DYLAN
Story by Elton Tonny
Familia, Kazi, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Unyanyasaji, Usaliti, Visasi, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa
(R-rated 18+)
Enjoy!
★★★★★★★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA THELATHINI NA TISA
★★★★★★★★★★★★★★★★★★
Dylan akabaki macho wazi, akiwa hajui ni jinsi gani angepaswa kuitikia wonyesho huu wa upendo kutoka kwa Fetty.
Fetty alipouachia mdomo wa Dylan kidogo, akaubusu tena kimahaba sana huku akiwa amefumba macho yake. Sasa mwanaume akaanza kupatwa na hisia kali zilizofanya aanze kurudisha busu hii. Akili yake ilikuwa ikijaribu kupingana na kitendo hiki lakini moyo wake ukamsukuma kuendelea kuipokea midomo laini ya bibie. Fetty alianza kuitembeza mikono yake kichwani kwa Dylan, naye Dylan akamshika kiunoni taratibu huku wakiwa wanaendelea na busu yao.
Miguno ya chini kutoka kinywani mwake Fetty ilisikika vyema kwa Dylan, na sasa jamaa akawa akitambua kuwa jambo hilo lingeenda mbele sana; sehemu ambayo haikutakiwa. Kumfikiria Leila, jinsi alivyomsaliti na kusababisha aachane naye, na Grace, ambaye alikuwa amemsaidia kwa mengi mpaka kuwa naye kimapenzi, kuliighafilisha akili ya Dylan kwa kadiri kubwa na kumfanya aushike uso wa Fetty na kuachanisha midomo yao.
Fetty alikuwa anapumua kwa kasi kutokana na kupandwa na hisia nyingi, na macho yake yalionyesha uhitaji mkubwa sana wa kutaka Dylan azitulize hisia hizo.
"Fetty..."
Kabla Dylan hajamalizia alichotaka kusema, Fetty akamwekea kidole chake juu ya mdomo wake ili kumzuia. Ni kama alikuwa ameshaelewa kile ambacho Dylan alitaka kusema, lakini akawa hataki kukisikia. Akakitoa kidole chake taratibu na kuusogeza mdomo wake mpaka kwenye mdomo wa Dylan na kuigusisha kwa wororo.
Harufu nzuri ya Fetty iliingia vizuri sana puani mwa Dylan, nayo kwa kiasi kikubwa ilimfanya aufurahie zaidi ukaribu huo wa mwanamke huyu. Midomo ya Fetty ikaanza kuikandamiza ya Dylan zaidi, na ulimi wake ukawa unatafuta njia ili kuweza kuingia ndani ya mdomo wa jamaa. Dylan akafungua mdomo wake na kuupokea wa mrembo huyu, na wote wakaanza kuzungushiana ndimi zao kimahaba tena.
Jambo hili lilikuwa linatembeza hisia kali sana mwilini mwa Dylan, na kwa sababu asiyoijua ilikuwa ni kama mawazo yake yote yaliyomuandama yalitoweka kadiri alivyoendelea kupiga busu na Fetty. Wakaendelea kuonyeshana penzi la mdomo kwa sekunde kadhaa, na sasa Fetty akawa anarudi nyuma-nyuma kuingia ndani ya chumba chake bila kuuachia mdomo wa Dylan.
Dylan alijihisi utofauti wa hali ya juu sana, na hasa hii ilitokana na ukweli wa kwamba hakuwahi kufanya jambo kama hilo akiwa kwenye uhusiano na mtu mwingine, kwa hiyo ngazi za kusisimuliwa na kitendo hiki zilikuwa za juu. Hakuna hata sekunde moja iliyopita ambayo Dylan aliendelea kufanya hivi bila kumfikiria Grace. Lakini ni kama kuna kitu kilimsukuma tu aendelee licha ya kwamba akilini alijua hakupaswa kufanya jambo hilo kwa kuwa, kama ni mambo mengi aliyochukia zaidi, ilikuwa ni kufanyiwa usaliti, lakini sasa yeye ndiyo alikuwa anaufanya.
(........).
(........).
(........).
(........).
Wote walibaki wakipumua kiuchovu baada ya kupeana mapenzi kwa mara ya kwanza.
Fetty ndiye aliyejihisi furaha isiyo na kifani baada ya kushiriki mwili wake na mwanaume aliyempenda sana. Dylan kwa upande wake alihisi kitulizo pia, ingawa alielewa kwamba hii ingekuwa ni kitu ya muda mfupi sana kwa kuwa tayari alikuwa wa mtu mwingine. Mwanaume akajigeuza na kulala chali pia, akiwa karibu kabisa na kichwa cha Fetty, wote wakitazama juu huku wameshikana viganja vyao kitandani hapo.
Fetty akamgeukia Dylan, kisha kwa upendo akambusu kwenye shavu lake. Dylan akamwangalia pia, naye Fetty akaanza kuibusu midomo yake taratibu.
"Ninajua unachowaza Dylan," Fetty akamwambia baada ya kujitoa mdomoni mwake.
"Nawaza nini?"
"Kwamba haya ni makosa."
"Hapana... siyo..."
"Usijali Dylan. Ninakujua vizuri. Ninajua huwa hupendi kusalitiwa, na jambo hili tulilofanya limekufanya ujione kama msaliti. Naelewa," Fetty akasema kwa hisia.
"Unajuaje hilo?"
"Kipindi kile niliona jinsi ulivyotaabika Harleen alipokusaliti, kwa hiyo najua jinsi unavyohisi."
"Harleen? Mtoto wa rafiki yake mama?"
"Ndiyo."
"Niliwahi kutoka naye?"
"Ndiyo."
Dylan akashusha pumzi huku akimwangalia bado.
"Usijichukie wala. Nikuombe tu samahani kwa sababu nimekuwa mbinafsi. Ninajua hatukupaswa ku..."
"No, please usiseme hivyo," Dylan akamkatisha.
Fetty akawa anamtazama tu kwa hisia.
