Simulizi: Lisa

Hamid alisema, "Zaidi ya hayo, nilikuwa na maingiliano machache na Cindy hapo awali. Mimi tayari ni mmoja wa wasimamizi bora katika kampuni. Hata mkurugenzi Mutui inabidi anitendee kwa heshima anaponiona. Lakini Cindy ananidharau kwa sababu tu anadhani yeye ni mwanamke wa Bwana Choka. Mtu kama yeye ana akili finyu. Akigundua kuwa una mahusiano na bwana’ake ataweza kukukandamiza.”
“Nimeelewa kila ulichosema. Ndiyo maana nimekuwa nikikataa mapendekezo ya Chester.” Eliza alikunja uso. "Watu kama yeye wanatuchukulia kama wanawake wepesi.”
“Ni vizuri kama umeelewa. Natumai Bwana Choka atakata tamaa hivi karibuni,” Hamid alimkumbusha, “Monte ni mfano bora zaidi.”
Akiongea juu ya Monte, Eliza alinyamaza.
Kwa kweli, hakuwa na hisia nyingi za Monte tena. Alipoamka, aligundua kuwa Eliza wa zamani alikuwa amejiua kwa ajili ya Monte. Hakuwa chochote ila mpuuzi mmoja tu.
“Pumzika kidogo. Acha Loida abaki hapa na akutunze. Bado natakiwa kusimamia mambo yako. Kuna kundi la wanahabari nje,” Hamid alisema, “By the way, tunapaswa kushughulikia vipi suala la baba yako?”
"Vyombo vya habari vinaripotije juu ya mambo?" Eliza aliuliza.
"Kwa bahati nzuri, tayari walichimba habari za Jacob na familia yake. Hata waliwasiliana na watu wengi wanaomfahamu Jacob na familia yake ili watoe taarifa. Hata hivyo, watu wa nje tayari wanajua kwamba wao ni familia ya wanyonyaji. Umma unakuonea huruma sana sasa.”
Eliza alifikiria na kusema, “Onyesha jina la mtaa wa Jacob na anwani ya kampuni ya mwanawe. Pia, tafuta wakili ili arudishe pesa nilizompa Jacob hapo awali. Wakati huo huo, mshitaki Jacob. Kwa kuwa alinijeruhi, anapaswa kwenda jela.”
Hamid alimtazama kwa mshangao.
"Nini?" Eliza aliuliza.
"Hakuna," Hamid alisema kwa hisia ngumu, "Nadhani umebadilika sana sasa. Hukuwa hivi hapo awali. Ulikuwa na moyo laini na uliendelea kujali uhusiano huo ambao haupo sawia kabisa wa baba na binti. Kwa kweli, ulikuwa dhaifu sana wakati huo.”
"Sitakuwa dhaifu tena," Eliza alisema, "Wale ambao hawakunitendea vizuri hawana haki ya kuninyang'anya vitu vyangu."
“Sawa.”
Hamid aliondoka.

Loida alimlisha Eliza uji. Haukupita muda mrefu, mlango ukafunguliwa tena. Mtu aliyeingia alikuwa Chester. Alivaa koti jeupe na miwani. Alikuwa na matatizo ya-kutoona mbali, kwa hiyo huwa anavaa miwani alipokuwa akifanya kazi. Lakini, hiyo haikuathiri sura yake nzuri. Kinyume chake, ilimfanya aonekane maridadi zaidi, muungwana, na mwenye akili.
Loida alikuwa akisikia watu wakisema kwamba Chester alikuwa anavutia zaidi alipovalia koti jeupe. Kwa wakati huo, karibu alisahau kugeuza macho yake alipojionea mwenyewe leo. Alikumbushwa tu baada ya Eliza kujisafisha koo lake kirahisi. Loida aliporudi kwenye fahamu zake, alihisi kuchanganyikiwa na kukosa utulivu.
Loida hakuelewa. Ni wazi kwamba Chester alikuwa mtu mchafu, lakini kwanini sura yake ilionekana wazi na angavu kama mwezi? Kama inavyotarajiwa, wanaume hawakuweza kuhukumiwa kwa sura zao.
"Unaweza kuondoka kwanza," Chester alimwambia Loida mara moja.
Loida alijieleza kwa wasiwasi. “Bwana Choka, jeraha la Eliza bado halijapona. Hupaswi—”
“Je, ninaonekana kuwa nataka kumfanyia kitendo kibaya?” Chester akamkatisha. “Zaidi ya hayo, mimi ndiye daktari wake ninayemsimamia. Mimi ndiye niliyemtibu jeraha lake.”
“Oh...” Loida hakuwa na la kufanya ila kuondoka.

Eliza alimtazama Chester kwa uso dhaifu na uliopauka. "Asante, Bwana Choka."
“Inatosha?” Chester aliketi kando ya kitanda, akitabasamu. “Eliza, mimi ni mtu ninayetii sheria. Lakini kwa ajili yako, nilifanya taarifa ya uongo kwa mara ya kwanza. Si hivyo tu, hata mimi ndiye niliyekuleta hospitalini.”
Eliza hakusema neno, na macho yake yalikuwa baridi kama barafu.
“Eliza, nimeona wanawake wengi wajanja kama wewe. Hata hivyo, sijawahi kuona mtu anayejitendea ukatili kama wewe.” Chester akarekebisha miwani yake. "Umefaulu kuamsha shauku yangu kwako."

Sura ya: 739
 
Eliza alicheka.
Chester hakufikiri ni kicheko cha furaha. “Unacheka nini?”
"Ah, unasikika kama wale mabwana wakuu katika drama ambazo nimeigiza hapo awali. Kama 'Mwanamke, ninavutiwa nawe,' au 'Mwanamke, nimekuangukia wewe.”' Midomo ya Eliza iliyopauka kidogo ikainuliwa. “Lakini hao mabwana wakubwa wanawabembeleza wake zao huku wewe unamtongoza mwanamke wa kando. Pia, unafanya hivyo wazi. Sijui nikupongeze kwa kuwa na ujasiri au kwa kukosa aibu?”
Uso mzuri wa Chester uligeuka kuwa mweusi kama sehemu ya chini ya sufuria. “Eliza nimekusaidia tu, kumbe unanidhalilisha sasa. Umenidhalilisha mara ngapi, huh?”

“Sikudhalilishi. Nilichosema ni kweli.” Eliza alishtuka. "Ikiwa unafikiri maneno yangu ya uaminifu yanafedhehesha, siwezi kufanya chochote kuhusu hilo."
“Eliza, wewe... unafikiri sithubutu kukufanyia chochote?” Chester akamshika mkono. Alipoivuta tu, Eliza alishusha pumzi kutokana na maumivu.
Alipoona kuwa anaumwa lakini alikuwa amekunja uso tu na kuvumilia, moyo wa Chester ukasisimka. Aliachilia mshiko wake kwa silika.
Eliza alichukua muda sana kupona kutokana na maumivu na akasema, “Je, mtu kama wewe anawezaje kuwa daktari anayenisimamia? Je, ninaweza kuomba daktari mwingine?”
Je! unajua ni watu wangapi ulimwenguni pote wanaoniomba nitibu magonjwa yao?” Chester akaachia kikohozi. "Haijalishi, Eliza, una deni kwangu wakati huu."
Eliza alizungusha kichwa na kusema. “Kwa kweli, naweza kukataa kuwa na deni hili kwako. Wewe ndiye ulihusika katika hili. Hata bila wewe, bado ningeweza kupiga simu kuita ambulance. Bado kungekuwa na madaktari wa kuniokoa hospitalini. Kwa sababu tu ulihusika, Hamid sasa anapaswa kufanya mipango na polisi ili kufidia ukweli kwamba ulikuwa nyumbani kwangu.”
Chester alikasirika kweli. Alikuwa amempeleka hospitali na kumwokoa, lakini alikuwa akisema kwamba alichofanya hakikuwa cha lazima.
"Eliza, lazima uwe na hamu ya kifo. Amini usiamini, nitafichua ukweli na kuwaruhusu watu wengine waone jinsi ulivyopanga njama dhidi ya baba yake na kumweka jela. Kufikia wakati huo, picha yako itaanguka. Kampuni za matangazo na wazalishaji wanaofanya kazi nawe wataomba fidia. Ikiwa Felix Media atapuuza jambo hili, utaishia pabaya.”
Eliza alikodoa macho. Alisema kwa baridi, "Kwa hivyo utafanya nini? Unitishie kulala na wewe? Kuwa mwanamke wako na mpenzi wa siri?"
Midomo maridadi ya Chester ikasogea. Mambo hayo yalionekana kuwa ya aibu sana, lakini kwa kweli alikuwa na hamu kubwa na mwanamke huyu. Lakini, kwa sababu fulani, alipojiona akijidhihirisha katika macho yake ya baridi, ghafla hakuweza kusema. Alianza kuhisi hasira kidogo pia.
Ghafla, mlango ukagongwa. Mwanamke mrefu, mrembo aliyevalia mavazi ya kulegea aliingia ndani akiwa na shada la maua. “Eliza, nimesikia umelazwa.”
Pamela alipomwona Chester, ambaye alikuwa amesimama wodini, alirudi nyuma.
Lisa, ambaye aliingia baadaye, naye alipigwa na butwaa. "Dokta Choka, kwa nini wewe pia uko hapa?"
“Mimi ndiye daktari wake,” Chester alisema kwa utulivu.
Lisa alishangaa. "Lakini si mara zote umekuwa ukisimamia wagonjwa katika idara ya saratani? Kwa nini...”
"Kumekuwa na uhaba wa wafanyikazi hapa hivi karibuni, kwa hivyo nilihamishiwa hapa kwa muda." Chester alimtazama Eliza aliyekuwa kitandani. "Nitaondoka kwanza. Nitakutafuta tena baadaye.”
Baada ya kuongea alitoka akiwa amependeza na miguu yake mirefu.
Pamela alimtazama kwa nyuma kwa macho ya ajabu. Kisha akamtazama Eliza. Alisema kwa sauti, “F*ck, Eliza. Je, Bwana Choka anakutaka?”
"Ananitaka?" Eliza alicheka. “Umenikadiria kupita kiasi.”
Lisa alikunja uso. Aliweka vyakula alivyopeleka kwenye meza ya kando ya kitanda. “Chester ni mwanamume mzuri, lakini ikiwa atakuwa mume au mpenzi, nadhani mtu yeyote ambaye atapendana naye atakuwa na bahati mbaya. Yeye si mtu ambaye atabaki mwaminifu kwa mwanamke yeyote.”
Pamela alisema, "Lakini si tayari ameamua kuoana na Cindy?"
“Unafikiri... Cindy anaweza kumdhibiti?” Lisa aliinua uso wake. "Kama angeweza, Chester asingekuwa anamuoa."
 
