Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA 16
alijiona kuwa mpenzi wa Patricia japokuwa bado hakuwa ameambiwa hivyo na msichana yule.
Martin akaamua kuanza kujipanga tayari kwa kumwambia Patricia ukweli wa moyo wake, kamwe hasingeweza kuvumilia na wakati moyo wake ulikuwa ukizidi kujisikia kiu ya kufanya kile ambacho alikuwa akihitaji kukifanya. Siku hiyo aliamua kukaa sana na Patricia chumbani kwake na hapo hapo ndipo alipoamua kulitoa duku duku lile ambalo lilikuwa moyoni mwake.
“Nafahamu hata kabla haujaniambia hivyo” Patricia alimwambia Martin na kuendelea.
“Sihitaji kujiingiza kwenye mapenzi Martin” Patricia alimwambia Martin maneno ambayo yalionekana kumvunja nguvu.
“Kwa nini Patricia? Kwa nini hautaki kuingia kwenye mahusiano ya mapenzi pamoja nami?” Martin aliuliza kwa sauti ndogo iliyojaa huruma.
“Unafahamu kwamba ninakupenda?” Patricia alimuuliza Martin.
“Nafahamu”
“Basi fahamu kwamba sitaki uumie” Patricia alimwambia Martin ambaye alionekana kuchanganywa na maneno yale.
“Hautaki niumie? Kivipi?” Martin aliuliza kwa mshangao.
“Wewe jua hivyo tu. Sitaki kukuumiza” Patricia alimwambia.
Patricia hakutaka kukaa sana chumbani humo, akatoka na kuanza kuongea na Bi Maria, mama yake Martin. Martin alibaki chumbani huku akionekana kuchoka kupita kawaida, maneno ambayo aliyaongea Patricia yalionekana kumuondoa nguvu zote. Mawazo yake katika kipindi hicho yakajipa uhakika kamba msichana huyo tayari alikuwa katika uhusiano na mtu mwingine na ndio maana hakutaka kuwa nae kwa kuwa aliamini angemuumiza tu.
Akainuka kitandani pale na moja kwa moja kueleka nje ya chumba kile. Kila alipokuwa akimwangalia Patricia alikuwa akichka zaidi, uzuri wa Patricia ambao alikuwa akiuona wala haikufaa kabisa kuwa rafiki yake. Patricia akaamua kuaga mahali hapo na kisha kuingia ndani ya gari pamoja na Martin.
Martin alikuwa ametulia katika kiti pembeni ya Patricia, muda wote alikuwa akimwangalia huku akionekana kumchunguza kutokana na uzuri wake ambao alikuwa nao, bado moyo wake atika kipindi hicho ulikuwa na hamu kubwa ya kuendelea kumwambia Patricia umuhimu wa msichana huyo katika maisha yake.
“Nakupenda Patricia. Nakupenda sana” Martin alimwambia Patricia.
“Nafahamu. Nakupenda pia Martin ila kuingia kwenye uhusiano pamoja nae ni kitu kisichowezekana kabisa” Patricia alimwambia Martin.
“Lakini kwa nini Patricia?”
alijiona kuwa mpenzi wa Patricia japokuwa bado hakuwa ameambiwa hivyo na msichana yule.
Martin akaamua kuanza kujipanga tayari kwa kumwambia Patricia ukweli wa moyo wake, kamwe hasingeweza kuvumilia na wakati moyo wake ulikuwa ukizidi kujisikia kiu ya kufanya kile ambacho alikuwa akihitaji kukifanya. Siku hiyo aliamua kukaa sana na Patricia chumbani kwake na hapo hapo ndipo alipoamua kulitoa duku duku lile ambalo lilikuwa moyoni mwake.
“Nafahamu hata kabla haujaniambia hivyo” Patricia alimwambia Martin na kuendelea.
“Sihitaji kujiingiza kwenye mapenzi Martin” Patricia alimwambia Martin maneno ambayo yalionekana kumvunja nguvu.
“Kwa nini Patricia? Kwa nini hautaki kuingia kwenye mahusiano ya mapenzi pamoja nami?” Martin aliuliza kwa sauti ndogo iliyojaa huruma.
“Unafahamu kwamba ninakupenda?” Patricia alimuuliza Martin.
“Nafahamu”
“Basi fahamu kwamba sitaki uumie” Patricia alimwambia Martin ambaye alionekana kuchanganywa na maneno yale.
“Hautaki niumie? Kivipi?” Martin aliuliza kwa mshangao.
“Wewe jua hivyo tu. Sitaki kukuumiza” Patricia alimwambia.
Patricia hakutaka kukaa sana chumbani humo, akatoka na kuanza kuongea na Bi Maria, mama yake Martin. Martin alibaki chumbani huku akionekana kuchoka kupita kawaida, maneno ambayo aliyaongea Patricia yalionekana kumuondoa nguvu zote. Mawazo yake katika kipindi hicho yakajipa uhakika kamba msichana huyo tayari alikuwa katika uhusiano na mtu mwingine na ndio maana hakutaka kuwa nae kwa kuwa aliamini angemuumiza tu.
Akainuka kitandani pale na moja kwa moja kueleka nje ya chumba kile. Kila alipokuwa akimwangalia Patricia alikuwa akichka zaidi, uzuri wa Patricia ambao alikuwa akiuona wala haikufaa kabisa kuwa rafiki yake. Patricia akaamua kuaga mahali hapo na kisha kuingia ndani ya gari pamoja na Martin.
Martin alikuwa ametulia katika kiti pembeni ya Patricia, muda wote alikuwa akimwangalia huku akionekana kumchunguza kutokana na uzuri wake ambao alikuwa nao, bado moyo wake atika kipindi hicho ulikuwa na hamu kubwa ya kuendelea kumwambia Patricia umuhimu wa msichana huyo katika maisha yake.
“Nakupenda Patricia. Nakupenda sana” Martin alimwambia Patricia.
“Nafahamu. Nakupenda pia Martin ila kuingia kwenye uhusiano pamoja nae ni kitu kisichowezekana kabisa” Patricia alimwambia Martin.
“Lakini kwa nini Patricia?”