SIMULIZI: Eliza na Ndoa Yangu (Kisa cha kweli cha kusisimua)

SIMULIZI: Eliza na Ndoa Yangu (Kisa cha kweli cha kusisimua)

SIMULIZI: ELIZA NA NDOA YANGU
SEHEMU YA 8
Man Middo: 0655 969 973
[emoji1427]
wakawa ananiambia wewe si unajiona unavaa wazi kuna wanaovaa wazi zaid yako.

Tulifika sehemu sikumbuki jina tukaingia tukaagiza chakula mimi niliagiza chipsi samaki, sasa chakushangaza wenzangu waliletewa waichokiagiza ila mimi sijaetewa akaniuliza

“Mbona hujaletewa au hujaagiza?”

“Nimeagiza ila sielewe kwanini hawaleti”
akaniambia

“Agiza tena huenda hukusikika vizuri”

Basi nikawaza ngoja niagize chipsi nyama tu maana mwanzo niliagiza chipsi samaki ndo hawakuleta nikaagiza pale wakaleta chipsi nyama.

Sasa ile naanza kula tu kumbe ile oda ya kwanza pia walikua wanandaa ikaja wee!! nilishia kutoa macho tu, Mudy ndo nilimjua siku ile yupoje upande wa hasira alifoka mpaka nilijihisi kutetema

“Tamaa tu unagizaje vitu viwili mtu mmoja mara samaki mara nyama utamaliza vyote na tamaa zako aah!”

Bahati nzuri rafiki yake akamwambia wenye kosa ni wahudumu sio huyu ndo akakaa kimya ila kwangu chakula hakikushuka kwa kweli cha kushukuru tu akalipia vyote tukafungiwa samaki.

Niliwahi kwenda kwenye gari maana niliumia sana hasa alivyoniaibisha mbele za watu nikajua hata atanibembeleza angalau nitoe upweke yeye kimya kwake hakuna kitu kama hicho.

Tukaondoka kuelekea coco beach na ndio ikawa mwanzo wangu wakuiona bahari, tulifika sasa tukawa tunaangalia watu wanavyo jitupa kwenye maji.

Mimi sikuwahi kuona meli live nikaiona meli kubwaa nilifrahi sana nikawa napiga picha tu, siku hiyo ilikua sikukuu ya pasaka nikamuomba Shem Godii atupige picha Mimi na bae.

Mmh! Sasa mwenzangu kila nikionesha ushirikiano wa mapozi yeye aibu tu kazi yake kushangaa wanawake wenye makalio makubwa yaani nilibaki kumshangaa tu.

Basi tukainjoy pale coco baadae tukaondoka tukapitia suparmaket uchumi kipindi hicho inaitwa Game tukapitia na Mlimani city kwa kweli siku ile nilinunua kila nilichokitaka.

Kwakua tulisoma sana chuo kuhusu vinywaji nilinunua vinywaji baadhi vingi kidogo akawa ananikataza kununua vinywaji vyenye vilevi akidai wewe huviwezi nilikazania akawa hana namna, tukanunua piza bagar siku hiyo ndio nilivila kwa raha kwasababu nilivyokua chuoni tunajifunza sikufaidi vizuri.

Tukarudi hadi nyumbani na mizigo kibao Shem Godii alishuka njiani kwake, sisi tukafika nyumbani tukaoga tukaenda kulala na kesho yake mimi safari ya kurudi Moro.
********

Basi ikafika muda wa chakula cha usiku kwa watu wazima, chakula kisichohitaji karaha na bughdha wakati wa kukila.

Basi ikawa mwendo wa pilau na viungo kama vyote siku hiyo na ukizingatia kesho yake naondoka! Hehee! Pilau ilikua tamu balaa usiku huo.

Asubuhi ikafika! Kama kwaida ya asubuhi lazima mpate chai hasa kabla hujashuka kitandani basi kwa upande wetu chakuagiana tulichagua kahawa ya moto kidogo na ukizingatia kale kabaridi kaasubuhi kahawa ilikua tamu mnoo!

Baada ya kahawa nzuri akaniambia nichukue kiasi cha pesa ninachotaka kwenye droo nikachukua pesa ila nikachukua tu kama anavyonipa elfu 70 kwa wiki na elfu 30 dharula akanambia

“Ongeza za wiki ya mbili chukua na za mandalizi ya kuanzia field kutuma na choka harafu nabanwa, muda mwingine nachoka kweli kutuma tuma”

Nikafanya hivyo nikaondoka kama na laki 4 hivi na makolokolo yakuondokanayo niliyonunua suparmakert.

Baada ya hapo nikampigia simu rafiki yangu kujua kafikia wapi ili turudi kama tulivyopanga ili ionekane tulikua kwao Dar nilimpigia akasema yupo anajiandaa.

Basi sisi tukapanda gari hadi ubungo, kufika ubungo tulisubiri wee!! Halima hatokei hadi Mudy akachukia akanza kufoka

“Huyo mwenzio anafikiri mimi sina kazi au?”

Akawa mkali yani tayari nilishia kumsoma Mudy kwa muda mchache kuwa ni mkali sana moyoni nikajiambia bora nimekujua mapema usinioe tu. Badae akaamua tu anikatie tu tiketi niondoke akasema

“Huyo rafiki yako atakua ananauli maana asinge sumbua hivi mimi nawahi kazini”

Nikamuaga pale nikapanda bus nikanza kurudi Moro

(kama kunaendeka nijue kama hakuendeki njue wapii? Dar mpaka Moro)……. ITAENDELEA

Inaitwa ELIZA NA NDOA YANGU je huu ndio mwanzo wa hiyo Ndoa?

Usikose kitakachojiri hapo baadae.

NUKUU “Muda upo Huru lakini Hauna gharama (Huwezi ukaununua muda) Huwezi ukamiliki muda lakini unaweza ukautumia muda. Huwezi ukautunza muda, lakini unaweza ukautumia muda. PINDI UKIUPOTEZA MUDA, KAMWE HUWEZI UKAUREJESHA MUDA”

Rudia kusoma [emoji1426] ukishasoma shusha like Yako,
Muendelezo mkuu sehemu ya tisa
 
SIMULIZI: ELIZA NA NDOA YANGU
SEHEMU YA SABA (07)
man Middo +255 655 969 973

ILIPOISHIA………….kufika ubungo tulisubiri wee!! Halima hatokei hadi Mudy akachukia akanza kufoka

“Huyo mwenzio anafikiri mimi sina kazi au?”

Akawa mkali yani tayari nilishia kumsoma Mudy kwa muda mchache kuwa ni mkali sana moyoni nikajiambia bora nimekujua mapema usinioe tu,

Basi badae akaamua tu anikatie tu tiketi niondoke tu akasema

“Huyo rafiki yako atakua ananauli maana asinge sumbua hivi mimi nawahi kazini”

Nikamuaga pale nikapanda basi nikanza kurudi Moro (kama kunaendeka nijue kama hakuendeki njue wapii? Dar mpaka Moro)……SONGANAYO

Nilifika salama moro nilishuka msavu nikapanda haisi mpaka standi ndogo. Baadae bodaboda hadi chuoni baada ya kufika tu chuo kichwa kikanza kuniuma sana tena na mafua juu.

