Simulizi: Shanga za Bibi zilivyonipa umaarufu

Simulizi: Shanga za Bibi zilivyonipa umaarufu

Simulizi ya kweli.......SHANGA YA BIBI ILIVYONIPA !!!!
Msimuliaji.............KIDAWA

Umri........ 18+

Sehemu ya 13

Ilipoishia.......James kamtangaza Kidawa kuwa si lolote si chochote kitandani ni kama gogo.Kama haitoshi kamtangaza mpaka kwenye mitandao ya kijamii.
Songa nayo....
Hi

Nilihisi machozi yakinitiririka kama maji nikaanza kulia kwa sauti Jenny akaanza kunibembeleza!
"Usilie rafiki yangu!"
"Ntaificha wapi hii aibu mimi?"
"Pole usilie Sasa!"
Hamna kipindi nilikuwa na maisha magumu kama kipindi hicho ,nikiishi kama sungura kujificha ficha tu.
Hiyo haikusaidia maana ilikuwa ni lazma niingie darasani,niliona vile walikuwa wananitolea mimacho.
James hakutosheka akaposti na picha zangu akinikashifu kwa maneno machafu sana!
Siku moja nilikutana na James nikamfuata!
"James!James!",nilimuita wala hakuitikia ,ikabidi nimsogelee nikamshika mkono,akageuka kwa hasira!
"Vipi?unanichafua!",alisema huku anautoa mkono wake.
"James nimekukosea nini?,mbona unanifanyia hivi kosa langu kukuruhusu uone mwili wangu!"
"Kwani nimeuona una nini?zaidi ya mat*ko hayo uliyobeba kama mizigo isiyokuwa na msaada!"
"James kama unataka tena sema ntakupa Niko tayari lakini siyo kunichafua hivi!!"
"Hahahaha!nikutake wewe?kwa kipi sit*mbani na magogo Mimi mwanamke hata hujigusi duhh,hujafundwa wewe eeh??!!"
James!alisema huku anaondoka nikajaribu kumuita!
"James!James!"
"Achana na Mimi!"
Niligeuka nikashangaa kumbe watu walikuwa wanatuangalia na wengine walikuwa wanapiga picha ambapo si muda mrefu zile picha zikasambaa mtandaoni!
Hiyo ilithibitisha maneno yake ,James akajizolea umaarufu ghafla kile kivideo kikasambaa kwenye status za watu nikapigiwa simu hadi na Bi Sandra!
"Haloo mwanangu!"
"Mama shikamoo!"
"Mwanangu hivi hii video naona ni wewe au mbona kama ni wewe unamlilia mwanaume hapa anakukataa?"
"Ni mimi mama Ila tulikuwa tunaigiza mama!"
"Nambie ukweli mwanangu?"
"Ndio kweli tulikuwa tunaigiza mama!"
"Unakumbuka nilikwambiaje?umeyaingilia mapenzi kichwa kichwa hujui A Wala CHE naomba ukifunga chuo uje nikupe somo,ulivyo unatakiwa kuliliwa sio kulilia ,umenielewa!
"Sawa mama!"
Unafikiri ningesemaje sasa?niliwaza vipi baba na mama wakiiona itakuwaje?
Maisha yalisonga ile hali ya kusemwa na kunyooshewa vidole nikaizoea,nikawa sijifichi tena japo kiukweli niliumia hata nikakonda nguo zangu baadhi zikawa hazinitoshi tena!
Wanaume hawakuacha kunisumbua huku wengine wakijifanya wananionea huruma kwa yanayotokea.
Nilijua lengo lao walitaka tu kuhakikisha kama maneno ya James ni kweli au vipi?
Sikuwapa hiyo nafasi kabisa niliwakataa wote na vishawishi vyao!
Tulimaliza mitihani nikiwa na shauku ya kutaka kurudi nyumbani nipate somo la Bi Sandra!pengine nami ntafurahi siku moja.
Siku namaliza mtihani nikamjulisha Bi Sandra kuwa kesho narudi.
"Haloo mama!"
"Naam mwanagu!"
"Narudi kesho mama!"
"Halafu mama na baba yako wapo!"
"Itakuwa vizuri nimewamiss pia!"
"Usijali ntakufundisha usiku namna ya kucheza na bakora najua kinachokutesa kesho ukija tutaanza somo!
Nilikusanya vitu vyangu ntakavyorudi navyo nyumbani.Nilikuwa na hamu sana ya kufika nyumbani niliona usiku mrefu sana nilichoka hizi aibu mimi!
Siku iliyofuata nilikodi teksi iliyonipeleka mpaka nyumbani.
Nililipa kisha nikaingia ndani kulikuwa na ukimya mkubwa!
Mlango wa sebuleni ulikuwa umefungwa na sikuwa na funguo!
