Simulizi : Safari Ndefu Kuelekea Kaburini

Simulizi : Safari Ndefu Kuelekea Kaburini

SEHEMU YA 16

alijiona kuwa mpenzi wa Patricia japokuwa bado hakuwa ameambiwa hivyo na msichana yule.
Martin akaamua kuanza kujipanga tayari kwa kumwambia Patricia ukweli wa moyo wake, kamwe hasingeweza kuvumilia na wakati moyo wake ulikuwa ukizidi kujisikia kiu ya kufanya kile ambacho alikuwa akihitaji kukifanya. Siku hiyo aliamua kukaa sana na Patricia chumbani kwake na hapo hapo ndipo alipoamua kulitoa duku duku lile ambalo lilikuwa moyoni mwake.
“Nafahamu hata kabla haujaniambia hivyo” Patricia alimwambia Martin na kuendelea.
“Sihitaji kujiingiza kwenye mapenzi Martin” Patricia alimwambia Martin maneno ambayo yalionekana kumvunja nguvu.
“Kwa nini Patricia? Kwa nini hautaki kuingia kwenye mahusiano ya mapenzi pamoja nami?” Martin aliuliza kwa sauti ndogo iliyojaa huruma.
“Unafahamu kwamba ninakupenda?” Patricia alimuuliza Martin.
“Nafahamu”
“Basi fahamu kwamba sitaki uumie” Patricia alimwambia Martin ambaye alionekana kuchanganywa na maneno yale.
“Hautaki niumie? Kivipi?” Martin aliuliza kwa mshangao.
“Wewe jua hivyo tu. Sitaki kukuumiza” Patricia alimwambia.
Patricia hakutaka kukaa sana chumbani humo, akatoka na kuanza kuongea na Bi Maria, mama yake Martin. Martin alibaki chumbani huku akionekana kuchoka kupita kawaida, maneno ambayo aliyaongea Patricia yalionekana kumuondoa nguvu zote. Mawazo yake katika kipindi hicho yakajipa uhakika kamba msichana huyo tayari alikuwa katika uhusiano na mtu mwingine na ndio maana hakutaka kuwa nae kwa kuwa aliamini angemuumiza tu.
Akainuka kitandani pale na moja kwa moja kueleka nje ya chumba kile. Kila alipokuwa akimwangalia Patricia alikuwa akichka zaidi, uzuri wa Patricia ambao alikuwa akiuona wala haikufaa kabisa kuwa rafiki yake. Patricia akaamua kuaga mahali hapo na kisha kuingia ndani ya gari pamoja na Martin.
Martin alikuwa ametulia katika kiti pembeni ya Patricia, muda wote alikuwa akimwangalia huku akionekana kumchunguza kutokana na uzuri wake ambao alikuwa nao, bado moyo wake atika kipindi hicho ulikuwa na hamu kubwa ya kuendelea kumwambia Patricia umuhimu wa msichana huyo katika maisha yake.
“Nakupenda Patricia. Nakupenda sana” Martin alimwambia Patricia.
“Nafahamu. Nakupenda pia Martin ila kuingia kwenye uhusiano pamoja nae ni kitu kisichowezekana kabisa” Patricia alimwambia Martin.
“Lakini kwa nini Patricia?”
 
SEHEMU YA 17

“Nimekwishakwambia kwamba sitaki kukuona ukiumia Martin. Ninakupenda sana tena sana tofauti na unavyofikiria. Sitaki kukuona ukiumia Martin” Patricia alimwambia Martin.
“Hautaki kuniona nikiumia! Kivipi? Una mvulana au? Hata kama una mvulana, niambie tu ili nijue sababu kuliko kuniweka kwenye hali kama hii” Martin alimwambia Patricia.
“Sina mvulana na wala sihitaji kuwa na mvulana. Na kama nitahitaji kuwana mvulana basi naamini wewe ndiye utakuwa mvulana wangu” Patricia alimwambia Martin.
“Lakini mbona hautaki kuniambia?”
“Muda bado. Muda ukifika nitakwambia. Tusome kwanza” Patricia alimwambia Martin.
Bado maneno yale yalionekana kumchanganya Martin, ilikuwaje msichana akatae kuwa nae kwa kuwa alihofia kumuumiza. Kwake, alikuwa amejitoa asilimia mia moja kuumia kwa ajili ya Martin hata kama kitu gani kitatokea huko mbele lakini ili mladi tu awe nae katika uhusiano wa kimapenzi.
“Labda kama una sababu nyingine”
“Wala hakuna. Sababu ni hiyo hiyo. SITAKI KUKUUMIZA” Patricia alimwambia Martin ambaye alionekana kuwa mpole.

