Simulizi:The President and I(Mimi Na Rais)

Simulizi:The President and I(Mimi Na Rais)

SEHEMU YA TANO

Joe Awasili Pyongyang. Siri Nzito Yawashtua Habibu Na Pius.

“선량한 동지들” seonlyanghan dongjideul (Habari za asubuhi kamaradi). Ndugu En Ki, waziri anayehusika na masuala ya kigeni wa Korea Kaskazini aliwasalimia kiKorea Joe na ujumbe wake mara tu baada ya kuwapokea uwanja wa ndege wa Pyongyang.

“좋은 아침” joh-eun achim(Salama) Joe nae alijibu kiKorea huku akiwa ameshikana mkono na ndugu En wakiwa wameinamishiana vichwa. “평양에 오신 것을 환영합니다. pyeong-yang-e osin geos-eul hwan-yeonghabnida, (Karibuni Pyongyang), Waziri En aliendelea.
“고마워. 우리의 즐거움 동지 야”gomawo. uliui jeulgeoum dongji ya. (Asante sana. Ni furaha yetu kubwa sana kuwa hapa), Joe nae alijibu huku akitabasamu.

Joe akiwa mwanadiplomasia mbobevu alielewa itifaki za mataifa mengi. Alikuwa ni mtu makini ambaye ukikutana nae unajua kabisa kuwa ameiva kwelikweli katika masuala ya mahusiano ya kimataifa, diplomasia na hata lugha za kigeni.

Ndugu En aliwaongoza Joe na ujumbe wake mpaka kwenye magari yaliyoandaliwa kwa ajili ya msafara kuelekea Ikulu ya Pyongyang. Kutokea uwanja wa ndege wa kimataifa wa Pyongyang Sunan jijini Pyongyang mpaka makazi ya Rais Kim ni mwendo wa kama dakika 40 hivi kwa gari, hivyo msafara ulianza kwa kuifuataHeeecheon Expressway.
Yalikuwa jumla ya magari manne, la mbele likiwa linaongoza msafara, la pili alipanda Waziri En na Joe, la tatu alipanda Habibu na Pius na la nne likiwa ni la ulinzi. Wakiwa njiani, Joe alikuwa akiongea mawili matatu na En. En alikuwa ni mjuzi wa lugha nne ukiacha ya kiKorea.

Alizungumza kwa ufasaha kiingereza, kichina, kirusi na kifilipino. Alikuwa ni mtu mwenye uelewa mkubwa sana wa masuala ya kimataifa na mwenye akili nyingi sana. Aliaminiwa na Rais Kim Jon Un wa Korea Kaskazini tangu alipoingia madarakani kurithi mikoba ya baba yake alipofariki.
“Comrade Kim has high expectations of your visit”, (Rais Kim ana matarajio makubwa na ujio wenu huu). En alimwambia Joe huku akitabasamu kwa shauku. “Same to President Costa”, (Hata Rais Costa), Joe nae alijibu kwa ufupi. Joe alijua mbinu za mazungumzo, alijua wapi pa kuongea sana na wapi pa kuongea kwa uchache, alijua lipi la kujibu na lipi la kukaa kimya. Tangu anawasili Pyongyang kila jambo analofanya alitumia umakini mkubwa.
Safari iliendelea huku Joe akishangaa na kustaajabu namna barabara ilivyokuwa tupu na nyeupe. Hakuona hata mtu mmoja tokea walipouacha uwanja wa ndege. Alikuwa akistaajabu na alipouliza kwa En alijibiwa hivyo ndivyo wanavyowaheshimu wageni muhimu kwa taifa. Joe hakuelewa.
**************************************
Ryongsong ndilo jina la makazi ya Rais Kim. Wengine hupenda kuyaita Residence No. 55 auCentral Luxury Mansionkutokana na umaridadi wake. Ni makazi yanayosemekana kulindwa na kuwa salama kuliko makazi yoyote duniani. Ukubwa wa eneo yaliyopo makazi haya ni kilometa za mraba 12 pakiwa na kila aina ya kitu kinachohitajika kwa kiongozi mkuu wa nchi.
Wataalamu wa masuala ya ulinzi na ujasusi wanaamini kuwa askari kati ya 95,000 – 120,000 wapo maalumu kwa ajili ya kulinda eneo hili pamoja na usalama wa Rais Kim na maeneo mengine yote yalipo makazi ya familia ya Rais Kim. Wakiwa chini ya kikosi namba 963wakiongozwa na Jenerali Yun Jong-Rin, wanakifanya kikosi hiki kuwa moja ya vikosi vikubwa kabisa vya ulinzi wa Rais duniani.
Ryongsong imezungukwa na machimbo yaliyotegwa kulipuka kama kuna mvamizi yeyote atataka kusogelea makazi haya kwa njia ya ardhi, lakini pia kuna wigo mkubwa wa umeme pamoja na vituo vingi vya ukaguzi kwenye njia ya kuingilia na kuzunguka makazi haya. Makazi haya pia yamezungukwa na vituo vya kijeshi vyenye makombora makubwa ya maangamizi na ya masafa marefu na mitambo ya kunasa chochote kinachoikaribia eneo lile bila taarifa na kuweza kutuma kombora kukisambaratisha.
Hakuna ndege wala kifaa chochote kinachoruhusiwa kupita juu ya anga lililopo jengo hili la sivyo kitatunguliwa hapohapo. Ndani ya makazi haya, chini ya ardhi kuna Sehemu salama ya kumficha Rais ikiwa itaonekana yupo hatarini. Eneo hilo limejengwa kwa kuta za chuma kizito na zege zito lililofunikwa na madini ya leadili kuzuia nyumba hiyo kuathirika hata kwa shambulio la nyuklia.
Lead ni moja ya madini yenye myeyuko hafifu (Low melting point), hivyo huhitajika joto la kuanzia nyuzi joto 327 ili yaweze kuyeyuka. Ni katika Sehemu hiyo Rais Kim huweza kuishi huko kwa usalama bila chochote kutoka kwa maadui kuweza kumvamia ama kumdhuru kwa miaka zaidi ya mitatu mfululizo bila kutoka, huku akiweza kutoa maelekezo ya kivita na kiutawala.
Makazi haya pia yameunganishwa na makazi mengine ya Rais ya Changgyongau huitwa Residence No.26. Makazi haya yote yamewekewa mfumo utakaoruhusu kutumia njia iliyopo chini ya ardhi ikitokea kuna uvamizi. Pia chini ya ardhi kutokea kwenye nyumba hii kuna reli maalumu kwa ajili ya Rais tu na kitu cha kustaajabisha kwa wachambuzi wengi wa masuala ya kiusalama ya peninsula ya Korea ni kuwa reli hii ilitengenezwa kuelekea mahali kusikojulikana.
Inadhaniwa kuwa mwisho wa reli hii hubadilikabadilika kulingana na mahitaji ya wakati husika lakini lengo kuu likiwa kuhakikisha kuwa Rais na familia yake wanakuwa salama likitoea shambulio. Mbali na mambo mengine mengi ya kiulinzi na kiusalama, nyumba hii imepambwa sana kwa nakshi, taa na samani nzuri. Nje kukiwa na bustani nzuri na za maua zenye kuvutia, mito na maziwa ya bandia yaliyotengenezwa kupendezesha eneo hili. Hakika makazi haya yalivutia.
Joe, Habibu na Pius walikuwa wanakuja kuingia hapa kwa mara ya kwanza.
*******************************************
“Wananchi wenzangu mlinichangua ili nilete maendeleo na maendeleo ndiyo haya. Nimesema na nimemwagiza Waziri wa Kilimo na Chakula hapa kuwa Sitaki kusikia mkulima yeyote anakatwa tozo eti ya kusafirisha mazao. Mtu hata kuuza hajauza unamkata tozo kivipi? Vibali vya kusafirisha mazao vitolewe bure kama mtu amelima mazao yake kihalali anayatoa shamba anayapeleka mjini ama mkoa fulani kuuza unamwambia alipe, sasa alipe na nini wakati hata kuuza hajauza? Tena sitataka kusikia ukiritimba katika kutolewa vibali hivi.
Waziri upo hapa unanisikia na viongozi wengine wote hili nalifuta kuanzia leo”, Rais Costa alikuwa akiongea huku akishangiliwa kwa nguvu na wananchi wa Kisasampara, Jimbo la Kengwe alipokwenda kuzindua ghala kubwa za chakula za hifadhi ya Taifa.
“Tumeanza mazungumzo na serikali ya China na tutaingia nao ubia kutujengea soko kubwa la kimataifa la matunda. Soko letu likikamilika litakuwa la kwanza kwa ukubwa bara la Afrika, hivyo vijana anzeni kujikita kuzalisha matunda. Neema inakuja!” Rais Costa aliendelea huku umati mkubwa wa watu ukimshangilia. Alikuwa ameanza utekelezaji wa ushauri aliowahi kupewa na Joe siku za nyuma namna ya kujadiliana na Rais wa China juu ya kuingiza vijana wa kichina zaidi ya laki moja kuja nchini Stanza kufanya biashara ndogondogo.
Rais Sylvester Costa alimaliza kuhutubia na kushuka jukwaani na kusalimiana na wananchi wawili watatu kisha kuanza kutembea kuelekea kwenye zile ghala kuzikagua. Alikuwa amefuatana na mawaziri, viongozi wengine wa serikali kuu na ya Jimbo pia alikuwepo na bi. Eliza, mke wa Joseph ambae kwa wakati huo ni Mkurugenzi wa Benki ya Kilimo ya Stanza. Aliingia akayakagua na kuridhika kisha msafara uliondoka kuelekea kwenye nyumba ya mapumziko ya viongozi wa kiserikali kwa ajili ya mapumziko iliyopo pale Kengwe.
Wakiwa kwenye nyumba ya mapumziko Rais alipata chakula pamoja na Waziri wa Kilimo na Chakula, Waziri wa Fedha ambaye ndiye alikuwa Waziri wa zamu kwa wiki hiyo, Gideon, mshauri wa karibu wa Rais Costa na Eliza mke wa Joe.
“Eliza Watoto wanaendeleaje”, Rais Costa aliuliza. “Wanaendelea vizuri Mh Rais’’, Eliza alijibu pasi kumtazama Rais usoni. “Nimeipata mikakati yako ya kuboresha ufanisi wa benki na hakika taifa lilikumisi sana”, Rais Costa aliendela kuongea huku akikata kipande cha nyama kwa uma na kisu. “Nafurahi kutoa mchango wangu kwa taifa”, Eliza alijibu kishupavu na maongezi mengine yaliendelea. Mara baada ya kumaliza kula Eliza, Waziri wa Fedha na Waziri wa Kilimo na Chakula waliaga na kuondoka kuelekea mahali walipoandaliwa kupumzika.
“Mh. Umeona wananchi wanavyokupenda? Umesikia walivyokuwa wapiga kelele uendelee kubaki madarakani? Mimi nadhani hata tulivyobadili katiba kuruhusu miula mitatu ya utawala tuliwarahisishia kazi sana”, Gideon alikuwa akimjaza upepo Rais Costa wakiwa pale sebuleni wakisoma magazeti huku wakitazama habari kwenye runinga.

