Simulizi: Mimi na Mimi

Simulizi: Mimi na Mimi

MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!

★★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA

★★★★★★★★★★★★★★★★★


Nikiwa nafikiria kurudi ndani kwanza kutokana na kiatu changu kukatika, Ankia ndiyo akawa amerejea. Alipendeza sana kichwani kwa kusuka nywele ngumu zenye mtindo wa mawimbi kama tambi, na zilikuwa nyekundu. Mkononi alishika mfuko mdogo ulioonyesha kitu kama karatasi, au bahasha nyeupe iliyotuna.

Alipofika karibu zaidi akasimama huku akitabasamu. "Vipi JC? Mbona umesimama hapa?" akaniuliza.

Nikiwa na uso makini, nikamwambia, "Nilikuwa nataka kutoka... ndala ikakatika. Inabidi nianze kuvaa zile mpya."

"Ee... pole."

"Umependeza."

"Asante. Zimenikaa vizuri?"

"Sana. Shi'ngapi hapo?"

"Elfu ishirini na tano."

"Ahaa... umependeza sana. Leo lazima nikutekenye," nikamtania.

"Ahahah... haya twende ndani. Nimeleta chips, saa nne sa'hivi, nisingeweza kuja kupika. Au? Ulikuwa unaenda wapi?" akaniuliza.

Alikuwa anaongea huku akitembea kuelekea kule ndani, lakini nikabakia hapo nikiwa nimeweka uso makini. Bado akili yangu ilikuwa imetekwa na suala la muda mfupi nyuma kuhusu Joshua.

"JC... vipi?" Ankia akarudi na kuuliza hivyo.

Nikamwangalia na kusema, "Poa. Namtafuta tu Tesha."

"Kumbe hamkuwa wote? Labda
atakuwa Masai... si kulikuwa na mechi leo?"

"Hapana. Masai hayupo."

"Kwao je?"

"Ndo' nilikuwa nataka niende ila... nimeahirisha," nikasema.

"Kwa nini? Kuna nini kwani?" akauliza.

"Twende ndani, nitakwambia," nikasema hivyo na kuanza kuelekea upande wa ndani pamoja naye.

Kweli nikawa nimemwelezea Ankia kilichotokea baada ya Joshua na mke wake kufika hapo nyumbani kwao Tesha, nami nikamjulisha kuwa bado watu hao walikuwa hapo ndiyo maana sikutaka kwenda nilipogundua hilo. Nilikuwa tu nataka kuhakikisha Tesha yuko poa maana mpango ulikuwa niondoke pamoja naye lakini akawa ameniacha tu, ikionekana ni hasira ndiyo zilimlemea.

Ankia akanituliza kwa kusema huyo kijana angekuwa poa tu maana alikuwa mjanja; labda alienda kwa mademu zake ama huko Mbagala kunywa pombe. Lakini na mwanamke huyu alishangaa sana suala la Miryam kumleta Joshua hapo baada ya kila kitu alichokuwa amewafanyia, ila akanishauri niachane na mambo ya hiyo familia maana hayakunihusu. Ila mimi sasa!

Tayari nilijua rangi za kweli za huyo Joshua, vitu vibaya sana ambavyo hata Ankia sikumwambia. Nisingeweza kuacha kujali hali ya Mariam huku nikijua kabisa kwamba kaka yake alikuwa na mpango wa kumuua, sijui na wakati huu alikuwa amepanga nini! Je kama alitaka kumuumiza Tesha? Mama wakubwa? Miryam?

Ningehitaji kuhakikisha naukomesha huo mchezo wake upesi ili asije kuleta shida kwa watu hao niliokuwa nimeanza kuwajali sana, yaani kwa maneno mengine, ningejitahidi kuilinda familia hiyo dhidi ya Joshua. Si alitaka watu wausikilizie muziki wake? Wakwangu angeucheza!

★★

Baada ya Ankia kuandaa vyakula mezani, tukala pamoja, chips kavu na mishikaki mitano-mitano. Ah hiki ni chakula pendwa na chepesi sana kupata kila kona ya eneo lolote, na angalau baada ya kushiba nikawa nimetulia zaidi kimwili. Nilikuwa nahisi uchovu-uchovu tu uliotokana na njaa, joto, bila kusahau mechi niliyocheza na Soraya pia, hivyo nikaamua kwenda kujimwagia ili kupunguza fukuto baada ya msosi kukaa mahali pake.

Mpaka inafika saa sita, sikuwa nimempata Tesha. Bi Zawadi alinipigia simu kuniuliza ikiwa nilikuwa na mwanaye huyo, lakini nikamwambia hapana. Walimpenda sana na walitaka kuhakikisha yuko salama, kwa hiyo nikawahakikishia angekuwa vizuri tu na angerudi, kwa hiyo wasijali.

Lakini mimi ndiyo nilikuwa najali zaidi, siyo kuhusu Tesha tu, ila wote hapo kwao. Nilikuwa nimemuuliza Bi Zawadi kama Joshua na mkewe waliendelea kuwepo hapo kwao, lakini akaniambia walikuwa wameondoka mida ya saa nne usiku huo, kumaanisha si muda mrefu sana uliokuwa umepita tokea nilipomsikia jamaa akiongea na jambazi mwenziye kwenye simu, ndiyo akawa ameondoka.

Nikaulizia tu na hali ya Mariam kwa muda huo, nami nikajulishwa kuwa binti alikuwa ameshapumzika usingizini. Sikutaka kuuliza mengi sana yasiyonihusu, kwa hiyo tuliachiana hapo tu.

Tesha sikuweza kumpata kabisa kwa simu. Bora hata mwanzoni ilikuwa ikiita mpaka kukata, lakini wakati huu haikupatikana kabisa. Dah! Sikuwa na namna ila kusubiri tu, nami nikakaa sebuleni mpaka saa nane kasoro usiku ndiyo hatimaye jambo jipya likaja.

Niliweza kusikia geti likigongwa huko nje, nami sikuwa na uhakika kama lilikuwa letu au la jirani, kwa hiyo nikatoka ili kwenda tu kuangalia ikiwa ilikuwa ni Tesha. Ankia alikuwa chumbani kwake lakini inaonekana alikuwa macho bado, kwani nilipoanza kufungua mlango wa kuingilia ndani hapa akawa ametoka chumbani na kuja kuniuliza naenda wapi. Nikamwambia naenda kuangalia ikiwa Tesha ndiyo amerudi, naye akasema poa.

Nikatoka mpaka nje, nikachungulia upande wa pili wa nyumba na kumwona bibie Miryam, ndani ya nightdress, akiwa hapo nje kwenye ubaraza wao. Alikuwa ndiyo ametoka ndani nafikiri, akitaka kwenda kufungua geti, nami nikadhani bila shaka ni kwake ndiyo paligongwa. Lakini geti lilipogongwa tena, nikatambua lilikuwa la kwetu.

Miryam akaonekana akienda kwenye geti lao na kufungua, kisha akaenda nje kabisa. Geti letu likaendelea kutoa kelele tu, nami nikaenda hapo na kukuta ni Tesha. Lakini hali niliyomkuta nayo haikuwa nzuri kabisa.

Alikuwa amechafuka kwenye suruali, huku akiwa anayumba kilevi na kofia yake kama kibandiko kichwani. Kuangalia jinsi alivyokuwa akiyumba lakini kwa kupindia upande mmoja kukanifanya nitambue kwamba alikuwa amepigwa.

Nikamwona Miryam akitokea pembeni yake na kumshika mkono, ikiwa wazi anataka ampeleke kwao, lakini Tesha akagoma.

"Hhh... sss... JC... kaka nifungulie..." Tesha akasema hivyo.

Hakuwa akitoa machozi, lakini alikuwa analia. Ile kulia ya kiume siyo kwa sababu umeumia mwilini, ila moyoni.

Miryam akaniangalia kifupi, kisha akamwambia mdogo wake, "Tesha... twende ndani. Ni usiku sasa hivi, na mimi hii tabia siipendi. Twende!"

"Niachie Mimi... nenda mwenyewe. Si unawajali hao mbuzi zaidi yetu... waambie wakae hapo... basi..." Tesha akasema hivyo.

Ikanibidi nirudi ndani upesi kwenda kuchukua funguo za hili geti letu, naye Ankia akawa ameniuliza kulikoni. Nikamwambia Tesha amerudi, lakini alikuwa vibaya, nasi sote tukatoka tena na kwenda nje. Tulikuta Miryam akiwa anamfokea mdogo wake lakini kwa sauti ya chini, nami nikafungua geti na kutoka.

"...maneno gani? Hebu jiangalie Tesha. Unafanya maisha yako yawe mabaya kisa hasira, unafikiri itakufikisha wapi?" Miryam akaendelea kumwambia hivyo.

"Mimi... niache... wewe fanya mambo yako... maana haujali hisia zangu..."

"Mimi sijali hisia zako Tesha? Unaniambia hivyo?" Miryam akamuuliza kwa hisia.

Nikamshika Tesha mkononi na kuuliza, "Tesha nini kimetokea?"

"Ah... sss... mwanangu..." akasema hivyo na kupiga ulimi mdomoni.

"Ulikuwa wapi? Umeanguka?" Ankia akamuuliza hivyo.

Tesha akawa anababaika, akionekana kuwa na maumivu.

"Umefanyaje? Nani amekupiga?" nikamuuliza hivyo kwa uthabiti.

"Amepigwa? Umepigwa Tesha?" Miryam akamuuliza hivyo na kusogea karibu zaidi.

"Ah... mwanangu nimekabwa... njiani..." Tesha akasema hivyo.

"Na vibaka? Sehemu gani?" nikamuuliza.

"Si huko Mbagala mwanangu... nilikuwa narudi... ah... mwanangu wamechukua simu yangu..." Tesha akaongea kwa kukaza hisia.

"Umetembea kutokea Mbagala?" Ankia akamuuliza hivyo.

"Jamani! Tesha umeona sasa mambo ya usiku? Nikwambie mara ngapi unisikilize?" Miryam akasema hivyo kwa huzuni.

"Ni kweli Tesha, usiku siyo mzuri... jamani, tuingieni ndani..." Ankia akasema hivyo.

"Twende Tesha ukalale..." Miryam akamwambia hivyo na kuuvuta mkono wake, lakini Tesha akaweka mgomo.

"Tesha... msikilize dada'ako..." Ankia akasema.

"Mbona yeye hanisikilizi? Anawaleta... ah... Ankia, sister anazingua... ona mpaka nimejikuta kwenye hii hali..." Tesha akasema hivyo.

"Yaani unanilaumu mimi kwa sababu ya upuuzi wako? Me nilikutuma uende huko? Ukoje wewe?" Miryam akasema hivyo na kusukuma kichwa cha mdogo wake kwa kidole.

"Miryam..." nikamwita hivyo kwa sauti ya chini.

"Nini?" akaniitikia hivyo.

"Nitaenda kulala naye. Yuko vibaya kama unavyoona... mwache tu, mtaongea asubuhi. Sawa?" nikamwambia hivyo kwa upole.

Miryam akamtazama mdogo wake, nikiona machozi yakiwa yamemlenga.

"Oya... twende ndani..." nikamwambia hivyo Tesha na kuanza kumvuta.

"Dah... JC, simu yangu..." akasema hivyo kwa huzuni.

"Twende kwanza upumzike... tutatafuta nyingine..." nikamwambia hivyo.

Nikamkokota vizuri mpaka ndani, Ankia na Miryam wakiwa wanatufata kwa ukaribu, nasi tukafika chumbani kwangu. Tesha akajitupia kitandani na kulala kifudifudi, huku uso wake akiugeuzia ukutani, na mwili wake ungeshtua kila mara kwa ile njia ya kulia kwa pumzi.

Nikawa namtia moyo tu ajikaze, na nikiangalia kama kuna sehemu aliyokuwa ameumia vibaya, huku wanawake wakiwa wanatutazama tu pale mlangoni, nami nikamwomba Ankia aifate feni sebuleni na kuileta huku, kisha aiwashe mpaka mwisho.

Akatii na kuileta, akiiwasha na kuielekeza upande aliolala Tesha, nami nikatoka kitandani na kusimama kumtazama dada mtu. Alikuwa anamwangalia mdogo wake hapo kitandani kwa macho yaliyojaa huzuni, na nilitambua kuna kiasi cha machozi kilichokuwa kimemtoka lakini akawa ameyafuta macho yake.

"Tumwache alale sasa, pombe ikimtoka mambo yataeleweka zaidi, eti Miryam?" Ankia akamwambia hivyo.

"Muda mwingine natamani hata nimkate masikio," Miryam akasema hivyo kwa sauti ya chini.

Ankia akatabasamu na kuniangalia.

Nilikuwa namwangalia Miryam kwa uelewa mwingi sana, naye aliponitazama machoni, nikasema, "Najua unawaza sana kuhusu hali yake, ila usijali. Hajaumia sana. Hao vibaka wamemkwarua kidogo tu."

"Na simu yake wamebeba," Ankia akasema.

"Kama angekaa kwa kutulia, haya yote yasingetokea... ah..." Miryam akasema hivyo kwa huzuni.

Ankia na mimi tukatazamana tu machoni, kisha tukamwangalia tena dada mkubwa.

"Sitaki akuletee shida Ankia jamani, ikiwa..."

"Hapana, hapana, Tesha siyo shida Miryam. Ni rafiki yetu, kwa hiyo lazima tumsaidie. Mbona we' umenisaidia kwa mengi magumu Miryam... sasa hiki tu ndo' kinipe shida? Hebu acha kuwaza hivyo bwana. Nenda kapumzike... asubuhi mambo yatakuwa sawa," Ankia akasema hivyo kwa upole.

Nikawa namwangalia tu Miryam, naye akashusha pumzi na kutoa shukrani, kisha akaanza kuondoka. Nikahakikisha namtoa mpaka nje na kumwacha kwenye mazingira salama mpaka alipoingia getini kwao, tukiwa hatujaongea chochote kabisa, nami nikarudi upande wetu.

Ankia akaanza kuniambia ni namna gani maisha ya hapo yalivyokuwa yakitengeneza drama moja baada ya nyingine, na hili suala la Tesha kupenda mno pombe mpaka anajikuta kwenye matatizo lingemfikisha pabaya mno ikiwa asingeangalia.

Akaniaga na kwenda kulala chumbani kwake, nami nikabaki chumbani pamoja na rafiki yangu mpya. Tayari usingizi ulikuwa umeshambeba zamani sana, si unajua alikuwa amegusa pombe? Kwa hiyo nikakaa hapo kwanza kutafakari vitu kidogo.

Alichosema Ankia kilikuwa sahihi. Tesha alikuwa kijana mzuri sana, lakini naona kuna kitu fulani kilichokuwa kikimsukuma apende mno pombe na kumfanya awe tofauti na alivyotakiwa kuwa. Kiuhakika, sisi wote tulikunywa, lakini hata sisi wengine tungeweza kuona kwamba alikuwa akipita kiasi.

Labda shauri ya msongo wa mawazo uliosababishwa na kitu fulani nisichofahamu ndiyo jambo lililofanya awe hivi, na kwa sababu nilikuwa namjali, nilitaka kuhakikisha namsaidia kwa ushauri, ikiwa ingewezekana, ili ajiepushe na mambo ambayo huenda yangekuja kumwingiza kwenye matatizo mabaya zaidi kuliko hata ya leo.

Sikutaka vitu vibaya zaidi vije kumpata huyu kijana, kwa hiyo darasa huru lingeitishwa siku ikishakucha ili kweli nisaidie kumweka huru.


★★★


Siku ikakucha. Niliamka cha kwanza ikiwa ni saa moja kasoro, nao usingizi bado ukawa unanivuta niendelee kulala. Kwa kuwa nililala na Tesha kwa kupishana miili, nilimchungulia tu na kuona kwamba bado alikuwa amesinzia, hivyo nami nikaingia usingizini tena.

Ndoto moja, mbili tena, nami nikaamka kwa mara nyingine. Zamu hii nilipoangalia muda nikakuta inakimbilia saa tatu asubuhi, nami nikamwangalia mwenzangu na kuona bado amelala kitandani, lakini macho yake yalikuwa wazi.

Tesha alitazama kuelekea juu, ikiwa kama vile anatafakari mambo fulani, nami nikampiga kidogo mguuni kwa mkono wangu.

"Oy, oy..." akasema hivyo kwa sauti ya chini.

"Uko macho muda?" nikasema hivyo na kupiga mihayo.

"Hamna... nimekata dakika 10 tu. Ankia kaja, akanicheki, ameenda sokoni kufata nyama. Wewe unalala kama umekufa mwanangu, hata hukumsikia," akaniambia hivyo.

"Ah wapi! Hahah... nimeamka kabla yako, nikakucheki, nikaona bado uko Dreamland, kwa hiyo na mi' nikarudi kulala pia..." nikasema hivyo.

"Dah, nimekunywa jana! Nashangaa sijapotea njia ya kurudi," akasema hivyo.

"Mlevi hata alewe vipi, hawezi kusahau kwake," nikamwambia.

"Ahahah... uhakika. Na mimi navyolalaga vibaya hivyo, sijakupiga mateke kweli?"

"Hamna... ila sema unajamba sana..." nikamtania.

"Aa, acha hizo mwanangu..."

Sote tukacheka kidogo.

"Unajisikiaje?" nikamuuliza.

"Dah! Kichwa kinagonga. Mbavu zinauma, hao wajinga jana walinipiga kabaroho la hatari," akaniambia.

"Kwani ulikuwa unatokea wapi kabisa? Jana nilikupigia kweli afu' baadaye ndiyo ukawa hupatikani kabisa..."

"Dah! Mwana me nilikuwa nimekasirika sana... ile ishu, si unaelewa?"

"Yeah."

"Nikaona niende zangu Tandika. Kule kuna demu wangu... anaitwa Happy... ananielewa sana. Nikaenda kwake, nikakaa pale wee... badae', jioni pale mechi imeisha, nikamwacha. Ah, afu' linapenda kunyonywa chenza!" akaniambia hivyo.

"Ahahahah... usinambie'!"

"Ah, siyo poa. Nimelila, likanigei na hela ya bia maana... linafanya kazi kwenye hoteli, kuna shift ya usiku kwo' lenyewe likaenda huko, nami ndo' nikaanza kurudi Mbagala..."

"Mm-hmm..."

"Basi mwanangu, nikaenda zangu pale Highway. Piga bia zangu kama nne hivi, wenye kushoboka wakaja, wakaongeza, nikaendelea kupiga tu. Nimekunywa jana! Halafu zilikuwa kama haziishi..."

"Haukufahamiana na hata mmoja?"

"Hamna, chawa tu zisizojulikana. Walikuwa wanafikiri me mtu mwenye hela ndo' maana..."

"Ikawaje?"

"Nimekunywa, nimekunywa, kuna demu akawa anataka niende naye Lodge ya hapo, ila me sikuwa na hela. Afu' lilikuwa la moto!"

"Wewe!"

"Acha mwanangu, bonge la pisi! Ningekuwa na 15 nisingerudi huku kabisa, ningelala nalo..."

Nilikuwa nasikiliza kwa umakini namna ambavyo kijana huyu aliongea, nikijaribu kuisoma saikolojia yake. Niliweza kutambua mambo fulani kuhusu utu wake kutokana na jinsi alivyozunguka kwenye maneno aliyotumia ili kufika kwenye pointi ya kile nilichotaka kujua. Alipenda ukweli wa mambo yote aliyofanya uelezeke mwanzo mwisho kwa msikilizaji, ili kumwaminisha zaidi.

"Nikatoka hapo, saa sita mwanangu, nikasema ah... si unajua na pombe? Nitembee tu... yaani napaona skani kama hapo tu. Nilikuwa hata siyumbi kivile mwanangu... mdogo mdogo tu mpaka lile eneo pale karibiaa... nanilii... kale ka-guest... Lasanga..."

"Ee..."

"Eee pale mbele mbele ukikaribia sasa kwenye lile dampo la machupa ya kuuzwa. Pale si ndiyo pamekaa vizuri kukojoa, nikasogea nishushe mvua. Ah!"

"Ndo' wakakuvamia hapo?"

"Yaani sijui hata walitokea wapi kaka!"

"Walikuwa wengi?"

"Kama watatu hivi. Wawili walinishika, mmoja akiwa amenikaba, afu' nikasikia nimepigwa kiunoni... hapa kwenye mbavu, ah! Isingekuwa ya pombe ningeruka nao! Wakachukua simu na wallet mwanangu, ila haikuwa na kitu hiyo..."

"Hakukuwa hata na kadi za maana? Vitambulisho?"

"Hamna. Uzuri sikuwa nimevibeba jana. Si ile nimeondoka kwa hasira, nilikuwa na buku tatu tu... ahahaha... mpaka kwa Happy huko Tandika, ndo' na yeye akanitoa kidogo baadaye. Ndiyo hivyo bro... wamenitia hasara hao wakuda..." akasema hivyo kwa kuudhika.

"Inabidi uje kwenda polisi... masuala ya laini, si unajua?"

"Ah! Nimeshachoka akili. Yaani kama nikija kukutana nao tena! Nitafanya kitu mbaya sana," akaniambia hivyo.

Nikajinyanyua na kukaa, yeye bado akiwa amelala chali huku mguu mmoja akiukanyagisha kitandani na mkono wake akiuweka kwenye paji la uso.

"Hiyo ni kama utakutana nao tena, na ni kitu kigumu sana. Hao ni watu wa kubadilisha maeneo, na wewe haukuwa target ya moja kwa moja. Walikuotea tu," nikamwambia hivyo.

"Ah... ndo' hivyo kaka. Mtihani wa kutafuta simu nyingine ni wangu... na ni mgumu kinoma," akasema hivyo.

"Unajua Tesha... nakuelewa. Vizuri sana. Wewe unavyoona mambo, ni tofauti na jinsi ambavyo dada yako au mama zako wakubwa wanayaona, kwa hiyo migongano lazima itokee msipokubaliana kwa jambo fulani, lakini...."

"Mimi ndo' nacholilia JC! Hivi kweli mwanangu, si na wewe ulikuwepo ile siku huyo mbwa ameitukana familia yetu? Tena we' hapo ilikuwa ni mara ya kwanza... me mwanangu namjua huyo mtu toka tupo wadogo, yaani hafai! Ni mchoyo, mkuda, mpumbavu, yaani ah! Halafu analeta ***** zake hapo afu' eti nimpokee 'njoo, karibu sana'? Yaani siwezi JC. Sijui Mimi anafikiria nini... ah..." akaongea kwa hisia sana.

"Hujaingia kwenye akili ya dada yako Tesha, na najua hamwezi kufanana kwa kila kitu. Unajua... we' ni mdogo wangu, sawa? Nakuelewa. Ninaelewa hasira uliyonayo haiko kwa familia yako, ila una hasira juu ya kitu kingine ambacho... ndiyo kinakufanya upende zaidi kujistarehesha... wanawake... pombe sana... ili ujipe njia ya kupotezea hizo hisia. Lakini Tesha... ushawahi kusikia kwamba huwezi kuepuka matatizo yote kwa kuyakimbia?" nikamwaongelesha hivyo kwa upole.

Akawa ananiangalia kwa macho yenye subira.