"Usijali, sikuwahi kufikiria kuwa pamoja naye." Eliza aliinua kichwa na kutabasamu kwa unyonge. "Ninaelewa kuwa ana nia ya muda kwangu tu. Hakuna kitakachotoka katika hili hata baada ya kupata kuwa na mimi. Isitoshe, simpendi hata kidogo.”
“Usijali. Ninaamini Eliza ni mtu mwenye akili zake. Sikuelewa kwanini Chester aliendelea kukulenga wakati wa chakula mara ya mwisho, lakini sasa nimeelewa. Chester lazima aliudhika kwa sababu hakuweza kukupata,” Pamela alisema huku akitabasamu.
Eliza alitabasamu na kubadili mada. “Sikutarajia nyie mje kunitembelea. Kwa kweli, mimi - "
“Sisi ni marafiki,” Pamela akamkatiza, “sijui ni kwanini, lakini nilifikiri kwamba nilikufahamu sana mara ya kwanza nilipokuona. Nadhani hii ndio maana ya damu kupatana na mtu. Chester alisema mambo mabaya kukuhusu, lakini kupata marafiki ni jambo linalopaswa kufanywa kupitia mwingiliano wa mtu mwenyewe. Hakuna mtu aliye wazi zaidi kuliko wao wenyewe ikiwa rafiki huyo anastahili au la.”
"Asante." Macho ya Eliza yalikuwa ya upole.
Ikiwa angelazimika kusema ni nani anayeweza kumfanya ajisikie kufahamiana, ingekuwa ni watu wawili tu walio mbele yake. Walikuwa marafiki zake zamani pia.
"Ikiwa kuna matatizo yoyote, unaweza kututafuta kwa usaidizi wakati wowote," Lisa alisema, "Alvin ni wakili bora. Ana rafiki ambaye anaendesha kampuni kubwa ya sheria. Ikiwa kesi hii itahitajika kuwasilishwa kama shauri mahakamani, unaweza kunitafuta wakati wowote."
“Sawa,” Eliza alifungua kinywa chake na kusema, “Kwa kweli, siogopi kuwaambia nyie kwamba nimepata jeraha hili kwa kujichoma kisu kimakusudi. Jacob aliendelea kunitisha tena na tena. Nimemchoka vya kutosha mtu huyo, kwa hivyo nilifikiria wazo hili.
Baada ya kuongea, alitabasamu kwa uchungu. “Sitaki kuwadanganya nyie. Mimi si mtu mwema.”
Lisa na Pamela walishangaa. Hata hivyo, ilikuwa ni kwa muda mfupi tu. Baadaye, kulikuwa na mshangao katika macho yao. Pamela alitabasamu na kusema, “Hiyo ni nzuri. Mimi na Lisa tunachukia wasichana wenye akili timamu wanaojifanya kuwa wema. Wanawake wanapaswa kuwa wakatili kidogo."
"Lakini hakuna haja ya kutumia mbinu ambazo zitakuumiza mwenyewe ili kuleta madhara kwa adui wakati ujao. Unaweza kututafuta msaada,” Lisa alisema.
"... Asante." Eliza aliinua kichwa chake na kuonesha tabasamu changamfu kutoka ndani ya moyo wake. Tangu kuzaliwa kwake upya, ilikuwa wakati huo kwamba alihisi wakati wa joto.


Lisa na Pamela walisimama tu na kuondoka baada ya kukaa wodini kwa saa moja.
Baada ya kuufunga mlango, Lisa aliinua kichwa chake na kumuona Chester akielekea kwake.

Pamela hakuweza kujizuia kusema, "Dokta Choka, upo huru kiasi cha kushughulika na mgonjwa mmoja tu kutwa nzima?"
Lisa alikunja uso kuelekea kwa Chester. “ Bwana Choka, giza linaingia hivi karibuni. Wakati wako wa mapumziko bado haujafika?”
"Eliza lazima awekewe dripu ya IV sasa," Chester alisema kwa upole.
“Bwana Choka, wewe ndiye daktari mkuu wa hospitali. Hakuna haja ya wewe kutunza jeraha la Eliza, sivyo?" Lisa alisema kwa mzaha.
“Yeye ndiye mgonjwa niliyemuokoa. Napenda kuwajibika kwa mgonjwa hadi mwisho,” Chester alijibu huku akitazama kwa utulivu.
Pamela alimdhihaki, "Inaonekana kama ni zaidi ya kuwajibika kwa jeraha lake, sivyo?"
"Nadhani nyinyi hamjajuana kwa muda mrefu. Ni bora kutojiingiza katika baadhi ya mambo.” Chester alimtazama Pamela kwa utulivu.

Sura ya: 740
 
Pamela alikasirika. Siku zote alikuwa mtu ambaye hawezi kushikilia hasira yake. Alisema mara moja, “Hata kama hatujafahamiana kwa muda mrefu, Eliza bado ni rafiki yetu. Naomba tu niongee ukweli. Tayari uko karibu kuoana na Cindy, kwa hivyo usimsumbue Eliza tena. Yeye ni mwanamke mzuri. Yeye si wale wanawake ambao umezoea kucheza nao.”
“Nyinyi wawili si watu wa ulimwengu mmoja,” Lisa alizungumza vilevile, “naamini hataki chochote kutoka kwako. Ikiwa unataka kucheza, unaweza kucheza na wanawake wengine huko nje wanaotaka vitu ulivyo navyo. Isitoshe, Cindy ni mtu wa kuudhika. Akigundua atamlenga Eliza.”
"Naweza kudili Cindy." Chester hakuwa na hakika.
Pamela akatoa mkoromo. “Kwa kuwa umesema maneno hayo, naweza kuthibitisha kuwa humwelewi kabisa Cindy. Cindy ana mawazo finyu kabisa. Hakika, huenda asifanye lolote mwanzoni, lakini ni mzuri katika kuweka kinyongo. Kisha, wakati kila mtu hayuko macho, atafungua kinywa chake na kumuuma sana mtu huyo hadi nyama ionekane.”
Lisa alisema, “Bwana Choka, usitufanye tufikirie vibaya juu yako. Ingawa nilifikiri wewe ni mwanamume wa kucheza na wanawake hapo awali, angalau sikufikiri kwamba wewe ni muhuni.”
“Umekosea. Nimekuwa mhuni muda wote. Pia, mimi kuwa mhuni au la si jambo lako.” Baada ya Chester kuzungumza, aliondoka kwa hatua ndefu.
Pamela alimtazama kwa nyuma na kukanyaga miguu yake. “Hii inatia hasira. Nilifikiri Rodney ndiye mtu niliyemchukia zaidi duniani. Sikutarajia Chester angekuwa anachukiza zaidi.”
Lisa alikunja uso. "Haijalishi, ikiwa Chester atatumia njia za kifisadi, lazima tumsaidie Eliza."
“Ndio, hatuwezi kumuacha aishie kuwa hawara. Chester hajali, lakini Eliza ni mtu mashuhuri. Ikiwa itatokea, maisha yake yote yataharibiwa, " Pamela alisema kwa kufadhaika.
•••
Katika wodi.
Chester aliusukuma mlango na kuingia. Loida alikuwa ameshikilia chungu chemba ili Eliza ajisaidie haja ndogo. Wote wawili waliingiwa na woga baada ya mtu kuingia kwa ghafla, kwa bahati nzuri kulikuwa na blanketi lililofunika sehemu ya chini ya mwili wa Eliza, lakini Eliza alikuwa bado amechanganyikiwa kutokana na kujisikia vibaya. "Chester, huwezi kubisha hodi kabla ya kuingia?"
"Samahani. Sikujua...” Chester pia hakutarajia. Akashusha mabega. "Lakini wewe ni mgonjwa, na mimi ni daktari. Nimeona mambo ya aina hii mara nyingi sana kila siku, kwa hivyo hakuna haja ya wewe kuona aibu.”
“Wewe...” Kifua cha Eliza kilimtoka kwa hasira.
Ilikuwa nadra kumuona akiwa na hasira. Chester ajabu alijisikia kupendeza. "Mbali na hilo, nilipokuokoa, tayari niliona nusu yako ya juu. Tayari nimeona kila kitu.”
Uso wa Loida ulikuwa mwekundu. Ilikuwa ni kwa sababu alijisikia vibaya, au alikuwa akiona haya badala ya Eliza.
“Umemaliza kukojoa?” Chester aliuliza.
"Unaendelea kuangalia upande wangu, nawezaje kukojoa?" Eliza hakuweza kuvumilia tena.
“Fanya haraka. Lazima uwekwe kwenye IV." Hapo ndipo Chester alipogeuka.
Baada ya Loida kumaliza kila kitu, Eliza alijilaza kitandani. Ilikuwa ni mara ya kwanza kujihisi mnyonge sana.
Chester alining'iniza IV na kumshika mkono Eliza. sauti yake ilikuwa ya upole na tulivu. "Pumzika kidogo."
Sauti hiyo… Eliza alikumbuka kwamba miaka mingi iliyopita, alisema maneno yaleyale katika sikio lake wakati wa mara yao ya kwanza kufanya ngono pamoja.
Hata hivyo... Walipokuwa wakubwa, sauti yake ilizidi kuwa ya mvuto na kuvutia.
Ingawa alijaribu kupuuza kadiri alivyoweza, masikio ya Eliza bado yalibadilika kuwa mekundu kidogo.
“Unawaza nini?” Chester alimtazama Eliza ghafla, tabasamu likiangaza machoni mwake.
"Ninaweza kuwa nafikiria nini? Ninataka tu ufanye hivi haraka." Eliza akageuza kichwa chake kwa ubaridi.
"Mambo haya hayawezi kufanywa haraka," Chester alisema.
Uso mzima wa Loida ulikuwa mwekundu aliposimama kando. Alitaka kufikiria tu, lakini maneno ya watu hao wawili yalimfanya ashindwe kuwaza mawazo safi.
Mwishowe, Eliza hakuweza kuvumilia tena. “Je, hospitali yako haina wauguzi? Kwanini daktari kama wewe lazima afanye jambo dogo kama vile kuingiza sindano ya dripu?”
 
