Simulizi: Before I die

Simulizi: Before I die

Mkuu LEGE habari za J'pili, mbona ratiba ya hii kitu haieleweki ?
 
Niliwahi kuisoma kwenye blog moja hivi, lkn aliishia njiani, nadhani hapa itafika hadi mwisho, ni story nzuri sana, hasa kwa upande wa Latoya kwani maisha yake hayaeleweki
 
leo kumbe nimewasahau daa kuna kitabu nakisoma ndio kimefanya j2 iwe mwanana kabisaaaa ngoja niwafanyie mpango
 
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 21
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Wazo zuri sana hilo dada Latoya.Nina imani hata Innocent ataliunga mkono.” Grace akasema
“kama tumekubaliana wote iwe hivyo ,basi mimi nianze maandalizi mapema iwezekanavyo..Kuna kampuni ya rafiki yangu mmoja nitaikodisha ili isimamie shughuli yote ya msiba huu.”
“ahsante sana dada latoya .Utakuwa umemsaidia sana Innocent” Sabrina na Grace wakasema kwa pamoja.
“Je kuna haja ya kuwataarifu wazazi wake kuhusiana na hili? Latoya akauliza
“dadaLatoya sidhani kama litakuwa ni jambo la busara kuwashirikisha wazazi wake kwa sababu toka mwanzo hawakuwa wamemkubali Marina kwa hiyo naamni hata Innocent asingependa kuwashirikisha katika suala la msiba.” Grace akasema
Bila kupoteza muda Latoya akachukua simu yake na kuanza kuwapigia simu watu mbali mbali akiwafahamisha kuhusiana na msiba ule.Akatoa malekezo kadhaa juu ya maandalizi ya msiba ule ambao alitaka ufanyike nyumbani kwake.


ENDELEA……………………………

Masaa manne yamepita toka Innocent alipozinduka.Baada tu ya kupata fahamu alikuwa ni kama mtu aliyechanganyikiwa na madaktari wakawasihi ndugu zake kuwa na utulivu kwa sababu hiyo ni hali ya kawaida.Innocent akaachwa apumzike ili akili yake itulie na baada ya saa nne akafumbua macho.Chumba kilikuwa na harufu kali ya dawa.Akapepesa macho na kugundua pale palikuwa ni hospitali.Akaanza kuvuta kumbu kumbu na kujiuliza alifikaje fikaje pale hospitali.Mara akakumbuka kwamba ilikuwa afanyiwe upasuaji wa kundoa figo ili awekewe Marina.Tayari kumbu kumbu zote zikarudi.Kitu kilicho mstaajabisha hakuwa akisikia maumivu yoyote ya sehemu iliyopasuliwa .Akanyoosha mkono wake na kugusa sehemu za tumbo lakini hakukuwa na dalili zozote za kupasuliwa.Akastuka akainuka na kukaa kitandani,akajifunua shuka akatazama mwili mzima hakukuwa na sehemu yoyote ile iliyokuwa imepasuliwa.Akainama na kukishika kichwa chake kwa mikono yake .
“Hivi ni kweli au nilikuwa ndotoni? Ninachokumbuka mara ya mwisho nilikuwa katika chumba cha upasuaji nikisubuiri kufanyiwa operesheni.Nini kimetokea? Am I crazy? …No ! No ! I’m not crazy.Akili yangu inafanya kazi vizuri.Nilitakiwa kufanyiwa operesheni kwa ajili ya kumuwekea figo Marina.Yes Marina.! Where is she? “Innocent akawaza huku jasho likimtiririka na mara akaingia muuguzi.
“Marina yuko wapi? Mbona sijafanyiwa upasuaji?” Inno akauliza maswali haraka haraka
“Innocent tafadhali endelea kupumzika.mwili wako bado hauna nguvu za kuitosha.tafadhali endelea kupumzika”
“Nesi akili yangu inafanya kazi vizuri na ninakumbuka mara ya mwisho nilikuwa katika chumba cha upasuaji nimelala nikisubiri kupasuliwa.Niambie nini kilitokea? Ni kwa nini sikufanyiwa upasuaji? Innocent akauliza kwa sauti kubwa ambayo ikawafanya ndugu zake waliokuwa wamekaa nje wakisubiri arejewe na fahamu waiingie mle chumbani.Innocent akastuka baada ya kuwaona wazazi wake wakiwa wameambatana na akina Grace na Sabrina.Mtu wa mwisho kuingia mle chumbani alikuwa ni Latoya.Innocent hakusita kuachia tabasamu baada ya kugonganisha macho na Latoya.
“Latoya umekuja? Akasema Inno
“Niko hapa Innocent na akina Grace ,Sabrina na wazazi wako.” Latoya akasema
“Ninashukuru sana.” Akasema huku akiwaangalia akina Grace na Sabrina waliokuwa wamekaa pembeni ya kitanda chake.
“Unajisikiaje sasa hivi? Mama yake akauliza
“najisikia vizuri kwa sasa.lakini ninachoshangaa ni kwa nini sijafanyiwa upasuaji wakati tayari nilikuwa katika katika chumba cha upasuaji nikisubiri kupasuliwa? Inno akauliza
“Innocent kuna mambo yalitokea ndiyo yaliyopelekea hadi kushindwa kufanyika operesheni .” baba yake Innocent akasema
“baba nini kimetokea? ….where is…..yuko wapi Marina? Inno akauliza kwa wasi wasi
“Inno tafadhali jitahidi uwe na moyo mgumu lakini huna budi kufahamu kwamba Marina amefariki dunia muda mfupi kabla ya kufanyika operesheni” baba yake Innocent akasema.Innocent akacheka kidogo na kusema
“No! That’s not true….Siyo kweli.Eti Grace ni kweli Marina amefariki dunia?
Grace akashindwa asema nini machozi yakamtoka. Inno akamgeukia Latoya.
“latoya niambie ni kweli Marina amefariki dunia?
Latoya akasita aseme nini akajikaza na kutikisa kichwa.
“Ni kweli Innocent.Maria amefariki dunia.”
Inno akayafunika macho yake kwa viganja vya mikono yake na kuinama.
“Ouh Marina ! “ akasema kwa uchungu.
Chumba chote kikawa kimya kabisa.Hali ikawa ni ya simanzi kubwa.mara daktari akaingia akiwa ameongozana na muuguzi.
“Dokta tafadhali naomba nipeleke nikamuone Marina.” Inno akasema kwa haraka huku macho yake yamejaa machozi
“Innocent tafadhali endelea kupumzika hadi hapo mwili wako utakapopata nguvu za kutosha.” Daktari akasema.
“Daktari naomba tafadhali nipeleke nikamuone marina.” Inno akasisitiza
Daktari akawaomba wale wote waliokuwamo mle chumbani watoke na wamuache yeye na Innocent.
“Inno nasikitika sana kwamba pamoja na jitihada zote zilizofanyika lakini hatukuweza kuyaokoa maisha ya Marina.Alifariki muda mfupi kabla ya kuanza kufanyika kwa operesheni.” Dokta akasema
“Ouh Marina I’m so sorry.Pamoja na jitihada zote lakini bado umepoteza maisha.” Inno akasema kwa uchungu.
“Innocent,kila lililohitajika kufanyika ,lilifanyika kwa hiyo naomba usijilaumu sana.Mungu alipenda iwe hivyo” daktari akasema
“Dokta naomba unipeleke nikamuone Marina” Inno akasisitiza.Daktari akamtuliza na kumweleza kwamba muda ule haukuwa muafaka kwa yeye kwenda kuiona maiti ya Marina hadi hapo baadae.Daktari akaondoka na kumuacha Inno pale kitandani
“Its because of them.Its because of you mom and daddy .Ninyi ndio mliosababisha kifo cha Marina...” Inno akasema kwa hasira baada ya kufungua mlango wa kile chumba na kuwakuta wazazi wake wamekaa katika viti pale nje
“Ninyi ni wazazi wangu nawapenda na kuwaheshimu sana lakini katika suala hili nawaomba mniache peke yangu.Niacheni mimi nikamzike Marina mwenyewe kwa sababu kama hamkutaka kumuona akiwa hai iweje muonyeshe huzuni wakati amefariki ? Naomba niwaambie wazazi wangu kwamba nimeumia sana.Kitendo cha kumkataa,kumdharau,na kumnyanyapaa Marina kimenisababishia jeraha kubwa moyoni mwangu.”Inno akasema kwa sauti ya juu na kumlazimu Latoya ainuke na kumfuata akamsihi aingie ndani na kutulia.


* * * *

Saa moja za jioni hali ya Innocent ilikuwa ya kuridhisha na madaktari walimruhusu arejee nyumbani.Alikuwa mkimya sana tofauti na alivyozoeleka.Kifo kile cha Marina kilimletea jeraha kubwa moyoni mwake.Mara tu Innocent alipopimwa na madaktari na wakathibitisha kwamba kwa sasa hali yake ni nzuri na anaweza kurudi nyumbani Latoya akaingia mle chumbani na kuketi karibu naye
“Inno pole sana.Naomba utambue kwamba tuko pamoja katika msiba huu.Huu ni msiba wetu sote na wote tumeguswa.Jipe moyo Innocent “ Latoya akasema huku amemshika mkono
“latoya nashukuru sana kwa ushirikiano wenu.Kifo cha Marina kimeniuma sana.Nilipambana kuyaokoa maisha yake lakini Mungu alimpenda zaidi” Inno akasema na kisha akatazama chini akakaa kimya
“Innocent kuna jambo nataka kukufahamisha.” Latoya akasema na kumfanya Innocent ainue kichwa chake kumsikiliza
“Nimeshauriana na Sabrina na Grace na kwa pamoja tumekubaliana kwamba kwa kuwa Marina hakuwa na ndugu yeyote hapa mjini basi shughuli zote za msiba zitafanyikia nyumbani kwangu na gharama zote zitakuwa ni juu yangu.Nilielezwa kuhusu matatizo yaliyotokea kule nyumbani kwenu hivyo tukaona halitakuwa jambo zuri kama msiba huu wa Marina utapelekwa pale kwenu.Tayari maandalizi ya msiba yameanza .Kuna kampuni ambayo nimeikodisha isimamie shughuli nzima ya msiba huu .Nimeona nikufahamishe mapema ili ufahamu nini kinachoendelea kwa sasa. “
Inno akamtazama Latoya ,halafu akasema.
“Latoya sijui hata niseme nini kwa jambo kubwa ulilolifanya.Napenda tu ufahamu kwamba toka ndani kabisa mwa moyo wangu ninasema ahsante sana kwa msaada huu mkubwa.Marina hakuwa na ndugu yeyote hapa mjini kwa hiyo hakuna mahala kokote ambako tungeweza kuupeleka msiba huu.Nashukuru kwa kujitolea shughuli za msiba huu zifanyike nyumbani kwako kwani nilikuwa naumiza kichwa mno kuhusu wapi ningeupeleka msiba huu.Nyumbani kwetu ni kama hivyo ulivyosikia,niliondoka baada ya kutopendezwa na mambo aliyofanyiwa Marina.Pamoja na hayo naomba niseme samahani sana Latoya kwa usumbufu huu mkubwa ulioupata.” Innocent akasema .Latoya akamwangalia kwa makini halafu akasema
”Innocent naomba uondoe hofu moyoni mwako.Hakuna usumbufu wowote utakaotokea.Nimeamua kwa dhati ya moyo wangu kuupeleka msiba huu nyumbani kwangu kwa sababu si msiba wako peke yako bali ni wetu sote.Sote tumeguswa sana na msiba huu .Marina alikuwa ni rafiki yako na kwa maana hiyo ni rafiki yetu vile vile.Nakuomba uwe na amani ya moyo Innocent na wala usitie shaka.Jiandae ili tuweze kuondoka hapa hospitali na kuelekea nyumbani kwangu ambako shughuli za msiba zinaendelea hivi sasa.”Latoya akasema
“Sijui nikushukuruje Latoya.Naomba ufahamu kwamba nina deni kubwa kwako la kurudisha fadhila hii kubwa .” Inno akasema
“Innocent tafadhali usiwaze kuhusu hilo.Sisi kama marafiki tuna jukumu la kusaidiana katika kila hali.tafadhali jiandae ili tuondoke hapa ukapumzike wakati taratibu nyingine zikiendelea” Akasema latoya kisha akatoka nje ya kile chumba na kumuacha Innocent akijiiandaa.Wazazi wa Innocent bado walikuwa pale nje na walipomuona Latoya ametoka mle ndani ya chumba wakamuita .
“Mwanangu sisi ni wazazi wake Innocent,hebu tuambie mwenzio anaendeleaje?’ mama Inno akauliza
“Anaendelea vizuri mama .Kwa sasa anajiandaa ili tuondoke hapa na kwenda kuendelea na shughuli za msiba.”
“Amesema shughuli za msiba zitafanyikia wapi? Huyu binti Marina alikuwa na ndugu zake hapa mjini? Baba yake Inno akauliza
“Marina hakuwa na ndugu hapa mjini kwa maana hiyo tumeafikiana kwamba msiba utakuwa nyumbani kwangu.” Latoya akasema na mara akatokea Sarah dada yake Innocent akakuta Latoya akiongea na wazazi wake.Akastuka sana na kusimama ghafla akaufumba mdomo wake kwa mkono wake wa kulia.Alikumbwa na mstuko wa ghafla.Latoya akageuka na kwa hatua za taratibu akaondoka zake na kuwaacha wazazi wa Innocent wakiwa kimya.
“Mama sikuweza kupata nafasi ya kufika hapa mapema.Uliponipigia simu na kunitaarifu kuhusu suala hili la Innocent nilikuwa Morogoro .Nimerudi sasa hivi nikaona ni bora nije moja kwa moja hapa hospitali.Innocent anaendeleaje? Akauliza Sarah kwa wasi wasi
“Mdogo wako anaendelea vizuri kwa sasa na tayari amepewa ruhusa ya kuondoka baada ya madaktari kuhakikisha kwamba hali yake ni nzuri.Kwa bahati mbaya yule binti aliyekuwa akimtolea figo alifariki kabla ya upasuaji kufanyika kwa hiyo Inno hakufanyiwa upasuaji wowote.” Mama yake akasema
“ Ouh ahsante Mungu ! “ Sarah akasema lakini bado sura yake ilionyesha mstuko
“Mbona umestuka?” Baba yake akauliza
“Nimestuka kusikia kwamba yule msichana amefariki dunia.Baba hivi hamuoni ni matatizo kiasi gani yanakwenda kutokea baada ya huyo binti kufariki ? Moyoni mwake tayari Innocent amejenga picha mbaya sana kwa ninyi kukataa yule msichana akae pale nyumbani.Atawalaumu sana na kusema kuwa mmechangia kifo chake .Ninamfahamu Inno vizuri,kifo hiki kitakuwa kimemuumiza mno.Lakini nashukuru kwa operesheni hii kutofanyika kwa sababu hata mimi sikuona sababu ya yeye kuamua kutoa figo yake kwa ajili ya msichana asiyemfahamu na tena kahaba.Angeidhalilisa sana familia yetu..” Sarah akasema
“Tayari amekwisha sema hilo na amesema kwamba sisi ndio tuliosababisha kifo cha binti yule.” Mama yake Inno akasema na kumtazama binti yake.
“Mama yule msichana mliyekuwa mkiongea naye hapa mnamfahamu? Sarah akawauliza wazazi wake.
“hapana hatumfahamu lakini kwa mujibu wa Grace ni kwamba yule ni rafiki wa Innocent na ndiye aliyempatia kazi Sabrina katika taasisi yake.Kwani vipi mbona unaonyesha wasi wasi na kustuka mara ulipomuona ? Mama Innocent akauliza
“Mama kwa taarifa yenu yule ndiye Latoya .Ni msichana bilionea mdogo kabisa afrika mashariki .Ni nadra sana kumuona mtu kama huyu sehemu kama hii na ndiyo maana nimestuka baada ya kumkuta hapa akiongea nanyi.Ni mtu anayeheshimika kupita maelezo kutokana na utajiri wake mkubwa. kinachowaumiza watu vichwa hadi leo hii ni wapi alikopata utajiri wake? Watu wanasema utajiri wake ni wa kichawi,wengine wanamuhisi kuwa mfuasi wa imani ya freemason ,wengine wanasema kwamba anaishi na jini ambalo huwa linampatia fedha kwa sababu hajawahi kuonekana na mwanaume yoyote na wala hajulikani kama ana mpenzi.Kwa muda mrefu watu wamekuwa wakijitahidi kuutafuta undani wake bila mafanikio.Hata wazazi wake waliwahi kuhojiwa na wakakiri kwamba hawafahamu mtoto wao aliupataje pataje utajiri mkubwa kiasi hiki.Hapo alipo anatembea na siri kubwa ya maisha yake.Nimeshangaa leo imetokea nini hadi awepo mahala hapa mida hii tena akiwa huru bila walinzi wake kwa sababu kila mahala anakoenda huwa ameongozana na walinzi wake.Ana ulinzi mkali mno na ndiyo maana nimestuka kumuona hapa hospitali akiwa peke yake ” Sarah akasema huku moyo ukimuenda mbio.Wazazi wake nao wakabaki wameduwaa
“Sarah unayoyasema ni ya kweli? Huyu Latoya niliyemsikia hivi majuzi kwamba amejenga nyumba mia moja na hamsini kama msaaada kwa waathirika wa mafuriko ndiye huyu?“ baba yake akauliza kwa mshangao
“Ndiye huyu mliyekuwa mkiongea naye baba.” Sarah akajibu huku ameyakaza macho yake akimtazama Latoya aliyekuwa amesimama akiongea na Sabrina na Garce.
“Unbeliavable !! Baba yake Innocent akasema huku akijishika kiuno.
“Baba.Latoya ni mtu adimu sana kuonekana hasa sehemu kama hii.Sidhani hata kama uongozi wa hospitali hii unafahamu kuhusu kuwepo kwa mtu kama huyu hapa hospitali” Akasema Sarah huku akiitoa simu yake katika mkoba wake mdogo
“Wakati tukiwa pale katika chumba cha upasuaji tukisubiri operesheni ifanyike alitokea mkurugenzi wa hospitali hii ambaye alimnyenyekea sana na kumtaka akakae sehemu iliyotengwa maalum kwa kupumzika watu mashuhuri.Sasa ndiyo napata picha kamili ni kwa nini mkurugenzi yule alionyesha heshima kubwa mbele ya msichana huyu mdogo” baba yake Innocent akasema
“Hii tayari ni habari.Ngoja niwapigie simu waandishi wenzangu ndipo mtakapoamini ninachokisema ” Sarah akasogea pembeni na kwa sauti ndogo kuogopa asisike akawapigia simu waandishi wenzake wa habari na kuwataarifku kwamba Latoya yuko pale hospitali na hana wale walinzi wake ambao huwa wanawazuia kumpiga picha au kumuuliza maswali
“Baba hii ni habari kubwa sana.Ninyi bado hamjafahamu mlikuwa mkiongea na mtu wa namna gani.Nadhani hata Inno bado hajafahamu huyo rafiki yake ni mtu wa namna gani.Kumuona Latoya ni zaidi ya kuonana na Rais.Kuwa karibu naye tu ni bahati kubwa.Nataka wapiga picha wawahi kumchukua picha akiwa na Innocent.Kitendo cha kuonekana wakiwa pamoja hapa hospitali kitamuweka Innocent katika daraja la juu mno.Magazeti yote siku ya kesho yatapambwa na picha hizo.Hata mimi sikuwa na wazo kama iko siku nitasimama karibu na Latoya Sielewi hata Sabrina alipataje kazi kwa Latoya? “Sarah akasema
“Nimekumbuka.Latoya ana taasisi yake ambayo inashughulika na masuala ya kusaidia wanawake hususan wale wenye maradhi ya kansa na kupitia taasisi hiyo mamia ya akina mama wanasaidiwa na kupona kabisa.Nadhani ilikuwa rahisi kwa Sabrina kupata kazi pale kwa kuwa ni mlemavu wa ngozi.Namuonea wivu sana kwani kwa sasa maisha yake yameshabadilika.Angalia anavyoongea na Latoya kama rafiki yake wa kawaida tu wakati mtu huyu ananyenyekewa hata na marais.Nasikia uchungu sana kwa mtu kama yeye ambaye alikuwa msichana wa kazi za ndani leo hii anaongea na kucheka na mtu mzito kama Latoya.Ama kweli maisha yanaweza kubadilika wakati wowote ule .Hili ni funzo kwamba katika haya maisha usimdharau mtu yeyote kwa sababu huwezi kujua kesho yake itakuwaje.” Sarah akawaza.Alionekana kama ni mtu aliyechanganyikiwa .Kila mara alikuwa akichukua simu yake na kuwapigia wenzake na kuwauliza kwa nini walikuwa wanachelewa.
“Mama hapa hospitali Latoya alikuja na nani? Sarah akauliza
“sisi tumekuja na kumkuta hapa akiwa na Sabrina.Nadhani ni yeye ndiye aliyemleta.” Mama yake akasema.Wote walikuwa wameyaelekeza macho yao kwa Latoya wakimshangaa wakasahau kabisa kuhusu Innocent.
“Kwa maana hiyo kutwa nzima ya leo ameshinda hapa? Latoya akauliza
“Ndiyo ameshinda hapa tena sijamuona hata akiinuka na kwenda kutafuta hata maji ya kunywa.Tumekuwa naye pale mlangoni tukimsubiri Innocent na mpaka muda huu bado yupo hapa hospitali” mama yake akasema
“kama kutwa nzima ya leo ameshinda hapa ina maana basi urafiki wao ni mkubwa.Ninavyofahamu Latoya ni mtu mwenye shughuli nyingi na hivyo asingeweza kuvunja ratiba yake ya siku na kuja hapa hospitali tena bila walinzi kama Innocent si mtu wake wa muhimu.Lakini ninachojiuliza ni kwamba huo urafiki wao umeanza lini? Innocent hajawahi kunieleza kama amewahi kukutana na Latoya.Nitamuuliza Innocent anieleze ukweli” Akawaza Sarah akiwa bado amemkazia macho Latoya.

TUKUTANE SEHEMU IJAYO………
 
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 22
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Mama hapa hospitali Latoya alikuja na nani? Sarah akauliza
“sisi tumekuja na kumkuta hapa akiwa na Sabrina.Nadhani ni yeye ndiye aliyemleta.” Mama yake akasema.Wote walikuwa wameyaelekeza macho yao kwa Latoya wakimshangaa wakasahau kabisa kuhusu Innocent.
“Kwa maana hiyo kutwa nzima ya leo ameshinda hapa? Latoya akauliza
“Ndiyo ameshinda hapa tena sijamuona hata akiinuka na kwenda kutafuta hata maji ya kunywa.Tumekuwa naye pale mlangoni tukimsubiri Innocent na mpaka muda huu bado yupo hapa hospitali” mama yake akasema
“kama kutwa nzima ya leo ameshinda hapa ina maana basi urafiki wao ni mkubwa.Ninavyofahamu Latoya ni mtu mwenye shughuli nyingi na hivyo asingeweza kuvunja ratiba yake ya siku na kuja hapa hospitali tena bila walinzi kama Innocent si mtu wake wa muhimu.Lakini ninachojiuliza ni kwamba huo urafiki wao umeanza lini? Innocent hajawahi kunieleza kama amewahi kukutana na Latoya.Nitamuuliza Innocent anieleze ukweli” Akawaza Sarah akiwa bado amemkazia macho Latoya.

