Simulizi: Lisa

Simulizi: Lisa

Sura ya 1279

Loida alisita, lakini bado alizungumza ukweli, “Si kwamba tu Chester alitoa amri ya kumtunza Cindy, bali hata Madam Choka na Mr. Choka mwenyewe walimtanguliza sana. Siku moja kabla ya jana, Cindy alipokuja kwenye kampuni, familia ya Choka ilituma dereva maalum kumchukua Cindy kwa chakula. Waandishi wa habari hata walipiga picha za shopping za Cindy na Madam Choka. Ni kwamba vyombo vya habari havikuthubutu kufichua picha hizo. Lakini, Hamad ana uhusiano mpana, kwa hivyo bado aligundua."

Loida alinyamaza kwa muda na kumtazama Eliza kwa huruma. “Lizzie, ni sawa. Kuwa wazi zaidi juu yake. Kwa kweli, Chester si mtu mzuri. Acha Cindy amshughulikie. Na wewe… Naam, wanawake wana mahitaji pia, sivyo? Nenda naye tu kwani umepata mtu wa kukukidhi."

"Asante. Hakika unajua jinsi ya kufariji mtu." Eliza alikosa la kusema kwa muda.

"Inaweza kuwa ... ujuzi wa Chester sio mzuri?" Aliuliza Loida kwa jazba kwani Eliza hakusema neno.

"... Sio hivyo."

Loida akashusha pumzi ya raha. "Nilijua. Chester ana umbo refu na pana. Hawezi kuwa na ujuzi mbaya."

Eliza kichwa kilimuuma sana hata hakutaka kuongea.

Akatoa simu yake na kuingia Facebook. Katika muda usiozidi nusu saa, habari kuhusu Simwendo zilikuwa zimeshuka hadi nafasi ya kumi kwenye orodha ya mada zinazovuma, huku utafutaji motomoto wa Gladys ukiwa wa kwanza. Wanamtandao hao walikuwa wamechimba kwa kina kila kitu kumhusu, kutia ndani habari kuhusu yeye kutongoza marafiki wa kiume wa watu wengine alipokuwa masomoni. Watu wengine pia walisema kwamba aliwahi kuwa mhudumu wa baa. Kimsingi, sifa ya Gladys iliharibiwa. Kila mtu alimchukia.

Wakati huo huo, Simwendo aliomba msamaha haraka hadharani na kukubali makosa yake.

Hata hivyo, barua hiyo ndefu ya kuomba msamaha ilidokeza zaidi kwamba alidanganya tu kwa sababu ya kutongozwa na Gladys. Alikiri kwamba alimdhulumu mkewe na bintiye. Angeweza kugeuza jani jipya na kumtunza mke wake na binti yake vizuri. Pia alimwomba kila mtu asimsumbue binti yake.

Baadaye, akaunti za barua taka zilimtetea Stuart kwa kusema kwamba alikuwa mwanamume halisi na kwamba Gladys alikuwa kahaba tu. Kwa hiyo, lazima awe amerogwa na Gladys.

Loida alikemea, “Makamu wa Mkurugenzi Joslin hana haya. Je, watu ndani ya kampuni hawajui tabia yake? Sio siku yake ya kwanza kulala na wafanyikazi wake. Namhurumia mke wake. Hata sasa bado anavumilia hili.”

"Ni mkakati wa kawaida wa ofisi ya uhusiano wa umma." Eliza alisema, “Nenda kwa kampuni ukaangalie hali ilivyo. Nitarudi kupumzika kwanza.”

“Sawa.”

Baada ya gari kumpeleka Eliza kwenye apartment yake, alienda kubadilisha nguo nyingine na kuvaa wigi. alitoka na gari nyeusi aina ya Buick.

Gari liliingia kwenye kilabu cha faragha sana. Eliza aliifuta kadi yake na kuingia kwenye chumba cha faragha mara moja.

Mwanamume zaidi ya miaka 30 aliketi ndani. Alivaa fulana ya polo nyeupe na suruali ya jeans ambayo ilikuwa ya kawaida na ya asili. Macho ya mshangao yalimtoka alipomuona Eliza.

Eliza akavua wigi lake na kulitupa kwenye sofa. Alinyoosha mkono wake. “Ni mara yetu ya kwanza kukutana, Bw. Levi Sweke. Nimefurahi kukutana nawe.”

“Nimefurahi kukutana nawe pia.” Levi alimshika mkono kwa msisimko kidogo. "Bi Robbins, inaonekana kama umemdanganya kila mtu. Sielewi kwa nini unamshambulia Gladys ambaye anatoka kampuni moja na wewe kupitia mimi? Je, ninyi wawili mna kinyongo?"

"Gladys sio kitu." Eliza aliutoa mkono wake na kukaa kwenye sofa.

Levi akamkabidhi glasi ya mvinyo mwekundu kwa haraka.

Eliza akatikisa kichwa. Macho yake mazuri yalionekana kutokuwa na mwisho. “Lengo langu ni Joslin Simwendo na Felix Media. Pia nataka kumfanya Chester aondoke kwenye tasnia ya burudani.”

Eliza alikuwa na hamu ya kujua ikiwa Cindy angeweza kufanikiwa kurudi ikiwa alihusika katika kashfa nyingine. Kwa upande wa Eliza, yeye hakuwa na wasiwasi kuhusu sifa yake hata kidogo.

Siku iliyofuata, Gladys alifadhaika sana. Aina zote za brands kubwa alizokuwa na mikataba nazo zilikuwa zikifanya kazi kusitisha mikataba yao naye, na alibadilishwa kutoka kwa maonyesho ambayo alipaswa kuigiza.
 
Kwa sababu ya mabadiliko ya dakika za mwisho ya waigizaji, maonyesho yote yalikuwa yamesimamishwa kwa siku chache hizi.

Eliza alifurahi kupumzika nyumbani. Wakati Loida alipomtembelea Eliza, alisema, “nilipokuja kutoka ofisini, kampuni kadhaa zilisisitiza kusitisha kandarasi zao na Gladys. Gladys alikuwa akilia ofisini, akiomba kukutana na Makamu wa Mkurugenzi Joslin Simwendo na Mkurugenzi Shadrack Mutui. Lakini hakuna mtu aliyekuwa na wasiwasi naye.”

“Anahitaji kuzoea. Ni rahisi kuanguka kutoka mbinguni hadi kuzimu katika tasnia ya burudani.” Eliza alikula nati bila kujali. "Usikubali maneno ya watu wowote wanapokubembeleza."

“Kweli.” Loida alikosoa kwa sauti nyororo, "Simwendo sio mzuri. Licha ya tukio hilo jana, bado alikwenda na kujiburudisha na watu wengine kwenye baa. Hakuwa na wasiwasi hata kidogo.”

Eliza aliposikia hivyo alikunja midomo yake. Anaweza kuwa hana wasiwasi sasa, lakini angetokwa na machozi kesho.

Siku ya tatu, vile vile kila mtu alifikiri kwamba jambo linalowahusu Gladys na Simwendo lisingeonekana tena, ghafla mtu fulani alivujisha jumbe za kutongozana kati ya Simwendo na wasanii wengine wa kampuni hiyo pamoja na picha za ndani. Picha na jumbe hizo hazikuwa sawa na zilivutia kila mtu.

Baadhi ya wasanii hao walikuwa wameachana na tasnia ya burudani, huku wengine wakiwa wapya. Wapo pia waliokuwa maarufu katika tasnia ya burudani kwa muda huo.

Mtu aliyevujisha picha hizo alinasa nyuso za wanawake hao kimakusudi, na kusababisha watumiaji wa mtandao kubahatisha.

[Damn. Huyu Simwendo anawachukulia wanawake katika tasnia ya burudani kama maharimu wake? Je, kweli amelala na wanawake wangapi?]

[Ninahisi kichefuchefu na jumbe hizo. Amekuwa akilala na watu mashuhuri na kupata faida?]

[Unafikiri msanii wa kike wa Felix Media mwenye jina la ukoo linaloanza na T ni nani? Savannah Tango au Cindy Tambwe?]

[Inawezekana zaidi kuwa Cindy. Hapo awali, kulikuwa na uvumi kwamba Cindy ana mtu anayemuunga mkono. Vinginevyo, hangeweza kurudi kwa kutumia rasilimali nyingi za Felix Media. Ilibainika kuwa anahusika na kigogo wa juu wa kampuni.]

[Nadhani ni Cindy pia. Mimi naamini hilo. Nilipenda sana nyimbo za Cindy baada ya kutazama 'The Treasured Voice' hivi majuzi. Lazima nimekuwa kipofu. Maoni yangu yamepotoshwa.]

[Vema, je, mahusiano katika tasnia ya burudani si ya fujo kila wakati? Kwa nini kusiwe na mafisadi kama Joslin Simwendo?]

[Hata hivyo, je, umeona kwamba Joslin hata hakuomba msamaha baada ya suala lake na Gladyskufichuliwa? Gladys alizomewa sana hadi akaambiwa atoke kwenye tasnia ya burudani. Ninachotaka kusema ni kwamba inachukua vidole viwili kuvunja chawa kwa aina hii ya kashfa.]

[Tunamkosoa Simwendo, lakini kulikuwa na maoni zaidi kutoka kwa watumiaji wa mtandao ambao waliunga mkono Felix Media. Felix Media ina vigogo wazito nyuma yake ambao ndiyo asili ya ufisadi huu.]

[Nani yuko nyuma ya Felix Media?]

[Chunguza tu na utajua. Mwanahisa mkubwa zaidi ni Chester Choka, bwana mdogo wa Choka Corporation. Anatengeneza pesa za kutosha katika uwanja wa matibabu, kwa hivyo anawekeza sana kwenye tasnia ya burudani.]

[Chester amekuwa maarufu kwa kubadilisha marafiki zake wa kike kana kwamba anabadilisha nguo. Lakini, vyombo vya habari vinaogopa sana kumfichua.]

[Chester Choka, je huwezi kutibiwa ugonjwa wako? Hakuna anayekuzuia kupata rafiki wa kike, lakini tafadhali usiharibu tasnia ya burudani.]

[Wacha tususie na Felix Media na tuache kutazama tamthilia na filamu zozote wanazowekeza.]
 
Sura ya 1280

Chester aliona maoni hayo.

Katika chumba cha mkutano, kwa hasira alichukua chupa ya maji kando yake na kumrushia Makamu Mkurugenzi Joslin Simwendo kichwani. “Nimekuwa nikikuambia nini? Nilikuambia uangalie, lakini hii ilifanyika. Je, nilikuwekea kampuni ya kuchagua wapenzi wako?”

Uso wa Simwendo uliojikunja ulijipinda kwa maumivu. Aliogopa sana hata hakuwa na ujasiri wa kukwepa chupa.

Baada ya hapo, alisema huku akivumilia maumivu, “Bwana Choka, ni lazima Ferra anajaribu kuleta matatizo kwa kampuni. Kampuni yetu ilinyakua rasilimali zao mwaka jana, kwa hivyo Levi Sweke lazima atakerwa nayo. Wakati huu, hakika nitamfanya ajutie matendo yake.”

“Sawa. Kwa kuwa una kipaji sana, nenda ukamfanyie fujo,” Chester alisema kwa uso wake wa baridi na mzuri.

Simwendo aliacha kuongea mara moja.

Levi Sweke hakuwa rahisi kushughulika naye katika tasnia ya burudani isipokuwa Chester angechukua hatua dhidi yake.

