Simulizi: Mimi na Mimi

Simulizi: Mimi na Mimi

MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

SEHEMU YA ISHIRINI NA NNE

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…


Ile nimemwona tu jamaa, pigo la moyo lilidunda kwa nguvu kiasi kutokana na kutotarajia jambo hilo, nami nikaliachia titi la Khadija. Mwanamke huyo akautoa mkono wake kwangu pia, akijikausha kwa kutazama pembeni, na Joshua alikuwa amesimama usawa wa sofa huku akitutazama. Nikawa namwangalia kwa umakini tu, nikishindwa kuelewa alikuwa ametokea wapi.

Cha ajabu ni kwamba, baada ya kuwa amesimama na kutuangalia namna hiyo, akaachia tabasamu hafifu huku akiniangalia kwa njia ya kirafiki usoni, nami nikaendelea kumtazama kwa umakini tu. Nilikuwa na uhakika kabisa kwamba aliona kile ambacho kilikuwa kinatokea hapo baina yangu na mke wake, lakini akajifanya kama hajaona ili kuendeleza unafiki wake.

Hapo ndiyo Bi Zawadi akawa ametokea jikoni, akiwa ameshika kikombe chenye chai na kusema, "Joshu... hadi nilikuwa nimeshasahau kama uko ndani jamani."

"Eeeh, nisamehe tu mama, huko tunakotoka hatuna vyoo vya kukaa. Hiki chenu kizuri hadi kidogo nisinzie," jamaa akasema hivyo.

Kumbe jamaa alikuwa chooni anajisaidia muda wote huo? Na inaonyesha alikuwa ameshusha limzigo lizito kweli maana alikaa zaidi ya nusu saa huko. Na wengine huwa wanakaa mpaka masaa!

Bi Zawadi akacheka kidogo na kuja kunipatia chai, naye akaenda kukaa kwenye sofa lake pale alipozoea.

Nikataka kunyanyuka ili nimpishe Joshua aketi na mke wake, lakini jamaa akasema, "Ah we kaa tu bro, me niko safi hapa."

Nikawa namwangalia tu kwa utulivu, naye akakaa kwenye mkono wa sofa huku akilaza mkono wake juu ya egamio la sofa karibu na Bi Zawadi. Mke wake alikuwa ameushona tu pembeni, akitulia kama malaika mpya aliyezaliwa leo. Ni hapa ndiyo Mariam akawa amerudi tena, na sijui kwa nini tu alikawia mno.

Akaja mpaka sofani akiwa ameshika penseli, boksi lenye rangi, pamoja na counter-book kubwa, naye akasema, "Hizi hapa. Tumchore sasa."

"Mamu subiri kwanza kaka anywe chai," Khadija akamwambia hivyo.

"Eeh, ngoja kwanza. Mtachora baadaye," Bi Zawadi akasema hivyo pia.

Mariam akaweka uso wenye kuonyesha kwamba alikwazika, nami sikupenda kumwona hivyo. Lakini ningefanyaje na sukari ilikuwa imeshakorogwa kwenye chai?

"Mamu... usinune mama, eti? Anamalizia tu kunywa chai halafu ndiyo mtachora. Tena na mimi nitachora na nyie, sawa?" Joshua akamsemesha hivyo kwa kubembeleza.

Mariam akawa bado amenuna, naye akanyanyua bega lake kuonyesha kwamba hataki.

Nikasema, "Haina shida, tutachora huku nakunywa na chai. Cheupe wangu, asante. Mamu... twende."

Nikasimama pamoja na Mariam, ambaye bado alikuwa kama amenuna lakini akaridhia kwenda nami upande wa dining, nasi tukakaa vitini na kuanza kuchora.

Nilikuwa namchorea mambo rahisi kama kiti, mpira, yai, kikombe, naye angeiga kwa kujitahidi kabisa kuvifananisha. Nikawa namsifia, hata Bi Zawadi na Joshua wangekuja hapo na kuangalia kazi za binti na kumpongeza, na hii ilisaidia kumwongezea Mariam hali ya kujiamini zaidi nilipoanza kumpa michoro ya mambo tata zaidi.

Aisee Joshua alikuwa anajua kuigiza! Yaani nilikuwa nikitazama namna alivyoongea na kuwatendea wanawake hawa kana kwamba alikuwa amezaliwa kwa mara ya pili na kuwa mtu tofauti kabisa, lakini ukweli wa utu wake mbaya bado ulikuwa pale pale.

Sikupenda kabisa alipomsogelea Mariam na kumsemesha ama kumgusa, na nilikuwa nimeona niendelee kutulia tu ili amani ambayo niliiona ndani yake Mariam kwa wakati huu ibaki hapo hapo kwanza. Huyu Joshua angehitaji kuumbuliwa na kuondoshwa hapa kwa nguvu ya Miryam pekee, ambaye alikuwa ndiyo njia iliyofanya jamaa akapata kiburi cha kurudi tena.

β˜…β˜…

Kufikia mida ya saa saba mchana tayari mke wake Joshua alikuwa ameshaanza kufanya harakati za mapishi hapo ndani, na sijui kwa nini tu lakini mpaka sasa hivi bado tu Tesha hakuwa amefika. Hali yake Mariam kwa wakati huu ilikuwa changamfu kweli baada ya mimi kufanya kitu kilichompa furaha sana.

Alikuwa ameleta picha moja nzuri sana ya Miryam kutoka kwenye album, naye alinitaka nimchore dada yake. Nilikuwa najua kuchora lakini ikifikaga kwenye pua za watu ndiyo huwaga naharibu kabisa, ila nilipoichora pua ya Miryam niliikuza sana kwa makusudi ya kumchekesha Mariam. Na walicheka mno! Bi Zawadi, Khadija, na hata Joshua Iskariote, wote wakawa wanaiongelea mno, na kilichokuwepo ilikuwa kuja kuwaonyesha wengine na hasa Miryam, ili waone itikio lake.

Halafu huyo Khadija, tokea muda ule Joshua katushtukiza, alikuwa analeta pigo za kimahaba kunielekea kwa kunitazama kwa yale macho na tabasamu la "ninakutaka," ama kujipitisha-pitisha dining ili niangalie jinsi kalio lake lilivyonesa huko nyuma, lakini mimi bado nilikuwa tu nawaza kuhusu usalama wa Mariam kwa ujumla kwa kuwaza zaidi juu ya mume wa huyo mwanamke.

Jamaa hakuwa amenisemesha tena kwa sababu nilionyesha wazi kwamba sikutaka mazoea naye hata kidogo, lakini niliweza kuona namna alivyokuwa ananitazama sana kama vile ananichora kutambua nimekaaje-kaaje, na nadhani alikuwa ameshatambua kwamba sitaki shobo naye kabisa.

Hazijapita dakika nyingi sana toka imeingia saa saba ndiyo tukasikia mlango wa geti nje ukifunguliwa na kufungwa, na baada ya hapo mlango wa kuingilia sebuleni hapo ukafunguka pia na Tesha kuingia. Mwonekano wake ulikuwa ule ule wa jana, lakini bila shaka kwa siku hii alikuwa ametoka huko kwa Dina akiwa ameoga.

Baada ya yeye kuingia, akamsalimu mama mkubwa wake na kuitikiwa vizuri tu, lakini nikaona anamtazama Joshua kwa njia ya kusita kutoa salamu. Akawa ameniona nikiwa na Mariam hapo dining, nami nikamtikisia kichwa kisalamu. Akairudisha salamu yangu namna hiyo hiyo, naye Joshua akaona amsemeshe.

"Vipi mdogo wangu?" jamaa akamuuliza hivyo Tesha.

"Poa," Tesha akamjibu kibaridi tu na kumpita.

Akaja mpaka upande wetu na kumsalimia Mariam, na binti akamwonyesha ule mchoro wa picha ya dada yao.

Tesha akacheka na kusema, "Dah! Kaka naona unataka kutangaza vita na Mimi! Akiiona anaweza akavimba wiki nzima."

"Kweli? Itabidi Mamu asimwonyeshe," nikamwambia.

Mariam akasema, "Tamwonyesha... atacheka."

"Eeh usiache kumwonecha... atacheka chana," Tesha akasema hivyo kwa kuiga ongea ya Mariam.

"Bado hizo silabi silabi hazijakaa safi mdomoni kwa Mamu eh? Ila baada ya muda ataongea vizuri kabisa kama zamani," Joshua akadakia kwa kusema hivyo kutokea pale masofani.

Tukaangaliana na Tesha machoni kwa njia ya kukerwa na hilo. Utafikiri alijua lolote, eti silabi silabi!

Bi Zawadi akamwambia Joshua, "Eeeh mazoezi yataendelea kumsaidia sana."

Tesha akakaa kitini na kutoa simu yake huku akiniambia, "Dah! JC
mwana bora jana usingeondoka yaani Dina alipika bonge la msosi."

Nikatabasamu tu.

"Hivi Dina hajamalizaga tu kusoma?" Bi Zawadi akamuuliza Tesha.

"Eti?! Yaani mpaka Leo bado tu anakomaa na vitabu. Siyo mbaya lakini, kwao wanazo kwo' lazima aongeze mamiaka," Tesha akamwambia hivyo.

Inaonyesha wanafamilia wa Tesha walimfahamu Dina pia kutokana na jinsi ambavyo Bi Zawadi alimwongelea, labda hata alikuwa mtoto wa rafiki wa karibu. Simu yangu ikaingiwa na ujumbe, nami nilipouangalia nikakuta ni Tesha ndiyo kanitumia. Sikumtazama kwa sababu tayari nilielewa kwamba alikuwa ananisemesha bila kutaka wengine wajue amesema nini, nami nikausoma.

'Huyu fala amekuja saa ngp,' ikasomeka hivyo sms yake.

Nikajibu, 'Nimemkut mapem. Labd amekuj asubh San'

Bi Zawadi na Joshua wakawa wanaendelea na maongezi mengine, huku mke wa jamaa akiwa ameenda kukaa sofani na mume wake kwa kile kilichoonekana kuwa kumaliza kupika mboga, naye Tesha akawa anamsemesha Mariam huku akiendelea kuchat na mimi.

'Bado analet maigizo yak tu hap,' ujumbe mwingine wa Tesha ukasomeka hivyo.

Nikajibu, 'Uhakika. Ila we mtulizie tu kwanz'

'Na Bi mkubw mbn simwon?'

'Dada yako kampelek kupim, hakuw frsh'

'Aa, barid. Tunakaa hapa hapa kuhakikisha huyu bwege haondok hat na bakul'

Nikatabasamu kidogo na kumwandikia, 'Kuna kitu ntakwambia, ila baadae'

'Kuhusu Joshu?'

'Mke wake.'

'Si uniambie now?'

'Tulia. Ni ubuyu mwing'

'Au siyo? Kama vile nshaanza kunusa haruf yak. We mkal san'

'Haha akil yako hiyo'

'Kam yakwako tu. Twend hat kw Ankia tukaongee'

'Poa.'

Nilipomaliza kumjibu hivyo, nikawatazama wale wengine pale sebuleni na kusimama, kisha nikasema, "Mrembo wangu, me wacha niwakimbie sasa."

Bi Zawadi akasema, "He! JC baba, tunaivisha."

"Ahah, usijali... na ningependa sana kuenjoy mlo. Sema... kuna ka-appointment sehemu... nahitajika kwenda," nikamwambia hivyo.

Nilikuwa nataka tu kwenda kwa Ankia ndiyo nikale maana alikuwa anaandaa msosi wa ukweli! Nilikuwa nimepitisha muda sijala pilau kwa hiyo masikio yalikuwa yamenisimama.

"Una kaapointinamenti wapi na wewe? Utafikiri umeoa!" Bi Zawadi akasema hivyo.

Tesha akacheka kwa furaha na kusema, "Kaapointinamenti? Ma' mkubwa hauendi mbinguni!"

Wengine wakacheka kidogo pia.

"Kisa?" Bi Zawadi akauliza.

Tesha akasimama na kusema, "Unaharibu lugha za watu bwana. Oya... unajua ile 'what's wrong' wazungu wanayoisemaga kuonyesha wanajalii? Mwambie ma' mkubwa aiseme... utacheka! Eti 'wothilong'o mai diya!'"

Wote tukacheka kwa pamoja, naye Mariam akasimama pia huku akiniangalia kwa furaha.

"Ila Tesha! Ahahah... ananizingua tu huyu. Me naisemaga hivyo?" Bi Zawadi akalalamika.

"Hebu iseme umpinge," Khadija akamwambia hivyo Bi Zawadi.

"Whots wrongg," Bi Zawadi akaivuta kama kwa lafudhi ya mzungu.

Tesha akacheka sana.

"Sasa je! Mbona ameisema vizuri?" Khadija akamwambia hivyo Tesha.

"Eeh, umeisema vizuri sana mama. Kama mzungu uliye wewe," Joshua akampamba namna hiyo.

"Muone kwanza! We' ndiyo huendi mbinguni Tesha," Bi Zawadi akasema hivyo kimaringo.

Tesha akasema, "Haya bwana, kisura umeshinda. Twende nikutoe nje bro."

Nikiwa natabasamu tu, nikamwambia Mariam, "Tutaonana baadaye rafiki yangu. Endelea kuchora-chora hizi hapa... na hizi... halafu uje umwonyeshe dada, sawa?"

Akatikisa kichwa kuonyesha uelewa, na baada ya Tesha kuyaangalia yale niliyomwambia Mariam ayachore, akatabasamu kidogo.

Nikaanza kuelekea hapo walipokaa wengine, Tesha na Mariam wakinifuata kwa nyuma, na ile tu ndiyo nataka kumpita Bi Zawadi, Joshua akasimama. Alikuwa amekaa pale ambapo niliketi na mke wake mwanzoni, Khadija akiwa pembeni yake wakati huu, kwa hiyo aliposimama ikawa ni kama vile amenizibia njia. Nikamtazama machoni kwa umakini.

"Kaka... ninaomba kuongea na wewe kabla hujaenda," akaniambia hivyo, kistaarabu tu.

Nikaendelea kumtazama kwa umakini, huku jicho pana likiona namna ambavyo mke wake alituangalia kama mtu mwenye wasiwasi.

"Maongezi tu mafupi ya kiume. Na Tesha pia. Twendeni hapo nje," Joshua akasema hivyo.

Nikatikisa kichwa kuonyesha nimekubali, nami nikamtazama Tesha na kukuta ananiangalia kwa umakini. Yale macho yanayojuana yaani. Haya, nikamuaga Bi Zawadi na Mariam kwa mara nyingine tena, na kisha sisi watatu tukatoka ndani hapo na kwenda pale kibarazani. Jua lilikuwa kali siyo mchezo!

Mimi na Tesha tukasimama kama vile tumemzingira Joshua, akiwa katikati ya ile pembetatu itengenezwayo na watu watatu kusimama pamoja, naye akawa anatuangalia kwa njia yenye upole.

"Eh bwana... nimeona nichukue hii nafasi kuzungumza na nyie kwa pamoja kwa sababu sisi wote ni wanaume, sawa? Tunaelewana kwa mapana zaidi ya vile ambavyo wanawake wanaweza kutuelewa... kwa hiyo... najua nitakayosema mtayaelewa kwa akili pana zaidi..." akaongea namna hiyo.

Alikuwa ameanza kuongea kwa njia iliyoonyesha kwamba alifanyia mazoezi kile ambacho alitaka kusema, nasi tukaendelea tu kutulia huku mimi nikitazama chini, na Tesha akimwangalia jamaa machoni kwa umakini.

"Najua kuna mambo mengi yametokea na... mengi niliyofanya ni mabaya..."

"Hapana, ni yote," Tesha akamkatisha kwa uthabiti.

Joshua akatulia kidogo, kisha akasema, "Ndiyo... yote niliyofanya ni mabaya. Siwezi kusema naweza... kufanya chochote kile kutangua mabaya yote niliyofanya, mabaya yote niliyosema, na kwa wewe Tesha... naelewa bado una hasira na mimi. Najua nimekufanya unichukie sana... na najua itachukua muda mpaka kufikia kipindi ambacho utanisamehe kabisa mdogo wangu... lakini hiyo ndiyo sababu niko hapa sasa hivi. Nimetambua kwamba niliwaumiza sana, na huwa natamani hata muda urudi nyuma ili paap, nifute yote mabaya, lakini haiwezekani kabisa. Ndiyo maana niko hapa sasa hivi... nimerudi ili tuijenge upya tena familia yetu... kuwe na amani tena. Hii yote naifanya ili niweze kuja kufa nikiwa na amani ya rohoni, siyo kuja kuingia kaburini nikiwa nachukiwa na ndugu zangu kabisa Tesha. Nyie ndiyo familia niliyonayo, niliyobakiza, na ninajua... najua nimewakosea sana kwa sababu ya kuendekeza tamaa lakini Tesha... Tesha nakuapia kwa majina ya marehemu wazazi wetu... niko hapa tena ili nirekebishe mambo upya... kwa ajili ya kumbukumbu ya wazazi wetu..." mwamba akaongea hivyo kwa upole.

Nilimtazama usoni kwa mkazo sana, nikiwa nahisi hasira ya kutaka hata kumtandika ngumi moja tu ya pua, lakini nikaendelea kutulia. Tesha akawa ameangalia pembeni baada ya kaka yake kusema hayo, naye Joshua akanitazama.

"Bro... nyie wote ni ndugu zangu. Najua mara ya kwanza tumekutana tulizinguana, na ilikuwa ni makosa yangu. Leo ndiyo nikuombe msamaha kaka. Kwa... kukutukana, kukutishia kukupiga, yaani..."

"Ahah... ungemweza sasa JC?" Tesha akamkatisha kwa kumuuliza hivyo.

Nikacheka kwa pumzi ya chini na kuangalia pembeni.

"Eee... tena unasema kweli. Nisingemuweza... angenivuruga kabisa. Unaona mdogo wangu... matatizo hayo yote ningejisababishia tu kwa kazi isiyokuwa na faida, na... Miryam ndiyo akanifanya nifungue akili yangu tena. Aliniita, akanikalisha, huyu mwenyewe alikuwepo hiyo siku ofisini kwake... aliniita, nikaenda kumsikiliza, nikamwelewa..." jamaa akaongea hivyo.

