Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #41
SEHEMU YA 34 YA 50
ameshampa, namba zote za siri za kadi zake za benki Mayasa alikuwa anazijua.
Tom alikuwa amechanganyikiwa! Penzi la Mayasa lilimchanganya sana kiasi kwamba, alikuwa kama chizi mwenye akili timamu! Hata yeye mwenyewe alishindwa kuelewa ni mapenzi ya aina gani yaliyokuwa na nguvu kiasi kile. Hata hivyo alipuuza na kuamini kwamba alikuwa akimpenda sana Mayasa na hapakuwa na kitu kingine zaidi ya hicho.
Kwa upande wa Mayasa ilikuwa tofauti sana, hata siku moja hakuwahi kuhisi kumpenda Tom, hilo hata yeye mwenyewe alilikiri moyoni mwake. Kama alikuwa akimpenda, basi ni kwasababu ya pesa alizokuwa nazo. Aifurahia kuishi maisha mazuri, huku akisiamia miradi mbalimbali ya Tom iliyokuwa jijini Dar es Salaam na mikoani. Mayasa alikuwa ni kila kitu.
Mara nyingi alikuwa akikutana na marafiki zake na kuzungumza nao juu ya mambo mbalimbali ya kimaisha, siku zote walishindwa kuelewa ni kwanini Tom alimpenda kiasi kile. Siku zote aliishia kuwaambia kwamba mapenzi yake ya kweli ndiyo nguzo kubwa inayomfanya aendelee kufaidi maisha mazuri kwa Tom.
“Shosti sema ukweli bwana, lazima kuna kitu kipo nyuma ya pazia!” Rukia, mmoja wa marafiki zake alimwuliza Mayasa.
“Zaidi ya penzi langu, nini kingine?”
“Sema shoga yetu na sisi tuwatulize wapenzi wetu, haiwezekani Papaa Bill mpaka anafikia hatua ya kumuacha mkewe kama hakuna kitu kingine nyuma ya pazia!”
“Aaaah! Bwana...kikubwa ni utaalamu kitandani...haya inatosha sana shoga zangu, nendeni mkajifunze mambo ya kitandani....tehe...tehe...tehe....” Mayasa alisema akicheka.
“Lakini ni vizuri ukatuambia ukweli bwana!”
“Sina ukweli mwingine zaidi ya huo...” Mayasa akazidi kusisitiza. Hakuwa tayari kutoa siri zake za ndani kiasi kile.
“Sawa shoga yetu lakini nina ushauri mzuri sana kwa ajili yako. Huwezi kuwa mjinga kiasi hicho, Papaa Bill ana pesa nyingi sana na tayari anakuamini kwa kiasi kikubwa, lakini kama hutakuwa makini, unaweza kuachana naye ukawa huna kitu!”
“Kwahiyo?”
“Lazima ufanye kitu fulani, uwe tajiri!”
“Kitu gani hicho shosti yangu?”
“KAMA UNATAKA UTAJIRI WA TOM, HUNA BUDI KUWA NA ROHO NGUMU! UNACHOTAKIWA WEWE KUFANYA NI KUMPOTEZA!”
“Kumpoteza? Unamaanisha nini?”
“PAPAA BILL ANATAKIWA AFE!” Rukia akambia Mayasa ambaye alikuwa kimya sana akiwasikiliza.
Lilionekana wazo lililomchanganya sana akili yake, alitumia kimya kwa muda mrefu sana bila kuzungumza kitu, lakini baadaye akafungua kinywa chake na kuzungumza; “Wazo lako ni zuri sana, lakini sasa nitamuuaje? Na watu wakijua?” Mayasa akasema akitetemeka kwa hofu.
“Acha ujinga Mayasa, wewe ni mtoto wa mjini, kama ni kweli unataka utajiri wa Papaa Bill lazima umwondoe duniani, kama upo tayari sema nikupe njia nzuri ambazo zitakuwa katika mazingira ya usiri mkubwa, yeye afe akuache na utajiri wako!”
“Nipo tayari, nakusikiliza!”
Pamoja na ushauri wa kitaalamu alioupata kutoka kwa Dk. Joseph Kisanga, bado Mariam hakuwa katika hali yake ya kawaida. Hata yeye mwenyewe alijishangaa, hapakuwa na kitu kingine akilini mwake zaidi ya Tom. Aliamini pasingetokea mwanaume atakayempenda kwa mapenzi yake yote kama ilivyokuwa kwa Tom!