"Labda mimi pia nitakuwa mbinafsi kwa kusema hivi, lakini ukweli ni kwamba nimefurahia penzi lako Fetty. Ni sawa kusema hii haikuwa sahihi, na mimi ningejuta sana kufanya hivi wakati nikiwa kwenye uhusiano na mtu mwingine nayempenda, lakini sijui ni kwa nini tu sihisi kujuta kufanya hivi na WEWE," Dylan akasema kwa hisia pia.
Fetty akaachia tabasamu hafifu kwa kuyapenda sana maneno ya Dylan. Akaanza kuushika uso wake na kutembeza vidole vyake kwenye nywele za jamaa, akimwangalia kwa upendo sana. Alipotaka tu kuifata midomo yake ili ambusu kwa mara nyingine, simu ya Dylan ikaanza kuita. Dylan akageuka taratibu na kuichukua, na hapo akapata kuona mpigaji hakuwa mwingine ila Grace. Akamwangalia Fetty, naye Fetty akamtikisia kichwa kumwonyesha kuwa ilikuwa ni sawa akipokea tu.
Dylan akaongea na Grace, ambaye aliuliza mwanaume wake huyu angerudi wakati gani kwa kuwa alihofia usalama wake na alikuwa amem-miss sana. Dylan akamwambia kuwa ni kesho ndiyo angerudi nyumbani, na kumwambia asiwaze sana kwa sababu alikuwa sehemu salama. Kwa umalizio, kumwambia Grace kwamba anampenda kilikuwa ni kitu kilichoichoma sana nafsi ya Fetty. Hakuweza kujizuia kutamani kwamba ingekuwa ni yeye ndiyo angepaswa kuambiwa maneno hayo, na kujua kwamba jambo hili alilofanya na Dylan halingewezekana kurudiwa tena kulimfadhaisha, lakini hakukuwa na jinsi.
Baada ya Dylan kumaliza kuongea na mpenzi wake halisi, akamgeukia tena mpenzi wake wa wakati huu na kumwangalia kwa hisia sana. Fetty akampa tu tabasamu dogo, kisha akanyanyuka na kwenda zake bafuni. Dylan alijua wazi kwamba hiki kilikuwa ni kizungumkuti kikubwa sana, na hisia zake zilivurugika mno kila mara alioomuwaza baby mama wake. Alijua ikiwa Grace angetambua kuhusu kitendo hiki, basi angevunjika moyo sana na huenda hata kukasirika. Lakini kitendo chenyewe kilikuwa kimempa aina fulani ya furaha ambayo ilimfanya ajiulize ni kwa nini ilikuwa hivyo. Labda alikuwa na hisia za upendo kumwelekea Fetty pia? Kama ni hivyo, zilianza lini? Alijikuna sana kichwa kwa kukosa majibu sahihi.
Fetty akatoka kujimwagia maji bafuni na kurudi chumbani. Alivaa tena night dress yake mbele ya Dylan, kisha akapanda kitandani na kujilaza kifuani kwa jamaa, bila kumwambia lolote. Hali hii ilimshangaza kiasi Dylan. Fetty alikuwa mwanamke wa aina tofauti kabisa. Yeye akamwekea tu mkono mgongoni na kumwacha alale hapo mpaka usingizi ulipowapitia wote bila kusemeshana chochote kabisa baada ya kupeana mapenzi yao ya marufuku usiku huo.
★★★
"Kweli?" Grace akamuuliza Jafari, wakiwa wanaongea kwa simu.
"Ndiyo. Nilipata tip kuhusu alipokuwa, lakini nilipofika sehemu hiyo nikakuta hayupo. Kilichoshangaza ni kwamba mlinzi wake alikuwa amezimia hapo kwa muda mrefu sana; karibia kufa kabisa," Jafari akamwambia.
"Kwa hiyo kuna mtu, au watu walimvamia na kumteka unataka kusema?" Grace akauliza.
"Inaonekana hivyo boss. Sina uhakika sana lakini... nadhani kwamba..."
"Itakuwa ni Dylan," akamalizia Grace.
"Ndiyo. Lakini amewezaje kufanya hivyo kwa kasi sana boss? Na Mr. Bernard atakuwa amemweka wapi?"
"Ngoja niongee naye ili nijue kama kwe...."
Kabla hajamaliza maneno yake, alisikia horn ya gari nje ya geti la nyumba. Akakisia kuwa huenda Dylan alikuwa karudi, na moyo wake ukaingiwa na furaha kwa tarajio hilo.
"Nitakupigia baadae Jafari, keep me updated," Grace akamwambia.
Baada ya kukata simu, akanyanyuka kutoka sehemu aliyokuwa amekaa sebuleni hapo na kutazama nje kupitia dirisha pana na refu usawa wa mlangoni. Aliona gari likiingia ndani na kuegeshwa, kisha Dylan akashuka na kuanza kuja usawa wa mlango wa nyumba. Mwanaume alipoingia ndani, aliweza kumwona Grace akiwa amesimama hapo, akimtazama kwa njia fulani iliyo serious. Akatulia tu usawa wa mlango akimwangalia kwa hisia sana, na kumbukumbu ya kwanza akilini mwake lilikuwa ni kile alichofanya na Fetty usiku wa jana. Alijihisi vibaya kwa kadiri kubwa kwa kuwa ikiwa asingemwambia, basi angekuwa bonge moja la mnafiki kwenye uhusiano wao. Lakini tena ikiwa angemwambia huenda ingesababisha matatizo ambayo yangevuruga umoja wao ambao ulikuwa muhimu hasa kwa ajili ya mtoto aliyekuwa njiani. Akashusha tu pumzi na kuanza kumfata mwanamke wake pale alipokuwa amesimama.
Baada ya kumfikia karibu zaidi, akamkumbatia kwa upendo huku akijihisi kuwa mwenye hatia sana, mpaka akawa anakaribia kulia. Grace akajitoa kwenye kumbatio lake na kumtazama tu usoni, akionyesha wazi kwamba alikuwa ameudhika.
"I'm sorry," Dylan akasema kwa sauti ya chini.
"Jana kwa kuwa hukuwa ofisini, closure nyingi..."
"Naelewa Grace. Nitazishughulikia... ninaomba unisamehe sana Grace... sana," Dylan akasema kwa hisia.
Grace akatazama pembeni.
