nasrimgambo
JF-Expert Member
- Jan 10, 2017
- 1,902
- 2,488
KARIBUNI KUSOMA SIMULIZI HII
SEHEMU YA KWANZA
Ilikuwa ni siku ya joto na jua kali, huku kama kawaida watu walikuwa wengi,
wakiwa kwenye pilika pilika, wengine wakiwahi usafiri na wengine wakishuka
kwenye mabasi na daladala wakiwa wamewasili.
Wafanyabiashara wadogowadogo
walikuwa bize na wateja wao, wengine walikuwa wakitumia vipaza sauti kunadi
biashara zao.
Watu kadhaa walioonekana wana hali duni na wamechoka, baadhi yao wakiwa
wazee, watoto na wenye ulemavu walionekana wameshika bakuli wakiombaomba
kwa wapita njia, huku wapita njia wachache wakitoa sarafu toka mifukoni mwao na
kuweka kwenye bakuli hizo.
Hali ndivyo ilivyokuwa hapo stendi ya Mbezi Luis, palikuwa pamechangamka na
kelele mtindo mmoja. Na hiyo ndiyo ilikuwa kawaida ya eneo hilo lililopo magharibi
ya jiji la Dar es Salaam.
Siku hiyo, wapendao wawili, kijana Haruna na mke wake Zara walikuwa kwenye
banda lao lao la biashara ya kuuza nguo za mitumba, lililokuwa moja kati ya
mabanda mengi ya biashara ndogondogo yaliyopo hapo stendi. Walikuwa wazoefu
na waliwashawishi wateja wengi wanunue nguo kwao.
Jioni walifunga biashara yao wakiwa na nyuso za furaha kwa kiasi cha fedha
walichokipata siku hiyo. Na wakarejea walikoishi, mitaa ya Goba.
Ndoa yao ilikuwa bado changa kabisa walikuwa wameoana miezi sita tu iliyopita
na maisha yao yalikuwa ni ya kawaida kabisa. Walikuwa wamepanga chumba kimoja.
Na humo waliishi wao, kitanda chao, viti, kabati, vyombo, viatu, madumu na madude
mengine kibao yote kwenye chumba hichohicho kimoja, na choo kilikuwa cha nje cha
kushea na mpangaji mwezao mwengine.
Pamoja na maisha yao ya kuwa ya kawaida sana, Haruna na Zara walipendana
mno. Na mapenzi yao katika ndoa yao changa yalikuwa motomoto.
Haijalishi siku iliwachosha kiasi gani, kila waliporejea kwenye chumba chao
kimoja walikuwa kwenye ulimwengu wa peke yao wa mapenzi walisahau uwepo wa
viumbe wengine wote.
Na usiku wa siku hiyo haukuwa tofauti ulikuwa ni wa furaha na mapenzi kwao.
Zara akiwa peke yake chumbani aliwasha redio yao na kuweka mziki mzuri wa
mapenzi, akijua fika utamnyanyua Haruna huko nje alikokuwako na kumrudisha
chumbani.
Kisha akajitupa kitandani huku kaukumbatia mto na kutupia macho yake
kwenye mlango wa chumba, akifahamu fika kuwa punde tu, Haruna angefungua
mlango na kuingia ndani.
Na kweli, sauti ya mziki mzuri wa mapenzi ilimfikia Haruna aliyekuwa amekaa
kwenye baraza nje ya nyumba, akajikuta akiweka tabasamu usoni. Alifahamu kuwa
ilikuwa ni mbinu ya Zara ya kumuita arejee ndani.
Basi Haruna alinyanyuka toka barazani alipokaa na kuelekea ndani, akafungua
mlango wa chumba alichoishi na mkewe na kuingia. Na akamuona mkewe akiwa
yupo kitandani kashikilia mto, usoni akiwa na tabasamu, huku mziki wa kimapenzi
ukiendelea kupiga.
Hakika Zara alivutia sana machoni mwa Haruna. Haruna alijiona mwenye bahati
sana kuwa mume wa Zara. Basi taratibu Haruna alisogea hadi karibu na kitanda na
kumnyooshea Zara mkono wa kulia, Zara akanyoosha mkono wake wa kushoto na
Haruna akaukamata mkono huo, kisha akamvuta Zara na kumnyanyua toka hapo
kitandani akamsimamisha na kumkumbatia, na kumshikilia huku wakianza kucheza
wimbo uliokuwa ukiendelea kupiga toka kwenye redio yao.
Walikuwa kwenye huba zito. Wote walipendana. Zara alimtazama Haruna usoni
na kuanza kumwambia, “mpenzi wangu mwenyezi Mungu muumba wa ardhi na
mbingu awe shahidi, wa penzi langu kwako, lililo moyoni mwangu”, aliongea Zara
huku Haruna akibaki anamtazama mkewe huyo, huku wakiendelea kucheza taratibu
wimbo wa mapenzi, kisha akaendelea kuongea, “tutulizane mpenzi tupendane”.