“Ujuzi wa wauguzi si mzuri kama wangu. Ninaogopa watakuchoma na kukuumiza.” Midomo mizuri ya Chester ikainuliwa na kuwa tabasamu la kuvutia. Ilikuwa na haiba ya mapenzi kabisa. Lakini, Eliza hakutetereka hata kidogo. "Ni sawa,
siogopi maumivu."

"Lakini moyo wangu utaumia kwa ajili yako," Chester alisema kwa tabasamu.
Eliza alicheka. Alikuwa amezoea hilo. Wakati mwanamume huyo alitaka kuwa na mwanamke, angeweza kusema kila aina ya maneno ya kimapenzi. Lakini, alipomchoka, mtazamo wake ungebadilika haraka kuliko mtu mwingine yeyote.
Ilikuwa kama vile alivyokuwa amepitia huko nyuma. Alipokuwa bado anasoma zamani, Chester alikuwa mzuri na mpole. Ingawa alikuwa ameufunga moyo wake kwa nguvu, bado alimpenda. Pia alikumbuka waziwazi usemi wake wa kinyama baada ya kubadili mtazamo wake.
“Bwana Choka, ni wanawake wangapi umewahi kuwaambia maneno hayo kabla? Uliwahi kumwambia Charity maneno hayo pia?" Eliza aliuliza ghafla.
Tabasamu machoni mwa Chester likaganda kidogo. Akainamisha kichwa, Eliza akaendelea kusema, “Nilisikia polisi wakitoa taarifa kwamba Charity hakuwa na hatia wakati ule. Aliandaliwa na mtu mwingine. Ilionekana kama mtu ambaye alienda kinyume naye katika mahakama mwaka huo alikuwa wakili bora zaidi uliyekuwa naye. Ulimpeleka mtu asiye na hatia jela kwa mikono yako mwenyewe. Unaonaje sasa?”
Mistari kwenye uso wa Chester ilibana inchi kwa inchi. Baada ya muda mrefu, alisema kwa sauti ya chini, "Nina deni lake."
“Wewe?” Eliza alicheka kwa kejeli. “Kwa bahati mbaya, wazazi wa Charity wamekufa. Charity amekufa pia. Kando na kusema kwamba una deni lake, inaonekana kama hakuna kinachoweza kubadilishwa.
“Eliza tusiongee hili tena. Ninaingiza sindano ndani yako. Ukiifanya hali yangu kuwa mbaya, ninaogopa nitakuchoma.” Macho ya Chester yalikuwa meusi kama usiku wa manane. Hata hivyo, sauti yake ilikuwa ya upole.
"Fanya iume," Eliza alisema kwa utulivu, "Ikiwa mwili wangu una maumivu zaidi, sitajisikia vibaya sana kukukabili."
Chester alishusha macho. Hatimaye, aliingiza sindano nyuma ya mkono wake. Ujuzi wake ulikuwa bora. Hakuhisi maumivu hata kidogo. Alihisi kama kuumwa na mbu tu.
“Baadaye, nitatuma mtu akuletee chakula. Baada ya IV kumalizika, bonyeza kengele. Nitakuja nikubadilishe. ” Chester aliondoka baada ya kuongea.
Loida akasogea na kusema, “Kama Bwana Choka hakuwa karibu kuoa, ningekaribia kutekwa na sauti yake. Sijui kama ni bora kusema yeye ni mhuni au mtu wa mapenzi.”
"Usichafue neno 'mpenzi'," Eliza alisema.
Chester akarudi ofisini kwake. Aliwasha sigara, na macho yake yasiyo na mwisho yalikuwa yakitazama nje ya dirisha ambapo anga lilikuwa likizidi kuwa jeusi. Alijua jina la Charity ni alama ambayo asingeweza kuifuta maisha yake yote.
•••
Wakati huo huo, Lisa aliingia katika ofisi ya mwenyekiti wa KIM International. Alvin, ambaye alikuwa amevalia suti ya bei ghali, alikuwa akizungumza na meneja mkuu. Meneja mkuu alipoona amefika, aliitikia kwa kichwa huku akitabasamu na kutoka nje.
“Nimewasumbua?” Lisa akasogea na kukaa mara moja. "Tayari ni saa kumi na mbili jioni na saa za kazi zimepita."

“Umeni’miss?” Alvin alishika kiuno chake chembamba. Macho yake yalionekana kupoa. "Kumekuwa na mambo mengi yanayoendelea hivi sasa. Siwezi kuondoka kazini kwa nyakati zilizopangwa kama wafanyakazi wengine.”
“Sijaku’miss sana maana nakuona kila siku... Ow... ” Wakati Lisa anaongea, alibanwa sana kiunoni.
Alimtazama Alvin kwa hasira. "Unafanya nini?"

“Ulithubutu kusema hukuni’miss,” Alvin alisema kwa sauti ya kuadhibu.
“Nakuona kila usiku. Kwanini niku’miss?” Lisa alipiga kelele. Alikuwa amehamia katika nyumba ya familia ya Kimaro. Mahali hapo palikuwa pakubwa hata hivyo. Yeye na watoto walikuwa na nyumba yao wenyewe, kwa hivyo hakuhitaji kuogopa kujisikia vibaya kila alipokabili wazee wa familia ya Kimaro kwa kuwa bado hajatalikiwa.
 
Tunaisubiro
Tunaisubirii kwa hamu 💔
 
Sura ya: 741



"Lakini hata nikikuona kila siku, bado ninakukumbuka." Alvin alipokuwa akiongea alinyanyua kidevu chake kidogo na kukaribia kumbusu.
Lisa alimkwepa haraka. “Usifanye fujo. Nilikuja kukutafuta kwa tatizo.”
“Mm?”
“Nilikwenda hospitali kumtembelea Eliza leo. Kitu fulani kilimtokea.”
Alvin akanyamaza kwa muda. Aliweza kukumbuka Eliza alikuwa nani baada ya muda mrefu. "Ni lini nyie mmekuwa karibu sana?"
“Kwa kweli, hatukuwasiliana baada ya kula mara ya mwisho lakini Pamela alisisitiza kuniburuza leo. Tulizungumza kwa muda. Ninamkubali sana.” Lisa alisema kwa unyoofu, “Unajua kwamba sina marafiki wengi hata baada ya kuja Nairobi kwa muda mrefu. Kulikuwa na Charity…”
Alvin aliposikia akimtaja Charity, mwili wake ulisisimka.
Lisa alimtazama, lakini hakuwahi kukawia kwenye mada hiyo. “Eliza ni msichana mzuri sana. Ingawa anajihusisha na tasnia ngumu ya burudani, bado anajitegemea. Nafikiri... Inahisi kana kwamba tumefahamiana kwa muda mrefu.”

"Ni vizuri kupata rafiki mwingine,"
Alvin alisema kwa kukubaliana.
“Lakini...” Lisa akanyamaza. "Chester ni wa kushangaza kidogo. Nilipoenda huko nilikuta ni daktari wa Eliza. Je, si yeye anayehusika na kesi kali katika idara ya oncology? Eliza alichomwa na kisu. Haijalishi ni nini, haipaswi kuwa ni Chester anayepaswa kuwa msimamizi wake, sawa?"

Alvin aliinua uso wake. “Unashuku kwamba anavutiwa na Eliza?”
"Ni dhahiri kwamba iko hivyo." Lisa alisema kwa hasira, “nilishamuuliza kuhusu hilo na hakukataa. Hata alizungumza kwa sauti iliyodokeza kwamba hatupaswi kuingilia biashara yake.
“Je, anafikiri kwamba nataka kuingilia biashara yake? Anaweza kufanya chochote anachotaka na wanawake wengine, lakini Eliza ni msichana mzuri. Tayari Chaster anaenda kumuoa Cindy, lakini bado anajihusisha na Eliza kwa wakati huu. Haoni aibu? Je, ana uadilifu? Je, wanawake ni vitu vya kuchezea tu kwake?”
Alvin alipiga piga nyuma ya kichwa chake kwa haraka. Alisema kwa upole, “Je, kuna kutokuelewana? Kulingana na kile ninachojua kuhusu Chester, yeye si mtu anayechukulia mahusiano kwa uzito. Hata akitafuta wanawake, hatawahi kuwalazimisha wengine. Pande zote mbili zitakubaliana kila wakati. Unajua kwa utambulisho wake, wanawake wengi hujirusha kwake, hasa wanawake katika tasnia ya burudani.”
"Unamaanisha nini?"
Lisa akautupa mkono wa Alvin. "Unamaanisha kwamba Eliza atakuwa alimtongoza?"
Alvin alikunja uso. “Lisa, usifadhaike sana. Labda... Kwani umemjua Eliza kwa muda gani?”
“Hapana, Eliza alipokuwa anazungumza nasi, alikuwa mkweli sana na muwazi. Hakuwahi kufikiria kuficha chochote.” Lisa alishuka kutoka kwa miguu yake kwa hasira. “Ni nyie wanaume wenye macho ya kutangatanga licha ya kuwa tayari mna mtu. Mwishowe, nyie bado mnamtuhumu mwanamke huyo kuwa hana adabu.”
"Lisa, mimi..."
“Alvin, siwezi kujisumbua kukujali tena,” Lisa alisema kwa hasira, “Kwa jinsi ninavyoona, humuelewi rafiki yako hata kidogo. Afadhali umpe ushauri. Anakaribia kuoa. Ikiwa ana mahitaji yoyote, anaweza tu kumtafuta Cindy. Hakuna haja ya kumsumbua Eliza." Aliondoka mara baada ya kuongea.
Kichwa cha Alvin kilisisimka. Hali za wanawake hazitabiriki kama hali ya hewa ya kiangazi.
Hakuwa na la kufanya zaidi ya kumfuata. “Sawa, Lisa. Usiwe na hasira. Nilisema vibaya sasa hivi. Nitamtafuta Chester baadaye na kumuuliza kuhusu hali hiyo, sawa? Pia, usinijumuishe katika jambo hili. Nina wewe tu moyoni mwangu sasa."
Lisa alimtazama kando. “Alvin, wewe ni mwanaume. Wanaume wana ufahamu wao wenyewe na njia ya kufikiri. Lakini, nina hakika kabisa kwamba Eliza sio mtu wa aina hiyo. Isitoshe, mwanamke mwenye akili asingechagua kufanya hivyo. Yeye ni maarufu sana sasa. Habari zikitoka na umma ukagundua kuwa anahusika na ndoa za watu wengine, kazi yake itaharibika. Isitoshe, mwanamke kama Cindy hatakiwi kuchanganyikiwa. Kwa kusema ukweli, Chester ni mbinafsi sana. Anafikiria tu na nusu yake ya chini. Hajui kwamba akifanya hivyo, ataharibu maisha ya baadaye ya mtu mwingine. Je, kumwangamiza Charity hakukutosha?”
"Sawa, uko sawa." Alvin alikubaliana naye kwa utiifu. Aliogopa kwamba angemkosea na kumkasirisha tena.
 