"Najua nimekukwaza, hapana... nimekuumiza. Grace, sitarudia tena kukutendea hivi. Nimekuwa mbinafsi sana, sana, sana. Ikiwezekana niadhibu maana... am so sorry. Yaani sijui..."
"Dylan stop, please..." Grace akamkatisha.
Dylan akabaki kumwangalia tu kwa huzuni.
"Kwa nini nikuadhibu? Ndiyo umekuwa mbinafsi, lakini ikiwa uliona ni sahihi kufanya vile ili umpate Mr. Bernard, basi hakuna haja ya kuomba samahani," Grace akamwambia.
Dylan akatazama chini kwa huzuni, akiwa anaelewa kwamba Grace hakujua samahani yake ilikuwa na mapana mengi.
"Ila usije kurudia kutoka tu... unaondoka kwa hasira... Dylan nakupenda sana. Ninajua ulikuwa na maumivu mengi kwa sababu ya Baraka lakini nami sitaki kukupoteza pia...unataka..."
Dylan akamkatisha kwa kuanza kumpiga busu taratibu kwa upendo mwingi sana. Grace aliitikia vyema pia na kuibusu midomo ya Dylan kwa shauku kubwa kimahaba, kisha Dylan akaiachia midomo yake taratibu na kuweka paji lake la uso kwenye paji la Grace.
"Nakupenda pia Grace. Sana. Hutanipoteza... I promise you that," Dylan akasema kiustaarabu.
"Shikamoo kaka Dylan," sauti ya Matilda ikasikika.
Dylan akajitoa kwenye paji la uso la Grace na kumwona msaidizi huyo wa kazi akiwa amesimama umbali mfupi kutokea walipokuwa.
"Marahaba Matilda. Za hapa?" Dylan akajibu.
"Nzuri."
"Anakula vizuri huyu?" Dylan akamuuliza Matilda.
"Ndiyo," Matilda akajibu akiwa anatabasamu.
Grace akatabasamu pia huku akiwa ameubana mwili wake kwenye mwili wa Dylan, akimwangalia kwa njia ya kudeka.
"Niwaandalie chakula?" Matilda akauliza.
"Ndiyo Matilda. Au ulikuwa umeshakula?" Grace akamuuliza Dylan.
Dylan akatikisa kichwa kukanusha.
Hivyo, Matilda akarudi jikoni kuwaandalia vyakula.
"Umetumia njia gani mpaka ukampata Bernard?" Grace akamuuliza Dylan.
"Aam... bado sijampata. Nimeomba msaada wa rafiki yangu anisaidie kumpata maana ana njia nyingi sana."
"Njia illegal?"
"Kwa kiasi fulani."
"Kwa hiyo huyo rafiki yako bado hajampata?"
"Ndiyo anamtafuta. Atanijulisha endapo..."
"Inaonekana ameshampata," Grace akamkatisha.
"What?"
"Jafari alikuwa amekaribia sana kumshika, lakini akakuta ameshachukuliwa na watu fulani," Grace akamwambia.
"Kumbe? Bado sija..."
Wakati akisema hivyo simu yake ikaanza kuita, naye akaitoa na kukuta ni Queen ndiye aliyekuwa anapiga. Akapokea.
"Queen..."
"Killmonger... we have your guy (tumempata mtu wako)," Queen akasema.
"Whoa! Mmempataje haraka namna hiyo? Nilifikiri itachukua siku kadhaa," Dylan akasema.
"Bullshit! Hapa Tanzania kuna sehemu ya kujificha sasa? Ninaye. Analetwa huku ASAP. Unataka nimfanye nini sweety?" Queen akasema.
"Nielekeze sehemu mtakayomweka ili nije hapo. Na tafadhali naomba favour moja...."
"Nini hiyo?"
"Pigeni mijeledi huo mwili mpaka nitakapofika, na asife."
Queen akacheka.
"Okay my Killmonger. Nakutumia location, wahi uje," Queen akamwambia.
Kisha Dylan akakata simu na kumtazama Grace, aliyekuwa anamwangalia kimaswali.
"Queen ni nani?"
Swali la Grace lingempa nafasi Dylan ya kuanza kumweleza kuhusu njia aliyotumia mpaka akafanikiwa kumpata Mr. Bernard, na baada ya kuwa ametumiwa kwa ujumbe sehemu aliyoshikiliwa mwanaume huyo, Grace akasema angekwenda pamoja naye pia ili hatimaye aweze kuonana naye ana kwa ana baada ya miaka mingi sana kupita.
★★★
Harleen alinunua vifaa vidogo sana vya kurekodia sauti (mini audio recorder), na kuvipachika kimoja kwenye gari la mama yake na kingine chumbani. Vilikuwa vimeunganishwa kwenye spika zake ndogo ambazo angekuwa nazo yeye muda wote ili kuweza kusikiliza mazungumzo ya mama yake wakati wowote ule. Ijapokuwa hakuwa na uhakika kama sehemu hizo alizotegeshea zingekuwa na matokeo mazuri, alitumaini angepata tu jambo fulani lenye kumjuza ni nini ambacho mama yake alikuwa anafanya wakati huu.
Sababu kuu ilikuwa hasa ni baada ya kuona video zile za kurekodiwa ambazo bila shaka alijua ni baba yake ndiye aliyezirekodi kupitia kwa mtu fulani. Lakini pia, usiku ule aliomkuta mama yake anaongea na simu chumbani, alikuwa amemsikia akisema "zote zimwishie mwilini," na kwa haraka hakuweza kuelewa maneno yake hayo yalimaanisha nini, lakini kwa sasa akayatilia maanani na kufikia mkataa kwamba kuna kitu ambacho mama yake alikuwa anafanya ambacho, hakikuwa sawa.
Ndani ya siku hizi chache ambazo alikuwa ameanza kumfatilia mama yake, hakupata kumsikia akisema jambo lolote lenye kushtusha, lakini akawa makini kutegea nyakati ambazo alikuwa angekuwa chumbani au kwenye gari ili asikilize. Ndipo siku hii ilipofika, akasikia mama yake akisema maneno yaliyomwacha akiwa haamini kabisa masikio yake, na sijui angeamini ya nani sasa!
