NYUMA YA MLANGO WA ADUI
SEHEMU YA MIA MOJA NA KUMI NA NNE
MTUNZI:
Mbogo EDGAR
WHATSAPP: 0743632247 (KWAMATUMIZI YA OFISI TU)
TULIPOISHIA SEHEMU YA MIA MOJA NA KUMI NA TATU :- “asante mfalme wangu, uwena Maisha marefu” alisema mzee James akionyesha tabasamu pana la furaha, “bwana James sasa ningependa kusikia kutoka kwako pia” alisema mfalme na kutulia kumsikiliza bwana James, “mtukufu mfalme, ukweli sikuwahi kujihusisha na watu hao hata mara moja, lakini jana usiku nilipigiwa simu na…..” alisema James na kusita kidogo, kisha akamtazama mke wake, “ni nani huyo alikupugia simu bwana James?” aliuliza king Elvis, kwa sauti, yenye shauku…..…. ENDELEA…
Ilimshtua kidogo James, ambae bado alikuwa anamtazama mke wake kama vile anamuomba msaada wa jibu, nae akamonyesha ishara ya mdomo kwamba amuambie ukweli, na kabla hajatoa jibu lolote, akasikia sauti ya mfalme Elvis, “hallow bwana James, bado unasikia?” hapo mzee James akaigeukia simu yake haraka, “ndio nipo na kusikia” alijibu mzee James ambae kichwani mwake alikuwa anatafakari jambo juu ya jibu ambalo analihitaji mfalme, je ni kweli amueleze aliepiga simu, ili hali hakuwa na ushaidi kuwa Chitopela ndie muhusika mkuu wa kikundi cha UMD, au akae kimya mpaka itakapo bainika.
Lakini baada ya kuchakata akaona ni vyema kufanya linalofaa kwa wakati ule,“ndio bwana James, ulisema ulipokea simu kutoka kwa nani?” aliuliza mfalme akionyesha hamu kubwa ya kumfahamu muhusika wa kundi hilo, “ndiyo mtukufu mfalme, nilipokea simu kutoka kwa mtu ambae hakujitambulisha akisema anahitaji kuongea na mimi juu ya biashara, nilipoenda nikawakuta wakina Kadumya, nao wakaniambia wanataka niwafadhili kuingiza silaha nchini, nilipokataa. walitka kuniuwa, bahati nzuri akatokea kijana mmoja hivi ni mtoto wa askari wa zamani wa #mbogo_land, bwana Deus Nyati, sidhani kama ni kweli yupo UMD, ila nae alikimbia nchini kwa kusingiziwa kuwa ni UMD” alielezea bwana James na wakaongea mawili matatu na king Elvis kabla ya kukata simu, huku wakipeana ahadi ya kuwasiliana kila itakapoitajika.********
Yap! sasa uchunguzi mkali chini ya TSA, ulianza kufanyika, juu ya wazazi wa kijana Deus, lengo ni kutaka kujuwa Deus ni nani asa na ametokea wapi, sababu shuku kubwa ni kwamba, Deus alikuwa ni askari wa MLA, alie jiunga na jeshi la Tanzania, pengine ni kwakutaka habari za kiusalama za jeshi la ulinzi la Tanzania, au alikuwa na mpango wa kuhujumu jeshi na serikali ya Tanzania kwa ujumla, tayari taarifa zilisha tawanywa sehemu tatu muhimu, ikiwemO TRA, ambako ndio sehemu ambayo taarifa zinaweza kupatikana kirahisi, TSA songea, na pia taarifa zilienda #mbogo_lan kwamakachero wa Tanzania waishio nchini humo, katika imvuri cha watumishi wa barozi.
Lakini ukiachilia ilo, TSA wengi sasa walikuwa mitaani wakiendelea msako wa siri, kama raia wengine, walikuwepo walio jifanya boda boda, walikuwepo waliojifanya maderva wa taxi, na wapo wengine, waliojifanya raia wa kawaida mitaani, mida hii mkurugenzi wa TSA kanda ya dar es salaam, bwana Elisha Eric, alikuwa ofisini, ana anasubiria taarifa toka sehemu mbali mbali, alizoweka mitego yake, mala akapokea toka kwa mmoja wa mawakara wake, aliekuwa mtaani anaendelea na ukusanyaji wa habari, “mkuruenzi, taarifa mpya zilizo naswa kwenye redio ya polisi, katika frequance 3, ni kwamba, dereva wa BMW jeusi, yani Deus Nyati, yupo na Veronica James, wameonekana mitaa ya Kufulu, barabara ya malamba mawili, kuelekea Kinyerezi, na wamefanikiwa kuwakimbia polisi” taarifa hii ilimshtua sana bwana Elisha, pamoja nawana usalama wenzake, aliokuwanao pale ofisini.