Je nini kitaendelea?
Je Patricia ataendelea na msimamo wake?
Je ni maumivu ya aina gani ambayo yanamfanya Patricia kutotaka kuingia katika mahusiano na Martin?

ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 18

Martin hakuonekana kuwa na furaha hata kidogo, usiku hakukulalika hata kidogo, muda wote alikuwa akionekana kuwa na mawazo tu. Kitendo cha Patricia kumkatalia kuingia katika mahusiano pamoja nae kulionekana kumuumiza kupita kawaida kwani kila siku ndoto zake zilikuwa ni kuwa katika mahusiano na msichana huyo mrembo.
Kila wakati alikuwa akiichukua simu yake na kisha kuliangalia jina la Patricia, alitamani sana kumpigia lakini kila alipokuwa akifikiria jinsi ambavyo msichana huyo alivyokuwa akikataa kuwa katika mahusiano pamoja nae alikosa nguvu za kumpigia. Hakujua ni kwa namna gani ambavyo angeumia hapo baadae kama tu Patricia angekubali kuingia katika mahusiano pamoja nae.
Kila alipokuwa akijiuliza, alikosa jibu kabisa. Alikuwa tayari kuyapata maumivu yoyote yale ambayo yangetokea hapo baadae lakini ili mladi tu akubaliwe kuingia katika mahusiano na msichana yule ambaye alikuwa ametokea kumpenda kupita kawaida. Kichwa chake bado kilikuwa kikifikiria namna ya maumivu ambayo angeyapata baadae lakini alikosa jibu ni aina gani ya maumivu ambayo angeyapata.
Akaanza kujifikiria labda Patricia alikuwa katika mahusiano ya kimapenzi na mvulana mwingine lakini hakuweza kukubaliana na hilo. Muda mwingi alikuwa pamoja na Patricia, je kama alikuwa na mwanaume, huyo mwanaume alikuwa wapi na alikuwa akiwasiliana nae vipi? Wazo hilo likaonekana kutokuwa na nguvu kichwani mwake jambo lililomfanya kuachana nalo.

Akaanza kufikiria kwamba labda Patricia alikuwa ameathirika lakini napo wazo hilo likaonekana kutokumuingilia akilini. Kila siku Patricia alikuwa akinawili zaidi na zaidi, je huo UKIMWI alikuwa ameupata wapi na wakati kuna kipindi alimwambia ukweli kwamba alikuwa msichana bikira, msichana ambaye hakuwahi kukutana kimwili na mwanaume yeyote yule.
Kila kitu ambacho alikuwa akikifikiria mahali hapo alikosa jibu kabisa, hakuelewa ni sababu zipi ambazo zilimfanya Patricia kutotaka kuingia katika mahusiano pamoja nae. Alijiona kuwa na kila sababu za kulalamika na kumlazimisha Patricia kuingia katika mahusiano pamoja nae.
Usiku ulionekana kuwa mgumu kwake, usingizi ambao alikuwa nao ukapotea kabisa, mawazo yake yalikuwa kwa Patricia tu, alitamani akubaliane na
 
SEHEMU YA 19

Patricia kwamba wasiingie katika mahusiano lakini jambo hilo likaonekana kuwa gumu kwake.
Moyo wake tayari ukaanza kupatwa na wasiwasi kwamba kuna siku Patricia angekuja kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mvulana mwingine jambo ambalo lingemfanya kuumia zaidi maishani mwake. Hakutaka kuliona jambo hilo likitokea katika maisha yake, alitamani kuwa na Patricia katika maisha yake yote.
Kichwa chake kikaanza kufikiria tena muziki, nyimbo ambazo zilikuwa zikija kichwani mwake ni zile ambazo zilikuwa na majonzi ya kuachwa na kukataliwa kuwa katika mahusiano. Martin alikuwa na kila sababu za kuandika aina hizo za nyimbo kutokana na kile ambacho alikuwa akikipitia kwa wakati huo.
******
Hali ambayo ilikuwa ikitokea kwa Martin ilikuwa ni hali ile ile ambayo ilikuwa ikimtokea Patricia. Muda wote alikuwa akimfikiria Martin, ni kweli kwamba alitamani kuingia katika mahusiano ya kimapenzi na Martin lakini bado moyo wake ulikuwa ukiogopa kumuumiza.
Alimpenda sana Martin hivyo hakuwa radhi kumuumiza, alipenda sana kumuona mvulana huyo akiishi katika maisha ya furaha, hakutaka yeye kuwa moja ya sababu ambayo ingemfanya Martin kutokuishi katika maisha ya furaha na amani, alikuwa akifanya kila liwezekanalo ili kumfurahisha Martin hasa katika kipindi cha baadae na si katika kipindi hicho.
*****
Mwaka ukakatika na hatimae kuingia kidato cha nne. Urafiki wao bado ulikuwa ukiendelea kama kawaida huku katika kipindi hiki ukiwa umezidi zaidi na zaidi. Bado walikuwa wakiendelea kusaidiana kwa kila kitu. Wanafunzi wote shuleni walikuwa wakiufahamu uhusiano huo kwamba watu hao walikuwa wapenzi.
Hapo ndipo mambo yalipoanza kubadilika. Martin na Patricia wakaanza kuishi maisha kama wapenzi. Wakaanza kunyonyana midomo na kuanza kutomasana hasa katika kipindi ambacho walikuwa ndani ya gari. Miili yao ilikuwa ikizidi kuwaka tamaa ya kufanya ngono katika maisha yao. Kila mmoja akawa na hamu ya kuuona mwili wa mwenzake, siku ambayo walitaka jambo hilo lifanyike ikapangwa na kila mtu kuisubiria kwa hamu.
 