Nikapiga simu ya Bi Sandra ikawa haipatikani,ndipo nikapiga simu ya mama!
"Haloo mama mko wapi Mimi niko nyumbani mlango umefungwa!"
",Tupo hospitali mwanangu Bi Sandra anaumwa sana!"
"Nini??anaumwa?"
"Ndiyo anaumwa tupo hospital!"
"Mbona Jana nimeongea nae!"
"Kaanguka leo bafuni alikuwa anaoga!"
Nilichanganyikiwa furaha yangu ikaingia huzuni kubwa,mtu anayetakiwa kurudisha tabasamu langu Sasa yupo hospitali eti anaumwa nilijiuliza nina mkosi gani Mimi?
Walinitajia jina la hospitali nikaacha mabegi yangu pale haraka nikatoka nikachukua bodaboda iliyonipeleka mpaka hospitali.
Nilifika nikawakuta baba na mama wako kwenye benchi,
"Mama!baba!Mama yuko wapi?",nilichanganyikiwa kwa kweli kwani huyu siyo tu mlezi wangu ni mama yangu japo hakunizaa Ila asilimia tisini ya malezi yangu yamepitia mikononi mwake!
"Yupo ndani,hataki kuonana na mtu yoyote zaidi yako!"
Niliingia chumbani nilichokiona sikuamini,Bi Sandra alikuwa amelala amefumba macho yake mashine ya kupumulia ikiwa imefunika pua na mdomo wake!
Niliganda kwanza nikiwa nahisi ni kama ndoto,haikuwa ivyo Bi Sandra alikuwa hoi akionekana wazi ni waleo wa kesho!
Taratibu nikapiga hatua zangu mpaka kilipo kitanda nikasimama kisha taratibu nikapiga magoti chini huku machozi yakinitiririka kama maji!!
Nilimuangalia Bi Sandra ambaye alikuwa amefumba macho yake!
"Mama!,nilimuita kwa sauti iliyoojaa simanzi na inayoonesha kukata tamaa kabisa!"
"Mama amka nimekuja!",nilimuita tena Safari hii nilitoa sauti kiasi,ghafla Bi Sandra akafungua macho yake akaniangalia Kisha akatabasamu.
Tabasamu lake lilitoka na machozi yaliyomwagika na kulowesha kitanda chake!
Nilitabasamu pia Ila nami nilitabasamu huku nalia!!
Dokta aliingia alipofika alishangaa sana hali aliyotukuta nayo,alishangaa hasa kumuona mgonjwa aliyekuwa mahututi anatabasamu!
Ilibidi awaite wazazi wangu kisha akawauliza
"Huyu mtoto ni nani kwa mama huyu?"
"Ni mama yake!",alijibu mama yangu mzazi huku anatabasamu,nadhani hata yeye anajua nampenda Bi Sandra kuliko yeye sababu wako bize na maisha kuliko familia!
"Ndio maana huyu mama anatabasamu na anaonekana kupumua vizuri sana tu haina haja ya mashine!"
Dokta aliongea kisha akamtolea zile mashine za kupumulia.
"Mamaaa"
"Mwanangu!",alijibu Bi Sandra kwa sauti ya chini,nikasimama nikamkumbatia pale kitandani huku natabasamu machozi yakinitoka!
Mama na baba nao walikuwa wamesimama pembeni wanatabasamu,tabasamu lilichanganyikana na huzuni ndani yake!
"Pole mamaangu utapona!"
"Ahsante nmefurahi sana umekuja nimekataa kusafiri hadi nikuone mwanangu!"
"Kwani ulitaka kusafiri mama!"
"Ndio nilikuwa safarini na tiketi nishaikata kabisa!"
"Mmmhh!unataka kuniacha na nani si ulisema utakuwepo uone ndoa yangu na uisimamie unipambe ning'ae kuliko bibi harusi yoyote!"
"Nimehairisha mwanangu ntakuwepo ntakupamba!"
"Sawa mama!"
Ilikuwa kama muujiza Ila Bi Sandra aliweza hadi kukaa,tulianza kupiga stori kama kawaida hadi mama akawa anatuonea wivu!!
"Nipikie kile chakula nachopenda mwanangu!"
Aliniambia Bi Sandra ikabidi nitoke niende nyumbani kumuandalia Niliondoka na mama na baba pia akaenda kwenye mishe zake!
Mgonjwa alikuwa na nafuu kubwa sana.Nilipitia sokoni nikanunua samaki wa Mwanza maarufu kama sangara na unga wa dona uliochanganywa na udaga kwa mbali Kisha nikapika vizuri.Nikarudi hospitali na mama.
Nilifika na kapu langu la chakula nikaingia wodini nilichokiona sikuamini!

