FOR YOU
Story by Elton Tonny
Familia, Urafiki, Mapenzi, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Uhalifu, Mauaji, Visasi, Vita, Mambo yasiyotazamiwa
R-rated 18+
Enjoy!
★★★★★★★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA AROBAINI NA NNE
★★★★★★★★★★★★★★★★★★
"Boss, we should arm ourselves (tunapaswa kubeba silaha)," Mensah akamwambia Kendrick.
"Hapana, don't panic. Tunaweza ku-solve hili kiurahisi," Torres akasema.
"Kiurahisi jinsi gani? Nora kawaleta hao wajing...."
"Hajawaleta Nora, LaKeisha. Hao sio watu wa serikali," akasema Kendrick.
"Unajuaje hilo?" akauliza Kevin.
"Kama siyo wa serikali ni wa nani?" akauliza LaKeisha.
Kendrick akasema, "Watakuwa watu wa Salim, I don't know. Lakini tunapaswa kuhakikisha hii inakuwa mara ya mwisho wanafika hapa. Lexi, mtoe Zelda umlete huku pamoja na Azra; Victor, Kevin, tengenezeni vizuri nyumba yake, Mensah, mimi nawe tulete kila kitu wasichotakiwa kuona huku, halafu Torres na Lakeisha...."
"Tunajua la kufanya," Torres akamalizia.
Lexi akaanza kuondoka haraka.
"Kwa hiyo tunajificha tu? Tungewapa hawa wajinga wanachostahili you know," akasema Kevin.
"Mna pungufu ya dakika tatu kufanya nilichowaagiza. Harakisheni," Kendrick akaamuru.
Wengine wakaanza kuondoka pia sehemu hiyo ya chini na kuelekea juu. Lexi alikuwa amekwenda kwenye chumba cha Azra, naye akamweleza hali iliyokuwepo na kumwambia akae humo humo mpaka akimpitisha Zelda. Akaenda na kwenye chumba chake na kuwakuta Isiminzile na Nora wakiwa wamekaa, naye akamwambia Nora kuwa kuna watu walikuwa wamefika hapo katika njia ya msako. Nora akashangaa, lakini pia kwa kufikiria labda ni yeye ndiyo alifuatiliwa akaanza kujilaumu, lakini Lexi akamtuliza na kumwambia haikuwa makosa yake. Lexi akawaambia walichopaswa kufanya ni kukaa hapo hapo ndani mpaka aje kuwaita, nao wakakubali na yeye akaondoka.
Alitoka mpaka nje na kwenda kumfungulia Zelda, ambaye tayari alikuwa amelala, naye akamwamsha na kuanza kumwongoza kuelekea ndani ya nyumba. Kufikia wakati huu, wengine wote walikuwa kwenye vyumba vyao isipokuwa Kendrick na LaKeisha, kwa sababu ni wao tu na Lexi ndiyo waliokuwa wamemzoea Zelda. Hivyo Lexi akampeleka Zelda mpaka kule chini, na ingawa mwanzoni mnyama wake huyu alisumbua, lakini mwishowe akaingia huko na kumfata Lexi mpaka kwenye kile chumba kidogo cha kupasha miili joto (steam room). Lakini alimwingiza humo bila kuwasha joto la ndani, kisha akamwacha tu Zelda na kuufunga mlango. Hii ilikuwa ni kwa sababu na wengine wangehitaji kuja chini huku kujificha, kwa hiyo Zelda angetakiwa kufungiwa ndani humo ili asidhuru mtu yeyote.
Baada ya kutoka huko chini, Lexi akawafata wakina Nora, Azra, na Isiminzile, huku Mensah, Victor, Kevin, na Kendrick wakijiunga nao pia kurudi huko chini wakiwa na vifaa mbalimbali. Hii ilikuwa ndiyo mara ya kwanza kwa Isiminzile na Nora kuingia chini huko, na kiukweli walistaajabishwa kiasi na ufundi wa kundi hili katika nyingi ya njia zao. Kwa hali ya kawaida tu isingekuwa rahisi kufikiri kwamba kungekuwa na chumba kipana sana chini ya ardhi, tena kilichofichika kitaalamu mno, hivyo iliwaacha wakiwa wanajiuliza mambo yote haya yalibuniwa na nani, na lini. Waliweza kuona vifaa vingi huko kwa ajili ya dharura, mitambo mingi ya kiteknolojia, na hata sehemu zenye vitanda vichache vya kulalia. Nora alikuwa na maswali mengi sana ya kumuuliza Lexi, lakini kwanza wangehitaji kutulia ili shida iliyokuwa ikiendelea ipite.
Lexi akawaelezea jinsi mpango wao ulivyokuwa. Wengine wote wangepaswa kubaki hapo chini, isipokuwa Torres na LaKeisha. Ni wawili hao tu ndiyo angalau mpaka sasa hawakuwa wamejulikana, ingawa hakukuwa na uhakika wa asilimia mia, hivyo wangetoka na kufanya maigizo ya hali ya juu ili kuwachengua watu wale waliofika hapo. Wakati Lexi alipokuwa anawaelezea Nora na Isiminzile haya, tayari LaKeisha na Torres walikuwa wameshapanda juu. Kwa hiyo kwa huko chini wangeendelea kukaa kwa utulivu mpaka wawili hao wakirejea.