"Mimi ni rafiki yako, na nimeshakusoma. Nimeelewa kwamba kuna kitu kinachokuumiza, lakini hautaki kuki-face... unakiepuka... kwa kuishi ile... kujiachia. Inaeleweka mwanangu, sawa? Hata mimi nimeshapita kwenye nyakati za namna hiyo... kwa hiyo nakuelewa. Lakini nitakwambia kitu. Ikiwa utaendelea kuiepuka hiyo hisia na kujifikirisha kwamba uko sawa, kwamba hauna tatizo... ndiyo itaendelea kukua zaidi. Inakuwa kama unapokuwa na kinyongo na mtu... lakini unaigiza kwamba ah mko fresh. Hiyo kitu inakuwa inakutafuna ndani kwa ndani, ndiyo maana unakuwa unafanya vitu kwa njia isiyo yako kabisa, hasa... hasa kama utakasirishwa na jambo hata dogo linalohusiana na hiyo hisia uliyoificha. Unanielewa rafiki yangu?"

Tesha alionekana kuzama ndani ya hisia fulani nzito sana baada ya kunisikia nikimwambia hivyo, naye akatikisa kichwa kuonyesha uelewa.

"Sisi siyo wakamilifu mwanangu. Hakuna mtu msafi yaani. Lakini tunapoona mwenzetu anajichafua haimaanishi tumwache tu. Tunakuwa tunasaidiana hivyo hivyo, uongo?" nikamwambia hivyo.

"Ni kweli," akajibu.

"Ee. Ila sasa... kuna watu kama Joshua. Sikupingi Tesha. Huyo kaka yako... hafai. Yaani ana ule uchafu sugu kwenye utu wake hata kuusugua kwa Jik wala msasa hautoki. Sawa?"

"Kwa hilo hupingwi JC..." Tesha akasema hivyo.

"Yeah. Ndivyo hali ilivyo, haipingiki. Lakini tukija kwa dada yako... Miryam ni mtu tofauti Tesha. Anajaribu kuona kitu fulani ndani ya mtu hata kama hakipo, na hiyo inamfanya awe mtu mwelewa sana... mpole... anayetaka amani hata kama nafasi ipo kidogo sana ya kuipata. Hayo siyo makosa yake, ndivyo alivyofundwa. Na dada yenu... anawapenda sana. Nadhani anataka kufanya kila kitu kuwaunganisha, maana anajua hatakuwa nanyi siku zote..." nikaeleza hivyo.

Tesha akaendelea kunisikiliza tu kwa utulivu.

"Ma' mkubwa wako alinielewesha kuhusu huo utu wa dada yako, kwa hiyo nimemwelewa namna hiyo. Anataka kutafuta amani hata na mtu kama Joshua kwa sababu ni ndugu yenu, sawa, huyo ni Miryam. Ila wewe ni Tesha. Ukishamwelewa kwamba 'dada yuko hivi,' we' kubaliana naye, kwa njia yake ya kuona mambo, lakini unakuwa unahakikisha kwamba uko macho kwa njia yako mwenyewe ya kuona mambo ili ukiona kwamba anakaribia kuanguka... unawahi kumdaka. Maana hata yeye anaweza akawa anakosea, si ndiyo?" nikamwambia hivyo.

"Ni kweli," akajibu.

"Ee, hawezi kuona vitu kama Bi Zawadi na Bi Jamila, ama Shadya na mashoga zake. Alivyo ndivyo alivyo tayari, we' mwelewe tu, halafu utulize hisia zake hata kama bado zako zinaruka-ruka. Si unaelewa mwanangu?"

Akatikisa kichwa kukubali.

"Ee. Haumwamini kaka yako, sawa, simama na hilo. Nenda na biti la dada yako la kutafuta amani lakini jicho lako makini lisitoke kwa huyo mtu unayejua anaweza kubadilika muda wowote. Si unanipata?" nikamwambia.

"Ee mwanangu, unasema kweli. Ah... mi' nakuwa sitaki hata awe karibu yetu maana..."

"Hata akiwa mbali Tesha, uwezekano wa kufanya mambo mabaya kwenu anao. Hicho ni kitu ambacho unatakiwa uwe nacho akilini. Kwa hiyo la muhimu kuangalia ni wale unaowapenda... basi. Wewe Tesha ndiyo mwanaume hapo... hebu, i-face hiyo hisia uliyoificha... ipe za uso... kitoe hicho kitu kinachoisumbua roho yako ili uache kujikimbia we' mwenyewe... ndiyo utaona umuhimu wa haya yote niliyokwambia ili uwe namna unavyotakiwa kuwa. Simaanishi utakuwa mtakatifu, ila najua utaanza kujitahidi kutotanguliza fikira zako tu na kuangalia faida za wapendwa wako zaidi. Hilo ndo' la muhimu. Au siyo?" nikamwambia hivyo kwa busara.

"Dah! Ahahah... kaka unaongea wewe! Fungua chaneli ya documentary..."

Akasema hivyo, nasi tukacheka kidogo.

"Me nimekuelewa JC. Uko sahihi. Unajua kuna kitu..."

Kabla hajamaliza kuongea, sote tukasikia mlango wa kuingilia ndani ya sebule ukigongwa, kuashiria mgeni kafika. Ah ingekuwa Ankia ndiyo karudi si angepita moja kwa moja? Huyo hakuwa yeye.

Nikaona nitoke tu kitandani na kuchukua T-shirt la kuvaa ili nikaone ni nani, maana nilikuwa kifua wazi na nimevaa pensi tu.

"Ankia kachelewa kweli kuleta supu," Tesha akasema hivyo.

"Labda ndo' katuma mtu ailete. Ngoja nikaone ni nani," nikamwambia huku nikivaa.

"Halafu mwana una kabode simple tu, ila kifua chako kiko mbele! Unaingiaga gym?" akaniuliza.

"Kitambo, niliacha. Ila nataka nije nianze tena kujenga kinga," nikamwambia hivyo.

"Na mimi nataka nianze pia, maana nilishakuwa legelege mpaka nakabwa kijinga," akasema hivyo.

Nikatabasamu kiasi, nami nikatoka chumbani na kwenda kufungua mlango.

Macho yangu yalikuwa na uzito kiasi, lakini baada ya kumwona bibie Miryam hapo nje ikawa kama yamepata wepesi. Alikuwa amevaa nguo kama dera, ya kijani, iliyokuwa imefungwa kwa mkanda laini sehemu ya kiuno. Kichwani alizibana nywele zake ndefu alizosuka kwa juu, na uso wake usiokuwa na virembesho vya aina yoyote ulipendeza sana kwa asubuhi hii.

"Za asubuhi?" akanisalimu kwa sauti yake nzuri.

"Salama. Vipi wewe?" nikamjibu.

"Safi tu. Huyo ameamka?"

"Ee yuko macho, ila... bado yuko kitandani... ingia..."

"Hapana, mwite tu. Nataka aje nyumbani."

"Bado ni mzito, Ankia ameenda kumfatia supu pia. We'... ingia tu umwone angalau. Tafadhali," nikamwomba hivyo.

Akaniangalia kwa macho yenye utathmini, kisha akavua ndala zake na kuingia ndani. Ngozi yake nyeupe iliyoonekana nyuma ya shingo yake ilipita hadi weupe wangu yaani, ikionekana kuwa nyororo sana.

Nikaacha kumtazama baada ya yeye kufika mbele zaidi na kunigeukia, nami nikaufunga mlango na kuelekea chumbani kwangu huku nikimwambia aje. Nikakuta Tesha akiwa amejilaza bado, nami nikamwambia dada yake amekuja.

Akajinyanyua na kuketi kitandani, huku dada yake akiwa anaingia chumbani sasa, nami nikaichukua simu yangu.

"Ngoja niwapishe kidogo... njoo ukae," nikamwambia hivyo Miryam.

"Hapana..."

Tesha akasema hivyo, nasi tukamwangalia.

"Usiondoke JC. Kuna vitu nataka niongee na we' usikie," akasema hivyo tena.

Nikamwangalia Miryam na kuona jinsi alivyomtazama mdogo wake kwa hisia, naye Tesha akasimama usawa wangu.

"Mimi... dada yangu... naomba unisamehe," Tesha akaanza kwa kusema hivyo.

Miryam akaingia ndani zaidi na kumfikia mdogo wake, akamshika mkono huku akimwangalia kwa hisia, naye akasema, "Usijali Tesha. Yameshapita. Wewe... twende nyumbani kwanza uka..."

"Hapana, Mimi, nataka unisikilize kwanza," Tesha akasema hivyo.

Miryam akabaki kimya.

Tesha akaanza kujipiga kifuani kwa kidole chake na kusema, "Kuna vitu vingi sana hapa dada. Nimejikaza muda mrefu mno. Unajua nikwambie kitu? Yaani kama ingekuwa... ingekuwa ni kuzaliwa kwenye maisha mengine... ningechagua kuwa na kaka wa damu kama JC... siyo Joshua."

Miryam akanitazama usoni, nami nikamtazama tu Tesha.

"Isingekuwa ya huyu kaka, leo nisingetambua kwa nini nimekuwa hivi. Mimi, hata wewe unajua sikuwa hivi... na japo... japo umeniacha tu niishi kama navyoishi sasa hivi lakini najua huwa nakuumiza sana. Najifumbisha tu macho... lakini ni kitu nachohisi... na roho inaniuma sana kwa sababu sipendi uumie..." Tesha akaongea kwa hisia.

Miryam akaanza kulengwa na machozi.

"Lakini... iko hivyo kwa sababu... yaani... nimekuwa hivi kwa sababu... kwa sababu uliniumiza Miryam..." Tesha akasema hivyo.

Miryam akamwangalia kwa njia iliyoonyesha hakuelewa, nami nikawa makini zaidi ili kuweza kuelewa sasa funguko la huyu kijana.

"Dada una moyo. Una moyo mzuri, sawa? Lakini Joshua siyo! Siyo mtu. JC... wazazi wetu wamekufa, sawa? Kwenye ajali. Walituachia kila kitu chao... wakatugawanyishia... lakini Joshua akawa anataka hadi na vya kwetu..."

"Tesha..." Miryam akasema hivyo kama kumzuia.

"Subiri kwanza Mimi, ngoja niongee. Mwanangu... Joshua alipewa vingi kuliko hata sisi, maana mama alikuwa anampendelea sana yaani. Lakini akavitumia vibaya, halafu ndiyo akageukia kwenye vyetu. Nilikuwa nimeachiwa shamba, nalimisha na Mimi, tunapata hela zinatumika kwenye maendeleo yangu, Mariam, na ndugu zetu wengine, lakini Joshua akaliiba... akaliuza serikalini!" Tesha akasema hivyo kwa sauti ya chini.

Hiki ni kitu ambacho nilifahamu, lakini nilidhani kwamba yeye Tesha hakujua. Nilipomtazama Miryam, alikuwa anamwangalia mdogo wake kwa njia iliyoonyesha hata yeye hakutarajia hilo.

"Da' Mimi alijua, lakini hakuniambia. Alikuwa anajaribu kulinda amani, kama ambavyo sikuzote anafanya, lakini nilipojua... niliumia sana kaka! Nilihisi kama vile na yeye anampendelea, ana... anakuwa kama mama..."

"Tesha..." Miryam akamwita hivyo huku machozi yakianza kumtoka.

"No, Mimi usilie, sikulaumu. Nakuelewa, sawa?" Tesha akasema hivyo na kumfuta dada yake machozi.

"Tesha..." Miryam akaita tena.

"Usijali. Nilikuelewa, ndiyo maana nikakaa kimya. Sasa... ah... JC ndiyo kanifungua macho leo. Hiyo kitu iliniumiza mno japo nilikuelewa... ndiyo maana nikawa namna hii. Kama ulivyoniambia mwanangu... nikawa naikimbia hiyo hisia. Ila me ni mtu mwenye hasira sana kaka, na nilikuwa sitaki ziende kwa Mimi. Nampenda mno..." Tesha akasema hivyo huku machozi yakionekana machoni mwake.

Nikaingiwa na simanzi baada ya kuwa nimemwelewa vizuri sasa. Unaona? Kadarasa huru nilikompa kakawa kameleta hiyo faida.

"Kwa hiyo dah! Me... Miryam siwezi kumchukia. Lakini ninakiri leo kwamba... kulikuwa na kitu hapa... kinanisukuma nimkasirikie... ndiyo maana nikaanza kunywa sana pombe, unajua inaweza ikawa ngumu kuelewa lakini... hii kitu ipo. Mimi... wewe ni mtu mmoja nayempenda sana. Nikikwambia naweza kuua mtu kwa ajili yako, namaanisha hata Joshua! Nikimwona anakuja hapo nyumbani... nakumbuka! Nakumbuka kila kitu... ndiyo maana nafanya mambo vibaya. Eh! Nisamehe dada'ngu. Kwa jana... ah, nisamehe tu..." Tesha akasema hivyo huku amemshika Miryam mabegani.

Dada mtu akawa anamwangalia tu mdogo wake kwa huzuni.

"Ila unajua nini? Sasa hivi... nimeshaliondoa hili kaa la moto rohoni. Sitaki tena. Sitaki... hasira niliyonayo iniongoze vibaya. Nakuahidi dada, nitabadilika. Labda... ila bia nitakuwa nakunywa kidogo tu, siyo mbaya..."

Kauli hiyo ikamfanya Miryam acheke kidogo kwa pumzi ingawa alikuwa na huzuni, nami nikatabasamu pia.

"Tuyaachie haya mambo hapa. Mimi... nakuahidi. Sitakuvunja moyo. Sawa? Amani unayoitaka utaipata... tena inaanzia kwangu, yaani usikonde," Tesha akasema hivyo kwa njia ya kuchangamsha.

Miryam akaangalia chini kiasi kwa huzuni.

"Oya... ndiyo hivyo. Asante sana kwa hiyo therapy... si umeona nimefunguka daktari-mchizi wangu?" Tesha akasema hivyo.

Nikatabasamu na kusema, "Nimekuelewa. Umefanya vizuri. Kumbuka tu hili. Haijalishi uliyoyafanya, sawa? Ila yale ambayo unataka kuyafanya ndiyo ya muhimu."

"Amen," Tesha akasema hivyo kiutani.

Nikafarijika kuona namna ambavyo kijana huyu alikuwa ameweza kuufungua moyo wake na kuonyesha utambuzi, nami nikamtazama dada yake na kukuta anamwangalia mdogo wake kwa hisia.

"Ngoja nikakojoe Mimi... nakuja..." Tesha akasema hivyo.

Miryam akatikisa kichwa kukubali, naye Tesha akampita na kutoka ndani hapo.

Ni baada tu ya mdogo wake kutoka ndiyo Miryam akakisogelea kitanda na kukaa, nami nikamtazama na kuona jinsi uso wake ulivyokunjamana kwa njia ya kulia. Oh alikuwa analia, sana!

Lakini ni machozi tu ndiyo yaliyoonekana kutiririka na kwikwi zake kushtua mwili, ila huyu mwanamke hakutoa sauti. Kilikuwa kile kilio cha ndani sana kutoka kwenye moyo wake, nami kumwona akilia namna hiyo kiukweli kulinipa hisia mbaya sana. Alitia huruma.

Nikasogea mpaka hapo na kukaa pembeni yake, nami nikasema, "Miryam... jikaze tu. Mdogo wako atakuwa sawa."

"Ahh... nakosea wapi? Hhh... kwa nini najitahidi kujenga ila tu ndiyo mambo yanabomoka?" akaongea hivyo kwa sauti ya kunong'oneza, na kwa hisia sana.

"Siyo..."

"Mimi ni mpumbavu, eti?" akaniuliza hivyo na kunitazama.

Nikabaki kumwangalia kwa huruma.

"Mimi nina moyo wa kipumbavu sana. Najaribu... nafikiri kufanya hivi ndiyo inafaa, lakini kumbe ndiyo naharibu. Naangukia pua... mwisho wa siku ni mimi tu ndiyo naangukia pua. Hadi mdogo wangu nimeshindwa kumwongoza vizuri? Mpaka ana... hivi kweli jamani... ni nini kama siyo upumbavu? Ndiyo maana hata na wewe uliweza kunifanya nionekane mjinga mara ya kwanza tumekutana, siyo? Ni kwa sababu ya upumbavu wangu..." Miryam akasema hivyo kwa huzuni.

"Hapana... siyo hivyo Miryam..." nikajaribu kumtuliza.

Akaendelea kulia bila kutoa sauti sana, nami hadi nikalengwa na machozi kabisa!

Nikapitisha mkono wangu kwenye bega lake kwa njia ya kumvuta kiasi, naye akalaza kichwa chake begani kwangu. Nilipatwa na hisia ya uvuguvugu moyoni, kwa sababu hali ya huyu mwanamke ilinigusa sana, naye akawa anaendelea kulia kwa kwikwi huku mimi nikimbembeleza kwa kusugua mkono wake taratibu.

Mapigo yangu ya moyo yalikimbia kwa kasi sana na sikujua shida ni nini. Kuna kitu fulani kilichokuwa kikijijenga ndani yangu ambacho bado sikuwa nimeelewa ni nini, ila kiliweka msingi wa hisia tofauti ndani yangu ambayo ilikwenda kinyume kabisa na hali ya utu niliokuwa nimejipatia kwa kipindi hiki. Sikujua kwa sasa, lakini huenda ingekuja kueleweka baadaye.



★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!

★★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI

★★★★★★★★★★★★★★★★★


Nikiwa naendelea kumpa Miryam bembelezo kwa kusugua mkono na bega lake taratibu, mlango wa kuingilia hapo chumbani ukafunguka, nami nikatazama hapo na kumwona Ankia akiwa amesimama. Bila shaka ndiyo alikuwa amerudi, na inaonekana alikuja moja kwa moja mpaka humu chumbani kutuangalia mimi na Tesha, lakini akakuta niko na dada mtu.

Miryam akawa amemwona pia, naye akajitoa begani kwangu na kuanza kujifuta machozi kwa viganja vyake. Ankia alikuwa amesimama hapo mlangoni akitutazama kama vile anasubiri maelezo.

"Ndiyo umerudi?" nikamuuliza hivyo.

"Ee... ndiyo nimefika. Kila kitu kiko sawa jamani?" Ankia akauliza hivyo kwa kujali.

Miryam akasimama baada ya kujikausha machozi, nami nikasimama pia. Akasema, "Ndiyo, nimemwijia Tesha."

"Yuko wapi?" Ankia akamuuliza.

"Ameingia uani. Ngoja niende nikamsubiri hapo nje," Miryam akasema hivyo.

Nilikuwa namtazama tu kwa utulivu, naye akaanza kuelekea mlangoni lakini Ankia akamshika mkono kumzuia. Sote tukamtazama.

"Nime... nimeleta supu. Kaa basi tunywe pamoja na mdogo wako, eti?" Ankia akamwambia hivyo.

Miryam akasema, "Sitaweza Ankia. Naingia kazini, nataka nikajiandae. Ila Tesha anaweza kubaki, na...."

"Ankia umerudi?" Tesha akawa amefika na kusema hivyo.

"Eee. Namwambia dada yako tunywe supu, nimeleta nyingi, ila anataka kuwahi kazini..." Ankia akasema.

"Aaa, Mimi... kunywa tu hata bakuli moja. Sikumbuki mara ya mwisho tumekunywa supu pamoja..." Tesha akamwambia hivyo dada yake.

Ankia akatabasamu na kusema, "Ee bwana, hata bakuli moja tu. Ngoja nikaweke, sawa?"

Miryam akaonekana kutaka kumridhisha mdogo wake, hivyo akatikisa kichwa kukubali.

"Haya twendeni jamani. JC... njoo," Ankia akaniita.

Nikatikisa kichwa kukubali, nami nikafata nyuma yao wote mpaka hapo sebuleni.

Hakukuwa na ile hali changamfu sana iliyozoeleka kutokana na uwepo wa Tesha, kwa sababu wakati huu alikuwa chini ya mvurugo wa kihisia. Angalau Ankia angeongea kwa njia nyepesi ili kurudisha hali iliyosawazika zaidi kwa sehemu hiyo. Kulikuwa na hotpot mezani na mfuko wenye kitu kwa ndani, naye Ankia akawa ameleta sahani ya udongo na mabakuli manne pamoja na vijiko.

Kwenye ule mfuko akatoa chapati sita za kusukumwa na kuziweka kwenye sahani, akisema ndizo zilizofanya akakawia kiasi kwa sababu ya kuhitaji kusubiri. Akaweka na supu kwenye mabakuli, nyama zikiwa zile zifananazo na maini (wanaita mapupu), naye akatusogezea kila mtu sehemu yake na kumsisitizia Miryam anywe na kula chapati.

Nilikuwa namwangalia mwanamke huyo na kuona namna alivyojitahidi kusitiri hisia zake. Kuna kitu kilichokuwa kinaisumbua nafsi yangu kutokana na kushindwa kumwambia maneno yenye kufariji alipokuwa anajilaumu kwa sababu ya matatizo yaliyokuwa yanatokea kwenye familia yake.

Hii ndiyo iliyokuwa mara ya pili kwangu kuweka ukaribu wa namna hiyo kwa huyu mwanamke, yaani vile nilivyombembeleza kidogo akiwa amenilalia begani, nikiwa nakumbukia mara ya kwanza aliponikumbatia kwa kutoa shukrani ya moyoni nilipomsaidia mdogo wake. Nilihisi kama ningeweza kujiweka karibu naye zaidi ili tushirikishane katika mambo yenye kujenga zaidi, lakini tatizo alikuwa wa kivyake mno.

Tukawa tunakunywa thupu, taratibu tu, naye Tesha akawa anasimulia kwa wanawake jinsi alivyojikuta anakabwa na vibaka na kuibiwa simu; bila kuongelea masuala ya wanawake aliokutana nao bar lakini. Akatania kwa kusema alitaka kurudi huko leo na kisu ili akawatafute hao vibaka, nasi tukamwambia awe mwangalifu kisije kikageuziwa kwake.

Kwa hiyo maongezi hapo yalikuwa mepesi tu mpaka tulipomaliza supu, Miryam na mimi tu ndiyo tukiwa tumekula chapati moja moja, kisha yeye na mdogo wake wakatuaga na kuelekea kwao. Tesha alikuwa anataka kwenda kuuweka mwili wake sawa zaidi ili baadaye nimsindikize kwenda kituo cha polisi kuangalia suala lake la simu, nami nilikuwa nimemwambia haina tatizo.

Bila shaka, wawili hao wangeenda kujaribu kuweka hali vizuri zaidi pale kwao, lakini bado nilikuwa na hofu kuelekea suala la huyo Joshua. Sikutaka kuwachanganyia habari kwa kuwaambia mambo niliyosikia huyo mjinga akisema, maana najua ningeizidisha tu hofu ya Miryam kutokana na vitu ambavyo mdogo wake angeweza kufanya.

Kwa sasa ingekuwa busara kutulia tu, lakini ningehakikisha nakuwa makini ili kuiepusha familia hiyo kutoka kwenye matatizo ambayo Joshua alitaka kuyaendeleza; hasa kumlinda Mariam.

★★

Muda mfupi baada ya Miryam na Tesha kuwa wameondoka hapa kwa Ankia, nikawa nimefanya usafi wa chumba na mwili, kisha nikavaa vizuri ili niweze kwenda pale kwao kushughulika na binti Mariam.

Ni leo ndiyo nilitaka kumpa Ankia hela ya kodi kwa ajili ya mwezi uliofuata, basi tu yaani ili wiki ambazo zingefuata nisiwaze kabisa kuhusu hilo suala. Nilipotazama matumizi yangu ya pesa za pembeni toka nimekuja mapumziko, nikaona nilikuwa nimetafuna nyingi kiasi, lakini hakukuwa na shida sana juu ya hilo.