SEHEMU YA 20

Siku ikafika. Gari aina ya Harrier nyeusi ilisimama katika eneo la hoteli ya Mtanzania. Patricia na Martin wakateremka na moja kwa moja kuelekea mapokezini na kisha kuchukua chumba. Walipoingia chumbani tu, wakaanza kukumbatiana, mabusu mfululizo yakaanza kupigwa jambo ambalo likawafanya kuanza kusaidiana kuvuana nguo.
Ni ndani ya dakika moja, wote walikuwa watupu. Martin akaanza kufanya mambo yake, japokuwa ndio kwanza ilikuwa mara yake ya kwanza kufanya kile ambacho alikuwa akikifanya lakini akaonekana kuwa kama mjuzi. Patricia alikuwa akilalamika tu pale kitandani jambo ambalo lilikuwa likimpa Martin nguvu ya kuendelea kufanya kile ambacho alikuwa akikifanya.
“Sijawahiiii....” Yalikuwa maneno ambayo yalisikika kutoka kwa Patricia.
Ni kweli. Patricia hakuwa amekutana kimwili na mvulana yeyote katika maisha yake, alikuwa bikira. Martin ndiye alikuwa mwanaume wa kwanza kuyaona matiti yake, alikuwa ndiye mwanaume wa kwanza kuyaona mapaja yake mazuri na pia alikuwa mwanaume wa kwanza kumvua nguo yake ya ndani.
Harufu nzuri ya manukato ambayo alikuwa akinukia Patricia mwilini mwake ndiyo ambayo ilimfanya Martin kuchanganyikiwa zaidi na zaidi. Alifanya kila awezalo kumlainisha Patricia mpaka pale ambapo wakaanza kuvunja amri ya sita mahali pale.
Patricia alikuwa akipiga kelele za maumivu chini ya kitovu lakini Martin hakuonekana kumuacha, bado alikuwa akiendelea na shughuli yake. Damu zikaanza kuonekana, moyo wa Martin ukaanza kuogopa lakini alipokumbuka kwamba jambo hilo hutokea kwa msichana yeyote ambaye alikuwa akifanya kitendo kile kwa mara ya kwanza, hofu ikamtoka na kuendelea.
Kitendo kile kilichukua saa moja, kila mmoja alikuwa amechoka, wakabaki wakiangaliana tu. Wakainuka na kuelekea bafuni ambako wakaoga na kisha kuondoka hotelini hapo. Hiyo ndio ilikuwa siku ya kwanza kwa wao kukutana kimwili. Hawakuishia hapo, kila siku walikuwa wakiendelea kufanya zaidi na zaidi. Walifanya ngono kila sehemu ambayo waliiona kustahili kufanyiwa mapenzi.
Patricia akazidi kunawili zaidi na zaidi, urembo wake ukazidi kuongezeka zaidi na zaidi, hipsi zake zikaanza kutanuka huku mwili wake ukizidi kutamanisha
 
