Simulizi: Kurudi Kwa Moza

Simulizi: Kurudi Kwa Moza

SEHEMU YA 61


Kulipokucha Patrick alitoka na kuruhusiwa kuondoka ila watoto wa rose walikuwa bado hawajazinduka, na baada ya Patrick kuondoka Ana nae aliondoka na kwenda shuleni kisha huku nyuma Rose aliingia chumbani kwa Sara na kuanza kuwaburuza wanae wale mapacha mmoja mmoja, hadi wote wawili akawaingiza chumbani kwako kisha akawaweka kitandani na kuwafunika mashuka halafu akaenda chumbani kwa Sara na kumuweka vizuri Sara kitandani kisha akamfunika na shuka. Baada ya muda wale mapacha walizinduka ila kila mmoja hakukumbuka kitu chochote kilichokuwa kimetokea ila walijikuta wamechoka sana na kuulizana kwa mshangao,
“Mbona tumechelewa sana kuamka!”
“Hata sielewi, sijui kwanini”
Basi ikabidi wajiandae haraka haraka na kuondoka, sebleni walimkuta mama yao na kumuaga.
“Sasa nataka niwaagize”
“Wapi tena mama?”
“Leo msafiri, muende kule shambani Morogoro”
Mmoja akadakia,
“Mama, kuna nini tena?”
“Sitaki maswali ila nataka muende kule shambani kwangu na mrudi kesho. Nadhani tunaelewana”
Akawapa na pesa kidogo ya kuwasaidia kwenye safari hiyo, waliondoka ila walijiuliza mambo mengi sana kuwa mama yao safari hii ana mpango gani maana mara ya mwisho aliwatuma Morogoro kumbe kuna kifo cha Moza, ila kwasababu hawakuwa na kumbukumbu yoyote ya kilichotokea usiku wakapuuzia na kuondoka zao.
Muda kidogo Sara nae aliamka, tena akaoga na kujiandaa kuondoka. Alipotoka sebleni akamkuta mama yao amekaa na akamuuliza swali,
“Unaenda wapi?”
“Naenda kwenye shughuli zangu mama”
“Nani amekuruhusu?”
“Mama jamani si nimepona! Je kutoka siruhusiwi?”
“Njoo ukae kwanza hapa nikuambie”
Sara alienda kukaa karibu na mama yake , kisha mama yake akamuuliza swali,
“Wewe umejizaa au nimekuzaa?”
“Umenizaa mama, ila kwanini umeniuliza hivyo?”
“Sasa niambie ukweli, ni kitu gani kimerudisha kuongea kwako na kuona kwako”
“Jamani mama inamaana haujapenda nilivyopona?”
“Wewe niambie tu umeponaje?”
“Nilikuwa nimelala hapa sebleni, mara nikasikia sauti ikisema inuka Sara umepona. Nikafungua macho yangu nikaona halafu nikajaribu kuongea napo nikaweza. Basi nikafurahi sana nimeweza kupona mama”
“Sara usinifiche, mimi ni mama yako niambie ukweli”
“Huo ndio ukweli mama wala hakuna ukweli mwingine zaidi ya huo”
“Sara, sitaki kutumia ukali mwanangu. Niambie ukweli”
“Huo ndio ukweli mama”
“Nadhani unataka kuona nitakufanya nini”
Rose akainuka na kuelekea chumbani, kisha Sara nae akainuka na kutaka kutoka nje ila akakuta mlango umefungwa kila alipojaribu kuufungua ilikuwa ni vigumu kuufungua ikabidi akae chini amsubirie tu mamake arudi.

 
SEHEMU YA 62


Bado Neema alikuwa akishangaa sana jinsi Salome alivyobadilika kwani mwanae hakuwa hivyo kabla, vitu vingi sana Salome alikuwa anavifanya vya tofauti. Muda huu alikuwa nae sebleni wakiangalia luninga, mara gafla Salome akashika kichwa chake kwa nguvu na kumfanya Neema amuulize kwa mshangao huku ameinuka na kumshikilia,
“Vipi Salome mwanangu!”
Ila Salome hakujibu zaidi aliinuka na kukimbilia chumbani halafu akafunga mlango. Kwakweli Neema alishindwa kuelewa kabisa kuwa imekuwaje lakini bado hakupata jibu kabisa, akawa tu anamgongea mlango,
“Jamani mwanangu Salome fungua, una matatizo gani mwanangu!”
Hakujibiwa wala mlango haukufunguliwa na kumfanya azidi kuchanganyikiwa lakini akaamua kwenda kukaa akisikilizia tu kipi kitajili baada ya hayo.
Baada kama ya lisaa limoja Salome alitoka ndani, na alimkuta mama yake akilia. Salome alimfata mama yake na kuanza kumbembeleza,
“Usilie mama, mimi ni mzima”
“Salome mwanangu, ulinifungia mlango lazima nihisi kuna kibaya kimekupata”
“Hakuna kibaya chochote mama”
“Sasa kwanini uliondoka gafla ukishika kichwa na kwenda kujifungia ndani?”
“Kichwa kiliniuma mama, sasa niliingia ndani na kunywa dawa na kupumzika sikutaka kuacha mlango wazi kwamaana niliona ungesumbuka”
“Jamani Salome mwanangu mbona siku hizi umebadilika sana, toka lini umefanya hivyo mwanangu?”
“Nisamehe mama yangu, naomba unisamehe sana”
Neema sasa alinyamaza ila akaja kushtuliwa tena na kauli ya Salome,
“Mama nataka kwenda kwa baba”
“Kivipi Salome?”
“Nataka kwenda kuishi na baba”
“Jamani Ssalome jamani, subiri basi kesho nitakujibu”
“Sitaki kusubiria kesho, nataka leo leo iende kwa baba”
“Hapana Salome, siwezi kukuruhusu leo. Subiri utaenda tu”
“Huwezi kubadilisha mawazo yangu mama, nishajipanga kwenda. Nitakuja tena tu hapa nyumbani ila kwa leo niache niende”
“Hapana Salome”
Ila Salome akainuka na kwenda chumbani kwake kisha akatoka na begi dogo na kumwambia mama yake,
“Baki salama mama”
Halafu akatoa milioni moja na kumkabidhi mama yake, hakutaka hata kusikia mama yake atasema nini kwani muda huo huo akatoka na kuondoka, kwakweli Neema alikuwa kama amepigwa na bumbuwazi hizi kwani aliona ni mambo ya ajabu sana kutokusikilizwa na mwanae.

