Simulizi: Harakati za maisha

Simulizi: Harakati za maisha

SEHEMU YA MWISHO.

Ilifikia hatua nikataka kuwashirikisha watu maana maji yalishafika kooni ama shingoni , Daniel nina jeuri, kiburi na najiamini ila kwa mke wangu nilikwama, loh!!
Mwanamke ni kiumbe mwenye nguvu ya ajabu mno tena sana wanaume acha tufe mapema.

Watu wengi sana wanateswa na mapenzi lakini kutokana na vifua vyao na Siri zao wanajikuta wanaumia ndani kwa ndani, all weman wakipenda wamependa, wakiamua kuvumilia wanavumilia, tena unaweza sema labda hawana pa kwenda, ila usiombe wakakuchoka , yaani mwanamke akifikia mwisho wa kuwa na wewe mmmmh, weka mbali na watoto.

Ndani ya siku tatu mke wangu hakupokea simu, niliwaza na kuwazua, nikipanga na kupangua lakini haikusaidia chochote.
Nilikula ili nisijekufa ila sikuiona ladha ya chakula.

Nakumbuka asubuhi sana meneja aliniita na kunitaka nijiandae na safari huku akinikumbusha kupeleka CV zangu upya ofisini , sikujua maana yake lakini nilitimiza nachoambiwa,
Nikapewa siku nne za kujiandaa na safari huku niliruhusiwa kubeba Kila kilicho changu mle ofisini, kwani niliambiwa nikirudi huenda nikafikia sehemu tofauti na ile.

Nakumbuka nilienda kwa katekista mmoja aliye mtaa wa pili kutoka kwangu , nikawa namueleza habari za wife, kuwa simpati kwenye simu kwani katoroka na pia hapokei simu.

Kwanza Katekista alishangaa huku akidai siyo muda mrefu mke wangu alikuwa anaongea na mke wake na anaonesha ni mwenye amani na walijua yupo tu nyumbani na pia hajawaambia kama hayupo , lakini pia walinilaumu kwa kitendo cha kukaa muda wote pasi na kutoa taarifa popote maana ilikuwa ni ndoa hivyo alichokifanya mke wangu hakikuwa sahihi na angetafutwa na pia angejibu mashtaka.
alifafanua katekista.

Baada ya hapo mke wa katekista alikuja Kisha akapiga simu mbele yangu, mke wangu akapokea kisha simu nikapewa Mimi lakini baada ya kusikia simu yangu alikata.
Katekista na mkewe waliangaliana Kisha nikatoka bila kuwaaga , lakini simu yangu iliita mpigaji akiwa mke wangu,

Nilitulia huku nikipark ngalawa pembeni, huku nikipanga kuwa na nidhamu na maongezi yale.

Mke wangu kumbuka nakupenda, kumbuka kwasasa sisi ni watu wazima jaribu kuwaza na kufikiria ni taswira gani tunawaonesha watoto wetu, vipi wakisikia hizi taarifa huoni zitaathiri maendeleo yao ya shule?
niliongea kwa sauti ya chini yenye kujihurumia.

Acha maigizo Daniel,
Nakuita Daniel kwasababu hata sifa ya kuwa mume wangu sidhani kama unayo lakini nikwambie tu kuwa , Sina mengi zaidi ya kusema sihitaji kuwa na wewe, hapa napumzisha akili yangu tu kisha taratibu za kuachana au kuvunja ndoa zitafuata, siwezi ishi na wewe tena , ni mlevi, hujiheshimu, na huniheshimu, ni mtu mwenye majanga kila siku , unatengeneza maadui kwa makusudi Kila siku, jamii haikukubali inakuona kama inaishi na mtu mwenye wazimu na kichaa,.

Niliolewa na wewe kwasababu ya Sheria mtu akifika umri fulani lazima awe na mwenza wa kuanzisha maisha, ni kweli wewe ni mtafutaji, ni mtu mwenye kuijali familia na mambo mengine mengi lakini hukujali hisia zangu, Kila nilichojaribu kukifanya ulipinga, Leo hii hata marafiki zangu wengi walinikataa sababu yako, mtu pekee nilikuwa namuelewa ni Jane ambaye naye ukamuumiza,na kumsababishia maumivu makubwa. Sasa baba imetosha wewe tafuta mke uoe Mimi siwezi kuishi na wewe , tutakuja tufe kwa moto humo ndani si nasikia Kuna watu walipanga kuchoma nyumba yako?

