Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #221
SEHEMU YA 155
Rose aliitwa tena na mganga ili atoe chaguo lake alilolifikiria,
“Muda unakwenda Rose, na usiku huo unaingia, chagua moja kumzika rafiki yako au kutoa kafara wanao”
“Hapana kwakweli, kuwatoa kafara wanangu hapana, nipo tayari kumzika rafiki yangu”
“Kumbuka utaenda kumzika peke yako na giza hili, hakuna wa kukusaidia. Chagua tena”
Rose hakuwa na jibu la zaidi ya kumzika rafiki yake,
“Kama umeamua hivyo sawa, inabidi azikwe leoleo yani maiti yake isilale tena maana yatatokea majanga bure”
“Majanga gani?”
“Usiniulize majanga gani, jua kuwa yatatokea majanga. Yani unatakiwa uizike maiti leoleo, ila kwa usalama wako ukiwa unatoka hapo mlangoni kwenda kuizika hiyo maiti usiongee na mtu yeyote Yule ila nenda moja kwa moja kuna mahali utakuta shimo halafu utamdumbukiza rafiki yako huku ukitaja majina yote ya watoto wako baada ya hapo utarudi na kulala hapa. Nadhani tumeelewana”
“Ndio tumeelewana”
“Haya lamba dawa hii na usiseme chochote”
Rose akalamba ile dawa na kutoka nje, ila kabla hajalisogelea gari lake akashangaa kumuona mwanae Ana akiwa amemfata kule kwa mganga, alishangaa sana na kujikuta akisema,
“Ana!”
“Ndio ni mimi mama, nimekufata nata……”
Ila kabla Ana hajamaliza sentensi yake, Rose alianguka chini na kuanza kutapatapa.
Rose akalamba ile dawa na kutoka nje, ila kabla hajalisogelea gari lake akashangaa kumuona mwanae Ana akiwa amemfata kule kwa mganga, alishangaa sana na kujikuta akisema,
“Ana!”
“Ndio ni mimi mama, nimekufata nata……”
Ila kabla Ana hajamaliza sentensi yake, Rose alianguka chini na kuanza kutapatapa.
Ana alipatwa na hofu sana baada ya kumuona mama yake katika hali ile ila gafla alijikuta akipata wazo la kutoa lile jiwe la dhahabu ila hakujua kuwa afanye nalo kitu gani.
Akalitoa lile jiwe la dhahabu na kujikuta akilishika na kuliweka kwenye kifua cha mama yake na gafla wakatoweka mahali pale.
Mganga alikuwa pembeni akiwaangalia na akiangalia kinachoendelea kwahiyo alishangazwa sana na kuona kuwa gafla watu wale hawaonekani ila gari ya Rose ilibaki pale pale na mwili wa mama Jack ulibaki mule mule kwenye gari, mganga alishangaa sana na kumwambia msaidizi wake,
“Mwanamke mshenzi sana Yule, ananiletea uchawi wake kwenye nyumba yangu pia! Kaacha maiti yake hapa, akimaanisha nini? Na nitamkomesha kwakweli yani nitamkomesha haswaa”
Msaidizi wa mganga alikaa kimya kwani hata yeye hakuelewa kitu chochote kile kinachoendelea, na pia hakuelewa kuwa yeye na mganga watafanya nini na maiti ambayo imeachwa ndani ya gari.
Rose aliitwa tena na mganga ili atoe chaguo lake alilolifikiria,
“Muda unakwenda Rose, na usiku huo unaingia, chagua moja kumzika rafiki yako au kutoa kafara wanao”
“Hapana kwakweli, kuwatoa kafara wanangu hapana, nipo tayari kumzika rafiki yangu”
“Kumbuka utaenda kumzika peke yako na giza hili, hakuna wa kukusaidia. Chagua tena”
Rose hakuwa na jibu la zaidi ya kumzika rafiki yake,
“Kama umeamua hivyo sawa, inabidi azikwe leoleo yani maiti yake isilale tena maana yatatokea majanga bure”
“Majanga gani?”
“Usiniulize majanga gani, jua kuwa yatatokea majanga. Yani unatakiwa uizike maiti leoleo, ila kwa usalama wako ukiwa unatoka hapo mlangoni kwenda kuizika hiyo maiti usiongee na mtu yeyote Yule ila nenda moja kwa moja kuna mahali utakuta shimo halafu utamdumbukiza rafiki yako huku ukitaja majina yote ya watoto wako baada ya hapo utarudi na kulala hapa. Nadhani tumeelewana”
“Ndio tumeelewana”
“Haya lamba dawa hii na usiseme chochote”
Rose akalamba ile dawa na kutoka nje, ila kabla hajalisogelea gari lake akashangaa kumuona mwanae Ana akiwa amemfata kule kwa mganga, alishangaa sana na kujikuta akisema,
“Ana!”
“Ndio ni mimi mama, nimekufata nata……”
Ila kabla Ana hajamaliza sentensi yake, Rose alianguka chini na kuanza kutapatapa.
Rose akalamba ile dawa na kutoka nje, ila kabla hajalisogelea gari lake akashangaa kumuona mwanae Ana akiwa amemfata kule kwa mganga, alishangaa sana na kujikuta akisema,
“Ana!”
“Ndio ni mimi mama, nimekufata nata……”
Ila kabla Ana hajamaliza sentensi yake, Rose alianguka chini na kuanza kutapatapa.
Ana alipatwa na hofu sana baada ya kumuona mama yake katika hali ile ila gafla alijikuta akipata wazo la kutoa lile jiwe la dhahabu ila hakujua kuwa afanye nalo kitu gani.
Akalitoa lile jiwe la dhahabu na kujikuta akilishika na kuliweka kwenye kifua cha mama yake na gafla wakatoweka mahali pale.
Mganga alikuwa pembeni akiwaangalia na akiangalia kinachoendelea kwahiyo alishangazwa sana na kuona kuwa gafla watu wale hawaonekani ila gari ya Rose ilibaki pale pale na mwili wa mama Jack ulibaki mule mule kwenye gari, mganga alishangaa sana na kumwambia msaidizi wake,
“Mwanamke mshenzi sana Yule, ananiletea uchawi wake kwenye nyumba yangu pia! Kaacha maiti yake hapa, akimaanisha nini? Na nitamkomesha kwakweli yani nitamkomesha haswaa”
Msaidizi wa mganga alikaa kimya kwani hata yeye hakuelewa kitu chochote kile kinachoendelea, na pia hakuelewa kuwa yeye na mganga watafanya nini na maiti ambayo imeachwa ndani ya gari.