Simulizi: Mimi na Mimi

Simulizi: Mimi na Mimi

MIMI NA MIMI 2

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Siri, Tamaa, Hila, Usaliti, Ukatili, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA SABA

★★★★★★★★★★★★★★


Safari ya kurudi Mbagala ikaanza nilipofanikiwa kufika Kawe stendi na kupanda daladala ambayo ingenifikisha huko moja kwa moja. Nilijihisi upya yaani. Kutembea nikiwa nimechomeka bastola kiunoni ilinifanya nijihisi kuwa mtu mwingine kabisa, sawa sikuwa nimeitumia bado, lakini mpaka kufikia hatua hii, ni wazi nilikuwa ndani ya badiliko kubwa kwenye maisha yangu. Na nilikuwa kwenye utayari wote kuishi nalo haijalishi matokeo yangekuwa vipi. Kistelingi yaani, au siyo?

Nikiwa mwendoni mpaka kufika Mbagala, niliona nitumie muda mfupi kumsalimia Soraya. Bwana, mwanamke huyo alikuwa amenikumbuka sana baada ya yale matembezi niliyomtembezea wiki kadhaa nyuma, na alikuwa tayari kukutana na mimi muda wowote ule hata kwa gharama yake mwenyewe. Kiukweli sikuwa nimefikiria tena kuja kutoka na Soraya, yaani kuna kitu tu ndani yangu kilihitaji suala la mimi na mwanamke huyo libaki kuwa historia, na tubaki kuwa na uhusiano kama niliokuwa nao na Ankia kwa sasa.

Lakini Soraya, dah! Alijua kusisitiza mpaka ungejihisi kuwa na hatia yaani. Aliniomba sana, sana, sana, tuje kukutana tena, nami nikamwambia sawa. Ila nikaweka sharti kuwa tutakapokutana tena ndiyo ingepaswa kuwa mara ya mwisho, kwa sababu sikutaka ishu yetu ije kuibua utata mkubwa mno kati yake na mume wake, naye akaonekana kuridhika na hilo.

Nimekuja kufika Mzinga ikiwa imeshaingia saa kumi na mbili jioni, na nilikuwa nahisi njaa. Ankia akawa amenipigia simu wakati nilipokuwa nikielekea kwake kuuliza nilikuwa wapi, maana mechi ilikuwa karibu kuanza, nami nikamwambia ndiyo nakaribia kufika. Nikamuuliza ikiwa tayari Adelina na yeye alikuwa amefika kwake, lakini akasema hapana, tena kwamba mwanamke huyo alimwambia kuwa hangeweza kuja leo shauri ya kubanwa na jambo fulani.

Adelina hakuwa amenitafuta kunijulisha kuhusu hilo, kwa hiyo nikaamua kumuaga Ankia ili nimpige yeye kumuuliza kama kila kitu kilikuwa sawa. Nikampigia mara mbili, lakini hakupokea, kwa hiyo nikamtumia ujumbe nikimpa pole kwa kutingwa na kwamba tungeonana tu wakati mwingine, hivyo amalizane salama na aliyokuwa akifanya.

Nikafika kwa Ankia giza likiwa limeshaanza kuvizia, na huko nilikopita shamra-shamra za mechi zilikuwa zimeshaamka mapema sana. Kilichokuwepo hapa ilikuwa ni mimi kufika hapo kwa Ankia na kuiweka bastola hii kwa kificho huko chumbani, kisha nijimwagie upesi na kuondoka na marafiki zangu hao. Nilikuwa natarajia kwamba bibie Miryam na Tesha wangekuwa tayari pia, kwa hiyo kweli nikajitahidi kuwahi. Angalau huu ungekuwa muda ambao ungenisahaulisha kidogo mambo mengine yenye kukwaza.

Ile nimefika tu ndani kwa Ankia, nikashangaa kidogo baada ya kumkuta mwanamke huyo akiwa sebuleni pamoja na Tesha, mama Chande, na Adelina mwenyewe. Kwa jinsi tu ambavyo niliachia tabasamu hafifu huku nikimwangalia mwanamke huyo ilifanya Ankia na Tesha waanze kucheka kwa furaha, naye Adelina akawa ananiangalia huku akitabasamu. Kumbe walikuwa wananizingua tu.

"Kwa kuniona kolo kiasi hicho, eti?" nikamwambia Ankia hivyo huku nikitabasamu.

Wote kwa pamoja wakacheka kidogo, nami nikatikisa kichwa na kuufunga mlango.

"Basi karoho kalikuwa kamekuuma masikini! Umepiga na simu kabisa mwanaume, usiniambie ulikuwa karibu kulia kisa Adela hajafika..." Ankia akasema hivyo na kucheka.

Nikasema, "Yaani huna idea! Ningeahirisha kabisa kama Adelina hangetokea."

Nikasogea karibu na sehemu ya sofa alilokuwa amekalia Adelina na Ankia, naye Adelina akasimama taratibu na kunifungulia mikono yake ili tukumbatiane. Nikajitahidi kumkumbatia kwa kutoubana mwili wangu kwake kabisa, ili asiweze kuhisi ugumu kiunoni kwangu ambao ungeweza kumfanya atambue nilikuwa nimebeba bastola.

"Adelina, karibu sana," nikamwambia hivyo.

"Asante," akaitikia.

Nikamwachia na kuendelea kumwangalia usoni kwa upendezi.

Alikuwa amevalia jezi nyeupe ya Simba kwa juu, iliyombana vizuri kuonyesha unawiri wake, pamoja na suruali nyeusi iliyombana vizuri sana kuonyesha umbo lake matata kuanzia kiunoni mpaka miguuni. Alisuka mtindo fulani hivi wa nywele nyeusi zilizoviringika-viringika, nyingi zikiwa juu ya kichwa chake mpaka kufikia uso na pembeni akiwa kama amesuka mistari miwili kwa mkono. Alipendeza usoni pia na macho yake ya kungu, na kilichofanya tuache kutazamana ikawa ni mguno wa kejeli alioutoa Tesha.

"Hmmm... basi JC hapo! Wengine hatatuona," Tesha akasema hivyo.

Nikamwangalia usoni kwa kuweka macho kizembe, nami nikamwambia, "Ulikuwepo kumbe?"

Wanawake wakacheka kidogo, naye mama Chande akanisalimu, "Mambo vipi jembe?"

"Fresh, Yanga lady. Naona uko tayari kwa mechi," nikamwambia hivyo.

"Yaani kama vile nimeiandaa mie!" mama Chande akasema hivyo huku akinyanyua tatu hewani.

"Hahaaa... leo lazima watu wachezee kipigoo," Ankia akaunga.

"Kaka... tuondoke, hawa bata leo lazima tuwachinje, wamezidisha mno kelele..." Tesha akasema hivyo huku akisimama.

Mama Chande akaanza kurusha michambo kwa Tesha, Ankia akimuunga mkono pia. Wanawake hawa kwa pamoja walikuwa wamevaa jezi za Yanga juu, Ankia nyeusi, mama Chande njano, huku suruali za skinny nyeusi zikitokelezesha makalio yao vyema, nami nikaona niwaulize swali muhimu zaidi.

"Miryam yuko wapi?"

Tesha akasema, "Yupo ndani huko, amesema tutangulie anakuja. Tutamwekea siti. Twende tuwahi, patajaa."

Nikaangalia saa mkononi na kumwambia, "Bado bado, nusu saa. Ngoja nikapige maji fasta halafu..."

"Aagh, mwana unazingua! Maji ya nini? Mbona unakuwa mrembo hivyo?" Tesha akalalamika.

"We' unafikiri mwenzako mchafu kama wewe? Mwaya JC kaoge... tutakusubiri," mama Chande akaongea hivyo.

"Yaani kanavyo... JC, hakuna kununulia mtu bia hapa..." Tesha akasema hivyo kama vile ananinong'oneza, makusudi yaani.

"Nyoo... kwani me sina hela yangu? Acha dharau we'! Mashabiki wa Simba mkoje?" mama Chande akamsuta.

"Na hapo umemaanisha na JC..." Tesha akasema hivyo.

"Basi jamani, msije kutoana meno wakati mechi yenyewe bado," Adelina akawaambia hivyo.

Sote tukacheka kidogo, kisha nikawaambia, "Sikieni. Tesha yuko sahihi, tangulieni, me nipige maji kwanza halafu nitawakuta. Nafasi zitajaa mkinisubiri, ila sichelewi sana. Tangulieni nakuja, eti?"

Nilikuwa nimemwangalia Adelina niliposema hivyo, naye akatikisa kichwa mara moja huku akinitazama kwa umakini. Basi eti wengine wakaangaliana na kujichekesha kimakusudi tu, nami pamoja na Adelina tukatabasamu pia.

Huyu mwanamke alionekana... tunasema 'kunimaindi,' na mimi nikaamua tu kuachana na hilo wazo upesi kwa sababu sikumchukulia namna hiyo hata kidogo, yaani nilimheshimu kama dada mkubwa fulani hivi. Lakini kwa wengine, sijui kwa nini waliona ulazima wa kusukumia uvutiano baina yangu pamoja naye, labda waliona tunapendezeana, sijui.

Mi' nikaamua tu kuelekea chumbani upesi, nikiwaacha marafiki zangu wakiwa kwenye harakati ya kuondoka, nami nikaichukua bastola niliyokuwa nimekabidhiwa na kuiweka sehemu nzuri iliyojificha. Angalau kwa usiku huu nilijua nisingeihitaji, kwa hiyo kilichofuata ikawa ni kwenda kuoga kwanza, kisha nikarejea na kuvaa vizuri. Masai hiyooo... nikaelekea.

★★

Nimefika Masai mechi ndiyo inataka tu kuanza, nami nikawaona wenzangu wakiwa wamekaa kwenye viti virefu vya plastiki kuzunguka meza ndefu ya mbao, ambayo tayari ilikuwa na vinywaji. Kuongezea kundi hapo alikuwa ni Bobo, ambaye alikaa pembeni kiasi, na baada ya Ankia na mama Chande kuniona eti wakaanza kushangilia kwamba mwamba nimefika. Walikuwa wameacha nafasi kwa viti viwili ambavyo hakuna mtu alipaswa kukalia isipokuwa mimi hapa na bibie Miryam, na bado hakuwa amefika.

Nikasalimiana na Bobo vizuri, kisha nikakaa pembeni yake Adelina. Watu walikuwa wamejaa haswa mpaka nje kabisa, na baada tu ya kuagiza vinywaji vyangu vichache, mechi ndiyo ikawa imeanza. Dakika zikatembea bila Miryam kuwa amefika, mpaka kuna watu wakawa wanataka kukibeba kiti chake shauri ya wateja fulani kukosa viti, naye Bobo akawaambia wachukue tu na kusema pindi ambayo Miryam angefika, basi angepata kiti bila wasiwasi wowote.

Yanga ikatangulia kufunga. Fujo! Kelele na maneno yakaongezeka, nasi wanasimba tukaendelea kuwa wapole. Kidogo Simba wakasawazisha. Wee! Ilikuwa kama vile ndiyo goli la ushindi yaani, fujo zilipita zile za mashabiki wa Yanga. Tukiwa suluhu mpaka mwisho wa kipindi cha kwanza, hali ikatuliapo kiasi huku ahadi za kukatana maneno zikitolewa kuhusu kipindi cha pili ambacho kingeanza muda si mrefu. Tukaendelea kusubiri huku tukinywa bila wasi, story za hapa na pale zikiniteka mimi na Adelina, na ndiyo Miryam akawa amefika.

Yaani ile nilipomwona tu, macho yangu hayakuondoka kwake. Aliingia na kusimama kwanza kututafuta, na baada ya kutuona, akaanza kuja kwetu. Ni hivi, watu, tena hasa wanaume, wote, walimwangalia utadhani ndiyo alikuwa kitu kitamu zaidi kwenye menyu zote ambazo wamewahi kuyaonjesha macho yao. Siyo siri ujio wake hapo ulifanya mioyo mingi iingie matatani. Na alikuwa amevaa kawaida tu, lakini yeye kama yeye hakuonekana kuwa wa kawaida kwa wengine.

Alikuwa amevaa blauzi nyepesi ya mikono mirefu, iliyochorwa mistari myeusi na ya kijivu kwa njia za pembetatu zinazojirudia kuizunguka, pamoja na suruali ya jeans ya blue iliyokoza sana, hips zake zikionekana kushiba kinoma, huku miguuni akivaa ndala zake nzuri za kike. Wakati huu, alikuwa amesuka nywele ndefu za rasta, zenye rangi iliyokaribia kuwa njano yenye weusi, uso wake ukionekana kuwa mweupeeh ndani hapo kuendana na ngozi ya mwili wake mwanga ulipommulika vyema. Alikuwa mzuri huyu dada! Sijui tu hata nisemeje.

Alipofikia meza yetu, Bobo akatoka kwenye kiti chake na kuja kukiweka upande wa pembeni na Adelina, na kuna watu walikuwa wameegamia hapo lakini wakapisha. Mwanamke akakaa. Hakushika kingine mkononi zaidi ya simu, nasi tukaanza kumsalimia vizuri huku Ankia na mama Chande wakimsifu kwa kupendeza sana na msuko wake. Miryam akiwa ni shabiki wa Yanga pia, wawili hao wakaanza kusema yeye ndiyo bahati nzuri iliyokuwa imekuja kuwapa ushindi wa magoli kumi kabisa ndani ya kipindi cha pili, na maneno baina yao na Tesha yakaanza tena Bobo alipofanikiwa kuleta kiti kingine ili akae.

Kwa jinsi tulivyokaa kuizunguka meza, kwenda mkono wa kushoto kwangu alikaa Adelina, kisha Miryam, Tesha, Ankia, mama Chande, Bobo, mpaka mimi tena. Kwa hiyo ni kama tulitazamana na Miryam sawia. Mhudumu akaja karibu yake Miryam, nami nikamponda na kisoda kisha kumwita aje kwangu. Miryam akanipa tabasamu na kutikisa kichwa chake kidogo, nami nikaelewa aliyokuwa akiwaza. Nikiwa nakumbuka vizuri kwamba bibie alipendelea wine tu, nikamwambia mhudumu alete chupa moja kubwa ya Dompo, pamoja na glasi, naye huyo akasepa.

Tesha alikuwa amechangamka sana hasa baada ya kumwona dada yake, akisema leo wangekunywa mpaka kukuche, na hata baada ya Miryam kuwekewa Dompo yake hapo, jamaa akasema yaani tutulie ndani ya dakika kumi tu, meza ingejaa bia kwa idhaa ya dada yake. Hata mimi nilikuwa nahisi uchangamfu kwa kweli, moyoni yaani, kuwa hapa na hawa watu, na pale kipindi cha pili cha mechi kilipoanza, mambo ndiyo yakavurugika. Aah! Yanga?

Wakaipiga Simba mabao manne zaidi na kufanya tupoteze mechi kwa jumla ya magoli matano kwa moja! Mashabiki wa Yanga walifurahia kupita maelezo, na kweli wachezaji wao walijituma mno. Tesha akazimishwa mdomo na Ankia na mama Chande, yaani walifurahia mpaka basi! Mimi, Adelina, na Bobo tukawa wapole tu, tukiwaangalia wenzetu walivyofurahia ushindi wao, na bibie Miryam alikuwa akitabasamu tu kwa utulivu huku akiendelea kunywa taratibu.

Na maneno ya Tesha yakawa kweli. Bia zilikuwa zikiongezeka tu mezani, wahudumu wakisema Miryam ananunuliwa na watu ambao hata hakujali kuwafahamu, kwa hiyo zikawa zinasambazwa tu kwetu ili tuburudike. Yaani maumivu ya Simba na utamu wa bia ukafanya nisahau hata kama nilikuwa na njaa, ila haimaanishi nilikuwa nimechomwa saaana na Simba kufungwa, mm... nilifurahi tu kuona furaha ya wengine, na muziki wa kuwapongeza watani ukapigwa na kuwanyanyua. Walicheza haswa! Pombe ikamwagwa! Viuno na makalio yakatikiswa, yaani eh!

Mama Chande na Ankia walikuwa wanampondea kweli Tesha, wakimwambia aongee sasa, mbona yuko kimya, na Tesha kweli akawa kimya tu huku akinywa bia na kuwaangalia wanawake hao kwa njia iliyoonyesha amekerwa. Mama Chande alikuwa anacheza muziki, kuendana na mashabiki wengi wa Yanga ambao waliserebuka na kupiga mavuvuzela kwa shangwe, naye hata akawa akimchanganyia Miryam pombe yake kwenye wine ya bibie, na wao na Ankia wakijichanganyia wine kwenye bia, yaani raha ya ushindi ikiwa imewateka haswa.

Adelina akawa amenisogelea sikioni kuninong'oneza. Akaniambia kwamba alihitaji kwenda msalani lakini hakupajua, hii ikiwa ndiyo mara ya kwanza amebanwa na mkojo, nami nikamwelekeza upande wa kuelekea. Akanyanyuka na kuondoka, huku nikimfatilia kwa macho kuhakikisha hakuna mtu anamchokoza, na ndiyo alipoishia huko vyooni nikawa nimemtazama Miryam. Mwanamke alikuwa ametulia tu kama vile hayupo ama siyo shabiki wa Yanga na makelele yao, walikuwa wananikera kweli lakini ni yeye tu ndiye ambaye hakukera. Angekunywa wine taratibu na kuendelea kubofya-bofya kioo cha simu yake, nami nikaendelea kunywa pia.

Kidogo tu akafika jamaa mmoja mweusi karibu zaidi na Miryam, akiwa ameshika chupa ya bia mkononi, naye akaanza kumsemesha. Alikuwa mweusi, akivaa kofia kichwani, na mwili wake ulikuwa mnene na mfupi kiasi. Nikamtazama kwa umakini alipokuwa akijaribu kumtongoza-fulani hivi Miryam, na alisema anaweza kumwongezea bibie bia na sisi wote kama Miryam angetaka, lakini Miryam hakumsemesha wala kumtazama. Nikachukua kisoda na kumponda jamaa, na akanitazama.

Nikamtolea ishara kwa kiganja kuwa aondoke huku nikimtazama kwa umakini, naye akaendelea tu kuniangalia. Wengine walikuwa bize na mambo yao isipokuwa Bobo, ambaye naye akamwonyesha huyo pimbi ishara kuwa aondoke. Jamaa akatunyooshea kidole na kukitingisha kidogo, akifikri tunamtania sijui, lakini nikaendelea kumkazia macho mpaka akaona asepe tu. Miryam alionekana kukerwa sana na hilo jambo, lakini akaendelea kutulia tu, na mimi sikujisikia vizuri kumwona akikosa raha. Ndiyo maana kumbe hakupenda sana kuja hizi sehemu.

Tesha akawa amenirushia kisoda ili nimwangalie, na nilipomwangalia akanionyesha ishara kuwa anataka tuondoke. Eti kero ya kipigo ilimzidia. Ah! Nikamwambia atulie tu. Mama Chande na Ankia wakamwongezea kero zaidi kwa kumsema-sema, huku Bobo pembeni yangu akisema kweli leo hao wanawake walikuwa mawinguni mno mpaka wangeenda kulala na chizi yeyote yule wa Yanga ambaye angewazoa. Nikamwambia acha mambo yako bana, hawako namna hiyo, naye akasema labda Ankia siyo mama Chande. Nikataka kumuuliza alikuwaje na uhakika kuhusu hilo, na ndipo nikahisi nashikwa begani kutokea nyuma yangu upande ambao sikuuangalia.

Nikageuka na kumtazama aliyenishika hivyo, maana hakuliachia kabisa bega langu, nami nikaendelea kumtazama kwa umakini kwa sababu nilimfahamu, lakini hatukujuana. Namaanisha sikuwa na ukaribu na huyu mtu, na alikuwa ni mwanamke, mweupe kiasi, mwili mnono, na nilimtambua upesi kuwa mdogo wake na yule Rukia. Yule yule Rukia niliyemrukia pia halafu nikamtosa.

Kunishika kwake huyu mwanamke hakukuishia begani, bali akauweka mkono wake kupita bega na kuishika shingo yangu, huku akinikaribia usoni kama vile anataka kunisemesha na macho yake yaliyowekewa kope ndefu. Ilikuwa njia ya kawaida ya kuvuta umakini wa mtu, lakini kutotarajia ujio wake wa moja kwa moja kwangu na kunishika utafikiri tulijuana sanaaa ndiyo uliofanya nimwangalie kwa macho ya 'we vipi?'

Huku macho yake yakionekana kukolezwa na pombe, akanisemesha namna hii, "Mambo handsome?"

Alikuwa amevaa nguo nyeusi, kama gauni, fupi kuyaacha mapaja yake wazi, na ilionyesha sehemu kubwa ya ndani ya mwili wake kama night dress vile. Yaani sidiria aliyovaa na nguo ya ndani viliweza kuonekana kwa mbali, na wigi lake la nywele ndefu za kizungu lilimkaa vizuri kichwani.

Nikiwa namwangalia kwa umakini, nikamwambia, "Poa, vipi?"

"Safi. Leo umeniweza... nimekufata mwenyewe..." akaongea hivyo.

Alikuwa ameanza kulielekea sikio langu ili aniambie jambo fulani kwa ukaribu zaidi, na nilipoangalia usawa wa sehemu ambayo Miryam alikaa, nikakuta mwanamke huyo ananitazama usoni sawia. Ah, sikupenda hiyo picha mbele yake aisee, na huyu mwanamke nilitakiwa kumtoa hapa upesi sana.

Akiwa amenisogelea sikioni, mwanamke huyo akasema, "Twende ukani(.....) basi!"

"Ih, hapana. Asante. Nenda katafute mtu mwingine," nikamwambia hivyo huku nikijaribu kuutoa mkono wake.

Akalazimisha kuning'ang'ania shingoni na kusema, "Jamani, hata kidogo tu. Wewe mzuri sana, ni(.....) hata kidogo tu... nimekuja na kondo...."

"Wewe, em' niachie..." nikamwambia hivyo kiukali.

Alikuwa amelewa, kwa hiyo nikautoa mkono wake kutoka kwangu kwa nguvu na kutazama pembeni.

Bobo akamwambia, "We' si uende? Jamaa hakutaki."

"E-eeh chonde! Sijakufata wewe," mwanamke huyo akamwambia hivyo Bobo.

Bobo akamnyooshea kiganja na kumwambia, "Aisee, nitakuzibua! Toka hapa!"

Nikakishika kiganja chake na kumtuliza.

"We' Naomi wewe... si una mume wako huko? Umalaya waziwazi, huna hata aibu? Hebu nenda, usilete fujo hapa wakati tuna-enjoy siye..." Mama Chande akamwambia hivyo.

"Ah kwenda huko, huna lolote! Mmekaa hapa na mwanaume mzuri mnajishaua tu, kumbe wote mnamtaka. Mwanamke halisi ni mimi, acheni nimwonyeshe raha astarehe," huyo Naomi akasema hivyo.

Mama Chande akamtukana tusi kubwa na kuanza kusemeshana naye kwa njia ya ugomvi, na huyo Naomi akashika chupa akitishia kuitupa kwa Mama Chande. Nikawahi kuinyakua kutoka mkononi mwake, na kasi ya kuivuta ikafanya ianguke chini na kupasuka. Watu wengi walikuwa wameshaanza kuangalia upande wetu shauri ya mama Chande kupaza makelele ya ugomvi kumwelekea mwanamke huyo huku akitaka kumfata, naye Bobo akamwita mwanamke mwingine ambaye alikuwa ni mhudumu wa hapo ili amwondoe huyo Naomi sehemu hiyo.

Nilijawa na hasira kiasi, maana sijui tu huyo mwanamke aliingiwa na nini kilichomsukuma aje kutuharibia amani hapa, na ndiyo akawa amefanikiwa kuondolewa hapo na kurudi kwa mashoga zake huko. Ikageuka kesi sasa, mama Chande akiwa na pombe kichwani hakuacha kuongea, akimsema huyo Naomi kwa Ankia na Tesha, huku Bobo akiwa ameenda huko ambako Naomi alielekea.

