Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #101
Dah umetuachia arosto mkuu dah
Arosto ipi mkuu story inaisha kesho [emoji91][emoji91]
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Dah umetuachia arosto mkuu dah
NotedSEHEMU YA 75
Daniel Mwaseba, Inspekta Jasmin, Martin Hisia, Richard, Dokta Yusha na Mwanasheria mlevi waliagana pale ikulu. Kila mmoja alirudi nyumbani kwake kwa ajili ya kujiandaa na safari ya kesho yake asubuhi. Daniel aliingia katika nyumba yake iliyopo huko Mikocheni saa sita usiku. Alipitiliza sebuleni na moja kwa moja kuelekea chumbani. Jicho lake lilipotua kitandani, alistuka sana! Katika kitanda chake alikutana na bahasha ambayo haikuwepo hapo siku aliyoondoka. Aliichukua ile bahasha. Akaisoma. Juu ya bahasha iliandikwa Daniel Mwaseba.
"Nini hii, kaleta nani? Kaingiaje humu?" Daniel Mwaseba alisema huku akiifungua ile bahasha. Alitoa karatasi kumi nyeupe ndani ya ile bahasha, juu ya karatasi ya kwanza kuliandikwa maneno kwa herufi kubwa NYARAKA ZA 001.
Daniel alistuka sana "Zimefikaje hapa hizi bahasha?" Nani kazileta?" Daniel Mwaseba alijiuliza maswali ambayo hakuwa na majibu nayo. Daniel alinyanyuka na kwenda chumba chake cha mitambo. Huko ndipo aliona kila kitu.
.....Video ilimuuonesha sebuleni mwanamke mmoja akiingia. Moja kwa moja bila wasiwasi mwanamke yule alienda chumbani kwake na kuiweka ile bahasha kitandani. Kisha alikaa kitandani na kuanza kuongea.
" Najua hapa namulikwa na Camera zako Daniel, na ndio maana naongea haya maana najua utakuwa unaniangalia muda huu. Kwa majina naitwa Elizabeth Neville. Mwanamke ukiyemsaka usiku na mchana tangu siku ile nilivyotoroka kwako baada ya kujua umenigundua kwamba mimi ni spy kutoka Cuba. Ulikuwa sahihi Daniel, sikuja kwako kwa bahati mbaya, nilikuja kwako kukumaliza kama nilivyotumwa na wakuu wangu na nilikuwa na uwezo wa kukuuwa lakini sikufanya hivyo. Sikukuuwa sio kwamba nakuogopa, la hasha! Sikukuuwa kwa sababu moja kuu Daniel, MAPENZI. Nilitokea kukupenda sana Daniel, na sikuona kama nitaweza kujisamehe endapo nitakuuwa mwanaume kama wewe ninayekupenda kuliko kitu chochote kile duniani. Ndoto yangu ni kuja kuishi mimi na wewe kama mke na mume, sikutaka kumuuwa mume wangu mtarajiwa.
Daniel, kuonesha upendo wangu wa dhati kwako nimeamua kukuachia nyaraka za siri za 001. Nyaraka muhimu sana kwa nchi yenu. Ila nakuomba ukamshauri rais akaziweke mahala sahihi nyaraka hizo kwani ni nyaraka muhimu sana ambazo serikali yangu ya Cuba wanazihitaji kwa udi na uvumba. Mimi ninarudi kwetu Daniel, nina asilimia ndogo sana za kusamehewa nitakavyorudi bila nyaraka za 001, lakini najua cha kusema na naamini watanielewa na kunipa nafasi nyingine, hapo ndipo nitakuja na kuishi na wewe kama mke na mume. Na kuachana sana mambo haya. Nakupenda sana Daniel, amini nakupenda kiasi cha kuisaliti nchi yangu. Na hiyo ni zawadi pekee niliyokuachia. Ngoja nikuibie siri Daniel, ni mimi ndiye niliyevujisha mpango wa wizi wa dhahabu Geita kabla hukatekelezwa, lengo ni kuinusuru nchi ya mwanaume ninayempenda. Ni mimi ndiye niliyemwambia msichana Bertha Fidelis kuhusu wizi ule.
Ahsante kwa kunisikiliza Daniel Mwaseba, mme wangu mtarajiwa"
Daniel Mwaseba alihemwa. Hakuamini kabisa macho yake. Elizabeth Neville alimwacha katika mshangao mkuu.
Harakaharaka alimpigia simu Rais Dr Joseph na kumueleza kila kitu. Dakika ishirini baadae Daniel Mwaseba alikuwa ikulu na kumuonesha rais Dr Joseph ile video na kumkabidhi nyaraka za 001. Rais Dr Joseph hakuamini macho yake. Alimshukuru sana Daniel.
Kwa furaha alisema" Kesho mtazikuta zawadi zenu katika akaunti zenu. Nimeshaongea na hazina" Rais Joseph alisema huku akizirudisha zile nyaraka za siri mahali pake.