ENDELEA…………………………

Mlango wa chumba ukafunguliwa na Innocent akajitokeza.Alikuwa akitembea kwa uchovu .Alionekana kudhoofika sana,hii ilitokana na kwamba hakuwa ametia kitu chochote tumboni kwa siku nzima .Kwa haraka Latoya akamfuata na kumshika mkono wakaanza kutembea hatua za taratibu.
“Innocent pole sana.Nimefika sasa hivi nilikuwa Morogoro.Unajisikiaje sasa?” sarah akasema akiwa na uso wenye simanzi
“Naendelea vizuri Sarah.Nashukuru kwa kuja kuniona.” Inno akasema.
“Vipi kuhusu msiba wa marina? Umepanga vipi?
“ Shughuli zote za msiba zitafanyikia nyumbani kwa Latoya ila mahali tutakapomzika bado hatujaamua ni wapi.Nitakufahamisha kila kitu kesho asubuhi ila kwa sasa naomba uniache nikapumzike.” Inno akamwambia sarah.
Kabla hawajaondoka watu watano wenye asili ya kihindi wakiwa na madaktari wawili waliokuwa wamevaa mavazi yao ya kidaktari wakafika eneo lile kwa kasi.Miongoni mwao alikuwa ni mkurugenzi wa hospitali ile Dr Rajiv.Moja kwa moja Dr rajiv akaenda kumpa mkono Latoya .
“Latoya pole sana kwa kilichotokea.Toka nilipoonana nawe mchana nilikuwa mkutanoni na nilipotaarifiwa kwamba operesheni ile ya ndugu yako haikufanikiwa na yule mgonjwa aliyetakiwa kuwekewa figo amefariki dunia nilistuka sana na ikanilazimu kutoka ndani ya kikao na kuja hapa haraka kukupa pole.Pole sana kwa tukio hili” Dr Rajiv akasema huku akiwa bado ameushikilia mkono wa Latoya kwa heshima kubwa.
“nashukuru sana Dr Rajiv.Huyu ndiye ndugu yangu ambaye alikuwa amejitolea figo yake.hali yake inaendelea vizuri na madaktari wamesema tunaweza kuondoka naye na sasa ndiyo tunaondoka ili walau akapate muda wa kupumzika”
Rajiv akamshika mkono Innocent
“Pole sana.You are so brave.Pole sana kwa jambo lililotokea” Rajiv akasema huku akimpiga piga begani Innocent halafu akaendelea na kuwapa mikono ya pole watu wengine.Wale wenzake aliokuja nao vile vile wakafanya kama alivyofanya Dr Rajiv yaani wakatoa pole zao kwa kila mtu pale na kisha safari ya kuelekea nje mahala yanakoegeshwa magari ikaendelea.Dr Rajiv ndiye aliyeufungua mlango wa gari la Latoya akaingia ndani halafu akaufungua mlango mwingine Innocent akaingia halafu akawafungulia tena milango Grace na Sabrina wakaingia garini.
“Latoya kesho asubuhi na mapema nitafika nyumbani kwako ili kuangalia namna tutakavyosaidiana katika shughuli nzima ya msiba na mazishi.Msiba huu ni wetu sote.” Dr Rajiv akasema akiwa amesimama katika dirisha la gari la Latoya.Innocent akashangazwa sana na kitendo kilichofanywa na Dr Rajiv mkurugenzi wa hospitali ile kubwa.Heshima aliyoionyesha kwa Latoya ilikuwa kubwa na kumfanya ajiulize ni kwa nini ilikuwa vile.
“nashukuru sana Dr Rajiv.Tutaonana hiyo asubuhi” Latoya akasema na kuliwasha gari lake akageuza na kuondoka eneo la hospitali.Wote walibaki wamesimama wakilitazama gari lile likiondoka hadi lilipofutika kabisa machoni pao.Dr Rajiv akaongozana na watu wake wakaelekea ndani ambako kwa haraka wakakaa kikao cha dharura ili kuangalia namna watakavyoshiriki katika msiba ule wa marina .Wazazi wa Innocent nao wakaingia katika magari yao na kuondoka.
Dakika chache baada ya gari la Latoya kuondoka wakafika waandishi wa habari wakiwa tayari na vifaa vyao ili kuweza kumpiga picha Latoya lakini walikwisha chelewa.Walijilaumu sana kwa kuikosa habari ile kubwa.


* * * *

Baada ya kutembea dakika thelathini katika barabara iliyokuwa kandoni mwa bahari wakaiacha barabara hiyo na kuifuata barabara iliyoelekea kushoto na kutembea kwa dakika kumi kisha taratibu gari la Latoya likapunguza mwendo na kusimama katika geti kubwa lililokuwa likilindwa na walinzi wanne na wawili kati yao wakiwa na silaha.Haraka haraka geti likafunguliwa na gari likaingia ndani.Walinzi wale wote wanainua mikono yao na kupiga saluti wakionyesha heshima .Latoya hakuwajali akakanyaga mafuta kuelekea ndani.Barabara ile ya lami ilikuwa imezungukwa na taa kubwa kila upande na kuifanya mandhari ya mahala pale ionekane kama mchana .Vile vile kulikuwa na miti na maua ya kupendeza.Toka pale getini kulikuwa na msitu wa miti mizuri ya kupendeza .Dakika kama tano za kutembea ndani ya msitu ule wenye kupendeza hata kwa usiku wakatokea katika mzunguko mkubwa uliokuwa na sanamu kubwa ya mtu iliyozungukwa na maua ya kupendeza na maji yaliyokuwa yakiruka juu na kuzidi kutia nakshi mzunguko ule.Haikuwa taabu kuweza kuitambua sanamu ile hata kwa usiku kwa sababu sura ya mtu iliyoonekana katika sanamu ile ilikuwa ni ya Latoya.Umbali wa kama mita mia tatu toka pale katika mzunguko likaonekana jumba kubwa la ghorofa lililokuwa likiwaka taa na kulifanya ling’ae .Toka kwa mbali jumba hili lilionekana kama kasri la kifalme.Innocent alikuwa akiustaajabia uzuri wa mahala hapa na kujiona kama yuko ndotoni.Japokuwa ni usiku lakini taa zilizokuwa zikimulika jumba hili zilipafanya paonekane kama mchana.Taratibu wakaanza kulikaribia jumba lile na mara wakalifikia kabisa.Katika uwanja mkubwa uliokuwa mbele ya jumba lile magari zaidi ya mia moja yalikuwa yameegeshwa.Latoya akaliingiza gari ndani ya nyumba yake ambako ana sehemu yake maalumu ya kuegesha magari yake.Gari nane za kifahari mno zilikuwa ndani ya gereji ile.Kwa Innocent ,Grace na Sabrina yalikuwa ni mambo ya kustaajabisha mno.Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Innocent kuona jumba kubwa na la kifahari kama lile nchini Tanzania.Majumba ya kifahari kama hili alizoea kuyatazama katika picha zitokazo huko falme za kiarabu katika makasri ya kifalme .
“Innocent karibu nyumbani kwangu.” Latoya akasema baada ya kushuka garini.
“Ahsante sana Latoya” Innocent akasema.Latoya akawageukia Grace na Sabrina akawaambia
“Grace,Sabrina karibuni sana hapa ni nyumbani kwangu”
“Ahsante sana “ Wakajibu kwa pamoja na kisha wakaanza kutembea wakimfuata.Latoya.Mlangoni alikuwepo kijana mmoja aliyekuwa amevaa mavazi meusi amesimama kwa adabu.
“Pole sana Madam” akasema kijana yule na kuufungua mlango,wakatembea katika varanda kubwa lenye picha na nakshi za kupendeza na mara wakajikuta wametokeza katika sebule moja kubwa lenye samani za gharama kubwa mno zilizonakshiwa kwa dhahabu.Innocent hakusita kuonyesha mshangao wake.Kila alichokiona katika jumba hili kilimfanya ashangae sana..Pale sebuleni walikuwepo wasichana wawili wazuri waliovaa mavazi meusi.Kwa heshima kubwa wakampa pole Latoya.Mambo haya yote yalikuwa yakimshangaza sana Innocent.Alihisi kama vile yuko katika ndoto nzuri lakini aliyoyaona yalikuwa ni kweli .Latoya akawakabidhi Sabrina na Grace kwa wasichana wale wahudumu ili wawahudumie halafu yeye na Innocent wakaelekea kushoto ambako kulikuwa na chumba cha lifti wakapanda hadi ghorofa ya nne ambayo ndiyo ya mwisho wakashuka na Innocent akaendelea kumfuata Latoya ambaye hakuwa akiongea jambo lolote.
Wakasimama nje ya mlango wa chumba kimoja ambacho Latoya akakifungua na kuingia ndani akakikagua na kisha akamuita Innocent.
“Innocent hiki ni chumba ambacho kimeandaliwa kwa ajili ya wewe kupumzika.Kwa kuwa kuna wageni tayari wamefika kuungana nasi katika msiba huu nakuomba ujiandae,ujiweke safi kisha tutakwenda kuwasalimu wageni halafu utarudi kupumzika.Nafahamu umechoka lakini wengi wa wageni wangependa kukupa pole.Ukisha jimwagia maji,tayari kuna nguo ziko kabatini maalum kwa ajili ya msiba huu utavaa kisha utapiga namba 277 katika simu ile pale mezani na nitafahamu kwamba tayari umeshajiandaa na kisha tutapata chakula chepesi kabla ya kwenda kuonana na baadhi ya waombolezaji ambao wamekwisha fika muda mrefu wako bustanini wakitusubiri..” Latoya akamwambia Innocent.Innocent alibaki amepigwa na butwaa asiamini kile kilichokuwa kinaendelea ni kweli au alikuwa ndotoni.
“Hapana siko ndotoni . Haya mambo yote ni kweli nayashuhudia.Latoya huyu ndiye Yule bilionea niliyewahui kumsikia nikiwa marekani? Inawezekana akawa ni mwenyewe kwani utajirihuu alionao si wa kawaida.Nina wasi wasi huyu anaweza akawa si binadamu wa kawaida.Huyu anaweza akawa ni moja kati ya viumbe vya kiroho.Sijawahi kuona jumba kubwa kama hili tena lenye samani za gharama kubwa namna hii.Majumba kama haya nimezoea kuyaona katika picha zitokazo nje ya nchi na hususani falme za kiarabu ambako kuna makasri makubwa ya kifalme kama hili.Jumba hili ni moja kati ya majumba ya maajabu katika Tanzania.Sasa ninapata picha ni kwa nini yule mkurugenzi wa hospitali ile Dr Rajiv alikuwa akimnyenyekea Latoya kupita kiasi.Kitendo kile kilinifanya nijiulize maswali mengi kulikoni hali hii lakini kumbe alifahamu alikuwa anaongea na nani.Halafu kitu kingine cha kushangaza ni gari za kifahari tulizozikuta zimeegeshwa hapo nje ambazo kwa madai yake ni kwamba zote zile ni za watu waliokuja kwenye msiba.Watu wote hawa wamekuja kutokana na heshima yao kwa Latoya.Iweje binti mdogo kama huyu aheshimiwe namna hii? Gari tulizozikuta katika gereji yake zilikuwa ni gari za kifahari mno,mambo haya yote yananifanya nijiulize maswali mengi juu ya binti huyu .Latoya ni nani hasa? Utajiri wote huu ameutoa wapi? Akawaza Innocent na kuvuta pumzi ndefu
“Sikuwahi kumuona hapo kabla.Nimefahamiana naye leo asubuhi baada ya kuelekezwa na Sabrina ambaye sifahamu alikutana vipi na Latoya hadi akapatiwa kazi na wakawa marafiki . Nikiwa ofisini kwake niliongea naye kwa muda mfupi nikapigiwa simu kwamba hali ya Marina imebadilika ,nikaachana naye na kukimbia hospitali.Nilivyoongea naye nilitambua alikuwa ni mtu mcheshi na mwenye roho ya ukarimu na kusaidia.Hicho ndicho kitu pekee ninachokifahamu kuhusu Latoya.Alikuwa ameahidi kunisaidia kutafuta figo kwa ajili ya Marina.” Akaendelea kuwaza Innocent.
“ Bado nina mashaka na siamini kama jumba hili ni la kwake kama anavyodai.Ninavyofikiri jumba hili litakuwa ni mali ya wazazi wake ambao aidha wanaishi ulaya au wameshafariki na kumrithisha utajiri huu mkubwai.Au kama si hivyo basi atakuwa na mume tajiri sana ambaye amemjengea kasri hili.Kumiliki jumba kama hili na magari ya kifahari kama yale si kitu kidogo.Lazima uwe bilionea.Kama ni kweli vyote hivi ni mali yake,yawezekana kweli Latoya akawa ndiye Yule bilionea niliyewahi kumsikia akitajwa katika vyombo vya habari vya Marekani.Kinachonishangaza ni kwa nini bilionea kama huyu aamue kuacha shughuli zake na kuja kukaa na ndugu zangu hospitali hadi usiku huu? Zaidi ya yote ameamua yeye mwenyewe kubeba jukumu zima la msiba wa Marina.Nini nimemfanyia na kumfanya afanye yote haya aliyoyafanya? Nashindwa kupata jibu ”
Innocent alikuwa amesimama akiwaza.Akakisogelea kitanda akalibonyeza godoro ili kuwa na uhakika kwamba ile haikuwa ni ndoto.Alikwisha anza kuwa na wasi wasi mwingi kuhusiana na Latoya.Akakaa kitandani
“Nimewahi kusimuliwa simulizi za zamani ambazo viumbe wa kiroho walikuwa wakiishi na binadamu .Nina wasi wasi Latoya anaweza akawa mmoja wao.Uzuri wake wenyewe unaogopesha.Ukiuangalia uzuri ule unaogopa hata kumsogelea.Macho yake mazuri meupe kama ya wale malaika ninaowaona katika picha mbali mbali.Ngozi yake laini na nyororo ambayo ukiitazama ni zaidi ya ngozi ya binadamu wa kawaida.Du ! kila kitu alicho nacho binti huyu kinastajaabisha na kushangaza.” Akawaza Inno kisha akakumbuka kwamba alitakiwa aoge li waelekee sehemu ya msiba akawasalimu waombolezaji waliokwisha fika baada ya kupata taarifa.Akafungua mlango na kuingia bafuni.Akafungua maji na kuweka mkono wake kwa wasi wasi.
“Kila kitu kilichopo ndani ya jumba hili kinanifanya niwe na wasi wasi mwingi.” Baada ya kufikiri kwa muda akapiga moyo konde na kuoga kisha akarudi chumbani akafungua kabati lile ambalo aliambiwa kumewekwa nguo za kuvaa.
“Pamoja na mambo yote haya ya ajabu ajabu sina budi kumshukuru Latoya kwa moyo wake wa ukarimu kwa kujitolea msiba huu ufanyike hapa nyumbani kwake.Kama si yeye sijui msiba huu ningeupeleka wapi.Sikuwa na mahala kokote ambako ningeweza kuupeleka msiba huu.Nitaendelea kumshukuru Latoya siku zote kwa jambo hili kubwa.” Akawaza Innocent wakati akilifungua kabati lile la nguo ambamo alikuta suti nyeusi kumi Zilikuwa ni suti mpya kabisa zikiwa ndani ya mifuko yake ya nailoni.Akaichukua moja na kuitoa ndani ya mfuko wake.Ilikuwa ni saizi ile ile ambayo huwa anavaa.Akashangaa sana.
“Kitu kingine cha kushangaza ni hiki hapa.Amejuaje kama ninavaa nguo za saizi hii? Ee Mungu nakuomba kama kuna jambo lolote ambalo si la kawaida linaloendelea hapa uniepushe nalo ..” akaomba kimoyomoyo huku akivaa suti ile iliyomkaa vyema.Akajiangalia katika kioo na kujiona jinsi alivyopendeza.Pembeni ya kabati lile kulikuwa na jozi tano za viatu vyeusi vipya kabisa.Alipovichunguza vyote vilikuwa ni saizi yake.Akachukua jozi moja na kuvaa.Akasimama akajiangalia na kuhakikisha yuko safi .Akaiendea simu na kubonyeza namba 277 kama alivyokuwa ameelekezwa na Latoya. Akauweka mkono wa simu sikioni.Ilikuwa ikiita
“Hallo Innocent” Ikasikika sauti laini ya Latoya
“Hallo latoya.Niko tayari”
“Sawa Innocent nakuja sasa hivi kukuchukua” akasema Latoya na simu ikakatwa.
“Sauti yake tu ukiisikia inakufanya mtu ubabaike hata kuongea.Ni mtu wa namna gani huyu? Innocent akazidi kuumiza kichwa chake na mara akasikia kengele ya mlangoni.Akaufungua mlango na kukutana na sura ya Latoya aliyekuwa amevaa kofia nyeusi ya mduara na gauni refu jeusi pamoja na koti jepesi jeusi lililomfika magotini.Usiku huu alizidi kuonekana mrembo na kumfanya Innocent astuke mara alipomuona.Simulizi zile za viumbe wa kiroho wanaoishi maisha ya kibinadamu iliendelea kumteza akili yake na hasa ukichukulia jumba lile la Latoya lilikuwa karibu na bahari
“Innocent kwa sasa tutaenda kwanza kupata chakula chepesi na kisha tutaelekea bustanini kuwasalimu waombolezaji ambao bado wanazidi kufika kwa wingi.Sielewi hata taarifa za msiba wanazipa wapi kwa sababu kuna watu wananipigia simu kunipa pole ambao hata sielewi wamejuaje kama tuna msiba.Wengi wangependa kukufahamu.Usistuke na wala usiogope kwa uwingi huu wa watu ,hawa wote ni rafiki zangu na watu wangu wa karibu .” Latoya akasema na kumshika mkono Innocent wakaelekea katika ukumbi wa chakula.Ulikuwa ni ukumbi mzuri ajabu uliokuwa umezungukwa na maua ya kila aina na taa za kupendeza.Meza kubwa ilizungukwa na viti kumi na mbili vyenye nakshi za dhahabu.Wahudumu wawili walikuwapo mle ukumbini .Wote walikuwa wamevalia suti nyeusi .Wakawakaribisha Latoya na Innocent.
“Akina Sabrina wako wapi? Latoya akamuuliza mmoja wa wale wasichana waliokuwa wakihudumia katika ukumbi ule.
“Jennifer amekwenda kuwachukua” akajibu yule msichana
Hata sekunde ishirini hazikupita wakatokea Sabrina na Grace wakiwa ndani ya suti nzuri nyeusi na kofia .Wakakaribishwa mezani na wahudumu wale wenye adabu .Innocent bado aliendelea kushangazwa na mambo yaliyomo ndani ya jumba lile.Latoya alikuwa akiheshimiwa kama malkia.
“Sabrina nomba utuongozee maombi ya chakula tafadhali.” Latoya akasema na wote wakafumba macho Grace akatoa maombi mafupi kukiombea chakula kile halafu Latoya akawakaribisha .
“Huyu hawezi kuwa kiumbe wa kiroho kama ninavyodhani kwani viumbe wale hawapendi maombi” akawaza Innocent huku akiweka chakula katika sahani yake
“Innocent hiyo ni pili pili samahani .Nafahamu kwamba hutumii pilipili kabisa” Latoya akamweleza Innocent mara tu alipomuona amelishika bakuli lililokuwa na pilipili iliyokuwa imetengenezwa vizuri.Innocent akashangaa na kuuliza huku aitabasamu
“Umejuaje kama situmii pili pili ?
Latoya akatabasamu na kusema
“Nilipewa vidokezo na Sabrina kwamba hutumii kabisa pilipili”
Wote wakaangua kicheko

TUKUTANE SEHEMU IJAYO……………
 
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 23
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Jennifer amekwenda kuwachukua” akajibu yule msichana
Hata sekunde ishirini hazikupita wakatokea Sabrina na Grace wakiwa ndani ya suti nzuri nyeusi na kofia .Wakakaribishwa mezani na wahudumu wale wenye adabu .Innocent bado aliendelea kushangazwa na mambo yaliyomo ndani ya jumba lile.Latoya alikuwa akiheshimiwa kama malkia.
“Sabrina nomba utuongozee maombi ya chakula tafadhali.” Latoya akasema na wote wakafumba macho Grace akatoa maombi mafupi kukiombea chakula kile halafu Latoya akawakaribisha .
“Huyu hawezi kuwa kiumbe wa kiroho kama ninavyodhani kwani viumbe wale hawapendi maombi” akawaza Innocent huku akiweka chakula katika sahani yake
“Innocent hiyo ni pili pili samahani .Nafahamu kwamba hutumii pilipili kabisa” Latoya akamweleza Innocent mara tu alipomuona amelishika bakuli lililokuwa na pilipili iliyokuwa imetengenezwa vizuri.Innocent akashangaa na kuuliza huku aitabasamu
“Umejuaje kama situmii pili pili ?
Latoya akatabasamu na kusema
“Nilipewa vidokezo na Sabrina kwamba hutumii kabisa pilipili”
Wote wakaangua kicheko