Baadae nikagundua kuwa nina allergy na AC maana nyumani kwa Mudy ipo, kwenye gari yake ipo na kwenye basi pia ilikuepo kwahiyo nilibwana kwakua nimetoka mazingira yale yenye AC.

Ilivyofika jioni rafiki yangu mnafiki Halima ndo anaingia akiniangalia anapepesa, macho nikamuuliza

“Kwanini kunitenda hivyo kumbe hukutaka kuongozana na mimi na kwanini usiseme tu ukweli?” aliishia tu kuniomba msamaha yakaisha.

Usiku kulikua na furaha sana pale room ukizingatia ndo tulikua tunatoka kalikizo kafupi na kesho yake tulikua ndio tunaenda tulikopangiwa field basi nikatoa vile vinywaji vyangu tukanywa kwa kuchanganya aisee tulilewaa hatari!

Asubuhi kila mtu alienda ofisini kuchukua form ya field na kuelekea alipochagua, wenzangu wengi walichagua Dar na mama yangu hakupenda nichague Dar hivyo nilibaki Moro.

Mama akaomba nikae kwa mama mdogo nisikae hostel ili awe anatoa hela ya nauli tu

(wakati huo kumbe rafiki yangu mnafiki Halima alikua bado anwasiliana na yule aliyekua boyfriend wangu na akamwambia kila kitu jinsi nilivyoenda Dar mpaka kurudi maana kuna muda nilikua najaribu kumtafuta anajibu shoti na baadae aliniambia kuwa najua kila kitu ndo nikagundua kuwa Halima bado anaendelea na unafiki wake, lakin mimi sikujali sana kwani boy mwenyewe ni mtu wakutaka kukaa tu bila kujishughulisha na alikua akinijibu hovyo nikimuambia swala la kujishughulisha. Mimi nilimuambia tu aendelee na huyo anaempa taarifa)

Baadae nikaanza field vizuri na ukizingatia nilikua na pesa kidogo, Kiukweli kipindi hicho nilikua na matunzo hata uzuri wangu niliona angalau japo mara nyingi sikuona kama watu walivyokua wanisifia.

Sasa nilivyofika ofisini kila mtu ananitaka Supervisor, mpishi mkuu yaani ikawa kila ninapopita nikutongozwa mpaka nikakosa amani yani.

Nilishangaa sana kwani hata huo uzuri wangu sikuuona kabisa kwani hata kujiremba sijirembi na nilikua navaa nguo ndefu sio kama wenzangu lakin ikawa kero kwangu.

Baadae niligundua kuwa kila atakaeenda pale kufanya field lazima atongozwe lakini mimi walizidisha yani, sasa ilifikia hatua supervisor ananitiashia kunipa aadhabu kama nisipomkubalia.

Kweli alikuja kinipa hadi adhabu ila sikujali sana. Pale field kuna mkaka mmoja aliitwa Matokeo siku moja aliniuliza

“Unaishi wapi?” nikamwambia akasema

“Kumbe tunaishi eneo moja nitakua nakupa lifti siku moja moja”

Kwasababu alikua na pikipiki basi tukanza urafiki na huyo mkaka, sasa supervisor alizidi kunichukia balaa...... ITAENDELEA.

Usikose kufuatilia episode ijayo.
On Twitter and Instagram [emoji1428]@middotz_[emoji1607]
 
SIMULIZI: ELIZA NA NDOA YANGU
SEHEMU YA NANE (08)
man Middo +255 655 969 973

[emoji1427]
Mudy alianza kupunguza mawasiliano taratibu, ule upendo wake wa mwanzo ulianza kupotea taratibu kwanza simu ilikua mpaka nipige mimi mara nyingi nikipiga simu anasema yupo bize ikiwa asubuhi, mchana hata usiku anasema amechoka analala.

Mara nyingi anasema eti mimi niongee tu ananisikia ila yeye hajibu chochote dah! Utafikiri mimi ndo nilimtongoza yani.

Mimi wakati huo ndo nilikolea kwake nikashindwa hata kumpotezea.

Kuna muda nilikaa kimya kwa siku tatu bila kumtafuta nikijua atanitafuta lakini wapi hakujaribu kabisa kunitafuta niliamua kumtafuta siku moja kwenye maongezi nikamwambia

“Mbona saivi hata hunitafuti?” alinijibu shoti tu

“Sio lazima tuongee kama hakuna cha kuongea na wewe”

Akakata simu harafu hakua mtu anaejali hata umtumie sms za aina gani ziwe za mahaba yeye hajali kujibu na mara nyingi alikua ananiambia hawezagi kuandika sms hivyo aliniambia nitume tu iliasome basi.

Lakini maajabu yake hakuwahi kuacha kunitumia hela hata nikae wiki mbili bila kumtafuta ila kila jumamosi bila kumuomba atanipigia simu atanisalimia harafu atanitumia, hakuwahi nitamkia nakupenda mara ya mwisho ni aliponitingoza hakuwahi pia kuniambia nimekumiss zaidi ya mimi.

Nilikuja kugundua Mudy nimbinfsi wa mapenzi anawajibika kitandani tu na kutuma pesa yeye masuala ya kumpetipeti mpenzi wake tupa kule. Basi nikaanza kuwaza

“Hivi umri huu nisisikie Nakupenda, nimekumiss na ninahamu na wewe”

Maana hata hao wanajeshi hawako hivyo. Kuna siku nilimpigia simu akaniambia anataka kulala nikamuliza mbona unawahi kulala nikamuacha alale akakata simu, Sasa kwangu nalala usingizi hauji nikasema

“Ngoja nimpigie tena kujua kama kalala”

(siunajua kupenda tena upo kama kipofu) sasa nampigia alipokea harafu nikashangaa kama yupo barabarani nikamuuliza

“Mbona kama upo barabarani ?” akajibu

“Kwani wewe unataka nini?” Nikamuambia

“Mbona sasaivi umebadilika mwanzo hukua hivyo kama hunitaki niambie”

weee nilijuta siku hiyo kama nilifungulia bomba la matusi alinitukana matusi makubwa ambayo hayasimuliki

“Wee msenge* nini mpuuzi mkubwa unawaza kitandan tu yani wee………………….. ningekua sikupendi ningekutumia pesa?, kama sikupendi kwangu ungekuja? Unakazania mapenzi tu utakula mapenzi wewe? Mbona nilikukuta hovyo kama mapenzi bila pesa mazuri? Mimi natafuta pesa wewe! Harafu unawaza ujinga ujinga tu”

Yani siku ile nilitetemeka niliia balaa nikakumbuka maneno ya Yule kaka wa kule field aitwae Matokeo aliniambia kuwa

“Kama hakujibu sms, haji kukuona, hakupigii simu zaid ya salamu mnaongea kama wazee ujue amewaweka foleni sio bure kuwa ni ubize na kazi”

Nikampigia simu matokeo nakumbuka ilikua saa 6 usiku nikamuelezea kila kitu akaniambia nimuache kwanza nione kama baada ya hapo hatanitafuta.