Shedrick alisema, “Jambo hili limekuwa zito sana. Kuajiri watumiaji wa mtandao kutoa maoni hakutafaa sana. Si hivyo tu hata wasanii wote wa kampuni yetu wameingizwa kwenye kashfa hiyo. Hadi sasa, zaidi ya makampuni kumi yamekuja kwangu na kuomba kusitishwa kwa mikataba yao na wasanii wetu. Sikukubali, na nilisema nitatafuta suluhu haraka iwezekanavyo.”

Chester alikoroma. “Mbali na wasanii wa kampuni yetu, mimi na Shedrick tumeingizwa kwenye fujo pia. Joslin, si una uwezo mzuri? Kwa sababu yako, sijawahi kuwa maarufu kama nilivyo leo.”

"Samahani." Kwa hofu, Joslin Simwendo alisihi, “Bwana Choka, nipe nafasi. Hakika nitabadilisha njia zangu katika siku zijazo. Kwanini msiniadhibu kwanza ili muelezee umma? Kisha, nitakusaidia kwa siri kuhusu suala hili.”

Macho ya Chester kwa Simwendo yalijaa chuki. "Utafanya mkutano na waandishi wa habari hivi sasa ili kuomba msamaha kwa umma na kujiuzulu. Kampuni pia itatoa taarifa ya kile tutakachokufanyia. Pia, unahitaji kubeba jukumu na fidia yote.”

“Sawa, sawa. Nitafanya sasa hivi.”

Simwendo aliondoka mara moja. Kwa kuwa tayari alikuwa na sifa mbaya, sasa hakuwa na woga.

Mbaya zaidi, angefanya kazi nyuma ya pazia. Wanamtandao hawangeweza kuendelea kumtazama katika kesi hiyo.

Shedrick aliutazama mgongo wa Simwendo huku akiwa amekunja uso. "Bwana Choka nilikuambia zamani kwamba Simwendo angevuruga mambo mapema au baadaye kwa sababu ya tamaa yake."

"Ikizingatiwa kuwa amekuwa kwenye tasnia ya burudani kwa miongo kadhaa, ana uzoefu zaidi na uhusiano mzuri kuliko sisi. Nitamfanya apotee atakapokuwa hana thamani.” Ilikuwa ni muda mrefu tangu Chester awe katika hali hiyo mbaya. " Y the way, weka mtu aondoe maoni yote yanayohusiana nami kwenye mtandao. Choka Corporation haiwezi kumudu kuhusika katika kashfa yoyote tena."

Shedrick aliitikia kwa kichwa. "Tayari kuna mtu amezifuta, lakini kuna suala moja ... Kwa sasa, Cindy ndiye msanii katika kampuni yetu ambaye ameingia kwenye kashfa kubwa zaidi ya Simwendo na wasanii wachache wa kike waliohusika naye. Kila mtu anadai kwamba Cindy anapata rasilimali nyingi na kwamba Simwendo anaweza kuwa na…”

Hakuendelea na sentensi yake.

Chester akakunja nyusi zake. "Weka mtu azuie suala hili."

Uso wa Shedrick uligeuka kuwa wa kuchukiza. “Nilitaka, lakini baada ya uchunguzi fulani, nilibaini kwamba wanaojadili suala hilo wengi wao ni wageni. Hata hivyo, nitajaribu tena kwa uwezo yangu. Natumai, inaweza kukandamizwa. ”

"Una hisia kuwa Ferra Film Group ndio ilifanya hivyo?" Chester aliuliza ghafla kwa sauti ya barafu.

“Pengine. Ni mtu kutoka Ferra Film Group ambaye alifichua habari hizo. Lakini, zaidi ya Ferra, kampuni zingine za burudani pia zinahusika, inaonekana wanajaribu kuiweka chini kampuni yetu. Baada ya yote, wamekuwa wakihusudu utendaji wa Felix Media katika miaka michache iliyopita."

"Levi Sweke ndiye CEO wa Ferra Film Group, sawa?" Chester alisimama kwa miguu yake, na macho yake yakawa meusi. "Nadhani amekuwa akiishi kwa raha sana. Nitashughulika na Levi. Sitaki kumuona tena kwenye tasnia ya burudani.”

Kwa hayo, Chester alisimama na kuondoka.
 
Shedrick alipapasa nyusi zake. Hakika, Levi alikuwa akijaribu kuuma zaidi kuliko angeweza kutafuna.

Ikiwa Levi angekuwa kimya, Chester asngejali kumruhusu abaki kwenye tasnia ya burudani. Kwa bahati mbaya alikuwa amemshika Simba masharubu yake.
***
Saa 5:00 jioni, Eliza aliwasiliana na Pamela. "Unafanya nini?"

“Nipo ofisini. Bado sijatoka kazini.” Pamela alisema huku akitabasamu, “Kwa kuchukua hatua ya kunipigia simu, unapanga kuniomba tukutane kwa chakula cha jioni? Lakini sipatikani leo. Nimemuahidi Ian kwamba nitaenda kwake.”

"Kuwa na wakati wako peke yako, huh?" Eliza alizidisha sauti yake. "Pamela, nifanyie upendeleo."

"Sema."

"Lazima umesikia kuhusu suala la Felix Media. Imekuwa mada moto hivi karibuni.”

"Kila mtu nchini Kenya anajua. Hata mlinzi katika kampuni yetu amesikia kuhusu hilo.” Kwa kutajwa kwa jambo hilo, Pamela alimuonea huruma Eliza. "Kama inavyotarajiwa kwa kampuni ya Chester. Wafanyakazi wake ni kama yeye, na Simwendo ni fisadi mmoja tu hivi. Anawachukulia wanawake kama nini? Pia, wanawake hao walikuwa tayari kufanya hivyo kwa ajili ya maisha yao ya baadaye? Sikurejelei wewe. Najua huna chaguo. Lizzie, umevutwa kwenye fujo?"

"Bado. Lakini natumai utamwomba Ian kuziomba idara zinazohusika kutazama Felix Media. Siwezi kumwacha Chester afiche suala hili.”

Pamela alipigwa na butwaa. “Lakini wewe pia uko katika kampuni hiyo. Nini kama-"

“Pamela, sijali. Sitaki tu kumwacha Chester. Ingawa siwezi kumpiga, ninaweza kuchukua hatua dhidi yake.”

“Sawa basi. Biashara yako ni biashara yangu. Hata kama Ian hakubaliani nayo, nitamlazimisha akubali.” Pamela alimuahidi.



Hisia ya uchangamfu iliufunika moyo wa Eliza. " Asante. Baada ya kusema hivyo, usimwambie Ian. Ni sawa kufanya hivyo mara moja au mbili, lakini ikiwa utaendelea kumlazimisha na utambulisho wako kama mpenzi wake, itaathiri uhusiano wako. Nitakutumia ninachotaka kusema, na unaweza kumtamkia vivyo hivyo. Ikizingatiwa kuwa Ian ni mtu mwerevu, hakika ataelewa jambo hilo. By the way, usimwambie mtu yeyote kuhusu hilo. Sitaki lifikie sikio la Chester.”

“Sawa.” Pamela hakuwa mjinga kiasi hicho.

Baada ya kazi, alienda kukutana na Ian.

ian sasa alikuwa anafanya masters yake, na alikuwa na darasa siku hiyo. Alipofika nyumbani kwake, bado alikuwa hajarudi.

Kwa hivyo, alichukua wakati wa kuanza kukata mboga na kupika.

Saa 6:30 jioni, Ian alifika nyumbani. Alipomwona mtu mmoja akikata mboga kwa taabu jikoni, alimkumbatia kwa furaha, “acha kukata. Acha nifanye. Ukikata kidole chako kwa bahati mbaya?"

“Sawa. Nitaacha kukata. Nimekusubiri kwa muda mrefu, na nina jambo la kukuambia.”

Pamela alimshika mkono, akimtoa jikoni. Uso wake mzuri ulionekana mpole.

Uso wake ulimfanya Ian ahisi woga kidogo. Wakati huo, alianza kujitafakari, akijiuliza ikiwa hivi karibuni alikuwa amefanya kosa.

"Bado unakumbuka nilikupigia simu jana usiku na kumkosoa Joslin Simwendo wa Felix Media?"

Kwa kutajwa kwa jambo hilo, mdomo wa Ian ulitetemeka. Angewezaje kusahau? Jana yake usiku, Pamela alimfundisha somo, akisema angemhasi ikiwa angethubutu kuwa kama Simwendo.

“Ndiyo. Mpenzi, nakuahidi kuwa mimi ni mtu mwenye tabia nzuri. Kwa kawaida huwa siingiliani na mtu wa aina hiyo.”

"Ian, nakuamini." Pamela alichukua nafasi ya kuzungusha mikono yake shingoni mwake. Kwa kuwa alitaka mwanaume huyo amfanyie upendeleo, ilimbidi awe mpole na romantic.

Macho ya Ian yalitiwa giza. Kisha, akatazama chini na alikuwa karibu kumbusu.
 
Sura ya 1281

Pamela mara moja alifunika midomo ya Ian. “Acha fujo. Nina jambo la kukuambia. Athari za jambo la Simwende kwa jamii ni mbaya sana. Je, hakuna anayelichunguza?”

“Haiwezekani kulichunguza. Suala liko katika uasherati wa mfanyakazi wa ndani katika Felix Media. Ingawa ni mbaya, Simwende amejitokeza, akaomba msamaha na kujiuzulu. Bila kujali kama kuna hadithi ya ndani ya jambo hilo, amebeba jukumu lote. Zaidi ya hayo, baadhi ya wanawake hao wanaweza kuwa wamefanya hivyo kwa hiari, lakini ni nani anayethubutu kusema na kukiri jambo hilo? Hata watakanusha, acha kusema.”

Pamela alidhihaki kwa kuudhika. “Kwa hiyo ikiwa ameomba msamaha? Anaweza kuendelea kuwa bosi kwa siri, sivyo?”

Ian akashusha pumzi kidogo, akihisi hana msaada.

“Ian, hukuona walichosema wanamtandao? Suala hili lina athari mbaya kwa jamii. Nadhani ikiwa idara husika inaweza kujua kilichotokea ni jambo moja, lakini lazima lichunguzwe. Vinginevyo, matukio zaidi kama haya yatatokea katika siku zijazo. Pia, unapaswa kupata baadhi ya vyombo vya habari vya kawaida ili kukosoa suala hili. Fikiri juu yake. Je, hufikirii Choka Corporation imekuwa na tamaa sana miaka michache iliyopita? Kwanza, wanachukua uwanja wa matibabu, na sasa, wanataka hata kudhibiti tasnia ya burudani. Ikiwa hii itaendelea, wakati ujao…”

Pamela aliuma ulimi wake na kumtazama. "Unaweza kuwa karibu zaidi na Alvin na Chester kwa sababu ya uhusiano wangu na Lisa, lakini ikiwa utamruhusu Chester
aendelea hivi, hakuna mtu hapa Kenya atakayeweza kuwadhibiti tena.

Ian alimtazama kwa kina, "ni nani aliyekuambia haya yote?"

"Unamaanisha nini? kwa nini nisingeweza kuja na hili mimi mwenyewe?” Pamela akakanyaga miguu yake.

"Ni tofauti na wewe kufikiria vitu kama hivyo." Ian alibana uso wake. “Niambie ukweli.”

“Sawa. Eliza ndiye aliyeniambia.” Pamela alisema kwa unyonge, "Chester anadharau. Eliza hampendi, hata hivyo amemtishia kukaa karibu naye. Sio tu kwamba alimtishia, lakini pia haonyeshi heshima yoyote kwake. Anamchukulia tu kama toy. Yeye ni mhuni sana."