Kwake Tom alikuwa ni kila kitu! Kilichomuumiza zaidi ni majibu ya wazazi wake, kwamba Tom aliwafukuza nyumbani kwake mbele ya mwanamke wake Mayasa, hilo lilimuumiza sana.
Hakika isingewezekana Mariam, akavumilia kumuona Tom akiendelea kutesa na Mayasa wake, mbele ya macho yake. Pengine angejifungia ndani, lakini bado angeweza kumuona kwenye magazeti na hata kwenye luninga akiwa katika shughuli mbalimbali za kijamii.
Tom asingekwepeka kirahisi! Kitu pekee kilichokuwa mbele yake ilikuwa ni lazima Mariam aondoke Dar es Salaam, aende mbali, kijijini, nje ya mji kusipokuwa na Teknolojia ya Mawasiliano kabisa. Hiyo ndiyo njia pekee ambayo Mariam alikuwa nayo.
“Ni bora niondoke, nihame kabisa, sina sababu ya kuendelea kuteseka, pengine ilikuwa lazima niteseke, niumie, nikose amani, lakini haya yote naamini Mungu wa mbinguni anaona na atanipigania kwa kila hali ili niweze kushindana na haya majaribu,” Mariam alimwambia mama yake kwa uchungu, muda mfupi kabla ya kuingia kwenye basi, eneo la Kituo Kikuu cha Mabasi ya Mikoani, Ubungo jijini Dar es Salaam.
“Usijali mwanangu, hakuna lenye mwanzo linalokosa mwisho, safiri salama mama, msalimie bibi yako. Hakikisha unatuliza akili yako mama, huna sababu ya kumfikiria mtu mbaya kama Tom tena katika maisha yako, fungua ukurasa mpya sasa mwanangu!”
“Nashukuru sana mama!”
“Usijali, lakini bado kuna kitu ambacho ni muhimu sana ukifahamu mwanangu!”
“Kitu gani mama?”
“Maombi! Unatakiwa uombe sana mwanangu, msaada pekee kwa sasa ambao upo mbele yako ni kuwa karibu na Mungu! Ukiweza kutimiza hilo itakuwa rahisi sana kushinda majaribu yaliyopo mbele yako.”
“Ahsante sana mama kwa ushauri wako, nafikiri unanijua vizuri sana kuhusu hilo mama yangu, nitakuwa karibu sana na Mungu wangu kwa kila kitu mama...nakuahidi na itakuwa hivyo kweli!”
“Nimefurahi sana, nakutakia safari njema!”
“Ahsante sana mama!”
“Halafu kitu kingine mwanangu, lazima ujue kwamba wewe bado ni mzuri sana, naamini kuna wanaume wengi ambao wanahitaji angalau kunywa soda na wewe, kwahiyo huna haja ya kuhuzunika sana!” Mama yake Mariam alisema akitabasamu.
Mariam naye akatabasamu, tabasamu la ushindi! Ulikuwa ushindi mkubwa sana kwa mama yake na Mariam, tangu alipoamka asubuhi, hakuwahi kumuona mwanaye akitabasamu, lakini tabasamu lake la muda ule, tena la ghafla lilikuwa faraja kubwa sana kwa mama Mariam, sasa alikuwa ana imani kwamba ufumbuzi umepatikana.
“Nafikiri umenielewa mwanangu!” Tabasamu la mama yake na Mariam, sasa liliongezeka.
“Mama, kwa utani na wewe!!!”
“Siyo utani mwanangu, wewe ni binti yangu na sina sababu ya kukutania, ninachokuambia ni kitu cha ukweli ambacho hata wewe utakidhibitisha, kama utaamua kutulia!”
“Ahsante mama, ahsante sana mama yangu kwa kuona uzuri wangu, lakini uzuri huu mama, ulikuwa kwa ajili ya Tom!”
“Tom?!” Mama Mariam akauliza akiwa ameukunja uso wake.
“Ndiyo mama, Tom!”
“Ndiyo hakutaki sasa mwanangu!”
“Najua siyo yeye!”
“Ni nani?”
“Shetani!”
“Hata kama ni shetani, ndiyo ampe nafasi kubwa kiasi kile? Wakati mwingine shetani huwa anakaribishwa na mtu mwenyewe, na ndivyo alivyofanya Tom, yeye ameamua kumkaribisha shetani, unafikiri kwanini asimchezee kama yeye mwenyewe amemruhusu?”
