Simulizi: Harakati za maisha

Simulizi: Harakati za maisha

SEHEMU YA ISHIRINI NA NNE

Karibuni sana,karibu Daniel.
alinikaribisha afande mmoja ambaye tunafahamiana sana tu.

Ahsante sana,
Nilijibu kiufupi.

Enheee (huku akiangalia saa ya ukutani iliyokaribu na picha ya IGP wa kipindi hicho)
Naona saa tano kasoro hii, vipi kwema Shemu?aliulizwa mke wangu.
Huku afande akiwa anatuangalia kwa zamu kwa mshangao.

Si kwema afande,si kwema kabisaa,
Ni kwamba kuna mtu leo hii siku inayoisha amekuja nyumbani mara mbili kipindi Mr yupo kazini,
Sikujali sana ujio wake japo alitoa vitisho akionesha ana bifu na mume wangu, lakini kubwa zaidi alikuja jioni Mida ya saa moja,akatoa vitisho zaidi,ndipo nilipochukua uamuzi wa kumtafuta mume wangu nimpe hizi taarifa cha ajabu wakati tunarudi dada wa kazi hatujamwona licha ya kuita mara nyingi ,baada ya hapo ndiyo tumekuja kuripoti.alifafanua mke wangu.

Bwana Daniel,vipi ukweli wa habari hizi maana mkeo anadai wewe ndiye unayetafutwa na huyo muhusika na vipi umeripoti kituo chochote cha polisi tofauti na hapa?aliuliza afande.

Hapana,kwakuwa habari nimepata muda si mrefu toka kwa wife,labda niseme naweza kuripoti tu kwani nimeshafika kwenye vyombo vya usalama.niliongea kwa sauti ya kilevi.

Dah sawa hebu tuanze na hili la upotevu wa huyo msichana wenu na shemeji ningekuomba usogee utoe maelezo maana naona wewe ndiye utakayenyoosha vizuri.aliongea afande yule huku akichukua maelezo ya mke wangu,wakati huo simu yangu iliita mpigaji akiwa ni Jirani yangu George.nikatoka nje nikapokea.

Kaka vipi mko wapi?
Salama lakini,binti yenu yupo hapa kwangu kaja muda huu anasema geti limefungwa anashindwa kuingia ndani.George aliongea bila breki.
Sikumjibu kitu nilikata simu kisha nikamtext tu kuwa nakuja.

Sorry afande nimepokea taarifa hivi punde kuwa binti tunayemtafuta yupo kwa jirani yetu palepale ningeomba basi niende nikasikilize.Niliongea huku nikiwa na pupa ya kutaka kutoka nje.

Subiri kwanza Daniel,ngoja nimalizie kuandika mlichokujia kwanza halafu pia huyo ambaye amekutishia si mnamfahamu? Aliuliza afande

Wote mimi na mke wangu tukaitikia kuwa tunamfahamu.

Eeeh tena ni vizuri,usitake kupambana naye hata kama unamuweza,wewe tumia sheria tu tunaandika maelezo yako kupitia mkeo ambaye ndiye anayeghasiwa,kisha mtaondoka na tutaacha mawasiliano ili pale ambapo huyo muhalifu atakuzidi nguvu basi utapiga simu.

Pia nikuonye bwana Daniel, tafadhali usije ukatafuta kulipa kisasi kiholela,wewe ni msomi na sitegemei nije kusikia umemalizana na huyo mshari wako kwa njia za kienyeji, acheni kuchezea uhuru wenu,namuona huyo mtu kama ni mhalifu tu kwasababu kama wewe ungekuwa na kosa basi angefuata sheria.afande alishauri vizuri huku nikimshukuru licha ya kuwa hawa jamaa huwa siwakubali hata sijui kwanini.

Tulifika nyumbani huku tukiwa na tahadhari sana nilishuka kwenye gari huku nikitaka mke wangu abaki kwenye gari tena mbali kama mita mia , nikafungua geti kwa tahadhari kisha nikakagua mazingira yote kuanzia sebuleni na vyumba vyote,nikajiridhisha kuwa kupo shwari kisha nikampigia George simu kuwa aje mahali ilipo gari yangu amlete binti yetu.

Baada ya kuja tulisalimiana huku naye akikosa amani kwani nilimuona akiwa anageukageuka kila saa, kiasi cha kunitisha hata mimi kisha akaniita pembeni ili maongezi yetu yasisikike na mke wangu wala yule dada.

