Simulizi: Mimi na Mimi

Simulizi: Mimi na Mimi

Festo is back πŸ˜‚πŸ”₯
Anaendelea alipoishia ...
Moto unaanza upya, huku Festo kule Diana

Stella nae anakuja Kasi πŸ˜‚, JC atapasha kiporo sio muda

Ila Tesha..bonge la midfielder kisheti πŸ˜‚πŸ”₯
Mwamba sana. Amenikumbusha jamaa yangu wa karibu sana alitokea kumpenda shemeji yangu mwenye figure ya hatari toka Rwanda ila akawa anaogopa kumface.

Basi baada ya kuona jamaa anaogopa na kuseka kila akimuona binti nikaomba anipe simu yake nimsaidie kuanza halafu yeye ataendelea baada mimi kumuanzishia hatua ya kwanza. Akanipa simu nikamtumia ujumbe wa mahaba shem ambaye ni mdogo wa mke wa bro kisha nikaufuta. Nikamwambia jamaa asubiri majibu atambae naye. Majibu kurudishwa wakaishia kuwa wapenzi. Mpaka leo jamaa hajui niliandika nini na sijawahi mwambia. Akiniuliza huwa namwambia endelea kula raha.
 
MIMI NA MIMI 3

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Siri, Tamaa, Hila, Usaliti, Ukatili, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

SEHEMU YA NNE

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…



Siku mbili zikapita. Ndiyo. Siku mbili, baada ya kuwa nimekutana na Miryam kule dukani kwake na kujaribu kufanya mazungumzo pamoja naye. Kwa kunitolea nje siku hiyo akisema kwamba tungeongea kesho yake, ni mpaka sasa hakuwa amenitafuta, wala mimi nilipomtafuta hakunijibu. Kilikuwa kitu chenye kukwaza sana. Sikufikiria ningewahi kumwona Miryam namna hii, lakini alianza kuwa mwongo. Tesha alikuwa ameniambia kwamba hiyo juzi dada yake alimwonyesha ukali kwa kitendo chake cha kunitumia ujumbe kupitia simu ya bibie, na kiukweli kijana alikuwa akijaribu tu kusaidia ila ndiyo ikamkasirisha dada yake. Haikuwa sahihi kwa Tesha kufanya vile, lakini tatizo hasa halikuwa hilo. Shida ilikuwa ni kwa nini Miryam hakutaka kuzungumza nami.

Kwa njia ya simu, nilikuwa nimewasiliana na Bi Zawadi, salamu tu iliyopelekea kuzungumzia ishu iliyozushwa na Bi Jamila na mama yangu, na kwa upande wake pia aliona ni jambo sahihi kwetu wote kukutana ili tuliongelee kwa kina na kujua tunasonga vipi mbele. Lakini aliona ni namna gani jambo hilo lilileta hali ya mgawanyo ndani ya familia yao, akiwa ameniambia jinsi ambavyo Miryam hakuwa tena namna alivyokuwa mwanzo, Bi Jamila akiwa na huzuni muda mwingi, na Mariam akianza kuwa wa kivyake mno. Tesha na Ankia kutokuwepo nyumbani muda mrefu sasa kulianza kumfanya Bi Zawadi ajihisi upweke mwingi, naye alitamani kweli kuniona tena. Yeye pia alikuwa na imani kwamba ningefanya jambo fulani ili kuleta hali nzuri kwa familia zetu sote, na mimi nikamtia tu moyo kwa kusema ningefanya jambo fulani.

Ila ukweli ni kuwa nilighafilika sana. Angalau ubize na kazi ulikuwa kichocheo kizuri cha kupisha muda lakini bado haya mambo yaliniharibia sana mudi. Mama yangu pia bado hakuwa kwenye hisia nzuri sana hata tu kumtafuta Miryam yeye mwenyewe, na hata Jasmine mambo kwake yalikuwa mengi mno kujaribu kunisaidia kwa hilo. Sasa ukiangalia na jinsi Miryam alivyokuwa akiweka mgomo usioeleweka sababu, ilinipa wakati mgumu. Kwa hiyo hapa muda ungeendelea tu kupita ameninyamazia, sivyo? Halafu nini, tungesahau na kusonga mbele? Nisingejua kwa kweli. Ila, angalau kwa siku ya leo jambo fulani zuri lingekuja upande wangu.

Ikiwa ni siku ya Ijumaa, rafiki yangu Simba ndiyo alikuwa anatokea Mwanza kuja jijini, na angefika usiku. Alikuja na basi, na kwa kuwa angefika na kuja kwangu moja kwa moja ingebidi kuwe na mtu wa kumpokea; ingawa hakuwa mgeni huku. Sema kilipita kitambo kirefu kutokea mara ya mwisho amekuja huko Bamaga, hivyo mwongozo angeuhitaji ili kufika kwangu. Kwa sababu ya kuwa kazini, nikamwomba Salumu anisaidie kwa hilo, na kweli rafiki yangu akawa ameingia jijini kwenye mida ya saa nane usiku. Basi lilipepea kweli, ila ingebidi ujenzi wa treni ya mwendokasi uifikie Mwanza pia ili mambo yawe rahisi zaidi.

Nikiwa hospitalini mpaka mida hiyo nikawasiliana na Simba kumkaribisha, yeye akiwa na uchovu wa safari na hivyo kuhitaji mapumziko ili kukikucha mengi zaidi yafuate; kama vile kukutana. Nikamweka wazi kuhusu ratiba yangu, kwamba kukikucha Jumamosi ningeendelea kuwa kazini hadi mida ya jioni ambapo ndiyo ningepata nafasi ya kupumzika mpaka Jumatatu tena, kwa hiyo bila shaka tungeonana kesho. Kama inavyokuwa, ratiba za matabibu hubana kiasi kwa wiki nzima mpaka tunapopewa siku moja ama mbili za kupumzika, na mimi kwangu hiyo ingekuwa Jumapili hasa. Hata sikuwa nimepata muda wa kwenda kumwona Evelyn tena na kuishia kuwasiliana naye kupitia video call, hivyo na yeye alikuwa orodhani kwa watu ambao ningehitajika kuwaona wakati wa kupumzika. Kwa sasa nikaingia tena kulala kwa masaa machache kuisogeza siku ili ikuche.


β˜…β˜…β˜…


Nimekuja kushtuka kwenye mida ya saa kumi na mbili, kwa kengele ya simu yangu, na kausingizi kakinivuta bado. Nikiwa na chumba binafsi hospitalini hapo, usingizi mara nyingi ulikuwa wa kuonja sana, kwa madaktari wengi, lakini hatukuwa na jinsi maana ndiyo uliokuwa wajibu kuwahi kazi. Upesi nikajisafisha na kuvaa vizuri, kazini nikaingia. Kama ilivyo ada, kuwasaidia watu waliohitaji msaada likawa jukumu langu kama nilivyolipenda, dakika na masaa yakipita nikiwa na ubize mwingi hadi kuusahau usingizi wa asubuhi. Nilipopata nafasi za kupumzika na kula ndiyo ningewasiliana na wapendwa wangu; Evelyn, Ankia, Jasmine, Simba, Tesha, na marafiki wengine pia.

Kuna watu niliofahamiana nao kwa kitambo kirefu ambao walitaka sana tuonane hapo jijini, washkaji kwa mademu, ila ndiyo nikawa nawapiga chini kwa kusingizia ratiba za kazi. Sikutaka tu yaani. Kulikuwa na sherehe ya kuzaliwa ya mmoja wa madaktari wenzangu hapo hospitali pia siku chache zijazo, na leo akanikumbusha kutoa mchango na kutokosekana kwenye hafla hiyo ambayo ilipangwa kufanyikia ukumbini. Angalau hiyo ndiyo mpango wa kuhudhuria nilikuwa nao. Kwa hiyo imekuja kufika mida ya saa kumi na moja ndiyo nikaondoka Muhimbili sasa, moja kwa moja mpaka kwangu.

Nikamkuta Simba, na mwamba alikuwa amebadilika kweli kutokea mara ya mwisho tulipoonana. Mwili wake uliongezeka, akionekana kuwa mbaba ingawa tulilingana kiumri, kimisuli na ukomavu akiwa vizuri nadhani shauri ya mazoezi ya huko jeshini, nami nilifurahia sana uwepo wake hapo. Tukasalimiana vizuri, nikionyesha uchovu kiasi wa kazi na hivyo akanishauri nikajimwagie halafu nirudi kukaa pamoja naye tule mastori. Ikawa hivyo. Baada ya kujimwagia na kuvaa nguo nyepesi, nikakaa naye sebuleni pale, akiwa amevuta chupa ya wine pamoja na glasi mbili ili tushiriki pamoja, na maongezi yakaanza. Akiwa ni mwanaume mchangamfu, Simba alinisimulia mengi ya huko Mwanza yenye kufurahishana, kuhusu mwanamke wake, akikumbushia mengi tuliyofanya pamoja, na alitarajia ningempa shauku ya hali kama ya kwake ila akatambua sikuwa sawa kihivyo.

Mwishowe, baada ya sote kushusha kileo cha kadiri, Simba akaniuliza, "Vipi mambo yako bro?"

"Safi tu. Kama unavyoniona, kazi ni kazi tu... maisha yanaenda," nikamwambia.

"Mbona kama vile unagwaya mood? Ama ni kuchoka tu?" akauliza.

Nikaangalia tu chini na kushusha pumzi.

"Niliwasiliana na mama juzi juzi akaniambia," Simba akasema hivyo.

Nikamwangalia, nikiwa nimeelewa kuwa alimaanisha mama yangu, nami nikauliza, "Kuhusu?"

"Mtoto wako. Aliniambia umeshaanza kuwa baby daddy sa'hivi..."

Nikatabasamu kiasi na kusema, "Yeah. Nimeanza-anza."

"Hapo pamekaaje?"

"Fresh. Bomba sana, yaani... napata raha nyingi kuwa baba kwa huyo mtoto."

"Umeona? Raha. Me nilikuwaga nakwambia, achana na ujinga wa Stella, yule ni mtoto wako. Sema tu we' si bado ulikuwa unajiona kama litoto, eti hutaki kulea!" akatania.

"Ahahah... acha ujinga..."

"Hahahah... kwa hiyo ukampa Stella vyake, akatulia?"

"Hamna, ye' ndiyo alikuwa ananitafuta. Kanisaka kweli mpaka nikalegeza..."

"Wewe..."

"Eeh, mwanzoni nikawa nakwepa ila sa'hivi nimemheshimu kwa jitihada alizoweka kunikutanisha na mwanangu. Amenifumbua macho," nikamwambia.

"Kwani nani alikuwa ameyafunga bado? Aisha?" akauliza.

"Agh..." nikafanya hivyo na kunywa kidogo.

"Ahahahah... usinambie mpaka leo unalialia kisa Aisha..."

"Hiyo meli imeshazama na kutoweka muda sana ndugu yangu," nikamwambia.

"Au siyo? Hata ukikutana naye hautajing'ata?"

"Aa wapi..."

"Hahahah... haya bana. Li-Aisha limeolewa sa'hivi, nasikia liko huko wanapaita Cape Town," akaniambia.

"Kumbe? Hapa hapa Dar?"

"Mmm. Halafu la moto sasa hivi, limekuwa na shepu, hilo pedeshee linakula hapo linagharamika kinoma..."

"Agh, hamna lolote..."

"Ahahahah... nakumbukia alivyokuwaga anakung'ang'ania kila mlikoenda bro, yaani Aisha! Mpaka alipiga mtu na chupa kisa JC..."

Nikacheka kidogo.

"Stella alizingua sana..."

"Ah wee, usiseme hivyo. Mama wa mtoto wangu huyo," nikamwambia.

"Fala nini, unajikuta baba bora mfuata tuzo eh? Au mmeshaanza kulana kizembe?"

"Acha mambo yako wewe, nimetulia sana sa'hivi," nikasema hivyo.

"Aaakh, labda umdanganye asiyekujua..."

Nikatabasamu tu na kuangalia simu yangu. Sikukuta ujumbe wala nini kutoka kwa Miryam, hapo nikiwa nimemtumia sms karibia kumi leo. Ilikuwa ni kama vile nachat peke yangu yaani kwa upande wake wa sms, na Simba akaona hilo.

"Nani huyo?" akauliza.

Nikamwangalia.

"Ndiyo anayekutoa misongo, au anakupa?" Simba akauliza tena.

Nikaiweka tu simu pembeni na kunywa kidogo. Akiwa ameona kwamba amani ilinipungua, Simba akawa makini zaidi na kuomba nimwambie kilichoonekana kunikosesha raha, maana hakunizoea hivi. Ni kweli, hakunizoea hivi, na mimi ilikuwa imefikia hatua ambayo nilihitaji kuzungumza yaliyonisumbua moyoni pamoja na mtu wangu wa karibu. Kwa hiyo tukaweka utani pembeni kwanza, na A mpaka Z iliyomhusu Miryam nikaanza kuielezea kwa rafiki yangu. Nikamsimulia kila kitu, kuanzia namna ambavyo nilisota sana kulipata penzi la Miryam mpaka hiyo juzi tulipopigwa na jambo zito lililoutia uhusiano wetu dosari. Mpaka nilipoweka kituo kwenye kuongea Simba hakusema chochote yaani, alinisikiliza kwa makini na kwa utambuzi kuwa niliumia sana moyoni.

Simba akaishia kupiga ulimi na kusema, "Aisee…"

"Ndiyo hivyo," nikamwambia huku nikihisi huzuni.

"Kwa hiyo ni kwamba... huyo mama yake alikuwa anajua muda wote kwamba nyie mna undugu?" akauliza.

"Hamna. Alihisi, yaani... kabla sijaanza mahusiano na Mimi, alimwonaga mama yangu kwenye picha lakini hakuwaza kwamba me ni mtoto wa mwanaye, huyo Tino... kwa hiyo alipokuja kujua nina uhusiano na Miryam ndiyo akapatwa na wasiwasi. Ila ilikuwa tu ule wasiwasi kum-face mama, sababu ya yale waliyomfanyia kipindi hicho mpaka kuwatenganisha yeye na baba yetu mzazi..." nikaeleza.

"Ahaa..."

"Yeah. Mama ndiyo alipasua ukweli alipogundua Miryam mtoto wa Tino, kwa jinsi inavyoonekana," nikasema.

"Usikute siyo wake," Simba akasema.

"Usikute ni wake. Lakini kwa vyovyote vile, bado hilo haliondoi upendo wangu kwa huyu mwanamke Simba," nikaongea kwa hisia.

"Mh! Huyo Miryam lazima awe mzuri sana, mpaka akugeuze we' playboy uwe wa mmoja tu!" akasema hivyo.

Nikatabasamu kiasi na kusema, "Me siyo playboy bwana. Na haupingwi. Ni mwanamke mzuri sana Miryam. Siyo sura tu..."

"Bali shepu na tabia," Simba akatania.

Nikatabasamu kidogo na kutikisa kichwa.

"Ila ndo' ashakuwa dada yako sasa," akasema.

"Na tena hata na hapo hatuna uhakika sana, ila uwezekano ni mkubwa mno. Yeye... na wadogo zake, ni ndugu zangu. Hiyo nzito sana bro," nikaongea kwa hisia.

"Na kufikiri hadi ulikuwa kwenye mikakati ya kuoa, dah! Kwa kweli ni nzito," akasema hivyo.

Nikabaki kimya nikimtafakari Miryam tu.

"Halafu kama sikosei tayari ulikuwa umeshakula," Simba akasema hivyo.

Nikamkata jicho la kuhukumu.

Akatabasamu kiasi na kusema, "Esyuksi me, lakini najua unajua najua. Ila maana yangu ni kwamba, kama mmechangia damu moja halafu ikatokea labda ameshika mimba, si inaweza kuwa problem?"

Nikaangalia pembeni kwa ufikirio. Sikuwa nimewaza hilo hata kidogo.

"Azae mtoto, halafu atakuita baba na mjomba, au baba na baba mdogo?" Simba akaendeleza masihara yake.

"Hapana, sidhani kama inaweza fika huko. Alikuwa anatumia dawa, mfumo wa kizazi chake haukuwa imara sana," nikamweleza.

"Sawa. Pole lakini kaka. Majanga ndo' kama ya Snura hayo," akasema.

"Asante."

"Na bado anakukwepa tu, hataki mwongelee hilo suala?" akauliza.

"Eeh. Najaribu kutafuta closure, lakini haipatikani maana ananisukumia mbali. Simba... nampenda sana Miryam. Yaani, akili yangu inajua kabisa kwamba hilo suala la undugu ni msingi wa kutuachanisha bila kupinga, lakini moyo wangu bado hautaki. Yaani nataka iwezekane tu kwamba yeye na mimi hatujachangia damu, sitajali mengine. Namhitaji sana," nikaongea kwa hisia.

"Na me naona. Unaogopa utarudi kuwa playboy tena akiondoka maishani mwako," akaniambia hivyo.

"Ah, tsk... naogopa mengi tu," nikasema hivyo na kuvuta kinywaji.

"Hafanyi vizuri kukwepa maongezi. Inabidi ufanye kitu hapo. Umeshaongea na ndugu zake? Labda na mama ameshajaribu kuwatafuta mkaongea kwa pamoja?"

Nikatikisa kichwa kukataa.

"Jaribu kuwaleta wote kwa pamoja mzungumze. Mama yako akimwita Miryam, labda..."

"Hapana Simba, mama pia bado yupo conflicted sana na hii hali. I mean, imagine kama tayari ningekuwa nimemwoa Miryam halafu tukaja kugundua haya baadaye, ingekuwaje? Wote tuko sehemu mbaya kwa sasa, ila hili ni la kukaa mimi na Miryam kuongelea na kujua tunafanyaje... hawa wengine wafate. Sasa yeye anakwepa..." nikaongea kwa mkazo.

"Mbembeleze tu..."

"Ah, ungejua! Nimemwaga sera kwa huyo mwanamke!"

"Wewe..."

"Ahiii... nikwambie mimi tu, usisikie kwa mwingine. Yaani tangu nimeanza kumtongoza, mpaka leo, nambembeleza haswa. Nampenda mno mpaka nimejua kubembeleza..."

Simba akacheka kidogo.

"Lakini sa'hivi mpaka nahisi kuchoka. Sijamchoka, yaani..."

"Anatakiwa ajue siyo yeye tu ndiyo ameumia, na wewe pia. Akikukwepa inakupa wakati mgumu, naelewa. Hata me ningechoka," Simba akasema hivyo.

Nikapiga ulimi kwa kusikitika.

"Sikia, najua unampenda, lakini sometimes kaka unajua huwa hatupati kila kitu tunacho...."

"No, no, Simba... yaani sitaki kukubali hilo..."

"Ndiyo maisha JC..."

"Kwa Miryam hapana. Nampenda sana, sidhani kama nitaweza kumwachia... ikiwa hicho ndo' unachojaribu kuniambia," nikaongea kwa hisia.

"Mbona Aisha uliweza?" akauliza.

"Miryam siyo Aisha, hiyo ni story nyingine," nikasema.

"Time. Mnahitaji muda tu. Hata kama useme huwezi kumwachia, halafu iwe ni kweli mme-share damu, JC... utafanyaje? Utafosi?"

"Sijui tu, lakini...."

"Hayo mambo ya wakina Kaini siku hizi hayapo, utajitafutia balaa ukijaribu kulazimisha vitu ambavyo vimeshindikana. Kuwa open minded ili unachokikazania kisipokwenda kwa matarajio yako, ujiokoe kutoumia zaidi bwege wewe," akanishauri namna hiyo.

"Ah, na we' naye unajiona simba kumbe swala tu," nikamwambia hivyo na kunywa kileo kidogo.

Akacheka kidogo na kunywa pia, naye akaniambia, "Kwenye ukweli lazima nikwambie kaka. Maisha siyo fair, halafu we' ya kwako yamejaa maigizo kinoma. Sikia..."

Simba akaendeleza ushauri-ushauri wake kwa lengo la kunisaidia nipate ahueni ya kihisia, na maongezi mepesi ya kirafiki yakaendelea kuhusiana na mambo hayo tuliyoongelea na mengine zaidi. Tukiwa hapo kuzungumzia jambo hili kukanifanya nipandwe na hisia za kukosa subira tena, yaani presha ya hali nzima iliyozungukia suala hilo ikanivaa kwa kasi sana, nami nikanyanyuka na kuweka glasi mezani.

Simba akauliza, "Vipi?"

Nikaangalia saa mkononi, ikiwa imeshaingia saa mbili usiku, nami nikamwambia, "Nakuja. Naenda hapo nje mara moja."

Akiwa hajui nilichowaza, akasema, "Poa. Rudi na chupa ingine basi, humu zimeisha."

Nikasema tu sawa, nami nikatoka ndani hapo na kwenda garini. Yaani nikalifata gari hapo huku wenge la mbali la pombe likiteka kichwa changu, lakini sikujali. Uvumilivu ulikuwa umenishinda aisee, nikiona huu kuwa kama ujinga sasa. Hata kama ningekaa na kuwaza na kuwazua vipi, hakuna lolote ambalo lingebadili ukweli kwamba nilimpenda yule mwanamke, na najua yeye pia alinipenda. Kusema nimwache tu aendelee kuninyamazia hakungerekebisha hali hii kwa vyovyote.

