Simulizi: Lisa

Simulizi: Lisa

jamani mnisamehee jana hakukuwa na umeme kwetu[emoji16][emoji16][emoji16] naelewa arosto lake[emoji23][emoji119] sema twendeni tu taratibu story bado ndefu sanaa yan[emoji119][emoji119] mwandishi anasemayupo sehemu ya 1000 na usheee[emoji2356][emoji22]
 
LISA KITABU CHA NANE (9) SIMULIZI........................LISA KURASA.................431 - 435
PRESENT: SIMULIZI ZA DULLY

Sura ya: 431
“Nilikuwa kwa Pamela tukijadili dili la fomula za vipodozi. Ningepoteza nafasi hiyo huenda mshindani wangu angenizidi kete.” Rodney alimwambia.
Sarah alikasirika. Hakufikiria kamwe kwamba Rodney, mpango wake wa kando, siku moja angemsahau. Hapo awali, alikuwa akimfikiria kila wakati, na maadamu angesema neno tu, Rodney angekuja haraka iwezekanavyo bila kujali alikuwa na shughuli nyingi au la. Aliumia sana kwa Rodney kumpotezea jioni hiyo kwa sababu ya Pamela Masanja.
Hata hivyo, hakuweza kusema hivyo, kwa hiyo alijifanya kuwa mstaarabu na mkarimu. "Ni sawa. Mazungumzo yaliendaje na Pamela?"
"Mazungumzo yamefikia muafaka, lakini

Pamela aliomba asilimia 10 ya hisa za kampuni," Rodney alisema kwa upole. “Kwa hiyo nilirudi kwenye kampuni ili kujadiliana na watendaji. Kila mtu anafikiri mpango huu unawezekana. Ikiwa tunaweza kumfunga Pamela Masanja na Osher, tutaweza kuidhibiti SE Group kwenye ushindani.”
“Asilimia 10?” Sauti ya Sarah haikuweza kujizuia kuinuka. "Huo ni wizi wa mchana, lakini nyinyi mnaukubali vipi?"
“Hakuna chaguo. Tunaamini, baada ya kampuni yetu kuzindua bidhaa mpya, thamani ya soko la Osher itaongezeka.”
Sarah alitaka sana kumwita Rodney nguruwe mjinga, lakini, aliweza kujizuia tu huku ndani yake kukilipuka kwa hasira.
 Baada ya kukata simu, mara akampigia Thomas.
“Unajua kwamba Rodney Shangwe

amevurugwa akili na huyo b *tch Pamela? Amempa asilimia 10 ya hisa za Osher? Anaweza hata kutupita kwa utajiri siku zijazo.” Thomas aliuma meno aliposikia hivyo.
Thamani ya soko ya Osher Corporation ilikuwa ni zaidi ya mamilioni ya dola. Thomas alipofikiri kwamba thamani ya Pamela ingekuwa karibu sawa na yake, alikosa furaha sana. Kwake, Pamela alikuwa mwanamke duni ambaye hakumfaa kwa lolote zaidi ya kutaka kumfunua mapaja tu basi.
“Kaka kwa kweli siwezi kuvumilia. Tafuta nafasi ya kukabiliana na Pamela." Sarah akauma meno yake na kusema, “Baada ya hapo, nitashughulika na Lisa.”
“Sihitaji uniambie hivyo. Pia sina nia ya kumwachia Pamela. Ninapanga kumaliza kile ambacho sikufanya miaka

mitatu iliyopita.” Thomas aliguna ghafla. “Hiyo ni nzuri. Ikiwa atakuwa na hisa za Osher, sitapoteza chochote kwa kumuoa.”
“Unamaanisha...” Macho ya Sarah yaliangaza. "Hilo ni wazo zuri. Nilisikia kwamba biashara ya familia yao pia imekuwa ikiongezeka na kukua katika miaka ya hivi karibuni, na wataipita hata kampuni yetu hivi karibuni. Ukimuoa, utaua ndege wawili kwa jiwe moja. Lakini unaweza kufanikisha?"
“Usijali. Nina mbinu nyingi za chinichini.” Thomas alicheka.
Sarah alisema kwa kuridhika, “Lakini Alvin hayupo nasi kukusafisha tena, kwa hivyo jiangalie. Usifanye jambo lolote lisilo halali.”
“Ninajua ninachofanya,” Thomas alisema. "Wewe je, utafanyaje na Lisa?"

"Heh, nina mpango wangu mwenyewe." •••
Siku iliyofuata, Pamela alipokea simu kutoka kwa Rodney. Alikubali masharti yake.
 Alasiri hiyo, Pamela alimwalika Lisa kwa chakula cha jioni kusherehekea.
“Ulifanya uamuzi sahihi. ” Lisa alitabasamu kimoyomoyo na kumpapasa. "Erick Malugu alikuwa ananiomba sana nikushawishi ushirikiane naye, lakini sikutaka kuingilia mambo yako ili nikuachie uhuru wa kufanya maamuzi yako mwenyewe. Hata hivyo Osher ni kampuni kubwa hapa nchini. Hii ni fursa nzuri kwako ikiwa kweli unataka kubaki Kenya."
Pamela akacheka. “Hatimaye nitashughulika na Thomas Njau. Nikiingia Osher, damu ya Sarah

itachemka.”
“Hakika. ” Lisa alicheka. "Baada ya yote, Sarah anamchukulia Rodney kama mpango wake wa kando."
"Sahau. Ninaogopa kwamba bado anamfikiria Alvin. Kwa kuwa Rodney amekataliwa kuwa mrithi wa familia ya Shangwe, siamini kwamba Sarah atakubali amuoe. Sarah anatafuta pesa na umashuhuri alionao Alvin.” Pamela alitikisa kichwa na ghafla akanung’unika, "Kwa kweli, Rodney ni mjinga sana. Ikiwa ningekuwa na mwanamume kama huyo ambaye alinipenda kama anavyofanya kwa Sarah, ningeweza kuolewa naye. ”
Lisa alishtuka sana hadi akasongwa na maji yake. “Usiniambie. Una mapenzi na Rodney, sivyo?”
“Bah, hapana. Namaanisha Sarah kweli

huwa na bahati nzuri nyakati fulani, lakini hajui jinsi ya kuithamini. Nitakuwa mkweli.
 Upikaji wa Rodney ni mzuri sana. Nyama yake aliyopika jana ilikuwa na ladha nzuri kabisa." Mdomo wa Pamela ulimwaga udenda kidogo huku akiwaza jambo hilo.
"Kwa hivyo, yeye sio bure kabisa. Kuna wanaume wachache sana wanaoweza kupika siku hizi.” Lisa alisema kwa kusikitika. “Tofauti na Alvin wangu, anataka tu nimpikiage kutwa nzima.”
“Lakini shoga ukiishi na mwanamume mwenye ujuzi wa kupika ni kazi? Atakosoa chakula chako kila siku.” Pamela alicheka.
Lisa alicheka na kuongeza. “Pamoja na hayo, kupikiwa na mwanamume kuna raha yake bwana. Nilitamani kweli kupata mwanamume wa kunipikia siku moja.”

"Kelvin anaweza." Pamela akakonyeza macho.
Lisa alinyamaza ghafla. Kwa muda mrefu Kelvin hakuwa amewasiliana naye kabisa kwa sababu ya mpango wake. Alikuwa na deni kubwa sana kwake.
Katikati ya chakula, Alvin alipiga. “Uko wapi?”
“Niko out nakula na Pamela.” Lisa alijibu kivivu.
Uso wa Alvin ukasinyaa mara moja. "Nataka kuwa na wewe, ndiyo maana Pamela nikamhamisha kwako. Lakini wewe unataka tu kuwa naye muda wote, why?"

“Siwezi kuwa na maisha mengine zaidi ya kazi na wewe? Nataka pia kufurahia muda wangu na rafiki yangu.” Lisa kisha akakata simu.
Baada ya chakula cha jioni, Lisa alienda saluni kusafisha uso na kucha pamoja na Pamela. Njiani, Alvin Kimaro aliendelea kutuma ujumbe: [Kwani ni lazima uende saluni ili kusafisha uso tu? Huwezi kuosha uso wako nyumbani?]
Lisa akatikisa kichwa, akakosa la kusema. [Alvin wewe ni mwanaume gani ambaye huelewi mambo ya wanawake? Haifai kuosha mwenyewe. Ninahitaji zana na mbinu za kitaalamu, unaelewa?]
[Sielewi. Nielekeze ulipo. Nitakufuata na kulipa bili.] Lisa alipoona maneno 'kulipa bili' akamtumia anwani.

Walipofika kwenye saluni hiyo, waliingia wanawake wawili warembo kuosha nyuso zao pia. Chumba kilichojaa harufu ya manukato na mafuta. Udi na uvumba pia ukawashwa na kusabisha hewa ya mle ndani kuwa ya kustarehesha sana mwili.
Muziki wa kutuliza ulikuwa ukicheza ndani ya chumba kile cha saluni, na Pamela akapiga miayo ghafla. "Ninahisi kulala ghafla. Hii ni ajabu. Nililala sana jana usiku na kuchelewa kuamka asubuhi.”
“Mimi pia nina usingizi kidogo. Lala tu ukitaka. ” Lisa akayapapasa macho yake. Alipokuwa tayari kuchukua usingizi, ghafla aligundua kwamba mwanamke anayeosha uso wake alikuwa na sura isiyo ya kawaida machoni pake. Mwili wake ulizidi kulainika na kuishiwa nguvu.
Ghafla, Lisa aliketi na kubonyeza kifaa

cha ‘air refresh’ kwenye kona kabla ya kumvuta Pamela haraka.
“Huh? Nini tatizo?" Pamela alipokuwa karibu kuketi, ghafla akasema, "Ni nini jamani, mbona najihisi dhaifu sana?" Wafanyikazi hao wawili walikimbia, na wakati huohuo, wanaume wanne waliofanana na shetani walijaa mlangoni.
"Halo, kumbe wanawake wenyewe ni wazuri hivi? Tutafaidi kweli siku ya leo." Mmoja wa wale wanaume wenye cheni nene za dhahabu alimfikia Lisa aliyekuwa dhaifu. Lisa alitumia mkono wake kumsukuma lakini alijikuta mwili mzima ukiwa umedhoofika.

"Nyie ni nani?" Pamela akajikaza kuamka. Lakini mwili ulikuwa mzito kama umegongelewa misumari pale kwenye kitanda cha kuoshea uso.

"Tuko hapa kukufundisha somo." Mwanamume huyo alipunga mkono wake, na wanaume watatu waliobaki wakaingia mara moja.
Sura ya: 432
Muda si muda, wakabanwa vitandani na wale watu wanne.
 "Boss, huyu ndiye Pamela Masanja." Mmoja wa watu hao alitoa picha iliyomtambulisha Pamela.
"Ndio, mchukue na mtangulie naye." Yule mtu mwenye cheni nene za dhahabu alipunga mikono kabla hajamtazama Lisa. “Nyie nendeni. Nitakaa hapa na kujiburudisha na huyu mrembo mwingine.”
"Bro, nataka kufurahia pia." Bwana

mdogo wa pembeni alilamba midomo yake huku akimkazia macho Pamela.
“Bosi alisema tusimguse.
” Jamaa mwenye cheni alionya.
“Sawa.”
Pamela akaondolewa. Lisa alishikwa na wazimu kuwaona watu hao wakimvamia na kuvuta nguo zake.
Wakati huo mlango uligongwa. Alvin aliingia ndani. Aliduwaakuona chumba cha saluni kimejaa wanaume. Alipoona nguo za Lisa zikiwa zimechanika nusu, macho yake yalibadilika mara moja na kujaa wazimu. “Unathubutu vipi kugusa mwili wa mwanamke wangu?”
“Nani... wewe ni nani?” Wale watu wanne walishtushwa na sura yake ya kutisha.


Kabla hawajafanya chochote, Alvin ambaye mara chache sana alitembea na bastola, alikuwa kishachomoa bastola yake ya kujihami kutoka kiunoni na mara moja akampiga risasi ya mguu yule jamaa mwenye cheni ya dhahabu aliyekuwa amemkamata Lisa.
Baada ya kipigo hicho alivua koti lake haraka haraka na kumfunika Lisa. Alipoona alama ya michubuko kwenye ngozi yake, aligeuka nyuma kwa hasira na kuvunja mguu wake wa pili pia.
“Bro, naomba tuondoke. Tuliajiriwa tu na mtu. ” Jamaa mwingine kati ya wale wanne akaomba kwa huruma.
Alvin aliuliza kwa ukali, "Ni nani aliyewatuma?"
Wale jamaa walisita kidogo lakini mmoja wao akaropoka kwa woga, "Mkurugenzi

wa SE Group, Erick Malugu."
"Kwa hivyo ni yeye, Erick Malugu?" Pamela alilaani kwa hasira.
“Ndiyo. Bwana Malugu aligundua kwamba umemzunguka na kushirikiana na Osher Corporation wakati yeye ndiye aliyekualika hapa Kenya na akasema kwamba umemdharau. Kwa hivyo alisema tukukamate na kukupeleka kwake.”
Yule mtu mwenye cheni ya dhahabu aliyevunjwa miguu yote akamtazama Alvin. “Bro, Baba yake na Erick si mtu wa kawaida. Unapaswa tu kuachana na jambo hili. Pia nimekuwa mitaani kwa miaka mingi. Labda tunaweza kuwa marafiki katika siku zijazo."
“Marafiki?” Alvin alicheka kwa sauti ya chini. Tabasamu lake lilikuwa la kikatili sana. "Unajua mimi ni nani?"

"Wewe ni nani?"
Alvin hakumjibu, alimkazia macho yake na kuvunja mikono yake pia.
“Nyie pia hamuwezi kuondoka hivhivi.” Kwa kusema hivyo, alivunja mguu mmoja mmoja wa wale jamaa watatu waliobaki. Waliingia wakiwa wazima lakini sasa ilibidi watoke wakiwa walemavu.
Chumba kidogo kilizikwa na sauti za mayowe ya watu wazima. Wanaume hao walimtazama Alvin kana kwamba walikuwa wakimtazama shetani. Hawakutarajia kwamba walikuwa wameshika na kuzichezea sharubu za simba wa Nairobi.
Baada ya Alvin kuwafundisha somo, alimnyanyua Lisa na kutoka nje.
“Subiri, Pamela...” Lisa akashusha

pumzi ndefu. Aliposhika kola yake, sauti yake ilikuwa dhaifu. "Hatuwezi kumuacha hapa peke yake."
Pamela kwa huruma aliinua kichwa chake na kutabasamu kwa uchungu. “Ni sawa. Nitapiga simu kuita ambulensi na kuwaambia wanipeleke hospitali.”
Alvin alisema bila kujali huku amekunja uso, “Umesikia hiyo? Hahitaji msaada wangu.”
"Hapana." Lisa alisema kwa wasiwasi, “Yeye ni rafiki yangu mkubwa. Hatuwezi kumuacha hapa.”
Alvin alikosa la kusema. "Lisa Jones, nimekwisha kuwaokoa, yupo salama. Unataka nifanye nini tena juu yake?”
“Sawa, umetuokoa tunashukuru. Basi na yeye mchukue, usimuache hapa. ” Lisa alitikisa kola yake taratibu. Hakuwa

na nguvu, kwa hiyo sauti yake ilikuwa nyororo hadi ikasikika kuwa ya kuchekesha.
Alvin akambeba Lisa kwa kumpakata kwa mikono yake miwili kama mtoto mchanga na kumpeleka kwenye gari, akamweka taratibu kwenye siti ya abiriakiti cha mbele na kumfunga mkanda wa usalama.
Alipomrudia Pamela, alimnyanyua tu na kumtupia begani kana kwamba amebeba mfuko wa simenti. Pamela alitaka kulia na kubaki akijiwazia. ‘Nahitaji kufanya haraka kutafuta mchumba.
 Huu ni unyanyasaji.’
Baada ya kufungua mlango wa gari, Pamela alitupwa bila huruma kwenye kiti cha nyuma kama furushi la pamba. “Puuuh!” Kisha kufunga mlango, akarudi kwenye siti ya dereva.

Akiwa amekasirishwa sana, Lisa alimwambia Alvin, “Mbona unafanya kama umelazimishwa?”
Alvin alimkazia macho. "Siwezi kuvumilia kuwagusa wanawake wengine isipokuwa wewe." Uso wa Lisa ulishtuka, na moyo wake ukaruka bila kutarajia.
Ingawa Pamela mnyonge hakuyasikia maneno yao, ghafla alihisi kana kwamba alikuwa amewashuhudia wakionyesha mapenzi hadharani. Alihisi huzuni. Lisa alikuwa amesisitiza njama yake ya kulipiza kisasi, lakini kama mtazamaji, kwanini alihisi kama walikuwa kwenye mapenzi mazito sana?
Wakiwa njiani, Alvin alimpigia simu Hans. “Wewe si ndiye uliyeniambia kuwa familia ya Malugu ni ya watu wastaarabu na wenye kujiheshimu?”

“Ndiyo Bwana Mkubwa. Hawana makuu na mtu...”
Alvin akamkatisha ghafla. “Bado unaongea upuuzi wako? Njoo haraka hapa Dada’s Best Salon na waandishi wa habari. Piga simu polisi na waandishi wa habari. Kuna bonge la kashfa kwao. Ninataka Erick Malugu na SE Group waharibiwe ndani ya siku moja. Hakikisha hakuna mtu anayejihusisha na saluni hiyo leo anayeondoka."
“Imeeleweka.” Hans, ambaye alikuwa kwenye miadi na mpenzi wake, hakuwa na la kufanya ila kwenda na kufanya kazi kwa saa za ziada usiku.

Ndani ya gari, uso mzuri wa Alvin ulikuwa umekunjamana kwa hasira tangu mwanzo. Ilimfanya aonekane kama mungu wa ghadhabu. Na kwa vile

alimchukia sana Erick Malugu kwa kumfuatilia Lisa, Alvin alipata sababu tosha ya kumuangamiza.
Lisa hakutaka kuchangia neno ila alikatishwa tamaa kabisa na Erick. Japo hakuwa amemlenga yeye katika tukio hilo, hakuamini kama angekuwa na moyo wa namna hiyo. Alionekana mstaarabu sana.
Pamela hakuthubutu kuongea, na hakuwa na nguvu ya kuzungumza.
Mara baada ya kufika hospitali, Pamela alitelekezwa bila huruma kwa muuguzi huku Alvin akiwa amemshika Lisa mikononi mwake na kumpeleka kwa daktari, akimsisitiza daktari kumhudumia kwa makini.
Wakati akisubiri majibu ya vipimo vya damu, hatimaye Alvin alimkaripia. "Hauruhusiwi kutoka na Pamela tena,

na wala Erick Malugu asikufuatilie tena. Mara nyingine, ukitaka kutoka na Pamela kwa ajili ya chakula, itabidi tuwasiliane nikupangie ulinzi wa uhakika."
“Leo ilikuwa ajali...”
“Ilikuwa ajali, na yote ni kwa sababu ya rafiki yako. ” Alvin alisema kwa ukali, “Alikuingiza kwenye matatizo yake.”
“Alvin Kimaro, inatosha. Pamela ni rafiki yangu.” Lisa hakujisikia vizuri. “Unamaanisha nini kwa kusema aliniingiza kwenye matatizo yake? Yeye ni kama ndugu yangu, huwa tunasaidiana kwenye shida na raha!"
Maneno ya Lisa yalizama huku akisema kwa kutoridhishwa, “Mbali na hilo, katika miaka hiyo mitatu tuliyokuwa nje ya nchi, tulitegemeana. Kwangu mimi ni sawa na familia. Pia, usisahau kwamba

ulimtishia na tukio la Thomas Njau miaka mitatu iliyopita. Aliacha kufuatilia kesi kwa sababu yangu na kubeba jukumu lote, ambalo liliharibu sifa yake.”
Alvin alikosa la kusema. Alipoteza sauti ghafla. Aliogopa sana kutaja matukio ya miaka mitatu iliyopita.
"Nilikosea. Haya yote ni makosa ya Rodney. Ikiwa asingechochea mambo, Pamela asingelengwa na Erick.” Alvin mara moja akabadilisha maneno yake.
Lisa alimtazama kwa unyonge.
“Usiniangalie hivyo.” Alvin aliinamisha kichwa chini. Kulikuwa na dalili ya malalamiko katika uso wake mzuri na usio na hatia. “Mimi bado ni mwokozi wako usiku wa leo, na pia nina hasira. Kama mwanamume, ni kawaida kuwa na hasira unapomuona mwanamke unayempenda anadhalilishwa.”

Lisa hakuzungumza. Alipofikiria matokeo, ubaridi ulishuka kwenye uti wa mgongo wake.
 Alinyoosha mkono na kuweka mikono yake shingoni mwa mwanaume huyo.
 Alvin aliinamisha kichwa chake na kumbusu taratibu.
Kwa upande mwingine wa pazia, Pamela aligeuza uso wake haraka huku moyo wake ukijawa na wivu. Walikuwa hawana aibu kiasi gani? Kulikuwa na watu wengine karibu!
Akiwa anawaza tu, Rodney akampigia simu. "Nimesikia juu juu tu kwamba Erick alikuletea shida. Uko salama?" “Bado una ujasiri wa kuuliza hivyo? Nimethibitisha tu ushirikiano wangu na wewe leo asubuhi. Erick alijuaje haraka hivyo?” Pamela akamrukia kwa maneno ya hasira.

Rodney alikaa kimya kwa muda kabla ya kusema kwa sauti ya chini, "Nilikutana na Erick mchana huu, na kwa bahati mbaya nikateleza ulimi wangu ..."
Pembe za mdomo wa Pamela zilitetemeka. “Ilikuwa bahati mbaya? Ulijionyesha kwa makusudi kwa sababu ulitaka kumringishia, sivyo?”
Rodney hakujua la kusema. Sura ya: 433
“Rodney! Nilikukosea nini katika maisha yangu ya nyuma?" Pamela hakuweza kujizuia na kulaani kwa sauti ya chini.
“Walikufanya nini?” Rodney alizidi kukosa raha.

Pamela alikuwa karibu kuongea wakati mkono mkubwa uliponyakua simu yake. Alvin kisha akasema, “Yupo hospitalini. Njoo hapa umpeleke nyumbani.”
“Alvin...”
"Vyombo vya habari vinaripoti kuhusu mambo mabaya ya Erick Malugu na SE Group. Jinsi unavyochukua fursa hii ili kumtoa mpinzani wako barabarani itategemea wewe mwenyewe.
 Juu ya hayo, unapaswa kuchukua hili kama somo. Ikiwa una mtu ambaye ni faida kubwa kwa kampuni, unapaswa kuwa macho kwa usalama wake."
Alvin akakata simu na kumtupia simu Pamela kabla hajageuka na kurudi kwa Lisa tena.
Dakika 20 baadaye, ripoti ya vipimo vya damu ilitoka. Daktari alithibitisha kuwa walikuwa sawa na walihitaji tu kupumzika vizuri usiku. Wangeweza

kurejesha nguvu zao kesho yake.
Alvin aliposikia hivyo mara moja akamnyanyua Lisa. “Tunarudi nyumbani.”
Lisa alimtazama Pamela kwa wasiwasi. “Na yeye...”
“Nipo hospitalini. Nitakuwa sawa. Ninyi wawili mnaweza kwenda. Rodney atakuja hivi karibuni.” Pamela alipunga mkono. "Mkiendelea kukaa hapa, Rodney anaweza kuishia kugombana nawe tena."
“Ndio. Yuko sawa. Sina mood ya kubishana naye pia. ” Alvin hakutaka pia kukutana na Rodney.

"Basi, kuwa mwangalifu. Asipokuijia, nipigie.” Lisa alipomaliza kusema tu, Alvin akambeba.

Pamela aliwatazama kwa huzuni na wivu kidogo. Alikuwa akifikiri kwamba marafiki wa kiume hawakuwa wa lazima, lakini sasa aliona ni vizuri kuwa naye.

Ilichukua dakika nyingine 20 kabla ya Rodney kuwasili. Alipomuona Pamela akiwa amelala kwenye kitanda cha hospitali mithili ya kiumbe laini, mwenye nywele zilizochafuka na kuvaa gauni la wagonjwa, alijiona kuwa na hatia kidogo.
“Alvin yuko wapi?”
"Ameondoka.”
“Nini kilitokea huko?” Rodney aliuliza.
“Wakati mimi na Lisa tukiwa kwenye saluni tukiosha nyuso na kucha, chumba kiliwashwa kwa udi na uvumba, wakaingia wanaume wachache, kwa

bahati nzuri Alvin alitokea kama malaika mlinzi. Viinginevyo tungekuwa tumekwisha.” Pamela alivuta kola yake, akifunua nguo zake zilizochanika na alama za michubuko ndani. “Angalia.”
Rodney alikunja uso. Lakini, kama mtu mwenye pesa na mamlaka, kwa kweli hakuweza kujishusha na kumwomba msamaha. “Hiyo ni...Huwezi kunilaumu mimi. Kuna jambo jingine ulilomkosea Erick? Yeye si mtu mzuri kwanza. Uliwahi kumuahidi kitu kabla...”
"Rodney Shangwe, funga mdomo wako. Nilimkosea kwa sababu yako.”
“Kwa sababu yangu? Kwa sababu nimekupa faida kubwa? Kwa sababu nilikupa hisa za Osher Corporation?”
“Kama usingekuwa na mdomo mkubwa hivi, Erick asingejua kuhusu ushirikiano wetu na asingenisumbua usiku huu.

Laiti ningejua Erick ameshajua kuhusu ushirikiano wetu, ningekuwa makini.”
“Ni kosa lako ulipokubali mwaliko wake... “
"Ikiwa ulikuja hapa kunifundisha, basi unaweza kuondoka." Pamela akashusha pumzi. Alikuwa hana nguvu hata hivyo.
“Sawa. Sahau. Sitagombana na mwanamke kama wewe. Nitakurudisha nyumbani.”
Rodney alinyanyua kitako chake na kumnyanyua ghafla. Hata hivyo, hakutarajia Pamela angekuwa mwepesi kiasi hicho.
 Akiwa ameshtuka, Pamela aliweka mikono yake shingoni mwake bila fahamu. Ishara hiyo ya karibu iliwafanya wote wawili kukosa raha, hivyo akaweka mikono yake chini haraka.

Baada ya Rodney kumtazama, alitoka nje huku akiwa amembeba. Kwa kila hatua aliyopiga, misuli ya mikono yake maridadi iliyokuwa nje ya shati lake la mikono mifupi ilijikunja kidogo. Pamela alikoroma. "Sikujuwa kuwa una misuli mikubwa hivi."
"Nyamaza. Ninafanya mazoezi mengi, sawa?" Rodney alidhihaki.
Wakati wa kurudi, muziki laini ulikuwa ukipigwa ndani ya gari. Kwa sababu ya uvumba wa kulevya aliokuwa ameuvuta hapo awali, Pamela hakuweza tena kuinua kope zake.
Walipofika Brighton Gardens, Rodney alisimamisha gari na kupaki, akawasha taa na kugeuka nyuma na kukuta Pamela amepitiwa na usingizi kwenye siti. Nywele zake ndefu zilifunika nusu ya uso wake, na nusu iliyobaki ilifunua

ngozi yake nyeupe iliyong'aa chini ya mwanga. Kawaida alikuwa na ulimi mkali, lakini wakati huo, alikuwa kama paka mpole na asiye na madhara, dhaifu na laini.
Alisita kabla hajatoa bkoti lake ili kumfunika. Kisha, akaketi na kusoma habari kwenye simu yake.

•••
Alvin alipomfikisha Lisa nyumbani kwake, alimuweka kwenye kitanda kikubwa kilichokuwa chumbani humo. Hakuweza hata kufunua kope zake wazi na alilala kwenye gari wakiwa njiani kurudi nyumbani.
Baada ya Alvin kumtazama kwa utulivu kwa muda, aligeuka kuchukua beseni la maji na kuvua nguo zake taratibu. Alipoona mikwaruzo mwilini mwake, uso wake mzuri uligeuka kwa hasira. Hata hivyo, kadri alivyozidi kumvua nguo, uso

wake haukuweza kujizuia kutokwa mate ya uchu kidogo.
Hakuwahi kumtazama Lisa kwa makini hivyo hapo awali. Alikuwa na umbo zuri sana. Alikuwa mdogo mahali alipohitaji kuwa mdogo, na mkubwa mahali ambapo alitakiwa pawe pakubwa. Mahali ambapo palitakiwa kujaa, palijaa sawasawa. Hakuzidi wala kupungua.
Akiwa kijana na mwenye nguvu, Alvin aliguna bila kutarajia, macho yake yakiwaka mwale wa uchu. Mara baada ya kumsafisha, alimvalisha pajama na kwenda kuoga maji baridi peke yake.
Alitumia taulo lake, ambalo lilikuwa na harufu iliyojulikana ya mwili wake. Ilikuwa nzuri sana. Baada ya kuoga, alijilaza na kulala pembeni yake kwenye shuka moja. Aliridhika sana na kunusa harufu ya mwili wake.
Kisha, hakuweza kupinga kumshika

mikononi mwake.
Lisa hakuamka. Hata hivyo, alimsugua uso wake mdogo kifuani mwake na kumkumbatia kwa mikono yake ndogo. Kitendo hicho kilikuwa cha asili sana. Ilikuwa kana kwamba walikuwa wamefanya hivyo mara nyingi sana hapo awali.
Siku inayofuata.
 Lisa alilkuwa amelala wakati Alvin aliposhtuka asubuhi na mapema, lakini hakujisumbua kumuamsha mpaka muda ukaenda sana. Alipofungua macho yake, Lisa alikabiliwa na misuli ya kifuani yenye rangi ya asali. Harufu iliyojulikana ya kiume iliyochanganywa na jeli ya kuogea aliyoitumia ilipepea puani mwake. Je, alimkumbatia Alvin usiku mzima? Haraka akainuka, lakini mkono wa kiunoni ukamkaza na kumrudisha nyuma.

“Umeamka?” Akiwa ameamka tu, sauti ya mwanamume huyo ilikuwa chini na ya kina kama kinubi, na kuufanya moyo wake udunde kwa kasi.
Lisa aliinua macho yake na kumuona Alvin akiwa na sura nzuri na iliyotulia vizuri. Aliuma midomo yake na akasema kwa hasira, “Kwanini unalala kitandani mwangu?”
“Babe, ulikuwa umedhoofika sana jana usiku. Nilikuwa na wasiwasi sana kukuacha ulale peke yako.” Alvin alitoa kicheko cha chini. Alikuwa amechukua fursa hiyo kujihesabia haki ya kulala pamoja naye.
“Huna aibu!” Lisa alimlaani. Aliketi, lakini kwa kuwa alikuwa hajapona kabisa, mara moja akaanguka kwenye kifua chake tena.
"Bado hujapata nguvu?" Ghafla macho ya Alvin yalimchoma kana kwamba

yalikuwa na miale ya moto. Alinyoosha mikono yake kumshika kwa nguvu.
'Si...” Lisa alijitahidi kwa muda mrefu lakini hakuweza kujinasua kwenye mikono yake. Badala yake, aliweza kuhisi macho ya mwanamume huyo yakizidi kuwa ya moto zaidi. Alikuwa anajua fika ni nini ambacho kingefuata.
“Niache niende. Sitaki ku...”
"Nimekukumbuka sana babe. Unataka nisubiri hadi lini?" Alvin alimpindua huku akiweka mikono yake yenye nguvu ubavuni mwake. Pumzi yake inayowaka ilianguka usoni mwake.
“Umesubiri kwa muda gani? Zimepita siku chache tu. ” Lisa aligeuka kwa kukataa. Alilegea sana hata hakuthubutu kumwangalia machoni.

Lakini, hakujua kuwa mkao wake ulikuwa ukimpa Alvin nafasi ya kuanzisha mashambulizi ya taratibu.
"Lisa, sisi ni wapenzi." Alvin aligeuza uso wake na kumbusu midomo yake.
"Hapana..." Lisa alijitahidi.
Licha ya hayo, mwanamume huyo alikuwa na nguvu nyingi sana, na alimfahamu vizuri sana. Mbali na hilo, kujua kutoka kwa Maya kwamba hakuwa amefanya hivyo na Sara kwa miaka mingi, kulimvua wasiwasi kwa sehemu kubwa. Lisa, ambaye awali alikusudia kuinuka, aliljilegeza kabisa na kumwacha Alvin afanye yake.
Sura ya: 434

Wakati huo huo, huko Brighton Gardens.
Pamela alipofumbua macho baada ya usingizi wa kuridhisha, alijikuta amelala kwenye siti ya nyuma ya gari huku akiwa koti zito mwilini mwake. Alikuwa ameduwaa na kuchanganyikiwa kwa muda kabla ya kukumbuka tukio la jana yake usiku. Rodney alipokuwa akimrudisha, hakuweza kuhimili tena na akalala ndani ya gari lake wakati.
Kwa maneno mengine, bado alikuwa ndani ya gari la Rodney. Koti zito liliwekwa juu yake na Rodney, na mto chini ya kichwa chake uliwekwa hapo na Rodney pia? Hisia za ajabu sana zilimjia moyoni.
Baada ya kumfanyia Rodney tukio lililomvunjia heshima majuzi kati, alidhani kwamba Rodney angemtoa nje ya gari au kutafuta watu wa kumlipizia

kisasi. Lakini wala Rodney wa watu hakuwa na mawazo hayo tena.
Pamela aliamka, akakaa kwenye siti na kumuona mwanaume huyo akiwa ameegemea kiti cha dereva bila kutikisika. Rodney alikuwa amepumzika huku akiwa amefumba macho. Kweli alizaliwa na mwonekano mzuri. Alikuwa na pua ndefu, midomo myembamba, ngozi safi, macho mazuri, ambayo kama yangemtazama mwanamke bila papara, yangeweza kumvuta kwake kama sumaku.
Hapo awali, Pamela alidhani kuwa Patrick ndiye mwanaume mzuri zaidi. Lakini, Patrick alibadilika kuwa duni sana kwa kulinganisha na sifa za Rodney.
Wakati huo, kope za Rodney zilicheza. Rodney alipapasa macho na kuzinduka. Alipogeuka, jozi mbili za macho

zilikutana. Ghafla hakuhisi usingizi hata kidogo. “Hatimaye umeamka.”
“Kwa nini hukuniamsha jana usiku?” Pamela alijifanya kutojali.
"Ulikuwa umelala kama nguruwe...”
"Rodney Shangwe, unajua unachozungumza?" Pamela alilipuka papo hapo. "Je, kuna nguruwe mzuri kama mimi?"
“Ndio. Nilimuona mmoja jana usiku. Bado yuko kwenye gari langu sasa hivi.” Rodney alikodoa macho na kudhihaki.
“Potelea mbali.” Pamela alimpiga kofi dogo na kufungua mlango wa gari kuondoka.
Rodney alishusha dirisha na kusema, “Usijali, Erick Malugu amekamatwa. Kama huna maadui zaidi, unaweza

kwenda nje kwa amani ya uhuru. Unapaswa kupumzika kwa siku mbili kabla ya kurudi kazini.
“Nipe pesa kwanza kisha tutazungumza.” Pamela alimkazia macho kabla hajapanda ghorofani.
Alipofika nyumbani, Pamela alipitia habari mtandanoni. Tukio la yeye na Lisa kuvamiwa jana yake usiku na watu wa Erick Malugu lilichukua nafasi kubwa mtandaoni. Watu waliwashambulia Erick Malugu, mkurugenzi wa SE Group, na baba yake Lincoln Malugu, ambaye ni mwenyekiti wa kampuni hiyo. Waliwashutumu kwa kutumia mbinu za kikatili kushindana kibiashara.
[Pia kuna kashafa kwamba Lincoln Malugu, baba yake Erick, mfanyabiashara mashuhuri wa vipodozi nchini Kenya, ametelekeza familia yake kwa ajili ya vimada]

[Mke wa Lincoln Malugu alilia na kumshutumu mumewe kwa kutorudi nyumbani kwa nusu mwaka na alikuwa hajawajalipia gharama za maisha.]
[Mke na binti mdogo wa Lincoln Malugu wanaishi katika nyumba kuukuu ya vyumba viwili vya kulala, huku vimada wake wakiishi katika majumba ya kifahari yenye thamani kubwa.]
[Erick Malugu naye anahisiwa kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja na wanaume kadhaa huko ughaibuni. Hana mke na hana mpango wa kuoa.]
[Bei ya hisa ya SE Group imeshuka. Wanawake wanatangaza kwamba wanaacha vipodozi vya SE.]
Uvumi mbaya kuhusu Erick Malugu

katika nyanja mbalimbali ulianza, na hata mama yake alihojiwa na vyombo vya habari kuhusu tabia mbaya na mumewe na mwanaye.
Tabia ya Erick na baba yake waliwakasirisha wanawake kote Kenya. Lincoln akiandamwa kwa tabia zake za kuendekeza michepuko na Erick akizomewa kwa tabia zake za ushoga. Wakati huo Erick alikuwa bado anachunguzwa katika kituo cha polisi.
Pamela alipoisoma, alifurahia kwa siri jinsi Alvin na Rodney walifanya haraka. SE Group ilipata pesa kutoka kwa wanawake lakini haikuwaheshimu wanawake. Zaidi ya hayo, Erick alikuwa ametumia njia zisizofaa kuwakandamiza wenzake. Ingekuwa vigumu kwa SE Group kurudi barabarani.
Aliwaza na kumpigia simu Lisa. Simu iliita, lakini hakuna aliyepokea.

Mpaka mchana ndipo Lisa alimpigia simu tena. "Rodney alikurudisha nyumbani jana usiku?"
“Umezidi sana. Nilikupigia simu asubuhi, lakini unajibu mchana? Siyo kawaida yako.” Pamela ghafla aligundua kitu na kucheka. “Mbona sauti yako imelegea hivi?"
“Unaongea upuuzi gani? Nilikuwa nimelala, sawa?" Lisa alimtazama Alvin pale kitandani kwa mshtuko.
 Kisha, kwa haraka akaburuta miguu yake yenye maumivu na kutoka nje.
"Ni sawa, Alvin alitumia gharama kubwa sana kunihamisha, wacha ajilie vyake ..." Pamela alitania na kucheka.
"Acha kufikiria ujinga basi!" Lisa akamkatisha kwa umakini.
“Nasikia harufu ya mapacha wengine,"

Pamela alimtupia dongo la mwisho na kuhamisha mada. "Nililala kwenye gari la Rodney jana usiku na kwa bahati mbaya nililala hadi asubuhi."
Lisa alipigwa na butwaa. “Hakukutupa nje? Alikuacha ulale mpaka asubuhi? Hujapata homa?"
“Ndio. Ndivyo nilivyofikiria pia. Sikutarajia pia. Hakuniamsha na hata akanifunika koti lake,” Pamela alisema kwa hisia tofauti.
“Sikujua kama anaweza kuwa mtu mzuri hivi. Anaweza kupika, na yuko makini. Kama si kutuchukia kwa sababu ya Sarah, Rodney angechukuliwa kuwa mtu bora. Kwa bahati mbaya, alimpenda mtu mbaya. Ana jicho baya kwa wanawake," Lisa alisema kwa majuto. "Huna mapenzi naye, sivyo?"
"Shindwa pepo!." Pamela mara moja

akakemea.
“Mbona unamuwazia sana?” Lisa alibonyeza ulimi wake na kukumbusha, “Lakini lazima nikukumbushe. Usijaribu kumpenda Rodney. Patrick ameshakufanya uteseke vya kutosha. Ikiwa utaangukia kwa Rodney, utateseka kuliko hapo awali. Mtu huyo ana macho kwa Sarah tu."
“Si lazima uniambie hivyo. Najua kuliko wewe.” Pamela mara moja akakata simu.
Lisaaliitazama ile simu huku akiwa na wasiwasi kidogo. Kulingana na miaka aliyoishi na kumfahamu Pamela, haikuwa kawaida kwa Pamela kumsifu mwanaume. Lazima kulikuwa na kitu ndani yake.
Alipokuwa ametekwa na mawazo hayo, mkono wa mwanamume ulikuja kutoka

nyuma na kumshika kwa nguvu. Alishtuka Alvin akimuuma sikio.
"Rodney ni mtu mzuri?"
Lisa alitetemeka ghafla na kugeuka huku akitaka kumwangalia. Lakini, Alvin alifunga midomo yake. "Mzuri kuliko mimi?"
"Alvin Kimaro. Swali gani hilo?”
"Unamsifia mtu mwanaume mwingine, unadhani mimi nitajisikiaje?" Alvin alifoka kwa maumivu, macho na sauti yake ilikuwa na uchungu.
Lisa alikosa la kusema. “Nimesema kitu kibaya? Nilikuwa nikifikiria kuwa Rodney hakuwa na maana isipokuwa sura yake, lakini ikawa kwamba ana pointi nzuri pia."
“Amekunyanyasa sana hapo awali...” Alvin aliuma meno yake na

kumkumbusha. Ilimkera sana kusikia mwanamke aliyempenda akimsifu mwanaume mwingine.
“Wewe hujawahi kuninyanyasa?” Lisa alimkumbusha. "Afadhali usiseme kwamba wengine ni wabaya, au nitaibua maudhi yako ya zamani tena."
Alvin akaachana nayo. Alizika uso wake mzuri kwenye shingo yake kimya. “Babe, nina njaa.”
Lisa alicheka. "Ni bahati mbaya. Nina njaa, pia. Sina hata nguvu ya kupika kiamsha kinywa, na sasa mwili wangu umedhoofika.”
“Nitakupikia.” Alvin alimwambia kwa upole. “Lakini kinaweza kisiwe kitamu kama chako. Usijiepushe nayo.”
“Kama kweli huwezi, basi pika mayai tu. Au na yenyewe yatakushinda?”

Sura ya: 435
Chini ya mapishi ya Alvin, walipata kifungua kinywa rahisi. Hata hivyo, kwa kuwa alikuwa na njaa sana, alihisi kuwa upishi wa Alvin kama takataka haungeweza kujaza matumbo yao.
Baada ya kula, Hans alipiga simu kuuliza kuhusu mambo fulani ya kampuni ambapo Alvin alisema, “Niletee baadhi ya nguo zangu hapa nyumbani kwa Lisa. Nitalala hapa siku kadhaa."
Hans akajibu, “Ahem. sawa.”
Lisa, hata hivyo, alimpokonya simu. "Hapana usilete. Hakuna haja." Kisha akakata simu.
“Lisa Jones...” Alvin aliuma meno.

“Sitaki kuishi pamoja na wewe kwa sasa. ” Lisa aliinuka. “Ikiwa kuna haja ya kulala usiku kucha, nitakuja kwako. Kumbuka kuajiri watumishi. Sitaki kuwa mtumishi wako wa nyumbani.”
Uso wa Alvin ukaingia simanzi, na Lisa akatabasamu. “Nimesema kitu kibaya? Nafasi yangu ni ndogo, na hakuna nafasi kwa mjakazi kuishi. Ukihamia hapa, nitalazimika kushughulikia kazi zote peke yangu. Samahani, lakini hadhi yangu ni ya juu na muda wangu ni wa thamani zaidi kwa sasa, kwa hivyo sitafanya chochote kitakachodhuru vidole vyangu maridadi. Hata hivyo, ni lazima nifurahie kama Sarah alivyokuwa akitendewa vizuri.”
Sura ya Alvin ilikuwa ya kusikitisha, na alipotaka kufungua mdomo wake, Lisa aliminya vidole vyake vyembamba kwenye midomo yake. “Usiongee nami

kuhusu kujitolea kwa ajili ya upendo. Ninaweza kukupenda, lakini nataka kujipenda zaidi.”
“Sawa. Tutafanya chochote utakachosema.” Alvin hakujua acheke au alie. Hakuwa amekusudia kumtendea ubaya. “Nitaajiri mpishi na mjakazi. Nitamwita Aunty Yasmine, kwanini usije kwangu ukae?”
"Hapana. Kunapaswa kuwa na umbali wa mara kwa mara kati ya watu wawili. Tutachokana haraka ikiwa tutakuwa pamoja kila wakati." Lisa akatingisha kichwa kwa uthabiti.
“Babe, mimi sitakuchoka,” Alvin alimbembeleza kwa upole.
Lisa alimtazama kwa ajabu. "Sawa, lakini mimi nitakuchoka ikiwa tutagandana muda wote kama kupe."

Alvin alishindwa cha kusema. Alisema nini? Angemchoka? Je, hisia zake hazikupaswa kuimarika zaidi alivyokuwa naye?
Alvin akashusha pumzi ndefu. Baada ya kupata pigo, uso wake mzuri sasa ulionekana kutopendeza sana, na akauma meno yake. "Lisa Jones, nitakupa nafasi moja ya kurekebisha kauli yako."
“Sijasema chochote kibaya... Ah...” Kabla Lisa hajamalizia sentensi yake, aligeuzwa na Alvin na kumpiga
kofi mara mbili matakoni.
Ingawa halikuwa kofi nzito, bado lilimtia hasira. "Alvin Kimaro, unathubutuje kunipiga?"
Alvin alishtushwa na hasira machoni

pake. "Nimekupiga kwa mahaba tu ..."
“Sijali. Mahaba gani hayo ya kuchapana makofi? Ipo siku utanitoa meno kisha useme ni mahaba tu. Nililala na wewe asubuhi tu, na mchana unaanza kunipiga, nakuchukia. Nenda zako.” Macho ya Lisa yalikuwa mekundu. Hapo awali alikuwa akijifanya tu, lakini baada ya kufikiria juu yake, alihisi huzuni pia.
Alvin mwenye kiburi naye alikasirika kidogo kwa kufukuzwa namna hiyo, lakini alipoona macho yake mekundu, mara akaingiwa na hofu na kumnyanyua kwa makini. “Babe, nilikosea. Usiwe na hasira. Unaweza kunipiga na wewe, sawa?"
"Sitaki kupiga matako yako." Lisa alitazama pembeni. Macho yake mazuri yalijawa na machozi, na mashavu yake yalituna kwa hasira za kujishaua, na kumfanya aonekane mzuri

iwezekanavyo.
Moyo wa Alvin ukayeyuka. Akamshika mkono na kuupigisha usoni mwake. “Hii ni sawa?”
"Hapana, ni jepesi sana." Lisa alishusha macho chini na kukoroma.
"Hili je?" Alvin akamshika mkono tena na kujipiga makofi mazito.
Ikiwa wengine wangeona tukio hilo, macho yao yangeanguka. Hakuna mtu ambaye angetarajia kwamba Alvin mwenye nguvu na mamlaka angejishusha kwa mwanamke kama huyo. Hata Sarah angeshtuka akiona hivyo.
"Hapo sawa." Lisa aliitazama alama nyekundu usoni mwake na kutabasamu.
Alvin alipoona tabasamu usoni mwake, moyo wake ukaanguka chini.

Hakuwahi kufikiria kwamba hata siku moja angeweza kumbembeleza mwanamke namna hiyo. Hakuwa hivyo hata alipokuwa akikabiliana na Sara siku za nyuma.
Kwa kweli, wakati fulani alikuwa akimbembeleza Sarah pia, lakini akimlinganisha na Lisa, alihisi kwamba alikuwa akimfurahisha Sarah tu. Ilionekana moyo wake haukuwa pamoja naye.
Akiwaza hayo, hakuonekana kuwa na wakati ambapo moyo wake ungeruka mapigo alipokuwa na Sarah. Hakukuwa na hasira nyingi, lakini hakukuwa na upendo wa kupendeza pia. Hiyo ilitokana na sauti kichwani mwake ambayo ilimtawala na kumwambia kuwa alimpenda Sara, kwa hiyo ilimbidi awe mwema kwake.
Lakini ... huo ulikuwa upendo? Je,

alimpenda Sara kweli? Mapenzi ya kweli yanapaswa kuwa hivi, ambapo kulikuwa na vicheko na utamu. Hata alipokuwa na hasira, alikuwa mrembo.
Ghafla, kulikuwa na maumivu makali katika kichwa chake. Akavuta pumzi ya baridi na kumuachia, akajikwaa hatua mbili nyuma na kushika kichwa chake.
“Alvin...” Lisa alishtuka na kumshika haraka. "Nini tatizo?"
"Kichwa changu kinauma ghafla." Alvin alishika kichwa chake.
Kuchanganyikiwa kuliangaza machoni mwa Lisa. “Ulikuwa unafikiria nini?”
“Nilikuwa nikifikiria... ” Koo la Alvin lilikwama ghafla alipogundua kuwa ubongo wake ulikuwa umechanganyikiwa kidogo. "Nilifikiri kwamba nilihisi kuwa na raha sana

kushirikiana nawe hivi sasa, na ulionekana mrembo sana ulipokuwa na hasira."
“Ni hayo tu?" Lisa hakuamini. Mara ya mwisho, pia alikuwa na maumivu ya kichwa wakati alikumbuka kitu huko mgahawani walipokuwa wakila na Suzie. "Ulikuwa na maumivu ya kichwa hapo awali?"
“Nimekuwa na maumivu machache ya kichwa tangu Sarah aliponisaidia kunitibu.” Alvin aliganda. “Inaonekana kila ninapoumwa na kichwa, nakuwa niko na wewe. Ninapaswa kushauriana na daktari wa ubongo...”
“Unaogopa kuwa una uvimbe kwenye ubongo wako?” Lisa alitania.
“Usiongee upuuzi. Hilo haliwezekani. Bado nataka kuwa na wewe.” Alvin alibana uso wake mdogo. "Lisa, wakati

mwingine, nahisi kama maisha ni ya ajabu, lakini siwezi kusema nini cha ajabu juu yake ... Kweli, nilikuwa nikifikiria tu kwamba ninapokuwa na Sarah, nakuwa sijaridhika naye kama ninapokuwa na wewe hivi.”
“Acha.” Lisa aliziba mdomo ghafla.
Sarah alimlaza akili, na Lisa alimwona daktari mzuri saikolojia kuhusu hilo hapo awali. Kwa aina hii ya hypnosis, hali mbaya zaidi ilikuwa kwamba siku moja, mgonjwa angevunja hypnosis mwenyewe na nafasi ya kupona ilikuwa ndogo. Kinachowezekana zaidi ni kwamba ukweli na kumbukumbu iliyopandikizwa ingegongana, na mgonjwa angepoteza akili yake.
"Nini tatizo?" Alvin alishangaa. “Hakuna kitu. Sitaki tu kusikia kuhusu

Sarah na wewe.” Lisa aligeuza uso wake kwa makusudi.
“Samahani.” Alvin aligeuza mwili wake na kumbusu kwa jazba na mapenzi. “Babe, nina uhakika wa ajabu sasa. Nakupenda."
Lisa aliduwazwa kidogo na busu lake na kuning'iniza mikono yake shingoni mwake. Hapo awali alipanga kwenda ofisini lakini hakufanikiwa mwishowe.
TUKUTANE KURASA 436-440
ONYO: Ni marufuku kusambaza, kukopi wala kuuza kazi hii kwani endapo kama tutakubaini basi sheria itachukua mkondo wake (By: Official Dully)
 
LISA KITABU CHA NANE (9) SIMULIZI........................LISA KURASA.................436 - 440
PRESENT: SIMULIZI ZA DULLY

Sura ya: 436
Siku iliyofuata, walipokuwa wakitoka kwenda kazini, Lisa alimsimamisha Alvin ghafla kando ya duka la madawa.
"Unataka kufanya nini?" "Kununua kitu."
Lisa alifungua mkanda wake na kushuka kwenye gari na kwenda kwenye duka la dawa. Aliomba vidonge vya uzazi wa mpango, akanywa na glasi ya maji kabla ya kutoka.
“Ulinunua nini?” Alvin alimtazama ghafla, uso wake mzuri ulikuwa na giza kidogo. Lisa alipepesa macho na kutoa boksi la vidonge kwenye mkoba wake.
Mikono ya Alvin ikakaza kwenye usukani, hata mishipa ilikuwa imemtoka. Uso wake haukuwa mzuri pia. “Usimeze

tena wakati mwingine. Ninapanga kutumia maisha yangu yote na wewe. Tunahitaji watoto pia...”
"Mara ya mwisho tulipokuwa pamoja, ulinirushia boksi la dawa za kupanga uzazi." Lisa alimkatisha. "Sasa nina hofu kidogo."
"Ilikuwa kwa sababu mimi ..."
“Pia, hali mbaya niliyokuwa nayo nilipokuwa mjamzito ilinitia kiwewe. Siko tayari kupata maumivu na woga wa aina hiyo tena, kwa sasa, kwa hivyo tafadhali jiweke kwenye viatu vyangu na ufikirie juu yake.” Lisa alisema bila huruma.
“Samahani.” Alvin alikasirika.
Akifikiria juu yake, alichukia utu wake wa zamani sana. Kwanini alikuwa mkatili sana? Hata kama hakumpenda wakati huo, bado alikuwa na mimba ya

watoto wake. Kwanini hakumjali zaidi? Kadiri alivyokuwa akifikiria juu yake, ndivyo alivyozidi kuhisi kuwa maisha yake ya nyuma yalikuwa ya kushangaza sana.
“Usinywe dawa za kupanga uzazi tena. Sio nzuri kwa afya yako." Akashusha pumzi. "Nitanunua kondomu."
“Sawa.” Lisa aliitikia kwa kichwa na hakukataa.
Alvin alimshusha Lisa Mawenzi Investiments na yeye akaelekea ofisini kwake. Muda si mrefu baada ya kupanda ghorofani, alipokea chokoleti iliyotengenezwa maalum kwa ajili yake. Ndani kulikuwa na kadi ya waridi: [Samahani, babe. Nitakutendea mema maisha yangu yote. Upendo, Alvin.]
Kisha, WhatsApp yake iliita. Alvin alituma ujumbe baada ya ujumbe.

[Lisa, I miss you.]
[Lisa, chokoleti ni nzuri?]
[Babe, nini kingine unataka kula?]
Lisa alikosa la kusema. Alitazama meseji zake za whatsapp na midomo yake ikalegea. Mtu huyu alikuwa kama mtu tofauti na Alvin wa zamani. Hakuwahi kumuona kama hivyo hapo awali.
Aliinamisha kichwa chake na kujibu, [Hakuna haja. Nina mipango yangu usiku wa leo.]
Alvin: [Unatoka na Pamela tena?]
Lisa: [Hapana, nina mambo mengine tu.]
Alvin: [Nikusindikize?]

Lisa: [Hapana.]
Alvin: [Nitakupangia ulinzi.]
Lisa: [Sitaki.]
Alvin alituma emoji yenye uso uliojawa na huzuni.

Lisa. [Kuwa mwema. Nina shughuli nyingi. Usifanye fujo.]
Alvin. [Sawa, sitafanya fujo. Nitamsikiliza mke wangu.]
Lisa, ambaye alikuwa akila chokoleti, karibu apaliwe. Ni nini eti? Je, huyu jamaa alikuwa na kizunguzungu?
Hata hivyo, alitabasamu kipumbavu huku akitazama meseji hizo.
•••

Usiku, kwenye baa.
Lisa aliketi kwenye stuli ndefu ya baa karibu na Logan, ambaye alikuwa ndiyo kwanza ameshuka kutoka safarini.
"Lazima ilikuwa safari ngumu kwenda Somalia. Uchunguzi ulikuwaje?” Lisa alifungua chupa ya bia na kuisukuma kwa Logan.
"Nimewafuatilia kwa siri Sarah na Thomas na kugundua jambo zito, naomba uweke siri hii kwa usalama wako.” Logan alikunywa bia na kusema kwa sauti ya chini. “Nilitumia muda huko na hatimaye nikapata upepo wa kitu. Kweli Thomas amekodi kundi la wasomali na kuwaleta nchini. Thomas alienda huko yeye binafsi na kutumia pesa nyingi kuwaajiri.”
“Kuna picha?”

“Hapana.”
Chini ya macho yake ambayo yalionekana kusema 'huna maana sana', Logan alichukizwa na kueleza, "Haikuwa rahisi kupata picha. Ingawa hapo ndio mahali penye machafuko zaidi ulimwenguni, bado wamejipanga. Nani atathubutu kuwaajiri ikiwa habari itafichuliwa kiholela?”
"Thomas, ana mpango gani kwa kuwaajiri watu hao hatari.”
Lisa alitafakari. "Kwa hiyo Sarah bado ana wasaidizi?"
"Hakika ana watu wanaomuunga mkono," Logan alisema kwa uhakika. "Lakini bado hajaonyesha kadi zake."
“Tusubiri. Lazima uvumilivu utakuwa umemshinda sasa, hatutangoja kwa muda mrefu na tutaona papara zake. ”

Lisa alikunywa bia na ghafla alionyesha uchovu kutoka kwenye uso wake.
"Nini tatizo? Mbona unaonekana kuchoka sana?" Logan aliinua uso wake. "Uko na Alvin tena, sivyo? Unajisikiaje kurudiana na mume wako wa zamani? Baada ya kukuacha anakuchukulia kama hazina sasa?"
Lisa alimkazia macho, na Logan akacheka. “Nina hamu ya kujua tu. Baada ya yote, alikuwa mtu unayempenda. Hutaishia kuwa na moyo laini, sivyo?
Lisa alitazama chini. Uso wake mzuri haukuweza kuonekana kwenye mwanga hafifu.
"Ni nini, wewe kweli ... umekuwa na moyo laini?" Logan alikosa la kusema kwa ukimya wake wa ajabu. “Huyo ndiye mtu aliyekuumiza sana hapo

awali. Huko nyuma, kama usingeigiza kifo chako, ungekufa. Watoto wako pia wasingekuewepo.”
“Najua.” Lisa alikunja uso kwa kero kubwa. Ikiwa asingegundua kutoka kwa Maya kwamba hakuna kilichotokea kati ya Sarah na Alvin, angeweza kuwa na wasiwasi. “Nina... nina hasira kidogo. Kwa kweli, najua hakukusudia kuniumiza wakati huo. Alilazwa tu akili na Sarah, lakini mambo yake ya siku za nyuma ni kama jeraha wazi kwangu. Wakati fulani, nafikiri kwamba nilipize kisasi kwa Sarah na nisiwe karibu sana na mwanamume huyu. Ana sumu...”
Ni wazi aliumizwa naye na akafikiri kuwa hampendi tena. Hata hivyo, siku mbili walizokuwa pamoja zilimfanya ajisikie kuwa alirejea wakati ambao wawili hao walikuwa wanapendana.
"Nifanye nini?" Aliuliza bila kuficha. Je,

aendelee au aache?
“Nikushauri nini? Sijawahi kuwa katika mapenzi kabla. Lakini unaweza kuolewa naye tena na na kupata naye watoto kana kwamba hakuna kitu kilichowahi kutokea?” Logan alisema, “Kusema ukweli, nadhani ikiwa angeweza kulazwa na Sarah hapo awali, ilimaanisha kwamba alimwamini kabisa Sarah. Zamani, alikuheshimu kiasi gani mlipokuwa kwenye ndoa? Hakufikiri kwamba alipaswa kujiweka mbali na mpenzi wake wa zamani kwa vile alikuwa na mke?”
Lisa alipigwa na butwaa. Ndiyo, Alvin alistahili kulipizwa kisasi. Ujinga wake ulimdhuru yeye na watoto wake.
“Sahau, tuondoke. Usiku umeenda sana.” Logan alipiga miayo. Alikuwa na uchovu wa safari na alikuwa hajapumzika vizuri. “Usiwaze sana.

Ikiwa bado kuna watu nyuma ya Sarah, basi bado kazi haijaisha. Isitoshe, usisahau, Sarah ndio ameachana na Alvin. Je, haya ndiyo matokeo pekee unayotaka, au unataka kulipiza kisasi zaidi?”
Macho ya Lisa yalipoa taratibu. Sarah aliua watu wengi sana na kuharibu familia ya Charity. Bila shaka angefanya maisha ya Sara kuwa mabaya zaidi kuliko kifo. Ikiwa Alvin angethubutu kumzuia, basi angemshughulikia pia.
Sura ya: 437
Lisa aliamka siku iliyofuata huku tumbo likiwa limechafuka kidogo kutokana na hungover za bia alizokunywa jana yake usiku. Alipoinuka na kunawa uso, alipokea simu kutoka kwa Alvin. Sauti yake ilikuwa chini na kali. “Ulienda wapi jana usiku?”

"Nilikuwa na jambo la kufanya na rafiki ..."
"Jambo gani la kunywa naye kwenye baa?" Alvin aliuma meno yake na kusema kwa huzuni, “Ingia mtandaoni usome habari zinazokuhusu, Lisa, nakuja baada ya dakika kumi. Afadhali unipe maelezo ya kueleweka.”
Kisha, akakata simu.
Lisa alishtuka na kutumia simu yake kutafuta habari hizo. Habari za hivi punde zaidi zilisema: [Mrithi wa Ngosha Corporation akizungumza na kucheka na mpenzi wake wa ajabu, wakionekana kuwa karibu sana.]
Picha hiyo ilikuwa ya Logan na umbo lake lilizofifia kwenye mwanga mdogo wa baa. Aliyakodoa macho yake na kuyapapasa. Kwa bahati nzuri, uso wa Logan haukufunuliwa, vinginevyo,

ingekuwa shida. Baada ya yote, Logan ndiye msaidizi wake pekee ambaye angeweza kumwamini kabisa.
Alikuwa ametoka tu kubadilisha nguo zake wakati aliposikia mtu akibisha mlango kwa nguvu. Alipofungua mlango, uso wa kutisha wa Alvin ulileta ubaridi wa kutisha.
“Ni nani huyo mtu?” Alvin alikuwa akipandisha kichaa kwa hasira. Alimjali sana na kumshikilia kila wakati, lakini alimzunguka na kwenda kwenye baa na mwanaume mwingine. Jambo lililo baya zaidi ni kwamba aliweza kutambua kupitia kwa mgongo wa mtu huyo kwamba hakuwa na sura mbaya. Mwili wake ulikuwa mzuri pia. Haikuwa rahisi kwake kumuondoa Kelvin na Erick Malugu, na sasa kulikuwa na mtu mwingine wa kumuumiza kichwa.
Alvin akamshika mabega kwa hasira.

“Lisa Jones, huwezi kunipa amani ya akili? Utakufa usipochokoza wanaume kutwa nzima? Au unamaanisha siwezi kukuridhisha?”
Mabega ya Lisa yalimuuma kutokana na mkandamizo wake. Alipomtazama mwanaume aliyekuwa mbele yake, maneno ya Logan jana yake usiku yakamjia kichwani. Alipaswa kudhibiti hisia zake. "Alvin Kimaro, nilikubali kuwa nawe, lakini huwezi kunizuia kuwasiliana na watu wa jinsia tofauti."
Uso wake ulijawa na hali ya kutojali, tofauti kabisa na sura ya aibu na haya aliyokuwa nayo kitandani jana yake. Alvin alihisi ndoo ya maji ya baridi inamwagiwa na kumtuliza.
"Lisa Jones, kwa kuwa uko pamoja nami, kujitenga na watu wa jinsia tofauti ndiyo kanuni ya msingi ya kuwa mpenzi wangu." Alvin alisema kwa uso wa

baridi, “Nilikuruhusu utoke jana, lakini ukatoka na mtu asiyejulikana. Unanichukulia mimi kama nani?”
"Nimekwambia kuwa ni rafiki tu. Ikiwa hutaki kuniamini, basi hakuna ninachoweza kufanya." Lisa aligeuka na kutoa maziwa kwenye jokofu bila kujali.
Alvin alimkazia macho mgongoni. “Usiponipa maelezo yaliyoshiba, nitamchunguza mtu huyo na kujua yeye ni nani.” Kisha, akageuka kwa hasira na kutoka nje.
“Subiri,” Lisa alimwita huku sauti yake ikipanda kwa hasira. “Umemaliza? Unachunguza watu walio karibu nami kama nani yaani? Wewe ni mume ni wangu? Ulimchunguza Erick hapo awali na sasa unamchunguza mtu mwingine. Alvin Kimaro, usiponipa heshima hata kidogo, basi tutaachana.”