“Ninaona hapa huyu Kibwe ameanza kupiga kelele juu ya azma yangu ya kubadili umri wa kugombea urais. Ni vyema tukamdhibiti mapema, si mtu wa kubeza, ana ushawishi mkubwa ndani na nje ya nchi. Hawa jamaa wa magharibi watatusumbua tukimwacha aliongelee ongelee”.
Badala ya kujibu aliloambiwa na Gideon, Rais Costa yeye alimwonyesha habari katika gazeti inayomwonyesha Julius Kibwe, kiongozi kijana na machachari wa upinzani akipinga vikali tetesi za muswada wa kutaka kubadili umri wa kugombea urais uongezwe kutoka miaka 40 mpaka miaka 55.
“Nitamshauri Waziri wa Sheria na Masuala ya Bunge njia nzuri ya kulipeleka hili, lakini wakati huo huo ni vema wewe ukazidi kuongeza imani na mapenzi kwa wananchi”, Gideon alimjibu Rais Costa.
‘’Umetoka kusema kuwa wananchi wananipenda. Hiyo Imani na mapenzi unayoshauri niongeze kwa wananchi ni kwa njia zipi?’’, Rais Costa alimuuliza Gideon akionekana wazi kuwa hajaelewa hilo lingefanyikaje kwani katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, pamoja na ukandamizaji wa demokrasia na kufunga wapinzani wake, lakini alianza kuhisi umaarufu wake umeshuka na kwa namna fulani wapinzani wake kisiasa walizidi kumkalia kooni wakimtaka aheshimu haki za binadamu, Sheria na Katiba ya nchi. Aliona kama alichosema Gideon hakiingii akilini kwa hali ya sasa.

‘’Tengeneza tatizo kupitia viongozi wa chini yako kisha wewe jiweke mbali nalo, hakikisha kuwa linamgusa kila mmoja au watu wengi, acha watu wapige kelele, wanasiasa waongee, kisha litatue na kulaumu watu wengine aidha kwa kuwataja hadharani au hata kwa kuwataja kwa ujumla tu katika makundi yao, ikiwezekana tumbua baadhi yao. Hii itakufanya wewe uonekane usiye na hatia, tena mkombozi haswa’’, Gideon alijibu na kumfanya Rais Costa kumpa usikivu zaidi na hata kubadilisha mkao.
“He he he he!”, Kwa mara ya kwanza baada ya kipindi kirefu, Rais Costa alicheka na kuonekana kuvutiwa na mipango ya Gideon ambayo ingemuongezea umaarufu na kupendwa. Rais Costa alipenda kusifiwa zaidi, hakutaka kusikia mtu anayemkosoa au asiyemuunga mkono. “Tatizo kama lipi kwa sasa?’’, Rais Costa alihoji kutaka kufahamu zaidi kuhusu mpango wa Gideon ambao ulishaanza kumvutia.
“Leo umetoka kuwafurahisha wakulima, ina maana vijijini tayari umezidi kupendwa kwani tozo hizi zilikuwa ni kero. Lakini ukumbuke kwa kufanya hivi umepunguza chanzo cha mapato kwa halmashauri nyingi hivyo ni lazima tutafute pa kulipia, sasa waite Waziri wa Fedha na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Taifa ya Mapato na Makusanyo. Wape maagizo waanze operesheni ya kukamata wote ambao hawajalipa kodi hata kama mhusika biashara yake mtaji ni wa chini ya shilingi laki moja, alazimishwe kulipa kodi kwanza kabla hajaanza bishara kwa kukadiriwa”, Gideon alishauri na kukaa kimya huku akimtazama Rais Costa.
“Ukweli kuna uliyosema ya msingi hasa kutafuta vyanzo mbadala vya mapato lakini hili la kulipisha watu kodi hata kabla ya biashara kuanza tena hata wenye mitaji ya chini kabisa sijaliunga mkono. Halina afya kwa mwananchi wa kawaida na tunajiua kiuchumi wenyewe”, Rais Costa alionekana kutoelewa.
Gideon alicheka sana kisha akamwambia Rais, “Hilo ndio litakuwa tatizo, na baada ya miezi mitatu hivi hadi sita ya watu kupata taabu na Mamlaka za Ukusanyaji Mapato na Kodi na kulalamika sana, utafuta huo utaratibu kwa kisingizo kuwa ni kumkandamiza mnyonge na wewe haupo kwa ajili ya kutesa wanyonge”, Gideon alimaliza.
Rais Costa alimwangalia Gideon kwa sekunde kama tatu akiwa kimya kisha aliangua kicheko kikubwa “Gideon you are a genius”, (Gideon una akili sana). Alifungua chupa ya wine na kuanza kummiminia Gideon.
***************************************
Msafara wa Joe na En uliwasili kwenye makazi ya Rais wa Korea. Rais Kim alikuwa mlangoni akiwasubiri na mara baada ya kushuka walipokelewa. Joe akiwa mbele ya Habibu na Pius alifika mbele ya Rais Kim kwa heshima kubwa, akainama kidogo na kumkabidhi nembo ya Rais wa Stanza (‘The Republic of Stanza’s Presidential Seal’), kama ishara haswa ya ujumbe maalumu wa Rais wa Stanza. “Karibuni sana”, kwa mshangao mkubwa Rais Kim aliwakaribisha kina Joe kwa kutumia Kiswahili. Walikumbatiana na kuelekea chumba maalum kwa ajili ya mazungumzo ya awali na kufikisha ujumbe Rais wa Stanza aliotaka umfikie Rais Kim.

Walifika na kuketi, Kim akiwa sambamba na En Waziri wake wa masuala ya kigeni huku kina Joe wakiwa wamepewa mkalimani waliulizana habari za hali na maendelo baina ya nchi hizo mbili. Joe alimkabidhi faili maalumu la siri alilopewa na Rais Costa lililo na barua na maelezo ya lengo la ujumbe ule. Hata hivyo maelezo yote aliyaandika Joe.
Baada ya Rais Kim kupokea faili lile alitoa maelekezo kuwa siku ile ya kwanza wangekutana ujumbe wa Joe na ujumbe wa serikali ya Korea Kaskazini. Joe na ujumbe wake wangeeleza kila jambo lililowapeleka Korea na kisha ujumbe wa Rais Kim ungeenda kutafakari na kisha kukutana nae kutafakari kabla ya kukutana tena wote kwa makubaliano na maazimio kesho yake.
Ilipangwa kuwa ni ugeni utakaodumu kwa siku mbili wakianza siku hiyo waliyowasili mpaka watakapoondoka. Mara baada ya kupata ratiba hiyo Joe na wenzake walielekezwa eneo la mapumziko na kuachwa hapo watatu wakiwa wamepewa kahawa kama walivyohitaji.

Joe akiwa na wenzake aliwaambia sasa muda wa kuonyesha vipawa vyao vya majadiliano ya kimataifa umefika. Wakiwa wanajadiliana, Pius alionekana kutotulia kiakili. Suala walilokuwa wamezungumza kwenye ndege lilikuwa likimsumbua sana.

“Upo sawa?”, Joe alimuhoji Pius. “Hapana, suala lile bado linanitafuna akili nataka kujua ni nani mwingine anafahamu”, Pius alimjibu Joe. Kwa kujua kuwa maongezi yao yaweza kuwa yanarekodiwa ndani ya makazi yale kwa kutumia vinasa sauti vyenye uwezo mkubwa ilikuwa ni lazima watumie maneno machache sana kuzungumza mambo yao au hata kwa ishara. Joe alishajua Pius anazungumzia nini, alijua anataka kujua ni nani mwingine yupo kwenye ule mpango aliowashirikisha wa kumpumzisha Rais Costa nje ya madaraka pasi yeye kutaka kwa hiari kuyaachia.
Joe aliwaangalia Habibu na Pius usoni. Aligundua kuwa bila kuwafumbulia fumbo hilo wasingefanya vizuri kwenye mazungumzo yao kwasababu akili zao zilitekwa na mpango ambao Joe aliwashirikisha kwa kifupi. “Ok, nitawaambia ili akili zenu mzirudishe hapa. Stanley Macha ni mmoja wapo kwenye mpango huu, mwingine sitawatajia kwa sasa” Joe aliwadokeza kwa kifupi.