Basi nikakubaliana nae nilikaa wiki nzima bila kumtafuta lakini ilivyofika Jumamosi alinitumia pesa kama kawaida, tuliendelea kuwa kimya kila mmoja bila kumtafuta mwenzake.

Siku moja nilimkumbuka kuna rafiki yake kipindi nilipokua kwake ndo alikua ananiletea chakula kipindi Mudy akiwa katoka, yeye aliitwa Afidh nilisachi kwenye simu yangu kumbe namba yake ilikuepo, nikampigia simu akapokea niamuelezea jinsi Mudy alivyobadilika akaanza kunieezea jinsi Mudy alivyo akaniambia

“Mudy umvumilie tu, kwanza kizuri kwake si mchoyo wa pesa wala starehe shida kubwa kwake yupo bize sana, anaheshimu kazi, anapenda kazi harafu furaha yake mpaka aamue yeye mimi pia ni rafiki yake anaweza kupita na gari nje hata mara tatu kazini kwangu tena nje hapa lakini asinisalimie na unaweza kupita mwezi hapo anafuraha zake ndo anakuja kukusalimia.

Kuhusu kukupenda Mudy anakupenda sana tatizo ubize wa kazi tu mimi namjua hana jipya anathamini kazi tu na mpaka mademu zake wengi humuachaga hivyo hivyo bora wewe kakusifia sana msafi, unajali huna kibuli harafu sio Malaya hawezi kukuacha mvumilie tu jaribu kumfundisha mapenzi hajui huyu dogo”

Afidh alinitia moyo sana lakini mimi nilipanaga kutomtafuta mwezi mzima ili nijue mwisho wake nipokee tu pesa zake basi kweli nilikaa mwezi mzima bila mawasiiano mazuri zaid ya kutumiwa pesa tu nakuulizwa kama imefika basi, kwahiyo nilikua na mtu anaenipa pesa tu ila nyege zilikua zinanibana zinakata zenyewe....... ITAENDELEA.

Usikose kujua kilichotokea sehemu ya 8,

On Twitter and Instagram @middotz_[emoji1427]
 
SIMULIZI: ELIZA NA NDOA YANGU
SEHEMU YA SABA (09)
man Middo +255 655 969 973

Siku moja nilianza kuumwa nikawa najiskia kizungu zungu mara kichefu chefu nikaenda kupima nikaambiwa nina UTI nikapewa dawa nikatumia nikapona lakin kichefu chefu kilikua bado kinaendelea nikaanza kuchagua vyakula vya kutumia machungwa mara ndimu kwa sana.

Watu wakawa wananitania kuwa itakua mimba mimi nilicheka tu kwani mwezi mzima sijatapika nikichefu chefu tu harafu nilikuaga na matatizo ya tumbo hivyo hata siku zangu nyingi hazikua zikiingia mara nyingi.

Basi nikaendelea kwenda field kama kawaida, siku zilivyozid kwenda nikaanza kunenepa yaani makalio na hips kubwa mpaka nikajiuliza nimeridhika na nini mimi Eliza.

Siku moja nikamkumbuka Mudy nikamtafuta nikamsalimia yeye akawa ananisikiliza tu niongee tu yeye hajibu chochote aisee mimi niliumia sana, nikakaa kimya nakukata simu nikamtumia sms

“Kwahiyo mimi mpenzi wangu pesa au?”
hakujibu akaja kupiga kesho yake tukanza kuongea

“Mh! Zasiku” nikamjibu

“Njema” Akaniambia

“Vipi nilisikia unaumwa vipi umepona?” nikamwambia

“Ndio"

"Maana hamchelewagi kusingizia watu mimba nyie”

Sijui kwanini moyo wangu ulipigwa kama na shoti hivi mmh! Niijichekesha tu pale akafurahi akakata simu.

Kesho yake nikatoka out na Matokeo nikarefresh mind tu maana nilitoka kazini nikiwa nimechoka, basi tukakutana bar flani hivi tukaanza kupiga stori Matokeo alikua ananiambia

“Kwanini unakubali kuwa na mtu mmoja harafu yupo mbali anatuma pesa tu mahitaji mengine vipi?”

“Najitunza ndo maana sitafuti mwingine labda aniache kabisa”

Basi akachukua simu yangu akakuta hamna sms nyingine zaid ya sms nilizomtumia Mudy tu, alishangaa sana tukanywa bia pale siku hiyo nilikunywa bia nyingi sana yani yote ilikua hasira tu kuona naishi bila furaha kwenye mahusino yangu lakini pesa ninayo ya matumizi.

Nilirudi nyumbani nikalala zangu, asubuhi niliamka nikatapika sana yani nilitapika sana mpaka nikakaa chooni, mama mdogo akaniambia

“Vipi mbona kutapika”

“Sijui tatizo” akaniambia

“Kapime kila kitu umenielewa”

Sikumuelewa anamaanisha nini, nikaenda zangu kazini (field) nilipofika uko nako nikatapika sana nikajua tu pombe za usiku nikamwambia mama kuwa sijiskii vizuri natapika wee! Kama namuona Mama yangu dah! akaniambia

“Hivi ninavyongea Kapime kila kitu usiniletee ujinga hapa”

Nikaanza kuwaza mama mdogo alivyoniambia na mama kaongea hivyo hivyo! Dah nikaomba ruhusa kazini nikaenda zangu hospitali.

Kipindi hicho nina mwezi nishamtoa Mudy moyoni hanitafuti simtafuti na nishaanza kuwa karibu na Matokeo kama rafiki yangu wakaribu wa kupiga nae stori tu lengo nimsahau tu Mudy kasha niachane nae tu.

Baada ya vipimo vyote nikaitwa kwa dokta kufika tu akaniambia

“Eliza Hongera sana, vipimo vyako vinaonyesha wewe ni mjazito wa miezi miwli na nusu”

Kwanza nilianza kuhisi kupigwa shoti, nilikosa nguvu ghafla, aisee ile siku sitoisahau nililia mithiri ya mtoto wa miaka mitano aliyefiwa na wazazi wake.

Kwa kweli nililia Sana huku natoka hospitali hata sijielewi huku najiuliza

“Nitamuambia nini mama ujinga huu, Je Mudy akikataa itakuaje na mama hawezi kunielewa, MUNGU WANGU WEE!”

Kuzaa na Mudy bora Yule boyfriend wangu wa kwanza, alinipenda tatizo lake hakuniamini na kupenda kupitiliza lakini hakuwahi nizarau wala kunitukana au kuruhusu alale bila kusikia sauti yangu! UUWIII!!!! Niilia macho live live njiani watu wananiangalia na kunishangaa peke yangu, nikakosea hadi kituo cha gari kwa kweli nilichanganyikiwa mweee…………….. ITAENDELEA.