Dani vipi kaka,mbona wajihi wako na hivi vituko hamuendani kwani yule mchizi umemfanya nini kiasi cha kukusaka vile na kwanini usiripoti polisi kaka? aliongea George huku akiwa anageukageuka kama vile anasakwa yeye.

Ndiyo natoka huko na wakati unanipigia kunipa taarifa za dada wa kazi nilikuwa polisi ,hivyo ondoa shaka huyo jastini ni jambazi kama walivyo wengine tu,vyombo vya sheria vipo kama mimi ni mkosefu lazima mngejua tu,kwanini ananipa tuhuma si zangu,yaani maisha aharibu yeye halafu lawama aniangushie mimi? Sikia G.mimi Jax hanifanyi chochote na uwe na amani.Niliongea huku nikimwambia mke wangu asogeze gari tuingie ndani

Kwa uoga mke wangu akapaki gari huku akiogopa hata kivuli chake tu.

Wewe ulikuwa wapi kiasi cha watu tukapata wasiwasi mkubwa?
nilimuuliza binti wa kazi.

Nilikuwa hapo nje,yule mtu aliyekuja mchana akamgombeza dada (akimaanisha mke wangu)
alikuja hapa akiwa na mwanamke mmoja hivyo niliogopa na kukimbia licha ya wao kutaka nisimame lakini niliwaogopa.alijibu binti yetu huku ikiniijia picha fulani.

Sasa ndiyo uache kila kitu wazi ,kama wangetaka kuiba?
Wangekuwa ni majambazi,na nilikwambia natoka namfuata shemeji yako nikitaka ukae ndani ujifungie kimya ,kwanini wewe ulitoka nje, huoni kama ulikuwa kwenye hatari zaidi na kwanini unakaidi maagizo yangu.mke wangu alifoka huku binti akiomba msamaha.

Mke mwema mimi sioni sababu ya kumlaumu huyu mtoto,ina maana hao watu kama wangekuwa ni majambazi yeye angewazuia?
nadhani tushukuru Mungu kila kitu kipo vizuri na hata yeye alikuwa anaokoa uhai wake, hata kama wewe mtu ambaye alitoka kutoa vitisho halafu tena uone anakuja utachukua hatua gani.hebu tuyaache hayo kwanza.

Saa nane usiku ndiyo tuliingia kulala huku mimi nikitoka nje na tochi kubwa nikijiridhisha kwenye angle zote ambapo muhalifu anaweza kujificha,lakini hakuna nilichokiona nikarudi kulala .

Kesho asubuhi na mapema niliwahi sana siku hiyo huku nikiacha tahadhari kwa familia lengo nikamuombe ruhusa boss wangu kuwa nina dharula.

Nilikutana na dada Vero mfanyakazi mwenzangu, mshauri wangu haswa kwakuwa amenizidi umri parefu,lakini siku hiyo niliona kama yupo mbali na mimi,licha ya kujichekesha lakini akawa bize kupita maelezo.

Lakini sikusita kumweleza maswahibu yangu licha ya kugundua namlazimisha tu, nilimweleza namna ambavyo nimepata vitisho toka kwa Jastini na hatua nilizochukua.

Kwa Da Vero alicheeeka huku akiniangalia kwa dharau sana ,

Hivi wewe Daniel unaishi maisha ya aina gani, mswahili si mswahili,yaani hueleweki au una laana?
Maana kila siku tunakushauri ni marafiki gani wa kuwa nao lakini wewe bado una watu ambao hawajaelimika,ona sasa mtu mwenye akili timamu anaweza kukufuata nyumbani kwa anayokuhisi?
Ndugu yangu acha kujifanya upo humble eti huna dharau wala nini,jaribu kuchagua watu sahihi wa kushirikiana nao,kwanini hamjifunzi kwa mume wangu,yah Mr yupo bize na akipiga stori na mtu basi ni mtu kweli,nakushauri tafuta mganga au kanisa pengine itasaidia.aliweka kituo huku nikishangaa mbona masimango.

Nikarudi ofisini huku nikizugazuga
Lakini hadi saa tano za asubuhi boss ambaye nilikusudia anipe ruhusa hakutokea nikipiga simu haipokelewi,basi nikawa niponipo tu.

Kuna ujumbe uliingia kwenye simu yangu, kuangalia unatoka kwa Jastini, moyo ulipiga paaah,ujumbe ukionesha amenitafuta zaidi ya mara saba.nikapiga lakini simu haikupokelewa.

