Nellove Da Presenter
New Member
- Aug 27, 2022
- 4
- 7
Story: MCHUNGAJI MCHAWI.
Mtunzi: Nelloveš
Episode: 01
WhatsApp: 0759941164
"Naitwa Juliana. Napenda kumshukuru sana Mungu mwenyezi kwa kunitendea muujiza mkubwa maishani mwangu. Sikuwahi kutegemea kama Mama yangu ataweza kutembea tena lakini kwa uwezo wa Mungu anatembea sasa" ilikuwa sauti ya mwanadada aliyesimama mbele ya madhabahu, mkononi mwake ameshika kipaza sauti anatoa ushuhuda.
"Mama yako yuko wapi?" Ilikuwa sauti ya mchungaji.
"Yule amekaa pale" alisema na kunyoosha kidole kuelekea mahali alipo Mama yake.
"Njoo Mama, njoo usiogope"
Aliita mchungaji kisha Mama yule wa makamo alisimama na kuanza kutembea kuelekea mbele.
"Mama unaitwa nani?"
"Naitwa Dorothea.
Namshukuru sana Mungu kwa kuniponya. Nilikuwa siwezi kutembea mimi, mguu wangu ulioza kabisa." Aliongea huku analia.
"Nimepoteza hela nyingi hospitalini na kwa waganga lakini sikuponywa ha..."
"Pole Mama, polepole sasa.
Enh! Ilikuwaje hadi unakuja kwa mchungaji?"
"Nilikuja hapa baada ya kusikia matangazo redioni kwamba kuna mchungaji anaponya sana" aliongea huku anatoa machozi.
"Tuambie Mama Ulipokuja ilikuwaje"
"Nilipokuja hapa niliguswa tu kidogo kisha nilipewa maji na mafuta ya upako. Nilipotumia tu nilipona kabisa".
"Halleluyaaaaaaaaah!!!!! Piga makofi na vigelegele. Mshangilie Mungu mpendwaaaa" sauti ya mchungaji iliunguruma, watu walishangilia mno.
"Hivi ndivyo utendaji wa Mungu ulivyo. Amekuumba ili uishi kwa amani. Naomba unisikilize mwanangu, Mungu hajakuumba ili uteseke na ndio maana mateso yanapokuja, yeye huwa tayari kukuondolea. Halleluyaaah!" Alizungumza mchungaji.
Baada ya hapo mchungaji alipiga hatua hadi nyuma ya madhabahu na kufunua kitambaa kirefu kilichofunika madhabahu ile. Aliingiza mkono na kugusa kitu alichokijua yeye mwenyewe kwa kidole kisha alipotoa mkono alilamba kidole kile huku akihisi nguvu za ajabu zikiingia mwilini mwake. Hili tukio la kulamba kidole halikuonekana na mtu yeyote,,, basi baada ya kufanya hivyo alirejea.
"Popote ulipo, naomba simama kwa miguu yako. Nahitaji kuomba nawe, nahitaji kumwambia Mungu akutoe katika shida uliyonayo, nahitaji kuomba mamlaka na nguvu za kufukuza mashetani yaliyofunga maisha yako, nguvu ya kutuma moto wa kwenda kuunguza wachawi wa maisha yako. Naisikia nguvu ya Mungu ndani yangu,,,, Motoooooooooooo!!!!!" alitamka maneno hayo kisha dakika chache baadae watu wengi walianza kuanguka na wengine walipiga kelele.
Wahudumu mbalimbali wa kanisa wakishirikiana na Mama mchungaji walijumuika kwa pamoja kutoa huduma kwa wote walioanguka na wenye mapepo. Mchungaji naye aliendelea kutoa huduma kwa kila mmoja aliyesogezwa mbele yake, alitumia kitambaa kirefu chenye rangi nyeupe kuwagusa wagonjwa na hakika kila aliyeguswa alipata kupona hapohapo. Miujiza iliendelea kufanyika kwa watu waliokuwa wamehudhuria kanisa hilo kubwa sana na lenye waumini wengi mno.
Na hivyo ndivyo ilivyokuwa siku hiyo na kila siku ya jumapili na jumatano, siku ambazo zilikuwa kwenye ratiba ya ibada ya kanisani hapo. Watu mbalimbali wenye shida kadha wa kadha waliponywa kwa miujiza ambayo iliendelea kukua siku hadi siku yaani muujiza mkubwa uliofanyika jana ni mdogo kuliko ule utakaofanyika leo na kesho. Miujiza iliendelea kuwa mikubwa mikubwa mikubwa,,,, miujiza ikasambaa sana na kufanya waumini waongezeke maradufu katika kanisa hilo.
Kila mmoja aliyeitambua shida aliyonayo hakutaka kusubiri, alikuwa tayari kutumia nauli ya kiasi chochote kile na muda wa masaa yoyote cha msingi afike kwa mchungaji na kupata huduma.
Watu wa sehemu mbalimbali ndani ya nchi waliweza kufika na hakika walizingatia muda kwani waliposikia ibada ni jumapili wao walifika mapema jumamosi, wapo wengine walifika Ijumaa na kulala hapo wakisubiri uponyaji.
Waumini waliongezeka na kuongezeka,,, nao walipokuwa wengi zaidi, kanisa lilifanyiwa ukarabati na kuongeza ukubwa.