Baada ya kupangilia mambo vyema, nikamfata Ankia na kumpatia pesa. Kama kawaida yake, alianza kujishaua mara JC mbona hivi, mbona vile, nami nikalazimisha azichukue na kumwambia akate mashauzi yake. Nikamuaga baada ya hapo, nikisema ndiyo naenda kwenye wajibu wangu wa kidaktari, nami nikaelekea mpaka kwa jirani yetu.

Tesha akawa amekuja kunifungulia geti, naye akasema kitu ambacho hata Bi Zawadi aliwahi kuniambia mapema sana kuhusu geti hilo. Ni kwamba kama mlango mdogo wa geti ungekuwa unaweza kufungukia kwa nje basi ningekuwa naingia tu badala ya kusumbuka kupiga hodi, hivyo nikaona nisaidie kuirekebisha hali hiyo kidogo.

Nikamwomba Tesha atafute kamba nyembamba, msumari, na nyundo ikiwezekana ili tujigeuze mafundi hapo. Akatii na kufata kamba nyembamba iliyoendana na zile walizoweka hapo nje kwa ajili ya kuanikia nguo, msumari mrefu, lakini hakukuwa na nyundo. Akaleta tu jiwe.

Nikaikata kamba hiyo kwa urefu uliotoshea upana wa kimlango hicho, kisha nikaifunga kwenye kale kadude ka kuvuta kwenye kifungio cha geti na kuipitisha nje kupitia uwazi mdogo mwanzoni mwa ukuta ambapo geti lilianzia. Nikatoka nje na kuugonga msumari ukutani, mwanzoni kabisa karibu na geti, kisha nikaifunga kamba hapo.

Tukaanza kufanya majaribio kwa kufunga kimlamgo cha geti, kisha naivuta kamba kiasi nikiwa kwa nje ili ikikivuta kile kidude kwa ndani, kiachie, na huo mlango ukafunguka. Akili mtu wangu! Ilikuwa ni njia ndogo tu ya kurahisisha kazi kwa sisi tuliozoea kuja hapo, naye Tesha akasema ilikuwa ni njia nzuri sema aliona uvivu tu kushughulika na geti hilo.

Nikaingia tena, na wakati huu ndiyo nikatilia maanani kuwa gari la Miryam halikuwepo, kumaanisha alikuwa ameshakwenda kazini. Nikamuuliza Tesha hali kwa sasa ilikuwaje, naye akaniambia tu twende ndani ili tukaongelee huko.

Kweli tukaenda, nami nikakuta hali isivyo kawaida na nilivyokuwa nimezoea. Sikuwakuta Bi Jamila na Bi Zawadi wakiwa wamekaa kwenye sofa lao kama kawaida, na sikumwona Mariam pia. Nikadhani labda wapo chumbani maana kulikuwa na hali ya utupu hapo.

Tukakaa na Tesha sofani, nami nikamuuliza, "Mariam yuko poa?"

"Eeh, ila ndo' hayupo. Wote hawapo," akasema hivyo.

"Wapi tena?"

"Da' Mimi kawachukua kuwapeleka kwa Joshua. Wakaongee huko," akasema hivyo kwa njia ya kukerwa.

Nikamwangalia kwa umakini na kuuliza, "Kampeleka Mariam kwa Joshua?"

"Ndo' maana yake."

"Lakini si Miryam amesema anaenda kazini?"

"Ndiyo, kawapeleka huko wote na mama wakubwa, halafu ataenda kazini... labda na baadaye ataenda tena huko... kuwafata."

"Mbona we' hujaenda?"

"Kwani haiko wazi? Sitaki tu. Lakini nimesingizia kwa dada kwamba sijisikii fresh bado. Hapo wanaenda kudanganywa-danganywa tu na huyo fala."

"Aisee! Yaani akimgusa Mamu, atanitambua," nikajikuta nimesema hivyo kwa hasira.

"Nini? Nani, Joshua? Anataka kumuumiza Mamu?" Tesha akaniuliza hivyo kwa mkazo.

Nikamwangalia na kusema, "Aa... hapana, yaani namaanisha... hali ya Mariam siyo nzuri kivile bado, ikiwa ataogopeshwa sana na kaka yako itakuwa kurudi nyuma tena. Nimeongea tu vibaya."

"Siyo vibaya, me mwenyewe nitamuua huyo mjinga ikiwa Mamu atarudi hapa bila unywele hata mmoja. Sema ndiyo nimemwahidi dada kuwa mpole, kwa hiyo natulia tu."

"Ila ungeenda nao Tesha, huwezi kujua," nikasisitiza.

"Usiogope bro. Me najua Joshua anachokifanya hapa mwanzoni ni kuigiza tu, kwa hiyo lazima na mimi niigize pia. Hawezi kumgusa mtu yeyote sa'hivi, utaona," akanihakikishia.

Nikaangalia pembeni nikiwa nimeudhika kiasi. Sikujua nifanye nini maana hali hii ilikuwa ya kushtukiza, na hii ikanipa somo kuhusu kuwa chonjo zaidi na hii familia ili Joshua asije kufanikiwa kwenye mipango yake, mimi nikabaki tu mdomo wazi.

"Wanarudi saa ngapi?" nikamuuliza hivyo.

"Jioni. Hapa doro tu kaka. Nataka nikazurure wee mpaka hiyo jioni," akaniambia hivyo.

Nikatulia tu na kushusha pumzi.

"Oy... kama vipi tuoshe, ama nini?" akaniuliza.

"Kuelekea wapi?"

"Nataka nikazunguke Kigamboni leo. Halafu baadaye tutazamia kwa mshkaji fulani hivi, nina siku sijamwona. Unasemaje?" akasema hivyo.

Lengo la kuja hapa ilikuwa kuendelea na mazoezi yangu pamoja na Mariam, lakini hakuwepo. Sikuwa na jambo lingine muhimu la kufanya kwa hiyo nikaona nimkubalie tu rafiki yangu. Labda na matembezi yangeleta jambo jipya mbali na yale niliyokuwa natazamia yafike.

Alikuwa ameshaoga kwa hiyo nikakaa kumsubiri alipokwenda kuvaa. Alivalia kawaida tu kama mimi, na kofia yake kama kibandiko kichwani ikanifanya na mimi nitake kwenda kuichukua ya kwangu, lakini nikaahirisha.

Tukatoka pamoja, akafunga milango na geti, nasi tukaenda kwa Ankia ili Tesha amwachie funguo za kwao ili endapo kama ndugu zake wangewahi kurudi kabla yake basi wazikute hapo. Ankia akatutakia matembezi mema huku akisema tukirudi tumletee zawadi, nasi tukaingia barabarani baada ya hayo.

★★

Basi, tukawa tunatembea mdogo mdogo kuelekea Mzinga. Baada ya kufika Mzinga, kibishoo tu yaani, tukaamua kuifata Kongowe kwa kutembea pia. Mwendo wa taratibu tu, huku tukipeana story nyingi za mambo yetu wanaume ukatufikisha mpaka hapo Kongowe, na hii ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika eneo hilo tokea nimepajua Mzinga; na hata Mbagala pia.

Mwanzoni mwa eneo hilo kunakuwa na sehemu nyingi zenye biashara ndogo na kubwa za wajasiriamali sanasana, nasi tukaelekea upande ambao daladala zingesimama kwa ajili ya kubeba abiria. Tukakuta moja ambayo ilikuwa ikielekea Kigamboni ndiyo, nasi tukaingia na kukaa siti za nyuma kabisa. Mwonekano wangu na Tesha ungefanya watu wafikiri sisi ni ndugu wa damu labda, maana kuna sehemu kubwa ya pigo zetu iliyokuwa inafanana sana.

Tukiwa tu ndiyo tumekaa, Tesha siti ya dirishani kabisa na mimi pembeni yake, nikapokea ujumbe kutoka kwa mtu ambaye sikuwa nimetarajia kabisa kwa muda huu. Ilikuwa ni Adelina, dada mkubwa wa Joy; ama niseme marehemu Joy.

Yaani tokea tumebadilishana namba pale msibani sikuwahi kumtumia salamu hata mara moja, ijapokuwa nilikuwa kwenye harakati za kumtafutia mdogo wake haki kwa mauaji yaliyomsibu. Alikuwa ametuma salamu fupi, 'habari yako,' nami nikatuma jibu kuwa 'niko salama' na kuuliza yeye aliendeleaje.

Nikaanza kumsikia konda kutokea nje akisema kwa abiria fulani waingie kukaa, kwamba siti hazikuwa zimeisha. Yaani alikuwa anawashawishi kwa kusema tena kuna waarabu ma-handsome wamekaa huko mwishoni, na ndiyo Tesha akanishtua nitazame nje.

Nikaangalia kupitia kioo na kuona wanawake wawili pamoja na mwanaume kijana mmoja, wote wakiwa ni waislamu, na mwanamke mmoja alivalia yale manguo meusi yanayoficha mpaka uso kasoro macho, lakini kale kengine uso ulikuwa wazi tu na kuzungukiwa kwa hijab kichwani. Kalikuwa kembamba, keupe, kenye macho mazuri kweli, na nahisi wao walikuwa waarabu kasoro huyo mwanaume kijana aliyekuwa mweusi kabisa; akionekana kuwa mwandamani wao.

Huyo mwanamke aliyeficha uso alikuwa kama hataki kuingia kwa kuwa labda hakupenda kukaa mwishoni, naye Tesha akawa ananishurutisha tufanye jambo ili hako kadada kaingie maana alikuwa amekaelewa tayari. Adelina akawa amenitumia ujumbe akisema yuko poa na kuuliza kama bado nilikuwa Mbagala, naye Tesha akaendelea kunibonyeza-bonyeza mpaka nikahisi kero.

Agh, nikasogea kufikia uwazi wa kioo na kuwaangalia wanawake hao, nami nikasema, "Dada, ingieni tu. Nafasi ziko tatu, yaani kama vile zimebaki kwa ajili yenu tu."

Mwanamke aliyekuwa amefunika mpaka uso akawa ananiangalia sana, naye konda akaongeza spidi ya kuwashawishi.

Nikakaa sawa tena na kumwambia Tesha, "Nimeweka jitihada hiyo kama ulivyotaka. Umefurahi?"

Akacheka kidogo na kusema, "We' ni chizi! Ndo' mpaka utuchoreshe? Ona washamba wanavyotuangalia."

"Unasumbua mno," nikamwambia hivyo nikiwa makini na simu.

Nikamjibu Adelina kwamba bado niko Mbagala ndiyo, na kumuuliza kama alisharudi Mbezi. Tesha akanibonyeza kidogo, nami nikaangalia mbele na kuona wale wanawake wameshapanda na kuja upande wa nyuma. Yule mwanaume kijana hakupanda, inawezekana labda alikuwa anawasindikiza tu, nao wakaja kukaa pamoja nasi; nafasi iliyobaki ikiwa imetutenganisha katikati.

Kale kadada kenyewe kakawa dirishani kabisa, huyo mficha uso akiwa pembeni yangu, nami nikamtazama Tesha na jamaa akajikausha tu kama vile siyo yeye aliyenisisitiza kuwashawishi waingie. Inaonekana kwa muda huu abiria waliokuwa wanataka kuelekea huko mbele walikuwa wachache, kwa sababu hakukuwa hata na mtu aliyesimama na safari ikaanza.

★★

Vuuu, mwendo ukaendelea huku na mimi nikiendelea kuchat na Adelina. Ilianza kidogo kidogo tu lakini mpaka ikafika hatua tukaanza kutaniana, kirafiki yaani. Akawa ameniambia kuwa kwa sasa hivi alikuwa amekwenda pale Mbagala kwa rafiki yake mmoja kumsalimia na ndiyo alifikiria uwezekano wa kupata nafasi ya kuja kunitembelea mimi na Ankia pale nyumbani.

Unajua, mpaka leo Adelina alikuwa anafikiri mimi ni mume wake Ankia, ndiyo ikabidi nimwambie kwamba ile ilikuwa danganya toto tu niliyofanya pamoja na Ankia; wala hata hakuwa mke wangu, na ndiyo matani baina yangu na Adelina yalianzia hapo.

Mwendo ulikuwa mrefu kiasi kuelekea Kigamboni, mara kwa mara watu wakiongezeka kwenye gari na kupungua, na uvumilivu ulikuwa unamshinda Tesha. Alitaka sana kuipata namba ya kale kadada keupe pembeni yetu, lakini alihofia kwamba huenda huyo mwanamke mwingine alikuwa mama yake kwa hiyo kungekuwa na utata.

Lakini akawa ananishawishi kwa kunitumia sms nijaribu kumsemesha maana alikuwa na uhakika kwamba mwanamke huyo aliingia tu kwenye gari kwa sababu yangu, nami nikamwambia Tesha aache umalaya la sivyo ungekuja kumuua siku moja.

Kama ninavyosemaga, mimi siyo mtu wa kuogopa mtu kabisa, na kama ningekuwa nataka kupata namba za mwanamke yeyote niliyekutana naye, ningezipata. Ila kuanza kumwelezea Tesha kwamba nilikuwa sitaki tu najua ingegonga mwamba, na hata hivyo nilikuwa nataka rafiki yangu huyu ajisikie vizuri tu baada ya mambo yote aliyokuwa amepitia jana, kwa hiyo nikamwambia atulie ili nimrekebishie mitambo.

Adelina bado nilikuwa nachat naye, akiwa amesema kwamba anaweza hata akaja leo kunitembelea mimi na Ankia pale nyumbani, nami nikaona nimjibu kwanza. Nikamwandikia kuwa kwa sasa nilielekea Kigamboni kwa hiyo endapo kama alikuwa na mpango wa kwenda kwa Ankia muda huu, asingenikuta, lakini labda kama ni jioni ndiyo tungeweza kuonana.

Ilishangaza kiasi kwamba hakuwa hata amemtafuta Ankia bado kuongelea suala la kwenda kumtembelea ilhali walikuwa ni marafiki, lakini labda ni kwa sababu tu hakuwa amewahi kuwasiliana nami kabisa, na kule kudhani mimi ndiyo kichwa sasa pale kwa Ankia.

Nilipomaliza kumweleza, nikamtazama mwanamke yule mwislamu. Hilo baibui jeusi alilovaa lilificha uzuri wa ngozi nyeupe aliokuwa nao, maana nilitazama vidole vyake vyenye kucha ndefu kidogo na nyekundu, vilivyoshikilia simu ya macho matatu, na kiuhakika nikaona kwamba havikuwa na hata chembe ndogo ya sugu nyeusi. Sijui walikuwa waarabu kweli?

Tesha akanibonyeza tena na kunipa ishara kwamba eti nichangamke, nami nikatabasamu kiasi na kufungua simu yangu tena upande wa sms.

Nikaandika pale patupu hivi, 'Habari? Naomba namb yako kam hutojal'

Nikanyoosha simu kwa chini kumwelekea mwanamke huyo, naye akaitazama. Sikuwa hata nikimwangalia lakini nikamwona akinyanyua uso wake kuniangalia, hivyo na mimi nikamwangalia. Huwa naweza kuweka macho fulani hivi ya kumvuta mwanamke aamshe upendezi kunielekea, macho ya ushawishi yaani, nami nikawa namtazama kwa hiyo njia.

Akaangalia mbele tu kama vile hataki, kisha akaichukua simu yangu kichinichini na kuiunganisha na yake. Nilikuwa nimeweka uso makini, nikiona wazi jinsi Tesha alivyojikausha kwa kujifanya anatazama nje tu, na kwa jicho la mbali nikaweza kuona mwanamke huyo anaandika kitu fulani kwenye simu yangu.

Kisha, akaitelezesha simu kwenye hiyo siti kuelekea upande wangu bila kuitazama, kukiwa na pete nene zenye kuonekana kuwa kama za dhahabu kwenye vidole vyake viwili, nami nikaipokea nikiwa nimeweka mwonekano makini bado. Mambo ya siri hayo, na Tesha ndiyo akawa ameniingiza majaribuni!

Wanawake wa hivi nawaelewa sana, yaani wanapoamuaga kujitafutia vitulizo vya nje huwa wanapenda mno usiri wa hali ya juu, na huyu inaonekana alikuwa amenielewa sana ndiyo maana akakubali kufanya hivyo akiwa pembeni ya binti yake, sijui mdogo wake, sikujua.

Tesha akakunja ngumi yake karibu na paja langu, akiwa anataka tugonge tano ya ushindi, nami nikaweka kiganja changu hapo huku nikimnyanyulia kidole cha kati. Nikatazama simu yangu na kukuta namba za simu zikiwa zimeandikwa hapo, nami nikazitumia ujumbe.

'Jina lako mremb?'

Nikajikausha kama simwangalii, nami nikaona anaandika kitu fulani kwenye simu yake kisha akatazama pembeni.

Ujumbe ukaingia kwenye simu yangu, namba hiyo hiyo, ukisomeka, 'niambie lako na wew.'

Nikajibu, 'JC'

'Ndiyo nn'

'Ndiyo my name'

'Me naitw Ibtisam'

'Ooh saw. Jina lako zur kam wew mremb'

'Uremb wang umeon wp'

Nikiwa bado sijajibu ujumbe wake huo ndiyo tukawa tumeingia maegesho ya daladala kwenye eneo la Kigamboni, na watu wakawa wanasimama ili washuke.

Nikamwandikia hivi, 'Ngj tushuke nikwambie'

Kweli tukaanza kushuka mpaka nje, nami pamoja na Tesha tukaenda upande wa nyuma wa gari na kuwaangalia wanawake hao waislamu. Wenyewe wakaelekea upande mwingine kwa pamoja, huku kale kembamba kakigeuka kututazama mara moja.

Nikaangalia simu na kukuta ujumbe wa huyo mwanamke akiwa amejibu, 'Saw, lkn ntakuchek badae. Kun shm naend sahiv'

Tesha akaniuliza, "Oy, umemwambiaje? Anasemaje?"

"Kaka utakuja kuniweka matatizoni siku moja!" nikamwambia hivyo.

Tukaanza kutembea kuelekea sehemu iliyoturuhusu kuiona vyema Bahari ya Hindi.

"Kwani vipi?" akaniuliza.

"We' kila demu unataka tu, wengine ni majini."

"Ahahahah... me kwani nilikwambia namtaka huyo jini wako? Mimi nilikuwa nakataka kale kengine, we' si umechukua namba ya huyo maza'ake kwa upendo wako?"

"Nimeomba namba yake ili uje kuipata ya hako unakokataka. Halafu Tesha!"

"Hahahah... JC bana! Kwo' jini linasemaje?"

"Atanicheki baadaye, na linaonekana limeolewa. Ah, sijui hata kwa nini nimemwomba namba!"

"Si kwa ajili yangu? We' ukishamzuzua utanifanyia unyama na mimi nipate ya hako kengine. We' utakula mazeli, mimi kimweli. Tena tutafanyia kwenye double deka kabisa."

Nikacheka kidogo tu na kusema, "Tesha tunaingia Kigamboni, wanawake wazuri kama wote, utawasahau hao uliowaona. Tulia mdogo wangu."

"Ah, kwenda huko! Huu ndiyo wakati wangu, we' ushazeeka ndo' maana. Twende tukapande meli huko."

Nikacheka na kutikisa kichwa, nami kweli nikaanza kumfata.

Tukapita sehemu nyingi zenye biashara, watu wengi, wadada wazuri ndiyo usiseme, nasi tukaelekea sehemu ya kununulia kadi za tiketi kwa ajili ya kuvuka bahari kwenda upande wa pili wa Kigamboni; ule wenye majengo ya ukweli. Tesha akapata kadi, nasi tukaenda kuvuka kwa kupanda meli ndogo ya uvukishaji abiria na magari. Watu walikuwa wengi kufikia kiasi kilichohitajika, na wakati tukiwa tumeanza kuvuka mvua ikaanza kunyesha.

Mpango ulikuwa kwenda kuzurura sehemu kadha wa kadha kwa eneo hilo, lakini mvua ikaongezeka mno kiasi kwamba jambo hilo likaingiwa na utata. Yaani ile tumeshuka tu, ikatubidi tuingie kwenye daladala ambazo zilielekea Kariakoo, na safari ikaanza tena. Hii haikuwa mara ya kwanza kutembelea Kigamboni na hata niliwahi kutoka na mwanamke fulani aliyekuwa wa pande hizi, ila hiyo ni hadithi nyingine, ya kusimuliwa kwa wakati mwingine.

★★

Mwendo wa dakika kadhaa ukatufikisha mpaka Kariakoo, na kwa huku mvua ilikuwa ishakatika. Tukashuka, Tesha akiwa bado anawashwa kutembea, hivyo tukachukua mwendokasi na kwenda pande za Ubungo. Tukazurura wee, Tesha hata akanipitisha kule alikokuwa anaenda kufata wanawake wa kulipwa, chimboni yaani, naye akawa akisema hizo mishe siku hizi hafanyi.

Tukatoka huko na kuzunguka mpaka Uhasibu, nasi tukashukia hapo. Tesha alikuwa na rafiki yake mwanachuo aliyekaa eneo la Uwanja wa Benjamin Mkapa, hivyo tukatembea mdogo mdogo kuelekea huko. Alikuwa ameshawasiliana naye. Yaani safari hii yote leo ilikuwa ni kwa udhamini wa Tesha, mimi ndiyo nilikuwa kama mtalii wake, nasi tulipokuwa tu ndiyo tumeyapita malango ya uwanja nikaanza kuona mdada fulani akija upande wetu taratibu.

Tesha alikuwa ameniambia kwamba tunaenda kumsalimia tu mshkaji wake, kwa hiyo sikuwa nimetarajia kwamba ingekuwa ni mwanamke mpaka mdada huyo alipotukaribia na kukumbatiana na Tesha kirafiki. Alikuwa mfupi kiasi, mweusi, mwili wa kawaida tu, na tabasamu lake lilionyesha mwanya mdogo katikati ya meno yake ya mbele.

Wakawa wanasemeshana kirafiki sana, naye akaniangalia na kunisalimu pia. Alikuwa mchangamfu sana, jina lake ikiwa ni Dina, naye akatuongoza kuelekea pale alipoishi. Ilikuwa ni kwenye zile nyumba za wapangaji zilizojaa hasa wanafunzi wa chuo, nasi tukaingia kwenye chumba chake.

Kilikuwa simple tu, safi, godoro chini kwenye sakafu ya vigae, friji ndogo, begi la nguo pembeni ya shehena ndogo ya vyombo, vifaa vya mapodozi na manukato, viti vitatu vya plastiki. Jiko dogo la gesi lilibeba sufuria lenye chakula kwa ndani bila shaka, nasi tukakaa na kuanza kupiga story.

Mimi nilikaa kwenye kiti, Tesha na Dina wakakaa kwenye godoro, na ni wao sanasana ndiyo walioongea huku mimi nikichangia mada mara moja moja kukoleza ucheshi. Dina akaniuliza natumia soda gani, nami nikamwambia Pepsi. Tesha vilevile akasema Pepsi ingawa alitania kutaka bia.

Dina akatoka kwenda kufata soda, nasi tukabaki hapo, nikisikiliza maneno ya kipuuzi ya Tesha kuhusu jinsi nilivyotakiwa kubaki hapa leo ili nifanye jambo fulani na Dina. Ni hapa ndiyo nikawa nimepokea ujumbe kutoka kwa yule mwanamke mwislamu tuliyekutana kwenye daladala, akiwa ametuma tu 'mambo,' nami kabla hata sijamjibu, simu yangu ikaanza kuita. Mpigaji? Bertha. Hatimaye!

Sikutaka Tesha asikie jambo lolote ambalo lingemfanya atambue nani naongea naye, hivyo nikapokea nikiwa nimejihakikishia kutosema lolote litakalomshtua jamaa.