“unauhakika kuwa, ulichokisikia ndio hicho unacho tueleza sisi?” aliuliza Elisha Eric, kwa sauti yenye mashaka, yani kuto kuamini kile alicho kisikia, toka kwa wakara wake, “ndiyo mkuu, hivyo ndivyo polisi walivyo peana taarifa, na hivi tunavyoongea lazima watakuwa Morogoro road, maeneo ya kuanzia mbezi mpaka kiluvya madukani” alisema yule wakara, akionyesha kuwa na uhakika na kile alichokisema, “sawa nimekupata, lakini mudawote, jitaidini muwe karibu na naeneo ambalo Deus anaonekana” alisema mkurugenzi na kukata simu.
Elisha Eric anaachia tabasamu, “jamani, ni mambo juu ya mambo, kazi inazidi kupamba moto” alisema Lisha akiwatazama wenzake kwa awamu, wemzale wanatega masikio kwa hamu ya kusikiliza taarifa mpya, “dakika chache baada ya Veronica kuonekana akishiriki wizi, tunapata taarifa kuwa alitekwa na UMD, lakini sasa inakuja taarifa kuwa yupo mikononi mwa Deus Frank Nyati, je yupo salama au nako ameteka?” aliuliza Elisha, na wenzake wakacheka kidogo, “kwa hiyo alimwokoa baba kisha akaenda kumteka mtoto?” aliuliza wakara mwingine, kwa sauti yenye mashaka, “hiyo aiwezekani, maana ni lazima ange mchukuwa moja kwa moja bwana James” alijibu mwingine, “sasa huyu Deus ni nani, na kwa nini anafanya hayo yote, au mzee James amemkodi kwenda kumchukuwa binti yake, maana kama alionekana kinyelezi, hiyo ilikuwa ni safari ya kurudi nyumbani” alisema bwan Elisha, wote wakatazamana.
Ni wazi kuna jmbo walilishuku, "kwahiyo mkuu, kama bwana James amemtuma huyu dereva akamwokoe binti yake, inamanisha kuwa, bwana james yupo katika mtandao wa watu, wanao tumia Deus Nyati, kama dereva kodi" alisema mmoja wa wanausalama waliokuwa na mle ndani na bwana Elisha, "kwahiyo unataka kusema kuwa, James anamfahamu Deus, muda mrefu uliopita?" aliuliza mkurugenzi Deus, huku anamtazama yule wakara, kabla ajajibu, hapo hapo wakara mwingine akadakia, "sizani kama inaweza kuwa hivyo, ila nahisi ni kwamba, Deus ni wakara wa serikali ya #mbogo_land. ambae baada ya kumwokoa bwana James, akapewa jukumu la kumwokoa Veronica" alisema wakara, wingine akipingana na yule wakwanza, "kwahiyo bado tunarudi kule kule, kwamba private Deus ni MLSA, na aliingia Jeshi la ulinzi kama mpelelezi wa siri" alisema mkurugenzi Elisha, na wengine wakaunga mkono, "basi tusubiri taarifa toka Songea kwa Haule (james bond, soma kiapo cha damu) na huko #mbogo_land, wao ndio wata tuonyesha mbivu na mbichi" alisema mkurugenzi Elisha, ambae akuonyeshaa dalili ya kwamba ata watawanyisha wajumbe wake, kwenda kupumzika.*******
Naam!! wakati kikundi maalumu cha jeshi la wananchi cha spcial marine force, kikiwa kina weka kituo kidogo maeneo ya kiluvya gogoni, wakati huo huo huku bwana Songoro na kikundi chake wakiwa wamesimama Kiluvya kwa komba hawajui waelekee wapi, maana tayari walishaachwa kama solemba, wakati huo huo magari takribani kumi na tano ya jeshi la polisi yanaonekana yakiwa katika speed ya ajabu yanakatiza mtaa ya Luguruni kuelekea mbezi, huku yakilindimisha ving'ora na bocon za rangi nyekundu na blue juu ya vichwa vya magari yao, huku askari wakionekana nyuma ya magari hayo wakining'inia na silaha zao, hizi zote ni mbio kuliwahi BMW jeus, kama wao walivyo liita farasi.
