Jack Daniel
JF-Expert Member
- Sep 23, 2021
- 2,912
- 12,904
- Thread starter
-
- #101
SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA
Usiku wa siku hiyo sikulala kabisa Kila nikiwaza namna Jastini alivyo nikawa napatwa na hofu.
Lakini Kuna hali fulani ya kiume ikawa inanijia.
Huwezi kunipelekesha wewe mjinga unadhani Mimi muoga kiasi hicho? Sasa jaribu kufanya unachotaka na Mimi nitakuonesha .
niliongea mwenyewe bila kujijua, kumbe mke wangu ananisikia.
Wewe vipi mbona sikuelewi,
Hebu amka kwanza, upo sawa kweli? aliuliza mke wangu.
Kwani Kuna Nini kimetokea,
Nilijibu nikijifanya sijui nini kinaendelea.
Naona unaongea peke yako!
Sijui nani hakuwezi, mara nini
Eeeeeh upo sawa kweli.
aliuliza mke wangu.
Nipo sawa, labda nilikuwa naota tu , hebu niache nilale bwana.
nilijitetea huku mke wangu akiwa hajaridhika na majibu yangu
Siku hiyo mke wangu aliamka mapema kuliko kawaida yake, akaendelea na shughuli zake ndogo ndogo za pale ndani kabla hajatoka kwenda kwenye biashara zake.
Na Mimi nilikuwa nishaamka niingie bafuni nijiswafi, mke wangu alikuja huku akiwa kabana mkoba wake kwapani .
Mimi natoka leo nataka niwahi kutokana na kuwa Kuna watu waliweka oda kwenye biashara zangu na waliniomba niwahi,lakini nikwambie tu kitu kimoja usiku wa leo nimegundua kuwa haupo sawa kiasi cha kunikosesha usingizi hata mimi, ushauri wangu ni kwamba ni vyema ukaniambia nini kinakusumbua tukusaidie. au habari za mpira nilizosema sitaki, ndiyo zinakusumbua? Lakini ujue utakuja kufa kutokana na kushindwa kuweka wazi matatizo yako mume wangu. alishauri.
Wee nishakuambia sina matatizo Sasa kwanini unalazimisha?
au unataka nizungumze uongo?
Hebu achana na mimi bwana.
nilikuwa mkali muda huo Kisha mke wangu akaondoka.
Nikiwa njiani kuelekea job, nilikuwa na mawazo sana, tena sana tu,
Mke wangu ameshagundua kuwa nina shida, halafu kajuaje?
Mbona nilijitahidi kujiweka sawa tu? au nimwambie ukweli tu, nisijekufa peke yangu, lakini nitaanzaje maana stori yenyewe ni ndefu inaanzia kwenye madini ambayo nilimficha sikutaka ajue.
Na mke wangu navyomjua kitendo Cha Mimi kumfichaficha vitu huwa hapendi kama nini, hili ni tatizo kubwa. nilijiwazia
Nilichukua simu nimpigie Jax haswa baada ya kuona huenda akawa kashusha hasira zake,lakini simu haikupatikana, nilishusha pumzi huku nikiona tayari Nina maadui wawili tena kesi moja wote wananituhumu kuwa nimeiba wake zao, na halafu ikiwa watakutana na kuambizana hili jambo si ndiyo watajua kabisa kwa asilimia miamoja kuwa ni kweli, hata yule afande ambaye hakuwa na Imani ya moja kwa moja anaweza kujua kuwa ni dhahiri shahiri Mimi nililala na mkewe, tena ni vyema kutuhumiwa na kesi nyingine lakini siyo tuhuma za wizi na wake za watu, hizi zimekaa vibaya mno. nilijiwazia huko moyo ukinidunda.
Lakini mbona inaonesha afande Hussein na Jastini wamedhulumiana pesa, huenda wakawa hawana maelewano mazuri, nikajikuta napata ahueni japo bado msala ulikuwa mkubwa.
Turudi nyuma kidogo.............
