Simulizi: Mimi na Mimi

Simulizi: Mimi na Mimi

MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA KUMI

★★★★★★★★★★★★


Baada ya mazungumzo hayo yenye kuchochea hisia pamoja na mama wakubwa, Bi Zawadi akasema angekwenda kuniwekea makande aliyopika ili nile hatimaye, nami nikakubali hilo na kisha kurudi kukaa sofani.

Wote kwa pamoja walitaka kujua mengi kuhusu udaktari wangu, nami nikawaelezea kwa njia nyepesi tu kuhusiana na masuala ya vitengo vya utabibu nilivyohusika navyo, muda ambao nilifanya kazi kwenye hospitali ile, mpaka kufikia wakati huu nilioamua kuchukua likizo fupi na kuja kukaa huku Mbagala.

Sasa wakaweza kunielewa vizuri hata zaidi, wakiniona kuwa kama mtu wa muhimu sana, lakini nikawaambia mimi kwao bado ni kijana mdogo mno na ninapenda kujiona kuwa chini ya wengine; hasa kama ninawaheshimu sana.

Nikaweka wazi kwao lengo langu la kuja kuishi huku kuwa kujaribu aina tofauti ya maisha niliyozoea kwa maeneo tofauti niliyopitia na kuishi, kama vile kujisahaulisha kwamba mimi nilikuwa daktari. Nimekaa kwenye vyumba vingi vya hospitali na kuzungukwa na watu wengi wenye kuhitaji msaada kwa muda mrefu kiasi, kwa hiyo nilihitaji kupumzika kidogo ndiyo nije kuendelea na wajibu wangu kama tabibu baadaye.

Kande lilikuwa tamu sana. Nikamaliza na kumshukuru Bi Zawadi, na ni hapo ndiyo sisi wote tukasikia honi ya gari nje ya geti la nyumba hii. Bi Zawadi akasema kwamba bila shaka huyo angekuwa ni Miryam, naye akataka kwenda kufungua geti lakini nikamwomba nimsaidie kufanya hivyo ili atulie tu ndani hapo. Akakubaliana na hilo.

Nikaangalia muda kwenye simu yangu na kuona ilikuwa ni saa tisa alasiri sasa; ikionyesha Miryam na Tesha walitumia muda mrefu sana huko ofisini kwa mwenyekiti, ama labda walikwenda na sehemu nyingine pia ukitegemea walitoka na gari.

Nikaenda hapo getini na kuiona pickup ya bibie ikiwa hapo nje, nami nikalifungua geti kuruhusu gari liingie. Vuuu likapita ndani, nami nikafunga tena geti.

Nilipokuwa ndiyo nimemaliza tu kulifunga, nikaangalia gari hilo na kuwaona Miryam, Tesha, pamoja na Shadya wakiwa wameshashuka, wanawake hao wakiwa wananitazama usoni kwa umakini, huku Tesha akija niliposimama.

Akanifikia karibu, nasi tukagonga tano huku akisema, "Vipi mwamba?"

"Poa tu. Za huko?" nikamuuliza.

Hakutoa jibu, bali akaangalia chini na kushusha pumzi, kisha akapigisha ulimi wake kidogo mdomoni kama vile kuonyesha amevunjwa moyo na jambo fulani, naye akageukia upande aliosimama Miryam. Mimi pia nikamwangalia mwanamke huyo, ambaye alikuwa ananiangalia kwa njia tulivu tu, nami nikampungia mkono kidogo kama kumpa salamu.

"We' JC? Vipi? Akina shangazi wameshakugeuza gateman?" Shadya akaniuliza hivyo kiutani.

Nikatabasamu na kumwambia, "Na mshahara wameshanipa."

Akacheka kidogo na kumwangalia Miryam, lakini mwanamke huyo alikuwa serious kama vile amemeza chura au nini, naye akaelekea tu ndani. Shadya akatoa mifuko fulani yenye kujaa vitu vingi ndani ya gari hilo na kumfata Miryam ndani huko pia, nikibaki mimi na kijana Tesha hapo nje.

"Mambo yameendaje?" nikamuuliza.

"Ah... sister anazingua JC..." Tesha akaniambia.

"Kafanyaje? Hamjamshtaki ka... a... huyo... huyo jamaa?" nikauliza tena.

"Umeona mwanangu? Hata wewe umetegemea tungemshtaki huyo fala, afungwe. Sasa Mimi si mama huruma sana? Kawaambia wamwachie," Tesha akaongea kwa sauti iliyoonyesha kuudhika kwake.

"Kawaambia wamwachie? Yaani kama vile amemwombea msamaha au?"

"Agh, mizinguo tu kaka! Hilo fala limemtukana hapa, lingeiba ishu ya Mamu, afu' tu eti anaenda kumwambia mzee Hamadi wamwachie jamaa! Imenidis sana..."

"Labda anaona kumfunga ndugu yenu haitafaa. Ameongea naye kwani?"

"Eee... Joshua ametoa makamasi hapo ndo' Mimi akamwonea huruma eti. Wamemwambia lakini wasije kusikia amezusha fujo wala chochote kile tena la sivyo watamfunga bila kujali huruma za dada. Ah... me nilikuwa natamani aende akanyee debe leo! Basi tu..." Tesha akasema hivyo.

Nikatabasamu kidogo na kusema, "Dada yako siyo mtu wa visasi inaonekana. Halafu... anaijali familia yenu, nyie wote yaani, hata kama huyo Joshua kapotea. Mwelewe tu... na umuunge mkono. Sawa?"

"Agh... bado inakera bana. Nilitaka nimwone huyo bwege amevaa karoti leo nije kula kuku mimi. Sasa sa'hivi nakuja kula tu kande huku nimevimba, ndo' nini? Ah..." akaongea kwa kuudhika.

"Ahahah... nenda kale kande, litapunguza hasira. Ni tamu," nikasema.

"Umeshakula?"

"Yah, Bi Zawadi kanionjesha."

"Au siyo? Sawa, ngoja na me nikale, nipige maji afu'... ah... mishe gani unafanya baadaye?"

"Nipo tu."

"Sijui twende tukazurure tu Mbagala? Ningekuwa na mshiko tungeshindia Masai..."

"Ahahaha... Gonga amenipigia mara kadhaa, sijui anataka nini..." nikamwambia.

"Ih, kweli? Hujapokea?"

"Hamna, sioni haja. Nahisi kama atan'sumbua tu..."

"A-ah... usizingue. Mtafute, najua anataka kukuita. Fanya mambo basi, uniunganishe na mimi angalau tukazimue za ofa, ama nini?"

"Ahahah... Tesha unapenda kunywa wewe!"

"Hahaha... aaa siyo sana. Ila hizi ofa kabambe siyo za kupitwa. Fanya mambo tuilambe hiyo," akasema hivyo na kuniwekea ngumi usawa wa kifua changu.

Nikaigonga kwa ngumi yangu pia na kusema, "Haya bana. We' nenda kale, tutashtuana baadaye. Waambie mama wakubwa nimeondoka eh? Tutaonana tu hata kesho."

"Haya poa kaka," akasema hivyo.

Tukaachana kiaina hiyo, nami nikarudi moja kwa moja mpaka ndani kwake Ankia.

Nilikuwa nimeijaza akili yangu mambo mengi kutokea asubuhi hii, lakini sasa angalau ilikuwa imepewa wepesi kiasi baada ya kuzungumza na Bi Zawadi na Bi Jamila kuhusiana na familia yao. Kilichokuwepo sasa ilikuwa kutafuta muda mzuri wa kuongea na dada mkubwa, Miryam, kuhusu suala la tatizo lililomwathiri mdogo wake, na ndiyo ningeanza kweli kumsaidia Mariam.

Nilipofika sebuleni hapo sikumkuta Ankia, nami nikasogea mpaka upande wa kuelekea jikoni nikidhani angekuwa huko lakini nikamkosa. Bila shaka angekuwa chumbani kwake, labda kalala, na nilipokuwa nimeamua tu kuelekea chumbani kwangu ili nikapumzike, mwanamke huyo akaniita kutokea chumbani kwake.

"JC..."

Nikaitika, "Naam..."

Sauti yake ikasema, "Ndo' umerudi?"

"Ndiyo. Ndo' naingia..."

"Funga basi huo mlango halafu uje..."

"Mlango wa sebule?"

"Eeee..."

"Kuna nini tena huko weye?" nikauliza kiutani.

Nikasikia akicheka, naye akasema, "Njoo bwana."

Tayari nilikuwa najua mambo ya kutarajia nikienda chumbani kwa mwanamke huyo, na kiukweli kwa muda huu nilikuwa na mhemko ufaao kukutana nayo hayo mambo. Si ni ile kuvutiana-vutiana sana na mwanamke huyo aliyekuwa amenielewa kupitiliza? Kwa hiyo kama alitaka nimpe alichokitaka sasa hivi, nilikuwa nimeamua kumtolea uvivu.

Nikaenda kuufunga mlango, yaani kuufunga kwa funguo, hiyo ikiwa ndiyo maana yake nilijua hivyo. Nikaenda mpaka kwenye mlango wa chumba cha mama mwenye nyumba wangu, nami nikaufungua na kuingia ndani humo.

Kilikuwa chumba chenye upana kiasi, kukiwa na kitanda kikubwa cha tano ya sita, kabati la nguo na stendi ya chuma ya kuning'iniza vitu kama nguo na mikoba, shehena ya kuwekea viatu, na dirisha kubwa ukutani lililofunikwa kwa pazia refu na kuacha upande mmoja tu ndiyo uwe wazi kupitisha hewa bila shaka.

Harufu ile nzuri ya Ankia ilikijaza vyema chumba hicho, nami nikaachia tabasamu hafifu baada ya kuona jinsi kitanda chake kilivyopambwa vizuri. Siyo mashuka wala mito, ila Ankia ndiye aliyekuwa pambo lenyewe.

Mwanamke huyo alikuwa amejilaza kwenye kitanda hicho kwa kulalia tumbo, huku miguu yake akiitandaza kiasi na mikono yake akiikunja na kuikutanisha usawa wa kichwa chake; akiulaza uso wake kwenye viganja vyake alivyoviunganisha pamoja.

Alikuwa amevaa khanga moja pekee mwilini, ikifanya mlima wake hapo nyuma uonekane vyema kwa jinsi ulivyotuna, na mapaja yake yenye nyamanyama yakiwa wazi kwa nyuma. Uhlalaah! Ilikuwa kama vile ni chakula kimewekwa mezani, na mimi nikitakiwa kuwa mlaji ningeamua tu nianze kukitafunia wapi.

Huyu mwanamke kweli alikuwa ameamua kunionyesha, na mimi nisingemvunja moyo. Alikuwa ananiangalia huku akitabasamu kwa njia ya shau, lile tabasamu la kuonyesha tunaelewana sana, nami nikaingia humo na kusimama usawa wa kitanda huku nikimwangalia.

"Keki hiyo..." nikamwambia hivyo kwa sauti ya chini.

Akaelekeza fikira zake katikati ya suruali niliyovaa kwa kutazama namna ilivyokuwa imeanza kuvimba, naye akaniangalia tena machoni.

"Naona umeuandaa msosi vyema. Ama ulikuwa unataka kulala?" nikamuuliza.

Akafumba macho yake na kutikisa kichwa kukataa.

Nikakaa kitandani usawa wa miguu yake, nami nikaanza kutembeza vidole viwili kwenye mguu wake wa kushoto kwa kuvipandisha kuelekea pajani.

"Siyo siri Ankia... umenona," nikamwambia hivyo.

"Asante," akanena hivyo kwa sauti ya chini.

"Nina njaa ujue... njaa ya kula hiki chakula chako. Ila nahitaji kujua kama itakuwa salama kula mpaka mwisho," nikamwambia hivyo.

"Ni salama. We' kula tu," akaniambia.

Huku nikitekenya mguu wake, nikamuuliza, "Kweli? Chombo ni safi?"

"Imetakata kabisa..."

"Kwa hiyo nijilie tu?"

"Kula. Yote yako..."

Ah! Kudadeki! Akaendelea kutulia tu, nikimwona namna alivyoibana na kuiachia midomo yake mara kwa mara, nami nikaamua kukatisha maneno ili nianze kushughulika kweli na hiyo keki.

(.........).

(.........).

(.........).

(.........).

(.........).

Miguu yake nikiwa nimeitanua na yeye kuishika ili ibaki hewani, nilipiga huyu mwanamke haswa mpaka akawa anaomba po kila mara. Angenisukuma niache kidogo, nami ningerejea tena na kuendelea kumtandika. Alikuwa anaongea maneno ya kiingereza na kikabila cha wazaramo, raha ikiwa imemkolea haswa, nami nikaendelea kupiga, piga, piga, PI-GA!

Kuna haka kamsukumo kalikonishawishi niendelee tu na mimi mpaka kufikia sehemu ya mridhiko, nayo ikaja. Nilikuwa naongeza kasi, huku nikiwa nimeushika kwa nguvu mkono wake Ankia aliourudisha nyuma, na alikuwa anatoa sauti ya juu kweli kwenye miguno yake huku jina langu akilitamka kwa njia yenye deko, nami nikajiachia ndani yake hatimaye.

Niikunja sura huku nikishtuka-shtuka, nami nikalibana tumbo lake kwa chini na yeye akiirudisha mikono yake kuning'ang'ania mapajani ili niendelee kumwagilia tu pango lake laini. Si alisema ilikuwa salama kabisa? Mimi nikaishushia kwa ndani ukweli. Ikafata sasa ile sehemu ambayo tukishagamaliza hiyo kitu tunaanza kuwaona wenzetu kuwa kama nguruwe!

Ila hapana, sikumwona Ankia kuwa nguruwe. Ni uchovu tu wa raha niliopata maana ni muda mrefu kiasi sikuwa nimejiachia namna hiyo kwa mwanamke, tena ndani kabisa. Nimefanya uhuni mwingi sana kiasi kwamba hata tu kumwambia mtu mimi ni daktari haikuonekana kuwa kweli, maana madaktari hupendaga kujionyesha wana aina fulani ya utakatifu lakini ndiyo watu wakatili na wachafu zaidi hapa duniani! Natania tu.

Riadha yangu na Ankia ikawa imeishia hapo, angalau kwa wakati huu. Mwanamke huyu akawa anazungusha nyonga yake taratibu huku bado nikiwa ndani yake, nikiwa nimemlalia kwa juu, na nikihisi jinsi ambavyo baadhi ya watoto wangu walivyokuwa wakimtoka kidogo-kidogo. Yeah... sikuwa nimemwagilia bustani muda mrefu.

Nikaanza kupitisha kiganja changu usoni kwake, naye akaingiza kidole changu kimoja mdomoni mwake na kuanza kukinyonya. Jasho lake na langu lilifanya ngozi ziteleze kwa namna tulivyoibana miili yetu, nami nikaitoa mashine yangu ndani yake na kulipiga kalio lake kofi zito kiasi.

"Hapo vipi? Umekaa sawa?" nikamuuliza hivyo baada ya kukitoa kidole mdomoni mwake.

"Mhm... una mapigo matamu JC..." akaniambia hivyo.

"Hata wewe uko vizuri. Utanifanya nioge kwa mara ya pili," nikamwambia.

Alionekana kuchoka, kwa kuwa aliendelea kulala namna hiyo hiyo huku akinitazama kilegevu.

"Makeke yamepungua sasa, au siyo? Ngoja me nikaoge..." nikamwambia hivyo.

"Tangulia nije..." akasema hivyo.

"A-ah... we' tulia, me naenda kuoga kwanza halafu ndiyo utafata..."

"Kwa nini tusioge wote?"

"Macho mengi."

"Asa' hapo nani atatuona? Halafu we' si huwa haujali watu? Unamwogopa nani sasa?"

"Simwogopi mtu. Ila mimi siyo wa hivyo. Napenda ya ndani yawe ya ndani, siyo mpaka kila mtu ajue. Na huu mtaa wenu umekaa kama wa Kazamoyo," nikamwambia.

"Mh? Haya baba. Chochote kile kwa ajili yako, mi' nitafanya. Umenipa raha kweli... we' siyo mchezo..." akasema hivyo.

Nikatabasamu kidogo na kuanza kuivaa boksa.

"Una mdude mzuri kweli," akaniambia hivyo.

"Hata we' kakwako kazuri..."

"Kana uzuri gani?"

"Kamevimba, katamu. Nilidhani ningekuta ndoo ila nilipoona siyo, nikashukuru Mungu," nikamtania.

Akacheka na kunitusi kimasihara, halafu akaziba mdomo wake baada ya kutambua amenitukana kwa kuponyokwa.

Nikakaa kitandani na kumsonta kwa kidole huku nimemkazia macho, kama kumwambia sijapenda jambo hilo, naye akakaa kabisa.

"Nisamehe... imenitoka tu..." akaniambia hivyo na kuibana midomo yake.

Nikatabasamu na kusema, "Usijali, nakutania tu. Ila ni kweli... we' ni mtamu sana."

Akatabasamu kidogo kwa haya, naye akasema, "Wewe pia."

"Me naenda sa' kujimwagia, af' naingia kulala. Sawa?" nikamwambia hivyo na kusimama.

"Hauli?" akaniuliza.

"Nimeshiba. Zawadi mweupe kanipa kande."

"Aaa... umeongea nao?"

"Ndiyo."

"Wamesemaje?"

"Wamenikubalia. Nataka nimsaidie Mariam na shida aliyonayo, ikiwa mambo yataenda vizuri, basi atakaa sawa."

"Unataka kumsaidiaje sasa?"

"Utaona. Ila ndo' napaswa niongee na dada yake kwanza."

"Walikuwa hawajarudi bado? Nimesikia kama gari limeingia..."

"Ndo' wamerudi me ninatoka, nitatafuta tu wakati mwingine niongee naye. Nataka sana nimsaidie huyu msichana. Niombee nifanikiwe," nikamwambia hivyo.

Akatabasamu.

"Nini?" nikamuuliza.

Akatikisa kichwa na kusema, "Una roho nzuri. Natamani ningekumiliki kimoja."

Nikatabasamu na kuokota nguo zangu huku nikimwambia, "Siyo roho nzuri, sema ni hicho kimoja nilichokupiga hapo ndiyo kimekumaliza akili kabisaa. Usijali. Utakipata tu tena. Endelea tu kuwa mtoto mzuri."

Akatabasamu na kuniangalia kwa madaha.

Nikamsogelea na kumpiga busu kavu mdomoni, hii ndiyo naiita busu ya kishkaji, nami nikatoka chumbani kwake hatimaye.

★★

Nilikuja kuamka mida ya saa kumi na mbili kasoro, jioni, nami nikanyanyuka kutoka kitandani na kuvaa nguo nyepesi. Tokea nilipomaliza tu ile ishu yangu na Ankia muda mfupi nyuma, nilienda kuoga na kisha kuja kulala kidogo, muda huu nikiwa ndiyo nimeamka sasa.

Nikachukua simu na kukuta jumbe chache pamoja na missed call kutoka kwa Chalii Gonga, nami nikaamua nimtolee jamaa uvivu hatimaye na kumpigia. Alipopokea, akaanza kuniuliza kwa nini sikuwa nikijibu miito yake, nami nikamwambia sikuwa karibu na simu leo kutokana na kuiacha ndani ipigwe chaji wakati nilipokuwa nimetoka.

Nilibuni hadithi hiyo upesi kwa kusema yaani ndiyo nilikuwa nimerudi tu sasa hivi, nami nikamuuliza ikiwa kulikuwa na jambo muhimu alitaka kunieleza. Akasema amenitafuta mno maana alitaka tukae pamoja sehemu nzuri tufurahie mambo matamu-matamu, na mimi nikiwa nimeshamwelewa vizuri nikamwambia tu tungetanya hivyo wakati mwingine.

Akaniuliza kama ningeenda Masai baadaye, nami nikasema haikuwa jambo la uhakika, lakini akasema tu nije kwenda huko na nikifika niagize chochote naye angekuja kulipia. Dah! Jamaa alikuwa ameanza kuleta mambo nisiyofagilia hata kidogo; shobo nyingi. Alisema na yeye hakuwa mtu wa shobo sana ila kwangu alikuwa ameanza kushoboka mno, na ili kumridhisha tu nikasema poa, ningefanya hivyo.

Tukaachiana hapo, nami nikaingia upande wa jumbe fupi na kumjibu Tesha, aliyekuwa anauliza kama tutaingia Masai ama tukatembee Mbagala. Nikamwambia tutaenda Masai mida ya saa moja, kwa hiyo apite hapa kwa Ankia ili twende.

Baada ya hapo, nikatoka chumbani hatimaye na kwenda sebuleni. Ankia hakuwepo sehemu yoyote kati ya sebule na jikoni, nami nikakisia kuwa huenda alikuwa amelala bado. Yeye pia aliniambia angelala, kwa hiyo nikaenda tu kwenye sofa na kukaa.

Nikapitia-pitia mitandao ya kijamii kidogo na kusoma vipengele fulani vifupi vya masuala ya kitabibu, kisha nikaachana na simu ili umakini wangu niuweke kwenye ile feni ya Ankia. Nikaifata na kuanza kuichunguza hapa na pale, nikijaribu kuiwasha na kubashiri tatizo lingekuwa wapi mpaka giza lilipoanza kuvizia kuingia, hali hiyo ikifanya ndani pawe na ugiza.

Ni taa ya sebule iliyowashwa ndiyo ikanifanya niachane na feni hiyo baada ya kumwona mama mwenye nyumba wangu akiwa amesimama sebuleni hapo. Nikampa tabasamu dogo la mapokezi, naye akatabasamu pia huku akifikicha jicho lake moja.

Akiwa ametoka kuamka, kasura kake kalivimba kiasi, na mwilini alivaa ile ile khanga moja niliyomkuta nayo muda ule chumbani, kitu ambacho kikanikumbusha mchezo wetu mzuri uliomwacha akinimwagia sifa za mimi kuwa fundi.

"Good morning," nikamwambia hivyo kiutani.

"Unaniona kama sijasoma? Morning sa'hivi?" akaniuliza.

"Angalia saa uone. Ndo' inaingia saa moja. Ubishi wa nini?"

"Kichwa chako! Iko saa moja moja kwani?"

"Ziko ngapi, ishirini?"

"Hebu acha mambo yako. Umeamka zamani?"

"Hamna, sina muda mrefu. We' ndo' unalala kama gogo."

"Nilikuwa nimechoka..."

Akasema hivyo na kuja kukaa kwenye sofa karibu na sehemu niliyochuchumaa kwa kupiga goti moja chini, huku feni ikiwa mkononi mwangu. Nikaendelea kuichokonoa.

"Umeweza kuitengeneza?" akaniuliza.

"Hamna... ila we' ngoja. Hii inazunguka sasa hivi tu, mapemaa..."

"Mhm... haya bwana. We' ndo' fundi, nakuaminia..."

"Haupingwi kwa hilo mama..."

Akatabasamu kidogo na kunishika begani. Akatulia na kuendelea kunitazama nilipoendelea kutia juhudi kuirekebisha feni hiyo, kisha nikaifunga na kujaribu kuiwasha. Si ikaanza kuzunguka! Ankia akaachama kimshangao, huku na mimi nikitabasamu kwa furaha, halafu nikamwangalia kwa macho yenye kiburi. Akacheka kwa furaha na kunikumbatia, akisema amekubali sana maajabu yangu.

Nikaiweka feni pembeni na kukaa karibu yake, ikiwa inatupuliza sasa angalau kupunguza joto, nami nikasema, "Mishe gani sa'hivi?"

Akashusha pumzi na kusema, "Labda kupika. Nilikutunzia ugali mchana... ila najua sa'hivi hautaliwa. Inabidi tu nikafate mboga sokoni halafu nije kupika na ubwabwa... tule."

"Mboga gani?"

"Sijui samaki... au nyama?"

"Ahirisha tu..."

"Kwa nini? Yaani tusile?"

"A-ah... tutakula. Nataka twende Masai. Tutakula huko," nikamwambia.

Akaachia tabasamu na kuuliza, "Unanitoa dinner eh?"

"Ahahah... hapana, usikijaze kichwa chako hayo mambo. Tunaenda na Tesha," nikamwambia.

"Aaaa.... nikafikiri mimi na wewe tu. Afadhali lakini, sitasumbuka. Mwanaume wangu anaenda kuninunulia msosi, nitake kipi kingine?"

"Ahaa... Basi nitakuwa nakupeleka tu kula msosi, sawa? Ila suala la kukupelekea moto sahau..." nikamtania.

"Ila wewe..."

"Nini sasa? Si hautaki kingine ila msosi?"

"Mm... me sitaki..."

"Unataka nini? Kula lazima, kuliwa hiari..."

Akacheka kidogo na kunilalia begani.

Simu yangu ikaanza kuita, nami nikaitoa na kukuta namba ngeni. Agh! Sikupenda kabisa kupokea namba nisizozifahamu maana usumbufu ulikuwa mwingi sana, naye Ankia alipoona sipokei, akaiangalia namba hiyo kwenye kioo cha simu yangu.

"Nani?" akaniuliza.

"Ah... sijui... me sipokei," nikamjibu.

"Kwa nini sasa? Je kama ni muhimu?"

"Atume ujumbe. Mimi simu nisizozifahamu huwa sipokei..."

"Sasa ndo' nini?"

"Ndiyo hivyo."

"Je kama ni Tesha? Au mtu mwingine mnayefahamiana naye?"

"Hakuna. Mimi watu naofahamiana nao huwa nawa-save. Sipendagi usumbufu wa namna hii..."

Simu ikakata, kisha ikaanza kuita tena; namba ikiwa hiyo hiyo.

"Agh..."

"Pokea tu JC. Hataacha kupiga usipopokea. Tuchukulie ni ndugu yako. Nisikilize tu. Pokea..."

"Na nikikuta siyo? Nikufanyeje?"

"Nifanye chochote unachotaka..." akanijibu kwa nyodo.

"Mmm... haya..."

Nikapokea simu hiyo hatimaye, nami nikaiweka sikioni. Sikuzungumza, lakini aliyekuwa upande wa pili alipoanza kuongea, nikaweka uso makini.

"JC... hhh... JC..."

Sauti hii niliifahamu, ikiwa ni ya mwanamke. Uzito wa namna ambayo ililiita jina langu uliniambia kwamba mwanamke huyu alikuwa akilia.

"JC... naomba unisaidie... njoo.... p... njoo tafadhali..."

Ilikuwa ni Joy.

Nilishangaa kiasi. Sikuwa na kumbukumbu ya kumpa namba yangu lakini hilo halikuwa lenye umuhimu sana kwa wakati huu. Nilijiuliza alikuwa amepatwa na nini kilichohitaji mimi ndiyo nimpe msaada. Sikutaka kujiingiza kwenye shida zingine zaidi za watu wa aina yake lakini jambo hili lilivuta hisia zangu za kujali kumwelekea. Alikuwa amekumbwa na nini huyu mwanamke?



★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA KUMI

★★★★★★★★★★★★


Baada ya mazungumzo hayo yenye kuchochea hisia pamoja na mama wakubwa, Bi Zawadi akasema angekwenda kuniwekea makande aliyopika ili nile hatimaye, nami nikakubali hilo na kisha kurudi kukaa sofani.

Wote kwa pamoja walitaka kujua mengi kuhusu udaktari wangu, nami nikawaelezea kwa njia nyepesi tu kuhusiana na masuala ya vitengo vya utabibu nilivyohusika navyo, muda ambao nilifanya kazi kwenye hospitali ile, mpaka kufikia wakati huu nilioamua kuchukua likizo fupi na kuja kukaa huku Mbagala.

Sasa wakaweza kunielewa vizuri hata zaidi, wakiniona kuwa kama mtu wa muhimu sana, lakini nikawaambia mimi kwao bado ni kijana mdogo mno na ninapenda kujiona kuwa chini ya wengine; hasa kama ninawaheshimu sana.

Nikaweka wazi kwao lengo langu la kuja kuishi huku kuwa kujaribu aina tofauti ya maisha niliyozoea kwa maeneo tofauti niliyopitia na kuishi, kama vile kujisahaulisha kwamba mimi nilikuwa daktari. Nimekaa kwenye vyumba vingi vya hospitali na kuzungukwa na watu wengi wenye kuhitaji msaada kwa muda mrefu kiasi, kwa hiyo nilihitaji kupumzika kidogo ndiyo nije kuendelea na wajibu wangu kama tabibu baadaye.

Kande lilikuwa tamu sana. Nikamaliza na kumshukuru Bi Zawadi, na ni hapo ndiyo sisi wote tukasikia honi ya gari nje ya geti la nyumba hii. Bi Zawadi akasema kwamba bila shaka huyo angekuwa ni Miryam, naye akataka kwenda kufungua geti lakini nikamwomba nimsaidie kufanya hivyo ili atulie tu ndani hapo. Akakubaliana na hilo.

Nikaangalia muda kwenye simu yangu na kuona ilikuwa ni saa tisa alasiri sasa; ikionyesha Miryam na Tesha walitumia muda mrefu sana huko ofisini kwa mwenyekiti, ama labda walikwenda na sehemu nyingine pia ukitegemea walitoka na gari.

Nikaenda hapo getini na kuiona pickup ya bibie ikiwa hapo nje, nami nikalifungua geti kuruhusu gari liingie. Vuuu likapita ndani, nami nikafunga tena geti.

Nilipokuwa ndiyo nimemaliza tu kulifunga, nikaangalia gari hilo na kuwaona Miryam, Tesha, pamoja na Shadya wakiwa wameshashuka, wanawake hao wakiwa wananitazama usoni kwa umakini, huku Tesha akija niliposimama.

Akanifikia karibu, nasi tukagonga tano huku akisema, "Vipi mwamba?"

"Poa tu. Za huko?" nikamuuliza.

Hakutoa jibu, bali akaangalia chini na kushusha pumzi, kisha akapigisha ulimi wake kidogo mdomoni kama vile kuonyesha amevunjwa moyo na jambo fulani, naye akageukia upande aliosimama Miryam. Mimi pia nikamwangalia mwanamke huyo, ambaye alikuwa ananiangalia kwa njia tulivu tu, nami nikampungia mkono kidogo kama kumpa salamu.

"We' JC? Vipi? Akina shangazi wameshakugeuza gateman?" Shadya akaniuliza hivyo kiutani.

Nikatabasamu na kumwambia, "Na mshahara wameshanipa."

Akacheka kidogo na kumwangalia Miryam, lakini mwanamke huyo alikuwa serious kama vile amemeza chura au nini, naye akaelekea tu ndani. Shadya akatoa mifuko fulani yenye kujaa vitu vingi ndani ya gari hilo na kumfata Miryam ndani huko pia, nikibaki mimi na kijana Tesha hapo nje.

"Mambo yameendaje?" nikamuuliza.

"Ah... sister anazingua JC..." Tesha akaniambia.

"Kafanyaje? Hamjamshtaki ka... a... huyo... huyo jamaa?" nikauliza tena.

"Umeona mwanangu? Hata wewe umetegemea tungemshtaki huyo fala, afungwe. Sasa Mimi si mama huruma sana? Kawaambia wamwachie," Tesha akaongea kwa sauti iliyoonyesha kuudhika kwake.

"Kawaambia wamwachie? Yaani kama vile amemwombea msamaha au?"

"Agh, mizinguo tu kaka! Hilo fala limemtukana hapa, lingeiba ishu ya Mamu, afu' tu eti anaenda kumwambia mzee Hamadi wamwachie jamaa! Imenidis sana..."

"Labda anaona kumfunga ndugu yenu haitafaa. Ameongea naye kwani?"

"Eee... Joshua ametoa makamasi hapo ndo' Mimi akamwonea huruma eti. Wamemwambia lakini wasije kusikia amezusha fujo wala chochote kile tena la sivyo watamfunga bila kujali huruma za dada. Ah... me nilikuwa natamani aende akanyee debe leo! Basi tu..." Tesha akasema hivyo.

Nikatabasamu kidogo na kusema, "Dada yako siyo mtu wa visasi inaonekana. Halafu... anaijali familia yenu, nyie wote yaani, hata kama huyo Joshua kapotea. Mwelewe tu... na umuunge mkono. Sawa?"

"Agh... bado inakera bana. Nilitaka nimwone huyo bwege amevaa karoti leo nije kula kuku mimi. Sasa sa'hivi nakuja kula tu kande huku nimevimba, ndo' nini? Ah..." akaongea kwa kuudhika.

"Ahahah... nenda kale kande, litapunguza hasira. Ni tamu," nikasema.

"Umeshakula?"

"Yah, Bi Zawadi kanionjesha."

"Au siyo? Sawa, ngoja na me nikale, nipige maji afu'... ah... mishe gani unafanya baadaye?"

"Nipo tu."

"Sijui twende tukazurure tu Mbagala? Ningekuwa na mshiko tungeshindia Masai..."

"Ahahaha... Gonga amenipigia mara kadhaa, sijui anataka nini..." nikamwambia.

"Ih, kweli? Hujapokea?"

"Hamna, sioni haja. Nahisi kama atan'sumbua tu..."

"A-ah... usizingue. Mtafute, najua anataka kukuita. Fanya mambo basi, uniunganishe na mimi angalau tukazimue za ofa, ama nini?"

"Ahahah... Tesha unapenda kunywa wewe!"

"Hahaha... aaa siyo sana. Ila hizi ofa kabambe siyo za kupitwa. Fanya mambo tuilambe hiyo," akasema hivyo na kuniwekea ngumi usawa wa kifua changu.

Nikaigonga kwa ngumi yangu pia na kusema, "Haya bana. We' nenda kale, tutashtuana baadaye. Waambie mama wakubwa nimeondoka eh? Tutaonana tu hata kesho."

"Haya poa kaka," akasema hivyo.

Tukaachana kiaina hiyo, nami nikarudi moja kwa moja mpaka ndani kwake Ankia.

Nilikuwa nimeijaza akili yangu mambo mengi kutokea asubuhi hii, lakini sasa angalau ilikuwa imepewa wepesi kiasi baada ya kuzungumza na Bi Zawadi na Bi Jamila kuhusiana na familia yao. Kilichokuwepo sasa ilikuwa kutafuta muda mzuri wa kuongea na dada mkubwa, Miryam, kuhusu suala la tatizo lililomwathiri mdogo wake, na ndiyo ningeanza kweli kumsaidia Mariam.

Nilipofika sebuleni hapo sikumkuta Ankia, nami nikasogea mpaka upande wa kuelekea jikoni nikidhani angekuwa huko lakini nikamkosa. Bila shaka angekuwa chumbani kwake, labda kalala, na nilipokuwa nimeamua tu kuelekea chumbani kwangu ili nikapumzike, mwanamke huyo akaniita kutokea chumbani kwake.

"JC..."

Nikaitika, "Naam..."

Sauti yake ikasema, "Ndo' umerudi?"

"Ndiyo. Ndo' naingia..."

"Funga basi huo mlango halafu uje..."

"Mlango wa sebule?"

"Eeee..."

"Kuna nini tena huko weye?" nikauliza kiutani.

Nikasikia akicheka, naye akasema, "Njoo bwana."

Tayari nilikuwa najua mambo ya kutarajia nikienda chumbani kwa mwanamke huyo, na kiukweli kwa muda huu nilikuwa na mhemko ufaao kukutana nayo hayo mambo. Si ni ile kuvutiana-vutiana sana na mwanamke huyo aliyekuwa amenielewa kupitiliza? Kwa hiyo kama alitaka nimpe alichokitaka sasa hivi, nilikuwa nimeamua kumtolea uvivu.

Nikaenda kuufunga mlango, yaani kuufunga kwa funguo, hiyo ikiwa ndiyo maana yake nilijua hivyo. Nikaenda mpaka kwenye mlango wa chumba cha mama mwenye nyumba wangu, nami nikaufungua na kuingia ndani humo.

Kilikuwa chumba chenye upana kiasi, kukiwa na kitanda kikubwa cha tano ya sita, kabati la nguo na stendi ya chuma ya kuning'iniza vitu kama nguo na mikoba, shehena ya kuwekea viatu, na dirisha kubwa ukutani lililofunikwa kwa pazia refu na kuacha upande mmoja tu ndiyo uwe wazi kupitisha hewa bila shaka.

Harufu ile nzuri ya Ankia ilikijaza vyema chumba hicho, nami nikaachia tabasamu hafifu baada ya kuona jinsi kitanda chake kilivyopambwa vizuri. Siyo mashuka wala mito, ila Ankia ndiye aliyekuwa pambo lenyewe.

Mwanamke huyo alikuwa amejilaza kwenye kitanda hicho kwa kulalia tumbo, huku miguu yake akiitandaza kiasi na mikono yake akiikunja na kuikutanisha usawa wa kichwa chake; akiulaza uso wake kwenye viganja vyake alivyoviunganisha pamoja.

Alikuwa amevaa khanga moja pekee mwilini, ikifanya mlima wake hapo nyuma uonekane vyema kwa jinsi ulivyotuna, na mapaja yake yenye nyamanyama yakiwa wazi kwa nyuma. Uhlalaah! Ilikuwa kama vile ni chakula kimewekwa mezani, na mimi nikitakiwa kuwa mlaji ningeamua tu nianze kukitafunia wapi.

Huyu mwanamke kweli alikuwa ameamua kunionyesha, na mimi nisingemvunja moyo. Alikuwa ananiangalia huku akitabasamu kwa njia ya shau, lile tabasamu la kuonyesha tunaelewana sana, nami nikaingia humo na kusimama usawa wa kitanda huku nikimwangalia.

"Keki hiyo..." nikamwambia hivyo kwa sauti ya chini.

Akaelekeza fikira zake katikati ya suruali niliyovaa kwa kutazama namna ilivyokuwa imeanza kuvimba, naye akaniangalia tena machoni.

"Naona umeuandaa msosi vyema. Ama ulikuwa unataka kulala?" nikamuuliza.

Akafumba macho yake na kutikisa kichwa kukataa.

Nikakaa kitandani usawa wa miguu yake, nami nikaanza kutembeza vidole viwili kwenye mguu wake wa kushoto kwa kuvipandisha kuelekea pajani.

"Siyo siri Ankia... umenona," nikamwambia hivyo.

"Asante," akanena hivyo kwa sauti ya chini.

"Nina njaa ujue... njaa ya kula hiki chakula chako. Ila nahitaji kujua kama itakuwa salama kula mpaka mwisho," nikamwambia hivyo.

"Ni salama. We' kula tu," akaniambia.

Huku nikitekenya mguu wake, nikamuuliza, "Kweli? Chombo ni safi?"

"Imetakata kabisa..."

"Kwa hiyo nijilie tu?"

"Kula. Yote yako..."

Ah! Kudadeki! Akaendelea kutulia tu, nikimwona namna alivyoibana na kuiachia midomo yake mara kwa mara, nami nikaamua kukatisha maneno ili nianze kushughulika kweli na hiyo keki.

(.........).