Ian alikunja uso huku yeye pia akichukizwa na tabia ya Chester.

Mahusiano yanapaswa kuwa ya maelewano. Wengine wamafanya hivyo kwa mapenzi, ilhali wengine wanafanya kwa ajili ya pesa, lakini haitakuwa na maana ikiwa mahusiano yatahusisha vitisho.

“Lakini Eliza yuko chini ya Felix Media. Mambo yakiwa mazito, hayatamnufaisha.”

Pamela alisema, “Eliza hajali. Zaidi, yeye ni rafiki yangu na Lisa. Hata kama hawezi kuendelea tena katika tasnia ya burudani, anaweza kuanzisha kampuni yake.”

Ian akatikisa kichwa kwa upole. “Wewe…”

“Je, utanifanyia wema huu?” Pamela alimtazama kwa mbwembwe.

“Ndiyo. Kwa kuwa umeliweka hivyo, lazima nikusaidie.” Ian alitabasamu huku mwanga mweusi ukiangaza machoni mwake.

Kwa kweli, familia ya Shangwe ingeweza kuchukua hatua ya kukandamiza Choka Corporation hata kama Pamela asingeileta.

Ingawa Ian alikuwa daima na uhusiano mzuri na Choka Corporation, Chester ilikuwa vigumu kumdhibiti kwa njia nyingi.

Ian hakufanya hivyo mapema kwa sababu hakukuwa na nafasi ya yeye kuifanya kwa kutumia njia sahihi.

Hata hivyo, mambo yalikuwa tofauti sasa.

• • •

Siku iliyofuata, Shedrick aliwaita wasanii wote ofisini kwa ajili ya kikao asubuhi.

Eliza alihudhuria mkutano huo pia.

Katikati ya mkutano, sekretari wa Shedrick aliingia chumbani haraka na kusema kitu karibu na sikio lake. Uso wa Shedrick ulibadilika kidogo kabla hajaondoka kwa mbwembwe.

Kisha, kila mtu katika chumba cha mkutano akaanza kunong’ona. "Je, Mkurugenzi Mutui aliondoka ghafla kwa sababu kuna jambo kubwa limetokea?"

"Labda."

Eliza alisimama na kuchukua mkoba wake. Alipokaribia kuondoka, Cindy alitembea kwa kiburi akiwa amevalia mavazi yake mapya ya maxi.

"Eliza, wewe ndiye uliyeajiri wanamtandao kunituhumu kwenye mtandao?" Cindy alitoa macho ya kifo kwa Eliza.

Mpango wake wa kurejea ulikaribia kufanikiwa hadi, kwa siku mbili zilizopita, watumiaji wengi wa mtandao walidai kwamba alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Simwende, ambayo iliharibu sifa yake tena.

Eliza alimfuata tu Cindy na kumzabua makofi mawili mazito moja kwa kila shavu.
 
Cindy alikasirika sana hadi akabubujikwa na machozi palepale. Madison alimtoa Cindy mara moja. Kisha, akamwonyesha Eliza na kusema, “Sawa. Kumbuka hili kwa sababu hatutaruhusu hili liende kwa urahisi. Mimi binafsi nitampigia simu Bosi Choka ili akufundishe somo.”

"Endelea. Hata hivyo mimi ni mwanamke wake.” Eliza alisema kwa jeuri, “Lakini mimi ni tofauti na Cindy. Ninapendelea kuruhusu uwezo wangu kuzungumza, tofauti na mtu ambaye hana rasilimali au pesa. Hatakuwa na budi ila kungoja kulazimishwa kutoka." Baada ya hapo, aligeuka na kuondoka kwa kiburi.

Cindy alimkazia macho Eliza mgongoni kwa hasira. "Nyie, rudufu haraka picha za uchunguzi na zipelekwe kwa Bwana Choka."

Lazima amuonyeshe Chester jinsi Eliza alivyokuwa na jeuri.

Hakuna aliyemwelewa Chester kuliko Cindy, na Chester aliwachukia zaidi wanawake wasiotii.

Ikizingatiwa alipigwa makofi mawili siku hiyo, angemfanya Eliza alipe zaidi ya mara kumi.

• • •

Katika korido ya ofisi, Loida alimfuata Eliza, ambaye alikuwa mbele yake. Wakati huo alikuwa amechanganyikiwa. Hakutarajia Eliza kuwa kichaa kiasi hicho.

Baada ya yote, hakuna mtu katika kampuni aliyethubutu kumkasirisha Cindy, na hata Shedrick alilazimika kuwa na adabu kwake.

Eliza alikasirika.

Cindy alilazimika kulalamika kuhusu Eliza.

"Eliza, ulikuwa na msukumo sana sasa hivi." Hamad alikasirika. “Najua unamchukia Cindy, lakini hukupaswa kumpiga kofi kwenye hafla ya aina hiyo. Ukiwa na mashahidi wengi, hutaweza kujieleza iwapo Cindy atalalamika kuhusu wewe kwa Chester.”

“Unafikiri Chester atanichukuliaje?” Eliza aligeuka ghafla na kuuliza.

Hamad alipumua.

Hakuwa na hakika jinsi ya kumwambia Eliza kwamba Chester alikuwa na wasiwasi juu ya Cindy. Kwa hivyo, Eliza bila shaka angekuwa katika hali mbaya ikilinganishwa na Cindy.



"Hamad, sio lazima uhisi huruma kwangu." Eliza alicheka. “Ninaelewa mambo mengi. Nilifanya hivyo leo ili kumfanya Chester atambue kuwa nimekuwa na kiburi tangu niwe mwanamke wake. Naam, ni mwanamke wa aina gani anayemchukia zaidi? Jibu ni wanawake wenye viburi. Tangu nilipoungana naye, sijawahi kupata manufaa yoyote, na siwezi kujihusisha naye hivi bila cheo au hadhi.”

Hamad aliona mwanga. Kwa kweli, alifurahi sana wakati Chester na Eliza walipokutana kwa mara ya kwanza. Hata hivyo, mpango wa Cindy kurejea ulimfanya Hamad atambue kuwa uhusiano wa Eliza na Chester haukuwa jambo zuri.

Kwanza, Chester hakumtunza Eliza vizuri.

Pili, hilo lingeamsha wivu wa Cindy.

Hakukuwa na haja ya uhusiano ikiwa hakuna faida.

Je! umewahi kufikiria kwa nini Chester akutoe nje kwa ajili ya Cindy?” Hamad alionyesha wasiwasi wake.

Loida, aliyekuwa nyuma ya Eliza, alisema, “Chester hawezi kuwa mkatili hivyo, sivyo? Ilikuwa ni makofi mawili tu. Baada ya yote, Lizzie amekuwa naye kwa muda mrefu, anastahili sifa hiyo."

Hamad alilazimisha tabasamu. Chester, mtu huyo mkatili, angewezaje kuwa na huruma?

Hakujua kwa nini Chester alimchukulia Cindy kama kipaumbele pia. Kwa Hamad, Cindy hakuweza kulinganishwa na Eliza hata kidogo.

"Pengine si mbaya zaidi, atanilazimisha kuomba msamaha kwa Cindy.”
Eliza akawafariji. “By the way, nyote wawili mnapaswa kuangalia kwa nini Mkurugenzi Mutui aliondoka kwa mwendo wa haraka katikati ya mkutano. Inaonekana kuna jambo kubwa limetokea.”

"Haki. Mimi karibu kusahau kuhusu hilo. Loida, unaweza kumrudisha Eliza.”

Baada ya kutoa agizo hilo, Hamad aliondoka.

Mara Eliza alipofika nyumbani, Loida aliwasiliana naye. "Idara ya usimamizi ilikuja na kufanya ukaguzi juu ya kampuni hivi sasa, kwa hivyo Rais Daley aliitwa kuhojiwa."

“Ilikuwa serious kiasi hicho?” Eliza aliuliza huku akionyesha mshangao.
 
Sura ya 1283

"Mbinu hii ni nzuri." Madam Choka alisema, “Eliza ni msanii wa kawaida tu.
Bila yeye, bado unaweza kumfanya msanii mwingine kuwa maarufu. Nilisikia vyombo vya habari vyote vitaripoti kuhusu Felix Media kupigwa faini usiku wa leo, na basi hakika itaendelea na utafutaji unaovuma. Mtu anahitaji kugeuza usikivu wa umma kwa wakati kama huu, na Eliza ndiye mtu anayefaa zaidi kutolewa kafala."

"Chester, Eliza alikutana kwa hiari na Monte wakati huo. Yeye ndiye aliyejitongozeshsa mwenyewe,” Cindy aliongeza.

Chester alimtazama Cindy kwa ubaya na kucheka. "Ni mpango mzuri sana, huh?"

Kutazama kwake kulifanya nywele za Cindy kusimama, na haraka akatazama chini. "Chester, uliahidi kwamba utaniunga mkono katika kurejea. Naamini wewe si mtu wa kutotimiza neno lako.

Uso wa Chester ulitiwa giza.

Ofisi ilikuwa kimya kwa muda kabla ya kusema, “Mama, bado nina kazi ya kufanya. Mchukue Cindy na muache kunisumbua.”

Kwa kutoridhika, Madam Choka alifungua kinywa chake, lakini Cindy akamvuta mara moja. "Mama, twende."

Madam Choka alikunja nyusi zake. “Hata hivyo, nitafanya hivyo hata kama hutafanya. Nitakuwa upande wa Cindy hata iweje.”

Kwa hayo, alimvuta Cindy na kuondoka zake.

Chester aliinamisha kichwa chake, akaweka vidole vyake virefu, vyembamba kwenye nywele zake, na kukikandamiza kwa upole.

Dakika kumi baadaye, aliwasiliana na Shedrick.

Shedrick alistaajabu aliposikia alichosema Chester. “Unapanga kufanya hivyo kweli? Eliza atakuwa amekasirika."

Chester alisema bila kujali, “Je, hakujiunga na tasnia ya burudani kwa ajili ya kutafuta pesa? Kitu chochote ambacho kinaweza kutatuliwa kwa pesa sio shida."

Shedrick hakujua ajibu nini.

Baada ya kupatana na Eliza, alihisi kwamba Eliza hakuwa mtu ambaye angeweza kushughulikiwa kwa kutumia pesa.

"La sivyo, una masuluhisho mengine?" Chester aliuliza.

Shedrick alihema. "Kuna kashfa za wasanii wengine wa orodha ya A kwenye tasnia ya burudani pia, lakini wana asili ya kuvutia, na kuwafichua kutawaudhi baadhi ya watu. Eliza ndiye msanii pekee asiye na historia ya kuvutia. Asili ya familia yake ni ya wastani, na anatoka katika mji mdogo."

"Imeamuliwa, basi," Chester alisema.

Shedrick alichanganyikiwa. “Unatuonea huruma. Je, nimjulishe Eliza mapema?”

“Mlete tukutane kesho.” Chester alifanya uamuzi kwa njia nyepesi.

• • •

Usiku huo, vyombo vya habari vyote viliripoti kuhusu Felix Media kupigwa faini kubwa.

Baada ya kutazama habari hiyo Eliza alikunywa wine yake kwa raha na kwenda kulala.

Siku iliyofuata, aliamshwa na kugongwa kwa mlango. Akiwa amevalia nguo za kulalia na bado anaonekana kusinzia, akaenda kufungua mlango. “Saa 6:00 asubuhi tu Mbona uko hapa?”