JE MAMA YAKE ATAMWAMBIAJE ATAKUBALI?

MAMA YAKE MDOGO ATASEMAJE ATAMFUKUZA KWAKE?

JE MUDY ATAKUBALI UJAUZITO AU ATAMTOLEA NJE?

BASI USIKUBALI KUKOSA SEHEMU IJAYO HAPA HAPA KWA MAN MIDDO.

UKISHASOMA LIKE NA COMMENT.

NUKUU “Siku zote utakachokipanda ndicho utakachovuna, huwezi ukapanda mahindi ukavuna ndizi. Hiki kilichomtokea Eliza kimewatokea wadada wengi sana, wengi walishawishika na tama za pesa bila kumchunguza mtu au kujua mapenzi ya mtu mwenyewe. Wadada wengi wameekuja kulaumu wanaume na kusema wanaume wote ndio walivyo baada ya kupewa mimba.

Lazima mjiulize na kuwachunguza hao mnaongia nao kwenye mahusiano nia yake kwako ni ipi? Sio kwasababu amekwambia nakupenda ndio sababu ya kujiachia hata ukiwa kwenye siku za hatari utakuja kulia kama Eliza. Mjifunze”

KAMA UNAHITAJI EPISODE IJAYO AU SIMULIZI YOTE NI inbox Man Middo
 
SIMULIZI: ELIZA NA NDOA YANGU SEHEMU YA KUMI (10)
NA Man Middo tz 0655 969 973

ILIPOISHIA…………..Huku tunapiga stori tukafika stendi tukakata tiketi na tukapewa hela tununue aple tutafune huku tusubir gari ije niondoke. Baade wifi akaanza kunisihi

“Wifi yangu mpendwa jitahidi kumvumilia Mudy ukali wake maana Mudy ni mkali mno hadi familia nzima tunamuogopa”

Nilimsihi asiwaze kwa kuwa nishakubali kuwa nae ila nilikua nawaza kuwa kama huyu mtu kwao tu wanamuogopa si itakua ishu sana na nani atakuja kunitetea akifanya kosa kama wanamuogopa hivi.

Baadae hatukusubiri sana gari ikaja nikapanda nikaondoka. Nikafika Moro salama nilifikia kwa mama mdogo maana bado nilikua naogopa kwa mama na ukizingatia aliniambia nije na huyo mwenzangu……….SONGANAYO

Basi nilipofika kwa mama mdogo nikamuelezea kichotokea, baadae nikampa bahasha yake akasoma. Mmh! Muda kidogo akamuita mama wakasoma ile barua kwa pamoja, Aisee wakapiga vigelegele kwa furaha mimi sikujua kichoandikwa nilibaki kuwashangaa tu.

Nilijiuliza kuwa juzi nilifokewa na kuwambiwa hawanitaki lakin saivi wanafurahi, ila angalau nilipata amani kuona kama wamekubaliana na kilichotokea japo si kitu ambacho mimi nilitarajia kuitwa mama kwa kipindi kile. Basi akaniuliza

“Sasa Eliza jibu letu litafiukaje?” nikawambia

“Amesema atatuma mtu”

Kweli wakajibu sasa ishu ilikua siku ya kuja kutoa mahari na sikujua ilikua shilingi ngapi mahari.

Kwa akina Mudy ndugu zao wengi walikua serikalini yani ni watu wenye mavyeo vyao serikalini hivyo ilikua ngumu kuwapanga kuja Moro kwasababu Mudy kuja peke yake isingeleta picha nzuri hivyo ilimbidi asubirie ahadi alizokua anapewa na ndugu zake ambao nao walikua wanampanaga kila siku.

Upande wa mama nae akanza kunisema kila kukicha kutokana na kuchelewa kwa akina Mudy.

“Ehee! Mume mwenyewe haji utajua mwenyewe si useme tu kuwa wamekutelekeza”

Yani mama aliongea kana kwamba wananiuza au kama kuna magari wanadai maana alikua na shauku ya Mudy kueta mahari balaa.

Baada ya kuona kelo mama mdogo ilibidi aingielie kati na kumwambia mama kuwa

“Usimwambie mtoto maneno hayo ni kama unamuuza harafu mwanume atahisi tunadhiki sana, sio kitu kizuri tuwe na subra mwanaume aje mwenyewe”

Dah! Nilizani ataacha kumbe ndo kama alikua studio kurekodi maana ilikua zaidi ya remix mama alianza kunitumia meseji za kunitukana

“Yupo wapi sasa endelea kusubiri tu na wakati umetelekezwa”

Na maneno mengine kama hayo nilibaki nikilia tu kila siku nikimuuliza Mudy nae ilikua kigugumizi kila siku na ndgu nao wakasikia nataka kutolewa mahari wakanza kunilaumu eti

“Ooh! Wewe kweli unataka kutolewa mahari na umri huu harafu na waislamu kweli, umewaza nini? Yani muislamu kabisa huwajui wale wewe hawaoi harafu wabinafsi mno”

Nilikua nalia tu kila siku maana ukikutana na mama ni wimbo ukikutana na ndugu hivyo hivyo.

Mtaani nako kero wanasema mimba ya boyfriend Yule niliyeachananae ilikua tabu tu nilibaki tu kujifungia ndani.

***
Baadae mama mdogo akanishauri niende kwa Mudy tena, niligoma kumwambia kuwa nikienda huenda asije kabis.

Basi ilifikia kipindi nikamjibu hadi mama vibaya ili tu asinitukane na kunisema vibaya kuhusu tamaa yake ya mahari nilimwambia

“Kwani wewe ulitolewa mahari achana na mimi na hata hapa nitaondoka nasitoenda kwa huyo mwanaume, wewe unataka nife tu nimekuchoka mama huna huruma na mwanao unataka tu pesa”

Kipindi hicho na hasira za ujauzito niliongea chochote harafu mwanamume simpendi ni tamaa tu.

Hata ndoa yenyewe siitaki mimba tu ndo ilipelekea nikubali, upande wandugu nao niliwatukana na kila mtu nikamtoa madhaifu yake.

Basi familia nzima sasa ilinigeukia mimi kila mtu Eliza! Eliza! Eliza! Mara mtoto gani huyu hasikii wakubwa anajifanya amekua yani mambo kibao.

Nakumbuka nilizima hadi na simu wiki nzima nilikua nawasha tu usiku natoa hela basi nazima.

Baade wazee watu wazima walimkalisha mama na kumuuliza

“Mbona mnagombania mahari na mwanao wakati mlikua mnaishi bila mahari” Mama akasema

“Huyu mtoto mshenzi ananijibu vibaya, anawezaje kunitukana Mimi”

Baade wazee wakamsihi kutambua kuwa Yule ni mtoto na bado ni mjamzito.

Basi kuna dada yangu ambae alikua Dar yeye ni mtoto wa mama mdogo akaingilia kati, alinipigia simu kupitia simu ya mama mdogo na kuniambia niwashe simu niligoma lakini aliniambia ameshaongea na mama hivyo niwashe ili anaipigie yaishe.