Jastini mtu mwenye miraba minne, akiwa na asili ya Kanda ya ziwa,wapo walidai si mtanzania,ni mchizi ambaye kwa mara ya kwanza tulikutana kwenye mitambo ya kuchimba visima huku yeye akiwa anadili na madini, huku akikataliwa na mafundi wenzangu msaada pekee nikawa ni Mimi, kwakuwa alikuwa ana hela na anajiweza aliamua kuonana na bosi wetu moja kwa moja na kufanikiwa zoezi lake japo madini hakupata kwani sehemu hiyo haikuwa na mwamba jike na pia mitambo yetu haikuwa ikifika mbali sana ardhini.
Baada ya hapo aliondoka tukapoteana , hadi pale tulipoonana mwaka fulani City centre akiwa na gari ndogo BMW kipindi hicho japo sikujua ni ya mwaka gani lakini hizi gari Ukiwa nazo mtu unaonekana wa maana sana kwa kipindi kile ambacho nilikuwa sina gari.
Ndipo tulipokumbushana wapi tulionana Kisha urafiki wetu ukaanzia hapo,huku nikigundua ni jamaa lenye pesa, lakini weeeeee badala ya kufilisika yeye akaporomoka kiasi kwamba akikuona na laki moja anapagawa , tulisaidiana mambo mengi sana lakini kwa siku hiyo akawa adui yangu huku nikiwaza kujificha.
Sasa endelea.....
Nilifika ofisini Nika assemble mambo yangu Kisha huyooo kwa Da Vero mtu nayemkubali sana, ushauri na hata kutunza Siri alikuwa mwanamke wa aina yake.
Daniel my brother niambie naona kama ulisahau kuwa Mr alikupa kadi ya mwaliko,mbona hujaja sasa , au humtaki mpwa awe kama wewe , maana tulikuwa tunamfanyia sherehe ndogo kama pongezi kwa kumaliza chuo kikuu. aliweka kituo da Vero.
Nikishika kichwa na kushangaa,
Dah jamani naombeni mnisamehe sana nilisahau na sijafanya makusudi. nilijitetea.
Vipi kwani ishu ya madini inakuvuruga nini bro maana ndicho kitu nilikuwa naona kinakunyima raha, aliuliza.
Bora hata ingekuwa hiyo , japo naweza sema hicho ndiyo chanzo kilichofanya nifike kwa Jastini.
nikaanza kumweleza mwanzo mwisho na jinsi Jastini alivyonitishia.
Mmmh pole sana halafu Dani kwanini huwa una marafiki wa ajabu ajabu hebu fikiria mtu hawezi hata kukusikiliza yeye anachokazania na kuamini ndicho hichohicho,
Halafu wifi umemwambia?
(akimaanisha mke wangu)
Nimwambie? Namwambiaje Sasa na wewe, hivi wewe mumeo aje na hizi habari , utamchukuliaje?
niliuliza
Daniel acha kumtolea mume wangu mfano, yaani Mimi na yeye tuache kwanza, jifikirie wewe kwanza .
Halafu hivi umewaza mkeo akizipata hizi habari na wewe umemficha unadhani itakuwaje,
Halafu Daniiiih, hivi kwani watu wawili wakupe tuhuma ya aina moja , mbona nakuwa njiapanda , natamani nikutetee lakini mmmmh bro!
Be careful naona Kuna kitu hakipo sawa , umri wako, wadhifa wako na jinsi ulivyojenga heshima ya jina lako hizi tuhuma hazikufai hata kidogo na watu wataanza kutuhisi vibaya na Mimi, eeeh maana unapenda sana wanawake so ukaribu wetu watu watahisi vibaya. aliweka kituo.
Dada Veroooo wewe si wakusema hayo,watu watuhisi vibaya kivipi?
Mimi na wewe tunaheshimiana Dada.
niliropoka.
Sasa chagua moja , uache kuniambia stori zako au uache ukaribu na Mimi, mtu mwenyewe tayari unaonekana Malaya, mume wangu akipata hizi habari zako, unadhani atapenda tena kuweka mifupa karibu na fisi, haiwezekani. aliweka kituo huku akinitaka niondoke kabisa ofisini kwake.
Nilirudi ofisini kwangu huku nikisikia baridi na hofu kuu , why nisingiziwe?
Nina mkosi gani?
Jastini na afande sijui hata wananiwazia Nini,
Vipi mke wangu akizipata hizi habari?
Nilijikuta nakosa amani.
Itaendelea.................
