Simulizi : Beyond Love (Zaidi Ya Mapenzi)

Simulizi : Beyond Love (Zaidi Ya Mapenzi)

SEHEMU YA 34 YA 50

ameshampa, namba zote za siri za kadi zake za benki Mayasa alikuwa anazijua.

Tom alikuwa amechanganyikiwa! Penzi la Mayasa lilimchanganya sana kiasi kwamba, alikuwa kama chizi mwenye akili timamu! Hata yeye mwenyewe alishindwa kuelewa ni mapenzi ya aina gani yaliyokuwa na nguvu kiasi kile. Hata hivyo alipuuza na kuamini kwamba alikuwa akimpenda sana Mayasa na hapakuwa na kitu kingine zaidi ya hicho.

Kwa upande wa Mayasa ilikuwa tofauti sana, hata siku moja hakuwahi kuhisi kumpenda Tom, hilo hata yeye mwenyewe alilikiri moyoni mwake. Kama alikuwa akimpenda, basi ni kwasababu ya pesa alizokuwa nazo. Aifurahia kuishi maisha mazuri, huku akisiamia miradi mbalimbali ya Tom iliyokuwa jijini Dar es Salaam na mikoani. Mayasa alikuwa ni kila kitu.

Mara nyingi alikuwa akikutana na marafiki zake na kuzungumza nao juu ya mambo mbalimbali ya kimaisha, siku zote walishindwa kuelewa ni kwanini Tom alimpenda kiasi kile. Siku zote aliishia kuwaambia kwamba mapenzi yake ya kweli ndiyo nguzo kubwa inayomfanya aendelee kufaidi maisha mazuri kwa Tom.

“Shosti sema ukweli bwana, lazima kuna kitu kipo nyuma ya pazia!” Rukia, mmoja wa marafiki zake alimwuliza Mayasa.

“Zaidi ya penzi langu, nini kingine?”

“Sema shoga yetu na sisi tuwatulize wapenzi wetu, haiwezekani Papaa Bill mpaka anafikia hatua ya kumuacha mkewe kama hakuna kitu kingine nyuma ya pazia!”

“Aaaah! Bwana...kikubwa ni utaalamu kitandani...haya inatosha sana shoga zangu, nendeni mkajifunze mambo ya kitandani....tehe...tehe...tehe....” Mayasa alisema akicheka.

“Lakini ni vizuri ukatuambia ukweli bwana!”

“Sina ukweli mwingine zaidi ya huo...” Mayasa akazidi kusisitiza. Hakuwa tayari kutoa siri zake za ndani kiasi kile.

“Sawa shoga yetu lakini nina ushauri mzuri sana kwa ajili yako. Huwezi kuwa mjinga kiasi hicho, Papaa Bill ana pesa nyingi sana na tayari anakuamini kwa kiasi kikubwa, lakini kama hutakuwa makini, unaweza kuachana naye ukawa huna kitu!”

“Kwahiyo?”

“Lazima ufanye kitu fulani, uwe tajiri!”

“Kitu gani hicho shosti yangu?”

“KAMA UNATAKA UTAJIRI WA TOM, HUNA BUDI KUWA NA ROHO NGUMU! UNACHOTAKIWA WEWE KUFANYA NI KUMPOTEZA!”

“Kumpoteza? Unamaanisha nini?”

“PAPAA BILL ANATAKIWA AFE!” Rukia akambia Mayasa ambaye alikuwa kimya sana akiwasikiliza.

Lilionekana wazo lililomchanganya sana akili yake, alitumia kimya kwa muda mrefu sana bila kuzungumza kitu, lakini baadaye akafungua kinywa chake na kuzungumza; “Wazo lako ni zuri sana, lakini sasa nitamuuaje? Na watu wakijua?” Mayasa akasema akitetemeka kwa hofu.

“Acha ujinga Mayasa, wewe ni mtoto wa mjini, kama ni kweli unataka utajiri wa Papaa Bill lazima umwondoe duniani, kama upo tayari sema nikupe njia nzuri ambazo zitakuwa katika mazingira ya usiri mkubwa, yeye afe akuache na utajiri wako!”

“Nipo tayari, nakusikiliza!”





Pamoja na ushauri wa kitaalamu alioupata kutoka kwa Dk. Joseph Kisanga, bado Mariam hakuwa katika hali yake ya kawaida. Hata yeye mwenyewe alijishangaa, hapakuwa na kitu kingine akilini mwake zaidi ya Tom. Aliamini pasingetokea mwanaume atakayempenda kwa mapenzi yake yote kama ilivyokuwa kwa Tom!

Kwake Tom alikuwa ni kila kitu! Kilichomuumiza zaidi ni majibu ya wazazi wake, kwamba Tom aliwafukuza nyumbani kwake mbele ya mwanamke wake Mayasa, hilo lilimuumiza sana.

Hakika isingewezekana Mariam, akavumilia kumuona Tom akiendelea kutesa na Mayasa wake, mbele ya macho yake. Pengine angejifungia ndani, lakini bado angeweza kumuona kwenye magazeti na hata kwenye luninga akiwa katika shughuli mbalimbali za kijamii.

Tom asingekwepeka kirahisi! Kitu pekee kilichokuwa mbele yake ilikuwa ni lazima Mariam aondoke Dar es Salaam, aende mbali, kijijini, nje ya mji kusipokuwa na Teknolojia ya Mawasiliano kabisa. Hiyo ndiyo njia pekee ambayo Mariam alikuwa nayo.

“Ni bora niondoke, nihame kabisa, sina sababu ya kuendelea kuteseka, pengine ilikuwa lazima niteseke, niumie, nikose amani, lakini haya yote naamini Mungu wa mbinguni anaona na atanipigania kwa kila hali ili niweze kushindana na haya majaribu,” Mariam alimwambia mama yake kwa uchungu, muda mfupi kabla ya kuingia kwenye basi, eneo la Kituo Kikuu cha Mabasi ya Mikoani, Ubungo jijini Dar es Salaam.

“Usijali mwanangu, hakuna lenye mwanzo linalokosa mwisho, safiri salama mama, msalimie bibi yako. Hakikisha unatuliza akili yako mama, huna sababu ya kumfikiria mtu mbaya kama Tom tena katika maisha yako, fungua ukurasa mpya sasa mwanangu!”

“Nashukuru sana mama!”

“Usijali, lakini bado kuna kitu ambacho ni muhimu sana ukifahamu mwanangu!”

“Kitu gani mama?”

“Maombi! Unatakiwa uombe sana mwanangu, msaada pekee kwa sasa ambao upo mbele yako ni kuwa karibu na Mungu! Ukiweza kutimiza hilo itakuwa rahisi sana kushinda majaribu yaliyopo mbele yako.”

“Ahsante sana mama kwa ushauri wako, nafikiri unanijua vizuri sana kuhusu hilo mama yangu, nitakuwa karibu sana na Mungu wangu kwa kila kitu mama...nakuahidi na itakuwa hivyo kweli!”

“Nimefurahi sana, nakutakia safari njema!”

“Ahsante sana mama!”

“Halafu kitu kingine mwanangu, lazima ujue kwamba wewe bado ni mzuri sana, naamini kuna wanaume wengi ambao wanahitaji angalau kunywa soda na wewe, kwahiyo huna haja ya kuhuzunika sana!” Mama yake Mariam alisema akitabasamu.

Mariam naye akatabasamu, tabasamu la ushindi! Ulikuwa ushindi mkubwa sana kwa mama yake na Mariam, tangu alipoamka asubuhi, hakuwahi kumuona mwanaye akitabasamu, lakini tabasamu lake la muda ule, tena la ghafla lilikuwa faraja kubwa sana kwa mama Mariam, sasa alikuwa ana imani kwamba ufumbuzi umepatikana.

“Nafikiri umenielewa mwanangu!” Tabasamu la mama yake na Mariam, sasa liliongezeka.

“Mama, kwa utani na wewe!!!”

“Siyo utani mwanangu, wewe ni binti yangu na sina sababu ya kukutania, ninachokuambia ni kitu cha ukweli ambacho hata wewe utakidhibitisha, kama utaamua kutulia!”

“Ahsante mama, ahsante sana mama yangu kwa kuona uzuri wangu, lakini uzuri huu mama, ulikuwa kwa ajili ya Tom!”

“Tom?!” Mama Mariam akauliza akiwa ameukunja uso wake.

“Ndiyo mama, Tom!”

“Ndiyo hakutaki sasa mwanangu!”

“Najua siyo yeye!”

“Ni nani?”

“Shetani!”

“Hata kama ni shetani, ndiyo ampe nafasi kubwa kiasi kile? Wakati mwingine shetani huwa anakaribishwa na mtu mwenyewe, na ndivyo alivyofanya Tom, yeye ameamua kumkaribisha shetani, unafikiri kwanini asimchezee kama yeye mwenyewe amemruhusu?”

“Usiseme hivyo mama!”

“Kumbe niseme nini Mariam, niseme nini?”

“Tunatakiwa kumuombea, naamini kwa kufanya hivyo siku moja atabadilika, niamini mama!”

Mama Mariam hakujibu kitu zaidi ya kumtulizia macho mwanaye, macho ambayo hayakuweza kuficha hasira na chuki za wazi alizokuwa nazo dhidi ya Tom.

“Naomba kukuuliza kitu mama!”

“Uliza!”

“Unamwamini Mungu?”

“Ndiyo, hata yeye anajua hilo!”

“Vizuri, nina swali lingine!”

“Uliza!”

“Kuna mahali popote ambapo Mungu amewahi kushindwa?”

“Hapana, yeye ni mshindi siku zote!”

“Basi ataendelea kuwa mshindi hata katika hili linalonisumbua na kunitesa mama!”

“Aaaamen!”

“Kwahiyo bado naendelea kukuomba umuombee!”

“Nitamuombea!”

“Nimefurahi kusikia hivyo, nimefurahi pia kwa wewe kuwa upande wangu. Nakupenda sana mama...nakupenda sana!”

“Nakupenda pia mwanangu mpenzi, nakutakia safari njema!”

“Ahsante mama!” Baada ya hapo mama Mariam aliondoka kwani dakika moja tu, baadaye basi liliondoka kituoni na safari ya kwenda Morogoro ikaanza.

Mariam aliweza kuwa macho hadi alipofika Kibaha tu, baada ya hapo alisinzia kabla ya kupitiwa na usingizi mzito. Hakujua Chalinze walipita muda gani, hata gari lilipoingia kwenye mizani eneo la Mikese hakujua, alishtuliwa na abiria aliyekuwa ameketi naye siti moja gari lilipokuwa likiingia katika katika Kituo cha Mabasi cha Msamvu.

“Tumefika sister amka!” Kijana huyo akamwambia akimtingisha.

“Mmmmh!” Mariam akaitikia akionekana kuwa na usingizi.

“Tumefika, inaonekana umechoka sana!”

“Ah! Ni kawaida, siku zote huwa napenda kulala nikiwa safarini!”

“Unashukia hapa?”

“Hapana, nitakwenda kushukia mjini!”

“Sawa basi, mimi nashuka hapa!” Baada ya abiria waliokuwa wakishukia pale Msamvu kuisha, gari likaondoka na kuingia katikati ya Mji ya Morogoro likawashusha abiria wote, eneo la Masika.

Mariam akanyoosha moja kwa moja akifuata barabara iliyokuwa ikielekea katika Kituo cha Daladala kilichokuwa kituo cha zamani cha mabasi yanayokwenda mikoani. Kwa bahati nzuri akapata gari la kwenda kwao, tena lililokuwa likikaribia kuondoka. Akaketi siti ya dirishani akiwa mkimya sana.

Muda mfupi baadaye safari ya kwenda Matombo ikaanza. Matombo siyo mbali sana kutokea Morogoro mjini, lakini kwasababu ya ubovu wa barabara na milima, ilimchukua saa mbili na nusu Mariam kufika kijijini kwao. Aliposhuka kituoni akakodisha baiskeli ambayo ilimpeleka nyumbani kwa bibi yake, katikati ya mashamba na mapori makubwa, mwendo ambao uliwachukua saa nzima na nusu njiani.

Hatimaye Mariam alifika akiwa amechoka sana, bibi yake alipomuona alimkimbilia na kumkumbatia kwa furaha. Hata hivyo alishangazwa sana na hali ya afya yake ilivyokuwa imezorota! Baada ya salamu, bibi alianza kuuliza habari za mjini.

“Wazee hawajambo?”

“Wazima kabisa bibi, wanakusalimia sana!”

“Nimefurahi sana kusikia hivyo....enheee, vipi wewe na mwenzako?”

Mariam hakuweza kujibu kitu, ni kama alikuwa amechomwa na chuma chenye moto katikati ya kidonda kibichi! Machozi yakaanza kumiminika machoni mwake. Akaanza kulia kwa sauti ya chini.

“Vipi, mbona unalia tena?”

Mariam hakujibu zaidi ya kuendelea kulia, tena safari hii alilia kwa sauti kubwa zaidi ya awali.
 
SEHEMU YA 35 YA 50

“Sema basi mjukuu wangu, kuna nini? Au amepata matatizo? Niambie mimi ni bibi yako, nitakusaidia!” Kauli hiyo ya bibi yake ilizidi kumchoma Mariam ambaye sasa alizidisha kilio chake.

Kazi aliyokuwa nayo bibi yake, ilikuwa moja tu, kumbembeleza!

*******

Kwa muda mfupi sana, roho ya Mayasa ilibadilika! Roho yake ilikuwa mbaya kuliko hata ya muuza sumu! Mayasa alikuwa na roho mbaya kuliko kawaida, hata yeye mwenyewe alijishangaa na alishindwa kuelewa roho hiyo ya paka alipoipata.

Macho yake mawili yalikuwa yamemuelekea Rukia ambaye kwa mwonekano wake wa nje, haikuwa rahisi kuamini kwamba anaweza kumshawishi mtu aondoe uhai wa mtu mwingine kirahisi kiasi kile. Tamaa ya mali ilimvaa, heshima na umaarufu ulikuwa umemtawala moyoni mwake. Alikuwa tayari kwa lolote.

“Ni kweli upo tayari?” Rukia akamwuliza akimkazia macho.

“Nipo tayari kwa moyo wangu wote!”

“Sawa, sasa ipo njia, lakini lazima uwe makini sana!”

“Nimeshasema nipo tayari kwa lolote!”

“Hatutaki utusaliti Mayasa!”

“Ni kitu ambacho hakiwezi kutokea.”

“Tom anatakiwa kufa, ndani ya mwezi huu, hatutakiwi kuwa na haraka, unachotakiwa kufanya kwa sasa ni kuongeza mapenzi yako kwa nguvu, mchanganye kimapenzi sana, toka naye mara nyingi, jamii ione mapenzi yenu na ikiwezekana wadaku waandike, baada ya hapo kazi itafanyika kiulaini kabisa!”

“Sawa kabisa...” kila mmoja alimuunga mkono.

“Lakini nina wasiwasi na jambo moja!” Mayasa akasema akitetemeka, hakuweza kuificha hofu yake.

Rukia akamkata jicho la chuki lililojaa mashaka, kwa ilivyoonekana, kama Mayasa angeongea jambo lolote kupingana na uamuzi wake wa awali, basi hatari ambayo ingekuwa mbele yake asingeisahau hadi atakapoingia kaburini!





Kuulizwa habari za Tom, ilikuwa ni sawa na kumchoma kwa msumari wenye moto, katikati ya kidonda kibichi kilichokuwa moyoni mwake. Alitegemea kuulizwa na bibi yake juu ya Tom, lakini siyo mapema kiasi kile. Hata kama asingeulizwa, lazima angesema, kwani ndiyo sababu hasa iliyomfanya awe kule kijijini.

Moyo wa Mariam ulimuuma sana, alishindwa kuelewa ni mapenzi ya aina gani aliyokuwa kwa Tom, aliumizwa zaidi na jinsi alivyokuwa akimpenda kwa moyo wake mtu ambaye hakuonyesha kushtuka kabisa na penzi lake. Bibi yake alikuwa amemtonesha!

“Nyamaza mjukuu wangu, lakini lazima unieleze ukweli wa kilichotokea!” Baada ya Mariam kutulia, bibi yake akamwambia.

“Bibi kuna matatizo!”

“Ni nini?”

“Tom bibi, Tom ameniacha!”

“Amekuacha?””

“Ndiyo bibi!”

“Sababu?”

“Hakuna!”

“Haiwezekani, lazima kuna kitu umemuudhi mwenzako, lakini wazee wameshindwa kumaliza huko nyumbani?”

“Walikwenda kwake lakini walifukuzwa na Tom na mwanamke wake!”

“Mwanamke wake? Unataka kusema kwamba Tom ana mwanamke mwingine?”

“Tena anaishi naye pale nyumbani, mimi nilikuwa nalala chumba cha wageni, baada ya kuchoshwa na mambo yao, ndiyo nikaondoka kwenda nyumbani, huko napo ndiyo....” Mariam akamsimulia bibi yake kila kitu, hadi alipofikia hatua ya kulazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

“Pole sana mjukuu wangu, wewe baki hapa nyumbani, pumzika kwanza, utulize akili yako, mambo mengine yatafuata baadaye, naamini hali yako itarudi kuwa nzuri. Hapa utakula kambale na mboga za majani na afya yako itarudi kama zamani, sawa mama?!” Bibi yake akamwambia kwa sauti iliyojaa mapenzi mazito.

“Ahsante bibi, nimefurahi sana, umenifurahisha sana kwakweli, naanza kujiona mpya sasa.”

“Kama ndivyo kweli, basi Mungu wa Mbinguni ashukuriwe!”

“Amen!”

Maisha yaliendelea kijijini kama kawaida, Mariam akiwa anamsaidia bibi yake kazi za kilimo. Aliyafurahia mno maisha ya pale kijijini, kwani kama alivyotarajia awali, hapakuwa na mawasiliano ya aina yoyote, kitu ambacho ndiyo haswa alikuwa akikitegemea.

Afya yake ikaanza kurejea taratibu hadi ilipotengemaa kabisa, wazazi wake kila walipokwenda kumtembelea walikuta mabadiliko! Furaha ikarudi katika maisha yake. Ingawa ilikuwa kazi ngumu sana, lakini alijishangaa aliwezaje kumsahau Tom, mwanaume ambaye kwake alikuwa sawa na Wimbo wa Taifa!

Alifurahishwa sana na mabadiliko yake, kwa bahati nzuri bibi yake alishajua kwamba kutaja jina la Tom ni sawa na kuchochea matatizo aliyokuwa nayo, hivyo hakuthubutu kutaja jina la Tom katika mazungumzo yao. Siku zote alikuwa akimfundisha maisha ya kijijini na jinsi wazee wa zamani walivyoweza kuishi maisha marefu kijijini kutokana na aina ya vyakula wanavyokula.

“Kwahiyo bibi, unataka kuniambia kwamba hata mimi sasa nitaishi maisha marefu kwasababu nipo huku?”

“Bila shaka mjukuu wangu!”

“Lakini bibi ukiachana na vyakula, ni nini kingine kilichowafanya wazee wa zamani waishi miaka mingi zaidi kuliko hivi sasa?”

“Mazingira pia yanachangia, unajua Mariam, huku kijijini kila kitu ni cha asili. Hakuna kuvuta moshi wa dizeli wala petroli, hakuna mionzi ya minara ya simu, moshi wa viwandani wala dawa zenye kemikali, hizi ni sababu kubwa sana zilizowafanya wazee wa zamani waishi umri mrefu!”

“Sasa naanza kuelewa!”

Mariam alikubali maisha mapya, akajifunza vitu vipya kila siku. Hakika aliyafurahia maisha ya kijijini. Aliona ni bora kuishi maisha yale kijijini, kuliko kuishi Dar es Salaam lakini akiumizwa na kukosa amani ya kuendelea na maisha. Maisha ya kijijini yalikuwa chaguo lake la kweli na hakuwahi kuyajutia.

********

Kitendo cha Mayasa kusema kuna jambo lililompa wasiwasi, kilitoa tafsiri tofauti kwa Rukia. Msichana huyu ni katili na siku zote hakupenda kabisa msaliti katika mipango yake. Alimwangalia Mayasa kwa jicho la hasira akisubiria azungumze jambo lolote ambalo ni kinyume na makubaliano yao ili amuadhibu.

Mayasa akawaangalia wote kwa zamu, kisha akatingisha kichwa kama anayesikitishwa na jambo ambalo angelitamka.

“Una nini?”

“Nimeshasema kwamba kuna jambo linanitatiza kidogo!”

“Sema ni nini?”

“Hivi Rukia, askari hawawezi kujua kweli?”

“Labda uwaambie wewe, tena naomba nikuambie jambo moja, sina muda wa kupoteza zaidi juu ya jambo hili...ni hivi, leo jioni tutakutana katika kikao cha siri na vijana tutakaowapa kazi hii!”

“Ni wapi?”

“Mbezi!”

*******

Kilikuwa chumba kidogo, lakini nadhifu na kinachovutia, kikiwa na uwezo wa kuhudumia watu ishirini kwa wakati mmoja. Ndani ya chumba hicho kilichokuwa na kiyoyozi, kulikuwa na watu sita waliokutana katika kikao cha siri usiku huo.

Watu hao walikuwa ni Rukia, Mayasa na vijana wanne ambao walikuwa maalumu kwa kukodiwa kwa ajili ya kufanya mauaji. Wote walikuwa kimya, vinywani mwao, ukitoka moshi mzito wa sigara ambao wakati mwingine walikuwa wakiutolea puani na masikioni! Baada ya ukimya wa muda kupita, Rukia aligonga meza kwa nguvu!

“Tumekutana hapa kwa kazi moja muhimu iliyopo mbele yetu, kama nilivyotangulia kusema awali, Papaa Bill anatakiwa aondoke duniani, tena ndani ya mwezi huu! Malipo yenu ni mazuri sana na leo mtapata malipo ya utangulizi!” Alisema Rukia, akiwatazama wote kwa zamu.

“Hakuna tabu sister Rukia, nafikiri unatuamini katika michongo hii, sisi hatuna noma, tupeni cash, tufanye kazi!”

“Hakuna shida, suala la pesa siyo tatizo kwangu, chukueni hizi kwanza na ninaomba baada ya wiki mbili Papaa Bill awe na jina lingine! Marehemu nadhani ni jina litakalomfaa zaidi!” Mayasa alisema akitoa shilingi milioni tano kama fedha za utangulizi na kuwapatia wale vijana.

“Hakuna tabu, tunakuhakikishia kazi nzuri baada ya huo muda uliosema.” Mmoja wao ambaye ndiye aliyepokea zile fedha alisema.

“Kilichobaki ni utekelezaji tu!” Mayasa akasema.

“Kuhusu hilo, usijali kabisa, hawa vijana nawaaminia!” Rukia akasema.

“Sawa, tutaona!” Kikao kikaahirishwa.

******

Alichokifanya Mayasa ni kuwa karibu zaidi na mume wake kuliko kipindi kingine chochote walipokuwa wakiishi na Tom. Alijifanya kumpenda zaidi, kuwa karibu naye zaidi kuliko kawaida. Tom akafurahi sana, akazidi kumpa siri zake za biashara akiamini alikuwa mke mwema wa maisha yake.

Hakujua kilichokuwa nyuma ya pazia, laiti kama angejua alikuwa katika hatari ya kufa wakati wowote, angeachana naye haraka sana, lakini jambo hilo hakulijua kwani lilikuwa siri kubwa sana. Maisha yaliendelea kama kawaida, Mayasa akiendelea kuwasiliana kwa karibu na vijana waliopewa kazi ya kumuua Tom na kuelekezekana kila kitu kwa hatua.

“Nadhani sasa kila kitu kipo tayari, mnaweza kukamilisha hiyo kazi!”

“Poa sister, ungependa iwe lini?”

“Kesho usiku, miye nitakuwa nyumbani, halafu nyie mtamtegea jirani na nyumbani mpaka atakapoingia, lakini muda wake mara nyingi ni saa mbili na madakika hivi, lakini haifiki saa tatu!”

“Umesomoka!”

Siku iliyofuata, kuanzia saa moja na nusu jioni, nyumba ya Tom ilikuwa imezungukwa na vijana sita wenye silaha, wakisubiria muda atakaorudi! Kama kawaida yake, saa mbili na robo alikuwa getini akipiga honi mfululizo ili afunguliwe lakini cha ajabu hakuna aliyetokea kumfungulia!

“Shiiit! Huyu mwanamke vipi, kwanini hanifungulii, ngoja nishuke nikagonge mwenyewe!” Tom akasema akifungua mlango wa mbele ili atoke, lakini kabla hajafanya hivyo akashangaa akihisi kitu cha baridi kikigusa shingoni mwake.

“Tulia hivyo hivyo, nyoosha mikono yako juu na ufuate maagizo yote tutakayokuambia!” Alisikia sauti ya mtu ikimuamrisha nyuma yake.

“Kuna nini tena jamani?”

“Hatubishani, lakini kama utaleta ubishi wa aina yoyote nakulipua sasa hivi!”

Sekunde chache baadaye, Tom alikuwa amezungukwa na watu sita waliokuwa wanaonekana dhahiri kuwa ni watu wa mazoezi. Alishajua kwamba kifo chake kilikuwa kimekaribia! Isingekuwa rahisi akubali kufa kijinga kiasi kile, alitakiwa kufanya jambo fulani ili aokoe roho yake.
 
SEHEMU YA 36 YA 50

“Jamani kama ni pesa au kitu chochote cha thamani mnataka, niambieni niwape lakini mniachie roho yangu, nawaombeni sana!”

“Hatuna shida na pesa zako!”

“Sasa kumbe mnataka nini jamani?!” Tom akasema akitetemeka kwa woga.

“Tunahitaji roho yako!”

“Roho yangu?”/



“Ndiyo, unatakiwa kufa Tom!” Tom akachanganyikiwa zaidi.

“Sikilizeni ndugu zangu, mnajua...” hakupewa nafasi ya kumalizia sentesi yake.

“Hivi kwanini tunamkawiza?”

“Mlipue!” Mwingine akadakia.

Hakuna aliyezungumza tena baada ya hapo, muda mfupi baadaye ulisikika mlio wa risasi. Wale vijana wakatoweka na kumuacha Tom akiwa ameanguka chini hoi, damu zikimvuja mwilini. Tom alikuwa hajitambui!





lio wa risasi ulisikika mara tatu, lakini baada ya hapo muungurumo wa gari ukasikika. Hiyo ilimaanisha tayari wauaji walikuwa wameshatoweka eneo la tukio. Ndani ya dakika tatu tu, watu walikuwa wamejaa getini mwa nyumba ya Tom wakishuhudia Tom alikiwa hajigusi chini, huku damu zikimtoka kwa wigi!

“Mume wangu oh! Mume wangu jamani...” Mayasa naye alitoka nje na kuanza kulia, akamlalia Tom, huku akisikilizia mapigo yake ya moyo kuhakikisha kwamba alikuwa amekufa au lah!

“Nitabaki na nani miye...Tom wangu jamani...” Mayasa alizidi kupiga kelele.

Watu walimuonea huruma sana, walijua ni kaisi gani alikuwa anaumia kutokana na matatizo aliyopata mumewe. Hakuna aliyejua kwamba yote aliyokuwa akiyafanya ilikuwa ni maigizo tu! Siri hiyo aliijua yeye mwenyewe.

“Lakini wezi gani wa mapema hivi?’ Mtu mmoja aliyekuwa kwenye tukio lile aliuliza.

“Hata mimi nashangaa...” mwingine akadakia.

“Mnashangazwa na nini jamani, kama watu wanaiba kwenye benki mchana inashindikana vipi kwa muda huu?”

“Lakini mbona hawajachukua kitu?”

“Hata mimi nashangaa!”

Kila mmoja alikuwa anaongea lake, lakini wengi walishangazwa sana na majambazi hao, ambao hawakuiba kitu chcohote zaidi ya kumdhuru Tom na kuondoka zao. Ilionekana kuwepo kwa kitu kilichojificha, kitu ambacho hakuna ambaye alikuwa anakijua.

Muda mfupi baadaye watu walijadiliana na kuamua kumkimbiza Tom katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Akalazwa kwa ajili ya kupatiwa matibabu. Muda wote huo Mayasa alikuwa analia sana, alionyesha huzuni kubwa, lakini moyoni mwake alikuwa akitamani sana Tom afe, hilo ndilo lililokuwa akilini mwake.

Kilichoonekana usoni mwa Mayasa kilikuwa tofauti kabisa na kilichokuwa moyoni mwake. Mayasa alikuwa na roho mbaya kuliko hata ya muuza sumu! Aliweka mbele masilahi yake baada ya kifo cha Tom.

“Samahani Dokta naweza kumuona mume wangu?”

“Hapana, yupo kwenye uangalizi maalum kwa sasa, tafadhali nenda urudi kesho asubuhi!”

“Lakini atapona?”

“Tumuombe Mungu, tutajitahidi kufanya kila tutakaloweza, lakini nguvu za Mungu ndizo zinazohitajika zaidi katika hili.”

“Ahsante sana Dokta.”

*****

Kilikuwa chumba kidogo, kizuri, chenye hewa safi ya kiyoyozi, ndani ya chumba hicho kulikuwa na vijana wanne na wasichana watatu, hiyo ndiyo ilikuwa Kamati nzima ya mauaji ya Tom. Wote walikuwa kimya, wakimtizama Rukia ambaye alikuwa ndiye Kiongozi wa Kamati hiyo. Rukia akapiga meza kwa nguvu!

“Nina furaha sana, nina furaha kwasababu kazi ambayo tuliwatuma, mmeikamilisha ingawa siyo kwa kiasi kikubwa!” Rukia alianza kuzungumza.

“Samahani sister!” Mmoja wa vijana wale akasema.

“Nakusikiliza!”

“Kwanini unasema siyo kwa kiasi kikubwa?”

“Acha wasiwasi kijana, nimesema siyo kwa kiwango kikubwa kwakuwa hajafa lakini nafikiri Mayasa atakuwa na majibu mazuri juu ya hilo kwakuwa yeye ndiye aliyeenda naye hospitalini!”

“Ni kweli Rukia, hali yake siyo nzuri, hana dalili za kupona kabisa, hadi sasa hivi hajazinduka, naona lazima atakufa tu!”

“Ni kweli kabisa!”

“Na hilo ndiyo lengo letu.”

“Kikubwa zaidi kilichotukutanisha hapa ni kuwalipa pesa zenu zilizobakia, lakini kama tukihitaji msaada wenu baadaye tutawajulisha na tafadhali mtoe ushirikiano.”

“Hakuna tabu sister Rukia.”

“Sawa.. Mayasa...” Rukia akaita.

“Nakusikiliza.”

“Wapatie mzigo wao uliobakia.”

Mayasa hakuwa na kitu cha kuzungumza zaidi ya kuchukua fedha kwenye pochi yake na kuwakabidhi.

“Tunashukuru sana kwa msaada wenu, lakini lazima jambo hili liwe siri,” Mayasa akasema.

“Siyo tu, siri bali kama tutaisikia mahali popote, basi mjue kuwa kifo kitakuwa jirani zaidi na nyie!”

“Kuhusu hilo huna sababu ya kuwa na wasiwasi nalo, kwani ni kazi ya kwanza tunafanya na wewe?”

“Lakini watu wanabadilika!”

‘Watakuwepo ila siyo sisi!”

“Nimefurahi kusikia hivyo!” Baada ya hapo kikao kikaahirishwa.

Siku iliyofuata, asubuhi na mapema Mayasa alikuwa ameshafika hospitalini, alikuwa makini sana na Tom, akihakikisha anamhudumia kwa karibu, lakini nia yake ya moyoni ilikuwa ni Tom afe, alichukia sana kumuona Tom akiwa bado anaendelea kuwa hai, ingawa alikuwa anapumua kwa msaada wa mashine.

Aliendelea kuwa karibu na Tom siku zote, hakuna aliyejua kilichokuwa akilini mwa Mayasa, kilichokuwa kikifanyika ilikuwa ni mchezo wa kuigiza tu, siri ambayo aliitunza moyoni mwake.

Wiki moja baadaye hakuona sababu ya kuendelea kumficha mama yake Tom juu ya hali ya mwanaye. Akafanya mawasiliano haraka, ambapo siku iliyofuata mama Tom alikuwa ameshafika Dar es Salaam, akipokelewa na Mayasa. Siku zote mama yake Tom, hakuwa akimpenda Mayasa, lakini kwasababu alishamuomba sana mwanaye aachane naye na akakataa, hakuwa na sababu ya kuendelea kuingilia mapenzi yao.

“Enhee vipi hali yake?” Mama Tom aliuliza mara baada ya kufika nyumbani na kuketi sofani.

“Pumzika kwanza mama!”

“Hapana, lazima nijue hali ya mwanangu!”

“Hana hali mbaya sana mama, lakini kesho asubuhi tutaongozana pamoja kwenda kumtizama, ila nimewasiliana na daktari wake amesema hali yake sasa siyo mbaya sana!”

“Fahamu zake zimesharudi?”

“Bado, lakini ana nafuu kubwa!”

Mama Tom alimpenda sana mwanaye, hakuwa tayari kumuona anakufa akiwa mdogo kiasi kile, kwa maisha ya shida ambayo amekulia, aliamini alipaswa kuendelea kuwa hai ili ale matunda ya jasho lake.

Kila alipokumbuka siku aliyotoka kwenye mgodi unaotitia akiwa na madini kwenye mfuko wake wa salufeti, alitokwa machozi. Kwake Tom alitakiwa aendelee kuyafaidi maisha! Kufa mapema kiasi kile ilikuwa ni pigo kubwa sana kwake. Mayasa alipata kazi ya kumbembeleza mama Tom, ambaye hakunyamaza mpaka sauti ilipoanza kukauka ndipo akanyamza na kupitiwa na usingizi.

Yeye ndiye aliyemwamsha Mayasa asubuhi, akimkumbusha kuwahi hospitani kumwona Tom. Walipoingia wodini na mama Tom kumuona mwanaye akiwa amefungwa mashine za kupumua, alichanganyikiwa! Tom alikuwa na hali mbaya sana na hadi wakati huo alikuwa hajitambui!

Ghafla mama Tom akaanza kuhisi kizunguzungu kikali, mwili wake ukaanza kupoteza nguvu taratibu, kisha akaanguka chini kama mzigo! Muda huo huo akakimbizwa wodini na kuanza kushughulikiwa. Hata hivyo hali yake ilizidi kuwa mbaya, usiku wa siku ile ile, mama Tom alifariki dunia!

“Pole sana dada, mgonjwa ni nani wako?” Daktari aliyekuwa akimhudumia alimwuliza Mayasa akifikiria jinsi ya kumweleza juu ya kifo cha mama huyo.

“Mama mkwe wangu, kwani vipi?”

“Kwa bahati mbaya sana, ameshafariki dunia!”

“Unasema?”

“Usijali ni mambo ya kawaida ambayo unapaswa kukubaliana nayo, hata kama ukilia, machozi yako hayataweza kumrudisha mama duniani, zaidi utakuwa unajiumiza mwenyewe.”

“Lakini kwanini inakuwa kwangu, nina mkosi gani mimi jamani! Mume wangu amelazwa na mpaka sasa hivi hajarejewa na fahamu, mama naye amefariki, nitakuwa mgeni wa nani mimi?”

“Usijali dada yangu, kubaliana na hali halisi, hatuwezi kubadilisha kilichotokea, zaidi unapaswa kumshukuru Mungu maana ameagiza tushukuru kwa kila jambo.”

“Ahsante sana Dokta, nashukuru. Acha nikawapashe habari ndugu zetu na kuandaa taratibu za mazishi.” Mayasa akasema na kuondoka.

“Sawa.”

Mayasa aliondoka akiwa na mawazo mengi sana kichwani mwake, hakuona sababu ya kuendelea kuishi nyumbani kwa Tom, alishachuma mali za kutosha kwa kipindi kifupi sana ambacho Tom alikuwa amelazwa hospitalini. Aliweza kufanya hivyo kwasababu Tom alikuwa akiweka mambo yake wazi.

Alishachukua fedha katika akaunti zote na kuziacha nyeupe kabisa, madini yaliyokuwa yakihifadhiwa chumbani nayo aliyachukua na kuyauza. Hakurudi tena hospitalini kumuangalia Tom wala kuuchukua mwili wa mama mkwe wake kwa ajili ya mazishi.

Wiki moja baadaye, kila kitu kilikuwa tayari na kilichokuwa mbele yake ilikuwa ni kuondoka nchini, kwenda zake kujichimbia Uingereza. Hilo ndilo lililofanyika, Mayasa akapanda ndege na kwenda zake Uingereza, akiwa hajui kabisa kilichoendelea huku nyuma.

******

Maisha ya kijijini Matombo, yalianza kumzoea Mariam, kama ilivyokuwa nia yake, kujitenga mbali na mji ili asiweze kujua habari zinazomhusu Tom na Mayasa. Alifurahia sana kuishi kijijini na aliyapenda maisha ya kule. Hata afya yake ilianza kuridhisha. Siku moja alitumwa na bibi yake mjini. Alipokuwa akikatiza eneo la Nunge akaona meza ya magazeti, hakutaka kuisogelea, maana alijua pengine angekutana na habari za Tom, jambo ambalo hakutaka litokee.

Katika hali ya kushangaza sana, akajikuta kuna kitu kinamlazimisha kwenda kwenye meza ile ya magazeti. Baadaye akaamua kwenda, akijipa moyo kwamba hata kama ataona habari zake, hazitamuuma sana kwasababu tayari ameshaanza kumzoea!

Magazeti karibu yote ya siku hiyo, yaliandika habari juu ya kifo cha mama yake Tom, Mariam alihisi kuchanganyikiwa! Macho yake yakatua juu ya gazeti la Ijumaa. Gazeti hilo lilikuwa limeandika kwa maandishi yaliyosomeka; ...wakati hali ya Papaa Bill ikizidi kuwa mbaya, MAMA YAKE MZAZI AFARIKI DUNIA! Chini ya maneno hayo, kulikuwa na maneno mengine yaliyosomeka; Mwenyewe yupo hoi Muhimbili, bado hajapata fahamu, mkewe amkimbia...soma habari kamili uk. 2

Zilikuwa habari mbaya sana kwa Mariam, akajikuta akipoteza nguvu taratibu, giza totoro likaanza kupita mbele ya macho yake. Akaanguka chini na kupoteza fahamu.
 
SEHEMU YA 37 YA 50

Alishaumia vya kutosha, alishateseka kiasi cha kutosha, aliamua kuishi kijijini Matombo ili asizidi kuteseka, alitaka kuwa mbali na maumivu ya mapenzi. Ni kweli alikuwa akimpenda sana Tom, hata moyo wake ulimhakikishia jambo hilo, lakini ilikuwa lazima awe mbali na matatizo!

Kumpenda mtu si tatizo, lakini kwa Mariam ilikuwa tatizo! Alikuwa na kila sababu ya kujitenga na matatizo. Hakutaka kuzidi kujipa mateso ambayo anaweza kuwa nayo mbali.

Mariam hakuwa na penzi la kinafiki, alikuwa na penzi la dhati ambalo siku zote lilikuwa hai, lakini hakutaka kumwaga machozi tena, hakutaka kuumia zaidi, lakini kwasababu tayari alishatambua kwamba moyo wake ulimpenda sana, akaona njia pekee ilikuwa ni kumkimbia!

Pengine ulikuwa uamuzi wa busara, lakini safari yake ya mjini ya siku hiyo, ilisababisha matatizo makubwa, ikatonesha kidonda kilichoanza kukauka. Mambo yakawa yale yale! Hakuweza kuvumilia kusoma habari za Tom akiwa amelazwa hospitalini, tena akiwa hana msaada wowote, mbaya zaidi mama mkwe wake akiwa amefariki! Hilo lilimuuma sana na kujikuta akianguka chini na kupoteza fahamu!

Hakuna aliyekuwa na taarifa za Mariam.

“Vipi jamani?!” Mmoja wa watu waliokuwa wamesimama mbele ya meza ile ya magazeti alisema.

“Siyo suala la kuuliza, kilichobaki hapa ni kumsaidia tu!”

“Lete gari bro,” jamaa mmoja alijitolea kumchukulia na teksi.

“Mshike huko...tusaidiane jamani...” watu wakasaidiana kumwingiza Mariam kwenye gari na safari ya kwenda Hospitali ya Mkoa wa Morogoro ikaanza.

Kutoka Nunge hadi Hospitali ya Mkoa, hapakuwa mbali, dakika tano tu tayari gari lilikuwa limeshaingia ndani ya Jengo la Hospitali hiyo. Walipofika mapokezi, waliruhusiwa kwenda moja kwa moja Chumba cha Mapumziko, akapokelewa vizuri na kuanzishiwa tiba haraka.

“Poleni sana jamani,” Dokta akawaambia wale watu waliompeleka Mariam hospitalini.

“Tunashukuru sana Dokta.”

“Nani anayehusika zaidi na huyu mgonjwa, nataka kufanya naye mazungumzo kidogo!”

“Kwakweli hakuna!”

“Hakuna?!”

“Ndiyo hakuna daktari!”

“Unamaanisha nini kusema hivyo, kwahiyo kati ya ninyi nyote hakuna ndugu wa huyu mgonjwa?”

“Hakuna!”

“Kivipi?!”

“Sisi ni wasamaria wema tu, ambao tumeamua kumsaidia baada ya kumuona ameanguka na kupoteza fahamu!”

“Ilikuwaje?”

“Kwakweli hatujui, lakini ilikuwa ni mbele ya meza ya magazeti!”

“Basi hakuna tabu, lakini mnaweza kujitolea pia kumsaidia malipo ya matibabu yake!”

“Hilo halina tabu.”

“Mungu akubariki kwa hilo, acha sisi tuendelee!”

“Sawa, sijui wewe ni dokta nani?”

“Naitwa Dk. Ringo, tena nilisahau kukufahamisha, sijui na wewe mwenzangu nani?”

“Naitwa Ramsey Muhando.”

“Nashukuru sana kukufahamu.”

“Nami pia.”

Kazi ya kumtibu Mariam ikaanza, huku gharama zote zikilipwa na Ramsey ambaye alijitolea.

******

“Sikiliza shoga yangu, mimi sijazoea mambo ya nuksi nyumbani kwangu, kama nilivyokuambia, mama yake Tom amefariki na sitaki kujihusisha na jambo lolote linalomuhusu yeye!” Mayasa alikuwa akimwambia Rukia katika kikao chao kilichofanyika usiku, ndani ya hoteli moja ya kifahari katikati ya Jiji la Dar es Salaam.

“Kwahiyo sasa utafanyaje?”

“Nawaachia watu wa Halmashauri ya Jiji wazike!”

“Lakini huoni kwamba mambo yanaweza kushtukiwa?”

“Kwanini?”

“Magazeti yameshaandika, halafu nyumbani hakuna msiba, unadhani utaelewekaje?”

“Kila kitu nimeshakamilisha, nimeshauza vitu vyote, fedha zilizokuwa benki pia nimekomba zote tena kwenye akaunti zake zote, kuna madini aliyokuwa akiyahifadhi ndani nayo nimeyachukua. Sina kinachonifanya niendelee kubaki kwenye ile nyumba, waache wenye moyo mwema watamzika, wakikosekana basi, bahati mbaya!”

“Safi sana, sasa vipi kuhusu mimi, naambulia nini?” Rukia akamwuliza Mayasa akiwa anamtizama kwa macho yenye kusubiria jambo fulani.

Mayasa hakumjibu kitu, zaidi ya kumwangalia kuanzia chini hadi juu, ni kama alikuwa akimchambua!

“Twende!” Mayasa akasema.

“Wapi? Mi’ nataka kujua changu!”

“Ndiyo maana nimekuambia twende!”

“Wapi sasa?”

“Nikakupe chako!”

“Ni nini?”

“Surprise!”

“Okay!” Wote kwa pamoja wakaondoka na kushuka chini ambapo walipanda kwenye gari la Mayasa na safari ya kwenda kusipojulikana ikaanza.

Rukia alikuwa kimya muda wote wa safari, akiwa hajui ni wapi hasa walipokuwa wakielekea, maswali tele kichwani mwake yalibaki yanazunguka. Baadaye gari likasimama nje ya geti jeusi, lenye nyumba moja nzuri sana. Mayasa akapiga honi mfululizo, mlango ukafunguliwa.

Wakaegesha gari kisha Mayasa akamshika mkono Rukia na kumtembeza kila kona ya nyumba ile. Ilikuwa nyumba ya kisasa iliyokuwa na kila kitu ndani, bwawa la kuogelea, gari ndogo ya kutembelea, samani ndani na bustani nzuri sana iliyokuwa nje.

“Sikiliza rafiki yangu...wewe ni rafiki yangu mpenzi, nakupenda na ninaheshimu sana msaada wako katika kufanikisha zoezi hili, kuanzia leo hii ni nyumba yako na kila kitu kilichomo ndani.

“Kwa bahati nzuri, hii nyumba nilijengewa na Tom mwenyewe, na hati zote zina majina yangu, kwahiyo usiwe na wasiwasi kabisa, hapa ni kwako na kila kilichomo ndani, kuanzia gari na samani zote, kuishi hapa au kuuza ni hiyari yako!” Mayasa akamwambia Rukia.

Rukia hakutegemea kama angepewa zawadi kubwa kiasi kile, kwanza alitumia muda mwingi kuwa kimya akijaribu kutafakari kama ni kweli kilichokuwa mbele yake kilikuwa yakini, Mayasa akampatia hati zote na kumtoa wasiwasi kwamba pale palikuwa ni nyumbani kwake na alikuwa na uhuru wa kufanya jambo lolote apendalo.

“Ahsante sana Mayasa shoga yangu, huu ndiyo urafiki wa kweli, ni wachache sana wanaweza kuwa kama wewe!”

“Usijali...sasa sijui utaishi hapa au utauza?”

“Nitauza, siwezi kuishi hapa!”

Ndivyo ilivyokuwa, siku iliyofuata nyumba ilitafutiwa mteja wa chapchap, ikauzwa kwa bei ya kutupwa! Jioni ya siku hiyo hiyo, Mayasa akaondoka kwenda zake Uingereza. Hakutaka kuendelea kuishi Tanzania tena, haikuwa sehemu salama kwake!

Hadi wiki moja baada ya mama yake Tom kufariki bila kutokea kwa ndugu yeyote, mwili huo ulichukuliwa na Halmashauri ya Jiji na kwenda kuzikwa. Kama kawaida, magazeti yaliripoti kila kitu, haikueleweka ni wapi Mayasa, mwanamke aliyekuwa akiishi naye baada ya Tom kumuacha mkewe Mariam, alipokwenda.

Kwakuwa hapakuwa na ndugu mwingine yeyote, mambo yaliendelea kuwa giza nene, mwenye majibu alikuwa ni Tom ambaye kwa wakati huo ni kama alikuwa nusu-mfu!

*******

“Toooom....Toom...Tooom, usife, bado nakupenda, bado nakuhitaji Tom wangu usife...” Ndiyo maneno aliyozungumza Mariam baada ya kuzinduka siku tatu baadaye katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro alipokuwa amelazwa.

“Vipi dada yangu, naomba utulie kwanza...tulia...” Ilikuwa sauti ya muuguzi ambaye alimwita mwenzake mara moja, ambapo alimuagiza akamwite dokta haraka.
 
SEHEMU YA 38 YA 50

“Afadhali amezinduka, vipi dada unaendeleaje sasa?” Dokta akamwuliza akiwa anamtizama usoni.

Mariam hakuwa na la kuongea, alianza kushangaa hadi aliporudisha fahamu vizuri, hapo ndipo Daktari alipomsimulia kila kitu. Bahati nzuri, Ramsey mmoja wa watu walioshuhudia tukio la yeye kuanguka, ambaye ndiye aliyekuwa akigharamia matibabu yake, akatokea. Alifurahi sana kumkuta katika hali nzuri. Akamsimulia kila kitu kilichotokea, Mariam naye hakuficha chochote kuhusu Papaa Bill ‘Tom’. Alizungumza kila ukweli unaohusu uhusiano wake na Tom. Historia yake ilihuzunisha sana, haikuwa rahisi kuamini kama msichana mdogo kama yeye aliwahi kupitia historia ngumu kiasi kile.

“Pole sana dada yangu, sasa nafikiri ni vyema nikurudishe nyumbani ukapumzike kwanza!” Ramsey akasema.

“Wapi?”

“Matombo, kwa bibi yako.”

“Haiwezekani!”

“Kwanini?”

“Sitaki!”

“Unataka kwenda wapi?’

“Kama ni kweli unataka kunisaidia, kwasasa nataka kwenda Muhimbili kuonana na Tom, pili kushughulikia mazishi ya mama mkwe wangu! Nampenda sana mama...nampenda, najua alikuwa akitamani sana niishi na mwanaye, lakini Tom alimpuuza mama yake. Lazima nionyeshe mapenzi yangu kwake hata kama amekufa!”

“Sawa nitakusaidia, lakini lazima hali yako itengemae kidogo!”

“Sawa!”

Siku tatu baadaye, hali ya Mariam ilipokuwa nzuri akaruhusiwa kutoka Hospitalini. Kama Ramsey alivyoahidi ndivyo alivyofanya, alifika Hospitalini akiwa amemnunulia nguo mpya na viatu. Mariam akaoga na kubadili nguo zake kisha wakaondoka na kwenda Msamvu ambapo walipanda basi la Hood kwa safari ya kwenda Dar es Salaam.

Safari ilikuwa ndefu sana kwa Mariam, lakini hatimaye walifika Ubungo, Ramsey akakodi teksi iliyowafikisha Muhimbili. Kutokana na umaarufu wa Tom ‘Papaa Bill’, haikuwa kazi kubwa kufahamu wodi aliyokuwa amelazwa. Ramsey na Mariam wakaongozana hadi kwenye kitanda cha Tom.

Mariam hakuamini macho yake, Tom alikuwa amelala kimya kitandani huku akipumua kwa kutumia mashine. Tom alikuwa hajitambui! Mariam akaanza kulia, hadi muuguzi alipofika eneo hilo na kumwita ofisini kwake.

“Vipi dada, wewe ni ndugu yake na Papaa Bill?”

“Ndiyo!”

“Nani wake?”

“Mume wangu.”

“Mumeo?

“Ndiyo!”

“Wewe ndiye Mariam, tunayekusoma kwenye magazeti?”

“Ndiyo!”

‘Pole sana mdogo wangu, una moyo wa peke yako kwakweli!”

“Ahsante sana sister, vipi maiti ya mama Tom? Nataka kushughulikia taratibu za mazishi!”

“Pole sana, ni juzi tu alizikwa na Halmashauri ya Jiji baada ya ndugu zake kutoonekana!”

“What?!” Mariam alitamka maneno hayo, macho yakimtoka.

Hakuwa tayari kuamini alichosikia.





Marehemu mama Tom alikuwa akimpenda sana Mariam, alimpenda kwa mapenzi yake yote. Alimfahamu vizuri sana Mariam, wema wake ulikuwa mkubwa sana, alikumbuka kila kitu alichokuwa akikifanya kwa ajili ya marehemu mume wake.

Alijua yote hayo yalifanyika kutokana na mapenzi ya kweli aliyokuwa nayo kwa mwanaye! Hilo pekee lilimfanya ajitahidi kumshauri mwanaye kwa kila hali aachane na wazo la kutoishi na Mariam. Alishazungumza sana, alionyesha kila dalili ya kuchukizwa na vitendo vya Tom, lakini kijana wake hakubadilika!

Pamoja na kwamba Mariam aliamua kwenda kujificha kijijini Matombo kwa ajili ya kukaa mbali na Tom, lakini hakuwa akimchukia mama yake! Siku alipoona habari kwenye gazeti la Ijumaa kuwa amefariki dunia, aliona fadhila aliyokuwa akitakiwa kufanya ni kumzika mama huyo kwa heshima!

Pengine angeumia sana baada ya kukuta amezikwa na jambo pekee ambalo lingefuata ingekuwa ni kwenda kutizama kaburi lake na kusoma dua pembeni ya kaburi lake, lakini sasa ndoto hizo zimezimika kama mshumaa!

Mama Tom amezikwa na Halmashauri ya Jiji, ni jambo ambalo lilimuumiza sana moyo wake. Machozi kama maji yakazidi kumiminika machoni mwake.

“Nyamaza Mariam, huna sababu ya kulia dada yangu, shukuru kwa kila jambo!” Ramsey, msamaria mwema aliyemsadia kuanzia Morogoro alimwambia.

“Siyo rahisi Ramsey, ni vigumu sana kaka yangu!”

“Kwanini....kubali kilichotokea, unajua hakuna kitakachobadilishwa na machozi yako!”

“Najua, lakini naamini machozi yangu yatakuwa yanaonyesha kujali kwangu!”

“Kwa mtu aliyekufa?”

“Ndiyo!”

“Ndiyo nasikia kwako...lakini Mariam, nyamaza kulia, huna sababu ya kulia kiasi hicho, utakuwa unajiumiza tu mdogo wangu!” Nesi naye akamwambia Mariam.

“Ahsante!”

“Pole sana!”

“Nashukuru!” Sasa Mariam akatulia kidogo.

Ramsey akamwangalia Mariam aliyekuwa akiendelea kutokwa na machozi mepesi, akachukua kitambaa chake na kumfuta machozi.

“Kwahiyo Sister ni nani anayemuuguza Tom kwa sasa?”

“Papaa Bill?”

“Ndiyo!”

“Hakuna mtu yeyote anayemhudumia, yupo peke yake!”

“Hali yake?”

“Kama ulivyomuona, hali yake siyo nzuri na amepoteza fahamu tangu siku aliyoletwa hapa!”

“Nini zaidi kinachomsumbua?”

“Kwani Mariam ulikuwa wapi hadi usijue yote hayo?”

“Acha tu dada’ngu, ni stori ndefu lakini fahamu kwamba sijui chochote kinachoendelea, nitakusimulia baadaye, lakini nafikiri ni vyema ukanieleza.”

“Alivamiwa na majambazi na kumpiga risasi, kwa bahati mbaya amepooza kuanzia shingoni kushuka chini, mbaya zaidi hajapata fahamu na anapumua kwa msaada wa mashine!”

“Mungu wangu!”

“Usijali Mariam, maadam unajua kuna Mungu, basi huyo ndiye msaada pekee uliobakia kwa sasa!”

“Nitaendelea kumuomba yeye siku zote!”

“Amen!”

“Sasa Mariam, kwahiyo utakuwa ukimuuguza Tom siyo?”

“Ndiyo, lazima nifanye hivyo!”

“Vizuri sana!”

Baada ya hayo, Ramsey na Mariam wakarudi tena wodini kumuangalia Tom, bado hakuwa amefumbua macho, hali yake ilikuwa mbaya sana. Mariam akamsogelea na kumbusu mashavuni mwake, kisha akamshika Ramsey mkono na kuondoka naye.

“Tunakwenda wapi?” Mariam akamwuliza Ramsey.

“Unamaanisha nini?”

“Namaanisha tunapokwenda!”

“Mariam kwani hujui nyumbani kwangu ni Morogoro?”

“Najua!”

“Sasa?”

“Nilikuwa nataka kujua kama unakwenda huko!”

“Ndiyo jibu lake!”

“Ramsey nashukuru sana kwa msaada wako, napenda kukuambia wazi kwamba wewe ni binadamu kamili, mwenye utu na unayetambua thamani ya ubinadamu. Mungu akubariki sana kwa hilo, lakini nilikuwa na ombi lingine!”

“Nini?”

“Sitaki kwenda nyumbani leo, nahitaji kulala hotelini kwa wiki nzima, unaweza kunisaidia fedha za kulipia pango na chakula kwa muda huo?”

“Hilo linawezekana, lakini kwanini hutaki kwenda nyumbani?”

“Nataka akili yangu ipumzike kidogo kwanza, nina mawazo mengi sana Ramsey!”

“Usijali lakini sioni kama ni busara kukuacha peke yako katika kipindi hiki kigumu, nafikiri tutafute hoteli kisha nitalipia vyumba viwili, niendelee kukupa kampani zaidi au unaonaje?”

“Sawa!” Ndivyo ilivyokuwa, wakaongozana hadi katika hoteli moja nzuri iliyopo Magomeni, wakalipia na kuingia ndani.

*****

Magazeti yote ya siku iliyofuata yalikuwa yamepambwa na habari ya Mariam kuonekana Muhimbili. Yaliandika habari ile kwa undani sana tena yakiwa na picha mbalimbali zinazomwonyesha Mariam akilia wodini na nyingine akimbusu Tom aliyekuwa amelala hoi kitandani!

Walielezea kitendo kile kuwa ni cha kijasiri na kwamba Mariam alikuwa na penzi la kweli. Habari hizo ziliwafikia wazazi wa Mariam ambao walikasirika sana. Kwanza walishindwa kuelewa ni kwanini mtoto wao alikuwa anaendelea kumsaidia Tom, mwanaume ambaye alimtesa, mbaya zaidi aliwatukana hata wao!

“Unaona mama Mariam, huyu mtoto ana akili kweli?”

“Sijui amempa nini mwanangu huyu Tom? Huyo mwanamke aliyemuona anafaa, amemkimbia na nasikia ameuza kila kitu, sasa kipindi cha matatizo ndiyo Mariam awe msaada kwake, haiwezekani!”

“Haiwezekani kabisa!”
 
SEHEMU YA 39 YA 50

“Sasa tutafanyaje?”

“Kilichopo hapa ni kwenda Muhimbili hadi kwenye wodi aliyolazwa, lazima tutamwona Mariam!” Wazo hilo liliungwa mkono na wote wawili ambapo waliingia kwenye gari na kwenda moja kwa moja Muhimbili.

Walipofika wakaingia katika wodi aliyolazwa Tom, kama walivyokuwa wakitarajia ndivyo ilivyokuwa. Walimkuta Mariam akimhudumia Tom, machozi mengi yakimtoka. Mama yake Mariam alipomuona mwanaye alikuwa na hasira sana, akamfuata na kumvuta pembeni uso wake ukiwa na makunyazi.

“Hivi we’ mtoto umelogwa? Una akili kweli? Kwani huyu hana ndugu, hana marafiki? Mabaya yote aliyokufanyia huyaoni? Matusi aliyotutukana sisi wazazi wako hayakuuma?

“Umelazwa mara ngapi kwa ajili yake, lakini leo wewe ndiyo unakuwa wa kumsaidia..sasa sisi kama wazazi wako, tunakuambia toka haraka sana hapo, unatakiwa tuongozane pamoja nyumbani!”

“Najua nyie ni wazazi wangu, najua kuwa mnanipenda, lakini lazima mzifahamu na kuheshimu hisia zangu. Mimi nampenda Tom kwa mapenzi yangu yote, siwezi kwenda na nyie nyumbani nikaamuacha Tom katika hali hii!”

“Unasemaje wewe mtoto, hivi una akili kweli wewe?” Baba yake Mariam akamwuliza kwa hasira sana.

“Akili ninazo tena nyingi sana, lakini penzi langu kwa Tom litaendelea kudumu siku zote za maisha yangu!”

“Sasa kama hujatoka kwenye tumbo langu mimi mama yako, endelea kubaki hapa hospitalini, lakini kama mimi ni mama yako, niliyekuzaa, urudi mwenyewe nyumbani!” Mama Mariam akasema kwa sauti ya ukali sana, kisha akamshika mumewe mkono na kutoka nje.

Baba Mariam alikuwa na hasira sana, hakuweza kuongea neno lolote zaidi ya kuwa msikilizaji! Baadaye Mariam naye alitoka kwa hasira, akachukua taxi na kwenda hotelini.

******

Mariam alipofika hotelini, aliingia chumbani kwake akiwa amechanganyikiwa sana. Kila alichokifanya aliona kama anakosea! Mawazo mengi yalimchanya kichwani.

Zaidi ya kufikiria kuhusu wazazi wake ambao walikuwa wanamzuia kumhudumia Tom, lakini pia aliumizwa na wema wa Ramsey. Hakutaka maumivu tena baadaye, alianza kuhisi kwamba Ramsey angehitaji kulipwa fadhila.

Hapo ndipo alipoamua kumpigia simu Ramsey, hakutaka kubaki na mawazo kichwani mwake. Akachukua mkonge wa simu, kisha akabonyeza namba za chumbani kwa Ramsey, simu ikaanza kuita, baadaye ikapokelewa na sauti tulivu sana ya Ramsey.

“Yes, Mariam hapa, naomba uje chumbani kwangu Ramsey!”

“Chumbani kwako?” Ramsey akauliza kwa mshangao.

“Ndiyo!”

“Kuna nini?”

“Njoo tu!” Dakika mbili baadaye Ramsey alikuwa chumbani kwa Mariam akiwa amevaa bukta na fulana nyepesi, uso wake ukionyesha wazi wasiwasi aliokuwa nao.

“Kuna nini dada Mariam?”

“Nataka kujua kwanini unanifanyia yote haya?”

Ramsey hakuwa na jibu la haraka. Aliangalia juu, kisha akarudisha macho yake chini kabla ya kuyatuliza usoni mwa Mariam.

“Unasema?” Ramsey akauliza.

“Kwanini umekuwa mwema kwangu kwa kiasi kikubwa namna hii?”

Ramsey alikuwa kimya.





Ramsey aliendelea kuwa kimya, katika siku ambazo alishangazwa sana na Mariam basi ni pamoja na siku ile. Swali aliloulizwa lilikuwa gumu sana, gumu kwa sababu hata mazingira ya swali lenyewe yalikuwa tata! Kuna wakati alianza kuwaza kwamba, inawezekana Mariam alikuwa akimtaka ndiyo maana akamwuliza swali lile kama mtego.

Macho ya Ramsey yalibaki usoni mwa Mariam kwa muda mrefu, akimtizama kwa makini na kumsoma uso wake kama ulifanana na aliyokuwa anayazungumza. Kwa kiasi kikubwa hakuweza kujua nia hasa ya Mariam ilikluwa nini kwani katika uso wake hapakuwa na kitu hata kimoja kilichoonekana kushabihiana na maneno yake.

Hakujua kama alikuwa anamtania au alikuwa anamwekea mitego! Ramsey akabaki anamwangalia Mariam bila kufungua kinywa chake kusema neno lolote. Sasa Ramsey akaamua kumwangalia Mariam kwa umakini zaidi, macho yake yalishuka hadi miguuni mwa Mariam, akaikagua.

Akayapandisha taratibu hadi kiunoni, hapo akakubali kwamba kweli Mariam alikuwa mwanamke mwenye mvuto wa kike! Akamwangalia macho yake ya mviringo ambayo yalikuwa pambo tosha katika chumba kile. Ramsey akahema kwa kasi, kisha akatizama “lips” za Mariam, hakika zilipendeza sana.

Lakini alikuwa na maswali yaliyomchanganya kichwani mwake, anaweza kuonekana mwenye tabasamu wakati alikuwa kwenye kipindi kigumu cha matatizo? Hilo lilizunguka ubongoni mwake bila kuwa na majibu ya moja kwa moja.

Kila kitu kilikuwa gizani. Maswali yote hayakuwa na majibu. Mariam ambaye muda wote alionekana kuwa kimya, sasa alifungua kinywa chake akionekana kuwa na jambo la msingi sana la kuzungumza naye. Akayatoa macho yake kwa kasi, kama alikuwa haoni vizuri, akameza fundo moja la mate ambayo bila shaka aliyakusanya kwa muda mrefu sana mdomoni mwake.

Akawa mtulivu sana, akaanza kuzungumza: “Nimekuuliza swali Ramsey!”

“Swali?”

“Ndiyo!”

“Mh!”

“Mbona unaguna?”

“Naguna sababu ya maneno yako Mariam!”

“Yanachekesha au hayana maana?”

“Siyo kwamba yanachekesha na wala siyo kwamba hayana maana.”

“Bali?”

“Nina wasiwasi na wewe.”

“Juu ya nini?”

“Ya ulipotoka, sijui kama umetoka sehemu salama.”

“Nini maana yako?”

“Siyo kawaida yako kuwa hivi Mariam, nahisi kuna tabia nyingine ambazo unazifanya ambazo mimi nilikuwa sizijui.”

“Kwanini unasema hivyo Ramsey?”

“Naweza kukuuliza kitu?”

“Uliza tu!”

“Unakunywa pombe?”

“Hapana.”

“Kweli?”

“Nakuhakikishia, kwani naonekana nimekunywa?”

“Hapana ila yanayotoka kinywani mwako ndiyo yanayosababisha nihisi hivyo.”

“Anyway...nisikilize Ramsey, tufanye hivi, mimi ni mnywaji wa pombe na leo nimekunywa. Halafu baada ya hapo jibu maswali yangu hata kama ni ya mlevi sawa?”

“Usiseme hivyo...”

“Sasa niseme nini? Inawezekana umesahau swali, nitakukumbusha...wewe ni kijana mzuri sana, ambaye roho yako inafanana na tabia yako! Nashukuru kwa hilo, lakini naamini una kazi nyingi za kufanya umeziacha na kuamua kunisaidia mimi katika kipindi hiki kigumu, je kwanini umeamua kufanya hivyo?” Mariam aliongea maneno hayo huku machozi yakimlengalenga machoni mwake.

“Mariam acha kulia, naomba ufahamu kitu kimoja, nimefanya yote hayo kwa sababu ya mapenzi tu, sina kitu kingine chochote ambacho kimenifanya nikaamua kukusaidia!”

“Unanipenda?”

“Ndiyo...kama dada yangu, rafiki yangu wa karibu lakini kubwa zaidi natimiza moja ya amri muhimu tulizopewa na Mungu, tuliagizwa tupendane Mariam, kwanini nisikusaidie kwa upendo huo?”

“Kweli?”

“Niamini!”

“Hakuna lingine?”

“Lipi tena?”

“Basi nashukuru sana kama ni kweli hakuna lingine zaidi ya hilo, umenifurahisha sana Ramsey.”

“Usijali.”

Wakaendelea kuzungumzia mambo mengine, hadi baadaye Ramsey alipoaga na kurudi chumbani mwake. Hata hivyo Ramsey aligundua kwamba lazima Mariam alikuwa na kitu kilichomchanganya hasa kutokana na maswali aliyokuwa akiuliza.

Jioni walikutana kwa ajili ya chakula cha jioni, baada ya kula Ramsey alishindwa kuvumilia kubaki na maswali mengi kichwani mwake, akaamua kumuuliza Mariam ili kupata ukweli. Mariam hakuona sababu ya kuficha jambo, akamweleza ukweli jinsi alivyokwaruzana na wazazi wake hadi kufikia hatua ya kuondoka wodini bila kuwepo kwa maelewano.

“Lakini wale ni wazazi wako Mariam, lazima uwasikilize!”

“Hujakosea Ramsey, lakini na wao hawawezi kunichangulia mtu nitakayeishi naye.”

“Ungewapa nafasi kwanza, hata kama unampenda huyo Tom kiasi gani lakini waliyokuambia yana maana, unampenda vipi mtu ambaye alikufukuza na kuwatukana wazazi wako?”

“Najua siyo yeye, ni yule shetani Mayasa niliyekupa habari zake.”

“Hata kama, lakini wazazi wako walikuwa na hoja ya msingi.”

“Sasa naona unataka kuniudhi,” Mariam akasema akionyesha hasira.

“Basi Mariam yaishe,” Ramsey akaamua kuwa mpole.

*******
 
SEHEMU YA 40 YA 50

Mariam akaendelea kumhudumia Tom kwa karibu sana, kila siku alikuwa akishinda Muhimbili na kurudi hotelini usiku. Hakutaka mpenzi wake apate shida, alikiri wazi kwamba hatatokea mwanaume ambaye atampenda kama alivyompenda Tom.

Tom alikuwa kila kitu kwake, alimkabidhi maisha yake yote, hakujali mateso na manyanyaso yote aliyompa. Imani kubwa aliyokuwa nayo moyoni mwake ni siku moja Tom angeamka na kuwa naye kama mke na mume maana Mayasa ambaye kwake alikuwa ni shetani alikuwa ameshatoroka.

Hakutaka kusikia kuhusu wazazi wake, aliamua kuishi maisha yake peke yake, huku mtu muhimu aliyekuwa mbele yake akiwa ni Tom pekee.

Siku moja Ramsey alimtoa Mariam na kwenda naye ufukweni, hiyo ni baada ya kumweleza alikuwa na mazungumzo ya muhimu sana ambayo yalihitaji sehemu iliyotulia ili aweze kumweleza vizuri jambo ambalo Mariam hakulipinga.

Wakiwa katika hoteli moja, ufukweni mwa Bahari ya Hindi, Mariam ndiye aliyeanzisha mazungumzo baada ya kuona Ramsey hazungumzi chochote.

“Enheee Ramsey, ulisema una mazungumzo muhimu na mimi, muda unazidi kwenda, naona ni bora ukaniambia.”

“Ni kweli, tena ni muhimu sana.”

“Nakusikiliza, bila shaka huu ndiyo muda muafaka.”

“Mariam nataka kukuambia jambo moja muhimu sana, muhimu kwako na kwangu, muhimu kwa maisha yako,” Ramsey alisema kwa sauti ya utulivu sana.

“Nakusikiliza Ramsey.”

“Nafikiri unakumbuka kuwa mimi ndiye niliyekuokota Morogoro na kukupeleka hospitalini kwa ajili ya matibabu!”

“Ndiyo nafahamu.”

“Pia mimi ndiye niliyekuleta Dar ba kukupeleka hadi hospitalini!”

“Ni kweli.”

“Kwamba mpaka sasa hivi mimi ndiye ninayegharamia mahitaji yote ya Tom na wewe.”

“Ndiyo!”

“Nimekufanyia mambo mengi sana ili kukufanya mwenye furaha!”

“Hilo halipingiki.”

“Unajua ni kwanini nimekufanyia yote haya?”

“Hilo litakuwa moyoni mwako.”

“Kipo kitu kilichonisukuma mimi kufanya yote hayo Mariam, kipo! Tangu nilipokuona siku ya kwanza, niliona kitu kwako Mariam, nakumbuka uliwahi kuniuliza sababu ya kukufanyia wema wote huu lakini nilikujibu jibu la uongo kwa sababu muda wa kukuambia haya ninayokuambia ulikuwa haujafika.

“Nisikilize kwa makini Mariam, wewe ni msichana mrembo sana, ambaye unahitaji matunzo, unatakiwa ukae mahali utulie ukila na kunywa kila unachokitaka. Hupaswi kuwa na huzuni wala mateso kama uliyonayo hivi sasa, hutakiwi kuwa na msiba mzito moyoni mwako kama ulionao sasa hivi. Urembo wako haufanani na matatizo uliyonayo. Mariam unatakiwa kubembelezwa!” Ramsey alipofika hapo alitulia kwa muda kisha akapeleka glasi yake ya maji ya matunda kinywani kabla ya kuanza tena kuzungumza.

“Mariam mimi nakupenda, tena nakupenda kwa mapenzi ya dhati kutoka moyoni mwangu, nipe nafasi nikuonyeshe raha za ulimwengu. Achana na yule mlemavu kule Muhimbili, kwanza inawezekana baada ya kupata fahamu akakufukuza, kwanini uumize moyo wako? Nipe nafasi nikuonyeshe ninavyokupenda Mariam,” Ramsey alizungumza kwa sauti ya upole sana, akiamini Mariam angemsikiliza.

“Umemaliza?” Mariam akamwuliza akivuta midomo.”

“Tayari...”

“Sikiliza....tena sikiliza kwa makini sana, hivyo vijimsaada vyako visiwe sababu ya kunitongoza. Mwili wangu una thamani sana, tena ni maalum kwa ajili ya mtu mmoja tu, Tom! Huyo ambaye kwako wewe umeona ni mlemavu lakini kwangu ni mwanaume, tena mume wa ndoa. Kama umechoka kunisaidia, acha! Sikulazimishi, lakini mwili wangu, sahau!” Mariam akasema kwa kujiamini sana.

Ramsey akavimba kwa hasira, hakuzungumza neno lolote zaidi ya kusimama na kuanza kupiga hatua moja baada ya nyingine akimwacha Mariam mwenyewe ufukweni.

Mariam akafikiria kwa haraka, akaona giza nene lililokuwa mbele yake, kumuacha Ramsey aondoke kulimaanisha yeye kutokuwa na mahali pa kulala kuanzia siku hiyo, pia asingeweza kumuhudumia Tom wake, achilia chakula chake yeye mwenyewe.

Mariam akaanza kulia. Ramsey aliendelea kutembea bila kugeuka nyuma, akiwa amedhamiria kabisa kuondoka na kumwacha Mariam pale ufukweni. Mariam akasimama na kuanza kumkimbilia Ramsey huku akiita jina lake kwa sauti kubwa.

“Ramseeeeeeeyyyy.....” Mariam aliita kwa sauti kubwa sana.

Ramsey akageuka nyuma, akasimama akiwa tayari kumsikiliza Mariam, hakuhitaji kitu kingine chochote zaidi ya penzi lake, vinginevyo aliamua kucha kusaidia tena Mariam.





Ni kama alikuwa amewahi kukimbia mbio za marathon, lakini haikuwa hivyo. Mariam hakuwahi kufanya mazoezi ya riadha hata mara moja, lakini siku hiyo alikimbia kwa mwendo wa ajabu. Hata yeye alijishangaa.

Alimfikia Ramsey akiwa anahema kwa kasi ya ajabu, akasimama mbele yake huku akiwa ameyatoa macho yake kama alikuwa akikimbizwa na mnyama hatari. Ghafla macho yake yakaanza kupatwa na unyevunyevu, baadaye kidogo machozi yakaanza kumiminika machoni mwake.

“Nyamaza Mariam, nyamaza...kulia kwako hakutasaidia kitu kama...”

“Kama sitakuambia nakupenda pia...”

“Ndiyo Mariam, kwanini unataka kuutesa moyo wangu kiasi hiki? Ni nani ambaye angeweza kufanya yote haya kwa ajili yako? Ni mimi ninayekupenda pekee ndiye niwezaye kufanya mambo haya.

“Lakini sasa, unadhani unafanya vyema kufanyiwa yote haya kwa mapenzi halafu wewe ulipe mabaya? Angalia mara mbili Mariam,” Ramsey alikuwa akizungumza kwa sauti laini, taratibu na macho yake yakiwa yameganda usoni mwa Mariam aliyekuwa akilia wakati wote.

Mariam hakuzungumza kitu, alitulia kwa muda kabla ya kwenda kujilaza kifuani mwa Ramsey. Ramsey alisikia raha sana kusikia pumzi za Mariam zikitoka kwa shida akiwa amelala juu ya kifua chake.

“Najua unanipenda sana Ramsey, najua...nafahamu kwamba ulifanya yote yale kwa sababu ya mapenzi yako kwangu...lakini pia unatakiwa kufahamu kwamba sikuwa nafahamu haya mambo mpaka leo uliponiambia, sikujua kama ulikuwa na jambo hilo moyoni mwako.

“Nashukuru sana kwa kunipenda na kunipa nafasi ya kwanza moyoni mwako, lakini unatakiwa kufahamu kwamba moyo wangu una makovu, kama ni sumu nilipewa kali, yenye kuua na kukausha kabisa! Hali yangu siyo nzuri kihisia....

“Najisikia kumpenda mtu mmoja tu, Tom! Lakini wema unaonipa nashindwa kujua nitakulipa vipi? Najua ni kiasi gani unavyoumia juu ya penzi lako kwangu, lakini nitafanyaje?” Mariam aliongea kwa sauti iliyojaa kwikwi huku machozi yakimiminika mgongoni mwa Ramsey aliyekuwa kimya akimsikiliza kwa makini sana.

“Kipo kitu cha kufanya Mariam, kipo...”

“Nini?”

“Kunipenda!”

“Ingeweza kuwa rahisi kukupenda, lakini siyo kukupenda wewe tu, Ramsey hata mwanaume mwingine yeyote. Ni kweli wewe ni kijana mzuri sana unayevutia kwa kila kitu, lakini moyo wangu una sumu, hauwezi tena kumpenda mtu mwingine zaidi ya Tom.

“Tafadhali usiumizwe na kauli zangu, ni hisia za kweli zinazotoka moyoni mwangu, naomba uzipokee kama zilivyo, nakupenda kama kaka yangu lakini siyo kimapenzi.”

“Kama hunipendi Mariam?”

“Nakupenda sana, tena sana lakini siyo kimapenzi, labda kama utanisaidia katika hilo!”

“Kukusaidia nini?”

“Kukupenda!”

“Unamaanisha nini?”

“Nisaidie niweze kupenda tena, moyo wangu sijui una matatizo gani?”

“Una uhakika na kauli yako?”

“Ndiyo!”

“Kweli?”

“Ndiyo...mbona unaniuliza mara mbilimbili, kwani huniamini?”

“Nakuamini sana...”

“Sema nakupenda sana Ramsey!”

“Nakupenda sana Ramsey!”
“Hebu niangalie!” Ramsey akamwambia Mariam ambaye alijitoa kifuani mwake na kusimama mbele yake huku akiwa ameyatuliza macho yake kwa Ramsey.

Ramsey akatabasamu, Mariam naye akatabasamu pia.

“Unahisi nini?”

“Kukupenda!”

“Kwahiyo mimi sasa ni mpenzi wako siyo?”

“Ndiyo, lakini nitaomba msaada mwingine kutoka kwako!”

“Unahitaji kiasi gani cha pesa?”

“Siyo pesa Ramsey, sizungumzii pesa!”

“Bali nini?”

“Tom!”

“Tom? Ameingia vipi tena kwenye mazungumzo yetu?”

“Naomba uniruhusu niendelee kumsaidia mpaka atakapopona!”

“Akifa je?”

“Hiyo itakuwa mipango ya Mungu!”

“Ok, hakuna tatizo katika hilo.”

Wakasogeleana tena, wakakumbatiana kwa nguvu, wakaanza kupeana mvua ya mabusu motomoto. Wakafungua ukurasa wa mapenzi. Hapo sasa wakarudi tena ufukweni ambapo walicheza michezo ya kimahaba mpaka usiku waliporudi zao hotelini.

*******

Moyo wa Mariam ulikuwa na maumivu makali sana, alikubali machoni tu kuwa na Ramsey lakini moyoni hakuwa na hata chembe ya mapenzi kwake. Moyoni mwake kulikuwa na mtu mmoja, Tom. Hakuwahi na wala hakufikiria kuwa na mtu mwingine zaidi ya Tom.
 
SEHEMU YA 8 YA 50

ndani ya gari kwenda hospitali ya Ocean Road, Tom akiwa ameacha maagizo kwa wauguzi kwamba ikitokea Mariam akaonekana na kuulizia basi aelekezwe mahali walikokuwa, wauguzi wakaahidi kumsaidia kufanya hivyo. Safari ya hospitali ya Ocean Road ikaanza, siku zote Tom alipita nje ya hospitali hiyo akielekea feri lakini hakuwahi kuwaza kwamba siku moja angeingia humo akiuguliwa na baba yake, hakuamini kama Saratani ingeweza kuingia ndani ya familia yake, aliuona ugonjwa wa watu wengine.

Matibabu yalianza siku hiyo hiyo kwa njia ya vidonge, mionzi na dawa za sindano ambazo badala ya kuonekana kumsaidia mzee Chacha zilimdhoofisha zaidi, afya yake ikaharibika kabisa na kupoteza uzito mwingi ndani ya muda mfupi! Nywele zote zikanyonyoka kichwani sababu ya ukali wa dawa alizokuwa akipewa.

Kila mara Tom alipomwangalia baba yake alishindwa kuvumilia na kutoka nje ambako alibubujikwa na machozi akitamani angalau Mariam angeonekana na kumpa maneno ya faraja lakini haikuwa hivyo, hatimaye wiki mbili zikakatika hali ya mzee Chacha ikizidi kuwa mbaya, madaktari wakashauri mgonjwa arudishwe nyumbani hasa baada ya kugundua alikuwa ni mtu wa Tarime na mke wake hakuwa tayari azikwe jijini Dar es Salaam kama kingetokea kifo jambo ambalo kila mtu alikuwa akilitarajia.

“Sawa tu daktari nimekubali, tatizo letu kubwa ni nauli, hatuna fedha kabisa!”

“Mimi na wafanyakazi wenzangu tutawachangia fedha kidogo lakini pia ninyi mnaweza mkajitahidi kutafuta kwa ndugu jamaa na marafiki!”

“Tutajitahidi!”

Alichokifanya mama yake Tom ni kuuza vyombo vyote vya ndani, akaenda Pepsi kazini kwa mume wake na kuomba msaada, Mkurugenzi wa kiwanda hicho akampa shilingi laki moja na nusu na kuja nazo hadi hospitali ya Ocean Road ambako wafanyakazi walimkabidhi shilingi laki moja, jumla akawa na shilingi laki sita pamoja na zilizopatikana kwa kuuza vyombo, mipango ya safari ikaanza kuandaliwa.

Siku mbili tu baadaye bila Tom kuonana na Mariam, moyo wake ukiwa umejaa hasira, walipanda daraja la tatu la treni kuelekea Mwanza ambako wangeunganisha kwa basi hadi Tarime, kwa jinsi hali ya mzee Chacha ilivyokuwa mbaya ilibidi abiria wote waliokuwa naye kwenye kiti, wanyanyuke kumpisha alale, hakuna aliyekuwa na uhakika angefika mzee huyo angefika Mwanza siku tatu baadaye akipumua.

Ulikuwa ni mlio mkubwa mno kwa mtu yeyote aliyekuwa jirani na eneo hilo kutosikia, watu wengi waliokuwa jirani walianza kukimbia kwenda mahali magari yalipogongana, baadhi wakiwa na nia ya kuokoa lakini wengine wakifikiria kuiba mali yoyote ambayo wangeikuta. Magari yaliyokuwa yakipita kwenye Barabara ya Nyerere kwenda au kutoka Uwanja wa Ndege yalishindwa kuendelea na safari sababu barabara ilikuwa imezibwa na magari mawili yaliyogongana uso kwa uso katikati ya barabara, hii iliwafanya abiria wote waliokuwa kwenye magari washuke kwenda kutoa msaada.

Kwenye daladala kulikuwa na abiria wengi walioumia, dereva wake akiwa amelaza kichwa kwenye usukani, damu zikimtoka puani na mdomoni, tayari alishakufa! Taratibu wakamwondoa na kumlaza chini. Sababu tairi za mbele za daladala zilikuwa zimesimama juu ya gari dogo lililogongwa, ilibidi watu wajitolee kulisukuma kurudi nyuma ili kutoa nafasi ya kuangalia kama kulikuwa na watu wengine ndani ya gari dogo. Hayo yalifanyika wakati abiria waliojeruhiwa wakipakiwa ndani ya magari mengine tayari kwa kupelekwa hospitali ikiwa ni pamoja na dereva wa daladala aliyekufa.

“Mungu wangu kuna mtoto mdogo, tena kwenye usukani, sijui ndiye aliyekuwa akiendesha? Mbona mdogo sana?” Mtu mmoja aliuliza baada ya daladala kuondolewa juu ya gari dogo.

“Ni mdogo mno huyu, hawezi kuwa dereva kama ni hivyo basi itakuwa aliiba gari, hawa watoto wa matajiri ndio wanasababisha sana ajali barabarani, si ajabu alikuwa ametoka zake disko akiwa amelewa!” Mwingine aliitikia.

Mariam alikuwa amelala ndani ya gari lililogongwa, akiwa kimya kabisa huku damu nyingi zikimtoka hasa kwenye paji la uso palipoonekana kuvimba, damu nyingine ilikuwa ikimtoka puani na masikioni. Kwa jinsi alivyokuwa amebanwa ilikuwa kazi ngumu kidogo kumtoa, hata hivyo baada ya muda si mrefu walifanikiwa na kumlaza chini kisha kuanza kumgusa kifuani kuona kama alikuwa na uzima.

“Anahema!” Aliongea mwanaume aliyekuwa akimgusa kifuani.

“Basi hajafa, tumkimbizeni hospitali!”

“Ni jambo jema, mleteni huku kwenye gari yangu nimpeleke mara moja Muhimbili!” Mwananchi mmoja alijitolea, Mariam akabebwa juu juu na kwenda kupakiwa kwenye gari dogo aina ya Mark II, safari kwenda hospitali ikaanza ambako walikuta pia majeruhi wengine wamekwishawasili.

Mapokezi hawakuona sababu ya kuuliza maswali mengi kwa jinsi hali ya mgonjwa ilivyokuwa mbaya, haraka akakimbizwa mpaka kwenye chumba cha daktari ambaye baada ya kumwona aliamuru akimbizwe haraka sana Chumba cha Upasuaji, kisha yeye kuwasiliana na madaktari wengine ambao walikutana kwenye chumba hicho na Mariam kuwekewa Mashine ya Hewa ya Oksijeni kisha kupandishwa kitandani ambako kazi ya kwanza iliyofanyika ni kuziba mishipa yote iliyokuwa ikivuja damu kuzuia upotevu mkubwa.

“Haraka sana mfanyieni CT-Scan!” Dk. Majaliwa, Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Uti wa Mgongo, alisema.

“Sawa daktari, acha tuwapigie simu hawa watu waje kuifanya kazi hiyo mara moja!”

“Fanyeni hivyo haraka kwani kwa dalili ninazoziona nahisi kuna tatizo kwenye ubongo wake!”

“Sawa daktari!”

Dakika ishirini baadaye Bingwa wa Kipimo cha CT-Scan alifika kwenye Chumba cha Upasuaji cha Hospitali ya Muhimbili na vifaa vyake na kumfunga Mariam kichwani, kisha yeye na madaktari wote wakaanza kuangalia, haikuhitaji muda mrefu sana kugundua kilichokuwa kikiendelea chini ya fuvu la Mariam; damu nyingi ilikuwa imevuja chini ya fuvu, kichwa chacke kilijipiga kwenye chuma sehemu ya paji la uso na ubongo kuumia kwa ndani.

“She has a subdural haemorrhrage!” (Anavuja damu chini ya fuvu!) Dk. Majaliwa aliongea baada ya kuitazama picha kwenye kompyuta.

“So?” (Kwahiyo?)

“She needs an urgent operation!” (Anahitaji upasuaji wa haraka)

“Are we ready?” (Tuko tayari?)

“Yes!” (Ndiyo)

“Can the people from laboratory do urgent blood grouping and cross matching check? As well as HB level?” (Watu wa maabara wanaweza kupima kundi lake la damu na anaweza kuongezewa na kundi gani? Pia kiasi cha damu alichobakiza?) Dk. Majaliwa alisema na wote wakakubaliana, watu wa maabara wakaitwa haraka na kuifanya kazi hiyo.

Hapakuwa na mtu wa kujiuliza mtu waliyekuwa wakimshughulikia aliitwa nani, mtoto wa nani na alitokea wapi. Kwao alikuwa ni mgonjwa na kazi yao kubwa ilikuwa ni kuokoa maisha yake, hilo ndilo madaktari walilotaka kulifanya. Damu ilipopatikana, vipimo vya moyo wake vikawa viko sawa, Mariam aliingizwa kwenye
Poor Mariam, huku Tom amekuchukia, kumbe unapigania uhai wako
 
SEHEMU YA 41 YA 50

Alikubali ili aweze kuendelea kupata misaada yake kwani asingeweza kumhudumia Tom akiwa hana fedha. Kumkubalia ulikuwa mtihani wa kwanza, lakini mtihani wa pili ambao ungekuwa mgumu zaidi kwake ni kufanya mapenzi na Ramsey.

Alijiapiza kukabiliana na hilo mpaka mwisho wa pumzi zake. Ni kweli hakuwa na mapenzi naye, lakini asingeshindwa kujifanya kuonyesha mapenzi yake kwa kila njia, lakini tatizo kubwa kwake likawa ni mapenzi, hakutaka kabisa kuruhusu mwili wake uguswe na mwanaume mwingine zaidi ya Tom wake.

Jioni walikuwa wanakula pamoja hotelini, Mariam akimlisha na kumbusu kila wakati, alionyesha kila dalili za wao kuwa wapenzi, ingawa Mariam alikuwa makini sana na kamera za waandishi wa habari hasa za waandishi wa magazeti ya udaku.

“Angalia bwana, haya maeneo siyo kabisa. Kuna mwandishi mmoja anaitwa Issa Mnally akituona tu, lazima atatupiga picha na utashangaa tumetoka kwenye gazeti la Risasi!”

“Issa Mnally?”

“Ndiyo...huyu ni mdaku balaa, hakuna asiyemjua hapa Bongo. Habari nyingi za Tom amekuwa akiziripoti yeye na kama siyo yeye basi ni Senchawa, hawa wadaku hawafai kabisa!”

“Usijali mpenzi wangu, tupo kwenye chimbo hapa hawawezi kutuona.”

“Lakini ni vyema tukichukua tahadhari.”

“Hakuna shida.”

Wakaendelea kula na kunywa kwa furaha hadi usiku kabisa, walipoamua kuondoka na kwenda vyumbani mwao kulala. Mariam aliingia chumbani kwake na Ramsey naye akaenda chumbani mwake. Muda mfupi baada ya Mariam kuingia chumbani kwake, simu ya mezani ikaita. Haraka akapokea akijua ni lazima angekuwa ni Ramsey.

“Vipi mpenzi wangu, si tumeachana muda huu tu,” Mariam alisema maneno hayo mara baada ya kupokea simu.

“Siyo shwari darling!”

“Kwanini?”

“Kuna baridi sana, siwezi kulala mwenyewe, nahitaji sana joto lako!”

“Lakini mbona bado mapema sana?”

“Mapema kupata joto lako? Mbona sikuelewi Mariam, naomba uje chumbani kwangu!”

“Sawa,” Mariam akajibu na kuamka haraka kisha akavaa na kwenda chumbani kwa Ramsey.

Hakutaka kumuudhi tena, lakini kikubwa ambacho kilikuwa akilini mwake ni kutomuachia kabisa mwili wake. Hilo alijihakikishia kabisa kwamba lilikuwa ndani ya uwezo wake. Akatoka nje, kisha akafunga mlango wake na kwenda chumbani kwa Ramsey.

“Karibu mpenzi wangu!”

“Ahsante sana!” Mariam akaingia na kwenda moja kwa moja kitandani.

Wakalala wakiwa wamekumbatiana. Katikati ya usiku, Mariam akiwa amelala fofofo, alisikia mikono laini ya Ramsey ikipita mwilini mwake. Mwanzoni alihisi alikuwa usingizini, lakini muda ulivyozidi kwenda ndivyo alivyogundua kwamba kila kilichokuwa kinatokea kilikuwa yakini!

Akashtuka zaidi alipogundua, Ramsey alikuwa ameshamvua nguo zake zote na alikuwa mtupu kabisa.

“Ramsey unataka kufanya nini?” Mariam akasema kwa ukali sana.

“Mbona hivyo mpenzi wangu? Kwani wewe ni nani wangu enheee? Sisi si ni wapenzi, sasa kuna ubaya gani kufanya mapenzi?”

“Ubaya upo!”

“Kivipi?”

“Hatujajuana vizuri Ramsey, lazima tupime kwanza kabla ya kuanza haya mambo!”

“Ninazo kondom!”

“Sipo tayari....kwanza huwa situmii kondom!”

“Mbona unakuwa hivyo?”

“Nooooo...haiwezekani Ramsey, naomba uelewe!” Mariam akajitoa kitandani kisha akavaa nguo zake haraka na kutoka nje, akarudi chumbani mwake.

*******

Hadi inafika saa moja kamili asubuhi, Mariam alikuwa hajafumba macho yake kulala. Alitumia usiku mzima kuwaza maisha yake. Hakuwa tayari kumsaliti Tom wake, lakini pia hakuwa tayari kupoteza misaada ya Ramsey.

“Nitafanya nini mimi jamani? Mbona dunia inanigeuka kiasi hiki?” Mariam akawaza akilia.

Usiku mzima alikuwa hapokei simu ya Ramsey, baadaye akaamua kuweka mkonge wa simu pembeni ili kukwepa usumbufu. Alipoanza kupiga simu yake ya mkononi akaamua kuizima kabisa. Akili yake ikawa ni juu ya mpenzi wake wa moyo wa Tom.

Akiwa anaendelea kuwaza, ghafla akasikia mlango ukigongwa, akaenda kufungua. Akakutana na Ramsey akiwa amebeba begi lake. Akamwangalia Mariam akionekana kuwa na chuki za wazi. Akaingiza mkono mfukoni kisha akatoa burungutu la pesa na kumrushia kitandani, baada ya hapo akaingiza tena mkono katika mfuko wa shati kisha akatoa karatasi iliyokuwa na maandishi na kumpatia.

“Maisha mema!” Ramsey akasema kisha akafunga mlango kwa nguvu na kuondoka.

Haraka Mariam akafungua lile karatasi kisha akaanza kusoma kwa makini. Ilikuwa imeandika hivi; Nilikupenda kwa mapenzi ya dhati, nikakupa kila kitu lakini hukuthamini penzi langu. Nilikuwa tayari kukupa kila aina ya msaada uliotaka, lakini ukanilipa machungu.

Kuondoka chumbani kwangu usiku, kumenipa taswira kwamba hunipendi, unanionea kinyaa na ni mwaume ambaye sina uwezo wa kuwa na wewe. Ahsante sana kwa hilo, naomba na mimi niishie hapa.

Nimekuachia hizo lakini tano, nikusaidie katika mwanzo mpya wa maisha yako, maana najua ni kiasi gani utakuwa katika hali ngumu. Maisha ya hapo hotelini hutayaweza, hivyo nakushauri rudi nyumbani, ukawaangukie wazazi wako, uwaombe radhi.

Hata hivyo, bado nakupenda, siku ukiona utaweza kuwa na mimi, basi nipigie simu kwa namba zangu nilizokuachia. Sina kingine zaidi ya kuendelea kukuambia nakupenda na sitaacha kukupenda. Huyo Tom ni msumari wako wa milele, lakini mwenye uamuzi wa kuutoa huo msumari ni wewe mwenyewe.

Akupendaye kwa dhati,

Ramsey.
 
SEHEMU YA 42 YA 50

Mariam alirudia kusoma yale maneno zaidi ya mara kumi na hakuna sehemu hata moja iliyobadilika! Yalikuwa maneno makali sana ambayo yaliuchoma moyo wake. Hakuwa na kitu kingine cha kufanya zaidi ya kulia. Mariam akaanza kulia.

“Lakini nimekumbuka, ipo njia ya kuepukana na haya matatizo yote, ipo...hapa natakiwa kufa tu, hakuna kingine. Nife, niende zangu kwa Mungu, yeye mwenyewe anajua kwanini nimeamua kwenda kwake mapema kabla yeye hajaniita. Nataka kufa, tena leo hii hii!” Mariam akasema maneno hayo kwa sauti ya chini huku akitokwa na machozi.





CHUMBA kilikuwa kichungu kwake, asingeweza kuendelea kuishi pale bila msaada wowote. Bado akilini mwake hakuweza kujua nini cha kufanya tofauti na uamuzi wa kufa ambao aliuona kuwa ni bora zaidi.

“Nitakuwa nimepotea kabisa, sitaonana na mtu yeyote tena, nitakuwa nimepumzika kwa Mungu, mateso na shida zote yatakuwa yameisha. Kwanini niendelee kuishi kwa shida kiasi hiki? Wazazi wangu hawanitaki, Ramsey amenikimbia, Tom naye ni mgonjwa, pamoja na kwamba nampenda lakini bado anaweza akapona na akaendelea kuwa na msimamo wake ule ule, sasa kwanini nijitese? Kwanini niendelee kuteseka?

“Ni bora kufa, ni bora niondoke, hiyo ndiyo inaweza kuwa salama yangu, sina kitu kingine cha kufanya zaidi ya hivyo, acha nikapumzike,” Mariam akawaza akilini mwake huku machozi mithili ya maji yakimiminika machoni mwake.

Alitulia kwa muda mrefu pale kitandani, akiendelea kulia, muda ukizidi kwenda. Alitumia muda mwingi akiwaza maisha yake, hapo ndipo alipokumbuka kwamba hakuwahi kufurahi kabisa katika maisha yake ya kimapenzi.

Mchana mzima alikuwa akilia, hakukumbuka kula siku hiyo, usiku akaamua kwenda kununua sumu ya panya ili ajitoe uhai. Alidhamiria kufa, baada ya kununua sumu yake ya panya, alirudi hotelini na kutulia kwa muda akijaribu kufikiria maisha yake baada ya kifo chake.

“Hakuna kitakachoharibika, sina thamani ya maisha hapa duniani, naamini kwa Mungu kuna afadhali, najua nitakuwa na dhambi ya kujiua lakini Mungu mwenyewe naamini atanisamehe kutokana na haya mateso niliyonayo. Sijapenda kufa, ila nalazimika kukimbia matatizo ya hapa duniani, siwezi kukabiliana nayo, yamenishinda,” Mariam alijisemea moyoni.

Mariam alibadilika sana, hakuona thamani yake tena duniani, aliamini kwa kufa pekee ndiyo angeweza kupumzika na kuepukana na matatizo anayoyapata. Alichokifanya ni kuchukua mkonge wa simu, kisha akabonyeza namba za hotelini.

“Hotelini!”

“Ndiyo habari yako?”

“Salama.”

“Naomba kukusikiliza!”

“Nahitaji soda ya badiri sana!”

“Soda gani?”

“Yoyote isiyo na gesi sana!”

“Soda gani sasa?”

“Yoyote.”

“Upo chumba namba ngapi?”

“206.”

“Ghorofa ya ngapi?”

“Tatu.”

“Ok! Baada ya muda mfupi utaletewa.”

Mariam akachukua kalamu na karatasi akaanza kuandika ujumbe ambao ungewasaidia wahudumu kufahamu alikuwa ni nani na ndugu zake ni akina nani. Ulikuwa ujumbe unaosikitisha sana, muda wote aliokuwa akiandika alikuwa akilia machozi.

Ujumbe huo, ulisomeka hivi; ‘Nimeamua kufa ili kukwepa fedheha ninayoipata hapa duniani, naamini kifo pekee ndicho kitakachoweza kunitenganisha na kero na matatizo yote ninayoyapata hapa duniani. Nimeteseka vya kutosha, ninayempenda hanipendi, wazazi wangu wamenifukuza nyumbani, sina msaada wowote.

Sioni thamani wala faida yangu duniani, ni heri nife tu, ni wengi wananifahamu, mimi ni mke halali wa Tom ambaye wengi wamekuwa wakimfahamu kwa jina la Papaa Bill. Naamini kwa utambulisho huu utawarahisishia kuwapa taarifa wazazi wangu ambao watakuja kuuchukua mwili wangu na kuuzika.

Naamini kifo ni safari ya kwenda mbinguni, hivyo basi ni imani yangu kwamba siku moja tutakutana katika enzi yake Mungu wa mbinguni. Kwaherini ya kuonana.

Mariam.’

Alipomaliza kuandika ujumbe huo, alirudia kuusoma mara mbili mbili huku akilia. Akiwa anarudia kwa mara ya tatu, mlango wa chumba chake ukagongwa, alijua lazima alikuwa mhudumu. Haraka akafuta machozi yake kisha akaficha karatasi yake, akasogea mlangoni, akafungua mlango.

“Vipi sister?”

“Salama.”

“Mbona kama ulikuwa unalia? Kuna tatizo?” mhudumu akamwuliza.

“Hapana macho yananisumbua kaka yangu!” Mariam akadanganya.

“Pole sana!”

“Ahsante!” Wakati Mariam anajibu hivyo, alijikuta machozi yakimwagika usoni mwake kama maji yanayotiririka kutoka mferejini.

“Mh! Dada inaonekana una tatizo, lakini unajaribu kunificha, kwanini usiseme ukweli, naweza kukusaidia mawazo,” yule mhudumu akamsisitizia.

“Kaka nimeshakuambia macho yananisumbua lakini kwanini unazidi kuning’ang’aniza niwe na matatizo? Kwanza siyo kazi yako kujua matatizo yangu, tafadhali fungua soda uondoke!” Mariam aliongea kwa ukali sana, alionyesha kudhamiria alichokuwa akizungumza.

Yule mhudumu hakuwa na maneno mengi, akafungua soda kisha akaondoka zake. Mariam akaimimina soda kwenye glasi kisha akachanganya na ile sumu aliyoinunua, baada ya hapo akaanza kuikoroga kwa pamoja. Akasimama mwili ukimsisimka, kisha akaiangalia ile glasi, baada ya hapo akaielekeza mdomoni mwake.

“Eeeh baba naomba upokee roho yangu,” Mariam akasema maneno hayo glasi ikikaribia kufika kinywani.

Aliamua kufa!

******

Nyumba ilipoteza amani, furaha yao haikuwepo tena, walishamtafuta Mariam hadi wamechoka na hawakufanikiwa kumpata. Mama yake Mariam alikuwa akilia muda wote.

Kila walipoenda Muhimbili kumtafuta Mariam, waliambiwa kuwa huwa anakwenda mara moja moja, jibu ambalo lilizidi kuwachanganya. Walishaamua kumchukua mtoto wao ili wafanye mazungumzo na kumuweka sawa, lakini waliumia sana walipomtafuta bila mafanikio.
 
Back
Top Bottom