Habibu na Pius walionekana kushtuka. Hawakuamini kama Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa nae yupo kwenye mpango huo. “This is serious guys”, (hili suala ni nyeti). Joe aliwaambia huku akiwatazama usoni. “Tutaamini vipi kama ni kweli?”, Habibu alihoji.
“Nitawapa namba za siri (codes). Sasa kila mtu kwa wakati wake na ikiwa umekubaliana na mpango huu kwa ustawi wa nchi yetu na kuwa mmoja kati ya watakaoleta chachu ya mabadiliko ya kweli, utamtumia Stanley hiyo namba ya siri kwa njia ya WhatsApp nae atajibu kama utakavyomwandikia, na baada ya hapo hamtaendelea na mazungumzo yoyote. Hiyo itakuwa ndio ishara kuwa nimeshawaambia na kuwa tupo pamoja”, Joe aliwaeleza.
“Tupe hizo codes”. Habibu na Pius walijikuta wakiuliza kwa pamoja. “Ego testor”, Joe aliwajibu (Hili ni neno la kilatini lenye maana ya kuapa/kula kiapo). Haraka Pius na Habibu walitoa simu zao za mkononi kwa shauku kutaka kuhakikisha kile wanachokisikia.

Waligundua simu zao hazinasi mtandao wowote, wapo ugenini lakini hata kama wangekua wanaweza kuwasiliana kwa wakati ule isingewezekana kwani ukikaribia tu makazi ya Rais Kim mawasiliano yote hukatika na ni mfumo wao tu maalumu wa mawasiliano ambao wanao watu wachache sana ndani ya makazi yale ndio hutumika. Walihema wote kwa pamoja na kutulia.
************************************
Je, Mazungumzo Jijini Pyongyang Yatafanikiwa?Vipi Usalama Wa Stanley Macha Baada Ya Kutajwa Na Joe?Usikose Sehemu Ya Sita
Safi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
VISASI

The President And I(Mimi Na Rais)- Sehemu Ya Tisa

Lello Mmassy January 22, 2019



Rais Costa Uso Kwa Uso Na Askofu Begere.Pius Atoweka Uwanja Wa Ndege Shenyang


“Mh.Rais, Askofu Begere ameomba miadi na wewe aje akuone”, Alikuwa ni Chaurembo Chalamila, Waziri wa Ardhi akimtaarifu Rais Costa juu ya ombi la Askofu Damian Begere kuomba kuonana nae kwa mazungumzo.

Kwa haraka Rais aliamini kuwa Begere anakuja kujisalimisha kwake na kuacha kumshambulia yeye na serikali yake. Rais Costa alifurahi ingawa alificha hilo usoni mwake.


“Anataka kuniambia nini? Au anataka kunihubiria na mimi kuhusu utawala bora?”. Rais Costa alijibu kwa dharau huku akiendelea kusoma makabrasha yaliyokuwa mezani kwake.


“Hapana anataka kujadiliana na wewe masuala mbalimbali hasa yanayohusu miradi yake ambayo umeikwamisha”, Waziri Chaurembo alijibu.


“Ha ha ha ha! Kwahivyo sasa ndio anatambua kuwa Rais wa nchi hii ni mimi na sio yeye? Mwambie sawa aje tujadiliane kesho saa nne asubuhi”, Rais Costa alimjibu Waziri Chaurembo.

************************************


Ilikuwa siku ya Jumatano, ilipofika saa nne kamili asubuhi tayari Rais Costa alikuwa ofisini kwake akisubiria kuja kuitwa ili akaonane na Askofu Begere. Aliendelea kusoma taarifa mbalimbali anazowekewa mezani na watu wa usalama na wasaidizi wake.


Rais Costa alikuwa akipenda sana kusoma taarifa. Ilikuwa ni ngumu awekewe taarifa na aache kuisoma. Katika vitu watu wa Ikulu wanaheshimu ni taarifa wanazoweka mezani kwa Rais. Ilikuwa ni rahisi sana mtu kupenyeza jambo lake. Ni kuhakikisha tu linafika kwenye meza ya Rais basi ni lazima angelisoma na kulifuatilia.


Akiwa anaendelea kusoma huku akinywa Kahawa mlango ulifunguliwa na kwa mshangao yeye akijua anaitwa ili aelekee chumba cha kukutania na askofu Begere badala yake aliingia Ketina.


“Mh. Rais Shikamoo”, Ketina, kimada wa Rais alisalimia kwa adabu ya kinafiki ili wasaidizi waliopo nje ya ofisi ya Rais wasielewe kinachoendelea.


“Ketina umekuja kufanya nini?” Rais Costa alihoji akiwa amestaajabu ujio ule bila mwaliko.


“Mh. Rais mimi si mteule wako? Katibu tawala wa Jimbo au? Nimeleta taarifa kwa boss wangu”, Ketina nae alijibu huku akiketi kwenye kiti kilicho mbele ya meza ya Rais.


“Nina kikao sasa na ‘Bishop’ Begere, utanisubiri pale eneo la wageni mpaka nikitoka”. Rais Costa alimwambia Ketina.


“Bishop ndio atasubiri sio mimi”, Ketina alianza kuonesha ukaidi kama kawaida yake.


Wakati wakijibizana mara aliingia tena msaidizi na kumtaarifu Rais Costa kuwa Askofu Begere yupo tayari kuonana nae. Rais Costa alianza kutoka na kumwacha Ketina pale ofisini kwake akiwa amekaa.


Rais alipotoka tu waliingia vijana wawili wa usalama na kumwomba Ketina atoke. Ketina alianza kuleta ukaidi kwa kuwauliza wanamjua yeye ni nani? Vijana wale walimsihi kwa mara nyingine atoke na kuwa ofisi ile haitakiwi iwe na mtu yeyote ndani kama Rais hayupo. Ketina aliendelea kuonesha kiburi na kujiamini kwakuwa tu alikuwa na mahusiano zaidi ya yale ya kikazi na Rais Costa. Wanausalama si watu wa kuwafanyia mzaha wakati mwingine, kufumba na kufumbua pasi kuamini Ketina alijikuta yupo chumba asichokifahamu pale Ikulu.


Ketina alipigwa shoti na kifaa cha umeme wanachokuwa nacho vijana wa usalama na kunyakuliwa mzobe mzobe kama mwewe anavyochukua kifaranga cha kuku na kuwekwa kwenye chumba maalumu cha uangalizi. Ketina aliposhtuka alianza kupiga kelele kwa nguvu pasi kuelewa kuwa chumba kile hakipitishi sauti hata desibeli moja. Aliachwa huko adabu imshike kwanza.

***************************************


“Mhashamu Baba Askofu, Tumsifu Yesu Kristu”, Rais Costa alimsalimia Askofu Begere kwa heshima huku akiibusu pete ya kiaskofu iliyopo kidoleni mwa askofu. Kiumri askofu Begere alikuwa ni mkubwa kwa Rais Costa. Wakati Rais Costa akiwa na miaka 56 askofu Begere alikuwa na miaka 73.


“Milele amina Mh. Rais”, Askofu Begere alijibu na wote waliketi. Mazungumzo yalianza.


“………Miradi hii ndiyo nilitaka kuitumia kama kilele cha utumishi wangu nitakapotimiza miaka 75 na kustaafu, na sasa nimebakiza miaka 2 tu. Nimeshamwandikia Baba Mtakatifu barua ya azma yangu ya kustaafu uaskofu na kupumzika, sasa miradi hii kukwama inaniumiza sana.” Askofu Begere aliongea kwa huruma kubwa.


“Mhashamu Baba Askofu, kwanza nikiri kanisa limekuwa na mchango mkubwa sana kwa maendeleo ya nchi yetu. Hata mimi nimesoma seminari ya kanisa hadi kidato cha sita. Lakini unachofanya wewe na kanisa kwa serikali yangu sioni kama ni sawa. Unanichonganisha na wananchi. Hivi siku ikitokea kutokana na msukumo wenu wananchi wakachukua hatua kwa kufanyia kazi unayohubiri, nchi ikakosa utulivu utaona raha gani?” Rais Costa alimweleza Askofu Begere, japo alikuwa akiongea kwa nidhamu lakini alitoa ya moyoni.


“Hayo tunayohubiri ni wajibu wetu. Kama tusiposimamia haki na usawa, utawala bora, matumizi sahihi ya fedha za umma na utii wa sheria na katiba ya nchi ni nani mwingine tumtarajie atasimamia? Nani atakemea? Kwani kuna la uongo ama la uchochezi tulilohubiri?”, Askofu Begere alionekana kutoelewa.