Lakini ni muda ambao boss alikuja huku akiwa na wageni kadhaa nikamuacha , kisha baada ya kugundua wale jamaa wageni wametoka nikaenda ofisini kwake.

Wewe nawe vipi simu tuuu unapenda sana kupiga simu eeeh,niliiona lakini niliipuuza tu,wewe unajua kabisa ni watu gani ambao ndiyo huwa wananitafuta kama kuna tatizo,acha mambo yako unaona fahari kubwa kupiga piga simu sitaki.aliongea boss kwa dharau.

Samahani nina matatizo nyumbani kwangu nilikuwa nakuomba ruhusa kwakuwa hata meneja mdogo hayupo amesafiri
nilijitetea.

Wewe nenda ila tambua mwezi unaokuja unatakiwa kwenda mkoani tena hili liwe akilini mwako maana ukitoka huko ndipo utapewa likizo.alinipa ruhusa ya siku kadhaa.

Lakini nikiwa najiandaa kutoka simu ya mke wangu iliingia nikapokea huku akinimbia kuwa Jastini na mkewe wapo nyumbani kwetu.

Nilishangaa huku nikijiuliza maswali mengi lakini nikaona majibu nitapata nikifika.

Itaendelea....................
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA TANO

Nilitoka kwa speed huku nikimpigia simu mke wangu na kumwambia akae mbali na watu wengine maana nilitaka kumuuliza maswali fulani.

Unasema Jax yupo hapo,vipi unavyomuona ana hali gani? nikiwa na hofu asiwe na chuki.

Yupo vizuri tu na tunapiga stori tu hapa japokuwa wananipa wasiwasi lakini si unakuja? utamuona mwenyewe.alijibu mke wangu kisha nikakata simu

Nikakoleza chombo na kuingia ndani kwa tahadhari kwani bado sikuwa na imani ya moja kwa moja na Jastini.

Niliingia ndani mwangu huku Jax na mkewe wakiwa na tabasamu,nadhani walitengeneza sura rafiki ili nitambue kuwa wamekuja kwa amani.
lakini mimi nikaweka sura ya hasira kimakusudi kabisa,
Kwanza sikusalimia ,ikabidi aanze yeye Jax kunisalimia huku mke wangu akinishangaa kwa nilivyo Muda ule.

Najua Daniel umekasirika sana kwa taarifa ambazo umezipata,
Natambua hilo lakini fahamu wazi kuwa nipo hapa kwaajili ya kurekebisha hilo suala.aliongea kwa tahadhari Jastini.

Kwani mimi wewe Jax unanionaje?
Yaani sikuelewi ujue,
Lakiniii ni wazi hatuheshimiani,na niseme wazi mbele ya mke wangu na mkeo pia ni kwamba nimepoteza imani na wewe kwa kitendo cha kunitishia maisha na kunidhalilisha.

Majirani wote wanajua mimi ni mtu fulani wa hovyo mwizi wa wake za watu na mtu nisiyejiheshimu,lakini pia nimepoteza imani kwa mke wangu kwa tuhuma ulizonipatia.unataka kuvunja ndoa yangu? nasikia umetamba sana hapa unakuja kila mara kama vile hapa ni sokoni huku ukitoa vitisho kwani unanichukuliaje? niliongea kwa hasira huku nikiinuka kama vile nataka kupigana lakini mke wangu na mke wa jamaa walinizuia nilijua tu watafanya hivyo,maana nipo kwangu nikawa najiamini.

Daniel ndugu yangu,
Nipo hapa kwaajili ya kurekebisha hili jambo kwanza naomba unisamehe sana................. kabla Jax hajamalizia sentensi yake nilidakia.

Bro njia uliyotumia wewe kunisaka kama jambazi si ile niliyotumia mimi ,mimi jana niliripoti kituo cha polisi,ni hapo tu police post wala siyo mbali, tunaweza kwenda ili kile unachotaka kurekebisha kwa mujibu wa maelezo yako utawaeleza polisi, maana hapa nilipo siwezi kuongea chochote na wewe ikiwa nilishakuripoti.maana kitendo cha kuelewana na wewe siku nyingine sitapata msaada maana nitaonekana mambo mengi ya hatari kama haya huwa namaliza mwenyewe.niliongea nikiwa sioneshi masikhara.

