mkushi wa kushi
JF-Expert Member
- Apr 27, 2021
- 657
- 993
Dah[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Dah[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Samson ushindi wa yanga unatupiga kimoko tu 😂 sio poaSEHEMU YA HAMSINI NA TANO
Safari rasmi ilianza baada ya kuachana na mwenyeji wangu Medi,na kuingia barabara ya lami.
Baada ya kutembea takribani dakika ishirini bila mazungumzo na yule dereva nilivunja ukimya.
Naitwa Daniel,bila shaka uliambiwa kuwa unanifuata mwenye jina hili.vipi mwenzangu unaitwa nani,maana kwenye taasisi yetu sijawahi kukuona.
Niliuliza huku nikichezea simu .
Ni kweli kabisa,mimi naitwa
Mark Rafael ni mgeni kwenye hii taasisi hasa kwa hii kazi ya udereva ,japo miaka mitano nyuma nilikuwa ni mmoja kati ya mafundi au warekebishaji wa umeme wa magari kwenye taasisi hii, na wewe nakufahamu mbona,na najua ni ngumu wewe kunitambua.alijibu kwa utulivu.
Unasema ulikuwa fundi,sasa ilikuwaje ukawa dereva leo hii.niliuliza
Kifupi nilikaa kama miaka miwili tu,ila kwa bahati mbaya kuna siku moja gari la boss liliharibika mifumo ya umeme
Na mimi nikaambiwa nikarekebishe,
Lakini naweza kusema bahati haikuwa yangu kwa siku ile kwani kila nikijitahidi nilishindwa kutatua tatizo lile ndipo boss kwa hasira akaagiza gari lingine na kutokomea huku akichukia kwa kudai mimi si fundi kwanini nimeshindwa kutatua tatizo dogo.
Na baada ya yeye kutoka nilifanikiwa kurekebisha lakini tayari nilishapoteza imani,kwani nilivyorudi tu,baada ya siku nne hivi nilipokea barua ya kusimamishwa kazi huku nikiambiwa nitaitwa lakini haikuwa hivyo
alifafanua.
Dah pole sana,sasa ilikuwaje ukawa dereva kwenye taasisi.niliuliza.
Mimi ni dereva mzuri tu kitambo sana ila kama unavyojua hizi taasisi kubwa zinataka drivers watoke vyuo vya kueleweka na madaraja ya kueleweka ,hivyo nilijikuta nakosa kazi kwani vigezo sikutimiza .
Ila ni wiki iliyopita nilijibiwa maombi yangu niliyotuma kwa muda mrefu sana baada ya kwenda mtaani na kujiongeza kutafuta cheti na daraja stahiki. Ndiyo hivi hii ni safari yangu ya kwanza na nimeambiwa ni kama interview na wewe ndiyo utatoa majibu kama ni dereva mzuri au la.
aliongea kwa hisia kali.
Sikumjibu kitu ila nilijikuta nawaza mbali sana niliwaza vitu vingi,ni kweli hakuwa dereva mzuri sana,kwani alikuwa akichapia gia kila mara huku nikigundua wamempa hili gari manual transmission makusudi kabisa, nilimgundua mapema sana lakini roho ya huruma iliniingia, maana mimi mwenyewe nilikuwa na hustle bado, nikitumia waganga, wachungaji lengo tu mambo yangu yaende.
Mmmmmh kama nikiulizwa vipi huyo ni dereva mzuri au la sijui nitajibuje,najua kwa kutengeneza uaminifu na maslahi mapana ya taasisi natakiwa kusema ukweli,huyu si dereva kuna vitu bado vinamshinda lakini........nilijikuta nawaza sana.
Tuliendelea kuchanja mbuga huku nikigundua ni muoga mno,lakini nikaona bora atembee mwendo huu huu maana ya Mungu mengi .
Tuliukaribia mkoa unaofuata kisha nikamwambia tutafute hotel tule maana tumbo lilidai chochote kitu,tulitumia kama dakika arobaini hivi kisha nikamuomba niendeshe.
Sasa mkuu itakuwaje maana nipo kwenye masomo ujue, aliuliza kwa sauti ya uoga huku akitabasamu.
Usijali naona nitalala ngoja nijikeep busy kwanza nitakuachia tu tukikaribia ,nilianza kusereresha ule mtumbwi huku nikigundua hata gari lenyewe kapewa bovu,looh inawezekana walimwambia achague yeye akaamua kuchagua huu mnisan Dah tutafika saa ngapi sasa ,kila magari yakituovertake nilichukia sana.