“Mh. Baba askofu kazi hizo zote ulizosema zina vyombo vyake vya kusimamia. Tuna Mahakama, Bunge, Mamlaka ya Makusanyo ya Taifa, Ofisi za wakaguzi wa hesabu n.k. Sidhani kama ni kazi yenu kukemea hayo. Kazi yenu ninyi na hata mimi nilijifunza seminari ni kuwaleta watu kwa Yesu Kristu. Hicho ndicho kipimo chenu baba askofu. Nisahihishe kama nimeongea uongo. Sasa ukisema ni kazi yenu kukemea inamaana na sisi tuiambie mahakama ianze kuhubiri Injili? Na bunge lianze kubatiza?” Rais Costa alianza kuongea kwa kuonyesha ghadhabu.


“Mh. Rais nadhani mbali ya mimi kuwa askofu lakini pia ni raia kama raia wengine na ninazo haki kikatiba kukemea pale ninapoona mambo hayaendi sawa” Askofu Begere alijibu kwa upole.


“Ndio ukemee kwa kutumia membari?” Rais Costa alimuuliza askofu Begere kwa ufupi sana.


“Je hayo ninayokemea sio haki? Ninasingizia?” Askofu Begere nae alihoji.


“Sasa kama unachohubiri ni haki, wewe kilichokuleta hapa ni nini Mhashamu?”, Rais Costa alionekana kutofurahishwa na majibu ya askofu Begere.


Baada ya kimya cha muda mchache huku wakitazamana, Askofu Begere aliuvunja ukimya “Sawa nimekuelewa Mh.Rais. Nimekuelewa unaamaanisha nini” alimwambia Rais Costa.


“Nashukuru sana Mhashamu Baba Askofu. Amani ya Kristu iwe nasi sote. Peleka salamu zangu kwa Baraza zima la maaskofu. Mnafanya mambo mengi makubwa kwa Taifa hili”, Rais Costa alikuwa akimwambia askofu Begere huku akiwa amesimama akishikana nae mkono.


“Nitawasalimia Mh. Rais”, Askofu Begere alijibu na kisha Rais Costa alitoka na kumwacha askofu bado ameketi.


Maongezi yalikuwa mafupi sana na ya moja kwa moja. Katika lugha ya wenzetu, Askofu Begere alionekana ameshafungwa mdomo ‘once and for all’, yaani si matarajio ya yeyote kwa Askofu kuendelea kuikosoa serikali ya Rais Costa. Angalau hivyo ndivyo Rais na wapambe wake waliamini baada ya mazungumzo hayo. Kwa mtizamo wa haraka wa mazungumzo yale, ilionekana wazi Askofu Begere amekubali kushindwa ili kutoharibu maendeleo ya miradi ambayo ingempa heshima ndani ya Kanisa na hata kwa taifa baada ya kustaafu kwake.

**********************************


“Guys, mtu mwingine ambae yupo kwenye mpango huu ni Bi. Sara, yaani mke wa Rais Costa. Kama mjuavyo hawapo nae vizuri na yeye kuna mambo hakubaliani nayo hivyo ametuunga mkono katika mkakati huu. Bi. Sara atatusaidia sana mbeleni, kwasasa nisielezee kwa undani ila ni kiungo muhimu sana kuliko mnavyoweza kuelewa.


Sasa basi, maswali kuwa nchi itaongozwa na nani niseme tu kuwa Habibu jitayarishe kuwa Rais wa Stanza. Pius utakuwa Mkuu wa Majeshi. Stanley atabaki palepale kwenye nafasi yake na mimi nitakaa nje ya mfumo.


Habibu unafahamu Rais Costa alikuondoa Stanza kwasababu ya nguvu uliyonayo kisiasa hivyo tutakurudisha ukaingie kwenye siasa kwa mwaka huu mmoja urudishe tena nguvu yako, wewe ni kijana pekee unayeweza kupambana na Julius Kibwe kwa hoja na kuleta kuaminiwa na kupata ufuasi mkubwa.


Stanley atabaki pale pale, the guy is more than a perfect match for that position. Habibu ukiingia utamteua Pius kuwa Mkuu wa Majeshi, naamini kwa njia hii nchi itakuwa kwenye mikono salama.


Tulichokubaliana na kula kiapo na Macha ni kuwa tunayafanya haya ili kurudisha Misingi ya Utawala bora, Demokrasia, Haki na kuleta maendeleo kwa wanastanza wote bila kujali ukanda wanaotokea, dini, itikadi za kisiasa na madaraja mengine ya kijamii.


Katiba yenye misingi bora ipo, ingawa inakiukwa kila mara kwa kutumia mabavu. Katika Stanza mpya inayofuata misingi ya utawala bora na misingi ya sheria, tunataka yeyote atakayekiuka mara tu baada ya kushika madaraka anawajibishwa, tunataka nchi ya watu wanaofurahia uhuru wao. Maendeleo bila uhuru ni ukoloni.


Sasa hatua gani tutaanza nazo? Kwanza tukifika nitatengeneza mazingira Habibu utolewe ubalozini aidha kwa kufukuzwa ama kwa kigezo cha kupangiwa majukumu mengine. Hili tutalifanya kitaalamu mimi na Macha ili lisiharibureputation yako lakini likupe nafasi wewe ya kurudi mtaani na kuanza kufanya siasa. Tutahakikisha Rais Costa hakugusi. Mipango mingine nyeti tutaambizana tukifika Stanza”, Joe alimalizia maelekezo yake kwa kirefu huku akiwatazama usoni.


Pius na Habibu walimeza mate, walijikuta wote wameshika bilauri ya maji na kunywa maji kushusha mshangao wao, hawakuamini jinsi mpango ule ulivyosukwa kitaalamu na kuwahusisha watu ambao hawakudhaniwa na mtu yeyote. Hawakuwahi kufikiri kuwa jambo hilo lingewezekana.


“Rais Costa mkishamtoa anakwenda wapi? Kwanini nguvu tunayotaka kuitumia kumtoa isitumike kuhakikisha miswada yake haipiti na kuwa uchaguzi ujao hashindi maana kama tunaweza kumtoa kwa nguvu kabla hata ya muda wake kuisha tunashindwaje kuhakikisha muda wake ukiisha hashindi tena?”, Pius alihoji.


“Kwa kutumia njia hiyo, ni rahisi kugundulika mapema na wapambe wake na kukutoa kwenye malengo. Unafahamu namna mambo yalivyo Stanza na ndiyo sababu tunataka kumtoa kwa kumshtukiza bila yeye kujipanga. Sasa swali mnalotaka kuniuliza kuwa yupo Makamu wa Rais, sijui na Waziri Mkuu ambao kama Rais akiwa hawezi kutimiza majukumu yake hao ndio hutakiwa kuchukua nafasi hiyo na sasa Habibu ataingiaje ingiaje hapo. Niwajibu tu kuwa hayo tunayafahamu na tutaambizana kadiri muda unavyosogea”Joe aliwaacha tena kina Pius na Habibu njiapanda.


Pius aliumiza akili, aliona kabisa mpango huu ni wa kumdhuru Rais Costa na yeye hakutaka litokee. Kiapo chake kilimtesa, alijiona siyo askari kabisa kwa kumsikiliza Joe. Aliwaza jambo kichwani ila akakaa kimya. Alitaka kwanza ajiridhishe kama kweli Macha anazo hizi taarifa ama ni tantalila za Joe tu. Alitaka atume kwanza yale maneno ya siri yajibiwe na Macha ndio aamue la kufanya.

*****************************************


Yule kijana wa kiVietinam aliwasili uwanja wa ndege wa kimataifa Beijing tayari kunasa maongezi ya kina Joe na wenzake. Alishajitega kwa namna ambayo kina Joe tangu wakiwa pale angeambatana nao bila wao kumjua na kunasa maongezi yao kutokea mbali.


Aliona ndege ya shirika la Korea Kaskazini, Air Koryo ikitua na alikaa tayari kufanya kazi aliyotumwa. Alistaajabu alipogundua kuwa kwenye ndege ile kina Joe hawakuwepo. Aliwasiliana na balozi Kimweri kumpa taarifa. Balozi alionekana kushangaa na haraka aliamua kuwasiliana na Ubalozi wa Korea Kaskazini pale China kuulizia kulikoni, alitaka kufahamu kwanini raia wake hawaonekani kama walivyopanga. Alijibiwa tu kiufupi kuwa Joe na Ujumbe wake wapo salama salimini na watawasili Ubalozini ndani ya muda mfupi.

************************************


Joe, mbali ya umaridadi wake katika masuala ya diplomasia lakini pia yu maridadi katika ujasusi kama sehemu ya msomo yake aliyosomea nchini Urusi miaka ya 1970 wakati nchi ya Stanza ikiwa na mahusiano thabiti na lililokuwa taifa la Umoja wa Kijamaa wa Jamhuri za Kisovieti (The Union of Soviet Socialist Republics)


Ni yeye aliporudishwa ndani kwa mazungumzo ya siri na Rais Kim akiwa peke yake, mbali na mambo mengine ya siri aliyoongea naye alimuomba usafiri wa tofauti kurudi China. Alijua Rais Costa anafuatilia nyendo zao na hivyo alitaka kumpiga chenga ili wapate wasaa wa kuongea na kina Pius na Habibu kwa kirefu.


Katika mambo walikubaliana japo ndani ya muda mfupi, Rais Kim alikubali moja ya ndege zakeChammae-5 iwabebe kina joe na kuwarudisha China. Joe alimwomba Rais Kim kuwa safari hiyo iwe ni ya kimya na Balozi Kimweri ashangae tu wamefika bila kujua utaratibu ulikuwaje. Pia alimwambia Rais Kim kuwa yeye atamwambia Rais Costa kuwa walipewa ndege ile kwa heshima kubwa ya undugu wanaoanza kuujenga baina ya mataifa yao mawili hivyo hakutakuwa na sintofahamu.