“Usiseme hivyo mama!”
“Kumbe niseme nini Mariam, niseme nini?”
“Tunatakiwa kumuombea, naamini kwa kufanya hivyo siku moja atabadilika, niamini mama!”
Mama Mariam hakujibu kitu zaidi ya kumtulizia macho mwanaye, macho ambayo hayakuweza kuficha hasira na chuki za wazi alizokuwa nazo dhidi ya Tom.
“Naomba kukuuliza kitu mama!”
“Uliza!”
“Unamwamini Mungu?”
“Ndiyo, hata yeye anajua hilo!”
“Vizuri, nina swali lingine!”
“Uliza!”
“Kuna mahali popote ambapo Mungu amewahi kushindwa?”
“Hapana, yeye ni mshindi siku zote!”
“Basi ataendelea kuwa mshindi hata katika hili linalonisumbua na kunitesa mama!”
“Aaaamen!”
“Kwahiyo bado naendelea kukuomba umuombee!”
“Nitamuombea!”
“Nimefurahi kusikia hivyo, nimefurahi pia kwa wewe kuwa upande wangu. Nakupenda sana mama...nakupenda sana!”
“Nakupenda pia mwanangu mpenzi, nakutakia safari njema!”
“Ahsante mama!” Baada ya hapo mama Mariam aliondoka kwani dakika moja tu, baadaye basi liliondoka kituoni na safari ya kwenda Morogoro ikaanza.
Mariam aliweza kuwa macho hadi alipofika Kibaha tu, baada ya hapo alisinzia kabla ya kupitiwa na usingizi mzito. Hakujua Chalinze walipita muda gani, hata gari lilipoingia kwenye mizani eneo la Mikese hakujua, alishtuliwa na abiria aliyekuwa ameketi naye siti moja gari lilipokuwa likiingia katika katika Kituo cha Mabasi cha Msamvu.
“Tumefika sister amka!” Kijana huyo akamwambia akimtingisha.
“Mmmmh!” Mariam akaitikia akionekana kuwa na usingizi.
“Tumefika, inaonekana umechoka sana!”
“Ah! Ni kawaida, siku zote huwa napenda kulala nikiwa safarini!”
“Unashukia hapa?”
“Hapana, nitakwenda kushukia mjini!”
“Sawa basi, mimi nashuka hapa!” Baada ya abiria waliokuwa wakishukia pale Msamvu kuisha, gari likaondoka na kuingia katikati ya Mji ya Morogoro likawashusha abiria wote, eneo la Masika.
Mariam akanyoosha moja kwa moja akifuata barabara iliyokuwa ikielekea katika Kituo cha Daladala kilichokuwa kituo cha zamani cha mabasi yanayokwenda mikoani. Kwa bahati nzuri akapata gari la kwenda kwao, tena lililokuwa likikaribia kuondoka. Akaketi siti ya dirishani akiwa mkimya sana.
Muda mfupi baadaye safari ya kwenda Matombo ikaanza. Matombo siyo mbali sana kutokea Morogoro mjini, lakini kwasababu ya ubovu wa barabara na milima, ilimchukua saa mbili na nusu Mariam kufika kijijini kwao. Aliposhuka kituoni akakodisha baiskeli ambayo ilimpeleka nyumbani kwa bibi yake, katikati ya mashamba na mapori makubwa, mwendo ambao uliwachukua saa nzima na nusu njiani.
Hatimaye Mariam alifika akiwa amechoka sana, bibi yake alipomuona alimkimbilia na kumkumbatia kwa furaha. Hata hivyo alishangazwa sana na hali ya afya yake ilivyokuwa imezorota! Baada ya salamu, bibi alianza kuuliza habari za mjini.
“Wazee hawajambo?”
“Wazima kabisa bibi, wanakusalimia sana!”
“Nimefurahi sana kusikia hivyo....enheee, vipi wewe na mwenzako?”
Mariam hakuweza kujibu kitu, ni kama alikuwa amechomwa na chuma chenye moto katikati ya kidonda kibichi! Machozi yakaanza kumiminika machoni mwake. Akaanza kulia kwa sauti ya chini.
“Vipi, mbona unalia tena?”