Nilikuwa tayari kuweka mengine kando ili niendelee kuwa na uhusiano pamoja naye, kabisa, kwa sababu ni vingi sana tulikuwa tumeshafanya kiasi kwamba hata kama damu zetu zingekuwa zimepita kwenye njia moja, isingewezekana kufuta. Utayari wa kuendeleza mahusiano pamoja na Miryam nilikuwa nao kwa asilimia zote haijalishi nani angesema nini, na nilitaka kujua kwa upande wake alihisije kuhusiana na hilo. Kwa kuwa hakutaka kujibu yoyote kati ya simu zangu na jumbe nilizomtumia, sasa ingekuwa ni kumfata huko huko ili nimlazimu kuongea. Washa gari, kanyaga mafuta, safari moja tu ndiyo ingefuata; Mbagala.

Ni kama maongezi niliyofanya na rafiki yangu yaliibua jini ndani yangu, alikuwa sahihi kabisa. Katika yote aliyosema, alikuwa sahihi kabisa kuniambia kwamba Miryam hakufanya vizuri kunikwepa namna hii, na ningetakiwa kufanya kitu. Alichosema kuhusu mimi kutakiwa kuwa tayari kumwacha Miryam bado nilipingana nacho, ila kuwa tu na akili iliyofunguka kuelekea tatizo hili kiujumla ilikuwa muhimu. Kwa kiwango kikubwa lilikuwa tatizo, lakini upande mwingine lilikuwa na uzuri wake kwa sababu hii ilimaanisha Tesha, Mariam, na wengine wa familia hiyo waliongezeka umuhimu zaidi kwangu kuliko hata awali. Ningepaswa kuitikia hilo kwa uchanya, kisha ingenibidi nitafute njia ya kumfanya Miryam aache kujiweka mbali na mimi kwa kudhani alifanya kilicho sahihi zaidi. Kuongea tulihitaji kuongea, na sasa hivi ingekuwa kwa lazima.

β˜…β˜…

Mwendo wa saa zima ukanifikisha hayo maeneo, ikiwa imeshaingia mida ya saa tatu usiku, na nilipofikisha gari langu eneo la nyumba ya Ankia nikakuta kuna gari lingine limeegeshwa usawa wa geti lake. Mwanzoni sikuliangalia vizuri na kudhani huenda kulikuwa na mgeni ama nini, na sikujali. Mimi nikalisogeza langu mpaka usawa wa nyumba ya Miryam na kushuka, na ndiyo nilipolitazama gari hilo lingine nikalitambua. Lilikuwa ndiyo lile lile aina ya Range Rover Discovery la kifahari, ambalo nikakumbuka nililiona likimshusha Miryam ile majuzi pale Mzinga. Hee!

Kuliona kwa ukaribu na nyumba yake sasa kulimaanisha kwamba mwenye nalo alikuwepo huko ndani, nami nikakaza meno tu na kwenda getini kujaribu kufungua, lakini mlango mdogo wa geti ukagoma kufunguka. Nilishikwa na hali fulani ya kukosa subira kiasi kwamba nikaanza kugonga geti kwa nguvu na mara nyingi sana, kileo kichwani kikinipa msukumo huo, na nikiona watu waliokuwepo nje waliponitazama kwa umakini, lakini sikuwajali. Nusu dakika hivi kupita na mlango huo ukafunguliwa kwa ndani, mbele yangu akisimama Tesha huku akinitazama kimaswali, nami nikaingia upesi huku nikimsukuma kiasi kusudi anipishe.

"JC?"

Tesha akasema hivyo, lakini mimi nikasogea mbele zaidi na kuona gari la Miryam likiwa pembezoni hapo, na kwamba Mariam alikuwa amesimama pale varandani pia, akiniangalia kiumakini. Hapo hapo Shadya naye akatokea pale ndani kwao, na mimi nikiwa bado napiga hatua, Tesha akanifikia na kuushika mkono wangu.

"Oya, subiri..." Tesha akanisimamisha.

Nikamgeukia na kusema, "Nimechoka kusubiri. Najua yupo ndani, naenda kuongea naye."

Shadya akawa amefika karibu zaidi na mimi bila kuvaa viatu, naye akasema kwa sauti ya chini, "We' JC, mbona fujo?"

"Nataka kuongea na Miryam," nikamwambia.

Tesha akasema, "Kaka, huu siyo muda mzuri, maana...."

Nikautoa mkono wake kwangu kwa nguvu na kumpita Shadya ili nielekee ndani, huku wawili hawa wakinifuata na Mariam akiwa amenikazia macho tu, na mlangoni akatoka Bi Zawadi pia, kitu kilichofanya nikatishe hatua zangu.

Akiwa ananitazama kwa hisia za kujali, Bi Zawadi akasema, "JC... we' ndiyo unagonga geti kwa nguvu hivyo? Utatutia presha."

"Ameingia kwa hasira kweli, najaribu kumsemesha, hasikilizi," Shadya akamwambia hivyo.

"Nataka kumwona Miryam," nikawaambia.

"JC... umelewa?" Bi Zawadi akaniuliza.

"Hapana," nikamjibu.

"JC, nimekwambia huu siyo muda mzuri. Twende nje au hapo kwa Ankia nikwambie kitu bro," Tesha akasema.

Walikuwa wanajitahidi kuongea kwa sauti isiyo ya juu sana, nami nikapata picha kwamba kuna kitu walificha, lakini sikukitilia maanani sana, sababu akili yote ilikuwa kwa Miryam tu.

Nikamwambia Tesha, "Tutaongea baadaye, nimekuja kuonana na Miryam. Kama amewapanga mmfiche ili tusiongee, basi mjue hilo limebuma. Leo siondoki hapa mpaka nionane naye."

Shadya akasema, "Siyo hivyo JC, sasa hivi kuna mgeni, ndo'...."

"Mgeni mwenye Range eh? Sijali," nikamkatisha.

"Baba, sikiliza. Tunajua mna mengi ya kuongea, lakini nakuomba utulie kwanza. Mtaongea tu," Bi Zawadi akasema hivyo.

"Kaka..." Tesha akaniita.

"Kwa nini ananikwepa? Wiki nzima namtafuta ananikaushia, hivi.... ah... Miryam!" nikaongea hivyo na kuita kwa sauti ya juu.

"He! JC, hebu acha sifa. Unaanza ku...."

"MIRYAAM!!" nikamkatisha Shadya na kuita kwa sauti ya juu zaidi.

"Oya, usiwe kama hujasoma basi. Mambo gani haya kuita matamasha?" Tesha akaniambia.

"Miryam acha utoto, naomba uje nje haraka. Siondoki hapa mpaka tuongee. Nitavunja mlango hata ukiufunga huko ndani, unanielewa?" nikanena kana kwamba nimerukwa na akili.

"Eh, makubwa!" Shadya akasema hivyo.

"JC jamani..." Bi Zawadi akaniita kwa upole.

Nikapiga ulimi kwa kusikitika na kumwambia Bi Zawadi, "Naingia ndani mama, naomba unipishe."

Tesha akanishika mkono kunizuia, nami nikautoa kwa nguvu na kumgeukia huku nikimnyooshea kidole kwa hasira. Shadya akasogea varandani karibu na Mariam, naye Tesha akabaki kunitazama kwa macho yenye mkazo. Nadhani sauti niliyotoa ilifanya ujirani uvutwe na yaliyokuwa yakiendelea hapa, nikiona watu wameanza kusogea kwenye kuta na hata geti likisikika kufunguka, lakini sikujali hayo zaidi ya kurudisha umakini wangu mlangoni ili nielekee ndani pale.

Bi Zawadi alikuwa amesimama kama vile kunizibia njia sijui, na sikutaka ionekane kwamba namvunjia heshima ila kama ni kwenda huko ndani nilikuwa ninaenda, haikujalisha chochote tena. Lakini kabla sijapiga hiyo hatua, hatimaye bibie akatoka na kuja hapo nje. Bibie Miryam. Taratibu tu. Mapigo yangu ya moyo yalishtua kana kwamba sikuwa nimemwona kwa muda mrefu kweli, na alikuja mbele yangu na kusimama huku akinitazama kwa njia ya kawaida kabisa, ila niliweza kuiona huzuni ilivyokuwa imejaa usoni kwake.

Kutokea nyuma yangu, nikasikia sauti ya Ankia akiniita, "JC..." nami nikageuka.

Hapo nikamwona Ankia kweli, akiwa na mwonekano kawaida wa nyumbani, pamoja na yule dada yake marehemu Joy, Adelina. Inaonekana walikuwa pamoja pale kwake, na endapo kama hii ingekuwa ni pindi nzuri sana, basi ningejawa na furaha kuwaona wanawake hawa kwa sababu walikuwa marafiki wazuri kwangu. Hasa Adelina ambaye nilikuwa nimemweka kando mno siku hizi. Lakini kutokana na haya yote yaliyoendelea nikashindwa kuonyesha chembe yoyote ya furaha na kumtazama Miryam kwa mara nyingine. Sasa alisimama mbele yake Bi Zawadi, akiniangalia kwa utulivu makini tu, na pale mlangoni akatoka Bi Jamila pia kufuatiwa na mtu mwingine aliyefanya mapigo yangu ya moyo yazidi kudunda kwa nguvu kwa sababu ya kutotarajia kumwona hapo muda huo. Nilimtazama kwa umakini nikiwa nimeshangaa sana, kwa sababu ilikuwa ni Festo mwenyewe!





β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

ITAENDELEA

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…


Whatsapp +255 678 017 280
 
MIMI NA MIMI 3

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Siri, Tamaa, Hila, Usaliti, Ukatili, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

SEHEMU YA NNE

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…



Siku mbili zikapita. Ndiyo. Siku mbili, baada ya kuwa nimekutana na Miryam kule dukani kwake na kujaribu kufanya mazungumzo pamoja naye. Kwa kunitolea nje siku hiyo akisema kwamba tungeongea kesho yake, ni mpaka sasa hakuwa amenitafuta, wala mimi nilipomtafuta hakunijibu. Kilikuwa kitu chenye kukwaza sana. Sikufikiria ningewahi kumwona Miryam namna hii, lakini alianza kuwa mwongo. Tesha alikuwa ameniambia kwamba hiyo juzi dada yake alimwonyesha ukali kwa kitendo chake cha kunitumia ujumbe kupitia simu ya bibie, na kiukweli kijana alikuwa akijaribu tu kusaidia ila ndiyo ikamkasirisha dada yake. Haikuwa sahihi kwa Tesha kufanya vile, lakini tatizo hasa halikuwa hilo. Shida ilikuwa ni kwa nini Miryam hakutaka kuzungumza nami.

Kwa njia ya simu, nilikuwa nimewasiliana na Bi Zawadi, salamu tu iliyopelekea kuzungumzia ishu iliyozushwa na Bi Jamila na mama yangu, na kwa upande wake pia aliona ni jambo sahihi kwetu wote kukutana ili tuliongelee kwa kina na kujua tunasonga vipi mbele. Lakini aliona ni namna gani jambo hilo lilileta hali ya mgawanyo ndani ya familia yao, akiwa ameniambia jinsi ambavyo Miryam hakuwa tena namna alivyokuwa mwanzo, Bi Jamila akiwa na huzuni muda mwingi, na Mariam akianza kuwa wa kivyake mno. Tesha na Ankia kutokuwepo nyumbani muda mrefu sasa kulianza kumfanya Bi Zawadi ajihisi upweke mwingi, naye alitamani kweli kuniona tena. Yeye pia alikuwa na imani kwamba ningefanya jambo fulani ili kuleta hali nzuri kwa familia zetu sote, na mimi nikamtia tu moyo kwa kusema ningefanya jambo fulani.

Ila ukweli ni kuwa nilighafilika sana. Angalau ubize na kazi ulikuwa kichocheo kizuri cha kupisha muda lakini bado haya mambo yaliniharibia sana mudi. Mama yangu pia bado hakuwa kwenye hisia nzuri sana hata tu kumtafuta Miryam yeye mwenyewe, na hata Jasmine mambo kwake yalikuwa mengi mno kujaribu kunisaidia kwa hilo. Sasa ukiangalia na jinsi Miryam alivyokuwa akiweka mgomo usioeleweka sababu, ilinipa wakati mgumu. Kwa hiyo hapa muda ungeendelea tu kupita ameninyamazia, sivyo? Halafu nini, tungesahau na kusonga mbele? Nisingejua kwa kweli. Ila, angalau kwa siku ya leo jambo fulani zuri lingekuja upande wangu.

Ikiwa ni siku ya Ijumaa, rafiki yangu Simba ndiyo alikuwa anatokea Mwanza kuja jijini, na angefika usiku. Alikuja na basi, na kwa kuwa angefika na kuja kwangu moja kwa moja ingebidi kuwe na mtu wa kumpokea; ingawa hakuwa mgeni huku. Sema kilipita kitambo kirefu kutokea mara ya mwisho amekuja huko Bamaga, hivyo mwongozo angeuhitaji ili kufika kwangu. Kwa sababu ya kuwa kazini, nikamwomba Salumu anisaidie kwa hilo, na kweli rafiki yangu akawa ameingia jijini kwenye mida ya saa nane usiku. Basi lilipepea kweli, ila ingebidi ujenzi wa treni ya mwendokasi uifikie Mwanza pia ili mambo yawe rahisi zaidi.

Nikiwa hospitalini mpaka mida hiyo nikawasiliana na Simba kumkaribisha, yeye akiwa na uchovu wa safari na hivyo kuhitaji mapumziko ili kukikucha mengi zaidi yafuate; kama vile kukutana. Nikamweka wazi kuhusu ratiba yangu, kwamba kukikucha Jumamosi ningeendelea kuwa kazini hadi mida ya jioni ambapo ndiyo ningepata nafasi ya kupumzika mpaka Jumatatu tena, kwa hiyo bila shaka tungeonana kesho. Kama inavyokuwa, ratiba za matabibu hubana kiasi kwa wiki nzima mpaka tunapopewa siku moja ama mbili za kupumzika, na mimi kwangu hiyo ingekuwa Jumapili hasa. Hata sikuwa nimepata muda wa kwenda kumwona Evelyn tena na kuishia kuwasiliana naye kupitia video call, hivyo na yeye alikuwa orodhani kwa watu ambao ningehitajika kuwaona wakati wa kupumzika. Kwa sasa nikaingia tena kulala kwa masaa machache kuisogeza siku ili ikuche.


β˜…β˜…β˜…


Nimekuja kushtuka kwenye mida ya saa kumi na mbili, kwa kengele ya simu yangu, na kausingizi kakinivuta bado. Nikiwa na chumba binafsi hospitalini hapo, usingizi mara nyingi ulikuwa wa kuonja sana, kwa madaktari wengi, lakini hatukuwa na jinsi maana ndiyo uliokuwa wajibu kuwahi kazi. Upesi nikajisafisha na kuvaa vizuri, kazini nikaingia. Kama ilivyo ada, kuwasaidia watu waliohitaji msaada likawa jukumu langu kama nilivyolipenda, dakika na masaa yakipita nikiwa na ubize mwingi hadi kuusahau usingizi wa asubuhi. Nilipopata nafasi za kupumzika na kula ndiyo ningewasiliana na wapendwa wangu; Evelyn, Ankia, Jasmine, Simba, Tesha, na marafiki wengine pia.

Kuna watu niliofahamiana nao kwa kitambo kirefu ambao walitaka sana tuonane hapo jijini, washkaji kwa mademu, ila ndiyo nikawa nawapiga chini kwa kusingizia ratiba za kazi. Sikutaka tu yaani. Kulikuwa na sherehe ya kuzaliwa ya mmoja wa madaktari wenzangu hapo hospitali pia siku chache zijazo, na leo akanikumbusha kutoa mchango na kutokosekana kwenye hafla hiyo ambayo ilipangwa kufanyikia ukumbini. Angalau hiyo ndiyo mpango wa kuhudhuria nilikuwa nao. Kwa hiyo imekuja kufika mida ya saa kumi na moja ndiyo nikaondoka Muhimbili sasa, moja kwa moja mpaka kwangu.

Nikamkuta Simba, na mwamba alikuwa amebadilika kweli kutokea mara ya mwisho tulipoonana. Mwili wake uliongezeka, akionekana kuwa mbaba ingawa tulilingana kiumri, kimisuli na ukomavu akiwa vizuri nadhani shauri ya mazoezi ya huko jeshini, nami nilifurahia sana uwepo wake hapo. Tukasalimiana vizuri, nikionyesha uchovu kiasi wa kazi na hivyo akanishauri nikajimwagie halafu nirudi kukaa pamoja naye tule mastori. Ikawa hivyo. Baada ya kujimwagia na kuvaa nguo nyepesi, nikakaa naye sebuleni pale, akiwa amevuta chupa ya wine pamoja na glasi mbili ili tushiriki pamoja, na maongezi yakaanza. Akiwa ni mwanaume mchangamfu, Simba alinisimulia mengi ya huko Mwanza yenye kufurahishana, kuhusu mwanamke wake, akikumbushia mengi tuliyofanya pamoja, na alitarajia ningempa shauku ya hali kama ya kwake ila akatambua sikuwa sawa kihivyo.

Mwishowe, baada ya sote kushusha kileo cha kadiri, Simba akaniuliza, "Vipi mambo yako bro?"

"Safi tu. Kama unavyoniona, kazi ni kazi tu... maisha yanaenda," nikamwambia.

"Mbona kama vile unagwaya mood? Ama ni kuchoka tu?" akauliza.

Nikaangalia tu chini na kushusha pumzi.

"Niliwasiliana na mama juzi juzi akaniambia," Simba akasema hivyo.

Nikamwangalia, nikiwa nimeelewa kuwa alimaanisha mama yangu, nami nikauliza, "Kuhusu?"

"Mtoto wako. Aliniambia umeshaanza kuwa baby daddy sa'hivi..."

Nikatabasamu kiasi na kusema, "Yeah. Nimeanza-anza."

"Hapo pamekaaje?"

"Fresh. Bomba sana, yaani... napata raha nyingi kuwa baba kwa huyo mtoto."

"Umeona? Raha. Me nilikuwaga nakwambia, achana na ujinga wa Stella, yule ni mtoto wako. Sema tu we' si bado ulikuwa unajiona kama litoto, eti hutaki kulea!" akatania.

"Ahahah... acha ujinga..."

"Hahahah... kwa hiyo ukampa Stella vyake, akatulia?"

"Hamna, ye' ndiyo alikuwa ananitafuta. Kanisaka kweli mpaka nikalegeza..."

"Wewe..."

"Eeh, mwanzoni nikawa nakwepa ila sa'hivi nimemheshimu kwa jitihada alizoweka kunikutanisha na mwanangu. Amenifumbua macho," nikamwambia.

"Kwani nani alikuwa ameyafunga bado? Aisha?" akauliza.

"Agh..." nikafanya hivyo na kunywa kidogo.

"Ahahahah... usinambie mpaka leo unalialia kisa Aisha..."

"Hiyo meli imeshazama na kutoweka muda sana ndugu yangu," nikamwambia.

"Au siyo? Hata ukikutana naye hautajing'ata?"

"Aa wapi..."

"Hahahah... haya bana. Li-Aisha limeolewa sa'hivi, nasikia liko huko wanapaita Cape Town," akaniambia.

"Kumbe? Hapa hapa Dar?"

"Mmm. Halafu la moto sasa hivi, limekuwa na shepu, hilo pedeshee linakula hapo linagharamika kinoma..."

"Agh, hamna lolote..."

"Ahahahah... nakumbukia alivyokuwaga anakung'ang'ania kila mlikoenda bro, yaani Aisha! Mpaka alipiga mtu na chupa kisa JC..."

Nikacheka kidogo.

"Stella alizingua sana..."

"Ah wee, usiseme hivyo. Mama wa mtoto wangu huyo," nikamwambia.

"Fala nini, unajikuta baba bora mfuata tuzo eh? Au mmeshaanza kulana kizembe?"

"Acha mambo yako wewe, nimetulia sana sa'hivi," nikasema hivyo.

"Aaakh, labda umdanganye asiyekujua..."

Nikatabasamu tu na kuangalia simu yangu. Sikukuta ujumbe wala nini kutoka kwa Miryam, hapo nikiwa nimemtumia sms karibia kumi leo. Ilikuwa ni kama vile nachat peke yangu yaani kwa upande wake wa sms, na Simba akaona hilo.

"Nani huyo?" akauliza.

Nikamwangalia.

"Ndiyo anayekutoa misongo, au anakupa?" Simba akauliza tena.

