Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #261
SEHEMU YA 182
Neema alipoamka alijikuta kasahau kila kitu hata kuhusu kutokuwaamsha wanae waende shule alikuwa amesahau huku akijua kuwa alishawaamsha wakaenda shule na yeye akarudi kulala, kwahiyo muda huu alioga na kujiweka sawa kisha kuanza kuandaa kifungua kinywa huku akisema kuwa yani Salome ametoka bila ya kumuaga, wakati anaandaa chai sebleni akakuta barua mezani kwake ikiwa imeandikwa kwa maneno machache tu,
“Kwako mama mpendwa, mimi naenda kuishi kwenye ile nyumba aliyokuwa akiishi baba yangu, nina maana yangu ya kufanya hivi. Nitarudi nikiwa nimekamilika. Kwaheri, ni mimi mtoto wako mpendwa Salome”
Neema alishangaa sana kwa uamuzi huo uliochukuliwa na Salome,
“Ataendaje kuishi kwenye nyumba ambayo hata baba yake hayupo, si ndio watamuua huko jamani? Kwanini kaamua kufanya hivi Salome?”
Halafu sasa akagundua kuwa hiyo sehemu wala haijui sababu hajawahi kufika zaidi ya siku waliyoenda kwenye msiba wa Moza na waliishia katikati sababu walikuta ndio wanaenda kuzika kwahiyo swala la yeye kufika nyumbani kwa Rose lilikuwa ni gumu sana, akaamua kunywa chai kwanza kisha kuchukua maamuzi mengine. Alipomaliza kunywa chai aligundua kuwa lile karatasi lenye ujumbe lilimwagikiwa na chai hivyo akachukua maamuzi ya kulitoa pamoja na vyombo vichafu kisha akaenda kulidumbukiza chooni. Kisha alienda kuchukua simu yake na kukaa sebleni ili ampigie Patrick na kumpa hiyo habari ila alipochukua alikutana na ujumbe kutoka kwa mama Pendo,
“Pole sana kwa maswahibu hayo ndugu yangu, ambayo kiuhalisia naona kama ni kiini macho kwakweli ila leo nitakuja na mchungaji hapo kwako. Mwambie mwanao asitoke, tunakuja kufanya maombi”
Neema alikuwa akishangaa huu ujumbe kutoka kwa mama Pendo kwani hata yeye hakuwa na kumbukumbu kuwa ni maswahibu gani aliyokuwa amemueleza mama Pendo,
“Kwani mama Pendo anaongelea kuhusu maswahibu gani jamani, kwani kuna maswahibu yoyote yamenipata au kaoteshwa huyu?”
Alijiuliza bila ya jibu sababu hakuwa na kumbukumbu ya aina yoyote ile kichwani mwake yani hata swala la kukumbuka kuwa alimkuta Salome amelala na gafla akamkuta mlangoni akigonga mlango haikuwepo hiyo kumbukumbu katika akili yake kabisa.
Kama ambavyo Mishi aliahidiwa na mumewe kwahiyo asubuhi asubuhi waliondoka na kwenda kwa mtaalamu lengo lilikuwa ni kuangaliziwa kuhusu huyo binti halafu na kuangaliziwa kuhusu mimba aliyokuwa nayo Mishi, walimkuta mganga na wateja wachache tu na walipoisha waliingia wao na kuanza kumuelezea matatizo yao,
“Yani cha kuwaambia tu huyo mtu ambaye mmeleta malalamiko yenu hapa, yupo nje anawasubiri”
“Anatusubiri!”
Walishtuka sana,
“Ndio anawasubiria”
“Sasa tutafanya nini?”
“Sio mtu mzuri Yule, ila yupo kwaajili ya kumkomesha mtu mmoja tu sema ukijiingiza kwenye familia hiyo imekula kwako kwahiyo na nyie swala la kuja kwangu ili niwasaidie itakula kwangu na kwenu”
“Tusaidie mganga, mi sioni kama mimba hiyo ina ukweli kwa mke wangu”
“Laiti kama mkeo akitoa hiyo mimba kaa ukijua kuwa si wewe wala mkeo utaweza tena kuwa na watoto katika maisha yenu. Mkeo alikuwa na makosa ndiomana akapewa hiyo adhabu”
“Makosa gani?”
Mishi alianza kuona aibu kwani hakumwambia ukweli mume wake kuhusu makosa yake mpaka kufikia hatua ya kubakwa ila alimwambia tu kuna vijana mapacha walidhania kuwa anawachanganya ndio huyo mtu akampa laana hiyo, basi Yule mganga akamuangalia Mishi na kumuuliza,
“Je nimwambie kuhusu makosa yako?”