ENDELEA……………………………

“Jenniffer naomba mkaendelee na shughuli nyingine.Nina maongezi kidogo na ndugu zangu” Latoya akawaambia wale wahudumu waliokuwa wakiwahudumia .Wakaondoka na kwenda kuendelea na shughuli nyingine.
“Innocent,Sabrina na Grace,kwanza kabisa napenda kuchukua nafasi hii kutoa pole nyingi kwa msiba uliotokea.Naomba mfahamu kwamba msiba huu ni wetu sote .Marina alikuwa ni rafiki wa Innocent ambaye ni kaka yetu na rafiki yetu.Kwa maana hiyo Marina pia alikuwa ni rafiki yetu sote.Naomba msiendelee kusema kwamba Marina hakuwa na ndugu hapa mjini.Ndugu zake wapo.Ndugu zake ni sisi .Kwa bahati mbaya sote tumemfahamu katika nyakati za mwisho za uhai wake.Laiti kama tungeweza kufahamiana naye kwa muda mrefu kabla tungeweza kufanya kitu kikubwa cha kuweza kumsaidia.Ni mapenzi ya mungu iwe hivi kwa sababu juhudi zilizofanywa na Innocent ni kubwa lakini Mungu alimpenda zaidi.Napenda niwahakikishie kwamba marina atasitiriwa kwa heshima kubwa tofauti na alivyokuwa akiishi.” Latoya akatulia kidogo na kuchukua glasi ya juice akanywa kisha akasema
“Jambo la pili ninapenda sana kuwakaribisha nyumbani kwangu.Hapa ni nyumbani kwangu .Ndipo ninapoishi.Nafahamu nyote bado mnaogopa nadhani ni kutokana na ukubwa wa jumba hili.Tafadhali naombeni msiogope.Jisikieni nyumbani.Masaa ishirini na manne ukihitaji kitu chochote kile kuna wahudumu wa kuwahudumia.Ninafurahi mno kuwa nanyi hapa saa hizi .Hakuna awezaye kuona furaha ya kuwa nanyi.Ninyi ni ndugu zangu .Kwa kuwa bado tuko katika kipindi cha majonzi sitaki kuongea mengi kwani bado tuna mambo mengi sana ya kuongea baada ya kumaliza msiba.Narudia tena kuwaomba kwamba jisikieni mko nyumbani.” Latoya akanyamaza tena akanywa juice yake na kuendelea
“jambo la tatu ni kwamba baada ya kumaliza kupata chakula tutakwenda kuonana na kuwasalimu waombolezaji ambao ni rafiki zangu na watu wangu wa karibu ambao kwa sasa naomba muwahesabu ni moja ya marafiki zenu pia .Wote hawa wamekuja kuungana nasi katika kuomboleza msiba huu tulioupata.Wengi wao watakesha pamoja nasi siku ya leo na watakuwa nasi mpaka hapo tutakapohitimisha msiba huu.Nategemea siku ya kesho idadi ya watu kuongezeka zaidi kwa sababu taarifa hizi za kuwapo kwa msiba hapa nyumbani kwangu zinasambaa kwa kasi sana.Baada ya kukaa na waombolezaji kwa muda mfupi,tutarejea ndani ili Innocent aweze kupata muda wa kupumzika,lakini kabla ya kupumzika tutakaa na viongozi wa kampuni niliyowakabidhi kazi ya kushughulikia msiba huu ambao wanahitaji maelekezo kadhaa toka kwetu.Kuna baadhi ya mambo kadhaa ambayo yalikuwa nje ya uwezo wangu kuyatolea maamuzi.masuala kama ya imani ya dini,sehemu ambayo ingependelewa kwenda kumsitiri marehemu na maelekezo mengineyo kama yatakuwepo.Kwa hiyo sisi kama ndugu wa marehemu, tutakaa na viongozi wa kampuni ile na kuwaelekeza mambo hayo ikiwamo siku gani tungependelea kumzika marehemu” latoya akatoa maelekezo .
Baada a kumaliza kupata chakula Latoya akawaongoza kuelekea bustanini ambako shughuli za msiba zilikuwa zikiendelea.Muziki wa maombolezo uliokuwa ukiwafariji waombolezaji ulikuwa ukipigwa na bendi maalum iliyoletwa kwa ajili ya shughuli hiyo.Kwa mbali mawimbi ya bahari yalikuwa yakisikika.Upepo mzuri wa bahari ulikuwa ukivuma na kuelekea mahala iliko bustani ile nzuri iliyokuwa imepambwa kwa maua na miti mizuri.Pamoja na familia yao kuwa na uwezo mkubwa wa kifedha lakini Innocent hakuota hata siku moja kama kuna watu hapa nchini Tanzania wanaishi maisha kama aliyoyaona hapa kwa Latoya.Bado aliendelea kushangazwa na kila kitu alichokiona.
“Ndugu waombolezaji,mabibi na mabwana watu tuliokuwa tukiwasubiri tayari wamefika..” Ilikuwa ni sauti ya muongozaji wa shughuli ile mara tu alipopewa taarifa kwamba Latoya na akina Innocent walikuwa wakija pale bustanini.
Watu wote pale bustanini wakasimama.Latoya akawaongoza akina Innocent,Grace na Sabrina hadi mahala walikokuwa wameandaliwa.Wakaketi katika sofa nyeusi .Innocent akastaajabu idadi ile kubwa ya watu waliokuwa wamekuja katika msiba wa Marina ndani ya kipindi kifupi namna ile cha kupata tarifa za kufariki kwa Marina.Wote walionekana ni watu wenye uwezo mkubwa kifedha.Walikuwepo pia watu wa mataifa tofauti kama wazungu ,na wahindi.
“ watu wote hawa wamefika hapa baada ya kupata taarifa kwamba Latoya amefiwa.Nikiwaangalia nawaona wote ni watu wenye uwezo mkubwa kifedha. Nina kila sababu ya kumfahamu kiundani mtu huyu.Amenifanya nisahau kama nina msiba mkubwa na kubaki nikimuwaza yeye na maisha yake ya kushangaza.Sikutegemea kama msiba wa Marina binti masikini anayejiuza mtaani ungewakusanya watu wazito namna hii.Yote imewezekana kwa sababu ya Latoya.” Akawaza Innocent wakati Latoya akijadiliana jambo na muongozaji wa shughuli.
Baada ya majadiliano mafupi Latoya akasimama akaongozana na muongoza shughuli hadi katika jukwaa dogo
“ndugu waombolezaji,naomba tafadhali tumsikilize ndugu yetu,mpendwa wetu Latoya anataka kuongea nasi machache" akasema muongoza shughuli
“ Ndugu waombolezaji,sipati neno la shukrani kwenu nyote ambao mmefika kuungana nasi mara tu baada ya kupata taarifa za msiba huu.Mimi na ndugu zangu wote tunawashukuru sana kwa kuja kuungana nasi katika usiku huu mgumu kwetu na hadi pale tutakapohitimisha safari ya mwisho ya mpendwa wetu Marina.Napenda nichukue nafasi hii niliyopewa ya kusema maneno machache,kuwaelezea kwa ufupi kuhusiana na msiba huu.Leo mchana tumempoteza ndugu yetu,mdogo wetu aitwaye Marina.Ndugu yetu huyu alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa figo na alifariki akiwa katika maadalizi ya kufanyiwa upasuaji ili abadilishiwe figo.Ndugu yangu Innocent ambaye ni yule pale mnayemuona alikuwa amejitolea figo yake ili awekewe ndugu yetu huyu lakini pamoja na jitihada zote hizo Marina alifariki dakika chache kabla ya upasuaji huo kufanyika.Ni msiba mkubwa sana umetupata mimi na ndugu zangu kwa sababu Marina amefariki akiwa bado mdogo .Amefariki akiwa ni binti wa miaka kumi na tisa.Hii yote ni kazi ya Mungu na siku zote kazi ya Mungu haina makosa.Bwana ametoa na na bwana ametwa.Jina lake lihimidiwe.Amen”
Watu wote wakaitika
“Amen”
Baada ya muitikio ule Latoya akaendelea
“Kwa niaba ya ndugu zangu,ninapenda kwa mara nyingine tena niwashukuru wote mliofika na kujumuika nasi katika msiba huu.Naomba moyo huo wa upendo mlio nao muendelee nao na Mungu awabariki .kwa kuwa ndugu yangu Innocent amechoka sana baada ya shughuli zote za hospitali ninaomba mumruhusu akapumzike na sisi wengine tuendelee na maombolezo .Kesho ratiba nzima itatolewa kuhusiana na msiba huu.Ahsanteni sana.”
Latoya akamaliza kuongea machache akarejea katika sehemu waliyokuwa wameandaliwa akamshika mkono Innocent wakaelekea ndani na kuacha maswali mengi miongoni mwa waombolezaji.Ilikuwa ni mara ya kwanza Latoya kuonekana akimshika mkono kijana wa kiume na kutembea pamoja.Kwa wengi waliomfahamu Latoya ilikuwa ni jambo la ajabu na la kushangaza sana .Kingine kilichowapa maswali mengi ni kutoonekana kwa wazazi wa Latoya msibani.Wengi walitegemea kwamba kwa kuwa msiba ule ni wa familia basi wazazi wa Latoya wangekuwepo msibani lakini wakashangazwa na kutomuona hata mzazi mmoja.Bado maswali kuhusiana na maisha ya Latoya yakazidi kuongezeka.
Latoya,Innocent ,Grace na Sabrina walitembea taratibu kuelekea ndani na kuwaacha watu wakiendelea na maombolezo.Kulikuwa na vinywaji vya kila aina,chakula cha kila namna kilikuwa kikipatikana.Matajiri walikuwa wakishindana katika kujitolea michango mbali mbali kwa ajili ya msiba ule.Gari zilizobeba vinywaji zilikuwa zikiingia na kuteremsha masanduku yaliyojaa vinywaji vya kila namna.Ilikuwa ni zaidi ya msiba.
“Innocent pamoja na kwamba umechoka na unahitaji kupumzika lakini kuna wawakilishi toka ile kampuni niliyoikabidhi kazi ya kushughulikia msiba huu wako tayari wakitusubiri.Naomba tuongee nao machache halafu uende kupumzika” Latoya akamweleza Innocent
“hakuna taabu Latoya.” Innocent akajibu kwa ufupi na moja kwa moja wakaelekea katika ukumbi ambao wawakilishi wa kampuni ile ya mazishi walikuwa wamekaa wakiwasubiri.
Mara tu walipoingia katika ule ukumbi mdogo ambao uliotumika kwa mikutano midogo,watu wote wapatao saba wakasimama ili kuonyesha heshima na Latoya akawafanyia ishara waketi.Akakohoa kidogo na kusema
“Ndugu zangu nawashukuru sana kwa kazi nzuri mliyoifanya toka nilipowapa taarifa ya msiba.Mmefanya kazi kubwa na kwa haraka licha ya idadi ya watu kuwa kubwa.Sikutegema kama kungekuwa na idadi hii kubwa ya watu namna hii .Sielewi hata taarifa hizi zinasambaa vipi kwa watu.” akasema Latoya
“Madam , hata sisi tunashangaa sana kwa jinsi taarifa zinavyosambaa kwa kasi.Tulitegemea kungekuwa na watu wachache lakini imekuwa tofauti kabisa.Tumeshangaa kuona idadi hii kubwa ya watu iliyofika kwa jioni hii.Kwa hali inavyoonekana ,siku ya kesho kutakuwa na idadi kubwa ya watu kwani kadiri muda unavyozidi kusonga taarifa zinazidi kusambaa.” Akasema mtu mmoja mnene ..
“Ok ! hakuna tatizo ila jitahidini kudhibiti idadi ya watu kwani eneo letu haliwezi kuhimili mkusanyiko mkubwa wa watu.Kwa ufupi tu ningependa kuchukua nafasi hii kumtambulisha kwenu ndugu yetu Innocent.Ndugu yetu huyu ndiye aliyekuwa na marehemu hadi dakika za mwisho za uhai wake na ndiye aliyekuwa amejitolea figo yake awekewe marehemu Marina.Innocent walioko mbele yako ni wawakilishi toka kampuni inayoratibu na kusimamia shughuli zote za msiba huu Kwa kuwa Innocent amechoka kutokana na pilika pilika nyingi za siku ya leo ,anahitaji kwenda kupumzika,kwa maana hiyo tunahitaji kuongea kwa kifupi sana kuhusu masuala ya muhimu ya msiba kwa usiku huu.Ningependa kwanza kupata taarifa wapi mlipofikia kuhusianana maandalizi ya mazishi na kama kuna tatizo lolote hadi hivi sasa.”
Sylivester kushishi ambaye ndiye alikuwa kiongozi akafungua faili lake na kusema
“Madam Latoya,mpaka sasa hivi tumekwisha kamilisha kila kitu kwa asilimia tisini.Watu wengi wamekuwa wakijtolea vitu mbalimbali kwa hiyo mpaka sasa hivi hakuna sehemu yenye upungufu wa kitu chochote kile.Chakula na vinywaji viko vya kutosha sana na bado vinazidi kuletwa.Kitu peke ambacho tungependa kupata maelekezo kutoka kwako ni lini mmepanga iwe ni siku ya mazishi na tumzike wapi.Hayo ndiyo mambo pekee ambayo yamebakia na tunasubiri maelekezo yako madam Latoya”
Latoya akamtazama Innocent na kumuuliza
“Innocent wewe ndiye mwenye kutoa uamuzi ni lini tumzike Marina na tumzike wapi”
Innocent akafikiri kidogo na kusema
“Latoya , hakuna haja ya kuweka siku nyingi za msiba kwani watu wanatakiwa waendelee na shughuli zao za maendeleo.Mimi nadhani hata kesho tunaweza tukafanya mazishi halafu kila mmoja akaendelee na shuguli zake.Suala la wapi atazikwa ni jambo la kuamua tu ,sehemu yoyote ile itakayoonekana inafaa mimi sina kipingamizi” Innocent akasema kwa sauti ndogo.
“nadhani mmemsikia Innocent alivyosema lakini na mimi ninapenda kuongezea machache katika hilo.Sioni tatizo lolote hata kama msiba huu utachukua mwezi mzima.Lakini kwa kuyaheshimu mawazo ya Innocent ningependekeza mazishi yafanyike kesho kutwa.Marina ni mtu muhimu kwetu na anastahili heshima kwa maana hiyo ninapendekeza azikwe katika makaburi ya Kivule wanakozikwa watu matajiri .Shughulikieni suala hilo na mpaka kesho jioni maandalizi ya kaburi yawe yamekamilika na kesho kutwa tufanye mazishi.Nataka mazishi haya yawe na hadhi na heshima ya kipekee sana.Tutaongea na kupanga zaidi siku ya kesho.Kama kuna jambo lolote ambalo litawasumbua msisite kunitaarifu mara moja..Naomba sasa nimruhusu Innocent akapumzike tutaonana tena kesho asubuhi” Latoya akasema na kisha akainuka na kumuongoza Innocent kuelekea chumbani kwake.
“Innocent naomba upumzike na tutaonana kesho.Iwapo utahitaji kitu chochote kile hata kwa usiku wa manane piga simu namba 200 wapo wahudumu ambao watakuhudumia mara moja .Kama una lolote la kuniambia unaweza ukanipigia simu muda wowote wa usiku lakini kuanzia saa tisa za usiku hadi saa kumi na moja za asubuhi huwa sipokei simu.Usiku mwema Innocent.”akasema Latoya na kuondoka.
“Sikutegemea kama msiba wa Marina ungekuwa namna hii.Mtu masikini asiye na ndugu yeyote,msichana ambaye anafanya biashara ya ukahaba lakini msiba wake umekuwa ni msiba wa kifahari na wa kitajiri.Kila mtu aliyefika hapa anajaribu kuonyesha uwezo wake wa kifedha kwa Latoya.Kwa mujibu wa Latoya shilingi millioni mia na hamsini tayari zimeshatolewa hadi hivi sasa kama mchango.Inanishangaza sana kwa watu kujitolea fedha hizo zote kwa ajili ya msiba badala ya kumsaidia mtu akiwa bado hai.Baada ya msiba huu nitaanzisha taasisi yangu ya kuwasaidia watu wenye matatizo kama ya Marina.Kuna watu wengi ambao nina imani wana matatizo makubwa na wanahitaji msaada mkubwa.Kuna kila sababu ya kuwaelimisha watu juu ya thamani ya mtu akiwa hai.Tusisubiri kumthamini mtu wakati amefariki.” Alikuwa akiwaza Innocent akiwa amekaa kitandani.Picha ya Latoya ikamjia kichwani
. ” Kuna kila sababu ya kumfahamu Latoya kwa undani.Ninataka nifahamu ni kwa nini binti mdogo namna ile ananyenyekewa na watu wakubwa na matajiri..Ni binti wa namna gani anayeweza kuwafanya watu wenye fedha na nyadhifa zao wajishushe kwake?.Nitajitahidi kumfahamu kiundani baada ya msiba huu kuisha.Kwa sasa nitakuwa nikiumiza kichwa changu bure.Ninachotakiwa ni kuelekeza mawazo yangu katika msiba huu mkubwa unaonikabili.Natakiwa kwanza kumzika Marina na kisha nijue nini kitakachofuata.Masikini Marina amekufa bado msichana mdogo .Hakufanikiwa kutimiza ndoto zake alizokuwa akifikiria kuzitimiza.Nasikitika sana kufahamiana naye katika siku za mwisho za maisha yake hapa duniani.Pamoja na kasoro zake ambazo zilichangiwa na maisha aliyoyaishi ,lakini nitakiri siku zote kwamba marina alikuwa na uzuri wa kipekee.Kinachoniuma zaidi ni kwamba tayari nilikwishavutiwa naye na alikuwa tayari kuyabadili maisha yake.Pamoja na jitihada zote nilizozifanya ili kuyaokoa maisha yake lakini Mungu amempenda zaidi.Nitazidi kumuombea siku zote ili apumzike kwa amani.”
Wakati Innocent akifumba macho yake na kulala,Latoya alikuwa amepiga magoti katika meza yake ambayo anayoitumia kila siku kwa ajili ya kufanyia maombi.Taa za chumbani kwake zilikuwa zimezimwa na mishumaa tisa ndiyo ilikuwa ikiwaka na kuleta mwanga mle chumbani.Uso wake ulikuwa umeloa machozi na alikuwa akilia kwa kwikwi.
“ni siku nyingi nimekuwa nikiota ili kabla sijafa niwe nimempata mtu ambaye nitampenda kwa moyo wangu wote.Ninahitaji kuwa na mtu nitakayempenda na ambaye atanipenda na kunithamini.Naamini nimekutana na Innocent kwa makusudi kabisa.Naamini Innocent ndiye yule mtu ambaye nimekuwa nikiomba kumpata mchana na usiku.Kadiri siku zinavyokwenda ninazidi kuwa dhaifu na nilikuwa ninaogopa ninaweza kufa kabla sijaitimiza ahadi hii niliyoiweka ya kumpata mtu nitakayemkabidhi moyo wangu.” Latoya alikuwa akiwaza huku uso wake umeloa machozi.Hali aliyokuwa nayo muda huu ilitia huruma sana.Taratibu akajiinua na kwenda kukaa katika kitanda chake kikubwa.Akakishika kichwa chake na kuzama katika mawazo mengi

TUKUTANE SEHEMU IJAYO…
 
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 24
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Wakati Innocent akifumba macho yake na kulala,Latoya alikuwa amepiga magoti katika meza yake ambayo anayoitumia kila siku kwa ajili ya kufanyia maombi.Taa za chumbani kwake zilikuwa zimezimwa na mishumaa tisa ndiyo ilikuwa ikiwaka na kuleta mwanga mle chumbani.Uso wake ulikuwa umeloa machozi na alikuwa akilia kwa kwikwi.
“ni siku nyingi nimekuwa nikiota ili kabla sijafa niwe nimempata mtu ambaye nitampenda kwa moyo wangu wote.Ninahitaji kuwa na mtu nitakayempenda na ambaye atanipenda na kunithamini.Naamini nimekutana na Innocent kwa makusudi kabisa.Naamini Innocent ndiye yule mtu ambaye nimekuwa nikiomba kumpata mchana na usiku.Kadiri siku zinavyokwenda ninazidi kuwa dhaifu na nilikuwa ninaogopa ninaweza kufa kabla sijaitimiza ahadi hii niliyoiweka ya kumpata mtu nitakayemkabidhi moyo wangu.” Latoya alikuwa akiwaza huku uso wake umeloa machozi.Hali aliyokuwa nayo muda huu ilitia huruma sana.Taratibu akajiinua na kwenda kukaa katika kitanda chake kikubwa.Akakishika kichwa chake na kuzama katika mawazo mengi

ENDELEA……………………………..

“Nina hakika kukutana na Innocent hakukuwa ni kwa bahati mbaya.Sina shaka kwamba Innocent ni yule mtu ambaye nimekuwa nikimsubiri kwa muda mrefu.Ninahitaji kuitimiza ahadi yangu kabla sijafa.Sehemu nyingi nimetembea duniani ili kumtafuta yule mmoja ambaye ataifanya ahadi yangu itimie lakini sijafanikiwa.Ni Innocent pekee ambaye moyo wangu una imani kubwa naye kwamba ndiye yule niliyekuwa nikimsubiri.” Latoya alikuwa katika mawazo mengi sana.Akazima mishumaa ile na chumba chote kikawa giza akalala”



* * * *

Siku iliyofuata ilikuwa ni siku yenye pilika pilika nyingi sana nyumbani kwa Latoya.Taarifa za kuwepo kwa msiba nyumbani kwa Latoya zilisambaa kwa kasi kubwa na kuwafanya watu wengi wahudhurie.Matajiri walikuwa wengi na walishindana katika viwango vya michango na rambi rambi.Walikuwepo pia viongozi wa serikali ,wawakilishi wa mashirika mbali mbali na hata viongozi wa dini.Wapo pia watu waliotoka nje ya nchi kwa ajili ya kuhudhuria msiba huu.Kwa maelekezo ya Innocent gari maalum ilitumwa na kuwaleta msibani baba na mama yake pamoja na dada yake Sarah.Vile vile waliletwa mzee Mustapha pamoja na wale wasichana ambao walikuwa wakiishi na Marina na kufanya naye biashara ya ukahaba.Wote hawakuamini kama msiba wa Marina ungekuwa ni msiba mkubwa namna ile.Wazazi wa Innocent walipigwa na bumbuwazi baada ya kuwasili eneo la msiba na kukutana na umati ule wa matajiri na watu mashuhuri.Matajiri hawa waliohudhuria msiba huu wote hawakuwa wakimfahamu Marina.Wote walifika kwa sababu ya Latoya.
Latoya ,Innocent ,Sabrina na Grace walikaa katika sofa nyeusi zilizokuwa zimewekwa katika sehemu iliyotengwa maalum kwa ajili ya wafiwa.Kila aliyefika msibani alikuwa akipita mbele na kwenda kuwapa pole wafiwa.Latoya akawatambulisha Innocent,Sabrina na Grace kwa wazazi wake ambao nao walihudhuria baada ya kupewa taarifa za msiba na Latoya mwenyewe.Bwana na Bi Curtis Stevens walikuwa ni wazee ambao umri wao ulikaribia miaka sitini hivi.Innocent akashangaa sana kwa kuwaona wazazi wa latoya.Latoya alionekana ni binti mdogo lakini wazazi wake walionekana ni watu wazima sana.Shughuli za msiba ziliendelea kwa siku nzima hadi usiku.