★
Wanaume wale waliokuwa nje, baada ya kuona dakika tano zimepita bila kujibiwa, wakatoa onyo la mwisho kwa kusema kwamba sasa wangelazimika kulifyatua geti kwa risasi na kuingia ndani kwa lazima. Lakini papo hapo geti hilo likaanza kufunguka lenyewe mbele yao, nao wakajiweka tayari na kuanza kuingia ndani hapo. Walishangaa kidogo kutoona mlinzi yeyote sehemu hiyo, na kiongozi wao akawapa ishara kwamba wangetakiwa kuwa makini, hivyo wote wakawa wanaelekea mbele huku wakielekeza bunduki zao kwa utayari.
Walipofika usawa wa geti la pili, nalo pia likafunguka, kisha wakaanza kwenda kwa pamoja. Hapo wakaweza kuiona nyumba hiyo jinsi ilivyokuwa kubwa, na mwanaume fulani akishuka kutoka kwenye ngazi kuwaelekea, yaani Torres. Wakati huu alikuwa amevalia nguo kwa ajili ya kulalia (pajamas), akionekana kama vile ametoka kupumzika au ndiyo alikuwa anajiandaa kupumzika. Wanaume wale kwa ujumla walikuwa 14, nao wakamkaribia zaidi na kusimama mbele yake.
"Habari zenu?" akauliza Torres.
"Ni nzuri. Wewe ndiyo mmiliki wa hii nyumba?" akauliza kiongozi wao.
"Ni mimi. Na nyie ni nani?" Torres akauliza.
"Tulikuwa tumeshajitambulisha kule nje. Kwa nini hakuna mlinzi getini?" mwanaume huyo akauliza.
"Walinzi wamepewa likizo fupi," Torres akasema.
"Likizo? Nyumba na sehemu kama hii inaondolewa ulinzi kwa ajili ya likizo?"
"Okay, sijui shida yenu ni nini lakini hilo ni suala la kibinafsi. Kuna tatizo lolote?" Torres akauliza.
"Hakutakuwa na tatizo lolote endapo utatuacha tufanye kazi yetu. Tunawatafuta wahalifu hatari sana, wanaojiita Mess Makers. Nadhani umeshawasikia," mwanaume huyo akamwambia.
"Ndiyo. Na sasa mnafikiri wako nyumbani kwangu... kwa nini?" Torres akauliza.
"Hili siyo suala la kibinafsi. Hii ni operesheni inayofanyika nchi nzima, kwa hiyo tunaomba ushirikiano wako tu..."
"Okay sawa. Naelewa mnahitaji kufanya kazi yenu. Mnaweza kutafuta sehemu yote, lakini ninajua mnatakiwa kuwa na mipaka. Sitazamii mharibu vitu vyangu vya gharama kutafuta kitu ambacho hamtapata," Torres akasema.
Mwanaume huyo akacheka kidogo na kuwapa wenzake ishara kuwa waingie ndani kufanya msako. Torres hata akamkaribisha kiongozi wao huyo waongozane ndani ili amwelekeze vizuri mambo ya huko, akijiweka katika hali fulani yenye kuonyesha urafiki. Wanaume wale wengine walitafuta nyumba nzima na kukosa mtu mwingine, isipokuwa LaKeisha, ambaye alikuwa chumbani akiwa amejilaza kitandani. Ikabidi naye atoke baada ya "kuvamiwa" na watu "asiowajua," naye akaelekea kule chini alipowakuta Torres na yule kiongozi wa kundi hilo. Alikuwa amevalia nguo ya kike ya kulalia pia, naye akasogea mpaka usawa wa Torres.
"Honey, what's going on? (mpenzi, nini kinaendelea?)" LaKeisha akamuuliza Torres.
"They're doing a search... Mess Makers thing (wanafanya upekuzi.. ishu ya Mess Makers)," Torres akajibu.
"Aaa... hi," LaKeisha akasema na kumsalimia hivyo mwanaume huyo.
Mwanaume huyo alikuwa anamtazama LaKeisha kwa njia iliyoonyesha upendezi, lakini akawa anajifanya kukaza.
"Unaitwa nani?" LaKeisha akamuuliza.
"Jina langu siyo muhimu hapa. Tukikosa tunachotafuta, hamtatuona tena," mwanaume huyo akajibu.
"Okay. Kwa hiyo ni nini kilichowafanya mkafikiri tunaficha wezi hapa?" LaKeisha akauliza.
"Kila mlango wa nyumba zote nchini unafanyiwa search. Siyo nyie tu..."
"Mmeshajaribu mpaka kwa Raisi?" LaKeisha akauliza kikejeli.
Torres akamkaza mkono kumzuia.
"Unasemaje?" mwanaume huyo akauliza.
"Aa... anatania tu. Kiukweli hatukufikiria mngekuja tu ghafla namna hii, kuna mambo tulikuwa tuna... si unajua? Imemkera kidogo," Torres akasema kiutani.
Mwanaume huyo akawa anamwangalia LaKeisha kwa umakini, huku LaKeisha akimpa tabasamu kwa ujasiri. Wenzake wote wakawa wamerudi, na kila mmoja wao akasema wametafuta vyumba vyote lakini hawakupata chochote chenye kutia mashaka.