Kanisa lilijengwa kisasa zaidi kwani ziliwekwa TV,, pia ziliwekwa kamera kunasa matukio yote yanayoendelea kwa ajili ya kurusha kwenye vyombo vya habari kama Televisheni maana walikuwepo waumini wengine ambao walikuwa wanafuatilia huduma kwa njia hiyo ya Televisheni. Si ndani ya nchi tu bali sasa waumini walitoka hata nje ya nchi pia.
Ilikuwa jumapili moja hivi muda wa maombi,, kabla ya kufanya chochote aliisogelea madhabahu na kupiga magoti huku akitamka maneno fulani ya ajabu. Nguvu zilimuingia kisha alianza kuwaponya watu wenye shida mbalimbali.
"Halleluyaaah Mungu ni mkuu sana. Najua mmesadiki ya kwamba hakuna jambo linaloweza kumshinda" mchungaji alisema baada ya kumgusa na kumponya mtu aliyekuwa hawezi kuona yani kipofu.
"Ni muujiza mojawapo kati ya mingi mliyoishuhudia kwa macho yenu. Wengi huwa hamuamini mpaka muone. Sasa mmeona hivyo sina shaka mnaamini. Sasa Hiyo imani uliyonayo ikunyanyue hapo ulipo,,, na wewe unayenitazama kupitia TV hapo nyumbani nikusihi simama na uguse kioo cha TV yako." Watu walisimama kwa imani huku wengine wakianza maombi yao ya chini chini.
"Kuna sauti inaniambia kwamba yupo Mama alichukuliwa damu na wachawi wakati wa siku zake. Na sasa huyu Mama hazai na amehangaika sana lakini hakuna mafanikio hivyo ameshakata tamaa" alisema mchungaji huku anatembea tembea.
"Yupo mwingine amefungwa tumbo lake ili asizae. Sasa natamka mkono wa Mungu ukafungue hiyo minyororo na nira zote ulizofungwa,,, na wewe Mama uliyechukuliwa damu yako nakutamkia uponyaji kwa nguvu za kiungu zenye kufukuza uchawi huo." Aliposema tu hivi vilisikika vilio kutoka nyuma ya kanisa.
Wamama watano walianguka na kubebwa msobemsobe hadi mbele.
"Wawekeni hapo" alisema kisha aliendelea
"Kuna sauti inaniambia tena. Kuna mtu mmoja nafsi yake imezikwa. Mnaweza kumuona anatembea na mmekaa naye hapo lakini ni mfu na ndio maana hapendwi, kila afanyacho kinaharibika na anakataliwa hata na familia yake. Nimetumwa kuokoa Taifa la Mungu, Sasa nakuita huko kaburini ama kuzimu uliko. Njooooooo!!!!!!" alitamka hayo kwa sauti nzito ya kuunguruma.
"Njoooooooooo!!!!!" alitamka tena na kumalizia mara ya mwisho ndipo mwanaume mmoja nyuma ya kanisa alipoanza kuruka ruka kama mtu aliyepandwa na mapepo.
Watu waliogopa kukaa karibu naye maana alitishia kukamata watu huku midomo yake ikitoa udenda na kitu kama povu hivi. Sauti ya kuunguruma ilisikika kutoka ndani yake na midomo yake iling'ata na kutafuna nyama za mikono yake. Damu ilitapakaa,, watu waliogopa zaidi.
Mchungaji alishuka madhabahuni na kupiga hatua za taratibu kuelekea nyuma ya kanisa.
Alikuwa pamoja na watumishi wake wapatao watatu walioongozana naye hadi mahali alipokuwepo yule mwanaume aliyekuwa anatisha watu.
Alimsogelea yule mtu na kukemea kwa nguvu lakini katika hali isiyo ya kawaida mchungaji alisikia kichomi na kujihisi kama anapigwa kofi zito usoni mwake. Kofi hili lilimpelekea kujisikia kizunguzungu na kuona giza kwa mbali lakini kabla hali haijawa mbaya zaidi alichukua kitambaa chake cheupe na kujifuta usoni.
Basi mchungaji alipoona kile kichomi na hali mbaya imetoweka alichukua kitambaa kile na kukirusha kwa yule mwanaume. Kitendo cha kuguswa na kitambaa kile, alianguka chini na kutapatapa kama mtu anayepigwa fimbo na kuugulia maumivu yake.
Dakika tatu baadaye yule mtu aliacha vurugu, alisimama taratibu kisha alianza kushangaa shangaa kama mtu anayeweweseka. Mchungaji alimtazama na kumgusa kwenye paji la uso huku anatamka maneno yake aliyoyafahamu yeye mwenyewe kisha alirudi madhabahuni.
Hata hivyo alishangaa sana kuona hali yake inaanza kuwa mbaya kwa mara nyingine. Alisimama taratibu na kuelekea kwenye chumba maalum cha kufanyia maombi yake mwenyewe,,, hakutaka yeyote amfuate. Alifunga mlango na madirisha, alifunika kichwa kwa kofia iliyokuwa imeshonwa kwenye kanzu yake Nyeusi kisha alifumba macho na kunyoosha mikono. Dakika chache tu baadaye š¹šFuvu lenye mapembe lilitokea na kuanza kuzunguka juu yake huku likifuka moshi, nayo ile hali mbaya ilipotea ghafla.
ITAENDELEA...