SEHEMU YA NNE
Mazungumzo Mazito.Yawaacha Njia Panda
“Mr. President, I respect the outstanding, long time bilateral relations our countries have enjoyed for the past 50 years. I, personally appreciate the two-way respect between you and I, but with all due respect, I will not allow your country to forcibly impose your culture on ours. We will not allow or legalize homosexuality in our country. It is against our normalcy, tradition, and culture as Africans. It is against our spiritual beliefs and the order of nature. If you have accepted it as your way of life, let it remain yours”
(Mh. Rais ninaheshimu mahusiano mazuri na ya muda mrefu baina ya nchi zetu mbili katika kipindi cha miaka 50 iliyopita. Na binafsi, ninaheshimu pia mahusiano tuliyo nayo sisi wawili, lakini kwa heshima kubwa niseme sintoruhusu taifa lako lilazimishe mapenzi ya jinsia moja kukubalika kwenye nchi yetu. Ni kinyume cha tamaduni na desturi zetu, kinyume na imani zetu, lakini zaidi na muhimu ni kinyume na asili ya mwanadamu. Kama mmekubaliana hayo kuwa Maisha yenu, basi ibaki kuwa hivyo huko kwenu.)
Rais Costa alikuwa akiongea na Rais wa Marekani, Chriss Donald masuala mbalimbali yanayohusu Stanza na hapo alikuwa akimjibu matakwa ya Marekani kutaka mataifa yanayopokea msaada kutoka kwao kuruhusu mahusiano ya jinsia moja (ushoga).
“Mr. President I understand your position, but I suggest that we talk about this in the next bilateral meeting. We will need to review most of our foreign relations policy with Stanza, if at all we do not come into a mutual understanding on the matter.
I can tell that after deliberations, your position will change, and Stanza will consider same-sex marriage as not only a private matter between two adult individuals who have chosen to love one another but also as a basic human right to associate and to form social relations. That I can guarantee”.
(Mh. Rais naelewa msimamo wako, ingawa nashauri kuwa tulizungumzie suala hili katika mkutano ujao kati ya nchi zetu. Tutalazimika kufanya mapitio ya sera yetu ya mambo ya kigeni na Stanza, ikiwa hatutofikia maelewano kuhusu suala hili.
Ninaweza kusema kuwa baada ya kukaa na kufikiria, msimamo wako utabadilika na Stanza itakubaliana na ndoa za jinsia moja si tu kuwa ni masuala ya faragha kati ya watu wazima wawili walioamua kupendana, bali pia kama haki ya msingi ya binadamu ya kuhusiana na kuanzisha mahusiano ya kijamii. Nakuhakikishia hilo). Rais Donald alimjibu Rais Costa kwa sauti ya kuamrisha kidogo. Rais Costa alighadhibika ila akakaa kimya.
“Again, it is interesting Mr. President to hear that your country is intending to amend the constitution that will change the legal age to run for presidency from 40 to 55 years.
(Nimepata taarifa kuwa Stanza inakusudia kufanya mabadiliko ya katiba yatakayofanya umri wa kisheria wa kugombea nafasi ya Urais kuwa miaka 55 tofauti na miaka 40 ya sasa). Rais Chriss Donald alimwambia Rais Costa kwa kebehi.
“I think you are crossing the line Mr. President, Stanza is a sovereign country. It is of best interest if each of our countries is let to freely define democracy according to their local context and choose what works best for them.
(Nafikiri unakwenda mbali Mh. Rais, Stanza ni taifa huru. Nibusara kuachia kila nchiijiamulie nini maana yademkorasia kwao kwa misingi yamuktadha na kile ambachokinafanya kazi katika nchihusika). Rais Joe nae alijibu kwakicheko cha kebehi lakinikilichojaa ghadhabu.
“No no no. It is not my intention, nor that of the United States to interfere with your internal affairs. I raised the matter so that we can both have the same understanding of the happenings. We shall see to that too”.
(Hapana! Hapana. Si lengo langu wala la Taifa la Marekani kuingilia masuala ya ndani ya nchi yenu. Nimelisemea suala hilo ili sote, mimi na wewe tuwe na uelewa unaofanana wa masuala yanayotokea. Tutaliangalia na hilo pia’’), Donald alimalizia.
“It was nice time speaking with you Mr. President” (Umekuwa muda mzuri kuongea nawe Mh. Rais) Rais Costa alimuaga Rais Donald kwa hasira kidogo.
“Pass my hello to Chairman, Mr. Kim”, (Salamu nyingi kwa Mr. Kim), Donald alimalizia na kukata simu akimwambia Rais Costa amsalimie Kim, Rais wa Korea Kaskazini.
