DR SANTOS
JF-Expert Member
- Mar 11, 2019
- 12,846
- 28,106
- Thread starter
- #41
Sura ya kumi na nne
ILIPOISHIA; “hapa uko brazil, kwenye kisiwa kilichosahaulika”. Aliongea malkia kauli iliyonifanya nistuke sana kwani sikutarajia kama ningekua brazili”.
“hmmm”. Niliishia kuguna tu kwani niliona maisha yangu yanakwenda kuishia kwenye kisiwa kilichosahaulika
SASA ENDELEA;siku za maandalizi zilikwisha na hatimaye siku ya kufanya uvamizi kwenye ufalme jirani iliwadia, hatukua na lengo baya zaidi ya kufuata vyakula tu.
Baada ya maandalizi yote kukamilika uliitishwa mkutano wa kutuaga na kututakia kila laheri katika safari ambayo ingetugharimu masaa arobaini na nane majini hadi kufika kwenye ufalme huo.
Tulipanda meli kubwa ya kivita ambayo ilikua na silaha za asili ikiwemo mishale ya moto pamoja na mafuta ya petroli, safari iliaza huku kila mmoja akitupungia mkono tukiwa tunaondoka na kukiacha kisiwa kilichosahaulika.
Majira ya usiku baridi ilikua kali sana iliyoambatana na upepo mkali wa bahari ilizdi kutuandama, sikuweza kuvumilia ijapokua nilikaa kisiwani pale kwa muda mrefu lakini sikiwahii huisikia baridi kama ile. Uzalendo ulinishinda kabisa kukaa juu ya meli na kuamua kushuka chini kwa lengo la kupumzika na kuiepuka baridi ile, si mimi tu bali kila mmoja aliyekua katika meli ile alitetemeka na ilitulazimu kukumbatiana lengo lilikua moja tu, kupata joto na hatimaye kila mmoja alipitiwa na usingizi
Tulikuja kuzinduka kukiwa kumepambazuka na jua lilishaanza kuchomoza, nahodha alichoka sana na alihitaji kupumzika, hio haikua shida nilipokea usukani na safari iliendelea, nikiwa naendelea kulisongesha jahazi alikuja sia ambaye ni mmoja wa wanajeshi na kunipa taarifa ambayo ilinistua kidogo
Hususani nilikua mgeni na masuala ya usafiri wa majini.
“mkuu kuna wanyang’anyi mbele yetu tufanyeje”. Aliongea sia kauli ambayo ilinifanya niachie usukani na kutoka hadi juu ambapo nilichukua darubini na kutazama,na niliona meli kubwa kuliko yetu ikiwa mbele yetu
“mwambie nahodha akate kona haraka tubadili uelekeo”. Niliongea lakini ni kama tulishachelewa kwani kombora kubwa lilitua kwenye meli yetu na kubomoa upande mmoja na kuifaya ianze kupitisha maji kwa kasi na kuanza kuzama taratibu.
Nilichanganyikiwa sana si kwaajili ya kuzama kwa meli bali sikua na uhakika kama ningeweza kusalimika kwa mara nyingine tena.
Na swali lilikuja akilini vipi kuhusu mabinti wale nilioongozana nao? Nikiendelea kujiuliza hayo tayari miguu yangu ilishaanza kuloa na maji baridi ya bahari kisha ,apaja yangu na kiuno kikafuata, niliamua kung’ang’ania ubao mmoja wa meli ambao ulinisaidia kuelea na nisiweze kuzama
Tayari wanyang’anyi walishafika mahali meli yetu ilipozama na walianza kuokoa mmoja baada ya mwingine ikiwemo mabinti niliokua nao msafara mmoja baada ya kuokolewa mabinti hao waliokua kumi na tisa kwa idadi name nilijisogeza maeneo ya meli ile ya wanyng’anyi lakini hawakuweza kununiona
Hakika niliona roho yangu ikiwa mkononi tena mkono usio na nguvu ambao ungeweza kuidondosha siku yoyote, saa yoyote na dakika yoyote
Pembeni ya meli ile kulikua na majina makubwa yaliyosomeka MOHAMED CARGO EXPORT LIMITED
“mungu wangu”. Nilijisemea moyoni na hasira iliwaka upya kwani nilijua bila shaka ni kampuni ya Mohamed bakantan na nilijua lazima ametoka kusafirisha mabinti kwenda kuwauza kwenye madangulo nje ya nchi.