(.........).

(.........).

(.........).

(.........).

Miguu yake nikiwa nimeitanua na yeye kuishika ili ibaki hewani, nilipiga huyu mwanamke haswa mpaka akawa anaomba po kila mara. Angenisukuma niache kidogo, nami ningerejea tena na kuendelea kumtandika. Alikuwa anaongea maneno ya kiingereza na kikabila cha wazaramo, raha ikiwa imemkolea haswa, nami nikaendelea kupiga, piga, piga, PI-GA!

Kuna haka kamsukumo kalikonishawishi niendelee tu na mimi mpaka kufikia sehemu ya mridhiko, nayo ikaja. Nilikuwa naongeza kasi, huku nikiwa nimeushika kwa nguvu mkono wake Ankia aliourudisha nyuma, na alikuwa anatoa sauti ya juu kweli kwenye miguno yake huku jina langu akilitamka kwa njia yenye deko, nami nikajiachia ndani yake hatimaye.

Niikunja sura huku nikishtuka-shtuka, nami nikalibana tumbo lake kwa chini na yeye akiirudisha mikono yake kuning'ang'ania mapajani ili niendelee kumwagilia tu pango lake laini. Si alisema ilikuwa salama kabisa? Mimi nikaishushia kwa ndani ukweli. Ikafata sasa ile sehemu ambayo tukishagamaliza hiyo kitu tunaanza kuwaona wenzetu kuwa kama nguruwe!

Ila hapana, sikumwona Ankia kuwa nguruwe. Ni uchovu tu wa raha niliopata maana ni muda mrefu kiasi sikuwa nimejiachia namna hiyo kwa mwanamke, tena ndani kabisa. Nimefanya uhuni mwingi sana kiasi kwamba hata tu kumwambia mtu mimi ni daktari haikuonekana kuwa kweli, maana madaktari hupendaga kujionyesha wana aina fulani ya utakatifu lakini ndiyo watu wakatili na wachafu zaidi hapa duniani! Natania tu.

Riadha yangu na Ankia ikawa imeishia hapo, angalau kwa wakati huu. Mwanamke huyu akawa anazungusha nyonga yake taratibu huku bado nikiwa ndani yake, nikiwa nimemlalia kwa juu, na nikihisi jinsi ambavyo baadhi ya watoto wangu walivyokuwa wakimtoka kidogo-kidogo. Yeah... sikuwa nimemwagilia bustani muda mrefu.

Nikaanza kupitisha kiganja changu usoni kwake, naye akaingiza kidole changu kimoja mdomoni mwake na kuanza kukinyonya. Jasho lake na langu lilifanya ngozi ziteleze kwa namna tulivyoibana miili yetu, nami nikaitoa mashine yangu ndani yake na kulipiga kalio lake kofi zito kiasi.

"Hapo vipi? Umekaa sawa?" nikamuuliza hivyo baada ya kukitoa kidole mdomoni mwake.

"Mhm... una mapigo matamu JC..." akaniambia hivyo.

"Hata wewe uko vizuri. Utanifanya nioge kwa mara ya pili," nikamwambia.

Alionekana kuchoka, kwa kuwa aliendelea kulala namna hiyo hiyo huku akinitazama kilegevu.

"Makeke yamepungua sasa, au siyo? Ngoja me nikaoge..." nikamwambia hivyo.

"Tangulia nije..." akasema hivyo.

"A-ah... we' tulia, me naenda kuoga kwanza halafu ndiyo utafata..."

"Kwa nini tusioge wote?"

"Macho mengi."

"Asa' hapo nani atatuona? Halafu we' si huwa haujali watu? Unamwogopa nani sasa?"

"Simwogopi mtu. Ila mimi siyo wa hivyo. Napenda ya ndani yawe ya ndani, siyo mpaka kila mtu ajue. Na huu mtaa wenu umekaa kama wa Kazamoyo," nikamwambia.

"Mh? Haya baba. Chochote kile kwa ajili yako, mi' nitafanya. Umenipa raha kweli... we' siyo mchezo..." akasema hivyo.

Nikatabasamu kidogo na kuanza kuivaa boksa.

"Una mdude mzuri kweli," akaniambia hivyo.

"Hata we' kakwako kazuri..."

"Kana uzuri gani?"

"Kamevimba, katamu. Nilidhani ningekuta ndoo ila nilipoona siyo, nikashukuru Mungu," nikamtania.

Akacheka na kunitusi kimasihara, halafu akaziba mdomo wake baada ya kutambua amenitukana kwa kuponyokwa.

Nikakaa kitandani na kumsonta kwa kidole huku nimemkazia macho, kama kumwambia sijapenda jambo hilo, naye akakaa kabisa.

"Nisamehe... imenitoka tu..." akaniambia hivyo na kuibana midomo yake.

Nikatabasamu na kusema, "Usijali, nakutania tu. Ila ni kweli... we' ni mtamu sana."

Akatabasamu kidogo kwa haya, naye akasema, "Wewe pia."

"Me naenda sa' kujimwagia, af' naingia kulala. Sawa?" nikamwambia hivyo na kusimama.

"Hauli?" akaniuliza.

"Nimeshiba. Zawadi mweupe kanipa kande."

"Aaa... umeongea nao?"

"Ndiyo."

"Wamesemaje?"

"Wamenikubalia. Nataka nimsaidie Mariam na shida aliyonayo, ikiwa mambo yataenda vizuri, basi atakaa sawa."

"Unataka kumsaidiaje sasa?"

"Utaona. Ila ndo' napaswa niongee na dada yake kwanza."

"Walikuwa hawajarudi bado? Nimesikia kama gari limeingia..."

"Ndo' wamerudi me ninatoka, nitatafuta tu wakati mwingine niongee naye. Nataka sana nimsaidie huyu msichana. Niombee nifanikiwe," nikamwambia hivyo.

Akatabasamu.

"Nini?" nikamuuliza.

Akatikisa kichwa na kusema, "Una roho nzuri. Natamani ningekumiliki kimoja."

Nikatabasamu na kuokota nguo zangu huku nikimwambia, "Siyo roho nzuri, sema ni hicho kimoja nilichokupiga hapo ndiyo kimekumaliza akili kabisaa. Usijali. Utakipata tu tena. Endelea tu kuwa mtoto mzuri."

Akatabasamu na kuniangalia kwa madaha.

Nikamsogelea na kumpiga busu kavu mdomoni, hii ndiyo naiita busu ya kishkaji, nami nikatoka chumbani kwake hatimaye.

★★

Nilikuja kuamka mida ya saa kumi na mbili kasoro, jioni, nami nikanyanyuka kutoka kitandani na kuvaa nguo nyepesi. Tokea nilipomaliza tu ile ishu yangu na Ankia muda mfupi nyuma, nilienda kuoga na kisha kuja kulala kidogo, muda huu nikiwa ndiyo nimeamka sasa.

Nikachukua simu na kukuta jumbe chache pamoja na missed call kutoka kwa Chalii Gonga, nami nikaamua nimtolee jamaa uvivu hatimaye na kumpigia. Alipopokea, akaanza kuniuliza kwa nini sikuwa nikijibu miito yake, nami nikamwambia sikuwa karibu na simu leo kutokana na kuiacha ndani ipigwe chaji wakati nilipokuwa nimetoka.

Nilibuni hadithi hiyo upesi kwa kusema yaani ndiyo nilikuwa nimerudi tu sasa hivi, nami nikamuuliza ikiwa kulikuwa na jambo muhimu alitaka kunieleza. Akasema amenitafuta mno maana alitaka tukae pamoja sehemu nzuri tufurahie mambo matamu-matamu, na mimi nikiwa nimeshamwelewa vizuri nikamwambia tu tungetanya hivyo wakati mwingine.

Akaniuliza kama ningeenda Masai baadaye, nami nikasema haikuwa jambo la uhakika, lakini akasema tu nije kwenda huko na nikifika niagize chochote naye angekuja kulipia. Dah! Jamaa alikuwa ameanza kuleta mambo nisiyofagilia hata kidogo; shobo nyingi. Alisema na yeye hakuwa mtu wa shobo sana ila kwangu alikuwa ameanza kushoboka mno, na ili kumridhisha tu nikasema poa, ningefanya hivyo.

Tukaachiana hapo, nami nikaingia upande wa jumbe fupi na kumjibu Tesha, aliyekuwa anauliza kama tutaingia Masai ama tukatembee Mbagala. Nikamwambia tutaenda Masai mida ya saa moja, kwa hiyo apite hapa kwa Ankia ili twende.

Baada ya hapo, nikatoka chumbani hatimaye na kwenda sebuleni. Ankia hakuwepo sehemu yoyote kati ya sebule na jikoni, nami nikakisia kuwa huenda alikuwa amelala bado. Yeye pia aliniambia angelala, kwa hiyo nikaenda tu kwenye sofa na kukaa.

Nikapitia-pitia mitandao ya kijamii kidogo na kusoma vipengele fulani vifupi vya masuala ya kitabibu, kisha nikaachana na simu ili umakini wangu niuweke kwenye ile feni ya Ankia. Nikaifata na kuanza kuichunguza hapa na pale, nikijaribu kuiwasha na kubashiri tatizo lingekuwa wapi mpaka giza lilipoanza kuvizia kuingia, hali hiyo ikifanya ndani pawe na ugiza.

Ni taa ya sebule iliyowashwa ndiyo ikanifanya niachane na feni hiyo baada ya kumwona mama mwenye nyumba wangu akiwa amesimama sebuleni hapo. Nikampa tabasamu dogo la mapokezi, naye akatabasamu pia huku akifikicha jicho lake moja.

Akiwa ametoka kuamka, kasura kake kalivimba kiasi, na mwilini alivaa ile ile khanga moja niliyomkuta nayo muda ule chumbani, kitu ambacho kikanikumbusha mchezo wetu mzuri uliomwacha akinimwagia sifa za mimi kuwa fundi.

"Good morning," nikamwambia hivyo kiutani.

"Unaniona kama sijasoma? Morning sa'hivi?" akaniuliza.

"Angalia saa uone. Ndo' inaingia saa moja. Ubishi wa nini?"

"Kichwa chako! Iko saa moja moja kwani?"

"Ziko ngapi, ishirini?"

"Hebu acha mambo yako. Umeamka zamani?"

"Hamna, sina muda mrefu. We' ndo' unalala kama gogo."

"Nilikuwa nimechoka..."

Akasema hivyo na kuja kukaa kwenye sofa karibu na sehemu niliyochuchumaa kwa kupiga goti moja chini, huku feni ikiwa mkononi mwangu. Nikaendelea kuichokonoa.

"Umeweza kuitengeneza?" akaniuliza.

"Hamna... ila we' ngoja. Hii inazunguka sasa hivi tu, mapemaa..."

"Mhm... haya bwana. We' ndo' fundi, nakuaminia..."

"Haupingwi kwa hilo mama..."

Akatabasamu kidogo na kunishika begani. Akatulia na kuendelea kunitazama nilipoendelea kutia juhudi kuirekebisha feni hiyo, kisha nikaifunga na kujaribu kuiwasha. Si ikaanza kuzunguka! Ankia akaachama kimshangao, huku na mimi nikitabasamu kwa furaha, halafu nikamwangalia kwa macho yenye kiburi. Akacheka kwa furaha na kunikumbatia, akisema amekubali sana maajabu yangu.

Nikaiweka feni pembeni na kukaa karibu yake, ikiwa inatupuliza sasa angalau kupunguza joto, nami nikasema, "Mishe gani sa'hivi?"

Akashusha pumzi na kusema, "Labda kupika. Nilikutunzia ugali mchana... ila najua sa'hivi hautaliwa. Inabidi tu nikafate mboga sokoni halafu nije kupika na ubwabwa... tule."

"Mboga gani?"

"Sijui samaki... au nyama?"

"Ahirisha tu..."

"Kwa nini? Yaani tusile?"

"A-ah... tutakula. Nataka twende Masai. Tutakula huko," nikamwambia.

Akaachia tabasamu na kuuliza, "Unanitoa dinner eh?"

"Ahahah... hapana, usikijaze kichwa chako hayo mambo. Tunaenda na Tesha," nikamwambia.

"Aaaa.... nikafikiri mimi na wewe tu. Afadhali lakini, sitasumbuka. Mwanaume wangu anaenda kuninunulia msosi, nitake kipi kingine?"

"Ahaa... Basi nitakuwa nakupeleka tu kula msosi, sawa? Ila suala la kukupelekea moto sahau..." nikamtania.

"Ila wewe..."

"Nini sasa? Si hautaki kingine ila msosi?"

"Mm... me sitaki..."

"Unataka nini? Kula lazima, kuliwa hiari..."

Akacheka kidogo na kunilalia begani.

Simu yangu ikaanza kuita, nami nikaitoa na kukuta namba ngeni. Agh! Sikupenda kabisa kupokea namba nisizozifahamu maana usumbufu ulikuwa mwingi sana, naye Ankia alipoona sipokei, akaiangalia namba hiyo kwenye kioo cha simu yangu.

"Nani?" akaniuliza.

"Ah... sijui... me sipokei," nikamjibu.

"Kwa nini sasa? Je kama ni muhimu?"

"Atume ujumbe. Mimi simu nisizozifahamu huwa sipokei..."

"Sasa ndo' nini?"

"Ndiyo hivyo."

"Je kama ni Tesha? Au mtu mwingine mnayefahamiana naye?"

"Hakuna. Mimi watu naofahamiana nao huwa nawa-save. Sipendagi usumbufu wa namna hii..."

Simu ikakata, kisha ikaanza kuita tena; namba ikiwa hiyo hiyo.

"Agh..."

"Pokea tu JC. Hataacha kupiga usipopokea. Tuchukulie ni ndugu yako. Nisikilize tu. Pokea..."

"Na nikikuta siyo? Nikufanyeje?"

"Nifanye chochote unachotaka..." akanijibu kwa nyodo.

"Mmm... haya..."

Nikapokea simu hiyo hatimaye, nami nikaiweka sikioni. Sikuzungumza, lakini aliyekuwa upande wa pili alipoanza kuongea, nikaweka uso makini.

"JC... hhh... JC..."

Sauti hii niliifahamu, ikiwa ni ya mwanamke. Uzito wa namna ambayo ililiita jina langu uliniambia kwamba mwanamke huyu alikuwa akilia.

"JC... naomba unisaidie... njoo.... p... njoo tafadhali..."

Ilikuwa ni Joy.

Nilishangaa kiasi. Sikuwa na kumbukumbu ya kumpa namba yangu lakini hilo halikuwa lenye umuhimu sana kwa wakati huu. Nilijiuliza alikuwa amepatwa na nini kilichohitaji mimi ndiyo nimpe msaada. Sikutaka kujiingiza kwenye shida zingine zaidi za watu wa aina yake lakini jambo hili lilivuta hisia zangu za kujali kumwelekea. Alikuwa amekumbwa na nini huyu mwanamke?



★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
Shukrani
 
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA KUMI NA MOJA

★★★★★★★★★★★★★★★★


"Joy..." nikaita hivyo huku nikimwangalia Ankia.

Ankia akaniangalia kiumakini pia.

"Njoo JC... nakuombaaa..." Joy akaendelea kulia.

"Wewe, umekuwaje? Nini shida?" nikamuuliza.

"JC nakuomba... nakuomba uje..."

"Nije wapi? Umefanyaje? Sikuelewi..."

"Hhh... njoo... nimepigwa... njoo JC..." akasema hivyo.

"Umepigwa na nani? Uko wapi?" nikamuuliza.

Hakujibu kitu na kuendelea kulia, nami nikamwangalia Ankia kimaswali. Akanionyesha ishara kwamba niweke mfumo wa kipaza sauti kwenye simu, nami nikafanya hivyo ili amsikie pia. Joy akawa akisikika vyema zaidi sasa namna alivyolia.

"We' Joy... niambie uko wapi..." nikasema hivyo.

"Hhh... Kongowe... nipo... hapa...."

"Nani amekupiga, amekupiga wapi? Eleweka basi..."

"Njoo JC... nakuomba... uje unitoe huku... JC nimeumia..."

Khh! Nikaona mwanamke huyo ananichanganya tu, hivyo nikakata simu na kuangalia pembeni kwa kuudhika.

Ankia akasema, "JC... mbona umekata simu? Joy... Joy anaonekana kuwa na shida... ameumia..."

"Me siyo mtoto mdogo Ankia. Tumia akili na wewe basi..." nikamwambia hivyo kwa kuudhika.

"Una maana gani?" akaniuliza.

"Huyu mwanamke anataka kunipanda. We' ndo' ulimpa namba yangu?" nikamuuliza.

Akabaki kunitazama tu usoni.

"Nijibu Ankia..." nikamwomba.

"Ee... alichukua namba yako kwangu... hiyo juzi. Aliichukua aliponisimulia mliyofanya chumbani kwako..." akaniambia hivyo.

"Achana na hayo. Huyu mwanamke anataka kunizoea vibaya, na mimi hiyo juzi nilikuwa nimelewa ndo' maana nikafanya naye. Asa' hapa ataanza kunisumbua kijinga tu..."

"Je kama amepigwa kweli? Labda yuko kwenye hali mbaya..."

"Asingekuwa ananifahamu angempigia nani?" nikauliza.

"Sijui, labda mabwana zake..."

"Awapigie hao hao sasa..." nikasema hivyo kwa kuudhika.

Simu ikaanza kuita tena, ikiwa ni Joy, nami nikakata upesi. Nikaiwekea namba hiyo ya Joy kizuizi (block) ili isinisumbue tena, haijalishi alikuwa anamwaga vipi machozi huko alikokuwa.

Ankia akatulia tu, akiona namna ambavyo hali hiyo ilikuwa imenikera sana, nami nikamwambia afanye kujiandaa kabla ya Tesha kuja ili tuelekee Masai kujichangamsha kidogo, kisha nikatoka hapo na kuelekea chumbani kwangu.

★★

Tesha hakukawia kuja hapo kwa Ankia baada ya mimi kuipuuzia simu ile iliyonikera kutoka kwa Joy, na alikuwa amevaa kwa njia ya kawaida ya kinyumbani tu. Hata mimi pia nilitinga nguo zangu za kawaida tu japo ningeonekana kupendeza mno kama kawaida yangu.

Ni Ankia ndiye aliyejiwekea mwonekano matata. Alivaa nguo kama shati laini tu lenye mikono mirefu, jeupe, lililoishia sehemu ya chini ya mapaja yake. Yaani kama angeinama kuokota kisoda, huko nyuma angeangusha tamasha!

Hilo shati, sijui gauni fupi, lilikuwa lenye kuonyesha ngozi yake ya ndani, kwa hiyo hata sidiria yake nyeupe pamoja na kikaptura cha skinny nyeusi kifupi sana alichovaa kwa chini zilionekana; na hapo ndiyo nikawa nimengundua kumbe huyu mwanamke alijua kujiachia. Jinsi alivyoiweka tu sidiria yake isogeze kifua mbele aisee! Ilikuwa ni makusudi yenye kutamanisha. Tesha alimsifia na kuniambia nijichukulie mtoto huyo, bila kujua kuwa nilikuwa nimeshalibeba!

Kwa hiyo tukasepa zetu kwenda Masai kwenye mida ya saa mbili kasoro, Tesha akiwa ametuambia kwamba dada yake alikuwa nyumbani, hasa kwa sababu leo ilikuwa Jumapili kwa hiyo alishinda hapo tu.

Akaeleza pia kwamba hapo nyumbani kwao angalau kwa wakati huu mambo yalikuwa vizuri tu kama nilivyoyaacha tokea Joshua aondolewe. Dada yake hakuwa mbanizi sana ila alimwambia Tesha awahi kurudi, ishu za kuingia ndani usiku mno hazikufaa, nami nikamwambia kweli leo tusingekaa muda mrefu.

Ankia akawa amemwambia kuhusu suala la Joy kunitafuta, naye Tesha akaniambia nilifanya la maana kumpuuzia kwa kuwa angenisumbua mno; na tayari alikuwa ameshanishauri juu ya sababu iliyofanya kwa nini kumpuuzia Joy iwe muhimu.

Basi tukafika Masai, nasi tukakaa sehemu iliyokuwa na viti vifupi vya mbao, vyenye muundo kama wa makochi marefu, vikizunguka meza pana ya mbao kwa pande mbili. Mimi na Ankia tukakaa upande mmoja, Tesha ule mwingine, kisha tukasubiri mhudumu aje.

Watu walikuwa wengi sana hapo, hata muziki ulikuwa ule wa nguvu zaidi maana kulikuwa na mhemko wa ukweli, hii ikiwa kawaida ya wikiendi kudadeki! Wanawake wengi waliniangalia, mimi na Tesha, lakini tukawa tunakula zetu tu. Mhudumu alipofika, nikamwambia aketi karibu nami ili kumpa maagizo kwa njia ambayo asingesahau, na baada ya kuelewa akaondoka.

Tukaendelea kutulia tu, huku baadhi ya watu waliopandwa na pombe wakiwa wameshaanza kucheza, Ankia akininong'oneza sikioni kuhusu namna watu walivyotuangalia na kunifahamisha fulani ni fulani, nikiona wazi kwamba mwanamke huyu alitaka watu waone nina ukaribu naye zaidi.

Muda si mrefu vinywaji vikaletwa; chupa tatu za Dompo baridi, pamoja na glasi za vioo. Zikagawanyishwa kwetu na huyo mhudumu, kisha akaondoka. Tesha alionekana kufurahi, lakini akatulia tu. Kidevu juu, si unajua? Kwa haraka hapo alielewa elfu thelathini ilikuwa imepita, na alijua vingine vilikuwa vinakuja kwa hiyo lazima angeweka ule mwonekano wa kutoshangaa.

Tukamimina kila mtu kwenye glasi yake, na Ankia hakuacha kuniambia kuhusu namna ambavyo watu walitutazama sana. Nikawa namwambia vitu vyenye kumchekesha, mara kwa mara Tesha naye akinitumia sms za utani kuelekea tabia tuliyoionyesha hapo ya ushua mwingi, na taratibu muda ukawa unaenda.

Wakawa wanakuja marafiki zao Tesha na Ankia pia, kutia ndani Bobo, wakitusalimu, kisha wanaondoka. Aliyekuja na kukaa hapo kabisa ilikuwa ni mama Chande, yule rafiki yake Ankia, naye nikamwagizia chupa 5 za bia aliyoipenda; Safari Lager.

Hazijapita dakika nyingi, wakaja wanaume vijana wawili wakiwa wamebeba sinia pana la mstatili lenye vyakula hapo. Kulikuwa na chips kavu nyingi, mishikaki ya ng'ombe mingi pia, pamoja na nyama za kuku. Meza ikaonekana kujaa kiasi, na mama Chande alikuwa anachekelea vibaya mno.

Tesha akanitumia ujumbe kuuliza ikiwa tungekula halafu tukimaliza tukimbie, maana alihofia hakukuwa na pesa ya kutosha, na kuniuliza ikiwa ni Chalii Gonga ndiye aliyelipia. Nikamwambia hapana, sikuwatoa hapa na Ankia kwa udhamini wa mtu yeyote; hii yote ilikuwa mimi, na yeye ajitahidi tu kuenjoy kisha tuondoke mapema.

Dah! Makamuzi yakaanza baada ya sisi wote kunawishwa mikono. Niliona jinsi wenzangu walivyojitahidi kuweka kauzungu kidogo kwenye ulaji na unywaji, na nilielewa kuna vitu vingi sana vingesemwa hapo Masai hata kuhusu haka kajambo kadogo tu tulikofanya, maana Tesha alisema fitina nyingi zilijaa sana sehemu hiyo. Niliangaliwa, yaani niliangaliwa mpaka ilikuwa inakera!

Angalau mama Chande akawa ameanza kunisemesha, akiniambia kweli kila mwanamke hapo alinitaka, eti kasoro yeye lakini! Shabiki wa Yanga na mashauzi yake huyo! Tukakata muda hapo mpaka imefika saa nne na nusu hivi, vibe la Dompo likiwa limenipanda kiasi, nami nikaletewa jambo jipya.

Mhudumu yule mwenye macho makubwa na kalio nene aliyetuhudumia jana pale VIP hadi Tesha akaanza kumchokoza, akawa amekuja hapo tulipokuwa, naye akanifata na kuniinamia sikioni, kisha akasema, "Nimeambiwa nikuletee hii."

Alinishikisha kitu kama karatasi kwenye kiganja changu, nami nikaitazama kwa njia ya kawaida tu. Hakuondoka. Akasimama nyuma yangu kama vile anasubiria jibu.

Nikaifungua hiyo karatasi, ikiwa ni bandiko dogo la kwenye chupa ya bia, na upande mweupe ulikuwa umeandikiwa maneno "njoo VIP, NINA SHIDA NA WEWE."

Aya?! Huyu angekuwa nani? Chalii Gonga? Hapana, yeye angenipigia tu simu. Huyu angekuwa mtu nisiyemfahamu, ama labda nilimfahamu lakini kwa hapo nisingejua ni nani. Fikira za haraka ikawa kwamba ni Joy, nami nikamwangalia Tesha na kukuta ananitazama kwa yale macho ya kuuliza 'vipi?'

Nikampa ishara huyo mhudumu kuwa ainame nimsemeshe, naye aliponikaribia nikamuuliza, "Nani amekupa hii?"

"Mke wake boss... boss wetu," akajibu hivyo.

"Bosi? Mke wake Chalii?" nikamuuliza.

Akatikisa kichwa kukubali.

"Nani, yule Joy?" nikauliza tena.

"A-ah... siyo Joy... mke wake boss kabisa... sijui anaitwa nani," akaniambia hivyo.

Dah! Kizungumkuti.

Ankia akaniuliza vipi, hapo tumacho twake tukiwa tumeshaanza kuwa lege, nami nikamwambia kuna mtu huko VIP ananiita... mke wa Gonga. Ankia aliposikia hivyo, akaniambia niende tu kumwona, maana alimjua lakini hakuwahi hata kuongea naye, ila nafsi yangu ikawa inapingana na hilo.

Nikamwambia yule mhudumu, "Nenda kamwambie hivi... ninakula. Kama anataka kuniona... yeye ndiyo aje hapa. Asipoweza, basi. Nenda."

Mhudumu akaondoka zake.

"Hadi mke wa Gonga ashaanza kutuma wajumbe!" Ankia akaniambia hivyo sikioni.

"Unamjua vizuri?" nikamuuliza.

"Ee, yupo hivi mwembamba kidogo, ila ana kashepu... mzuri mzuri... anapendaga kukaa huko juu akijaga hapa," akasema hivyo.

Nikapiga tu fundo dogo la wine.

"Si ukamwone?" Ankia akasema hivyo.

"Ah... ili iweje?"

"Atakuwa anakutaka..."

"Me simtaki sasa. Hebu kula tuondoke bwana..."

Ankia akacheka na kunilalia mgongoni, kisha akaendelea kula na kupiga umbeya na mama Chande.

Tesha akanitumia ujumbe kuniambia kwamba niwe mwangalifu sana kwa jambo lolote lile ambalo ningejiingiza kufanya na watu wake Chalii Gonga, nami nikamwambia asijali, nilikuwa macho. Dogo pia alikuwa makini hata ingawa kwenye kukubali bia za ofa kutoka kwa watu hao lilikuwa jambo rahisi kwake.

Ni baada tu ya dakika kama mbili kupita na yule mhudumu akawa amerudi tena. Zamu hii akanipa kikaratasi kingine tena, nami nikahisi kukerwa. Alikuwa ameshaanza kunichoresha kwa watu maana wajanja wangejua tu kwamba alikuwa anatumwa kwangu, na mimi nilitaka hiyo ikome. Nikaifungua karatasi na kusoma.

"Njoo, pametulia zaid huku. Kuna ishu muhm natak tuongee. Nitagharamia order zako zote hata ukitaka. We njoo"

Ikasomeka hivyo. Nikawaangalia wenzangu na kuona wananitazama usoni kwa umakini, nami nikasimama na kumwambia huyo mhudumu aende zake; sikuhitaji msindikizaji, VIP nilipajua.

Nikatoka na tembea yangu ya kujiamini, nikiwapita watu walioserebuka hapo, na nilipofikia usawa wa sehemu ya DJ nikakuta ni Bobo ndiye anaongoza mitambo. Alikuwa pia ameshika maiki na kufanya kama u-MC, na baada ya kuniona nakuja upande wake, akaelekeza sifa kwangu.

"Oyo, oyo, vibe kama lotee... mchina, mchina, kasimama mchina... kelele kwakeee!"

Bobo alikuwa anasema hivyo huku akinionyeshea kwa watu, na kweli shobo zikaanza kutoka kwa watu ambao hata sikuwafahamu; wanawake wakiwa wanatoa sauti za shangwe. Nikacheka kidogo nilipomfikia na kumwambia 'acha basi mwanangu,' naye akagongesha kiganja chake kwenye changu kabla ya kumpita na kwenda upande wa vyoo.

Baada ya kutoa haja ndogo ndefu kweli, nikatoka hapo na kuelekea VIP. Moja kwa moja mpaka ndani. Nilipoingia, nikakuta ndani humo kukiwa na utupu wa watu isipokuwa ya mwanamke mmoja aliyekuwa amekaa kwenye sofa upande wa mbele zaidi. Alikuwa amekaa kwa utulivu tu, simu ikiwa kiganjani, na macho yake yakiwa kwangu.

Alikuwa mzuri kwa kiasi chake, mwembamba lakini kutokea kiunoni mpaka miguuni alikuwa na unawiri mzuri, akiwa amevalia gauni refu lenye kubana mwili wake, jeusi, lenye kupambwa na vitu vinavyomeremeta kulizunguka, na lilikuwa na mpasuo mrefu kufikia juu ya hip yake uliolionyesha vizuri sana paja lake jeupe.

Sura yake ilitaka kufanana na ya mwigizaji Rose Ndauka, ingawa huyu alikuwa mweupe. Alishonea wigi la nywele za kizungu kichwani, na midomo yake ilikuwa mikubwa; ikionyesha mtapakao wa lipstick nyekundu iliyong'aa. Ah mimi kwa kusoma figure za wanawake nilikuwa sijambo!

Alivutia kwa mwonekano aliokuwa nao, wadhifa wa kuwa mke wa mwenye Masai na hoteli kubwa huko Buza ukimfaa kabisa, lakini hakuwa Hamisa Mobeto! Nilimwona kuwa wa kawaida sana, na nilitaka kujua alichohitaji kuzungumza nami ili niondoke haraka.

"Ingia. Mbona umesimama huko? Njoo..."

Akasema hivyo, sauti yake ikiwa na utulivu tu, nami nikauachia mlango na kusogea mbele kidogo.

"Wewe ndiyo unaniita?" nikamuuliza.

"Ndiyo, ni mimi. Mpaka kusumbuana sana... si ungekuja tu mara ya kwanza nilipomtuma huyo?" akasema hivyo.

"Sikujui, ndiyo maana..."

"Kwani sasa hivi umenijua? Ama ni ile tu kwamba... nitalipia kila kitu ulichoagiza ndiyo imekunyanyua?"

"Sikuja hapa nikitarajia kulipiwa chochote na mtu yeyote, unanielewa? Ongea shida yako niondoke," nikamwambia hivyo kwa sauti makini.

Akaachia tabasamu la kuhukumu fulani hivi, nami nikaona ana dharau tu.

"Unaitwa nani?" akaniuliza.

Nikabaki kimya tu.

"Mimi ni Bertha. Naimiliki hii sehemu na mume wangu...."

"Unataka nini?" nikamkatisha.

"Mhm... una kiburi sana inaonekana..."

"Ah..."

Nikafanya hivyo na kupiga ulimi mdomoni, nami nikageuka ili niondoke.

"Unajua kwamba mpenzi wako amevamiwa?" akaniuliza hivyo.

Nikageuka na kumtazama.

"Eee. Wamemvamia... wamempiga vibaya sana... hadi polisi wameitwa," akasema hivyo.

"Sielewi. Mpenzi wangu gani?" nikamuuliza.

"Lazima utakuwa nao wengi kwa hiyo kukuchanganya ni rahisi..."

Nikaendelea tu kumwangalia, naye akasimama na kuanza kuja upande wangu. Oh alikuwa mrefu, na ulizidishwa kwa viatu vya kuchuchumia alivyovaa.

Akanikaribia na kusema, "Kwa hiyo huna habari yoyote kama Joyce amevamiwa?"

"Joyce? Joy?“

"Mmm."

"Amevamiwa wapi?"

"Huko Kongowe..."

"Ih! Kwa hiyo umeniita hapa kuniambia kwamba Joy amevamiwa, sijui amepigwa, kwa nini?"

"Si ni mpenzi wako?"

"Siyo mpe.... aisee! Watu mkoje? Joy ni mpenzi wangu? Haya, sawa. Ni mpenzi wangu. Akipigwa inakuhusu nini? Wewe unataka nini?" nikamuuliza kwa kuudhika.

"Nataka ujue kwamba mimi ndiyo nimewatuma hao watu wakamvamia," akaniambia hivyo kwa sauti kuu.

Kauli hiyo ikavuta umakini wangu.

"Isingekuwa ya mazingira, ningehakikisha wanamuua! Wewe kijana ni mjinga sana. Unashindwa vipi kujua kwamba mpenzi wako anatembea na mume wangu na ukamdhibiti? Tena kwa jinsi navyosikia ni kwamba unajua kabisa, lakini umetulia tu. Kwa nini, kwa sababu unamwogopa Gonga?" akaongea kwa hisia kali.

"Unasikia kutoka kwa nani?" nikamuuliza hivyo kwa sauti ya chini.

"Nisikilize. Sipendi mchezo. Sawa? Kama unafikiri Gonga ndiyo wa kuogopa, umekosea. Niogope mimi hapa. Kila kitu anachofanya Gonga kinapita kwangu, na sitaki aguswe na malaya yeyote yule. Yeye ni mume wangu tu. Usipoangalia na wewe nitakuja nikuumize vibaya mno kwa sababu unaendekeza unafiki tu wa kipuuzi. Huna hata aibu? Yaani mwanamke wako anatoka na mwanaume wangu halafu umekaa tu?" akasema hivyo kwa mkazo.

Ka! Huyu mwanamke alikuwa mjinga, ama? Nikabaki nikimtazama kwa mkazo sana, nikiwa naona wazi kwamba akili yake haikuwa na ule usawa sawa.

"Nimekwambia ni mimi ndiyo nimemfanya hivyo ili usihangaike kutafuta nani kampiga... wala nini. Na ushahidi hauna kama ni mimi, na ninakuambia ili nikuonye... wewe na huyo malaya wako. Habari zenu zote ninazo. Nikija kusikia tena... nawaua nyie wote. Unanielewa?" akasema hivyo.

Nikatazama chini nikiwa najaribu kuelewa hali ya mtu huyu mbele yangu.

Akanipiga begani kidogo na kusema, "Wewe! Unanielewa?"

Nikamnyooshea kidole kwa njia ya hasira na kumkazia macho kiukali.

Akabaki kunitazama kwa ujasiri.

"Na wewe nisikilize. Kama una kawaida ya kutengeneza drama kwa kufanya vituko vya kijinga, na unataka kuitengeneza na mimi hapa... nitaicheza. Unanielewa? Sipendi ujinga. Unanipotezea muda kuniambia vitu visivyonihusu, sijui umefanyaje, sijui utafanyaje, ili iweje? Kama unataka kufanya, fanya! Nimekuzuia? Sitaki ujinga. Narudia tena, sitaki ujinga. Hunijui, sikujui, ila ukitaka kunijua na mimi... endelea kunichokonoa," nikamwambia hivyo kwa hasira.

"Mhm... kwa hiyo unajifanya unaniweza mimi si ndiyo?"

"Na nitakuharibu vibaya mno! Niguse tena uone," nikamwambia hivyo kiukali.

Akabaki kuniangalia tu.

"Hivi wewe... yaani unaonekana.... eti 'nimempiga mpenzi wako,' kwa hiyo unataka nikusaidie nini? Ama unafikiri nitakupigia magoti? Tena yaani... waambie na hao waliompiga Joy waje kwangu... walete kwangu na mimi wanipige, sawa?" nikamsemesha kwa ujasiri.

Akawa ananiangalia kama vile bado hanielewi sijui, na mimi hapo tayari nilikuwa nimeshapandwa na hasira pia.

"Mtu kweli unakosa kazi, unakaa kufanya michezo ya kipumbavu tu? Tuko kwenye movie hapa? Haya ni maisha, darling. Hata upige na kuua malaya wangapi, mume wako atatoka nje tu! Unang'ang'aniza ujinga, eti 'nakuambia ili nikuonye,' mimi ndiyo natoka na mume wako? Unashindwa kutafuta suluhisho linalofaa unaendekeza ujinga tu wa Sinema Zetu? Utaendelea kukalia chupa ya moto tu, mjinga wewe!" nikamwambia hivyo kwa hasira.

Alikuwa amenikera sana. Hii ilikuwa nje ya matarajio yangu kabisa. Akanisukuma kifuani kwa mikono yake, kama kutaka kunifukuza, lakini nikaishika mikono hiyo yenye bangili nyingi kwa nguvu sana, halafu nikamvuta mpaka karibu na uso wangu.

"Niachie, msenge wewe!" akanitukana.

"Nakwambia hivi... waite hao watu wako na mimi wanivamie, sawa? Uone kama Gonga ataacha kulala na wanawake wengine. Ikikupa faida yoyote kuumiza watu wengine kwa sababu ya vitu unavyoshindwa kucontrol... niite mwehu. Nitakula makapi yako kila siku! Mjinga wewe!" nikamwambia hivyo.

Kisha nikamsukuma mpaka akadondokea kwenye meza na kukaa huku akiniangalia kwa hasira.

Nikaufungua mlango, na kabla sijatoka nikamwambia, "Na sikuja ili unilipie chochote. Hauna hata hela wewe, unazitoa tu kwa mume wako afu' unajifanya eti 'kila kitu kinapita kwangu,' 'nitakuumiza!' Uje ujaribu kunisogelea tena uone."

Alibaki akiniangalia kama vile kweli alikuwa amekalia chupa ya moto, nami nikatoka hapo na kurudi kwa wenzangu tena.

Nilikuwa nimeshaudhika sana, na baada ya kufika pale walipokuwepo marafiki zangu, nikakuta ni Ankia na Tesha tu ndiyo waliobaki, huku mama Chande akiwa na watu wengine kwenye kucheza muziki. Ankia akaniuliza mke wake Chalii Gonga alitaka nini, nami sikujibu hilo, nikamwomba tu Tesha aniitie yule mhudumu niliyeongea naye mwanzoni ili nilipe, tuondoke.

Ilikuwa imeshafika saa tano na nusu hivi, na baada ya huyo dada kuja tukapiga mahesabu na kujua gharama iliyonihusu hapo ilikuwa 83500. Nikatoa wallet na kumpatia elfu tisini, naye Tesha akanionyesha ishara ya kushangaa kwa mdomo. Mhudumu huyo akaondoka, akiwa anatakiwa kurudi na chenji na mzigo mwingine.