JE KAONA NINI KIDAWA?NINI KIMETOKEA NA JE BI SANDRA ATAPONA AU NDIYO BASI NA VIPI FURAHA YA KIDAWA? USIKOSEEEEEE
 
.
Simulizi ya kweli....... SHANGA YA BIBI ILIVYONIPA UMAARUFU!!!!
Msimuliaji............ KIDAWA

Umri .......... 18+

Sehemu ya 14

Tulipoishia...... Kidawa anarudi nyumbani akiwa na shauku ya kumuona Bi Sandra ili ampe ufundi asionekane gogo kitandani kama wanavyosema lakini anakuta wamefunga Bi Sandra yuko hospital,anaenda hospital Bi Sandra anapata nafuu hadi anamtuma Kidawa ampikie chakula anachopenda......
Songa nayo.......

Nilipika vizuri,maana kwenye mapishi niko vizuri nilifundishwa vzuri na Bi Sandra mwenyewe!
Nilivyomaliza nilijiandaa kisha tukatoka na mama pia kwenda hospitali,tulipanda gari ya mama mpaka hospitali.
Nilikuwa na tabasamu pana usoni nikiamini sio muda mrefu ntakuwa kungwi wa mapenzi,usoni nilijawa na tabasamu pana lenye matumaini!
Tulifika tukashuka mimi na mama tukaanza kupiga hatua zetu kwenda kwenye wodi binafsi alikolazwa Bi Sandra.
Njiani tulikutana na machela iliyobeba mwili wa mtu ambaye ni wazi kashapoteza uhai wake,hiyo haikutushitua,maana pale ni hospital ivyo kufa na kuzaliwa ni kila siku,tuliingia ndani ya wodi nilichokiona kiliniogopesha nilikuta kitanda kikiwa kitupu tena kimetandikwa vizuri kama hakuna mtu alilala pale!
Mkono wangu ulioshika kapu uliachia likaanguka chini,mikono nikaiweka kichwani huku nimepigwa butwaa!!
Nilitoka nakimbia mbio nikielekea njia niliyokutana na ile machela huku nyuma mama akawa ananifuata huku ananiita!!
"Kidawa!Kidawa mwanangu we kidawaaa!!!"
Sikujali nilikimbia huku machozi yakinitiririka kwa kasi,watu walibaki wananishangaa tu hawakujua kwanini nakimbia,walinzi walianza kunikimbiza Ila hawakunipata mpaka nikawaona wale manesi wanaosukuma ile machela!
Nilifika nikasimama mbele yao ghafla nao wakasimama wakawa wananiangalia kama wananishangaa.
Sikuwajali nilifika nikafunua shuka jeupe sikuamini nilimuona Bi Sandra wangu kafumba macho yake hatikisiki wala hawezi tena kugeuza shingo yake kuniangalia!
Bi Sandra alikuwa amefumba macho huku anatabasamu,machozi yalinitoka safari hii nililia peke yangu,Bi Sandra hakulia tena sikuona chozi lake Ila tabasamu lake!!!
Mama naye alifika pale pamoja na wale walinzi,waliotaka kunishika mama akawazuia..
"Hapana msimguse,muacheni amlilie mama yake!"
Mama alinisogelea akapiga magoti pembeni yangu na yeye machozi yalimtoka pia .
"Mama!Bi Sandra ameondoka mama,aliniambia hawezi kusafiri hadi anione mama,Bi Sandra kanisaliti mama,alisema atahairisha safari kwa ajili yangu mamaa!"
Mama alilia tu hakuongea neno lolote wote tulimpenda Bi Sandra.
"Mamaaaaaa!!,amkaaaaaaa mama yangu amkaaaa mamaaaaaa nani atanipikiaaaaaa mamaaaaaaa umeondokaaaa nani atanifundishaaaaaaaa mamaaa wananicheka chuoniiiiiiii!"
Wale manesi walianza kusukuma machela yao wakionyesha huzuni kubwa ,kilio changu kiliwafanya baadhi wamwage machozi!
Nilitaka kuizuia machela Ila walinzi wakanizuia nikabaki nimekaa chini nikigalagala zaidi ya yule jamaa aliyeachwa na Hamida!
Nikiwa pale alikuja Daktari aliyekuwa anamhudumia Bi Sandra akasimama kisha akatoa karatasi akanipatia!!
"Huu ni ujumbe wa marehemu kwako alisema usimpe mtu asome zaidi yako hata mimi sijasoma,tunza ahadi yake!"
Nilichukua ule ujumbe nikauweka kwenye sindiria,mama akanishikria mkono tukaanza kuondoka hadi kwenye gari sikuwa na nguvu za kutembea peke yangu.
Tulirudi nyumbani tukakuta kumbe baba kaishatangaza msiba nyumbani,baadhi ya watu walishafika!
Taratibu zillifanyika Bi Sandra akapumzishwa kesho yake.