Nilianza kukata mawimbi, kwa hasira iliyo kuu huku meli ile ikianza kuniacha, lakini niliamini ilikua ikielekea Tanzania hivyo niliogelea kufuata uelekeo wa meli ile hata iliponiacha sikukata tama nilizidi kunyoosha hivyo hivyo.
Nilichoka sana kuogelea, kwenye maji ya chumvi ambayo yalifanya macho yangu kuwa mekundu kama nimevuta kaya mbichi (bangi). Nilizidi kuogelea huku nikibadili mitindo mbalimbali ya kuogelea ambayo nilijifunza kisiwani ambako niliishi kwa muda mrefu sana ambao sikutambua ni ilikua miezi wiki au miaka.
Pumzi zilianza kuniisha kabisa mikono ilichoka na sikua na uwezo wa kuogelea tena, nilimuomba mungu aninusuru kwa mara nyingine kwani lengo langu ni kwenda kuwaokoa watu wengine na nafsi zao kutoka kwenye mikono ya Mohamed bakantan na nilipanga kumuadabisha mzee bakantan na kufichua maovu yake yote endapo tu ningeweza kukanyaga ardhi ya Tanzania.
Hakika hayo ni mawazo yaliyokitawala kichwa change huku baridi kali ikizidi kunipiga na nguvu zikizidi kuniisha,
kwa mbali niliweza kuona mwanga wa taa ya kandili ikija upande wangu, nami sikutaka kupoteza wakati nilizidi kukata mawimbi na hapo nguvu ziliniisha kabisa, kiza kinene kilitanda kwenye macho yangu.
Je nini kilifuata
ILIPOISHIA; “hapa uko brazil, kwenye kisiwa kilichosahaulika”. Aliongea malkia kauli iliyonifanya nistuke sana kwani sikutarajia kama ningekua brazili”.
“hmmm”. Niliishia kuguna tu kwani niliona maisha yangu yanakwenda kuishia kwenye kisiwa kilichosahaulika
SASA ENDELEA;siku za maandalizi zilikwisha na hatimaye siku ya kufanya uvamizi kwenye ufalme jirani iliwadia, hatukua na lengo baya zaidi ya kufuata vyakula tu.
Baada ya maandalizi yote kukamilika uliitishwa mkutano wa kutuaga na kututakia kila laheri katika safari ambayo ingetugharimu masaa arobaini na nane majini hadi kufika kwenye ufalme huo.
Tulipanda meli kubwa ya kivita ambayo ilikua na silaha za asili ikiwemo mishale ya moto pamoja na mafuta ya petroli, safari iliaza huku kila mmoja akitupungia mkono tukiwa tunaondoka na kukiacha kisiwa kilichosahaulika.
Majira ya usiku baridi ilikua kali sana iliyoambatana na upepo mkali wa bahari ilizdi kutuandama, sikuweza kuvumilia ijapokua nilikaa kisiwani pale kwa muda mrefu lakini sikiwahii huisikia baridi kama ile. Uzalendo ulinishinda kabisa kukaa juu ya meli na kuamua kushuka chini kwa lengo la kupumzika na kuiepuka baridi ile, si mimi tu bali kila mmoja aliyekua katika meli ile alitetemeka na ilitulazimu kukumbatiana lengo lilikua moja tu, kupata joto na hatimaye kila mmoja alipitiwa na usingizi
Tulikuja kuzinduka kukiwa kumepambazuka na jua lilishaanza kuchomoza, nahodha alichoka sana na alihitaji kupumzika, hio haikua shida nilipokea usukani na safari iliendelea, nikiwa naendelea kulisongesha jahazi alikuja sia ambaye ni mmoja wa wanajeshi na kunipa taarifa ambayo ilinistua kidogo
Hususani nilikua mgeni na masuala ya usafiri wa majini.