Ilkiwa ni usiku wa siku hii sasa, wakati wote wakiwa nyumbani kwao wakila, Beatrice akapigiwa simu na kunyanyuka kwenda kuongelea chumbani kwake. Harleen naye akanyanyuka na kwenda kwenye chumba chake ili aweze kusikiliza maongezi hayo kupitia kifaa chake.
"...wakati mwingine ninatamani tu niwafate na kuwa-shoot wote! Wananikera sana.... Hakuna.... Nimesema hapana Bernard, acha nifanye mambo navyojua kuwa sahihi... hawawezi kunishinda hata siku moja.... Kama wanafikiri wamepiga hatua mbili mbele zaidi yangu wamefeli sana, mimi niko tatu mbele zaidi! Kama vipi wakamuulize yule kachero wao Baraka... na bado...."
Harleen alikuwa anajua kuhusu msiba uliompata Baraka. Kilichomshangaza ilikuwa ni kwa nini mama yake angesema maneno hayo kuhusu mwanaume huyo aliyeuawa kikatili namna ile.
"....natafuta tu nafasi nzuri nimkarabati huyo Dylan... nikimmaliza huyo nafata na Jaquelin... nimeshachoka kuigiza kuwa BFF sasa! ... Sitaki kutumia mtu kwa hili Bernard, nitadili nalo mimi mwenyewe... Una mpango gani huko uliko? ...."
Harleen aliendelea kusikiliza maongezi hayo akiwa amechoka kihisia. Ikiwa mama yake ndiye aliyemuua Baraka, na alikuwa akipanga kumuua Dylan na Jaquelin, basi ni yeye pia ndiye aliyemuua baba yake! Lakini alijiuliza ni kwa nini mama yake alikuwa anafanya haya yote. Ndiyo alielewa kwamba inaonekana zilikuwa ni hasira tu kwa sababu hakuendelea kuwa na Gilbert tena. Ila mpaka kufikia hatua ya kuua watu, tena wengine wasio na hatia, ni kitu ambacho kilimuumiza sana Harleen. Hangeweza kuruhusu maovu haya yaendelee tena, hivyo akaamua kufikisha taarifa hizi kwa Dylan ili achukue hatua ya kumdhibiti mama yake kabla hajaumiza mtu mwingine yeyote.
Wakati Harleen akijiandaa ili aondoke, Beatrice alikuwa amemaliza kuongea na simu yake pale alipotaka kuiweka kwenye meza yake ndogo ya humo na kuangusha kilainishi cha uso chini baada ya kukipamia. Akachuchumaa ili kukiokota, na hapo akaanza kuona mwanga mwekundu wenye kufifia ukitokea chini ya meza hiyo. Hii ikavuta umakini wake, naye akasogeza mkono wake na kugusa hapo kwa chini. Alihisi kitu fulani kigumu kiasi kwenye kidole, hivyo akakishika na kukichomoa hapo. Alishtuka sana baada ya kutambua kilikuwa ni kifaa cha kusikilizia sauti na kurekodi pia.
Maswali mengi yaliingia akilini mwake. Ni nani aliyeweka kifaa hicho humo, kwa usahihi kabisa kuonyesha kwamba alikuwa anamfatilia? Hakukuwa na yeyote aliyekuja kwake, na hapo kwake walioishi ilikuwa ni yeye, watoto wake wawili, na wasaidizi wa kazi, pamoja na mlinzi wa nyumba. David hangeweza kupata kifaa cha namna hiyo kwa sababu kwa kukiangalia kilikuwa na gharama. Hivyo ikawa wazi kwake kwamba ni binti yake ndiye aliyekitega humo. Lakini kwa nini angefanya hivyo? Na alikuwa ameanza kumpeleleza tokea wakati gani?
Kutokana na maswali mengi aliyokuwa nayo kichwani, na kutambua kwamba ni muda mfupi tu alikuwa ametoka kuongea na Mr. Bernard ikimaanisha alikuwa amesikiwa, akatoka haraka sana kwenye chumba chake na kukifata cha Harleen. Alipofika, akamkuta binti yake akiwa anavaa sweta jeusi, huku chini akivalia suruali ya jeans na sneaker nyeupe miguuni. Alipomwangalia machoni, alitambua kwamba Harleen alikuwa analia, na hapo hapo Harleen akaacha kumtazama mama yake na kujifuta machozi huku anaweka simu yake mfukoni.
Beatrice akaingia ndani humo akitembea taratibu, mapigo ya moyo yakimkimbia kwa kasi kutokana na wasiwasi mwingi aliokuwa nao.
"Harleen... ni wewe ndiyo umeweka hiki kidude chumbani kwangu?"
Beatrice akauliza hivyo, naye Harleen akamwangalia. Lakini hakusumbuliwa tena na hilo kwa kuwa tayari ukweli aliujua, hivyo akampita ili aondoke. Lakini Beatrice akamshika mkono na kumng'ang'ania.
"Nijibu... wewe ndiye..."
"Ndiyo. Ni mimi," Harleen akamkatisha.
Pumzi za Beatrice zikaanza kupanda. Harleen akawa anatikisa kichwa kwa kuhuzunika.
"Harleen... nisikilize. Chochote kile ulichosikia usichukulie kwa njia... haiko kama unavyofikiria..."
"Ila ikoje?"
Beatrice akashindwa kuongea.
"Nielezee. Baraka, rafiki yake Dylan, umemuua. Unataka kumuua Dylan na mama yake pia. Hebu nipe sababu moja muhimu ya kujitetea ambayo itahalalisha unyama unaofanya mama!" Harleen akasema huku analia.
"Hapana... hapana... hapana... Siyo hivyo Harley... nisikilize baby. Mimi ni mama yako. Sawa? Nina maana yangu... usiamini kila kitu ulicho..."
"Nisiamini nini mama? Kwamba wewe ni muuaji? Ingekuwa nimeambiwa tu na mtu... nimesikia mimi mwenyewe! Mama why? Just... unawezaje kufanya hivi?" Harleen akaongea kwa simanzi nzito.
