Simulizi: Before I die

Simulizi: Before I die

Hii story niliisoma zamani safi sana LEGE tuletee nyingine ambazo tumezisahau
 
Before I die ni story Kali sana Peniela inasubiri miaka buku nane
 
bado hamjamaliza tuu kusoma
 
bado hamjamaliza tuu kusoma
Mkuu Lege Ishushe Huku hii before I die, niliwahi ifuatilia 2013 kabla haijasitishwa.... Wakati Peniela is loading, before I die iwepo hapa tuburudike nayo
 
Mkuu Lege Ishushe Huku hii before I die, niliwahi ifuatilia 2013 kabla haijasitishwa.... Wakati Peniela is loading, before I die iwepo hapa tuburudike nayo
powa mkuu ngoja niishushe .sie walevi wa haya makitu
 
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 16
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“My God why her? “ Innocent akasema taratibu baada ya Marina na Dr Peter kutoka mle ofisini mwake.
“kwa nini mzigo wa mambo yote haya umuelemee yeye peke yake? Lakini Leo nimegundua kitu ambacho sikuwa nimekigundua hapo awali.Marina ana uzuri wa asili uliojificha .Mtoto yule ni mzuri.Kuna kitu nimekiona katika macho yake ambacho kimenisisimua mwili wangu wote.Sielewi kama niko sahihi kwa hisia zangu lakini nahisi hisia zangu ziko sahihi.There is a connection between us.Kuna nguvu inayonivuta kuwa karibu na Marina.” Innocent akawaza halafu akainuka na kusimama huku mikono yake imeshikilia kiti
“No ! No No Innocent you are wrong.Marina isn’t the one”” Innocent akasema kwa sauti ndogo huku akizunguka zunguka mle ofisini.Akaenda na kusimama dirishani.
“ A woman of my deams must be simple,educated,full of love,…and…..” Innocent akawaza akahisi kama kichwa kikimuuma.
“marina is a simple girl,asiyekuwa na elimu but I can see something in her eyez..I can see passion..I can see love..Kama akibadilika anaweza akanifaa.” Mawazo ya innocent yakakatizwa na simu ya mezani iliyolia mle ofisini.