* * * *

Siku iliyofuata ilikuwa ni siku ya mazishi ya Marina.Asubuhi hii tayari watu wengi walikwisha kuwasili.Wengine walilala hapo hapo.Saa mbili za asubuhi Innocent alikuwa tayari amejiandaa kwa ajili ya kuelekea hospitali kuchukua mwili wa Marina na kuuleta nyumbani kwa ajili ya heshima za mwisho kabla ya kupelekwa katika makaburi ya watu matajiri ya Kivule.
“Innocent nafahamu ugumu wa siku hii.Ni moja kati ya siku ngumu sana kwani mtu uliyemzoea na kumpenda anakwenda kuwekwa kaburini.Tafadhali naomba uwe jasiri kwani haya ndiyo maisha yetu sote.Uko tayari kwenda hospitali kwa ajili ya kuuchukua mwili wa Marina ? Latoya akamuuliza Innocent aliyekuwa amevaa suti nyeusi iliyomkaa vyema.
“Latoya kifo ni jambo ambalo hatuwezi kulikwepa.Sote tutakufa na tutafiwa.Siku kama hii huwa ni ngumu sana kwa wale wote waliofiwa kwa sababu ni siku ambayo huwa inawapa uhakika kwamba hawatamuona tena mpendwa wao hadi siku ya mwisho.Ni siku ngumu lazima nikiri.Niko tayari kwenda hospitali kuuchukua mwili wa Marina” Innocent akasema huku akiirekebisha tai yake
Walipotoka ndani ya jumba lile wakakuta msafara wa magari zaidi ya ishirini yote meusi yakiwa yamepangwa tayari kwa kuelekea hospitali kuuchukua mwili wa Marina.Latoya na Innocent wakaelekezwa gari liliokuwa limeandaliwa kwa ajili yao wakapanda na safari ya kuelekea hospitali ikaanza.
Saa nne za asubuhi wakawasili hospitali na moja kwa moja Latoya Innocent,Sabrina na Grace wakaelekea katika chumba cha maiti.Ulinzi ulikuwa mkali na kwa mara ya kwanza Innocent akashuhudia jinsi Latoya alivyokuwa akilindwa.Alikuwa na walinzi wake binafsi ambao hawakuruhusu mtu yeyote kumkaribia.Ndani ya chumba cha maiti tayari mwili wa Marina ulikwishaandaliwa na kuwekwa katika jeneza la gharama kubwa.Innocent ,Latoya ,Sabrina na Grace wakalizunguka jeneza lile , likafunguliwa .Marina alikuwa amelala ndani ya jeneza .Alionekana ni kama mtu aliyelala usingizi mzito.Innocent akavua miwani yake myeusi aliyokuwa ameivaa akainama na kukilaza kichwa chake katika kichwa cha Marina.machozi yalikuwa yakimtoka.
“Pumzika kwa amani Marina.Nitakuombea daima” akatamka maneno hayo machache kwa uchungu Sabrina na Grace walishindwa kujizuia kuangusha machozi.Ilikuwa ni hali ya simanzi kubwa sana.Michirizi ya machozi ilionekana katika macho ya Latoya.Akatoa kitambaa na kujifuta kisha akavaa miwani yake.Mlinzi mmoja akasogea taratibu na kutaka kumuinua Innocent juu ya mwili wa Marina lakini Latoya akamzuia.
“Muache Innocent amlilie Marina kwa mara ya mwisho.”
Dakika kumi baadae Innocent akainuka .Latoya akachukua kitambaa chake na kumfuta machozi huku akimpiga piga mgongoni.
“Be strong Innocent”
Jeneza likafungwa ,wakasogea watu sita waliokuwa wamevaa suti nyeusi wakalibeba jeneza lile na kuanza kutoka kuelekea nje.Gari maalum la kubebea maiti lilikwisha sogea na jeneza likapakiwa garini ,Sabrina na Grace wakapanda katika gari lile lililobeba mwili wa Marina na kisha msafara wa kurudi nyumbani kwa Latoya ukaanza.
Saa tano kamili kama ratiba ilivyokuwa imepangwa shughuli zikaanza.Ibada iliyoongozwa na askofu ikafanyika na baada ya ibada zikafuata salamu za wasemaji ambao walipangwa kuwa wawili tu Marina na Innocent.Mtu wa kwanza kupewa nafasi ya kuongea alikuwa ni Marina ambaye katika maongezi yake aliwashukuru watu wote kwa kuhudhuria msiba ule toka siku ya kwanza na kwa kila kitu walichojitolea.Baada ya Latoya akapewa nafasi Innocent. Taratibu akajongea katika sehemu iliyotengwa rasmi kwa ajili ya kusemea.Akautazama umati ule wa watu waliojazana pale kisha akasema
“Ndugu zangu mimi naitwa Innocent Benard mtoto wa bwana na bibi Vincent Benard.Nadhani wengi wenu si wageni kwa mzee huyu ambaye ni mmoja wa wafanya biashara maarufu.Naomba usimame mzee Benard popote ulipo”
Mzee Benard baba yake Innocent akasimama na kupunga mikono hewani huku akitabasamu .Alijisikia fahari kubwa kuwapo katika hadhira ile kubwa iliyojaza matajiri wakubwa.
“Ndugu zangu ,tumekusanyika hapa leo kwa ajili ya kumsindikiza ndugu yetu Marina katika safari yake ya mwisho.Hatutamuona tena katika maisha yetu ya kimwili lakini kiroho bado atazidi kuwa nasi.Nyote mmehudhuria msiba huu lakini ni wachache wenye kufahamu binti huyu ambaye ametukutanisha sote hapa leo hii ni nani.Nilikutana na Marina siku moja usiku, mimi na dada yangu Sarah tulipokwenda kupata burudani katika klabu moja ya usiku .Katika lango la kuingilia sehemu ile tuliyokuwa tukienda nililiona kundi la wasichana wanaofanya biashara ya kuuza miili na miongoni mwao alikuwepo binti mdogo.Nilistuka sana baada ya kumuona binti yule akiwa mahala pale na wasichana wale,nikapata shauku ya kutaka kufahamu ni kwa nini alikuwepo pale mida ile.Nilifanya kila juhudi nikampata na kwenda naye mahala ambako nilimdadisi na akanieleza historia yake kwa urefu na kwa nini ilimpasa kuwa pale saa zile.Aliniambia kwamba hakuwa na wazazi.Mama yake ambaye ndiye alikuwa tegemeo lake pekee alifariki wakati yeye akiwa mdogo na kwa hiyo ilimlazimu kukatisha masomo yake na kutafuta namna ambayo angeweza kuishi.Hakuwa na elimu ya kumuwezesha kupata ajira au mtaji wa biashara ambao ungemuwezesha kuanzisha biashara japo ndogo hivyo akaona njia pekee ya kumuwezesha kumudu maisha ni kushiriki katika biashara ya mwili.Kutokana na umbo lake dogo na la kuvutia watu wengi walivutiwa naye lakini hakuna hata mmoja wao ambaye alimuonea huruma badala yake wengi walimtumia kwa kuridhisha miili yao na kisha kumlipa pesa kidogo..Niliguswa sana na maelezo aliyonipa na nikaahidi kumsaidia.Nikiwa katika harakati za kumsaidia ili ayabadili maisha yake na kuanza maisha mapya ,akaanza kuumwa na tulipompeleka hospitali ikagundulika kwamba alikuwa akisumbuliwa na figo.Ilikuokoa maisha yake alihitajii kubadilishiwa figo.Juhudi za kutafuta figo ziliendelea nikishiriana na Latoya lakini hali yake ilibadilika ghafla na hivyo ikanilazimu niamue kujitolea figo yangu mwenyewe ili kuyaokoa maisha yake.kwa bahati mbaya Marina alifariki dakika chache kabla ya operesheni kufanyika.Mungu ampumzishe kwa amani Amina”
Umati wote ulionekana kuguswa sana na maelezo yale ukaitika “Amina”
Innocent akautazama umati ule na kisha akaendelea.
“Ndugu zangu nimeamua kuyasema haya yote si kwa nia mbaya bali muweze kupata picha kamili ni nini hasa kilichotokea.Marina alikuwa ni binti masikini ambaye hakuwa akimilki hata sahani ya kulia chakula lakini msiba wake umekuwa ni msiba wa kifahari na kitajiri.Ufahari huu na utajiri huu unaonyesha ni kwa namna gani jamii yetu inavyothamini mtu akisha fariki kuliko kumjali akiwa hai.Laiti michango hii mikubwa iliyotolewa hapa ingepatikana wakati Marina yuko hai nina imani tungeweza kuokoa maisha yake na kumsaidia yeye na wasichana wenzake wengi ambao wanaishi katika mazingira magumu sana.Katika jamii yetu kuna maelfu ya watu walio kama Marina ambao hawana hakika na kesho yao.Kuna watu wana umasikini wa kutisha.Kuna watu ni wagonjwa na hawajui watapata wapi msaada.Kuna watu wanakosa elimu kutokana na ukosefu wa fedha,kuna watu ambao wanakosa haki zao za msingi kutokana na umasikini walio nao.Wote hawa wanahitaji msaada mkubwa kutoka kwetu sisi ambao Mungu huyo huyo aliyewanyima wao ndiye aliyetupa sisi.Nawaomba ndugu zangu ,kuanzia sasa tubadilike.Tubadili mawazo na mitazamo yetu.Tujifunze kushuka chini na kuwasaidia wale wenye mahitaji .Na wala tusiwanyanyapae kwa ajili ya umasikini wao na tusisubiri kuonyesha ufahari na kushindanisha michango ya fedha na vitu katika misiba wakati tulikuwa na uwezo wa kutoa msaada mapema.Marina alikuwa ni binti mzuri,mwenye upeo na ambaye alikuwa na ndoto nyingi katika maisha yake.Nimepata bahati ya kuwa naye karibu katika siku za mwisho za uhai wake na nilibahatika kumfahamu vyema.Alikuwa ni binti jasiri ambaye hakufahamu neno kushindwa.Alikumbana na changamoto nyingi lakini hakukata tamaa na maisha yake.Laiti kama angepatiwa msaada asingeweza kujihusisha tena na biashara aliyokuwa akiifanya.Tujenge moyo wa kusaidia wengine wenye matatizo na uhitaji.Mwisho napenda kuchukua nafasi hii kuwahukuru nyote kwa kuhudhuria kwenu .Mimi na ndugu zangu tumefarijika sana .Ahsanteni na Mungu awabariki”.
Innocent akamaliza na kurejea kukaa mahala pake.Maneno yale aliyoyasema yalimfanya Latoya atokwe na machozi.Alichomwa mno na maneno yale yaliyojaa ukweli.Si Latoya tu aliyeguswa na maneno yale bali hata waombolezaji walibaki wakinong’ona wao kwa wao.
Shughuli za kuuaga mwili zilianza na watu walipita mbele ya Jeneza la mwili wa Marina na kutoa heshima zao za mwisho.Baada ya zoezi hilo kukamilika safari ya kumsindikiza Marina katika nyumba yake ya milele ikaanza.Saa kumi za jioni Marina akazikwa katika makaburi ya Kivule maalum kwa watu maarufu na matajiri.
Baada ya mazishi ya Marina yaliyokutanisha vigogo na matajiri wakubwa wa ndani na nje ya nchi msafara mkubwa wa magari ukarejea nyumbani kwa Latoya ili kuendelea na shughuli za kumalizia msiba.Kilichoendelea ilikuwa ni chakula na vinywaji pamoja na salamu nyingi za pole na rambi rambi kutoka kwa watu mbali mbali .Saa mbili za usiku Latoya akamuomba Innocent aende kupumzika kutokana na shughuli ndefu ya siku ile.Wakawaaga waombolezaji ambao walikuwa bado wamejazana katika bustani ile wakiendelea kula na kunywa na kisha wakaingia ndani.
“Latoya narudia tena kukushukuru kwa msaada huu mkubwa ulionisaidia kwa kukubali kuubeba msiba huu wa Marina.Upendo na ukarimu wako hautaweza kufutika moyoni mwangu mpaka siku ninaingia kabuirini.Umeonyesha upendo mkubwa kiasi cha kumshangaza kila mtu.Kila mtu aliyefika msibani hakuna aliyekuwa akifahamu mtu aliyefariki ni nani.Kwa mtu mwenye hadhi yako si rahisi kuruhusu msiba wa mtu kama Marina ufanyike nyumbani kwako.Umeonyesha upendo wa hali ya juu sana na kwa hilo nitakukumbuka milele na milele.” Innocent akamweleza Latoya wakati wakiwa katika sehemu ya mapumziko maalum kwa ajili ya Latoya pekee.
“Innocent mara zote umekuwa na maneno mazuri kiasi ninapenda niwe ninakusikiliza wakati wote.Ninachotaka kukueleza ni kwamba huna sababu ya kunishukuru mimi .Sote tunapaswa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa sababu kila jambo linafanyika kwa maongozi yake.Ni kweli kwamba katika dunia ya sasa kumekuwa na matabaka mawili makubwa.Tabaka la wenye nacho na wasio kuwa nacho.Ni nadra sana kwa wenye nacho kuchangamana na wasio kuwa nacho.Katika msiba huu wa Marina idadi kubwa iliyohudhuria msibani ni watu matajiri wenye uwezo wao mkubwa .Wote walikuja kwa sababu ya jina langu .Nashukuru sana Innocent kwa maneno uliyoyatoa msibani ambayo kila nikikaa mwenywe nayasikia yakinijia masikioni.maneno yako yamewachoma watu sana.Umewafundisha kitu kikubwa sana na nina imani mwenye masikio amesikia " .Latoya akasema na kumtazama Innocent.ambaye alikuwa akitabasamu
“ Msiba huu wa Marina umenifundisha mambo mengi sana na kubwa ni sababu ya mimi kuwepo hapa duniani.Pamoja na kwamba hayuko nasi leo hii lakini kifo chake kimenifanya nijifunze mambo mengi .Pumzika kwa amani Marina” akasema Innocent na kwa mbali macho yake yalianza kulengwa na machozi.Latoya akampeleka Innocent chumbani kwake kupumzika halafu naye akaelekea chumbani kwake.Kama ilivyo kuwa kawaida yake akazima taa zote na kuwasha mishumaa tisa.Akainama na kwa muda wa kama robo saa hivi akainua uso wake ambao tayari ulikuwa umelowa machozi.Huku akilia kwa kwikwi akainua kichwa na kusema kwa sauti ndogo .
“Ee Mungu naomba na nitaendelea tena kukuomba kila siku kwamba tafadhali naomba unifunulie kama Inocent ndiye yule nliyekuwa nikikuomba unipatie kabla sijafa.Kama ni yeye nakuomba usimuache akaondoka mikononi mwangu.Moyo wangu unaniambia kwamba yeye ndiye, lakini bado nahitaji ufunuo kwamba ni yeye yule ninayemsubiri” Wakati akiomba akahisi kitu kama maji maji mgongoni wake.Akapeleka mkono taratibu kisha akagusa maji maji yale na alipoutoa mkono wake ulikuwa umeloa damu.Machozi mengi yakamporomoka
“Its time “ akasema Latoya kwa sauti ndogo
Ghafla akaanza kusikia maumivu makali kupita kiasi.Akapiga kelele kubwa kutokana na maumivu yale yasiyovumilika na mara akaanguka chini na kupoteza fahamu.

TUKUTANE SEHEMU IJAYO………
 
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 25
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Msiba huu wa Marina umenifundisha mambo mengi sana na kubwa ni sababu ya mimi kuwepo hapa duniani.Pamoja na kwamba hayuko nasi leo hii lakini kifo chake kimenifanya nijifunze mambo mengi .Pumzika kwa amani Marina” akasema Innocent na kwa mbali macho yake yalianza kulengwa na machozi.Latoya akampeleka Innocent chumbani kwake kupumzika halafu naye akaelekea chumbani kwake.Kama ilivyo kuwa kawaida yake akazima taa zote na kuwasha mishumaa tisa.Akainama na kwa muda wa kama robo saa hivi akainua uso wake ambao tayari ulikuwa umelowa machozi.Huku akilia kwa kwikwi akainua kichwa na kusema kwa sauti ndogo .
“Ee Mungu naomba na nitaendelea tena kukuomba kila siku kwamba tafadhali naomba unifunulie kama Inocent ndiye yule nliyekuwa nikikuomba unipatie kabla sijafa.Kama ni yeye nakuomba usimuache akaondoka mikononi mwangu.Moyo wangu unaniambia kwamba yeye ndiye, lakini bado nahitaji ufunuo kwamba ni yeye yule ninayemsubiri” Wakati akiomba akahisi kitu kama maji maji mgongoni wake.Akapeleka mkono taratibu kisha akagusa maji maji yale na alipoutoa mkono wake ulikuwa umeloa damu.Machozi mengi yakamporomoka
“Its time “ akasema Latoya kwa sauti ndogo
Ghafla akaanza kusikia maumivu makali kupita kiasi.Akapiga kelele kubwa kutokana na maumivu yale yasiyovumilika na mara akaanguka chini na kupoteza fahamu.

ENDELEA……………………………

Hakuna aliyekuwa akiongea ndani ya gari.Wote walikuwa kimya kabisa.Kila mmoja alikuwa akiwaza lake.Mzee Benard baba yake Innocent ndiye aliyekuwa akiendesha gari usiku huu wakiwa wanarejea nyumbani baada ya kuhudhuria mazishi ya Marina.Ndani ya gari ile alikuwemo pia mke wake na mwanae Sarah.
“mama Edson kuna mambo ambayo tunahitaji kuongea.”Akasema mzee Benard
“mambo gani hayo baba Eddy? Akauliza mke wake.
Mzee benard akavuta pumzi ndefu akalipita gari lililokuwa mbele yao kisha akasema
“Tulikosea sana.Tulifanya makosa makubwa mno.”
“makosa gani baba Eddy?
“Kumfukuza yule binti nyumbani kwetu tulifanya makosa makubwa mno.Maneno aliyoyaongea Innocent pale kwenye msiba yalinichoma moyo sana .Kitendo tulichokifanya kilimuumiza mno Innocent.Tunatakiwa tumuombe mtoto msamaha na tuanze upya”akasema mzee Benard huku mkewe akimuangalia kwa macho makali
“baba Eddy mimi sijakosea.Nilikuwa sahihi kabisa.Innocent anatakiwa ajifunze kwamba kuna ukomo wa kutoa misaada.Si kila mtu anafaa kusaidiwa.Yule binti alikuwa kahaba kama yeye mwenyewe alivyosema huoni kwamba kama angeendelea kuwa naye angehatarisha maisha ya mtoto wetu? Akasema mama yake Inno kwa ghadhabu.
“Nimesikia aibu kubwa sana na sintakuwa na amani katika maisha yangu yote mpaka siku nitakapoyamaliza mambo haya na Innocent.Kuna haja ya mabadiliko makubwa mno katika familia yetu.Inno anahitaji msaada wetu sisi kama wazazi wake.” akasema mzee Banard
“baba Eddy mimi katu sintaweza kupiga magoti na kumuomba msamaha mtoto wa kumzaa mwenyewe.Innocent aliondoka nyumbani mwenyewe kwa kiburi kabisa na hata kifo cha huyo kahaba wake ni pigo toka kwa Mungu.Ka…” mama yake Inno akasema kwa ukali lakini kabla hajaendelea mbele zaidi Sarah aliyekuwa amekaa kiti cha nyuma akaingilia kati
“mama si vizuri kutamka maneno hayo.Baba yuko sahihi kwamba tumefanya makosa.Hata wale wasichana wengine Grace na Sabrina tumekuwa tukiwatendea visivyo.Mimi naungana na baba kwamba kuna kila sababu ya kubadilika na kuwa familia yenye upendo mkubwa.Angalia matajiri waliojazana katika msiba ule.Wote waliokuja pale hakuna hata mmoja ambaye anamfahamu Marina.Wote walikuja pale kwa sababu ya roho ya upendo aliyonayo Latoya.Ni binti mdogo mwenye utajiri wa kutisha lakini ana roho nzuri mno na ndiyo sababu akakubali kuubeba msiba wa mtu masikini kama Marina.Kama angekuwa na roho ya kibinafsi na kujivuna kwa utajiri alionao ,wasingejitokeza watu kama wale msibani.” Saraha akamweleza mama yake ambaye alikuwa amenuna ameangalia pembeni.Hakutaka kuongea kitu chochote tena.


* * * *

Bado picha ya Marina imekuwa inamjia kichwani.Alikumbuka jinsi Marina alivyokuwa akitabasamu na vishimo kuonekana katika mashavu yake.Alikumbuka kicheko chake na sauti yake iliyokuwa inakwaruza kwaruza anapoongea.
“Alikuwa na uzuri wa kipekee ambao mtu unaweza ukautambua kama ukipata bahati ya kukaa naye kwa karibu” akawaza Innocent.
Picha ambayo kila alipokuwa akiikumbuka ilikuwa ikimtoa machozi ni ile ambayo Marina alikwa ametulia tuli katika jeneza .
“Ukurasa wa Marina ninaufunga rasmi.Nitamuombea kila siku ili aweze kupumzika kwa amani huko aliko.Nini kitakachofuata baada ya hapa? Moyo wangu unaniambia kuna kitu ninatakiwa kufanya lakini sielewi ni kitu gani hicho ninachotakiwa kukifanya.Ninajihisi kama nina kazi kubwa ya kufanya baada ya kumpoteza Marina.Ni kazi gani hiyo? Na nini yatakuwa maisha yangu baada ya hapa? “ Innocent akainuka na kukaa Mara sura ya Latoya ikamjia kichwani akatabaasmu
“Binti mzuri,mwenye sura ya kupendeza na kuvutia.Ana uzuri wa ajabu sana.Ana sura kama ya malaika.Uzuri wake unanifanya mara nyingine nihisi labda si binadamu wa kawaida.Ni binti mdogo lakini mwenye mambo makubwa mno.Latoya ni nani?? Kwa nini kila mtu anampa heshima kubwa namna ile.Nimeshuhudia kwa macho yangu jinsi matajiri wakubwa wa nchi hii ninaowafahamu na hata wale nisio wafahamu wakitoa heshima kubwa kwa binti huyu. Anafanya biashara gani kiasi cha kumfanya awe na utajiri mkubwa na kuheshimika namna hii? Vipi kuhusu masuala ya kimahusiano? Yawezekana akawa ameolewa? Kama kaolewa ni kwa nini basi huyo mume wake sijamuona msibani na wala hakugusia jambo lolote kuhusu suala hilo ? Pale msibani alinitambulisha wazazi wake ambao wanaonekana wana umri mkubwa wakati Latoya bado binti mdogo.je inawezekana walimpata Latoya wakita tayari ni wazee? Latoya ana ndugu wengine? Mbona sikuwaona msibani?” Innocent akahisi kuumwa kichwa kwa mawazo yale mengi kuhusiana na Latoya
“Halafu kitu kingine kinachonifanya niwe na udadisi mkubwa kuhusiana na binti huyu ni kwamba kwa nini katika ghorofa hii ya juu anaishi yeye pekee? Wafanyakazi wake wote wanaishi katika ghorofa za chini na toka nimefika hapa sijaona mfanyakazi yeyote akipanda huku ghorofa ya juu.Kulikoni? Swali jingine ninalojiuliza ni kwamba nimeonana naye kwa siku moja tu imetokea nini mpaka akawa karibu na mimi namna hii? Mbona ameniamini kwa kiasi kikubwa kama hiki? Kwa jinsi anavyonijali kila mtu anaamini kwamba mimi ni rafiki yake wa siku nyingi.Kuna kila ulazima wa kuanza kumfahamu Latoya ni nani kwani hata mimi nimeanza kuvutiwa naye,si kwa utajiri alionao lakini nahisi kuna kitu kinaanza kujengeka ndani ya moyo wangu kuhusu Latoya.Kila mara picha ya sura yake ikinijia ninasisimkwa mwili” Akawaza Innocent.
“Nimekumbuka zile namba alizoniambia nimpigie kama nina shida naye nyakati za usiku.Ngoja nimpigie nimwambie kitu chochote kile hata usiku mwema inatosha.Ili kumfahamu vizuri ninatakiwa kuanza kujenga mazoea ya karibu sana naye” akawaza Inno huku akiandika namba alizopewa na Latoya na kupiga.simu ikaita lakini haikupokelewa.Akapiga tena lakini haikupokelewa.
“Inawezekana amelala usingizi mzito sana.Amechoka mno .Ngoja na mimi nilale” akawaza Innocent na kisha akalala