Alvin alishtuka. Uso wake ulikuwa umejawa na uhasama na alikuwa na hasira sana hadi akaupiga mlango kwa ngumi, huku akitoa sauti nzito ya mguno. Lakini, Lisa alimimina tu kikombe cha maziwa na uso uliotulia, bila kuathiriwa kabisa na hasira yake.
Kwa muda, Alvin alishtuka kidogo. Alikuwa amekasirika waziwazi, lakini kwa nini Lisa hakumfariji kwa upole, au kujielezea? Maadamu angemsihi na kuahidi kutotoka na mtu wa jinsia tofauti siku zijazo, angeweza kujilazimisha kumsamehe. Lakini, mtazamo wa mwanamke huyu ulikuwa wa kiburi sana.
"Lisa Jones, sidhani kama unatambua, lakini kwa kuwa wewe ni mwanamke wangu, si rahisi kuachana. Nitakutupa mbali ikiwa sikutaki, lakini haiwezekani wewe kuanza kuniacha.” Kisha akaufunga mlango kwa nguvu na

kuondoka zake.
Chumbani, Lisa alimpigia Logan kinyonge. "Ulipigwa picha na mtu kwenye baa. Jifiche kwa sasa na usijionyeshe hadharani. Nitawasiliana nawe ikiwa chochote kitatokea."
Siku iliyofuata, Alvin hakuwasiliana naye. Lisa alikwenda kwenye jumba la familia ya Ngosha ili kumsalimia Lucas. Alipofika, Lucas alikuwa akicheza na seti ya Lego Star Wars.
"Babu alikununulia hii?" Lisa alitazama sanduku. Ilikuwa toleo ndogo, kwa hivyo ilikuwa ghali kabisa.
“Anko Kelvin alinipa. Alikuja shule ya chekechea kuniona jana.” Lucas alitazama juu na kutabasamu, akifunua safu ya meno ya lulu.
Lisa alishangaa. Alijua kuwa Lucas

alitabasamu mara chache, lakini sasa alikuwa akicheka kwa sababu ya zawadi ya Kelvin. Ilionyesha kwamba alikuwa akiipenda sana zawadi hiyo.
Kelvin alikuwa hivyo kila mara. Alikumbuka kile watoto wale wawili walipenda, na alikuwa mpole na msikivu. Moyo wake ukawa mzito ghafla. Alijua kwamba Kelvin alikuwa akimfuatilia kimyakimya kwa nyuma. Aliogopa kuvuruga mpango wake na mara chache sana aliwasilina naye.
"Lucas, unampenda Anko Kelvin sana?" Lisa aliuliza kwa upole.
"Mama, najua kwamba anakupenda na atakuwa mwema kwangu," Lucas alisema kwa uzito. “Jambo muhimu zaidi kwangu ni kwamba Mama atakuwa na furaha na hataumia.” Lisa aliinamisha kichwa chini na kubusu paji la uso la mwanae.

Joel alikuja huku akitabasamu. “Lucas ndiye mtoto mwenye busara zaidi ambaye nimemwona. Ana akili sana tofauti na umri wake.”
“Ndiyo.” Lisa alikigusa kichwa cha mwanae. "Baba, unajisikia vizuri?"
"Chembechembe za sumu ziliondolewa hivi majuzi, kwa hivyo sasa najisikia bora zaidi." Joel akahema. “Nilienda ofisini jana na nikagundua kuwa babu yako alichukua nafasi ya kuongoza. Alitaka nifanye mazoezi nyumbani kwa muda na akasema kwamba angetazama kampuni. Bila kuficha, lazima awe amejazwa upepo na Damien. Babu yako hata alikubali kuanzisha ubia na Kampuni ya Campos. Sina hisia nzuri kuhusu hili...”
"Baba, ukiniuliza, unapaswa kuwaacha wafanye wapendavyo," Lisa alisema

kwa unyogovu. “Uza tu hisa zako na uachane na kampuni ya Ngosha. Afya yako itakapokuwa bora, unaweza kuanzisha kampuni nyingine peke yako.”
Uso wa Joel ulizama. “Lisa, Ngosha Corporation ni moyo na roho ya Baba. Nilitumia muda mwingi wa maisha yangu kuijenga kampuni hiyo...”
“Baba, nitakuwa mkweli. Sina matumaini kuhusu ushirikiano wa Campos na Ngosha. Nilisikia kidogo kutoka kwa Alvin. Familia ya Campos ni bora katika kujifanya dhaifu, lakini wanataka kuipita familia ya Kimaro na kuwa familia kuu nchini. Nadhani anataka kutumia familia ya Ngosha kama hatua.” Lisa alieleza, “Fikiria jambo hilo. Kuanzisha kampuni ya ubia. Familia ya Ngosha haijui chochote kuhusu biashara ya fedha na haina timu inayojulikana au wataalamu. Hatutajua

jinsi familia ya Campos itakavyobadilika katika siku zijazo.
“Zaidi ya hayo, babu amerudi na kujihusisha na mambo yote ya kampuni. Damien na Melanie ni sawa tu na wanahisa wake. Ikiwa unataka kupata udhibiti tena, huwezi kupambana na Damien tena. Ukigombana na babu, na mambo yakienda kusini, utaitwa mtu asiyefaa.”
Uso wa Joel ukawa mzito. Aliona hilo likija. Ubaridi ulikimbia chini ya uti wa mgongo wake huku akifikiria juu ya kile baba yake alichofanya. Damien na binti yake walifanya mambo mengi sana ili kumdhuru Joel, lakini bado baba yake aliwasamehe.
Lisa aliongeza, “Ikiwa ni lazima niseme, thamani ya soko ya Ngosha Corporation iko juu sasa, na hisa ziko katika bei kubwa zaidi. Kuziuza mapema ni wazo

bora. Baba, wakati mwingine, kung’ang’ania kitu ni kujikosehsa fursa ya mafanikio. ”
“Labda uko sawa...” Joel alishangazwa na maneno yake kwa muda na akaugua kwa huzuni.
Lisa alipoona anasitasita akasema, “Baba ukishindwa niachie mimi hili jambo. Baada ya yote yaliyotokea, huelewi? Unathamini sana mapenzi. Mapenzi yako kwa Nina, upendo wako wa kindugu kwa Damien, na upendo wako kwa Bibi na Babu. Kama si wote hao, je wewe na mama yangu mngeanguka hadi mlipo leo? Niambie kwa uaminifu. Una furaha?"
Joel alitabasamu kwa uchungu. Angewezaje kuwa na furaha? Tangu alipogundua kuwa Melanie hakuwa mtoto wake, alijuta kila dakika.
 Watu hao walimchukulia kama mpumbavu na

kumuumiza na hakukuwa na msamaha wa dhati hata kidogo.
“Sawa, Lisa. Nitakuachia hili.” Joel aliitikia kwa kichwa. "Nitakabidhi haki zangu zote kwako."
"Baba, unapoanzisha kampuni mpya, bado unaweza kufungua mipaka mipya na kikundi cha watu ambao ni waaminifu kwako." Lisa alimkumbusha. “Lakini usiweke jambo hili hadharani. La sivyo, Bibi na Babu watakasirika wakijua.”
Sura ya: 438
Siku iliyofuata, Lisa aliunda kamati ndogo ofisini kwake ili kufuatilia habari fulani katika mzunguko wa biashara.
Muda mfupi baadaye, Amba alimletea habari hiyo. “Mwenyekiti Jones, Bwana Kawada kutoka Delta Co., Ltd. nchini

Japani anavutiwa sana na Ngosha Corporation. Kwa bahati mbaya, anasafiri kwa ndege kwenda Afrika Kusini leo kuhudhuria maonyesho ya kimataifa ya sanaa ya Afrika Kusini.”
"Kawada anapenda sanaa?" Lisa aliinua uso wake.
"Ndiyo, Bwana Kawada anavutiwa sana na picha za kubuni," Amba alielezea.
“Nikatie tiketi ya ndege. Nitasafiri kwa ndege hadi Johannesburg leo. ”
Lisa alisema mara moja.
•••
Ndani ya Kampuni ya KIM International, Saa mbili usiku, taa katika ofisi ya Alvin ilikuwa bado inawaka. Wale waliokuwa katika ofisi ya sekretari walipiga miayo na kumtazama Hans kwa kusihi. “Hans, tafadhali umsihi bosi asichelewe sana na kuturuhusu twende nyumbani mapema. Hatuwezi kuvumilia tena.”

"Unasema hivyo kama naweza." Hans alitaka kulia.
Alichukua picha ya nyuso za huzuni za kila mtu ndani ya idara ya sekretari na kuzituma kwa Lisa. [Bi. Jones, unaweza kumshawishi Bwana Kimaro asifanye kazi ya ziada kwa kuchelewa sana? Tunataka kwenda nyumbani. PS: Tulifanya kazi ya ziada hadi saa saba usiku jana.]
Lisa alijibu: [Mmemwendekeza, komaeni tu. Sijawahi kuwalazimisha wafanyakazi wangu wanisubiri kila wakati ninapofanya kazi saa za ziada.]
Hans: [Sio kila mtu ni mzuri kama wewe.]
Lisa: [Niko busy. Nina safari ya ndege, kwa hivyo ninazima simu yangu.]

Hans akaingiwa wazimu kusikia Lisa hakuwa Nairobi tena. Haraka akaangalia mashirika ya ndege. Dakika kumi baadaye, aligonga mlango wa bosi wake. “Bwana Kimaro...”
“Usinisumbue,” Alvin alionya kwa ukali na kuchukua simu yake na kuitazama. Jamani. Mwanamke huyo alikuwa hata hajampigia simu kumwomba msamaha bado? Je, alikuwa akimfanyia mjinga? Je, hii ilikuwa malipo kwa nyakati hizo ambapo alimkosea walipokuwa kwenye ndoa hapo awali? Alipofikiria uwezekano huo, moyo wake ukaingiwa na maumivu makali.
"Hapana, Bwana Mkubwa. Nilitaka kukujulisha kwamba Bi Jones alichukua ndege hadi Johannesburg. ” Hans alisema kwa unyonge.
Alvin ghafla akaketi kwenye kiti cha ngozi na kumtazama kwa macho

makali. “Anaenda huko kwa ajili ya nini?”
"Kuna maonyesho ya sanaa ya kimataifa huko kesho. Pengine yupo kuhudhuria.”
Alvin alikasirika. Sio tu kwamba Lisa hakumwomba msamaha, hata alienda kuhudhuria maonyesho ya sanaa nje ya nchi bila kumuaga? Vizuri. Vizuri sana, Lisa Jones.
"Sawa, ulijuaje kwamba alienda huko?" Alvin aliuliza kwa ukali ghafla. “Nilimtumia ujumbe wa WhatsApp. Yeye...”
“Unayo WhatsApp yake?” Alvin alimkazia macho Hans. "Na ulizungumza naye kwa faragha?" Hans alishuka. “Kama msaidizi wako, niliongeza WhatsApp ya Bi Jones kwa manufaa yako. Kwa mfano,

unapokasirika, naweza kumwomba akufariji.”
“Lakini sijafarijiwa naye kwa sasa.” Alvin alikoroma kwa ukali. "Je, alikuambia kwamba anaenda Johannesburg?"
"Alitaja, lakini mimi ..."
“Najua. Alitaka kunieleza kuhusu jambo hili kwa kutumia mdomo wako.” Alvin alicheka kwa kujifariji. “Anafikiri ningekuwa na wasiwasi akiondoka Nairobi. Anaweza kuendelea kuota.”
Hans alikosa la kusema.
 Alishuku kuwa Alvin alikuwa akiwaza sana.
“Nikatie tiketi ya ndege sasa hivi. Ninaenda Johannesburg usiku wa leo.” Alvin aliamuru ghafla.
"Utaenda ... kumfuata Bi Jones?" Hans alipigwa na butwaa na kushtushwa na

maamuzi yake ya ghafla.
"Bila shaka hapana. Nitaenda kununua baadhi ya kazi za sanaa, inaelekea Lisa anapenda sanaa. ” Alvin alinyanyuka na kufungasha vitu vyake.
Hans alitamani kulia. Tayari muda ulikuwa umekwenda sana, hata hivyo ilimbidi aandamane na Alvin hadi Johannesburg. Kihelehele chake kilimponza. Kuwa msaidizi wabosi kama Alvin kulichosha sana.
•••
Usiku, Lisa alifikia katika hoteli ya nyota nne huko Johannesburg.
Kwa kuwa kulikuwa na watu wengi sana waliofika kutoka kote ulimwenguni kuhudhuria maonyesho hayo, hoteli nyingi nzuri zilichukuliwa mapema, kwa hivyo hiyo ndiyo ilikuwa hoteli bora zaidi ambayo angeweza kupata.
Baada ya kuoga alitoka kwenda kulala.

Ghafla aliamshwa na milango ikigongwa kwenye chumba kilichofuata.
"Hawa watu wana wazimu? Kwanini wanagonga mlango kwa nguvu namna hii?” Lisa alifoka moyoni.
Chini ya dakika kumi baadaye, kulikuwa na muziki wa mdundo mzito wa ‘amapiano’ kwenye chumba hicho. Kulikuwa na kelele kiasi kwamba hakuweza kulala. Hakuweza kujizuia na kupiga simu mapokezi kulalamika.
Dakika tano baadaye, mhudumu wa mapokezi alimpigia simu na kumjibu. "Samahani bibiye. Wafanyikazi wetu walienda kumtafuta bwana huyo wa chumba jirani, lakini alisema kuwa muziki wake hauzidi decibel 50, ambacho ni kiwango kinachokubalika kisichoweza kusababisha kero. Hata polisi hawawezi kufanya lolote kuhusu hilo.”

"Inawezekanaje kuwa ni kiwango cha kawaida kwa kelele zote hizo?" Lisa alikasirika. “Sauti iko juu sana. Lazima iwe zaidi ya decibel 50."
“Tumepima. Ni decibel 49 tu."
Lisa alikosa la kusema. Jamani. Alikuwa akimfanyia makusudi au? Ni lazima awe mtu aliyeijua sheria vizuri.
"Unaweza kunibadilishia chumba changu?" Lisa aliomba.
"Samahani, hatuna vyumba vingine vilivyobaki."
Lisa aliumwa na kichwa. Alichoweza kufanya tu ni kuingiza tishu kwenye masikio yake kujaribu kupunguza sauti kuingia masikioni mwake. Mwishowe, hakuweza kulala vizuri usiku na aliendelea kuota ndoto mbaya.

Siku iliyofuata, aliamka mapema na kujipodoa vizuri kabla ya kuelekea kwenye maonyesho ya sanaa. Baada ya kuangaza sana kwenye umati mkubwa wa watu, hatimaye akamwona bwana Kawada. Alikuwa mtu wa miaka arobaini, lakini alionekana kijana
sana. Wakati huo, Bwana Kawada alikuwa akitazama picha kubwa ya michoro ya mtindo wa Tingatinga. Wajapani wanaipenda sana michoro hiyo.
Muuzaji alisema, “Hii ni michoro maarufu ya Tingatinga, na ni mkono halisi wa Said Tingatinga, mwanzilishi wa mtindo huo wa michoro. Ni hazina kubwa kabisa. Sikuiuza hata wakati mtu alitoa milioni 4 mara ya mwisho.”
"Naweza kuangalia kwa karibu?" Lisa akasogea na kuuliza huku akitabasamu. Bwana Kawada

akamkabidhi ile picha kubwa na kutabasamu.
"Je, mwanamke huyu anajua jinsi ya kutathmini kazi za sanaa?" Muuzaji aliuliza kwa wasiwasi.
"Najua kidogo." Lisa aliitazama na kutikisa kichwa. "Hii ni bandia."
"Haya, usizungumze ujinga." Muuzaji alimtazama kwa hasira. "Hujui chochote, msichana mjinga wewe."
Lisa aliashiria motifu ya joka kubwa na kusema, “Ikiwa ni mchoro halisi wa mwanzilishi wa mtindo wa tingatinga, ilipaswa kuwa imechorwa mwanzoni mwa miaka ya sitini kwani yeye alifariki mwaka 1965 au 1966 hivi kama sikosei. Ukitazama saini yake hapa inaonyesha picha hii imechorwa mwaka 1971. Ni mwigo mzuri lakini siyo kazi original ya Said Tingatinga. Natoa elfu mbili.”

Uso wa muuzaji ulikuwa mwekundu kwa aibu kwa madai ya Lisa.
Bwana Kawada alimkazia macho. “Ulitumia kazi bandia kunitapeli. Unafikiri mimi ni rahisi kudanganya kwa sababu mimi ni Mjapani?”
"Sio. Hata mimi sijui historia ya kweli ya Tingatinga.” Muuzaji alinyanyuka na picha mikononi mwake kwa aibu.
Sura ya: 439
“Asante, Bibi.” Bwana Kawada akatabasamu. "Unaonekana si mgeni kwenye macho yangu, nilishawahi kukuona wapi?"
"Watu wengi wanasema kwamba wamewahi kuniona mahali, ila wengi wao ni kwenye vyombo vya habari." Lisa aligeuka na kumjibu Kawada.

“Subiri, nakukumbuka sasa. Wewe ni mrithi wa Ngosha Corporation. Jina lako la mwisho ni... Jones...” Kawada alisema kwa haraka. "Baba yako ni Joel Ngosha, sawa?"
“Maelezo sahihi kabisa. Umekuwa ukitufiatilia kabla8? ” Lisa alipunga mkono kwa mshangao.
“Niliwahi kukutana na baba yako.” Kawada alicheka na kumkabidhi kadi yake ya biashara.
Lisa aliisoma na mara moja akampa mkono. “Halo Bwana Kawada. Mimi kwa kweli ni shabiki wa picha za kubuni pia. Niliruka hapa kwa siri ili nifurahie kazi hizi za sanaa kwa sababu sikutaka wengine wanitambue.”
"Naelewa. Daima kuna watu ambao watataka kujipendekeza kwa faida zao

wenyewe. Ni shida sana.” Kawada akacheka. "Ni bahati kwamba tumeweza kukutana wote tukiwa na hobi zinazofanana. Angalia kipande hicho."
“Hakika.” Lisa alimfuata, na saa moja ikapita wakishangaa kazi mbalimbali za sanaa za michoro. Wawili hao walizungumza mambo mengi.
Ilipofika wakati wa chakula cha mchana, Kawada alisema, “Kwa kweli, siku zote nimekuwa nikifurahia maendeleo ya Kampuni ya Ngosha katika eneo la vifaa. Kwa kuwa wewe ni mrithi wa Ngosha Corporation, unapanga kuchukua lini kampuni hiyo?”
“Si rahisi hivyo kuchukua madaraka. Lisa alitabasamu kwa uchungu. “Kwa sasa maendeleo ya Ngosha Corporation ni mazuri sana, na bei ya hisa pia ilipanda, lakini usimamizi wa ndani wa

kampuni ni mgumu. Kuna watu wengi wanaotamani nafasi yangu.”
“Hiyo ni kweli." Macho ya Kawada yalimtoka. “Lakini huwezi kuachia nafasi hii kirahisi. Ni kazi ngumu ya baba yako.”
“Baba yangu hana afya nzuri na anataka niiongoze kampuni, lakini bado nina kampuni nyingine. Sina nguvu nyingi hivyo. Ninaweza kuishia kuuza hisa zangu. ” Lisa alichomokea. “Lakini ninaogopa baba yangu hatakubali, na babu yangu anaweza kukasirika pia. Lakini kwa vyovyote vile, jina langu la mwisho ni Jones, kwa hivyo sijali kuhusu hilo sana.”
Kawada alitoa kikohozi kirefu. "Hiyo ni kweli. Bado wewe ni mdogo sana, na hao Uncle na babu yako ni wazee na wajanja, kwa hivyo inaweza kuwa bora kuziuza. Msichana lazima aolewe

hatimaye."
“Ni kweli. Wakati fulani huwa nataka kupata mpenzi, lakini nina shughuli nyingi sana. Ninachotaka sasa ni kuolewa kwa furaha sasa... " Lisa alipomaliza kusema, ghafla alionekana kusikia sauti ya kitu kikivunjika kutoka kwa jirani. Aliganda!
Wakati huo, Kawada alisema kwa sauti ya chini, “Nitakuwa mkweli. Kwa kweli ninavutiwa sana na biashara ya usafirishaji. Kwa nini usiniuzie hisa? Unaweza kutaja bei."
“Huu?” Lisa alishtuka na kutazama huku na huko kwa fujo. “Hilo...Hilo halitawezekana. Ikiwa babu yangu atagundua ... "
“Nilisikia kuwa babu yako alirudi Ngosha Corporation. Nadhani hataachilia cheo chake kwa muda.” Kawada alisema kwa

kumaanisha, “Wewe pia hukupata malezi ya babu yako. Si rahisi kwa yeye kuwa upande wako."
“Umeyajuaje hayo na wewe ni mgeni?” Lisa alishangaa.
“Kama nilivyokuambia, nimevutiwa na kampuni hiyo muda mrefu kwa hiyo nilikuwa nikiifuatilia chinichini. Ukiwa tayari kuniuzia hisa, ninaweza nikabadilisha mambo ndani ya kampuni.”
Lisa alipigwa na butwaa na kusema. "Ningeiuza kwa dola milioni 60..."
“Milioni 60?” Kawada alishtuka. Hiyo ilikuwa bei ya juu kabisa. “Nakumbuka thamani ya soko ya kampuni ya Ngosha ni chini ya milioni tu. Ninaogopa hakuna mtu atakayeinunua ikiwa utaiuza kwa milioni 60, lakini nitakuwa tayari kuinunua ikiwa unaweza kuiacha kwa

milioni 45.
Tazama, kuna kampuni nyingi sana za usafirishaji siku hizi...” Kisha, Kawada bila kukoma akajaribu kumshawishi Lisa.
Lisa alijifanya kusikiliza na kupendezwa zaidi na hatimaye akakubali kuuza hisa za Ngosha Corporation kwa dola milioni 50.
Kawada alifurahi sana. “Basi tusaini mkataba usiku. Hakuna wakati kama wa sasa. ”
Aliogopa msichana huyu mdogo angegeuka nyuma na kumwambia baba yake, na Joel angekataa. Baada ya yote, Ngosha Corporation ilikuwa kampuni kubwa zaidi ya usafirishaji wa barabarani nchini Kenya, na walikuwa wakipanuka sana katika usafiri wa anga na majini pia. Alikuwa akitaka kununua Ngosha Corporation kwa muda mrefu.

“Sawa, basi tutakutana usiku wa leo. Nahitaji sekretari aandae mkataba. Lakini usimwambie mtu yeyote kuhusu hilo. Naogopa kuzomewa na baba yangu. Tutaenda kwenye kampuni baada ya siku chache kuhamisha hisa.” Lisa alisema kwa wasiwasi.
"Hakika, hakika. Imetulia basi.” Kawada akampa mkono na kuondoka zake kwa furaha. Alipotoka tu, Lisa alitabasamu. Kuuza 40% ya hisa za Shirika la Ngosha kwa milioni 50. Sio mbaya. Baada ya Kawada kuingia kwenye kampuni ya Ngosha, hakika ingezua dhoruba. Damien, Melanie, na Jerome bila shaka wangepandwa wazimu.

“Mhudumu, ningependa kikombe kingine cha kahawa...” Lisa aligeuza kichwa chake na papo hapo alipigwa na butwaa alipomwona mtu mrefu mwenye sura ya kutawala akiwa amesimama

kando ya mlango. Alvin Kimaro. Kwa nini alikuwa hapa? Macho yake meusi yalikuwa wazi.
"Njoo nje." Alvin akauma meno yake na kumtazama kwa ukali, moja kwa moja akamtoa nje.
Alikuwa akimfuatilia tangu asubuhi na kumwangalia mara kwa mara akiandamana kutizama na kununua kazi za sanaa na mwanamume wa makamo wa Kijapani, na hatimaye akaanzisha mazungumzo naye. Kisha, walizungumza na kucheka wakati wa chakula cha mchana.
Mwanzoni alikasirika, lakini moyo wake ulizidi kuwa mgumu zaidi na zaidi alipoenda kwenye chumba kilichokuwa karibu na chao.
Mwanamke huyu alikuwa anazidi kutoka nje ya mstari. Alimkaribia mwanamume yule bila kupepesa kope na hata

kumchezea kiganja cha mikono yake.
Walipotoka nje ya hoteli, Alvin alimuuliza. “Ulikuja huku kufanya nini?”
“Na wewe umekuja kufanya nini?” Lisa alirudisha swali mahali lilikotoka.
"Nimekuwa nikikufuatilia tangu ulipoondoka jana," Alvin alisema kwa huzuni.
Lisa alipigwa na butwaa lakini kwa haraka akajibu kwa sauti kali. "Wewe ndiye ulikuwa ukipiga muziki mkubwa kama mwendawazimu jirani na chumba changu usiku wa kuamkia jana?"
"Unamwita nani mwendawazimu?" Uso mzuri wa Alvin ukawa mweusi.
“Ni kweli ulikuwa wewe?” Lisa alishangaa. “Alvin una kichaa? Sikuweza kulala hata kidogo kwa

sababu ya kelele.”
“Tuko kwenye mashua moja. Ulinitesa hadi nikakosa kulala, kwa hiyo usifikiri hata kupata usingizi.” Alvin alikoroma kwa ujeuri. Alikuwa na siku mbili bila usingizi kwa sababu yake.
Lisa alikosa la kusema. "Haukuwa unakunywa pombe kwenye hicho kweli?" Alitazama mikono yake, ambapo kulikuwa na makovu na alama za damu, na akakumbuka kwamba alisikia kitu kilivunjwa mapema.
Alvin alisema kwa huzuni, “Hapo awali nilitaka kuona kama ungenifanyia kitu fulani na Kawada, lakini niliishia kusikia kwamba unataka kupata mpenzi wa kukuoa kwa furaha. Kumbe mimi sio mpenzi wako bado. Kwa hivyo, mpenzi wako ni nani? Yule jamaa uliyekwenda kunywa naye baa usiku?”

Lisa alicheka huku midomo yake ikitetemeka. Hatimaye aliona jinsi akili za Alvin zilivyokuwa hazimtoshi. "Nilisema hivyo kwa makusudi ili kumpumbaza."
"LisaJones, unapanga nini?" Mtazamo wa Alvin haukuwa wa kawaida. “Unauza hisa za Ngosha Corporation kwa siri. Baba yako anajua?"
Sura ya: 440
Ngosha Corporation ilikuwa kampuni kubwa zaidi ya usafirishaji nchini Kenya na imekuwa ikiendelea kwa kasi katika biashara ya usafirishaji mtandaoni hasa katika miaka ya hivi majuzi. Watu wengi walikuwa wakikimezea kipande hicho cha nyama chenye kunona, lakini Lisa alikitoa kwa urahisi.
"Ndio, nilimshawishi aiuze." Lisa alishtuka kwa utulivu. "Kuna ugomvi wa ndani katika Kampuni ya Ngosha, babu

yangu bado ana hamu kubwa katika uzee wake, Damien na binti yake wanatutazama kwa tamaa, na wanahisa wamefumbwa macho kwa ukungu wa Damien na Melanie. Ni bora kuziuza zote tu.
“Delta Co. Ltd. ni kampuni kubwa nchini Japani. Baada ya Rais Kawada kuingia Ngosha Corporation, hakika atafikiria kugombea madaraka na babu na Anko zangu. Itakuwa ya kuvutia sana kutazama wakati huo."
Alvin alikosa la kusema. Akiiwazia sura ya Mzee Ngosha pengine angetaka kutapika damu kwa hasira. Mababu wa familia ya Ngosha wangepanda kutoka kaburini ikiwa wangejua juu yake. Kampuni hiyo ilikuwa juhudi kubwa za familia ya Ngosha kwa vizazi, lakini aliiuza kama hivyo, na kwa mtu kutoka Japani.

“Wewe ni kweli...”
Lisa alimkatisha. “Kuna jambo moja zaidi. Ninahisi kama ubia na Campos Corporation kwa wakati huu ni
mtego. Bwana Kawada pia ana ufahamu mkubwa katika masuala ya fedha. Atakapojiunga, atavuruga azma ya Jerome ya kuwa familia bora zaidi nchini. ”
"Mwishowe, unajaribu kunisaidia?" Macho ya Alvin ghafla yakaangaza.

"Unafikiria sana." Lisa alijihisi jasho na kutema mate, akasonga mbele.
Hata hivyo, baada ya kupiga hatua chache tu, mkono wake ukashikwa na Alvin na kuvutwa kwenye mikono yake. Akamtazama kwa jicho la huzuni na kero.
“Lisa Jones, kweli unataka kuachana na

mimi? Nimekuwa nikisubiri uniombe msamaha, lakini kimya!”
"Samahani, lakini sina nia ya kuomba msamaha," Lisa alisema kwa upole. “Wewe...” Macho ya Alvin yalimkodolea. Ikiwa sura inaweza kuua, angekuwa amekufa mara nyingi tayari. Tayari alikuwa amemfuata hadi huko. Kwanini hakuweza kuinamisha kichwa chake? Je, angekufa akiomba msamaha?
“Kwa hiyo unataka kuachana na mimi?” Alvin alishusha pumzi kwa nguvu. "Ulinizunguka usiku na mwanaume mwingine na kunywa pombe kwenye baa na kufanya kashfa, lakini siwezi kusema chochote juu yake? Hufikirii kuwa wewe ni mwingi sana?”
Lisa alimtazama. Hakuna aliyemuelewa zaidi yake. Hasira yake ilikuwa karibu kufikia kikomo. “Sijaribu kuachana na wewe. Nilisema nina mambo ya

kushughulikia, ambayo ninafanya. Nani alisema kuwa watu hawawezi kuzungumza kwenye baa? Isitoshe, je, picha hiyo ilinionyesha nikimbusu au nikimkumbatia mwanaume mwingine?”
"Kwa vyovyote vile, ni ukweli usiopingika kwamba ulinizunguka na mwanaume mwingine." Sauti ya Alvin ilipungua kidogo alipoelezea, lakini uso wake bado ulikuwa wa hasira ngumu. "Naweza kukusamehe wakati huu, lakini ... usirudie tena." Alisema kwa ukali na sauti hiyo ilifanya ionekane kama Lisa alikuwa akimwomba msamaha.
Lisa alikataa unyonge. “Kwanini nikusikilize? Mbona wewe huwa unakutana na Sarah hata kama nikikuzuia?”
Alvin alinyamaza kwa muda na kusema, "Sitakutana naye sana katika siku zijazo."

“Kweli?" Lisa alidanganya tabasamu.
“Kwa nini nikudanganye?” Alvin alikoroma kwa sauti ya hali ya juu. "Sahau. Kwa kuwa una mtazamo mzuri na umekubali kosa lako, nitaacha jambo hili lipite.”
Lisa alicheka tu kwa mshangao. Alikuwa na mtazamo mzuri na alikubali kosa lake? Tangu lini alikubali makosa yake?
“Mbona unanitazama hivyo?” Alvin alishindwa kujizuia kumkodolea macho. “Lisa, nimekuwa nikifanya maelewano mara kwa mara kwa ajili yako. Hakuna mwanamke aliyethubutu kunichokoza hivi kabla.”
“Nimekuchokoza vipi? sikufanya lolote.” Lisaalimkazia macho. "Nipishe. Narudi hotelini kupumzika. Jua ni kali sana.”

“Usiende kwenye hiyo hoteli uliyokwenda jana. Ni nafuu sana.” Alvin alimpeleka Lisa kwenye gari. "Nina chumba cha kibinafsi cha hadhi ya Rais katika hoteli ya nyota tano hapa."
Lisa alishangaa. "Uliwekeza lini kwenye hoteli?"
“Nimekuwa nikiwekeza katika majiji mengi. Utagundua polepole katika siku zijazo.” Alvin alipapasa ncha ya pua yake. "Unahitaji kujua kuwa hakuna mwanaume katika Kenya yote anayeweza kulinganishwa na mimi."
Akijua kwamba alikuwa akijaribu kumaanisha jambo fulani tena, Lisa alijifanya kuwa haelewi maneno
yake. Mara walipofika kwenye chumba cha kifahari cha hoteli hiyo, ghafla alibebwa kabla hata hajatazama huku na kule.

“Alvin...” Alimzungushia mikono yake shingoni. Kuangalia ndani ya macho ya mtu anayewaka, alikuwa na hisia ya kuzama. “Unapanga kufanya nini mchana kweupe...”
“Siyo kana kwamba hatujawahi kufanya mchana.” Alvin mara moja akamweka kitandani na kuweka mikono yake pande zote mbili. Aliongeza kwa sauti ya huzuni, "Umekuwa ukinipa wakati mgumu kwa usiku tatu zilizopita."
"Hebu tuzungumze kuhusu usiku wa leo, sawa? Amba atatua hapa muda si mrefu, nimemwambia alete mkataba, na nitakutana na Bwana Kawada usiku wa leo kusaini makubaliano.”
Lisa alijaribu kuusukuma mwili wake uliokuwa na misuli, lakini hakusogea hata kidogo.
"Amba anapanda ndege hapa, kwa

hivyo itamchukua muda. Bado tuna muda wa kufanya hivyo.” Alvin alipomaliza kuongea tu, alimbeba na kumbusu kwa mahaba ili kumzuia asizungumze.
•••
Katika ukumbi wa chakula wa hoteli usiku.
Baada ya kusubiri kwa muda mrefu, hatimaye Bwana Kawada alimuona Lisa ambaye alikuwa amechelewa. Alishusha pumzi ya raha kisha akasema kwa tabasamu, “Nilifikiri umeghairi na ukaamua kutokuja.”
"Nilikuwa nikiufanyia kazi mkataba wetu. ” Lisa alijitahidi kadri ya uwezo wake kujiweka sawa na kuketi. Moyoni alikuwa akimlaani Alvin kwa kumcelewesha. Alvin ndiye aliyesema kwamba wangeweza kumaliza kwa wakati. Mwishowe, alimfanya Amba

asubiri nje kwa zaidi ya saa moja kabla ya kufungua mlango. Alikuwa ameona aibu kabisa.
Baada ya kusaini makubaliano hayo, Lisa alishiriki mazungumzo madogo na Bwana Kawada kabla ya kufanya utaratibu wa kuchukua ndege ya usiku kurejea Nairobi.
Lisa alipokaribia kukata tiketi ya ndege ili arudi, Alvin alinyakua simu yake. “Hakuna haja ya kuharakisha kurudi. Tunaweza kukaa hapa na kufurahia kwa muda."
Afrika Kusini ilikuwa na historia ndefu na vivutio kadhaa. Lisa alipigwa na butwaa. Muda mfupi baadaye, alitikisa kichwa. “Hakika. Hatujawahi kwenda safari pamoja.”
“Nitakupeleka nje mara nyingi zaidi siku zijazo," Alvin alijibu kwa upole huku

akiwa amembeba.
Siku iliyofuata, Alvin alimpeleka hadi kwenye mbuda za wanyama za Transvaal. Baada ya kuegesha gari, wawili hao walianza kutembea hadi Transvaal Park. Wakiwa katikati ya matembezi yao, Lisa alichoka sana hivi kwamba aliendelea kumsumbua Alvin ambebe.Kwa kuwaona wageni waliokuwa wakienda na kutoka karibu nao, Alvin alijisikia vibaya.
“Wewe tayari ni mtu mzima lakini unategemea nikubebe?”
“Sijisikii vizuri. Nataka unibebe.” Lisa alipiga kelele kwa hasira kama mtoto.
Tabia yake ilimfanya Alvin awe mtu wa kuchanganyikiwa. Hakuweza kumwambia hapana, hakuwa na jinsi zaidi ya kumbeba mgongoni. Wakati wa matembezi yao, watu wengi

waliwatazama kwa sura ya kupendeza.
“Angalia jinsi mumewe alivyo mzuri. Anambeba mkewe kwa mapenzi mazito.”
"Zaidi ya yote, yeye ni mzuri."
Ndani ya sekunde chache, watu wengi walikuwa wamepiga picha kwa siri za Alvin na Lisa, kuzisambaza mtandaoni. Katika siku hizi ambapo mtandao ni teknolojia inayokua kwa kasi, watumiaji wa mtandao nchini Kenya waligundua kwamba Lisa na Alvin walikuwa kwenye safari pamoja.
TUKUTANE KURASA 441-445
ONYO: Ni marufuku kusambaza, kukopi wala kuuza kazi hii kwani endapo kama

tutakubaini basi sheria itachukua mkondo wake (By: Official Dully)
 
LISA KITABU CHA NANE (9) SIMULIZI........................LISA KURASA.................441 - 445
PRESENT: SIMULIZI ZA DULLY

Sura ya: 441
Maono ya wanamtandao yalikuwa mengi.
[Je, kuna kitu kibaya na kumbukumbu yangu? Bwana Kimaro hakufunga ndoa na Sarah hivi majuzi?]
[Hawakuoana mwishowe. Nilisikia polisi walimchukua Sarah wakati wa harusi. Kulingana na mtu wa ndani, Sarah alionekana kumkosea Bwana Kimaro.]
[Kwa hiyo Mkubwa Alvin Kimaro anarudiana na mke wake wa zamani? Kwa njia fulani, ninamwona Bwana Kimaro kama mkorofi kabisa.]
[Bi. Jones ana nini na Bwana Kimaro? Baada ya yote, sio tu kwamba yeye ni mrithi wa kike wa mojawapo ya familia tajiri zaidi nchini Kenya, lakini pia ndiye tajiri mkuu wa kike nchini. Je, hakuna wanaume wengine duniani mpaka arudi

kwa Alvin?]
[Bwana Kimaro kweli ni mzuri na tajiri. Nadhani hakuna mwanamke anayeweza kumpinga.]
[Kwanini ninahisi kuwa Bwana Kimaro anampenda zaidi Lisa? Kwa jinsi anavyombeba, anaonekana kumdekeza sana.]
[Nafikiri hivyo pia. Wakati Bwana Kimaro alipokuwa kwenye uhusiano na Sarah hapo awali, ilikuwa nadra kumpata akifanya naye shopping, sembuse kumbeba.]
Sarah, ambaye alikuwa mbali katika jumba lake la kifahari, alipandwa na hasira alipoona maoni ya wanamtandao hao. Kwa kweli, walikuwa sahihi. Ingawa alikuwa amekaa pamoja na Alvin kwa zaidi ya miaka kumi, Alvin hakuwahi kwenda naye safarini,

sembuse kumbeba mgongoni.
Dokezo la chuki likaangaza kwenye macho yake yenye huzuni. Mara moja alimpigia simu mtu...
•••
Jijini Johannesburg katikati ya mlima usiku.
Katika jumba la mbao la kitalii, Lisa alilala kitandani huku akisoma maoni ya wanamtandao. Alvin alimtazama kimya kimya baada ya kutoka kuoga..
“Babe, unatazama nini?” Alvin akamsogelea. Alipozitazama habari zake kwenye simu yake, aibu ilienea katika uso wake mzuri mara moja.
"Angalia jinsi maoni ya watumiaji wa mtandao yanavyovutia." Lisa alinyoosha kidole kwenye maoni yaliyomvutia zaidi na kusema, "Kila mtu anasema kwamba wewe ni mwaminifu kwa sababu

hurukiruki hovyo na wanawake. Una mimi na Sarah tu. Unapochagua kuachana na Sarah, unaweza kuwa nami, na kinyume chake. Hutafuti wanawake wengine kamwe."
Huku akiwa na uso wa kusitasita, Alvin akaitupa pembeni simu ya Lisa. “Imekufurahisha?”
“Ndio. Huoni kuwa ina maana?” Lisa aliinua kichwa chake na kumkazia macho huku akitabasamu.
Alipomuona Lisa akimcheka bila huruma, Alvin alihisi hisia kali ndani yake na kukunja uso. Alimshika uso na kumbusu kwa mapenzi hadi wawili hao wakaanguka kitandani tena.
Lisa akamzuia. "Unafanya nini? Hii haina mwisho, kama jana. Ni kana kwamba hujawahi kulala na wanawake wengine kwa miaka kadhaa.”

Alvin aliuma meno kwa siri. Alikuwa sahihi, lakini hakuweza kukubali kwa kuzingatia utu wake. Kwa hivyo, hakuwa na chaguo ila kunung'unika, "Siwezi kupinga hirizi zako."
"Nilidhani utasema kuwa haujawahi kulala na wanawake wengine." Huku kidole kikitembea kifuani mwake, Lisa aliweza kuhisi waziwazi kwamba mwili wake ulikuwa umeganda kwa maneno yake.
Alvin aliinamisha kichwa na kukaa kimya. Alichokuwa akitaka ni kuendelea kumbusu. Lakini, Lisa alifunika mdomo wake na kuanza kuonekana kuwa mbaya. “Kwa kuwa unakataa kunijibu, ina maana kwamba umelala na Sarah sana katika miaka ya mapenzi yenu, sivyo? Huenda nyinyi mlilala pamoja mara moja kwa siku au mara moja kwa wiki—”

“Lisa Jones...” Alvin alimkatisha Lisa huku akiwa ameuma meno. Uso wake mzuri ulijaa aibu. "Acha kutuunganisha mimi na Sarah, sawa?"
“Hapana, nasisitiza kujua kuhusu hilo.” Lisa akaizungushia mikono yake shingoni. "Je, mimi ni mtamu zaidi, au au yeye ndiye mtamu zaidi? Usiponipa jibu leo hutasikia mwisho wake kutoka kwangu.”
Alvin kichwa kilimuuma. Japokuwa alihisi kupandwa na hasira, mwanamke huyo alionekana kupendeza sana hata alipokuwa akimtania. Angewezaje kuwa mkali naye?
"Je, ni vigumu kujibu? Ukikaa kimya jibu lake litakuwa umelala na Sarah sana.” Alijifanya kuwa na hasira na kumsukuma mbali. Kisha, akasimama na kutaka kuondoka.

Akiwa katika hali ya woga, Alvin alimkumbatia kwa kasi kwa nyuma. “Babe, nitakujibu, sawa? Kwa kweli... Kwa kweli, sijawahi kufanya hivyo na Sarah.”
Lisa aliganda. Aligeuka na kumtazama kwa kutoamini. “Acha kunidanganya. Kwa kuwa ulimpenda sana hapo awali, ungeachaje kufanya naye? Alvin, huu ni uwongo mtupu.”
"Sisemi uwongo." Alvin akatoa kicheko cha uchungu. "Kila nilipojaribu kulala naye, tumbo langu lilivurugika kabisa. Nimetapika hata mara chache. Nilipokuja kukutafuta wewe, sikuwa na tatizo lolote. Ukweli ni kwamba Sarah alijaribu kunifanyia kitu lakini alishindwa. Niliishia kutapika.”
Lisa alipigwa na butwaa. Alikuwa tu akitaka kudhibitisha hilo kwa sauti yake.

Hakutarajia kile Maya alisema kuwa kweli.
"Uliniona nikitembelea kitengo cha andrology kabla ya hii, sivyo?" Alvin alimshika mkono akiwa hoi. "Nilidhani kulikuwa na shida kwangu, lakini nilipokuwa na wewe baadaye ... niliweza kufanya kazi kama kawaida. Nilifikiri nisingeweza kushughulika na Sarah tu, kwa hiyo nilijaribu na wanawake wengine wachache. Mwishowe, walinifanya nihisi kutapika.”
"Ulijaribu hata na wanawake wengine ...?" Lisa alikodoa macho.
“Nilifanya hivyo kwa ajili ya kuelewa hali yangu. Lakini, sikuwahi kupanga kuifanya nao. Usinielewe vibaya. Kwa kweli, maisha yangu ya kibinafsi ni ya heshima sana, "Alvin alielezea haraka.
“Lakini kwanini hukunijulisha mapema?”

Lisa alishtuka kutoka kwenye mshiko wake. "Uliamua kuwa nami kwa sababu tu ninaweza kukidhi mahitaji yako, huh?"
“Hii ndiyo sababu hasa sikukuambia. Niliogopa ungekuwa na wazo kama hilo." Alvin alisema kwa upole, “Nataka kuwa nawe kwa sababu tu nakupenda. Ninahisi kama nyumbani ninapokuwa na wewe. Ninapokuwa peke yangu, huwa nafikiria juu yako. Hata wakati wa mikutano, siwezi kujizuia kuangalia simu yangu mara kwa mara. Ninaogopa unaweza kuwa umenitumia ujumbe nikachelewa kujibu. Sijawahi kubadilika kwa sababu ya mtu yeyote. Ikiwa sio upendo, hii ni nini?"
Moyo wa Lisa ulimshtuka..
Alvin aligeuza uso wake kwa upole na kumbusu kwa upendo. “Lisa, acha kuwaza kupita kiasi, sawa? Hakuna

shaka kwamba ninakupenda.”
"Kwa hiyo, Sarah alienda hospitalini kupandikizwa ujauzito hivi majuzi. Ulifanya-"
"Hapana. Niliandamana naye mara mbili tu kwa uchunguzi wa afya. Sikuidhinisha. Sitaki anizalie mtoto,” Alvin alijibu bila kufafanua.
Lisa kisha akamkumbatia bila kusema kitu kingine chochote.
Vivyo hivyo, wangeendelea kukaa pamoja kwa muda mrefu kadri walivyoweza. Ingawa alikuwa na ajenda ya siri, alifikiria kuiweka kando hadi muda fulani baadaye.
Muda huo simu ya Alvin iliita ghafla. Hakupokea simu. Simu iliita bila kukoma hadi akainuka bila kupenda na kujibu kwa jazba. "Rodney Shangwe, unauliza kifo?"

“Wewe ndio unaomba kifo Alvin. Kwa kweli uko katika hali ya kufanya safari ya kufurahi na Lisa wakati Sarah yuko taabani!” Rodney alinguruma, “Sarah ametekwa nyara! ”
Macho mekundu ya Alvin yalitiwa giza. "Nini kimetokea?"
Sura ya: 442
Rodney alisema kwa hasira, “Sarah alipotea mchana huu alipotoka kununua kitu. Sikuweza hata kuwasiliana naye. Ni wakati tu nilipomuuliza mlinzi wa nyumba ndipo nilipopata habari kwamba hakuwa amerudi nyumbani tangu alipondoka. Nilikagua kamera za uchunguzi na nikagundua kuwa mtu fulani alimshika na kumziba mdomo wake na kumwingiza ndani ya gari alipokuwa kwenye maegesho ya magari ya duka moja.

“Rudi sasa hivi! Sasa kwa kuwa umemtupa, huenda asiweze kuishi ikiwa kundi hili la watu waliomteka watakuwa ni wauaji.”
“Narudi sasa hivi.” Alvin akasimama.
Lisa alimkumbatia kwa nyuma na kumtazama kwa mbwembwe. "Alvin, utaniacha peke yangu?"
"Tunaweza kwenda pamoja," Alvin alinong'ona.
“Lakini sitaki kuingilia mambo ya Sarah. Acha tu Rodney na Chester wamuokoe,” Lisa alijibu kwa sauti ya chini. Maneno yale yalimfanya Alvin kuangaza macho yake kwa huzuni.
Baadaye, sauti ya Rodney ilisikika kutoka kwenye simu kwani simu haikukatika. “Lisa Jones, wewe ni

mwanamke katili sana! Sarah ametekwa nyara na watekaji nyara wanaweza kumuua. Kwa wakati kama huo, bado unahisi wivu! Je, huna huruma hata kidogo? Kwanini Alvin aliangukia kwa mwanamke kama wewe?"
“Rodney!” Alvin alikata simu bila kumruhusu Rodney kuendelea. Aligeuka na kumwambia Lisa kwa sauti ya ukali, *Kama hutaki kuondoka nami, unaweza kukaa hapa. Nitamwambia Shani akuijie kesho au hata mtakaa naye hapa kwa siku chache.”
“Hukumpeleka Shani nje ya nchi?”
"Nitamwambiaa arudi sasa hivi." Kwa hayo, Alvin alivaa nguo zake haraka na kuchukua simu yake.
Alipofungua mlango, upepo wa mlimani ulivuma usiku huo wenye baridi kali. Alvin alikuwa tayari alikuwa ameondoka.

Huku mikono yake ikizunguka magotini, Lisa alitoa tabasamu hafifu.
Hapo awali, alishtuka aliposikia maneno yake matamu. Hakutarajia kofi la usoni muda mfupi baadaye. Halikuwa jambo baya, baada ya yote. Angalau, alikuwa akijifunza kutoguswa kwa urahisi na maneno yake.
Ilibidi amshukuru Sarah kwa hilo.
Safari yake na Alvin ilifanya habari wakati wa mchana, na Sarah alitekwa nyara usiku. Ni bahati mbaya iliyoje. Ni lazima ulikuwa mpango wake mwingine mpya. Labda ilihusiana na watu wale waliokodiwa kutoka Somalia.
Lisa alijaribu kumpigia simu Logan, lakini hakuweza kumpata. Kwa namna fulani, alihisi kana kwamba kivuli cheusi kilikuwa kimemtupa. Ilikuwa ni kama anga la usiku nje.

Haraka akakurupuka na kumtafuta mmiliki wa nyumba ile ya kitalii. “Bwana, unaweza kumwomba mtu anishushe mlimani mara moja? Nina jambo la dharura la kushughulikia.”
“Mh? Tuna uhaba wa wafanyakazi nyakati za usiku. Kwanini hukwenda na mpenzi wako? Umemwacha aondoke peke yake na wewe unataka uondoke peke yako.” Mmiliki alipiga miayo. “Nikukumbushe barabara za hapa zinapinda. Si rahisi kusafiri katikati ya usiku.”
“Kwa kweli nina jambo la dharura la kushughulikia. Tafadhali nipatie dereva mzuri. Niko tayari kulipa kiasi chochote.” 6:00 asubuhi.
••• Nairobi.

Alvin aliingia kwenye jumba lake la zamani chini ya jua la asubuhi. Mdukuzi mkuu na wanachama wa ONA pamoja na watu mahiri wa familia ya Choka walikuwa tayari hapo. Kwa kuongezea, kulikuwa na idadi kubwa ya watu kutoka idara ya polisi.
Rodney alimpiga Alvin dakika tu alipomwona. “Yote ni kwa sababu yako! Ikiwa usingewafukuza watu wa ONA kumlinda Sarah, asingetekwa nyara, wewe b*star! Ikitokea lolote kwake, sitakuacha uondoke”
Alvin alishika ngumi ya Rodney na kumkazia macho. "Badala ya kuzua fujo hapa, kwa nini usiende kumtafuta?" Baada ya muda, aligeuka na kumuuliza Master Ganja. “Kuna maendeleo gani?”
Ganja alimtaka mdukuzi acheze video iliyorekodiwa. “Gari ambalo lilitumiwa kumteka nyara Miss Njau liliondoka

kwenye maegesho ya magari ya duka kubwa na kuelekea eneo la maegesho la uwanja wa michezo wa karibu katika kitongoji hicho. Tulifuatilia na tulipofika pale, hakukuwa na mtu ndani ya gari. Kwa vile uwanja wa michezo
hauna kamera za uchunguzi, hatukuweza kujua kilichoendelea baada ya hapo. Tunashuku kuwa watekaji nyara wameondoka na gari lingine. Kupitia uchunguzi wetu wa jana usiku, tunaweza kuthibitisha kuwa ni Santana nyeusi.”
Chester alisema, "Kutokana na kile nilichosikia hivi punde, gari hilo aina ya Santana lilisafiri hadi msitu wa vilima vya Cherangany kabla ya kutoweka."
“Acha kuropoka. Hebu tufike huko kwanza,” Rodney alisema kwa hasira, “Imekuwa usiku mmoja. Mambo mengi yanaweza kuwa tayari yametokea.”

Maneno yale yalifanya uso wa kila mtu kuwa na huzuni. Baada ya Alvin kuingia ndani ya gari, alipita kwa kasi na kuyapita magari yaliyokuwa barabarani kuelekea kitongojini. Akiwa njiani kwenda huko, aliuliza, “Umejua ni nani aliyefanya hivyo?”
“Bado hatuoni sura za watekaji nyara, kwa hivyo hatuna uhakika. Inaweza kuwa washindani wako wa biashara pia." Chester aliongeza kwa kusitasita, “Kwa miaka mingi, watu wengi wamekua wakichukia kukuona. Kwa kuzingatia kwamba una uhusiano wa karibu na Sarah, huenda wengi wanapanga kukutisha naye. Mmiliki wa Gloway alikufanyia kitu kama hiki hapo awali, sivyo?”
Alvin akakunja uso wake. Rodney alimtazama Alvin kwa ukali. “Hao watekaji lazima wawe vipofu! Walipaswa kumteka nyara Lisa badala

yake. Je, ina uhusiano gani na Sara? Umemuumiza vya kutosha. Ni bahati mbaya sana kuwa ameanguka kwa ajili yako."
Akiwa anaminya midomo yake myembamba kwa hasira, Alvin alibaki kimya.
"Afadhali uombe kwamba Sarah awe sawa." Rodney alikuwa na wasiwasi kiasi kwamba mishipa yake ilikuwa ikitoka nje.
Muda mfupi baadaye, umati wa watu ulionekana katika eneo jirani la msitu wa vilima vya Cherangany. Chini ya nusu saa baadaye, mtu mmoja alipiga simu na kudai kuwa gari hiyo aina ya Santana ilipatikana magharibi.
Alvin na wengine mara moja walikimbilia huko. Ganja alisema, "Tumetafuta kila mahali, na nadhani mtekaji nyara

alimleta Sarah kwa njia hii."
“Mtekaji nyara?” Alvin aliinua uso wake kwa huzuni. "Kwa hiyo ni mtu mmoja tu anayehusika?"
"Kulingana na nyayo, nadhani hivyo."
“Nenda mkamuwinde. Bado anapaswa kuwa mahali fulani hapa.” Alvin alitoa amri kwa haraka.
Dakika kumi baadaye, ghafla walisikia mwanamke akipiga kelele.
"Ni Sarah." Uso wa Rodney ulibadilika sana. Alikimbia hadi eneo ambalo sauti hiyo ilitoka.
Alvin alimfuata kwa hatua kubwa. Baada ya muda, waligundua pango nyuma ya msitu. Kila mtu aliingia ndani ya pango na taa za tochi. Ni kijana mtanashati tu ndiye alionekana

akimkandamiza Sarah ambaye shati lake lilikuwa limechanwa katikati. Kutokana na uso wake kuvimba, ilionekana wazi kuwa alikuwa amepigwa kofi kali.
"Mjinga gani huyu?" Rodney alikimbia kwenda kwa mtu huyo ili kumpiga, lakini mara mtu huyo aligeuka kana kwamba alikuwa na macho nyuma ya kichwa chake. Aliingia kwenye vita na Rodney.
Alvin kwa haraka akavua shati lake na kumfunga Sarah. “Alvinic, Alvinic, ninaota? Hatimaye umekuja kuniokoa.” Sara alianguka mikononi mwake huku akilia.
“Samahani.” Muda huo Alvin alianza kuongea, ghafla Sarah alimsukuma kwa nguvu. Kisha, akajikunja na kujificha upande mmoja. “Usinishike. Mimi ni mchafu. mimi ni mchafu sana.”

“Wewe si mchafu. Tuko hapa, na utakuwa sawa. ” Alvin alimfariji kwa upole. "Ngoja nikupeleke nyumbani, sawa?"
“Hapana, nimetosha. Sitaki kuishi tena. ” Sarah alipomaliza kusema aligeuka na kujibamiza kwenye jiwe la ukuta pango.
“Sarah...” Alvin alimkimbilia upesi na kumbeba.
Kichwa cha Sarah kilitapakaa damu. Wakati akijitahidi kuinua kichwa chake, alimgusa usoni na kulia kwa huzuni. “Alvinic, usijisumbue kuniokoa tena, kwa kweli. Mimi... niko katika kuzimu hai. Kwa kweli... nilitaka kufa vibaya sana wakati huo. Mimi... sijisikii... kuishi tena. Nachukia... jinsi nilivyo mchafu. Nachukia... jinsi..wewe na Lisa ni... Inaniuma... Hii ni sawa... ninaweza kuwa huru sasa...”

Sarah alipomaliza kusema tu, alifumba macho kana kwamba amekufa.
Sura ya: 443
“Sarah!” Alvin alipiga kelele kwa wasiwasi. Aliweka mkono wake karibu na pua yake na kugundua kuwa bado alikuwa akipumua kwa kina. "Chester, njoo umuokoe mara moja!" Akiwa amefadhaika, Alvin alimfokea Chester.
Kwa upande mwingine, Rodney alikasirika sana hadi macho yake yakawa mekundu. "Chester, lazima umwokoe, tafadhali."
“Nitajitahidi.” Chester mara moja akamwomba Alvin amlaze Sarah chini. Kwa bahati nzuri, alikuwa amebeba kifurushi cha huduma ya kwanza asubuhi hiyo.
 Baada ya kutumia zaidi ya dakika kumi kumtibu Sarah, aliachia mguno akiwa amepoteza fahamu. Bado

alibaki amepoteza fahamu.

“Nimejaribu niwezavyo. Ingawa yuko hatarini kwa sasa, anahitaji kupelekwa hospitalini haraka iwezekanavyo, la sivyo atapatwa na mshtuko kwenye ubongo,” Chester alisema kwa sauti nzito.
“Sawa. Nitampeleka hospitali sasa hivi.” Alvin akambeba Sarah kwa kasi na kukimbia kuelekea kwenye gari lake. Baada ya kupata gari lake, alikimbia hadi hospitali kwa kasi ya
umeme. Baada ya matibabu ya dharura, hatimaye Sarah aliokolewa.
Alvin aliegemea kiti, na mikono yake ilikuwa imejaa damu. Uchovu alioupata haukuelezeka.
“Bwana Mkubwa, mtekaji nyara amefungiwa kwenye jela ya
ONA," Ganja alimwendea Alvin na

kumjulisha.
Alvin aliinua kichwa chake na kuyatazama majeraha ya uso
wa Ganja. Alipomtazama Rodney ambaye pia alikuwa katika hali mbaya, alikunja uso kwa huzuni. “Wewe na Rodney mlikuwa mnashughulika na mtu mmoja tu. Umejeruhiwa vipi?"
Ganja akakohoa kidogo. "Ningeweza kushughulika naye peke yangu tulipokuwa shingo na shingo, lakini Bwana Shangwe alinizuia kidogo ..."
"Unamaanisha nini? Unasema sina uwezo? ” Rodney alishindwa kujizuia.
Sura isiyo ya kawaida iliosha uso
wa Ganja. Hata hivyo, macho ya Alvin yaliyowekwa ndani kabisa yaliangaza kwa sura ya barafu. "Hata hivyo, jamaa huyo hafanani na raia wa Kenya. Mtu huyu ni nani? Kwanini alimteka nyara

Sarah? Nani mpangaji wa tukio hili? Fanya haraka uchunguze.”
“Sawa, nitafanya sasa hivi.” Ganja aligeuka na kuondoka.
Sarah aliposukumwa ndani ya wodi ya watu mashuhuri, Alvin alijihisi mnyonge sana kwa kuona kichwa chake kimefungwa bandeji. Hakuwahi kufikiria kwamba angethubutu kugonga kichwa chake ukutani ili kujiua.
Je, alikuwa amemuumiza sana hivi kwamba hakutaka kuishi tena? Alihisi kama angekuwa na deni lake milele.
“Alvin...” Rodney alimsogelea Alvin huku macho yakiwa yamemwagika damu kwani hakuwa amelala hata siku moja. Zaidi ya hayo, alikuwa ameingia kwenye vita pia, jambo ambalo lilimfanya aonekane mwenye huzuni.
Alvin alisema kwa mshtuko, “Ikiwa

unapanga kupigana nami...” Kabla hajamaliza sentensi yake, Rodney alipiga magoti mbele yake. Uso wa Alvin ulibadilika. “Unafanya nini Rodney Shangwe? Simama."
"Alvin, unajua sijawahi kumwomba mtu yeyote wala kupiga magoti mbele ya mtu yeyote." Rodney alitoa tabasamu la uchungu huku akiwa karibu na machozi. “Nakuomba mara hii moja tu. Muoe Sarah na achana na Lisa. Ukimwacha Sara baada ya mambo haya yote, atakufa. Hakuna kingine nitakuomba. Nataka tu kumuona Sarah akiwa hai.”
Alvin alishindwa cha kusema. Ikiwa angeachana na Lisa na kuvumilia na kuoana na Sarah, angekuwa mnyonge sana. Alikuwa amepitia penzi tamu la Lisa, na kumuoa mtu ambaye hakuwa na hisia naye kungemfanya akose furaha kabisa. Angekuwa tayari kupoteza furaha yake kwa ajili ya mtu

mwingine?
"Amka." Alvin alikunja ngumi.
"Hapana." Rodney alisaga meno yake kwa macho ya kusihi. “Alvin, daktari amefanikiwa kumwokoa, lakini vipi ikiwa hana kitu kingine cha kutarajia baada ya hapa? Vipi kesho na kesho kutwa? Ikiwa asingekutia moyo ulipokuwa katika hospitali ya magonjwa ya akili, labda ungekata tamaa. Baadaye, alichukua saikolojia kwa sababu yako. Kama si yeye miaka mitatu iliyopita, ungekuwa mwendawazimu. Kwanini huwezi kumuonea huruma kidogo? Kwanini unakuwa mkatili sana, huh?"
Alvin alitikiswa. Akageuka na kutoka nje ya wodi moja kwa moja.
Rodney akaushika mguu wake. “Alvin, nakuomba. Usipokubali, nitaendelea kupiga magoti hapa.”

"Rodney, kama rafiki yangu, hutakiwi kunitishia hivi." Alvin alijiondoa kwenye mtego wake na kutoka nje.
"Rodney, amka." Chester akashusha pumzi. "Ninaelewa kuwa unataka Sarah awe na furaha, lakini huwezi kujenga furaha yake juu ya maumivu ya mtu mwingine. Alvin amekuwa akijisikia hatia kwa kile kilichotokea kwa Sarah na maisha yake. Ana msongo wa mawazo pia.” Kwa hayo, Chester naye akatoka nje.
Alvin aliwasha sigara kwenye korido na kusema, "Wakati mwingine, nadhani ingekuwa bora kama Sarah asingeniokoa miaka mitatu iliyopita."
“Alvin, usijitie shinikizo kubwa. Kwa kweli... haujafanya chochote kibaya.” Chester alimgonga Alvin begani. "Naelewa. Hapo awali, ulikuwa

ukijilazimisha tu kumuoa Sarah na hata hukuwa na furaha.”
"Asante." Alvin alilazimisha
tabasamu. Akatoa simu yake na kuangalia mawasiliano ya Lisa kwenye WhatsApp. Hata hivyo, hakuwa amepokea ujumbe wala simu kutoka kwake. Akabonyeza simu huku akipanga kumuuliza kitu. Wakati huo, alikumbuka Sarah akigonga kichwa chake ukutani kwa dhamira. Hatimaye alisitisha lengo lake. Alikuwa amechoka kiakili pia.
Jioni, Ganja alikuja kwa Alvin na habari alizochunguza. Hata hivyo, aliuma ulimi baada ya kuwatazama Rodney na Chester.
“Sema tu. Wao si watu wa nje hata hivyo,” Alvin alisema bila kujali.
"Huyu ndiye mtu aliyemteka nyara

Sarah." Ganja akamwonyesha picha.
Alvin alichukua picha ile na kupigwa na butwaa kwa kuiona. Kamwe katika ndoto zake mbaya zaidi hakufikiria kwamba mtekaji nyara angekuwa kijana mdogo katika miaka yake ya mapema ya 20. Ingawa uso wake ulikuwa na makovu mabaya, alikuwa anaonekana mzuri na mwenye kuvutia.
Ganja aliongeza, “Tulipata hati yake ya kusafiria, na inaonyesha kwamba yeye si Mkenya. Anatoka Marekani, na jina lake ni Logan Law. Aliingia Kenya chini ya mdhamini aitwaye, Lisa Jones."
Alvin aliganda. Mwili wake uliokuwa na misuli ulionekana kulegea ghafla.
"Umesema nini? Lisa ndiye aliyemhakikishia kuingia kwake?" Rodney alikasirika sana hivi kwamba alikunja vidole vyake kwa nguvu. "Kwa

hiyo Lisa ndiye mpangaji mkuu wa tukio la utekaji nyara jana?"
“Hii haiwezekani,” Alvin alikatiza kwa ukali huku akiikunja picha iliyokuwa mkononi mwake.
“Nina uhakika ni yeye!” Rodney alinguruma. "Ana nia mbaya. Bila shaka, anamchukia Sarah kwa kudai kwamba alikuwa na ugonjwa wa akili miaka mitatu iliyopita na anamchukia Thomas kwa kumdhalilisha Pamela. Baadaye, Thomas aliachiliwa kwa sababu ya Sarah. Isitoshe, Sara alikunyakua kutoka kwake, kwa hiyo amekuwa akimwekea kinyongo.”
"Funga mdomo wako!" Alvin alimtazama Rodney kwa huzuni. Chester akawatazama wawili hao. “Tulieni nyie. Mnaweza kumwacha Ganja amalize kwanza?"

Ganja aliendelea, “Bwana Mkubwa, sina uhakika kama bado unamkumbuka yule ripota aliyemkamata Miss Jones akinywa pombe na mtu wa ajabu kwenye baa siku chache zilizopita.”
“Ndiyo.” Alvin akauma meno. Angekumbuka tukio hili hadi siku atakayokufa. "Unajaribu kuniambia kuwa mwanaume huyo ni Logan?"
“Hii ndiyo picha iliyopigwa kwenye baa wakati huo. Unaweza kuwalinganisha.” Ganja akatoa picha nyingine. “Ingawa ni mgongo wake tu ndio ulitekwa wakati huo, staili ya mwanamume huyu ni sawa kabisa na ya Logan. Ukiangalia sikio lake la kushoto, utagundua kuwa sikio lake la kushoto limevishwa hereni inayofanana.”
Sura ya: 444

Alvin aliendelea kuitazama ile picha. Umbo lake refu na lililonyooka lilionekana kuzungukwa na baridi kali. Alikuwa ameduwaa kabisa. Hakuamini kabisa kuwa Lisa ndiye aliyemfanya mtu huyu amteke Sarah.
"Bado unamwamini, huh?" Rodney aliinyakua ile picha na kuipeperusha mbele yake. “Angalia, wako sawa. Je, bado hujaelewa? Huu ni mtego wa Lisa. Umenaswa!
“Kwa muda mrefu amepanga mtu wa kumteka nyara Sarah. Baada ya hapo, alikuvutia hadi Johannesburg ili aweze kumfanya mtu huyo amteke Sarah. Kama sikujua kuhusu jambo hilo na kufika huko upesi, huenda Sarah angeuawa. Huyu mwanamke ni mkatili sana!”
Alvin alibaki kimya. Alimtazama tu Chester. "Nini unadhani; unafikiria nini?"

