tinerdewaizer
Member
- Jan 26, 2025
- 26
- 7
Karibu Mkuu 😅
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
🤔🤔🤔🤔Mbona hamna kitu ??
🍿🍺🍺Mida imekaribia wanaolala watasoma kukikucha wale mapopo muda mfupi ujao namwaga episode
NzuriNYUMA YA MLANGO WA ADUI
SEHEMU YA TANO
MTUNZI : Mbogo EDGAR
WATSAPP: 0743632247
ILIPOISHIA SEHEMU YA NNE: “ok! nipe hali ya uzito wa mzigo, daraja la mzigo, na usalama wa usafirishaji” aliuliza kijana wetu, ambae alikuwa anaendelea kuendesha gari kwa speed kama vile analazimika kwenda na muda flani, wakati huo walikuwa wanakaribia njia panda ya Moroco, “uzito, haufiki hata kilo, usalama ni mkubwa sana, thamani yake laki mbili” alijibu yule mwanamke kwa sauti ile ile, ambayo kama unauwezo wa kujaji mtu kupitia sauti ungejuwa kwa, uzuri wa mwanamke huyu, siyo wataratibu, na ni mwanamke wa mjini, mwenye maisha ya hali ya juu. endelea
Hapo dereva wetu akashusha pumzi ndevu ya kuchoka, maana yeye amezowea kusafirisha mizigo ya hatari, lakini sasa anaambiwa kuwa, mzigo hakuwa na hatari yoyote, na thamni yake ni laki mbili, hapo akaona kuwa ni utani, lakini kutokana na utaratibu wake namba 7, hakutakiwa kudharau kitu wala mtu, “ok! malipo elfu hamsini, utanipatia nikifisha mzigo, lakini utatakiwa kuzingatia kuwa, hakuna ujanja, huo ni utaratibu namba 5” alisema dereva, akitaja elfu hamasini kwa kutegemea kuwa mwanamke huyu, angeona bei kubwa, na kughairi mpango, “wala usiwe na wasi wasi, natukienda sawa, nita kuongezea mala dufu ya elfu hamsini” alisema yule mwanamke, huku akizidi kuipooza sauti yake, “ok! mpango umekubaliwa” alisema dereva na kukata simu, wakati huo, anapunguza mwendo kuingia njia panda ya Moroco, na kukata kushoto kuelekea barabara ya mwenge, kisha akaongeza mwendo, pasipo kujari sms zilizokuwa zinaingia kwenye ile simu yake nyingine, muda wote mschana mdogo Zamda akiwa anamtazama kijana huyu, kwa macho ya viulizo, na kushindwa kupata jibu.*******
Yap! wakati kama huu, kusini mashariki mwa Tanzania, pembezoni mwa mto Ruvuma, kaskazini mashariki mwa msumbiji, ndani ya nchi ndogo ya kifalme, nchi iliyosaahulika katika ramani ya dunia, kutokana na kuchelewa kutambuliwa na umoja wa mataifa, nchi ya mbogo #land_land, inayoongozwa na mfalme Elvis Mbogo wa kwanza, mwenye makazi yake katika ngome ya dhadhabu, kwamaana ya Golden Castle, iliyopo ndani ya jiji la Treanch Town, kwa maana ya Treanch Town City.
Tuachane na King Elvis, twende kusini mwa mji huu wa TT, mpaka nje kidogo ya jiji Hilo la Trench Town, ni pembezoni mwa barabara ya kuelekea upande wa msumbiji, katika kitongoji kidogo cha Mmajile, (mmemaliza), mji ulikuwa umechangamka kwa burudani, kama ujuwavyo mji huu, jioni na nyakati kama hizi, watu hutumia muda wao na familia zao, au wapenzi wao, kupata burudani katika bustani za viunga vya jiji, huku wakipata vinywaji na vitafunwa mbali mbali.
Hayatuhusu hayo, sisi twendeni moja kwamoja mpaka kwenye jengo moja kubwa, la ghorofa kumi na mbili, ambao lilikuwa alijamaliziwa ujenzi wake, lililokuwa limezungushiwa uzio wa mabati, kama wafanyavyo wakandarasi wengine wanapofanya ujenzi mkubwa kama huu.
Ndani ya uzio huo yana onekana magari nane ya kifahari, ni jambo la kawaida kwa nchi hii kuona magari kama haya, maana wanachi wengi ni mtajiri, lakini licha ya magari hayo nane, pia kulionekana vijana kumi na tano, walio valia nguo nyeusi, kwa maana ya suruali nyeusi za jinsi, na tishert nyeusi, zilizo kamata miili yao, kichwani kofia nyeusi za cap, waswaili uita kapelo, mikononi mwao wakiwa na bunduki aina ya HECKLER &KOCH G95 toka GERMANY ASSAULT RFLE 5.56MM, H K G 95, yaani hecler & koch G 95, iliyotengenezwa nchi germany assault refle yenye mtutu wa mzingo mill miter 5.56, kwa faida ya msomaji, ni aina ya silah iliyotumika kumuuwa Osama bin laden mwaka 2011.