“Naondoka. Rudi tu baada ya kumshawishi.” Baada ya Lisa kuongea, alichukua begi lake na kuondoka.
Alvin alicheka kwa uchungu huku akimtazama kwa nyuma. Lakini, ikiwa kila kitu alichosema kilikuwa ni kweli, vitendo vya Chester vilikuwa vimepitiliza sana. Baada ya kumaliza kazi yake, Alvin aliendesha gari hadi hospitali kwa Chester mara moja.
Baada ya Alvin kuingia ofisini, alimtazama Chester aliyekuwa amevaa koti jeupe kwa mshangao.Chester alikuwa tofauti na madaktari wengine. Sio tu kwamba alikuwa bosi wa makampuni yote ya familia ya Choka, lakini ujuzi wake wa matibabu pia ulikuwa bora kuliko madaktari wote wa hospitali hizo. Wagonjwa wengi nchini humo walikuwa tayari kutumia kiasi kikubwa cha pesa kumwajiri kutibu magonjwa yao. Hata hivyo, pamoja na sifa zake, ikiwa si kufanya upasuaji usiku au ikiwa hakuna wagonjwa wa dharura, hakuwa na haja ya kuwa kwenye zamu ya usiku.
“Lisa alikuambia uje? ” Chester aliinua macho yake. Nyuma ya lenzi, macho yake tulivu yalikuwa makali sana.
Alvin akatoa kiti na kuketi. Akamtolea jicho la ajabu Chester. “Lisa aliponiambia kuhusu jambo hilo hapo awali, sikulichukulia kwa uzito.
Hata hivyo, kwa kuangalia hali ilivyo sasa, hakika sina budi kuuliza... Una tatizo gani?”
Alvin ghafla akakumbuka kuwa usiku wa kuamkia jana yake wakati wanacheza pool, Chester alionekana kuwa katika hali mbaya sana. Rodney alikuwa amezungumza na Chester kwa muda mrefu, lakini uso wa Chester bado ulikuwa mbaya sana.
"Nadhani anavutia sana." Chester akafungua kola ya shati lake. Midomo yake myembamba ikainua tabasamu.
"Je, alikubali kuwa na uhusiano usio na utata na wewe? Au alikuahidi kitu?" Alvin aliuliza. Alishangaa.
Baada ya kimya cha muda, Chester alikanusha. "... Hapana."
Alvin alishangaa. “Huu si mtindo wako.
Chester, hautawahi kuwalazimisha wanawake."

"Sijawahi kumlazimisha." Chester alishtuka. "Bado niko katika harakati za kumfuatilia."
“Kumfuatilia?”
Alvin alikunja uso. “Pole kusema ukweli, lakini tayari unakaribia kuoa. Huna haki ya kutafuta wanawake tena. Chester, najua haumuoi Cindy kwa mapenzi, lakini ndoa ni ndoa. Bila shaka, ni kawaida sana kwa wanaume matajiri kuwa na wanawake wachache kando yao hata baada ya kuoa.
"Hata hivyo, lazima utafute mwanamke ambaye anaweza kukubali kitu cha aina hii. Ukweli kwamba Eliza anaweza kuwa na marafiki wazuri kama Pamela na Lisa inamaanisha kuwa watatu hao wana haiba sawa na ni watu wa aina moja. Si wa kuchezewa. Hawajali kupata mtu mwenye ushawishi kwa sababu wana utajiri wa kiroho. Wanapenda kujitegemea zaidi.”
Sura ya: 742
 
“Najua.”
Chester alisokota kalamu mkononi mwake.
Alielewa kila kitu alichosema Alvin baada ya kukataliwa na Eliza mara kadhaa. Alipomtilia maanani Charity, naye alifikiri ajitenge na Eliza.
Lakini, wakati mwingine, watu walikuwa wa ajabu sana. Chester hakuweza kuelewa kwanini alienda mahali pake ghafla asubuhi. Alijua tu baada ya kuona Eliza anampiga Jacob kwa hali ile, hakudhania kuwa ana sura mbili. Badala yake, alihisi hisia ya ajabu ya kupendeza.
Chester hakupenda wanawake wepesi waliojifanya dhaifu. Eliza alipokichukua kile kisu na kujichoma mgongoni, Chester alihisi pia amechomwa na kitu kwa muda huo.
Ni wazi alikuwa mwanamke mwenye hila, na aliwachukia zaidi wanawake wadanganyifu. Lakini, Eliza alikuwa tofauti. Mwanzoni, Chester alimbusu kwa sababu ya macho yake. Baadaye, alivutiwa na utu wake.
"Hapana, una hisia naye?" Alvin ghafla alisema kwa macho ya ajabu baada ya kumuona Chester akiwa kimya.
“Hisia?” Chester alipigwa na butwaa. Kalamu aliyokuwa akiizungusha iliangukia mezani. Akacheka. "Ikiwa unazungumza juu ya kuwa na hisia kitandani, nilipata uzoefu huo hapo awali. Lakini kuwa na hisia nje ya kitanda ... " Chester alikuwa ameduwaa. Alikumbuka kipindi ambacho alianza kuchumbiana na Charity muda mrefu uliopita. "Alvin, sijui," Chester alisema kwa sauti ya chini, "Ninahisi tu kama lazima niwe na mwanamke huyu."
"Hujawahi kuwa na hisia za aina hii ambapo lazima uwe na mwanamke. Neno ‘kusitasita’ halimo katika kamusi yako.” Alvin alisimama na kumpapasa bega Chester. “Chester, humpendi Cindy kikweli. Hakuna haja ya kumuoa. Hata ikibidi kuoa, unaweza kupata angalau mwanamke wa kuvutia ambaye hutachukia kukutana naye kila siku. Ikiwa unataka kuwa na Eliza, lazima ughairi uchumba wako na Cindy. Vinginevyo, ukijaribu kuvuta mti kwa nguvu, utaishia kuuvunja mti huo.”
“Unadhani wazazi wangu wataniruhusu kufuta ndoa yangu na Cindy? Hata mialiko imekamilika," Chester alisema bila kujali.
“Basi kaa mbali na Eliza. Kuna umuhimu gani ikiwa tayari unajua nyinyi wawili sio watu kutoka ulimwengu mmoja? Tayari nimesema yote ninayopaswa kufanya. Ni lazima nirudi sasa hivi.” Alvin alifungua mlango.
Chester ghafla akasema, “Mlipokutana na Lisa enzi hizo, hamjawahi kufikiria kwamba nyinyi wawili hamkuwa watu wa ulimwengu mmoja? Lakini bado ukaendelea?”
Alvin alishikwa na butwaa. “Kumbukumbu yangu ya siku za nyuma ni finyu kidogo, lakini mimi ni tofauti na wewe. Nilijua wazi kuwa nilimpenda. Ni tofauti na wewe unayetaka kummiliki Eliza.”
"Ni tofauti gani?"
"Ya kwanza hudumu kwa maisha yote, wakati ya pili ni ya muda tu. Si Eliza pekee kwako.” Alvin aliondoka moja kwa moja baada ya kuongea.
Alvin aliporudi kwenye nyumba ya familia ya Kimaro, Lisa alimwendea. “Ulienda kumtafuta Chester, sivyo? Iliendaje?"
"Nimesema kila kitu nilichopaswa kufanya." Alvin alitafakari kwa muda. Kisha, alikunja uso na kusema, "Lakini nahisi kama Chester yuko tofauti kidogo wakati huu."
"Ni sehemu gani yake tofauti?" Lisa alishangaa.
"Anaweza kuwa na hisia kwa Eliza," Alvin alisema, "angalau, zaidi ya Charity wakati huo, sijawahi kumuona akijaribu kumwelezea mwanamke kwa njia hii."
“Usimtaje Charity,” Lisa alisema kwa hasira, “Je, Chester hakutaka tu kuchezea Charity alipokuwa anachumbiana naye wakati huo? Baada ya kumpata, aliondoka tu.”
“Haikuonekana hivyo,” Alvin alinong’ona, “Alipokuwa akichumbiana na Charity, alikuwa mvumilivu sana. Ni mtu ambaye hana subira sana kwa wanawake. Charity ndiye mtu pekee ambaye alikuwa tayari kumsubiri. Baadaye, waliachana ghafla. Isitoshe, Chester aliendelea kuwaza kuwa Charity alikuwa akimdhulumu Sarah wakati huo. Wote wawili wanaweza kuwa na matatizo mengine.”
“Lini Charity alimnyanyasa Sarah? Sarah ndiye aliyejifanya mnyonge na kuwafanya watu wafikirie kuwa wengine walikuwa wanamnyanyasa,” Lisa alisema kwa kufadhaika.
"Hatukujua wakati huo." Alvin alimshika mikono kwa haraka. “Tusitaje tena yaliyopita. Lisa, bado sijala. Nina njaa."
 