Shemeji yangu samahani sana nakuomba basi kuwa na imani msamehe mume wangu tupo tayari kueleza kila kitu jambo lako si lipo tu polisi? Kwani ni mahakamani huko?kwamba huwezi kusuluhisha jambo lililo kwenye Sheria?
Tupo chini ya miguu yako Shemu, tunahitaji huruma yako tu mitihani aliyonayo mume wangu ni mingi na anakabiliwa na madeni chungu mzima.mimi nadhani shemeji wewe ni mchamungu mzuri mwenye hofu ya Mungu na pia ni muelewa.aliweka kituo mke wa Jastini huku na mimi nikishusha hasira.

Kaka najua ni jinsi gani mke wako alikuwa kwenye wakati mgumu kwa Yale niliyomueleza Jana kuwa wewe umemtorosha mke wangu, nikikumbuka hali aliyokuwa nayo kiukweli, kwanza shemeji naomba nisamehe Mimi nilikuwa kwenye wakati mgumu sana. Jax alimuomba msamaha mke wangu.

Shemu sihitaji longolongo, nyoosha maelezo vizuri msinichezee akili yangu, nataka kujua ile A to Z ilikuwaje, hadi mume wangu kuhusishwa na maswala hayo.
Mke wangu aling'aka.

Ndipo Jastini alipoeleza mwanzo mwisho tangu tulipokutana na ishu ya madini, huku yeye akiwa mtu wa kati na afande Hussein ndiye muuzaji na Mimi Daniel ni mnunuzi.
aliongea na kufafanua vizuri sana Jastini.

Ahaaaa kwahiyo baba Jack, unaingia kwenye biashara zako bila kunishirikisha hiyo moja, halafu kwanini ufanye biashara ambayo huna uzoefu nayo,mara unakurupuka unanunua vitu kwa hela nyingi sana kwanini lakini? Maana kwa maelezo ya shemeji hapa ni dhahiri hamkuchukua hata wiki moja tayari ulikuwa umeshatoa hela ya kununua hivyo vitu. Kweli mume wangu?
Hata kunishirikisha?
Na ulifanya utafiti kweli?
mke wangu aliniuliza kwa upole huku nikiona aibu sana, ni kweli huwa namshirikisha mambo mengi japo siyo Kila kitu.

Sawa hayo mume wangu huwezi kujibu, enhee na wewe shemu Jastini mkeo umempataje maana mpaka hapa naona kama mnanizunguka tu. mke wangu aliuliza huku akionesha bado hana Imani na mimi,

Iko hivi mimi baada ya kupokea hela niliongea na afande Hussein kuwa niende Mkoa xxxx nikanunue mzigo ili tuendelee na biashara yetu, kifupi hela iwe inazunguka, na kitu ambacho wewe Daniel hujui ni kwamba afande Hussein madini huwa anatumiwa na mkewe ambaye anafanya kazi TANAPA, madini huwa anayapataje Mimi sijui ila huwa anayatuma kwa mumewe Kisha Mimi kwakuwa nawajua matajiri wengi basi tunauza,Kisha akaendelea kumfafanulia mke wangu.......

Baada ya kurudi kutoka mkoani nilipata taarifa kuwa mumeo Daniel alikuwa anaonekana nyumbani kwangu , Hilo sikujali Wala sikuwa na wasiwasi sana , nilijua alikuwa ananitafuta kwakuwa yupo na mzigo ambao hajui atauzia wapi na kwakuwa sikuwa napatikana kwenye simu basi nilijua wazi lazima atakuwa na wasiwasi. alifafanua Jastini.

Na ndicho kipindi ambacho mke wangu uliniuliza mbona sipo sawa lakini nilikuwa najikaza sikutaka kukusumbua sana. nilimwambia ukweli mke wangu.

Jastini akaendelea.........
Lakini baada ya kufika kule Mkoa nilikutana na watu wanaonidai hivyo niliishia kukaa lockup tu kwa siku tatu Kisha nikajidhimini na kupunguza deni kwa kutumia hela ambayo ni ya afande Hussein, ambapo naye si yake ni ya mkewe.kipande hiki hata Mimi nilikuwa makini kumsikiliza jamaa kwani tangu atoke mkoani tuliishia kwenye matatizo tu hakukuwa na maelewano hivyo siku hiyo nikawa makini sana.

Akaendelea......

Baada ya kuwa pesa zaidi ya million tatu nimeishia kulipa deni, ndipo nilipoazima nauli na kurudi Dar es salaam, na nikiri wazi kuwa Mimi zamani nilikuwa nafanya hii biashara na Fatma mke wa afande Hussein, baada ya dhuluma za hapa na pale Fatma akakataa kunipa mzigo huku akiwa Hana pakuuzia ,huku akimtaka mumewe amfanyie mpango kwa matajiri wengine, lakini yule afande Hussein hakufanikiwa kupata matajiri wa Ruby ni Mimi tu ndiye nawajua hivyo Kwa Siri afande akawa ananipa mzigo nimuuzie huku akitaka mkewe asijue kuwa bado na Mimi nipo kwenye ile cycle.

