mireille
JF-Expert Member
- Mar 4, 2020
- 529
- 589
PETE YA MFALME WA EDEN
MTUNZI:JAFARI MPOLE
SEHEMU YA 01
Asubuhi ya Saa mbili kijana Jafari alikurupuka kutoka kitandani,alipotazama saa yake ya mkononi ambayo aliiweka karibu na mto alipolala kwa lengo la kumuamsha kwa kutegesha alamu,lakini ajabu siku hiyo hakuweza kusikia muito wa saa ile ikimuamsha jambo lililomfanya haraka anyanyuke na kuanza kuvaa nguo zake za shule haraka haraka.
“yaani leo nachezea stiki za Bokeloo, na u timekeeper niliopewa ndio mimi nimekuwa mchelewaji,Mungu wangu leo mh“alisema kijana Jafari akiwa anavaa viatu vyake haraka bila ya soksi,alipohakikisha yupo sawa alinawa uso wake kisha akachukua begi lake na kuanza safari ya kuelekea shuleni ambapo ni mbali kidogo kutoka kijiji cha Kabuku ambacho ndipo anaishi kijana huyo na alipogika njiani akakata kipande cha tawi la muarobaini na kutengeneza mswaki wa kijiti huku safari ikiendelea kuelekea shule. Ilimchukua dakika 35 za kukimbia tu hadi kufika mazingira ya shuleni hapo huku akionekana kuhema sana kwa kuchoka na jasho likimmiminika kiasi cha kulowesha nguo zake. Alisogea mbele kidogo akaanza kunyata na kwa mbali alisikia bakora zikitua mwilini kwa mtu hali iliyomfanya ajibanze kwanza mahali.Alipotazama kwa makini mbele alipata kushuhudia rafiki yake wa darasani Fanuel akiwa amelala chini akichapwa bakora kwenye makalio.
“duh hata jamaa leo kachelewa? Mungu wangu nisaidie"alisema Jafari na kuanza kutafuta njama ya kuingia darasani bila kuonekana maana wanafunzi wote walikuwa washaingia darasani wakichungulia tu kuona watu walio chelewa wakipata adhabu ya viboko kutoka kwa Mwalimu mkuu wa shule hiyo ya KWALUDEGE SECONDARY. Alipotazama pembeni akaona kuna wanafunzi watano wanatembea wakielekea kwenye bustani hivyo akaona njia pekee ya yeye kuepuka bakora ni kujichanganya kwa wale wanafunzi apate kupenya hadi kuingia darasani. Taratibu akanyata kwa ustadi wa hali ya juu hadi kufanikiwa kuzama kwenye lile kundi ambalo walipomuona Jafari walicheka tu na kuendelea na kazi zao za pale kwenye bustani huku naye akishirikiana nao huku akipanga njama ya kuingia darasana ambapo ni karibu na bustani hiyo waliyopo. Alipo piga ramani na kuona Mwalimu mkuu yule amezubaa akakimbia haraka hadi darasani kwao akaingia na kikimbia kukaa kwenye kiti chake huku baadhi ya wenzake wakianza kucheka maana walishamuona tangu anafanya ujanja wake.Dakika moja mbele akaja kijana mmoja pale karibu yake.
“mwanangu sio kama umesevu ulivyoingia humu.. Bokeloo anakuja huku kashatuhesabu tuliowahi ana namba zake na tuliopo humu ni 36 tu.“alisema kijana huyo na kumfanya Jafari ashtuke kusikia vile. Akaona ni msala wa yeye kuendelea kuwa pale darasani bora atoke tu, na alipotaka kufanya hivyo gafla tu aliona mlango unafunguliwa na kuingia Mwalimu mkuu Bokeloo akiwa ameshika bakora zake tatu huku sura yake ikionesha kuwa na hasira. Alipiga macho darasa zima huku akihesabu watu waliopo mule ndani,akajikuta akirudia tena na tena.
“hesabu zangu zinakataa, kuna mtu amezidi humu“alisema Mkuu huyo na baadhi ya wanafunzi wakaanza kumtazama Jafari aliye onekana kutetema mwili huku akijitahidi asionekane hali ile akawa anatoa vitabu vyake kwenye begi na kuanza kuvipanga.