Tesha akaniangalia na kuuliza, "Da' Mimi alimwita huyu ofisini kwake? Na wewe ulikuwepo?"

Kabla sijamjibu, Joshua akadakia, "Eeh, aliniona pale, nilienda. Miryam huyu! Miryam ndiyo dada! Yaani kama nisingekuwa fala fala huko mwanzo, sasa hivi tungekuwa tunaishi bila misukosuko yote. Na ni makosa yangu..."

Aliongea, yaani, kama mtu mwenye huzuni sana, nami nikatazamana na Tesha kama vile bado hatumwelewi jamaa.

"Sikilizeni. Mimi hapa nipo... kutafuta tu amani tena... kuwaenzi wazazi wetu Tesha, na... ili Miryam na Mariam wawe na furaha. Nakuomba tu Tesha yale mapito ujaribu kuyaweka pembeni mdogo wangu. Hata kama itakuchukua muda mrefu kunisamehe, haina kwere, la muhimu tu kuwe na amani kwa muda huu wote. Mimi sitaacha kuwaonyesha jinsi nilivyobadilika... na Miryam amenisaidia sana, mpaka sasa hivi Mamu haniogopi tena, umeona? Kwa hiyo ni hivyo. Halafu nyie yaani... washkaji sana, tena huyu... JC... msomi hahah... tukiwa good hapa mambo mengi sana yatanyooka," Joshua akasema hivyo.

Alipokuwa ametamka jina langu, alinishika begani kwa njia ya kirafiki, lakini Tesha akautoa mkono wake kwangu taratibu.

"Sikia Joshua. Kama ulivyosema... kukusamehe itachukua muda. Sijui kuhusu wengine, ila mimi... itachukua muda. Kwa hiyo, we' endelea na shenanigan yako ya kutafuta amani, fresh, hakuna shida. Me nimetulia. Sikugusi, sikufukuzi tena. Ila... nitoe tu kaonyo. Ikitokea tu yaani, kale kashetani kako kakakurudia... kakakuingia tu tena ukaamsha majini-wizi yako, aisee! Siyo Mimi, ma' mkubwa, wala Mzee Hamadi watakaoweza kukusave tena. Zamu hii tutatibuana haswa... na nakwambia haya yote JC yuko hapa anasikia, kwa hiyo tusije tukalaumiana. Ushanisoma?" Tesha akasema hivyo kwa sauti ya chini lakini imara.

Kijana huyu alikuwa ameongea kile kitu ambacho hata mimi ningesema pia, lakini kwa wakati huu nilikuwa nataka kuyatimiza hayo maneno ya Tesha kwa sababu nilijua vizuri sana kwamba hako kashetani bado kalikuwa kichwani kwa huyo mwanaume.

Joshua akajichekesha kidogo na kusema, "Haina shida mdogo wangu. Usikonde. Umekuwa simba kweli, nakuaminia sana."

"Imeisha hiyo," Tesha akasema hivyo na kutazama pembeni.

Simu yangu ikaanza kuita papo hapo, nami nikaitoa na kukuta ni Ankia ndiye aliyekuwa ananipigia. Nikapokea na kumsikia mwenye nyumba wangu akiniambia niende kunywa supu ya kuku na pilau ilikuwa mbioni kuiva, nami nikamwambia poa.

Nikashusha simu na kusema, "Nahitaji kuwahi."

Niliongea hivyo bila kumwangalia Joshua hata kidogo, huku nikiona yeye ananikodolea tu, nami nikampa Tesha ishara ya kichwa kuwa anifuate. Tukatoka hapo kibarazani bila kusema lolote lile kwa huyo Joshua, tukimwacha anatusindikiza tu kwa macho mpaka tulipokwenda nje.

Nikawa nimemweleza Tesha kwa ufupi kuhusiana na lile suala la kukutana na Joshua kazini kwake Miryam, nikimwambia ilikuwa ni wakati ambao nilienda kwa dada yake ili kumzungumzia Mariam, ikionekana ni kutokea kipindi hicho Miryam ndiyo alikuwa ameanza kumvuta tena Joshua kwa ajili ya kuleta amani na ndugu yake. Lakini ndugu mwenyewe alikuwa ovyo!

Nilikuwa najihisi kuchafukwa rohoni yaani! Basi tu yaani huyo mwanaume hakuwa muungwana kabisa hata kwa jicho la kawaida tu, yaani hakufaa. Mpaka anatumia uzito wa kumbukumbu ya vifo vya wazazi wao ili tu ajionyeshe kuwa mtu mpya eti, kiukweli alinifanya nimchukie mno. Ila zake zingetimia tu, na hazingekawia.

Tukaingia kwa Ankia pamoja na kumkuta akiwa na mama Chande, best yake. Ndani palinukia kweli pilau na vitunguu swaumu na kuku, na kama kawaida yake, Tesha akaanza kutaniana na wanawake na kuwafanya wacheke kwa furaha. Inaonyesha Ankia alikuwa amepata msaada wa mapishi kutoka kwa mama Chande ndiyo maana aliwahi kutengeneza vyakula, na kwa msukumo wa jiko la gesi mambo yalikuwa fasta tu.

Wanawake wakiwa wamekaa hapo sebuleni, sisi tukaelekea chumbani kwangu ili kwanza tusimuliane mambo yetu vijana ambayo Tesha alipenda kupita maelezo. Alitaka kujua kuhusu mke wake Joshua, lakini mimi nikataka aanze yeye kunisimulia kuhusiana na yule Winny. Yaani siku wamekutana ilikuwa vipi na mpaka sasa hivi walikuwa wapi.

Ah, akasema yaani yule alikuwa na dharau sana. Eti alipokwenda kukutana naye, mwanamke huyo alimwona kuwa kama mtoto mdogo na alifikiri hangeweza kazi. Winny hakuwa wa aibu, alimpa Tesha penzi lakini alikuwa haridhiki. Tesha akasema alipiga vitano bila kutumia dawa na bado mwanamke akawa anataka waendelee!

Nikacheka na kumwambia huyo alikuwa anataka kumkomoa tu, na yeye akasema ni kweli kabisa kwa kuwa baada ya hapo alipoendelea kumtafuta kwa simu demu akawa anamkwepa tu; kumaanisha alikuwa na mishe zake nyingine za kuzungushia utamu. Ila akadai kwamba alimkubali sana huyo mwanamke kwenye ukataji wa viuno, na angalau alimla bila gharama!

Hiyo yote ilinifurahisha sana hasa kutokana na njia yake Tesha ya kuongea, na sasa ndiyo akataka kujua kuhusu mke wa kaka yake. Nikamwambia kwamba huyo mwanamke alikuwa ananitaka, nami nikamwelezea mambo yote yaliyotokea pale kwao baina yangu na huyo Khadija.

Akashangaa! Yaani haingeingia akilini mwake kufikiri huyo mwanamke alikuwa wa hivyo, akieleza sababu kuwa Khadija alikuwa mpole sana na mtulivu wa ndoa, ila ndiyo hapa akaona ukweli wa ule msemo 'kamwe usichukulie kuyajua yaliyo ndani ya kitabu kwa kuhukumu tu jalada lake.'

Nikamwambia sikuwa na uhakika wa kitu cha kufanya kuelekea suala hilo, lakini Tesha akasema ish! Piga tu! Kama mwanamke aliitaka kwa nini anyimwe? Nikacheka na kumuuliza hana kwere kwa sababu ya mwanamke huyo kuwa shemeji yake? Akaniambia hakuna kitu kama hicho, yaani hata kama Khadija angekuwa amejisogeza kwake na kuanza kumsugua-sugua miguu, hata yeye angepiga tu!

Aisee, nikamwambia ndiyo hivyo, na mimi sikuwa na ile kusema nimemtaka sana huyo mwanamke ila kama angelazimisha mambo basi ningemkoa tu na yeye. Tesha akasema tena kwa hilo aliniunga mkono wake kwa asilimia zote, akifikiri ni masuala ya kujifurahisha tu, kumbe mimi nilikuwa nataka kuchimba zaidi ndani ya suala la maovu ya Joshua.

Maongezi hayo yote yalifanywa kwa sauti ya chini ili wanawake pale sebuleni wasitusikie, na ndipo Ankia akawa ametuita twende huko. Nikamwambia Tesha huo ulikuwa ni mwito wa kunywa "thupu" ya kuku, na sikuwa nimekosea.

Kweli tukakuta Ankia akiwa ametuwekea mimi na Tesha supu pamoja na nyama kwenye mabakuli, nasi tukakaa ili kujinywea. Alikuwa kwenye harakati za kwenda kuanza kukaanga nyama za kuku ili aziunge vizuri kwa mchuzi wa nyanya na mapocho ya upishi wajuayo wanawake, nasi tukaendelea kunywa huku tukipiga story.

Mada ilikuwa sanasana kuhusiana na Simba na Yanga, jinsi timu hizi zilivyokuwa zimeingia kwenye michuano ya kimataifa barani mwetu, na mechi ya watani wa jadi iliyokuwa inakaribia kuchezwa. Ubishi na maneno ya sutu uliwajaa sana Tesha na mama Chande, hadi Tesha alikuwa anamfanyia mwanamke huyo zile pigo za kike za "ng'oo ng'oo" huku akikandamiza pua kwa kidole, nasi tukawa tunacheka sana. Wanaume tulikuwa Simba, wanawake Yanga, kwa hiyo utani wa maneno hapa ulikuwa mwingi sana.

Tukiwa tunaendelea kufurahia maongezi bwana si simu yangu ikaita? Mpigaji hakuwa mwingine ila madam Bertha, mwanamke shupavu, muuaji, na mwenye jeuri kama lote. Nikapokea hapo hapo na kumsikiliza. Alikuwa ananitaka niende kule Royal Village sasa, ikiwa ndiyo muda alioona unafaa wa mimi kutoka huku nilikokuwa. Akasema nisisahau kubeba na unyama wote niliokuwa nimetengeneza, nami nikamwambia poa. Akakata simu.

Nikaangalia muda; saa tisa kasoro. Dah! Huyo mwanamke alijua kunikatishia hamu! Yaani na hapa pilau na kuku ningezikosa tu kisa kufuata amri zake! Lakini haikuwa na noma. Nikamtaarifu Ankia kuhusu safari yangu ya ghafla kuelekea jijini zaidi, naye akaanza kununa. Eti yaani kanipikia pilau halafu naondoka? Sawa tu.

Nikacheka kidogo na kumwambia hapo naenda kusaka hela za likizo ndiyo maana, ila nikamwambia ningekuja tu kuila pilau yake baadaye. Tesha akaniuliza ikiwa hii ndiyo dharura iliyokuwa imefanya niondoke na kwao pia, nami nikakubali, nikisema kuna jamaa aliniita ili akanipange juu ya mambo fulani.

Kwa hiyo nikatoka hapo sebuleni na kwenda chumbani tena, na nilikuwa nawaza labda niende kuoga tena ila kutokana na uharakishi wa madam nikaamua tu nibadili mavazi na kuvaa kwa mtoko bomba zaidi. Nikajitengeneza vyema, kisha nikachukua lile begi langu la mgongoni na kulipunguzia vitu nilivyokuwa nimeweka humo, halafu nikachukua mifuko ile yenye madawa ya cocaine na kuitumbukiza kwenye begi.

Nilihakikisha kuacha nguo chache na vifaa nilivyochukua hospitali ili dawa zifichike pia, kisha nikavaa viatu na kutoka hatimaye. Marafiki zangu walifikiri labda nataka kusafiri kwa siku kadhaa kutoka huku, lakini nikawahakikishia kwamba ningerudi leo leo, ama kesho. Tukaagana vizuri baada ya hapo, nami nikaondoka kwenda kupanda daladala.

β˜…β˜…

Safari ya kuelekea Makumbusho ilidumu kwa masaa mawili kabisa. Hii ilisababishwa na msongamano wa magari hasa tulipofikia eneo la Keko, na kwenye ile round-about pale sipajui jina, lakini ilikuwa jam kali kweli mpaka kuhitaji mwongozo wa askari wa usalama barabarani. Kwa hiyo nimekuja kufika Makumbusho ikiwa ni saa kumi na moja jioni, na kwa muda wa nusu safari nilikuwa nimesimama baada ya kumpisha mwanamke mjamzito aketi kwenye siti yangu, hivyo miguu ilikuwa inaita kwa kiasi fulani.

Nikatoka Makumbusho, kama kawaida nikapanda Uber na kuanza kuitafuta Royal Village Hotel. Nikiwa njiani, nikaona nimpigie madam Bertha kumuuliza kama na leo nilitakiwa nipande lifti pale hotelini, kisha labda kwenye lifti hiyo ningekutana na mwanamke ambaye angenipa funguo ya chumba ambacho madam angekuwepo. Akaniambia niache ujinga na nifike kule tu kisha nimjulishe, na ile nataka tu kusema kwamba nimekaribia, akakata simu. Doh!

Nikajikuta tu nacheka mwenyewe, lakini hiyo haikumaanisha kwamba nilikuwa nimeshasahau dhumuni langu la kufanya haya yote. Bado, pamoja na kuwa nimejiweka upande wake, huyo mwanamke alikuwa ni adui yangu. Tumeangalia filamu nyingi zinazoonyesha kwamba mara nyingi ukitaka kufanikiwa kuwaangusha maadui zako, basi jiweke karibu nao ili uweze kufanikiwa kuwaangusha kwa njia bora.

Ndiyo nilichokuwa nikikifanya wakati huu. Ningeendelea kujichekesha tu heheh ili siku huyo mwanamke akija kunikuta serious, ajue kuna watu wasiopenda michezo kwenye maisha ya wengine kama ile aliyoifanya kwangu mpaka kuua mwanadamu mwenzetu. Na sikuwa nimempa taarifa askari mpelelezi Ramadhan kuhusu mkutano wangu huu na mwanamke huyo, ili nione kwanza huu mchezo ungenipeleka wapi kwa leo.

Nikaifikia Royal Village hatimaye, nami nikamlipa dereva na kwenda ndani ya geti. Nikatembea mpaka kufikia usawa wa bustani na kisha nikampigia tena madam. 'Haya ndiyo nimefika, niende juu au?' Akarusha dongo kwa kusema niache kuwa na kiherehere, na kwamba bado yeye hakuwa amefika hapo hotelini ingawa alikuwa anakaribia.

Nikamuuliza yuko sehemu ipi kwa sasa. Akasisitiza tu tena kwa kusema ndiyo alikuwa amekaribia kufika hotelini hapo, yaani ni dakika mbili tu angeingia, hivyo niende kumsubiri ule upande wa maegesho ya magari ya nyuma kwenye jengo hilo. Sikudhani kwenye hoteli hiyo kulikuwa na maegesho ya namna hiyo lakini hilo lilikuwa jambo hakika, hivyo nikamkubalia na kukata simu, kisha nikazungukia mpaka upande huo kwenda kumsubiri. Ah kumbe na hoteli hii ilikuwa ya ubora bwana!

Maegesho ya huku nyuma yalikuwa mapana, safi, nguzo ama ngome nyingi nene zikilibeba jengo hilo la hoteli na magari ya maana yakionekana kuegeshwa hapa na kule. Hizi ndiyo zile sehemu ambazo mara nyingi tunaonaga kwenye filamu hasa za wazungu jinsi ambavyo majambazi hupenda kuzitumia kwa ajili ya kutoroka wakishafanya maovu yao, na kweli hapa nilikuwa nimekuja kukutana na majambazi!

Nilitembea mpaka kufikia sehemu ambayo iliniruhusu kuuona mlango wa lifti ya nyuma kwenye jengo hilo, na bila shaka baada ya Bertha kufika tungeitumia hiyo kuelekea juu, hivyo nikasimama usawa wa nguzo moja na begi langu mgongoni kumsubiri madam afike.

Hakukuwa na nafsi hata moja iliyoonekana kwa upande huu, pakiwa kimya kweli, nami nikawa naangalia mpangilio maridadi wa sehemu hiyo pamoja na CCTV camera zilizowekwa kwenye kila pembe. Nikasikia kengele ya mlango wa lifti iliyoashiria kwamba kuna watu walikuwa wanatoka, na ile nimenyanyua tu uso wangu kutazama huko, nikajikuta nakunja sura kimaswali kutokana na kutotegemea kabisa kumwona niliyemwona.

Mwanamke niliyemfahamu, akiwa amevaa gauni jeupe lililo la mtindo mzito kama sweta laini, refu kufikia miguuni, lenye kubana mwili wake ulioumbika vyema. Alikuwa ameshika mkoba mkononi, na hilo gauni liliacha mikono yake myeupee wazi kutokea mabegani, na aisee alinifanya nibaki nikimtazama kwa mshangao sana. Bibie Miryam!

Yaani sikuwahi kutegemea kumwona hapo kabisa, tena akiwa ndani ya mtindo mzuri kama huo uliompendezesha vibaya mno. Alikuwa amevaa viatu vya kuchuchumia vyekundu, vikiwa vimeendana na rangi ya mkoba wake, na mwonekano huo uliniambia kwamba alikuwa sehemu hiyo kwa mkutano wa masuala binafsi; labda date na mtu wake, na huku ilikuwa ni mbali kweli!

Ila ilimfaa, nami nikaona nijibanze kwenye nguzo hiyo ili asiweze kuniona kabisa. Nisingefikiria hata mara moja kwamba ningemwona hapo hasa kwa kujua alikwenda zake kazini baada ya kumpeleka mama mkubwa wake hospitali. Alikuwa anakuja upande wangu lakini kwa kupitilizia sehemu iliyokuwa imeegeshewa magari, nami ndiyo nikawa nimeiona ile pickup yake.

Pamoja na kuwa mwanamke mwenye mvuto sana lakini hakupenda makuu mno, na kuwa mtu aliyethamini zaidi mambo yaliyokuwa na maana kwake kuliko kutafuta vitu vya kumpa sifa tu; yaani huyu hata kama angekuwa ameamua kutembelea gari aina ya Range Rover Evoque asingeshindwa, lakini aliendelea kutumia pickup iliyokuwa ya baba yake ili kumuenzi. Lakini dah! Miryam ndiyo alikuwa maana ya mwanamke. Sijui nani tu alikuwa anakula hapo!