"Kama tu nilivyowaambia, hapa tupo sisi tu. God, natumaini hawa Mess Makers wakamatwe haraka maana wanaumiza vichwa sana," Torres akasema.
"Nyumba yako ni kubwa sana. Ina vyumba vingi mno kuishi watu wawili tu. Una uhakika hakuna wapangaji hapa?" mwanaume huyo akauliza.
"Mimi ni mjasiriamali mkubwa ndugu yangu. Nina watu wengi, nina mikutano mingi, nina party nyingi. Napokuwa sijisikii kutoka hata kwa mwaka mzima, kila kitu kinafanyikia hapa. Kwa hiyo kuwa na vyumba vingi ni sehemu ndogo tu ya kutumia kile nilichonacho. Na hii siyo nyumba yangu pekee. Kwa hiyo... ikiwa ni hayo tu, tunawashukuru sana, na tunatumaini mtai-note sehemu hii kutokuwa nyumba ya wezi. Asanteni sana," Torres akaongea kwa uhakika.
Mwanaume huyo akamtazama kwa umakini na kumwangalia LaKeisha kwa umakini pia, kisha akatoa ishara kwa wengine kuwa wangeweza kuondoka hatimaye.
"Poleni kwa usumbufu. Mnaweza kuendelea na mliyokuwa mnayafanya," mwanaume huyo akasema.
Torres akatabasamu na kusema, "Kwa tahadhima yote, bila shaka."
LaKeisha akacheka kidogo kwa kiburi.
Mwanaume huyo pamoja na kundi lake lililojitambulisha kuwa la "serikali" wakaondoka hapo hatimaye. Baada ya hayo kuhitimika, LaKeisha akafurahi sana na kumrukia Torres, akimpa busu ya ushindi. Wakarejea kwa wenzao kule chini na kuwaambia mambo yalikuwa safi huku juu, nao wakatoka wakiwa wanauliza ni yapi yaliyoendelea. Torres akawaelezea kwamba bila shaka wanaume hao hawakuwa watu wa "serikali" moja kwa moja, bali inaonekana walikuwa ni watu kutoka kundi fulani maalum kati ya makundi ya kijeshi yaliyotumiwa kwa umakini sana.
Azra akawa ametambua kwamba hao bila shaka walikuwa ni watu wa Luteni Jenerali Weisiko, kwa sababu alifahamu njia za mwanaume yule kutokana na kutumiwa kwake kwenye mishe kadhaa, lakini hakuwaambia wengine kuhusiana na hilo. Kendrick akawaambia vijana wake kwamba wangetakiwa kuwa makini zaidi, kwa sababu kadiri siku zinavyozidi kwenda ndiyo watu kutoka nje wangeendelea kuwakaribia, kwa hiyo akawaasa waende kupumzika ili kuja kupanga mambo yao vizuri kwa kesho.
Nora mpaka kufikia sasa alikuwa anajiuliza mwanamke yule mdogo alikuwa nani, yaani Azra, kwa sababu kati ya wote waliotambulishwa kwake ni yeye tu ndiyo hakuwa ametambulishwa bado, na aliona ufanani baina yake na Lexi, lakini akakaa kimya tu ili aje kumuuliza Lexi vizuri. Wengine walipotawanyika kurudi vyumbani kwao, Lexi akamwongoza Nora pia mpaka kwenye chumba chao na kumwambia amsubiri na asitoke ili aweze kumrudisha Zelda kwenye nyumba yake ndogo. Tena na hapa Nora akawa anajiuliza Zelda ndiyo nani, na baada ya Lexi kuondoka, ikabidi asimame karibu na mlango ili aweze kumwona huyo Zelda wakati Lexi angempitisha. Si ndiyo akapata sasa kumwona akiwa na mnyama aliyefanana na simba huku akimwongoza kuelekea nje!
Nora aliendelea kuchoshwa akili na hawa watu. Yaani alianza kujiona ni kama yuko kwenye sinema fulani isiyoisha vituko kila alipodhani amejua mambo yote kuihusu. Ikabidi tu akae kitandani na kumsubiri Lexi mpaka aliporejea, na baada ya yeye kufika akaketi usawa wa kitanda pia huku akimtazama kwa umakini. Nora akaangalia chini na kutikisa kichwa kwa njia iliyoonyesha ameachwa njia panda, naye Lexi akatabasamu kidogo.
"Yaani Lexi kiukweli... hizi wiki chache zilizopita zimebadili kabisa aina ya mtu niliyedhani ulikuwa. Everything about you is just... a mystery (kila kitu kuhusu wewe ni fumbo)," akasema Nora.
"Pole Nora. Lakini usijali, I'll get you up to speed," Lexi akasema.
"Hicho kilikuwa ni nini? Na wewe ni Tarzan sasa?" Nora akauliza.
"Ahahah... huyo ni Zelda. Ninamfuga. Tokea Ghana. Ni kipenzi changu," Lexi akasema.
"Alikuwa wapi wakati tuko huko chini?"
"Alikuwepo huko huko... ila nilikuwa nimemfungia ili asije kuwaumiza..."
"Yaani unataka kusema kwamba tulikuwa kwenye banda moja na simba?"
"Ahahah... ndiyo..."
"Ahah... hivi hata ulimwingizaje humu nchini?"
"Njia ni nyingi. Bandarini, kwenye kontena..."
"Okay, inatosha. Sitauliza njia zenu tena," Nora akasema.