Hicho ndicho kilichotokea na sasa kwa mara nyingine tena, Rais Costa na Balozi Kimweri wanapigwa chenga ya mwili na gwiji Joseph Kaduma.

**********************************


Mara baada ya kuwasili uwanja mdogo wa ndege Shenyang simu za Joe na wenzake zilianza kushika mtandao tena. Tayari walikuwa na mipangilio iliyoruhusu watumie mtandao wa simu wakiwa China,(roaming) za China hivyo WhatsApp na mitandao mingine iliweza kufanya kazi vyema.


Kila mmoja kwa shauku kubwa alimtumia ujumbe Stanley Macha wenye yale maneno ya siri ego testor. Ndani ya dakika tatu hivi alienza kujibiwa alikuwa ni Habibu “Ego testor”, Ujumbe wa WhatsApp kutoka kwa Macha uliingia. Habibu alitabasamu kwa mshangao asiamini kuwa kumbe mpango ule ni hakika na kweli.


“Ego testor”, Ujumbe uliingia kwa Pius pia. Pius alishangaa na kuzungusha macho huku na huku na alipoona si Habibu wala Joe anayemtazama alipotea katika mazingira ya kutatanisha.


Joe na Habibu walipiga hatua kwa haraka wakijua Pius yupo nyuma anawafuata. Joe nae alikuwa anatembea huku akiwa WhatsApp akitumiana jumbe na Stanley Macha kwani tangu waingie Korea hawakuwa wamewasiliana. Macha alimwambia Joe kuwa ni punde tu ametoka kuwajibu kina Pius na Habibu yale maneno ya siri.


Macha alimuuliza kama ana hakika vijana wake wamemuelewa? Joe alijibu ndio huku akicheka na alinyanyua kichwa ili awatazame kina Habibu wana sura gani baada ya kujibiwa na Macha. Alistaajabu kutomuona Pius. Alisimama.


“Habibu Pius yupo wapi?”, Joe alimuuliza Habibu aliyekuwa nae ameinamisha kichwa akituma jumbe kwa WhatsApp. Habibu nae alisimamisha shingo na kushangaa kutomuona Pius.


“Macha, we have a problem. Pius is missing” (Macha tuna tatizo. Pius haonekani). Joe alimwandikia Macha ujumbe huo kwa haraka huku mapigo yake ya moyo yakizidi kuongezeka kasi kila sekunde moja inapopita. Alianza kutoka jasho japo palikuwa na baridi kali.

*************************************

Nini Kitatukia? Tukutane Ijumaa.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
The President And I(Mimi Na Rais)- SEHEMU YA SABA
Cc. Ibney hearly kuku mweus Munamuge Atikinson samson nchimbi ram kisukari moneytalk Tater Litro Madame S BssU Shunie The Book baba swalehe nipo2 kanonb boy lanugo


Mazungumzo Yakamilika Pyongyang. Rais Costa Ndani Ya Mgogoro Na Askofu Begere


Rais Sylvester Costa aliwasili Ikulu ya Stanza akitokea jimbo la Kengwe alipokuwa akizindua maghala ya taifa ya kuhifadhia chakula. Akiwa amesikiliza na kufuatilia vyema mahojiano kati ya Julius Kibwe na Katibu Mkuu wa chama chake tawala bwana Stanslaus alikasirika kwa jinsi Julius alivyomshambulia yeye na Serikali yake.


Akiwa amepokelewa na Stanley Macha na viongozi wengine wakitembea kwenye korido za Ikulu huku akisindikizwa na Gideon na Waziri wa Fedha, Rais Costa alitoa maagizo; “Gideon, mtaarifu Waziri wa Sheria na Masuala ya Bunge kuwa kesho asubuhi anione akiwa na taarifa amefikia wapi kuhusu ule muswada wa kubadili umri wa kugombea uRais.


Tamara wewe tutaonana mchana kesho, kuna maagizo nitakupa, uje na Mkurugenzi wako wa Mamlaka Ya Mapato na Makusanyo. Macha wewe ukiambatana na Waziri wa Polisi na Magereza mje na mpango mkakati wa namna ya kumdhibiti Julius Kibwe. Ni vyema akadhibitiwa mapema kabla hajawa tishio la kweli. Asanteni”. Rais Costa alimaliza kutoa maagizo na kuwashukuru wote waliokuwa wakitembea nae kuelekea kwenye makazi yake na kisha kuwaaga. Aidan Tamara ni Waziri wa Fedha wa Stanza.

***************************************


“Tunafanyaje hapa?”. Joe alianzisha majadiliano baada ya kusogelewa kwa karibu sana na Habibu na Pius.


“Kwa sababu hili ni moja la hitaji lao la lazima japo hatujajua kwanini lakini nadhani tukubali ili tufanikiwe. Ni lazima tukubaliane nao, hivyo tuwaambie suala la silaha za nyuklia liwe ni siri kubwa. Lakini ninajua kwa sababu wanajua tuna madini ya Uranium watataka kuzalisha baadhi ya silaha kule kule”, Habibu alidakia.


“Habibu, hakutakuwa na siri yoyote, Marekani wakijua tuna ushirikiano na Korea ni lazima watakuja kung’amua kuwa tunazalisha silaha za kivita za kinyuklia baada ya muda na watataka ukaguzi wa wataalamu wa kimataifa kama ambavyo wamelazimisha kwa kipindi kirefu kwa Iran’’, Joe alimjibu Habibu.


“Kwanza nadhani tuwape Korea wawe na ngome yao ya kijeshi Stanza. Hii itakuwa ngome yao ya kwanza nje ya Taifa lao. Ngome hii tuwape kwenye milima ya Usungulilo ambapo ndio tumegundua madini ya Uranium na ardhi ile iwe ni miliki halali ya Korea na hapo ndipo pawe panakaa vifaa vyote vya nyuklia. Hivyo tutamshauri Rais Costa awape haki miliki ya miaka hamsini kwa kuanzia.


Kwa namna hii tutahakikisha kuwa hata Marekani wakisema tunamiliki silaha hizo tunakana na wakitaka kukagua tunawaruhusu. Tunafahamu kabisa hawatapata na ikiwa watapata Ushahidi wa namna yoyote katika kukagua milima ya Usungulilo, ina maana wanaingilia ardhi ya Korea jambo ambalo halitawezekana hivyo tutakuwa tumeondoa mzigo wa kesi mabegani mwetu na kuuhamishia kwa waKorea”, Pius alichangia.


“Wataingia kwa nguvu Pius na hiyo ni vita sasa”, Joe alimwambia Pius.


“Hawataweza labda kama wanataka vita kati yao na Korea. Korea inamiliki makombora ya masafa marefu (Intercontinental Ballistic Missiles) ambayo kwa sasa Marekani yote ipo kwenye uzio wao (within target).


Wakati Marekani wakiwa wanamiliki Exoatmospheric Kill vehicle (EKV), teknolojia inayotumika kulipua makombora ya masafa marefu kabla ya kufikia tageti, tayari Korea hawa wana Multi-Object Kill Vehicle (MOKV) ambayo haizuii tu makombora yaliyotumwa bali pia yenyewe inazuia na wakati huohuo inatuma kombora muelekeo uleule kombora la adui lilipotokea na kwenda kuharibu chanzo. Hii ni teknolojia ya hali juu kabisa kwa sasa.


Aidha, ndege ya kishushushu iliyozinduliwa na China yenye uwezo wa kuruka bila kunaswa na rada yoyote na uwezo mkubwa wa kupiga picha kutokea juu sana ni zao la ushirikiano wa Korea na China. Marekani hana ubavu wa kuwasumbua Korea kwasasa”, Pius alionekana kushirikisha uzoefu wa kijeshi.


“Pius, lazima utambue kuwa kama mapigano haya yakianza ni dhahiri kuwa yanatokea katika ardhi yetu. Je, tungependa tuingie kwenye vitabu vya historia kuwa ni sisi tuliyaleta haya? na Je, haya yote yana tija gani kwa maendeleo na maisha ya watu wa Stanza au ni kukidhi tu matakwa ya Rais Costa?” Joe alionekana kuwa makini sana.


“Joe, chagua moja urudi umwambie Rais Costa umeshindwa haya mazungumzo au ukubali tuendelee”. Pius alihoji na kusimama. Walibaki na ukimya.

************************************


“Gentlemen, it’s time” (Jamaa, muda umefika), alikuwa ni Waziri En akiwaalika tena waelekee chumba namba 441 kuendelea na mazungumzo.


Baada ya kupeana muda wa mapumziko timu ya Waziri En ilikuwa imeelekea kuonana na Rais Kim ili kumpa kinachoendelea na yeye atoe maoni yake. Ilikuwa watakapomaliza haya mazungumzo ya awamu ya pili, watapumzika mpaka kesho yake ambapo watakutana wote na Rais Kim kumalizia mazungumzo.


Joe na ujumbe wake ulikuwa ukielekea kwenye mazungumzo bila muafaka na hakuna aliekuwa anajua nini wataongea. Joe alikuwa akitembea huku akiwaza sana. Alichakata akili kuliko wakati wowote katika maisha yake, ni kama mtu aliepewa nafasi atoe hukumu kati ya mauti ama uzima. Pius na Habibu wote walikuwa wakimtegemea yeye. Waliingia na kuketi.