Nikaiweka tu simu pembeni na kunywa kidogo. Akiwa ameona kwamba amani ilinipungua, Simba akawa makini zaidi na kuomba nimwambie kilichoonekana kunikosesha raha, maana hakunizoea hivi. Ni kweli, hakunizoea hivi, na mimi ilikuwa imefikia hatua ambayo nilihitaji kuzungumza yaliyonisumbua moyoni pamoja na mtu wangu wa karibu. Kwa hiyo tukaweka utani pembeni kwanza, na A mpaka Z iliyomhusu Miryam nikaanza kuielezea kwa rafiki yangu. Nikamsimulia kila kitu, kuanzia namna ambavyo nilisota sana kulipata penzi la Miryam mpaka hiyo juzi tulipopigwa na jambo zito lililoutia uhusiano wetu dosari. Mpaka nilipoweka kituo kwenye kuongea Simba hakusema chochote yaani, alinisikiliza kwa makini na kwa utambuzi kuwa niliumia sana moyoni.

Simba akaishia kupiga ulimi na kusema, "Aisee…"

"Ndiyo hivyo," nikamwambia huku nikihisi huzuni.

"Kwa hiyo ni kwamba... huyo mama yake alikuwa anajua muda wote kwamba nyie mna undugu?" akauliza.

"Hamna. Alihisi, yaani... kabla sijaanza mahusiano na Mimi, alimwonaga mama yangu kwenye picha lakini hakuwaza kwamba me ni mtoto wa mwanaye, huyo Tino... kwa hiyo alipokuja kujua nina uhusiano na Miryam ndiyo akapatwa na wasiwasi. Ila ilikuwa tu ule wasiwasi kum-face mama, sababu ya yale waliyomfanyia kipindi hicho mpaka kuwatenganisha yeye na baba yetu mzazi..." nikaeleza.

"Ahaa..."

"Yeah. Mama ndiyo alipasua ukweli alipogundua Miryam mtoto wa Tino, kwa jinsi inavyoonekana," nikasema.

"Usikute siyo wake," Simba akasema.

"Usikute ni wake. Lakini kwa vyovyote vile, bado hilo haliondoi upendo wangu kwa huyu mwanamke Simba," nikaongea kwa hisia.

"Mh! Huyo Miryam lazima awe mzuri sana, mpaka akugeuze we' playboy uwe wa mmoja tu!" akasema hivyo.

Nikatabasamu kiasi na kusema, "Me siyo playboy bwana. Na haupingwi. Ni mwanamke mzuri sana Miryam. Siyo sura tu..."

"Bali shepu na tabia," Simba akatania.

Nikatabasamu kidogo na kutikisa kichwa.

"Ila ndo' ashakuwa dada yako sasa," akasema.

"Na tena hata na hapo hatuna uhakika sana, ila uwezekano ni mkubwa mno. Yeye... na wadogo zake, ni ndugu zangu. Hiyo nzito sana bro," nikaongea kwa hisia.

"Na kufikiri hadi ulikuwa kwenye mikakati ya kuoa, dah! Kwa kweli ni nzito," akasema hivyo.

Nikabaki kimya nikimtafakari Miryam tu.

"Halafu kama sikosei tayari ulikuwa umeshakula," Simba akasema hivyo.

Nikamkata jicho la kuhukumu.

Akatabasamu kiasi na kusema, "Esyuksi me, lakini najua unajua najua. Ila maana yangu ni kwamba, kama mmechangia damu moja halafu ikatokea labda ameshika mimba, si inaweza kuwa problem?"

Nikaangalia pembeni kwa ufikirio. Sikuwa nimewaza hilo hata kidogo.

"Azae mtoto, halafu atakuita baba na mjomba, au baba na baba mdogo?" Simba akaendeleza masihara yake.

"Hapana, sidhani kama inaweza fika huko. Alikuwa anatumia dawa, mfumo wa kizazi chake haukuwa imara sana," nikamweleza.

"Sawa. Pole lakini kaka. Majanga ndo' kama ya Snura hayo," akasema.

"Asante."

"Na bado anakukwepa tu, hataki mwongelee hilo suala?" akauliza.

"Eeh. Najaribu kutafuta closure, lakini haipatikani maana ananisukumia mbali. Simba... nampenda sana Miryam. Yaani, akili yangu inajua kabisa kwamba hilo suala la undugu ni msingi wa kutuachanisha bila kupinga, lakini moyo wangu bado hautaki. Yaani nataka iwezekane tu kwamba yeye na mimi hatujachangia damu, sitajali mengine. Namhitaji sana," nikaongea kwa hisia.

"Na me naona. Unaogopa utarudi kuwa playboy tena akiondoka maishani mwako," akaniambia hivyo.

"Ah, tsk... naogopa mengi tu," nikasema hivyo na kuvuta kinywaji.

"Hafanyi vizuri kukwepa maongezi. Inabidi ufanye kitu hapo. Umeshaongea na ndugu zake? Labda na mama ameshajaribu kuwatafuta mkaongea kwa pamoja?"

Nikatikisa kichwa kukataa.

"Jaribu kuwaleta wote kwa pamoja mzungumze. Mama yako akimwita Miryam, labda..."

"Hapana Simba, mama pia bado yupo conflicted sana na hii hali. I mean, imagine kama tayari ningekuwa nimemwoa Miryam halafu tukaja kugundua haya baadaye, ingekuwaje? Wote tuko sehemu mbaya kwa sasa, ila hili ni la kukaa mimi na Miryam kuongelea na kujua tunafanyaje... hawa wengine wafate. Sasa yeye anakwepa..." nikaongea kwa mkazo.

"Mbembeleze tu..."

"Ah, ungejua! Nimemwaga sera kwa huyo mwanamke!"

"Wewe..."

"Ahiii... nikwambie mimi tu, usisikie kwa mwingine. Yaani tangu nimeanza kumtongoza, mpaka leo, nambembeleza haswa. Nampenda mno mpaka nimejua kubembeleza..."

Simba akacheka kidogo.

"Lakini sa'hivi mpaka nahisi kuchoka. Sijamchoka, yaani..."

"Anatakiwa ajue siyo yeye tu ndiyo ameumia, na wewe pia. Akikukwepa inakupa wakati mgumu, naelewa. Hata me ningechoka," Simba akasema hivyo.

Nikapiga ulimi kwa kusikitika.

"Sikia, najua unampenda, lakini sometimes kaka unajua huwa hatupati kila kitu tunacho...."

"No, no, Simba... yaani sitaki kukubali hilo..."

"Ndiyo maisha JC..."

"Kwa Miryam hapana. Nampenda sana, sidhani kama nitaweza kumwachia... ikiwa hicho ndo' unachojaribu kuniambia," nikaongea kwa hisia.

"Mbona Aisha uliweza?" akauliza.

"Miryam siyo Aisha, hiyo ni story nyingine," nikasema.

"Time. Mnahitaji muda tu. Hata kama useme huwezi kumwachia, halafu iwe ni kweli mme-share damu, JC... utafanyaje? Utafosi?"

"Sijui tu, lakini...."

"Hayo mambo ya wakina Kaini siku hizi hayapo, utajitafutia balaa ukijaribu kulazimisha vitu ambavyo vimeshindikana. Kuwa open minded ili unachokikazania kisipokwenda kwa matarajio yako, ujiokoe kutoumia zaidi bwege wewe," akanishauri namna hiyo.

"Ah, na we' naye unajiona simba kumbe swala tu," nikamwambia hivyo na kunywa kileo kidogo.

Akacheka kidogo na kunywa pia, naye akaniambia, "Kwenye ukweli lazima nikwambie kaka. Maisha siyo fair, halafu we' ya kwako yamejaa maigizo kinoma. Sikia..."

Simba akaendeleza ushauri-ushauri wake kwa lengo la kunisaidia nipate ahueni ya kihisia, na maongezi mepesi ya kirafiki yakaendelea kuhusiana na mambo hayo tuliyoongelea na mengine zaidi. Tukiwa hapo kuzungumzia jambo hili kukanifanya nipandwe na hisia za kukosa subira tena, yaani presha ya hali nzima iliyozungukia suala hilo ikanivaa kwa kasi sana, nami nikanyanyuka na kuweka glasi mezani.

Simba akauliza, "Vipi?"

Nikaangalia saa mkononi, ikiwa imeshaingia saa mbili usiku, nami nikamwambia, "Nakuja. Naenda hapo nje mara moja."

Akiwa hajui nilichowaza, akasema, "Poa. Rudi na chupa ingine basi, humu zimeisha."

Nikasema tu sawa, nami nikatoka ndani hapo na kwenda garini. Yaani nikalifata gari hapo huku wenge la mbali la pombe likiteka kichwa changu, lakini sikujali. Uvumilivu ulikuwa umenishinda aisee, nikiona huu kuwa kama ujinga sasa. Hata kama ningekaa na kuwaza na kuwazua vipi, hakuna lolote ambalo lingebadili ukweli kwamba nilimpenda yule mwanamke, na najua yeye pia alinipenda. Kusema nimwache tu aendelee kuninyamazia hakungerekebisha hali hii kwa vyovyote.

Nilikuwa tayari kuweka mengine kando ili niendelee kuwa na uhusiano pamoja naye, kabisa, kwa sababu ni vingi sana tulikuwa tumeshafanya kiasi kwamba hata kama damu zetu zingekuwa zimepita kwenye njia moja, isingewezekana kufuta. Utayari wa kuendeleza mahusiano pamoja na Miryam nilikuwa nao kwa asilimia zote haijalishi nani angesema nini, na nilitaka kujua kwa upande wake alihisije kuhusiana na hilo. Kwa kuwa hakutaka kujibu yoyote kati ya simu zangu na jumbe nilizomtumia, sasa ingekuwa ni kumfata huko huko ili nimlazimu kuongea. Washa gari, kanyaga mafuta, safari moja tu ndiyo ingefuata; Mbagala.

Ni kama maongezi niliyofanya na rafiki yangu yaliibua jini ndani yangu, alikuwa sahihi kabisa. Katika yote aliyosema, alikuwa sahihi kabisa kuniambia kwamba Miryam hakufanya vizuri kunikwepa namna hii, na ningetakiwa kufanya kitu. Alichosema kuhusu mimi kutakiwa kuwa tayari kumwacha Miryam bado nilipingana nacho, ila kuwa tu na akili iliyofunguka kuelekea tatizo hili kiujumla ilikuwa muhimu. Kwa kiwango kikubwa lilikuwa tatizo, lakini upande mwingine lilikuwa na uzuri wake kwa sababu hii ilimaanisha Tesha, Mariam, na wengine wa familia hiyo waliongezeka umuhimu zaidi kwangu kuliko hata awali. Ningepaswa kuitikia hilo kwa uchanya, kisha ingenibidi nitafute njia ya kumfanya Miryam aache kujiweka mbali na mimi kwa kudhani alifanya kilicho sahihi zaidi. Kuongea tulihitaji kuongea, na sasa hivi ingekuwa kwa lazima.

β˜…β˜…

Mwendo wa saa zima ukanifikisha hayo maeneo, ikiwa imeshaingia mida ya saa tatu usiku, na nilipofikisha gari langu eneo la nyumba ya Ankia nikakuta kuna gari lingine limeegeshwa usawa wa geti lake. Mwanzoni sikuliangalia vizuri na kudhani huenda kulikuwa na mgeni ama nini, na sikujali. Mimi nikalisogeza langu mpaka usawa wa nyumba ya Miryam na kushuka, na ndiyo nilipolitazama gari hilo lingine nikalitambua. Lilikuwa ndiyo lile lile aina ya Range Rover Discovery la kifahari, ambalo nikakumbuka nililiona likimshusha Miryam ile majuzi pale Mzinga. Hee!

Kuliona kwa ukaribu na nyumba yake sasa kulimaanisha kwamba mwenye nalo alikuwepo huko ndani, nami nikakaza meno tu na kwenda getini kujaribu kufungua, lakini mlango mdogo wa geti ukagoma kufunguka. Nilishikwa na hali fulani ya kukosa subira kiasi kwamba nikaanza kugonga geti kwa nguvu na mara nyingi sana, kileo kichwani kikinipa msukumo huo, na nikiona watu waliokuwepo nje waliponitazama kwa umakini, lakini sikuwajali. Nusu dakika hivi kupita na mlango huo ukafunguliwa kwa ndani, mbele yangu akisimama Tesha huku akinitazama kimaswali, nami nikaingia upesi huku nikimsukuma kiasi kusudi anipishe.

"JC?"

Tesha akasema hivyo, lakini mimi nikasogea mbele zaidi na kuona gari la Miryam likiwa pembezoni hapo, na kwamba Mariam alikuwa amesimama pale varandani pia, akiniangalia kiumakini. Hapo hapo Shadya naye akatokea pale ndani kwao, na mimi nikiwa bado napiga hatua, Tesha akanifikia na kuushika mkono wangu.

"Oya, subiri..." Tesha akanisimamisha.

Nikamgeukia na kusema, "Nimechoka kusubiri. Najua yupo ndani, naenda kuongea naye."

Shadya akawa amefika karibu zaidi na mimi bila kuvaa viatu, naye akasema kwa sauti ya chini, "We' JC, mbona fujo?"

"Nataka kuongea na Miryam," nikamwambia.

Tesha akasema, "Kaka, huu siyo muda mzuri, maana...."

Nikautoa mkono wake kwangu kwa nguvu na kumpita Shadya ili nielekee ndani, huku wawili hawa wakinifuata na Mariam akiwa amenikazia macho tu, na mlangoni akatoka Bi Zawadi pia, kitu kilichofanya nikatishe hatua zangu.

Akiwa ananitazama kwa hisia za kujali, Bi Zawadi akasema, "JC... we' ndiyo unagonga geti kwa nguvu hivyo? Utatutia presha."

"Ameingia kwa hasira kweli, najaribu kumsemesha, hasikilizi," Shadya akamwambia hivyo.

"Nataka kumwona Miryam," nikawaambia.

"JC... umelewa?" Bi Zawadi akaniuliza.

"Hapana," nikamjibu.

"JC, nimekwambia huu siyo muda mzuri. Twende nje au hapo kwa Ankia nikwambie kitu bro," Tesha akasema.

Walikuwa wanajitahidi kuongea kwa sauti isiyo ya juu sana, nami nikapata picha kwamba kuna kitu walificha, lakini sikukitilia maanani sana, sababu akili yote ilikuwa kwa Miryam tu.

Nikamwambia Tesha, "Tutaongea baadaye, nimekuja kuonana na Miryam. Kama amewapanga mmfiche ili tusiongee, basi mjue hilo limebuma. Leo siondoki hapa mpaka nionane naye."

Shadya akasema, "Siyo hivyo JC, sasa hivi kuna mgeni, ndo'...."

"Mgeni mwenye Range eh? Sijali," nikamkatisha.

"Baba, sikiliza. Tunajua mna mengi ya kuongea, lakini nakuomba utulie kwanza. Mtaongea tu," Bi Zawadi akasema hivyo.

"Kaka..." Tesha akaniita.

"Kwa nini ananikwepa? Wiki nzima namtafuta ananikaushia, hivi.... ah... Miryam!" nikaongea hivyo na kuita kwa sauti ya juu.

"He! JC, hebu acha sifa. Unaanza ku...."

"MIRYAAM!!" nikamkatisha Shadya na kuita kwa sauti ya juu zaidi.

"Oya, usiwe kama hujasoma basi. Mambo gani haya kuita matamasha?" Tesha akaniambia.

"Miryam acha utoto, naomba uje nje haraka. Siondoki hapa mpaka tuongee. Nitavunja mlango hata ukiufunga huko ndani, unanielewa?" nikanena kana kwamba nimerukwa na akili.

"Eh, makubwa!" Shadya akasema hivyo.

"JC jamani..." Bi Zawadi akaniita kwa upole.

Nikapiga ulimi kwa kusikitika na kumwambia Bi Zawadi, "Naingia ndani mama, naomba unipishe."

Tesha akanishika mkono kunizuia, nami nikautoa kwa nguvu na kumgeukia huku nikimnyooshea kidole kwa hasira. Shadya akasogea varandani karibu na Mariam, naye Tesha akabaki kunitazama kwa macho yenye mkazo. Nadhani sauti niliyotoa ilifanya ujirani uvutwe na yaliyokuwa yakiendelea hapa, nikiona watu wameanza kusogea kwenye kuta na hata geti likisikika kufunguka, lakini sikujali hayo zaidi ya kurudisha umakini wangu mlangoni ili nielekee ndani pale.

Bi Zawadi alikuwa amesimama kama vile kunizibia njia sijui, na sikutaka ionekane kwamba namvunjia heshima ila kama ni kwenda huko ndani nilikuwa ninaenda, haikujalisha chochote tena. Lakini kabla sijapiga hiyo hatua, hatimaye bibie akatoka na kuja hapo nje. Bibie Miryam. Taratibu tu. Mapigo yangu ya moyo yalishtua kana kwamba sikuwa nimemwona kwa muda mrefu kweli, na alikuja mbele yangu na kusimama huku akinitazama kwa njia ya kawaida kabisa, ila niliweza kuiona huzuni ilivyokuwa imejaa usoni kwake.

Kutokea nyuma yangu, nikasikia sauti ya Ankia akiniita, "JC..." nami nikageuka.

Hapo nikamwona Ankia kweli, akiwa na mwonekano kawaida wa nyumbani, pamoja na yule dada yake marehemu Joy, Adelina. Inaonekana walikuwa pamoja pale kwake, na endapo kama hii ingekuwa ni pindi nzuri sana, basi ningejawa na furaha kuwaona wanawake hawa kwa sababu walikuwa marafiki wazuri kwangu. Hasa Adelina ambaye nilikuwa nimemweka kando mno siku hizi. Lakini kutokana na haya yote yaliyoendelea nikashindwa kuonyesha chembe yoyote ya furaha na kumtazama Miryam kwa mara nyingine. Sasa alisimama mbele yake Bi Zawadi, akiniangalia kwa utulivu makini tu, na pale mlangoni akatoka Bi Jamila pia kufuatiwa na mtu mwingine aliyefanya mapigo yangu ya moyo yazidi kudunda kwa nguvu kwa sababu ya kutotarajia kumwona hapo muda huo. Nilimtazama kwa umakini nikiwa nimeshangaa sana, kwa sababu ilikuwa ni Festo mwenyewe!





β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

ITAENDELEA

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…


Whatsapp +255 678 017 280
Woow! another twist.
 
MIMI NA MIMI 3

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Siri, Tamaa, Hila, Usaliti, Ukatili, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

SEHEMU YA TANO

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…



Niliishiwa pozi. Huyo ndiye mgeni mwenye Range ambaye Shadya alisema amefika hapo? Kwa nini sikuwaza kabisa kwamba ingeweza kuwa yeye? Festo alifikaje huku wakati kama huu, na alikuja kwa dhumuni lipi? Ilinishtua kwa kweli, kwa sababu ni kwa wakati mwafaka kabisa ambao mimi na Miryam tulikuwa tukipitia hali yenye kutatanisha ndiyo jamaa akawa amefika ghafla namna hiyo. Alijua kuhusu haya yaliyokuwa yanatokea? Yaani... sikuelewa.

Alitoka tu mlangoni hapo na kusimama nyuma yake Bi Jamila na Bi Zawadi, nasi tukabaki kutazamana usoni kwa macho yaliyofahamiana vyema sana. Alikuwa amevalia kwa njia nadhifu, asiwe na utofauti wowote kutoka kwa jinsi nilivyomkumbuka kimwonekano. Nikaacha kumwangalia na kutazama pembeni kwanza, nikiwa najaribu kuusoma mchezo uliokuwepo hapa, kisha nikamwangalia Miryam usoni tena. Alitulia tu na kunitazama kama vile kusubiri niseme lolote lile ili nimwondolee kero, na ni kitu kilichonivunja sana moyo. Kwamba nilihisi ameanza kuniona kuwa kero. Wote hapo nje walitulia kimya tu, wakitutazama mimi na bibie kungoja drama.

Kwa sauti tulivu, nikamuuliza Miryam, "Umepoteza simu?"

Akabaki kuniangalia kama vile hataki kujibu.

"Kwa nini haukuja?" nikamuuliza.

"Wapi?" akaniuliza.

"Najua umeziona sms zangu zote. Kwa nini haukujibu? Na kwa nini haukuja?" nikamuuliza pia.

"Nina mambo mengi," akanijibu hivyo.

"Mmm... kwa hiyo kama usingekuwa na mambo mengi ungekuja?"

"Labda," akajibu kibaridi.

"Okay. Nimekurahisishia kazi basi. Nimeona nikufate me mwenyewe. Twende nje tukaongee," nikamwambia hivyo.

"Hatuna chochote cha kuongelea," akasema hivyo.

"Kabisa?"

"Kabisa."

"Kwa hiyo... kila kitu kiko poa?"

"Yeah, kila kitu kiko poa."

Nikatulia kidogo nikimtazamaaa, kisha nikamuuliza, "Unapofanya haya unayoyafanya Miryam, unakuwa unamaanisha nini?"

"Simaanishi chochote. Na sijafanya lolote. Ni wewe tu ndiyo umebaki kulazimisha vitu visivyowezekana," akaniambia hivyo.

