SIMULIZI: Eliza na Ndoa Yangu (Kisa cha kweli cha kusisimua)

SIMULIZI: Eliza na Ndoa Yangu (Kisa cha kweli cha kusisimua)

SIMULIZI: ELIZA NA NDOA YANGU
SEHEMU YA 15
Man Middo Tz +255 655 969 973

Mimi nilikua najua vitu vingi tu hata kutumia hiyo laptop nilijua lakin niliogopa kufanya baadhi ya vitu maana ananidharau mno anajua mimi wa hovyo tu.

Kuna siku niliunganisha Tv na spika za redio yeye hakujua. Baadae pia simu na radio akaniangalia huku akishangaa harafu akasema

“Kumbe ni hivyo”

Yani hata kusema nielekeze yeye kimya, hata kwenye Muvi za kizungu mimi nilikua mwepesi kuelewa kuliko yeye lakin alijifanya kujua.

Kuna baadhi ya vipande mimi ndo namuelekeza wamemaanisha nini, sasa akawa analeta tukiangalia sehemu akiwa hajaelewa ananiangalia eti niseme maana yake, ahahaha yani hata kuomba au kuuliza hana hicho yani anadharau mnoo.

Siku moja niliamua kutumia laptop na yeye alikua anajua kuwa mimi sijui kuitumia hivyo alikua anaiacha tu kila siku na kuikuta hivyo hivyo.

Basi siku hiyo alivyoenda kazin nikajaribu kufungua kumbe hajaweka password nikaanza kupekua nikakuta kumbe muvi zake za ngono bado anazo yani.

Baadae ninaendelea kuangalia nikakuta chat zao na mwanamke nilikuta amemtamkia maneno mazuri mno ya kimahaba ambayo sikuwahi tamkiwa niliangalia tarehe walizo chat, maana siku nyingine anaenda nayo kazini nikagundua kuwa ni mwanmke wa muda mrefu mno na wanajuana.

Aisee nilipandwa na uchungu nilianza kulia nilia wee nakiwaza kuwa kumbe naishi na lifuska la kiume.

Baade akaja binti ambae alikua akimuita Baba mdogo nikamuonyesha angalie baba yake anayofanya maana Yule binti alitokea kuwa mtu wangu wa karibu kwa kipindi kile hivyo nikamuonyesha

“Hebu ona baba yako mshenzi anayonifanyia yani hajali kabisa hali yangu ya ujauzito”

Niliendelea kulia kama kuna msiba. Baadae Yule bint alienda kumwambia baba mkwe kuwa mama kule analia, baba mkwe akaja akaniuliza nalia nini nikamueleza kila kitu toka mwanzo alivyokua anidharau hadi akanipiga na muvi zake za ngono basi baba mkwe akaniambia

“Sasa utulie usubiri mwenzako akirudi ndio tuyaongee” Mimi nikakataa nikamuambia

“Baba haina haja ya kuongea nae ngoja tu alee mimba basi mi sitaki tena kuishi na mtu kama huyu” akanisihi pale baadae akaondoka.

Baada ya baba mkwe kuondoka ni kama nilishikwa na wazimu, nilienda hadi ndani kupekua kila sehemu nikakutana na picha ya mwanamke wake ipo kwenye fremu kabisa nikajikuta naumia mara mbili harafu alificha mbali mno.

Na kweli Yule mdada kwenye picha uongo dhambi alikua mzuri sana na kwa kipindi kile naweza sema kwake naingia mara tatu kwa uzuri wake.

Basi nikaanza kujishisi sifanani na mume wangu, Niliona kumbe anahaki ya kunidharau nilichanyanyikiwa balaa.

Baadae nikatoa laini zangu zote nikaacha pale ndani nikatoka nakuondoka sijui naelekea wapi (hapo nimepndwa na wazimu simpendi tena yani) maana hata njia sikuijua kabisa nilitembea mnoo na hapo sijala chochote toka asubuhi.

Baadae nikafika barabarani nikaendelea kutembea nikaona kabisa hapa napotea sikujali kikubwa kwangu nirudi Moro lakini nisione tena uso wa Mudy................ITAENDELEA……..

Usikose kufuatilia sehemu ya 12 KUJUA ELIZA ALIFIKIA WAPI BAADA YA KUONDOKA NA KWENDA ASIKOJUA? JE ATAKUA SALAMA NA UJAUZITO WAKE?

ANAENDA MOROGORO KWA MGUU KUTOKA KIBAHA JE INAWEZEKANA KWA MWANAMKE TENA MJAMZITO WA MIEZI 7?

“Kuna vitu vingi vya kumuomba mungu akubariki kabla hujamuomba pesa tazama eliza kapata mwanaume mwenye pesa, akitaka kwenda popote anatoka kwa gari lakini hana furaha, hapati mapenzi, na ujauzito anadiliki kuodoka bila kujua aendako mbali”

NUKUU “Sekunde moja ya kugombana na kutokuelewana ni SUMU KUBWA inayotufanya tusahau mamia ya mambo tuliyofanya katika MAPENZI YETU” Zingatia kujua thamani ya hisia za yule umpendae au uliyechagua kuishi nae.

JAMANI MWENDELEZO UPO UKIHITAJI NAKUPATIA TIME YOYOTE, CHAKUFANYA NITEXT “Naomba mwendelezo” KISHA NITAKUPA MAELEKEZO 0655 969 973
 
SIMULIZI: ELIZA NA NDOA YANGU
SEHEMU YA 16
Man Middo Tz +255 655 969 973

Nilitembea sana hadi nikafika sehemu moja kuna fremu ni zile library za wanaouza na wanaokodisha CD pamoja na kuingiza nyimbo.

Nikaenda nilikua nimechoka vibaya mno maana tumboni vichomi, miguu nayo inauma balaa na mtoto tumboni amecheza mpaka akaacha, nilipofika pale nikaomba kuingiziwa nyimbo lakini nia yangu ilikua kupumzika tu nikaona tu nizuge kwanza pale.

Sikua hata na shida ya nyimbo niliomba nyimbo mbili akaingiza chap nikaona mbona huyu anataka nisipumzike nikamwambia bado niliendelea kumwambia aingize kila alipomaliza ili tu niendelee kupumzika.

Baadae alipomaliza na nilipoona nimepumzika kiasi flani nikamuuliza anielekeze njia ya kutokea barabarani. Basi akanielekeza nikafika barabarani, Sasa pale barabarani niliwaza kuwa

“Usiku huu nitaweza kweli kurudi kwetu harafu sijala toka asubuhi, si nitaumwa mimi na ujauzito huu harafu nimeacha laini kule”

Baada ya hapo nikaona nirudi tu kwa Mudy, Nikaanza kufuatisha barabara (Ila siku ile ningejua barabara mapema ningerudi nyumani kwetu) nilianza kurudi taratibu huku nawaza sana

“Kwanini huyu mwanaume haridhiki nimempa mahitaji yote ya kimwili lakini haridhiki”

(simaanishi kinyume na maumbile) namaanisha mapenzi ya kama wanandoa.
Niliwaza sana na kujiulaumu kuwa ningemsikiliza mama haya yote yasingetokea.

Baadae nikafika kwa Mudy nikakuta gari nje, nilistuka kwanza sikutaka kumkuta muda ule, nikajua tayari ashafika huyu nilipofika mlangoni nikakuta viatu vya watu wawili, nikanza kuwaza

“Huyu mwingine ni nani?”

Baadae nikasikia maongezi Mudy akiwa anajitetea

“Huyu atakua hajangalia vizuri, hii laptop hamna kitu kabisa yani amekosea tu kuangalia”

Kumbe alikua baba yake basi nikangia zangu kwa hasira nikawapita sebleni baba yake akawa anaita

“Mkwe ,mkwe njoo tuyajenge”

Sikujali nikaenda zangu hadi chumbani. Baadae Mudy akaja akaniambia

“Njoo tukaongee sebuleni baba anakuita”

Baba mkwe kweli alikua ananiita.Basi hata mimi mwenyewe nilihisi kaaibu kidogo nikatoka hadi sebleni nikakaa nilikua na hasira za ajabu hata kuongea sikuweza, Yani kama kuna kitu kilikua kinanikaba yani ilikua ni kwikwi tu nikitaka kuongea.

Nilikaa nusu saa nzima nikilia tu, baadae nilielezea kila kitu kwa baba mkwe Mudy anavyonidharau hajawahi kuniita hata mpenzi lakini nimekuta majina yote ya kimahaba nikamwambia kuwa

“Nilijua hajui kutamka kumbe yeye anadharau tu, mimi nimechoka nahisi mimba ndio imemponza ila nishajua nani anampenda ngoja mimi nikijifungua nitaleta mtoto amuoe amtakae” nilivyomaliza baba mkwe akamuuliza Mwanae

“Mudy umesikia hayo” Mudy akabaki kimya kichwa chini, mimi nikasema

“Nataka jibu narudi lini kwetu nimechoka!” Akaanza kusema

“NISAMEHE”

Kwa mara ya kwanza ndio aliweza kutamka maneno yale lakini sikufurahi nilitaka kujua lini nitarudi. Mudy akanza kusema

“Mimi sijafanya kitu ila ni kweli nimekosea, ila huyo mwanamke nimeongea nae kawaida tu!” Baba yake akasema

“Hebu acha ujinga, mimi nishasoma kabisa ujinga wako umekuja hapa umefuta, Sasa binti hamna kuondoka ila natoa onyo ni hivi hii laptop siitaki kwanzia Leo, Mudy chukua hii laptop kauze pesa zote mpe huyu binti kisha wewe binti hii pesa kwakua laptop alikua anaitumia kwa ujinga wake, sasa na wewe hiyo pesa usinunue kitu chochote humu ndani cha gharama wewe tumia tu utakavyo.