“We have decided to go on and accept your terms. However, we would like to know more details about it, and whether there are any other demands as a result of your military aid to Stanza so that we can determine if we can meet them or not’’.

(Tumeamua kukubali sharti lenu lakini tungependa kufahamu taarifa zaidi za sababu ya kutaka silaha za nyuklia ziwepo nchini kwetu, lakini pia tunapenda kujua matakwa yenu mengine ili tuweze kutathmini ikiwa tunaweza kukubali au kukataa). Joe alianzisha mazungumzo yaliyowaacha Habibu na Pius mdomo wazi.


Waziri En alitabasamu na kisha kumweleza Joe na wenzake kuwa chanzo hasa cha kutaka wawe na silaha za nyuklia Afrika, kwanza ni kutaka kuwa na sehemu mbadala wanapozalisha silaha hizo nje ya nchini kwao kama sehemu yao kimkakati na kiulinzi.


Lakini pili, wangependa Stanza ndiyo iwe sehemu yao ya kimkakati kupata mashirikiano mengine Afrika kwa maana ya kuzitoa woga nchi za kiAfrika kutokuwa na mahusiano nao na hivyo kuwa kama Ushahidi kuwa hakuna lolote wanaweza kufanywa na yeyote eti tu kwa sababu wana mashirikiano na taifa lao.


Sababu ya tatu aliyotoa Waziri En ni kuwa Korea wanataka chanzo kipya cha kupata madini ya Urani ambayo ni malighafi muhimu sana kwa utengenezaji wa silaha za nyuklia. Madini hayo usafirishwaji wake ni hatari zaidi kuliko yakiwa tayari yameshatengenezewa silaha.


Waziri En alienedelea kuwa mahitaji mengine mawili watahitaji. Kwanza, mazao ya chakula na pili wapatiwe sehemu ya mgodi wa dhahabu ili kwa kutumia shirika lao la Mansudae waweze kuchimba na kuitumia kama sehemu ya kunyanyua uchumi wao.


Joe na wenzake walikubali kwani mazao ya chakula na madini ya dhahabu ni rasilimali ambazo zipo kwa wingi nchini Stanza. Majadiliano ya awamu ya pili hayakuwa marefu na walikubaliana na kuafikiana kukutana kesho kumalizia mazungumzo na Rais Kim.


Waziri En akishirikiana na Ujumbe wake waliwachukua Joe na wenzake tayari kuwapeleka nyumba watakayolala usiku huo ili wakutane kesho yake. Walitembea kwenye korido kuelekea mashariki kisha waliingia kwenye lifti iliyowashusha chini ya ardhi umbali kama wa mita mia moja, kisha walitoka na kuingia kwenye treni dogo kabisa.


Ilikuwa ni jambo la kushangaza kidogo kwa Joe. “Where are we going En?” (Tunaelekea wapi En), Joe alishindwa kuvumilia na kumuuliza Waziri En. Waziri En alicheka kidogo na kumweleza kuwa wanaelekea Kangdong Residence, moja ya makazi mengine ya Rais Kim.


Ni umbali wa mwendo wa kama dakika 6 kwa treni ile ipitayo chini ya ardhi. Ni treni ya umeme na maalum tu kwa ajili ya Rais Kim ama ugeni wake. Katika njia (tunnel) ile Joe alishangaa jambo moja, ni kuwa ipo giza totoro na treni ile hutumia sensor tu na haina dereva.


En alimweleza kuwa njia ile haiwezi kulipuka hata kwa bomu la nyuklia ni salama kabisa sawa na Rais Kim akiwa kwenye nyumba yake. Alimweleza pia ndani ya njia ile kama ikijulikana kuna hatari basi kunaweza kuachiliwa joto kali lenye uwezo wa kuyeyusha chuma kizito na kukigeuka uji ndani ya dakika tatu. Ilikuwa ni hatari.


Pius alikuwa akisikiliza hayo maongezi na akilini alikiri kuwa ulinzi alio nao Rais Costa wa Stanza ni sawa na hakuna. Alitabasamu akabaki kimya.


“You may have thought that the president of America is the most protected in the world, now you know who is. If you want to harm President Kim, he must be the last one alive in this nation’’.

(Unaweza kufikiri kuwa Rais wa Marekani ndiye anayelindwa zaidi duniani, sasa unajua ukweli ni nani analindwa zaidi. Ukitaka kumdhuru Rais Kim, labda awe ndiye mtu wa mwisho aliyebaki hai ndani ya taifa hili). Waziri En alimalizia kwa majigambo huku wakishuka kwenye ile treni na kuingia kwenye lifti iliyowapandisha juu.


Walitokea kwenye jengo hilo na kama kawaida kuna watu wachache sana wanaoonekana katika viunga vyake. Walipewa wana usalama wawili watakaokuwa wanawasaidia mahitaji yao. Waziri En aliwaaga, “Don’t worry today, no Methylbenzene here. Ha ha” (Msiwe na hofu, leo hakunaMethylbenzene hapa. Ha ha), En aliwatania kwa kukumbushia kilichompata Pius. Aliondoka.

***********************


“Nimesema wasipewe hili eneo. Waziri hakikisha hili eneo hawalipati, tena na hata lile eneo la Kiberege walipoanza kujenga ile seminari yao wabomoe. Hamfahamu kuwa lipo karibu na mto, sehemu ambayo serikali yangu inakusudia kuweka mradi wa kuzalisha umeme?”. Alikuwa ni Rais Costa akiongea kwa hasira jioni ile huku akimfokea Waziri wake wa Ardhi, ndugu Chaurembo Chalamila Ikulu ya Stanza.


“Mh. Rais, eneo lile la Kanisa pale Kiberege lipo mbali sana na mto na sehemu yenye maporomoko ya kuzalisha umeme na kuwa halitaathiri mradi. Lakini pia, ujenzi wa ile seminari yao ambayo ni kubwa kuliko zote nchini umekamilika kwa asilimia kubwa. Na eneo hili wanaloomba la Kilungulula kufanya mradi wa hospitali ya kisasa una manufaa kwa wananchi wa eneo lile kwani katika kanda nzima hakuna kabisa hospitali ya rufaa”, Waziri Chaurembo alimjibu Rais Costa kwa unyenyekevu mkubwa.


“Chaurembo, sidhani kama wewe unajua manufaa ya wananchi kuliko mimi,kwa hiyo usianze kunipa darasa la manufaa ya wananchi hapa. Nimesema eneo wasipewe na ile seminari yao kule wabomoe. Kama waliuziwa eneo lile na serikali za awamu iliyopita iliyokuwa imejaa rushwa, siwezi kuacha kuwapa wananchi wangu umeme kwa sababu eti watu wajenge shule ya kusomea kusali na kupiga cheteso (cheteso ni chombo kinachotumika kufukizia ubani kwenye madhabahu ya kanisa. Mara nyingi kanisa katoliki na yale ya Orthodoxy)


Hii nchi ina watu zaidi ya wakatoliki. Hata kama ni fidia nitatoa hela za kuwalipa ninazo ila wabomoe waondoke”, Rais Costa alisisitiza kwa hasira.


“Sawa Mheshimiwa Rais. Nitafanyia kazi maelekezo yote mkuu”. Waziri Chaurembo alijibu huku akiwa ameinamisha kichwa na kuanza kuondoka.


“Sasa mpelekee Askofu Begere salamu, mwambie aendelee kuhubiri sana kuhusu demokrasia, matumizi ya pesa za serikali na utawala bora. Mwambie akitaka aje agombee uRais kabisa. Mpuuzi!”, Rais Costa alionekana kughadhabika sana.


Chaurembo alisikiliza akatabasamu na kutoka. Katika hali ile kutia neno ni kujihakikishia kufukuzwa kazi palepale. Rais Costa alifahamika zaidi kwa tabia ya kuwa na hasira za haraka.

Alifukuza kazi watendaji asiokubaliana nao akiwa sehemu yoyote, katikati ya hotuba, kwenye mikutano ya hadhara na hata katika vikao vya kawaida tena bila kufanya uchunguzi na kujiridhisha kuwa kweli walikosea au vinginevyo. Alifanya hivyo kutafuta umaarufu na kuonesha tu mabavu yake kama Rais.

**************************************


Damian Begere, Askofu Mkuu wa jimbo kuu Katoliki Peron na mwanashirika wa shirika la Wajesuiti alikuwa kwenye sintofahamu na Rais Costa. Askofu Begere ni kiongozi mwadilifu wa kanisa katoliki Stanza alitambulika sio tu Stanza bali na Afrika nzima kwa misimamo yake isiyotetereka juu ya tawala za kidhalimu, zilizokosa kufuata misingi ya utawala bora, haki za binadamu na matumizi sahihi ya pesa za umma.


Nchini Stanza alikuwa ni mwiba kwa serikali ya Rais Costa. Ni Askofu asiyeogopa kusema mawazo au kutoa msimamo wake kuhusu masuala mbalimbali. Asiemung’unya maneno tena mwenye kupenda kusema ukweli. Alijizolea umaarufu na kuheshimika miongoni mwa wananchi wengi wa Stanza. Vyombo vya habari vilipenda kumtumia kama rejeo la masuala mbalimbali ya kitaifa na kimataifa.