Kwa kweli kwa kipindi hicho niliwaza tu kunywa sumu tu nife nilichoka kulia kila siku maana ujauzito wenyewe kama waugonjwa ni kuumwa tu.

Nikitembea kero nilihisi kuna kitu nimekosea dunaia maana niliona manyanyaso huishi kwa raha, ujauzito ukusumbue, mama nae ndugu nao na mwanaume nae ndo hivyo nilitamani kufa kwa kweli.

Baadae nilimpa taarifa Mudy akaniambia kuwa wiki haiishi watakuja kweli walikuja wakatoa mahari ya watu iliyokua inaleta tafrani.

Huwezi kuamini tena walikuja kwa mbwe mbwe na ukizingatia kwao zipo walikuja na mzigo wao wote, lakini upande wa kwetu wakasema hawapaswi kutoa yote nilitoewa mahari nzuri tu ya kikristu.

Sasa mama sio kunipa hongera huko lakini ukaribu ulipungua sio kama zamani na ndugu nao mawasiliano yalikata ni kama walinitenga.…..... ITAENDELEA

Usikose sehemu ya 11 kufuatilia kilichoendelea.

Kama unahitaji mwendelezo Nitafute 0655 969 973

Facebook [emoji1428]man Middo
Instagram [emoji1428] @middotz_
Twitter [emoji1428]@ManMiddo
 
SIMULIZI: ELIZA NA NDOA YANGU SEHEMU YA 11
NA Man Middo tz 0655 969 973
[emoji1427][emoji1427][emoji1427]

Baade mama mdogo akaniruhusu kwenda kwa Mudy akaniambia

“Sasa unaweza kwenda kukutana kuongeza njia”

(Aliingiza kautani kidogo) basi kabla sijaenda kwa Mudy nikaenda kliniki nikakutana na dokta akaniuliza

“Kwanini umeamua kuzaa na umri mdogo?” Nikamwambia ivyokua akaniuliza kuwa

“Mpaka imefika miezi mitatu umekutana na mhusika na je anakutafuta”

“Ndio ananitafuta” akaniambia

“Sasa jitahidi muwe mnakutana kimwili ili kuongeza njia, ili siku ya mwisho kisu kisihusike na kazi ufanye sana maana ni kama umelegea”

Na ni kweli nilipungua sana kilo na ukiniona nilikua kama mgonjwa. Nilirudi nyumani nikamtaarifu Mudy kuwa nahitaji kuja akanambia sawa, akapanga siku kweli akaja na toka siku hiyo nilisuka nywele za vitunguu.

Mudy aliniambia kwenye simu kuwa hatoshuka wala kukaa atakapofika tu ananichukua tunaenda kwa mama then tunaondoka kwake nikasema sawa.

Basi toka kipindi tunagombana kuhusu mahari na wao waje watoe mahari sijaonana na mama wala kufika nyumbani.

Mudy alikuja na rafiki yake akapiga honi nikatoka, wee! Mudy alinishangaa sana kwa hasira akaniambia

“Panda chap tuondoke”

Mimi nilijua sababu ya yeye kuchukia ni kuwa nilikua nimekonda sana na nilikua nimetoka vipele na nywele za vitunguu. Shem akashindwa kuvumilia akaniuliza

“Mbona uko hivyo unakula kweli?”

Sikua na jibu sahihi nilikaa kimya tu Mudy alikua na hasira alibakia kusonya tu.

Basi tukafika nyumbani kwa mama yangu akatukaribisha tulikuta ashapika kumbe Mudy alishampa taarifa.

Sasa mama kuniona tu ile hali yangu akaanza kulia

“Mwanagu nini! kulikoni mbona kama huli na kwanini huli?”

Bado nilibaki kimya tu mama aliumia sana pamoja na yaliyopita lakin alijua kule kwa mama mdogo muangalizi hakuna maana mama mdogo anaenda kazini na mimi kipindi kile nisingeweza kubaki kwa mama kwasababu ya maneno yake.

Ndugu zangu na mtaa mzima walijua nilimuacha yule boy wa pale mtaani kwasababu ya pesa kitu ambacho si kweli. Mama akaniuliza

“Unakula kweli?”

“Ndio Mama nakula” Mudy akasema

“Sio kweli niliongea na mama mdogo wake alinambia huwa anakunywa maziwa, maji na tikiti maji tu” nikawa kimya tu.

Basi wakandaa chakula mama akanipakulia chakula nikamwambia

“Nipe maji kwanza” Mudy akamwambia

“Mama usimpe ukimpa hatokula ale kwanza” nilinuna nikachukua ili nile lakini nilishia vijiko viwili tu, tena kwa usimamizi wa mama. Akaniambia

“Kula mwanangu, kula hiyo hali bila kula ni sawa na bure, unajua oparesheni sio nzuri” Nilijaribu nilishindwa Mudy akanambia

“Hutaki kula subiri tufike nyumani kwetu hujawahi kuonana na mama mkwe wako ndo mtaenda kuonana”

Sasa mh! kusikia hivyo niliwaza maana sikuwahi kumuona kweli, Basi tukala tukatoka nje tukaagana na mama tukanza safar ya kwenda Pwani.

Njiani ikafika usiku Mudy akasimamisha gari sheli flani hivi yenye supermarket akasema

“Haya tushuke tuchukue chakutafuna ili tufike bila njaaa”

Mimi sikushuka yani kutembea ilikua ishu harafu nilikua najihisi mbaya muda wote nilijichukia ghafla kwasababu Mudy alionyesha nimekuwa hovyo au mbaya hivi kwa hiyo nilikosa ujasiri. Nikamuomba aniletee alinijibu kwa dharau

“Sifanyi ujinga huo kama huwezi kushuka basi” Shem akasema nitakuletea, Mudy akamjibu

“Usimletee! Umletee ili iweje achana nae”

Wakaondoka mimi nikabaki nikaona sawa tu, hata wasipoleta kwanza nilikua siskii njaaa kabsaaa yani.

Baadae wakarudi huku wanakula Mimi nikaa kimya tu, Mudy alijua nitachukia au nitadai lakini nilikua kimya akanza kuongea

“Mimi siwezi kukaa na mtu asie kula yani twende lakin ukizidi kukaa bila kula nitakurudisha kwenu, siwez Mimi ujinga huo yani tumbo lako kula tuhusike wengine. Nakwambia nitakurudusha kwenu labda kwenu ndo utakula yani umeniuzi sana, inafikia hatua mpaka mama yako analia mbele yangu kana kwamba sijui unakosa nini”

Aliongea mpaka nilijiskia vibaya nikajiona kama nimemkosea sana mama nikaumia sana kwa kitendo kile mpaka mama kulia. Akamwambia Godii

“Hebu mpe”

Kumbe walinunua vitu vingi tu waliweka kwenye mifuko nikachukua nikawa natafuta huku natafakari ukali wake kuwa haoni kuwa mimi sipendi pia hiyo hali.

