Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #41
SEHEMU YA 41
Wakati anaendesha gari akasikia sauti,
“Rose, umenigonga nimekufa halafu kwenye maizishi yangu unakimbia!”
Rose alishtuka na kusimamisha gari kwa haraka huku akiwa amejawa na hofu iliyomfanya ashindwe hata kutazama nyuma ya gari kuwa hiyo sauti inatoka wapi. Akiwa amejawa na hofu zaidi, ile sauti ikajirudia tena, na kumfanya Rose ashuke kabisa kwenye gari ile, alipokuwa chini akatazama kwenye kioo cha gari gafla alimuona kama Yule babu yupo ndani ya lile gari.
Uoga ulizidi kumshika Rose na kujikuta akiacha gari kisha kuanza kukimbia hovyo, alikimbia sana hadi akachoka kwakweli. Alifika kwenye mti mmoja na kukaa chini yake huku akiwaza kuwa alikuwa anaota au ni vipi maana yale mambo yalikuwa kama ndoto.
“Hivi ni kweli au naota? Lakini mimi uoga umeanza lini kwangu? Hivi mi naweza kuwa na uoga wa namna hii kweli? Ningeweza kuwafuga wale wajinga wangu? Hapana kwakweli, mimi ndio mimi uoga kwangu ni mwiko”
Akainuka na kuanza safari ya kurudi kwenye gari yake ila aligundua kuwa ni mbali sana ameiacha hiyo gari.
Alitembea kwa umbali mrefu sana hadi kuifikia, alivyofika alikuwa amechoka vilivyo, akafungua na kuingia ndani ya gari yani ingawa milango ya gari hakufunga na funguo ila ilionyesha wazi hakuna mtu aliyeingia kwenye gari ile kwani kila kitu alikuta kama kilivyo. Aliendesha gari na kwenda moja kwa moja hotelini, hakutaka kwenda nyumbani kwake kwanza kwahiyo aliamua kwa wakati huo akalale hotelini kwanza.
Kwa upande wa nyumbani kwa Neema, ilipofika usiku Salome aligoma kwenda kulala na mamake mdogo Ashura, kitendo hiko kilimshangaza sana Neema kwani kwake ilikuwa ni ajabu,
“Kwahiyo, Salome unataka ukalale wapi?”
“Nataka leo nikalale na wewe mama”
“Una nini lakini Salome jamani?’
“Sina chochote mama ila nataka nikalale na wewe”
Neema hakuwa na jinsi zaidi ya kukubali tu vile alivyoambiwa na mtoto wake ila Ashura nae kwakweli alimshangaa sana Salome ila hakusema chochote.
Muda wa kulala ulipofika, moja kwa moja Salome alikwenda na mama yake chumbani ila walipotaka tu kulala, Salome akaanza kumwambia vitu Neema vilivyomshangaza sana, tena muda mwingine akamuuliza maswali ambayo Neema hakufikiria kama kuna siku Salome atamuuliza maswali ya namna hiyo,
“Mama, baba yangu yuko wapi?”
“Mmmh Salome, ndio maswali gani hayo?”
“Kila mtu kwenye ulimwengu huu ana baba yake, mimi je baba yangu yuko wapi?”
“Jamani, Sa lome kwanini kutaka kunikumbushia machungu yaliyopita? Wewe ni mwanamke pia, ukikua vizuri utatambua nazungumzia nini”
“Mama, mimi ni mkubwa tayari au unataka nikue mara ngapi? Nataka kujua baba yangu alipo”
“Baba yako alishakufa”
‘Si kweli mama”
“Sasa ukweli ni upi? Baba yako alishakufa, wewe huna baba”
“Sawa, baba yangu alishakufa. Je baba wa hawa wadogo zangu je nae alikufa? Maana nae sijawahi kumuona na wote tunatumia majina ya babu!”
“Salome, tafadhali niache nilale, wala sitaki maswali zaidi”
Neema aliona maswali ya Salome yanamchanganya kichwa tu, ila Salome hakuendelea na maswali zaidi halafu akajifanya muda huo huo amelala ila kumbe alikuwa kijicho kimoja akimchungulia mama yake kila alichofanya kwa muda huo, kwani Neema nae hakulala tena maswali ya Salome yalimkumbusha mbali sana hivyo hakuyataka tena, Ila kabla hajalala aliinuka pale kitandani na kupekua vitu kwenye kabiti lake, kuna kitu alikitoa kilikuwa kama daftari dogo, akakiangalia sana kisha akakirudisha na kurudi kitandani halafu akalala sasa.
Salome akainuka pia na kwenda pale alipokuwa anapekua Neema, akapata kile kitu kumbe ilikuwa ni kadi ya kliniki ya miaka ya nyuma, iliandikwa jina la mtoto Maria Patrick. Alitazama vizuri ile kadi kisha akairudisha na kwenda kulala pia.