Mishi alitikisa kichwa kwa ishara kuwa asimwambie, ila Yule mganga aliendelea,
“Hata nisipomwambia, ilimradi anawasuburia nje, basi napo atamwambia tu. Bora nimwambie mimi”
Mume wa Mishi akamuomba mganga amwambie maana alihisi kufichwa mambo mengine, ila Mishi aliona aibu sana na kuinuka kisha akatoka nje, ila mumewe bado alikomaa kuwa aambiwe, Yule mganga aligoma kusema sababu muhusika kainuka,
“Yani mimi kusema siwezi maana mwenyewe kainuka lakini mfate tu mtaonana na Yule mtu na atakwambia ukweli maana hatakuficha lolote”
Ikabidi mume wa Mishi ainuke tu ili amfate mkewe nje maana mkewe alishatoka eneo hilo, ila alipofika alipo mkewe alishangaa kumuona mkewe kasimama na binti Fulani ambaye yeye hakumjua binti huyo, ikabidi awafate ila huyu binti kabla hata ya salamu alianza kumwambia mume wa Mishi,
“Mkeo nimempa adhabu hiyo sababu amekuwa akiumiza moyo wa wenzie sana, bora angekuwa anajiuza tungejua moja kuliko alichokuwa anafanya huyu. Yani anakuwa na wanaume zaidi ya watano kwa wakati mmoja halafu wote anawadanganya kuwa anawapenda, je ni nafasi za mabinti wangapi anaziziba ambao wangependwa na hao wanaume? Ile familia aliumiza mioyo ya watu watatu, sasa ni zamu yake nay eye kuumia moyo. Kuhusu wanaume wengine aliokuwa nao atakwambia mwenyewe, huyu mkeo ni zaidi ya wanawake wanaojiuza ila nimemwambia akithubutu kufanya hivyo na kwenye ndoa yenu nitamkomesha”
Kisha Salome akaondoka na kuwaacha, Mishi alikuwa na aibu sana. Mumewe akamuangalia kwa jicho la gadhabu na kumwambia,
“Kumbe nimeoa changudoa, mwenyewe nilijisifu kuwa mwanamke anamsimamo hataki nimuoe ananipima kwanza kumbe ni changudoa. Kwakweli Mishi umeniangusha sana, yani unajua uovu ulikuwa unautenda nab ado bila ya aibu unataka tuje kwa mganga wa kienyeji ulidhani afanyeje sasa na wakati una laana? Unafikiri machozi ya watu wote uliowaliza yameenda bure? Tena uwe mpole kabisa maana ukileta kidomo domo chako nitawaeleza ndugu zako wote ukweli kuwa ulibakwa”
Mume wa Mishi akaondoka zake ikabidi Mishi amfate nyuma huku aibu tele ikimshika moyoni kwani hakutegemea kama angeaibika kwa kiasi hicho, alikuwa akitembea kwa aibu tele tele usoni.
Neema alipoamka alijikuta kasahau kila kitu hata kuhusu kutokuwaamsha wanae waende shule alikuwa amesahau huku akijua kuwa alishawaamsha wakaenda shule na yeye akarudi kulala, kwahiyo muda huu alioga na kujiweka sawa kisha kuanza kuandaa kifungua kinywa huku akisema kuwa yani Salome ametoka bila ya kumuaga, wakati anaandaa chai sebleni akakuta barua mezani kwake ikiwa imeandikwa kwa maneno machache tu,
“Kwako mama mpendwa, mimi naenda kuishi kwenye ile nyumba aliyokuwa akiishi baba yangu, nina maana yangu ya kufanya hivi. Nitarudi nikiwa nimekamilika. Kwaheri, ni mimi mtoto wako mpendwa Salome”
Neema alishangaa sana kwa uamuzi huo uliochukuliwa na Salome,
“Ataendaje kuishi kwenye nyumba ambayo hata baba yake hayupo, si ndio watamuua huko jamani? Kwanini kaamua kufanya hivi Salome?”
Halafu sasa akagundua kuwa hiyo sehemu wala haijui sababu hajawahi kufika zaidi ya siku waliyoenda kwenye msiba wa Moza na waliishia katikati sababu walikuta ndio wanaenda kuzika kwahiyo swala la yeye kufika nyumbani kwa Rose lilikuwa ni gumu sana, akaamua kunywa chai kwanza kisha kuchukua maamuzi mengine. Alipomaliza kunywa chai aligundua kuwa lile karatasi lenye ujumbe lilimwagikiwa na chai hivyo akachukua maamuzi ya kulitoa pamoja na vyombo vichafu kisha akaenda kulidumbukiza chooni. Kisha alienda kuchukua simu yake na kukaa sebleni ili ampigie Patrick na kumpa hiyo habari ila alipochukua alikutana na ujumbe kutoka kwa mama Pendo,
“Pole sana kwa maswahibu hayo ndugu yangu, ambayo kiuhalisia naona kama ni kiini macho kwakweli ila leo nitakuja na mchungaji hapo kwako. Mwambie mwanao asitoke, tunakuja kufanya maombi”
Neema alikuwa akishangaa huu ujumbe kutoka kwa mama Pendo kwani hata yeye hakuwa na kumbukumbu kuwa ni maswahibu gani aliyokuwa amemueleza mama Pendo,
“Kwani mama Pendo anaongelea kuhusu maswahibu gani jamani, kwani kuna maswahibu yoyote yamenipata au kaoteshwa huyu?”