Baadae mama yake akampigia simu akamuliza

“uko wapi?” Akajibu

“Tupo njiani tunakaribia”

“Sawa amekula huyo?” akaanza kumwambia sasa

“Hali yani tumetoka kwao hajala chochote hapa nimenunua vitu vya kijinga ndo anajifanya kupapatikia yana anauzi sana ngoja aje uone”

Basi tukaendelea na safari tukafika njiani akashuka shem tukafika nyubmani.

Usiku ule alienda kwao kuchukua chakula sikuweza kula kabisa yani ikabidi aagize tu chipsi na mshikaki zilipanda kidogo nikala nusu tu harafu nikatapika alikua anakunja sura huyo, basi nikaenda kulala.

Nikakumbuka kuongeza njia basi tukafanya wee!!! Asubuhi niliamka nguvu sina wakati nimekaa sebleni Mudy anajiandaa kwenda kazini nikasikia hodi! Kumbe alikua mama mkwe akaingia nikamsalimu pale alionekana kuwa na taarifa zangu zote basi akaanza kunipa risala ya vyakula maana yeye alikua nesi mstaafu akaniambia

“Ni lazima ule bila hivyo itakua ngumu kuwa salama na mtoto tumboni cha msingi useme chochote unachotaka harafu usilale muda wote” akaongea weee! Aksema

“Ngoja nikuetee chai unywe” Nilianza kusema

“Haya sasa ya kusimamiwa ni mateso”

Baade akaleta trei la chakula yani kuna kila aina ya vitafunwa viwili viwili na chai aina tatu nichague kipi kinapanda nilionja kila kitu nikaona bagia na uji ndo vinapanda kidogo lakini nilitaka sana ubuyu na soda………. ITAENDELEA

HIVI MIMBA ZINAKUAGA HIVI UNAPENDA TU UBUYU NA SODA? WANAWAKE TUAMBIE YAKO ILIKUAJE?

MWANAUME TUAMBIE MKEO ALIKUA ANAPENDA NINI KIPINDI MJAZITO MPAKA UKANZA KUCHUKIA?

JE UNAJUA KIFUATACHO?BASI UKO TUELEKEAKO NIKUTAM BALAA, KUNAHUZUN ISHA NA KUNAFURAHISHA.

NUKUU “Katika maisha wakati wa furaha, Rafiki na ndugu zako watapata kujua WEWE NI NANI. Wakati wa matatizo utapata kujua yupi ni rafiki yako”

Hata Eliza mama yake alishamgombeza kwa kupata ujauzito lakini barua ilivyokuja akapiga vigelegele.

(Hapa tunajifunza wazazi wetu kuna muda wanangalia maslahi kuliko utu wa mwanae)

Kingine Mudy anakunja sura mke wake akitapika lakini akiwa faragha mambo yanakua mazuri

(Jifunze kumpenda mwenzi wako katika kila hali anazopitia, jitahidi sana kumjua mpenzi wako, jitahidi uwe rafiki wa mpenzi wako kwani ukiwa rafiki utajua matatizo yake yote”

Whatsapp 0655 969 973
 
SIMULIZI: ELIZA NA NDOA YANGU SEHEMU YA 12
man Middo +255 655 969 973

TULIPOISHIA………….Nikakumbuka kuongeza njia basi tukafanya wee!!! Asubuhi niliamka nguvu sina wakati nimekaa sebleni Mudy anajiandaa kwenda kazini nikasikia hodi! Kumbe alikua mama mkwe akaingia nikamsalimu pale alionekana kuwa na taarifa zangu zote basi akaanza kunipa risala ya vyakula maana yeye alikua nesi mstaafu akaniambia

“Ni lazima ule bila hivyo itakua ngumu kuwa salama na mtoto tumboni cha msingi useme chochote unachotaka harafu usilale muda wote” akaongea weee! Aksema

“Ngoja nikuetee chai unywe” Nilianza kusema

“Haya sasa ya kusimamiwa ni mateso”

Baade akaleta trei la chakula yani kuna kila aina ya vitafunwa viwili viwili na chai aina tatu nichague kipi kinapanda nilionja kila kitu nikaona bagia na uji ndo vinapanda kidogo lakini nilitaka sana ubuyu na soda……….TIRIRIKA NAYO

Basi Nikanywa chai, mchana hivyo hivyo naletewa ugali na mboga kama zote yani, harafu nakusimamiwa juu na mama mkwe mpaka pale nilipotengemaaa ndio nikaanza kupika mwenyewe.

Lakin pamoja na hivyo bado kula ilikua ileile ya kijilazimisha ila maajabu ya Mudy nilishangaa sana, alijua vizuri hali yangu lakin mimi ndo niikua namuulizaga akiwa kazini kuwa amekula nini au kashindaje.

Basi hapo ndo yeye anaiulize. Bila mimi mkupigia yeye hanitafuti kabisa nikajisemea kuwa

“Yani huyu anaona mtu kuwa na pesa ndio mapenzi yenyewe”.

Upande wa mama mkwe mara nyingine alikuaga bize hasa siku za wiki labda siku za jumamosi na jumapili ndo anakuja kujua naendeleaje.

Sasa kuna siku nilikua nashindwa kabisa kupika kama nilivyosema ujauzito wangu ulikua kama wa ugonjwa, maana kuna muda nashindwaga kabisa kuamka.

Katika marafiki wa Mudy, rafiki ambae yupo karibu kuliko wote ni Gody, lakini mimi nilimzoea sana Afidh kuliko Gody.

Afidh ndio ambae nilikua namuelezea jinsi hali yangu ilivyo na kila kinachomuhusu Mudy na alikua ananisihi kuwa Mudy ananipenda sana nimvumilie tu.

***

Kwa kweli Mudy hakuwa romantic kabisa maana hata arudi kazini ukimwambia pole na kazi hata kusema asante kwake ngumu anaishia tu kuanzisha mada nyingine.

Yani pole yake ni mkiwa faragha kitandani ndo utasikia pole ukimwambia asanteh mpenzi wangu pole na wewe yeye kimya.

Akila hasemi asanteh au kusema chochote chakula kiwe kizuri yeye kimya kikiwa kibaya anakula kidogo tu anaacha harafu anakwambia nitakula kesho.

Akiwa kazini ukimuuliza nipike nini anajibu chochote na akikaribia kutoka kazini ndo anauliza kuwa umepika? Ukijibu ndio anakuja kama bado unasikia

“Usipike nakuja na chakula au jiandae tukale nje”

Tabu nayo sasa mkienda huko nje kula njia nzima hamuongei, Na ikitokea ukianzisha tu mada anachukua simu anampigia mtu yoyote anaongea chochote tu mpaka mtakapofika huko.

Na huko hakuna kuongea mpaka mnamaliza tunarudi mwendo huo huo yeye na simu au anaweka mziki kwa sauti anafuatisha kuimba.

Muda wote mimi nakua tu kama bubu kimya mpaka nyumbani, akifika tu nyumbani cha kwanza laptop yake.