"No, no, no, no.... Harleen.... baby tukae chini tuongee...nitakueleza kila kitu honey. Ona... hiyo simu... huyo nilikuwa namzingua tu, mimi siwezi kufanya mambo hayo. Kwa nini kwanza nifanye hivyo? Siwezi. Harleen...unanijua vizuri... siwezi kuua mwanadamu mwenzangu bila saba...."
"INATOSHA!" Harleen akasema kwa sauti ya juu.
Beatrice akabaki kumtazama kwa presha.
"Mimi siyo mtoto mdogo. Na uko sahihi. Nilfikiri ninakujua. Lakini kumbe sijakujua hata kidogo. Niachie... nimesema niachie! Mikono yako yenye umwagaji wa damu inanichafua!"
"Harleen...."
"Eti natafuta nafasi nzuri nimkarabati huyo Dylan! Mama, kijana wa watu amekukosea nini? Hivi kweli unataka kusema obsession yako kwa uncle Gilbert ndiyo imekupoteza namna hiyo?"
Maneno ya Harleen yakamfanya Beatrice atoe macho kwa mshangao. Hakutarajia kwamba Harleen alikuwa anajua kuhusu yeye na Gilbert.
"Ndiyo mama. Ninajua mlikuwa mna affair na baba yake Dylan. Lakini hata yeye alikuelezea kwamba hamkupaswa kuendelea kwa ajili ya familia zenu. Kwa nini umeamua kuwa chizi wa mapenzi kwa mtu ambaye ni wazi hakutaka tena kuwa na wewe?" Harleen akasema kwa hisia.
"Umejuaje hayo yote?" Beatrice akauliza kimshangao.
"Does it matter? Ni kwamba nimeshajua ukweli mama. Nini kinafata? Na mimi mtaniua kama mlivyomuua baba?" Harleen akasema kwa hisia kali.
Beatrice akaanza kurudi nyuma akiwa ameshtushwa na maneno ya binti yake. Alipandwa na presha ghafla. Harleen akawa anamwangalia huku machozi yakimtiririka
"Ni wewe na uncle Gilbert ndiyo mlimuua baba, si ndiyo? Niambie mama!" Harleen akasema kwa hisia.
Beatrice akaanza kutetemeka, hadi jasho likaanza kumtoka.
"Wewe ni mnyama mama! Najihisi kama... hhh... I hate you!" Harleen akasema kwa sauti kali sana.
Beatrice akashindwa kujikaza na kuanza kulia kwa majonzi sana.
"Ni lazima nihakikishe ubaya wako unakomeshwa. Siwezi kuruhusu uumize watu wasio na hatia kwa tamaa zako za kijinga... never," Harleen akasema.
"Harleen please... nisikilize my..."
"Don't touch me... don't..touch me!"
Harleen akamsukuma mama yake kwa nguvu na kusababisha aangukie chini.
Beatrice alikuwa analia sana.
Bila kuchelewa Harleen akatoka ndani humo ili aondoke, na mlangoni aliweza kumkuta David akiwa amesimama huku analia pia. Akamwangalia kwa sekunde chache, akishindwa hata amwambie nini mdogo wake, naye akatoka upesi na kwenda mpaka kwenye gari lake. Beatrice alibaki kulia tu ndani ya chumba cha Harleen, akihisi maumivu mengi sana kutokana na maneno ya binti yake.
★★★
Dylan pamoja na Grace walifika eneo ambalo walikuwa wameelekezwa na Queen. Kulikuwa na jengo dogo sehemu hiyo liliozungukwa na gari chache, na huu ulikuwa ni upande wa mji wao wa kule walikoishi familia yake; yaani Gilbert na Jaquelin. Eneo hilo lilizungukwa na miti mirefu na giza zito pia, lakini mwanga wa taa za gari ulimulika vyema kuwaonyesha wawili hawa mambo vizuri. Waliposhuka kutoka ndani ya gari, walifatwa na wanaume wawili ambao walikuwa ni kama walinzi wa Queen, nao wakawaambia wawafuate ili kuwapeleka hadi ndani ya nyumba ile.
Walipofika kule ndani, walikuta ilikuwa ni sehemu ya wazi kabisa isiyokuwa na vitu vingi. Queen alikuwa amesimama hapo pia na mabaunsa wengine wawili, akimwangalia Dylan kwa hamu sana kadiri alivyozidi kusogea karibu. Palikuwa na giza pia ndani hapo lililopambanishwa na mwanga hafifu wa tochi walizoshika wanaume wale. Alipomkaribia Queen zaidi, Dylan akaushika mkono wa Grace ili wawe karibu hata zaidi. Queen akaachia tabasamu la mbali huku anamwangalia Grace.
"Who's your good looking friend? (rafiki yako huyu mzuri ni nani?)" Queen akauliza.
"Huyu ni Grace. Grace, huyu ni Queen," Dylan akasema.
"Sikujua ulikuwa unakuja na dada yako," Queen akasema.
"Mimi siyo dada kwake. Ni mpenzi wake," Grace akasema.
"Ooooh... kweli? Too bad. The boy was already turning me on (...basi hiyo mbaya. Huyu kijana alikuwa ameanza kunipagawisha sana)," Queen akasema kikejeli.
"Mimi na Grace letu ni moja. Tunamtaka huyo mpumbavu kwa hali na mali," Dylan akasema.
"I can see that... all the desperation. Amewafanya nini kwani?" Queen akauliza.
"Amefanya vitu vingi vibaya. Amewatesa wasichana wengi na kuwadhulumu watu haki zao. Na hata alijaribu kuniua mimi na Dylan," Grace akasema.
"Oh! Kumbe ndiyo hivyo? Alijaribu kukuua kwa sababu gani?"
"Hakuwa na sababu yoyote zaidi ya kuwa mwenye tamaa za kibinafsi," Grace akajibu.
"Mmmm... so all this is to exact revenge? You could have just told me to handle him for ya...(kwa hiyo hii yote ni kulipiza kisasi? si mngeniambia tu mapema ili nimshughulikie kwa ajili yenu...)" Queen akauliza.
Grace akamsogelea karibu zaidi.
"I want to make him feel all the pain he has caused many people. Killing him will not make him feel it. I'll deal with him in such a way that he'll wish it was better if he was dead! (ninataka kumfanya ahisi maumivu aliyowasababishia watu wengi. Kumuua haitamfanya ayahisi. Nitashughulika naye kwa njia ambayo itamfanya aone kifo kuwa bora!)" Grace akasema kwa mkazo.