Saa kumi na moja tulikuwa kwenye jiji lenye kila aina ya kipaji,na kila aina ya maisha yapo kwenye jiji hili.
Sasa ndugu yangu njoo ukae kwenye usukani wako kisha utaniacha njia panda X ili mimi nielekee nyumbani,vipi gari walisema ulale nalo au upeleke ofisini? niliuliza.
Mkuu hata najua basi,ila ni vema nipeleke tu .alijiongeza.
Nilitafuta taxi nikapakia mizigo yangu niliyopewa kama zawadi toka mkoa wenye watu wenye mioyo safi.nikashika barabara kuelekea pembeni ya mji ambako ndiyo maskani kwangu.
Nilifika nyumbani huku nikipokelewa vizuri na dada wa kazi pamoja na wageni kadhaa,nisiowajua.
Tukasalimiana.
Vipi dada yako yuko wapi?
Nilimuuliza dada wa kazi.
Nadhani bado yupo dukani kwake,na hata hawa wageni wanamsubiri yeye.alijibu huku tukisaidiana kuingiza mizigo yangu ndani.
Kama kawaida yangu (hili ni kwa watu wengi) nilianza kuizunguka nyumba kukagua kagua sehemu kibao kuangalia kama kuna mabadiliko yeyote maana wiki zaidi tatu ni nyingi unaweza kuta nyumba imeweka ufa lakini wake zetu yeye anaishi tu akisafisha tu basi mengine haangalii.
Wale wanawake wageni nilioambiwa wanamsubiri mke wangu walikuwa wakiniangalia sana,lakini nilipanga kumsema mke wangu,kwanini anapenda watu wanasubiri nyumbani ikiwa yeye hayupo.
Dunia ya sasa usalama ni mdogo mno ,ni jambo la hatari kumuamini mtu hata kama ni ndugu wa tumbo moja sembuse watu baki.nilijiwazia.
Shemeji samahani ,utakuwa labda umeongea na mkeo ujue yupo wapi maana sisi tunamsubiri yeye,aliuliza mmoja wa wale wageni.
Mimi yule ni mke wangu na sijaambiwa ana matatizo,na sioni haja ya kumpigia simu kwani si atarudi?niliwajibu kishujaa nikiwa sipendi uwepo wao kisha nikaingia ndani chumbani nikaanza kukaguakagua vitu mara nifungue droo hii mara nivute hiki,
Mara paaap nikakutana na mizigo,pesa nyingi tu.
Mmmmmh hizi pesa za nani halafu mbona mpya na nyingi?
Mke wangu amepata wapi?
Na kwanini akae na pesa ndani asiniambie amepata wapi?
Mzigo mpya wenye nembo ya benki fulani maarufu nchini.
Halafu huyu ameshaanza kiburi siku hizi mambo yake mengi sana haniambii nashtuka vitu vipya mara hiki mara kile.ngoja arudi atanieleza.nilipanga kumhoji maana yasije kunikuta ya Shabani aliyeachana na mkewe.
Nilitoka nikija usawa wa sebule huku kupitia dirishani nikiliona gari la mke wangu linakuja
Huku wale wanawake wakimsogelea na kuonesha kwa ishara kuwa mume wako yupo ndani.alipaki gari kisha akaanza kuja ndani ,nikaketi huku nikijaribu kuweka sura ngumu ili nimsome ana jipya gani.wakati huo giza linaingia.
Jifunze,
Elimika,
Burudika.
Loading...............
Muongeze kimojaNourhan nimekupiga viwili au niongeze viwe vitatu,[emoji23]
Pamoja mkuuu,shusha vitu mzee wa yangaSEHEMU YA HAMSINI NA SABA
Ndugu msomaji wa simulizi hii,
Si kila jambo ni la kujaribu kwa kutaka heshima au uogopwe ohooooo...
Sasa endelea......
Nilipiga simu mara kadhaa lakini haikupokelewa,nikaamua kuendelea na kazi zingine huku kila mara nikipiga,najua yupo dukani na si rahisi kuwa mbali na simu sasa kwanini hapokei?
Nilijiuliza huku roho ya wivu ikiniingia kwa mara ya kwanza tangu nimuoe mke wangu,kwanza niliwaza namna milivyomfanyia nikawaza kuwa naye ni binadamu anayoyafanya nyuma ya pazia siyajui,na kuendelea kuleta jeuri basi nitakuwa kama nimemruhusu afanye ayawezayo . maana kwanza kuna mzigo wa pesa nimeuona ndani sijui ni sponsor gani katoa.
