Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #41
nakukubaliii[emoji91][emoji91]
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
nakukubaliii[emoji91][emoji91]
Aisee kitu kinazidi kuwa kitamu yani nasoma huku natamani isiisheSEHEMU YA 42
"Usinambie Elizabeth. Usinambie hiyo siri sina haja ya kuijua. Don't tell me Elizabeth" Mwanasheria mlevi alisema kwa nguvu.
"Wewe ni mtu wa ajabu miongoni mwa watu wa ajabu. Nataka nikwambie kitu ambacho kila mtu anataka kujua. Nataka nikwambie kuhusu 001. Kubali nikwambie ili ujue utafanya nini?. Nitakuwa nimefanya dhambi kubwa sana endapo nikifa bila kumwambia mtu kuhusu 001. Sikili..." Elizabeth Neville alitaka kusema lakini Mwanasheria mlevi alimkatisha.
"Don't tell my sister pleeease. Don't tell meeee" Alisema kwa nguvu Mwanasheria.
Katika chumba kingine kilichokuwa na watu wawili katika nyumba hiyohiyo kulikuwa na taharuki. Watu hao walikuwa mbele ya kompyuta zao huku wakiwaangalia Elizabeth na yule jamaa. Mwanzoni sura zao zilikuwa zimejawa na furaha pale Elizabeth alipokuwa tayari kutoa siri kabla ya yule kijana kukataa kuambiwa hiyo siri.
"Huyu jamaa anazingua. Tulikuwa tunaimaliza kazi hii leo. Elizabeth Neville alikuwa tayari kutoa siri kuhusu 001 ila huyu jamaa katurudisha nyuma.
"Sasa tufanyaje. Naona na mpango huu unaelekea kufeli" Zungu alisema.
"Elizabeth Neville apelekwe katika chumba cha mateso akakutane na Richard, nahisi leo atasema kila kitu. Ameingiwa na uwoga kuona kile anachotaka kufanywa mwenzie. Mpeleke kule leo atatapika" Sam aliamrisha.
Simu ikapigwa kule chumba cha mateso. Felix naye akapiga kwa walinzi wakiowalinda wakina Elizabeth Neville. Harakaharaka Elizabeth alitolewa katika kile chumba na kupelekwa katika chumba cha mateso. Na Dokta Yusha akarudishwa kule katika chumba cha awali.
"Aisee that man is monster. Na ujanja wangu wote leo mkojo umenitoka. Ni nani yule Richard. Sura yake nzuri lakini inabadilika awapo kazini. Maneno yake hatanii, ananena atakacho kutenda. Alikuwa ananitumbua korodani leo!" Dokta Yusha alisema pindi tu alipopelekwa kile chumba kingine.
"Tumeona kila kitu. Tumeona ukivyotetemeka pindi alivyotaka kukufanya yule jamaa. Hata Elizabeth huku alikuwa anatetemeka. Akataka kunambia siri lakini nikakataa" Mwanasheria mlevi alisema.
"Hee! Kwanini umekataa sasa. Hiko ndio kitu tulichotumwa na Chifu. Tumeishi miezi kadhaa Mbeya kuisaka hiyo siri. Kwanini sasa umeikataa?"
"Nimekataa kwa sababu ya Camera hizo. Ningesema tu nikubali kuambiwa basi tungewarahisishia kazi hawa jamaa. Hawa nao bila shaka wanaisaka hiyo siri. Sikutaka kuwasaidia kwa namna hiyo" Mwanasheria mlevi alisema.
"Sasa Elizabeth kapelelekwa kule. Je hawezi kuisema hiyo siri baada ya kupewa mateso?" Dokta Yusha aliuliza.
"Ni suara la kuangalia mbele kwenye ile runinga tutapata jibu" Mwanasheria mlevi alisema.
Wote macho yao yalielekea mbele. Kushuhudia Richard akiwa amekutana na Elizabeth Neville. Kuona je atasema?"
***
ITAENDELEA
PSEUDEPIGRAPHAS
SIMULIZI