Harafu Mudy nimekuona sana ukimnyanyasa huyu binti unasafiri mwezi mzima wakati unajua mwenzio mjamzito unamsumbua hujali hali ya mwenzio, pia kama ulimpenda huyo binti wa kwenye simu si ungemuoa huyo kwanini unasumbua watu umetutoa hapa mpaka Morogoro vijijini kabisaa kule, si ungeoa huyo uliyemtaka kama ulikua huna nia ya kumuoa huyu ungesema”

Yani alimsema sana siku ile angekua wa kusikia angeskia……………….ITAENDELEA.

Yani huwezi kuamini alichofanya Mudy...

Usikose kufuatilia episode ijayo.

Mwendelezo Nitafute kupitia namba 0655 969 973. Whatsapp
 
SIMULIZI: ELIZA NA NDOA YANGU
SEHEMU YA 17
Man Middo Tz +255 655 969 973

Basi kweli Mudy alienda kuuza ile laptop akaniletea pesa zote nikanunua dressingtable na begi la nguo, na nyingine zote nikatumia tu mwenyewe hapo angalau nikaanza kupata furaha na amani.

Na kwa kweli alianza kubadilika, kwanza aliawahi kurudi kazini na akirudi tulikua tunangalia muvi, muda wa kulala tunaenda wote hakuna tena ile kuchat na simu au ile kukaa sebleni na laptop.

Kwa kipindi kile hicho nikawa nampenda sana nilikua napenda kumchokoza michezo ya kimahaba ili tu asiboleke kukosa laptop yake, Na yeye pia alionyesha ushirikiano kwa kiasi kikubwa.

Basi miezi ilisogea ilipofika miezi 8 nikarudi nyumbani Moro Kama maandalizi ya kujifungua, Nilifika Moro nikaendelea kuhesabu siku na kwenda kliniki kucheki afya.

Siku ya kujifungua ikafika nikaenda hospitali ya kwaida nikaambiwa kwa umri wangu lazima niende hospitali ya mkoa niliogopa kidogo, lakini hakukua na namna nikaenda hadi hospitali ya mkoa.

Huko nako nikalazwa wakaniambia kwa umri wangu lazima kubaki pale kwanza ndipo niondoke nikiwa na mwanangu, nakumbuka nilikaa wodini wiki mbili peke yangu kabla ya kujifungua.

Mudy nilimuamwambia hali niliyokuanayo lakin hakuingiwa hata na moyo wa kuja kuniona pamoja na kumuomba aje alinipiga chenga mno niliumia sana hasa baada ya kuona wenzangu wanakuja kutembelewa na waume zao mimi hakuna hata mtu.

Kwani hata mama nae hakuruhusiwa kazini aliambiwa acahgue kukaa hospitali nikiwa sijajifungua au kuniuguza nikishajifungua, hivyo hakua na namna zaid ya kusubiri nijifungue.

Kwa kipindi kile mama mdogo nae alikua na matatizo yake binafsi kuna muda analeta chakula na muda mwingine haleti, mimi nilibaki tu nanunua chakula maana tuliruhusiwa kutoka kuchukua chakula kwa wale ambao hawana wasaidizi na pia ilikua kama mazoezi kumbuka hapo sijajifungua......itaendelea.

JE ELIZA ATAJIFUNGUA SALAMA? NANI ATAMPA MSAADA HAPO HOSPITALI AKISHAJIFUNGUA?

JE MUDY ATAKUJA AU BADO ATAPIGA CHENGA? BASI USIKOSE EPISODE YA 18.

Kama unataka episodes zote au ijayoo nicheki Inbox Man Middo au 0655 969 973 SIO LAZIMA KUONGOJA HADI NIKIPOST.

NUKUU “Hakuna Faraja Mwanamke Anaipenda Kama Ile Itokayo Kwa Yule Aliyeamua Kuwa Wa Maisha Yake, Hakuna Kitu Kibaya Kama Kuchezea Hisia Za Yule Anaekupenda. Mwanaume mwenzangu usomae hapa jifunze kumpenda mkeo kwasababu wewe ndio mfariji wake katika matatizo” Nyie mnaowadharau wake zenu kuweni makini.
 
SIMULIZI: ELIZA NA NDOA YANGUS
EHEMU YA 18
Man Middo Tz +255 655 969 973

Siku hiyo asubuhi uchungu ukanianza, hapo wiki ya pili sasa nipo hospitali basi nikapelekwa leba, Kwa kweli siku ile nilijifunza mengi na nilijua maana ya upendo ni nini maana niliwaza sana kuwa kumbe mama sio alikua ananipenda eeh! Kumbe Mudy ananidharau kwakua hana uchungu na mimi Dah! Kumbe mama alilia sana nilipopata mimba ya uzinzi.

Mama alilia sana nilipokonda ni kwasababu ya uchungu huu, kwa kweli siku ile nilijifunza namna ya kumpenda na kumheshimu mama.

Nilijua umuhimu wa mama, niliumia sana kipindi namjibu mama vibaya niliwaza sana huku uchungu unauma. Kwa kweli kujifungua kwangu kulikua kwa maajabu maana uchungu umenishika toka asubuhi nimekuja kujifungua saa 4 usiku tena baada tu ya kuongea na Mudy kwa simu huwezi amini baada ya yeye kupiga simu hapo hapo nikapiga kelele nikisema

“MUDY UNANIUAAAAA”

Hapo hapo mtoto huyooo nikaongezewa njia nikashonwa maana mtoto kichwa kilikua kikubwa kiasi, nilijifungua mtoto wakike.

**
Basi baadae nikaruhusiwa nikarudi zangu nyumbani kwa mama, nilitegemea Mudy angekuja kesho yake lakini akakataa kabisa yani, eti hadi aje na ndugu zake niliwaza huyu mwanaume anamatatizo gani. Kweli walikaa wiki nzima ndio wakaja, nakumbuka walileta kila kitu cha mtoto.

Mudy alifurahi sana alikua ananiangalia mara mbili mbili, ni kama alikua haamini kama nimemletea alichokua anakitaka. Siku hiyo walikaa siku nzima ilivyofika jioni wakaondoka.

Baada ya hapo maisha ya uzazi yaliendelea nikiwa kwetu mpaka ilipofika miezi mitatu nikarudi kwa Mudy sasa. Siku ambayo nilienda mama alinionya kuwa

“Mkajitahidi sio vizuri mkafika leo leo harafu mkafanya mambo yenu bila kinga mimba itaingia tena, kumbuka bado upo wazi jitahidi ukajizuie”

Nilimuitikia mama baadae nikasindikizwa na rafiki yangu mpaka kwangu nakumbuka Mudy alimtuma mtu hadi Moro kuja kutuchukua na tulipofika alikua kazini.

Usiku ulipofika alirudi alifurahi sana kumuona mtoto na ndugu zake ndo balaa mama mkwe na baba mkwe ndo usiseme ilikua furaha tupu hadi nikashangaa.

Muda wakulala ulipofika Mudy si akataka kunipalamia nikakumbuka mama alichoniambia nikasema hapa nikileta udhaifu tu nitaitwa mama tena baada ya miezi 9 mingine.

Basi nikamwambia leo hapana na hakua na kinga na hapendagi kinga nikamwambia subiri hadi nianze uzazi wa mpango alikubali kusubiri kesho.

Siku hiyo alikesha kumtazama mtoto mimi ndio nilikua na usingizi wa uzazi maana miezi 9 sio mchezo.

Basi Mudy alikua anamshangaa mtoto yani kama mshamba flani hivi. Kesho yake ikafika nikajiunga uzazi wa mpango basi ilipofika usiku alikua na hamu balaa maana alikua na papala mno.

Tukashirikiana kwa kuandana vizuri kucheza machi ya kimataifa naweza kuifananisha na mechi kati ya Simba na As Vita maana kila mmoja alitaka kufuzu robo fainali au Ile ya Yanga na Club Africain kule Tunisia, tulianza mechi vizuri mpaka tukatoana ugwadu wotee wa miezi mingi alijisifu sana siku hiyo baada ya kupata goli la ushindi dakika 89 basi akafuzu.

***
Tuliishi kwa furaha sana kipindi mtoto mdogo nilimjali alinijali tuliongea vizuri alikua anawahi kurudi kwajili ya mtoto maana alimpenda mtoto sana.

Kwa kweli akitoka kazini tu anamuogesha mtoto yani alikua ana upendo na mtoto sana alinijali alitujali huwezi amini kama atafanya mambo ya kinyoko. Basi mtoto alipofikisha miezi 9 yale mambo ya kinyoko yalianza upyaaaaa……… ITAENDELEA.