ENDELEA……………………..
Saa kumi na mbili za jioni Innocent akamaliza kazi ,yeye na Marina wakaelekea nyumbani kwao.Tayari giza lilikwisha tanda walipowasili nyumbani.Akiwa ametangulia mbele na Marina akimfuata nyuma Inno akafungua mlango wa sebuleni na kukutana na sura ya mama yake iliyostuka ghafla baada ya kumuona Marina akiwa nyuma ya Inno.
“Inno ukitaka tuelewane leo ,mtoe huyo kahaba ndani mwangu.” Mama Innocent akainuika na kusema kwa hasira
“Mama tafadhali……..” Inno akajaribu kuongea lakini akakatishwa na sauti ya juu iliyojaa ukali ya mama yake.
“Nakwambia Innocent kama unataka tuelewane leo muondoe huyo kahaba wako haraka sana.Sitaki kumuona ndani ya nyumba yangu.Innocent umekuwaje siku hizi? Sikutegemea kama iko siku utakuja kuwa na uhusiano na watu kama hawa.” Mama yake akafoka
“mama tafadhali naomba unisikilize japo kidogo” Innocent akasema
“Inno nimekwisha sema kwamba kahaba huyu halali humu ndani leo.Kama huamini leo ndiyo atanitambua..” Mama Innocent kwa hasira akamsukuma Inno akaanguka pembeni halafu akamvaa Marina akamsukuma nje akaanguka chini na kutoa ukelele wa maumivu.
“Nimekwambia toka asubuhi kwamba sitaki nikuone ukiwa na mwanangu.Unachomfuata fuata mwanangu ni kitu gani wewe kahaba? “ mama Innocent akasema kwa hasira huku akimvuta Marina mkono ili kumtoa nje.Innocent alikiona kitendo kile kikamuumiza sana.Kwa nguvu akamvuta mama yake akamwachia Marina.
“Mama imetosha.Siwezi tena kuvumilia matukano na manyanyaso kama haya kwa binti masikini kama huyu.Sitaki kusema lolote mama ila naomba uelewe kwamba kwa vile hutaki Marina akae hapa basi na mimi naondoka.” Innocent akasema huku akihema kwa hasira.Akamfuata Marina pale chini alipokuwa amelala akamwambia
“Marina nyamaza kulia.Nisubiri nikachukue baadhi ya vitu vyangu tunaondoka wote” Marina hakujibu kitu alikuwa akilia kwa maumivu.Innocent akaenda chumbani kwake akachukua begi lake na kupakia baadhi ya vitu vyake muhimu kama nguo na baadhi ya nyaraka za kiofisi ,mara Sabrina akaingia
“Kaka Innocent ni kweli unaondoka? Sabrina akauliza huku akitokwa na machozi
“Sabrina nimeamua niondoke.Nimechoka na vituko vya mama yangu.”
Huku akilia Sabrina akauliza
“sasa Innocent usiku huu unaenda kulala wapi?
“Sabrina sijajua bado lakini nitalala sehemu yoyote ile.Mimi mtoto wa kiume siwezi kushindwa maisha” Innocent akasema huku akimalizia kufunga zipu za begi lile kubwa
“Innocent kama unaondoka basi hata sisi tunaondoka.Siwezi kuendelea kuishi hapa kama wewe haupo.Wewe ndiye uliyekuwa mtetezi wetu.kama wewe haupo hakuna mtu mwingine atakayetujali” Sabrina akasema kwa hisia kali
“Sabrina tafadhali msiondoke hapa nyumbani.wewe na Grace ni sehemu ya familia hii .Subirini kwanza nirekebishe sehemu ya makaazi halafu nitawachukua tukaishi wote.” Innocent akasema huku akimpiga piga Sabrina mgongoni.
“Kaka Innocent suala la mahala pa kukaa halina taabu.Nimechelewa kukutaarifu kwamba nimepata kazi katika taasisi moja isiyo ya kiserikali inayoshughulika na kuwasaidia wanawake wenye kansa na matatizo mbali mbali .Dada Latoya ambaye ndiye mwenye taasisi hiyo ameniahidi kunipatia nyumba ya kuishi .Nitakupigia simu nikutaarifu zaidi.” Grace akasema huku akilibeba begi la Innocent wakatoka mle chumbani.Innocent akastuka kidogo na kumuangalia Sabrina
“ Unasema Latoya?
“ ndiyo Latoya.Unamfahamu?
“ Latoya huyu bilionea? Akauliza Innocent
“ Sifahamu kama ndiye huyo Latoya bilionea unayemsema lakini yeey ana taasisi ya kusaidia walemavu na watu watu wenye matatizo mbali mbali.Umewahi kumuona?
“ Hapana sijaahi kumuona lakini nimewahi kusikia kwamba kuna bilionea mkubwa wa Kitanzani anaitwa Latoya anyway hongera sana kwa kufanikiwa kupata kazi.Tafadhali nipigie simu kesho ili tuongee kwa undani zaidi.Kwa sasa bado nina hasira sana” Innocent akasema .Walipotokeza sebuleni mama yake Innocent bado alikuwa amesimama amefura kwa hasira Wakatazamana usoni kwa sekunde kadhaa halafu Inno akasema
“Mama mimi naondoka.Nitatafuta mahala pengine pa kuishi .Siwezi kuvumilia kumuona Marina akiteseka na kunyanyaswa.Laiti ungejua matatizo makubwa aliyonayo binti huyu usingethubutu kumtolea maneno makali kama uliyomtolea.Nitamtuma dereva kuja kumalizia vitu vyangu vilivyobakia kesho.” Innocent akamuaga mama yake.Akamuinua Marina ambaye alikuwa akigugumia kwa maumivu makali na kwa kusaidiana na Grace na Sabrina wakampakia katika gari ,akaliwasha na kuondoka huku kila mmoja akiwa haamini kama ni kweli Innocent alichukua maamuzi ya kuondoka nyumbani kwao.Mpaka taa za gari zinafutika machoni pake bado mama yake aliendelea kusimama pale nje akiwa na hasira zisizomithilika.
Innocent akageuka na kumtazama Marina aliyekuwa amekaa kiti cha pembeni.Alikuwa akigugumia kwa maumivu.
“Unajisikiaje Marina? akauliza
“Nasikia maumivu makali sana tumboni” Marina akasema kwa sauti yenye kuonyesha ni wazi alikuwa akisikia maumivu makali mno
“Kesho nitakupeleka hospitali ili ukaanze matibabu.” Akasema Innocent.
“nashukuru sana Innocent kwa msaada wako.lakini Inno hukupaswa kuondoka nyumbani kwenu kwa ajili yangu.Ungeniacha mimi nirudi nikaendelee kuishi kule ninakoishi” marina akasema