Macho ya Chester yalibeba sura ngumu. “Nafikiri... alichosema Rodney kina mantiki. Lisa ana nia, na zaidi, anafahamiana na mtekaji nyara. Hapo awali nilikukumbusha kwamba anaweza kuwa na ajenda iliyofichika atakapoamua kuwa nawe tena.”
"Ikiwa bado unakataa kuamini wakati huu, kimsingi unajidanganya. Nadhani huwezi kujiletea kumtendea Lisa kwa ukali. Ninataka kulipiza kisasi kwa niaba ya Sarah. Nitampeleka Lisa kituo cha polisi.” Rodney alisema na kugeuka na kutoka nje ya wodi.
Baada ya kupigwa na butwaa kwa muda, mara Alvin alimfuata. Muda mfupi baadaye, Rodney aliingia kwenye lifti. Alvin hakuwa na la kufanya zaidi ya kushuka ngazi huku akiongeza mwendo.

Kwa wakati huu, Lisa, ambaye hakufanikiwa kumpata Logan baada ya muda mrefu, alituma ujumbe kwa nambari huko Marekani. [Rudi Kenya kwa haraka, Austin Lord. Logan anaweza kuwa hatarini.]
Baada ya kutuma ujumbe huo, alirejea nyumbani kwake. Wakati huo huo, wasiwasi ulikua ndani yake. Katika miaka miwili aliyomfahamu Logan, Lisa hakuwahi kushindwa kuwasiliana naye. Baada ya kurudi Kenya kwa muda mrefu hivyo, ilikuwa mara yake ya kwanza kujihisi hoi. Baada ya yote, Logan alikuwa mtu wake wa mkono wa kulia.
Mara tu alipoegesha gari lake, gari moja lilimsogelea ghafla. Kabla hajaikwepa, gari lake liligonga ukutani nyuma yake. Mkoba wa hewa ulituna, ukimlinda, lakini damu ilikuwa ikimwagika ndani yake.

Baadaye, alimwona Rodney akitoka kwenye gari hilo lililokuwa karibu naye. Akafungua mlango wa gari lake na kumtoa nje moja kwa moja.
“Lisa Jones, tangu zamani nilitaka kukuua lakini niliendelea kukuvumilia. Lakini wakati huu, ulithubutu kumdhuru Sara. Sitakuacha kwa hili! ”
Kwa usemi wa kikatili, Rodney alinyoosha mkono wake kumkaba kooni.
Lisa alifumba macho huku akijitahidi kadiri awezavyo kukitawala kichwa chake ili asihisi kizunguzungu. Baada ya hapo, akanyanyua mikono yake na kumvamia Rodney.
Punde wawili hao waliingia kwenye vita. Rodney aliuliza watu wake wamtii. Binafsi nitakulipa kwa yale uliyomfanyia Sarah. Rodney alimwonyesha kwa hasira.

“Sijui unachokisema! ” Lisa aliona ni ujinga. “Unashuku kwamba nilimteka nyara Sarah?”
“Kama si wewe, nani mwingine angefanya hivyo? Hata aliye chini yako amekamatwa.” Rodney alimtupia picha hiyo. “Mtazame mtu huyu. Unamfahamu?”
Lisa aliinamisha kichwa chini na kumuona Logan akiwa amefungwa kwenye rafu. Kulikuwa na alama za mijeledi mwili mzima, na uso wake mzuri ulijeruhiwa vibaya sana. Macho yake ghafla yalitoa hisia ya huzuni.
"Yuko wapi?”
"Kizuizini." Rodney alidhihaki. “Lisa Jones, nakupa chaguzi mbili sasa. Unaweza kwenda jela au kuwaruhusu wasaidizi wangu wafurahie na wewe.

Hapo ndipo nitakuacha uachane na hili.”
Lisa alicheka. "Kwa mtu kama wewe ambaye hata hastahili kurithi mali ya familia ya Shangwe, wewe si kitu. Nina hakika kundi hili la watu sio mabwana kutoka Shangwe Corporation. Ikiwa nyinyi watu mna ujasiri, mnaweza kuungana na kunishambulia. Hebu nione jinsi ulivyo mkuu.”
Rodney alikasirika sana hivi kwamba sura yake ilibadilika sana. Wakati huu, Alvin alikuwa amekimbia.
 Akapiga breki ili kusimama mbele ya magari yao. Mara akatoka nje.
 Bado alikuwa amevaa shati lile lile alilokuwa ametoka kwa haraka asubuhi na mapema. Lakini, uso wake wa kupendeza ulionekana mkali sana, ambao ulikuwa tofauti kabisa na sura yake ya upole ya jana.
Alipomwona Alvin, Rodney alikoroma.

“Alvin, umekuja kwa wakati sahihi. Amekiri kuwa alikuwa anafanya. Wakati huu, inabidi unipe maelezo. Mwanamke huyu katili lazima aadhibiwe ipasavyo.”
Lisa alishindwa cha kusema. “Ni lini nilikubali kumteka nyara Sarah?”
“Ulikubali kuwa mteka nyara anakufanyia kazi. Kama usingemwagiza, angemteka nyara Sarah kwa hiari yake mwenyewe?” Rodney alimkosoa.
Lisa alikunja nyusi zake. Ingawa Logan alimfanyia kazi, asingeweza kuteka nyara mtu bila agizo lake- isipokuwa mtu alikuwa amemseti.
Siku zote alikuwa akimficha Logan. Hakuna aliyejua juu yake isipokuwa marafiki zake wachache wa karibu.
Je, inawezekana kuwa kuna mtu amegundua kuhusu hilo baada ya

mwandishi kunasa mkutano wake na Logan kwenye baa siku chache zilizopita? Baada ya kusema hivyo, mtu huyo anaweza kuwa nani?
Je, anaweza kuwa ni wale watu waliokidiwa na Thomas kutoka Somalia?
Labda... ulikuwa mpango mpya wa Sarah. Kusudi la Sarah lilikuwa kuzidisha mzozo kati ya Alvin na yeye. Kisha, angemwangamiza mtu wake wa mkono wa kulia, Logan. Mpangaji wa tukio hili hakuwa na huruma, kweli.
Ilikuwa imepita muda tangu arudi Kenya na ilikuwa mara yake ya kwanza kuchanganyikiwa sana. Alikuwa amemdharau Sarah. Kwa wakati huu, bado haikujulikana ni nani aliyekuwa akimsaidia Sarah kwa siri. Lakini, kilichokuwa muhimu sasa ni kumokoa Logan. Hakuweza kumwacha juu na kavu.

"Angalia, Alvin. Anajiona kuwa na hatia sana hivi kwamba anashindwa kusema.” Rodney alidhihaki.
Alvin alitembea taratibu kuelekea kwa Lisa. Jana yake usiku, alijiwazia kuwa naye milele, lakini kwa wakati huo, alihisi kuwa hawezi kuona kupitia kwake. “Kwanini ulifanya hivyo?” Akamtazama kwa hasira huku macho yakiwa yana damu. “Kama una kinyongo, unaweza kulipiza kisasi kwangu. Mimi ndiye niliyekuumiza hapo awali, sio Sarah. Unaweza kunifanyia chochote unachotaka, lakini kwanini umepata mtu wa kumdhalilisha Sarah?”
Kwa mwanamke, hakuna kitu kikatili zaidi ya kumshtaki kwa kitu ambacho hakufanya. Hata hivyo, ni mwanamke wake mpendwa ambaye alifanya jambo hilo la kutisha.

Lisa alitazama macho yake bila huruma na kwa utulivu. “Alvin, umeniambia hivi majuzi tu kwamba utajaribu kuniamini. Je, hivi ndivyo unavyoniamini? Kila linapokuja suala la Sarah, huwa unanishuku bila kufikiria tena.”
“Sitaki kukushuku pia, lakini nimemkamata mtu anayekufanyia kazi!" Alvin alinguruma, “Ulipokutana naye kwenye baa siku hiyo, ulikuwa ukimuelekeza kumteka nyara Sarah, sivyo? Ukikataa na kukataa uhusiano wako naye, nitapata mtu wa kumuua mara moja."
"Hapana!" Lisa alisema kinyonge, “Alvin, lazima kutakuwa na kutokuelewana. Natumai utalichunguza suala hili kwa kina. Ni kweli kwamba Logan inanifanyia kazi. Yeye ndiye mlinzi niliyemwajiri kutoka ng'ambo. Niliporudi Kenya, nyinyi bado mlikuwa maadui zangu, kwa hiyo ilinibidi kupata

mtu wa kunilinda. Ninaelewa tabia yake. Asingefanya jambo kama hilo.”
“Acha kukana,” Rodney akajibu, “Ukweli tayari uko mbele ya macho yako. Logan alitenda kulingana na maagizo yako. Nani mwingine angemuagiza kufanya hivyo kama si wewe? Katika Kenya yote, ni wewe na Pamela pekee mnayemchukia Sarah.”
Sura ya: 445
Alvin alikaa kimya, lakini alikubaliana na Rodney waziwazi.
Lisa alipotazama mwanga wa macho ya Alvin ukififia kidogo kidogo, moyo wake ulitawaliwa na kejeli. Alijidhihaki kwa kuguswa na maneno yake saa 24 zilizopita. Baada ya kupitia magumu mengi, bado haikumpata kuwa mtu huyu ni mwongo? Alipomtaka, angeweza kusema kila kitu.

“Alvin, nataka kukuuliza jambo moja tu. Nifanye nini ili umruhusu Logan aende zake?” Lisa aliuliza kwa sauti ya chini.
“Amwache aende zake?” Rodney aliitikia kana kwamba amesikia mzaha. “Unaota? Kamuumiza Sarah, halafu aachwe hivihivi tu? Watu kama yeye wanapaswa kuteswa hadi kufa. Hata hivyo, kwanini una wasiwasi naye sana? Inawezekana una uhusiano naye wa kimapenzi?”
"Angalia mdomo wako." Mara tu Lisa alipomwonya Rodney kwa ukali, aliweza kuhisi hasira ya ghafla katika macho ya Alvin yenye baridi kali.
Moyoni alikuwa akimlaani Rodney.
"Ninaweza kumwacha aende," Alvin alitamka kila neno kwa uchungu, "lakini ni sehemu moja tu anayopaswa kwenda, nako ni kaburini!"

“Alvin, Logan na mimi hatuna hatia. Afadhali uamini maneno ya Rodney kuliko yangu licha ya kulala na mimi kitandani? Hatimaye nimeelewa sasa.” Lisa alishusha macho chini, kope zake zikificha mng'ao wa hasira machoni pake.
Alvin aliumia moyoni baada ya kuona sura yake. Alikuwa akijaribu kumbana kupitia sehemu zake dhaifu, yote ni kwa sababu ya msisitizo wake wa kumokoa Logan.
“Lisa Jones, umeniangusha. Sikuwahi kufikiria kama ungekuwa mwovu sana.” Alvin alimtazama Lisa kwa moyo uliovunjika, hakuweza kujizuia kutoa tabasamu hafifu.
Macho ya Lisa yakawa mekundu. Alikuwa akimwita mwovu? Ni nani aliyekuwa mwovu kati yake na Sarah? Baada ya miaka mitatu, bado alikuwa

kipofu kama zamani. Bado alishindwa kuona rangi halisi za Sarah.
“Vipi bado unatabasamu wakati huu?!” Rodney alifoka kwa hasira.
“Inachekesha sana, kwanini nisitabasamu? Lisa alijifuta pembe za macho yake kabla hajageuka na kuelekea kwenye lifti.
“Simama.” Rodney mara moja aliamuru wasaidizi wake kumzunguka. “Unapanga kwenda wapi?”
“Kwanini? Unapanga kunikamata?" Sura ya mawe iliangaza machoni mwa Lisa. “Nyinyi si ndio mnaongoza Kenya sasa. Mnadai kuwa nilimteka nyara Sarah, lakini mna ushahidi? Kwa sababu tu mlimshika mtu ninayemjua, mna uhakika kwamba ilikuwa kazi yangu. Je, mtu mliyemkamata aliwaambia kuwa mimi ndiye

niliyemuagiza kufanya hivyo?”
Akiwa ameudhishwa na shutuma zake, Rodney alikasirika sana hivi kwamba akafungua macho yake. “Sijali! Ikiwa unakubali au la, huwezi kuondoka leo.”
"Vema, Bwana Mdogo Shangwe, hii inamaanisha kuwa unaniteka nyara kwa nguvu." Lisa akamsogelea ghafla. "Naweza kujua kama wewe ni afisa wa polisi?"
“Polisi? Polisi watanifanya nini nikiamua kukukamata?”
"Umesahau kwamba baba mdogo wako atagombea Urais mwakani? Je, unafikiri unaweza kujifanya jeuri na kumshika mtu yeyote bila mpangilio? Sasa, unajaribu kuweka mikono yako juu ya mwenyekiti wa kampuni kubwa kama Mawenzi. Zaidi ya hayo, mimi ni binti wa Joel Ngosha, mmoja wa watu kumi bora

zaidi mahiri nchini Kenya.”
Macho ya Lisa yalimtoka kwa ukali. "Bwana Shangwe, ba’mdogo wako ana washindani wengi sasa. Kila mtu katika familia ya Shangwe amekuwa na tabia ya tahadhari kwa ajili ya uchaguzi mwaka ujao, lakini wewe unataka kumburuta ba’mdogo wako chini.
 Una uhakika unataka kuharibu sifa ya familia yako na kuwa mtu wa kulaumiwa?”
“Wewe...” Mishipa ya Rodney ilibubujika kwa hasira. Alihisi hamu kubwa ya kutaka kumnyonga. Hata hivyo, aliyosema Lisa yalimwingia taratibu. Alijua vizuri jinsi uchaguzi wa ba’mdogo wake mwaka ujao ulivyokuwa muhimu.
Rodney aliwahi kuharibu sifa ya familia ya Shangwe hapo awali, lakini hiyo ilihusiana na maisha yake ya kibinafsi. Ikiwa angechukua hatua dhidi ya Lisa wakati huo tena, pengine ingesababisha

kila mtu kususia familia ya Shangwe kwa ajili ya uchaguzi mwaka ujao.
“Ikiwa unapanga kunikamata, afadhali uwe na ushahidi kwanza,” Lisa alisema bila kujali. Kwa hayo, akageuka ili kuondoka.
"Subiri. Unaondoka, nani amekuruhusu?" Alvin alimsogelea kwa sura nzito.
“Nilisema unaweza kuondoka?” Macho ya Rodney yakaangaza. "Alvin, mshike na umpeleke ONA kumtesa."
“Unapanga kunikamata, huh?” Lisa alitazama machoni mwa Alvin, macho yake yakionyesha sura adimu ya huzuni.
Moyo wake ukasisimka mara moja. Ghafla, hakujua la kusema. Alijua akifanya hivyo, mzozo kati yao ungezidi.

Hata hivyo, kwa kuwa sasa alikuwa amefanya jambo hilo baya, je, angeweza kujiafanya kwamba hakuna jambo lolote lililotukia?
"Alvin, mbona unasitasita?" Rodney alinguruma, “Umesahau kwamba Sarah alikaribia kupoteza maisha yake? Je, umesahau sura ya kukata tamaa usoni mwake alipotaka kujiua?”
Lisa alipigwa na butwaa. Kweli Sarah alijaribu kujiua? Hakika, alikuwa amedhamiria kujifanyia ukatili kwa ajili ya Alvin.
"Wewe, utaenda ONA pamoja nami." Macho ya Alvin yalionyesha hali ya mshangao. Kisha, alinyoosha mkono wake kumshika Lisa.
Kabla hajamsogelea, yule mwanamke aliyekuwa mbele yake, akatoa bastola na kumlenga nayo. Tangu litokee lile tukio la kuvamiwa saluni, Lisa alimua

kuchukua hatua biafsi ya kuimarisha ulinzi wake kwa kununua bastola.
Alvin aliganda palepale huku akionekana kutokuamini machoni mwake. Haikuwa wazi kama alishtuka kwa sababu alimuona Lisa akiwa na bastola au kwa sababu alikuwa akimlenga nayo.
“Sitaondoka na wewe. Ukithubutu kuniondoa kwa nguvu, sitakuwa na budi ila kukupiga risasi.” Lisa alionya bila masihara yoyote machoni.
Macho ya Lisa yalikuwa tulivu isivyo kawaida. Alihisi kama angempiga risasi kweli ikiwa angesisitiza
kumchukua. Huzuni ilimtawala Alvin ndani kabisa. Alisema kwa sauti ya kishindo, “Unathubutu vipi kuwa na wazo la kunipiga risasi?”
"Kwa hiyo nikae tu kizembezembe na

kukuacha unishike badala yake?" Lisa alikoroma. “Sikufanya kosa lolote, kwanini nikubali nikateswe huko ONA? Alvin, ninafanya hivi kwa kujilinda. Unaweza kufikiri kwamba ninakuumiza kwa kukunyooshea bunduki, lakini vipi kuhusu wewe? Unajaribu kunishika, si unaniumiza pia? Kwa kuwa unaweza kuniumiza bila kufikiria mara mbili, kwanini mimi usiweze?”
Aliinua bastola kidogo na kulenga mguu wake. "Unaweza kujaribu kunisogelea ikiwa unadhani natania. Jaribu tu.”
"Ukithubutu kunipiga risasi, utaenda kunyea debe gerezani," Alvin alionya vikali.
“Ukithubutu kunisogelea, utakuwa kilema,” Lisa alimkumbusha bila kulegea.
Alvin alikunja ngumi kwa nguvu. Macho

yake yalijawa na hasira, hatia, huzuni, na kukata tamaa. Lakini, Lisa hakuonekana kuliona hilo. Alirudi nyuma hadi akaingia kwenye lifti. Ni baada tu ya lifti kupanda ndipo moyo wake uliokuwa na wasiwasi ulianza kutulia.
Hakuna aliyejua kwamba alikuwa amepitia mambo mengi sana. Tangu alipovamiwa nyumbani kwake, na baadaye saluni akiwa na Pamela, alikuwa ameweka bastola kwenye gari lake ili tu apate silaha ya
kujihami.
 Baada ya yote, alijua Sarah angetaka kumuua dakika yoyote. Hata hivyo, hakuwa amepanga kufyatua risasi kwa Alvin, alikuwa akimtisha tu ili asimkamate.
Baada ya kusema hivyo, Lisa hakuweza kumruhusu Alvin ampeleke ONA. Ilimjaza hofu sana. Miaka mitatu iliyopita, Alvin alimpeleka hospitali ya magonjwa ya akili na karibu kumfanya

awe mwendawazimu. Miaka mitatu baadaye, ni nani alijua ni matokeo gani ambayo angeyapata katika makucha yake?
Pia, ni nani angemuokoa Logan ikiwa angechukuliwa? Kwa bahati nzuri, alikisia sawa. Alvin hakumfuata tena.
TUKUTANE KURASA 446-450
ONYO: Ni marufuku kusambaza, kukopi wala kuuza kazi hii kwani endapo kama tutakubaini basi sheria itachukua mkondo wake (By: Official Dully)
 
LISA KITABU CHA NANE (9) SIMULIZI........................LISA
KURASA.................446 - 450
PRESENT: SIMULIZI ZA DULLY

Sura ya: 446
Kwenye maegesho ya magari. Baada
ya lifti kupanda juu, Alvin alipiga kwa
nguvu ngumi kwenye kioo cha gari lake.
Damu zilimtoka kwenye ngumi hadi
chini, hata hivyo hakusikia maumivu
hata kidogo. Macho yake yalikuwa
mekundu, na huzuni nyingi zilimjaa.
Lisa kweli... akamnyooshea bastola? Ni
nini kinachoweza kuwa na uchungu
zaidi kuliko kujua kwamba mwanamke
wake mpendwa alikuwa na wazo la
kumpiga risasi? Ha! Je, hata alikuwa
anampenda? Angewezaje kuwa mkatili
hivyo?
"Alvin, si tayari umeelewa tabia ya Lisa
kwa sasa? Amebadilika kwa muda
mrefu. Amebadilika sana hivi kwamba

hatuwezi kuona kupitia kwake sasa.
Nani angetarajia kuwa angekutishia kwa
bastola?” Rodney alisema kwa hasira,
“Amekuwa akificha mambo mengi
kutoka kwako. Pengine yeye si mkweli
kuwa katika uhusiano huu na wewe.
Hata hakupendi. Alirudiana na wewe
kwa sababu tu alitaka kulipiza kisasi
kwa Sarah.
 Je, huoni?”
"Nyamaza!" Alvin alimtazama kwa ukali.
“Nasema ukweli tu. Amka na uangalie
kilicho mbele yako. Angalia ni nani
anayekupenda kweli." Rodney
alipomaliza tu sentensi yake, alifungua
mlango wa gari kwa mshituko.
“Sijamaliza na hili
jambo bado. Hata ingawa angeweza
kutoroka leo, sitamwacha atoke kwenye

hili. Naenda ONA sasa kumhoji huyo
bwege wake.”
Muda mfupi baada ya kuondoka,
Pamela alikuja kwa haraka kwa Lisa. "Ni
kweli Alvin alimkamata Logan?"
“Mm.” Lisa alikuwa ametoka bafuni na
kubadilisha nguo safi.
Kwa vile hakuwa amelala kwa usiku
mmoja, uso wake mzuri ulijawa na
uchovu. “Kulingana na walivyosema,
Logan alinaswa akimfanyia Sarah
kitendo kichafu eneo la tukio. Baada ya
Sarah kuokolewa, alihisi aibu sana hivi
kwamba alijigonga kichwa chake
kwenye mwamba ili kujiua.”
"Ni wazi, yote ni mipango ya Sarah. Je,
Logan angewezaje kupendezwa na
mwanamke kama Sarah? Anamjua

Saraha vizuri na anaogopa kupata
ugonjwa! ” Pamela alitukana kwa hasira.
Lisa alikuwa anaumwa na kichwa na
kujipapasa paji la uso. “Hii ni ajabu
sana. Lakini siwezi kumuacha Logan
huko ONA kwani Alvin atachukua
maisha yake.”
“Una mpango gani?” Pamela aliuliza.
"Sijafikiria chochote bado." Macho ya
Lisa yalimtoka kwa
kuchanganyikiwa. "Nahitaji kukutana na
Logan ili kufahamu suala hilo ili niweze
kuthibitisha kuwa hana hatia."
“Sahau kuhusu hilo. Mastaa hao wawili,
Rodney na Alvin, wamevurugwa na
Sarah. Wana imani naye kabisa. Mara
Sarah atakapolia na kuwatishia, bado

watamwamini hata kama kuna ushahidi
dhidi yake. Pamela akashusha pumzi.
"Sielewi kwanini wanaume hao
wanamwamini sana Sarah ingawa yeye
ni mbaya sana."
“Hasa.” Lisa alikunja ngumi. "Kwa kuwa
siwezi kulishughulikia hili peke yangu,
wacha nimshilikishe baba."
•••
Saa moja na nusu baadaye.
Joel na Lisa walikwenda kwenye makazi
ya familia ya Shangwe pamoja.
Familia ya Shangwe ilikuwa imemaliza
kula chakula chao cha jioni. Mbali na
Mzee Shangwe, wanawe na wajukuu
pia walikuwepo. Hata Nathan Shangwe,
ambaye angegombea Urais wa Kenya
mwaka ujao, alikuwepo.

"Joel, nini kimekuleta hapa saa hizi?"
Mzee Shangwe aliuliza huku
akitabasamu.
"Bwana Shangwe, nina jambo la
dharura la kuzungumza nawe."
Mwonekano wa hasira ukauosha uso
wa Joel. “Kama ningekuwa na chaguo
lingine, nisingemleta binti yangu hapa.
Jason, ukizingatia sisi ni marafiki,
natumai utaendelea kumfuatilia
mwanao.”
Jason alipigwa na butwaa. Alikuwa na
watoto wawili. “Unamaanisha...”
"Mchana wa leo, Rodney alienda Karen
Estate kwa Lisa na kumletea shida."
Lisa aliwasha simu yake na

kumuonyesha video. "Hii ni picha
niliyopata kutoka kwa kamera ya
uchunguzi. Iangalie. Alinigonga na
kuharibu gari langu.”
Washiriki wengine wa familia ya
Shangwe walikuja kutazama video
kwenye simu. Wote wakamuona
Rodney akimvuta nywele Lisa huku
akimtoa nje ya gari. Hata alimnyonga
baada ya kuligonga gari lake. Kutokana
na picha hizo, waliweza kuona kwamba
aliambatana na watu wengi pia. Mzee
Shangwe, Jason, na wengine wote
waligeuka kwa hasira mbaya mara
moja.
Familia ya Shangwe ilikabiliwa na suala
muhimu wakati huo. Ikiwa video kama
hiyo ingeenea kwa umma, ingempa
wakati mgumu Nathan Shangwe

kwenye kampeni zake za Urais.
“Ni nini hasa kilitokea?” Jason punde
akajivuta. "Lazima kuna sababu nyuma
ya hii."
“Bwana Shangwe, ikizingatiwa kuwa
wewe ni mtu mwenye busara na pia mtu
wa hekima, nitakuwa wazi na wewe.
Sarah alitekwa nyara jana. Ikatokea mtu
aliyenaswa ni mlinzi wangu. Kwa
sababu hiyo, Rodney alikuwa anashuku
kwamba mimi ndiye nilifanya hivyo.
“Kwa kweli tukio hili naona ni la ajabu.
Nilikuwa Johannesburg siku chache
zilizopita. Niliporudi, Rodney
aliniangukia akiwa na gari lake na hata
akajaribu kunishika ili... kuwafanya watu
wake kunishambulia. ”

Uso wa Jason ukawa giza mara moja.
Kulikuwa na giza zaidi kuliko mkaa. Kila
kizazi cha familia ya Shangwe kilikuwa
kikikwepa sana kashfa na kiliimarisha
sifa safi kama filimbi. Jason hakutarajia
kuwa angekuwa na mtoto wa hovyo
kama huyo.
Lisa aliendelea kinyonge, “Nilijaribu
kubishana naye, lakini aliendelea
kushuku kuwa mimi ndiye
niliyesababisha utekaji nyara wa Sarah.
Nisingejali kama angetaka kuwaita
polisi, lakini lazima awe na ushahidi.
Hata yule aliyemkamata hakusema
kuwa mimi ndiye nilitoa maagizo.
“Nilitaka kumwelewesha Rodney, lakini
hakuweza kujisumbua kunisikiliza hata
kidogo. Alichokifanya ni kunifokea na
kunipiga ngumi. Kusema kweli, sidhani

kama mlinzi wangu angemteka nyara
Sarah. Kunaweza kuwa na mbinu chafu
kuhusiana na suala hili.”
“Bi Jones, ni kweli kwamba hukumteka
nyara Sarah?” Mzee Shangwe aliuliza
ghafla kwa sauti nzito. "Nijuavyo, una
kisasi cha kibinafsi dhidi ya Sarah."
“Mzee Shangwe, kama ningetaka
kumteka nyara Sarah, nisingemwomba
mlinzi wangu kufanya hivyo. Sikuhitaji
kuajiri mtu mwingine kufanya hivyo.”
Lisa alitoa kicheko cha uchungu. "Zaidi
ya hayo, nimekuwa kwenye urafiki na
maeleweno mazuri na Alvin siku hizi.
Hata tulienda safari pamoja siku mbili
zilizopita. Kwanini nijisumbue kumteka
nyara Sarah na kusababisha uhusiano
wangu na Alvin kuwa mbaya?”

Familia ya Shangwe ilikuwa smart.
Baada ya kusikia maneno ya Lisa,
waligundua kuwa alikuwa sahihi. Kando
na hayo, Mzee Shangwe bado
alikumbuka kwamba Alvin alikuja
kumchukua Lisa pale kwake ana kwa
ana siku kadhaa nyuma.
Joel alisema kwa mkoromo, “Binti yangu
asingemteka nyara Sarah. Kwa upande
mwingine, Sara ni mwovu sana. Licha
ya kujua kuwa Alvin na Lisa walikuwa
tayari wameoana enzi hizo, bado
alimsogelea Alvin na kumtongoza bila
aibu. Baada ya wawili hao kunaswa na
waandishi, watu wengi walimkosoa
Sarah kama mchepuko.
“Lakini Alvin alimfanya Lisa atangaze
kuwa wameachana kutokana na
ugonjwa wake. Pia alilazimika kusema

kwamba alikuwa akimpenda sana Sara.
Wakati kwa kweli, Alvin na Lisa
waliachana tu mwezi uliopita. Ikiwa
huniamini, unaweza kwenda kwa ofisi
ya usajili na uangalie tarehe yao ya
talaka. ”
Baada ya kusikia haya, wanawake wote
katika familia ya Shangwe walikasirika
juu yake. Wendy alishangaa. "Hii ina
maana kwamba Sarah amekuwa
mchepuko tu kwa Alvin katika miaka hii
mitatu?”
"Sarah alikuwa mpenzi wake wa
kwanza na pia mchumba wake wa
utotoni. Ninajilaumu tu kwa kuangukia
mtu ambaye alikuwa akimpenda mtu
mwingine kwa siri.” Lisa alisema kwa
huzuni, “Huenda hamjui kwamba Alvin
alikuwa akipanga kumuoa Sarah kabla

ya hapo, lakini... Nadhani nyote mliona
jinsi polisi walivyomchukua Sarah
wakati wa harusi yao. ”
“Ndio. Sarah hakuolewa na Alvin
mwishoni, na nikasikia... Alikuwa na
uhusiano wa kimapenzi na
mwanamume mwingine?” Jason
alikohoa kidogo na kujibu.
“Ndiyo. Sarah alipokuwa kwenye
uhusiano na Alvin, alikuwa na uhusiano
wa kimapenzi na mteka nyara wake wa
zamani ambaye alikuwa pia ni mraibu
wa madawa ya kulevya. Kama
sijakosea, walijuana tangu alipokuwa
ametekwa. Kila juma, Sarah alikuwa
akienda kwenye nyumba yake na kulala
naye.
 Mtu aliyemuua mtu huyo
hajapatikana. Hapo awali, polisi

walimshuku Sarah, lakini hawakupata
ushahidi wowote wa kumtia hatiani.”
Sura ya: 447
Taarifa hii ilishangaza kila mtu katika
familia ya Shangwe. Baada ya yote,
hawakufikiria kwamba Rodney alikuwa
akimlinda Sarah kwa siri.
Ijapokuwa sifa mbaya ya Sarah ilizua
ghasia hivi majuzi, ulikuwa uvumi tu.
Maelezo mahususi ya tukio hilo
hayakujulikana.
“Una uhakika kuwa unasema ukweli?”
Mtazamo wa kusikitisha uliosha uso wa
Jessica.
“Kwa kweli, Rodney anafahamu jambo
hili pia, lakini anamchukulia Sarah kama
mungu wa kike. Huenda Sara

aliwadanganya wanaume hao kwa
kudai kwamba alikuwa amelazimishwa
kufanya mambo hayo.”
Lisa aliongea kwa sauti ya unyonge,
“Mwanaume akisharogwa na
mwanamke ataamini chochote
atakachosema. Zaidi ya hayo, ukweli
kwamba Alvin alichagua kutomuoa
mwishowe unathibitisha kwamba sisemi
uwongo. Ni vigumu kwa mwanaume
yeyote kukubali kusalitiwa na
mwanamke wake.”
Familia ya Shangwe ilikaa kimya. Siku
nyingine, Alvin alikuwa amesema
kwamba angepanga upya harusi wakati
fulani baadaye. Hata hivyo, haikutajwa
tena. Familia ya Kimaro ilipoulizwa
kuhusu jambo hilo, hawakusema lolote
kuhusu hilo.

Joel alipotambua kwamba binti yake
alikuwa karibu kumaliza, alisema kwa
upole, “Nilikuja hapa kuwaambia ninyi
nyote mambo haya kwa kuzingatia
uhusiano kati yetu kwa miaka mingi.
Pia, ninaelewa tabia ya Mzee Shangwe.
Natumai kwamba nyote mtaendelea
kumtazama Rodney. Nilikuonyesha
video hiyo kuhusu tabia yake isiyo halali
na ya kiburi ili kukukumbusha kuwa
ikiwa video hii ingekuwa mikononi mwa
wale wenye nia mbaya, ninahofia
Nathan asingeweza kugombea Urais
mwakani.”
Akiwa na uso mzuri na wa kupendeza,
Nathan aliuliza kwa woga, “Ndugu Joel,
picha...”
“Zimefutwa,” Joel alijibu kwa ukarimu.

Familia ya Shangwe ilishusha pumzi ya
raha liipoisikia hivyo. Pia walionyesha
shukrani zao kuelekea Joel na Lisa.
“Asante Joel.” Mzee Shangwe kisha
akasema kwa pumzi, “Lazima
imekuogopesha, Lisa. Usijali,
nitaendelea kumuangalia Rodney na
kumfundisha somo kwa niaba yako.”
“Asante, Mzee Shangwe,” Lisa alisema
kwa bidii, “Kwa kweli, Pamela
alipomhadaa Rodney hapo awali, watu
wa nje walikuwa wamezungumza
kuhusu familia ya Shangwe lakini ninyi
hamkufanya fujoi kuhusu hilo. Ninaweza
kusema kwamba ninyi ni watu wenye
akili timamu.”
Familia ya Shangwe ilifurahia kusikia
hivyo. Kisha, Wendy akasema, “Kwa

kweli hata mimi simpendi Sarah pia,
lakini inaonekana Rodney amerogwa na
hawezi kuishi bila yeye.”
Lisa akahema. “Mtu akimpenda mtu bila
kulalamika si ni sawa tu na aliyerogwa?
Kuiangalia kutoka kwa mtazamo
mwingine, tunaweza kusema kwamba
Rodney ni mtu mwenye upendo. Kwa
kusikitisha, alianguka kwa mtu mbaya.
Akikutana na mtu anayemthamini, nina
uhakika mwanamke huyo atathamini
uhusiano wao.”
“Uko sawa.” Wendy aliitikia kwa kichwa
kwa kuridhika. Baada ya yote, Rodney
alikuwa mtoto wake. Hakutaka kusikia
mtu wa nje akimdharau. Maneno ya
Lisa yalimpa raha kubwa. "Kwa bahati
mbaya, tunahisi kwamba Sarah
anamchukulia kama mpango wake wa

kando tu lakini haonekani kuwa anajua."
“Anti Wendy, Sarah ni mtu mjanja. Sasa
kwa kuwa Rodney hatarithi Shangwe
Corporation, hatamkubali isipokuwa
awe amekata tamaa.”
Lisa alimtazama kwa kina Nathan. "Bila
shaka, ikiwa Sarah na Alvin bado
hawajafunga ndoa mwaka ujao na
Anko Nathan anakuwa Rais mpya,
utamwona Sarah aking’ang’ana
kuolewa na familia ya Shangwe."
Familia ya Shangwe ilishtuka.
Alipogundua kwamba walikuwa
wamewaelewa vya kutosha, Joel
alisema, “Tayari tumechelewa.
Tutaondoka sasa hivi.”
“Unaondoka hivyo hivyo? Kwanini

usikae na kunywa kahawa?” Jason
akasimama kwa heshima.
“Hapana, tutachunguza suala la mlinzi
wa Lisa ili kujua ni nani
anayemtengezea njama kwa siri.
Lazima tujue ukweli.” Joel alipunga
mkono kabla hajaondoka na Lisa.
Baada ya wao kuondoka, Mzee
Shangwe aliuliza kwa sauti nzito, "Je,
unafikiri kile Joel na binti yake walisema
ni kweli?"
Jason alikunja uso. “Nafikiri... Lisa
alikuwa anasema ukweli. Pia Joel ni
muungwana.”
“Ndiyo.” Wendy naye akaitikia kwa
kichwa. "Joel anaujua uchungu baada
ya kulizwa na Nina ambaye alikuwa na

uhusiano wa kimapenzi na Damien kwa
zaidi ya miaka kumi. Mbali na hilo,
nimekuwa nikiwapenda Lisa na Pamela
tangu mara ya mwisho nilipokutana nao.
Wao ni tofauti na wale watu ambao
wana nia mbaya.
Uzuri ni kwamba, watazamaji wanaona
sehemu kubwa ya mchezo. Rodney na
Alvin wote wamefunikwa na ukungu wa
Sarah, kwa hivyo hawawezi kuelewa
ukweli. Wanadai kuwa Lisa alimteka
nyara Sarah, lakini ukitafakari kwa
makini tukio hilo linatia shaka.”
"Ninashuku kwamba Sarah ndiye
aliyeandaa tukio la utekaji nyara akiwa
peke yake," Jessica alisema ghafla,
"Kwa mwonekano wa mambo, Sarah
hata ana matumaini ya kuolewa na
Alvin. Kwa mujibu wa habari za hivi

punde, Alvin na Lisa wamerudiana, kwa
hiyo inawezekana Sarah
anamtengenezea Lisa mbinu chafu za
kumtenganisha na Alvin.”
Kila mtu alimtazama Jessica kwa
mshangao kwa nusu sekunde. Kisha,
Mzee Shangwe akaitikia kwa kichwa.
"Inawezekana."
Nathan alianza kuonekana hana subira.
“Hata hivyo, nyie lazima mumfundishe
Rodney somo. Kwa bahati nzuri, ni
familia ya Ngosha waliokuja. Ikiwa ni
familia zingine, zingeweza kufichua
familia yetu kwa kuwaonea wengine na
kupuuza sheria. Nyie mnajua kabisa
kwamba tumetumia zaidi ya miaka kumi
kujiandaa na uchaguzi wa mwakani.”
Mzee Shangwe aligonga mkono wa kiti

kabla ya kuinua kichwa chake.
"Waamuru walinzi wa Shangwe
wamrudishe Rodney. Usimruhusu
kwenda popote katika kipindi hiki.”
"Baba, ikiwa Rodney hatasikiliza ..."
"Apigwe mara moja," Mzee Shangwe
alijibu bila huruma, "Unaweza kumpiga
popote, isipokuwa kwenye kichwa
chake tu. Yeye ni mjinga vya kutosha.
Ikiwa utapiga kichwa chake, anaweza
kuwa mjinga zaidi. Wakati huo maisha
yake yatakuwa magumu.”
Kila mtu katika familia ya Shangwe
alipoteza maneno.
Mzee Shangwe kweli alikuwa na hoja.
Baada ya Bentley nyeusi iliyowabeba
kuondoka katika jumba la kifahari la
familia ya Shangwe, Joel alimfariji Lisa,

akisema, “Usijali. Familia ya Shangwe
itashughulika na Rodney. Mimi na
Nathan tulikuwa wanafunzi wenza, na
zaidi ya hayo, familia ya Shangwe ni
watu wenye akili timamu.”
Lisa alishangaa. “Baba, wewe na
Nathan mmesoma pamoja?”
“Ndiyo. Nathan ni mtu mwenye busara.
Wagombea wengine wanaogombea
Urais hawawezi kushindana naye.
Kama mtu mzuri katika familia ya
Shangwe, Nathan atapaa angani
mapema au baadaye. Kwa hivyo...
tusiwaudhi au kuwa na ugomvi nao,”
Joel alimkumbusha kwa tahadhari.
“Sawa...” Lisa alijipapasa paji la uso
wake baada ya kusikia hivyo. “Kama ni
hivyo, nisimruhusu Sarah aolewe na

Rodney. Ikiwa Nathan ataishia kuwa
Rais, Sarah atafanya mambo yasiyo na
maadili zaidi kama ataolewa naye.”
“Usijali. Tayari umefichua rangi halisi za
Sarah leo. Ikiwa Rodney atathubutu
kumuoa Sarah, atafukuzwa kutoka kwa
familia ya Shangwe."
Lisa alitikisa kichwa. Alifurahi kwa siri
kwamba alienda kwa familia ya
Shangwe siku hiyo. Angalau, aliharibu
kabisa uwezekano wa Sarah kuolewa
na Rodney.
Akiwa kwenye mawazo tele, simu yake
ikaita. Alikuwa ni Kelvin ambaye
hakuwa amewasiliana naye kwa muda
mrefu. "Lisa, nilisikia tukio kuhusu
Logan kutoka kwa Pamela."

Lisa alikosa la kusema. "Pamela hana
dogo, anataka tu kukusaidia tukutane.”
Kelvin alisema, “Hebu tujadili
tunachoweza kufanya.”
Lisa hakufikiri kwamba Kelvin angeweza
kushindana dhidi ya ONA, lakini
hakuweza kuvumilia kukataa wema
wake. Mwishowe, alitikisa kichwa.
Sura ya: 448
Katika kambi ya ONA.
Sauti ya Rodney akiongea,
ilipishana na sauti ya kuchapwa viboko.
"Sema! Je, ni Lisa aliyekuagiza?”
“Hapana, sikufanya chochote. ” Logan
akakunja uso. Aliposhindwa kuvumilia
tena, akazimia.

“F*ck, huyu mpumbavu ni bubu? Yeye
ni mkaidi sana.” Rodney aligeuka na
kuondoka kwenye chumba cha chini
kwa hasira. Alipopanda, Alvin alikuwa
ameketi kwenye baa, akinywa mvinyo.
Uso wake ulikuwa umepooza kwa
hasira.
"Alvin, yule jamaa amezimia," Rodney
alisema kwa hasira.
“Hajasema lolote?” Alvin alikodoa
macho. Alidhani Logan alikuwa mlinzi
wa kawaida tu. Hakutarajia angekuwa
mwaminifu kiasi hicho kwa Lisa. Si
ajabu kwamba Lisa alikuwa amekosa
subira kumwambia amwachie Logan.
"Hapana.” Rodney akatikisa kichwa.
“Ninaenda hospitali kumtembelea

Sarah. Unataka kwenda pamoja nami?”
“Nitakwenda baadae baada ya kuoga,”
Alvin alisema bila kujieleza huku
akimimina glasi ya mvinyo.
Rodney alimtazama. Midomo yake
ikasogea, lakini alikata tamaa ya
kusema chochote na kuondoka tu.
Alipowasha tu gari lake, alizungukwa na
magari machache.
Muda si mrefu, mmoja wa wanaume wa
Shangweden (walinzi wa familia ya
Shangwe) alishuka kutoka kwenye moja
ya magari.
Rodney alishuka kwenye gari lake
baada ya kuwaona. "Mwamba, kwa nini
unazuia gari langu? Ondoka, nina kitu
cha kufanya."

"Samahani, Bwana Mdogo Shangwe.
Mzee Shangwe ameniamuru
nikukamate. Inabidi ukae ndani kwa
muda. Katika kipindi hiki, unapaswa
ndani ili kuepusha shari." Mwamba
alikuwa na mwili wa kutisha, lakini
alikuwa akiongea kwa sauti ya upole.
“Unamaanisha nini kwa kukaa ndani?”
Rodney alishangaa. "Babu yangu
anataka kunifungia?"
“Umekuwa ukisababisha matatizo
mengi hivi karibuni. Ili kuepuka kuathiri
kampeni za Urais za Nathan Shangwe,
unapaswa kurudi kwenye nyumba ya
familia na kukaa huko. Usitoke na
kusababisha shida kwa familia ya
Shangwe tena, " Mwamba alisema kwa
utulivu.

"Ni lini nimesababisha shida kwa familia
ya Shangwe?" Rodney aligundua kitu
ghafla. Alikasirika. "Lisa alimfuata babu
yangu na kumwambia kitu?"
“Twende zetu.” Mwamba hakutaka
kubishana naye.
“Nilifanya hivyo kwa sababu—”
Mwamba aliushika mkono wa Rodney
mara moja kabla hajamaliza
kuzungumza.
"Sitarudi." Rodney alikwepa na kupinga.
Ilikuwa sawa kama ingekuwa siku
nyingine yoyote, lakini Sarah alikuwa
bado hospitalini sasa. Hakujisikia
salama kabisa kuondoka na kumwacha
Sarah hospitalini. "Mwamba, mimi ndiye
bwana mdogo wa familia ya Shangwe.

Siamini kama utathubutu kuniwekea
mkono.”
"Katika hali hiyo, usitulaumu kwa
kukosa adabu." Mwamba alipunga
mkono wake. Wanachama wa
Shangweden walimzunguka Rodney
papo hapo. Wote walikuwa watu wenye
ujuzi. Ngumi za Rodney hazikuweza
kwenda popote mbele ya watu wale.
Alipigwa sana na hakuweza hata
kusimama baada yake.
“Acha!” Wakati huo, milango ya ONA
ilifunguliwa. Alvin na Ganja walitoka nje
huku wanachama wa ONA wakiwa
nyuma yao. Uso wa Alvin ulizidi kuwa
mbaya kwa hasira. “Rodney ni rafiki
yangu mzuri, lakini mnampiga mbele
yangu. Bado mna heshima yoyote kwa
familia ya Kimaro?"

Mwamba akasonga mbele. Alisema kwa
unyenyekevu, “Bwana Kimaro, Master
Ganja, Shangweden, na ONA daima
haziingiliani kwenye mambo yao
wenyewe. Ningekushauri usijiingize
katika maswala ya ndani ya familia ya
Shangwe."
"Familia ya Shangwe inawaruhusu
walinzi wa Shangweden kumpiga
mjukuu wao?" Alvin aliona haiaminiki.
Rodney, ambaye alipigwa hadi mbavu
zake karibu kuvunjika, alisema kwa
hasira, "Ni Lisa ambaye alimchochea
babu yangu. Anajaribu kuweka kabari
kati yetu.”
Chembe ya hasira ilitanda machoni
mwa Alvin. Mwanamke huyo alikuwa

mjanja sana na mwenye kiburi.
Mwamba alisema bila kujali, “Mzee
Shangwe ametoa maagizo yake. Ikiwa
Bwana Mdogo Shangwe atapinga,
tunaweza kumpiga tunavyotaka. Hii ni
kumzuia asilete matatizo kila mahali na
kuaibisha familia ya Shangwe.”
“Babu yangu lazima amepagawa...”
Rodney alipomaliza kumkemea babu
yake, mtu mmoja alimpiga ngumi ya
tumbo kwa nyuma.
"Wewe ni kichaa!" Mwamba
alimkumbusha kwa upole, "Uchaguzi wa
Rais umekaribia. Kila mtu katika familia
ya Shangwe yuko makini hivi sasa na
anafanya mipango kwa ajili ya kampeni
ya Nathan Shangwe. Ni wewe pekee
ambaye kila siku unamsumbua na

kumsumbua mwanamke. Mzee
Shangwe anataka urudi ili urejeshwe
kwenye fahamu zako."
Baada ya Mwamba kuongea, alipunga
mkono. Washiriki wa Shangweden mara
moja walimtupa Rodney ndani ya gari.
"Bwana Kimaro, nitaondoka sasa."
Mwamba aligeuka na kuondoka.
Ganja alitazama sura mbaya ya Alvin.
"Bwana Mkubwa ..."
"Hakuna haja ya kuwafuata. Kwa kweli
hili ni suala la familia ya Shangwe.
Nikiingilia kati kwa nguvu, ONA na
Shangweden wanaweza kupigana leo.”
Alvin akatikisa kichwa.
Familia ya Shangwe haikuwa mojawapo

ya familia tatu bora nchini Kenya, lakini,
ni Alvin pekee alijua juu ya nguvu
ambayo familia ya Shangwe ilikuwa
nayo nyuma ya pazia. Familia ya
Shangwe ilikuwa imevumilia kwa miaka
mingi ili kumsaidia Nathan kupata kiti
cha Urais.
Kwa hiyo, daima walikuwa
wanapambana chini kwa chini katika
ulimwengu wa biashara. Hawakutaka
kujionyesha kama ni familia tajiri sana.
Hata hivyo, kama ONA wangekabiliana
dhidi ya Shangweden, ingewezekana
wasingetoboa. Ilikuwa tu kwamba
hakuwahi kutarajia kwamba kitendo cha
Lisa kuchombeza maneno kwa familia
ya Shangwe kingeinua mkono wake
dhidi ya Rodney wao wa thamani.
Alifanya nini? Je, mwanamke huyo
alikuwa akisisitiza kwenda kinyume

naye?
•••
Lisa alienda kwenye jumba la Kelvin
moja kwa moja. Kwa vile kulikuwa na
waandishi wa habari ambao walipiga
picha zake na Logan mara ya mwisho,
hakuthubutu kukutana na Kelvin
hadharani.
"Lisa, unaonekana kama unahitaji
kupumzika." Kelvin alimpa sahani ya
tambi. "Nadhani haujapata mlo unaofaa
baada ya kujua Logan yuko taabani."
“Umesema kweli, nina njaa. Nisingejua
kama usingenikumbusha.” Lisa
alitazama sahani ya moto ya pasta.
Ilionekana kana kwamba kuna kitu
kilikuwa kimemzuia kooni.

Kila ambapo Alvin, mwanaume
aliyesema anampenda aliendelea
kumuumiza, Kelvin pekee ndiye
aliyempa joto. Alikuwa kama bandari
ambapo angeweza kujificha kutokana
na dhoruba.
Alikula pasta haraka. “Kula taratibu.”
Kelvin alimmiminia glasi ya maziwa ya
joto. “Najua Logan ni muhimu kwako.
Yeye ni mwaminifu.”
“Ni kweli. Inabidi nimuokoe. Itakuwa
hatari zaidi kila kukicha ikiwa atabaki
ONA. Alvin na wengine hakika
watamtesa. Huenda hata usiku wa leo
asimalize.” Lisa alikaza mkono wake
kwenye uma.
“Nitakusaidia,” Kelvin alisema ghafla.

Lisa alipigwa na butwaa. Kelvin
aliinamisha kichwa chake na kusema,
“Kwa kweli, nina uhusiano wa kibinafsi
na Jerome Campos baada ya kufanya
kazi hapa Nairobi miaka hii yote.
Amekuwa akitaka fomula za virutubisho
vinavyouzwa zaidi vya kampuni yetu.
Ninaweza kufanya naye makubaliano
na kuungana na familia ya Campos
kumuokoa Logan.”
"Hapana." Lisa akatikisa kichwa kwa
haraka. "Ukitoa fomula hizo kwa familia
ya Campos, faida ya kampuni yako
itapunguzwa nusu. Kando na hilo,
kampuni kubwa kama Campos
Corporation haitaipa kampuni yako
nafasi ya kuishi.
Sura ya: 449

Kelvin alimtazama Lisa kwa upendo. Alisema kwa upole, “Ikilinganishwa na kampuni, ni afadhali nisikuone ukiwa umefadhaika sana.”
Lisa alishtuka. Ingawa alijua kwamba Kelvin anampenda, hakufikiria kamwe kwamba angetoa maisha ya baadaye ya kampuni yake kwa ajili yake.
 “Kelvin sistahili...” alisema kwa sauti ya chini. Alikuwa hoi lakini mkweli.
“Kwa nini hustahili? Wewe ni mkurugenzi wa kampuni ambayo ina thamani ya jumla ya dola bilioni, binti pekee wa Joel, mwanamke tajiri kuliko wore Anchi nzima, mwanamke tajiri kuliko wote Kenya, mwanamke namba moja wa Kitanzania uliyefanikiwa nje ya nchi na ndani ya nchi, na mkurugenzi mkuu wa Kilimani Group. Una vitambulisho vingi sana. Idadi ya wanaume wanaotaka kukuoa

wanaweza hata kupanga foleni, lakini hapa unasema kwamba hufai.” Kelvin alitabasamu. "Kwa upande mwingine, nadhani wewe ndiye uliyetoka kwenye ligi yangu."
“Acha utani. Nafasi ya Golden Corporation tayari imeingia kwenye makampuni 50 ya juu ya taifa zima. Vyombo vya habari siku zote hukuangazia wewe, CEO kijana anayekuja kwa kasi. Mabinti wa familia nyingi za tajiri wanataka kuolewa na wewe...”
“Lakini sitaki kuoa mtu ambaye simpendi,” Kelvin akamkatisha. "Kwangu, sitaki kufanya maelewano inapokuja suala la ndoa."
Lisa alishindwa cha kusema.
“Nitawasiliana na Jerome sasa hivi...” Kelvin alisimama.

“Subiri.” Lisa akamzuia. Aliuma mdomo. "Nataka kumtafuta Alvin na kuzungumza naye tena."
“Unafikiri kuna manufaa yoyote kuzungumza naye?” Kelvin alikataa wazo hilo. Dokezo la huzuni likaangaza machoni pake. “Lisa, unaogopa kwamba utanidai sana? Au una hisia zisizoweza kudhibitiwa kwa Alvin tena baada ya kukaa naye katika kipindi hiki?”
"Sio hivyo." Lisa alishindwa kuvumilia kumuumiza. Alikanusha mara moja, akisema, "Kelvin hali si mbaya kiasi kwamba tunahitaji kutumia kampuni yako kumuokoa Logan. Huna haja ya kujitoa hivyo juu yake. Bado kutakuwa na mivutano tu kati yangu na Alvin katika siku zijazo. Ikiwa tutacheza karata zetu zote sasa hivi, tutashindana vipi na ONA baadaye?”

“Lakini...”
“Nina njia zangu. Ninakubali nia yako nzuri. Angalau najua wewe ndiye unayenijali vizuri zaidi. ” Lisa alisimama. “Nimechelewa, lazima niende.”
“Lisa...” Kelvin alimkumbatia kutoka nyuma ghafla. Sauti yake ilijaa uchungu. “Sijali jinsi mambo yalivyo kati yako na Alvin kwa sasa. Nitaifumbia macho tu. Nisipoifikiria, sitahisi kukosa hewa. Lakini baada ya kila kitu kuisha, unaweza kuniahidi... nitakuoa?”
"...Kelvin sistahili tena kuolewa na wewe." Lisa alihisi mgongano. Alifikiri hakumstahili Kelvin.
"Naelewa. Ili kumfanya Alvin kukupenda tena, lazima... ulilala naye.” Maumivu yaliangaza machoni pa Kelvin lakini bado alikuwa na tabasamu usoni

mwake. “Katika wakati huu na umri huu, wanawake wengi si mabikira tena wanapoolewa. Kila mtu ana wapenzi wachache wa zamani, na wengine hata walitoa mimba. Mimi sijali hilo. Ninachotaka ni maisha yako ya baadaye, sio maisha yako ya nyuma."
"Sawa..." Baada ya kimya kirefu, hatimaye Lisa alitikisa kichwa. "Mradi tu uko tayari kunioa, nitaolewa na wewe."
Katika maisha haya, alikuwa na deni kubwa kwa mtu huyu ambaye alikuwa akimwangalia kimya kimya. Hakuweza tena kumkatisha tamaa.
Baada ya kutoka kwenye makazi ya Kelvin Lisa alipiga namba ya Jack. “Mmoja wa watu wangu yuko mikononi mwa Alvin. Nataka kwenda ONA kesho asubuhi, lakini lazima nihakikishe kwamba ninaweza kuingia huko kiulaini. Nataka kumuazima Suzie.”

Jack alikamatwa mara moja. “Unataka kumtishia Alvin na Suzie?”
“Mm, Alvin hajui kuhusu uhusiano wangu na Suzie. Sina chaguo lingine.” Lisa alitabasamu kwa uchungu.
“Wewe ni mama Suzie. Hakika hutamuumiza, lakini Alvin anaweza asifikiri hivyo hivyo,” Jack alisema kwa wasiwasi, “Utaharibu kabisa uhusiano wako na Alvin kwa njia hii. Si hivyo tu, atanikataza nisikuruhusu kukutana na Suzie tena.”
“Ndio maana nina haraka ya kukutana na Logan ili kuthibitisha kwamba hana hatia. ” Lisa alikazia macho. "Ni kwa njia hii tu ndipo Alvin ataacha kuniandama."
“Una uhakika unaweza kupata ushahidi?” Jack alikuwa na shaka.


"Naweza." Lisa alijibu.” Lisa alijibu. "“Hakuna mpango usio na dosari kabisa. ”
Saa Tisa usikutisa usiku, Lisa alipokea simu kutoka kwa Austin. "Bi Jones, nimefika NairobiNairobi."
“Nenda ukamchukue Suzie kwa Jack asubuhi hii ya leo kwa Kack Kimaro. Ukishamchukua nitakupa maelezo mengine.” Lisa alimkabidhi kazi.
“Hivyo tu?” Austin alipigwa na butwaa. Hakuamini kwamba ameitwa kutoka Marekani kwa ajili ya kazi hiyo tu.
“Ndiyo. Usiruhusu mtu yeyote akutambue isipokuwa Suzie.”
“Sawa.”
Saa kumi na mbili na nusu asubuhi Lisa alipokuwa

Saa kumi na mbili , njiani kuelekea ONA, alimpigia simu Alvin.
“Mwishowe unawasiliana nami.” Kicheko jeurijeuri na cha sauti cha Alvin kilisikika. ."
“Nataka kukutana na Logan. Nitafika ONA baada ya dakika 40,”
Lisa alisema.
“Unataka? Una haki gani ya kuniamuru?" Alvin alisema kwa ukali, “Lisa, nimekudharau. Ulienda kwa familia ya Shangwe na kuchochea maneno Kati yaochonganisha maneno. Umemkashifu Rodney vibaya sana. Siwezi hata kuwasiliana naye hadi sasa. Amefungwa na familia ya Shangwe."
"Sikutarajia
“ Mzee Shangwe kuwa na ufanisi kiasi

hicho." Lisa alitabasamu. Hii ndiyo habari njema pekee aliyoisikia ndani ya siku mbili.
"Kwa hiyo ni wewe?" Alvin alisema kwa upole, "Ulitafuta mtu aliyemteka nyara Sarah na kisha ukaenda kwenye familia ya Shangwe ili kukabiliana na
Rodney. Sijawahi kumuona mwanamke mchafu kama wewe.”
Lisa alicheka sana. “Bila shaka, na hutawahi kumwona kwa sababu macho yako yamepofuka.”
"Kwanini unacheka?" Alvin alikerwa na kicheko chake.
"Njoo hapa. Nataka kukutana nawe. ” Sauti ya Lisa ilikuwa ya chini sana kana kwamba ni ya kunong’ona kati ya wapendanao.
Akili ya Alvin ilizunguka kwa muda.

Walipokuwa mapenzini wakati huo, hakuwa amewahi kutumia sauti kama hiyo kuzungumza hapo awali.
Midomo yake myembamba ikacheza. Alipokuwa karibu kusema kitu, mlezi alikuja kwa haraka na kusema, "Bwana Kimaro, Bi. Njau ameamka." Alikata simu mara moja na kukimbilia wodini.
Ndani ya gari, Lisa alitazama simu iliyokatika. Pembe za midomo yake ziliinuliwa kwa tabasamu la kebehi. Alvin alikuwa na wasiwasi sana juu ya Sarah. Sio tu kwamba alikaa kando yake usiku mzima, lakini hata alikata simu mara moja alipoamka. Macho na moyo wake ulijaa mwanamke huyo pekee.
Ghafla alihisi wimbi la uchovu. Hapo awali Lisa alipanga kumfanya Alvin ampende tena. Alitaka kumfanya Sarah aonje hisia za kunyang'anywa

mwanamume anayemjali zaidi. Kisha, angem’mwaga Alvin ili kumuacha ahisi uchungu aliokuwa nao hapo
awali. Alifikiri alikuwa karibu kufanikiwa. Lakini, aligundua juhudi zake zote zilikuwa ni kama hatua za mlevi, anaenda mbele hatua mbili na kurudi nyuma hatua sita.
Ilikuwa na maana gani kwamba mwanamume huyo alisema anampenda? Asingeweza kamwe kumshinda Sarah. Kama Sarah angeweza kutosheleza mahitaji ya mwili wake, kusingekuwa na nafasi kwa ajili yake kati yao wote wawili. Ghafla alihisi kama bidii yake yote hapo awali haikuwa na maana. Alitaka kulipiza kisasi kwao, lakini badala yake alijikuta anakuwa mnyonge.
Sura ya: 450
Katika wodi, Sarah alifumbua macho

yake kwa unyonge. “Bado niko hai. Kwanini... mimi sijafa?”
"Sarah acha kuongea upuuzi" Alvin alimfariji kwa sauti ya chini.
“Hiyo ni kweli, Sarah.” Thomas aliingilia kati, “Tangu ulipoumia jana, Shemeji Kimaro amekaa kando yako bila kuchukua hatua. Atafanya nini ikiwa kitu kitakupata?"
Alvin alikunja uso baada ya kusikia maneno hayo. Hata hivyo, alipoona mwanga wa tumaini machoni pa Sara, hakuweza kusema lolote.
“Kweli?” Sarah alimtazama kwa kutarajia kwa macho yake mekundu. “Alvinic, hunidharau? Mimi ni mchafu sana, karibu nipate-”
“Hukufanya hivyo,” Alvin akamkatisha. “Usiwaze upuuzi. Tulifika huko kwa

wakati na tukazuia isitokee.”
“Kwanini mambo haya yananipata siku zote?” Uso wa Sarah ulijaa kukata tamaa. “Simfahamu mtu huyo hata kidogo. Ilikuwa inatisha sana. Alirarua nguo zangu zote—ahh!” Ghafla alikumbatia kichwa chake kwa maumivu.
"Acha kufikiria juu yake." Alvin akamshika mkono.
Sara alijitupa kwenye kumbato lake, na kuuzika uso katika mikono yake huku akitetemeka. “Alvinic kwanini umeniokoa? Nilitamani sana kufa. Nimechoka. Jana ilinifanya nikumbuke kile kilichotokea huko Garisa wakati natekwa kipindi kile. Nina bahati mbaya sana. Usiniache tafadhali?”
"Sawa, nitakuwa hapa." Alvin alimbembeleza. Sarah taratibu akawa

kimya katika kumbato lake.
Baada ya kutulia, Thomas aliuliza mara moja, “Sarah, nini hasa kilitokea? Kwanini mtu huyo alikuteka nyara?”
“Hata mimi sijui pia. Nilitaka tu kwenda kufanya shopping kwa sababu nilikuwa na hali mbaya, lakini alinikaba na kunikokota hadi kwenye gari kwenye maegesho. Nilipozinduka, tayari nilikuwa ndani ya pango lile. Mtu huyo... Alisema... Alisema alitaka kunifanya kitu kibaya maishani mwangu. Alinuia hata kupiga picha kwa ajili ya kuzisambaza mtandaoni kila mtu anione... nikiwa katika hali hiyo.” Sarah alisema kwa kufoka kwa huzuni, “Mtu huyo alitaka kuniangamiza, lakini simjui hata kidogo.”
Thomas alikasirika. “Shemeji Kimaro, nilimsikia Rodney akisema kuwa mtekaji nyara ni mmoja wa watu wa Lisa.

Inabidi umpe Sarah maelezo.”
"Ilikuwa ... ni Lisa ndiye aliyepanga?" Sara aliishiwa nguvu na kuingiwa na hofu. “Kwanini alifanya hivyo? Tayari alishakunyakua. Ni nini kingine ambacho haridhiki nacho? Ananichukia kwa kusema kwamba alikuwa mgonjwa wa akili hapo awali? Au ananichukia kwa kukunyakua kutoka kwake? Labda anamchukia Thomas kwa kutaka kumbaka rafiki yake wakati huo. Lakini angeweza kunitafuta moja kwa moja. Kwanini alilazimika kutumia njia za kikatili namna hii?”
Uso mzuri wa Alvin uliingia simanzi baada ya kusikia hivyo.
Baada ya kumpanga Alvin, Thomas alijifanya kama amekasirika na kusema, "dada, hujaelewa? Hataki tu kulipiza kisasi kwako, anataka kukuangamiza kabisa ili upotee kabisa kwenye ramani. Hakuna mwanaume atakayethubutu

kukuoa siku zijazo na hata utapoteza ujasiri wa kuendelea kuishi.”
“Inatisha sana.” Sarah aliendelea kutetemeka. Alimtazama Alvin kwa kusihi na kwa woga. “Alvinic, najua unampenda Lisa sasa hivi. Hutaniumiza kwa sababu yake, sawa?”
"Hapana, nitakulinda." Alvin alimbembeleza kwa upole.
Thomas alisema kwa kutoridhika, “Bwana Kimaro, lazima umpe Sarah maelezo kuhusu jambo hili. Usiruhusu Sarah aonewe bila sababu kwa sababu tu familia ya Njau ni dhaifu. Amekuwa na maisha magumu. Alipelekwa katika hospitali ya magonjwa ya akili alipokuwa mdogo kwa sababu wazazi wake walimnyanyasa. Baada ya kutoka nje, familia ya Njau ilimpenda tu Charity na wakambagua Sarah. Alienda kusoma kwenye chuo kikuu Garisa akaishia

kutekwa nyara na magaidi na hata alipotea kwa miaka mingi tukadhania amekufa. Maisha yake yamekuwa ni magumu mno. Kwanini mbingu zinamtendea isivyo haki?”
“Nitampa maelezo.” Alvin aliinamisha kichwa chake na kumuuliza Sarah, “Unataka nifanye nini?”
Sarah akatikisa kichwa na kusema, “Kwa mantiki, mtu huyo alipaswa kufungwa jela. Lakini ninachukia sana kwa kunigusa kwa mikono yake. Alvinic, unaweza kukata mkono aliotumia kunishika? Sitaki wasichana wengine wasio na hatia wateseke kwa ajili yake.”
"Sawa." Alvin alishikwa na butwaa lakini akaitikia kwa kichwa. * Nitamalizana naye baadaye.”
Baada ya dakika kumi hivi, Sarah alichoka na kurudi kulala. Alvin

akasimama. Akamwambia Thomas, “Kaa hapa na umtunze Sara.”
"Utamkata kweli huyo mtu mkono wake?" Thomas alijipa ujasiri na kuuliza, “Bwana Kimaro, hutaweza kutudanganya, sivyo? Baada ya
yote, tangu wewe na Lisa mlipokutana, hata humjali Sarah hata kidogo.”
Alvin aligeuka na kuondoka huku akiwa na sura ya ukali.
Muda mfupi baada ya Alvin kuondoka, Sarah, ambaye alikuwa kitandani, alifungua macho yake.
"Sarah, wewe ni wa ajabu." Thomas akampa dole gumba. Alinong'ona, "Sema, Lisa atakuwa na hasira kiasi gani ikiwa atajua kuwa mtu wake muhimu zaidi anaenda kukatwa mkono wake?"