USIKOSE KUJUA MAMBO GANI YA KINYOKO MUDY ALIANZA? basi usikose kifutacho.

NUKUU “Kumbuka kama hujifunzi hapa basi hautajifunza tena, kama bado hujaoa au kuolewa jifunze hapa ni kipi hutakiwi kufanya ukiwa katika ndoa, sio kila kitu lazima upewe na kungwi”

Kama unaitaka yote au sehemu ijayo nicheki 0655 969 973
 
SIMULIZI: ELIZA NA NDOA YANGU
SEHEMU YA 19
Man Middo Tz +255 655 969 973

Baada ya miezi 9 hiyo Mudy aliamua kunifungulia duka, kwa maana nisiwe mama wa nyumbani tu niwe najishughulisha.

Aliamua kumleta rafikiyake Godii ambaye amesema kuwa ndio ataweza kunilekeza mpaka nitakapojifunza ataniachia.

Mume wangu aliniambia kuwa atakaa wiki mbili lakini ikawa tofauti alikaa miezi mitatu kasoro, Baada ya wiki mbili kuisha nilimuuliza Mudy

“Mbona rafiki yako haniachii dukani?”

“Wewe unaharaka gani subiri atakuachia”

Sikubishana nae nikabaki kimya.Lakini Katika hizo wiki mbili hajawahi kunielekeza chochote yani kazi yangu ilikua kumpikia na kumpelekea chakula asubuhi, mchana na jioni.

Kwanza sikuona sababu ya kuelekezwa bei za vitu maana kila kitu nilikua najua reja reja na jumla nilijua maana maduka yaliyokuepo eneo lile nilijua bei zao na hazikutofautiana kwa chochote.

Baada ya mwezi mwingine kuisha nilimuuliza tena kwanini haniachii na pia hanielekezi chochote yeye alibaki kimya tu. Kwa muda huo kuna rafiki yangu aliniambiaga nitafute mtu tumwajili ili tusaidiane kwasababu ya mtoto dah!

Basi Yule rafiki yangu alikaa pale mpaka akaondoka maana Godii hakuonyesha dalii zozote zakuachia duka.

Niliendelea kumwambia Mudy kuwa naweza kubaki mwenyewe lakini hakuonyesha kujali kabisa.Kuna siku shem Afidh akamuliza Mudy kuwa

“Mbona dukani anakaa Godii kwani yeye hana kazi ya kufanya mbona anajibana kwa watu”

Na kweli hadi watu hapo mtaani walikua wanamshangaa kung’ang’ania dukani wakati mimi nipo, Mudy kama kawaida yake hakua na jibu lolote ni mzee wa kimya tu ukiuliza swala la Godii kukaa dukani.

Godii nilikua na mheshimu kama shemeji lakin nilianza kumpuuza kwakua alianza kunidharau, alianza kunipelekesha kama mkewe mara aulize

“Umepika nini?”

Mara akatae mboga niliyopika, mara asuse yani tafrani kila kukicha. Siku moja nikaenda kulalamika kwa wakwe kuwa Godii pamoja na kukaa dukani lakin ananidharau sana, nilisikilizwa tu na kuniambia watamuambia Mudy lakin wapi.

Sasa siku ziliendelea hivyo hivyo nikimwambia shida Mudy ananiambia kamwambie Godii yani hata iwe pesa ya kula kauli yake ni nenda kwa Godii, basi nikimwambia huyo Godii nae ananiuliza

“Pesa ya nini?” Nikisema kuna shida anauliza

“Shida gani?” Harafu anasema

“Mbona mimi hiyo pesa utakayo sina, mimi nina kiasi fulani tu” Yani ili tu anidharau.

Kuna kipindi Mudy ananidharau mbele ya huyo rafiki yake yani kitu kidogo tu anakuambia unanini wewe! Unajua nini wewe mwanamke! Nikawaza kuwa huyu ananidharau kwakua Mudy ananijibu hovyo mbele yake.

Godii alikua anajua kila kitu cha Mudy kudrive alitumia magari yote ya pale atakavyo, mambo ya pesa za Mudy benki yeye ndio alijua, biashara aliachiwa yeye yani kila kitu yeye alikua ni muamuzi yani hata huyo Mudy akiwa na shida ya pesa utasikia ngoja nimuombe Godii utafikiri Duka sio lake.

Akiwa mbali hata mkoani analalamika sina kitu nafikiria kumuomba Godii, yani nilikua naumia mno tena mno hasa ukizingatia mimi kama mkewe hanishirikishi kwenye vitu vya msingi.

Yeye anamshirikisha mtu baki tena hawana undugu wowote maana afadhali angekua mtoto wa mjomba yake au shangazi kidogo lakini yeye alipitiliza sana.

Basi Godii akaanza kuniachia dukani lakini ikiwa ana matembezi yake ndio huniachia kwa masaa anaenda nikiuza akija huku amenuna anauliza

“Umeuza kiasi gani?”

Namjibu harafu namkabidhi kisha mimi naondoka zangu. Ikaendelea hivyo hivyo baadae akanza kuniachia hata wiki lakini wiki ikiisha tu akija anakusanya pesa zote anasepa, baadae nikamuuliza Mudy kuwa

“Hivi Godii pesa zote anazokusanya yeye anapeleka wapi?” Nikaishia kuambiwa

“Wewe hujui mahesabu ngoja ujaziwe duka kisha uuze mwenyewe shida iko wapi?”

Niliumia ikawa ugomvi hauishi kila siku kisa GODII, yani kila nikikutana na Mudy lazima jila la Godii litajwe………………..ITAENDELEA.

Urafiki ni mzuri lakini usivuke mipaka kama huu wa Mudy na Godii.

Nitafute Whatsapp nikupatie mwendelezo
0655 969 973
 
SIMULIZI: ELIZA NA NDOA YANGU
SEHEMU YA 20
Man Middo Tz +255 655 969 973

Kuna siku ndugu wa Godii wakaja dukani kuchukua vitu kisha wakawa wanaondoka nikauliza

“Mbona mnaondoka harafu pesa hamjatoa?” wakajibu

“Godii anajua”

Harafu walijibu kwa dharau flani ivi, niliumia sana ikawa ndio mtindo wanakuja wanachukua nakusepa kama kwa kwao tu.

Duka likaanza kupukutika yani vitu vya juu kama vyakupendezeshea duka viliisha viibaki vya chini tu.

Kuna siku kuna mchele ulibaki harafu ulikua umeharibika haukua mzuri ila mimi nikajitahidi nikaupepeta nikamuambia Godii

“Huu mchele usiutupe kuna mtu nitaenda kumpatia”

Akaniitikia pale na pia nikamtaarifu Mudy kuwa kuna mchele nitauchukua pale hauko vizuri kwa kuuza, basi baadae naenda kuuchukua siukuti namuuliza

“Godii ule mchele uko wapi?” Ananiuliza

“Wa nini?”

“Nina shida nao” akasema tu jibu rahis kuwa

“Haupo”

Harafu Akakaa kimya niliumia sana, niliamua tu kuondoka maana nilitamani kumtusi lakin nikasema itakua lawama tu baadae, nilikuja kumwambia Mudy akanipuuzia tu kama kawaida yake.

****

Siku moja Godii aliniacha dukani alikua ameenda kwao, baadae alikuja mdogo wake.

Sasa kwakua mimi nalea nilikua ndani Yule mdogo wake aliita mimi sikusikia akaja binti akaniambia unaitwa dukani nikasema na nani akasema na mdogo wake Godii nikamuambia asubirie kidogo kwakua ni mwenyeji ili nimbeleze huyu mtoto na mtoto alikua analia kweli.

Basi baadae nikaenda kumhudumia ila kama kawaida yao hajalipa chochote akaondoka, Sasa baadae akaja Godii nilikua ndani pia kwakua sikua na binti wa kazi ilikua shida na sikuona haja ya kuwa na binti wa kazi kwani kipindi kile Godii hakuniachia duka, basi Godii akaja ndani nilikua jikoni akaniuliza kwa dharau na jaziba kaniuliza

“Mbona wewe unadharau sana” nikasema

“Dharau gani”

“Nimemtuma ndugu yangu hapa dukani harafu unamrudisha kwa dharau zako za hovyo tena kwa kumjibu hovyo hovyo unafikiri mimi silipii kama wewe na pia wakichukua naandika kama mteja mwingine tu”

(wakati kipindi hicho nilikua nakagua madftari yote hakuna sehemu aliyojiandika wala ndugu yake)

Nilibaki kumshangaa tu alivyokua ananizodoa aiseee sitakaa nisahauu nililia nililia sana kwa uchungu, kilichokua kinaniumiza ni kuwa Mudy hajanipa haki yoyote kama mkewe hadi kumfanya rafiki yake anaidharau kiasi hiki, rafiki yake ananichukulia tu kama binti wa kazi, Aisee yani pale ndio nilimchukia Mudy kabisaaa yani sikutaka hata kuongea nae kama zamani......ITAENDEEA

KAMA HUJUI YANAYOTOKEA KATIKA NDOA NYINGI BASI ENDELEA KUFUATILIA SIMULIZI HII. HUKO MBELENI NDIO INANOGA ZAIDI.