Rais Costa alibaki na mshangao ulioonekana waziwazi usoni mwake. Alijiuliza maswali mengi, muhimu zaidi ikiwa imekuwaje Rais Donald akamtaja Kim muda ambao Joe na wenzake wanatekeleza misheni aliyowatuma ambayo kwa wakati huo alitambua ni siri.
“Macha wapigie simu kina Joe, nataka kufahamu wamefikia wapi. Haraka nitafutie nani amevujisha mpango huu kwa Marekani kabla hata ya Joe kukutana na Rais Kim”, Rais Costa alimwambia Stanley Macha kwa ghadhabu kisha alijiegamiza kwenye kochi na kupumua kwa nguvu. Alichanganyikiwa. Anafahamu mabavu ya Marekani katika siasa za kimataifa. Katika kipindi cha miongo miwili iliyopita, mataifa yaliyotofautiana na Marekani yameingia katika misukosuko mikubwa ya kiuchumi na kijamii.
**************************************
Ndege waliyopanda Joe na wenzake iliondoka mishale ya saa moja asubuhi kwa saa za China kuelekea Pyongyang ikitokea uwanja wa Beijing Capital International Airport. Joe na wenzake waliwekewa nafasi kwenye daraja la watu muhimu, ulikuwa ni ujumbe maalum unaosubiriwa sana na uongozi wa Korea Kaskazini. Kutoka Beijing mpaka Pyongyang ni safari ya masaa mawili hivi, hivyo mara tu baada ya ndege kutulia juu ya anga Joe aliwapa alama Habibu na Pius wasogee kwenye nafasi yake karibu. Nafasi zao zilifuatana.
Joe aliwaambia kwa kifupi kwanini aliwaondosha pale mgahawani. Aliwaambia kuwa Rais Costa alikuwa akifatilia maongezi yao kwa kuwatumiadrone yenye umbo la Nzi ili inase maongezi yao. Pius na Habibu bado walikuwa hawajaelewa kwanini hayo yanatokea. Joe alitambua hilo na haraka alianza kuwaweka bayana, “Nadhani kati yenu hakuna anaefurahia namna Costa anaipeleka nchi, ni jukumu letu sasa kumpumzisha kwa amani na usalama”.
“Najua mnaweza kudhani ninataka kulipa kisasi lakini nayasema haya kwa nia njema ya kizazi kijacho na ustawi wa nchi yetu ya Stanza”, Joe alikuwa akiongea kwa kunong’ona sana huku akiwakazia macho Pius na Habibu. “Ninawaambia haya kwa sababu ni ninyi mnaoweza kutekeleza hili. Ninawategemea kama vijana wangu, lakini ikiwa mtaona haya si ya msingi, basi tunaweza kuachana na mpango huu kabla hata hatujauanza. Tafakarini na tutaamua kwa pamoja uelekeo ambao ninyi mnatamani taifa letu lichukue”. Joe alimalizia na kukaa kimya kuwasikiliza.
Baada ya sekunde kadhaa za ukimya, Habibu ndiye aliyekuwa wa kwanza kuuvunja ukimya. “Joe, unachomaanisha ni kututaka tushiriki kumpindua Rais aliyepo madarakani kihalali?”. Habibu alionekana kutoelewa anachoshauri Joe. Habibu ni mtiifu kwa Joe lakini katika hili aliona ukakasi.
“Hapana, hatumpindui, tunampumzisha kwa ustawi wa Stanza.” Joe alijibu kiufupi. “Unampumzishaje mtu kabla ya muda wake wa kukaa madarakani kihalali kuisha?”, Habibu alizidi kuuliza.
“Muda wake kihalali uliisha 2015, nini kilitokea baada ya pale? Costa hana uhalali na nilazima ataibadili katiba na sasa nadhani Pius anafahamu, labda wewe kwa sababu upo mbali na varanda za Ikulu hujui, anataka kuhakikisha uchaguzi ujao anapandisha umri wa mtu kugombea Urais ili abakie yeye. Costa hana muda wa uhalali”. Joe alijibu huku akiwatazama usoni Habibu na Pius.
“Joe, nimekula kiapo cha kumlinda Rais, unachoniambia hapa ni Uhaini, na ni lazima utambue nafasi yangu katika jeshi”. Luteni Jenerali Pius Kihaka alionekana kumjibu Joe huku akiwa amekunja ndita.