Askofu Begere sio tu alikuwa na hamasa kwa wananchi wa kawaida Stanza, bali hata katika jumuiya yao ya maaskofu alikuwa na ushawishi mkubwa. Kwanza, ni kwa sababu ya umri wa utumishi katika nafasi ile, lakini pia kwasababu ya ukomavu wa mawazo yake katika masuala mtambuka ya kitaifa.

Ilikuwa ni vigumu atoe neno halafu lije kukanushwa na Askofu mwingine yeyote hata wale wasio wakatoliki. Aliheshimika sana na viongozi wa dini ya Kikristo na hata dini nyingine.


Ni katika muktadha huo, Askofu Begere alikuwa na uhasimu mkubwa na Rais Costa. Uhasimu ulichagizwa zaidi hasa kipindi Rais Costa alipoanza harakati za kutaka kubadili katiba iliyomruhusu kugombea tena Urais kwa awamu ya tatu. Lakini na sasa kukiwa na vuguvugu la tetesi za kuongeza umri wa kugombea Urais.


Isitoshe, yamekuwepo matukio kadhaa ya uvunjifu wa haki za raia na demokrasia lakini lililomgusa zaidi Askofu Begere na Jumuiya nzima ya viongozi wa dini ni kusudio la serikali kufuta kabisa Ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali. Wengi wanaamini kuwa kwa kufutwa ofisi hii, hakutokuwa na anayekagua matumizi ya fedha za umma na hivyo kutoa mwanya wa kukithiri kwa rushwa na ufisadi katika taifa la Stanza.


Rais Costa na Askofu Begere hawakuweza kupikika chungu kimoja na sasa kwa hasira Rais Costa anatumia mamlaka yake kuhujumu miradi mbalimbali ya kanisa Katoliki anayojua ina mkono na msukumo wa Askofu Begere.

************************************


Usiku wa siku ile hakuna alielala. Japo waliwekwa vyumba tofauti lakini kila mmoja alikuwa akijitahidi kuingia kwenye kichwa cha mwenzake kimawazo. Joe alikuwa akiwaza nini Habibu na Pius wanawaza kwa wakati ule na wanachukuliaje mpango aliowashirikisha .Lakini Pius nae alikuwa akiwaza na kutokuwa na hakika kama je, ni kweli Joe na mipango yake ya kumpumzisha Rais Costa ni hakika ama anapimwa?


Habibu yeye alikuwa hawazi kupumzishwa kwa Rais Costa bali hatima nzima ya nchi yao kuanza kuzalisha silaha za kinyuklia. Kila mtu kwenye chumba chake alilala akiwa anaangalia juu. Wakiwa na mawazo yale waliendelea kustaajabu uzuri wa makazi yale ya pili ya Rais Kim. Ni katikati ya mawazo hayo walijikuta kunapambazuka bila kupata lepe la usingizi. Hawakuamini.

***************************************

the Legend☆
 
The President And I(Mimi Na Rais)- SEHEMU YA NANE
Cc. Ibney hearly kuku mweus Munamuge Atikinson samson nchimbi ram kisukari moneytalk Tater Litro Madame S BssU Shunie The Book baba swalehe nipo2 kanonb boy lanugo

Rais Kim Awaaga Joe Na Ujumbe Wake. Rais Costa Akarahishwa Na Utendaji Wa Waziri Wake


“Kinyamagoha huwa nakwazika sana na tabia ya mimi kutoa maagizo kisha nianze kufuatilia utekelezaji, ikiwa umechoka niambie nikupumzishe”. Alikuwa ni Rais Costa akiongea na Gambani Kimampala Kinyamagoha, Waziri wa Sheria na masuala ya Bunge wa Stanza.


“Samahani mkuu”, Kinyamagoha alijibu kwa utaratibu.


“Suala nililokupa la kuhakikisha muswada unaandaliwa wa marekebisho ya umri wa kugombea Urais umefikia wapi”, Rais Costa aliuliza.


“Mkuu, suala hili nilikuwa nafikiria njia nzuri ya kulienenda bila kuathiri hali ya kisiasa ya nchi…”


“Kinya acha ujinga”, Rais Costa aling’aka kwa hasira na kumkatiza Kinyamagoha kabla hajamaliza kujieleza.


“Unafikiria suala hili mara tatu tatu kwanini? Hivi nchi hii nani kiongozi?’’, Rais alihoji.


“Wewe mkuu”, Kinyamagoha alijibu.


“Bungeni Spika ni chama gani, na chama gani kina wabunge wengi”? Costa alihoji.


“Chama cha Ukombozi Stanza Mh. Rais” Kinyamagoha alijibu kwa upole.


Rais Costa aliendelea kuhoji kwa ghadhabu na kuonesha ukubwa wake ndani ya taifa la Stanza.


“Nani Mwenyekiti wa hicho chama Kinya?”, Rais Costa aliuliza.


“Ni wewe muheshimiwa”, Kinyamagoha alijibu tena kwa kutetemeka. Alishahisi kuwa Rais angeweza kumvua nafasi yake wakati uleule.


“Sasa wewe unavyoniambia unalitafakari hili una maanisha nini? Hii ni ishara tosha kuwa wewe ndio hutaki. Haya toka”, Rais Costa alimfukuza Kinyamagoha atoke.


“Mh. Rais nilikuwa naomba…….”, “Nimesema toka”, Rais Costa alimkatiza Kinyamagoha kwa hasira. Kinyamagoha aliondoka.


Rais Costa alibaki kimya akiwa amevimba kwa hasira kwa dakika kadhaa.


“Mh. Rais nina wazo”, Gideon mshauri na mpambe wa karibu wa Rais alidakia. Rais Costa alimwangalia Gideon machoni kuashiria kuwa anamsikiliza anachotaka kumwambia. Gideoni alijua haswa pa kujipatia sifa mbele ya Rais Costa. Alikuwa ni kama mkoba wake, hakumwacha kila alipoelekea. Alimwamini sana.


“Kuna watu wengi wenye uwezo sana wa kukusaidia hii kazi”, Gideon alianza kumshauri Rais.


“Kama nani”, Rais Costa alihoji.


“Yule binti, Katibu tawala wa Jimbo la Kichumbi, anaitwa Ketina nadhani angeweza sana kukusaidia hapa. Kwanza ni msomi wa sheria na ni mchapakazi kwelikweli”, Gideoni alimaliza.


Rais Costa alionekana kushtuka kusikia ushauri ule hasa ukizingatia Ketina ni kimada wake na alifanya siri kubwa watu wasijue. Alianza kuhisi kuwa Gideoni ameshajua nini? Ukweli ni kuwa Gideon alikuwa akicheza na akili ya Rais Costa. Alishapenyezewa taarifa na mmoja wa vijana wa usalama wanaotumiwa na Rais Costa kuwakutanisha na Ketina na hivyo Gideon aliamua atumie nafasi hiyo kuzidi kujipendekeza kwa Rais Costa.


“Ketina bado hajakomaa. Atapata tabu kwenye kufanya lobbying ya wabunge, pia hajajua mambo mengi ya kiutawala. Ngoja akomae kwanza”, Rais costa alimjibu Gideon kiutu uzima.


“Kwani ni nani Rais? Spika wa bunge ni chama gani na chama gani kina wabunge wengi ndani ya bunge? Nani mwenyekiti wa chama hicho?” Gideoni alirudia maswali yote ambayo Rais Costa alimuhoji Kinyamagoha. Baada ya maswali hayo Rais Costa alibaki kimya.


“Sawa nipe muda”, Rais Costa alimjibu Gideon kwa ufupi.

**************************************

Mchana wa siku hiyo Rais Costa alikutana na Waziri wake wa Fedha ndugu Aidan Tamara akiwa ameambatana na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mapato na Makusanyo ya Taifa.


Aliwapa maagizo kuwa sasa waanze kukusanya kodi kwa nguvu. Wahahakikishe kila mtu anayefanya chochote kinachomwingizia kipato analipa kodi. Haijalishi ndio anaanza ama biashara imeshakua, kama anaanza alipe kodi kwanza ndio aanzishe biashara. Alitaka kodi kwa nguvu na kuwawekea lengo kubwa la makusanyo kuliko kawaida.


Katika kikao kile hakuna aliehoji, wote waliitikia na kuahidi utii na utekelezaji. Waliondoka.


Gideon alifurahi na kumwambia Rais sasa ategemee kilio kila kona ya nchi, asubirie kwa miezi michache kisha ajitokeze kukemea na kuagiza utaratibu mpya wa ukusanywaji wa kodi. Ni kwa namna hiyo atakuwa ametengeneza tatizo na kulitatua na hivyo kuzidi kupendwa na wananchi na kumwimbia nyimbo za ‘atawale milele’


Jioni, Macha aliingia akiwa ameambatana na Waziri wa Polisi na Magereza.


“Mnajua nilichowaitia right?’’ Rais Costa alikuwa amechoka na hakutaka kupoteza muda.


“Ndio Mkuu. Mimi nadhani tumpoteze kabisa huyu kijana”, Kirondori Rugara, Waziri wa Polisi na Magereza alijibu kwa pupa.


Rais Costa alikuwa akiwauliza wamefikia wapi na mpango alioagiza wa kuhakikisha kijana na kiongozi mkuu wa chama cha upinzani ndugu Julius Kibwe anadhibitiwa kwani anaonekana ataleta kelele nyingi kwenye muswada anaotaka upelekwe bungeni wa yeye kubadilisha umri wa kugombea uRais kutoka miaka 40 mpaka kuwa miaka 55.