“simameni wote“alitoa amri hiyo mkuu na wote wanafunzi wa darasa hilo la Form 4 wasimame.
“namba moja apite mbele“alisema Mkuu na mwanafunzi mwenye namba hiyo akapita mbele,hali hiyo ikazidi kumfanya Jafari akose amani na kukumbuka ule usemi KIFO CHA NYANI MITI YOTE HUTELEZA, hakukuwa na ujanja wowote ikabidi asubiri tu kukamatwa. Namba ziliendelea hadi kufika 34 na kubaki wanafunzi watatu waliosimama akiwemo Jafari ambaye alijikuta akiomba Mungu tu kwa woga uliomjaa.
“eh Mungu wangu nishushie muujiza huyu mzee hata akinikamata asiniadhibu hata bakola moja, unajua nilivyo mbovu katika kuvulia bakora mimi mja wako,doh saa imeniponza leo“alijisemea moyoni Jafari huku tumbo likiunguruma kwa woga akabaki ameinamisha tu kichwa chini huku wenzake wawili waliobaki wamesimama naye wakasogea mbele baada ya kutajwa namba zao akabaki yeye tu. Hapo ndipo akasikia vicheko vya wenzake wakicheka baada ya kumuona amebaki yeye tu kwenye viti.
“wewe ndio ulikuwa unanisumbua muda wote hapa hebu kuja huku, nyie rudini mkakae wewe kima njoo hapa alaah.“alisema Mkuu na wanafunzi wakarudi kwenye viti vyao huku Jafari akisogea pale mbele na kushikwa mkono na Bokeloo.
“wewe una makosa mawili kwanza, kwanza wewe ni TIME KEEPER ulipaswa uwahi kugonga kengele ndio watu wahesabu namba saa moja kamili,leo kengele nimegonga mimi mwenyewe saa moja na dakika 15 hivyo umeharibu ratiba nzima ya shule leo mpaka sasa vipindi havijaanza,utabeba adhabu hii peke yako lazima uwajibike,twende huku.“alisema Mkuu akitoka nje na kijana Jafari aliyeshikwa mkono. Watu wakawa wanatazama tu madirishani wakitaka kushuhudia adhabu gani atakayopatiwa.
Upande wa pili katika nchi ya kifalme kunaonekana kuna mkusanyiko wa watu katika uwanja mmoja nje ya jengo la kifalme. Kwenye jukwaa ambalo ni maalumu kwaajili ya kutoa hukumu anaonekana babu mmoja akiwa amefungwa kamba kwenye nguzo ya mti mrefu huku mwili wake ukiharibika kwa kupigwa sana na askari wa kifalme. Alichoka mwili mzima akisubiri hukumu yake tu ambayo ilisadikika mzee huyo ni mchawi na baya zaidi ameweza kumroga mpaka binti wa kifalme ambaye hadi sasa bado yu taabani kitandani hanyanyuki. Mzee huyo alipokamatwa na kubinywa ili aweze kueleza dawa ya kumtibu binti huyo alikataa katakata na kusema hawezi kusaidia falme haramu inayoongozwa na Mfalme Siddik hivyo ilibidi Mfalme Siddik atoe amri ya kumnyonga mzee huyo kwa kumkashifu Mfalme kisha waangalie namna nyengine ya kumsaidia binti wake maana hakukuwa na jinsi maana mzee yule aliapa kutomponesha binti huyo. Basi siku hiyo ya hukumu watu walifurika sana akiwemo hata binti wa mzee huyo aliyeitwa Nadhra. Yeye alikuwa mstari wa mbele kabisa akiwa mwenye huzuni sana akimtazama baba yake huyo akiwa amenin‘ginizwa kwenye nguzo kubwa akisubiri hukumu yake ambayo kila mmoja aliifahamu hukumu ya mtu mchawi,ni kunyongwa mpaka kufa.
Mzee huyo akiwa pale juu huku damu zikimtiririka alipata kumuona mwanaye pale mbele akiwa analia tu,alitabasamu baada ya kumuona mwanaye.
