CHANGE
Story by Elton Tonny
Urafiki, Familia, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Ukatili, Mauaji, Mambo yasiyotazamiwa, Mambo yenye kuhofisha
R-rated 18+
Enjoy!
★★★★★★★★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA THELATHINI NA TISA
★★★★★★★★★★★★★★★★★★★
Usiku huo huo, ndani ya nyumba ya Efraim Donald na Namouih wote walikuwa wameshapumzika kwa kupiga usingizi mwanana ili kukikucha waweze kufurahia siku hiyo ambayo ingekuwa muhimu kwa Namouih. Ikiwa ni mida ya saa kumi usiku, mlango wa chumba alichotumia Sasha ukafunguka taratibu, na hapo akaanza kuingia mtu kwa njia ya kunyata. Binti alikuwa amelala kitandani, lakini hakuwa amesinzia. Aliweza kuhisi vyema namna ambavyo mtu huyo aliingia ndani ya chumba chake, naye hakujisumbua kugeuka hata mara moja kwa sababu tayari alijua ni nani.
Ilikuwa ni Efraim Donald mwenyewe, naye akakielekea kitanda cha Sasha na kupanda taratibu. Mwanadada huyo alikuwa amelala kwa ubavu huku akitazama upande mwingine, kwa hiyo alimhisi vyema Efraim pale alipoukaribia mwili wake kwa nyuma na kulala kando ya mgongo wake. Sasha aliendelea tu kuwa mtulivu, kwa sababu hali hii mpya tayari alikuwa ameanza kuizoea, na hata kwa kadiri fulani, alikuwa anafurahia. Kumuua Shomari kulithibitisha hilo, na Efraim kumwahidi kwamba angekuwa nguvu yake kuu kuanzia sasa kulimfanya ajihisi tofauti na utayari wa kubadilika kutoka kuwa Sasha wa zamani na kuwa Sasha mpya.
"Mrembo wangu..."
Sauti hiyo ya chini kutoka kwa Efraim ikasikika vyema masikioni mwa binti. Sasha akaendelea kutulia tu, naye Efraim Donald akaupitisha mkono wake kwenye kiuno cha binti na kuuingiza ndani ya kinguo chake chepesi mpaka kulishika titi lake laini, naye Sasha akaendelea kutulia. Mwanaume huyo akawa ameubananiza zaidi mwili wake nyuma ya mwili wa binti, huku akitumia vidole vyake kuliminya-minya na mdomo wake kuubusu mgongo safi wa mrembo wake mpya.
"Nisamehe nimechelewa. Najua umenisubiri sana," Efraim akasema.
Sasha akabaki kimya tu.
"Najua umenimiss pia mrembo wangu," Efraim akasema.
Wakati huu, mwanaume huyo alikuwa analifinya titi la Sasha kwa nguvu kiasi, naye binti akawa amekunja uso huku akipumua kwa njia legevu.
"Mke wangu alipokuja kukuona... mliongea nini?" Efraim akauliza.
Sasha hakutoa jibu lolote, bali akawa anaitikia tu kwa pumzi zake hisia za kimahaba alizopata. Efraim Donald akautoa mkono wake kwenye kifua cha binti na kuupeleka mpaka sehemu yake ya chini. (........).
"Alikuhoji kuhusu tulipoenda?" Efraim akauliza.
"Mm-mmm..." Sasha akakanusha kwa mguno huo.
(........).
"Nimempa mama yako gari leo. Na wewe? Ungependa nikupe nini?" Efraim akamuuliza.
Sasha akatoa mguno wa juu wa pumzi, kisha bila kutoa jibu akarudisha mkono wake kwa nyuma na kumshika Efraim sehemu ya siri iliyokuwa imetuna ndani ya boksa. Mwanaume hakubaki kujiuliza ni nini ambacho mtoto alikuwa anataka, alielewa fika kwamba alikitaka, na yeye alikuwa hapo kumpatia. (........).
(.........).
Sasha alikuwa amekunja sura yake huku akijikaza kutoa sauti za juu sana, lakini miguno yake ya kooni ilimhamasisha zaidi Efraim kumpatia dozi mpaka akome. Si aliiomba? Kuipata akaipata. Efraim Donald akaikaba shingo ya binti huyo huku akiendelea kumkuna kwa nguvu, na miguno ya Sasha ikazidi kuongezeka sauti. (........).
(.........).
Sasha aliona ni kama amejiingiza kwenye karama fulani hivi, na ilikuwa moja iliyomsisimua sana. Alikuwa ameitandaza miguu yake hewani huku akigugumia mahaba hayo ya kijeuri, uso wake mweupe ukibadilika kuwa mwekundu, na mishipa ya shingo na kichwa ikimsimama mithili ya mizizi ya mihogo. Efraim Donald akamfikisha mlimbwende huyo mahali pazuri, kwani binti alianza kutetemeka kiunoni na miguu pia, naye Efraim Donald akajitoa kwenye kito hicho safi na hapo hapo binti akaanza kurusha juisi zake za utamu kwa mfululizo.
(........).
(........).
(........).
Sasha alikuwa anapumua kwa nguvu na kilegevu sana, akijihisi wa ajabu sana, lakini kwa wakati huo huo akifurahia hilo moyoni, na hakujua ni kwa nini.
Efraim Donald akaishika shingo ya binti kama anataka kumkaba, kisha akasema, "We' ni mtamu sana Sasha. Inaonekana ni kitu mlichobarikiwa nacho nyie wote watatu."
"Na nani mwingine? Mama yangu?" Sasha akaongea hatimaye.
"Hahahah... siwezi kujua. Ndiyo maana nimesema 'inaonekana.'"
"Utakuwa umenichubua..."
"Pole. Ila si unafurahia nikiwa... aggressive?"
Sasha akatulia kidogo, kisha akasema, "Ndiyo."