Sasa kwanini nife wakati inawezekana kukuepuka na hata wanangu nimewaambia wasirudi hapo hata likizo ikifika, hata hao wafanyakazi wako nimewaambia waondoke na huyo dada wa kazi nilimpa na nauli yake aondoke kabisa.aliweka kituo mke wangu.

Sasa uko wapi nije maana Nina maongezi na wewe , tafadhali nihurumie mke wangu umeondoka kipindi nakuhitaji sana. Kumbuka Kila lenye mwanzo halikosi mwisho. nilimbembeleza lakini alikata simu huku licha ya kupiga mara kadhaa sikufanikiwa.

Niliwaambia wanajumuiya wake juu ya maamuzi ya mke wangu lakini walidai hawawezi kunisaidia kwasababu kwanza huwa sisali na pia tabia zangu zinajulikana mno hivyo itakuwa ngumu.

Nikahamia kwa wachungaji ambao walinipa moyo kuwa ni shetani yupo kazini na muda wowote mke wangu atarudi kama zamani .

Baada ya hapo niliondoka nchini nikiwa bado sijafanikisha lolote juu ya kurudi kwa mke wangu.

Nikiwa kwenye Moja ya Nchi nzuri yenye kudumisha mila na tamaduni
za muafrika , nilienjoy na kujifunza vingi sana, huku nikificha huzuni na kulazimisha furaha ili tu nisije kuwa kituko kwenye semina ile muhimu.

Siku moja nikiwa nimelala usiku, nilimpigia mke wangu kwa namba nyingine, ya Nchi ya kule akapokea ...

Mimi ni mume wako Niko nchi ya (nikitaja jina) vipi kwema huko!! nilisalimia

Ni kwema, vipi Nini kimekupeleka huko? aliuliza.

Nimeamua kutoka kwasababu wewe unaniumiza mno , nimeamua kuja kupunguza mawazo, mke wangu tafadhali ikiwezekana rudisha moyo wako kumbuka tutaharibu saikolojia ya watoto wetu. Niliweka kituo huku nikigundua ule ukali wa mwanzo umepungua.(nilimdanganya sikutaka ajue kama ni mambo ya kiofisi)

Usinichekeshe, wataharibika kivipi , na mbona wanajua kama sipo na wewe, ningekufa wasingesoma?
Nilipita shule zote wanakosoma na nimeshawaambia Mimi sipo nyumbani, lazima wajue na wazoee tu niwafiche ili iweje?

Tuliongea mengi huku msimamo wake ukiwa vile vile hakutaka kabisa ushirikiano na mimi.


Naam, siku za semina ziliisha huku nikiwa na madini kibao, hakika Mungu ni mwema, nakumbuka nilirudi Nchini huku nikihuzunika maana mtu pekee wa kunipokea alipaswa awe mke wangu lakini
Kweli shetani anajua anachokifanya.

Baada ya kwenda ofisini niliambiwa natakiwa kuandaa taarifa fulani kama feedback kutokana na nilichojifunza
Kule hivyo nikapewa wiki mbili,
Wiki ya kwanza nitaenda pembeni ya mji kwaajili ya kufanya kwa vitendo kile nilichojifunza lakini , wiki ya pili nitaandaa taarifa nyingine inayohusu computer.

Nikiwa pembeni ya mji nilikumbuka ni Kijiji nakifahamu niliwahi kufika kwaajili ya kumtafuta mtaalamu au mganga wa jadi ambaye alinikatalia kuwa ni kazi alishaiacha na kuamua kumrudia mwenyezi MUNGU.

Baada ya kumaliza kilichonipeleka, niliamua kwenda kumsalimia , akiwa kashanisahau , ila baada ya kumkumbusha alifurahi sana.

Enhee matatizo yako ulishayamaliza ? aliuliza.

Mzee wangu , kiukweli yaliisha ila kwasasa yapo mengine ambayo yananinyima raha mno ,Tena ni Bora Yale ya zamani nilikuwa nafarijiwa na mke wangu, lakini kwasasa mke wangu ndiye kanikimbia, yaani yapata mwezi na kitu sasa. Nilifafanua.

(Kwanza akacheka sana tu)
Loh mwanangu kweli una matatizo, lakini si uoe mwingine, mbona wanawake ni wengi mno , isitoshe wewe ni mwanaume unayeonekana si haba Sasa kwanini uhangaike na wanawake, hujui dawa ya moto ni Moto? aliuliza.