Lexi akacheka kidogo.
"Unaweza kuniambia yule msichana ni nani?" Nora akauliza.
"Anaitwa Azra. Ni mdogo wangu," Lexi akajibu.
"Yeah, nimeona mnafanana, na tayari nilikuwa nimekisia hilo. Lakini... nimesoma taarifa kuhusu familia yako, na inasemekana wote walikufa... kutia ndani wewe... miaka nane iliyopita. Mambo haya yote yaliwezekanaje?" Nora akauliza.
Lexi akashusha pumzi ya utulivu, naye Nora akawa anamwangalia kwa umakini.
"Kwanza kabisa Nora... nataka nikushukuru sana kwa kunisaidia usiku ule. Isingekuwa ya wewe labda ningekuwa nimekufa sasa," Lexi akamwambia.
"Ahah... unajua sikufikiri kiukweli kama ungeweza kuwatoroka wale wanaume, ila nikaweka tu matumaini..."
"Ndiyo Nora, naelewa. Na jambo hilo hilo ndiyo lilinipa nguvu. Nilikuwa nimeshavunjika moyo na kuamua liwalo na liwe, lakini nilivyotambua kwamba unaniamini... na mimi nikajitahidi kufanya yote ili nisikuangushe..."
"Kwa hiyo... ulipigana vile ili utoke... kwa ajili yangu?"
"Yeah... for you," Lexi akasema kwa hisia.
Nora akamwangalia kwa hisia pia.
"Nilijihakikishia kuwa kama ningetoka mikononi mwao, ningetumia kila njia ili nikufikie na niweze kukueleza kila kitu, kwa kuwa sikutaka kukuacha gizani. Nora... baba yako ni mtu anayefanya mambo mengi mabaya sana..."
"Mambo gani?"
"Unakumbuka kisa cha Demba Group kilichotokea hapa nchini miaka kadhaa nyuma?"
"Ndiyo..."
"Ni yeye pamoja na watu wengine ndiyo waliowaongoza baadhi ya wanajeshi kufanya matendo yale... wakijiita Demba Group..."
"Nini?"
"Ndiyo..."
"I don't understand..."
"Wakati huo... baba yangu na uncle Kendrick walikuwa wanajeshi pia... Uncle Kendrick akiwa kama Captain alikuja kubaini mpango wa baba yako na Lieutenant Weisiko wa kutaka kumwondoa Raisi madarakani ili wamweke makamu wake ndo awe Raisi..."
"Mdeme?"
"Yeah. Njia waliyotumia ilikuwa ni hiyo ya Demba Group, na walifanya mambo yao kwa umakini sana ili wasijulikane, lakini uncle Kendrick akajua. Walikuwa wameua watu wengi sana ili tu kupata mambo waliyotaka. Yeye ndiyo chanzo cha wazazi wangu na ndugu zangu kuuawa. Usiku ule maisha yangu yalibadilika sana. Nilimwangalia mama yangu, na baba yangu na dada zangu wawili walipouliwa na Weisiko... na mimi nisingekuwa hai ikiwa uncle Kendrick asingeniokoa," Lexi akasema kwa hisia sana.
Nora alimwonea huruma, mpaka machozi yakawa yanamlenga.
"Najua kila kitu nachokwambia huenda kikaonekana kama kimebuniwa tu... lakini usijali, nitakuthibitishia kila kitu," Lexi akasema.
"Nafahamu baba yangu siyo mtu mzuri sana kama anavyojionyesha kwa wengine... lakini sikuwahi kufikiria yeye ni mnyama kiasi hicho. Ni kwa nini alifanya hayo yote? I can't believe this," Nora akasema kwa huzuni sana.
"Yeye pamoja na wote walioshirikiana naye walinibadili sana... nilitaka sana kuwaua wote siku ambayo ningekutana nao. Lakini uncle Kendrick... yeye ndiye aliyenifundisha jinsi ya kuzuia hasira yangu... akanifundisha vitu vingi sana vilivyonifanya nitambue hasa njia nzuri ya kuwaangusha wabaya wetu wote. Kuwaua kusingetosha... nilitaka kuwafanya wajulikane kwa mabaya yao yote waliyofanya, na maumivu yote waliyosababishia mamia ya watu kwenye hii nchi wapitie na wao wangeyapitia," Lexi akasema huku chozi likimtoka.
"Oh Lexi..." Nora akamshika shavu na kumfuta chozi.
"Mhm... najua hii ni ajabu kwa kuwa nayemwongelea ni baba yako..."
"Hapana. Nakuelewa vizuri. Wakati mwingine kufuata njia ya haki hakuleti matokeo mazuri sana hasa kama unadili na mtu anayetumia ukatili kama njia yake kuu, hivyo ninafurahi kujua kwamba ulichagua kufichua mabaya yao badala ya kufanya umwagaji wa damu," Nora akasema.
"Oh Nora... mimi sitakuwa mnafiki kwako. Nitaua yeyote yule anayejaribu kuingilia kati kwenye njia yangu ya kufanya mambo. Yote niliyopitia kipindi cha nyuma... sitaki tena yeyote ayapitie. Tulijaribu kuwakomesha kwa namna yetu, lakini kiukweli...."
"Its okay. Naelewa Lexi. Naelewa," Nora akamkatisha huku akimshika usoni.