"You talk big, girl. Ungekuwa na fire ya namna hiyo hiyo kwenye kumtafuta mbona ungekuwa umempata tayari? Ni kama ulikuwa ume-relax tu," Queen akamwambia Grace.
"Nilikuwa napanga mambo mengi carefully. Mpelelezi wangu alikuwa ameshampata wakati wewe ulipomteka," Grace akamwambia kwa uthabiti.
"Ahahahah... kwa hiyo nilipomchukua tu ndiyo huyo mpelelezi wako akampata? What a coincidence," Queen akasema.
"Unataka kusema nini?" Grace akauliza.
"You gotta be careful on whom you put your faith in sweetheart (kuwa mwangalifu kuhusu watu unaowaamini mpenzi)," Queen akamwambia.
Dylan alihangaishwa na jinsi wanawake hawa walivyopeana maneno kwa njia hiyo. Lakini alianza kuona ni kama Queen alikuwa sahihi. Jafari alikuwa akiwasaidia ndiyo, lakini ilipokuja kwenye suala la Mr. Bernard, ni kama alikuwa anajirudisha nyuma. Alifikiria wakati ambao Pius alikufa, yeye ndiye aliyempatia taarifa mapema, lakini bado kutokea wakati huo mpaka sasa eti hakuwa amempata Mr. Bernard. Kwa upande mwingine, haikuonekana kwamba ingewezekana kumfikiria Jafari kuwa mtu anayemlinda Mr. Bernard, kwa kuwa kama ingekuwa hivyo basi huenda Grace asingekuwa hai leo. Kwa hiyo Dylan akayaona maneno ya Queen kuwa kama ya tahadhari tu isiyokuwa na hatari kubwa.
"Unataka kusema nini? Kwamba mpelelezi wangu ananisaliti?" Grace akauliza.
"Wewe ndiyo umesema hivyo," Queen akamwambia.
Wanawake hawa walikuwa wanatazamana kwa hisia kali, ikionekana wazi kila mmoja alionyesha yuko makini sana. Dylan akasogea karibu yao ili kuvunja hali hiyo tata.
"Queen, yuko wapi huyo mpumbavu? Ninataka kumuuliza mambo mengi," Dylan akasema.
Queen, akiwa bado anamwangalia Grace machoni, akatoa ishara kwa kupiga vidole vyake viwili vilivyotoa sauti iliyosikika vyema, na hapo hapo taa zikawashwa kuelekea mwishoni mwa nyumba hii. Dylan na Grace waliweza kumwona Mr. Bernard akiwa kwa mbele kule, mikononi akifungwa kwa kamba nene zilizokazwa kwenye nguzo za ndani hapo; zilizoinyanyua mikono yake juu. Alikuwa amepiga magoti chini, huku kichwa chake akiwa amekiinamisha, na kifua chake chenye vinyweleo vingi kilikuwa wazi.
Queen akaanza kuwaongoza kumwelekea, na walipomkaribia, akawaangalia wawili hao huku anatabasamu.
"Here's your guy. Fucker was hiding in a truck self-contained room... what a bitch! (huyu hapa mtu wenu. alikuwa anajificha kwenye chumba cha kontena kubwa la gari..malaya kweli!)" Queen akasema.
Grace alikuwa akimwangalia kwa hasira sana.
"Amezimia?" Dylan akauliza.
"Amesinzia. He's all yours," Queen akamwambia.
Dylan akamsogelea Mr. Bernard karibu, kisha akamwasha kofi la nguvu usoni na kusababisha mzee huyo akurupuke kutoka usingizini. Akawa anawaangalia wote hapo kwa taharuki kubwa, lakini alipomwona tu Grace, akagandisha macho yake kwake kiudadisi. Alitambua kwamba mwanamke huyu alimjua, lakini hakuweza kukumbuka kikamili alikomjulia.
"Dylan... kijana wangu... naomba tuongee... usichukue hatua ambayo...."
"Shut up!" Dylan akamfokea.
Mr. Bernard akawa anaogopa sana huku akimwangalia tena Grace.
"Ninakuuliza swali moja. Ninataka jibu moja. Ni wewe ndiyo ulimuua Baraka?" Dylan akauliza.
Mr. Bernard akawa anapumua kwa presha kubwa tu. Hakujua aseme nini.
"Sidhani kama leo ndiyo siku yako ya kwanza kuwa na hizo lips nyeusi... ongea," akasema Queen.
"Siyo mimi!" Mr. Bernard akasema.
"Ni nani?" akauliza Dylan.
"Nitakwambia. Lakini kwanza, nifungue... halafu unilinde kwa kuwa..."
"Hivi we ni mshenzi eti? Mlijaribu kuniua mimi, mkamuua Pius na Baraka, halafu unajifanya unaweza ku-demand chochote kutoka kwangu? Niambie ni nani aliyekuwa akikusaidia... NOW!" Dylan akapaaza sauti kwa hasira.
Mr. Bernard akawa kimya tu, kama hataki kujibu.
"Okay this is getting old. You want me to make him talk? (hii inaboa. Nikusaidie kumfanya aongee?)" Queen akamwambia Dylan.
"Hapana. Ataongea tu," Dylan akasema.
Kisha akamshika na kumnyanyua ili asimame, na hapo hapo akaanza kumtandika ngumi nyingi sana hasa tumboni na usoni. Mr. Bernard alitoa kelele nyingi za maumivu, huku Dylan akiwa anamwambia aseme ni nani aliyekuwa akimsaidia. Mwishowe, alipoona hangeweza kuendelea kuficha tena kutokana na maumivu ambayo alipata, akamwomba Dylan aache kumpiga, naye angemwambia ni nani. Dylan akaacha, huku Mr. Bernard sasa akiwa amepiga magoti chini na damu zikimtoka mdomoni na puani mwake.
"Ongea..." Dylan akamwamuru.
Mr. Bernard akawa amelegea kwelikweli huku akiyasikilizia maumivu aliyohisi. Hapa hakuwa na ujanja tena kwa kuwa siku za wizi wake zilikuwa zimefikia arobaini.