"Mafuta yako motoni," Loida alisema kwa haraka. “Lizzie, uhusiano wako na Monte Karanja umefichuliwa. Sasa, ofisi imejaa waandishi wa habari. Kuna hata waandishi wa habari nje ya mtaa wako. Kila mtu kwenye Mtandao anazungumza juu ya jinsi ulivyokuwa mpenzi wake hapo awali. Zaidi ya hayo, Monte tayari ana mchumba.”

Eliza alikuwa macho kabisa sasa. aliwasha simu yake na kuona watu wengi wakisambaza picha zake za karibu sana na Monte wakati wa miaka yake ya chuo kikuu kwenye Mtandao. Baadhi ya watumiaji waliothibitishwa walidai kuwa alikuwa mwanamke wa Monte Karanja wakati wa miaka yake ya chuo kikuu na kwamba baadaye aliingia katika tasnia ya burudani kwa sababu ya uhusiano wake na Monte. Lakini, Monte alimwacha mara tu alipomchoka, lakini Eliza alijaribu kumlazimisha Monte kumuoa kwa kujiua.

Kulikuwa hata na rekodi za kukaa hospitalini na kufanyiwa upasuaji.

Eliza alikuwa Charity, lakini alikuwa anautumia mwili wa Eliza. Ingawa roho ndani yake ilikuwa imebadilika, kile kilichotokea siku za nyuma hakikuweza kufutika.

Hata hivyo, hakuweza kuelewa. Tayari alikuwa na watu kufuta mambo hayo yote alipoamka wakati huo, kwa hivyo hakuna mtu wa nje aliyejua juu yake. Vipi imekuwaje tena…?
 
Kisha, Eliza akaona kwamba baada ya kashfa yake kufichuliwa kwenye orodha inayovuma, habari za Felix Media kupigwa faini na uchafu wa Cindy ulikuwa umetoweka kwenye orodha hiyo. Kwa wakati huo, Eliza alielewa kila kitu.
Oh. Ilibainika kuwa alikuwa kondoo wa dhabihu kwa kampuni.

Damu ya ubaridi ikaingia moyoni mwake. Ilikuwa ni hisia zile zile alizohisi wakati anatuhumiwa kwa mauaji.

"Lizzie, tufanye nini?" Loida alichanganyikiwa. “Hamad ameenda kwa kampuni hiyo kumtafuta Mkurugenzi Mutui. Natumai, kampuni inaweza kukuondoa kwenye orodha inayovuma haraka iwezekanavyo."

"Shedrick Mutui?" Eliza alimtazama msaidizi wake asiyejua kitu kama vile amesikia mzaha. "Kweli Hamad hajui chochote?"

“Unajua nini?” Loida hakuwa na habari.

"Hiki ni kitendo kilichopangwa na Felix Media. Wananitumia kama mwana-kondoo wa dhabihu.” Eliza alicheka kwa ubaridi. “Tazama! Kashfa ya mwanamke mashuhuri wa orodha ya A ni ya kupendeza sana hivi kwamba umakini wa kashfa za Felix Media umepuuzwa mara moja."

Loida alipigwa na butwaa na kutoamini. "Kampuni lazima iwe kichaa. Wewe ndiye msanii maarufu katika kampuni. Unaingiza pesa nyingi zaidi kila mwaka."

"Kila mtu anaweza kuchukua nafasi yake." Eliza akaweka simu yake chini. "Nitabadilisha, nipate kifungua kinywa, na nielekee kwenye kampuni."

"-Bado uko katika hali ya kupata kifungua kinywa?" Loida alikuwa karibu kwenda kichaa.

"Kwa nini isiwe hivyo? Ninakaribia kupoteza kazi yangu. Je, nijiue kwa njaa pia?”

Kwa hayo, Eliza aligeuka kwa ubaridi. Ikiwa angekuwa mzembe, angeweza kupoteza udhibiti kwa sababu ya hasira au hata kufanya mambo yasiyo ya maana.
Lakini, tayari alikuwa amepitia kifo hapo awali, kwa hivyo ni nini kingine angeogopa?

Alimuonea huruma tu Eliza halisi.

Eliza wa kweli alikosea nini? Alichofanya ni kumpenda mtu asiye sahihi na kujiua kwa sababu ya uhusiano. Lakini, mwishowe, kila mtu aliona uhusiano huo kama mtoto mchanga.

Haikuwa ni haki.

Isitoshe, Eliza alitendewa isivyo haki kwa sababu ya mtu fulani.

Katika chumba cha kuvaa, Eliza alibadilisha nguo za kawaida. Kisha, alikaanga mayai na kuchemsha maziwa. Wakati wa kifungua kinywa, Lisa alimpigia. “Lizzie, uko sawa?”

Onyesho rahisi tu la kujali lilimfanya Eliza ahisi kana kwamba joto kidogo lilikuwa limepenya kwenye moyo wake baridi.

“Hunishuku hata kidogo?” Eliza alishangaa.

Lisa alisema kwa huzuni, “Huniamini kama rafiki? Wewe ndiye uliniambia wakati huo. Ikiwa sio wewe, je, niamini kile watu kwenye mtandao wanasema? Ninakuuliza kama uko sawa, maana yake ninakuuliza ikiwa unaumia kwamba kampuni yako ilikugeuka?"
 
Sura ya 1282

"Hasa, ni kwa sababu suala la Makamu wa MkurugenziJoslin limekuwa na athari mbaya kwa jamii." Loida alisema kwa pumzi, “Hata hivyo, sikuwahi kufikiria kwamba kwa uhusiano aliokuwa nao Chester, wangeweza kumchunguza. Nilisikia alipigwa faini pia. Nadhani kuanzia sasa Felix Media italazimika kuweka hadhi ya chini katika tasnia ya burudani kwa muda mrefu.”

Baada ya Eliza kuongea kwa muda mfupi kwenye simu na Loida, muda si mrefu Levi akampigia. Alisikika kusisimka. “Eliza, una kipaji. Iwapo idara ya uangalizi itaichunguza Felix Media, hakika hawataweza kuiondoa kwa urahisi hivyo.”

“Mambo vipi mwisho wako?” Eliza aliuliza bila kujali.

"Kuhusu hilo ... sithubutu kwenda nje." Levi alinong’ona, “Nilihisi kama kuna mtu alikuwa akinishika mkia nilipoenda ofisini jana."
.

"Unahitaji kujitengenezea ajali." Eliza alitoa pendekezo. "Fanya ionekane kama mtu alijaribu kulipiza kisasi kwa makusudi kwako."

"Unamaanisha nini?" Levi alikuwa mnyonge.

“Umma unajua wewe ndiye uliyefichua suala la Joslin Simwende. Iwapo kitu kitakutokea kwa kuwa idara ya usimamizi inachunguza suala hilo, unafikiri… idara husika itafikiria nini?” Eliza alimkumbusha kwa utulivu.

Hapo ndipo Levi alipoelewa hoja yake. "Eliza, wewe ni kweli ..."

“Nitakata simu sasa hivi.”

Eliza hakutaka kumsikiliza akiendelea. Ilikuwa juu ya Levi kufanya anachotaka.

Lakini, hakufikiria kamwe Levi alikuwa mkatili sana. Mchana, alisikia kwamba CEO wa Ferra Film Group aligongwa gari alipoondoka nyumbani. Tangu wakati huo, alikuwa amepelekwa hospitalini, lakini alikuwa katika hali mbaya.
***
Katika hospitali.

Chester aliposikia kuhusu jambo hilo, alisema kwa hasira, “Je, sikukuambia ughairi mpango wetu wa kuchukua hatua dhidi ya Levi kwa kuwa idara ya usimamizi inaichunguza Felix Media?”

"Bwana Choka, haikuwa kazi yetu," msaidizi wake alisema. “Tulikusikiliza na tumerudi nyuma mapema. Sasa tunakula chakula cha jioni nyumbani.”

Chester aliona mwanga. Levi ndiye aliyemdanganya. Ilikuwa ni muda tangu mtu awe na ujasiri wa kupanga njama dhidi yake.

Ni hila gani nzuri.

Akakaribia kuitupa laptop yake sakafuni.

Hapo hapo akapokea simu kutoka kwa Shedrick. "Hii ni mbaya, Bwana Choka. Idara ya usimamizi inasababisha matatizo kwa kampuni. Walitoza faini ya dola za Marekani milioni 10 na hata wakatoa onyo kali kwa kampuni kwamba iwapo kesi mbaya kama ya Makamu wa Mkurugenzi Joslin itatokea tena, wataifungia kampuni yetu.”

Kwa kweli, dola milioni 10 zilikuwa kiasi kidogo tu kwa Chester. Lakini, uharibifu wa sifa yao haungeweza kutenduliwa. Pia wangekuwa kicheko katika tasnia ya burudani.

Chester hakuwahi kuwa katika hali ya aibu kama hiyo hapo awali katika maisha yake.

Akakoroma. "Wacha watoze faini, basi."

Shedrick hakuweza kujizuia kulalamika, “Kwa kweli, walituonya tu kwa maneno, lakini suala la Levi liliwachochea. Nilipoenda kwa uchunguzi, walidai kuwa Felix Media ilikuwa na kiburi sana."

"Kata mawasiliano na Simwendo kwa sasa." Chester akaitupa simu yake pembeni. Kisha, akatoa sigara na kuiwasha.

Muda si mrefu, Hunter Choka alimpigia ili kumpa Chester kipande cha mawazo yake. “Bwege wewe. Nimekuambia usijihusishe na tasnia ya burudani, na sasa, angalia. Hata umepigwa faini. Wakurugenzi wameniambia nikuonye usiburute kampuni ya Choka kwenye fujo. Mbali na hilo, nikukumbushe kuwa kuwa na tamaa ni jambo jema, lakini unapaswa kuelewa kuwa watu wengi huko nje wanatuonea wivu. Jason hata aliwasiliana nami kibinafsi wakati huu."

“Alisema nini?” Chester akabonyeza sigara na kuivuta sana.

“Ridhika.”

Chester alicheka. "Inaonekana kama familia ya Shangwe inapanga kunikandamiza."

"Ni onyo tu wakati huu, lakini ni bora usiichukue mbali sana." Kwa hayo, Hunter akakata simu.

Chester alivuta sigara chache ofisini, uso wake mzuri ukiwa umefunikwa na moshi.

Hakuna mtu aliyeweza kuona vizuri sura yake, zaidi ya baridi na giza la macho yake.

Muda huohuo, mtu aligonga mlango.

“Ingia ndani.”

Sauti isiyojali ilisikika, Madam Choka akaingia na Cindy ambaye alikuwa amevalia barakoa na miwani ya jua. Hakuna mtu ambaye angeweza kumtambua bila kumwangalia kwa karibu.
 
"Mama, mbona upo hapa badala ya kupumzika nyumbani?" Chester alikasirika

Alitoa sigara mdomoni na kukunja uso. Baada ya hapo, alimtazama Cindy bila subira.

“Njoo, Cindy. Vua barakoa yako,” Madam Choka alisema.

Cindy mara moja akatoa barakoa yake na miwani, akionyesha uso uliovimba, akalia. "Chester, unahitaji kusimama kwa ajili yangu."

Macho ya Chester yaliutazama uso wa Cindy, bila kuficha karaha machoni mwake. "Ni mbaya sana."

“Chester…” Akiwa amehuzunika, Cindy akavuta, alionekana kana kwamba aliumizwa sana na kofi hilo.

Madam Choka akavuta uso mrefu. "Unasema nini? Mwanamke wako Eliza ndiye aliyempiga kofi Cindy machoni pa watu wote. Unahitaji kusimama kwa ajili ya Cindy. Eliza ana kiburi sana. ”

Kwa kweli, Chester alikuwa amesikia kuhusu tukio hilo katika chumba cha mikutano.