Wakionekana kuwa makini sana, katika ulinzi wa eneo hilo, lenye mwanga hafifu, vijana hawa walionekana wakiwa wamejipanga kwa kuachiana nafasi ya mita kati ya kumi mpaka kumi natano eneo lote la mbele.
Achana na eneo ili kwa nje, huko ndani katika moja kumbi za jengo hilo, lenye giza, zilionekana taswira za vimvuli vya giza, vya watu kama sita hivi, ambao kiukweli usingeweza kuona sura zao, walionekana kuwa katika mpango flani mzito sana, “bwana James Carvin, alitoroka nchini mwaka 1988, na kukimbilia tanzania, ambako anaalianzisha tena biashara zake na kuwa mfanyabiashra mkubwa na tajiri” alisema mmoja wao, aliekuwa amesimama mbele yao, huku wengine watano, wakiwa wamesima kwa kutengeneza nusu mwezi, huku wakionekana kumsikiliza kwa umakini mkubwa sana.
“bwana James Carvin, ambae kwa sasa anamiliki viwanda vikubwa vya vyakula unga na vinywaji, huko Tanzania, alikimbia nchini, akikwepa tuhuma za uhaini, alionekana kuwa alikuwa anafadhiri kikundi cha kijeshi cha waasi wa zamani, kilicho fahamika kwa jina la harakati za uhuru kwa damu” alisema tena yule ambae walikuwa wanamtazama, ambae kwa haraka alionekana kuwa na umri mkubwa zaidi yao, “naamini bwana James atakuwa na hasira kali sana na serikali, hivyo akielezwa anachotakiwa kufanya juu yetu, lazima ataungana na sisi, na kutusaidia kulipia kontena ishirini za silaha mabomu na risasi, kwaaajili ya mapinduzi, pamoja na kutusaidia chakula kwaajili ya askari wetu waliopo msituni” alisema yule jamaa, ambae licha ya kuwa gizani, na rangi yake kuwa nyeusi, pia alikuwa amevalia koti refu jeusi, suruali nyeusi, viatu vyeusi, na kofia ya duara yeusi yenye kuziba uso wake.
“Lakini mheshimiwa, itakuwaje kama atakataa, maana Jemes nikama mtu wa kufata sheria pia” aliuliza mmoja kati yao, ambae alionekana kuvalia nguo zinazofanana na wale vijana wa nje, “sikia bwana Tambwe, fanya kama nilivyo kuagiza, mweleze kwamba, mimi nimesema, kuwa, endapo tutachukuwa nchi hii, yeye atakuwa huru kuchimba dhahabu, kufanya biashara bila ushuru wowote, pia atapewa eneo kubwa sana la kufungua biashara yake na pia atapewa kandarasi ya kuchimba gass na mafuta, lazima atakubari tu, na kumbukeni kuwa mzigo hupo njiani, sikutatu baadae unatia nanga Queen Irine Bay, lazima tuwe na fedha ya kulipia kwa wale jamaa watukabidhi mzigo wetu” alisema yule alie itwa Mheshimiwa, safari hii akionyesha msisitizo mkubwa, “lakini mheshimiwa, nadhani itakuwa vizuri kama tukiwa na mpango mwingine, maana uwezi kujuwa James atasemaje” safari hii alishauri mtu mwingine, na siyo yule alie itwa Tambwe, huyu alikuwa amevaa suit nyeusi na kofia nyeusi.
Hapo mheshimiwa akatulia kidogo kama sekunde tano hivi, kisha akamtazama yule alie shauri, “sasa nimekuelewa, bwana Kadumya, mpango wapili upo, na utatekelezwa muda mchache sana baada ya huu wa kwanza kushindikana” alisema mheshimiwa ambae mpaka sasa hatuja mfahamu kwa jina, huku wale wengine wakimsikiliza kwa umakini mkubwa sana, “Kadumya hakikisha vijana wako wanafwata maelezo, ikiwa pamoja na endapo huu wakwanza utashindikana, wamuuwe James, kisha watahamia kwenye mpango wa pili, ambao nita wapa muda mfupi baada ya mpango wa kwanza, japo sitegemei kama James akiona mitutu ya bunduki usoni mwake, ataweza kusema hapana” alisema Mheshimiwa akionekana kuwa mwenye uhakika zaidi.
Naam baada ya hapo hawa kutumia muda mrefu mahala pale, wakaagana, “Kadumya, hakikisha vijana wako, wanapanda ndege kesho mapema, kuelekea Tanzania, nguo na silaha watazikuta huko huko, kwa bwana Mbwambo, kule temeke kaburi moja” alielekeza Mheshimiwa, kabla hawajaondoka zao, kwa namna ya siri kama vile Hawakuwa pamoja.******
Naam turudi kigamboni, ambako tayari polisi walisha kagua magari yote yaliyokuwa yana subiri kuingia kwenye kivuko yani Pantoni, pasipo kuliona BMW jeusi, na kuamua kurudi walikotoka, huku CP Ulenje akitoa maagizo askari wasambae maeneo yote kulisaka gari ilo, na yeye pamoja na askari watano wakaelekea upande wa mji mwema, kwenda kumwona bwana Songoro.