“Huwezi kwenda jikoni kutafuta chakula ikiwa una njaa? Mimi si mpishi wako.” Lisa akatupa mkono wake mbali. “Hmph, nikimzungumzia Sarah, sijamuona kwa muda mrefu. Usifikirie nitaruhusu hii kuteleza. Nitamfundisha somo taratibu.”
Alipuuza Alvin na kuondoka baada ya kuongea.
Suzie na Lucas walitembea, wakitazama tu kwa furaha. "Baba, umemkosea mama tena?" Alvin akashusha pumzi ndefu.
Dar es Salaam.
Ndege kutoka nje ya nchi ilitua kwenye Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam.
Baada ya kusubiri kwa zaidi ya dakika kumi nje, Mathew alimuona Titus akimzunguka Sheryl huku wakitoka pamoja. Wote wawili walikuwa tayari wameoana kwa makumi ya miaka, lakini bado walikuwa kama wanandoa wachanga—hasa baba yake, ambaye alitamani kuwa na mama yake kila wakati.
Lina alifuata nyuma. Alikuwa kama binti wa kifalme huku walinzi wachache wakimfuata nyuma huku wakiwa wamebeba mizigo.
"Baba, mama, dada." Matthew akaenda mbele.
“Matt.” Lina alitabasamu kwa upole. “Kwanini ulirudi Tanzania kwanza? Hukutungoja. Laiti si kwa sababu nilitaka kuandamana na Mama zaidi, ningerudi na wewe pia.”
"Nilirudi mapema ili kuwatoa mjomba Jones na Shangazi Mama Masawe gerezani." Matthew alitabasamu huku akimtazama Sheryl. “Mama ngoja nikupeleke kwa mjomba Jones na Shangazi Mama Masawe. Hapo awali walitaka kukufuata wewe huku, lakini niliwaacha wangojee kwenye jumba lao.
“Sawa.” Sheryl aliitikia kwa kichwa. Alihisi hisia kidogo.
Baada ya kupoteza kumbukumbu zake kwa zaidi ya miaka kumi, hatimaye alikuwa katika nchi yake. Njiani, Matthew aliendesha gari kuelekea katikati ya jiji. Sheryl alichungulia nje ya dirisha huku Lina akimtambulisha majina ya baadhi ya maeneo maarufu ya jiji.
Sheryl alitafuta kwa muda na ghafla akasema, "Nadhani mahali hapa panajulikana sana." Titus alimkumbatia mke wake mpendwa na kumuuliza, “Je, unakumbuka jambo fulani?”
"Nadhani ninakumbuka mambo kadhaa, haswa shule tuliyopita hivi sasa. Nilisoma hapo awali?" Sheryl aliuliza ghafla.
Moyo wa Lina ulirukaruka aliposikia hivyo. “Sijui kuhusu hilo, Mama. Uliondoka mapema sana. Bibi hakuzungumza nami kuhusu hilo hapo awali.”
“Oh.” Sheryl alijuta kidogo. "Nataka kuzunguka Dar es Salaam zaidi katika siku hizi chache. Kama vile mahali niliposomea hapo awali na nyumba niliyokuwa nikiishi. Labda itasaidia kurejesha kumbukumbu zangu. ”
Kumbukumbu za wakati uliopita ni muhimu sana? Je, tayari hatukufanikiwa kumpata Lina?” Titus alisema ghafla huku akijisikia kukosa raha.
Sheryl alimtazama kwa hasira. "Unasema nini? Je, kumbukumbu hizo zinawezaje kuwa zisiwe muhimu? Nimepoteza zaidi ya miaka 2o ya kumbukumbu zangu. Nusu ya maisha yangu ni tupu. Nani anaweza kukubali?”
Matthew alitabasamu na kusema, “Mama, Baba anaogopa kuwa utakumbuka uhusiano wako wa zamani. Ana wivu.”
“Nyamaza wewe, hakuna mtu atakayefikiri wewe ni bubu hata kama husemi chochote.” Titus alionekana kana kwamba kuna mtu amemkanyaga. Akamkazia macho mwanae kwa ukali.
“Tumekuwa pamoja kwa muda mrefu sana. Unafikiri bado nitajali kuhusu uhusiano huo hapo awali? Bado hujanielewa?” Sheryl aliushika mkono wa mume wake bila la kujali na kusema, “Nakumbuka vizuri jinsi umekuwa ukinitendea vyema katika makumi ya miaka hii.”
Hapo ndipo uso baridi wa Titus ulipolegea kidogo. Alinong’ona katika sikio la Sheryl, “Tunaporudi baadaye, sema kwamba unanipenda.”
Sheryl. “.....”
Kwa kweli alishindwa kuvumilia mzee huyu aliyejifanya mtoto kiasi kile.

Sura ya: 743


Matthew alijifanya hakuwaona. Kwa hali yoyote, tayari alikuwa ameizoea. Kwa wazazi wake, alikuwa tu zawadi ya bure.

Lina hakuwa na mawazo kama hayo. Akili yake ilikuwa katika kelele sasa. Hakutarajia kamwe Sheryl kukumbuka kitu mara tu atakaporudi Dar es Salaam. Labda hakuwahi kurejesha kumbukumbu zake hapo awali kwa sababu hakwenda sehemu zozote alizozifahamu, lakini kama angekaa hapa kwa muda mrefu na kwenda sehemu alizoishi hapo awali, angeweza kurejesha kumbukumbu yake. Ikiwa hilo lingetokea, angejua kwamba binti yake aliitwa Lisa Jones. Ilibidi Lina amzuie Sheryl asirejeshe kumbukumbu yake. Angefanyaje hivyo?
 
Hivi karibuni walifika kwenye villa. John Jones na mkewe Mama Masawe walikuwa wamengoja mlangoni kwa muda. Baada ya gari kusimama, Titus mwenye nguvu na mrefu alishuka kwanza, akifuatiwa na mwanamke mrembo na mzuri. Mwanamke huyo alikuwa ametoweka ndani ya jiji hili kwa miaka zaidi ya 30.
John Jones Masawe alimtazama kwa muda na kuhisi macho yake kuwa mekundu. “Sherry...” Alilia na kukimbilia lakini alizuiwa na Titus mbabe.

“Baba, huyu ni Mjomba na Shangazi,” Matthew alimkumbusha kumzuia baba yake kuwa na wivu sana.

“Naweza kusema,” Titus alisema kwa unyonge. Hakutaka tu kuruhusu wanaume asiowafahamu wamkumbatie Sheryl. "Wewe ni kaka yangu, sivyo?" Sheryl alimtazama Mzee Jones Masawe. Alipomwona, alionekana kuwa na uzoefu na hisia inayojulikana.

“Sherry, sikutarajia hilo... bado uko hai. ” Mzee Jones Masawe alisisimka kwelikweli. Baada ya yote, alikua na dada yake mdogo mmoja tu. Ni baada ya Sheryl kuondoka ndipo hatua kwa hatua akapofushwa na pupa.

“Sherry, mimi ni wifi yako. Bado wewe ni mchanga na mrembo kama hapo awali. ” Mama Masawe alihema kwa hisia. “Wewe si kama mimi na kaka yako. Tumezeeka sana tunaonekana kama tuko katika miaka yetu ya 60."

"Shangazi, nyinyi wawili lazima mmeteseka gerezani," Lina alisema kwa haraka, akimkumbusha Sheryl kwamba kaka yake na shemeji yake wamekuwa hivyo kwa sababu ya Lisa.

Mzee Jones Masawe aliduwaa aliposikia Lina akimwita mama yake 'Shangazi', lakini kwa bahati nzuri, Mama Masawe aliitikia haraka na kusema, “Tusiongee hilo. Ingia ndani.”

“Jones Masawe, Mama Masawe, asante kwa kumtunza Mama, Baba, na Lina miaka hii yote,” Sheryl alisema kwa shukrani. “Umemlea vizuri sana.”

Mzee Jones Masawe alikaa kimya, lakini mkewe alisema kwa hatia, “Usiseme hivyo. Ilikuwa ni kosa letu kwamba Lina alitekwa nyara na watu wabaya wakati huo. Kwa bahati nzuri, hatukukata tamaa na tukafanikiwa kumrudisha. Pia, samahani sana, Sherry. Kampuni ya Mawenzi Investments uliloanzisha wakati huo lilipaswa kuachiwa Lina, lakini binti yangu alikuwa mkatili sana na alichukua mali zote za familia. mimi-”
“Usiseme zaidi. Sikulaumu,” Sherry alimkatisha kwa macho ya baridi. "Ingawa sijali kuhusu mali hiyo, watu wengine wanapaswa kupata adhabu wanayostahili."

Mzee Jones Masawe alisema kwa kigugumizi, “S— Sherry, yeye bado ni nyama na damu yangu. Unaweza kumfundisha somo, lakini kuokoa maisha yake, sawa? Mwacheni aishi.”

"Wewe una moyo laini sana." Sheryl alipumua. “Lakini ninaelewa. Usijali. Kwa uchache zaidi, nitamruhusu apoteze sifa yake na kuachwa bila chochote. Nitamlipa malipo ya matendo yake.”

Matthew aliyekuwa pembeni alishindwa kujizuia kukunja uso. Alimfikiria Lisa na alishangaa kidogo. Je, alikuwa mtu mbaya hivyo?

“Je, Mzee Jones Masawe, unaweza kunipeleka mahali nilipokuwa nikiishi hapo awali? Ninataka kurudisha kumbukumbu yangu haraka iwezekanavyo,” Sheryl alisema.

“Kumbukumbu?” Mama Masawe aliganda kwa muda kabla ya kutikisa kichwa haraka. "Bila shaka, bila shaka."

Baada ya chakula cha mchana.
Mzee Jones Masawe na mkewe walimwita Lina kwenye chumba cha kusomea. Mama Masawe alipunguza sauti yake na kusema kwa fadhaa, “Lina, nini kinaendelea? Hukusema hapo awali kwamba hawezi kukumbuka chochote kuhusu siku za nyuma? Ikiwa atakumbuka, basi tumemalizika. Mwangalie Titus. Yeye si mtu tunayeweza kumchezea.”

“Yote ni makosa yako. Kwanini ulilazimika kusema uwongo?" Mzee Jones Masawe nusura aingie kichaa kutokana na hasira. “Hata umejifanya kuwa wewe ni Lisa. Unataka kufa?"

“Mama, baba, kama nisingekuwa mimi, ninyi wawili bado mngekuwa gerezani,” Lina alisema kwa upole. “Isitoshe, umewahi kufikiria hili? Ikiwa siku moja Lisa atakubaliwa na Sheryl, itakuwa mchezo wa kitoto ikiwa anataka kushughulika nami. Nitateswa naye hadi kufa.”

“Mzee, mesahau jinsi Alvin alivyomuuza binti yetu kwenye misitu?" Mama Masawe alizuia machozi yake na kumkumbusha mkewe kwa ukali.

Mzee Jones Masawe alishtuka ghafla. Hasira yake ilikuwa imetulia baada ya kufungwa kwa miaka kadhaa, lakini uzoefu wa uchungu wa Lina pia ulimfanya kuwa na hasira.
 
“Mama, baba, msijali. Nitafikiria njia. Jihadharini tu na msiruhusu chochote kuteleza,” Lina alisema.

"Je, kweli tutampeleka katika maeneo ambayo alikuwa akienda zamani?" Mzee Jones Masawe aliuliza bila kuficha.

"Mpeleke katika sehemu zisizojulikana na umzuie kwa siku mbili." Lina aliwakumbusha, “Kumbukeni. Ikumbukwee katika vichwa vyenu kwamba Lisa Jones ni binti yenu wa kumzaa.” Mzee Jones Masawe na mkewe walitikisa kichwa.