Nikakaa kitini tena nikiwa nahisi kuvurugwa, na macho yangu yalipomwangukia Miryam tena, nikakuta akiwa ananiangalia kwa utulivu tu, kisha akaendelea na mambo yake kwenye simu. Nikajiona kama fala tu yaani, sijui kwa nini ila nikawa nafikiria kama vile bibie alikuwa amenisoma vibaya shauri ya hilo tukio, nami nikajitahidi kutulia huku nikiwasikiliza Tesha na mama Chande wakiwa wanatoa kero zao kuelekea wanawake malaya.

Adelina akawa amerejea na kukuta mhudumu anasafisha vipande vya chupa hapo chini, naye akauliza kulikoni. Ndiyo alipokaa na yeye akaanza kusimuliwa yaliyotokea.

"Yuko wapi huyo mwanamke?" Adelina akawa amemuuliza Ankia.

Mama Chande akanyoosha kidole kuelekea kule ambako Naomi alikuwepo, naye Adelina akawa amemwona.

"Yule pale, malaya tu aliyeshindikana..." mama Chande akasema hivyo.

"Amelewa tu, hata sijui ni nini kingine kimempa kiburi akamfata JC," Ankia akamwambia Adelina.

"Kwani sisi hatujalewa? Mbona akijaga na mume wake huwa analewa na hamfati JC? Ni umalaya tu. Kaona mpenzi wake JC ameenda chooni ndiyo akajua amepata nafasi... hana hata aibu..." mama Chande akaongea hivyo na kusonya.

Aliposema hivyo, nikamtazama usoni kiumakini, naye Tesha akauliza kikejeli, "Mpenzi wake JC tena? Ndiyo yuko wapi?"

Mama Chande akamnyooshea kidole Adelina huku akimwambia Tesha, "Huyu ndiyo mtoto sasa JC ameleta. Huyo mjinga anakuja hapa, eti anatusema wote tunamtaka lakini tunajishaua. Amekuwa Mungu? Eti akafikiri kijana wetu atahangaishwa na hilo limtako lake bayaa lililomshuka kama chupi ya mtoto iliyoning'iniza mavi... toto hilo hapo pembeni yake JC, halina nyash kwani? Tena nyash iliyoenda chuo kikuu, limetuliaaa... zuri, safi... halafu huyo mk(....) analeta bangi zake hapa?"

Aliongea hayo na kusonya kuondoa kero, naye Tesha na Ankia wakacheka sana na kujaribu kumtuliza huku mama Chande akicheza-cheza muziki. Pombe hii!

Nikamwangalia Adelina pembeni yangu, naye akaniangalia usoni pia na kutabasamu kwa njia yenye hisia kiasi, kisha akavuta na kunywa bia yake taratibu. Itikio lake kwa maneno aliyosema mama Chande lilionyesha dhahiri kwamba aliyafurahia kwa kiasi fulani, kwa hiyo ikawa wazi kwamba alikuwa na upendezi wa hali ya juu kunielekea.

Lakini mimi kiukweli niliboeka. Nilikuwa nimeingiwa na hali ya umakini kiasi kwa kutofurahishwa na kile kitendo cha Naomi, na bila kujizuia nikawa nimemwangalia Miryam tena. Niliganda kumtazama tu kwa sekunde chache, yeye akionekana kuwa bize na simu yake, ndiyo alipovuta glasi yenye wine ili anywe akakutanisha macho yake na yangu na kutulia pia. Yaani glasi alikuwa ameshainyanyua, lakini ikaishia njiani kabla ya kuufikia mdomo wake, naye akawa ananiangalia kwa macho yenye utulivu.

Tukaangalianaa... mimi nikihisi kabisa kuwepo na maana kubwa na nzuri mno kwa jinsi tulivyotazamana, naye ndiyo akaacha kunitazama na kuangalia pembeni huku akinywa kileo chake. Nikamwangalia na Ankia pia kukuta amenikazia macho yake kwa umakini, nami nikampa tabasamu hafifu, na yeye akatabasamu pia kwa furaha.

Baada ya dakika chache Bobo akawa amerejea tena, na chupa za bia zilikuwa zinaisha mezani kwetu, hivyo Adelina akafanya wema wa kuongeza zingine ili tuendelee kupoza koo. Inaonekana jamaa tuliyemfukuza alikoma kuongeza zingine, najua ilikuwa ni yeye ndiye aliyetuwekea bia kwa kudhani angejipatia Miryam. Ha! Ikawa imekula kwake.

Pombe ilikuwa inanigonga haswa maana nilikuwa nimepitisha muda sijanywa, kwa hiyo niliendelea tu kukaa kwa utulivu huku nikisindikiza story za akina Tesha, mama Chande, na Bobo, kwa kusema hiki au kile. Na sasa angalau Adelina na Miryam walikuwa wameanza kupatana maana walianzisha mazungumzo baina yao yaliyoonekana kufurahisha. Nilipenda sana kuwaangalia.

Katika kumtazama tena Ankia, nikakuta bado akiwa ananiangaliaaa, yaani kama vile alikuwa ananisoma sijui, mpaka nikamuuliza 'wewe, nini?' lakini akaacha kunitazama na kutabasamu tu huku akitikisa kichwa kuonyesha hakuna kitu. Sijui pombe labda ilikuwa imemkolea sana ama ishu ya mdogo wake Rukia kunifata hapo mpaka kumfukuza ndiyo ilimfanya aniangalie kwa hiyo njia, lakini nikapotezea tu na kuendelea kunywa taratibu.

★★

Tukaendelea kunywa kistaarabu tu, na kufikia sasa wote tuliokuwa tunakunywa kistaarabu zaidi tulikuwa tumeshalegezwa na nguvu ya pombe, yaani hadi Miryam alikuwa akitaniwa na Tesha kwa jinsi macho yake yalivyokuwa yakirembua mno shauri ya kileo chake kumwingia. Lakini baada ya muda mfupi nikawa nimetambua kwamba Miryam hakujisikia vizuri sana, ikionekana kichefuchefu kilikuwa kinampanda ama anaelekea kutapika, hivyo nikamwomba Adelina amuulize ikiwa alihitaji usaidizi.

Adelina mwenyewe alikuwa ameshapaa kwa pombe, lakini ustaarabu wake bado ulikuwepo, hivyo akanong'onezana kidogo na Miryam, kisha akaniambia kwamba Miryam alihisi vibaya mwilini ndiyo, shauri ya kutokunywa sana kwa kipindi kirefu, na hivyo huenda sasa alihitaji tu kurudi nyumbani ili akapumzike. Lakini nikaona hiyo kuwa haifai, najua kilichomkoroga zaidi ilikuwa kuchanganyiwa bia kwenye wine yake, nami nikamuuliza Bobo ikiwa kulikuwa na supu za mbuzi au ng'ombe hapo Masai kwa muda huo, na kwa sababu ya kutokuwa na uhakika sana, akaamua kumwita mhudumu ili amuulizie.

Mhudumu akaleta jibu kwamba supu zilikuwa zimeisha. Baada ya Miryam kutambua kwamba nilikuwa nataka nimtafutie supu, akasema nisijali kwa kuwa kama angetapika basi hali hiyo ingemwisha kufikia asubuhi, lakini mimi nikakataa. Nikamwambia angetakiwa kunywa supu usiku huu huu la sivyo angeumwa vibaya sana kesho, ila yeye bado akasisitiza haikuwa na shida. Hata wengine wakawa wanasema haitawezekana kupata supu mpaka asubuhi, lakini sikutaka hilo.

Nikawaambia tunyanyuke, twende kule Mzinga barabarani kuna sehemu wangekuwa wanatengeneza supu, nami nikatoka kwenye siti yangu na kwenda kumshika Miryam mkono. Alionekana kunishangaa kiasi, mpaka na wengine walinishangaa, ila ni pombe tu ndiyo iliyokuwa inaongoza hisia zangu zinifanye nitende namna hiyo. Nikawaambia wote tuondoke ili tukanywe supu kabla ya kurudi nyumbani, na sauti yangu ilisikika kama amri yaani.

Nikaanza kuungwa mkono na Bobo na Tesha, ambao waliona kwamba kileo cha Miryam kilikuwa kimemkoroga vibaya, hivyo tukaamua kuyaacha mambo yote ya hapo Masai hapo hapo Masai. Nikamwomba Tesha akachukue na maji ya kunywa ya baridi sana pale kaunta ili tuondoke nayo kama tahadhari, naye akatii na kwenda.

Miryam aliposhuka kutoka kitini, alikuwa akitembea kwa kuyumba kiasi, kwa hiyo nikawa nimemshikilia kwa kuuingiza mkono wake ndani ya kiwiko changu, hivyo mwili wake ukawa umeegamia zaidi kwenye wangu akiwa kama hana habari yaani. Tesha akarejea na kujiunga nasi, sisi wote tukiondoka hapo kasoro mama Chande, aliyeamua kubaki na mwanaume fulani wa Yanga aliyejuana naye. Bobo alikuwa sahihi kumbe!

Watu walikuwa wameanza kututazama sana tulipokuwa tunaondoka, lakini tukaendelea kujali yetu. Ilikuwa ni suala la kuchukua boda mpaka huko mbele shauri ya uzito aliokuwa nao Miryam, lakini yeye mwenyewe akasema tutembee tu; uzuri mimi, Tesha, na Bobo tulikuwepo na wanawake, kwa hiyo hakuona haja ya kuchukua bodaboda kwenda eneo la karibu mno.

Basi, tukaendelea kutembea mdogo mdogo. Kiukweli kwa mtu ambaye angetuona jinsi ambavyo nilitembea kwa ukaribu sana na Miryam, angefikiri tuna ule ukaribu wa ndaniii, lakini hata mimi mwenyewe nilielewa kwamba kumshika mwanamke huyu namna nilivyokuwa nimemshika sasa hivi, ilikuwa ngumu sana. Lakini alistareheka, pamoja na kwamba alijisikia vibaya, ila tulipokuwa tunaongea na wengine yeye pia alichangia maongezi na kuonyesha uchangamfu.

Nilifurahia sana mwili wake karibu yangu. Nilijisikia vizuri mno. Si unajua kwenye pindi za namna hii unakuwa unajifanya kama vile hiki ni kitu ambacho haukitilii maanani sana, kumbe moyoni unarukaruka. Nilitamani wakati ambao ungefika nimshike mwanamke huyu namna hiyo na nisimwachie tena. Mguso wake ulinitia uradhi wa hali ya juu sana mpaka... ngoja kwanza, hivi haya mawazo yalikuwa yanatoka wapi? Akili yangu ilikuwa sawa kweli?

Ile tulipokuwa tunaelekea kufikia lami, Miryam akaonekana kuzidiwa zaidi na kuanza kuyumbia upande mmoja, nami nikamwelewa. Ikanibidi nimshike pande za mikono yake na kumsogeza pembeni ya barabara, huku mwili wake ukiwa umeinama, naye akaanza kutapika hapo hapo. Wengine wakawa wamesimama na kutuangalia, Tesha akimtania dada yake kwa kusema huo ndiyo ulevi, na kwa kweli Miryam alikuwa amelewa.

Alipomaliza kumwaga matapishi, Ankia akanipatia chupa ya maji ya baridi ili nimpe Miryam anywe, naye akaanza kunywa taratibu. Nilikuwa namnywesha. Yaani nilimtendea kama yai vile, Tesha akiendelea na masihara yake tu kuhusu dada yake kunywa supu na kurudi kupiga bia tena, na ndiyo hapo jambo jipya likazuka.

Bobo akasema, "Tatizo hilo linakuja."

Nikageukia upande wake na kuona maaskari watatu wa usalama wa mtaa, polisi jamii, wakiwa wanakuja upande wetu kutokea upande mwingine wa barabara, nami nikamshikilia Miryam vizuri alipokuwa ametulia kidogo baada ya kunywa maji ya baridi.

"Wanakuja kutuzingua sasa hivi..." Ankia akasema hivyo kwa sauti ya chini.

"Watuzingue, tumeiba?" nikamuuliza.

"Si tunatembea usiku?" Ankia akasema.

"Agh..." nikafanya hivyo na kutoa kitambaa changu ili nimfute Miryam mdomoni.

Na alikuwa amelegea kweli sasa hivi, sijui kama supu ingenyweka.

Hao polisi viazi wakawa wametufikia, wakibeba na silaha nakwambia, wote wakiwa ni wanaume, na mmoja wao akauliza, "Na nyie? Mnatoka wapi?"

"Tulikuwa Masai hapo... ndiyo tunaenda nyumbani... mwenzetu anaumwa," Bobo akasema ukweli lakini kwa kudanganya.

"Kuumwa, kuumwa na nini? Pombe? Ndiyo imemng'ata?" polisi mwingine akauliza.

"Ndiyo tulikuwa tunarudi nyumbani..." Ankia akamwambia hivyo.

"Ee, wewe! Sikukuuliza wewe, sawa? Naongea na bwana wako. Kaa kimya," polisi namba 1 akamwambia hivyo Ankia.

"Nimepewa mdomo wa kuongea na Muumba. Nitaongea ninapojisikia, nikae kimya kwa nini?" Ankia akamwambia hivyo.

"Una jeuri eeh?" polisi namba 2 akamuuliza hivyo Ankia.

"Sikieni. Hapa hamna shida. Sisi tunaenda tu hapo mbele, tunapita hivi... tunaingia home. Na hata muda haujaenda kihivyo," Tesha akasema hivyo huku macho yake yakiwa yamelegea.

"Muda haujaenda? Ni mchana sasa hivi?" polisi namba 1 akamuuliza Tesha.

"Kwani sa'hivi saa ngapi?" nikamuuliza kistaarabu.

Akaniangalia na kuuliza, "Yaani unaniuliza mimi sasa hivi saa ngapi?"

"Eeh, nimekuuliza wewe, sa'hivi saa ngapi?" nikamsemesha kwa sauti makini.

"JC..." Adelina akaniita hivyo kwa sauti ya chini kama kunizuia.

Polisi namba 1 akanisogelea na kusema, "Wewe nakujua. Ndo' yule jamaa aliyejifanyaga shujaa kipindi kile mpaka wakamfunga yule jamaa, eti?"

Alikuwa kama anawasemesha wenzake, nami nikamuuliza, "Kwa hiyo unasemaje?"

"Usiniongeleshe hivyo, nitakuchafua!" jamaa akaniambia hivyo.

"Kwani tumefanyaje jamani? Si tunarudi nyumbani?" Ankia akawauliza.

"Unaulizia hivyo kama vile hujui sheria za kutembea usiku? Tena mkiwa mmelewa?" polisi namba 3 akauliza pia.

Bado nilikuwa nikitazamana na polisi namba 1 kwa mkazo, nikisubiri akorome tena.

Bobo akasema, "Sisi ni wa hii hii mitaa, tunatambulika kabisa, mjumbe wetu ni Yusufu. Sasa hivi saa tano, tunatoka kunywa kidogo ndiyo tunarudi nyumbani. Sa' shida ni nini?"

"Shida umeisema. Mnatembea usiku sasa hivi, mnatafuta nini?" polisi namba 2 akamuuliza hivyo.

"Kwa hiyo mtaa wooote ni sisi tu ndiyo tunaotembea sasa hivi? Mbona Emirate hamfiki? Wale wavuta bangi wanaokaa pale kila siku mpaka saa nane mbona hamwasogelei kuwaambia wamevunja sheria? Mnachotaka kwetu ni nini eh?" Ankia akasema hayo na pombe yake kichwani.

"Halafu we' ndo' unajifanya una mdomo sana," polisi namba 3 akamwambia Ankia huku akimnyooshea rungu-bunduki.

"A-ah... msamehe tu bro, amechangamka sana..." Tesha akasema hivyo.

"Hapa hatujali mmechangamka wala nini. Twendeni hapo ndani sasa hivi!" polisi namba 1 akasema hivyo.

Eh!

Ankia akaanza kulalamika, twende huko pamoja nao, KWA NINI? Ilionekana kuwa uonevu, Bobo na Tesha wakijaribu kuendelea kutuliza upande wa maaskari hawa, lakini umakini wangu ukavutwa zaidi na Miryam. Ikaonekana anakaribia kutapika tena, naye akainamia pembeni na kuanza kutoa maji mengi mdomoni, kwa kasi. Kichefuchefu kilikuwa kimemkaba haswa, ni lazima alikuwa anajutia.

Nikawa nimesimama karibu yake zaidi, nikisugua mgongo wake kwa kiganja changu, naye akachuchumaa kabisa na kuendelea kuinamisha uso wake. Polisi wale wakaendelea kulazimisha kwamba twende nao, eti tutajibu kila kitu huko huko, na wenye maneno mengi haswa ilikuwa ni Ankia na polisi namba 3, huku Bobo akiwa refa wao kwenye maongezi.

Ikanibidi niwageukie na kusema, "Aisee, tunarudi tu nyumbani, drama za nini? Tunaonekana kama watu wabaya sisi, au basi tu mnatafuta sababu ya kuonea mtu? Angalia tunawaambia kuna mtu hajisikii vizuri hapa, halafu mnataka tumpeleke huko ili...."

"Kaa kimya!" polisi namba 1 akanifokea namna hiyo.

Nikamtazama kwa umakini sana.

"Huko! Nimesema tembeeni! Huko!" akaamrisha hivyo.

Nikamtazama Miryam, ambaye bado alikuwa ameinama hapo pembeni, na ile nimemwangalia tena polisi namba 1, nikakuta ametoa kitu kama waya mweupe, wenye muundo kama jinsi siafu hutengeneza mstari wao, naye akaukunjia kiganjani kwake na kuacha sehemu ndogo inaning'inia. Alikuwa akitaka kutishia kunichapa sijui?

Akasema, "Anzeni kutembea sasa hivi. Wewe! Nyanyuka hapo!"

Alielekeza hayo maneno kwa Miryam, nami sikutarajia hili aisee. Akamsogelea na kutumia hicho kisiafu kumtandika mgongoni! Eh, eh, eh, eh, eh, eh!

Miryam akatoa sauti ya maumivu na kujikunja kiasi mgongoni, naye Ankia akapiga kelele ya kushangaa sana baada ya huyo jamaa kufanya hicho kitendo. Aisee, hapana... huyu angekuwa Joshua wa pili!

Nikang'ata meno kwa nguvu nikihisi hasira kali vibaya mno, nami nikamfata kwa kasi na kumsukuma kwa nguvu mno! Polisi namba 1 akawa ameweweseka vibaya na kuanguka chini kwa kishindo, nami nikamrukia hapo hapo chini wakati akijaribu kusimama na kumtandika ngumi mbili nzito kwenye taya yake, naye akaufunika uso kwa mkono.

Mapolisi wenzake wakaja juu yangu na kuanza kunipiga mgongoni kwa virungu, kisha wakanitoa na kunisukuma. Bobo alikuwa mwenye nguvu sana, naye pamoja na Tesha wakaweka kama ukuta kuendana na sehemu niliyokuwa nimesimama, huku Adelina na Ankia wakiwa wamesaidizana kumwondoa Miryam pale alipokuwa na kusogea mbali kidogo.

Polisi namba 1 akasimama, na yule namba 2 ndiye ambaye alikuwa ameshikilia bunduki kabisa, na sasa akawa ametunyooshea huku kwa pamoja wakituamrisha tupige magoti chini. Nilikuwa nikiwatazama kwa hasira sana, hasa yule ambaye alithubutu kunyanyua mkono wake dhidi ya Miryam, naye Bobo akawa akiwaambia watulize jazba huku akitusihi mimi na Tesha tupige magoti. Yeye na Tesha wakaanza kupiga magoti chini, kisha mimi pia nikafata.

Polisi hao wakatusogelea na kuanza kutusengenya kwa kutupiga-piga vibao, huku wakiwaita na wanawake waje upande wetu, na kwa ujasiri, Miryam akawaacha nyuma Adelina na Ankia na kuanza kuja tulipokuwa, kisha nao wakafuata. Bado alikuwa akiyumba na alionekana kuchoka, lakini akaja kando yetu na kupiga magoti pembeni yangu, nami nikamtazama usoni kwa hisia sana.





★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★


Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
jc wewe ndiyo uliyesababisha shefu said Àuwawe,,,, kwann???,,, siku umefika pale ulianza kuleta ukaribu na yule bwana ukuishia hapo na namba za simu mkabadilishana mbaya zaidi yote haya mliyafanyia ndani ya nyumba ya Festo ,,,

Sasa sijui hukufikiria ,,, kuwa festo siyo mjinga aamini walinzi tu peke yake ,,, bwana huyu lazima atakuwa kafunga Camera zakutosha nje na ndani ya hilo jumba lake ,,, sasa ikiwa niwazavyo ni sahihi,,, maongezi yako weww na shefu zaidi siku ile aliyaona na kuyasikia ,,, lakini pia kitendo cha weww kukaa na mpishi yule mkala chakula pamoja pia kilimuongezea matatizo ..

Sheria zilikuwa wazi ,,, kazi ya shefu said ilikuwa ni kupika tu na kuondoka zake,,, siyo kuanza kula na kuongea na wageni wasio muhusu ,, na kwenda mbali zaidi hata kuchukua namba zao kwa mawasiliano huu ulikuwa ni ukiukwaji mkubwa sana wa sheria na usaliti wa kiwango cha juu hivyo kama ulivyo sema festo ni mtu makini ,,, hivyo ilikuwa lazima ampoteze huyu bwana...
Wewe utakuwa ni Festus a.k.a Festo.
 
MIMI NA MIMI 2

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Siri, Tamaa, Hila, Usaliti, Ukatili, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA NANE

★★★★★★★★★★★★★★


Adelina na Ankia wakaja nyuma yetu na kupiga magoti pia, hivyo sote tukawa tumewekwa "chini ya ulinzi." Wakati wa burudani ukawa umeingiwa na jini kisirani. Tukawa tumepigishwa magoti kwa kunyooshewa bunduki kutokana tu na mimi kujaribu kumtetea Miryam, lakini sikupiga magoti kwa sababu ya kuogopa watu hawa, bali tu ilikuwa kuangalia usalama wa wenzangu.

Mapolisi wenyewe walionekana kuwa wavutaji tu, hawakuwa na ufundi uliofikia nyenzo halisi za kuwa katika nguvu waliyokuwa nayo, ni basi tu kushikishwa mitutu na virungu ndiyo mambo yaliyowajaza viburi kufikiri wanaweza kufanya lolote lile kwa raia. Nilitaka kuhakikisha ninawapa somo leo hii.

Kufikia wakati huu, kuna watu wa ujirani ambao walikuwa wametoka majumbani mwao na kuonekana hapa na kule wakitazama yaliyokuwa yametokea, na ndiyo maaskari uchwara wakawa wametuambia tusimame ili watupeleke kwenye kituo chao eti kutupa adhabu. Mhm... haya.

Sote tukasimama, huku bado Miryam akiwa hajiwezi vizuri shauri ya hali yake, lakini angalau kutapika vile kulikuwa kumemwondolea uzito mzito mno, sema bado alikuwa mzito kiasi, kwa hiyo alishikamana na Ankia pamoja na Adelina katika utembeaji. Mimi nilihisi maumivu mgongoni kutokana na virungu walivyonitandika hao mbwa, lakini sikuyajali sana.

Tukaelekea huko walikokuwa wanataka twende, nikiwa bado nina hasira kali mno iliyozidi kupanda tu shauri ya polisi namba 1 kupenda sana kunisukuma-sukuma, na mpaka tunalifikia jengo lile lile lililotumiwa kama ofisi ya mwenyekiti au mtendaji, bado ilikuwa ni saa tano. Wakatupeleka huko ndani ambako kulikuwa na chumba maalumu cha kuwafungia wahalifu, nao wakatuambia tuingie humo; yaani eti tungelala hapo mpaka kesho na hatua zaidi ndiyo ingechukuliwa.

Nikawauliza, "Hivi nyie mna matatizo, eti?"

Polisi namba 1 akasema, "Haki ya Mungu we' mjinga ukisema neno lingine tena nitakufanyi..."

"Nimeshaanza kuongea, na nataka unisikilize kwa umakini," nikamwambia hivyo kwa ujasiri.