“Marina nimechoshwa na vitendo vya unyanyasaji vinavyofanyika katika ile nyumba.Mungu ametujalia uwezo lakini isiwe ni sababu ya kuwanyanyasa wale wasiokuwa na uwezo.Kitendo cha leo alichokifanya mama kimeniumiza mno…” Innocent akasema na kuongeza mwendo wa gari.
“Bado sijapata jibu kwa nini mama amfanyie Marina namna ile.Kama mama alipaswa kumuhurumia na kumpokea .Alipaswa kuonyesha ile huruma ya kimama.Bila ya kutambua kwamba Marina ni mgonjwa amemsukuma na kumsababishia maumivu makubwa.Siku zote nimemvumilia lakini leo mama ameniumiza kupita kiasi.” Innocent akawaza huku moyoni bado akiwa na hasira kila akikumbuka kitendo kile
“Usiku huu itanibidi nitafuate mahala nikalale.Marina anahitaji kupumzika na kesho asubuhi nimpeleke hospitali.Kesho ndipo nitapanga vizuri nini kifuate baada ya hatua hii ya kuondoka nyumbani.Nitahitaji kupata mahala pa kuishi lakini isiwe ni sehemu inayohusiana na familia yangu.Familia yangu imejaa watu wasio hata na chembe ya ubinadamu.Nitatafuta nyumba ya kupanga na kuwachukua Sabrina na Grace na kuishi nao kwani najua baada ya mimi kuondoka pale nyumbani maisha yao yatakuwa magumu sana”
Usiku huu hakuwa na mahala pengine alipokuwa akipaamini zaidi ya 104 lodge.Ni hoteli tulivu mno na ya kupendeza.Ni katika hoteli hii ndipo Inno alimleta Marina siku ya kwanza walipoonana.Pale hotelini wakapewa chumba na wahudumu wakawasaidia kubeba mabegi ya Inno hadi chumbani.
“Marina utakula chakula gani usiku huu” Inno akamuuliza Marina aliyekuwa amekaa sofani
“Sijisikii kula chakula chochote Inno”
“hapana Marina unapaswa ule chakula ili mwili uwe na nguvu.” Inno akasema akaiendea simu na kuagiza waletewe chakula chumbani kwao.
Haikuchukua muda chakula kikaletwa na kuwekwa mezani.Inno akambembeleza Marina ajitahidi kula japo kidogo.Marina akala kijiko cha kwanza na cha pili akashindwa kuendelea zaidi.Inno akamsogelea karibu akakishika kijiko chake na kuchota chakula.
“marina tafadhali naomba jitahidi kula.Chakula hiki ndicho kitakupa nguvu “ Inno akasema huku akimuangalia Marina ambaye pamoja na maumivu aliyoyasikia akatabasamu na kufungua mdomo Innocent akamlisha chakula.
“Jitahidi karibu unamaliza” Inno akaendelea kumbembeleza hadi alipomaliza sahani nzima
“ Safi sana.Sasa unaweza kupanda kitandani kupumzika.Mimi nitalala hapa katika sofa” Innocent akamwambia Marina .Marina akamtazama Inno usoni kwa sekunde kadhaa na kusema
“Inno nashukuru sana “
“Usijali Marina.” Akasema Inno na kumsaidia Marina kuinuka pale sofani na kumpeleka kitandani akamlaza na kumfunika shuka.
“Pumzika Marina ,kesho nitakupeleka hospitali na kisha nitashughulikia suala la wapi tutakwenda kuishi.Siwezi kukuruhusu urejee tena kule ulikokuwa ukiishi”
Marina hakujibu kitu ,aliendelea kumtazama Inno usoni ambaye aligeuka na kwenda kuketi sofani .Alionekana mwingi wa mawazo.
Pale sofani Inno alikuwa ameinama akijaribu kufikiri juu ya mambo kadhaa ambayo anahitaji kuyafanya.Mara akasikia sauti ya Marina ikimuita.Akainuka pale sofani na kumfuata Marina kitandani
“Innocent naomba kukuuliza”
“Uliza Marina “
“Ni kwa nini unanifanyia mambo yote haya? Najaribu kuwaza lakini sipati jibu .Inawezakanaje mtu ambaye sina undugu naye wowote,sina urafiki naye wowote,na kikubwa zaidi mtu kutoka katika familia ya kitajiri anifanyie mambo kama haya mimi masikini ninayefanya biashara ya kujiuza?.Hebu niweke wazi Innocent ni kwa nini umejitolea kunifanyia mambo yote haya hadi ukaamua kuliacha jumba lenu la kifahari kwa sababu yangu? Marina alisema huku akilia.Innocent akamtazama,akasikia uchungu moyoni.Akainama na kumfuta machozi
“Usilie Marina.Nimefanya haya yote kwa sababu ninapaswa kufanya hivi” Inno akajibu kwa ufupi.
“Innocent bado hujajibu swali langu.Nataka kufahamu sababu ya wewe kunifanyia mambo haya yote.Kila siku umekuwa ukipoteza muda mwingi na kuacha kazi zako ili kunishughulikia mimi.”
Innocent akatafakari ajibu nini.Akamtazama Marina aliyekuwa akisubiri apewe jibu
“Marina mimi ndivyo nilivyo.Huwa ninaumia sana kila nimuonapo binadamu mwenzangu akiteseka hivyo kama uwezo unaniruhusu kwa wakati huo,lazima nimsaidie.”
“nakubali Innocent una roho nzuri lakini kwa nini uamue kunichagua mimi ? Marina akauliza
“Marina nafikiri hayo ni maongozi ya Mungu.Hata mimi sifahamu ni kwa nini macho yangu yalikuona wewe tu na si mwingine.Pumzika Marina tutaongea zaidi kesho”Akasema Innocent na kugeuka akaanza kupiga hatua kurejea katika sofa.Marina akamuita tena,Inno akageuka
“Innocent unaniogopa?
Huku akitabasamu Innocent akajibu
“kwa nini nikuogope Marina”
“Siwezi kujua ,lakini ninaona kama bado unaniogopa .Innocent nakubali nimeishi maisha mabaya sana lakini kwa sasa sitaki tena kuishi maisha ya namna ile.Nataka kubadilika.Naomba usiniogope tena Innocent.Nisaidie niweze kuanza maisha mapya” Marina akasema na kumfanya Innocent acheke kicheko kidogo
“Marina nafurahi sana kusikia kwamba uko tayari kubadilika.Nakuahidi nitafanya kila niwezalo ili kuhakikisha kwamba unakuwa na maisha mazuri na yenye furaha.”
“Nashukuru sana Innocent.Sijawahi kukutana na binadamu mwenye roho nzuri kama ya kwako.” Marina akasema .Innocent akarudi na kuketi sofani.

