Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #41
SEHEMU YA 23
Mama mchungaji hakuamini kuwa kundi lote lile la watu lilikuwa limemaliza safari yao mbele yake,mapigo ya moyo yaliongeza kasi sana aliukamata mkoba wake kwa nguvu mno kwani kwa upande mwingine alidhani wale pale ni wezi wanataka kumwibia kwa staili ya kumzingira.
"nini? Nini?" kwa uoga mama mchungaji alianza kujitetea mbele ya kundi lile,ile sukumwa sukumwa ya hapa na pale ilipelekea kuanguka kwake,lakini kabla hajafika chini tayari ile kanga aliyokuwa amejitanda kichwani ilikuwa imetolewa na kumwacha uso na kichwa wazi.
"ana bahati kumbe mwanamke kweli" alisema mmoja kati ya waliokuwa kwenye lile kundi kisha kila mmoja akatoweka na kumwacha mama mchungaji peke yake eneo lile. Juhudi zake za kuubana mkoba wake zilikwisha wakati anapepesuka kuelekea chini ni katika kipindi hicho hicho mikono ya kijanja ya kijana mmoja ilizama na kutoka na simu moja ya mama mchungaji.
"Mungu wangu na simu wamechukua maskini wee nitafanyaje sasa mimi" alijiuliza mama mchungaji huku akitazamwa na wananchi wengine kana kwamba ni mwendawazimu fulani aliyetoroka hospitali,mwili wake ulijaa vumbi na nywele zake zilikuwa zimevurugwa sana na wale vijana wakati wa varangati lile.
"eeh! Mwenyezi Mungu nisaidie waumini wa kanisa wasiwepo mitaa hii" huku akitetemeka alizungumza na wakati huo huo akijaribu kurudishia khanga yake kichwani na usoni. Kwa kuelewa kwamba heshima yake imeshuka tayari eneo lile mama huyu hakutaka kuongeleshana na mtu yeyote badala yake hatua kwa hatua akajitoa eneo lile kuelekea katika mitaa iliyochangamka zaidi kutokana na wingi wa nyumba zilizojengwa pale na kusababisha msongamano wa watu.
"sijui ni njia hii hapa sijui ni kule,mama yangu leo napotea hapa na sijui itakuwaje sasa..kwaheri ndoa yangu" alijisemea kwa upole na sauti ya chini mama mchungaji huku akitazama pete aliyovishwa na mchungaji siku walipofunga ndoa takatifu kanisani.
"Zinduna..nasema niachie we m¥€&** tena malaya mkubwa,niachie nisije nikakuchania blauzi yako huo mtindi ukabaki nje sasa hivi"
"umchanie nani blauzi,unaijua thamani yake wewe,nakuuliza bwana yako anaweza kununua? Ashura nitakukun'guta mpaka uione dunia chungu"
ulikuwa ni ugomvi kati ya wanawake wawili ambao kwa hali na matusi ya nguoni waliyotukanana walionekana kuwa katika mtafaruku mkubwa wa kugombea bwana,umati uliowazunguka haukuwa hata na wazo la kuwatenganisha katika ugomvi wao,zilikuwepo pande mbili na kila mmoja akishabikia mtu wake ili aweze kushinda.
Mama mchungaji alipita jirani kabisa na eneo hilo macho yake yalivutia kwenda kutazama visa alivyovikosa kwa siku nyingi tangu aolewe na mchungaji.
"he! Sio zinduna yule...ha! Na yule pale mbona ni Ashura" alisema kimoyomoyo mama mchungaji alipofika eneo lile
"au nawafananisha jamani" alizidi kuwaza.
Mama mchungaji hakuamini kuwa kundi lote lile la watu lilikuwa limemaliza safari yao mbele yake,mapigo ya moyo yaliongeza kasi sana aliukamata mkoba wake kwa nguvu mno kwani kwa upande mwingine alidhani wale pale ni wezi wanataka kumwibia kwa staili ya kumzingira.
"nini? Nini?" kwa uoga mama mchungaji alianza kujitetea mbele ya kundi lile,ile sukumwa sukumwa ya hapa na pale ilipelekea kuanguka kwake,lakini kabla hajafika chini tayari ile kanga aliyokuwa amejitanda kichwani ilikuwa imetolewa na kumwacha uso na kichwa wazi.
"ana bahati kumbe mwanamke kweli" alisema mmoja kati ya waliokuwa kwenye lile kundi kisha kila mmoja akatoweka na kumwacha mama mchungaji peke yake eneo lile. Juhudi zake za kuubana mkoba wake zilikwisha wakati anapepesuka kuelekea chini ni katika kipindi hicho hicho mikono ya kijanja ya kijana mmoja ilizama na kutoka na simu moja ya mama mchungaji.
"Mungu wangu na simu wamechukua maskini wee nitafanyaje sasa mimi" alijiuliza mama mchungaji huku akitazamwa na wananchi wengine kana kwamba ni mwendawazimu fulani aliyetoroka hospitali,mwili wake ulijaa vumbi na nywele zake zilikuwa zimevurugwa sana na wale vijana wakati wa varangati lile.
"eeh! Mwenyezi Mungu nisaidie waumini wa kanisa wasiwepo mitaa hii" huku akitetemeka alizungumza na wakati huo huo akijaribu kurudishia khanga yake kichwani na usoni. Kwa kuelewa kwamba heshima yake imeshuka tayari eneo lile mama huyu hakutaka kuongeleshana na mtu yeyote badala yake hatua kwa hatua akajitoa eneo lile kuelekea katika mitaa iliyochangamka zaidi kutokana na wingi wa nyumba zilizojengwa pale na kusababisha msongamano wa watu.
"sijui ni njia hii hapa sijui ni kule,mama yangu leo napotea hapa na sijui itakuwaje sasa..kwaheri ndoa yangu" alijisemea kwa upole na sauti ya chini mama mchungaji huku akitazama pete aliyovishwa na mchungaji siku walipofunga ndoa takatifu kanisani.
"Zinduna..nasema niachie we m¥€&** tena malaya mkubwa,niachie nisije nikakuchania blauzi yako huo mtindi ukabaki nje sasa hivi"
"umchanie nani blauzi,unaijua thamani yake wewe,nakuuliza bwana yako anaweza kununua? Ashura nitakukun'guta mpaka uione dunia chungu"
ulikuwa ni ugomvi kati ya wanawake wawili ambao kwa hali na matusi ya nguoni waliyotukanana walionekana kuwa katika mtafaruku mkubwa wa kugombea bwana,umati uliowazunguka haukuwa hata na wazo la kuwatenganisha katika ugomvi wao,zilikuwepo pande mbili na kila mmoja akishabikia mtu wake ili aweze kushinda.
Mama mchungaji alipita jirani kabisa na eneo hilo macho yake yalivutia kwenda kutazama visa alivyovikosa kwa siku nyingi tangu aolewe na mchungaji.
"he! Sio zinduna yule...ha! Na yule pale mbona ni Ashura" alisema kimoyomoyo mama mchungaji alipofika eneo lile
"au nawafananisha jamani" alizidi kuwaza.