Mapolisi wote walikuwa wananiangalia kwa umakini, na hatukuwa tumeingia kwenye hicho chumba, bali Miryam alikuwa amekaa kwenye benchi moja pembezoni mwa ukuta pamoja na Tesha huku Bobo, Adelina, na Ankia wakisimama kando yangu.

"Msije mkafikiri kila mtu huwa ni wa kuonea tu. Sijaja na nyie hapa kwa sababu ninaogopa hilo bunduki lenu, ila nina watu naowapenda, na nyie mkiwaumiza watu naowapenda, ni lazima nitawaumiza nyinyi," nikawaambia hivyo kwa mkazo.

"We' panyammoja unafikiri unaweza kunifanya nini mimi? Unajifanya unajua sana kupigana kisa nimemgusa huyo mwanamke wako?" polisi namba 1 akasema hivyo.

"Umemgusa? Wakati umempiga! Tena umempiga na hicho kiwaya chako wakati tumekwambia anaumwa!" Ankia akaongea kwa hasira.

"Ndiyo nimempiga! Ni haki yake kupigwa!" polisi namba 1 akaongea kwa kiburi.

"Wewe ni fala sana! Mwanaume gani unajitoa akili kupiga mwanamke? Kama unataka kupiga mtu, pigana na sisi hapa... waachie hawa waende nyumbani, tupige sisi hapa sasa!" Tesha akaongea kwa hisia kali pia.

"Kumbe mnataka na nyie eh?" polisi namba 2 akasema hivyo.

"Ingieni huko ndani la sivyo tutawacharaza virungu wote!" polisi namba 3 akapayuka.

"Niambieni ni sheria gani inawaruhusu kupiga raia wakati hajafanya jambo lolote la kuwadhuru nyinyi? Mh? Sheria ipi?" Adelina akasema hivyo kwa hisia kali pia.

"Wameshazoea kuwatisha watu wote, wengine wanawaburuzaga kabisa wakati hata hawajafanya lolote..." Ankia akasema hivyo pia.

"Kwa hiyo hamtaki kuingia huko ndani si ndiyo?" polisi namba 2 akasema hivyo.

"Bobo, mpigie mzee Hamadi. Una namba zake?" nikamuuliza hivyo.

Bobo akasema, "Ninazo," na kutoa simu yake.

"Mmpigie ili iweje? Mnafikiri ndiyo atawatoa hapa? Aisee, nimesema ingieni huko!" polisi namba 2 akasema hivyo na kumshika Adelina kwa kutaka kumsukuma.

Nikautoa mkono wake kwake kwa nguvu na kusimama mbele yake, naye akanipandishia kidevu juu.

"We' ndo' una damu ya moto sana eti?" polisi namba 1 akaniuliza hivyo.

"Jibuni swali lake. Ni sheria gani inawaruhusu kumpiga raia wakati hana kosa? Huyu, au mimi, tumekuwa ng'ombe? Tunawaambia tuko njiani kurudi nyumbani halafu mnampiga mwanamke anayeumwa? Kwa nini?" nikauliza hivyo kwa hasira.

Bobo alikuwa ameshampigia mzee Hamadi na kuanza kuongea naye, na Miryam alikuwa amekaa tu kwenye benchi akionekana kuchoka huku Tesha akimshika kwa ukaribu.

"Na wewe unajua adhabu ya kumpiga askari ngumi? Eh? Umenirukia ukanirushia ngumi, unafikiri tutakuacha tu?" polisi namba 1 akaniuliza hivyo kwa hasira pia.

"A-ah... kwa nini umpige? Kwa nini umpige huyu mwanamke? Jibu swali langu. Unajua ni kosa gani umefanya we' mwanaume? Unajua? Au unafikiri kila mtu atakuwa mwoga wa vitendo vyenu vya kikatili mnavyofanyia raia kwa kujisikia tu? Alikufanya nini huyo dada? Alikufanya nini mpaka unyanyue huo mkono wako kumpiga?" nikaongea kwa hasira ya wazi kabisa.

"Basi, JC... acha tu," Adelina akaniambia hivyo huku akinishika mkono.

Mapolisi wakawa wananiangalia kama vile wananipangia njama mbaya kwa pamoja.

Bobo akasema, "JC, mzee Hamadi amesema yuko hapo karibu... anakuja. Anataka kuongea na sisi wote..."

"Kwa hiyo mnafikiri mmemaliza sasa kwa sababu mnajuana na mwenyekiti?" polisi namba 1 akasema hivyo.

"Hapa hamwondoki, na mpaka mtoe faini!" polisi namba 3 akasema hivyo.

"Unamaanisha rushwa?" Adelina akamuuliza.

"Tena faini ya nini? Tumefanya nini? Hivi nyie mnafikiri... ehee... yaani watu! Wewe utatoa faini ya kumpiga Miryam? Tena na JC mmempiga na mavirungu yenu!" Ankia akafoka.

"Eeeh tena tunawapiga tena! Mtafanya nini?" polisi namba 2 huyo.

"Jaribu! Jaribu!" Ankia akawa anafoka huku Bobo akimshikilia.

"Msijione mnaweza sana kuongea. Hatujali nyie mnatoka wapi. Ingieni huko ndani, la sivyo..." polisi namba 1 akatishia.

"Mtatufanyaje? Mtatufanyaje?" Ankia akaendelea kufoka.

"Ankia, tulia..." Bobo akaendelea kumtuliza.

Ankia, akiwa hadi ameanza kutokwa na machozi, akasema, "Niachie Bobo. Waache na me wanipige, ama waniue. Kwa nini wampige Miryam? Eh? Aliwakosea nini? Eee... baba, njooni mtufanyie sasa. Na huko ndani hatuingii. Fanyeni mnachotaka, si mnajiona mnaweza sana? Fanyeni halafu mwone itakavyokuwa!"

Hao mapolisi jamii wakacheka na kuendelea kumwangalia Ankia na sisi wote kwa dharau.

Nikamnyooshea mkono Bobo ili amwachie Ankia, naye akatii. Ankia akaja mpaka usawa wangu na kusimama, nami nikawaambia hao viazi, "Huyu hapa mwanamke mwingine mnayeona ana haki ya kupigwa. Pigeni."

Polisi namba 1 akaniambia, "We' jamaa huwa unajisikiaga sanaaa... unafikiri kila kitu unajua yaani... huwaga nakuangalia tu ila, nakupania siku moja tuje tukutane sehemu..."

Nikasogea mbele yake na kusema, "Kwani hii si sehemu? Isingekuwa ya Mir.... isingekuwa ya hawa marafiki zangu leo, ungetumia hata hilo bunduki lako kunifanyia unachotaka, lakini mimi siwezi, kamwe, kuogopa mtu mdogo kama wewe."

"Mdogo eh?" akaniuliza hivyo.

"Tena mwanangu wa kuzaa kabisa!" nikamwambia hivyo.

Akanisogelea usoni na kusema, "Ingia. Wewe na familia yako, sijui wapenzi wako, nimesema ingieni HUKO NDANI!!!"

Nikatulia tu na kuendelea kumwangalia usoni kwa umakini.

"Yaani nyie jamaa nawashangaa sana. Sijui ni chuki binafsi tu?" Tesha akasema hivyo.

"Eti?!" Ankia akadakia.

"Na ni viburi tu, hamna lolote. Tumefanya nini kibaya, na mnataka kuthibitisha nini sasa?" Adelina akaongea hivyo.

"Wanataka hela tu, eti faini! Tumekojoa ukutani kwa mtu? Hatutoi hata senti yaani," Tesha akasema hivyo.

"Halafu we' dogo!" polisi namba 3 akamnyooshea Tesha kirungu.

"Nini? Haki ya Mungu, naweza kucheza sindimba na wewe mpaka asubuhi na ukalala mimi bado nacheza tu, hunitishi kwa lolote! Nilikuwa mpole mwanzoni, halafu mkaona mmpige dada'angu?! Yaani JC... usingekuwa hapa, hakuna cha kumsubiri mzee Hamadi wala nani, tungeuana tu na hawa mafala!" Tesha akasema hivyo kwa hisia kali.

Polisi namba 2 akafanya kutuelekezea bunduki lake na kusema, "Ingieni huko!"

"Piga! Piga!" Ankia akamwambia hivyo kwa ujasiri.

"Hey, hey nyie! Kulikoni hapa?"

Mzee Hamadi akawa amefika hatimaye na kuuliza hivyo, na alikuwa amevalia jezi ya Simba kwa juu pamoja na suruali ya kitambaa, huku kichwani asikose kibaghalashee chake.

"Juma, hebu shusha hiyo bunduki," mzee Hamadi akamwambia hivyo polisi namba 2.

Jamaa akaishusha na kusema, "Hawa wajinga wamevunja sheria halafu wakamvamia Mzamiru na kumpiga... huyu hapa mwarabu huyu!"

"Kwenda huko! Unaongea kwa kudeka kama litoto ili iweje? Tulia na sisi tuongee suruali ikushuke, halafu mjinga mwenyewe!" Ankia akamwambia hivyo.

"Umeona walivyo na dharau?" polisi namba 3 akadakia.

Mzee Hamadi akamwambia polisi namba 1, "Bobo amesema nyie ndo' mmewavamia halafu mkampiga mgonjwa wakati wanarudi kwao. Ni kweli Mzami?"

"Siyo mgonjwa, amelewa. Wote hawa wamelewa, husikii wanavyonuka mapombe?" polisi namba 1 akalalamika.

"Ndiyo ikupe ruhusa ya kumchapa huyu dada? Kosa lake ni kunywa? Mbona hukwenda Masai kuwachapa wote waliokuwa wanakunywa?" Bobo akamuuliza hivyo.

"Si ndiyo hapo?" Ankia akaongea pia.

"Kwa hiyo hii shida yote imeanza kwa sababu umempiga Miryam? Miryam mama... Miryam..." mzee Hamadi akajaribu kumwita.

Miryam alikuwa amekaa kimya tu, akiunganisha viganja vyake kwa pamoja na kuinamishia uso wake hapo, nami nikamtazama kwa hisia sana.

"Hajisikii vizuri. Tena alikuwa anatapika, huyo msenge akampiga eti kuonyesha anaweza sana kupiga wanawake!" Tesha akamwambia hivyo mwenyekiti.

"Umeniitaje we' mjinga?" polisi namba 1 akafoka na kutishia kumfata Tesha.

"Kama ulivyosikia, msenge wewe!" Tesha akaongea kwa sauti na kusimama, akija upande wetu kwa hasira pia.

Mzee Hamadi akamwambia polisi namba 1, "Basi! Hebu acheni haya mambo bana!"

Nikamwekea Tesha kiganja kifuani ili atulie pia. Nilikuwa kimya tu kwa sababu ya kumkazia macho huyo Mzamiru. Alikuwa amenichukiza sana. Sana!

Mzee Hamadi akasema, "Hivi nyie kuna amani kweli kabisa kwenye familia yenu? Eh? Kwa nini mizozo kila mara?"

"Kila mara katika maana gani? Sisi ni watu tuliotulia, lakini wajinga kama hawa ndiyo wanapenda kutuchokoza tu wakifikiri sisi ni wa kuyumbishwa sijui? Hawa kama hawajatumwa na mtu kutufata na kutuzingua leo... basi shida yao ni hela tu. Walikuwa wanataka hongo, eti wanasema 'faini,' faini itoke wapi? Tumekojolea hii ofisi au? Baba... hapa lazima haki ipatikane. Wametuonea sana. Wamempiga Miryam, amewakosea nini? Ah!" Ankia akaongea kwa hisia sana.

Alifanya mpaka hasira yangu ikaniweka kwenye ukaribu wa kutokwa na machozi, maana kitendo alichofanyiwa Miryam kiliendelea kujirudia akilini mwangu kila mara yaani. Nafikiri kulikuwa na watu huko nje ambao walisikia yaliyokuwa yakiendelea hapa, kwa hiyo kuna ambao walisogea karibu zaidi na jengo hilo, na polisi uchwara wengine watano wakawa wameongezeka hapo na kuwafukuza. Kundi lao likaongezeka.

Polisi namba 1 akasema, "Mwenyekiti, hakuna kuwasikiliza hawa! Walale humo mpaka asubuhi! Na lazima walipie kwa kuvunja sheria... wamenirukia wakanipiga mimi askari!"

"Nyooo... askari gani wewe?" Ankia akasema hivyo.

"Na nani alikudanganyaga kwamba maaskari huwa hawapigwi? Mkivunja sheria, kwa nini tuwaache?" Bobo akamuuliza hivyo.

"Nini kinaendelea?" polisi uchwara mwingine akauliza.

"Hebu tulieni basi!" mzee Hamadi akaongea kwa kukereka.

"Hawa ni wapumbavu! Nimewakuta wanatembea usiku, wamelewa, halafu...."

"Wewe Mzamiru, nimesema kaa kimya! Mbona huelewi?" mzee Hamadi akamwambia polisi namba 1 hivyo.

"Hawa siyo wa kunyenyekea mwenyekiti! Sisi siyo Joshua aisee! Na hatuogopi hiyo ngozi yenu. Mkizingua, tunawazingua kweli. Na hamuwezi kutufanya lolote!" polisi namba 1 akasema hivyo huku akiniangalia usoni.

"Unajua... huwa sipendi kutumia maneno makali, ila Tesha yuko sahihi. We' ni msenge sana," nikamwambia hivyo polisi namba 1.

"Jayden..."

Hatimaye Miryam akawa amezungumza kwa mara ya kwanza kabisa toka tumefika hapo, na sauti yake ilikuwa ya chini, akiniita kama vile kuniambia hakufurahishwa na maneno yangu hasa kwa sababu yalitoka kwangu, nami nikageuka na kumwangalia. Wote tulimwangalia.

"Inatosha... please..." akasema tena hivyo bila kuinua uso wake.

Polisi namba 1 akacheka kidogo na kuwaambia wenzake, "Eti wazungu sasa..."

Nikakunja ngumi kwa nguvu, nami nikamgeukia mzee Hamadi, na kwa sauti tulivu nikamwambia, "Mzee... nisikilize. Mimi siyo mjinga. Ninajua sheria vizuri sana, na najua wewe pia unaijua, kwa hiyo unajua kuwa huu upuuzi waliofanya watu wako uko kinyume na sheria. Hawa siyo maaskari, ni walinzi tu. Lakini hata IGP Wambura ashasema, vitendo kama hivi vinavunja code of conduct waliyonayo wanausalama wa taifa wote, na kuna hatua za kinidhamu zinazochukuliwa dhidi yao wakibainika. Mzee Hamadi nimekupigia ili tusifike mbali, lakini kwa huu ujinga unaoendelea tutafika huko, kwa sababu hawa watu hawatutendei sisi tu hivyo... kuna wengi wameshazoea kuwatendea hivyo. Ninakutaka uchukue hatua kuukomesha huu utawala wao wa kipuuzi wanaoufanya badala ya kazi jamii iliyowaweka kufanya, unajua nina tie in kubwa sana na watu kama detective Ramadhan. Nikivuta waya wangu hapa kumpigia akaleta mvua yake ya moto huku... hawa vijana wako watakwisha. Sijui umenipata?"

Niliongea maneno hayo kwa mkazo sana, na wote walikuwa wakiniangalia kwa umakini.

Mzee Hamadi akasema, "A-ah, JC... mbona unataka kwenda mbali sana?"

"Unamaanisha nini tutakwisha?" polisi jamii mmoja akauliza hivyo.

"We' Karim hayakuhusu. Pita hivi," Bobo akamwambia.

"Hapana Bobo, ni wote! Wote wako hivyo hivyo," Tesha akamwambia hivyo.

Mzee Hamadi akasema, "Kimya, nasema kimya!"

Wote wakatulia.

Mwenyekiti akaniangalia usoni na kusema, "Nimekuelewa JC. Hii haifai najua, ni... imeenda mbali, na haikupaswa kufika mbali. Nawaomba nyie wote mwondoke, nendeni tu nyumbani. Nitaongea na vijana hawa..."

"Tunajua toka mwanzo tulikuwa na haki ya kutokuwa hapa mpaka wakati huu, kwa sababu tumeonewa. Na zaidi... wamemwonea huyu dada, wamempiga bila sababu..." nikamwambia hivyo mwenyekiti.

"Tena na JC wamempiga na marungu mgongoni! Anajikaza, lakini wamemuumiza," Ankia akasema hivyo.

"Haina shida Ankia, niko sawa," nikamwambia.

"Kwa hiyo unachotaka ni nini?" mzee Hamadi akaniuliza.

Nikamwangalia huyo polisi namba 1 usoni na kusema, "Ninataka huyu... amwombe msamaha Miryam."

"Eeh... amwombe msamaha Miryam kwa alivyompiga!" Tesha akaongea pia.

"Kwa hiyo nikimwomba msamaha ndiyo atasahau kwamba alipigwa?" polisi namba 1 akaniuliza hivyo.

"Nimekurudishia ya kumpiga. Nataka umwombe msamaha... na upige magoti!" nikamwambia hivyo.

"Nini?!" jamaa akashangaa.

"Kama ulivyosikia!" Tesha akamwambia hivyo.

Polisi uchwara wakaanza kuongea kwa ubishi, wakisema huo ni upuuzi usiowezekana hata kidogo.

"Yaani mimi nipige magoti? Wewe ni mwendawazimu eti? Nikipiga magoti, yaani naacha na kazi leo leo hii..." polisi namba 1 akaongea kwa kujitutumua.

"Ni leo hii hii, yaani hata kiswahili kuongea ni matatizo... hayajui," Ankia akasema hivyo, naye Bobo akacheka kidogo.

"Simama hapo hapo mpaka kesho, uone kama nitapiga magoti!" jamaa akaniambia hivyo.

Nikamwangalia mzee Hamadi kwa mkazo, naye akasema, "JC... si mngeenda tu nyumbani? Eh? Miryam amechoka, nyie wote mmechoka, haya yote ya nini? Usiku umeishaingia, em' nendeni..."

"Kweli JC, tuondoke tu. Haina faida yoyote," Adelina akaniambia hivyo.

"Nasema hivi... apige magoti amwombe Miryam msamaha. Mzee Hamadi haunijui vizuri, lakini niamini nikikwambia kwamba tukiondoka hapa huyu mbuzi hajamwomba msamaha Miryam, nitaitia hii ofisi dosari. Sikutanii," nikaongea hivyo bila utani hata kidogo.

"Yaani wewe! Unafikiri unatutisha sisi? Ulete nini labda wewe mbwa tukiogope?" jamaa akaongea kwa dharau.

Mzee Hamadi akamwangalia na kusema, "Mwombe msamaha huyo dada, Mzamiru."

Wote tukamwangalia jamaa.

"Nimwombe... haki ya Mungu! Mzee... huyu mkorogo huyu ndiyo anakutetemesha huyu... akija kukwambia ule mavi utakula kwa hiyo?"

"Nimesema mwombe huyo dada msamaha. Ulichomfanyia siyo kizuri. Hakuna kosa lolote hawa wamefanya, na usiendekeze jeuri. Mwombe msamaha, yaishe," mzee Hamadi akamwambia hivyo.

Polisi namba 1 akasema, "Wewe siyo boss wetu mwenyekiti kutuamulia..."

"Nani anawalipa pesa mnayotumia kula ili mzurure usiku kulinda mitaa? Hmm?" mzee Hamadi akamkatisha kwa kuuliza hivyo.

"Si ni wajumbe?" polisi namba 2 akajibu hivyo.

Tesha akacheka kidogo kwa pumzi na kusema, "Yaani... bogus!"

Mzee Hamadi akasema, "Hao wajumbe wanazitoa wapi? Kabla hujajibu, nitakwambia. Wanawatoza hawa hawa raia ambao mnawaonea, wanaziwasilisha kwa viongozi wenu, mnapewa share yenu. Lakini hayo yote hayakamiliki nisipohusika, kwa sababu hao hao wajumbe wanategemea nguvu yangu, sijui mnanipata? Kwa hiyo ni mimi ndiye nayewalipa nyie, hao ni wasaidizi wangu tu. Akili zenu inaonekana bado ndogo sana hata hayo hamwelewi!"

"Sana!" Bobo akawaambia hivyo.

"Huyu dada ni moja ya watu wastaarabu sana hapa mtaani, hanaga zogo na mtu. Imekupa raha gani kumpiga hivyo, eh? Umejiona super sasa? Mzamiru, nasema mwombe msamaha. Mwombe msamaha haraka," mzee Hamadi akamwambia hivyo kwa uthabiti.

Huyo Mzamiru, akacheka kidogo kama vile hataki eti, halafu akasema, "Haya, nisamehe... we' dada? Nisamehe kukupiga, sawa eh?"

Alikuwa anajiona ana dharau mno, nami nikasema, "Piga... magoti."

Akaniangalia usoni kwa umakini.

"Kama ulinisikia tu kwa watu kwamba nilimfunga mtu kwa sababu ya upuuzi wake, basi cheza na mimi uje uone mwisho wake, siyo kuusikia tu. Unaongelea kuacha kazi? Nitahakikisha unafutwa na hupati kazi kwingine tena kwa sababu ya huu upumbavu ili uhangaike mpaka familia yako iteseke. Acha kucheza na watu usiojua mwanangu, siyo wote wameumbwa kuonewa, na usichezee kazi yako ukajiona umefika sana na kuitumia kama fimbo kumchapa yeyote unayetaka... wengine siyo wa kuguswa. Piga magoti umwombe huyu dada msamaha, sasa hivi..." nikaongea hayo kwa hisia kali.

Yaani niliongea kwa sauti yenye mamlaka, pakatulia mpaka tuli. Sasa watu wote hapo walikuwa wakitutazama, na sikujua Miryam alikuwa vipi huku nyuma yangu lakini nilitaka kuhakikisha hili jambo linakubali ili iwe somo kwa wote kutokuja kamwe kurudia kitendo kama kile. Haingefanya kazi kwa wote, najua, lakini baada ya hapa ningekuwa nimehakikisha wote wanamwona Miryam kuwa malkia.

Niliona wazi kwamba jamaa alianza kuogopa, na alikuwa akiona aibu; kiburi chake pia kikimfanya awaangalie wenzake ili kupewa 'support,' lakini wote walibaki kimya zamu hii na kubaki kuangalia angefanya nini.

Akasema, "Kwa hiyo...."

"Nimesema piga magoti!" nikamkatisha kwa ukali.

We! Mpaka mzee Hamadi akanishangaa.

"Jayden..." sauti ya Miryam ikasikika akiniita hivyo.

Nikageuka na kumwangalia, na sasa alikuwa amenyanyuka kutoka kitini huku akiniangalia usoni kwa macho makini ingawa yalikuwa mazito, na kwa sauti ya chini nikamwambia, "Hautoki hapa Miryam kabla huyu hajakuomba msamaha."

Akaendelea tu kuniangalia kimkazo kiasi.

Nikamgeukia polisi namba 1 na kusema, "Fanya hivyo."

Mzee Hamadi akashusha pumzi na kusema, "Aisee! Mzamiru harakisha, yote ni makosa yako. Piga magoti."

Heeee!

Ilionekana kuwa kizungumkuti na bonge moja la drama ya kuigiza, lakini mbona jamaa akaenda chini! Alishuka kwa mguu mmoja, kisha wa pili, akapiga magoti huku sote tukimtazama kwa umakini.

"Nisamehe," akamwambia hivyo Miryam kama hataki.

"Iseme vizuri," nikamwambia hivyo.

"JC..." Adelina akaniita kama kuniambia imetosha.

Nikamgeukia na kusema, "Nini Adelina? Sasa hivi me ndo' naonekana namwonea, au? Hicho kitu hakipo. Hakipo!"

Nilikuwa nimefura!

Nikamwangalia jamaa usoni tena hapo chini, akiwa amepiga magoti kama litoto, nami nikamwambia, "Iseme vizuri."

Akamwangalia Miryam na kusema, "Naomba nisamehe dada. Nisamehe kukupiga."

"Angalau," Tesha akasema hivyo akiwa amekunjia mikono yake kifuani.

Nikamwangalia Miryam usoni, yeye akiwa anamtazama huyo polisi mwenye akili 0 kwa mkazo, kisha akaniangalia machoni pia.