 
SEHEMU YA 63


Wale mapacha walipokuwa wanajiandaa ili wapande basi waende Morogoro maana walichelewa sana kutokana na mambo waliyokuwa wanayafanya ndiomana ikawachelewesha, wakasikia mtu akiwaita,
“Kulwa na Doto”
Walishtuka na kumuangalia aliyewaita, kwakweli sura ya Yule mtu ilikuwa ni ngeni machoni mwao ila walipomuangalia zaidi waligundua kuwa mtu Yule amefanana na baba yao wa kambo Mr.Patrick. Walimsogelea Yule binti na kumsikiliza vizuri,
“Naitwa Salome”
Wakatazamana na kumuuliza,
“Unatujua sisi?”
“Ndio nawajua”
“Na je umetuitia nini?”
“Nimetumwa na mama ambaye ni mama yenu”
“Kwani na wewe ni mama yako?”
“Ndio ni mama yangu, kaolewa na baba yangu”
Wakashangaana kwa muda na kuuliza kwa makini kuhusu baba wa Salome, naye akawaelezea,
“Mzee Patrick ni baba yangu mzazi, nz mimi ni mtoto wake wa pekee na analitambua hilo. Nimefika leo rasmi nyumbani nyie mmeondoka, ndio mama kasema niwafate hapa stendi turudi nyumbani akawatambulishe vizuri. Hata hivyo amesema huko Morogoro ameshamalizana na wakulima tayari kwahiyo hakuna cha kuendea.”
Wale mapacha wakaangaliana na kujikuta wakikubaliana nae kile alichowaambia na kuamua kughaili kwenda Morogoro na kurudi nyumbani ila Salome aliwaaga kuwa yeye anapitia mahali kwahiyo ataonana nao nyumbani.
Wakati wanarudi njiani walikutana na baba yao ambaye ni Mr.Patrick nae akiwa kwenye gari yake akirudi nyumbani kwahiyo walimsimamisha na kushuka kwenye gari ya kukodi waliyopanda kisha kuingia kwenye gari ya Patrick.
“Baba mbona na wewe unarudi nyumbani muda huu?”
“Nimejisikia tu kurudi”
Wakaona si vyema waongee sana labda baba yao anaenda kufanyiwa kitu cha kushtukiza kwahiyo wakimwambia watakuwa wameharibu ila baba yao aliwaomba wapiti kumchukua Ana maana amepigiwa simu na walimu wa Ana kuwa arudi kwao.
Basi wakapita shuleni kwakina Ana, halafu Patrick akakabidhiwa Ana arudi nae nyumbani. Walimu walimkabidhi na barua mr.Patrick aende nayo. Walirudi na kupanda kwenye gari, kaka zake wakamuuliza kwa mshangao,
“Kwani Ana imekuwaje mdogo wetu mbona mapema sana, halafu umerudishwa nyumbani na barua juu”
“Achaneni na mimi”
“Mmmh haya bhana, tunaachana na wewe ila kumbuka elimu ndio kila kitu katika maisha”
“Naweza kupata kila kitu bila ya elimu, achaneni na mimi kabisa”
“Haya tumekuacha”
Basi safari ilikuwa inafanyika ya kurudi nyumbani.
Rose alikuwa anampango wa kumfanyia mambo ya ajabu sana Sara kwavile alimficha bado ila kila alichotaka kufanya aliona kuna kitu kinapingana nae na kushindwa kuelewa kuwa ni kitu gani ambacho kilikuwa kikimshinda kufanya vile alivyotaka kufanya, akamuita Sara kwa nguvu kiasi cha kufanya hadi nyumba yake itikisike ila Sara alishindwa kuinuka pale alipokuwa amekaaa ikabidi amfate kwa hasira na kutaka kumuinua kwa nguvu ila wakati anakazana kumuinua mara gafla nguo zake zote zikaanguka chini hata asielewe kwanini zimeanguka kwahiyo akawa kama alivyozaliwa, gafla mlango ulifunguliwa na waliingia ndani watoto wake na mume wake, kwakweli wote walimshangaa mama yao kuwa kama alivyozaliwa. Ikabidi Ana akimbilie nguo na kumfunika mama yake kisha wale mapacha nao wakatoka nje kwa aibu. Kwakweli siku ya leo ilikuwa ni siku ya aibu kubwa kwa Rose ambayo hajawahi kuitegemea kwa siku zote, hajawahi kutegemea kama kuna siku atadhalilika kiasi kile.
Ana alimchukua mama yake na kwenda nae chumbani huku akisikitika sana kwa kilichotokea na kumpa mama yake pole,
“Imekuwaje mama?”
“Sijui ila nguvu zangu zimepotea mwanangu, yani sina nguvu kama mwanzo. Nimedhalilika sana”
“Pole mama, ni kitu gani kimetokea?”
“Sijui ila kila nilipokuwa nafanya dawa zilikuwa zinapingana na vitu vingine. Hapo ndipo nilipotaka kwenda kumchukua kwa nguvu Sara ila ndio nguo zikanidondoka halafu nyie mkaingia”
Mara wakasikia sauti ya Sara ikiongea kwa nguvu tena kwa ujasiri,
“Sasa huyu ndio kiboko ya Ana”
Ikabidi watoke ili wakamuone huyo kiboko ya Ana, kwakweli Rose alishtushwa sana kumuona Salome.

 
SEHEMU YA 64


Mara wakasikia sauti ya Sara ikiongea kwa nguvu tena kwa ujasiri,
“Sasa huyu ndio kiboko ya Ana”
Ikabidi watoke ili wakamuone huyo kiboko ya Ana, kwakweli Rose alishtushwa sana kumuona Salome. Kitendo cha Rose kumuona Salome kilimkosesha furaha na kujikuta akipatwa kama presha na kuanguka kwani mawazo yake ilikuwa ni Salome amekufa kwahiyo kitendo cha kumuona akiwa mzima kilimshangaza kabisa. Watoto wake wote walimfata pale chini na kumpeleka chumbani ambako walimuwashia feni ilia pate upepo na wazo hilo la kumuwashia feni walilipata kwa Ana, kisha wakarudi sebleni na kumuacha Ana akiwa chumbani na mama yao.
Katika watu ambao walikuwa hawaelewi kinachoendelea ni Patrick maana yeye aliona kila kitu ni cha ajabu tu hapo, alikuwa akimuangalia Salome kama mgeni kabisa machoni pake ila Salome akamtoa mashaka,
“Usiniangalie hivyo, mimi ni mtoto wako”
“Nakuangalia sababu sielewi elewi”
“Mimi ni mtoto wako, na mama yangu ni Neema”
“Yeye yuko wapi?”
“Sijaja nae sababu alikuwa hataki nije huku”
Patrick alimuangalia Salome na kujikuta akimsogelea na kumkumbatia,
“Kumbe nina binti mkubwa tu”
“Ndio ni mimi mtoto wako”
“Karibu sana hapa nyumbani”
“Asante”
Muda watoto wa Rose wanarudi sebleni ni muda ambao Salome alikuwa anaondoka na kuelekea chumbani, wote wakajikuta wakisimama na kumuangalia ataelekea kwenye chumba kipi ila alielekea kwenye chumba kile alichokuwa analala Moza. Hapo iliwashangaza sana kwani hawakutegemea kama Salome angeelekea kwenye chumba cha Moza, na baada ya muda akarudi sebleni na kuwakuta wamekaa.
“Nimeshaenda kuweka begi langu”
Pacha mmoja akamuuliza Salome,
“Mbona chumba cha kulala umeenda bila kuonyeshwa na yeyote?”
“Mbona hapa nilishawahi kuja kipindi yupo dada Moza! Nishawahi kuja hapa, najua kila sehemu. Vipi leo tunakula nini?”
Wote walikuwa kimya ila huyu mgeni wa leo aliwashangaza sana kwani alikuwa na mambo ya ajabu ajabu, kafika tu mara mama yao kazimia, mara anaenda chumbani bila kuonyeshwa saivi anawauliza watakula nini, na alipoona kimya alienda yeye jikoni kupika. Kila mtu alikuwa kimya hata Sara mwenyewe alikuwa kimya kabisa.

 
SEHEMU YA 65


Rose alipozinduka bado alikuwa na mkaranganyiko wa mawazo kwani bado hakuelewa kitu chochote, akachukua simu yake na kuanza kumpigia Ashura lakini haikupatikana. Akachukua tena simu na kuwapigia wale vijana, kisha akaongea nao
“Hivi nyie mmenifanya nini? Si mlisema Yule mtoto mmeenda kumtupa mbali na hakuna wa kumuokoa iweje anaonekana tena nyumbani kwangu”
Wale vijana wakamuelezea ilivyokuwa kisha rose akawatuma waende pale alipokuwa anaishi Ashura ili kama yupo wamkamate mpaka aseme ukweli.
Alipokata tu ile simu akashangaa akipata ujumbe kutoka kwa Ashura,
“Samahani dada yangu, mimi sikuona kosa la huyu mtoto Salome na sikuona kama bi vizuri kumuua. Wale vijana niliwawekea mbwa kwenye kile kiroba ili wakuaminishe kuwa ni kweli nilimuua Salome ila kiukweli Salome sikumuua na mimi nimeondoka sipo kabisa mjini nimeenda kijijini kweli na sitaki tena kujishughulisha na hizo kazi zako.”
Kwakweli ujumbe huu aliusoma mara mbili mbili bila ya kumaliza na akiwa haamini kile anachokisoma kuwa Ashura anaweza akamgeuka namna hiyo, akaamua amtumie ujumbe pia,
“Ashura unajifanya umesahau tulivyoahidiana, hivi ningesema ukweli wa mambo yako na wewe ungeweza kukaa huko unapokaa? Mbona wewe pia una maovu mengi Ashura, umesahau Yule mganga babu ni wewe ndiye ulinipeleka? Umesahau hawa wasichana niliowafunga humu ndani ni ushauri wako, eti leo unajifanya kunigeuka Ashura! Kwanza jina lako sio Ashura wewe ila subiri nitakupata tu, mimi nina pesa”
Muda kidogo akajibiwa,
“Pesa zako wala hazinibabaishi hata mimi nina pesa, tena kwa taarifa yako ni mimi nimemueleza ukweli wote huyo Salome kuwa baba yake ni Patrick kwahiyo usishangae akija kuishi hapo. Ukweli wote nishamwambia, ujipange upya na hunipati ng’ooo, hao misukule uliowatunza utajijua nao mwenyewe”
Rose alichukizwa sana na ujumbe huu ila kila alipojaribu kupiga simu hiyo namba ya Ashura haikupatikana, yani alichukia hadi akarusha simu yak echini.