Efraim akatabasamu na kusema, "Kila nafasi tutakayopata, nitakupa unachotaka. Nimeshajua unayotaka, kwa hiyo nitakupatia tu. Mimi ni wako sasa hivi."
"Na dada? Yeye si ndiyo mmiliki halali?"
"Haijalishi. Mbona yeye anani-cheat?"
"Kwa nini unafanya ionekane kama kitu cha kawaida sana? Haikuumizi kwamba mke wako anakusaliti?"
"Hata chembe."
"Mhm... mwongo."
"Really? Kwa nini unasema hivyo?"
"Inakuumiza, ila naona una sababu nyingine tu inayofanya umwache. Na mimi ndiyo unanitumia kama kisasi," Sasha akasema.
Efraim Donald akatabasamu na kusema, "Una akili sana, lakini siyo hivyo. Wewe... ni kama tuzo yangu. Tuzo kuu kwa ajili ya jambo moja muhimu sana. Sitaki mtu yeyote akusumbue kuanzia sasa... we' ni mali yangu."
"Na wewe ni nguvu yangu. Ninataka kufanya lolote nalotaka kuanzia sasa, na wewe utanisaidia hata iwe nini," Sasha akaongea kwa ujasiri.
"Ahahahah.... uko kama dada yako tu..."
"Usinilinganishe na mke wako, mimi ni mimi. Dada anaweza akawa amechanganywa na maisha ya ndoa lakini mimi najua nachotaka. Sitapindisha mambo. Nitakupa unachokihitaji kutoka kwangu, na mimi utanipa lolote nalotaka wakati wowote ule."
Efraim Donald akamtazama kwa umakini, kisha akasema, "Muda mfupi uliopita ulikuwa mwoga kweli, ila sa'hivi naona umeanza kuzoea utu wako. Ahadi yangu iko pale pale. Kwa hiyo niambie unataka nini."
"Nataka umkamate... umkamate mwanamke aliyetoka na Shomari..." Sasha akasema hivyo.
Efraim Donald akatabasamu kwa mbali, kisha akauliza, "Halafu?"
"Nitadili naye mimi," Sasha akasema.
Efraim akacheka kidogo, kisha akamshika shavuni na kusema, "Roho ya kisasi iliyo moyoni mwako... inanifanya nitamani hata kubaki na wewe daima. Haitakuwa hivyo sikuzote Sasha, lakini kwa muda tutakaokuwa pamoja, nitakutimizia yote unayotaka. Huyo mwanamke nitamtafuta. Nitamshika haraka, nitakuachia ucheze naye. Ila na me si ninaalikwa kutazama hiyo drama?"
Sasha akabaki kumtazama tu usoni.
Efraim Donald akatabasamu, kisha akaipandisha boksa na kuificha mashine yake. "Umenyeshea kitanda, mvua nyingi haswa. Esma ana kazi kweli."
"Nitafua mwenyewe. Nilikuwa nina...."
Kabla Sasha hajamaliza kuongea, wote wakasikia sauti ya mlango kufungwa, kisha hatua za mtu zikija upande wa chumba cha Sasha zikasikika. Sasha akatazama mlangoni kwa umakini, naye Efraim Donald akawa ameweka kiganja chake kifuani kwa binti kama kumtuliza hapo hapo. Hatua hizo zikakipita chumba cha Sasha na kutokomea, naye Efraim akamgeukia binti.
"Ni Esma, ameamka kuanza kazi. Wewe rudi kulala. Tutaonana baadaye," Efraim akamwambia.
Kisha akageuka tena ili ajiondoe kitandani, lakini Sasha akakishika kichwa chake na kumvutia kwake, akianza kumpa denda taratibu mdomoni. Efraim akairudisha busu ya binti pia huku analiminya kalio lake, kisha akajitoa kwake na kusema 'yaani we mtoto wewe!' halafu ndiyo akashuka na kuondoka. Sasha akajirudisha kulala taratibu kama alivyokuwa mwanzoni, akiwa anatafakari alichokuwa amepania kufanya pindi ambapo Efraim angemkamata mwanamke aliyemrubuni Shomari mpaka akamsaliti, kwa sababu bado alitaka kuzimaliza hasira alizokuwa nazo kwa hatua kama aliyochukua siku ya jana. Baada ya muda mrefu wa kuwazia mambo mengi, akajinyanyua na kuanza kukisafisha kitanda ili pawe papya kadiri siku ilivyoanza kupambazuka.
★★
Siku hii ilianza kwa Blandina kujiandaa vyema kuelekea kazini kwa upande wake. Tokea waliporudi jijini na Namouih, ni leo ndiyo alikuwa amerejea kazini rasmi, na angekuwa akishughulika na usaidizi wa masuala ya kesi za baadhi ya wanasheria wa hapo wakati huu ambao mwanasheria wake mkuu hakuwepo. Draxton alipomsaidia kupigania kesi ya yule mzee Douglas na kuishinda, mwanaume huyo alikuwa ameitoa zawadi yake ya shukrani kama alivyoahidi, akiwa amewalenga wote waliomsaidia, lakini Draxton alikuwa amempa Blandina yote kabisa.
Mwanamke huyu aliwaza sana kuhusu hali ya uhusiano wake na yule mtu maana haikueleweka hatma yao ingekuwa nini hasa ukitegemea Draxton hakupatikana kabisa, na kusema tu aendelee kukaa kusubiri hakukutosha. Alihitaji kujihakikishia kwamba pendo lake halijavuliwa bila utambuzi wake, kwa hiyo akawa haachi kumtafuta. Mida fulani hata Namouih akawa amempigia simu na kuuliza ikiwa angekwenda nyumbani kwake pamoja na Natasha na Draxton, naye Blandina akamjulisha kwamba kwa mama yake mdogo uhakika ulikuwepo ila kwa Draxton bado hakujua. Namouih akampa ushauri kwamba aende kwake Draxton kabisa ili aangalie kama yupo au hata kumuulizia mwanaume huyo, akisema huenda alikuwa tu nyumbani, naye Blandina akakubali kufanya hivyo.