"JC, basi. Miryam mama... nenda nyumbani ukapumzike, sawa? Nendeni tu. Hey nyie wote, nendeni... toka hapo," mzee Hamadi akaongea hivyo na kuwaambia hivyo wengine huko nje.

Miryam akaanza kuja upande wangu taratibu huku akiniangalia usoni kwa sura iliyoonekana kukwazwa sana, naye akanipita tu na kuelekea nje huku Adelina akimfuata.

Nikafumba macho na kung'ata meno kiasi kutokana na kuhisi kwamba sababu ya yeye kukwazika ilitokana na mimi kulazimisha aombwe msamaha namna hiyo, haijalishi kama kweli huyo polisi alistahili hiyo fedheha. Na aliistahili, nilikuwa natamani hata na yeye atandikwe na hako kamjeledi, basi tu!

Bobo na Tesha wakaniambia tuondoke, huku Ankia akiwa ameshatangulia nje pia, na huyo polisi akawa ameshasimama na kuonekana kuudhika sana kutokana na "kudhalilishwa" mbele ya wenzake. Na wote walinitazama kwa macho makali kweli.

Lakini nikamsogelea huyo jamaa karibu na kumwambia, "Huo ndiyo wendawazimu wangu sasa. Nitafute tu kwenye ile siku uliyoisema, niko tayari kwa ajili yako."

Jamaa akaniangaliaaa, yaani kama vile haelewi kabisa ujasiri niliokuwa nao ulitoka wapi, na mzee Hamadi akasema, "Ah, JC! We' kijana hapana. Hebu nenda kale ugali ulale. A-ah..."

Tukaondoka tu hapo hatimaye pamoja na wenzangu, ikiwa imeingia saa saba usiku sasa, na bado kukiwa na watu kadhaa ambao walitutazama sana tulipokuwa tukitoka kwenye eneo la hiyo ofisi. Miryam, Adelina, na Ankia walikuwa wakitembea taratibu tu mbele yetu, huku nikiona jinsi Ankia alivyowasemesha wenzake kwa manung'uniko, vilevile na Tesha upande wetu aliyekuwa akiongea haswa na Bobo kuhusiana na hiyo ishu. Nilikuwa kimya tu, wenzangu wakiona kwamba bado nina hasira, na ndiyo ikawa imepita bajaji isiyokuwa na wateja kando yetu.

Nikawaza upesi kwamba ingekuwa vizuri wanawake wakipanda kwenda mpaka nyumbani, kwa hiyo nikaisimamisha na kumlipa mwendeshaji na kumwambia akawabebe. Bajaji ilipowafikia, ilionekana wameelewa kuhusu kupanda lakini wakawa wanataka kupanda pamoja nasi, kwa hiyo tulipowafikia karibu tukawaambia watangulie tu; sisi wanaume tungekuja mdogo mdogo.

Ni Miryam ndiye ambaye akaonekana kutopenda hilo wazo, kwa hiyo akaanza kutembea tena taratibu kuelekea mbele. Tesha akawa anamwita, Ankia vilevile, lakini hakusimama, hivyo mimi nikamfata upesi na kumshika mkono. Akaniangalia usoni kwa njia iliyoonyesha kuchoka sana kihisia, nami nikamsihi kwa upole kuwa aingie kwenye bajaji, sisi tungekuwa sawa na tungefika. Awahi tu kupumzika.

Ndipo akautoa mkono wangu kwake taratibu na kuacha kunitazama, halafu polepole akarudi kwenye bajaji na kwenda kuingia humo, akiniacha nimesimama tu hapo huku nikimtazama. Adelina na Ankia wakaingia bajajini pia, nayo hiyo ikatuacha wanaume tukitembea mdogo mdogo kuelekea majumbani. Siku hiyo kwa kweli haikuwa imeenda kama nilivyodhani ingekwenda. Tofauti kabisa na nilivyokuwa nimetarajia.

★★

Mimi na Tesha tumekuja kufika makwetu ikiwa inaelekea kuingia saa nane kabisa, maana tulianza kupita Masai kwanza na Bobo, ambako bado kulikuwa na watu, na kwa ushawishi wa hawa wenzangu nikawa nimeshusha bia moja tu ili niende kulala usingizi mzito. Tesha alihakikisha amepiga mbili zaidi ili aongezee kulewa, na ndiyo tukawa tumerudi sasa vichwa vikiwa vimepondeka haswa. Na nilihitaji tu kulala aisee.

Ile nimefika ndani tu, nikamkuta Ankia sebuleni, kwenye sofa, akiwa anaangalia marudio ya tamthilia fulani ya wagiriki kwenye TV. Inaonekana alikuwa ananisubiria tu, kwa hiyo bila hata kumsemesha nikachukua funguo na kwenda kufunga geti, kisha nikarejea hapo sebuleni na kukaa sofani nikihisi kuchoka mwilini.

"Mmepita Masai tena?" Ankia akaniuliza hivyo na macho yake legevu.

Sikumjiibu, bali nikawa nimetazama mbele tu.

"Mhm... ya leo makubwa jamani. Hao wajinga wametuonaje sisi?" akauliza hivyo.

"Adelina?" nikamuuliza hivyo, nikiwa sitaki kuongelea hayo mambo.

"Amelala."

"Na wewe? Si ukalale?"

"Nimelewa lakini sina usingizi."

"Kaulazimishe. Muda umeenda," nikamwambia hivyo.

"Halafu wewe?"

"Naenda kuoga kwanza..."

"Ngoja, hhkh... kun... kuna kitu nataka nikuulize..." akasema hivyo na kunishika begani.

"Utaniuliza kesho Ankia, twende tukalale. Zima TV..."

"A-aah... nisikie kwanza..."

"Sitaki kuongelea hayo mambo sa'hivi, me nataka nikalale... kesho nayo siku," nikamwambia hivyo.

"Tayari hiyo kesho unayoisema ni leo... haijakucha tu bado..."

"Agh..." nikafanya hivyo na kusimama.

Ankia akasimama pia na kuniambia, "Ngoja, nataka nikuulize kitu..."

"Utaniuliza kesho Ankia. Halafu ukiwahi kuamka, na me uniamshe pia, nipige nikigoma, sawa? Ndiyo utaniuliza maswali yote ya dunia. Baadaye..." nikamwambia hivyo na kutaka kumpita.

Akanizibia njia na kusema, "Subiri! Nataka nikuulize kitu kuhusu Miryam."

Nikamwangalia usoni kwa umakini na kumuuliza, "Amefanyaje? Halafu nimesahau, hujaniambia... am-amefika... yuko huko kwao... amefika salama?"

"Enhee... umeona? Hicho hicho..." Ankia akasema hivyo huku akinikazia macho.

Nikaendelea kumwangalia kwa umakini.

"Sisi wote tumekasirika... hao wapumbavu walivyotufanyia... tena hasa walivyomfanyia Miryam. Lakini wewe JC.... maneno yako... jinsi ulivyokuwa unatenda... hapo mwishoni yaani... mpaka nimeshangaa. Kwa nini?" akaongea hivyo.

"Sikuelewi bana..." nikamwambia.

"Nimeanza kukuona toka tupo Masai, nimekuangaliaaa... ulivyokuwa ukimtizama Miryam... tulipokuwa tunatembea, hata alipokuwa anatapika ukamfuta kabisa matapishi, mpaka kuwapigisha magoti watu wababe... ili uwe mbabe... kwa ajili ya Miryam tu... nimeona kuna kitu hakipo sawa kabisaaaa..." akaongea kama vile hana akili.

Nikamnyooshea kidole na kumwambia, "We' umelewa wewe. Zima hiyo TV, ukalale. Me naenda kuoga kwanza..."

"'Hauondoki hapa mpaka akuombe msamaha!'" Ankia akaiga maneno yangu niliyoyasema kumwelekea Miryam muda ule.

Nikabaki nikimtazama kwa umakini.

"'Nitahakikisha hauajiriwi sehemu yoyote...' JC! Leo nimemwona mtu mwingine kabisa... diffarant kabisa na niliyefikiri ni wewe tokea umekuja," Ankia akasema hivyo.

"Sijui unajaribu kuongea nini. Na ni different, siyo diffarant," nikamwambia hivyo.

"Sijalewa kufanya akili yangu ipotee, najua nayomaanisha. JC uliniambia kwamba wewe siyo mtu wa hisia za... mpaka kulazimisha vitu, kwamba haujali sana na nini... lakini today? Hapana. Huyo hakuwa wewe niliyemjua. Kuna kitu kinakusumbua... na nakwambia kwa sababu nimekujua, hao wengine siyo rahisi, me ndiyo nakaa na wewe. Nakujua. JC, umebadilika. Utafanya kitu CHOCHOTE kile kwa ajili ya Miryam. Chochote! Yaani nimeshaona, siyo Bi Zawadi, Tesha, Shadya, Mamu... yaani, nimeshaona. Ni Miryam. Unafanya hhkh... yote, ili kuhakikisha Miryam... haumii," Ankia akaongea hivyo kwa sauti tulivu.

Nikaangalia pembeni kwanza.

"Ahah... si unaona, niko sahihi. Kwa hiyo imeanza lini hii? Nini... ni wapi ambapo alikugusa sana mpaka...."

"Ankia naomba uniache, nenda ukalale!" nikamkatisha na kuanza kuondoka huku nikivua T-shirt..

Akanishika mkono kwa nguvu na kusema, "Hapana JC, nataka uniambie..."

Nikamgeukia na kuuliza, "Nikwambie nini?"

"Unampenda Miryam, JC?"

"What the.... yaani nikwambie hivyo... nijibu hilo swali ili iweje? Ume...? Hebu niachie!" nikautoa mkono wake kwangu.

"Niambie ukweli tu JC. Nimeshakuona. Niambie. Unampenda huyo dada, si ndiyo?" Ankia akaniuliza hivyo kwa sauti ya chini.

Nikabaki nikimtazama machoni bila kuwa na uhakika wa jibu la kumpa.

"Eti? Tena siyo... siyo ile kwamba tu unamtamani yaani, kama ulivyosemaga na besi lako 'tunaanzaga kutamani kwanza, kupenda baadaye,' a-ah! Hii hapa ya sasa hivi ni kwamba umeanza kumpenda Miryam kwanza, na baadaye utaendelea kumpenda si ndiyo? Kile kitu ambacho ulikuwa unajaribu kuepuka kwangu eh?" akaniuliza hivyo huku akiniangalia kwa hisia.

Dah! Maneno yake yalinigusa!

Akanishika shingoni kwa mikono yake yote na kusema, "Niambie JC. Unampenda Miryam?"

Nikashusha macho taratibu na kuangalia chini tu, nikiwa nimekazwa na hisia nzito sana moyoni, nami nikatikisa kichwa na kusema, "Ndiyo Ankia. Nampenda Miryam."

Hatimaye, hatimaye... nikawa nimefunguka!

Ankia akaachia tabasamu hafifu tu, lakini alionekana kuwa amefurahi sana. Sijui hata kwa nini!

Nikamwangalia usoni na kusema, "Ah, aisee! Mpaka nakuwa sijielewi... haikupaswa kuwa hivi Ankia..."

"We' ulitaka iweje?"

"Sikutaka iwe chochote mimi! Haya mambo ya nampenda, nakupenda, Ankia...."

"Wewe ni mwanadamu JC. Hata ukimbie vipi upendo wa kweli lazima utautaka tu. Hauwezi kuwa Playboy maisha yako yote..."

"Mimi siyo Playboy... na hata kama, ningekuwa... Playboy... ningeweza kuwa wa maisha yote..."

"Ahahah... nimeangalia movie ya Tony Stark, na yeye alikuwa kama wewe tu... anafikiri maisha ya mapenzi ni mchezo...."

"Sijawahi kusema nafikiri ni mchezo... acha kuangalia movie za kipuuzi..."

"Lakini umekuwa ukiishi kwa namna hiyo..."

"Ankia... please... basi," nikaona tupumzike kwanza, maana mabishano yasingeisha.

Ankia akarudi nyuma kidogo huku akinitazama na tabasamu lake mwanana, nami nikajishika kiuno na kuinamisha uso huku nikitabasamu pia.

"Aww... JC is in love!" Ankia akasema hivyo.

Nikamnyooshea kidole nikijifanya kuudhika, naye akaziba kicheko chake kwa kiganja.

"So... umepanga kumwambia lini?" akaniuliza hivyo.

"Kumwambia?! Ankia are you serious?" nikamuuliza hivyo kwa sauti ya chini.

"Yes. I mean... siyo pombe tu, yaani I'm deadass serious..."

"Hapana, you're not deadass serious..."

"Unaogopa nini kwani?"

"Siogopi lolote, Ankia. Sitaki tu kujiumiza. Faida itakuwa wapi kwenye hilo?" nikamwambia hivyo.

"Oooh, kwa hiyo unafikiri ukiendelea kukaa kimya ndiyo hautaumia?"

"Unataka nifanye nini? Unamjua vizuri. Hawezi kukubali, Ankia. Yaani... Miryam? Kwa nini ilipaswa kuwa Miryam? Yaani... pisi kibao... and I had to fall in love with Miryam? Ah..." nikaongea hivyo kwa hisia.

"JC, najua mapenzi hayalazimishwi, sawa, hata mimi nilifeli kwako, baada ya muda nikazoea. Lakini sikukaa kimya. Nilikwambia. Usipomwambia Miryam ukweli wakati upendo wako kwake unazidi kukua, JC... utaumia vibaya zaidi... hasa kama muda mrefu utapita. Nina experience, najua. Nimekuangalia, siyo leo tu, toka muda nilikuwa nimeshaona unampenda huyu dada. Tafuta nafasi umwambie, uondoe hicho kilongolongo moyoni maana naona kimeshaanza kukutafuna... usione hata mende anamsogelea yaani uko tayari kumuua kwa panga..."

Nikajikuta nacheka tu mwenyewe utadhani alikuwa anatania.

"I'm serious JC. Mwambie tu. You never know," akasema hivyo.

"Na ukweli ni kwamba I'll never know. Ankia... kilichofanya mpaka nikampenda huyu dada ni kwa sababu yuko tofauti sana, tofauti ambayo mpaka inanifanya nijione kuwa simfai yaani. Nina dhambi nyingi kinoma, achana na umri tu kuwa mdogo, yaani kweli unafikiri Miryam anaweza kuniangalia mimi kwa macho ya mara mbili mbili... hata tu akasema 'ngoja nifikirie upuuzi wako?'"

"Kwa nini unajikatisha tamaa hivyo?"

"Kwa sababu sitaki kuumia zaidi ya ninavyoumia sasa. Kuumia kwa kutomwambia ni bora kuliko kumwambia halafu anikatae. Sijajua kama nitaweza kubeba hilo Ankia. Miryam... yuko kwenye level nyingine yaani ya kina cha upendo naohisi kumwelekea. Ni bora nizame mwenyewe tu, kuliko yeye ndiyo aje kuwa mtu wa kunizamisha kabisa na kuniacha nijifie humo..." nikamwambia hivyo.

Ankia akawa ananiangalia kwa utulivu tu.

"A... hhh... yaani... sijui hata... sijui hata naongea nini. Ila Ankia... please... nakuomba usije kumwambia mtu yeyote kuhusu hili," nikamwomba hivyo kwa hisia.

"Unanichukuliaje JC? Nimwambie nani sasa?" akasema hivyo.

"Wewe ukiwa na mama Chande, huwa zinapaa. Kuanzia leo, hakuna kunywa pombe tena! Sitaki ulewe ukaja ukaropoka!" nikamwambia hivyo.

"Ahahahah... we' ni mjinga! Niongezee zingine now uone kama nitamropokea hata Adela. Kichwa changu siyo lege namna hiyo," akasema hivyo.

Nikashusha pumzi tu na kutikisa kichwa, kisha nikasema, "Nilipitiliza sana leo kuwa mkali namna ile."

"Haukufanya lolote baya wala. Mimi tu hapa ndiyo ilinipa picha kamili. Na ni jambo zuri JC," akaniambia hivyo.

Nikamwangalia usoni kwa hisia.

Akanisogelea na kusema, "Usijali. Nimekuelewa. Fanya unayoona ni sawa, ila usisahau na maneno yangu pia. Yanaweza yakajalisha siku moja."

"Ahah... yatajalisha ukija kusikia nimepondwa na chupa ya chai usoni..."

Ankia akacheka kwa furaha sana.

"Na ndo' unachotaka..."

"Mbona umeanza kuwa mwoga? Hauogopi kuwapigisha magoti polisi jamii, ndiyo unamwogopa Miryam hivyo?" akaniuliza.

Nikamkazia macho.

"Okay, sawa naelewa. Nakutania tu. We' nenda kaoge, me pia nakuja kujimwagia. Tutaongea zaidi kesho. Sawa?" akaniambia hivyo.

Nikatikisa kichwa kuonyesha uelewa, naye akatabasamu kiasi na kuanza kuelekea chumbani kwake.

Nikatoka hapo na kuelekea chumbani kwanza, nikiwa natafakari maongezi yangu na Ankia, na mpaka nimeenda kuoga na kurudi chumbani tena, bado nilikuwa nawaza tu. Nilijitahidi kuonyesha kwamba nilikuwa imara sanaaa mbele yake Ankia, lakini ukweli ni kwamba nilikuwa naogopa. Yaani nilikuwa nikiogopa hisia zangu mwenyewe, kwa sababu sikuwa nimetaka zinifikishe huku kote, lakini sasa nikiwa ndiyo nimefika, na sikujua zingenipeleka wapi.

Miryam nilimpenda. Sana. Lakini hata baada ya mimi mwenyewe kuwa nimekiri ukweli huu, bado sikujua ikiwa ungenipa faida kutoka kwa upande wake yeye mwenyewe. Kukaa kimya tu kungeendelea kunitafuna kama Ankia alivyoniambia, na kumwambia Miryam ukweli halafu akatae upendo wangu kwake ndiyo kungenipasua-pasua hata zaidi. Lakini najua bado hisia zangu zingekuwa pale pale tu. Ningefanya nini sasa?





★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★


Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
Upo sahihi Jc ,,, wanawake inabidi walijue hili ,,, mara nyingi mwanaume anapopenda kweli huingia na woga ,, kiwango cha kujiamini mbele ya yule ampendaye hupungua ,, na hapa ndiyo ile kauli ya kamoyo kanadundaga ti !! ti !! ti ,, huwa inazaliwa ..
Najua fika hapo mrembo miryamu akimkubalia tu ,,, kesho yake tu muhuni anatangaza ndoa hato fikiria mara mbili juu ya jambo hilo
 
"Unataka nifanye nini? Unamjua vizuri. Hawezi kukubali, Ankia. Yaani... Miryam? Kwa nini ilipaswa kuwa Miryam? Yaani... pisi kibao... and I had to fall in love with Miryam? Ah..."
Umeshaingia kwenye Mfumo JC hautoki ndugu yangu 😀😀😀😀
 
MIMI NA MIMI 2

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Siri, Tamaa, Hila, Usaliti, Ukatili, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA TISA

★★★★★★★★★★★★★★


"JC... we' JC... amka..."

Nilikuwa nasikia sauti hiyo ikiniita, lakini sikutaka kuamka kabisa maana nilijihisi uzito wa ajabu. Ndipo nikashtukia nawashwa kofi mkononi lililofanya niumie kiasi, nami nikajitahidi kufumbua macho.

"Amka! Amka... pameshakucha."

Ilikuwa ni Ankia bwana.

Nikaangalia mazingira vizuri; ndiyo, bado nilikuwa kitandani, na kweli palikuwa pamekucha. Nikamuuliza, "Ndiyo nini na wewe kuamshana na makofi?"

"Uliniambia nikuamshe mapema, na nikupige ukizingua. Ahadi ni deni, imetimia," akasema hivyo.

Nilikuwa nahisi kichwa changu ni kizito kweli, nami nikiwa nimelala kwa ubavu, nikaendelea tu kufumba macho na kumwambia, "Umefanya vizuri, ila bado nina usingizi!"

"Kwani unataka kwenda wapi? Huko Sinza kwenu, au?"

Nikatikisa kichwa kukubali.

"Ndo' unyanyuke sasa. Me nataka nikatafute supu, ukisinzia tena shauri yako..."

"Saa ngapi?"

"Saa mbili," akajibu.

"Niletee basi maji ya baridi darling..." nikamwambia hivyo.

"Umeme umekatika... friji haijawaka."

"Kanunue basi. Unaenda kufata supu yako tu?"

"Eeeh, na Adelina. Ila ye' bado kalala. Unataka na we' nikuletee? Niongezee hela basi.." akasema hivyo.

"Kuna elfu tano hapo... juu ya droo. Kachukue supu ya elfu nne, na... maji ya baridii... ongezea, utaona," nikamsemesha huku bado nikiwa nimejisinzisha.

"Mhm... haya ngoja niwahi basi," akasema hivyo.

"Poa."

Nikahisi alipokuwa amenyanyuka kutoka kitandani na kuondoka, nami nikajivuta hivyo hivyo tu na kukaa. Matukio ya usiku uliotangulia yakajirudia wee akilini mwangu, huku nikihisi maumivu mgongoni kutokana na marungu niliyoshushiwa jana, nami nikaamua kuifata simu kutoka chajini. Ndiyo, niliiweka chaji kabla ya kulala.

Nikajitahidi kupambana na wenge la kichwani, nami nikaona kwamba kuna watu walikuwa wamenipigia, na jumbe chache kuingia. Bertha, Soraya, yule Kevin, namba fulani ngeni, pamoja na Bi Zawadi walikuwa wamenipigia kwa asubuhi hii, huku jumbe zikitumwa na Soraya pamoja na hiyo namba ngeni. Nikaona nianze na Bertha.

Nikampigia, na baada ya kupokea, akauliza nilikuwa wapi. Nikamwambia ndiyo nilikuwa najiandaa kwenda kule supermarket Ubungo, yaani sikuwa nimeondoka bado, naye akasema niende kwake kwanza. Kwa kuwa hii ilikuwa Jumatatu, yeye angefanya kawaida yake ya kwenda pale supermarket na sehemu zingine, na ndiyo ningemwonea huko, ila leo alitaka niende kwake kwanza. Bila kuuliza sababu, nikamwambia nakuja, naye akasema nisichelewe.

Wa pili akawa Soraya. Huyu nikamtumia tu ujumbe kuwa bado nilibanwa na kazi fulani, maana alikuwa anataka nimpe ratiba ya makutano, na aisee! Kutokea hapa sidhani kama ingekuwa rahisi tena kwa kweli. Yaani, nilikuwa nimetoka tu kukiri hata mbele ya Ankia kuwa nilimpenda Miryam, na kukumbuka hilo kila mara kukawa kunanifanya nitake kuwa mtu mpya ingawa bado hata sikuwa nimemfikishia mwanamke huyo hisia zangu, na nilikumbuka vizuri sana kwamba bado upande wa Bertha ungeendelea kunipa changamoto.

Yaani hako katabia ka kutoka na huyu na yule nilitaka na nilipaswa nikakomeshe kutokea hapa, na kwa kujua kwamba bado Bertha angekuwa kikwazo, nikaona nimtafute askari Ramadhan. Nikamtumia sms nikiuliza tu 'imefika wapi?' nikiwa na lengo la kutaka kujua kama siku yetu ya kuyamaliza hayo mambo ya Bertha ilikuwa imekaribia. Sawa alisema wiki na nini, lakini nilitaka tu iwepo njia ya kuharakisha haya yote ili hatimaye niwe na uhuru uliotosha kufanya jambo fulani ambalo moyo wangu ulitamani sana kufanya. Kumsemesha Miryam.

Maneno ya Ankia huo usiku kwa kweli yalikuwa yanazunguka mno kichwani. Kwa kiasi kikubwa nilikuwa nataka sana kujaribu kumfikishia Miryam hisia zangu, sema tu niliona muda kuwa haufai, na yeye vilevile angeweza kuukataa upendo wangu. Kama hilo la pili lingetokea, ningetakiwa kuwa nimeshaona mwelekeo kabla hata ya kujaribu kumwambia nampenda, kwa hiyo nilihitaji kuwa na uhakika KWANZA. Hivyo yaani.