"Visivyowezekana kivipi? Miryam mimi na wewe hatuja-share damu, na haya yote hakuna ambaye angeweza kuyaona...."

"Jayden, inatosha. Hakuna lolote ambalo utasema wala kufanya litabadili hali," akanikatisha.

"Hali ipi? Kweli unataka kusema kwa sababu tu tumejua kuna uhusiano wa kifamilia basi ndiyo ifute kila kitu ambacho mimi na wewe tumepitia? Eh? Kila kitu ambacho tumefanya?" nikamuuliza kwa hisia.

Akabaki kuniangalia kwa hisia makini.

Bi Jamila akasema, "JC mwanangu, tutafute muda, au mtafute muda mwingine mzuri wa kuongelea haya mambo kwa sababu huu siyo wakati mzuri."

"Nini, kwa sababu Festo amekuja?" nikamuuliza.

Wote wakabaki kimya, huku jamaa akiwa ananiangalia kwa utulivu pale nyuma.

"Ahah, Miryam bana! Kwa hiyo, una mambo mengi, huwezi kukutana nami, ila kupanda Range za watu kuzurura mpaka usiku ndo' unaweza..." nikamwambia hivyo.

Akabaki kuniangalia tu kwa mkazo.

"Kwa hiyo kilichokuwa kinakufanya uwe bize eti, ni kutafuta... backup plan ya kumwondoa JC kwenye taswira, si ndiyo? Umemwita na huyu jamaa ili akusaidie kunipotezea, au?" nikamuuliza Miryam.

"JC, acha kuongea hivyo," Bi Zawadi akaniambia.

"Amekunywa huyu," Shadya akasema.

"JC, twende huku ndani basi...." Ankia akajaribu kunisemesha na kunishika, lakini nikauondoa mkono wake kwangu taratibu.

Nikamsogelea Miryam karibu zaidi na kumwambia, "Mimi, come on... let's talk about this, eti? Just me and you."

Nilimsemesha kwa kubembeleza na kuishika mikono yake, lakini akaitoa taratibu mwilini mwake na kuniambia, "Hakuna lolote limebaki la kuzungumzia, Jayden. Jinsi mambo yalivyo ndiyo yanapaswa kuwa hivyo hivyo. Naomba uende nyumbani."

Nilibaki nikimwangalia kwa kutoamini yaani, kwa kuwa maneno yake yalituma maana fulani kwangu ambayo bado sikutaka kukubaliana nayo. Akafumba macho kiufupi, kisha akageuka na kutaka kurejea ndani, lakini nikauwahi mkono wake na kumgeuzia kwangu kwa kasi.

"Miryam..." nikamwita kwa hisia.

"Jayden, niachie..." akaniambia hivyo.

"Unamaanisha nini? Hm? Nini, kwamba mimi na wewe ndiyo basi, au?" nikamuuliza.

Shadya akasema, "Tumeshagundua kwamba nyie ni ndugu JC... kuendeleza mahusiano haita...."

"Shangazi..." Tesha akamwita kama kumzuia asiendelee kuongea.

Festo akasema, "JC, tuliza hisia. Haya mambo mnaweza...."

"Kaa kimya, Festo! Hayakuhusu!" nikamwambia hivyo kwa hisia kali na kumnyooshea kidole.

"Eh, Mungu wangu!" Bi Zawadi akasema hivyo.

Festo alibaki kuniangalia kwa utulivu tu, mimi hapo nikiwa nimeshapandwa na mzuka yaani kama angeleta ujinga wake nisingesubiri kuvuruga hali ya hewa.

Miryam akautoa mkono wake kwangu na kusema, "Jayden, sitaki malumbano sasa hivi. Nimekwambia uondoke."

"Siondoki mpaka ieleweke una tatizo gani Miryam. Kwa nini hutaki tukae tuzungumze kuhusu hili jambo? Kunikwepa ndiyo itasuluhisha lolote linalofanya unione kuwa kama kero sasa hivi, ama?" nikamuuliza kwa hisia.

"Jayden, familia zetu zinaingiliana. Hatuwezi kuendelea kuwa karibu tena! Ni kipi ambacho huelewi na unahitaji kuzungumzia zaidi, eh?" Miryam akanisemesha kwa uthabiti.

"Miryam suala la familia zetu kujuana haliondoi uhusiano tuliojenga kufikia sasa. Hata kama damu zetu zingekuwa zinaingiliana, hiyo haimaanishi tungeacha kupendana, kwa sababu tulikuwa tumeshapendana kabla hatujajua hilo..."

"Hivi Jayden, unaelewa unachokiongea kweli?" akaniuliza.

"Sijui, labda we' ndiyo unieleweshe..." nikamwambia.

"Tesha na Mariam ni wadogo zetu. Mimi na wewe hatuwezi kuwa kitu kimoja kwa kuwa tuna damu zao ndani ya mishipa yetu. Unataka tuendekeze ubinafsi na kufumbia jicho jambo zito kama hilo?" Miryam akaongea kwa hisia.

"Tatizo ni hilo kweli Miryam, au basi tu unataka tuanze kuzungushana mpaka tufike pasikofikiwa? Ikiwa tusingejua kuhusu haya mpaka tunafunga ndoa, ingetuzuia kuendelea kupendana eti tu kwa sababu tumechangia uzazi kwa wadogo zetu?" nikamuuliza.

"Lakini Jayden, kwa nini unakuwa huelewi?" Miryam akaongea kwa hisia.

"Shida siyo suala la undugu Miryam, kuna kitu kingine tu kinakusumbua mpaka ufanye haya. Una tatizo gani? Kwa nini hutaki kuniambia? Kwa nini unakuwa hivi?" nikamuuliza kwa hisia mpaka machozi yakaanza kunivizia.

Akawa ananitazama kwa hisia huku akipumua kwa nguvu.

"Niambie. Nini kinakusumbua?" nikamuuliza.

Akakaza hisia zake zaidi, naye akasema, "Siwezi tena Jayden. Yote... yote tuliyofanya... nikifikiria tu ukweli kwamba tumefanya mengi endapo kama... kama mimi na wewe tungekuwa ndugu wa damu kweli... ingekuwaje?"

Nikabaki nikimtazama kwa huzuni na kutikisa kichwa.

"Hili jambo siyo dogo. Tungeweza kuwashawishi wengine namna tunavyoelewana haijalishi ni namna gani nimekuacha kiumri, lakini sasa hivi tutawashawishi vipi waelewe...."

"Miryam, kwa nini ujali kuhusu watu...."

"... waelewe mahusiano yetu, no Jayden, usipuuzie ukweli kwamba mahusiano yangu me na wewe yanawaathiri watu wengine pia ndani ya familia zetu. Tutajenga suto kubwa ambayo sidhani kama niko tayari kuibeba," akaongea kwa hisia.

"Nilikwambia nini kuhusu wewe kubeba kila kitu mwenyewe? Hili siyo pambano lako pekee, Miryam, niko nawe, niko kando yako, kwa lolote lile tutakalo-face, itakuwa ni sisi wawili, kwa pamoja...."

Akawa anatikisa kichwa kukataa.

"... mpaka tutashinda. Miryam... Miryam..."

Nikamsogelea karibu zaidi na kumshika shingoni, lakini akajirudisha nyuma.

"Mi.... ah, Miryam nashindwa kuelewa... unataka nini? Tutaondoka ukitaka, sawa? Tutaenda mbali ikiwa hutaki ku...."

"Jayden, hapana. Hii imeshakuwa too much. Tumeshajaribu mengi, lakini nimeona... na wewe umeshaona kabisa kwamba... labda me na wewe hatujapangiwa kuwa pamoja. Labda fate zetu haziendani, na hizi ndiyo ishara..." akaniambia.

"Oh, God..." nikanena hivyo kwa huzuni.

"Inabidi tu tulikubali hilo. Unanielewa?" akaniambia.

Nikamtazama machoni kwa mkazo.

Akajifuta machozi upesi kwa uimara na kusema, "Naomba uende nyumbani. Familia yangu imeshakuwa na rep ya kutosha kutengeneza drama hapa nje, imetosha. Nenda Jayden."

Nikaendelea kumwangalia tu, yaani kama vile sijasikia yote aliyotoka kusema.

Ankia akanisogelea na kusema, "JC... hebu twende."

"Halafu nini?" nikamuuliza Miryam hivyo.

Miryam na wengine wakaendelea kunitazama tu.

"Niende nyumbani, halafu nini? Nisahau kila kitu? Ni... nikusahau Miryam?" nikamuuliza hivyo.

Miryam akabaki kimya tu.

"Unajua Miryam vitu vingine siyo vya kuongelea juu juu tu bila kufikiria. Unaposema imekuwa too much kwako kupokea maumivu wakati hujajipa muda wa kuya-face pamoja nami, wewe ndiyo unakuwa mbinafsi. Unafikiri kila kitu utabeba wewe tu, hujafikiria kwamba hili pia linaniathiri mimi? Lakini uko shuta kweli kunitolea.... eti unaniambia niondoke... niondoke? Unataka nikuache Miryam? Kweli umeshalifikiria hilo vizuri kabisa, au ni pressure tu ndiyo inakufanya uongee hivyo?" nikamuuliza.

"Unataka niseme nini, Jayden?" Miryam akaniuliza kwa mkazo.

"Nataka useme kwamba unanipenda," nikamwambia hivyo kwa uhakika.

Akabaki kuniangalia kwa hisia.

"Nataka useme kwamba unanihitaji, kwamba hutaki niende... kwamba unajua nikiondoka hautakuwa na furaha tena, kwa sababu unajua moyo wako utafunga... na itakuwa ni milele," nikamwambia hivyo kwa hisia.

Miryam akadondosha chozi na kulifuta haraka, huku wengine wakiwa bado wanatazama igizo hili lililozidi kuwa zito sana, naye akajikaza na kuniangalia kwa uimara, kisha akasema, "Hayo mambo hayawezekani tena."

Nikatikisa kichwa kwa huzuni na kupiga ulimi mdomoni.

"Na wala usijali kuhusu moyo wangu. Utapata tu mwingine wa kupenda," akaniambia hivyo.

"Ohh please... wewe Miryam? Umpende nani mwingine, huh? Huyu?" nikaongea kwa hisia kali huku nikimnyooshea kidole Festo.

"JC..." Ankia akaniita kwa upole.

"Huyu ndiyo mtu unayefikiri unaweza kumpenda?" nikamuuliza Miryam kwa mkazo.

Miryam akasema, "Ndiyo."

Nikamwangalia machoni. Hata na wengine wakamtazama Miryam baada ya yeye kusema hivyo.

"Nitampenda yeye," Miryam akaniambia hivyo.

Mkono niliokuwa nimeunyoosha kumwelekea Festo ukashuka taratibu, baada ya kuhisi kitu kikali kikiwa kimeuchoma moyo wangu kutokana na kusikia maneno ya Miryam. Sikuamini yaani. Yaani alikuwa kabisa ametoka kuniambia kwamba atampenda Festo badala yangu? Alinimaliza! Nikaangalia chini nikiwa nimeishiwa pozi hata zaidi, na chozi nililojitahidi kuzuia lisitiririke likanitoka.

"Dah! JC, kaka nisikilize..." Tesha akanisemesha hivyo.

"JC... Mimi..." Bi Zawadi akasikika pia akituita.

Nikamtazama Miryam usoni na kuona alivyokuwa akiniangalia kwa huzuni, machozi akijitahidi kuyazuia, nami nikamwambia, "Unajua Miryam... yaani ingekuwa bora kama ungenikata-kata kwa mapanga kuliko kuniambia hivyo. Ulichokisema... kwangu ni kibaya kuliko hata kifo!"

"We' JC wewe!" Shadya akasema hivyo.

"JC... acha kuongea hivyo. Hey... nakuomba uje nasi," Adelina akanisemesha hivyo hatimaye na kunishika mkononi.

"JC... hebu twende," Ankia naye akaniambia hivyo.

Miryam aliendelea kunitazama tu kwa njia imara, nami nikamwangalia Festo pale nyuma yake. Mwanaume huyo alinitazama kwa umakini, akijifanya mtulivu tu wakati bado sikuwa nimesahau rangi zake zote alizokuwa nazo, lakini kwa wakati huu sikuona uhitaji tena wa kuendelea kulazimisha mambo hapo. Miryam alikuwa ameusema uamuzi wake mpya, tena hadharani, na mimi sikuwa sehemu ya huo uamuzi hata chembe. Nilikuwa nafanya nini hapa?

Nikageuka hapo hapo na kuanza kuelekea upande wa geti, Ankia na Adelina wakija nyuma yangu, na kuna baadhi ya watu waliokuwa wamesimama sehemu hiyo, wakinipisha nilipojitoa getini hapo. Yaani sikutaka kujali tena yaliyoendelea pale, moyo wangu ulikuwa umevunjika sana baada ya mwanamke huyo kuniambia yale maneno. Nilipofika nje sikwenda garini, bali nikaelekea kwenye nyumba ya Ankia mpaka kule ndani kwake. Nadhani wanawake hawa walifikiri nilitaka kwenda kukaa nao na kuzungumza kidogo, lakini mie nikakielekea chumba nilichokuwa natumia hapo na kuanza kuzitoa nguo zangu kabatini, upesi nikizishindilia ndani ya begi. Najua walikuwa nyuma yangu wakinitazama, na ni Ankia ndiye akaanza kunisemesha.

"JC, mbona unapaki nguo?" akaniuliza hivyo.

Sikujibu. Nikaendelea tu mpaka nikamaliza na kulifunga begi.

Akaendelea kusema, "Tukae basi kwanza tuongee, eh? Najua unaumia lakini nakuomba kwanza... ukae... JC..."

Nikawa nimeshalibeba begi na kuanza kuelekea mlangoni, nami nikasimama na kuwatazama kwa njia iliyowapa ujumbe kuwa nilihitaji wanipishe ili niondoke.

"JC, sikiliza. Tuongee kwanza, eti? Weka begi chini tuongee," Ankia akaniambia hivyo.

Nikatikisa kichwa kukataa, nami nikataka kupita katikati yao kwa lazima. Lakini Adelina akaweka kiganja chake kifuani kwangu kunizuia, nami nikamtazama machoni kwa hisia za mkazo.

"Siyo salama kwako kuendesha ukiwa umekunywa JC. Nitakuja na wewe," Adelina akaniambia hivyo.

"Adela..." Ankia akamwita kama kumzuia.

"Nipe funguo, nitaendesha," Adelina akaniambia hivyo.

Nikamtazama kwa hisia makini kwanza, nami nikasema, "Nimefika hapa bila shida. Nitarudi hivyo hivyo."

"Hapana JC. Siwezi kukubali uendeshe ukiwa namna hii. Nipe funguo," Adelina akaniongelesha kwa ustaarabu thabiti.

Nikiwa sitaki kuvurugwa zaidi, na kwa heshima niliyokuwa nayo kumwelekea, nikatoa tu funguo mfukoni na kumpatia, kisha nikawapita bila kusema lolote na kuelekea huko nje.

Nikamsikia Ankia akisema, "Lakini Adela, tulikuwa hata hatuja...."

"Haina shida Ankia, nitamsindikiza tu halafu nitaenda kwangu pia. Anahitaji kupumzika, lakini nataka kuhakikisha anafika salama," Adelina akasema hivyo.

Nikatoka hapo ndani na kwenda mpaka garini kwangu, bado watu wakiwepo sehemu hiyo ya nje, nami nikaingia tu na kutupia begi langu siti za nyuma. Nikiwa nimeketi siti ya pembeni na usukani, nilikuwa nikiitazama nyumba yake Miryam kwa mkazo sana, nikimwona Tesha anakuja sehemu ya hapo nje na kusimama pamoja na vijana kama wawili-watatu hivi, ambao walionekana kuongea na kuelekeza macho yao upande wa gari langu. Adelina akaja mpaka ndani ya gari langu na kuingia kwenye usukani, naye akaniangalia kwa ufupi usoni. Nikiwa nataka tu kuondoka eneo hili, nikatulia na kufumba macho nisisubiri kingine zaidi. Gari likawaka, na mwanamke huyu akaniondoa taratibu eneo hilo lililokuwa limeniacha na majonzi mengi moyoni mwangu.

β˜…β˜…

Adelina akaniendesha kwa mwendo usio wa haraka kabisa, na mwanamke huyu mtulivu alikuwa akijaribu kunisemesha mara kadhaa kuhusu hali yangu, lakini sikumjibu hata kidogo. Nilikuwa ndani ya hisia mbaya sana kiasi kwamba sikujua tunaenda wapi na sikujibu hata aliponiuliza uelekeo aliopaswa kupita ili anifikishe kwangu. Na kiukweli sikumtendea haki dada wa watu, maana alichokuwa akifanya ni kujitahidi tu kunisaidia. Lakini mawazo na hisia zangu hazikuwa mahala sahihi kwa pindi hii, nilivurugwa ile mbaya. Yaani nilihisi hasira kali mno kwa maneno ambayo Miryam aliyasema mbele ya kila mtu. Eti ingekuwa afadhali ampende Festo na si mimi? Ningeweza kuua mtu aisee, na sikudhani ningewahi kuwaza kufanya hivyo.

Kuna mahali tukafika, barabarani, na askari wa usalama kwa eneo hilo akatusimamisha. Ilikuwa ni kuchekiwa tu kwa gari na mwendeshaji, na Adelina alionyesha leseni yake na kufanya maongezi mafupi na askari huyo, kisha akatuachia tusonge mbele. Kiukweli alikuwa amenisaidia sana maana endapo kama ningeshikwa naendesha huku nimelewa ingekuwa kujitia hatiani. Ila bado nilikuwa kwenye hisia za kutojali, na Adelina aliendelea kujaribu kunisemesha bila kupata itikio lolote. Ikafikia hatua akasimamisha gari eneo moja, na kuliangalia nikatambua palikuwa kwenye barabara iliyoelekea Kimara.

Adelina akanishika begani na kuniambia ninavyokaa kimya inamkosesha amani sana, na ile nimemwangalia tu, niliona sura yenye kujali sana ya mwanamke huyu ilivyokuwa ikinitazama, lakini umakini wangu ukawa huko nje zaidi. Niliona jengo lenye kumbi ya starehe na baa ya vinywaji, nami bila kusema lolote, nikafungua mlango na kutoka ndani ya gari. Nikavuka barabara na kwenda huko bila kujali kuangalia kushoto wala kulia, nikimwacha Adelina anajiuliza ninakwenda wapi bila shaka.

Akili mbele tu, nikaingia kwenye kumbi hiyo na moja kwa moja kuelekea kaunta kupombeka. Aloo! Najua niliwavutia wengi waliokuwepo, nikafuatwa kabisa na baadhi ya wanawake ili wapate baraka kutoka kwangu, lakini sikuwa na muda nao. Nikakaa kitini na kuagiza kileo kikali, spirit yaani, na sikuwa na mpango wa kuichanganyia na soda wala nini, yaani chupa nzima nilipanga kuinywa hadi iishe. Ndiyo nilikuwa nimetoka tu kuimimina kwenye glasi kidogo pale niliposhikwa mkono kwa chini, na aliyenishika nilipomgeukia nikakuta ni Adelina.

"Wewe, JC... mambo gani haya?" akaniuliza kiumakini.

Nikabaki nikimtazama kwa umakini pia, na hatimaye nikamwambia, "Nakunywa kidogo. Kaa nikuagizie."

Akabaki kuniangalia kwa kukereka, nami nikavuta glasi yenye kileo na kuishusha yote kooni kwa kishindo. Ilikuwa kali! Nikatulia kwa sekunde chache nikisikilizia hilo pigo, kisha nikatulia na kumwita bartender, mwanamke mtu mzima ila matata.

"Mpe huyu yoyote anayotaka," nikamwambia huku nikimshika Adelina begani.

Adelina akautoa mkono wangu begani kwake na kumwambia mwanamke huyo, "Sitaki chochote."

Mwanamke huyo akabaki kututazama.

Nikiwa nimeshamimina kinywaji tena, nikasema, "Kama hutaki kunywa agiza msosi ule."

Adelina akabaki kuniangalia kwa mkazo.

"Au ulikula kwa Ankia?" nikamuuliza.

Tayari divai ilikuwa imeanza kunikoroga vyema, naye Adelina akasema, "Kwa hiyo muda wote nimekusemesha kwenye gari ulikuwa husikii? Ulitaka kuja kuongelea bar?"

Nikapuuzia swali lake na kupachika goli la pili la pombe hiyo kali balaa.

"JC mbona unakuwa hivi? Nikuache tu si ndiyo?" Adelina akasema.

"Hamna... kaa unywe," nikaongea kilevi.

"Hebu twende JC..."

Adelina akajaribu kunivuta lakini nikamwekea mgomo.

"Tabia si nzuri hii, kulewa haitasaidia lolote. Unajidanganya ukifikiri ndiyo itasuluhisha matatizo yako..." akaniambia hivyo.

"Hamna... ila inayapunguza," nikamwambia hivyo na kutabasamu.