Kuna wakati ambao Blandina alikuwa anaweka kituo na kutafakari mambo kwa kina kirefu. Sawa alikuwa anajaribu kutofikiria mambo mengi vibaya, lakini hiyo haikumaaniaha alikuwa kipofu namna hiyo. Wonyesho aliotoa Namouih wa kujali sana ikiwa Draxton angekwenda nyumbani kwake leo ulimfanya Blandina awazie kuhusu namna ambavyo rafiki yake alikuwa ameanza kutenda kumwelekea mpenzi wake kwa hizi siku chache toka kifo cha Nasma, na jambo hilo lilimsumbua sana moyoni. Hakutaka kumhukumu vibaya rafiki yake kipenzi, kwamba labda ameanza kumpenda mwanaume wake, lakini hizo hisia hazikuacha kucheza karibu sana na moyo wake ingawa alijitahidi mno kutowazia mambo kwa njia kama hiyo. Akaamua kuitafuta tena simu ya Draxton, na wakati huu, ikaita hatimaye!
Alihisi kama moyo wake umechangamka sana baada ya kuipata simu ya mpenzi wake tena, naye akawa anangoja kwa hamu apokee lakini hakupokea. Akapiga kwa mara nyingine lakini ikawa inaita tu, hivyo akakata na kunyanyuka kutoka kwenye kiti cha meza yake ya ofisi na kubeba mkoba wake. Upesi akaondoka kutoka hapo kwenye kampuni ili aende kule mpenzi wake alikoishi kuona kama angempata. Mapenzi yalikuwa yakisumbua sana akili ya mwanamke huyu kwa sababu ilikuwa imeshazama sana kwa Draxton, naye angefanya tu lolote lile ili kuhakikisha anakuwa karibu yake haijalishi wanapitia nini kwenye uhusiano wao. Akachukua gari lake na kuanza kuelekea huko upesi akiwa hana hata uhakika kama angemkuta mpenzi wake.
★★
Mwendo wa dakika kadhaa ukatosha kumfikisha mwanamke huyu nje ya nyumba aliyoishi mpenzi wake, na hakuna kitu kilichompa ridhiko kubwa moyoni kama kuliona gari la Draxton hapo nje. Blandina alikuwa ametumia muda fulani siku mbili zilizopita kufika kwenye nyumba hii kumtafuta mpenzi wake bila kumkuta, kwa hiyo kuliona gari lake hapo sasa kulimaanisha angekwenda ndani huko ili apate majibu kamili ya maswali mengi aliyokuwa amejiuliza mpaka akachoka. Yaani leo kingeeleweka, na kama angekuta mwanamke mwingine ndiyo analiwa huko ndani angehakikisha anaondoka na jicho lake moja! Hakutaka kabisa mchezo na penzi lake.
Draxton kutopokea simu yake kulimaanisha alikuwa anamkwepa makusudi kabisa, kwa hiyo Blandina angekwenda ndani kwa lazima ili aubambe ukweli yeye mwenyewe. Akatoka ndani ya gari lake baada ya kuegesha na kwenda ndani moja kwa moja kwa kuwa geti lilikuwa wazi. Aliwakuta wanawake wenyeji wa pale sehemu ya nje na kuwasalimu tu kikawaida, halafu akawapita na kwenda mpaka kwenye mlango wa chumba cha Draxton; kukuta kimefungwa kwa ndani. Akaanza kugonga mlango huo kwa njia fulani kama mtu asiye na subira hata kidogo, na aliweza kutambua kwamba dirisha la majirani wa hapo liliacha uwazi kidogo kumwambia kwamba walikuwa wanamchungulia kutokea huko ndani, lakini akawapuuzia. Akaendelea kuugonga mlango namna hiyo hiyo, na ndipo ukafunguliwa.
Macho yake yakakutana kwa mara nyingine tena na macho mazuri sana ya mwanaume huyo aliyempenda kwa dhati, lakini yalionekana kuchoka kama mtu aliyekuwa ametoka kulala. Hapo mbele yake Blandina, Draxton alisimama huku akiwa kifua wazi, pensi nyepesi ya kijani ikimsitiri kwa chini, na akimtazama mwanamke huyu kwa njia fulani iliyoonyesha simanzi. Blandina hakujua ni nini tu, lakini angeweza kusema kwamba mwanaume huyo alisumbuliwa na jambo fulani kwa kumwangalia tu. Alikuwa amemkosa sana. Akamfata haraka mlangoni hapo na kumkumbatia kwa nguvu, kana kwamba hakuwa ameonana naye kwa mwaka mzima. Draxton alikuwa ametulia tu, kisha taratibu akarudishia mlango na kuzungushia mikono yake mwilini kwa mpenzi wake, akimbana kwa hisia sana. Alikuwa amerudisha mwonekano wake wa kawaida sasa, na akilini kwake kulikuwa na mambo mengi sana yaliyoongezeka kwa sababu hizi siku chache zilizopita tokea alipomwacha Blandina hazikumwendea vyema kabisa, kwa hiyo kumbatio la huyu mwanamke lilimfanya ajihisi vizuri sana.
Blandina akamwachia taratibu huku bado miili yao ikiwa kwa ukaribu, naye akaudondosha mkoba wake chini na kumshika usoni. Alikuwa anamwangalia mwanaume wake kwa upendo sana, kisha hapo hapo akaanza kumbusu mdomoni mwake. Akaendelea kumbusu tu kwa hamu nyingi, naye Draxton akawa anajibu busu hiyo kwa hisia huku amekishika kiuno cha mwanamke huyo.
Alipouachia mdomo wake, Blandina akasema kwa hisia, "Yaani hukosi njia za kunitesa we' mwanaume. Wakati mwingine najiuliza kwa nini... ila nimegundua kwamba inakupa furaha."
"Blandina...."