Kwa kuwa Bertha alinitaka niwahi, nikaona nipitie ile namba ngeni upesi kwanza; Bi Zawadi ningemwambia tu niliwahi mahali fulani maana kama siyo kuongea nami kuhusiana na yaliyotokea usiku wa kuamkia sasa, basi huenda ilimhusu tu Mariam. Nilipoangalia ujumbe wa hiyo namba ngeni, nikakunja uso kiumakini kwa sababu haukunipendeza kabisa. Ulisomeka, 'Muda umekwisha JC. Nipe jibu haraka, mengine yafate.'

Moja kwa moja nikawa nimeelewa kwamba ujumbe huo ulitoka kwa Sudi, kama siyo Chalii Gonga. Uharaka wao wa kutaka jibu langu ulionyesha kwamba walipanga kutimiza hila zao kumwelekea Bertha upesi sana, na sijui ni kwa nini tu waliona umuhimu wa kunitaka mimi niwe kama mpiga muhuri wao, ama kuwapa ruhusa. Walikuwa wanajishaua, na inawezekana hata yule jamaa aliyenifatilia kule Kariakoo alikuwa mtu wao, kwa hiyo nikaamua kwamba kutokea hapa mpaka huko nitakapofika, bastola ingekihusu kiuno changu.

Hii ndiyo ingekuwa mara ya pili ambayo ningetembea na hiyo silaha, lakini ndiyo ingekuwa mara ya kwanza ambayo ningehisi uhitaji wa kuitumia. Lolote lile lingeweza kutokea, hasa kwa sababu sikutaka kuwajibu, na sikujibu ujumbe huo alioutuma. Nikaifuta na hiyo namba, kisha nikaanza kufanya maandalizi ya kuondoka huku nikihisi kichwa kimeanza kuachia kabisa shauri ya jambo hilo kunitatiza na kunipa umakini ulionifanya nihisi nguvu mpya.

★★

Kufikia mida ya saa nne nikawa nimeshaondoka hapo kwa Ankia baada ya kuvaa vizuri na kunywa supu na maji ya baridi aliyoleta mwanamke huyo. Niliondoka Adelina akiwa bado amelala, kwa hiyo nilimwambia Ankia ampe salamu yangu na tungewasiliana baadaye. Nikiwa nimeshapanda gari la kuelekea Makumbusho ndiyo nikapata nafasi ya kumpigia Bi Zawadi na kumsalimu.

Sikuwa nimekosea kuwa alitaka kunijulia hali baada ya yaliyotokea jana, nadhani Tesha akiwa amemwambia kwamba nilipigwa na virungu, kwa hiyo nikamtuliza kwa kusema nilikuwa sawa na tungeongea zaidi nikirejea. Alinijali kweli huyo mama. Lakini ningepaswa kufanya jambo fulani kuhusu maumivu ya mgongoni maana nilihisi yakiendelea kuongezeka kwa ndani kila dakika.

Toka nilipokuwa nimepanda daladala ya kuelekea Makumbusho, nilikuwa nimesimama, na watu kadhaa na nini walikuwa wakiniangalia kama nilivyozoea, lakini kulikuwepo na mwanamke mmoja aliyevutia sana kwa sura na mwonekano wake ambaye alisimama karibu nami zaidi kwa muda mrefu. Hata muda mwingine angepisha mtu mwingine akae kwenye nafasi zilizoachwa ili tu aendelee kusimama, nikiona wazi kuwa alipendezwa nami, lakini sikutaka tena majaribu mimi. Moyo wangu ulikuwa kwingine kabisa.

Dakika kadhaa zikakatika mpaka tulipofika maeneo ya Vunja Bei, Mkwajuni hapo, nami nikaanza kushuka. Huyo mwanamke akaanza kutembea pia nyuma yangu, ikionekana alitaka kushukia hapo, na mimi sikujali sana yaani, nilikuwa nimetangulia mbele tu, sema tulitazamwa mno utadhani tulikuwa pamoja. Nikiwa ndiyo nimeshuka tu na kusimama pembeni ya barabara, mwanamke huyo akaja karibu zaidi na nilipokuwa. Kwa kufikiri anataka kupita, nikampisha, lakini akanifata huku akinitazama moja kwa moja. Nikamwangalia pia.

Alikuwa mweupe, mrefu kiasi, akivaa gauni refu lenye kubana mwili wake lililokuwa na rangi ya blue, lililobana umbo lake lenye hips nene na kalio lililotokeza kwelikweli mpaka kulichoreshea gauni lake mistari ya nguo aliyovaa ndani. Alionekana kutovaa sidiria, kwa kuwa matiti yake yasiyo makubwa sana yalichoresha vizuri chukuchuku zake hapo kifuani, na alisuka mtindo wa rasta za kahawia ndefu sana kufikia mpaka kwenye kalio lake. Alikuwa na sura na mdomo mzuri, macho makubwa yaliyorembwa kwa wanja kopeni, na alishika kimkoba kidogo kiganjani mwake.

Mrembo akasema, "Mambo kaka?"

Alikuwa na sauti ya kipole.

Nikamwambia, "Fresh. Niaje?"

"Poa tu. Samahani, nilikuwa naomba kuongea nawe..." akaongea kwa njia ya kawaida.

"Ah, usijali, toa hiyo samahani. Nambie..." nikamwambia hivyo.

"Wewe ni mwenyeji wa haya maeneo?" akaniuliza.

"Hapana. Me ni mgeni huku," nikamdanganya.

"Umekuja kutembea?"

"Yeah, kuna sehemu nimealikwa. Ndiyo nawahi sasa hivi..."

"Ahaa, sawa... basi, kama una haraka naomba tuachiane mawasiliano," akasema hivyo.

"Kwa nini?"

Akabana midomo yake na kuangalia pembeni, akionekana kuwa na wasiwasi sijui, nami nikaelewa kuwa aliniogopa kidogo. Najua alichokuwa anakitaka, ila kujitoa akili ilikuwa lazima. Na bado nilikuwa nawaza kwamba huenda huyu angekuwa ametumwa hata na hao wakina Sudi, kwa hiyo nilihitaji kuwa mwangalifu. Na tulikuwa tunaangaliwa sana na baadhi ya watu eneo hilo.

"Unaitwa nani?" nikamuuliza mrembo.

Akaniangalia na kusema, "Pendo."

"Wewe ni mwenyeji wa huku?"

Akatikisa kichwa kukubali.

"Unasoma?"

"Me nesi," akajibu.

"Wapi?"

"Agha Khan," akajibu.

"Kumbe? Okay. Sa' Pendo, kwa nini unataka kuwasiliana na mimi?"

"Kuna kitu nataka nikwambie..."

"Niambie sasa hivi."

"Ni vitu vingi. Si umesema una haraka?"

"We' sema."

"Eh... aheh... mpaka niseme jamani... we' si ni mtu mzima?"

"Ahah... sawa. Ila hatujuani, unaweza ukawa mke wa mtu," nikamwambia.

"Me sijaolewa mbona," akasema hivyo.

"Kwa hiyo umenielewa eh?"

Akatabasamu kwa haya na kuangalia chini.

Nikasema, "Okay. Nimekuelewa. Ila Pendo, me ni mume wa mtu. Na ninampenda huyo mtu. Sidhani kama nitaweza kukupa unachotaka."

"Kwani ni lazima mke wako ajue?"

"Kumbe na we' wa hivyo? Nilikuona mpole, nikadhani utaelewa," nikamwambia.

"Mhm... haya. Kwa hiyo hujanipenda?" akaniuliza hivyo.

"We' mzuri. Ila me wa mtu. Siwezi kumdanganya mwenzangu, hata wewe itafika mahala tutadanganyana mno nikifanya hilo. Siyo wa hivyo mimi," nikamwambia hivyo.

"Ahaa... basi. Safari njema," kakasema hivyo bila kuniangalia.

"Na we' pia," nikamjibu.

"Poa," akasema hivyo.

Huyoo akaendelea na mwendo kuelekea upande mwingine, nami nikajiondokea hapo kama vile siyo mimi. Yaani huyo angekuwa amenikuta kipindi kile! Ningemwonyesha ushetani wangu maana alikuwa wa moto, siyo mchezo. Ila sasa hivi nilitaka kutulia tu mpaka suala langu kwa Miryam lieleweke kabisa, la Bertha limalizike pia, ndiyo ningejua nisimame wapi baada ya hapo.

Nikiwa naelekea Royal Village sasa, nikampigia simu madam Bertha kumwambia ndiyo nilikuwa nimeingia getini na ningefika huko juu upesi, na alipopokea, kabla hata sijaongea akaniambia nielekee kule nyuma alikopenda kuegeshea gari lake halafu nimsubiri hapo; maana ndiyo alikuwa anashuka. Ilikuwa kama vile anajua nimeshafika yaani, nami nikasema tu sawa, ninaelekea huko, ndiyo nikaanza kuelekea huko kweli.

Nikiwa ndiyo nimefika huko kwenye egesho la magari, nikaona kitu kilichofanya niingiwe na umakini zaidi. Ilikuwa ni Dotto, akiwa amesimama usawa wa magari mawili; moja ikiwa ni lile la madam Bertha la Harrier, na lingine likiwa la aina ya Lexus LX570, kubwa na zuri, likiwa na mwonekano mpya wa rangi ya shaba (silver) iliyoelekea kuwa dhahabu kabisa.
Lexus.jpg


Alisimama karibu nalo hilo kama vile lilikuwa lake ama labda yeye ndiye aliyekuwa dereva wake, nami nikamwangalia kwa umakini zaidi.

Alikuwa amevalia T-shirt nyeusi ya mikono mirefu, iliyobana mwili wake vizuri kuonyesha namna misuli yake iliyokuwa imara, pamoja na suruali nyeusi pia na kiatu cheusi. Akawa ametazama upande wangu na kuniona, naye akaacha kuniangalia na kutazama pembeni kama vile hanijali. Kuna kitu tu kikanisukuma nimfate mpaka hapo alipokuwa na kusimama mbele yake, nikiwa nahisi hata uwezekano wa kutoa bastola hapo hapo ungetokea, lakini sikutaka ifike huko. Yeye akanitazama usoni kwa umakini.

"Imekuwa hivi tokea lini?" nikamuuliza hivyo.

Akaniangalia kwa njia ya kuonyesha kwamba hakuelewa nilichomaanisha, lakini najua alinielewa vizuri.

"Oh, hujaelewa? Okay, let me rephrase that. Umeanza kumfanyia usaliti madam tokea lini?" nikamuuliza tena.

"Usaliti? Usaliti gani?" akajitoa akili kabisa na kuniuliza hivyo.

"Naongelea usaliti ambao hadi ukafanya utamke maneno 'tutamuua' with such ease..."

"Ah, ongea kiswahili dogo, wengine hatukwenda shule..."

"Mbona 'game on' uliweza kuisema?" nikamuuliza hivyo kwa kuudhika.

Akacheka kidogo na kuifuta-futa pua yake kwa kidole, halafu akaniambia, "Ukijua nini kimeanza lini, itasaidia nini? We' si uangalie kile ambacho kipo sasa hivi, hayo mengine yatakupa faida gani?"

"Ah, nashangaa tu yaani, ghafla tu... goon namba moja wa madam kamgeuka, akiwa pamoja na mume wake wanapanga kumuua. Sishawishiki kirahisi na bullshit yote eti kisa Chalii ni kaka yako... mbona kipindi hicho chote ulikuwa umetulia tu? Eh? Tena ukifanya bidding zake madam... zote? Nini kime-change ghafla? Sudi amekuahidi mengi mazuri zaidi ya unayopata kutoka kwa madam, au?" nikamuuliza hivyo.

"Hayo hayakuhusu. Jiangalie wewe. Umepewa muda kutoa jibu, utumie vizuri," akaniambia hivyo.

"Sihitaji kujibu chochote. Mngekuwa mmeniambia labda mnataka kumwibia sijui... labda ningekubali. Yote ya kumuua ya nini? Halafu eti mnafikiri nitaogopa kumwambia kwa kusema sijui ataniua kwa sababu anakuamini zaidi wewe..."

"Mbona bado hujamwambia sasa? Mwambie. Si anakuja hapa hata sasa hivi... mwambie tu," Dotto akaongea kwa kutojali.

Nikabaki nikimtazama usoni kwa umakini.

Akanisogelea karibu zaidi na kusema, "Fanya uamuzi dogo. We' si una akili sana? Kila kitu kipo juu yako. Wala usiwaze kuhusu mimi."

Baada ya Dotto kusema maneno hayo, sote tukabaki kutazamana machoni umakini sana, akinionyeshea ubabe wake, na mimi nikimwonyeshea ujasiri wangu. Kutokana na hali kuwa nzito hapo hatukutambua upesi kwamba kuna mtu alikuwa akija upande wetu mpaka sauti yake iliposikika akisema...

"Hey..."

Nikatazama pembeni na kumwona madam Bertha akiwa anakuja upande wetu. Dotto akasogea nyuma kidogo huku naye pia akimwangalia madam, na kama kawaida yake alikuwa amependeza sana.

Alivalia nguo laini sana ya moja kwa moja mpaka miguuni, ikiwa ya suruali, na iliyokuwa na rangi kama ya ngozi ya mtu anayeelekea kuwa mweupe. Kwa kuwa ilimbana, yaani ilionekana kama vile ni ngozi yake kabisa, kwa hiyo kwa kumtazama vibaya ungedhani alikuwa uchi. Mabuti marefu ya kike ya kuchuchumia ya rangi ya maziwa yalimrefusha zaidi, na nywele zake nyekundu za kusuka alikuwa ameziachia kama namna ile ile nilipomwona majuzi. Mikononi aliweka mkoba mweusi pamoja na koti zito la nanyonya lenye rangi ya maziwa, na aliyaficha macho yake kwa miwani nyeusi ya urembo.

Akiwa anatembea kwa mwendo kama wa miss, akatukaribia zaidi na kuuliza, "Kuna nini hapa? Mbona kama mnataka kupigana?"

Nikamtazama Dotto usoni, yeye pia akinitazama kwa utulivu, nami nikamwambia Bertha, "Hamna kitu. Tulikuwa tu tunasalimiana."

Bertha akamwangalia Dotto.

Jamaa akasema, "Umependeza madam..."

"Shut up! Shika... tangulia kwenye gari," Bertha akamwambia hivyo.

Alikuwa akimkabidhi koti na mkoba wake, na jamaa akavipokea na kuniangalia kwa jicho la chini lenye hila. Nikaendelea kumtazama tu mpaka alipoanza kuondoka kwa kudunda na kuviingiza vitu vya Bertha kwenye lile gari la Lexus, ndiyo na yeye akaingia humo. Nikamtazama madam usoni, naye akaitoa miwani yake na kunisogelea zaidi huku akitabasamu kwa njia yenye kuonyesha madaha.

Sikutarajia anipe hilo upesi, kwa hiyo nikiwa makini tu nikamuuliza, "Umenunua gari jipya?"

Akatikisa nyusi kukubali.

"Zuri. Hongera," nikamwambia hivyo.

"Sifa ziende kwako," akasema hivyo huku akinishika mkono.

Nikatulia kidogo nikitafakari kitu, kisha nikamuuliza, "Kila kitu kiko poa madam?"

Akapitisha mikono yake kiunoni kwangu na kuuegemia mwili wangu huku akinitazama kwa hisia, naye akasema, "Kwa nini kila kitu kisiwe poa?"

Nikajitahidi kuupa mwili wangu wepesi ili asinikandamize sana kiunoni na kuihisi bastola, nami nikamshika shingoni na kumwambia, "Mara ya mwisho nimekuja, tuliishia sehemu siyo nzuri sana, nikafikiri labda...."

"Ah, achana na hayo. Nilikuelewa. Na sasa hivi tuta-focus kwenye mimi na wewe tu... mengine pembeni."

Nikakunja uso kimaswali kiasi, kwa sababu sikutarajia angekuwa ameliachilia lile suala kiurahisi namna hiyo, lakini wala hakuonekana kama ameliweka moyoni kabisa. Tena akakishika kidevu changu kwa makucha yake na kujing'ata mdomo wake wa chini huku akiuelekea wa kwangu, halafu akanipiga busu moja laini na kunifuta-futa lipstick iliyobaki kwa kidole chake kimoja.

"Umekunywa pombe asubuhi-asubuhi?" akaniuliza hivyo.

"Jana. Nilikunywa kidogo wakati wa game la Simba," nikamwambia.

"Haikuwa kidogo, bado harufu ipo japo umesugua ulimi. Pole... inaonekana ni machungu ya Simba kubondwa ndo' yalikufanya ukalewa wewe..." akasema hivyo na kucheka kidogo.

Nikatabasamu kwa kutoamini kabisa huu wonyesho wa upendo, au nia nzuri aliyokuwa ameanza kuijenga kwangu, nami nikamuuliza "Mood nzuri namna hii unaitoa wapi wakati nilikuwa nimeku-diss?"

"Lini umeni-diss?"

"Si ile juzi?"

"Well... wewe ndiyo unaifanya day inakuwa nzuri. Ya juzi hata siyakumbuki maana umenifurahisha sana leo," akasema hivyo.

"Kwa kipi?"

"Kumkataa Pendo," akasema hivyo.

Nikamkazia macho kiasi, naye akatikisa nyusi kimchezo, ndiyo nikamuuliza, "Pendo? That was you?"

Akatikisa kichwa kukubali huku akitabasamu kiasi.

"Ahah... kwa hiyo, kumbe ulikuwa umemtuma huyo mwanamke anitongoze, ili..."

"Ili nione kama kichwa chako kiko kwenye game, na moyo wako uko kwangu. Ilikuwa ni test ndogo tu, ila kumkataa Pendo ni ishu kubwa. Huyo mwanamke huwa hakataliwi kirahisi hata na wazee wa upako na maaskofu," akaniambia hivyo.

"Ameanza kunifatilia tokea... tokea Mbagala? Yaani... ulikuwa umeshampanga asimame nami mpaka huku?"

"Me hayo siyajui. Karudisha taarifa kuwa umemkataa, that's what I wanted..."

"Utajuaje hilo kuwa kweli? Je kama nimemkubali na amekudanganya?"

"Nilikuwa nasikia maongezi yenu yote," akaniambia hivyo.

Nikanyanyua kidevu juu kiasi huku nikimwangalia kwa utambuzi, nami nikasema, "Alikuwa anachukua sauti..."

"Mm-hmm. Na kama ingetokea umemkubali, me na we' ndiyo ingekuwa bye bye... na tena una bahati yako. Ipo siku nitakushika kivingine," akajibu hivyo.

Nikatulia kidogo, kisha nikamuuliza, "Kwa nini Bertha? Mpaka ufanye hayo yote... why?"

Akasema, "Kwa sababu nataka uwe wangu peke yangu. Sasa hivi sitajali sijui nini, au nini... JC, nataka uwe WANGU PEKE YANGU. Sahau ishu ya me kutaka mtoto, tutauangalia huo mpango baadaye. Sasa hivi nataka kichwa chako kiwe sehemu moja, na moyo wako hapa tu. La sivyo, mimi na wewe kuachana inamaanisha itakuwa vibaya. Unaelewa jinsi navyokuwa nikipenda kitu sana, si ndiyo?"

Hmm! Hili lingekuwa tatizo haswa, ila ni ikiwa tu nisingekuwa mwangalifu. Nikatikisa kichwa tu kuonyesha uelewa.

"Good. Umepita kamtihani kangu. Ngoja tuendelee kuona ya mbele," akasema hivyo.

Nikawa nikimtazama kwa ufikirio sana, nami nikasema, "Bertha... popote pale ambapo me na wewe tutaishia, ninaomba ujue tu kwamba sehemu kubwa ya moyo wangu haitaki kuona unaumia. Hatujaanza vizuri... na... sijui kama tutaishia pazuri, lakini...."

"Shhh..." akaninyamazisha kwa kuweka kidole chake kimoja mdomoni kwangu.

Nikatulia tu.

"Usiwaze negative. Sasa hivi nataka kuhakikisha kila kitu changu na wewe kinajengeka kwa njia positive, tena kuanzia leo leo. Na nitafanikiwa. Utaona tu," akaniambia hivyo kwa uhakika.

Nikashusha macho yangu chini, nikiwa najihisi vibaya kiasi moyoni. Maneno niliyokuwa nataka kumwambia yalikuwa yamebeba maana pana sana, hakujua tu.

Akatoa kidole chake mdomoni kwangu na kusema, "Twend'zetu. Kuna watu muhimu nataka tukakutane nao."

Nikamwangalia na kutikisa kichwa kukubali, naye akanishika mkono na kuanza kuniongoza mpaka tulipoingia kwenye Lexus yake na kuketi siti za nyuma, kisha Dotto akaliwasha na kuanza kuendesha.

Bado tu nikawa nawaza vitu vingi sana, mara kwa mara nikitazamana na Dotto kupitia kile kioo cha mbele pale juu kwa macho yaliyojuana mno, na maswali ya ni wapi haya yote yangekuja kuishia yakaendelea kuisumbua nafsi yangu hasa baada ya Bertha kuonyesha kwamba ni kweli alikuwa ananipenda. Kama tu maneno ya Dotto muda mfupi nyuma, kwa kweli ningetakiwa kufanya uamuzi haraka ikiwa Ramadhan na wenzake wangekawia kuyamaliza haya.

★★

Kulikuwa na mkutano fulani maalumu huko Kinondoni ambao ulibeba matembezi ya wafanyabiashara na viongozi fulani wa juu serikalini, na Bertha alikuwa na lengo la kwenda kumzuzua mfanyabiashara mmoja mkubwa sana awekeze kwenye ishu yake Bertha ambayo bado sikufahamu ni nini. Yaani kuna kitu Bertha alikuwa ameanza kujenga, bila mimi kujua, ila nafikiri kilikuwa pembeni ya ishu zao za madawa ingawa angekijenga kwa kutegemea nguvu ya biashara yake ya madawa.

Sijui alikuwa anataka kufungua kampuni labda? Na ndiyo alitaka kuwa na mtu kama huyo mfanyabiashara mkubwa wa kusaidia kulikuza jambo hilo upesi na kwa njia isiyo haramu, kwa hiyo hii ndiyo ikawa "mission" yetu ya leo. Asingekwenda huko supermarket wala wapi, na alitaka niwe pamoja naye ili nimpe ushirika wangu kama "mpenzi" wake. Kwa hiyo tulipita kwenye duka moja kubwa la nguo, nami nikavalishwa suti na kiatu cheusi bila kupenda. Nilikuwa mwangalifu sana kuhakikisha hawatambui kwamba nilikuwa na bastola, na Bertha akiwa amependeza tayari, tukaelekea huko Kinondoni.

Zilikuwa ni hafla zenye kuboa sana. Tulisubiri kwa muda mrefu, ndani ya ukumbi kwenye jengo kubwa kweli, na ilinikera kutembea kwenye vigae vilivyoteleza na maviatu haya, kila dakika nilihisi ningeweza kuanguka. Lakini hatimaye madam akawa amepata nafasi yake kuongea na jamaa, akitumia ushawishi wake mzuri kwenye maneno na nguvu ya kuwa mwanamke ili kumzuzua kwelikweli jamaa, na jamaa akatoa kadi yake ya mawasiliano na kumuahidi kupanga makutano "binafsi" ili waongee biashara zaidi. Ikawa ni mwanzo mzuri kwa madam.

Kwa hiyo tumekuja kumalizana na hayo jioni kabisa, na baada ya hapo ndiyo tukaelekea sehemu nzuri pamoja na madam kupata msosi. Bertha alikuwa kwenye hali nzuri kihisia, alionyesha furaha yake waziwazi alipoongea, hata akawa ananilisha eti mbele za watu, na mimi nilijitahidi kufanya ionekane nafurahia sana muda huu pamoja naye, lakini kila nilipomwangalia huyo Dotto aliyekuwa amesimama "kibodigadi" huko pembeni, nilihisi hasira tu iliyonifanya nikose amani hata ya kunisaidia kuendelea kuigiza. Lakini ningefanyaje?