Inaendelea............................
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA SITA

Moyo wangu ulisisimka sana kwa kile alichokisema Jastini huku nikimuona jamaa siyo wa kawaida hana uoga kwenye Mali ya mtu.

Jastini akaendelea........

Kwahiyo baada ya kukaa lockup kule mkoani kwa zaidi ya siku tatu Kisha nikarudi Dar es salaam kwa kuungaunga, ndipo nilipomtafuta afande Hussein nimpe habari kuwa mchongo umeharibika ,
Alipokea taarifa ile kishingo upande huku nikigundua amekasirika sana Lakini hakusema chochote, tukaachana kisha nikakupigia wewe simu ili tukutane unipe madini ili tukauze nikijua Kuna chochote kitu nitapata ili nisogeze maisha Lakini ukaniambia umeuza
Hakika nilichanganyikiwa sana , Lakini nashukuru ukaniambia kama ni asilimia zangu za udalali utanipa , tukapanga tukutane kwenye hotel ya (akitaja jina)ambapo kabla hujafika tayari nilishadakwa na maaskari nikapelekwa kituoni nikitambua afande Hussein ameshanichora. alifafanua Jastini.

Maelezo ya Jastini yalitugusa wote mle ndani si mkewe, si mke wangu, Wala Mimi mwenyewe, nyuso za wanawake wawili zilionesha huruma sana hata Mimi Kuna muda nilimuhurumia Jastini licha ya kuwa ni jana tu alitoka Kunitishia Mimi na familiar yangu ila harakati zake ambazo hazikuwa na matunda zilitia huruma.

Jastini akaendelea..........
Nilikaa kituo kidogo cha polisi kwa masaa zaidi ya nane kabla sijahamishwa na kupelekwa Kituo cha kati, hata hivyo niliwaza Ina maana Dani hana taarifa yeyote kuhusu kukamatwa kwangu? shukrani ziende kwa ndugu zangu ambao walikuja kunidhamini huku wakati natoka nikakutana na wewe Daniel pale nje kabla hatujatibuana kwa kukosana kiswahili.

Nilifika nyumbani kwangu nikaangalia huku na huko sikumuona mke wangu, nikaulizia kwa majirani wakasema hawajui huku wakikuhusisha wewe Dani kuhusu kupotea kwa mke wangu maana asubuhi ya siku hiyo kabla sijadhaminiwa ulionekana nyumbani kwangu huku ukimpa kiasi kikubwa cha pesa. aliweka kituo Jastini.

Ni kweli nilionekana nikitaka kumpa taarifa za wewe kuwa mahabusu Lakini kwa hali niliyomkuta nayo , nikaona nitamuongezea matatizo zaidi na sikumpa kiasi cha pesa wanachosema, Mimi nilitoa hela ya vocha tu kuwa anitafute baadaye ili tuwe tunawasiliana, nadhani ilikuwa ni noti moja ya elfu kumi. nilifafanua huku point ile nikimlenga mke wangu na nashukuru MUNGU kwanini siku ile nilijikuta nakuwa bahili? Ni kwamba my Lord alikuwa upande wangu.

Jastini akaendelea.......
kiukweli baada ya hapo sikuwa na imani na wewe tena na nilikuchukia huku nikiwa na asilimia miamoja kuwa wewe unahusika na upotevu wa mke wangu, lakini cha ajabu jana baada ya kutoka hapa mchana nilimkuta mke wangu nyumbani ambapo aliponieleza alipokuwa niliridhika ni kwamba alikuwa kwa ndugu zangu, na nilichelewa kujua haya kwakuwa simu yangu muda mwingine naizima kwasababu ya madeni niliyokuwa nayo, na Kwa taarifa za chini chini nasikia yule mke wa afande Hussein yupo mji huu toka huko porini anakofanyia kazi na atakuwa amekuja kwaajili yangu. aliweka kituo Jastini akionesha ni mwenye wasiwasi sana.

Kwahiyo hiyo million tatu shemeji huwezi kuilipa kwa namna yeyote ili uwe na amani? mke wangu aliuliza.

Lakini Jastini alicheka kidogo Kisha akaniangalia mimi na huku akikohoa kidogo.