Akawa amenipita bila kuniona maana nilijibanza vizuri, nami nikawa naangalia miondoko yake ya taratibu ambayo ingemfanya mwanaume yeyote agande kumtazama kwa jinsi alivyokuwa amebarikiwa huyo dada. Siyo kwa sura tu, siyo kwa shepu tu, hata tabia, yaani kila kitu kwake ni kama kilikuwa kamili.

Sikutaka anione maana mishe zilizokuwa zimenileta huku hazikuwa nzuri kuendana na jinsi dada wa watu alivyokuwa ananifahamu, lakini Shetani bana, akaona aniharibie tu. Sijui labda namsingizia bure? Simu yangu ikaanza kuita. Muito wa simu ulikuwa ni mdundo wa wimbo wa Ozuna uitwao "Una Lodura," wabrazili hao na ni ngoma kali, hivyo sauti ya mwanzoni tu ikawa imesikika kwa bibie. Agh!

Nimeshtuka ile nataka kuitolea sauti, sauti ya viatu vya Miryam ikakata, na hilo likaniambia kwamba alikuwa amesimama, kwa hiyo ikanibidi nitoke hapo kwenye hiyo nguzo na mimi nijifanye kwamba ndiyo nilikuwa nimetokea tu upande huo na sikuwa nimemwona. Nikaweka uso makini kweli nikiiangalia simu, na nilikuwa nimeanza kupiga hatua chache kisha nikasimama.

Mpigaji alikuwa ni rafiki yangu mmoja wa Mwanza, hivyo nikaitolea tu simu sauti huku nikimrushia laana ya kimoyomoyo huko alikokuwa kwa kusababisha nikachomeshwa namna hiyo. Nikajifanya naangalia tu pembeni kama vile sina habari na mwanamke huyo ambaye nilijua wazi kwamba alikuwa amesimama na anaangalia upande wangu, na ndipo hatua zake kunielekea zikaanza kusikika.

Nikafumba macho kwa kutotaka jambo hilo kabisa, kwa sababu nilihofia sana kuhusiana na mambo ambayo yangetokea ikiwa Bertha angefika na kunikuta nikiwa na Miryam hapo. Sijui ni kwa nini tu yaani mwanamke huyu alitakiwa kuwa hapo kwa muda huo! Ningepaswa nimwepuke upesi, kwa njia yoyote ile.

Nikamgeukia na kujifanya kushangaa, kama vile ndiyo nimemwona sasa, naye akawa ananifata huku funguo ya gari lake ikiwa kiganjani, na akitabasamu kiasi.

"Hey, vipi?" akaniuliza hivyo.

"Safi tu. Ih! Upo huku kumbe?" nikamsemesha namna hiyo.

"Ndiyo," akajibu hivyo na kusimama mbele yangu.

"Mishe gani?"

"Aa... nimekuja tu kukutana na mtu, alikuwa ameniita huku ndiyo nikaja haraka," akaniambia hivyo na kasauti kake katamu.

"Aaa... umedamshi kweli. Lazima uwe mkutano wa maana," nikazungumza kwa wasiwasi kiasi.

"Ahah... acha bwana. Ni mikutano tu ya kikazi," akasema.

"Aaa... sawa. Si ndiyo unaondoka?"

"Eeh."

"Haya sawa, basi,... baadaye. Kama kawaida tu, nitakuja kwa Mamu," nikamwambia hivyo kama namfukuza yaani.

Akauliza, "Na wewe? Mbona uko huku?"

"Kuna... na mimi kuna mtu nakutana naye... hapa. Ni rafiki. Kwa hiyo, we' nenda tu, si unaenda kuendelea na kazi? Nisikucheleweshe," nikamwambia.

Akawa ananiangalia kwa utafakari, naye akasema, "Mbona kama una wasiwasi? Kuna tatizo lolote?"

"Hapana. Kila kitu kiko sawa," nikamwambia hivyo na kutabasamu.

Akatikisa kichwa kuonyesha uelewa, naye akasema, "Okay. Basi... tutaonana baadaye... kama ulivyosema."

Nikatikisa kichwa kukubali hilo.

Akageuka na kuanza kuondoka, nami nikaangalia pembeni na kushusha pumzi ya utulivu. Nikawaza kuwa angalau tu kama dada wa watu angeondoka, maana, hapo sikuwa sehemu nzuri kabisa ya....

Ilikuwa mapema sana kufikiri kwamba nilipata ushindi kwa kumwondoa Miryam upesi, kwa sababu alikuwa amepiga hatua chache tu kisha akasimama tena. Nikamwangalia. Akanigeukia tena na kunitazama, kisha akaanza tena kurudi kwangu. Aisee! Sijui alikuwa amesahau nini!

Akafika karibu tena, nami nikajitahidi kuonyesha utulivu usoni lakini moyoni palidundika mithili ya ngoma, naye akasema, "Nilikuwa nataka nikwambie jambo fulani."

Nikatikisa kichwa kuonyesha aendelee.

"Ni kuhusu jana... na... kila kitu ambacho kimeendelea kwa Tesha na Mamu. Huwa... sitegemei sana mtu yeyote anisaidie kwa... mambo ya familia yaani, sijazoea... ila... kwa yote ambayo wewe unafanya... nataka tu kusema asante..." akaongea hayo.

Dah! Hii ingepaswa kuwa pindi moja nzuri sana maana huyu dada alikuwa ameanza na kunisemesha kabisa, tena kunishukuru, lakini muda na sehemu ya tukio hili haikufaa. Nilikuwa naangalia upande ule wa mwingilio wa magari kwa wasiwasi kiasi, nikiomba Mungu Bertha aendelee kukawia tu.

Miryam akaendelea kusema, "Niliongea na Tesha hiyo jana... na jinsi alivyokuwa ameonyesha kutulia kiakili kwa kweli... sijaiona kwa muda mrefu kiasi. Anasema yote hiyo imewezekana eti kwa sababu ulimpa therapy ahahah..."

Nikalazimisha kicheko pia na kusema, "Eeh, ndiyo, ndiyo..."

"Yaani una effect nzuri hata kwa Mamu, mpaka ameanza na kuongea tena. Niseme tu... yaani, hatujawahi kuzungumza sana ndiyo maana nimeona nichukue hii nafasi ku..."

Maneno ya Miryam yakakatishwa baada ya sote kuona gari aina ya Harrier new model ya silver likiwa linaingia, nami nikajiambia eh Mungu! Huyu mwanamke alipaswa kutoka hapa sasa hivi!

Miryam yeye akiwa haelewi somo akaona aendelee kuzungumza tu kutoa shukrani yake, na hilo gari likaingia sehemu ya maegesho isiyo mbali sana na hapo tulipokuwa tumesimama. Dereva aliposhuka hakuwa mwingine ila yule baunsa wa madam, naye akaonekana kuufungua mlango wa nyuma wa gari.

Nikamgeukia Miryam na kumkatisha kwa kusema, "Miryam... tafadhali... tuta... tutaongea wakati mwingine... yaani, tukionana tena, sawa?"

Akaibana midomo yake taratibu huku macho yake yakiwa kwangu kwa utulivu tu.

"Unaweza kwenda tu Miryam. Naowasubiri wamefika, we'... kaingie kwenye gari dada..."

Yaani nilikuwa najaribu kumfukuza kistaarabu, na nilihitaji sana aondoke maana sikutaka Bertha amjue Miryam. Katika watu ambao sikutaka mwanamke huyo awaingie kabisa ilikuwa ni huyu dada, lakini kwa hapo nikawa nimechelewa.

"HB..." sauti ya Bertha ikasikika akiniita.

Ah!

Nikageuka kumwangalia, Miryam bado akiwa hapo hapo, nami nikamwona madam akiwa anakuja kwa mwendo wa madoido. Alikuwa amevaa gauni jeupe fupi sana lililoubana mwili wake. Mapaja yalikuwa wazi, mikono na mabega yalikuwa wazi pia, na sehemu ya mbavu zake ilikuwa wazi pia kama vile gauni hilo limechanwa humo pembeni kwa njia ya urembo.

Miguuni alivaa mabuti ya kike yenye rangi ya kahawia, na usoni alikuwa amevaa miwani pana nyeusi ya urembo. Baunsa wake alikuwa anafata nyuma huku ameitanua mikono na sura yake ikiwa makini, nao wakafika karibu yetu; Bertha akisimama karibu nasi zaidi na kuitoa miwani yake machoni.

Nikaendelea kuonyesha utulivu tu, huku nikiona jinsi Bertha alivyokuwa akimtazama Miryam kwa macho yenye udadisi, kisha akaniangalia mimi. "Za jioni?" akauliza hivyo.

"Fresh tu," nikajibu hivyo kwa sauti ya chini.

"Nimefika wakati mbaya? Mlikuwa mna..." Bertha akasema hivyo.

"Hamna, me ndiyo nimefika tu upande huu sa'hivi..."

"Sikumbuki kukwambia uje na mtu," Bertha akanikatisha kwa kusema hivyo.

Nikamwangalia Miryam kiufupi, ambaye alikuwa ananiangalia kwa utulivu tu, nami nikamwambia Bertha, "Hapana. Nimekuja mwenyewe. Sijaja na mtu."

"Huyu ni nani?" Bertha akaniuliza.

Miryam akaanza kusema, "Mimi ni..."

"Nimekutana tu na huyu dada hapa, alikuwa amedondosha funguo yake hiyo... ndo'... nikamsaidia kuipata..." nikamkatisha Miryam.

Jinsi ambavyo mwanamke huyo aliniangalia, yaani, alikuwa ndani ya mshangao mzito bila shaka, na ilieleweka kwamba hakuwa amenielewa.

Bertha akaniuliza, "Kwa hiyo ndiyo mmekutana hapa hapa?"

Nikatikisa kichwa kukubali.

"Hamfahamiani kabisa?" Bertha akaniuliza tena.

Macho yake Miryam yakanitazama kwa njia ya subira, na najua alikuwa anataka kuona ningejibu nini, na aisee! Roho iliniuma sana kwa kitendo nilchokifanya.

Nikatikisa kichwa kukataa na kumwambia Bertha, "Hapana. Simjui."

Siwezi kujua undani wa mshtuko niliofanya Miryam auhisi hapo aisee! Aliniangalia kwa njia ya kawaida tu, lakini naelewa alikuwa akinishangaa sana. Sana!



β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

ITAENDELEA

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

SEHEMU YA ISHIRINI NA TANO

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…


Miryam akaacha kuniangalia na kumtazama Bertha, ambaye alikuwa amesimama kama vile amemzibia njia.

"We' dada mzuri. Unamwonaje HB wetu, umempenda?" Bertha akamsemesha hivyo Miryam.

Miryam akabaki kimya, nami nikamtazama usoni kwa hisia za hatia.

Bertha akacheka kikejeli na kusema, "Nisamehe shoga, nilikuwa nakutania tu. Ila... kama mlikuwa bado hamjapeana namba, nisiwe kikwazo. Chukua tu namba za HB boy. Hana baya."

"Madam, acha bwana. Ni..."

Nikaishia hapo tu huku nikimwonyesha Bertha kwa ishara za mikono kwamba kumzingua mtu mzima namna hiyo haikuwa jambo zuri, lakini huyu mwanamke alijali sasa? Miryam alipotaka kupiga hatua kuondoka, Bertha akamwahi na kumzibia njia kwa kusimama mbele yake zaidi, nami nikapandwa na hisia zilizofanya nikunje ngumi kwa chini.

Mwanamke huyo mbabe akawa anamwangalia Miryam huku akitabasamu kichokozi, na yule baunsa wake akaja karibu yangu na kupitisha mkono begani kwangu kirafiki. Eti ile kwamba kwa sababu madam alikuwa ameanza kumzingua mtu, basi lilikuwa ni jambo letu moja, nami nikaendelea tu kutulia huku nikiwatazama wanawake.

Bertha akazishika nywele zake Miryam kwa chini, naye akasema, "Mbona haraka hivyo? Unawahi wapi? Tuongee kidogo."

"Naomba unipishe," Miryam akamwambia hivyo.

"Hee! Nyie... mmeisikia hiyo sauti? Dada, em' ongea tena..." Bertha akasema hivyo.

Miryam akabaki kimya tu.

"Ongea baasi... hata kidogo. Nitakupa pesa. Nisemeshe tu walau kidogo," Bertha akaendelea kumshurutisha.

"Labda tukusaidie kumfanya aongee?" baunsa Dotto akasema hivyo.

"Wewe... mmfanye nini tena? Mtoto mzuri kama huyu siyo wa kulazimisha. Huoni alivyo wa moto? Darling... nitakupa pesa yoyote unayotaka yaani. Wewe unaweza kuwa sehemu muhimu sana ya biashara yangu kuubwa kuliko... yaani unafaa kabisa. Uko perfect sana."

Miryam akabaki kumwangalia Bertha kwa njia iliyoonyesha hakuelewa, nami nikawa nimeelewa ni biashara ya aina gani mwanamke huyo alikuwa akimaanisha. Aisee! Yaani kule kule ambako sikutaka tufike ndiyo Bertha akawa anatupeleka kabisa!

"Nimekuelewa sana yaani... nataka tuwe karibu. Ushawahi kusagana?" Bertha akamuuliza hivyo.

Nikafumba macho na kuinamisha uso, huku baunsa Dotto akicheka kidogo.

"Una matatizo ya akili?" Miryam akamuuliza hivyo.

"Ahahah... inawezekana yamenipata nilipokutana tu na wewe. We' unaonaje mpenzi?" Bertha akasema hivyo na kumshika kiunoni.

Miryam akaupiga mkono wake kwa nguvu ili asiendelee kushikwa, na akiwa anamnyooshea Bertha kidole akasema, "Jichunge we' mwanamke! Siyo kila mtu anaishi maisha ya kibatili kama wewe. Katafute malaya wengine wa kusagana nao, sikujui, hunijui, kwa hiyo nikome!"

Aliongea kwa uthabiti kabisa, na akiwa bado amemnyooshea Bertha kidole, Dotto akataka kwenda hapo sijui kumpiga, lakini nikamshika mkono kumzuia, na hata Bertha akawa amenyanyua kiganja chake kumzuia jamaa asiende hapo.

"Madam... achana naye tu. Kwanza... pisi kali nyingi, tutatafuta hata baadaye. Muda unaenda, si unajua?" nikamwambia hivyo.

Bertha akaniangalia, kisha akamtazama Miryam kwa macho makini.

"Nimekwambia nipishe. Usifanye nikakuitia polisi sasa hivi," Miryam akamwambia hivyo Bertha.

"Ahah... wacha! Kwa hiyo hutaki kabisa tuchezee mito, darling?" Bertha akasema hivyo kwa sifa.

Miryam akasonya na kutaka kumpita tena, lakini Bertha akamzuia kwa kutumia nguvu zaidi.

Hali ikaonekana kutaka kuingia sehemu mbaya zaidi ya nilivyokuwa nimetarajia, nami nikashindwa kujua pa kusimama kabisa. Miryam ndiyo angekuwa chaguo la kwanza katika kutetewa na mimi lakini hilo lingenifanya nipoteze mchezo wote niliokuwa nimeanzisha kwa Bertha.

Miryam akamshusha na kumpandisha mwanamke huyo kwa hisia kali, naye Bertha akamsogelea dada wa watu karibu zaidi kama anataka kuanzisha ndondi. Ilikuwa ni ile chick Vs chick kama kwenye WWE, na inaonekana Dotto alitaka kuwa mwamuzi kabisa kwa jinsi alivyotaka kuona wanawake hao wakianza kutoboana!

Ila Mungu si Athumani bwana? Watu kadhaa kutoka kwenye lifti wakaanza kuja huku, na hata magari mengine yakaingia pande hizi. Hiyo ikawa ni ponea chupu chupu niliyohitaji sana itokee, naye madam akasogea nyuma kiasi na kuachia tabasamu ili bila shaka watu waliopita waone mambo yalikuwa shwari hapo.

"Una bahati. Huwa sipendi kusemeshwa kama ulivyonisemesha. HB angekupa mawaidha ya nini naweza kukufanya... ila muda hautoshi sweety. Kwa hiyo... nenda," Bertha akamwambia hivyo Miryam huku akitabasamu kinafiki.

Niliona wazi kwamba Miryam alikuwa amekasirishwa na haya yote, naye akanigeukia na kunitazama kwa mkazo.

Kama ilivyokuwa siku fulani ya nyuma, nilipatwa na ile hisia ya hofu, sijui woga, yaani ni kitu ambacho kilitokea tu pindi ambayo Miryam angeniangalia namna hiyo. Sijui ilikuwa kwa nini tu, lakini ni kitu kilichofanya hadi ujasiri wa kumtazama machoni unitoke, nami nikaangalia pembeni kama vile simjali.

"Ondoka," Bertha akamwambia hivyo Miryam.

Miryam akamtazama na kumshusha kwanza, kisha huyoo akaenda zake mpaka kwenye gari.

Bertha alikuwa anamwangalia tu Miryam mpaka alipoingia garini, na kiukweli nilikuwa najihisi vibaya kusimama tu hapo na kuangalia hayo yote yalipokuwa yakiendelea. Yaani sijui hata ningemtazama vipi tena huyo dada wakati ambao ningerudi kule nyumbani.

Nilijisikia vibaya sana kumkana namna ile, lakini sikuwa na jinsi. Hakuelewa, ila nilikuwa namlinda. Sikutaka Bertha aanze mambo yake ya kufatilia huyo alikuwa nani maana sikuwa na uhakika ikiwa alikuwa ameshaniamini kwa asilimia zote, na kunikuta hapo na mtu bila shaka kungempa shuku. Bora kama ingekuwa ni mtu mwingine tu lakini Miryam, hapana. Sikutaka aguswe pabaya kabisa. Nilimheshimu mno.

Gari la Miryam likatoka sehemu ya maegesho huku sisi wote tukiliangalia, naye Dotto akasema, "Pisi la maana, lakini akili hamna."

"Kinajikuta kisafi, eti 'malaya wenzako...' unafikiri kimekuja huku kufanyaje kama siyo ku(.....)? Bado kitaendelea kudrive mistubishi mpaka kitakufa. Na ni kweli, hana akili kabisa. Demu wa wapi mkali namna hiyo akandesha usenge kama huo? Mpuuzi mkubwa tu!" Bertha akasema hivyo kwa dharau.

Aisee, nilisikia hasira! Basi tu.