"Ulikuwa wapi? Kwa nini hupatikani? Unanipima na kupima mpaka lini Draxton? Bado tu unanipa mitihani ili niteseke mno kukufanya uone kwamba nakupenda sana au?"
"La. Samahani...."
"Usiniambie samahani tu Draxton, leo haitatosha. Ikiwa kweli unathamini kile tulichojenga kufikia sasa naomba unieleze kwa nini mapenzi yetu yako namna hii. Sitaki kukuchoka... ila unanilazimu nianze kufanya hivyo..."
Blandina aliongea maneno hayo kwa hisia sana, naye Draxton akaangalia chini kwa huzuni. Akakiachia kiuno chake taratibu na kukishika kiganja chake, kisha akauokota mkoba wa mwanamke huyo na kuanza kuongozana naye kuelekea sehemu ya sebule. Wakalifikia sofa na kukaa pamoja, huku Blandina akiwa amejiweka karibu naye zaidi, akimwangalia kwa upendo sana, na Draxton akionekana kuwa kwenye wimbi la mawazo.
"Uko sahihi. Samahani haitoshi hata kidogo. Nimekuweka gizani kwa mambo mengi na sasa yameongezeka na kuwa mengi zaidi mpaka nashindwa nianze wapi kuelezea," Draxton akasema kwa upole.
"Draxton niambie. Nataka kukuelewa. Umeshaniambia mambo fulani kuhusu wewe lakini ambayo hujasema ndiyo yanayovuruga penzi letu. Unapotea tu kila tukijaribu ku... unakuwa unaenda wapi? Hiyo shida yako ni nini? Draxton usiponiambia utamwambia nani jamani, eh? Nakujali sana, nakupenda mno, nataka kusaidia lakini unaniweka pembeni tu. Hebu nionee huruma basi..." Blandina akasema kwa hisia.
"Nisamehe Blandina. Kweli sijakutendea haki kwa mambo mengi... ilitakiwa wewe ndiyo uwe wa kwanza kujua yaani hata sielewi kwa nini ilipaswa kuwa hivi..."
"Kuwa nini? Unamaanisha umemwambia mtu mwingine tatizo lako kwanza kabla yangu?"
Draxton akamtazama tu usoni.
"Unajua ninawaza sana. Pamoja na yote nayojitahidi kufanya kuonyesha navyokupenda lakini ni kama unazichukua hisia zangu for granted... ni kama tumekwama sehemu moja tu kwa sababu hutaki kuniambia matatizo yako... unahisi siwezi kukusaidia kuubeba mzigo ulionao mpenzi wangu... na hiyo inaniumiza sana..." Blandina akasema hivyo na kuanza kudondosha machozi.
Draxton akamshika shavuni na kuanza kumfuta machozi, kisha akasema, "Am sorry. Nisamehe Blandina. Nataka nikuelezee kila kitu... na ninahitaji uelewe kwamba kufanya niliyofanya... kumenibomoa sana... na sijui kama nitawahi kuondoa vikwazo vinavyosababisha maisha yangu yayumbe. Ni kitu kinachoniumiza kwa kuwa yanakuathiri vibaya hata ingawa najaribu kujiweka sawa... ninakosea sana yaani... ninakukosea sana Blandina..."
Blandina akawa anaendelea kulia na kuishika mikono ya mpenzi wake, kisha akasema, "Niambie. Usijali. Niambie mpenzi wangu. Sitakuchukulia vibaya. Nahitaji tu kuujua ukweli kutoka kwako hata kama sitaweza kusaidia moja kwa moja lakini nahitaji unionyeshe kwamba unaniamini. Please..."
Draxton akashusha pumzi taratibu, kisha akaanza kusema, "Maisha yangu ni kitu cha ajabu sana Blandina. Vitu navyotaka kukwambia... inabidi u...."
Simu ya Blandina ikakatisha maneno ya Draxton baada ya kuanza kutoa mwito wa kupigiwa. Blandina akaitoa mkobani haraka akiwa na lengo la kukata ili aendelee kumsikiliza mpenzi wake, lakini akasitisha kufanya hivyo baada ya kuona ni 'boss' wake ndiyo alikuwa anapiga, yaani Mr. Edward Thomas. Akamwangalia Draxton kiufupi, na mwanaume huyu akamtikisia kichwa mara moja kama kumwambia 'pokea.'
Blandina akajiweka sawa kihisia na kupokea simu yake. Akaanza kuongea na Mr. Edward, aliyemwambia kwamba alimhitaji ofisini haraka kwa kuwa kuna kazi ilihitaji usaidizi wake mzuri. Alikuwa anauliza alikoenda, naye Blandina akasema alitoka tu mara moja na hakuwa mbali. Akamuuliza ikiwa ilikuwa lazima yeye ndiyo afanye hiyo kazi, naye Edward akasema ndiyo, na alitaka awahi kuimaliza kwa sababu alijua mwanamke huyu angekwenda kwenye sherehe ya Namouih jioni hiyo kama yeye tu. Blandina akamtazama Draxton machoni kwa hisia, na mwanaume huyo akamwonyeaha kwa ishara ya kichwa akubali tu mwito wa mkuu wake. Blandina hakuwa na namna ila kukubali, akimwambia 'boss' wake kuwa angejitahidi kuwahi, kisha akakata simu na kumwangalia mpenzi wake tena.
"Draxton...."
"Usijali. Wewe nenda, tutaongea tu tena. Nimefurahi kukuona," Draxton akasema kwa upendo.
"Sawa. Lakini tafadhali usipotee tu tena. Naomba uje leo kwa Donald. Ni party ndogo ya birthday ya Namouih. Ulikuwa unajua?" Blandina akasema.
Draxton akaangalia chini, kisha akatikisa kichwa kukanusha.
"Unapaswa uje Draxton. Please usiache... niahidi utakuja," Blandina akamsihi.