*************
Ilikuwa ni ngumu sana kuamini yaliyotokea kwangu kiukweli nilikuwa katika wakati mgumu sana.
Ilinichukua wiki nzima kuanza kuzoea na kula japo si sana muda mwingi nilimkumbuka mama yangu wa hiyari!!
Nikienda jikoni nakuwa kama namuona anapika,sebuleni namuona akifanya usafi na nikiwa ndani mtu akija kuniamsha nahisi ni yeye ndiyo ananiita!
Ndipo nulipokumbuka ile barua aliyonipa yule daktari niliitoa nilipoihifadhi nikaanza kuisoma!
Iliandikwa hivi....

Kwako mwanangu,binti yangu wa pekee,popote ntakapokuwa ntakutambulisha kama mwanangu umeishi ukiniaminisha ivyo binti yangu Kidawa,hujui tu vile nilikuwa nafurahi ulipokuwa unaniita mama!
Wewe ndiyo unanifanya niende safarini nikiwa natabasamu,chozi lako limenionyesha ni jinsi gani una upendo wa kweli kwangu.
Japo roho yangu inaniuma nimekufundisha kupika,nimekufundisha vyote Ila nilisahau kukufundisha kitu kinachokusumbua Sasa mwanangu! Sijakufundisha mapenzi najuta Kidawa mwanangu.
Naskitika uzuri wako umefunikwa na kufichwa na kasoro ndogo iliyopo ndani yako .
Kama nilivyokwambia Safari yangu ilifika na tiketi nilikuwa nayo,Ila sikupanda basi nikagoma kuondoka mpaka nikuone mwanangu kipenzi!
Nashukuru ulikuja,Israel akakubali kunipa pumzi tena niongee na wewe.nimefurahi sana mwanangu.
Sasa sina sababu tena basi limenirudia,namuona mama na baba zangu wananiita namuona pia na mpenzi wa moyo wangu ananiita,mwanaume niliyempenda kuliko mwanaume yoyote duniani ananiita sio muda ntaonana nae!
Najua sikuachi vizuri mwanangu Ila ntakupa maelekezo yupo wa kukutendea makubwa zaidi yangu.
Funga Safari hadi Tanga wilaya ya Lushoto shukia sehemu moja wanapaita vuga road pale utachukua pikipiki wakupeleke kwenye Kijiji cha Kilwai ukifika ulizia kw Bi Mwana mtoto,kama tatzo ni mapenzi atakufanya uwe kungwi wa mahaba na kama kuna uchawi atakutibu pia!!!
Sina mengi mikono inakosa nguvu ya kuandika angalau nina amani nina amini utatabasamu na utakuwa kungwi kati ya makungwi!......
Narudi nyumbani ntakusubiri huko safari yako ikifika ntakutumia tiketi mwanangu,ntakupokea huku ni kuzuri kuliko huko mwanangu!!!!
...............

Nilimaliza kusoma machozi yakanitoka nikaanza kupanga nguo zangu kwenye kibegi changu,sikupanga nguo nyingi sana nilichukua tu kama tatu.Mama aliingia akanikuta napanga nguo zangu
"Mwanangu una Safari?"
"Narudi chuo mama!"
"Hakijafunguliwa bado lakini?"
"Siwezi kukaa hapa mama,namuona Bi Sandra kila Kona!"
"Basi safiri na Baba yako anaenda Dubai kesho kutwa!"
"Sisafiri mama naenda chuo kuna rafiki zangu nimewazoea huko!"
"Sawa nenda mwanangu!!"
"Ahsante mama!"
"Akaunti yako ina pesa!"
"Ina laki nne!"
"Ntakuingizia laki sita nadhani zinatosha utumie!"
"Ntashukuru!"
"Mbona hauna furaha mwanangu?"
"Unahisi huu ni wakati wa furaha kwangu?"
Nilimuuliza swali mama ambaye aliondoka bila kunijibu,ndivyo walivyo wazazi wangu wanaamini pesa ni kila kitu, nikikohoa tu pesa hawana muda wa kujua nasumbuliwa na nini.Waliniingizia pesa ambazo sikuwa hata na matumizi nazo ,nimemwambia lakini nne lakini ukweli Nina kama milioni mbili benki.
Muda mwingine mama ananiingizia pesa baba naye ananitumia sijui hawaambiani?mi sijui!!

Kulikucha nikabeba begi langu nikawaaga wakataka wanibebe mpaka chuoni nikakataa,nikatoka nikachuka bodaboda mpaka ubungo nikakata tiketi ya Basi la Tanga linaloenda Lushoto!
Safari ikaanza!!!!