 
SEHEMU YA 66


Kwa upande wa Salome ilikuwa furaha sana kwake na alijikuta akigundua siri nyingi sana za Rose maana muda wote Rose alijua anayejibishana nae kwenye ujumbe mfupi ni Ashura kumbe kuna mtu mwingine, na huyo ashura mwenyewe ni marahemu wa muda mrefu sana.
Salome alikuwa ameingia na chakula chumbani na alikuwa anakula humo, mara Sara alienda kumgongea na kuingia ila alipomkuta anakula chumbani alishtuka sana, ikabidi Salome amuulize ameshtuka kwasababu ipi,
“Hapa nyumbani hakuna mtu anayeruhusiwa kula chakula chumbani”
“Mmmh kwanini?”
“Sijui ni kwanini ila mama anakataa kabisa mtu kula chakula chumbani”
“Hujui sababu kweli! Labda ungesema mama anaogopa panya watazaliana au mende watajaa. Ila ni leo tu haitajirudia kula chakula chumbani”
“Na kwanini umechagua kulala chumba hiki?”
“Sababu hiki ni chumba alichokuwa analala mpendwa wangu Moza, namkumbuka sana ndiomana nimekuja kulala hapa”
“Ila unafikiri Moza tulimzika! Alitoweka kimiujiza”
“Alitoweka!”
“Ndio alitoweka, yani kuna binti alitumbukia kwenye kaburi walipompeleka hospitali basin a mwili wa Moza ulipotea”
“Maskini Moza wangu, kwahiyo hakuna kaburi la Moza!”
“Ndio hakuna”
“Kwa staili hiyo inamaana basi Moza hakufa, labda kwa mfano hakufa!”
“Mmmh usiongee habari hizo, mimi ni muoga nitashindwa kulala hapa usiku”
“Basi usijali”
“Ila huku ndani kuwa nako makini sana, ulisaidia macho yangu yakaona tena na mdomo wangu ukaweza kuongea ila chakula nilichopika siku ile kuna kilichopotea na sijui kimeenda wapi. Kuwa makini sana na humu ndani kuna mambo ya ajabu sana”
“Usijali, nipo makini sana”
Sara alijikuta akimpenda sana huyu Salome yani alimpenda sana kutokana na jinsi alivyomsaidia matatizo yake ya kurogwa na mdogo wake. Walipomaliza maongezi, Sara akamuomba Salome waende nae sebleni ambapo alifanya hivyo na pale sebleni walikuwepo wale mapacha na mr.Patrick ambae toka amerudi hakwenda kabisa chumbani kwa mke wake. Baada ya kimya kirefu pale sebleni, Salome akaanza kusema,
“Hata hamniulizi jamani kuwa nimejuaje kama huyu baba ni baba yangu”
Pacha mmoja akadakia,
“Eeh tuambie umejuaje!”
“Unajua mimi nimeishi bila kumjua baba kwa miaka yote hii mpaka sasa nilikuwa kidato cha tatu ila baba yangu simjui. Alipotokea msamalia mwema na kuniambia kuwa huyu ni baba yangu nilifurahi sana ndiomana sikutaka hata kupoteza muda zaidi ya kuja hapa ili nifurahi na ndugu zangu wengine. Jamani ndugu zangu, mimi ni ndugu yenu ni mtoto wa Mr.Patrick kama mlivyo nyie”
Mmoja akahamaki,
“Wewe si ulituambia pale kuwa wewe ndiye mtoto wa pekee wa mzee Patrick, haya saivi unasema na sisi ni watoto wa huyu mzee. Hapana, sisi ni watoto wake wa kambo. Labda Ana sijui”
Sara akadakia,
“Ana nae ana baba yake mwingine, ni hakika kabisa wewe Salome ndiye mtoto wa pekee wa baba”
Mama yao akiwa ameambatana na Ana walitoka chumbani na waliisikia vilivyo kauli ya Sara na iliwakera sana. Rose kabla ya kukaa alianza kwa kumuuliza Sara,
“Hivi wewe Sara una nini wewe? Kitu gani kinakuwasha mdomoni kwako?”
Kisha Rose alikaa na kumuangalia Salome na kusema,
“Haya na wewe nani kakukaribisha kwenye nyumba hii?”
“Nimekuja kwa baba yangu”
Salome alijibu kwa kujiamini kabisa.
“Sikuelewi”
“Mamdogo Ashura kaniambia kuwa hapa ni kwa babangu, hata ameshakwambia kuwa nakuja hapa”
“Kwahiyo hapa kwangu unalala chumba gani sasa?”
“Kile chumba alichokuwa analala dada Moza”
Rose akamuangalia mume wake na kumwambia waelekee chumbani ana mazungumzo nae, kwahiyo sebleni walibaki watoto tu. Ambapo Ana alimuangalia Salome na kumwambia,
“Utaondoka kama ulivyokuja, hakuna anayekutambua hapa. Ndiomana unalala chumba cha marehemu”
Kisha akaenda zake chumbani kwake, ila Sara alimuangalia Salome na kumwambia,
“Hata usijali, nitakuwa na wewe bega kwa bega”
Wale mapacha wakainuka na kwenda chumbani kwao ila Sara aliinuka na Salome na kumkaribisha Salome kwenye chumba chake,
“Humu ni chumbani kwangu Salome, muda wowote unaruhusiwa kuingia. Ukiwa na shida ya kitu chochote unaruhusiwa kuja kuchukua”
“Asante dada”
“Nimefurahi sana kupata mdogo mwenye upendo kama wewe, kwanza umeniponya macho yangu na mdomo wangu. Halafu ngoja nikuhadithie kitu bhana”
Basi Sara akaanza kumueleza Salome jinsi Ana alivyokuwa akishangaa mwalimu wake amepona kimiujiza,
“Niambie Salome, ni wewe uliyemsaidia Yule mwalimu”
Salome akacheka kidogo,
“Hapana bhana si mimi ila nimefurahi kusikia kuna mtu alifanyiwa hivyo na amepona pia”
“Mmh si wewe kweli! Sasa mimi ulijuaje kama naumwa?”
“Nilioteshwa na nilioteshwa dawa za kuja kukupa ndiomana nimekwambia hawatakusumbua tena”
“Ila mimi nimefurahi sana umekuja kuishi hapa, naomba uishi hapa milele yote”
Salome akacheka tu na kufurahi pale na Sara kisha usiku ulipoingia alimuaga na kwenda kulala kwani nyumba hiyo huwa chakula kinakuwa mezani na mwenye njaa anaenda kula mezani na kama siku hiyo hakijapikwa basi kila mmoja anajijua mwenyewe.