Hata hivyo, hakuweza kuwa na wasiwasi kuhusu hilo, kutokana na kwamba mambo mengi yamekuwa yakifanyika ndani ya Felix Media. Sasa Cindy alipomleta Madam Choka ili wamuone, alikasirika sana.

Alikasirishwa na jinsi Cindy alivyokuwa akitengeneza matukio.

Alikerwa na jinsi Eliza alivyokuwa na kiburi.

Wanawake hao walikuwa walimletea shida hata katika kipindi kigumu kama hicho.

"Ikiwa huniamini, tazama video mwenyewe." Madam Choka moja kwa moja akamkabidhi simu ya Cindy, ambayo ilionyesha picha za uchunguzi wa chumba cha mkutano. Chester hakuipokea bali aliweka mkono wake kwenye skrini. Hakukuwa na sauti kwenye video, lakini ilikuwa ukweli kwamba Eliza alimshambulia Cindy kwanza. Zaidi ya hayo, Eliza alionekana mwenye kiburi sana baada ya hapo.

Chester alionekana kutopenda.



Alipoona hivyo, Cindy alisema, “Kwa kweli sikumkasirisha. Kila mtu katika chumba cha mikutano aliona kwamba alinipiga makofi na kunisukuma chini bila hata kuniomba msamaha. Baadaye, alinikasirisha tena. Anadhani anaweza kunionea anavyotaka kwa sababu yeye ni mwanamke wako.”

Madam Choka alisema kwa hasira, “Yule mwanamke amekwenda mbali sana. hata aliajiri watumiaji wa mtandao kumshtaki Cindy na kudai kwamba Cindy alilala na Simwendo. Mpango wa Cindy wa kumfanya arudi ulikuwa unaenda vizuri sana. Lakini sasa, timu ya watayarishaji ambayo ilikuwa imemsajili hapo awali inamzuia kuendelea na mpango huo labda kwa sababu wanataka kusitisha mikataba yao naye. Chester, lazima umfundishe mwanamke huyo somo wakati huu.”

“Mnataka nifanye nini?” Chester aliinua uso wake. "Kwa kuwa nyote wawili mlikuja pamoja, lazima mtakuwa na mpango tayari."

Moyo wa Cindy ulitetemeka chini ya macho yake. Kwa bahati nzuri, alikuwa na akili ya kutosha kuambatana na Madam Choka pamoja naye wakati huo."

Madam Choka alisema, “Unajua vizuri kama Cindy ni mwanamke wa Simwendo au la. Laiti Cindy asingenipa damu yake katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, ningepoteza maisha muda mrefu uliopita. Kwa vile Eliza alimpiga makofi Cindy na kisha kulipaka jina la Cindy kwa kueneza uvumi, lazima alipe gharama. Ikiwa unataka watu wengine wasahau kuhusu suala la Cindy, lazima ufichue habari kubwa zaidi ili kugeuza usikivu wa watumiaji wa mtandao. Nilisikia Eliza alikuwa na Monte…”

Mambo mengine yalikuwa yanajieleza.

Chester hakuelekeza macho yake kwa Mama yake. Badala yake, alimkazia macho Cindy, macho yake yakimeta kwa ubaridi. "Unajaribu kunifanya nifichue kilichotokea kati ya Eliza na Monte?"

Madam Choka alisema huku amekunja uso, “mbona unamkodolea macho Cindy? Hili lilikuwa wazo langu.”

"Mama, ninyi nyote hamna uzoefu wa kutosha kucheza hila mbele yangu." Chester alikaza macho yake na kusema kwa sauti ya baridi, "Ninaelewa tabia ya Cindy kuliko mtu mwingine yeyote."

Cindy aliona aibu haswa. “Na- ninafanya hivi kwa faida yako mwenyewe. Wasanii wa kampuni yetu wamekuwa gumzo kati ya wanamtandao kwa siku chache zilizopita, na Eliza ndiye pekee ambaye ameathiriwa kidogo na jambo hili. Chester, Eliza ni msanii wa orodha A. Ukifichua kashfa yake sasa, itageuza hisia za umma kutoka kwako, Felix Media, mimi na hata wasanii wengine.
 
Sura ya 1284

“Umegundua?” Pembe za midomo ya Eliza zilijipinda na kuwa tabasamu.

“Ni dhahiri. Kufichua kashfa kwa wakati huu hakuna nia nyingine ila kugeuza umakini." Lisa naye alikasirika. "Nilidhani Chester alikuwa mtu baridi na mwanamume wa kucheza, lakini sasa ninagundua kuwa hana haya kabisa na hana dira ya maadili."

"Je, mtu ambaye hana haya na mwenye dira ya maadili atakuwa na hadhi yake leo?" Eliza alicheka kwa madaha.

Moyo wa Lisa ulizidi kumuuma sana Eliza alipokuwa anasikiliza. “Usijali. Nitafikiria njia ya kukuondoa kwenye orodha inayovuma. Pia, nitawasiliana na familia ya Monte Karanja ili kuwazuia wasikusumbue. Kuhusu Chester, ingawa siwezi kumwangusha, naweza kuyafanya maisha yake kuwa magumu kidogo.”

"Hakuna haja ya hilo." Eliza alikataa. "Uhusiano wake na Alvin ni maalum. Hupaswi kumweka Alvin katika wakati mgumu.”

"Nitamfanya Alvin asiingiliane kidogo na Chester." Lisa alisema kwa hasira, “Sitaki awe na athari mbaya kwa mume wangu.”

"Alvinn amemfahamu Chester kwa makumi ya miaka. Angekuwa amepotoshwa zamani kama ingekuwa hivyo. Lisa, nisikilize. Wakati Alvinn alipokuwa katika nyakati ngumu zaidi za maisha yake, Chester hakumuacha. Itakuwa haina huruma kwa Alvin ikiwa utamfanya ajitenge na Chester kwa ajili yangu. Tatizo hili ni kati ya Chester, Felix Media, na mimi. Sitaki nyie mhusike.”

“Lakini-”

"Niamini. Nitalimaliza hili.” Eliza alisema kwa dhati, “Usiende kutafuta watunzi wa mtandao ili kukandamiza jambo hilo. Suala hili tayari limeenea. Ikiwa watu watagundua kuwa niliondolewa kwenye orodha inayovuma, inaweza kuwachukiza. Ni bora kuwa mkweli.”

“Sawa.” Lisa alijihisi mnyonge. Hakujua tasnia ya burudani vizuri. Lakini, kwa kuwa Eliza alikuwa amesema hivyo, alipaswa kuwa na wazo jinsi ya kukabiliana nayo. "Wasiliana nami wakati wowote unahitaji msaada."

Baada ya kukata simu, Lisa alimkazia macho Alvin ambaye alikuwa ametoka kunawa na kutoka.

Kulikuwa na athari za kubembeleza na hatia kwenye uso mzuri wa Alvin. “Wifey, sijui kabisa kuhusu hili. Sikuwahi kufikiria Chester angefanya jambo kama hilo pia. Nitamtafuta na kuzungumza naye, sawa?”



“Tunazungumza nini?” Lisa alikasirika kwa kumwangalia tu Alvin. “Suala hilo limeongezeka kwa kiwango ambacho kila mtu anajua kulihusu. Kila mtu anamdharau Eliza. Umeona wanachosema kwenye mtandao? Ni maneno makali sana. Sifa ya Eliza katika tasnia ya burudani imeharibika kabisa. Si hivyo tu, lakini kwa sababu yeye ni mtu wa umma, inabidi kubeba sifa ya kuwa Sugar mamy kwa maisha yake yote. Je, unatarajia atapata mpenzi siku zijazo?

"Chester hajui aibu. Hata kama hampendi Eliza, bado ni mwanamke wake."

“Angalia marafiki zako. Chester na Rodney ni watu wa aina gani wenye uchafu? Tabia zao zinazidi kuwa mbaya kwa kila mtu."

Lisa alikasirika zaidi alipozungumza, “Hatimaye ninaelewa maana ya ndege wa aina moja huruka pamoja. Si ajabu na wewe pia ulikuwa huna huruma sana kwangu.”

Akiwa amekabiliwa na hasira za mkewe, Alvin alitamani kupiga magoti pale pale. “Mke, mimi ni tofauti na wao. Miongoni mwa marafiki zangu, Sam pia sio mbaya. Je, hukuwa na uhusiano mzuri naye sikuzote?”

Lisa alilalamika. "Siwezi kufanya chochote kwa Chester, lakini usifikirie hata kulala kitandani mwangu mwezi huu."

Baada ya hapo, alinyanyuka kwa hasira.

Suzie alienda upande wa baba yake kana kwamba alikuwa anatazama furaha. "Baba, kwanini umemkasirisha mama tena?"

“Alichagua marafiki wasiofaa,” Lucas alisema kwa upole huku akipita.

Pembe za mdomo wa Alvinn zilitetemeka. Kisha, alimpigia Chester kwani hakuweza kuvumilia tena. "Kwa kweli umeniingiza kwenye matatizo makubwa wakati huu, Chester. Je, wewe ndiye unayehusika na suala la Eliza?”

“Usinisumbue. Bado sijaamka.” Sauti ya Chester ilisikika ya kutisha na kusinzia.

Alvinn alikasirika. "Bado una hamu ya kulala?"

"Eliza hafai kunipoteza usingizi wangu." Sauti ya Chester ilikuwa ya barafu isivyo kawaida.
 
Alvinn alikosa la kusema. Alikuwa na mashaka juu yake hapo awali, lakini sasa, alikuwa na hakika. “Chester, huoni kuwa umeichukulia mbali sana? Tunaweza kwenda kwa urefu wowote kufanya mambo, lakini tunapaswa kuwa na mpaka. Zaidi ya hayo, Eliza ni mwanamke wako. ”

“Yeye ni mfanyakazi wangu pia. Mbali na hilo… Hilo ndilo alilofanya kweli, sivyo?” Chester hakujali. “Mwambie Lisa kwamba ni kwa ajili ya kujionyesha tu na kwamba hatakiwi kulitia moyoni. Si thamani yake."

Baada ya simu kukatika, Alvinn alikunja uso.

Hata kama Eliza alikuwa mwigizaji, mwigizaji pia alikuwa binadamu. Zaidi ya hayo, alikuwa mwanamke ambaye Chester alitaka kuwa naye kwa nguvu.

Chester hakuwa akimchukulia Eliza kwa uzito. Haishangazi mke wake alikuwa na hasira sana.

Alvinn alihisi kweli kwamba Chester aliwabagua wanawake na hakuwachukulia kwa uzito.

Kulikuwa na msemo wa kutochoma madaraja ya mtu. Chester alifanya ngono na Eliza, lakini hakumpa nafasi yoyote. Mtazamo wake bila shaka ungemletea matatizo mapema au baadaye.

• • •

9:00 asubuhi

Wakati Eliza akiendesha gari lake nje ya apartment, alizuiwa na kundi kubwa la waandishi wa habari na mashabiki nje mara tu alipotoka kwenye lango.

“Eliza, kashfa iliyopo kwenye mtandao ni kweli? Umekuwa mchepuko tangu ukiwa chuo kikuu?"

“Eliza, nilisikia ulitoa mimba kwa ajili ya Monte Karanja hapo awali. Je, unaweza kuishi kulingana na mashabiki ambao wamekuamini siku zote?”

"Monte Karanja ana mchumba. Je, mchumba wake anajua kuhusu wewe na uhusiano wa Monte? Kutokana na matendo yako, wewe ni kama mvunja nyumba.”