JE KIDAWA ATAFANIKIWA KUMPATA BI MWANA MTOTO ,NA JE HUYU BIBI NI NANI?? USIKOSEEEEEE
 
Simulizi ya kweli......SHANGA YA BIBI ILIVYONIPA UMAARUFU!!!!
Msimuliaji........ KIDAWA

Umri........18+

Sehemu ya 15

Tulipoishia...... Kidawa alikuwa kwenye Basi akisafiri kwenda Tanga Wilaya ya Lushoto katika Kijiji kinachoitwa Kilwai.Anakwenda kumtafuta mtu atakayemfanya kuwa kungwi wa mapenzi!!

Songa nayo......

Safari ilikuwa ndefu sana,nilisinzia nikaamka nikalala nikaamka.
Nilikuwa kimya sikuwa na stori na mtu yeyote,nashukuru nilikaa na mdada mwenzangu.Kama unavyojua mwanamke na mwanamke kuanzisha stori ni ngumu.tulisafiri kibubu bubu.
Nilifika Lushoto saa nane nikashukia kwenye kituo cha Vuga road kama barua ilivyoelekeza.
Nilikuta pikipiki nikachukua kuelekea Kijiji cha kilwai.
"Samahani kaka naelekea kwa Bi Mwana Mtoto sijui unamjua!"
"Namjua yule Bibi kumbe ana mtoto tunajuaga yule Bibi hanaga watoto!"
"Ndio mimi ni mwanae!"
"Aiseeh!atafurahi sana una siku hujamtembelea!
"Sio muda sana namtembeleaga!"
Safari ilituchukua dakika arobaini mpaka kufika Kijiji cha Kilwai.
Boda boda alisimama nje ya nyumba ya nyasi iliyoezekwa kwa makuti.
"Saivi atakuwa shambani!"
"Ntamsubiri ni shingapi unadai?"
"Elfu tano tu dada!"
Nilichomoa noti ya elfu kumi nikampa nikamuachia na chenji nikamuomba namba yake ya simu akanipatia ili niwe namuagiza vitu maana kule ni kijijini na sijui itanichukua siku ngapi kuwa fundi wa mapenzi!
Nilikaa pembeni kulikuwa na kigoda nikimsubiri Bi Mwana Mtoto nikiwa na shauku kubwa ya kumuona!
Masaa yalipita hatimaye Bi Mwana Mtoto alifika alikuwa ni mzee kama wa miaka 65 au 70.
Alikuwa amebeba jembe na kapu lililosheheni mazao mbali mbali.Nilisimama nikampokea jembe na kapu lake nikavisogeza hadi mlangoni.
"Bibi shikamoo!"
"Marahaba Karibu sana!"
Aliongea kisha akaniacha nimekaa pale nje chini ya mti!
Alitoka ameshikilia chungu akaja akakaa pembeni yangu,ndani ya kile chungu kulikuwa na maziwa yaliyoganda!Akaniangalia wala hakuniuliza mimi ni nani,akaanza kuongea?
"Nina wiki sasa sijaangalia haya maziwa,nilikuwa nayaangalia kila siku tangu aondoke hapa akisema anaenda mjini kutafuta furaha baada ya misukosuko mingi sana ya maisha aliyopitia,aliondoka hapa akiwa binti mdogo sana na siku anaondoka nilikamua maziwa ya ng'ombe nikamwambia ateme mate humu nikamwambia angali yupo hai maziwa haya hayatoganda!
Sandra,Sandra mwanangu umeganda,umeganda sijui niko bize na shughuli za shamba mwanangu,Sandra umeganda!"
Alisema Bi Mwana Mtoto huku machozi yakimtoka.Machozi yalinikumbusha siku ile hospital nilipolia pamoja na Bi Sandra!
Aliinuka akachukua jembe akaniambia
"Beba hicho chungu unifuate!"
Nikabeba kile chungu tukazunguka nyuma ya nyumba akaniambia nichimbe shimo,nikachimba shimo hapo nikitoka jasho ambapo si muda nilianza kuchoka si unajua binti wa mjini sijawahi hata kushika jembe!
"Ndiyo maana bakora inakushinda chimba vizuri hilo shimo!"
Nilishangaa huyu bibi kajuaje mimi bakora inanishinda duh!nilikuuliza nikakosa jibu!!Nilichimba lile shimo mpaka usawa wa magoti.Nilimaliza nikihema sana ilikuwa kazi nzito kijasho chembamba kikinitoka!
Alikishika kile chungu akafumba macho akaanza kuongea maneno ambayo sikuyaelewa Kisha akakifukia ndani ya lile shimo!!
Tukarudi ambapo aliniambia niingie ndani nikabadili nguo nije tupike!Nikabeba kibegi changu nikaingia ndani nikavaaa dela kisha nikatoka!