Draxton akamwangalia usoni na kutikisa kichwa kukubali, kisha Blandina akaanza tena kuibusu midomo ya mwanaume huyo kwa upendo.
"Nitakupigia. Zamu hii usinikwepe Drax... I need to know everything, sawa?" Blandina akasema.
"Okay. Nitakwambia kila kitu. Usijali," Draxton akasema kwa upole.
Blandina akanyanyuka kutoka sofani na kusimama, kisha akaufata tena uso wa Draxton na kumpiga busu mara kadhaa mdomoni, halafu ndiyo akaondoka sehemu hiyo ili awahi kazini tena. Draxton akabaki kwenye sofa akiwa ameweka kiganja usawa wa mdomo wake, akiwaza na kuwazua mambo mengi sana yaliyofanya ahisi ni kama dunia imemlemea. Hakuna mtu ambaye angeweza kuelewa ni aina gani ya maisha aliyokuwa anapitia, lakini kukutana kwake na yule Mark usiku uliotangulia kulimpatia mwanga fulani mpya, mwanga ambao ulizusha masuala mengi makubwa ambayo yangemhitaji achukue maamuzi magumu si kwa ajili yake tu, bali kwa ajili ya wale aliowapenda, na ambao hakuwahi kudhani angekuja kutakiwa kuwapenda.
★★
Maandalizi ya sherehe ndogo ya Namouih yaliendelea nyumbani kwake, kukipambwa kwa njia ya kawaida na kutengenezwa kwa vyakula mbalimbali pamoja na vinywaji kwa ajili ya wote ambao wangekwenda. Waliokuwa wamealikwa hapo hawakuwa wengi, sanasana Blandina, Natasha, Mwantum, Godwin Shigela, Marietta na Dantu ambao waliahidi kuja pia kutokana na kukosa msiba wa mdogo wake Namouih, Salome, Mr. Edward Thomas, na watu wengine wachache sana ambao wangetoshea vyema sehemu ya ndani ya nyumba kubwa ya Efraim Donald. Mama ya mwanaume huyu, Halima, alikuwa analetwa jijini huku leo pia, akiwa mmoja wa wageni muhimu sana hapo.
Baada tu ya kuwa wamemaliza kupata kiamsha kinywa asubuhi hiyo, familia hii iligawanyika kama jana tu, lakini wakati huu Namouih akienda kutembea na Sasha huku Efraim Donald aliondoka na Zakia. Namouih alitaka kuhakikisha anampendezesha sana Sasha kwa ajili ya siku hiyo maana aliona uhitaji wa kumfanya ajihisi vizuri baada ya binti kufunguka kwake jana. Walitembelea nyumba za urembo na maduka ya saluni kupata huduma kadhaa za kimwili ili kuwa ng'ari ng'ari.
Wakiwa huko, Namouih alijaribu kumtafuta Draxton hatimaye kwa kumtumia ujumbe mrefu, akimwomba asikose kufika kwake leo kwa sababu alikuwa anahitaji sana kumwona. Akasema amekuwa akimuwaza sana tokea mara ya mwisho walipoonana na kuomba samahani kutomtafuta, ila ujio wake leo ungekuwa wa muhimu sana. Hakupata jibu lolote, na wala hakutegemea ajibiwe. Bado hakujua Draxton alikuwa chini ya hali ipi kwa sasa, lakini alitumaini yupo huku bado na angekuja kumwona baadaye. Isingekuwa ya wajibu kwa wanafamilia wake, angekuwa ameshakwenda kumtafuta pale kwake au kule msituni, kwa hiyo angehitaji kuwa na subira kuona mambo yangekwendaje jioni hii.
Kwa upande wake Efraim Donald, bado alisumbuliwa na akili na suala la Suleiman kutopatikana ghafla tu tokea asubuhi ile. Hakuhitaji kuendelea kufanya makisio, alielewa fika kwamba kijakazi wake alikuwa amepatwa na masaibu huko alikokuwa. Lakini akaamua kuweka hilo pembeni kwanza kwa kuwa sasa alitaka kufanya jambo lingine. Alikuwa ameondoka na Zakia asubuhi hiyo kwa kutumia lile gari la Toyota Fortuner alilomzawadia mama-mkwe wake jana, naye akawapeleka mpaka sehemu iliyokuwa na uwanja mpana ili aanze kumfundisha vitu vingi kuhusu uendeshaji. Zakia alijitahidi sana kufuata maelekezo mazuri ya Efraim, na ingawa mwanzoni aliona ugumu kushika mambo mengi lakini yale muhimu zaidi hakukawia kuyazoea, na kwa siku hii akawa amejitahidi sana kuonyesha ameelewa darasa.
Basi imefika mida ya saa saba mchana, Efraim Donald akapendekeza waende hotelini na Zakia kupata angalau juice kisha warudi nyumbani baada ya kuwa ametumia kama masaa mawili ya kumfundisha gari. Zakia akaridhia, kisha Efraim akawaendesha mpaka kufikia hoteli moja kubwa sana na ya kifahari. Akaelekea naye huko ndani, akimwongoza mpaka ndani ya lifti na kuanza kuelekea naye ghorofa za juu. Wakiwa ndani ya lifti, wawili hawa hawakusemeshana lolote kabisa, lakini mara ambazo wangetazamana Efraim angetabasamu kidogo, naye Zakia angetabasamu pia. Wakafika ghorofa ya mwisho kabisa, kisha Efraim akatangulia mbele huku Zakia akimfuata kwa nyuma. Mwanaume huyo alikuwa akisema kwamba Zakia ni mwanafunzi mzuri na hangechukua muda mrefu sana angekuwa ameshajua kuendesha vizuri zaidi hata ya Namouih, na mwanamke huyu akawa anafurahia sana sifa za mwana-mkwe wake.