* * * *

Saa nane na dakika nane za usiku Innocent akasikia sauti ya Marina akiugulia kwa maumivu makali.Akainuka kwa haraka na kwenda kumtazama .
“marina ! Marina !……” Innocent akamuita Marina lakini hakuitika zaidi ya kuendelea kutoa miguno ya maumivu.
“Hali yake imebadilika sana.Siwezi kusubiri hadi asubuhi.Ngoja nimuwahishe hospitali” Innocent akawaza huku akivaa viatu vyake halafu akambeba Marina na kumpakia katika gari lake na kwa kasi ya ajabu akaelekea hospitali.
“Kwa kuwa vipimo alivyofanyiwa jana vinaonyesha kwamba kinachomsumbua ni figo sina haja ya kumpeleka hospitali nyingine zaidi ya Agape kidney hospital.Nasikia pale kuna madaktari mabingwa wa masuala ya figo wanatokea Marekani.” Akawaza Inno .Usiku huu hakukuwa na magari mengi barabarani kitu kilichomfanya atumie dakika thelathini na tano kufika katika hospitali hii maalum kwa ajili ya magonjwa ya figo.Hospitali hii inayoongozwa na wamisionari ,ilifanya kazi kwa saa ishirini na nne.Mara tu Inno alipowasili ,marina akachukuliwa na kupelekwa katika chumba maalum kwa ajili ya huduma ya kwanza wakati wakisubiri maelekezo ya daktari.Innocent akaitwa ofisini kwa daktari na kutoa maelezo ya ugonjwa wa Marina ikiwa ni pamoja na majibu ya vipimo alivyofanyiwa siku iliyopita.Daktari akamuomba Inno akaendelee kusubiri katika sehemu ya kupumzikia wakati wakiendelea na zoezi la kuchukua vipimo zaidi ili walifahamu tatizo la Marina kiundani zaidi .


