moneytalk
JF-Expert Member
- Jan 23, 2017
- 7,976
- 16,769
mbona hivyo sasa[emoji849][emoji40]
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
mbona hivyo sasa[emoji849][emoji40]
Eti hataki 😁mbona hivyo sasa
tumependana wenyeweEti hataki [emoji16]
Yng [emoji102]mbona hivyo sasa
DaahDYLAN
Story by Elton Tonny
Familia, Kazi, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Unyanyasaji, Usaliti, Visasi, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa
(R-rated 18+)
Enjoy!
★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA NANE
★★★★★★★★★★★★
"Hospitali gani?" Fetty akauliza kwa presha.
Kisha akaishusha simu kutoka sikioni na kumwangalia Dylan usoni kwa hofu.
"Vipi Fetty?" Dylan akauliza kwa kujali.
"M..mdogo wangu....amegongwa na gari!" akasema huku anaanza kulia.
Dylan akashangaa sana.
"Nahitaji kwenda Dylan...asante kwa kila kitu..." Fetty akasema huku akianza kuondoka.
"Subiri kwanza Fetty. Siwezi kukuacha uende mwenyewe, ninakuja nawe. Wamempeleka hospitali gani?" Dylan akamuuliza huku anamwita muhudumu kwa kiganja.
Baada ya Dylan kulipa pesa ya chakula ambacho hata hawakuwa wamemaliza, walianza kuondoka kutoka hapo upesi sana na kuingia kwenye gari, kisha kuanza safari huku Fetty akimwelekeza hospitali ilipokuwa. Binti alikuwa na wasiwasi sana, naye Dylan alijitahidi kuendesha kwa kasi ili waweze kuwahi kule. Ilikuwa sehemu ya mbali kiasi kwa kuwa iliwachukua dakika kama 30 kufika kule. Fetty alishuka upesi kutoka ndani ya gari na kukimbilia mule ndani ya hospitali, Dylan akimfuata kwa nyuma.
Mwanadada huyu alimkuta mama yake, mvulana mwingine mdogo, mwanaume fulani mwenye umri mkubwa kidogo kumzidi Fetty, pamoja na kijana fulani wakiwa eneo la nje ya chumba cha matibabu. Mama yake Fetty alikuwa analia, na baada ya kumwona binti yake akazidi kulia na kumfata. Fetty akamkumbatia na kuanza kuuliza hali ya mdogo wake aliyegongwa na gari.
"Wamekataaaa....wamekataaa..."mama yake akawa anasema huku analia.
"Wamekataa nini? Mama..." Fetty akasema kwa huzuni.
"Wanasema hawawezi kumfanyia matibabu kwa sababu hatuwezi kulipia!" yule mwanaume akamtaarifu.
"Nini?! Yaani....wamesema...kwa hiyo Sophia...Sophia wamemwacha tu?!" Fetty akauliza huku analia.
"Eee..." mwanaume huyo akajibu.
"Ameumia vibaya sana Fatuma...wanataka hela ili kulipia mambo yatakayohitajika kumtibia....na ni hela nyingi sisi hatuna...aaahahaaaa....nitafanyaje mama anguu mimi...Sophia atakufaaa!" mama yake akaendelea kulia kwa uchungu mwingi.
Fetty alichanganyikiwa. Hakujua afanye nini, kwa sababu hakutegemea jambo hili hata kidogo la sivyo angekuja hata na hela kidogo alizotunza. Dylan alikuwa pembeni anasikia kila kitu, na hapo hapo akaja daktari na muuguzi mmoja. Mama yake Fetty akawafata na kuanza kulia sana akiwaomba wamsaidie ili binti yake asipatwe na madhara, lakini daktari huyo akasisitiza kwamba ni LAZIMA Sophia alipiwe KWANZA ndiyo apewe matibabu.
Dylan alimshangaa. Alijiuliza ikiwa hapo palikuwa ni hospitali kweli au kituo cha biashara! Yaani kuna msichana ambaye bila shaka alikuwa mdogo sana hapo na alikuwa anapambania maisha yake, lakini hawa watu walichojali ilikuwa pesa tu. Akamfata daktari huyo na kumgeuza ili amtazame.
"Nisikilize. Ninataka madaktari wote waliopo hapa waje kumhudumia huyo msichana kimatibabu haraka. Sasa hivi!" Dylan anatoa amri.
Wote waliokuwepo hapo walimshangaa. Daktari akamwangalia kwa njia ya kujiuliza ni nani huyo, naye Dylan akamtazama muuguzi.
"Nenda kawaite wote wanaohitajika hapa na waje na madude yao yote ya kumsaidia, haraka sana. Pesa yote nalipia mimi," akasema kwa uhakika.
Muuguzi akabaki kumwangalia tu kama kachanganyikiwa.
"Harakisha!" Dylan akafoka.
Muuguzi huyo akatoka hapo haraka na kwenda kufanya alivyoagizwa. Daktari huyo akashusha pumzi kisha kwenda upesi kwenye chumba alichokuwepo Sophia, mdogo wake Fetty. Mama yake Fetty alimtazama sana Dylan kwa matumaini, naye akamsogelea na kuanza kumshukuru sana kwa jambo hilo, ijapokuwa hakumfahamu. Dylan alimwonea huruma sana mama huyo, kwa kuwa alilia kwa njia iliyomfanya kijana ahisi simanzi nzito ndani yake.
Sekunde chache tu, madaktari wawili na wauguzi kadhaa wakapita hapo kuelekea kile chumba, wakiwa wamebeba vifaa mbalimbali vya kimatibabu. Fetty alikuwa analia bado huku anamwangalia sana Dylan, na mama yake akawa amemkumbatia yule mvulana mdogo huku anasali ili Mungu asaidie binti yake awe salama.
Hospitali hii haikuwa kubwa, hivyo Dylan alijua wazi matibabu ya hapo yangekuwa na kikomo fulani, kwa hiyo ingekuwa muhimu binti huyo akipelekwa kwenye hospitali kubwa ili apate matibabu mazuri. Lakini kwa kuwa alihitaji uangalizi fulani baada ya kuachwa tu muda wote huo, Dylan aliona ni sawa wakimshughulikia kwanza, ili akiwa kwenye uafadhali kutoka hatarini, basi wamwamishe. Dylan akatoka hapo ili kwenda sehemu ya malipo, naye Fetty akamfata.
Walipofika kule, waliuliza gharama iliyohitajiwa, na baada ya mahesabu kupigwa ya kila jambo lililohitajiwa,wakasema ni kwenye laki 4. Fetty aliona ni kama walikuwa wanafanya wizi, lakini hangeweza kusema lolote na kubaki kumtazama tu Dylan. Mwanaume akatoa wallet yake na kuchomoa kadi ndogo ya benki, kisha akampatia mhusika wa malipo na kusema atoe laki 5 kamili. Baada ya kukamilisha hilo, akachukua kadi yake na kumwangalia Fetty, ambaye alikuwa anamtazama sana machoni. Binti akaanza kumshukuru mno na kumwambia angefanya yote awezayo kumlipa siku moja, lakini Dylan akakanusha na kumwambia hakuhitaji kufanya hivyo. Wote wakarejea kwa wengine kule walikowaacha, na baada ya Fetty kumwambia mama yake kwamba Dylan alilipia, mama huyo akaanza kumshukuru jamaa huku akilia. Dylan akamtuliza kwa kumkumbatia; kitu ambacho kiliufariji sana moyo wa Fetty.
Waliendelea kukaa hapo mpaka inafika saa 6 usiku. Mama yake Fetty alikuwa amewasimulia kilichompata Sophia. Binti huyo, alikuwa ameagizwa na mama yake kufata mzigo fulani kwa rafiki yake kwenye mida ya saa 3, ndipo akapigiwa simu baadae na kuambiwa binti yake aligongwa na gari. Kwa hiyo kwa kiasi kikubwa mama huyo alijilaumu kwamba ni makosa yake bintiye kugongwa kwa kuwa ni yeye ndiye aliyemtuma, lakini Fetty na yule mwanaume mwingine wakawa wakimwambia asijilaumu na kumtia moyo kwamba Sophia angekuwa sawa. Wauguzi walitoka na kuingia mara kwa mara kwenye chumba hicho bila kusema lolote kuhusu hali ya binti, kisha baadae madaktari watatu wakatoka pia.
"Dokta, dokta, mwanangu anaendeleaje?" mama yake Fetty akauliza baada ya kuwafata.
Daktari mmoja akaondoka, akiwaacha wawili hapo; mmojawapo akiwa ni yule wa kwanza kabisa kufika.
"Tumejitahidi kuzuia damu zisiendelee kuvuja na tumeziwekea mihogo sehemu za shingo na mguu wake mmoja kwa kuwa zimevunjika. Bado amepoteza fahamu lakini tutaendelea kumwangalia ili kuhaki...."
"Nani anamwangalia sasa hivi wakati wauguzi wote wameondoka?" Dylan akamkatisha daktari huyo kwa uthabiti.
Madaktari hao wakamwangalia kwa hisia kali.
"Huyu ndiyo aliyekuwa anafoka hapa?" daktari yule wa pili kuingia kwenye chumba cha Sophia akamuuliza mwenzake kwa kiburi.
"Siyo kufoka...mlichokuwa mnafanya hakikuwa sahihi," Dylan akamwambia.
"Kijana nisikilize... hii ni hospitali na ina sheria zake. Hautakiwi kuongea vitu usivyovijua. Bila sisi unajua huyo binti hangekuwa salama..."
"Nyie mlichokuwa mnajali si ni pesa tu? Inaamanisha mgemwacha tu mpaka akafa!" Fetty akasema kwa hisia za huzuni.
"Fatuma usiongee hivyo..." yule mwanaume akamwambia.
"Haujui mambo vizuri dada. Sehemu hii ina sheria zake za kufata kama sehemu zingine, na ni lazima tuzifate tu. Kama hamjui, ni kwamba mgonjwa hawezi kuhudumiwa ikiwa hawezi kulipia. Hilo ni jambo halali hata kisheria... kwa hiyo hakuna njia yoyote ya kuweza kutulaumu hata kama nini kingetokea," daktari akasema.
"Nyie ndiyo mnaokosea! Sheria za wapi hizo zinazowaruhusu mmwangalie tu mtu aliye hatarini eti kisa hawezi kulipia?" Dylan akauliza.
"Ni mambo ambayo sisi tumebobea...wewe huwezi kuelewa. Kwa kuwa umeshatoa hela endeleeni kusubiria tu, sisi ndiyo tunaojua mambo vizuri zaidi ya NYINYI," daktari yule mwenye kiburi akasema.
"Wewe ndiyo unajifanya unajua sana lakini hujui lolote!" Dylan akamwambia kwa uthabiti.
"Basi jamani inatosha. Haina haja ya kulaumiana," mama yake Fetty akawaomba.
"Kwa hiyo we ndiyo unajua sana sheria za hospitali? Hebu nielezee..." daktari huyo akamwambia Dylan.
"Najua ndiyo kwamba huwa inahitajika hospitali na madaktari wapewe malipo mgonjwa anapohitaji huduma, na mnaruhusiwa kukataa kutoa huduma ikiwa mgonjwa hawezi kulipa. Lakini hamruhusiwi kukataa IKIWA kufanya hivyo kutamsababishia madhara makubwa," Dylan akawaambia.
"Ndiyo unavyojidanganya?" daktari huyo akamwambia Dylan.
"Wewe ndiyo unajidanganya. Madaktari wanatakiwa wawe watu wanaohangaikia hali za wanaoumia siyo tu kwa sababu ya kupata pesa, bali kwa sababu wanawajali. Unapotambua kwamba mtu ana Urinary Tract Infection (UTI) mbaya sana kwa mfano, halafu ukakataa kumsaidia, ni lazima utawajibika kisheria ikiwa tatizo hilo litaongezeka na kuidhuru figo yake. Huyu hakuwa mgonjwa, alikuwa amejeruhiwa vibaya ghafla sana. Mnakosa hata ubinadamu kweli? Ikitokea huyu msichana akapatwa na madhara kwa sababu ya ujinga huu ninawaahidi lazima nitawafungulia kesi kwa sababu mnafanya medical malpractice kwa kisingizio kisicho na kichwa wala miguu."
Dylan aliongea yote hayo kwa mkazo sana. Wote walikuwa wakimwangalia kwa makini, hata madaktari wakabaki kumtazama tu kwa kushangaa jinsi alivyosema mambo kwa uhakika. Baadhi ya watu wachache walikuwa wamesogea hapo kuangalia malumbano hayo, hivyo Dylan akaondoka ili asije akatenda kwa njia ambayo isingependeza. Fetty alimwangalia kwa hisia sana hadi alipoishia kwenye kona na kutokomea.
"Huyo mwanaume anajiona yeye ni nani?" daktari akawauliza waliobaki hapo.