Mariam hakujibu zaidi ya kuendelea kulia, tena safari hii alilia kwa sauti kubwa zaidi ya awali.
ameshampa, namba zote za siri za kadi zake za benki Mayasa alikuwa anazijua.
Tom alikuwa amechanganyikiwa! Penzi la Mayasa lilimchanganya sana kiasi kwamba, alikuwa kama chizi mwenye akili timamu! Hata yeye mwenyewe alishindwa kuelewa ni mapenzi ya aina gani yaliyokuwa na nguvu kiasi kile. Hata hivyo alipuuza na kuamini kwamba alikuwa akimpenda sana Mayasa na hapakuwa na kitu kingine zaidi ya hicho.
Kwa upande wa Mayasa ilikuwa tofauti sana, hata siku moja hakuwahi kuhisi kumpenda Tom, hilo hata yeye mwenyewe alilikiri moyoni mwake. Kama alikuwa akimpenda, basi ni kwasababu ya pesa alizokuwa nazo. Aifurahia kuishi maisha mazuri, huku akisiamia miradi mbalimbali ya Tom iliyokuwa jijini Dar es Salaam na mikoani. Mayasa alikuwa ni kila kitu.
Mara nyingi alikuwa akikutana na marafiki zake na kuzungumza nao juu ya mambo mbalimbali ya kimaisha, siku zote walishindwa kuelewa ni kwanini Tom alimpenda kiasi kile. Siku zote aliishia kuwaambia kwamba mapenzi yake ya kweli ndiyo nguzo kubwa inayomfanya aendelee kufaidi maisha mazuri kwa Tom.
“Shosti sema ukweli bwana, lazima kuna kitu kipo nyuma ya pazia!” Rukia, mmoja wa marafiki zake alimwuliza Mayasa.
“Zaidi ya penzi langu, nini kingine?”
“Sema shoga yetu na sisi tuwatulize wapenzi wetu, haiwezekani Papaa Bill mpaka anafikia hatua ya kumuacha mkewe kama hakuna kitu kingine nyuma ya pazia!”
“Aaaah! Bwana...kikubwa ni utaalamu kitandani...haya inatosha sana shoga zangu, nendeni mkajifunze mambo ya kitandani....tehe...tehe...tehe....” Mayasa alisema akicheka.
“Lakini ni vizuri ukatuambia ukweli bwana!”
“Sina ukweli mwingine zaidi ya huo...” Mayasa akazidi kusisitiza. Hakuwa tayari kutoa siri zake za ndani kiasi kile.
“Sawa shoga yetu lakini nina ushauri mzuri sana kwa ajili yako. Huwezi kuwa mjinga kiasi hicho, Papaa Bill ana pesa nyingi sana na tayari anakuamini kwa kiasi kikubwa, lakini kama hutakuwa makini, unaweza kuachana naye ukawa huna kitu!”
“Kwahiyo?”
“Lazima ufanye kitu fulani, uwe tajiri!”
“Kitu gani hicho shosti yangu?”
“KAMA UNATAKA UTAJIRI WA TOM, HUNA BUDI KUWA NA ROHO NGUMU! UNACHOTAKIWA WEWE KUFANYA NI KUMPOTEZA!”
“Kumpoteza? Unamaanisha nini?”
“PAPAA BILL ANATAKIWA AFE!” Rukia akambia Mayasa ambaye alikuwa kimya sana akiwasikiliza.
Lilionekana wazo lililomchanganya sana akili yake, alitumia kimya kwa muda mrefu sana bila kuzungumza kitu, lakini baadaye akafungua kinywa chake na kuzungumza; “Wazo lako ni zuri sana, lakini sasa nitamuuaje? Na watu wakijua?” Mayasa akasema akitetemeka kwa hofu.
“Acha ujinga Mayasa, wewe ni mtoto wa mjini, kama ni kweli unataka utajiri wa Papaa Bill lazima umwondoe duniani, kama upo tayari sema nikupe njia nzuri ambazo zitakuwa katika mazingira ya usiri mkubwa, yeye afe akuache na utajiri wako!”
“Nipo tayari, nakusikiliza!”
Pamoja na ushauri wa kitaalamu alioupata kutoka kwa Dk. Joseph Kisanga, bado Mariam hakuwa katika hali yake ya kawaida. Hata yeye mwenyewe alijishangaa, hapakuwa na kitu kingine akilini mwake zaidi ya Tom. Aliamini pasingetokea mwanaume atakayempenda kwa mapenzi yake yote kama ilivyokuwa kwa Tom!