TUKUTANE SEHEMU IJAYO….
 
BEFORE I DIE
SEHEMU YA 17
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Hali yake imebadilika sana.Siwezi kusubiri hadi asubuhi.Ngoja nimuwahishe hospitali” Innocent akawaza huku akivaa viatu vyake halafu akambeba Marina na kumpakia katika gari lake na kwa kasi ya ajabu akaelekea hospitali.
“Kwa kuwa vipimo alivyofanyiwa jana vinaonyesha kwamba kinachomsumbua ni figo sina haja ya kumpeleka hospitali nyingine zaidi ya Agape kidney hospital.Nasikia pale kuna madaktari mabingwa wa masuala ya figo wanatokea Marekani.” Akawaza Inno .Usiku huu hakukuwa na magari mengi barabarani kitu kilichomfanya atumie dakika thelathini na tano kufika katika hospitali hii maalum kwa ajili ya magonjwa ya figo.Hospitali hii inayoongozwa na wamisionari ,ilifanya kazi kwa saa ishirini na nne.Mara tu Inno alipowasili ,marina akachukuliwa na kupelekwa katika chumba maalum kwa ajili ya huduma ya kwanza wakati wakisubiri maelekezo ya daktari.Innocent akaitwa ofisini kwa daktari na kutoa maelezo ya ugonjwa wa Marina ikiwa ni pamoja na majibu ya vipimo alivyofanyiwa siku iliyopita.Daktari akamuomba Inno akaendelee kusubiri katika sehemu ya kupumzikia wakati wakiendelea na zoezi la kuchukua vipimo zaidi ili walifahamu tatizo la Marina kiundani zaidi .