Sent from my TECNO LC6a using JamiiForums mobile app
Usiku wa siku hiyo sikulala kabisa Kila nikiwaza namna Jastini alivyo nikawa napatwa na hofu.
Lakini Kuna hali fulani ya kiume ikawa inanijia.
Huwezi kunipelekesha wewe mjinga unadhani Mimi muoga kiasi hicho? Sasa jaribu kufanya unachotaka na Mimi nitakuonesha .
niliongea mwenyewe bila kujijua, kumbe mke wangu ananisikia.
Wewe vipi mbona sikuelewi,
Hebu amka kwanza, upo sawa kweli? aliuliza mke wangu.
Kwani Kuna Nini kimetokea,
Nilijibu nikijifanya sijui nini kinaendelea.
Naona unaongea peke yako!
Sijui nani hakuwezi, mara nini
Eeeeeh upo sawa kweli.
aliuliza mke wangu.
Nipo sawa, labda nilikuwa naota tu , hebu niache nilale bwana.
nilijitetea huku mke wangu akiwa hajaridhika na majibu yangu
Siku hiyo mke wangu aliamka mapema kuliko kawaida yake, akaendelea na shughuli zake ndogo ndogo za pale ndani kabla hajatoka kwenda kwenye biashara zake.
Na Mimi nilikuwa nishaamka niingie bafuni nijiswafi, mke wangu alikuja huku akiwa kabana mkoba wake kwapani .
Mimi natoka leo nataka niwahi kutokana na kuwa Kuna watu waliweka oda kwenye biashara zangu na waliniomba niwahi,lakini nikwambie tu kitu kimoja usiku wa leo nimegundua kuwa haupo sawa kiasi cha kunikosesha usingizi hata mimi, ushauri wangu ni kwamba ni vyema ukaniambia nini kinakusumbua tukusaidie. au habari za mpira nilizosema sitaki, ndiyo zinakusumbua? Lakini ujue utakuja kufa kutokana na kushindwa kuweka wazi matatizo yako mume wangu. alishauri.
Wee nishakuambia sina matatizo Sasa kwanini unalazimisha?
au unataka nizungumze uongo?
Hebu achana na mimi bwana.
nilikuwa mkali muda huo Kisha mke wangu akaondoka.
Nikiwa njiani kuelekea job, nilikuwa na mawazo sana, tena sana tu,
Mke wangu ameshagundua kuwa nina shida, halafu kajuaje?
Mbona nilijitahidi kujiweka sawa tu? au nimwambie ukweli tu, nisijekufa peke yangu, lakini nitaanzaje maana stori yenyewe ni ndefu inaanzia kwenye madini ambayo nilimficha sikutaka ajue.
Na mke wangu navyomjua kitendo Cha Mimi kumfichaficha vitu huwa hapendi kama nini, hili ni tatizo kubwa. nilijiwazia
Nilichukua simu nimpigie Jax haswa baada ya kuona huenda akawa kashusha hasira zake,lakini simu haikupatikana, nilishusha pumzi huku nikiona tayari Nina maadui wawili tena kesi moja wote wananituhumu kuwa nimeiba wake zao, na halafu ikiwa watakutana na kuambizana hili jambo si ndiyo watajua kabisa kwa asilimia miamoja kuwa ni kweli, hata yule afande ambaye hakuwa na Imani ya moja kwa moja anaweza kujua kuwa ni dhahiri shahiri Mimi nililala na mkewe, tena ni vyema kutuhumiwa na kesi nyingine lakini siyo tuhuma za wizi na wake za watu, hizi zimekaa vibaya mno. nilijiwazia huko moyo ukinidunda.
Lakini mbona inaonesha afande Hussein na Jastini wamedhulumiana pesa, huenda wakawa hawana maelewano mazuri, nikajikuta napata ahueni japo bado msala ulikuwa mkubwa.
Turudi nyuma kidogo.............
