SASHA MLINZI WA NAFSI
Sehemu ya..........15
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
ILIPOISHIA...
"Shiiiiiiiiiiiiii...." Alisema mtu huyo ikiwa ni ishara kwa Tesha kwamba anyamaze kimya.
SASA ENDELEA...
"Kaka...!!" Tesha aliita kwa mshangao mara baada ya kuutoa mkono wa mtu huyo mdomoni kwake na kumtazama.
"Tuondoke hapa sasa hivi" Alisema yule mtu, alikuwa ni Godfrey kaka yake Tesha
"Umefikaje hapa?" Tesha aliuliza
"Huu sio wakati wake tuondoke kwanza hapa" Godfrey alisisitiza huku akiushika mkono wa Tesha akaanza kumvuta kuelekea kwenye gari lake, wakafika na kuingia ndani. Wakati huo ile sauti ya king'ora kutoka ndani ya mgahawa iliacha kusikika kukawa kimya.
"Vipi jamani kwema?" Aliuliza Dereva wa Tesha mara baada ya kuona mtu na kaka yake wameingia mkukumkuku ndani ya gari.
"Kaka God nini kinaendelea mbona sielewi, wale watu mle ndani ni akina nani?" Tesha naye akaongeza swali lingine huku akimtazama kaka yake kwa macho ya kuuliza. Ni kweli Tesha hakuwa akielewa chochote hadi dakika hiyo. Mambo aliyoyaona mle mgahawani na baadae kaka yake Godfrey anatokea ghafula kumtoa yalizidi kumshangaza.
"Endesha gari bro, tuondoke hapa haraka"Alisema Godfrey, Dereva akatii na kuwasha gari tayari kuondoka.
"Hebu subiri kwanza, usiondoke" Mara Godfrey alimzuia tena dereva huku akiwa ametoa macho kutazama kwenye 'site mirror'
"Pandisha vioo vya gari haraka" Alisema Godfrey, dereva akafanya kama anavyoagizwa.
Godfrey, Tesha na dereva wake waligeuka kutazama kule mgahawani wakawaona wale wanaume waliovaa helmet wanatoka getini mmoja baada ya mwingine huku wakiwa wamewabeba wale wanawake wa ajabu yaani Zucc na Femi ambao walikuwa wamepoteza fahamu wakati huo.
Mwanaume wa mwisho kutoka naye alikuwa amembeba kijana David begani kwake. David naye hakuwa akijilewa alikuwa amepoteza fahamu vilevile.
"David...!" Tesha aliita kwa sauti ya chini akajaribu kufungua mlango wa gari ili atoke lakini Godfrey akamzuia.
"Unafanya nini Tesha hebu jitulize kwanza!"
"Ni David wamemteka David.."
"Sawa, lakini ni hatari kama utatoka. Unataka na wewe uingie kwenye matatizo au?"
"Basi tupige simu Polisi haraka" Alisema Tesha kisha akachukua mkoba wake akatoa simu na kubinya namba 111.
"Acha usipige..." Alisema Godfrey
"Kwa nini kaka, mbona sikuelewi lakini..."
Alisima Tesha, Godfrey hakujibu kitu, akachukua simu yake akawa anawapiga picha wale wanaume wanne ambao waliingia kwenye gari wakiwa wamewabeba watu watatu yaani Femi, Zucc na David. Wakawasha gari lao na kuondoka kwa kasi eneo hilo.
Godfrey aliacha zoezi lake la kupiga picha, akavuta pumzi ndefu na kuitoa taratibu, alionekana mtu mwenye mawazo na wasiwasi mwingi. Akageuka na kumtazama mdogo wake Tesha.
"Nenda nyumbani Tesha nitakuja then tutaongea vizuri.."
"No tuonge hapa hapa, watu wametekwa mbele ya macho yetu alafu wewe kirahisi tu unanizuia nisipige simu polisi kwa nini ani! Istoshe aliyetekwa ni David mwanaume wangu"
"Mwanaume wako how!?" Aliuliza Godfrey huku akimtazama Tesha usoni, Tesha akatazama pembeni kwa aibu ni kama neno hilo lilimtoka kwa bahati mbaya.