Kwake Tom alikuwa ni kila kitu! Kilichomuumiza zaidi ni majibu ya wazazi wake, kwamba Tom aliwafukuza nyumbani kwake mbele ya mwanamke wake Mayasa, hilo lilimuumiza sana.
Hakika isingewezekana Mariam, akavumilia kumuona Tom akiendelea kutesa na Mayasa wake, mbele ya macho yake. Pengine angejifungia ndani, lakini bado angeweza kumuona kwenye magazeti na hata kwenye luninga akiwa katika shughuli mbalimbali za kijamii.
Tom asingekwepeka kirahisi! Kitu pekee kilichokuwa mbele yake ilikuwa ni lazima Mariam aondoke Dar es Salaam, aende mbali, kijijini, nje ya mji kusipokuwa na Teknolojia ya Mawasiliano kabisa. Hiyo ndiyo njia pekee ambayo Mariam alikuwa nayo.
“Ni bora niondoke, nihame kabisa, sina sababu ya kuendelea kuteseka, pengine ilikuwa lazima niteseke, niumie, nikose amani, lakini haya yote naamini Mungu wa mbinguni anaona na atanipigania kwa kila hali ili niweze kushindana na haya majaribu,” Mariam alimwambia mama yake kwa uchungu, muda mfupi kabla ya kuingia kwenye basi, eneo la Kituo Kikuu cha Mabasi ya Mikoani, Ubungo jijini Dar es Salaam.
“Usijali mwanangu, hakuna lenye mwanzo linalokosa mwisho, safiri salama mama, msalimie bibi yako. Hakikisha unatuliza akili yako mama, huna sababu ya kumfikiria mtu mbaya kama Tom tena katika maisha yako, fungua ukurasa mpya sasa mwanangu!”
“Nashukuru sana mama!”
“Usijali, lakini bado kuna kitu ambacho ni muhimu sana ukifahamu mwanangu!”
“Kitu gani mama?”
“Maombi! Unatakiwa uombe sana mwanangu, msaada pekee kwa sasa ambao upo mbele yako ni kuwa karibu na Mungu! Ukiweza kutimiza hilo itakuwa rahisi sana kushinda majaribu yaliyopo mbele yako.”
“Ahsante sana mama kwa ushauri wako, nafikiri unanijua vizuri sana kuhusu hilo mama yangu, nitakuwa karibu sana na Mungu wangu kwa kila kitu mama...nakuahidi na itakuwa hivyo kweli!”
“Nimefurahi sana, nakutakia safari njema!”
“Ahsante sana mama!”
“Halafu kitu kingine mwanangu, lazima ujue kwamba wewe bado ni mzuri sana, naamini kuna wanaume wengi ambao wanahitaji angalau kunywa soda na wewe, kwahiyo huna haja ya kuhuzunika sana!” Mama yake Mariam alisema akitabasamu.
Mariam naye akatabasamu, tabasamu la ushindi! Ulikuwa ushindi mkubwa sana kwa mama yake na Mariam, tangu alipoamka asubuhi, hakuwahi kumuona mwanaye akitabasamu, lakini tabasamu lake la muda ule, tena la ghafla lilikuwa faraja kubwa sana kwa mama Mariam, sasa alikuwa ana imani kwamba ufumbuzi umepatikana.
“Nafikiri umenielewa mwanangu!” Tabasamu la mama yake na Mariam, sasa liliongezeka.
“Mama, kwa utani na wewe!!!”
“Siyo utani mwanangu, wewe ni binti yangu na sina sababu ya kukutania, ninachokuambia ni kitu cha ukweli ambacho hata wewe utakidhibitisha, kama utaamua kutulia!”
“Ahsante mama, ahsante sana mama yangu kwa kuona uzuri wangu, lakini uzuri huu mama, ulikuwa kwa ajili ya Tom!”
“Tom?!” Mama Mariam akauliza akiwa ameukunja uso wake.
“Ndiyo mama, Tom!”
“Ndiyo hakutaki sasa mwanangu!”
“Najua siyo yeye!”
“Ni nani?”
“Shetani!”
“Hata kama ni shetani, ndiyo ampe nafasi kubwa kiasi kile? Wakati mwingine shetani huwa anakaribishwa na mtu mwenyewe, na ndivyo alivyofanya Tom, yeye ameamua kumkaribisha shetani, unafikiri kwanini asimchezee kama yeye mwenyewe amemruhusu?”