Naye Haruna akafungua kinywa chake na kuanza kumwambia mkewe, “Mke
wangu naahidi kukupenda na kukujali milele. Mimi nimekuchagua uwe wangu,
wangu wa maisha wa kufa na kuzikana”.
Mara wakajikuta wamesukumana kitandani, huku wakitupiana mabusu, huku
wakitoa nguo zilizo miilini mwao, na kushikanashikana kimapenzi. Hakika ulikuwa ni
usiku wa aina yake kwao.
….……………………………………………………
Pengine mapenzi ya Haruna na Zara yalitokana na kufanana kwa historia za
maisha yao. Wote walikuwa wametoka familia zenye maisha ya kawaida sana.
Haruna alikulia mitaa ya Mburahati huku baba yake aliyeitwa Mzee Nzowa
alikuwa ni mtengeneza majiko ya mkaa na mama yake alikuwa anajishughulisha na
kuuza chakula na vitafunwa mtaani. Wazazi wake walimpenda sana na walifanikiwa
kumsomesha na Haruna alikuwa amehitimu shahada ya kwanza katika masuala ya
teknolojia ya mawasiliano.
Zara alikuwa amezaliwa mitaa ya Kigogo, alikuwa mtoto wa mwisho kwenye
familia yao ya watoto watatu. Baba yake alikuwa mlinzi kipindi Zara anazaliwa, ila
siku moja ajali mbaya ilisababisha babake apoteze miguu yake, hivyo kufanya
ashindwe kuendelea kutunza familia kupitia kazi yake ya ulinzi.
Na hivyo ilimbidi mama yake Zara ajiingize kwenye biashara za kuuza chakula
mtaani ili aweze kutunza familia yao.
Kupitia shughuli za kuuza chakula mtaani mama yake Haruna na mamake Zara
walifahamiana na kuunda urafiki, urafiki ambao uliwakutanisha Zara na Haruna na
wao wakawa marafiki.
Kutokana na urafiki wao, Zara alikuwako kwenye nyakati nyingi za muhimu za
maisha ya Haruna kama kwenye mahafali yake pamoja na sherehe zake nyingi za
kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa.
Hata Haruna alipoingia chuo, Zara aliendelea kumtembelea hadi chuoni. Taratibu
uhusiano wao ukageuka kuwa mapenzi na hawakuficha wakaweka wazi kwa familia
zao.
Miezi kadhaa baada ya Haruna kuhitimu chuo, janga la mafuriko lililikumba jiji la
Dar es salaam na kuleta maafa makubwa na kubomoa nyumba na kuzoa mali za watu.
Miongoni mwa maeneo yaliyoathirika yalikuwa ni Kigogo mtaa alioishi Zara ambapo
mafuriko yalibomoa nyumba yao na kufanya walale nje pale mafuriko yalipopita.
Haruna akiwa bado hajapata kazi yoyote ya maana aliamua kufanya maamuzi ya
kumuoa Zara.
Hakutaka kuona binti aliyempenda akilala nje kisa nyumba yao
imebomolewa na mvua, na aliona kuwa kwa kumuoa basi angeweza moja kwa moja
kumuondoa Zara kutoka kwenye kuishi maisha ya kulala nje, na pia wao kupata
nafasi ya kuanza maisha yao mapya kabisa kama mume na mke.
Basi ndoa ikafungwa. Na Haruna na mkewe Zara wakapanga chumba chao kimoja
mitaa ya Goba, huku wakibahatika kufungua biashara yao ya kuuza mitumba stendi
ya Mbezi baada ya babake Haruna, Mzee Nzowa kutoa fedha toka kwenye akiba zake
na kuwapa kama zawadi ya mtaji kwao, waanzie maisha.
Maisha yao yalikuwa na furaha sana hapo Goba. Walipendana na kujaliana.
Walifanya kazi kwa bidii kwenye biashara yao. Walikuwa na ndoto kubwa. Walipanga
kuja kuzaa watoto na kukuza familia. Walipanga kununua kiwanja na kujenga.
Walipanga kununua magari. Walipanga kusafiri na kwenda maeneo ya kitalii
kufurahia maisha na mapenzi yao hapo baadae.
Wao waliona maisha yao yana nuru kubwa. Walisadiki yote waotayo yatatimia.
Wao hawakujiuliza kama ndoto zao zitatimia, walijiuliza ni lini ndoto zao zitatimia,
waliona lilikuwa ni suala la muda kwa yao yote kutokea na walitumaini na kuamini
kuwa Mungu alikuwa upande wao na atawatetea kwenye safari yao ya maisha.