Alijiuliza bila ya jibu sababu hakuwa na kumbukumbu ya aina yoyote ile kichwani mwake yani hata swala la kukumbuka kuwa alimkuta Salome amelala na gafla akamkuta mlangoni akigonga mlango haikuwepo hiyo kumbukumbu katika akili yake kabisa.
Kama ambavyo Mishi aliahidiwa na mumewe kwahiyo asubuhi asubuhi waliondoka na kwenda kwa mtaalamu lengo lilikuwa ni kuangaliziwa kuhusu huyo binti halafu na kuangaliziwa kuhusu mimba aliyokuwa nayo Mishi, walimkuta mganga na wateja wachache tu na walipoisha waliingia wao na kuanza kumuelezea matatizo yao,
“Yani cha kuwaambia tu huyo mtu ambaye mmeleta malalamiko yenu hapa, yupo nje anawasubiri”
“Anatusubiri!”
Walishtuka sana,
“Ndio anawasubiria”
“Sasa tutafanya nini?”
“Sio mtu mzuri Yule, ila yupo kwaajili ya kumkomesha mtu mmoja tu sema ukijiingiza kwenye familia hiyo imekula kwako kwahiyo na nyie swala la kuja kwangu ili niwasaidie itakula kwangu na kwenu”
“Tusaidie mganga, mi sioni kama mimba hiyo ina ukweli kwa mke wangu”
“Laiti kama mkeo akitoa hiyo mimba kaa ukijua kuwa si wewe wala mkeo utaweza tena kuwa na watoto katika maisha yenu. Mkeo alikuwa na makosa ndiomana akapewa hiyo adhabu”
“Makosa gani?”
Mishi alianza kuona aibu kwani hakumwambia ukweli mume wake kuhusu makosa yake mpaka kufikia hatua ya kubakwa ila alimwambia tu kuna vijana mapacha walidhania kuwa anawachanganya ndio huyo mtu akampa laana hiyo, basi Yule mganga akamuangalia Mishi na kumuuliza,
“Je nimwambie kuhusu makosa yako?”
Mishi alitikisa kichwa kwa ishara kuwa asimwambie, ila Yule mganga aliendelea,
“Hata nisipomwambia, ilimradi anawasuburia nje, basi napo atamwambia tu. Bora nimwambie mimi”
Mume wa Mishi akamuomba mganga amwambie maana alihisi kufichwa mambo mengine, ila Mishi aliona aibu sana na kuinuka kisha akatoka nje, ila mumewe bado alikomaa kuwa aambiwe, Yule mganga aligoma kusema sababu muhusika kainuka,
“Yani mimi kusema siwezi maana mwenyewe kainuka lakini mfate tu mtaonana na Yule mtu na atakwambia ukweli maana hatakuficha lolote”
Ikabidi mume wa Mishi ainuke tu ili amfate mkewe nje maana mkewe alishatoka eneo hilo, ila alipofika alipo mkewe alishangaa kumuona mkewe kasimama na binti Fulani ambaye yeye hakumjua binti huyo, ikabidi awafate ila huyu binti kabla hata ya salamu alianza kumwambia mume wa Mishi,
“Mkeo nimempa adhabu hiyo sababu amekuwa akiumiza moyo wa wenzie sana, bora angekuwa anajiuza tungejua moja kuliko alichokuwa anafanya huyu. Yani anakuwa na wanaume zaidi ya watano kwa wakati mmoja halafu wote anawadanganya kuwa anawapenda, je ni nafasi za mabinti wangapi anaziziba ambao wangependwa na hao wanaume? Ile familia aliumiza mioyo ya watu watatu, sasa ni zamu yake nay eye kuumia moyo. Kuhusu wanaume wengine aliokuwa nao atakwambia mwenyewe, huyu mkeo ni zaidi ya wanawake wanaojiuza ila nimemwambia akithubutu kufanya hivyo na kwenye ndoa yenu nitamkomesha”
Kisha Salome akaondoka na kuwaacha, Mishi alikuwa na aibu sana. Mumewe akamuangalia kwa jicho la gadhabu na kumwambia,
“Kumbe nimeoa changudoa, mwenyewe nilijisifu kuwa mwanamke anamsimamo hataki nimuoe ananipima kwanza kumbe ni changudoa. Kwakweli Mishi umeniangusha sana, yani unajua uovu ulikuwa unautenda nab ado bila ya aibu unataka tuje kwa mganga wa kienyeji ulidhani afanyeje sasa na wakati una laana? Unafikiri machozi ya watu wote uliowaliza yameenda bure? Tena uwe mpole kabisa maana ukileta kidomo domo chako nitawaeleza ndugu zako wote ukweli kuwa ulibakwa”
Mume wa Mishi akaondoka zake ikabidi Mishi amfate nyuma huku aibu tele ikimshika moyoni kwani hakutegemea kama angeaibika kwa kiasi hicho, alikuwa akitembea kwa aibu tele tele usoni.