Nikashusha pumzi na kusema, "Harakati zinaendaje sasa? Maana saa moja inaingia."

Bertha akaanza kuelekea upande wa lifti huku na sisi tukimfuata, naye akasema, "Utajua huko juu. Na iwe mara ya mwisho kukuona umesimama na mpumbavu yeyote tukiwa tunakutana, sijui unanielewa?"

Nikasema, "Yes madam."

Tukaifikia lifti na kuingia, kisha tukaanza kuelekea juu. Bado nilikuwa nikimwaza Miryam tu, yaani ni jinsi gani ambavyo tukio la muda mfupi nyuma lingefanya nipoteze kabisa kiasi chochote cha imani alichokuwa nacho kunielekea kwa wakati huu. Sijui alikuwa ananifikiriaje! Lakini hakukuwa na njia ya kuepuka yaliyotokea maana nilikuwa na malengo kwenye haya yote niliyofanya, kwa hiyo ningepaswa kuendelea kujitahidi kuyafikia.

Tukiwa bado ndani ya lifti, Bertha akapigiwa simu na mtu fulani, naye akaanza kuongea naye kwa shauku. Alikuwa anamwambia kwamba asiogope, hangekawia kufika huko na alikuwa na zawadi nzuri sana ambayo ingewafanya wote wa huko wachanganyikiwe ile mbaya, nami nikaelewa hilo lilimaanisha sehemu ambayo mwanamke huyu ndiyo alikuwa anataka twende muda huu.

Kwa sababu sikujua mengi ya kutegemea japo nilijiandaa kwa lolote lile, nisingeweza kufanya kitu cha ujanja-ujanja mpaka niwe na uhakika wa kile ambacho kingetokea. Yaani namaanisha kama siku ile huyu mwanamke ameniita nije hapa kwa mara ya kwanza, nilifanya kurekodi sauti za mambo tuliyozungumzia na kumpelekea yule mpelelezi, lakini kwa sasa hivi nisingefanya kitu kama hicho mpaka nihakikishe mazingira ambayo ningekuwepo yangeruhusu.

Mpaka tumetoka ndani ya lifti na kwenda kwenye kile kile chumba kwenye ghorofa ya saba, madam bado aliendelea kuongea na huyo mtu wake kwenye simu, naye akaenda kukaa kwenye sofa lililokuwa na muundo kama kitanda, kwa hiyo akawa amekaa kama amelalia ubavu wake mmoja na kuendelea kuongea kwa madaha.

Mimi nikaweka begi langu kitandani, huku Dotto akiwa amesimama pembeni yangu kama vile anasubiria nimpe kitu fulani, na nilijua tu kile ambacho alikuwa anataka. Nikachomoa dawa ya kwenye kifuko kidogo na kumpatia, naye akakipokea na kunigongea tano kuonyesha furaha. Nikamwangalia Bertha, ambaye bado alikuwa kwenye raha ya maongezi yake, nami nikakaa kitandani hapo.

Dotto alikuwa kwenye kiti kimoja kati ya viwili karibu na meza fupi, vyote vikiwa vya plastiki, naye akawa ameifungua dawa na kuweka kiasi mezani, kisha akaitenganisha kwa mistari mifupi na kujisawazisha vizuri. Akaniangalia na kunitolea ishara ya kwenda hapo ili nijiunge naye, lakini nikamwonyesha kwamba niko vizuri tu, hivyo yeye aendelee.

Akaiinamia meza na kuziba tundu moja la pua yake, kisha akavuta mstari mmoja wa madawa hayo mpaka ukaisha. Kwa jinsi ilivyokuwa kali, hiyo ingempaisha mbali sana kiasi kwamba sidhani kama angeweza kuendesha gari vizuri tena. Akawa anakunakuna pua huku akitikisa kichwa kuonyesha msisimko, nami nikampa tabasamu hafifu tu aliponitazama machoni.

Nikamwangalia na madam, ambaye sasa alikuwa amemaliza kuongea na simu na kuonekana akichat sijui? Bado sikuwa nikiambiwa yatakayofuata lakini nikaona nibaki tu kimya na kutoa simu yangu pia.

Wakati huu, nilikuta yule mwanamke mwislamu aliyeitwa Ibtisam akiwa amenitumia ujumbe, akisema kuwa anataka tukutane tena na angeandaa mazingira yeye mwenyewe, lakini sikumjibu jumbe hata moja. Alikuwa amenichunia toka nilipomwambia nimemwelewa, na sasa ghafla tu akawa anataka tukutane. Je kama ilikuwa ni mume wake au ndugu zake wa Mafia? Isingekuwa busara kufia ujinga, kwa hiyo nikaamua kumweka pembeni.

Nikaanza tu kucheza "game" maana niliona wazi kwamba hapo ingekuwa ni kusubiri tu; Bertha alikuwa bize na mambo yake, na Dotto alikuwa kwenye raha ya vibe la madawa niliyotengeneza. Kidogo tu ndiyo jamaa akaanza kuongea, akisifia hayo madawa na kunipigisha story za mambo mengine ambayo hayakuwa na umuhimu wowote ule kwangu.

Niliangalia kwa umakini namna ambavyo mwanaume huyo alizungumza kwa njia huru sana mbele ya Bertha, kitu kilichoonyesha kwamba walikuwa na mazoea ya muda mrefu. Kwa jinsi alivyokuwa na ukaribu naye, bila shaka alijua siri nyingi za mambo ya huyo mwanamke, na kama alishiriki katika mauaji ya Joy basi na yeye angekuwa amejiweka ndani ya shabaha yangu ya maangamizi. Siyo mbaya kujipa kichwa kidogo!

Nikawa nasindikiza tu mongezi yake na kumwambia mambo yaliyomchekesha, naye akaendelea tu kushusha madawa puani kila robo saa.

β˜…β˜…

Bertha kama boss alikuwa kivyake tu mpaka inaingia saa tatu usiku, nami nikajiuliza ikiwa kweli ningewahi kutoka huku. Na hapo bado kuna sehemu tulitakiwa twende, kuna kitu tulikuwa tunasubiria, kwa hiyo bila shaka hiyo sehemu ingekuwa ya mambo yaliyohitaji giza nene.

Ah nikaona hii kuwa usumbufu tu maana huyo mwanamke aliniwahisha kweli kuja huku mpaka nikajikuta nakutana na Miryam, wakati tu angeweza kuniambia nianze kuja hata jioni ili nifike huku usiku. Hakukuwa na namna ya kubadili mambo tena, ila kiukweli bado ishu ya kukutana na Miryam hapo hotelini mpaka Bertha kumwanzishia fujo ilinisumbua sana akilini.

Nikawa nimeanza tena kumwaza mwanamke huyo pale mlango wa kuingilia ndani hapo ulipogongwa kwa nje. Nikamwangalia madam usoni, naye akaninyooshea kiganja kuuelekea mlango kuashiria nikaufungue, hivyo nikanyanyuka na kuchukua kadi ya kufungulia kisha kwenda mlangoni.

Bila shaka aliyekuwa anasubiriwa ndiyo alikuwa amefika, na baada ya kufungua mlango, nikakutana uso kwa uso na mwanaume kijana aliyekuwa amevalia suti iliyombana haswa, na alikuwa na kipara huku akivalia miwani pana yenye kuonyesha macho yake. Alikuwa amesimama mbele ya wanaume wengine wawili wenye miili mikubwa na warefu, waliokuwa wamevaa suti pia, na wakiwa wamebeba maboksi mapana ya kutunzia nguo pamoja na fuko la kutunzia suti; likiwa na suti.

Huyu mwanaume aliyevalia miwani akawa ananiangalia kwa njia fulani kama ananishangaa, lakini jinsi ambayo alifanya hivyo yaani sikuielewa-elewa. Alikuwa kama anarembua kwa mbali, shingo yake ikinesa-nesa kwa maringo utadhani alikuwa.... subiri kwanza, nini?

"We' nyau ndo' unafika sasa hivi?"

Swali hilo liliulizwa na Bertha humo ndani, nami nikaelewa kwamba lilimhusu mmoja wa hawa watu waliofika hapa. Ila ni huyu wa mbele tu ndiye aliyekuwa akifanana na nyau kwa hiyo bila shaka swali lilikuwa lake kujibu!

Huyo jamaa akacheka kidogo kwa pumzi na kusema, "Jamani dear, nisamehe. Kazi zilikuwa piled up, na msongamano wa magari hukutuacha salama."

Eh! Alisema hivyo huku akinipita na kuingia ndani, nami kiukweli sikuwa nimetegemea kabisa namna yake ya kuongea. Yaani aliongea kike, 'jomooni deear,' hivyo! Wale jamaa wengine wakaingia pia, nami nikaufunga mlango na kuwatazama wote kwa umakini.

"Utakuja kuni-cost wewe, unajua nimesubiria kwa muda gani hapa?" Bertha akamwambia hivyo huyo jomooni deear.

"Mmmm, shoga, acha ukali bwana. Ilikuwa nje ya uwezo wetu," jamaa akamwambia hivyo.

Aisee!

"Kwenda huko! Nje ya uwezo wapi, ukinikosesha alama leo? Hee. Mizigo ndiyo hiyo?" Bertha akamuuliza.

"Hundred percent! Yaani kama uliyoagiza darling, parcel za ukweli, suti na hizo dress, yaani unakoenda na mume wako itakuwa kama nyie ndiyo mnaimiliki Bongo nzima! Hahahaaah..."

Nikajikuta tu natabasamu na kutikisa kichwa kwa kutoamini huu upuuzi. Kumbe tulikuwa tumekaa hapa muda huo wote kumsubiri huyu bwege alete nguo za kuvaa ili ndiyo twende tulikopaswa kwenda, naye akawa amezileta kwa mbembwe zile za yule jamaa anayependaga kusema dhambi za fashoon. Na walikuwa ni wale wale kabisa!

Bertha akasema, "Huna lolote Eliya."

Eliya, ikiwa ndiyo jina la huyo jamaa, akasema, "Si utaona? Kwani me huwaga nafeli? Insta kote nafahamika, hata wa duka la Mobetto hawawezi kufikia hizi design. We' mwenyewe unanijua, ndiyo maana bado umezama kwa fashion designer Eliyah! Hahaaa mtoto vaa, ng'ara, pendeza, hakuna atakayefikia show yako huu usiku, yaani hakuna yeyote yule atakayefikia mng'ao wako kwa hii kitu. Au nadanganya Mandonga zangu? Sasa! Kitu ng'ari ng'ari, yaani ukivaa kila mtoto wa mjini unamgeuza mshamba... yaani ndoigee!"

Dotto na wale mabaunsa wakacheka kidogo, hata Bertha pia akacheka huku akitikisa kichwa taratibu, kwa sababu jamaa aliongea huku amenyanyua tatu hewani kana kwamba alikuwa anachamba mtu kama mwanamke!

Inaonekana Bertha alipenda sana misifa ya namna hiyo, tabasamu lake la kiburi lilithibitisha hilo, naye akawa amesimama na kufungua maboksi kuziangalia nguo hizo. Akazitoa kabisa, moja baada nyingine, akizipima-pima mwilini kwake, na huyo Eliya akaendelea kusifia tu kama kawaida yake.

Hivi huwa ni lazima watengenezaji mitindo ya wanawake ambao ni wanaume sikuzote wawe namna hiyo, ama? Tena jamaa hadi akawa ananiangalia kwa yale macho yaani dah! Kungekuwa na mawe humo!

Bertha sasa akawa ameshika nguo hizo mbili mikononi mwake, akiwa anajishauri atumie ipi maana zote zilikuwa nzuri, naye akaniangalia na kusema, "Njoo mpenzi."

Wengine wakanitazama usoni, na mpaka kufikia hapo bado nilikuwa nimesimama karibu na mlango. Bertha alikuwa na michezo yenye kushtukiza maana alifanya iwe ngumu kwangu kujua namna ya kuitikia masuala fulani ambayo yangekuwa tofauti na misingi ya uhusiano tuliokuwa nao, lakini mimi ningekwenda tu na mabiti namna hiyo hiyo.

Nikatembea taratibu mpaka kufikia aliposimama, naye akaniuliza, "Eti honey... nivae lipi?"

Wakati huu huyu mwanamke alikuwa anatumia sauti fulani kama vile anadeka kwangu eti, bila shaka akiwa ananioshea kwa hawa wengine walioingia, nami nikajitoa tu akili na kumwonyesha gauni aliloshika mkono wa kulia.

Lilikuwa ni gauni lenye kubana bila shaka, lililokuwa na rangi ya maroon, na lilipambwa kwa vitu kama vialmasi vingi kulizunguka vilivyofanya limeremete sana kwa mng'ao wa mwanga wa taa. Lile lingine lilikuwa la blue-bahari, likiwa la mtindo ambao sikuuelewa na sikujali; mimi nilimwonyesha tu la maroon avae, tuondoke.

Akaliangalia gauni nililomchagulia na kuniuliza, "Kwa nini unataka damu ya mzee? Kwa nini nisivae hili?"

Khh! Kero!

Nikamwambia, "Ngozi yako ni nyeupe, mpenzi wangu. Ukivaa hii inayomeremeta halafu usiku... ndiyo utaonekana kuwa zaidi ya malaika kabisa."

Bertha akabaki kunitazama kwa umakini baada ya mimi kumwambia hivyo. Nafikiri sifa ikawa imemwingia.

Eliya akasema, "Kweli shem, si umeona? Atang'ara vibaya mno! Madam... vaa maroon upendeze, hata mwanaume wako amesema... utakuwa zaidi ya malaika. Yaani watu watakaposema 'haki ya Mungu,' watamaanisha wewe! Wape vitu vyao heshima yako iendelee."

Jamaa alikuwa anasifia kwa bidii kweli bidhaa zake, kitu kilichoonyesha kwamba pesa ambayo madam angeitoa ilikuwa ndefu. Bertha akaonekana kuridhia gauni hilo, naye akamwambia Eliya kwamba angeyachukua yote na pesa angemwekea kwenye namba yake ya akaunti ya benki ikifika kesho, na kwa hilo Eliya hakuwa na neno.

Mimi nikakaa kitandani tena, nisitake shobo na mtu yeyote hasa baada ya huyo Eliya kuanza kunisifia-sifia kwa Bertha akisema kwamba alikuwa amepata mtu aliyeendana na hadhi yake kutokana na mimi kuwa na sura nzuri, naye akasema tungezaa watoto waliofunika uzuri wa watoto wa mastaa kama wa Hemedy PhD.

Aliongea huyo kaka, na hivi alikuwa shoga! Mpaka Bertha akakatisha kelele zake na kumwambia aondoke sasa ili sisi tuvae na kwenda kuenjoy. Eliya na mabaunsa wake hawakuwa na neno, nao wakaondoka hapo ikiwa ni mida ya saa nne wakati huu. Dotto akawa amesimama huku akionekana wazi kuwa amelewa, naye akampa ishara Bertha kama kumuuliza 'niende?' naye Bertha akazungusha macho yake kidogo na kumruhusu aende.

Nikawa nimeelewa kwamba jamaa alitaka kumwahi Eliya ili bila shaka aende kuchukua namba kama siyo kupiga sound, ikionekana alipenda mashoga. Maisha haya! Ndiyo maana nilisema mwanzoni kwamba maisha hutofautiana, na kila mtu ana namna ya kuyaendesha kwa uchaguzi wake, kwa hiyo nisingehukumu lolote na kuendelea kuangalia tu pale ugali wangu ulipo. Basi.

Baada ya Dotto kuondoka, Bertha akasema, "Chukua hiyo suti uvae. Tumeshachelewa."

Nikauchukua mfuko wenye suti hiyo, ikiwa ni ya zambarau, safi, mpya, yenye tai maridadi, na boksi la pembeni lilikuwa na viatu vyeusi vipya pia. Yaani haya mambo yote, bure bure tu? Bertha alikuwa anataka kunipeleka wapi?

Nikamuuliza, "Suti na hili joto lote kweli? Tunaingia pande gani?"

"Kigamboni. Na ni lazima uonekane smart, siyo sehemu ya watoto," akajibu hivyo.

"Ahaa, sawa. Kigamboni... ndo' kwenye ile ishu uliyoniambia?"

"Yeah. Twende tukacheze karata," akasema hivyo.

Mh?

Mwanamke huyo akaanza kuvua kigauni kifupi alichokuwa amevaa, nami nikabaki nikimwangalia. Alikuwa amebaki na sidiria nyeupe ambayo ilikuwa na urembo uliofanya rangi ya 'chukuchuku' zake ionekane kwenye matiti yake yenye ujazo mkubwa, na hata nguo yake ya ndani ilikuwa ya mtindo huo huo lakini kito chake kilifichwa vyema kwa mbele.

Nikaona nitie umakusudi wa kuendelea kumtazama, ili aone kwamba nilikuwa nimezubaishwa na mwili wake. Alikuwa na tumbo dogo la mazoezi, hips nene kiasi ingawa alikuwa na mwili mwembamba, naye akaanza kulivaa gauni aliloletewa na Eliya huku akiniangalia kwa umakini pia.

"Unavaa ama?" akaniuliza hivyo.

Nikajifanya kushtuka kiasi na kuliondoa T-shirt langu mwilini, kisha nikalirushia kitandani na kuanza kuitoa suti.

"Hauendi kujimwagia?" nikamuuliza hivyo bila kumtazama.

"Nimekwambia tumechelewa... kwani hujaoga?" akasema hivyo.

Nikatabasamu kidogo tu.

Nikamwangalia na kukuta ameshalivaa gauni lake, lililokuwa refu na lenye mpasuo mpaka kufikia pajani usawa wa kalio kabisa, huku likiwa na mikanda myembamba iliyopitishwa mabegani. Kwenye kifua chake kulikuwa na uwazi mpana ulioonyesha mstari uliotenganisha matiti yake, na kiukweli lilimpendezea.

Akawa ananitazama kifuani kwangu, naye akasema, "Una kamwili kazuri. Gym inakuhusu eh?"

"Ah... hamna hata. Nimenyanyua chuma zamani sana, sa'hivi nimeacha, labda push-up za mara moja moja tu," nikamwambia hivyo kwa kujishaua.

Akawa ananitazama kwa yale macho ya kuhukumu.