 
SEHEMU YA 67


Salome akiwa chumbani kwake aliona ujumbe kwenye simu ya Ashura ukionekana umetoka kwa wale vijana,
“Sista mbona umefanya tupate lawama, ila mbona hupatikani hewani? Sasa ni mtu gani Yule tuliyemtupa kama sio Yule mtoto? Mama ametupa oda kuwa twende kwenye ile nyumba na tumalize yeyote tutakayemkuta pale”
Ujumbe huu ulimchanganya sana Salome, akawaza kwanza cha kuwaambia hawa vijana kisha akawatumia ujumbe,
“Basi kama nyie mnataka kuwateketeza wale wote ngojeni kwanza, msiende hivi karibuni. Subirini mpaka mwezi upite”
‘Haiwezekani sista, sisi tunataka pesa na si vinginevyo”
“Hatakama mnataka pesa, kumbukeni Yule Rose ni dada yangu, kwahiyo msifanye kitu chochote bila kuwaruhusu mimi. Yule Rose ametumia hasira tu”
“Kwahiyo tusubiri hadi lini?”
“Subirini hadi keshokutwa”
Wakamjibu tu poa, na hapo Salome akawaza cha kufanya maana ingawa kaihamisha familia yake ila waliohamia hapo watapata matatizo kwahiyo alikuwa anafikiria cha kuweza kuwasaidia na wale wengine.
Ila kabla hajalala, alianza kupekua kwanza vitu vya mule ndani ambapo alipata kijitabu kidogo ambacho kimeandikwa vitu vya maelekezo yaliyokuwa kama historia hivi ya mtu aliyeonekana ameandika hicho kitabu. Kurasa ya kwanza kabisa akaona,
“Nimeanza kazi leo kwenye hii nyumba ila usiku nilipolala nimegundua kuna chumba walichowekwa wadada wawili kama misukule. Natakiwa niwasaidie watoke”
Salome alisoma mara mbili mbili sehemu hiyo na kuwaza jambo Fulani ila kabla hajaendelea na kile kitabu, alikuja Sara chumbani kwake ikabidi kile kitabu akiweke pembeni, Sara akaanza kumwambia Salome,
“Naomba tukalale wote chumbani kwangu”
Salome alikuwa anakataa ila Sara alimbembeleza sana hadi alikubali na kwenda kulala nae.

 
SEHEMU YA 68


Kulipokucha siku ya leo ilikuwa ni ya ajabu sana kwani Patrick aliwaita watoto wake wote sebleni kisha akaanza kuongea,
“Salome, sikutambui kwahiyo naomba uondoke. Jamani hatuna undugu na huyu wakuitwa Salome, simtambui mimi”
Salome akacheka kisha akamuangalia Rose na kumwambia,
“Ndio mlivyohamua hivi!”
“Ndio. Uondoke Salome, hakuna anayekutambua kwenye nyumba hii. Kama huyo unayedai ni baba yako hakutambui, je sisi tutakutambua?”
“Basi naombeni nafasi kidogo niongee na huyu baba ndio nitaondoka”
Wote walitoka pale sebleni kasoro Rose ila salome alimsihi aondoke ili yeye aweze kuzungumza na mzee Patrick halafu ataondoka, Rose alikubali kuondoka kwani alijua mzee Patrick hawezi kubadilisha maamuzi yake yoyote kutokana na alichomfanya usiku wa jana.
Kwahiyo sebleni alibaki Salome na Patrick, kisha Salome akamuangalia vizuri Patrick na kumuuliza,
“Hunitambui mimi!”
Patrick alikuwa kimya tu, ila Salome akamsogelea karibu na kumkazia macho. Mzee Patrick akashtuka na kusema,
“Aaaah kumbe Moza!”
Akaanguka chini na kuzimia.


Kwahiyo sebleni alibaki Salome na Patrick, kisha Salome akamuangalia vizuri Patrick na kumuuliza,
“Hunitambui mimi!”
Patrick alikuwa kimya tu, ila Salome akamsogelea karibu na kumkazia macho. Mzee Patrick akashtuka na kusema,
“Aaaah kumbe Moza!”
Akaanguka chini na kuzimia. Salome alihakikisha ile sauti wengine wote hawajaisikia pia alimpulizia Yule mzee maji na kumfanya azinduke muda ule ule, ila alipozinduka sasa alikuwa na swaga mpya kwani alimsogelea Salome na kumwambia,
“Nisamehe mwanangu, jamani nisamehe wewe ni mwanangu. Damu yangu jamani nisamehe, nisamehe kwa kipindi chote bila kuwa karibu na wewe nisamehe sana mwanangu. Nataka unipeleke na kwa mamako nikamwombe msamaha”
“Usijali nitakupeleka”
Kisha Mr. Patrick akawaita tena wote sebleni, na walipokuja aliwaambia,
“Jamani huyu ni ndugu yenu, naomba tumpende”
Halafu akainuka na kutoka nje ya nyumba, kwakweli hichi kitendo kilimkera sana Rose yani alitamani sijui afanye kitu gani, alimuangalia Salome kwa hasira sana, ila alipotoka nje ili kumuangalia mume wake alikuta ameshaondoka,
“Yani leo Patrick ameondoka bila ruhusa yangu? Nitamfundisha huyu Salome na atanijua mimi ni nani”
Rose alirudi tena ndani akiwa na hasira sana na moja kwa moja akaenda chumbani kwake.
Watoto wake walikuwa sebleni wakijadiliana kasoro Ana,
“Mmmh nyie huyu mzee kama anakuwaga anaugua vile, kwajinsi alivyofanana na huyu dogo anaanzaje kumkataa!”
Walijadiliana na kuondoka kisha wakamuacha Salome akiwa na Sara, halafu Sara akamwambia Salome
“Usijali hata nyumba nzima ikikutenga jua ya kwamba nitakuwa pamoja na wewe”
“Nashukuru”
Kisha Salome akamuaga Sara kuwa anatoka kidogo, basi akaondoka kumbe mr.Patrick aliwekwa nje ya geti akimsubiria Salome, na alipotoka aliingia kwenye gari ya Patrick kisha safari ya kwenda nyumbani kwao ikaanza.

 
SEHEMU YA 69

Walifika nyumbani kwakina salome na kumkuta Neema akiwa anafanya usafi, kwakweli nae alishangaa sana kumuona Patrick akiambatana na Salome ila aliwakaribisha ndani hivyo hivyo cha kushangaza Patrick alianza kwa kupiga magoti na kuomba msamaha kwa Neema,
“Nisamehe Neema, naomba unisamehe. Nisamehe sana, nimefanya makosa makubwa sana, sikumtambua mwanangu naomba unisamehe”
Kwajinsi Patrick alivyokuwa anatia huruma ikambidi Neema amuhurumie kwani hajawahi kuwaza kama ipo siku Patrick atakuja na kumpigia magoti ya kumuomba msamaha. Neema akamshika mkono Patrick na kumkaribisha kwenye kochi,
“Usijali Patrick, yale yamepita ni mapito tu na nimeshasahau. Mtoto amekua sasa na amekutambua”
“Kwakweli moyo unaniuma sana yani sana, kumkosa mwanangu mpendwa kwa kipindi chote hiki. Nisamehe kabisa Neema”
Kisha Patrick akamuuliza Neema kuhusu pale anapoishi na alimwambia kama alipanga, kwakweli Patrick alisikitika sana maana nyumba nyingi tu alikuwa nazo ila mwanamke aliyezaa nae amepanga, akamuahidi kumpa nyumba moja.
“Kweli utanipa?”
“Ni haki yako Neema, kila kitu change ni haki yako. Nitakuja tu nikukabidhi”
Muda huu Salome alikuwa chumbani kwake ila gafla akashtuka na kusema,
“Muda umeisha, itabidi nimtoe huyu mzee haraka sana mpaka kwa wakati mwingine”
Basi akatoka chumbani na kumuomba baba yake kuwa waondoke, ila Patrick alitoa begi lake na kumpatia Neema pesa zote zilizokuwepo kwenye begi hilo wala yeye hakuzihesabu ila alimpa Neema pesa zote na begi lake kisha akaondoka na Salome ambapo Salome alishuka mahali na kumuacha akiendelea na safari zake zingine.
Salome alienda kwanza kule walipokuwa wanaishi mwanzo na kumuomba mama mwenye nyumba asiweke mpangaji mwingine mpaka miezi miwili iishe kwani wao walikuwa na hatihati ya kurudi na ukizingatia kodi yao ilikuwa bado kuisha ikabidi mama mwenye nyumba asikilizane nao kumbe Salome alifanya vile ili kuepusha wale wakija wasikute mtu katika nyumba ile. Kisha Salome akarudi tena kwa mama yake ili akahesabu nae pesa zilizokuwemo kwenye lile begi.