“Eliza, toka uweke mambo wazi. Picha yako baridi na nzuri iliyoonyeshwa kwenye mtandao ni ya uwongo, sivyo? Kwa nini ulitudanganya?”

“Eliza, nimekatishwa tamaa na wewe. Kufikiri kwamba nilikupenda wakati wote. Sikuwahi kufikiria kuwa wewe ni mpumbavu hivyo.”

"Ulikuwa mrembo sana moyoni mwangu, na hiyo ndio kiwango cha jinsi nadhani ulivyo sasa."

“Kufa tu Eliza. Ninawachukia zaidi waharibifu wa mapenzi ya watu.”

“Eliza, tafadhali ondoka kwenye tasnia ya burudani. Hatutaki kukuona tena. Ulisema uwongo kwa kila mtu aliyekuamini.”

Kundi la waandishi wa habari na mashabiki walilizunguka gari la Eliza.

Kila mtu alikuwa akigonga vioo vya gari kwa hasira. Baadhi ya watu hata walipiga mlango wa kiti cha dereva.

Loida aliogopa. Eliza alikuwa na macho makali na mikono ya haraka. Mara moja alizima injini na kufunga milango.

Hata hivyo, baadhi ya mashabiki walikuwa wazimu sana hivi kwamba waliruka kwenye gari na kugonga kioo cha mbele kwa mawe. Muda mfupi baadaye, nyufa zilionekana.

Hamad alipiga kelele, “Je, watu hawa ni wazimu?”

"Hebu tupigie simu polisi." Eliza haraka akapiga simu polisi.

Polisi walipokea na kusema watatuma watu wao haraka. Lakini, haijalishi walikuwa na kasi gani, mashabiki hawakuweza kusimamishwa. Walikuwa wamegonga kioo cha mbele hadi kikavunjika.

"Eliza, toa ujinga. Lazima utoe maelezo leo.” Shabiki mmoja aliruka mbele ya gari na kumpiga Eliza aliyekuwa kwenye kiti cha abiria.

"Unafanya nini? Acha niende.” Loida alichukua mkoba na kugonga mkono wa fanboy kwa fadhaa.

Waandishi wa habari waliokuwa pembeni walipiga haraka picha za tukio hilo. “Mfanyakazi wa Eliza anawapiga mashabiki. Kila mtu, tazama."

“Eliza, umezidi sana. Sisi ni mashabiki wako waaminifu. Tulitumia pesa nyingi kwako. Kwa wakati huu, hurejeshi pesa zetu wala kutubu. Badala yake, unatupiga hata sisi mashabiki wanaokuunga mkono.”

Kioo cha mbele kikavunjwa sasa, mashabiki wachache walijitokeza kumtoa Eliza nje.

Bado kulikuwa na vingi ilizovyovunjika.

Eliza bila shaka angepata majeraha makubwa ikiwa angetolewa nje hivi.

“Acha.” Loida alikuwa kwenye hatihati ya kulia kutokana na wasiwasi. "Eliza utaumia ukifanya hivi."

Hata hivyo, eneo hilo lilikuwa na fujo. Hakuna aliyekuwa akimsikiliza Loida hata kidogo.

Eliza alihisi mkono wake utavunjika kutokana na kuvutwa.

Akauma meno na kufungua gari. Aliusukuma mlango na kutoka nje.

“Eliza katoka. Kila mtu, njooni." Mtu mmoja alipiga kelele.

Umati ulisongamana kwa mawimbi.

Kulikuwa na shabiki ambaye alichukua fursa ya kugusa mwili wake.
 
Sura ya 1285

Macho ya Eliza yalipoa. Alishika kifundo cha mkono cha mtu huyo na kukizungusha nyuma.

Yule shabiki alilia kwa uchungu pale pale. “Eliza ananiumiza. Msaada! ”

"Ikiwa mtu yeyote atathubutu kunigusa, utapata hatima kama hiyo."

Eliza aliushika mkono wa mtu huyo na kuubonyeza pembeni ya mlango wa gari. Kisha akausukuma mlango kwa nguvu na kuubana. Mkono wake ulikuwa umekwama katikati ya mlango wa gari. Mwanaume huyo alilia kwa uchungu kutokana na shinikizo hilo.

Tukio hilo lilikuwa la kuogofya sana hivi kwamba liliwashtua watu waliokuwa jirani mara moja. Mashabiki wachache ambao hapo awali walitaka kuchukua faida ya Eliza hawakuthubutu kuhama tena.

"Wewe b*tch. Sitakuacha kwenye ndoano! ” mwanaume huyo alifoka kwa hasira.

"Inaonekana bado haujajifunza somo lako." Eliza akatumia nguvu tena. Watu waliokuwa karibu nao waliona damu ikitoka kando ya mlango.

Kila mtu alishtuka. Lakini, Eliza, ambaye ndiye alikuwa sababu ya yote, alikuwa na sura ya baridi kwenye uso wake wa kushangaza wakati wote. Macho yake yalikuwa makali kama upanga.

"Tengeneza njia, fanya njia." Wakati huo, polisi waliingia.

“Niokoe. Anataka kuharibu mkono wangu na kuniua! Mkamate, haraka. Anamshambulia mtu hadharani! ” Uso wa shabiki huyo ulikuwa umepauka kutokana na maumivu.

Afisa wa polisi alimwendea kwa maneno makali na kuonya, “Mwache aende sasa.”

Eliza alifungua mlango wa gari bila haraka. Alimsukuma shabiki huyo na kueleza kwa sauti tulivu, “Nilifanya hivyo tu kwa sababu alijaribu kunitumia wakati wa ghasia. Isitoshe, walivunja gari langu pia.”

“Sikufanya hivyo. Nilimshika mkono tu kumuuliza kwa nini amekuwa mharibifu wa nyumbani.” Mshabiki huyo aliinua vidole vyake vinne vinavyovuja damu na kulalamika kwa macho mekundu. "Tulimpenda kwa muda mrefu na tumemuunga mkono wakati wote."

"Hiyo ni sawa." Mashabiki wengine na fangirls pia walisema, “Eliza, wewe ni mkatili sana. Umewashambulia hata mashabiki wako? Hakika utakufa kifo kichungu."

"Kufa tu." Mtu alichukua mboga zilizooza na matunda na kumtupia Eliza usoni kwa hasira.

“Acha!” Afisa wa polisi alifoka na kuwatazama watu wale kwa tahadhari. Kisha, akamtazama Eliza kwa uchungu, “Ulimjeruhi mtu kimakusudi. Inabidi ufuatane nasi hadi kituo cha polisi.”

“Watu hao walivunja gari langu. Je, ningekaa kushambuliwe tu pasi na kujihami?" Eliza alisema kwa upole, “Gari langu la michezo lina thamani ya dola laki tano. Litahitaji mamia ya maelfu ya dola kurekebisha gari ambalo limeharibiwa kwa kiwango hiki."

"Eliza, wewe bado ni binadamu?" Fangirl mmoja aliyevaa miwani hakuweza kuvumilia tena na akapiga hatua. “Kama si sisi kukuunga mkono, ungekuwa na umaarufu wako wa sasa? Je, ungeweza kuendesha gari la kifahari ambalo ni mamilioni ya shilingi? Nakwambia wewe si kitu bila sisi.”

"Ulisema unaniunga mkono." Eliza alicheka. Macho yake yalikuwa makali. "Unakumbuka tamthilia yangu ya kwanza nilipoanza? Je, unakumbuka siku yangu ya kuzaliwa na nilihitimu chuo kikuu gani? Unakumbuka ni filamu yangu ipi ambayo ina watazamaji wengi zaidi?"

Msururu wa maswali ulimfanya fangirl huyo kukosa maneno. Alisema kwa kigugumizi, “Mambo hayo si muhimu tena. Hata hivyo, nimekatishwa tamaa na wewe. Sitakupenda tena.”

Eliza alidhihaki, akasema kwa ukali, “Je, ni vigumu sana kujibu maswali yangu? Kadiri utakavyojibu maswali yangu, nitakuomba msamaha hadharani. Unaweza kuniambia kiasi cha pesa ulichonitumia miaka yote hii na nitakurudishia mara kumi.”

Rangi ya uso wa fangirl ilibadilika. “Mimi…Sijali pesa zako…”

“Wewe si shabiki wangu hata kidogo,” Eliza alimkatiza yule fangirl kwa ubaridi. Kisha, akawatazama wale wengine kwa macho makali. “Sijali nani kawaambia anwani ya makazi yangu, wala sijali nani kati yenu ni mashabiki wangu wa kweli. Lakini, tafadhali kumbuka kuwa hata mdudu atageuka. Ni mkono wa mtu huyu leo, lakini siwezi kukuhakikishia mambo mengine ya kizembe ninayoweza kufanya kesho. Kuhusu habari kuhusu mimi kwenye mtandao, naweza kusema tu kwamba mimi, Eliza Robbins, sijawahi kufanya jambo lolote linaloenda kinyume na dhamiri yangu.”
 
Baada ya kuongea, aliwafuata polisi kwenye gari la polisi na kuondoka.

Kwa vile alikuwa amemjeruhi mtu, alipelekwa moja kwa moja kwenye kituo cha polisi na polisi.

Nusu saa baadaye, Hamad alikimbia na mtu fulani na kumtaka wakili amtoe Eliza nje.

Walikutana kwenye ukumbi wa kituo cha polisi. Hamad alimtazama Eliza kwa hisia ngumu.

Eliza aligeuza kichwa na kumuuliza wakili, “Je, suala la mimi kumjeruhi mtu limetatuliwa?”

Mwanasheria alikuwa katika wakati mgumu. "Bado. Mtu huyo anataka fidia ya milioni mia mbili."

“Milioni mia mbili?” Eliza alionekana kana kwamba amesikia mzaha. "Ana historia gani ambayo mkono wake mmoja una thamani ya milioni mbili?"

Hamad alipumua. Hapo ndipo Eliza alipomtazama. "Nani alivujisha anwani ya apartment yangu? Nani aliwaambia watu waje huku wakijifanya mashabiki wangu wazue zogo?”

"Sijui. Bado wako katikati ya uchunguzi.” Hamad hakuthubutu kukutana na macho ya Eliza.

"Lazima iwe kampuni, sawa? Nimehamia huko muda si mrefu uliopita. Nani angejua mahali ninapoishi kando na wafanyakazi wa ndani wa kampuni?” Tabasamu la kejeli lilionekana kwenye pembe za mdomo wa Eliza. "Hamad, ulienda kwenye kampuni asubuhi ya leo. Shedrick alisema nini?"

"Mkurugenzi anataka umtafute Chester." Uso wa Hamad ulijawa na uchovu na kukosa msaada. “Eliza, sijui kwa nini mambo yamekuwa hivi. Niamini. Mimi ndiye niliyekulea. Sitamani kukuona ukikabiliwa na hali hii kuliko mtu mwingine yeyote.”

"Naelewa." Moyo wa Eliza ulikuwa wa baridi sana. Hata hivyo, akimkabili Hamad, bado alisema kwa upole, “Hamad, nakuamini. Sijawahi kukulaumu pia. Nimekata tamaa tu.”

“Eliza…” Mwili mzima wa Hamad ulitetemeka.

“Niazime funguo za gari lako. Nitamtafuta Chester.” Eliza alinyoosha mkono wake.

Hamad akaweka funguo za gari mkononi mwa Eliza. "Chester ana mkutano katika makao makuu ya Choka Corporation leo."

Eliza aliendesha gari na kuondoka.