Sarah alikodoa macho. Lisa atakuwa na hasira kiasi gani? Kulingana na habari aliyopata, mtu huyo alikuwa chini ya Lisa, lakini Lisa alimchukulia kama familia. Lisa alithamini hisia kuliko kitu chochote. Je, angekasirika vipi ikiwa mkono wa mwanafamilia wake ungekatwa? Alvin asingeweza kamwe kuwa pamoja na Lisa katika maisha haya.
•••
Huko ONA, baada ya Lisa kuegesha gari lake, alitembea kuelekea mlango mkuu. Mlinzi aliyekuwa mlangoni alipomwona, mara moja akaingia ndani kuripoti.
Dakika chache baadaye, Shani alitoka nje akiwa na watu wengine. Alipomuona Lisa alipigwa na butwaa. "Bibi mdogo -"
“Usiniite ‘Bi Mdogo’ tena. Sijawahi kuwa hivyo tangu zamani na sitakuwa.” Lisa alimtazama huku akitabasamu.

Walikuwa hawajaonana kwa miaka mitatu. Ngozi ya Shani ilikuwa imefifia sana. Ilionekana wazi kwamba alihamishiwa sehemu ambayo haikuwa nzuri sana.
"Shani, hatujaonana kwa muda mrefu. Umekuwa ukifanyaje miaka hii?"
"Mm, nimerudishwa hapa siku chache zilizopita." Aliposikia sauti ya Lisa iliyojaa wasiwasi, Shani alisema kwa uchungu, “Maisha yangu yalikuwa ya kawaida tu, lakini najua hayakuwa magumu kulinganisha na yako.”
Alikuwa ameshuhudia unyama wa Alvin dhidi ya Lisa. Kwa bahati mbaya, hakuweza kuwa na msaada wowote kwani alikuwa chini. “Bi Jones, tafadhali rudi kabla Bwana Mkubwa hajaja. Haifai wewe kujitoa kiasi hiki kwa ajili
ya mlinzi tu,” Shani alimshauri Lisa kwa

haraka.
Lisa alisema kwa uchungu, “Walinzi pia ni binadamu. Isitoshe, yeye si mlinzi kwangu tu bali ni mwanafamilia muhimu pia. Maadamu mtu huyu ni mwaminifu kwangu, nitamlinda kwa nguvu zangu zote kama mkuu wake.”
Shani alipigwa na butwaa. "Wewe bado ni sawa na hapo awali. Lakini... nina wasiwasi kwamba huenda usiweze kutoka mara tu unapoingia hapa. Bwana Mkubwa amekasirika sana wakati huu."
"Kwa kuwa nimekuja, sitarudi nyuma hata nini kitokee." Lisa aliingia ndani akiwa amekunja mgongo.
Ganja alionekana na kumkaribisha kwenye ukumbi. "Bibi Jones, tafadhali keti hapa ili kumngoja Bwana Kimaro."
Uhusiano wa Alvin na Lisa ulikuwa

mgumu sana na usioeleweka. Kama wasaidizi, hawakuthubutu kufanya chochote kwa Lisa. Kwani, ikiwa wote wawili wangepatana tena wakati ujao, mambo yangekuwa magumu kwao.
“Naweza kwenda kumuona Logan? Sina chochote cha hatari. Sitaweza kumuondoa,” Lisa alieleza.
"Samahani. Tunahitaji kibali cha Bwana Mkubwa Kimaro.” Ganja alimkataa moja kwa moja.
Lisa hakusema neno lingine. Kulikuwa na mtu anayelinda mlango hivyo hakuweza kwenda popote.
Dakika 20 baadaye, umbo la Alvin liliingia. Alivaa shati jeusi na suruali ndefu nyeusi. Mwonekano mzuri na mgumu wa uso wake ulionekana kuwa mkali.

Ingawa walikuwa mbali, Lisa aliweza kuhisi kwamba Alvin alikuwa katika hali mbaya sana. Hata macho yake yalijawa na uadui. Alipokumbuka kwamba alikuwa ametoka hospitalini, alijua yule b*tch, Sarah, alifanya jambo la kuzusha mfarakano kati yao tena.
Ganja alijitokeza na kusema. "Bwana Mkubwa, Miss Jones alisema anataka kukutana na Logan,"
Midomo myembamba ya Alvin iliinuliwa kwa dharau. "Unaweza kwenda kukutana naye, lakini hutatoka tena baada ya kuingia ndani. Unasemaje?"
Uso wa Lisa ulijikunja kwa nguvu. “Alvin, nipo hapa kwa sababu nataka kwa dhati kuwa na mazungumzo ya amani na wewe. Ni lazima tufanye mambo kama haya kati yetu?"

“Unadhani niko tayari? Wewe ndiye uliyenilazimisha.” Kifua cha Alvin kilikuwa kimejaa uhasama. Ilifanya sauti yake kujawa na kero pia.
"Lisa, ulifikiria juu ya hisia zangu wakati ulininyooshea bastola? Ulifanya jambo baya sana kwa Sara pia. Unataka kumwangamiza, na hata kumfanya atamani kufa. Unalingana na maelezo ya kuwa mtu mkatili zaidi.”
Lisa akashusha pumzi ndefu. Moyo wake uliotulia hapo awali ulighadhabishwa na maneno yake mara moja. Lisa alitabasamu kwa huzuni. "Sababu nataka kukutana na Logan ni kuelewa kilichotokea siku ile. Alvin, hata mfungwa anayesubiri kunyongwa atapelekwa mahakamani, kuhojiwa, na kuchunguzwa na polisi mara nyingi. Una haki gani ya kuamua mara moja kuwa mimi ndiye niliyemuagiza Logan? Umenipa hata nafasi ya kujitetea? Ikiwa huniamini, unaweza kusimama kando

baadaye.”
Alvin alidhihaki, “Sawa, nitakuruhusu kukutana naye. Lakini usifikirie kutoka nje kwa sasa.” Baada ya kuzungumza, aligeuza kichwa chake bila huruma na kumwambia Ganja, "Mlete kwenye ghorofa ya chini."
"Bwana Mkubwa... " Shani alikuwa na wasiwasi.
"Nyamaza! Ashukuru Mungu kwamba simpeleki kituo cha polisi. Hili ni somo kwake. ” Alvin alimkazia macho Lisa kwa ukali. “Kaa humo ndani na ujitafakari. Fikiria ulichokosea, weka mbali mawazo yako maovu, na usimlenge Sara wala kumchukia tena. Ninaweza kufikiria kukuruhusu utoke.” Aligeuka baada ya kusema na kugeukia dirisha.
Lisa alitazama kivuli chake kutoka

nyuma. Hakuwa na huruma na asiyejali. Huyu ndiye mwanaume ambaye aliwahi kumpenda sana? Huyu ndiye mwanaume ambaye bado alikuwa akivutiwa naye hata baada ya
kurudi? Wakati huo, moyo wake ulikua mchungu sana. Hakuweza tena kuhisi kuvutiwa naye.
LISA ITAENDELEA KITABU CHA 10
ONYO: Ni marufuku kusambaza, kukopi wala kuuza kazi hii kwani endapo kama tutakubaini basi sheria itachukua mkondo wake (By: Official Dully)
 
LISA KITABU CHA NANE (10) SIMULIZI...........................LISA
KURASA....................451- 455
PRESENT: SIMULIZI ZA DULLY

Sura ya: 451
Alvin aligeuka nyuma na kuelekeza mgongo wake kwa Lisa. Lisa alipotazama kivuli chake kwa nyuma, kulikuwa na uchungu unaozunguka machoni mwake.
Shani alipiga magoti chini. “Bwana Mkubwa Kimaro, Sidhani kama Bi Jones anaweza kuwa anahusika na hili— ”
Alvin alimpiga jicho kali kabla hajamaliza sentensi yake. "Shani, wewe ni sawa na Maya. Nyote wawili mlifanya makosa sawa. Ninyi nyote ni wanachama wa ONA, lakini mnaruhusu hisia zenu kutawala matendo yenu.”
"Ninaelewa. Ndiyo maana Bwana Mkubwa ulinihamisha mwaka huo.” Shani alitabasamu kwa uchungu. "Hata hivyo, nilikuwa nikimlinda Bi. Jones kando yake kama ulivyoagiza zamani.

Kwa kweli yeye si mtu mbaya. Bwana Mkubwa, ninafanya hivi kwa ajili yako pia. Hatimaye uliweza kurudiana pamoja naye. Kama utakuwa mkatili sana na kukata hisia za pekee ulizo nazo kwake, unaweza usipate wakati mwingine baada ya hili."
“Unadhani najali kuhusu hilo? Je, aliwahi kufikiria kuhusu hisia zangu alipofanya mambo hayo? Anajua wazi Sarah ndiye mfadhili wangu. Tayari nina deni kubwa la Sarah, akidhurika Sarah ni sawa na kudhurika mimi, lakini anaendelea kunilfanya nijihisi hatia kwake tena na tena. Labda... hajawahi kunipenda hata kidogo.” Alvin akacheka vibaya.
“Bwana Mkubwa, naamini si yeye... “
Shani akakatishwa kwa ukali. "Peleka hii hospitalini." Alvin aliinua mkono wake na kumtupia Shani begi mkononi.

Shani aliangalia. Uso wake ulibadilika mara moja. " Hii ni..."
"Kidole cha Logan. Ni ahadi yangu kwa Sarah, aliniomba nimkate mkono, lakini kidole kinatosha. Hiyo ndiyo huruma ya pekee kwangu kwake.” Alvin alisema.
Shani alifungua kinywa chake na kusema kwa kusitasita, “Nilipokutana na Miss Jones mlangoni, alisema kwamba ingawa Logan ni mlinzi wake, anamchukulia kama familia yake. Nawaza tu, Bwana Mkubwa, ungejisikiaje ikiwa mtu angekata kidole cha mtu wa familia yako?"
Moyo wa Alvin ulitetemeka. Akafinya macho. " Unamaanisha nini?"
“Namaanisha huenda Lisa asikusamehe tena baada ya hili, hasa utakapogundua ukweli kuwa si yeye aliyehusika na kumteka Sarah.” Shani alitabasamu kwa

uchungu. Akainama na kuokota kidole pale sakafuni na kwenda nacho hospitali.
Alvin alisimama palepale, huku akiwa hana wasiwasi. Majira ya joto yalikuwa yanakaribia, lakini alihisi ndani yake kuwa baridi. Hapana, haiwezi kuwa. Alikuwa ni mlinzi tu. Isitoshe, ilimbidi kumfundisha Lisa somo. Kama sivyo, asingeweza kumpa Sarah maelezo.
Lisa aliletwa ndani baada ya mlango kufunguliwa na mara akasikia harufu ya damu. Kisha, akaona Logan ametupwa sakafuni kama gunia. Tayari alikuwa amepoteza fahamu. Uso wake, ambao ulikuwa na kiburi na msimamo, ulikuwa na majeraha makubwa. Mwili wake wote ulikuwa umejaa majeraha yaliyotokana na mjeledi.
Lisa alipitisha macho juu ya mwili wake wote. Hatimaye, macho yake yakatua

kwenye mkono wake. Macho yake yalipungua ghafla.
“Kidole chake...”
"Bwana Kimaro alikikata sasa hivi," mlinzi wa ONA alisema. Baada ya hapo, alifunga mlango na kuondoka.
“Sasa hivi?” Akili ya Lisa ililipuka. Sasa hivi, Alvin alikuwa humo alipokuwa akisubiri nje? Alikunja ngumi hadi kucha zikachimba kwenye nyama yake. Alvin anawezaje kuwa mkatili hivyo? Ilikuwa ni ukatili kupita kiasi! Hakuwa binadamu hata kidogo! Chozi lilidondoka kutoka kwenye jicho lake. Wakati huo, macho yake hayakuwa na joto na yalijaa chuki tu.
"Logan ... Logan." Aliita jina lake kwa upole.
Hakuna aliyejua jinsi Logan alikuwa

muhimu kwake. Alikuwa mdogo tu kwake kwa miaka mitano. Alianza kumchukulia kama kaka yake zamani.
“Bosi...” Logan alijitahidi kufumbua macho. “Kwanini uko hapa? Alvin... Alvin alikufunga wewe pia?”
"Mimi ... nimekuja kukutoa hapa," Lisa alisema kwa macho mekundu, "Lakini kidole chako ..."
“Ni sawa. Si... Si ni kidole tu?” Logan alivuta pumzi kutokana na maumivu. Baada ya muda, mwili wake ulianza kutetemeka huku macho yake yakirudi nyuma.
"Una tatizo gani?" Lisa alishtuka sana. “Mimi... nilidungwa dawa za kulevya. ”
Logan alihema kwa pumzi kubwa. "Alvin ndiye aliyefanya hivi?" Lisa

aliuliza kwa sauti ya kutetemeka.
“Hapana...Si yeye.” Logan alipiga chini ngumi kwa uchungu. "Uliponimbia kuwa nisionekane hadharani baada ya paparazi kutupiga picha kule baa, nilikuwa nikijificha ... kulingana na maagizo yako. Nilikuwa mwangalifu, lakini sikuwahi kutarajia kwamba mtu aliyekuwa akiniletea chakula angetia dawa za kulevya kwenye chakula changu. Nilipokula ndipo nikapoteza fahamu. Nilipoamka... nilijikuta nimetupwa pangoni.
“Sarah alikuwa pembeni pia. Nilianza kujitahidi kujiondoa wakati huo, lakini sikuweza, sikuwa na nguvu hata kidogo. Baada ya hapo... Alvin na wengine wakaja. Ulikuwa ni mpango."
Lisa aliogopa sana. Alijua kuwa kuna mtu alikuwa akijaribu kuwatengenezea kesi nzito ya utekaji nyara na ubakaji.

Hata hivyo, kulingana na maneno ya Logan, ilikuwa ni kana kwamba kuna mtu alikuwa amefuatilia mambo yote ya Logan na mienendo yake.
“Haya yote... lazima yaunganishwe na Sarah. Lakini... kinachotisha zaidi ni mtu anayejificha nyuma ya Sarah. ” Logan alihangaika na kusema, "Tayari ... anatulenga."
Lisa alitetemeka. "Ulimwambia Alvin kuhusu hili?"
"Nilimwambia, lakini hakuamini hata kidogo... wanafikiri ninadanganya." Logan alicheka kwa uchungu. “Bosi, wewe... Una jicho baya, ni mtu gani huyu ulichagua kwenye maisha yako?”
"Samahani. Unaweza kustahimili?” Lisa alimtazama kwa wasiwasi.
"Jambo la muhimu zaidi ni njia za

kujiokoa." Logan alikuwa akihema. "Lakini maumivu katika mwili wangu hunisaidia kukaa macho na kujidhibiti mwenyewe. Isitoshe, kifo si kitu. Nina deni kwako maisha yangu hata hivyo.”
“Usiseme zaidi. Nitakutoa hapa.” Lisa alishika mikono yake na kuapa kwa macho mekundu.
Milango ya chuma ilifunguliwa ghafla. Alvin alisimama mlangoni. Alipoona mikono yao yote miwili imefungwa pamoja, uhasama ulitanda machoni pake.
"Inaonekana hujaridhika na kukatwa kidole chako, labda tuukate kabisa mkono wako tena." Alvin alitembea kwa hatua ndefu. Akamtoa Lisa na kumkanyaga Logan kwa nguvu.
"Acha!" Lisa alishindwa kuvumilia tena akampiga ngumi Alvin.

Alvin alishikwa na butwaa na kujikongoja nyuma baada ya kupigwa. Alihisi damu yake ikichemka kifuani. Hata hivyo, uchungu aliokuwa nao haukuweza kulinganishwa na uchungu uliokuwa moyoni mwake.
“Umenipiga kwa ajili ya mwanaume mwingine?” Alvin alimkazia macho Lisa kwa hasira mithili ya simba anayetaka kwenda kumrarua adui.
"Kwa kuwa unamjali sana, nitamuua."
“Alvin, ukithubutu kumuua, nitakufa mbele yako,” Lisa alimtishia kwa hasira.
"Unampenda?" Macho ya Alvin yalikuwa kama macho ya pepo.
"Nampenda kwa kuwa yeye ni mtu muhimu wa familia yangu." Lisa alifumbua macho yake mekundu. “Katika miaka hiyo mitatu, mimi na

Pamela tulipitia magumu mengi tulipokuwa Marekani. Kama isingekuwa ulinzi wa Logan, ningekuwa tayari nimekufa. Nilimwokoa na hatari fulani hapo awali, na aliahidi kunilinda kwa miaka kumi. Katika miaka hii kumi, siwezi kumwacha afe.”
Macho ya Alvin yalipoa, lakini bado yalikuwa ya kutisha. “Kama ndivyo, kwanini ulikuwa unamshika mkono sasa hivi? Wewe ni mwanamke wangu. Sikuruhusu kushika mkono wa mwanaume mwingine yeyote.”
"Mke wako? ” Lisa alicheka, lakini tabasamu lake lilionekana kuwa baya kuliko mtu aliyekuwa akilia. "Sahau. Sikuwahi kuwa mwanamke wako tangu mwanzo. Ni Sarah ndiye mwanamke wako. Sitakuwa na ndoto za aina hiyo tena.”
Uso wa Alvin ulibadilika. “Inatosha.

Kama usingemuumiza Sarah, nisingekuwa nakutendea hivi. Wewe ndiye uliye katika makosa. Hujawahi hata siku moja kujiweka katika viatu vyangu. Hata ninashuku ... uliingia tu kwenye uhusiano na mimi ili kulipiza visasi. Kwanza ilikuwa ni kisasi kwa Lina na Ethan na sasa ni kisasi kwa Sarah na mimi.”
“Ndiyo, ninalipiza kisasi kwako. Nilikuhudumia hadi ukaridhika kila usiku.” Lisa alicheka kwa uchungu. “Sikuwahi kutaka ulinzi wako wala mali yako. Hata nilikupikia na kukipasha moto kitanda chako. Alvin Kimaro, niambie, unaweza kupata wapi mwanamke kama mimi?"
Alvin alikosa la kusema kutokana na maneno yake, lakini alichohisi zaidi ni majuto. “Maadamu unatubu kwa dhati, omba msamaha kwa Sarah, na ukishakuomba msamaha, ninaweza

kukusamehe.”
“Haha.” Logan, ambaye alikuwa amejilaza sakafuni, alicheka ghafla. “Bosi, huyu ndiye mwanaume uliyempenda? Yeye ni rundo gani la takataka?”
"Inaonekana nimekuwa mpole sana kwako." Alvin alikodoa macho kwa kutisha.
Uso mzuri wa Lisa haukuonyesha hisia. “Alvin, huna haja ya kunisamehe tena.”
"Unamaanisha nini?" Alvin alishikwa na butwaa.
“Anamaanisha nini? Bado hujaelewa?” Logan alicheka kwa kejeli. “Inamaanisha kwamba... hahitaji kuwa na wewe tena. Je, unafikiri wewe ndiwe... mwanamume pekee duniani?”

Sura ya: 452
Uso wa Alvin ulibadilika. Akamtazama Lisa bila kuyumba.
Macho ya Lisa yalikuwa kama maji ya ziwa yaliyotuama- tulivu bila mawimbi yoyote.
“Alichosema ni sawa. Ikiwa tulikuwa wapenzi rasmi hapo awali, basi ninasema hivi rasmi, Alvin, tuachane. Haiwezekani niwe na wewe tena. Haitawezekana tena. Kwa hiyo, si muhimu kama unisamehe au la.”
Alvin alimtazama mwanamke aliyekuwa mbele yake ambaye alikuwa ametulia na kujieleza. Moyo wake wenye nguvu ulitetemeka sana. Hali ya unyonge isiyoelezeka ilimfunika.
Lisa alikuwa karibu naye wakati huo, lakini ilikuwa kana kwamba kulikuwa na

milima na mito kati yao. Kwenye akili yake hakufikiria tena kutengana na Lisa. Hata Rodney alipopiga magoti mbele yake na kumsihi amwoe Sarah... Hata alipojua kuwa yeye ndiye aliyemwagiza Logan, hakuwa tayari kumuacha Lisa. alitaka tu kumtumia Logan mbuzi wa kafara.
Baada ya muda mrefu, alizungumza kwa sauti ya ukali. “Usithubutu.”
"Alvin, haukupaswa kamwe kumkata Logan kidole. Macho ya Lisa yalijawa na dharau. “Yeye ni familia yangu. Ninamchukulia kama kaka yangu. Je, umewahi kufikiria utakavyojisikia kuona mtu wa familia yako anakatwa kidole? Bora kidonda cha nyama au mfupa uliovunjika kinaweza kupona. Hata hivyo, kidole hakiwezi kuota tena! Wewe ni pepo mkatili na mtu wa ajabu. Mtu kama wewe anapaswa kuwa pamoja na Sarah maisha yako yote!”

"Katika ndoto zako!" Alvin alimfokea kama mwendawazimu. “Hata nikioana na Sarah, bado itabidi uwe mwanamke wangu. Ikiwa unataka nikuache uende, hakuna nafasi isipokuwa nife."
“Basi unaweza kufa. Mwanamume katili na mbaya kama wewe hustahili kuishi katika ulimwengu huu hata hivyo,” Lisa alianza kupiga kelele, “Familia ya Kimaro ilifanya jambo sahihi hapo awali. Ni sawa kwa mtu kama wewe kufungiwa katika hospitali ya magonjwa ya akili na kukaa humo milele. Kwanini nilikukingia kifua? Kwanini nisingekuacha tu ukafie huko?!"
Alvin alimkazia macho Lisa. Macho yake yaliyokuwa yakiwaka moto wa damu yalikuwa yakimtoka machozi. Uso wake mzuri ulikuwa umejikunja na kumfanya aonekane kichaa. Hakuwahi kufikiria kuwa ipo siku mwanamke

aliyempenda atamlaani hivyo. Alikuwa mkali sana hivi kwamba alitamani kifo chake.
Alihisi kana kwamba moyo wake ulikuwa ukivunjwa kwa nguvu na kusema, "Utathubutu kusema hivyo wakati mwingine?" Alitembea kuelekea kwake hatua kwa hatua kama mwendawazimu aliyekata tamaa.
“Nimesema kitu kibaya? Nilisema Logan alishtakiwa kimakosa na alifanyiwa njama na mtu mwingine. Kwanini hukuchunguza ipasavyo?! Tangu nilipokutana nawe, umekuwa ukinilaumu mimi kila mara na kumuomba msamaha Sarah. Sikufanya hata jambo lolote la f*cking. Acha kusema kwamba unanipenda! Nakuomba, kaa mbali nami siku zijazo. Siwezi kumudu kuishi na wewe, Alvin Kimaro!”
Baada ya kuongea hayo, Lisa alimsaidia

Logan kunyanyuka.
“Unajaribu kufanya nini?” Alvin alimtolea macho ya kejeli. "Ikiwa unataka kumwondoa, endelea kuota! Lisa Jones, kuanzia sasa mtakaa hapa milele. Ukija kwangu na kuniomba nifanye mapenzi na wewe, labda nitakuruhusu ulione jua la nje.”
"Kwa kuwa nilithubutu kuja, basi hakika nina ujasiri wa kutoka.” Lisa alicheka. “Alvin, mbona hutambui ni yupi kati ya wanafamilia wako amepotea?”
Uso wa Alvin ulikunjamana kwa mshangao. "Umefanya nini?"
“Unaweza kumpigia simu Suzie kumuuliza yuko wapi sasa hivi?” Lisa aliinua uso wake na kumkumbusha Alvin.

Moyo wa Alvin ulitetemeka. Suzie alikuwa na simu ndogo ya saa. Akaipata namba ya Suzie na kuipiga kwa haraka, lakini haikupatikana.
“Ulimfanya nini Suzie?” Macho yake yalikuwa yamejaa nia ya kuua kana kwamba anataka kumuua.
"Ninaweza kukuonyesha mahali alipo, lakini itabidi unirudishie simu yangu ili nimpigie mtu mmoja simu ya video." Lisa alinyoosha mkono wake kuelekea kwake.
Mara moja Alvin akaomba mtu alete simu yake. Lisa alimpigia Austin. Mwanamume aliyevaa kinyago usoni mwake alionekana kwenye skrini.
“Bi Jones...”
“Muache amuone mtoto,” Lisa aliamuru. Muda si muda, Austin akampa simu Suzie.

“Anko Alvin...” Suzie aliinua kichwa chake kwa tabasamu angavu. Alvin alitazama pia. Aliona haikuwa Karen Estate bali ni sehemu isiyojulikana kabisa.
“Suzie, kwanini haukwenda shule leo?” Aliuliza kwa haraka.
“Aunty Lisa alisema ananileta nicheze leo. Alimwomba Anko huyu anichukue. Anko Alvin, unaweza kumuuliza Aunty Lisa ataniijia saa ngapi? Suzie alisema kwa sauti ya kitoto, "Nimechoka sana."
“Suzie, unajua ulipo?”
“Hapana, hii ni mara yangu ya kwanza kuja hapa—”
“Mtoto mdogo, ni wakati wa kurudisha simu kwa Anko. ” Austin alimpokonya simu Suzie. Kisha akatazama kwenye

kamera huku akitabasamu.
“Bi Jones, rudi haraka. Mtoto mdogo anakuhitaji. Sijawahi kulea mtoto hapo awali, kwa hiyo sina subira sana.” Alikata simu baada ya kusema hivyo.
Alvin akamtupia simu Lisa. "B*tch, unadiriki hata kumdhuru mtoto anayekuamini kabisa! Bado wewe ni binadamu? Lazima nimekuwa kipofu kwa kuanguka katika mapenzi na wewe. ”
Simu ile nzito ikampiga kwa nguvu Lisa kwenye paji la uso. Wakati huo, kichwa chake kilikuwa kikiunguruma kwa maumivu na karibu azimie. Alishindwa hata kusimama ikabidi akae chini. Aligusa paji la uso wake, na hapo ndipo alipogundua kuwa paji lake la uso lilikuwa limevimba vibaya.

“Si ulisema mimi ni mkorofi? Kwa vile mimi ni mtu mkorofi, usipotutoa ndani ya dakika kumi siwezi kukuahidi kuwa Suzie atakuwa sawa,” Lisa alimtishia Alvin kwa ujeuri.
“Unathubutu kunitishia?” Umbo kubwa la Alvin lilimsogelea hatua kwa hatua. Uso wake mzuri ulijaa nia ya kuua.
"Ungependa kujaribu?" Lisa alimkumbusha kwa tabasamu, “Umesahau jinsi Suzie anavyokupenda na jinsi anavyopendeza anapotabasamu?”
Mwili wa Alvin ulitulia. Kwa namna fulani, alipofikiria jinsi ambavyo asingeweza kukutana tena na msichana huyo mdogo, alihisi kama mtu anaupeleka mbali moyo wake.
"Lisa Jones, kosa langu kubwa katika maisha haya ni kukupenda? Potelea

mbali! Mchukue mtu wako na mpotee!” Alvin alimzomea kwa dharau, "Lakini ngoja nikuambie hivi, baada ya kutoka nje ya mlango huu, nina njia milioni moja za kufanya maisha yako kuwa kuzimu hai."
“Kwani umeshayafanya maisha yangu kuwa kuzimu hai mara ngapi? Sioni hata kipya utakachonifanya.” Lisa alimsaidia Logan kunyanyuka, ambaye alikuwa na damu nyingi juu yake, na kutoka nje ya chumba cha chini hatua kwa hatua.
Wanachama wa ONA waliwazunguka, lakini Lisa akawafumbia macho. Alipomsaidia Logan kutoka nje ya ONA, mara polisi walifika.
“Tulipokea ripoti ya polisi saa moja iliyopita, na maelekezo ya GPS ya eneo hili kwamba kuna mtu anashikiliwa isivyo halali. Ni nani aliyetoa taarifa?”

Polisi walipofika na kuona eneo hilo, walikuwa na maumivu ya kichwa. Baada ya yote, ONA walikuwa ni watu ambao hata polisi wenyewe hawakuthubutu kuwaudhi.
"Mimi ndiye niliyewaita polisi," Lisa alisema, akiinua mkono wake. “Siku mbili zilizopita, Bi Sarah Langa Njau alitekwa nyara. Alvin alipoenda kumuokoa alimuona mtu huyu pale pangoni na Bi Njau. Alihitimisha kuwa mtu huyu ndiye mtekaji nyara mwenyewe, wakamchukua na kumleta humu kumtesa, kwa hivyo nikapiga simu polisi. Baada ya yote, kila mtu anapaswa kuhojiwa na kutolewa hukumu na mahakama ili kuhukumiwa, sivyo?”
"Uko sahihi, na umefanya jambo sahihi." Polisi alitikisa kichwa. Akamtazama Logan aliyekuwa ametapakaa damu. Alionya, "Hakuna mtu anayepaswa

kutoa adhabu isiyo ya kisheria kwa mwingine. Ingekuwa hivyo, ulimwengu si ungekuwa katika machafuko?”
Uso wa Alvin ulizidi kukunjamana kutokana na hasira. Hakutarajia kamwe Lisa angekuwa mjanja kiasi hicho. Kweli aliita polisi kabla?
Sura ya: 453
Mara baada ya Logan kupelekwa kituo cha polisi, angelazwa kwa matibabu na kuhojiwa tena kulingana na utaratibu wa kawaida. Si hivyo tu, angekuwa mikononi mwa polisi, hivyo Alvin asingeweza kumfundisha Logan somo.
“Nitatoa ripoti kwa polisi pia." Alvin akashuka ngazi huku akimuelekezea Lisa. “Mwanamke huyu alimteka nyara mtoto wa ndugu yangu na anakusudia kumuumiza. Tafadhali chunguza suala hili mara moja.”

"Sawa, Bi Jones na Bw. Kimaro, tafadhali tufuateni hadi kituo cha polisi," polisi walisema. Kisha, Logan alipelekwa hospitalini kwa gari la wagonjwa.
Lisa alikaa kwenye gari la polisi huku Alvin akifuata nyuma kwa Sedan iliyopangwa na ONA.
Muda si mrefu baada ya kufika kituo cha polisi, Jack alimleta Suzie.
“Habari, Bwana Polisi,” Suzie aliwasalimia polisi kwa furaha mara tu alipoingia.
"Halo, mpenzi mdogo." Polisi alikandamiza mashavu ya Suzie kwa upole.
Alvin alimtazama Jack kwa uchungu. "Nini kimetokea? Kwanini Suzie yuko na wewe? Yuko wapi yule mtu aliyekuwa

naye?”
“Unamaanisha Austin? Alikuwa anacheza na Suzie sasa hivi.” Jack akajifanya kama amechanganyikiwa.
Polisi walimtazama Alvin kwa mshangao. "“Bwana Kimaro, si ulisema kuna mtoto alitekwa nyara?” Polisi walihoji.
Jack akamuuliza Alvin, “kaka, kwanini ulisema kuwa Suzie alitekwa nyara?”
“Jack, ulikula njama na Lisa ili kunidanganya! ” Alvin alipandwa na hasira. Akashika kola ya Jack. “Mtu kama wewe anastahili kweli hata kuwa babake Suzie?”
"Anti Lisa, nini kimetokea kwenye paji la uso wako?" Sauti ya Suzie ilisikika. Alikimbia kuelekea kwa Lisa na akawa anatokwa na machozi kwa kuona paji la

uso wake.
“Niliumia nilipoanguka chini kimakosa." Lisa alinyoosha mikono, akitaka kumbeba Suzie, lakini, Alvin alimuwahi haraka na kumbeba kwanza. “Huna haki ya kumbeba. Potelea mbali!”
Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Suzie kumuona Alvin akiwa na hasira sana. Alikuwa katika butwaa kutokana na mshtuko. Kisha, akaanza kulia kwa sauti kubwa. “Sipendi unamkasirikia sana Aunty
Lisa! Unatisha sana. Sitakupenda tena.”
“Suzie, huelewi. ” Alvin aliposikia kilio cha mtoto, moyo wake ulikuwa karibu kutoka kwa maumivu.
“Najua! Wewe ndiye
uliyemuumiza Aunty Lisa usoni, sivyo? Wewe ni mkatili sana. Nenda zako!” Suzie aliendelea kupiga mabega yake.

Jack alipoona sura mbaya ya Alvin, aliingiwa na wasiwasi kuwa Alvin angeweza kumuumiza Suzie. Hapo hapo akamtoa Suzie kwenye kumbato la Alvin.
“Baba tuondoke na Aunty Lisa. ” Suzie aliufungua mkono wake mmoja ili kumshika Lisa.
"Sawa, twende." Lisa akakipapasa kichwa cha Suzie. Kisha akaondoka kituo cha polisi na Jack.
Alvin akawatazama kwa nyuma. Walikuwa kama familia ya watu watatu.
Moyo wake ulikuwa ukimuuma hadi kumziba. Kwanini Suzie hakumuelewa? Alitaka kumwokoa, lakini hakuweza kutambua wema wake na akasema hatampenda tena. Hah! Ilionekana kuwa kila mtu hakumpenda. Lisa pia alikuwa ameuliza kwanini hakufungiwa katika

hospitali ya magonjwa ya akili na kwanini hakuwa amekufa.
Je, alikuwa anachukiwa kiasi hicho?
Wimbi la uhasama lilizidi kumpanda. Alionekana kama volkano ambayo ilikuwa karibu kulipuka. Hakuna aliyethubutu kumsogelea.
Ndani ya gari, Suzie alilala kwenye kumbato la Lisa. Machozi yalimtoka. “Mama, inauma sana? Simpendi tena baba mchafu. Usiwe pamoja naye tena.”
“Ni sawa. Sijambo.” Lisa akagusa kichwa cha Suzie. “Suzie, umefanya kazi nzuri leo. Samahani kwa kukutumia.” Ikiwa angeweza, hakutaka watoto wake waone mambo machafu kama hayo.
“Ni sawa, ulifanya hivyo tu ili kumwokoa Anko Logan. Isitoshe, Anko Austin aliendelea kunitunza,” Suzie

alinong’ona.
“Nenda ukacheze na Anko Jack baadaye. Bado nahitaji kutafuta ushahidi kuthibitisha kuwa Anko Logan hana hatia.” Lisa akambusu paji la uso la Suzie. “Nitakutafuta baada ya kumaliza kazi yangu, sawa? Mm, Suzie atakuwa msichana mzuri."
“Unahitaji msaada?” Jack aliuliza.
“Hapana, nahitaji tu unisaidie kumtunza vizuri Suzie.” Lisa akatikisa kichwa. Jambo hilo lilikuwa gumu sana. Aliogopa kwamba jambo lingetokea kwa Jack pia.
"Ni kosa langu kwa kutokuwa na maana." Jack alitabasamu kwa uchungu.
“Usiseme hivyo. Nadhani una akili sana, angalau ukilinganisha na kaka yako,”

Lisa alisema kwa dhati.
“Una hoja hapo. Kwa kweli sielewi jinsi Sarah alivyomroga.” Jack akahema.
Baada ya kuachana na Jack, Lisa aliwasiliana haraka na Austin. Alimtaka Austin aende kufanya uchunguzi kwenye pango ambalo kisa hicho kilitokea. Wakati akienda huko, alipita kwenye nyumba aliyokaa Logan aliposhambuliwa.
Alipofika, aliangalia picha za usalama za nyumba hiyo. Aligundua kuwa rekodi ya mtu anayesafirisha chakula akimpelekea Logan chakula chake cha jioni ilifutwa. Hakukuwa na picha kabisa kutoka saa mbili hadi saa mbili na nusu usiku.
Alitafuta picha za usalama katika maeneo ya karibu pia lakini hakukuwa na chochote. Hatimaye, ilibidi aelekeze

mawazo yake kwenye dashibodi za magari yaliyoegeshwa chini...
•••
Siku iliyofuata katika kampuni ya KIM International.
Ofisini, Alvin alikuwa akisikiliza taarifa za wasimamizi waandamizi huku akionyesha giza totoro. Hakuwa amefika kwenye kampuni hiyo kwa siku chache. Kulikuwa na mambo mengi ambayo wasimamizi wakuu walipaswa kuripoti kwake.
Hata hivyo, walikuwa wameanza kuripoti ndipo mlango wa ofisi hiyo ulipopigwa teke. Jack aliingia kwa hasira. “Alvin unamaanisha nini kusema hivyo? Unaniagiza niende Uganda kujenga kiwanda cha cement na nisirudi kabla hakijakamilika? Unatumia vibaya uwezo wako kunikomoa. Unatumia njia kama hizi za kijinga kila wakati ninapokukasirisha. Unajua wazi kuwa

siwezi kuondoka Nairobi kwa muda mrefu sana. Suzie anahitaji uangalizi wangu.”
"Mwenyekiti ... Mwenyekiti Kimaro, tutarudi baadaye." Wasimamizi wakuu walihisi kuwa kuna kitu kibaya katika hali hiyo. Walitoka nje kwa haraka huku wakiwa wameinamisha vichwa chini.
Walibaki Alvin na Jack tu kwenye ofisi kubwa.
Alvin aliikunja mikono yake kifuani. Alikuwa hana cha kujieleza. “Hustahili kuwa babake Suzie.”
“Kama sistahili, ni nani sasa awe baba yake!” Jack alicheka kwa hasira. Akasema, "Kila mtu ana haki ya kusema hivyo isipokuwa wewe."
Alvin alikodoa macho. Alimuuliza Jack kwa ukali, "Unamaanisha nini kwa hilo?" Moyo wa Jack ulirukaruka, akasema

kwa hasira. "Ikiwa una haki, kwanini mapacha wako walipotea wakati huo?"
“Thubutu kusema hivyo tena.” Alvin alisimama ghafla. Sauti na macho yake yalionekana ya kutisha kabisa.
Jack alihisi hofu ikimpiga moyoni. Alihisi kwamba Alvin alikuwa akitoa harufu ya umwagaji damu, kama mwendawazimu. Na muda wowote kingenuka!
Jack alikunja ngumi na kusema bila kuridhika, “Siwezi kuondoka sasa. Suzie ni mdogo sana. Unaweza kuagiza watu wengine kufanya hivi...”
“Kuna watu wengi wa kumtunza Suzie. Isitoshe, uko karibu sana na mwanamke huyo katili, Lisa. Sina imani kama unafaa kumlea Suzie. Ni shaka huenda kutakuwa na siku nyingine Suzie atakapokuwa mateka tena. Yeye ni mchanga na hajui chochote. Wewe ni

baba yake, lakini uliungana mkono na mtu mwingine na kumtumia Suzie kunitisha. Je, umewahi kufikiria kama Lisa angefanya uzembe, huenda Suzie angekufa wakati wowote?”
Alvin alimkodolea macho Jack. “Mimi ndiye mkuu wa familia ya Kimaro na Suzie ni sehemu ya familia ya Kimaro. Nina haki ya kuamua kila jambo linalohusiana na nyinyi nyote.”
“Wewe ni mtu wa kiburi na jeuri kweli. ” Jack alikasirika. “Kwanini unamuwazia vibaya Lisa? Kupendana naye kweli ni bahati yake mbaya.”
“Upendo?” Alvin alicheka. “Mtu kama yeye hastahili upendo wangu. Nilikuwa kipofu wakati huo. Kuanzia sasa sitaki kumuona Suzie akiwa karibu naye.”
"Ninakuambia, sitaenda Uganda" Jack akatikisa kichwa. Hakuweza kumuacha

Suzie peke yake kwenye nyumba ile. Pia alikuwa amemuahidi Lisa atamlinda Suzie na kuwaruhusu wakutane mara kwa mara.”
“Kama hutaki kwenda, basi usiwe meneja mkuu tena. Nenda ukafanye kazi kwenye madaraja ya chini,” Alvin alisema kwa ukali.
"Sawa, amua lolote unalotaka kuamua." Jack alihisi chuki na fedheha zikiendelea ndani ya moyo wake. Akageuka na kuondoka kwa hatua ndefu.
Alipofika mlangoni, alisimama na kugeuka. "Alvin, ninamchukulia Lisa kama rafiki mzuri na ninaweza kumwamini bila masharti. Lakini wewe? Yeye hulala kando yako kila usiku, lakini imani yako kwake haiwezi kulinganishwa na yangu. Si hivyo tu, hata polisi wanachunguza kesi ya

Logan kwa utaratibu wa kawaida. Wewe ndiye pekee ambaye hauko tayari kumpa nafasi ya kudhibitisha kuwa hana hatia. Wewe ni mkatili sana. Utakuja kujuta siku moja." Baada ya kuongea aliufunga mlango kwa nguvu na kuondoka bila kuangalia nyuma.
Sura ya: 454
Ofisini, Alvin alipiga meza kwa ngumi. Macho yake yalionekana kuduwaa. Je, alikuwa mkatili? Si yeye ndiye aliyemlazimisha? Alimtumia hata Suzie kumtishia safari hii. Alikuwa amemchochea kabisa.
Wakati huo simu yake iliita. Thomas alikuwa akimpigia simu kutoka hospitali. “Shemeji Kimaro, unakuja lini? Baada ya kuondoka asubuhi, Sarah hajala kabisa. Hana hata hamu ya kula. Kwa kawaida, Rodney angekuja, lakini

hatujaona hata kivuli chake siku hizi.”
"Nilikuwa na kazi katika kampuni. Nitakuja mara moja."
Alvin harakaharaka akakimbilia hospitali. Sarah alipomwona, roho yake ilipata nafuu na hata akala chakula. "Alvinic, nilisikia ... Logan alipelekwa kituo cha polisi."
“Mmh!” Mtazamo wa Alvin ukiwa mkali. “Polisi tayari wamefungua kesi. Muda ukifika, kutakuwa na kesi mahakamani.”
“Ni vizuri...” Sarah alitoa tabasamu la faraja. "Baada ya yote, haifai kutoa adhabu isiyo ya kisheria. Ni bora kesi hii ipelekwe polisi.”
Thomas alifoka, "Lakini kesi za utekaji nyara kama hizi zitapokea tu kifungo cha miaka michache jela."

“Naamini atatubu kwa moyo wote jela. Tunapaswa kutii sheria pia,” Sarah alisema kwa kujieleza kwa dhati.
Thomas akahema. "Wewe ni mkarimu sana."
Alvin alishusha macho yake chini, akiitazama sura laini na ya upole ya Sarah. Hakuweza kujizuia kufikiria sura mbaya ya Lisa.
Hakuweza kujizuia kuomboleza. Je, kweli alimpenda mtu asiyefaa? Huenda hakumpenda Sara tena, lakini angalau alikuwa mtu mwenye fadhili. Hata hivyo, alikuwa amemuumiza tena na tena kwa ajili ya mtu kama Lisa.
"Shemeji Kimaro, utakuwa wakili wa Sarah kwa kesi yake, sivyo?" Thomas alisema ghafla, “ Nina wasiwasi kwamba Lisa ataajiri wakili stadi. Itakuwa shida ikiwa Logan ataachiliwa

huru."
“Hilo halitatokea. Nitaisimamia kesi mwenyewe,” Alvin alisema kwa sauti ya chini.
“Hapo sawa. Hakuna kesi ambayo Alvinic hawezi kushinda.” Sarah aliinua kichwa chake na kutabasamu kumtazama.
•••
Usiku, katika makazi ya familia ya Kimaro.
Alvin alirudi, ingawa ilikuwa nadra kwake. Bibi Kimaro hakujisikia raha baada ya kumtazama. “Je, jua limechomoza kutoka magharibi leo? Leo umerudi? Ni nini hicho mkononi mwako?”
"Mdoli mpya zaidi wa Barbie. ” Alvin alimletea Suzie ambaye alikuwa akipata

vitafunwa. "Ninakupa hii, sawa?"
Hakuwa mtu wa kujali hisia za mtoto, lakini maneno ya Suzie jana yake yaliuumiza moyo wake. Hakuweza kulala kwa usiku mzima. Hakuelewa kwa nini alikuwa na wasiwasi juu ya binti wa Jack. Ilikuwa ni ajabu sana.
"Hapana." Suzie alimkwepa. Alikimbia hadi upande wa Bibi Kimaro na kuinamisha kichwa chake.
Bibi Kimaro alimkodolea macho Alvin na kufoka, “Ulimpokonya umeneja baba yake na kumpa kazi za chini na kumfanya kuwa kicheko, lakini bado unathubutu kuja kumfurahisha Suzie?”
"Jack alikwambia hivyo?" Uso wa Alvin ulisinyaa.
“Hapana kabisa.” Bibi Kimaro aliinua kichwa chake, akasema kwa sauti,

“Suzie aliwasikia Jack na Lisa wakijadili jambo hili. Baba yake alikukosea nini hata ukamtendea hivyo?”
Alvin alishindwa cha kusema. Hakuweza kumwambia ukweli.
"Najua, lazima iwe kama vile Aunty Sarah alisema Anko Alvin na baba yangu wana baba tofauti, hivyo Anko Alvin hampendi baba yangu,” Suzie alisema kwa uchungu huku macho yakiwa na machozi.
"Sarah alikuambia hivyo?" Maneno ya Bibi Kimaro yalibadilika papo hapo. “Ni mwanamke wa aina gani? Angewezaje kusema hivyo mbele ya mtoto? Amezidi sana.”
“Bibi...” Alvin alionekana kutoridhika.
Bibi Kimaro alisema kwa ukali, “Nilisikia kwamba umekuwa ukikaa karibu na

Sarah kila siku hospitalini hivi majuzi. Je, hukuwa na mwanamke katika maisha yako ya nyuma? Tayari amekusaliti. Kila mtu hapa mjini anazungumza juu yake. Mbona wewe ni mjinga sana?”
Alvin aliweka uso mrefu. Hakusema neno.
Mzee Kimaro aliingia kwa msaada wa fimbo yake. “Acha kuongea. Huyu mjukuu wako hawezi kuishi bila wanawake hata hivyo. Afanye chochote anachotaka. Yeye ndiye mkuu wa familia ya Kimaro sasa. Haifai mtu kusema lolote.”
“Nifanye nini tena? Ikiwa unataka kumuoa Sarah, nenda kafunge naye ndoa nje ya nchi.
Usitualike. Hatutahudhuria harusi. Inatia aibu,” Bibi Kimaro alisema kwa hasira.

“Naenda chumbani kwangu.” Alvin aliweka mdoli wa Barbie juu ya meza kabla ya kugeuka na kuondoka.
Wakati anakaribia kupanda ngazi, alisikia sauti ya Suzie kwa nyuma. "Anko Alvin, subiri."
“Suzie, nilifikiri hunipendi tena?” Alvin akageuka nyuma. Dokezo la uchungu likaangaza machoni pake.
Suzie aliuma mdomo wake, na macho yake safi yalikuwa mekundu. “Nataka tu kukuambia hivi. Siku hiyo, Aunty Lisa hakuniteka nyara. Kabla sijaenda, Aunty Lisa alikuwa ameshanieleza kila kitu. Alisema alitaka kumuokoa rafiki kwani rafiki huyo alitekwa na wewe. Hakuwa na chaguo ila kukufanya ufikiri kwamba nilitekwa nyara. Hapo ndipo ungemruhusu huyo Anko aende zake.”

"Ulijua tangu mwanzo." Alvin alishtuka. Alidhani Suzie asiye na hatia alikuwa amefichwa ukweli wa mambo.
Suzie alisema kwa umakini, “Mm, baba alisema Anko Logan ni mtu mzuri pia. Alimsaidia sana Aunty Lisa hapo awali, kwa hiyo nilitaka kumsaidia. Samahani nilikudanganya. Nataka tu kukuambia kuwa Aunty Lisa hakuwahi kuniumiza. Yeye pia hakuwahi kunidanganya. Ninampenda sana, na nitaendelea kumpenda katika siku zijazo. Ingawa mimi ni mdogo, bado ninaweza kuwatofautisha watu wazuri.”
Alvin alipigwa na butwaa. "Mtoto mdogo kama wewe anaweza kutofautisha nini?"
"Bila shaka, naweza." Suzie aliweka mikono yake kwenye kiuno chake kidogo. “Katika nyumba hii kubwa,

Anko, Grand’ma, Grand’pa, Bibi mkubwa, Babu mkubwa, na maanti wote wananipenda kikweli, lakini Babu, Babu mkubwa na Bibi yangu, na maanko na maanti kutoka upande wa baba yangu hawanipendi.”
Alvin alishtuka na kujibu baada ya muda mrefu. "Ina maana babu yako na bibi, Aunt zako na Uncle zako kutoka kwa familia ya Campos hawakupendi?"
"Ndio, Baba aliponipeleka kwa familia ya Campos, wote hawakunipenda. Kaka mwingine mkubwa hata alininyanyasa. Aliponichokoza, lakini babu aliniambia nimuombe msamaha.” Suzie aliinamisha kichwa chini na kukunja ngumi zake ndogo. “Nililelewa na Mama tangu nilipokuwa mdogo, kwa hiyo nina uwezo wa kusoma maneno ya watu.”
Moyo wa Alvin uliinama kwa uchungu, lakini hakuweza kujua ni kwanini.

“Usiende kwa familia ya Campos tena. Ikiwa umechoka, njoo unitafute.”
"Hapana. Simpendi Aunty Sarah, na najua hata mimi pia hanipendi.” Suzie alitikisa kichwa na kupunga mkono. “Kwaheri, Anko.”
Kisha, alikimbia kurudi ndani ya nyumba.
Alvin alimtazama mgongoni kwa muda mrefu na kuchukua simu yake kupiga idara ya Human Resources. "Wacha Jack aendelee kuhudumu kama meneja mkuu wa kampuni."
Meneja wa idara ya Human Resources alikosa la kusema. "Bado anahitaji kwenda Uganda kujenga kiwanda?" "Hakuna haja. Nitapanga mtu mwingine aende.”
Alvin akahema. Kwa nini Jack alikuwa na binti ambaye angeweza kumfanya

Alvin afadhaike hivyo? Iwapo angemvua Jack umeneja na kumtupa kwenye vyeo vya chini katika kampuni, Suzie angedharauliwa kama binti yake. Alvin asingeruhusu mtu yeyote kumdharau Suzie.
Hata hivyo... hakutarajia kwamba Mason Campos angemchukia sana Suzie. Suzie alikuwa ni mjukuu wake. Ni babu yupi hawakupenda wajukuu zake? Watu wa familia ya Campos walikuwa wa ajabu sana.
Sura ya: 455
Alvin aliporudi kwenye jumba lake la kifahari, Aunty Yasmine alimkaribisha kwa tabasamu. “Bwana Mkubwa Kimaro, utamrudisha lini Bibi Jones?"
Uso wa Alvin ulibadilika ghafla, lakini Aunty Yasmine hakugundua na aliendelea na tabasamu, "Nilitazama

habari siku hiyo. Uliandamana na Miss Jones nje ya nchi. Nyinyi wawili mmerudiana pamoja? Nina furaha sana nikiwaona mkiwa pamoja.”
"Tumeachana tena," Alvin alisema bila kufafanua.
Aunty Yasmine aliganda. "Kivipi..."
“Usirudie kumtaja tena huyo mwanamke siku zijazo,” Alvin alisema na kupanda ghorofani.
Baada ya Alvin kuingia chumbani, alifunga mlango kwa kishindo. Akawasha sigara na kukumbuka maneno ya Suzie. Je, ni kweli Lisa alimtumia Suzie kumtishia? Vipi ikiwa angemdhuru Suzie? Athari ya kuchanganyikiwa ilionekana machoni pake.
Kisha, Hans akaingia. “Bwana Mkubwa

Kimaro, hii ndiyo taarifa kuhusu kesi ya Logan Law.”
Alvin aliduwaa na ghafla akakumbuka kuwa aliamua kuchukua kesi ya Sarah. Ikabidi apokee taarifa husika.
Wakati huo, Lisa na yeye wangekutana mahakamani.
Kwa kuwa Lisa alimjali sana Logan Law, yeye binafsi angempeleka mtu huyo jela.
Baada ya yote, neno 'kushindwa' halikuwepo katika kamusi yake.
“Bwana Mkubwa, hujasimamia kesi mahakamani kwa miaka mingi. Mbona imekuwa ghafla? Kwa heshima zote, haijalishi ni nani atashinda kesi hii, Bi Jones na wewe mtakuwa maadui kabisa mwisho wake,” Hans alisema kwa ujasiri.
Alvin alipigwa na butwaa kidogo. Ilikuwa ni kweli kwamba ilikuwa imepita miaka

mingi tangu achukue kesi ya mwisho. Ikiwa Thomas asingezungumza hospitalini siku hiyo, labda asingechagua kwenda kortini kibinafsi. Ilibidi akiri maneno ya Thomas yalimsukuma sana kuchukua uamuzi huo.
Ndani ya moyo wake, kulikuwa na mlipuko mkali wa kuwashwa na kuudhika. Hata hivyo, alipotafakari kwa makini, alijua Lisa tayari ameshakatisha penzi lao la mwisho pale alipomtumia Suzie kumtishia.
“Inatosha, najua ninachofanya. Nenda nje,” Alvin alisema kwa ukali.
Hans alifunga mlango nyuma yake na kuhema.
•••
Nyumbani kwa Lisa huko Karen Estate.
Katika siku mbili zilizopita, Lisa alikuwa

ametingwa nyumbani na kutazama video za dashcam hadi macho yake yakawa ukungu ili kutafuta ushahidi. Kwa bahati nzuri, Pamela alikuwepo kumsaidia. Hata hivyo, iliwachosha sana hivi kwamba walikosa usingizi.
Mchana, Hans aliwapelekea makaratasi husika kwa kesi ya Logan. “Kesi imepangwa kufanyika Jumatano ijayo.
Wakili wa upande mwingine ni Alvin Kimaro.”
"Alvin Kimaro?" Pamela nusura aigeuze laptop mbele yake. “Amedhamiria kumsaidia Sarah tena, sivyo? Kila mtu nchini anajua kuwa Alvin hajawahi kupoteza kesi yoyote hapo awali. Haijalishi ni ushahidi gani uliopo, anaweza kupindua meza.”
Pamela alikumbuka jinsi Alvin alivyosimamia kesi ya Lisa kumuokoa hapo awali, kwa hivyo hakutarajia

angeenda kinyume na kumpeleka gerezani mlinzi wake aliyeaminika zaidi.
“Hatuwezi kukata tamaa,” Lisa alisema, “Kwa uso wa ushahidi kamili, wakili yeyote mwenye nguvu ana uwezekano wa kushinda. Kwa kuwa hajawahi kushindwa, safari hii ataonja machungu ya kupoteza kesi katika vita dhidi yangu.”
Pamela akampa dole gumba. “Wewe unajiamini sana!”
Hans alisema, "Kila wakili ambaye alikuwa ameenda mahakamani dhidi ya Alvin Kimaro alisema hivyo pia, lakini wote walishindwa kabisa. Hakuna uwezekano wa kushinda hata kidogo ikiwa Alvin ataenda mahakamani kwa ajili ya Sarah.”
Lisa aliinamisha macho yake. Kope zake nyeusi na nzito zilizuia mwanga

hafifu machoni pake. "Haijalishi Alvin anashangaza kiasi gani, au yeye ndiye mwenye nguvu zaidi hapa nchini. Siku zote kutakuwa na mtu mwenye nguvu zaidi yake huko nje. Ilimradi mtu huyo anaweza kupatikana na kuwa tayari kuja, niko tayari kutumia kiasi chochote cha pesa.”
“Kweli...” Hans alisita na kusema, “Alvin Kimaro aliwahi kushindana na wakili aliyeshika nafasi ya pili hapa nchini na wawili hao wakafungana. Kwa sasa, mwanasheria anayeweza kupambana naye ana zaidi ya miaka 60 na amestaafu kwa zaidi ya miaka kumi. Hataonekana hata mtu tajiri zaidi duniani atamwomba afanye hivyo.”
Lisa, akaguna. Pamela alikosa la kusema. "Kwa maneno mengine, Alvin Kimaro hashikiki kwenye uwanja wa sheria?"

"Kitu kama hicho." Hans aliitikia kwa kichwa kwa kusisitiza.
Pamela naye akanyamaza ghafla. Kwa maoni yake aliamini kwamba hata kama Alvin angefahamu kuwa Suzie na Lucas ni watoto wake na Lisa, ilionekana kwamba daima angempendelea Sarah bila masharti. Hata angekua anampenda Lisa, hakuna kitu ambachokingebadilika. Ulinzi wake juu ya Sara ulichongwa ndani ya mifupa yake.
Siku chache zilizofuata, Lisa na Austin walikuwa wanahangaika kutafuta ushahidi. Ilikuwa ni Jumanne, na siku ya kesi ilikuwa imekaribia katika kupepesa macho. Kelvin alipokuja kumtembelea, aliona macho yake yakiwa yametapakaa damu na uso wake ulionekana kuwa umepungua. Moyo wake ulikunjamana.

“Unaenda mahakamani kesho. Umepata ushahidi wowote?"
“Ndiyo.” Lisa aliyapapasa macho yake yaliyochoka. "Tulipata ushahidi fulani. Kuna nafasi ya kushinda, lakini sio kubwa."
“Oh?” Macho ya Kelvin yaliangaza kumaanisha. “Ni nini? Nina hamu sana ya kujua.”
“Sitasema sasa. Utajua kesho,” Lisa alisema kwa wasiwasi, “Lakini uwezekano wa kushinda ni mdogo sana. Baada ya yote... wakili wa upande unaopingana ni Alvin Kimaro, ambaye hajawahi kushindwa hapo awali. Kesho, badala ya kumtegemea hakimu kutamka kwamba Logan hana hatia, tunajaribu kumshawishi Alvin. Alimradi afahamu kuwa Logan alichezewa mchezo mchafu, kuna nafasi tunaweza kushinda."

"Sio lazima," Kelvin alimkumbusha, "Hata kama atatambua kuwa Logan kachezewa mchezo mchafu, itakuwa ni kushindwa kwake kwa mara ya kwanza katika taaluma yake kama wakili ikiwa atakubali. Hata akijua amekosea, kwa kuangalia tabia yake ya kiburi, ataendelea kupambana ili kushinda.”
Lisa alipigwa na butwaa na kutabasamu kwa uchungu. “Uko sahihi. Watu kama yeye wanajali sana hadhi zao machoni kwa watu, hata kama hali halisi inapingana na ukweli.”
"Lakini ... utashinda." Kelvin ghafla alimkandamiza begani mwake. “Najua umekuwa na shughuli nyingi na umechoka sana, kwa hivyo pia sijakaa bure bila kufanya kazi. Nilipata gari ambalo lilitumika kumteka Sarah. Hakukuwa na alama yoyote ya Logan ndani yake.

“Kweli?” Lisa akaketi ghafla, macho yake yakiwa yamejawa na mwanga.
“Ndiyo.” Kelvin akamkabidhi faili. “Nimeziomba mamlaka husika kulikagua gari na hata kutafuta alama za vidole. Ni bodi la gari pekee ndilo lenye alama za vidole za Logan.”
"Hiyo ni safi sana." Lisa alichukua faili na kuhisi mlipuko wa furaha. "Kwa hili, tutashinda kabisa. Kelvin asante sana. Siwezi kamwe kulipa—”
“Usiongee kuhusu kunilipa. Hisia zangu kwako zinanifanya niwe tayari kufanya lolote kwa ajili yako wewe.” Kelvin alishika mikono yake kwa upole. Macho yake yalijawa na upendo aliposema, “Ikiwa unataka kumlinda Logan, nitamlinda pamoja nawe.”
Moyo wa Lisa ulitetemeka sana.

Muda wote huo, alifahamu hisia za Kelvin kwake, lakini siku zote alikuwa amemkataa.
Wakati huo, aliguswa kabisa. Kwa kweli, alipaswa kutambua zamani kwamba alikuwa mtu ambaye alimtendea vyema zaidi. Miaka hii yote, alikuwa ameandamana naye bila malalamiko. Angeweza kumsaidia kila alipohitaji, na aliwatendea vizuri Suzie na Lucas pia.
Kwa upande wa Alvin, alimuumiza tu bila kikomo.
Alijuta ghafla. Alijuta kwamba alitambua kuwa amechelewa. "Samahani, Kelvin. Ninatambua kwamba nimefanya makosa,” Lisa alisema kwa uchungu, “Sikupaswa kumwendea Alvin tena na kurudiana naye. Ninaendelea kukuumiza mara kwa mara, lakini sitarudia tena.”
"Unamaanisha...?" Kelvin alitazama juu

kwa mshangao.
"Zamani, nilifikiria tu kumrudia Alvin na kumwacha baadaye ili aonje uchungu wa kuachwa na mpendwa wake." Lisa alisema kwa uchungu, “Lakini sikujua kwamba uhusiano kati yake na Sarah hauwezi kuvunjwa na mtu yeyote. Kwa kweli, hata kama Sarah asingemsaliti Alvin, asingeweza kuvunja uhusiano wake naye. Kwa muda mrefu, tungekuwa tumetalikiana hata hivyo. Ni sasa tu ndipo hatimaye ninaelewa kwamba mimi na Alvin tuliachana wakati huo si kwa sababu ya Sarah kuilaza akili yake bali kwa sababu anampenda sana na Sarah. Katika maisha haya, Sarah daima atakuwa kipenzi cha kwanza cha moyo wake.”
"Ni vizuri unajua," Kelvin alisema huku akitabasamu. “Ni kama vile nilivyo na wewe moyoni mwangu. Hata nikijua hutanikubali, bado nitaweka mstari wazi

moja kwa moja na wanawake wengine. Kwa maoni yangu, upendo wa kweli na uaminifu unapaswa kuwa hivi.”
"Ndio, najua ni nani anayestahili kuthaminiwa sasa." Lisa alimshika mkono Kelvin. “Asante kwa kunisubiri kila wakati. sitaki kukuangusha tena.”
“Hiyo ni nzuri.” Uso mpole na maridadi wa Kelvin uliingiwa na furaha. Alimkumbatia Lisa kwa furaha na kumzungusha huku na kule. “Lisa, nimeisubiri sana siku hii. Hii siyo ndoto tu, sivyo? Hutaniacha kwa Alvin tena baadaye, sivyo?”
“Hapana, lakini sitawaacha Sarah na kaka yake. Lazima nilipize kisasi kwa niaba ya familia ya Charity,” Lisa aliuma meno na kusema.
“Sawa, nitakusaidia siku zote. ” Kelvin alinyoosha mkono kumshika kwa nguvu,

uso wake ukiwa umejaa furaha na kuridhika.
TUKUTANE KURASA 456-460
ONYO: Ni marufuku kusambaza, kukopi wala kuuza kazi hii kwani endapo kama tutakubaini basi sheria itachukua mkondo wake (By: Official Dully)
 
LISA KITABU CHA NANE (10) SIMULIZI...........................LISA
KURASA....................456- 460
PRESENT: SIMULIZI ZA DULLY

Sura ya: 456
Saa mbili asubuhi siku iliyofuata.
Bentley nyeusi ya Alvin ilikuwa ya gari
ya kwanza kufika mahakamani. Baada
ya gari kuegeshwa, Alvin alishuka na
kumfungulia mlango wa gari Sarah.
Wakati huo huo, Thomas alishuka
kutoka kwenye kiti cha nyuma.
Mlangoni, mwandishi wa habari
mwenye macho makali akaenda mara
moja. "Alvin Kimaro, umerudiana
pamoja na Bi.
Njau? Nilisikia kwamba ulisafiri hadi
Johannesburg siku chache tu zilizopita
pamoja na Miss Jones. Wewe
unawamiliki wote sasa...?”
“Usichukue video...” Sarah aliuzuia uso
wake kwa mkono wake na kujificha
kwenye mikono ya Alvin kwa woga.
Alvin alimkodolea macho mwandishi.