JE UNAFIKIRI MUDY AKIAMBIWA ATAJIBU NINI?

VIPI GODII ATAENDELEA KUWA MTAWALA KWA MUDY?

USIKOSE KIFUATACHO HAPA HAPA KWA GROUP LETU PENDWA?

NUKUU “Mwanaume uliyeoa tayari au ambae unatarajia kuoa, Kumbuka katika ndoa mkeo ni muhimu zaidi kuliko mtu mwingine, yeye ndo anajua udhaifu wako, yeye ndo anajua siri zako, yeye ndo anakuhudumia, yeye ndo ukiumwa anakuogesha na hawezi kukukatia tamaa,

NOTE! Jamaa mmoja alimnyanyasa mwanamke kwa miaka 8 kila mwanamke akimwambia wafunge ndoa jamaa anakataa huku akijidai kwakua amemzalisha watoto wawili hawezi kwenda popote na kweli alikua anampiga, kumdharau lakini mwanamke hakuwahi kwenda kwao, kila siku neno

‘NENDA KWENU KWANI UNAFAIDA GANI HAPA’

halikuacha kutoka kinywani mwake lakini siku moja mwanamke alichoka akaondoka na kumuachia mwanaume watoto. Jamaa amekaa na watoto kwa miezi mitatu tu, narudia miezi mitatu tuu akaanza kuhaha kumtafuta mwanamke akampata akanza kumuomba msamaha akimwambia siwezi kuishi bila wewe na siwezi kulea wale watoto peke yangu.

Mwanamke alibaki na msimamo akamwambia tayari nimepata kazi najihisi kuwa na amani sana kuwa na maisha yangu nazani ulisema sina faida yoyote pale kwako, hivyo nitakuja tu kutembelea watoto wangu siku nikipata muda. Huwezi amini jamaa alipiga magoti akilia kama mtoto akimuomba mkewe arudi lakin mwanamke moyo wake haukutaka kurudia ya nyuma’
 
SIMULIZI: ELIZA NA NDOA YANGU
SEHEMU YA 21
Man Middo Tz
-eif8m5.jpg

ILIPOISHIA………..Siku hiyo tukaenda hadi kwa wakwe na dada, ilibidi tuwahi sana maana dada alikua na watoto na hana mtu maalum wa kumwachia wanae, hivyo alipanga nanipeleke ili jioni arudi. Lakini nilikua naumia na kumuwaza tu Mudy kuwa

“Kwanini ananizungusha hivi hasemi tu ukweli kwa ndugu zangu kuwa hanipendi”

Nilikua kama mtu wa kuburuzwa tu, kwanza aliweza kuwashika ufahamu ndugu zangu akiwemo mama (wamama wakinyakyusa shikamooni kwa kuheshimu wakwe) maana Mudy aliwajua ndugu zangu kuwa wanamheshimu hivyo akinifukuza nikifika kwetu anasema “Sijamfukuza”

mama nae bila kufikiria anasema “Rudi kwa mumeo kumbe hujafukuzwa” nikirudi anasema “Nilikwambia utarudi tu na hivyo kwenu masikini utaenda wapi.”
Basi njia nzima nikiwaza hayo nilikua nalia tu, dada alinisihi kuwa maisha ndio yalivyo........SONGANAYO

Dada njia nzima alikua ananisihi tu kuwa
“Maisha ndio yalivyo mdogo wangu na siku Mudy atajua anachokufanyia ni upumbavu, ila ukifika akisema baki wewe baki ila uishi nae kwa akili sana”
Basi tukafika kwa wakwe tukawakuta, kumbe walikua wanajua ujaji wetu, wakati huo mimi nilikua na hasira zangu tu haswa nikikumbuka wamesema hawajui kama nimeondoka.
Baade tuliletewa chakula mimi hata sikula, baada ya chakula dada akaanza kujieleza kuwa

“Baba huyu Eliza ni mdogo wangu na ni kama ilivyo kwa Mudy tu, naweza sema wote wadogo zangu, tunafahamu Eliza aliondoka kwa mumewe baada ya kufukuzwa na Mumewe. Kutokana na maelezo aliyotoa na barua aliyokuja nayo kama talaka lakini pamoja na hayo imeonekana sio kweli kama amefukuzwa, sasa ikaonekana kuwa kwakua hajafukuzwa anatakiwa arudi hapa ili muyaongee kama wazazi kisha waendelee na maisha yao.

Pia sisi upande wetu nazani hata kwenu pia tunafahamu kuondoka bila taarifa kwa mumewe si vizuri na nichukue nafasi hii kwa niaba ya mama tunaomba radhi kwa mgongano wa nyie wazazi hivyo tunaomba Mudy akirudi myaongee muamalize”

Mama mkwe akadakia

“Waongee wapi? Hapa sio mahakamani hapa kwangu hatutaki vikao tena wakongee huko huko kwao hapa hakuna kitu kama hicho, kila mtu anamisha yake hatutaki ujinga hapa” baba mkwe nae akadakia

“Kwani huyo Eliza ni nani? Sisi hatumtambui! Tunamuona kama hawala tu wa mtoto wetu, hebu muulize ni lini walifunga ndoa? Na kama walifunga ndoa sisi tulikuja? Au huyo mama yake alikuja? Narudia sisi hatumtambui huyu ni kama hawala tu wa mtoto wetu lakini sio mke wa mtoto wetu, aende tu akamsubirie nje hapo akija watajuana wenyewe huko huko, sisi hatumjui hata kumkaribisha hapa tumefanya makosa mnoo alipaswa asiingie hapa”

Muda wote dada alikua kichwa chini ni kama amebeba mzigo usiomhusu kwa kweli nimelia yani nimelia nilikua siamini kama yale maneno yanatoka kwa wakwe. Baba mkwe aliyekua ananipenda vile na mama mkwe niliyekua namchukulia kama mama yangu leo hii wanaongea vile tena kana kwamba kipindi naondoka sikuondoka katika mikono yao, harafu tena kwa karatasi waliosema ni talaka, eti leo hii hawanitambui niliumia mnoo.

Baadae dada akaniomba ninyamaze akiniambia hatuwezi kupata suruhu kwa kulia hivyo. Mama mkwe akarudi tena kwa kasi kuwa

“Hapa hakuna kikao vikao mtakaa huko huko hapa tulishanawa mikono maana kila siku nyie tu, kazi ya kumtuhumu mwanangu Malaya kutwa kucha, sasaivi kuna mwanaume msafi? eti wewe dada yake kuna mwanaume msafi sikuhizi”

Baba mkwe allikua kimya kwa muda akimuacha mkwewe ajimwage aisee aliongea siku ile na nilichogundua Mudy alikua anaongea vitu vingi vya kusingizia ili mimi nionekane mbaya kwa wazazi wake. Alifanikiwa kwa kiasi kikubwa sana na mimi kwa ujinga wangu nilikua sisemi makosa makubwa ukweni hapo nilijiona boya baada ya kuona Mudy ameweza kuwashawishi wazazi wake.

***

Baadae dada akaanza kuomba msamaha akawambia

“Msameheni huyu bado ni mtoto na hata hiyo ndoa kaikimbilia tu hebu msameheni au nisameheni kwa niaba yake” basi baba mkwe akasema

“Nimekusamehe wewe dada mtu kwakua unaheshima sana lakini Eliza angekua peke yake nisingempokea hapa, sasa utalala tu hadi kesho kwakua muda umeenda huyo Mudy akirudi nitamuliza anatakaje akikataa unarudi kwenu asubuhi”

Dada akashukuru pale na akaomba kuondoka ili awahi watoto wake, Baadae usiku Mudy alirudi kwake akamuita baba yake na mdogo wake wakiume wakaenda kuongea huko kwake mimi nilibaki tu kuwaza kama atanirudisha au kuamua tu nirudi kwetu hata usingizi haukuja. Baadae walirudi saa 8 usiku ila Mudy hakuja, na usiku huo huo wakawa wanajadili kitu na mama mkwe nikahisi labda nitaitwa ila walikua kama mipango flani wanapanga.

**
Baadae wakaingia zao kulala bila kuitwa, basi asubuhi ilivyofika nikaamka nikafanya usafi nikapika chai tukanywa ndipo baba mkwe akanita akanipa tena elf 20 hapa niliwaza “Narudi nyumbani lakin pia hawazi hata huyu mtoto wananipa hela ya nauli tu” basi baba mkwe aliniambia kuwa
“Hii hela uende nyumani Mudy amesema atakuja huko huko sasaivi yupo bize na kazi”

Nikapoke ile hela nikaenda zangu kuvaa na mwanangu tukapelekwa hadi staendi nikapanda gari nikarudi Morogoro.

****

Nilivyofika na maumivu yangu nikamlilia mama kwa uchungu nikimwambia

“Mama naomba unipeleke kusoma Mudy ameamua tu kufanya dharau nimeenda kule lakini hakuna jipya zaid ya kutukanwa na kuonyesha dharau ya pesa zao, naomba sana mama nipeleke chuo mimi sio wa kuitwa hawala mama yangu naomba please nipeleke chuo nikiwa na kazi haya yataisha”

Mama nikama hakuona uchungu nilionao wala yale machozi yangu, achilia mbali yale ya kila siku lakini muda ule yalikua ya uchungu mno.