Ankia akaniuliza mbona kama hela ilipita hata vile ambavyo tulichukua, na ndiyo hapo hapo akapata jibu. Mhudumu aliporejea na chenji, akawa ameleta na mfuko uliowekewa nyama ya kitimoto iliyotengenezwa vizuri sana, ikiwa imegawangishwa kwenye vifungo viwili. Moja ilikuwa kilo, na nyingine kilo tatu.

Nikampatia Ankia abebe huo mfuko, nasi tukaanza kuondoka. Bila shaka watu walijiuliza kwa nini tunaondoka mapema sana, ila sababu zilikuwa zetu kujua. Kwa sababu Ankia alikuwa anamalizia kuagana na rafiki yake aliyekutana naye langoni, mimi na Tesha tukawa tumetangulia nje, na ndiyo kijana akapata nafasi ya kuniuliza yaliyojiri kule VIP.

"Umemwona huyo mwanamke?" akaniuliza hivyo.

Nikatikisa kichwa mara moja kukubali.

"Alikuwa anataka nini?"

"Ah... ananichanganyia habari tu. Anaanza kuniambia eti sijui katuma watu wampige Joy kisa anatoka na mume wake..."

"Wewee... kweli?"

"Ndiyo hivyo kaka. Asa' me inanihusu nini? Eti anasema anajua me ni mpenzi wa Joy, kwa hiyo ananiambia ili kunionya. Ana akili kweli?"

"Ahahee... mwanangu siyo poa. Mabalaa yashaanza kukutafuta mapema hata wiki haijaisha!"

"Ananiogopesha sasa unafikiri?"

"Kwani ni kweli alivyosema?"

"Hata kama ni kweli, hanibandulii chochote. Siogopi mtu Tesha, nayemwogopa ni Mungu tu. Sijui watu wana matatizo gani... mimi kuja hapa sijui nawazuia wasile kwao? Tayari washaanza kusambaza me mtu wake Joy, wakati hata sijui anatokea wapi! Fitina za hapa ulizoniambia ndiyo nimeanza kuziona... mpaka natamani nisirudi tena," nikamwambia hivyo kwa kuudhika.

Tesha akanisimamisha karibu na nguzo, naye akasema, "Oy, tusimame hapa, tumsubirie huyu. Sikia. Me nilikwambia. Masai ndo' palivyo. Yaani mtu akishakugusa tu kidogo, ndiyo atataka hadi afunue na nguo yako auone mwili wote."

"Unafikiri kwa huyu mwanamke ni hicho Tesha? Basi tu, sijui ana akili gani yaani... nilikuwa hata simwelewi..."

"Huwa anavuta," Tesha akasema hivyo kwa sauti ya chini.

"Bangi?"

"Unga."

"Kumbe?"

"Ee. Bobo si mwana? Huwa ananiambia. Kamemganda sana Chalii, na hata wakigombanaga... akikapa tu unga kanatulia. Sasa kakiwa high huwaga kanafanya vituko hapa ama kule... Chalii muda mwingine anakafungiaga wanasema..." Tesha akaniambia.

"Ahaa... kumbe ni addict?"

"Eee. Usikute hapo kalikuwa kamepiga. Kanajionaga matawiii, shauri nasikia kwao kwanza wana hela sana..."

"Aaa, kumbe ka kishua?"

"Ndo' hivyo. Ila ishu zake siyo, sometime huwa hadi nasikia kanampelekaga Chalii kombo na ye' anaanza kufanya vitu kwa sifa.... wana akili zile zile tu, sijui walitoana wapi mpaka kufaana... yaani mwanangu! Me huwa najichekesha kwao tu lakini sijiwekagi karibu kabisa. Kuna mambo mengi figisu huko, unashangaa tu umekuja kuuziwa kesi. Kisa? Ulionwa umeingia VIP na mke wa Gonga. Kakishapeleka maneno ya kijinga kwa mume wake huko kakamroga-roga kwa uwongo? Ohooo... unajikuta kwa Maimuna mzee. Kuwa makini..." Tesha akasema hivyo.

Nikaangalia pembeni kiufupi nikiwa natafakari maneno hayo. Alikuwa sahihi kabisa. Tena hata nilipomwambia huyo mwanamke hana hela, nilisema hivyo kwa sababu ya hasira zilizonifanya kutongalia vitu kwa umakini, lakini si ajabu kwamba kweli mwanamke huyo ndiye aliyekuwa mwenye nguvu zaidi hata ya Chalii Gonga. Ni kwamba tu ugeni wa maeneo na watu ndiyo uliokuwa mpya, lakini si kwamba vitu vya namna hiyo vilikuwa vigeni kwangu.

Kwa vyovyote vile nisingetaka kujiingiza kwenye shida zaidi na watu hao, japo nilikuwa tayari kupambana nazo kama wangezileta kwangu, kwa hiyo kuanzia wakati huu ningepaswa kujitahidi kuweka kigingi kikali kuzuia mazoea yasiyo na faida yoyote pamoja na watu hao; hasa huyo Chalii Gonga.

Nilihisi kabisa kwamba mwanaume huyo angekuja kuniletea shida endapo kama ningejiingiza kwenye mambo aliyojihusisha nayo, haijalishi ikiwa na mke wake alihusika, hivyo huu ndiyo ungekuwa mwanzo wa mwisho wa ukaribu wowote uliokuwa umejitengeneza baina yangu na mwanaume huyo.

Sikutaka kuangalia faida zozote zile za muda mfupi ambazo ningepata kutoka kwa mtu aliyefanya mambo haramu mpaka kutembea na mabastola, bali kukazia fikira hasara ambazo zingenipata kwa kuweka ukaribu naye ndiyo kungenisaidia niwe makini kwa muda wote ambao ningekuwa huku.

Mwanzoni si ilionekana kama shobo tu lakini sasa ndiyo nikawa nimeanza kutilia maanani ukweli wa kwamba si kila mtu anayecheka na wewe anakutakia mazuri, na kama Gonga Chalii na wenzake wangekuwa wananipangia mabaya, basi na mimi ningewarudishia ubaya tu. Daktari mwenye kiburi ndiyo lakini nilikuwa makini. Waje kunifata, ndiyo wangeelewa maana ya jina langu!



★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA KUMI NA MBILI

★★★★★★★★★★★★★★★★


Ankia akawa amefika hapo, naye Tesha akabadili mada upesi huku tukianza kutembea tena.

"Dah, kaka yaani nilikuwa sijategemea. Hilo ni bonge la mtoko, yaani halikufaa kuletwa Masai, au siyo Ankita?" Tesha akasema hivyo.

"Mmm... JC umegharamika kweli, yaani! Hiyo Dompo ilivyo tamu! Kweli tuje tupate kamshiko tufanye hii kitu kama hii," Ankia akasema hivyo.

"Yeah. Tutaenda sehemu nyingine nzuri siku moja," nikawaambia hivyo.

"Mwamba nikaona manoti tu unatoa, dah! Halafu ulikuwa unakataa eti siyo wa kishua," Tesha akasema hivyo.

"Ahahaha... siyo lazima kuwa wa kishua. Je kama nimeziiba, utajuaje?" nikamuuliza.

"Aa wapi. Ma' mkubwa kaniambia we' doctor. Ankia ulikuwa unajua jamaa ni doctor?" Tesha akamuuliza.

"Wewe... kweli?" Ankia akamuuliza hivyo.

"Uhakika. Anafanya kazi Muhimbili kabisa..."

"Wacha we! Mwanaume ana siri huyu!" Ankia akasema hivyo na kunisukuma.

Nikatabasamu kidogo.

"Tena anayo siri nzito kinoma. Ndo' umchune sasa. Oy JC, mkifika ndani mwonyeshe sugar mommy tiba ni nini," Tesha akasema hivyo kiutani.

Sote tukacheka kidogo, na masihara yakaendelea mpaka tulipofika getini kwao Tesha.

Nikachukua mfuko aliobeba Ankia na kutoa nyama ya kitimoto kilo moja, nami nikamwambia Tesha apeleke hiyo kilo tatu kwao ili wakajikamulie pia. Akasema Mariam angefurahi kweli maana alizipenda, na ndiyo lililokuwa lengo langu.

Ankia akawa ameenda kufungua geti letu, nami nikamwambia Tesha asiseme kwa watu wa familia yake kwamba mimi ndiyo nilinunua hicho chakula, na ni kitu kilichofanya aniulize kwa nini.

Nikamwambia tu aseme yeye ndiyo kanunua au hata asiseme lolote, maana kutokana na maelezo ya mama zake wakubwa kumhusu Miryam waliyonipa leo, sikufikiri hiki ni kitu ambacho dada yake angefurahishwa nacho; yaani kujua nimewanunulia kitu fulani.

Lakini sikumwambia Tesha kuhusu hilo, naye akaridhia tu kwa hicho nilichomwambia na kwenda kwao baada ya kuagana kirafiki. Ankia wangu alikuwa ananisubiria getini, nami nikajiunga naye na kuelekea ndani.

Mwanamke alionekana kutosheka kiasi na Dompo moja aliyokuwa amekunywa maana alikuwa na uchangamfu kweli, akinikumbushia kuhusu namna ambavyo watu walikuwa wanatutazama sana kwa macho yenye husuda, nami nikamsaidia tu kuingiza vitu vilivyotakiwa kuingia ndani na kufunga mlango.

Nilipokuwa tu ndiyo nimemaliza kufunga mlango na kugeuka kumwangalia, nikakuta akiwa ameinama karibu na sehemu yenye extension iliyochomekea nyaya za TV na king'amuzi, akionekana kutaka kuweka simu yake chaji. Kuinama kwake kulifanya shati lake lipande juu na kufunua mapaja yake mpaka kalio, lililositiriwa kiasi tu na kiboksa-skinny chake. Alikuwa na makalio makubwa! Mambo yangu ikaanza kupanda, bila kupenda.

Alikuwa anahangaika kuichomekea simu waya sijui, nami nikawa namwangalia tu kwa matamanio kiasi. Nasema kiasi kwa kuwa mawazo yangu yalikuwa mbali na kile ambacho mwili wangu ulitaka, kwa hiyo sikuwa nimeelekeza fikira zangu zote kwa Ankia japo alinivuta. Akawa amemaliza kuweka simu yake na kusimama vizuri tena, naye akaniangalia na kusema kitu fulani ambacho sikukazia fikira haraka.

"Mbona umesimama tu hapo?" akaniuliza hivyo tena.

"Naam?" nikawa kama nimeshtuka.

"Nimekuuliza mbona umeufunga mlango? Hauendi kujimwagia kama kawaida yako?" akasema hivyo.

"Ah... nimeona uvivu hata kwenda kujimwagia... feni itanihusu," nikamwambia hivyo na kusogea usawa wa sofa.

"Tukae kidogo... bado mapema..."

"Ishaingia saa sita mbona... na we' si unapendaga kulala mapema, vipi leo?"

"Sijachoka kihivyo," akaniambia hivyo na kunipita.

Alikuwa akielekea upande wa chumba chake, kalio lake likitikisika si mchezo, nami nikamwambia, "Kumbe unataka kuchoka ndo' ulale?"

"Eee, bado nimechangamka," akajibu.

"Nikusaidie?" nikamuuliza.

Akawa ameufikia mlango wake na kunigeukia, naye akatabasamu na kuuliza, "Unisaidieje?"

Nikamfata mpaka kufikia hapo aliposimama na kusema, "Kukuchosha."

Akasema, "Haya... nichoshe."

Alikuwa ananiangalia kwa macho yenye uvutio, nami nikamshika kiunoni kwa nguvu na kumvuta kwangu. Alipodhani nataka kumbusu mdomoni, mimi nikamgeuza na kumfanya anipe mgongo, kisha nikamsukumia ukutani na kumkandamiza hapo kiasi.

"Ah... JC... mbona hivyo?"

Akasema hivyo kwa deko, nami nikaishika shingo yake kutokea nyuma na kukivuta kidevu chake ili nimtazamishe kwangu.

Kwa sababu alikuwa mfupi alijipinda vyema kwa mbinuko wa mgongo, huku kalio lake likiwa linaukandamiza uanaume wangu, naye akawa ananiangalia kilegevu kukubali utesaji huo wa mwanzo. Unajua ni pombe tu ndiyo ilinipandishia mzuka namna hiyo la sivyo nisingejishughulisha naye kabisa.

(........).

(........).

Bado tulikuwa na nguo mwilini, kwa hiyo hiki kilikuwa cha kuchoshana haraka tu. Mkono wake mmoja alikuwa anaurudisha nyuma kama kuniambia nipunguze kasi, lakini nikawa naushikilia kwa nguvu na kuendelea kumtandika tu. Alikuwa analia siyo mchezo.

(........).

(........).

(........).

Tukatoka ukutani mpaka kwenye sofa. Piga haswa, naye akapasua bomba. Nikamuuliza tukiachia hapo vipi, lakini akanijibu kwa kuirudisha ndani yeye mwenyewe. Dah! Kazi!

Pombe ilikuwa inazunguka vizuri mwilini kwa kuwa sikudhani kama ningeweza kukata dakika nyingi sana nikicheza naye tu namna hiyo, na ndipo alipopasua lingine mimi pia nikalisaka goli langu. Lakini halikutoka. Nilichokuwa nasikia kimenibana ilikuwa ni mkojo, nami nikakwazika kiasi kwa sababu sikupata kale kahisia ka mridhiko kanakoletwaga na ile kitu kutoka. Ah mwanaume anaelewa!

Ila kumtandika Ankia namna hiyo kwa mara nyingine kuliridhisha sana, nami nikaona nimwache tu hapo sofani na kwenda zangu jikoni. Nilichukua chupa tupu ya maji ili nikojoe humo maana choo kilikuwa nje na mlango nilikuwa nimeshafunga. Kisha nikaenda pamoja nayo chumbani na kuiacha huko.

Nikaitoa feni na kuipeleka hapo sebuleni, kisha nikaiwasha na kuielekeza kwa mwenye nyumba wangu. Alikuwa amelala kwa kujiachia huku jasho kama lote likimtoka, nayo feni ikaanza kutupuliza vizuri nilipokaa karibu yake pia.

Kwa kuwa nilikaa karibu na alipolaza kichwa chake, akajinyanyua na kuishika mashine yangu, kisha akaitumbukiza mdomoni. Ah yaani kama alijua. Nikawa mgumu hata zaidi na hatimaye kurusha risasi kama zote. Aah kale kahisia sasa!

Nikawa nashtuka-shtuka huku nikiona nyota tu, nami nilipomwangalia mtoto nikakuta nimemlowanisha usoni kabisa, kitu ambacho kilifanya nicheke kidogo maana ni kama alikuwa amemwagikiwa na uji!

Akajinyanyua na kuelekea chumbani kwake bila kusema lolote, nami nikamwahi kabla hajafikia mlango na kumpiga kofi kalioni. Akanigeukia na kuachia tabasamu hafifu, naye akanipiga begani kidogo.

"Si umechoka sasa?" nikamuuliza.

Akatikisa kichwa kidogo kukanusha.

"Aaaa... kwa hiyo tuendelee? Njoo," nikamwambia hivyo huku nikimvuta.

"Hamna, natania tu... nimechoka..." akawa anakataa huku akicheka.

"Twende nikumwagie uji mwinginee..." nikamwambia kwa sauti nzito ya mchezo.

"Iih wewe... sitaki..." akasema hivyo huku akicheka.

Akakimbilia chumbani kwake na kufunga mlango, nami nikasema, "Njoo tuchoshane bwanaa..."

"Choka wewe tu. Mtu mwenyewe hata huchoki, sijui binadamu wa aina gani..."

Akasikika akisema hivyo, nami nikacheka kidogo. Alifikri sijachoka kwa sababu ya muda niliotumia bila kufika mwisho mapema, lakini kimwili nilikuwa nimechoka.

Tayari ikawa imeingia saa saba usiku, nami nikaona tu nizime taa na kuibeba feni, maana Ankia hakutaka kutoka tena. Kwa hiyo tungekuja kuonana kukishakucha, na nilikuwa sijasahau mipango mingine ya kushughulika nayo kwa siku hii ambayo ingefuata; mipango ya kumsaidia binti Mariam. Nikaingia zangu chumbani na kulala.


★★★


Asubuhi na mapema ya saa tatu tu nikawa nimeamka. Oh hii kwangu ndiyo ilikuwa mapema sana kwa hizi siku za mapumziko yangu huku, na cha kwanza nilichokuwa nataka kufanya kabla ya mengine ni kujisafisha kinywa na mwili; hasa kwa kuwa nililala bila kujimwagia usiku uliopita.

Nikapitia jumbe mbalimbali kwanza kwenye simu na kujibu chache, kisha nikachukua vifaa vya usafi na kutoka ndani ya chumba. Nilidhani labda Ankia angekuwa hajaamka bado kutokana na uchovu wa usiku lakini mwanamke huyo alikuwa na bidii.

Tayari, alikuwa ameshaamka, ameshafanya usafi, bila shaka mapema sana, nami nikatoka nje na kumkuta akiwa anamalizia kufua mashuka yake pamoja na yale ambayo niliyaondoa kitandani kwangu usiku ule nimefanya mapenzi na Joy. Na nilikuwa nimeyaweka tu pembeni ili kuja kuyafua baadaye, ila Ankia akawa ameniwahi.

Alikuwa amevalia T-shirt lake la Yanga na khanga kutokea kiunoni, nami nikampa salamu kwa kuliminya shavu la kalio lake alipokuwa akianika shuka. Akatabasamu kwa furaha na kunipa salamu pia, nami nikamtania kwa kuuliza ikiwa alitaka kunywa uji mwingine asubuhi hii. Akacheka tu na kunipiga kidogo begani, nami nikamshukuru kwa kunisaidia kufua, kisha nikamwacha na kwenda upande wa sinki kuosha domo.

Nilitazama upande wa nyumba yao kina Tesha na kuona kwamba gari la Miryam halikuwepo, kumaanisha tayari alikuwa ameenda kazini kwake. Nikaelekea bafuni baada ya kuweka maji kwenye ndoo na kuoga, kisha nikarudi ndani tena. Ankia alikuwa ameshamaliza kufua na wakati huu alikuwa anatengeneza chai jikoni, hivyo nikaelekea chumbani na kujitengeneza vyema pia kwa sababu nilitaka kuondoka.

Nikavaa jeans yangu nyeusi, kisha nikaenda kumwomba Ankia pasi ya umeme ili ninyooshe T-shirt langu jeupe la mikono mifupi (Manga). Akawa ndiyo ameniuliza ninakwenda wapi, nami nikamwambia tu naenda huko Mbagala kukutana na mtu kifupi kisha ningerudi. Alikuwa anasisitiza ninywe chai kwanza, yaani amalize kuichemsha kisha afate chapati upesi kwa ajili yetu, lakini nikamwambia asijali; ningekunywa chai huko huko tu, kwa hiyo asiharakishe chochote.

Basi, nikamaliza kunyoosha kiwalo changu na kukitupia mwilini, nikahakikisha niko vizuri kichwani, na kufikia wakati huu nilikuwa na uhitaji wa kunyoa kiasi ama kuchonga nywele. Lingekuwa jambo la kufanya baadaye. Nikatoka na kumkuta Ankia sebuleni, akiwa amesimama usawa wa sofa huku akitazama jambo fulani kwenye TV, nami nikafika karibu yake na kusimama pia.

Akaniambia kwamba kiukweli, bila unafiki wowote, nilijaliwa kuwa na sura nzuri sana, na hata ile kumwambia tu kwamba ninatoka kwenda kukutana na mtu fulani ilimfanya ahisi wivu kwa kukisia kwamba ni mwanamke, japo tulikuwa tumeshakubaliana kwamba hakupaswa kuziacha hisia za namna hiyo zimtawale.

Mimi nikatabasamu tu kwa kumwelewa, nami nikaona nimpe busu laini tu ya kupoza roho. Akauliza ikiwa nilihitaji anitunzie chakula kwa ajili ya mchana, nami nikasema ningemjulisha kwa njia ya ujumbe endapo kama ningechelewa. Nikamwachia elfu kumi nikimtania kwamba kama akitaka basi akanunue Dompo aje kupigia ndani, naye akafurahi sana na kunibusu tena, kisha mimi huyo nikaondoka zangu.

★★

Sikupata shida kufika Mzinga na kuchukua usafiri wa kuelekea Mbagala, na kama kawaida, nilivuta macho ya wengi. Ah hiyo ni kunipandishia tu hisia za kujiamini lakini ililemea mno. Watu wa huku walijua kukodolea macho mpaka ilichosha!

Nikafika Mbagala, nami nikakunja kona mpaka kufikia Zakhem, kisha nikachukua bajaji kuelekea Kijichi. Ndiyo, Kijichi. Mpango ulikuwa kwenda kukutana na bibie Miryam ili nizungumze naye kuhusiana na mdogo wake, Mariam, na nilitaka mazungumzo yetu yaende vizuri sana maana yule mwanamke alionekana kupenda vitu vilivyonyooka; masihara pembeni yaani, na kwa jambo hilo sikutaka ahisi labda namchezea.

Kwenye bajaji niliyopanda niliketi nyuma pamoja na wadada wawili kwenye miaka ya ishirini na kitu mpaka thelathini hivi, wenye mionekano mizuri kweli kwa jinsi walivyovaa na kusuka, na dereva wa bajaji alikuwa anaongea nao kwa njia ya kichokozi na kuwafanya wafurahie. Mimi nilikuwa makini tu, na kila mara ambayo ningemwangalia aliyekaa karibu nami, alikuwa ananikata jicho la upendezi huku akilishusha kimadoido, na hatimaye akanifanya nitabasamu.

Dereva wa bajaji alikuwa mwongeaji sana, akihamishia mpaka mazungumzo yao kunielekea mimi kwa kuwaambia waniombe namba maana mimi ndiye niliyekuwa mwanaume mzuri wa kutoka nao, lakini walionekana kuniogopa kutokana na jinsi nilivyoonyesha kutokuwa na habari nao. Sasa si dereva akaongeza presha? Nikaona nitende jambo.

Ile tumefika kituo cha Upendo hatimaye, nikashuka, nikalipa, kisha nikawasemesha hao wanawake. Nikamwomba huyo mmoja simu yake niandike namba, naye akacheka tu. Dereva akawa anawapampu wachukue namba la sivyo wangepoteza bahati eti.

Mwenzake na huyo dada aliyeona aibu hakupoteza muda na kunipa ya kwake, nami nikaandika namba yangu na kumrudishia, kisha nikamwambia 'nitext,' halafu nikaanza kuondoka. Nilifanya hivyo kwa sababu kiukweli wanawake hao walikuwa wazuri, ila sikuwa na nia yoyote ile ya kutoka nao. Nia yangu ilikuwa nyingine tu.

Nikafika pale kwenye duka la bibie Miryam, na hapo nje nikakuta gari lake pamoja gari lingine jeusi aina ya Toyota Kluger. Bila shaka angekuwa na mgeni wa masuala yao ya kibiashara, nami nikaelekea mpaka ndani huko. Nikamkuta Mamacita Soraya akiwa ameketi kwenye kiti chake mezani kwa mapokezi, na tabasamu aliloachia lilitosha kueleza ni namna gani alivyokuwa amefurahi kuniona.

Akiwa amevaa ushungi kichwani kama kawaida yake, uso wake mweupe ulipendeza sana. Nyusi zilizotindwa vyema na lipstick ya zambarau mdomoni, pamoja na macho yake makubwa kama ya kiarabu yalivutia mno. Nguo aliyovaa ilikuwa kama gauni la njano lakini lenye mtindo wa sari lenye kubana kufunika mwili wake wote kutokea kifuani, na kwa sababu ya kukaa sikuweza kumchora vizuri.

"JC!" akaniita kwa shauku tulivu.

"Mambo vipi Cute Soraah?" nikamwambia hivyo.

"Hee! Umelitoa wapi hilo jina?"

"We' kwani umeliandika wapi?"

"Hahah... umeshanitafuta mpaka Facebook?"

"Ndiyo maana yake. Una tupicha tukali kweli, siyo rahisi kuamini una miaka 30..."

"Ahahaha... kwa nini?"

"Unaonekana mdogo kweli. Upo sahihi kujiita Cute... na me sa'hivi nitakuwa nakuita Soraah..."

Akacheka kidogo kwa haya.

"Ama ni la mume wako tu kukuita?" nikamuuliza.

"Hamna... niite tu hivyo. Napenda."

"Eti eh?"

Akatikisa kichwa kukubali.

Ni hapa ndiyo simu yangu ikatoa mtetemo kutokea mfukoni mwa suruali yangu kuashiria kuna ujumbe umeingia, nami nikautoa ili kuona ni nani.

"Na me itabidi nikutafute FB nijue una miaka mingapi," Soraya akaniambia hivyo.

Nikatabasamu kidogo na kusema, "Itakuwa vizuri."

Nikaona ujumbe huo ulioingia kwenye simu kutoka kwa namba ngeni, aliyetuma akisema 'mambo,' nami nikakisia kuwa huenda ni yule mwanamke wa kwenye bajaji.

"Na wewe lazima uwe na tupicha tuzuri FB. Nitakuona," Soraya akasema hivyo.

"Hamna hata, mbaya," nikamwambia hivyo kiutani.

"Mh... labda umdanganye mtu ambaye hajawahi kukuona," akasema hivyo na kucheka kidogo.

Nikamjibu aliyenitumia ujumbe 'saf, nan?' naye akajibu, 'me naitwa Winny tumekutan kw bajaj.' Nikaona Soraya ananitazama tu kwa utulivu, nami nikampa tabasamu hafifu na kumjibu huyo "Winny" kwamba ningemtafuta baadaye maana kuna jambo nilikuwa nashughulika nalo.

"Sawa. Vipi... boss wetu yupo na mgeni?" nikamuuliza hivyo na kuweka simu mfukoni.

"Eeeh. Umekuja kuonana naye?"

"Ndiyo, nimekuja kuongea naye. Itabidi kusubiri eh?"

"Ee, ila ngoja tu nimpigie nimwambie ana mgeni hapa mwingine..."

"Hapana, acha tu. Nitasubiri. Na sisi tupige story zetu kwa huo muda. Za nyumbani?" nikamuuliza hivyo.

"Nzuri tu. Ndo' ukanichunia jana..."

"Mh? Saa ngapi?"

"Jana, si nilikutext mida ya saa nne hivi, lakini hukujibu," akaniambia hivyo.

"Kweli? Itakuwa hazikufika labda. Pole," nikamwambia hivyo.

"Haina shida."

"Basi ukaumia?"

"Wala hata..."

"Hahah... sema tu... nitafidishia hilo kwa chochote utakachotaka..."

"Mh... ahahaa... wanaume bwana..."

Nilipenda sana alivyofanya macho yake aliposema hivyo, na kiukweli niliweza kuhisi uvutio wangu kumwelekea ukiongezeka. Nikaanza kumtamani sana mwanamke huyu, ikiwa ni hisia iliyojijenga upesi sana.

"Mbona sasa ukanitafuta saa nne usiku kabisa?" nikamuuliza.

Akaniangalia tu na kutabasamu kiasi.

"Ulikuwa unataka tuimbiane na nyimbo za kupeana usingizi eti?" nikamuuliza kiutani.

Akapandisha nyusi zake kukubali, nami nikacheka kidogo kwa kuelewa alikuwa anatania pia.

Hapo hapo mlango wa ofisi ya Miryam ukafunguka, nasi sote tukautazama. Tabasamu nililokuwa nalo usoni likaondoka, nami nikaweka uso makini zaidi baada ya kumwona Festo akiwa anatoka ndani huko. Yule yule mchumba Festo aliyedhaniwa kuwa ndiyo mimi hapa mara ya kwanza kabisa nimefika nyumbani kwake Miryam, ndiyo alikuwa hapo.

Miryam pia akatoka ofisini na kusimama baada ya kuniona sehemu hiyo, nami nikaendelea kujituliza tu. Kulikuwa na ukimya mfupi ulioijaza sehemu hiyo hali nyingi tofauti kifikira, kwa sababu niliona Festo akinitazama kwa macho yenye udadisi, kisha akamwangalia Miryam pia. Bibie Miryam alikuwa ananitazama tu kwa umakini, yeye bila shaka akijiuliza kwa nini niko hapo, lakini Festo akiwa kama anahukumu kwa nini niko hapo.

Nikawaza sijui jamaa bado alikuwa anafukuzia manzi huyo, manzi mwenyewe alikuwa mgumu kweli kulainika! Ni lazima tu Festo hakuwa amefika hapo kibiashara, bali lengo lake lilikuwa kuongea zaidi na Miryam kumshawishi waweze kuungana kimahusiano. Ilieleweka alikuwa amemwelewa.

Lakini mimi nisingejua undani wa mambo yaliyoendelea baina yao, na hayakunihusu. Ila kwa jinsi Festo alivyoniangalia, ilikuwa ni kama vile fahali mpya kaingizwa kwenye zizi lenye fahali mwingine, na hiyo ilifanya nijiulize sababu ni nini.

Huenda alikuwa anafikiri mimi pia namfukuzia huyo dada maana alinikuta huko kwao siku ile amekuja kumchumbia, kwa hiyo labda alifikiria katika sababu zilizofanya akataliwe siku ile na mimi nilikuwemo. Ah! Kama ndiyo ilikuwa hivyo basi ningepaswa kuwa mwangalifu sana nisije kujikuta napigwa mshale kifuani bila kuelewa somo, si unajua wivu wa mapenzi?

Jamaa akaniangalia tena, kisha akasogea karibu nami na kusimama. Nikawa namwangalia tu kwa utulivu, naye akaninyooshea mkono wake kwa njia ya salamu. Nikaupokea, tukaitingisha kwa pamoja bila kusemeshana chochote, kisha mwamba akaondoka. Alikuwa nadhifu kweli, nguo zake zikionekana wazi kuwa za gharama, nami nikamwangalia Miryam usoni.

Kama kawaida yake, katika uzuri hakuangusha hata kwa kidogo alichoweka mwilini. Alikuwa amevaa blauzi nyeupe yenye mikono mirefu pamoja na sketi ndefu ya jeans ya blue, na nywele zake alizibana kwa nyuma. Bado aliniangalia kwa macho yenye subira tu, nami nikawa natafuta salamu iliyofaa kumpa kwa wakati huu.

"Dada... JC ndiyo kafika. Anataka mfanye mazungumzo," Soraya akaingilia kati ukimya wetu.

Miryam akanitazama usoni tena, kisha akatikisa kichwa kukubali na kuingia ofisini kwake.

Nikamwonyesha Soraya ishara ya mapigo ya moyo kudunda kwa nguvu, naye akacheka kidogo bila kutoa sauti, kisha nikaenda zangu ofisini kwa bibie.

Sikuwa na hofu, ila kwenye kuongea na huyo mwanamke kuhusu suala la familia yake kungehitaji busara. Sikuwa nimeisahau motto yake hata kidogo: sipendi michezo isiyo na faida. Kwa hiyo hapa ningehakikisha namwonyesha kuwa sikuja kufanya mchezo, ili kutokea hapa aanze kunichukulia 'serious.'

Nikaingia ofisini humo na kwenda kukaa kwenye kiti sehemu ya meza yake mkurugenzi, huku yeye akiwa amekaa kwenye chake cha kibosi. Alipendeza sana huyu mwanamke kwa namna alivyojiweka tu yaani. Kawaida. Hakupenda makuu, lakini alionekana kupenda sana maendeleo ndiyo maana hata na sehemu hii ya kikazi alikuwa ameipanua vizuri sana. Nilihisi kama vile niko kwenye kampuni kabisa!

Akiwa ananiangalia kwa macho yenye subira, nikamwambia, "Habari za kazi dada yangu?"

"Ni nzuri. Mbona umekuja hapa? Kuna tatizo lolote?" akaniuliza hivyo.

"Ha..pana... siyo hivyo. Hamna tatizo. Kwa nini unafikiri mimi kuja ni mpaka kuwe na tatizo? Sura yangu imeandikwa 'matatizo' au?" nikamwambia hivyo kiutani.

Nikaona anatoa tabasamu hafifu na kuangalia chini, nami nikacheka kidogo kwa kupata kitulizo kiasi.

"Sawa. Niambie," akasema hivyo.

Nikasafisha koo kidogo na kusema, "Nimekuja ili tuzungumze kuhusu mdogo wako... Mariam."

Akabaki kimya na kuendelea kunitazama kwa utulivu.

"Sijui ikiwa... mama zako walikwambia kuhusu maongezi yetu jana?" nikamuuliza.

"Ndiyo waliniambia. Wewe unataka kipi kutoka kwa Mariam?" akaniuliza.

"Nataka kumsaidia. Mdogo wako ana kasoro ndogo kwenye ubongo wake ambayo nina imani inaweza kushugulikiwa na kuondolewa kwa njia ya... ya kwake yaani. Nimemwangalia nikaona ana njia tofauti za kuitikia mambo...."

"Ni kasoro gani unayoongelea?" akanikatisha.

"Sijawa na uhakika sana, ila nafikiri mdogo wako atakuwa amepatwa na kitu kinachofanana na ASD," nikamwambia hivyo.

"Ndiyo nini hiyo?" akauliza.

"Autism Spectrum Disorder. Ni ugonjwa unaozuia maendeleo ya utimamu kwa mtu unaosababishwa na tofauti zinazojitokeza kwenye ubongo. Wanaokuwa na hii kasoro huwa wana matatizo ya kuwasiliana, ama tabia na mapendezi yanayojirudia-rudia, na... njia zao za kujifunza zinakuwa tofauti sana na ukawaida wa watu wengine. Hii huwapataga sanasana watoto wadogo kwa sababu ubongo wa mtoto bado unakuwa unaendelea kukua mpaka anapofikisha miaka kama 15, ndiyo unakuwa umekomaa. Ubongo wake Mariam tayari ulikuwa umeshakomaa alipopatwa na shida kama hii, kwa hiyo nafikiri tunaweza kumsaidia arudishe utimamu wake mzuri licha ya kwamba muda umepita..." nikamwelezea.

Akawa ananitazama tu machoni kwa umakini.

"Unaonaje kuhusu hilo?" nikamuuliza.

Akaangalia chini kiasi, kisha akanitazama na kuuliza, "Wewe... ni daktari kweli?"

Swali lake likaniacha namwangalia tu usoni kwa ufikirio, kwa sababu ilikuwa wazi kwamba mpaka kufikia hapo bado alikuwa haniamini; haijalishi hata kama suala la mdogo wake kuokolewa asigongwe kwa gari lilitoka kwangu. Bila shaka aliambiwa na mama zake wakubwa kwamba mimi ni tabibu, lakini bado bibie alikuwa na mashaka yake kunielekea.

Nikashusha pumzi kiitulivu, nami nikamwambia, "Ndiyo. Mimi ni daktari."

"Unajua... Mariam nimeshampeleka hospitali na... wanasema nimwache wodi za vichaa. Kwa haya uliyoniambia unamaanisha kwamba mdogo wangu siyo kichaa, si ndiyo?" akaniuliza.

"Ndiyo. Mariam siyo kichaa, anaumwa tu kwenye ubongo."

"Sasa kwa nini walikuwa wananiambia mdogo wangu ni kichaa, sijui... amepoteza kabisa utimamu wa akili?"

"Hapana, hajapoteza utimamu wa akili. Unajua labda kwa kipindi hicho... Mariam ndiyo alikuwa amepatwa tu na hiyo shida ghafla kwa hiyo hata hao waliomwangalia inaonekana hawakumwelewa vizuri. Madaktari wengine ni wajinga, wana... wanafanya vitu haraka-haraka bila kuchunguza vizuri..." nikamwambia hivyo.

Akapiga ulimi wake mdomoni na kuangalia pembeni.

"Ila usijali. Mariam anaweza kusaidika. Ninaomba tu unipe ruhusa ili niweze kumsaidia," nikamwambia hivyo kwa upole.

"Unataka kumpa msaada gani sasa? Kama ni madawa ameshatumia mengi mpaka nikaogopa angejazwa sumu mwilini..."

"Hapana, usijali. Msaada naotaka kumpatia ni wa kisaikolojia. Nataka nicheze na akili yake kwanza, nimwelewe vizuri zaidi, kisha ndiyo nitampa msaada unaomfaa YEYE. Hawezi kufanana na wagonjwa wengine... kwa hiyo atakuwa na njia tofauti ya kupona," nikamwambia.

Macho mazuri ya mwanamke huyu yakawa yananitazama bila kukwepesha hata kidogo, nami mpaka nikahisi ajabu kiasi.

"Unanipa uhakika kwamba... atapona?" akaniuliza hivyo.

Sauti yake tamu sana ilijaa matumaini aliponiuliza hivyo, nami nikasema, "Ndiyo. Atapona."

Akaangalia chini kiasi akionekana kutafakari vitu.

"Nitahitaji kwenda naye hospitali kwanza... tuonane na daktari aliye-specialize zaidi kwenye magonjwa ya hivi ili nijue mambo ya kufanya kwa uhakika," nikamwambia.

"Hospitali gani?" akaniuliza hivyo.

"Muhimbili," nikamjibu.

Akaniangalia kwa macho yenye umakini.

Najua alikuwa anajaribu kusawazisha wazo la mimi kwenda na mdogo wake sehemu ya mbali, ile hali ya kutoniamini bado ikionekana wazi, nami nikamwambia, "Tutaenda pamoja na Tesha, ukiona ni sawa. Maana wewe unakuwa kazini. Unaonaje?"

Akatikisa kichwa kukubali.

Nikatabasamu kidogo na kusema, "Sawa basi... nashukuru. Uta... fanya unachotaka kumwandaa ili labda kesho twende huko... nitakuwa nimeshawasiliana na huyo daktari."

"Gharama ya haya yote haitakuwa nyingi?" akaniuliza.

"Hapana, wala... sifanyi hivi ili unilipe. Unafikiri kila kitu ni pesa tu?"

"Nilidhani wewe ndiyo unafikiri hivyo. Kwamba mtu akikusaidia basi ni lazima anataka kulipwa. Au nakosea?" akaniuliza hivyo kwa umakini.

Ohohoo, povu!

Pozi likaniisha kidogo kwa sababu nilielewa maana ya kauli hiyo vizuri sana. Alikuwa ananiunguza, tena kunichoma kwa ule moto mkali wa kumbukumbu ya kile nilichomfanyia mara ya kwanza tumekutana. Si nikakumbuka kweli nilitoa elfu mbili na kujaribu kumpatia kama malipo kwa ule msaada alionipa?