"Endelea kurekodi video ikiwa haujali
kampuni yako kupotea kabisa kwenye
uso wa dunia."
Mwanahabari huyo alikumbuka ghafla
kwamba kampuni ya vyombo vya habari
iliyoripoti kuhusu kurudiana kwa Alvin
na Lisa siku chache zilizopita ilifungwa
ghafla. Miguu yake ilitetemeka na
kuondoka kwa haraka kutafuta habari
nyingine za kuripoti.
"Alvin, kesi ya leo inapaswa kuwa
faragha, sawa?" Sarah alisema kwa
woga na wasiwasi, “Sitaki habari za
kutekwa nyara kwangu zienee...”
“Ni kesi ya faragha hata hivyo,
haitakuwa na watazamaji baki. Usijali,
habari zake hazitaenea.” Alvin
akampiga bega taratibu.
Wakati huo, gari jingine lilipita na
kuegesha karibu na Bentley la Alvin.

Kisha, Lisa, Pamela, na Austin
wakatoka nje ya gari. Sarah alipomuona
Lisa, aliogopa sana na mara moja
akajificha mikononi mwa Alvin akiwa na
uso uliopauka.
Alvin alifikiri kwamba alikuwa
akikumbuka mambo yale ya kutisha
tena na hakuweza kujizuia kumtazama
Lisa. “Nilifikiri usingethubutu kuja.”
“Kwanini nisingethubutu? Nina dhamiri
safi.” Lisa alimtazama Sarah aliyekuwa
amebebwa mikononi mwake bila
viwimbi machoni mwake. Alikuwa
amepitia baadhi ya mambo baada ya
kuyatafakari.
"Ni aibu kwamba hakika utapoteza
ingawa uko hapa." Thomas alicheka
kwa ujeuri. “Alvin Kimaro ndiye
anayeshughulikia kesi ya Sarah leo.
Yeye ndiye wakili bora zaidi nchini na
hajawahi kushindwa.”

“Hiyo si lazima iwe kweli. Labda leo ndio
siku ambayo rekodi yake ya unbeaten
inakwenda kuvunjwa kama Yanga na
Ihefu?" Lisa alitabasamu kwa utulivu.
Thomas alikoroma kwa kicheko. "Ni
wakili gani anayekusimamia mpaka
unajiamini sana kisi hicho?"
Lisa alitazama nyuma yake na ghafla
akatabasamu. "Bwana Nelly,
nitakutegemea."
Alvin na wengine waligeuka kutazama
na kumwona mzee wa makamo
mwenye kichwa kinachong'aa akitoka
kwenye gari aina ya Santana.
“Unamaanisha yeye...?” Pembe za
mdomo wa Thomas zilitetemeka. Alifikiri
kwamba Lisa angetafuta wakili wa
angalau kiwango cha Alvin huko Nairobi

au nje ya nchi, lakini aliishia kupata
wakili asiyejulikana ambaye alikuwa
mfupi na alionekana maskini. Jamani,
mtu huyo hata alikuwa akiendesha
Santana ambayo ilikuwa na thamani
ndogo sana. Je, hakuwa na uwezo kiasi
gani?
“Ndiyo, huyu ni Bw. Nelly.” Lisa alipeana
mkono na mwanasheria kwa shauku.
Tabasamu la Bw. Nelly lilikuwa la
kujilazimisha sana. Wakati mstari mkali
wa macho wa Alvin ulipompita, miguu
yake ilianza kutetemeka pia.
"Mungu wangu! Umempata wapi
wakili takataka kama huyo?" Thomas
alishindwa kujizuia kuangua kicheko.
“Alvin Kimaro, angalia nguo zake.
Nadhani ni mitumba iliyotumika Ulaya.
Hata soli za viatu vyake vya ngozi
zimechubuka. Tumbo langu litauma
kutokana na kucheka huku.”

Alvin naye alikunja uso na kumtazama
kwa kina Lisa. “Huyu ndiye wakili
anayemtetea Logan?”
Lisa alitabasamu bila kusema lolote
mwanzo mwisho. Aliwatazama tu kwa
utulivu.
Thomas alipomaliza kucheka, alifuta
machozi machoni pake na kusema,
“Bw. Nelly, nikikuuliza, alitumia kiasi
gani kukuajiri?”
"Si nyingi, karibu dola 2,000," Bw.Nelly
alisema, kwa aibu.
“Ajabu! ” Thomas kwa mzaha alimpa
dole gumba Lisa. “Lisa, najua umekata
tamaa ya kushinda kwa sababu
unashughulika na wakili msomi Alvin
Kimaro, lakini si unamuonea huruma
Logan Law? Mbona hauko tayari
kutumia pesa nyingi kidogo zaidi kuajiri

wakili bora. Dola 2,000, tsk. Ikiwa
unasitasita, ningekukopesha pesa,
kuliko kuangukia kwa wakili wa hali ya
chini kama huyo.”
“Umeelewa vibaya.” Lisa alitabasamu
kwa unyonge. "Nilifikiria tu kuwa
kushughulika na wakili kama Alvin
Kimaro, hakuna haja ya kuajiri mtu wa
gharama kubwa sana. Baada ya yote,
tutashinda hata hivyo, haijalishi yeye ni
nani.”
"Nini? Nasikia vitu au bado unaota?
Unajiingiza katika mawazo yako.”
Thomas alicheka. "Alvin Kimaro,
anasema kwamba wakili mbovu kama
huyu hapa anaweza kukushinda."
“Ota ndotoni,” midomo myembamba ya
Alvin ilitamka maneno hayo mawili bila
huruma. Machoni mwake, Lisa alikuwa
tayari amekata tamaa.
Hata hivyo, alielewa hali hiyo. Ilikuwa ni

kawaida kwa watu kukata tamaa
wanapokuwa wanamkabili kama
mpinzani wao.
"Unaweza kuridhika sasa," Pamela
alidhihaki, "Kesi itakapokwisha, watu
katika ulimwengu wa nje wataanguka
sakafuni wakicheka wanapojua kwamba
gwiji huyo mashuhuri ambaye hajawahi
kushindwa alipoteza kwa wakili
aliyegharimu dola 2,000."
“Kwa kweli sielewi kwanini nyie mna
ndoto zisizo za kweli. ” Safari hii hata
Sarah alitikisa kichwa. Alimshika mkono
Alvin. “Alvin twende ndani. Tusipoteze
muda tena hapa.”
“Mmh.” Alvin alitembea na kuondoka.
Nyuma yake, Thomas alimwambia Lisa
kwa sauti ya chini, “Haiwezekani
ushinde, lakini ukipiga magoti na

kuniomba na kumuacha Pamela alale
na mimi kwa usiku kadhaa, naweza
nikamsihi dada yangu ampunguzie
Logan. kifungo cha miaka michache.”
“F*ck off,” Lisa alitema mate pembeni
kwa hasira.
Pamela alimlaani moja kwa moja,
“Kipande cha takataka kama wewe
unataka mwili wa thamani kama huu?
Potelea mbali. Hustahili hata kushika
viatu vyangu.”
"Pamela Masanja, nitakufanya ujute
mapema au baadaye."
Thomas alitabasamu vibaya. "Hata
hivyo, nilisahau kukuambia, kidole cha
Logan kililiwa na mbwa. Ni kwa sababu
Shemeji Kimaro anamjali sana Sarah.
Sarah alipoomba kidole cha Logan,
Bwana Kimaro alikikata na kukipeleka
bila neno lolote. Mbwa alikula kana
kwamba ni kipande cha soseji. ”

Lisa alitazama juu. Hali ya joto machoni
mwake ilishuka ghafla hadi kiwango cha
baridi, na ngumi zake zikakunjamana
kwa hasira.
Thomas aliona na akacheka kabla ya
kuondoka.
"Mwana wa b*tch!" Pamela alilaani.
“Mapema au baadaye, nitawafanya
ndugu hao waishi maisha mabaya zaidi
kuliko kifo.”
"Ndio," Lisaalijibu kwa sauti ya chini.
Alikuwa na mawazo sawa.
Sura ya: 457
Kesi ilianza rasmi. Logan alitolewa nje.
Baada ya kutibiwa hospitalini kwa siku
kadhaa alikuwa na hali bora kidogo.
Hata hivyo, bado alijikunyata
alipotembea na mkono wake ulikuwa
umefungwa kwa bendeji nene.

Uso wa Austin ulibadilika. Alikuwa
anakaribia kuinuka lakini Lisa
alimkandamiza begani huku
akimwangalia.
Austin akauma meno yake kwa hasira
na kukaa chini.
Hakimu alitazama kila mtu na kugonga
meza, na kutangaza kuanza kusikilizwa
kwa kesi. “Mlalamikaji, Sarah Njau,
anamshutumu Logan Law kwa kumteka
nyara mnamo tarehe 28 mwezi huu.
Mshtakiwa ana nini cha kusema?"
Bw. Nelly akasafisha koo lake na
kusimama chini ya macho ya umati ya
watu ya ajabu na ya kuudhi. “Mshtakiwa
anakana hatia. Mshtakiwa alichezewa
njama."
Alvin alisimama, sura zake za
kupendeza na kuvutia zikionekana nzuri
isiyo na kifani. “Mheshimiwa, hizi ni

shuhuda za mashahidi watatu
waliokuwa kwenye pango wakati huo.
Wote walishuhudia nia ya Logan Law
kumshambulia Bi. Sarah Njau. Ikiwa
tusingemzuia kwa wakati, matokeo
yangekuwa yasiyowezekana.

Hakimu alisoma shuhuda na kutikisa
kichwa. "Kwa kweli huu ni ushahidi wa
kutia hatiani."
Bw. Nelly alisema kwa haraka, “Tuna
ushahidi mkononi kwamba mteja wangu
alitengenezewa njama. Mheshimiwa,
mteja wangu alisema kwamba usiku
kabla ya tukio, alikuwa peke yake katika
nyumba yake na aliagiza chakula
kutoka nje. Alizimia baada ya kula
chakula hicho na baadaye kuzinduka
pangoni.
"Kwa mujibu wa Logan, tuliangalia
kamera za uchunguzi wa nyumba

anayoishi lakini kwa bahati mbaya,
picha zote ndani ya nusu saa baada ya
mtu aliyempelekea chakula kuwasili,
zilifutwa."
Alvin alidhihaki, “Pengine ulizifuta picha
wenyewe ili kufanya mambo kuwa
magumu.”
"Tuna ushahidi zaidi." Bw. Nelly
aliwasilisha picha za uchunguzi. "Hii ni
picha ya dashcam ya gari tulilopata
kwenye maegesho ya ghorofa ya chini
mali ya mtu fulani katika jamii. Saa 8:20
usiku wa tarehe 28 walionekana watu
wawili wakiwa wamebeba begi kubwa
na kupita sehemu ya maegesho. Mteja
wangu alisema kwamba mmoja wao ni
mtu aliyempelekea chakula.”
Wafanyakazi wa mahakama walicheza
picha hiyo. Katika eneo la maegesho
yenye mwanga hafifu, watu wawili
walioonekana kuwa na shaka walikuwa

wamebeba begi kubwa kwenye sehemu
ya gari.
Bw. Nelly alisema, "Mkoba huu
unaweza kutoshea kumbeba mteja
wangu kikamilifu."
Macho ya Alvin yaliganda kidogo.
Kando yake, macho ya Sarah yalimtoka
kwa hofu huku akiushika mkono wa
Alvin bila kujijua.
"Alvin, tutapoteza?"
Sarah alipiga piga nyuma ya mkono
wake na kuinuka bila haraka. “Mjinga!
Ulisema kwamba kuna mtu alibebwa
ndani ya begi hili kubwa, lakini hayo ni
mawazo yako tu. Hakuna ushahidi wa
moja kwa moja wa kuthibitisha hilo.”
Hakimu aliitikia kwa kichwa. "Nakubali.
Wakili wa utetezi, una ushahidi
mwingine wowote?”

“Ndiyo, kuna mengi,” Bw. Nelly alitikisa
kichwa na kusema, “Tulipata wakulima
kadhaa wa eneo hilo karibu na pango.
Kuna mashahidi ambao walisema
kwamba asubuhi hiyo mapema,
kulikuwa na watu wawili walioonekana
kuwa na shaka wakitembea kuelekea
mlimani. Walisema Bi Sarah Njau
alikuwa akitembea nyuma yao.
Hakutekwa nyara.”
“Unaongea upuuzi...” Sarah alisimama
kwa hasira na ghadhabu. “Umeenda
mbali sana! Ni wazi mimi ndiye
niliyetekwa, lakini unanitukana hivi.”
"Mshtaki, nyamaza." Hakimu alibisha
hodi na kumwonya Bw. Nelly kwa
kukunja uso, “Wakili wa utetezi, una
ushahidi wa kuunga mkono maneno
yako?”
“Kunao— ”

Bw. Nelly alikuwa bado hajamaliza
kuzungumza. Hata hivyo, Alvin ghafla
alisema kwa ukali, “Bw. Nelly, ulisema
kwamba mashahidi waliona tukio hili
asubuhi na mapema lakini nakumbuka
kwamba anga ya asubuhi siku hizi huwa
na ukungu, sembuse msituni ambapo
tukio hilo lilitokea. Ulisema shahidi
alimwona Sarah Njau akiingia msituni
nyuma ya wanaume wawili na
hakutekwa nyara. Katika ukungu huo,
wangeweza kuona vizuri ikiwa Sarah
Njau asingekuwa amefungwa mikono
yake?”
Bw. Nelly alipigwa na butwaa kwa
muda. "Nadhani tunaweza kuwaruhusu
waje mahakamani kwanza..."
Alvin alisema kwa ukali, “Wakulima wa
ndani lazima wawe na uhaba mkubwa
wa pesa. Ingekuwa rahisi kuwanunua
kwa pesa ili kuwafanya wakubali
maungamo yao.”

“Napinga...”
Alvin alidhihaki, “Bw. Nelly, sihitaji
kukukumbusha kuwa kununua
mashahidi wa uwongo ni kinyume cha
sheria. Kwa kweli, ni ujinga kwao
kusema katika kauli zao kwamba Sarah
Njau hakuwa amefungwa na chochote.
“Mheshimiwa, tafadhali angalia mikono
ya mteja wangu. Michubuko mikononi
mwake bado ni mibichi. Alama hizi
zilitokana na kufungwa mikono yake
siku hiyo."
Alvin alinyanyua mikono ya Sarah huku
akisema, mara Sarah akajishika
mdomo. Macho yake yalikuwa mekundu
na kusababisha watu waliokuwa
mahakamani hapo kumuonea huruma.
Alvin aliendelea kushambulia kwa ukali,
akisema, “Uwe wakili au mtu, lazima

kuwe na msingi. Mteja wangu amepata
majeraha mengi wakati huu, lakini sasa,
unamaanisha kwamba alitunga njama
hizi kimakusudi. Unaenda mbali sana.”
"Ndio, ni juu kidogo." Watu katika
hadhira walinong'ona.
Lisa alimkazia macho Alvin, macho
yake mazuri yakionyesha kuchukizwa.
Pamela alikasirika. "Alvin Kimaro ni
mbaya sana. Anachochea hisia za
hakimu na kumfanya awe na maoni hasi
kuhusu Bw. Nelly. Mashahidi Austin
alijaribu sana kupata hawawezi hata
kuingia katika mahakama sasa. Kwa
ufasaha wa Alvin na wasifu wake,
nadhani hata wale walioshuhudia
wangeingia, angewafanya waonekane
kana kwamba wamehongwa na sisi.”
“Kwa bahati nzuri, Kelvin alipata
ushahidi zaidi kwa ajili yetu, au bila

shaka tungepoteza,” Lisa alilalamika.
"Kelvin bado ndiye bora zaidi. Alvin
Kimaro ni rundo la takataka.” Pamela
alikashifu.
Lisa alikunja uso kwa nguvu huku mwili
ukimsisimka.
Wakati kila mtu alipofikiri kwamba Bw.
Nelly alikuwa amepotea, alisema tena,
“Bw. Kimaro, hatujawahi kununua
mashahidi wowote. Huenda hujui, lakini
tumepata gari ambalo lilitumiwa
kumteka nyara Bi. Sarah Njau. Hii ni
Santana nyeusi, sawa?"
Bw. Nelly alichukua picha. Alvin
aliitazama na kutikisa kichwa.
Sarah ghafla alikuwa na hisia mbaya
sana.
Bw. Nelly alisema, “Tumeitaka idara ya
mwanasheria mkuu kufanya tathmini.
Cha ajabu ni kwamba kwenye siti ya

nyuma ya gari la mtekaji kulikuwa na
begi kubwa ambalo ni sawa kabisa na
lile lililopigwa picha na dashcam hapo
awali.”
Bw. Nelly aliwaruhusu wafanyakazi wa
mahakama kuleta video ya kwanza
iliyowasilishwa na kuisimamisha katika
eneo mahususi. Begi kubwa lililokuwa
limebebwa na mleta mizigo na yule mtu
mwingine kwenye fremu lilikuwa sawa
na lile begi kubwa kwenye picha ya gari.
Uso mzuri wa Alvin ulibadilika kidogo.
Vidole vyake vyembamba havikuweza
kujizuia kushika kalamu iliyokuwa juu ya
meza, na kuikamata kwa nguvu.
Bw. Nelly alisema, “Isitoshe, alama za
vidole za Logan Law zilipatikana ndani
ya begi lakini alama za vidole kwenye
vipini vya begi si za mteja wangu bali
wanaume wawili wasiojulikana.

“Kwa maneno mengine, unadai kuwa ni
Logan Law aliyemteka nyara Bi Sarah
Njau, lakini alipotekwa nyara, Bw. Law
alijazwa kwenye begi. Je, kunaweza
kuwa na mtekaji nyara kama huyo, Bw.
Kimaro? Au unajaribu kusema kwamba
hili ni jambo ambalo mteja wangu
amepanga?"
Sura ya: 458
Alvin akaminya midomo yake myembamba kwa kasi. Alijua kwamba kama wakili, Sarah angepoteza ikiwa hatazungumza.
Hata hivyo, ushahidi ulipokuwa mbele yake, ulimlazimu kuyumba.
Thomas alishauri kwa wasiwasi alipoona Alvin hasogei. “Alvin Kimaro, fanya haraka na umtetee Sarah.
Logan ataachiliwa ikiwa hautapingana naye.”

Bw. Nelly aliona hilo na kusema, “Bw. Kimaro, najua wewe ni gwiji maarufu katika ulimwengu wa sheria na hujawahi kupoteza, lakini kama ulivyosema, mawakili pia wanahitaji kuwa waangalifu. Kwa upande wa sophistry, hakika mimi ni duni kwako, lakini, kuna mambo mengi ya shaka katika kesi hii. Logan Law ni kijana tu ambaye ana umri wa miaka 21 tu. Ikiwa ataishia kwenda jela kwa hili, atakuwa amekosa miaka ya dhahabu ya maisha yake baada ya kuachiliwa. Jambo la kusikitisha zaidi ni kwamba yeye ndiye mtu aliyetekwa. Aliwekewa dawa za kulevya, akatekwa na kupelekwa pangoni.”
Maneno haya yalipozungumzwa, watazamaji walikuwa katika ghasia. Kifua cha Alvin kilimtoka. Alichosema wakili Nelly ghafla kiliangaza akilini mwake. Polisi walikuwa wakichunguza kesi hiyo, lakini yeye shutuma zote

alikuwa amezisukumia kwa Lisa bila kuwa na ushahidi wa kutosha.
Akili yake ilimtoka ghafla. Macho yake yalimtazama Lisa ambaye alikuwa amekaa kwenye upande wa watazamaji, lakini hata hakumwangalia. Alimlenga tu Bw. Nelly. Moyo wake ulijawa na hisia nyingi za kutokuwa na uhakika na kutojiamini.
Hakuwahi kuhisi hivi hapo awali.
Wakati huo, Bw. O'Neill alizungumza tena, “Hii ni ripoti ya uchunguzi wa damu kutoka hospitalini. Damu ya Logan ilipimwa kuona kuwa kama ana uraibu wa dawa za kulevya, lakini muundo wake wa damu ulionyesha kuwa alikuwa ametumia dawa mara chache sana. Yaani siku hiyo ilikuwa ni mara yake ya kwanza, lakini alipotupwa pangoni tena, alidungwa dawa kali iliyomsababishia aone maluweluwe, ndiyo maana alimvamia Sarah Njau.”

"Ngoja nione. ” Hakimu alinyoosha mkono na kuchukua ripoti ya Bw. Nelly.
Baada ya Bw. Nelly kunywa maji, alihitimisha, “Kweli, mlolongo wa matukio katika kesi hii ni rahisi sana. Logan Law alikula chakula alichokabidhiwa na mtu katika chumba chake na kuzirai. Kisha watu wawili wakambeba kwa kutumia mfuko mkubwa na kumpeleka kwenye pango na kumtia dawa. Baada ya kuamka, Bi Njau naye alikuwepo na alishindwa kujizuia.”
Hakimu alimtazama Sarah pale pale. “Mlalamikaji, bado unakumbuka kilichotokea kwenye pango wakati huo?”
Akili ya Sarah ilikuwa ikivuma. Alijua kwamba kwa ushahidi mwingi kama ule, ingekuwa ngumu kumtia hatiani Lagan. Sasa, jambo la muhimu zaidi lilikuwa ni

kuondoa mashaka yao juu yake.
“Mimi... pia nilikuwa nimezimia, na nilipoamka, nilikuwa pangoni. Nilipofungua macho yangu, niliona kuwa Logan alikuwa akijaribu...
kunivua nguo zangu.”
Thomas aliapa kwa hasira, “Kwa maneno mengine, Logan Law alikuwa akijaribu kumbaka dada yangu!”
“Wasikilizaji, nyamazeni! ” Hakimu alimpa Thomas mwangaza wa onyo. Sarah alikaribia kutapika damu. Thomas hakujua jinsi ya kuhukumu hali hiyo. Angekufa kwa sababu ya ujinga wake mapema au baadaye.
Bw. Nelly alitabasamu. "Nijuavyo, Bi. Njau na Logan Law pia wanahusiana kwa kiasi fulani."
"Hatuna uhusiano wowote. Simjui hata

kidogo. Alvin, sema kitu.” Sarah kwa wasiwasi akamvuta Alvin aliyekuwa kimya.
Thomas pia alisema, “Ndiyo, Bwana Kimaro. Ukishindwa katika kesi hii, utakuwa kituko cha kila mtu.”
Alvin alichanganyikiwa na kukaza ngumi. Alikuwa karibu kufungua kinywa chake wakati Bw. Nelly alipozungumza kwanza, “Bw. Kimaro, kwa kweli, ushiriki huu unahusiana na wewe. Unataka kusikia?”
"Inahusiana nami kivipi?" Alvin alikunja uso kwa chini ya fahamu.
“Ndiyo.” Bw. Nelly alitikisa kichwa. "Logan Law ni mlinzi wa Miss Lisa Jones. Nijuavyo, ulikuwa ulichumbiana na Miss Jones hadi siku kadhaa zilizopita na Sarah Njau ni mpenzi wako

wa zamani. Ulimshika Logan Law akijaribu kumshambulia Sarah Njau kwenye tukio hili, kwa hivyo ukafikiri kwamba ni Lisa Jones aliyemwomba Logan Law kufanya hivyo.
"Kwa hivyo, ulipandwa na hasira na ukawa na mzozo mkali na Miss Jones. Ninyi wawili hata mliachana tena. Ulikwenda kwa Sarah Njau, mwathirika, tena kwa hatia. Wakati huo huo, uliamua moyoni mwako kwamba Lisa Jones alikuwa mwanamke mwovu asiyestahili kupendwa na wewe.
“Unamaanisha nini kusema hivyo?” Sarah alisimama kwa fadhaa. “Nilikaribia kuharibiwa na mtu mwingine, lakini unazungumza kana kwamba nilimtengenezea njama Logan Law kimakusudi. Tafadhali, angalia majeraha yangu. Nilikaribia kufa. Ikiwa ningejua kwamba ningetukanwa hivi, nisingemwacha daktari aniokoe mara ya

kwanza.”
"Sarah, tulia." Thomas akamshika mara moja. “Usiwe na haraka. Mkuu, hilo haliwezekani. Dada yangu alijibamiza ukutani ili kujiua kutokana na aibu isiyovumilika. Angekufa kama asingepelekwa hospitali kwa wakati.”
"Ni bahati mbaya gani," Pamela alisimama ghafla na kusema kwa sauti kubwa, "nakumbuka kwamba mmoja wa mashahidi ni Chester Choka, daktari maarufu nchini, sivyo? Angewezaje kufa?”
Mara baada ya kutamka maneno haya, kila mtu alianza kumtazama Sarah kwa namna tofauti. Ubongo wa Alvin ulihisi kuwa karibu kulipuka.
Wazo ambalo hakuthubutu kulifikiria lilijitokeza. Je, ikiwa haya yote yalipangwa kwa makusudi na Sarah? Ndiyo, alikuwa amejaribu kujiua wakati huo, lakini Chester alikuwepo.

Haikuwezekana kwamba angekufa, lakini, sio wanawake wengi wangeweza kupanga mpango mbaya kama huo, sivyo?
“Inatosha, acha kuongea! ” Sarah alikatiza kwa kilio cha uchungu. “Unachosema ni kwamba nilitunga njama dhidi ya Logan, lakini vipi kuhusu ushahidi? Umewahi kufikiria kwamba ikiwa watu waliokuja kuniokoa wakati huo wangechelewa hata dakika moja baadaye, ningekuwa nimeharibiwa kweli? Je, ni wanawake wangapi wangethubutu kujitoa kafara ya kutokuwa na hatia na kucheza kamari na miili yao wenyewe? Hujui ni maumivu kiasi gani nimekuwa nayo hivi majuzi.”
Alilia kwa uchungu.
Hakimu alikunja uso na kumtazama Bwana Nelly kwa onyo. “Una ushahidi wa hayo uliyosema?”

“Nabahatisha tu. Baada ya yote, kuna haja ya kuamini kuwa Logan alitengenezwa, lakini ni hakika kwamba ni mtu mwingine aliyemteka nyara Bi Njau. Mheshimiwa Logan pia ni mwathirika.”
Hakimu aliitikia kwa kichwa. "Ninatangaza kwamba Logan Law hana hatia ya uhalifu. Kuhusu mtekaji nyara halisi wa Sarah Njau, nitakabidhi video na taarifa hizi kwa polisi ili kuwachunguza watu hao wawili wanaotiliwa shaka. Isitoshe, baada ya majeraha ya Logan Law kupona, atapelekwa katika kituo cha kurekebisha tabia za dawa za kulevya.”
Baada ya kusikilizwa kwa mahakama, kila mtu alipigwa na butwaa. Kila mtu hakuweza kuamini kwamba wakili asiyejulikana kama Bw. Nelly alikuwa amemshinda gwiji wa tasnia hiyo, Alvin

Kimaro.
Bw. Nelly alisisimka zaidi. "Bibi Jones, hii ni ajabu! Kweli nilimshinda Alvin Kimaro! Hahaha, ninaota?"
“Siyo ndoto, Mheshimiwa Nelly. Asante." Lisa alishukuru kwa dhati.
“Hapana, hapana, hapana, najua sikufanya lolote. Ni kwa sababu umepata ushahidi wote.” Bwana Nelly alicheka.
Wakati huo huo, Logan pia alilegea. Uso wake mzuri na mkorofi ulionekana kuwa na hisia. "Bosi, hakuna kitu kingine cha kusema. Nitaishi kama msaidizi wako kwa maisha yangu yote. Hata roho yangu itakuwa yako.”
Austin akacheka. “Ndio. Bosi alilala chini ya saa tatu kwa siku tano mfululizo

kwa sababu yako.”
"Asante." Macho ya Logan yalikuwa mekundu.
"Hapana, badala yake ningesema samahani." Macho ya Lisa yalitua kwenye kidole chake kilichokosekana na hatia kubwa ikazidi machoni mwake. "Kama singekuwa mimi, usingelengwa mara ya kwanza."
“Hiyo ni kawaida. Ninajilaumu tu kwa kutokuwa makini sana.” Logan akatabasamu kwa uchungu. "Niligundua kitu wakati ulionyesha picha sasa hivi. Migongo ya wateka nyara hao wawili ilikuwa sawa na wale wanaume waliohusika na kifo cha Hisan Ghadaffi siku ile.”
Lisa alipigwa na butwaa. "Inaonekana ni kundi moja la watu. Ni aibu kwamba

bado hatujawafichua watu nyuma ya Sarah.”
"Lazima tuchukue hatua moja baada ya nyingine." Logan alifoka. “Jeraha langu linauma kupita kiasi. Nitarudi hospitalini.”
“Rudi baada ya kupata nafuu,” Lisa alimkumbusha kwa sauti ya chini. “Ndio. Austin, mtunze vizuri bosi. Ikitokea lolote kwake, nitakufanya ulipe nikirudi,” Logan alionya kabla ya kuondoka na polisi.
Sura ya: 459
Kwa upande mwingine, Alvin alikaa kwenye kiti bila kuamini kilichotokea. Macho yake yalikuwa kwa Lisa. Kila mtu alifikiri kwamba alikuwa amekasirika kwa sababu sifa yake kama wakili asiyeshindwa ilipotea kwa sababu ya wakili mdogo.

Hii haikuwa kweli. Sio kwamba hakuwa na nafasi ya kushinda. Kwa ufasaha wake, angeweza kupata sababu ya kupingana bila kujali ushahidi ulikuwa nini. Lakini, ushahidi ulipowekwa mbele yake, aligundua kuwa Logan alikuwa ameandaliwa. Sasa ni nani aliyefanya mchezo huo mchafu? Je, lengo lake lilikuwa ni kumharibia tu uhusiano wake na Lisa ama kulikuwa na sababu nyingine?
Kwa kweli, alipaswa kuchunguza kwa uwazi tangu mwanzo. Yeye aliamini tu pale pale pangoni siku hiyo, alipomuona Logan akimshambulia Sarah na kumfanya ajaribu kujiua. Kwa hivyo, alifikia hitimisho. Baadaye, aligundua kwamba Logan alifanya kazi kwa Lisa. Isitoshe, Logan na Lisa walikuwa wamekutana kwenye baa hivi majuzi, kwa hiyo alifikiri Lisa ndiye aliyempa agizo hilo. Ilikuwa ni kwa sababu Lisa

alikuwa na nia ya kulipiza kisasi, na alimchukia Sarah na yeye.
Alisahau kuhusu kukusanya alama za vidole kwenye gari na kusahau kwamba hakukuwa na picha yoyote iliyoonyesha sura ya Logan wakati wa mchakato mzima wa utekaji nyara. Yote ilikuwa njama.
Labda Bw. Nelly alikuwa sahihi. Ilikuwa ni njama ya kuharibu kabisa uhusiano ambao Lisa na yeye walikuwa wameanzisha. Kwa kweli, haikupaswa kwenda mbali hivi. Kwanini alifanya hivi? Kwanini alimkata kidole Logan? Kwanini aliamua yeye binafsi kuchukua kesi kwa Sarah? Shani na Hans walikuwa wamesema kwamba Lisa alikimchukulia Logan kama mtu wa familia. Mwishowe, alimkata kidole cha mtu wa familia yake.
Hans alisema kwamba ikiwa

angechukua kesi ya Sarah, ingemaliza uhusiano wake na Lisa, bila kujali ni nani angeshinda. Kila hatua yake ya ukatili ilikuwa imesukuma uhusiano wao juu ya makali ya kuachana kabisa.
Lakini, hakutaka kufanya mambo haya pia. Alikuwa Sarah ambaye alisema kwamba anataka Kidole cha Logan, na Thomas ndiye alisema ni yeye pekee ndiye anayeweza kushinda kesi au Logan angeachiwa huru. Kwa hivyo, alikubali changamoto.
“Alvin twende...” Sarah kwa wasiwasi na kwa woga aliutazama uso wake mzuri ukiwa mtupu kabisa. Aliishiwa na mawazo, na kisha akawa mpole na mwenye huzuni.
Alinyoosha mkono kumshika mkono, lakini kabla hajaweza, alimkwepa. Mwili wake ukakakamaa, na Thomas haraka akasema, “Bwana Kimaro, kwa

nini uko hivi? Sarah tayari ni mnyonge sana.
Leo hajaumia vya kutosha?”
"Ndio, tayari ana huzuni sana." Alvin akatabasamu.
Alipofikiria jambo hilo kwa makini, je, Sarah alibakwa na Logan? Hapana. Badala yake, vipi kuhusu Logan? Kidole chake kilikatwa, akadungwa madawa ya kulevya ambayo hakuwahi kuyatumia hata kidogo, na mwili wake ulikuwa na makovu.
"Alvin, huniamini?" Sarah alimtazama kwa huzuni kwa uso uliopauka.
Alvin naye alimkazia macho. Huyu ndiye mwanamke aliyekuwa akimpenda. Hata kama hakumpenda tena, alitaka pia kumlinda vyema. Lakini, ghafla aligundua kuwa hakuweza kumuelewa

tena.
Tukio la Hisan lilikuwa limenyong’onyesha sana.
Kwa wakati huu, ghafla alitekwa nyara wakati Lisa na yeye walikuwa wanaendelea vizuri. Kisha, kila kitu kilibadilika. Laiti si hawa ndugu, asingemkata Logan kidole na pia asingechukua kesi hiyo. Ikiwa haya yote yalipangwa na Sarah, yangemfanya adhalilike sana.
“Sarah, kesi yako itachukuliwa rasmi na polisi kuanzia leo. Watajaribu wawezavyo kukusaidia kuwapata watekaji nyara hao wawili.
Tayari nimeachana na wewe, kwa hivyo usije kwangu tena siku zijazo. ” Alvin alishusha macho chini na kumaliza kuongea kabla ya kunyanyua miguu na kujiandaa kuondoka.
Sarah alimshika mkono na kulia, “Alvin, haijalishi kama wengine wananitilia

shaka, lakini tumefahamiana kwa miaka 20.
Je, huniamini? Mimi ni mwanamke dhaifu tu. Ningewezaje kuwa na uwezo wa kumteka nyara Logan? Uwezo wake wa kupigana ni sawa na wa Master Ganja. Isitoshe, sikujua kwamba Logan pia alitekwa nyara. Kitu cha kwanza nilichoona nilipofungua macho yangu ni yeye.”
“Hiyo ni kweli,” Thomas alisema kwa haraka, "Hata nikiharibu, mimi huharibu tu na punk ndogo ndogo. Sijawahi kugusa madawa hapo awali. Watu hawa ni dhahiri ni nguvu iliyopangwa. Nini kingetokea ikiwa wangefanikisha adhma yao juu ya Sarah tena?”
Sarah alimtazama Thomas kwa shukrani. Mtu huyu hatimaye alisema jambo muhimu.
Kichwa cha Alvin kilitikisika kwa kelele

za ndugu wale wawili. Hakuwahi kuchanganyikiwa hivyo hapo awali. Alijisikia kama alikuwa akielea katikati ya hewa, bila nguvu na mwenye hofu. Alishtuka sana alipomuona Lisa akitoka nje ya chumba cha mahakama.
“Nitatafuta mtu wa kukulinda kwa muda, lakini tafadhali usiwasiliane nami tena." Alvin aliushika mkono wa Sarah. "Sarah, lazima uelewe. Nilipoachana na wewe, nilikupa nyumba, gari, na mabilioni ya pesa taslimu. Na wewe, Thomas, nimeilinda familia yako kwa miaka mingi sana na hata kukuokoa mara kadhaa. sina deni nanyi tena.”
Uso wa Sarah ulionyesha kushindwa na ulikuwa mweupe kama karatasi. Machozi yake yalimtoka.
Lakini, Alvin hakuweza kujali. Alikuwa amechoka sana kwa sababu alitambua kwamba uhusiano wake na Sarah

ulikuwa umeharibu kabisa hisia ambazo yeye na Lisa walijenga kwa bidii.
Alvin alirudi nyuma hatua kwa hatua na kugeuka kumfuata Lisa bila kuangalia nyuma.
Kwenye korido, Pamela na Lisa walisimama wakingojea lifti.
Alvin akapiga hatua kubwa kuelekea kwa Lisa. Mwendo wake ulikuwa wa shauku, lakini kabla hajamkaribia, Austin alimzuia.
"Ondoka njiani. Nahitaji kuzungumza naye.”
Alvin alimtazama tu Lisa kwa wasiwasi. Aligundua kuwa japo siku chache tu zimepita bila kumuona, alikuwa ameshakuwa mnyonge. Macho yake yalikuwa mekundu na yakiwa na damu. Kwa kuongezea, kulikuwa na duru za giza chini ya macho yake. Lazima alikuwa na wasiwasi sana juu ya kesi ya

Logan na labda hakulala kwa siku kadhaa.
Moyo wake ulimuuma sana.
Alikuwa amelazimisha haya yote yatokee. Ikiwa angekuwa na imani naye zaidi, mambo yasingekuwa hivyo.
Pamela alidhihaki, “Alvin Kimaro, unawezaje kukosa aibu kuja hapa? Sarah alipomshutumu Lisa, ulikuwa mkatili na huna huruma, ukimwita mwanamke katili. Hukuwa na imani naye hata kidogo. Sasa kwa kuwa umegundua kuwa hana hatia, unataka kuja kurudiana naye tena?”
Kifua cha Alvin kiliumia kwa maneno ya Pamela. Aliutazama uso wa Lisa uliokuwa umechoka na ghafla akakumbuka kuwa siku mbili tu ziliopita, wawili hao walikuwa wakila bata huko Afrika Kusini. Macho yake angavu na tulivu, jinsi alivyokuwa akijivinjari naye mara kwa mara, na jinsi kicheko chake

kilivyokuwa kitamu... Je, yote yalibadilikaje kwa kufumba na kufumbua?
“Sorry...”
"Sio lazima useme samahani." Sauti safi na tulivu ya Lisa ilimkatisha. "Kwa sababu sitakusamehe kamwe."
"Afadhali uende kumlinda Sarah wako mpendwa," Pamela alisema kwa dhihaka, "Baada ya yote, ikiwa kitu kitamtokea, kila wakati na bila masharti utatoka mbio kwenda kumlinda,. Alvin Kimaro, machoni pako, na moyoni mwako, msimamo wa Sarah ni maalum sana. Kwa nini huwezi kukubali?”
“Kwa upande mmoja, unafikiri humpendi, lakini unataka kumlinda. Kwa upande mwingine, unataka penzi la Lisa, lakini unataka arudi kwako bila kujali jinsi ulivyomuumiza. Unafikiri unarekodi tamthilia?”

Uso maridadi na mzuri wa Alvin ulipauka. Pamela alikuwa na furaha isiyoelezeka kwa maneno yake. “Kumbe nilisikia kwa bahati mbaya kuwa ulimpa Sarah nyumba, gari na mabilioni ya pesa ulipoachana naye? Mungu wangu. Hiyo lazima iwe ada ya gharama kubwa zaidi ya kuvunja uhusiano katika ulimwengu huu. Naomba kuuliza ulimpa nini Lisa ulipoachana naye?”
“Lisa, sitafanya hivyo tena. Naapa! ” Alvin aliingiwa na hofu.
Kadri Pamela alivyozidi kuongea ndivyo alivyozidi kufahamu kuwa hakuwa akimtendea haki Lisa.
“Acha kutukana. Ahadi zako zinaniumiza. Alvin Kimaro, kaa mbali nami siku zijazo. Unachoweza kunipa si furaha; ni maumivu ambayo yananipeleka kwenye shimo mara kwa mara. Siwezi kamwe kukusamehe, kwa

hivyo usije kunitafuta tena. Unanichukiza.” Lisa aliingia kwenye lifti
bila kuangalia nyuma.
Miguu ya Alvin ilijihisi kama imefungwa mawe wakati alipokabiliana na macho yake ya chuki. Alijaribu kumsogelea lakini hakuweza kusogea.
Ni mpaka alipoondoka ndipo alipohisi mwili wake umeishiwa nguvu zote.
Hakujua jinsi alivyotoka nje ya mahakama.
Alitembea mtaani peke yake kwa muda mrefu hadi akachoka kutembea. Alikaa kwenye kiti kando ya barabara kama kikaragosi asiye na roho.
Hans alitembea na mwavuli. “Bwana Mkubwa Kimaro, kuna jua sana. Unapaswa kurudi kwenye gari kwanza."
"Hans, unafikiri atanisamehe?" Alvin alitazama mikono yake kwa huzuni. Mikono hii imemkata Logan kidole.

Alikuwa amemwomba mara kwa mara amwamini. Vipi kuhusu yeye? Alisema kwamba anampenda, lakini hakuwahi hata mara moja kumpa imani. Alijaribu kumfungia Logan na yeye kwenye chumba cha chini pia.
Ikiwa Lisa asingemtumia Suzie kutoroka na Logan, labda asingeweza kutambua ukweli.
Haishangazi aliuliza kwanini hakufungiwa katika hospitali ya magonjwa ya akili na kwa chuki nyingi. Angewezaje kuwa kipofu hivyo? Ndiyo, imekuwaje akawa kipofu hivyo? Je, alipatwa na kichaa gani cha kumuumiza mwanamke aliyempenda namna hiyo?
Hans aliitazama sura ya Alvin isiyo na matumaini na kugundua kuwa ilikuwa ni mara yake ya kwanza kumuona Alvin hivi. Ni kana kwamba alikuwa amepoteza hazina yake aipendayo sana

na alikuwa amepotea. Sura ya: 460
"Bwana Mkubwa, unapaswa kusahau kuhusu Miss Jones na kufanya mambo yako tofauti." Hans alihema moyoni mwake.
Alikuwa amemwonya bosi wake huyo mkaidi usiku huo, lakini kwa bahati mbaya, hakusikiliza. Alvin alimwamini Sarah kupita kiasi. Alijuta sasa, lakini hapakuwa na dawa ya majuto duniani.
“Nimsahau?” Alvin ghafla akainua macho, akainuka na kumshika kola Hans. Alionekana kama simba ambaye alikuwa karibu kuanguka. “Nitamsahau vipi?! ”
“Ulipomsaidia Bi. Njau katika kesi yake, si tayari umeacha kufikiria maisha ya baadaye na Miss Jones? Katika hali hiyo, ulipaswa kuwa tayari umejiandaa

kiakili muda mrefu uliopita, "Hans alimkumbusha.
Alvin aliganda. Sauti ya Hans ilikuwa kama kofi kali usoni mwake.
Ndiyo, hapo awali alikuwa ameamua kutompenda Lisa tena, kwa nini asimwache aende zake sasa? Kwa nini ahisi kama maelfu ya mchwa walikuwa wakiutafuna moyo wake?
Hans aliendelea, “Je, unamuonea huruma Bi Jones? Lakini kwake, msamaha bora ni kuacha kumsumbua. Yuko sawa. Kama asingekuwa karibu nawe, labda asingeumia sana.”
“Hans...” Alvin alimkazia macho. Hakuwahi kufikiria kuwa Hans angekuwa na ujasiri wa kumwambia jambo kama hilo.
“Bwana Mkubwa Kimaro, samahani. Labda nimejikwaa maneno yangu leo."

Hans alitabasamu kwa uchungu. "Kama mtazamaji, nadhani Bi Jones anasikitisha sana. Kabla ya kuachana naye mara ya mwisho, Maya alimvua nguo mbele ya Roy na wengine. Uliweza kukabiliana na Maya na kumfanya Miss Jones ahisi kuguswa kidogo, lakini tukio hili la utekaji nyara limeharibu matumaini yake. Ulimwomba akusamehe, lakini atakabiliana vipi na Logan na kidole chake kilichopotea katika siku zijazo?"
"Ndio, aliniambia mwenyewe kwamba kidole hakiwezi kukua tena."
Alvin alitabasamu kwa huzuni huku akirudi nyuma hatua mbili. Akageuka kuondoka.
“Bwana Mkubwa ...” Hans alitaka kumfuata.
Alvin alisema kwa uchovu, “Nenda. Nataka wakati wa utulivu peke yangu."

•••
Katika gari, Pamela alipiga kelele kwa furaha, "Lisa, unafikiri Alvin Kimaro atamtilia shaka Sarah wakati huu?"
"Sina hakika, lakini nadhani Sarah atajaribu kila kitu kujiondoa tuhuma." Lisa hakuwahi kuthubutu kumdharau Sarah.
"Hiyo ni kweli. Nilidhani ulimshinda Alvin kabisa mara ya mwisho, lakini ni nani angetarajia aje na kesi ya utekaji nyara?” Pamela alibofya ulimi wake. "Alvin hakika anajuta hivi sasa. Nadhani atakuja kukutafuta tena. Hukuiona sura yake tulipotoka mahakamani. Majuto na huzuni machoni pake ... Hehe, anatia huruma sana."
"Kwa bahati mbaya, haijalishi anatia huruma kiasi gani, kidole cha Logan bado hakipo." Lisa hakuweza kujizuia kuinua vidole vyake vyema na

vyembamba.
Pamela alipoona hivyo moyo wake ukaingiwa na huzuni. "Ni sawa. Hivi karibuni au baadaye, tutashughulika na Sarah na kaka yake.
“Unapaswa kuwa mwangalifu,” Lisa alimkumbusha, “Sarah anaweza kuwa kichaa. Alijaribu hata kujiua ili kupata imani ya Alvin. Mwanamke wa aina hii anatisha."
"Ndio, nitakuwa mwangalifu sana."
Pamela aliona sura nzuri ya Kelvin imesimama nje ya jengo la nyumba ya Lisa kwa mbali. “Umeamua kweli kuolewa na Kelvin?”
"Ndio, yeye ni mzuri kwangu. Sitaki kumwangusha tena.” Lisa alilitazama sura ile na macho yake yaling’aa kwa

mwanga wa upole.
Pamela alipigwa na butwaa. Aliweza kuhisi kwamba baada ya tukio hili, Lisa alikuwa akimtendea tofauti Kelvin. Zamani, mara nyingi alipinga alipogusia tu habari zake, lakini sasa, hakuwa hivyo tena. Kelvin alikuwa amepata faida wakati huu, sivyo?
“Naam, hiyo ni nzuri. Wanaume kama yeye ni wachache sana. Lakini ikiwa Alvin atagundua, hatakutishia kutengana kama hapo awali?" Pamela aliuliza kwa wasiwasi.
“Ndiyo maana sitaiweka hadharani. Angalau, hadi tutakapopata cheti cha ndoa." Lisa alitabasamu kwa unyonge.
"Hilo ni wazo zuri. Kisha, nitasubiri kuwa mpambe wako. Nimekuwa nikiisubiri siku hii kwa muda mrefu.” Pamela alikuwa na furaha ya dhati kwa Lisa.

Lisa alipigwa na butwaa. Ndio, aliolewa hapo awali, lakini hakuwahi kufanya harusi. Kufikiria juu yake, kwa kweli alikuwa na huzuni sana. "Sawa, basi jiandae kuwa mpambe."
Gari likasimama mbele ya Kelvin, Lisa akashuka.
"Nilisikia umeshinda." Kelvin alitabasamu na kuushika mkono wake kawaida.
“Ndio. Ni shukrani kwa ushahidi ulionipa. ” Lisa alimtazama. “Nitakupikia jioni ya leo ili kusherehekea?”
"Bila shaka, tunapaswa kusherehekea." Kelvin aliinua mkono wake na kutoa pete ya almasi kutoka mfukoni mwake, akamvisha.
Lisa aliitazama pete kubwa ya almasi kwenye kidole chake cha kati na

kupigwa na butwaa. "Hii ni...?"
“Uko tayari?” Kelvin alimtazama kwa umakini. “Sitaki mambo ya uchumba wakati huu. Je, tunaweza kuoana tu mara moja?”
Lisa alipigwa na butwaa kidogo. Ingawa alikuwa ametaja ndoa na Pamela kwenye gari mapema, hakutarajia angependekeza hivi karibuni.
"Samahani, inaonekana nimekuogopesha." Kelvin alitabasamu kumtoa hofu. "Ninaogopa sana kwamba utakimbia tena."
“Sitaweza.” Lisa aliweka mkono wake chini na kutabasamu. “Sawa, nimekubali.”
“Kweli?” Kelvin alishangaa, lakini kulikuwa na tabasamu la furaha kwenye uso wake wa kifahari na mzuri.

“Bila shaka.” Lisa alinyamaza na kusitasita kabla ya kusema, “Lakini natumai hatutaiweka hadharani kwa wakati huu. Baada ya yote, unajua kwamba Alvin ana nguvu sana na mbinafsi. Ninaogopa kwamba anaweza kujaribu kukomesha ikiwa atajua kuwa tuko pamoja. Ngoja tusubiri baada ya harusi.”
“Hilo ndilo nililokuwa nikifikiria pia. Ni bora utangaze baada ya kupata mtoto,” Kelvin alisema kwa mzaha. Lisa alipigwa na butwaa na ghafla akawafikiria Lucas na Suzie.
“Usinielewe vibaya.” Kelvin alikisia alichokuwa akifikiria. “Nitawachukulia Lucas na Suzie kama wanangu, lakini napenda watoto. Bila shaka, ni sawa ikiwa hutaki...”
“Hapana, tukifunga ndoa, hakika nitapata watoto wako. Vinginevyo,

itakuwa si haki kwako." Lisa alitabasamu. Hakuwa mbinafsi kiasi hicho.
“Lisa, asante. Bado nitakusikiliza. Maadamu ni watoto wako, nitawapenda wote sawa.” Kelvin alitabasamu na kumshika mkono.
“Twende nyumbani kwako. Nina wasiwasi kwamba Alvin atakuja hapa.”
"Ndio, pia ninapanga kuhamia kwa baba yangu kwanza. Angalau ninaweza kuwa karibu na Lucas kila siku katika siku zijazo.
Alikuwa akiishi hapo kwa urahisi tu wa kumtongoza Alvin, lakini kwa kuwa hakuwa na mawazo hayo tena, haikuwa na haja ya yeye kuendelea kuishi hapo. Zaidi ya hayo, aliomba msamaha kwa kutomjali Lucas katika kipindi hicho cha wakati.

“Sawa, nitakusaidia kuhama kesho.” Kelvin alishikilia mkono wake kwenye gari.
TUKUTANE KURASA 461-465
ONYO: Ni marufuku kusambaza, kukopi wala kuuza kazi hii kwani endapo kama tutakubaini basi sheria itachukua mkondo wake (By: Official Dully)
 
LISA KITABU CHA NANE (10) SIMULIZI...........................LISA
KURASA....................461- 465
PRESENT: SIMULIZI ZA DULLY

Sura ya: 461
Usiku sana kwenye jumba la klabu. Chester alipompata Alvin, tayari alikuwa amelewa. Hata hivyo, mwanaume huyo bado alikuwa ameshikilia chupa ya kileo mkononi huku akimwaga mdomoni. “Acha pombe. Tumbo lako halitaweza kustahimili.” Chester alichukua chupa ya mvinyo.
"Nipe chupa!" Macho ya Alvin ya kileo yalikuwa mekundu kidogo. Alijipapasa kifuani kwa nguvu na sauti yake ilikuwa ya kishindo. “Ni pombe pekee ndiyo itanifanya niisiumie sana hapa. Mimi si binadamu kweli? Ningewezaje kumdhuru hivyo?”
Kulikuwa na sura ngumu katika macho ya Chester. Licha ya kumfahamu Alvin kwa muda mrefu, ilikuwa ni mara ya kwanza kumuona Alvin... akilia.
Alikuwa akilia kweli.

“Usiseme hivyo.” Chester akaketi kando yake na kuwasha sigara. "Hakuna aliyetarajia kwamba Logan angechezewwa mchezo mchafu."
"Chester, unafikiri ... haya yote yalikuwa ya Sarah?" Alvin alimuangalia kwa uchungu. "Sitaki kumshuku, lakini kama hakufanya hivyo alisema kwamba alitaka kidole cha Logan, nisingekikata. Ikiwa Thomas hangeniuliza niende kwenye kesi, nisingefika mahakamani leo. Ni kutokana na haya yote siwezi kurudi kwa Lisa.”
"Sijui pia, lakini ikiwa ni Sarah, basi jinsi anavyoficha rangi zake halisi inatisha sana. Ninaogopa sio watu wengi wanaweza kupanga kutishia kwa kutumia kifo. Lakini kwa kweli siamini kama anaweza kufanya hivyo. Sarah na Thomas hawapaswi kuwa na uwezo huo.”

Chester akashusha pumzi kubwa. Pia alikua karibu sana na Sarah na alimfikiria kama dada mdogo moyoni mwake. Katika akili yake, alikuwa mtu simple, asiye na hatia, na mwenye fadhili. Hata hivyo, mambo yote yaliyotokea pia yalimfanya aanze kushuku kuwa huenda Sarah alikuwa amebadilika.
“Kama si yeye, basi ni nani anayejaribu kumtumia Logan ili kunifanya mimi na Lisa tuachane? Ni nani angefaidika na mimi na Lisa kutengana?” Midomo ya Alvin ilipinda. Hakutaka pia kumtilia mashaka Sarah, lakini ikabidi akubali kwamba inawezekana Sarah ndiye aliyepanga tukio hilo.
Hata kama si yeye, baada ya tukio hilo, Sarah na kaka yake walikuwa wamewasha moto kwa makusudi ili kuzidisha mgogoro kati yake na Lisa.

Kwa bahati mbaya, hakuwa na akili ya kutosha kufikiria juu yake wakati huo kwa sababu alimuhurumia Sarah kupita kiasi.
"Watazamaji wanaona mchezo wa bao bora kuliko wachezaji." Alvin alitabasamu kwa uchungu. “Hapo awali, sikuelewa kwa nini Babu Derek alitaka kumzuia Rodney. Labda ni kwa sababu aliweza kuiona kwa uwazi zaidi kuliko sisi.”
"Ndio, kama Rodney angekuwa karibu, kwa hasira yake, Logan ... angeweza kupoteza maisha yake." Moyo wa Chester ulizidi kuwa baridi kadri alivyozidi kuwaza jambo hilo.
Ilionekana kana kwamba kulikuwa na nguvu nyuma ya ujanja huo. Wote watatu kwa kawaida walikuwa wastadi wa kupanga mikakati na kuitekeleza, lakini ilionekana kwamba siku zote

hawakuweza kutulia Sarah alipohusika.
"Chester, kuanzia leo... kaa mbali na Sarah." Alvin alihisi baridi ndani. "Ikiwa hii ina uhusiano wowote naye, ninahisi kuwa yeye ni mtu hatari sana."
“Hilo ni jambo unalopaswa kujishauri mwenyewe. Wewe ndiye uliye na uhusiano wa karibu zaidi naye. ” Chester akatikisa kichwa. "Kuhusu Rodney, labda hatakubali kuamini."
“Hilo ni juu yake, lakini... kuanzia leo, sitamwacha Rodney amdhuru tena Lisa...” Baada ya Alvin kuzungumza, alitabasamu kwa huzuni. "Sahau. Aliyemuumiza zaidi ni mimi.”
“Alvin, acha. Usimtafute tena.”
Chester ghafla alihisi kwamba alikuwa amepitia mengi kupita kiasi na Lisa. Ingawa hakuwa amemletea matatizo

kama Rodney, alifikiri kwamba moyoni mwake ni mwanamke mkorofi. Hasa Lisa alipojenga urafiki wa karibu na Charity. Hakumpenda Lisa hata zaidi wakati huo na alifikiria kwamba ndege wa manyoya huruka pamoja.
“Hapana, nitamuomba anisamehe. ” Alvin alishika chupa na kunywa mpaka tumbo likashindwa kustahimili maumivu makali. Alikimbilia uani na kutapika sana. Kulikuwa na hata damu iliyochanganyika kwenye nyongo.
"Shrt" Chester alitoa laana ya chini chini na kumpeleka hospitali haraka.
Daktari aligundua kuwa ni shida ya kutoboka kwa utumbo na kusema upasuaji wa haraka ulihitajika.
Hata hivyo, kabla ya upasuaji... Alvin aliuma meno na kuvumilia

maumivu makali, akairusha simu yake kwa Chester. “Tafuta namba ya Lisa. mpigie kwa simu yako.”
Walikuwa ndugu kwa miaka mingi, hivyo Chester alijua mara moja kile Alvin alikuwa akifikiria. Hata hivyo, alihisi kwamba Lisa asingeenda. Hata hivyo, kwa jinsi sura ya Alvin ilivyokuwa imebadilika rangi, alishindwa kujizuia kumpigia simu Lisa kwenye simu yake.
“Hujambo.” Sauti nyororo ya kike ilisikika.
Chester akasafisha koo lake. “Huyu ndiye Chester. Alvin alikunywa pombe kupita kiasi na kupata tundu kwenye utumbo wake. Anahitaji kufanyiwa upasuaji— ”
“Mimi sio daktari,” Lisa alimkatisha moja kwa moja na kwa kiburi.
"Alitapika damu." Chester alitabasamu

kwa uchungu. "Alvin anajuta sana sasa. Sijawahi kumuona akiteseka hivi. Je, unaweza kuja? Anakuhitaji sana.”
“Umempigia mtu asiyefaa. Nadhani anayehitajika ni Sarah. Usinipigie tena. Hata akifa, hakuna haja ya kunijulisha. Sitaleta hata maua. Baada ya yote, maua hugharimu pesa. Sitaki kupoteza hata senti moja kwa mtu kama yeye.” Lisa alikata simu moja kwa moja.
Sauti ilikuwa kwenye loudspika. Alvin alikuwa amelazwa kwenye kitanda cha hospitali, akikaribia kuzimia kutokana na maumivu. Aliposikia mazungumzo hayo, tumaini dogo lililokuwa machoni pake lilizimika taratibu, na mahali pake pakaja giza na taabu zisizo na mwisho.
Tundu la utumbo lilimuuma, lakini halikuwa na uchungu kama uchungu uliosababishwa na ukali wa maneno yake. Chester alipumua na kumwomba

daktari amsukume ndani kwa ajili ya upasuaji.
•••
Katika jumba la Joel Ngosha.
Lisa kwa kawaida aliitupa simu pembeni huku akiwa na uso usiojali. Hakuonyesha hisia zozote za kuguswa hata kidogo. Alifikiri kwamba moyo wake ungeuma kwa sababu tu kulikuwa na tundu kwenye tumbo lake? Je, alifikiri kwamba angekimbia katikati ya usiku? Alimfikiria sana kama mwanamke ambaye alikuwa na wasiwasi juu yake. Sivyo tena.
"Mama, kuna kitu kimetokea kwa baba mchafu?" Akiwa amejilaza kitandani, Lucas alifumbua macho akiwa ameduwaa.
"Ndio, una wasiwasi juu yake?" Lisa aliuliza kwa sauti ya chini.

"Hapana. Lakini unajua nini? Watu wazuri hawadumu, wabaya hayafi. Hatakufa kirahisi hivyo,” Lucas alisema kwa unyonge.
Lisa alikoroma kicheko. “Ndiyo hivyo mpenzi. Nenda kitandani mapema. Mama hajapumzika kwa siku kadhaa sasa.”
Lucas alitazama uso wa mama yake aliyelala na kufinya macho yake.
•••
Wakati huo huo, Sarah aliendelea kumpigia simu Alvin lakini hakupokea. Jibu alilopata lilikuwa ni sauti ya kiotomatiki ikimwambia kuwa simu yake ilikuwa imezimwa.
Alimpigia simu Chester, lakini hakupokea pia. Simu zake kwa Rodney pia ziliachwa bila kuunganishwa.
Alishindwa kujizuia katika jumba lake na kupiga kelele kwa hasira. Hakutarajia

kamwe kwamba katika usiku mmoja tu, mabwana watatu katika jiji kuu wote wangezisusia simu zake. Baada ya yote, siku za nyuma, wote watatu walikuwa wakimkumbatia muda wote katika viganja vya mikono yao.
Sura ya: 462
Thomas alikuwa na wasiwasi. “Sarah, tufanye nini? Ikiwa watatupuuza katika siku zijazo, itakuwa ngumu sana kwetu kupata nafasi katika jiji hili.”
“Alvin anaigiza tu kwa hasira na hataniacha. Mbali na hilo, Rodney amefungwa kwa muda tu. Familia ya Shangwe haiwezi kumfungia maisha yake yote,” Sarah aliuma mdomo na kusema.
"Lo, nilifikiri ungeweza kutumia fursa hii kurudiana pamoja na Alvin Kimaro, lakini tumeikosa.

Nani alifikiri kwamba Lisa angeshinda kesi hiyo?” Thomas alimtazama kwa makini. "Sarah, wale watekaji nyara wawili walikodiwa nawe, sawa?"
“Usiongee upuuzi. sikufanya lolote.” Sarah alimtazama kwa ukali. "Usirudie tena."
“Sawa.” Thomas alishtuka. Alikana, lakini hakuamini.
Baada ya Thomas kuondoka mara moja Sarah akapiga namba kwa hasira. “Mbona watu wako wazembe sana? Ilikuwa sawa na kesi ya Hisan. Muda huu, kulikuwa na picha za ufuatiliaji zilizosalia baada ya kuniteka nyara, na hata alama za vidole kwenye gari hazikusafishwa. Logan Law alipaswa kufungwa, lakini mahakama iliishia kumtangaza kuwa hana hatia. Hata Alvin ananishuku sasa. Unakaribia kuniua.”

“Kukuua?” Mwanaume wa upande wa pili akaachia kicheko cha chinichini. "Kwa kuwa ulikuja na mpango huo mbaya, unapaswa kuwa tayari kubeba matokeo mabaya zaidi. Utekaji nyara ulifanyika kwa hiari yako, na ulinipa chini ya nusu siku tu kupanga. Kwanini hukuweka mambo haya wazi kabla? Nilifuta picha zote za ufuatiliaji kwa mujibu wa maagizo yako, lakini siwezi kufuta dash-camera zote kwenye magari ya jumuiya.”
"Ikiwa ungeharibu gari tu, basi kila kitu kingeenda sawa," Sarah alimwambia.
“Wewe ni mjinga? Je, Alvin Kimaro angekupata vipi katika muda mfupi iwezekanavyo ikiwa gari liliharibiwa? Logan Law kweli alidungwa dawa za kulevya. Ikiwa Alvin asingefika ndani ya muda tuliopanga, ungevamiwa na Logan,” mtu huyo alifoka kwa ubaridi.

Sarah alikosa la kusema kwa muda.
Kisha, akasema, “Sarah Njau, nimekusaidia mara mbili lakini inaonekana, bado huna uwezo wa kurudiana na Alvin Kimaro. Usije kwangu tena. Huna faida kwangu— ”
“Sina faida gani? Hata kama Alvin hataki kunioa, Rodney bado anajitolea kwangu. Mara Uncle wake atakapokuwa Rais mwaka ujao, kufikia wakati huo, hadhi ya familia ya Shangwe itapanda pia.” Sarah alisema kwa haraka.
Ikiwa marafiki wale matajiri watatu hawakuwa wa kutegemewa tena, ilimbidi ahakikishe kuwa anamshikilia sana msaidizi huyu.
"Isitoshe, si ulikuwa unampenda Lisa Jones siku zote? Wakati huu, yeye na Alvin wamegeuka dhidi ya kila mmoja. Naogopa kuna hakuna njia ya wao kurudiana pamoja. Fursa yako imekuja.

Unapaswa kunishukuru,” Sarah alidhihaki.
Mtu huyo alicheka kwa sauti ya chini. “Sarah Njau, nimekusaidia mara mbili. Kwa kweli sitakusaidia tena isipokuwa unaweza kufikiria ni thamani gani bado unaweza kuniletea. Hakuna haja ya kunitisha pia. Jambo hili likifichuliwa, ninaogopa pia utapoteza sifa ya kuolewa na Rodney Shangwe. Mbali na hilo, ni rahisi sana kwangu kumfanya mwanamke asiye na nguvu kutoweka.”
Simu iliisha kwa mlio na baridi ikaujaza moyo wa Sarah.
•••
Katika jumba la kifahari jijini, Kelvin Mushi alisimama mbele ya dirisha la sebule akiwa na simu yake. Dirisha lililokuwa mbele yake lilionyesha umbo lake jembamba na lililo wima. Pajama

zake za bluu iliyokolea zilikuwa zimezungushiwa mwili wake. Uso wake msafi na mzuri ulitoa hali ya kutisha na ya kina, ambayo ilikuwa tofauti sana na mwonekano wake wa upole na wa kifahari wakati wa mchana.
Muda si muda simu yake iliita na sauti nyingine isiyoeleweka ikasikika. “Mambo yanaendeleaje?”
“Nakaribia,” Kelvin alijibu kwa heshima.
"Vizuri sana. Familia ya Kimaro imesimama juu kwa muda mrefu sana. Ni wakati wao kuanguka. Nitakungoja,” mtu huyo alisema kwa furaha, “Umefanya kazi nzuri hivi majuzi. Nina matumaini makubwa juu yako.”
"Asante." Baada ya kukata simu, macho ya joto ya Kelvin yalionyesha chuki na hasira.
Alvin Kimaro. Muda si muda,

angemburuta mtu huyo chini! Asingeweza kusahau jinsi Alvin alivyomdhalilisha mbele ya macho ya watu wakati wa sherehe ya kuzaliwa kwa Mzee Ngosha, na asingesahau pia jinsi mtu huyo alivyomnyakua Lisa kwa ukatili kutoka kwake. Alikuwa amelala chini kwa miaka mitatu, lakini, angekaa katika nafasi ya juu ya nchi hivi karibuni.
•••
Siku iliyofuata.
Lisa akiwa anaandaa kifungua kinywa
kwa ajili ya Lucas, ghafla Joel akapigiwa simu na Mzee Ngosha.
“Joel kweli umeuza hisa za kampuni. Hii ni biashara ya familia ya Ngosha ambayo mababu zetu walituachia. Nenda kwa kampuni sasa hivi. Hata kama huwezi kuja hapa kimwili, lazima utambae, wewe mwovu!”