Na mke wangu naye ni mzuri na ndiyo maana watu hutuita mapacha,akiamua kutumia uzuri wake kujipatia riziki kwenye hii Dunia ya digitali,sina uwezo wa kubaini jambo labda kwa bahati.
Basi ikawa kila simu ikiita najua ni yeye kumbe ni watu wengine tu,
Nikituma sms hazijibiwi,weweeee siku ya jumanne ikawa mbaya kwangu huku hasira ikija na kutoka
Au nikampige maana huyu hapokei simu kisa niliyomfanyia jana,sasa nitamuonesha kuwa mimi ni nani na atanieleza zile pesa ni za nani!
Na hata kitendo cha watu kujakuja nyumbani pale ,ngoja nikampige marufuku,hawezi kuniletea mishangingi na mijitu iliyokosa mabwana ,pale ni kwangu na siyo danguro au kasino,halafu ngoja nitahakikisha anavunja urafiki na wale watu kwasababu sidhani kama ni marafiki sahihi.nilijiwazia huku nikitafuta sababu hata zisizo na mashiko lengo nikamgombeze mke wangu.
Lakini ikawa kila baada ya dakika kadhaa napiga simu,lakini haikupokelewa.
Baada ya muda fulani simu iliita mpigaji akiwa ni dada wa kazi,
Nikapokea kwa pupa.
Hey niambie kuna habari gani hapo kwema, niliuliza.
Ni kwema ilaaaaaa ,......dada wa kazi aliongea kwa kubabaika kisha akanitumia sms iliyosomeka hivi,
Dada kasema hataki usumbufu,anasema usimpigie,ila samahani shemeji mimi sijui ana maana gani na nimefikisha ujumbe tu,na kila nikimkatalia kuwa jambo hili ni gumu kwangu ananilazimisha.
Niliamua kutulia huku nikishusha pumzi ndeeeefu kwasababu nilikuwa nawaza mambo mengi sana yenye wivu ndani yake.
Muda wa lunch tuliongozana kama wanne ,wanaume watatu, mwanamke mmoja ambaye ndiye aliyetualika huku kila mtu akishangaa imekuwaje kwa Veronica tunayemjua kwa ubahili akalipe yeye ,tukajikuta kila mmoja anatabasamu.
Nilijitahidi kuificha ile hali isionekane kwa watu na kwa kiasi fulani nilifanikiwa,ila ilikuwa ni moja ya siku mbaya kwangu.
Muda wa kuondoka ulifika huku huku
Ulifika huku nikiwa nalaumu foleni kama vile ndiyo kwanza naiona kumbe ni kawaida kutokana na miundo mbinu yenyewe,lakini hata hivyo watu wanapiga hatua,ni rahisi sana mtu kumiliki usafiri tofauti na zamani,hii ni new era.
Nilifika nyumbani huku nikijaribu kuweka uso wa mbuzi , mdomoni nikipangilia maneno ya mashambulizi yatakayonipa points .
Lakini mke wangu aliinuka na kuja kunisalimia huku akinipokea handbag........
Vipi habari za kazi mume wangu ,
alisalimia.
Ni nzuri tu vipi mmeshindaje hapa,
Na mbona dukani hujaenda huoni kama utapoteza wateja, kumbuka watu tunapenda kuona sehemu ambayo iko available masaa 24.
niliongea huku nikishangaa utulivu wa mke wangu licha ya kuwa tuna kasoro zetu.
Niliingia ndani nika change nguo kisha nikatoka na panga nikiwa nazuga kukata kata majani ya mgomba huku nikimwangalia mke wangu na kilemba chake,huruma ilijaa,mawazo yaligonga kichwa, nilitupa panga pale chini na kuamua kurudi ndani kisha nikamuita mke wangu aje ndani chumbani .
Mke wangu mbona hukupokea simu nimepiga zaidi ya masaa manne kila baada ya dakika kadhaa ,vipi niambie kulikuwa na tatizo gani.
Niliuliza kwa upole.
Tatizo lipo,ila labda nikuulize kitu Mume wangu, kwasababu nakuogopa nahisi nipo na mtu mwenye ukichaa ,japo samahani kama nakutukana ila tambua nashindwa kabisa nikuweke kwenye fungu gani.aliweka kituo mke wangu.
Sawa ,najua umegundua kuwa nimechukia lakini hujui sababu .
Ila naomba kujua pesa ambazo zipo humu ndani ni za nani.
hapa nilibadilika kidogo sikuweka sura ya masihara.