“Nadhra...usilie binti yangu,ukifanya hivyo utanifanya huko niendako niwe na huzuni kuwa nimemuacha binti muoga,simama kwenye msimamo nilio kwambia na hiyo pete kaitupe sehemu yeyote ya kengele kabla ya hukumu yangu kama unataka niwe nawe kiroho siku zote“alisema Mzee huyo moyoni mwake lakini kwa uwezo alio nao Nadhra alipata kusikia yote aliyosema baba yake.
“mimi naamini nguvu zako baba sio za kudhuru mtu, wana kuhukumu bure tu hawa watu wa kifalme.“alisema Nadhra moyoni mwake akiwa anawasiliana na baba yake aliyekuwa juu ya nguzo.
“hilo sio la kuliongelea kwasasa,fanya kile nilichokueleza hapo awali haraka.“alisema Mzee yule na binti yake akamuelewa. Waliangalina kwa mara ya mwisho mtu na mwanaye kila mtu akitokwa na machozi kisha Nadhra akageuka na kuondoka zake akipita katikati ya halaiki ya watu waliofurika kushuhudia hukumu hiyo.
“PISHA NJIA MFALME ANAPITA...“ilisikika sauti ya maaskari na kuwafanya watu waache njia kubwa ya msafara wa Kifalme ukiwasili sehemu ile.Nadhra alipata kuutazama tu msafara ule ukimpita akiwa naye amesimama pembeni hadi Mfalme Siddik alipopita akiwa juu ya farasi na wafuasi wake na kufika kwenye jukwaa lile alilopo baba wa Nadhra. Kiliandaliwa kitanzi maalumu kwaajili ya kukamilisha hukumu hiyo na hapo ndipo Nadhra akapata akili kumbe aliagizwa kufanya jambo. Haraka akaanza kukimbia sasa kwenda kutafuta mahala popote pale palipo kengele ili apate kuitupa pete aliyo agizwa na baba yake upate kusikika mlio kutoka kwenye kengele kwa imani yao ndio itakuwa afadhari ya baba yake atakuwa amejitoa kiroho katika mwili ambao utanyongwa hivyo ataendelea kuishi kama kawaida lakini hataweza kuonekana kama awali. Na asipofanikiwa Nadhra ni kwamba baba yake atakufa kabisa pindi atakapo nyongwa.
ITAENDELEA
MTUNZI:JAFARI MPOLE
SEHEMU YA 01
Asubuhi ya Saa mbili kijana Jafari alikurupuka kutoka kitandani,alipotazama saa yake ya mkononi ambayo aliiweka karibu na mto alipolala kwa lengo la kumuamsha kwa kutegesha alamu,lakini ajabu siku hiyo hakuweza kusikia muito wa saa ile ikimuamsha jambo lililomfanya haraka anyanyuke na kuanza kuvaa nguo zake za shule haraka haraka.
“yaani leo nachezea stiki za Bokeloo, na u timekeeper niliopewa ndio mimi nimekuwa mchelewaji,Mungu wangu leo mh“alisema kijana Jafari akiwa anavaa viatu vyake haraka bila ya soksi,alipohakikisha yupo sawa alinawa uso wake kisha akachukua begi lake na kuanza safari ya kuelekea shuleni ambapo ni mbali kidogo kutoka kijiji cha Kabuku ambacho ndipo anaishi kijana huyo na alipogika njiani akakata kipande cha tawi la muarobaini na kutengeneza mswaki wa kijiti huku safari ikiendelea kuelekea shule. Ilimchukua dakika 35 za kukimbia tu hadi kufika mazingira ya shuleni hapo huku akionekana kuhema sana kwa kuchoka na jasho likimmiminika kiasi cha kulowesha nguo zake. Alisogea mbele kidogo akaanza kunyata na kwa mbali alisikia bakora zikitua mwilini kwa mtu hali iliyomfanya ajibanze kwanza mahali.Alipotazama kwa makini mbele alipata kushuhudia rafiki yake wa darasani Fanuel akiwa amelala chini akichapwa bakora kwenye makalio.