Inaonekana hiki ni kitu ambacho bado kilifanya awe na shuku kunielekea japo hakuniona kuwa mtu mbaya, oh nasema hivyo kwa sababu sikuwa nimesahau namna alivyonikumbatia ule usiku alipotoa shukrani kwa ajili ya msaada niliompa mdogo wake, na hapo kiukweli nikawa nimejifunza somo muhimu.

Shukrani zetu zilitofautiana, na ya kwake ndiyo iliyofaa zaidi. Mimi kumpa hela siku ile amenisaidia labda kulifanya ahisi nimemdharau hata kama sikuwa na nia hiyo, lakini yeye aliponikumbatia kwa shukrani japo nilikuwa nimelewa, alionyesha ni kitu kilichotoka moyoni mwake, na ni jambo lililonigusa sana usiku huo.

Kwa hiyo hapa kiukweli alikuwa amenipa fundisho dogo lakini lenye maana kubwa sana, nami nikatabasamu tu kidogo na kutikisa kichwa kuonyesha uelewa wa kauli yake kwa njia nzuri.

Akashusha pumzi na kusema, "Okay. Nashukuru pia kwa... jitihada yako. Nitamwandaa Mamu baadaye ili kesho mwende. Tesha atakuwa nanyi."

Nikatikisa kichwa kukubali, nami nikasema, "Asante kwa kukubali. Ngoja niende sasa. Tutaonana... labda baadaye... au... kesho..."

Alikuwa ananitazama tu machoni kwa mkazo kama vile ananishangaa kutokana na kubabaika kwa yale niliyosema, nami nikaibana cheko yangu na kusimama. Nikampungia kiganja kwa chini kama kumuaga, naye akatikisa kichwa kukubali.

Nikatoka hapo ofisini nikiwa nimefarijika kutokana na kukubaliwa ombi langu, japo mwanamke huyo alinipiga bomu zito kiasi la rohoni. Ile ndiyo nimegeuka tu na kutazama upande wake Soraya, nikakunja uso kimaswali kiasi baada ya kukuta kuna mtu mwingine aliyekuwa amesimama usawa wa meza hiyo ya mapokezi, naye hakuwa mwingine ila yule Joshua!

Nikamtazama machoni kwa mkazo kiasi, nikiwa najiuliza kwa nini alikuwa amekuja hapo. Kumwona mwanaume huyo kazini kwa Miryam ilinifanya nipatwe na hisia mbaya kwamba huenda alikuwa amekuja kumfanyia fujo dada mkubwa na huku tena, wakati alipewa msamaha wa kutofungwa jela na Miryam mwenyewe.

Alisimama kwa utulivu huku akiniangalia kwa njia ya kawaida, nami nikamwona Soraya akimwonyesha ishara ya kumruhusu aje upande huu wa ofisi. Jamaa akatembea taratibu na kufika karibu zaidi na niliposimama.

Nikawa namwangalia kwa ujasiri machoni, na kwa sababu alizozijua yeye, wakati huu hakuwa akinitazama kwa njia ya chuki kama vile alivyoniangalia mara ya mwisho tumeonana.

"Niaje mtu wangu?" akanisalimia hivyo.

Mh?

Ilikuwa ni kama kumpiga kofi kidogo Shetani ili kuona ikiwa atakurudishia la kwake kwa utani, lakini mimi sikutaka kufanya matani yoyote na huyu mtu. Sikuwa na uhakika, lakini kwa kumwangalia tu, nilihisi ujio wake hapa ulikuwa wa nia mbili; yaani bado singeweza kuamini kuwa alikuja hapa kwa lengo la kusaka amani. Zamu hii angekuwa anataka nini kutoka Miryam?



★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA KUMI NA MBILI

★★★★★★★★★★★★★★★★


Ankia akawa amefika hapo, naye Tesha akabadili mada upesi huku tukianza kutembea tena.

"Dah, kaka yaani nilikuwa sijategemea. Hilo ni bonge la mtoko, yaani halikufaa kuletwa Masai, au siyo Ankita?" Tesha akasema hivyo.

"Mmm... JC umegharamika kweli, yaani! Hiyo Dompo ilivyo tamu! Kweli tuje tupate kamshiko tufanye hii kitu kama hii," Ankia akasema hivyo.

"Yeah. Tutaenda sehemu nyingine nzuri siku moja," nikawaambia hivyo.

"Mwamba nikaona manoti tu unatoa, dah! Halafu ulikuwa unakataa eti siyo wa kishua," Tesha akasema hivyo.

"Ahahaha... siyo lazima kuwa wa kishua. Je kama nimeziiba, utajuaje?" nikamuuliza.

"Aa wapi. Ma' mkubwa kaniambia we' doctor. Ankia ulikuwa unajua jamaa ni doctor?" Tesha akamuuliza.

"Wewe... kweli?" Ankia akamuuliza hivyo.

"Uhakika. Anafanya kazi Muhimbili kabisa..."

"Wacha we! Mwanaume ana siri huyu!" Ankia akasema hivyo na kunisukuma.

Nikatabasamu kidogo.

"Tena anayo siri nzito kinoma. Ndo' umchune sasa. Oy JC, mkifika ndani mwonyeshe sugar mommy tiba ni nini," Tesha akasema hivyo kiutani.

Sote tukacheka kidogo, na masihara yakaendelea mpaka tulipofika getini kwao Tesha.

Nikachukua mfuko aliobeba Ankia na kutoa nyama ya kitimoto kilo moja, nami nikamwambia Tesha apeleke hiyo kilo tatu kwao ili wakajikamulie pia. Akasema Mariam angefurahi kweli maana alizipenda, na ndiyo lililokuwa lengo langu.

Ankia akawa ameenda kufungua geti letu, nami nikamwambia Tesha asiseme kwa watu wa familia yake kwamba mimi ndiyo nilinunua hicho chakula, na ni kitu kilichofanya aniulize kwa nini.

Nikamwambia tu aseme yeye ndiyo kanunua au hata asiseme lolote, maana kutokana na maelezo ya mama zake wakubwa kumhusu Miryam waliyonipa leo, sikufikiri hiki ni kitu ambacho dada yake angefurahishwa nacho; yaani kujua nimewanunulia kitu fulani.

Lakini sikumwambia Tesha kuhusu hilo, naye akaridhia tu kwa hicho nilichomwambia na kwenda kwao baada ya kuagana kirafiki. Ankia wangu alikuwa ananisubiria getini, nami nikajiunga naye na kuelekea ndani.

Mwanamke alionekana kutosheka kiasi na Dompo moja aliyokuwa amekunywa maana alikuwa na uchangamfu kweli, akinikumbushia kuhusu namna ambavyo watu walikuwa wanatutazama sana kwa macho yenye husuda, nami nikamsaidia tu kuingiza vitu vilivyotakiwa kuingia ndani na kufunga mlango.

Nilipokuwa tu ndiyo nimemaliza kufunga mlango na kugeuka kumwangalia, nikakuta akiwa ameinama karibu na sehemu yenye extension iliyochomekea nyaya za TV na king'amuzi, akionekana kutaka kuweka simu yake chaji. Kuinama kwake kulifanya shati lake lipande juu na kufunua mapaja yake mpaka kalio, lililositiriwa kiasi tu na kiboksa-skinny chake. Alikuwa na makalio makubwa! Mambo yangu ikaanza kupanda, bila kupenda.

Alikuwa anahangaika kuichomekea simu waya sijui, nami nikawa namwangalia tu kwa matamanio kiasi. Nasema kiasi kwa kuwa mawazo yangu yalikuwa mbali na kile ambacho mwili wangu ulitaka, kwa hiyo sikuwa nimeelekeza fikira zangu zote kwa Ankia japo alinivuta. Akawa amemaliza kuweka simu yake na kusimama vizuri tena, naye akaniangalia na kusema kitu fulani ambacho sikukazia fikira haraka.

"Mbona umesimama tu hapo?" akaniuliza hivyo tena.

"Naam?" nikawa kama nimeshtuka.

"Nimekuuliza mbona umeufunga mlango? Hauendi kujimwagia kama kawaida yako?" akasema hivyo.

"Ah... nimeona uvivu hata kwenda kujimwagia... feni itanihusu," nikamwambia hivyo na kusogea usawa wa sofa.

"Tukae kidogo... bado mapema..."

"Ishaingia saa sita mbona... na we' si unapendaga kulala mapema, vipi leo?"

"Sijachoka kihivyo," akaniambia hivyo na kunipita.

Alikuwa akielekea upande wa chumba chake, kalio lake likitikisika si mchezo, nami nikamwambia, "Kumbe unataka kuchoka ndo' ulale?"

"Eee, bado nimechangamka," akajibu.

"Nikusaidie?" nikamuuliza.

Akawa ameufikia mlango wake na kunigeukia, naye akatabasamu na kuuliza, "Unisaidieje?"

Nikamfata mpaka kufikia hapo aliposimama na kusema, "Kukuchosha."

Akasema, "Haya... nichoshe."

Alikuwa ananiangalia kwa macho yenye uvutio, nami nikamshika kiunoni kwa nguvu na kumvuta kwangu. Alipodhani nataka kumbusu mdomoni, mimi nikamgeuza na kumfanya anipe mgongo, kisha nikamsukumia ukutani na kumkandamiza hapo kiasi.

"Ah... JC... mbona hivyo?"

Akasema hivyo kwa deko, nami nikaishika shingo yake kutokea nyuma na kukivuta kidevu chake ili nimtazamishe kwangu.

Kwa sababu alikuwa mfupi alijipinda vyema kwa mbinuko wa mgongo, huku kalio lake likiwa linaukandamiza uanaume wangu, naye akawa ananiangalia kilegevu kukubali utesaji huo wa mwanzo. Unajua ni pombe tu ndiyo ilinipandishia mzuka namna hiyo la sivyo nisingejishughulisha naye kabisa.

(........).

(........).

Bado tulikuwa na nguo mwilini, kwa hiyo hiki kilikuwa cha kuchoshana haraka tu. Mkono wake mmoja alikuwa anaurudisha nyuma kama kuniambia nipunguze kasi, lakini nikawa naushikilia kwa nguvu na kuendelea kumtandika tu. Alikuwa analia siyo mchezo.

(........).

(........).

(........).

Tukatoka ukutani mpaka kwenye sofa. Piga haswa, naye akapasua bomba. Nikamuuliza tukiachia hapo vipi, lakini akanijibu kwa kuirudisha ndani yeye mwenyewe. Dah! Kazi!

Pombe ilikuwa inazunguka vizuri mwilini kwa kuwa sikudhani kama ningeweza kukata dakika nyingi sana nikicheza naye tu namna hiyo, na ndipo alipopasua lingine mimi pia nikalisaka goli langu. Lakini halikutoka. Nilichokuwa nasikia kimenibana ilikuwa ni mkojo, nami nikakwazika kiasi kwa sababu sikupata kale kahisia ka mridhiko kanakoletwaga na ile kitu kutoka. Ah mwanaume anaelewa!

Ila kumtandika Ankia namna hiyo kwa mara nyingine kuliridhisha sana, nami nikaona nimwache tu hapo sofani na kwenda zangu jikoni. Nilichukua chupa tupu ya maji ili nikojoe humo maana choo kilikuwa nje na mlango nilikuwa nimeshafunga. Kisha nikaenda pamoja nayo chumbani na kuiacha huko.

Nikaitoa feni na kuipeleka hapo sebuleni, kisha nikaiwasha na kuielekeza kwa mwenye nyumba wangu. Alikuwa amelala kwa kujiachia huku jasho kama lote likimtoka, nayo feni ikaanza kutupuliza vizuri nilipokaa karibu yake pia.

Kwa kuwa nilikaa karibu na alipolaza kichwa chake, akajinyanyua na kuishika mashine yangu, kisha akaitumbukiza mdomoni. Ah yaani kama alijua. Nikawa mgumu hata zaidi na hatimaye kurusha risasi kama zote. Aah kale kahisia sasa!

Nikawa nashtuka-shtuka huku nikiona nyota tu, nami nilipomwangalia mtoto nikakuta nimemlowanisha usoni kabisa, kitu ambacho kilifanya nicheke kidogo maana ni kama alikuwa amemwagikiwa na uji!

Akajinyanyua na kuelekea chumbani kwake bila kusema lolote, nami nikamwahi kabla hajafikia mlango na kumpiga kofi kalioni. Akanigeukia na kuachia tabasamu hafifu, naye akanipiga begani kidogo.

"Si umechoka sasa?" nikamuuliza.

Akatikisa kichwa kidogo kukanusha.

"Aaaa... kwa hiyo tuendelee? Njoo," nikamwambia hivyo huku nikimvuta.

"Hamna, natania tu... nimechoka..." akawa anakataa huku akicheka.

"Twende nikumwagie uji mwinginee..." nikamwambia kwa sauti nzito ya mchezo.

"Iih wewe... sitaki..." akasema hivyo huku akicheka.

Akakimbilia chumbani kwake na kufunga mlango, nami nikasema, "Njoo tuchoshane bwanaa..."

"Choka wewe tu. Mtu mwenyewe hata huchoki, sijui binadamu wa aina gani..."

Akasikika akisema hivyo, nami nikacheka kidogo. Alifikri sijachoka kwa sababu ya muda niliotumia bila kufika mwisho mapema, lakini kimwili nilikuwa nimechoka.

Tayari ikawa imeingia saa saba usiku, nami nikaona tu nizime taa na kuibeba feni, maana Ankia hakutaka kutoka tena. Kwa hiyo tungekuja kuonana kukishakucha, na nilikuwa sijasahau mipango mingine ya kushughulika nayo kwa siku hii ambayo ingefuata; mipango ya kumsaidia binti Mariam. Nikaingia zangu chumbani na kulala.


★★★


Asubuhi na mapema ya saa tatu tu nikawa nimeamka. Oh hii kwangu ndiyo ilikuwa mapema sana kwa hizi siku za mapumziko yangu huku, na cha kwanza nilichokuwa nataka kufanya kabla ya mengine ni kujisafisha kinywa na mwili; hasa kwa kuwa nililala bila kujimwagia usiku uliopita.

Nikapitia jumbe mbalimbali kwanza kwenye simu na kujibu chache, kisha nikachukua vifaa vya usafi na kutoka ndani ya chumba. Nilidhani labda Ankia angekuwa hajaamka bado kutokana na uchovu wa usiku lakini mwanamke huyo alikuwa na bidii.

Tayari, alikuwa ameshaamka, ameshafanya usafi, bila shaka mapema sana, nami nikatoka nje na kumkuta akiwa anamalizia kufua mashuka yake pamoja na yale ambayo niliyaondoa kitandani kwangu usiku ule nimefanya mapenzi na Joy. Na nilikuwa nimeyaweka tu pembeni ili kuja kuyafua baadaye, ila Ankia akawa ameniwahi.

Alikuwa amevalia T-shirt lake la Yanga na khanga kutokea kiunoni, nami nikampa salamu kwa kuliminya shavu la kalio lake alipokuwa akianika shuka. Akatabasamu kwa furaha na kunipa salamu pia, nami nikamtania kwa kuuliza ikiwa alitaka kunywa uji mwingine asubuhi hii. Akacheka tu na kunipiga kidogo begani, nami nikamshukuru kwa kunisaidia kufua, kisha nikamwacha na kwenda upande wa sinki kuosha domo.

Nilitazama upande wa nyumba yao kina Tesha na kuona kwamba gari la Miryam halikuwepo, kumaanisha tayari alikuwa ameenda kazini kwake. Nikaelekea bafuni baada ya kuweka maji kwenye ndoo na kuoga, kisha nikarudi ndani tena. Ankia alikuwa ameshamaliza kufua na wakati huu alikuwa anatengeneza chai jikoni, hivyo nikaelekea chumbani na kujitengeneza vyema pia kwa sababu nilitaka kuondoka.

Nikavaa jeans yangu nyeusi, kisha nikaenda kumwomba Ankia pasi ya umeme ili ninyooshe T-shirt langu jeupe la mikono mifupi (Manga). Akawa ndiyo ameniuliza ninakwenda wapi, nami nikamwambia tu naenda huko Mbagala kukutana na mtu kifupi kisha ningerudi. Alikuwa anasisitiza ninywe chai kwanza, yaani amalize kuichemsha kisha afate chapati upesi kwa ajili yetu, lakini nikamwambia asijali; ningekunywa chai huko huko tu, kwa hiyo asiharakishe chochote.

Basi, nikamaliza kunyoosha kiwalo changu na kukitupia mwilini, nikahakikisha niko vizuri kichwani, na kufikia wakati huu nilikuwa na uhitaji wa kunyoa kiasi ama kuchonga nywele. Lingekuwa jambo la kufanya baadaye. Nikatoka na kumkuta Ankia sebuleni, akiwa amesimama usawa wa sofa huku akitazama jambo fulani kwenye TV, nami nikafika karibu yake na kusimama pia.

Akaniambia kwamba kiukweli, bila unafiki wowote, nilijaliwa kuwa na sura nzuri sana, na hata ile kumwambia tu kwamba ninatoka kwenda kukutana na mtu fulani ilimfanya ahisi wivu kwa kukisia kwamba ni mwanamke, japo tulikuwa tumeshakubaliana kwamba hakupaswa kuziacha hisia za namna hiyo zimtawale.

Mimi nikatabasamu tu kwa kumwelewa, nami nikaona nimpe busu laini tu ya kupoza roho. Akauliza ikiwa nilihitaji anitunzie chakula kwa ajili ya mchana, nami nikasema ningemjulisha kwa njia ya ujumbe endapo kama ningechelewa. Nikamwachia elfu kumi nikimtania kwamba kama akitaka basi akanunue Dompo aje kupigia ndani, naye akafurahi sana na kunibusu tena, kisha mimi huyo nikaondoka zangu.

★★

Sikupata shida kufika Mzinga na kuchukua usafiri wa kuelekea Mbagala, na kama kawaida, nilivuta macho ya wengi. Ah hiyo ni kunipandishia tu hisia za kujiamini lakini ililemea mno. Watu wa huku walijua kukodolea macho mpaka ilichosha!

Nikafika Mbagala, nami nikakunja kona mpaka kufikia Zakhem, kisha nikachukua bajaji kuelekea Kijichi. Ndiyo, Kijichi. Mpango ulikuwa kwenda kukutana na bibie Miryam ili nizungumze naye kuhusiana na mdogo wake, Mariam, na nilitaka mazungumzo yetu yaende vizuri sana maana yule mwanamke alionekana kupenda vitu vilivyonyooka; masihara pembeni yaani, na kwa jambo hilo sikutaka ahisi labda namchezea.

Kwenye bajaji niliyopanda niliketi nyuma pamoja na wadada wawili kwenye miaka ya ishirini na kitu mpaka thelathini hivi, wenye mionekano mizuri kweli kwa jinsi walivyovaa na kusuka, na dereva wa bajaji alikuwa anaongea nao kwa njia ya kichokozi na kuwafanya wafurahie. Mimi nilikuwa makini tu, na kila mara ambayo ningemwangalia aliyekaa karibu nami, alikuwa ananikata jicho la upendezi huku akilishusha kimadoido, na hatimaye akanifanya nitabasamu.

Dereva wa bajaji alikuwa mwongeaji sana, akihamishia mpaka mazungumzo yao kunielekea mimi kwa kuwaambia waniombe namba maana mimi ndiye niliyekuwa mwanaume mzuri wa kutoka nao, lakini walionekana kuniogopa kutokana na jinsi nilivyoonyesha kutokuwa na habari nao. Sasa si dereva akaongeza presha? Nikaona nitende jambo.

Ile tumefika kituo cha Upendo hatimaye, nikashuka, nikalipa, kisha nikawasemesha hao wanawake. Nikamwomba huyo mmoja simu yake niandike namba, naye akacheka tu. Dereva akawa anawapampu wachukue namba la sivyo wangepoteza bahati eti.

Mwenzake na huyo dada aliyeona aibu hakupoteza muda na kunipa ya kwake, nami nikaandika namba yangu na kumrudishia, kisha nikamwambia 'nitext,' halafu nikaanza kuondoka. Nilifanya hivyo kwa sababu kiukweli wanawake hao walikuwa wazuri, ila sikuwa na nia yoyote ile ya kutoka nao. Nia yangu ilikuwa nyingine tu.

Nikafika pale kwenye duka la bibie Miryam, na hapo nje nikakuta gari lake pamoja gari lingine jeusi aina ya Toyota Kluger. Bila shaka angekuwa na mgeni wa masuala yao ya kibiashara, nami nikaelekea mpaka ndani huko. Nikamkuta Mamacita Soraya akiwa ameketi kwenye kiti chake mezani kwa mapokezi, na tabasamu aliloachia lilitosha kueleza ni namna gani alivyokuwa amefurahi kuniona.

Akiwa amevaa ushungi kichwani kama kawaida yake, uso wake mweupe ulipendeza sana. Nyusi zilizotindwa vyema na lipstick ya zambarau mdomoni, pamoja na macho yake makubwa kama ya kiarabu yalivutia mno. Nguo aliyovaa ilikuwa kama gauni la njano lakini lenye mtindo wa sari lenye kubana kufunika mwili wake wote kutokea kifuani, na kwa sababu ya kukaa sikuweza kumchora vizuri.

"JC!" akaniita kwa shauku tulivu.

"Mambo vipi Cute Soraah?" nikamwambia hivyo.

"Hee! Umelitoa wapi hilo jina?"

"We' kwani umeliandika wapi?"

"Hahah... umeshanitafuta mpaka Facebook?"

"Ndiyo maana yake. Una tupicha tukali kweli, siyo rahisi kuamini una miaka 30..."

"Ahahaha... kwa nini?"

"Unaonekana mdogo kweli. Upo sahihi kujiita Cute... na me sa'hivi nitakuwa nakuita Soraah..."

Akacheka kidogo kwa haya.

"Ama ni la mume wako tu kukuita?" nikamuuliza.

"Hamna... niite tu hivyo. Napenda."

"Eti eh?"

Akatikisa kichwa kukubali.

Ni hapa ndiyo simu yangu ikatoa mtetemo kutokea mfukoni mwa suruali yangu kuashiria kuna ujumbe umeingia, nami nikautoa ili kuona ni nani.

"Na me itabidi nikutafute FB nijue una miaka mingapi," Soraya akaniambia hivyo.

Nikatabasamu kidogo na kusema, "Itakuwa vizuri."

Nikaona ujumbe huo ulioingia kwenye simu kutoka kwa namba ngeni, aliyetuma akisema 'mambo,' nami nikakisia kuwa huenda ni yule mwanamke wa kwenye bajaji.

"Na wewe lazima uwe na tupicha tuzuri FB. Nitakuona," Soraya akasema hivyo.

"Hamna hata, mbaya," nikamwambia hivyo kiutani.

"Mh... labda umdanganye mtu ambaye hajawahi kukuona," akasema hivyo na kucheka kidogo.

Nikamjibu aliyenitumia ujumbe 'saf, nan?' naye akajibu, 'me naitwa Winny tumekutan kw bajaj.' Nikaona Soraya ananitazama tu kwa utulivu, nami nikampa tabasamu hafifu na kumjibu huyo "Winny" kwamba ningemtafuta baadaye maana kuna jambo nilikuwa nashughulika nalo.

"Sawa. Vipi... boss wetu yupo na mgeni?" nikamuuliza hivyo na kuweka simu mfukoni.

"Eeeh. Umekuja kuonana naye?"

"Ndiyo, nimekuja kuongea naye. Itabidi kusubiri eh?"

"Ee, ila ngoja tu nimpigie nimwambie ana mgeni hapa mwingine..."

"Hapana, acha tu. Nitasubiri. Na sisi tupige story zetu kwa huo muda. Za nyumbani?" nikamuuliza hivyo.

"Nzuri tu. Ndo' ukanichunia jana..."

"Mh? Saa ngapi?"

"Jana, si nilikutext mida ya saa nne hivi, lakini hukujibu," akaniambia hivyo.

"Kweli? Itakuwa hazikufika labda. Pole," nikamwambia hivyo.

"Haina shida."

"Basi ukaumia?"

"Wala hata..."

"Hahah... sema tu... nitafidishia hilo kwa chochote utakachotaka..."

"Mh... ahahaa... wanaume bwana..."

Nilipenda sana alivyofanya macho yake aliposema hivyo, na kiukweli niliweza kuhisi uvutio wangu kumwelekea ukiongezeka. Nikaanza kumtamani sana mwanamke huyu, ikiwa ni hisia iliyojijenga upesi sana.

"Mbona sasa ukanitafuta saa nne usiku kabisa?" nikamuuliza.

Akaniangalia tu na kutabasamu kiasi.

"Ulikuwa unataka tuimbiane na nyimbo za kupeana usingizi eti?" nikamuuliza kiutani.

Akapandisha nyusi zake kukubali, nami nikacheka kidogo kwa kuelewa alikuwa anatania pia.

Hapo hapo mlango wa ofisi ya Miryam ukafunguka, nasi sote tukautazama. Tabasamu nililokuwa nalo usoni likaondoka, nami nikaweka uso makini zaidi baada ya kumwona Festo akiwa anatoka ndani huko. Yule yule mchumba Festo aliyedhaniwa kuwa ndiyo mimi hapa mara ya kwanza kabisa nimefika nyumbani kwake Miryam, ndiyo alikuwa hapo.

Miryam pia akatoka ofisini na kusimama baada ya kuniona sehemu hiyo, nami nikaendelea kujituliza tu. Kulikuwa na ukimya mfupi ulioijaza sehemu hiyo hali nyingi tofauti kifikira, kwa sababu niliona Festo akinitazama kwa macho yenye udadisi, kisha akamwangalia Miryam pia. Bibie Miryam alikuwa ananitazama tu kwa umakini, yeye bila shaka akijiuliza kwa nini niko hapo, lakini Festo akiwa kama anahukumu kwa nini niko hapo.

Nikawaza sijui jamaa bado alikuwa anafukuzia manzi huyo, manzi mwenyewe alikuwa mgumu kweli kulainika! Ni lazima tu Festo hakuwa amefika hapo kibiashara, bali lengo lake lilikuwa kuongea zaidi na Miryam kumshawishi waweze kuungana kimahusiano. Ilieleweka alikuwa amemwelewa.

Lakini mimi nisingejua undani wa mambo yaliyoendelea baina yao, na hayakunihusu. Ila kwa jinsi Festo alivyoniangalia, ilikuwa ni kama vile fahali mpya kaingizwa kwenye zizi lenye fahali mwingine, na hiyo ilifanya nijiulize sababu ni nini.

Huenda alikuwa anafikiri mimi pia namfukuzia huyo dada maana alinikuta huko kwao siku ile amekuja kumchumbia, kwa hiyo labda alifikiria katika sababu zilizofanya akataliwe siku ile na mimi nilikuwemo. Ah! Kama ndiyo ilikuwa hivyo basi ningepaswa kuwa mwangalifu sana nisije kujikuta napigwa mshale kifuani bila kuelewa somo, si unajua wivu wa mapenzi?

Jamaa akaniangalia tena, kisha akasogea karibu nami na kusimama. Nikawa namwangalia tu kwa utulivu, naye akaninyooshea mkono wake kwa njia ya salamu. Nikaupokea, tukaitingisha kwa pamoja bila kusemeshana chochote, kisha mwamba akaondoka. Alikuwa nadhifu kweli, nguo zake zikionekana wazi kuwa za gharama, nami nikamwangalia Miryam usoni.

Kama kawaida yake, katika uzuri hakuangusha hata kwa kidogo alichoweka mwilini. Alikuwa amevaa blauzi nyeupe yenye mikono mirefu pamoja na sketi ndefu ya jeans ya blue, na nywele zake alizibana kwa nyuma. Bado aliniangalia kwa macho yenye subira tu, nami nikawa natafuta salamu iliyofaa kumpa kwa wakati huu.

"Dada... JC ndiyo kafika. Anataka mfanye mazungumzo," Soraya akaingilia kati ukimya wetu.

Miryam akanitazama usoni tena, kisha akatikisa kichwa kukubali na kuingia ofisini kwake.

Nikamwonyesha Soraya ishara ya mapigo ya moyo kudunda kwa nguvu, naye akacheka kidogo bila kutoa sauti, kisha nikaenda zangu ofisini kwa bibie.

Sikuwa na hofu, ila kwenye kuongea na huyo mwanamke kuhusu suala la familia yake kungehitaji busara. Sikuwa nimeisahau motto yake hata kidogo: sipendi michezo isiyo na faida. Kwa hiyo hapa ningehakikisha namwonyesha kuwa sikuja kufanya mchezo, ili kutokea hapa aanze kunichukulia 'serious.'

Nikaingia ofisini humo na kwenda kukaa kwenye kiti sehemu ya meza yake mkurugenzi, huku yeye akiwa amekaa kwenye chake cha kibosi. Alipendeza sana huyu mwanamke kwa namna alivyojiweka tu yaani. Kawaida. Hakupenda makuu, lakini alionekana kupenda sana maendeleo ndiyo maana hata na sehemu hii ya kikazi alikuwa ameipanua vizuri sana. Nilihisi kama vile niko kwenye kampuni kabisa!

Akiwa ananiangalia kwa macho yenye subira, nikamwambia, "Habari za kazi dada yangu?"

"Ni nzuri. Mbona umekuja hapa? Kuna tatizo lolote?" akaniuliza hivyo.

"Ha..pana... siyo hivyo. Hamna tatizo. Kwa nini unafikiri mimi kuja ni mpaka kuwe na tatizo? Sura yangu imeandikwa 'matatizo' au?" nikamwambia hivyo kiutani.

Nikaona anatoa tabasamu hafifu na kuangalia chini, nami nikacheka kidogo kwa kupata kitulizo kiasi.

"Sawa. Niambie," akasema hivyo.

Nikasafisha koo kidogo na kusema, "Nimekuja ili tuzungumze kuhusu mdogo wako... Mariam."

Akabaki kimya na kuendelea kunitazama kwa utulivu.

"Sijui ikiwa... mama zako walikwambia kuhusu maongezi yetu jana?" nikamuuliza.

"Ndiyo waliniambia. Wewe unataka kipi kutoka kwa Mariam?" akaniuliza.

"Nataka kumsaidia. Mdogo wako ana kasoro ndogo kwenye ubongo wake ambayo nina imani inaweza kushugulikiwa na kuondolewa kwa njia ya... ya kwake yaani. Nimemwangalia nikaona ana njia tofauti za kuitikia mambo...."

"Ni kasoro gani unayoongelea?" akanikatisha.

"Sijawa na uhakika sana, ila nafikiri mdogo wako atakuwa amepatwa na kitu kinachofanana na ASD," nikamwambia hivyo.

"Ndiyo nini hiyo?" akauliza.

"Autism Spectrum Disorder. Ni ugonjwa unaozuia maendeleo ya utimamu kwa mtu unaosababishwa na tofauti zinazojitokeza kwenye ubongo. Wanaokuwa na hii kasoro huwa wana matatizo ya kuwasiliana, ama tabia na mapendezi yanayojirudia-rudia, na... njia zao za kujifunza zinakuwa tofauti sana na ukawaida wa watu wengine. Hii huwapataga sanasana watoto wadogo kwa sababu ubongo wa mtoto bado unakuwa unaendelea kukua mpaka anapofikisha miaka kama 15, ndiyo unakuwa umekomaa. Ubongo wake Mariam tayari ulikuwa umeshakomaa alipopatwa na shida kama hii, kwa hiyo nafikiri tunaweza kumsaidia arudishe utimamu wake mzuri licha ya kwamba muda umepita..." nikamwelezea.

Akawa ananitazama tu machoni kwa umakini.

"Unaonaje kuhusu hilo?" nikamuuliza.

Akaangalia chini kiasi, kisha akanitazama na kuuliza, "Wewe... ni daktari kweli?"

Swali lake likaniacha namwangalia tu usoni kwa ufikirio, kwa sababu ilikuwa wazi kwamba mpaka kufikia hapo bado alikuwa haniamini; haijalishi hata kama suala la mdogo wake kuokolewa asigongwe kwa gari lilitoka kwangu. Bila shaka aliambiwa na mama zake wakubwa kwamba mimi ni tabibu, lakini bado bibie alikuwa na mashaka yake kunielekea.

Nikashusha pumzi kiitulivu, nami nikamwambia, "Ndiyo. Mimi ni daktari."

"Unajua... Mariam nimeshampeleka hospitali na... wanasema nimwache wodi za vichaa. Kwa haya uliyoniambia unamaanisha kwamba mdogo wangu siyo kichaa, si ndiyo?" akaniuliza.

"Ndiyo. Mariam siyo kichaa, anaumwa tu kwenye ubongo."

"Sasa kwa nini walikuwa wananiambia mdogo wangu ni kichaa, sijui... amepoteza kabisa utimamu wa akili?"

"Hapana, hajapoteza utimamu wa akili. Unajua labda kwa kipindi hicho... Mariam ndiyo alikuwa amepatwa tu na hiyo shida ghafla kwa hiyo hata hao waliomwangalia inaonekana hawakumwelewa vizuri. Madaktari wengine ni wajinga, wana... wanafanya vitu haraka-haraka bila kuchunguza vizuri..." nikamwambia hivyo.

Akapiga ulimi wake mdomoni na kuangalia pembeni.

"Ila usijali. Mariam anaweza kusaidika. Ninaomba tu unipe ruhusa ili niweze kumsaidia," nikamwambia hivyo kwa upole.

"Unataka kumpa msaada gani sasa? Kama ni madawa ameshatumia mengi mpaka nikaogopa angejazwa sumu mwilini..."

"Hapana, usijali. Msaada naotaka kumpatia ni wa kisaikolojia. Nataka nicheze na akili yake kwanza, nimwelewe vizuri zaidi, kisha ndiyo nitampa msaada unaomfaa YEYE. Hawezi kufanana na wagonjwa wengine... kwa hiyo atakuwa na njia tofauti ya kupona," nikamwambia.

Macho mazuri ya mwanamke huyu yakawa yananitazama bila kukwepesha hata kidogo, nami mpaka nikahisi ajabu kiasi.

"Unanipa uhakika kwamba... atapona?" akaniuliza hivyo.

Sauti yake tamu sana ilijaa matumaini aliponiuliza hivyo, nami nikasema, "Ndiyo. Atapona."

Akaangalia chini kiasi akionekana kutafakari vitu.

"Nitahitaji kwenda naye hospitali kwanza... tuonane na daktari aliye-specialize zaidi kwenye magonjwa ya hivi ili nijue mambo ya kufanya kwa uhakika," nikamwambia.

"Hospitali gani?" akaniuliza hivyo.

"Muhimbili," nikamjibu.

Akaniangalia kwa macho yenye umakini.

Najua alikuwa anajaribu kusawazisha wazo la mimi kwenda na mdogo wake sehemu ya mbali, ile hali ya kutoniamini bado ikionekana wazi, nami nikamwambia, "Tutaenda pamoja na Tesha, ukiona ni sawa. Maana wewe unakuwa kazini. Unaonaje?"

Akatikisa kichwa kukubali.

Nikatabasamu kidogo na kusema, "Sawa basi... nashukuru. Uta... fanya unachotaka kumwandaa ili labda kesho twende huko... nitakuwa nimeshawasiliana na huyo daktari."

"Gharama ya haya yote haitakuwa nyingi?" akaniuliza.

"Hapana, wala... sifanyi hivi ili unilipe. Unafikiri kila kitu ni pesa tu?"

"Nilidhani wewe ndiyo unafikiri hivyo. Kwamba mtu akikusaidia basi ni lazima anataka kulipwa. Au nakosea?" akaniuliza hivyo kwa umakini.

Ohohoo, povu!

Pozi likaniisha kidogo kwa sababu nilielewa maana ya kauli hiyo vizuri sana. Alikuwa ananiunguza, tena kunichoma kwa ule moto mkali wa kumbukumbu ya kile nilichomfanyia mara ya kwanza tumekutana. Si nikakumbuka kweli nilitoa elfu mbili na kujaribu kumpatia kama malipo kwa ule msaada alionipa?

Inaonekana hiki ni kitu ambacho bado kilifanya awe na shuku kunielekea japo hakuniona kuwa mtu mbaya, oh nasema hivyo kwa sababu sikuwa nimesahau namna alivyonikumbatia ule usiku alipotoa shukrani kwa ajili ya msaada niliompa mdogo wake, na hapo kiukweli nikawa nimejifunza somo muhimu.

Shukrani zetu zilitofautiana, na ya kwake ndiyo iliyofaa zaidi. Mimi kumpa hela siku ile amenisaidia labda kulifanya ahisi nimemdharau hata kama sikuwa na nia hiyo, lakini yeye aliponikumbatia kwa shukrani japo nilikuwa nimelewa, alionyesha ni kitu kilichotoka moyoni mwake, na ni jambo lililonigusa sana usiku huo.

Kwa hiyo hapa kiukweli alikuwa amenipa fundisho dogo lakini lenye maana kubwa sana, nami nikatabasamu tu kidogo na kutikisa kichwa kuonyesha uelewa wa kauli yake kwa njia nzuri.

Akashusha pumzi na kusema, "Okay. Nashukuru pia kwa... jitihada yako. Nitamwandaa Mamu baadaye ili kesho mwende. Tesha atakuwa nanyi."

Nikatikisa kichwa kukubali, nami nikasema, "Asante kwa kukubali. Ngoja niende sasa. Tutaonana... labda baadaye... au... kesho..."

Alikuwa ananitazama tu machoni kwa mkazo kama vile ananishangaa kutokana na kubabaika kwa yale niliyosema, nami nikaibana cheko yangu na kusimama. Nikampungia kiganja kwa chini kama kumuaga, naye akatikisa kichwa kukubali.

Nikatoka hapo ofisini nikiwa nimefarijika kutokana na kukubaliwa ombi langu, japo mwanamke huyo alinipiga bomu zito kiasi la rohoni. Ile ndiyo nimegeuka tu na kutazama upande wake Soraya, nikakunja uso kimaswali kiasi baada ya kukuta kuna mtu mwingine aliyekuwa amesimama usawa wa meza hiyo ya mapokezi, naye hakuwa mwingine ila yule Joshua!

Nikamtazama machoni kwa mkazo kiasi, nikiwa najiuliza kwa nini alikuwa amekuja hapo. Kumwona mwanaume huyo kazini kwa Miryam ilinifanya nipatwe na hisia mbaya kwamba huenda alikuwa amekuja kumfanyia fujo dada mkubwa na huku tena, wakati alipewa msamaha wa kutofungwa jela na Miryam mwenyewe.

Alisimama kwa utulivu huku akiniangalia kwa njia ya kawaida, nami nikamwona Soraya akimwonyesha ishara ya kumruhusu aje upande huu wa ofisi. Jamaa akatembea taratibu na kufika karibu zaidi na niliposimama.

Nikawa namwangalia kwa ujasiri machoni, na kwa sababu alizozijua yeye, wakati huu hakuwa akinitazama kwa njia ya chuki kama vile alivyoniangalia mara ya mwisho tumeonana.

"Niaje mtu wangu?" akanisalimia hivyo.

Mh?