Basi mama akaniambia “Subiri kikao! Wewe bado ni mke wa mtu nitapoteza pesa zangu bure kwako ngojea aje huyo mwenzako tujue kuwa unarudi au hurudi”

Niliumizwa sana na maneno ya mama, nilitarajia angekua na maamuzi magumu juu yangu lakini ndo hivyo. Dah! Baadae nilikaa tu mtaani bila cha kufanya kila siku kazi yangu ilikua kumkumbusha mama ampigie Mudy nijue kama anakuja lakin cha ajabu Mudy alikua anatangaza mtaani kuwa sitaki asome nataka maisha yampige kwanza mpaka aombe msamaha.
*
Nilizidi kukonda siku hadi siku, nikawa mweusi chu wakati hata sio mweusi. Muda wote huo hajawai kumkumbuka mwanae hata kwa chochcote, nikazoea tu maisha ya mtaani kama ndio yalivyo na tukakaa kimya hatuwatafuti. Sasa walivyoona tupo kimya siku hiyo wakapiga simu kuwa

“Tunakuja kuyaongea wiki ijayo” basi siku ikafika wakaja kwaajili ya kikao…….ITAENDELEA.

JE UNAJUA KWENYE KIKAO WALIAMUA NINI? JE ELIZA ATARUDI TENA KWA MUDY? SOMA NUKUU HARAFU USIKOSE SEHEMU YA 22.

NUKUU “Kumbuka Mwishoe utaishia kuumia tu kama unafikiri watu watafanya wema kwajili yako Kama wewe ujitoavyo kwajili yao, SIO KILA MTU ANAMOYO SAWA NA WAKO” ELIZA ametenda wema mwingi kwa wakwe zake lakini hakuna malipo yoyote, hapa ndio unaweza kuchukua ile dhana kuwa “Tenda wema harafu nenda zako na usubiri malipo kwa Mungu” lakini Mungu anaona kila chozi lilidondokalo na sababu za chozi hilo, Nyie mabingwa wa kumwaga machozi ya watu hakika malipo yenu yapo hapa hapa duniani.
Kumbuka “Mtu kufikia hatua ya kulia sio kwamba ni dhaifu NOO, Ila hii ni kwakua amebaki imara kwa muda mrefu”

Kama unahitaji episode ijayo kujua maamuzi ya kikao nicheki Inbox man Middo au Whtasapp 0655 969 973 Upate mwendelezo.

Usikose kujua waliamua nini katika kikao chao, Je Eliza atarudi tena kwa Mudy au atabaki,
hakikisha unalike ukurasa wangu wa Man Middo tz
 
SIMULIZI: ELIZA NA NDOA YANGU
SEHEMU YA 22
INSTAGRAM: @middotz_

ILIPOISHIA…… Nilizidi kukonda siku hadi siku, nikawa mweusi chu wakati hata sio mweusi. Muda wote huo hajawai kumkumbuka mwanae hata kwa chochcote, nikazoea tu maisha ya mtaani kama ndio yalivyo na tukakaa kimya hatuwatafuti. Sasa walivyoona tupo kimya siku hiyo wakapiga simu kuwa “Tunakuja kuyaongea wiki ijayo” basi siku ikafika wakaja kwaajili ya kikao…….SONGANAYO

Basi siku waliyokuja mama nilimshangaa Sana yani alimjali Mudy, aliandaa chakula cha adabu! Yani cha heshima eti kuwapokea wageni. Sijui kwanini aliwanyenyekea vile nikafikiaria nikahisi kwasababu eti wanapesa ila utafikiri sio yule Mudy aliyekua anamjibu vibaya niliumia mno lakini sikua na namna.
Kikao tulienda kufanyia sehemu ambayo ni nje kidogo na nyumabani kwetu, ilikua kuogopa tu majirani wasifuatilie kinachoendelea maana nyumbani kwa mama kwenyewe ni nyumba za kota. Sasa mwanzo niliongea na mshenga wangu aliniambia kuwa kwenye kikao atanza kuongea Mudy, nilifurahi kidogo ili nijue uongo wake ili nipate kumkosoa.

**

Baadae basi kwenye kikao upande wetu tulikua saba ni mimi na mama harafu na baba zangu wengine tu waheshima maana mama walishatengana na baba kitambo sana. Kwa wakati huo baba mwenyewe mzazi alikua Mbeya na mama yupo Morogoro kazini. Upande wa Mudy walikua wanne kwa hiyo jumla kikao kilikua na watu 11. Sisi ndio tulikua wengi kwenye kikao ingawa pamoja na uwingi wetu wale wazee hawa kujua sana kuhusu mimi na kuteswa na ukizingatia familia nyingi wanaona ukiolewa na mtu mwenye pesa basi kukitokea mkwaruzano wanaona mwanamke ndio mwenye tatizo tu na sio mwanaume.

***

Kikao kilianza na maombi watu tukaomba vizuri pale Mungu akasimamie kikao kikawe na muafaka mzuri na wenye faida, baada ya maombi baba wa upande wetu akaanza kuongea

“Jamani kwanza poleni na safari na pia kwa kujali kuja kwenye hili suala, kuja kwenu kunaonyesha ni kwa namna gani na nyie mnahitaji muafaka wa jambo hili. Basi kama mnavyojua hapa tuna watoto ambao hawaelewani, ndoa yao bado changa tena na pia wanamtoto mchanga. Wao pia bado wadogo maana hakuna anaempa mwenzake nafasi ya kukubali kosa. Sasa ili yaishe waendelee na maisha yao kama ilivyo lengo ni kupata suruhu na tumeona tuanze kusikiliza kero zao kwanza ndipo baadae tujue waishi au wasiishi.(mzee akameza mate kisha akasema) sasa kwa kuanza tuanze na Eliza”

Kwanza moyo ulistuka nikasema kweli wanaume wanalindana huyu mzee aliniambia ataanza Mudy leo hii kanisukumizia nianze mimi.

Dah! Nikakaa kimya kidogo, nikakohoa kidogo ili kuweka koo sawa kisha nikaanza kuongea, nilielezea yote Mudy aliyonifanyia kunitesa kunidharau na kunipiga ila sikuongelea mambo ya rafiki yake Godii wala wapangaji kwasababu niliona hao ni watu baki tu.Niliona Wazee wanaweza kusema umeolewa na Mudy sio hao. Basi baada ya kuelezea kila kitu kuhusu Mudy, wakaniuliza maswali kuwa

“Kwanini ulipokua unafukuzwa hukumwambia mshenga wako? Kwanini ulipokua unadharauliwa na kuteswa hukumwambia mama mkwe wako mpaka imefikia hatua mbaya? Kwanini ulikubali kuishi na mtu ikiwa hakupendi na humpendi? Maswali yote nilijibu kwa ufasaha sasa ikafika zamu ya Mudy (aisee huyu jamaa ni Nyoko) hahahaha! Nacheka tu kwa maumivu jamani, Maana hakuongea ya ndani aliongelea wengine nje kabisa.

Basi mzee baba akanza “Wewe Eliza kwanza nilikupiga wapi? Umemwambia mama yako kuwa nilikupiga na huyo mama yako ananipigia simu kuniuliza kwanini nimekupiga, nilikurudisha ili nimuulize wapi umeumia, yani mama yako amenikwaza kweli yani bila kufikiria anakupokea tu” (watu midomo wazi wanashangaa tu kinachoendelea)

“Harafu nakushangaa sana wewe mama huyu mwanao toka yupo kwa mama yake mdogo nikija napitia kwako naleta sukari, mchele, niseme naleta kila kitu harafu leo unasema mwanao simpendi ningekua simpendi mwanao ningeleta hivyo vitu au mnasema tu” (JEURI YA PESA UNAONGEA CHOCHOTE) niliumia nikajikuta nalia tu.