Fetty akamwangalia tu, kisha akaondoka ili amfate Dylan. Alimtafuta huku na kule bila kumwona, kisha akaamua kutoka hadi nje na kumkuta akiwa amesimama pembeni ya gari lake; akionekana kuongea na mtu fulani kwenye simu. Fetty akamwangalia sana kwa sekunde kadhaa hadi alipomaliza kuongea na simu, naye akamfata pale alipokuwa amesimama.
"Dylan..." akaita baada ya kumkaribia.
"Fetty..." Dylan akasema baada ya kumwona.
Fetty akasogea karibu yake na kumtazama tu.
"...samahani Fetty...sija...sijatenda kwa njia nzuri mule ndani," akamwambia.
"Acha masihara basi! Yaani isingekuwa wewe kuwaambia ukweli mimi hata ningepigana nao kabisa," Fetty akasema.
"Ahahahah... kweli?"
"Ndiyo. Wamezidi sana kutuonea yaani... kwa sababu tu hatuna hela wanatutendea kama hatufai. Kuna kipindi mmama mmoja jirani yetu, mwanae aliumwa sana. Akamleta akiwa amembeba mgongoni akiwaomba wamsaidie lakini wakawa tu wanamweka pembeni. Kakaa kusubiri analia, analia, analilia msaada... wapi. Mtoto wake akafa akiwa mgongoni kwake!" Fetty akasema kwa huzuni.
Dylan alitikisa kichwa kwa kutoamini kabisa. Hakuelewa watu hawa walikuwa na mafunzo ya aina gani ya kutoa huduma kwa wagonjwa, lakini ni wazi watu wengi waliumizwa na vitendo hivyo.
"Dylan, ninaomba nikushukuru tena kwa kutusaidia. Ninakuahidi nitajitahidi...."
Dylan akamkatisha kwa kuweka kidole mdomoni mwake. Fetty akabaki kumwangalia tu usoni.
"Na mimi ninakuomba usije kurudia tena kusema utanilipa. La sivyo sitakusemesha milele," akamtania.
Fetty akatabasamu kwa kufarijika, naye Dylan akamkumbatia. Kumbatio hili lilikuwa la faraja kutoka kwa Dylan, kwa maana yeye alizoea sana vitu kama hivi vya wazungu-wazungu kwa sababu ya kuishi muda mrefu Brazil. Lakini kwa Fetty, liliamsha hisia fulani kumwelekea Dylan ambazo kwa kiasi fulani alikuwa akijaribu kupingana nazo, ila ni kama zikawa zinakita mizizi tu.
Baada ya kumwachia, wakarudi ndani pia, kukuta mama yake na yule mvulana mdogo wamekaa huku wakisinzia. Yule mwanaume aliyekuwa hapo, akamwambia Fetty kwamba alihitaji kurudi nyumbani, na angekuja kesho kuangalia hali ya Sophia. Akaondoka pamoja na yule kijana mwingine, na ni hapa ndipo Fetty akamjulisha Dylan kwamba huyo mwanaume alikuwa mdogo wa mama yake, yaani mjomba wake Fetty, na yule kijana alikuwa ni mtoto wa rafiki yake aliyekuwa akiishi kwake. Mvulana yule mdogo aliyekuwa amelala hapo pamoja na mama yake ni mdogo wake Fetty pia, aliyeitwa Japhet. Dylan akapendekeza kwamba itafaa kama akiwapeleka nyumbani mama yake na mdogo wake, halafu yeye na Fetty wakae hapo hospitali mpaka asubuhi.
Wakawaamsha, na ijapokuwa mwanzoni mama yake aliweka kipingamizi cha kutotaka kurudi nyumbani, Fetty alimshawishi kwa kumwambia alihitajika kuwa na Japhet nyumbani pia kwa kuwa ni mdogo, hivyo yeye angebaki kumwangalia Sophia ili wenyewe wakapumzike. Baada ya kukubali, Dylan akambeba Japhet na kutangulia naye nje, na ni hapa ndipo mama yake Fetty akamuuliza binti yake Dylan alikuwa ni nani hasa. Fetty akamweleza ni rafiki yake tu mzuri na mkarimu sana, na baada ya hapo wakaenda nje pia mpaka kwenye gari la jamaa.
Fetty yeye alibaki hospitalini, kwa hiyo Dylan aliwapeleka mama yake binti na mtoto nyumbani kwa kuelekezwa na mama huyo. Hapakuwa mbali mno, mwendo wa dakika kama 7 hivi ulitosha kuwafikisha, kisha Dylan akarejea hospitalini tena; ikiwa ni saa 7 usiku sasa. Alimkuta binti akiwa ameketi tu kwenye benchi, naye akaenda kukaa pamoja naye. Aliuliza kama kulikuwa na jipya, naye binti akakanusha.
"Uko sawa Fetty?" Dylan akauliza kwa kujali.
"Ndiyo. Niko sawa," Fetty akajibu kwa hisia.
Dylan akatulia kidogo na kuuliza, "Sophia ana miaka mingapi?"
"18."
"Anasoma?"
"Amemaliza kidato cha nne. Amefaulu vizuri unajua...ndiyo najitahidi kumtunzia ili aendelee...lakini sikuzote maisha yana njia ya kunifanya nivunjike tu moyo," Fetty akasema huku machozi yakianza kumtoka.
Dylan akaanza kuusugua-sugua mgongo wake kwa njia ya kubembeleza.
"Baba yetu alikufa nilipokuwa naingia chuo, siyo kikuu... nilikuwa tu nimemaliza form four nikaona niende chuo kwa kuwa sikutaka kupita kule juu kote...niliona mizunguko ingekuwa mingi. Yeye ndiyo alikuwa ananilipia... kwa hiyo kifo chake kilifanya isiwezekane kuanza. Lakini mama, na kazi yake ya ushonaji, alijitahidi kutusaidia sisi wote watatu tuendelee na elimu...na mimi nikawa nafanya shughuli ndogo ndogo nilipopata nafasi. Baadae nikaanza chuo... nika... nilipenda sana sheria...nikasoma kwa miezi michache ndipo tukagundua mama'angu ana shida fulani... kiafya..."
Yote haya Fetty aliyasimulia huku analia kwa kujikaza sana, naye Dylan akawa anamtazama kwa simanzi sana kadiri binti alivyoendelea kufunguka.
".....alihitaji kutibiwa...na pesa haikutosha... hata zile ndogo ndogo nilizopata hazikufikia kiwango kilichohitajiwa. Kwa hiyo ikabidi niachane tu na chuo...nikaanzakufanya kazi... za ndani. Karibu kila sehemu niliyofanya, walioniajiri walinitaka kimapenzi...nami nilijua wazi wangenitumia tu Dylan... sikuwa na akili chafu ya kutaka kukubali vitu hivyo...kwa hiyo ilikuwa ni kutoka hapa kwenda hapa kwenda kule....ahhhh...."
Akainamisha uso wake na kuufunika kwa viganja vyake. Dylan akaanza kuzilaza-laza nywele zake kwa wororo ili kumbembeleza. Kisha taratibu Fetty akaunyanyua uso wake na kutazama mbele.
"Nimejitahidi sana. Mambo mengi yalikuwa yanakatisha tamaa lakini nilijua sikupaswa kufanya hivyo. Familia yangu ilinihitaji sasa, kwa hiyo nilijua lazima nifanye yote kujitoa kwao...lakini siyo kwa njia za mkato. Angalau nilikuja kupata kazi kama hii niliyonayo sasa, nikatunza na kumsaidia mama...na wadogo zangu pia. Kwa hiyo... kwa muda fulani niliona niliweke suala la chuo pembeni ili...niitegemeze familia yangu pia. Ndugu zetu wa ukoo hawakujali kuhusu afya ya mama hata kidogo, ukitoa huyu mjomba wangu, angalau ni yeye tu ndiye aliyetusaidia mpaka kuhakikisha tunamsaidia mama... yaani Dylan wakati mwingine nahisi kushindwa sana... sana. Nina miaka 25 sa'hivi, na kilichopo akilini mwangu ni hali nzuri tu ya familia yangu... basi. Mdogo wangu huyu....I wanted her to have a bright future...and she's so intelligent... nini hiki sasa? Aah..."
Fetty aliongea kwa simanzi nzito mno mpaka Dylan akadondosha machozi. Dylan hakuwa mzuri sana wa maneno ya kufariji, hivyo akazungushia tu mkono wake mpaka kwenye bega la Fetty na kumvutia kwake, naye Fetty akalaza kichwa chake kwenye sehemu ya juu ya kifua cha jamaa, akiruhusu amfariji kwa njia hiyo kwa muda mrefu hapo.
Mpaka asubuhi inafika wawili hawa hawakusinzia hata kidogo. Dylan alikuwa ametafutwa mara kadhaa na Jaquelin, aliyeuliza kijana wake huyo alikokuwa, naye Dylan akasema tu alilala kwenye ile nyumba yake nyingine. Alimwambia huenda angechelewa kufika kazini, hivyo mambo ambayo angehitajika kushughulika nayo angeyafanya baadae. Ilipofika mida ya saa 2 asubuhi, madaktari walikuja kumwangalia Sophia, kisha wakawataarifu wawili hao kuwa inaonekana matibabu waliyompa jana yamesaidia kwa kuwa alionekana kutoka kwenye hatari. Dylan akawauliza ikiwa itakuwa sawa kumtoa hapo na kumpeleka kwenye hospitali nyingine, na wote wakamshangaa kwa kiasi fulani. Walijibu kuwa ndiyo inawezekana, lakini mpaka apelekwe kwa kutumia ambulance, na hata kabla hawajamaliza kuelezea, Dylan akatoka tu nje upesi.
Madaktari walimwona Dylan kama mtu fulani mwenye kujisikia sana, lakini kihalisi hilo halikuwa kweli. Alitoka na kumpigia simu Harleen. Alimweleza kwamba alihitaji msaada wake kwa kuwa rafiki yake alikuwa ameumia, hivyo angetaka apatiwe uangalizi bora kwenye hospitali kubwa kama aliyofanyia kazi Harleen. Harleen akakubali na kumwambia afanye mpango ili ampeleke huko haraka, hivyo bila kuchelewa akaenda sehemu ambayo angefanya mipango ya kuchukua ambulance ili wamtoe Sophia pale haraka.
Baada ya kurudi chumbani kwa Sophia, alimkuta Fetty humo na kumwambia kila kitu alichofanya, akimwacha binti anashangaa. Fetty alihofia gharama, lakini Dylan akamwambia asiwaze kabisa kuhusu hilo. Hivyo ikabidi Fetty ampigie mama yake ili kumjulisha yaliyojiri, na mama huyo akamwambia Fetty amshukuru sana Dylan kwa niaba yake.
Muda fulani baadae, Sophia alipelekwa taratibu mpaka kwenye ambulance ili safari ianze kuelekea hospitali kuu ya jiji. Wakati huu mama yake alikuwepo pia, naye alikuwa amewaambia kwamba alimwomba mdogo wake yule mwanaume awe kwake pamoja na Japhet kwa muda ambao angekwenda pamoja na Sophia kule hospitali kuu.
★★★
Zilipita siku tano baada ya Sophia kuamishwa kutoka kwenye hospitali ile, na bado alikuwa kwenye usingizi wa kupoteza fahamu (coma). Kwenye hospitali hii kulikuwa na madaktari wenye uzoefu wa hali ya juu, dawa za kila aina na vifaa vingi vyenye ubora, hivyo binti alihudumiwa vizuri sana. Sophia alilazwa kwenye chumba cha peke yake ghorofa ya tano ya jengo la hospitali hii, na ni Dylan ndiye aliyekuwa akilipia matibabu ya msichana huyo hapo hospitalini. Mama yake alikuja kila siku kwa usafiri ambao ni Dylan aligharamia nauli pia, ili aje kumwona binti yake na kurudi nyumbani pia wakati ambao angehitaji kuwa pamoja na Japhet. Ratiba ya Fetty ilimruhusu kwenda hospitalini kwenye mida ya saa 12 au saa 1 jioni pindi ambapo angemaliza kazi, hivyo ni muda huo ndiyo mama yake angerudi kule nyumbani kwake.
Mama yake Fetty alitaka sana kujua ikiwa Fetty alikuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na Dylan, kwa kuwa aliona msaada huo wote ambao kijana huyu aliwapatia haukuwa bure. Mara zote Fetty alimhakikishia kwamba wao ni marafiki tu, tena wamejuana kipindi cha karibuni tu. Mama yake alipendezwa sana na Dylan, hivyo alikuwa akimshawishi Fetty amzuzue jamaa (seduce) ili waweze kuwa pamoja, lakini Fetty hakuafikiana na wazo hilo. Hakutaka kufanya hali hii ionekane kama alitakiwa kujitoa namna hiyo kwa Dylan kwa sababu tu amemsaidia; aliona ingekuwa ni kama anajiuza kwake. Mama yake alikuwa mwenye nia nzuri tu, lakini bado binti akayapiga chini matarajio yake.