Ilikuwa ni kama kumpiga kofi kidogo Shetani ili kuona ikiwa atakurudishia la kwake kwa utani, lakini mimi sikutaka kufanya matani yoyote na huyu mtu. Sikuwa na uhakika, lakini kwa kumwangalia tu, nilihisi ujio wake hapa ulikuwa wa nia mbili; yaani bado singeweza kuamini kuwa alikuja hapa kwa lengo la kusaka amani. Zamu hii angekuwa anataka nini kutoka Miryam?



★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
Sawa mzee
 
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!

★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA KUMI NA TATU

★★★★★★★★★★★★★★★★


Kwa kuona sijatoa jibu lolote kwa salamu aliyonipa, Joshua akatabasamu kidogo na kuinamisha uso, kitakatifu eti, kisha akanipita na kuingia ndani humo. Alitoa vibe za 'bad guy' kama kwenye filamu za wazungu, nami sikuweza kujizuia kutaka kujua ni jambo gani alilokuwa amelileta mezani kwa bibie Miryam. Ama labda ni Miryam ndiyo alikuwa amemwita?

Nisingeweza kujua, na mtu yeyote angeweza kuniambia sikupaswa kujua maana haikunihusu. Au uwongo? Lakini nisingeweza kupuuzia uwezekano wa mwanaume huyo kufanya jambo lingine la kipuuzi kwa sehemu hii, kwa hiyo nikataka kuhakikisha.

Nikatoka sehemu hiyo ya mlango wa ofisini na kuifikia meza ya msaidizi, nami nikapokewa kwa tabasamu mwanana na mwanamke mrembo Soraya.

"Vipi?" nikamuuliza hivyo nikiwa nimesimama karibu na meza hiyo.

"Safi. Naona mmemaliza maongezi yenu," akasema hivyo.

"Ndiyo. Bosi wako mtata kweli."

"Ahahah... labda ukimchokonoa, ila ni mstaarabu sana..."

"Eti eh? Na huyu jamaa aliyeingia sa'hivi? Unamjua?" nikamuuliza hivyo.

"Eee, ni ndugu yake. Kaka yake sijui... sina uhakika sana, ila najua ni ndugu yake," akanijibu.

"Aaa, kwa hiyo hatamchokonoa boss eh?"

"Ahahah... sidhani. Amekuja kiupole, sioni kama kutakuwa na baya."

"Alipanga mapema kuja leo?"

"Yeah, da' Miryam aliniambia angekuja. Ndiyo alipofika nikamwambia asubiri kwanza maana mgeni bado ulikuwa ndani," akaniambia hivyo.

"Au siyo? Ukanipa heshima yangu mtoto.." nikamwambia hivyo, naye akacheka kidogo.

Kwa kujua sasa kwamba ni Miryam ndiye aliyemwita huyo jamaa hapo, nikaona labda mambo yasingeenda vibaya. Alikuwa na maana yake.

Nikamwambia Soraya, "Haya bana. Me ndo' natoka. Ushagakataa kuja kututembelea."

"Aam... nitakuja tu. Mambo mengi, si unajua? Kama hivi..."

"Wala hamna presha, usijali. Sema naona unapendezea sana kubadili mazingira, maana unakaa sana hapa. Huwa hata unatembea?" nikamuuliza hivyo.

Akatikisa kichwa kidogo kukataa.

"Kweli? We' ni wa kitako tu na hicho kiti?" nikauliza tena.

Akacheka na kusema, "Kawaida tu. Majukumu. Nikitoka hapa... ni kuwahi nyumbani. Nitatembea saa ngapi?"

"Wikiendi je?"

"Hata Jumapili nakuwa zangu ndani. Sizururagi mimi. Ijumaa hapa naenda zangu msikitini saa sita, da' Miryam ananiachia niende nyumbani. Sinaga mipango mingi ya kutoka wala labda iwe na ulazima kwa hiyo... ndiyo hivyo," akaniambia hayo.

Nikawa namwangalia tu usoni huku nikitabasamu kimchezo, naye akacheka kidogo kwa pumzi na kuung'ata mdomo wake wa chini.

"Mbona unaniangalia hivyo?" akaniuliza.

"Kwani we' umenionea nini?" nikamuuliza.

"Unaniangalia kama unanijaji. Unafikiri nakudanganya au?"

"Macho yangu hayajasema hivyo, we' ndo' umeyajaji vibaya..."

"Kumbe? Yanasemaje kwani?"

"Yanasema kama vipi baadaye nikutoe out... ila we' usiyependa kuzurura najua hautaweza," nikamwambia hivyo.

"Mhm... unaongea wewe..."

"Ahahah... bado hujanisikia nikiongea. Utachoka..."

Akaniangalia kwa macho mazuri, naye akasema, "Kwa hiyo unataka kunitoa out?"

"Ee fresh tu, kama ukitaka..." nikamwambia.

"Me muda sina JC..."

"Kwani unatoka saa ngapi?"

"Saa kumi na moja."

"Na uliniambia unakaa Sabasaba?"

Akatikisa kichwa kukubali.

"Asa' si hapo tu? We' ukitoka, nambie, tukutane, tule hata mishkaki, uende home. Ndo' urafiki huo, siyo kwenye simu tu," nikamwambia.

"Mmm?"

"Eeeh."

"Na nikichelewa?"

"Kwani... ahah... we' ni mtoto? Au mume mkali?"

"Hapana... me..." akababaisha jibu.

"Usijing'ate Soraah. We' ukimaliza tu nicheki..." nikapigilia msumari ndani zaidi kwenye ushawishi.

Nadhani alielewa vizuri kabisa kwamba nilikuwa namwonyesha kuvutiwa naye ingawa sikwenda huko moja kwa moja, na yeye pia akafanya ionekane kwamba hakufikiria huko.

Akasema, "Sawa. Nikiwahi, n'takwambia. Mishkaki si unaninunulia?"

"Usiwaze. Hayo ndiyo mambo sasa. Unamaliza kazi, unabembea kidogo na rafiki, ndiyo unaingia makwenu, au siyo?"

"Mh... kubembea tena?"

"Ahahahah... uko innocent sana, hadi raha. Me ngoja niwahi, naingia Kariakoo sa'hivi. Ukinijali utanitext. Usiponitext, basi ndo' ntaila mishikaki mwenyewe," nikamwambia hivyo kiutani.

Akacheka kidogo na kusema, "Haya bwana. Unaenda Kariakoo kufanya nini?"

"Naenda kuchukua nguo fulani, afu' nageuka..."

"Sawa."

"Haya, baadaye beauty Soraah..." nikamuaga kiaina hiyo.

Akatabasamu na kutikisa kichwa kidogo, nami nikampita na kwenda nje.

Huyu mwanamke nilitaka kuhakikisha napita naye, maana alionekana kuficha utamu fulani hivi ndani ya huo upole wake mwingi aliokuwa nao. Haikujalisha suala la yeye kuwa ameolewa, maana mpaka kufikia wakati huu bado nilikuwa kwenye zile nyendo za kuharibu mitambo niliyoielewa hata kama ilikuwa imeshaunganishwa kwenye nyumba za wengine. Na Soraya alikuwa mtambo material.

Sikujua sana ikiwa angeridhia kufika na mimi kule ambako ningetaka tufike, lakini kama angekataa wala nisingemlazimisha. Ila nilimtamani sana. Kwa hiyo nikajiondokea pande za Kijichi baada ya hayo, nami nikachukua daladala zilizoelekea Kariakoo.

Nilikuwa nikifikiria mambo mengi kuhusiana na vitu nilivyotakiwa kufanya ili kuanza kumpatia Mariam msaada wa kisaikolojia ambao ungefaana na hali aliyokuwa nayo. Sikubobea sana kwenye masuala ya saikolojia wala magonjwa ya akili, lakini nilijua mengi kuhusu hali iliyomwandama, na utundu wangu ungesaidia niweze kucheza na akili yake vyema mpaka ikae sawa tena.

Nilipofika Karikoo, nilizunguka pande tofauti mpaka nikafikia Msimbazi, kisha nikaingia kwenye duka moja lenye kuuza bidhaa kama nguo, suruali, viatu, na ndala nzuri. Nikanunua T-shirt zuri sana la mikono mirefu, lenye rangi ya blue-nyeusi na mistari myembamba kifuani, pamoja na ndala nzuri zenye rangi mchanganyiko wa nyekundu, blue, na nyeupe.

Nilipenda mionekano mizuri sana kimavazi, na kutumia hela niliyokuwa nayo kwenye mavazi lilikuwa jambo la kawaida sana kwangu. Nani asiyependa kupendeza?

Baada ya kutoka hapo, nikaelekea kwenye mgahawa mzuri wa kisasa ili kupata chakula, maana sikuwa nimeweka kitu chochote tumboni kutokea asubuhi. Nikawa nimemjulisha Ankia kuwa asinitinzie chakula cha mchana maana ningechelewa kurudi na hivyo kula huku huku nilikokuwa. Nilikaa kivyangu tu huku nikiendelea kula na kuchat na marafiki kwenye simu, kisha nikaondoka hapo baada ya kushiba.

Nikaenda sehemu zingine pande hizo za Kariakoo na kununua kinanda kidogo kwenye duka la vifaa vya ala za muziki, chenye vibonyezeo vilivyowekewa sauti ambazo zimesharekodiwa. Yaani, ukibonyeza kimoja kinatoa mlio (instrumental) wa twinkle twinkle star, ama mlio wa happy birthday, kwa midundo ya kinanda. Kilikuwa kizuri sana, chenye umbo la mstatili na mwonekano kama wa boksi dogo la viatu vya dukani. Nilikinunua kwa ajili ya Mariam.

★★

Nikatoka huko Kariakoo ikiwa inaingia mida ya saa kumi jioni sasa. Kuna pisi kali nilikuwa napishana nazo, kali vibaya mno, na zilikuwa zinaniangalia hizo! Siyo poa. Yaani kuna wanawake wengine unaweza kuwaona ukatamani hata uwabebe wote uende nao kwako. Wengi watasema ooh wanaume ni malaya lakini uchaguzi mmoja tu wa mwanamke anayekufaa huwa ni mgumu sana aisee, ukitegemea wako mamilioni hapa duniani. Ndiyo sababu tunakulagakulaga wengi kwanza, na bado tunakuwa hatutosheki!

Bwana, nikawa nimeiacha Kariakoo hatimaye kwa mwendo wa taratibu wa daladala, na aisee! Nilikoma kupanda hizi daladala za kutokea Gerezani mpaka Kisemvule. Yaani watu wanabanana mpaka unakosa pozi na pumzi, hasa ukiwa umesimama kama mie ilivyokuwa wakati huu. Pigia picha ingekuwaje wakati wa usiku ikiwa tu gari liliweza kushonana namna hiyo kukiwa jioni ya mapema, na niliombea asitokee mtu wa kujamba la sivyo ningezimia!

Lengo lilikuwa kuwahi nyumbani, niweke mizigo, kisha niangalie utaratibu unaofaa ili nikamjali mamacita Soraya. Hakuwa amenipotea akilini hata kidogo, na kama ningefanikiwa kutoka na yule mwanamke, leo ningeweza hata kulala na mbu wananing'ata huku natabasamu. Yule alikuwa wa ukweli, na sikuwa nimepanga kumwambia Tesha lolote hata kama maangamizi yangetokea!

Lakini msongamano wa magari ukafanya dakika za kukawizwa barabarani ziwe nyingi hasa kuanzia maeneo ya Uhasibu, mpaka inaingia saa kumi na moja bado tukawa tunaisaka Sabasaba. Sijui shida ilikuwa nini. Hivyo hivyo mdogo mdogo tukaendelea kusogea, nami nikapata ujumbe kutoka kwa Soraya.

'Ndo natoka.'

Agh! Siyo lazima mpaka mtu awe amesoma saana ili kuelewa kwamba mtoto alikuwa anataka kuelekezewa fikira, na zangu kwa wakati huu zilikuwa kwake kweli, kwa hiyo ningejitahidi nisimvunje moyo.

Nikamjulisha kuwa nilikuwa maeneo ya karibu na Rangi Tatu, naye akasema tayari yuko kwenye bajaji kuelekea huko pia. Duh! Hapa isingewezekana kwenda kwanza kule nilikokaa na kurudi tena, kwa hiyo ingebidi nikutane naye nikiwa na mifuko ya bidhaa nilizonunua.

Kwa kuwa ilionekana yeye ndiye ambaye angewahi kabla yangu, nikamwambia kwa kuwa bajaji kutokea Kijichi zinashushia eneo la hapo Zakhem, akishuka basi aende kwenye mgahawa wowote wa karibu hata pale pale Zakhem Hotel, ndiyo sehemu ambayo tungekutana maana bado nami nilikuwa kwenye gari. Akanikumbusha kuhusu kupaswa kuwahi, nami nikamwambia asiwaze.

Dakika chache kupita nasi tukawa tumefika Rangi Tatu. Ile nimeanza kutembea tu kuelekea Zakhem Soraya akanipigia, 'wewe uko waapi' na kasauti kake ka upole, nami nikamwambia niko karibu.

Nikajitahidi kutembea haraka kiasi mpaka nilipofika eneo la mgahawa wa Zakhem, nami nikampigia kumuuliza yuko upande gani. Akaniambia ameniona na ananifata, nami kweli nikamwona akija kutokea kwenye duka dogo la bidhaa upande wa nyuma niliouvuka kabla ya kuufikia mgahawa huu maridadi.

Nikakata simu. Alikuwa anakuja kwa mwendo wa taratibu tu, gauni lake laini na refu mpaka chini likipeperuka kiasi kwa upepo uliopuliza kwa nguvu, na uso wake uliochorwa duara la ushungi aliovaa ukimpa mwonekano mzuri sana. Hii ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kumtazama vizuri akiwa amesimama, kwa hiyo nilipendezwa hata zaidi na mwonekano wake.

Akawa amenifikia karibu zaidi, tukiwa tumesimama karibu na mwingilio wa mgahawa wa Zakhem, naye akatabasamu kiasi huku mimi nikimwangalia kwa umakini.

"Nimechelewa sana?" nikamuuliza.

Akatikisa kichwa kidogo kukanusha.

"Twende sa' hata ukanywe soda na mishikaki kidogo," nikamwambia hivyo.

"Hapana... JC... nitachelewa," akasema.

"Utachelewa wapi? Saa kumi na mbili hii kweli?"

"Saa moja tu natakiwa niwe nimeshafika nyumbani. Nahitaji kuwapikia wanangu."

"Sawa. Basi... angalau nipe tu hata kimoja Soraah," nikamwambia hivyo.

Akakunja uso wake kimaswali na kuuliza, "Kimoja?"

"Ee, fasta tu," nikamwambia.

"Sijakuelewa JC..."

"Nataka nisafishe chumba na wewe," nikasema hivyo.

"Ku... kusafishaje? Kusafisha chumba?"

"Acha kujitoa akili, najua unanielewa bwana..."

"Eh... ahah... eheh... makubwa jamani..."

"Nini sasa?"

"Wewe... sasa... si nilikwambia nimeolewa?"

"Ndiyo, najua. Ila me nakuelewa, na we' najua unanielewa..."

"Mm... me hapana... siwezi... dini yangu hairuhusu..."

"Hairuhusu nini? Mbona mwenzako anaruhusiwa kuwa na wanawake mpaka wanne? Huoni siyo fair?"

"Ye' ni mwanaume... ndiyo imeshaandikwa hivyo..."

"Hakuna kitu, huo ni uonevu bwana. Ona... najua unataka kuwahi, kwa hiyo... nipe tu kidogo maana... nakuhamu sana Soraah..." nikamwambia hivyo huku namwangalia kwa macho yenye ushawishi.

"Eh... hamna... natakiwa kuwahi, kwanza me siwezi... maana..."

Akawa anajizungusha kimaneno sana, akiongea kwa namna yake ya upole lakini nikiona wazi kwamba alitaka nimbembeleze zaidi, ila kama nilivyokuwa nimesema mwanzo, ikiwa asingeridhia, nisingemlazimisha.

Nikamwambia, "Basi poa. Haina shida. Twende hivi ukapande gari uende nyumbani."

Akabaki kunitazama kama vile hakuwa amenisikia.

"Vipi?" nikamuuliza.

"Umekasirika?" akaniuliza pia.

"Sijakasirika. Si umesema unataka kuwahi? Twende ukapande gari uende."

Akaangalia chini kiasi kwa huzuni.

"Nini, mbona unakuwa hivyo?" nikamuuliza.

"Usichukulie vibaya JC, me..."

"Sijachukulia vibaya, Soraya. Si una haraka, majukumu? Ndiyo nakwambia haina shida. Nenda uwahi," nikasema hivyo.

"Sa' mbona kama umechukia?"

"Sijach... Okay. Nimehisi vibaya, lakini nitafanyaje? Una mambo muhimu ya kufanya pia. Kayafanye."

"Siyo hivyo tu, najua umechukia kwa sababu nimekukatalia. Usichukie JC..." akaongea kwa kubembeleza.

Sijui alikuwa ananiona kama keki? Hii ndiyo raha ya kutokea wanawake wenye umri mkubwa, wanajua sana kudekeza!

Nikamwambia, "Hapana, we' usiwaze. Twende ukachukue tu usafiri na me niende home. Nitapambana na hali yangu."

Akawa ananiangalia kama anataka kulia eti, kisha anaangalia pembeni, mara huku, mara kule, nami nikawa nimeshachoshwa na presha ya kutazamwa sana na watu kwenye eneo hilo.

"Soraah twende. Au vipi?" nikamuuliza hivyo kwa sauti makini.

Akaniangalia na kuuliza, "Kwani ulikuwa unataka twende wapi?"

Ohohoo! Pasi ndefu kuelekea goli la ushindi!

Sikutoa jibu. Nikaushika mkono wake na kuelekea naye kwenye jengo refu la hoteli iliyokuwa karibu na hapo, nisijali hata kuangalia jina wala nini. Nilikuwa namvuta Soraya kama vile natembea na mtoto, nami nikaiona sehemu ya mapokezi na kwenda kuzungumza na mhudumu.

Huku Soraya akiwa amesimama nyuma yangu, nikauliza gharama ya vyumba vya kulala wageni sehemu hiyo, nami nikajulishwa kuwa kuna vyumba vya shilingi elfu thelathini mpaka elfu themanini kwa siku eti. Nikatoa elfu thelathini chap kulipia kimoja, na huyo mhudumu akaniongoza mimi na Soraya kuelekea kwenye vyumba.

Eh, huyu mwanamke alikuwa na aibu! Kwa wengi mambo ya hivi ni kawaida lakini kwake yeye haikuwa hivyo, maana alitembea kwa kuficha uso wake utadhani dunia nzima ilikuwa inamwangalia yeye. Huyo mhudumu akatufikisha kwenye chumba kimoja kwenye ghorofa ya pili, nasi tukaingia ndani.

Kilikuwa na mwonekano mzuri, safi sana. Kitanda kilikuwa kipana na kirefu, kilichotandikwa shuka jeupe na kuwekewa mito, huku juu kukiwa na neti. TV ya flat screen ukutani, meza yenye droo kadhaa na viti vya kukalia, kabati la ukutani la nguo, mlango ulioelekea kwenye bafu na choo safi, pamoja na taulo mbili zilizokunjwa na kuwekwa kitandani pia, mapazia marefu yaliyofunika madirisha makubwa, vyote vilikuwemo.

Huyo mhudumu akatuacha mimi na mali safi humo ndani, nami nikafunga mlango kwa funguo baada ya kuiweka mifuko yangu mezani. Soraya alikuwa amesimama usawa wa kitanda akionekana kutafakari vitu, nami nikaona nisimcheleweshe.

Nikaja nyuma yake na kukibana kiuno chake kwa mikono yangu, huku nikibusu shavu lake usoni kutokea nyuma, lakini akashtuka na kujitoa kwangu, naye akakaa kitandani. Alionekana kuogopa.

"Vipi Soraah?"

"Me... bado naona kama tumepeleka mambo haraka sana," akaniambia.

"Bado hata hatujaanza!" nikamwambia.

"Simaanishi hivyo..."

"Nakuelewa. Ndiyo maana hii ya mwanzo nimetaka tuifanye chap tu, maana una haraka. Ama?"

"Me bado naogopa jC..."

"Unaogopa nini? We' si mkubwa kwangu? Unaogopa nini sasa?"

"Sijawahi kucheat."

"Ndo' ujifunze," nikamwambia hivyo.

Akaniangalia kimkazo na kucheka kwa kuguna.

"Usiwe hivi bwana... muda unaenda..."

Nikamwambia hivyo na kumsogelea, nami nikapiga magoti chini katikati ya miguu yake iliyofichwa kwa gauni na kuushika uso wake, nikitaka kumbusu, lakini akawa ameinamisha tu uso wake.

"Soraah, ni nini?" nikamuuliza.

Akabaki kimya.

"Unaumwa? Uko P?" nikauliza tena.

Akatikisa kichwa kukataa.

"Nini sasa? Tutumie muda vizuri basi, saa moja itakukuta bado unajing'ata... eleweka basi..."

Akaniangalia kwa macho yaliyojaa hisia nzito sana, na hivi yalikuwa lege, nami nikaifata midomo yake na kuanza kumbusu.

Piga denda nzito sana na taratibu ili nimhemshe mtoto, hapo nikiwa nimeshavimba kwa nguvu zote, nami nikashika upande mmoja wa kifua chake uliofichwa kwa nguo. Akaushika mkono wangu na kuutoa kifuani kwake, lakini nikalazimisha kuminya-minya hapo, naye akautoa tena na kukatisha busu yetu.

Nikamwangalia na kuona namna alivyokuwa anajishauri bado, na kiukweli hii sitaki-nataka ilikuwa inaniboa sana, basi tu. Nikakishika kidevu chake ili nimtazamishe kwangu, naye akaniangalia machoni kwa hisia za woga-woga tu, kitu ambacho kilifanya nihisi stimu inanitoka.

Agh, nikamwachia na kusimama, kisha nikakaa kitandani pia na kutazama pembeni nikiwa nimeudhika. Niliweza kuona uso wake ukiniangalia mara kwa mara japo sikumtazama kabisa, nami nikaangalia saa mkononi na kukuta ni saa kumi na mbili na dakika arobaini na kitu.

Hapo nikaona ni kazi bure tu kulipia elfu thelathini yote halafu mwanamke mwenyewe akawa analeta swaga za kishamba; wakati nilikuwa namkubali mno.

"JC..." akaniiita kwa sauti ya chini.

Nikamwangalia, nikiwa na uso makini.

"Umekasirika?" akaniuliza hivyo.

Nikamkazia macho tu, kisha nikatazama pembeni tena.

"Hautaki kunijibu?"

"Nikujibu nini? Unataka nifanye nini sasa? Maana sikuelewi..."

"Mmh... JC... mimi... siyo kwamba nafanya makusudi, ila... nina aibu..."

"Agh..." nikafanya hivyo na kupiga ulimi mdomoni.

"Mbona unafanya hivyo?"

"Unazingua, Soraah. Unasema una haraka, me nimekujali nikakwambia tupige mambo fasta, bado unajivuta. Asa' muda si umeshakata?" nikamwambia hivyo kwa kuudhika.

"Siyo hivyo... sijazoea tu..."

"Haya nenda," nikamkatisha.

"Bee?"

"NE-NDA! Wahi nyumbani," nikamwambia hivyo kwa mkazo.

Akabaki kunitazama kwa huzuni.

Nikasimama na kwenda kuufungua mlango kwa funguo, naye akasimama pia. Nikarudi sehemu ile yenye meza ili niichukue mifuko, naye akaja nyuma yangu.

"JC... usikasirike..." akawa ananiomba hivyo.

"Ishaisha hii. We' chukua mkoba wako, tuondoke," nikamwambia hivyo.

Nikaichukua mifuko yangu nikiwa nimeudhika kweli, lakini akaikwapua kutoka mikononi mwangu na kuiweka mezani tena. Akawa ananiangalia kama vile anataka kulia.

"Soraah mbona sikuelewi? Unataka nini sasa?" nikamuuliza.

"Mm... nakutaka weewe..." akasema hivyo kwa sauti yenye upole.

Nikabaki kumtazama usoni kwa umakini.

"Ila... ninaogopa tu JC. Sijawahi kufanya kitu kama hiki... sija... nakuogopa yaani... unanifanya nasisimka sana mpaka... mpaka naogopa... sijawahi kuwa na mwanaume mzuri kama wewe... yaani...."

Nilimwangalia kwa njia ya uelewa sasa, nikianza kumwona kama Ankia tu. Ila yeye hakuwa mzoefu, kwa hiyo sasa nisingejali tena masuala ya muda; hapa ningetakiwa nimnyooshe ili na yeye ajue kwamba tupo kwenye karne ya 21, baby!

Nikamshika usoni kwa viganja vyangu, nikiyakandamiza mashavu yake na kumsogelea karibu zaidi, nami nikamuuliza, "Haujafanya vitu vingi eh?"

Akatikisa kichwa kukubali.

"Sawa. Nilifikiri ni mashauzi tu. Nisamehe kwa kuudhika," nikamwambia hivyo kwa upole.

Nikahisi mikono yake ikikishika kiuno changu na makucha yake yakinichoma kiasi.

"We' ni mwanamke mstaarabu, naona hilo sasa. Ila kama unanitaka kweli... jiachie. Mimi ndo' najaza nafasi zilizoachwa wazi... we' ziache tu ziwe wazi. Sijui umenisoma?" nikamuuliza hivyo.

Akatikisa kichwa kukubali.

Dah! Midomo yake ilikuwa imelowana kwa mate, uso wake mweupe ukionyesha hamu nzito kunielekea, nami nikaanza tena kumbusu. Nilimpiga busu ya taratibu, pigo za wazungu zile, kisha nikashusha mkono wangu mmoja mpaka kwenye kalio lake.

(.........).

(.........).

Huyu alikuwa kama wale wanawake unaoenda kupiga halafu kazi yao inakuwa ni kulala tu huku wamefunika uso kwa mkono, kwa sababu Soraya alikuwa mpole mno na mwenye aibu. Kwa hiyo mimi nikaanza tu kujilia keki.

(.........).

(.........).

(.........).

(.........).

Hakuwa na mambo mengi ya ajabu; ni miguno tu ya upole. Nikamwacha na kwenda kuwasha taa, ikiwa imeshaingia saa moja usiku, kisha nikamrudia tena. Alikuwa ameshakolezwa utamu asiambilike chochote yaani, na kiukweli nilimfurahia mno. Nilijihisi vizuri sana. Joto lililokuwa limepanda ndani yangu lilisisimua mno nilipolishusha namna hiyo kwa huyu kamama. Nilikuwa nimeamua kuwahisha mambo ili kweli dada wa watu awahi nyumbani, lakini si utamu ukawa umemkolea?

Nikamwambia, "Soraah... saa moja ishaingia. Jisafishe uende."

"Mmm... bado..."

"Bado nini?"

"Mmm..."

"Unataka tuendelee?"

Akatikisa kichwa kukubali bila kuniangalia.

"Asa' si utachelewa?"

"Ah... chomekaa..." akaongea hivyo kwa deko.

Nikatabasamu kidogo na kutikisa kichwa, kisha nikamvuta tena. Zamu hii akiwa amebinuka kwangu, nikalisambaza kalio lake na kuingia tena, kisha nikaanza shambulizi. Alikuwa analia huyo!

Nikafumua bila kumpumzisha, akiirudisha mikono yake yote nyuma, nami nikaibania mgongoni kwake na kuendelea kupiga haswa. Nadhani alikuwa anataka kufika ukingoni kwake kwa kumwaga juisi japo tayari alikuwa ameshatetema mara kadhaa nyuma, na mimi nikajitahidi ili aridhike kweli. Alikuwa ameiva balaa!

Nikaendelea tu kumtandika huku nikimsemesha. "Utamu umekukolea, si utafika nyumbani vibaya?"

Likaendelea tu kuguna.

"Wewe... si ulikuwa unakataa-kataa, unaogopa muda... unaogopa kuchelewa?"

"Mmm... sikujuaa..."

"Hukujua nini?"

"Sikujuaa... sikujua kama we' ni mtamu hivi..."

"Ahahah... wanao si watalala njaa sasa...."

"Mmm...."

Mwanamke bwana akawa anaonyesha raha tu na malalamiko yake, na hatimaye hiyo sikujua yake ikashika hatamu.

Akapasua bomba lenye maji marefu mpaka nikashangaa! Alishtuka kwa nguvu kama vile mwili mzima umepatwa na kwikwi, nami nikawa nalisugua linyama lake kwa vidole ili asafishe haja yake yote mpaka mwisho. Ikaeleweka kwangu kwamba hakuwa amefikia ukingo kwa muda mrefu sana.

Akalala hoi kitandani, huku akijing'ata mdomo na kupumua kilegevu, nami nikamgeuza alale chali ili nichezee mwili wake. Alikuwa anarembua mno, nami nikampiga kofi laini shavuni.

"Wewe... amka... amka tuondoke. Saa mbili sa'hivi," nikamwambia.

Akawa ananiangalia kilegevu tu.

"Soraah... sitaki kuja kusikia umepigwa huko, maana mna ratiba zenu. Nyanyuka twende," nikamwambia hivyo.

Nikataka kunyanyuka, lakini akanishika mkononi na kunivuta kwake tena, asitake kuniachia.

"Nini?" nikamuuliza.

"Tukae kidogo..." akasema hivyo.

Nikatabasamu na kuuliza, "Na nyumbani?"

"Mmh... nitaenda baadaye... nimechoka..."

"Aa wee... unataka wanao walale njaa? Saa mbili sa'hivi, kwanza ulikuwa unaenda kupika nini?"

"Ubwabwa..."

"Ndo' unyanyuke sasa, washaanza kulia njaa..."

"Ah... me nitasema kulikuwa na foleni... baba yao atawanunulia chakula..." akaongea kwa deko.

Unaona? Hawa viumbe wakishagalishwa utamu ndiyo wanakumbuka kwamba kuna kitu kinaitwa kudanganya. Si muda ule alikuwa anapiga kelele eti ooh nitachelewa, sasa hivi kiko wapi? Nikacheka tu kidogo na kuushika uso wake taratibu.

"Siyo vizuri hivyo unajua?" nikamwambia.

"Me nataka tukae kidogo..."

"Kwa nini?"

Akanishika shingoni na kusema, "Bado nawashwa."

"Ahahahah... sa'hivi aibu imekutoka eh?"

Akatikisa kichwa kukubali.

"Usijali. Nitakukuna tu. Ila sa'hivi muda unatupinga. We' vaa na me nivae twende. Tutapanga siku nyingine tukutane. Si umeshanizoea sasa hivi?" nikamwambia hayo.

Akatikisa kichwa kukubali.

"Fresh. Fanya hivyo," nikamwambia.

Nikapeana naye busu tamu huku, kisha nikajitoa kitandani hapo. Aisee alikuwa amelowanisha shuka siyo poa! Ingetubidi tuondoke haraka kabla hatujaitwa kufanyia usafi maana kwenye hiyo hoteli kulikuwa na sheria za "by utawala."

Nikavaa, nikamsaidia mwanamke avae pia, na kiukweli Soraya alionekana kutaka sana tuendelee maana aliniangalia kwa yale macho ya turudi kitandani tena. Mimi nikampiga tu busu na kumwambia muda mwingine tukipata nafasi basi ningempa mapenzi zaidi hata ya leo, naye akaonekana kufurahi.

Nikafungua droo moja kwenye ile meza na kutoa chanuo. Nikachana nywele na kujiweka vizuri, na yeye pia akajiweka vizuri mwilini kwa kujipulizia manukato yake ili asifike nyumbani ananukia mimi. Uzuri hakuwa ameutoa ushungi wake pindi nzima ya mechi yetu, kwa hiyo tukabeba vilago vyetu na kuondoka.

Tukaingia tena barabara ya Zakhem kuelekea Rangi Tatu pale, tukitembea taratibu tu huku nikiwa nimemtangulia mamaa. Tulipoufikia mgahawa wa Zakhem, nikamwambia twende hapo, nami nikaenda kununua nyama za kuku pamoja na mishikaki mingi, kisha ikafungwa nasi tukaanza kurudi barabarani.

Mpaka kufikia muda huu, Soraya hakuwa ametafutwa na mume wake, kwa hiyo yeye akawa amemtafuta na kusema alikuwa amepatwa na dharura lakini ndiyo alikuwa njiani kurudi nyumbani. Dah! Dhambi hizi!

Hivyo vyakula nikawa nimempatia mwanamke ili avipeleke kwa watoto huko kwake kama zawadi ya upendo, na niliona wazi kwamba Soraya alifurahia sana. Tukaachana kwenye mazingira mazuri baada ya kuhakikisha amepanda gari la kwenda huko kwake, nami pia nikapanda la kuelekea Mzinga. Mission accomplished!

★★

Nikawa nimefika nyumbani kwake Ankia hatimaye na kumkuta mwanamke huyo akiwa amekaa sebuleni pamoja na mama Chande, na kulikuwa na mvulana mdogo hapo pia wa miaka kama 10 hivi.

Kwa haraka nilitambua kwamba mvulana huyo alikuwa mtoto wa mama Chande, labda ndiyo Chande mwenyewe, na nilipowapa wanawake hao salamu za wakati huu wa usiku, waliziitikia huku wakiniangalia kwa njia iliyoniambia kwamba kulikuwa na tatizo.

Nikaona nipite tu kwanza na kuelekea chumbani kuiweka mizigo, nikiwa nadhani labda walikuwa tu na ishu zao zisizonihusu hata kidogo, na baada ya kutoa mavazi yangu, nikavaa nguo nyepesi ili niende kuoga. Si unajua joto la mwili lingekuwa juu baada ya mechi niliyocheza na Soraya?

Kwa hiyo nikatoka chumbani ili nielekee bafuni, lakini nilipofika hapo sebuleni tena, nikakuta Ankia akiwa ameinamisha uso wake, viganja akiviunganishia usoni, huku machozi yakionekana kumtoka. Hali hiyo ikanitatiza sana.

Mama Chande alikuwa ananiangalia kwa macho yenye subira, bila shaka akitaka nijue nini kilichokuwa kinaendelea hapo, nami nikasimama karibu na sofa alilokalia yule mvulana mdogo huku nikimwangalia mama Chande pia.

"Vipi? Mbona huyu analia?" nikamuuliza hivyo mama Chande.

"Eh... kaka... ni makubwa yametokea. Kuna msiba," akasema hivyo.

Kauli hiyo ikanifanya nimwangalie Ankia, nikiwa nimehisi labda msiba huo ulikuwa wa mtu wa karibu zaidi na mwenye nyumba wangu. Lakini kabla hata sijauliza nani kafa, mama Chande akanipa jibu, na ni jibu ambalo sikuwa nimetegemea kabisa!

"Haujasikia kumbe?" akaniuliza hivyo.

Nikatikisa kichwa kukanusha.

"Joy amefariki," akaniambia.

Nilihisi kama vile pozi lilinitoka kabisa baada ya kusikia maneno hayo, lakini nikaendelea tu kumwangalia mwanamke huyo kwa utulivu.

"Unamfahamu Joy, si ndiyo? Amefariki. Tena... ameuawa," mama Chande akasema hivyo.

Eh! Haya sasa! Nikabaki nimesimama hapo hapo bila kusema lolote, nami nikatazama pembeni nikiwa najaribu kuisawazisha vyema taarifa hiyo kichwani kwangu.

Ingepaswa kuwa kitu chenye kushtua mno, na kilinishtua, lakini mshtuko nilioupata ulitokana haswa na fikira za ni nini ambacho kilikuwa kimesababisha mwanamke huyo afe ghafla. Tena kujua kwamba alikuwa ameuawa ndiyo kuliongezea fikira hizo ukali wa moto wake, kwa sababu tayari ningeweza kukisia ni nani aliyekuwa msababishi. Aisee!

Kumbe mambo yalikuwa serious namna hii? Aliyefanya hivyo alikuwa anataka kuonyesha hatanii, na nilimjua vizuri sana. Sasa kutokea hapa huu mchezo ungeelekea wapi?



★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!

★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA KUMI NA TATU

★★★★★★★★★★★★★★★★


Kwa kuona sijatoa jibu lolote kwa salamu aliyonipa, Joshua akatabasamu kidogo na kuinamisha uso, kitakatifu eti, kisha akanipita na kuingia ndani humo. Alitoa vibe za 'bad guy' kama kwenye filamu za wazungu, nami sikuweza kujizuia kutaka kujua ni jambo gani alilokuwa amelileta mezani kwa bibie Miryam. Ama labda ni Miryam ndiyo alikuwa amemwita?

Nisingeweza kujua, na mtu yeyote angeweza kuniambia sikupaswa kujua maana haikunihusu. Au uwongo? Lakini nisingeweza kupuuzia uwezekano wa mwanaume huyo kufanya jambo lingine la kipuuzi kwa sehemu hii, kwa hiyo nikataka kuhakikisha.

Nikatoka sehemu hiyo ya mlango wa ofisini na kuifikia meza ya msaidizi, nami nikapokewa kwa tabasamu mwanana na mwanamke mrembo Soraya.

"Vipi?" nikamuuliza hivyo nikiwa nimesimama karibu na meza hiyo.

"Safi. Naona mmemaliza maongezi yenu," akasema hivyo.

"Ndiyo. Bosi wako mtata kweli."

"Ahahah... labda ukimchokonoa, ila ni mstaarabu sana..."

"Eti eh? Na huyu jamaa aliyeingia sa'hivi? Unamjua?" nikamuuliza hivyo.

"Eee, ni ndugu yake. Kaka yake sijui... sina uhakika sana, ila najua ni ndugu yake," akanijibu.

"Aaa, kwa hiyo hatamchokonoa boss eh?"

"Ahahah... sidhani. Amekuja kiupole, sioni kama kutakuwa na baya."

"Alipanga mapema kuja leo?"

"Yeah, da' Miryam aliniambia angekuja. Ndiyo alipofika nikamwambia asubiri kwanza maana mgeni bado ulikuwa ndani," akaniambia hivyo.

"Au siyo? Ukanipa heshima yangu mtoto.." nikamwambia hivyo, naye akacheka kidogo.

Kwa kujua sasa kwamba ni Miryam ndiye aliyemwita huyo jamaa hapo, nikaona labda mambo yasingeenda vibaya. Alikuwa na maana yake.

Nikamwambia Soraya, "Haya bana. Me ndo' natoka. Ushagakataa kuja kututembelea."

"Aam... nitakuja tu. Mambo mengi, si unajua? Kama hivi..."

"Wala hamna presha, usijali. Sema naona unapendezea sana kubadili mazingira, maana unakaa sana hapa. Huwa hata unatembea?" nikamuuliza hivyo.

Akatikisa kichwa kidogo kukataa.

"Kweli? We' ni wa kitako tu na hicho kiti?" nikauliza tena.