Bwana, tumekuja kurudi kwake Bertha saa tatu usiku baada ya mimi kuamua kupita kwenye gym fulani huko Morocco (ya Dar siyo Africa), ili ninyooshe viungo kidogo. Nilifanya hivi kutokana na maumivu niliyokuwa nayo, na Bertha alilazimisha kuja nami ili anitazame eti. Kulikuwa na wanaume vifutu siyo mchezo, waliomtazama madam na kuonyesha ngangali zao, lakini madam wangu alikuwa na mimi tu, hata akipiga makofi ya pongezi alipoona nimetandika push-up mia moja. Yaani mtu mwingine mpaka angehisi raha!

Kwa hiyo nilijisafishia huko huko baada ya tizi, na tulipofika kwake alikuwa ananitaka nilale naye, lakini nikamwambia hata mimi nilitamani sana kubaki hapo ila kwa leo isingewezekana, maana kuna ishu nilitaka kushughulikia huko Mbagala. Nikajitoa akili na kumpetipeti kwa maneno na miguso na nini, naye akalegeza. Alikuwa hadi ameanza kudeka, yaani hakuwa Bertha niliyemfahamu kabisa, dah!

Ila kuna nyakati nilikuwa namwangaliaaa, jinsi ambavyo hakuwa na dokezo lolote la mambo ya mbeleni yaani, lakini sikuwa na jinsi ila kubaki njia kuu mchezoni. Kuna vitu tu ningepaswa kuamua kuacha vitokee, na vingine ningejitahidi kuvizuia visitokee, lakini kwa kweli kuna sehemu zilizokuwa mpaka zinanifanya nihisi kujuta, basi tu, sikuwa na namna tena. Mchezo ungepaswa kuendelea. Kwa hiyo alipokubali kuniachia, nikaondoka hapo upesi sana ili kurudi Mbagala, madam akiwa pia amenikabidhi suti na viatu vipya viwe vyangu kimoja, huyooo nikatembea.

Alikuwa amenipa ofa ya kusindikizwa na Dotto mpaka nyumbani kwa kutumia gari lake, lakini nikaikataa kistaarabu tu. Jamaa asingeweza kumgusa madam hata kama wangeachwa peke yao kwa sababu najua alikuwa akifuata mipango ya Sudi, kwa hiyo na mimi ningeendelea kukausha tu kwa wakati huu mpaka nikiona wazi kwamba hatua waliyotaka kuchukua dhidi ya madam ingechukuliwa. Nikachukua tu usafiri wa umma, nikiwa kwenye umakini wangu kama ilivyotakiwa kwa wakati huu.

★★

Nimekuja kuifikia Mzinga ikiwa imeshaingia saa sita usiku, kama kawaida, usafiri na changamoto zake. Zamu hii hakukuwa na majangili ama akina Pendo walioagizwa kunifatilia, na nilihakikisha bastola ipo mahala pake ili timbwili lolote likizuka basi nitimbwilishane nalo ipasavyo. Mpaka nafika kwa Ankia sikuchokozwa na yeyote yule, walioniona wakiniangalia tu kama vile hawanijui, ila walishawahi kunisikia.

Nilikuwa nimeshamtumia ujumbe Ankia kumjulisha niko njiani kuja huku, na katikati ya safari hiyo nilikuwa nimewasiliana na Adelina pia. Mwanamke yule tayari alikuwa ameondoka kurudi kwao ile mchana, na nilimwomba radhi tu kutokana na kuwahi kuondoka asubuhi bila kuonana naye, lakini akasema haina shida, na alitarajia tungekuja kukutana tena panapo majaaliwa na mambo kwenda vyema zaidi ya jana. Na hiyo jana aisee! Basi tu, ningepaswa kuisahau baada ya muda.

Ile ndiyo nimefika getini kwa Ankia, kama kawaida nikatazama upande wa jirani zetu, na ikiwa kama bahati tu, nikamwona bibie Miryam akiwa amekaa hapo nje; varandani kwake. Kwa kuwa kutembea kwangu kulifanya sauti za hatua zisikike kutoka chini, nikamwona akinyanyua uso wake na kutazama upande wangu, na kwa sekunde chache tukabaki kuangaliana tu bila wonyesho wa hisia yoyote.

Lakini kiukweli mimi bado nilikuwa nikiteseka sana rohoni, hasa tu baada ya kumwona namna hiyo ghafla kukafanya moyo wangu upige ngoma yenye mdundo mzito sana kifuani utadhani nilikuwa nimemwibia kitu. Ila ni yeye ndiye ambaye alikuwa ameiba moyo wangu, na sijui kama angeweza kutambua hilo, yaani ingenibidi tu niache kuwa kama kuku aisee. Nilimwelewa mno, na nilitaka ifike siku ajue hilo japo sikuwa na uhakika kama angelipenda.

Baada ya kuendelea kumwangalia tu kupitia matundu ya ukuta wa uzio, nikanyanyua kiganja changu na kukitikisa kama kumpa salamu, naye akanyanyua chake na kunipa ishara ya "njoo." Ah! Nikageuka fasta, yaani hakukuwa na ubishi wala uchovu tena hapo, malkia aliniita kwa nini nijizungushe? Nikaenda kufungua geti lao na kumfata hapo ubarazani.

Kama kawaida, alivalia kinguo chake cha kulalia huku akijifunika kwa kikoti chepesi cha nguo hiyo, na nywele zake alizosuka zilikuwa zimefichwa kwa kikofia laini cha kusitiri nywele chenye rangi zambarau. Alikaa kitini akiniangalia kwa utulivu, simu ikiwa mkononi, na pia kulikuwa na kiti kingine pembeni yake ambacho hakikuwa na mtu. Hebu ngoja kwanza. Nilikuwa nimewekewa mimi, ama? Alikuwa ananisubiri? Hapana, ilikuwa bado mapema mno kuwaza hivyo, ila hako kawazo kalisisimua!

Nikajisogeza tu hapo, yeye akiwa ananitazama kwa utulivu usoni, nami nikamwambia, "Uko poa?"

Akatikisa kichwa kukubali na kuendelea kunitazama.

"Mbona umekaa kwenye baridi?" nikawauliza.

Akapandisha mabega kiasi huku akifumba na kufumbua macho yake, kama kusema basi tu amependa.

Nikatabasamu kiasi na kusema, "Wengine watakuwa wameshalala, eh?"

"Yeah, wako vyumbani..."

"Mbona kama haukuwa peke yako hapa?"

"Nilikuwa nimekaa na Tesha. Ndiyo ameingia ndani muda siyo mrefu kuongea na simu, atakuwa ni demu wake," akasema hivyo.

Akanifanya nicheke ghafla kwa sababu ya kutotarajia aseme hivyo.

"Nini?" akaniuliza.

"Hamna. Sikuwahi tu kufikiri na wewe unasemaga maneno kama 'demu,'" nikamwambia.

"Si ndiyo lugha mnayopenda? Nitafanyaje sasa?" akaniuliza hivyo.

"Ni neno la kawaida. Sema tu watu wameshazoea kulitumia kihuni mno," nikamwambia.

"Mhm... kaa basi unipe company kidogo. Au ume...."

Nikakatisha maneno yake kwa kukaa kitini upesi, naye akatabasamu kiasi.

"Inaonekana umetokea pazuri," akasema hivyo.

"Kwa nini?" nikamuuliza.

"Uko na mood nzuri sana," akasema.

"Ah, hamna. Kawaida mbona?"

"Eti eh?"

"Yeah. Hata nikiwa na stress, mood yangu huwa iko juu tu. Hiyo inasaidia stress zinaondoka zenyewe," nikamwambia.

"Naona una balance nzuri kwenye kupunguza stress, ila mtu akikuudhi humwachi salama," akaniambia hivyo.

"Ahahahah... najua unajua. Sipendi wachokozi," nikamwambia hivyo pia.

Sote tukacheka kidogo maana tulikuwa tunakomea njiani kufika kule ambako upana wa maneno yetu ulikuwa unaelekea.

Akauliza, "Ni sawa. Ila ni hasa ulipokuja huku Mbagala, ama ni kutokea zamani ulikuwa hivyo?"

"Nimekuwa hivyo tokea muda. Kama ni kitu ambacho sipendi zaidi maishani... ni uonevu. Mengine tutavumiliana ila... hata wakati nipo shule, yaani mwalimu tu akimwonea mwanafunzi mwenzangu, ama wanafunzi wenzangu kuoneana, nilikuwa najisikia vibaya sana. Nisingeweza kuzuia yote, lakini kila ilipokuja kwangu..."

"Ungewaka!"

"Wee! Hakuna aliyekuwa ananisogelea," nikajitutumua eti.

"Na bila shaka kwenye masomo ulikuwa mkali pia," akaniambia hivyo.

"Yeah, toka nimeanza shule mpaka nimemaliza. Nilijitahidi sana nisianguke hata mara moja," nikamwambia.

"Hukuwahi kurudia darasa hata moja?" akauliza.

Nikatikisa kichwa kukubali.

"Mambo kwako yalikuwa easy eh?" akauliza.

Nilianza kuona kwamba Miryam alitaka kunielewa zaidi, kwa hiyo nafasi hii ningeitumia vizuri.

Nikamwambia, "Siyo sana. Mungu alinipa tu ubongo mzuri, lakini bidii ilihitajika ili ufanye kazi vizuri. Nilikuwa napenda sana kusoma, na hali za kimaisha hazikuwa rahisi sana wakati nakua, ila... angalau nilifanikiwa kutoka vizuri shuleni," nikamwambia.

"Ulimaliza shule una miaka mingapi?"

"Form four nimemaliza nina miaka 16," nikamwambia hivyo.

"Eh, mdogo!" akasema hivyo huku akitabasamu.

"Ahah... nilianza shule mdogo, na sikurudiaga, kwa hiyo nikamaliza mdogo," nikasema hivyo.

"Baada ya form four?"

"Nikaenda advance, nilichaguliwa kwenye shule moja huku nzuri, nilipata alama nzuri necta. Yeah... kwa hiyo, nikasoma hiyo miaka miwili, nikafaulu vizuri tena, moja kwa moja UDSM..."

"Wow... udaktari..."

"Ndiyo. Nikapiga miaka mitano, na ndani ya hiyo miaka tayari nilikuwa nimeshaanza kupelekwa sehemu hizi au zile kusaidia na kazi... mahospitalini kabisa, kwa hiyo nikawa naona mambo mengi yaliyonisaidia niwe na experience zaidi. Lilipokuja suala la masomo, yaani sikutakaga kuwa mtu wa kuanguka kabisa, sometimes hata nilikuwa napewa chaki niwaelekeze wanafunzi wenzangu maana mpaka walimu walielewa nilikuwa genius..."

"Wacha we!"

"Ahahahah... usipime. Nimetoka chuo nimeiva, nikaenda kufanya internship Bugando, kule Mwanza, halafu...." nikajikuta nimeishia hapo baada ya kukumbukia kitu fulani cha zamani.

Miryam akasema, "Halafu..."

Nikamwangalia na kusema, "Yeah, halafu... ilikuwa kwa mwaka mmoja, ndiyo... nikaja sasa Muhimbili."

"Ni Muhimbili ya Mloganzila, au hiyo ya hapo?"

"Kotekote, ila sanasana hii ya huku. Nilikuwa wa kitengo fulani maalumu, na sikuwa daktari mmoja tu kwenye hicho... kwa hiyo ni kama tuseme zamu zinakuwa zinabadilishwa, lakini baada ya muda nikawa nakaa hii Muhimbili ya huku Kariakoo zaidi..."

"Sawa."

"Yeah. Ndiyo hivyo."

"Na hiyo ni... umekaa kwa muda gani yaani?"

"Miaka kama mitatu," nikamwambia.

"Mh? Miaka mitatu?" akaonekana kushaangaa.

"Ee. Michache?"

"Ahah... me nikafikiri labda hata kumi! Asa' unahitaji likizo ya nini, ni kwamba hupendi wagonjwa ama uvivu tu?" akauliza hivyo.

Nikacheka kidogo, kisha nikamwambia, "Kiukweli, sikuwa mtu wa kupumzika sana tokea nimemaliza chuo, mpaka kuingia kazini, mambo yalikuwa mengi. Sometimes nilikuwa silali, unakuta nakaa macho hata saa za kazi zikiisha me nabaki kuangalia mahitaji ya wagonjwa..."

"Hiyo si ni kazi ya wauguzi?"

"Yes, ila siyo wote. Kuna hizi scenario unakuta... wanakuwepo tu kwa ajili ya wagonjwa kuwaangalia, na hata kama madaktari wengine wanakuwa wameshughulika na wagonjwa wao, me napenda tu pia kuwafanyia double checking ili kuhakikisha kwamba wanaendelea kuwa sawa," nikamwambia hivyo.

"Si... sijui kama nimeelewa vizuri..." akasema hivyo.

"Iliwahi kutokea... kuna mgonjwa ambaye alikuwa hospitalini amelazwa baada ya msaada wa madaktari, akawa amepoteza maisha baada ya wao kufikiri msaada wanaotoa unatosha. Na inatokea mara nyingi. Najua kazi zinakuwa rundo, ila... me nilishagaona ni muhimu tu kuhakikisha. Naongelea wagonjwa ambao unakuta wanakuwa wamelazwa, na hali zao ni..."

"Ndiyo, ndiyo, naelewa," akanihakikishia.

"Yeah, ndiyo hivyo. Huwa tu sijisikii vizuri mgonjwa akipoteza uhai wakati yuko hapo hapo hospitali. Kuna vingine haviwezi kuzuilika, ila me nikiwepo... nakuwa nataka kuhakikisha usalama unachekiwa mara mbili zaidi ya ile wanayoona inatosha. Kwa hiyo, nilikuwa mtu wa kutaka kusaidia kila mtu... hata kama nisingeweza kuwasaidia wote... popote ambapo ningeweza, hapo hapo. Mpaka ikawa inazidi. Nikachoka kiasi, ndiyo maana nikapewa haka kalikizo," nikamwambia hivyo.

"Kumbe haukuiomba?" akauliza.

"Hamna. Nilipewa kama break, ili nikirudi niwe kwenye game vizuri hata zaidi kupiga miaka mingine vyema," nikamwambia hivyo.

Akatabasamu kiasi na kuniambia, "Ndiyo maana ukamsaidia na Mariam."

Nikatabasamu kiasi.

"Unapenda kusaidia sana watu. Mpaka unajiingiza kwenye vitu hatari sana ili tu uwasaidie wengine," akasema hivyo.

Nikatabasamu zaidi na kusema, "Eeh."

Lakini nilipomwangalia, nikakuta akinitazama kwa hisia makini zaidi usoni, kama vile alikuwa akinitafakari sanaaa, nami nikajikuta nafifisha tabasamu langu na kubaki nimemtazama usoni kwa umakini pia. Akaacha kuniangalia na kushusha pumzi taratibu, na kiukweli hapo niliweza kuona kwamba alikuwa amezama ndani ya fikira fulani kunielekea, na kuwaza ingekuwa ni fikira gani, kulisisimua sana akili yangu.

Nikamwambia, "Ona... Miryam... kuhusu ile jana..."

"It's okay, Jayden. Tuyasahau tu ya jana, sawa? Tusonge mbele," akaniambia hivyo kwa upole.

Nikatabasamu kiasi na kumwambia, "Sawa. Unajisikiaje lakini? Mgongo I mean..."

"Oh, niko sawa kabisa. Ule mkanda ulipiga zaidi nguo ya ndani, na ilikuwa ngumu, kwa hiyo sijaumia sana..."

"Hata kutia alama?"

"Hapana. Niko poa," akanihakikishia.

Nikatikisa kichwa kuonyesha uelewa.

"Na wewe? Vipi mgongo?" akauliza.

"Yeah, nimeamka unauma-uma, ila sa'hivi umeachia. Leo imenibidi niingie gym tena," nikamwambia hivyo.

"Ili uongeze maumivu kufanya yaliyokuwepo yapungue?" akauliza.

"Yep. Na kesho nitaamka yamenikaza zaidi, kwa hiyo sitapaswa kuacha," nikamwambia hivyo.

Akatikisa kichwa taratibu na kusema, "Pole lakini."

"Usijali. Halafu... nimewaza kitu..." nikamwambia.

"Mm-hmm..." akatega sikio.

"Vipi tukiwatoa... familia... out ya pamoja yaani, watembee..." nikamwambia hivyo.

"Mh! Wapi?" akauliza pia huku akitabasamu.

"Popote. Iwe sehemu nzuri, halafu iwape kale ka-sense ka ugeni yaani..."

"Yaani iwe kama lunch au dinner hivi?"

"Eeeh. Ila ukisema lunch... ndo' inafaa. Vipi tukiwatoa wote, Mamu, warembo wangu, Tesha, Ankia... twende tukapige kisinia?" nikamuuliza hivyo kwa uchangamfu.

"Ahahah... kisinia! Nina muda sijafanya hiyo kitu..." akasema hivyo.

"Itakuwa poa sana. Najua Mamu atafurahia sana..."

"Na bado hujamsema Tesha..."

"Ahahahah... tufanye hivyo. Tena mapema yaani, iwe kama tunaamshia-amshia na birthday ya cheupe wangu," nikamwambia.

"Ni sawa. Sema, nilikuwa sijajiandaa, kwa hiyo..."

"Usijali Miryam. Zamu hii itakuwa my treat," nikamwambia hivyo.

"Mm? Wewe mwenyewe?" akauliza.

"Mmm. Na tena ikiwa utaona inafaa... kesho," nikamwambia hivyo kwa uhakika.

"Jayden..."

"Usijali Miryam, everithingi niachie mimi, wewe ni kuja tu. Kila kitu kitakuwepo tayari," nikamwambia hivyo.

"Ahah... ni wazo zuri, sema unapeleka mambo fast mno Jayden..." akasema hivyo.

"Mjini kuchangamka Miryam, hujui?"

Akatabasamu na kuangalia pembeni.

"Come on, ni idea nzuri, we' mwenyewe umesema. Tena nimeshafikiria mahala pazuri pa kulia kisinia kesho. Kubali tu," nikamshawishi.

"Wapi?" akauliza.

"Huko kwetu Sinza," nikamwambia.

"Wewe!" akaonekana kushangaa kidogo.

"Eeh, nakwambia ni pazuri kweli. Familia yako itafurahi sa...."

"Jayden, kuwapeleka huko akina mama, me naona ni mbali. Halafu kesho ninaenda kazini. Bora kama ingekuwa...."

"Siyo siku ya kazi, najua utasema hivyo, lakini hiyo wala siyo shida. Wewe nenda dukani, fanya kazi, ukimaliza unamwacha tu Soraya halafu unakuja. Utatukuta. Mimi ndiyo nitawaongoza hawa wote, tutapanda daladala, halafu tukifika huko nakutumia address kabisa ili uje mwenyewe kwa raha zako..." nikamwambia hivyo kwa ushawishi zaidi.

Akacheka kidogo kwa pumzi na kutikisa kichwa chake.

"Eeh, fanya hivyo. Angalau kesho wote watakuwa na mengi ya kuona... na najua wakifurahia, hata wewe utafurahia pia. Unastahili hilo," nikamwambia hivyo kwa sauti tulivu.

Akaniangalia machoni kwa utulivu tu, mimi nikimpa tabasamu hafifu, naye akasema, "Sawa basi... nitawaambia. Na uhakikishe kila kitu una-handle vizuri..."

Nikanyoosha kiganja kimoja juu na kingine nikiweka moyoni, nami nikasema, "I cross my die, and hope to heart. Kila kitu kitakuwa sawa."

Akacheka kidogo na kusema, "We' ni shida Jayden..."

Akanifanya nicheke kidogo kwa furaha, ndiyo nikamwambia, "Asante Miryam. Hautajutia hii."

"Hapana, mimi ndiyo nikwambie asante Jayden. Unaleta vitu vingi vizuri kwenye familia yangu, na hauchoki yaani. Nathamini sana," akaniambia hivyo kwa sauti yake nyorororo.

Mpaka nikajihisi haya, ile ku-blush, na ndiyo hapa bibie akawa amesema ingefaa aelekee ndani ili autafute usingizi sasa. Basi, na mimi nikaona ninyanyuke, nikamsaidia kuingiza kiti ndani na kumuaga vizuri tena, kisha ndiyo nikaelekea kwa Ankia. Mwanamke tayari alikuwa ameingia kulala, kwa hiyo nikaamua kuelekea tu chumbani kwangu moja kwa moja.

Nilifika tu chumbani na kujitupia kitandani, nikijilaza chali huku mkono wangu nikiukunjia nyuma ya kichwa. Nikajikuta tu natabasamu mwenyewe kutokana na kuhisi raha sana. Yaani eti raha tu kukaa vile na Miryam hapo nje, kuongea kidogo, halafu sasa na vile alivyokuwa ananitazama. Dah! Tule tumawazo tulikuwa tunanifanya najihisi kama Cinderella yaani, ningeweza hata kung'ata kidole kimoja mdomoni kwa shau!

Ilikuwa wazi kwangu zaidi na zaidi kwamba nilimpenda sana huyu mwanamke, na ningetakiwa kufikiria wakati sahihi na njia nzuri ya kumweleza hisia zangu bila ya matatizo yoyote kutokea. Sikujua ikiwa angeweza kunichukulia serious, ila ningehakikisha anajua tu. Iwe isiwe. Nikaamua kujiondoa kwenye ulimwengu wangu wa ndoto za mapenzi ya kweli na kwenda kuoga kwanza, kisha nikarejea na kulala hatimaye. Mbu hao!





★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★


Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
MIMI NA MIMI 2

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Siri, Tamaa, Hila, Usaliti, Ukatili, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA TISA

★★★★★★★★★★★★★★


"JC... we' JC... amka..."

Nilikuwa nasikia sauti hiyo ikiniita, lakini sikutaka kuamka kabisa maana nilijihisi uzito wa ajabu. Ndipo nikashtukia nawashwa kofi mkononi lililofanya niumie kiasi, nami nikajitahidi kufumbua macho.

"Amka! Amka... pameshakucha."

Ilikuwa ni Ankia bwana.

Nikaangalia mazingira vizuri; ndiyo, bado nilikuwa kitandani, na kweli palikuwa pamekucha. Nikamuuliza, "Ndiyo nini na wewe kuamshana na makofi?"

"Uliniambia nikuamshe mapema, na nikupige ukizingua. Ahadi ni deni, imetimia," akasema hivyo.

Nilikuwa nahisi kichwa changu ni kizito kweli, nami nikiwa nimelala kwa ubavu, nikaendelea tu kufumba macho na kumwambia, "Umefanya vizuri, ila bado nina usingizi!"

"Kwani unataka kwenda wapi? Huko Sinza kwenu, au?"

Nikatikisa kichwa kukubali.

"Ndo' unyanyuke sasa. Me nataka nikatafute supu, ukisinzia tena shauri yako..."

"Saa ngapi?"

"Saa mbili," akajibu.

"Niletee basi maji ya baridi darling..." nikamwambia hivyo.

"Umeme umekatika... friji haijawaka."

"Kanunue basi. Unaenda kufata supu yako tu?"

"Eeeh, na Adelina. Ila ye' bado kalala. Unataka na we' nikuletee? Niongezee hela basi.." akasema hivyo.

"Kuna elfu tano hapo... juu ya droo. Kachukue supu ya elfu nne, na... maji ya baridii... ongezea, utaona," nikamsemesha huku bado nikiwa nimejisinzisha.

"Mhm... haya ngoja niwahi basi," akasema hivyo.

"Poa."

Nikahisi alipokuwa amenyanyuka kutoka kitandani na kuondoka, nami nikajivuta hivyo hivyo tu na kukaa. Matukio ya usiku uliotangulia yakajirudia wee akilini mwangu, huku nikihisi maumivu mgongoni kutokana na marungu niliyoshushiwa jana, nami nikaamua kuifata simu kutoka chajini. Ndiyo, niliiweka chaji kabla ya kulala.

Nikajitahidi kupambana na wenge la kichwani, nami nikaona kwamba kuna watu walikuwa wamenipigia, na jumbe chache kuingia. Bertha, Soraya, yule Kevin, namba fulani ngeni, pamoja na Bi Zawadi walikuwa wamenipigia kwa asubuhi hii, huku jumbe zikitumwa na Soraya pamoja na hiyo namba ngeni. Nikaona nianze na Bertha.