Dylan alikuwa akija pia kila jioni kumwona. Mara kwa mara alikutana na Harleen hapo, nao wangetazamana sana kisha Dylan angempa tu tabasamu na kuelekea upande mwingine. Bado roho ilimuuma sana Harleen, na mpaka wakati huu hakuwa ameachana na Alex, kwa sababu kihalisi alimpenda. Lakini tatizo lilikuwa kwamba alimpenda Dylan pia, hivyo hakujua jinsi ya kupima uzito wa upendo wake kwa wanaume hawa, na ni hicho ndicho kilichomfanya apoteze amani ya moyo kabisa.
Jioni hii Dylan alipokuja hapo hospitali kwenye mida ya saa 1, alimkuta mama yake Fetty akiwa mwenyewe kwenye chumba cha Sophia. Mara zote alipofika alikuta Fetty tayari yupo, lakini leo haikuwa hivyo. Akamuuliza mama yake kama amewasiliana naye, lakini akamjibu kuwa amempigia sana simu ila binti yake huyo hakupokea hata mara moja. Dylan pia akampigia, lakini hakupokea simu yake pia. Akapiga simu kwa rafiki yake kumuuliza kama bado wako kazini, lakini akamjulisha kwamba Fetty aliondoka mapema tu ili awahi nyumbani kujiandaa kwenda hospitalini. Hivyo Dylan akamwambia mama yake Fetty kuwa angemfata binti yake kule kule ili arudi pamoja naye upesi.
Alifika nje ya ile nyumba alikopanga Fetty, naye akaelekea moja kwa moja mpaka mule ndani akitumaini angemkuta. Kulikuwa na vyumba kadhaa vilivyopangiliwa kwa mzunguko, naye akapata kumwona mwanamke fulani hapo nje akiwa ameketi huku anakuna nazi. Akamsogelea na kumsalimu, kisha akauliza chumba cha Fetty kilikuwa ni kipi, na kama Fetty alikuwepo. Mwanamke huyo akakubali kwamba yupo, na baada ya kumwonyesha Dylan chumba hicho kilipokuwa, akakifata na kukuta mlango uko wazi kidogo. Akamwita Fetty huku anausukuma mlango na kuingia, na hapo akasimama kwa kutotarajia alichokikuta.
Fetty alikuwa amesimama huku akimtazama, na kulikuwa na mwanaume mwingine mweusi na mrefu humo akimtazama pia, bila shaka wote wakiwa wameshtushwa na Dylan baada ya kuingia tu humo ndani. Ilionekana ni kama walikuwa na maongezi, naye Dylan akajisikia vibaya kiasi kwa sababu aliingilia ubinafsi wa watu. Akatambua haikuwa adabu hata kidogo.
"Oh... samahani jamani. Ngoja nisubiri hapa nje..." Dylan akasema.
Fetty akamfata na kumshika mkono ili asitoke nje.
"Haina haja... tumeshamaliza kuongea," Fetty akasema.
"Huyu ni nani?" mwanamume huyo akauliza.
"Ni rafiki yangu, anaitwa Dylan. Dylan... huyu ni Sam," Fetty akawatambulisha.
"Niaje kaka?" Dylan akamsalimu jamaa.
"Aaaa... kwo' kumbe ni huyu ndiyo anafanya unanitendea hivi eti?" Sam akasema kiukali huku akianza kumwelekea Dylan.
Dylan akashangaa.
"Sam, Sam... siyo hivyo. Huyu ni rafiki yangu. Agh... me sitaki hayo mambo bwana, unajua sipendi," Fetty akasema kwa hisia kali.
"Kama umeshaanza kusuguliwa na mtu mwingine si useme tu? Unanizingua kisa nini sasa?" Sam akasema kwa hisia.
"Sam nakuomba uende... tutaongea wakati mwingine, nimeshakwambia nataka kwenda hospitalini mbona huelewi?" Fetty akamwambia.
Dylan alikuwa ameachwa njia panda kwa kuwa hakuelewa nini kinaendelea, lakini kwa akili ya haraka akatambua mwanaume huyo bila shaka alikuwa na uhusiano wa kimapenzi pamoja na Fetty. Sam akamwangalia Fetty kwa mkazo sana, kisha akampita na kumpamia Dylan kimakusudi kabla ya kutoka nje na kuondoka. Dylan akatikisa kichwa chake huku akicheka kimasihara, kisha akamwangalia Fetty, ambaye alionekana kutangatanga sana kiakili.
"Hivi ni kwa nini sikuzote wanawake wazuri lazima muwe na watu wenye akili kama za yule mwigizaji Zimwi?" Dylan akatania.
Bado Fetty alionyesha kutangatanga sana, hivyo, kwa huruma Dylan akamfata na kumkumbatia ili kumtuliza. Fetty alijibana kwenye mwili wa Dylan akijihisi vizuri sana kuonyeshwa na Dylan kwamba alimjali, huku pia bado akiwa na huzuni kwa sababu ya mambo yaliyotokea kati yake na Sam, naye Dylan akaendelea kumpa mwanamke huyu kumbatio hilo la faraja.
★★★★★★★★★★★★
ITAENDELEA
★★★★★★★★★★★★
Usikose sehemu za mwendelezo wa DYLAN. Waweza ipata yote kwa sh. 2000 tu WhatsApp. [emoji6]
WhatsApp no: +255 787 604 893
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]Yng [emoji102]
hahahaa elton umetisha sana na hicho kithungu cha hapo mwishoniDYLAN
Story by Elton Tonny
Familia, Kazi, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Unyanyasaji, Usaliti, Visasi, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa
(R-rated 18+)
Enjoy!
★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA TISA
★★★★★★★★★★★★
"Najua mambo ni mengi, lakini tunahitaji kwenda hospitalini... mama anasubiri," Dylan akasema kwa upole huku akiwa bado amemkumbatia Fetty.
Kisha akamwachia na kumwambia angemsubiri nje ili avae nguo alizohitaji kuvaa.
Baada ya kubadili nguo, Fetty akaenda pamoja na Dylan kwenye gari na kuelekea mpaka hospitali. Njia nzima ni kama Dylan alikuwa anaongea mwenyewe, kwa kuwa Fetty alijibu kifupi tu au kuwa kimya mpaka ikabidi Dylan akaushe tu. Walipofika kwenye chumba alicholazwa Sophia, mama yake Fetty alimuuliza kwa nini hakuwa akipokea simu wakati anampigia, naye binti akajibu kuwa aliiacha kwa jirani ili ipate chaji kwa kuwa umeme kwenye nyumba yao ulikuwa umeisha. Baada ya hapo mama yake akaondoka, akiwaacha wawili hao kwenye chumba hicho. Fetty aliketi kwenye kiti kidogo pembeni huku sura yake ikiwa bado inaonyesha ana huzuni.
"Ulikula?" Dylan akaanzisha maongezi.
"Ndiyo. Nimekula," Fetty akajibu bila kumwangalia.
"Hey mbona hivyo? Usinitendee kama boyfriend wako yule," Dylan akasema kimasihara.
Fetty akamwangalia, kisha akasema, "Samahani Dylan. Nimepatwa na stress tu basi ila siyo kwamba..."
"Fetty relax. Natania tu," Dylan akamtuliza.
Fetty akashusha pumzi na kuangalia chini.
"Sam umekuwa naye kwa muda gani?" Dylan akauliza.
Fetty akamtazama tu bila kutoa jibu.
"Haina haja ya kubeba mzigo huu mwenyewe. Mimi ni rafiki yako, tambua niko hapa kwa ajili yako," Dylan akasema kwa upole.
"Samwel ni.... nilikuwa natoka naye kimapenzi lakini..." akashindwa kuendelea.
"Kwa hiyo mliachana au?" Dylan akauliza.
"Aa... hapana. Ni muda mrefu sana yaani... baada ya muda unajua tu kwamba unahitaji kukua... nilihitaji muda wa kuwa mwenyewe... nafasi ya kuyajenga maisha yangu..."
"Okay, okay, nimeelewa. Ulihitaji muda wa kuyajenga maisha yako hivyo mahusiano ukaona uyaweke pembeni... lakini ukashindwa kumwambia jamaa hivyo," Dylan akasema.
"Siyo kushindwa Dylan yaani... nilimwambia kabisa kuwa ninahitaji muda sema... aahh jamani..." Fetty akaongea kwa kuvunjika moyo.
"Inaeleweka. Lakini, bado siyo fresh kumzungusha. Kama utaendelea naye mwambie, kama huwezi tena... sema. Ukifanya hivyo unakuwa unamwonea kwa kiasi fulani na bichwa lake lile," Dylan akasema.
Fetty akacheka kidogo na kumwangalia usoni. Dylan akatabasamu kidogo baada ya kumwona binti ameonyesha itikio zuri. Binti alijua alichosema Dylan kilikuwa sahihi na alihitaji afanye uamuzi haraka, kwa kuwa Sam alikuwa akisubiri kwa muda mrefu sana.
"Kesho nafungua rasmi restaurant yangu," Dylan akamwambia.
"Kweli?" Fetty akauliza kwa shauku.
"Ndiyo."
"Eh hongera. Uliniambia utaiitaje kweli?"
"Dy-Foods."
"Dah, haya bwana. Kwa hiyo kesho kutakuwa na pilau ya sherehe?"
"Pilau ya nini? Nafungua ili watu waanze kazi, siyo wacheze dansi."
"Umeshaweka na watu tayari? Umewaajiri lini wakati hujaufungua bado?" Fetty akauliza.
Dylan alianza kumwelezea jinsi alivyopangilia mambo mengi vizuri kwenye suala la mgahawa wake mpya. Fetty alipendezwa sana na werevu mwingi wa Dylan. Akatambua pia kwamba Dylan hakuwa aina ya mtu mwenye pesa anayejivuna sana, bali alikuwa mwenye usawaziko na mkarimu, ijapokuwa alikuwa mwenye utundu mwingi mno. Fetty akaahidi angekwenda kuuona wakati ambao angepata nafasi. Wakaendelea kupeana maongezi huku wakimwangalia Sophia, na baada ya muda Dylan akaondoka.
★★★
Upande wa Mr. Bernard, mipango yake pamoja na yule mtu mwingine ya kumwangusha Gilbert ilikuwa nyendoni. Mr. Bernard alikuwa mtu wa kutekeleza tu kile alichoambiwa na mtu huyo, kwa sababu yeye hakuwa mwanaume mwenye subira sana. Lakini mtu huyo alikuwa amemwambia wasubirie wakati mwafaka ili waweze kupiga hatua yao kwa umakini wa hali ya juu, na sasa wakati huo ukawa umewadia. Walichokuwa wanasubiri tu, ni ndege wao kuingia mtegoni, halafu wao waufyatue.
★★★
Ilikuwa ni furaha kubwa sana upande wa Fetty, kwa kuwa sasa Sophia alikuwa amerejesha fahamu tena! Binti huyo aliamka siku mbili kutokea usiku ule ambao Dylan alikutana na boyfriend wa Fetty, Samwel. Baada ya kupata taarifa, Dylan alikwenda hospitali upesi siku hiyo kwenda kumwangalia. Alimkuta mama yake Fetty pamoja na Fetty pia, nao wakamwambia Sophia kwamba wa kumshukuru kwa matibabu yake ni Dylan. Lakini Dylan hakutaka kuelekezewa sana fikra, na kwa busara akasema tu kwamba alisaidia kama mama na dada yake walivyosaidia pia.
Sofia alikuwa amewekewa kifaa cha kuizuia shingo yake isishtuke, kwa kuwa ilihitaji muda mrefu wa kukaa usawa mmoja ili kupona, hivyo hangeweza kuigeuza. Mguu wake mmoja ulikuwa umevunjika kwa ndani na hivyo kuwekewa vifaa vya kuusaidia unyooke tena; ukizibwa kwa muhogo mnene sana kuanzia kwenye goti mpaka nyayoni. Hakuweza kutoa sauti vizuri, hivyo Dylan akampa njia ya kuwasiliana kwa kumwambia atumie macho kujibu walipomsemesha; mfano kama akikubali kitu, anafumba na kufumbua, lakini akikataa, asifumbe macho hata kidogo.
Baada ya muda fulani, mama yake Fetty akasema kwamba Japhet, aliyekuwa kule nyumbani kwao, aliomba sana aje huku kumsalimia dada yake baada ya mama yake kumwambia ameamka, hivyo mama Fetty akasema angeondoka ili kumfata. Lakini Dylan akamwambia haikuwa na haja ya kwenda, bali yeye mwenyewe angemfata ili mama huyu awe na binti yake hapo. Fetty akasema angekwenda pamoja naye pia, hivyo wakaondoka na kuanza kuelekea nyumbani huko.
Kufikia sasa Dylan alikuwa ameshaufungua rasmi mgahawa wake wa Dy-Foods, na ulikuwa wa kisasa sana wenye kuvutia wengi. Ijapokuwa mwonekano wa mgahawa huo ulikuwa wa kifahari kwa kadiri fulani, hiyo hsikumaanisha kwamba ulikuwa kwa ajili ya wenye pesa tu, kwa kuwa watu wote walikaribishwa pale. Alikuwa ameajiri wahudumu sita, wapishi wanne, na mwanaume fulani aliyeitwa Tony ambaye alikuwa kama msimamizi hapo (manager). Alikuwa anataka kuajiri mtu mwingine awe ndiyo msimamizi msaidizi (assistant manager) hapo, na wa kwanza kwenye akili yake hakuwa mwingine ila Fetty.