Lakini mpaka wanafika njia panda ya malamba mawili na wanakutana ambapo walikutana na magari mengine manne ya polisi, tatu yakitokea upande wa mjini na jingine ni lile la wakina Cheleji, lakini hawakuwa wameliona BMW jeus, wala dalili ya gari hilo, hakika ilishangaza sana, “atakuwa amepitia wapi huyu mshenzi, tena amemteka mtoto wa mzee James” alisema koplo Cheleji, huku wengine wakimsikiliza, tena kati yao walikuwepo waliomzidi cheo, wakiwepo ma sajent na major, ma inspector ma super lutenat, hakuna alieamini kilichotokea, maana licha ya speed kali na uharaka walio utumia kuwahi pale mbezi, lakini bado wanalikosa gari lile, cha kushangaza zaidi ni kwamba, ukiachilia magari yaliyotokea kibaha na huku kinyerezi, pia kulikuwa na magari yaliyotokea mjini, kwa maana kama BMW lilielekea upande huo wangekutana nalo, “hakuna haja ya kuzubaa hapa, tunaingia mitaani kulisaka hilo gari, lazima litakuwa halijafika huku” alisema polisi mmoja mwenye cheo cha lutendant, na hapo polisi wakaingia kwenye magari na kuanza kuondoka kuelekea maeneo mbali mbali ya pale mbezi wakipishana na magari mawili aina ya land rover puma yaliyokuwa yanaelekea upande wa kibaha.******
Naam, sasa basi wakati vyombo vya ulinzi na usalama vikiwa mitaani vina msaka kijana Deus Nyati vikisahau kuhusu UMD, kitu ambacho wao hawakukijua ni kwamba tayari BMW S7, lilikuwa limesha kamata barabara ya vumbi ya kisarawe kupitia kisopwa mkoani pwani na kwenda kutokea kwenye reli ya kati, kisha taratibu likaanza kuambaa ambaa na njia hiyo hafifu yenye mawe mengi, na sasa mwendo wa BMW ulikuwa mdogo mdogo, giza lilikuwa nene na la kutisha, misitu minene na vichaka vikubwa, hapakuwa na dalili za makazi ya watu wala dalili ya mwanga wa taa au karabai maeneo ya karibu na pale, zaidi ya taa zilizo onekana mbali sana za mji wa kibaha na dar es salaam, pengine ni mwanga wa taa za gari hili aina ya BMW s7 ambalo sasa, lilikuwa linaangazia mwanga hafifu, uliowekwa makusudi kuepuka kuonekana mbali, yani ngao mbele ya adui zake.
Safari ilikuwa kimya kimya watu wawili yani Deus Nyati na mschana Veronica, kila mmoja akiwaza la kwake kichwani, wakati mwadada Veronica alikuwa anawaza juu ya usalama wake, hasa ukichukulia kwamba alishaona kuwa mambo yamekuwa mazito upande wake, maana hata baadhi ya askari wa jeshi la polisi ni maadui zake, na vipi kuhusu huyu kijana dereva mwenye uso wa upole, ambae kuuwa ni kazi ndogo sana kwake, huku anampeleka wapi na itakuwaje kama akienda kumfanyia vitendo visivyo faa, ukichukulia yeye ni mzuri na anatamanisha.
Lakini hata hivyo kijana huyu ambae hakuonyesha kuwa na nia ovu juu yake ndio msaada wa pekee kwake, maana hata kama akiomba ashushwe na yule dereva angekubari, unadhani yeye angefika wapi na ule msitu, hata kama kusingekuwa na hatari ya watu au wanyama lakini kwa uoga angejikuta anazimia, hivyo kilicho bakia ni kutengeneza urafiki na kijana huyu ili usalama wake uendelee kuwepo.
Deus yeye alikuwa anawaza juu ya muunganiko wa matukio yanayoendelea, matukio yanayohusiana na UMD, kundi ambalo ukiachilia kumteka mzee James na binti yake ni kundi ambalo pia, lilihusika kumsababishia baba yake matatizo makubwa huko #mbogo_land mwaka 1992, “naitwa doctor Veronica, nipo hospita ya mkoa wa pwani” alijitambulisha Veronica huku anaachia tabasamu, ambalo hata yeye alitamani dereva aone hilo tabasamu ambalo mara zote huamsha matamanio ya wanaume, “umevunja sheria namba moja” alisema Dereva kwa sauti tulivu ya upole, ambae hakuonyesha dalili ya kumtazama Veronica...Naam Usiache Kufuatilia mkasa huu wa
NYUMA YA MLANGO WA ADUI unaokujia hapahapa
jamii forums