* * * *

Curtis Stevens mtu ambaye kwa miaka kumi na mitano amekuwa balozi wa Tanzania katika nchi za Uholanzi ,Denmark Ufilipino na Marekani bado alikuwa amekaa katika sofa sebuleni kwake na pembeni yake kulikuwa na kikombe cha kahawa.Toka amerejea kutoka katika mazishi ya Marina Mr Curtis amekuwa ni mtu mwenye mawazo mengi .
“Curtis ,unawaza nini? Akauliza mke wake .
“Nina mawazo mengi sana kuhusiana na huyu binti yetu Latoya”
“Nimekwisha kuambia Curtis mambo ya Latoya ni mambo magumu sana na sisi kuendelea kumfuatilia ni kupoteza muda wetu bure.Kila siku nimekuwa nikikueleza kuhusiana na suala hili kwamba muda ukifika Latoya mwenyewe atatueleza kuhusiana na maisha yake yenye utata mkubwa” mama yake Latioya akasema
“nakubaliana nawe mke wangu lakini kuna jambo nimejifunza pale msibani.”
“Jambo gani hilo?
“Ni kuhusu uhusiano uliopo baina ya Latoya na yule kijana Innocent.Umeuonaje urafiki wao?
“Kwa mara ya kwanza katika maisha ya Latoya nimeshuhudia akiwa na urafiki wa karibu na kijana wa kiume.Sijawahi kumuona au hata kusikia akiwa na urafiki wa karibu na kijana yeyote kama alionao kwa Yule kijana Innocent.” akasema mzee Curtis..
“Hata mimi nimehisi kama kuna kitu kinaendelea baina yao japokuwa hakiko wazi lakini kama mzazi na mtu ninayemfahamu Latoya vizuri nimekiona kitu hicho.Kwa upande mmoja nimefurahi kwa sababu tunaweza tukamtumia kijana yule katika kuutafuta undani wa Latoya.Kama wazazi hatuwezi kamwe kumuona binti yetu akiwa na utajiri mkubwa kama ule bila kufahamu ni wapi alikoutoa na hataki kusema ameupata wapi utajiri wa namna hii akiwa binti mdogo.Mambo mengi sana yanasemwa kuhusiana na binti yetu.Kama tulivyo sisi wazazi wake ,hakuna anayefahamu chanzo cha utajiri wake na aina ya maisha anayoyaishi na ndiyo maana kila mmoja anatamka lake.Wengine wanasema kwamba ni mshirika wa imani hii ya freemason ambayo inasemekana watu wanaojiunga na imani hii huwa wanapata utajiri mkubwa sana.Wengine wanadai kwamba pesa yake inatokana na imani za kishirikina ili mradi kila mmoja anatamka maneno yake.Lakini ukweli ninaoufahamu ni kwamba Latoya nimemlea katika misingi imara ya kidini na sina hakika kama anaweza akashiriki katika hayo mambo wanayosema anashiriki.Lakini lisemwalo lipo kwa sababu vijana hawa wa siku hizi wamekuwa na tamaa kubwa ya utajiri wa haraka haraka.Kinachonifanya hata mimi niwe na wasi wasi na Latoya na niamini baadhi ya maneno wanayoyasema watu ni jinsi utajiri wake ulivyokuja ghafla na bila kumueleza mtu yeyote ameupata wapi utajiri ule mkubwa “ akasema Mr Curtis akanyanyua kikombe chake cha kahawa akanywa kidogo na kusema
“Nakumbuka baada ya kumaliza muda wangu kama balozi wa Tanzania nchini Marekani tulimuacha Latoya akiendelea na masomo yake huko huko Marekani.Baada ya mwaka mmoja kupita ndipo alipotueleza kwamba ana mpango wa kufungua biashara hapa Tanzania ingawa hakusema pesa za kuanzisha biashara hiyo amezitoa wapi.Kama utani alianzisha kiwanda cha kutengeneza nguo na baadae biashara zake zikaanza kuongezeka na kuongezeka na ghafla tukasikia kwamba binti yetu amekuwa ni bilionea.Jambo hili si la kufumbia macho mama Latoya tunatakiwa tufahamu ni wapi binti yetu alikoupata utajiri huu mkubwa sana.Ukiachana na maswali hayo kwamba ni wapi alikotoa utajiri huu Latoya amekuwa ni mtu mgumu sana kuweza kuyaweka wazi maisha yake.Maisha yake yametawaliwa na usiri mkubwa sana.Jumba lake kubwa lina watumishi ambao hakuna hata mmoja ambaye amewahi kukiona chumba cha Latoya.Hakuna mfanyakazi anayeruhusiwa kufika katika ghorofa ya juu ambako ndiko anakolala Latoya.Unadhani ni kwa nini amefanya hivi ? Ni wazi kuna kitu anakificha.Kuna siri kubwa anyoificha na ambayo ni lazima tuifahamu.Nafikiri muda umewadia kwa sisi kuupata ukweli kupitia kwa huyu kijana Innocent ambaye anaonekana kuwa karibu sana na Latoya.Inaonekana ni marafiki wakubwa.” Mzee Curtis akamwambia mkewe ambaye alikuwa amekaa kimya akimsikiliza kwa makini
“Curtis nakubaliana nawe kwa yote uliyoyasema.Ni kweli kwamba Latoya ni binti ambaye tumempata kwa shida baada ya kukaa kwa muda mrefu bila kujaliwa mtoto.Ni mtoto ambaye tulimpata kama muujiza vile kutokana na umri wetu kuwa umekwenda sana kwa maana hiyo tuna kila sababu ya kumchunga kama mboni ya jicho letu japokuwa amekwisha kuwa binti mkubwa sasa.Kusema ukweli utajiri wake unatia mashaka sana .Umekuwa ni utajiri wa ghafla mno kwa binti mdogo kama yeye.Katika umri wake huu mdogo tayari amekuwa billionea kweli nijambo la kushangaza mno.Kinachowashangaza watu ni kwamba sisi wazazi wake tunaishi maisha ya kawaida na wala hatuna utajiri wowote.Suala hili linawafanya watu wajiulize maswali mengi sana kuhusiana na wapi Latoya ameupata utajiri huu mkubwa.Kuna mtu aliwahi kuniambia kwamba alisikia tetesi kwamba eti Latoya anaishi na kiumbe wa ajabu sana chumbani kwake ambaye ndiye anayempatia utajiri huo na ndiyo sababu amekuwa hataki mtu yeyote aingie chumbani kwake.Kila mtu anaongea la kwake.Kuna ulazima wa kuutafuta ukweli kuhusiana na binti yetu.” Akasema mama Latoya
“Kuanzia kesho nitaanza kutafuta namna ya kuweza kuonana na yule kijana Innocent ili niweze kumuomba atusaidie kuupata ukweli halisi kuhusiana na Latoya.Twende tukalale mke wangu .Mambo ya Latoya ni magumu sana .” akasema mzee Curtis huku akiinuka pale sofani na kuongozana na mkewe kwenda kulala.

TUKUTANE SEHEMU IJAYO……
 
BEFORE I DIE

SEHEMU YA 26

ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Kusema ukweli utajiri wake unatia mashaka sana .Umekuwa ni utajiri wa ghafla mno kwa binti mdogo kama yeye.Katika umri wake huu mdogo tayari amekuwa billionea kweli nijambo la kushangaza mno.Kinachowashangaza watu ni kwamba sisi wazazi wake tunaishi maisha ya kawaida na wala hatuna utajiri wowote.Suala hili linawafanya watu wajiulize maswali mengi sana kuhusiana na wapi Latoya ameupata utajiri huu mkubwa.Kuna mtu aliwahi kuniambia kwamba alisikia tetesi kwamba eti Latoya anaishi na kiumbe wa ajabu sana chumbani kwake ambaye ndiye anayempatia utajiri huo na ndiyo sababu amekuwa hataki mtu yeyote aingie chumbani kwake.Kila mtu anaongea la kwake.Kuna ulazima wa kuutafuta ukweli kuhusiana na binti yetu.” Akasema mama Latoya
“Kuanzia kesho nitaanza kutafuta namna ya kuweza kuonana na yule kijana Innocent ili niweze kumuomba atusaidie kuupata ukweli halisi kuhusiana na Latoya.Twende tukalale mke wangu .Mambo ya Latoya ni magumu sana .” akasema mzee Curtis huku akiinuka pale sofani na kuongozana na mkewe kwenda kulala.


ENDELEA……………………………..


Hali ya unyevu nyevu na ubaridi ndivyo vilimfanya Latoya auinue mkono wake ili kuangalia kama alikuwa ndotoni ama vipi.Akausogeza mkono wake sehemu ile aliyohisi kuna unyevu nyevu akakutana na maji maji.Taratibu akainuka na kuketi kitako.fahamu zikamrudia akakumbuka kilichotokea muda mfupi uliopita.Alikuwa amepoteza fahamu baada ya kupatwa na maumivu makali.Mahala alipokuwa amekaa alikuwa amekalia dimbwi la damu.Akainama na machozi mengi yakamtoka.
“Kila siku zinavyozidi kusonga mbele ndivyo maumivu yanavyozidi kuwa makali na mateso kuongezeka.Ninazidi kuwa dhaifu kila uchao.Itanibidi nimuite daktari wangu aje mara moja ili anihudumie kwa sababu kwa wiki mbili sasa nimekuwa nikipoteza damu kwa wingi.” Latoya akawaza na kisha akainuka akawasha taa na kuitazama damu ile iliyoweka dimbwi pale sakafuni.Machozi yakamtoka tena.Taratibu akaenda bafuni akachukua ndoo iliyokuwa na maji na kitambaa akaifuta damu ile halafu akachukua vidonge katika kabati lake akameza akakaa kitandani.

“Nina wasi wasi ninaweza nikafa kabla sijaitimiza ahadi yangu niliyoiweka.Ninatakiwa kufanya kila linalowezekana ili kuweza kumpata mtu ambaye nitampenda naye atanipenda kwa dhati japokuwa ni kwa muda mfupi sana niliobaki nao.Mpaka sasa nina imani kabisa kwamba Innocent ni kijana pekee katika mamilioni ya vijana wa ulimwengu huu ambaye moyo wangu umetokea kumkubali na nina imani ni yeye pekee anayeweza kunipenda na kunijali katika kipindi hiki kifupi nilichobaki nacho.Ni kijana mwenye utofauti mkubwa na vijana wengine.Sijawahi kuona kijana kama yeye.” akawaza Latoya huku ameinama na machozi yakimchuruzika.
“Moyo wangu umemkubali na kumpenda Innocent.Tatizo lililopo ni kwamba nitawezaje kumweleza kwamba nahitaji kuwa naye? Atanielewa?..” Latoya akasimama na kuanza kuzunguka zunguka mle chumbani mwake halafu akavua mavazi yake na kuingia bafuni kuoga kisha akapanda kitandani kulala.

“Sidhani kama nitaweza kuishi maisha yangu yaliyobaki bila ya kuwa na Innocent.Nitajitahidi kadiri nitakavyoweza ili niweze kumpata kijana huyu ambaye nahisi kukutana naye ni mipango ya Mungu.Kuanzia kesho nitaanza kumuweka karibu ili aweze kunizoea.Japokuwa nimejaribu kuwa naye karibu kwa siku hizi mbili lakini bado naona ananiogopa.Yawezekana tayari atakuwa amesikia maneno yanayosemwa huko mitaani kuhusu mimi.Kama ni kweli atakuwa ameyasikia maneno hayo itanilazimu kufanya kazi ya ziada ili niweze kumuhakikishia kwamba mambo hayo yote si kweli,ni uzushi wa watu…Ooh ! Nilitaka kusahau kumtaarifu Dr Godwin aweze kuja mara moja siku ya kesho .” akawaza Latoya kisha akaichukua simu iliyokuwa pembeni yake akaandika namba za simu za daktari wake akampigia na kumuomba afike kesho yake bila kukosa.Baada ya kupiga simu ile akalala.



* * * *




Saa ya ukutani ilionyesha ilipata saa tatu na dakika nane asubuhi.Innocent akayafikicha macho na kisha akainua mikono akajinyoosha.
“Nahisi uchovu mwingi sana.Siku hizi mbili zimekuwa ni siku zenye pilika nyingi.Namshukuru Mungu kwa kunisaidia kupata wahisani walionisaidia kufanikisha mazishi ya Marina.Katika siku zote za maisha yangu sintamsahau Latoya .Bila yeye ningepata wakati mgumu sana.Kwa moyo wake wa upendo alikubali kuuchukua msiba ule na kuuleta hapa kwake na akahakikisha tunamsitiri Marina kwa heshima zote.Kwa sababu yake msiba wa binti masikini umekuwa ni msiba wa kihistoria hapa nchini.Kwa hili nina deni kubwa kwake na sioni kitu cha kumlipa ambacho kinaweza kulingana na thamani ya utu wake.Ni mtu mwenye roho ya huruma sana na utu. Jinsi alivyo na matendo yake ni vitu viwili tofauti kabisa.Watu wengi wenye utajiri mkubwa kama wa Latoya ni nadra sana kufanya kama alichokifanya Latoya.” Innocent akawaza huku akiinuka na kuingia bafuni kuoga na kisha oga akafungua kabati la nguo na kuchagua kuvaa suti nyeupe.Akajiangalia kwenye kioo na kutabasamu kwa namna alivyokuwa amependeza.
Akiwa katika kioo akijitazama na kutabasamu,kengele ya mlango ikalia ,kwa haraka akausogelea mlango na kuufungua.Akakutana na sura iliyomfanya astuke kidogo.Alikuwa ni latoya.Sura yake ilikuwa iking’aa na kila kila alivyotabasamu ndivyo uzuri wake uliongezeka mara dufu.Innocent akayakaza macho yake kumuangalia kana kwamba ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuonana na Latoya aliyekuwa amevaa suruari nyeupe na fulana nyeupe na kama kawaida yake alikuwa amevaa koti jeusi lililomfika magotini.

“Mbona unaniangalia hivyo? Akauliza Latoya huku akitabasamu
“Nimestuka baada ya kukuona nikadhani nimeonana na malaika.Umependeza sana leo” Innocent akasema na kumfanya Latoya acheke kicheko kikubwa na kusema
“hata wewe umependeza mno leo.Napenda sana rangi nyeupe.”
Innocent hakujibu kitu zaidi ya kutabasamu
“Umeamkaje Innocent? Tumekimbilia katika muonekano kabla ya kujuliana hali” akasema Latoya
“Nimeamka vizuri sana japokuwa nasikia uchovu mwingi kutokana na pilika pilika za siku hizi mbili.Vipi wewe umeamkaje?
“Nashukuru kama umeamka vizuri.Hata mimi nimeamka vizuri.”
Kisha salimiana Latoya akamuomba Innocent waelekee katika ukumbi wa chakula kwa ajili ya kupata kifungua kinywa.Tayari kifungua kinywa kilikwisha andaliwa na watumishi wawili waliokuwa wamevaa sare nyeupe na nyeusi walikuwa wamesimama kando kidogo ya meza kwa ajili ya kutoa huduma pindi ikihitajika.

“Grace na Sabrina wako wapi? Latoya akauliza

“Bado wamelala Madam.Kila mmoja anasema anajisikia uchovu mwingi” akajibu mmoja wa wale wasichana wawili waliokuwa wamesimama pembeni kidogo ya meza kwa ajili ya kutoa huduma.
“Wamechoka sana kwa shughuli za juzi na jana.Wanahitaji mapumziko “ akasema Latoya na kumkaribisha Innocent mezani.Kisha maliza kupata kifungua kinywa Latoya akatoa maelekezo kadhaa kwa Irene mwanamke ambaye alionekana ni mwenye umri mkubwa kuliko wafanyakazi wote wa nyumba ile .Alimuelekeza mambo kadhaa ya kufanya kwa siku ile na kisha akamkumbusha jambo.

“mama Irene , leo nahitaji kupumzika na sitaki kuonana na mgeni yeyote .Yeyote atakayeniulizia mwambie kwamba sipatikani kwa leo.Godwin daktari wangu atakuja baadae ,tuma dereva akampokee uwanja wa ndege.Akisha fika utanitaarifu mara moja.Nitakuwa bustanini kwangu ninapumzika,naomba unipelekee vinywaji” Latoya akamwambia Irene ambaye ndiye msimamizi wa watumishi wote katika jumba hili .Kutokana na utofauti mkubwa wa kiumri ,Latoya alimheshimu sana Irene na siku zote alikuwa akaimuita Mama.Ni Irene pekee ambaye alikuwa akiruhusiwa kufika katika bustani ya latoya iliyoko juu kabisa ya jumba hili .Hata Irene aliweza kufika huko kwa ruhusa maalum.
Latoya akamuongoza Innocent hadi katika bustani yake iliyokuwa juu kabisa ya jumba lake.Innocent akapigwa a mshangao mkubwa baada ya kuishuhudia bustani ile kubwa na nzuri ajabu iliyokuwa juu ya jumba lile.Kulikuwa na maua mazuri ya kupendeza sana .Bwawa kubwa la kuogelea .Sehemu ya kupumzikia kama utajisikia uchovu na kila aina ya vitu vizuri vilipatikana katika bustani hii ambayo Innocent aliiona ni kama bustani ya ajabu sana .Pamoja na kila aina ya maua mazuri yaliyoifanya bustani hii iwe ni ya kipekee kabisa kulikuwa vile vile na upepo mzuri sana kutoka baharini kwa sababu jumba hili lilikuwa mita kadhaa kutoka baharini.Ndege mbali mbali waliovutika na uzuri wa bustani ile walikuwa wakiruka na kuifanya bustani hii kuwa ni ya kipekee sana.Inocent hakuwahi kushuhudia bustani yenye uzuri wa kipekee kama hii.
“Amazing ! “ Innocent akasema kwa mshangao.Latoya akatabasamu na kusema

“hapa ndipo mahala ambapo nikihitaji kujipumzisha akili yangu huwa ninakuja .Kuna nyakati huwa ninahitaji kuwa katika ukimya na kutafakari mambo mbali mbali kuhusiana na maisha ya kila siku kwa hiyo huwa nakuja huku na kupumzika.Nikiwa huku huwa najiona kama vile niko nje ya ulimwengu huu kwa sababu ya mandhari yake na utulivu wa kipekee ulioko huku.” Latoya akasema huku akitembea taratibu na kumuonyesha Innocent sehemu mbali mbali za kuvutia katika bustani ile.
“Nimeipenda sana bustani yako.Sijawahi kuona bustani yenye kupendeza kama hii.Ningefurahi kama ungeniajiri kama mfanyakazi wa kuishughulikia bustani hii” akasema Inno na kumfanya Latoya acheke kicheko kikubwa

“Hata mimi ningefurahi sana kuajiri kijana mwenye nguvu kwa ajili ya kuihudumia bustani hii lakini kwa bahati mbaya siwezi kufanya hivyo kwa sababu kazi zote za bustani hii huwa nazifanya mimi mwenyewe.” Akasema Latoya
“si kweli Latoya. Wewe !! “ Innocent akauliza kwa mshangao
“kwani mimi unanionaje Inno? Ninaonekena kama mtu nisiyewea kufanya kazi za bustani? Latoya akauliza huku akitabasamu
“Sikumaanisha hivyo Latoya.Kilichonishangaza ni muda unaopata katika kuihudumia bustani yako hadi kuwa ya kupendeza namna hii.Nafahamu wewe ni mtu mwenye shughuli nyingi sana kwa maana hiyo muda uupatao ni kidogo sana wa kuweza kushughulika na bustani yako” Inno akasema.

“Ni kweli hayo unayoyasema Innocent.Muda ninaoupata kwa ajili ya mapumziko yangu binafsi ni mdogo sana na kusema ule ukweli mara nyingi Irene ndiye ambaye amekuwa akishughulika na kuifanyia usafi bustani hii na mara moja moja nipatapo wasaa huwa ninamsaidia.” Latoya akasema
‘Inaonekana katika watumishi wako wote unamuamini sana Irene” Inno akauliza

“Kweli kabisa.Irene ni mtu ambaye ninamuamini mno kuliko watumishi wangu wote.Yeye ndiye mtumishi wangu wa kwanza kabisa kwa hiyo ninamuamini kupita kiasi na ndiyo sababu ni yeye pekee ninayemruhusu aingie katika bustani hii.Hakuna mtu mwingine anayeruhusiwa kuingia katika bustani hii bila ruhusa yangu.” Latoya akasema na kumfanya Innocent apatwe na shauku ya kutaka kuuliza jambo lakini Latoya akamuwahi
“Zile nyumba nyeupe unazoziona kule ni nyumba za watumishi wangu” akasema Latoya huku akimuonyesha Inocent kijiji chenye nyumba nyeupe zilizokuwa zikionekana kwa mbali

“Zile zote ?
“Ndiyo.Nyumba zile zote unazoziona zinakaliwa na watumishi wangu.Kuna nyumba zaidi ya mia moja pale.”akasema Latoya na kisha akapiga hatua kuelekea katika sehemu ambayo kulikuwa na kijumba ambacho ndani yake kulikuwa friji lenye vinywaji mbali mbali akalifungua na kuchukua kinywaji anachokipenda.Innocent naye halikadhalika akachukua kinywaji na kisha wakaelekea katika sehemu iliyokuwa na viti vizuri vya kupumzika vilivyokuwa pembeni ya bwawa la kuogelea.Kila dakika iliyokatika Inno alizidi kujiuliza maswali mengi kuhusiana na Latoya.Alitamani apate nafasi ya kuweza kumuuliza Latoya kuhusiana na maisha yake.
“Latoya napenda kuchukua nafasi hii kukushukuru sana kwa msaada mkubwa ulionisaidia .kwa kweli sipati neno ambalo linaweza likaelezea shukrani zangu kwako kwa kitendo cha kuchukua jukumu kubwa la kuhakikisha kwamba Marina anasitiriwa kwa heshima zote.Nina deni kubwa kwako na hata sijui nitalilipaje kwa sababu wema ulionitendea ni mkubwa sana kiasi kwamba sioni kitu cha kukulipa ambacho kinaweza kulingana na wema huu.Toka ndani kabisa ya moyo wangu ninasema ahsante sana.Nitaendelea kukushukuru katika siku zote za maisha yangu hapa duniani.Nitakuombea sana ili Mungu akupe baraka zake nyingi kwa moyo wako huu wa huruma.Naomba ufahamu kwamba siku zote utakuwa hapa moyoni mwangu.Sintakusahau kamwe katika maisha yangu.” Innocent akasema kwa hisia kubwa
“Innocent nakushukuru sana kwa maneno yako ya shukrani kwangu.Inno naomba ufahamu kwamba kila kitu kinafanyika kutokana na maongozi ya mwenyezi Mungu.Sikutegemea kama ningeweza kuonana nawe siku ile.Lakini ni Mungu aliyetukutanisha katika mazingira kama yale .Nimekuwa nikisaidia watu mbali mbali kupata msaada wa matibabu ndani na nje ya nchi.Mpaka sasa hivi taasisi yangu imekwisha okoa maisha ya watu zaidi ya 2000 waliopata msaada wa kimatibabu katika hositali za ndani na nje ya nchi.Pamoja na msaada huo mkubwa ambao nimekuwa nikiutoa kwa watu wsiokuwa na uwezo wa kulipia gharama za matibabu ,sijawahi kuguswa kama nilivyoguswa na suala la marina.Nilisikia uchungu mwingi sana kwa jinsi ulivyonielezea hali yake.Kwa maana hiyo Innocent sote tuliguswa kwa namna moja au nyingine kwa msiba ule wa marina.Sote tuliumia na kwa maana hiyo msiba ule haukuwa wako peke yako.Ulikuwa ni wetu sote.Tumshukuru Mungu kwa kutusaidia tumefanikiwa kumsitiri mwenzetu kwa heshima zote na kinachobaki kwetu ni kuzidi kumuombea ili aweze kupumzika kwa amani huko aliko.” Latoya akasema akachukua kinywaji chake akanywa kidogo
“Pamoja na hayo yote uliyoyasema Latoya ,napenda nikiri kwamba u mwanamke mwenye roho ya huruma sana.Ninakuona uko tofauti sana na watu wengine wenye uwezo mkubwa kifedha .Kuna nyakati huwa ninajisahau na kufikiri labda wewe ni mmoja wa wale malaika ambao tunasimuliwa kwamba huwa wanashushwa na Mungu ili waweze kuishi na binadamu na kuwasaidia” Inno akasema na kumfanya Latoya acheke kwa nguvu.
“Innocent umenifurahisha sana leo.Malaika hawana mwili kama huu.Huu ni mwili wa kawaida wa kibinadamu.Kwa hiyo mimi ni binadamu wa kawaida na si malaika.” Latoya akasema huku akiendelea kucheka halafu akasema
“Innocent naomba nikufahamishe kwamba ni nchi chache sana za ulimwengu huu ambazo sijafika.Katika nchi zote nilizozitembelea sijawahi kukutana na kijana mwenye roho ya huruma kama yako.Nimepata taarifa zako nyingi toka kwa Sabrina ambaye anakuona wewe kama mzazi wake kwa sababu bila wewe haelewi angekuwa wapi leo hii.Ni vijana wachache sana katika ulimwengu wa sasa ambao wanaweza wakajitoa kwa ajili ya watu wengine kama ulivyofanya wewe..” Latoya akasema na kumtazama Innocent.
“Nakubaliana nawe Latoya kwamba katika dunia ya sasa sehemu kubwa ya watu wametawaliwa na ubinafsi.Watu wamekuwa ni wenye kujipenda wenyewe na hivyo kuisahau sehemu kubwa ya jamii ya watu masikini na wenye uhitaji.Ninafurahi sana kukutana na mtu ambaye ana maono kama yangu yaani kujitoa kwa ajili ya kuwasaidia watu wenye uhitaji.Suala la Marina hata mimi lilinigusa kwa namna ya kipekee kabisa na ndiyo maana nikafanya kila nililoweza kwa ajili ya kutaka kumsaidia na kumuondoa toka katika maisha aliyokuwa akiyaishi na kumjengea maisha mengine mazuri yenye nuru.Sielewi ni kwa nini nilijikuta nikiguswa sana na Marina .Kupitia kwake nimeweza kujifunza mambo mengi sana na muhimu .Akili yangu imeweza kufunguka zaidi.Kwa kifupi tu nimegundua kwamba wengi wa wasichana hawa wenye maisha kama ya Marina wanajikuta wakiingia katika biashara hii ya kuuza miili yao kwa sababu mbali mbali .Kikubwa zaidi ni hali mbaya ya maisha inayowakabili huko watokako katika familia zao ndiyo inayosababisha wasichana wengi wakubwa kwa wadogo waweze kujihusisha na biashara hii ya ngono.Nimefika hadi mahala alipokuwa akiishi Marina.Nimekutana na maisha ya ajabu sana.Chumba kimoja kidogo kinakaliwa na wasichana zaidi ya saba.Wanaishi kama wanyama.Toka moyoni nimeguswa sana na maisha haya wanayoyaishi wasichana hawa na niko katika kufikiri ni namna gani nitakavyoweza kuwakomboa kutokana na umasikini walio nao.Nimefikir………………..” kabla hajaendelea mbele simu ya mezani iliyokuwa pembeni kidogo na mahala alipokaa Latoya ikalia.Latoya akauchukua mkono wa simu na kuita
“hallo”
“Madam Latoya Daktari Godwin tayari amewasili ” Ilikuwa ni sauti ya Irene

“ Ok Irene ninakuja hapo muda si mrefu “ Akasema Latoya na kumgeukia Innocent

“Innocet tutaendelea baadae na maongezi yetu.Kuna mgeni wangu amefika ninahitaji kwenda kumuona” akasema Latoya huku wakiinuka na kutoka mle bustanini.
Katika sebule maalum kwa ajili ya Latoya na wageni wake wa muhimu alikuwepo mzungu mmoja mwenye nywele ndefu na ndevu nyingi akiwa amekaa akimsubiri Latoya.Huyu alikuwa ni Dr Godwin ambaye ndiye daktari anayemtibu Latoya.
“Dr Godwin.karibu sana” akasema Latoya

“Ahsante sana Latoya nimekaribia.” Akasema Godwin huku akitoa tabasamu kubwa sana na kisha wakakumbatiana
“Dr Godwin,kutana na rafiki yangu anaitwa Innocent.Innocent kutana na daktari wangu anaitwa Godwin” Latoya akatoa utambulisho mfupi
Innocent akampa mkono Godwin

“nafurahi sana kukufahamu Dr Godwin”
Dr Godwin akajaribu kufunua mdomo wake lakini hakuweza kuongea kitu.Alikuwa akiongea kama bubu.Innocent akastuka.