“Luteni ulikula kiapo kuilinda katiba na Rais anayeitii misingi ya katiba. Utamlinda Rais pale tu akiitii katiba na si vinginevyo. Rais asiyetaka kuitii katiba, misingi ya haki na utawala bora anageuka kuwa muhalifu kama wahalifu wengine. Sasa nikuulize kiapo chako kinakuelekeza kumtii na kumlinda muhalifu?” Joe alimjibu Pius.
“Nahitajika kumtii yeyote alieshikilia nafasi inayoitwa Rais bila kujali anafuata katiba ama vinginevyo. Hivyo ndivyo mafunzo na miiko yangu jeshini inavyoniongoza. Wananchi ndio wanatakiwa waseme huyu haifuati katiba na wamtoe kwa chaguzi za kidemokrasia lakini sio mimi. Lakini je, wewe ndio kipimo cha kuhalalisha kuwa huyu anavunja katiba ama la? Au wewe ndio wa kusema huyu hafuati haki na utawala bora ama la? Nijuavyo mimi mamlaka hayo imepewa Mahakama au angalau Bunge na sio hisia za mtu binafsi Joe” Pius alisisitiza kwa maswali mfululizo.
“Pius, nadharia ya mgawanyo wa kimamlaka kati ya Serikali kuu, Bunge na Mahakama kiuhalisia haupo kwenye nchi zetu nyingi za kiAfrika achilia mbali Stanza. Nadharia hizo zimewekwa kwenye katiba kwa mkono mmoja na kuporwa kwa mkono mwingine. Tuliyajadili haya kwa kina sana nilipokuwa nawafundisha pale chuo cha diplomasia. Pius ulionekana kukasirishwa sana na hali hii, Habibu uliniahidi siku ukipata nafasi ya uongozi ungerekebisha haya, lakini tazama leo baada ya kuzipata nafasi mbalimbali mmesahau mara moja hii? Leo ninyi nanyi mnaona hali hii ni sawa na kunihoji maswali kana kwamba hamfahamu ukweli huu?” Joe aliongea kwa hisia kubwa na kuanza kuwapa darasa.
Aliongea nao kwa kina na kuwapa mifano mingi ya uvunjifu wa haki za raia, unyanyasaji na uteswaji. Aliwaambia jinsi hali inavyokwenda kuwa Mbaya baada ya Rais Costa kuweka sera nyingi mbovu na kuharibu sana mahusiano na mataifa rafiki. Aliwaambia hata safari yao ile ni kwa sababu Stanza inakosa marafiki na sasa inatafuta marafiki wapya kwa nguvu.
Aliwaeleza kinagaubaga namna mihimili miwili ya Bunge na Mahakama jinsi ilivyo ghoshiwa na Rais Costa na kuwa hakuna chochote kinaweza kuendelea ndani ya mihimili hiyo kilicho kinyume na Rais Costa hata kama kina maslahi makubwa kiasi gani na nchi ya Stanza. Aliwashangaa ni kwanini wao kwa nafasi zao inawawia vigumu kuling’amua hilo vipi kwa mtu wa kawaida.
Aliwaambia, wao wanaweza kukataa kwa sababu wana nafasi serikalini lakini wajueakumulikaye mchana usiku atakuchoma hivyo wasishangae siku moja kugeukwa na kuingia kwenye mateso makubwa. Aliwauliza nani katika serikali ile alikuwa rafiki wa karibu na Rais Costa kuliko yeye? Na je wanajua kilichompata?
Alimalizia kwa kuwaambia kuwa ili kutoka katika hali ile inahitajika juhudi za mmoja mmoja na sio kutegemea wengi. Wao kwa nafasi zao wapo kwenye nafasi nzuri za kuhakikisha Rais Costa anapumzishwa nje ya madaraka na marekebisho makubwa ya kimfumo,kisera na kikatiba yanafanyika kwa maslahi mapana ya wana Stanza. Joe aliongea kwa hisia, na baada ya kumaliza Habibu na Pius walionekana kuanza kuelewa.
“Kwa hiyo kwenye mpango huu upo na nani?”, Pius alihoji. “Ni mapema sana kuwaambia. Kwanza nilitaka nipate nafasi hii kuwapa huu muhtasari na kutaka utayari wenu kisha nitawaambia wote waliopo kwenye mkakati huu” Joe alijibu.
“Kwa hiyo jambo hili linafanikishwaje”, Habibu alihoji. “Nitawaambia, but first, let’s focus on what brought us all the way here”. Joe alijibu akikusudia kufunga ule mjadala, na kabla hajamaliza muhudumu wa ndege aliwasogelea na kuwauliza kama kuna kitu wanahitaji. Waliagiza Chai. Joe na Habibu wakarudi kukaa kila mtu akionekana kujaa mawazo. Mawazo ya jinsi gani watampumzisha Rais Costa nje ya madaraka, nani ataongoza Stanza na nini kitafuata baada ya hayo?