"Hallo?" sauti yake Bertha ikasikika.

"Hello, vipi?" nikasema hivyo.

"Poa. Uko wapi?"

"Niko kwa Mkapa hapa."

"Unafanyeje huko?"

"Nimekuja kwa mshkaji wangu, niambie..."

Tesha akaniuliza kwa ishara, "nani?" nami nikamwonyesha ishara pia kuwa atulie.

"Nataka uje. Au biashara uliyonayo sasa hivi huko ni muhimu sana?"

"Hakuna chochote muhimu zaidi yako dear."

"Usiniite dear, mazoea ya hivyo sitaki."

"Sawa dear," nikasema hivyo makusudi.

"Halafu wewe!" akasikika kwa ukali.

Nikajikaza nisicheke na kumwambia, "Pole, nimejikwaa tu. Ulimi hauna mfupa."

"Na nitakuja kuuwekea mfupa usipoangalia."

"Sorry."

"Toka huko sasa hivi. Niko Masai," akaniambia hivyo.

Ni muda huu ndiyo Dina akawa ameingia ndani tena, lakini wakati huu alikuwa pamoja na mwanadada mwingine mweupe, mwembamba, mrefu kiasi, aliyekuwa amevalia T-shirt nyeusi na suruali ya jeans ya samawati iliyobana. Nywele zake zilisukwa kwa mtindo wa dread nyeusi na fupi, naye akaenda kukaa godoroni baada ya Tesha kunyanyuka na kukaa kwenye kiti.

"Umeelewa?" Bertha akasikika kwenye simu.

Nikasema, "Eeh, nimeelewa. Ila... niko mbali kama hivi, naweza kuchelewa kidogo."

Dina akawa ametufungulia soda zetu na kutupatia, na ukimya mfupi uliofuata kwenye simu ukanifanya nitambue kwamba Bertha alikuwa amekasirishwa na maneno yangu.

Nikamwambia, "Ila nakuja. Nitakuwa nimeshafika muda siyo mrefu."

Likakata simu!

Kazi nilikuwa nayo. Nikashusha pumzi na kumwangalia Tesha, aliyekuwa akinitazama kama anasubiri nijielezee.

"Kuna dharura bro. Natakiwa nifike location mara moja," nikamwambia hivyo.

"Tumekuja wote, unataka kuondokaje mwenyewe bana?" Tesha akaniuliza kwa uthabiti.

"Iih, unataka kutukimbia?" Dina akaniuliza hivyo.

"Kuna dharura imetokea, nahitajika sehemu haraka ndo' maana..."

"Acha bangi! Hautoki hapa. Keki tamu kama hizi unakimbia kweli?" Tesha akasema hivyo kiutani.

Tukacheka kidogo, na Dina akamsonta huku akisema, "Afu' wewe!"

"Inanibidi tu kaka," nikamwambia Tesha.

"Jamani, mbona ghafla? Chakula hiki napakua," akasema Dina.

"Oh usijali Dina, niko poa. Labda umpakulie huyu mbwa," nikamwambia hivyo.

Akacheka kidogo, naye Tesha akasema, "Em' pakua mama, tule."

"Basi kunywa hata soda, imeshafunguliwa," akaniambia hivyo yule mdada mwingine.

"Ee, kunywa soda ndiyo uende kaka," Dina akaniambia.

"Poa," nikajibu.

Ingenibidi nipige hii soda fasta maana huyo Bertha hakuwa mtu wa subira hata kidogo, na hiki ni kitu ambacho nilikuwa nimekisubiria sana kwa hiyo wiki nzima kwa hiyo nisingeweza kuchezea nafasi hata kama ningepewa ofa ya utatu na hawa wadada!

Nikawa napiga fundo ndefu ndefu, huku nikiwa nimeanza kuchat na yule mwanamke mwislamu pia. Alikuwa mmoja kati ya wale wanawake ambao walipenda mtu aende moja kwa moja kwenye pointi ya kitu ambacho alitaka kutoka kwake, nami nikamwambia ndiyo, nilimkubali sana kutokana na kupenda macho yake na ngozi yake.

Akaniambia ooh nimeshaolewa, kwa hiyo ukinitaka lazima upande ngazi, nami nikamwambia hakuna ngazi za kupanda; ikiwa alinikubali pia basi tuje kucheza, lakini asipotaka basi sitalazimisha. Kwa kauli hiyo akawa ametulia kwanza, nami nikawa nimemaliza soda.

Nikamshukuru Dina na kusimama, Tesha bado akiwa analalama kuhusu mimi kuondoka, hivyo ikanibidi nitoe ahadi ya kuja naye tena kesho ikiwezekana kumtembelea rafiki yetu. Dina alipenda sana hilo wazo na kusisitiza nisije kuacha kuja, nami nikamwambia aondoe shaka. Huyo rafiki yake mwingine alikuwa akiniangalia sana kwa sura yake ya kiupole, nami nikamuaga pia nikiwa hata simjui jina.

Nikawaacha marafiki hao hapo na kuanza kuelekea barabarani, nikiwa natumaini kuwahi, na Tesha asijue kwamba sehemu niliyokwenda ilikuwa ni Masai. Angeshangaa sana!

★★

Nilifanikiwa kupata usafiri wa daladala zilizoelekea Mbagala, na mpaka kufikia huko tayari ilikuwa inaelekea kuingia saa moja. Nilikuwa nikijiuliza ni kwa nini madam Bertha alikuwa ameamua kuja Masai mapema sana leo, lakini hayo yote ningeyajua nikishafika pale.

Badala ya kuchukua daladala tena kutokea Rangi Tatu, nikaamua kupanda bodaboda ili niwahi zaidi, brrrr mpaka Mzinga, nami nikaunganisha moja kwa moja kufikia Masai, lakini nikaona nielekee kwa Ankia kwanza.

Nikafika hapo dukani kwa Fatuma na kumkuta huyo dada pamoja na wanawake wengine wengine wakiwa wamekaa kama kikundi cha kupiga umbeya, nami nikamwambia bodaboda anisubirie nikachukue mzigo ndani kisha anirudishe Masai upesi. Nikawapita hao wavaa dera kama siwaoni, nami nikaelekea mpaka ndani na kuingia.

Akili yangu ilikuwa imekazia fikira jambo moja tu kiasi kwamba mpaka nikashtuka kiasi moyoni baada ya kuingia na kumkuta Ankia akiwa amekaa pamoja na Adelina! Ile hali ya kutotegemea kumkuta mwanamke huyu hapa ingawa tulikuwa tumewasiliana ilikuwepo yaani, halafu nilikuwa kwenye kasi kwelikweli.

Wawili hao, baada ya kuniona, wakatabasamu kwa pamoja, nami nikatabasamu pia na kusogea karibu zaidi na walipokaa.

"Mume amerudi," Adelina akasema hivyo.

"Ee, baba mwenye nyumba ndiyo kafika," Ankia akasema hivyo pia.

Nikajikuta tu natenda bila kufikiri sana kwa kuinama na kumkumbatia Adelina, nami nikamwambia, "Karibu."

Nafikiri alikuwa ameshangaa kiasi lakini akaweza kucheka kidogo kwa pumzi, naye akasema, "Asante."

Nikamwachia na kusema tena, "Karibu sana."

Kisha nikaelekea chumbani, bila shaka nikiwaacha wanawake hao wanatazama haraka yangu.

Nikaingia chumbani na kutoa yale madawa niliyotengeneza, nami nikachukua kiasi kidogo na kukiweka kwenye karatasi tu baada ya kuwa nimekosa pa kuwekea, kwa kuwa sehemu niliyohifadhia dawa yote ilikuwa ndani ya mifuko minene; madawa yakionekana kama glucose. Nikachomeka hicho kikaratasi mfukoni, kisha nikaelekea sebuleni tena.

"Unatoka?" Ankia akauliza hivyo.

"Ndiyo, kuna sehemu nafika mara moja lakini... sikawii, nakuja. Sawa?" nikaongea hivyo nikiwa nimeelekeza fikira zangu kwa Adelina.

Akatikisa kichwa kukubali, naye Ankia akasema, "Unawahi nini kinachokutoa kijasho hivyo? Tuambiane..."

"Utajua tu, ngoja nirudi," nikasema hivyo na kuelekea mlango.

Nikawaacha wanawake hao wakicheka kidogo, nami nikaenda mpaka nje tena. Nikapanda bodaboda na kugeuza kuirudia Masai, nasi tukafika hapo huku sasa giza likiwa limeshaingia. Nikamlipa jamaa na kumwambia atokomee, kisha nikaelekea pale ndani.

Wanywaji walikuwepo na nafikiri kuna wahudumu wapya waliokuwa wameongezwa hapa na wachache niliowajua kuondoka, nami nikawa nimemwona Bobo pamoja na DJ fulani hivi wa hapo Masai. Nikamfata.

"Oyo, mchina..." akaniambia hivyo tukiwa tunagonganisha mabega yetu kirafiki.

Nikagongesha tano kwa yule DJ pia, kisha nikamwambia Bobo, "Oya umepotea kweli."

"Ah, mimi, wewe? Yaani hutokei Masai siku hizi mwanangu. Check watu wanavyokuangalia kama vile hujawahi kuonwa hapa," akasema hivyo.

Nikatabasamu na kusema, "Na mimi nimetingwa kaka, ila mdogo mdogo narudi. Ishu zinakwendaje?"

"Kama kawa budha. Oy... mtu wako yupo huko ndani," akaniambia hivyo kwa kuninong'onezea sikioni.

"Eeh, nimeona gari nje," nikamwambia.

"Yuko VIP, kamchangamkie..."

"Ndo' mpango mzima," nikasema hivyo.

Tukacheka tena pamoja, kisha nikamwacha hapo na kuelekea pande ya VIP. Na Bobo alikuwa sahihi kabisa, watu walikuwa wananiangalia kweli, lakini umakini wangu wote ulikuwa kumfikia huyo madam.

Nilipofika mlangoni, nikajiwekea hali ya utulivu, kisha nikaingia ndani hapo. Nikamkuta madam Bertha akiwa amekaa sofani, glasi yenye wine kiganjani, na kwenye sofa la pembeni alikaa yule baunsa wake; a.k.a shemeji.

Kama kawaida ya mwanamke huyo, alikuwa amependeza kwa kuvaa kigauni kifupi chekundu, kilichoyaacha mapaja yake meupe wazi kutokana na namna alivyokuwa amepiga nne, na inaonekana kilikuwa cha mgongo wazi. Wakati huu alishonea wigi la nywele za kizungu kichwani, na baunsa wake alikuwa amevaa kaushi tu na suruali nyeusi, akionyesha misuli yake imara.

Nikasogea usawa wa meza moja hapo, nami nikamtikisia kichwa jamaa kama salamu, naye akairudisha. Nikamwangalia Bertha, ambaye alikuwa akinitazama tu kwa utulivu, nami nikamwambia, "Nimefika madam."

"Umechelewa," akaniambia hivyo.

"Kweli? Mbona naona kama bado party haijaanza?" nikamuuliza hivyo.

Baunsa wake akamwangalia na kucheka kidogo, naye Bertha akawa amenikazia macho yake.

"Tupishe," Bertha akamwambia hivyo jamaa.

Baunsa akasimama na kuja upande wangu, naye akaniuliza, "Una ule unyama jembe?"

"Nakosaje labda?" nikamuuliza hivyo.

Akatabasamu huku akitikisa kichwa taratibu, nami nikaitoa ile dawa na kumfungulia.

"Si iko kama ile?" akaniuliza hivyo.

"Kwa asilimia zote," nikamwambia.

Akachovya kwa kidole na kulamba, kisha akatikisa kichwa kwa nguvu kiasi na kunishika begani. "We' dogo ni nyoko!" akaniambia hivyo.

Nikatabasamu kidogo, naye akanipita na kutoka ndani humo.

Nikabaki na madam. Alikuwa ananitazama kwa yale macho ya kuhukumu bado, naye akasema, "Njoo."

Nikatii na kumfata. Sikuwa na hofu kumwelekea huyu mwanamke, ila kujifanya mnyenyekevu sana ilikuwa lazima. Nikasimama usawa wa sofa alilokalia na kubaki mtulivu.

"We' vipi, si ukae?" akaniambia hivyo.

Nikasogea na kukaa kwenye sofa karibu yake.

Akawa ananitazama sana, naye akasema, "Yaani hiyo sura! Kama mwanamke!"

Dah! Kashfa hizo.

Nikatabasamu kwa kujilazimisha na kusema, "Asante. Moja kati ya silaha zinazonisaidia kupita huku na kule ni hii sura."

Akacheka kwa mguno, kisha akaweka glasi yake pembeni.
"Nimekufatilia kwa hiyo wiki dogo, naona una maisha magumu sana mpaka ukaamua kutoka Goba Center kuja kuishi Mbagala," akaniambia hivyo.

Umeona sasa? Nilikuwa sahihi. Huyu mwanamke alikuwa amefanya uchunguzi kunihusu mpaka kujua kitu ambacho bado sijaelezea kujihusu. Nikataka kujua anaelewa mambo mengi kadiri gani kuhusu maisha yangu.

"Ahah... eeh... maisha magumu. Nimekaa sehemu nzuri lakini... hazijanifiti ndo' maana nimeangukia huku sasa hivi," nikaongea hivyo kiupole, ikiwa kimtego zaidi.

Akasema, "Me sijali ulikuwa unaishi vipi. Nataka tu ujue nikiamua kukuharibia maisha yako endapo kama utanigeuka basi sitosita kuanza hata na familia yako."

"Usiwe na hofu juu ya hilo madam. Siwezi kukusaliti. Kwanza... familia yangu iko Mwanza, mimi huku ni mtafutaji tu kwa hiyo niko mwenyewe," nikamdanganya.

"Una uhakika na kile ulichojiingiza kukifanya huku dogo?" akaniuliza.

"Ndiyo najua. Nina ujanja mwingi, usinichukulie poa. Sema mambo huko Goba hayakwenda fresh tu ndo' maana nikaja huku kujitafuta, na najua nimejipata tena kwa kuwa chini yako. Sitakuangusha madam. Najua nachokifanya, na nitafata utakachonielekeza kufanya," nikamwambia hivyo.

Akatulia kidogo, kisha akasema, "Sawa. Nipe hiyo kitu nionje."

Nikamfungulia kikaratasi chenye dawa ya cocaine, naye akachovya na kulamba kidole chake huku akinitazama kwa macho makini. Kidogo tu yakalegea naye akawa ananiangalia utadhani ananitaka kimapenzi. Ah mimi nilikuwa mtaalamu bwana!

Na angalau kufikia hapa nikawa nimetambua kwamba hakujua mengi zaidi kuhusu maisha yangu isipokuwa tu kuwa amefatilia na kujua nilikotokea kihalisi kabla ya kufika huku, kwa hiyo mchezo wangu kwake ungeendelea taratibu.

Vibe likiwa limemgonga, akaniambia, "Unyama mzuri huu."

Nikatabasamu kidogo.

"Kuna ishu nataka nikushirikishe," akasema hivyo.

Pasi ndefu hiyoo! Nikatikisa kichwa kuonyesha namsikiliza.

"Kesho utakuja pale pale ulipokuja siku ile, uje jioni," akasema hivyo.

"Sawa. Nije na unyama wetu?" nikamuuliza.

Akaweka macho ya udadisi, naye akauliza, "Unamaanisha kwamba unao mwingi?"

"Nimetengeneza kiasi fulani. Hakijazi mifuko mikubwa lakini si unajua ni tamu mno, kwa hiyo kidogo tu...."

"Ni nyingi," akamalizia maneno yangu.

Nikatikisa kichwa kukubali.

Akaninyooshea kidole chake na kunipiga kofi laini shavuni, naye akasema, "Safi sana. Kumbe we' kweli wa faida. Uje nao kesho. Nitakuelekeza mengine ukishafika."

"Imeisha hiyo," nikamwambia hivyo.

Akawa ananitazama kwa njia fulani utadhani alikuwa ananisoma, naye akasema, "Nataka kuona kama we' siyo mwanaume sura tu."

Nikamsogelea karibu zaidi na uso wake na kumuuliza, "Kivipi?"

"Kesho. Kesho ndiyo nitaona," akasema hivyo huku akipindisha shingo yake kiasi, midomo yetu ikiwa karibu sana.

Nikasema, "Ahaa... nilidhani unataka nikuonyeshe sasa hivi."

Akatabasamu na kuangalia chini, kisha akatoa tusi kunielekea bila kuniangalia.

Nikatabasamu pia baada ya kuona kwamba alikuwa ameanza kuonyesha roho ya kuniamini kiasi, na bila shaka ishu hiyo ya kesho ingehusiana na mengi ya vitu nilivyotaka kuhakikisha vinaporomoka kwa msaada wa askari Ramadhan. Ingebidi kusubiri kuona.

Akawa amekivuta kinywaji chake tena na kuikunjua miguu yake, naye akaniangalia usoni. "Kwa hiyo toka mpenzi wako amekufa, haujaingiza substitute?" akaniuliza hivyo.

Nikatazama chini kwa ufupi, nikielewa alimaanisha Joy.

"Oh, nimegusa pabaya? Mhm... inawezekana ulikuwa unampenda sana."

"Joy na mimi ilikuwa kama biashara tu. Wala hakukuwa na kitu tense kivile," nikamwambia.

"Mm? Unanidanganya mimi? Ahah... unajua bado natakiwa niwe mwangalifu sana juu yako maana inaweza ikawa unataka kumlipizia kisasi mpenzi wako," akasema hivyo.

Dah! Lina akili!

Nikatoa kicheko cha kujilazimisha na kusema, "Madam una vituko. Najua hauamini hilo kwa sababu tayari unaniamini mimi."

"Unajuaje?"

"Usingemwambia bodyguard wako atoke nje kama ungeamini naweza kukufanyia kitu kibaya. Hadi dawa nayotengeneza unakula, kama ingekuwa kukuua si ningewekea hata sumu?"

Akatulia kidogo akiniangalia kwa umakini, naye akasema, "Huwezi kuwa na uhakika sikuzote. Ndiyo maana bado nataka nikupime."

Nikaegamia sofa, huku nikimwangalia kizembe na kusema, "Fanya chochote madam... JC ni mali yako sasa hivi."

"Nhhaa... unanifurahisha. Bado akili yako ni ndogo sana."

Nikamshika kiunoni taratibu, naye akawa makini na kuniangalia machoni. "Ndiyo unifunze sasa. Mi' wa faida kweli," nikamwambia hivyo kwa sauti ya chini.

Akabaki kuniangalia tu huku akizungusha-zungusha kinywaji ndani ya glasi aliyoshika, na ni hapo ndiyo mlango wa kuingilia ndani humo ukasikika ukifunguka. Kwa sababu nilikuwa nimeupa mlango mgongo, nisingeweza kujua nani kaingia upesi, lakini nikaona macho yake Bertha yakimtazama aliyeingia kwa njia ya kukerwa.

Nikiwa nafikiri ni mhudumu labda au yule baunsa, nikageuka bila kuwa na utayari wa kumchukulia serious huyo mtu aliyeingia mpaka nilipojikuta nashangaa kiasi baada ya kuona ni Chalii Gonga mwenyewe!



★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!

★★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI

★★★★★★★★★★★★★★★★★


Nikiwa naendelea kumpa Miryam bembelezo kwa kusugua mkono na bega lake taratibu, mlango wa kuingilia hapo chumbani ukafunguka, nami nikatazama hapo na kumwona Ankia akiwa amesimama. Bila shaka ndiyo alikuwa amerudi, na inaonekana alikuja moja kwa moja mpaka humu chumbani kutuangalia mimi na Tesha, lakini akakuta niko na dada mtu.

Miryam akawa amemwona pia, naye akajitoa begani kwangu na kuanza kujifuta machozi kwa viganja vyake. Ankia alikuwa amesimama hapo mlangoni akitutazama kama vile anasubiri maelezo.

"Ndiyo umerudi?" nikamuuliza hivyo.

"Ee... ndiyo nimefika. Kila kitu kiko sawa jamani?" Ankia akauliza hivyo kwa kujali.

Miryam akasimama baada ya kujikausha machozi, nami nikasimama pia. Akasema, "Ndiyo, nimemwijia Tesha."

"Yuko wapi?" Ankia akamuuliza.

"Ameingia uani. Ngoja niende nikamsubiri hapo nje," Miryam akasema hivyo.

Nilikuwa namtazama tu kwa utulivu, naye akaanza kuelekea mlangoni lakini Ankia akamshika mkono kumzuia. Sote tukamtazama.

"Nime... nimeleta supu. Kaa basi tunywe pamoja na mdogo wako, eti?" Ankia akamwambia hivyo.

Miryam akasema, "Sitaweza Ankia. Naingia kazini, nataka nikajiandae. Ila Tesha anaweza kubaki, na...."

"Ankia umerudi?" Tesha akawa amefika na kusema hivyo.

"Eee. Namwambia dada yako tunywe supu, nimeleta nyingi, ila anataka kuwahi kazini..." Ankia akasema.

"Aaa, Mimi... kunywa tu hata bakuli moja. Sikumbuki mara ya mwisho tumekunywa supu pamoja..." Tesha akamwambia hivyo dada yake.

Ankia akatabasamu na kusema, "Ee bwana, hata bakuli moja tu. Ngoja nikaweke, sawa?"

Miryam akaonekana kutaka kumridhisha mdogo wake, hivyo akatikisa kichwa kukubali.

"Haya twendeni jamani. JC... njoo," Ankia akaniita.

Nikatikisa kichwa kukubali, nami nikafata nyuma yao wote mpaka hapo sebuleni.

Hakukuwa na ile hali changamfu sana iliyozoeleka kutokana na uwepo wa Tesha, kwa sababu wakati huu alikuwa chini ya mvurugo wa kihisia. Angalau Ankia angeongea kwa njia nyepesi ili kurudisha hali iliyosawazika zaidi kwa sehemu hiyo. Kulikuwa na hotpot mezani na mfuko wenye kitu kwa ndani, naye Ankia akawa ameleta sahani ya udongo na mabakuli manne pamoja na vijiko.

Kwenye ule mfuko akatoa chapati sita za kusukumwa na kuziweka kwenye sahani, akisema ndizo zilizofanya akakawia kiasi kwa sababu ya kuhitaji kusubiri. Akaweka na supu kwenye mabakuli, nyama zikiwa zile zifananazo na maini (wanaita mapupu), naye akatusogezea kila mtu sehemu yake na kumsisitizia Miryam anywe na kula chapati.

Nilikuwa namwangalia mwanamke huyo na kuona namna alivyojitahidi kusitiri hisia zake. Kuna kitu kilichokuwa kinaisumbua nafsi yangu kutokana na kushindwa kumwambia maneno yenye kufariji alipokuwa anajilaumu kwa sababu ya matatizo yaliyokuwa yanatokea kwenye familia yake.

Hii ndiyo iliyokuwa mara ya pili kwangu kuweka ukaribu wa namna hiyo kwa huyu mwanamke, yaani vile nilivyombembeleza kidogo akiwa amenilalia begani, nikiwa nakumbukia mara ya kwanza aliponikumbatia kwa kutoa shukrani ya moyoni nilipomsaidia mdogo wake. Nilihisi kama ningeweza kujiweka karibu naye zaidi ili tushirikishane katika mambo yenye kujenga zaidi, lakini tatizo alikuwa wa kivyake mno.

Tukawa tunakunywa thupu, taratibu tu, naye Tesha akawa anasimulia kwa wanawake jinsi alivyojikuta anakabwa na vibaka na kuibiwa simu; bila kuongelea masuala ya wanawake aliokutana nao bar lakini. Akatania kwa kusema alitaka kurudi huko leo na kisu ili akawatafute hao vibaka, nasi tukamwambia awe mwangalifu kisije kikageuziwa kwake.