Akacheka na kusema, "Kawaida tu. Majukumu. Nikitoka hapa... ni kuwahi nyumbani. Nitatembea saa ngapi?"

"Wikiendi je?"

"Hata Jumapili nakuwa zangu ndani. Sizururagi mimi. Ijumaa hapa naenda zangu msikitini saa sita, da' Miryam ananiachia niende nyumbani. Sinaga mipango mingi ya kutoka wala labda iwe na ulazima kwa hiyo... ndiyo hivyo," akaniambia hayo.

Nikawa namwangalia tu usoni huku nikitabasamu kimchezo, naye akacheka kidogo kwa pumzi na kuung'ata mdomo wake wa chini.

"Mbona unaniangalia hivyo?" akaniuliza.

"Kwani we' umenionea nini?" nikamuuliza.

"Unaniangalia kama unanijaji. Unafikiri nakudanganya au?"

"Macho yangu hayajasema hivyo, we' ndo' umeyajaji vibaya..."

"Kumbe? Yanasemaje kwani?"

"Yanasema kama vipi baadaye nikutoe out... ila we' usiyependa kuzurura najua hautaweza," nikamwambia hivyo.

"Mhm... unaongea wewe..."

"Ahahah... bado hujanisikia nikiongea. Utachoka..."

Akaniangalia kwa macho mazuri, naye akasema, "Kwa hiyo unataka kunitoa out?"

"Ee fresh tu, kama ukitaka..." nikamwambia.

"Me muda sina JC..."

"Kwani unatoka saa ngapi?"

"Saa kumi na moja."

"Na uliniambia unakaa Sabasaba?"

Akatikisa kichwa kukubali.

"Asa' si hapo tu? We' ukitoka, nambie, tukutane, tule hata mishkaki, uende home. Ndo' urafiki huo, siyo kwenye simu tu," nikamwambia.

"Mmm?"

"Eeeh."

"Na nikichelewa?"

"Kwani... ahah... we' ni mtoto? Au mume mkali?"

"Hapana... me..." akababaisha jibu.

"Usijing'ate Soraah. We' ukimaliza tu nicheki..." nikapigilia msumari ndani zaidi kwenye ushawishi.

Nadhani alielewa vizuri kabisa kwamba nilikuwa namwonyesha kuvutiwa naye ingawa sikwenda huko moja kwa moja, na yeye pia akafanya ionekane kwamba hakufikiria huko.

Akasema, "Sawa. Nikiwahi, n'takwambia. Mishkaki si unaninunulia?"

"Usiwaze. Hayo ndiyo mambo sasa. Unamaliza kazi, unabembea kidogo na rafiki, ndiyo unaingia makwenu, au siyo?"

"Mh... kubembea tena?"

"Ahahahah... uko innocent sana, hadi raha. Me ngoja niwahi, naingia Kariakoo sa'hivi. Ukinijali utanitext. Usiponitext, basi ndo' ntaila mishikaki mwenyewe," nikamwambia hivyo kiutani.

Akacheka kidogo na kusema, "Haya bwana. Unaenda Kariakoo kufanya nini?"

"Naenda kuchukua nguo fulani, afu' nageuka..."

"Sawa."

"Haya, baadaye beauty Soraah..." nikamuaga kiaina hiyo.

Akatabasamu na kutikisa kichwa kidogo, nami nikampita na kwenda nje.

Huyu mwanamke nilitaka kuhakikisha napita naye, maana alionekana kuficha utamu fulani hivi ndani ya huo upole wake mwingi aliokuwa nao. Haikujalisha suala la yeye kuwa ameolewa, maana mpaka kufikia wakati huu bado nilikuwa kwenye zile nyendo za kuharibu mitambo niliyoielewa hata kama ilikuwa imeshaunganishwa kwenye nyumba za wengine. Na Soraya alikuwa mtambo material.

Sikujua sana ikiwa angeridhia kufika na mimi kule ambako ningetaka tufike, lakini kama angekataa wala nisingemlazimisha. Ila nilimtamani sana. Kwa hiyo nikajiondokea pande za Kijichi baada ya hayo, nami nikachukua daladala zilizoelekea Kariakoo.

Nilikuwa nikifikiria mambo mengi kuhusiana na vitu nilivyotakiwa kufanya ili kuanza kumpatia Mariam msaada wa kisaikolojia ambao ungefaana na hali aliyokuwa nayo. Sikubobea sana kwenye masuala ya saikolojia wala magonjwa ya akili, lakini nilijua mengi kuhusu hali iliyomwandama, na utundu wangu ungesaidia niweze kucheza na akili yake vyema mpaka ikae sawa tena.

Nilipofika Karikoo, nilizunguka pande tofauti mpaka nikafikia Msimbazi, kisha nikaingia kwenye duka moja lenye kuuza bidhaa kama nguo, suruali, viatu, na ndala nzuri. Nikanunua T-shirt zuri sana la mikono mirefu, lenye rangi ya blue-nyeusi na mistari myembamba kifuani, pamoja na ndala nzuri zenye rangi mchanganyiko wa nyekundu, blue, na nyeupe.

Nilipenda mionekano mizuri sana kimavazi, na kutumia hela niliyokuwa nayo kwenye mavazi lilikuwa jambo la kawaida sana kwangu. Nani asiyependa kupendeza?

Baada ya kutoka hapo, nikaelekea kwenye mgahawa mzuri wa kisasa ili kupata chakula, maana sikuwa nimeweka kitu chochote tumboni kutokea asubuhi. Nikawa nimemjulisha Ankia kuwa asinitinzie chakula cha mchana maana ningechelewa kurudi na hivyo kula huku huku nilikokuwa. Nilikaa kivyangu tu huku nikiendelea kula na kuchat na marafiki kwenye simu, kisha nikaondoka hapo baada ya kushiba.

Nikaenda sehemu zingine pande hizo za Kariakoo na kununua kinanda kidogo kwenye duka la vifaa vya ala za muziki, chenye vibonyezeo vilivyowekewa sauti ambazo zimesharekodiwa. Yaani, ukibonyeza kimoja kinatoa mlio (instrumental) wa twinkle twinkle star, ama mlio wa happy birthday, kwa midundo ya kinanda. Kilikuwa kizuri sana, chenye umbo la mstatili na mwonekano kama wa boksi dogo la viatu vya dukani. Nilikinunua kwa ajili ya Mariam.

★★

Nikatoka huko Kariakoo ikiwa inaingia mida ya saa kumi jioni sasa. Kuna pisi kali nilikuwa napishana nazo, kali vibaya mno, na zilikuwa zinaniangalia hizo! Siyo poa. Yaani kuna wanawake wengine unaweza kuwaona ukatamani hata uwabebe wote uende nao kwako. Wengi watasema ooh wanaume ni malaya lakini uchaguzi mmoja tu wa mwanamke anayekufaa huwa ni mgumu sana aisee, ukitegemea wako mamilioni hapa duniani. Ndiyo sababu tunakulagakulaga wengi kwanza, na bado tunakuwa hatutosheki!

Bwana, nikawa nimeiacha Kariakoo hatimaye kwa mwendo wa taratibu wa daladala, na aisee! Nilikoma kupanda hizi daladala za kutokea Gerezani mpaka Kisemvule. Yaani watu wanabanana mpaka unakosa pozi na pumzi, hasa ukiwa umesimama kama mie ilivyokuwa wakati huu. Pigia picha ingekuwaje wakati wa usiku ikiwa tu gari liliweza kushonana namna hiyo kukiwa jioni ya mapema, na niliombea asitokee mtu wa kujamba la sivyo ningezimia!

Lengo lilikuwa kuwahi nyumbani, niweke mizigo, kisha niangalie utaratibu unaofaa ili nikamjali mamacita Soraya. Hakuwa amenipotea akilini hata kidogo, na kama ningefanikiwa kutoka na yule mwanamke, leo ningeweza hata kulala na mbu wananing'ata huku natabasamu. Yule alikuwa wa ukweli, na sikuwa nimepanga kumwambia Tesha lolote hata kama maangamizi yangetokea!

Lakini msongamano wa magari ukafanya dakika za kukawizwa barabarani ziwe nyingi hasa kuanzia maeneo ya Uhasibu, mpaka inaingia saa kumi na moja bado tukawa tunaisaka Sabasaba. Sijui shida ilikuwa nini. Hivyo hivyo mdogo mdogo tukaendelea kusogea, nami nikapata ujumbe kutoka kwa Soraya.

'Ndo natoka.'

Agh! Siyo lazima mpaka mtu awe amesoma saana ili kuelewa kwamba mtoto alikuwa anataka kuelekezewa fikira, na zangu kwa wakati huu zilikuwa kwake kweli, kwa hiyo ningejitahidi nisimvunje moyo.

Nikamjulisha kuwa nilikuwa maeneo ya karibu na Rangi Tatu, naye akasema tayari yuko kwenye bajaji kuelekea huko pia. Duh! Hapa isingewezekana kwenda kwanza kule nilikokaa na kurudi tena, kwa hiyo ingebidi nikutane naye nikiwa na mifuko ya bidhaa nilizonunua.

Kwa kuwa ilionekana yeye ndiye ambaye angewahi kabla yangu, nikamwambia kwa kuwa bajaji kutokea Kijichi zinashushia eneo la hapo Zakhem, akishuka basi aende kwenye mgahawa wowote wa karibu hata pale pale Zakhem Hotel, ndiyo sehemu ambayo tungekutana maana bado nami nilikuwa kwenye gari. Akanikumbusha kuhusu kupaswa kuwahi, nami nikamwambia asiwaze.

Dakika chache kupita nasi tukawa tumefika Rangi Tatu. Ile nimeanza kutembea tu kuelekea Zakhem Soraya akanipigia, 'wewe uko waapi' na kasauti kake ka upole, nami nikamwambia niko karibu.

Nikajitahidi kutembea haraka kiasi mpaka nilipofika eneo la mgahawa wa Zakhem, nami nikampigia kumuuliza yuko upande gani. Akaniambia ameniona na ananifata, nami kweli nikamwona akija kutokea kwenye duka dogo la bidhaa upande wa nyuma niliouvuka kabla ya kuufikia mgahawa huu maridadi.

Nikakata simu. Alikuwa anakuja kwa mwendo wa taratibu tu, gauni lake laini na refu mpaka chini likipeperuka kiasi kwa upepo uliopuliza kwa nguvu, na uso wake uliochorwa duara la ushungi aliovaa ukimpa mwonekano mzuri sana. Hii ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kumtazama vizuri akiwa amesimama, kwa hiyo nilipendezwa hata zaidi na mwonekano wake.

Akawa amenifikia karibu zaidi, tukiwa tumesimama karibu na mwingilio wa mgahawa wa Zakhem, naye akatabasamu kiasi huku mimi nikimwangalia kwa umakini.

"Nimechelewa sana?" nikamuuliza.

Akatikisa kichwa kidogo kukanusha.

"Twende sa' hata ukanywe soda na mishikaki kidogo," nikamwambia hivyo.

"Hapana... JC... nitachelewa," akasema.

"Utachelewa wapi? Saa kumi na mbili hii kweli?"

"Saa moja tu natakiwa niwe nimeshafika nyumbani. Nahitaji kuwapikia wanangu."

"Sawa. Basi... angalau nipe tu hata kimoja Soraah," nikamwambia hivyo.

Akakunja uso wake kimaswali na kuuliza, "Kimoja?"

"Ee, fasta tu," nikamwambia.

"Sijakuelewa JC..."

"Nataka nisafishe chumba na wewe," nikasema hivyo.

"Ku... kusafishaje? Kusafisha chumba?"

"Acha kujitoa akili, najua unanielewa bwana..."

"Eh... ahah... eheh... makubwa jamani..."

"Nini sasa?"

"Wewe... sasa... si nilikwambia nimeolewa?"

"Ndiyo, najua. Ila me nakuelewa, na we' najua unanielewa..."

"Mm... me hapana... siwezi... dini yangu hairuhusu..."

"Hairuhusu nini? Mbona mwenzako anaruhusiwa kuwa na wanawake mpaka wanne? Huoni siyo fair?"

"Ye' ni mwanaume... ndiyo imeshaandikwa hivyo..."

"Hakuna kitu, huo ni uonevu bwana. Ona... najua unataka kuwahi, kwa hiyo... nipe tu kidogo maana... nakuhamu sana Soraah..." nikamwambia hivyo huku namwangalia kwa macho yenye ushawishi.

"Eh... hamna... natakiwa kuwahi, kwanza me siwezi... maana..."

Akawa anajizungusha kimaneno sana, akiongea kwa namna yake ya upole lakini nikiona wazi kwamba alitaka nimbembeleze zaidi, ila kama nilivyokuwa nimesema mwanzo, ikiwa asingeridhia, nisingemlazimisha.

Nikamwambia, "Basi poa. Haina shida. Twende hivi ukapande gari uende nyumbani."

Akabaki kunitazama kama vile hakuwa amenisikia.

"Vipi?" nikamuuliza.

"Umekasirika?" akaniuliza pia.

"Sijakasirika. Si umesema unataka kuwahi? Twende ukapande gari uende."

Akaangalia chini kiasi kwa huzuni.

"Nini, mbona unakuwa hivyo?" nikamuuliza.

"Usichukulie vibaya JC, me..."

"Sijachukulia vibaya, Soraya. Si una haraka, majukumu? Ndiyo nakwambia haina shida. Nenda uwahi," nikasema hivyo.

"Sa' mbona kama umechukia?"

"Sijach... Okay. Nimehisi vibaya, lakini nitafanyaje? Una mambo muhimu ya kufanya pia. Kayafanye."

"Siyo hivyo tu, najua umechukia kwa sababu nimekukatalia. Usichukie JC..." akaongea kwa kubembeleza.

Sijui alikuwa ananiona kama keki? Hii ndiyo raha ya kutokea wanawake wenye umri mkubwa, wanajua sana kudekeza!

Nikamwambia, "Hapana, we' usiwaze. Twende ukachukue tu usafiri na me niende home. Nitapambana na hali yangu."

Akawa ananiangalia kama anataka kulia eti, kisha anaangalia pembeni, mara huku, mara kule, nami nikawa nimeshachoshwa na presha ya kutazamwa sana na watu kwenye eneo hilo.

"Soraah twende. Au vipi?" nikamuuliza hivyo kwa sauti makini.

Akaniangalia na kuuliza, "Kwani ulikuwa unataka twende wapi?"

Ohohoo! Pasi ndefu kuelekea goli la ushindi!

Sikutoa jibu. Nikaushika mkono wake na kuelekea naye kwenye jengo refu la hoteli iliyokuwa karibu na hapo, nisijali hata kuangalia jina wala nini. Nilikuwa namvuta Soraya kama vile natembea na mtoto, nami nikaiona sehemu ya mapokezi na kwenda kuzungumza na mhudumu.

Huku Soraya akiwa amesimama nyuma yangu, nikauliza gharama ya vyumba vya kulala wageni sehemu hiyo, nami nikajulishwa kuwa kuna vyumba vya shilingi elfu thelathini mpaka elfu themanini kwa siku eti. Nikatoa elfu thelathini chap kulipia kimoja, na huyo mhudumu akaniongoza mimi na Soraya kuelekea kwenye vyumba.

Eh, huyu mwanamke alikuwa na aibu! Kwa wengi mambo ya hivi ni kawaida lakini kwake yeye haikuwa hivyo, maana alitembea kwa kuficha uso wake utadhani dunia nzima ilikuwa inamwangalia yeye. Huyo mhudumu akatufikisha kwenye chumba kimoja kwenye ghorofa ya pili, nasi tukaingia ndani.

Kilikuwa na mwonekano mzuri, safi sana. Kitanda kilikuwa kipana na kirefu, kilichotandikwa shuka jeupe na kuwekewa mito, huku juu kukiwa na neti. TV ya flat screen ukutani, meza yenye droo kadhaa na viti vya kukalia, kabati la ukutani la nguo, mlango ulioelekea kwenye bafu na choo safi, pamoja na taulo mbili zilizokunjwa na kuwekwa kitandani pia, mapazia marefu yaliyofunika madirisha makubwa, vyote vilikuwemo.

Huyo mhudumu akatuacha mimi na mali safi humo ndani, nami nikafunga mlango kwa funguo baada ya kuiweka mifuko yangu mezani. Soraya alikuwa amesimama usawa wa kitanda akionekana kutafakari vitu, nami nikaona nisimcheleweshe.

Nikaja nyuma yake na kukibana kiuno chake kwa mikono yangu, huku nikibusu shavu lake usoni kutokea nyuma, lakini akashtuka na kujitoa kwangu, naye akakaa kitandani. Alionekana kuogopa.

"Vipi Soraah?"

"Me... bado naona kama tumepeleka mambo haraka sana," akaniambia.

"Bado hata hatujaanza!" nikamwambia.

"Simaanishi hivyo..."

"Nakuelewa. Ndiyo maana hii ya mwanzo nimetaka tuifanye chap tu, maana una haraka. Ama?"

"Me bado naogopa jC..."

"Unaogopa nini? We' si mkubwa kwangu? Unaogopa nini sasa?"

"Sijawahi kucheat."

"Ndo' ujifunze," nikamwambia hivyo.

Akaniangalia kimkazo na kucheka kwa kuguna.

"Usiwe hivi bwana... muda unaenda..."

Nikamwambia hivyo na kumsogelea, nami nikapiga magoti chini katikati ya miguu yake iliyofichwa kwa gauni na kuushika uso wake, nikitaka kumbusu, lakini akawa ameinamisha tu uso wake.

"Soraah, ni nini?" nikamuuliza.

Akabaki kimya.

"Unaumwa? Uko P?" nikauliza tena.

Akatikisa kichwa kukataa.

"Nini sasa? Tutumie muda vizuri basi, saa moja itakukuta bado unajing'ata... eleweka basi..."

Akaniangalia kwa macho yaliyojaa hisia nzito sana, na hivi yalikuwa lege, nami nikaifata midomo yake na kuanza kumbusu.

Piga denda nzito sana na taratibu ili nimhemshe mtoto, hapo nikiwa nimeshavimba kwa nguvu zote, nami nikashika upande mmoja wa kifua chake uliofichwa kwa nguo. Akaushika mkono wangu na kuutoa kifuani kwake, lakini nikalazimisha kuminya-minya hapo, naye akautoa tena na kukatisha busu yetu.

Nikamwangalia na kuona namna alivyokuwa anajishauri bado, na kiukweli hii sitaki-nataka ilikuwa inaniboa sana, basi tu. Nikakishika kidevu chake ili nimtazamishe kwangu, naye akaniangalia machoni kwa hisia za woga-woga tu, kitu ambacho kilifanya nihisi stimu inanitoka.

Agh, nikamwachia na kusimama, kisha nikakaa kitandani pia na kutazama pembeni nikiwa nimeudhika. Niliweza kuona uso wake ukiniangalia mara kwa mara japo sikumtazama kabisa, nami nikaangalia saa mkononi na kukuta ni saa kumi na mbili na dakika arobaini na kitu.

Hapo nikaona ni kazi bure tu kulipia elfu thelathini yote halafu mwanamke mwenyewe akawa analeta swaga za kishamba; wakati nilikuwa namkubali mno.

"JC..." akaniiita kwa sauti ya chini.

Nikamwangalia, nikiwa na uso makini.

"Umekasirika?" akaniuliza hivyo.

Nikamkazia macho tu, kisha nikatazama pembeni tena.

"Hautaki kunijibu?"

"Nikujibu nini? Unataka nifanye nini sasa? Maana sikuelewi..."

"Mmh... JC... mimi... siyo kwamba nafanya makusudi, ila... nina aibu..."

"Agh..." nikafanya hivyo na kupiga ulimi mdomoni.

"Mbona unafanya hivyo?"

"Unazingua, Soraah. Unasema una haraka, me nimekujali nikakwambia tupige mambo fasta, bado unajivuta. Asa' muda si umeshakata?" nikamwambia hivyo kwa kuudhika.

"Siyo hivyo... sijazoea tu..."

"Haya nenda," nikamkatisha.

"Bee?"

"NE-NDA! Wahi nyumbani," nikamwambia hivyo kwa mkazo.

Akabaki kunitazama kwa huzuni.

Nikasimama na kwenda kuufungua mlango kwa funguo, naye akasimama pia. Nikarudi sehemu ile yenye meza ili niichukue mifuko, naye akaja nyuma yangu.

"JC... usikasirike..." akawa ananiomba hivyo.

"Ishaisha hii. We' chukua mkoba wako, tuondoke," nikamwambia hivyo.

Nikaichukua mifuko yangu nikiwa nimeudhika kweli, lakini akaikwapua kutoka mikononi mwangu na kuiweka mezani tena. Akawa ananiangalia kama vile anataka kulia.

"Soraah mbona sikuelewi? Unataka nini sasa?" nikamuuliza.

"Mm... nakutaka weewe..." akasema hivyo kwa sauti yenye upole.

Nikabaki kumtazama usoni kwa umakini.

"Ila... ninaogopa tu JC. Sijawahi kufanya kitu kama hiki... sija... nakuogopa yaani... unanifanya nasisimka sana mpaka... mpaka naogopa... sijawahi kuwa na mwanaume mzuri kama wewe... yaani...."

Nilimwangalia kwa njia ya uelewa sasa, nikianza kumwona kama Ankia tu. Ila yeye hakuwa mzoefu, kwa hiyo sasa nisingejali tena masuala ya muda; hapa ningetakiwa nimnyooshe ili na yeye ajue kwamba tupo kwenye karne ya 21, baby!

Nikamshika usoni kwa viganja vyangu, nikiyakandamiza mashavu yake na kumsogelea karibu zaidi, nami nikamuuliza, "Haujafanya vitu vingi eh?"

Akatikisa kichwa kukubali.

"Sawa. Nilifikiri ni mashauzi tu. Nisamehe kwa kuudhika," nikamwambia hivyo kwa upole.

Nikahisi mikono yake ikikishika kiuno changu na makucha yake yakinichoma kiasi.

"We' ni mwanamke mstaarabu, naona hilo sasa. Ila kama unanitaka kweli... jiachie. Mimi ndo' najaza nafasi zilizoachwa wazi... we' ziache tu ziwe wazi. Sijui umenisoma?" nikamuuliza hivyo.

Akatikisa kichwa kukubali.

Dah! Midomo yake ilikuwa imelowana kwa mate, uso wake mweupe ukionyesha hamu nzito kunielekea, nami nikaanza tena kumbusu. Nilimpiga busu ya taratibu, pigo za wazungu zile, kisha nikashusha mkono wangu mmoja mpaka kwenye kalio lake.

(.........).

(.........).

Huyu alikuwa kama wale wanawake unaoenda kupiga halafu kazi yao inakuwa ni kulala tu huku wamefunika uso kwa mkono, kwa sababu Soraya alikuwa mpole mno na mwenye aibu. Kwa hiyo mimi nikaanza tu kujilia keki.

(.........).

(.........).

(.........).

(.........).

Hakuwa na mambo mengi ya ajabu; ni miguno tu ya upole. Nikamwacha na kwenda kuwasha taa, ikiwa imeshaingia saa moja usiku, kisha nikamrudia tena. Alikuwa ameshakolezwa utamu asiambilike chochote yaani, na kiukweli nilimfurahia mno. Nilijihisi vizuri sana. Joto lililokuwa limepanda ndani yangu lilisisimua mno nilipolishusha namna hiyo kwa huyu kamama. Nilikuwa nimeamua kuwahisha mambo ili kweli dada wa watu awahi nyumbani, lakini si utamu ukawa umemkolea?

Nikamwambia, "Soraah... saa moja ishaingia. Jisafishe uende."

"Mmm... bado..."

"Bado nini?"

"Mmm..."

"Unataka tuendelee?"

Akatikisa kichwa kukubali bila kuniangalia.

"Asa' si utachelewa?"

"Ah... chomekaa..." akaongea hivyo kwa deko.

Nikatabasamu kidogo na kutikisa kichwa, kisha nikamvuta tena. Zamu hii akiwa amebinuka kwangu, nikalisambaza kalio lake na kuingia tena, kisha nikaanza shambulizi. Alikuwa analia huyo!

Nikafumua bila kumpumzisha, akiirudisha mikono yake yote nyuma, nami nikaibania mgongoni kwake na kuendelea kupiga haswa. Nadhani alikuwa anataka kufika ukingoni kwake kwa kumwaga juisi japo tayari alikuwa ameshatetema mara kadhaa nyuma, na mimi nikajitahidi ili aridhike kweli. Alikuwa ameiva balaa!

Nikaendelea tu kumtandika huku nikimsemesha. "Utamu umekukolea, si utafika nyumbani vibaya?"

Likaendelea tu kuguna.

"Wewe... si ulikuwa unakataa-kataa, unaogopa muda... unaogopa kuchelewa?"

"Mmm... sikujuaa..."

"Hukujua nini?"

"Sikujuaa... sikujua kama we' ni mtamu hivi..."

"Ahahah... wanao si watalala njaa sasa...."

"Mmm...."

Mwanamke bwana akawa anaonyesha raha tu na malalamiko yake, na hatimaye hiyo sikujua yake ikashika hatamu.

Akapasua bomba lenye maji marefu mpaka nikashangaa! Alishtuka kwa nguvu kama vile mwili mzima umepatwa na kwikwi, nami nikawa nalisugua linyama lake kwa vidole ili asafishe haja yake yote mpaka mwisho. Ikaeleweka kwangu kwamba hakuwa amefikia ukingo kwa muda mrefu sana.

Akalala hoi kitandani, huku akijing'ata mdomo na kupumua kilegevu, nami nikamgeuza alale chali ili nichezee mwili wake. Alikuwa anarembua mno, nami nikampiga kofi laini shavuni.

"Wewe... amka... amka tuondoke. Saa mbili sa'hivi," nikamwambia.

Akawa ananiangalia kilegevu tu.

"Soraah... sitaki kuja kusikia umepigwa huko, maana mna ratiba zenu. Nyanyuka twende," nikamwambia hivyo.

Nikataka kunyanyuka, lakini akanishika mkononi na kunivuta kwake tena, asitake kuniachia.

"Nini?" nikamuuliza.

"Tukae kidogo..." akasema hivyo.

Nikatabasamu na kuuliza, "Na nyumbani?"

"Mmh... nitaenda baadaye... nimechoka..."

"Aa wee... unataka wanao walale njaa? Saa mbili sa'hivi, kwanza ulikuwa unaenda kupika nini?"

"Ubwabwa..."

"Ndo' unyanyuke sasa, washaanza kulia njaa..."

"Ah... me nitasema kulikuwa na foleni... baba yao atawanunulia chakula..." akaongea kwa deko.

Unaona? Hawa viumbe wakishagalishwa utamu ndiyo wanakumbuka kwamba kuna kitu kinaitwa kudanganya. Si muda ule alikuwa anapiga kelele eti ooh nitachelewa, sasa hivi kiko wapi? Nikacheka tu kidogo na kuushika uso wake taratibu.

"Siyo vizuri hivyo unajua?" nikamwambia.

"Me nataka tukae kidogo..."

"Kwa nini?"

Akanishika shingoni na kusema, "Bado nawashwa."

"Ahahahah... sa'hivi aibu imekutoka eh?"

Akatikisa kichwa kukubali.

"Usijali. Nitakukuna tu. Ila sa'hivi muda unatupinga. We' vaa na me nivae twende. Tutapanga siku nyingine tukutane. Si umeshanizoea sasa hivi?" nikamwambia hayo.

Akatikisa kichwa kukubali.

"Fresh. Fanya hivyo," nikamwambia.

Nikapeana naye busu tamu huku, kisha nikajitoa kitandani hapo. Aisee alikuwa amelowanisha shuka siyo poa! Ingetubidi tuondoke haraka kabla hatujaitwa kufanyia usafi maana kwenye hiyo hoteli kulikuwa na sheria za "by utawala."

Nikavaa, nikamsaidia mwanamke avae pia, na kiukweli Soraya alionekana kutaka sana tuendelee maana aliniangalia kwa yale macho ya turudi kitandani tena. Mimi nikampiga tu busu na kumwambia muda mwingine tukipata nafasi basi ningempa mapenzi zaidi hata ya leo, naye akaonekana kufurahi.

Nikafungua droo moja kwenye ile meza na kutoa chanuo. Nikachana nywele na kujiweka vizuri, na yeye pia akajiweka vizuri mwilini kwa kujipulizia manukato yake ili asifike nyumbani ananukia mimi. Uzuri hakuwa ameutoa ushungi wake pindi nzima ya mechi yetu, kwa hiyo tukabeba vilago vyetu na kuondoka.

Tukaingia tena barabara ya Zakhem kuelekea Rangi Tatu pale, tukitembea taratibu tu huku nikiwa nimemtangulia mamaa. Tulipoufikia mgahawa wa Zakhem, nikamwambia twende hapo, nami nikaenda kununua nyama za kuku pamoja na mishikaki mingi, kisha ikafungwa nasi tukaanza kurudi barabarani.

Mpaka kufikia muda huu, Soraya hakuwa ametafutwa na mume wake, kwa hiyo yeye akawa amemtafuta na kusema alikuwa amepatwa na dharura lakini ndiyo alikuwa njiani kurudi nyumbani. Dah! Dhambi hizi!

Hivyo vyakula nikawa nimempatia mwanamke ili avipeleke kwa watoto huko kwake kama zawadi ya upendo, na niliona wazi kwamba Soraya alifurahia sana. Tukaachana kwenye mazingira mazuri baada ya kuhakikisha amepanda gari la kwenda huko kwake, nami pia nikapanda la kuelekea Mzinga. Mission accomplished!

★★

Nikawa nimefika nyumbani kwake Ankia hatimaye na kumkuta mwanamke huyo akiwa amekaa sebuleni pamoja na mama Chande, na kulikuwa na mvulana mdogo hapo pia wa miaka kama 10 hivi.

Kwa haraka nilitambua kwamba mvulana huyo alikuwa mtoto wa mama Chande, labda ndiyo Chande mwenyewe, na nilipowapa wanawake hao salamu za wakati huu wa usiku, waliziitikia huku wakiniangalia kwa njia iliyoniambia kwamba kulikuwa na tatizo.

Nikaona nipite tu kwanza na kuelekea chumbani kuiweka mizigo, nikiwa nadhani labda walikuwa tu na ishu zao zisizonihusu hata kidogo, na baada ya kutoa mavazi yangu, nikavaa nguo nyepesi ili niende kuoga. Si unajua joto la mwili lingekuwa juu baada ya mechi niliyocheza na Soraya?

Kwa hiyo nikatoka chumbani ili nielekee bafuni, lakini nilipofika hapo sebuleni tena, nikakuta Ankia akiwa ameinamisha uso wake, viganja akiviunganishia usoni, huku machozi yakionekana kumtoka. Hali hiyo ikanitatiza sana.

Mama Chande alikuwa ananiangalia kwa macho yenye subira, bila shaka akitaka nijue nini kilichokuwa kinaendelea hapo, nami nikasimama karibu na sofa alilokalia yule mvulana mdogo huku nikimwangalia mama Chande pia.

"Vipi? Mbona huyu analia?" nikamuuliza hivyo mama Chande.

"Eh... kaka... ni makubwa yametokea. Kuna msiba," akasema hivyo.

Kauli hiyo ikanifanya nimwangalie Ankia, nikiwa nimehisi labda msiba huo ulikuwa wa mtu wa karibu zaidi na mwenye nyumba wangu. Lakini kabla hata sijauliza nani kafa, mama Chande akanipa jibu, na ni jibu ambalo sikuwa nimetegemea kabisa!

"Haujasikia kumbe?" akaniuliza hivyo.

Nikatikisa kichwa kukanusha.

"Joy amefariki," akaniambia.

Nilihisi kama vile pozi lilinitoka kabisa baada ya kusikia maneno hayo, lakini nikaendelea tu kumwangalia mwanamke huyo kwa utulivu.

"Unamfahamu Joy, si ndiyo? Amefariki. Tena... ameuawa," mama Chande akasema hivyo.

Eh! Haya sasa! Nikabaki nimesimama hapo hapo bila kusema lolote, nami nikatazama pembeni nikiwa najaribu kuisawazisha vyema taarifa hiyo kichwani kwangu.

Ingepaswa kuwa kitu chenye kushtua mno, na kilinishtua, lakini mshtuko nilioupata ulitokana haswa na fikira za ni nini ambacho kilikuwa kimesababisha mwanamke huyo afe ghafla. Tena kujua kwamba alikuwa ameuawa ndiyo kuliongezea fikira hizo ukali wa moto wake, kwa sababu tayari ningeweza kukisia ni nani aliyekuwa msababishi. Aisee!

Kumbe mambo yalikuwa serious namna hii? Aliyefanya hivyo alikuwa anataka kuonyesha hatanii, na nilimjua vizuri sana. Sasa kutokea hapa huu mchezo ungeelekea wapi?



★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
Ohoooo ahsante sanaa dear
 
Halaf kwann huzifanyii kazi?
emoji1751.png
emoji1751.png

MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA KUMI NA MOJA

★★★★★★★★★★★★★★★★


"Joy..." nikaita hivyo huku nikimwangalia Ankia.

Ankia akaniangalia kiumakini pia.

"Njoo JC... nakuombaaa..." Joy akaendelea kulia.

"Wewe, umekuwaje? Nini shida?" nikamuuliza.

"JC nakuomba... nakuomba uje..."

"Nije wapi? Umefanyaje? Sikuelewi..."

"Hhh... njoo... nimepigwa... njoo JC..." akasema hivyo.

"Umepigwa na nani? Uko wapi?" nikamuuliza.

Hakujibu kitu na kuendelea kulia, nami nikamwangalia Ankia kimaswali. Akanionyesha ishara kwamba niweke mfumo wa kipaza sauti kwenye simu, nami nikafanya hivyo ili amsikie pia. Joy akawa akisikika vyema zaidi sasa namna alivyolia.

"We' Joy... niambie uko wapi..." nikasema hivyo.

"Hhh... Kongowe... nipo... hapa...."

"Nani amekupiga, amekupiga wapi? Eleweka basi..."

"Njoo JC... nakuomba... uje unitoe huku... JC nimeumia..."

Khh! Nikaona mwanamke huyo ananichanganya tu, hivyo nikakata simu na kuangalia pembeni kwa kuudhika.

Ankia akasema, "JC... mbona umekata simu? Joy... Joy anaonekana kuwa na shida... ameumia..."

"Me siyo mtoto mdogo Ankia. Tumia akili na wewe basi..." nikamwambia hivyo kwa kuudhika.

"Una maana gani?" akaniuliza.

"Huyu mwanamke anataka kunipanda. We' ndo' ulimpa namba yangu?" nikamuuliza.

Akabaki kunitazama tu usoni.

"Nijibu Ankia..." nikamwomba.

"Ee... alichukua namba yako kwangu... hiyo juzi. Aliichukua aliponisimulia mliyofanya chumbani kwako..." akaniambia hivyo.

"Achana na hayo. Huyu mwanamke anataka kunizoea vibaya, na mimi hiyo juzi nilikuwa nimelewa ndo' maana nikafanya naye. Asa' hapa ataanza kunisumbua kijinga tu..."

"Je kama amepigwa kweli? Labda yuko kwenye hali mbaya..."

"Asingekuwa ananifahamu angempigia nani?" nikauliza.

"Sijui, labda mabwana zake..."

"Awapigie hao hao sasa..." nikasema hivyo kwa kuudhika.

Simu ikaanza kuita tena, ikiwa ni Joy, nami nikakata upesi. Nikaiwekea namba hiyo ya Joy kizuizi (block) ili isinisumbue tena, haijalishi alikuwa anamwaga vipi machozi huko alikokuwa.

Ankia akatulia tu, akiona namna ambavyo hali hiyo ilikuwa imenikera sana, nami nikamwambia afanye kujiandaa kabla ya Tesha kuja ili tuelekee Masai kujichangamsha kidogo, kisha nikatoka hapo na kuelekea chumbani kwangu.

★★

Tesha hakukawia kuja hapo kwa Ankia baada ya mimi kuipuuzia simu ile iliyonikera kutoka kwa Joy, na alikuwa amevaa kwa njia ya kawaida ya kinyumbani tu. Hata mimi pia nilitinga nguo zangu za kawaida tu japo ningeonekana kupendeza mno kama kawaida yangu.

Ni Ankia ndiye aliyejiwekea mwonekano matata. Alivaa nguo kama shati laini tu lenye mikono mirefu, jeupe, lililoishia sehemu ya chini ya mapaja yake. Yaani kama angeinama kuokota kisoda, huko nyuma angeangusha tamasha!

Hilo shati, sijui gauni fupi, lilikuwa lenye kuonyesha ngozi yake ya ndani, kwa hiyo hata sidiria yake nyeupe pamoja na kikaptura cha skinny nyeusi kifupi sana alichovaa kwa chini zilionekana; na hapo ndiyo nikawa nimengundua kumbe huyu mwanamke alijua kujiachia. Jinsi alivyoiweka tu sidiria yake isogeze kifua mbele aisee! Ilikuwa ni makusudi yenye kutamanisha. Tesha alimsifia na kuniambia nijichukulie mtoto huyo, bila kujua kuwa nilikuwa nimeshalibeba!

Kwa hiyo tukasepa zetu kwenda Masai kwenye mida ya saa mbili kasoro, Tesha akiwa ametuambia kwamba dada yake alikuwa nyumbani, hasa kwa sababu leo ilikuwa Jumapili kwa hiyo alishinda hapo tu.

Akaeleza pia kwamba hapo nyumbani kwao angalau kwa wakati huu mambo yalikuwa vizuri tu kama nilivyoyaacha tokea Joshua aondolewe. Dada yake hakuwa mbanizi sana ila alimwambia Tesha awahi kurudi, ishu za kuingia ndani usiku mno hazikufaa, nami nikamwambia kweli leo tusingekaa muda mrefu.

Ankia akawa amemwambia kuhusu suala la Joy kunitafuta, naye Tesha akaniambia nilifanya la maana kumpuuzia kwa kuwa angenisumbua mno; na tayari alikuwa ameshanishauri juu ya sababu iliyofanya kwa nini kumpuuzia Joy iwe muhimu.

Basi tukafika Masai, nasi tukakaa sehemu iliyokuwa na viti vifupi vya mbao, vyenye muundo kama wa makochi marefu, vikizunguka meza pana ya mbao kwa pande mbili. Mimi na Ankia tukakaa upande mmoja, Tesha ule mwingine, kisha tukasubiri mhudumu aje.

Watu walikuwa wengi sana hapo, hata muziki ulikuwa ule wa nguvu zaidi maana kulikuwa na mhemko wa ukweli, hii ikiwa kawaida ya wikiendi kudadeki! Wanawake wengi waliniangalia, mimi na Tesha, lakini tukawa tunakula zetu tu. Mhudumu alipofika, nikamwambia aketi karibu nami ili kumpa maagizo kwa njia ambayo asingesahau, na baada ya kuelewa akaondoka.