*************************************
“Sikiliza Sylvester, haya sio makubaliano yetu. Ulinitoa Canada kwa ahadi kuwa unakuja kunipa Uwaziri, umeishia kunipa Ukatibu Tawala wa jimbo tena huku kijijini, kweli? Ungeniacha Canada kule kule bwana”. Alikuwa ni mrembo, Ketina, kimada wa Rais Costa akiongea nae kwa simu kutokea Jimbo la Kichumbi alikomteua kama Katibu tawala.
“Keti, mbona una haraka mpenzi? Hujakaa kwenye hiyo nafasi hata miezi sita unataka nikupe Uwaziri? Hatuendi hivyo mpenzi wangu. Subiri angalau umalize mwaka nitakupa Ubunge kwa kutumia nafasi zangu kwa mujibu wa katiba halafu utaanza na Unaibu Waziri”. Rais Costa alijibu kwa utaratibu na kubembeleza.
“Nani asubiri mwaka mzima Costa? Mimi Keti au nani? Wachezee hao hao watu wako wa Stanza sio mimi. Hakuna linaloshindikana ukiamua. Wewe ni mtu mwenye nguvu kuliko wote chini ya jua la Stanza. Katiba imekupa mamlaka ya kuamua uzima na kifo cha yeyote nchi hii sembuse kunipa uwaziri mimi? Ketina alichachamaa.
“Kwanza ndani ya siku mbili tatu hizi nitakuja Peron kuonana na wewe nimeku miss”, Ketina alimalizia kwa sauti ya upole. Alimtaarifu Rais Costa kuwa anakuja Peron mji mkuu wa Stanza ilipo Ikulu ya Rais Costa kwa ajili ya kuonana nae.
“No, no Keti, I have pressing issues that I am dealing with right now. I will tell you when to come” (Hapana Keti, nina masuala nyeti ninayoshughulikia sasa hivi. Nitakwambia lini uje), Rais Costa nae alijibu kwa upole.
“Midts of your pressing issues, you can always slot a time to hang on with your bae, aren’t you Mr. President?”. (Hata katikati ya masuala yako nyeti huwezi kukosa muda wa kukutana na mpenzi wako, au sio Mh. Rais?). Ketina aliongea kwa sauti ya kimahaba iliyomlainisha Rais Costa. “Aaa…. aaaa. Ok Keti just come”, (Aaaa…. aaaaa. Sawa Keti njoo basi). Rais Costa alijikuta anakosa kauli. “That’s my baby” (Huyo ndio mpenzi wangu), Ketina alimalizia na kukata simu.
***************************************
Kwa macho na mbele ya wananchi na watendaji wa Serikali, Rais Sylvester Costa alikuwa akionekana mkali na mtu asiesogeleka. Ilikuwa ni ngumu kumwangalia machoni mara mbili akiwa anaongea na wewe. Hata watendaji wa serikali ikiwemo na mawaziri wake huongea nae wakiwa wameinamisha kichwa. Alikuwa mkali na mbabe kwelikweli.
Ketina Nikodemas, msichana mdogo kiumri aliyekutana nae nchini Canada miaka mitatu iliyopita katika moja ya ziara zake, ndiye pekee aliyeweza kumuendesha Rais Costa jinsi alivyotaka. Ketina akiwa nchini Canada kumalizia masomo yake ya Uzamili alionana na Rais Costa na katika kumsalimia, Rais Costa alivutiwa nae na hivyo kuagiza kuonana nae Hoteli aliyofikia.
Rais Costa alianzisha mahusiano na binti Ketina na hakika binti huyu alijua kumteka Rais. Ni katika mapenzi hayo ambapo Ketina alitaka apewe Uwaziri na hivyo Rais Costa alimrudisha nchini Stanza na kuanza kwa kumpa Ukatibu Tawala wa jimbo.
Ketina hakufurahishwa na uteuzi huo na sasa alikuwa akimlazimisha Rais ampe Uwaziri kamili. Hakuna aliyekuwa akijua kinachoendelea nyuma ya pazia kati ya Rais Costa na Ketina isipokuwa kwa wafanyakazi wachache wa Ikulu hasa vijana wa Usalama wanaotumiwa na Rais kupanga na kuandaa mazingira ya kukutana kwao mara kwa mara sehemu mbalimbali.
**********************************
Je, Habibu Na Pius Wamemuelewa Joe?Vipi Kuhusu Rais Costa Na Chriss Donald Wa Marekani?Vipi Kimada Ketina?.....