Nikamkuta kawasha jiko la kuni anachochea juu kabandika sufuria lenye maji mengi!
Sikujua anataka kupika nini Ila baadae alirudi akakaa kwenye kigoda chake akaanza kuita kuku,walikuja kuku wake pale akawa anawamwagia mahindi wanakula,kuku walikuwa wamemzoea kiasi kwamba wakawa wanamsogelea mpaka miguuni!
Akamkamata jogoo mmoja aliyenona kisha akaniita
"Kidawa!",nilishangaa sana kwa kweli,sikuwahi kumtamkia jina langu Ila aliniita kwa jina langu,sikumpa taarifa ya kifo cha Bi Sabra ila alijua kutokana na maziwa yalivyoganda na pia alishaijua shida yangu kabla sijamwambia!
"Abeee Bibi!"
Niliitika nikamsogelea akanipa yule kuku akaniambia.
Nenda nyumba ya pili ukawaambie umetumwa na Mwana Moto wakuchijie huyo kuku!
"Nyumba ipi bibi?"
"Iyo yenye bati lekundu!"
Nilitoka nikaenda sikupata tabu nyumba ile yenye bati jekundu kidogo kuna utofauti na kwa Bibi wao walipikia mkaa na hata nyumba yao ilikuwa imejengwa kwa tofali za kuchoma!
Nilifika nikamkuta kijana mmoja aliyekuwa amevalia msuli huku akiwa kifua wazi,mwili wake ulijengeka kimazoezi nadhani ni kwa sababu ya shughuli za shamba!
"Wenyewe!"
"Karibu!"
"Wewe ni mhusika hapa!"
"Ndio mimi ni kijana wa hapa naitwa Said!"
"Mimi naitwa Kidawa ni mgeni mtoto wa Bi Mwana amenituma nimlete huyu kuku mnichinjie!"
"Bila shaka, nisubiri!"
Alisema akiingia ndani akatoka akiwa ameshika kisu ameshikia jagi lenye maji akanikabidhi nikampa kuku akanichinjia Kisha Yale maji akamsafishia!
Nilichukua kuku nikamshukuru nikaanza kuondoka kumbuka nilikuwa nimevaa dela tu na chupi ndani wowowo langu lilijichora nikajua tu huko Said tabu anaipata!
Sikufika mbali Said akaniita....
"Dada",nikageuka
"Abee Kaka!"
"Umesema unaitwa kidawa eeh!"
"Ndio Kaka!"
"Ntakuja kukutembelea!"
"Karibu sana!"
Nilimjibu moyoni nikahisi tayari ameshanitamani,na hayo mambo sikuyataka muda ule hasije kunitangaza mtaani kama mambo yalivyo chuoni!
Nilifika nikamkuta Bi Mwana akiwa anakuna nazi,nilifika aliponiona akatabasamu.
"Mjukuu wangu una nyota kali sana ila tu ilo balaa lililo ndani yako ndio linakusumbua!"
"Unamaanisha nini Bibi?"
"Wanaume wanakupenda sana ila wakizama huko baharini chumvi nyingi wanakimbia!!"
"Mmmhh!", niliguna tu nikaendelea na shughuli zingine nilimnyonyoa kuku nikamchemsha ambapo nilimuunga vizuri kama Bi Sandra alivyonifundisha,kisha nikapika wali wa nazi!
"Unanikumbusha mwanangu Sandra!"
"Kwanini Bibi??"
"Alijua kupika mtoto yule alitamani sana kumpikia mumewe kila siku ila maskini mumewe Wala hakufaidi chakula chake!"
"Kwani ilikuwaje Bibi?"
"Mmmhh!mjukuu tuyaache hayo!
Tulikula tukamaliza nikatoa vyombo Kisha akaniambia!
"Umenifurahisha sana Kidawa!"
"Kwa lipi Bibi?
"Kwanza ulivyojitambulisha kwa yule boda boda kuwa wewe ni mwanangu nilifarijika sana!Hata said umemwambia hivyo kwa kweli umeniheshimisha sana!"
"Ahsante Bibi sikujua kama ungependa mimi kufanya ivyo!"
"Niite mama napenda uniite mama uzibe pengo la mwanangu wa hiyari Sandra niite mama Kidawa!"
"Sawa mama!"
"Ngoja nikuandalie mahali pa kulala ,utalala kule chumba cha pili mimi ntalala chumbani kwangu baba yako atakuja leo amenimiss sana!"
Nilishangaa eti baba anakuja jamani na uzee wote huo kumbe Bi Mwana bado yumo,niliapa lazima nimpige chabo usiku!

JE NINI KITAENDELEA KIDAWA ATAMPIGA CHABO BI MWANA?KIDAWA ATAFANIKIWA KUPATA ANACHOTAKA!!