Tukaendelea kutulia tu, huku baadhi ya watu waliopandwa na pombe wakiwa wameshaanza kucheza, Ankia akininong'oneza sikioni kuhusu namna watu walivyotuangalia na kunifahamisha fulani ni fulani, nikiona wazi kwamba mwanamke huyu alitaka watu waone nina ukaribu naye zaidi.

Muda si mrefu vinywaji vikaletwa; chupa tatu za Dompo baridi, pamoja na glasi za vioo. Zikagawanyishwa kwetu na huyo mhudumu, kisha akaondoka. Tesha alionekana kufurahi, lakini akatulia tu. Kidevu juu, si unajua? Kwa haraka hapo alielewa elfu thelathini ilikuwa imepita, na alijua vingine vilikuwa vinakuja kwa hiyo lazima angeweka ule mwonekano wa kutoshangaa.

Tukamimina kila mtu kwenye glasi yake, na Ankia hakuacha kuniambia kuhusu namna ambavyo watu walitutazama sana. Nikawa namwambia vitu vyenye kumchekesha, mara kwa mara Tesha naye akinitumia sms za utani kuelekea tabia tuliyoionyesha hapo ya ushua mwingi, na taratibu muda ukawa unaenda.

Wakawa wanakuja marafiki zao Tesha na Ankia pia, kutia ndani Bobo, wakitusalimu, kisha wanaondoka. Aliyekuja na kukaa hapo kabisa ilikuwa ni mama Chande, yule rafiki yake Ankia, naye nikamwagizia chupa 5 za bia aliyoipenda; Safari Lager.

Hazijapita dakika nyingi, wakaja wanaume vijana wawili wakiwa wamebeba sinia pana la mstatili lenye vyakula hapo. Kulikuwa na chips kavu nyingi, mishikaki ya ng'ombe mingi pia, pamoja na nyama za kuku. Meza ikaonekana kujaa kiasi, na mama Chande alikuwa anachekelea vibaya mno.

Tesha akanitumia ujumbe kuuliza ikiwa tungekula halafu tukimaliza tukimbie, maana alihofia hakukuwa na pesa ya kutosha, na kuniuliza ikiwa ni Chalii Gonga ndiye aliyelipia. Nikamwambia hapana, sikuwatoa hapa na Ankia kwa udhamini wa mtu yeyote; hii yote ilikuwa mimi, na yeye ajitahidi tu kuenjoy kisha tuondoke mapema.

Dah! Makamuzi yakaanza baada ya sisi wote kunawishwa mikono. Niliona jinsi wenzangu walivyojitahidi kuweka kauzungu kidogo kwenye ulaji na unywaji, na nilielewa kuna vitu vingi sana vingesemwa hapo Masai hata kuhusu haka kajambo kadogo tu tulikofanya, maana Tesha alisema fitina nyingi zilijaa sana sehemu hiyo. Niliangaliwa, yaani niliangaliwa mpaka ilikuwa inakera!

Angalau mama Chande akawa ameanza kunisemesha, akiniambia kweli kila mwanamke hapo alinitaka, eti kasoro yeye lakini! Shabiki wa Yanga na mashauzi yake huyo! Tukakata muda hapo mpaka imefika saa nne na nusu hivi, vibe la Dompo likiwa limenipanda kiasi, nami nikaletewa jambo jipya.

Mhudumu yule mwenye macho makubwa na kalio nene aliyetuhudumia jana pale VIP hadi Tesha akaanza kumchokoza, akawa amekuja hapo tulipokuwa, naye akanifata na kuniinamia sikioni, kisha akasema, "Nimeambiwa nikuletee hii."

Alinishikisha kitu kama karatasi kwenye kiganja changu, nami nikaitazama kwa njia ya kawaida tu. Hakuondoka. Akasimama nyuma yangu kama vile anasubiria jibu.

Nikaifungua hiyo karatasi, ikiwa ni bandiko dogo la kwenye chupa ya bia, na upande mweupe ulikuwa umeandikiwa maneno "njoo VIP, NINA SHIDA NA WEWE."

Aya?! Huyu angekuwa nani? Chalii Gonga? Hapana, yeye angenipigia tu simu. Huyu angekuwa mtu nisiyemfahamu, ama labda nilimfahamu lakini kwa hapo nisingejua ni nani. Fikira za haraka ikawa kwamba ni Joy, nami nikamwangalia Tesha na kukuta ananitazama kwa yale macho ya kuuliza 'vipi?'

Nikampa ishara huyo mhudumu kuwa ainame nimsemeshe, naye aliponikaribia nikamuuliza, "Nani amekupa hii?"

"Mke wake boss... boss wetu," akajibu hivyo.

"Bosi? Mke wake Chalii?" nikamuuliza.

Akatikisa kichwa kukubali.

"Nani, yule Joy?" nikauliza tena.

"A-ah... siyo Joy... mke wake boss kabisa... sijui anaitwa nani," akaniambia hivyo.

Dah! Kizungumkuti.

Ankia akaniuliza vipi, hapo tumacho twake tukiwa tumeshaanza kuwa lege, nami nikamwambia kuna mtu huko VIP ananiita... mke wa Gonga. Ankia aliposikia hivyo, akaniambia niende tu kumwona, maana alimjua lakini hakuwahi hata kuongea naye, ila nafsi yangu ikawa inapingana na hilo.

Nikamwambia yule mhudumu, "Nenda kamwambie hivi... ninakula. Kama anataka kuniona... yeye ndiyo aje hapa. Asipoweza, basi. Nenda."

Mhudumu akaondoka zake.

"Hadi mke wa Gonga ashaanza kutuma wajumbe!" Ankia akaniambia hivyo sikioni.

"Unamjua vizuri?" nikamuuliza.

"Ee, yupo hivi mwembamba kidogo, ila ana kashepu... mzuri mzuri... anapendaga kukaa huko juu akijaga hapa," akasema hivyo.

Nikapiga tu fundo dogo la wine.

"Si ukamwone?" Ankia akasema hivyo.

"Ah... ili iweje?"

"Atakuwa anakutaka..."

"Me simtaki sasa. Hebu kula tuondoke bwana..."

Ankia akacheka na kunilalia mgongoni, kisha akaendelea kula na kupiga umbeya na mama Chande.

Tesha akanitumia ujumbe kuniambia kwamba niwe mwangalifu sana kwa jambo lolote lile ambalo ningejiingiza kufanya na watu wake Chalii Gonga, nami nikamwambia asijali, nilikuwa macho. Dogo pia alikuwa makini hata ingawa kwenye kukubali bia za ofa kutoka kwa watu hao lilikuwa jambo rahisi kwake.

Ni baada tu ya dakika kama mbili kupita na yule mhudumu akawa amerudi tena. Zamu hii akanipa kikaratasi kingine tena, nami nikahisi kukerwa. Alikuwa ameshaanza kunichoresha kwa watu maana wajanja wangejua tu kwamba alikuwa anatumwa kwangu, na mimi nilitaka hiyo ikome. Nikaifungua karatasi na kusoma.

"Njoo, pametulia zaid huku. Kuna ishu muhm natak tuongee. Nitagharamia order zako zote hata ukitaka. We njoo"

Ikasomeka hivyo. Nikawaangalia wenzangu na kuona wananitazama usoni kwa umakini, nami nikasimama na kumwambia huyo mhudumu aende zake; sikuhitaji msindikizaji, VIP nilipajua.

Nikatoka na tembea yangu ya kujiamini, nikiwapita watu walioserebuka hapo, na nilipofikia usawa wa sehemu ya DJ nikakuta ni Bobo ndiye anaongoza mitambo. Alikuwa pia ameshika maiki na kufanya kama u-MC, na baada ya kuniona nakuja upande wake, akaelekeza sifa kwangu.

"Oyo, oyo, vibe kama lotee... mchina, mchina, kasimama mchina... kelele kwakeee!"

Bobo alikuwa anasema hivyo huku akinionyeshea kwa watu, na kweli shobo zikaanza kutoka kwa watu ambao hata sikuwafahamu; wanawake wakiwa wanatoa sauti za shangwe. Nikacheka kidogo nilipomfikia na kumwambia 'acha basi mwanangu,' naye akagongesha kiganja chake kwenye changu kabla ya kumpita na kwenda upande wa vyoo.

Baada ya kutoa haja ndogo ndefu kweli, nikatoka hapo na kuelekea VIP. Moja kwa moja mpaka ndani. Nilipoingia, nikakuta ndani humo kukiwa na utupu wa watu isipokuwa ya mwanamke mmoja aliyekuwa amekaa kwenye sofa upande wa mbele zaidi. Alikuwa amekaa kwa utulivu tu, simu ikiwa kiganjani, na macho yake yakiwa kwangu.

Alikuwa mzuri kwa kiasi chake, mwembamba lakini kutokea kiunoni mpaka miguuni alikuwa na unawiri mzuri, akiwa amevalia gauni refu lenye kubana mwili wake, jeusi, lenye kupambwa na vitu vinavyomeremeta kulizunguka, na lilikuwa na mpasuo mrefu kufikia juu ya hip yake uliolionyesha vizuri sana paja lake jeupe.

Sura yake ilitaka kufanana na ya mwigizaji Rose Ndauka, ingawa huyu alikuwa mweupe. Alishonea wigi la nywele za kizungu kichwani, na midomo yake ilikuwa mikubwa; ikionyesha mtapakao wa lipstick nyekundu iliyong'aa. Ah mimi kwa kusoma figure za wanawake nilikuwa sijambo!

Alivutia kwa mwonekano aliokuwa nao, wadhifa wa kuwa mke wa mwenye Masai na hoteli kubwa huko Buza ukimfaa kabisa, lakini hakuwa Hamisa Mobeto! Nilimwona kuwa wa kawaida sana, na nilitaka kujua alichohitaji kuzungumza nami ili niondoke haraka.

"Ingia. Mbona umesimama huko? Njoo..."

Akasema hivyo, sauti yake ikiwa na utulivu tu, nami nikauachia mlango na kusogea mbele kidogo.

"Wewe ndiyo unaniita?" nikamuuliza.

"Ndiyo, ni mimi. Mpaka kusumbuana sana... si ungekuja tu mara ya kwanza nilipomtuma huyo?" akasema hivyo.

"Sikujui, ndiyo maana..."

"Kwani sasa hivi umenijua? Ama ni ile tu kwamba... nitalipia kila kitu ulichoagiza ndiyo imekunyanyua?"

"Sikuja hapa nikitarajia kulipiwa chochote na mtu yeyote, unanielewa? Ongea shida yako niondoke," nikamwambia hivyo kwa sauti makini.

Akaachia tabasamu la kuhukumu fulani hivi, nami nikaona ana dharau tu.

"Unaitwa nani?" akaniuliza.

Nikabaki kimya tu.

"Mimi ni Bertha. Naimiliki hii sehemu na mume wangu...."

"Unataka nini?" nikamkatisha.

"Mhm... una kiburi sana inaonekana..."

"Ah..."

Nikafanya hivyo na kupiga ulimi mdomoni, nami nikageuka ili niondoke.

"Unajua kwamba mpenzi wako amevamiwa?" akaniuliza hivyo.

Nikageuka na kumtazama.

"Eee. Wamemvamia... wamempiga vibaya sana... hadi polisi wameitwa," akasema hivyo.

"Sielewi. Mpenzi wangu gani?" nikamuuliza.

"Lazima utakuwa nao wengi kwa hiyo kukuchanganya ni rahisi..."

Nikaendelea tu kumwangalia, naye akasimama na kuanza kuja upande wangu. Oh alikuwa mrefu, na ulizidishwa kwa viatu vya kuchuchumia alivyovaa.

Akanikaribia na kusema, "Kwa hiyo huna habari yoyote kama Joyce amevamiwa?"

"Joyce? Joy?“

"Mmm."

"Amevamiwa wapi?"

"Huko Kongowe..."

"Ih! Kwa hiyo umeniita hapa kuniambia kwamba Joy amevamiwa, sijui amepigwa, kwa nini?"

"Si ni mpenzi wako?"

"Siyo mpe.... aisee! Watu mkoje? Joy ni mpenzi wangu? Haya, sawa. Ni mpenzi wangu. Akipigwa inakuhusu nini? Wewe unataka nini?" nikamuuliza kwa kuudhika.

"Nataka ujue kwamba mimi ndiyo nimewatuma hao watu wakamvamia," akaniambia hivyo kwa sauti kuu.

Kauli hiyo ikavuta umakini wangu.

"Isingekuwa ya mazingira, ningehakikisha wanamuua! Wewe kijana ni mjinga sana. Unashindwa vipi kujua kwamba mpenzi wako anatembea na mume wangu na ukamdhibiti? Tena kwa jinsi navyosikia ni kwamba unajua kabisa, lakini umetulia tu. Kwa nini, kwa sababu unamwogopa Gonga?" akaongea kwa hisia kali.

"Unasikia kutoka kwa nani?" nikamuuliza hivyo kwa sauti ya chini.

"Nisikilize. Sipendi mchezo. Sawa? Kama unafikiri Gonga ndiyo wa kuogopa, umekosea. Niogope mimi hapa. Kila kitu anachofanya Gonga kinapita kwangu, na sitaki aguswe na malaya yeyote yule. Yeye ni mume wangu tu. Usipoangalia na wewe nitakuja nikuumize vibaya mno kwa sababu unaendekeza unafiki tu wa kipuuzi. Huna hata aibu? Yaani mwanamke wako anatoka na mwanaume wangu halafu umekaa tu?" akasema hivyo kwa mkazo.

Ka! Huyu mwanamke alikuwa mjinga, ama? Nikabaki nikimtazama kwa mkazo sana, nikiwa naona wazi kwamba akili yake haikuwa na ule usawa sawa.

"Nimekwambia ni mimi ndiyo nimemfanya hivyo ili usihangaike kutafuta nani kampiga... wala nini. Na ushahidi hauna kama ni mimi, na ninakuambia ili nikuonye... wewe na huyo malaya wako. Habari zenu zote ninazo. Nikija kusikia tena... nawaua nyie wote. Unanielewa?" akasema hivyo.

Nikatazama chini nikiwa najaribu kuelewa hali ya mtu huyu mbele yangu.

Akanipiga begani kidogo na kusema, "Wewe! Unanielewa?"

Nikamnyooshea kidole kwa njia ya hasira na kumkazia macho kiukali.

Akabaki kunitazama kwa ujasiri.

"Na wewe nisikilize. Kama una kawaida ya kutengeneza drama kwa kufanya vituko vya kijinga, na unataka kuitengeneza na mimi hapa... nitaicheza. Unanielewa? Sipendi ujinga. Unanipotezea muda kuniambia vitu visivyonihusu, sijui umefanyaje, sijui utafanyaje, ili iweje? Kama unataka kufanya, fanya! Nimekuzuia? Sitaki ujinga. Narudia tena, sitaki ujinga. Hunijui, sikujui, ila ukitaka kunijua na mimi... endelea kunichokonoa," nikamwambia hivyo kwa hasira.

"Mhm... kwa hiyo unajifanya unaniweza mimi si ndiyo?"

"Na nitakuharibu vibaya mno! Niguse tena uone," nikamwambia hivyo kiukali.

Akabaki kuniangalia tu.

"Hivi wewe... yaani unaonekana.... eti 'nimempiga mpenzi wako,' kwa hiyo unataka nikusaidie nini? Ama unafikiri nitakupigia magoti? Tena yaani... waambie na hao waliompiga Joy waje kwangu... walete kwangu na mimi wanipige, sawa?" nikamsemesha kwa ujasiri.

Akawa ananiangalia kama vile bado hanielewi sijui, na mimi hapo tayari nilikuwa nimeshapandwa na hasira pia.

"Mtu kweli unakosa kazi, unakaa kufanya michezo ya kipumbavu tu? Tuko kwenye movie hapa? Haya ni maisha, darling. Hata upige na kuua malaya wangapi, mume wako atatoka nje tu! Unang'ang'aniza ujinga, eti 'nakuambia ili nikuonye,' mimi ndiyo natoka na mume wako? Unashindwa kutafuta suluhisho linalofaa unaendekeza ujinga tu wa Sinema Zetu? Utaendelea kukalia chupa ya moto tu, mjinga wewe!" nikamwambia hivyo kwa hasira.

Alikuwa amenikera sana. Hii ilikuwa nje ya matarajio yangu kabisa. Akanisukuma kifuani kwa mikono yake, kama kutaka kunifukuza, lakini nikaishika mikono hiyo yenye bangili nyingi kwa nguvu sana, halafu nikamvuta mpaka karibu na uso wangu.

"Niachie, msenge wewe!" akanitukana.

"Nakwambia hivi... waite hao watu wako na mimi wanivamie, sawa? Uone kama Gonga ataacha kulala na wanawake wengine. Ikikupa faida yoyote kuumiza watu wengine kwa sababu ya vitu unavyoshindwa kucontrol... niite mwehu. Nitakula makapi yako kila siku! Mjinga wewe!" nikamwambia hivyo.

Kisha nikamsukuma mpaka akadondokea kwenye meza na kukaa huku akiniangalia kwa hasira.

Nikaufungua mlango, na kabla sijatoka nikamwambia, "Na sikuja ili unilipie chochote. Hauna hata hela wewe, unazitoa tu kwa mume wako afu' unajifanya eti 'kila kitu kinapita kwangu,' 'nitakuumiza!' Uje ujaribu kunisogelea tena uone."

Alibaki akiniangalia kama vile kweli alikuwa amekalia chupa ya moto, nami nikatoka hapo na kurudi kwa wenzangu tena.

Nilikuwa nimeshaudhika sana, na baada ya kufika pale walipokuwepo marafiki zangu, nikakuta ni Ankia na Tesha tu ndiyo waliobaki, huku mama Chande akiwa na watu wengine kwenye kucheza muziki. Ankia akaniuliza mke wake Chalii Gonga alitaka nini, nami sikujibu hilo, nikamwomba tu Tesha aniitie yule mhudumu niliyeongea naye mwanzoni ili nilipe, tuondoke.

Ilikuwa imeshafika saa tano na nusu hivi, na baada ya huyo dada kuja tukapiga mahesabu na kujua gharama iliyonihusu hapo ilikuwa 83500. Nikatoa wallet na kumpatia elfu tisini, naye Tesha akanionyesha ishara ya kushangaa kwa mdomo. Mhudumu huyo akaondoka, akiwa anatakiwa kurudi na chenji na mzigo mwingine.

Ankia akaniuliza mbona kama hela ilipita hata vile ambavyo tulichukua, na ndiyo hapo hapo akapata jibu. Mhudumu aliporejea na chenji, akawa ameleta na mfuko uliowekewa nyama ya kitimoto iliyotengenezwa vizuri sana, ikiwa imegawangishwa kwenye vifungo viwili. Moja ilikuwa kilo, na nyingine kilo tatu.

Nikampatia Ankia abebe huo mfuko, nasi tukaanza kuondoka. Bila shaka watu walijiuliza kwa nini tunaondoka mapema sana, ila sababu zilikuwa zetu kujua. Kwa sababu Ankia alikuwa anamalizia kuagana na rafiki yake aliyekutana naye langoni, mimi na Tesha tukawa tumetangulia nje, na ndiyo kijana akapata nafasi ya kuniuliza yaliyojiri kule VIP.

"Umemwona huyo mwanamke?" akaniuliza hivyo.

Nikatikisa kichwa mara moja kukubali.

"Alikuwa anataka nini?"

"Ah... ananichanganyia habari tu. Anaanza kuniambia eti sijui katuma watu wampige Joy kisa anatoka na mume wake..."

"Wewee... kweli?"

"Ndiyo hivyo kaka. Asa' me inanihusu nini? Eti anasema anajua me ni mpenzi wa Joy, kwa hiyo ananiambia ili kunionya. Ana akili kweli?"

"Ahahee... mwanangu siyo poa. Mabalaa yashaanza kukutafuta mapema hata wiki haijaisha!"

"Ananiogopesha sasa unafikiri?"

"Kwani ni kweli alivyosema?"

"Hata kama ni kweli, hanibandulii chochote. Siogopi mtu Tesha, nayemwogopa ni Mungu tu. Sijui watu wana matatizo gani... mimi kuja hapa sijui nawazuia wasile kwao? Tayari washaanza kusambaza me mtu wake Joy, wakati hata sijui anatokea wapi! Fitina za hapa ulizoniambia ndiyo nimeanza kuziona... mpaka natamani nisirudi tena," nikamwambia hivyo kwa kuudhika.

Tesha akanisimamisha karibu na nguzo, naye akasema, "Oy, tusimame hapa, tumsubirie huyu. Sikia. Me nilikwambia. Masai ndo' palivyo. Yaani mtu akishakugusa tu kidogo, ndiyo atataka hadi afunue na nguo yako auone mwili wote."

"Unafikiri kwa huyu mwanamke ni hicho Tesha? Basi tu, sijui ana akili gani yaani... nilikuwa hata simwelewi..."

"Huwa anavuta," Tesha akasema hivyo kwa sauti ya chini.

"Bangi?"

"Unga."

"Kumbe?"

"Ee. Bobo si mwana? Huwa ananiambia. Kamemganda sana Chalii, na hata wakigombanaga... akikapa tu unga kanatulia. Sasa kakiwa high huwaga kanafanya vituko hapa ama kule... Chalii muda mwingine anakafungiaga wanasema..." Tesha akaniambia.

"Ahaa... kumbe ni addict?"

"Eee. Usikute hapo kalikuwa kamepiga. Kanajionaga matawiii, shauri nasikia kwao kwanza wana hela sana..."

"Aaa, kumbe ka kishua?"

"Ndo' hivyo. Ila ishu zake siyo, sometime huwa hadi nasikia kanampelekaga Chalii kombo na ye' anaanza kufanya vitu kwa sifa.... wana akili zile zile tu, sijui walitoana wapi mpaka kufaana... yaani mwanangu! Me huwa najichekesha kwao tu lakini sijiwekagi karibu kabisa. Kuna mambo mengi figisu huko, unashangaa tu umekuja kuuziwa kesi. Kisa? Ulionwa umeingia VIP na mke wa Gonga. Kakishapeleka maneno ya kijinga kwa mume wake huko kakamroga-roga kwa uwongo? Ohooo... unajikuta kwa Maimuna mzee. Kuwa makini..." Tesha akasema hivyo.

Nikaangalia pembeni kiufupi nikiwa natafakari maneno hayo. Alikuwa sahihi kabisa. Tena hata nilipomwambia huyo mwanamke hana hela, nilisema hivyo kwa sababu ya hasira zilizonifanya kutongalia vitu kwa umakini, lakini si ajabu kwamba kweli mwanamke huyo ndiye aliyekuwa mwenye nguvu zaidi hata ya Chalii Gonga. Ni kwamba tu ugeni wa maeneo na watu ndiyo uliokuwa mpya, lakini si kwamba vitu vya namna hiyo vilikuwa vigeni kwangu.

Kwa vyovyote vile nisingetaka kujiingiza kwenye shida zaidi na watu hao, japo nilikuwa tayari kupambana nazo kama wangezileta kwangu, kwa hiyo kuanzia wakati huu ningepaswa kujitahidi kuweka kigingi kikali kuzuia mazoea yasiyo na faida yoyote pamoja na watu hao; hasa huyo Chalii Gonga.

Nilihisi kabisa kwamba mwanaume huyo angekuja kuniletea shida endapo kama ningejiingiza kwenye mambo aliyojihusisha nayo, haijalishi ikiwa na mke wake alihusika, hivyo huu ndiyo ungekuwa mwanzo wa mwisho wa ukaribu wowote uliokuwa umejitengeneza baina yangu na mwanaume huyo.

Sikutaka kuangalia faida zozote zile za muda mfupi ambazo ningepata kutoka kwa mtu aliyefanya mambo haramu mpaka kutembea na mabastola, bali kukazia fikira hasara ambazo zingenipata kwa kuweka ukaribu naye ndiyo kungenisaidia niwe makini kwa muda wote ambao ningekuwa huku.

Mwanzoni si ilionekana kama shobo tu lakini sasa ndiyo nikawa nimeanza kutilia maanani ukweli wa kwamba si kila mtu anayecheka na wewe anakutakia mazuri, na kama Gonga Chalii na wenzake wangekuwa wananipangia mabaya, basi na mimi ningewarudishia ubaya tu. Daktari mwenye kiburi ndiyo lakini nilikuwa makini. Waje kunifata, ndiyo wangeelewa maana ya jina langu!



★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
Story ni nzuri haswaa! Naomba kujua, ni ya kweli au ya kutunga?
 
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA KUMI NA NNE

★★★★★★★★★★★★★★★★


Mama Chande akaendelea kusema, "Ile jana nilipata taarifa eti Joy alikuwa amevamiwa, akapigwa, lakini hakujua amepigwa na nani. Yaani wakaenda mpaka polisi... akawa amehojiwa. Aliulizwa kama alifahamu watakaokuwa wamefanya hayo kwa sababu mapolisi waliona hao watu walimlenga yeye kabisa, lakini akasema hajui. Leo ndo' tunapata hizi taarifa. Jamani!"

Nikamwangalia Ankia kwa ufupi, akiwa bado ameinamisha tu uso wake, nami nikauliza, "Ameuawa vipi?"

"Nasikia sijui amechomwa na visu, sijui amekatwa na mapanga... eh, yaani bado sijaelewa," mama Chande akasema.

Nikafumba macho kwa ufupi, kisha nikafumbua na kuuliza, "Wapi?"

"Nasikia alikuwa huko mitaa ya Buza. Jamani dada wa watu alikuwa mzuri! Alikuwa rafiki yetu sana, akija anatuchangamkia kweli, yaani ni kama tumetoka mbali kweli japo tumekutania huku tu. Sijui hao watu walikuwa wanamtaka nini! Na ni kweli kama mapolisi walivyosema, walikuwa wanamlenga yeye hata kwenye hiyo ya kupigwa. Nimeogopa sana jamani yaani... ah! Ankia... jikaze dada, ndo' maisha... yamempata mwenzetu, tuombe tu yasitufikie na sisi! Hei..." mama Chande akasema hayo kwa huzuni.

Safari ya kwenda bafuni kuoga ikawa imekatikia hapo hapo, nami nikakaa kwenye mkono wa sofa pembeni yake Ankia na kutulia hapo kwanza. Maswali kadhaa yalipita kichwani kwangu, na sikuweza kujizuia kuhisi vibaya sana moyoni kutokana na tukio hili kunihusu mimi pia kwa njia fulani.

Nikakumbuka namna ambavyo Joy alikuwa akiongea kwa huzuni sana jana aliponipigia na mimi nikampa bega la baridi kwa kudhani alikuwa ananifanyia tu kituko kingine. Nikawaza kuwa huenda kwa njia kubwa nilisababisha kilichompata kitokee, kwa sababu nilichukulia vitisho vya mke wa Gonga kuwa hewa tu japo alionekana kuwa serious. Na sasa akawa amethibitisha kwamba hakutania. Aisee!

Nilijua kabisa kwamba ingekuwa ni yeye ndiye aliyefanya hayo, na kama haikuwa yeye, basi ningehakikisha nafanya utafiti wa ndani zaidi kujua ni nani aliyemwondoa mwanamke yule duniani.

Sehemu hii sasa ikawa imejawa na simanzi kutokana na hii ishu, nami sikusema lolote lile na kuendeleza utulivu wangu tu. Mama Chande akasema kwamba amesikia mapolisi walikuwa wanafatilia sakata hilo la mauaji ya Joy ili wawapate waliohusika, nami nikawa nimeingiwa na wazo lililonitia wasiwasi kiasi.

Tesha alisema kitu kuhusu mke wa Chalii Gonga kuwa mtu mwenye hila sana, na kama ilikuwa yeye ndiye amemuua Joy, uwezekano wa kuligeuzia suala hilo kwangu ulikuwepo. Si alikuwa anataka kunikomesha? Huwezi jua, ningeshangaa tu mapopo hao wanafika mlangoni hapo na kusema niko chini ya ulinzi kwa sababu mimi ndiyo muuaji!

Huyo mwanamke angeweza kunikamatisha kinamna hiyo kabisa kwa kutumia hila zake, na hili lilikuwa ni wazo la kutochukulia kirahisi hata kama uhakika wa mambo kwenda namna hiyo haukuwa wa asilimia mia.

Nikiwa bado nawaza mengi, nikasikia sauti ya mlio wa simu yangu kutokea chumbani, nami nikanyanyuka kwenda kuona mpigaji ni nani. Nikakuta ni Tesha, na baada ya kupokea, rafiki yangu huyo naye akawa amenipa taarifa za kifo cha Joy. Ila yeye kama kawaida yake ndiyo alikuwa na habari kamili.

Akaniambia kwamba Joy aliuawa maeneo ya kule Buza baada ya kuwa ametoka kwenye ile hoteli yake Chalii Gonga kwenye mida ya jioni kabla giza kuingia, sehemu ya mauaji hayo ikiwa ni kwenye ghetto lake lililokuwa maeneo ya huko huko. Nikamuuliza ikiwa alisikia kuhusu kuvamiwa kwake pale Kongowe, na alipokubali, nikauliza Kongowe alivamiwa akiwa kwa nani. Akasema alivamiwa akiwa kwenye nyumba isiyo ya kwake, ila hakuwa na uhakika sana ni ya nani.

Akaeleza kwamba alikisia hayo yote yalihusiana na suala la mke wa Chalii Gonga kujua kuhusu Joy kutoka na mume wake, naye akaeleza kwamba alihuzunika sana. Alikuwa anatamani hata afanye jambo fulani ili kulipiza kisasi kwa ajili ya kifo cha mwanamke yule, kwa sababu aliuliwa vibaya sana kwa kuchomwa na visu mara nyingi mno mwilini. Roho iliniuma.

Tukaagana na Tesha baada ya yeye kuniambia yupo njiani kurudi kutokea Tandika, na hakuwa ameniambia alikwenda huko saa ngapi wala kufanya nini kwa hiyo nikachukulia alikuwa na mambo yake tu mengine. Mimi kiukweli nilivurugwa mno na msiba huo. Nikawa hadi nashindwa kuacha kumtafakari mwanamke yule japo nilijitahidi kiasi kuondoa fikira zangu zote kwake.

Mpaka mama Chande na mwanaye walipoondoka, nikakaa na Ankia kidogo na kumsikiliza alipotoa maneno yake yenye kuonyesha huzuni kuelekea kifo cha rafiki yake, nami nikajitahidi kumbembeleza kwa upole mwingi. Hapa kilichokuwepo kwa Ankia hiyo kesho ilikuwa kwenda msibani ili kuwaunga mkono ndugu na marafiki zake Joy, na mimi pia nikamwambia ningekwenda.

Nikiwa nimeshatafakari mambo mengi kuhusiana na hali hii, nikawa nimejiweka vizuri kiakili ili nifanye jambo fulani ambalo lingesaidia kurudisha haki ya kilichompata Joy. Siyo kwamba labda nilijiona kuwa na hatia sana ama kama mpelelezi mahiri mno, hapana, bali ikiwa kama ni kweli mke wake Chalii Gonga ndiye aliyekuwa amehusika na suala hilo, nisingemwacha salama. Ningehakikisha analipia.


★★★


Asubuhi ikafika. Niliamshwa mapema kwa sababu ya simu yangu kuita mara kadhaa, na baada ya kuichukua nikaona mpigaji kuwa Tesha. Baada ya kupokea, jamaa akaniuliza ni muda upi tungeenda pamoja na Mariam kumwona daktari huko hospitali, akisema kuwa dada yake alimwambia kuhusu suala hilo, na wakati huu Miryam alikuwa anamwandaa Mariam kwa ajili ya kwenda huko. Nikamwambia ni muda siyo mrefu ningefika hapo kwao ili tushughulike na jambo hilo, naye akakubali.

Kwa hiyo nikaamka na kuanza kufanya maandalizi. Nikaoga, nikavaa vizuri, hii ikiwa ni saa tatu kasoro, na mwenye nyumba wangu alikuwa chumbani kwake tu mpaka wakati ambao nilikuwa nimemaliza kuuweka mwili wangu safi.

Nikaona niende huko chumbani kwake kumwona, nami nikamkuta amejilaza tu kitandani kwake huku akionekana kuchat kwenye simu ama kusoma; alijua yeye. Nilielewa kwamba tayari alijua nimeingia, lakini hakuniangalia hata mara moja, akionekana kuwa makini kweli, nami nikamsemesha.

"Ankia... umeamkaje?"

Akanitazama usoni, naye akasema, "Kawaida tu. Unataka kutoka?"

"Ndiyo."

"Sawa. Nisamehe sija... sijachemsha chai...."

"Usijali, we' pumzika mpaka utakapojisikia kunyanyuka," nikamwambia.

"Unaenda wapi?"

"Natoka na Tesha kumpeleka Mamu hospitali," nikamjulisha.

"Aaa... sawa."

"Na wewe? Umepanga kwenda msibani mida gani?"

"Baadaye. Si na wewe utakuja?"

"Ndiyo, nafikiri Tesha ata...."

Kabla sijamaliza kumjibu, simu yangu ikaanza kuita, nami nikaitoa na kuangalia mpigaji kukuta ni Chalii Gonga. Nikakaza macho kwa umakini.

"Vipi?" Ankia akauliza.

Nikamwangalia na kusema, "Ee... labda nitakuja na Tesha. Tukishatoka hospitali. Sipajui kwo' kuja naye lazima... ngoja nipokee simu," nikamwambia hivyo.

Akatikisa kichwa kukubali, nami nikatoka chumbani hapo na kusogea mpaka kufikia mlango wa kuingilia sebuleni. Mawazo yakiwa ni mengi kichwani kutokana na kujua mambo mazito yaliyokuwa nyuma ya mtu huyu aliyenipigia, nikapokea na kuiweka sikioni.

"Oya dogo langu..." sauti ya Chalii Gonga ikasikika.

"Naam kaka..." nikaitika.

"Mbona nakutafuta sana lakini unanikaushia?"

"Mambo mengi tu. Vipi kwani?"

"Umesikia kilichompata Joy jana?"

"Ndiyo nimesikia."

"Unaweza kuniambia nini kinaendelea?" akaniuliza hivyo.

Nikakunja uso kimaswali kiasi na kusema, "Kwa nini uniulize mimi hivyo?"

"Nimeuliza tu... labda ukawa unajua kitu fulani..."

"Ah... sijui. Hilo jibu linatosha au?"

"Mhm... usipandishe jazba mdogo wangu..."

"Sijapandisha jazba. Ongea point yako," nikamwambia hivyo kwa sauti makini.

"Nimeanza kusikia Joy kapigwa hiyo juzi. Sijui unanielewa? Na alipopigwa, mtu wa kwanza kupigiwa ilikuwa wewe. Nataka kujua alitaka nini kutoka kwako... ama labda na wewe pia ulihusika kwenye hiyo ishu," akaniambia hivyo.

"Ishu gani? Kumpiga? Kwa nini nimpige Joy?"

"Ndiyo uniambie..."

"Nisikilize Chalii. Wewe si una watu wako? Fanya utafiti mwenyewe uujue ukweli, sawa? Kama unafikiri mimi ndiyo nimemuua Joy, thibitisha, halafu uje kwangu umlipizie kisasi. Sawa?"

"Mbona unaenda mbali sana? Mimi nataka tu kujua ukweli..."

"Ndiyo maana nimekwambia fanya uchunguzi. Ukikuta nimehusika... nifanye chochote unachotaka. Si alikuwa mtu wako? Utaamua mwenyewe cha kufanya. Nimemaliza. Kuna kingine?" nikamwambia hivyo kwa ujasiri.

Akacheka tu na kusema, "Usijali. Uchunguzi nafanya. Sikutaka kuamini ni wewe ndiyo umemuua Joy, ila nikikuta ni wewe... utajuta mdogo wangu."

"Ah... utajua mwenyewe. Hivyo vitisho vyote ungevitunza kwa ajili ya wahusika halisi na si mimi Chalii. Hapa unapoteza tu muda wako... na naomba usinisumbue tena," nikamwambia hivyo kwa kukereka.

Kabla hajasema lolote tena, nikakata simu na kushusha pumzi kwa nguvu. Kuna mtu aliyekuwa anazungusha mchezo huu wa mauaji ya Joy kunielekea mimi, na tayari nilijua huyo kuwa mke wake Chalii.

Hako kajinga kalikuwa kanataka kuniharibia wakati wangu mzuri niliokuwa nimekuja kujijengea huku, na kitendo cha Chalii Gonga kunipigia wakati huu na kuanza kutema vitisho ndiyo kilichochea kuni za moto kwenye nia yangu ya kutaka kupambana nao na kuwaangusha. Wote kwa pamoja walikuwa wameshanigeuza mimi kuwa adui yao, na ningewaonyesha urafiki mzuri wa kuwa adui yangu.

Nikaweka suala hilo pembeni na kutafuta namba za daktari fulani pale Muhimbili, kisha nikampigia na yeye akapokea. Daktari huyu alibobea kwenye masuala ya maendeleo na ukuzi wa ubongo, hivyo alikuwa ni mtaalamu wa mambo mengi yaliyohusisha kichwa. Tulijuana sana na ni moja ya walimu niliowahi kuwa chini yao wakati ndiyo niko kwenye mbio za kuwa daktari rasmi hospitalini pale (tunaita internship).

Nikamwambia kuhusu ishu ya Mariam, nikimwomba nafasi ya kuonana naye kwa asubuhi hii ili anipatie ushauri mzuri kuhusu hali ya "mdogo wangu," naye akaridhia. Akaniambia niende tu na nikifika nimjulishe hasa kama nisingemkuta kwenye ofisi yake, nami nikamshukuru kwa hilo. Oh na ni mhindi, kwa hiyo maongezi yetu yalibeba kimombo sanasana!

Nikaweka simu mfukoni baada ya kumalizana naye, nami nikaelekea nyumbani kwao Tesha. Sikuwa hata nimempa Ankia kwa heri nyingine tena maana nilihisi kuvurugwa kiakili kiasi, na baada ya kufika getini pale, nikaligonga na kusubiri lifunguliwe.

Dakika moja nyingi nalo likawa limefunguliwa, na sikuwa nimetarajia mfunguaji awe bibie Miryam mwenyewe. Nikatoa tabasamu hafifu kama kumpa salamu, naye akawa ananiangalia kama vile anasubiria niseme kitu fulani. Nikampa hilo.

"Za asubuhi dada?" nikamsalimu.

"Nzuri. Karibu," akaniitikia na kuachia uwazi zaidi ili niingie.

Nikapita na kuingia sehemu hiyo ya ndani ila nje ya nyumba yao, na nilikuta mama mkubwa mweusi, Bi Jamila, akiwa ameshikilia mpira mrefu wa maji uliounganishwa kwenye bomba hapo nje, akimwangalia maua yaliyotunzwa kwenye vyombo kuzungukia nyumba yao.

