Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #201
SEHEMU YA 145
Mama Jack alifika nyumbani kwakina Yule binti na kukaribishwa vizuri sana, mama Jack hakuelewa kuwa alikuwa mtegoni maana Yule binti alikuwa ni Salome ambapo alipitia hospitali kumchukua Doto kwahiyo mama Jack alifika kwenye nyumba ya Rose bila kujua kuwa pale ni nyumbani kwa Rose, na kwavile mama Jack hakuwazoea watoto wa Rose kwahiyo ilikuwa vigumu sana kwa yeye kugundua kuwa wale ni watoto wa Rose, mtoto pekee wa Rose aliyemfahamu alikuwa ni Ana na muda huo aliofika Ana alikuwa bado yupo shuleni.
Walimkaribisha vizuri sana huku Salome akiwaambia kuwa Yule mama kamsaidia sana bila ya kusema kuwa kamsaidia vitu gani, ila Salome alimuomba huyu mama asubiri mama yao atarudi nyumbani muda sio mrefu, Sara alimuuliza Salome,
“Una uhakika mama atarudi leo?”
Salome alimuangalia kwa jicho kali Sara na kumfanya Sara ainuke tu pale alipokuwa amekaa kanakwamba alimwambia kuwa aondoke, kisha Salome akabadilisha mada na kuanza kuongea na Doto habari za hospitali na jinsi anavyojisikia, kwavile habari ilibadilika kidogo, Sara alijikuta akirudi tena sebleni huku akiwa ameongozana na Kulwa ambaye alifurahi kusikia kuwa Doto ametoka hospitali.
Patrick alirudi moja kwa moja kwa Neema na kujikuta akimueleza Neema kile ambacho kaelezwa na vijana aliokutana nao, kwakweli Neema alishangaa sana na kuuliza kwa makini
“Kwahiyo Ashura amekufa?”
“Ndio, nimeona hivi picha akiwa ameanza kuoza kwakweli sijui kama ile picha itatoka akilini mwangu ila siamini kama Salome anaweza kutenda kitu cha namna hiyo”
“Nimeumia sana, ingawa kuna mengi nimeyagundua kijijini lakini Ashura niliishi nae kama ndugu yangu kabisa, alikuwa kama mdogo wangu na aliwapenda wanangu. Ila siamini kama Salome anaweza kutenda kitu cha namna hiyo, hapana kwakweli. Salome ni mwanangu, namjua vyema sana, hawezi kufanya jambo la namna hiyo. Salome hawezi kuua”
“Hata mimi nimekataa kuwa Salome hawezi kuua”
“Naomba hao vijana watupeleke huko nikaone jambo alipotupiwa ndugu yangu Ashura jamani nimeumia sana, sasa mbona nilikuwa nawasiliana nae jamani aaah haiwezekani”
Akajikuta akikumbuka kuwa wanae hawa wadogo wamewahi kumwambia kuwa mama yao mdogo Ashura alianguka na povu kumtoka halafu Salome akawaambia ni mchezo wanacheza, akajikuta anasema,
“Ina maana……”
“Ina maana nini?”
“Aaah tuachane na habari hizo, jamani Ashura ndugu yangu hapana jamani. Hata kama hakuwa ndugu yangu, hakustahili kuzikwa kinyama hivyo”
Alichukua simu yake na kujaribisha ile namba aliyokuwa anawasiliana na Ashura ila hakuipata hewani na kumfanya hadi tumbo limuume na kuzidi kuamini kuwa itakuwa kweli ashura kauwawa ila bado moyo wake ulikataa kuwa kauliwa na Salome kwani hakutegemea kama mwanae anauwezo wa kuua.
Mama Jack alifika nyumbani kwakina Yule binti na kukaribishwa vizuri sana, mama Jack hakuelewa kuwa alikuwa mtegoni maana Yule binti alikuwa ni Salome ambapo alipitia hospitali kumchukua Doto kwahiyo mama Jack alifika kwenye nyumba ya Rose bila kujua kuwa pale ni nyumbani kwa Rose, na kwavile mama Jack hakuwazoea watoto wa Rose kwahiyo ilikuwa vigumu sana kwa yeye kugundua kuwa wale ni watoto wa Rose, mtoto pekee wa Rose aliyemfahamu alikuwa ni Ana na muda huo aliofika Ana alikuwa bado yupo shuleni.
Walimkaribisha vizuri sana huku Salome akiwaambia kuwa Yule mama kamsaidia sana bila ya kusema kuwa kamsaidia vitu gani, ila Salome alimuomba huyu mama asubiri mama yao atarudi nyumbani muda sio mrefu, Sara alimuuliza Salome,
“Una uhakika mama atarudi leo?”
Salome alimuangalia kwa jicho kali Sara na kumfanya Sara ainuke tu pale alipokuwa amekaa kanakwamba alimwambia kuwa aondoke, kisha Salome akabadilisha mada na kuanza kuongea na Doto habari za hospitali na jinsi anavyojisikia, kwavile habari ilibadilika kidogo, Sara alijikuta akirudi tena sebleni huku akiwa ameongozana na Kulwa ambaye alifurahi kusikia kuwa Doto ametoka hospitali.
Patrick alirudi moja kwa moja kwa Neema na kujikuta akimueleza Neema kile ambacho kaelezwa na vijana aliokutana nao, kwakweli Neema alishangaa sana na kuuliza kwa makini
“Kwahiyo Ashura amekufa?”
“Ndio, nimeona hivi picha akiwa ameanza kuoza kwakweli sijui kama ile picha itatoka akilini mwangu ila siamini kama Salome anaweza kutenda kitu cha namna hiyo”
“Nimeumia sana, ingawa kuna mengi nimeyagundua kijijini lakini Ashura niliishi nae kama ndugu yangu kabisa, alikuwa kama mdogo wangu na aliwapenda wanangu. Ila siamini kama Salome anaweza kutenda kitu cha namna hiyo, hapana kwakweli. Salome ni mwanangu, namjua vyema sana, hawezi kufanya jambo la namna hiyo. Salome hawezi kuua”
“Hata mimi nimekataa kuwa Salome hawezi kuua”
“Naomba hao vijana watupeleke huko nikaone jambo alipotupiwa ndugu yangu Ashura jamani nimeumia sana, sasa mbona nilikuwa nawasiliana nae jamani aaah haiwezekani”
Akajikuta akikumbuka kuwa wanae hawa wadogo wamewahi kumwambia kuwa mama yao mdogo Ashura alianguka na povu kumtoka halafu Salome akawaambia ni mchezo wanacheza, akajikuta anasema,
“Ina maana……”
“Ina maana nini?”
“Aaah tuachane na habari hizo, jamani Ashura ndugu yangu hapana jamani. Hata kama hakuwa ndugu yangu, hakustahili kuzikwa kinyama hivyo”
Alichukua simu yake na kujaribisha ile namba aliyokuwa anawasiliana na Ashura ila hakuipata hewani na kumfanya hadi tumbo limuume na kuzidi kuamini kuwa itakuwa kweli ashura kauwawa ila bado moyo wake ulikataa kuwa kauliwa na Salome kwani hakutegemea kama mwanae anauwezo wa kuua.