Y
 
Simulizi ya kweli...... SHANGA YA BIBI ILIVYONIPA UMAARUFU!!!!!
Msimuliaji.......... KIDAWA


Sehemu ya 16

Tulipoishia.....Kidawa kafika Tanga,kampata Bi Mwana ambaye anaonekana kujua matatizo yake yote kabla hajamwambia je atafanikiwa kupata alichofuata?
Songa nayo......

Moyoni nilisema lazima nimpige chabo usiku haiwekani na uzee ule eti aseme babu anakuja!
Mzee Kama yule anawezaje kumudu kucheza Na bakora? Kwa kweli nilitamani kiza kiingie mapema!
Wakati nao ulikuwa na mimi muda ulikimbia haswa hatimaye ikafika saa mbili usiku tofauti na mjini huku watu wanalala mapema sana!
Niliingia kwenye chumba nilichoelekezwa nikakuta kigodoro kidogo tu na shuka zilizochanika Ila zilikuwa safi.
Nikalala kwenye kigodoro changu, kiukweli Yale maisha yalikuwa magumu sana kwangu nilishazoea maisha mazuri, sikuwahi kuota kama kina siku ntalala kwenye kidogoro Kama hiki!
Nilitoa simu yangu bahati nzuri kulikuwa na mtandao nikakuta nimepigiwa simu na mama na baba!
Sikutaka kuwasiliana nao, niliingia upande wa meseji nikakuta meseji kutoka benki nimetumiwa kaki sita na nusu kwenye akaunti yangu nikaizima simu nikalala.
Ghafla! Bi Mwana akaingia kabla sijapata usingizi akanambia.
"Umekubali kuacha vitanda mjini umekuja huku kulalia kigodoro changu na hujalalamika umenifurahisha sana, umefaulu mitihani yangu mwanangu mafunzo yataanza leo usiku!!
"Kwa hiyo niamke mama? "
"Hapana utaamka muda ukifika, ngoja nimsubiri baba yako anipeleke duniani sijaenda Siku nyingi! "
Nililala nikisubiri huo muda wa mafunzo,nilikuwa na shauku kiasi kwamba hadi nilishindwa kulala usingizi haukuja ilifika mpka saa sita bado Bi Mwana hakuniita nilikuja kupitiwa na usingizi mzito!
Nikiwa usingizini nilisikia kama kitanda cha chuma kinalia kwichikwichi kwichi kwichi!
Niliamka nikagundua Ila sauti inatoka kwenye chumba cha Bi Mwana nikaamka nikasogea mlangoni kwa Bi Mwana!
"Ooohhhssshhh!!!!wekaaaa!!!aahhhhshhhii nipeeee babaaaaa ooohhh tamuuuuuu aaaaaaaahhhhooooohhh hapo !!ongezaaaaaaa!"
Hizo ndiyo sauti nilizoziskia nikashangaa sana nikijiuliza ivi ni Bi Mwana huyu au nani anayechezea bakora humo ndani?
Na kama ni Bi Mwana ndiye anayetoa kisauti kama binti wa miaka kumi na nane!Yaani analia vizuri kuibembelezea bakora kuliko hata mimi Kidawa!!!???
Nilijiuliza maswali ndani kipigo kiliendelea kiasi kwamba mpaka nikaanza kujikunja kwa utamu mwanga wa koroboi ndani haukutosha kunionyesha yanayotokea ndani.
Ile sauti iliendelea vilio alivyotoa Bi Mwana vilinifanya niloweshe chupi yangu nikapitisha kidole nikaanza kuichezea k yangu huku nimefumba macho,ghafla sauti zile zilikata nikanyata kurudi chumbani kwangu!
Sijui ni nini Ila moyoni nilijikuta natamani na mimi nikikutana na mwanaume nitoe milio ilee,milio inayo muhamasisha kidume yoyote kuingia nyavuni haraka!!!
Nilirudi nikajifunika shuka langu usingizi ukanipitia nikasinzia,nilikuja kushituka asubuhi kumeshakucha mida kama saa mbili asubuhi Bi Mwana tayari alikuwa kashaamka nilijilaumu kulala sana maana nilitamani kumuona huyo kidume aliyekuwa anamuendesha Bi Mwana akalia kama kabinti wakati mvi Karibu zinafunika kichwa chake!
"Shikamoo mama!"
"Marahaba mwanangu!"
"Umeshaamka Mama!"
"Hahahahaaa! mwanamke unatakiwa kuamka mapema kabla ya mumeo mwanangu!"
"Lakini hujaolewa mama!"
"Hahahahaaa!Mwanamke anaejiamini huwa anaishi akiamini ataolewa kesho!hivyo hujifunza na kuyaishi yote yampasayo kufanya kwenye ndoa,ukibweteka hata siku ukiolewa utakuwa wa hivyo hivyo!"