“Usiseme hivyo mama!”
“Kumbe niseme nini Mariam, niseme nini?”
“Tunatakiwa kumuombea, naamini kwa kufanya hivyo siku moja atabadilika, niamini mama!”
Mama Mariam hakujibu kitu zaidi ya kumtulizia macho mwanaye, macho ambayo hayakuweza kuficha hasira na chuki za wazi alizokuwa nazo dhidi ya Tom.
“Naomba kukuuliza kitu mama!”
“Uliza!”
“Unamwamini Mungu?”
“Ndiyo, hata yeye anajua hilo!”
“Vizuri, nina swali lingine!”
“Uliza!”
“Kuna mahali popote ambapo Mungu amewahi kushindwa?”
“Hapana, yeye ni mshindi siku zote!”
“Basi ataendelea kuwa mshindi hata katika hili linalonisumbua na kunitesa mama!”
“Aaaamen!”
“Kwahiyo bado naendelea kukuomba umuombee!”
“Nitamuombea!”
“Nimefurahi kusikia hivyo, nimefurahi pia kwa wewe kuwa upande wangu. Nakupenda sana mama...nakupenda sana!”
“Nakupenda pia mwanangu mpenzi, nakutakia safari njema!”
“Ahsante mama!” Baada ya hapo mama Mariam aliondoka kwani dakika moja tu, baadaye basi liliondoka kituoni na safari ya kwenda Morogoro ikaanza.
Mariam aliweza kuwa macho hadi alipofika Kibaha tu, baada ya hapo alisinzia kabla ya kupitiwa na usingizi mzito. Hakujua Chalinze walipita muda gani, hata gari lilipoingia kwenye mizani eneo la Mikese hakujua, alishtuliwa na abiria aliyekuwa ameketi naye siti moja gari lilipokuwa likiingia katika katika Kituo cha Mabasi cha Msamvu.
“Tumefika sister amka!” Kijana huyo akamwambia akimtingisha.
“Mmmmh!” Mariam akaitikia akionekana kuwa na usingizi.
“Tumefika, inaonekana umechoka sana!”
“Ah! Ni kawaida, siku zote huwa napenda kulala nikiwa safarini!”
“Unashukia hapa?”
“Hapana, nitakwenda kushukia mjini!”
“Sawa basi, mimi nashuka hapa!” Baada ya abiria waliokuwa wakishukia pale Msamvu kuisha, gari likaondoka na kuingia katikati ya Mji ya Morogoro likawashusha abiria wote, eneo la Masika.
Mariam akanyoosha moja kwa moja akifuata barabara iliyokuwa ikielekea katika Kituo cha Daladala kilichokuwa kituo cha zamani cha mabasi yanayokwenda mikoani. Kwa bahati nzuri akapata gari la kwenda kwao, tena lililokuwa likikaribia kuondoka. Akaketi siti ya dirishani akiwa mkimya sana.
Muda mfupi baadaye safari ya kwenda Matombo ikaanza. Matombo siyo mbali sana kutokea Morogoro mjini, lakini kwasababu ya ubovu wa barabara na milima, ilimchukua saa mbili na nusu Mariam kufika kijijini kwao. Aliposhuka kituoni akakodisha baiskeli ambayo ilimpeleka nyumbani kwa bibi yake, katikati ya mashamba na mapori makubwa, mwendo ambao uliwachukua saa nzima na nusu njiani.
Hatimaye Mariam alifika akiwa amechoka sana, bibi yake alipomuona alimkimbilia na kumkumbatia kwa furaha. Hata hivyo alishangazwa sana na hali ya afya yake ilivyokuwa imezorota! Baada ya salamu, bibi alianza kuuliza habari za mjini.
“Wazee hawajambo?”
“Wazima kabisa bibi, wanakusalimia sana!”
“Nimefurahi sana kusikia hivyo....enheee, vipi wewe na mwenzako?”
Mariam hakuweza kujibu kitu, ni kama alikuwa amechomwa na chuma chenye moto katikati ya kidonda kibichi! Machozi yakaanza kumiminika machoni mwake. Akaanza kulia kwa sauti ya chini.
“Vipi, mbona unalia tena?”
Mariam hakujibu zaidi ya kuendelea kulia, tena safari hii alilia kwa sauti kubwa zaidi ya awali.