Lexi akatazama tu pembeni akiwa na huzuni.
"Nitaelewa mambo mengi vizuri ukishanipa uthibitisho zaidi. Lakini ninajua unayosema ni kweli. Nakuamini," akasema Nora.
Lexi akamtazama na kutabasamu.
"Aam... vipi kuhusu... ulichoniambia siku ile?" Nora akauliza.
"Jambo gani?"
"Ulisema kwamba wewe... unatamani kuoa. Ijapokuwa mwanzoni nilidhani labda uliongea bila kufikiri lakini baadae niliendelea sana kutafakari hayo maneno. Ulikuwa unamaanisha nini?"
"Ahah... kwani mwanamke hawezi kuoa?"
"Hapana, nilihisi ulikuwa na maana tofauti Lexi..." Nora akasema.
"Kuna jambo lilitokea... mimi na dada yangu tuli-switch miili... mpaka leo sijajua ni nini kilisababisha hilo. Mwili huu ni wa pacha wangu, na yeye ndiye aliyekuwa ndani ya mwili wangu wakati Weisiko alipomuua," Lexi akaeleza.
"What? Hiyo inawezekanaje?" Nora akashangaa.
"Ilitushangaza sisi sote, lakini hatukuweza kujua kilichotokea. Kwa hiyo miaka mingi baada ya Sandra kufa ilibidi tu nizoee kuwa ndani ya mwili wake...," Lexi akasema.
Nora akamwangalia kwa kujali.
"Maisha yangu ni kama fumbo kubwa sana, hilo ni kweli. Na najua mambo yote nayokwambia yanakuchanganya sana," Lexi akasema.
"Ndiyo ni kweli. Lakini sijui tu ni kwa nini kila kitu unachosema nakuwa... nakiamini," Nora akamwambia.
"Asante Nora. Nilitokea kuwachukia sana mapolisi na wanajeshi wengi hasa kwa sababu ya matendo ya watu kama Weisiko... lakini wewe...." Lexi akaishia hapo.
Nora akatabasamu kwa mbali.
"Kwa hiyo... ukiwa ndani ya mwili wa dada yako... bado unapata... hisia kama mwanaume?" Nora akauliza.
"Ni tofauti. Bado nahisi kuwa mimi, lakini mwili huu ni wa mwanamke kwa hiyo kuna vitu siwezi kubadili. Naishi kulingana na hali," Lexi akasema.
"Okay. Kwa uzuri wako Lexi, bila shaka umeshatongozwa karibia mara buku," Nora akasema.
"Ahahahah... ndiyo, wanaume wengi sana wamejaribu kunitokea. Wakati tumefika Tanzania, Kevin alijaribu kunitongoza eti..."
"Ahahahah... alikuwa anajibebisha?"
"Ahahahah... yeah."
"Ikawaje?"
"Nikampiga stop kali kama yule Luka wa siku ile Sea House," Lexi akasema, naye Nora akacheka.
Lexi akatulia kidogo, kisha akaanza kusema, "Ona... samahani kwa kukuambia mambo mengi yenye kuchanganya kwa..."
"Hapana, usiombe samahani," Nora akamwambia kwa sauti ya chini.
Nora akaanza kusogea karibu zaidi na Lexi na kukishika kiganja chake. Akawa ameukaribia zaidi uso wa Lexi sasa, naye Lexi akawa ameelewa jambo hili lilikotaka kuelekea.
"Nora..." Lexi akaita kwa sauti ya chini.
"Yes..." Nora akaitika na kutulia.
"Kuwa na... mimi kama mwanamke... siyo ajabu kwako?"
"Hapana, kwa nini iwe ajabu?"
"Usiku ule... ulisema ulihisi labda nimekuroga tu, kwamba haungeweza
kamwe kutoka nami katika hali ya kawai...."
"No, no, Lexi... nisamehe. Samahani sana kwa kusema maneno yale. Nilikuwa na hasira, niliumia, nilifikiri labda umeniumiza kwa makusudi maovu... sikumaanisha nilichosema," Nora akaongea kwa kujali.
"Nora... mimi ni mwanaume kwa ndani, lakini nje siko hivyo. Samahani lakini... siwezi kukupa kile unachohitaji kwa njia nayotamani kufanya hivyo," Lexi akasema kwa hisia.
"Acha kuomba samahani Lexi. Kiukweli... sijui ni kwa nini lakini wanaume wengi ambao nimekuwa nao hawajawahi kunifanya nihisi vile navyotaka kuhisi... ila kwako... ilikuwa tofauti kabla hata sijajua ndani ulikuwa mwanaume. Ni ngumu kuelezea lakini...." akaishia hapo.
"Samahani Nora..."
"Kwa nini unaomba samahani?"
"Ni kwamba tu... sina uhakika sana... yaani... samahani...."
"Agh, Lexi ukisema samahani kwa mara nyingine nitakupiga ngumi!" Nora akamwambia.
Lexi akaangalia pembeni tu.
Nora alikuwa amekwishamwelewa, na alitaka sana kumwonyesha kwamba kile alichowaza hakikuwa na shida yoyote kubwa.
"Lexi... niangalie..." Nora akasema.
Lexi akageuka na kumwangalia machoni. Nora akamshika kidevuni na kutelezesha mkono wake mpaka shavuni.