Ndugu zanguni Mimi nadhalilika hapa mjini Nini million tatu? Kwa hela anazonidai yule mwanamke ni nyingi yaani million tatu ni kama elfu tatu tu kwa hela anazodai ni kwa kipindi kirefu, mbaya zaidi alishakataa ushirikiano na mimi, halafu Nina madeni kwa watu wengine pia hakika safari na nyumba ile naona inaenda kuuzwa. aliongea kwa hisia kali Jastini kiasi cha kudondosha chozi.

Jastini mtu mwenye kiburi na anayejiamini pande la mtu,jitu lenye kipara muda wote, aliwahi kusema huwa hapendi kufuga nywele kwani huwa zinachukua asilimia kadhaa za ubongo,na pia mwenyewe aliwahi kusema kamwe hawezi kudondosha machozi kizembe ,akidai machozi ni ya thamani kubwa kwa mwanaume lakini,hatimaye alilia mbele ya wanawake wawili,huku aibu nikiiona Mimi, hakika hakuna kitu kibaya sana kama shida.

Wakati huo mke wangu alikuwa na imani tena kwangu kwani maelezo ya Jastini yalijitosheleza mno. Kazi ilikuwa kwa mke wa Jastini ambaye alikuwa analia kama mfiwa haswa baada ya kusikia kuwa nyumba wanayoishi huenda ikauzwa muda si mrefu.

Tulifanikiwa kumbembeleza Kisha yale mambo yakawa yameisha na tukaendelea kupiga stori za kawaida tu, hakuna aliyewaza kwenda polisi eti Jastini aliyetutishia hatimaye yupo mikononi mwetu kama ambavyo mke wangu alishauri tupige simu polisi kimya kimya then waje wamkamate, lakini kwa harakati za maisha yake hakuna aliyewaza mambo mengine yasiyofaa.

Lakini hofu ya Jastini bado niliiona nilitambua licha ya kutueleza mambo mengi lakini bado Kuna vitu anaficha ikabidi nimuulize haswa baada ya kuwa wanawake wameondoka.

Jax haupo sawa hebu niambie Kuna nini kingie tofauti na maelezo yako kama ni m3 nipo tayari kulipa niliropoka.

Daniel mwanangu,
Fatma yupo mjini, na amekuja kwaajili yangu nilimdhulumu pesa nyingi sana,na kumbuka Hawa wote ni maaskari yeye na mumewe hivyo Wana msaada mkubwa sana, wanaweza kunipoteza mara moja.
aliongea kwa upole Jastini.

Niliinama chini nikawaza sana, nakumbuka ni Jana tu nilionana na Fatma, pisikali ya maana almanusura nijipendekeze kwa mara nyingine jana lakini mpango uliharibika baada ya mke wangu kuja kunipa taarifa za kusema kuna vitisho nyumbani , nilishawahi kutengeneza mazingira ili nilale naye lakini ilishindikana, Fatma mbona kama ni zaidi ya nimuonavyo kwanini Jastini anamuogopa hivi?
nilijiuliza sana.

Kumbe wakati tupo ndani Kuna mtego uliwekwa nje na hakuna aliyejua, geti liligongwa wakaingia watu watatu mbavu kwelikweli wakasalimia huku haraka wakitoa vitambulisho vyao na kunionesha.
Walikuwa ni askari polisi sura ngeni hakuna niliyemjua hata mmoja.

Bila shaka wewe ni Daniel (akitaja majina matatu)

Yeah ni Mimi karibuni.
Niliwakaribisha huku nikimuona Jastini akija tulipo

Kwahiyo kumbe plan na mipango yenu huwa mnafanyia hapa si ndiyo?
Yaani nyinyi mnajifunza utapeli,Wala si wazoefu Sasa jeshi la polisi linawasaka watu kama nyinyi , Tena mlivyo wajanja Kuna muda mnajifanya mmegombana ili kutuzuga lakini timu yetu imefanikiwa kujua mbinu zenu.jana tu umeenda kituo cha polisi eti unamshitaki huyu jambazi mwenzio kakutishia, kumbe lengo mnatuchezea ili tusijue mipango yenu. aliongea huku akikunja sura akionesha hatanii.

Afande unaongea nini na Hawa?
Maelezo haya watapewa kituoni . aliamrisha askari aliyekuwa na silaha akisema muda unapotea.

Licha ya kujaribu kutaka kuuliza Kuna Nini lakini nilitishiwa na kubwa zaidi baada ya kujaribu kugoma kwenye gari lao lenye vioo vya tinted. Nilipigwa vizuri nikaona isiwe tabu na nitaumia nikaingia kwenye gari.