ENDELEA………………………………

Saa mbili na nusu za asubuhi daktari akamuita Innocent ofisini kwake.
“Innocent mgonjwa wako anaumwa sana.Tumemfanyia uchunguzi wa hali ya juu na tumegundua kwamba kwa sasa hali yake si nzuri kwa sababu figo zake zinashindwa kufanya kazi” Akasema daktari yule na kumtazama Innocent usoni.
“Daktari kuna namna yoyote mnayoweza kufanya ili figo zake ziweze kufanya kazi tena? Inno akauliza
“Hilo ndilo limenifanya nikuite hapa ofisini.” Akasema daktari na Innocent akamuangalia kwa wasi wasi.
“mgonjwa wako anatakiwa kubadilishiwa figo.Akipata walau figo moja inaweza kusaidia kuokoa maisha yake” Daktari akamwambia Innocent , akastuka na kusimama.
“Dokta ina maana figo nyingine ikikosekana Marina anaweza kufariki?
“Uwezekano wa kupona kama hatabadilishiwa figo ni mdogo sana” Daktari akasema na kuzidi kumchanganya Innocent ambaye alikuwa akimtazama daktari kwa wasi wasi mkubwa.
“Hizo figo zinapatikana wapi dokta.Niambie kiasi chochote cha pesa nitatoa ilimradi marina apone” Inno akasema
“Innocent nasikitika kwamba figo inatakiwa kutolewa kwa mtu.Unatakiwa kutafuta mtu ambaye atajitolea figo yake moja kwa ajili ya mgonjwa wako.Hakuna figo ya kununua” Dokta akazidi kumkatisha tamaa Innocent.
“My Gosh ! Marina is going to die.I cant let that happen” Akaongea mwenyewe na kumfanya daktari amuangalie kwa makini.
“Daktari iwapo akijitokeza mtu wa kutoa figo yake kwa ajili ya Marina itamlazimu kusafirishwa nje ya nchi kwa upasuaji? Innocent akauliza
“hapana Innocent,hii ni hospitali maalum kwa ajili ya magonjwa ya figo na kuna madkatari bingwa wa figo wako hapa kwa hiyo kila kitu kinafanyika hapa hapa.hakuna haja ya kumpeleka mgonjwa nje ya nchi.”
Maneno yale ya daktari yanampa moyo Innocent
“Daktari nashukuru naomba unipe muda nikatafute namna ya kuweza kupata mtu wa kujitolea figo.Nitapata figo daktari .marina hawezi kupoteza uhai kwa sababu ya Figo” Innocent akasema huku akiondoka mle ofisini akapanda gari lake na kuondoka .
“Lazima figo ipatikane.Siwezi kukubali kumpoteza Marina kwa sababu ya figo.Ngoja kwanza niende ofisini nikaangalie shughuli zinakwendaje halafu nianze jitihada za kutafuta mtu wa kujitolea figo” Akawaza Inno akiwa njiani kuelekea ofisini.
Alipofika ofisni akashuka garini na kutembea kwa haraka kuelekea ofisini kwake.Kila aliyemuona alikuwa akimshangaa kwa hali aliyokuwa nayo.Alikuwa amesawajika mno.Hawakuzoea kumuona katika hali ile.Kila mmoja alijua kuna jambo limemsibu.Mara tu alipoingia ofisini kwake akakutana na sura ya baba yake.Kwa muonekano wa baba yake ulivyokuwa alihisi kuna jambo si zuri.
“baba shikamoo” Inno akamsalimia baba yake.
“marahaba Inno.” Baba yake akaitika
Inno akaketi kitini na kumpigia simu katibu muhtasi wake.
“Devotha siko kikazi leo.Naomba futa ahadi zote za kukutana na watu niliokuwa nikutane nao leo”
baba yake akamuangalia kwa jicho kali.
“Innocent jana umelala wapi? Baba yake akauliza mara tu alipoweka chini mkono wa simu.
“Baba ni hadithi ndefu nadhani mama alikwisha kueleza.Niliamua kuondoka nyumbani”
“Uliondoka nyumbani kwa ruhusa ya nani? Akauliza mzee Benard na muda huo simu ya Innocent ikaita.Akatazama mpigaji alikuwa ni Sabrina.
“samahani baba naomba kupokea hii simu ni muhimu” Akasema Inno akiinuka na kusogea pembeni
“Hallo Sabrina”
“Kaka Innocent habari za toka jana? Sabrina akauliza
“habari si nzuri sana Sabrina”
“marina anaendeleaje?
“Marina ana hali mbaya sana.Amezidiwa usiku nikampeleka hospitali na amelazwa .Kwa mujibu wa madaktari ni kwamba figo zake zinashindwa kufanya kazi kwa maana hiyo ili kuokoa maisha yake anahitaji kubadilishiwa figo.”
“Ouh Mungu wangu !” Sabrina akastuka.
“sasa umefikia wapi katika kupata figo? Sabrina akauliza
“Bado natafuta mtu wa kuweza kujitolea figo moja.” Innocent akajibu.