Efraim Donald akafikia usawa wa mlango fulani na kutoa kadi kama ya benki mfukoni mwake, naye akaiingiza kadi hiyo hapo na kisha kuufungua mlango. Akawa amesimama mlangoni kwa njia ya kumpisha Zakia apite na kuingia, na mwanamama huyo akaingia ndani na kisha Efraim kuingia pia. Mazingira ambayo Zakia aliyakuta humo yalikuwa mazuri sana, lakini hayakuwa yale mazingira kwa ajili ya sehemu ya kupata chakula, bali kwa ajili ya kulala kabisa. Kulikuwa na kitanda kikubwa kilichotengenezwa vizuri sana, dirisha pana lenye mapazia marefu, TV kubwa ya flat screen ukutani na upande wenye masofa mawili na meza ya kioo katikati. Kulikuwa na mlango mwingine pembeni ambao bila shaka ulielekea kwenye bafu na choo cha humo, naye Zakia akatabasamu kwa kupendezwa na mpangilio mzuri sana ndani humo.
"Kila chumba hapa hotelini kiko hivi?" Zakia akauliza baada ya kumgeukia Efraim.
"Hapana... siyo vyote. Hiki ni special kwa ajili ya watu kama sisi," Efraim Donald akasema.
"Aaah... umeshakuja na Namouih hapa eti? Pako juu... halafu pazuri kweli..." Zakia akasema.
Efraim Donald akawa amebaki tu kumwangalia machoni.
Zakia akatazama chini kidogo na kuuliza, "Kwa hiyo... wahudumu wako wapi? Tumeingia tu humu... wanatuletea menu au?"
Efraim Donald akatabasamu kwa mbali, kisha akaanza kumsogelea mama-mkwe wake. Zakia akawa anamwangalia kwa umakini mpaka alipokaribiwa na mkwe wake huyo, kisha Efraim akasema, "Watakuja. Nilikuwa nataka upumzike kidogo."
Mwanaume huyo alikuwa amesimama mbele ya mama ya mke wake huku akimwangalia kwa upendezi, na kiukweli hali hii haikuwa imetarajiwa kwa Zakia.
"Kupumzika... yaani kama... kutulia hapa?" Zakia akauliza.
"Ndiyo."
"Kunywa juice au kufanya nini?"
"Ni wewe tu," Efraim akajibu kwa sauti ya chini.
Zakia akawa ameanza kupatwa na hisi za haya, akishangazwa na njia ambayo mwana-mkwe wake alitumia kuzungumza naye.
"Najua umepitia mambo mengi sana... na mimi... mimi nataka tu kuhakikisha unapata kitulizo bora kabisa," Efraim Donald akasema.
Zakia akawa anamwangalia kwa njia ya kushangaa, kisha akacheka kidogo na kuangalia pembeni.
"Mbona unacheka?" Efraim Donald akauliza.
"Sijacheka mbona? Hivi... ninachofikiria unamaanisha ndiyo hicho unachomaanisha?" Zakia akauliza.
"Kwani we' unafikiri namaanisha nini?" Efraim akauliza.
Zakia akapiga hatua chache kurudi nyuma, na Efraim akamfata tena taratibu na wote kusimama kwa ukaribu. "Haya ni makubwa jamani. Baba, mbona unataka kunitia majaribuni?"
"Majaribu? Sidhani kama hilo ndiyo neno unalotakiwa kusema. Unatakiwa kusema 'utamu,'" Efraim akaongea kwa njia ya utongozi.
"Yesu wangu!" Zakia akashangaa.
"Hhahahahah... naelewa. Kwa jinsi unavyopenda utamu wa vijana wadogo nadhani hata huyo Yesu umeshampa vyote..."
"Jamani! Mwanangu mbona sielewi... yaani hivi...."
"Kwa nini unaniita mwanangu? Hivi Zakia kweli unaniona mimi kama mtoto kwako? Au wewe unajiona kama mzee? Hebu acha hizo bwana... wewe ni binti, tena kimwali mzuri sana. Una miaka mingapi... si 40 tu?"
"49."
"Sasa je!"
"Lakini Ef...."
Efraim Donald akamsogelea karibu zaidi na kukishika kiuno chake. Zakia akapandisha pumzi na kuziba mdomo wake kwa viganja vyake. Mwanaume akaanza kukiminya kiuno hicho na kupitilizisha mkono wake mmoja mpaka kwenye kalio la Zakia. Mwanamama huyu alikuwa amevaa nguo nyepesi ya rangi ya maziwa kwa juu, huku miguuni ikiwa ni suruali nyeusi ya skinny iliyobana vyema umbo lake na kultokeza vyema kalio lake. Ni kweli alikuwa na umri mkubwa, lakini kama Namouih tu, hata yeye alibarikiwa kwa uzuri uliomfanya aonekane mdogo bado kwa kuwa alipenda kuendelea kuonekana namna hiyo. Jambo hili ambalo mwana-mkwe wake alionyesha kutaka kutoka kwake lilikuwa nje ya matarajio kabisa, na ni kama mshtuko alioupata ndiyo ukamfanya ashindwe kutoa itikio sahihi maana hakuelewa ilifikiaje mpaka mume wa binti yake akaanza kumwonyesha upendezi wa kimahaba.
Efraim Donald akawa karibu kabisa na uso wa Zakia sasa, huku akiliminya kalio lake kwa nyuma, na mwanamke huyo akawa ameziba tu midomo yake bado huku akiangalia chini. Mwanaume akaitoa mikono ya Zakia mdomoni, kisha akaishika shingo yake na kumvutia usoni kwake, na hapo hapo akaanza kuinyonya midomo ya mama-mkwe wake. Hapana cheza na Efraim Donald! Zakia alipewa denda ambayo hakuwa ameitarajia kabisa, kisha akajitoa mdomoni kwa Efraim kwa ufupi na kusema kwa sauti tetemeshi, "Ef.... Efraim... tutachelewa... siwezi... Namouih atakasi...."