 
SEHEMU YA 70


Rose akiwa na hasira sana, kwanza alipoingia chumbani kwao na kufanya mambo yake akagundua kitu. Akagundua kuwa Patrick aliondoka na gari yake ambapo kwenye gari hiyo aliweka begi lenye pesa ili akawalipe wajenzi kwenye saiti yao na lile begi aliliweka asubuhi ya siku hiyo akiwa na lengo la kumaliza yale mazungumzo ajiandae na kwenda saiti ila sasa Patrick alishaondoka na lilke gari lenye begi,
“Mungu wangu, Patrick kaondoka na lile begi eti! Na hivi akili yake haipo sawa litakuwa limepona kweli? Ila natumai limepona maana sidhani kama anaweza kufanya ujinga.”
Ikabidi Rose ajiandae haraka haraka na kuelekea saiti.
Kufika kule alimkuta Patrick amekaa chini ya mti, akamshtua na Patrick alishtuka sana kama kashtuliwa na kitu gani. Swali la kwanza ambalo Rose alimuuliza Patrick,
“Kwanini umeondoka na gari yangu?”
“Hata mimi mwenyewe nashangaa sijui hata imekuwaje nimeondoka na gari langu”
“Natumaini hujafanya ujinga”
“Ujinga gani tena?”
Rose akainuka na kwenda kuangalia begi la hela kwenye gari, ila lile begi halikuwepo. Kwakweli Rose alikuwa na hasira sana na kumuuliza tena Patrick,
“Begi la hela liko wapi?”
“Begi! Begi lipi?”
“Inamaana hukuona begi kwenye gari hilo?”
“Sijaona begi”
“Patrick usinitanie na hela zangu, tafadhali begi langu liko wapi?”
Patrick alionekana pia akishangaa yani kama mtu anayeonewa vile kwani ilionyesha wazi hajui begi la hela limeenda wapi.
“Patrick, Patrick. Begi la hela limeenda wapi?”
“Sijui kweli mke wangu unanionea tu”
“Nakuonea kitu gani, haya sasa tutawalipa nini hawa mafundi?”
“Kachukue hela nyingine benki tuwalipe”
“Hivi wewe Patrick una matatizo gani? Yani unarahisisha tu. Haya twende nyumbani ndio utanieleza vizuri”
Akapanda kwenye gari kisha Patrick akawa gari ya mbele akiongoza kwenda nyumbani halafu Rose akiwa nyuma yake, kwakweli Patrick alikuwa haelewi kabisa kwa muda huo kuwa begi limeenda wapi na kwenye begi kulikuwa na kiasi gani.

 
SEHEMU YA 71


Salome alienda tena kwa mama yake ambaye bado alikuwa akitetemeka tu kuziangalia zile hela za kwenye begi,
“Usitetemeke mama, ni zako hizo”
“Mmmh mwanangu ni miujiza hii”
“Usiwe na mashaka mama yangu, nimekuja nikusaidie kuhesabu”
Basi wakaanza kuhesabu zile hela wakakuta ni milioni thelathini na tano, kwakweli Neema alipagawa kabisa kwani hajawahi kushika hela za namna hiyo katika maisha yake kwahiyo alihisi kuchanganyikiwa.
“Sasa mwanangu nafanyaje? Nizipeleke benki!”
“Usiwe na haraka mama, benki tutazipeleka kwa utaratibu. Usizipeleke hivyo kwa mkupuo, na huo wasiwasi wako watahisi hata umeiba. Nitakupekea mwenyewe benki, yani wewe hata usiwe na mashaka”
Haya mambo Neema hakuyaamini kabisa na kwake yalikuwa kama ndoto vile hadi alijikuta akitetemeka tu, na kumfanya ashindwe kumuuliza maswali zaidi Salome kwani aliona kama kawa mokozi wake kwa kipindi hiko. Alijikuta akimwambia,
“Salome, ni kweli nimekuzaa na nimekulea ila sikutegemea kama kuna siku ungeweza kuja kufanya kitu cha namna hii. Baba yako nimemsamehe na nimefuta yote aliyonitendea, yani yote kabisa nimeyafuta. Kwahiyo mwanangu unaenda tena kwa baba yak oleo?”
“Siendi leo mama, nitaenda keshokutwa hadi nikamilishe hizi hela zako kukuwekea benki. Hata usiwe na mashaka mama yangu”
Neema alifurahi kusikia hivi na kisha Salome alikaa na mama yake huyo na kumueleza utaratibu watakaotumia kuziweka hizo hela benki.


 
SEHEMU YA 72


Patrick na Rose walifika nyumbani ila kwakweli Rose alikuwa na hasira sana kwa kile kilichofanywa na Patrick kuondoka na gari lenye begi la hela na eti kujifanya hajui begi limeenda wapi, akaenda moja kwa moja na Patrick chumbani kisha akaanza kumuuliza tena,
“Patrick, hebu kumbuka vizuri begi limeenda wapi?”
“Hata sijui mke wangu yani sijui kabisa”
“Hebu kwanza niambie ulipotoka hapa ulienda wapi?”
“Yani ninachokumbuka ni kuwa nimejikuta tu nipo kule saiti, nikaa chini nikawa najifikiria bila kupata jibu kuwa nimeenda kule kufanya nini. Na mara ukaja wewe yani sielewi kabisa”
“Haya, vipi kuhusu kumkubali Salome wakati mimi nimekwambia umkatae Yule mtoto!”
“Pale nakumbuka ndio, Yule mtoto nilimkataa ila nilikuja na kumkubali. Unajua ni mwanangu Yule!”
“Hivi wewe Patrick una nini lakini? Yule kawa mwanao tangia lini jamani? Mwanao wewe si Ana!”
“Yule ni mwanangu Rose”
“Yule si mwanao, inamaana hunielewi au”
Rose akampulizia kitu uoni na Patrick akapatwa na usingizi na kulala. Kisha Rose akatoka sebleni, mara akaingia ndani Sara akiwa ameambatana na ommy, kwakweli Rose alivyowaona alichefukwa sana ukizingatia akili yake ilishavurugika kwa wakati huo,
“Na wewe kijana mwanga unataka nini nyumbani kwangu?”
Ommy alianza kwa kumsalimia ila Rose hakuitaka salamu ya Ommy zaidi ya kumfukuza tu nyumbani kwake, ikabidi Sara aingilie kati,
“Mama jamani, utamfukuzaje rafiki yangu?”
“Sara, hii ni nyumba yangu sio nyumba yako unanisikia! Sitaki ujinga kwenye nyumba yangu”
“Lakini mama huyu Ommy ni rafiki yangu”
“Kama ni rafiki yako ishia nae huko huko sio nyumbani kwangu tena usinikere”
Sara alibaki tu anamshangaa mama yake, lakini Rose alipoona wamesimama tu wakimshangaa akainuka na yeye na kumsukumia mlangoni Ommy ambaye alijikwaa kwenye mlango na kuaguka kisha damu zikamtoka ikabidi Sara ainame pale alipoangukia Ommy na kuanza kumsaidia kwenda nje ila kabla hawajafika getini Ommy alionekana akianza kuugulia kichwa ni kitu ambacho kilimshtua sana Sara na kumfanya akimbilie ndani ili akamletee huduma ya kwanza ila aliporudi hakumkuta Ommy, alimuita lakini hakumsikia sehemu yoyote ikabidi fike getini na kumuuliza mlinzi,
“Eti Ommy ametoka hapa?”
“Nimemuona tu akiingia ila kutoka sijamuona”
“Mungu wangu jamani, Ommy atakuwa ameenda wapi wakati alikuwa anaumwa. Hivi hukumuona kama nakokotana nae pale na alilala pale chini?”
“Sijawaona kabisa madam yani hata mimi unakuja kuniuliza muda huu nashangaa tu”
Sara akaangalia kwa makini pale ambapo alilala Ommy kwani alijua lazima damu zitakuwa zimebaki na kama kaelekea mahali basi ataona matone ya damu ila alipoangalia hakuona damu yoyote na hadi alipoingia ndani pale alipojigonga ommy hakuona damu yoyote. Kwkweli hiki kitu kilimuumiza sana Sara kwani hakuelewa kabisa aliona kama ndoto kwa ommy kutoweka mbele ya macho yake mwenyewe.
Akataka kumuuliza mama yake ila hakumkuta sebleni na alienda kumgongea mlango chumbani kwake ila hakuitikiwa na kujiuliza inamaana mama yake amelala kwa muda mfupi huo, hakupata jibu kwakweli na alibaki anashangaa tu ila bado alikazana kumuita mama yake ili ampe jibu.