"Yes he's my Man, kwani sikukwambia nina kazi naye? alafu kaka Godfrey hebu kuwa serious basi niambie ni nini kinaendelea..."
"Tesha nenda nyumbani kwanza kwa sasa sina muda wa kukueleza ila nakuahidi baada ya saa moja nitakuwa home tutaongea vizuri na kuhusu usalama wa huyo mwanaume wako niachie mimi" Alieleza Godfrey kisha akapokea simu yake iliyokuwa ikiita.
Tesha alipiga jicho la kuibia kutaza jina la mpigaji akalisoma
'Brandina-usalama'
"Hallo..." Godfrey alianzisha mazungumzo.
"Ndio nimefika hapa mbona sikuoni" Ilisikika sauti ya kike simuni.
"Nipo ndani ya hii gari mbele yako, nimeshakuona nakuja" Alijibu Godfrey kisha akakata simu. Nyuma yao aliliona gari dogo aina ya Toyota IST likifunga breki.
"Tesha nikukute nyumbani, just one hour okay" Alisema Godfrey. Kishingo upande Tesha akatikisa kichwa kukubali. Godfrey alishuka garini akapiga hatua na kuingia kwenye ile Toyota, wakati huo dereva wa Tesha naye aliwasha gari wakaondoka eneo hilo.
"Pole" Brandina mwanamke mmoja mweusi na mrembo aliyekuwa ndani ya gari alianzisha mazungumzo mara tu baada ya Godfrey kuingia na kuketi pembeni yake.
"Asante lakini sijafanikiwa kuwafuatilia"alijibu Godfrey
"Kwa nini?" Aliuliza Brandina huku akivua miwani yake
"Mdogo wangu alikuwa hapa, ikabidi nimtoe kwanza, ndiye aliyenichelewesha"
"Mdogo wako yupi Tesha?"
"Ndiyo"
"Tesha huyu super star'.."
"Yap"
"Sasa alikuwa anafanya nini kwenye huu mgahawa wa hadhi ya chini"
"Nafikiri kuna mtu alikuwa anakutana naye na hakutaka kuonekana, ni kijana mmoja anaitwa David naye kachukuliwa na hao majamaa tunao wafuatilia"
"Wamewachukua watu wangapi leo?"
"Watatu, nimeona wanawake wawili na huyu jamaa David ni watatu"
"Oops! Hawa jamaa wanatuumiza akili sana ni kheri serikali itangaze tu jambo hili na kuliweka wazi kuliko kufanya siri na watu wanaendelea kutoweka kila kukicha"
"Sasa kwa nini haitangazi, unajua siwaelewi kabisa?"
"Hawataki kutengeneza taharuki kwa raia, unajua hawa jamaa ni kama wana nguvu flani ambazo sio za kawaida yani ni kama wanatumia nguvu za giza hivi hata sielewi, huwezi kuamini ni miaka mitatu sasa tunaendelea kuwasaka kimya kimya lakini hakuna kitu tumewahi kupata hadi leo zaidi ya kukumbana na matukio ya ajabu ajabu yenye miujiza kibao"
"Lakini mbona kama hawa wanawake waliowateka leo sio wa kawaida yaani kwa kuwatazama tu wanamuonekano tofauti kabisa"
"Ndio maana nakwambia hili suala sio jepesi Godfrey. Kuna wakati hawa jamaa wenye helmet huwa wanaviteka viumbe vya ajabu kama hivyo unavyosema na kuna wakati huwa wanawateka binadamu wa kawaida kama walivyomteka mpenzi wako Dayana mwaka jana"
"Mmh! Sasa ni akina nani hawa?"
"Hatuelewi kabisa, vipi umepiga picha hata moja"
"Yap! Kuna hizi picha nimefanikiwa kuwapiga"
"Okay Good" Aliesema Brandina huku akiipokea simu ya David
Akawa anatazama picha zile moja baada ya nyingine.
"Si unaona hawa wanawake waliowabeba.. wamevaa magauni ya ajabu alafu yanafanana. Kwa Dunia yetu hii ni nani anaweza kuvaa kama hivi na akatoka mtaani kutembea"
"Ni ajabu sana, angalia hata gari la hawa jamaa halina plete number. Ni ngumu kuwapata" Godfrey aliongezea.