"Hakuna! Unayaongeza tu na unajiumiza. Hebu acha," akaongea kwa hisia kali.

"Adelina nenda ukalale... matatizo... matatizo yangu... hayakuhusu..." nikamwambia hivyo.

Nikaongeza pombe na kutaka kunywa tena, hapo wenge zito kichwani likiwa limeshaniteka, lakini Adelina akaikwapua glasi hiyo na kuiweka pembeni kwa hasira.

Akamwita bartender na kutoa hela yake mwenyewe kumpatia. "Shi'ngapi hiyo?" akamuuliza.

Nikacheka kilegevu, na baada ya kuambiwa bei Adelina akalipia na kisha kunishika mkono kwa nguvu.

"JC nyanyuka," Adelina akaniambia.

"Sijamaliza kilichoni...."

"Nimesema twende!" akanikatisha kwa kunikaripia.

Nikautoa mkono wangu kutoka kwake kwa nguvu sana na kusema kwa hasira, "Niache bana! We' vipi?!"

Niliuvuta mkono wangu kwa njia iliyosababisha Adelina aweweseke kunielekea, na ikawa kama vile nimemsukumia upande wa kaunta nusu ajipige hapo. Kuna watu najua walianza kututazama sana, hata bartender, naye Adelina akaniangalia usoni kwa kutatizika. Nikapatwa na hisia mbaya baada ya kutambua nilichofanya, na mwanamke huyu akaangalia tu chini kwa ufupi, kisha akaniwekea funguo za gari langu ndani ya mfuko wa suruali na kuanza kuondoka sehemu hiyo. Aliondoka huku nikimtazama bila kuacha, nami nikarudiwa na utambuzi ulionifanya nitoke hapo pia ili niwahi kumfata.

Pombe niliyokunywa kabla sijaenda kwa Miryam kujumuisha na hii ya sasa ilifanya nihisi kulewa hata zaidi, kwa hiyo nguvu mwilini ilivutwa. Lakini nikajitahidi kutoka na kuanza kuelekea kule nilikoliona gari langu, na kwa hakika sikuweza kumwona Adelina upande huo. Nilipoangaza huko na kule, nikamwona mwanamke huyo akielekea sehemu ambayo angesimama ili kungoja daladala, na kiukweli hisia mbaya zikazidi kunipata. Sikumtendea kwa heshima. Akafika hiyo sehemu na kusimama pamoja na watu wengine, nami nikaelekeza hatua zangu huko kumfuata. Nilipomkaribia, aliniangalia kwa njia ya kawaida tu, hivyo nikajitahidi kuuweka utimamu kisawasawa ili nisiongee pumba na kumwomba samahani kwa kilichotokea.

"Adelina..."

Akanyanyua kiganja chake kwa chini kama kunizuia nisiendelee, halafu akatazama upande mwingine kuonyesha namna gani alikwazika.

"Adelina samahani... sija...." nikakosa hata cha kusema.

Inaonekana gari alilokuwa akilingojea likawa limefika, naye akaashiria kutaka kulifata lakini nikamshika mkono ili nimzuie.

"Adelina please... nisikilize..." nikamwomba.

"Niachie bwana JC..." akaniambia hivyo kwa kuudhika.

Konda alikuwa akisubiria tupande kwa kuona nyendo za Adelina, lakini nikamwambia, "Hatuendi bro. Tembea."

"Hauendi wewe, me naenda," Adelina akasema hivyo na kujaribu kuutoa mkono wangu kwake.

"No, hauwezi... bro tembeeni tu," nikasema hivyo nikiendelea kuukaza mkono wa Adelina.

Konda alikuwa akinitazama kwa hasira, eti namkosesha buku, na dereva wake akampigia kelele waondoke upesi, hivyo wakatuacha hapo nikimshikilia rafiki yangu bado.

"JC ni nini lakini? Si umeniambia nikuache, unataka nini?" Adelina akaongea kwa hisia.

"Nis.. nisamehe, samahani, unajua... unajua..." nikaishia tu hapo kwa kubabaika.

Akabaki kuniangalia kwa mkazo.

"Tafadhali... naomba uniendeshe. Ni.. siwezi ku... kuendesha ma... sisemi hauna budi, ni makosa yangu... najua... ila...."

Adelina akapiga ulimi kwa kuudhika na kisha kunishika mkononi, naye akaanza kuelekea upande tuliotoka kwa njia ya kunivuta. Na pombe juu lakini mpaka nilihisi aibu. Alinishika hivyo ili kuhakikisha tunavuka barabara kwa usalama, na baada ya kuvuka moja kwa moja tukaelekea kwenye gari langu. Nikampatia funguo, kisha tukaingia na safari kuanza.

Sikujaribu tena kumsemesha kwa kuwa niliona bado aliudhika. Na tena pombe yangu kichwani haikuwa nzito kunisahaulisha mambo kivile, lakini wenge nililohisi likanifanya hadi nisahau simu yangu ilikuwa wapi. Ndiyo nikamuuliza Adelina, nikimwambia mara mbili kwamba nimeimisi simu yangu, lakini wakati huu ikawa ni zamu yake kuninyamazia. Dah! Haya bwana. Nikaona nisitoe kero zaidi, kwa sababu wakati huu mimi ndiye niliyekuwa mkosaji. Nikatulia tu kwenye siti nisijue tulikoelekea.

β˜…β˜…

Mwendo ulikuwa mrefu kiasi, na kuna mara ambazo ningetazama nje na kutambua kwamba tupo Kimara, Temboni, kuelekea kituo cha mabasi cha Magufuli Mbezi. Pindi nyingi tulisimama sana kutokana na msongamano, na baada ya muda ulioonekana kuwa mrefu tukaingia eneo lililoiacha lami na kusonga kwa dakika chache, kisha gari likatulia. Kichwani pombe ilikuwa imeanza kufifia ingawa bado wenge lilikuwepo, na nikaona Adelina akitoka ndani ya gari. Kuangalia mbele lilikuwa geti lisilopakwa rangi, likiwa la uchuma yaani, naye akaingia hapo na kisha kuanza kulifungua lote kutokea ndani. Sikujua ikiwa hapa palikuwa kwake ama vipi, lakini akarejea tena kwenye gari na kuliingiza ndani, kisha akashuka tena. Hakutaka kunisemesha kabisa.

Bwana, nikajiongeza tu na mipombe yangu kushuka pia, na yeye akiwa ndiyo anamalizia kulifunga geti. Nikapatazama hapo kuyaelewa mazingira, na mbele yangu ilikuwa ni nyumba yenye ukubwa mkubwa kiasi, iliyoonekana kuwa ya kupangisha watu. Millango kwa nje ilikuwa kwa pande mbili, hivyo nikafikiria lazima kuwe na mpangaji mwingine tofauti na Adelina hapo. Moja kwa moja nikaelewa huku palikuwa Kinyerezi, ambako mara nyingi mwanamke huyu alinisisitiza nije kumtembelea, na ni jambo ambalo nilikuwa nikimwahidi kufanya bila kulitimiza. Ona sasa mazingira yaliyokuwa yamefanya nikafika kwake kwa mara ya kwanza! Yalikuwa mabaya, na hilo likanitia huzuni.

Kumwangalia, Adelina akaja niliposimama na kunishika mkononi, naye akaanza kunielekeza kuelekea mlango ambao bila shaka ulikuwa wa ndani alikoishi yeye. Sikuwa na namna ila kuwa mtiifu tu, na aliponiachia ili anitangulie nikawa namfuata taratibu hadi alipofikia sehemu yenye ngazi kama mbili hivi, kisha akaufungua mlango huo. Sikujua ilikuwa saa ngapi, ila palikuwa kimya kweli kuzungukia eneo lote kutokea huko nje. Alipoufungua mlango akanishika tena mkono kunikaribisha ndani bila maneno, nami nikainama na mapombe yangu ili nifanye ustaarabu wa kuvua viatu kwanza.

"A-ah, usivue. Ingia tu."

Akanisemesha hatimaye. Nikasimama vizuri na kumtazama, naye akageuka na kuingia ndani kwa kusimama usawa wa mlango, halafu akawasha taa na kuendelea kusimama hapo hapo kama kusubiri nipite. Haikuwa na neno, nikapita. Ndani hapo palikuwa simple tu, masofa matatu ya samawati marefu na mazuri aliyoyapanga kwa kuzungukia kuta, zulia safi na laini chini, nikaona na friji, kiyoyozi cha juu na cha kuongoza kwa mkono pembeni, pamoja na TV pana ya flat screen, bufa, king'amuzi, na vitu-vitu vingine. Kulikuwa na mlango upande wa kushoto ambao ulikuwa wa jikoni, na upande wa kulia chumbani kwake bila shaka. Nikasimama hapo kati nikimwangalia Adelina alipokuwa akimalizia kufunga mlango vizuri, kisha akasogea mbele yangu na kuniangalia machoni.

"Unasikia njaa?" akaniuliza hivyo.

Nikatikisa kichwa kukanusha.

Yeye pia akatikisa kichwa mara moja na kuangalia pembeni, kisha akasema, "Sawa. Itabidi ulale hapo hivi, kwenye sofa, maana... kitanda ni kimo...."

"Haina shida Adelina," nikamkatisha.

Akiwa hataki kunitazama bado, akasema, "Sawa, basi... me naenda kulala. Upumzike pia, hapa hamna mbu... ukitaka nikuwashie na fe..."

"Adelina..." nikamwita kwa upole.

Akaacha kuongea na kunitazama kichini, si machoni.

Nikamwambia, "Adelina naomba unisamehe."

Akasema, "Ah, usijali JC, yashapita hayo achana nayo. Wote tumechoka kwa hiyo... usiku mwema..."

Alitaka na kuondoka lakini nikaushika mkono wake na kumgeuzia kwangu kwa nguvu kiasi, naye akatulia.

Nikiwa namwangalia kwa kujali, nikasema, "Adelina niangalie."

Macho yake hayakuwa mbali sana kuyafikia yangu sababu ya urefu wa mwili wake, lakini bado akaendelea tu kuniangalia kichini. Nikatumia kiganja changu kulishika shavu lake taratibu, naye ndiyo akanitazama machoni hatimaye.

"Nisamehe," nikaongea kwa upole na macho yangu lege.

Adelina hakutoa jibu kwa maneno na kuendelea kuniangalia tu, na kisha matendo yake ndiyo yakaongea. Akapitisha mikono yake kufikia mgongoni kwangu na kunikumbatia taratibu, akiusugua taratibu kama kuniambia nisijali, nami nikapata ahueni moyoni. Nikalirudisha kumbatio hilo na kisha kumwachia, nikimtazama usoni kwa uthamini. Tukiwa tumekaribiana zaidi namna hiyo, tukabaki kuangaliana kwa njia fulani ya subira; mimi nikingoja aseme jambo fulani, na nisijue yeye akingoja nini. Lakini kungoja kwangu aseme jambo fulani kukabadilika ghafla kutokana na kuanza kupatwa na hisia kumwelekea mwanamke huyu. Sikuwahi kumtazama Adelina kwa njia hii, ya hisia, ila sasa ikawepo. Sijui ni pombe tu, au ilikuwa moyo kabisa?

Nadhani hali ikawa namna hiyo hiyo hata kwake pia, kwa sababu baada ya kuangaliana kihivyo, nikahisi mkono wake ukipita ubavuni kwangu na kufanya kama kuishika T-shirt niliyovaa kwa kuivuta fulani hivi, nami nikauangalia mkono wake. Niliporudisha macho yangu usoni kwake, wakati huu ukawa tofauti na jinsi ulivyokuwa awali; si wa kuudhika tena, bali wa hisia. Ah! Hee. Ujumbe ukawa delivadi. Mimi nikiwa mzee wa kupandisha mizuka, sikuchelewa. Huko chini nikaanza kunyanyuka, kwa nguvu hatari, na hali hii ikaniongezea hamu ya kutaka jambo hili liendelee. Tukiwa bado tunatazamana kwa ukaribu, na Adelina akinishikilia ubavuni bado, nikajikuta naifuata midomo yake papo hapo na kuanza kuipiga busu. Mluzi!





β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

ITAENDELEA

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…


Whatsapp +255 678 017 280
 
MIMI NA MIMI 3

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Siri, Tamaa, Hila, Usaliti, Ukatili, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

SEHEMU YA TANO

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…



Niliishiwa pozi. Huyo ndiye mgeni mwenye Range ambaye Shadya alisema amefika hapo? Kwa nini sikuwaza kabisa kwamba ingeweza kuwa yeye? Festo alifikaje huku wakati kama huu, na alikuja kwa dhumuni lipi? Ilinishtua kwa kweli, kwa sababu ni kwa wakati mwafaka kabisa ambao mimi na Miryam tulikuwa tukipitia hali yenye kutatanisha ndiyo jamaa akawa amefika ghafla namna hiyo. Alijua kuhusu haya yaliyokuwa yanatokea? Yaani... sikuelewa.

Alitoka tu mlangoni hapo na kusimama nyuma yake Bi Jamila na Bi Zawadi, nasi tukabaki kutazamana usoni kwa macho yaliyofahamiana vyema sana. Alikuwa amevalia kwa njia nadhifu, asiwe na utofauti wowote kutoka kwa jinsi nilivyomkumbuka kimwonekano. Nikaacha kumwangalia na kutazama pembeni kwanza, nikiwa najaribu kuusoma mchezo uliokuwepo hapa, kisha nikamwangalia Miryam usoni tena. Alitulia tu na kunitazama kama vile kusubiri niseme lolote lile ili nimwondolee kero, na ni kitu kilichonivunja sana moyo. Kwamba nilihisi ameanza kuniona kuwa kero. Wote hapo nje walitulia kimya tu, wakitutazama mimi na bibie kungoja drama.

Kwa sauti tulivu, nikamuuliza Miryam, "Umepoteza simu?"

Akabaki kuniangalia kama vile hataki kujibu.

"Kwa nini haukuja?" nikamuuliza.

"Wapi?" akaniuliza.

"Najua umeziona sms zangu zote. Kwa nini haukujibu? Na kwa nini haukuja?" nikamuuliza pia.

"Nina mambo mengi," akanijibu hivyo.

"Mmm... kwa hiyo kama usingekuwa na mambo mengi ungekuja?"

"Labda," akajibu kibaridi.

"Okay. Nimekurahisishia kazi basi. Nimeona nikufate me mwenyewe. Twende nje tukaongee," nikamwambia hivyo.

"Hatuna chochote cha kuongelea," akasema hivyo.

"Kabisa?"

"Kabisa."

"Kwa hiyo... kila kitu kiko poa?"

"Yeah, kila kitu kiko poa."

Nikatulia kidogo nikimtazamaaa, kisha nikamuuliza, "Unapofanya haya unayoyafanya Miryam, unakuwa unamaanisha nini?"

"Simaanishi chochote. Na sijafanya lolote. Ni wewe tu ndiyo umebaki kulazimisha vitu visivyowezekana," akaniambia hivyo.

"Visivyowezekana kivipi? Miryam mimi na wewe hatuja-share damu, na haya yote hakuna ambaye angeweza kuyaona...."

"Jayden, inatosha. Hakuna lolote ambalo utasema wala kufanya litabadili hali," akanikatisha.

"Hali ipi? Kweli unataka kusema kwa sababu tu tumejua kuna uhusiano wa kifamilia basi ndiyo ifute kila kitu ambacho mimi na wewe tumepitia? Eh? Kila kitu ambacho tumefanya?" nikamuuliza kwa hisia.

Akabaki kuniangalia kwa hisia makini.

Bi Jamila akasema, "JC mwanangu, tutafute muda, au mtafute muda mwingine mzuri wa kuongelea haya mambo kwa sababu huu siyo wakati mzuri."

"Nini, kwa sababu Festo amekuja?" nikamuuliza.

Wote wakabaki kimya, huku jamaa akiwa ananiangalia kwa utulivu pale nyuma.

"Ahah, Miryam bana! Kwa hiyo, una mambo mengi, huwezi kukutana nami, ila kupanda Range za watu kuzurura mpaka usiku ndo' unaweza..." nikamwambia hivyo.

Akabaki kuniangalia tu kwa mkazo.

"Kwa hiyo kilichokuwa kinakufanya uwe bize eti, ni kutafuta... backup plan ya kumwondoa JC kwenye taswira, si ndiyo? Umemwita na huyu jamaa ili akusaidie kunipotezea, au?" nikamuuliza Miryam.

"JC, acha kuongea hivyo," Bi Zawadi akaniambia.

"Amekunywa huyu," Shadya akasema.

"JC, twende huku ndani basi...." Ankia akajaribu kunisemesha na kunishika, lakini nikauondoa mkono wake kwangu taratibu.

Nikamsogelea Miryam karibu zaidi na kumwambia, "Mimi, come on... let's talk about this, eti? Just me and you."

Nilimsemesha kwa kubembeleza na kuishika mikono yake, lakini akaitoa taratibu mwilini mwake na kuniambia, "Hakuna lolote limebaki la kuzungumzia, Jayden. Jinsi mambo yalivyo ndiyo yanapaswa kuwa hivyo hivyo. Naomba uende nyumbani."

Nilibaki nikimwangalia kwa kutoamini yaani, kwa kuwa maneno yake yalituma maana fulani kwangu ambayo bado sikutaka kukubaliana nayo. Akafumba macho kiufupi, kisha akageuka na kutaka kurejea ndani, lakini nikauwahi mkono wake na kumgeuzia kwangu kwa kasi.

"Miryam..." nikamwita kwa hisia.

"Jayden, niachie..." akaniambia hivyo.

"Unamaanisha nini? Hm? Nini, kwamba mimi na wewe ndiyo basi, au?" nikamuuliza.

Shadya akasema, "Tumeshagundua kwamba nyie ni ndugu JC... kuendeleza mahusiano haita...."

"Shangazi..." Tesha akamwita kama kumzuia asiendelee kuongea.

Festo akasema, "JC, tuliza hisia. Haya mambo mnaweza...."

"Kaa kimya, Festo! Hayakuhusu!" nikamwambia hivyo kwa hisia kali na kumnyooshea kidole.

"Eh, Mungu wangu!" Bi Zawadi akasema hivyo.

Festo alibaki kuniangalia kwa utulivu tu, mimi hapo nikiwa nimeshapandwa na mzuka yaani kama angeleta ujinga wake nisingesubiri kuvuruga hali ya hewa.

Miryam akautoa mkono wake kwangu na kusema, "Jayden, sitaki malumbano sasa hivi. Nimekwambia uondoke."

"Siondoki mpaka ieleweke una tatizo gani Miryam. Kwa nini hutaki tukae tuzungumze kuhusu hili jambo? Kunikwepa ndiyo itasuluhisha lolote linalofanya unione kuwa kama kero sasa hivi, ama?" nikamuuliza kwa hisia.

"Jayden, familia zetu zinaingiliana. Hatuwezi kuendelea kuwa karibu tena! Ni kipi ambacho huelewi na unahitaji kuzungumzia zaidi, eh?" Miryam akanisemesha kwa uthabiti.

"Miryam suala la familia zetu kujuana haliondoi uhusiano tuliojenga kufikia sasa. Hata kama damu zetu zingekuwa zinaingiliana, hiyo haimaanishi tungeacha kupendana, kwa sababu tulikuwa tumeshapendana kabla hatujajua hilo..."

"Hivi Jayden, unaelewa unachokiongea kweli?" akaniuliza.

"Sijui, labda we' ndiyo unieleweshe..." nikamwambia.

"Tesha na Mariam ni wadogo zetu. Mimi na wewe hatuwezi kuwa kitu kimoja kwa kuwa tuna damu zao ndani ya mishipa yetu. Unataka tuendekeze ubinafsi na kufumbia jicho jambo zito kama hilo?" Miryam akaongea kwa hisia.

"Tatizo ni hilo kweli Miryam, au basi tu unataka tuanze kuzungushana mpaka tufike pasikofikiwa? Ikiwa tusingejua kuhusu haya mpaka tunafunga ndoa, ingetuzuia kuendelea kupendana eti tu kwa sababu tumechangia uzazi kwa wadogo zetu?" nikamuuliza.

"Lakini Jayden, kwa nini unakuwa huelewi?" Miryam akaongea kwa hisia.

"Shida siyo suala la undugu Miryam, kuna kitu kingine tu kinakusumbua mpaka ufanye haya. Una tatizo gani? Kwa nini hutaki kuniambia? Kwa nini unakuwa hivi?" nikamuuliza kwa hisia mpaka machozi yakaanza kunivizia.

Akawa ananitazama kwa hisia huku akipumua kwa nguvu.

"Niambie. Nini kinakusumbua?" nikamuuliza.

Akakaza hisia zake zaidi, naye akasema, "Siwezi tena Jayden. Yote... yote tuliyofanya... nikifikiria tu ukweli kwamba tumefanya mengi endapo kama... kama mimi na wewe tungekuwa ndugu wa damu kweli... ingekuwaje?"

Nikabaki nikimtazama kwa huzuni na kutikisa kichwa.