Dylan alijua Fetty alikuwa na uzoefu pia kwenye masuala ya migahawa, hivyo bila shaka jambo hilo lingemsaidia, kama Fetty alivyosema kipindi kile, kuyajenga vizuri maisha yake. Hakuwa mwanamke aliyetaka vitu maishani kwa njia ya mkato, bali kuvifanyia kazi, kwa hiyo Dylan alihisi hiyo ingekuwa njia nzuri ya mwanzo ya kumsaidia kwa kadiri fulani. Wazo hili alimpatia wakati wakielekea kule kwao, naye Fetty alionekana kutokuwa na uhakika ikiwa angeweza. Lakini Dylan alimhakikishia kwamba aliamini aliweza, hivyo aamue ikiwa angekubali ofa hiyo. Fetty akamwambia angelifikiria kwanza suala hilo, naye Dylan akaridhia kwa kusema angesubiri jibu.
Walifika kwao binti baada ya dakika kadhaa, kisha wote wakashuka na kuelekea usawa wa nyumba yao. Dylan akamwambia Fetty aende tu ndani kumpanga dogo na yeye angemsubiri hapo nje. Binti akaingia ndani na kumkuta Japhet pamoja na mjomba wake wakiwa wamekaa, naye akaanza kuwaambia kuhusu hali ya Sophia kule hospitali. Akamwambia Japhet aende kujiandaa haraka ili waondoke, kisha akamuuliza na mjomba pia ikiwa alitaka kwenda, lakini akakanusha na kusema alihitaji kufanya jambo fulani, hivyo angeenda kesho.
Basi baada ya hapo Japhet akawa amerudi, akiwa amevaa nguo nyingine pamoja na viatu, kisha yeye na dada yake wakamuaga mjomba wao na kuanza kuelekea nje. Walipofika nje tu, Japhet akasema amesahau kitu chumbani, hivyo dada yake akamwambia awahi kukifata na angemkuta nje anamsubiria. Fetty alimkuta Dylan akiwa ameketi kwenye benchi dogo huku anatazama upande mwingine pale nje. Alipomwangalia vizuri, aliona Dylan akicheka peke yake na kumfanya ajiulize ni nini kilichomchekesha.
Akamfata mpaka hapo alipokuwa amekaa.
"Dylan..." Fetty akaita.
Dylan akageuka na kusimama baada ya Fetty kusogea karibu.
*Vipi... mbona unacheka mwenyewe?" Fetty akauliza.
Dylan akaachia tabasamu na kutazama upande ule aliokuwa anaangalia. Baada ya Fetty kuangalia huko pia, aliweza kuona mtoto mdogo wa jirani, mwenye miaka kama miwili hivi, akiwa amevaa chupi iliyotera kwa nyuma kufikia chini ya mapaja, huku akiwa anachukua michanga chini na kujimwagia kwa kuigiza kama anaoga! Fetty alishangaa na kuanza kucheka, kisha akamwita mama ya mtoto huyo kwa sauti kubwa, ambaye alikuwa jikoni akipika, na kumwambia amzuie mwanae. Mwanamke huyo akafika hapo na kumtoa mwanae haraka.
"Yaani Dylan, badala umsaidie mtoto we unamcheka!" Fetty akamwambia.
"Ahahahah... dogo alikuwa ameweka show nzuri hapo, lakini siyo yeye tu ndiyo amenifanya nicheke," Dylan akasema.
"Kilichokuchekesha ni nini sasa?" Fetty akauliza.
"Nilikuwa nakuwaza... umekuzwa huku pia kwa hiyo... nikapigia picha kwamba ulivyokuwa mtoto ulikuwa unafanana na vile huyo dogo amepauka," Dylan akasema kiutani.
Fetty akacheka na kumwambia, "Nilikuwa zaidi ya hapo."
"Kweli?! Ahahahah... sipati picha jinsi enzi hizo ulivyokuwa kachafuuu... afu' leo mishebeduo kama yote..." Dylan akamtania.
"Em' toka hapa!" Fetty akamwambia huku akicheka.
Ni wakati huu ndipo Japhet akawa amerejea.
"Sh'kamoo..." kakamsalimu Dylan.
"Aam... mahaba," Dylan akaitikia.
Fetty akacheka.
"Yaani hujui hata kuitikia shikamoo?" Fetty akamuuliza.
"Sijazoea," Dylan akasema.
"Nani alikulazimisha ukasome nje ya nchi? Ni mama yako eti?" Fetty akauliza.
"Umesema kwa usahihi, lakini umeotea," Dylan akajibu.
"Ahahahah... eti nimeotea!" Fetty akasema.
"Okay, kwa hiyo... ndani mambo yako fresh?" Dylan akauliza.
"Ndiyo. Tuondoke sasa," Fetty akasema.
"Sawa."
Walirudi kwenye gari na kuanza kuelekea hospitalini. Njiani Dylan alinunua vyakula mbalimbali vizuri sana ili waende kukamua pamoja kule hospitali. Kiukweli mambo yote Dylan aliyofanya yalizidi kuongeza upendezi ambao Fetty alikuwa nao kumwelekea, bila kupenda! Wakafika hospitalini mida ya saa 12 jioni, naye Japhet akapelekwa hadi kwenye chumba cha dada yake. Sophia alifurahi sana kumwona mdogo wake tena, na wote wakaanza kumtuliza kwa kuwa alikuwa akilia kwa furaha baada ya kuwaona watu aliowapenda wakiwa hapo.
Dylan aliondoka baadae kwenye mida ya saa mbili, akiwaacha wote pale baada ya kushiriki nao chakula alichowaletea. Japhet alimtania sana Fetty kwamba 'amepata mchumba,' na kwa kiasi fulani maoni hayo yalimkosha moyoni huyu dada ijapokuwa alikanusha mara nyingi kwa kusema walikuwa ni marafiki tu. Bila wao kujua, Dylan alikuwa amefanya mpango wa kumlipia Sophia huduma ZOTE alizohitaji hospitalini hapo mpaka wakati ambao angeachiwa na kwenda nyumbani. Hiyo ilikuwa ni pesa ndefu kwa sababu alitaka Sophia atendewe kama vile ni mtoto wa mfalme hapo hospitalini.
★★★
Baada ya Dylan kufika nyumbani, alienda zake chumbani kuoga, na kisha akarudi tena sehemu ya sebule na kuketi. Mama yake hakuwa amefika bado, lakini baba yake alikuwa hapo ameketi tu kwenye sofa. Dylan akamuuliza Gilbert mama yake yuko wapi, naye akamwambia ametoka na rafiki yake mmoja ila yuko njiani kurudi. Dylan akataka kuondoka apande juu kwenda kwenye chumba chake, lakini Gilbert akamwambia aketi ili waongee kidogo. Ijapokuwa sasa hivi walifanya kazi za kampuni pamoja, bado uhusiano wao haukuwa wa karibu sana, hivyo kwa kiasi fulani Dylan aliona hii ingekuwa na uajabu. Lakini akatii na kukaa ili amsikilize mzee wake.
"Ulikuwa hospital?" Gilbert akauliza.
"Yeah," Dylan akajibu.
"Anaendeleaje huyo binti?"
"Ndiyo ameamka tu. Bado baadhi ya viungo vyake havijakaa sawa lakini...with time, ata-heal," Dylan akajibu.
"Sawa. Nafurahi sana kujua kwamba unatoa msaada kwa mtu namna hiyo."
"Asante."
"Unajua... nilienda kumwangalia jana," Gilbert akasema.
Dylan akakunja sura kimaswali.
"Yeah. Nilimkuta mama yake, na huyo msichana...Sophia...alikuwa bado hajaamka," Gilbert akamwambia.
Dylan alishangaa kiasi.
"Kwa nini ulifanya hivyo?" Dylan akamuuliza.
"Nilitaka tu kumwona. Umekuwa...adamant sana kutaka kumsaidia, na sasa naelewa ni kwa nini."
"Unamaanisha nini?" Dylan akauliza.
"Kwa sababu ya dada yake... Fetty, si ndiyo?" Gilbert akauliza kichokozi.
Dylan akashindwa kujizuia kutabasamu kwa kustaajabishwa na hili.
"Ahah... yeah actually, namjua Sophia kupitia kwa dada yake...na ninamsaidia kwa kuwa ni rafiki yangu," Dylan akajibu kwa unyoofu.
"Rafiki?" Gilbert akauliza.
"Ndiyo."
"Kweli?"
"Ahahah...unataka kusema nini?"
"Nothing. I found something to be very interesting. Medical bill zake zote unazilipia wewe...na umelipia mpaka wakati ambao ataruhusiwa kwenda nyumbani."
"Yeah, so?"
"Hiyo ni pesa nyingi sana Dylan. Sidhani ikiwa 'rafiki logic' ni ya kweli."
"Ahah... kwani siwezi kutoa msaada kwa mtu mpaka awe ni zaidi ya rafiki?"
"Hapana. Nachotaka kukwambia ni kwamba... usiogope hisia zako mwenyewe. Unahitaji kupanua moyo wako Dylan kutambua kwa nini unafanya vitu...siyo kukazia fikira kile unachodhani ndiyo sababu," Gilbert akamshauri.
Dylan akabaki kimya akiyatafakari maneno ya baba yake. Aliongea kwa fumbo, lakini alimwelewa kwa asilimia zote.
"Unaonaje ukimleta "rafiki" yako hapa siku moja...atutembelee?" Gilbert akamwambia.
Dylan akatabasamu, na kisha akasema, "Ni wazo zuri."
Gilbert akatabasamu pia. Huyu ndiyo Gilbert ambaye Dylan alimpenda sana akiwa mdogo. Nyakati hizi ambazo walikuwa mbali kiukaribu wa mahusiano, ilionekana ni kama alikuwa amebadilika, lakini sasa Dylan akapata kuona kwa kiasi fulani kwamba Gilbert bado ni yule yule; ijapokuwa bado hangeweza kusitawisha ukaribu kama waliokuwa nao zamani.
"Vipi kuhusu kesho kutwa? Mipango inakwendaje?" Gilbert akauliza.
"Oh yeah...aaam...mkutano utafanyika. Wamesema watatuma taarifa ya eneo husika, lakini najua haitakuwa ndani ya huu mkoa. Ninaona uvivu kwenda," Dylan akasema.
"Ahahah... ni must Dylan. Unajua kwamba wewe sasa hivi ndiyo the face of the company," Gilbert akamwambia.
"Sitaki ifike mbali kote huko. Itanipa tu furaha nikiendelea kusaidia kwenu huku nauendesha mgahawa wangu pia," Dylan akasema.
"Ahahahah... yeah hongera sana kwa hilo pia. Nafikiri...kesho nitapita pale ili nipate msosi," Gilbert akasema.
Dylan akacheka kidogo, kisha akamwambia, "Karibu sana."
Wawili hawa hawakuwa wametengeneza maongezi yenye kufurahisha kama haya tokea Dylan aliporudi kutoka Brazil. Pindi hii ilimfariji sana Gilbert; kuona Dylan ameweza kumpa itikio zuri sana kwenye maongezi yao. Dylan yeye akanyanyuka tu na kuelekea chumbani, akijitahidi kupotezea jambo hilo. Lakini alishindwa kuacha kufikiria maneno ya baba yake kuhusu hisia zake, kwa sababu ndani ya moyo wake alijua mzee wake alichoongea ni kweli. Akakaa kumtafakari Fetty kwa kina, ili aone kama kweli alikuwa tu akizizuia hisia zake za upendo kumwelekea.
Kila alipowaza kuhusu mambo mengi yenye kuvunja moyo aliyopitia kwenye mahusiano, alijikataza asipaparukie mapenzi tena, kwa kuwa hakutaka kuangukia pua. Isitoshe, alijiaminisha kuwa Fetty tayari alikuwa na mtu ampendaye, yaani Samwel, ijapokuwa uhusiano wao haukuwa kwenye mstari ulionyooka. Hivyo wazo la kumwelekezea Fetty fikira za kimapenzi akaliweka pembeni yake, na kuendelea kumwona tu kama rafiki mzuri.
★★★
"Yaani watu siku hizi jamani! Mtoto wa watu mzuri kweli, nilienda kumwona ile juzi pale na Fetty," akasema dada fulani aliyeitwa Patricia.
"Kwa hiyo mpaka sasa hivi hajaweza kunyanyuka eeh?" akauliza mwanamke mwingine; mmama.
"Ndiyo. Itachukua muda ila tumeambiwa atarudia hali yake ya kawaida," Fetty akasema.
"Inshaallah Mola amjalie apone," akasema mwanamke huyo.