Kiukweli sijui anangaliaga nini mpaka naenda kulala nikijakustuka yupo kitandani sijui kaja sangapi, lakini nikijigeuza tu kanidaka hakuna kuandaana wala nini yeye nikufanya tu akimaliza haja yake basi anajigeuza analala.

Ni kama alikua ananibaka lakin niliendelea kuvumilia nikijua ndoa mwanzo mgumu.

**
Shem Afidh mkewe alikua anatoka kujifungua hivyo alikua najua vyakula vingi, asubuhi alikua ananiuliza unakula nini kama ni supu au chochote basi yeye anamtuma mtu ananiletea.

Ikifika mchana hivyo hivyo ikawa mtindo huo huo, yani akawa anajali sana ilikua akileta vyakula aina tofauti tofauti ili tu nichague kinachopanda basi nikawa nafurahi kujali kwake yani.

Lakini Mudy kama mhusika hakufanya hivyo hata mara moja na nilikua namuagizia kila siku na isitoshe yeye alikua anaona hali yangu, maana nilikua nashindwa kabisa hadi kuamka lakin yeye hakujali na akirudi usiku ndo anasema

“ooh! Nilisahau hakuna hata cha samahani mkeo wangu wala nini”.

**
Siku moja baada ya kutenga chakula Mudy akala vizuri tu, mimi kwa kweli sikula sana zaid ya kugusagusa tu kwanza nilikua napenda kunywa soda sana ,biskuti, ubuyu, tambi yani vitu kama hivyo ndo nilikua nakula sana.

Sasa baada ya kula Mudy akachukua laptop yake kwa kweli nilitokea kuichukia ile laptop. Basi alikua anachat tu mtandaoni kaweka Modem nikamuuliza

“Unafanya nini twende tukalale” nakumbuka ilikua saa 6 usiku akaniambia

“Wewe kalale mimi niache nitakuja”

Mmh! Nilikua naumia sana ila baada ya kuniambia hivyo sikutaka mabishano nikaenda zangu kitandani sasa kulala, Ila sasa usingizi hauji mwenzangu.

Basi ikawa inafika saa 8 kasoro hivi usiku anachat tu yani yupo bize na laptop balaa. Nikasema huyu asinitanie mie, nikanyanta taratibu bila yeye kujua nikafika nakusoma anachoandika ilikua facebook nikakuta anachat na mwanamke tena kimahaba mno yani alikua anampetipeti balaa wakati mimi hata neno

“NAKUPENDA narudia neno NAKUPENDA” hajawahi nitamkia hajawahi nionyesha mapenzi yoyote zaidi ya hizo pesa zake.

Duuh! kwa kweli uchungu wa siku ile sitousahau nilishia kupiga kelele kwa sauti, nilishindwa kuvumilia maana muda huo ni usiku sana mimi kama mkewe nipo kitandani haji kulala yeye anachati na wanawake wengine kwa mahaba ambayo mimi najitahidi kuonyesha ushirikiano yeye hajali........... ITAENDELEA.

Usikose kufuatilia episode ijayo.
@middotz on Twitter and Instagram
 
SIMULIZI: ELIZA NA NDOA YANGU SEHEMU YA 13
man Middo +255 655 969 973
[emoji1427][emoji1427][emoji1427]

Basi baada ya mimi kupiga kelele yeye alistuka akafunga laptop yake na kuanza kunifuata nakuniuliza kwa kufoka

“Si nilikuambia ukalale imekuaje umeanza kunifuata fuata nakuuliza wewe?” alianza kunitukana

“Nakuliza wewe Malaya eeh! Wewe ku* kwanini…..”

Akanza kutoa mkanda wake wa suruali tena ile ngozi na muda huo nilikua uchi kabisa maana kulikua na joto lilikua kali sikuliweza, tulikua tunafunga mlango na madilisha na kuwasha feni, kipindi hicho AC yake haikutumika sana na mara nyingi ilitumika sebleni.

Basi akaanza kunipiga na ule mkanda wake wa ngozi tena uchi wa mnyama weeeh! Mama yangu weweee! Nililia sana na kupiga kelele kiasi ila yeye hakujali kuwa mimi ni mjamzito huku naugulia na kipigo kinazidi niliamua kulalia tumbo akanipiga!

Akanipiga! Wee! Mpaka akaacha mwenyewe nikabaki nalia tu niliumia na ule mkanda wake, yani na uweupe wangu zilionekana sehemu ambazo ule mkanda ulipokua unapita.

Siku hiyo nililia kwa kubana sauti ili wapangaji wasisikie maana kwa njee alipangisha, Sasa niliwaza ubaya wangu ni upi na wakati saa 6 alitakiwa awe kitandani nililia sana huku nasema

“ OOH!Mama nisamehe sana ulinionya mimi kwenda Dar lakini nikakaidi baadala yake sasaivi naumbuka napigwa uchi wa mnyama”

Nilikua naongea huku anasikia, nililia hadi akaingiwa na huruma akaja kananiambia

“Nenda kalale” niliendelea tu kulia pale chini. Akasema tena

“Nenda kalale” nikakataa, akasema

“Nakupiga tena”

Kwakua niliogopa kupigwa tena nikamka nikaenda zangu chumbani kulala lakin niliendelea kulia.Baade akaja akanza kuniomba radhi Eti

“Najuta kukupiga tatizo unapenda sana kunifuata kunichunguza mimi huwa sipendi ujue, wewe ndio ninaekupenda sio mwingine kumbuka kabla yako nilikua na binti mwingine mzuri kama wewe, na mchapa kazi kama wewe nae nilitaka nimuoe lakini ulipopata mimba tu nikaona nibaki na wewe, ningekua sikupendi nisingetoa mahari, nisingekuleta hapa ningeamua kulea mimba tu kwani wangapi wanalea mimba tu lakin hakuna cha ndoa?

Nisamehe sitokupiga tena na nikikupiga tena waambie nyumbani, sihuwahi waza kuja kumpiga mwanamke hata siku moja na sijui leo ilikuaje” Aliapa na kuramba ardhi kabisa kuwa hatorudia mimi nilikaa kimya tu nikalala.

***
Asubuhi nikamka nikampikia chai akaja akakuta nimeshandaa, akaenda kuoga nikapasi nguo za kuvaa kwani ilikua usipoandaa nguo alivaa hovyo hovyo mimi sikupenda awe rafu harafu nipo.

Baadae alipotoka bafuni akakuta ndio namalizia kuweka boxa akanifuata nyuma yangu akanikumbatia akanivua kanga na ndani sikuvaa kitu akaniandaa tukananii akarudi kuoga tena.

Akarudi akavaa akaenda kunywa chai kisha akaenda zake kazini. Kawaida yangu huwa siamkagi na hasira za jana na ilikua hivyo na kitendo cha kupigwa sikumwambia Afidh kuwa nilipigwa kisa meseji za mwanamke wake.

Afidh niliendelea kumtegemea tu kama siku nikizidiwa kuhusu chakula, Na nilikua napenda sana story zake tulikua tunaongea sana na simu maana aligundua nikiwa Pwani nakuaga mpweke sana harafu sikuwa natokaga nje, hiyo hali hata nikiwa nyumbani kwetu nilishaizoea.