Baada ya kurudi chumbani kwake, Lina alimpigia simu Kelvin. "Je, kuna njia yoyote ya kumzuia Sheryl kurejesha kumbukumbu yake? Tuko kwenye mashua moja sasa. Nikifichuliwa, nitakukatisha tamaa pia. Usisahau, wewe pia uko katika hali mbaya sasa hivi.”

Kelvin alikuna kichwa chake. "Kuna mtu ambaye anaweza kusaidia hilo, lakini nataka kukuuliza. Ni lini watafanya harakati zao dhidi ya Alvin na Lisa? Alvin yuko kwenye kilele cha uwezo wake sasa. Ananikandamiza kwa nguvu sana nashindwa kupumua.”

"Tutakuja Nairobi baada ya siku chache. ” Lina akakata simu.

Kelvin haraka akaendesha gari kwa Sarah. “Wewe ni mwanasaikolojia. Je, kuna njia ya kumfanya mtu aliyepoteza kumbukumbu kwa sababu ya ajali asirudishe kumbukumbu yake?”
"Kamwe?" Sarah aliinua uso wake na kumpa sura ya kushangaza.

"Baada ya suala hili kutatuliwa, sitakutendea vibaya," Kelvin alisema kwa sauti ya chini.

"Nisamehe kwa kusema hivi, Bwana Mushi, lakini unawezaje kurejea tena kwenye nafasi yako?" Sarah alikuwa na shaka. Alikuwa amejionea jinsi Alvin alivyonyanyuka tena madarakani ghafla.

“Unadhani nitashushwa kirahisi hivyo? Kabla ya Mason kuanguka, tayari nimepata sehemu ya miunganisho yake nje ya nchi. Alvin na familia ya Choka wameungana kunikandamiza siku hizi, lakini watu watakaoshughulika na Alvin na Lisa wamejitokeza.” Kelvin akaachia kicheko kidogo. "Mtu huyo ndiye ninayehitaji msaada wako ili kumzuia mtu kurejesha kumbukumbu yake."

Sarah aliinua uso wake. "Ninajua dawa ya kutibu magonjwa ya akili. Baada ya kuichukuka, itasababisha mtu huyo kushindwa kurejesha kumbukumbu yake kwa muda. Lakini kutakuwa na athari mbaya."

"Madhara gani?"

"Itasababisha ndoto mbaya wakati mwingine." Sarah alitabasamu. “Unaitaka?”

Kelvin alinyamaza kwa muda kabla ya kuuliza, “Je, madhara yatakuwa dhahiri?”

"Ikiwa hataitumia sana, athari zake hazitaonekana mwanzoni. Lakini akiitumia kwa muda mrefu... siwezi kukuhakikishia chochote,” Sarah alisema kwa uaminifu.

"Muda mrefu... Nusu yake ni ya muda gani?"

"Takriban miaka miwili hadi mitatu."

"Inatosha. Nipe dawa.” Nuru ya kikatili ilimulika machoni pa Kelvin. Miaka miwili hadi mitatu ilimtosha kusimama juu ya dunia.

Mbali na hilo, mtu ambaye Titus Tshombe alimjali sana alikuwa Sheryl. Ikiwa Sheryl angepatwa na mshtuko wa neva, bila shaka Titus angeathiriwa. Pia kulikuwa na Lina, hivyo wangeweza kubadilisha mambo mengi katika miaka miwili hadi mitatu.

Sura ya: 744



Dar es Salaam.

Katika siku mbili zilizopita, Mzee Jones Masawe aliwatembeza Sheryl na Titus mahali pengi.

“Sherry, hii ni kampuni ya zamani ya familia yetu, Kibo Group. Hapo awali, ulikuwa ukimsaidia Baba hapa wakati wa mapumziko ya kiangazi. Kwa bahati mbaya, si mali yetu sasa, kwa hiyo unaweza kuangalia mlangoni tu.” Mzee Jones Masawe alifichua kwa majuto.

Sheryl alilitazama jengo lililo mbele yake. Hisia ya kufahamiana ilitoweka kabisa baada ya kuhisi siku ya kwanza. "Ikiwa ilikuwa biashara iliyoachwa na baba yetu, kwanini sio ya familia ya Jones?"

Mzee Jones Masawe aliinamisha kichwa chake kwa aibu, na mkewe akapumua kabla ya kusema, “Ni kwa sababu ya Alvin. Baada ya kumrejesha Lina, tulimsajili kwenye Kibo Group ili kujaribu kumsaidia, lakini Lisa hakufurahishwa nayo. Alifikiri kwamba Lina alitaka kuiba Kibo Group na alituchukia, hivyo alipokutana na Alvin, alijaribu kutumia mbinu za siri kwenda kinyume na Kibo Group, na kusababisha hali ya Kibo Group kuwa mbaya. Baada ya kushuka kifedha... ilibidi tuuze Kibo Group.”
“Shangazi, Mjomba, samahani,” Lina aliomba msamaha mara moja. "Sikupaswa kurudi basi."

“Usiseme hivyo. Ni kwa sababu hatukumfundisha binti yetu vizuri.” Mama Masawe alijifanya kuwa na huzuni.
 
Sheryl alikasirika zaidi kadiri alivyosikiliza, na maoni yake juu ya Lisa yalizidi kuwa mbaya. Tangu aliporudi, alikuwa amesikia hadithi nyingi za mambo ambayo Lisa aliwafanyia wazazi wake na Lina. Mtu anawezaje kuwa mkatili hivyo?

Baada ya kurudi hotelini, mara moja akampigia simu Matthew. “Si ulienda Nairobi kwa siku chache? Je, maandalizi ya kumfundisha Lisa somo yanaendeleaje? Kwa kuwa Mawenzi Investments ilianzishwa nami na kuondoka kwa Lina, ni wakati wa mimi kuirejesha.”

Macho meusi ya Matthew yalipepesuka kwa mzozo. Baada ya muda kidogo, alisema, “Mama, kuna jambo hujui kulihusu. Niliitazama Mawenzi na kugundua kuwa Lisa ndiye mwenye hisa pekee. Kwa maneno mengine, nguvu zote ziko mikononi mwake. Wanahisa waliotangulia wote walifukuzwa naye. Kimsingi haiwezekani kuirudisha Mawenzi.”

"Mwanamke huyo ... ni mjanja sana." Sheryl alishangaa kidogo. Ikiwa Lisa asingefanya maovu mengi sana, angeweza hata kumvutia.

"Ninachojua, alichukua Mawenzi katika miaka ya hivi karibuni. Yeye ni mwanamke mchanga, lakini aliweza kuwafukuza wanahisa wote wa zamani. Hakika ni mtu mkatili na jasiri.” Titus alikaa kimya.

"Sahau. Ni kampuni ndogo tu. Ni sawa hata tusipoipata tena. Wasiliana na baadhi ya watu, fanya matatizo, na ufadhili wao ukikatizwa, kwa kawaida Mawenzi haitaweza kudumu,” Sheryl alisema kwa unyonge, “Acha tu ianguke.”
Matthew alikunja uso. "Lisa ana KIM International inayomuunga mkono. Ikiwa ufadhili wao utakatwa, KIM International itamsaidia bila shaka. Pia... amemkubali Joel Ngosha kama babake. Ingawa Joel ameondoka Ngosha Corporation, yeye alifungua kampuni ya usafirishaji peke yake ambayo imekuwa moja ya kampuni kuu za usafirishaji nchini Kenya baada ya mwaka mmoja tu. Wanaweza hata kupanuka kimataifa hivi karibuni.”

“Joel Ngosha?” Sheryl alikunja uso. “Mjinga gani. Hawezi hata kujua binti yake halisi ni nani?”

Titus aliyekuwa pembeni alikasirika mara moja. "Ni sawa ikiwa hawezi kufahamu. Unapanga kwenda kwa mlango wake na kuelezea kibinafsi kwa mpenzi wako wa zamani? Sitaki uwe na uhusiano wowote naye. Zaidi ya hayo, una binti naye na nilisikia kuwa hajaoa sasa. Nahofia atapata wazo lisilo sahihi.”

Sheryl awali alifikiria kwenda kwa Joel mwenyewe, lakini alitupilia mbali wazo hilo baada ya maneno ya Titus.

"Ukiniuliza, hakuna haja ya kuwa na wasiwasi kuhusu Joel hata kidogo," Titus alisema kwa unyogovu, "kampuni ya Joel inapanuka, kwa hivyo pesa zao lazima zipunguzwe. Hataweza kumsaidia Lisa hata kidogo. Kitu pekee tunachopaswa kushughulika nacho ni KIM International”

Sheryl aliitikia kwa kichwa. “Si unamfahamu mtu huko? Wasiliana na mtu huyo."

"Hilo ndilo nililokuwa nikifikiria pia." Titus alimkumbatia. "Tutasafiri kwa ndege hadi Nairobi kesho na kula chakula na mtu huyo. Ni jambo dogo.”

Matthew alisikiliza sauti ya kawaida ya wazazi wake na akakunja uso kidogo. Kwa kawaida alijua mbinu za baba yake. Titus alikuwa na uhusiano na watu duniani kote. Hakuwa na hisia nzuri ya Alvin, lakini Lisa ...


Siku iliyofuata.
Sheryl, Titus, Matthew, na Lina walisafiri kwa ndege hadi Nairobi. Ndege ilipotua, Lina akashusha pumzi ndefu. 'Nairobi, nimerudi.'

Mwaka huo alikuwa amekimbia kutoka mahali hapa katika hali mbaya. Sasa, alikuwa amerudi. Punde, Rolls-Royce iliyopanuliwa iliwapeleka kibinafsi kwenye nyumba iliyojitenga na maridadi. Baada ya karamu, Matthew aliwarudisha kwenye jumba la kifahari alilokuwa amenunua katika jiji kuu. Aliamua kununua jumba hilo Nairobi kutokana na hali ya hewa kufafana kabisa na ya huko Ulaya walikoishi wazazi wake, tofauti na huko Dar kulikokuwa na joto kali muda wote.

Wale wanawake wawili walipoenda kunawa, Matthew akamwita Titus, “Baba...”
“Kunanini?”

Macho ya heshima ya Titus yalimtazama. "Unaonekana kama una kitu cha kuniambia."

Matthew alikasirika kidogo. Alitaka kuongea na Titus, lakini baba yake alikuwa ameshikamana na Sheryl mara kwa mara na Lina alikuwepo pia.

“Baba, tuzungumze kwenye maktaba,” Matthew alisema kwa sauti ya chini.
 