 
SEHEMU YA 73


Rose alichoshwa na kelele za Sara, na baada ya lisaa limoja rose alitoka ndani na kumfata Sara alipokuwa kisha akamuangalia kwa jicho kali sana na kuanza kumvuta hadi chumbani kwa Sara kisha akamwambia,
“Laiti kama ungejua leo ninavyojisikia au yaliyonitokea wala usingethubutu kunipigia kelele”
“Sasa mama yaliyokutokea yanamahusiano gani na kupotea kwa Ommy!”
“Hivi unajua leo nimepoteza kiasi gani cha pesa? Unajua! Yani wewe mtoto tafadhali niache usitake kukorofisha akili yangu kabisa”
“Basi mama niambie alipo Ommy wangu”
“Kwahiyo mimi huyo Ommy wako nimemla au? Wewe mtoto wewe hebu niache”
Rose akatoka na kumfungia Sara mlango kwa nje ambapo alikuwa akiugonga tu bila ya mafanikio yoyote.
Rose akaenda zake sebleni na baada ya muda watoto wake walianza kurudi na wote wakawa pale sebleni na kuzisikia kelele za Sara kuwa afunguliwe, wale mapacha walimuhurumia sana dada yao,
“Mama jamani, msamehe dada Sara, nadhani hatorudia tena”
“Hebu na nyie niacheni”
Gafla ikasikika sauti kali sana ya kelele za Sara ikisema,
“Mozaaaaaaaaa”
Na gafla kukawa kimya kabisa.

 
SEHEMU YA 74



Rose akaenda zake sebleni na baada ya muda watoto wake walianza kurudi na wote wakawa pale sebleni na kuzisikia kelele za Sara kuwa afunguliwe, wale mapacha walimuhurumia sana dada yao,
“Mama jamani, msamehe dada Sara, nadhani hatorudia tena”
“Hebu na nyie niacheni”
Gafla ikasikika sauti kali sana ya kelele za Sara ikisema,
“Mozaaaaaaaaa”
Na gafla kukawa kimya kabisa.
Kitendo hicho kiliwashtua wote sebleni hata Rose mwenyewe akashtuka na kujikuta akienda kumfungulia Sara ili kujua tatizo ni nini, ila alipomfungulia alimuona Sara akiwa ameanguka chini na kuzimia, kwakweli Rose alichanganyikiwa sana kwani hakudhania kama mwanae kumfungia mule chumbani angezimia basi akamuinua mwenyewe na kumbeba hadi sebleni kisha akawaambia wale mapacha wasaidiane nae kumpepea hata wao wakashangaa kuwa mama yao kuna wakati kumbe anakuwa na huruma dhidi yao. Ana alimwambia mama yake,
“Unajichosha bure mama”
“Ni mwanangu huyu”
Ana akaondoka zake huku Rose akiendelea na wale mapacha wake kumpepea Sara, na ilimchukua muda sana kuzinduka na hata alipozinduka hakukumbuka kitu chochote yani cha kushangaza hata kuhusu kuanguka kwa Ommy na kutoweka hakukumbuka pia.
Rose alimsogelea mwanae na kumpa pole kisha akainuka nae na kwenda chumbani, akakaa nae kuzungumza,
“Mwanangu una hakika hukumbuki chochote?”
“Sikumbuki kitu mama”
“Yani vilivyofanyika leo hukumbuki?”
“Yani sikumbuki hata kuhusu leo nilitoka nimejua wewe ulivyosema ila sikumbuki chochote”
“Kheee makubwa haya, hivi anayefanya kutoa kumbukumbu kwa watu wangu wa karibu ni nani!”
Akakumbuka kuwa kauli ya mwisho ya mwanae kabla ya kuzimia ilikuwa ni neno ‘Moza’ na ilionyesha aliona kitu cha kustaajabisha sana ila akajiuliza kuwa inamaana huyo Moza karudi kama mzimu au ni kitu gani.
“Ila inawezekana maana alitoweka pale makaburini na hatukumzika. Lazima nifatilie na nijue mbichi na mbivu”
Akapanga pale na halmashauri ya kichwa chake kuwa kesho aende kwa mtaalamu mwingine ili kujua ukweli kuhusu Moza maana kitendo cha mtoto wake kusema Moza na kuzimia halafu kupoteza kumbukumbu zote kilimstaajabisha ingawa kilimfurahisha kwa kiasi Fulani kwani mwanae hakuwa na kumbukumbu za kupotea kwa Ommy. Alimuangalia pale mtoto wake aliyeonyesha kuwa hana kumbukumbu ya aina yoyote kisha akaondoka na kumuaga pale.
“Mwanangu naenda chumbani, ikiwa utapatwa na tatizo lolote usisite kuniambia. Sawa mwanangu eeh!”
“Sawa mama”
Rose alitoka ila Sara alibaki akijiuliza sana upendo wa mama yake wa siku hiyo ni waajabu sana ukizingatia na siku zingine.
Kaka zake mapacha nao wakaenda chumbani kwake na kumuuliza tena dada yao hali yake ila bado walimshangaa kuwa hana kumbukumbu ya aina yoyote.
“Yani dada hukumbuki kitu chochote!”
“Sikumbuki ndio, kwani ilikuwaje?”
“Sisi wenyewe hatuelewi ila tulisikia tu ukipiga kelele kuwa ufunguliwe na mara ukapiga kelele za nguvu ukitaja Moza, halafu kimya kikatawala. Mama alikuja kukufungulia na kukuta umezimia ndio akakuleta sebleni tukupepee”
“Kheee mama alinibeba pekeyake?”
“Ndio alikubeba peke yake”
“Mama amewezaje kunibeba peke yake jamani wakati anasemaga siku hizi nimenenepa sana, amewezaje kunibeba peke yake nikiwa mzito hivi!”
“Yule ni mama, ametubeba wakati watoto na anaweza kutubeba hata sasa”
“Mmh jamani kaka zangu, ni mama kweli sijakataa. Katubeba wakati watoto, sijakataa lakini kumbukeni utotoni tulikuwa wadogo ila kadri tunavyokua na uzito nao unaongezeka. Mama angembeba mtu kama Ana sawa ila sio mimi na ubonge huu, yani hata nyie hamjapata mashaka. Sikumbuki kitu ila swala la kusema mama alinibeba peke yake limenishtua kidogo”
“Mmmh basi tuachane na habari hizo dada, cha muhimu unaendelea vizuri”
Kaka zake nao waliondoka na kumuacha mule chumbani.

 
SEHEMU YA 75


Usiku wake Sara alikuwa amelala ila akajiwa na njozi kuwa Ommy yupo mahali anateseka sana huku akimuomba Sara msaada aokolewe,
“Nisaidie Sara, nateseka naumia kwa kosa nisilolijua. Nisaidie Sara”
“Uko wapi kwani?”
Sara akashtuka na swali lake hilo, jasho likawa linamtoka tu ingawa chumbani kule feni ilikuwa inawaka. Alikaa na kujaribu kufikiria sana kuwa Ommy amepatwa na nini ila hakuelewa, akaamua achukue simu na kumpigia Ommy ila hiyo simu ilipoanza kuita aliiona chumbani kwake na kushangaa kuwa simu ya Ommy ipo chumbani kwake, hakuelewa imekuwaje hadi simu ipo pale na ni nani aliyeiingiza ile simu chumbani kwake. Akachukua simu ya Ommy na kuanza kuipitia kwani kwa upande mwingine alifurahi kuona simu ya Ommy kuwa ataweza kuona meseji zake. Na kweli alipochukua simu ya Ommy tu alibambana na ujumbe kutoka kwa Mishi, ujumbe ulikuwa unasema,
“Mpenzi wangu Ommy uko wapi jamani? Nimekumisi sana, mpaka muda huu kweli hujaja! Nakupenda sana mpenzi wangu”
Sara alijikuta akiumia moyo kupita maelezo ya kawaida, roho ya wivu iliingia ndani kwake na hapo akajikuta akisahau kabisa kama ameota kuwa Ommy yupo kwenye matatizo zaidi kilichomuuma ni kusalitiwa na Ommy basi, akajikuta akimjibu huyu Mishi,
“Usinisumbue nipo kwa mwanamke wa maisha yangu Sara. Nampenda sana”
Akatumia hiyo meseji ila moyo wangu ulijawa na wivu kiasi kwamba alijikuta akishindwa hata kulala,
“Yani huyu Ommy nampenda kwa moyo wwangu wote, hakuna chochote anachonipa ila mimi nampa upendo. Shida yoyote kiipata namsaidia. Kila kitu nampa, eti leo ananisaliti na mwanamke sijui wa kuitwa Mishi! Lazima nimjue huyo mwanamke nijue tofauti ya mimi na yeye ni nini kwani mimi nina ubaya gani wa kuchanganywa kimapenzi na mwanamke mingine! Yani wanaume hawa”
Alijikuta machozi yakimtoka tu na hakupata usingizi hadi kunakucha, wazo lake lilikuwa moja tu la kwenda kumtafuta Mishi ili ajue ni kwanini Ommy amemsaliti kwa huyo mwanamke.