Baada ya hapo walishuka na kuingia mgahawani wakakagua mazingira na baadae walifanikiwa kumuona yule dada muhudumu aliyeanguka na kupoteza fahamu.
Brandina alipiga simu kutoa taarifa na punde gari ya wagonjwa ikafika na kumchukua.
"Huyu binti akiamka asizungumze na mtu yeyote hadi nifike mimi sawa" Brandina alitoa maelezo kwa mmoja kati ya watoa huduma wa afya waliofika mahali hapo.
"Sawa afande"
"God naomba unikutanishe na Tesha anaweza kuwa aliona chochote cha kutusaidia"
"Hapana, mdogo wangu hajaona chochote"
"Usijali sitamuingiza kwenye hii kesi isipokuwa nataka maelezo yake kidogo tu" Brandina alimtoa wasiwasi Godfrey.
[emoji294][emoji294][emoji294]
ISRA...
Jitihada za kumvuta Handan kutoka shimoni ziliendelea, farasi walizidi kusogea mbele huku kamba ya Handan nayo ikizidi kusogea juu taratibu kutoka shimoni. Wakati huo hali ya hewa ilikuwa shwari kabisa kile kimbunga na tetemeko la ardhi vilitoweka ghafula mara tu baada ya Sasha kuzama shimoni akiwa na farasi wake.
Baada ya jitihada kubwa za wale wanawake walinzi wa Sasha kufanyika mwisho kamba ilifika ukomo, watu hawakuamini macho yao mara baada ya kumuona Handan akichomoza kutoka shimoni huku akiwa amemkumbatia Sasha kifuani mwake.
Handan na Sasha walitoka nje ya shimo, wale wanawake wawili walinzi walikimbia na kwenda kuwapokea kwa furaha.
Miili ya Sasha na Handan ilikuwa imejeruhiwa vibaya mno kutokana na misukosuko waliyokutana nayo shimoni. Damu yenye rangi ya kijani ilikuwa ikiwatoka katika maeneo mbalimbali waliyojeruhiwa.
"Asante Handan..." Alisema Sasha huku akimtazama Handan usoni mlinzi wake namba moja aliyejitoa kuyaokoa maisha yake.
"Usijali, lakini kwa nini ukafanya hivyo Sasha? Uliingia kufanya nini msituni?" Aliuliza Handan wote wakawa makini kusikiliza Sasha atajibu nini. Sasha naye akawa anawaza ni jibu gani sahihi la kuwapa kwani tayari alishaelezwa kuwa kila alichoongea na Bi Noha kilikuwa ni siri kubwa. Hakutakiwa kabisa kuufungua mdomo wake kuzungumza kuhusu jukumu zito alilopewa la kumlinda mwanadamu David.
Akiwa anawaza nini ajibu mara watu zaidi ya kumi na tano walifika na kuwazunguuka huku wakiwa wamenyoosha panga zao mbele. Walikuwa ni wale watu kutoka msafara wa Dumayo mjomba wa Sasha.
"Kuna nini? Mnataka nini?" Aliuliza Sasha huku akiwatazama watu hao kwa macho makali.
"Hawajui kitu hawa, mtu wa kumuuliza ni mjomba wako" Handan aliongea kwa sauti ya chini huku akiwapa ishara wale wanawake wengine walinzi wa Sasha wasijaribu kufanya lolote.
Sekunde chache baada Dumayo mjomba wa Sasha naye akasogea karibu akiwa juu ya farasi wake.
"Tunawakamata kwa kosa la kuingia ndani ya msitu bila ruhusa, mmesababisha majanga makubwa sana ndani ya ISRA, kutoweka kwa msitu wa Bi Noha ni laana kubwa ndani ya ISRA, ni lazima muwajibike kwa hili" Alisema Dumayo.
0756862047 Full kwa tsh ELF 1 TU
Je nini kitafuata?
David kapelekwa wapi?
Ni akina nani wamemchukua?
Kwa nini?
ITAENDELEA...