"Hili jambo siyo dogo. Tungeweza kuwashawishi wengine namna tunavyoelewana haijalishi ni namna gani nimekuacha kiumri, lakini sasa hivi tutawashawishi vipi waelewe...."

"Miryam, kwa nini ujali kuhusu watu...."

"... waelewe mahusiano yetu, no Jayden, usipuuzie ukweli kwamba mahusiano yangu me na wewe yanawaathiri watu wengine pia ndani ya familia zetu. Tutajenga suto kubwa ambayo sidhani kama niko tayari kuibeba," akaongea kwa hisia.

"Nilikwambia nini kuhusu wewe kubeba kila kitu mwenyewe? Hili siyo pambano lako pekee, Miryam, niko nawe, niko kando yako, kwa lolote lile tutakalo-face, itakuwa ni sisi wawili, kwa pamoja...."

Akawa anatikisa kichwa kukataa.

"... mpaka tutashinda. Miryam... Miryam..."

Nikamsogelea karibu zaidi na kumshika shingoni, lakini akajirudisha nyuma.

"Mi.... ah, Miryam nashindwa kuelewa... unataka nini? Tutaondoka ukitaka, sawa? Tutaenda mbali ikiwa hutaki ku...."

"Jayden, hapana. Hii imeshakuwa too much. Tumeshajaribu mengi, lakini nimeona... na wewe umeshaona kabisa kwamba... labda me na wewe hatujapangiwa kuwa pamoja. Labda fate zetu haziendani, na hizi ndiyo ishara..." akaniambia.

"Oh, God..." nikanena hivyo kwa huzuni.

"Inabidi tu tulikubali hilo. Unanielewa?" akaniambia.

Nikamtazama machoni kwa mkazo.

Akajifuta machozi upesi kwa uimara na kusema, "Naomba uende nyumbani. Familia yangu imeshakuwa na rep ya kutosha kutengeneza drama hapa nje, imetosha. Nenda Jayden."

Nikaendelea kumwangalia tu, yaani kama vile sijasikia yote aliyotoka kusema.

Ankia akanisogelea na kusema, "JC... hebu twende."

"Halafu nini?" nikamuuliza Miryam hivyo.

Miryam na wengine wakaendelea kunitazama tu.

"Niende nyumbani, halafu nini? Nisahau kila kitu? Ni... nikusahau Miryam?" nikamuuliza hivyo.

Miryam akabaki kimya tu.

"Unajua Miryam vitu vingine siyo vya kuongelea juu juu tu bila kufikiria. Unaposema imekuwa too much kwako kupokea maumivu wakati hujajipa muda wa kuya-face pamoja nami, wewe ndiyo unakuwa mbinafsi. Unafikiri kila kitu utabeba wewe tu, hujafikiria kwamba hili pia linaniathiri mimi? Lakini uko shuta kweli kunitolea.... eti unaniambia niondoke... niondoke? Unataka nikuache Miryam? Kweli umeshalifikiria hilo vizuri kabisa, au ni pressure tu ndiyo inakufanya uongee hivyo?" nikamuuliza.

"Unataka niseme nini, Jayden?" Miryam akaniuliza kwa mkazo.

"Nataka useme kwamba unanipenda," nikamwambia hivyo kwa uhakika.

Akabaki kuniangalia kwa hisia.

"Nataka useme kwamba unanihitaji, kwamba hutaki niende... kwamba unajua nikiondoka hautakuwa na furaha tena, kwa sababu unajua moyo wako utafunga... na itakuwa ni milele," nikamwambia hivyo kwa hisia.

Miryam akadondosha chozi na kulifuta haraka, huku wengine wakiwa bado wanatazama igizo hili lililozidi kuwa zito sana, naye akajikaza na kuniangalia kwa uimara, kisha akasema, "Hayo mambo hayawezekani tena."

Nikatikisa kichwa kwa huzuni na kupiga ulimi mdomoni.

"Na wala usijali kuhusu moyo wangu. Utapata tu mwingine wa kupenda," akaniambia hivyo.

"Ohh please... wewe Miryam? Umpende nani mwingine, huh? Huyu?" nikaongea kwa hisia kali huku nikimnyooshea kidole Festo.

"JC..." Ankia akaniita kwa upole.

"Huyu ndiyo mtu unayefikiri unaweza kumpenda?" nikamuuliza Miryam kwa mkazo.

Miryam akasema, "Ndiyo."

Nikamwangalia machoni. Hata na wengine wakamtazama Miryam baada ya yeye kusema hivyo.

"Nitampenda yeye," Miryam akaniambia hivyo.

Mkono niliokuwa nimeunyoosha kumwelekea Festo ukashuka taratibu, baada ya kuhisi kitu kikali kikiwa kimeuchoma moyo wangu kutokana na kusikia maneno ya Miryam. Sikuamini yaani. Yaani alikuwa kabisa ametoka kuniambia kwamba atampenda Festo badala yangu? Alinimaliza! Nikaangalia chini nikiwa nimeishiwa pozi hata zaidi, na chozi nililojitahidi kuzuia lisitiririke likanitoka.

"Dah! JC, kaka nisikilize..." Tesha akanisemesha hivyo.

"JC... Mimi..." Bi Zawadi akasikika pia akituita.

Nikamtazama Miryam usoni na kuona alivyokuwa akiniangalia kwa huzuni, machozi akijitahidi kuyazuia, nami nikamwambia, "Unajua Miryam... yaani ingekuwa bora kama ungenikata-kata kwa mapanga kuliko kuniambia hivyo. Ulichokisema... kwangu ni kibaya kuliko hata kifo!"

"We' JC wewe!" Shadya akasema hivyo.

"JC... acha kuongea hivyo. Hey... nakuomba uje nasi," Adelina akanisemesha hivyo hatimaye na kunishika mkononi.

"JC... hebu twende," Ankia naye akaniambia hivyo.

Miryam aliendelea kunitazama tu kwa njia imara, nami nikamwangalia Festo pale nyuma yake. Mwanaume huyo alinitazama kwa umakini, akijifanya mtulivu tu wakati bado sikuwa nimesahau rangi zake zote alizokuwa nazo, lakini kwa wakati huu sikuona uhitaji tena wa kuendelea kulazimisha mambo hapo. Miryam alikuwa ameusema uamuzi wake mpya, tena hadharani, na mimi sikuwa sehemu ya huo uamuzi hata chembe. Nilikuwa nafanya nini hapa?

Nikageuka hapo hapo na kuanza kuelekea upande wa geti, Ankia na Adelina wakija nyuma yangu, na kuna baadhi ya watu waliokuwa wamesimama sehemu hiyo, wakinipisha nilipojitoa getini hapo. Yaani sikutaka kujali tena yaliyoendelea pale, moyo wangu ulikuwa umevunjika sana baada ya mwanamke huyo kuniambia yale maneno. Nilipofika nje sikwenda garini, bali nikaelekea kwenye nyumba ya Ankia mpaka kule ndani kwake. Nadhani wanawake hawa walifikiri nilitaka kwenda kukaa nao na kuzungumza kidogo, lakini mie nikakielekea chumba nilichokuwa natumia hapo na kuanza kuzitoa nguo zangu kabatini, upesi nikizishindilia ndani ya begi. Najua walikuwa nyuma yangu wakinitazama, na ni Ankia ndiye akaanza kunisemesha.

"JC, mbona unapaki nguo?" akaniuliza hivyo.

Sikujibu. Nikaendelea tu mpaka nikamaliza na kulifunga begi.

Akaendelea kusema, "Tukae basi kwanza tuongee, eh? Najua unaumia lakini nakuomba kwanza... ukae... JC..."

Nikawa nimeshalibeba begi na kuanza kuelekea mlangoni, nami nikasimama na kuwatazama kwa njia iliyowapa ujumbe kuwa nilihitaji wanipishe ili niondoke.

"JC, sikiliza. Tuongee kwanza, eti? Weka begi chini tuongee," Ankia akaniambia hivyo.

Nikatikisa kichwa kukataa, nami nikataka kupita katikati yao kwa lazima. Lakini Adelina akaweka kiganja chake kifuani kwangu kunizuia, nami nikamtazama machoni kwa hisia za mkazo.

"Siyo salama kwako kuendesha ukiwa umekunywa JC. Nitakuja na wewe," Adelina akaniambia hivyo.

"Adela..." Ankia akamwita kama kumzuia.

"Nipe funguo, nitaendesha," Adelina akaniambia hivyo.

Nikamtazama kwa hisia makini kwanza, nami nikasema, "Nimefika hapa bila shida. Nitarudi hivyo hivyo."

"Hapana JC. Siwezi kukubali uendeshe ukiwa namna hii. Nipe funguo," Adelina akaniongelesha kwa ustaarabu thabiti.

Nikiwa sitaki kuvurugwa zaidi, na kwa heshima niliyokuwa nayo kumwelekea, nikatoa tu funguo mfukoni na kumpatia, kisha nikawapita bila kusema lolote na kuelekea huko nje.

Nikamsikia Ankia akisema, "Lakini Adela, tulikuwa hata hatuja...."

"Haina shida Ankia, nitamsindikiza tu halafu nitaenda kwangu pia. Anahitaji kupumzika, lakini nataka kuhakikisha anafika salama," Adelina akasema hivyo.

Nikatoka hapo ndani na kwenda mpaka garini kwangu, bado watu wakiwepo sehemu hiyo ya nje, nami nikaingia tu na kutupia begi langu siti za nyuma. Nikiwa nimeketi siti ya pembeni na usukani, nilikuwa nikiitazama nyumba yake Miryam kwa mkazo sana, nikimwona Tesha anakuja sehemu ya hapo nje na kusimama pamoja na vijana kama wawili-watatu hivi, ambao walionekana kuongea na kuelekeza macho yao upande wa gari langu. Adelina akaja mpaka ndani ya gari langu na kuingia kwenye usukani, naye akaniangalia kwa ufupi usoni. Nikiwa nataka tu kuondoka eneo hili, nikatulia na kufumba macho nisisubiri kingine zaidi. Gari likawaka, na mwanamke huyu akaniondoa taratibu eneo hilo lililokuwa limeniacha na majonzi mengi moyoni mwangu.

β˜…β˜…

Adelina akaniendesha kwa mwendo usio wa haraka kabisa, na mwanamke huyu mtulivu alikuwa akijaribu kunisemesha mara kadhaa kuhusu hali yangu, lakini sikumjibu hata kidogo. Nilikuwa ndani ya hisia mbaya sana kiasi kwamba sikujua tunaenda wapi na sikujibu hata aliponiuliza uelekeo aliopaswa kupita ili anifikishe kwangu. Na kiukweli sikumtendea haki dada wa watu, maana alichokuwa akifanya ni kujitahidi tu kunisaidia. Lakini mawazo na hisia zangu hazikuwa mahala sahihi kwa pindi hii, nilivurugwa ile mbaya. Yaani nilihisi hasira kali mno kwa maneno ambayo Miryam aliyasema mbele ya kila mtu. Eti ingekuwa afadhali ampende Festo na si mimi? Ningeweza kuua mtu aisee, na sikudhani ningewahi kuwaza kufanya hivyo.

Kuna mahali tukafika, barabarani, na askari wa usalama kwa eneo hilo akatusimamisha. Ilikuwa ni kuchekiwa tu kwa gari na mwendeshaji, na Adelina alionyesha leseni yake na kufanya maongezi mafupi na askari huyo, kisha akatuachia tusonge mbele. Kiukweli alikuwa amenisaidia sana maana endapo kama ningeshikwa naendesha huku nimelewa ingekuwa kujitia hatiani. Ila bado nilikuwa kwenye hisia za kutojali, na Adelina aliendelea kujaribu kunisemesha bila kupata itikio lolote. Ikafikia hatua akasimamisha gari eneo moja, na kuliangalia nikatambua palikuwa kwenye barabara iliyoelekea Kimara.

Adelina akanishika begani na kuniambia ninavyokaa kimya inamkosesha amani sana, na ile nimemwangalia tu, niliona sura yenye kujali sana ya mwanamke huyu ilivyokuwa ikinitazama, lakini umakini wangu ukawa huko nje zaidi. Niliona jengo lenye kumbi ya starehe na baa ya vinywaji, nami bila kusema lolote, nikafungua mlango na kutoka ndani ya gari. Nikavuka barabara na kwenda huko bila kujali kuangalia kushoto wala kulia, nikimwacha Adelina anajiuliza ninakwenda wapi bila shaka.

Akili mbele tu, nikaingia kwenye kumbi hiyo na moja kwa moja kuelekea kaunta kupombeka. Aloo! Najua niliwavutia wengi waliokuwepo, nikafuatwa kabisa na baadhi ya wanawake ili wapate baraka kutoka kwangu, lakini sikuwa na muda nao. Nikakaa kitini na kuagiza kileo kikali, spirit yaani, na sikuwa na mpango wa kuichanganyia na soda wala nini, yaani chupa nzima nilipanga kuinywa hadi iishe. Ndiyo nilikuwa nimetoka tu kuimimina kwenye glasi kidogo pale niliposhikwa mkono kwa chini, na aliyenishika nilipomgeukia nikakuta ni Adelina.

"Wewe, JC... mambo gani haya?" akaniuliza kiumakini.

Nikabaki nikimtazama kwa umakini pia, na hatimaye nikamwambia, "Nakunywa kidogo. Kaa nikuagizie."

Akabaki kuniangalia kwa kukereka, nami nikavuta glasi yenye kileo na kuishusha yote kooni kwa kishindo. Ilikuwa kali! Nikatulia kwa sekunde chache nikisikilizia hilo pigo, kisha nikatulia na kumwita bartender, mwanamke mtu mzima ila matata.

"Mpe huyu yoyote anayotaka," nikamwambia huku nikimshika Adelina begani.

Adelina akautoa mkono wangu begani kwake na kumwambia mwanamke huyo, "Sitaki chochote."

Mwanamke huyo akabaki kututazama.

Nikiwa nimeshamimina kinywaji tena, nikasema, "Kama hutaki kunywa agiza msosi ule."

Adelina akabaki kuniangalia kwa mkazo.

"Au ulikula kwa Ankia?" nikamuuliza.

Tayari divai ilikuwa imeanza kunikoroga vyema, naye Adelina akasema, "Kwa hiyo muda wote nimekusemesha kwenye gari ulikuwa husikii? Ulitaka kuja kuongelea bar?"

Nikapuuzia swali lake na kupachika goli la pili la pombe hiyo kali balaa.

"JC mbona unakuwa hivi? Nikuache tu si ndiyo?" Adelina akasema.

"Hamna... kaa unywe," nikaongea kilevi.

"Hebu twende JC..."

Adelina akajaribu kunivuta lakini nikamwekea mgomo.

"Tabia si nzuri hii, kulewa haitasaidia lolote. Unajidanganya ukifikiri ndiyo itasuluhisha matatizo yako..." akaniambia hivyo.

"Hamna... ila inayapunguza," nikamwambia hivyo na kutabasamu.

"Hakuna! Unayaongeza tu na unajiumiza. Hebu acha," akaongea kwa hisia kali.

"Adelina nenda ukalale... matatizo... matatizo yangu... hayakuhusu..." nikamwambia hivyo.

Nikaongeza pombe na kutaka kunywa tena, hapo wenge zito kichwani likiwa limeshaniteka, lakini Adelina akaikwapua glasi hiyo na kuiweka pembeni kwa hasira.

Akamwita bartender na kutoa hela yake mwenyewe kumpatia. "Shi'ngapi hiyo?" akamuuliza.

Nikacheka kilegevu, na baada ya kuambiwa bei Adelina akalipia na kisha kunishika mkono kwa nguvu.

"JC nyanyuka," Adelina akaniambia.

"Sijamaliza kilichoni...."

"Nimesema twende!" akanikatisha kwa kunikaripia.

Nikautoa mkono wangu kutoka kwake kwa nguvu sana na kusema kwa hasira, "Niache bana! We' vipi?!"

Niliuvuta mkono wangu kwa njia iliyosababisha Adelina aweweseke kunielekea, na ikawa kama vile nimemsukumia upande wa kaunta nusu ajipige hapo. Kuna watu najua walianza kututazama sana, hata bartender, naye Adelina akaniangalia usoni kwa kutatizika. Nikapatwa na hisia mbaya baada ya kutambua nilichofanya, na mwanamke huyu akaangalia tu chini kwa ufupi, kisha akaniwekea funguo za gari langu ndani ya mfuko wa suruali na kuanza kuondoka sehemu hiyo. Aliondoka huku nikimtazama bila kuacha, nami nikarudiwa na utambuzi ulionifanya nitoke hapo pia ili niwahi kumfata.

Pombe niliyokunywa kabla sijaenda kwa Miryam kujumuisha na hii ya sasa ilifanya nihisi kulewa hata zaidi, kwa hiyo nguvu mwilini ilivutwa. Lakini nikajitahidi kutoka na kuanza kuelekea kule nilikoliona gari langu, na kwa hakika sikuweza kumwona Adelina upande huo. Nilipoangaza huko na kule, nikamwona mwanamke huyo akielekea sehemu ambayo angesimama ili kungoja daladala, na kiukweli hisia mbaya zikazidi kunipata. Sikumtendea kwa heshima. Akafika hiyo sehemu na kusimama pamoja na watu wengine, nami nikaelekeza hatua zangu huko kumfuata. Nilipomkaribia, aliniangalia kwa njia ya kawaida tu, hivyo nikajitahidi kuuweka utimamu kisawasawa ili nisiongee pumba na kumwomba samahani kwa kilichotokea.

"Adelina..."

Akanyanyua kiganja chake kwa chini kama kunizuia nisiendelee, halafu akatazama upande mwingine kuonyesha namna gani alikwazika.

"Adelina samahani... sija...." nikakosa hata cha kusema.

Inaonekana gari alilokuwa akilingojea likawa limefika, naye akaashiria kutaka kulifata lakini nikamshika mkono ili nimzuie.

"Adelina please... nisikilize..." nikamwomba.

"Niachie bwana JC..." akaniambia hivyo kwa kuudhika.

Konda alikuwa akisubiria tupande kwa kuona nyendo za Adelina, lakini nikamwambia, "Hatuendi bro. Tembea."

"Hauendi wewe, me naenda," Adelina akasema hivyo na kujaribu kuutoa mkono wangu kwake.

"No, hauwezi... bro tembeeni tu," nikasema hivyo nikiendelea kuukaza mkono wa Adelina.

Konda alikuwa akinitazama kwa hasira, eti namkosesha buku, na dereva wake akampigia kelele waondoke upesi, hivyo wakatuacha hapo nikimshikilia rafiki yangu bado.

"JC ni nini lakini? Si umeniambia nikuache, unataka nini?" Adelina akaongea kwa hisia.

"Nis.. nisamehe, samahani, unajua... unajua..." nikaishia tu hapo kwa kubabaika.

Akabaki kuniangalia kwa mkazo.

"Tafadhali... naomba uniendeshe. Ni.. siwezi ku... kuendesha ma... sisemi hauna budi, ni makosa yangu... najua... ila...."

Adelina akapiga ulimi kwa kuudhika na kisha kunishika mkononi, naye akaanza kuelekea upande tuliotoka kwa njia ya kunivuta. Na pombe juu lakini mpaka nilihisi aibu. Alinishika hivyo ili kuhakikisha tunavuka barabara kwa usalama, na baada ya kuvuka moja kwa moja tukaelekea kwenye gari langu. Nikampatia funguo, kisha tukaingia na safari kuanza.

Sikujaribu tena kumsemesha kwa kuwa niliona bado aliudhika. Na tena pombe yangu kichwani haikuwa nzito kunisahaulisha mambo kivile, lakini wenge nililohisi likanifanya hadi nisahau simu yangu ilikuwa wapi. Ndiyo nikamuuliza Adelina, nikimwambia mara mbili kwamba nimeimisi simu yangu, lakini wakati huu ikawa ni zamu yake kuninyamazia. Dah! Haya bwana. Nikaona nisitoe kero zaidi, kwa sababu wakati huu mimi ndiye niliyekuwa mkosaji. Nikatulia tu kwenye siti nisijue tulikoelekea.

β˜…β˜…

Mwendo ulikuwa mrefu kiasi, na kuna mara ambazo ningetazama nje na kutambua kwamba tupo Kimara, Temboni, kuelekea kituo cha mabasi cha Magufuli Mbezi. Pindi nyingi tulisimama sana kutokana na msongamano, na baada ya muda ulioonekana kuwa mrefu tukaingia eneo lililoiacha lami na kusonga kwa dakika chache, kisha gari likatulia. Kichwani pombe ilikuwa imeanza kufifia ingawa bado wenge lilikuwepo, na nikaona Adelina akitoka ndani ya gari. Kuangalia mbele lilikuwa geti lisilopakwa rangi, likiwa la uchuma yaani, naye akaingia hapo na kisha kuanza kulifungua lote kutokea ndani. Sikujua ikiwa hapa palikuwa kwake ama vipi, lakini akarejea tena kwenye gari na kuliingiza ndani, kisha akashuka tena. Hakutaka kunisemesha kabisa.