"...ni... ni Beatrice... ni Beatrice ndiyo ana.... ndiyo amenisaidia... amemuua yule mwanaume..."
"Beatrice gani?" akauliza Dylan.
"Rafiki yake na mama yako..." akajibu Mr. Bernard.
Dylan akashindwa kuelewa.
"Beatrice?!" Grace akauliza.
"Kwa nini afanye hivyo?" Dylan akamuuliza Mr. Bernard.
Mzee akawa anapumua kivivu tu. Dylan akamshika kichwa na kumtazama usoni kwa ukaribu.
"Sitaki unifanye mimi fala mwenzio. Niambie ukweli," Dylan akamwamuru.
"Ni kweli... ni yeye. Mimi sijaua mtu... sijafanya chochote kibaya Dylan niamini..."
Dylan akakisukumiza kichwa chake kwa kukerwa.
"Nipe sababu moja kuu ya kuamini maneno yako," Dylan akamwambia.
"....yule mwanamke anataka... anamtaka baba yako. Anataka... anataka kuivuruga familia yenu... Anaweza kuwafanya chochote anachojisikia... ni mkatili sana ndiyo maana me nikaogopa hata... nikafanya mabaya yake lakini..."
"Acha kujifaraghua, fala wewe. Umekuwa mtoto upelekeshwe kwani? Tunajua nature yako Mr. Bernard wala usijilambe-lambe. Huyo Beatrice ndiyo wa kuua mtu kisa tu anamtaka baba yangu? Bado hujani-convince," Dylan akasema.
"Hapana sikudanganyi. Ni yeye...aah ssss...alinitafuta nika... alinipanga ili tuwaangushe Gilbert na Jaquelin kwa pamoja. Mpango ulikuwa kuichukua kampuni... mimi sikutaka kuhusika kwenye mauaji ila yeye ndiye aliyesema ufe kwa kuwa aliogopa ungemletea matatizo. Yule ndiyo mbaya wenu... siyo mimi. I'm a victim here too..."
Grace akasonya kwa kukerwa sana na mwanaume huyo. Dylan akamwangalia Grace akiwa anayatafakari maneno ya Mr. Bernard kuhusu Beatrice. Hili kwa kweli lilikuwa ni jambo lisilowazika kabisa.
"Msinifanyie kitu kibaya tafadhali nawaombeni. Yule mwanamke ni sumu, niko tayari kufichua mabaya yake ili...."
"Huyo Beatrice... mpaka sasa... oh God! Nahitaji kuwaonya wazazi wangu," Dylan akamwambia Grace.
"Kikulacho hah..." Queen akasema.
"Ndiyo. Ni jambo la muhimu sana kuwaambia haraka. Halafu inabidi tuhakikishe anakamatwa bila yeye kutarajia," Grace akasema.
Dylan akatoa simu yake ili ampigie Gilbert.
"Vipi kuhusu huyu? Nitafurahi mkiniambia nimkatekate ili nimtengenezee mbwa wangu supu," Queen akawaambia.
"No please... tafadhali nina..." Mr. Bernard akawa anaomba asidhurike.
Dylan alimpigia baba yake simu, lakini hakupokea. Hivyo akaona ampigie mama yake badala. Ila kabla hajafanikiwa, simu yake ikaanza kuita, na mpigaji alikuwa ni Harleen. Dylan alikumbuka vizuri kuwa huyu alikuwa ni binti wa Beatrice, ambaye sasa alikuwa amepata kujua kuwa ndiye adui yake mkubwa. Akapokea akiwa makini sana.
"Hello... Dylan?" sauti ya Harleen ikasikika.
"Naam..." Dylan akaitikia.
"Dylan... kuna jambo muhimu nataka tuzungumze. Naomba tukutane."
"Jambo gani?"
"Tafadhali Dylan, naomba tukutane. Ni muhimu mno kwa kuwa... inahusiana na mtu anayejaribu kukuua. Nimemjua... nataka nikwambie ni nani, na nina ushahidi wa kukusaidia ili akamatwe. Please kutana na mimi," Harleen akaomba.
Dylan akamwangalia Grace, ambaye alikuwa anamtazama asijue mwanaume anaongea na nani, kisha Dylan akakubali na kumwambia Harleen wakutane. Kwa kuwa alikuwa jijini kwao, Harleen alimwelekeza sehemu ya kukutana ambayo haikuwa na watu ili aweze kumpa kile alichomwambia. Baada ya hapo, Dylan akakata simu na kumsogelea Grace.
"Grace, huyo alikuwa ni Harleen. Anasema ana ushahidi wa kunipa kuhusu mtu anayetaka kuniua," akamwambia.
"Nini?" Grace akauliza akiwa hajaelewa.
"Mtoto wa Beatrice yule wa kike, Harleen, anataka kunipatia ushahidi wa mtu aliyekuwa...."
"Una uhakika hiyo ni genuine? Je kama yeye na mama yake wanakuzunguka?" Grace akauliza.
"I'm not sure, sijui lakini... kuna chance kwamba anachosema ni ukweli. Nahitaji kujionea," Dylan akasema.
"Okay. Twende wote. Ikiwa kweli..."
"No Grace. Hatutaenda pamoja," Dylan akamkatisha.
"What?"
"Nahitaji kuwa mwangalifu. Kama ulivyosema, ikiwa ni mchezo nafanyiwa basi nahitaji kuwa makini. Lakini... wewe na hali yako, haitakuwa salama..."
"But Dylan..."
"Usijali Grace, mimi nitakuwa sawa. Nachohitaji zaidi wakati huu ni wewe kuwa salama, tafadhali."
Grace akashusha pumzi.
"Kwa hiyo unaenda mwenyewe?" Queen akamuuliza.
"Hapana. Nipe wanaume wako niende nao, just in case," Dylan akasema.
"Ahahahah... unavyoongea utafikiri umewaajiri. Wakifa huko?"
"Hawawezi, nawajua wako vizuri sana. Nisaidie Queen tafadhali, ninataka kuikomesha hii hali yote milele, please..."