Itaendelea.................
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA SITA

Moyo wangu ulisisimka sana kwa kile alichokisema Jastini huku nikimuona jamaa siyo wa kawaida hana uoga kwenye Mali ya mtu.

Jastini akaendelea........

Kwahiyo baada ya kukaa lockup kule mkoani kwa zaidi ya siku tatu Kisha nikarudi Dar es salaam kwa kuungaunga, ndipo nilipomtafuta afande Hussein nimpe habari kuwa mchongo umeharibika ,
Alipokea taarifa ile kishingo upande huku nikigundua amekasirika sana Lakini hakusema chochote, tukaachana kisha nikakupigia wewe simu ili tukutane unipe madini ili tukauze nikijua Kuna chochote kitu nitapata ili nisogeze maisha Lakini ukaniambia umeuza
Hakika nilichanganyikiwa sana , Lakini nashukuru ukaniambia kama ni asilimia zangu za udalali utanipa , tukapanga tukutane kwenye hotel ya (akitaja jina)ambapo kabla hujafika tayari nilishadakwa na maaskari nikapelekwa kituoni nikitambua afande Hussein ameshanichora. alifafanua Jastini.

Maelezo ya Jastini yalitugusa wote mle ndani si mkewe, si mke wangu, Wala Mimi mwenyewe, nyuso za wanawake wawili zilionesha huruma sana hata Mimi Kuna muda nilimuhurumia Jastini licha ya kuwa ni jana tu alitoka Kunitishia Mimi na familiar yangu ila harakati zake ambazo hazikuwa na matunda zilitia huruma.

Jastini akaendelea..........
Nilikaa kituo kidogo cha polisi kwa masaa zaidi ya nane kabla sijahamishwa na kupelekwa Kituo cha kati, hata hivyo niliwaza Ina maana Dani hana taarifa yeyote kuhusu kukamatwa kwangu? shukrani ziende kwa ndugu zangu ambao walikuja kunidhamini huku wakati natoka nikakutana na wewe Daniel pale nje kabla hatujatibuana kwa kukosana kiswahili.

Nilifika nyumbani kwangu nikaangalia huku na huko sikumuona mke wangu, nikaulizia kwa majirani wakasema hawajui huku wakikuhusisha wewe Dani kuhusu kupotea kwa mke wangu maana asubuhi ya siku hiyo kabla sijadhaminiwa ulionekana nyumbani kwangu huku ukimpa kiasi kikubwa cha pesa. aliweka kituo Jastini.

Ni kweli nilionekana nikitaka kumpa taarifa za wewe kuwa mahabusu Lakini kwa hali niliyomkuta nayo , nikaona nitamuongezea matatizo zaidi na sikumpa kiasi cha pesa wanachosema, Mimi nilitoa hela ya vocha tu kuwa anitafute baadaye ili tuwe tunawasiliana, nadhani ilikuwa ni noti moja ya elfu kumi. nilifafanua huku point ile nikimlenga mke wangu na nashukuru MUNGU kwanini siku ile nilijikuta nakuwa bahili? Ni kwamba my Lord alikuwa upande wangu.

Jastini akaendelea.......
kiukweli baada ya hapo sikuwa na imani na wewe tena na nilikuchukia huku nikiwa na asilimia miamoja kuwa wewe unahusika na upotevu wa mke wangu, lakini cha ajabu jana baada ya kutoka hapa mchana nilimkuta mke wangu nyumbani ambapo aliponieleza alipokuwa niliridhika ni kwamba alikuwa kwa ndugu zangu, na nilichelewa kujua haya kwakuwa simu yangu muda mwingine naizima kwasababu ya madeni niliyokuwa nayo, na Kwa taarifa za chini chini nasikia yule mke wa afande Hussein yupo mji huu toka huko porini anakofanyia kazi na atakuwa amekuja kwaajili yangu. aliweka kituo Jastini akionesha ni mwenye wasiwasi sana.

Kwahiyo hiyo million tatu shemeji huwezi kuilipa kwa namna yeyote ili uwe na amani? mke wangu aliuliza.

Lakini Jastini alicheka kidogo Kisha akaniangalia mimi na huku akikohoa kidogo.