Efraim akamkatisha kwa kuendelea kumbusu mdomoni, na sasa akawa kama anamsukuma taratibu kuelekea usawa ule ambao kulikuwa na masofa na meza. Mwanamama huyo akaivunja busu hiyo na kuweka mikono yake kifuani kwa Efraim kama kumzuia, na ndipo Efraim akaishusha suruali ya Zakia mpaka usawa wa mapaja yake na kuyashika makalio yake makubwa kiasi yaliyobebwa kwa chupi safi nyeupe.
Zakia akashtuka na kuanza kuitoa mikono ya Efraim huku akijaribu kuukwepa mdomo wake, naye akasema, "Hii ni dhambi. Dhambi kubwa sana, siwezi ku... kama ni kwa sababu umenipa gari basi lichukue ila me siwezi kwa kweli..."
"Hahah... hiko kigari ndo unafikiri kimenitia kiburi nifanye hivi? Hamna. Nimekutamani tokea muda mrefu sana," Efraim akasema.
"Ati?!" Zakia akashangaa.
"Hao watoto ulotoka nao hawawezi kukupa kile unachostahili Zakia. Leo nataka ukipate kutoka kwangu," Efraim akasema.
"Siyo sawa... ah-ah. Namouih akijua... yaani leo birthday yake halafu tufanye hivi kweli?"
"Mbona we' ulitoka kula bata wakati Nasma anapitia mambo magumu sana?"
Zakia akabaki kumtazama.
"Samahani. Namaanisha... haupaswi kuacha mambo mengine yakuzuie kufurahia unachotaka... na mimi naweza kukupa hiyo furaha. Hali yako haijawa nzuri tokea mzee Masoud alipopanda juu, na nilitamani sana kukupa comfort ila kama ujuavyo mambo ni mengi huku. Sasa hivi nimeipata hiyo nafasi... nataka ujiachie tu kwangu ewe mrembo," Efraim akaongea kwa ushawishi huku akilitomasa kalio la Zakia.
"Mimi... sielewi jamani... Efraim..."
Mwanaume akawa ameanza kuibusu shingo ya mama-mkwe wake taratibu, naye Zakia akawa bado anababaika. Kisha, Efraim Donald akaishika blauzi ya Zakia na kupandisha juu, kitu kilichomfanya afichue tumbo la mwanamke huyo, naye Zakia akalegea na kunyoosha mikono hewani ili kumruhusu aitoe yote. Alikuwa amevaa sidiria nyeusi iliyoyanyanyua juu matiti yake makubwa kiasi, naye akabaki kuangalia chini kwa njia ya aibu. Kiukweli, ingawa alijua jambo hilo halikuwa sahihi, Zakia alikuwa mwanamke aliyependa sana kuonyeshwa kwamba "anatakwa," kwamba yeye bado ni mwanamwali mzuri anayeweza kutoa utamu kama binti mdogo tu, na kwa hilo alikuwa hajakosea. Aliyajua vizuri mapenzi, lakini hakuwahi tu kutazamia kuja kuombwa ayafanye na mkwe wake aliyemheshimu sana, na sasa hali hii ikawa inampa aina fulani ya msisimko uliompagawisha sana.
Kwa upande wake Efraim, kuweza kufanya mambo hayo na familia hii ilikuwa njia ya kujiburudisha tu kutokana na aina ya utu mbovu aliokuwa amejijengea. Alimuua Masoud kwa makusudi, akatumia matatizo ya Sasha kumrubuni msichana yule, na sasa akawa anaiharibu hadhi ya mama wa mwanamke aliyemwoa. Kwake ilikuwa ni sehemu tu ya ushindi wa mambo aliyotarajia kuvuna, na bado kuna mengi aliyotaka kuhakikisha anafanikisha. Ila kama ilivyokuwa kwa Sasha, jambo hili pia lilimsisimua sana, na alikuwa amepanga kuliweka kuwa historia isiyosahaulika akishatoka hapo.
Zakia akiwa anajishauri bado, Efraim akaanza tena kumpiga denda, ikiwa ni kama analazimishwa kufanya hivyo. Lakini mwanaume huyo hakuwa na shaka yoyote kwamba mama-mkwe wake aliyatamani sana mambo hayo, na hapa alikuwa hatoki bila kumwonyesha nini maana ya jina lake. Efraim Donald! Akamsukuma kidogo baada ya kuacha kumnyonya mdomo na kufanya Zakia aangukie kwenye sofa, uso wake bado ukionyesha kutokuwa na uhakika sana, naye Efraim akavua T-shirt aliyovaa na kuirusha pembeni, kisha akaanza kuufungua mkanda wa suruali yake. Zakia alikuwa anamwangalia kwa njia ya hofu kiasi, akiwa ameikunjia mikono yake kifuani kama vile anakificha, naye Efraim akatabasamu kwa kiburi.
Ni baada tu ya mwanaume huyo kuifungua zipu ya suruali na kuishusha ndipo Zakia akaangalia pembeni kama vile hataki kuona kilichotolewa mbele yake. Efraim Donald akaushika uso wake na kuutazamisha upande wake, naye Zakia akamwangalia machoni.
"Najua we' ni mjuzi. Usione aibu. Jiachie kabisa. Sidhani kama hata Namouih anakuzidi kwenye nyanja za mapenzi maana kama sikosei wewe ndiyo uliyemfundisha, si ndiyo?" Efraim akasema.
Zakia akabaki kimya na kuibana midomo yake kana kwamba amezila.
Efraim Donald akaitoa suruali yake yote baada ya kuvua viatu kwa chini, akiwa amebaki na boksa nyeusi tu sasa, kisha akasema, "Nionyeshe mautamu yako mama... na mimi nitakupa chochote kile hata usipokiomba."
"Kwa hiyo ni sawa na kusema unataka kuninunua," Zakia akamwambia.
"Hapana. Nataka tu kuula utamu wako mama... nimesubiri kwa muda mrefu. Usiogope, Namouih hawezi kujua. Na hautajuta," Efraim akaongea kwa ushawishi.