Mzee wangu,
Ingekuwa nimemuoa miaka mitano, au miaka ya hivi karibuni , ningemuacha lakini tatizo nimezeeka naye, yaani naona anguko mbele yangu ikiwa nitaoa kwa kutaka kuziba pengo, na pia sipo tayari kuoa kirahisi hivyo. Nilijibu Kisha akakubali kwa kutikisa kichwa.

Sasa mwanangu Mimi nitakusaidia kwa hilo, unajua Mungu hataki ramli chonganishi na shirki zingine ila kwa hili ngoja tumuombe Mungu, zipo sura za kuomba ustahimilivu kama wako kwanza nakuonea huruma sana ujue mke anauma na mbaya zaidi hujui kajificha kwa nani hapo na wivu unatafuna mifupa yako. alifafanua huku akizidi kuniumiza.

Tukakubaliana kuwa nikaoge niwe safi Kisha nirudi nikiwa nadhifu.
Kisha nikaenda pale gesti bubu nikajiswafi na kurudi kwa yule Mzee ambaye naye nilimkuta akiwa kwenye kanzu yake nzuri na safi licha ya watu wa vijijini kuwa na muonekano fulani rural.

Tuliingia ndani akaanza kusoma Aya kwa kiarabu huku akiwa ni mwenye hisia Kali , ilifikia hatua Hadi machozi yalimtoka huenda alimaanisha alichokuwa anakisoma.

Baada ya hapo akasema nimfuatishe akisoma maneno fulani, nikafanya vile Kisha tukaagana huku akinihakikishia kuwa kama huyo mkeo ni halali yako na Mungu alipanga uwe na wewe basi atarudi, ikiwa ni kinyume chake nayo ni kheri pia kwani mwenyezi Mungu anajua Kila analolifanya, tukapeana namba za simu Kisha nikaondoka. Nikiwa na tumaini jipya.

Basi niliendelea kumsumbua kwa kumpigia simu , hatimaye akaniambia alipo, alikuwa kwa ndugu zake fulani ambao ni wenye uwezo mzuri tu kipesa hawapo kinyonge ,japo ilikuwa ngumu kuwashawishi kumchukua lakini hekima na busara nilizotumia huku nikimshirikisha Mungu kwa Kila hatua, nikafanikiwa kumrudisha nyumbani.

Maisha mapya ofisini yalikuwa poa sana tena mno, heshima iliongezeka , wigo wa kufahamiana na watu uliongezeka, na mengine mengi mazuri, ila kumbuka tangu mke wangu arudi tulikaa vyumba tofauti kwa takribani mwezi mzima, huku nikigundua mapenzi yake kwangu yalishuka kwa kiasi kikubwa kama siyo kuporomoka kabisa.nilionesha
Udhaifu wa wazi kwa mke wangu
Kiasi cha kunigeuzageuza kama samaki kwenye kikaango.

Lakini ni udhaifu wangu ,wapo ambao mke hawasumbui kwa wanaacha mara moja lakini nao wana madhaifu sehemu nyingine,ndicho tulivyo ,mimi nikilizwa na hiki mwingine atalizwa na kile,ambacho huenda ni cha kijinga kwangu.

Dharau, vitisho vya kukimbiwa tena na mambo kibao ilikuwa ni kawaida kuambiwa, kifupi ni baadaye sana nilifanikiwa kuirudisha ndoa yangu kama zamani huku nikiwa natii vitu kibao ili tu ninusuru ndoa yangu.wanaume wenzangu wanajua.

Maisha yaliendelea hivyohivyo ,Kila kitu kikirudi taratibu, na kulingana na umri wangu vipo nilivyopunguza kama pombe,vipo nilivyoviacha na kufanikiwa kurudisha amani na upendo kwenye familia, jamii na hata Imani kwa waajiri wangu.

Harakati ni nyingi huwezi kuandika Mikasa ukaimaliza hii ni sehemu ya mwisho kwenye simulizi hii,
Huku lengo kubwa likiwa ni kujifunza, kuelimika na kuburudika pia.

1. Ndugu wasomaji na wafuatiliaji, kwa wote niliowakwaza haswa kuchelewa kwa simulizi mnisamehe tu,mambo ni mengi mno na pia members waliokwazana wenyewe kwa wenyewe, msameheane
Ni kawaida tu kwenye maisha.

2.Makosa ya kiuandishi, typing error na mengineyo mnisamehe sometimes haraka haraka inachangia.

Nawapenda sana wote.

Jack Daniel.
Hatimae 🙏Asante sana JD Be bless Samson 😁
 
Back
Top Bottom