Chubbylady
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 621
- 1,018
Hamid alisema, "Zaidi ya hayo, nilikuwa na maingiliano machache na Cindy hapo awali. Mimi tayari ni mmoja wa wasimamizi bora katika kampuni. Hata mkurugenzi Mutui inabidi anitendee kwa heshima anaponiona. Lakini Cindy ananidharau kwa sababu tu anadhani yeye ni mwanamke wa Bwana Choka. Mtu kama yeye ana akili finyu. Akigundua kuwa una mahusiano na bwana’ake ataweza kukukandamiza.”
“Nimeelewa kila ulichosema. Ndiyo maana nimekuwa nikikataa mapendekezo ya Chester.” Eliza alikunja uso. "Watu kama yeye wanatuchukulia kama wanawake wepesi.”
“Ni vizuri kama umeelewa. Natumai Bwana Choka atakata tamaa hivi karibuni,” Hamid alimkumbusha, “Monte ni mfano bora zaidi.”
Akiongea juu ya Monte, Eliza alinyamaza.
Kwa kweli, hakuwa na hisia nyingi za Monte tena. Alipoamka, aligundua kuwa Eliza wa zamani alikuwa amejiua kwa ajili ya Monte. Hakuwa chochote ila mpuuzi mmoja tu.
“Pumzika kidogo. Acha Loida abaki hapa na akutunze. Bado natakiwa kusimamia mambo yako. Kuna kundi la wanahabari nje,” Hamid alisema, “By the way, tunapaswa kushughulikia vipi suala la baba yako?”
"Vyombo vya habari vinaripotije juu ya mambo?" Eliza aliuliza.
"Kwa bahati nzuri, tayari walichimba habari za Jacob na familia yake. Hata waliwasiliana na watu wengi wanaomfahamu Jacob na familia yake ili watoe taarifa. Hata hivyo, watu wa nje tayari wanajua kwamba wao ni familia ya wanyonyaji. Umma unakuonea huruma sana sasa.”
Eliza alifikiria na kusema, “Onyesha jina la mtaa wa Jacob na anwani ya kampuni ya mwanawe. Pia, tafuta wakili ili arudishe pesa nilizompa Jacob hapo awali. Wakati huo huo, mshitaki Jacob. Kwa kuwa alinijeruhi, anapaswa kwenda jela.”
Hamid alimtazama kwa mshangao.
"Nini?" Eliza aliuliza.
"Hakuna," Hamid alisema kwa hisia ngumu, "Nadhani umebadilika sana sasa. Hukuwa hivi hapo awali. Ulikuwa na moyo laini na uliendelea kujali uhusiano huo ambao haupo sawia kabisa wa baba na binti. Kwa kweli, ulikuwa dhaifu sana wakati huo.”
"Sitakuwa dhaifu tena," Eliza alisema, "Wale ambao hawakunitendea vizuri hawana haki ya kuninyang'anya vitu vyangu."
“Sawa.”
Hamid aliondoka.
Loida alimlisha Eliza uji. Haukupita muda mrefu, mlango ukafunguliwa tena. Mtu aliyeingia alikuwa Chester. Alivaa koti jeupe na miwani. Alikuwa na matatizo ya-kutoona mbali, kwa hiyo huwa anavaa miwani alipokuwa akifanya kazi. Lakini, hiyo haikuathiri sura yake nzuri. Kinyume chake, ilimfanya aonekane maridadi zaidi, muungwana, na mwenye akili.
Loida alikuwa akisikia watu wakisema kwamba Chester alikuwa anavutia zaidi alipovalia koti jeupe. Kwa wakati huo, karibu alisahau kugeuza macho yake alipojionea mwenyewe leo. Alikumbushwa tu baada ya Eliza kujisafisha koo lake kirahisi. Loida aliporudi kwenye fahamu zake, alihisi kuchanganyikiwa na kukosa utulivu.
Loida hakuelewa. Ni wazi kwamba Chester alikuwa mtu mchafu, lakini kwanini sura yake ilionekana wazi na angavu kama mwezi? Kama inavyotarajiwa, wanaume hawakuweza kuhukumiwa kwa sura zao.
"Unaweza kuondoka kwanza," Chester alimwambia Loida mara moja.
Loida alijieleza kwa wasiwasi. “Bwana Choka, jeraha la Eliza bado halijapona. Hupaswi—”
“Je, ninaonekana kuwa nataka kumfanyia kitendo kibaya?” Chester akamkatisha. “Zaidi ya hayo, mimi ndiye daktari wake ninayemsimamia. Mimi ndiye niliyemtibu jeraha lake.”
“Oh...” Loida hakuwa na la kufanya ila kuondoka.
Eliza alimtazama Chester kwa uso dhaifu na uliopauka. "Asante, Bwana Choka."
“Inatosha?” Chester aliketi kando ya kitanda, akitabasamu. “Eliza, mimi ni mtu ninayetii sheria. Lakini kwa ajili yako, nilifanya taarifa ya uongo kwa mara ya kwanza. Si hivyo tu, hata mimi ndiye niliyekuleta hospitalini.”
Eliza hakusema neno, na macho yake yalikuwa baridi kama barafu.