Yalikuwa ni maongezi kati ya wanawake hawa waliofanya kazi kwenye mgahawa aliofanyia kazi Fetty. Huyo mwanamke mwislamu ndiye aliyekuwa mwenye mgahawa, na hapa ilikuwa ni asubuhi wakiongelea kuhusiana na ajali iliyompata mdogo wake Fetty huku wanaendelea na kazi kadha wa kadha sehemu ya jikoni. Akaja dada mwingine aliyefanyia kazi hapo pia.
"Fetty, yule kaka amekuja... anakutaka," huyo dada akasema.
"Yule mkaka wa Fetty handsome handsome?" akauliza Patricia.
Wote wakacheka na kisha dada yule akakubali.
"Hivi ulimfanyaje maana kila akija lazima aagize wewe tu," huyo mama akamwambia Fetty.
"Haka si kachawi tu...kanatumia unga wa ngano, sijui upupu!" Patricia akatania.
"Hamna, ni tako tu hilo," yule dada aliyekuja akasema.
Wote wakacheka.
"Nenda kamsikilize mteja wako, halafu ndiyo utaenda sasa," huyo mama akamwambia Fetty.
"Haya," Fetty akajibu.
Fetty alikuwa amemwomba mama huyo ambaye ni mwajiri wake ruhusa ya kwenda mapema hospitalini kwa Sophia. Kwa hiyo hapo alivyomwambia kwamba akimaliza kumhudumia Dylan ndiyo angeenda, alimaanisha hospitalini. Binti akatoka na kwenda kule ndani, akimkuta Dylan ameketi huku anatabasamu baada ya kumwona mrembo akija. Kulikuwa na wateja wengine wakipiga misosi yao ya asubuhi hapo, naye Fetty akapita meza kadhaa na kumfikia Dylan.
Walisalimiana vizuri, kisha Dylan akamwambia Fetty amletee chai ya maziwa, chapati mbili, na supu ya nyama yenye nyama nyingi kama alivyopenda. Sikuzote hata kama angeagiza nini, lazima malipo yalikuwa ni elfu kumi kamili; bila kujali chenji iliyobaki. Hivyo, Fetty akaondoka kwenda kumfatia vitu hivyo, huku wanaume hapo wakiangalia jinsi kalio lake lilivyonesa-nesa kila alipopiga hatua. Hata Dylan mwenyewe alipenda sana.
Baada ya dakika chache, akarudi akiwa amebeba sinia pana lililowekewa vyakula alivyoagiza Dylan. Akaviweka mezani huku anatahasamu, naye Dylan alikuwa akimwangalia tu kiunoni. Yaani jinsi mwili wa Fetty ulivyokuwa mnono kutokea kiunoni na ulivyojichora kulimdatisha sana Dylan, lakini akajizuia tu asipitilizishe mawazo yake mpaka mbali mno.
"Nikuwekee vingapi?" Fetty akauliza.
Alikuwa anamaanisha amwekee vijiko vidogo vingapi vya sukari kwenye chai yake.
"Viwili tu vinatosha. Sitaki chai yangu iwe tamu mno kukuzidi wewe," Dylan akatania.
Fetty akamwangalia kwa upendezi mwingi, kisha akamuuliza, "Ulishawahi kunionja?"
Tabasamu lililokuwa usoni mwa Dylan likafifia taratibu, naye akaanza kumwangalia Fetty kwa kushangazwa na maneno yake kiasi. Binti yeye akawa anakoroga tu sukari kwenye chai huku akitambua kwamba Dylan anamtazama sana, kisha akabeba sinia lake na kuondoka bila kumwangalia wala kusema lolote, akimwacha Dylan anamsindikiza tu kwa macho.
Dylan akabaki anayatafakari maneno yale. Yeye kumtania vile ilikuwa masihara tu kutokana na jinsi alivyo, lakini maneno ya binti yalikuja kivingine kabisa. Yaani ilikuwa ni kama Fetty alimpa ujumbe fulani usio wa moja kwa moja, lakini bado akawa tu anaizuia akili yake isifike huko kwa kuwa alijitahidi kwa kadiri ya uwezo wake wote kujidhibiti.
Alipomaliza kula, Fetty alirudi tena, naye akampatia pesa ya malipo. Binti akashukuru huku akimtazama jamaa kwa njia fulani ambayo kwa Dylan ilikuwa ngeni. Hakuwahi kumtazama jinsi alivyomtazama sasa.
"Fetty..." akamwita.
"Bee..." akaitika.
"Nataka leo nikutoe... out. Ungependa?" Dylan akauliza.
Fetty akaangalia pembeni na kutabasamu, kisha akauliza, "Saa ngapi?"
"Jioni. Ukimaliza kazi si unaenda hospital baadae?"
"Actually... ninaondoka sasa hivi kuelekea hospitalini. Nimeomba ruhusa," Fetty akamjulisha.
"Oh kumbe! Basi, twende pamoja nikupitishe hospitalini."
"Si unaenda kazini lakini?"
"Ndiyo. Nakupeleka huko, halafu nageuza. Baadae ndiyo nitakupitia kwa ajili ya outing," Dylan akasema huku ananyanyua nyusi zake kichokozi.
"Sawa. Kwenye mida ya saa ngapi kabisa?"
"Kwenye mida ya saa 1 au 2...ni wewe tu," Dylan akasema.
"Mmmm...hiyo inamaanisha hakutakuwa na mtu kwa Sophia maana mama ataondoka," Fetty akamkumbusha.
"Usijali kuhusu hilo. Nitaweka muuguzi maalum ili awe nae karibu," Dylan akamwambia.
"Sawa basi. Tutaenda. Ni wapi?" Fetty akauliza.
"Utapaona. Utapapenda sana. Pendeza mtoto," Dylan akamwambia.
Fetty akatabasamu. Alifurahi mno moyoni mwake na kuwa na matarajio mengi mazuri. Ijapokuwa Dylan alijiaminisha kwamba alifanya haya yote kirafiki tu, furaha aliyohisi pia ilipita hisia za kawaida za urafiki. Alitazamia kwa hamu 'date' hii kwa kuwa alipanga kumpeleka sehemu ya muhimu.
Baada ya hapo, Dylan akakaa kama dakika 5 hivi akimsubiria Fetty apange mambo yake hapo, kisha wote wakaondoka pamoja. Wakiwa mwendoni, kwa mara ya kwanza kabisa ndiyo Dylan aliweza kumsimulia Fetty kuhusu maisha yake kule Brazil. Wakati wa nyuma alikuwa tu amemwambia kwamba alisomea nje ya nchi, lakini sasa akamwelezea kwa sehemu maisha yake ya huko. Sasa binti akaweza kuelewa zaidi ni kwa nini sikuzote aliiona lafudhi ya Dylan kuwa yenye utofauti, na sababu ilikuwa ni kukaa huko kwa muda mrefu. Alimwambia kuhusu mambo mengi mazuri ya kule, chuo alichosomea, na shangazi yake mdogo pia.
Wakiwa wanaelekea huko bado, Dylan alipigiwa simu kutoka kwenye kampuni yao na kujulishwa kwamba kulikuwa na makaratasi muhimu sana yaliyohitaji sahihi yake. Ni Jaquelin mwenyewe ndiye aliyemwambia aharakishe ili waweze kuyatuma yalikohitajika, hivyo Dylan akamwambia Fetty kwamba wangepita kwenye kampuni yao kwanza mara moja ili ashughulikie hilo, ndipo angempeleka hospitalini sasa.
Binti hakuwa na kipingamizi, na baada ya dakika kadhaa wakafika nje ya jengo la kampuni yao. Dylan akashuka na kumwambia Fetty waende pamoja, na ijapokuwa mwanzoni binti alisita, Dylan akamshurutisha kwa kumshika mkono na kwenda pamoja naye mpaka ndani. Ilikuwa ndiyo mara ya kwanza kwa Fetty kuingia kwenye jengo hilo, naye alipendezwa sana na umaridadi wake. Alitazamwa mno na wafanyakazi wa hapo waliojiuliza alikuwa ni nani kwa Dylan mpaka aende naye hapo akiwa amemshika mkono. Dylan hakujali macho ya watu na kwenda moja kwa moja mpaka kwenye lifti pamoja na Fetty, kisha wakaelekea juu. Alimpeleka Fetty mpaka ofisini kwake na kumwambia amsubiri humo, kisha yeye akaenda kwenye ofisi ya mama yake upesi.
Baada ya muda mfupi, Dylan akarejea na kumkuta Fetty akiwa ofisini kwake bado, naye akamjulisha kuwa kazi yake ilikamilika hivyo wangeweza kuondoka. Wakatoka pamoja tena mpaka kwenye gari, kisha wakaendeleza safari yao ya kuelekea hospitalini. Alimfikisha binti na kuwasalimu Sophia na mama yao, na baada ya hapo akarejea tena kwenye kampuni akiiacha familia hiyo.
★★★
Jioni ilionekana kufika haraka sana. Fetty aliwahi kuondoka hospitalini na kuelekea ghetto kwake kujiandaa vizuri. Alihisi uchangamfu mwingi mno kana kwamba alikuwa anatoka na mpenzi wake, na ni kama aliona mambo yangeelekea huko, ijapokuwa naye pia bado alijidhibiti. Alijisafisha vizuri sana, kisha akavaa kigauni chekundu kilichoyaacha mabega na mikono yake wazi, kilichoishia magotini, na kilichoubana mwili wake vizuri sana kulichora umbo lake matata vyema. Akazichana nywele zake vizuri na kuupamba uso kiasi, miguuni akivaa viatu vyekundu vya kuchuchumia vilivyoonyesha kucha zake zilizopakwa rangi nyekundu miguuni.
Hazikupita dakika nyingi akiwa anajiweka sawa mbele ya kioo, na simu yake ikaita. Akapokea baada ya kuona ni Dylan ndiyo anapiga, naye akamwambia alikuwa nje tayari anamsubiria. Binti akamjulisha kuwa anatoka muda siyo mrefu, kisha akakata simu. Akajipulizia manukato mtoto, na baada ya hapo akatoka na kuufunga mlango wake. Majirani wenzake walikuwa wanamsifia hapo nje kwa mwonekano wake, huku wengine wakiona wivu na kwenda kumchungulia mpaka alipoingia ndani ya gari la Dylan na kuondoka.
Dylan alimsifia sana kwa kupendeza, mpaka Fetty alihisi aibu. Yaani mwendo mzima jamaa alichoongelea sanasana ilikuwa ni mwonekano wa Fetty tu, hata ingawa binti alijitahidi kuzungumzia mambo mengine pamoja naye. Walifika hospitalini, naye mama yake Fetty alipendezwa na mwonekano wa binti yake. Fetty alikuwa mstaarabu lakini alijua kupendeza pia hata kwa hivyo hivyo vitu vichache alivyokuwa navyo. Dylan akamwambia mama yake Fetty kuwa walikuwa wanaenda sehemu fulani, hivyo wangeacha muuguzi maalum wa kumwangalia Sophia.
Mama yake alifurahi sana kujua walikuwa wanatoka pamoja, kwa kuwa matarajio mengi aliyokuwa nayo yalionekana kushika hatamu sasa. Akawatakia matembezi mema, kisha baada ya dakika kadhaa, Dylan akaenda kumpanga muuguzi yule aliyesema angemwangalia Sophia. Akarudi pamoja naye, kisha wawili hao wakamuaga mama Fetty na Sophia, nao wakaondoka hapo. Mama yake pia angeondoka muda siyo mrefu.
Ilikuwa ni saa 1 jioni hivi tayari, naye Dylan akawa anamwendesha Fetty kuelekea sehemu ambayo binti hakutambua ni wapi. Matarajio yake mengi yalikwenda tofauti na alivyotazamia baada ya Dylan kulifikisha gari nje ya geti la nyumba kubwa sana na kupiga horn ya gari lake. Fetty akashangaa.
"Dylan hapa ni wapi?" akamuuliza.
"Karibu kwetu," Dylan akasema huku anatabasamu.
Fetty akatoa macho asiamini kama kweli Dylan alikuwa amempeleka kwao.
"Kwenu? Kwa nini umenileta kwenu Dylan?" akauliza kimashaka.
Ni wakati huu ndipo geti la nyumba yao likafunguliwa na mlinzi.
"Hukumbuki uliniambia ulitamani kupaona kwetu siku moja? Leo ndiyo hiyo siku sasa," Dylan akasema huku akiliingiza gari ndani.
"No...Dylan... nilikuwa natania tu...hivi kweli....yaani umenileta kwenu...nimevaa hivi..."
Dylan akacheka.
"Dylan acha michezo yako bwana. Twende unirudishe sasa hivi," Fetty akasema.
Wakati huu, Dylan alikuwa amekwishaliegesha gari, lakini akawa anaangalia gari lingine hapo nje ambalo halikuwa la kwao. Akakisia kuwa huenda kulikuwa na mgeni mwingine tu amekuja.
"Tumeshafika. Shuka," Dylan akamwambia.
"Mm-mm...me sishuki," Fetty akagoma.
"Fetty come on..." Dylan akambembeleza.
"We hujaniambia kama unanileta kwenu....kweli Dylan unategeme..."