 
SEHEMU YA 76


Rose siku ya leo alijiandaa kwenda kwa mganga wa kienyeji kwani bado swala la kupotelewa kwa pesa yake lilimuumiza sana na alitaka kujua huyo anayewatoa kumbukumbu familia yake bila yay eye mwenyewe kujua. Alimsihi mume wake asitoke kabisa siku ya leo,
“Tafadhali usiende popote”
“Sawa, sitaenda popote”
“Nitakuagizia mtu wa kukuletea chakula, tafadhali leo usitoke. Narudia tena na tena tafadhali sana leo usitoke”
“Nimekuelewa mke wangu sitatoka”
“Na Yule panya ambaye jana hajarudi, sitaki uende kumtafuta wala sitaki umkaribishe hapa tena”
“Panya gani huyo?”
“Si huyo shetani wa kuitwa Salome, simtaki katika nyumba yangu. Tafadhali Patrick huyo mtoto simtaki, usitake kabisa kunikera”
“Nimekuelewa mke wangu, sitafanya kinyume chako”
Rose akatoka na safari yake ikaanza ila alipitia kwanza shuleni na kumuacha mwanae Ana shuleni kisha yeye akaenda na safari yake ya kumtafuta mganga, akiwa njiani akaanza kuwaza jinsi hela zake zilivyopotea kizembe halafu jinsi mume wake akiwa hana kumbukumbu yoyote kuhusu alipozipeleka hizo pesa yani aliwaza sana, ila gafla alifunga breki ya gari kwani mbele yake aliona begi jeusi likiwa na mfanano wa lile lile begi ambalo aliliweka kwenye gari yake na mumewe akaondoka nalo. Rose alishuka kwenda kuliangalia, akasogea na kulichukua kisha akapanda nalo kwenye gari yake na kulifungua, alishangaa kuona pesa nyingi, kwakweli alishangaa sana na kujiuliza,
“Sio begi langu kweli hili? Ndio lenyewe bhana”
Alilifunga na kuweka pembezoni mwake kisha akacheka,
“Yani wamesikia naenda kwa mtaalamu wamerudisha begi, atakuwa kiboko sana Yule ninayemuendea. Na wala sirudi, naenda tu nimkomeshe huyo kidudu mtu asiyejulikana anayesumbua familia yangu”
Akawasha gari yake na kuendelea na safari.

 
SEHEMU YA 77


Sara aliwasiliana na Mishi kwa njia ya ujumbe na kujifanya ni Ommy huku akimuomba msamaha kwa kauli ya jana yake, nia yake kubwa ilikuwa ni kumuona huyo Mishi anafananaje. Alifika hadi eneo alilopanga kukutana na huyo Mishi na akabahatika kumuona kabla Mishi hjamuona yeye, hasira zilimpata yani muda huo hata hakutaka kujua kuwa Ommy yuko wapi au kitu gani kimemkuta ila yeye alikuwa akiumizwa na wivu tu muda huo. Alitamani aende amsogelee huyo Mishi na amuanzishie varangati ikiwezekana amdunde maana alijiona yeye ni bonge ni Mishi ni mwembamba kwahiyo alihisi kuwa angemudu kumdunda ila kabla hajaenda kufanya chochote alishangaa akishikwa bega, kugeuka nyuma alishangaa sana maana alimuona Salome,
“Kheeee Salome! Unafanya nini hapa?”
“Nikuulize wewe dada unafanya nini hapa?”
“Kuna mtu nilikuwa namsubiri maeneo haya”
“Mmmh dada wakati ulikuwa unampango wa kwenda kupigana na Yule dada wa kuitwa Mishi”
“Umejuaje?”
“Najua tu, katu usipende kuruhusu mapenzi yakakutawala hivyo dada yangu hadi ushindwe kufanya vitu vyako vya maana”
“Sikuelewi Salome”
“Mapenzi yapo tu na siku zote yatakuwepo ila heshima yako ni kubwa sana kuliko hayo mapenzi, mfano ukaenda na kupigana na Yule Mishi akakupiga itakuwaje? Si aibu hiyo mtu bonge kupigwa na kimbau mbau. Na mfano ukaenda mkapigana weee ila ashishinde yoyote itakuwaje? Ni kujidhalilisha huko, na mfano ukaenda kupigana na mtoto wa watu bahati mbaya akaanguka na kufa, huoni kama utapata kesi ya kujibu! Dadangu usitake mapenzi yakutawale kiasi hiko, tafadhali twende nyumbani”
Maneno ya Salome yalimuingia akilini Sara kwa kiasi chake, na kujikuta akitoa wazo la kutaka kwenda kupigana na Mishi badala yake kugeuza na Salome na kurudi nyumbani.
Walifika nyumbani na moja kwa moja Sara alienda chumbani kwake ambapo Salome alimfuata kwa nyuma, Sara alifika na kulia sana ila Salome alikuwa akimuangalia tu. Sara alilia sana kuhusu mapenzi ila alipotulia kiasi Salome alisogea na kumbembeleza. Sara alimuangalia Salome,
“Wewe ni mtoto mdogo, mapenzi huyajui vizuri”
“Mimi ni mtoto kwa kuniangalia ila sio mtoto kivile unavyonifikiria. Nimekuacha ulie ili utoe uchungu wako, dada yangu narudia tena usipende mapenzi yakutawale”
“Ila kwanini Ommy anifanyie hivi? Kwanini Ommy anisaliti?”
“Ila dada jamani mara nyingine unaweza kumlaumu bure huyo Ommy ingawa ni kweli ana makosa, Ommy anakupenda sana na alitaka kukuoa ila mama yako hataki hata kunuona akikusogelea, mama yako hataki hata upate muda wa kwenda kuonana na Ommy. Jamani nae ni binadamu anamatamanio jamani”
“Khabari za Ommy wewe umezijuaje?”
“Usiniulize tu habari za Ommy nimezijuaje bali niulize pia habari za Mishi nimezijuaje, ila nakwambia tena usiruhusu mapenzi yakutawale kiasi hicho. Ommy ni binadamu kama binadamu wengine, si malaika Yule kusema atakuwa sahihi kwenye kila kitu”
“Unasema tu kwasababu huyajui mapenzi, simtaki tena Ommy. Sitaki hata kumuona, akaendelea na hiko kimishi chake si kaniona mimi bonge sifai”
“Hizo ni hasira Sara, tena hasira ni hasara. Hapo ulipo hata hujui Ommy yuko wapi ila unasema hutaki tena kumuona”
“Sitaki ndio, sitaki kujua hata alipo”
“Ila moyo unakuuma, jambo lolote usilitafutie jawabu wewe mwenyewe. Ni Ommy pekee anayeweza kukujibu kati yako wewe na Mishi anampenda nani. Tunatakiwa tufanye jitihada za kumrudisha Ommy”
“Kumrudisha kwani yuko wapi?”
“Ngoja nikuache ulale kidogo ila ukiamka utakuwa na kumbukumbu zote kuhusu Ommy”
Sara alimshangaa sana Salome ila Salome alimuaga saran a kumuacha mule chumbani kisha yeye akatoka zake.