Zakia akakunja midomo na kuangalia pembeni kama mwanamke anayedengua, naye Efraim akamsukumia tena kwenye sofa hilo ili aliegamie kwa njia ya kuulaza mgongo wake. Zakia alikuwa anamwangalia kwa kumshusha na kupandisha haraka-haraka, naye Efraim akaivuta suruali ya mwanamke huyo na kuitoa yote, akimwacha na chupi yake na sidiria pekee mwilini. Zakia akatoa ishara ya msalaba huku akiwa amefumba macho, na baada ya Efraim kuona hilo akachekea kwa chini. (........).
(........).
(........).
(........).
(........).
(........).
Wakati akiwa anampa mahaba kwa mtindo huo, Efraim akaiokota suruali yake hapo chini na kuitoa simu yake, kisha akawasha camera yake na kuweka katika mfumo wa kurekodi. Akawa anachukua mkanda mzima wa namna alivyokuwa anakula penzi la mama-mkwe wake, na hata maneno ambayo Zakia angeongea yaliingizwa vyema ndani ya spika za simu hiyo. Akaendelea kumpa mahaba hayo na kumhamishia kitandani, Zakia akijihisi hoi, naye akampa cha mwisho baada ya mama-mkwe wake kuwa amemwaga raha zake mara nne mfululizo. Efraim Donald akajiachia ndani kabisa ya Zakia, kisha akalala pamoja naye kitandani na kuanza kucheka kwa sauti ya chini baada ya kumwangalia mama huyo na kuona jinsi alivyokuwa amelegea.
"Ahahah... sasa je? Nani mtamu kama wewe?" Efraim akasema.
"Hhh... hhh... hii ni dhambi nzito sana Efraim..." Zakia akasema huku amefumba macho.
"Dhambi yenye uzito mtamu. Yaani mmebarikiwa sana nyie watatu, siyo siri," Efraim akamwambia.
Zakia akamwangalia, kisha akauliza, "Watatu? Unamaanisha nini?"
Efraim akaachia tu tabasamu la kiburi.
"Nani mwingine? Unamaanisha mimi, Namouih... na Sasha?" Zakia akauliza.
"We' unafikiri nani mwingine?"
"Unataka kuniambia na Sasha ume...."
"Tena bado bichi na litaendelea kuiva," Efraim akajibu kwa kejeli.
Zakia akajiketisha akiwa anamwangalia kwa mkazo, kisha akasema, "Yaani umeshatembea na Sasha pia? Lini? Jana? Jana mlivyoondoka?"
"Hebu acha kuigiza kwamba unajali saana Zakia, haikupendezi. Najua ulikuwa unam-despise sana huyo mtoto, kwa hiyo maigizo yako hayana faida yoyote hapa."
"Sasha ni mtoto wangu. Siwezi nikamruhusu mtu yeyote amharibu!"
"Aharibike kwa kipi wakati yeye mwenyewe anaiomba hii kitu uliyotoka kuililia sasa hivi tu?"
"Wewe ni mtu wa aina gani?"
"Mtoa utamu... hhahahahah...."
"Haiwezekani. Namouih lazima ajue kila kitu... nitamwambia unayofanya..."
"Halafu? Umesahau kwamba na wewe uko ndani ya hilo duara au?"
Zakia akabaki kimya.
Efraim Donald akajinyanyua na kuketi pia, kisha akamwambia, "Najua una akili kuliko unavyojionyesha Zakia. Acha kujifaraghua na ufurahie kile utakachopata kutoka kwangu, full stop. Mambo nitakayofanya na Sasha au Namouih, ni yetu binafsi, kama tu ambavyo na wewe umekuwa jambo langu binafsi. Imenipa furaha sana kupita nanyi warembo, mzee Masoud aliniachia vitu vizuri sana... ahhahahah..."
Zakia akawa anamwangalia kwa njia ya hasira.
"Hhh... two down, one to go. Haitakuchukua muda mrefu wala. Ukimwambia Namouih lolote lile ni wewe tu ndiyo utakayeumia. Jitahidi kutumia akili yako uliyopewa na ufanye ulichobakiza kufanya tu; kuwa mama mzuri... bila kusahau kunipa utamu," Efraim akamwambia kwa dharau.
Akakishika kidevu cha Zakia akiwa na lengo la kumbusu mdomoni, lakini Zakia akatazama pembeni kwa hasira na kuutoa mkono huo kwa nguvu.
Efraim Donald akacheka kidogo, kisha akaweka uso makini na kusema, "Kavae nguo. Tunaondoka... mama-mkwe."
Zakia akamwangalia kwa hisia kali, naye Efraim akampa ishara ya busu kwa midomo yake, kisha akatoka kitandani hapo na kwenda kuvaa nguo zake. Alipomaliza hadi kuvaa bado Zakia alikuwa amekaa tu kitandani akitazama chini kwa kuhisi majuto na aibu, naye Efraim Donald akamkubusha kuwahi ili waondoke haraka, akionyesha wazi kwamba hakujali hisia za mwanamke huyo baada ya kupata alichotaka. Akaanza kulia sana ndani ya chumba hicho akijilaumu kwa kushindwa kutenda kwa busara kabisa, na hakujua angeweza vipi kuwatazama tena binti zake machoni baada ya haya yote.
Efraim Donald alikuwa anahakikisha anaiachia familia hii mvurugo wa hali ya juu, na hata baada ya kutoka hapo moyoni mwake alikuwa akijisemea "na bado."
★★★★★★★★★★★★
ITAENDELEA
★★★★★★★★★★★★
Usikose sehemu za mwendelezo wa hadithi hii kali ya CHANGE. Ni story nzuri na ndefu sana. Waweza ipata nakala yote kwa gharama nafuu sana. Karibu WhatsApp au kwa inbox ya hapa hapa JF.
WhatsApp no: +255 678 017 280