Mzee Ngosha alifoka sana hata Lisa akasikia jikoni.
“Baba...” Alimtazama Joel kwa wasiwasi. "Nadhani Bw. Kawada alienda kwenye kampuni."
“Ni sawa. Kwa vile nilikuwa nimeamua kuziuza, nilikuwa tayari kukemewa na babu yako.” Joel alitabasamu kwa uchungu.
“Babu ana hasira sana sasa. Ninaogopa hataacha kukukemea tu.” Lisa alikunja uso.
"Jambo baya zaidi linaweza kutokea ni kunifukuza kutoka kwa familia
ya Ngosha. Sijali tena.” Joel akashusha pumzi ndefu. “Nimewatii babu na bibi zako maisha yangu yote. Hapo zamani, ni wao ambao walisisitiza niwe na Nina, jambo ambalo lilinifanya nitengane na mama yako. Upendo wa kibaba ambao

ulipaswa kuwa wako wote alipewa Melanie, lakini jambo la kipuuzi zaidi ni kwamba Melanie hata si binti yangu. Hata hivyo, babu na bibi yako bado wanawalinda Damien na Melanie. Nimetosheka na maisha haya.”
“Babu, hauko peke yako. Mama na mimi tutakuwa pamoja nawe.” Lucas aliinua uso wake mdogo mzuri na kumfariji.
“Wewe ni mvulana mzuri. Katika siku zijazo, kila kitu ambacho Babu anacho kitakuwa kwa ajili yako, mama yako, na Suzie.” Joel akatabasamu. "Nikifikiria juu ya. Nataka kuanzisha kampuni nyingine.”
“Baba, utakuwa na msaada wangu kila wakati.” Lisa alitabasamu. “Nitakwenda na wewe kwa kampuni baada ya kifungua kinywa. Baada ya yote, mimi ndiye niliyeuza hisa. Mheshimiwa Kawada lazima awe ameenda kwenye

kampuni ana kwa ana. Lazima nizungumze naye ana kwa ana.”
Saa 8:00 asubuhi, baba na binti waliendesha gari hadi Ngosha Corporation. Wawili hao walipoingia kwenye kampuni, wafanyakazi wote waliwatupia wawili hao macho yasiyo ya kawaida na ya kukasirika.
“Mtu anayesimamia Kampuni ya Ngosha anaweza kubadilika hivi karibuni. Nashangaa kama bado tutaitwa Ngosha Corporation.”
“Hiyo ina maana gani? Mnazungumza nini nyie?”
“Mungu wangu, ni tukio kubwa sana lakini bado hulijui? Leo Bwana Kawada kutoka kampuni ya Delta Co. amekuja kujitambulisha. Bwana Kawada atakuwa mwanahisa mkubwa zaidi katika siku zijazo.”

“Je, Delta Co. Ltd. haitoki Japani? Kwa hivyo kampuni yetu itakuwa kampuni inayofadhiliwa na nchi za nje katika siku zijazo?”
“Ndio. Muhimu zaidi, haiwezekani kwa Mzee Ngosha kupata tena udhibiti wa kampuni.
Hakika Kawada hatamruhusu kusimamia Ngosha Corporation. Nadhani mambo katika menejimenti ya juu yatakuwa na msukosuko.”
“Joel Ngosha lazima awe kichaa. Kampuni ya Ngosha ndio msingi wa familia ya Ngosha.”
“Hakuna utani! Wanahisa wote wameshikwa wazimu kwa hasira. Hukuwaona wakikimbia asubuhi ya leo? Wote wako kwenye chumba cha mikutano sasa. ”
Lisa alipuuza kabisa gumzo la

wafanyakazi hao na moja kwa moja akaingia kwenye chumba cha mikutano akiwa na Joel.
Chumba cha mkutano kilikuwa na kelele, na Mzee Ngosha alikuwa akimfokea Bwana Kawada, “Katika Kampuni ya Ngosha, ninachosema, huenda.
Bila ridhaa yangu, hana sifa ya kuuza hisa zake kwa mtu yeyote. Unaweza kuendelea kuota ikiwa unataka kuingia katika kampuni yetu.”
"Bwana. Ngosha, usifanye hasira. Tazama, Bi Jones na Bwana Ngosha wako hapa.” Bwana Kawada aliguna. "Ilikuwa Miss Jones ambaye alikubali kuniuzia hisa. Hata tulitia saini mkataba wa uhamisho na tayari nimetuma pesa. Ukirudisha pesa sasa, ninaweza kukushtaki kwa utapeli.”
Sura ya: 463

"Lisa Jones, unawezaje kufanya jambo kama hilo?"
Melanie alimfokea Lisa kwa hasira. "Ilichukua miaka kwa babu zetu kukuza Kampuni ya Ngosha hadi hapa lilipo, lakini uliishia kuiuza kwa mtu kutoka Japan. Je, huogopi kwamba babu zetu watatambaa kutoka kwenye makaburi yao ili kukulaani?”
“Kaka, umechanganyikiwa sana—una kichwa. Je, ulitiwa moyo na Lisa? Je, unajaribu kuwafanya Mama na Baba wafe kwa hasira? Walikupa hisa za kampuni kwa sababu walikuamini. Ikiwa hukuzitaka, ungeweza kutuambia. Tungeweza kununua hisa mikononi mwako kama wanahisa. Kwanini umewauzia wengine?” Damien alikasirika sana akataka kutapika damu. Hapo awali alidhani kwamba kwa kumtia moyo bwana mzee arudi kwenye kampuni, angeweza kurudi na kupata

udhibiti wa kampuni.
Hata hivyo, Joel aliuza hisa na Kawada akajiunga. Baada ya hapo, Kawada angeweza kudhibiti Ngosha Corporation atakavyo.
“Wewe b*tch!” Mzee Ngosha alinyakua kikombe kilichokuwa mbele yake na kumtupia Lisa usoni. Hata hivyo, ilikosa. Lisa alisogeza kichwa na kukwepa kikombe.
"Nilikosea. Sikupaswa kukukubali tena katika familia ya Ngosha. Hapo awali nilikuwa na matarajio kwako. Nilifanya nini katika maisha yangu ya nyuma hadi kubahatika kuwa na mjukuu kama wewe?!
“Mweke wazi Mheshimiwa Kawada mara moja. Mkataba ulisainiwa na wewe na hauna uhusiano wowote na baba yako. Haina uhusiano wowote na Ngosha Corporation. Sitakubali

mkataba huu. ” Mzee Ngosha alishindwa kujizuia na kuunguruma.
Lisa aliinua uso wake uliokuwa umepoa kama maji. “Babu, hukusikia alichosema Bwana Kawada? Nikizirudisha, nitakuwa nimefanya ulaghai wa kibiashara. Nitalazimika kwenda jela.”
“Ni afadhali uende jela kuliko hisa za Ngosha Corporation zianguke mikononi mwa Mjapani," Damien alisema kwa sauti nzito, "Kaka, nakushauri umshawishi vizuri. Najua nilishawahi kukuangusha, lakini mwishowe bado ni ndugu. Haijalishi tunapigana kiasi gani, sisi bado ni familia. Jina la kampuni hiyo ni Ngosha. Ukiiuza, jina la kampuni linaweza kubadilishwa katika siku zijazo. Unaweza kuvumilia kuona hivyo?"
Mwanahisa mwingine, Mkurugenzi Pan, mara moja alisema, “Ndiyo. Joel,

umefanya kazi katika Ngosha Corporation kwa miongo kadhaa. Sote tumejitahidi kukuza kampuni kufikia jinsi ilivyo leo. Sote tunafikiria Ngosha Corporation kama mtoto wetu. Fikiri kwa makini. Usifanye jambo ambalo utajutia.”
"Inabidi unilazimishe mimi baba yako nipige magoti mbele yako?" Mzee Ngosha alilia kwa kusihi.
“Baba samahani. Lisa ni binti yangu. Siwezi kumwacha aende jela.” Joel akashusha pumzi ndefu.
“Wewe...” Mzee Ngosha alikasirika sana mpaka shinikizo la damu likapanda. Alijikongoja kwa hatua kadhaa na kuzimia.
“Babu!” Melanie mara moja akakimbilia kumuunga mkono mzee huyo.
"Fanya haraka na upige gari la wagonjwa."

Joel haraka akapiga 000 na gari la wagonjwa likaja kwa haraka kumpeleka Bwana Mzee hospitali. Ni Damien pekee ambaye hakuenda kwa vile hakuweza kutembea.
Chumba cha mikutano kilikuwa na ghasia. "Kwa kuwa Mzee Ngosha amezirai, tutajadili jambo hili siku nyingine," Damien aliamuru kwa ukali na kujiandaa kuondoka mara moja.
Kawada akatabasamu kwa upole. “Samahani, lakini kwa vile nimekuja leo, sina nia ya kuondoka. Kuanzia leo na kuendelea, mimi ndiye mbia mkubwa zaidi wa Ngosha Corporation, kwa hivyo naomba mkutano wa bodi ufanyike Jumatatu ijayo. Nina haki ya kujua mambo mengi kuhusu kampuni, na mwenyekiti pia atahitaji kuchaguliwa tena.” Kisha, Bwana Kawada akaondoka moja kwa moja.

Kichwa cha Mkurugenzi Pan kiliwaka. “Damien, Kawada ni mjanja sana. Hakika si rahisi kukabiliana naye.”
“Najua. Delta Co., Ltd. ni mojawapo ya makampuni kumi bora nchini Japani. Bwana Kawada anawezaje kuwa mtu wa kawaida? Amekuwa akiitazama kampuni ya Ngosha kwa muda mrefu.” Damien aliuma meno kwa hasira. "Lisa Jones amenipa shida kubwa sana."
•••
Katika hospitali.
Mbele ya chumba cha dharura, Melanie alishindwa kujizuia kumtazama Lisa baada ya kukata simu.
“Angalia ulichofanya. Hivi sasa, Bwana Kawada alisema kikao cha bodi kitafanyika wiki ijayo. Kwa sauti yake, inaonekana anataka kuketi katika nafasi

ya mwenyekiti.”
Lisa alimsikiliza bila kujali na akampa mtazamo wa upande. “Hilo haliko wazi? Je, ulifikiri mtu kama Bwana Kawada angetaka tu kuchukua sehemu ya gawio baada ya kujiunga na Ngosha Corporation?”
“Wewe...” Melanie alikasirika. "Lisa Jones, unafanya hivi makusudi? Hiyo ni sawa. Baada ya yote, jina lako la mwisho sio Ngosha.
Hujali Ngosha Corporation ni mali ya nani. Watu wote kama wewe wanachojali ni pesa tu."
“Husemi! Hata hivyo, hata kama mimi ndiye mrithi wa baba yangu, ninyi nyote mnapenda kunipuuza na hamnitambui kabisa katika kampuni. Niliwashauri wanahisa wasifungue kampuni ya ubia na Campos Corporation, lakini nyote mlikataa kusikiliza.

Kwa hiyo, nilimshawishi baba yangu auze hisa zake. Isitoshe, je, wewe na baba yako hamkumhimiza Babu kwa bidii kuwaruhusu ninyi nyote wawili kurudi Ngosha Corporation? Kwa muda mrefu mmekula njama na wanahisa wa kampuni.” Lisa alisema huku uso wake ukiwa na tabasamu la uwongo, “Sasa mimi na baba hatupo, hatuna uhusiano tena na Ngosha Corporation. Unapaswa kuwa na furaha badala yake.”
Melanie alitaka kutapika damu. Angewezaje kuwa na furaha? Joel alikuwa na afya mbaya, hivyo muda wote Mzee Ngosha alikuwa karibu, aliweza kumshikilia Joel kwa nguvu. Hata hivyo, ikiwa Bwana Kawada alijiunga, haijalishi ni kiasi gani Babu yake alimshinikiza, Kawada asingewaelewa kiurahisi. Isitoshe, Bwana Kawada anaweza asimjali kabisa Mzee Ngosha.

“Uncle, hukuona? Babu alizimia kwa hasira sasa hivi.” Ilibidi Melanie aelekeze mawazo yake kwa Joel. “Kama Kawada atakuwa mwenyekiti wa kampuni, Babu anaweza kufa kwa hasira. Yeye ni baba yako.”
“Tayari nimeuza hisa. Na siwezi kumwacha Lisa aende jela,” Joel alijibu kwa sauti ya kawaida.
"Acha tu aende jela." Bibi Ngosha alitokea ghafla akiwa na fimbo.
“Mama...” Joel alikuwa anataka kuongea lakini bibi mzee alimpiga kofi usoni.
“Unataka kutukasirisha baba yako na mimi hadi tufe? Je, baba yako alikufanya uwe mbia mkuu wa kampuni ili tu uuze hisa zako? Alitaka uchukue jukumu la kampuni na kuifanya listawi. Joeli, ungewezaje kufanya jambo kama hilo?” Bibi mzee alimshutumu kwa

huzuni na kukata tamaa. "Yote ni shukrani kwa matarajio makubwa tuliyokuwa nayo kwako. Kama tungejua, tungekabidhi kampuni kwa Damien badala yake.”
Moyo wa Joel ulipasuka kwa simanzi. “Mama, umesahau alichonifanyia Damien? Nina na yeye —”
“Alitongozwa na Nina. Ndugu yako ni dhaifu na mwenye hisia. Hajawahi kuwa na rafiki wa kike katika maisha yake kabla ya hii. Nina alimpumbaza. Isitoshe, ana kujistahi chini na amekuwa akiteseka miaka hii yote. Je, huwezi kuelewa zaidi kama kaka?” Bibi Ngosha alisema kwa chuki.
Moyo wa Joel ulitulia, lakini Lisa hakuweza kuvumilia tena kusikia hivyo. “Damien Ngosha aliteseka, lakini si baba yangu pia aliteseka? Mke ambaye alimuoa kwa makumi ya miaka, na hata

mtoto aliyemlea hakuwa wake. Umefikiria juu ya hisia za baba yangu? Alipewa sumu inayofanya kazi polepole na hata sasa mwili wake bado haujaimarika.”
“Babu yako anajua kuwa mwili wake hauko sawa. Ndio maana alirudi kwa Ngosha Corporation katika umri wake," Bibi Ngosha alisema kwa hasira, "Kama hutaki kusimamia kampuni, ungeweza kumpa Damien hisa. Kwanini uliziuza kwa wengine? Unahitaji pesa sana?"
“Bibi, si unaelewa bado? Uncle... anadhani kwamba baada ya Babu kurudi kwenye kampuni, amekuwa akimzuia Lisa kupanda juu,” Melanie alisema kwa hasira, “Mara ya mwisho Lisa alipokuja kwenye kampuni hiyo, Babu hakumsikiliza na akakubali kushirikiana na kampuni ya Campos.” “Upuuzi! Je, Ngosha Corporation ni mali yako? Kwanini babu yako akusikilize?”

Bibi Ngosha alimkazia macho Lisa kwa chuki. “Unafikiri wewe ni nani?”
Mama...” Joel alikasirika.
"Nini? Utabishana nami kuhusu binti wa haramu?” Bibi Ngosha alishindwa kujizuia.
"Lisa si mtoto wa haramu."
“Kwa kuwa hukumuoa mama yake, ina maana yeye ni mtoto wa nje ya ndoa. Mtu wa aina hii hajastahili kuwa sehemu ya nyumba ya familia ya Ngosha. Ukisisitiza kumkubali, wewe si mwanangu tena.” Bibi Ngosha alimtishia Joel.
“Baba bado yuko kwenye chumba cha dharura, kwa hiyo sitaki kubishana nawe.” Joel alihema huku akigeuka. Alikuwa amekasirika sana hivi kwamba mwili wake dhaifu ulikuwa ukitetemeka.

"Kaa kwanza baba." Lisa alimshika kiti mara moja. “Nitashuka ili nikununulie chupa ya maji.”
Melanie alitania kwa sauti ya ajabu, “Hata Bibi bado hajaketi licha ya uzee wake. Wewe ni mzuri sana katika kupeana fadhila. Si ajabu umemfunga Anko Joel mikononi mwako.” Kisha, akageuka na kumweka Bibi Ngosha kwenye kiti.
"Una adabu sana, tofauti na mtu fulani." Bibi Ngosha akatikisa kichwa. Alichukizwa sana na Lisa.
Joel alikasirika sana hadi uso wake ukawa mwekundu. Isingekuwa ukweli kwamba kwa muda huo Mzee Ngosha alikuwa kwenye matibabu ya dharura, angeondoka bila kufikiria tena.
Haijalishi, Baba. Babu na Bibi

hawajanipenda tangu mwanzo hata hivyo, na baada ya yote, sio wao walionilea. Kwa bahati nzuri, sina nia ya kurudi nyumbani kwa akina Ngosha pia.” Baada ya kumfariji Joel, aligeuka na kushuka kwenda kumletea maji.
Sura ya: 464
Katika kata ya VIP.
Alvin alikuwa amejilaza kitandani huku akiingiziwa infusion ya sodium chloride IV (dripu). Uso wake haukuwa na hisia, na macho yake yalikuwa tupu. Kana kwamba alikuwa hajisikii kabisa kuendelea kuwepo juu ya ulimwengu huu, alionyesha hali ya kukata tamaa.
Hata ule mwonekano wa mamlaka, ukali, na ubabe aliokuwa nao haukuwepo. Wakati huo, alikuwa tu kama mtu katika akili yake mwisho.
Alipoona hali yake, Hans alimhurumia.

"Bwana Mkubwa, unapaswa kula kitu. Tangu upasuaji wako ulipoisha jana, haujala chochote. Mwili wako hautaweza kuvumilia hata kama unafaa kwa kawaida.”
Alvin akabetua midomo yake nyembamba bila kutamka neno lolote. Hakuwa hata katika hali ya kusema chochote. Hakuwahi kuuchukia mdomo wake kiasi hicho. Kwanini hakuwa bubu? Vinginevyo, asingemtupia Lisa maneno ya kuumiza.
Wakati huo, mtu anayemfahamu aliangaza mbele ya mlango. Alikaa huku akitetemeka na moja kwa moja akatoa mirija mkononi kabla hajaifuata ile sura.
Hans alipigwa na butwaa. “Mwalimu Mkubwa Kijana, mkono wako bado unavuja damu... Umefanyiwa upasuaji. Daktari alisema huwezi kunyanyuka, la sivyo kidonda chako kitapasuka.”

Hata hivyo, Alvin alijifanya kana kwamba hakusikia. Badala yake, alikimbia kwa kasi alivyoweza hadi akamshika yule mtu mwembamba aliyekuwa mbele yake.
“Lisa...”
Lisa akiwa anasonga mbele ghafla alihisi mtu amemshika na kusikia sauti ya kicheko ya mwanaume kwa wakati mmoja.
Alipogeuka, aliona macho ya Alvin yakiwa yamejawa na uchungu.
Bado alionekana mtanashati licha ya kuwa ndani ya gauni jeupe la hospitali. Kwa kweli, mavazi hayo yalifichua udhaifu wa mtu huyo ambaye kwa kawaida alikuwa na nguvu, na kumfanya aonekane kama mtoto mdogo ambaye alihitaji kutunzwa na kulindwa.
“Umekuja kunitembelea?” Alvin

alimkazia macho ya uchoyo. Sauti yake ilijaa tahadhari na kubembeleza, jambo ambalo lilikuwa nadra. "Wadi yangu iko nyuma."
Lisa aliweka macho yake ya mawe kwenye sura ya tahadhari ya Alvin. Aliona ni ujinga. Pembe za mdomo wake zilikunja kwa tabasamu la kejeli.
“Unafikiri nipo hapa kukutembelea?” Lisa alishtuka kutoka kwenye mkono wake. "Hatuna uhusiano wowote mimi na wewe tena."
Kisha akageuka ili kuondoka, lakini Alvin alikuwa mwepesi wa kusimama mbele yake. Ingawa alikuwa mgonjwa, sauti yake ilikuwa ya kiburi kama kawaida. “Niliachana na wewe lini? Lisa, wewe bado ni mpenzi wangu.”
"Bwana. Kimaro, una kumbukumbu mbaya sana. Acha nikukumbushe

kwamba ulikuwa umeshikilia mikono ya Sarah kwa ukaribu ulipofika mahakamani jana.” Lisa alishangazwa sana na tabia yake ya kukosa aibu. "Mtu ambaye ana aibu hatajiaribu kusema mambo kama hayo."
"Unaweza kunichukulia kama mtu asiye na aibu, basi." Alvin alisita kuuachia mkono wake. Alijua kuwa alikuwa amemkosea sana, kwa hivyo labda asimsumbue kama Hans alivyosema. Hata hivyo, hakuweza kuacha kumfikiria tangu jana yake usiku.
Alikuwa amesikia msemo ambao mtu angemfikiria mtu aliyempenda wanapokuwa wagonjwa.
Kwa bahati mbaya, alikuwa ameielewa kwa kuchelewa.
“Lisa, samahani. Sikukusudia. Ilikuwa ni kwa sababu nilimwona Logan akirarua nguo za Sarah pangoni juzi...”

“Acha kuniambia jinsi unavyojisikia kwa Sarah. Naona ni chukizo.” Lisa alimkatisha. "Kwa kweli, ulidhani ni sawa, ngoja nikwambie ukweli Alvin. Nilikubali tu kurudiana pamoja na wewe kwa nia ya kulipiza kisasi kwako. Nilitaka Sarah ahisi hisia za kunyakuliwa mtu wake mpendwa.”
"Umesema nini? ” Alvin alipigwa na butwaa. Moyo wake ulihisi kama umepigwa na kitu kizito. “Hii haiwezekani...”
“Haiwezekani?” Lisa alikoroma, “Ni nini kinakufanya ujiamini hivyo? Fikiria juu ya mambo yote uliyonifanyia hapo awali. Unataka niyaorodheshe moja baada ya nyingine? Kwanza, ulipokuwa na uhusiano wa kimapenzi na Sarah lakini ukaogopa kukosolewa na umma, ulinitisha na baba yangu na kunilazimisha kuuambia umma kuwa tumepeana talaka. Kisha, wanamtandao

walinipiga vijembe.
"Tukio la pili lilikuwa wakati ulisisitiza kumuokoa Thomas, ambaye alitaka kumbaka Pamela, ambayo iliongeza mafuta kwenye moto. Mwishowe, Thomas alitoka na kumchafua Pamela mbele ya vyombo vya habari.
“Tatu, ulinitendea kama mbwa na ukanifungia. Ulipanga hata kumuacha Sarah awe mama wa watoto wangu nitakapojifungua.
“Nne, ulinisukuma na kunisababishia mimba kuharibika.
“Ya tano ni pale Sarah alipodai kuwa nina msongo wa mawazo, hivyo ukamwomba daktari anifungie na kunipiga sindanona dawa kila siku. Nilikuambia mara nyingi kwamba nilikuwa sawa na sikuwa mgonjwa wakati huo, hukunisikiliza.

“Sita ulimuacha Sarah kusimamia kampuni pekee ambayo mama yangu alikuwa ameniachia baada ya kujifanya kuwa nimekufa. Una makampuni mengi, lakini ilibidi tu kumpa Mawenzi. Hukuweza kumpa kitu kingine?”
Kadiri Lisa alivyozidi kueleza ndivyo alivyozidi kuwa na hasira na kuhamaki. Macho yake mazuri yalikuwa yakiwaka kwa hasira.
Alvin alipigwa na butwaa kabisa. Hatimaye ilimgusa kwamba hajawahi kuacha kumchukia. Je, ilimaanisha kwamba tabasamu, hangaiko, na upole wake wote wa hapo awali ulikuwa wa uwongo? Ilimuuma sana hata akashindwa kupumua. Inaweza kuwa ni kutokana na ukweli kwamba alikuwa amefanyiwa upasuaji, lakini alihisi kuwa angezimia muda wowote.

Lisa alijifanya hajaona na kuendelea kukosoa kwa kejeli, “Yote niliyoyataja yalitokea kabla ya kurudi kwangu. Sasa, nitaorodhesha mambo uliyonifanyia baada ya kurudi. Jambo la kwanza ni kwamba uliwataka wanahisa na washirika wa kampuni yangu kunigomea kwa sababu Sarah alikushawishi kufanya hivyo. Kama nisingekuwa mwerevu, Mawenzi Investments ingeanguka kwa muda mrefu kwa sababu yako. “Pili, Sarah alikuwekea dawa, lakini ulikuja kwangu kujisaidia. Baada ya hapo ulinionya hata ninywe tembe za kuzuia mimba ili nisiwe na mimba ya watoto wako.”
“Tatu, nitapuuza ukweli kwamba ulinilazimisha kupata talaka kwa sababu ulitaka kuoana na Sarah, lakini kwanini ulilazimika kumwambia Maya kunivua nguo? Ndiyo, umenisaidia kulipiza kisasi kwake, lakini unaelewa uchungu na fedheha ya kubanwa sakafuni na

kuvuliwa nguo kidogo kidogo? Kimsingi uliikanyaga heshima yangu.
"Suala la nne lazima liwe la Logan. Baada ya kujua kwamba Sarah alitekwa nyara, uliniacha kwenye Mlima huko Afrika Kusini katikati ya usiku. Nilikusihi usiende, lakini bado uliondoka bila moyo.
“Logan ni familia yangu, lakini ulimchukuliaje? Ulimkata kidole ili kumfurahisha Sarah. Alvin, huoni kuwa unatisha?”
Inatisha? Alikuwa anatisha? Mikono ya Alvin ilikuwa ikitetemeka.
Kama asingeorodhesha mambo hayo moja baada ya jingine, angalisahau maovu haya yote aliyokuwa kayafanya kwake.
Kwa asili hakuwa mkatili. Lakini, angeweza kubadilika kwa urahisi kuwa shetani inapokuja suala la Sarah.

“Samahani, Lisa Sitafanya tena, naapa...”
“Acha kutukana. Tulipokuwa kwenye uhusiano, uliahidi kuwa mwaminifu. Lakini tulikuwa pamoja kwa siku ngapi?" Sura ya Lisa ilionekana kuchukia. "Alvin, umenifanya nitambue kuwa siwezi kuamini maneno yako kwa sababu hakuna mtu anajua ni lini utanigeuka.”
“Sitakugeuka. Ninaahidi." Alvin, ambaye alikuwa mwishoni mwa akili yake, akashika mkono wake. “Ulisema hapo awali kwamba unataka kulipiza kisasi kwa mimi na Sarah, sivyo? Ulisema unataka kuninyakua kutoka kwa Sarah na kumtesa, sivyo? Ninakupa nafasi sasa.”
Hakujali kuteswa na Lisa ilimradi tu asiachane naye.
Kwa wakati huu, Alvin alikuwa kama

mtoto asiyejiweza. Alichotegemea ni kwa Lisa kumpa nafasi nyingine.
“Asante, lakini sitaki nafasi hii tena. ” Lisa alimtazama Alvin, ambaye alikuwa akitaka kumuweka pembeni yake. Ikiwa hii ingetokea mapema, angefurahia. “Alvin, ulikuwa unafikiri mimi sina thamani, lakini nina uhakika kwamba hukuwahi kufikiria kwamba siku moja ungeogopa na kuhuzunika sana.”
Hata hivyo, ilibidi akubali kwamba pia aliumia katika harakati za kumfanya aanguke tena.
“Kwanini hutaki tena kulipiza kisasi kwangu?”
Ikizingatiwa kuwa mtu mwenye kiburi kama yeye aliishia katika hali hii, Alvin alijidhihaki. Hata hivyo, jambo lililokuwa likimuogopesha zaidi ni kwamba hakutaka kulipiza kisasi kwa sababu hilo lilimaanisha kwamba wasingekuwa na

uhusiano wowote tena.
Mapigo marefu ya moyo wa Lisa yalipungua. “Alvin, mimi pia ni binadamu. Nilishawishika tulipokuwa wapenzi, haswa nilipogundua kuwa hukulala na Sarah, na uliponirudisha nyuma wakati wa kupanda Mlima huko Afrika Kusini.
“Lakini likaja suala la Logan, ukanipiga kofi kali ambalo liliniamsha. Nilikuwa najipanga kuutoa mwili wangu ili unianguke ili nikutese, lakini lilikuwa ni wazo la kipumbavu kiasi gani. Nilikuwa najaribu kulipiza kisasi kwako au kukuruhusu unifaidi?”
"Hapana. Ulinilipiza kisasi, kama vile unavyofanya sasa. Moyo wangu unauma sana...” Alvin alimtazama kwa huzuni. "Kaa hapa. Unaweza kunitesa upendavyo mradi tu uwe na furaha.”
"Hakuna haja." Lisa akatikisa kichwa.

“Nilipokusihi pkule ONA, ulisema utanifungia. Kisha, nilipokuona ukikata kidole cha Logan, hisia zangu kwako zilipotea. Kuanzia leo, nitalipiza kisasi changu kwa Sarah Njau. Sifanyi kwa ajili yako bali kwa ajili ya Charity. Hebu tusahau kuhusu mahusiano yetu ya uchungu katika siku za nyuma. Sijisikii kutumia uhusiano wetu kama chombo cha kulipiza kisasi tena.”
Sura ya: 465
Lisa mwenyewe alisema kwamba hakuwa na hisia tena kwa Alvin.
Pembe za macho ya Alvin zilibadilika na kuwa mekundu kwa maumivu.
Ikawa kwamba alimpa nafasi, na akakubali. Hata hivyo, alikosa nafasi hiyo usiku ambao alimwacha peke yake kwenye Mlima huko Afrika Kusini bila kufikiria tena. Alvin, oh, Alvin. Kwa Sarah umemuumiza kiasi gani huyu mwanamke aliyekuwa anakupenda?

“Alvin, najua hutamwacha Sarah kamwe. Katika kesi hii, tutakuwa wapinzani katika siku zijazo.” Lisa alirudi nyuma kutoka kwa mguso wake na kuondoka bila kuangalia nyuma.
“Usiniache, Lisa...” Kadiri Alvin alivyotaka kumfuata, jeraha lake la baada ya upasuaji lilikuwa limefunguka, na damu ikamchafua gauni. Kwa kila hatua aliyopiga, jeraha lake lilihisi kana kwamba linapasuka upya. Maumivu yalikuwa makali sana hadi uso wake ukawa mweupe kama karatasi.
Alitaka kumjulisha kuwa hataki kuwa mpinzani wake. Badala yake, alitaka awe mpenzi wake na mke wake. Asingejisumbua tena na mambo ya Sara. Licha ya hayo, mwili wake haukumruhusu kusogea zaidi.
Alvin alianguka chini kwa maumivu. Alipoinua kichwa chake, alimwona Lisa

kwa mbali akigeuza kichwa chake na kumtazama huku akiwa na maono hafifu. Hata hivyo, mtazamo wake ulikuwa wa kiburi, na akaondoka bila nia ya kugeuka. Pamoja na hayo, aliondoka.
Ijapokuwa aliona shati lake likiwa limetapakaa damu na kugundua kuwa ana maumivu makali sana kiasi kwamba angezimia, hakugeuka nyuma. Hata hakuwa na wasiwasi, wasiwasi, au hofu. Ha!? Macho yake yakawa mekundu tena.
“Bwana Mkubwa, kidonda chako kimefunguka. ” Sauti ya wasiwasi ya Hans ilisikika kando ya sikio lake. "Dokta, njoo haraka." Punde, mtu alimchukua Alvin hadi kitandani na kumpeleka kwenye chumba cha dharura ili kushona jeraha lake upya. •••
Baada ya kununua chakula na maji,

Lisa alielekea ghorofani. Mzee Ngosha tayari alikuwa ametoka kwenye chumba cha dharura na kutoka kwenye hatari kwa muda huo, lakini bado alikuwa amepoteza fahamu.
Bibi Ngosha alimuonya Joel kwa jazba, “Uking’ang’ania kuuza hisa, hutakuwa mwanangu tena. Usijisumbue kurudi nyumbani."
Uchungu uliangaza machoni mwa Joel. Badala ya kujibu alimuomba tu daktari amtibu Mzee Ngosha kabla hajajiandaa kuondoka na Lisa.
Joel na Lisa walipotoka tu mlangoni, wakakutana uso kwa uso na Jerome akitembea kwa haraka. Alipomwona Lisa, macho ya Jerome yalibadilika kuwa makali. Jambo la kwanza ambalo Jerome alisema lilikuwa, "Anko Joel, lazima uwe mgonjwa."

Lisa aliuma mdomo. “Baba yangu hana akili timamu. Lakini unapaswa kuwa na wasiwasi juu yako mwenyewe. Sasa kwa kuwa Bwana Kawada ndiye mwanahisa mkubwa zaidi katika Kampuni ya Ngosha, unafikiri atawapanga watu wake kwa kampuni yako mpya ya uwekezaji iliyoanzishwa?”
Uso wa Jerome ulibadilika. Hili ndilo lililomtia wasiwasi zaidi. Hapo awali alikuwa amepanga kutumia kampuni yao kuchukua Ngosha Corporation, ambayo ingewezesha familia ya Campos kuwa familia yenye ushawishi mkubwa zaidi nchini Kenya. Hata hivyo, aligundua kuwa Kawada aliwahi kujihusisha na sekta ya fedha. Katika hali hiyo, Kawada bila shaka angeshindana kutawala ubia baadaye.
"Lisa Jones, nina hakika ulifanya hivi makusudi." Jerome akasaga meno yake.

Lisa alitabasamu kwa unyonge. "Hata hivyo, hatuna uhusiano wowote tena na Ngosha Corporation. Ni juu yako kufanya chochote unachotaka, Bwana Campos. Lakini baada ya kusema hivyo, acha niwakumbushe kwamba huenda Damien na binti yake wasiweze kumpinga Kawada.” Kwa hayo, Lisa aliondoka bila kuhangaika kuona sura ya Jerome.
Punde, Melanie alitoka wodini na kumtazama kwa wasiwasi. “Jerome, tufanye nini sasa? Inaonekana Joel yuko tayari kuuza hisa, na hakuna anayeweza kumzuia.”
Moyo wa Jerome ulifanya mgeuko kabla ya kuhema. “Hatuwezi kumuacha Kawada awe mwenyekiti, zaidi ya kupata nafasi ya kujihusisha na mambo ya ndani ya Kampuni ya Ngosha. Vinginevyo, ataifanya familia ya Ngosha

kuwa watu mashuhuri mapema au baadaye.
Uso wa Melanie ulipauka mara moja. Kwa kweli, alitarajia hii. “Kawada ni mtu mjanja, kwa hiyo hakika hufanani naye.”
“Tunapaswa kumtegemea baba yako. Kama baba yako hawezi kumpinga, basi wewe na baba yako...” Jerome akatikisa kichwa huku akisema, “Nyinyi watu mnaweza tu kukaa na kufurahia faida. Lakini unaweza tu kuchukua kiasi ambacho yuko tayari kuwapa.”
“Hapana...” Melanie alishtuka sana hivi kwamba akatikisa kichwa haraka. "Jerome, kama mume wangu, unahitaji kunisaidia. Tumeunganishwa pamoja. Zaidi ya hayo, familia ya Campos na familia ya Ngosha wamekuwa wakifanya kazi kwa karibu na kila mmoja. Nikipoteza nafasi yangu katika Ngosha Corporation, hakika itaathiri

ubia wetu.”
"Bila kusema, nina wasiwasi kuhusu hili pia." Jerome akazungusha mkono wake mabegani mwake. “Vipi kuhusu kumfanya Mike akusaidie? Nitamfanya awe msaidizi wako.”
Macho ya Melanie yakaangaza kwa kusitasita. Hakutaka kuwa na watu wa Jerome katika Ngosha Corporation, na Mike Kalonzo alikuwa katibu wa Jerome.
"Wifey, sasa ni wakati wa sisi kuungana na kuwapinga watu wa nje," Jerome alinong'ona. “Kama mume wako, kwa hakika nataka familia ya mke wangu iwe salama. Nina heshima yangu ya kuhifadhi pia. Natumai, Babu yako anaweza kuwa na udhibiti kamili juu ya Ngosha Corporation wakati huu.”
“Sawa.” Melanie aliitikia kwa kichwa bila

kusita.
Aliamini kuwa Jerome angeshughulika
na Kawada kwa niaba yake, ikizingatiwa kuwa ni mke wake.
Hakujua kwamba kwa pembe ya macho yake, macho ya Jerome yaligeuka polepole.
Mara Jerome alipotoka hospitalini, alimtafuta Mike Kalonzo, msaidizi wake. "Tafuta njia ya kuwasiliana na Bwana Kawada."
"Bwana Campos, unajaribu ku..."
"Kushirikiana." Jerome alikaza macho yake.
Mike alipigwa na butwaa. “Lakini hata Kawada humjui. Je, atakubali kushirikiana nawe?”
"Mpinzani anaweza kuwa rafiki yako mradi tu unamshawishi vya kutosha."

Jerome akakoroma. “Melanie na baba yake wana nini kingine wakati huu? Huku zikiwa zimesalia hisa chache tu za kampuni ya Ngosha Corporation, wawili hao hawalingani na Kawada, ambaye ni tofauti kwa kuwa ana kampuni ya kimataifa. Tutafanikiwa ikiwa tutafanya kazi pamoja. Nimekuagiza umfanyie kazi Melanie. Nataka uungane mkono na Kawada na kuifanya Ngosha Corporation iwe yetu ndani ya miezi miwili.”
Akitazama sura za Jerome kwenye uso wake mzuri, Mike hakuweza kujizuia kutetemeka.
Umma mara nyingi walimwita Alvin mkatili, lakini hawakujua jinsi familia ya Campos ilivyokuwa wakatili. Jerome angeweza hata kuchukua faida ya mke wake ili kupata mamlaka..

•••
Katika wodi.
Hans alimwarifu Alvin, "Bwana Mkubwa, Bibi Jones alikuja hospitalini kwa sababu Mzee Ngosha aliletwa hapa baada ya kuzirai kutokana na hasira wakati wa mkutano."
"Je, ni kwa sababu Joel aliuza hisa?" Alvin aliuliza kwa sauti ya kufoka.
“Ndio. Imeenea kama moto wa nyika na kusababisha ghasia miongoni mwa wafanyabiashara nchini Kenya. ” Hans alishangaa, “Kutakuwa na mabadiliko makubwa katika Ngosha Corporation.”
"Sio mbaya. Kwa kuzingatia ushirikiano wa karibu kati ya Campos Corporation na Ngosha Corporation, Jerome lazima awe na ajenda ya siri. Ilikuwa salama na busara kwa Lisa kuondokana na kimbunga hiki."

Midomo ya Alvin ya kupendeza na myembamba ililazimisha tabasamu la kujifariji.
Hans alimtania Alvin kwa siri, 'Umeachana na Lisa, lakini unafanya kana kwamba bado wewe ni mpenzi wake. Bwana Mkubwa, tafadhali zingatia kupata afya kwanza." Hans alikumbusha, “Tunakaribia kufaulu na mradi wetu wa mpya wa kiwanda cha smartphone. Itakuwa hatua kubwa kwa KIM Internaional wakati huo.”
Alvin alikaa kimya.
Hakika, KIM International ingeenda
mbali zaidi, na angekuwa na pesa hata za kuchoma. Hata hivyo, faida ya kupata pesa nyingi hivyo ilikuwa nini? Mwanamke ambaye angependa kutumia naye pesa alikuwa amemchukia sana.
Simu ya Alvin ilitetemeka ghafla

Ilikuwa ni Simu kutoka kwa Sarah. Hakuwa katika hali ya kumsikiliza hata kidogo. Kwa kweli, aliona inakera tu.
TUKUTANE KURASA 466-470
ONYO: Ni marufuku kusambaza, kukopi wala kuuza kazi hii kwani endapo kama tutakubaini basi sheria itachukua mkondo wake (By: Official Dully)
 
LISA KITABU CHA NANE (10) SIMULIZI...........................LISA
KURASA....................466- 470
PRESENT: SIMULIZI ZA DULLY

Sura ya: 466
Usiku, Ivan kutoka ONA alimpigia simu. "Bwana Mkubwa, Bi Njau amejaribu kujiua kwenye sinki la bafu la nyumba ya kifahari."
Alvin aliketi mara moja na kuuliza kwa sauti ya wasiwasi, "Vipi sasa?"
"Kwa bahati nzuri, tuligundua haraka na kumpeleka hospitalini kwa matibabu ya dharura. Ameumia mkono wake. Sasa niko kwenye gari la wagonjwa kuelekea hospitali, na tayari nimemjulisha Thomas. Bwana Mkubwa, unakuja...?”
Alvin alijibu bila kujali, “Nimefanyiwa upasuaji. Ninawezaje kuja?”
“Oh, sawa...” Ivan alishangaa kidogo huku akifikiri Alvin angekimbilia huko kwa wasiwasi.

Kwa kawaida Alvin alikuwa akiharakisha kumuona Sarah bila kufikiria mara moja kila jambo lilipomtokea. Hii ilitia ndani hata kama alikuwa katika safari ya kikazi nje ya nchi, au akishughulika na mambo fulani muhimu.
Ivan aliinamisha kichwa chake na kumtazama Sarah, ambaye alikuwa amelala kwenye gari la wagonjwa huku uso wake ukiwa umepauka. Akiwa mwanamume, aliwahi kumuonea huruma pia, lakini alishaona alishamuonea huruma sana hata akaishiwa na tone na mwisho la huruma.Kwani, haikuwa mara ya kwanza kwa Sarah kujiua. Alikuwa amelazwa hospitalini mara kwa mara kwa matukio ya kujiumiza kiasi kwamba ilionekana kana kwamba hospitali ilikuwa nyumbani kwake.
Wakiwa wodini, Alvin alimpigia Chester simu. Chester alikuwa amemaliza tu

upasuaji wa kuchosha wa saa sita, akitaka kupumzika, baada ya kusikia maneno ya Alvin ambayo yalimtia hasira sana asijue la kusema.
“Ana pepo la kujiua? Anaweza pia kukodisha wodi yz hospitali na kukaa huko mazima.”
"Kwa kweli ni mkatili sana kwa nafsi yake." Alvin alicheka kwa uchungu.
Tangu kesi yake na Logan isikilizwe, hakuweza tena kufikiria kwa busara kuhusu mambo ya Sarah.Isitoshe, Sarah alikuwa amelazwa hospitalini hivi majuzi, kwa hiyo alikuwa akienda mara kwa mara kati ya hospitali, ofisi na nyumbani. Tangu wakati huo hakuwa amepumzika vizuri. Yeye, pia, alikuwa amechoka.
“Ndio. Ni kana kwamba ni lazima tuwajibike kwa maisha yake tu,

tunakuwa kama watumwa sasa.” Chester alihisi uchungu mwingi.
Alikuwa akimchukulia Sara kama dada yake na alisikitikia yale aliyopitia.
Hata hivyo, si Alvin na Chester waliochangia mateso yake. Alikuwa katika matatizo yasiyo na mwisho. Dakika moja, alianguka kutoka kwenye ngazi, na iliyofuata, karibu ajiue kwa sababu alitendewa kikatili. Sasa, alijaribu kujiua ndani ya nyumba.
Akiwa daktari, Chester alikuwa ameona wagonjwa wengi walioaga dunia kutokana na magonjwa mazito. Kwa hiyo, alithamini uhai, lakini hakuhisi hivyo kwa Sara.
Asubuhi. Sarah aliamka taratibu, akamuona Thomas akichezea simu yake kando yake. Macho yake yalizunguka wodi, na karibu kuzimia.
“Alvinic yuko wapi? Si alikuja? Na

Chester yuko wapi?"
"Chester alikuja hapa kwa muda mfupi jana usiku, lakini Alvin hajafika." Thomas aliweka simu yake chini na kusema kwa hasira, “ Bwana Kimaro hana moyo. Unakaribia kufa, lakini hajali kabisa. Simama, Sarah, nafikiri wamechoshwa na mbinu yako ya kujiua.”
"Nyamaza." Sarah alimkazia macho. “Unadhani napenda kufanya hivi? Alikataa kupokea simu zangu wala kukutana nami. Nalazimika kumfanya aamini kuwa sina uhusiano wowote na suala la Logan.”
"Lakini nadhani anakushuku." Thomas akashusha pumzi. “Nadhani unapaswa kuachana na Alvin. Rodney pia si mbaya.”
“Usimtaje. Mtu huyo asiyefaa bado

amefungwa na familia ya Shangwe." Sarah akafumba macho.
Hakuna mtu huko Kenya ambaye angeweza kulinganishwa na mwanamume mashuhuri kama Alvin, kwa hiyo alisitasita kuachana naye. Isitoshe, alikuwa akimpenda sana Alvin. Vinginevyo, asingekuwa karibu naye ingawa hakuweza kumgusa kwa muda wa miaka mitatu iliyopita. Hii ndiyo mara pekee ambayo Alvin alimpuuza alipokuwa amelazwa hospitalini.
Siku iliyofuata, hakuweza kujizuia tena kwani alishindwa kujizuia na kuvunja vitu vilivyokuwa ndani ya wodi. Hata alifanya tukio na kujaribu kujiua tena. Alikuwa na uhakika kwamba wanachama wa ONA waliokuwa nje ya wodi wangemjulisha Alvin kuhusu hilo.
Kwa bahati nzuri, Alvin hatimaye alijitokeza siku ya tatu, lakini, alikuwa

ameketi kwenye kiti cha magurudumu na amevaa gauni la hospitali sawa na yeye. Uso wake mzuri ulikuwa umepwaya sana, na kufanya sura yake ionekane wazi zaidi na iliyopoa zaidi. Huku macho yake meusi yakiwa yamemkazia, Sarah alihisi kukosa raha kusikoelezeka.
“Alvinic, kuna nini... Una tatizo gani?” Sarah alimtazama kwa mshangao mkubwa. “Umejeruhiwa?”
Hans alisema kwa unyonge, "Bwana Mkubwa amefanyiwa upasuaji wa utumbo. Daktari alisema hatakiwi kuamka kitandani, lakini umekuwa ukizua kelele kila siku, kwa hiyo hakuwa na la kufanya zaidi ya kuja.”
"S-Samahani. Sikumaanisha, sikujua.” Sarah alikuwa akitokwa na machozi, lakini moyoni mwake alifurahi. Ilimgusa kwamba kutokuwepo kwake mapema ni

kwa sababu alifanyiwa upasuaji, si kwa sababu hakuwa na wasiwasi naye. Sasa alipokuja, ilionyesha kwamba kweli alimjali.
“Kwa kuwa unajua kwa nini sikufika mapema, unaweza kuniacha peke yangu sasa hivi?” Macho ya kuvutia ya Alvin yalizama, na kulikuwa na hisia ya uchovu usoni pake.
Sarah alipigwa na butwaa, na wimbi la wasiwasi likamkumba. “Alvinic, umenielewa vibaya. Sikuwa na nia ya kuanzisha ugomvi ukiwa mgonjwa. Nilikuwa mnyonge sana, haswa nilipofikiria kuwa umenielewa vibaya...”
"Ndio maana umeamua kufanya jaribio la kujiua?" Alvin alimkatisha huku akimtazama. "Kwa kuwa hupendi kuishi tena, umeshanunua jeneza?"
"W-nini?" Sarah aliganda. Hakuamini

kuwa Alvin angesema vile.
Akiwa amechanganyikiwa, Thomas alianza kupiga kelele, “Mwalimu Mdogo, umeenda mbali sana. Je! unajaribu kumfukuza Sarah hadi kifo chake?" “Nimekosea kusema hivyo? Aliomba kifo, kwa hiyo unawezaje kusema kwamba ninamlazimisha?” Alvin alidhihaki.
Thomas alishindwa cha kusema.
Mdomo wa Alvin ukasisimka ghafla. Alijiuliza kwanini alikuwa mjinga sana kabla ya kutotambua jinsi Sarah na Thomas walivyokuwa wakiimba wimbo mmoja. Walimfanya ahisi kuwa mtenda dhambi alipompuuza Sara.
“Sarah, kuna ugumu gani kuacha kunisumbua na kuniacha peke yangu? Niambie tu.”
Sarah akatetemeka. Ilikuwa ni mara

yake ya kwanza kusikia maneno hayo ya kinyama kutoka kwa Alvin. Ilionekana kana kwamba alikuwa amemchosha sana.
"Samahani, Alvinic." Alifunika uso wake na kulia. “Sitaki kuwa hivi pia. Najua nimekuwa nikikusababishia matatizo...”
"Sarah, hakuna kitu cha kusikitikia." Thomas alisema kwa hasira, “Bwana Kimaro, wewe huna huruma kabisa. Umesahau ni nani aliyeponya ugonjwa wako wakati huo? Ameshikamana nawe kupitia unene na mwembamba. Hata kama ninyi wawili hamwezi kuwa wanandoa, bado mnaweza kuwa marafiki, sawa?”
Sura ya: 467
“Marafiki?” Alvin alicheka. “Unamaanisha rafiki wa aina gani anayempigia simu, lakini akinipigia simu

na nikichelewa kufika, atafanya tukio? Wakati huo huo, ni lazima niwajibike kwa usalama na furaha yake maisha yake yote.”
Sarah akabishana mara moja, “Hapana...”
"Sarah, ni lini uligeuka kuwa mtu wa aina hii?" Alvin alikatisha sentensi yake bila subira. "Tulikuwa katika uhusiano tu, na hatujawahi kulala pamoja hadi leo. Nimekupa hata mali na pesa nyingi tulipoachana.
Lakini kwanini huwa unanitishia kujiua ikiwa nitakataa kuwa nawe?”
Alvin alitoboa ukweli. Alikuwa ametosha kwa kila kitu. Alikuwa ametosha kuwajibika kwa Sara kwa maisha yake yote. Alitosha kumuumiza Lisa mara kwa mara kwa sababu ya Sarah.
Sarah alishtushwa na usemi wake mkali. “Umeelewa vibaya. Nilitaka kujiua

kwa sababu nilihisi kwamba mimi ni... mchafu.
Alvinic, nakupenda. Upendo wangu kwako haujawahi kubadilika."
"Kwa bahati mbaya, sikupendi tena." Alvin alisema moja kwa moja na bila kujali, “Sarah, unapaswa kuridhika. Lisa nilimuoa na hata kuharibika mimba yake ni kwa sababu yangu, lakini sikumpa hata senti moja tulipoachana. Kwa mtu mkatili na asiye na moyo kama mimi, ninachukuliwa kuwa mkarimu kwako. Niliweza hata kumlinda na kumwangalia kaka yako asiyefaa. Ingawa uliponya ugonjwa wangu, nimerudisha neema.
Niambie, bado nina deni kwako katika nyanja gani?"
Sarah na Thomas wote walikuwa wameduwaa.
Alvin anaweza kuwa amekaa kwenye kiti cha magurudumu, lakini hasira machoni mwake iliwajaza hofu.

Muda kidogo baadaye, Sarah alisema kwa huzuni, “Je, unafikiri jambo la Logan lilikuwa ni mimi niliyefanya? Sikuifanya. Naapa.”
"Ikiwa ulifanya au la, haijalishi tena. Cha muhimu ni kwamba ukiendelea kuninyanyasa hivi siwezi kupata mwanamke mwingine wa kuoa.” Paji la uso wa Alvin lilijaa kero. “Hivi karibuni nitatangaza kwa umma kwamba tumeachana ili kuwazuia waandishi hao kutupiga picha bila mpangilio. Sarah, tumemalizana. Ukipanga kujiua tena usinipigie simu, nami nitamuondoa mwanachama wa ONA kwako pia. Ikiwa utatekwa nyara, mwambie mtekaji nyara amtafute Thomas. Siwezi kuwajibika kwako kwa maisha yako yote.”
Kwa hayo, Alvin akasogeza kiti chake cha magurudumu. Mara Hans alipoelewa nia yake, mara moja akamsukuma nje.

"Hapana, Alvinic. Usiondoke.” Sarah alimfuata Alvin huku akilia. Kadiri alivyotaka kumshika Alvin, Hans alimzuia.
“Alvinic, siwezi kuishi bila wewe. Je, umesahau ahadi yetu? Unawezaje kuwa mkatili hivyo? Je, ni kwa sababu ya Lisa? Hata hakupendi kama mimi.”
Alvin alitazama nyuma na kumwangalia uso wake uliokuwa na machozi. Ikiwa hii ingekuwa wakati huo, angeguswa. Hata hivyo, matukio aliyomfanyia Lisa aliyevunjika moyo na kumuumiza mara kwa mara yalijitokeza mbele ya macho yake. Ghafla, moyo wake ulianza kumuuma.Ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuudhika kwa Sarah.
“Hata kama hanipendi ni sawa ilimradi nampenda. Kwa upande wako, sina hisia na wewe tena.” Alvin alikuwa

amejiweka wazi kwake. Hakutaka kukaa tena, alimwambia Hans amsukume nje ya wodi ile. Hapo ndipo ilipomjia akilini kwamba ilikuwa haiwezekani kumlinda Sarah kwa upande mmoja na kujaribu kuuteka moyo wa Lisa kwa upande mwingine.
Sauti za kilio cha Sarah zilisikika wodini. Thomas pia alikuwa katika hali mbaya. “Tumelikoroga. Kama nilivyosema, mbinu yako ya kujiua imemkasirisha Alvin. Sasa kwa kuwa tumepoteza usaidizi mkubwa, tutafanya nini?"
“Nyamaza,” Sarah alimfokea kwa huzuni. Macho yake yalikuwa yakiungua kwa chuki kali. 'Alvin, wewe ni mkatili sana.”
Alimpenda sana hata alikuwa ameuumiza mwili wake kwa ajili yake tena na tena. Lakini, bado alimwacha mwishowe, na kwa hilo, lazima alipe!

•••
Siku iliyofuata.
Alvin alitangaza kwenye akaunti yake rasmi kwenye Facebook:
[Tetesi za hivi majuzi kuhusu Sarah Njau na mimi kuoana na kurudiana zinaenea kama moto wa nyika. Leo, niko hapa kuthibitisha kwamba mimi na Miss Njau tumeachana rasmi kwa sababu hatuna hisia tena kwa kila mmoja. Hatutarudiana tena.]
Mara baada ya habari hiyo kutolewa, ilisababisha ghasia kwenye Facebook.
[Alvin Kimaro kweli ni fisadi. Ni mara yangu ya kwanza kuona mwanamume fisadi akisema hivyo... kwa majigambo. Sijui la kusema tena.]
[Walikuwa tu wakijiandaa kwa ajili ya

harusi yao juzi tu, lakini sasa, hawana hisia tena kwa kila mmoja wao. Tsk, kusema wazi, amebadilisha mawazo yake.]
[Inaonekana Bwana Kimaro bado anafikiria kuhusu Binti Lisa Jones. Je, Bwana Mkubwa atatangaza rasmi uhusiano wake na Bi Jones? Siwezi kusubiri.]
[Hilo lina uwezekano mkubwa. Niliwaona wakienda kwenye matembezi pamoja siku kadhaa huko nyuma.]
Kwa hivyo, wanamtandao walienda pia kwenye wasifu wa Lisa na kuacha maoni yao.
[Lisa, utaoana tena Alvin rasmi? Lini mtatoa tangazo rasmi kuhusu hilo? Nitakuwa wa kwanza kukutumia baraka zangu.]

[Usirudiane na Alvin. Nadhani unastahili mtu bora zaidi.]
Lisa, ambaye alikuwa akifanya kazi huko Mawenzi, alikosa la kusema alipojiona kwa namna fulani kwenye utafutaji unaovuma.
Muda mfupi baadaye, alitoa tangazo kupitia akaunti yake.
[Alvin na mimi tulijaribu kurudiana pamoja kitambo, lakini tuligundua kuwa hatuwezani. Binafsi huwa napenda sana wanaume wenye maamuzi kwenye mahusiano kwahiyo haiwezekani turudiane tena. Natumai nyie hamtanivuta kwenye uhusiano wa Alvin tena. Kuanzia sasa na kuendelea, tutatakiana mema.]
Mara baada ya taarifa hiyo kutolewa, ilizua tafrani kwa wanamtandao waliokuwa wakisubiri habari hiyo.

[Unamaanisha nini kwa kuwapenda wanaume wenye maamuzi katika mahusiano? Lisa, je, Alvin alikuwa akiwasiliana na Sarah wakati wote alipokuwa kwenye uhusiano na wewe?]
[Maskini Lisa, usikasirike kwa sababu ya Alvin tena. Unastahili mtu bora zaidi.]
[Nilimsikia Alvin hata alifungua kesi dhidi ya Lisa siku chache zilizopita kwa ajili ya Sarah. Wawili hao walikabiliana mahakamani.]
[Damn. Alvin lazima awe mtu mchafu zaidi duniani.]
Wakati huo Alvin alikuwa amekaa wodini. Dakika alipoiona post ya Lisa, alihisi kana kwamba kuna kitu kimetoboa tundu moyoni mwake, akatetemeka. Hakutarajia angekuwa mkatili kiasi hicho. Hata alitangaza hadharani kwamba hawatarudiana

kamwe na kutakiana mema? Angewezaje kuwa sawa bila yeye?
Mara moja alichukua kalamu na kuchora sura ya moyo kwenye karatasi. Baada ya hapo, aliipiga picha na kuisambaza kwenye Facebook. [Nitakusubiri Maishani.]
Wanamtandao wakatoa maoni yao:
[Akiwa na umbo la moyo na msemo 'nitakusubiri maishani', je, anamaanisha kwamba atatumia maisha yake yote akimngoja Lisa?]
[Oh jamani, Bwana Kimaro anafanya nini? Sijamzoea kuwa mwenye mapenzi badala ya kuwa mkorofi.]
[Hatutaelewa ulimwengu wa matajiri. Miaka mitatu iliyopita, alisema kwamba Sara ndiye mpenzi wake wa kweli. Miaka mitatu baadaye, alisema angetumia maisha yake yote akimngoja

Lisa. Bah, sielewi!]
Lisa aliona chapisho ambalo Alvin alishiriki, akatoa tabasamu la kejeli. Nitakusubiri Maishani? Sahau kuhusu hilo!
Sura ya 468
Alvin alikuwa amengoja kwa muda mrefu, lakini Lisa hakuposti chochote kwenye Facebook tena. Moyo wake ukakata tamaa.
Ingawa alikana kuwa na uhusiano wowote naye hapo awali, bado walikuwa na mwingiliano, ambayo ilionyesha kuwa anamjali. Sasa hakukuwa na habari yoyote kutoka kwake, ilimaanisha kuwa alikuwa amempuuza kabisa. Hisia ya kupuuzwa ilikuwa ya kusikitisha. Alvin akaitupa simu yake pembeni na kuinuka. Jeraha lake lilianza kumuuma tena.

Hans alikosa la kusema. “Bwana Mkubwa, daktari amefanya upendeleo na kuidhinisha urudi ofisini japo kidonda chako hakijapona. Unapaswa kuacha kujitesa.”
"Nirudishe kwa Mzee Kimaro."
Hans alipumua, akijua kuwa hatamtafuta Lisa. Vinginevyo, ingekuwa shida ikiwa jeraha lake litafunguka kama jinsi lilivyofanya mara ya mwisho na kumpa homa.
"Kabla ya hapo, ninunulie vitu vya kuchezea zaidi vya Suzie," Alvin alikumbusha.
Hans alipigwa na butwaa, lakini mara moja alitikisa kichwa. Kuandamana na binti yake mara nyingi ilikuwa chaguo bora zaidi kuliko kuingia kwenye uhusiano.

Saa kumi na moja jioni, Jack alimchukua Suzie kutoka shule ya awali. Suzie aliruka huku na kule huku akiwa ameshikilia pipi ya big boom. Hata hivyo, mtoto mdogo alipomwona Alvin kwenye kiti cha magurudumu, aliganda. "Anko Alvin, mbona mguu wako ni mlemavu?"
“Hapana, nimefanyiwa upasuaji. Jeraha langu bado halijapona, hivyo siwezi kutembea,” Alvin alijibu kwa upole.
"Anko Alvin, unatia huruma sana." Macho ya Suzie yalimtoka kwa huruma. Ingawa alikuwa mvivu, bado alikuwa baba yake mzazi. "Hebu nione jeraha lako, sawa?"
“Ni sawa. Tayari ninajisikia vizuri zaidi.” Moyo wa Alvin ukayeyuka. “Nimekununulia midoli mingi. Anko Hans tayari ameiweka kwenye chumba chako. Kuna vyombo vya jikoni,

sanduku la mapambo, na mengine mengi.
“Hiyo ni nzuri. Asante, Anko Alvin.” Suzie aliruka kwa furaha, lakini alitulia upesi. "Subiri. Mama yangu alisema hakuna kitu cha bure.”
Alvin alikosa la kusema.
Jack hakuweza kujizuia kumcheka. “Suzie, mama yako yuko sahihi kabisa. ...”
“Jack...” Alvin alimkatisha kwa ukali.
"Nimekukumbusha kwa muda mrefu Alvin." Jack alikoroma. “Sasa, hatimaye unajuta. Lakini cha kusikitisha ni kwamba hakuna kitu duniani kinachoweza kutibu majuto. Wale waliojeruhiwa hawawezi kujifanya kuwa hakuna kilichotokea. Nini zaidi... Logan ni muhimu sana kwa Lisa.”

Alvin alikunja mkono wa kiti chake cha magurudumu. “Wewe ndiye uliyempeleka ng’ambo enzi hizo, kwa hiyo unapaswa kuifahamu vyema historia kati ya Logan na yeye. Unaweza kuniambia kuhusu hilo?”
“Je, huna kinyongo na mimi kwa kumhonga daktari ili kughushi kifo chake na kumpeleka ng’ambo?” Jack alimdhihaki. "Bado nakumbuka jinsi ulivyonipiga."
Moyo wa Alvin ulivutika kuashiria na dalili ya kero. Ndio, alimpiga Jack, lakini angepaswa kuomba msamaha kwa Jack? Ili kumuelewa Lisa vizuri, Alvin hakuwa na la kufanya zaidi ya kuvuta pumzi ndefu na kusema bila kupenda, “Jack, lazima nikiri kwamba siku hizo nilikuwa na msukumo wa hasira. Ulikuwa sahihi.”
Wakati huo, hakuhisi hivyo kwani

hakuwa akimpenda Lisa. Sasa kwa kuwa alikumbuka, bila shaka angekuwa mnyonge ikiwa Lisa angekufa.
Jack alimtazama kwa mshangao. Hakutarajia kuwa Alvin angemuomba msamaha. Labda nguruwe wanaweza kupaa!
“Sawa. Nitakuambia. Logan na Austin wote walilelewa katika vitongoji duni vya jiji la New York huko Marekani. Ili kuishi, walitumwa na genge lao wakiwa na umri mdogo sana kutekeleza misheni. Hata hivyo, mambo waliyofanya yalikuwa ya aibu. Logan na Austin wwalijikuta wakichokozana na magenge mengine hasimu, wakaanza kuwindwa ili wauawe.
"Lisa, ambaye alienda huko miaka minne iliyopita, alitokea kuwaokoa kwa kuwahifadhi na kuwapa chakula walipokuwa wamejificha, na

wanachopaswa kufanya ni kumfanyia kazi bila masharti kwa miaka mitano. Wawili hao ni watu wa mkono wa kulia wa Lisa, na wamekuwa waaminifu sana kwake.”
"Wakati Lisa alikumbana na hatari chache nje ya nchi, alibahatika kuwa na Logan na Austin kumlinda. Ni Logan ambaye alimfundisha Lisa ujuzi wa kujilinda pia. Wote wawili ni makocha wake na familia yake.”
"Kwanini alikuwa katika hatari nje ya nchi?" Alvin aliuliza kwa jazba.
“Tafadhali, unafikiri Marekani ni salama kwa mwanamke mrembo kama yeye ambaye hafahamu nchi hiyo?” Jack alimdhihaki. "Ameteseka sana kuwa kama alivyo leo."
“Kwa kweli, kama si wewe na Sarah, asingelazimika kwenda ng’ambo.”