SEHEMU YA 21

zaidi na zaidi kwa kila mvulana ambaye alikuwa akimwangalia.
Wakaendelea kusoma, juhudi zao za kusoma zikaogezeka zaidi na zaidi mpaka pale ambapo wakaja kufanya mtihani wa Taifa wa kidato cha nne. Walipomaliza, wakapata uhuru wa kukaa nyumbani, ukaribu wao ukazidi zaidi na zaidi lakini huku Patricia akionekana kuwa mpweke zaidi. Kila siku Martin alikuwa na kazi ya kumuuliza Patricia sababu ambayo ilikuwa imemfanya kuwa katika hali ile lakini Patricia hakuwa radhi kuzungumza.
“Lakini kwa nini Patricia? Kwa nini unakuwa hivyo?” Martin aliuliza.
“Usijali Martin. Nipo salama” Patricia alijibu kiunyonge.
“Sasa kwa nini upo hivyo? Una mimba?”
“Hapana”
“Sasa tatizo nini?”
“Usijali. Achana na hayo”
“Sawa. Uko tayari kwa sasa kuwa mpenzi wangu?” Martin alimuuliza Patricia swali ambao likamuongezea majonzi zaidi.
Martin akaonekana kubadilia, katika maisha yake hakutamani kumuona Patricia akiwa katika hali ile, majonzi ambayo alikuwa nayo yalionekana kumsikitisha. Akamsogelea na kumkumbatia. Patricia akaanza kulia, alilia sana kama mtu ambaye alikuwa amefiwa na mtu ampendae.
“Uko tayari?”
“Hapana Martin” Patricia alijibu.
“Lakini kwa nini?”
“Sitaki kukuumiza. Najua utaumia tu”
“Nitaumia? Kivipi?”
Patricia hakujibu swali hilo, alibaki kimya huku akimwangalia Martin usoni. Macho ya Martin tayari yakaanza kuonyesha wasiwasi mkubwa jambo ambalo lilimfanya Patricia kuonekana kuwa na majonzi zaidi na zaidi. Wakakumbatiana tena na kisha kuanza kupiga stori nyingine.
Muda ulikuwa umekwenda sana na hivyo Patricia kuaga mahali hapo. Wote kwa pamoja wakaanza kupiga hatua kulifuata gari lile, walipolifikia, Patricia akasimama kwa nje, akamshika mikono Martin na kisha kuuinamisha uso wake chini.
Siku hiyo Patricia alionekana kuwa na majonzi kuliko siku zote, machozi yalikuwa yakimtoka muda wote, alionekana kuumia kupita kawaida. Akamvuta Martin kwake na kumkumbatia. Siku ilionekana kuwa ya majonzi kwa Patricia jambo ambao lilimchanganya sana Martin.
“Mbona unaonekana hivyo?” Martin alimuuliza Patricia ambaye wala hakujibu chochote. Wakakumbatiana tena. Yaani ulikuwa ni muda wa kukumbatiana wakati wote.
 
SEHEMU YA 22



Patricia akatoka kifuani mwa Martin na kisha kuufungua mlango wa gari na kutoa boksi moja ambalo lilikuwa limerembwa na lilionekana kuwa na zawadi fulani ndani yake. Akamkabidhi Martin ambaye alikuwa akitetemeka kwa hofu kwani tayari alikuwa amekwishaona mabadiliko fulani.
“Asante. Ila kuna nini?” Martin aliuliza huku akitaka kufungua.
“Usifungue. Utafungua chumbani kwako katika kipindi ambacho nitakuwa nimeondoka” Patricia alimwambia Martin ambaye akatii.
Patricia akamkumbatia tena Martin na kisha kuingia garini ambako akaliwasha na kuondoka mahali hapo huku ikiwa imetimia saa tano kasoro usiku. Martin akaonekana kuwa na kimuemue, akaondoka mahali hapo na kuelekea chumbani kwake, akakaa kitandani na kuanza kulifungua boksi lile.
Mwili wake ulikuwa ukitetemeka, hali ambayo aliionyesha Patricia tayari ilionekana kumtia wasiwasi moyoni. Kijasho chembamba kikaanza kumtoka huku akizidi kutetemeka zaidi na zaidi. Kitu cha kwanza ambacho alikuwa amekutana nacho katika boksi lile ilikuwa ni karatasi ambayo akaifungua kwa haraka haraka na kukutana na mwandiko mzuri. Hakutaka kupoteza muda, akaanza kuisoma barua ile ambayo ilionekana kuanza kumtia wasiwasi. Kadri ambavyo alivyokuwa akisoma na ndivyo ambavyo wasiwasi ukazidi kumshika zaidi na zaidi, alipomaliza kuisoma tu, machozi yalikuwa yakimtoka, kila alipokuwa akijaribu kuyafuta, yalikuwa yakimtoka zaidi na zaidi.
“Patricia......Patricia....” Martin alijikuta akiita kwa uchungu, akasimama na kuanza kwenda nje huku akionekana kuchanganyikiwa.
Barua ile tayari ikaonekana kumchanganya, akaanza kukimbia kuelekea nyumbani kwa kina Patricia, japokuwa alikuwa akikaa Mwananyamala na Patricia alikuwa akikaa Mikocheni B lakini hakuonekana kujali, alikuwa akikimbia kwa kasi kuelekea nyumbani kwa kina Patricia huku akionekana kuchanganyikiwa.
Barua ile ambayo alikuwa ameisoma, ilikuwa imeandikwa hivi.

