DR SANTOS
JF-Expert Member
- Mar 11, 2019
- 12,846
- 28,106
Mwanzo
“Huyu tumuue kwani bosi amemleta huku lengo lake afe tu”.
“Hapana nafikiri kumuua sio jambo jema, kiubinadamu pia huyu ni mwanaume mwenzetu”
“Kibarua kitaota nyasi shauri yako,sasa unashauri nini”.
“Tumtupe kwenye maji tu akacheze na papa huko”
Mabishano hayo niliweza kuyapata vyema, yalipenya kwenye ngoma za masikio yangu barabara kabisa kwani hakukua na kelele yoyote ambayo ingeweza kufanya nisisikie kilicho zungumzwa zaidi ya sauti za mawimbi ya bahari ya hindi, pamoja na injini ya boti ambayo ilizidi kuchanja mbuga kwani mlio wa injini ulionesha dhahiri boti hio ilikua ikienda kwa kasi sana, baridi njaa kali pamoja na kiu vilizidi kuniandama.
Nikiwa kwenye chemba ndogo ya boti maalum kabisa kwaajili ya kuhifadhi vifaa vya ukarabati , pamoja na madumu ya mafuta na makorokoro mengine yaliyofanya chemba hio kuwa na harufu ya dizeli na mafuta ya petrol ambayo ilifanya mavazi yangu yaweze kunukia petrol vile vile.
Muda mchache baada ya mazungumzo hayo kusikika mlango wa chemba ile uliweza kufunguliwa na kijana mmoja ambaye kwa makadirio alikua na umri wa miaka ishirini hadi ishirini na nne, ambaye alinipokea kwa maneno ya kejeli “nataka leo nikupigishe stori na papa mzee baba”.
Aliongea kijana huyo ambapo sikutaka kubishana nae kwanza nilihitaji kukusanya nguvu pia kunyoosha viungo vyangu vizuri na ukizingatia nilikua sijaona jua kwa muda mrefu sana zaidi ya kukaa kwenye chumba chenye kiza kinene cha boti ile.
Tofauti na nilivyotarajia kijana Yule alizidi kunipa kejeli na sikujua kwanini alifanya hivyo kwani nilimuona ni mbwa tu tena koko aliyejishikiza kwenye utajiri haramu wa Mohamed bakantan.
Nilimtazama kwa hasira sana kijana Yule ambapo niliona akizidi kunishuhia maneno ya matusi, hakika kwa binadamu wa kawaida asingeliweza kuvumilia kabisa, kutukanwa na mwanaume ambaye anaona angeweza kummudu.
Nilimkadiria nikatazama na kamba walizonifunga niliwaona ni wazembe sana na sikutaka kupigana wala kujibizana na yoyote kwa chochote, nilichohitaji kwa muda huo ni kuhakikisha najitoa mikononi mwa Mohamed bakantan na timu yake.
“nifungue hizi kamba kama wewe ni mwanaume, nikuzibue”.
Niliongea kwa hasira nikimchimba mkwara kijana huyo ambapo hii ilipelekea apunguze kuongea kwani nilimtisha sana na aliweza kutambua mimi ni mtu wa aina gani, jua lilizidi kuwaka na kukomaa kabisa hii ilionesha ulikua ni wakati wa mchana.
Nikiwa sielewi nini hatma yangu,njaa nayo ilikua kama rafiki yangu wa karibu hakika nilikua na wakati mgumu sana, bado boti ilizidi kuchana mawimbi kabla ya kijana mmoja kunifuata na kunipa chakula nile ambapo ilikua ni mkate na soda kama kawaida na maneno ya kejeli yalihusika.
“Wewe fala kula kwa mara ya mwisho tutakutupa kwenye maji ukawe rafiki wa papa mkapige soga huko majinii mbwa wewe, ili siku nyingine uache kufuatilia mabinti za watu. Unajifanya unajua kupenda eeeeh”.
Sikuyajali maneno hayo nilichojali nimekula chakula ambacho niliamini kitaniongezea nguvu. Kwakua ilikua ni kipindi cha baridi kali kuna maeneo jua halikuwaka kabisa siku hio na kupelekea maji kuganda na kutengeneza miamba migumu ya barafu, boti yetu iligonga moja ya mwamba na kutoboka kupelekea maji yanze kujaa nayo kuzama taratibu.
Haraka nilijifungua kamba zile nilichojali ni kujiokoa nafsi yangu tu bila kusahau kumlipa fadhila Yule aliyenitukana
“wewe mbwa wa bakantan hebu kafie mbele, na utaliwa na papa leo nyau wewe”.
Baada ya kumaliza kumpa maneno ya kejeli nilijitosa baharini bila kusahau kubeba koti maalumu kabisa kwa kutozama majini, nikiwaacha wakiendelea kuhaha na boti lao.