Maneno yake yalinichoma,maana yalinilenga mimi moja kwa moja,nilichukua ufagio nikaanza kufagia uwanja!Bi Mwana alikuwa zake anaota jua huku anatafuna mihogo mibichi!
"Unaonekana ulielewa somo la Jana!"
Nilishtuka nikajiuliza ni somo gani nilisoma jana wakati ni ni yeye alikuwa anachezea bakora ndani huko!
"Kwani Jana ulinifundisha Bi Mwana!"
"Hahahahaaa!sauti ni siraha kubwa ya mwanamke mwanangu jifunze kulia,usijibane ikiwekezekana hata machozi yamwage tu!"
Nilisimama kwanza nikaacha kufagia nikajiuliza kumbe ile sauti aliyokuwa anaitoa ilikuwa somo mmmhh!ana mambo Bibi huyu looh!!!
"Aya mama ahsante kwa somo!",nilisema nikiona aibu maana nikikumbuka ile sauti ilinisisimua hadi nikaanza kuchezea kisimi nikahisi pengine aliniona maana huyu Bi Mwana nae mambo yake kama mganga mganga!
"Chemsha mihogo iyo tule twende shamba!"
Aliongea Bi Mwana nikaduwaa kusikia shamba maana jembe lenyewe tu sijui kushika itakuwaje?
Niliwasha jiko la kuni hapo moshi ukiniingia hadi machoni machozi yakanitoka haswa nilijuta kwa kweli Ila moyoni nilijisemea hii mitihani lazima nishinde na John na James watanijua tu waache waringe na viswaswadu vyao!
Tulimaliza kunywa chai na mihogo kisha tukatoka nikabeba jembe langu na Bi Mwana lake ikaanza safari ya shamba!
Tulitembea sana kama saa zima ndiyo tukafika shambani,picha linaanza tu nilifika nimechoka na natakiwa kulima!
"Mwanangu mwanamke ndiyo nguvu ya familia?"
"Ukiachana mwanaume watoto wako utalea mwenyewe,ni aslimia chache ya wanaume wanaotoa msaada wa malezi kwa watoto wa wanawake walioachana nao!"
"Kwa hiyo inatakiwa uwe imara katika nyanja zote,hakuna mwanamke anayeheshimika kama mwenye biashara zake na elimu yake pia hata mapenzi hayatamyumbisha, sababu hata mwanaume atakayekuwa naye atamheshimu kama siyo kumuogopa kabisa, umenielewa!"
"Nakuelewa mama!"
"Haya shika jembe,utalima hapa mpaka kule ndiyo tuondoke bila hivyo mwanangu tutakesha hapa!"
"Lakini mama,mi siwezi kulima sijawahi!"
"Hahahahaaa!unataka kujifunza mapenzi Ila jembe hutaki lima hapo hutaki basi,rudi nyumbani!"
Machozi yalinitoka nikiangalia ile sehemu ilivyo kubwa halafu nilime mwenyewe!
Nilianza kinyonge kuanza kulima hatimaye nikakaza mkono,hadi jua kali la mchana likapotelea utosini.
"We mwana weeh! hata nusu hujafika?"
"Jamani mama nimechoka!"
"Pole,umejitahidi sana!Sasa nikuulize kitu?"
"Ndiyo mama!"
"Hilo jembe nimekushikia?si umeshika ukalima mwenyewe?"
"Ndiyo mama!"
"Umejuaje kwamba jembe linashikwa hivi na linalima hivi?"
"Nilikuwa naona tu mama!"
"Sawa,hivyo hivyo na kwenye bakora mwanangu,jitume kuwa mbunifu tutakufundisha mume yuko hivi na vile kaa naye ivi mpe hivi na vile lakini wengi sio wabunifu,mapenzi matamu ni akiba,ukimpa mpenzi wako penzi tamu akafurahi hata kama alikuwa na nia ya kuondoka atakuganda kama luba!"
Nilikaa kimya,nikimsikiliza mama kwa maneno yake!
"Twende nyumbani!"
Tulirudi nyumbani,tukala tukapumzika.Jioni baada ya kula Bi Mwana aliniita nikakaa naye kwenye mkeka!
"Kidawa!"
"Abee Mama!"
"Utotoni wakati unacheza ile michezo ya baba na mama ilikuwaje?"
"Sijawahi kucheza mama!"
"Kombolela!"
"Sijawahi pia naskia tu!"
"Pole mwanangu,kuna vitu inatakiwa upitie ukiwa mtoto,kuna vitu pia inatakiwa upitie ukiwa kijana ili usije kusumbua watu ukizeeka!"
"Unamaanisha nini mama!"
 
Back
Top Bottom