TUKUTANE SEHEMU IJAYO…
 
BEFORE I DIE

SEHEMU YA 27

ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Katika sebule maalum kwa ajili ya Latoya na wageni wake wa muhimu alikuwepo mzungu mmoja mwenye nywele ndefu na ndevu nyingi akiwa amekaa akimsubiri Latoya.Huyu alikuwa ni Dr Godwin ambaye ndiye daktari anayemtibu Latoya.
“Dr Godwin.karibu sana” akasema Latoya

“Ahsante sana Latoya nimekaribia.” Akasema Godwin huku akitoa tabasamu kubwa sana na kisha wakakumbatiana
“Dr Godwin,kutana na rafiki yangu anaitwa Innocent.Innocent kutana na daktari wangu anaitwa Godwin” Latoya akatoa utambulisho mfupi
Innocent akampa mkono Godwin
“nafurahi sana kukufahamu Dr Godwin”
Dr Godwin akajaribu kufunua mdomo wake lakini hakuweza kuongea kitu.Alikuwa akiongea kama bubu.Innocent akastuka.


ENDELEA……………………………


“mama Irene naomba ukae na Innocent kwa muda huu ambao nina maongezi na daktari wangu.”Latoya akamwambia Irene halafu akamgeukia Innocent
“Innocent ninakuacha kidogo na mama Irene nina maongezi na daktari wangu.Nitarejea baada ya muda mfupi”
Latoya na Godwin wakaondoka huku wakiongea na kucheka kwa furaha.Innocent alizidi kuchanganyikiwa.
“Irene huyu dokta Godwin ana matatizo gani? Mbona alipotaka kuongea na mimi alishindwa na kuanza kuzungumza kama bubu? Innocent akamuuliza Irene
Irene akamuangalia Innocent kwa makini sana akatabasamu na kusema
“Innocent ,katika nyumba hii kuna mambo mengi sana ambayo utayaona na yatakushangaza kwa kiasi kikubwa sana.Ninachokuomba ni wewe kuwa mvumilivu kwa kila utakachokiona katika jumba hili.Kwa ufupi ni kwamba yule daktari hawezi kuongea na mtu mwingine yeyote zaidi ya Latoya.Ni Latoya pekee mwenye uwezo wa kumfanya dokta Godwin aongee.Akiwa na Latoya Godwin anaweza akaongea vizuri kabisa lakini akisha achana na Latoya anakuwa bubu.Hawezi tena kuongea na mtu yeyote yule.Nimekaa na Latoya kwa muda wa miaka zaidi ya tisa sasa na ni mtu mwenye roho ya ajabu.Ana wema uliopindukia.Nina watoto wangu wawili wanaosoma Ulaya na ni yeye ndiye anayewagharamia.Latoya ni mtu mzuri ,ana roho nzuri Mimi nimekuwa mtu wake wa karibu na ananiamini kupita mtu yeyote yule lakini katika siku zote hizo sijawahi kukiona chumba cha Latoya.Ni mimi pekee ninayeruhusiwa kuingia katika ghorofa ya juu ambayo ndiko anaishi Latoya.Ni mimi pekee ninayeruhusiwa kuingia katika bustani yake pekee iliyoko juu ya jumba hili lakini napenda nikiri kwamba sijawahi kukiona chumba cha Latoya hata mara moja .mwisho wangu mimi ni katika ule mlango mkubwa mweupe.Siruhusiwi kuvuka pale.” Irene akamwambia Innocent ambaye alikuwa akitiririkwa na jasho jingi.Alizidi kuchanganyikiwa.
“ Irene maneno yako yananiogopesha sana Maneno yako yananifanya nihisi mambo mengi a kuhusiana na Latoya. Kuna nyakati nimekuwa nikihisi pengine huyu si binadamu wa kawaida kutokana na mambo yake na hata muonekano wake ulivyo” akasema Innocent akiwa na sura iliyoonyesha uoga fulani kutokana na yale aliyoyasikia.
“Innocent tafadhali naomba usiogope kwa sababu Latoya ni mtu mwenye roho nzuri mno kama nilivyokueleza.Amekuwa akisaidia mamia ya watu wenye matatizo mbali mbali ndani na nje ya nchi.Hivi majuzi tu ametoa msaada wa kuwajengea nyumba wale waathirika wote wa mafuriko.Ni mtu ambaye ana roho ya huruma sana .Ninachoweza kukushauri ni kwamba katu usimuogope Latoya .Ni mtu mzuri anayependa watu .Nimekuwa na Latoya kwa muda mrefu sasa ninamfahamu vizuri sana na ninaweza kusema kwamba una bahati ya aina yake kwa sababu toka nimemfahamu sijawahi kumuona akiwa karibu na kijana wa kiume kama ulivyo naye wewe kwa sasa.Sijawahi kumuona Latoya akiwa na uso uliojaa nuru kama ilivyo sasa hivi.Tafadhali jaribu kumsoma na kumfahamu vizuri .Ukiweka pembeni mambo yake fulani fulani ambayo yanaonekana kama si ya kawaida Latoya ni mtu mzuri sijapata kuona .” Irene akamwambia Innocent

“Irene kusema ukweli unazidi kunichanganya sana .Unaposema mambo yake ya ajabu ajabu ambayo si ya kawaida unamaanisha nini? Hebu nieleze Irene kwa sababu umekaa na Latoya kwa muda mrefu zaidi kupita mtumishi yeyote yule.Ni mambo ya namna gani hayo? Niweke wazi tafadhali” akasema Innoent

“Innocent kuna mambo mengi ambayo ukikaa na Latoya utayagundua ambayo utayaona kama si ya kawaida lakini sisi tunaoishi naye siku zote tumekwisaha yazoea na kuyaona ni mambo ya kawaida sana.Kwa mfano ni kama vile nilivyokueleza kwamba hakuna mtu yeyote isipokuwa mimi anayeruhusiwa kufika katika ghorofa ya juu kabisa anayoishi latoya.jambo lingine ni kwmba hakuna mtu yeyote aliyewahi kukiona chumba cha Latoya zaidi ya Dr Godwin ambaye naye hawezi kuongea na mtu mwingine yeyote zaidi ya Latoya pekee kwa maana hiyo ni kwamba hakuna ajuaye mahala anakolala latoya kukoje.Kitu kingine ambacho unaweza ukakiona kama si cha kawaida ni kwamba hata siku moja Latoya hajawahi kuacha kuvaa koti jeusi.” Irene akazidi kumchanganya Innocent

“Kuna siku aliwahi kukueleza anaumwa ugonjwa gani? Akauliza Innocent
“hapana Innocent ,hata siku moja hajawahi kunieleza anaumwa kitu gani.Daktari wake huwa anakuja na kuondoka mara kwa mara lakini sijafahamu Latoya anasumbuliwa na ugonjwa gani kwa sababu siku zote amekuwa mzima wa afya.Toka nimemfahamu Latoya sijawahi hata mara moja kusikia au kumuona akiumwa.” akasema Irene na mara akatokea mtumishi mmoja aliyekuwa amevaa suti nyeusi na shati jeupe
“mama Irene ,kuna mgeni wa madam Latoya sebuleni.Ni mzee Curtis” akasema msichana yule aliyekuwa amependeza sana kwa mavazi aliyokuwa ameyavaa

“ Innocent baba mzazi wa Latoya amekuja ngoja nikamkaribishe tafadhali” akasema Irene

“Tunaweza kwenda wote ? Hata mimi ninataka kwenda kumsalimu mzee Curtis kwa sababu nilionana naye mara moja tu msibani na hatukupata wasaa wa kutosha wa kujuana”
Irene akakubaliana na Innocent na kuongozana kwenda kuonana na baba wa Latoya balozi mstaafu mzee Curtis.

“ Baba shikamoo” Irene akamsalimu mzee Curtis
“marahaba mama.Hamjambo hapa? Akasema mzee Curtis.
“hatujambo baba.habari za nyumbani?” Akasema Irene akiwa amepiga magoti
‘ Tunamshukuru Mungu sisi wazima tunaendelea vizuri sana.Poleni na shughuli za msiba “ akasema mzee Curtis
“Tumekwisha poa baba” akasema Irene.

“karibu sana “ Irene akaendelea kumkaribisha balozi mzee Curtis.
“mzee shikamoo” Innocent akamsalimu mzee Curtis
“Ouh kijana..marahaba mwanangu hujambo? Nimelisahau jina lako unaitwa nani tena? Akasema mzee Curtis akiwa katika tabasamu huku ameshikana mkono na Innocent
“Ninaitwa Innocent “
“Exactly ! ..Innocent.Nafurahi sana kukutana nawe tena.Pole sana na matatizo yaliyotokea”
“Tumekwisha poa mzee.Ni mambo ya kawaida katika dunia”

“kweli Innocent.Matatizo ni sehemu ya maisha ya binadamu na hatuna budi kuyakubali.Tunapopatwa na matatizo ndipo tunakomaa kiakili” akasema mzee Curtis
“Kweli kabisa mzee.Mama hajambo nyumbani? Innocent akasema
“mama yako mzima nimemuacha amekwenda kuangalia mifugo huko shambani na mimi nikasema ngoja nipite hapa niwajulieni hali kwanza kwa sababu toka msiba umemalizika sijapata wasaa wa kufahamu mnaendeleaje.”
“Sisi tunaendelea vizuri sana baba” Irene ambaye alikuwa ameketi sofani akajibu
“Latoya yuko wapi? Akauliza mzee Curtis.

“Madam Latoya yuko na daktari wake ambaye amefika muda si mrefu” akasema Irene

“Ok ..kama yuko na daktari wake hakuna tatizo mimi nitakuwepo kule bustanini nikipumzika .Atakapomalizana na daktari wake utanipa taarifa.” Mzee Curtis akasema huku akiinuka sofani
“innocent unaonaje kama tukienda kupoteza wakati bustanini?
“hakuna tatizo mzee” Inocent akasema na kisha wakaongozana kuelekea bustanini.Ni katika bustani hii ambayo siku mbili zilizopita ilitumika katika msiba wa Marina.Ilikuwa ni bustani nzuri ajabu iliyokuwa pembeni ya ufukwe wa bahari.

“Innocent nimeshukuru sana kwa kumkuta Latoya akiwa na mgeni wake kwani safari hii ya kuja huku ilikuwa ni kwa ajili yako.”akaanzisha mazungumzo mzee Curtis

“Innocent pamoja na pole zangu nyingi sana za kupotelewa na rafiki yako ambaye tumemzika siku moja iliyopta nimefurahi sana kugundua kwamba mwanangu Latoya anao marafiki kama wewe .Sikujua hapo kabla kama Latoya ana marafiki wenye akili na upeo mkubwa kama ulivyo wewe.Nimefurahi sana baada ya kukuona ukiwa na mwanangu” akasema mzee Curtis na kumfanya Inno atabasamu
“Mzee Curtis,hata mimi ninafurahi sana kuwa na rafiki kama Latoya ambaye ni mtu mwenye huruma na ukarimu wa kipekee sana.hana dharau hata kidogo na anawaheshimu watu wote wakubwa kwa wadogo licha ya utajiri na uwezo mkubwa kifedha alionao.Mzee Curtis ninaweza kusema kwamba una bahati sana kuwa na binti kama Latoya.” Innocent akamwambia mzee Curtis

“Siku zote huwa namshukuru sana Mungu kwa baraka hii kubwa ya mtoto aliyotupatia.Mimi na mama yake Latoya tulikaa muda mrefu sana bila kujaaliwa mtoto na tumekuja kupata baraka ya mtoto wakati tayari umri umekwenda sana ndiyo maana unaona tayari sisi ni wazee lakini Latoya bado ni binti mdogo.Nilimpata Latoya muda mfupi kabla ya kuwa balozi wa Tanzania nchini Marekani” akasema mzee Curtis

“Umewahi kuwa balozi wa Tanzania nchini marekani? Akauliza Innocent
“Ndiyo.Na si marekani tu .Nimekuwa balozi wa Tanzania katika nchi mbali mbali na nchi ya mwisho ilikuwa marekani.Nimefanya kazi pale ubalozini hadi nilipostaafu na kurejea nyumbani.Ina maana Latoya hajakufahamisha lolote kuhusiana na familia yake?” Akasema mzee Curis

“Hapana mzee.Latoya hajanieleza lolote kuhusiana na familia yake” Inno akajibu

“Sishangai kwa sababu Latoya ni mtu mmoja msiri sana na siku zote huwa hapendi kuzungumza mambo yake ya ndani .kwa ufupi tu ni kwamba mimi na mke wangu tulijaaliwa kumpata mtoto tukiwa wazee.Latoya ni binti pekee ambaye tulifanikiwa kumpata.Tulimlea katika makuzi mazuri yaliyojaa maadili na imani.Toka akiwa mdogo tulimfundisha kupenda watu,kuwaheshimu watu wengine na zaidi ya yote tulimfundisha kuishi katika imani.Baada ya kumaliza muda wangu wa utumishi nchini marekani nilirejea nyumbani na kumuacha latoya akiendelea na masomo yake nchini marekani.Baada ya kama miaka miwili hivi,Latoya alinipa taarifa kwamba anataka kuanza kufanya biashara.Nilimuuliza kwamba mtaji wa kufanya biashara hiyo ameupata wapi na akasema kwamba kuna mtu ambaye ameahidi kumkopesha fedha za kufanya biashara hiyo.Ni kweli kama alivyosema alikuja na kuianzisha kiwanda kidogo cha nguo biashara ambayo taratibu ikaanza kukua na kupanuka na hatimaye baada ya muda mfupi Latoya akaanza kujulikana kama msichana mdogo lakini mwenye mafaniko makubwa.Sifa za Latoya zikaanza kuvuma kama upepo na sasa ikawa si kwa Tanzania tu bali afrika kwa ujumla.Huo ndio ukawa mwanzo wa latoya huyu tunayemfahamu leo ambaye kwa mujibu wa tathmini iliyofanyika kuhusiana na watu matajiri katika ukanda huu wa kusini ya jangwa la sahara latoya anaongoza .Utajiri wake unaongezeka kwa kasi kila kukicha.Ni suala hili ambalo limeacha maswali mengi sana katika jamii.Maisha yake yametawaliwa na siri kubwa mno .Hakuna anayefahamu latoya ameupata wapi utajiri huu mkubwa.Hata sisi wazazi wake tunashangaa sana kwa maisha haya ya mwana wetu ambayo yanasiri nzito nyuma yake.Aina ya maisha anayoyaishi inawachanganya watu zaidi.Mpaka leo hii hakuna mtu ambaye amewahi kukiona chumba anacholala latoya.Ni mtumishi wake mmoja tu ambaye anaruhusiwa kufika katika ghorofa ya juu ambayo anaishi yeye peke yake lakini hata mtumishi huyo kuna mahala ambako anatakiwa kuishia na kutokuendelea mbele.Mtu mwingine yeyote ambaye utaingia katika ghorofa ile bila ruhusa maalum unapatwa na mambo ya ajabu ajabu sana.kwa mfano kuna mtumishi mmoja ambaye aliamua kwenda ghorofani kule ili akachunguze Latoya anaishi vipi lakini hakufanikiwa kuona kitu chochote na badala yake akakutwa amelala ufukweni katika pwani ya Zanzibari.Mpaka leo hii mtu huyo yuko Ulaya akitunzwa katika kituo cha kuwatunzia wagonjwa wa akili kwa sababu akili yake haiko sawa.Mtu wa pili alikuwa ni mlinzi wake ambaye naye alitaka kwenda kuchunguza namna gani Latoya anaishi lakini naye aliokotwa katika mapango ya Amboni huko Tanga.Kwa bahati mbaya mtu huyu alifariki siku chache baadae.Toka wakati huo hakuna tena mtu yeyote anayethubutu kutaka kumchunguza Latoya.Toka nimemfahamu binti yangu huyu nina imani kwamba wewe ni kijana wa kwanza wa kiume kuwa naye karibu kwa sababu toka akiwa mdogo alikuwa akipenda sana siku moja awe mtawa.Hakupenda kuzoeana na vijana wa kiume..hata hivyo….” Ghafla mzee Curtis akastushwa na kishindo cha muanguko.Innocent alikuwa amejikwaa katika kisiki na kuanguka chini..haraka haraka mzee Curtis akamtazama kama ameumia ama la.
“Pole sana Innocent.”
“Ahsante mzee” Innocent akasema huku akijifuta futa.
“Innocent nafahamu nimekueleza mambo mengi kuhusiana na Latoya na nina imani tayari umekwisha ingiwa na uoga mkubwa.Si lengo langu kukuogopesha na ninakuomba tafadhali usiogope hata kidogo.Latoya ni mtu mwenye roho nzuri kupindukia.Nimekueleza haya yote kwa sababu nahitaji umfahamu mwenzako vizuri .Pamoja na hayo kuna jambo ambalo ningeomba unisasidie kulifanya” akasema mzee Curtis
“jambo gani hilo mzee? Innocent akauliza

“Innocent wewe ni mtu ambaye naweza kusema kwamba ni wa kwanza katika maisha ya Latoya kuwa karibu naye ukiacha yule daktari wake ambaye hakuna mtu mpaka leo anayefahamu huwa anamtibu ugonjwa gani latoya.Kutokana na ukaribu huo ninakuomba unisaidie kufanya uchunguzi juu nini siri ya maisha yake anayoificha”
“No ! Mr Curtis No…I Cant do that….” Innocent akasema kwa haraka
“Innocent…………………”

“No ! Nimesema siwezi kufanya hivyo mzee Curtis.Siwezi kabisa kufanya jambo la hatari kama hilo.Umenielezea wewe mwenyewe mambo yaliyowapata wale waliojaribu kuyachunguza maisha ya Latoya.Mimi sitaki yanikute kama yaliyowakuta watu hao.Kuna watu wengi ambao bado wanahitaji msaada wangu kwa sasa.tafadhali naomba usinishawishi kufanya hivyo…” Innocent akasema kwa sauti ya ukali kidogo na kuanza kutembea kwa haraka kurudi katika jumba la Latoya “Innocent nimekuambia haya yote si kwa ajili yangu mimi .Its for you own good…Tafadhali Innocent fanya kama nilivyokuomba” Mzee Curtis naye alikuwa akitembea kwa kasi akimfuata nyuma Innocent ambaye hakuwa akijibu kitu.
Kila mtu alishangazwa na hali iliyotokea kwani Innocent aliingia mle ndani kwa kasi ya ajabu na huku uso wake ukiwa na hasira na mara akafuatia mzee Curtis ambaye naye alikuwa akitembea kwa kasi akimfuata Innocent.Watumishi pamoja na walinzi walibaki wakijiuliza nini kimetokea kwa sababu watu hawa wawili waliondoka kama marafiki wakubwa lakini ghafla wamerudi wakiwa katika hali hii.
Innocent akapanda ngazi za kuelekea ghorofani katika chumba chake na mee Curtis naye akamfuata.Irene alililiona hilo na akaanza kupanda ghorofa kwa kasi huku akimpigia kekele mzee Curtis kutokuendelea na kumfuatilia Innocent lakini mzee Curtis alikwisha ghafilika na hakutaka kumsikiliza mtu yeyote.Innocent akaufungua mlango mkubwa wa kuingilia katika ghorofa ya mwisho ambayo ndiyo ghorofa asiyoruhusiwa kuingia mtu ambaye hana ruhusa maalum toka kwa Latoya.Jitihada za Irene kiumpigia kelele mzee Curtis ziligonga mwamba kwani tayari alikwisha ufikia mlango na kutaka kuingia ndani lakini ghafla kikatokea kitu kama mwanga mkali sana na wenye nguvu kubwa na kumpiga mzee Curtis na kumrusha hadi ghorofa ya chini yake na kisha milango ikajifunga.Irene akaogopa sana na kuchanganyikiwa asijue afanye nini.Hakuwahi kuona kitu cha namna hiyo kikitokea .Mzee Curtis alikuwa amelala chini akitokwa na damu puani na masikioni.Irene akapiga kelele kuomba msaada na mara walinzi wakafika na kumchukua mzee Curtis wakampakia garini na kwa haraka wakamkimbiza hospitali


TUKUTANE SEHEMU IJAYO……
 
BEFORE I DIE

SEHEMU YA 28

ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Kila mtu alishangazwa na hali iliyotokea kwani Innocent aliingia mle ndani kwa kasi ya ajabu na huku uso wake ukiwa na hasira na mara akafuatia mzee Curtis ambaye naye alikuwa akitembea kwa kasi akimfuata Innocent.Watumishi pamoja na walinzi walibaki wakijiuliza nini kimetokea kwa sababu watu hawa wawili waliondoka kama marafiki wakubwa lakini ghafla wamerudi wakiwa katika hali hii.
Innocent akapanda ngazi za kuelekea ghorofani katika chumba chake na mee Curtis naye akamfuata.Irene alililiona hilo na akaanza kupanda ghorofa kwa kasi huku akimpigia kekele mzee Curtis kutokuendelea na kumfuatilia Innocent lakini mzee Curtis alikwisha ghafilika na hakutaka kumsikiliza mtu yeyote.Innocent akaufungua mlango mkubwa wa kuingilia katika ghorofa ya mwisho ambayo ndiyo ghorofa asiyoruhusiwa kuingia mtu ambaye hana ruhusa maalum toka kwa Latoya.Jitihada za Irene kiumpigia kelele mzee Curtis ziligonga mwamba kwani tayari alikwisha ufikia mlango na kutaka kuingia ndani lakini ghafla kikatokea kitu kama mwanga mkali sana na wenye nguvu kubwa na kumpiga mzee Curtis na kumrusha hadi ghorofa ya chini yake na kisha milango ikajifunga.Irene akaogopa sana na kuchanganyikiwa asijue afanye nini.Hakuwahi kuona kitu cha namna hiyo kikitokea .Mzee Curtis alikuwa amelala chini akitokwa na damu puani na masikioni


ENDELEA……………………..