“mkuu kuna wanyang’anyi mbele yetu tufanyeje”. Aliongea sia kauli ambayo ilinifanya niachie usukani na kutoka hadi juu ambapo nilichukua darubini na kutazama,na niliona meli kubwa kuliko yetu ikiwa mbele yetu
“mwambie nahodha akate kona haraka tubadili uelekeo”. Niliongea lakini ni kama tulishachelewa kwani kombora kubwa lilitua kwenye meli yetu na kubomoa upande mmoja na kuifaya ianze kupitisha maji kwa kasi na kuanza kuzama taratibu.
Nilichanganyikiwa sana si kwaajili ya kuzama kwa meli bali sikua na uhakika kama ningeweza kusalimika kwa mara nyingine tena.
Na swali lilikuja akilini vipi kuhusu mabinti wale nilioongozana nao? Nikiendelea kujiuliza hayo tayari miguu yangu ilishaanza kuloa na maji baridi ya bahari kisha ,apaja yangu na kiuno kikafuata, niliamua kung’ang’ania ubao mmoja wa meli ambao ulinisaidia kuelea na nisiweze kuzama
Tayari wanyang’anyi walishafika mahali meli yetu ilipozama na walianza kuokoa mmoja baada ya mwingine ikiwemo mabinti niliokua nao msafara mmoja baada ya kuokolewa mabinti hao waliokua kumi na tisa kwa idadi name nilijisogeza maeneo ya meli ile ya wanyng’anyi lakini hawakuweza kununiona
Hakika niliona roho yangu ikiwa mkononi tena mkono usio na nguvu ambao ungeweza kuidondosha siku yoyote, saa yoyote na dakika yoyote
Pembeni ya meli ile kulikua na majina makubwa yaliyosomeka MOHAMED CARGO EXPORT LIMITED
“mungu wangu”. Nilijisemea moyoni na hasira iliwaka upya kwani nilijua bila shaka ni kampuni ya Mohamed bakantan na nilijua lazima ametoka kusafirisha mabinti kwenda kuwauza kwenye madangulo nje ya nchi.
Nilianza kukata mawimbi, kwa hasira iliyo kuu huku meli ile ikianza kuniacha, lakini niliamini ilikua ikielekea Tanzania hivyo niliogelea kufuata uelekeo wa meli ile hata iliponiacha sikukata tama nilizidi kunyoosha hivyo hivyo.
Nilichoka sana kuogelea, kwenye maji ya chumvi ambayo yalifanya macho yangu kuwa mekundu kama nimevuta kaya mbichi (bangi). Nilizidi kuogelea huku nikibadili mitindo mbalimbali ya kuogelea ambayo nilijifunza kisiwani ambako niliishi kwa muda mrefu sana ambao sikutambua ni ilikua miezi wiki au miaka.
Pumzi zilianza kuniisha kabisa mikono ilichoka na sikua na uwezo wa kuogelea tena, nilimuomba mungu aninusuru kwa mara nyingine kwani lengo langu ni kwenda kuwaokoa watu wengine na nafsi zao kutoka kwenye mikono ya Mohamed bakantan na nilipanga kumuadabisha mzee bakantan na kufichua maovu yake yote endapo tu ningeweza kukanyaga ardhi ya Tanzania.
Hakika hayo ni mawazo yaliyokitawala kichwa change huku baridi kali ikizidi kunipiga na nguvu zikizidi kuniisha,
kwa mbali niliweza kuona mwanga wa taa ya kandili ikija upande wangu, nami sikutaka kupoteza wakati nilizidi kukata mawimbi na hapo nguvu ziliniisha kabisa, kiza kinene kilitanda kwenye macho yangu.
Je nini kilifuata