Nikampigia, na baada ya kupokea, akauliza nilikuwa wapi. Nikamwambia ndiyo nilikuwa najiandaa kwenda kule supermarket Ubungo, yaani sikuwa nimeondoka bado, naye akasema niende kwake kwanza. Kwa kuwa hii ilikuwa Jumatatu, yeye angefanya kawaida yake ya kwenda pale supermarket na sehemu zingine, na ndiyo ningemwonea huko, ila leo alitaka niende kwake kwanza. Bila kuuliza sababu, nikamwambia nakuja, naye akasema nisichelewe.

Wa pili akawa Soraya. Huyu nikamtumia tu ujumbe kuwa bado nilibanwa na kazi fulani, maana alikuwa anataka nimpe ratiba ya makutano, na aisee! Kutokea hapa sidhani kama ingekuwa rahisi tena kwa kweli. Yaani, nilikuwa nimetoka tu kukiri hata mbele ya Ankia kuwa nilimpenda Miryam, na kukumbuka hilo kila mara kukawa kunanifanya nitake kuwa mtu mpya ingawa bado hata sikuwa nimemfikishia mwanamke huyo hisia zangu, na nilikumbuka vizuri sana kwamba bado upande wa Bertha ungeendelea kunipa changamoto.

Yaani hako katabia ka kutoka na huyu na yule nilitaka na nilipaswa nikakomeshe kutokea hapa, na kwa kujua kwamba bado Bertha angekuwa kikwazo, nikaona nimtafute askari Ramadhan. Nikamtumia sms nikiuliza tu 'imefika wapi?' nikiwa na lengo la kutaka kujua kama siku yetu ya kuyamaliza hayo mambo ya Bertha ilikuwa imekaribia. Sawa alisema wiki na nini, lakini nilitaka tu iwepo njia ya kuharakisha haya yote ili hatimaye niwe na uhuru uliotosha kufanya jambo fulani ambalo moyo wangu ulitamani sana kufanya. Kumsemesha Miryam.

Maneno ya Ankia huo usiku kwa kweli yalikuwa yanazunguka mno kichwani. Kwa kiasi kikubwa nilikuwa nataka sana kujaribu kumfikishia Miryam hisia zangu, sema tu niliona muda kuwa haufai, na yeye vilevile angeweza kuukataa upendo wangu. Kama hilo la pili lingetokea, ningetakiwa kuwa nimeshaona mwelekeo kabla hata ya kujaribu kumwambia nampenda, kwa hiyo nilihitaji kuwa na uhakika KWANZA. Hivyo yaani.

Kwa kuwa Bertha alinitaka niwahi, nikaona nipitie ile namba ngeni upesi kwanza; Bi Zawadi ningemwambia tu niliwahi mahali fulani maana kama siyo kuongea nami kuhusiana na yaliyotokea usiku wa kuamkia sasa, basi huenda ilimhusu tu Mariam. Nilipoangalia ujumbe wa hiyo namba ngeni, nikakunja uso kiumakini kwa sababu haukunipendeza kabisa. Ulisomeka, 'Muda umekwisha JC. Nipe jibu haraka, mengine yafate.'

Moja kwa moja nikawa nimeelewa kwamba ujumbe huo ulitoka kwa Sudi, kama siyo Chalii Gonga. Uharaka wao wa kutaka jibu langu ulionyesha kwamba walipanga kutimiza hila zao kumwelekea Bertha upesi sana, na sijui ni kwa nini tu waliona umuhimu wa kunitaka mimi niwe kama mpiga muhuri wao, ama kuwapa ruhusa. Walikuwa wanajishaua, na inawezekana hata yule jamaa aliyenifatilia kule Kariakoo alikuwa mtu wao, kwa hiyo nikaamua kwamba kutokea hapa mpaka huko nitakapofika, bastola ingekihusu kiuno changu.

Hii ndiyo ingekuwa mara ya pili ambayo ningetembea na hiyo silaha, lakini ndiyo ingekuwa mara ya kwanza ambayo ningehisi uhitaji wa kuitumia. Lolote lile lingeweza kutokea, hasa kwa sababu sikutaka kuwajibu, na sikujibu ujumbe huo alioutuma. Nikaifuta na hiyo namba, kisha nikaanza kufanya maandalizi ya kuondoka huku nikihisi kichwa kimeanza kuachia kabisa shauri ya jambo hilo kunitatiza na kunipa umakini ulionifanya nihisi nguvu mpya.

★★

Kufikia mida ya saa nne nikawa nimeshaondoka hapo kwa Ankia baada ya kuvaa vizuri na kunywa supu na maji ya baridi aliyoleta mwanamke huyo. Niliondoka Adelina akiwa bado amelala, kwa hiyo nilimwambia Ankia ampe salamu yangu na tungewasiliana baadaye. Nikiwa nimeshapanda gari la kuelekea Makumbusho ndiyo nikapata nafasi ya kumpigia Bi Zawadi na kumsalimu.

Sikuwa nimekosea kuwa alitaka kunijulia hali baada ya yaliyotokea jana, nadhani Tesha akiwa amemwambia kwamba nilipigwa na virungu, kwa hiyo nikamtuliza kwa kusema nilikuwa sawa na tungeongea zaidi nikirejea. Alinijali kweli huyo mama. Lakini ningepaswa kufanya jambo fulani kuhusu maumivu ya mgongoni maana nilihisi yakiendelea kuongezeka kwa ndani kila dakika.

Toka nilipokuwa nimepanda daladala ya kuelekea Makumbusho, nilikuwa nimesimama, na watu kadhaa na nini walikuwa wakiniangalia kama nilivyozoea, lakini kulikuwepo na mwanamke mmoja aliyevutia sana kwa sura na mwonekano wake ambaye alisimama karibu nami zaidi kwa muda mrefu. Hata muda mwingine angepisha mtu mwingine akae kwenye nafasi zilizoachwa ili tu aendelee kusimama, nikiona wazi kuwa alipendezwa nami, lakini sikutaka tena majaribu mimi. Moyo wangu ulikuwa kwingine kabisa.

Dakika kadhaa zikakatika mpaka tulipofika maeneo ya Vunja Bei, Mkwajuni hapo, nami nikaanza kushuka. Huyo mwanamke akaanza kutembea pia nyuma yangu, ikionekana alitaka kushukia hapo, na mimi sikujali sana yaani, nilikuwa nimetangulia mbele tu, sema tulitazamwa mno utadhani tulikuwa pamoja. Nikiwa ndiyo nimeshuka tu na kusimama pembeni ya barabara, mwanamke huyo akaja karibu zaidi na nilipokuwa. Kwa kufikiri anataka kupita, nikampisha, lakini akanifata huku akinitazama moja kwa moja. Nikamwangalia pia.

Alikuwa mweupe, mrefu kiasi, akivaa gauni refu lenye kubana mwili wake lililokuwa na rangi ya blue, lililobana umbo lake lenye hips nene na kalio lililotokeza kwelikweli mpaka kulichoreshea gauni lake mistari ya nguo aliyovaa ndani. Alionekana kutovaa sidiria, kwa kuwa matiti yake yasiyo makubwa sana yalichoresha vizuri chukuchuku zake hapo kifuani, na alisuka mtindo wa rasta za kahawia ndefu sana kufikia mpaka kwenye kalio lake. Alikuwa na sura na mdomo mzuri, macho makubwa yaliyorembwa kwa wanja kopeni, na alishika kimkoba kidogo kiganjani mwake.

Mrembo akasema, "Mambo kaka?"

Alikuwa na sauti ya kipole.

Nikamwambia, "Fresh. Niaje?"

"Poa tu. Samahani, nilikuwa naomba kuongea nawe..." akaongea kwa njia ya kawaida.

"Ah, usijali, toa hiyo samahani. Nambie..." nikamwambia hivyo.

"Wewe ni mwenyeji wa haya maeneo?" akaniuliza.

"Hapana. Me ni mgeni huku," nikamdanganya.

"Umekuja kutembea?"

"Yeah, kuna sehemu nimealikwa. Ndiyo nawahi sasa hivi..."

"Ahaa, sawa... basi, kama una haraka naomba tuachiane mawasiliano," akasema hivyo.

"Kwa nini?"

Akabana midomo yake na kuangalia pembeni, akionekana kuwa na wasiwasi sijui, nami nikaelewa kuwa aliniogopa kidogo. Najua alichokuwa anakitaka, ila kujitoa akili ilikuwa lazima. Na bado nilikuwa nawaza kwamba huenda huyu angekuwa ametumwa hata na hao wakina Sudi, kwa hiyo nilihitaji kuwa mwangalifu. Na tulikuwa tunaangaliwa sana na baadhi ya watu eneo hilo.

"Unaitwa nani?" nikamuuliza mrembo.

Akaniangalia na kusema, "Pendo."

"Wewe ni mwenyeji wa huku?"

Akatikisa kichwa kukubali.

"Unasoma?"

"Me nesi," akajibu.

"Wapi?"

"Agha Khan," akajibu.

"Kumbe? Okay. Sa' Pendo, kwa nini unataka kuwasiliana na mimi?"

"Kuna kitu nataka nikwambie..."

"Niambie sasa hivi."

"Ni vitu vingi. Si umesema una haraka?"

"We' sema."

"Eh... aheh... mpaka niseme jamani... we' si ni mtu mzima?"

"Ahah... sawa. Ila hatujuani, unaweza ukawa mke wa mtu," nikamwambia.

"Me sijaolewa mbona," akasema hivyo.

"Kwa hiyo umenielewa eh?"

Akatabasamu kwa haya na kuangalia chini.

Nikasema, "Okay. Nimekuelewa. Ila Pendo, me ni mume wa mtu. Na ninampenda huyo mtu. Sidhani kama nitaweza kukupa unachotaka."

"Kwani ni lazima mke wako ajue?"

"Kumbe na we' wa hivyo? Nilikuona mpole, nikadhani utaelewa," nikamwambia.

"Mhm... haya. Kwa hiyo hujanipenda?" akaniuliza hivyo.

"We' mzuri. Ila me wa mtu. Siwezi kumdanganya mwenzangu, hata wewe itafika mahala tutadanganyana mno nikifanya hilo. Siyo wa hivyo mimi," nikamwambia hivyo.

"Ahaa... basi. Safari njema," kakasema hivyo bila kuniangalia.

"Na we' pia," nikamjibu.

"Poa," akasema hivyo.

Huyoo akaendelea na mwendo kuelekea upande mwingine, nami nikajiondokea hapo kama vile siyo mimi. Yaani huyo angekuwa amenikuta kipindi kile! Ningemwonyesha ushetani wangu maana alikuwa wa moto, siyo mchezo. Ila sasa hivi nilitaka kutulia tu mpaka suala langu kwa Miryam lieleweke kabisa, la Bertha limalizike pia, ndiyo ningejua nisimame wapi baada ya hapo.

Nikiwa naelekea Royal Village sasa, nikampigia simu madam Bertha kumwambia ndiyo nilikuwa nimeingia getini na ningefika huko juu upesi, na alipopokea, kabla hata sijaongea akaniambia nielekee kule nyuma alikopenda kuegeshea gari lake halafu nimsubiri hapo; maana ndiyo alikuwa anashuka. Ilikuwa kama vile anajua nimeshafika yaani, nami nikasema tu sawa, ninaelekea huko, ndiyo nikaanza kuelekea huko kweli.

Nikiwa ndiyo nimefika huko kwenye egesho la magari, nikaona kitu kilichofanya niingiwe na umakini zaidi. Ilikuwa ni Dotto, akiwa amesimama usawa wa magari mawili; moja ikiwa ni lile la madam Bertha la Harrier, na lingine likiwa la aina ya Lexus LX570, kubwa na zuri, likiwa na mwonekano mpya wa rangi ya shaba (silver) iliyoelekea kuwa dhahabu kabisa.
View attachment 3057392

Alisimama karibu nalo hilo kama vile lilikuwa lake ama labda yeye ndiye aliyekuwa dereva wake, nami nikamwangalia kwa umakini zaidi.

Alikuwa amevalia T-shirt nyeusi ya mikono mirefu, iliyobana mwili wake vizuri kuonyesha namna misuli yake iliyokuwa imara, pamoja na suruali nyeusi pia na kiatu cheusi. Akawa ametazama upande wangu na kuniona, naye akaacha kuniangalia na kutazama pembeni kama vile hanijali. Kuna kitu tu kikanisukuma nimfate mpaka hapo alipokuwa na kusimama mbele yake, nikiwa nahisi hata uwezekano wa kutoa bastola hapo hapo ungetokea, lakini sikutaka ifike huko. Yeye akanitazama usoni kwa umakini.

"Imekuwa hivi tokea lini?" nikamuuliza hivyo.

Akaniangalia kwa njia ya kuonyesha kwamba hakuelewa nilichomaanisha, lakini najua alinielewa vizuri.

"Oh, hujaelewa? Okay, let me rephrase that. Umeanza kumfanyia usaliti madam tokea lini?" nikamuuliza tena.

"Usaliti? Usaliti gani?" akajitoa akili kabisa na kuniuliza hivyo.

"Naongelea usaliti ambao hadi ukafanya utamke maneno 'tutamuua' with such ease..."

"Ah, ongea kiswahili dogo, wengine hatukwenda shule..."

"Mbona 'game on' uliweza kuisema?" nikamuuliza hivyo kwa kuudhika.

Akacheka kidogo na kuifuta-futa pua yake kwa kidole, halafu akaniambia, "Ukijua nini kimeanza lini, itasaidia nini? We' si uangalie kile ambacho kipo sasa hivi, hayo mengine yatakupa faida gani?"

"Ah, nashangaa tu yaani, ghafla tu... goon namba moja wa madam kamgeuka, akiwa pamoja na mume wake wanapanga kumuua. Sishawishiki kirahisi na bullshit yote eti kisa Chalii ni kaka yako... mbona kipindi hicho chote ulikuwa umetulia tu? Eh? Tena ukifanya bidding zake madam... zote? Nini kime-change ghafla? Sudi amekuahidi mengi mazuri zaidi ya unayopata kutoka kwa madam, au?" nikamuuliza hivyo.

"Hayo hayakuhusu. Jiangalie wewe. Umepewa muda kutoa jibu, utumie vizuri," akaniambia hivyo.

"Sihitaji kujibu chochote. Mngekuwa mmeniambia labda mnataka kumwibia sijui... labda ningekubali. Yote ya kumuua ya nini? Halafu eti mnafikiri nitaogopa kumwambia kwa kusema sijui ataniua kwa sababu anakuamini zaidi wewe..."

"Mbona bado hujamwambia sasa? Mwambie. Si anakuja hapa hata sasa hivi... mwambie tu," Dotto akaongea kwa kutojali.

Nikabaki nikimtazama usoni kwa umakini.

Akanisogelea karibu zaidi na kusema, "Fanya uamuzi dogo. We' si una akili sana? Kila kitu kipo juu yako. Wala usiwaze kuhusu mimi."

Baada ya Dotto kusema maneno hayo, sote tukabaki kutazamana machoni umakini sana, akinionyeshea ubabe wake, na mimi nikimwonyeshea ujasiri wangu. Kutokana na hali kuwa nzito hapo hatukutambua upesi kwamba kuna mtu alikuwa akija upande wetu mpaka sauti yake iliposikika akisema...

"Hey..."

Nikatazama pembeni na kumwona madam Bertha akiwa anakuja upande wetu. Dotto akasogea nyuma kidogo huku naye pia akimwangalia madam, na kama kawaida yake alikuwa amependeza sana.

Alivalia nguo laini sana ya moja kwa moja mpaka miguuni, ikiwa ya suruali, na iliyokuwa na rangi kama ya ngozi ya mtu anayeelekea kuwa mweupe. Kwa kuwa ilimbana, yaani ilionekana kama vile ni ngozi yake kabisa, kwa hiyo kwa kumtazama vibaya ungedhani alikuwa uchi. Mabuti marefu ya kike ya kuchuchumia ya rangi ya maziwa yalimrefusha zaidi, na nywele zake nyekundu za kusuka alikuwa ameziachia kama namna ile ile nilipomwona majuzi. Mikononi aliweka mkoba mweusi pamoja na koti zito la nanyonya lenye rangi ya maziwa, na aliyaficha macho yake kwa miwani nyeusi ya urembo.

Akiwa anatembea kwa mwendo kama wa miss, akatukaribia zaidi na kuuliza, "Kuna nini hapa? Mbona kama mnataka kupigana?"

Nikamtazama Dotto usoni, yeye pia akinitazama kwa utulivu, nami nikamwambia Bertha, "Hamna kitu. Tulikuwa tu tunasalimiana."

Bertha akamwangalia Dotto.

Jamaa akasema, "Umependeza madam..."

"Shut up! Shika... tangulia kwenye gari," Bertha akamwambia hivyo.

Alikuwa akimkabidhi koti na mkoba wake, na jamaa akavipokea na kuniangalia kwa jicho la chini lenye hila. Nikaendelea kumtazama tu mpaka alipoanza kuondoka kwa kudunda na kuviingiza vitu vya Bertha kwenye lile gari la Lexus, ndiyo na yeye akaingia humo. Nikamtazama madam usoni, naye akaitoa miwani yake na kunisogelea zaidi huku akitabasamu kwa njia yenye kuonyesha madaha.

Sikutarajia anipe hilo upesi, kwa hiyo nikiwa makini tu nikamuuliza, "Umenunua gari jipya?"

Akatikisa nyusi kukubali.

"Zuri. Hongera," nikamwambia hivyo.

"Sifa ziende kwako," akasema hivyo huku akinishika mkono.

Nikatulia kidogo nikitafakari kitu, kisha nikamuuliza, "Kila kitu kiko poa madam?"

Akapitisha mikono yake kiunoni kwangu na kuuegemia mwili wangu huku akinitazama kwa hisia, naye akasema, "Kwa nini kila kitu kisiwe poa?"

Nikajitahidi kuupa mwili wangu wepesi ili asinikandamize sana kiunoni na kuihisi bastola, nami nikamshika shingoni na kumwambia, "Mara ya mwisho nimekuja, tuliishia sehemu siyo nzuri sana, nikafikiri labda...."

"Ah, achana na hayo. Nilikuelewa. Na sasa hivi tuta-focus kwenye mimi na wewe tu... mengine pembeni."

Nikakunja uso kimaswali kiasi, kwa sababu sikutarajia angekuwa ameliachilia lile suala kiurahisi namna hiyo, lakini wala hakuonekana kama ameliweka moyoni kabisa. Tena akakishika kidevu changu kwa makucha yake na kujing'ata mdomo wake wa chini huku akiuelekea wa kwangu, halafu akanipiga busu moja laini na kunifuta-futa lipstick iliyobaki kwa kidole chake kimoja.

"Umekunywa pombe asubuhi-asubuhi?" akaniuliza hivyo.

"Jana. Nilikunywa kidogo wakati wa game la Simba," nikamwambia.

"Haikuwa kidogo, bado harufu ipo japo umesugua ulimi. Pole... inaonekana ni machungu ya Simba kubondwa ndo' yalikufanya ukalewa wewe..." akasema hivyo na kucheka kidogo.

Nikatabasamu kwa kutoamini kabisa huu wonyesho wa upendo, au nia nzuri aliyokuwa ameanza kuijenga kwangu, nami nikamuuliza "Mood nzuri namna hii unaitoa wapi wakati nilikuwa nimeku-diss?"

"Lini umeni-diss?"

"Si ile juzi?"

"Well... wewe ndiyo unaifanya day inakuwa nzuri. Ya juzi hata siyakumbuki maana umenifurahisha sana leo," akasema hivyo.

"Kwa kipi?"

"Kumkataa Pendo," akasema hivyo.

Nikamkazia macho kiasi, naye akatikisa nyusi kimchezo, ndiyo nikamuuliza, "Pendo? That was you?"

Akatikisa kichwa kukubali huku akitabasamu kiasi.

"Ahah... kwa hiyo, kumbe ulikuwa umemtuma huyo mwanamke anitongoze, ili..."

"Ili nione kama kichwa chako kiko kwenye game, na moyo wako uko kwangu. Ilikuwa ni test ndogo tu, ila kumkataa Pendo ni ishu kubwa. Huyo mwanamke huwa hakataliwi kirahisi hata na wazee wa upako na maaskofu," akaniambia hivyo.

"Ameanza kunifatilia tokea... tokea Mbagala? Yaani... ulikuwa umeshampanga asimame nami mpaka huku?"

"Me hayo siyajui. Karudisha taarifa kuwa umemkataa, that's what I wanted..."

"Utajuaje hilo kuwa kweli? Je kama nimemkubali na amekudanganya?"

"Nilikuwa nasikia maongezi yenu yote," akaniambia hivyo.

Nikanyanyua kidevu juu kiasi huku nikimwangalia kwa utambuzi, nami nikasema, "Alikuwa anachukua sauti..."

"Mm-hmm. Na kama ingetokea umemkubali, me na we' ndiyo ingekuwa bye bye... na tena una bahati yako. Ipo siku nitakushika kivingine," akajibu hivyo.

Nikatulia kidogo, kisha nikamuuliza, "Kwa nini Bertha? Mpaka ufanye hayo yote... why?"

Akasema, "Kwa sababu nataka uwe wangu peke yangu. Sasa hivi sitajali sijui nini, au nini... JC, nataka uwe WANGU PEKE YANGU. Sahau ishu ya me kutaka mtoto, tutauangalia huo mpango baadaye. Sasa hivi nataka kichwa chako kiwe sehemu moja, na moyo wako hapa tu. La sivyo, mimi na wewe kuachana inamaanisha itakuwa vibaya. Unaelewa jinsi navyokuwa nikipenda kitu sana, si ndiyo?"

Hmm! Hili lingekuwa tatizo haswa, ila ni ikiwa tu nisingekuwa mwangalifu. Nikatikisa kichwa tu kuonyesha uelewa.

"Good. Umepita kamtihani kangu. Ngoja tuendelee kuona ya mbele," akasema hivyo.

Nikawa nikimtazama kwa ufikirio sana, nami nikasema, "Bertha... popote pale ambapo me na wewe tutaishia, ninaomba ujue tu kwamba sehemu kubwa ya moyo wangu haitaki kuona unaumia. Hatujaanza vizuri... na... sijui kama tutaishia pazuri, lakini...."

"Shhh..." akaninyamazisha kwa kuweka kidole chake kimoja mdomoni kwangu.

Nikatulia tu.

"Usiwaze negative. Sasa hivi nataka kuhakikisha kila kitu changu na wewe kinajengeka kwa njia positive, tena kuanzia leo leo. Na nitafanikiwa. Utaona tu," akaniambia hivyo kwa uhakika.

Nikashusha macho yangu chini, nikiwa najihisi vibaya kiasi moyoni. Maneno niliyokuwa nataka kumwambia yalikuwa yamebeba maana pana sana, hakujua tu.

Akatoa kidole chake mdomoni kwangu na kusema, "Twend'zetu. Kuna watu muhimu nataka tukakutane nao."

Nikamwangalia na kutikisa kichwa kukubali, naye akanishika mkono na kuanza kuniongoza mpaka tulipoingia kwenye Lexus yake na kuketi siti za nyuma, kisha Dotto akaliwasha na kuanza kuendesha.

Bado tu nikawa nawaza vitu vingi sana, mara kwa mara nikitazamana na Dotto kupitia kile kioo cha mbele pale juu kwa macho yaliyojuana mno, na maswali ya ni wapi haya yote yangekuja kuishia yakaendelea kuisumbua nafsi yangu hasa baada ya Bertha kuonyesha kwamba ni kweli alikuwa ananipenda. Kama tu maneno ya Dotto muda mfupi nyuma, kwa kweli ningetakiwa kufanya uamuzi haraka ikiwa Ramadhan na wenzake wangekawia kuyamaliza haya.

★★

Kulikuwa na mkutano fulani maalumu huko Kinondoni ambao ulibeba matembezi ya wafanyabiashara na viongozi fulani wa juu serikalini, na Bertha alikuwa na lengo la kwenda kumzuzua mfanyabiashara mmoja mkubwa sana awekeze kwenye ishu yake Bertha ambayo bado sikufahamu ni nini. Yaani kuna kitu Bertha alikuwa ameanza kujenga, bila mimi kujua, ila nafikiri kilikuwa pembeni ya ishu zao za madawa ingawa angekijenga kwa kutegemea nguvu ya biashara yake ya madawa.