“duh hata jamaa leo kachelewa? Mungu wangu nisaidie"alisema Jafari na kuanza kutafuta njama ya kuingia darasani bila kuonekana maana wanafunzi wote walikuwa washaingia darasani wakichungulia tu kuona watu walio chelewa wakipata adhabu ya viboko kutoka kwa Mwalimu mkuu wa shule hiyo ya KWALUDEGE SECONDARY. Alipotazama pembeni akaona kuna wanafunzi watano wanatembea wakielekea kwenye bustani hivyo akaona njia pekee ya yeye kuepuka bakora ni kujichanganya kwa wale wanafunzi apate kupenya hadi kuingia darasani. Taratibu akanyata kwa ustadi wa hali ya juu hadi kufanikiwa kuzama kwenye lile kundi ambalo walipomuona Jafari walicheka tu na kuendelea na kazi zao za pale kwenye bustani huku naye akishirikiana nao huku akipanga njama ya kuingia darasana ambapo ni karibu na bustani hiyo waliyopo. Alipo piga ramani na kuona Mwalimu mkuu yule amezubaa akakimbia haraka hadi darasani kwao akaingia na kikimbia kukaa kwenye kiti chake huku baadhi ya wenzake wakianza kucheka maana walishamuona tangu anafanya ujanja wake.Dakika moja mbele akaja kijana mmoja pale karibu yake.
“mwanangu sio kama umesevu ulivyoingia humu.. Bokeloo anakuja huku kashatuhesabu tuliowahi ana namba zake na tuliopo humu ni 36 tu.“alisema kijana huyo na kumfanya Jafari ashtuke kusikia vile. Akaona ni msala wa yeye kuendelea kuwa pale darasani bora atoke tu, na alipotaka kufanya hivyo gafla tu aliona mlango unafunguliwa na kuingia Mwalimu mkuu Bokeloo akiwa ameshika bakora zake tatu huku sura yake ikionesha kuwa na hasira. Alipiga macho darasa zima huku akihesabu watu waliopo mule ndani,akajikuta akirudia tena na tena.
“hesabu zangu zinakataa, kuna mtu amezidi humu“alisema Mkuu huyo na baadhi ya wanafunzi wakaanza kumtazama Jafari aliye onekana kutetema mwili huku akijitahidi asionekane hali ile akawa anatoa vitabu vyake kwenye begi na kuanza kuvipanga.
“simameni wote“alitoa amri hiyo mkuu na wote wanafunzi wa darasa hilo la Form 4 wasimame.
“namba moja apite mbele“alisema Mkuu na mwanafunzi mwenye namba hiyo akapita mbele,hali hiyo ikazidi kumfanya Jafari akose amani na kukumbuka ule usemi KIFO CHA NYANI MITI YOTE HUTELEZA, hakukuwa na ujanja wowote ikabidi asubiri tu kukamatwa. Namba ziliendelea hadi kufika 34 na kubaki wanafunzi watatu waliosimama akiwemo Jafari ambaye alijikuta akiomba Mungu tu kwa woga uliomjaa.
“eh Mungu wangu nishushie muujiza huyu mzee hata akinikamata asiniadhibu hata bakola moja, unajua nilivyo mbovu katika kuvulia bakora mimi mja wako,doh saa imeniponza leo“alijisemea moyoni Jafari huku tumbo likiunguruma kwa woga akabaki ameinamisha tu kichwa chini huku wenzake wawili waliobaki wamesimama naye wakasogea mbele baada ya kutajwa namba zao akabaki yeye tu. Hapo ndipo akasikia vicheko vya wenzake wakicheka baada ya kumuona amebaki yeye tu kwenye viti.
“wewe ndio ulikuwa unanisumbua muda wote hapa hebu kuja huku, nyie rudini mkakae wewe kima njoo hapa alaah.“alisema Mkuu na wanafunzi wakarudi kwenye viti vyao huku Jafari akisogea pale mbele na kushikwa mkono na Bokeloo.
“wewe una makosa mawili kwanza, kwanza wewe ni TIME KEEPER ulipaswa uwahi kugonga kengele ndio watu wahesabu namba saa moja kamili,leo kengele nimegonga mimi mwenyewe saa moja na dakika 15 hivyo umeharibu ratiba nzima ya shule leo mpaka sasa vipindi havijaanza,utabeba adhabu hii peke yako lazima uwajibike,twende huku.“alisema Mkuu akitoka nje na kijana Jafari aliyeshikwa mkono. Watu wakawa wanatazama tu madirishani wakitaka kushuhudia adhabu gani atakayopatiwa.