….……………………………
SEHEMU YA KWANZA
Ilikuwa ni siku ya joto na jua kali, huku kama kawaida watu walikuwa wengi,
wakiwa kwenye pilika pilika, wengine wakiwahi usafiri na wengine wakishuka
kwenye mabasi na daladala wakiwa wamewasili.
Wafanyabiashara wadogowadogo
walikuwa bize na wateja wao, wengine walikuwa wakitumia vipaza sauti kunadi
biashara zao.
Watu kadhaa walioonekana wana hali duni na wamechoka, baadhi yao wakiwa
wazee, watoto na wenye ulemavu walionekana wameshika bakuli wakiombaomba
kwa wapita njia, huku wapita njia wachache wakitoa sarafu toka mifukoni mwao na
kuweka kwenye bakuli hizo.
Hali ndivyo ilivyokuwa hapo stendi ya Mbezi Luis, palikuwa pamechangamka na
kelele mtindo mmoja. Na hiyo ndiyo ilikuwa kawaida ya eneo hilo lililopo magharibi
ya jiji la Dar es Salaam.
Siku hiyo, wapendao wawili, kijana Haruna na mke wake Zara walikuwa kwenye
banda lao lao la biashara ya kuuza nguo za mitumba, lililokuwa moja kati ya
mabanda mengi ya biashara ndogondogo yaliyopo hapo stendi. Walikuwa wazoefu
na waliwashawishi wateja wengi wanunue nguo kwao.
Jioni walifunga biashara yao wakiwa na nyuso za furaha kwa kiasi cha fedha
walichokipata siku hiyo. Na wakarejea walikoishi, mitaa ya Goba.
Ndoa yao ilikuwa bado changa kabisa walikuwa wameoana miezi sita tu iliyopita
na maisha yao yalikuwa ni ya kawaida kabisa. Walikuwa wamepanga chumba kimoja.
Na humo waliishi wao, kitanda chao, viti, kabati, vyombo, viatu, madumu na madude
mengine kibao yote kwenye chumba hichohicho kimoja, na choo kilikuwa cha nje cha
kushea na mpangaji mwezao mwengine.
Pamoja na maisha yao ya kuwa ya kawaida sana, Haruna na Zara walipendana
mno. Na mapenzi yao katika ndoa yao changa yalikuwa motomoto.
Haijalishi siku iliwachosha kiasi gani, kila waliporejea kwenye chumba chao
kimoja walikuwa kwenye ulimwengu wa peke yao wa mapenzi walisahau uwepo wa
viumbe wengine wote.
Na usiku wa siku hiyo haukuwa tofauti ulikuwa ni wa furaha na mapenzi kwao.
Zara akiwa peke yake chumbani aliwasha redio yao na kuweka mziki mzuri wa
mapenzi, akijua fika utamnyanyua Haruna huko nje alikokuwako na kumrudisha
chumbani.
Kisha akajitupa kitandani huku kaukumbatia mto na kutupia macho yake
kwenye mlango wa chumba, akifahamu fika kuwa punde tu, Haruna angefungua
mlango na kuingia ndani.
Na kweli, sauti ya mziki mzuri wa mapenzi ilimfikia Haruna aliyekuwa amekaa
kwenye baraza nje ya nyumba, akajikuta akiweka tabasamu usoni. Alifahamu kuwa
ilikuwa ni mbinu ya Zara ya kumuita arejee ndani.
Basi Haruna alinyanyuka toka barazani alipokaa na kuelekea ndani, akafungua
mlango wa chumba alichoishi na mkewe na kuingia. Na akamuona mkewe akiwa
yupo kitandani kashikilia mto, usoni akiwa na tabasamu, huku mziki wa kimapenzi
ukiendelea kupiga.
Hakika Zara alivutia sana machoni mwa Haruna. Haruna alijiona mwenye bahati
sana kuwa mume wa Zara. Basi taratibu Haruna alisogea hadi karibu na kitanda na
kumnyooshea Zara mkono wa kulia, Zara akanyoosha mkono wake wa kushoto na
Haruna akaukamata mkono huo, kisha akamvuta Zara na kumnyanyua toka hapo
kitandani akamsimamisha na kumkumbatia, na kumshikilia huku wakianza kucheza
wimbo uliokuwa ukiendelea kupiga toka kwenye redio yao.
Walikuwa kwenye huba zito. Wote walipendana. Zara alimtazama Haruna usoni
na kuanza kumwambia, “mpenzi wangu mwenyezi Mungu muumba wa ardhi na
mbingu awe shahidi, wa penzi langu kwako, lililo moyoni mwangu”, aliongea Zara
huku Haruna akibaki anamtazama mkewe huyo, huku wakiendelea kucheza taratibu
wimbo wa mapenzi, kisha akaendelea kuongea, “tutulizane mpenzi tupendane”.