Ndugu zanguni Mimi nadhalilika hapa mjini Nini million tatu? Kwa hela anazonidai yule mwanamke ni nyingi yaani million tatu ni kama elfu tatu tu kwa hela anazodai ni kwa kipindi kirefu, mbaya zaidi alishakataa ushirikiano na mimi, halafu Nina madeni kwa watu wengine pia hakika safari na nyumba ile naona inaenda kuuzwa. aliongea kwa hisia kali Jastini kiasi cha kudondosha chozi.

Jastini mtu mwenye kiburi na anayejiamini pande la mtu,jitu lenye kipara muda wote, aliwahi kusema huwa hapendi kufuga nywele kwani huwa zinachukua asilimia kadhaa za ubongo,na pia mwenyewe aliwahi kusema kamwe hawezi kudondosha machozi kizembe ,akidai machozi ni ya thamani kubwa kwa mwanaume lakini,hatimaye alilia mbele ya wanawake wawili,huku aibu nikiiona Mimi, hakika hakuna kitu kibaya sana kama shida.

Wakati huo mke wangu alikuwa na imani tena kwangu kwani maelezo ya Jastini yalijitosheleza mno. Kazi ilikuwa kwa mke wa Jastini ambaye alikuwa analia kama mfiwa haswa baada ya kusikia kuwa nyumba wanayoishi huenda ikauzwa muda si mrefu.

Tulifanikiwa kumbembeleza Kisha yale mambo yakawa yameisha na tukaendelea kupiga stori za kawaida tu, hakuna aliyewaza kwenda polisi eti Jastini aliyetutishia hatimaye yupo mikononi mwetu kama ambavyo mke wangu alishauri tupige simu polisi kimya kimya then waje wamkamate, lakini kwa harakati za maisha yake hakuna aliyewaza mambo mengine yasiyofaa.

Lakini hofu ya Jastini bado niliiona nilitambua licha ya kutueleza mambo mengi lakini bado Kuna vitu anaficha ikabidi nimuulize haswa baada ya kuwa wanawake wameondoka.

Jax haupo sawa hebu niambie Kuna nini kingie tofauti na maelezo yako kama ni m3 nipo tayari kulipa niliropoka.

Daniel mwanangu,
Fatma yupo mjini, na amekuja kwaajili yangu nilimdhulumu pesa nyingi sana,na kumbuka Hawa wote ni maaskari yeye na mumewe hivyo Wana msaada mkubwa sana, wanaweza kunipoteza mara moja.
aliongea kwa upole Jastini.

Niliinama chini nikawaza sana, nakumbuka ni Jana tu nilionana na Fatma, pisikali ya maana almanusura nijipendekeze kwa mara nyingine jana lakini mpango uliharibika baada ya mke wangu kuja kunipa taarifa za kusema kuna vitisho nyumbani , nilishawahi kutengeneza mazingira ili nilale naye lakini ilishindikana, Fatma mbona kama ni zaidi ya nimuonavyo kwanini Jastini anamuogopa hivi?
nilijiuliza sana.

Kumbe wakati tupo ndani Kuna mtego uliwekwa nje na hakuna aliyejua, geti liligongwa wakaingia watu watatu mbavu kwelikweli wakasalimia huku haraka wakitoa vitambulisho vyao na kunionesha.
Walikuwa ni askari polisi sura ngeni hakuna niliyemjua hata mmoja.

Bila shaka wewe ni Daniel (akitaja majina matatu)

Yeah ni Mimi karibuni.
Niliwakaribisha huku nikimuona Jastini akija tulipo

Kwahiyo kumbe plan na mipango yenu huwa mnafanyia hapa si ndiyo?
Yaani nyinyi mnajifunza utapeli,Wala si wazoefu Sasa jeshi la polisi linawasaka watu kama nyinyi , Tena mlivyo wajanja Kuna muda mnajifanya mmegombana ili kutuzuga lakini timu yetu imefanikiwa kujua mbinu zenu.jana tu umeenda kituo cha polisi eti unamshitaki huyu jambazi mwenzio kakutishia, kumbe lengo mnatuchezea ili tusijue mipango yenu. aliongea huku akikunja sura akionesha hatanii.

Afande unaongea nini na Hawa?
Maelezo haya watapewa kituoni . aliamrisha askari aliyekuwa na silaha akisema muda unapotea.

Licha ya kujaribu kutaka kuuliza Kuna Nini lakini nilitishiwa na kubwa zaidi baada ya kujaribu kugoma kwenye gari lao lenye vioo vya tinted. Nilipigwa vizuri nikaona isiwe tabu na nitaumia nikaingia kwenye gari.

Itaendelea.................
Msala mwingine Dani

Sent from my CPH1923 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom