Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #41
SEHEMU YA 41
Ilipita kama miezi miwili, Babuu alikosa mawasiliano na Erica kabisa na alipojaribu kwenda chuoni kwao hakuweza kuonana nae, ikabidi aende tena ili ajaribu kuonana hata na Yule Dora ambaye ni rafiki wa Erica. Na alikuwa akienda mara kwa mara ila mara zote hakumpata yeyote kati ya Erica wala Dora, mpaka siku hiyo ilikuwa kama bahati maana alimuona Dora na kumuita,
“Dora”
Dora aligeuka nyuma kuangalia ni nani anamuita na akamuona ni Babuu, akaitika na kusogea ili kumsikiliza kuwa ana ujumbe gani.
“Naomba kuzungumza na wewe Dora”
“Hakuna shida, twende tukakae pale kwenye kimbweta”
Basi wakaenda kukaa kisha Babuu akaanza kutoa maelezo yake.
“Nina matatizo Dora, naomba unisaidie niweze kuonana na Erica”
“Si umpigie simu”
“Mwanzoni alikuwa hapokei simu yangu ila kwasasa simpati kabisa hewani, yani huwezi amini kila siku nakuja hapa chuoni ili kuangalia kama nitamuona ila leo Mungu mkubwa nimekuona wewe. Tafadhari naomba nisaidie kuonana na Erica”
“Nikuulize swali Babuu?”
“Niulize”
“Hivi huwezi kuwa na msichana mwingine zaidi ya Erica?”
“Jamani dora! Natumai unajua kuhusu kupenda, nampenda kweli Erica ninampenda sana”
“Na kama yeye hakupendi tena je?”
“Kama yeye hanipendi tena sijui ila ninachojua nina mpenda sana”
“Hivi huwezi hata kujiongeza, mwanamke ulikuwa unampigia simu hapokei simu zako na siku hizi ukimpigia humpati hewani yani unashindwa kujiongeza tu kuwa umeachwa?”
“Jamani Dora usiniumize moyo wangu, unajua nampenda sana Erica yani nampenda sana”
Dora alimuangalia jinsi Babuu alivyokuwa akiongea kwa huruma, na mbele yake kidogo akawaona Erica pamoja na George wakiwa wameongozana huku wameshikana mikono, Dora alimuangalia Babuu na kumwambia,
“Angalia kule ujionee”
Babuu aligeuka na kuangalia, kwakweli hakuamini macho yake na kuyafikicha fikicha yani hakuamini kabisa kama Erica aliyemopenda kupita maelezo ya kawaida yupo kwa mtu mwingine,
“Hapana Dora, yani Erica kaniacha kweli?”
“Ndio umeachwa, wakati anakupigia simu wewe na hupokei ulikuwa unamaanisha nini? Kama kuwekwa rumande alikutuma wewe kwenda kuchokoza polisi?”
“Dah! Unaniumiza Dora ila nashukuru sana ingawa roho inaniuma. Mimi nilikamwatwa na polisi baada ya kutoka kuonana na Erica yani siku hiyo nilichelewa sana kurudi, ila kama Erica kaamua kunifanyia hivi sawa bhana Mungu atannilipia”
Dora alicheka sana na kumwambia,
“Akulipie kwa lipi? Usinichekeshe mie, haya ni mapenzi tu, ukitendwa sehemu moja tafuta sehemu nyingine ujiliwaze. Pole sana”
Babuu hakuweza kuendelea kukaa mahali pale na kuamua kuondoka kwani aliona akizidi kuumia tu kwahiyo hakutaka kuendelea kujiumiza moyo kwa kitu ambacho ameona kwa ushahidi kabisa kuwa Erica ameamua kuachana nae na kuwa na mwingine kabisa kabisa.
Ilipita kama miezi miwili, Babuu alikosa mawasiliano na Erica kabisa na alipojaribu kwenda chuoni kwao hakuweza kuonana nae, ikabidi aende tena ili ajaribu kuonana hata na Yule Dora ambaye ni rafiki wa Erica. Na alikuwa akienda mara kwa mara ila mara zote hakumpata yeyote kati ya Erica wala Dora, mpaka siku hiyo ilikuwa kama bahati maana alimuona Dora na kumuita,
“Dora”
Dora aligeuka nyuma kuangalia ni nani anamuita na akamuona ni Babuu, akaitika na kusogea ili kumsikiliza kuwa ana ujumbe gani.
“Naomba kuzungumza na wewe Dora”
“Hakuna shida, twende tukakae pale kwenye kimbweta”
Basi wakaenda kukaa kisha Babuu akaanza kutoa maelezo yake.
“Nina matatizo Dora, naomba unisaidie niweze kuonana na Erica”
“Si umpigie simu”
“Mwanzoni alikuwa hapokei simu yangu ila kwasasa simpati kabisa hewani, yani huwezi amini kila siku nakuja hapa chuoni ili kuangalia kama nitamuona ila leo Mungu mkubwa nimekuona wewe. Tafadhari naomba nisaidie kuonana na Erica”
“Nikuulize swali Babuu?”
“Niulize”
“Hivi huwezi kuwa na msichana mwingine zaidi ya Erica?”
“Jamani dora! Natumai unajua kuhusu kupenda, nampenda kweli Erica ninampenda sana”
“Na kama yeye hakupendi tena je?”
“Kama yeye hanipendi tena sijui ila ninachojua nina mpenda sana”
“Hivi huwezi hata kujiongeza, mwanamke ulikuwa unampigia simu hapokei simu zako na siku hizi ukimpigia humpati hewani yani unashindwa kujiongeza tu kuwa umeachwa?”
“Jamani Dora usiniumize moyo wangu, unajua nampenda sana Erica yani nampenda sana”
Dora alimuangalia jinsi Babuu alivyokuwa akiongea kwa huruma, na mbele yake kidogo akawaona Erica pamoja na George wakiwa wameongozana huku wameshikana mikono, Dora alimuangalia Babuu na kumwambia,
“Angalia kule ujionee”
Babuu aligeuka na kuangalia, kwakweli hakuamini macho yake na kuyafikicha fikicha yani hakuamini kabisa kama Erica aliyemopenda kupita maelezo ya kawaida yupo kwa mtu mwingine,
“Hapana Dora, yani Erica kaniacha kweli?”
“Ndio umeachwa, wakati anakupigia simu wewe na hupokei ulikuwa unamaanisha nini? Kama kuwekwa rumande alikutuma wewe kwenda kuchokoza polisi?”
“Dah! Unaniumiza Dora ila nashukuru sana ingawa roho inaniuma. Mimi nilikamwatwa na polisi baada ya kutoka kuonana na Erica yani siku hiyo nilichelewa sana kurudi, ila kama Erica kaamua kunifanyia hivi sawa bhana Mungu atannilipia”
Dora alicheka sana na kumwambia,
“Akulipie kwa lipi? Usinichekeshe mie, haya ni mapenzi tu, ukitendwa sehemu moja tafuta sehemu nyingine ujiliwaze. Pole sana”
Babuu hakuweza kuendelea kukaa mahali pale na kuamua kuondoka kwani aliona akizidi kuumia tu kwahiyo hakutaka kuendelea kujiumiza moyo kwa kitu ambacho ameona kwa ushahidi kabisa kuwa Erica ameamua kuachana nae na kuwa na mwingine kabisa kabisa.