***

Mshenga wake akamnyamazisha akimwambia kuwa

“Wewe Mudy hawatajagi vitu wanavyopeleka kwa mama mkwe wako, tambua huyo ni sawa na mama yako ukipeleka kitu huhesabu kuwa na adabu”

Yani nikama walimuongezea nguvu hata hakusikia chochote akaendelea

“Wewe mama sijui ukoje kakitu kadogo tu wewe kuingilia mwanangu! Mwanangu! Basi kaanae sasa kwanza hata hiki kikao sikukitaka”

Ilivyofika hapo wazazi wake ikabidi waingilie mama yake akafoka akamwambia

“Wewe hebu kaa kimya kama huna cha kuongea, hebu ongea kero zenu sio mama zenu kwani mnaishi na wazazi?”
****

Baadae akaendelea “Ehee! Huyu Eliza hampendi rafiki yangu Godii hataki akae dukani mimi nilimuweka dukani kwa muda ili amfundishe mahesabu maana hajui hata kurudisha chenji yani hata elf 5….” Wakamkatisha

“Hee! Wewe Mudy hivi kweli Eliza na elimu yake ya Form 4 hajui kurudisha chenji ya elf 5 hizo ni dharau, alipitaje darasa la saba hebu acha kumdharau mwenzio”, (sasa alivyoona kaambiwa ukweli akanza sasa habari za uongo akaendelea sasa)

“….kwanza huyu mwanamke hawapendi wapangaji yani haongei nao vizuri, wale wapangaji ni kama ndugu zangu tena kabila moja, sasa huyu anawalingishia maisha nikiondoka anawambia ‘samaki sizipendi zimenifika hapa nataka hadi kutapika’,...harafu anamwambia maneno, kuna mbibi flani hivi tena anakaa mbali na kwangu anamwambia eti mimi nina pesa mpaka zinamwagika, sasa huko sikudharau huko na kunichoresha je wakiniibia au kunivamia. Ndio maana kuna siku moja tuliibiwa pesa na simu yake kumbe anatangaza, huyu mwanamke muuaji anataka kuniua huyu mimi”

Kila mtu alianza kumshangaa akanendelea tena “Harafu huyu mwanamke usiku anatabia kuniamsha kwa kunimwagia maji usoni kama ananiamsha nikalale chumbani, kwanza hata hapo nyumbani sitamani kabisa kurudi yani nyumba naiona ya moto. Nyumba naona chungu bora nirudi zangu tu usiku ili nikifika nalala tu. Na akianza kununa wiki hata mbili haongei” kila mtu alianza kunishangaa nikaona sasa kibao kinarudi kwangu.

Muda wote Mudy anabwabwaja mimi machozi yananitoka tu niliumia nakujiuliza “Nia yake ni ipi haswa kwamba amekuja kunidhalilisha au anataka tu mama asinisomeshe” niliumia sana sikuamini macho yangu, muda wote nampa heshima kama mume wangu namfanyia kila kinachostahili kufanyiwa na mkewe namfichia siri zake hata kwenye hiki kikao angalau ili hata ajiulize na kuona kuwa bado nimempa heshima lakini kujiona anapesa ananidharau na kuniaibisha tena sio mimi tu mpaka mama yangu. Niliumia sana Mudy hakuwahi kumpa mama senti zake kwanza mama ni mfanyakazi hivyo alijiweza pamoja na kwamba mshahara mdogo lakin aliweza hadi kunilipia ada chuo, yeye anafikia hatua ya kumtukana mama yangu.
**

Basi kibao kikageukia kwangu (shikamoo uongo wa wanaume kama Mudy) sasa wale wazee wakanza kumtetea mwenzao

“Wewe mwanamke gani kitu kidogo kwa mama yako, hivi unafikiri ndoa zote ingekua kitu kidogo tu kwa mama watu wangeishi katika ndoa? Kwanini umwagie mumeo maji na ujue kabisa katika vitu hatupendi kufanyiwa wanaume ni kumwagiwa maji, hilo ni jambo baya sana. Wewe unatakiwa uwe mfariji wa mwenzako na sio mtu wa kumtesa. Mwanaume katoka kazini kajipumzisha unammwagia maji je akifa dah! Kumbe hufai wewe mtoto” walinisema sana.

Baadae wakamgeukia mama “Hivi mnakazania kulea watoto harafu kumbe wanawashinda na bora tu huyu mtoto anageishi na baba yake maana sio kwa dharau unazompa kwani umeambiwa ukimuacha hivyo hivyo akae hata kama anateseka unaharibikiwa nini eti. Kitu kidogo tu mrudishe mwanangu haya sasa kumbe mwanao ndio kichomi” Mama alishindwa kujizuia akanza kulia akawambia

“Huyu mtoto hii ndio mara ya kwanza kumwambia rudi lakini hizo siku nyingine akirudi anasemaga narudi kama likizo, mpaka mimi namfukuza maana mumewe hajawahi kumuita akiwa kwangu, nikimuliza kuna tatizo maana toka aolewe anapungua tu lakin ananiambia mumuwe kamuaga na kamruhusu nafikia hatua nampigia simu Mudy kumwambia nimechoka ujaji wa mwenzako huku yeye ananimbia muache tu akae akichoka atarudi.

Namulizaga Mudy kama anampenda mkewe na kwanini akija huku hamkatazi, yeye ananiambia hawezi kumkataza maana anakuja kwao, mimi ndio nachukuaga maamuzi ya kumfukuza huyu”

Basi mama alivyomaliza kueleza yake wakanza kuchambua makosa, ikaonekana mimi ni mkorofi na sijui kutunza siri maana kazi kukimbilia kwa mama, kitu kidogo tu kwa mama harafu namtesa mwanaume na nyumba yake, mama yake akasema

“Huyu Eliza inaonekana anahasira sana huwa namsihi sana avumilie maana hata hapa tulipofika sisi mama zako tumevumilia mengi mno tena afadhali kabisa yeye, sasa mwenzetu kutwa kulia tu kama vile kaonewa, sasa nimeona bora mumsikilize nyie mnaweza kujua shida iko wapi”

Wakanza kunipa mausia ya ndoa wakaongea wewe na kuniambia “Eliza inaonyesha humpendi mumeo na humjali ndio maana ni rahisi ukifukuzwa unaondoka tu, mtu anaempenda mumewe hawezi kubali kirahisi rahisi tu akiambiwa ondoka. Hatafu majirani zako ndio kila kitu kumbuka uliwakuta na wakakupokea unatakiwa uishi nao vizuri. Kingine rafiki wa mumeo unatakiwa kumuheshimu kama mumeo wa ndoa sio kumchukia”

Niliwaza sana kuwa hawa wote wanachuki zao, upande wetu hawanitetei kwasababu pia wananiita nina dharau hivyo waliendelea kunigandamiza, upande wa Mudy wanaongea uongo tu hivyo kwakua anaejua kila kitu ni mimi na mama basi lazima tu nigandamizwe. Baadae wakamua kuwa

“Kutokana na sababu zenu ni za kitoto, sasa hakuna kuchana hapa sasa mnarudiana upya na maisha yaendelee”
Mimi nikakataa na Mudy pia akakataa, wazee wakasema

“Nyie mnajifikiria wenyewe hamumuwazi mtoto wenu, sasa kama hamtokubali kuendelea na ndoa na hamtokubali kuachana kwa amani basi itawaumiza wenyewe. Wewe Mudy ukimuacha Eliza kwa hivi visababu vyako hutaoa mke mwingine utaoa tu na kuacha unaweza kufikisha hata wanawake 200 ila utacha hivi hivi na wewe Eliza hivyo hivyo utaolewa na kuachika, sasa ni bora haya mambo yaishe muendelee na maisha yenu”…………….USIKOSE SEHEMU YA 23 KUJUA KIKAO KILIISHAJE

Ama kweli pesa inanguvu kubwa, leo siongei mengi maana kikao hakijaisha. Swali ingekua wewe mpaka hapo walipofikia ungefanya maamuzi gani, mama yako anadharauliwa, anatukanwa na ndugu zako nao wanakugandamiza unalazimishwa urudi motoni utafanyaje? Au ingekua Eliza ni binti yako utaamua nini?

NUKUU “KUNA WATU NI MASIKINI KIASI KWAMBA KITU PEKEE WALICHONACHO NI PESA” Mudy anayopesa lakini ni masikini wa NIDHAMU, masikini wa BUSARA NA HEKIMA, masikini wa UTU nk (anajali kitu kuliko utu, kumpelekea mama mkwe sukari na mchele eti ndio mapenzi, eti ndio kupenda ajuavyo yeye hajui hata anaetaka kukuwekea sumu anaweza kufanya hivyo pia)

Usingoje kesho kama unataka mwendelezo ni rahisi tu nicheki INBOX au WHATSAPP 0655 969 973 LI
 
ELIZA NA NDOA YANGU
SEHEMU YA 23
Man Middo Tz
ILIPOISHIA..... Baadae wakamua kuwa
“Kutokana na sababu zenu ni za kitoto, sasa hakuna kuchana hapa sasa mnarudiana upya na maisha yaendelee”
Mimi nikakataa na Mudy pia akakataa, wazee wakasema

“Nyie mnajifikiria wenyewe hamumuwazi mtoto wenu, sasa kama hamtokubali kuendelea na ndoa na hamtokubali kuachana kwa amani basi itawaumiza wenyewe. Wewe Mudy ukimuacha Eliza kwa hivi visababu vyako hutaoa mke mwingine utaoa tu na kuacha unaweza kufikisha hata wanawake 200 ila utacha hivi hivi na wewe Eliza hivyo hivyo utaolewa na kuachika, sasa ni bora haya mambo yaishe muendelee na maisha yenu”…………….SONGANAYO

Baadae mama yake Mudy akaingilia kati kasema “Kwanza mimi nashangaa ugomvi wa hawa watoto, huyu Eliza kwake na kwangu ni jirani naenda kwake na yeye anakuja kwangu lakini hajawahi kunidharau wala kudharau watu au kutusema vibaya. Kwa kweli sijawahi kusikia hata kwa majirani, sasa wanachogombana hatukijui haswa maana hatujui wameanziana nini, sisi wazazi tunampenda mno maana ni msaada kwetu tunashangaa tu wanagombana”

Kikao kikarudi tena kwa Mudy kaulizwa “Wewe Mudy huenda huyu Eliza sio mbaya kama unavyoeleza kwasababu inawezekanaje awe mbaya kwako tu wewe unaeishi nae. Kutwa nzima haupo wale anaoshindanao kutwa hawaoni ubaya wake, huenda kuna kitu hapa kimejificha au ni wivu tu unawasumbua, sasa mtake mistake lazima mrudiane”
Dah! Nililia mno yani kikao kizima mimi nalia tu maana sikutaka kurudi tena kwa Mudy, moyo wangu ulishakufa kurudi tena kwa Mudy.

Siku ya kikao ndio nilijua kuwa kumbe Godii na wale wapangaji walikua wanamwambia Mudy mambo mengi ya uongo ambayo mimi sikuwahi fikiri kuwa watasema. Nikajisemea kumbe nilikua nafanya makosa kuwaacha waingilie mambo ya ndoa yangu. Mshenga akasema hapa lazima muelewanae Mudy kasema

“Mimi nimeshamsamehe lakini mumfunde, mumfunze namna ya kuishi na mwanaume ndio arudi kwangu na lazima arudi kwangu baada ya wiki mbili. Msipomfunza vizuri sitompokea, hapa anajidai analia kwa uchungu lakini akija kwangu hasira zote kwangu mimi staki”.
Mama akaenda kwa Mudy kupiga magoti huku akisema

“Asanteh baba yangu, Mungu akubariki nisamehe kwa kumsikiliza Eliza kuliko wewe”

Daaah! Nililia mara mbili yake kwa mama kumpigia magoti Mudy bila sababu yoyote niliwaza huyu Mudy na upuuzi wake wote ndio wakupigiwa magoti na mama yangu harafu Mudy kwa dharau akamjibu mama

“Ndio uongee na mwanao mimi sichelewi kumuacha na hii ni mara ya mwisho sitomsaidia tena, kwanza hampendi baba yake toka nianze kuishi nae hajawahi nipeleka kwa baba yake anakupenda wewe tu” Mudy aliongea mambo mengi ambayo ni yakuumiza sana sana kuongea.

Basi baadae niligoma niliwambia siwezi tena kurudi kwa Mudy, nikanza kusema ukweli wote Mudy alionifanyia mpaka kunifumua mshono kwa kuniingilia, Mudy akanywea na watu wote pale ni kama wanamshangaa sasa, baadae wakasema

“Kwakua ashasema urudi nyie sameheaneni tu mrudiane yaishe na msirudie hayo makosa tena mkaumizana, kuanzia leo wewe Eliza kama kuna kitu unawambia wakwe zako na wewe Mudy unawambia wakwe zako sio wazazi wako” wakainuka wakasali eti kikao kimeisha mimi nalia tu.
Wakati wanataka kusali mara Mdogo wake Mudy akanza kusema

“Kwanza huyu Eliza hampendi kaka yangu yani makosa afanye yeye harafu kazi kumsingizia kaka yangu mimi simuelewi kabisa huyu”
Watu wote wakamshangaa wakamwambia

“Kama humpendi mke wa kaka yako subiri ukioa wa kwako na kikao kizima umekaa kimya huongei sasa kimeisha ndio unajifanya kuongea kama mmekuja kuacha sasa ndio mjue kuwa sisi ndio wanyakyusa hutachwi ila tunaacha sasa subir afundwe arudi”

Yule dogo hakupenda lakin mama yake alifurahi sana akenda kumkumbatia mama tukaambiwa tuinuke tukumbatiane maana tuliyataka wenyewe. Mimi nilikua nawaza tu kuwa isingekua mimba nisingeishi na huyu mwanaume nikagundua Mudy, Godii, wapangaji na majirani wote hawanipendi kwahiyo nilivyoondoka ilikua sherehe sasa narudi inakua msiba tena na wataamini kweli kwetu masikini ndio maana nimerudi na tunamnyenyekea sana Mudy.

***
Ilivyofika jioni wakaondoka kurudi Pwani, mimi niliondoka pale kwenye kikao peke yangu mtoto alienda na mama kwa bodaboda. Sasa wakati narudi simu yangu ikaita alikua ni yule mpenzi wangu wa zamani yule wa kabla ya Mudy mmh nikapokea akaniambia

“Nimesikia upo kwa mzee mwaipopo mna kikao”

Kweli kile kikao tulifanya kwa mzee huyo aitwae mwaipopo akaniambia

“Nilikua maeneo hayo ila nimesikia ukilia sana kikao kizima, kwanini wewe ndio ulilia sana? Sikupata jibu sahihi la kumpa nilikua bado nalia tu.

Akaniambia “Njoo stendi tuongee” kweli nikaenda hadi stendi kwanza sikuona umuhimu wa kuwahi nyumbani na pia niliona mama hakunitetea chochote, ameniuzi kukubali kurudi kwa Mudy.

Mama Kusema kabisa kuwa na kwangu asirudi tena wakigombana wasuruhishe huko huko niliona mama ananichimbia kaburi bila kujua. Basi nilitembea kwa mguu hadi stendi sio mbali sana na sehemu niliyokuepo, sasa kumbe ex wangu kawa dereva boda boda akanipandisha tuakenda hadi sehemu flani hivi kuna poli, hiyo ni sehemu ambayo kipindi tunasoma tulikua tunasindikizana na huku tunapiga stori sana sana ikiwa tumekosana.

****

Basi tulipofika huku naendelea kulia nikamwambia

“John nisamehe sana ni bora ningevumilia wivu wako na kunibana kwako kuliko kumvumilia Mudy ananiua kimya kimya” huku naendelea kulia nikajikuta namwambia “Naomba tuendelee na mahuasiano kama zamani kama huna mtu kwasasa na kama unamtu nitakubali tu iwe siri yetu” alikataa akaniambia

“Eliza nakupenda lakini uliniumiza sana na sasaivi nina mtu wangu ananipenda sana staki kumuumiza kama ambavyo umeniumiza, nataka kuwa muaminifu kwenye uhusiano wangu na pia hata mumeo akijua nitakuongezea matatizo wewe, ila mimi nitakua nakusabahi tu muda wowote ukihitaji kuongea na mimi lakini swala la mahusiano hapana” niliumia maana nilijiona kama takataka machozi hayaachi kutoka.

Baadae akanza kunibembeleza akanikumbatia nikahisi msisimko wa kipekee toka niwe na Mudy hakuwahi hata kunikumbatia, lile kumbato la John lilinifanya nimiss aliyokua ananifanyia zamani nilijikuta nimeganda machozi yanatoka tu, alinikumbatia muda mrefu huku akinisihi kuwa

“Eliza haya ni mapito tu, yote haya yatakwisha na natambua kuwa wenye pesa huwa hawaridhiki na mmoja. Sasa mpo wengi ndio maana hata robo ya mapenzi hupati, kipindi kwangu ulikua peke yako sikua na pesa huenda ningekua na pesa ungetulia kwangu na unafahamu jinsi nilivyokua nakupenda sidhani kama ningefikia hatua hii ya kukutesa hadi unajiona kuna thamani mbele za ulimwengu huu, ila kwasasa ni ngumu kuwa na wewe watu wengi mtaani hapa wanajua uliniacha na hunitaki sijui nanzaje kukurudia na nikimsaliti nilienae itakua dhambi pia naomba unisamehe”

Pale pale simu yangu ikaita kuangalia alikua ni mama akaniambia
“Uko wapi wewe mtoto hujampa uji mpaka saaizi”

kipindi hicho mtoto ana miezi 9 nishamuachisha kunyonya alikua anatumia uji na maziwa tu………ITAENDELEA.

Usikose kujua sehemu ijayo kilichoendelea na kufahamu kama atarudi au atafanyaje.


NUKUU “Mwanamke ambae haombi chochote anastahili kupewa kila kitu” Eliza anastahili kupewa kila kitu. “Kufeli ni sehemu ya maisha kama hautafeli hautajifunza, Kama hautajifunza basi kamwe huwezi kubadilika” Eliza amejifunza kitu ndio maana amerudi kwa John kumuomba warudiane. “MTU ANAEKUPENDA KWELI , NI YULE ANAYEONA MAUMIVU KATIKA MACHO YAKO, WAKATI KILA MTU ANAAMINI KATIKA TABASAMU USONI MWAKO” kwenye kikao wote wamemuona Eliza kama anaigiza tu alipolia lakini John pamoja na kuwa wana miaka hawajaonana lakini amegundua Eliza yupo na maumivu makubwa mnoo. Mwisho chukua hii na ujifunze “Vitu vitatu ambavyo hutakiwi kuvivunja
AHADI
IMANI na
MOYO WA MTU”
Kama unahitaji mwendelezo nicheki Inbox au WHATSAPP 0655 969 973
 
SIMULIZI: ELIZA NA NDOA YANGU
SEHEMU YA 24
Na Man Middo tz

ILIPOISHIA………….akanza kunibembeleza akanikumbatia nikahisi msisimko wa kipekee toka niwe na Mudy hakuwahi hata kunikumbatia, lile kumbato la John lilinifanya nimiss aliyokua ananifanyia zamani nilijikuta nimeganda machozi yanatoka tu, alinikumbatia muda mrefu huku akinisihi kuwa

“Eliza haya ni mapito tu, yote haya yatakwisha na natambua kuwa wenye pesa huwa hawaridhiki na mmoja. Sasa mpo wengi ndio maana hata robo ya mapenzi hupati, kipindi kwangu ulikua peke yako sikua na pesa huenda ningekua na pesa ungetulia kwangu na unafahamu jinsi nilivyokua nakupenda sidhani kama ningefikia hatua hii ya kukutesa hadi unajiona kuna thamani mbele za ulimwengu huu, ila kwasasa ni ngumu kuwa na wewe watu wengi mtaani hapa wanajua uliniacha na hunitaki sijui nanzaje kukurudia na nikimsaliti nilienae itakua dhambi pia naomba unisamehe”

Pale pale simu yangu ikaita kuangalia alikua ni mama akaniambia
“Uko wapi wewe mtoto hujampa uji mpaka saaizi”
kipindi hicho mtoto ana miezi 9 nishamuachisha kunyonya alikua anatumia uji na maziwa tu…………SONGANAYO

Baada ya kupigiwa simu John akaniambia

“Ngoja nikupeleke tu nyumbani mtoto akanywe uji, hata hivyo sio vizuri kumtesa mtoto maana yeye hana hatia”
Basi nikapanda pikipiki yake akanipeleka hadi nyumbani, yeye akaondoka baada ya kuondoka nikaingia ndani. Mama hakunisemesha kitu chochote nikashukuru maana sikutaka kusikia tena masuala ya kikao kwa wakati ule, Nikampa mtoto uji siku ikapita hivyo.

**
Baada ya wiki moja mama ndio akanikumbusha tena masula ya kikao cha kufundwa, japo nilikua naumia kwa kwenda kufundwa kitu ambacho sijawahi mtendea vibaya mtu lakini nikaona hii itakua fursa kwangu kuongea japo ukweli wa kila kilichoendelea kwa Mudy, ili tu anagalau wawe na imani kwa uapande wangu au anagalau nitoe ile tofauti ya kuonekana mbaya pande zote.

Basi siku hiyo jioni tukaenda kwa mjomba ni jirani tu na kwetu ni mjomba wangu tu kiheshima, tulipofika tukafanya maombi kikao kikaanza nikaulizwa

“Binti yale maneno tuliyosikia kuwa hata chenji ya elf 5 hujui kurudisha ni ya kweli? Na je ni kweli wanavyosema kuwa unamtanagazia mumeo kuwa anapesa hadi zinamwagika? Hebu nieleze ukweli wote hadi yale ya kipindi anakuja kwangu”

(kuna kipindi Mudy alienda mbeya alifika hadi kwa mjomba sasa alivyorudi akaniambia kuwa mjomba wako kaniambia kuwa umemuoa binti ambae utajuta maana hafai hana adabu, sasa kipindi hicho mama alimchukia sana mjomba nakumgombeza lakin kumbe Mudy alitunga tu ili atugombanishe, mjomba alichukia sana kipindi kile )
Basi niliwaeleza kila kitu kuwa Mudy ni muongo anachopenda nikunigombanisha na kila ndugu yangu ninaekuwa na ukaribu nae. Watu walishangaa sana yale ambayo nimeyaeleza baada ya kueleza kila kitu, baba mlezi akaniambia

“Eliza sikia nikuambie mwanangu hapa unapotuona ni watu wazima na mtu muongo tunamfahamu sana mimi kwa kazi yangu namfahamu mtu muongo kwa macho tu, hayo ya kuongea ni ziada tu, sasa ni hivi huyo mumeo tushamsoma sana, ujana ni mwingi kwake na ndio unamsumbua akili yake haijatulia. Wewe una akili japokua bado mdogo, sasa chakushangaza yeye na ukubwa wote ule akili zake ndogo labda nikuambie tu kuwa Mudy, mama yeke na yule mdogo wake wote walikuja kwa nia ya kukuacha sasa baba mkwe wako hajapenda hicho kitu ndio maana hakuja kwenye kile kikao.

Sasa kama hujui naomba ujue kuwa sisi wanyakyusa huwa hatuachwi ila tunaacha haswa kwa mtu mjinga kama yeye. Ukweli ni kuwa kwa Mudy ulikosea na umekosea, Mudy kama nilivyosema ni mtu anaetaka kukuacha ila anatafuta pakukuachia, alitafuta nani wakumpa lawama akaona kwa mama yako ndio wakumuangushia jumba bovu ili iwe kama chanzo. Sasa mimi nasema hivi hapa haachwi mtu na ndio maana tulikukandamiza kwenye kikao ili aumie yeye na nia yake ya kukuacha sasa baada ya kurudi tumia akili ya namna ya kuondoka ila tafuta pakwenda kwa mama yako tena basi, ulikua umepanda sasa huu ni wakati wa mavuno naomba uvune hakuna wakumpa lawama tena, sasa nenda wakaaibike Godii, wapanaji pamoja na majirani zake aliowatambia kuwa amekuja kukuacha”,

Kwa kweli nililia sikutaka tena kurudi kwa Mudy niliona labda watanisikiliza na kukubali nisirudi niliona kama wananipeleka motoni kwa makusudi, mama nae akasema kuwa

“Kuanzia leo sitaki tena kujihusisha na ndoa yako kwa lolote lile labda ugonjwa tu, kwangu naomba kabisa usije bila sababu na likikupata jambo mwambie mumeo sio mimi nimemchukia sana amenidhalilisha kikaoni kuwa mimi kila jambo nawasha moto kwake au nikikugombeza jambo wewe ukirudi unamuwashia moto kana kwamba kuna kitu nafaidika na hiyo ndoa yenu , naonekana naongeza kitu ili mgombane sasa sitaki tena”

Niliumia sana maana kila aliyepaswa kunipa msaada alinikataa kwa wakati ule, mamuuzi ni kunitupa kwenye moto, nilijiuliza kabisa “kama mtu mshajua kabisa akili zake ni ndogo wapangaji, rafiki na majirani wanamuendesha sasa yanini kunipeleka kwa watu wanamna hiyo” pale ndio nilichukia mila za ajabu tu “eti wanyakyusa hatuachwi ila tunaacha”
Basi baadae mama mmoja pale kwenye kikao akaniuliza kama naishi vizuri na majirani nilimwambia sijawahi kuwadharau kwa chochote, yeye akaniambia kuwa sumu kubwa ipo kwa huyo Godii, wapangaji na pia majirani zako sasa itakubidi ufanye jambo laasivyo mateso yatazidi.

***

Kikao kikaisha na wakanionya kuwa nisimtishie Mudy kwa chochote kwasababu yeye anatafuta sababu tu, baadae wakaniambia kuwa jumatatu wataenda kunikabidhi kwa wakwe zangu, nilikubali tu kishingo upande na kuna muda niliona nisahihi tu kwa wakati ule kwasababu hao niliowategemea ndio wamenisukumiza kurudi. Bado nina mtoto mchanga nikisema niondoke sikujua niende wapi, na umri wangu niliona nitakayoelekezwa ndio sahihi.
Maisha kwangu yalikua magumu sana nilikua nimekonda mnoo pamoja na kuwa nimemuachisha mtoto kunyonya hela yangu ya akiba yote iliisha. Yani kila nilichofikiria akili ikakwama, yani ningepaona pakuishi ningeenda maana kwa Dada ningesumbuliwa tu.

Baada ya kikao ikawa muda wa kutoka nilivyofika stendi kikamwambia mama atangulie, basi John akaja tukaenda tena hadi kwenye ile sehemu tunapokaaga kwenye kale kapoli ketu tulivyofika tukaanza stori akaniuliza kilichojili kikaoni nikamwambia kila kitu akawa anashangaa tu. Akaniambia kuwa
"Kwahiyo wazazi wako wanataka wakupeleke kwenye moto kabisa"......ITAENDELEA.

ELIZA ANARUDI TENA KWA MUDY, JE UNAJUA ATAENDA KUISHIJE UKO? ATAELEWANA NA MUDY AU NDO ATAZIDI KUDHARAULIWA.

KUMBUKA MWENDELEZO UNAUPATA CHAP WHATSAPP 0655 969 973 AU KWA MESSENGER.

NUKUU “Usitamani kiatu changu ukikivaa hautembei” hivyo usitamani cha Eliza, “Kuna siku mbili pekee katika mwaka ambazo huwezi kuzifanyia chochote, ya kwanza inaitwa JANA na nyingine inaitwa KESHO, Hivyo LEO ni siku sahihi ya KUIPENDA, KUIAMINI, KUIFANYIA KITU NA KUIISHI” Mungu akubariki msomaji wa simulizi hii siku ya LEO ukafanye maamuzi yaliyosahihi, usiwaze ya jana yatakumiza na Hujui ya kesho yako fanya kitu leo, “Usilipize kisasi, tambua kisasi kikubwa na kizuri ni kuchagua FURAHA YAKO TU”

JE UNAJUA KINACHOENDA KUTOKEA UKO KWA MUDY? BASI TWENDE WOTE
Nakutumia inbox kwako na whatsapp nicheki Man Middo au whatsapp 0655 969 973
 
Back
Top Bottom