"Usijali, ninakuelewa. Ninajua yote uliyopaswa kupitia toka ulipobadilishwa mwili na dada yako hayakuwa rahisi... ninaelewa. Lakini usijifungie namna hii. Huu ni mwili WAKO sasa. Usiwaze kuhusu kile ambacho huna.... fuata tu moyo wako.... kama mimi nilivyochagua kufanya," Nora akasema kwa hisia sana.
Lexi alimwangalia sana Nora kwa hisia za upendo.
Ni kweli kwa ndani yeye bado alikuwa "Xander," na kuishi kwenye mwili wa mwanamke ilikuwa ni mtihani mgumu sana kwake tokea hali hiyo ilipompata. Alifikiria kwamba hangeweza kumfurahisha mwanamke kwa njia aliyozoea kufanya zamani, hasa kwa kuwa mwanamke aliyempenda kama Valentina hakukubaliana na hali yake hiyo mpya, hivyo aliona ni kama hata kwa mwingine ingeweza kuwa namna hiyo. Lakini Nora alionyesha kwamba hakujali kuhusiana na hilo, kwa kuwa alimpenda YEYE, yaani utu wake, na siyo kwa kuangalia sura wala mwili tu.
Nora akawa anamtazama Lexi kwa njia iliyoonyesha kwamba alimhitaji sana. Ilimchukua ujasiri kiasi kuushika mkono wa Lexi na kuuingiza ndani ya uwazi mdogo wa T-shirt yake kwa chini, na pale tu kiganja cha Lexi kilipoigusa sehemu ya mbavu yake, Nora akasisimka sana. Lexi pia alipatwa na hisia ambazo kwa kipindi kirefu aliziona kuwa za ajabu kwa sababu ya kuwa kwenye mwili wa mwanamke, lakini kwa Nora ziligeuka na kuwa nzuri sana kwake. Nora akiwa anamwangalia Lexi kama anasubiri afanye jambo fulani, Lexi akaipeleka midomo yake polepole kwenye midomo ya Nora na kumpa busu laini.
Wawili hawa wakaendelea kupeana busu kwa midomo taratibu, kisha wakaifungua midomo yao na kuanza kuzungushiana ndimi kimahaba sana. Mawazo yote ya Lexi kuwa ndani ya mwili wa pacha wake, yaliyomfanya ajizuie kujitoa kwa mtu yeyote kwa muda mrefu sana, yalififia kwa Nora. Tokea mara ya kwanza na ya mwisho alipojitoa kwa LaKeisha hakuwa amejiweka katika hali hii tena, ila sasa akajiachia tena. Alikuwa amejenga upendezi wa hali ya juu sana kumwelekea Nora. Ni jambo ambalo wote walikuwa wamejenga kwa muda fulani sasa, lakini kutokana na hali zilizowazunguka haikuwa rahisi kuonyeshana hilo.
Sasa Lexi akiwa ameondoa vikwazo vyote akilini mwake na kuamua kumwonyesha mwanamke huyu upendo, alianza kufanya mambo kwa njia ambayo angeyafanya kama Xander. Yeye kuwa "Lexi" ilimaanisha alipaswa kukumbuka kwamba kuwa ndani ya mwili wa dada yake bado kunamuunganisha naye, ijapokuwa tayari alikuwa amekufa, na ndiyo maana aliamua kuupa mwili wake heshima hiyo ya kuwa kitu kimoja tokea Alexandra alipokufa. Lakini sasa Nora alikuwa amemsaidia kuona kwamba hakupaswa kuhisi hatia ikiwa angeamua kushiriki mwili huu na mtu mwingine aliyempenda, kwa sababu kihalisi mwili huu sasa ulikuwa ni WAKE.
(.........).
Kisha Lexi akajitoa mdomoni mwake na kumwangalia machoni kwa hisia sana. Nora pia akawa anamwangalia huku akitabasamu kwa mbali, naye Lexi akaweka paji lake la uso kwenye paji la Nora akiwa amefumba macho. Nywele chache za Nora zilikuwa mbele ya uso wake, hivyo Lexi akatumia kiganja chake kingine kuzirudisha nyuma ya sikio la Nora taratibu. Kisha akalishika shavu la Nora na kumwangalia tena machoni, huku Nora akiwa amelegeza sana shingo yake na kumwangalia Lexi kama vile anamsubiria atende chochote kile anachojisikia.
Lexi akasogeza mdomo wake karibu kabisa na wa Nora, na hapo aliweza kuhisi joto la pumzi zake.
"This is going to be crazy... (hii itakuwa hali yenye kuchizisha)" Lexi akanong'oneza karibu zaidi na mdomo wa Nora.
Nora akatabasamu kilegevu na kusema kwa kunong'oneza, "Yeah."
(.........).
(.........).
Ndimi zao ziliendelea kuchezeana kwa sekunde kadhaa na bila papara yoyote. Lexi alianza kufurahia hata zaidi ukaribu huo, hasa kwa sababu ilikuwa ni Nora. Alipandwa na hisia nyingi sana zilizomfanya atake kufanya mambo kwa haraka, lakini alijidhibiti kwa kuwa hakutaka aongozwe na hisia za mwili wake huu ambao bado alielewa ulikuwa ni wa mwanamke. Kilichokuwepo hapa ilikuwa ni jambo moja tu; kumfurahisha Nora, na hiyo ndiyo ingekuwa furaha tosha kwake.