Mwonekano wa Miryam uliniambia kwamba bado, ama labda hakuwa na mpango wa kwenda kazini kwa leo, kwa sababu alikuwa ndani ya T-shirt nyeusi yenye mikono mifupi pamoja na khanga kutokea kiunoni, na nywele zake hakuwa amezitengeneza vizuri kimtoko; zikiwa na mvurugo kiasi wa kazi za asubuhi nadhani.

Nikasimama usawa wa gari lake na kumwamkia Bi Jamila. "Mama shikamoo?"

Akaniangalia na kuitikia, "Marahaba baba. Hujambo?"

"Sijambo. Naona unawaogesha watoto," nikamjibu.

Akacheka na kusema, "Ee wanangu hawa wanapenda kweli maji, kila asubuhi na jioni lazima waoge."

"Ni vyema. Hapo lazima wanenepe mno," nikamwambia kiutani.

Alipotabasamu kidogo, nikamwangalia Miryam na kukuta ananitazama kwa yale macho yake yenye udadisi fulani hivi, nami nikashindwa kujizuia kutabasamu na kuangalia chini. Hata sikujua sababu ni nini!

"Nini?" akaniuliza hivyo.

Nikatikisa kichwa kuonyesha kwamba hamna kitu, nami nikamtazama machoni kwa mara nyingine.

"Ingia ndani. Mariam yuko tayari ila anapaswa anywe chai kwanza. Tesha ndiyo bado hata hajaoga," Miryam akasema hivyo.

"Dah! Halafu kameniwahisha kweli, kumbe bado hata hajaamka!" nikasema hivyo kiutani.

"Nini? Nani?" akaniuliza hivyo.

"Mdogo wako, tumeongea muda si mrefu, nikadhani na yeye alikuwa tayari tayari. Kwa hiyo nakaa kuwasubiri," nikasema hivyo.

"Yeah... au unapotezewa wakati?"

"Hapana. Nataka nitumie muda wangu wote nitakaokuwa hapa kumsaidia Mamu... kwa hiyo yeye ndiyo mmiliki wa wakati wangu," nikamwambia hivyo.

Itikio alilotoa baada ya mimi kusema hivyo lilikuwa kunishusha na kunipandisha mara moja kama vile anajaribu kunisoma, nami nikatabasamu kidogo.

"Mbona unaniangalia hivyo?" nikamuuliza.

Akaachia tabasamu hafifu la kuhukumu fulani hivi, naye akanipita na kuanza kuelekea ndani ya nyumba. Nikajizuia kutotabasamu zaidi kwa sababu ni wazi kwamba mwanamke huyu bado aliniona kuwa mtu asiyeeleweka, labda sijatulia kiakili, huenda akiniona kama Tesha vile, na mimi nikaridhia tu kuwa angalau mambo baina yetu yalikuwa sawa.

Nikaingia ndani kwao na kumkuta Mariam, akiwa amekaa upande wa dining, na akipata kiamsha kinywa pamoja na Bi Zawadi. Mwanamama huyo akanisalimu kwa uchangamfu wake na kunikaribisha ninywe chai, nami nikashukuru na kusema nilikuwa sawa kabisa, kisha nikakaa sofani kumsubiri binti.

Miryam alikuwa ameenda chumbani nadhani, na hakutoka tena tokea aliponikaribisha ndani hapo. Tesha akaja kutokea upande wa bafuni, akiwa amevaa pensi ya kijani pekee, huku mwili wake ukionekana kulowana. Bila shaka ndiyo alikuwa ametoka kuoga, nasi tukasalimiana vizuri na jamaa kwenda chumbani kwake kuvaa nguo ili tuondoke.

Nilikuwa nikipata mazungumzo mawili matatu pamoja na Bi Zawadi kuhusiana na masuala ya dawa za kienyeji na za hospitali, na mwanamke huyo alionekana kupenda sana matumizi ya dawa za kienyeji zaidi ya za hospitali kwa jinsi alivyozisifia.

Nilimtazama Mariam kwa usomi mwingi alipokuwa akila, nikiona jinsi alivyofurahia kupata chakula kwa njia kama ya mtoto mdogo. Akawa ameshiba, Bi Zawadi akamsaidia kunawa, kisha wakaja upande wa masofa hapo sebuleni na kukaa.

Binti alikuwa akionyeshwa mimi ili anisalimie, lakini akawa anaangalia chini tu kama hataki. Nilielewa kwamba bado hakuwa amejenga uzoefu kwangu, na njia ya kwanza ya kufanikisha kumsaidia vizuri ingenihitaji nijenge mazoea naye ili akishaweza kujiachia zaidi kwangu, ndiyo nianze kumwekea tiba akilini.

Wakati ambao Bi Jamila ndiyo alikuwa amerudi kutoka kumwagilia maua yake, Tesha naye akawa ametoka chumbani, akiwa amevaa vizuri sana, naye akamwita dada mkubwa ili apewe funguo za gari. Nikamwambia isingekuwa mbaya tukichukua usafiri tu maana bila shaka Miryam angehitaji gari kwenda kazini, lakini akasema ni yeye Miryam mwenyewe ndiye aliyetaka tuchukue pickup yake ili twende hospitali na Mariam akiwa ndani ya gari lisilo na purukushani nyingi. Upendo wa dada.

Kweli Miryam akawa ametoka na kumpa Tesha funguo, naye akamsihi mdogo wake awe makini sana na Mariam mpaka tutakaporudi. Nikamuuliza Miryam angekwendaje kazini, naye akasema angechukua usafiri. Basi kwa kuwa mambo yalionekana kunyooka kwa sehemu hiyo, tukatoka kwa pamoja, Mariam akaingia siti za nyuma ya gari, Miryam akafungua geti, nasi tukaingia mbele ya gari na Tesha kulitoa nje.

Niliona jinsi gani Mariam alimpenda sana dada yake, kwa kuwa aliweka uso wake kwenye kioo huku akimtazama sana huko nje kana kwamba ni mtoto asiyetaka kumwacha mama yake, nami nikaweka hilo akilini ili nije kulitumia katika msaada niliotaka kumpatia. Kila jambo lingekwenda taratibu tu mpaka ningehakikisha huyu binti amekaa sawa tena.

★★

Vuuu, mwendoni kuelekea hospitali. Gari hili lilikuwa modeli ya zamani ya manual kwa hiyo kulikuwa na gia ya kusukuma na kurudisha nyuma karibia kila dakika, na Tesha alitia mbwembwe kweli kwenye kuendesha ili kunionyesha kwamba alijua sana. Na alijua. Alikuwa dereva mzuri.

Nikamwangalia Mariam nyuma na kumwona akiwa ameshika simu ya Tesha akitazama katuni ambazo kaka yake alimwekea ili binti atulie, nami nikamtazama rafiki yangu.

"Oya unaona navyoweka vitu hapa?" akaniambia hivyo kwa kujisifu.

"Naona. Miryam ndiyo alikufundisha kuendesha?" nikamuuliza.

"Hamna, nimejifunzia Arusha. Miezi miwili tu Veta nikatoka nimeiva," akasema.

"Aaa sawa."

"Na wewe mtoto wa kishua? Unajua kuendesha?"

"Ahahah... ndiyo, najua."

"Ulijfunzia chuo gani?"

"Hamna, me sikujifunzia Veta wala popote. Nilichukua tu gari la mtu nikaanza kuendesha mwenyewe mpaka nikaweza..."

"Aa wewe... unazingua..."

"Kweli tena."

"Una leseni?"

"Ee."

"Uliitolea wapi sasa kama hukwenda chuo?"

"Ahahahah... shortcut tu. Yaani me nimeweza gari mdogo, nilipofika legal age nikamtafuta askari mmoja wa usalama barabarani... hadi nilishamsahau jina ila, yaani, yule ulikuwa unampa hela tu anaenda anakutengenezea leseni, fwii unaingia barabarani," nikamwambia.

"Kweli eh? Nishagasikia wanafanya hivyo ila siku hizi sidhani sana maana kuna kushikwa kwingi..."

"Ee, ndiyo hivyo. Me nilipita nayo namna hiyo."

"Ulikuwa unatoa shi'ngapi?"

"Kwa ajili ya leseni? Laki tatu tu."

"Laki tatu tu, au siyo? Kama buku tatu yaani..."

"Wee, nilihangaika kuipata! Hata kipindi hicho mambo hayakuwa easy sema ukishajuana tu na watu si unajua vichochoro vinajinyoosha..."

"Ahehehe... mwana me napenda sana hizi manual. Kucheza hapa mbele nakubali mno, yaani auto zinakera, unaweza hata ukanyoosha miguu hapa juu maana nyepesi mno," aksema hivyo.

"Na dada yako anapenda za hivi eh?"

"Da' Mimi? Sijui sana. Hii ni ya kuenzi tu unajua? Angeweza hata kuiuza na kuchukua nyingine ila anapenda mno kutunza kumbukumbu," akaniambia hivyo.

"Unamaanisha nini?" nikamuuliza.

"Hili lilikuwa gari la baba," akaniambia hivyo.

"Aaa..."

"Eee, walikuwa tight sana na da' Mimi."

"Sawa. Inaonekana ya zamani, lakini anajua kutunza."

"Ina muda. Sema mzee alipoenda, Miryam akaichukua. Sa' siunajua ye' mrembo kwa hiyo na gari lazima itarembwa tu hata kama ishazeeka," akasema hivyo.

Nikacheka na kumwambia, "Kweli. Hivi... yule jamaa, Joshua, umeshamwona tena?"

"Toka walipomwachia? Sijamwona. Wa kazi gani kwanza? Akae huko huko, next time akileta bangi zake nitamtoboa kabisa..."

Nilikuwa nimekumbuka namna ambavyo huyo Joshua alimtukana Miryam siku ile kuhusu mwanamke huyo kutumia gari hili aliloliona kuwa la kizee, na sasa baada ya mimi kuelewa kwa nini mwanamke huyo alilitumia, kweli kashfa za jamaa zilizidi kuonekana kuwa mbaya sana.

Lakini kitendo cha kumwona jana ofisini kwake Miryam akijionyesha kuwa mtakatifu na sasa Tesha kuonekana hajui kuhusiana na hilo, kilifanya nielewe kwamba kuna jambo lililokuwa likiendelea ambalo kijana huyu, labda na familia yao wote kwa ujumla, walifichwa kwanza, kwa hiyo nikaona nisimwambie kuhusiana nalo. Bila shaka dada yake alikuwa anapanga mambo fulani bila kuwaambia wengine, ama huyo Joshua alijipeleka huko kazini kwa Miryam yeye mwenyewe. Ningeona.

"Tuachane na habari za huyo mjinga. Oya, hivi... hii ishu ya Joy mwanangu unaionaje?" akaniuliza hivyo.

Nikawa makini zaidi na kusema, "Iko hivyo tu. Kauliwa... labda shauri ya yale mambo uliyoniambia."

"Yale yake na Chalii Gonga, au ile ishu nyingine?"

"Ishu gani?"

"Acha kujitoa akili JC. Mke wake Chalii si kakuita ile juzi kukutisha eti atafanya kitu kibaya, halafu kweli kimetokea. Hujahisi labda ni yeye?"

Nikamwangalia Tesha. Kijana alikuwa na akili nyepesi, lakini nikamwambia, "Huwezi kuwa na uhakika. Labda tu tuyaache jinsi yalivyo."

"Dah! Me naacha kwenda Masai kwa wiki kabisa. Nisije kujikuta naamkia motoni kesho tu. Sijasema mbinguni maana najua nishakataliwa huko," akasema hivyo

Nikacheka kidogo na kusema, "Kweli kaka, hilo ndiyo la muhimu kufanya. Jiweke kushoto kabisa."

"Fact," akasema hivyo.

Mawazo yake Tesha kuhusiana na jambo hilo yalifanana na ya kwangu, lakini sikutaka kuchangia sana upande wa mawazo yangu kwa sababu sikuhitaji kijana huyu avutwe kiundani zaidi kwa yale niliyofikiria kufanya. Ndiyo, bado nilikuwa na mpango wa kumtafutia haki Joy endapo kama kweli mke wake Chalii alihusika na kifo chake, lakini nilitaka Tesha akae pembeni kabisa na suala hili. Ingekuwa bora kwa ajili yake.

★★

Kwa hiyo mwendo wa kupita robo tatu ya saa kuelekea Muhimbili ukatufikisha hospitalini huko, nasi tukaelekea majengoni baada ya kuegesha gari. Sikudhani ningekuja kurudi hospitalini hapa mapema namna hiyo, yaani baada ya kuingia tu kwenye siku za likizo, lakini Mariam aliustahili umuhimu wa kilichofanya nirudi tena hapa.

Kwa kuwa tayari nilikuwa nimeshawasiliana na yule daktari, nikampigia simu tena kumjulisha kwamba tulikuwa tumefika, lakini hakupokea. Ah nikaona tu nitulie mpaka tukifika ofisini kwake, labda kwa sasa alikuwa bize kidogo. Lakini hazijapita sekunde nyingi akawa amenipigia na kusema kwamba niende tu moja kwa moja mpaka ofisini kwake, alikuwepo huko, maana hakusahau kuhusu ujio wangu. Hiyo ikawa imeenda!

Tulipita majengo ya chuo cha Muhimbili na aisee! Watoto! Kuna wanawake warembo ukanda huo wa wanavyuo mpaka Tesha alikuwa anashindwa kujizuia kuwaangalia. Hasa wale weupe wavaa shungi! Lakini hakuonekana kuwa na shobo za kishamba kama wanaume wengine wanavyokuwaga, na kwa hilo nilimkubali sana.

Ujio wangu kwa sehemu hiyo kama kawaida ulivuta macho ya baadhi ya watu walionifahamu na wasionifahamu, na wale walionijua wangenipa salamu kwa kupunga mikono na mimi pia kuwarudishia.

Mariam alikuwa amependezeshwa kiasi na dada yake isingekuwa rahisi kwa yeyote aliyemwona kwa mara ya kwanza kudhani ana tatizo kwenye akili yake. Alitembea kwa ukaribu sana na Tesha, akiung'ang'ania mkono wake ili asijikute anapotea kwenye mazingira hayo mapya kwake, na kwa kweli hiyo ilionyesha kwamba alijua dunia ni mbaya, na si kila mtu angepaswa kumwamini zaidi ya yule aliyejua angeweza kumwamini.

Kwa hiyo tukasonga mbele zaidi, tukipita majengo ya kantini, majengo ya vyumba vya madaktari, mpaka kufikia upande wa hospitali yenyewe. Kama kawaida watu walikuwa ni wengi, na kama isingekuwa ya mimi kuja na ndugu hawa basi wangekaa mno kusubiri, lakini nikawapeleka moja kwa moja mpaka kwenye ofisi ya yule daktari na kusimama nje ya mlango wa kuingilia ndani hapo.

Nikawaomba wanisubiri kwanza, kisha nikaingia na kumkuta daktari huyo akiwa na mgonjwa mwingine hapo. Alionekana kumjazia ripoti fulani, na baada ya kuniona, akatabasamu kiasi na kunisalimu. Nikamsalimu pia pamoja na huyo mgonjwa, kisha nikasimama pembeni kusubiri.

Daktari huyu aliitwa Roshan Sotto, naye alikuwa mtu mzima karibu kufikia kama miaka 60 hivi. Alipomaliza kuandika ripoti ya mgonjwa wake, akampa maelekezo fulani, kisha mgonjwa huyo akaipokea karatasi na kunyanyuka ili aondoke. Alipotoka ndiyo nikapata sasa nafasi ya kuongea na daktari mwenzangu, akiuliza naendelea vipi huko nilikokuwa nimeenda.

Mimi nikamwambia niliendelea vizuri tu, naye akasema kiukweli nilikuwa nimetia pengo fulani hapo hospitalini kwa kuondoka, akinitania ni namna gani muuguzi mmoja wa kike hapo hospitalini aliyeitwa Latifah alivyonitafuta sana. Si unajua sikuzote lazima uwe na yule mtu anayekupenda sana kazini mpaka unabambikiziwa ndoa ya kiutani pamoja naye? Ndiyo alikuwa huyo Latifah sasa.

Karibia kila mtu aliyenifahamu hapa hospitali aliniita mimi na Latifah mume na mke. Tulizoewa namna hiyo. Kwa hiyo daktari Roshan aliponikumbusha kumhusu, nikacheka sana na kumwambia kwamba nilijitahidi kuingia tena huku kisiri ili asinione maana kama angeniona ndiyo angening'ang'ania mpaka basi.

Baada ya kuweka utani pembeni, daktari mwenzangu akaniambia sasa nimlete mgonjwa wangu ili amcheki haraka, nami nikamfata Tesha na Mariam pale nje. Wakaingia na kukaa kwenye viti kutazamana na daktari Roshan, mimi nikiwa nimesimama, na baada ya utambulisho wa ndugu hawa wawili, Tesha akaombwa aelezee hali ya mdogo wake ilikuwa vipi. Akaeleza kila kitu kwa namna nilivyofahamu pia, naye daktari Roshan akajaribu kumsemesha Mariam.

Binti hakujibu hata mara moja, nami nikamwambia daktari kwamba kutokana na namna ya Mariam ya kuitikia kwa vitu fulani na dalili kadhaa alizozionyesha, nilifikiri alikuwa na tatizo lililofanana na ASD, na ndiyo nilikuwa nimekuja kupata uhakika kutoka kwake ili apendekeze tiba sahihi zaidi ya kumpa. Na nilikuwa natumia kiingereza.

Daktari Roshan akanyanyuka, akafata kifaa fulani cha kielektroni kwenye chumba cha pembeni ndani humo humo na kumfata Mariam, kisha akamvalisha kichwani na kuanza kusoma namba-namba na maherufi-herufi. Alikuwa akimpima, na baada ya kumaliza, akamtolea na kurudi kukaa kwenye kiti chake.

Akamuuliza Tesha, "Huyu mdogo wako, amekuwa hivyo kwa muda gani?"

Tesha akasema, "Ni... miaka kama mitatu na miezi kadhaa. Inaelekea miaka minne."

Daktari Roshan akasema, "Sawa. Sasa ni hivi... aam, utasamehe na Kiswahili changu, ila si kibaya sana..."

Nikatabasamu kidogo, naye Tesha akasema, "Haina shida doctor."

"Her brain isn't damaged... aah... ubongo wa Mariam uko sawa... kabisa, hakukuwa na kitu kama... uvimbe au shimo dogo kutokana na ugonjwa, ama accident... ajali, kwa hiyo bila shaka... alikuwa na tatizo kwenye... mishipa midogo iliyosawazisha taarifa kwenye ubongo wake..." daktari akaelezea.

Aliongea kwa kutumia kauli za wakati uliopita lakini sote tulielewa alimaanishia wakati huu aliotoka kumpima binti, na alielekeza maneno hayo kwangu. Nikatikisa kichwa kuonyesha uelewa.

Akaendelea. "Yaani... kwa wakati huu mishipa hiyo haikuweza kusawazisha... vizuri... taarifa mbalimbali ubongoni mwake, na... ni kweli... tatizo lililompata lilifanana na ASD."

"ASD ndiyo nini? Au... utanielezea baadaye JC?" Tesha akaniuliza.

"Yeah, nitakwambia. Ngoja nimuulize kuhusu tiba. Kwa hiyo doctor Rosh... what approach should be taken towards her treatment?" nikasema hivyo.

"It depends. Matibabu kwa ajili ya ugonjwa... wa ASD, yanalenga kupunguza... dalili zilizoingilia utaratibu mzuri wa kuishi au kutenda kwa njia kawaida... mtu aliyeathiriwa. ASD inawapata na... kuwaathiri watu... kwa njia tofauti, hiyo ilimaanisha kwamba waathiriwa hawawezi kuonyesha dalili zilezile... so... na njia za kuwatibu... haziwezi kufanana. Unaelewa... Tesha?" daktari Roshan akamuuliza hivyo.

"Ndiyo doctor," Tesha akajibu.

"Yes. Matibabu hayo ya ndani... tabia, maendeleo ya kiakili, kielimu, psychology, mazungumzo, na vitendo. Yanaweza kumix kwa... kwa pamoja... ama kukazia fikira kimoja tu kati ya hayo, ikitegemea na hali ya mwathiriwa. Kwa hiyo cha msingi kufanya kwa ajili ya binti huyo... ingekuwa kuangalia nini... kinavuta zaidi akili yake, kisha kutafuta njia za kumfanya akaze fikira... zake... kuzungukia kitu hicho... au vitu hivyo, ili ubongo wake... urudi kwenye ukuzi mzuri wa awali..."

Ah, blah blah blah kutoka kwa daktari mwenzangu zilikuwa nyingi sana, lakini nilielewa zaidi sasa kwamba Mariam angehitaji vitu viwili tu kwenye jambo moja; michezo ya kiakili, na mafundisho ndani ya hiyo hiyo michezo ya kiakili. Ningeweza kujua tayari alipenda mambo yapi yaliyoichezesha vyema akili yake, kwa hiyo ningeyatumia hayo hayo kwa njia ya kidaktari zaidi ili akili yake itiki.

Daktari Roshan alieleza kwamba kwa jinsi hali yake Mariam ilivyokuwa, angehitaji msaada wa kitaalamu kutoka kwa wataalamu ambao wangemwangalia kwa ukaribu. Hii ingemaanisha akae sehemu fulani hususa mbali na kwao, kama tu wodi za vichaa, lakini ya peke yake, na nilijua hiki ni kitu ambacho dada yake asingekubaliana nacho; achilia mbali tu na gharama ambazo zingehitajika kuwalipa wataalamu hao.

Kwa hiyo nikiwa na uhakika wa mambo ya kufanya sasa kutokea hapo, nikamshukuru tu daktari huyu na kumwambia tungeshughulika vyema kumpatia msaada binti huyo ili kusaidia hali yake irudi kuwa sawa tena, nasi tukamuaga upesi ili aweze kuangalia mahitaji ya wagonjwa wengine waliokuwa wakimsubiri.

Hivyo tukaondoka hatimaye sehemu hiyo ya hospitali, ikiwa ni mida ya saa sita kasoro sasa, nami nikawa natembea pamoja na ndugu hawa wawili kuelekea nje huku nikimwelezea Tesha vitu alivyotaka kujua.

Tesha kiukweli bado alikuwa haamini-amini ikiwa mimi nilikuwa daktari, maana aliniona kuwa wa aina ya kihuni zaidi, lakini nikamwambia hata madaktari huwa wana maisha mengine bwana. Na mimi nilikuwa nimeishi maisha mengi. Kwa hiyo baada ya kuwa ameelewa vizuri hali ya mdogo wake, akasema angesaidia pia katika chochote ambacho ningefanya kuipa akili ya Mariam "boost," yaani kuibustisha.

Nikawaongoza ndugu hawa wawili kuelekea kwenye jengo la maabara moja hospitalini hapo, nami nikamwomba Tesha anisubirie nje kwa ufupi tulipofikia mlango wa kuingilia ndani hapo. Nikaingia maabarani, kukiwa na vifaa vingi vya matumizi ya vipimo vya masuala ya kisayansi, nami nikamkuta mwangalizi wa sehemu hiyo ambaye ndiyo nilikuwa na lengo la kumwona.

Huyu hakuwa mwingine ila mwanadada Latifah, mke wangu wa hospitali. Yeye ndiyo alikuwa msimamizi kwa sehemu hii na kwa sababu nilikuwa na nia ya kupata vitu fulani kutoka kwenye maabara hii, kuonana naye ilikuwa lazima. Kama ingekuwa ni ndani ya uwezo wangu basi ningefanya kila kitu kumkwepa kabisa maana nilijua kama angeniona ndiyo angening'ang'ania mno, na sikuwa nimekosea.

Aliponiona tu ndani hapo, akaacha mambo aliyokuwa anafanya na kunifata kwa kasi huku akifurahi mno, naye akanikumbatia. Alikuwa mweusi wa maji ya kunde, mwembamba kiasi na mwenye miguu mirefu iliyoupa mwili wake umbo la umiss maridadi. Alikuwa na midomo minene na mizito kama vile iko tayari kudondosha udende muda wowote.

Ijapokuwa tulikuwa tumebambikiziwa ndoa ya kiutani hapa hospitalini, mimi na Latifah tulikuwa tumeshafanya michezo mingi sana kwa sababu alinielewa mno. Kwa wengine tulijionyesha kuwa wapenzi wa kikazi tu, lakini nilikuwa nimeshampigisha kazi nyingi sana huyu mwanamke kiasi kwamba alitamani hata nimuoe!

Kwa hiyo hata na hapa akaanza kudeka kwangu, akisema amenimiss, akiniambia mimi mbaya, nimeondoka bila kumuaga ili nimkimbie na niende kwa wanawake wengine. Nikamwambia hapana, ni mambo mengi tu yalikuwa yameingiliana na hata laini ya mtandao niliyokuwa natumia kuwasiliana naye awali ilikuwa imepotea kwa hiyo namba yake ilipotea pia nilipoingia likizo, lakini nilimmiss pia ndiyo maana nikaja wakati huu. Hizo zote zilikuwa fix tu.

Tukajuliana hali, kisha nikamweleza lengo langu la kuja hapo. Nilihitaji vifaa vichache vya maabara pamoja na kemikali kiasi za kugawanyisha virutubisho vya madawa, naye akaniuliza vya kazi gani. Nikamwambia kuna dawa nilikuwa nataka kutengeneza, na singechukua muda mrefu sana na vifaa hivyo ningevirudisha.

Akakubali ila akaniomba nimjali kidogo kwanza, unaelewa, lakini nikamwambia haingewezekana maana kuna Serikali ilikuwa inanisubiri hapo nje, lakini akasisitiza tu na kutaka kunibusu mdomoni. Nikamzuia, nikimkumbusha kwamba kuna CCTV camera humo, lakini akaendelea kufosi.

Alikuwa mkaidi kweli, lakini mara zote alipoona niko makini alitulia, na mimi nikamwonyesha kweli kwamba sikuwa na muda wa kufanya kile alichokuwa anakitaka. Nikamwambia kama hataki kunipa basi tu mimi niondoke, ndiyo akashusha makeke na kunituliza. Akanifatia vifaa hivyo, naye akaniwekea kwenye mfuko na kuniletea.

Latifah alikuwa mwanamke aliyezoea watu upesi sana na hapa hospitali alipendwa mno mpaka na wasimamizi wa majuu kutokana na utu wake wa kirafiki, kwa hiyo alijiachia sana kwa mambo mengi aliyofanya japo si kwamba alikuwa binti mapepe. Nasema hivyo kwa kuwa baada ya yeye kunipa vitu nilivyohitaji, akaanza kunipiga busu mdomoni bila kujali uwepo wa CCTV camera, nami nikamwambia awe makini asije kusababisha akajikuta anafutwa kazi kwa sababu ya kuchanganya kazi na starehe.

Akasema hiyo haiwezi tokea kamwe, naye akaniomba namba zangu za sasa ili tuanze kuwasiliana tena. Wala hata sikuwa nimepoteza laini na chochote bali nilikuwa nimempiga tu block ili wakati wa likizo uwe wa mambo mengine, lakini sasa nikawa sina jinsi. Nikampa namba ya laini nyingine, kisha ndiyo nikamuaga na kurudi kwa wenzangu.

Tesha na mdogo wake walikuwa wamesimama kwenye kingo ya pembeni karibu na ngome zilizoshika ukuta, nami nikamwambia nilikuwa nimepata nilivyovitaka kwa hiyo tuondoke hapo hatimaye. Hakuwa na habari yoyote kuhusu mimi kukutana na mke wangu wa kubambikiziwa, nasi tukaendelea tu kuongelea mambo mengine kadiri tulivyoelekea upande wa kutokea kwenye hospitali.

Tulipokuwa tumefika eneo lenye zile kantini, nikawaongoza ndugu hawa kwenye kantini moja ili tupate chakula chepesi. Nilihisi njaa kiasi na hata Tesha hakuwa amekunywa chai pia, kwa hiyo nikaagiza na kuwaagizia ndugu hawa msosi mtamu, nasi tukala kwa pamoja.

Kila mara ambayo Tesha angeona pisi kali zilizoelekeza umakini wao kwetu, angenibonyeza ili kunionyeshea bila yeye kufanya ionekane wazi kwamba ameukamata umakini wao, nasi tungeongea mengi kuhusiana na namna ambavyo wanawake wa chuo waliishi kihalisi tofauti na jinsi ilivyookekana waliishi. Wanaojua maisha yao wanaelewa, hata mimi niliyaona pia!

Mariam alipenda sana vyakula vitamu kama chips mayai na kuku, na alikula bila kujali nani anamwangalia. Midomo yake iling'aa mafuta kumfanya Tesha amfute kila dakika kwa tishu, na nilipenda sana kautoto alikokuwa nako huyo mwanadada. Ila ndiyo ningepaswa kumsaidia kukaondoa ili kasiteke maisha yake yote mpaka mwisho.

★★

Tulipomaliza kula na kujisafisha, tukaondoka hospitalini hapo hatimaye. Mwendo ungekuwa mmoja tu wa kuturudisha nyumbani ili Mariam akapumzike, na Tesha alikuwa analalama kuhusu kuondoka bila namba ya pisi yeyote wa hapo Muhimbili. Nikamwambia wa huko wangemsumbua tu kwa kumnyonya mno hela mpaka angekauka.

Lakini malalamiko yake ya kutaka pisi kali yakanifanya nikumbuke kitu fulani. Winny. Mmoja wa wale wadada niliokutana nao kwenye bajaji jana. Na nilikuwa nimemsahau kabisa maana mambo mengi yalikuwa yameingiliana. Nikamwambia Tesha kuhusu mwanamke huyo, nikisema ni mzuri na nilichukua namba yake.

Masikio yakamsimama jamaa akinitaka nimpatie, lakini nikamwambia atulie kwanza; mpaka nimtafute Winny mwenyewe, nimpange kuhusu rafiki yangu, halafu ikiwezekana niwakutanishe. Jamaa akakubali hilo huku akitaka nimhakikishie kwamba kweli huyo mwanamke alikuwa mzuri, nami nikamwambia nisingechukua namba yake endapo kama angekuwa wa ovyo.

Tukiwa tumekaribia kuifikia Mbagala, simu yangu ikaanza kuita. Mpigaji? Soraya. Tabasamu hafifu likaniponyoka, na sikuwa na mpango bado wa kumwambia Tesha lolote kuhusu mimi na yule mwanamke, lakini jicho la mwewe la jamaa likaona jina la huyo Mamacita hapo akinipigia, naye akaanza kunisema sasa.

Nikamwambia acha zako wewe, huyu anapiga kunisalimia tu, nami nikapokea na kumsikiliza mtoto mzuri. Alinijulia hali, akaniambia yuko kazini, na alitaka tuje tukutane tena. Yaani leo leo, maana kama tu msemo aliokuwa ametumia jana, ni kwamba bado "aliwashwa."

Sikujibu kauli zake za kimapenzi moja kwa moja, lakini kitendo cha mimi kusema kwa leo haitawezekana maana nilibanwa na mambo mengi, kikafanya Tesha ashtukie dili. Nikamwambia tu Soraya ningemtafuta baadaye maana hapa nilikuwa na mpango wa kuelekea kwenye msiba wa rafiki, naye akaridhia. Na alikuwa anataka kweli tuonane huyo mwanamke, lakini mie wala sikuwa na presha.

Baada ya mazungumzo pamoja na Soraya, Tesha akaanza kunichokoza sasa. Alitaka kujua. Ajue, ajue, ajue! Nikamwambia dogo tulia, Soraya anataka tu tuelekee kule kwenye mambo zetu lakini mimi nampiga chenga, ila Tesha hakutaka kukubali. Na akasema haina shida, mimi hata nikimficha, angejua tu. Alinifurahisha sana maana alikuwa na akili nyepesi na mwingi wa maneno, na mimi bado sikutaka tu kumwambia kuhusu jambo langu na Soraya ili asiwe na makeke mengi.

Kwa hiyo baada ya dakika kadhaa kupita kutokea hapo, tukawa tumefika Mzinga hatimaye na kuendelea kuelekea nyumbani, huku tukiwa tumeshaongelea suala la kwenda Buza kwenye msiba wake Joy. Kwa kuwa tulikuwa tumekula kule hospitali, hapo ilikuwa ni kumwacha tu Mariam nyumbani kisha sisi tugeuke tena; uzuri leo Miryam alikuwa amemwachia mdogo wake gari.

Lakini tulipofikia eneo la Masai, nikamwambia Tesha anishushie hapo kwanza. Akaniuliza nilitaka kwenda kunywa bia au, nami nikamwambia hapana, kuna deni nilikuwa naenda kulipa hapo, hivyo yeye ampeleke mtoto nyumbani kisha akigeuka atanikuta hapo ili tuondoke. Hakuwa na neno. Nikashuka, kisha nikaanza kwenda kule ndani kwenye bar.

Hii ikiwa ni saa saba mchana, bado Masai ilikuwa imetulia, kukiwa na watu watatu tu walioonekana kukaa na kunywa pombe, ikiwa wazi kwamba hata muda wa jirushe haukuwa umefika. Lengo langu kuja huku lilikuwa kumtafuta Bobo, nami nikawa nimemwona.

Mwanaume tolu, asiyeonekana kuwa na figisu za kijinga, Bobo alikuwa amesimama usawa wa kaunta akizungumza na wanawake wadogo wawili, bila shaka wahudumu wa hapo. Alikuwa akiwapa maelekezo sijui, na aliponiona, akanipa ile salamu yake ya uchangamfu ah nakuona mchina!

Nikatoa tabasamu hafifu na kuwasalimu wale wanawake, nao wakaitikia na kuendelea kunitazama. Bobo akaanza utani wake, akimsukumia mmoja kwangu na kusema kama nikitaka basi anilipie chumba hapo kwenye lodge ya Masai ili nikamtandike, lakini nikacheka tu na kumwambia ni yeye ndiye aliyefanya nikaja hapo. Nilitaka tuongee kibinafsi, na kwa hilo akasema hamna noma.

Tukasogea pembeni kabisa na kusimama kwa ukaribu.

"Oy, si unajua kilichomkumba Joy?" nikamuuliza.

"Ee, najua. Dah mwanangu! Wamemchana vibaya yaani! Wanaingiza vipisi kwenye jeneza. Inatisha kinyama," Bobo akasema.

"Dah! Kwa hiyo... utaenda msibani?"

"Nitaenda kuchungulia tena. Unajua... nilienda kuona tukio baada tu ya kusikia na... mambo kule hayaeleweki. Huo mwili wake wenyewe ungetakiwa kuachwa kwa mapolisi huko, lakini wameona waipe tu familia yake heshima ili uzikwe. Mwanangu, Joy hakuwa wa kufa kihivyo... tukiwapata waliomuua, hata mimi nitachangia kuwachinja..."

"Labda ni masuala ya makundi, si unajua? Ikiwa kuna kundi linalopingana na kundi la Chalii labda kumuua Joy ilikuwa kukomoana..."

"Ah mwana una akili! Umekuja juzi tu tayari umeshaotea hivyo..."

"Nimeshaona mengi."

"Ee, inawezekana masuala ya makundi. Sijui sana, ila... maneno ni mengi, si unajua? Maaskari wanaweza kuja hadi hapa kuipekenyua Masai wakijua Joy alipenda kutimkia na huku, kwo' tumejiweka sawa pote hapa ili hiyo ikitokea maelezo yanyooke. Sijaelewa undani wa kilichompata ila... Chalii na yeye anawatafuta hao mbwa wal'omuua. Si unajua alikuwa demu wake?"

"Najua."

"Ndo' hivyo. Amepanga fanya kitu mbaya akiwanasa. Me nasubiri mchezo tu," Bobo akasema.

Nikatulia kidogo kutafakari mambo. Aidha Bobo alijua ama hakujua kwamba Chalii Gonga alinishuku mimi pia mpaka kunipigia simu leo kunitisha, lakini hicho siyo kilichokuwa kimenileta hapa.

"Wewe unaenda huko?" akaniuliza.

"Ee, ndo' tunaenda sa'hivi na Tesha," nikamwambia hivyo.

"Aaa, isingekuwa ya biashara na mimi ningeunga. Ulikuwa umekuja kunipitia?"

"Hamna. Nilikuja kwa sababu... nataka tuwe washkaji Bobo. Tight yaani. Nimekuangalia... nimekusoma... wewe uko poa sana. Japo uko upande mbaya lakini naona unajua upande sahihi wa mambo ni upi," nikamwambia.

"Ehehe... sikuelewi mwanangu, sijui ndo' unaongea nini," akasema hivyo.

Nikacheka kidogo na kusema, "Nataka unisaidie kitu, lakini iwe baina yetu."

"Nambie kamanda... usikonde," akasema.

"Una namba za mke wa Chalii?"

"Mke... Bertha?"

"Yah."

"Aaaa... kumbe!" akasema hivyo.

Nikatabasamu kidogo.

"Ah! Mwanangu umezunguka kichizi. Si ungesema tu?"

"Ndiyo nimekwambia sasa."

"Ah, maji laini mbona? Unamkubali eh?"

"Sana. Sema shida... kama unavyojua..."

"Ah... wewe Chalii asikuumize kichwa. Sikiliza nikwambie. Huyo manzi huwa ni mtata, lakini we' kama mjanja pale unaingia vizuri mbona? Halafu tena wewe... yaani yule unakula mapema. Si ile juzi alikuita ye' mwenyewe hapa?" Bobo akasema.

"Mh! Habari zinasambaa haraka!" nikasema.

"Hahaha... watu tuna macho. Yaani wewe Chalii asikupe presha wala, usimwogope. Namba nakupa... ukitaka huyo mutoto unakula vizuri sana... ila uende na swaga zilizonyooka, maana..." akasema hivyo huku akitoa simu.

"Anaweza akazingua, namwelewa. Usihofu. Najua pa kumtekenyea. Sema tu Chalii asijue, au siyo?"

"Uhakika. Ila ukim(.....) chukua video uje unionyeshe. Nataka kuona kama ana mabaka au ngozi ya tembo!" Bobo akasema hivyo.

Nikacheka kidogo na kutoa simu yangu, nami nikaanza kuandika namba ya mwanamke yule na kisha kuitunza. Nikabadilishana namba na Bobo ili tuwe tunawasiliana pia, naye akanisevu kama alivyopenda kuniita, "Mchina."

Ilikuwa sawa kwangu kuigiza kwa Bobo kwamba nilimtaka kimapenzi huyo Bertha ili anipe namba yake, na nilipeleka maigizo haya mbali kwa kufanya ionekane kuwa nilimhofu sana Chalii, lakini nilikuwa na lengo lingine kabisa kwa kufanya haya yote. Baada ya kuwa nimeipata namba, sasa ingekuwa ni kula sahani moja na huyo Bertha.



★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
Back
Top Bottom