Mbona hukuuliza mara tu baada ya kuziona huoni kama utapoteza ushahidi ,hivi kwa mfano tupo mahakamani unaweza kuonesha hizo pesa? Mke wangu ajibu kiupole.
Niliinuka kama kipanga na kwenda kufungua droo ya lile kabati lakini ilionesha imefungwa.
Pesa niliziona humu ,hebu nioneshe funguo na leo utanieleza nani kakupa hizo hela.sikuonesha utani.
Aliinuka na kutoa funguo zilizokuwa kwenye mkoba wake na kunisaidia kufungua huku nikiziona zile pesa kama nilivyoziona jana.
Haya (huku nikitaja jina lake halisi)
Niambie umepata wapi pesa zote hizi ? niliuliza nikiwa sina masikhara kabisa
Daniel,wewe ni mume wangu tena nakupenda sana,si kwasababu unanifanyia mazuri sana ila ni kwasababu kuu mbili,
Kwanza wewe ni baba wa wanangu na unawajibika vyema kama mume na baba wa familia.
Pili ni kwasababu tu nimekuzoea ,yaani naishi na wewe kimazoea.lakini kiukweli nje ya hapo sikupendi Daniel,laiti ningeambiwa nirudi zama za usichana wangu halafu nichague ni mume gani niolewe naye , sidhani kama kwenye miamoja bora ungekuwepo.
Naomba usichukie kwasababu nimekuambia sikupendi,
Bali nimeamua kukwambia ukweli,
Tabia zako haziniridhishi ,hebu fikiria umekaa huko mkoani kwa wiki tatu halafu unafika hapa unanuna tu ,
haya tufanye hizi pesa za watu ndiyo zimekuudhi kwanini usingeuliza,
Mbona kama siyo Daniel ninayekujua au unayejulikana na wengi.
Ni mjanja,ni mwenye ushawishi,ni mtu msomi kiasi chake,unaaminiwa lakini sasa hizi umekuwa kama mlevi wa vilabuni haupo kama zamani au unataka kuoa,maana kuoa ndiyo maana unanicharura charura kisha uone nitafanyaje.
Mtu nakungojea kwa hamu akili yangu inajiandaa kwa hamu mume anarudi,lakini badala yake unarudi na kuniongezea maumivu,sasa nagundua huenda hata ulikoenda hukwenda kazini bali ni kwa mwanamke mwingine.
Sasa nikwambie hivi mimi (akijitaja jina halisi) nakuruhusu fanya chochote kuanzia muda huu kama unataka kuniacha niache tu baba,hakuna sababu ya kujisumbua kutafuta visingizio visivyo na msingi ,nipo radhi kuondoka sitajuta kuyaanza upya maisha.
aliongea kisha akainuka na kuchukua Documents fulani kwenye mkoba wake akanipa.
Hizo karatasi ni za kikundi chetu cha kipindi kile na hizi ni pesa tumekopeshwa na kama mbunge alivyokuwa ametuahidi ,na jana tulifanikiwa kutoa hicho kiasi unachokiona ili tujue pakuanzia,kuna watu walikuja kwaajili ya kikao tupange tuanze na mradi gani kati ya miradi kadhaa tuliyonayo.na leo ilikuwa ni siku ya kikao husika ila nimeshindwa kwasababu Daniel umeharibu siku yangu vilivyo nashindwa nifanyeje.
Najua kikundi hiki hukukipenda tangu mwanzo na ndiyo maana hata hujui nina nafasi gani au naaminika vipi kwenye chama.
Tukiwa tunaendelea na maongezi dada wa kazi aliita kuashiria kuna ugeni nje.nilitoka na kukutana na sura za akina mama kama nane zikiwa hazina tabasamu kabisa.
Mkeo yuko wapi , anapigiwa simu hapokei tangu asubuhi na hatumuelewi.waliongea huku wakilazimisha kuingia ndani kwa nguvu.
Jifunze,
Elimika,
Burudika.
Itaendelea.............
Kwani ukisoma usipo soma unapungukiwa niniTupia basi story unataka ubembelezwe kama vile unaombwa k.
Saa kumi jioni usikose kuchungulia,Tupia basi story unataka ubembelezwe kama vile unaombwa k.
sawa tunasubiriSaa kumi jioni usikose kuchungulia,
Lakini punguza lugha zisizofaa, maisha ni hayahaya
Utoto mwingiSaa kumi jioni usikose kuchungulia,
Lakini punguza lugha zisizofaa, maisha ni hayahaya