Naye Haruna akafungua kinywa chake na kuanza kumwambia mkewe, “Mke
wangu naahidi kukupenda na kukujali milele. Mimi nimekuchagua uwe wangu,
wangu wa maisha wa kufa na kuzikana”.
Mara wakajikuta wamesukumana kitandani, huku wakitupiana mabusu, huku
wakitoa nguo zilizo miilini mwao, na kushikanashikana kimapenzi. Hakika ulikuwa ni
usiku wa aina yake kwao.
….……………………………………………………
Pengine mapenzi ya Haruna na Zara yalitokana na kufanana kwa historia za
maisha yao. Wote walikuwa wametoka familia zenye maisha ya kawaida sana.
Haruna alikulia mitaa ya Mburahati huku baba yake aliyeitwa Mzee Nzowa
alikuwa ni mtengeneza majiko ya mkaa na mama yake alikuwa anajishughulisha na
kuuza chakula na vitafunwa mtaani. Wazazi wake walimpenda sana na walifanikiwa
kumsomesha na Haruna alikuwa amehitimu shahada ya kwanza katika masuala ya
teknolojia ya mawasiliano.
Zara alikuwa amezaliwa mitaa ya Kigogo, alikuwa mtoto wa mwisho kwenye
familia yao ya watoto watatu. Baba yake alikuwa mlinzi kipindi Zara anazaliwa, ila
siku moja ajali mbaya ilisababisha babake apoteze miguu yake, hivyo kufanya
ashindwe kuendelea kutunza familia kupitia kazi yake ya ulinzi.
Na hivyo ilimbidi mama yake Zara ajiingize kwenye biashara za kuuza chakula
mtaani ili aweze kutunza familia yao.
Kupitia shughuli za kuuza chakula mtaani mama yake Haruna na mamake Zara
walifahamiana na kuunda urafiki, urafiki ambao uliwakutanisha Zara na Haruna na
wao wakawa marafiki.
Kutokana na urafiki wao, Zara alikuwako kwenye nyakati nyingi za muhimu za
maisha ya Haruna kama kwenye mahafali yake pamoja na sherehe zake nyingi za
kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa.
Hata Haruna alipoingia chuo, Zara aliendelea kumtembelea hadi chuoni. Taratibu
uhusiano wao ukageuka kuwa mapenzi na hawakuficha wakaweka wazi kwa familia
zao.
Miezi kadhaa baada ya Haruna kuhitimu chuo, janga la mafuriko lililikumba jiji la
Dar es salaam na kuleta maafa makubwa na kubomoa nyumba na kuzoa mali za watu.
Miongoni mwa maeneo yaliyoathirika yalikuwa ni Kigogo mtaa alioishi Zara ambapo
mafuriko yalibomoa nyumba yao na kufanya walale nje pale mafuriko yalipopita.
Haruna akiwa bado hajapata kazi yoyote ya maana aliamua kufanya maamuzi ya
kumuoa Zara.
Hakutaka kuona binti aliyempenda akilala nje kisa nyumba yao
imebomolewa na mvua, na aliona kuwa kwa kumuoa basi angeweza moja kwa moja
kumuondoa Zara kutoka kwenye kuishi maisha ya kulala nje, na pia wao kupata
nafasi ya kuanza maisha yao mapya kabisa kama mume na mke.
Basi ndoa ikafungwa. Na Haruna na mkewe Zara wakapanga chumba chao kimoja
mitaa ya Goba, huku wakibahatika kufungua biashara yao ya kuuza mitumba stendi
ya Mbezi baada ya babake Haruna, Mzee Nzowa kutoa fedha toka kwenye akiba zake
na kuwapa kama zawadi ya mtaji kwao, waanzie maisha.
Maisha yao yalikuwa na furaha sana hapo Goba. Walipendana na kujaliana.
Walifanya kazi kwa bidii kwenye biashara yao. Walikuwa na ndoto kubwa. Walipanga
kuja kuzaa watoto na kukuza familia. Walipanga kununua kiwanja na kujenga.
Walipanga kununua magari. Walipanga kusafiri na kwenda maeneo ya kitalii
kufurahia maisha na mapenzi yao hapo baadae.
Wao waliona maisha yao yana nuru kubwa. Walisadiki yote waotayo yatatimia.
Wao hawakujiuliza kama ndoto zao zitatimia, walijiuliza ni lini ndoto zao zitatimia,
waliona lilikuwa ni suala la muda kwa yao yote kutokea na walitumaini na kuamini
kuwa Mungu alikuwa upande wao na atawatetea kwenye safari yao ya maisha.
….……………………………