Nikafanya kuanza kuivua suruali yangu taratibu huku nikisema, "Angalau lakini nilijaribu-jaribu kuukata mwili... kidogo. Ila... hauna ile sifa ya kuniruhusu niwe bodyguard wa mtu, au siyo?"

Nikawa namwangalia sasa baada ya kuvua suruali yangu, nikiwa nimebaki na boksa pekee, nami nikamchezeshea matiti ya kifua changu kwa uchokozi kidogo.

Akatabasamu kiasi na kutikisa kichwa kuonyesha utani umemwingia, naye akasema, "Hauna baya. Umeumbwa kwa ajili ya mwanamke kweli."

"Siyo yeyote tu lakini... wale wa maana," nikamwambia.

"Kama nani vile?"

"Hamisa Mobeto."

Akacheka kidogo na kusema, "Unamkubali sana eh?"

"Mno. Ni kipenzi changu toka niko la saba. Mademu wote niliotoka nao walikuwa wakali ila bado sijapata anayefikia pale..."

"Ni mpaka uje umpate yeye mwenyewe, na ukishampata utamwona wa kawaida sana," akasema hivyo.

Kisha akaanza kunifata mpaka niliposimama huku akiniangalia usoni kwa umakini, nami nikatulia tu. Akageuka na kunipa mgongo, na ni kweli alinipa maana mgongoni palikuwa wazi, akiwa anataka nimsaidie kupandisha zipu ya nguo hiyo.

Nikatii na kuanza kumpandishia, taratibu, nikifanya makusudi kwa kusugua kucha ya kidole changu mgongoni kwake kadiri nilivyokuwa napandisha. Nikaona ameinamisha uso wake kiasi na shavu lake kunyanyuka kidogo, kitu ambacho kilionyesha kwamba alikuwa anatabasamu, nami nikamaliza kumfungia na kuachia zipu hiyo.

Akanigeukia tena na kuniangalia machoni, mimi nikiwa nimesimama kwa utulivu tu, kisha akashusha macho yake mpaka usawa wa boksa yangu na kusema, "Fanya haraka kibamia. Hatuna muda wa kupoteza."

Dah! Yaani huyu mwanamke!

Nikatabasamu kidogo tu na kutikisa kichwa, naye akaniacha hapo na kwenda pamoja na mkoba wake sehemu yenye kioo ili ajitengeneze usoni na kichwani. Akavaa na mikufu, mabangili, na pete zingine zilizoonekana kuwa za gharama, ama inawezekana zilikuwa ghoroka.

Mwanaume mimi nikatia suti na tai mwilini, na ilinikaa vyema sana japo sikuwa nimepimwa. Ilikuwa ya ki-modo yaani, koti na suruali za zambarau pamoja na kizibao, shati jeupe, kiatu cheusi, na kwa kujumuisha na saa yangu kali mkononi ilinifanya nitokelezee ile mbaya. Lakini joto sasa!

Nikawa nimemwomba Bertha chanuo ili nisawazishe nywele zangu vizuri, naye akanipa huku akinitazama kwa umakini. Nikajitengeneza vyema kisha nami nikamwangalia, nikiona wazi namna alivyokuwa anatathmini mwonekano wangu.

"Hapa vipi? Nakimbilia kuifikia hadhi yako, au siyo?" nikamuuliza hivyo.

Akatoa tabasamu la kiburi kiasi, naye akachukua manukato yake yaliyoonekana kuwa ya gharama na kunipulizia hapa na pale kwenye nguo nilizovaa, kisha ndiyo akaniangalia machoni na kusema, "Unakaribia."

Nikatabasamu kidogo, naye akaacha kuniangalia na kuifuata simu yake.

Jinsi ambavyo mwanamke huyu alikuwa ameanza kujiachia kiuhusiano kunielekea tofauti na mwanzoni ilionyesha alitaka kunizoea, na mimi nilikuwa na nia ya kuendelea kulisukuma hilo kwa kuwa ningemfanya azidi kuweka imani kwangu zaidi, na hivyo iwe rahisi kuzielewa kazi zake na kuziporomosha. Akawa anaongea na mtu kwenye simu, akisema aweke gari tayari kwa kuwa tungeshuka sasa hivi mpaka huko chini.

Alipokata simu, nikamuuliza ikiwa huyo aliyekuwa anazungumza naye ni Dotto, maana jamaa alionekana kuwa anga ya 18 kuweza kuendesha gari vizuri tena. Akasema hapana, huyo alikuwa dereva mwingine ambaye usafiri wake ulikuwa ni wa kulipia, na ndiyo angetutoa hapo hotelini mpaka Kigamboni.

Nikamuuliza kwa nini ilimpasa alipie usafiri ikiwa alikuwa na gari lake kabisa, naye hakunijibu lolote isipokuwa kunishusha na kunipandisha tu. Akanipita na kulifuata begi langu, naye akalifungua na kukunguta kwa nguvu mpaka kila kitu kikadondokea kitandani. Hadi vile ambavyo nilipaswa kumrudishia Latifah hospitali. Alikuwa na fujo!

Akayaona yale madawa, yakiwa kwenye mifuko minne kama tu glucose zikaavyo, naye akayaweka kwenye mkoba wake uliokuwa mpana vya kutosha kuyaweka. Akaniambia nibebe kadi/funguo ya mlango, nami nikatii na sote tukaelekea nje ya chumba. Ningekuja kulirudia begi langu baada ya kutoka huko alikokuwa ananipeleka.

Tulikuwa tumependeza sana, yaani tulipendezeana mbele ya macho ya wengi ambao wangetuona, hukumu ya kwanza kwa yeyote ikiwa ni sisi kuwa wapenzi. Bertha alitembea kwa mwendo uliofanya ionekane ni kama vile kiuno chake kinazunguka, na kalio lake lililotokeza nyuma ya hicho kigauni lilionekana kuwa jeupee. Yaani kwa jinsi ambavyo mpasuo ulikuwa umefikia hadi karibu na kiuno chake, kama tu ungeuvuta upande wa nyuma wa hiyo nguo basi ungeona tako lake lote!

Tukachukua lifti ile ile ya upande wa nyuma, nasi tukaelekea maegesho. Kufika hapo kulinifanya nimwaze tena bibie Miryam, jinsi niliyokuwa nimemkana. Ke! Nahisi angekuwa amenikasirikia si sababu tu nilikana kumjua, ila hasa kwa jinsi ambavyo Bertha alimtendea. Lakini hilo lingekuwa la kusuluhisha baadaye.

Hapa tulikuwa tukielekea pale ambapo nakumbuka Dotto aliegesha Harrier ya madam, lakini wakati huu haikuwa hapo na badala yake lilisimama gari jeusi aina ya Range Rover, safi kinoma. Pembeni alisimama mwanaume aliyevaa suti kabisa, ikiwa ndiyo dereva bila shaka, na aisee huu ungekuwa ni usafiri wa gharama.

Huyu mwanamke hakuonekana kuwa mraibu tu wa madawa ya kulevya, bali inawezekana alihusika katika masuala ya kununua na/ama kusambaza, "Drug Lord" wa kike, na ni huko huko nilikokuwa nataka anipeleke ili nikapaumbue maana alionekana kufanya vitu hivi kwa mpangilio makini sana.

Tukalifikia gari hllo, jamaa akafungua mlango wa siti za nyuma, naye madam akatangulia kisha nikafuata. Gari maridadi siyo mchezo! Na nilijua pointi ya kulitumia hili ilikuwa ni kuoshea huko tulipokuwa tunaenda kucheza karata, nami nikamuuliza ikiwa tungekutana na Dotto huko lakini akakanusha.

Akasema tu Dotto alielekea sehemu nyingine kwa masuala yake binafsi, nami nikaelewa tu kwamba jamaa alikuwa ameenda kula misele na mupenzi wake! Haya bwana, nikatulia tu. Dereva akaingia kwenye usukani, ndinga ika-vruum, safari ikaanza.

β˜…β˜…

Tulizunguka barabara za hapa na kule jijini, tukipita maghorofa, nyumba, maduka, magari, na sikuwa nikikazia fikira sana kuhusu njia tuliyotumia kuelekea Kigamboni, kwa sababu mwendo ndani ya gari hilo ulitengeneza hali fulani tulivu iliyonipa nafasi ya kutumia simu kwa muda mrefu. Ndani ya saa kama moja na nusu hivi tayari tukawa tumeingia Kigamboni kwenye majengo mengi maridadi sana hapa jijini, na ndiyo huyo dereva akawa anaitafuta sehemu tuliyopaswa kuelekea.

Nilikuwa nikiwasiliana na marafiki WhatsApp, pia na mama yangu aliyekuwa akinijulia hali, na yule mwanamke mwislamu aliyeitwa Ibtisam. Bado alikuwa ananitafuta, na wakati huu nikawa nimemwambia kwamba mambo yalikuwa yameingiliana kwa hiyo kukutana isingekuwa rahisi mpaka wakati mwingine. Yaani alikuwa anataka tukutane saa hii hii.

Angalau muda huu nilithibitisha kwamba ni yeye maana tulihamishia maongezi WhatsApp, ndiyo akapiga video call ili nimwone. Sikuona noma kupokea nikiwa pamoja na Bertha maana alikuwa bize na simu yake pia, nami ndiyo kwa mara ya kwanza nikawa nimeiona sura ya Ibtisam bila kificha uso. Alikuwa mwarabu, mweupee, macho mazuri kweli, naye alikuwa na ongea ya taratibu sana kama hataki yaani.

Nikawa namwambia vitu vya kujenga mazoea zaidi, akiwa anasema anapenda sana macho yangu na anatamani anione tena ana kwa ana, nami nikamsisitizia kwamba tungekutana muda mwingine uliofaa. Aliona kwamba nilikuwa nimependeza kwa kuvaa suti, na alitambua nilikuwa kwenye gari, hivyo akauliza ninaelekea wapi kwa wakati huu. Nikamwambia ni matembezi tu, lakini ndiyo ule utani wa 'ama uko unaenda kula bata na wanawake wengine' ukawa umeanza.

Nikamwambia mimi sina hizo, ila nilikuwa naelekea sehemu muhimu sana ndiyo maana nilivaa mpaka na suti, naye eti akawa anataka kujua ni wapi kabisa. Nilikuwa nataka hata nimkatie simu kwa sababu alianza kuonyesha kuniganda mno, lakini ndiyo hapo akauliza ikiwa labda niliogopa kumwambia kwa sababu nilikuwa na mke wangu. Bila matarajio, nikashtukia simu yangu inakwapuliwa upesi na Bertha, nami nikamtazama.

Sasa alikuwa akiangaliana na Ibtisam hapo kwenye video call, naye akasema, "Ndiyo, yupo na mke wake, malaya wewe! Lione kwanza, hadi Kanumba alikwambia una minywele kama fidudidu lakini hukomi tu kutoka na waume za watu! Zima simu ukalale, shenzi wewe!"

Kisha mwanamke huyu akasonya na kuirusha simu yangu kwenye uwazi wa katikati kwenye siti tulizokalia. Nikabaki namwangalia tu usoni, yeye akiwa amerudia ubize wake kwenye simu yake, nami nikaichukua ya kwangu na kukuta kweli Ibtisam amekata mawasiliano. Nikamtazama tena Bertha usoni.

Akaniangalia kwa jicho kali kiasi, naye akauliza, "Nini?"

Nikashindwa kujizuia kuanza kucheka, nami nikageukia upande wa kioo na kuendelea kucheka tu.

"Nini kimekupa raha?" akaniuliza hivyo tena.

Nikamwangalia na kusema, "Yaani kumbe ulikuwa unasikiliza ya huku?"

"Kwani niko nje ya gari?" akauliza hivyo.

Nikacheka tena kidogo.

"Unaongea na malaya zako ukiwa na mimi, una akili sawa sawa?" akaniuliza hivyo.

Aisee! Yaani yeye kila kitu kwake ni kibaya tu.

Nikamwambia, "Basi yaishe. Sitarudia."

Akasonya kidogo kuondoa kero.

Nikaendelea kumwangalia kwa jicho makini sana, yeye asijue ni namna gani nilivyokuwa nawaza mengi mno juu yake, nami nikaipumzisha simu yangu na kuendelea kutulia.

β˜…β˜…

Si dakika nyingi kutokea hapo nasi tukawa tumeingia upande wa jengo moja maridadi sana, na gari likapelekwa eneo la maegesho ambalo lilikuwa limejaa magari ya watu wengine. Ikanibidi nihakikishe ikiwa sehemu hiyo ndiyo iliyokuwa yenyewe, na kweli ilikuwa ni yenyewe. Wapi? Jengo la Casino ya The African Princess!

Mh? Nikamtazama Bertha kwa umakini, ambaye alikuwa akiongea na dereva kuhusu kutuacha malangoni mwa jengo hilo kisha akatafute sehemu nyingine ya kuegesha gari kutokana na maegesho ya hapo kujaa. Sikushangaa kuja sehemu kama hii, lakini sikufikiria hata kidogo kwamba ingekuwa hapo. Msemo wa Bertha kuhusu kuja kucheza karata ukawa umeeleweka vizuri zaidi sasa, ila najua hilo halikuwa lengo pekee la kufika hapo. Nikatulia tu.

Dereva akalisogeza gari usawa wa malango ya jengo hilo maridadi sana, kisha akatoka na kutufungulia mlango, nasi tukashuka. Niliigiza vyema kuwa "gentleman" kwa kukishika kiganja chake madam kama wazungu vile, naye dereva akaliondoa gari hapo baada ya sisi kuanza kuyaelekea malango.

Haipingwi kwamba hii ilikuwa ni sehemu ya watu wenye pesa, na angalau Bertha alijitahidi sana kutufanya tuonekane kuwa pea moja ya watu wa majuu. Na mpaka mwanamke huyu kunivalisha vizuri namna hii na kunileta hapo kwa njia fulani kama vile sisi ni wanandoa, ilionyesha alikuwa amenikubali sana. Ila akili yangu ilikuwa imetekwa zaidi na yale ambayo yangetokea huko ndani ya jumba hilo la kamari.

Hakukuwa na wengi tulioingia nao, na hata kuona kwamba eneo la maegesho lilijaa ilimaanisha ni kweli kabisa yale Bertha aliyokuwa akisema kuhusu kuchelewa. Ikiwa ni saa tano ya saa sita sasa, tukafikia hapo malangoni, nasi tukakutana na mabaunsa wawili, tena nafikiri walikuwa kama wale makomando wa jeshi kabisa, naye Bertha akasalimiana nao kwa njia iliyoonyesha kwamba walimfahamu.

Mwanamke alikuwa amepitisha mkono wake ndani ya kiwiko changu nilichokunjia usawa wa ubavu, nami nikiwa makini, nikawatikisia jamaa kichwa kisalamu. Mmoja wao akatumia kile kifaa cha kupima vitu vyovyote hatarishi mwilini kwa kukipitisha kuanzia mabegani kwangu mpaka viatuni, kisha akaturuhusu tupite bila hata kumkagua Bertha. Alifahamika hapo.

Tukaingia. Hii ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kuingia sehemu hii, na aisee! Walioijenga walifanya kweli. Palikuwa pazuri. Sana. Watu wengi wenye pesa zao walikuwa hapa na kule, aidha wakifanya michezo tofauti tofauti ya kamari, ama kujitumbuiza kwa muziki, pombe, na wanawake.

Aisee, wanawake! Yaani... PISI! Sikuona mzembe hata mmoja humo, yaani wote walikuwa wazuri, shepu hizo, sura, vinguo walivyovaa sasa, ai! Tesha angezimika sana kuwa sehemu kama hii. Yaani kuna mambo mengi kiasi kwamba siwezi kuyaelezea yote hapa!

Kuingia kwetu hapo kulifanya wengi wao watutazame sana. Unajua kutokana na Bertha kuwa amezoeleka hapo sidhani kama yeye ndiyo alikuwa kitovu cha hayo macho kodo, ila juu ya ni nani aliyekuwa pamoja naye wakati huu. Mzee mwenyewe. Niliendelea kuweka mwonekano wangu makini usoni kama sijali lolote lile kabisa, naye Bertha akaninong'oneza sikioni akisema kwamba niendelee kuwapa mikazo ya namna hiyo hiyo. Alikuwa anataka tupite kwenye kona na kumbi zenye watu ambao wangetutazama sana, na kwa hilo niliridhia.

Tukaendelea kutembea, kwa mwendo wa taratibu wa wapendanao, na nilikuwa namwambia mambo yenye kufurahisha sana ingawa hakuwa mwanamke chekelea, ili nijenge mazingira yenye ukaribu zaidi kadiri ambavyo mchezo huu ungeendelea kusonga.

Tukaanza kufatwa na washobokaji japo wenye hela, wakitusalimia, huku wanawake wakali wakipita-pita karibu nami na wengine wakinitazama mno. Samaki mpya kwenye bahari ya papa, yaani wote wanataka kuning'ata! Mpaka kuna watu kadhaa wakawa wameomba kupiga picha na sisi, wakituona kuwa kama watu maarufu, naye Bertha akawakubalia na kuniruhusu nimshike kiunoni na kumbusu shavuni. Nilikuwa sahihi kabisa, alikuwa ananioshea huyu.

β˜…β˜…

Baada ya kuchangamana na mataita wawili watatu waliomwelewa madam na kushusha wine kali pamoja nao, Bertha akaniambia sasa ulikuwa umefika muda wa kunipeleka sehemu ambayo ilidili na suala la unyama wetu, ili aweze kuniingiza kundini.

Wakati huu ilikuwa ni saa saba usiku, naye akanishika mkono na kunitoa sehemu ya VIP tuliyokuwa tumekaa, kisha akaanza kunipeleka upande mwingine wa jengo ambao ulitufikisha kwenye ngazi zilizoelekea chini. Haikuonekana kama tulikuwa juu, kwa hiyo bila shaka kulikuwa na sehemu iliyojengwa chini ya ardhi kwenye jengo hilo, nasi tukashuka.

Bertha alikuwa ameshachangamka kutokana na wine alizopiga, na najua huko tulikoenda ndiyo kungekuwa na mizuka zaidi. Hata huko tulipotoka palikuwa pamechangamka, ila tulipofika huku chini, hadi mimi mwenyewe nikakubali. Palikuwa pa moto! Watu waliokuwepo walifanya kila aina ya ujinga, waziwazi, bila aibu, bila vizuizi. Yaani ilikuwa ni kama nimeingia kwenye zile zama za waroma na Spartacus! Sikuamini.