Wakati anaendesha gari akasikia sauti,
“Rose, umenigonga nimekufa halafu kwenye maizishi yangu unakimbia!”
Rose alishtuka na kusimamisha gari kwa haraka huku akiwa amejawa na hofu iliyomfanya ashindwe hata kutazama nyuma ya gari kuwa hiyo sauti inatoka wapi. Akiwa amejawa na hofu zaidi, ile sauti ikajirudia tena, na kumfanya Rose ashuke kabisa kwenye gari ile, alipokuwa chini akatazama kwenye kioo cha gari gafla alimuona kama Yule babu yupo ndani ya lile gari.
Uoga ulizidi kumshika Rose na kujikuta akiacha gari kisha kuanza kukimbia hovyo, alikimbia sana hadi akachoka kwakweli. Alifika kwenye mti mmoja na kukaa chini yake huku akiwaza kuwa alikuwa anaota au ni vipi maana yale mambo yalikuwa kama ndoto.
“Hivi ni kweli au naota? Lakini mimi uoga umeanza lini kwangu? Hivi mi naweza kuwa na uoga wa namna hii kweli? Ningeweza kuwafuga wale wajinga wangu? Hapana kwakweli, mimi ndio mimi uoga kwangu ni mwiko”
Akainuka na kuanza safari ya kurudi kwenye gari yake ila aligundua kuwa ni mbali sana ameiacha hiyo gari.
Alitembea kwa umbali mrefu sana hadi kuifikia, alivyofika alikuwa amechoka vilivyo, akafungua na kuingia ndani ya gari yani ingawa milango ya gari hakufunga na funguo ila ilionyesha wazi hakuna mtu aliyeingia kwenye gari ile kwani kila kitu alikuta kama kilivyo. Aliendesha gari na kwenda moja kwa moja hotelini, hakutaka kwenda nyumbani kwake kwanza kwahiyo aliamua kwa wakati huo akalale hotelini kwanza.
Kwa upande wa nyumbani kwa Neema, ilipofika usiku Salome aligoma kwenda kulala na mamake mdogo Ashura, kitendo hiko kilimshangaza sana Neema kwani kwake ilikuwa ni ajabu,
“Kwahiyo, Salome unataka ukalale wapi?”
“Nataka leo nikalale na wewe mama”
“Una nini lakini Salome jamani?’
“Sina chochote mama ila nataka nikalale na wewe”
Neema hakuwa na jinsi zaidi ya kukubali tu vile alivyoambiwa na mtoto wake ila Ashura nae kwakweli alimshangaa sana Salome ila hakusema chochote.
Muda wa kulala ulipofika, moja kwa moja Salome alikwenda na mama yake chumbani ila walipotaka tu kulala, Salome akaanza kumwambia vitu Neema vilivyomshangaza sana, tena muda mwingine akamuuliza maswali ambayo Neema hakufikiria kama kuna siku Salome atamuuliza maswali ya namna hiyo,
“Mama, baba yangu yuko wapi?”
“Mmmh Salome, ndio maswali gani hayo?”
“Kila mtu kwenye ulimwengu huu ana baba yake, mimi je baba yangu yuko wapi?”
“Jamani, Sa lome kwanini kutaka kunikumbushia machungu yaliyopita? Wewe ni mwanamke pia, ukikua vizuri utatambua nazungumzia nini”
“Mama, mimi ni mkubwa tayari au unataka nikue mara ngapi? Nataka kujua baba yangu alipo”
“Baba yako alishakufa”
‘Si kweli mama”
“Sasa ukweli ni upi? Baba yako alishakufa, wewe huna baba”
“Sawa, baba yangu alishakufa. Je baba wa hawa wadogo zangu je nae alikufa? Maana nae sijawahi kumuona na wote tunatumia majina ya babu!”
“Salome, tafadhali niache nilale, wala sitaki maswali zaidi”
Neema aliona maswali ya Salome yanamchanganya kichwa tu, ila Salome hakuendelea na maswali zaidi halafu akajifanya muda huo huo amelala ila kumbe alikuwa kijicho kimoja akimchungulia mama yake kila alichofanya kwa muda huo, kwani Neema nae hakulala tena maswali ya Salome yalimkumbusha mbali sana hivyo hakuyataka tena, Ila kabla hajalala aliinuka pale kitandani na kupekua vitu kwenye kabiti lake, kuna kitu alikitoa kilikuwa kama daftari dogo, akakiangalia sana kisha akakirudisha na kurudi kitandani halafu akalala sasa.
Salome akainuka pia na kwenda pale alipokuwa anapekua Neema, akapata kile kitu kumbe ilikuwa ni kadi ya kliniki ya miaka ya nyuma, iliandikwa jina la mtoto Maria Patrick. Alitazama vizuri ile kadi kisha akairudisha na kwenda kulala pia.