“Eliza, nimeona wanawake wengi wajanja kama wewe. Hata hivyo, sijawahi kuona mtu anayejitendea ukatili kama wewe.” Chester akarekebisha miwani yake. "Umefaulu kuamsha shauku yangu kwako."
Sura ya: 739
“Nimeelewa kila ulichosema. Ndiyo maana nimekuwa nikikataa mapendekezo ya Chester.” Eliza alikunja uso. "Watu kama yeye wanatuchukulia kama wanawake wepesi.”
“Ni vizuri kama umeelewa. Natumai Bwana Choka atakata tamaa hivi karibuni,” Hamid alimkumbusha, “Monte ni mfano bora zaidi.”
Akiongea juu ya Monte, Eliza alinyamaza.
Kwa kweli, hakuwa na hisia nyingi za Monte tena. Alipoamka, aligundua kuwa Eliza wa zamani alikuwa amejiua kwa ajili ya Monte. Hakuwa chochote ila mpuuzi mmoja tu.
“Pumzika kidogo. Acha Loida abaki hapa na akutunze. Bado natakiwa kusimamia mambo yako. Kuna kundi la wanahabari nje,” Hamid alisema, “By the way, tunapaswa kushughulikia vipi suala la baba yako?”
"Vyombo vya habari vinaripotije juu ya mambo?" Eliza aliuliza.
"Kwa bahati nzuri, tayari walichimba habari za Jacob na familia yake. Hata waliwasiliana na watu wengi wanaomfahamu Jacob na familia yake ili watoe taarifa. Hata hivyo, watu wa nje tayari wanajua kwamba wao ni familia ya wanyonyaji. Umma unakuonea huruma sana sasa.”
Eliza alifikiria na kusema, “Onyesha jina la mtaa wa Jacob na anwani ya kampuni ya mwanawe. Pia, tafuta wakili ili arudishe pesa nilizompa Jacob hapo awali. Wakati huo huo, mshitaki Jacob. Kwa kuwa alinijeruhi, anapaswa kwenda jela.”
Hamid alimtazama kwa mshangao.
"Nini?" Eliza aliuliza.
"Hakuna," Hamid alisema kwa hisia ngumu, "Nadhani umebadilika sana sasa. Hukuwa hivi hapo awali. Ulikuwa na moyo laini na uliendelea kujali uhusiano huo ambao haupo sawia kabisa wa baba na binti. Kwa kweli, ulikuwa dhaifu sana wakati huo.”
"Sitakuwa dhaifu tena," Eliza alisema, "Wale ambao hawakunitendea vizuri hawana haki ya kuninyang'anya vitu vyangu."
“Sawa.”
Hamid aliondoka.
Loida alimlisha Eliza uji. Haukupita muda mrefu, mlango ukafunguliwa tena. Mtu aliyeingia alikuwa Chester. Alivaa koti jeupe na miwani. Alikuwa na matatizo ya-kutoona mbali, kwa hiyo huwa anavaa miwani alipokuwa akifanya kazi. Lakini, hiyo haikuathiri sura yake nzuri. Kinyume chake, ilimfanya aonekane maridadi zaidi, muungwana, na mwenye akili.
Loida alikuwa akisikia watu wakisema kwamba Chester alikuwa anavutia zaidi alipovalia koti jeupe. Kwa wakati huo, karibu alisahau kugeuza macho yake alipojionea mwenyewe leo. Alikumbushwa tu baada ya Eliza kujisafisha koo lake kirahisi. Loida aliporudi kwenye fahamu zake, alihisi kuchanganyikiwa na kukosa utulivu.
Loida hakuelewa. Ni wazi kwamba Chester alikuwa mtu mchafu, lakini kwanini sura yake ilionekana wazi na angavu kama mwezi? Kama inavyotarajiwa, wanaume hawakuweza kuhukumiwa kwa sura zao.
"Unaweza kuondoka kwanza," Chester alimwambia Loida mara moja.
Loida alijieleza kwa wasiwasi. “Bwana Choka, jeraha la Eliza bado halijapona. Hupaswi—”
“Je, ninaonekana kuwa nataka kumfanyia kitendo kibaya?” Chester akamkatisha. “Zaidi ya hayo, mimi ndiye daktari wake ninayemsimamia. Mimi ndiye niliyemtibu jeraha lake.”
“Oh...” Loida hakuwa na la kufanya ila kuondoka.
Eliza alimtazama Chester kwa uso dhaifu na uliopauka. "Asante, Bwana Choka."
“Inatosha?” Chester aliketi kando ya kitanda, akitabasamu. “Eliza, mimi ni mtu ninayetii sheria. Lakini kwa ajili yako, nilifanya taarifa ya uongo kwa mara ya kwanza. Si hivyo tu, hata mimi ndiye niliyekuleta hospitalini.”
Eliza hakusema neno, na macho yake yalikuwa baridi kama barafu.
“Eliza, nimeona wanawake wengi wajanja kama wewe. Hata hivyo, sijawahi kuona mtu anayejitendea ukatili kama wewe.” Chester akarekebisha miwani yake. "Umefaulu kuamsha shauku yangu kwako."
Sura ya: 739