Bwana, nikajiongeza tu na mipombe yangu kushuka pia, na yeye akiwa ndiyo anamalizia kulifunga geti. Nikapatazama hapo kuyaelewa mazingira, na mbele yangu ilikuwa ni nyumba yenye ukubwa mkubwa kiasi, iliyoonekana kuwa ya kupangisha watu. Millango kwa nje ilikuwa kwa pande mbili, hivyo nikafikiria lazima kuwe na mpangaji mwingine tofauti na Adelina hapo. Moja kwa moja nikaelewa huku palikuwa Kinyerezi, ambako mara nyingi mwanamke huyu alinisisitiza nije kumtembelea, na ni jambo ambalo nilikuwa nikimwahidi kufanya bila kulitimiza. Ona sasa mazingira yaliyokuwa yamefanya nikafika kwake kwa mara ya kwanza! Yalikuwa mabaya, na hilo likanitia huzuni.

Kumwangalia, Adelina akaja niliposimama na kunishika mkononi, naye akaanza kunielekeza kuelekea mlango ambao bila shaka ulikuwa wa ndani alikoishi yeye. Sikuwa na namna ila kuwa mtiifu tu, na aliponiachia ili anitangulie nikawa namfuata taratibu hadi alipofikia sehemu yenye ngazi kama mbili hivi, kisha akaufungua mlango huo. Sikujua ilikuwa saa ngapi, ila palikuwa kimya kweli kuzungukia eneo lote kutokea huko nje. Alipoufungua mlango akanishika tena mkono kunikaribisha ndani bila maneno, nami nikainama na mapombe yangu ili nifanye ustaarabu wa kuvua viatu kwanza.

"A-ah, usivue. Ingia tu."

Akanisemesha hatimaye. Nikasimama vizuri na kumtazama, naye akageuka na kuingia ndani kwa kusimama usawa wa mlango, halafu akawasha taa na kuendelea kusimama hapo hapo kama kusubiri nipite. Haikuwa na neno, nikapita. Ndani hapo palikuwa simple tu, masofa matatu ya samawati marefu na mazuri aliyoyapanga kwa kuzungukia kuta, zulia safi na laini chini, nikaona na friji, kiyoyozi cha juu na cha kuongoza kwa mkono pembeni, pamoja na TV pana ya flat screen, bufa, king'amuzi, na vitu-vitu vingine. Kulikuwa na mlango upande wa kushoto ambao ulikuwa wa jikoni, na upande wa kulia chumbani kwake bila shaka. Nikasimama hapo kati nikimwangalia Adelina alipokuwa akimalizia kufunga mlango vizuri, kisha akasogea mbele yangu na kuniangalia machoni.

"Unasikia njaa?" akaniuliza hivyo.

Nikatikisa kichwa kukanusha.

Yeye pia akatikisa kichwa mara moja na kuangalia pembeni, kisha akasema, "Sawa. Itabidi ulale hapo hivi, kwenye sofa, maana... kitanda ni kimo...."

"Haina shida Adelina," nikamkatisha.

Akiwa hataki kunitazama bado, akasema, "Sawa, basi... me naenda kulala. Upumzike pia, hapa hamna mbu... ukitaka nikuwashie na fe..."

"Adelina..." nikamwita kwa upole.

Akaacha kuongea na kunitazama kichini, si machoni.

Nikamwambia, "Adelina naomba unisamehe."

Akasema, "Ah, usijali JC, yashapita hayo achana nayo. Wote tumechoka kwa hiyo... usiku mwema..."

Alitaka na kuondoka lakini nikaushika mkono wake na kumgeuzia kwangu kwa nguvu kiasi, naye akatulia.

Nikiwa namwangalia kwa kujali, nikasema, "Adelina niangalie."

Macho yake hayakuwa mbali sana kuyafikia yangu sababu ya urefu wa mwili wake, lakini bado akaendelea tu kuniangalia kichini. Nikatumia kiganja changu kulishika shavu lake taratibu, naye ndiyo akanitazama machoni hatimaye.

"Nisamehe," nikaongea kwa upole na macho yangu lege.

Adelina hakutoa jibu kwa maneno na kuendelea kuniangalia tu, na kisha matendo yake ndiyo yakaongea. Akapitisha mikono yake kufikia mgongoni kwangu na kunikumbatia taratibu, akiusugua taratibu kama kuniambia nisijali, nami nikapata ahueni moyoni. Nikalirudisha kumbatio hilo na kisha kumwachia, nikimtazama usoni kwa uthamini. Tukiwa tumekaribiana zaidi namna hiyo, tukabaki kuangaliana kwa njia fulani ya subira; mimi nikingoja aseme jambo fulani, na nisijue yeye akingoja nini. Lakini kungoja kwangu aseme jambo fulani kukabadilika ghafla kutokana na kuanza kupatwa na hisia kumwelekea mwanamke huyu. Sikuwahi kumtazama Adelina kwa njia hii, ya hisia, ila sasa ikawepo. Sijui ni pombe tu, au ilikuwa moyo kabisa?

Nadhani hali ikawa namna hiyo hiyo hata kwake pia, kwa sababu baada ya kuangaliana kihivyo, nikahisi mkono wake ukipita ubavuni kwangu na kufanya kama kuishika T-shirt niliyovaa kwa kuivuta fulani hivi, nami nikauangalia mkono wake. Niliporudisha macho yangu usoni kwake, wakati huu ukawa tofauti na jinsi ulivyokuwa awali; si wa kuudhika tena, bali wa hisia. Ah! Hee. Ujumbe ukawa delivadi. Mimi nikiwa mzee wa kupandisha mizuka, sikuchelewa. Huko chini nikaanza kunyanyuka, kwa nguvu hatari, na hali hii ikaniongezea hamu ya kutaka jambo hili liendelee. Tukiwa bado tunatazamana kwa ukaribu, na Adelina akinishikilia ubavuni bado, nikajikuta naifuata midomo yake papo hapo na kuanza kuipiga busu. Mluzi!





β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

ITAENDELEA

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…


Whatsapp +255 678 017 280
Festo kama kawaida yake...jamaa ni mpole sana mbele za watu πŸ˜‚ ila kumbe mafia wa kuogopwa
Sema Mimi buana πŸ’”πŸŒ
 
MIMI NA MIMI 3

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Siri, Tamaa, Hila, Usaliti, Ukatili, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

SEHEMU YA TANO

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…



Niliishiwa pozi. Huyo ndiye mgeni mwenye Range ambaye Shadya alisema amefika hapo? Kwa nini sikuwaza kabisa kwamba ingeweza kuwa yeye? Festo alifikaje huku wakati kama huu, na alikuja kwa dhumuni lipi? Ilinishtua kwa kweli, kwa sababu ni kwa wakati mwafaka kabisa ambao mimi na Miryam tulikuwa tukipitia hali yenye kutatanisha ndiyo jamaa akawa amefika ghafla namna hiyo. Alijua kuhusu haya yaliyokuwa yanatokea? Yaani... sikuelewa.

Alitoka tu mlangoni hapo na kusimama nyuma yake Bi Jamila na Bi Zawadi, nasi tukabaki kutazamana usoni kwa macho yaliyofahamiana vyema sana. Alikuwa amevalia kwa njia nadhifu, asiwe na utofauti wowote kutoka kwa jinsi nilivyomkumbuka kimwonekano. Nikaacha kumwangalia na kutazama pembeni kwanza, nikiwa najaribu kuusoma mchezo uliokuwepo hapa, kisha nikamwangalia Miryam usoni tena. Alitulia tu na kunitazama kama vile kusubiri niseme lolote lile ili nimwondolee kero, na ni kitu kilichonivunja sana moyo. Kwamba nilihisi ameanza kuniona kuwa kero. Wote hapo nje walitulia kimya tu, wakitutazama mimi na bibie kungoja drama.

Kwa sauti tulivu, nikamuuliza Miryam, "Umepoteza simu?"

Akabaki kuniangalia kama vile hataki kujibu.

"Kwa nini haukuja?" nikamuuliza.

"Wapi?" akaniuliza.

"Najua umeziona sms zangu zote. Kwa nini haukujibu? Na kwa nini haukuja?" nikamuuliza pia.

"Nina mambo mengi," akanijibu hivyo.

"Mmm... kwa hiyo kama usingekuwa na mambo mengi ungekuja?"

"Labda," akajibu kibaridi.

"Okay. Nimekurahisishia kazi basi. Nimeona nikufate me mwenyewe. Twende nje tukaongee," nikamwambia hivyo.

"Hatuna chochote cha kuongelea," akasema hivyo.

"Kabisa?"

"Kabisa."

"Kwa hiyo... kila kitu kiko poa?"

"Yeah, kila kitu kiko poa."

Nikatulia kidogo nikimtazamaaa, kisha nikamuuliza, "Unapofanya haya unayoyafanya Miryam, unakuwa unamaanisha nini?"

"Simaanishi chochote. Na sijafanya lolote. Ni wewe tu ndiyo umebaki kulazimisha vitu visivyowezekana," akaniambia hivyo.

"Visivyowezekana kivipi? Miryam mimi na wewe hatuja-share damu, na haya yote hakuna ambaye angeweza kuyaona...."

"Jayden, inatosha. Hakuna lolote ambalo utasema wala kufanya litabadili hali," akanikatisha.

"Hali ipi? Kweli unataka kusema kwa sababu tu tumejua kuna uhusiano wa kifamilia basi ndiyo ifute kila kitu ambacho mimi na wewe tumepitia? Eh? Kila kitu ambacho tumefanya?" nikamuuliza kwa hisia.

Akabaki kuniangalia kwa hisia makini.

Bi Jamila akasema, "JC mwanangu, tutafute muda, au mtafute muda mwingine mzuri wa kuongelea haya mambo kwa sababu huu siyo wakati mzuri."

"Nini, kwa sababu Festo amekuja?" nikamuuliza.

Wote wakabaki kimya, huku jamaa akiwa ananiangalia kwa utulivu pale nyuma.

"Ahah, Miryam bana! Kwa hiyo, una mambo mengi, huwezi kukutana nami, ila kupanda Range za watu kuzurura mpaka usiku ndo' unaweza..." nikamwambia hivyo.

Akabaki kuniangalia tu kwa mkazo.

"Kwa hiyo kilichokuwa kinakufanya uwe bize eti, ni kutafuta... backup plan ya kumwondoa JC kwenye taswira, si ndiyo? Umemwita na huyu jamaa ili akusaidie kunipotezea, au?" nikamuuliza Miryam.

"JC, acha kuongea hivyo," Bi Zawadi akaniambia.

"Amekunywa huyu," Shadya akasema.

"JC, twende huku ndani basi...." Ankia akajaribu kunisemesha na kunishika, lakini nikauondoa mkono wake kwangu taratibu.

Nikamsogelea Miryam karibu zaidi na kumwambia, "Mimi, come on... let's talk about this, eti? Just me and you."

Nilimsemesha kwa kubembeleza na kuishika mikono yake, lakini akaitoa taratibu mwilini mwake na kuniambia, "Hakuna lolote limebaki la kuzungumzia, Jayden. Jinsi mambo yalivyo ndiyo yanapaswa kuwa hivyo hivyo. Naomba uende nyumbani."

Nilibaki nikimwangalia kwa kutoamini yaani, kwa kuwa maneno yake yalituma maana fulani kwangu ambayo bado sikutaka kukubaliana nayo. Akafumba macho kiufupi, kisha akageuka na kutaka kurejea ndani, lakini nikauwahi mkono wake na kumgeuzia kwangu kwa kasi.

"Miryam..." nikamwita kwa hisia.

"Jayden, niachie..." akaniambia hivyo.

"Unamaanisha nini? Hm? Nini, kwamba mimi na wewe ndiyo basi, au?" nikamuuliza.

Shadya akasema, "Tumeshagundua kwamba nyie ni ndugu JC... kuendeleza mahusiano haita...."

"Shangazi..." Tesha akamwita kama kumzuia asiendelee kuongea.

Festo akasema, "JC, tuliza hisia. Haya mambo mnaweza...."

"Kaa kimya, Festo! Hayakuhusu!" nikamwambia hivyo kwa hisia kali na kumnyooshea kidole.

"Eh, Mungu wangu!" Bi Zawadi akasema hivyo.

Festo alibaki kuniangalia kwa utulivu tu, mimi hapo nikiwa nimeshapandwa na mzuka yaani kama angeleta ujinga wake nisingesubiri kuvuruga hali ya hewa.

Miryam akautoa mkono wake kwangu na kusema, "Jayden, sitaki malumbano sasa hivi. Nimekwambia uondoke."

"Siondoki mpaka ieleweke una tatizo gani Miryam. Kwa nini hutaki tukae tuzungumze kuhusu hili jambo? Kunikwepa ndiyo itasuluhisha lolote linalofanya unione kuwa kama kero sasa hivi, ama?" nikamuuliza kwa hisia.

"Jayden, familia zetu zinaingiliana. Hatuwezi kuendelea kuwa karibu tena! Ni kipi ambacho huelewi na unahitaji kuzungumzia zaidi, eh?" Miryam akanisemesha kwa uthabiti.

"Miryam suala la familia zetu kujuana haliondoi uhusiano tuliojenga kufikia sasa. Hata kama damu zetu zingekuwa zinaingiliana, hiyo haimaanishi tungeacha kupendana, kwa sababu tulikuwa tumeshapendana kabla hatujajua hilo..."

"Hivi Jayden, unaelewa unachokiongea kweli?" akaniuliza.

"Sijui, labda we' ndiyo unieleweshe..." nikamwambia.

"Tesha na Mariam ni wadogo zetu. Mimi na wewe hatuwezi kuwa kitu kimoja kwa kuwa tuna damu zao ndani ya mishipa yetu. Unataka tuendekeze ubinafsi na kufumbia jicho jambo zito kama hilo?" Miryam akaongea kwa hisia.

"Tatizo ni hilo kweli Miryam, au basi tu unataka tuanze kuzungushana mpaka tufike pasikofikiwa? Ikiwa tusingejua kuhusu haya mpaka tunafunga ndoa, ingetuzuia kuendelea kupendana eti tu kwa sababu tumechangia uzazi kwa wadogo zetu?" nikamuuliza.

"Lakini Jayden, kwa nini unakuwa huelewi?" Miryam akaongea kwa hisia.

"Shida siyo suala la undugu Miryam, kuna kitu kingine tu kinakusumbua mpaka ufanye haya. Una tatizo gani? Kwa nini hutaki kuniambia? Kwa nini unakuwa hivi?" nikamuuliza kwa hisia mpaka machozi yakaanza kunivizia.

Akawa ananitazama kwa hisia huku akipumua kwa nguvu.

"Niambie. Nini kinakusumbua?" nikamuuliza.

Akakaza hisia zake zaidi, naye akasema, "Siwezi tena Jayden. Yote... yote tuliyofanya... nikifikiria tu ukweli kwamba tumefanya mengi endapo kama... kama mimi na wewe tungekuwa ndugu wa damu kweli... ingekuwaje?"

Nikabaki nikimtazama kwa huzuni na kutikisa kichwa.

"Hili jambo siyo dogo. Tungeweza kuwashawishi wengine namna tunavyoelewana haijalishi ni namna gani nimekuacha kiumri, lakini sasa hivi tutawashawishi vipi waelewe...."

"Miryam, kwa nini ujali kuhusu watu...."

"... waelewe mahusiano yetu, no Jayden, usipuuzie ukweli kwamba mahusiano yangu me na wewe yanawaathiri watu wengine pia ndani ya familia zetu. Tutajenga suto kubwa ambayo sidhani kama niko tayari kuibeba," akaongea kwa hisia.

"Nilikwambia nini kuhusu wewe kubeba kila kitu mwenyewe? Hili siyo pambano lako pekee, Miryam, niko nawe, niko kando yako, kwa lolote lile tutakalo-face, itakuwa ni sisi wawili, kwa pamoja...."

Akawa anatikisa kichwa kukataa.

"... mpaka tutashinda. Miryam... Miryam..."

Nikamsogelea karibu zaidi na kumshika shingoni, lakini akajirudisha nyuma.

"Mi.... ah, Miryam nashindwa kuelewa... unataka nini? Tutaondoka ukitaka, sawa? Tutaenda mbali ikiwa hutaki ku...."

"Jayden, hapana. Hii imeshakuwa too much. Tumeshajaribu mengi, lakini nimeona... na wewe umeshaona kabisa kwamba... labda me na wewe hatujapangiwa kuwa pamoja. Labda fate zetu haziendani, na hizi ndiyo ishara..." akaniambia.

"Oh, God..." nikanena hivyo kwa huzuni.

"Inabidi tu tulikubali hilo. Unanielewa?" akaniambia.

Nikamtazama machoni kwa mkazo.

Akajifuta machozi upesi kwa uimara na kusema, "Naomba uende nyumbani. Familia yangu imeshakuwa na rep ya kutosha kutengeneza drama hapa nje, imetosha. Nenda Jayden."

Nikaendelea kumwangalia tu, yaani kama vile sijasikia yote aliyotoka kusema.

Ankia akanisogelea na kusema, "JC... hebu twende."

"Halafu nini?" nikamuuliza Miryam hivyo.

Miryam na wengine wakaendelea kunitazama tu.

"Niende nyumbani, halafu nini? Nisahau kila kitu? Ni... nikusahau Miryam?" nikamuuliza hivyo.

Miryam akabaki kimya tu.

"Unajua Miryam vitu vingine siyo vya kuongelea juu juu tu bila kufikiria. Unaposema imekuwa too much kwako kupokea maumivu wakati hujajipa muda wa kuya-face pamoja nami, wewe ndiyo unakuwa mbinafsi. Unafikiri kila kitu utabeba wewe tu, hujafikiria kwamba hili pia linaniathiri mimi? Lakini uko shuta kweli kunitolea.... eti unaniambia niondoke... niondoke? Unataka nikuache Miryam? Kweli umeshalifikiria hilo vizuri kabisa, au ni pressure tu ndiyo inakufanya uongee hivyo?" nikamuuliza.

"Unataka niseme nini, Jayden?" Miryam akaniuliza kwa mkazo.

"Nataka useme kwamba unanipenda," nikamwambia hivyo kwa uhakika.

Akabaki kuniangalia kwa hisia.

"Nataka useme kwamba unanihitaji, kwamba hutaki niende... kwamba unajua nikiondoka hautakuwa na furaha tena, kwa sababu unajua moyo wako utafunga... na itakuwa ni milele," nikamwambia hivyo kwa hisia.

Miryam akadondosha chozi na kulifuta haraka, huku wengine wakiwa bado wanatazama igizo hili lililozidi kuwa zito sana, naye akajikaza na kuniangalia kwa uimara, kisha akasema, "Hayo mambo hayawezekani tena."

Nikatikisa kichwa kwa huzuni na kupiga ulimi mdomoni.

"Na wala usijali kuhusu moyo wangu. Utapata tu mwingine wa kupenda," akaniambia hivyo.

"Ohh please... wewe Miryam? Umpende nani mwingine, huh? Huyu?" nikaongea kwa hisia kali huku nikimnyooshea kidole Festo.

"JC..." Ankia akaniita kwa upole.

"Huyu ndiyo mtu unayefikiri unaweza kumpenda?" nikamuuliza Miryam kwa mkazo.

Miryam akasema, "Ndiyo."

Nikamwangalia machoni. Hata na wengine wakamtazama Miryam baada ya yeye kusema hivyo.

"Nitampenda yeye," Miryam akaniambia hivyo.

Mkono niliokuwa nimeunyoosha kumwelekea Festo ukashuka taratibu, baada ya kuhisi kitu kikali kikiwa kimeuchoma moyo wangu kutokana na kusikia maneno ya Miryam. Sikuamini yaani. Yaani alikuwa kabisa ametoka kuniambia kwamba atampenda Festo badala yangu? Alinimaliza! Nikaangalia chini nikiwa nimeishiwa pozi hata zaidi, na chozi nililojitahidi kuzuia lisitiririke likanitoka.

"Dah! JC, kaka nisikilize..." Tesha akanisemesha hivyo.

"JC... Mimi..." Bi Zawadi akasikika pia akituita.

Nikamtazama Miryam usoni na kuona alivyokuwa akiniangalia kwa huzuni, machozi akijitahidi kuyazuia, nami nikamwambia, "Unajua Miryam... yaani ingekuwa bora kama ungenikata-kata kwa mapanga kuliko kuniambia hivyo. Ulichokisema... kwangu ni kibaya kuliko hata kifo!"

"We' JC wewe!" Shadya akasema hivyo.

"JC... acha kuongea hivyo. Hey... nakuomba uje nasi," Adelina akanisemesha hivyo hatimaye na kunishika mkononi.

"JC... hebu twende," Ankia naye akaniambia hivyo.

Miryam aliendelea kunitazama tu kwa njia imara, nami nikamwangalia Festo pale nyuma yake. Mwanaume huyo alinitazama kwa umakini, akijifanya mtulivu tu wakati bado sikuwa nimesahau rangi zake zote alizokuwa nazo, lakini kwa wakati huu sikuona uhitaji tena wa kuendelea kulazimisha mambo hapo. Miryam alikuwa ameusema uamuzi wake mpya, tena hadharani, na mimi sikuwa sehemu ya huo uamuzi hata chembe. Nilikuwa nafanya nini hapa?