Kwako Martin.

Najua kwamba utachanganyikiwa sana kile ambacho utakisoma katika karatasi hii lakini naomba uamini kwamba huu ndio ukweli wenyewe ambao umenifanya mimi kutotaka kuingia katika mahusiano pamoja na wewe. Naomba ujipe nguvu ya kusoma mpaka pale ambapo utamaliza kuisoma barua hii ambayo itakushtua sana na kukufanya kutokuwa na furaha kabisa.
Najua kwamba umetokea kunipenda sana ila sidhani kama ulikuwa
 
SEHEMU YA 23

ukinipenda kama ambavyo nilitokea kukupenda Martin. Tumekuwa marafiki kwa muda mrefu sana, tukazoeana mpaka kufikia hatua ya kufanya kila kitu ambacho wapenzi wanastahili kukifanya hasa wanapokuwa faragha. Naomba uamini kitu kimoja Martin kwamba sisi hatukuwa wapenzi bali tulikuwa marafiki wa kawaida kama wengine.
Huu ni muda wangu wa kukwambia kwamba sitoweza kuwa pamoja nawe tena kwa sababu moja kubwa kwamba ninahama nchini Tanzania na kuhamia nchini Marekani ambako nitakwenda kuishi na baba yangu mzazi, mzee Thomson.
Maisha yangu yataanza nchini Marekani na kumalizia nchini humo bila ya kuwa na ndoto zozote za kurudi nchini Tanzania. Najua kwamba umeshtuka sana Martin ila naomba ujipe nguvu moyoni mwako. Kila siku ulikuwa ukinitaka niingie katika mahusiano pamoja nawe ila nilikuwa nikikataa kila siku, na hii ndio ilikuwa sababu kubwa.
Kamwe nisingeweza kuingia katika mahusiano na wakati nilikuwa na mikakati ya kuondoka nchini Tanzania. Ningeweza vipi kuingia kwenye mahusiano na wakati nilikuwa na muda mchache wa kuishi nchini Tanzania? Najua ungeumia sana hata zaidi ya unavyoumia kwa sasa endapo tu ningekuwa mpenzi wako Martin.
Sikutaka kukuaga Martin kwa sababu sikutaka kukuona ukiwa na majonzi, sikutaka kukuona ukilia kwa ajili yangu na wakati nilikuwa ninatimiza ahadi ambayo nilimuahidi baba yangu ya kuishi pamoja nae mara nitakapomaliza kidato cha nne. Sikutaka kuyaona machozi yako, sikutaka kuisikia sauti yako ya kilio chako masikioni mwangu.
Najua kwamba maisha yako yatategemea zaidi muziki, naomba ufanye muziki Martin na achana na masomo kwani naamini kama utaingia kwenye masomo hautofanya vizuri kwa kuwa tu utakuwa kwenye hali ya mawazo mengi.. Nakuomba uendelee na muziki kwani nyimbo zako nzuri natumaini zitakufanya kupata mashabiki wengi watakaokupenda na kuvutiwa nawe.
Katika boksi hili nimekuwekea kadi yangu ya benki ambayo ina kiasi cha zaidi ya milioni kumi na tano. Naomba uzitumie fedha hizo katika kuyaendeleza maisha yako huku nami nikikutumia kiasi cha zaidi ya milioni tatu kila mwezi
 