Upande wa pili katika nchi ya kifalme kunaonekana kuna mkusanyiko wa watu katika uwanja mmoja nje ya jengo la kifalme. Kwenye jukwaa ambalo ni maalumu kwaajili ya kutoa hukumu anaonekana babu mmoja akiwa amefungwa kamba kwenye nguzo ya mti mrefu huku mwili wake ukiharibika kwa kupigwa sana na askari wa kifalme. Alichoka mwili mzima akisubiri hukumu yake tu ambayo ilisadikika mzee huyo ni mchawi na baya zaidi ameweza kumroga mpaka binti wa kifalme ambaye hadi sasa bado yu taabani kitandani hanyanyuki. Mzee huyo alipokamatwa na kubinywa ili aweze kueleza dawa ya kumtibu binti huyo alikataa katakata na kusema hawezi kusaidia falme haramu inayoongozwa na Mfalme Siddik hivyo ilibidi Mfalme Siddik atoe amri ya kumnyonga mzee huyo kwa kumkashifu Mfalme kisha waangalie namna nyengine ya kumsaidia binti wake maana hakukuwa na jinsi maana mzee yule aliapa kutomponesha binti huyo. Basi siku hiyo ya hukumu watu walifurika sana akiwemo hata binti wa mzee huyo aliyeitwa Nadhra. Yeye alikuwa mstari wa mbele kabisa akiwa mwenye huzuni sana akimtazama baba yake huyo akiwa amenin‘ginizwa kwenye nguzo kubwa akisubiri hukumu yake ambayo kila mmoja aliifahamu hukumu ya mtu mchawi,ni kunyongwa mpaka kufa.
Mzee huyo akiwa pale juu huku damu zikimtiririka alipata kumuona mwanaye pale mbele akiwa analia tu,alitabasamu baada ya kumuona mwanaye.
“Nadhra...usilie binti yangu,ukifanya hivyo utanifanya huko niendako niwe na huzuni kuwa nimemuacha binti muoga,simama kwenye msimamo nilio kwambia na hiyo pete kaitupe sehemu yeyote ya kengele kabla ya hukumu yangu kama unataka niwe nawe kiroho siku zote“alisema Mzee huyo moyoni mwake lakini kwa uwezo alio nao Nadhra alipata kusikia yote aliyosema baba yake.
“mimi naamini nguvu zako baba sio za kudhuru mtu, wana kuhukumu bure tu hawa watu wa kifalme.“alisema Nadhra moyoni mwake akiwa anawasiliana na baba yake aliyekuwa juu ya nguzo.
“hilo sio la kuliongelea kwasasa,fanya kile nilichokueleza hapo awali haraka.“alisema Mzee yule na binti yake akamuelewa. Waliangalina kwa mara ya mwisho mtu na mwanaye kila mtu akitokwa na machozi kisha Nadhra akageuka na kuondoka zake akipita katikati ya halaiki ya watu waliofurika kushuhudia hukumu hiyo.
“PISHA NJIA MFALME ANAPITA...“ilisikika sauti ya maaskari na kuwafanya watu waache njia kubwa ya msafara wa Kifalme ukiwasili sehemu ile.Nadhra alipata kuutazama tu msafara ule ukimpita akiwa naye amesimama pembeni hadi Mfalme Siddik alipopita akiwa juu ya farasi na wafuasi wake na kufika kwenye jukwaa lile alilopo baba wa Nadhra. Kiliandaliwa kitanzi maalumu kwaajili ya kukamilisha hukumu hiyo na hapo ndipo Nadhra akapata akili kumbe aliagizwa kufanya jambo. Haraka akaanza kukimbia sasa kwenda kutafuta mahala popote pale palipo kengele ili apate kuitupa pete aliyo agizwa na baba yake upate kusikika mlio kutoka kwenye kengele kwa imani yao ndio itakuwa afadhari ya baba yake atakuwa amejitoa kiroho katika mwili ambao utanyongwa hivyo ataendelea kuishi kama kawaida lakini hataweza kuonekana kama awali. Na asipofanikiwa Nadhra ni kwamba baba yake atakufa kabisa pindi atakapo nyongwa.
ITAENDELEA