“Huyu tumuue kwani bosi amemleta huku lengo lake afe tu”.
“Hapana nafikiri kumuua sio jambo jema, kiubinadamu pia huyu ni mwanaume mwenzetu”
“Kibarua kitaota nyasi shauri yako,sasa unashauri nini”.
“Tumtupe kwenye maji tu akacheze na papa huko”
Mabishano hayo niliweza kuyapata vyema, yalipenya kwenye ngoma za masikio yangu barabara kabisa kwani hakukua na kelele yoyote ambayo ingeweza kufanya nisisikie kilicho zungumzwa zaidi ya sauti za mawimbi ya bahari ya hindi, pamoja na injini ya boti ambayo ilizidi kuchanja mbuga kwani mlio wa injini ulionesha dhahiri boti hio ilikua ikienda kwa kasi sana, baridi njaa kali pamoja na kiu vilizidi kuniandama.
Nikiwa kwenye chemba ndogo ya boti maalum kabisa kwaajili ya kuhifadhi vifaa vya ukarabati , pamoja na madumu ya mafuta na makorokoro mengine yaliyofanya chemba hio kuwa na harufu ya dizeli na mafuta ya petrol ambayo ilifanya mavazi yangu yaweze kunukia petrol vile vile.
Muda mchache baada ya mazungumzo hayo kusikika mlango wa chemba ile uliweza kufunguliwa na kijana mmoja ambaye kwa makadirio alikua na umri wa miaka ishirini hadi ishirini na nne, ambaye alinipokea kwa maneno ya kejeli “nataka leo nikupigishe stori na papa mzee baba”.
Aliongea kijana huyo ambapo sikutaka kubishana nae kwanza nilihitaji kukusanya nguvu pia kunyoosha viungo vyangu vizuri na ukizingatia nilikua sijaona jua kwa muda mrefu sana zaidi ya kukaa kwenye chumba chenye kiza kinene cha boti ile.
Tofauti na nilivyotarajia kijana Yule alizidi kunipa kejeli na sikujua kwanini alifanya hivyo kwani nilimuona ni mbwa tu tena koko aliyejishikiza kwenye utajiri haramu wa Mohamed bakantan.
Nilimtazama kwa hasira sana kijana Yule ambapo niliona akizidi kunishuhia maneno ya matusi, hakika kwa binadamu wa kawaida asingeliweza kuvumilia kabisa, kutukanwa na mwanaume ambaye anaona angeweza kummudu.
Nilimkadiria nikatazama na kamba walizonifunga niliwaona ni wazembe sana na sikutaka kupigana wala kujibizana na yoyote kwa chochote, nilichohitaji kwa muda huo ni kuhakikisha najitoa mikononi mwa Mohamed bakantan na timu yake.
“nifungue hizi kamba kama wewe ni mwanaume, nikuzibue”.
Niliongea kwa hasira nikimchimba mkwara kijana huyo ambapo hii ilipelekea apunguze kuongea kwani nilimtisha sana na aliweza kutambua mimi ni mtu wa aina gani, jua lilizidi kuwaka na kukomaa kabisa hii ilionesha ulikua ni wakati wa mchana.
Nikiwa sielewi nini hatma yangu,njaa nayo ilikua kama rafiki yangu wa karibu hakika nilikua na wakati mgumu sana, bado boti ilizidi kuchana mawimbi kabla ya kijana mmoja kunifuata na kunipa chakula nile ambapo ilikua ni mkate na soda kama kawaida na maneno ya kejeli yalihusika.
“Wewe fala kula kwa mara ya mwisho tutakutupa kwenye maji ukawe rafiki wa papa mkapige soga huko majinii mbwa wewe, ili siku nyingine uache kufuatilia mabinti za watu. Unajifanya unajua kupenda eeeeh”.
Sikuyajali maneno hayo nilichojali nimekula chakula ambacho niliamini kitaniongezea nguvu. Kwakua ilikua ni kipindi cha baridi kali kuna maeneo jua halikuwaka kabisa siku hio na kupelekea maji kuganda na kutengeneza miamba migumu ya barafu, boti yetu iligonga moja ya mwamba na kutoboka kupelekea maji yanze kujaa nayo kuzama taratibu.
Haraka nilijifungua kamba zile nilichojali ni kujiokoa nafsi yangu tu bila kusahau kumlipa fadhila Yule aliyenitukana
“wewe mbwa wa bakantan hebu kafie mbele, na utaliwa na papa leo nyau wewe”.
Baada ya kumaliza kumpa maneno ya kejeli nilijitosa baharini bila kusahau kubeba koti maalumu kabisa kwa kutozama majini, nikiwaacha wakiendelea kuhaha na boti lao.