Mwisho
Imeletwa kwenu kwa udhamini wa Pseudepigraphas
Ahsanteni sana kwa kuwa wote mwanzo hadi mwisho.
SEHEMU YA 75
Daniel Mwaseba, Inspekta Jasmin, Martin Hisia, Richard, Dokta Yusha na Mwanasheria mlevi waliagana pale ikulu. Kila mmoja alirudi nyumbani kwake kwa ajili ya kujiandaa na safari ya kesho yake asubuhi. Daniel aliingia katika nyumba yake iliyopo huko Mikocheni saa sita usiku. Alipitiliza sebuleni na moja kwa moja kuelekea chumbani. Jicho lake lilipotua kitandani, alistuka sana! Katika kitanda chake alikutana na bahasha ambayo haikuwepo hapo siku aliyoondoka. Aliichukua ile bahasha. Akaisoma. Juu ya bahasha iliandikwa Daniel Mwaseba.
"Nini hii, kaleta nani? Kaingiaje humu?" Daniel Mwaseba alisema huku akiifungua ile bahasha. Alitoa karatasi kumi nyeupe ndani ya ile bahasha, juu ya karatasi ya kwanza kuliandikwa maneno kwa herufi kubwa NYARAKA ZA 001.
Daniel alistuka sana "Zimefikaje hapa hizi bahasha?" Nani kazileta?" Daniel Mwaseba alijiuliza maswali ambayo hakuwa na majibu nayo. Daniel alinyanyuka na kwenda chumba chake cha mitambo. Huko ndipo aliona kila kitu.
.....Video ilimuuonesha sebuleni mwanamke mmoja akiingia. Moja kwa moja bila wasiwasi mwanamke yule alienda chumbani kwake na kuiweka ile bahasha kitandani. Kisha alikaa kitandani na kuanza kuongea.
" Najua hapa namulikwa na Camera zako Daniel, na ndio maana naongea haya maana najua utakuwa unaniangalia muda huu. Kwa majina naitwa Elizabeth Neville. Mwanamke ukiyemsaka usiku na mchana tangu siku ile nilivyotoroka kwako baada ya kujua umenigundua kwamba mimi ni spy kutoka Cuba. Ulikuwa sahihi Daniel, sikuja kwako kwa bahati mbaya, nilikuja kwako kukumaliza kama nilivyotumwa na wakuu wangu na nilikuwa na uwezo wa kukuuwa lakini sikufanya hivyo. Sikukuuwa sio kwamba nakuogopa, la hasha! Sikukuuwa kwa sababu moja kuu Daniel, MAPENZI. Nilitokea kukupenda sana Daniel, na sikuona kama nitaweza kujisamehe endapo nitakuuwa mwanaume kama wewe ninayekupenda kuliko kitu chochote kile duniani. Ndoto yangu ni kuja kuishi mimi na wewe kama mke na mume, sikutaka kumuuwa mume wangu mtarajiwa.
Daniel, kuonesha upendo wangu wa dhati kwako nimeamua kukuachia nyaraka za siri za 001. Nyaraka muhimu sana kwa nchi yenu. Ila nakuomba ukamshauri rais akaziweke mahala sahihi nyaraka hizo kwani ni nyaraka muhimu sana ambazo serikali yangu ya Cuba wanazihitaji kwa udi na uvumba. Mimi ninarudi kwetu Daniel, nina asilimia ndogo sana za kusamehewa nitakavyorudi bila nyaraka za 001, lakini najua cha kusema na naamini watanielewa na kunipa nafasi nyingine, hapo ndipo nitakuja na kuishi na wewe kama mke na mume. Na kuachana sana mambo haya. Nakupenda sana Daniel, amini nakupenda kiasi cha kuisaliti nchi yangu. Na hiyo ni zawadi pekee niliyokuachia. Ngoja nikuibie siri Daniel, ni mimi ndiye niliyevujisha mpango wa wizi wa dhahabu Geita kabla hukatekelezwa, lengo ni kuinusuru nchi ya mwanaume ninayempenda. Ni mimi ndiye niliyemwambia msichana Bertha Fidelis kuhusu wizi ule.
Ahsante kwa kunisikiliza Daniel Mwaseba, mme wangu mtarajiwa"
Daniel Mwaseba alihemwa. Hakuamini kabisa macho yake. Elizabeth Neville alimwacha katika mshangao mkuu.
Harakaharaka alimpigia simu Rais Dr Joseph na kumueleza kila kitu. Dakika ishirini baadae Daniel Mwaseba alikuwa ikulu na kumuonesha rais Dr Joseph ile video na kumkabidhi nyaraka za 001. Rais Dr Joseph hakuamini macho yake. Alimshukuru sana Daniel.
Kwa furaha alisema" Kesho mtazikuta zawadi zenu katika akaunti zenu. Nimeshaongea na hazina" Rais Joseph alisema huku akizirudisha zile nyaraka za siri mahali pake.
Mwisho
Imeletwa kwenu kwa udhamini wa Pseudepigraphas
Ahsanteni sana kwa kuwa wote mwanzo hadi mwisho.