Alienda kwa Kampuni ya Choka Corporation. Alipofika, mhudumu wa mapokezi alimwona na kusema, “Bi Robbins, Boss alitoa maagizo kwa wewe kwenda ofisini kumsubiri ikiwa utakuja. Bado yuko kwenye mkutano.”

"Asante."

Eliza alipoelekea kwenye lifti alisikia sauti za watu wakijadili nyuma yake.

“Siyo Eliza? Kwa nini yuko hapa?”

"Labda anataka kumtafuta Bwana Choka na kumsihi amlinde."

"Ha, amewahi kuwa na wanaume wengine hapo awali. Hata kama atatumia mwili wake, Chester anaweza hata asipendezwe naye.”

Eliza hakuwahi kutarajia kwamba angeishia katika hali ambayo wafanyikazi wadogo wa Choka Corporation wanaweza kumdhihaki nyuma yake hata baada ya kuzaliwa tena. Katika maisha yake ya awali, alikuwa ameaibishwa na Chester mara nyingi sana.

Hata katika maisha yake ya zamani, hakuwahi kufikiria kulipiza kisasi kwa Chester baada ya kumpeleka gerezani kwa sababu kwa maoni yake, Chester pia alidanganywa na wengine.

Ilikuwa pia kwa sababu Chester alikuwa na nguvu sana. Hakuweza kumshusha hata kidogo.

Wakati huo, alitaka tu kuondoka na kutoroka kutoka kwake.

Lakini, ilionekana kama hatima haikutaka kuruhusu Chester kumwachilia Eliza.

Eliza akahema. Alikuwa ameanzisha mpango kwa Chester, lakini alimtumia kama ngao.

Ilikuwa ni ujinga sana.
 
Sura ya 1286

Eliza alisubiri ofisini kwa saa moja.

Chester aliingia kutoka nje. Alikuwa amevalia suruali nyeusi na shati jeupe. Mabega yake yalikuwa mapana, na alikuwa na miguu mirefu. Sura yake ilikuwa ya kipekee. Mikono yake ilikuwa imekunjwa, ikionyesha mistari laini ya misuli kwenye mikono yake.

Baada ya mlango kufungwa, Chester alikaa kwenye kiti cha ofisi. Uso wake usio na mpinzani, mzuri uliinuliwa kidogo. Macho yake nyuma ya lenzi yalimtazama Eliza bila kujali.

"Kuna nini?"

'Kuna nini?' Eliza aliwaza moyoni mwake. Hayo yalikuwa maneno ya kuchekesha zaidi aliyowahi kuyasikia.

Ingawa siku zote alikuwa mtulivu, alishindwa kuuzuia mwili wake kutetemeka kwa wakati huo.

“Jina langu limechafuliwa. Watangazaji na waongozaji wote wa filamu wananipigia simu na kunikaripia, wakitaka kukatisha mikataba yao nami. Sasa ninachukiwa na kila mtu. Je, hujui haya yote?”

Eliza hakutaka kuvumilia tena. Alichukua chombo kutoka kwenye rafu ya mapambo na alikuwa karibu kukivunja sakafuni kwa hasira.

Chester ghafla akamkumbusha kwa upole, “ Chombo kilicho mkononi mwako ni cha gharama kubwa mno. Kivunje ukithubutu.”

Mkono wa Eliza ukakakamaa. Vase ambayo ilikuwa na thamani ya milioni tatu haikuwa kitu kwake. Lakini, ilikuwa pesa kubwa kwa Eliza ambayo Chester alijua.

Katika mvutano huo, Eliza aliuma meno yake na kurudisha chombo nyuma. Kisha, alikimbilia upande wa Chester akiwa na macho mekundu. "Ulinitumia kama ngao ya kampuni bila neno. Hufikirii unahitaji kunipa maelezo? Chester, hata kama hunipendi na ingawa huenda nisiwe muhimu kama Cindy, mimi pia ni binadamu. Nimeingiza faida kubwa kwa kampuni, lakini umeniharibia kirahisi.
Unanichukua kama nini?”

Aliporudisha chombo nyuma kwa woga, Chester alianza kumdharau.
Wakati huo, alikuwa mvivu sana kupigana naye. Alichukua kadi kutoka kwenye droo mara moja na kuitupa kwenye meza. "Kuna dola milioni 10 ndani yake. Ni fidia yako.”

Eliza akatoa macho. Baada ya yote, alikuwa mwigizaji wa kitaaluma. Kwa hiyo, sura yake ilionekana kana kwamba kadi hiyo ilikuwa ya aibu. "Ninaweza kuzalisha faida ya milioni mia chache kwa kampuni kila mwaka. Umeharibu taaluma yangu ya uigizaji katika tasnia ya burudani milele, na sasa unanifukuza kwa dola milioni 10 pekee. Unafikiri mimi ni ombaomba?”

“Ombaomba?” Chester alicheka kwa kejeli. “Je, ombaomba anaweza kuwa na pesa nyingi hivyo? acha kukejeli watu.”

Uso wa Eliza ulikunjamana kwa hasira. "Thamani yangu sio dola milioni 10 tu. Sihitaji pesa. Nataka tu maisha yajayo yenye matumaini.”

“Siwezi kufanya hivyo.” Chester alimtazama kwa macho yaliyojaa dharau. "Ukweli kwamba umekuwa na Monte Karanja ndio ukweli. Unaweza kujilaumu tu kwa kuwa mzinzi. Zaidi ya hayo, nadhani inatosha kuwa una thamani ya dola milioni 10. Tasnia ya burudani inabadilika kila wakati. Ni kweli kwamba wewe ni maarufu mwaka huu, lakini vipi kuhusu mwaka ujao na mwaka baada ya hapo? Hata kashfa ndogo inaweza kuharibu mtu mashuhuri, bila kusahau kuwa uhusiano wako na Monte ni kashfa iliyopigwa mawe."

"Kama si kampuni kutunga njama ili kugeuza umakini, hakuna mtu ambaye angegundua kuihusu." Eliza alimkodolea macho Chester. "Zaidi ya hayo, kuweka kando mkataba wangu na kampuni, mimi bado ni mwanamke wako. Chester, wewe ni mkatili sana kwangu. Wewe kweli ni mkatili sana.”

Machozi machoni mwake yalimtoka.

Chester aliyatazama hayo macho. Siku za nyuma, alifikiri Eliza anafanana na Charity alipokuwa baridi. Hata hivyo, aligundua kuwa hawakufanana hata kidogo baada ya kuangalia kwa karibu.

Alisimama kwa hasira. “Vipi hata kama wewe ni mwanamke wangu? Nilikuwa nikitosheleza mahitaji yangu tu.”

Eliza alitoa macho na kumtazama Chester. “Huna aibu sana. Hukupaswa kunilazimisha kwa kutumia watu wengine kama tishio wakati huo.”

Kumbuka kwamba Chester alimlazimisha Eliza kulala naye kwa kutumia vitisho vya wale jamaa waliomsaidia Eliza kumteka nyara Sarah ambao Chester alikuwa anawashikilia bado.

“Kwahiyo kama nilikulazimisha? Hukujisikia vizuri ulipokuwa kitandani kwangu?” Chester alifungua sanduku la sigara. Alichukua sigara katikati ya vidole vyake na kumuelekezea.
 
“Eliza, ngoja nikuambie hili. Wewe ni msanii wa kampuni yangu. Baada ya kusaini mkataba, kama mfanyakazi wa kampuni, unapaswa kuweka faida ya kampuni na bosi wake kwanza kila wakati. Fikiri juu yake. Je, kampuni si ndiyo iliyokupa ulichofanikiwa leo? Huu ni ushauri kutoka kwangu. Chukua hii dola milioni 10
na kuondoka. Baada ya kashfa hiyo kuisha, kampuni bado inaweza kupata fursa kwako kurejea."

Eliza alishindwa kuvumilia kuendelea kusikiliza. Alifagia nyaraka zote za Chester kwenye meza hadi sakafuni kana kwamba alipagawa. “Usinichukulie kama mjinga. Je, kurudi ni rahisi hivyo? Mimi ni mtu mashuhuri wa list-A sasa, lakini ulininyonya kikamilifu. Je, itachukua miaka mingapi kabla ya tukio hili kufa? Kufikia wakati huo, sitakuwa na faida ya kuwa mchanga tena. Wewe pia hutanipenda. Ushindani ndani ya kampuni ni mkali. Je, bado kutakuwa na matumaini ya mimi kurudi tena?”

"Una hamu ya kifo." Chester alimshika mkono na kuutupa kwa nguvu. Eliza alitupwa chini.

“Unadhani wewe ni nani wa kupiga kelele ofisini kwangu? Je, hukujifunza kutokana na somo mara ya mwisho?”

Chester alimtazama Eliza kwa juu. “Nakuonya. Usisukume bahati yako. Ukiniudhi, nitafanya hivyo ili usipate nafasi ya kurudi tena.”

"Je, huoni hatia hata kidogo kwangu?" Eliza alikuwa amejilaza chini na kumtazama Chester akiwa katika hali ya fujo.

“Hatia ya nini?” Chester alicheka kwa ubaridi. "Wewe ni kitu gani hata ambacho kinastahili kunifanya nijisikie hatia?"

Eliza alibaki mdomo wazi kana kwamba amepata mshtuko mkubwa.

Siku hiyo alitumia vipodozi vya bei nafuu usoni mwake. Baada ya kulia sasa hivi, vipodozi vyake vilikuwa vimechafuka kabisa kama paji yenye unyevunyevu.

Chester alichukizwa na mtazamo huo. “Chukua kadi uondoke. Ikiwa unaona ni pesa kidogo sana, usichukue."

Eliza alionekana kuogopa baada ya kusikia hivyo. Mara akainuka na kushika kadi.

Macho ya Chester yakazidi kuwa ya dharau. Akawaza huku akimcheka kimoyomoyo. 'Angalia hilo, alisema pesa ni kidogo sana na akazidharau, lakini bado alishikilia kadi kwa nguvu mwishowe.'

Wanawake wote walikuwa sawa.


"Msichana mzuri." Uso wa Chester ulionekana bora zaidi. “Eliza, najua kampuni ina deni kwako katika suala hili. Kwa kweli, kama ungekuja na kuzungumza nami kwa sauti nzuri sasa hivi, maneno yangu yasingekuwa makali hivyo. Ichukue kama kampuni inadaiwa kukufadhili wakati huu. Kampuni itarudisha fadhila kwako katika siku zijazo."

Eliza alicheka. Ilikuwa ni sawa na kutoa peremende ili kurekebisha mambo baada ya kumpiga mtoto makofi kadhaa. Alikuwa akiwatendea watu kama wapumbavu.

Alitikisa kichwa huku akitokwa na machozi. “Sitaki kuidai kampuni. Siwezi kumudu kukukasirisha wewe au kampuni. Mimi si muhimu sana sasa hata hivyo. Siwezi kuleta faida kwa kampuni pia. Ninafikiria kuvunja mkataba wangu.”

"Kukatisha mkataba?" Chester aliwasha sigara kwa kiberiti na kuivuta. Kisha, akasema, "Hufikirii kulala na watu wengine ili kurudi, sawa?"

"Hapana." Eliza aliinua kichwa chake huku akiwa na hofu. Alieleza kwa huzuni, “Sitaki tu kubaki katika kampuni hii tena. Nilikuwa nyota ya juu, lakini ikilinganishwa na Cindy, sasa ninadhihakiwa na kudharauliwa popote ninapoenda. Mimi si kitu sasa. Nitadhihakiwa zaidi na watu wengine. Ikiwa unadhani kampuni ina deni kwangu, wacha nisitishe mkataba. Angalau sitakuwa nikipokea macho mengi ya uvundo.