Kwa hiyo maongezi hapo yalikuwa mepesi tu mpaka tulipomaliza supu, Miryam na mimi tu ndiyo tukiwa tumekula chapati moja moja, kisha yeye na mdogo wake wakatuaga na kuelekea kwao. Tesha alikuwa anataka kwenda kuuweka mwili wake sawa zaidi ili baadaye nimsindikize kwenda kituo cha polisi kuangalia suala lake la simu, nami nilikuwa nimemwambia haina tatizo.

Bila shaka, wawili hao wangeenda kujaribu kuweka hali vizuri zaidi pale kwao, lakini bado nilikuwa na hofu kuelekea suala la huyo Joshua. Sikutaka kuwachanganyia habari kwa kuwaambia mambo niliyosikia huyo mjinga akisema, maana najua ningeizidisha tu hofu ya Miryam kutokana na vitu ambavyo mdogo wake angeweza kufanya.

Kwa sasa ingekuwa busara kutulia tu, lakini ningehakikisha nakuwa makini ili kuiepusha familia hiyo kutoka kwenye matatizo ambayo Joshua alitaka kuyaendeleza; hasa kumlinda Mariam.

★★

Muda mfupi baada ya Miryam na Tesha kuwa wameondoka hapa kwa Ankia, nikawa nimefanya usafi wa chumba na mwili, kisha nikavaa vizuri ili niweze kwenda pale kwao kushughulika na binti Mariam.

Ni leo ndiyo nilitaka kumpa Ankia hela ya kodi kwa ajili ya mwezi uliofuata, basi tu yaani ili wiki ambazo zingefuata nisiwaze kabisa kuhusu hilo suala. Nilipotazama matumizi yangu ya pesa za pembeni toka nimekuja mapumziko, nikaona nilikuwa nimetafuna nyingi kiasi, lakini hakukuwa na shida sana juu ya hilo.

Baada ya kupangilia mambo vyema, nikamfata Ankia na kumpatia pesa. Kama kawaida yake, alianza kujishaua mara JC mbona hivi, mbona vile, nami nikalazimisha azichukue na kumwambia akate mashauzi yake. Nikamuaga baada ya hapo, nikisema ndiyo naenda kwenye wajibu wangu wa kidaktari, nami nikaelekea mpaka kwa jirani yetu.

Tesha akawa amekuja kunifungulia geti, naye akasema kitu ambacho hata Bi Zawadi aliwahi kuniambia mapema sana kuhusu geti hilo. Ni kwamba kama mlango mdogo wa geti ungekuwa unaweza kufungukia kwa nje basi ningekuwa naingia tu badala ya kusumbuka kupiga hodi, hivyo nikaona nisaidie kuirekebisha hali hiyo kidogo.

Nikamwomba Tesha atafute kamba nyembamba, msumari, na nyundo ikiwezekana ili tujigeuze mafundi hapo. Akatii na kufata kamba nyembamba iliyoendana na zile walizoweka hapo nje kwa ajili ya kuanikia nguo, msumari mrefu, lakini hakukuwa na nyundo. Akaleta tu jiwe.

Nikaikata kamba hiyo kwa urefu uliotoshea upana wa kimlango hicho, kisha nikaifunga kwenye kale kadude ka kuvuta kwenye kifungio cha geti na kuipitisha nje kupitia uwazi mdogo mwanzoni mwa ukuta ambapo geti lilianzia. Nikatoka nje na kuugonga msumari ukutani, mwanzoni kabisa karibu na geti, kisha nikaifunga kamba hapo.

Tukaanza kufanya majaribio kwa kufunga kimlamgo cha geti, kisha naivuta kamba kiasi nikiwa kwa nje ili ikikivuta kile kidude kwa ndani, kiachie, na huo mlango ukafunguka. Akili mtu wangu! Ilikuwa ni njia ndogo tu ya kurahisisha kazi kwa sisi tuliozoea kuja hapo, naye Tesha akasema ilikuwa ni njia nzuri sema aliona uvivu tu kushughulika na geti hilo.

Nikaingia tena, na wakati huu ndiyo nikatilia maanani kuwa gari la Miryam halikuwepo, kumaanisha alikuwa ameshakwenda kazini. Nikamuuliza Tesha hali kwa sasa ilikuwaje, naye akaniambia tu twende ndani ili tukaongelee huko.

Kweli tukaenda, nami nikakuta hali isivyo kawaida na nilivyokuwa nimezoea. Sikuwakuta Bi Jamila na Bi Zawadi wakiwa wamekaa kwenye sofa lao kama kawaida, na sikumwona Mariam pia. Nikadhani labda wapo chumbani maana kulikuwa na hali ya utupu hapo.

Tukakaa na Tesha sofani, nami nikamuuliza, "Mariam yuko poa?"

"Eeh, ila ndo' hayupo. Wote hawapo," akasema hivyo.

"Wapi tena?"

"Da' Mimi kawachukua kuwapeleka kwa Joshua. Wakaongee huko," akasema hivyo kwa njia ya kukerwa.

Nikamwangalia kwa umakini na kuuliza, "Kampeleka Mariam kwa Joshua?"

"Ndo' maana yake."

"Lakini si Miryam amesema anaenda kazini?"

"Ndiyo, kawapeleka huko wote na mama wakubwa, halafu ataenda kazini... labda na baadaye ataenda tena huko... kuwafata."

"Mbona we' hujaenda?"

"Kwani haiko wazi? Sitaki tu. Lakini nimesingizia kwa dada kwamba sijisikii fresh bado. Hapo wanaenda kudanganywa-danganywa tu na huyo fala."

"Aisee! Yaani akimgusa Mamu, atanitambua," nikajikuta nimesema hivyo kwa hasira.

"Nini? Nani, Joshua? Anataka kumuumiza Mamu?" Tesha akaniuliza hivyo kwa mkazo.

Nikamwangalia na kusema, "Aa... hapana, yaani namaanisha... hali ya Mariam siyo nzuri kivile bado, ikiwa ataogopeshwa sana na kaka yako itakuwa kurudi nyuma tena. Nimeongea tu vibaya."

"Siyo vibaya, me mwenyewe nitamuua huyo mjinga ikiwa Mamu atarudi hapa bila unywele hata mmoja. Sema ndiyo nimemwahidi dada kuwa mpole, kwa hiyo natulia tu."

"Ila ungeenda nao Tesha, huwezi kujua," nikasisitiza.

"Usiogope bro. Me najua Joshua anachokifanya hapa mwanzoni ni kuigiza tu, kwa hiyo lazima na mimi niigize pia. Hawezi kumgusa mtu yeyote sa'hivi, utaona," akanihakikishia.

Nikaangalia pembeni nikiwa nimeudhika kiasi. Sikujua nifanye nini maana hali hii ilikuwa ya kushtukiza, na hii ikanipa somo kuhusu kuwa chonjo zaidi na hii familia ili Joshua asije kufanikiwa kwenye mipango yake, mimi nikabaki tu mdomo wazi.

"Wanarudi saa ngapi?" nikamuuliza hivyo.

"Jioni. Hapa doro tu kaka. Nataka nikazurure wee mpaka hiyo jioni," akaniambia hivyo.

Nikatulia tu na kushusha pumzi.

"Oy... kama vipi tuoshe, ama nini?" akaniuliza.

"Kuelekea wapi?"

"Nataka nikazunguke Kigamboni leo. Halafu baadaye tutazamia kwa mshkaji fulani hivi, nina siku sijamwona. Unasemaje?" akasema hivyo.

Lengo la kuja hapa ilikuwa kuendelea na mazoezi yangu pamoja na Mariam, lakini hakuwepo. Sikuwa na jambo lingine muhimu la kufanya kwa hiyo nikaona nimkubalie tu rafiki yangu. Labda na matembezi yangeleta jambo jipya mbali na yale niliyokuwa natazamia yafike.

Alikuwa ameshaoga kwa hiyo nikakaa kumsubiri alipokwenda kuvaa. Alivalia kawaida tu kama mimi, na kofia yake kama kibandiko kichwani ikanifanya na mimi nitake kwenda kuichukua ya kwangu, lakini nikaahirisha.

Tukatoka pamoja, akafunga milango na geti, nasi tukaenda kwa Ankia ili Tesha amwachie funguo za kwao ili endapo kama ndugu zake wangewahi kurudi kabla yake basi wazikute hapo. Ankia akatutakia matembezi mema huku akisema tukirudi tumletee zawadi, nasi tukaingia barabarani baada ya hayo.

★★

Basi, tukawa tunatembea mdogo mdogo kuelekea Mzinga. Baada ya kufika Mzinga, kibishoo tu yaani, tukaamua kuifata Kongowe kwa kutembea pia. Mwendo wa taratibu tu, huku tukipeana story nyingi za mambo yetu wanaume ukatufikisha mpaka hapo Kongowe, na hii ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika eneo hilo tokea nimepajua Mzinga; na hata Mbagala pia.

Mwanzoni mwa eneo hilo kunakuwa na sehemu nyingi zenye biashara ndogo na kubwa za wajasiriamali sanasana, nasi tukaelekea upande ambao daladala zingesimama kwa ajili ya kubeba abiria. Tukakuta moja ambayo ilikuwa ikielekea Kigamboni ndiyo, nasi tukaingia na kukaa siti za nyuma kabisa. Mwonekano wangu na Tesha ungefanya watu wafikiri sisi ni ndugu wa damu labda, maana kuna sehemu kubwa ya pigo zetu iliyokuwa inafanana sana.

Tukiwa tu ndiyo tumekaa, Tesha siti ya dirishani kabisa na mimi pembeni yake, nikapokea ujumbe kutoka kwa mtu ambaye sikuwa nimetarajia kabisa kwa muda huu. Ilikuwa ni Adelina, dada mkubwa wa Joy; ama niseme marehemu Joy.

Yaani tokea tumebadilishana namba pale msibani sikuwahi kumtumia salamu hata mara moja, ijapokuwa nilikuwa kwenye harakati za kumtafutia mdogo wake haki kwa mauaji yaliyomsibu. Alikuwa ametuma salamu fupi, 'habari yako,' nami nikatuma jibu kuwa 'niko salama' na kuuliza yeye aliendeleaje.

Nikaanza kumsikia konda kutokea nje akisema kwa abiria fulani waingie kukaa, kwamba siti hazikuwa zimeisha. Yaani alikuwa anawashawishi kwa kusema tena kuna waarabu ma-handsome wamekaa huko mwishoni, na ndiyo Tesha akanishtua nitazame nje.

Nikaangalia kupitia kioo na kuona wanawake wawili pamoja na mwanaume kijana mmoja, wote wakiwa ni waislamu, na mwanamke mmoja alivalia yale manguo meusi yanayoficha mpaka uso kasoro macho, lakini kale kengine uso ulikuwa wazi tu na kuzungukiwa kwa hijab kichwani. Kalikuwa kembamba, keupe, kenye macho mazuri kweli, na nahisi wao walikuwa waarabu kasoro huyo mwanaume kijana aliyekuwa mweusi kabisa; akionekana kuwa mwandamani wao.

Huyo mwanamke aliyeficha uso alikuwa kama hataki kuingia kwa kuwa labda hakupenda kukaa mwishoni, naye Tesha akawa ananishurutisha tufanye jambo ili hako kadada kaingie maana alikuwa amekaelewa tayari. Adelina akawa amenitumia ujumbe akisema yuko poa na kuuliza kama bado nilikuwa Mbagala, naye Tesha akaendelea kunibonyeza-bonyeza mpaka nikahisi kero.

Agh, nikasogea kufikia uwazi wa kioo na kuwaangalia wanawake hao, nami nikasema, "Dada, ingieni tu. Nafasi ziko tatu, yaani kama vile zimebaki kwa ajili yenu tu."

Mwanamke aliyekuwa amefunika mpaka uso akawa ananiangalia sana, naye konda akaongeza spidi ya kuwashawishi.

Nikakaa sawa tena na kumwambia Tesha, "Nimeweka jitihada hiyo kama ulivyotaka. Umefurahi?"

Akacheka kidogo na kusema, "We' ni chizi! Ndo' mpaka utuchoreshe? Ona washamba wanavyotuangalia."

"Unasumbua mno," nikamwambia hivyo nikiwa makini na simu.

Nikamjibu Adelina kwamba bado niko Mbagala ndiyo, na kumuuliza kama alisharudi Mbezi. Tesha akanibonyeza kidogo, nami nikaangalia mbele na kuona wale wanawake wameshapanda na kuja upande wa nyuma. Yule mwanaume kijana hakupanda, inawezekana labda alikuwa anawasindikiza tu, nao wakaja kukaa pamoja nasi; nafasi iliyobaki ikiwa imetutenganisha katikati.

Kale kadada kenyewe kakawa dirishani kabisa, huyo mficha uso akiwa pembeni yangu, nami nikamtazama Tesha na jamaa akajikausha tu kama vile siyo yeye aliyenisisitiza kuwashawishi waingie. Inaonekana kwa muda huu abiria waliokuwa wanataka kuelekea huko mbele walikuwa wachache, kwa sababu hakukuwa hata na mtu aliyesimama na safari ikaanza.

★★

Vuuu, mwendo ukaendelea huku na mimi nikiendelea kuchat na Adelina. Ilianza kidogo kidogo tu lakini mpaka ikafika hatua tukaanza kutaniana, kirafiki yaani. Akawa ameniambia kuwa kwa sasa hivi alikuwa amekwenda pale Mbagala kwa rafiki yake mmoja kumsalimia na ndiyo alifikiria uwezekano wa kupata nafasi ya kuja kunitembelea mimi na Ankia pale nyumbani.

Unajua, mpaka leo Adelina alikuwa anafikiri mimi ni mume wake Ankia, ndiyo ikabidi nimwambie kwamba ile ilikuwa danganya toto tu niliyofanya pamoja na Ankia; wala hata hakuwa mke wangu, na ndiyo matani baina yangu na Adelina yalianzia hapo.

Mwendo ulikuwa mrefu kiasi kuelekea Kigamboni, mara kwa mara watu wakiongezeka kwenye gari na kupungua, na uvumilivu ulikuwa unamshinda Tesha. Alitaka sana kuipata namba ya kale kadada keupe pembeni yetu, lakini alihofia kwamba huenda huyo mwanamke mwingine alikuwa mama yake kwa hiyo kungekuwa na utata.

Lakini akawa ananishawishi kwa kunitumia sms nijaribu kumsemesha maana alikuwa na uhakika kwamba mwanamke huyo aliingia tu kwenye gari kwa sababu yangu, nami nikamwambia Tesha aache umalaya la sivyo ungekuja kumuua siku moja.

Kama ninavyosemaga, mimi siyo mtu wa kuogopa mtu kabisa, na kama ningekuwa nataka kupata namba za mwanamke yeyote niliyekutana naye, ningezipata. Ila kuanza kumwelezea Tesha kwamba nilikuwa sitaki tu najua ingegonga mwamba, na hata hivyo nilikuwa nataka rafiki yangu huyu ajisikie vizuri tu baada ya mambo yote aliyokuwa amepitia jana, kwa hiyo nikamwambia atulie ili nimrekebishie mitambo.

Adelina bado nilikuwa nachat naye, akiwa amesema kwamba anaweza hata akaja leo kunitembelea mimi na Ankia pale nyumbani, nami nikaona nimjibu kwanza. Nikamwandikia kuwa kwa sasa nilielekea Kigamboni kwa hiyo endapo kama alikuwa na mpango wa kwenda kwa Ankia muda huu, asingenikuta, lakini labda kama ni jioni ndiyo tungeweza kuonana.

Ilishangaza kiasi kwamba hakuwa hata amemtafuta Ankia bado kuongelea suala la kwenda kumtembelea ilhali walikuwa ni marafiki, lakini labda ni kwa sababu tu hakuwa amewahi kuwasiliana nami kabisa, na kule kudhani mimi ndiyo kichwa sasa pale kwa Ankia.

Nilipomaliza kumweleza, nikamtazama mwanamke yule mwislamu. Hilo baibui jeusi alilovaa lilificha uzuri wa ngozi nyeupe aliokuwa nao, maana nilitazama vidole vyake vyenye kucha ndefu kidogo na nyekundu, vilivyoshikilia simu ya macho matatu, na kiuhakika nikaona kwamba havikuwa na hata chembe ndogo ya sugu nyeusi. Sijui walikuwa waarabu kweli?

Tesha akanibonyeza tena na kunipa ishara kwamba eti nichangamke, nami nikatabasamu kiasi na kufungua simu yangu tena upande wa sms.

Nikaandika pale patupu hivi, 'Habari? Naomba namb yako kam hutojal'

Nikanyoosha simu kwa chini kumwelekea mwanamke huyo, naye akaitazama. Sikuwa hata nikimwangalia lakini nikamwona akinyanyua uso wake kuniangalia, hivyo na mimi nikamwangalia. Huwa naweza kuweka macho fulani hivi ya kumvuta mwanamke aamshe upendezi kunielekea, macho ya ushawishi yaani, nami nikawa namtazama kwa hiyo njia.

Akaangalia mbele tu kama vile hataki, kisha akaichukua simu yangu kichinichini na kuiunganisha na yake. Nilikuwa nimeweka uso makini, nikiona wazi jinsi Tesha alivyojikausha kwa kujifanya anatazama nje tu, na kwa jicho la mbali nikaweza kuona mwanamke huyo anaandika kitu fulani kwenye simu yangu.

Kisha, akaitelezesha simu kwenye hiyo siti kuelekea upande wangu bila kuitazama, kukiwa na pete nene zenye kuonekana kuwa kama za dhahabu kwenye vidole vyake viwili, nami nikaipokea nikiwa nimeweka mwonekano makini bado. Mambo ya siri hayo, na Tesha ndiyo akawa ameniingiza majaribuni!

Wanawake wa hivi nawaelewa sana, yaani wanapoamuaga kujitafutia vitulizo vya nje huwa wanapenda mno usiri wa hali ya juu, na huyu inaonekana alikuwa amenielewa sana ndiyo maana akakubali kufanya hivyo akiwa pembeni ya binti yake, sijui mdogo wake, sikujua.

Tesha akakunja ngumi yake karibu na paja langu, akiwa anataka tugonge tano ya ushindi, nami nikaweka kiganja changu hapo huku nikimnyanyulia kidole cha kati. Nikatazama simu yangu na kukuta namba za simu zikiwa zimeandikwa hapo, nami nikazitumia ujumbe.

'Jina lako mremb?'

Nikajikausha kama simwangalii, nami nikaona anaandika kitu fulani kwenye simu yake kisha akatazama pembeni.

Ujumbe ukaingia kwenye simu yangu, namba hiyo hiyo, ukisomeka, 'niambie lako na wew.'

Nikajibu, 'JC'

'Ndiyo nn'

'Ndiyo my name'

'Me naitw Ibtisam'

'Ooh saw. Jina lako zur kam wew mremb'

'Uremb wang umeon wp'

Nikiwa bado sijajibu ujumbe wake huo ndiyo tukawa tumeingia maegesho ya daladala kwenye eneo la Kigamboni, na watu wakawa wanasimama ili washuke.

Nikamwandikia hivi, 'Ngj tushuke nikwambie'

Kweli tukaanza kushuka mpaka nje, nami pamoja na Tesha tukaenda upande wa nyuma wa gari na kuwaangalia wanawake hao waislamu. Wenyewe wakaelekea upande mwingine kwa pamoja, huku kale kembamba kakigeuka kututazama mara moja.

Nikaangalia simu na kukuta ujumbe wa huyo mwanamke akiwa amejibu, 'Saw, lkn ntakuchek badae. Kun shm naend sahiv'

Tesha akaniuliza, "Oy, umemwambiaje? Anasemaje?"

"Kaka utakuja kuniweka matatizoni siku moja!" nikamwambia hivyo.

Tukaanza kutembea kuelekea sehemu iliyoturuhusu kuiona vyema Bahari ya Hindi.

"Kwani vipi?" akaniuliza.

"We' kila demu unataka tu, wengine ni majini."

"Ahahahah... me kwani nilikwambia namtaka huyo jini wako? Mimi nilikuwa nakataka kale kengine, we' si umechukua namba ya huyo maza'ake kwa upendo wako?"

"Nimeomba namba yake ili uje kuipata ya hako unakokataka. Halafu Tesha!"

"Hahahah... JC bana! Kwo' jini linasemaje?"

"Atanicheki baadaye, na linaonekana limeolewa. Ah, sijui hata kwa nini nimemwomba namba!"

"Si kwa ajili yangu? We' ukishamzuzua utanifanyia unyama na mimi nipate ya hako kengine. We' utakula mazeli, mimi kimweli. Tena tutafanyia kwenye double deka kabisa."

Nikacheka kidogo tu na kusema, "Tesha tunaingia Kigamboni, wanawake wazuri kama wote, utawasahau hao uliowaona. Tulia mdogo wangu."

"Ah, kwenda huko! Huu ndiyo wakati wangu, we' ushazeeka ndo' maana. Twende tukapande meli huko."

Nikacheka na kutikisa kichwa, nami kweli nikaanza kumfata.

Tukapita sehemu nyingi zenye biashara, watu wengi, wadada wazuri ndiyo usiseme, nasi tukaelekea sehemu ya kununulia kadi za tiketi kwa ajili ya kuvuka bahari kwenda upande wa pili wa Kigamboni; ule wenye majengo ya ukweli. Tesha akapata kadi, nasi tukaenda kuvuka kwa kupanda meli ndogo ya uvukishaji abiria na magari. Watu walikuwa wengi kufikia kiasi kilichohitajika, na wakati tukiwa tumeanza kuvuka mvua ikaanza kunyesha.

Mpango ulikuwa kwenda kuzurura sehemu kadha wa kadha kwa eneo hilo, lakini mvua ikaongezeka mno kiasi kwamba jambo hilo likaingiwa na utata. Yaani ile tumeshuka tu, ikatubidi tuingie kwenye daladala ambazo zilielekea Kariakoo, na safari ikaanza tena. Hii haikuwa mara ya kwanza kutembelea Kigamboni na hata niliwahi kutoka na mwanamke fulani aliyekuwa wa pande hizi, ila hiyo ni hadithi nyingine, ya kusimuliwa kwa wakati mwingine.

★★

Mwendo wa dakika kadhaa ukatufikisha mpaka Kariakoo, na kwa huku mvua ilikuwa ishakatika. Tukashuka, Tesha akiwa bado anawashwa kutembea, hivyo tukachukua mwendokasi na kwenda pande za Ubungo. Tukazurura wee, Tesha hata akanipitisha kule alikokuwa anaenda kufata wanawake wa kulipwa, chimboni yaani, naye akawa akisema hizo mishe siku hizi hafanyi.

Tukatoka huko na kuzunguka mpaka Uhasibu, nasi tukashukia hapo. Tesha alikuwa na rafiki yake mwanachuo aliyekaa eneo la Uwanja wa Benjamin Mkapa, hivyo tukatembea mdogo mdogo kuelekea huko. Alikuwa ameshawasiliana naye. Yaani safari hii yote leo ilikuwa ni kwa udhamini wa Tesha, mimi ndiyo nilikuwa kama mtalii wake, nasi tulipokuwa tu ndiyo tumeyapita malango ya uwanja nikaanza kuona mdada fulani akija upande wetu taratibu.