"Okay fine. Jacob na Hussein, nendeni na Killmonger. Mpeni protection endapo kutatokea shida," Queen akawaambia walinzi wake, nao wakakubali.
"Killmonger?" Grace akauliza.
"Aam... hiyo ni nickname yangu... nilikuwa natumia zamani. Queen, thanks, I really owe you a lot," Dylan akasema na kumshukuru Queen.
"Yeah you do. Nenda kashughulike na huyo mwingine, na sisi tutashughulika na huyu, au siyo... Grace?" Queen akasema.
Grace akatikisa kichwa kukubali, kisha akamgeukia Dylan na kumpiga busu ya kumuaga, na hapo hapo Dylan akatoka akiwa na wale wanaume kwenda mpaka kwenye gari ili waelekee kule walikokubaliana kukutana na Harleen.
★★★
Harleen alikuwa akisubiri ujio wa Dylan usiku huo peke yake. Sehemu hii ilikuwa ni ya jengo la ofisi lililoachwa na kutotumiwa kwa muda mrefu. Alikuwa peke yake nje hapo, akimsubiria Dylan ili aweze kumwambia ukweli wote, haidhuru ikiwa mama yake angechukuliwa hatua ya kisheria, kwa kuwa aliyoyafanya hayakuwa mazuri hata kidogo. Ilipita zaidi ya nusu saa tokea Harleen alipomwambia Dylan wakutane hapo, na sasa aliweza kusikia gari ikiwa inakuja upande huo alipokuwa. Likafika hatimaye na kuingia sehemu hiyo mpaka nyuma ya gari lake na kusimama hapo.
Lakini gari hili alilijua vizuri sana, na kwa haraka angeweza kusema halikuwa la Dylan hata kidogo. Lilikuwa gari la mama yake. Akaingiwa na hasira hata zaidi baada ya kumwona mama yake akishuka na kumfata, huku nyuma akisindikizwa na yule mlinzi wake gaidi. Alikuwa ametumia simu yake kumfatilia Harleen, na hivyo ndivyo alivyoweza kumpata huku. Mikononi mwake Harleen alikuwa ameshika kile kifaa cha kurekodia sauti alichotoka nacho nyumbani, naye akakirudisha nyuma ili kukificha.
Beatrice akamsogelea mpaka karibu akiwa na uso ulioonyesha mfadhaiko mkubwa sana.
"Harleen..."
"Unataka nini?"
"Harleen nisikilize. Mimi ni mama yako..."
"Kwa hiyo?"
"Nakupenda Harleen. Kila kitu nachofanya ni kwa ajili yako... na David..."
"Bullshit!"
"Harleen, tafuta kote utakapoenda lakini hautapata mama mwingine zaidi yangu. Mimi nimekuzaa, nimekulea, nimekutunza mpaka umekuwa hivi, huwezi kusema utanichukia kwa sababu... hhh... Look, hayo ni mambo yaliyopita binti yangu... eeh? Yasahau, mimi niko tayari..."
"Yaani yooote unayoyasema hayana faida yoyote kwangu mimi. Ongea chochote kile unachotaka, lakini kuanzia wakati huu sitaki tena kuwa na lolote la kufanya linalokuhusu. Hesabu hauna binti hapa, kwa sababu mimi siwezi kuwa na mama ambaye ni mfano wa Shetani!" Harleen akamwambia.
"Harleen usiongee hivyo. Kumbuka mambo yote ambayo..."
"Ninachokumbuka tu sasa hivi ni kile nilichokiona kwenye zile video. Ninachoona ni wewe ukimuua baba. Hakuna chochote kingine ninachoona zaidi ya ushetani wako mkubwa!" Harleen akaongea kwa hisia sana.
Beatrice akaanza kulia.
"Siwezi kukuachilia uendeleze mabaya haya. Nitayaweka wazi kwa wote uliowakosea..."
"Harleen..."
"....kama ndiyo itakuwa fundisho kwako ni bora uende jela kabisa ili ulipwe kwa mabaya yote uliyoyafanya. Unanifanya najihisi mchafu sana mama... how could you do this?" Harleen akawa anasema huku akilia.
"I'm sorry... I'm sorry...I'm...I'm...I'm sorry... Harleen please...."
"Mm-mm...usiniguse... don't touch me..."
"Harleen my baby... usimpe yeyote hiyo record... mimi ni mama yako... huna... tafadhali..."
"Niache. Ni lazima ufundishwe somo... siwezi kukubali umuumize Dylan hata siku moja..."
"Yaani... kwa ajili ya Dylan uko tayari kuni..."
"Ndiyo!"
"Harleen...."
Kulikuwa na hali nzito sana ya kihisia baina ya wawili hawa wakati huu. Beatrice akawa aking'ang'aniza kumkumbatia Harleen ambaye hakutaka hilo hata kidogo. Alimsukuma mara kadhaa ili kukataa kumbatio lake, lakini bado Beatrice akaendelea kulazimisha. Mwishowe, Harleen akatulia tu na kumwacha mama yake amkumbatie huku analia sana na kuomba amsamehe na asifichue mabaya yake.
"...please... baby I love you.... please usifanye hivi...."
"Its too late mommy. Siwezi kurudi nyuma tena..."
Beatrice akakaza macho yake kwa nguvu sana akihisi uchungu mwingi moyoni mwake.
"I'm sorry... nisamehe Harleen... nisamehe.... nakupenda my daughter... nakupenda sana...."
Mkono mmoja wa Beatrice ulirudi mpaka nyuma ya kiuno chake, naye akatoa bastola yake na kuipandisha taratibu mpaka usawa wa tumbo la binti yake. Harleen aliweza kuhisi kitu kigumu kikigusa tumbo lake, na ijapokuwa aliingiwa na hofu kubwa baada ya kutambua ilikuwa ni nini, akatulia tu hivyo hivyo na kufumba macho yake huku akitokwa na machozi. Beatrice alikuwa analia huku mkono wake mwingine ukizishika-shika nywele za kichwani za binti yake kwa wororo, kisha akavuta kidole chake kwenye kivutio cha bastola yake.
"Paahh!"
★★★★★★★★★★
ITAENDELEA
★★★★★★★★★★
WhatsApp +255 787 604 893