SEHEMU YA 24

katika akaunti hiyo hiyo. Usijali kuhusu kuitumia kadi yangu, kabla sijaondoka, kila dokumenti nimebadilisha na kuliandika jina lako kama mmiliki wa akaunti hiyo.
Nakupenda sana Martin ila haina jinsi, inanipasa kuondoka kuanza maisha na baba yangu mbali nawe. Najua tutaweza kuonana, ila katika kipindi hicho nadhani utakuwa tayari una familia yako na mimi pia nitakuwa na familia yangu. Kama utaweza, naomba unitoe moyoni mwako, na kama kutatokea msichana ambaye atatamani kuwa nawe, naomba umkubalie tu ila kama utakuwa na uhakika kwamba hatokuja kukuumiza maishani mwako.
Najua kuna wengi watakupenda kwa kuwa naamini utakuwa supastaa ila itakupasa kuwa makini Martin kwa kuamini kwamba si kila anayekupenda atakuwa na mapenzi ya dhati kwako kama niliyo nayo. Pamoja na hayo, nitafanya kila liwezekanalo maishani mwangu kukununulia nyumba nzuri ya kuishi nchini Tanzania. Nafikiri baada ya mwaka mmoja, nitahitaji utafute nyumba nzuri ambayo itakuwa na hadhi kubwa ya kuishi kwa mtu kama wewe nami nitakununulia kwa kukutumia kiasi hicho cha fedha.
Natumaini baba yangu atanisaidia kufanikisha kila kitu ambacho ninakuahidi kwa sababu ana uwezo mkubwa kifedha.
Usiku wa leo ndio nitapanda ndege kuelekea nchini Marekani. Mama amekwishanipelekea mabegi yangu uwanja wa ndege na ni mimi tu ndiye ninayesubiriwa. Nakuomba Martin jipe moyo wa ushujaa, nakuomba ujipe moyo kwamba utampata msichana mzuri na atakayekupenda zaidi yangu.
Nakutakia maisha mema, naomba uniagie kwa mama na umwambie kuhusu mapenzi mazito niliyo nayo juu yako. Nakupenda Martin.

Ni mimi
Patricia Thomson.

******

Bado Martin alikuwa akikimbia kwa kasi kuelekea nyumbani kwa kina Patricia huku jasho likimtoka. Machozi yalikuwa yakimtoka muda wote, bado alikuwa akilia kwa uchungu. Kasi ambayo alikuwa akiitumia ilionekana kumshangaza kila mtu ambaye alikuwa akimwangalia mahali pale.
“Ungeniambia Patricia....ungeniambia Patricia” Martin alikuwa akijisemea huku akizidi kukimbia kuelekea Mikocheni B huku tayari akiwa amekwishafika Sayansi, Kijitonyama.

Martin aliingia katika eneo la nyumba ya kina Patricia huku saa yake ikimwambia kwamba tayari ilikuwa saa sita usiku. Alikuwa akihema kupita
 
SEHEMU YA 25

kawaida. Sauti mbalimbali za mbwa ambazo zilikuwa zikisikika masikioni mwake zilikuwa zikimtia wasiwasi. Akaanza kumfuata mlinzi na kuanza kuongea nae.
Muda wote Martin alionekana kutokuwa na furaha moyoni mwake, alikuwa akiongea kwa uchungu jambo ambalo lilimfanya hata yule mlinzi kumshangaa. Hali ambayo alikuwa nayo Martin alikuwa akitia huruma kupita kawaida, uso wake ulikuwa katika majonzi makubwa.
“Nadhani ndege yenyewe itakuwa imekwishapaa kwani ratiba yake ilikuwa saa sita na nusu” Mlinzi alimwambia Martin ambaye akaangalia saa yake na kukuta kwamba tayari ilikuwa saa sita na dakika ishirini na saba.
Martin akakaa chini, machozi bado yalikuwa yakimtoka kupita kawaida. Moyo wake ulikuwa katika maumivu makali kuliko kipindi chochote katika maisha yake. Kama ambavyo alitabiri Patricia ndivyo ambavyo ilivyotokea, Martin alikuwa ameumia kupita kawaida. Hakutaka kuondoka mahali hapo siku hiyo, alichokifanya ni kumsubiri mama yake Patricia, Bi Beatrice.
Zilipita dakika hamsini, gari aina ya Harrier ambalo alikuwa ameondoka nalo Patricia likaanza kulisogelea geti la nyumba ile na kisha kuanza kupiga honi. Mlinzi akaanza kulifuata geti lile na kisha kulifungua na gari kupita. Bi Beatrice akateremka, macho yake yakatua usoni mwa Martin ambaye alikuwa amelia vya kutosha.
Bi Beatrice akamsogelea Martin na kisha kumkumbatia. Moyo wake ulifahamu ni kwa kiasi gani Martin alikuwa ameumia moyoni mwake kutokana na kitendo cha Patricia kuondoka nchini huku akimuaga katika hatua za mwisho kabisa.
“Nyamaza Martin.....Nyamaza mwanangu” Bi Beatrice alimbembeleza Martin ambaye alikuwa akiendelea kulia.
Martin hakunyamaza, tukio ambalo lilikuwa limetokea lilionekana kumuumiza kuliko matukio yoyote ambayo yalikuwa yametokea katika maisha yake. Alimpenda sana Patricia zaidi ya msichana yeyote katika dunia hii, aliona kuwa na haki za kuishi na Patricia katika kipindi chote cha maisha yake ambacho angeishi katika dunia hii.
Bi Beatrice akamchukua Martin na kwenda nae ndani na kisha kukaa nae kochini. Muda wote Martin alikuwa akionekana kuwa na huzuni, machozi kwake hayakukauka hata kidogo. Bado alikuwa akimhitaji Patricia wake ambaye alikuwa ameondoka kuelekea nchini Marekani kuishi na baba yake.

ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 26

Bi Beatrice hakutaka kumchelewesha Martin, alichokifanya ni kumpakiza kwenye gari lake na kurudisha nyumbani kwao huku ikiwa imetimia saa nane kasoro usiku. Ndani ya gari, Martin hakuongea kitu chochote kile, muda wote macho yake yalikuwa yakiangalia nje.
Alipofika nyumbani kwao, akateremka na kumuaga Bi Beatrice na kisha kuanza kuelekea chumbani kwake. Mama yake hakuwa amelala, muda wote alikuwa macho akimsubiria Martin ambaye hakuwa amejua ameelekea mahali gani.
“Mbona unaonekana hivyo?” Mama yake, Bi Evadia alimuuliza.
Martin hakutoa jibu lolote lile, akaanza kupiga hatua kuelekea chumbani kwake na kisha kujitupa kitandani. Bi Evadia hakuonekana kuridhika, akaanza kupiga hatua kumfuata chumbani kule na kumuuliza swali lile lile zaidi ya mara tatu.
“Patricia ameondoka” Martin alimwambia mama yake.
“Usijali. Kesho si atarudi tena”
“Hapana mama. Hawezi. Ameondoka kuelekea nchini Marekani. Hatorudi tena” Martin alimwambia mama yake huku machozi yakianza kumtoka tena.
Bi Evadia akaonekana kushtushwa na maneno yale, akakataa kuamini kwamba kile ambacho alikuwa amekizungumzia Martin kilikuwa na ukweli wowote ule. Alichokifanya Martin ni kuichukua ile barua na kumgawia mama yake.
“Fedha si kitu kwangu. Muhimu kwangu ni mapenzi yake tu” Martin alijisemea.
*****
Patricia alikuwa akiendesha gari kuelekea uwanja wa ndege, uso wake ulikuwa na majonzi makubwa huku muda wote macho yake yakitoa machozi. Moyo wake ulikuwa ukimuuma kupita kawaida, kitendo cha kuondoka nchini Tanzania kuelekea nchini Marekani huku akimuacha Martin nchini Tanzania.
Moyoni hakupenda kabisa kuondoka lakini hakuwa na jinsi, kwa wakati huo alikuwa na wajibu wote wa kutekeleza ahadi ambayo alikuwa amemuahidi baba yake, Bwana Thomson ya kwenda kuishi nchini Marekani
Kichwani alikuwa na mawazo tele, bado machozi yalikuwa yakiendelea kumtoka. Alichokifanya baada ya kufika Boma ni kulipaki gari pembeni na kuegemea usukani wa gari lake. Kilio cha sauti kikaanza kusikika kutoka kwake. Alikaa katika eneo hilo kwa dakika kadhaa na ndipo alipoamua kuendelea na safari yake.
Akafika uwanja wa ndege na kuingia katika eneo la uwanja huo ambako
 