Ingawa alikuwa ametoka kujimwagia muda mfupi nyuma, Nora alikuwa na ngozi yenye joto sana kutokana na kusisimka mno. Lexi akaona apeleke penzi hili hatua nyingine. Mkono mmoja wa Lexi ukafungua kifungo laini cha suruali ya Nora, kisha ule ulio ndani ukashuka moja kwa moja mpaka kwenye paja la Nora lililokuwa nene kiasi na kuanza kuishusha suruali yake. Alitambua haraka kwamba Nora alijua anapoelekea kwa kuwa mwanamke huyu alijinyanyua ili yote itolewe, kisha akayaachanisha mapaja yake yaliyokuwa yamegusana na kufanya mkono wa Lexi uweze kutomasa paja moja kuelekea katikati.
(........).
Kufikia wakati huu Lexi alikuwa na T-shirt nyepesi tu ya mikono mirefu na suruali. Kisha akaacha kulitomasa paja la Nora na kumbusu, akijitoa kabisa kwake na kusimama kutoka alipokuwa amekaa.
Nora akamwangalia akiwa ameshangazwa kiasi na jambo hili, naye Lexi akaelekea upande mwingine wa kitanda hiki na kuchukua kifaa kidogo kama rimoti kutoka kwenye droo ya pembeni, kisha akarudi usawa alioketi Nora. Akampa tabasamu la mbali, kisha akabonyeza rimoti hiyo, naye Nora akatazama upande uliokuwa na sebule na kuona kitu kama pazia nene sana likishuka kutokea juu katikati mpaka chini; lililofanya kama kuitenganisha sehemu ile ya sebule na upande wa huu wa kitanda, hivyo hawangeweza kuonwa kutokea upande wa pili. Akamwangalia Lexi kwa kupendezwa na jambo hilo, naye Lexi akaketi tena kitandani karibu yake.
"Naona hii nyumba imejengwa kiteknolojia sana," Nora akasema kwa sauti ya chini.
"Yeah, ni kazi ya Torres," Lexi akajibu.
"Mbona sasa ulikuwa unaniuliza ikiwa ulitakiwa kutoka nje ili nivae... kama tu ungeweza kufanya hivyo?" Nora akamuuliza.
Lexi akachezesha macho yake huku na huku, kisha akasema, "Zilikuwa swagger!"
Nora akacheka kidogo na kumshika shavuni. Kisha akasimama karibu kabisa na uso wa Lexi, akiwa anamwangalia kwa hisia, naye akaitoa T-shirt yake na nguo yake ya ndani, akiiacha ianguke chini. Sasa mwili wake wote ukawa wazi mbele ya Lexi. Lexi aliutazama kwa matamanio mengi, akipendezwa na rangi ya maji ya kunde ya mwanamke huyu. Ijapokuwa alikuwa askari lakini aliutunza mwili wake vyema, kwa sababu haukuwa umekakamaa kama wa mwanamke mkomao.
(.........).
Alipojitoa mdomoni mwake, Nora akapanda mpaka katikati ya kitanda polepole, akiwa anatambaa na kulielekeza kalio lake kwa Lexi ili ayaone maungo hayo vizuri. Lexi akawa anamwangalia huku anatabasamu, naye Nora akakaa akiwa ameibana miguu yake, akimwangalia kwa njia fulani ya kichokozi, naye Lexi akatabasamu na kumfata mpaka hapo. Nora akaishika sehemu ya chini ya T-shirt la Lexi na kuanza kulipandisha juu, naye Lexi akamruhsu kwa kuinyoosha mikono yake juu.
Kwa mara ya kwanza, Nora (.......). Lakini alipendezwa hata zaidi na michoro ya tattoo kuzunguka kifua cha Lexi mpaka tumboni na mikononi. Yaani ilikuwa ni kama amevaa nguo nyingine kwa jinsi tattoo hizo zilivyochorwa kwenye ngozi yake nyeupe kwa ubunifu sana, kuanzia sehemu ya juu ya kifua kufikia sehemu ya chini ya tumbo, na mikononi mwake mpaka kufikia mgongoni.
Akawa anazitazama huku anatembeza kiganja chake kuzifatisha jinsi zilivyochorwa.
"Nani alikuchora hizi?" Nora akauliza.
"LaKeisha," Lexi akajibu.
"Ooooh... kumbe anajua eeh?"
"Ndiyo..."
"Lazima awe special. Wewe kumwachia akuchore hivi I mean..."
"Ndiyo, tumetoka mbali. Lakini pia tuliwahi ku.... ila siyo sana," Lexi akasema.
"Ahaaa... kumbe ndiyo maana alikuwa ananifanyia vile..."
"Ahah... yeah," Lexi akasema.
Nora akamkazia macho kwenye upande wa kushoto wa kifua chake, na hapo akaona majina fulani yakiwa ndani ya mchoro wa tattoo ya kopa (love), na kwa kuyasoma akatambua ilikuwa ni watu wa familia yake Lexi; Casmir, Alice, Sandra, Azra, Salome. Akamtazama machoni na kukuta Lexi anamwangalia kwa hisia pia, hivyo akaifata midomo yake ili waweze kuendelea na penzi lao. Lakini wakati alipoizungushia mikono yake nyuma ya mgongo wa Lexi, akahisi kitu fulani kilichofanya ajitoe mdomoni mwake kwa mara nyingine. Akamtazama kimaswali sana.