Tesha alikuwa ameniambia kwamba tunaenda kumsalimia tu mshkaji wake, kwa hiyo sikuwa nimetarajia kwamba ingekuwa ni mwanamke mpaka mdada huyo alipotukaribia na kukumbatiana na Tesha kirafiki. Alikuwa mfupi kiasi, mweusi, mwili wa kawaida tu, na tabasamu lake lilionyesha mwanya mdogo katikati ya meno yake ya mbele.

Wakawa wanasemeshana kirafiki sana, naye akaniangalia na kunisalimu pia. Alikuwa mchangamfu sana, jina lake ikiwa ni Dina, naye akatuongoza kuelekea pale alipoishi. Ilikuwa ni kwenye zile nyumba za wapangaji zilizojaa hasa wanafunzi wa chuo, nasi tukaingia kwenye chumba chake.

Kilikuwa simple tu, safi, godoro chini kwenye sakafu ya vigae, friji ndogo, begi la nguo pembeni ya shehena ndogo ya vyombo, vifaa vya mapodozi na manukato, viti vitatu vya plastiki. Jiko dogo la gesi lilibeba sufuria lenye chakula kwa ndani bila shaka, nasi tukakaa na kuanza kupiga story.

Mimi nilikaa kwenye kiti, Tesha na Dina wakakaa kwenye godoro, na ni wao sanasana ndiyo walioongea huku mimi nikichangia mada mara moja moja kukoleza ucheshi. Dina akaniuliza natumia soda gani, nami nikamwambia Pepsi. Tesha vilevile akasema Pepsi ingawa alitania kutaka bia.

Dina akatoka kwenda kufata soda, nasi tukabaki hapo, nikisikiliza maneno ya kipuuzi ya Tesha kuhusu jinsi nilivyotakiwa kubaki hapa leo ili nifanye jambo fulani na Dina. Ni hapa ndiyo nikawa nimepokea ujumbe kutoka kwa yule mwanamke mwislamu tuliyekutana kwenye daladala, akiwa ametuma tu 'mambo,' nami kabla hata sijamjibu, simu yangu ikaanza kuita. Mpigaji? Bertha. Hatimaye!

Sikutaka Tesha asikie jambo lolote ambalo lingemfanya atambue nani naongea naye, hivyo nikapokea nikiwa nimejihakikishia kutosema lolote litakalomshtua jamaa.

"Hallo?" sauti yake Bertha ikasikika.

"Hello, vipi?" nikasema hivyo.

"Poa. Uko wapi?"

"Niko kwa Mkapa hapa."

"Unafanyeje huko?"

"Nimekuja kwa mshkaji wangu, niambie..."

Tesha akaniuliza kwa ishara, "nani?" nami nikamwonyesha ishara pia kuwa atulie.

"Nataka uje. Au biashara uliyonayo sasa hivi huko ni muhimu sana?"

"Hakuna chochote muhimu zaidi yako dear."

"Usiniite dear, mazoea ya hivyo sitaki."

"Sawa dear," nikasema hivyo makusudi.

"Halafu wewe!" akasikika kwa ukali.

Nikajikaza nisicheke na kumwambia, "Pole, nimejikwaa tu. Ulimi hauna mfupa."

"Na nitakuja kuuwekea mfupa usipoangalia."

"Sorry."

"Toka huko sasa hivi. Niko Masai," akaniambia hivyo.

Ni muda huu ndiyo Dina akawa ameingia ndani tena, lakini wakati huu alikuwa pamoja na mwanadada mwingine mweupe, mwembamba, mrefu kiasi, aliyekuwa amevalia T-shirt nyeusi na suruali ya jeans ya samawati iliyobana. Nywele zake zilisukwa kwa mtindo wa dread nyeusi na fupi, naye akaenda kukaa godoroni baada ya Tesha kunyanyuka na kukaa kwenye kiti.

"Umeelewa?" Bertha akasikika kwenye simu.

Nikasema, "Eeh, nimeelewa. Ila... niko mbali kama hivi, naweza kuchelewa kidogo."

Dina akawa ametufungulia soda zetu na kutupatia, na ukimya mfupi uliofuata kwenye simu ukanifanya nitambue kwamba Bertha alikuwa amekasirishwa na maneno yangu.

Nikamwambia, "Ila nakuja. Nitakuwa nimeshafika muda siyo mrefu."

Likakata simu!

Kazi nilikuwa nayo. Nikashusha pumzi na kumwangalia Tesha, aliyekuwa akinitazama kama anasubiri nijielezee.

"Kuna dharura bro. Natakiwa nifike location mara moja," nikamwambia hivyo.

"Tumekuja wote, unataka kuondokaje mwenyewe bana?" Tesha akaniuliza kwa uthabiti.

"Iih, unataka kutukimbia?" Dina akaniuliza hivyo.

"Kuna dharura imetokea, nahitajika sehemu haraka ndo' maana..."

"Acha bangi! Hautoki hapa. Keki tamu kama hizi unakimbia kweli?" Tesha akasema hivyo kiutani.

Tukacheka kidogo, na Dina akamsonta huku akisema, "Afu' wewe!"

"Inanibidi tu kaka," nikamwambia Tesha.

"Jamani, mbona ghafla? Chakula hiki napakua," akasema Dina.

"Oh usijali Dina, niko poa. Labda umpakulie huyu mbwa," nikamwambia hivyo.

Akacheka kidogo, naye Tesha akasema, "Em' pakua mama, tule."

"Basi kunywa hata soda, imeshafunguliwa," akaniambia hivyo yule mdada mwingine.

"Ee, kunywa soda ndiyo uende kaka," Dina akaniambia.

"Poa," nikajibu.

Ingenibidi nipige hii soda fasta maana huyo Bertha hakuwa mtu wa subira hata kidogo, na hiki ni kitu ambacho nilikuwa nimekisubiria sana kwa hiyo wiki nzima kwa hiyo nisingeweza kuchezea nafasi hata kama ningepewa ofa ya utatu na hawa wadada!

Nikawa napiga fundo ndefu ndefu, huku nikiwa nimeanza kuchat na yule mwanamke mwislamu pia. Alikuwa mmoja kati ya wale wanawake ambao walipenda mtu aende moja kwa moja kwenye pointi ya kitu ambacho alitaka kutoka kwake, nami nikamwambia ndiyo, nilimkubali sana kutokana na kupenda macho yake na ngozi yake.

Akaniambia ooh nimeshaolewa, kwa hiyo ukinitaka lazima upande ngazi, nami nikamwambia hakuna ngazi za kupanda; ikiwa alinikubali pia basi tuje kucheza, lakini asipotaka basi sitalazimisha. Kwa kauli hiyo akawa ametulia kwanza, nami nikawa nimemaliza soda.

Nikamshukuru Dina na kusimama, Tesha bado akiwa analalama kuhusu mimi kuondoka, hivyo ikanibidi nitoe ahadi ya kuja naye tena kesho ikiwezekana kumtembelea rafiki yetu. Dina alipenda sana hilo wazo na kusisitiza nisije kuacha kuja, nami nikamwambia aondoe shaka. Huyo rafiki yake mwingine alikuwa akiniangalia sana kwa sura yake ya kiupole, nami nikamuaga pia nikiwa hata simjui jina.

Nikawaacha marafiki hao hapo na kuanza kuelekea barabarani, nikiwa natumaini kuwahi, na Tesha asijue kwamba sehemu niliyokwenda ilikuwa ni Masai. Angeshangaa sana!

★★

Nilifanikiwa kupata usafiri wa daladala zilizoelekea Mbagala, na mpaka kufikia huko tayari ilikuwa inaelekea kuingia saa moja. Nilikuwa nikijiuliza ni kwa nini madam Bertha alikuwa ameamua kuja Masai mapema sana leo, lakini hayo yote ningeyajua nikishafika pale.

Badala ya kuchukua daladala tena kutokea Rangi Tatu, nikaamua kupanda bodaboda ili niwahi zaidi, brrrr mpaka Mzinga, nami nikaunganisha moja kwa moja kufikia Masai, lakini nikaona nielekee kwa Ankia kwanza.

Nikafika hapo dukani kwa Fatuma na kumkuta huyo dada pamoja na wanawake wengine wengine wakiwa wamekaa kama kikundi cha kupiga umbeya, nami nikamwambia bodaboda anisubirie nikachukue mzigo ndani kisha anirudishe Masai upesi. Nikawapita hao wavaa dera kama siwaoni, nami nikaelekea mpaka ndani na kuingia.

Akili yangu ilikuwa imekazia fikira jambo moja tu kiasi kwamba mpaka nikashtuka kiasi moyoni baada ya kuingia na kumkuta Ankia akiwa amekaa pamoja na Adelina! Ile hali ya kutotegemea kumkuta mwanamke huyu hapa ingawa tulikuwa tumewasiliana ilikuwepo yaani, halafu nilikuwa kwenye kasi kwelikweli.

Wawili hao, baada ya kuniona, wakatabasamu kwa pamoja, nami nikatabasamu pia na kusogea karibu zaidi na walipokaa.

"Mume amerudi," Adelina akasema hivyo.

"Ee, baba mwenye nyumba ndiyo kafika," Ankia akasema hivyo pia.

Nikajikuta tu natenda bila kufikiri sana kwa kuinama na kumkumbatia Adelina, nami nikamwambia, "Karibu."

Nafikiri alikuwa ameshangaa kiasi lakini akaweza kucheka kidogo kwa pumzi, naye akasema, "Asante."

Nikamwachia na kusema tena, "Karibu sana."

Kisha nikaelekea chumbani, bila shaka nikiwaacha wanawake hao wanatazama haraka yangu.

Nikaingia chumbani na kutoa yale madawa niliyotengeneza, nami nikachukua kiasi kidogo na kukiweka kwenye karatasi tu baada ya kuwa nimekosa pa kuwekea, kwa kuwa sehemu niliyohifadhia dawa yote ilikuwa ndani ya mifuko minene; madawa yakionekana kama glucose. Nikachomeka hicho kikaratasi mfukoni, kisha nikaelekea sebuleni tena.

"Unatoka?" Ankia akauliza hivyo.

"Ndiyo, kuna sehemu nafika mara moja lakini... sikawii, nakuja. Sawa?" nikaongea hivyo nikiwa nimeelekeza fikira zangu kwa Adelina.

Akatikisa kichwa kukubali, naye Ankia akasema, "Unawahi nini kinachokutoa kijasho hivyo? Tuambiane..."

"Utajua tu, ngoja nirudi," nikasema hivyo na kuelekea mlango.

Nikawaacha wanawake hao wakicheka kidogo, nami nikaenda mpaka nje tena. Nikapanda bodaboda na kugeuza kuirudia Masai, nasi tukafika hapo huku sasa giza likiwa limeshaingia. Nikamlipa jamaa na kumwambia atokomee, kisha nikaelekea pale ndani.

Wanywaji walikuwepo na nafikiri kuna wahudumu wapya waliokuwa wameongezwa hapa na wachache niliowajua kuondoka, nami nikawa nimemwona Bobo pamoja na DJ fulani hivi wa hapo Masai. Nikamfata.

"Oyo, mchina..." akaniambia hivyo tukiwa tunagonganisha mabega yetu kirafiki.

Nikagongesha tano kwa yule DJ pia, kisha nikamwambia Bobo, "Oya umepotea kweli."

"Ah, mimi, wewe? Yaani hutokei Masai siku hizi mwanangu. Check watu wanavyokuangalia kama vile hujawahi kuonwa hapa," akasema hivyo.

Nikatabasamu na kusema, "Na mimi nimetingwa kaka, ila mdogo mdogo narudi. Ishu zinakwendaje?"

"Kama kawa budha. Oy... mtu wako yupo huko ndani," akaniambia hivyo kwa kuninong'onezea sikioni.

"Eeh, nimeona gari nje," nikamwambia.

"Yuko VIP, kamchangamkie..."

"Ndo' mpango mzima," nikasema hivyo.

Tukacheka tena pamoja, kisha nikamwacha hapo na kuelekea pande ya VIP. Na Bobo alikuwa sahihi kabisa, watu walikuwa wananiangalia kweli, lakini umakini wangu wote ulikuwa kumfikia huyo madam.

Nilipofika mlangoni, nikajiwekea hali ya utulivu, kisha nikaingia ndani hapo. Nikamkuta madam Bertha akiwa amekaa sofani, glasi yenye wine kiganjani, na kwenye sofa la pembeni alikaa yule baunsa wake; a.k.a shemeji.

Kama kawaida ya mwanamke huyo, alikuwa amependeza kwa kuvaa kigauni kifupi chekundu, kilichoyaacha mapaja yake meupe wazi kutokana na namna alivyokuwa amepiga nne, na inaonekana kilikuwa cha mgongo wazi. Wakati huu alishonea wigi la nywele za kizungu kichwani, na baunsa wake alikuwa amevaa kaushi tu na suruali nyeusi, akionyesha misuli yake imara.

Nikasogea usawa wa meza moja hapo, nami nikamtikisia kichwa jamaa kama salamu, naye akairudisha. Nikamwangalia Bertha, ambaye alikuwa akinitazama tu kwa utulivu, nami nikamwambia, "Nimefika madam."

"Umechelewa," akaniambia hivyo.

"Kweli? Mbona naona kama bado party haijaanza?" nikamuuliza hivyo.

Baunsa wake akamwangalia na kucheka kidogo, naye Bertha akawa amenikazia macho yake.

"Tupishe," Bertha akamwambia hivyo jamaa.

Baunsa akasimama na kuja upande wangu, naye akaniuliza, "Una ule unyama jembe?"

"Nakosaje labda?" nikamuuliza hivyo.

Akatabasamu huku akitikisa kichwa taratibu, nami nikaitoa ile dawa na kumfungulia.

"Si iko kama ile?" akaniuliza hivyo.

"Kwa asilimia zote," nikamwambia.

Akachovya kwa kidole na kulamba, kisha akatikisa kichwa kwa nguvu kiasi na kunishika begani. "We' dogo ni nyoko!" akaniambia hivyo.

Nikatabasamu kidogo, naye akanipita na kutoka ndani humo.

Nikabaki na madam. Alikuwa ananitazama kwa yale macho ya kuhukumu bado, naye akasema, "Njoo."

Nikatii na kumfata. Sikuwa na hofu kumwelekea huyu mwanamke, ila kujifanya mnyenyekevu sana ilikuwa lazima. Nikasimama usawa wa sofa alilokalia na kubaki mtulivu.

"We' vipi, si ukae?" akaniambia hivyo.

Nikasogea na kukaa kwenye sofa karibu yake.

Akawa ananitazama sana, naye akasema, "Yaani hiyo sura! Kama mwanamke!"

Dah! Kashfa hizo.

Nikatabasamu kwa kujilazimisha na kusema, "Asante. Moja kati ya silaha zinazonisaidia kupita huku na kule ni hii sura."

Akacheka kwa mguno, kisha akaweka glasi yake pembeni.
"Nimekufatilia kwa hiyo wiki dogo, naona una maisha magumu sana mpaka ukaamua kutoka Goba Center kuja kuishi Mbagala," akaniambia hivyo.

Umeona sasa? Nilikuwa sahihi. Huyu mwanamke alikuwa amefanya uchunguzi kunihusu mpaka kujua kitu ambacho bado sijaelezea kujihusu. Nikataka kujua anaelewa mambo mengi kadiri gani kuhusu maisha yangu.

"Ahah... eeh... maisha magumu. Nimekaa sehemu nzuri lakini... hazijanifiti ndo' maana nimeangukia huku sasa hivi," nikaongea hivyo kiupole, ikiwa kimtego zaidi.

Akasema, "Me sijali ulikuwa unaishi vipi. Nataka tu ujue nikiamua kukuharibia maisha yako endapo kama utanigeuka basi sitosita kuanza hata na familia yako."

"Usiwe na hofu juu ya hilo madam. Siwezi kukusaliti. Kwanza... familia yangu iko Mwanza, mimi huku ni mtafutaji tu kwa hiyo niko mwenyewe," nikamdanganya.

"Una uhakika na kile ulichojiingiza kukifanya huku dogo?" akaniuliza.

"Ndiyo najua. Nina ujanja mwingi, usinichukulie poa. Sema mambo huko Goba hayakwenda fresh tu ndo' maana nikaja huku kujitafuta, na najua nimejipata tena kwa kuwa chini yako. Sitakuangusha madam. Najua nachokifanya, na nitafata utakachonielekeza kufanya," nikamwambia hivyo.

Akatulia kidogo, kisha akasema, "Sawa. Nipe hiyo kitu nionje."

Nikamfungulia kikaratasi chenye dawa ya cocaine, naye akachovya na kulamba kidole chake huku akinitazama kwa macho makini. Kidogo tu yakalegea naye akawa ananiangalia utadhani ananitaka kimapenzi. Ah mimi nilikuwa mtaalamu bwana!

Na angalau kufikia hapa nikawa nimetambua kwamba hakujua mengi zaidi kuhusu maisha yangu isipokuwa tu kuwa amefatilia na kujua nilikotokea kihalisi kabla ya kufika huku, kwa hiyo mchezo wangu kwake ungeendelea taratibu.

Vibe likiwa limemgonga, akaniambia, "Unyama mzuri huu."

Nikatabasamu kidogo.

"Kuna ishu nataka nikushirikishe," akasema hivyo.

Pasi ndefu hiyoo! Nikatikisa kichwa kuonyesha namsikiliza.

"Kesho utakuja pale pale ulipokuja siku ile, uje jioni," akasema hivyo.

"Sawa. Nije na unyama wetu?" nikamuuliza.

Akaweka macho ya udadisi, naye akauliza, "Unamaanisha kwamba unao mwingi?"

"Nimetengeneza kiasi fulani. Hakijazi mifuko mikubwa lakini si unajua ni tamu mno, kwa hiyo kidogo tu...."

"Ni nyingi," akamalizia maneno yangu.

Nikatikisa kichwa kukubali.

Akaninyooshea kidole chake na kunipiga kofi laini shavuni, naye akasema, "Safi sana. Kumbe we' kweli wa faida. Uje nao kesho. Nitakuelekeza mengine ukishafika."

"Imeisha hiyo," nikamwambia hivyo.

Akawa ananitazama kwa njia fulani utadhani alikuwa ananisoma, naye akasema, "Nataka kuona kama we' siyo mwanaume sura tu."

Nikamsogelea karibu zaidi na uso wake na kumuuliza, "Kivipi?"

"Kesho. Kesho ndiyo nitaona," akasema hivyo huku akipindisha shingo yake kiasi, midomo yetu ikiwa karibu sana.

Nikasema, "Ahaa... nilidhani unataka nikuonyeshe sasa hivi."

Akatabasamu na kuangalia chini, kisha akatoa tusi kunielekea bila kuniangalia.

Nikatabasamu pia baada ya kuona kwamba alikuwa ameanza kuonyesha roho ya kuniamini kiasi, na bila shaka ishu hiyo ya kesho ingehusiana na mengi ya vitu nilivyotaka kuhakikisha vinaporomoka kwa msaada wa askari Ramadhan. Ingebidi kusubiri kuona.

Akawa amekivuta kinywaji chake tena na kuikunjua miguu yake, naye akaniangalia usoni. "Kwa hiyo toka mpenzi wako amekufa, haujaingiza substitute?" akaniuliza hivyo.

Nikatazama chini kwa ufupi, nikielewa alimaanisha Joy.

"Oh, nimegusa pabaya? Mhm... inawezekana ulikuwa unampenda sana."

"Joy na mimi ilikuwa kama biashara tu. Wala hakukuwa na kitu tense kivile," nikamwambia.

"Mm? Unanidanganya mimi? Ahah... unajua bado natakiwa niwe mwangalifu sana juu yako maana inaweza ikawa unataka kumlipizia kisasi mpenzi wako," akasema hivyo.

Dah! Lina akili!

Nikatoa kicheko cha kujilazimisha na kusema, "Madam una vituko. Najua hauamini hilo kwa sababu tayari unaniamini mimi."

"Unajuaje?"

"Usingemwambia bodyguard wako atoke nje kama ungeamini naweza kukufanyia kitu kibaya. Hadi dawa nayotengeneza unakula, kama ingekuwa kukuua si ningewekea hata sumu?"

Akatulia kidogo akiniangalia kwa umakini, naye akasema, "Huwezi kuwa na uhakika sikuzote. Ndiyo maana bado nataka nikupime."

Nikaegamia sofa, huku nikimwangalia kizembe na kusema, "Fanya chochote madam... JC ni mali yako sasa hivi."

"Nhhaa... unanifurahisha. Bado akili yako ni ndogo sana."

Nikamshika kiunoni taratibu, naye akawa makini na kuniangalia machoni. "Ndiyo unifunze sasa. Mi' wa faida kweli," nikamwambia hivyo kwa sauti ya chini.

Akabaki kuniangalia tu huku akizungusha-zungusha kinywaji ndani ya glasi aliyoshika, na ni hapo ndiyo mlango wa kuingilia ndani humo ukasikika ukifunguka. Kwa sababu nilikuwa nimeupa mlango mgongo, nisingeweza kujua nani kaingia upesi, lakini nikaona macho yake Bertha yakimtazama aliyeingia kwa njia ya kukerwa.

Nikiwa nafikiri ni mhudumu labda au yule baunsa, nikageuka bila kuwa na utayari wa kumchukulia serious huyo mtu aliyeingia mpaka nilipojikuta nashangaa kiasi baada ya kuona ni Chalii Gonga mwenyewe!



★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 2
 
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!

★★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI

★★★★★★★★★★★★★★★★★


Nikiwa naendelea kumpa Miryam bembelezo kwa kusugua mkono na bega lake taratibu, mlango wa kuingilia hapo chumbani ukafunguka, nami nikatazama hapo na kumwona Ankia akiwa amesimama. Bila shaka ndiyo alikuwa amerudi, na inaonekana alikuja moja kwa moja mpaka humu chumbani kutuangalia mimi na Tesha, lakini akakuta niko na dada mtu.

Miryam akawa amemwona pia, naye akajitoa begani kwangu na kuanza kujifuta machozi kwa viganja vyake. Ankia alikuwa amesimama hapo mlangoni akitutazama kama vile anasubiri maelezo.

"Ndiyo umerudi?" nikamuuliza hivyo.

"Ee... ndiyo nimefika. Kila kitu kiko sawa jamani?" Ankia akauliza hivyo kwa kujali.

Miryam akasimama baada ya kujikausha machozi, nami nikasimama pia. Akasema, "Ndiyo, nimemwijia Tesha."

"Yuko wapi?" Ankia akamuuliza.

"Ameingia uani. Ngoja niende nikamsubiri hapo nje," Miryam akasema hivyo.

Nilikuwa namtazama tu kwa utulivu, naye akaanza kuelekea mlangoni lakini Ankia akamshika mkono kumzuia. Sote tukamtazama.

"Nime... nimeleta supu. Kaa basi tunywe pamoja na mdogo wako, eti?" Ankia akamwambia hivyo.

Miryam akasema, "Sitaweza Ankia. Naingia kazini, nataka nikajiandae. Ila Tesha anaweza kubaki, na...."

"Ankia umerudi?" Tesha akawa amefika na kusema hivyo.

"Eee. Namwambia dada yako tunywe supu, nimeleta nyingi, ila anataka kuwahi kazini..." Ankia akasema.

"Aaa, Mimi... kunywa tu hata bakuli moja. Sikumbuki mara ya mwisho tumekunywa supu pamoja..." Tesha akamwambia hivyo dada yake.

Ankia akatabasamu na kusema, "Ee bwana, hata bakuli moja tu. Ngoja nikaweke, sawa?"

Miryam akaonekana kutaka kumridhisha mdogo wake, hivyo akatikisa kichwa kukubali.