 
SEHEMU YA 78


Rose alifika kwa mganga wake na kukuta watu wengi sana kwenye foleni ila alishangaa akiitwa yeye ndani na kuwapita wote kwenye foleni huku wengine wakilalamika,
“Sababu kaja na gari, yani waganga wanapenda matajiri sababu wanajua wanahela”
Rose alitembea kwa madaha sana na kuingia kwenye kibanda cha mganga ila alishangaa kuona kibanda kile kikiwa tofauti na kwa waganga alipopazoea, na cha kushangaza alikaribishwa na sauti ya kike. Rose alikaa lakini alikuwa na wasiwasi mwingi sana, kulikuwa na mwanamke kajifunika na khanga mbele yake, mganga aliyemfata hapo ni mwanaume kwahiyo kitendo cha kuona mwanamke amekaa hapo kilimshangaza sana. Na kujikuta hata ameshindwa kusema chochote,
“Elezea matatizo yako”
Rose alishtushwa na sauti ya huyu mganga kwani ilikuwa ni sauti ya mtu anayemfahamu, akajikuta akisema kwa mshangao,
“Mozaa!!!”
Yule mganga alifunua sura yake na kumfanya Rose ashtuke zaidi kwani ni kweli alikuwa ni Moza.


Rose alishtushwa na sauti ya huyu mganga kwani ilikuwa ni sauti ya mtu anayemfahamu, akajikuta akisema kwa mshangao,
“Mozaa!!!”
Yule mganga alifunua sura yake na kumfanya Rose ashtuke zaidi kwani ni kweli alikuwa ni Moza.
Kwakweli Rose alitetemeka sana na kupata ujasiri wa gafla wa kutoka mule ndani na kuanza kukimbia yani kila mtu aliyekuwa pale alimshangaa, alikimbia sana kufika mbele akakumbuka gari yake na kujiuliza kurudi tena kuifuata, leo Rose alipatikana yani alipatikana haswaa kupita siku zote anazopatikana. Alichoka sana na kuanza kurudi kufata gari yake.
Alipofika kwenye gari yake alifungua na kuingia ndani ya gari, watu wapale karibu walimfata na kumuuliza kuwa ana tatizo gani lakini hakuna aliyemjibu zaidi ya kuondoa gari yake na kuondoka zake. Njia zima aliona kilichotokea kamavile ni ndoto tena ndoto haswaa, hadi hakujielewa jinsi anavyoendesha gari. Akapata wazo la kuangalia lile begi la hela aliloliokota kama lipo ila aliliona pale pale alipoliweka, kidogo akapata nafuu moyoni mwake kuwa begi lipo huku akiendelea na safari ya kurudi nyumbani kwake.

 
SEHEMU YA 79


Salome alikuwa amekaa sebleni kwa Rose ila Patrick alitoka chumbani na kushangaa kumkuta tena Salome kwenye nyumba hiyo, alimuuliza kwa mshangao
“Wewe tena umefuata nini kwenye nyumba hii?”
“Jamani baba si nimekuja kwako, kuishi kwa baba yangu!”
“Kwani wewe ni mwanangu?”
“Ndio mimi ni mwanao, naitwa Maria”
“Maria!! Ndio yupi?”
“Mama yangu ni Neema na alinipa jina la mama yako ambaye ni bibi yangu”
Patrick alikuwa kama akitafakari jambo na alionyesha kumkumbuka sana mama yake, kisha akainuka na kumkumbatia Salome,
“Jamani kumbe ndio wewe mtoto ambaye mama aliniambia kuwa natakiwa kumfahamu, masikini mama yangu nilimkuta amekufa”
“Pole sana baba, ila mimi ndio Maria”
“Naomba uishi hapa siku zote, mama alinihusia nikupende na nikutunze ila mama yangu alikufa na sikujua kama mwanangu huyo alikuwepo”
Yani akili za Patrick zilikuwa zinakuja na kuondoka kiasi kwamba alikuwa anashindwa kutambua jambo lolote kwa wakati mmoja yani mara nyingine ilimlazimu kutafakari kwanza.
Waliongea mengi sana, Patrick alijikuta akimwambia Salome kuhusu familia yake.
“Lakini mama yangu ndio alikuwa mke wako wa ndoa!”
“Ni kweli mama yako alikuwa mke wangu wa ndoa ila alinitendea jambo bay asana siwezi kusahau ila sikutaka tu kumfungulia mashtaka mama yako, na siku zote sikujua kama wewe upo yani kulikuwa na kauli mbili kuwa ni kweli nina mtoto kwakwe ila kauli nyingine ilikuwa mtoto si wa kwangu ila ana baba mwingine”
“Alikufanyia jambo gani baya?”
“Unajua mama yako niliishi nae kwa muda mrefu sana bila kupata mtoto, hivi unafikiri ni nani anayeweza kuvumilia muishi kwa miaka karibu ishirini bila mtoto! Ni nani anayeweza kuvumilia hilo? Niliondoka takribani miaka mitatu, kurudi kidogo tu mamako akasema amepata mimba yangu, unafikiri ni rahisi kwangu kuamini hilo? Nilimfukuza nakiri hilo kabisa, na nilimfukuza kwa hasira kwani sikuwa na imani hata kidogo kuwa amepata mimba yangu. Baada ya miezi kadhaa nikapata habari kuwa anaishi kwa mamangu na mama akasema mtoto anafanana sana na mimi na wamempa jina lake. Nilifurahi kusikia hivyo na nikawa na lengo moja kwenda kumchukua mamako kwa mamangu na wewe tuishi pamoja. Cha kushangaza siku niliyoenda nilimkuta mama yangu ameuwawa kikatili sana na watu wote wakasema ni Neema tu ndiye amehusika na kifo cha mama yangu. Kiukweli niliumia san asana, yani niliumia kupita maelezo. Nilitaka kumtafuta Neema nimfungulie mashtaka akaozee jela huko ila mke wangu Rose akanishauri kuwa nisifanye hivyo na nisahau habari za Neema, nimejitahidi kuzisahau hata na mtoto aliyemzaa habari zake zilipotea kwenye akili yangu ingawa kuna baadhi ya ndugu zangu walikuwa wananishauri nimtafute mwanangu, ila napenda sana kusikia ushauri wa mke wangu na aliniambia nisifanye hivyo kwani hakuna ushahidi wowote kuwa ni mwanangu. Ila leo umenikumbusha mbali sana, kwakweli Maria mwanangu nakumbuka kifo cha mama yangu. Naomba unikutanishe na mama yako aniambie kwanini alimuua mama yangu kikatili kiasi kile”
Salome loe alimuangalia kwa makini huyu mzee aliyeonyesha anaongea kwa kujiamini kabisa halafu anaonyesha kamavile akili yake ipo salama kabisa kwa siku hii, Salome alijikuta akisema,
“Sasa huyu ndio mzee Patrick ninayeweza kuongea nae kwasasa”
“Sikuelewi”
“Utanielewa tu, kwanza tambua kuwa mama yangu hakuhusika na kifo cha bibi ila ukweli wote utaupata kwenye ndoto”
“Kwenye ndoto?”
“Ndio kwenye ndoto”
“Kivipi?”
“Subiri”
Salome alitoka nje na baada ya muda kidogo akarudi ndani na kitu kidogo kama kipande cha mkaa kisha akampa Patrick atafune naye akafanya hivyo halafu akamwambia,
“Leo ukilala utaona kila kitu kama sinema jinsi mama yako alivyouwawa”
“Mmmh kwani wewe mwanangu ni mganga wa kienyeji?”
Salome akacheka na kumuuliza,
“Mbona nilivyokupa dawa utafune hukuniuliza chochote? Mimi si mganga baba, ila fanya vile nilivyokuelekeza”
Patrick alitamani hata aende akalale muda huo ili kama hiyo ndoto aipate muda huo kwani miaka yote alikuwa akifikiri kuwa Neema ndiye aliyemuua mama yake ndiomana hakupenda hata kumuona na wala kile kitendo cha kwenda kwa Neema hakijui maana kilifanyika kwa namna nyingine. Patrick aliinuka pale sebleni na kumuacha Salome peke yake kisha yeye akaelekea chumbani.

 
Back
Top Bottom