Titus akaitikia kwa kichwa. Baada ya kuingia kwenye maktaba, alisema kwa ghafula, “Kwa kweli, ulitaja hapo awali kwamba ulikutana na mwanamke mrembo sana na ukampenda mara ya kwanza, sivyo?”

Matthew akanyamaza. Ikiwa alimwambia Titus kwamba alikuwa amempenda Lisa mara ya kwanza, Titus angeweza kumuua. “Oh, hapana. Niligundua baadaye kuwa tayari ameolewa.”

Titus alimtazama kwa huruma kidogo. Haikuwa rahisi kwa Matthew kumpenda mtu, lakini mwanamke huyo aliishia kuolewa.

“Baba kweli... nataka tuongee na wewe kuhusu Lisa...” Titus alijipiga moyo konde na kusema. "Usiniambie kwamba mwanamke aliyeolewa unayependa ni yeye," Titus alisema ghafla.

Matthew akaguna.
Ilionekana hakukuwa na njia ya kuendelea na mazungumzo hayo.

Kumwona Matthew akinyamaza kimya, uso wa Titus ulibadilika mara moja. “Alikutongoza.”

“Hapana, Baba. Nilikutana naye kwa bahati siku nilipokuja Nairobi. Sikujua hata alikuwa Lisa wakati huo. Aliniokoa,” Matthew alieleza kwa haraka.

“Unafikiri alikuokoa kutokana na wema wa moyo wake?” Titus alidhihaki. “Umesahau ni watu wangapi walijaribu kuwa karibu nawe tangu utotoni? Ulikulia Lubumbashi. Vipi bado unakuwa mjinga?”

“Baba, hakujua utambulisho wangu wakati huo. Nilikuwa tu nimewasili Dar es Salaam. Isitoshe, angejuaje utambulisho wangu?” Matthew hakukubaliana na maneno ya baba yake. "Kwa kweli, pia nilimshuku hapo awali. Baada ya kufika Nairobi, nilikutana naye tena mara kadhaa baada ya mara ya kwanza. Nadhani... Lisa si mwanamke mbaya hivyo.”

"Kuna wanawake wengi ambao ni wazuri katika uigizaji." Titus alikunja uso kwa ubaridi. “Hata hakuwaacha wazazi wake wa kumzaa. Baada ya yote aliyofanya, bado unamtetea? Mama yako akisikia kuhusu hili, ona atakufanyia tu.”

"Ndio maana simwambii." Matthew alipiga kelele. "Baba, kwa kweli ... nadhani wakati mwingine, kile unachosikia kinaweza kuwa sio ukweli."

“Hiyo ina maana gani?” Titus alikodoa macho. “Je, unashuku kwamba Lina na John Jones Masawe wanadanganya? Matthew, angalia unachosema. Lina alifanya kipimo cha DNA. Ni binti wa damu wa mama yako, na wewe ndiye uliyelileta hili.”

“Sijui baba. Labda ... ukikutana na Lisa, utagundua kuwa yeye sio mbaya," Titus alisema, "Alvin pia haonekani kuwa mbaya. Anamjali sana mke wake.”
“Kwanini nikutane naye? Usisahau, nilikuja hapa kutatua maswala haraka iwezekanavyo na kumrudisha mama yako. ” Titus aliusogelea mlango na kugeuka na kumwambia Matthew, “Nimesikia ulichosema. Mazungumzo haya yanaishia hapa." Titus akaondoka na Matthew akashusha pumzi kwa hasira.

Sura ya: 745


Saa sita mchana siku iliyofuata.

Lina aliingia kwenye mgahawa wa hali ya juu akiwa na begi la mbunifu maarufu.

"Lina, ni wewe kweli."

Linda alisimama, na macho yake yakatetemeka alipomwona Lina. Pia alikuwa mtu ambaye alinunua na kuvaa vitu vya anasa, hivyo aliweza kuona kwa haraka tu kwamba begi la Lina ni moja ambalo lilikuwa limetoka tu kutolewa nchini Paris Ufaransa. Bado lilikuwa halijaanza kuuzwa nchini Kenya, na bei yake ilikuwa karibu dola elfu makumi kadhaa.Zaidi ya hayo, ilikuwa wazi kwa mtazamo wa kwanza kwamba mavazi ya Lina yalikuwa ya gharama kubwa pia.

"Linda, ni muda mrefu." Lina alisalimia na kumkumbatia. " Inaonekana hauko vizuri. Uso wako unaonekana mnyonge.”

"Imekuwa ngumu." Linda akatabasamu kwa uchungu. "Huenda usijue hili kwa vile umerudi tu lakini Pamela alilipiza kisasi kwa Jackson & Sons Company siku chache zilizopita. Pamela ana familia ya Shangwe nyuma yake, na familia ya Shangwe imekuwa ikikandamiza familia ya Shebi na Jackson. Kitu pekee ambacho Jackson & Sons Company imebakisha ni jina lake, na Patrick... aliwekwa jela na hawezi kuokolewa.”
Macho yake yalikuwa mekundu alipokuwa akiongea. Alikuwa anampenda sana Patrick.

“Yeye ni mwanamume tu,” Lina alitabasamu kwa unyonge. "Patrick anaweza kuchukuliwa kuwa mtu bora huko Dar es Salaam, lakini ukimweka dhidi ya wanaume nje ya nchi, hawezi kulinganishwa nao. Unaweza tu kupata mwanaume bora. Nitakutambulisha kwa mmoja.”
 
Linda akatingisha kichwa bila kufikiria. “Nilikua na Patrick na nimempenda tangu hapo tulikuwa watoto. Sikuanza kumpenda hivi majuzi. Lina, unaweza…” Baada ya kutulia, alisema kwa uchungu, “Usijali. Aliichukiza familia ya Shangwe. Ungewezaje kumsaidia?”

“Usiseme hivyo. Nina njia,” Lina alicheza na vidole vyake na kusema kwa kawaida. Linda alimtazama. “Usinidanganye.”

“Kwanini nikudanganye? Kwa kuwa ulinisaidia kwa kuniambia kuhusu Pamela kufanya kipimo cha DNA, niko tayari kukusaidia wakati huu pia.” Lina akatabasamu. "Natumai ... tunaweza kuendelea kufanya kazi pamoja katika siku zijazo. Kwa kweli, humchukii Pamela?"

“Bila shaka.” Linda akaitikia kwa kichwa. Macho yake yalidhihirisha chuki. "Rafiki ya Lisa ni adui yangu." Lina alitabasamu bila dhati na kuchukua kikombe chake. "Wacha tufurahie kurudi kwangu."
•••
Kwenye Jumba La kifahari La Kimaro.

Saa mbili kamili asubuhi, Lisa alitayarisha kifungua kinywa. Lucas alikuwa amevalia vizuri sare yake ya shule na akaketi kula kifungua kinywa chake kwa utii, lakini Suzie hakuwa na tabia hiyo. Hakupenda kula kifungua kinywa na alitaka tu kula chokolets na donuts.

"Suzie, huwezi kula vyakula vitamu asubuhi." Alvin alimbembeleza binti yake na kumlisha kijiko kwa kijiko.

Tukio hilo lilimfurahisha sana Lisa. Hapo zamani, yeye ndiye alilazimika kufanya kitu cha aina hii, lakini mwishowe hakuhitaji kufanya hivyo tena.
“Baba mchafu, sitaki kula mie. ” Suzie aliyainua mashavu yake madogo.

Lucas alikoroma kwa ukali. “Ukila vitafunwa kila siku, utanenepa. Sitakubali kuwa wewe ni dada yangu mdogo katika shule ya chekechea wakati huo.

"Mama, ananisumbua tena." Suzie alianza kulalamika.

Lisa alipapasa paji la uso.

Simu ambayo Alvin aliiacha mezani iliita ghafla. Ilikuwa kutoka kwa Hans. Aliitikia wito, na baada ya muda, uso wake mzuri ukaingia giza. "Nitakuja kwa kampuni mara moja."

Lisa alimtazama. “Si ulisema unataka kuwapeleka shule ya awali pamoja? Unaondoka sasa hivi?”

"Kitu kilikuja kwenye kampuni." Alvin alinyoosha mkono kusugua nywele zake. "Lazima niende sasa."

Lisa alitazama sura yake ya dhati na kutikisa kichwa.

Baada ya kifungua kinywa, aliwapeleka watoto wawili hadi shule ya chekechea chini ya mlima. Watoto wawili walipoingia ndani, aliendesha gari hadi kwenye kampuni.

Akiwa njiani ghafla alipokea simu kutoka kwa Pamela. "Patrick aliachiliwa."

“Huu?” Lisa alipigwa na butwaa. Je! familia ya Shangwe ilimwacha aende haraka hivi? Si walisema angefungwa kwa miongo kadhaa?”

"Ndio, ndivyo nilivyofikiria mwanzoni," Pamela alisema kwa sauti ya chini, "nilimuuliza mama yangu wa kufikia kuhusu hilo. Familia ya Shangwe haijawahi kukusudia kumwachilia Patrick. Alitakiwa kufungwa angalau kwa miaka kumi, lakini aliachiliwa ghafla. Mama alisema ni agizo la halmashauri kuu...”

“Patrick ni mkubwa kiasi cha kuokolewa na wananchi katika halmashauri kuu? Lisa alichanganyikiwa.

“Pia naona ni ajabu. Ikiwa familia ya Jackson ingekuwa na uwezo huo, wazazi wake wasingehitaji kuwasihi wazazi wangu. Pamela naye alichanganyikiwa. “Lakini cha ajabu, Patrick yuko huru sasa.”

Kadiri Lisa alivyozidi kusikiliza ndivyo alivyohisi kuwa ni jambo la ajabu.
"Kwa njia, unajua kuwa kuna kitu kilitokea kwa KIM International?" Pamela aliuliza ghafla.

"Nini kimetokea?" Lisa alikuwa amepoteza akili yake kabisa.

"Alvin hakukuambia?" Pamela alishangaa. "KIM International imejumuishwa katika orodha isiyofaa ya makampuni yanayohitaji kufanyiwa uchunguzi. Kwa sasa, idara zote zinazohusika zimeunda timu za uchunguzi kuichunguza KIM International.”

Lisa ghafla akakumbuka jinsi Alvin alivyoondoka kwa haraka asubuhi ya siku hiyo na kupata hisia mbaya. "Kwanini KIM International imeorodheshwa ghafla bila sababu? Halafu, Alvin si yuko karibu na familia ya Shangwe?"