Kumbi ilikuwa inalindwa hiyo, na Bertha alitoa pesa fulani ndefu inayofanana na dola, kama kiingilio sijui, kisha ndiyo tukapita. Kulikuwa na taa za rangi mchanganyiko. Moshi ulitawala. Harufu zilikuwa nyingi sana; harufu si ya bangi, shisha, mirungi, manukato, madawa ya kuchoma, makalio, na bila kusahau makwapa! Zote zilichanganyika huku.

Joto lilikuwa kali ukitegemea na nilikuwa nimevaa suti, naye Bertha akaendelea kunivuta kuelekea upande mwingine wa mbele zaidi. Tulikuwa tunawapita watu huku nikishikwa-shikwa na kuvutwa kabisa, si na wanawake, si na wanaume, yaani ah! Mola nisaidie!

Mimi na madam tukafika mpaka kwenye mlango mmoja mfupi sana, kukiwa na baunsa mmoja aliyekaa kitini akitutazama kwa umakini, na akiwa na bunduki ndefu, naye Bertha akatoa ufunguo fulani mkobani mwake na kisha kuuchomeka kwenye tundu lisilo na kitasa, nami nikaona kitaa fulani cha kijani kinawaka kwa juu.

Akasukuma huo mlango, nasi tukaingia kwa kuinama, kisha akaufunga tena. Bila shaka hii ndiyo ilikuwa sehemu ya "Top Secret," na ile nimesimama vizuri na kupaangalia ndani humo, nikajikuta nashangaa kiasi baada ya kumwona mtu fulani niliyemfahamu. Oh, kulikuwa na watu kadhaa ndani hapo lakini ni huyu tu ndiye aliyevuta umakini wangu zaidi.

Mwanaume mtu mzima, akiwa amekaa kwenye sofa la sakafuni, yaani yale ya chini bila mbao, na wanawake wawili wakiwa nusu uchi huku wakimtikisia makalio na matiti yao kumzunguka usoni na mwilini, na alikuwa anayalamba. Ilikuwa ni mchumba Festo! Yule yule jamaa aliyekwenda kwake Miryam ili kumtolea mwanamke huyo posa, na ambaye nadhani mpaka kufikia kipindi hiki bado alikuwa anajibebisha kwa mwanamke huyo, ndiyo alikuwa sehemu hii ya madhambi akipewa burudani.

Lakini kwa nini awe ndani ya sehemu hii iliyokuwa ya maovu zaidi na ya siri sana? Alihusika wapi kwenye haya yote ambayo Bertha alitaka kunionyesha?



β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

ITAENDELEA

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

SEHEMU YA ISHIRINI NA SABA

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…


Nikafumba macho yangu kidogo tena na kufumbua, na haikuonekana kama nilikuwa naota. Maaskari hao, hawakuwa maaskari wa usalama barabarani, ila wale ambao huwa wanavaa kofia fulani hivi nyekundu kichwani zilizopindia upande mmoja wa kichwa. Kudadadadadeki!

Nikaanza kujitahidi kunyanyuka, lakini nilikuwa mzito vibaya mno, na Bertha kunilalia ndiyo kuliniongezea uzito. Nikajaribu kumwamsha, wapi. Hadi mate laini yalikuwa yanadondoka kutoka mdomoni mwake! Nikaangalia tena hapo nje na kuona kwamba askari mmoja alikuwa ameanza kuja huku kwenye gari, akishikilia libunduki hilo, nami nikasema "Toba!"

Hakukuwa na muda wa kufikiri aisee. Nikauchukua mkoba wa madam upesi sana na kutoa bastola na kifuko chenye cocaine, kisha nikaurusha kwenye siti na kuinama. Nikalifunua kanyagio la miguu upande wangu na kuvisukumia vitu hivi kwa chini, kisha nikalifunika na kuweka miguu yangu hapo hapo, huku nikijikalisha tena kwenye siti kwa kumweka Bertha aniegamie vile vile. Nikajifanya kuwa ndiyo nimetoka usingizini kwa kufikicha macho yangu taratibu, huku mapigo yangu ya moyo yakifanya riadha hiyo! Siyo poa.

Ni hapo hapo mlango wa upande wake Bertha ukafunguka, nami nikatazamana ana kwa ana na njemba iliyokuwa inaonekana makini kweli. Alikuwa mwanaume mtu mzima, mwenye mwili wa mazoezi bila shaka kutokana na mafunzo yao ya kivita, naye akawa anaangalia mbinuko wa paja la Bertha kwa jinsi alivyokuwa amejilaza, kisha akanitazama na mimi pia. Yaani hapa kama isingekuwa kurukishwa vichura! Sijui tu.

Nikajitoa akili na kumpungia jamaa mkono kiasi, kisha nikasema, "Habari ya kazi mkuu?"

Hakujibu salamu yangu na kuendelea kunitazama kwa umakini, kisha ndiyo akasema, "Mnafanya nini kutembea usiku wote huu?"

"Ah... kumradhi mkuu. Tumetoka kwenye sherehe, sasa... tukachelewa kidogo, ndiyo..."

"Kuchelewa kidogo? Unajua sa'hivi saa ngapi?" akanikatisha kwa kuuliza hivyo.

Nikaona yule dereva akianza kuletwa na yule askari mwingine, nami nikamwambia huyu wa mlangoni, "Najua muda umeenda... na najua kuna sheria, ila... imeenda tu nje ya uwezo wetu yaani... ni kwa sababu sisi tuna...."

Mlango wa upande wangu kufunguliwa ukakatisha maneno yangu, nami nikawatazama waliokuwa nje hapo.

"Habari za kazi mheshimiwa?" nikamsalimu hivyo huyo askari.

Ke! Nilikuwa najikaza kiume yaani, ila hofu iliyokuwepo!

Huyo askari wa pili akauliza, "Wewe ndiyo mmiliki wa hili gari?"

Nikasema, "Ni usafiri wa kulipia kutoka makampuni."

Dereva wetu akaanza kusema, "Boss... tuna... tumesimamishwa shauri ya kuwa mwendoni kwenye hii barabara muda ukiwa umeenda, ila nilikuwa najaribu kuwaelezea kwamba kuna hali zilizosababisha tukachelewa..."

"Haina shida... usijali," nikamtuliza, nikijifanya kuwa bosi kweli.

Yule askari wa kwanza akasema, "Endelea na uliyokuwa unasema."

Halafu nahisi alikuwa mhaya huyo jamaa, nami nikamwambia, "Ndiyo, yaani... tunaishi huku Sinza, sherehe ilikuwa pale Kigamboni na ni mwendo mrefu kama mjuavyo. Ugeni wetu ulikuwa rasmi kwa hiyo... tulitegemewa kukaa mpaka mwisho, so... ndiyo hivyo..."

Askari wa kwanza akauliza, "Huyu ni nani?"

Alielekeza swali lake kwa kunionyesha Bertha, nami nikamwambia, "Mke wangu."

"Amefanyaje? Mbona yuko hivyo?" akauliza tena.

"Ahah... uchovu tu. Amekunywa-kunywa pia, kwa hiyo hapo yupo ndotoni," nikamwambia hivyo.

Yule askari wa pili akasema, "Nionyeshe vitambulisho vyako."

Doh! Nikaitoa wallet yangu kutoka mfukoni mwa suruali, kisha nikapekua na kuvichomoa vitambulisho vyangu viwili; kimoja cha utaifa, kingine cha kikazi. Nikampatia.

Yule askari wa kwanza akafanya kitu ambacho nilikuwa nimehofia zaidi mwanzoni baada tu ya yeye kuingiza mkono wake ndani ya gari na kuuchukua mkoba wake Bertha, kisha akaanza kutafuta-tafuta ndani yake. Kijasho hicho nilichohisi! Niliombea tu asikute fuko lingine la unga ama hapo ndiyo ingekuwa mwisho wa safari!

Yule askari wa pili akasema, "Wewe ni daktari kumbe? Muhimbili?"

Nikamwangalia na kutikisa kichwa kukubali.

"Mnakaa wapi?" akaniuliza tena.

"Tuko hapo... siyo mbali na Makumbusho, tuna apartment Royal Village..." nikasema hivyo kwa kujiamini zaidi wakati huu.

"Ile hoteli kubwa?" akauliza tena.

"Eeh," nikajibu.

Nilitengeneza mazingira ya kuonyesha kwamba tulikuwa na hela sana, na huyo askari wa pili akanirudishia vitambulisho vyangu.

"Aisee, niwaombe radhi kwa mara nyingine tena. Najua hii haifai, na mnatimiza wajibu wenu kutulinda. Sema... inabidi hata niwape pole ya usumbufu, maana... mnapiga kazi sana..."

Niliongea hivyo huku nikiomba kwa ishara kumwelekea askari wa kwanza kuwa anipe mkoba wa Bertha, naye akanipatia. Sikuwa hata na uhakika kama kulikuwa na pesa lakini nikatafuta na kukuta kuna kakibunda ka laki moja. Oh shukrani kwa Mungu!

Nikaifungua huku nikisema, "Siyo mbaya mkiendelea kupiga kazi na ka kitu ka kuwapa boost baadaye mkija kutazama mechi ya watani wa jadi, au siyo?"

Nikamnyooshea askari wa kwanza elfu hamsini, naye akazipokea huku akisema, "Huo muda tunaupata sasa? Hahahah..."

Nikajichekesha pia utafikiri hata alikuwa ametoa utani mkubwa zaidi ya vituko vya Joti! Si unajua wahaya kwa sifa?

Nikampa na yule askari wa pili hamsini pia, naye akazipokea huku akisema, "Hii tuiiteje? Rushwa au?"

"Faini hiyo mkuu. Nimewakosea. Na tena mmenikuta vibaya, yaani ilitakiwa kutoka kubwa zaidi. Na nimemchomolea huyu ya kwake, kwa hiyo mnajua tu tukifika huko akaamka, heee ataniwashia moto huo!" nikawaambia hivyo.

Wakacheka kidogo, mibichwa sasa ikiwa imewajaa.

"Haya bwana. We'... ingia tu kwenye gari uwawahishe huko," askari wa pili akamwambia hivyo dereva wetu huku akimrudishia kadi iliyoonekana kuwa leseni yake.

Dereva na suti yake huyo akazungukia mpaka upande wa usukani. Saa kumi hiyo.

"Kuweni waangalifu next time. Wengine siyo waelewa sana, mngefanya tu hata kulala huko huko kwenye sherehe," askari wa kwanza akasema hivyo.

"Ah, imeeleweka mheshimiwa. Sema na masuala ya kazi si unajua nikaona kurudi home muhimu kwa ajili ya kesho. Na tena siyo kesho, ni leo, yaani dah!"

Wakacheka kidogo tena, na yule wa pili akasema, "Haya nendeni sasa. Lakini huyo akiamka akauliza pochi yake imeenda wapi? Utamwambiaje?"

"Nitamwambia niliinywea wine. Akininyonga sawa tu," nikasema hivyo kama vile sijali.

Wakacheka na kutikisa vichwa vyao, kisha ndiyo wakanitakia safari njema na kutuacha tuondoke. Raa!

Mwendo ulipoanza tena, dereva akawa amenisimulia kuhusu namna ambavyo maaskari hao walimsimamisha na jinsi ambavyo hali hiyo ilimfanya ahisi hasira kutokana na kutoona jambo lolote lile baya tulilokuwa tumefanya, nami nikamwambia tu haikuwa na haja ya kuangalia tena kisa hicho maana ilikuwa ishapita. Nikamwambia tu awe makini asije kutupitisha njia yenye watu wa namna hiyo tena.

Tukaipita Shekilango, na sijui ni kwa nini alikuwa amezungukia mpaka huku, ila labda ndiyo ilikuwa kufuata agizo la kupita sehemu ambazo hatungesimamishwa na yeyote tena. Akachanganya njia ya hapa na pale mpaka tukalifikia jengo la hoteli ya Royal Village hatimaye. Ah, nilikuwa nimechoka!

Tukawapita walinzi getini na kuelekea mpaka maegesho, na jitihada ya kumwamsha Bertha ikagonga mwamba kwa sababu alikuwa mbali mno kiusingizi. Hivyo nikaamua kumbeba tu mikononi, na kufikia wakati huu tayari nilikuwa nimesharudisha bastola na yale madawa mkobani mwake na kuufunga vizuri.

Dereva akasaidia kubeba vitu vyetu na kutusindikiza mpaka kufikia kwenye lifti, nasi tukaanza kuelekea ghorofani mpaka tukaingia chumbani kwake madam kwa msaada wa jamaa nilipomwongoza kutumia kadi ya kufungulia mlango wa kuingilia ndani hapo.

Nikamlaza mwanamke huyo kitandani, na inaonekana dereva huyu alikuwa akifikiri mimi ni mume wake Bertha kiukweli, kwa hiyo mpaka sasa alikuwa akiniita boss. Akaaga hatimaye, ikionekana kuwa huduma yake ndiyo ilikuwa imefikia mwisho, na nadhani tayari alikuwa ameshalipwa na Bertha; labda kupitia njia fulani ya kampuni jamaa aliyofanyia kazi.

Akatuacha, nami nikafunga mlango na kutazama muda. Ilikuwa saa kumi na moja alfajiri, na kiukweli hapa sikutaka kujali kingine tena. Nikavua ushenzi wote aliokuwa amenivalisha huyo mwanamke na kuzima taa, kisha nikawasha kiyoyozi na kwenda kujitupia kitandani hapo; pembeni ya madam. Muda haukupita mwingi sana usingizi ukawa umenibeba pia.


β˜…β˜…β˜…


Nimekuja kuamka asubuhi nisiyofahamu muda wake, na tena hata sikuwa na uhakika ikiwa ni asubuhi. Macho yalikuwa mazito mno, usingizi bado ukiendelea kuyatongoza ili yafumbe na kulala tena, lakini nikajitahidi kutulia kwanza na kuufukuza usingizi kistaarabu.

Matukio yote ya usiku uliotangulia yakacheza vyema tena kichwani kwangu, na aisee, nilikuwa nahisi kiu kikali na njaa! Na hivyo vitu viwili ndiyo vilifanya nihisi uchovu mzito hata kusema ninyanyuke kwenda kutafuta maji, na ndiyo nikawa nimegeukia upande wa pili wa kitanda na kumwona madam Bertha akiwa amelala bado.

Sura yake nyeupe ya Rose Ndauka ilitazama upande wangu, akiwa amelala kwa ule mtindo chali huku mguu mmoja akiwa ameukunjia usawa wa kiuno kwa kujiachia. Hii ilifanya gauni lake lililokuwa na mpasuo matata liwe limefunuka kwenye huo huo mguu uliokunjwa, kwa hiyo wote ulionekana wazi mpaka kuionyesha nguo yake ya ndani nyeupe.

Nikajigeuza vizuri na kumtazama kwa umakini. Alikuwa amelala kama amekufa, pua yake ikionekana kutoa umafuta wa jasho ingawa kiyoyozi cha kitaalamu kilikuwa kinatupuliza, na hiyo ilionyesha kwamba alikuwa na joto kali mwilini kutokana na kutumia madawa mengi jana; ama niseme leo.

Nikaona niachane naye tu na kujinyanyua, nami nikakaa na kuikanyagisha miguu sakafuni. Mapazia yaliyotundikwa kwenye madirisha yalikuwa yameyafunika kwa hiyo mwanga wa hapo ndani ulikuwa hafifu kuelekea kuwa giza, na ni kitu kilichofanya macho yangu yatulie japo kulikuwa na kizunguzungu kichwani.

Nikaichukua simu yangu kutoka kwenye meza ndogo yenye taa pembeni, nikiwa niliiweka hapo kabla sijajitupia kitandani ile alfajiri, na ndiyo kutazama muda nikakuta ni saa sita mchana, siku ya Jumatano.

Nilikuwa nimekuta wapendwa wangu wengi wakiwa wamenitafuta, wa huku nilikotoka na kule Mbagala, na ujumbe wa salamu kutoka kwa yule Ibtisam ndiyo ulionifanya nitabasamu baada ya kukumbuka kile ambacho Bertha alimwambia jana. Nikamtumia ujumbe wa salamu pia, kisha nikaweka simu pembeni.

Nikasimama na kuelekea kwenye dirisha la upande mmoja, kubwa kweli, nami nikasogeza pazia kiasi na kuangalia nje. Kutokea hapo juu, niliweza kuona pande todauti-tofauti za jiji, watu, majengo, magari, na nilitambua kwamba mvua ilikuwa imenyesha kutokana na ardhi zenye lami kulowana na mawimgu kuwa mazito. Jua halikuonekana pia.

Nikaanza kusikia sauti za miguno kutokea nyuma yangu baada ya kusimama hapo kwa sekunde chache, nami nikageuka na kumwona madam akiwa anajinyoosha na kuviringika hapo kitandani mpaka kufikia upande niliokuwa nimelala mimi. Lakini alikuwa anaendelea tu kuviringika kuelekea mwishoni kabisa, nami nikakimbilia hapo ili kumwahi asije kuanguka.

Ilikuwa imebaki kidogo tu apigize likisogo lake, ila nikawa nimemdaka, na nafikiri mshtuko wa jambo hilo ukafanya aamke. Akawa ananitazama kwa kutoelewa-elewa nini kinaendelea, nami nikamsaidia kurudi kitandani tena huku nikimwambia alikuwa karibu kudondoka. Akajilaza chali tena na kukandamiza pua yake kwa vidole, huku akifumba macho kwa mkazo, nami pia nikaona nijilaze tu pembeni yake.

Nikawa nimeangalia juu tu nikiwaza kwenda kuoga kisha niondoke hapa, lakini ingekuwa muhimu kwanza kusikia propaganda za huyu kiumbe. Inaonekana alikuwa anajisikia ovyo tu, nami nikamuuliza ikiwa kuna chochote alihitaji. Cha kwanza kabisa alichotaka ilikuwa ni kujua kwa nini nimelala pamoja naye kwenye kitanda chake, na Dotto alikuwa wapi.