Latoya alikuwa katika chumba kidogo kilichokuwa pembeni ya chumba chake ambacho kimesheheni vifaa lukuki na kuonekana kama hospitali ndogo.Alikuwa amelala katika kitandani na mkononi alikuwa ameunganishwa na mpira uliotoka katika chupa ya damu iliyokuwa imetundikwa juu ya kitanda.Hii ilikuwa ni chupa ya pili.Usoni machozi yalikuwa yakimtoka.

“Unalia nini Latoya? Akauliza daktari wake Godwin
“Godwin ninasikitika sana kwa sababu sijawahi kuishiwa damu kiasi hiki.Ninazidi kudhoofu ingawa hakuna mtu ambaye anaweza akalitambua hilo kwani katika macho ya kawaida ninaonekana ni mzima wa afya tele.Ninaogopa ninaweza nikafa kabla sijaitimiza ahadi yangu” latoya akasema huku akishindwa kuyazuia machozi kumtoka

“Latoya ni kweli hali yako kiafya inaonyesha unazidi kudhoofu.nakuomba kwa sasa uanze kupunguza baadhi ya mambo na uanze kuwa na mapumziko marefu. Hali uliyokuwa nayo hata mimi ilinistua sana.” Godwi akasema
“Nitajitahidi kufanya hivyo lakini kuna jambo moja ambalo linanipa mateso makubwa.”

“jambo gani hilo Latoya”
“Ni ahadi yangu niliyoiweka kwamba ni lazima niitimize kabla sijafa” akasema latoya na ghafla mpira uliokuwa ukipeleka damu mwilini mwa Latoya ukapasuka na damu nyingi kumrukia usoni.Godwin akastuka sana kwa hali ile.

“something is wrong !!! akasema Latoya akiwa anahema kwa nguvu.

“Godwin simamisha kila kitu.Something is wrong here” akasema Latoya ambaye alikuwa amekaa kitandani.
“Latoya ,bado chupa ya mwisho ya damu haijamalizika kuingia mwilini” akasema Dr Godwin
“Listen to me Godwin.something isn’t right here…damu uliyoniwekea inatosha kwa sasa” akasema Latoya huku akiifungua plasta toka katika mkono wake na kuitupa pembeni.
“Kuna kitu ambacho hakiko sawa.Ninahisi kuna kitu kimetokea .Moyo wangu umesikia uzito usio wa kawaida.Kitu gani kinaweza kuwa kimetokea? Akawaza Latoya kisha akainuka na kuelekea bafuni kuoga na kujifuta damu ile ambayo ilikuwa imemtapakaa mwilini baada ya mpira ule wa damu kupasuka.
“Godwin nafikiri kazi yako kwa leo imekwisha .Kama hali yangu itakuwa na mabadiliko nitakufahamisha mara moja” akasema Latoya akimwambia Dr Godwin

“Ok Latoya ,lakini nilihitaji kukaa hapa kwa muda zaidi kwa sababu ni nyakati kama hizi ninapata na mimi nafasi ya kuzungumza kama binadamu wengine.Ninapokuwa nawe najiona kama mtu ninayeishi.I feel life when I’m with you ”akasema Godwin kwa upole
“Godwin please kazi yako imekwisha na tafadhali naomba uelekee uwanja wa ndege uondoke.Nitakupigia simu kama kuna tatizo lolote litakalotokea” akasema Latoya akiwa ni mwingi wa wasi wasi

“Ok Latoya naomba usisahau kuyazingatia yale yote niliyokueleza.Jitahidi kupata mapumziko ya muda mrefu “ akasisitiza Dr Godwin.
“Nitajitahidi “ akasema Latoya huku akimsaidia Dr Godwin kubeba begi lake lenye vifaa na kumfungulia mlango wa chumba na Dr Godwin akaanza kupiga hatua kuondoka.

“Nini kinaweza kuwa kimetokea? Naogopa hata kuuliza ni jambo gani lililotokea.Naogopa Innocent asije kuwa amepatwa na matatizo” akawaza Latoya akiwa amekaa kitandani kwake.Baada ya tafakari ya muda akachukua simu yake na kumpigia Irene.
“Mama Irene kuna tatizo lolote huko chini? Akauliza Latoya
“Ndiyo madam Latoya.Kuna tatizo limetokea muda mfupi uliopita”
“tatizo gani limetokea? Akauliza Latoya kwa wasi wasi
“madam Latoya ni mzee Curtis”
“Curtis !! my father? Akauliza Latoya kwa mstuko
“Ndiyo Madam ”akajibu Irene
“Nini kimetokea mama Irene? Latoya akauliza kwa wasi wasi

“Mzee Curtis alifika hapa wakati ukiwa chumbani na Dr Godwin.Nilimwambia kwamba uko na daktari wako akasema hakuna tatizo atakusbiri mpaka utakapomaliza matibabu.Akasema kwamba anakwenda kupumzika bustanini.Kwa kuwa Innocent alikuwepo karibu mzee Curtis akamuomba waende bustanini Innocent akakubali”
“What !!…Daddy alikwenda bustanini na Innocent? Ouh My God ….” Akauliza latoya

“Ndiyo Madam Latoya.Waliongozana kwenda bustanini na baada ya kama nusu saa hivi nikamuoa Innocent akirejea kwa kasi na alionekana ni kama alikuwa amekasirishwa na kitu Fulani.Baada ya muda mfupi akatokea tena mzee Curtis naye akitembea kwa kasi kumfuata Innocent.Inaonekana kuna jambo walikuwa wameshindwa kuelewana .Innocent alipandisha ngazi za kuelekea chumbani kwake na mzee Curtis naye akaanza kupandisha ngazi kumfuata.Nilimkimbilia mzee Curtis na kumzuia asiendelee kumfuata Innocent lakini hakunisikia na akiwa na hasira akaendelea kumfuata Innocent”
“Ouh My God ! My father ….” Akasema Latoya akiwa ameinamisha kichwa chini.Baada ya kama dakika mbili hivi akauliza
“Irene yuko wapi baba?

“madam Latoya ,mzee Curtis alipofika mlangoni……..”
“Irene naomba unieleze yuko wapi Curtis ? akauliza Latoya
“Amekimbizwa hospitali haraka kwani hali yake iilikuwa mbaya na alikuwa akivuja damu puani na mdomoni”

“Ouh God ! amepelekwa hospitali gani ?
“ Latoya akasema kwa uchungu mkubwa.

“Maria Theresa hospital”
“Irene andaa security ..nataka kwenda hospitali sasa hivi kujua maendeleo ya baba” akasema Latoya huku akishindwa kuyazuia machozi kumdondoka
“Daddy nimekwambia mara nyingi kuhusiana na kuyafuatilia maisha yangu lakini hukutaka kunisikia.Ouh my father kwa nini lakini unaniongezea maumivu zaidi ya yale ninayostahili? “ akaongea Latoya huku akitoa machozi.Taratibu akavua viatu na kisha akaenda katika ile sehemu yake ambayo huwa anaitumia kwa maombi ,akawasha mishumaa tisa kuizunguka meza ile halafu akapiga magoti na kuinama kwa takribani dakika tano na kisha akainuka.Uso wake ulikuwa umejaa machozi.Akaenda katika meza yake ya vipodozi akarekebisha uso wake na kisha akavaa miwani na kushuka kuelekea chini. Walinzi wake tayari walikuwa wamejiandaa kama walivyokuwa wameelekezwa na Irene .Latoya akafunguliwa mlango akaingia garini na safari ya kuelekea hospitali ikaanza..Akiwa ndani ya gari lake mara simu yake inaita.Alikuwa ni mama yake.
“Shikamoo mama” akasema latoya
“Sina haja na salamu yako.Mwanangu umekosa nini hadi uamue kumuumiza baba yako kiasi hiki? Mwanangu tumekukosea nini?’ akalalamika mama yake
“mama plea……………………..” Latoya akataka kusema neno lakini mama yake akamzuia
“Usiseme lolote Latoya.Ila tambua kwamba umeniumiza sana mimi mama yako.Sikutegemea kama iko siku unaweza ukamfanyia mzazi wako jambo la kikatili kama hili.Hiyo tamaa ya mali na utajiri itakupeleka pabaya mwanangu na ninakuonya kwamba kama baba yako akifariki nitapambana na wewe hadi tone la mwisho la damu yangu.Mchawi mkubw…………….” Kabla mama yake hajamaliza neno alilotaka kulisema Latoya akakata simu.Alishindwa kujizuia akaanza kulia.Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa dereva wake kumshuhudia Latoya akiangua kilio.

“madam are you ok? Akauliza dereva wake huku akipunguza mwendo wa gari

“ I’m ok” akajibu kwa ufupi Latoya.Akatoa kitambaa na kuyafuta machozi .
“Mateso haya yatakwisha lini? Kadiri siku zangu za kuishi hapa duniani zinavyozidi kupungua na ndivyo mateso yanavyozidi kuongezeka.Ninauhakika mkubwa kwamba kuna kitu baba alimwambia Innocent ambacho kilimuudhi na kufanya washindwe kuelewana.Ni jambo gani hilo? Nitaongea na Innocent anieleze baba alimwambia nini.Najua ni lazima atakuwa alitaka kumlisha maneno kuhusiana na mimi kwa sababu si mara yake ya kwanza kuyachimba maisha yangu na nilikwisha muonya mara nyingi kuhusiana na kuyafuatilia maisha yangu lakini hakutaka kunisikia.” Akawaza Latoya wakiwa njiani kuelekea hospitali.
Katika geti la kuingilia hospitali kuu ya Maria Theresa Latoya alistushwa na umati mkubwa wa watu uliokuwapo nje ya geti.Waandishi wa habari walikuwa wamejazana pale nje ya geti la hospitali wakiwa na kamera zao tayari kabisa kuweza kupiga picha au kupata mawili matatu ya kuandika.Tayari walikwisha pata taarifa za jambo lililotokea nymbani kwa Latoya.Walinzi wa Latoya wakashuka katika magari na kuwasogeza pembeni waandishi wa habari waliokuwa wamezuia barabara kutokana na uwingi wao.Gari la Latoya likaingia ndani hospitalini na kuwaacha waandishi wa habari wakiishia kulipiga picha kwa nyuma.Gari liliposimama walinzi wake waliokuwa wamevaa suti nyeupe wakalizunguka gari na baada ya dakika mbili mlango ukafunguliwa na kwa kasi huku wakimuweka kati kati yao wakamuongoza Latoya kuelekea katika chumba alimokuwa amelazwa baba yake.Taarifa za uwepo wa Latoya katika hospitali ile zilisambaa kwa kasi sana zikichagizwa na vyombo mbalimbali vya habari na hivyo kusababisha umati wa watu waliotaka kumuona binti huyu bilionea ambaye anaumiza vichwa vya watu wengi na wengi walitaka wamuone kwa macho yao wenyewe.

“Pino tafadhali jaribu kutafuta ni kwa namna gani taarifa za tukio hili zimevifikia vyombo vya habari mapema namna hii.” Akasema Latoya akimwambia mmoja wa wasaidizi wake.
“Ok Madam” akajibu Pino kwa heshima.
“Stevie shughulikia ndege iwe tayari kwani tunamuhamisha baba na kumpeleka Marekani atatibiwa huko” akaamuru tena Latoya
“sawa madam” Stevie akasema kwa unyenyekevu mkubwa
Latoya akapokelewa na daktari mkuu wa hospitali hii Dr Alberto raia wa Italia ambaye alimpa taarifa fupi ya hali ya mgonjwa kisha akamuongoza kuelekea katika chumba alimolazwa baba yake.
“Mgonjwa anaendelea vizuri.Tayari tumemfanyia uchunguzi wa awali na vipimo vinaonyesha kwamba hakuna mahala kokote alikoumia.Tulidhani labda amepatwa na majeraha ya ndani lakini vipimo havionyeshi kama kuna jeraha lolote la ndani alilolipata.Tunataka kufanya uchunguzi wa mara ya pili ili tujiridhishe kwamba ni kweli mgonjwa hajapata majeraha yoyote .Hii ni ajabu sana kwa sababu hali aliyokuja nayo mzee Curtis ni tofauti kabisa na vipimo vinavyoonyesha.” Akasema daktari mkuu wa hospitali huku wakitembea kwa kasi kuelekea katika chumba alimolazwa mzee Curtis.

“nashukuru sana dokta kwa huduma mlizompatia baba yangu lakini hataendelea kukaa hapa kwa sababu ndege iko tayari tunamuhamisha kumpeleka Marekani kwa matibabu ya juu zaidi” akasema Latoya.
Chumba alimolazwa mzee Curtis kikafunguliwa mlango na Latoya akiwa ameongozana na daktari wakaingia ndani.Wengine wote wakabaki nje.Latoya akamshika kichwa baba yake akamtazama akashindwa kuyazuia machozi kumtoka.

“Doka tafadhali naomba uniache peke yangu na baba kwa dakika chache” Latoya akaomba na daktari akatoka mle chumbani.Latoya akamkumbatia baba yake ambaye alikuwa amelala pale kitandani na macho ameyafumba
“Dady kwa nini lakini ulifanya vile? Kwa nini hukuacha kuyafuatilia maisha yangu? Nilikukanya muda mrefu sana kuhusu jambo hili lakini hukunisikia.Dady unazidi kuniongezea mateso.Nilipokukataza kuhusiana na kuujua undani wangu nilikuwa na maana kubwa.Ninawapenda wazazi wangu kupita mnavyoweza kufikiri na sikuwa tayari jambo kama hili limfike mmoja kati yenu na ndiyo maana nimekuwa nikijaribu kujiweka mbali nanyi ili msipate nafasi ya kuliendeleza jambo hili.Dady nimeumia sana roho yangu kukuona ukiwa hapa kitandani.Huwezi kufahamu ni mateso kiasi gani umeniongezea kwa kitendo hiki cha leo..Ouh Daddy please talk to me why you did that? What you wanted to see? I already told you that there are questions not to be asked and answers not to be given but why you kept on asking the same forbidden question?.” Akasema Latoya huku akilia akiwa amemkubatia baba yake pale kitandani.Ghafla mzee Curtis akauinua mkono na kuishika shingo ya Latoya na kumfanya anyamaze kulia ghafla.

“ Daddy !! Latoya akasema kwa mstuko mkubwa sana.

“M..my..l ..lllo.oo.ve…….pleaa..aaa..sse…for..g..gi..giv..e me..” Mzee Curtis akasema kwa taabu.Latoya akamtazama baba yake na kuangusha machozi.
“Ouh My daddy you are alive..! Ouh daddy” akasema Latoya na kisha akamkumbatia tena baba yake kwa nguvu.Ghafla Latoya akasikia makelele nje ya mlango
“Nasema niachieni nikapambane na huyu mchawi humo ndani.Niachieni nikamfundishe adabu.Amekuja kummalizia mume wangu.Niacheni nikamtoe humo ndani” Baada ya kutega sikio kwa makini Latoya akaitambua sauti ile ilikuwa ni ya mama yake.

“Ouh My God another problem” akasema Latoya kwa sauti ndogo huku akiinuka na kusimama akafungua mlango na kukuta walinzi wake wakiwa wamemzuia mama yake kuingia mle chumbani.Akawaomba wamuache aingie chumbani.Mama yake Latoya akiwa amefura kwa hasira akasimama mlangoni .
“Umekuja kummalizia mume wangu? Sasa leo nataka nipambane mimi na wewe.Uchawi wako umevuka mipaka “ akasema mama yake Latoya na kisha akachomoka kwa kasi pale mlangoni akimuelekea latoya.
“Leo ni mimi au wewe” alisikika akisema mama Yule mwenye nguvu.Kwa kasi na nguvu zote alizokuja nazo akaruka kwa lengo la kumvamia Latoya na mara maajabu yakatokea.Mama yake Latoya aliamini kwamba alikuwa amemvamia Latoya na ghafla akiwa amenyoosha mikono yake kwa dhumuni la kuishika shingo ya mwanae akajikuta mikono yake ikishikana yenyewe Latoya alipotea machoni pake hivyo akapita mzima mzima kama yuko sehemu tupu na kwa nguvu alizokuwa amekuja nazo alijibamiza kichwa ukutani na kishindo kikubwa kikasikika.Kila mtu akafumba macho.Mama yake Latoya akaanguka chini na hakuongea tena

TUKUTANE SEHEMU IJAYO…
 
BEFORE I DIE


SEHEMU YA 29

ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Ouh My God another problem” akasema Latoya kwa sauti ndogo huku akiinuka na kusimama akafungua mlango na kukuta walinzi wake wakiwa wamemzuia mama yake kuingia mle chumbani.Akawaomba wamuache aingie chumbani.Mama yake Latoya akiwa amefura kwa hasira akasimama mlangoni .
“Umekuja kummalizia mume wangu? Sasa leo nataka nipambane mimi na wewe.Uchawi wako umevuka mipaka “ akasema mama yake Latoya na kisha akachomoka kwa kasi pale mlangoni akimuelekea latoya.
“Leo ni mimi au wewe” alisikika akisema mama Yule mwenye nguvu.Kwa kasi na nguvu zote alizokuja nazo akaruka kwa lengo la kumvamia Latoya na mara maajabu yakatokea.Mama yake Latoya aliamini kwamba alikuwa amemvamia Latoya na ghafla akiwa amenyoosha mikono yake kwa dhumuni la kuishika shingo ya mwanae akajikuta mikono yake ikishikana yenyewe Latoya alipotea machoni pake hivyo akapita mzima mzima kama yuko sehemu tupu na kwa nguvu alizokuwa amekuja nazo alijibamiza kichwa ukutani na kishindo kikubwa kikasikika.Kila mtu akafumba macho.Mama yake Latoya akaanguka chini na hakuongea tena


ENDELEA……………………….


Latoya alikuwa amesimama pembeni akishangaa kilichotokea.Kwa haraka daktari mkuu ambaye alikuwa mlangoni pamoja na watu walinzi wa Latoya wakaingia mle ndani na kumuangalia mama yake Latoya aliyekuwa amelala pale chini damu zikimtoka mdomoni.dr Alberto akachukua kifaa chake ha kupimia mapigo ya moyo akapima na kisha akainua kichwa.
“Tell me doctor how’s she? Akauliza Latoya
“I’m sorry Madam Latoya….she’s dead”.
"Doctor No ! Its a lie...my mother is not dead..please doctor tell me its not true" akasema Latoya huku machozi yakimtoka.Daktari akamuangalia na kisha akawaangalia watu wengine waliokuwamo mle chumbani na kwa masikitiko akasema
"I 'm sorry madam Latoya..your mother is dead" akasema daktari na kuinuka akawapigia simu wauguzi wafike na kitanda mara moja na kuuchukua mwili wa mama yake Latoya.Kila mtu alikuwa kimya kabisa.Taratibu Latoya akapiga magoti na kukishika kichwa cha mama yake.Akafumba macho akakaa kimya kwa dakika kama tano hivi halafu akainua kichwa.Macho yake yalikuwa yamejaa machozi. Akainuka na kwenda kumkumbatia baba yake ambaye naye machozi yalikuwa yakimtoka.

" I love you daddy" akambusu baba yake shavuni na kuwageukia watumishi wake.

" Stevie sitisha lile zoezi nililokwambia la ndege ya kumpeleka baba Marekani mpaka baada ya msiba huu kumalizika..Kwa sasa shughulikia mwili wa mama yangu uende ukakae katika chumba cha maiti katika hospitali ya masista ya St Magdalene .Nataka na baba yangu pia ahamishiwe katika hospitali hiyo haraka iwezekanavyo" akaamuru Latoya huku akiendelea kufuta machozi yaliyokuwa yakimtiririka.

" Yes maam.." akajibu Stevie akiwa amesimama kwa adabu na majonzi.
" Ukisha maliza suala hilo tukutane nyumbani kwangu kwa ajili ya maelekezo zaidi" akasema Latoya na kuanza kuondoka mle chumbani huku akiwekwa kati kati na walinzi wake.Alikuwa akilia.Taarifa za kifo cha ajabu cha mama yake Latoya zilisambaa kwa kasi sana pale hospitali na hivyo kuzua taharuki kubwa.Hali hii iliwafanya hata wagonjwa wale ambao walikuwa na unafuu wa kuweza kupiga hatua kutoka nje ya wodi zao kwa lengo moja tu la kutaka kumshuhudia huyu binti mdogo ambaye anasemekana kuwa na maisha yenye maajabu mengi.Latoya akaingia garini na msafara wake ukaondoka maeneo hayo ya hospitali huku waandishi wa habari wakijaribu kupata picha ambazo watazitumia katika habari watakazoziandika..
"Mungu wangu naomba usiniache katika wakati huu mgmu nilionao sasa.Ninahitaji sana kuwa na nguvu za kuweza kuvumilia katika kipindi hiki kigumu sana kwangu" akaomba kimoyo moyo Latoya huku ameinama chini machozi yakimtoka

" Siku zote nimekuwa nikijaribu kukaa mbali na wazazi wangu ili niweze kuwaepusha na mambo kama haya yaliyotokea.Siku zote nimekuwa nikikwepa kuwa karibu nao kwa sababu ninafahamu lengo lao kubwa ni kutaka kuyafahamu maisha yangu.I'm so sorry mom..I'm so sorry....." Latoya akawaza na kuendelea kulia.

" Kadiri siku zinavyozidi kwenda ndivyo mateso yanavyozidi kuongezeka.Kila siku linaibuka jambo jipya.Masikini mama yangu sitampata tena mama kama yeye.Nimepitia vipindi vingi vigumu katika maisha yangu lakini hiki kinaonekana kuwa ni kipindi kigumu sana kupita vyote." Latoya akaendelea kulia garini akielekea nyumbani kwake.
Akiwa amekaribia geti la kuingilia nyumbani kwake akakutana na gari mbili zilizokuwa zikitoka.Zikasimama baada ya kuuona msafara wa Latoya.Katika gari moja kati ya zile mbili alishuka Irene mtumishi wa Latoya anayemuamini sana.Moja kwa moja akaelekea katika gari la Latoya na alipomuona Irene akija akafungua mlango na kushuka garini.