Nikageuka hapo hapo na kuanza kuelekea upande wa geti, Ankia na Adelina wakija nyuma yangu, na kuna baadhi ya watu waliokuwa wamesimama sehemu hiyo, wakinipisha nilipojitoa getini hapo. Yaani sikutaka kujali tena yaliyoendelea pale, moyo wangu ulikuwa umevunjika sana baada ya mwanamke huyo kuniambia yale maneno. Nilipofika nje sikwenda garini, bali nikaelekea kwenye nyumba ya Ankia mpaka kule ndani kwake. Nadhani wanawake hawa walifikiri nilitaka kwenda kukaa nao na kuzungumza kidogo, lakini mie nikakielekea chumba nilichokuwa natumia hapo na kuanza kuzitoa nguo zangu kabatini, upesi nikizishindilia ndani ya begi. Najua walikuwa nyuma yangu wakinitazama, na ni Ankia ndiye akaanza kunisemesha.

"JC, mbona unapaki nguo?" akaniuliza hivyo.

Sikujibu. Nikaendelea tu mpaka nikamaliza na kulifunga begi.

Akaendelea kusema, "Tukae basi kwanza tuongee, eh? Najua unaumia lakini nakuomba kwanza... ukae... JC..."

Nikawa nimeshalibeba begi na kuanza kuelekea mlangoni, nami nikasimama na kuwatazama kwa njia iliyowapa ujumbe kuwa nilihitaji wanipishe ili niondoke.

"JC, sikiliza. Tuongee kwanza, eti? Weka begi chini tuongee," Ankia akaniambia hivyo.

Nikatikisa kichwa kukataa, nami nikataka kupita katikati yao kwa lazima. Lakini Adelina akaweka kiganja chake kifuani kwangu kunizuia, nami nikamtazama machoni kwa hisia za mkazo.

"Siyo salama kwako kuendesha ukiwa umekunywa JC. Nitakuja na wewe," Adelina akaniambia hivyo.

"Adela..." Ankia akamwita kama kumzuia.

"Nipe funguo, nitaendesha," Adelina akaniambia hivyo.

Nikamtazama kwa hisia makini kwanza, nami nikasema, "Nimefika hapa bila shida. Nitarudi hivyo hivyo."

"Hapana JC. Siwezi kukubali uendeshe ukiwa namna hii. Nipe funguo," Adelina akaniongelesha kwa ustaarabu thabiti.

Nikiwa sitaki kuvurugwa zaidi, na kwa heshima niliyokuwa nayo kumwelekea, nikatoa tu funguo mfukoni na kumpatia, kisha nikawapita bila kusema lolote na kuelekea huko nje.

Nikamsikia Ankia akisema, "Lakini Adela, tulikuwa hata hatuja...."

"Haina shida Ankia, nitamsindikiza tu halafu nitaenda kwangu pia. Anahitaji kupumzika, lakini nataka kuhakikisha anafika salama," Adelina akasema hivyo.

Nikatoka hapo ndani na kwenda mpaka garini kwangu, bado watu wakiwepo sehemu hiyo ya nje, nami nikaingia tu na kutupia begi langu siti za nyuma. Nikiwa nimeketi siti ya pembeni na usukani, nilikuwa nikiitazama nyumba yake Miryam kwa mkazo sana, nikimwona Tesha anakuja sehemu ya hapo nje na kusimama pamoja na vijana kama wawili-watatu hivi, ambao walionekana kuongea na kuelekeza macho yao upande wa gari langu. Adelina akaja mpaka ndani ya gari langu na kuingia kwenye usukani, naye akaniangalia kwa ufupi usoni. Nikiwa nataka tu kuondoka eneo hili, nikatulia na kufumba macho nisisubiri kingine zaidi. Gari likawaka, na mwanamke huyu akaniondoa taratibu eneo hilo lililokuwa limeniacha na majonzi mengi moyoni mwangu.

β˜…β˜…

Adelina akaniendesha kwa mwendo usio wa haraka kabisa, na mwanamke huyu mtulivu alikuwa akijaribu kunisemesha mara kadhaa kuhusu hali yangu, lakini sikumjibu hata kidogo. Nilikuwa ndani ya hisia mbaya sana kiasi kwamba sikujua tunaenda wapi na sikujibu hata aliponiuliza uelekeo aliopaswa kupita ili anifikishe kwangu. Na kiukweli sikumtendea haki dada wa watu, maana alichokuwa akifanya ni kujitahidi tu kunisaidia. Lakini mawazo na hisia zangu hazikuwa mahala sahihi kwa pindi hii, nilivurugwa ile mbaya. Yaani nilihisi hasira kali mno kwa maneno ambayo Miryam aliyasema mbele ya kila mtu. Eti ingekuwa afadhali ampende Festo na si mimi? Ningeweza kuua mtu aisee, na sikudhani ningewahi kuwaza kufanya hivyo.

Kuna mahali tukafika, barabarani, na askari wa usalama kwa eneo hilo akatusimamisha. Ilikuwa ni kuchekiwa tu kwa gari na mwendeshaji, na Adelina alionyesha leseni yake na kufanya maongezi mafupi na askari huyo, kisha akatuachia tusonge mbele. Kiukweli alikuwa amenisaidia sana maana endapo kama ningeshikwa naendesha huku nimelewa ingekuwa kujitia hatiani. Ila bado nilikuwa kwenye hisia za kutojali, na Adelina aliendelea kujaribu kunisemesha bila kupata itikio lolote. Ikafikia hatua akasimamisha gari eneo moja, na kuliangalia nikatambua palikuwa kwenye barabara iliyoelekea Kimara.

Adelina akanishika begani na kuniambia ninavyokaa kimya inamkosesha amani sana, na ile nimemwangalia tu, niliona sura yenye kujali sana ya mwanamke huyu ilivyokuwa ikinitazama, lakini umakini wangu ukawa huko nje zaidi. Niliona jengo lenye kumbi ya starehe na baa ya vinywaji, nami bila kusema lolote, nikafungua mlango na kutoka ndani ya gari. Nikavuka barabara na kwenda huko bila kujali kuangalia kushoto wala kulia, nikimwacha Adelina anajiuliza ninakwenda wapi bila shaka.

Akili mbele tu, nikaingia kwenye kumbi hiyo na moja kwa moja kuelekea kaunta kupombeka. Aloo! Najua niliwavutia wengi waliokuwepo, nikafuatwa kabisa na baadhi ya wanawake ili wapate baraka kutoka kwangu, lakini sikuwa na muda nao. Nikakaa kitini na kuagiza kileo kikali, spirit yaani, na sikuwa na mpango wa kuichanganyia na soda wala nini, yaani chupa nzima nilipanga kuinywa hadi iishe. Ndiyo nilikuwa nimetoka tu kuimimina kwenye glasi kidogo pale niliposhikwa mkono kwa chini, na aliyenishika nilipomgeukia nikakuta ni Adelina.

"Wewe, JC... mambo gani haya?" akaniuliza kiumakini.

Nikabaki nikimtazama kwa umakini pia, na hatimaye nikamwambia, "Nakunywa kidogo. Kaa nikuagizie."

Akabaki kuniangalia kwa kukereka, nami nikavuta glasi yenye kileo na kuishusha yote kooni kwa kishindo. Ilikuwa kali! Nikatulia kwa sekunde chache nikisikilizia hilo pigo, kisha nikatulia na kumwita bartender, mwanamke mtu mzima ila matata.

"Mpe huyu yoyote anayotaka," nikamwambia huku nikimshika Adelina begani.

Adelina akautoa mkono wangu begani kwake na kumwambia mwanamke huyo, "Sitaki chochote."

Mwanamke huyo akabaki kututazama.

Nikiwa nimeshamimina kinywaji tena, nikasema, "Kama hutaki kunywa agiza msosi ule."

Adelina akabaki kuniangalia kwa mkazo.

"Au ulikula kwa Ankia?" nikamuuliza.

Tayari divai ilikuwa imeanza kunikoroga vyema, naye Adelina akasema, "Kwa hiyo muda wote nimekusemesha kwenye gari ulikuwa husikii? Ulitaka kuja kuongelea bar?"

Nikapuuzia swali lake na kupachika goli la pili la pombe hiyo kali balaa.

"JC mbona unakuwa hivi? Nikuache tu si ndiyo?" Adelina akasema.

"Hamna... kaa unywe," nikaongea kilevi.

"Hebu twende JC..."

Adelina akajaribu kunivuta lakini nikamwekea mgomo.

"Tabia si nzuri hii, kulewa haitasaidia lolote. Unajidanganya ukifikiri ndiyo itasuluhisha matatizo yako..." akaniambia hivyo.

"Hamna... ila inayapunguza," nikamwambia hivyo na kutabasamu.

"Hakuna! Unayaongeza tu na unajiumiza. Hebu acha," akaongea kwa hisia kali.

"Adelina nenda ukalale... matatizo... matatizo yangu... hayakuhusu..." nikamwambia hivyo.

Nikaongeza pombe na kutaka kunywa tena, hapo wenge zito kichwani likiwa limeshaniteka, lakini Adelina akaikwapua glasi hiyo na kuiweka pembeni kwa hasira.

Akamwita bartender na kutoa hela yake mwenyewe kumpatia. "Shi'ngapi hiyo?" akamuuliza.

Nikacheka kilegevu, na baada ya kuambiwa bei Adelina akalipia na kisha kunishika mkono kwa nguvu.

"JC nyanyuka," Adelina akaniambia.

"Sijamaliza kilichoni...."

"Nimesema twende!" akanikatisha kwa kunikaripia.

Nikautoa mkono wangu kutoka kwake kwa nguvu sana na kusema kwa hasira, "Niache bana! We' vipi?!"

Niliuvuta mkono wangu kwa njia iliyosababisha Adelina aweweseke kunielekea, na ikawa kama vile nimemsukumia upande wa kaunta nusu ajipige hapo. Kuna watu najua walianza kututazama sana, hata bartender, naye Adelina akaniangalia usoni kwa kutatizika. Nikapatwa na hisia mbaya baada ya kutambua nilichofanya, na mwanamke huyu akaangalia tu chini kwa ufupi, kisha akaniwekea funguo za gari langu ndani ya mfuko wa suruali na kuanza kuondoka sehemu hiyo. Aliondoka huku nikimtazama bila kuacha, nami nikarudiwa na utambuzi ulionifanya nitoke hapo pia ili niwahi kumfata.

Pombe niliyokunywa kabla sijaenda kwa Miryam kujumuisha na hii ya sasa ilifanya nihisi kulewa hata zaidi, kwa hiyo nguvu mwilini ilivutwa. Lakini nikajitahidi kutoka na kuanza kuelekea kule nilikoliona gari langu, na kwa hakika sikuweza kumwona Adelina upande huo. Nilipoangaza huko na kule, nikamwona mwanamke huyo akielekea sehemu ambayo angesimama ili kungoja daladala, na kiukweli hisia mbaya zikazidi kunipata. Sikumtendea kwa heshima. Akafika hiyo sehemu na kusimama pamoja na watu wengine, nami nikaelekeza hatua zangu huko kumfuata. Nilipomkaribia, aliniangalia kwa njia ya kawaida tu, hivyo nikajitahidi kuuweka utimamu kisawasawa ili nisiongee pumba na kumwomba samahani kwa kilichotokea.

"Adelina..."

Akanyanyua kiganja chake kwa chini kama kunizuia nisiendelee, halafu akatazama upande mwingine kuonyesha namna gani alikwazika.

"Adelina samahani... sija...." nikakosa hata cha kusema.

Inaonekana gari alilokuwa akilingojea likawa limefika, naye akaashiria kutaka kulifata lakini nikamshika mkono ili nimzuie.

"Adelina please... nisikilize..." nikamwomba.

"Niachie bwana JC..." akaniambia hivyo kwa kuudhika.

Konda alikuwa akisubiria tupande kwa kuona nyendo za Adelina, lakini nikamwambia, "Hatuendi bro. Tembea."

"Hauendi wewe, me naenda," Adelina akasema hivyo na kujaribu kuutoa mkono wangu kwake.

"No, hauwezi... bro tembeeni tu," nikasema hivyo nikiendelea kuukaza mkono wa Adelina.

Konda alikuwa akinitazama kwa hasira, eti namkosesha buku, na dereva wake akampigia kelele waondoke upesi, hivyo wakatuacha hapo nikimshikilia rafiki yangu bado.

"JC ni nini lakini? Si umeniambia nikuache, unataka nini?" Adelina akaongea kwa hisia.

"Nis.. nisamehe, samahani, unajua... unajua..." nikaishia tu hapo kwa kubabaika.

Akabaki kuniangalia kwa mkazo.

"Tafadhali... naomba uniendeshe. Ni.. siwezi ku... kuendesha ma... sisemi hauna budi, ni makosa yangu... najua... ila...."

Adelina akapiga ulimi kwa kuudhika na kisha kunishika mkononi, naye akaanza kuelekea upande tuliotoka kwa njia ya kunivuta. Na pombe juu lakini mpaka nilihisi aibu. Alinishika hivyo ili kuhakikisha tunavuka barabara kwa usalama, na baada ya kuvuka moja kwa moja tukaelekea kwenye gari langu. Nikampatia funguo, kisha tukaingia na safari kuanza.

Sikujaribu tena kumsemesha kwa kuwa niliona bado aliudhika. Na tena pombe yangu kichwani haikuwa nzito kunisahaulisha mambo kivile, lakini wenge nililohisi likanifanya hadi nisahau simu yangu ilikuwa wapi. Ndiyo nikamuuliza Adelina, nikimwambia mara mbili kwamba nimeimisi simu yangu, lakini wakati huu ikawa ni zamu yake kuninyamazia. Dah! Haya bwana. Nikaona nisitoe kero zaidi, kwa sababu wakati huu mimi ndiye niliyekuwa mkosaji. Nikatulia tu kwenye siti nisijue tulikoelekea.

β˜…β˜…

Mwendo ulikuwa mrefu kiasi, na kuna mara ambazo ningetazama nje na kutambua kwamba tupo Kimara, Temboni, kuelekea kituo cha mabasi cha Magufuli Mbezi. Pindi nyingi tulisimama sana kutokana na msongamano, na baada ya muda ulioonekana kuwa mrefu tukaingia eneo lililoiacha lami na kusonga kwa dakika chache, kisha gari likatulia. Kichwani pombe ilikuwa imeanza kufifia ingawa bado wenge lilikuwepo, na nikaona Adelina akitoka ndani ya gari. Kuangalia mbele lilikuwa geti lisilopakwa rangi, likiwa la uchuma yaani, naye akaingia hapo na kisha kuanza kulifungua lote kutokea ndani. Sikujua ikiwa hapa palikuwa kwake ama vipi, lakini akarejea tena kwenye gari na kuliingiza ndani, kisha akashuka tena. Hakutaka kunisemesha kabisa.

Bwana, nikajiongeza tu na mipombe yangu kushuka pia, na yeye akiwa ndiyo anamalizia kulifunga geti. Nikapatazama hapo kuyaelewa mazingira, na mbele yangu ilikuwa ni nyumba yenye ukubwa mkubwa kiasi, iliyoonekana kuwa ya kupangisha watu. Millango kwa nje ilikuwa kwa pande mbili, hivyo nikafikiria lazima kuwe na mpangaji mwingine tofauti na Adelina hapo. Moja kwa moja nikaelewa huku palikuwa Kinyerezi, ambako mara nyingi mwanamke huyu alinisisitiza nije kumtembelea, na ni jambo ambalo nilikuwa nikimwahidi kufanya bila kulitimiza. Ona sasa mazingira yaliyokuwa yamefanya nikafika kwake kwa mara ya kwanza! Yalikuwa mabaya, na hilo likanitia huzuni.

Kumwangalia, Adelina akaja niliposimama na kunishika mkononi, naye akaanza kunielekeza kuelekea mlango ambao bila shaka ulikuwa wa ndani alikoishi yeye. Sikuwa na namna ila kuwa mtiifu tu, na aliponiachia ili anitangulie nikawa namfuata taratibu hadi alipofikia sehemu yenye ngazi kama mbili hivi, kisha akaufungua mlango huo. Sikujua ilikuwa saa ngapi, ila palikuwa kimya kweli kuzungukia eneo lote kutokea huko nje. Alipoufungua mlango akanishika tena mkono kunikaribisha ndani bila maneno, nami nikainama na mapombe yangu ili nifanye ustaarabu wa kuvua viatu kwanza.

"A-ah, usivue. Ingia tu."

Akanisemesha hatimaye. Nikasimama vizuri na kumtazama, naye akageuka na kuingia ndani kwa kusimama usawa wa mlango, halafu akawasha taa na kuendelea kusimama hapo hapo kama kusubiri nipite. Haikuwa na neno, nikapita. Ndani hapo palikuwa simple tu, masofa matatu ya samawati marefu na mazuri aliyoyapanga kwa kuzungukia kuta, zulia safi na laini chini, nikaona na friji, kiyoyozi cha juu na cha kuongoza kwa mkono pembeni, pamoja na TV pana ya flat screen, bufa, king'amuzi, na vitu-vitu vingine. Kulikuwa na mlango upande wa kushoto ambao ulikuwa wa jikoni, na upande wa kulia chumbani kwake bila shaka. Nikasimama hapo kati nikimwangalia Adelina alipokuwa akimalizia kufunga mlango vizuri, kisha akasogea mbele yangu na kuniangalia machoni.

"Unasikia njaa?" akaniuliza hivyo.

Nikatikisa kichwa kukanusha.

Yeye pia akatikisa kichwa mara moja na kuangalia pembeni, kisha akasema, "Sawa. Itabidi ulale hapo hivi, kwenye sofa, maana... kitanda ni kimo...."

"Haina shida Adelina," nikamkatisha.

Akiwa hataki kunitazama bado, akasema, "Sawa, basi... me naenda kulala. Upumzike pia, hapa hamna mbu... ukitaka nikuwashie na fe..."

"Adelina..." nikamwita kwa upole.

Akaacha kuongea na kunitazama kichini, si machoni.

Nikamwambia, "Adelina naomba unisamehe."

Akasema, "Ah, usijali JC, yashapita hayo achana nayo. Wote tumechoka kwa hiyo... usiku mwema..."

Alitaka na kuondoka lakini nikaushika mkono wake na kumgeuzia kwangu kwa nguvu kiasi, naye akatulia.

Nikiwa namwangalia kwa kujali, nikasema, "Adelina niangalie."

Macho yake hayakuwa mbali sana kuyafikia yangu sababu ya urefu wa mwili wake, lakini bado akaendelea tu kuniangalia kichini. Nikatumia kiganja changu kulishika shavu lake taratibu, naye ndiyo akanitazama machoni hatimaye.

"Nisamehe," nikaongea kwa upole na macho yangu lege.

Adelina hakutoa jibu kwa maneno na kuendelea kuniangalia tu, na kisha matendo yake ndiyo yakaongea. Akapitisha mikono yake kufikia mgongoni kwangu na kunikumbatia taratibu, akiusugua taratibu kama kuniambia nisijali, nami nikapata ahueni moyoni. Nikalirudisha kumbatio hilo na kisha kumwachia, nikimtazama usoni kwa uthamini. Tukiwa tumekaribiana zaidi namna hiyo, tukabaki kuangaliana kwa njia fulani ya subira; mimi nikingoja aseme jambo fulani, na nisijue yeye akingoja nini. Lakini kungoja kwangu aseme jambo fulani kukabadilika ghafla kutokana na kuanza kupatwa na hisia kumwelekea mwanamke huyu. Sikuwahi kumtazama Adelina kwa njia hii, ya hisia, ila sasa ikawepo. Sijui ni pombe tu, au ilikuwa moyo kabisa?

Nadhani hali ikawa namna hiyo hiyo hata kwake pia, kwa sababu baada ya kuangaliana kihivyo, nikahisi mkono wake ukipita ubavuni kwangu na kufanya kama kuishika T-shirt niliyovaa kwa kuivuta fulani hivi, nami nikauangalia mkono wake. Niliporudisha macho yangu usoni kwake, wakati huu ukawa tofauti na jinsi ulivyokuwa awali; si wa kuudhika tena, bali wa hisia. Ah! Hee. Ujumbe ukawa delivadi. Mimi nikiwa mzee wa kupandisha mizuka, sikuchelewa. Huko chini nikaanza kunyanyuka, kwa nguvu hatari, na hali hii ikaniongezea hamu ya kutaka jambo hili liendelee. Tukiwa bado tunatazamana kwa ukaribu, na Adelina akinishikilia ubavuni bado, nikajikuta naifuata midomo yake papo hapo na kuanza kuipiga busu. Mluzi!





β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…

ITAENDELEA

β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…β˜…


Whatsapp +255 678 017 280
One mistake one goal
 
Back
Top Bottom