"Haya twendeni jamani. JC... njoo," Ankia akaniita.

Nikatikisa kichwa kukubali, nami nikafata nyuma yao wote mpaka hapo sebuleni.

Hakukuwa na ile hali changamfu sana iliyozoeleka kutokana na uwepo wa Tesha, kwa sababu wakati huu alikuwa chini ya mvurugo wa kihisia. Angalau Ankia angeongea kwa njia nyepesi ili kurudisha hali iliyosawazika zaidi kwa sehemu hiyo. Kulikuwa na hotpot mezani na mfuko wenye kitu kwa ndani, naye Ankia akawa ameleta sahani ya udongo na mabakuli manne pamoja na vijiko.

Kwenye ule mfuko akatoa chapati sita za kusukumwa na kuziweka kwenye sahani, akisema ndizo zilizofanya akakawia kiasi kwa sababu ya kuhitaji kusubiri. Akaweka na supu kwenye mabakuli, nyama zikiwa zile zifananazo na maini (wanaita mapupu), naye akatusogezea kila mtu sehemu yake na kumsisitizia Miryam anywe na kula chapati.

Nilikuwa namwangalia mwanamke huyo na kuona namna alivyojitahidi kusitiri hisia zake. Kuna kitu kilichokuwa kinaisumbua nafsi yangu kutokana na kushindwa kumwambia maneno yenye kufariji alipokuwa anajilaumu kwa sababu ya matatizo yaliyokuwa yanatokea kwenye familia yake.

Hii ndiyo iliyokuwa mara ya pili kwangu kuweka ukaribu wa namna hiyo kwa huyu mwanamke, yaani vile nilivyombembeleza kidogo akiwa amenilalia begani, nikiwa nakumbukia mara ya kwanza aliponikumbatia kwa kutoa shukrani ya moyoni nilipomsaidia mdogo wake. Nilihisi kama ningeweza kujiweka karibu naye zaidi ili tushirikishane katika mambo yenye kujenga zaidi, lakini tatizo alikuwa wa kivyake mno.

Tukawa tunakunywa thupu, taratibu tu, naye Tesha akawa anasimulia kwa wanawake jinsi alivyojikuta anakabwa na vibaka na kuibiwa simu; bila kuongelea masuala ya wanawake aliokutana nao bar lakini. Akatania kwa kusema alitaka kurudi huko leo na kisu ili akawatafute hao vibaka, nasi tukamwambia awe mwangalifu kisije kikageuziwa kwake.

Kwa hiyo maongezi hapo yalikuwa mepesi tu mpaka tulipomaliza supu, Miryam na mimi tu ndiyo tukiwa tumekula chapati moja moja, kisha yeye na mdogo wake wakatuaga na kuelekea kwao. Tesha alikuwa anataka kwenda kuuweka mwili wake sawa zaidi ili baadaye nimsindikize kwenda kituo cha polisi kuangalia suala lake la simu, nami nilikuwa nimemwambia haina tatizo.

Bila shaka, wawili hao wangeenda kujaribu kuweka hali vizuri zaidi pale kwao, lakini bado nilikuwa na hofu kuelekea suala la huyo Joshua. Sikutaka kuwachanganyia habari kwa kuwaambia mambo niliyosikia huyo mjinga akisema, maana najua ningeizidisha tu hofu ya Miryam kutokana na vitu ambavyo mdogo wake angeweza kufanya.

Kwa sasa ingekuwa busara kutulia tu, lakini ningehakikisha nakuwa makini ili kuiepusha familia hiyo kutoka kwenye matatizo ambayo Joshua alitaka kuyaendeleza; hasa kumlinda Mariam.

★★

Muda mfupi baada ya Miryam na Tesha kuwa wameondoka hapa kwa Ankia, nikawa nimefanya usafi wa chumba na mwili, kisha nikavaa vizuri ili niweze kwenda pale kwao kushughulika na binti Mariam.

Ni leo ndiyo nilitaka kumpa Ankia hela ya kodi kwa ajili ya mwezi uliofuata, basi tu yaani ili wiki ambazo zingefuata nisiwaze kabisa kuhusu hilo suala. Nilipotazama matumizi yangu ya pesa za pembeni toka nimekuja mapumziko, nikaona nilikuwa nimetafuna nyingi kiasi, lakini hakukuwa na shida sana juu ya hilo.

Baada ya kupangilia mambo vyema, nikamfata Ankia na kumpatia pesa. Kama kawaida yake, alianza kujishaua mara JC mbona hivi, mbona vile, nami nikalazimisha azichukue na kumwambia akate mashauzi yake. Nikamuaga baada ya hapo, nikisema ndiyo naenda kwenye wajibu wangu wa kidaktari, nami nikaelekea mpaka kwa jirani yetu.

Tesha akawa amekuja kunifungulia geti, naye akasema kitu ambacho hata Bi Zawadi aliwahi kuniambia mapema sana kuhusu geti hilo. Ni kwamba kama mlango mdogo wa geti ungekuwa unaweza kufungukia kwa nje basi ningekuwa naingia tu badala ya kusumbuka kupiga hodi, hivyo nikaona nisaidie kuirekebisha hali hiyo kidogo.

Nikamwomba Tesha atafute kamba nyembamba, msumari, na nyundo ikiwezekana ili tujigeuze mafundi hapo. Akatii na kufata kamba nyembamba iliyoendana na zile walizoweka hapo nje kwa ajili ya kuanikia nguo, msumari mrefu, lakini hakukuwa na nyundo. Akaleta tu jiwe.

Nikaikata kamba hiyo kwa urefu uliotoshea upana wa kimlango hicho, kisha nikaifunga kwenye kale kadude ka kuvuta kwenye kifungio cha geti na kuipitisha nje kupitia uwazi mdogo mwanzoni mwa ukuta ambapo geti lilianzia. Nikatoka nje na kuugonga msumari ukutani, mwanzoni kabisa karibu na geti, kisha nikaifunga kamba hapo.

Tukaanza kufanya majaribio kwa kufunga kimlamgo cha geti, kisha naivuta kamba kiasi nikiwa kwa nje ili ikikivuta kile kidude kwa ndani, kiachie, na huo mlango ukafunguka. Akili mtu wangu! Ilikuwa ni njia ndogo tu ya kurahisisha kazi kwa sisi tuliozoea kuja hapo, naye Tesha akasema ilikuwa ni njia nzuri sema aliona uvivu tu kushughulika na geti hilo.

Nikaingia tena, na wakati huu ndiyo nikatilia maanani kuwa gari la Miryam halikuwepo, kumaanisha alikuwa ameshakwenda kazini. Nikamuuliza Tesha hali kwa sasa ilikuwaje, naye akaniambia tu twende ndani ili tukaongelee huko.

Kweli tukaenda, nami nikakuta hali isivyo kawaida na nilivyokuwa nimezoea. Sikuwakuta Bi Jamila na Bi Zawadi wakiwa wamekaa kwenye sofa lao kama kawaida, na sikumwona Mariam pia. Nikadhani labda wapo chumbani maana kulikuwa na hali ya utupu hapo.

Tukakaa na Tesha sofani, nami nikamuuliza, "Mariam yuko poa?"

"Eeh, ila ndo' hayupo. Wote hawapo," akasema hivyo.

"Wapi tena?"

"Da' Mimi kawachukua kuwapeleka kwa Joshua. Wakaongee huko," akasema hivyo kwa njia ya kukerwa.

Nikamwangalia kwa umakini na kuuliza, "Kampeleka Mariam kwa Joshua?"

"Ndo' maana yake."

"Lakini si Miryam amesema anaenda kazini?"

"Ndiyo, kawapeleka huko wote na mama wakubwa, halafu ataenda kazini... labda na baadaye ataenda tena huko... kuwafata."

"Mbona we' hujaenda?"

"Kwani haiko wazi? Sitaki tu. Lakini nimesingizia kwa dada kwamba sijisikii fresh bado. Hapo wanaenda kudanganywa-danganywa tu na huyo fala."

"Aisee! Yaani akimgusa Mamu, atanitambua," nikajikuta nimesema hivyo kwa hasira.

"Nini? Nani, Joshua? Anataka kumuumiza Mamu?" Tesha akaniuliza hivyo kwa mkazo.

Nikamwangalia na kusema, "Aa... hapana, yaani namaanisha... hali ya Mariam siyo nzuri kivile bado, ikiwa ataogopeshwa sana na kaka yako itakuwa kurudi nyuma tena. Nimeongea tu vibaya."

"Siyo vibaya, me mwenyewe nitamuua huyo mjinga ikiwa Mamu atarudi hapa bila unywele hata mmoja. Sema ndiyo nimemwahidi dada kuwa mpole, kwa hiyo natulia tu."

"Ila ungeenda nao Tesha, huwezi kujua," nikasisitiza.

"Usiogope bro. Me najua Joshua anachokifanya hapa mwanzoni ni kuigiza tu, kwa hiyo lazima na mimi niigize pia. Hawezi kumgusa mtu yeyote sa'hivi, utaona," akanihakikishia.

Nikaangalia pembeni nikiwa nimeudhika kiasi. Sikujua nifanye nini maana hali hii ilikuwa ya kushtukiza, na hii ikanipa somo kuhusu kuwa chonjo zaidi na hii familia ili Joshua asije kufanikiwa kwenye mipango yake, mimi nikabaki tu mdomo wazi.

"Wanarudi saa ngapi?" nikamuuliza hivyo.

"Jioni. Hapa doro tu kaka. Nataka nikazurure wee mpaka hiyo jioni," akaniambia hivyo.

Nikatulia tu na kushusha pumzi.

"Oy... kama vipi tuoshe, ama nini?" akaniuliza.

"Kuelekea wapi?"

"Nataka nikazunguke Kigamboni leo. Halafu baadaye tutazamia kwa mshkaji fulani hivi, nina siku sijamwona. Unasemaje?" akasema hivyo.

Lengo la kuja hapa ilikuwa kuendelea na mazoezi yangu pamoja na Mariam, lakini hakuwepo. Sikuwa na jambo lingine muhimu la kufanya kwa hiyo nikaona nimkubalie tu rafiki yangu. Labda na matembezi yangeleta jambo jipya mbali na yale niliyokuwa natazamia yafike.

Alikuwa ameshaoga kwa hiyo nikakaa kumsubiri alipokwenda kuvaa. Alivalia kawaida tu kama mimi, na kofia yake kama kibandiko kichwani ikanifanya na mimi nitake kwenda kuichukua ya kwangu, lakini nikaahirisha.

Tukatoka pamoja, akafunga milango na geti, nasi tukaenda kwa Ankia ili Tesha amwachie funguo za kwao ili endapo kama ndugu zake wangewahi kurudi kabla yake basi wazikute hapo. Ankia akatutakia matembezi mema huku akisema tukirudi tumletee zawadi, nasi tukaingia barabarani baada ya hayo.

★★

Basi, tukawa tunatembea mdogo mdogo kuelekea Mzinga. Baada ya kufika Mzinga, kibishoo tu yaani, tukaamua kuifata Kongowe kwa kutembea pia. Mwendo wa taratibu tu, huku tukipeana story nyingi za mambo yetu wanaume ukatufikisha mpaka hapo Kongowe, na hii ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika eneo hilo tokea nimepajua Mzinga; na hata Mbagala pia.

Mwanzoni mwa eneo hilo kunakuwa na sehemu nyingi zenye biashara ndogo na kubwa za wajasiriamali sanasana, nasi tukaelekea upande ambao daladala zingesimama kwa ajili ya kubeba abiria. Tukakuta moja ambayo ilikuwa ikielekea Kigamboni ndiyo, nasi tukaingia na kukaa siti za nyuma kabisa. Mwonekano wangu na Tesha ungefanya watu wafikiri sisi ni ndugu wa damu labda, maana kuna sehemu kubwa ya pigo zetu iliyokuwa inafanana sana.

Tukiwa tu ndiyo tumekaa, Tesha siti ya dirishani kabisa na mimi pembeni yake, nikapokea ujumbe kutoka kwa mtu ambaye sikuwa nimetarajia kabisa kwa muda huu. Ilikuwa ni Adelina, dada mkubwa wa Joy; ama niseme marehemu Joy.

Yaani tokea tumebadilishana namba pale msibani sikuwahi kumtumia salamu hata mara moja, ijapokuwa nilikuwa kwenye harakati za kumtafutia mdogo wake haki kwa mauaji yaliyomsibu. Alikuwa ametuma salamu fupi, 'habari yako,' nami nikatuma jibu kuwa 'niko salama' na kuuliza yeye aliendeleaje.

Nikaanza kumsikia konda kutokea nje akisema kwa abiria fulani waingie kukaa, kwamba siti hazikuwa zimeisha. Yaani alikuwa anawashawishi kwa kusema tena kuna waarabu ma-handsome wamekaa huko mwishoni, na ndiyo Tesha akanishtua nitazame nje.

Nikaangalia kupitia kioo na kuona wanawake wawili pamoja na mwanaume kijana mmoja, wote wakiwa ni waislamu, na mwanamke mmoja alivalia yale manguo meusi yanayoficha mpaka uso kasoro macho, lakini kale kengine uso ulikuwa wazi tu na kuzungukiwa kwa hijab kichwani. Kalikuwa kembamba, keupe, kenye macho mazuri kweli, na nahisi wao walikuwa waarabu kasoro huyo mwanaume kijana aliyekuwa mweusi kabisa; akionekana kuwa mwandamani wao.

Huyo mwanamke aliyeficha uso alikuwa kama hataki kuingia kwa kuwa labda hakupenda kukaa mwishoni, naye Tesha akawa ananishurutisha tufanye jambo ili hako kadada kaingie maana alikuwa amekaelewa tayari. Adelina akawa amenitumia ujumbe akisema yuko poa na kuuliza kama bado nilikuwa Mbagala, naye Tesha akaendelea kunibonyeza-bonyeza mpaka nikahisi kero.

Agh, nikasogea kufikia uwazi wa kioo na kuwaangalia wanawake hao, nami nikasema, "Dada, ingieni tu. Nafasi ziko tatu, yaani kama vile zimebaki kwa ajili yenu tu."

Mwanamke aliyekuwa amefunika mpaka uso akawa ananiangalia sana, naye konda akaongeza spidi ya kuwashawishi.

Nikakaa sawa tena na kumwambia Tesha, "Nimeweka jitihada hiyo kama ulivyotaka. Umefurahi?"

Akacheka kidogo na kusema, "We' ni chizi! Ndo' mpaka utuchoreshe? Ona washamba wanavyotuangalia."

"Unasumbua mno," nikamwambia hivyo nikiwa makini na simu.

Nikamjibu Adelina kwamba bado niko Mbagala ndiyo, na kumuuliza kama alisharudi Mbezi. Tesha akanibonyeza kidogo, nami nikaangalia mbele na kuona wale wanawake wameshapanda na kuja upande wa nyuma. Yule mwanaume kijana hakupanda, inawezekana labda alikuwa anawasindikiza tu, nao wakaja kukaa pamoja nasi; nafasi iliyobaki ikiwa imetutenganisha katikati.

Kale kadada kenyewe kakawa dirishani kabisa, huyo mficha uso akiwa pembeni yangu, nami nikamtazama Tesha na jamaa akajikausha tu kama vile siyo yeye aliyenisisitiza kuwashawishi waingie. Inaonekana kwa muda huu abiria waliokuwa wanataka kuelekea huko mbele walikuwa wachache, kwa sababu hakukuwa hata na mtu aliyesimama na safari ikaanza.

★★

Vuuu, mwendo ukaendelea huku na mimi nikiendelea kuchat na Adelina. Ilianza kidogo kidogo tu lakini mpaka ikafika hatua tukaanza kutaniana, kirafiki yaani. Akawa ameniambia kuwa kwa sasa hivi alikuwa amekwenda pale Mbagala kwa rafiki yake mmoja kumsalimia na ndiyo alifikiria uwezekano wa kupata nafasi ya kuja kunitembelea mimi na Ankia pale nyumbani.

Unajua, mpaka leo Adelina alikuwa anafikiri mimi ni mume wake Ankia, ndiyo ikabidi nimwambie kwamba ile ilikuwa danganya toto tu niliyofanya pamoja na Ankia; wala hata hakuwa mke wangu, na ndiyo matani baina yangu na Adelina yalianzia hapo.

Mwendo ulikuwa mrefu kiasi kuelekea Kigamboni, mara kwa mara watu wakiongezeka kwenye gari na kupungua, na uvumilivu ulikuwa unamshinda Tesha. Alitaka sana kuipata namba ya kale kadada keupe pembeni yetu, lakini alihofia kwamba huenda huyo mwanamke mwingine alikuwa mama yake kwa hiyo kungekuwa na utata.

Lakini akawa ananishawishi kwa kunitumia sms nijaribu kumsemesha maana alikuwa na uhakika kwamba mwanamke huyo aliingia tu kwenye gari kwa sababu yangu, nami nikamwambia Tesha aache umalaya la sivyo ungekuja kumuua siku moja.

Kama ninavyosemaga, mimi siyo mtu wa kuogopa mtu kabisa, na kama ningekuwa nataka kupata namba za mwanamke yeyote niliyekutana naye, ningezipata. Ila kuanza kumwelezea Tesha kwamba nilikuwa sitaki tu najua ingegonga mwamba, na hata hivyo nilikuwa nataka rafiki yangu huyu ajisikie vizuri tu baada ya mambo yote aliyokuwa amepitia jana, kwa hiyo nikamwambia atulie ili nimrekebishie mitambo.

Adelina bado nilikuwa nachat naye, akiwa amesema kwamba anaweza hata akaja leo kunitembelea mimi na Ankia pale nyumbani, nami nikaona nimjibu kwanza. Nikamwandikia kuwa kwa sasa nilielekea Kigamboni kwa hiyo endapo kama alikuwa na mpango wa kwenda kwa Ankia muda huu, asingenikuta, lakini labda kama ni jioni ndiyo tungeweza kuonana.

Ilishangaza kiasi kwamba hakuwa hata amemtafuta Ankia bado kuongelea suala la kwenda kumtembelea ilhali walikuwa ni marafiki, lakini labda ni kwa sababu tu hakuwa amewahi kuwasiliana nami kabisa, na kule kudhani mimi ndiyo kichwa sasa pale kwa Ankia.

Nilipomaliza kumweleza, nikamtazama mwanamke yule mwislamu. Hilo baibui jeusi alilovaa lilificha uzuri wa ngozi nyeupe aliokuwa nao, maana nilitazama vidole vyake vyenye kucha ndefu kidogo na nyekundu, vilivyoshikilia simu ya macho matatu, na kiuhakika nikaona kwamba havikuwa na hata chembe ndogo ya sugu nyeusi. Sijui walikuwa waarabu kweli?

Tesha akanibonyeza tena na kunipa ishara kwamba eti nichangamke, nami nikatabasamu kiasi na kufungua simu yangu tena upande wa sms.

Nikaandika pale patupu hivi, 'Habari? Naomba namb yako kam hutojal'

Nikanyoosha simu kwa chini kumwelekea mwanamke huyo, naye akaitazama. Sikuwa hata nikimwangalia lakini nikamwona akinyanyua uso wake kuniangalia, hivyo na mimi nikamwangalia. Huwa naweza kuweka macho fulani hivi ya kumvuta mwanamke aamshe upendezi kunielekea, macho ya ushawishi yaani, nami nikawa namtazama kwa hiyo njia.

Akaangalia mbele tu kama vile hataki, kisha akaichukua simu yangu kichinichini na kuiunganisha na yake. Nilikuwa nimeweka uso makini, nikiona wazi jinsi Tesha alivyojikausha kwa kujifanya anatazama nje tu, na kwa jicho la mbali nikaweza kuona mwanamke huyo anaandika kitu fulani kwenye simu yangu.

Kisha, akaitelezesha simu kwenye hiyo siti kuelekea upande wangu bila kuitazama, kukiwa na pete nene zenye kuonekana kuwa kama za dhahabu kwenye vidole vyake viwili, nami nikaipokea nikiwa nimeweka mwonekano makini bado. Mambo ya siri hayo, na Tesha ndiyo akawa ameniingiza majaribuni!

Wanawake wa hivi nawaelewa sana, yaani wanapoamuaga kujitafutia vitulizo vya nje huwa wanapenda mno usiri wa hali ya juu, na huyu inaonekana alikuwa amenielewa sana ndiyo maana akakubali kufanya hivyo akiwa pembeni ya binti yake, sijui mdogo wake, sikujua.

Tesha akakunja ngumi yake karibu na paja langu, akiwa anataka tugonge tano ya ushindi, nami nikaweka kiganja changu hapo huku nikimnyanyulia kidole cha kati. Nikatazama simu yangu na kukuta namba za simu zikiwa zimeandikwa hapo, nami nikazitumia ujumbe.

'Jina lako mremb?'

Nikajikausha kama simwangalii, nami nikaona anaandika kitu fulani kwenye simu yake kisha akatazama pembeni.

Ujumbe ukaingia kwenye simu yangu, namba hiyo hiyo, ukisomeka, 'niambie lako na wew.'

Nikajibu, 'JC'

'Ndiyo nn'

'Ndiyo my name'

'Me naitw Ibtisam'

'Ooh saw. Jina lako zur kam wew mremb'

'Uremb wang umeon wp'

Nikiwa bado sijajibu ujumbe wake huo ndiyo tukawa tumeingia maegesho ya daladala kwenye eneo la Kigamboni, na watu wakawa wanasimama ili washuke.

Nikamwandikia hivi, 'Ngj tushuke nikwambie'

Kweli tukaanza kushuka mpaka nje, nami pamoja na Tesha tukaenda upande wa nyuma wa gari na kuwaangalia wanawake hao waislamu. Wenyewe wakaelekea upande mwingine kwa pamoja, huku kale kembamba kakigeuka kututazama mara moja.

Nikaangalia simu na kukuta ujumbe wa huyo mwanamke akiwa amejibu, 'Saw, lkn ntakuchek badae. Kun shm naend sahiv'

Tesha akaniuliza, "Oy, umemwambiaje? Anasemaje?"

"Kaka utakuja kuniweka matatizoni siku moja!" nikamwambia hivyo.

Tukaanza kutembea kuelekea sehemu iliyoturuhusu kuiona vyema Bahari ya Hindi.

"Kwani vipi?" akaniuliza.

"We' kila demu unataka tu, wengine ni majini."

"Ahahahah... me kwani nilikwambia namtaka huyo jini wako? Mimi nilikuwa nakataka kale kengine, we' si umechukua namba ya huyo maza'ake kwa upendo wako?"

"Nimeomba namba yake ili uje kuipata ya hako unakokataka. Halafu Tesha!"

"Hahahah... JC bana! Kwo' jini linasemaje?"

"Atanicheki baadaye, na linaonekana limeolewa. Ah, sijui hata kwa nini nimemwomba namba!"

"Si kwa ajili yangu? We' ukishamzuzua utanifanyia unyama na mimi nipate ya hako kengine. We' utakula mazeli, mimi kimweli. Tena tutafanyia kwenye double deka kabisa."

Nikacheka kidogo tu na kusema, "Tesha tunaingia Kigamboni, wanawake wazuri kama wote, utawasahau hao uliowaona. Tulia mdogo wangu."

"Ah, kwenda huko! Huu ndiyo wakati wangu, we' ushazeeka ndo' maana. Twende tukapande meli huko."

Nikacheka na kutikisa kichwa, nami kweli nikaanza kumfata.