Dylan akakishika kiganja chake ili kumtuliza, naye Fetty akatulia kidogo na kumwangalia.
"Usiogope. Uko na mimi. Nakuahidi kila kitu kitakuwa sawa. Niamini," Dylan akamwambia kwa sauti ya upole.
Fetty akamwangalia tu huku akiwa na wasiwasi bado, naye Dylan akashuka na kuzunguka gari mpaka kwenye mlango wa siti aliyoketi Fetty. Akaufungua na kumnyooshea mkono ili amsaidie kutoka, naye Fetty akampa mkono na kutoka; kama wazungu wafanyavyo. Binti aliitazama nyumba yao Dylan, jinsi ilivyokuwa kubwa na yenye umaridadi wa hali ya juu. Akamwangalia Dylan kimashaka bado, naye jamaa akatabasamu tu na kumshika mkono, kisha akaanza kuelekea sehemu ya mlangoni pamoja naye.
Walipofika mlangoni, Dylan akamhakikishia Fetty kwamba kila jambo lingekwenda vizuri, kisha akaufungua mlango na kupiga hatua chache kuingia ndani. Ile anayapeleka macho yake pale sehemu ya sebule, tabasamu alilokuwa nalo usoni likageuka na kuwa butwaa kubwa sana baada ya kumwona mtu ambaye hakutarajia kumkuta hapo hata kidogo! Akabaki amesimama tu akishangaa, na sehemu hiyo walikuwa wameketi watu watatu kwenye masofa; Gilbert, Jaquelin, na nwanamke mwingine ambaye alimjua VIZURI sana.
Huyu alikuwa ni shangazi yake mdogo, yaani dada mdogo wa Gilbert, yule yule aliyekwenda kuishi naye kule Brazil. Alikuwa hapa wakati huu, na ni jambo ambalo Dylan hakuwa ametarajia kabisa. Baada ya Jaquelin kumwona Dylan, alisimama akiwa na uso ulioonyesha ana furaha sana.
"Hey Dylan... look who's here! (Dylan..ona aliye hapa!)" Jaquelin akasema kwa shauku.
Shangazi yake akasimama pia baada ya kumwona mpwa wake huyu, akimtazama kwa hisia sana. Dylan akabaki kumwangalia tu kimashangao, akiwa amerudiwa na kumbukumbu nyingi za wakati uliopita baada ya kumwona shangazi yake tena........
JE, WATI DU YU SINKI DAILANI IZ SINKING?
★★★★★★★★★★★
ITAENDELEA
★★★★★★★★★★★
Full story ni 2000 tu.
WhatsApp no: +255 787 604 893 (hii ni namba ya WhatsApp, siyo ya malipo. Ya malipo utaipata ukija WhatsApp. Karibu sana)
The the story the is the very the cool the right?hahahaa elton umetisha sana na hicho kithungu cha hapo mwishoni
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]daahThe the story the is the very the cool the right?
Mmh babe siku hizi unanifanya nikose hata chakucommentDYLAN
Story by Elton Tonny
Familia, Kazi, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Unyanyasaji, Usaliti, Visasi, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa
(R-rated 18+)
ILIPOISHIA.....
Dylan anafika kwao pamoja na Fetty kwa mara ya kwanza. Anamhakikishia Fetty kwamba kila jambo lingekwenda vizuri kwa kuwa yuko pamoja naye, hivyo asiogope chochote. Wanafika mlangoni naye Dylan anaufungua na kupiga hatua chache kuingia ndani. Ile anayapeleka macho yake pale sehemu ya sebule, tabasamu alilokuwa nalo usoni likageuka na kuwa butwaa kubwa sana baada ya kumwona mtu ambaye hakutarajia kumkuta hapo hata kidogo! Akabaki amesimama tu akishangaa, na sehemu hiyo walikuwa wameketi watu watatu kwenye masofa; Gilbert, Jaquelin, na nwanamke mwingine ambaye alimjua VIZURI sana.
Huyu alikuwa ni shangazi yake mdogo, yaani dada mdogo wa Gilbert, yule yule aliyekwenda kuishi naye kule Brazil. Alikuwa hapa wakati huu, na ni jambo ambalo Dylan hakuwa ametarajia kabisa. Baada ya Jaquelin kumwona Dylan, alisimama akiwa na uso ulioonyesha ana furaha sana.
"Hey Dylan... look who's here! (Dylan..ona aliye hapa!)" Jaquelin akasema kwa shauku.
Shangazi yake akasimama pia baada ya kumwona mpwa wake huyu, akimtazama kwa hisia sana. Dylan akabaki kumwangalia tu kimashangao, akiwa amerudiwa na kumbukumbu nyingi za wakati uliopita baada ya kumwona shangazi yake tena........
★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA KUMI
★★★★★★★★★★★
2014
SAÕ PAULO, BRAZIL
Ulikuwa ni mwaka ambao Dylan alihitaji kufanya uamuzi wa muhimu sana. Alikuwa amesoma shule kadhaa ambazo zilimwongezea ujuzi na kumpa tuzo za kitaaluma kutokana na bidii yake na mafanikio mazuri katika masomo na michezo. Alishauriwa na baadhi ya walimu na watu aliofahamiana nao huko kwenda chuo kusomea mambo ambayo yangemfanya aajiriwe kwenye sekta kubwa za jamii kwenye nchi hiyo.
Lakini yeye alipenda zaidi masuala ya ukandarasi, na upendo huu ulirithishwa kwake kutoka kwa baba yake, ambaye alikuwa mjenzi na mkandarasi mzuri sana. Alitaka kuwa kama baba yake kwa mambo mengi sana, hivyo aliamua kuchagua kozi ya 'Civil Engineering' ambayo angesoma kwa miaka 6. Alifanikiwa na kuchaguliwa kwenye chuo kikuu cha USP (University of Saõ Paulo), ambacho kilikuwa cha hali ya juu sana na kilichotoa masomo bure kabisa kwa wachaguliwa hapo.
Kufikia wakati huu, bado alikuwa akiishi nyumba moja na shangazi yake, yaani mdogo wake baba yake. Waliishi pamoja kwa miaka mingi sana tokea Dylan alipokwenda huko. Shangazi yake huyu alikuwa akifanya kazi ya kutengeneza mitindo ya mavazi iliyopendwa sana, na alikuwa ameolewa na mwanaume fulani mbrazili miaka mingi iliyopita ambaye ndiye alimleta kwenye nchi hii.
Baadae waliachana na kutalikiana miaka michache nyuma, na sasa alikuwa kwenye mahusiano na mwanaume fulani mwingine ambaye alikuwa na tabia za ajabu-ajabu tu. Dylan hakupendezwa naye hata kidogo kwa kuwa angekuja hapo nyumbani na kujifanya yeye ndiyo kichwa kwenye kila kitu, na mara nyingi alimpelekesha sana shangazi yake kufanya mambo alivyotaka yeye. Dylan hata alikuwa akimshangaa sana shangazi yake kwa kuwa na mtu kama huyo, lakini hakuwa na jinsi ila kumwacha tu ayaongoze maisha yake jinsi alivyotaka.
Shangazi yake aliitwa Camila, naye alikuwa mwanamke mrembo sana mwenye miaka 35 WAKATI HUU, na hakuwa na mtoto hata mmoja. Kipindi hiki alikuwa ameajiriwa kwenye kampuni ndogo ya mitindo kama 'fashion designer' wa mitindo ya nguo na urembo. Kufikia kipindi hiki, Dylan alikuwa kijana mwenye sura na umbo la kiume lenye kuvutia wanawake wengi. Alikuwa amefikisha miaka 20 miezi michache iliyopita, na alikuwa na mwili mpana wenye kujijenga vizuri sana kutokana na mazoezi yake ya viungo na upenzi wa sarakasi.
Dylan alikuwa na mpenzi wa kibrazili, aliyeitwa Amanda, ambaye aliishi mtaa wa jirani na maeneo ilipokuwepo nyumba ya shangazi yake. Walikuwa wamedumisha uhusiano wao kwa zaidi ya mwaka mmoja na nusu sasa. Wakati huu alikuwa kwenye matatizo pamoja na mpenzi wake huyo kwa sababu alianza kufanya mambo kwa njia isiyoeleweka; mara amdanganye vitu fulani, mara anune-nune bila sababu, visa visa vya kitoto, kiufupi Amanda alikuwa anajaribu kutengeneza njia ya kumkwepa Dylan, ijapokuwa Dylan hakumkatia tamaa kwa sababu alimpenda sana.
Ndipo siku moja Dylan alipata habari iliyomshtua sana. Alitumiwa ujumbe usiku na mtu asiyejulikana kuwa Amanda alikuwa akitoka kimapenzi pamoja na mwanaume mwingine. Akaambiwa ikiwa alitaka kuthibitisha, aende sehemu fulani ambayo angemkuta Amanda pamoja na huyo mtu wake.
Bila kukawia, Dylan alikwenda huko upesi ili kujionea ikiwa kweli alichoambiwa kilikuwa sahihi. Alimwamini Amanda, lakini kutokana na jinsi tabia yake ilivyokuwa imebadilika, alihisi uhitaji wa kutaka kuthibitisha ikiwa kweli bado Amanda alistahili kuaminiwa. Ni mpaka alipofika eneo lile na kukuta vijana kadhaa wakiwa hapo; Amanda akishikwa-shikwa mwilini na kijana fulani, kisha wakaanza kudendeshana huku wengine wakifanya mambo kama kucheza muziki na kuvuta sigara na kunywa pombe.
Dylan aliingiwa na majonzi sana baada ya kuona vile. Alihisi hasira pia iliyomfanya awafate pale na kumpiga ngumi yule jamaa. Amanda alishtushwa na uwepo wa Dylan hapo ambao hakuutarajia, na vijana wale wengine wakaacha mambo yao na kumwangalia Dylan kwa mshangao. Alimuuliza Amanda kwa nini alimfanyia hivyo, lakini binti hakusema kitu chochote. Alipomshurutisha aseme, wale vijana wengine wakamfata na kuanza kumpiga.
Kutokana na hasira alizokuwa nazo, aliwachangamkia wote upesi kwa kuwapiga kwa mtindo wake wa 'capoeira' uliowachanganya wote na kuwaacha wamelala chini baada ya kupigwa vibaya; kutia ndani jamaa wake Amanda. Amanda aliogopa sana na kuanza kukimbia, na ndiyo hapo mapolisi wakawa wamefika. Walimchukua Dylan na kumpeleka kituoni, ambako baada ya muda fulani, Camila alifika na kufanikiwa kumtoa ili amrudishe nyumbani. Alikasirishwa sana na kitendo ambacho mpwa wake alifanya, naye akamfokea mno kuhusu jinsi ambavyo alimweka kwenye wakati mgumu.
Dylan hakuwahi kutenda kwa namna hiyo hata mara moja, kwa hiyo alijihisi vibaya kwa kuwa shangazi yake hakusikiliza maoni yake kuhusu jambo lililotokea na badala yake kumlaumu tu. Kwa maumivu aliyokuwa nayo baada ya kusalitiwa na mtu aliyempenda, alihisi ni kama hakutendewa haki hata kidogo.
"But aunt... (Lakini shangazi..)" akajaribu kujitetea.
"No. You stay quiet. Do you have any idea how much all this takes away your good reputation? What... just what got into you? You just go out there, and beat up someone just 'cause you can? What insufferable behavior is this suppo... (hapana. Kaa kimya. Hivi unajua ni jinsi gani haya yote yanasababisha sifa yako nzuri ipotee? Ni nini kimekuingilia kichwani? Unatoka tu huko nje na kupiga mtu jwa sababu tu unaweza? Ni aina gani mbaya ya tabia ambayo umei...)"
"Enough! (Inatosha!)" Dylan akamkatisha.
Camila alishtuka kiasi baada ya kuona Dylan amekuwa mkali kwake kwa mara ya kwanza.
"I care a damn about reputation! (sijali chochote kuhusu sifa nzuri!)" Dylan akasema kwa ukali.
"Dylan... unawezaje kuongea nami kwa njia hiyo?" Camila akauliza.
"Just leave me alone. My opinions don't matter anyway (niache tu. mambo ninayosema huwa hayana maana hata hivyo)," akasema Dylan, kisha akaondoka na kwenda kwenye chumba chake.
Alimwacha Camila akiwa anashangaa sana. Hakuwahi kumwona Dylan namna hiyo, hata kama angekuwa na tatizo, sikuzote wangeongea vizuri tu, haijalishi ikiwa alimfokea au la. Lakini pia hasira ya Camila haikuwa kwa sababu tu ya kile alichofanya Dylan, bali ilikuwa kutokana na mkazo alioupata kutoka kwa mwanaume wake. Aliketi hapo sebuleni akitafakari mambo kidogo, kisha akaelekea chumbani kupumzika.
Ijapokuwa kihalisi wawili hawa walikuwa ni watanzania, maisha waliyoishi huku yaliendana kabisa na tamaduni za wabrazili. Walivaa, walikula, waliongea kwa njia za utamaduni wa huku, hivyo ni kama wao pia walikuwa ni wabrazili. Camila na Dylan walizungumza lugha tatu; kiswahili, kiingereza, na kispanish cha wabrazili, mara nyingi wakipendelea kuchanganya lugha hizo kwenye maongezi yao ya kila siku.