Kadiri Jack alivyokuwa akiendelea na jambo hilo ndivyo alivyokuwa akipandwa na hasira, hivyo akamchukua Suzie na kuondoka zake.
Suzie aliingia mara moja kwenye chumba chake cha kucheza. Ingawa hakuweza kumuona mama yake, familia ya Kimaro ilimtendea vizuri sana kwa matunzo na vitu vya kuchezea walivyomnunulia.
Alikuwa amecheza kwa muda mfupi tu, Alvin alikuja kwenye kiti cha magurudumu. “Suzie, nahitaji msaada wako. Tafadhali sana,” Alvin alinong’ona. Hakuwahi kufikiria kwamba siku moja angehitaji kumsihi binti yake. “Unaweza kunisaidia kumuita Aunty Lisa? Sema tu kwamba ungependa kucheza naye.”
“Anko Alvin, si ulinizuia kuwasiliana na Aunty Lisa?” Suzie aliinua kichwa chake

na kusema kimakusudi, “Ulisema yeye ni mwanamke mwovu kwa kuniteka nyara.”
Alvin aliweka mkono wake kwenye paji la uso wake. Alitamani ang'oe ulimi wake. "Sikumuelewa wakati huo. Mimi...ninampenda sana, na ninataka kuwa naye. Suzie, nisaidie. Maadamu utaniahidi, nitafanya chochote unachotaka nifanye.”
“Sitaki ufanye lolote. Sitaki tena umuumize Aunty Lisa.” Suzie alipiga kelele. “Baba alisema umemuumiza sana Aunty Lisa safari hii. Ulimsaidia hata Aunty Sarah kumuumiza Aunty Lisa, ambaye hata hakupumzika kabisa maana ilibidi atafute ushahidi. Sitakukutanisha wewe na Aunty Lisa tena.”
Alvin alijisikia mnyonge. “Nimejitafakari. Mara tu nitakaporudiana pamoja naye,

hakika nitamtunza na kumpenda... ” “Ni sawa. Kuna mtu anaweza kufanya hivi vizuri kuliko wewe,” Suzie alifoka.
Alvin alipigwa na butwaa. Hata hivyo, upesi uso wake mzuri uligeuka kuwa mbaya, na akainua sauti yake licha ya nafsi yake. "Nani?"
Nani angeweza kufanya vizuri zaidi yake? Je, inawezekana kwamba Lisa alikuwa na mwanaume mwingine? Kwa kufikiria uwezekano huu, kifua cha Alvin kiliwaka.
“Oh hapana. Anko, unaonekana kutisha.” Suzie alipojua kuwa amemwaga maharage, aliogopa sana akataka kukimbia.
“Suzie, usiogope. ” Alvin alivumilia maumivu na kutoka kwenye kiti chake cha magurudumu. Alimkumbatia na kusema kwa kusihi, “Nampenda sana Lisa. Ndiyo, nimewahi kumuumiza mara

nyingi, na inaniumiza pia. Najua sipaswi kumsumbua, lakini siwezi kuacha kumfikiria kila wakati...”
“Kwanini hukuhisi hivyo juu yake ulipokuwa na Aunty Sarah?” Suzie aliongea kwa sauti ya chini huku akionekana kuduwaa.
“Mimi...” Alvin alishindwa cha kusema. “Nilifikiria juu yake, lakini sikuficha hisia zangu kwa sababu sikumwelewa wakati huo. Nilidhani ni mwanamke mbaya... "
“Kwa hiyo humpendi Aunty Lisa kwa vile tu ni mbaya? Inaonyesha kuwa unapenda wanawake wema tu. Lakini kuna wanawake wengi wema huko nje. Ina maana unawapenda wote?” Swali la Suzie likamfanya Alvin kukosa la kusema tena.
Sura ya: 469

Hakika, Alvin alizungumza kila wakati juu ya jinsi Lisa alivyokuwa mbaya na mbaya. Kwa kuwa kulikuwa na wanawake wengi wema huko nje, je, aliwapenda wote? Hapana.
Suzie alipiga kelele. “Kwanini unampenda Aunty Lisa basi? Humpendi akiwa mbaya, kwa hiyo unampenda tu wakati yeye si mbaya?”
Alvin alimtupia Suzie sura ya ajabu. "Niligundua kuwa ... unaweza kuonekana sawa na Jack, lakini haujarithi tabia zake. Wewe unaongea sana katika umri mdogo, na nadhani wewe ni kama mimi. Unaweza kuwa wakili katika siku zijazo."
Ndani kabisa, Suzie aligugumia. Hakuwa binti wa Jack, kitu cha kwanza. “Sitaki kuwa kama wewe. Bibi-mkubwa alisema kuwa wewe ni fisadi. Sitaki kuwa fisadi.”

Alvin aligusa pua yake kwa uchungu. Ilionekana kana kwamba kila mtu a alikuwa amethibitisha kwamba yeye ni fisadi.
“Umesema kweli, Suzie. Hapo zamani, nilikuwa fisadi... nilizidi sana. Sasa nimejifunza kwamba ninapompenda mtu, ninapaswa kupenda pande zake nzuri na mbaya. Kwa bahati mbaya, niliielewa kwa kuchelewa. Tafadhali nisaidie..."
"Hapana." Suzie alimkataa bila huruma. “Nikimdanganya Aunty Lisa kwa ajili yako, huenda hatataka kuniona tena. Kwa kuwa ulifanya jambo baya, unapaswa kutatua tatizo hilo wewe mwenyewe.”
"Lakini hataki kukutana nami." Uso wa Alvin ulijawa na ukiwa.

Suzie aliutazama uso wake uliofanana na wake. Kama binti yake, alimhurumia kidogo. “Mama alikuwa akiniambia kwamba mradi tu uweke akilini mwako, unaweza kufanya hivyo. Pia, inaonyeshwa kwenye TV kwamba mwanamume mwenye kuvumilia anaweza hatimaye kulainisha moyo wa mwanamke. Unapaswa kutafakari juu yake."
Kwa hayo, mtoto mdogo alikimbia haraka.
Alvin alipigwa na butwaa. Hakutarajia kwamba siku moja angekuwa na mtoto mdogo wa kumuongoza kupitia mahusiano. Lakini, alipofikiria juu yake, aliona kuwa ni sawa. Angeweza pia kuendelea kumsumbua kwa kuamini kwamba atamsamehe siku moja.
Baada ya chakula cha jioni, Alvin alitafakari kwa muda kabla ya kumwomba dereva wake ampeleke Karen Estate. Huku akibeba maumivu

kwenye kidonda chake, aliinama na kuweka mishumaa chini ya jengo la ghorofa ambalo Lisa aliishi na kutengeneza neno 'samahani'.
Kila alipokuwa akiinama, ilimuuma sana hadi kidonda chake kilipasuka.
Hata hivyo, alijitahidi kadiri awezavyo kuvumilia maumivu hayo.
Hatimaye alipowasha mishumaa, tayari alikuwa amewavutia watazamaji wengi katika ujirani huo.
Kijana mmoja akamsogelea Alvin na kumtazama. "Bwana, ni wewe tena."
Ndani ya sekunde chache, Alvin alimtambua kuwa ni mvulana aliyekuwa akiishi karibu na Lisa. Alikuwa amegongana naye mara kadhaa. “Ndio. Nilimkosea.”
"Lo, lakini kuweka mishumaa kama hii haitafanya kazi." Mvulana aliinamisha

kichwa chake na kusema, “Yule mwanamke alihama jana asubuhi. Hata niligongana naye, na aliniambia kwamba hatarudi tena.”
Simu katika mkono wa Alvin ilianguka kwenye sakafu. Kichwa chake kilianza kuvuma. Hakutarajia kwamba Lisa angehama hivyo hivyo. Je, ilimaanisha kwamba hakutaka tena kumuona? Hisia isiyoelezeka ya uchungu ilisambaa ndani ya mwili wake.
Mvulana huyo alimtazama Alvin kwa huruma na kusema, “Mama yangu alisema kwamba nyote wawili ni wanandoa wenye huzuni zaidi kuwahi kuwaona. Nyie mnagombana mara kadhaa kwa mwezi. Yule mwanamke pengine kachoka kugombana nawe wakati huu. We fanya haraka tu uondoke. Acha kuweka mishumaa hapa, au inaweza kusababisha ajali ya moto.” Yule kijana aliondoka mara

baada ya kumaliza kuongea.
Alvin aliinua kichwa chake na kuitazama ghorofa ambayo Lisa alikuwa akiishi. Pembe za mdomo wake zilivuta tabasamu la huzuni.
•••
Alvin alipata shida kulala usiku tena. Asubuhi alipoamka na kuvaa nguo zake, ghafla sauti ya Rodney kwenye mlango ilisikika kutoka nje. Alipofungua tu mlango, Rodney akaingia ndani kwa kasi. Jeraha usoni mwake lilikuwa halijapona, na macho yake ya kuvutia yalijaa hasira.
“Alvin Kimaro, unathubutu vipi kutangaza hadharani kwamba umeachana na Sarah. Hata ulidai kuwa nyote wawili hamtarudiana tena. wewe ni binadamu? Amejiumiza vibaya sana. Kwanini umtese?”

Zoezi alilofanya Rodney lilisababisha kichwa cha Alvin kumuuma. “Familia ya Shangwe ilikuachilia tu?"
“Duh. Nilienda kumtembelea Sarah, na amejikata kifundo cha mkono ili kujiua tena kwa sababu yako. Alvin, nahisi ninataka kukuua.”
Akiwa na hasira, Rodney alimwelekezea kidole. “Hajateseka vya kutosha kutokana na kutekwa nyara mara ya mwisho? Nilidhani utamlinda wakati familia ya Shangwe iliponifungia. Lakini inageuka kuwa unaamini nini watu wengine wanasema kuhusu Sarah kupanga tukio hilo. Haingehitaji mjinga kujua kwamba Sarah asingeweza kufanya jambo kama hilo.”
Baada ya kuona majibu ya Rodney, Alvin alijikuta akipandwa na hasira hata asijue la kusema. Alionekana kufahamu kwa nini Lisa alizoea kumwita kipofu kila

wakati. Pengine ilikuwa ni kwa sababu kila Lisa alipomkabili, alikuwa akitenda kama vile Rodney alivyofanya. Alitamani sana kumpiga nyundo kichwani Rodney.
"Rodney, ni kweli kwamba suala hilo halihusiani na Lisa na Logan ..."
“Hata hivyo, una upendeleo kwa Lisa. Umelogwa naye kiasi kwamba huwezi kutofautisha mema na mabaya,” Rodney alimfokea.
Maruwani ya Alvin yaligongana, na akasema bila kujali, “Imetosha. Haijalishi utanikosoa na kunishauri vipi, nimeamua. Kwa kuwa sina hisia tena na Sarah, ni lazima nijitenge naye. Anapaswa kuwa na maisha yake mwenyewe pia. Siwezi kumlinda milele. Kwa hivyo nyote wawili mtakapokutana wakati ujao, hamna haja ya kunialika. Hata ukipiga magoti mbele yangu sasa sitabadili mawazo yangu.”

"Sawa, Alvin. Nitakumbuka maneno yako. Kuanzia sasa na kuendelea, mimi, Rodney Shangwe, sina rafiki katili kama wewe tena. Kwa kuwa humtaki Sarah, mimi namtamani. Nitawajibika kwa maisha yake yote.”
Rodney aliupiga mlango kwa teke na kuondoka zake huku akihema.
Akiwa amekata tamaa, Alvin alipapasa paji la uso wake. Hakutarajia kwamba siku moja uhusiano wake na Rodney ungeisha katika hali hiyo kwa sababu ya mwanamke.
Hata hivyo, hakutaka mtu yeyote aathiri au kutishia uhusiano wake tena.
Iwe alimpenda mtu au la, ilimbidi aseme wazi.
•••
Katika maduka, Sarah alikuwa anafanya

manunuzi ya kawaida.
Ghafla, mwanamume mmoja mnene na mrefu akashika mkono wake. “Haya, Sarah. Je, unafanya ununuzi kote? Unapanga kununua nini? Ninaweza kukununulia mradi tu uwe mwanamke wangu.”
“Bwana Yusto, niachie.” Sarah alijitahidi kwa nguvu zake zote, na uso
wake ulijaa hofu.
Hata hivyo, Yusto alijitahidi zaidi kumtuliza kadiri alivyohangaika zaidi. “Mbona bado unatubania? Ingekuwa zamani ungekuwa na Alvin na Chester wanakulinda, lakini nilisikia hawakujali tena. Alvin hata alitangaza kwa umma kwamba hatarudiana tena na wewe. Lakini ninavutiwa sana na mwanamke wa mwanamume tajiri zaidi wa Kenya.
“Yusto Herman, hata sikupendi. Niache sasa. Unaniumiza.” Sarah aliomba kwa

upole.
Herman Yusto aliyeyuka alipomsikia. “Sarah, unaonekana mtamu sana. Nina hamu sana ya kulala nawe. Twende zetu. Hata iweje, ni lazima nikuchukue leo.” Akamkokota kwa nguvu.
Wakati Maya alipomwona Herman karibu kumkumbatia Lisa, alikimbia na kumpiga teke kabla ya kumlinda Sarah mikononi mwake haraka.
“Unathubutuje kunipiga teke. Umeishi...” Herman aliinua kichwa chake, na kuona sura ya hasira ya Maya. Mara akawa mpole.
“Fanya haraka na upotee,” Maya alionya.
Herman alimkazia macho kwa hasira, lakini angeweza tu kufanya kama alivyoambiwa. Kwani, hakuweza kumudu kumchokoza Alvin.

Hata hivyo, Sarah hakufikiri kwamba kuna mtu kutoka ONA bado anamlinda. Alvin alikuwa amemwomba Maya aondoke, sivyo?
Baada tu ya Herman kuondoka,
Maya alimwinua Sarah kwa miguu yake mara moja. “Uko sawa, Bi Njau? Ni kosa langu. Nilifanikiwa kutoroka kuja Kenya siku chache zilizopita, na sikutarajia...”
“Maya, ninakushukuru sana. Vinginevyo, ningeruka kutoka kwenye jengo leo. ” Sarah alimkumbatia Maya na kububujikwa na machozi. "Sasa kwa kuwa kila mtu anajua kuwa nimepoteza nguzo yangu, wengi wao wamekuja kunidhalilisha."
Maya alivunjika moyo na hasira kusikia hivyo. “Bwana Mkubwa Kimaro ni mkatili kweli. Umemfahamu kwa zaidi ya miaka

kumi. Ni sawa ikiwa hakutaki, lakini hakulazimika kuutangazia umma.”
"Acha, Maya. Ikiwa Alvinic atagundua kuwa umerudi, anaweza kuharibu maisha yako. ” Sarah alimsukuma kwa hofu kubwa. "Anaweza kuwa asiye na huruma kwangu, sembuse wewe?"
Maya alishtuka na kumkumbuka Alvin akifikiria kumfukuza ONA.
“Maya, usikae karibu nami tena. Ikiwa Alvinic atarudiana pamoja na Lisa katika siku zijazo, lazima ukumbuke kumfurahisha Lisa, sawa? Sarah alimkumbusha kwa wasiwasi, “Haifai kukaa nami.”
Maya alikuwa karibu kulia. Umma siku zote uliwaogopa watu kutoka ONA, lakini hawakujua kwamba alikuwa mlinzi tu katika familia ya Kimaro ambaye alimtendea kama mbwa. Sara pekee ndiye aliyemchukua kama rafiki. Hata

hadi leo, Sara alikuwa amemtafuta kwa dhati.
“Ondoka sasa hivi.” Sarah alimsukuma huku machozi yakimtoka.
Baada ya Maya kuondoka tu Sarah alimpigia mtu simu. “Ameondoka...”
Wakiwa wamejitenga, Maya alikuwa karibu kuingia kwenye gari lake kwenye maegesho ya magari wakati mwanamume wa makamo akiwa na miwani ya jua alimkaribia ghafla. "Bi Chande, ningependa kuwa na neno na wewe."
"Wewe ni nani? Nenda zako.” Maya alimkasirikia.
Hata hivyo, mtu huyo alimzuia njia, akatabasamu kinafiki na kumwambia. "Najua wewe ni mwanachama wa ONA, lakini unapanga kuwa mbwa wa Alvin

milele?"
Maya alishikwa na butwaa!
Kwenye sakafu ya juu ya duka, Sarah alikuwa ameagiza kikombe cha kahawa. Alipokuwa anakoroga taratibu, muziki kwenye mgahawa ulibadilika ghafla na kuwa wimbo mtamu.
Baada ya hapo, mtumishi alisukuma keki kubwa ya ngazi tatu kuelekea kwake. Juu ya keki hiyo kulikuwa na maneno mawili 'Marry Me' yaliyoandikwa kwa jam. Wakati Sarah akiwa amepigwa na butwaa, alimuona Rodney akija kwake akiwa na shada kubwa la maua. Kisha, akapiga magoti mbele yake. “Sarah, naomba nikuoe. Kusema kweli nimekuwa nikikupenda kwa muda mrefu sasa tangu tunasoma ila ulikuwa kwenye mahusiano na Alvin enzi hizo. Kwa kuwa Alvin hawezi kukuoa tena, nitafanya hivyo. Labda

nisiwe bora kama yeye, lakini nitatoa moyo wangu wote kwa ajili yako, na hili halitabadilika kamwe.”
“Rodney...” Sarah aliduwaa kwa muda, lakini mara moja akachezesha macho yake mekundu. "Mimi ... sistahili kuwa na wewe."
“Inatosha. Machoni mwangu, wewe ndiye mwanamke mzuri zaidi, na ninataka uwe mke wangu. Tafadhali nipe nafasi.” Rodney aliinua kichwa chake kwa upendo. “Usinikatae.”
",..sawa." Hatimaye Sarah alitikisa kichwa. Kwa sasa, ilikuwa haiwezekani kwake kurudiana tena na Alvin, hivyo angeweza kuolewa na Rodney kwa kusita. Ingawa Rodney asingeweza kurithi Shangwe Corporation, angalau angepata kichaka cha kujihifadhi tena.
“Hiyo ni ajabu, Sarrah. Asante." Rodney

kwa tahadhari alimvisha pete kidoleni na kumfunga mikononi mwake.
Kando, baadhi ya watu walikuwa wamechukua video na picha zao na kuzishiriki mtandaoni.
[Rodeney Shangwe Proposed To Sarah.] Ilikuwa ni habari iliyovumakwa muda mfupi sana.
[Damn, Sarah ana bahati sana. Alvin alikuwa ametoka tu kumtupa, lakini huyu hapa Bwana Mdogo wa Shangwe kamchumbia muda mfupi tu baadaye.]
[Je, Sarah anajaribu kulipiza kisasi kwa Bwana Kimaro? Ikiwa sivyo, kwa nini akubali kuolewa na Bwana Shangwe hivi karibuni?]
[Kofi lililoje usoni. Nashangaa kama Bwana Kimaro anajuta.]

Sura ya: 470
Pamela alikuwa amelala kwenye kochi huko Brighton Gardens huku Lisa akimpikia. Mara tu alipoziona habari hizo, alishtuka sana hadi akakaribia kuchomwa na chips.
“Haya, Lisa. Tazama hii. Rodney, mwanaume huyo mwenye kuudhi, amemchumbia Sarah.” Pamela alikimbia haraka kwa Lisa ili kushiriki naye uvumi huo. “Ni mechi mbaya sana! Hii ni sawa na nguruwe kulishwa keki."
Lisa akapepesa macho. "Machoni pako, Rodney amekuwa keki?"
Pamela akaangaza macho. “Namuonea huruma tu. Kwa kweli, yeye si mtu mbaya kihivyo ingawa matamshi yake yanaweza kuwa mabaya nyakati fulani. Kuna kitu kibaya tu akilini mwake, kama Alvin. Hapana, nadhani suala lake ni

zito kuliko lile la Alvin.”
"Sikutarajia familia ya Shangwe kumwachilia hivi karibuni. Nadhani... damu ya familia ya Shangwe lazima iwe inachemka sasa hivi.” Lisa alitafakari. “Tukio lao limezua tafrani. Iimefanikiwa hata kuingia kwenye utaftaji wa juu."
"Nina hakika amelipa kuwa katika utafutaji wa juu." Pamela alidhihaki, “Ni siku chache tu zimepita tangu Alvin atangaze hadharani kwamba hatarudiana tena na Sarah. Lakini sasa, amekubali kuolewa na Rodney. Ni nini hiki?"
“Hii si kawaida? Kwa kuwa Alvin amekataa kurudi pamoja naye, anaweza tu kumshikilia Rodney." Uso wa Lisa ulijawa na kejeli. "Nasubiri kuona jinsi Alvin atafanya kwa hili."
“Haha. Lazima atakuwa anachemka

kwa hasira. Huenda alifikiri kwamba Sara angekuwa mshikamanifu kwake milele, wakati kwa kweli, yeye ni mtu mjanja njanja tu.”
•••
Katika ofisi ya KIM International.
Alvin alipopokea picha ya Rodney akimchumbia Sarah, hakuwa na wivu wala kukasirika kuwaona wawili hao wakiwa wamekumbatiana. Lakini, alishangaa sana!
Labda alishangazwa na jinsi Sarah alivyokubali pendekezo la Rodney upesi baada ya kummwaga rasmi siku chache zilizopita. Alikuwa anajaribu kulipiza kisasi kwake? Au alijua kwamba asingeweza tena kuweka matumaini yake kwake, hivyo akamshikilia Rodney? Baada ya yote, bila kujali asili ya familia yao kupenda kujificha sana, Rodney alikuwa mmoja wa Vijana watano wa Juu huko Nairobi. Hatimaye

Alvin aligundua kuwa Rodney hamwelewi Sarah.
Akiwa katika mawazo yake, Rodney akampigia simu. “Umeona? Nimemchumbia Sarah. Kwa kuwa humthamini, nitamthamini, na nitakaa naye kuanzia sasa na kuendelea.”
"Naam ... Hongera." Alvin alifikiria kwa muda kabla ya kumpongeza Rodney. Hata hivyo, hili halikuwa jambo baya. Sarah angeacha kumsumbua, na Rodney angeweza kutimiza matakwa yake kwa wakati mmoja.
"Hujachukia?” Rodney alikatishwa tamaa kidogo kuona kwamba kitendo chake hakikumshtua hata kidogo Alvin.
“Nichukie kwa lipi basi? Sasa kwa kuwa umemchumbia Sarah, ulitaka nimpokonye kutoka kwako?” Alvin alisema bila huruma, “Nilimaanisha

niliposema kwamba simpendi tena. Unaweza kunitumia mwaliko wa harusi wakati ukifika.”
Baada ya hapo, Alvin akakata simu. Rodney aliitazama simu ile kwa hisia za ajabu. Alimchumbia Sarah akiwa na shauku ya kumuona Alvin akijuta, lakini Alvin hakuwa na kinyongo hata kidogo.
Rodney alipokuwa ameshuka, simu ya Mzee Shangwe iliingia ghafla.
Rodney aliogopa sana hata akakaribia kuitupa simu yake. Kuona simu kutoka kwa familia ya Shangwe sasa ilikuwa kama kumwona mfalme wa kuzimu akija kunyakua maisha yake. Aliipuuzia tu ikiita na kuita.
Kisha, simu ikaacha kuita, lakini punde, simu nyingine ikaingia. Mzunguko uliendelea na kuendelea na kuendelea.
Akiwa hana chaguo, Rodney aliweza tu

kupokea simu. “Babu...”
“Unathubutu vipi bado kuniita babu yako kwa kuziba masikio kusikia maneno yangu? Wewe kijana mbaya sana. Sikupaswa kukutoa nje. ” Mzee Shangwe alikasirika. “Nimekuacha tu kutoka asubuhi ya leo, na umemchumbia Sarah kufikia jioni. Rudi nyumbani haraka, nitakupiga hadi kufa.”
“Babu, Sarah anatia huruma sana. Lazima nisimame kumlinda wakati huu. Sielewi kwanini nyote mna chuki kama hiyo dhidi ya Sarah.”
Rodney alisema kwa kufadhaika, “Lisa ni mgeni, lakini nyote mnaamini kila anachosema. Mimi ni mjukuu wako wa damu. Unafikiri siwezi kujua kama Sarah ni mtu mzuri au la?”
"Funga mdomo wako, mjinga," Mzee Shangwe alifoka. "Ikiwa utathubutu kumuoa Sarah, usijisumbue kurudi

kwenye familia ya Shangwe tena."
"Samahani, babu. Lazima
niomuoe Sarah,” Rodney alijibu bila kusita.
"Vema sana, Radney Shangwe. Usijutie hili.” Mzee Shangwe aliitupa simu kando kwa hasira. Mzee huyo alikasirika sana hata akakaribia kuzirai.
"Baba, tulia." Jason alijaribu kumtuliza.
“Potelea mbali. Una mwana mwovu kiasi gani. Yupo ili kunitia hasira tu.” Mzee Shangwe alizama kabisa kwenye hasira.
Jason akahema. Mzee Shangwe alikuwa amesahau kwamba Rodney alikuwa mjukuu wa kwanza wa familia ya Shangwe. Rodney alipozaliwa, Mzee Shangwe alitega sikio kila siku na kumtendea Rodney kwa thamani sana.

“Nenda. Nenda ukamwite Jessica,” Mzee Shangwe aliamuru.
Punde Jessica alifika. Mzee Shangwe alisema, “Jessica, nina kazi kwa ajili yako. Sijali ni njia gani utakayotumia, lakini hupaswi kumruhusu Rodney kumuoa mwanamke huyo, Sarah, simtaki katika familia.”
Jessica kichwa kilimuuma. Kwanini aina hiyo ya kazi ndogondogo za kijinga daima zilianguka kwenye mabega yake?
"Hakuna njia nyingine." Mzee Shangwe alikuwa hoi. "Wewe ndiye mtu mwenye moyo mgumu zaidi katika familia ya Shangwe. Ni wewe pekee unayeweza kuvumilia kufanya hivi.”
Jessica alitabasamu kwa uchungu. Hakujua kama alipaswa kuwa na furaha au huzuni kwa ukweli huo.

•••
Siku inayofuata.
Wakati wa karamu ya uzinduzi wa bidhaa mpya ya Osher Corporation, Rodney alikuwa akijisikia furaha sana. Alikuwa amempata mpenzi wa masiha yake, na pia alikuwa anazindua bidhaa mpya ya ngozi kwenye kampuni yake. Pamela alikuwa ameiwezesha kampuni kuzindua cream mpya ya kuimarisha ngozi. Wafanyakazi wengi tayari walikuwa wameijaribu cream hiyo, na matokeo yalikuwa bora. Kwa hivyo, angeweza kuona mafanikio katika mauzo ya Osher Corporation tena. Kuhusu maisha yake ya mapenzi, Sara, ambaye alikuwa akimpenda kwa siri kwa zaidi ya miaka kumi, hatimaye alikubali pendekezo lake. Kwa wakati huu, alihisi kama maisha yake yalikuwa kamili.

Chester, ambaye alikuwa ameshika glasi ya mvinyo, alimpa jicho la pembeni. “Ondoa hilo tabasamu lako la kipumbavu. Hujaacha kutabasamu tangu nilipoingia mlangoni.”
Cindy akatabasamu. “Haiwezi kusaidiwa. Bwana Rodney sasa ana kazi yake na mpenzi wa maisha yake. Kumbe, Bwana Shangwe lazima awe amemwalika Sarah usiku wa leo, lakini kwa nini siwezi kumwona?”
“Yupo hapa.” Baada ya Rodney kuongea hayo, macho yake yakaangaza kumtazama mwanamke aliyeingia chumbani humo.
Usiku huo, Sarah alivaa vazi jekundu la mtindo wa nguva la velvet lililokuwa na mpasuko mrefu pembeni na utepe mkubwa wa kike kwenye shingo. Nguo hiyo ilimfanya aonekane mzuri zaidi. Alipotokea, ni kana kwamba taa zote

zilikuwa juu yake. Rangi nyekundu ilivutia sana macho.
Kando yake, Thomas alivaa suti nyeusi. Kaka na dada walipokuwa wakitembea, waliteka macho ya husuda na wivu ya kila mtu. Ikiwa kungekuwa na mwanamke ambaye wanawake wote wa Kenya walimwonea wivu kwa wakati huo, kwa kawaida angekuwa Sarah.
TUKUTANE KURASA 471-475
ONYO: Ni marufuku kusambaza, kukopi wala kuuza kazi hii kwani endapo kama tutakubaini basi sheria itachukua mkondo wake (By: Official Dully)
 
LISA KITABU CHA NANE (10) SIMULIZI...........................LISA
KURASA....................471- 475
PRESENT: SIMULIZI ZA DULLY

Sura ya: 471
Ingawa Sarah alikuwa amepoteza Bwana Kimaro, bado alikuwa na Bwana Shangwe, ambaye familia yake pengine ingetoa Rais mpya kwa mwaka ujao.
"Si ajabu Bwana Mdogo Shangwe hakuweza kumsahau. Yeye ni mrembo sana.”
“Umeona, eeh? Umbo lake ni zuri sana, na anavutia sana sana.”
Sarah aliposikia msururu wa pongezi hizo, alianza kujihisi nguvu sana moyoni mwake. Kwa hivyo ni nini ikiwa angempoteza Alvin? Bado angeweza kuwa kitovu cha umakini wa kila mtu.
Cindy alihisi wivu kwa siri huku akimtazama. Hapo awali alimtazama

Sarah wakati Alvin alipomtupa, lakini ni nani angetarajia...
Chester pekee ndiye aliyekuwa amekunja uso. Alikuwa amenasa ubadhirifu uliojificha machoni mwa Sarah wakati anaingia ndani muda huo. Ingawa ilitoweka mara moja, ilikuwa ya kushangaza. Ni wazi alimpenda Alvin kwa zaidi ya miaka 10 na alikuwa ameachana tu. Alijaribu hata kujiua kwa ajili ya Alvin hapo awali. Je, angeweza kujiingiza katika uhusiano na Rodney katika siku chache tu? Ghafla aligundua kuwa labda hawakumwelewa Sarah hapo awali. Alikuwa amebadilika muda mrefu uliopita.
Hata hivyo... Alimtazama Rodney, ambaye alikuwa akitabasamu kwa utamu, na akashusha pumzi kwa siri. Sahau. Ilikuwa sawa mradi Rodney alipenda mwenyewe bila kulazaimishwa. Hatimaye alitimiza

matakwa yake.
“Sarah...” Rodney alienda mbele mara moja na kumshika Sarah mkono.
“Rodney, usifanye hivi. Watu wengi wanatazama, na bado sijaridhika nayo.” Chembe ya unyonge iliangaza machoni mwa Sarah, haswa alipoona macho ya Chester. "Chester, umekuja pia ..." Macho yake yalizunguka kwa kusitasita baada ya kusema.
"Sikumualika Alvin." Rodney angeweza kukisia mawazo yake.
“Hilo ni wazo zuri kweli?” Sarah alisema kwa wasiwasi, “Hata hivyo, yeye ni rafiki yako mkubwa. Ulimwalika Chester, lakini sio yeye. Watu wengine watafikiria nini?"
"Sarah, Alvin amekuumiza sana, lakini bado unamjali sana," Rodney alisema kwa upendo

.
"Sitaki kuathiri uhusiano kati yenu wawili." Baada ya maongezi yote, Sarah aligundua kwamba ingawa Rodney aliguswa, lakini Chester alikuwa bado hamjali. Moyo wake ukafadhaika. Je, Chester aliona kitu?
“Sawa, Rodney. Mkutano na waandishi wa habari unakaribia kuanza,” Chester alimkumbusha.
Punde, Pamela, ambaye alikuwa kwenye maabara ya vipodozi, alishuka. Alivaa vazi jekundu la zamani la mtindo wa nguva lililoweka wazi mabega yake. Ngozi yake ilikuwa nzuri kama theluji, na kulikuwa na mkufu wa almasi kwenye shingo yake nzuri. Ulijumuisha na uzuri wake wa asili, hakuna mtu aliyeweza kujizuia kumtolea macho.
"Wow, huyu lazima awe mkurugenzi mpya wa utafiti na maendeleo wa Osher

Corporation. Yeye ni mrembo sana.”
“Ndoyeye? Wote wawili wamevaa nguo nyekundu, lakini amemshinda Sarah kabisa.”
“Kweli. Sarah ni mchumba wa Rodney Shangwe baada ya yote. Lakini wote wawili ni tofauti. Sarah ana sura nzuri tu, wakati Pamela ni mrembo na mwenye uwezo.”
"Nilisikia Osher Corporation ilimpa Pamela baadhi ya hisa kama malipo ya kujiunga na kampuni hiyo. Sasa yeye ni mbia wa Osher Corporation.”
“Nashangaa kama anatafuta mpenzi. Nataka sana kufahamiana naye.”
Majadiliano hayo yalifanya damu ya Sarah ichemke. Kwa muonekano wa usiku huo, alikuwa amejiandaa kwa siku nzima ili kufunika kabisa karamu nzima,

lakini ilionekana kwamba kulikuwa na mtu aliyempiku.
Sarah alishuku kuwa yeye, Lisa, na Pamela walikuwa maadui wa kuapishwa. Vinginevyo, kwa nini wangechukiana popote walipokutana?
Thomas, ambaye alikuwa kando yake, alimtazama Pamela kwa uchungu na uchu ulioonekana machoni pake.
"Sarah, lazima nimpate mwanamke huyu leo." Thomas alimnong’oneza Sarah kwenye sikio, “Sikufikiri kwamba Pamela angekuwa mrembo wa kung’aa hivyo. Hakuna hasara kwangu ikiwa nitamuoa.”
“Sawa, nakuunga mkono. Inatokea kwamba kuna waandishi wengi hapa usiku wa leo. Unaweza kutumia fursa hii, lakini uwe mwangalifu.” Sarah akashusha pumzi ndefu. Angeweza

kulipiza kisasi bila kujali. Mara tu Pamela angeolewa na Thomas, angekuwa na nafasi nyingi za kushughulika naye.
“I will.” Thomas alitikisa kichwa kwa upole.
Kwenye jukwaa, Pamela alikuwa tayari akitambulisha bidhaa hiyo mpya kwa kila mtu. "Habari za jioni, Mabibi na Mabwana. Mimi ni Pamela, mwanakemia wa vipodozi na mgunduzi wa bidhaa mpya ya ulinzi wa ngozi iitwayo...”
Rodney alimtazama Pamela kwa woga. Mwanzoni, alikuwa na wasiwasi juu ya kumruhusu atambulishe bidhaa kwenye jukwaa lake, llakini, hakujua kwamba angekuwa mzuri na wa asili mbele ya vyombo vya habari vyote. Juu ya sura yake hiyo nzuri, alipendeza sana machoni. Ilikuwa nadra kwake kuvutiwa

na Pamela. Ilionekana kana kwamba kumwalika kujiunga na Osher Corporation ulikuwa uamuzi wa busara.
“Rodney...” Sarah aliuzungusha mkono wake ghafla. Alilazimisha tabasamu na kusema, “Sikufikiri Bi. Masanja angevaa gauni jekundu pia usiku wa leo. Nisingevaa nguo nyekundu pia kama ningejua.”
Rodney alipigwa na butwaa.
Thomas alipumua mara moja na kusema, “Ni sadfa iliyoje kwamba Sarah alivaa nguo nyekundu pia. Kila mtu alikuwa akiwalinganisha wote wawili sasa hivi. Walisema Pamela amemfunika kabisa Sarah au kitu...”
“Kaka...” Sarah alimkazia macho Thomas. "Haijaandikwa kuwa mimi pekee ndiye ninaweza kuvaa nguo nyekundu."

"Ninashuku alifanya hivyo kwa makusudi. Sio kama Lisa hajafanya kitu kama hicho hapo awali. Kwa kuwa Pamela na Lisa ni marafiki wazuri, kwa kawaida hujifunza kutoka kwa kila mmoja. Hata hivyo, wewe na Alvin tayari mmeachana. Hana sababu ya kukulenga,” Thomas alilalamika.
Rodney alikunja uso kwa ukali. Hakusema neno.
“Rodney, usijali kuhusu yeye. Kaka yangundivyo alivyo,” Sarah alisema kwa haraka.
“Ni sawa. Alichosema ndugu yako ni sawa. Wewe ni mpenzi wangu sasa. Unawezaje kulinganishwa na mwanakemia wa vipodozi?” Rodney aliongea kwa sauti ya chini huku akimwangalia Pamela aliyekuwa jukwaani.

Sarah na Thomas walitazamana kwa siri. Kulikuwa na ladha ya ushindi katika macho yao.
Baada ya Pamela kumaliza hotuba yake, alishuka jukwaani kwa msaada wa mfanyakazi. Hapo ndipo Katibu wa Rodney alipokuja na kusema, “Bi. Masanja, Bosi Shangwe ameomba kukuona ghorofani.”
Pamela akaitikia kwa kichwa. Alifikiri Rodney alitaka kujadili jambo linalohusiana na kazi. Alipofika kwenye chumba cha juu, Rodney alikuwa amesimama mbele ya dirisha. Alivalia suti nyeupe iliyoambatana na shati la pinki ndani. Mikono yake ilikuwa imefungwa kwa uvivu kwenye mifuko yake.
Iwapo wangekuwa wanaume wengine, wangeonekana wastaarabu sana

wakiwa wamevalia hivyo. Hata hivyo, sura kali ya Rodney yenye hasira haikuweza kubeba vazi hilo maridadi.
Kati ya mambo yote, alionekana kama kipande cha keki kilichotiwa doa na kinyesi cha ng'ombe, ambaye alikuwa Sara.
'Nimekuandalia mavazi. Badilisha haraka kabla hujashuka." Rodney alinyoosha kidole kwenye nguo ya kijani kibichi kwenye sofa na kidevu chake.
“Nguo zangu ziko sawa. Kwanini ni lazima nibadilishe?” Pamela alishangaa.
“Rangi ya mavazi yako ni sawa na ya Sarah,” Rodney alisema kwa utulivu. "Kwa kuwa yeye ni mchumba wangu na mke mtarajiwa wa bosi wa kampuni, sitakuruhusu uvae rangi sawa na yeye."

Sura ya: 472
Baada ya mshangao wa muda, kifua cha Pamela kilihisi kama kinaweza kulipuka kutokana na hasira. "Kuna nini? Kwa nini usiseme kuwa hautaruhusu mimi na Sarah tuwe na jinsia moja pia?”
Rodney alikunja uso kwa maneno yake. “Wewe ni binti kutoka katika familia yenye heshima, lakini mdomo wako umejaa maneno machafu. Mchafu kiasi gani.”
“Kwanini hukusema nilikuwa mchafu uliponiajiri kuwa mkemia wakowa vipodozi?” Pamela alidhihaki. “Muundo wa mavazi yangu ni tofauti na Sarah. Kwanini siwezi kuvaa nguo nyekundu kwa sababu tu Sarah alivaa? Je, unajifikiria kama kijana wa Rais wa Kenya tayari? Anko wako hata

hajachukua nafasi hiyo. Kila mtu katika familia ya Shangwe hana majivuno kama wewe, kwa hivyo walipataje mtoto kama wewe? Rodney, unaweza kuacha kuwa fedheha kwa familia yako?" Baada ya hapo, aligeuka ili kuondoka.
Rodney alikasirika. “Pamela Masanja, usifikiri sijui kwamba ulifananisha rangi na Sarah makusudi. Unachotaka ni kuwaacha watu hapa usiku wa leo wafikiri kuwa wewe ni mrembo kuliko Sarah na kuwafanya watu wamdhihaki. Tayari ana huzuni sana. Kwanini wewe na Lisa hamuwezi kumuacha peke yake?”
Pamela akashusha pumzi ndefu. Alikuwa akihema kwa hasira. “Una kichaa? Ikiwa una mawazo mazuri, kwanini ulianzisha kampuni ya vipodozi? Unapaswa kuwa mwandishi badala yake. Unafikiri ninaweza kusoma mawazo ya Sarah? Ningejuaje angevaa

nguo nyekundu? Na hata kama ningekuwa najua, ni uamuzi wangu kuvaa nguo yoyote ninayotaka. Sarah ni malkia kwenye moyo wako tu, siyo kwenye mioyo ya watu wote."
"Mwanamke mshenzi kama wewe ipo siku yako tu." Rodney alikoroma.
“Siwezi kujisumbua kukujali. Hata hivyo, usifikirie kunifanya nibadilishe nguo zangu, isipokuwa nife. ” Pamela aliendelea kutembea. Hakutaka kubishana na mpumbavu huyo tena.
“Simama hapo hapo...” Akiwa amekasirika, Rodney alinyoosha mkono wake ili kushika mikono yake iliyojaa majimaji. Nguo yake haikuwa
na mabega, na alipoivuta alipokuwa kwa mbele, nusu ya upande wa vazi hilo iliteleza. Hata kifuniko chake cha chuchu kilichomoza.

Rodney alikitazama kifua chake kikiwa bubu, ambacho hakikuwa na chochote cha kukifunika. Ilionekana kana kwamba alikuwa na busta kwenye kifua chake wakati akivaa vazi hilo, lakini Rodney alishangaa kuona dodo zake zikiwa pyua kabisa!
Damu ikammwagika hadi kichwani, na uso wake mzuri ukaganda kama sanamu.
“Rodney, wewe mwanaharamu. Unaangalia nini? ” Pamela alipiga kelele na kujifunika kifua kwa mkono mmoja huku akimpiga kofi usoni na mwingine.
“Unawezaje kunipiga?” Rodney alifunika uso wake. Macho yake ya kuvutia yalitoka kwa hasira.
“Umenivua nguo kwa makusudi, nitaachaje kukupiga?” Uso mzuri wa Pamela ulikunjamana, ama kutokana na

hasira au aibu. Mwanaume hakuwahi kumwona mtupu hapo awali katika maisha yake yote.
"Wewe ndiye ambaye hutaki kubadilisha nguo zako." Rodney alimtishia bila kujiamini, “Ikiwa hutabadilisha, nitakubalisha mimi mwenyewe.”
“Haya basi. Unaweza kunibadilishia nguo.” Pamela alimkaribia kwa hasira. "Ikiwa una ujasiri, nivue nguo zangu. Mbaya zaidi, nitapiga simu polisi na kusema mmenitumia vibaya. Hili likishakuwa suala kubwa, tuone nani ataaibika zaidi. Nimepitia mambo ya aibu zaidi ya haya miaka mitatu iliyopita.”
Kwa hivyo, Rodney alilazimika kuchukua hatua chache nyuma. Alikuwa mrefu zaidi yake, hivyo pumzi yake ilipanda juu alipotazama chini kwenye kifua chake.

“Sawa. Vaa nguo zako haraka na utoke nje,” aliamuru. Hatimaye angemtia kichaa.
Baada ya kumkodolea macho Rodney, Pamela alienda bafuni kuweka nguo zake vizuri. Muda mfupi baadaye, kichwa chake kilitoka bafuni kwa kuchanganyikiwa. "Rodney, nipatiee kifuniko cha chuchu zangu."
Rodney alishikwa na butwaa. Alipoona kile kitu cha waridi sakafuni, alijisikia vibaya sana. "Njoo uchukue mwenyewe, mimi sitaweza kufanya hata kidogo.” “Rodney, lazima uwe mjinga. Unatarajiaje nitoke humu ndani bila kuvaa hivyo?" Pamela akauma meno.
“Unamwita nani mjinga? Sema hivyo kwa mara nyingine, nami nitatupa kitu chako hiki.” Rodney alikasirika.

“Nimekosea, samahani, Rodney Shangwe. Unaweza kunipitishia kifuniko cha chuchu zangu?” Pamela mara moja akaweka tabasamu. "Ikiwa hutaki, naweza tu kukimbia katika hali hii na kupiga kelele kwamba Rais Shangwe ana nia mbaya kwangu. Kuna wanahabari wengi nje, na mpenzi wako Sarah yupo pia.”
"Umecheza vizuri." Tishio la Pamela halikumpa Rodney chaguo ila kujizatiti kuokota na kumpitishia Pamela sidiria yake.
Akiutazama uso wake uliokuwa na haya, Pamela alijikuta hana la kusema na bado anachekesha. Ilibidi achukue tu sidiria yake!
“Mbona unaona haya hivyo? Kwa hiyo, hujawahi kufanya ngono na mwanamke?"

“Sijawahi kufanya mapenzi na mwanamke? Ha! Unatania?" Rodney alicheka kwa kejeli, lakini kwa kweli, hakuwa na ujasiri hata kidogo. Baada ya yote, kwa kweli ilikuwa aibu kwa kijana wa miaka 30 kujulikana kuwa hajawahi kufanya mapenzi.
“Kwa hiyo ulishawahi kufanya ngono? Na nani? Kwa vile Sarah yuko nje niende kumwambia kuwa mchumba wake alikuwa na mwanamke kabla yake? ” Uso wa Pamela wenye tabasamu ulimfanya Rodney ahisi kutaka kumpiga kipigo kizuri.
“Pamela Masanja, hakuna mtu atakayefikiri kuwa wewe ni bubu hata kama husemi chochote,” Rodney alimuonya kwa hali ya huzuni.
“Nilikuwa na hamu ya kutaka kujua tu. Halo, umeniona sasa hivi. Haiwezi kuwa mara yako ya kwanza kumtazama

mwanamke...”
Rodney hakuweza kumvumilia tena, akaufunga mlango wa bafu kwa nguvu na kuondoka kabla Pamela hajamalizia sentensi yake. Ule mshindo mkubwa alipoubamiza mlango ulikuwa wa ajabu kwa Pamela.
Alikuwa na hasira kutokana na aibu. Anawezaje kuwa msafi hivyo? Tsk tsk, Sarah alipata bahati kweli.
Katika ukumbi wa karamu, Rodney alishusha glasi ya divai. Jamani. Hakujua ni kwa sababu Pamela alikuwa amemkera au ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuona laivu chuchu za mwanamke, lakini sehemu maalum ya mwili wake ilihisi joto.
Alipofikiria jambo hilo, ukweli kwamba alikuwa mtu mzima na bado hajagusa uchi wa mwanamke kwa hakika ilimtia aibu sana.

“Rodney, una tatizo gani? Mbona unaonekana katika hali mbaya?" Sarah alimgeukia huku akiwa na wasiwasi.
"Kama sio Pamela ambaye alinikasirisha." Rodney alikasirika. "Inawezekanaje kuwa na mwanamke asiye na aibu katika ulimwengu huu?"
"Alifanya nini?"
"Kwa kweli ... Yeye ... Hakuna chochote." Rodney alipokuwa akikumbuka tukio la chumbani muda mfupi uliopita, hali mbaya ya usoni ilimwangazia.
Moyo wa Sarah ulishtuka alipoona hivyo. Alifanya nini na Pamela hata asingeweza kumwambia kuhusu hilo? Wakati huo huo, alimuona Pamela akitembea kwa uzuri chini ya ngazi, na bado alikuwa amevaa nguo hiyohiyo nyekundu. Ishara ya kuchanganyikiwa

iliangaza machoni pa Sarah. Pamela hakuwa amebadilisha nguo zake.
“Samahani, Sarah. Nilimwomba abadilishe mavazi yake, lakini alikataa.” Rodney alionekana kuwa na hatia. "Siwezi hata kumvua."
“Najua. Ni sawa. Ni mavazi tu. Huna haja ya kuwa na wasiwasi kuhusu hilo.” Sarah alijilazimisha kumfariji.
"Hujambo, Bi. Njau, Bwana Shangwe... " Pamela aliwasalimia ghafla. "Samahani sikubadilisha nguo zangu mwishowe."
Sauti yake ilikuwa kubwa, watu wengi katika jumba la karamu walimtazama.
“Bi. Pamela, kwa nini unahitaji kubadilisha nguo zako?" Meneja Mkuu aliuliza. "Nguo yako usiku wa leo ni ya kushangaza sana."

Sarah alipatwa na hisia mbaya ghafla, na Rodney pia alikuwa ametambua. Kwa hivyo, alionya mara moja, "Pamela ..."
“Bwana Shangwe, samahani. Kwa kweli sikujua kwamba vazi langu lingekuwa la rangi sawa na la Bi Njau.”
Sura ya: 473
Pamela aliinua sauti yake ya hofu na huzuni, akiogopa kwamba watu wa kando hawakuweza kumsikia. "Gauni la kijani kibichi ulilonipa nibadilishe lilikuwa dogo sana. Sikuweza kulivaa. Bi. Njau, tafadhali nijulishe kabla rangi ya mavazi utakayovaa wakati ujao. Ninaogopa nitapata karipio kutoka kwa
Bosi Shangwe ikiwa nitagongana na wewe tena.”
Watu waliokuwa karibu walimtazama

Sarah kwa dharau na kuanza kujadiliana wao kwa wao.
“Hii haina maana sana. Je, ni yeye pekee anayeweza kuvaa rangi nyekundu?”
“Hasa. Rangi ya nguo yake si nzuri kama ya Bi. Masanja, kwa hivyo alimtaka Bi Masanja kuibadilisha. Kwa kweli sikuweza kujua kwamba alikuwa mtu wa aina hii.”
"Bwana Shangwe, pia. Bi. Masanja ndiye mkemia wa vipodozi na mvumbuzi wa bidhaa hii na amechangia pakubwa kwa Osher Corporation, si wa kukosolewa kwa kuvaa mavazi ya rangi sawa na Sarah. Yeye ni bosi sana.”
Nyuso za Rodney na Sarah zilikuwa na rangi zilipwaya kutokana na kukosolewa. Rodney alitaka sana kumpiga Pamela akiwa hai.

Meneja Mkuu alinung'unika kwa siri pia. Hakupaswa kuuliza swali kama hilo. Kwa hiyo, haraka akafikiria njia ya kubadilisha mada kuelekea bidhaa hiyo mpya, lakini habari zilienea kama moto wa nyika. Kufikia wakati huo, tukio kuhusu vazi hilo lilikuwa limesafirishwa katika mkutano na waandishi wa habari.
Macho ya kila mtu kwa Sarah yalijawa na dharau. Sarah alimchukia Pamela hadi kufa. Kwa hayo, alimwita Thomas. "Leo usiku, haijalishi unatumia njia gani, nataka Pamela atamani angekufa."
“Usijali Sarah. Tayari kuna mtu anauchanganya mvinyo ambayo Pamela anakunywa sasa.” Thomas alitabasamu vibaya na kusema, "Leo usiku, kitandani, nitampa mateso mabaya zaidi kuliko kifo."
"Ninatazamia habari zako njema." Sarah alimtazama kwa kuridhika.

Wakati huo huo, Chester alienda kwa Rodney. “Bado nina biashara nyingine ya kushughulikia. Nitaondoka kwanza.”
“Sawa. basi sitakuona ukiwa mbali.” Rodney akampiga bega.
Chester alimtazama Rodney kwa mawazo. “Rodney, ni mavazi tu. Hakuna haja ya kwenda mbali hivyo."
Rodney alikuwa na wasiwasi kutokana na kuambiwa na kaka yake. “Umeelewa vibaya. Mimi...”
"Rodney, hutakiwi kutibua mambo. Kampeni ya Anko wako inakuja, kwa hivyo usiende kuleta shida kwa familia ya Shangwe. Niko mkweli kwako kwa sababu nakuona kama ndugu yangu.” Kisha, Chester akaondoka na Cindy.
Ndani ya gari, Cindy alikuwa akijaribu

kukisia usemi wa Chester kwa makini. “Chester, unafikiri usiku wa leo...”
"Sikufikiri kama Sarah alikuwa mtu wa aina hii." Chester akatoa sigara na kuing'ata katikati ya midomo yake kwa umaridadi. “Hawezi hata kuvumilia mtu aliyevaa mavazi yanayofanana na yake. Kwa kweli hatukumfahamu vizuri hivyo.”
"Hiyo ni sawa. ” Cindy alitabasamu kwa unyonge. Ilionekana kana kwamba alipaswa kukaa mbali na Sarah katika siku zijazo.
“Kwa utu wake, si jambo zuri kwa Rodney kuwa naye,” Chester alilalamika.
•••
Saa tano usiku.
Pamela alihisi kichwa kikizidi kupata kizunguzungu. Alishuku kuwa alikuwa amelewa, hivyo akaondoka zake na

kupanda lifti kwenda kwenye chumba chake cha juu kwa ajili ya kupumzika.
Hata hivyo, wakati anatoka kwenye lifti, kichwa chake kilianza kuzunguka kabla ya kuzimia na kuanguka chini. Thomas alitoka kwenye kona kwa tabasamu mbaya na kumnyanyua kutoka chini.
Kiuno chembamba kile cha Pamela nusura kimfanya ashindwe kujidhibiti hapohapo. “Little b*tch, usiku wa leo ndio umeanza. Subiri uone nitakufanyia nini.” Thomas alibana mashavu yake huku akimbeba Pamela kuelekea chumbani.
Alipokaribia kuufungua mlango, aligundua kwamba kwa bahati mbaya alikuwa ameacha kadi yake ya ufunguo kwenye sofa la jumba la karamu.
Muda mfupi baada ya Thomas kuondoka, Jessica Shangwe akiwa na msaidizi wake walipita eneo hilo.

Jessica Shangwe alikuwa ni mmoja wa wageni waalikwa kwenye karamu hiyo. Pamoja na hayo, alikuwa na kazi aliyopewa na Mzee Shangwe kuzuia uhusiano wa Sarah na Rodney. Osher Corporation ilikuwa imekodi karibu vyumba vyote vya hoteli hiyo kwa ajili ya kupumzika wafanyakazi na wageni waalikwa baada ya karamu hiyo.
Mara walipomwona Pamela amelala chini mlangoni, msaidizi wa Jessica alienda kumsaidia kumyanyua. Pamela aliamka kutokana na joto. Mwili wake ulikuwa unawaka moto, akasimama akiwa anaona ukungu, asijue ni wapi alipo. Alipojikwaa na kugongana na yule mwanaume, alihisi kana kwamba amepata kiyoyozi, hivyo akamshikilia mtu huyo na kukataa kumwachia.
“Bibi Mkubwa, si Pamela Masanja huyu...” Msaidizi alitazama kwa woga

uso wa Jessica uliojikunja. Alimfahamu, kwani alimwona alipoitwa nyumbani kwa Mzee Shangwe.
"Kuna mtu amemfanyia kitu." Jessica aliutazama uso wa Pamela uliokuwa umekunjamana.
Msaidizi alishikwa na butwaa. "Lakini huu ni mkutano wa waandishi wa habari wa Osher Corporation. Yeye ndiye mkurugenzi wa utafiti na maendeleo na mhusika mkuu wa usiku wa leo. Ni nani anayethubutu kutmfanyia hivyo?"
“Niletee chumbani kwangu. Unapaswa kufuatilia hapa. Mtu anayemtafuta mtu hapa labda ndiye aliyemdhuru.”
Baada ya kutoa agizo hilo, Jessica alimsaidia Pamela kurudi chumbani kwake.
Walipofika chumbani, mwili wa Pamela

ulikuwa na joto kali kiasi kwamba hakuweza kuvumilia tena, hivyo aliendelea kubingiria pale kitandani.
Jessica alipata maumivu ya kichwa kwa kumtazama. Kwa hivyo, hakuwa na chaguo ila kujaza beseni la maji baridi na kumweka Pamela ndani.
Wakati anamaliza, msaidizi alikuwa amerudi pia.
"Bibi Mkubwa, Thomas alirudi kutafuta mtu sasa hivi. Nilimwona akiingia kwenye njia ya kutokea, ambapo alitembea juu na chini, akitafuta mara nyingi.”
“Thomas...” Jessica alikazia macho. Thomas alikuwa kaka ya Sarah, na alifahamu jina lake kwa mambo yote mabaya ambayo alikuwa amefanya kwa miaka mingi. Rodney alikuwa ametoka tu kuchumbiana na Sarah, lakini Thomas alikuwa tayari hana kizuizi.

Katika siku zijazo, ikiwa Nathan Shangwe angechukua nafasi ya Uais na Sarah akafanikiwa kuwa sehemu ya familia ya Shangwe, je Thomas angekuwa na woga wa sheria?
Babu yake alikuwa sahihi. Haijalishi ni njia gani walitumia, Sarah hakutakiwa kuolewa katika familia ya Shangwe.
“Bibi Mdogo, Bi. Masanja anaonekana kama... hana raha sana. ” Msaidizi aliona haya kwa kusikia sauti ya Pamela.
Jessica alimtazama. "Fahamu Rodney yuko wapi."
Kwenye jumba la karamu chini, Rodney alikuwa akishirikiana na kundi moja la wageni baada ya jingine. Zaidi ya hayo, siku hiyo alikuwa katika hali nzuri, hivyo alikunywa hadi akalewa.

Sarah alimsaidia hadi kwenye lifti. "Rodney, kuwa mwangalifu." “Hapana, Sarah. Nina furaha. ” Rodney alimkumbatia na kucheka.
Sarah alibaki kimya huku akiegemea kwenye kumbatio lake. Alikuwa akifikiria iwapo afanye mapenzi na Rodney usiku ule kwa vile alikuwa amelewa.
Ingawa Rodney alikuwa tayari amemchumbia, familia ya Shangwe ilikuwa dhahiri dhidi yake. Pia haikujulikana ni lini harusi yao ingefanyika. Katika hali hiyo, angeweza pia kupata mimba ya mtoto wa Rodney kwanza. Kufikia wakati huo, familia ya Shangwe ingeachwa bila kuwa na chaguo.
"Rodney, nitakusaidia kurudi chumbani." Alijaribu kumgeuza kwa kumgusa kwa mikono yake.
Akiwa hana uzoefu katika jambo hilo,

Rodney alihisi kana kwamba mwali umewashwa mwilini mwake, na kwa kweli alikosa raha. Hatimaye walipofika kwenye mlango wa chumba chake, Sarah alipapasa-papasa mwilini mwake kwa makusudi kuitafuta ile kadi ya kufungulia chumba. Kwa hivyo, kupumua kwa Rodney kukawa shida kutokana mihemko.
“Bi. Njau unaonekana kuwa muwazi sana kuhusu ngono. Nakumbuka muda si mrefu uliachana na Alvin. ” Sauti ya mwanamke ya dhihaka ilitoka nyuma ya Sarah.
Sura ya: 474
Sarah alishtuka na kugeuza kichwa chake na kumuona Jessica akiwa amesimama nyuma yake. Jessica na Rodney walionekana kufanana kidogo. Walikuwa na macho yaleyale ya kuvutia, lakini macho ya Jessica

yalikuwa yametulia na makali kana kwamba Sarah hakuwa chochote ila chungu tu kwake.
“Dada... Jessica.” Sarah kwa silika aliogopa. Tabia ya Jessica ilikuwa tofauti kabisa na Rodney tangu wakiwa wadogo. Alikuwa jeuri na asiye na moyo.
“Usiniite dada. Sikujui vizuri hivyo.” Jessica alimdokeza msaidizi wake kwa macho. "Nenda ukamchukue Rodney."
Msaidizi alitikisa kichwa kabla hajamchukua Rodney kutoka mikononi mwa Sarah. Sarah aliuma midomo yake. Alikasirika kwamba mipango yake ya awali ilikuwa imevurugika.
“Bi. Shangwe, najua unanidharau kwa sababu familia ya Njau haiwezi kulinganishwa na familia ya Shangwe. Hata hivyo, Rodney ananitendea vizuri

sana. Amejitolea sana kwa ajili yangu hata sitaki kumuumiza tena. Baada ya kupitia mambo mengi, najua ni nani anayestahili kuthaminiwa. Ilimradi Rodney hataniacha, sitamuacha.”
“Sawa, ulirudi kwenye fahamu zako kwa wakati ufaao, pale tu Alvin alipotangaza hadharani kwamba hatarudiana nawe. Kabla ya hapo, hujawahi hata kugundua jinsi Rodney alivyokutendea vyema.” Sauti ya Jessica ilikuwa ya kejeli.
Maneno yake yalikuwa butu, na uso mzuri wa Sarah ulibadilika kutokana na pigo hadi kiburi chake. Jessica hakuwa mwanamume, kwa hiyo hakumuhurumia Sarah hata kidogo. Kwa hayo, alimtaka msaidizi wake kumchukua Rodney na kuondoka moja kwa moja.
Mara tu walipoingia kwenye lifti, Jessica aliamuru, "Mpeleke kwenye chumba changu." Msaidizi alishtuka. “Lakini Bi.

Pamela yumo ndani, na kwa sasa yuko...” Ikiwa wangempeleka Rodney ndani wakati huo, je, hawakuwa wakituma kondoo kwenye tundu la simba?
“Yeye ndiye aliyemwalika Thomas. Ukweli kwamba Thomas alithubutu kuweka kitu kwenye kinywaji cha Pamela ni matokeo ya yeye kumwendekeza Sarah. Katika hali hiyo, anapaswa kuchukua jukumu la kumsaidia Pamela. Jessica alipumua baada ya kusema. “Isitoshe, babu alinipa kazi, na sina la kufanya. Hatuwezi kumruhusu Sarah ajiunge na familia ya Shangwe hata iweje. La sivyo, haitadhuru Rodney pekee bali familia ya Shangwe pia...”
Msaidizi akanyamaza ghafla. Yeye, pia, alipendezwa na ukatili wa Jessica wakati mwingine, lakini kwa bahati mbaya, hakuwa mtu wa kawaida.

Rodney, ambaye alikuwa amelewa kabisa, hakujua kwamba alikuwa anapambanishwa. Akatupwa chumbani. Alipofika kitandani, alianza kuvua nguo na viatu bila kujielewa.
Pamela bado alijisikia vibaya sana hata baada ya kulowekwa kwenye maji baridi kwa muda mrefu. Alijilazimisha na kunyata kutoka bafuni. Alipomwona mwanamume mwenye sura nzuri juu ya kitanda, alikuwa kama mwindaji aliyepata mawindo yake. Hakuweza kupinga kumkaribia...
***
Saa nne asubuhi.
Baada ya Rodney kufumbua macho yake kwa ulegevu, kitu cha kwanza alichokiona ni mwanamke aliyekuwa amelala kwenye kumbatio lake, huku uso wake ukiwa umeziba kifuani mwake. Blanketi liliwafunika kwa shida wote wawili. Hata hivyo, bega nzuri la

mwanamke huyo lilifanya damu ya Rodney iende mbio tena. Anaweza kuwa hakuwa na uzoefu, lakini alijua kilichotokea jana yake usiku.
Ingawa ilitokea katika ukungu, alikumbuka alikuwa na usiku mzuri. Hakutarajia kamwe Sarah kuwa mkali kiasi hicho.
“Sarah...” Akainamisha kichwa chake na kumbusu sikio lake.
Mwanamke mikononi mwake aliinua uso wake uliochoka, mdogo mzuri.
Macho yao yakakutana, wakatazamana. Yowe la mshangao likawatoka kwa wakati mmoja.
Rodney alishtuka sana hadi akaruka kitandani, huku Pamela akiogopa sana hivi kwamba alijifunika blanketi haraka.
“F*ck, Rodney Shangwe. Umenifanya

nini?” Pamela alimkazia macho. Macho yake yalionekana kana kwamba alitaka kumla akiwa hai.
“Mimi ndiye napaswa kuuliza swali hilo. ” Rodney alikuwa karibu kuvunjika. “Mbona upo chumbani kwangu? Mbona upo kitandani kwangu?”
“Hiki ndicho chumba chako?” Pamela alipigwa na butwaa.
“Upuuzi. Bila shaka hii ni...” Rodney alitazama huku na kule. Ghafla, alihisi kutojiamini. Hicho hakikuonekana kama chumba chake pia.
“Hiki si chumba chako pia, sawa? Macho ya Pamela yalikuwa mekundu kwa hasira. "Rodney Shangwe, wewe mpumbavu. Kwanini umemzunguka Sarah na kuja kwangu? Ulionekana kumpenda sana. Unapungukiwa na wanawake? Kwanini hukwenda kulala na Sarah?”

"Una uhakika mimi ndiye niliyekuleta humu?" Rodney alikasirika. "Wewe ndiye uliyejipendekeza kwangu na kuingia kisiri nikiwa nimelewa." Alikuwa karibu kupandwa kichaa. Hatimaye alimchumbia Sara baada ya kuuhifhadi kwa bidii ubikira wake, lakini yote yakaharibiwa na mwanamke huyo usiku ndani ya usiku mmoja tu.
“Uh, kwa huo ubongo wako mbovu, nisingependa kufanya mapenzi na wewe hata ukiniomba sana. Mbali na hilo... jana usiku ilikuwa mara yangu ya kwanza pia, sawa?” Pamela alikasirika sana hivi kwamba alitamani kulia.
“Inatosha. Usinichukulie mjinga. Hakuna jinsi mwanamke kigeugeu kama wewe bado awe ni bikira. Nimekuona ukiwa na wanaume wengine...”
Kabla hajamalizia sentensi yake, aliona

madoa ya damu kwenye shuka nyeupe, akaganda ghafla. Madoa ya damu hayakuweza kughushiwa. Hakutarajia kwamba ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Pamela pia. Alikuwa katika butwaa na kupoteza akili yake. “Haya, usitafute mimi niwajibike. Sitawajibika kwako.”
"Mjinga wewe, lazima nitakuua." Pamela alichukua mto na alikuwa karibu kugonga mwili wake.
Wakati huo, mlango wa chumba ulifunguliwa, na kundi la waandishi wa habari wakaingia.
Tukio hilo lilijulikana sana. Rodney angeweza kuvunjika hapo hapo. Kwa nini alikutana na vitu kama hivyo kila wakati? “Bwana Shangwe, si uko kwenye uhusiano na Sarah? Kwa nini ulilala na Director Masanja?"
"Bwana Shangwe, hii inamaanisha kuwa una uhusiano wa kimapenzi?"