Nikamwambia sijui habari za Dotto, lakini kuhusu kwa nini nimelala hapa, nikamwelezea kila kitu kuanzia wakati alipolewa sana mpaka tukakutana na maaskari na kufika huku hotelini alfajiri ya saa kumi na moja. Aliniangalia kwa mkazo sana, asielewe kwa nini haelewi. Akajilaza kwa ubavu ili aniangalie vizuri zaidi, nami nikamtazama pia kwa kujiamini ingawa nilielewa alitaka kuanza kuangusha mabomu yake.

"Yaani ukawapa laki moja kabisa, hivi we' una akili au matope?" akaniuliza hivyo.

"Kwa hiyo ulitaka nifanyeje? Wale walikuwa FFU, siyo migambo," nikamwambia hivyo.

"Ndo' uwape laki yangu? Hivi wewe... na toka lini FFU wakakubali rushwa, walikuwa mashoga au?"

"Ah, me sijui bana. Ilikuwa tu bahati ya ngekewa..."

"Ama umeiminya hiyo hela, halafu unawasingizia tu hapa FFU?"

"Aa wee... mtafute dereva wako wa jana akusimulie yeye mwenyewe. Me siyo boya kama unavyofikiria."

"We' dogo mbona unazingua mapema sana?"

"Tumia akili yako vizuri basi sometime na we' naye!" nikamwambia hivyo kwa kuudhika.

Akaniangalia kwa umakini na kuuliza, "Unamaanisha nini?"

"Wale polisi siyo wa mchezo, sawa? Kidogo tu hadi walikuwa washashika mkoba wako kupekua, wangetusondeka kwenye Defender je? Ungepimwa wakaona unakula unga je? Ile bastola wangeiona tu kama wangetushusha pale, we' ulikuwa mawinguni madam, nilihitaji ku-act fasta ili wasitutoe mule. Sa'hivi ingekuwa story nyingine hapa, ah..." nikaongea hivyo kwa mkazo.

Akawa ananitazama kwa umakini, kisha akafanya ile cheko ya pumzi huku midomo akiikunja, naye akasema, "Kwa hiyo ndiyo umekuza sauti sasa... eti hero..."

"Ni lazima mpaka useme hivyo? Si uniambie tu asante?"

"Asante ya nini wakati umewapa hela yangu? Kwani hawalipwi? Na utairudisha, bogus wewe... nilikuwa nimeipangia mambo mengine halafu we' uje uwape tu hao wajinga!"

"Asa' madam, kweli, laki moja tu? Unanilalamikia hivyo wakati unajua nitakutengenezea mamilioni kabisa? Huoni kama unanionea?" nikamwambia hivyo kwa kujiamini.

Akabaki kunitazama huku midomo yake ikikunjamana kwa njia ya kuzuia tabasamu lake lisionekane wazi, lakini najua alikuwa akifurahi sana. Nikakunjia mikono kifuani na kutazama juu, naye ndiyo akacheka kidogo na kushusha pumzi kwa sauti kabisa.

"Watu wengine ni wakuda tu. Hawakuona magari mengine ya kusimamisha ila letu tu?" akasema hivyo.

Nikabaki kimya tu.

Akanitazama usoni na kuuliza, "Umekunywa chai?"

Nikamwangalia na kusema, "Itoke wapi? Ndiyo nimeamka tu na mimi... na ni saa sita sasa hivi, ngoja nijimwagie halafu nisepe."

"Wewe, unaenda wapi?"

"Ku... naondoka, naenda nyumbani. Nasikia njaa."

"Hivi wewe mbona una mashauzi sana? Mbona ulikuwa umekaa hapa huo muda wote kama ulikuwa unasikia njaa sana?" akaniuliza kwa njia ya kuhukumu.

"Nilikuwa nataka kuhakikisha naondoka nikikuacha upo sawa. Umeshaamka sasa, na uko good. Kwa hiyo ndiyo naenda..." nikamwambia hivyo kistaarabu.

Alibaki akiniangalia kwa macho yenye utulivu kiasi, nisijue ni sehemu ipi ya maneno yangu ndiyo alikuwa anaitafakari.

Nikajikalisha na kuashiria kutaka kutoka kitandani huku nikisema, "Utanisamehe kwa kulala kitandani kwako, lakini sipendi kulala chini. Ngoja nikuache tu, tuta..."

"Wewe, em' subiri," akanikatisha na kuushika mkono wangu kabisa.

Nikamwangalia usoni.

"Hebu kaa hapo utulie," akaniambia hivyo.

Alionekana kuwa makini zaidi wakati huu, ule u-madam ukiwa umerudi, nami kweli nikaona nitulie na kumsikilizia.

Akageukia kule pembeni na kuchukua kimkono cha simu ya mezani, kisha akakiweka sikioni na kubofya namba tatu tu. Baada ya sekunde chache, akaanza kuongea na mtu fulani, akimwambia anahitaji huduma ya vyakula vitamu kwenye chumba hiki namba 101, kisha ndiyo akairudisha simu mahala pake.

Akanitazama na kusema, "Uwe unaacha kujiendekeza na we' naye. Vitu vingine siyo mpaka uanze 'natako kuondokoo'... si unasema tu uletewe chakula, we' vipi?"

Aliongea kwa njia ya michambo na kunitazama kwa mkazo wa kiutani, nami nikatazama tu pembeni bila kutabasamu wala nini.

Akajinyanyua kutoka kitandani na kusimama karibu na kitanda, nami nikamtazama machoni na kukuta ananitazama pia. Tulikuwa tunapeana utizami makini sana, naye akaanza kuitoa mikanda ya nguo yake mabegani, akiishusha huku bado macho yake yakiwa kwangu. Ilipomtoka mikononi, ikafanya nguo yake idondoke mpaka chini, mwili wake mweupe ukiwa wazi, lakini sikuacha kumtazama machoni.

Sidiria na nguo yake ya ndani vilimsitiri vyema kwa mbele, na najua alikuwa amefanya hivyo kwa makusudi, ila mimi nikaendelea tu kumwangalia usoni na si mwilini mwake. Akatoa tabasamu la upande kwa kiburi, kisha akavua mikufu, mabangili, na pete zake na kuzirusha kitandani, halafu akageuka. Hapo sasa ndiyo macho yangu yakashuka. Hiyo nguo ya ndani aliyokuwa amevaa iliacha mashavu ya kalio lake nje, na yalikuwa meupe kama tu mwili wake.

Nafikiri Bertha alikuwa na makusudi iliyokithiri sana, kwa kuwa alianza kutembea kuelekea upande wenye mlango wa kioo kizito, ikiwa ni bafuni bila shaka, naye alitembea taratibu huku akifungua sidiria yake kutokea mgongoni kwake, kisha akaitupa chini. Nilikuwa nimeshaanza kuvimba bila kupenda, japo sikuona kifua chake kwa mbele, hali hiyo tu alivyoitengeneza ilisisimua.

Alipoufikia huo mlango, akavua nguo yake ya ndani huku akiwa ameibana miguu yake kwa uangalifu ili nisiweze kuona mengine zaidi ya kalio lake na miguu tu, naye akaitoa miguuni pake huku akiwa amenigeuzia shingo kunitazama kwa macho ya uchokozi. Huyu alikuwa ni mtu mkubwa ananifanyia hivyo! Ingekuwa ni bwege mwingine hapo tayari angekuwa ameshavua nguo akifikiri huo ni mwaliko, ila mimi nilikuwa na akili bwana.

Haya yote yalikuwa majaribio ya huyu mwanamke ili kuona akili yangu inatik-tok sehemu gani zaidi, nami nikaacha kumwangalia na kuchukua tu simu yangu. Nilijitahidi kuukazia msuli ulale upande mmoja ili asije kuona kwamba alichokuwa amefanya kilinisisimua, maana ni boksa laini tu ndiyo iliyokuwa mwilini bado, naye akawa ameingia mule bafuni kuoga.

Alipokuja kutoka, alikuwa amejifunika kwa taulo fupi kutokea kifuani, na alikuwa amezivalisha nywele zake kimfuko fulani cha kuzuia zisiguswe na maji, naye akasema naweza kwenda kuoga sasa. Alikuwa kama ameshapotezea kile alichotoka kufanya muda mfupi nyuma, nami kweli nikaelekea bafuni kuoga.

Damu ilikuwa inakimbia kweli shauri ya njaa, nami nikawa nimemaliza na kujikausha maji kwa taulo nyingine, kisha nikajifunga hiyo hiyo kiunoni na kutoka. Nikakuta kukiwa na mtu mwingine ndani hapo, mwanamke mhudumu wa vyakula hotelini, ambaye alikuwa ameleta vyakula vya ukweli na chai za chocolate kama vile bado ilikuwa asubuhi.

Wakati huu Bertha alikuwa amekaa kitandani akiwa amevaa nguo ya taulo iliyoufunika mwili wake wote, na nywele zake kuziachia, na mhudumu huyo alikuwa amesimama pembeni yake akiwa ameshika kifaa cha kielektroni cha kupokea pesa. Yaani, Bertha akawa amempa kadi yake ya benki, na huyu mhudumu akaipachika tu hapo kwenye hicho kifaa ili kivute hela ya malipo kwa ajili ya chakula. Mambo hayo!

Huyo mhudumu aliponiona nakuja upande wao nikiwa kifua wazi, akaendelea tu kuniangalia, nami nikamsalimia. Akaitikia vizuri, nami nikafika hapo kitandani na kukaa upande mwingine karibu na pale chakula kilipowekwa.

Nikiwa najali zaidi hamsini zangu, nikashtuka kiasi baada ya Bertha kufoka kwa sauti ya juu, akiwa amempigia kelele huyo mhudumu kuwa aache kuzubaa na akaendelee na kazi zake. Nikawaangalia wote na kukuta huyo mhudumu akiwa ameanza kusukuma katoroli kake ka kubebea vyakula huku akiniangalia mara kwa mara, naye Bertha akasonya. Dah!

Inaonekana dada wa watu alikuwa amezubaa kuniangalia mpaka Bertha ndiyo akampigia huo mwano, nami nikaendelea kumtazama tu mpaka alipoondoka masikini. Nikamwangalia Bertha, ambaye alikuwa akinitazama kwa macho yenye kukerwa, nami nikacheka kidogo kwa pumzi na kuangalia pembeni.

Haikuwa muda mrefu baada ya hapo nasi tukaanza kula kwa pamoja. Ugali mzuri, nyama hizo, mboga mchanganyiko zilizokaangwa, soseji, chai ya kupashia matumbo mwanzoni, pamoja na maji ya kunywa. Nilifikiri huyu mwanamke alishindia madawa tu lakini kumbe alijua nini maana ya mlo pia.

Hatukusemeshana kwa lolote tena mpaka tuliposhiba kabisa, ndiyo nikampa shukrani na kuanza kuvaa nguo zangu nilizokuja nazo jana. Akawa bize tu na simu yake, akiwa hajamuulizia Dotto tena, nami nikaweka vifaa vyangu begini na kulibeba, kisha ndiyo nikamuuliza ikiwa kuna jambo lolote alitaka nifanye kuhusiana na zile ishu zetu; nikiwa hasa namaanisha kutengeneza madawa mengine.

Alichoniambia ikawa 'nenda tu, nitakwambia,' nami huyoo nikageuka zangu na kunyoosha njia. Hata hakuwa akinilipa! Ila siyo mbaya, maana nilikuwa nimeshajazwa matumaini ya kuja kumtoza malipo makubwa sana kwa kukomesha maovu yake, na angelipia bila kupenda.

β˜…β˜…

Ilinichukua masaa karibia matatu kabisa kutokea huko kwa madam Bertha mpaka kuja kufika kwa Ankia. Nilipoondoka hotelini pale, nilichukua usafiri wa bodaboda mpaka kwenye kituo cha mabasi ya mwendokasi ili nielekee Muhimbili kwanza.

Nilikuwa na lengo la kwenda kurudisha vifaa nilivyochukua hospitali pamoja na kumwona Latifah, lakini pia, nilitaka tu kuonana na daktari Roshan ili nizungumze naye kwa machache. Hayo machache yalikwenda kwa jina la Mariam. Nilitaka nimweleze kwa ufupi kuhusu maendeleo ya binti ili anipe mawazo zaidi juu ya mambo ambayo ningeweza kuboresha katika zoezi langu la kumsaidia binti, nami nilitekeleza hilo baada ya kufika hospitalini hapo.

Latifah ndiye aliyekuwa mlaji wa muda wangu zaidi maana hakuishiwa maneno na malalamiko kuhusu mimi kumweka pembeni sana, na alifanya kunikutanisha na watu wengine tuliofanya nao kazi hospitalini hapo ili tu niendelee kukaa pamoja nao kwa muda mrefu.

Ila Tesha kunipigia na kuniuliza kama ningeenda kwao leo ndiyo iliyokuwa njia yangu ya kumtoroka mwanamke huyo, nikiitumia kama dharura fulani iliyonihitaji kuwahi kuondoka. Nikamwambia rafiki yangu kwamba ndiyo nilikuwa njiani kurudi Mbagala, naye akasema sawa. Latifah alikuwa anajua kung'ang'ania mtu wewe, siyo poa!

Ndiyo nikafanikiwa kumkimbia baada ya kumwachia vifaa vile, nami nikaenda kupanda daladala pale Kariakoo zilizoandikwa Gerezani mpaka Mbagala. Na aisee! Sikutaka tena kuja kurudia kupanda hizo daladala, yaani mshono ni mshono, watu tulikuwa tumebanana haswa mpaka kupumua ilikuwa ni mateso. Sijui shida ilikuwa ni nini tu, yaani gari zinakuja watu wamejaa kinoma, na hapo ni jioni ya mapema tu, sikupata picha usiku hiyo biashara ilikuwa vipi! Na hii ilikuwa ni mara ya pili kuzipanda.

Kwa hiyo baada ya kuwa nimefika kwake Ankia, mida ya saa kumi na nusu hivi jioni, nilimkuta akiwa pamoja na wale marafiki zake wawili vijana, wale wavaa pini puani kama yeye pia, nami nikapokelewa kwa salamu nzuri na kuzirudisha, kisha nikaenda zangu chumbani. Ankia alikuwa amenimiss huyo! Akaja chumbani nilipokuwa nimeanza kutoa nguo mwilini, naye bado akawa analalamika kuhusu mimi kuikosa pilau yake jana.

Nikalikamata kiuno na kuanza kulipiga denda laini, na kidogo tu nilikuwa nimeshaamka maana nilikuwa na hamu kweli, hasa baada ya madam kunianzishia uchokozi wake usiokuwa na maana kule hotelini, lakini nisingeweza kwenda na Ankia mazima kwa wakati huu. Alikuwa na wageni, halafu bado alikuwa "mgonjwa," kwa hiyo mbio hiyo ya dendani ikaishia midomoni tu.

Lilikuwa limelegea kweli, likiniangalia kwa hamu pia, nami nikamwambia asiwaze; akipika msosi mzuri tena kwa ajili yangu tutakula pamoja, yaani mimi na yeye tu.

Nikamwambia kwamba nilihisi uchovu kiasi maana nilitokea hospitalini kutimiza wajibu fulani, ila na sasa nilitaka kuvaa ili kwenda kumwona Mariam pia. Ndiyo akawa ameniambia kwamba alikuwa amekuja chumbani humu ili kuwaumiza mioyo hao rafiki zake, akisema eti wote walikuwa wananitaka. Nikamwambia amefanya jambo la maana, naye akacheka kidogo na kisha ndiyo akatoka ndani hapo.

Kweli bado nilikuwa nikijihisi mzito mzito, kama vile nilitakiwa kuendelea kulala, na kukiangalia kitanda kulinifanya nitamani kweli kukirukia ili nijisinzishe kidogo, lakini nisingeweza kuvunja ahadi yangu ya kwenda kumwona Mariam. Na nilikuwa nawaza kuhusu dada yake pia, ikiwa alikuwa amewaambia mama zake labda kuhusu jinsi nilivyomkana jioni ya jana, ila ndiyo ningetakiwa kwenda huko na kujua.

Nikatia viwalo vingine safi mwilini, kisha nikatoka hapo tena na kuwapita wanawake wakiendelea kukaa pamoja. Akili yote ilikuwa kwa Mariam wakati huu. Nikafika hapo kwao, nami nikaelekea mpaka ndani na kupiga hodi mlangoni. Aliyekuja kunifungulia mlango hakuwa mwingine ila binti Mariam mwenyewe, naye akanikaribisha kwa tabasamu la furaha na kunikumbatia.

Nikaingia ndani hapo huku bado akiwa amenikumbatia, na ndiyo nikawakuta wenyeji wangu wengine wakiwa wamekaa kwenye masofa na wakiniangalia kwa furaha. Warembo wangu wawili walikuwepo, Tesha, pamoja na Shadya pia, nami nikasalimiana nao na kuanza mazungumzo yenye kufurahisha pamoja nao wote. Walikuwa wamenikosa tokea jana, hasa Mariam, ambaye hakutaka kuniachia yaani mpaka nikahisi aibu.

Kwa hiyo nikakaa naye sofani, nami nikamwambia nimekuja sasa na kama kawaida, leo pia tungechora. Akafurahi sana na kwenda chumbani upesi kama mshale, ili akalete vifaa vya kuandikia. Tesha akasema yaani dogo alikuwa kama hana amani kutoniona leo, ila kufika kwangu ndiyo kukamrudishia furaha yake, nami nikamwambia huo ni uhakika. Nikawa nimeulizia hali yake Bi Jamila na kujua kwamba aliendelea vizuri zaidi wakati huu, akiwa alipata dawa za kutumia walipokwenda hospitali jana na Miryam kuangalia afya yake.

Angalau sasa nikawa nimehakikisha kwamba hali ilikuwa shwari kwa upande wa familia nzima ya bibie Miryam kunielekea, kitu ambacho kilionyesha kwamba hakuwa amenitibulia kwa lolote. Ila kuongea naye bado lingekuwa jambo la lazima; kwanza nimweleweshe kuhusu suala la jana, halafu nimwambie ukweli wote wa matendo ya Joshua ambayo yangekuja kuivuruga amani hii niliyoikuta hapa.

Najua angenielewa tu, kwa sababu aliipenda familia yake, kwa hiyo ningepaswa kumsubiri bibie afike ili nisahihishe mambo. Kila kitu kingekuwa sawa.