★★★
Ilipofika asubuhi, Dylan alikuwa ameketi sehemu yake ya kulala tu akitafakari mambo kwa upana. Alifikiria kuhusu usaliti wa Amanda, ugomvi wake na Camila, na chuo pia, ambacho angeanza ndani ya siku chache. Mambo yote yalikuwa yenye kukonga moyo wake, lakini jambo muhimu wakati huu ilikuwa shangazi yake. Alijihisi hatia sana kwa kuongea naye kiukali usiku wa jana, naye alitambua angepaswa kumwomba samahani.
Hivyo akajitoa hapo na kuelekea chumbani kwa Camila. Alikuta mlango ukiwa wazi kiasi, hivyo akajua tayari shangazi yake alikuwa ameamka. Akavuta pumzi na kuishusha, kisha akaingia ndani hapo.
"Aunt Cami..."
Alikuwa anataka kumwita pale alipokatishwa na kile alichokiona mbele yake. Camila alikuwa amesimama karibu na kitanda, akiwa hajavaa nguo hata moja mwilini! Alikuwa amempa mgongo, hivyo Dylan aliweza kuona sehemu ya nyuma ya mwili wake vyema. Camila alikuwa na umbo zuri; mrefu kiasi, mwenye hips nene na kalio lililotokeza vyema nyuma, huku ngozi yake ikipendezeshwa na weupe wa mbali aliokuwa nao.
Dylan alishindwa kufanya jambo lolote na kubaki kumtazama tu. Ndipo Camila akageuka na kumwona akiwa amesimama hapo, kisha kwa haraka akachukua taulo iliyokuwa kitandani hapo na kujifunika kifuani huku anamtazama Dylan kwa kushtushwa na uwepo wake hapo. Dylan akabaki anamwangalia machoni tu, naye Camila akaonekana kuweka uso wenye utulivu kiasi, akimwangalia mpwa wake kama anasubiri jambo fulani litokee huku kashika taulo yake.
Kijana huyu akamshusha na kumpandisha taratibu Camila kwa macho yake, kwa njia ambayo ilionyesha....upendezi. Camila hakuweza kusema chochote ila kumwangalia tu, akijaribu kutafakari ni kitu gani ambacho Dylan alikuwa anafikiria, na alikuwa amesimama hapo chumbani kwake kwa muda gani pia.
Dylan akatazama chini akiwa na uso wenye huzuni kwa njia ya kawaida kabisa, kisha taratibu akarudi nyuma na kuufunga mlango akimwacha Camila anauangalia. Camila alishindwa kuelewa maana ya Dylan kufanya hivyo, kwa kuwa alifikiri huenda kijana huyu alikuwa amemwangalia akiwa mtupu kwa muda mrefu chumbani hapo. Akaanza kufanya jitihada za kuvaa nguo ili atoke kwenda kuongea naye.
Alipomaliza, alienda sehemu ya sebule na kuanza kumwita Dylan, lakini hakuitika. Ikabidi amfate chumbani na kumsisitizia atoke waongee, na baada ya kuona kimya tu, akausukuma mlango na kuingia. Hakukuwa na uwepo wa mpwa wake ndani humo, naye akawa ametambua kuwa kijana wake huyo alikuwa ameondoka baada ya kuangalia na mazingira ya nje na kumkosa.
Ilikuwa ni siku iliyomfanya Dylan ahisi upweke sana. Alikwenda sehemu mbalimbali pamoja na baadhi ya rafiki zake ili kujifurahisha, lakini kwake ilikuwa ni kupoteza muda tu kwa sababu ijapokuwa alijitahidi kusahau mambo yaliyotokea, ilikuwa ngumu kuyafuta akilini kwa kuwa mara kwa mara yalijirudia kichwani. Alipoachana na rafiki zake, alitembea mwenyewe jijini na kukaa sehemu fulani kutafakari mambo.
Zilikuwa zimebaki siku chache tu aondoke nyumbani pale kwenda chuo. Hakutaka kuondoka akiwa kwenye hali ya sintofahamu pamoja na shangazi yake kipenzi. Camila alikuwa mwanamke mwenye kujali sana, mpole, mstaarabu, na kwa miaka yote 9 ambayo Dylan aliishi naye, hakuwahi kugombana namna hiyo pamoja naye; yaani kumpandishia sauti. Dylan alijilaumu sana kufanywa mpenzi kipofu na Amanda. Yeye ndiye aliyekuwa amesababisha hasira ya Dylan iwake na kumfanya ashindwe kujidhibiti.
Dylan alifikiria kumpigia simu Camila, lakini bado akawa na wasiwasi fulani uliomfanya aache. Alijua angepaswa tu kurudi nyumbani, hivyo akaamua kuwa wakati ambao angerudi angeongea naye; kwa kuwa sasa aliweza kuituliza zaidi akili yake. Kuna wakati ambao angekumbukia jinsi Camila alivyoonekana chumbani kwake ile asubuhi, na kumwaza namna hiyo kulimfanya ahisi hatia kiasi. Hakujua ni kwa nini jambo lile liliendelea kuzunguka akilini mwake ijapokuwa alifanya juu chini kuliondoa kichwani.
★★★
Ilifika mida ya saa 2 usiku, naye Dylan akawa anarejea nyumbani sasa. Hakuwa amerudi tokea alipoondoka asubuhi, na alijua bila shaka shangazi yake alimsubiri kwa hamu. Nyumba yao ilikuwa imejitenga kiasi na nyumba zingine eneo la hapo, na majirani wengi waliishi kwa kutengana-tengana. Ilikuwa nyumba ya kulipia, kama ya kupangishwa, nayo ilikuwa na uzio mfupi na geti dogo la kuingilia ndani umbali mfupi kutokea barabarani.
Wakati Dylan alipokuwa amelikaribia geti, alianza kusikia sauti za juu ndani mule, kama watu wanafokeana. Akatembea upesi zaidi na kuingia getini hapo, naye akapata kuona kupitia dirisha shangazi yake akifokeana na yule mwanaume ambaye alikuwa mpenzi wake. Akaudhika mno kwa kuwa kama kawaida, bila shaka mwanaume huyu alikuwa anamletea fujo shangazi yake hapo. Sikuzote walipogombana, Dylan aliwasikia akiwa chumbani kwake, na mara nyingi ilikuwa ni bangi tu za kibrazili zilizompanda huyo jamaa. Lakini wangepatana tena na kuonekana wanayajenga, kisha ugomvi lazima tu ungetokea tena.
Lakini wakati huu, inaonekana mambo yalikuwa tata zaidi. Dylan alimsikia Camila akisema kwa hasira kwamba amechoka, na anavunja uhusiano huu kwa kuwa mwanaume huyo hakumtendea kwa heshima na staha. Ndipo Dylan akamwona jamaa amemshika shangazi yake kwa nguvu mikononi, na kwa hasira, akamtikisa-tikisa huku anamwambia hawezi kuachana naye kwa kuwa hatapata mwanaume mwingine. Kisha akamsukuma na kumfanya Camila aangukie vitu fulani vilivyotoa sauti ya juu ya kudondoka.
Dylan alikuwa amesimama hapo karibu na dirisha akiona kila kitu, kisha akafanya, "Ahah..," kicheko cha kuashiria alikuwa anataka amwonyeshe jamaa huyo adabu maana yake nini. Akaweka uso ulio 'serious' na kuingia ndani hapo. Mwanaume huyo hakutambua ujio wa Dylan kwa kuwa alikuwa anamfokea Camila aliyekuwa chini bado huku analia kwa huzuni na hasira. Dylan alitembea kwa njia ya kawaida tu kama vile hakukuwa na tatizo, kisha akafika hapo na kumsukuma jamaa, ambaye aliwewesekea mbele na kuangukia kwenye sofa.
"Dylan!" Camila akaita baada ya kumwona hapo ghafla.
Kijana akageuka na kuchuchumaa chini, kisha akamshika shangazi yake na kumsaidia anyanyuke.
"Niñito engreido! (mvulana mpumbavu wewe!)" jamaa akasema kwa hasira.
Kisha akanyanyuka na kumfata Dylan, akimshika kwenye kola ya shati lake huku anamwangalia kikatili. Camila alikuwa anamwambia amwachie mpwa wake kwa kuwa ni mdogo, huku Dylan anamtazama mwanaume huyo bila woga wowote. Jamaa akatoa mkono wake mmoja kwenye kola ya Dylan na kutaka kumpiga ngumi, lakini kwa kasi Dylan akakwepa na kumpiga mbavuni kwa kiwiko, jambo lililomuumiza sana jamaa na kumfanya arudi nyuma kidogo.
Camila alishikwa na taharuki kubwa kwa kuwa sasa walikuwa wameanza kupigana. Jamaa alipositiri maumivu kiasi, akamfata Dylan ili amrukie, lakini upesi Dylan akatumia mtindo fulani wa sarakasi kuirudisha miguu yake kwa nyuma na kukibana kiuno cha Camila, halafu akajigeuza kwa mikono na kurukia upande mwingine, akiizungusha miguu yake. Hii ilifanya Camila awewesekee upande mwingine huku mwili wake ukizunguka na kukaribia kuanguka, lakini ndiyo huo upande ambao Dylan alikuwa amerukia, hivyo akamdaka kwa utulivu na kumkalisha kwenye sofa. Hii ilikuwa ni njia ya kumlinda Camila asipamiwe na jamaa, kwa kuwa jamaa alipitilizia mpaka kwenye TV na kuiangukia vibaya.
Camila alishangazwa na ustadi huo wa Dylan, huku akipumua kwa hofu kubwa. Dylan akamwangalia kwa kujali, kisha akasimama na kumtazama jamaa. Jamaa akanyanyuka kibishi-bishi ili aendeleze ubabe wake, lakini Dylan hakutetemeshwa na hilo. Jamaa akaanza kumfata, na alipotaka kumshika, Dylan akampiga kwa mitindo mingi yenye kushtukiza; mara begani, hajakaa sawa, pajani, hajasikilizia maumivu, tumboni, yaani haraka-haraka na kwa nguvu sana. Camila alikuwa analia huku akijaribu kuwaambia waache kwa huzuni sana, lakini vilio hivyo ndiyo vilikuwa vinamwongezea tu hamasa kijana wake aendelee kumtandika huyo mjinga.
"Dylan stop! Please..."
Kufikia hapa, kwa Dylan ilikuwa imepita kiasi kuendelea kuona mwanaume huyu anamsumbua shangazi yake, hivyo aliazimia kumpa somo kuwa akimzingua tena, atamnyoosha. Akamburuza mpaka nje ya nyumba, huku sasa mwanaume huyo akiwa amelegea kwa kupigwa sehemu nyingi zenye udhaifu. Camila alishangazwa sana na njia ya Dylan ya kufanya mambo. Hakuwahi kumwona anapigana na mtu, na hakufikiria angeweza kumpiga mwanaume huyo mtu mzima jinsi hiyo.
Dylan akamtoa jamaa mpaka nje ya geti na kumsukuma chini. Kulikuwa na watu wachache hapo ambao walisogea baada ya kusikia sauti zilizozidi za kelele kutoka humo ndani. Baadhi walimfahamu Dylan tokea alipofika hapo, na walimzoea kuwa mtu mchangamfu na mtundu, lakini hawakuwahi kumwona akiwa amekasirika namna hiyo.
Dylan akamshika tena jamaa na kuanza kumnyanyua, kisha akamsukumia kwenye geti akimkandamizia hapo. Mwanaume mmoja alijaribu kumshika Dylan ili amzuie, lakini Dylan akamgeukia kwa hasira na kumsonta, akimwambia bila kutoa maneno kuwa asiguswe. Badiliko hilo la Dylan liliwaogopesha sana waliokuwa hapo. Mwanaume huyo aliyepigwa na Dylan hakuonyesha ujanja tena, bali maumivu tu na damu zilizomtoka usoni. Yaani hakumkwaruza Dylan hata sehemu moja!
Camila akaja nyuma ya mpwa wake na kumsihi amwache huyo bwege, kwa kuwa alikuwa amekwishamfukuza kwenye maisha yake, hivyo Dylan akamwambia jamaa apotee haraka sana. Kwa woga, mwanaume huyo akaanza kuondoka huku anachechemea, akisindikizwa na macho ya wengi hapo. Camila akamshika Dylan mkono na kuanza kumvuta ili warudi ndani, na baada ya kuingia getini akalibamiza kwa nguvu na kulifunga akiwa amevurugika akili.
"Que te pasa? (una shida gani?)" Camila akamuuliza kwa ukali.
"Que pasa? (shida gani?)" naye Dylan akauliza kwa ukali.
"How could you do something like that? (unawezaje kufanya jambo kama hilo?)" Camila akauliza kwa ukali.
"Ulitaka nifanye nini aunt Camila? Nimwimbie sé preparo?" Dylan akauliza pia.