"Nini hiki?" Nora akauliza.
Alikuwa ameishika sehemu ya nyuma ya bega la Lexi. Lexi hakumjibu, bali akaangaalia tu chini. Nora akazungukia nyuma na kuangalia sehemu hiyo ya begani, na hapo akaona plasta nene ya jeraha iliyotuna kiasi, na kwa haraka alitambua lilikuwa ni jeraha la risasi.
Lexi akamgeukia taratibu.
"Hiki bado kiko fresh... Lexi... nini kilitokea?" Nora akauliza kwa kujali.
"Wakati natoroka... mmoja wao alinifyatulia...." Lexi akaishia hivyo.
"Oh Lexi... kwa nini hukuni.... sikupaswa...."
"Heey... niko sawa, kimeshapoa. Hakiko fresh kama kinavyoonekana, kwa hiyo usijali," Lexi akamwambia.
Kisha akaifata midomo ya Nora na kuanza kumbusu tena.
Nora alipenda sana jinsi Lexi alivyoupa mwili wake umakini, kwa kuwa alimshika hapa na pale kwa kuminya-minya na kumtekenya kwenye sehemu za mwili wake. Akajitahidi kurudisha upendo namna hiyo lakini akawa makini kutomkandamiza sehemu ya begani. (.........).
(........). Lakini baada ya Lexi kujitoa tu mdomoni mwake ili afanye hivyo, Nora akaendelea kuifata midomo yake na kuipiga denda tena, akikataa kuivunja busu yao tamu. Lexi alifurahi kuona jinsi Nora alivyoonyesha kupenda sana jambo hili.
(........).
(........).
(........).
Hii ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Nora kufanya mapenzi na "mwanamke," ijapokuwa Lexi alikuwa mwanaume kwa ndani, hivyo Nora alikuwa akitaka kuona nini kingefuata ndani ya penzi hili jipya kwa kuwa hakujua sana atarajie nini kama alivyozoea kwa mwanaume. Kila kitu alichofanya Lexi kilimpagawisha sana Nora kadiri dakika ulivyozidi kwenda.
(........).
(........).
(........).
Mapigo ya moyo wake Lexi yalidunda kwa nguvu sana kwa kuwa hili ni jambo alilokuwa akitamani sana kufanya.
(........).
(........).
(........).
(........).
Lexi alipomtazama Nora kutokea katikati ya mapaja yake, akamwona jinsi alivyomtazama kwa hisia nyingi nzito za mahaba. Mkono wa Nora ulikuwa umekishika kichwa cha Lexi huku mwingine uking'ang'ania shuka kwa nguvu, naye akaliachia na kujiziba mdomo huku akikirudisha kichwa chake kitandani kwa nguvu. Lexi aliweza kusikia sauti zilizozibwa za kelele kutoka kwa Nora, lakini akautoa mkono huo mdomoni mwake, kwa sababu alijua hata kama akipiga kelele wengine hawangeweza kusikia, hivyo akawa anataka kumhakikishia hilo.
Alipenda sana sauti za Nora za miguno, ikiwa kama sauti za msichana mdogo anayedeka, naye akawa anamtekenya taratibu mwanamke huyo baada ya kuwa amemaliza kumwaga raha zake. Nora akabaki kupumua kiuchovu huku akiusugua mkono wa Lexi taratibu, bila kumwangalia, lakini akizungusha shingo yake huku na huku.
Lexi akaanza kumbusu taratibu kuanzia kitovuni kuelekea mpaka mdomoni. Wakaanza kudendeshana tena, kisha Lexi akajitoa mdomoni mwake na kumwangalia machoni. Nora akawa anamtazama huku akizichezea nywele za Lexi.
"Pelvis to pelvis," Lexi akamwambia.
Nora akacheka kidogo.
"Uko tayari kuendelea kuwa nami... hata ikiwa...."
"Lexi... stop," Nora akamkatisha.
Lexi akawa anamwangalia kwa hisia.
"Nakupenda," Nora akasema.
Lexi akaachia tabasamu kwa hisia nzuri sana aliyoipata.
Nora akatabasamu pia na kumvuta Lexi kwake, nao wakaanza kupiga busu tena.
Baada ya kuwa wamepeana mapenzi kwa mara hiyo ya kwanza, wawili hawa wakajilaza kitandani hapo pamoja na kuvuta shuka nene kuifunika miili yao; Nora akiwa amempa mgongo Lexi, na Lexi akiubana mwili wake nyuma ya mwanamke huyo huku wakiwa wameshikana.
Nora akawa wa kwanza kufumba macho yake, naye Lexi akawa kwa nyuma akizihisi pumzi za mwanamke huyo jinsi zilivyoonyesha kutulia kwake na kuridhika. Yeye pia Lexi alihisi uchovu kiasi ingawa hakuwa ametendeshwa kama yeye alivyomtendesha Nora, hivyo naye akafumba macho na kuanza kuutafuta usingizi, akihisi amani moyoni kuwa pamoja na mwanamke huyu aliyemkubali bila kujali hali aliyokuwa nayo.
★★★★★★★★★★★★★
ITAENDELEA
★★★★★★★★★★★★★
WHATSAPP +255 787 604 893