Chester hakusema neno. Alimtazama tu Eliza kwa jicho la uchunguzi kana kwamba alikuwa akiamua ukweli wa maneno yake.

"Zaidi ya hayo ... nimepoteza thamani yangu yote sasa." Eliza alitabasamu kwa huzuni. "Kuhusu kurejea tena… Chester, umeona watu mashuhuri wa kike wakiweza kurejea baada ya kashfa zao za kutoa mimba au kuwa waharibifu wa nyumbani kufichuliwa? Vituo vya utangazaji havitajitia hatarini kuwekeza katika tamthilia nilizomo. Ikiwa hakuna mtu atakayewekeza kwenye tamthilia zangu, waongozaji wa filamu hawatanipendekeza hata kidogo. Ni nini kingine ninachoweza kufanya zaidi ya kudhihakiwa ikiwa nitabaki kwenye kampuni?”

"Ikiwa ni hivyo, fanya kama unavyotaka." Chester alidondosha majivu ya sigara na kusema kwa upole baadaye.

Alikuwa mtu halisi.
 
Eliza alipotoa ombi hilo, tayari alikuwa ametathmini kiakili thamani yake.
Kwa kweli, zaidi ya kupoteza pesa za kampuni kwenye mshahara wake wa msingi, hakukuwa na matumizi mengine katika kumbakishs Eliza.
 
Sura ya 1287

Isitoshe, kashfa ya Eliza ilikuwa kali zaidi kuliko kashfa ya Cindy hapo awali. Ingekuwa vyema kutumia pesa kumruhusu Eliza aende kwenye maonyesho mbalimbali, lakini kurejea katika drama kunaweza isiwe rahisi hivyo.

Mbali na hilo, hata watu mashuhuri wa kike walio na fanbase kubwa za mashabiki wanaweza kubadilishwa kwa urahisi. Katika miaka mingine miwili baada ya tukio hilo kufa, bila shaka kungekuwa na watu mashuhuri wengi wachanga na warembo ambao wangeonekana kwenye tasnia ya burudani. Ingekuwa ngumu sana kwa Eliza kuinuka.

Kwa kuongezea, kwa tabia ya Cindy na msaada wa Madam Choka nyuma yake, bila shaka angemnyanyasa Eliza.

Hata hivyo, wakati huo… Chester alikuwa mgonjwa sana na Eliza.

Kukatisha mkataba huo lilikuwa chaguo bora zaidi kumzuia Eliza asije kwake kwa kufoka na kulalamika baadaye.

"Asante, Bwana Choka." Eliza aliuma mdomo kwa kusitasita. “Kisha… Baada ya kandarasi yangu kusitishwa, apartment ambayo kampuni ilikodisha kwa ajili yangu hakika itarejeshwa. Je, ninaweza kuhamia mahali pako kwa muda?"

“Unaota ndoto?” Chester alichukizwa.

Mwili wa Eliza ulitetemeka. “Lakini wewe ndiye uliyesema naweza kwenda kwako wakati wowote ninapotaka. Umeninunulia nguo nyingi sana…”

“Hiyo ni siku za nyuma. Hujui kuwa wanaume ni wepesi wa kubadilika?” Chester alisema kwa uso usio na hisia. “Je, Monte hakukufundisha somo kuhusu hili? Je, hujajifunza somo lako?”

Eliza alionekana kushtuka sana. Machozi ya kimya kimya yakamdondoka tena kwenye kona ya macho yake. “Vipi… Unawezaje kufanya hivi? Je, bado ninaweza kukutafuta?”

Hapo awali, Chester alitaka kusema kwamba hakuhitaji kuja kumtafuta tena. Hata hivyo, baada ya kufikiri juu yake, vipi ikiwa alikuwa na mahitaji wakati fulani? Kwani, ikilinganishwa na kumgusa Cindy, kumgusa Eliza hakukumfanyila ajisikie kuwa amechukizwa. Japokuwa tayari alikuwa ameshapoteza kabisa hamu na Eliza.

“Subiri hadi nitakapokuhitaji. Sio lazima uje kwangu nisipowasiliana nawe,” Chester alisema bila kujali.

Eliza alikata tamaa kidogo. Alifikiri hatataka tena kumgusa. Ilionekana kama bado alilazimika kuweka bidii zaidi.

"Basi ... nitasubiri ujumbe wako." Eliza aliruhusu dokezo la kukata tamaa limweke machoni mwake kwa makusudi. “Unaweza kuwasiliana nami wakati wowote. Sina kazi sasa, kwa hiyo niko huru kabisa.”

Chester aliachia tabasamu na kumtazama Eliza. "Eliza, ni lini umekuwa mjanja sana?"

Uso mzuri wa Eliza ulipauka, akauma mdomo na kuonekana kana kwamba anapitia wakati mgumu. “Bwana Choka, kampuni nyingi zimesitisha mikataba yao na mimi. Sitalazimika kulipa ada zote za fidia, sivyo? Ikiwa nitalazimika kulipa, mimi..."

“Usijali. Hutalazimika kuwalipa. Kampuni itashughulikia." Kando na pesa, alizungumza tu juu ya kuvuna faida.

Chester alikasirika sana asiendelee kusikiliza. “Ondoka. Bado ni lazima nifanye kazi. Usije tena kwenye kampuni kunitafuta.”

"Nina ... ninaelewa." Eliza alijibu kwa upole kabla ya kugeuka. Aliondoka huku akirudisha kichwa nyuma kwa matamanio.

Chester alichukia sana sura hiyo. Baada ya kuondoka, mara moja alimpigia simu Shedrick. “ Tengeneza makubaliano ya kusitisha mkataba wa Eliza. Hatakuwa tena msanii wa kampuni yetu katika siku zijazo."

Shedrick alishtuka. “Kusitisha mkataba?”

“Nini tena?” Chester alisema kwa upole, “Sifa ya Eliza imeharibiwa. Pesa anazoweza kupata haziwezi hata kufikia ile ya mfanyakazi wa ngazi ya kuingia wa kampuni. Kwa nini tumweke?”

"...T-Huu ni ukatili sana." Shedrick alihisi ubaridi ukipita kwenye uti wa mgongo wake. Alifikiri kwamba Chester alikuwa mkatili kwa Eliza, lakini hakuwahi kufikiria kuwa angekuwa mtu asiye na moyo kiasi hicho. Baada ya yote, Chester alifanya mapenzi naye hapo awali.

"Alipendekeza mwenyewe." Chester hakuwa na wasiwasi. "Ni vizuri kwamba tunakatisha mkataba pia. Tunaweza kuepuka kutumia pesa ili kuunga mkono kwa nguvu kurudi kwake. Mbali na hilo, kuna watu wanaowatendea watu wengine tofauti kulingana na hali zao, haswa Cindy. Tukimhifadhi Eliza, Cindy anaweza kufanya jambo.”
 
“Una hoja hapo…” Shedrick alishawishika. "Cindy ana uwezo wa kufanya vitu kama hicho. Bado hujui kuhusu hili, lakini anwani ya jumba la Eliza ilivuja alipokuwa akitoka asubuhi ya leo. Kulikuwa na kundi la wapinzani kati ya watu. Walizuia na kuvunja gari lake. Kwa bahati nzuri, polisi walifika huko kwa wakati na hakuna chochote kikali kilichotokea. Polisi wanaichunguza sasa hivi. Wale wapinga mashabiki labda walielekezwa na mtu, lakini hawatakubali."

Chester alipigwa na butwaa. Akakunja uso. Hakumsikia Eliza akitaja alipokuja sasa hivi. “Unashuku ni Cindy ndiye aliyefanya hivyo?”

“Hata mimi sina uhakika sana.” Shedrick akaweka koo lake. Madam Choka alikuwa akimlinda sana Cindy, hivyo hakuweza kusema chochote. Baada ya yote, alikuwa mfanyakazi tu.

“Sawa, ninaelewa.” Chester akabonyeza katikati ya nyusi zake. Chuki yake dhidi ya Cindy iliongezeka zaidi. "Unaweza kwenda kupanga kusitishwa kwa mkataba."

Muda mfupi baada ya Eliza kuondoka Choka Corporation, alipokea simu ya Shedrick. Akamwambia aende kwenye kampuni.

Nusu saa baadaye, alifika Felix Media.

Alipoingia tu mlangoni, kundi la wafanyakazi waliokuwa wakipita hapo walimnyooshea vidole na kumjadili nyuma yake.

"Uongozi katika Felix Media utabadilika katika siku zijazo. Hadhi ya nyota ya juu pengine itakuwa ya mtu mwingine.”

"Nilisikia kampuni imemkabidhi Hamad kwa Cameron Otieno, hatashughulikia masuala ya Eliza tena."

“Tafadhali. Hamad ni mmoja wa wasimamizi bora katika kampuni. Bila shaka, hawezi kupoteza muda kwa mtu mashuhuri aliyechafuliwa.”

“Ah, Eliza hakuwahi kukutana na Chester hapo awali? Tofauti yake ikilinganishwa na Cindy ni kubwa mno.”

“Anaweza hata kufananishwa na Cindy? Mbali na hilo, Cindy amekuwa pamoja na Chester pekee, tofauti na Eliza, ambaye amewahi kuwa na wanaume wengine hapo awali. Eliza hata alitoa mimba kwa ajili ya mwanamume mwingine.”

Ingawa Eliza alikuwa amezoea watu wengine kumjadili, lakini maneno ya watu wale yalizidi kuwa ya kipuuzi. Walikuwa hata wakisema kwamba alitoa mimba?

Nyuso za Eliza zilikunjamana. Alipotaka kugeuka tu, sauti za makaripio ya Cindy zilisikika nyuma yake.

"Nyie watu mnajadili nini badala ya kufanya kazi ipasavyo?" Cindy alimtazama Eliza kwa madaha. "Sio nafasi yenu kuzungumza juu ya ukweli kwamba mrembo wetu wa ulimwengu mwingine, Eliza, alitoa mimba."

Wafanyakazi wale walipomwona Cindy, mara moja walitetemeka kwa hofu. Walisema kwa heshima, “Samahani, Bi Tambwe. Hatutazungumza tena juu yake."

“Ni vyema mkatambua makosa yenu. Endeleeni na kazi yenu. ” Cindy alipunga mkono. Wale ambao hawakujua chochote wangefikiri kwamba kampuni hiyo ilikuwa yake.

Eliza hakujisumbua kuhusu Cindy na alitazama tu mashauzi yake kimya kimya.

“Ah, samahani, Eliza. Walikuwa wakizungumza juu ya uvumi wako, kwa hivyo walipaswa kukuomba msamaha. Lakini…Hadhi yako katika kampuni iko chini sana sasa.” Cindy alimsogelea Eliza huku akitabasamu. Uso wake ulikuwa wa kihuni. “Ndiyo maana watu hawapaswi kuteremka. Angalia, unapokuwa katika hali duni, hata wafanyakazi tu huthubutu kukupa mtazamo duni.”

"Hiyo inategemea mtu. Je, baadhi ya watu si wataalamu wa kuwachukulia watu wengine kulingana na hali zao?” Eliza aliwatazama walinzi na msaidizi nyuma ya Cindy kwa ubaridi.

Ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuona mtu ana walinzi katika kampuni hiyo. Kulingana na sheria za kampuni hiyo, walinzi walikuwa wakiachwa kwenye lango la getini.
 
Back
Top Bottom