“Bi. Masanja, unaweza kuelezea uhusiano wako na Bwana Shangwe?"
"Inaonekana usiku wa jana ulikuwa mtamu sana."
Waandishi wa habari waliendelea kupiga kamera zao kwa Pamela na Rodney. Pamela haraka akajifunga blanketi na kutorokea bafuni. Je, hili halikuwa wazo ambalo alikuwa ametumia dhidi ya Rodney mara ya mwisho? Kamwe hakutarajia kwamba angepigwa picha siku hiyo na hisia hiyo ikamtia wazimu. Kwanini alikuwa na bahati mbaya? Alimkosea nani hasa?
Kwa bahati nzuri, walinzi wa hoteli hiyo walikimbia na kusafisha eneo la tukio. Baada ya Pamela kubadilisha nguo na kutoka bafuni kisiri, Rodney alimfokea meneja wa hoteli hiyo kwa sauti ya hasira.

"Wanahabari hao walikimbia moja kwa moja bila hata kuhitaji kubisha hodi. Hii ina maana kwamba walikuwa na kadi muhimu. Hoteli yako inafanya nini?"
“Bwana Shangwe, ulifanya mkutano na waandishi wa habari hapa jana usiku. Ilikuwa Osher Corporation ambaye alikodi vyumba kwa ajili ya waandishi wa habari. Walilala kwenye vyumba vya chini jana usiku. Kuhusu kwamba waliingia kwa sababu walikuwa na kadi muhimu, sijui iliishiaje mikononi mwao,” meneja wa hoteli alieleza kwa aibu.
“Nendeni mkachunguze hili kwa kina. Sasa hivi.” Akiwa amekasirika, Rodney alimuonya Pamela, “Ikiwa vyombo vya habari vitakuuliza, unapaswa kusema wewe ndiye uliyenitongoza. Unaelewa? Una mwanaume hata hivyo, ilhali mimi ni tofauti. Sara ataachana nami.”

“Nilikutongoza?” Pamela alikosa la kusema. “Hata wewe ni mwanaume? Je, huoni aibu? Unachofanya ni kujifikiria mwenyewe. Umewahi kufikiria jinsi jambo hili ni muhimu kwangu, nikiwa kama mwanamke?"
“Acha kuongea upuuzi. Nikigundua kuwa wewe ndiye uliyeniingiza hapa jana usiku, matokeo yake yatakuwa mabaya sana,” Rodney alimuonya kwa huzuni.
"Vivyo hivyo kwako." Pamela alitoka nje kwa hasira, lakini alipokuwa mlangoni, aligeuza kichwa chake. “Usijali, Sarah hataachana nawe. Sasa kwa kuwa hana Alvin, wewe ndiye pekee mtu ambaye anaweza kumtegemea. Atakachofanya ni kutupa hasira kidogo na kujifanya kana kwamba anataka kukuacha. Ukimbembeleza, atakusamehe. Kwa hiyo, hakika atasema kwamba kosa haliko na wewe na kwamba huna hatia.

Atapata kisingizio cha kukutoa katika hili.”
Baada ya hapo, Pamela alifunga mlango kwa nguvu na kuondoka na kumwacha Rodney akishangazwa na maneno yake.
Sura ya: 475
Wakati Pamela alikuwa ametoka tu nje ya hoteli na miguu yake inauma, Lisa akampigia simu.
"Dada, wewe ni wa ajabu." Lisa alicheka sana. "Rodney alimchumbia Sarah tu, na mlifanya naye ngono siku iliyofuata. Unafanya kazi kwa bidii ili kulipiza kisasi kwa Sarah. Wewe na Rodney mko kwenye habari zinazovuma hapa mjini kwa sasa. Kila mtu anajua kuhusu hilo.”
“Achana na mimi Lisa.” Pamela alijihisi mnyonge. “Sijui chochote, sawa?

Nilikunywa pombe kupita kiasi jana usiku, na nikazimia. Ni mara yangu ya kwanza, na ninaharibiwa na yule mpumbavu, Rodney. Najisikia kulia.”
“Lazima kuna mtu amekuchezea chezo,” Lisa alimkumbusha, “Je, umetumia vidonge vya kuzuia mimba? Haraka nenda ukanunue.”
“Uko sawa.” Pamela mara moja alipita kwenye duka la dawa karibu.
Mfanyakazi wa duka la dawa alipogeuka tu ili kumpatia Pamela vidonge vya kudhibiti mimba, simu ya mezani ililia ghafla. Mfanyakazi alipochukua simu, sura yake ilibadilika kidogo.
Alipokata simu, alimwambia Pamela, “Dawa zitakuwa stoo. Nitaenda kuzichukua, kwa hiyo tafadhali subiri kidogo.”

Ndani, mfanyakazi alibadilisha vidonge vya uzazi wa mpango na kutia vidonge vya minyoo kabla hajarudi kwa Pamela. Pamela alilipia kabla hajatoka na kumeza dawa haraka.
Bila kujua, Jessica alikuwa ameketi kwenye Sedan kando ya barabara. Baada ya Pamela kuondoka, Jessica alimpigia Mzee Shangwe simu. "Babu, tayari nimemwomba mfanyakazi wa duka la dawa kubadili tembe za kuzuia mimba."
“Mm, umefanya vizuri. Hii sio haki kwa Pamela, lakini tutafidia familia ya Masanja mara tu atakapokuwa sehemu ya familia ya Shangwe."
Wakati huohuo, Sarah alipoona picha ya Pamela na Rodney wakiwa kwenye chumba kimoja kwenye habari, uso wake mzuri ulikunjamana papo hapo. Je, Jessica hakumchukua Rodney jana

yake usiku? Aliishiaje kulala na Pamela?
Alikasirika sana hadi akampigia simu Thomas kwa haraka. “Pumbavu wewe, jana usiku ulifanya nini hasa? Si ulisema unataka kulala na Pamela? Kwanini ulimruhusu alale na Rodney badala yake?”
"Sijui.” Rodney alikasirika pia. "Nilisahau kadi yangu ya chumba jana, kwa hivyo nilimwacha Pamela kwenye korido. Alikuwa ameenda niliporudi. Nilienda hata chumbani kwake kumtafuta, lakini hakuwepo.”
“Usio na maana wewe! Je, huwezi kufanya lolote ipasavyo?” Sarah alimkaripia.
Haijalishi alikuwa mjinga kiasi gani, alijua kwamba Jessica alikuwa akimfuatilia jana yake usiku. Hili lazima

lilifanywa na Jessica.
Alipokuwa karibu kumlalamikia Rodney, video ya taarifa kutoka kwa mkurugenzi wa Shangwe Corporation mwenyewe, Jason Shangwe, iliibuka ghafla. Alipoingia kwenye video, alikuwa Jason akiwa na mahojiano kwenye mlango wa nyumba yake.
Mwandishi wa habari aliuliza, “Mkurugenzi Shangwe, mwanao, Rodney Shangwe, alilala jana usiku na Pamela Masanja. Umesikia juu yake?" Jason alisema, “Ninayo taarifa, lakini hii si kitu. Pamela ni mchumba wa mwanangu tangu mwanzo.”
"Nini? Lakini je, Rodney hakumchumbia Sarah Njau siku chache zilizopita? Sarah si ndiye mchumba wake halisi?”
Jason alisema, “Ndoa si mchezo wa kitoto. Kuchumbiwa kwa Sarah ni

pendekezo la Rodney mwenyewe. Lakini, familia ya Shangwe haitawahi kuidhinisha ndoa yake wala Sarah kujiunga na familia ya Shangwe. Kuhusu Pamela, yeye ndiye mchumba ambaye kila mtu katika familia ya Shangwe amemchagulia Rodney. Kwa kuwa jambo hili limetokea, familia ya Masanja itakuja Nairobi hivi karibuni kujadili ndoa hiyo.
“Basi, itakuwaje kwa Sara?” aliuliza mwandishi.
"Sisi, familia ya Shangwe, tuna sheria kali za familia. Hatutamruhusu Rodney kuwa na hawara au
mchepuko." Pamoja na hayo, video iliisha.
Mikono ya Sarah ilikuwa ikitetemeka. Aliporudi kwenye fahamu zake, alianza kupiga kelele na kuvunja vitu kwa hasira. Hakuwahi kutarajia familia ya

Shangwe kutomjali sana. Kwa vile walisema hadharani kwamba Pamela ni mchumba wa Rodney, basi yeye alikuwa nani?
Miaka mitatu iliyopita, sifa ya Pamela iliharibiwa kwa sababu ya Thomas. Miaka mitatu baadaye, familia ya Shangwe ingependelea kumkubali b*tch kama Pamela ajiunge na familia
yao. Alikosa nini kulinganisha na Pamela? Kulikuwa na yule mjinga, Rodney pia. Alisema alimpenda jana yake, lakini alifanya ngono na Pamela siku iliyofuata. Wanaume wote walikuwa wazuri bure.
Wakati huo Rodney alipiga simu. Mara moja akaivunja simu yake.
Hata hivyo, alitulia haraka. Rodney hakuweza kusamehewa kirahisi hivyo, lakini pia hakuweza kumuacha. Baada ya yote, mwanamume pekee aliyekuwa naye karibu naye alikuwa Rodney.

Kwa upande mwingine, Rodney alipoona taarifa ya Jason, alikimbia kurudi kwa familia ya Shangwe.
“Baba ulisema upuuzi gani mbele ya waandishi? Pamela alikua mchumba wangu lini? Hata simfahamu. Mchumba wangu ni Sarah.”
Wakiwa njiani Sarah hakupokea simu zake hata kidogo. Alikuwa karibu kushikwa na kichaa. Ilibidi aeleze kila kitu kwa uwazi.
“Umetoa mahari kwa Sarah?” Jason aliuliza kwa ubaridi. "Je, sherehe ya uchumba ilifanyika kati ya familia ya Shangwe na familia ya Njau? Je, Sarah alikutana na wazazi wako na kula chakula pamoja nasi?”
Rodney alishikwa na butwaa. “Tayari nimempendekeza na kumpa pete.

Vyombo vya habari vinafahamu...”
"Mradi tu utaratibu wa uchumba haujafanyika, Sarah sio mchumba wako." Mzee Shangwe alimkata maini kwa ukali. "Zaidi ya hayo, ulilala na Pamela, kwa hivyo unapaswa kuwajibika. Familia ya Shangwe haichezi na wanawake na kuwaacha baadaye.”
"Nikizungumza ya jana usiku, nilifanyiwa mchezo na Jessica. ” Rodney alimtazama Jessica kwa hasira. “Tayari nimeichunguza. Chumba nilicholala jana usiku kilikodiwa chini ya jina lako. Kamera ya ulinzi iliyokuwa mlangoni ilionyesha ni wewe uliyenipeleka chumbani. Ulifanya makusudi.”
"Hiyo ni sawa. Ilikuwa ni mimi.” Uso wa Jessica ulikuwa mtulivu.
“Wewe ni dada yangu. Ungewezaje

kunifanyia hivi?” Rodney akatupa ndimi kali. "Wewe ni mnyama mwenye damu baridi. Utafanya chochote kile ili kupata kibali cha Babu.”
"Funga mdomo wako." Jessica alimtazama kwa macho yake baridi. “Unajua kwanini nilikutupa chumbani jana usiku? Kwa sababu mtu fulani alimwekea Pamela dawa za kumsisimua hisia za mapenzi kwenye ukumbi wa karamu. Mkurugenzi wa utafiti na maendeleo wa kampuni yako alifanyiwa jambo fulani wakati wa mkutano na waandishi wa habari. Kwa kweli sielewi jinsi unavyosimamia kampuni."
'Haiwezekani...” Rodney alishtuka.
"Ikiwa Pamela hakuwa na fahamu, unafikiri angefanya ngono na wewe?" Uso wa Jessica ulijaa kejeli. "Kama hujui, mtu ambaye alimwekea dawa

hizo alikuwa ni kaka mzuri wa Sara."
“Unamaanisha Thomas?” Rodney alishtuka kwa mshangao. Ingekuwa ni watu wengine, asingeamini. Hata hivyo, alipokumbuka mambo ambayo Thomas alimfanyia Pamela hapo awali, hakuthubutu kukataa.
“Kuna kutokuelewana...”
“Nilipoenda hotelini jana usiku, niliona kuna kitu kibaya kwa Pamela. Hakuweza hata kutembea vizuri, kwa hiyo nikamwambia msaidizi wangu ampeleke chumbani kwangu. Baadaye, Thomas alikuwa akitafuta mtu mahali pale nilipomwona Pamela. Alienda hata chumbani kwake kumtafuta.
Kisha, nilifikiria kuangalia kamera za usalama, lakini kwa bahati mbaya, kamera za usalama kwenye ghorofa ya 28 hazikufanya kazi.”

Baada ya Jessica kuongea, Mzee Shangwe alipiga meza kwa hasira. "Thomas ana ujasiri sana."
“Yeye hana ujasiri. Wafanyakazi wa hoteli walijua kuwa dada yake ni mpenzi wa Pili wa Bwana Shangwe, kwa hiyo hawakuthubutu kumuudhi.”
Jessica alimtazama Rodney kwa ujeuri. “Kama si wewe, Thomas asingekuja. Katika hali hiyo, mimi kukutumia kumsaidia Pamela ni suala la haki pia. Ulitatua shida uliyojitengenezea mwenyewe. Je! hiyo si nzuri?
"Zaidi ya hayo, na hali ya Pamela jana usiku, ilikuwa dhahiri kwamba dawa hiyo ilikuwa na nguvu. Hata kumloweka kwenye bafu la maji baridi hakukuwa na maana, na nilihofia huenda jambo fulani lingempata.”

TUKUTANE KURASA 476-480
ONYO: Ni marufuku kusambaza, kukopi wala kuuza kazi hii kwani endapo kama tutakubaini basi sheria itachukua mkondo wake (By: Official Dully)
 
LISA KITABU CHA NANE (10) SIMULIZI...........................LISA
KURASA......................476- 480
PRESENT: SIMULIZI ZA DULLY

Sura ya: 476
Rodney hakuweza kupata neno lolote la kusema. Hakuwahi kufikiria Thomas angethubutu kumwekea dawa Pamela wakati wa mkutano na waandishi wa habari. Haijalishi nini, Pamela alikuwa mbia wa kampuni yake. Zaidi na zaidi, alikuwa mkurugenzi wa idara ya utafiti na maendeleo ambaye alimkabidhi majukumu makubwa. Alipokumbuka jinsi alivyomkaripia Pamela kwa kumtongoza, alihisi majuto na hatia.
"Sis, wewe ndiye uliyewaita waandishi?" Aliuliza huku akiuma mdomo.
“Mmh. Ikiwa nisingelifanya hili kuwa suala kubwa, ungechukuaje jukumu kwa Pamela?" Jessica aliitikia bila hatia yoyote.

“Wewe ni mtu mbaya sana!” Rodney alisema kwa upole, “Kwa bahati mbaya, haina maana hata kama uliwaita waandishi. Sitamuoa Pamela hata nikifa. Sitawahi kumuumiza Sarah maishani mwangu. Mara moja nitafafanua kila kitu kwenye vyombo vya habari.” Kwa hayo, akageuka na kuelekea nje.
Sauti ya Jessica tulivu ilitoka nyuma. “Unaweza kwenda. Ukithubutu kufanya hivyo, hakuna haja ya Osher Corporation kuzindua bidhaa zao mpya tena. Ninachohitaji kufanya ni kufahamisha mamlaka husika. Nina njia nyingi za kuizuia. Sio tu bidhaa mpya, lakini ninaweza hata kufanya kaunta za Osher Corporation kufungwa ndani ya usiku mmoja. Unaweza kujaribu.”
“Wewe...” Rodney alimkazia macho. Ikiwa macho yake yangeweza kumtenganisha, basi angeweza kuwa

vipande vipande. "Babu, baba, mwangalie ..."
"Jessica, ikiwa kuna jambo lolote ambalo huwezi kulisimamia, unaweza kunitafuta wakati wowote," Mzee Shangwe alisema kwa upole. "Tunaweza kuifunga Osher Corporation yake. Inawezekana kumfanya asipate hata senti moja.”
“Asante, babu.” Jessica alitabasamu. Damu ya Rodney ilichemka.
•••
Brighton Gardens.
Pamela alipoona video ya Jason, alijisikia vibaya sana. "Je, wanafamilia wa Shangwe ni wajinga? Ni lini nimekuwa mchumba wa Rodney? Mbona mimi mwenyewe siijui?”

Lisa alimtazama kwa wasiwasi. "Wanafamilia wa Shangwe hawataki Rodney amuoe na Sarah. Ndiyo maana walikusukuma ndani ya hili ili kuwazuia wote wawili.”
“Haha, sitaolewa naye kamwe. Anaweza kufanya chochote anachotaka na Sarah,” Pamela alisema kwa hasira.
Lisa akahema. “Unaweza tu kukiri hilo sasa. Ukikanusha wanamtandao watakuzomea kuwa wewe ni hawara na kusema umeharibu uhusiano wa Rodney na Sarah. Je! unataka kuitwa mchepuko, au ungependa Sarah atambe?"
Pamela alipigwa na butwaa. Alikuwa amekasirika. “Kwanini iko hivi?”
“Ni rahisi. Familia ya Shangwe lazima wamepanga waandishi wa habari

asubuhi ya leo. Labda wanaenda na mtiririko." Lisa alikunja uso. "Kuhusu ukweli kwamba ulinyweshwa dawa jana usiku, nadhani familia ya Shangwe isingefanya hivyo. Je, ulikuwa ukilengwa na mtu mbaya jana?”
“Si kawaida kwa mrembo kama mimi kulengwa na wanaume wenye uchu na tamaa?” Pamela alisema kwa kupigwa na butwaa, “Hapana, Thomas alikuwepo jana. Ni lazima alikuwa mpuuzi huyo.”
Lisa alishangaa, lakini haraka akaamini. “Hiyo lazima iwe hivyo. Ikiwa angethubutu kuingia ndani ya nyumba yako na watu wengine, haishangazi kwamba angekufanyia kitu wakati wa mkutano na waandishi wa habari jana. Baada ya yote, anadhani anaweza kufanya chochote anachotaka kwa kuwa Rodney anamuunga mkono Sarah.
Maadamu Sarah yuko hapa, Rodney

hatathubutu kumfanya chochote.”
"Anachekesha sana." Pamela alitetemeka kwa dharau. "Je, nilikuwa na kinyongo na mtu huyu mchafu katika maisha yangu ya awali?"
“Kwanza, ni wazi kwa sababu ya uzuri wako. Pili, anaweza kutaka kukuoa.” Lisa aliichambua kwa busara. “Wewe ni mwanakemia wa hali ya juu sasa. Zaidi ya hayo, biashara ya familia ya Masanja imekuwa ikikua chini ya usimamizi wa kaka yako. Kwa kweli, sababu New Era Advertisings inayosimamiwa na Thomas bado ipo ni kwamba walitegemea miunganisho ya Alvin.
"Kwa kuwa wamepoteza uungwaji mkono wa Alvin, na Rodney hana uwezo kama huo, Thomas anaweza kufikiria unamfaa. Hajali kufanya mapenzi na wewe kwanza kisha kukuoa baadaye.”

"Zinamtosha lakini?" Pamela alikosa la kusema. "Hakuna mwanamke msomi katika Kenya yote ambaye atataka kuolewa na fisadi kama yeye."
Lisa alicheka. “Usiiweke hivyo. Watu kama Thomas na Sarah wanajiamini sana. Wanaweza hata kufikiri kwamba hatuwezi kujilinganisha nao hata kidogo.”
Pamela alitoa mawazo na kugundua kuwa uwezekano wa kutokea ni mkubwa. Alizidi kuchukizwa na kukosa raha kadri alivyozidi kuwaza juu yake.
“Nafikiri Sarah alijua kuhusu jambo hili pia,” Lisa alisema. “Hawezi kustahimili mbele yako. Nadhani anataka kusubiri hadi Thomas akuharibu na kukuoa. Baada ya hapo, anaweza kukutesa kwa yote anayotaka na, wakati huo huo, kufikia lengo lake la kulipiza kisasi kwangu. Lakini, sidhani walitarajia kuwa

ungelala na Rodney. Nadhani damu ya Sarah lazima inachemka sasa.”
“Kesi mbili hizo.” Pamela alitetemeka kwa hasira. "Sitawaacha wakae kwa amani. Nimeamua. Nataka kuwa mchumba wa Rodney. Maadamu familia ya Shangwe inanikubali rasmi, Sarah atakuwa mchepuko ambaye kila mtu atamdharau.”
Lisa alikosa la kusema. Ilibidi akubali kwamba Pamela hakuwa na chaguo jingine kwa kuwa mambo yalikuwa yameenda hivyo.
“Kwa sasa wewe ni mchumba wa Rodney tu. Bado unaweza kughairi uchumba baadaye. Kufikia wakati huo, Rodney atakuwa bado anahusika na Sarah hata hivyo. Baada ya muda, unaweza kusema Rodney alikuwa akikudanganya wakati nyinyi mkiwa wachumba, kwa hivyo ukaamua

kughairi uchumba. Wakati huo huo, unaweza kupata huruma kutoka kwa umma na kuharibu sifa ya Sarah na Rodney pia.”
“Lisa, mbinu yako ni ya ajabu. ” Pamela alimpa dole gumba. “Siyo Sarah pekee, bali nataka kumfundisha Rodney somo pia. Yule mjinga alisema nimemtongoza asubuhi ya leo. Hata hivyo, Rodney hatakubali mimi ni mchumba wake.”
“Usijali. Familia ya Shangwe tayari inakukubali. Mbali na hilo, waandishi wa habari walipiga picha zenu wawili kitandani wenyewe. Ikiwa atakataa, unaweza kwenda kwa waandishi wa habari na kuwalalamikia kwa machozi, .... ‘Rodney hakusema hivyo aliponibembeleza nilale naye.
Alisema nina uwezo, nina mwili mzuri, na mimi ni mzuri. Vinginevyo, nisingerudi kwa Osher Corporation kwa hiari kufanya kazi kwa ajili yake’...” Lisa aliigiza kwa Pamela.

Pamela alipigwa na butwaa. "Lisa, natambua ... wewe pia ni mjanja sana sasa."
Lisa akatoa macho. “Nimeelewa mikakati yao yote baada ya kutangamana na wengi wao. Jifunze.” “Kwenye akili, una akili sana. La sivyo, Sara asingepoteza kwako.” Pamela alitoa dole gumba.
“Unawaza sana. Sikumpoteza. Mimi ndiye niliyepoteza muda wote. La sivyo, Logan asingepoteza kidole chake.” Lisa alitabasamu kwa uchungu. Hayo ndiyo yalikuwa maumivu yasiyokubalika kabisa moyoni mwake.
Pamela hakujua kujibu, lakini kwa bahati mbaya, baba yake alimpigia simu wakati huu.
“Pamela, mjinga wewe. Unathubutu vipi

kulala na mwanaume mwingine kabla ya kuolewa? Nilikufundisha nini kuhusu kujipenda kama msichana? Isitoshe, huna wanaume wengine wa kulala nao? Rodney tayari ana mpenzi...”
“Baba, hukuelewa. Nilichezewa mchezo mchafu.” Pamela hakuwa na la kufanya zaidi ya kueleza tukio zima.
Mzee Masanja alikaa kimya kwa muda mrefu kabla ya kusema, “Katika hali hiyo, Rodney lazima awajibike kwako. Familia ya Shangwe tayari imewasiliana nami. Mimi na mama yako tunakuja Nairobi leo kula mlo na familia ya Shangwe.”
“Oh!” Pamela hakutarajia familia ya Shangwe kuwa wepesi sana katika vitendo vyao. Kwa hivyo, alifikiria na kumwambia Mheshimiwa Masanja mpango wake.

Mheshimiwa Masanja alikasirika aliposikia. "Nini? Rodney alisema umemtongoza? Lazima awe kipofu. Binti yangu ni mrembo sana, hiyo ni dharau kubwa sana kwako. Sawa. Nitaenda pamoja na chochote unachotaka kufanya. Ingawa familia ya Shangwe ni familia tajiri, familia ya Masanja haijawahi kufikiria kuwategemea. Mimi na mama yako tutashirikiana nawe katika kitendo hiki.”
“Asante, Baba.” Pamela aliguswa sana hivi kwamba akampiga busu.
Lisa, ambaye alimtazama kwa pembeni, alikuwa na wivu. Kwa kweli, aliona wivu mazingira ambayo familia ya Pamela ilikuwa nayo. Pamela alipendwa sana na wazazi na kaka yake tangu alipokuwa mdogo, tofauti na yeye. Ingawa Lisa alikuwa na Joel, bado haikuweza kulinganishwa na familia ya Masanja.

Sura ya: 477
Katika Jumba la Kifahari la Sarah.
Rodney aliendesha gari harakaharaka na kuingia ndani na kumuona Sarah akiwa amekaa kwenye sofa huku akilia. Uso wake ulikuwa na michirizi ya machozi.
“Kwanini uko hapa? Ondoka. Sitaki kukuona.” Sarah alimrushia hasira na kupiga kelele huku akilia, “Ni nani aliyesema atanipenda milele? Hata hivyo, kabla sijajua, ulifanya ngono na mwanamke mwingine. Ninachukia zaidi usaliti maishani mwangu.”
“Sarah, samahani. Naweza kueleza.” Rodney alikasirika mwanzoni, lakini alifadhaika alipomwona usoni. "Jana usiku, Pamela aliwekwa dawa na Thomas, kwa hivyo Jessica alinitupa

kwa Pamela ili kumsaidia. Nilikuwa nimelewa sana wakati huo. Sikujua kilichotokea hata kidogo.”
“Thomas?” Sarah aliogopa sana. Hakufikiri kwamba Rodney angejua jambo hilo haraka hivyo. "Hii ... Hili haliwezekani."
“Dada yangu aliiona kwa macho yake. Pia nilitaka kumtafuta Thomas sasa hivi, lakini nikagundua kuwa alikuwa ametorokea ng'ambo. Ni wazi ana hatia.” Rodney alikasirika. “Sarah, kwanini ulimleta Thomas jana usiku? Baada ya yote, Pamela ni mkurugenzi katika Osher Corporation. Thomas anajiamini kijinga sana. Unapaswa kuweka umbali kutoka kwake katika siku zijazo. Sitaki kumuona tena katika maisha yangu.”
“Wewe... Unanilaumu mimi? Mimi ndiye mwathirika hapa, sawa?"

Sarah alizidi kusononeka, machozi yalizidi kumtoka. “Sitaki pia kuwa na kaka kama yeye, lakini nina chaguo gani? Hii ni hatima yangu. Kama ningelijua, bila shaka ningemzuia.”
"Sikulaumu.” Rodney alitabasamu kwa uchungu. "Sarah, nataka tu uelewe kwamba sikukusaliti kwa makusudi."
“Usiseme zaidi.” Sarah alimsukuma mbali huku macho yake yakiwa mekundu. "Baba yako alisema mwenyewe. Pamela ndiye waliyemchagua kuwa mchumba wako, na mimi ni hawara tu. Sitaki tena kuwa katikati yenu...”
“Sarah, wewe ndiye mwanamke ninayempenda.” Rodney aliushika mkono wake kwa hamaki na kusema kwa shauku, "Kwa ajili yako, naweza kuacha kila kitu."

“Nini... unamaanisha nini?” Sarah alikuwa na hisia mbaya kuhusu hili. Rodney alicheka kwa uchungu.
“Dada yangu aliniambia ikiwa sitamtambua Pamela kama mchumba wangu, familia ya Shangwe itaifunga Osher Corporation. Na yule mwanamke mwenye damu baridi, Jessica, anaweza kweli kufanya hivyo. Ikiwa familia ya Shangwe inanikandamiza, ninaweza kupoteza kila kitu, lakini ni sawa. Bado nina akiba. Nina furaha maadamu niko na wewe.”
Sarah alipigwa na butwaa. Tayari alimchukia Rodney kwa kupoteza haki yake ya urithi wa familia, kampuni ya hangwe. Ikiwa angepoteza na Osher Corporation pia, basi angekuwa na nini kingine? Ilibidi waendelee na hiyo akiba kidogo aliyokuwa nayo? Kiasi hicho kidogo cha akiba kinaweza kudumu kwa muda gani? Labda angelazimika

kuwatunza Rodney na Thomas, vitu viwili visivyo na maana, kwa yale mabilioni ya ada ya kutengana ambayo Alvin alikuwa amempa? Isitoshe, ikiwa angekuwa na Rodney, ambaye alikuwa amepoteza kila kitu, je, wengine hawangemcheka?
"Rodney, asante kwa kunipenda sana." Sarah aliinua macho yake ya machozi. “Nafahamu dhabihu zote ulizonitolea, lakini siwezi kukudhuru. Umejitahidi sana baada ya kuhitimu kuanzisha Osher Corporation. Kuna bidii nyingi sana ndani yake. Kama mwanaume, unapaswa kutanguliza kazi yako. Sitaki udharauliwe na wengine kwa sababu yangu.”
Rodney aliguswa sana. "Sarah, ni sawa. Sijali kudharauliwa na watu wengine. ”
Damu ya Sarah ilichemka. Rodney alipaswa kuwa mjinga, lakini hakuweza

kueleza waziwazi.
“Lakini mimi Siwezi kuruhusu wengine wakudharau. Isitoshe, huenda usijute sasa, lakini ni nani anayejua kama ungejuta katika siku zijazo?” Sarah akahema. "Ikiwa tunaweza kuwa pamoja, natumai huu utakuwa uhusiano usio na majuto."
"Unamaanisha nini? Unanitosa?” Rodney alikuwa katika uchungu.
"Hapana. Tutengane kwa muda. Hata hivyo, umesema unamkubali Pamela tu kama mchumba wako, sio mke. Kwa sasa, nitafanya niwezavyo ili kupata idhini ya familia ya Shangwe.
“Nafikiri watu wawili wanapokuwa pamoja, bado wanahitaji msaada wa wazazi wao. Sitaki kukuona ukitofautiana na familia yako, na ninatumai unaweza kukomaa haraka

pia, kiasi kwamba hakuna mtu anayeweza kukutisha. Naamini unaweza kufanya hivyo.” Sarah alimtazama kwa kumtia moyo.
Rodney aliguswa moyo sana, lakini alizidi kumuonea huruma. "Lakini Sarah, ikiwa nitamkubali Pamela kama mchumba wangu, wengine watakudhihaki."
“Kwako sijali hata nikidhihakiwa. Ilimradi... niko moyoni mwako.” Sarah alishusha macho chini na kuhema. Alikuwa na sura ya huzuni, isiyo na msaada. “Labda mbingu zinataka kunitesa. Maisha yangu ya mapenzi yanaonekana kujawa na magumu. ”
"Sarah, asante kwa dhabihu uliyojitolea kwa ajili yangu." Rodney aliinua mkono wake. “Mimi, Rodney Shangwe, naapa kwamba wewe ndiye pekee

nitakayekupenda milele. Hakika nitakuoa. Subiri tu uone, nami nitakomaa haraka. Nilikuwa mpumbavu sana zamani, bila hamu ya kujiboresha. Nitaitengeneza Osher Corporation kuwa brand bora zaidi ya kimataifa ya vipodozi haraka iwezekanavyo. Nina imani ya kuifanikisha ndoto hii baada ya mwaka mmoja. Kufikia wakati huo, hakuna anayeweza kutuzuia tusiwe pamoja.”
“Sawa. Nitakuwa nakusubiri.”
•••
Baada ya kuondoka kwenye jumba la kifahari la Sarah, Rodney alimwita Chester nje. Alikuwa katika hali mbaya. Hata hivyo, alipokwenda kule, aligundua kuwa Alvin pia alikuwa pale. Alvin alikuwa na uso ulionyooka, na alivaa shati jeusi na suruali nyeusi. Alifanana kabisa na mfalme aliye hai wa kuzimu.
“Kwanini upo hapa pia?” Rodney hakuweza kusimama mbele ya Alvin.

Alvin alikunja uso wake na kumwangalia, ambapo Chester alisema kwa haraka, “Alvin alisikia umepata matatizo, hivyo alikuwa na wasiwasi sana. Rodney, sisi sote ni marafiki wa utotoni ambao tulikua pamoja. Tunapaswa kuwa hivi kwa sababu ya mwanamke?"
“Siyo mwanamke mwingine yeyote. Ni Sarah! ” Sauti ya Rodney ilikuwa ya ukali sana. “Alvin, mwishowe, ni kosa lako kwamba Sarah ni mnyonge sana. Ikiwa sio wewe, familia ya Shangwe isingempinga.
Hakika ni mwanamke mzuri. Ingawa nilimkosea, bado ananijali sana.”
“Kweli?” Chester akarekebisha miwani yake na kubadilishana macho na Alvin.
"Anakujali kwa njia gani?" Alvin alidadisi kidogo.

Rodney alieleza kwa huzuni jinsi familia ya Shangwe ilivyomtisha.
"Sio tu kwamba Sarah hakunilaumu, hata alijali kampuni yangu. Hakutaka wengine wanidharau, kwa hivyo alisema atajitahidi kuwafanya wanafamilia wa Shangwe kukubaliana na yeye. Sarah ni mkarimu sana, lakini wewe, Alvin, hujui hata jinsi ya kumtunza mwanamke mzuri kama huyo. Lazima ujutie sana sasa, lakini kujutia ni bure.”
Alvin aliinua uso wake. Kama ingekuwa hapo awali, huenda angevutiwa na Sara. Angekuwa na mawazo sawa na Rodney. Hata hivyo, hakumpenda Sara tena. Alipotulia na kutafakari, kwa namna fulani alihisi kwamba Rodney alikuwa mtu wa kawaida.
Alitaka sana kumkumbusha Rodney kwamba ikiwa atapoteza kila kitu, mwanamke wa kawaida anaweza hata asitamani kuwa naye.

Lakini, Sarah alikuwa bora kwa ukweli kwamba ingawa alimdharau Rodney, bado angeweza kuonekana kama alikuwa akimfikiria. Kadri Alvin alivyokuwa akimwangalia Rodney ndivyo alivyozidi kuhisi kuwa Rodney anafanana na mzee wake.
Zamani alishuku utu wa Sara, lakini sasa alikuwa na hakika kwamba Sara hakuwa mtu asiye na hatia na mwenye fadhili kama alivyofikiri.
Kwa bahati mbaya, alikuwa amemuumiza Lisa, ambaye alimpenda sana, kwa ajili ya mtu wa aina hiyo.
"Kwa kweli ... Yeye ni mkarimu sana." Baada ya kukutana na macho ya Alvin, Chester alishika glasi yake na kusafisha koo lake. “Kwa hiyo unapanga kufanya nini baadaye?”
Rodney alicheka kwa uchungu. "Ninaweza tu kujifanya kuchumbiana na

Pamela na kuifanya familia ya Shangwe kuacha tahadhari yao. Baada ya hapo, nitatoka nje na kufanya kazi kwa bidii kwa ajili ya Sarah. Nitakuwa na nguvu sana kwamba hakuna mtu katika familia ya Shangwe anayeweza kunizuia. Ngoja. Nilikuwa mvivu sana zamani. Sitakuwa hivyo tena katika siku zijazo.”
"Umewahi kumfikiria Pamela?" Alvin aliongea ghafla. "Umeharibu usichana wake, lakini bado unataka kumtumia."
Sura ya: 478
Rodney aliganda. Baada ya kuhisi hatia ya muda mfupi, mara moja alisema, “Unawaza sana. Mwanamke huyu pia si rahisi kushughulika naye. Nyie hamjui hili, lakini familia ya Masanja inakuja Nairobi leo. Familia hizo mbili zitakula pamoja kesho. Ha! Nadhani lazima alifikiria kuchukua faida ya familia ya Shangwe kwa muda mrefu sasa.

Sitawahi kuoa mwanamke kama yeye.”
Alvin alikunja uso. "Mwanamke anapopatwa na jambo kama hili na hatambuliki kama ni mchumba wako, atasakamwa na maneno ya watu. Watu wengine watasema kwamba alivunja...”
“Alvin, una tatizo gani? Kwanini unaendelea kumtetea Pamela?" Rodney alimkatisha kwa hasira. "Watu wengine wanaweza wasijue hili, lakini nyinyi wawili mnapaswa kujua. Huyo mwanamke ameharibu pia usafi wangu ambao nimeutunza kwa miaka 30. Anapaswa kujua kuhusu hisia zangu kumwelekea Sarah, lakini ilimbidi tu aingie katika hali hii mbaya. Basi, hawezi kunilaumu kwa kupoteza usichana wake kwangu.”
Kuona upendeleo wa Rodney kwa Sarah kulimfanya Alvin atamani sana kumtupa chooni na kumwagia maji ya

baridi ili aamke. Lakini, isingekuwa na manufaa, kama vile yeye alivyokuwa hapo awali. Hakuamini chochote alichosema mtu. Ni kana kwamba alikuwa amepagawa.
“Haya. Kunywa ikiwa uko katika hali mbaya. Hutakuwa na wasiwasi ukiwa mlevi.” Chester alimmiminia Rodney bia.
Rodney alipokuwa amelewa na kulala kwenye sofa ndipo Chester akawasha sigara na kuhema kwa nguvu.
“Kwanini nahisi Sarah siyo kwamba anajaribu kumsaidia kufanikiwa hata kidogo? Ukweli ni kwamba hatampenda bila Osher, kwa sababu kwa sasa familia haimuungi mkono."
“Naamini hivyo pia." Alvin alimpa sura ya ajabu.
"Je, hukumwamini Sarah hapo awali?"

"Yeye ni mzuri sana katika kujifanya. Labda Sarah alibadilika miaka mitatu iliyopita, lakini hatukutambua.”
Chester alimtazama. "Haukwenda kwenye mkutano na waandishi wa habari jana, lakini ilikuwa ajabu sana. Pamela alivaa mavazi ya rangi sawa na Sarah, na Rodney akamkokota Pamela hadi ghorofani na kumlazimisha abadilishe. Unadhani mzee Rodney angefanya hivyo bila kuambiwa na Sarah? Kwa bahati mbaya, vazi jekundu la Pamela jana usiku lilionekana bora kuliko lile la Sarah.”
Alvin alishtuka. Kulingana na uelewa wake wa Rodney, hakika asingefanya jambo kama hilo bila sababu. Rodney alikuwa mtu wa kuropoka na asingefikiria rangi ya nguo za mtu isipokuwa mtu angemchochea. Ni wazi kwamba hakukuwa na mtu mwingine

zaidi ya Sarah ambaye angejali, na Rodney alijali zaidi hisia za Sarah.
"Chester, asante... namshukuru Mungu sikumuoa wakati huo." Alvin alilalamika ghafla, “Je, unafikiri yote aliyosema kuhusu Hisan yalikuwa ya kweli?”
Chester alikuwa na sura ya ajabu machoni pake. Kama ingekuwa hapo awali, angesema alimwamini kabisa, lakini sasa...”Ni vigumu kusema.”
Alvin alitabasamu kwa uchungu. “Sina sifa ya kumcheka Rodney. Nilikuwa kama yeye pia.”
"Nilikuwa vile vile." Chester akahema. “Ndiyo maana sikusema mambo fulani mapema. Anampenda Sara hadi kufa. Nikisema jambo moja baya juu yake, atanirushia mikono kwa kweli.”
"Ikiwa Lisa anajua kwamba Rodney

anamtendea Pamela hivi, nina hakika atakasirika sana," Alvin alinong'ona.
Zamani upumbavu wake ulimuumiza Lisa. Kuanzia siku hiyo, hakutaka mtu yeyote karibu naye aumie tena.
•••
Siku inayofuata.
Gari la Alvin liliingia kwenye maegesho ya Mawenzi Investments. Alipiga honi kwa muda mrefu, lakini mlinzi hakufungua milango. Msimamizi alipokuja, Alvin alifungua mlango.
Baada ya kuona uso tulivu na mzuri wa Alvin, tabasamu la msimamizi lilitetemeka. “Samahani, Bwana Kimaro. Mwenyekiti wetu alisema kuwa magari tusiyoyafahamu hayaruhusiwi kuingia, hasa... yako.”

Alvin akakunja usukani kwa uchungu. Hakufikiri angekuwa mkatili kiasi hicho. Hakuruhusiwa hata kuingia kwenye maegesho ya Mawenzi?
“Ondoka njiani,” Alvin alisema kwa ukali.
“Samahani,...”
Kabla ya msimamizi kumaliza sentensi yake, hundi ya fedha iliwekwa mkononi mwake. "Hizi ndizo pesa za
kunifidia kugonga geti."
Kisha, Alvin akawasha gari na kuelekea getini kwa kishindo. Msimamizi alijihisi hofu.
Muda si mrefu, gari la Lisa lilitokezea. Aliona na kukunja uso kwa macho yaliyokuwa yamemtoka kama mjusi kabanwa na mlango.
“Mwenyekiti Jones, alikuwa ni Bwana Kimaro ndiye aliyegonga geti na

kuvunja. Hata alinipa cheki,” msimamizi alieleza.
Lisa alikunja uso, lakini hakuwa na sababu ya kumfokea msimamizi.
Lisa aliingia ndani na kuona Aston Martin nyeusi ikiwa imeegeshwa kando ya nafasi yake ya kipekee ya kuegesha. Alvin alikaa mbele ya gari huku akiwa amevalia shati jeupe lililokuwa limechomekewa ovyo kwenye suruali yake. Huenda alikuwa amepungua uzito hivi majuzi kwani nguo zake zilionekana kulegea kidogo.
"Alvin Kimaro, kwanini uko hapa? Naamini nimejiweka wazi sana kwako.” Lisa alifunga mlango kwa nguvu baada ya kushuka. Sauti yake ilionekana kukosa subira.
Moyo wa Alvin ulimuuma. Wakati wote huo, hakuja kumtafuta kwenye kampuni kwa sababu aliogopa kwamba

angemtazama kwa macho makali.
“Nina jambo la kuzungumza nawe. Inahusiana na rafiki yako, Pamela.
“Ni nini?” Lisa akanyamaza.
“Tutazungumza hapa? Twende ofisini kwako.” Alvin akatembea kuelekea kwake.
“Sawa.” Lisa alikunja uso. Ikiwa ilikuwa juu ya Pamela, basi ilibidi akubali.
Mara walipofika juu, Lisa alisema moja kwa moja, "Sema."
Alvin akatazama pande zote. “Hivi ndivyo unavyowatendea wageni wako? Kikombe cha kahawa kiko wapi?"
"Ikiwa uko hapa kwa ajili ya kahawa, unaweza kutoka na kugeuka kulia, na kuchukua lifti na kushuka moja kwa

moja." Lisa alisisitiza kwa mikono yake. "Niko busy sana. Sina muda wa kunywa kahawa na Bwana Kimaro.
"Huna huruma kabisa." Moyo wa Alvin ulikuwa na uchungu sana. Hakuwahi kufikiria kwamba angemtumia Pamela kama kisingizio ili tu kumuona. “Kwa nini ulihama?”
"Alvin Kimaro, nilikubali tu kukusikiliza kwa sababu ya Pamela." Lisa alikuwa akipata papara.
“Hutaki kuniona kiasi hicho?” Alvin alimtazama kwa macho yake mazito.
“Hilo si jambo la lazima? Kukutazama tu kunanichukiza.” Lisa hakuficha karaha machoni mwake.
“Nimejishusha sasa kwako vya kutosha. Wewe ni wa hivyo daima. Unapojiona upo sawa, unanidharau kutoka juu, na

matendo yako kwangu ni mabaya zaidi kuliko kifo. Lakini mara tu unapojua kuwa umekosea, unarudi mara moja kunibembeleza na kuomba msamaha. Imetokea zaidi ya mara moja au mbili tu. Sasa nimchoka, naudhika!”
Uso mzuri wa Alvin uligeuka kuwa mnyonge sana kwa maneno yake. Hakuna mtu aliyewahi kumkemea hivi. Hata hivyo, sasa alitambua kwamba alikuwa tayari kuvumilia karipio hilo mradi tu angemwona.
Tangu waachane tena, amekuwa akifikiria juu yake kila siku. Hasa hatia na hamu ambayo ilimfanya ateseke.
"Nipo hapa kukukumbusha tu kwamba ni bora kutomruhusu Pamela kukubaliana na uchumba na Rodney." Alvin alisema kwa shida, “Rodney amelogwa kabisa na Sarah, na hakuna jinsi atamuoa Pamela. Kujifanya

anamchumbia Pamela ni mkakati tu anaotumia kuichelewesha familia ya Shangwe...”
"Hilo ndilo tu ulitaka kusema?" Lisa alimkatisha kwa hasira. “Sihitaji uniambie ninachojua tayari. Je, unafikiri mimi ni mjinga kiasi cha kufikiri kwamba Rodney anampenda Pamela ghafla kwa sababu walilala pamoja usiku mmoja?
"Umewahi kufikiria jinsi watu watakavyomkashifu Pamela ikiwa asingekubali kuwa walikuwa wachumba? Wangesema aliharibu uhusiano wa watu wengine na kumwita malaya.”
Alvin aliguna. Kwa kweli, pia alikuwa amefikiria hilo.
“Unasema haya yote kwa sababu unataka kumzuia Pamela asiingie kati ya Rodney na Sarah, sivyo? Pia

unafanya bidii ili kuhakikisha Sarah anapata furaha.” Lisa alicheka.
“Sio hivyo. Lisa, sikumjua Sarah vizuri hapo awali. Lakini mambo mengi sana yametokea hivi majuzi hivi kwamba sasa ninatambua kwamba nilikuwa kipofu hapo awali. Yeye si rahisi hivyo.” Alvin alijitetea kwa haraka, “Kama Pamela ataendelea na hili, atakuwa lishe ya kanuni kati ya Sarah na Rodney. Rodney amevurugwa akili kabisa na Sarah. Hisia zake kwake ni kubwa mno.”
“Oh,” Lisa alijibu kwa unyonge. “Umemaliza? Basi unaweza kwenda.”
Jambo hilo lilimuudhi Alvin. Ni mara ngapi alimwambia aondoke siku hiyo?
“Lisa, nitamfidia Logan, sawa? Nipo tayari kumlipa hata kwa kidole changu.”

Sura ya: 479
Lisa alionekana kushangaa. Hakuwahi kufikiria kwamba Alvin Kimaro, mtu wa juu na mwenye nguvu angependekeza fidia kama hiyo. Machoni mwake, Logan alikuwa ni mlinzi tu. Kwa tabia ya awali ya Alvin, hakukuwa na jinsi angeweza kutumia vidole vyake mwenyewe kufidia.
Alvin alipoona ameacha kuongea, dokezo la dhamira likaangaza kwenye macho yake membamba yenye giza. “Kadiri unavyoweza kunisamehe, niko tayari kumfidia kwa kidole changu mwenyewe. Anaweza hata kukikata yeye mwenyewe.”
Alinyoosha mkono wake na kumtazama kwa macho ya moto. Ilikuwa ni kidole tu. Baada ya hivyo, bado angeweza kumkumbatia na kumbusu. Maumivu ya kupoteza kidole bila shaka

hayangekuwa makubwa kama maumivu ya kumchukia na kumkwepa.
Lisa alitazama vidole vyake. Alijua hapo awali kwamba vidole vyake vilikuwa vyembamba na safi, lakini hajawahi kuona vidole vya mtu vikionekana vizuri kama vyake.
"Hakuna haja." Lisa aligeuka na kusema kwa unyonge, “Kuna faida gani ya kukata kidole chako? Logan hawezi kukibandika kwenye mkono wake hata hivyo.”
Uso mzuri wa Alvin ulidhihirisha tabasamu, na hata macho yake yalikuwa yameng'aa kama mwanga wa nyota. “Lisa, ni kwa sababu unanihisi vibaya? Huwezi kuvumilia nikate kidole changu.”
“Unawaza kupita kiasi.” Lisa alikataa mara moja. “Ni kwa sababu sitaki

kukusamehe, na sitaki kurudiana na wewe. Alvin Kimaro, bado hujanielewa? Kuwa na wewe ni shida sana, na sijawahi kuwa na siku ya amani. Mbali na hilo, unaweza hata kuumiza watoto wako mwenyewe. Siwezi kurudiana tena na mwanaume kama wewe." Alipomaliza tu, aliinuka.
Uso mzuri wa Alvin ulipauka, na bila fahamu akamshika mkono wake. "Unaenda wapi?"
"Ni wazi, ikiwa hutaondoka, basi nitaondoka nikuachie ofisi," Lisa alisema kwa utulivu.
Koo la Alvin likahama kwa maumivu, na mkono wake juu yake ukakaza kidogo. Alipomtazama kwa nusu sekunde, unyonge machoni pake ikabadilishwa na dimbwi la giza. “Lisa, huelewi? Kwa kuwa ulinipata katika maisha haya, usifikirie hata kuniacha.”

"Alvin Kimaro, unaota." Lisa alitazama kwa macho yaliyojaa hasira.
Hata hivyo, Alvin alitabasamu tu. Ilikuwa sawa ikiwa alimchukia au kama alikuwa na hasira naye. Alimradi angeweza kuiona sura yake kuanzia wakati huo tena, angeridhika. Kuhusu wengine, haikujalisha. Kwa kadri ambavyo angekuwa akionana naye, angeweza kumlainisha hatimaye. Lakini, ikiwa angemwachilia sasa, hawangekuwa na uhusiano wowote kati yao.
“Lisa, hukupaswa kurudi kwangu kulipiza kisasi.” Alvin alimkazia macho. “Kama ningeoana na Sarah, hakuna kitu ambacho kingetokea kwako. Lakini uliamua tu kunifanya nikupende sana. Sema, unafikiri ningemwacha mwanamke niliyempenda sana?”
“Kwanini? Utanitishia nini muda huu?”

Lisa alidhihaki. "Samahani kusema hivi, lakini ugonjwa wa baba yangu umepona, na Ngosha Corporation haina uhusiano nami tena. Je, unataka kushughulika na Mawenzi tena? Endelea. Nina pesa nyingi hata hivyo, kwa hivyo ni sawa ikiwa nitaiuza tu Mawenzi Investments. Pesa ni mali tu ya ulimwengu.”
Alvin alishindwa cha kusema. Ndiyo, hakuna kitu ambacho angeweza kumtishia tena. Angeweza kufanya nini kingine?
“Lisa, usinilazimishe. Katika maisha haya, unaweza tu kuwa wangu.” Alimtazama kwa muda na kuyaacha maneno yale aliyodhamiria, na kugeuka kuondoka.
Vile vile, hali nzuri ya Lisa iliharibiwa kwa siku hiyo. Kwa tabia ya Alvin, alikuwa na uhakika kwamba asingekata

tamaa kirahisi. Lakini, hakujua angefanya nini wakati huo.
•••
Saa kumi na moja jioni.
Kelvin aliendesha gari kwenda kumchukua. Alipoingia ndani ya gari, macho yake yalimtoka kwa wasiwasi. "Kelvin, unapaswa kuja kuniona mara chache kwa sasa. Alvin alikuja kwenye kampuni leo. Nahofia hata anaweza kushughulika na wewe kunitishia tena iwapo atajua kuhusu uhusiano wetu.”
“Amekuwa hivyo siku zote. Ni mjinga sana huyu jamaa.” Kelvin alicheka kwa hasira.
“Ndio. ” Lisa alihema kwa sauti ndogo. "Lakini ana nguvu zaidi kuliko alivyokuwa hapo awali. Hakuna kitu kizuri kitakachotokea ikiwa tutapambana naye kwa nguvu."

Kelvin alimtazama sana machoni mwake. Alitaka kumfariji kwamba KIM International ingeanguka hivi karibuni, lakini kwa bahati mbaya, asingemwelewa sasa. “Lisa, kwanini tusi... tusisajili ndoa yetu. Tukishafunga ndoa kihalali, na Alvin hataweza kufanya lolote.”
“Tufunge ndoa?” Lisa alishtuka sana.
Alikuwa amekubali tu pendekezo lake la kuoana, lakini alitaka wafunge ndoa mapema hivyo? Alipigwa butwaa kwa muda.
“Ndiyo. Je, ni ghafla sana? Nilikutisha?” Kelvin alisema kwa aibu, “Lisa, sina chaguo pia. Sitaki kukupoteza tena. Usijali, ndoa na harusi zitafanyika kwa wakati mmoja. Wacha tufanye harusi yetu huko Dar es Salaam ili tumzuie Alvin. Sitaki kuwa kama Alvin. Ingawa

uliolewa naye, hukupata hata harusi ya heshima.”
"Asante." Lisa alihisi utulivu aliposikia maneno yake, na wasiwasi ndani yake ukaondoka. Katika hali ya wakati huo, ilionekana hakuna haja ya kusita tena. Mbali na hilo, Kelvin alikuwa amemngoja kwa muda mrefu sana. Hakutakiwa kumfanya asubiri tena.
“Sawa. nitakubali.” Aliitikia kwa kichwa baada ya muda.
“Basi vizuri. Mara moja nitawaambia watu walioko Dar es Salaam wajiandae. Harusi haitakuwa kubwa ili kuepusha umakini wa watu sana, lakini hakika nitahakikisha kuwa ni nzuri. Wazazi wetu wote wa pande mbili watakuwepo. Sawa, wacha Suzie na Lucas wawe flower girl na page boy wetu,” Kelvin alisema kwa furaha.

“Sawa.” Lisa aliitikia kwa kusitasita. "Lakini ikiwa wazazi wako watagundua kuwa nina watoto wawili ..."
“Wanajua tayari, lakini hakuna wanachoweza kufanya kwa sababu nakupenda sana. Niliwaambia kuwa sitaoa mtu yeyote isipokuwa wewe. Vinginevyo, ningependelea kuacha familia na kuwa mtawa. Hawawezi kufanya lolote kuhusu hilo.”
Kelvin alilitazama tumbo lake na kusema, “Mbali na hilo, kwa vile ulikuwa na mapacha hapo awali, labda utapata wengine wakati ujao. Kisha, familia itakuwa hai.”
Lisa aliona haya kwa aibu. “Usiseme hivyo. Inanifanya nipate shinikizo kidogo...”
“Natania tu. Maadamu ni watoto wako, nitawapenda.” Kelvin akainama na kumbusu paji la uso wake.

Lisa alifumba macho na kujisemea, 'Na iwe hivyo.' Hivi karibuni, angeolewa tena. Katika ndoa hii, alitaka kuzeeka na Kelvin.
Sura ya: 480
Katika mgahawa, familia za Shangwe na Masanja zilikula pamoja.
Mzee Shangwe alikuwepo. Kando yake alikaa Jason na mkewe, pamoja na Carson na Jessica. Mhusika mkuu pekee, Rodney, ndiye aliyekuwa hayupo.
Kujieleza kwa Mheshimiwa Masanja kulikuwa kwa hasira na kutojiamini. Ingawa familia ya Shangwe ilikuwa kubwa zaidi kuliko familia ya Masanja katika biashara na mamlaka, kutokuwepo kwa Rodney kulikuwa ni dharau sana kwa Pamela.

"Mzee Shangwe, kwa kuona kwamba Rodney hajitokezi, kunanitia wasiwasi sana. Pengine hana nia ya kumuoa binti yetu. Hakuna kitu cha kulazimishwa kitakachokuwa kizuri..."
"Labda amekwama kwenye trafiki." Mzee Shangwe alimtazama Jessica. Jessica alichukua simu yake na kutoka nje kupiga simu. “Nitakupa dakika kumi. Ikiwa hutafika hapa kwa wakati, usijisumbue hata kidogo.
"Jessica Shangwe, usiwe mkali sana. Nimekwama kwenye foleni.” Sauti ya hasira ya Rodney ilisikika.
"Unajua vizuri ikiwa umekwama kwenye trafiki au unacheza kwa makusudi." Jessica alisema kwa upole, “Unataka nifanye maamuzi magumu kwa Osher? Kama pia unataka pia kuwapa familia ya Masanja na mimi wakati mgumu, usitegemee maisha yako yatakuwa

rahisi. Nadhani huelewi hali yako.” Hapo akakata simu.
Baada ya kurudi chumbani, hakuna aliyeuliza ni muda gani Rodney angekuja. Hata hivyo, dakika kumi baadaye, Rodney alikimbilia chumbani humo huku akihema. Uso wake mzuri ulikuwa umetulia kwa sababu alikimbia kilomita tatu kwa dakika chache, na hakuweza kutamka neno kwa muda mrefu.
Jason alitabasamu na kusema, “Mzee Masanja, unaweza kuwa na uhakika sasa. Rodney wetu ni mwaminifu sana. Tazama, alitumia nguvu zake zote kukimbia kuja huku.”
Bwana Masanja alimtazama Rodney lakini hakumfikiria sana. Rodney alikuwa amevaa suruali ya jeans ya kimodo na shati ya maua. Alionekana mtanashati, lakini kwanini apendelee

mavazi ya kihuni?
Kabla ya hili, Patrick alikuwa mzuri pia, lakini tabia yake haikuwa nzuri. Kwanini binti yake alikutana na wanaume kama hao kila wakati? Kwa bahati nzuri, Pamela hakukusudia kuolewa naye.
"Rodney, hawa ni wazazi wa Pamela." Jason alianzisha mazungumzo rasmi. “Fanya haraka uwasalimie.”
“Anko, Aunty, Shikamooni”
Rodney alisalimia kwa utii na alikuwa karibu kuketi. Carson alivuta kiti moja kwa moja. "Kaka, nenda ukaketi na shemeji."
Shemeji...?! Pembe za mdomo wa Rodney zilitetemeka, na Pamela pia hakujisikia vizuri.
“Niite tu Pamela. Tunapaswa kuwa karibu na umri sawa."

“Hilo halitapendeza. Familia ya Shangwe inatilia maanani sana heshima katika familia. Hata kama wewe ni mdogo kwangu, lazima nikuite shemeji.” Carson alitabasamu. “Shemeji tuongezane WhatsApp.”
Pamela alidhani Carson alikuwa mkarimu zaidi kuliko Rodney.
Baada ya kutoa simu yake na kumuongeza Carson, Wendy, mama wa Rodney, pia alisema, “Pamela, niongeze na mimi pia. Kwa njia hii, tunaweza kuwasiliana kila wakati. Wazazi wako wako Dar, kwa hivyo unaweza kufikiria tu familia ya Shangwe kama familia yako kuanzia sasa na kuendelea unapokuwa hapa Nairobi.”
“Sawa.” Kwa hayo, Pamela aliongeza WhatsApp ya wanafamilia wote wa Shangwe kabla ya Wendy kutoa

kisanduku cha zawadi na kukabidhi.
“Kwa kuwa ni uchumba, lazima kuwe na zawadi ya uchumba. Hii ni kwa ajili yako.”
Pamela aliifungua na kuona kuna mikufu, vidani, hereni na pete za madini mbalimbali ya thamani kama dhahabu, alamsi na tanzanite na rubby. Mtindo ulikuwa wa kisasa sana na wa asili, na mikufu ilikuwa angavu na safi kama maji.
Rodney alishtuka. Mama yake alikuwa ametumia makumi ya mamilioni ya pesa kununua hivyo vitu katika mnada miaka michache iliyopita. Alidai kuwa ilikuwa ya mke wake wa baadaye, lakini hakutarajia angempa Pamela sasa.
"Mama..."
"Nyamaza." Wendy alimpa mwanga wa

onyo.
Pamela alipigwa na butwaa kidogo. Hakujua chochote kuhusu vito vya thamani hata kidogo.
Hata hivyo, Bi Masanja aliweza kusema. “Hiyo ni ghali sana. Nadhani lazima iwe na thamani ya makumi ya mamilioni ya pesa."
“Kuna zaidi. Nimeahidi hapo awali mradi Pamela yuko tayari kuolewa na familia ya Shangwe, ninaweza kumpa asilimia 10 ya hisa za Shangwe Corporation. Mzee Shangwe alisema kwa sauti nzito, “Ichukue. Hakuna njia ambayo familia ya Shangwe itamtendea vibaya Pamela.”
Familia ya Masanja ilipigwa na butwaa. Bwana Masanja alishangaa zaidi. Familia ya Shangwe ilikuwa kweli familia nzuri, lakini ilikuwa ni huruma kwamba hakumpenda Rodney.

Baada ya chakula, Mzee Shangwe alisema, “Rodney, wapeleke wakwe zako kwenye uwanja wa ndege. Wanarudi Dar es Salaam usiku wa leo.”
“Sawa,” Rodney alijibu.
Alipoenda kuchukua gari, Bw. Masanja alilalamika, “Isipokuwa kwa tabia mbovu ya Rodney, familia nyingine ya Shangwe ni nzuri sana. Hawana kiburi ambacho familia kubwa na tajiri huwa nacho."
“Uko sahihi kabisa baba.” Pamela alikubali kwa kichwa.
Hata hivyo, Bibi Masanja alimhurumia. "Kwa kweli, Carson ni mzuri sana. Kwanini hukuchumbiwa naye badala yake?”
Punde, Rodney aliendesha gari. Kwake

ilikuwa ni vigumu kuzungumza na Bw. na Bi. Masanja, lakini njiani, Pamela alikuwa akidekezwa sana na wazazi wake. Ilikuwa wazi kuwa familia ya Masanja ilimpenda Pamela sana. Hali ya familia ya Masanja ilionekana kuwa nzuri, tofauti na baadhi ya familia ndogo za wenyeji ambao walijaribu kujipendekeza kwake mara tu waliposikia kwamba alikuwa kutoka kwa familia ya Shangwe.
Baada tu ya Bwana na Bibi Masanja kuingia kwenye ndege, Pamela na Rodney waliondoka.
Rodney alisema moja kwa moja, “Sina chaguo ila kukubaliana na ndoa hii kwa sasa, lakini usifikirie sana kuihusu. Sitawahi kukupenda, na sitawahi kuwajibika kwako. Kwa hiyo, nirudishie sanduku la zawadi ambalo mama yangu alikupa."

Pamela alipigwa na butwaa. Alijua kwamba Rodney hakuwa na akili kabisa, lakini hakutegemea angekosa na busara pia hadi akataka kumpokonya zawadi ambayo hakumpa yeye.
“Fanya haraka unipe.” Rodney aliaibishwa na macho yake, lakini hakuwa na chaguo. Hakuweza kumuumiza Sarah. "Nitampa Sarah."
Pamela alisema, “Ikiwa mama yako atajua, atakufa kwa hasira"
“Hutaki kurudisha?” Rodney alimkazia macho. "Pamela Masanja, kisanduku hiki cha vito ni ghali kama mimi. Sio kitu ambacho unaweza kumudu kubaki nacho. ”
“Ndiyo ... ni ghali kabisa." Pamela akakitoa na kukipungia kwa makusudi mbele yake. "Lakini wewe? Sahau.

Ingawa wewe ni sehemu ya familia ya Shangwe, huna hadhi yoyote, na huna haki yoyote ya kurithi. Kuhusu Osher, kama singekupa fomula, ingekuwa imeshuka katika miaka miwili ijayo.”
“Wewe...” Uso wa Rodney ulikunjamana kwa hasira. Alikuwa mtu mzuri sana, lakini alizungumza kana kwamba hana thamani.
“Kama mwanaume, huoni aibu kuishi hivi?" Pamela kisha akatoa simu yake ili kupiga simu.
Rodney hakujua anachofanya mpaka alipomsikia Pamela akiita kwa utamu neno ‘Aunty’. Hapo ndipo alipogundua kuwa mwanamke huyu alikuwa amempigia simu mama yake.
"Pamela Masanja, nipe simu." Rodney alinyoosha mkono kuinyakua.

"Rodney Shangwe, unathubutu kunipiga?" Pamela alifoka huku akikwepa. “Sawa, Aunty. Rodney alisema anataka kifurushi cha zawadi uliyonipa. Alisema kwamba si kitu ninachoweza kustahili, na anataka kumpa Sarah.”
“Mama, sikufanya hivyo. Usimsikilize... ” Rodney alikuwa na wasiwasi sana hivi kwamba alimkumbatia Pamela akijaribu kunyakua simu yake na kujieleza, ndipo akagundua kuwa alipiga nambari isiyo sahihi.
Pamela aliangua kicheko. “Si ulikuwa na kiburi mapema? Je! hukutaka kumpa Sara?”
"Pamela Masanja, unanidanganya." Rodney alipandwa na hasira. Alitaka kumfundisha somo, lakini ghafla akagundua kuwa alikuwa akimkumbatia kwa nguvu. Akamsukuma.

“Mmmh... Nahitaji kwenda kuoga. Ninaogopa kuwa mgonjwa kwa kumkumbatia mtu kama wewe.” Pamela alitoka nje ya uwanja wa ndege akiwa na uso uliochukizwa.
"Wewe ndiye mgonjwa." Rodney alifoka.
“Oh, ulikuwa hujui?” Pamela alimtazama tena kwa sura ngumu. “Baada ya Lisa kulala na Alvin mara ya mwisho, ilimbidi kukimbilia hospitali kufanyiwa uchunguzi. Aliogopa kupata ugonjwa kwa sababu Alvin alikuwa kwenye uhusiano na Sarah, ambaye alilala na yule Hisan Gadaffi... Unahitaji niongee kuhusu Hisan? Alitumia madawa ya kulevya na alipenda kulala na kila aina ya wanawake. Nani alijua kama alipata ugonjwa? Kwanini tena ulifikiri Alvin alikataa kumgusa Sarah? Yeye pia ana wasiwasi wake mwenyewe."

TUKUTANE KURASA 481-485
ONYO: Ni marufuku kusambaza, kukopi wala kuuza kazi hii kwani endapo kama tutakubaini basi sheria itachukua mkondo wake (By: Official Dully)
 
Back
Top Bottom