“Kaka Innocent jana nilikwambia kuhusiana na dada Latoya ambaye ndiye mwenye hii taasisi ninayofanya kazi.Anasaidia sana wanawake wenye matatizo kama ya kansa za matiti ,vizazi n.k.Unaonaje kama nitakuunganisha naye uone kama anaweza kuwa na namna yoyote ya kukusaidia? Ni mtu mwenye roho ya huruma sana.”
Sabrina akamwambia Innocent ambaye baada ya kufikiri kwa sekunde chache akasema
“Ok Sabrina nitafurahi kuonana naye”
‘Usijali kaka Innocent.Ninakwenda kuongea naye sasa hivi na kumweleza kuhusu umuhimu wa jambo hili.Nitakupigia simu baada ya muda mfupi”
Walipomaliza maongezi Innocent akarudi mezani na kuketi kitini.
“Innocent yule Marina ni nani wako? Baba yake akauliza
“Ni rafiki yangu”
“Innocent katika watoto niliokuwa nawategemea ni wewe.Sikutegemea hata siku moja kwamba ungeweza kufanya jambo kama ulilolifanya jana.Kwa ajili ya mwanamke kahaba unadiriki kuhama nyumbani kwenu? Umeidhalilisha sana familia yetu.Wewe ni kijana msomi ,ambaye unatakiwa utafute binti mzuri,msomi mwenzako ambaye atakupenda na mtaishi wote na kutengeneza familia na si hawa makahaba mnaowaokota mitaani ambao hawana lolote zaidi ya kutumia fedha zako na kukuachia maradhi.Nimekuja hapa kwa lengo moja tu ,kutaka kuisikia kauli yako kwamba unachagua kitu gani kati ya familia yako au huyo kahaba wako.Innocent tunakupenda na hatutaki upotezwe na hawa wasichana wasiokuwa na mwelekeo.Naomba urudi nyumbani na kama utasisitiza kuendelea na huyo kahaba wako basi utakuwa umejiondoa katika familia wewe mwenyewe.Sisi hatutakutambua tena.Sitaki hayo yatokee Innocent ,nakuomba uniahidi kwamba utaachana na huyo msichana wa mitaani” Mzee Benard akasema kwa sauti isiyo na masihara.Innocent anamfahamu vizuri baba yake,akiwa katika hali kama hii huwa hana masihara.Ni wazi alimaanisha kile alichokisema.Maneno yale ya baba yake yakamchoma moyo Inno.Aliumizwa sana na maneno yale.Sura ya Marina akiwa katika maumivu makali hospitali ikamjia tena kichwani akawaza.
“hapana siwezi kumuacha Marina apoteze maisha .Pesa mali na kila kitu vinapita lakini uhai wa Marina ni muhimu mno kwangu.Akipotea leo hakuna pesa itakayoweza kumrudisha.I cant let that happen”
Kwa sura iliyojaa simanzi,Innocent akaenda juu ya kabati akachukua funguo nyingi na kuziweka mezani.Baba yake akazidi kumshangaa.
“Baba funguo hizo hapo”
“Za nini” baba yake akauliza
“I quit.I’m out of here”
Mzee Benard akastuka sana kwa kauli ile ya Innocent
“Ina maana kahaba ni bora zaidi kuliko familia yako?
“baba vyovyote itakavyokuwa ninyi mtabaki kuwa familia yangu mpaka kufa.lakini kwa sasa uhai wa Marina ni kitu muhimu sana kwangu.I cant let her die.Nimekurudishia ofisi baba.” Innocent akasema na kutoka mle ofisini.
“Innocent !!..Innocent !……” mzee Benard akaita kwa sauti ya juu iliyowastua wafanyakazi wengine lakini Innocent hakugeuka ,akaingia garini na kuondoka.
“Sikutegemea kama baba angeweza kunitamkia maneno kama yale.Nashindwa kuelewa ni kwa nini familia yangu wamekuwa hawapendezwi kila ninapojitahidi kuwasaidia watu wenye matatizo.Mungu ameibariki familia yetu na kuipatia mali na fedha,lakini isiwe ni sababu ya kutowapenda na kuwabagua wale ambao hawakujaliwa kuwa navyo.Huu ni msimamo wangu na sintakubali mtu yeyote aniyumbishe katika msimamo wangu huu.Nitamsaidia yeyote mwenye shida kama nitakuwa nacho.Familia yangu ni muhimu sana lakini kuokoa uhai wa Marina ni muhimu zaidi kwangu sasa.Natakiwa nipambane kadiri nitakavyoweza ili niweze kuokoa maisha ya binti yule masikini.” Mawazo ya Innocent yakakatishwa na simu yake iliyokuwa ikiita.Akapungua mwendo wa gari na kutazama mpigaji.Alikuwa ni Sabrina.
“Helo Sabrina” Innocent akasema baada ya kubonyeza kitufe cha kupokelea simu
“Kaka innocent uko wapi sasa hivi? Sabrina akauliza
“Niko barabarani naenda kuonana na rafiki yangu mmoja ni daktari nione kama atanisaidia”