Pamela alifungua kinywa chake, na baada ya muda, alisema kwa shida, "Nilimsikia Nathan Shangwe akisema kwamba KIM International inaweza kukabiliwa na shida ambayo haijawahi kutokea wakati huu. Sio sawa na yale yaliyotokea mara ya mwisho. Alvin anaweza kupoteza kila kitu.”
 
“Unatania, sawa?” Lisa hakuamini. "KIM International imerejea sasa na ni wakati wao kuinuka..."

"Inaonekana kuwa amemchukiza mtu wa kutisha.
Hata familia ya Shangwe haiwezi kumpinga
mtu huyo,” Pamela alimkatisha na kusema huku akionekana kutojiweza. Ubongo wa Lisa ulimshtua kwa kelele.
Alvin na yeye walikuwa wamepitia mengi sana kuweza kufika pale walipo sasa. Mason alienda jela na hatimaye wangeweza kummaliza Kelvin, lakini sasa, inaonekana walikuwa wamemkosea mtu wa kutisha zaidi. Alikuwa ni nani? Alikuwa amechoka sana na kupoteza.
Iwe ni Alvin au yeye mwenyewe, haikuwa rahisi kwao kufikia hatua hii.



"Uko salama?" Pamela aliuliza kwa wasiwasi.


"Sijui, Pamela. Nitaenda KIM International nikaangalie,” Lisa alisema kwa uchovu.

Baada ya kukata simu, alipita kwenye kampuni ya KIM International.
Muda huo, wanahabari walikuwa wakipiga kelele nje ya KIM International. Kwa hivyo, Lisa aliingia kutoka kwa maegesho ya nyuma. Alipofika ghorofa ya juu, aliona watu kadhaa waliovalia sare za bluu wakitembea na masanduku kadhaa.

Wafanyikazi wa kampuni hiyo walisimama pande mbili hadi mtu kutoka ofisi ya katibu alipomwona. "Bi Jones..."

"Alvin yuko wapi?" Lisa aliuliza.
"Bwana Kimaro na wakurugenzi wachache wako ndani." Katibu akamuingiza ndani.

Katika ofisi kubwa, Alvin, Lea, Spencer, na wakurugenzi mbalimbali walikuwepo. Wote walikuwa na sura zisizopendeza kwenye nyuso zao.

"Bwana Kimaro, natumai kwamba unaweza kujua kuhusu hali hiyo kutoka kwa Seneta Shangwe haraka iwezekanavyo," mmoja wa wakurugenzi alisema, "Hata iweje, KIM International inachunguzwa ghafla, kwa mbwembwe nyingi bila sababu. Waandishi wa habari wamejaa nje ya kampuni. Wengine watafikiria nini kuhusu KIM International?"

"Jamani, nini kinatokea kwa KIM International mwaka huu? Haikuwa rahisi kuwaangusha familia ya Campos na kupanda tena, lakini sasa tunachunguzwa tena. Makampuni mengi yamepiga simu kuuliza kuhusu hali hiyo. Tumesaini mikataba mingi sana. Ikiwa kazi yote itacheleweshwa tena kama mara ya mwisho, tutapoteza kila kitu wakati huu. Spencer naye alishindwa kujizuia.

“Kila mtu rudini mkapumzike kwa sasa. Mimi binafsi nitaenda kumtafuta Seneta Shangwe baadaye,” Alvin alisema kwa sauti ya chini.

Wakurugenzi walipoondoka mmoja baada ya mwingine, Lisa alienda upande wa Alvin. “Kwanini hukuniambia kuhusu jambo muhimu hivyo?”

"Sikutaka ufikirie kupita kiasi." Alvin akauweka mkono wake taratibu kwenye kiganja chake kikubwa.

Lisa alimkazia macho. “Niligundua hata hivyo. Pamela alinipigia simu mapema na kusema kwamba ... tunaweza kuwa tumemkosea mtu wa kutisha. Ninaogopa haitakuwa rahisi kutatua hili. Sote wawili tunajua kwamba hofu kubwa katika ulimwengu wa biashara si washindani bali uchunguzi...”

Sura ya: 746


Hasa uchunguzi ambao unafanyika bila sababu. Ikiwa chochote kitapatikana, kinaweza kufanya kampuni kupoteza sifa yake na bei yake ya hisa kushuka - hata kusababisha kampuni hiyo kufutwa. Hasa KIM International, ambayo ilikuwa imezindua bidhaa mpya. Ingesababisha kampuni nyingi ambazo hapo awali zilitaka kushirikiana ili kuzuia KIM International badala yake.

“Lisa, usiruhusu mawazo yako yaende ovyo. Nimepitia kila aina ya mambo kufikia hapa nilipo leo.” Uso mzuri wa Alvin ulitabasamu. "Lazima uniamini mimi."
“Alvlisa...”
Midomo myekundu ya Lisa iliachana. Alishtuka ghafla wakati mawazo yalipomjia kichwani.

"Nini tatizo?" Alvin aliuliza kwa upole.

"Nilikumbuka kitu," Lisa alisema, "Pamela alisema kwamba Patrick aliachiliwa kwa amri kutoka kwa halmashauri kuu, na sasa KIM International inachunguzwa. Ninashangaa ikiwa mambo haya mawili yanaunganishwa. Katika nchi hii, nguvu pekee ambayo familia ya Shangwe haina mamlaka dhidi yake ni baraza kuu.”
 
Alvin alikunja uso. Baada ya muda, alisema, “Sikuwaza kuhusu familia ya akina Jackson, lakini maneno yako yamenikumbusha. Lisa, nenda kwa kampuni. Nitaenda kwenye makazi ya Shangwe...”
“Nitakwenda nawe.” Mara Lisa akasimama. “Alvilisa, nataka kukabiliana na hili na wewe. Ikiwa huwezi kushinda kikwazo hiki, itabidi niondoke upande wako.” Alvin aliganda na kumtazama kwa sura isiyopendeza. “Alvlisa, samahani. Hata kama nilichosema ni kigumu kukisikia, ni lazima niwafanyie watoto,” Lisa alibana mdomo na kusema kwa sauti ya chini.

“Hapana, sina furaha kwa sababu unaniona sina maana. Haijalishi bwana ni nani, sitaweza kushushwa kirahisi hivyo.” Alvin akamkumbatia kwa upole. “Kama kweli itafika siku siwezi kukulinda wewe na watoto, huna haja ya kusema lolote zaidi, nitakuacha uende.”

Lisa hakusema chochote, lakini macho yake yalimchoma. Alimpenda, naye alimpenda. Lakini, ukweli haukuwa hadithi ya hadithi. Walipaswa kuwajibika kwa watoto wao.

Baada ya kufikia makazi ya Shangwe. Mjakazi mkuu alipowapeleka ndani, walisikia sauti ya Rodney walipofika mlangoni. "Ba’mdogo, Alvin ni kama kaka yangu na ana uhusiano mzuri na familia ya Shangwe. Inabidi umsaidie.”

"Bwana Mdogo Shangwe, Alvin Kimaro na Miss Jones wako hapa," mjakazi mkuu alisema.


Alvin na Lisa walitazama na kuwaona kwa mbali na Nathan, Pamela na Rodney pia walikuwepo. Alvin akawaitikia kwa kichwa na kumpiga bega Rodney taratibu. “Asante.”

"Sisi ni ndugu." Rodney alicheka na kusugua pua yake.

Alvin hakuzungumza kitu kingine chochote akamtazama Nathan. “Uncle Nathan, unajua jinsi nilivyo. Familia ya Kimaro imesimama kileleni mwa ulimwengu wa biashara wa Kenya kwa zaidi ya miaka hamsini na imekuwa ikifuata sheria kila wakati. Hii ni mara ya kwanza kwa uchunguzi huo mkubwa kufanyika. Nataka tu kujua wanataka nini."

"Alvin, nitakuambia ukweli." Nathan aliwasha sigara. “Niliwasiliana na Halmashauri Kuu, wakanionya nisiingilie kati suala hili. Vinginevyo, sitaweza kumudu matokeo.”

Maneno ya kila mtu yalibadilika. Rodney alisimama kwa hasira. “Wanataka kuharibu KIM International?”

“Inawezekana,” Nathan aliitikia kwa kichwa na kusema bila msaada, “Ingawa umekuja kwangu ili kupata usaidizi, kitu pekee ninachoweza kukupa ni kuomba msamaha.”

Uso mzuri wa Alvin ulizama. “Utakuwa Rais wa Kenya mwezi ujao. Itakuwaje nikichelewesha hadi wakati huo?”

“Alvin, ninashuku kwamba si baraza kuu linalokulenga wewe. Huenda kuna mtu aliwaambia wafanye hivyo, na nguvu hiyo ni ile ambayo halmashauri kuu haiwezi kumudu kuiudhi. Nadhani ni muhimu kujua ni nani ulimkosea kwanza. Hapo ndipo utaweza kupata suluhisho,” Nathan alimkumbusha.

"Naelewa." Alvin akaitikia kwa kichwa.

Rodney alipigwa na butwaa. “Hilo haliwezi kuwa. Alvin ana maadui wengi, lakini ni takataka za kiwango cha tatu kama Mason na Kelvin. Alimchokozaje mtu ambaye hata mamlaka ya juu kabisa ya nchi haiwezi kumudu kumuudhi?”

"Hujui, lakini daima kuna watu wenye nguvu zaidi duniani," Nathan alisema kwa kumaanisha.
•••
Baada ya kuondoka kwenye makazi ya Shangwe. Alvin na Rodney walikuwa wakitembea sambamba. Lisa na Pamela walitembea nyuma yao.

“Lisa, usijali. Hakika kutakuwa na njia." Pamela hakujua jinsi ya kumfariji Lisa, lakini alisema hata hivyo.
"Kuna njia, lakini Pamela, nahitaji msaada wako," Lisa alisema ghafla, "Inaweza kuwa njia pekee ya kupata fununu juu ya mtu huyu ni nani."

“Mimi?”
Pamela alipigwa na butwaa kidogo. "Una uhakika?"

"Kwa kweli, ninashuku kuwa watu waliomwokoa Patrick kutoka gerezani na watu wanaolenga KIM International ni walewale," Lisa alisema kwa sauti ngumu, "Ni bahati mbaya sana. Matukio yote mawili yalitokea kwa wakati mmoja na maagizo yalitoka kwa Halmashauri Kuu.”

“Unamaanisha... kwa sababu nilimkosea Patrick, wale watu wanalenga KIM International kwani wewe ni rafiki yangu na Alvin ni mpenzi wako?”
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…