****
Siku moja Afidh akamuuliza Mudy kwa simu mimi nikiwa nae kuwa

“Hivi wewe Mudy mwenzako ulimuachaje nyumbani? Amekula asubuhi ulivyomuacha na mchana huu umemuuliza amekula nini?” alibaki kujiumauma tu eti

“Ooh! Nitampigia baadae”

Wakati muda huo ilikua saa 9 na nimechoka hatari maana nilitapika mpaka natoa hewa tu na aliniacha nimelala asubuhi.

Shem Afidh alimpigia mtu simu akaleta chakula akawa ananibembeleza kuwa

“Shem kula ili anangalau upate nguvu maana tukikupeleka hospitali kule hutorususiwa mapema kwa ulaji wako huo utakesha”

Basi nilikula kidogo nikakaa kama nusu saa hivi shem Afidh akaondoka yani yeye ndio alikua anajua ratiba zangua za kula Mudy yeye muda wote alidai yupo bize, cha ajabu akija jioni anakuja na Muvi nikimuliza kazipata wapi ananiambia

“Nimepata muda nikadownload”, mara aniambie

“Nilipokua sina kazi ya kufanya nimelala kwenye gari nimekuja kustuka jion nikapitia kwa Afidh kupiga stori ndio nikarudi”

Lakin hakua na muda wa kuniuliza mimi wakati huo akiongea mimi ilikua kuitikia tu maana stori kwake kama sheria yani apige yeye tu nikiwa mimi anajifanya kufanya mambo mengine yani aliniona kama mpuuzi flani ivi.......ITAENDELEA.

Usikose kufuatilia episode ijayo....

NUKUU “MOJA YA KOSA KUBWA TUFANYALO WANAUME NI KUMRUHUSU MWANAUME MWENZAKO KUMFANYA MKEO AWE NA FURAHA KATIKA KIPINDI AMBACHO WEWE MWENYEWE UPO”

Bila shaka kama umemsoma vizuri Eliza tayari mapenzi yake ashanza kuyahamishia kwa yule anaemjali ambae ni shemeji yake Afidhi.

Katika maisha ya kawaida hivi ndivyo baadhi ya wanawake hushawishika kuchepuka.

FUNZO: Mwanaume timiza majukumu yako vizuri, tumia nafasi yako vizuri kama kichwa cha familia, mpende mkeo, mfanye we rafiki yako harafu uone amani na furaha utakayopata. wenye ndoa zenu mzingataie hili.

Kama unataka episode ijayo nicheki Inbox Man Middo Tz “Naomba mwendelezo” nitakupa maelekezo 0655 969 973
 
SIMULIZI: ELIZA NA NDOA YANGU
SEHEMU YA 14
Man Middo Tz +255 655 969 973

Kuna kitu nilikuja kushanngaa kwa Mudy ambacho hakikua sawa, siku moja nikwa nafanya usafi juu ya kabati nikakutana na Muvi nyingi za ngono.

Siku hiyo nilishangaa sana ila nikazichukua nakuzichoma moto, baadae nikaja kumuuliza

“Kwanini unangalia uchafu?” akaniambia

“Kuna kipindi niliachana kabisa na mambo ya wanawake kwa hiyo nilikua naangalia hizo nikiwa kwenye gari na njiani nikimuona mwanamke nimemtamani namuangalia nikifika nyumbani naangalia X harafu navuta taswira ya Yule mwanamke naanza kujichua mpaka namaliza haja zangu kisha nalala”

“Jaman Mudy! Hivi unajua madharea yake lakini?”

“Ndio nayajua” nikamwambia

“Usijaribu tena utakuja kuona mwanmke kama sanamu tu zikikukaa kichwani, pia utakuja kujifunza mambo ya ajabu ajabu. Na madhara makubwa nguvu za kiume zitapotea harafu mimi niteseke ujue”
akaniambia

“Hakuna madhara bwana”

“Acha kuwa mbishi misuri italegea hiyo” akajifanya kunielewa pale huku akiniambia sasaivi

“Siwezi tena sishaoa bwana” nikamuitika tu.

****
Nilikaa miezi miwili nikarudi Moro kwa mam mdogo, sijui kwanini sikuwa nawaza tu kukaa moja kwa moja, Yani bado Mudy nilimuona kama ni mchumba tu mpaka tufunge ndoa.

Basi moro nilikaa ilipofika miezi 6 nilirudi tena kwa Mudy bila hata kuitwa kumbuka alikua ni mtu asiyejali hakuna kunipigia simu kunambia unaendeleaje, nimekumis au ninahamu na wewe njoo mke wangu.

Yani hayo hakuna hata uage yeye anakuruhusu tu hakuna usiondoke mke wangu hakuwahi kusema chochote, lakini mtu wa nje asiyejua kinachoendelea akituona tunatoka nipo kwenye gari anaweza sema nakula raha sana.

Yeye kitu alichokua anajali ni kunitoa tu na gari yake, yeye hakupenda kabisa nitumie daladala au bus kwenda sehemu, naweza sema huko ndo kujali kwake basi.

Lakini mimi pamoja na mateso ya mimba yangu nilijitahid kumtamkia maneno yote mazuri lakin hakuwahi kujibu. Mudy aliendelea hivyo hivyo na hata akirudi kazini nikienda kumpokea ananishushua tena kwa kunifukuza kabisa na anafanya hivyo akiona watu, utasikia

“Toka unanipokea nini bhna nenda tu”

Vuta picha mtu ni mumeo anarudi kazini anashuka kwenye gari na mizigo na kuna watu unaona umpokee yeye anakurudisha mbele za watu tena kwa mashushu harafu baade mkiwa peke yenu anajifanya kukusifia eti kumbe unajua wajibu wako nilikua nachukia sana.

Niliendelea kutimiza wajibu wangu Kama mke na mimba ya miezi 6 nafanya kazi zote hali yakuumwa ilipungua kiasi flani nilijishusha sana hata maji ya kikatika nilienda kuchota kisimani sikuwaza kununua au kumlipa mtu maana yeye pesa ilimfanya aone anaweza kununua kila kitu.

Maisha ya visa visa yaliendelea vilevile na mimi nilikomaa hivyo hivyo nikiangalia Tv yeye yupo bize na laptop yake kama kawaida.

Niliichukia sana laptop na baadae hata baadhi ya tabia zangu ambazo niliziona muhimu nilianza kuziacha.

Mimi sikua mtu wa kuwa sirias muda wote nilipenda kucheka na kutabasamu sana, hata shule watu walinijua sana kwa kuchekesha ilikua huwezi kaa na mimi robo saa hujacheka lakin kwa Mudy kipaji hicho kilipotea.

Ilikua hata nangalia Tv nikicheka tu yeye tanipiga jicho balaa yani hata kuongea ilikua mtihani.…………………………..ITAENDELEA.

USIKOSE KIFUATACHO KATIKA EPISODE YA 15
 
Back
Top Bottom