Sijui alikuwa anataka kufungua kampuni labda? Na ndiyo alitaka kuwa na mtu kama huyo mfanyabiashara mkubwa wa kusaidia kulikuza jambo hilo upesi na kwa njia isiyo haramu, kwa hiyo hii ndiyo ikawa "mission" yetu ya leo. Asingekwenda huko supermarket wala wapi, na alitaka niwe pamoja naye ili nimpe ushirika wangu kama "mpenzi" wake. Kwa hiyo tulipita kwenye duka moja kubwa la nguo, nami nikavalishwa suti na kiatu cheusi bila kupenda. Nilikuwa mwangalifu sana kuhakikisha hawatambui kwamba nilikuwa na bastola, na Bertha akiwa amependeza tayari, tukaelekea huko Kinondoni.

Zilikuwa ni hafla zenye kuboa sana. Tulisubiri kwa muda mrefu, ndani ya ukumbi kwenye jengo kubwa kweli, na ilinikera kutembea kwenye vigae vilivyoteleza na maviatu haya, kila dakika nilihisi ningeweza kuanguka. Lakini hatimaye madam akawa amepata nafasi yake kuongea na jamaa, akitumia ushawishi wake mzuri kwenye maneno na nguvu ya kuwa mwanamke ili kumzuzua kwelikweli jamaa, na jamaa akatoa kadi yake ya mawasiliano na kumuahidi kupanga makutano "binafsi" ili waongee biashara zaidi. Ikawa ni mwanzo mzuri kwa madam.

Kwa hiyo tumekuja kumalizana na hayo jioni kabisa, na baada ya hapo ndiyo tukaelekea sehemu nzuri pamoja na madam kupata msosi. Bertha alikuwa kwenye hali nzuri kihisia, alionyesha furaha yake waziwazi alipoongea, hata akawa ananilisha eti mbele za watu, na mimi nilijitahidi kufanya ionekane nafurahia sana muda huu pamoja naye, lakini kila nilipomwangalia huyo Dotto aliyekuwa amesimama "kibodigadi" huko pembeni, nilihisi hasira tu iliyonifanya nikose amani hata ya kunisaidia kuendelea kuigiza. Lakini ningefanyaje?

Bwana, tumekuja kurudi kwake Bertha saa tatu usiku baada ya mimi kuamua kupita kwenye gym fulani huko Morocco (ya Dar siyo Africa), ili ninyooshe viungo kidogo. Nilifanya hivi kutokana na maumivu niliyokuwa nayo, na Bertha alilazimisha kuja nami ili anitazame eti. Kulikuwa na wanaume vifutu siyo mchezo, waliomtazama madam na kuonyesha ngangali zao, lakini madam wangu alikuwa na mimi tu, hata akipiga makofi ya pongezi alipoona nimetandika push-up mia moja. Yaani mtu mwingine mpaka angehisi raha!

Kwa hiyo nilijisafishia huko huko baada ya tizi, na tulipofika kwake alikuwa ananitaka nilale naye, lakini nikamwambia hata mimi nilitamani sana kubaki hapo ila kwa leo isingewezekana, maana kuna ishu nilitaka kushughulikia huko Mbagala. Nikajitoa akili na kumpetipeti kwa maneno na miguso na nini, naye akalegeza. Alikuwa hadi ameanza kudeka, yaani hakuwa Bertha niliyemfahamu kabisa, dah!

Ila kuna nyakati nilikuwa namwangaliaaa, jinsi ambavyo hakuwa na dokezo lolote la mambo ya mbeleni yaani, lakini sikuwa na jinsi ila kubaki njia kuu mchezoni. Kuna vitu tu ningepaswa kuamua kuacha vitokee, na vingine ningejitahidi kuvizuia visitokee, lakini kwa kweli kuna sehemu zilizokuwa mpaka zinanifanya nihisi kujuta, basi tu, sikuwa na namna tena. Mchezo ungepaswa kuendelea. Kwa hiyo alipokubali kuniachia, nikaondoka hapo upesi sana ili kurudi Mbagala, madam akiwa pia amenikabidhi suti na viatu vipya viwe vyangu kimoja, huyooo nikatembea.

Alikuwa amenipa ofa ya kusindikizwa na Dotto mpaka nyumbani kwa kutumia gari lake, lakini nikaikataa kistaarabu tu. Jamaa asingeweza kumgusa madam hata kama wangeachwa peke yao kwa sababu najua alikuwa akifuata mipango ya Sudi, kwa hiyo na mimi ningeendelea kukausha tu kwa wakati huu mpaka nikiona wazi kwamba hatua waliyotaka kuchukua dhidi ya madam ingechukuliwa. Nikachukua tu usafiri wa umma, nikiwa kwenye umakini wangu kama ilivyotakiwa kwa wakati huu.

★★

Nimekuja kuifikia Mzinga ikiwa imeshaingia saa sita usiku, kama kawaida, usafiri na changamoto zake. Zamu hii hakukuwa na majangili ama akina Pendo walioagizwa kunifatilia, na nilihakikisha bastola ipo mahala pake ili timbwili lolote likizuka basi nitimbwilishane nalo ipasavyo. Mpaka nafika kwa Ankia sikuchokozwa na yeyote yule, walioniona wakiniangalia tu kama vile hawanijui, ila walishawahi kunisikia.

Nilikuwa nimeshamtumia ujumbe Ankia kumjulisha niko njiani kuja huku, na katikati ya safari hiyo nilikuwa nimewasiliana na Adelina pia. Mwanamke yule tayari alikuwa ameondoka kurudi kwao ile mchana, na nilimwomba radhi tu kutokana na kuwahi kuondoka asubuhi bila kuonana naye, lakini akasema haina shida, na alitarajia tungekuja kukutana tena panapo majaaliwa na mambo kwenda vyema zaidi ya jana. Na hiyo jana aisee! Basi tu, ningepaswa kuisahau baada ya muda.

Ile ndiyo nimefika getini kwa Ankia, kama kawaida nikatazama upande wa jirani zetu, na ikiwa kama bahati tu, nikamwona bibie Miryam akiwa amekaa hapo nje; varandani kwake. Kwa kuwa kutembea kwangu kulifanya sauti za hatua zisikike kutoka chini, nikamwona akinyanyua uso wake na kutazama upande wangu, na kwa sekunde chache tukabaki kuangaliana tu bila wonyesho wa hisia yoyote.

Lakini kiukweli mimi bado nilikuwa nikiteseka sana rohoni, hasa tu baada ya kumwona namna hiyo ghafla kukafanya moyo wangu upige ngoma yenye mdundo mzito sana kifuani utadhani nilikuwa nimemwibia kitu. Ila ni yeye ndiye ambaye alikuwa ameiba moyo wangu, na sijui kama angeweza kutambua hilo, yaani ingenibidi tu niache kuwa kama kuku aisee. Nilimwelewa mno, na nilitaka ifike siku ajue hilo japo sikuwa na uhakika kama angelipenda.

Baada ya kuendelea kumwangalia tu kupitia matundu ya ukuta wa uzio, nikanyanyua kiganja changu na kukitikisa kama kumpa salamu, naye akanyanyua chake na kunipa ishara ya "njoo." Ah! Nikageuka fasta, yaani hakukuwa na ubishi wala uchovu tena hapo, malkia aliniita kwa nini nijizungushe? Nikaenda kufungua geti lao na kumfata hapo ubarazani.

Kama kawaida, alivalia kinguo chake cha kulalia huku akijifunika kwa kikoti chepesi cha nguo hiyo, na nywele zake alizosuka zilikuwa zimefichwa kwa kikofia laini cha kusitiri nywele chenye rangi zambarau. Alikaa kitini akiniangalia kwa utulivu, simu ikiwa mkononi, na pia kulikuwa na kiti kingine pembeni yake ambacho hakikuwa na mtu. Hebu ngoja kwanza. Nilikuwa nimewekewa mimi, ama? Alikuwa ananisubiri? Hapana, ilikuwa bado mapema mno kuwaza hivyo, ila hako kawazo kalisisimua!

Nikajisogeza tu hapo, yeye akiwa ananitazama kwa utulivu usoni, nami nikamwambia, "Uko poa?"

Akatikisa kichwa kukubali na kuendelea kunitazama.

"Mbona umekaa kwenye baridi?" nikawauliza.

Akapandisha mabega kiasi huku akifumba na kufumbua macho yake, kama kusema basi tu amependa.

Nikatabasamu kiasi na kusema, "Wengine watakuwa wameshalala, eh?"

"Yeah, wako vyumbani..."

"Mbona kama haukuwa peke yako hapa?"

"Nilikuwa nimekaa na Tesha. Ndiyo ameingia ndani muda siyo mrefu kuongea na simu, atakuwa ni demu wake," akasema hivyo.

Akanifanya nicheke ghafla kwa sababu ya kutotarajia aseme hivyo.

"Nini?" akaniuliza.

"Hamna. Sikuwahi tu kufikiri na wewe unasemaga maneno kama 'demu,'" nikamwambia.

"Si ndiyo lugha mnayopenda? Nitafanyaje sasa?" akaniuliza hivyo.

"Ni neno la kawaida. Sema tu watu wameshazoea kulitumia kihuni mno," nikamwambia.

"Mhm... kaa basi unipe company kidogo. Au ume...."

Nikakatisha maneno yake kwa kukaa kitini upesi, naye akatabasamu kiasi.

"Inaonekana umetokea pazuri," akasema hivyo.

"Kwa nini?" nikamuuliza.

"Uko na mood nzuri sana," akasema.

"Ah, hamna. Kawaida mbona?"

"Eti eh?"

"Yeah. Hata nikiwa na stress, mood yangu huwa iko juu tu. Hiyo inasaidia stress zinaondoka zenyewe," nikamwambia.

"Naona una balance nzuri kwenye kupunguza stress, ila mtu akikuudhi humwachi salama," akaniambia hivyo.

"Ahahahah... najua unajua. Sipendi wachokozi," nikamwambia hivyo pia.

Sote tukacheka kidogo maana tulikuwa tunakomea njiani kufika kule ambako upana wa maneno yetu ulikuwa unaelekea.

Akauliza, "Ni sawa. Ila ni hasa ulipokuja huku Mbagala, ama ni kutokea zamani ulikuwa hivyo?"

"Nimekuwa hivyo tokea muda. Kama ni kitu ambacho sipendi zaidi maishani... ni uonevu. Mengine tutavumiliana ila... hata wakati nipo shule, yaani mwalimu tu akimwonea mwanafunzi mwenzangu, ama wanafunzi wenzangu kuoneana, nilikuwa najisikia vibaya sana. Nisingeweza kuzuia yote, lakini kila ilipokuja kwangu..."

"Ungewaka!"

"Wee! Hakuna aliyekuwa ananisogelea," nikajitutumua eti.

"Na bila shaka kwenye masomo ulikuwa mkali pia," akaniambia hivyo.

"Yeah, toka nimeanza shule mpaka nimemaliza. Nilijitahidi sana nisianguke hata mara moja," nikamwambia.

"Hukuwahi kurudia darasa hata moja?" akauliza.

Nikatikisa kichwa kukubali.

"Mambo kwako yalikuwa easy eh?" akauliza.

Nilianza kuona kwamba Miryam alitaka kunielewa zaidi, kwa hiyo nafasi hii ningeitumia vizuri.

Nikamwambia, "Siyo sana. Mungu alinipa tu ubongo mzuri, lakini bidii ilihitajika ili ufanye kazi vizuri. Nilikuwa napenda sana kusoma, na hali za kimaisha hazikuwa rahisi sana wakati nakua, ila... angalau nilifanikiwa kutoka vizuri shuleni," nikamwambia.

"Ulimaliza shule una miaka mingapi?"

"Form four nimemaliza nina miaka 16," nikamwambia hivyo.

"Eh, mdogo!" akasema hivyo huku akitabasamu.

"Ahah... nilianza shule mdogo, na sikurudiaga, kwa hiyo nikamaliza mdogo," nikasema hivyo.

"Baada ya form four?"

"Nikaenda advance, nilichaguliwa kwenye shule moja huku nzuri, nilipata alama nzuri necta. Yeah... kwa hiyo, nikasoma hiyo miaka miwili, nikafaulu vizuri tena, moja kwa moja UDSM..."

"Wow... udaktari..."

"Ndiyo. Nikapiga miaka mitano, na ndani ya hiyo miaka tayari nilikuwa nimeshaanza kupelekwa sehemu hizi au zile kusaidia na kazi... mahospitalini kabisa, kwa hiyo nikawa naona mambo mengi yaliyonisaidia niwe na experience zaidi. Lilipokuja suala la masomo, yaani sikutakaga kuwa mtu wa kuanguka kabisa, sometimes hata nilikuwa napewa chaki niwaelekeze wanafunzi wenzangu maana mpaka walimu walielewa nilikuwa genius..."

"Wacha we!"

"Ahahahah... usipime. Nimetoka chuo nimeiva, nikaenda kufanya internship Bugando, kule Mwanza, halafu...." nikajikuta nimeishia hapo baada ya kukumbukia kitu fulani cha zamani.

Miryam akasema, "Halafu..."

Nikamwangalia na kusema, "Yeah, halafu... ilikuwa kwa mwaka mmoja, ndiyo... nikaja sasa Muhimbili."

"Ni Muhimbili ya Mloganzila, au hiyo ya hapo?"

"Kotekote, ila sanasana hii ya huku. Nilikuwa wa kitengo fulani maalumu, na sikuwa daktari mmoja tu kwenye hicho... kwa hiyo ni kama tuseme zamu zinakuwa zinabadilishwa, lakini baada ya muda nikawa nakaa hii Muhimbili ya huku Kariakoo zaidi..."

"Sawa."

"Yeah. Ndiyo hivyo."

"Na hiyo ni... umekaa kwa muda gani yaani?"

"Miaka kama mitatu," nikamwambia.

"Mh? Miaka mitatu?" akaonekana kushaangaa.

"Ee. Michache?"

"Ahah... me nikafikiri labda hata kumi! Asa' unahitaji likizo ya nini, ni kwamba hupendi wagonjwa ama uvivu tu?" akauliza hivyo.

Nikacheka kidogo, kisha nikamwambia, "Kiukweli, sikuwa mtu wa kupumzika sana tokea nimemaliza chuo, mpaka kuingia kazini, mambo yalikuwa mengi. Sometimes nilikuwa silali, unakuta nakaa macho hata saa za kazi zikiisha me nabaki kuangalia mahitaji ya wagonjwa..."

"Hiyo si ni kazi ya wauguzi?"

"Yes, ila siyo wote. Kuna hizi scenario unakuta... wanakuwepo tu kwa ajili ya wagonjwa kuwaangalia, na hata kama madaktari wengine wanakuwa wameshughulika na wagonjwa wao, me napenda tu pia kuwafanyia double checking ili kuhakikisha kwamba wanaendelea kuwa sawa," nikamwambia hivyo.

"Si... sijui kama nimeelewa vizuri..." akasema hivyo.

"Iliwahi kutokea... kuna mgonjwa ambaye alikuwa hospitalini amelazwa baada ya msaada wa madaktari, akawa amepoteza maisha baada ya wao kufikiri msaada wanaotoa unatosha. Na inatokea mara nyingi. Najua kazi zinakuwa rundo, ila... me nilishagaona ni muhimu tu kuhakikisha. Naongelea wagonjwa ambao unakuta wanakuwa wamelazwa, na hali zao ni..."

"Ndiyo, ndiyo, naelewa," akanihakikishia.

"Yeah, ndiyo hivyo. Huwa tu sijisikii vizuri mgonjwa akipoteza uhai wakati yuko hapo hapo hospitali. Kuna vingine haviwezi kuzuilika, ila me nikiwepo... nakuwa nataka kuhakikisha usalama unachekiwa mara mbili zaidi ya ile wanayoona inatosha. Kwa hiyo, nilikuwa mtu wa kutaka kusaidia kila mtu... hata kama nisingeweza kuwasaidia wote... popote ambapo ningeweza, hapo hapo. Mpaka ikawa inazidi. Nikachoka kiasi, ndiyo maana nikapewa haka kalikizo," nikamwambia hivyo.

"Kumbe haukuiomba?" akauliza.

"Hamna. Nilipewa kama break, ili nikirudi niwe kwenye game vizuri hata zaidi kupiga miaka mingine vyema," nikamwambia hivyo.

Akatabasamu kiasi na kuniambia, "Ndiyo maana ukamsaidia na Mariam."

Nikatabasamu kiasi.

"Unapenda kusaidia sana watu. Mpaka unajiingiza kwenye vitu hatari sana ili tu uwasaidie wengine," akasema hivyo.

Nikatabasamu zaidi na kusema, "Eeh."

Lakini nilipomwangalia, nikakuta akinitazama kwa hisia makini zaidi usoni, kama vile alikuwa akinitafakari sanaaa, nami nikajikuta nafifisha tabasamu langu na kubaki nimemtazama usoni kwa umakini pia. Akaacha kuniangalia na kushusha pumzi taratibu, na kiukweli hapo niliweza kuona kwamba alikuwa amezama ndani ya fikira fulani kunielekea, na kuwaza ingekuwa ni fikira gani, kulisisimua sana akili yangu.

Nikamwambia, "Ona... Miryam... kuhusu ile jana..."

"It's okay, Jayden. Tuyasahau tu ya jana, sawa? Tusonge mbele," akaniambia hivyo kwa upole.

Nikatabasamu kiasi na kumwambia, "Sawa. Unajisikiaje lakini? Mgongo I mean..."

"Oh, niko sawa kabisa. Ule mkanda ulipiga zaidi nguo ya ndani, na ilikuwa ngumu, kwa hiyo sijaumia sana..."

"Hata kutia alama?"

"Hapana. Niko poa," akanihakikishia.

Nikatikisa kichwa kuonyesha uelewa.

"Na wewe? Vipi mgongo?" akauliza.

"Yeah, nimeamka unauma-uma, ila sa'hivi umeachia. Leo imenibidi niingie gym tena," nikamwambia hivyo.

"Ili uongeze maumivu kufanya yaliyokuwepo yapungue?" akauliza.

"Yep. Na kesho nitaamka yamenikaza zaidi, kwa hiyo sitapaswa kuacha," nikamwambia hivyo.

Akatikisa kichwa taratibu na kusema, "Pole lakini."

"Usijali. Halafu... nimewaza kitu..." nikamwambia.

"Mm-hmm..." akatega sikio.

"Vipi tukiwatoa... familia... out ya pamoja yaani, watembee..." nikamwambia hivyo.

"Mh! Wapi?" akauliza pia huku akitabasamu.

"Popote. Iwe sehemu nzuri, halafu iwape kale ka-sense ka ugeni yaani..."

"Yaani iwe kama lunch au dinner hivi?"

"Eeeh. Ila ukisema lunch... ndo' inafaa. Vipi tukiwatoa wote, Mamu, warembo wangu, Tesha, Ankia... twende tukapige kisinia?" nikamuuliza hivyo kwa uchangamfu.

"Ahahah... kisinia! Nina muda sijafanya hiyo kitu..." akasema hivyo.

"Itakuwa poa sana. Najua Mamu atafurahia sana..."

"Na bado hujamsema Tesha..."

"Ahahahah... tufanye hivyo. Tena mapema yaani, iwe kama tunaamshia-amshia na birthday ya cheupe wangu," nikamwambia.

"Ni sawa. Sema, nilikuwa sijajiandaa, kwa hiyo..."

"Usijali Miryam. Zamu hii itakuwa my treat," nikamwambia hivyo.

"Mm? Wewe mwenyewe?" akauliza.

"Mmm. Na tena ikiwa utaona inafaa... kesho," nikamwambia hivyo kwa uhakika.

"Jayden..."

"Usijali Miryam, everithingi niachie mimi, wewe ni kuja tu. Kila kitu kitakuwepo tayari," nikamwambia hivyo.

"Ahah... ni wazo zuri, sema unapeleka mambo fast mno Jayden..." akasema hivyo.

"Mjini kuchangamka Miryam, hujui?"

Akatabasamu na kuangalia pembeni.

"Come on, ni idea nzuri, we' mwenyewe umesema. Tena nimeshafikiria mahala pazuri pa kulia kisinia kesho. Kubali tu," nikamshawishi.

"Wapi?" akauliza.

"Huko kwetu Sinza," nikamwambia.

"Wewe!" akaonekana kushangaa kidogo.

"Eeh, nakwambia ni pazuri kweli. Familia yako itafurahi sa...."

"Jayden, kuwapeleka huko akina mama, me naona ni mbali. Halafu kesho ninaenda kazini. Bora kama ingekuwa...."

"Siyo siku ya kazi, najua utasema hivyo, lakini hiyo wala siyo shida. Wewe nenda dukani, fanya kazi, ukimaliza unamwacha tu Soraya halafu unakuja. Utatukuta. Mimi ndiyo nitawaongoza hawa wote, tutapanda daladala, halafu tukifika huko nakutumia address kabisa ili uje mwenyewe kwa raha zako..." nikamwambia hivyo kwa ushawishi zaidi.

Akacheka kidogo kwa pumzi na kutikisa kichwa chake.

"Eeh, fanya hivyo. Angalau kesho wote watakuwa na mengi ya kuona... na najua wakifurahia, hata wewe utafurahia pia. Unastahili hilo," nikamwambia hivyo kwa sauti tulivu.

Akaniangalia machoni kwa utulivu tu, mimi nikimpa tabasamu hafifu, naye akasema, "Sawa basi... nitawaambia. Na uhakikishe kila kitu una-handle vizuri..."

Nikanyoosha kiganja kimoja juu na kingine nikiweka moyoni, nami nikasema, "I cross my die, and hope to heart. Kila kitu kitakuwa sawa."

Akacheka kidogo na kusema, "We' ni shida Jayden..."

Akanifanya nicheke kidogo kwa furaha, ndiyo nikamwambia, "Asante Miryam. Hautajutia hii."

"Hapana, mimi ndiyo nikwambie asante Jayden. Unaleta vitu vingi vizuri kwenye familia yangu, na hauchoki yaani. Nathamini sana," akaniambia hivyo kwa sauti yake nyorororo.

Mpaka nikajihisi haya, ile ku-blush, na ndiyo hapa bibie akawa amesema ingefaa aelekee ndani ili autafute usingizi sasa. Basi, na mimi nikaona ninyanyuke, nikamsaidia kuingiza kiti ndani na kumuaga vizuri tena, kisha ndiyo nikaelekea kwa Ankia. Mwanamke tayari alikuwa ameingia kulala, kwa hiyo nikaamua kuelekea tu chumbani kwangu moja kwa moja.

Nilifika tu chumbani na kujitupia kitandani, nikijilaza chali huku mkono wangu nikiukunjia nyuma ya kichwa. Nikajikuta tu natabasamu mwenyewe kutokana na kuhisi raha sana. Yaani eti raha tu kukaa vile na Miryam hapo nje, kuongea kidogo, halafu sasa na vile alivyokuwa ananitazama. Dah! Tule tumawazo tulikuwa tunanifanya najihisi kama Cinderella yaani, ningeweza hata kung'ata kidole kimoja mdomoni kwa shau!

Ilikuwa wazi kwangu zaidi na zaidi kwamba nilimpenda sana huyu mwanamke, na ningetakiwa kufikiria wakati sahihi na njia nzuri ya kumweleza hisia zangu bila ya matatizo yoyote kutokea. Sikujua ikiwa angeweza kunichukulia serious, ila ningehakikisha anajua tu. Iwe isiwe. Nikaamua kujiondoa kwenye ulimwengu wangu wa ndoto za mapenzi ya kweli na kwenda kuoga kwanza, kisha nikarejea na kulala hatimaye. Mbu hao!





★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★


Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
JC JC JC nimekuita mara tatu kuwa makini ndugu yangu Festo atakuchomoa bandama kwa MIMI halafu Bertha ndo atakunywa SUPU hahahaha
 
Back
Top Bottom