SEHEMU YA 27

akaanza kumtafuta mama yake. Wala hakuchukua sekunde zaidi ya thelathini, akamkuta ndani akiwa anamsubiri. Patricia hakuonekana kuwa na furaha kabisa, bado hali ya majonzi ilikuwa ikionekana usoni mwake.
Akamsogelea mama yake na kumkumbatia. Bi Beatrice akapata wakati mgumu wa kuanza kumbembeleza Patricia. Kadri alivyokuwa akibembelezwa na ndivyo ambavyo alizidi kulia zaidi na zaidi. Muda mwingi Patricia alikuwa akilitaja jina la Martin, mwanaume ambaye alikuwa ametokea kuuteka moyo wake kupita kawaida.
Tangazo likatolewa kwamba abiria wote ambao walikuwa wakielekea nchini Marekani kwa kutumia ndege ya shirika la American Airways walikuwa wakihitajika. Beatrice akamkubatia tena mama yake na kisha kuchukua mabegi yake mawili ambayo akayapeleka sehemu ya uchunguzi huku yeye akitangulia ndani ya ndege na mabegi yake kuchukuliwa na wahusika wa mizigo.
Patricia akaingia ndani ya ndege, akachukua nafasi isiyokuwa na mtu na kisha kutulia, Bado majonzi yalikuwa mengi moyoni mwake, hakuonekana kuwa na furaha hata kidogo. Abiria wakazidi kuingia ndani ya ndege ile mpaka idadi ya abiria mia na hamsini kutimia na kisha abiria wote kutakiwa kufunga mikanda.
Hilo ndilo lilikuwa tukio ambalo liliuchoma moyo wa Patricia kuliko matukio yote ambayo alikuwa amepitia katika maisha yake kabla ya hapo. Akabaki akiangalia dirishani, mianga ya taa ilikuwa ikionekana kwa mbali machoni mwake, majonzi ambayo alikuwa nayo yalizidi kuongezeka zaidi na zaidi kwani aliamini kwamba wala asingeweza kumuona Martin katika kipindi chote cha maisha yake japokuwa wangezidi kuwasiliana kwa kutumia simu.
******
Ndege ya shirika la ndege la American Airways ilikuwa ikitua katika uwanja wa ndege wa John F Kennedy uliokuwa katika jiji la New York nchini Marekani. Ndege ile ikaanza kutembea katika ardhi ya nchi hiyo mpaka pale iliposimama na abiria kuanza kuteremka.
Macho ya Patricia yalikuwa yakiangalia katika kila upande katika uwanja ule, maghorofa yalikuwa yakionekana kwa mbali huku hali ya hewa ya kiubaridi kikiwa kinaupiga mwili wake. Patricia pamoja na abiria wengine wakaanza kutembea kuelekea katika jengo la uwanja ule na kisha kuchukua mabegi yao
 
SEHEMU YA 28

mara tu yalipomalizwa kuchunguzwa.
Patricia akayachukua mabegi yake mawili na kisha kuanza kupiga hatua kuelekea nje. Ghafla macho yake yakagongana na macho ya mwanaume mmoja ambaye alikuwa na ndevu aina ya mustachi, akamsogelea na kumkumbatia, alikuwa baba yake, Bwana Thomson.
Ilikuwa ni furaha kwa Patricia, ingawa katika kipindi kilichopita alikuwa na huzuni kwa kuwa alikuwa ameondoka nchini Tanzania lakini muda huo kidogo furaha ikaonekana kurudi japokuwa haikurudi kwa asilimia mia moja.
Bwana Thomson pamoja na binti yake, Patricia wakaanza kupiga hatua kuelekea nje ya jengo lile huku mabegi yakibebwa na kijana mmoja ambaye alionekana kuwa mfanyakazi wa Bwana Thomson. Walipofika nje, gari zuri na la gharama, Mc Lloyd lilikuwa likiwasubiri, mizigo ikapakiwa na kisha safari ya kuelekea katika mtaa wa kitajiri wa Frankline Square kuanza.
Muda mwingi macho ya Patricia yalikuwa yakiangalia nje, mandhari mazuri ya jiji la New York yalionekana kumvutia kupita kawaida. Moyoni alikuwa akifurahia muda wote, kuingia nchini Marekani huku akiwana baba yake kulionekana kumfariji kupita kawaida.
Dereva akachukua barabara ya St’ Peters na kunyooka moja kwa moja kama umbali wa kilometa tatu na kisha kuchukua barabara ya magari yaendayo kasi ya Smallville. Gari lilikuwa likiendeshwa kwa mwendo wa kasi kupita kawaida, barabara ilionekana kuwa bize muda wote, magari yalikuwa yakiendeshwa kwa kasi ya zaidi kilometa 200 kwa saa.
Walitumia muda wa dakika kumi na ndipo wakachukua barabara ya Rangers Park ambayo ilikuwa ikitumiwa sana na watu waliokuwa wakielekea katika jengo la kampuni ya kutengeneza majarida ya Cow Boy. Walitumia muda wa dakika mbili na ndipo wakaingia katika mtaa wa Frankline Square, mtaa ambao ulikuwa ukikaliwa na watu matajiri wakiwemo wafanyabiashara wakubwa, wacheza filamu, wanamichezo na watu wengine wengi.
Gari likaanza kusogea katika geti la nyumba moja iliyozungushiwa ukuta mkubwa na geti lile kujifungua. Gari likaanza kupita kuingia ndani. Kamera nyingi zilikuwa zikionekana ndani ya eneo lile huku zikizunguka katika kila
 
Back
Top Bottom