“Kaka Innocent ,nimeshaongea na dada Latoya na ameonyesha kuguswa na jambo hilo na yuko tayari kukusaidia.Kwa kuwa anatakiwa kuhudhuria kikao muhimu mchana huu amesema kwamba kama una nafasi fika sasa hivi hapa ofisini kwake ili muweze kuongea na kuangalia ni namna gani mnaweza mkayaokoa maisha ya Marina”
“Ok Sabrina nielekeze zilipo ofisi zenu nifike hapo mara moja”
Sabrina akamuelekeza Innocent zilipo ofisi zao ,akageuza gari na kuelekea huko.
“Nadhani kuna haja ya kuanzisha mfuko maalum wa kuwasaidia watu wenye matatizo kama anavyofanya huyo Latoya.Nimegundua kwamba ukiwa na maisha ya juu kamwe huwezi kuzitambua shida walizonazo watu wenye maisha ya chini.Watu wenye uwezo mkubwa kifedha hawafahamu nini maana ya kulala njaa,nini maana ya kukosa ada ya kumsomesha mtoto,kiujumla hawafahamu nini maana ya shida.Hii ni sababu hata wazazi na ndugu zangu hawaniungi mkono katika jitihada zangu za kuwasaidia watu wenye matatizo mbali mbali.Nashukuru Mungu kwa kunipa moyo huu wa kuguswa na matatizo ya watu.Laiti kama ningekuwa na uwezo wa kuweza kuyatafutia ufumbuzi matatizo yao,lakini uwezo wangu ni mdogo na bado una mipaka na ndiyo maana nafikiria kuwa na taasisi yangu mwenyewe ya kuwasaidia watu kama Marina na wengine wenye matatizo mbali mbali makubwa.” Akawaza Innocent wakati akielekea ofisini kwa Latoya
“kwa sasa najiona ni mwenye furaha kusikia kwamba Sabrina amepata kazi ambayo itamuwezesha kujitegemea yeye mwenyewe.Sabrina ni mlemavu wa ngozi na hakuwa akipewa thamani yoyote na familia yangu,alitengwa na kubaguliwa kwa kitu kimoja tu ulemavu wa ngozi yake..Leo hii amesoma na amepata kazi ya kufanya na muda si mrefu ataanza maisha yake mwenyewe.Haya ni mafanikio.Grace naye ni msichana ambaye amepitia magumu mengi na ambaye alikwisha kata tamaa ya maisha kwa kuamini kwamba ni muathirika wa ukimwi,kwa sasa anaendelea na mafunzo ya upishi na nina uhakika kwamba baada ya kumaliza mafunzo yake atapata kazi au atajiajiri yeye mwenyewe.Haya ni mafanikio makubwa sana ambayo ninaweza kujivunia.Nimeweza kuyabadili maisha ya wasichana hawa.Nimewasaidia kuzitimiza ndoto zao walizokwisha poteza matumaini ya kuzitimiza tena.Wasichana hawa ni wachache lakini katika jamii wapo wengi zaidi ya hawa wawili,ambao hawana mtu wa kumsemea shida zao.Kwa sasa natakiwa kuelekeza nguvu kwa Marina.Ni lazima niokoe maisha ya Marina na kumsaida kuzitimia ndoto zake vile vile.Baada ya hapo ndipo nitafikiria namna ya kuweza kuanzisha taasisi yangu mwenyewe itakayokuwa ikiwasaidia watu wenye matatizo mbali mbali makubwa katika jamii” Innocent alikuwa na mawazo mengi.Kitendo cha baba yake mzee Benard kumtamkia maneno makali namna ile kilimuumiza sana moyo.
Hatimaye akawasili katika jengo zilimo ofisi za taasisi binafsi inayoendeshwa na mwanadada Latoya. Aliposhuka garini akapanda lifti ya jengo lile hadi ghorofa ya tisa ambamo ndimo zilimokuwa ofisi za taasisi hiyo.Mtu wa kwanza kumtambua Inno alikuwa ni Sabrina.
“kaka Innocent karibu sana” Sabrina akamkaribisha Inno kwa furaha huku akitabasamu
“Hii ndiyo ofisi yetu kaka Innocent karibu sana.” Sabrina akasema huku akimtambulisha Inno kwa wafanyakazi waliokuwa pale ofisini.Innocent hakuificha furaha yake.Kwa muda huu mfupi aliowasili hapa kila mmoja alionekana kuufurahia ucheshi na uchangamfu wa Innocent. Baada ya maongezi na utani wa hapa na pale kama kawaida yake ,Sabrina akamchukua Inno na kumpeleka katika ofisi ya Latoya.
“Dada huyu ndiye Innocent,amekuja kukuona kwa ajili ya lile suala nililokueleza” Sabrina akamtambulisha Innocent kwa Latoya.Kwa sekunde kadhaa walibaki wanatazamana halafu Latoya akasema
“Karibu sana Innocent,nafurahi kukufahamu” Latoya akasema huku akisimama na kumpa mkono
“Hata mimi nafurahi sana kukufahamu “ Innocent akajibu huku akihisi kama vile macho yake yalikuwa yakimdanganya kwa msichana aliyekuwa mbele yake.

TUKUTANE SEHEMU IJAYO……
 
Back
Top Bottom