β˜…β˜…

Mambo yakaendelea kuwa mazuri tu sehemu hii baada ya masaa machache kupita mpaka kufikia saa mbili usiku. Nilikuwa nimefanya michezo ya uchoraji wa herufi pamoja na Mariam, yaani kuzichora alfabeti na kuzipamba kwa rangi zake binti pia.

Nilikuwa namwelekeza apangilie herufi kadha wa kadha kwa mtiririko hususa ili kutokeza maneno kama "MY NAME IS MARIAM," "MY BROTHER IS TESHA," na mengine mengi kwenye karatasi nyingi, kisha mimi na Tesha tungemsaidia kuyatamka kwa kusoma pamoja naye. Alifurahia sana huyu binti na kuwaonyesha mama zake kila mara, nao wangempongeza sana.

Shadya alikuwa amekwishaondoka kwenda kwake kwenye mida ya saa kumi na mbili, kwa kuwa kipindi hiki tayari mume wake alikuwa amesharudi kutoka safari. Alikuwa hapa leo kwa ajili ya kupangana na mama wakubwa na hata Tesha pia kuhusu kufanya sherehe ndogo ya siku yake Bi Zawadi ya kuzaliwa, iliyokuwa ikikaribia kufika, na walikuwa wamepanga ije kufanyiwa hapa hapa nyumbani maana eti mama wakubwa walikuwa wazito mno kwenda kumbini.

Walikuwa wameshaanza kupanga bajeti, nani aje, nani asije, na katika watu wa kuja mmoja wao alikuwa yule Dina tuliyeenda kumtembelea siku fulani ya juzi pamoja na Tesha. Kijana ndiyo akawa ameniambia sasa kwamba alikuwa amewasiliana na Dina leo leo, na mdada huyo alisema eti alikuwa ameumia baada ya mimi kutotimiza ahadi ya kwenda pale kwake kumtembelea tena.

Tesha akasema inaonekana Dina alikuwa amenielewa sana, lakini hata alipomjaribu kumpa namba zangu, alikataa, mwanadada huyo akiona hiyo kuwa siyo busara, ama labda tu aliogopa. Nikamwambia Tesha inaonekana huyo Dina alikuwa na usawaziko mzuri wa kiakili, nami nikasema tungepanga kwenda kumtembelea siku nyingine tena.

Basi, tukiwa tunaendelea kufurahia wakati huu kwa pamoja hapo sebuleni, honi ya gari nje ya geti la nyumba hii ikaashiria kuwa mkurugenzi alikuwa amefika. Tesha akanyanyuka na kwenda nje ili amfungulie dada yake, nami nikawa najiandaa kwa yale ambayo yangefuata nikionana na Miryam tena.

Kale ka hisia ka msisimko wa hofu kiasi kalikuwepo, siyo hofu ya woga bali ya kutarajia mengi mno. Sikujua mwanamke huyo angenitendea vipi baada ya kile kilichotokea baina yangu, yeye, na Bertha ile jana jioni, na ndiyo nikawa nasubiri kuona. Sijui ingekuwa vipi endapo kama angefika na gia ya kwanza kuingiza ikawa kunifukuza!

Baada ya gari kuingia na geti kufungwa, bibie Miryam akawa wa kwanza kuingia ndani, kisha Tesha akafuata nyuma yake. Mwanamke huyo alikuwa amevalia shati jeupe la kike lenye mikono mirefu lakini iliyokunjwa mpaka usawa wa viwiko, pamoja na suruali nyeusi ya kitambaa iliyokuwa imembana kiasi usawa wa hips zake na kuchanua kwa upana zaidi kufikia miguuni. Nywele zake ndefu za kusukwa alikuwa amezilaza upande wa mbele kwenye bega la kushoto, na mkononi alishikilia mkoba mweusi.

Alipokuwa ameingia tu na kuniona, nilitambua upesi sana kwamba hakufurahishwa na uwepo wangu hapo kwa sababu hakunitazama tena na kuelekeza fikira zake kwa wengine hapo sebuleni. Akakaa kwenye sofa pamoja na Mariam, huku akizungumza na mama zake wakubwa kuhusu masuala ya hapa na pale yaliyokuwa yametokea kwa muda aliokuwa kazini. Tesha alikuwa amepeleka mifuko fulani jikoni, bila shaka Miryam akiwa ndiyo amekuja nayo, kisha akarudi na kukaa karibu nami tena.

Mariam akafata karatasi moja aliloandikia na kwenda kumwonyesha dada yake, naye Miryam akatabasamu kiasi. Akamuuliza ikiwa aliandika yeye mwenyewe, na Mariam akatikisa kichwa kukubali. Miryam akamwomba ayaseme maneno hayo kwa sauti, naye Mariam akayatamka vizuri sana. "I LOVE YOU MIRYAM." Sisi wengine tukacheka kidogo, na nilikuwa nimemkaririsha kwelikweli hayo maneno, naye Miryam akaonekana kufurahi sana.

Bi Zawadi alipoanza kumzungumzia Mariam kwa kugusia namna ambavyo nilichangia kumfanya achangamke namna hiyo, Miryam hakuniangalia, wala kunisemesha hata kidogo, akikwepa kuendeleza mazungumzo kwenye mada ambazo ningehusika zaidi. Alikuwa na hasira mimi, na ilieleweka kwa nini. Nikaona nitulie kimya tu mpaka Tesha akauliza kwa nini sikuwa nikiongea, na ndiyo nikawa nimemtazama Miryam. Nikakuta akiwa ameniangalia, kisha akaacha na kumtazama Mariam tu.

Ah, hii hali sikuipenda kabisa, na kwa sababu haikutakiwa kuendelea kuwa namna hiyo, ningepaswa niongee na huyu dada. Ningepaswa nimweleweshe. Miryam alikuwa mstaarabu na mwelewa kwa hiyo najua angenisikiliza na kuelewa maana ya yale niliyoyafanya jana. Haingekuwa busara kumwacha anikasirikie na kujenga kitu kama uadui wakati bado mdogo wake alinihitaji, kwa hiyo ningetakiwa kuongea naye; sasa hivi.

Baada ya Tesha kuniuliza kwa nini nilikuwa kimya tu, sikutoa jibu lolote kutokana na kuwa ndani ya fikira zilizozama kwa dada yake, naye akanishika mkononi na kusema, "JC? Vipi bro, mbona umezubaa?"

"Uko sawa JC?" Bi Jamila akaniuliza pia.

"Ndiyo, niko sawa," nikajibu hivyo kwa utulivu.

Wengine wakawa kama wameelekeza umakini wao kwangu, isipokuwa Miryam tu, aliyekuwa anapekua mkoba wake kutafuta nini sijui.

"Miryam..." nikamwita.

Mkono wake ukakatisha kutafuta alichokuwa anasaka mkobani, na macho yake mazuri yakapanda taratibu kunitazama usoni.

"Naomba kuongea na wewe... tafadhali..." nikamwambia hivyo.

Akaendelea kuniangalia kwa umakini, na Mariam akamwangalia pia kwa njia makini. Hata binti alionekana kuelewa kwamba kulikuwa na jambo zito, siyo mama wakubwa na Tesha pekee tu walioonekana kuhisi hilo kutokana na jinsi ambavyo wao pia walimwangalia Miryam.

Sikuhitaji mwanamke huyo anipe jibu. Nikanyanyuka tu kutoka sofani na kuuelekea mlango, nami nikatoka hapo na kwenda kibarazani. Nilielewa kwamba bila shaka niliwaacha wengine pale ndani wanajiuliza tatizo lilikuwa nini, ila lilikuwa langu na Miryam pekee kutambua na kutatua.

Sekunde tatu tu na mwanamke huyo akawa amekuja nje pia, naye akasimama umbali mfupi kutoka pale nilipokuwa nimesimama.

"Kuna mambo mengi sana ambayo nataka.... nashindwa kujua nianzie wapi yaani..." nikaanza kwa kumwambia hivyo.

Akawa ananitazama tu machoni kwa umakini.

"Miryam... kwanza... kile ambacho kimetokea jana najua hukukielewa vizuri, kwa hiyo..."

"Nilielewa vizuri sana," akanikatisha kwa kusema hivyo.

Nikatulia kidogo na kumuuliza, "Ulielewaje?"

"Mimi na wewe hatufahamiani," akasema hivyo.

Nikaishiwa pozi kiasi. Lakini nikamwambia, "Haiko kama unavyofikiria. Pale yaani... yale mazingira hayakuwa mazuri, sikutaka wale watu wakufahamu kwa sababu...." nikashindwa kuendelea.

Akasogea karibu zaidi na mimi, naye akasema, "Unakuwa mtu mwingine kabisa mbele yetu halafu unapokuwa na watu wako unabadilika, si ndiyo? Sasa nitakwambia kitu fulani. Sijali kuhusu nani unakutana naye, na sijui ni nini unafanya, lakini kuanzia wakati huu sitaki tena ujihusishe kwa lolote lile linalohusu familia yangu. Umenielewa?"

Alinifanya nibaki nikimtazama kwa mshangao mzito bila hata kuachama mdomo na kukodoa macho. Aliongea kwa sauti ya chini lakini ilipiga roho ya masikio yangu mpaka kufikia hisia kwa kishindo chenye nguvu sana, naye akaashiria kutaka kurudi ndani tena.

Nikamwambia, "Miryam, subiri. Unamaanisha nini?"

Akaniangalia na kusema, "Sitaki tena uwe karibu na mdogo wangu!"

"Kwa nini?"

"Ahah... "kwa nini?""

"Miryam haujui sababu iliyonifanya nikatenda kama vile jana..."

"Na sijali. Nimekwambia sitaki tena u..."

"Miryam, em' kwanza... tulia. Sawa? Huo uamuzi unaufanya kwa sababu tu ya hasira, hauoni utam-cost mdogo wako?"

Akaniangalia kwa macho makali na kunisogelea karibu zaidi, naye akasema, "Kwani nilikuomba huo msaada wako?"

Nikatulia kidogo, ikiwa imechoma hiyo, nami nikamwambia, "Ndiyo, hukuniomba. Nilijitolea mwenyewe, kwa sababu ninataka kumsaidia Mariam... apone. Haya mambo mengine hayahusiani naye."

"Lakini si ni mambo yako? Kwa hiyo nini... ukiwa hapa unajifanya daktari mwema, unajali, halafu ukiwa na watu wako ndiyo hatujuani? Ya nini uendelee kumzunguka mdogo wangu ikiwa hata na yeye unaweza ukamkana mbele ya watu kwamba humjui?" akaniambia hivyo kwa hisia kali kiasi.

"Miryam hapana, hiyo siyo maana ya kile nilichokifanya jana," nikamwambia hivyo kwa sauti yenye hisia.

Akabaki kuniangalia tu kwa mkazo.

"Wale siyo watu wazuri Miryam. Ndiyo waliosababisha kifo cha Joy, na mimi niko nao ili nije kusaidia kuwakamatisha... wakalipie kwa maovu wanayofanya..."

"Kwa hiyo na we' umekuwa askari sasa hivi?" akanikatisha.

"Hapana, ila ninafanya kazi na maaskari," nikamwambia hivyo.

"Ahah... unbelievable. Yaani unaweza kusema chochote, na kufanya chochote ili kudanganya tu. Uko hapa, unamsaidia mdogo wangu, sijui ili uthibitishe kwamba wewe ni mtu mzuri wakati siyo! Sitaki tena... we' kaka... sitaki tena ujihusishe na Mamu. Hiyo influence yako... na mashirikiano uliyonayo na hayo makundi yafanyie huko huko, sitaki tujuane tena kama ulivyokataa kunijua. Unafikiri nitakuwa na amani kujua unafanya mambo hatari wakati uko na mdogo wangu? Ili na yeye aje apelekwe kwenye hizo biashara zenu za kusagana?"

"Miryam..." nikamwita kwa upole.

Akanyanyua kidole chake na kusema, "Uliyoyafanya kwa ajili ya Mamu yanatosha. Kama kukushukuru nimeshakushukuru, kwa hiyo nakuomba... utajua mwenyewe namna ya kuwaelezea hawa wengine lakini nakuomba uache... mazoea na familia yangu."

"Yaani Miryam kweli... unaongea haya yote kama vile hunijui?"

"Ninajua nini kuhusu wewe kwani? Zaidi ya kwamba ikiwa sitachukua hatua haraka basi utasababisha matatizo kwenye familia yangu?"

"Mimi? Mimi niwasababishie matatizo? Siyo mimi nitakayewaletea shida Miryam, ila usipoangalia, ni wewe mwenyewe ndiye utakayefanya familia yako ianguke," nikamwambia hivyo.

Akakaza sura yake na kuuliza, "Unasemaje?"

"Usiwaze kuhusu mimi kuwa mbaya kwako kwa sababu hujui hata kwa kile nilichokifanya jana, nilikifanya ili kukulinda. Siwezi kuwatakia nyie mabaya hata kidogo. Ila huyo Joshua wa sasa siye mtu unayemdhania Miryam. Bado ana lengo la kuwaharibu nyie kama familia... na atafanya kitu kibaya tena kwa Mariam ili achukue shamba lake," nikamwambia hivyo.

Akawa ananitazama kwa hisia kali kiasi, naye akauliza, "Umemaliza?"

"Sikutanii Miryam. Nina uhakika na ninachosema. Kaka yako siyo mtu, hana uthamini wa familia, anajali tumbo na koo lake tu. Mtu anaweza kubadili matendo lakini kubadili utu huwa ni ngumu, na utu wa Joshua umeshaharibu mpaka dhamiri yake kiasi kwamba hawezi akabadili matendo yake tena. Anachofanya ni maigizo tu. Nafikiri hayo yote unayajua Miryam, lakini sidhani kama unajua kwamba ni yeye ndiyo alipanga Mariam agongwe na gari siku ile nimemwokoa... hiyo ilipofeli ndiyo akaja hapo getini na zile paper, na alipofeli tena ndiyo sasa hivi ameona aje kivingine. Unaona? Anataka kufanya Mamu atoweke Miryam, na usipoangalia... atatoweka kweli. Ni yeye ndiyo unapaswa kujihadhari naye Miryam... siyo mimi," nikamweleza hayo kwa hisia.

Akawa ananitazama kwa umakini tu, naye akasema tena, "Umemaliza?"

Nikabaki nikimwangalia kwa utulivu.

"Wewe ni mwongo sana. Sawa? Nakwambia leo... wewe ni mwongo, halafu mnafiki," akaniambia hivyo.

Dah!

Nikaendelea kumwangalia kwa macho yenye umakini.

"Unajua kila mara ambayo nilikuwa najitahidi kuona kwamba labda nilikujaji vibaya mwanzoni... umerudi tena kunithibitishia kwamba nilikuwa nakosea. Wewe ndiyo mwongo. Unaweza mpaka kudanganya mtu kwamba uko karibu kufa ili tu upate lifti, unashindwa vipi kudanganya kuhusu matendo ya mtu mwingine ambaye hata humfahamu?" akaniambia hivyo.

"Ahh... God!" nikasema hivyo kwa sauti ya chini huku nikitikisa kichwa kwa kutoamini jinsi ambavyo jambo hili lilizidi kwenda upande mbaya tu.

"Unadanganya kwamba Joshua alitaka kumgonga Mariam kwa gari, ulimwona? Oh, kama una ushahidi utoe. Utaniaminishaje? Kwa kuanza kukohoa na kusema unaumwa kifua, au?" akaniuliza hivyo.

Nikamwangalia kwa mkazo kiasi na kusema, "Kwa hiyo kumbe bado tuko kule kule tu? Mpaka leo bado hujanielewa vizuri kiasi kwamba unatumia hicho kisa nilichokifanya mara ya kwanza tumekutana ili kufumbia macho mambo mazito ya wakati huu? Ningekuwa nataka kuwaletea matatizo ningemsaidia mdogo wako?"

"Kwa hiyo nini... unanisimangia Mamu? Kwamba niamini kila kitu unachosema kwa sababu unamsaidia mdogo wangu bila kulipwa, si ndiyo?" akaniuliza hivyo kwa hisia kali.

"Okay Miryam, sijamaanisha hivyo unavyofikiria... no," nikamwambia hivyo kwa ukali kiasi.

Hisia zilikuwa zimeanza kupanda!

"Sikukuomba umsaidie Mamu, ulikuja mwenyewe kwangu. Ukitaka kuacha, acha... na sitaki tena uendelee. Acha niibebe familia yangu mwenyewe, haikuhusu kwa lolote," akanisemesha hivyo kwa sauti ya juu kiasi.

Inaonekana sauti yake ilisikika mpaka pale ndani, kwa kuwa mlango ulifunguka na wa kwanza kutoka akawa ni Tesha.

"Hakuna anayekuzuia Miryam, lakini hata wewe ni mwanadamu. Hutabeba kila kitu peke yako, kuna vitu vingine vitakushinda na utahitaji msaada. Huwezi kuona kila kitu..."

"Nimesema uniache! Sihitaji msaada wako kwa lolote!" Miryam akanikatisha kwa ukali.

Tesha akawa amesimama nyuma yake, akionekana kushangaa, na mama zao wakubwa wakawa wamekuja nje pia na kusimama karibu na Miryam.

"Mimi... kuna tatizo gani?" Bi Zawadi akamuuliza hivyo.

"Nakuomba uondoke," Miryam akaniambia hivyo.

"Da' Mimi... JC kaka, ishu ni nini?" Tesha akauliza hivyo.

Nikasema, "Miryam nakuomba utulize akili... ili uone mambo kama...."

"Nimekwambia ondoka, ushauri wako siuhitaji. Mizigo yangu ni yangu kubeba, haikuhusu," Miryam akaniambia hivyo.

Nikamwambia, "Miryam, unavyofikiria siyo. Hicho kimeanza kuwa kiburi sasa...."

Miryam akanitandika kofi zito shavuni ghafla sana!

"Mimi!" Bi Zawadi akaita hivyo kwa mshangao.

Nilibaki nikiwa nimeinamishia uso wangu pembeni baada ya mwanamke huyu kunilabua namna hiyo, na kiliuma kweli! Ila maumivu ya hicho kibao kwangu mimi hayakuwa shavuni, bali moyoni. Mambo yalikwenda tofauti kabisa na matarajio yoyote niliyokuwa nayo.



β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

ITAENDELEA

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
Back
Top Bottom