Ilikuwa ni safari ya dakika kumi na tano, mpaka kufika kwenye nyumba ya bwana Songoro, iliyo jitenga ndani ya eneo moja kubwa lililozingikwa na vichaka vifupi na minazi mirefu, sehemu ambayo walipofika tu, wakapokelewa na bwana Songoro alie simama sambamba na yule mwanamke, ambae sasa alikuwa amevalia chupi aina ya bikini na sidilia kifuani kwake, kati kati ya eneo la mbele la ile yumba kubwa, huku wakionekana watu waliokuwa wanagala gala chini kwa maumivu makali, huku wengine wakiwa wamepoteza fahamu zao, idadi yao ikifika zaidi ya kumi, huku zikionekana silaha mbali mbali zajadi na zile za kisasa, yani visu mapanga na bastora, vikiwa vimetawanyika eneo lile, huku baadhi ya ya watu hao wakionekana kuvujwa na damu , toka kwenye majelaha mbakubwa, katika sehemu mbali mbali za miili yao.
CP Ulenje alitoa macho kwa mshangao, “Songoro unasema alikuwa kijana mmoja tu?” aliuliza CP Ulenje kwa mshangao, “ukweli sikuwai kufikiria kama kuna mtu anaweza kuwa kama yule kijana, hakika namwitaji na tena namwitaji nimkate kiungo kimoja baada ya kingine” alisema Songoro kwa sauti iliyo jaa chukizo na kasiriko, “vijana tayari wapo kazini, naamini muda siyo mrefu watamtia nguvuni” alisema Ulenje, wakati huo wanaingia ndani, na kukagua watu wengine walio kuwa bado wanagala gala kwa maumivu, wapo waliolalamikia mbavu wapo waliolalamikia nyuso zao, na wapo walio lalamikia miguu yao, ilimradi kila mmoja wao alipata anacho stahili, “unampango gani na hawa watu Songoro” aliuliza Uledi , wakati wanaendelea kukagua mle ndani, “wajinga hawa wanawezaje kupigwa na mtoto mrembo kama yule” alisema Songoro ambae hakuonyesha dalili ya kuwa saidia vijana wake, waliokuwa wanataabika pale chini, “huyo kijana atakuwa tatizo hapa mjini, inabidi apatikane haraka sana” alisema CP Ulenje, huku anatoa simu, kubofya namba kisha akaipiga na kuweka sikioni.
Simu haikuita muda mrefu, ikapokelewa, “OCD mambo ni mazito, kuna uvamizi mkubwa umetokea huku mji mwema kigamboni, kwa mfanyabiashara Songoro, agiza gari la wagonjwa lije huku, pia peleka taarifa vituo vyote vya polisi, hapa mjini, msako mkali uendelee, malengo ni BMW jeusi, kamata kila anae hisiwa mpaka apatikane, na taarifa itolewe kuwa ni mtu hatari sana huyo” alisema CP Ulenje, mara tu baada ya simu kupokelewa, “sawa mkuu inatekelezwa” alijibu OCD, na hapo Ulenje akakata simu, kisha akamtazama Songoro, “hakiki hakikisha unaondoa hizo silaha hapo nje” alisema Ulenje, kwa msisitizo.*******
Naam barabara ya bagamoyo, mtaa wa tegeta, njia panda ya kwasharifu, linaonekana gari moja jeusi aina ya ford ranger likiwa limesimama pembeni ya barabara hiyo, huku mtu mmoja, mwenye mwonekano wa miaka 40, akiwa amesimama ubavuni mwa gari ilo, huku uso wake, ukionekana kujawa na mashaka mengi, mara kwa mara alikuwa anatazama saa yake, na kisha kutazama upande wa mjini, ni wazi alikuwa anatarajia kuona mtu au gari likitokea upande huo….. hivi huyo mzee James atakubari mpango wa mheshimiwa, ebu tuone kitakacho tokea. basi… endelea kufwatilia mkasa huu wa #NYUMA_YA_MLANGO_WA_ADUI, inayo kujia hapa hapa jamii forums
Ndio kwanza upo sehemu ya 5 wewe utafaida kwasababu utasoma bila arosto, acha niwashushie episode kabla hawajanitukana 😅Nzuri
Kesho ndio sasa mkuu hii ni saa saba kamili sema wewe tu umewahi kulala,😅Nilodhani keshabandika.
Basi tusubiri subirie japo hadi kesho.
Wala sijalala na nimeisha isoma.Kesho ndio sasa mkuu hii ni saa saba kamili sema wewe tu umewahi kulala,😅
Haya bhna mukiamka mutaendelea kuenjoy na stori yetu.
Deusi atageuza hilo pagale lao kuwa machinjio kisha ataondoka na mchumba Ili wakajuane kuwa wao ndio pacha na Mchoraji pembeni wakiwa na manoti yaliyochukuliwa bank.Imeishia pazuri ngoja tuone kama deus atatoka na happ