Jastini mtu mwenye miraba minne, akiwa na asili ya Kanda ya ziwa,wapo walidai si mtanzania,ni mchizi ambaye kwa mara ya kwanza tulikutana kwenye mitambo ya kuchimba visima huku yeye akiwa anadili na madini, huku akikataliwa na mafundi wenzangu msaada pekee nikawa ni Mimi, kwakuwa alikuwa ana hela na anajiweza aliamua kuonana na bosi wetu moja kwa moja na kufanikiwa zoezi lake japo madini hakupata kwani sehemu hiyo haikuwa na mwamba jike na pia mitambo yetu haikuwa ikifika mbali sana ardhini.
Baada ya hapo aliondoka tukapoteana , hadi pale tulipoonana mwaka fulani City centre akiwa na gari ndogo BMW kipindi hicho japo sikujua ni ya mwaka gani lakini hizi gari Ukiwa nazo mtu unaonekana wa maana sana kwa kipindi kile ambacho nilikuwa sina gari.
Ndipo tulipokumbushana wapi tulionana Kisha urafiki wetu ukaanzia hapo,huku nikigundua ni jamaa lenye pesa, lakini weeeeee badala ya kufilisika yeye akaporomoka kiasi kwamba akikuona na laki moja anapagawa , tulisaidiana mambo mengi sana lakini kwa siku hiyo akawa adui yangu huku nikiwaza kujificha.
Sasa endelea.....
Nilifika ofisini Nika assemble mambo yangu Kisha huyooo kwa Da Vero mtu nayemkubali sana, ushauri na hata kutunza Siri alikuwa mwanamke wa aina yake.
Daniel my brother niambie naona kama ulisahau kuwa Mr alikupa kadi ya mwaliko,mbona hujaja sasa , au humtaki mpwa awe kama wewe , maana tulikuwa tunamfanyia sherehe ndogo kama pongezi kwa kumaliza chuo kikuu. aliweka kituo da Vero.
Nikishika kichwa na kushangaa,
Dah jamani naombeni mnisamehe sana nilisahau na sijafanya makusudi. nilijitetea.
Vipi kwani ishu ya madini inakuvuruga nini bro maana ndicho kitu nilikuwa naona kinakunyima raha, aliuliza.
Bora hata ingekuwa hiyo , japo naweza sema hicho ndiyo chanzo kilichofanya nifike kwa Jastini.
nikaanza kumweleza mwanzo mwisho na jinsi Jastini alivyonitishia.
Mmmh pole sana halafu Dani kwanini huwa una marafiki wa ajabu ajabu hebu fikiria mtu hawezi hata kukusikiliza yeye anachokazania na kuamini ndicho hichohicho,
Halafu wifi umemwambia?
(akimaanisha mke wangu)
Nimwambie? Namwambiaje Sasa na wewe, hivi wewe mumeo aje na hizi habari , utamchukuliaje?
niliuliza
Daniel acha kumtolea mume wangu mfano, yaani Mimi na yeye tuache kwanza, jifikirie wewe kwanza .
Halafu hivi umewaza mkeo akizipata hizi habari na wewe umemficha unadhani itakuwaje,
Halafu Daniiiih, hivi kwani watu wawili wakupe tuhuma ya aina moja , mbona nakuwa njiapanda , natamani nikutetee lakini mmmmh bro!
Be careful naona Kuna kitu hakipo sawa , umri wako, wadhifa wako na jinsi ulivyojenga heshima ya jina lako hizi tuhuma hazikufai hata kidogo na watu wataanza kutuhisi vibaya na Mimi, eeeh maana unapenda sana wanawake so ukaribu wetu watu watahisi vibaya. aliweka kituo.
Dada Veroooo wewe si wakusema hayo,watu watuhisi vibaya kivipi?
Mimi na wewe tunaheshimiana Dada.
niliropoka.
Sasa chagua moja , uache kuniambia stori zako au uache ukaribu na Mimi, mtu mwenyewe tayari unaonekana Malaya, mume wangu akipata hizi habari zako, unadhani atapenda tena kuweka mifupa karibu na fisi, haiwezekani. aliweka kituo huku akinitaka niondoke kabisa ofisini kwake.
Nilirudi ofisini kwangu huku nikisikia baridi na hofu kuu , why nisingiziwe?
Nina mkosi gani?
Jastini na afande sijui hata wananiwazia Nini,
Vipi mke wangu akizipata hizi habari?
Nilijikuta nakosa amani.
Itaendelea.................
Sent from my TECNO LC6a using JamiiForums mobile app