Tukapita sehemu nyingi zenye biashara, watu wengi, wadada wazuri ndiyo usiseme, nasi tukaelekea sehemu ya kununulia kadi za tiketi kwa ajili ya kuvuka bahari kwenda upande wa pili wa Kigamboni; ule wenye majengo ya ukweli. Tesha akapata kadi, nasi tukaenda kuvuka kwa kupanda meli ndogo ya uvukishaji abiria na magari. Watu walikuwa wengi kufikia kiasi kilichohitajika, na wakati tukiwa tumeanza kuvuka mvua ikaanza kunyesha.

Mpango ulikuwa kwenda kuzurura sehemu kadha wa kadha kwa eneo hilo, lakini mvua ikaongezeka mno kiasi kwamba jambo hilo likaingiwa na utata. Yaani ile tumeshuka tu, ikatubidi tuingie kwenye daladala ambazo zilielekea Kariakoo, na safari ikaanza tena. Hii haikuwa mara ya kwanza kutembelea Kigamboni na hata niliwahi kutoka na mwanamke fulani aliyekuwa wa pande hizi, ila hiyo ni hadithi nyingine, ya kusimuliwa kwa wakati mwingine.

★★

Mwendo wa dakika kadhaa ukatufikisha mpaka Kariakoo, na kwa huku mvua ilikuwa ishakatika. Tukashuka, Tesha akiwa bado anawashwa kutembea, hivyo tukachukua mwendokasi na kwenda pande za Ubungo. Tukazurura wee, Tesha hata akanipitisha kule alikokuwa anaenda kufata wanawake wa kulipwa, chimboni yaani, naye akawa akisema hizo mishe siku hizi hafanyi.

Tukatoka huko na kuzunguka mpaka Uhasibu, nasi tukashukia hapo. Tesha alikuwa na rafiki yake mwanachuo aliyekaa eneo la Uwanja wa Benjamin Mkapa, hivyo tukatembea mdogo mdogo kuelekea huko. Alikuwa ameshawasiliana naye. Yaani safari hii yote leo ilikuwa ni kwa udhamini wa Tesha, mimi ndiyo nilikuwa kama mtalii wake, nasi tulipokuwa tu ndiyo tumeyapita malango ya uwanja nikaanza kuona mdada fulani akija upande wetu taratibu.

Tesha alikuwa ameniambia kwamba tunaenda kumsalimia tu mshkaji wake, kwa hiyo sikuwa nimetarajia kwamba ingekuwa ni mwanamke mpaka mdada huyo alipotukaribia na kukumbatiana na Tesha kirafiki. Alikuwa mfupi kiasi, mweusi, mwili wa kawaida tu, na tabasamu lake lilionyesha mwanya mdogo katikati ya meno yake ya mbele.

Wakawa wanasemeshana kirafiki sana, naye akaniangalia na kunisalimu pia. Alikuwa mchangamfu sana, jina lake ikiwa ni Dina, naye akatuongoza kuelekea pale alipoishi. Ilikuwa ni kwenye zile nyumba za wapangaji zilizojaa hasa wanafunzi wa chuo, nasi tukaingia kwenye chumba chake.

Kilikuwa simple tu, safi, godoro chini kwenye sakafu ya vigae, friji ndogo, begi la nguo pembeni ya shehena ndogo ya vyombo, vifaa vya mapodozi na manukato, viti vitatu vya plastiki. Jiko dogo la gesi lilibeba sufuria lenye chakula kwa ndani bila shaka, nasi tukakaa na kuanza kupiga story.

Mimi nilikaa kwenye kiti, Tesha na Dina wakakaa kwenye godoro, na ni wao sanasana ndiyo walioongea huku mimi nikichangia mada mara moja moja kukoleza ucheshi. Dina akaniuliza natumia soda gani, nami nikamwambia Pepsi. Tesha vilevile akasema Pepsi ingawa alitania kutaka bia.

Dina akatoka kwenda kufata soda, nasi tukabaki hapo, nikisikiliza maneno ya kipuuzi ya Tesha kuhusu jinsi nilivyotakiwa kubaki hapa leo ili nifanye jambo fulani na Dina. Ni hapa ndiyo nikawa nimepokea ujumbe kutoka kwa yule mwanamke mwislamu tuliyekutana kwenye daladala, akiwa ametuma tu 'mambo,' nami kabla hata sijamjibu, simu yangu ikaanza kuita. Mpigaji? Bertha. Hatimaye!

Sikutaka Tesha asikie jambo lolote ambalo lingemfanya atambue nani naongea naye, hivyo nikapokea nikiwa nimejihakikishia kutosema lolote litakalomshtua jamaa.

"Hallo?" sauti yake Bertha ikasikika.

"Hello, vipi?" nikasema hivyo.

"Poa. Uko wapi?"

"Niko kwa Mkapa hapa."

"Unafanyeje huko?"

"Nimekuja kwa mshkaji wangu, niambie..."

Tesha akaniuliza kwa ishara, "nani?" nami nikamwonyesha ishara pia kuwa atulie.

"Nataka uje. Au biashara uliyonayo sasa hivi huko ni muhimu sana?"

"Hakuna chochote muhimu zaidi yako dear."

"Usiniite dear, mazoea ya hivyo sitaki."

"Sawa dear," nikasema hivyo makusudi.

"Halafu wewe!" akasikika kwa ukali.

Nikajikaza nisicheke na kumwambia, "Pole, nimejikwaa tu. Ulimi hauna mfupa."

"Na nitakuja kuuwekea mfupa usipoangalia."

"Sorry."

"Toka huko sasa hivi. Niko Masai," akaniambia hivyo.

Ni muda huu ndiyo Dina akawa ameingia ndani tena, lakini wakati huu alikuwa pamoja na mwanadada mwingine mweupe, mwembamba, mrefu kiasi, aliyekuwa amevalia T-shirt nyeusi na suruali ya jeans ya samawati iliyobana. Nywele zake zilisukwa kwa mtindo wa dread nyeusi na fupi, naye akaenda kukaa godoroni baada ya Tesha kunyanyuka na kukaa kwenye kiti.

"Umeelewa?" Bertha akasikika kwenye simu.

Nikasema, "Eeh, nimeelewa. Ila... niko mbali kama hivi, naweza kuchelewa kidogo."

Dina akawa ametufungulia soda zetu na kutupatia, na ukimya mfupi uliofuata kwenye simu ukanifanya nitambue kwamba Bertha alikuwa amekasirishwa na maneno yangu.

Nikamwambia, "Ila nakuja. Nitakuwa nimeshafika muda siyo mrefu."

Likakata simu!

Kazi nilikuwa nayo. Nikashusha pumzi na kumwangalia Tesha, aliyekuwa akinitazama kama anasubiri nijielezee.

"Kuna dharura bro. Natakiwa nifike location mara moja," nikamwambia hivyo.

"Tumekuja wote, unataka kuondokaje mwenyewe bana?" Tesha akaniuliza kwa uthabiti.

"Iih, unataka kutukimbia?" Dina akaniuliza hivyo.

"Kuna dharura imetokea, nahitajika sehemu haraka ndo' maana..."

"Acha bangi! Hautoki hapa. Keki tamu kama hizi unakimbia kweli?" Tesha akasema hivyo kiutani.

Tukacheka kidogo, na Dina akamsonta huku akisema, "Afu' wewe!"

"Inanibidi tu kaka," nikamwambia Tesha.

"Jamani, mbona ghafla? Chakula hiki napakua," akasema Dina.

"Oh usijali Dina, niko poa. Labda umpakulie huyu mbwa," nikamwambia hivyo.

Akacheka kidogo, naye Tesha akasema, "Em' pakua mama, tule."

"Basi kunywa hata soda, imeshafunguliwa," akaniambia hivyo yule mdada mwingine.

"Ee, kunywa soda ndiyo uende kaka," Dina akaniambia.

"Poa," nikajibu.

Ingenibidi nipige hii soda fasta maana huyo Bertha hakuwa mtu wa subira hata kidogo, na hiki ni kitu ambacho nilikuwa nimekisubiria sana kwa hiyo wiki nzima kwa hiyo nisingeweza kuchezea nafasi hata kama ningepewa ofa ya utatu na hawa wadada!

Nikawa napiga fundo ndefu ndefu, huku nikiwa nimeanza kuchat na yule mwanamke mwislamu pia. Alikuwa mmoja kati ya wale wanawake ambao walipenda mtu aende moja kwa moja kwenye pointi ya kitu ambacho alitaka kutoka kwake, nami nikamwambia ndiyo, nilimkubali sana kutokana na kupenda macho yake na ngozi yake.

Akaniambia ooh nimeshaolewa, kwa hiyo ukinitaka lazima upande ngazi, nami nikamwambia hakuna ngazi za kupanda; ikiwa alinikubali pia basi tuje kucheza, lakini asipotaka basi sitalazimisha. Kwa kauli hiyo akawa ametulia kwanza, nami nikawa nimemaliza soda.

Nikamshukuru Dina na kusimama, Tesha bado akiwa analalama kuhusu mimi kuondoka, hivyo ikanibidi nitoe ahadi ya kuja naye tena kesho ikiwezekana kumtembelea rafiki yetu. Dina alipenda sana hilo wazo na kusisitiza nisije kuacha kuja, nami nikamwambia aondoe shaka. Huyo rafiki yake mwingine alikuwa akiniangalia sana kwa sura yake ya kiupole, nami nikamuaga pia nikiwa hata simjui jina.

Nikawaacha marafiki hao hapo na kuanza kuelekea barabarani, nikiwa natumaini kuwahi, na Tesha asijue kwamba sehemu niliyokwenda ilikuwa ni Masai. Angeshangaa sana!

★★

Nilifanikiwa kupata usafiri wa daladala zilizoelekea Mbagala, na mpaka kufikia huko tayari ilikuwa inaelekea kuingia saa moja. Nilikuwa nikijiuliza ni kwa nini madam Bertha alikuwa ameamua kuja Masai mapema sana leo, lakini hayo yote ningeyajua nikishafika pale.

Badala ya kuchukua daladala tena kutokea Rangi Tatu, nikaamua kupanda bodaboda ili niwahi zaidi, brrrr mpaka Mzinga, nami nikaunganisha moja kwa moja kufikia Masai, lakini nikaona nielekee kwa Ankia kwanza.

Nikafika hapo dukani kwa Fatuma na kumkuta huyo dada pamoja na wanawake wengine wengine wakiwa wamekaa kama kikundi cha kupiga umbeya, nami nikamwambia bodaboda anisubirie nikachukue mzigo ndani kisha anirudishe Masai upesi. Nikawapita hao wavaa dera kama siwaoni, nami nikaelekea mpaka ndani na kuingia.

Akili yangu ilikuwa imekazia fikira jambo moja tu kiasi kwamba mpaka nikashtuka kiasi moyoni baada ya kuingia na kumkuta Ankia akiwa amekaa pamoja na Adelina! Ile hali ya kutotegemea kumkuta mwanamke huyu hapa ingawa tulikuwa tumewasiliana ilikuwepo yaani, halafu nilikuwa kwenye kasi kwelikweli.

Wawili hao, baada ya kuniona, wakatabasamu kwa pamoja, nami nikatabasamu pia na kusogea karibu zaidi na walipokaa.

"Mume amerudi," Adelina akasema hivyo.

"Ee, baba mwenye nyumba ndiyo kafika," Ankia akasema hivyo pia.

Nikajikuta tu natenda bila kufikiri sana kwa kuinama na kumkumbatia Adelina, nami nikamwambia, "Karibu."

Nafikiri alikuwa ameshangaa kiasi lakini akaweza kucheka kidogo kwa pumzi, naye akasema, "Asante."

Nikamwachia na kusema tena, "Karibu sana."

Kisha nikaelekea chumbani, bila shaka nikiwaacha wanawake hao wanatazama haraka yangu.

Nikaingia chumbani na kutoa yale madawa niliyotengeneza, nami nikachukua kiasi kidogo na kukiweka kwenye karatasi tu baada ya kuwa nimekosa pa kuwekea, kwa kuwa sehemu niliyohifadhia dawa yote ilikuwa ndani ya mifuko minene; madawa yakionekana kama glucose. Nikachomeka hicho kikaratasi mfukoni, kisha nikaelekea sebuleni tena.

"Unatoka?" Ankia akauliza hivyo.

"Ndiyo, kuna sehemu nafika mara moja lakini... sikawii, nakuja. Sawa?" nikaongea hivyo nikiwa nimeelekeza fikira zangu kwa Adelina.

Akatikisa kichwa kukubali, naye Ankia akasema, "Unawahi nini kinachokutoa kijasho hivyo? Tuambiane..."

"Utajua tu, ngoja nirudi," nikasema hivyo na kuelekea mlango.

Nikawaacha wanawake hao wakicheka kidogo, nami nikaenda mpaka nje tena. Nikapanda bodaboda na kugeuza kuirudia Masai, nasi tukafika hapo huku sasa giza likiwa limeshaingia. Nikamlipa jamaa na kumwambia atokomee, kisha nikaelekea pale ndani.

Wanywaji walikuwepo na nafikiri kuna wahudumu wapya waliokuwa wameongezwa hapa na wachache niliowajua kuondoka, nami nikawa nimemwona Bobo pamoja na DJ fulani hivi wa hapo Masai. Nikamfata.

"Oyo, mchina..." akaniambia hivyo tukiwa tunagonganisha mabega yetu kirafiki.

Nikagongesha tano kwa yule DJ pia, kisha nikamwambia Bobo, "Oya umepotea kweli."

"Ah, mimi, wewe? Yaani hutokei Masai siku hizi mwanangu. Check watu wanavyokuangalia kama vile hujawahi kuonwa hapa," akasema hivyo.

Nikatabasamu na kusema, "Na mimi nimetingwa kaka, ila mdogo mdogo narudi. Ishu zinakwendaje?"

"Kama kawa budha. Oy... mtu wako yupo huko ndani," akaniambia hivyo kwa kuninong'onezea sikioni.

"Eeh, nimeona gari nje," nikamwambia.

"Yuko VIP, kamchangamkie..."

"Ndo' mpango mzima," nikasema hivyo.

Tukacheka tena pamoja, kisha nikamwacha hapo na kuelekea pande ya VIP. Na Bobo alikuwa sahihi kabisa, watu walikuwa wananiangalia kweli, lakini umakini wangu wote ulikuwa kumfikia huyo madam.

Nilipofika mlangoni, nikajiwekea hali ya utulivu, kisha nikaingia ndani hapo. Nikamkuta madam Bertha akiwa amekaa sofani, glasi yenye wine kiganjani, na kwenye sofa la pembeni alikaa yule baunsa wake; a.k.a shemeji.

Kama kawaida ya mwanamke huyo, alikuwa amependeza kwa kuvaa kigauni kifupi chekundu, kilichoyaacha mapaja yake meupe wazi kutokana na namna alivyokuwa amepiga nne, na inaonekana kilikuwa cha mgongo wazi. Wakati huu alishonea wigi la nywele za kizungu kichwani, na baunsa wake alikuwa amevaa kaushi tu na suruali nyeusi, akionyesha misuli yake imara.

Nikasogea usawa wa meza moja hapo, nami nikamtikisia kichwa jamaa kama salamu, naye akairudisha. Nikamwangalia Bertha, ambaye alikuwa akinitazama tu kwa utulivu, nami nikamwambia, "Nimefika madam."

"Umechelewa," akaniambia hivyo.

"Kweli? Mbona naona kama bado party haijaanza?" nikamuuliza hivyo.

Baunsa wake akamwangalia na kucheka kidogo, naye Bertha akawa amenikazia macho yake.

"Tupishe," Bertha akamwambia hivyo jamaa.

Baunsa akasimama na kuja upande wangu, naye akaniuliza, "Una ule unyama jembe?"

"Nakosaje labda?" nikamuuliza hivyo.

Akatabasamu huku akitikisa kichwa taratibu, nami nikaitoa ile dawa na kumfungulia.

"Si iko kama ile?" akaniuliza hivyo.

"Kwa asilimia zote," nikamwambia.

Akachovya kwa kidole na kulamba, kisha akatikisa kichwa kwa nguvu kiasi na kunishika begani. "We' dogo ni nyoko!" akaniambia hivyo.

Nikatabasamu kidogo, naye akanipita na kutoka ndani humo.

Nikabaki na madam. Alikuwa ananitazama kwa yale macho ya kuhukumu bado, naye akasema, "Njoo."

Nikatii na kumfata. Sikuwa na hofu kumwelekea huyu mwanamke, ila kujifanya mnyenyekevu sana ilikuwa lazima. Nikasimama usawa wa sofa alilokalia na kubaki mtulivu.

"We' vipi, si ukae?" akaniambia hivyo.

Nikasogea na kukaa kwenye sofa karibu yake.

Akawa ananitazama sana, naye akasema, "Yaani hiyo sura! Kama mwanamke!"

Dah! Kashfa hizo.

Nikatabasamu kwa kujilazimisha na kusema, "Asante. Moja kati ya silaha zinazonisaidia kupita huku na kule ni hii sura."

Akacheka kwa mguno, kisha akaweka glasi yake pembeni.
"Nimekufatilia kwa hiyo wiki dogo, naona una maisha magumu sana mpaka ukaamua kutoka Goba Center kuja kuishi Mbagala," akaniambia hivyo.

Umeona sasa? Nilikuwa sahihi. Huyu mwanamke alikuwa amefanya uchunguzi kunihusu mpaka kujua kitu ambacho bado sijaelezea kujihusu. Nikataka kujua anaelewa mambo mengi kadiri gani kuhusu maisha yangu.

"Ahah... eeh... maisha magumu. Nimekaa sehemu nzuri lakini... hazijanifiti ndo' maana nimeangukia huku sasa hivi," nikaongea hivyo kiupole, ikiwa kimtego zaidi.

Akasema, "Me sijali ulikuwa unaishi vipi. Nataka tu ujue nikiamua kukuharibia maisha yako endapo kama utanigeuka basi sitosita kuanza hata na familia yako."

"Usiwe na hofu juu ya hilo madam. Siwezi kukusaliti. Kwanza... familia yangu iko Mwanza, mimi huku ni mtafutaji tu kwa hiyo niko mwenyewe," nikamdanganya.

"Una uhakika na kile ulichojiingiza kukifanya huku dogo?" akaniuliza.

"Ndiyo najua. Nina ujanja mwingi, usinichukulie poa. Sema mambo huko Goba hayakwenda fresh tu ndo' maana nikaja huku kujitafuta, na najua nimejipata tena kwa kuwa chini yako. Sitakuangusha madam. Najua nachokifanya, na nitafata utakachonielekeza kufanya," nikamwambia hivyo.

Akatulia kidogo, kisha akasema, "Sawa. Nipe hiyo kitu nionje."

Nikamfungulia kikaratasi chenye dawa ya cocaine, naye akachovya na kulamba kidole chake huku akinitazama kwa macho makini. Kidogo tu yakalegea naye akawa ananiangalia utadhani ananitaka kimapenzi. Ah mimi nilikuwa mtaalamu bwana!

Na angalau kufikia hapa nikawa nimetambua kwamba hakujua mengi zaidi kuhusu maisha yangu isipokuwa tu kuwa amefatilia na kujua nilikotokea kihalisi kabla ya kufika huku, kwa hiyo mchezo wangu kwake ungeendelea taratibu.

Vibe likiwa limemgonga, akaniambia, "Unyama mzuri huu."

Nikatabasamu kidogo.

"Kuna ishu nataka nikushirikishe," akasema hivyo.

Pasi ndefu hiyoo! Nikatikisa kichwa kuonyesha namsikiliza.

"Kesho utakuja pale pale ulipokuja siku ile, uje jioni," akasema hivyo.

"Sawa. Nije na unyama wetu?" nikamuuliza.

Akaweka macho ya udadisi, naye akauliza, "Unamaanisha kwamba unao mwingi?"

"Nimetengeneza kiasi fulani. Hakijazi mifuko mikubwa lakini si unajua ni tamu mno, kwa hiyo kidogo tu...."

"Ni nyingi," akamalizia maneno yangu.

Nikatikisa kichwa kukubali.

Akaninyooshea kidole chake na kunipiga kofi laini shavuni, naye akasema, "Safi sana. Kumbe we' kweli wa faida. Uje nao kesho. Nitakuelekeza mengine ukishafika."

"Imeisha hiyo," nikamwambia hivyo.

Akawa ananitazama kwa njia fulani utadhani alikuwa ananisoma, naye akasema, "Nataka kuona kama we' siyo mwanaume sura tu."

Nikamsogelea karibu zaidi na uso wake na kumuuliza, "Kivipi?"

"Kesho. Kesho ndiyo nitaona," akasema hivyo huku akipindisha shingo yake kiasi, midomo yetu ikiwa karibu sana.

Nikasema, "Ahaa... nilidhani unataka nikuonyeshe sasa hivi."

Akatabasamu na kuangalia chini, kisha akatoa tusi kunielekea bila kuniangalia.

Nikatabasamu pia baada ya kuona kwamba alikuwa ameanza kuonyesha roho ya kuniamini kiasi, na bila shaka ishu hiyo ya kesho ingehusiana na mengi ya vitu nilivyotaka kuhakikisha vinaporomoka kwa msaada wa askari Ramadhan. Ingebidi kusubiri kuona.

Akawa amekivuta kinywaji chake tena na kuikunjua miguu yake, naye akaniangalia usoni. "Kwa hiyo toka mpenzi wako amekufa, haujaingiza substitute?" akaniuliza hivyo.

Nikatazama chini kwa ufupi, nikielewa alimaanisha Joy.

"Oh, nimegusa pabaya? Mhm... inawezekana ulikuwa unampenda sana."

"Joy na mimi ilikuwa kama biashara tu. Wala hakukuwa na kitu tense kivile," nikamwambia.

"Mm? Unanidanganya mimi? Ahah... unajua bado natakiwa niwe mwangalifu sana juu yako maana inaweza ikawa unataka kumlipizia kisasi mpenzi wako," akasema hivyo.

Dah! Lina akili!

Nikatoa kicheko cha kujilazimisha na kusema, "Madam una vituko. Najua hauamini hilo kwa sababu tayari unaniamini mimi."

"Unajuaje?"

"Usingemwambia bodyguard wako atoke nje kama ungeamini naweza kukufanyia kitu kibaya. Hadi dawa nayotengeneza unakula, kama ingekuwa kukuua si ningewekea hata sumu?"

Akatulia kidogo akiniangalia kwa umakini, naye akasema, "Huwezi kuwa na uhakika sikuzote. Ndiyo maana bado nataka nikupime."

Nikaegamia sofa, huku nikimwangalia kizembe na kusema, "Fanya chochote madam... JC ni mali yako sasa hivi."

"Nhhaa... unanifurahisha. Bado akili yako ni ndogo sana."

Nikamshika kiunoni taratibu, naye akawa makini na kuniangalia machoni. "Ndiyo unifunze sasa. Mi' wa faida kweli," nikamwambia hivyo kwa sauti ya chini.

Akabaki kuniangalia tu huku akizungusha-zungusha kinywaji ndani ya glasi aliyoshika, na ni hapo ndiyo mlango wa kuingilia ndani humo ukasikika ukifunguka. Kwa sababu nilikuwa nimeupa mlango mgongo, nisingeweza kujua nani kaingia upesi, lakini nikaona macho yake Bertha yakimtazama aliyeingia kwa njia ya kukerwa.

Nikiwa nafikiri ni mhudumu labda au yule baunsa, nikageuka bila kuwa na utayari wa kumchukulia serious huyo mtu aliyeingia mpaka nilipojikuta nashangaa kiasi baada ya kuona ni Chalii Gonga mwenyewe!



★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
Ok
 
Back
Top Bottom