" mama Irene kuna tatizo gani tena? akauliza Latoya
"Madam Latoya kuna tatizo limetokea wakati mmeondoka.Stephano mmoja wa wafanyakazi wetu alipatwa na matatizo ya ghafla ya kutokuongea.Amekuwa bubu ghafla.Tulijaribu kumuhoji kwa kuandika katika karatasi na akakiri kwamba ni yeye ndiye aliyepiga simu kwa waandishi wa habari kwamba baba yako amepatwa na matatizo na amepelekwa hospitali.Kwa sasa hali yake ni mbaya sana na tumelazimika kumkimbiza hospitali.Kabla hali yake haijabadilika aliandika ujumbe huu na kunitaka mtu yeyote yule asiusome zaidi yako" akasema Irene huku akimpatia Latoya bahasha yenye ujumbe ulioandikwa na Stephano.Latoya akaifungua bahasha ile na kuitoa barua iliyokuwamo ndani akaanza kuisoma.





" Kwako Madam Latoya
Nimelazimika kuandika waraka huu mfupi kwako kwa sababu sina hakika wakati unausoma waraka huu nitakuwa hai.Madam Latoya naomba kwanza nikuombe msamaha toka ndani ya moyo wangu kwa kuvunja moja ya masharti yaliyomo katika mkataba wangu.Ninakiri nimefanya kosa kubwa sana kwa tamaa ya pesa.Naomba nikiri kwamba nimekuwa nikitoa taarifa mbalimbali kwa waandishi wa habari ambao wamekuwa wakinilipa pesa nyingi kila ninapowapa habari yoyote inayohusiana nawe.Hivi leo ni mimi ndiye niliyewataarifu kuhusu tukio lililotokea nyumbani kwako lililomuhusu baba yako mzee Curtis.Madam Latoya nakufahamu sana kwamba wewe si mtu mbaya hata kidogo na utanisamehe kwa kosa hili nililolifanya.Siku zote umekuwa mtu mwema sana kwangu na kwa familia yangu lakini tamaa yangu ya kutokuridhika na kile nikipatacho ndiyo imesababisha mambo haya kunipata.Niandikapo waraka huu niko katka maumivu makali sana na ninastahili mateso haya kwa kosa nililolifanya.Narudia tena naomba unisamehe na kama nkifariki nakuomba usiache kunisomeshea watoto wangu uliokuwa ukiwagharamia kuwasomesha.
Natumai utanisamehe
Stephano"
Latoya alipomaliza kuisoma barua ile machozi yakaanza kumtoka akavua miwani yake mikubwa akafuta machozi.

"Yuko wapi Stephano? akauliza Latoya

" ndani ya gari" akajibu Irene na kisha Latoya akapiga hatua kuelekea katika gari ambalo Stephano alikuwamo.Machozi yakamtoka baada ya kumuona Stephano akiwa katika mateso makali sana.Akamuonea huruma.

" Kwa nini ulifanya hivi Stephano? Kwa nini ulifanya hivi? akasema Latoya kwa sauti ndogo huku akimshika Stephano kichwani.
"Mrudisheni nyumbani" akaamuru Latoya huku akirejea katika gari lake
Nyumbani kwa Latoya wafanyakazi wote walikuwa wamesimama kila mmoja akiwa katika taharuki kwa mambo ambayo yalikuwa yametokea muda mfupi uliopita.kwanza kwa mzee Curtis na kisha kwa Stephano.Kila mmoja alianza kuogopa.Walipouona msafara wa Latoya ukirejea wote wakatawanyika na kurejea katika sehemu zao za kazi kwa haraka.
Stephano akashushwa katika gari na Latoya akaamuru apelekwe sehemu ya kupumzika ili aweze kupata mapumziko.
" Mama Irene naomba uwaite watumishi wote ninataka kuongea nao" akasema Latoya

" Sawa madam" akajibu Irene

" Innocent yuko wapi ? akauliza Latoya

" Toka wakati ule alipopanda chumbani kwake baada ya kutokuelewana na mzee Curtis sijamuona tena huku chini.Inaonekana atakuwa amelala." akajibu Irene na kisha Latoya akapadisha ngazi kuelekea chumbani kwake.Alipofika chumbani kwake akakaa kitandani na kuanza kulia.Alilia sana hadi machozi yakamkauka.Katika maisha yake hakuwahi kulia namna hii.Alikuwa akimlilia mama yake.Taratibu akainuka na kwenda katika kabati lake akatoa mshumaa mkubwa mwekundu akauweka katika ile sehemu yake ya ibada akauwasha halafu akapiga magoti na kuinama akaanza kuomba na mara mle ndani kukawa na mwanga mkali sana akaacha kufanya maombi yake akageuza shingo kutazama mle chumbani.
" It Starts again........." Latoya akasema kwa sauti ya chini iliyojaa uoga.
Taratibu akaanza kuhisi kitu kama kisu chenye makali kikipita mgongoni mwake na kumpa maumivu makali sana.Akakunja uso wake na kugugumia kwa maumivu makali mwishowe akashindwa kuvumilia baada ya maumivu kuwa makali zaidi akapiga ukelele mkubwa "Aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaagggggggggghhhhhhhhhhhhhhhhhhhhh...!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!............. " Latoya akaanguka na kupoteza fahamu



TUKUTANE SEHEMU IJAYO……………………
: BEFORE I DIE

SEHEMU YA 30

ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA


" Toka wakati ule alipopanda chumbani kwake baada ya kutokuelewana na mzee Curtis sijamuona tena huku chini.Inaonekana atakuwa amelala." akajibu Irene na kisha Latoya akapadisha ngazi kuelekea chumbani kwake.Alipofika chumbani kwake akakaa kitandani na kuanza kulia.Alilia sana hadi machozi yakamkauka.Katika maisha yake hakuwahi kulia namna hii.Alikuwa akimlilia mama yake.Taratibu akainuka na kwenda katika kabati lake akatoa mshumaa mkubwa mwekundu akauweka katika ile sehemu yake ya ibada akauwasha halafu akapiga magoti na kuinama akaanza kuomba na mara mle ndani kukawa na mwanga mkali sana akaacha kufanya maombi yake akageuza shingo kutazama mle chumbani.
" It Starts again........." Latoya akasema kwa sauti ya chini iliyojaa uoga.
Taratibu akaanza kuhisi kitu kama kisu chenye makali kikipita mgongoni mwake na kumpa maumivu makali sana.Akakunja uso wake na kugugumia kwa maumivu makali mwishowe akashindwa kuvumilia baada ya maumivu kuwa makali zaidi akapiga ukelele mkubwa "Aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaagggggggggghhhhhhhhhhhhhhhhhhhhh...!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!............. " Latoya akaanguka na kupoteza fahamu


ENDELEA………………………..


Baada ya kushindwa kuelewana na mzee Curtis Innocent akapanda kwa haraka chumbani kwake na baada ya kuingia akafunga mlango kwa funguo .Hakutaka kabisa kuonana tena na mzee Curtis .Akasimama na kuhema kwa nguvu kutokana na kupanda ngazi kwa kasi kubwa.

" Huyu mzee sijui vipi? haoni kwamba anataka kunisababishia matatizo makubwa? Kwa nini asifanye huo uchunguzi wake yeye mwenyewe hadi anitumie mimi? Siwezi kamwe kufanya vile alivyonitaka nifanye...." akawaza Innocent akiwa amesimama amejiegemeza katika kabati la nguo.Taratibu akaketi kitandani akalivua koti lake na kulitupa pembeni.Jasho lilikuwa likimtoka kutokana na nguvu kubwa aliyoitumia kuzipanda ngazi za ghorofa lile.
"Latoya ni mtu mzuri sana na mwenye roho ya huruma.Kama ana madhaifu mengine hayo ni ya kwake lakini lazima nikiri kwamba ni mtu mwenye roho nzuri sijapata kuona.Nilipopatwa na msiba wa kufiwa na Marina,Latoya alijitolea kuubeba msiba ule kama wa kwake.Hili ni jambo jema sana na ambalo nitaendelea kumshukuru hadi mwisho wa uhai wangu.Sikuwa na fedha wala mahala pa kuupeleka msiba ule lakini kwa moyo wake wa huruma Latoya akakubali shughuli nzima ya msiba wa Marina ifanyike hapa nyumbani kwake.Siwezi kwenda kinyume na kuanza kuchunguza aina ya maisha anayoyaishi.Kama kuna mtu ambaye anaona kwamba Latoya ana matatizo basi aje yeye mwenye amuulize lakini si kwa kuwatumia watu wengine kama mimi.Latoya ameniheshmu kwa kiwango cha juu sana na kunipa nafasi katika ghorofa hii ya juu ambayo ni yake yeye pekee.Amenipa nafasi ya kuweza kuifikia bustani yake ambayo hakuna mtu mwingine zaidi ya Irene ambaye anaruhusiwa kuingia.Mtu huyu lazima nimuheshimu sana na kamwe siwezi kufanya jambo lolote la kumkosea heshima.Nafahamu ukaribu huu wetu unaweza ukazua maswali mengi sana kwa watu wakihoji ni kwa nini tumekuwa marafiki wa karibu namna hii.Atakaye hoji jambo kama hilo hamfahamu Latoya vizuri” akawaza Innocent halafu akaenda kuketi kitandani

" Latoya anaumwa nini hasa? Kwa nini dakari wake Godwin hawezi kuzungumza na mtu mwingine yeyote zaidi yake? Kwa nini matibabu yake yawe ya siri? Hapa lazima kuna jambo zito limejificha.Nikijaribu kulifikiri jambo hili na yale aliyoniambia Irene ninahisi Latoya ana siri nzito sana.Sitaki kuufahamu pande wa pili wa Latoya ukoje.Upande mmoja ninaomfahamu Latoya unanitosha sana .Ninamfahamu Latoya kama mtu mwenye roho nzuri na ya huruma na kusaidia.Mambo megine yoyote zaidi ya hapo sitaki kufahamu.Nina mambo mengi sana ya kufanya kwa sasa kwa hiyo sitaki kuumiza kichwa kwa mambo yasiyonihusu.Nitaendelea kuwa rafiki na Latoya na hata siku moja sintajaribu kutaka kuutafuta undani wake." akawaza Innocent na taratibu akaanza kuhisi macho yanakuwa mazito taaratibu akaanza kusinzia.
"Innocent amka unaitwa" Ilikuwa ni sauti ya mtoto mdogo ambaye umri wake ulikaribia miaka nane au tisa hivi.Innocent akafumbua macho na kujikuta akiwa amelala katika majani ndani ya bustani nzuri yenye miti mizuri ya kupendeza na maua yanayovutia mno.Ndege wa kila aina ,wa kila rangi walikuwa wakiruka na kuzidi kupafanya mahala hapa kuwa pazuri na pa kuvutia sana.Pembeni ya mahala alipokuwa amelala Innocent kulikuwa na kijito cha maji safi .Ilikuwa ni bustani nzuri ajabu.Innocent akajikuta akitabasamu kwa uzuri huu wa ajabu uliokuwamo katika bustani hii ambayo kwa kiasi fulani aliifananisha na bustani kama aliyowahi kuiona sehemu fulani

" Wow ! Bustani nzuri sana..." akasema Innocent huku uso wake ukiwa umechanua kwa tabasamu pana sana.

" Umeipenda bustani hii? akauliza yule mtoto ambaye alikuwa ameshika fimbo nyembamba
" Nimeipenda sana.Bustani hii ninaifananisha na bustani ya rafiki yangu mmoja anaitwa Latoya.Naye ana buistani nzuri kama hii lakini hii imeizidi ile ya Latoya kwa uzuri" akasema Innocent

" unamfahamu Latoya? akauliza yule mtoto
" Ndiyo ninamfahamu.Wewe umemfahamia wapi? Innocent akamuuliza yule mtoto.

" Latoya ni rafiki yangu sana tena wa siku nyingi" akajibu yule mtoto

" Kwani wewe una miaka mingapi? Inno akauliza

" Nina miaka mingi kukushinda hata wewe" akajibu yule mtoto katika hali ya utani na kumfanya Innocent acheke sana.

" Inocent nimetumwa nije nikuite.Baba anahitaji kukuona" akasema yule mtoto.

" Baba yako yuko wapi?

" Yuko kule nyumbani "

" Nyumbani kwenu ni wapi?

" Hapo chini si mbali sana " akajibu yule mtoto na kuanza kumuongoza Innocent kuelekea nyumbani kwao.Njiani Innocent hakukaukiwa na tabasamu kwa uzuri wa asili wa bustani ile.
Mara wakafika katika nyumba moja iliyokuwa chini ya mti mkubwa.Pale nje ya nyumba alikuwa amekaa mzee mmoja mwenye ndevu nyingi aliyevaa kanzu nyeupe na mshipi mwekundu kiunoni.Nguo zake zilifanana sana na nguo wazivaazo maaskofu wa kanisa katoliki.Alipomuona Innocent akasimama na kusalimiana naye.
" Karibu sana Innocent" akasema yule mzee na kumfanya Innocent ashangae kidogo kwa sababu hajawahi kuonana na mzee yule na hakufahamu aliwezaje kumfahamu

" Nashukuru sana mzee" akasema Innocent huku akiketi katika kiti kilichokuwa pembeni ya kile alichokuwa amekalia yule mzee
" Innocent umeyaonaje mazingira yetu? akauliza yule mzee
"Nimeyapenda sana.Yanavutia." akasema Innocent
"Twende nikakuonyeshe zaidi uzuri wa mahali hapa" akasema yule mzee na kisha akazunguka nyuma ya nyumba na kurejea akiwa amepanda gari la kukokotwa na farasi akamwambia Innocent apande kisha wakaanza kupanda juu ya kilima huku yule mzee akiendelea kumuonyesha sehemu mbali mbali za kuvutia.Hatimaye wakafika juu kabisa ya kilima.
" Huu ni upande mwingine wa nchi hii " akasema yule mzee akimuonyesha Innocent sehemu ya pili ya nchi ile iliyozidi kumfanya Inno apafurahie zaidi.Wakati Innocent akiendelea kuonyeshwa nchi ile mara kwa mbali likaonekana kundi kubwa la farasi likija kwa kasi.

" Nani wale? Innocent akauliza na kumfanya mzee yule kuvuta pumzi ndefu kisha akasema
" Wamekuja tena."
" Akina nani wamekuja tena? akauliza Innocent kwa mshangao
"Twende tuondoke.Tuna kazi kubwa leo" akasema yule mzee na kumuamuru Inno waondoke wakapanda gari lao la farasi na kuondoka kwa kasi.Walipofika nyumbani kwa yule mzee akaingia ndani kwa haraka na kutoka na upanga mrefu wenye kung'aa akampa Innocent.

" kamata upanga huu twende katika mapambano" akasema yule mzee,wakapanda tena gari la farasi na kuondoka kwa kasi.
" Mzee mbona sikuelewi tunakwenda kupambana na nani? akauliza Innocent kwa wasi wasi lakini yule mzee hakujibu kitu.Walifika karibu na nyumba moja ndogo wakashuka na kuanza kutembea kwa miguu.Wakaifikia nyumba ile na nje wakakuta kuna farasi wengi wamefungwa.Idadi yao ilizidi mia moja
" Watu hawa wenye hizi farasi wako wapi? akauliza Innocent
" Shhhhhhhhh !!...usiseme kitu" akasema mzee yule huku taratibu wakinyata kuelekea nyuma ya ile nyumba.Innocent akachungulia kilichokuwa kikiendelea uani na ghafla bila kutazamia akamuoa Latoya akiwa amefungwa katika gogo moja kubwa kama lile ambao huwa linatumika katika kukatia nyama buchani.Wale watu walikuwa wakiimba na kucheza kwa furaha sana.Mtu mmoja alishika kisu kikali sana akaanza kukipitisha mgongoni mwa Latoya na kumfanya apige ukelele mkubwa wa maumivu .

“ Latoya !! Innocent akastuka kumuona Latoya pale.Akamgeukia yule mzee na kumkaba shingo.

" Niambie Latoya amefikaje huku?: na wale wanaotaka kumuua ni akina nani? akasema Inno akiwa ametumbua macho kwa hasira.
" Nenda kamuokoe" akasema yule mzee.
"Nitamuokoaje wakati amezingirwa na watu zaidi ya mia moja? Inno akauliza
" Usipoteze muda nenda kamuokoe.Ni wewe pekee unayeweza kumuokoa kwa sasa.Nenda usipoteze muda" mzee yule akasema.Innocent akamshuhudia Latoya akilia kwa maumivu makali sana baada ya kisu kile chenye makali kuendelea kupita mgongoni mwake.Kwa hasira Innocent akaruka toka mahala alipokuwa amejificha akapaaza sauti
"Nasema muache Latoya haraka sana !!!!!..............
Sauti ile ya innocent ikawastua wale jamaa na kuwafanya waogope sana.Taratibu wakaanza kupiga hatua kurudi nyuma kila Inno alipopiga hatua kumkaribia Latoya.

" wewe ni nani? nani amekupa huo upanga wa moto? akasema jamaa mmoja mwenye sauti ya kukwaruza.

" Ninasema ondokeni haraka sana mahali hapa na msirudie tena kumfuata fuata Latoya.Kuanzia sasa mimi ndiye nitakayekuwa mlinzi wake na yeyote atakayekuja kumsumbua nitamkata kichwa kwa upanga huu" Innocent akasema kwa ukali na sauti yake ilisikika kama vile alikuwa akiunguruma.
Taratibu na kwa uoga watu wale wakaanza kurudi nyuma na kurukia farasi wao wakaondoka kwa kasi sana.Innocent akamfungua Latoya kamba zile alizokuwa amefungwa na kutokana na maumivu makali aliyoyapata alikuwa amepoteza fahamu.Damu nyingi ilikuwa ikimtoka.Akamuinamia Latoya kwa uchungu kisha akasikia sauti ya yule mzee ikimuita ,akageuka.

" Innocent watu wale wamekwenda kujipanga kwa ajili ya kurudi tena.Unatakiwa kusimama kidete kumlinda Latoya.Kwa sasa ni wewe pekee ambaye unaweza kumlinda ." akasema yule mzee
" kwa nini mimi pekee? Nitawezaje kupambana na mijitu ile yenye kutisha ?Watu wale ni akina nani na kwa nini wanataka kumdhuru Latoya? akauliza Innocent
" Wewe unaweza ukapambana nao kwa sababu una nguvu hizo.Kuanzia sasa ninakukabidhi kazi ya kumlinda Latoya.Leta mkono wako wa kulia" Innocent akampa yule mzee mkono wake wa kulia akaushika kwa mikono yake miwili
" Innocent kuanzia sasa wewe ndiye utakayekuwa mlinzi wa Latoya .Utapambana na kila ajaye kwa lengo la kumdhuru au kumuumiza.Wengi wa watu utakaopambana nao wana nguvu kubwa kwa hiyo ninaupa mkono wako wa kulia nguvu ya kuweza kuushika upanga wa moto na kupambana na kila mwovu ajaye kwa nia ya kumdhuru Latoya.Hakikisha umemuokoa Latoya na muiokoe dunia.” Akasema Yule mzee halafu akautazama mkono wa Innocent na kusema
“Shuka sasa nguvu na uwezo katika mkono huu" akasema yule mzee na ghafla mkono wa Innocent ukaanza kuwaka moto.Akahisi maumivu makali sana akaanguka chini.
Ghafla innocent akafumbua macho na kuhema kwa nguvu.Alikuwa akiota.Mwili wote ulikuwa umelowa jasho kutokana na ndoto ile ya kutisha.
“Ee Mungu hii ni ndoto ya namna gani? .........akasema Inno huku akivua shati lililoloa kutokana na jasho jingi.Alihisi maumivu makali sana katika mkono wake wa kulia.Akaushika na kuutazama mkono wake kwa wasiwasi mkubwa.Ulikuwa na maumivu makali sana.Inno akaogopa akautazama mkono wake kwa mshangao mkubwa.Akajaribu kuuinua juu lakini akaurudisha chini haraka kutokana na kuhisi maumivu makali sana.Mkono haukuonyesha dalili zozote za kuungua moto kwa nje lakini ulikuwa ukiuma sana kwa ndani.Innocent akajiuliza maswali mengi.

" Mungu wangu haya mambo gani tena? Hii ndoto niliyoota inaweza ikawa ni kweli? .Innocent akajiuliza bila kupata jibu.Bado aliendelea kusikia maumivu makali katika mkono wake wa kulia na jasho likaendelea kumtoka.

"Ndoto niliyoota ni ya maajabu sana .Latoya alikuwa amefungwa kamba katika mti na alikuwa akiteswa na watu wale walioonekana makatili sana.Yule mzee akanipa upanga na kuniambia nikamuokoe Latoya na kweli nilipowanyooshea upanga ule wale jamaa wakaogopa wakapanda farasi wao na kukimbia.Baada ya mijitu ile kukimbia nakumbuka kuna maneno mzee yule aliniambia.Nakumbuka alisema " “Innocent kuanzia sasa wewe ndiye utakayekuwa mlinzi wa Latoya .Utapambana na kila ajaye kwa lengo la kumdhuru au kumuumiza.Wengi wa watu utakaopambana nao wana nguvu kubwa kwa hiyo ninaupa mkono wako wa kulia nguvu ya kuweza kuushika upanga wa moto na kupambana na kila mwovu ajaye kwa nia ya kumdhuru Latoya. Hakikisha umemuokoa Latoya na muiokoe dunia " “Nakumbuka baada ya maneno hayo ya yule mzee ulishuka moyo mkali sana na kuniunguza mkono nikasikia maumivu makali na kuanguka nikapoteza fahamu na ndipo hapo nikastuka toka usingizini na kuukuta kweli mkono wangu una maumivu makali.Naanza kuchanganyikiwa na mambo haya ,inawezekana ndoto ile ikawa ni kweli? Inawezekana yote niliyoyaona ndotoni ni ya kweli?" akawaza Innocent akiwa bado ameushikilia mkono wake uliokuwa na maumivu makali.Akainama na kuendelea kuwaza.
" Kama ndoto ile isingekuwa ya kweli nisingeamka na kujikuta na maumivu haya ninayoyasikia katika mkono ule ule ambao niliota ukiunguzwa moto.Naanza kuwa na wasi wasi mkubwa na maisha ya hapa.Nyumba hii inaonekana kuwa na mauza uza mengi .Nakumbuka Irene aliniambia kuhusu mambo yaliyowapata watu waliojaribu kutaka kuchungulia ndani ya ghorofa hii ya juu ambayo ni ya Latoya pekee.Sikuwa nikiamini mambo yale aliyonieleza Irene lakini baada ya ndoto hii niliyoota nikiunguzwa moto na kweli baada ya kuamka nakuta kweli mkono wangu ukiwa na maumivu makali sana nimeanza kuamini kwamba hapa kuna mambo mazito sana yanayoendelea.Latoya ni nani hasa? Mbona anaanza kunipa wasi wasi? Binti mzuri namna hii mwenye uzuri uliotukuka kwa nini anaishi katika maisha yaliyojaa utata mwingi namna hii? Ninaanza sasa kupata picha kwa nini mzee Curtis alikuwa akinitaka nimchunguze Latoya kwa sababu maisha yake yenye utata hata yeye kama baba yake yamemshangaza sana." akawaza Innocent kisha akainuka akaenda katika kabati la nguo na kuchukua shati lingine akavaa.Mkono wake wa kulia alihisi kama umekufa ganzi.


TUKUTANE SEHEMU IJAYO…………………………
 
Back
Top Bottom