"Usinichanganye Dylan. You have no idea what I'm going through! (haujui ninapitia nini!)" akasema Camila kwa hisia za majonzi.
"I do! Ninajua vizuri sana kwamba mwanaume huyo hakufai. Ni woga wako tu ndiyo..."
"Dylan!"
Dylan akasitisha kuongea na kumtazama shangazi yake usoni. Aliona jinsi shangazi yake huyu alivyokuwa ameghafilika kweli. Lakini ukitegemea hali ambazo Dylan alikuwa ametoka kupitia na Amanda, alihisi kama vile alihitaji kumwambia ukweli shangazi yake ili aone mambo kihalisi.
"Ndiyo hakufai. El solamente te hace dudar de ti misma y de tus (anakufanya unajishuku tu mwenyewe na uwezo wako ukiwa mwanamke)," Dylan akasema.
"How dare you!" Camila akasema kwa hisia.
"El está no es el indicado si prefiere salir con sus amigos en lugar de hacer algun plan contigo... (mwanaume huyo siyo sahihi kwako ikiwa anaona ni bora kutumia muda wake na marafiki zake badala ya kukaa nawe na kuyapanga maisha yenu...)" akasema Dylan kwa hisia kali.
"Sufficiente... (Inatosha)" Camila akamwambia.
"...si durante el dia no te llama o no te escribe para saber de ti, creéme, siempre hay tiempo para hacerlo por muy ocupado que se esté (...ikiwa hakupigii wala kukutumia ujumbe ndani ya siku kukujulia hali, niamini, sikuzote huo muda upo hata kuwe na ubize mwingi kiasi gani)" Dylan akaendelea kumwambia ukweli.
"Sufficiente Dylan..! (Dylan inatosha!)" akasema Camila huku anapumua kwa kasi.
"Ndiyo... hakufai! Ulijilazimisha tu kufikiri bado unampenda lakini ilikuwa ni kwamba unaogopa tu kuachwa," Dylan akasema kwa mkazo sana.
Camila alinyanyua mkono wake na kumpiga kofi la nguvu usoni. Dylan akawa ametazama pembeni, kisha akamgeukia na kumwangalia kwa hisia. Camila alikuwa ameziba mdomo wake kwa kiganja chake huku analia, akijisikia vibaya baada ya kumpiga mpwa wake hivyo. Mambo yote aliyosema Dylan yalikuwa kweli, na ni kwa sababu ya huo ukweli ndiyo Camila aliumizwa sana na maneno ya Dylan. Akakimbilia ndani haraka na kwenda kujifungia chumbani kwake huku analia kwa huzuni.
Dylan alibaki hapo getini akihisi simanzi nzito sana iliyoambatana na hisia za majuto. Alianza kujilaumu kwa nini alimwambia shangazi yake mambo hayo yenye kuumiza sana. Muda mfupi uliopita alitaka tu kurudi nyumbani na kurekebisha hali ya hewa baina yao, lakini sasa tena mambo yakavurugika zaidi. Akakaa chini na kuegamia geti, akiwa amefumba macho kwa huzuni.
Baada ya dakika kadhaa kupita, akanyanyuka na kwenda ndani. Alienda mpaka kwenye mlango wa chumba cha Camila na kutaka kupiga hodi, lakini akasita, akifikiria huenda shangazi yake hata hakutaka kumwona. Akaahirisha na kurudi sebuleni pale. Akarekebisha baadhi ya vitu vilivyokuwa vimevurugwa na kusafisha vile vilivyovunjika.Akachukua matunda kiasi na kula, huku akimfikiria sana Camila.
Baada ya muda fulani kupita, aliona afunge milango ya nyumba nzima na kuingia chumbani kwake ili apumzike. Matukio ya siku hii yalizidi kumfanya ajihisi upweke wa hali ya juu, kwa kuwa mfariji wake aliyekuwa huku wakati huu alihitaji kufarijiwa, huku yeye ndiye ambaye alimwongezea huzuni. Akajaribu kusoma vitu fulani kwenye simu yake, kisha baada ya hapo akalala.
Alikuja kuamka asubuhi ya saa 2, naye akaingia bafuni kujisafisha mwili na kinywa pia. Alihisi wasiwasi mwingi kwa kuwa alijua angehitaji kutoka na kwenda kuongea na shangazi yake, ambaye huenda bado alikuwa kwenye huzuni, na ambaye huenda hangetaka hata kumwona baada ya kilichotokea jana. Lakini akajikaza kiume na kuelekea sebuleni pale. Hakukuwa na mtu, lakini aliweza kutambua kuwa chai na vitafunwa vilikuwa vimeshaandaliwa mezani, hivyo bila shaka shangazi yake alikuwa ameamka mapema na kuvitengeneza; Dylan akiamka afike na kula tu.
Lakini mawazo ya Dylan yalikuwa mbali sana kutoka kwenye chai. Alihitaji sana kuiweka hali baina yao iwe sawa kwa haraka, hivyo akaona amfuate chumbani kwake. Alipofika, alikuta mlango uko wazi kuruhusu nusu mwili upite, na kwa sababu hakuwa na uhakika ikiwa Camila angetaka kumwona, akaona aingie tu wayamalize mapema.
Alipoingia, hakumwona sehemu hiyo. Ile anataka kumwita, Camila akatokea kwenye bafu la humo humo chumbani akiwa amejifunga taulo kuanzia kifuani mpaka ilipoishia mapajani. Kichwani kwake alijifunga taulo kubwa kwa ajili ya kukausha nywele zake, naye akaenda usawa wa kitanda na kusimama akiwa amempa mgongo Dylan, bila kujua yuko nyuma yake.
Kwa mara nyingine tena Dylan alipatwa na hisia za ajabu-ajabu baada ya kumwona shangazi yake namna hiyo. Fikira ya kwanza iliyomjia akilini ilikuwa ni kuondoka haraka ili ampishe avae, lakini kukawa na kitu fulani ambacho kilikuwa kinamsukuma aendelee kumtazama tu. Alimwangalia kwa njia yenye uvutio mwingi sana, kuanzia miguuni, alipandisha macho yake taratibu mpaka mgongoni kwa Camila akipendezwa na mwonekano wake.
Hakuwahi kumtazama kwa njia hiyo kabla, ijapokuwa hata pindi ambazo waliwahi kwenda sehemu kama beach pamoja, alimwona akiwa amevaa nguo nyepesi za kuogelea zilizoonyesha viungo vyake, lakini hakumtazama jinsi alivyomtazama sasa. Wimbi kubwa la hisia ambazo zilimchanganya liliuvaa mwili wake na kumfanya ashindwe kujua cha kufanya. Alijua hakupaswa kuendelea kumwangalia, lakini akaendelea tu.
Camila alikuwa ameanza kuitoa taulo ile iliyokuwa kichwani huku anafuta-futa nywele zake laini zilizolowana, pale alipomwona Dylan nyuma yake kupitia kioo kilichokuwa upande wa pembeni kwenye kabati. Alishtuka na kugeuka nyuma kumwangalia, naye Dylan akamtazama machoni kwa hisia. Camila hakusema chochote, akageukia tu mbele baada ya kukumbukia kilichotokea usiku wa jana; jinsi kijana wake alivyompa ukweli kwa njia yenye kuumiza. Akabaki amesimama tu akizizuia hisia zake za maumivu.
"Unaonaje ukiniacha nivae?"
Camila akamwambia maneno hayo kwa sauti ya chini yenye utulivu sana. Dylan alisikia, lakini hakutii maneno hayo aliyoambiwa. Kuna kitu kilianza kumsukuma, siyo kitu kabisa, yaani, hisia fulani ambayo ilikuwa mpya kabisa kwake. Akaanza kupiga hatua kuelekea aliposimama Camila taratibu, kama vile anasita-sita. Camila aliweza kumwona kupitia kioo kuwa alikuwa anamfata, naye akatulia tu hapo hapo, huku akianza kuingiwa na hali fulani ya woga wenye kusisimua. Hakujua mpwa wake alifikiria nini, hivyo akataka aone alikuwa anataka kuchukua hatua gani.
Dylan alipofika karibu kabisa nyuma ya Camila, alipendezwa na nywele zake nyeusi, laini, na ndefu, zilizokuwa zimelala kutokana na kulowana na maji. Umbo lake lililochoreka vizuri ndani ya taulo lilipendeza sana pia machoni pake. Alikuwa anafikiria kumsemesha shangazi yake, labda aombe samahani, lakini jambo hilo lote likabadilika baada ya kumsogelea karibu hivyo.
Dylan alianza kumwangalia Camila, siyo kama mdogo wake na baba yake tena, bali kama mwanamke mwenye kuvutia sana! Hisia hii mpya kumwelekea Camila ilimfanya ajihisi kama mtenda dhambi mkubwa sana, lakini moyo wake ulitaka kuitalii hisia hiyo; haijalishi matokeo yangekuwa vipi. Camila alihisi waziwazi kabisa kwamba Dylan alikuwa nyuma yake, karibu sana, lakini hakumzuia, ball akaendelea kutulia akisikilizia ni kitu gani ambacho mpwa wake huyu angefanya, huku mapigo ya moyo wake yakikimbia kwa kasi.
Kisha Dylan akakigusa kiganja cha Camila kwa vidole vyake taratibu, na hii ikafanya Camila asisimke mpaka mishipa ya shingoni kuikaza. Angeweza kukisia kwa usahihi sasa kwamba Dylan hakutaka kumsemesha, bali kumtendesha! Ni kama Dylan alikuwa amepumbazika, yeye mwenyewe hakuelewa kwa nini alifikia hatua hii ya kumwonyesha shangazi yake upendezi wa kimahaba kumwelekea. Lakini bado alitaka kuendelea.
Akaanza kupandisha vidole vyake ta-ra-ti-bu kuelekea juu ya mkono wa Camila, kama vile anauchorea njia, na hii ikamsisimua hata zaidi shangazi yake, ambaye alikuwa akipumua kwa kasi kiasi huku uso wake ukionyesha hofu. Vidole vya Dylan vikaendelea kupanda mpaka begani kwa Camila, kisha akavitembeza kufikia kwenye shingo yake. Akaisugua-sugua kwa ulaini sana na kuvipandisha mpaka kwenye shavu. Camila akafumba macho, huku pumzi zake za hofu zikigeuka na kuwa mihemo ya mbali ya kimahaba. Dylan alikuwa amempandishia hisia zake za mahaba, na alikuwa amesisimka kupita kawaida.
Dylan akashusha tena kiganja chake hicho cha kushoto mpaka begani kwa Camila, huku na yeye pia akiwa amesisimka sana na kufanya mashine yake ivimbe ndani ya kaptura nyepesi aliyokuwa amevaa. Akasogeza uso wake karibu zaidi na kichwa cha Camila, kisha akaiweka midomo yake kwenye sikio lake na kulibusu kama analinyonya kwa wororo sana. Camila alifumba macho tena, akiwa haamini kabisa kwamba mpwa wake angeweza kufanya hivyo.
"Dylan....what...what are you..." Camila akauliza kwa kunong'oneza.
"I don't know....I don't...I don't know..." Dylan akajibu kwa kunong'oneza pia.
Alianza kusugua uso wake nyuma ya kichwa cha Camila, kimahaba sana, naye Camila alitokwa na fikira zote za kutaka kumzuia, kwa kuwa aliishiwa nguvu kutokana na uzito wa hisia za mahaba zilizomvaa hapa. Kama ndiyo ilikuwa njia ya kumwomba samahani, basi Dylan aliipeleka samahani hiyo mbali mno. Akakishusha kiganja chake mpaka kwenye ubavu wa Camila, kisha akakipandisha taratibu kufikia sehemu ya taulo iliyoibana kwenye mwili wa Camila.
"Dylan..." Camila akaita huku anatazama mbele kwa wasiwasi.
Dylan akaivuta sehemu hiyo, nayo ikaachia huku bado akiwa ameendelea kuishikilia.
"Oh my God!"
Camila akanong'oneza kwa hofu huku amefumba macho baada ya Dylan kufanya hivyo.
DYLAN IS A BAD BOY!
UNAFIKIRI NI NINI KILIFUATA BAADA YA HAPO?
★★★★★★★★★
ITAENDELEA
★★★★★★★★★
Usikose sehemu za mwendelezo wa hadithi kali ya DYLAN. Waweza ipata yote kwa sh. 2000 tu WhatsApp.
WhatsApp no: +255 787 604 893 (hii ni namba ya WhatsApp, siyo ya malipo. Ya malipo utaipata ukija WhatsApp. Karibu sana)
Why's that lovely?Mmh babe siku hizi unanifanya nikose hata chakucomment
utamu unazidi kunoga hadi najikuta nakosa lakuongeaWhy's that lovely?
Nimependa zaidi neno "utamu" kwenye hayo uliyoandika 😂. Asante sanautamu unazidi kunoga hadi najikuta nakosa lakuongea
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Nimependa zaidi neno "utamu" kwenye hayo uliyoandika [emoji23]. Asante sana