“Tumpoteze vipi Kirondori? Acha kuwaza kama kichaa bwana”, Stanley Macha alijikuta akimkatiza kirondori kwa hasira.


Macha akiwa mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa alikuwa katika mipango ya siri na Joe. Lakini aliifanya katika weledi uliokithiri. Alichukizwa na jibu la Kirondori kuwa Julius Kibwe apotezwe. Kupotezwa ina maana auawe. Hakuwa tayari, hakutaka. Alijua fika Kirondori alijibu vile ili kujipendekeza kwa Rais na si vinginevyo.


“Mh. Rais mimi nilikuwa nawaza tofauti kwa sababu tukianza mambo ya kupotezana hapa tutawapoteza wangapi? Suala hili mbona ni dogo sana na huyu bado hajafikia kuwa tishio la kupoteza uhai wake.


Halafu nafikiri hawa jamaa wa magharibi wanatufuatilia kila hatua na wanajua kinachoendelea, kumpoteza kwa namna yoyote ile ni kukaribisha kufuatiliwa na kubughudhiwa na mataifa ya magharibi kila siku. Tusije kuishia kupunguza wahisani kabla bajeti yetu haijajitegemea kikamilifu’’, Macha alianza kuelezea kwa utofauti jinsi ya kukabiliana na Kibwe badala ya kummaliza kama ilivyoshauriwa.


‘’Ninafikiri kuwa kwasababu chama hiki hakina wabunge wengi, wabunge 100 kati ya 500 ni wachahe sana na hivyo sehemu kubwa ya mapato yao hutegemea misaada ya wahisani na hasa matajiri wawili wakubwa hapa nchini, ninapendekeza tuwabane hawa matajiri wakate pesa zao kwake.


Hatua hii itampunguza nguvu ya kuendesha chama chake na pia safari zake mikoani zitapungua. Hatua ya pili, tuongee na wamiliki wawili wa hivi vituo vya redio kuzuia mahojiano nae ama habari zake kuziandika katika hali ambayo hazitakuwa na hamasa. Hii ni njia rahisi sana ya kumpunguza nguvu”, Stanley Macha alishauri.


“Unajua ana wafuasi wangapi kwenye mitandao yake ya kijamii au unasema tu?”, Kirondori alihoji kwa haraka.


“Ulishawahi lini kuona Stanza watu wakafuatilia mambo kwa umakini huko kwenye mitandao? Kule wanapiga kelele tu yanaishia kule, Stanza mitandao ya kijamii bado haijawa tishio, wanapiga kelele tu.


Hata hivyo hao wafuasi ni wa hapa mjini hawana madhara hata kidogo. Mh. Rais hii kazi niachie mimi nitamdhibiti bila madhara kabisa. Labda Kirondori awe anamshikilia kila mara na kumpeleka mahakamani kwa kauli zake ama vikao visivyo halali, awe anashinda mahakamani Januari mpaka Disemba na kukosa muda wa kupambana na serikali. Wananchi watamsahau tu”, Macha alimalizia.


Rais Costa alionekana kukubaliana na Macha kwanza kwasababu ya uaminifu alionao kwake katika kuhakikisha usalama wake lakini pia kwa njia aliyopendekeza ambayo haitakuwa na utata hata kwa jumuiya za kimataifa. Kikao kilimalizika.

************************************

Siku ile ilikuwa ni ya msisimko mkubwa kwa Joe na wenzake. Ni siku ambayo walikuwa wanakutana na Rais Kim mwenyewe na ndipo hapo Rais Kim angesaini hati ya kukubali ama kukataa maombi yao na wao kundoka nayo kuelekea Stanza. Ilikuwa ni siku ya ama warudi Stanza kishujaa au kiunyonge. Joe alipenda la kwanza. Asingependa kabisa arudi na majibu kuwa imeshindikana.


Timu aliyoongozana nayo haikumuangusha, ilikuwa ni ya vijana Hodari kwelikweli. Katika mawazo yake wakiwa wanaelekea Upande wa mashariki mwa makazi namba 55, makazi rasmi ya Rais Kim na upande ambao ndio hasa zilipo ofisi zake, moyo wa Joe ulijawa furaha sana. Alijiona mshindi na mtu aliefikia Kilele cha mafanikio katika Nyanja ya kidiplomasia. Walifika wakaingia na Rais Kim akawapokea.


“힘들지만 좋은 토론을했다는 말을 들었습니다. 이것은 이정표이자 역사적인 이야기였습니다. 추가 할 내용이 없지만 모든 부분이 우리가 동의 한 부분에 서 있는지 확인합시다. 너무 잘 했어. En은 앞으로가는 길에 대해 계속 연락 할 것입니다”


himdeuljiman joh-eun tolon-eulhaessdaneun mal-eul deul-eossseubnida. geos-eun ijeongpyoija yeogsajeog-in iyagiyeossseubnida. chuga hal naeyong-i eobsjiman modeun bubun-i uliga dong-ui han bubun-e seo issneunji hwag-inhabsida. neomu jal haess-eo. Eneun ap-euloganeun gil-e daehae gyesog yeonlag hal geos-ibnida.


(Nimetaarifiwa kuwa mlikuwa na majadiliano magumu lakini mazuri. Majadiliano haya ni ya kihistoria na muhimu sana kwa pande zote mbili. Tunachotakiwa kuhakikisha ni kila upande kuona namna gani unakidhi matakwa ya mwenzake vyema. Hivyo niwatakieni heri na En ataendelea kuwasiliana nanyi kwa yote yanayofuata). Rais Kim alimaliza kuongea huku akimalizia kuweka sahihi kwenye nyaraka zile ziliandikwa vyema kabisa yote waliyojadiliana na kukubaliana kati ya ujumbe wa Joe na Waziri En.


“Thank you, Mr. President,” (Asante Mh. Rais), baada ya kupata tafsiri Joe alishukuru.


Ilikuwa ni hatua kubwa sana katika utumishi wa Joe. Habibu na Pius walionekana kutabasamu kwa kulifanikisha jambo lile. Kila mmoja alikuwa na mchango mkubwa katika makubaliano yale.


Joe asingekubali vifaa vya nyuklia vitengenezwe Stanza kama sio Pius kuwashirikisha nguvu ya Korea Kaskazini kijeshi na kuwahakikishia kuwa watalindwa. Habibu nae taarifa zake na umakini na uhodari wa kuhoji masuala uliwafungua macho kwa namna fulani Pius na Joe. Yeye Joe kama kiungo mchezeshaji alikuwa na kazi moja tu ya kuchuja na kuamua. Hakika walipongezana na baada ya dakika kadhaa waliagana na Rais Kim ili waondoke.


Wakiwa wanatoka jambo moja lilimshangaza Joe alivutwa nyuma na kurudishwa ndani ya ofisi alimokuwa Rais Kim na wenzake kubakia nje.


“If president Costa declines our offer, I will want you to make it happen in one way or another. Can I count on you? (Kama Rais Costa akikataa matakwa yetu nitakuhitaji wewe uyafanikishe kwa njia moja au nyingine. Naweza kukutegemea?). Rais Kim alimwambia Joe.


Joe alikosa la kujibu alipozungusha macho alikuta watu wote waliokuwa pale ofisini mwa Rais Kim wanamtazama yeye.


“Can I?” (Ninaweza kukutegemea?), Rais Kim alihoji tena. Joe hakujua ajibu nini.

*****************************************

“Kimweri, umeshapata nafasi ya kuwasiliana na kina Joe?”, Rais Costa alimuliza Kimweri balozi wa Stanza huko Beijing China.


“Hapana Mkuu lakini kutokana na ratiba watawasili leo saa kumi na moja jioni na ndege ya Air Koryo ile ile waliyoondoka nayo”. Kimweri alimjibu Rais Costa walipokuwa kwenye mazungumzo yao ya kufuatilia ujumbe wa Joe na wenzake.


Rais Costa alikuwa akimtumia Kimweri kufuatilia mazungumzo ya Joe na wenzake pindi wanapokuwa kwenye ardhi ya China. Alijua fika yapo watakayokuwa wanazungumza na japo hawezi yapata yote lakini machache yanaweza kumsaidia kuunganisha nukta na kujua kama Joe hana mpango mwingine ambao hauna maslahi mema kwake.


“Yule kijana umeshampanga hapo kiwanjani? Nataka wakati huu isishindikane”, Rais Costa alisisitiza.


“Sawa Mtukufu Rais”, Kimweri alijibu kwa kuinamisha kichwa japo yeye yupo China na Rais Costa yupo Stanza.


Kijana wa kiVietinam alishawekwa tayari kufatilia mienendo yote ya Joe na wenzake. Wakati huu wakitumia teknolojia ya MCC3G-R Voice ampliefier.


Hii ni teknolojia ya hali ya juu kabisa kutoka Vietnam ambayo mtu huweza kurekodiwa mazungumzo yake kwa anayerekodi kukaa mbali na kuweza kuelekeza kifaa hicho mahali anayerokodiwa alipo, kisha kifaa hicho huweza kuweka uzio wa mawimbi sauti katika eneo litakaloamuliwa na anaetaka kurekodi. Baada ya hapo chochote kitakachozungumzwa ndani ya uzio ule uliowekwa kitanaswa kutokea mbali na kisha sauti ile kukuzwa.


Kinachofanyika ni kuwa mtu yule anayerekodiwa akitembea ama kuhama ni shurti kifaa kile kigeuzwe ili mtu anayerekodiwa abakie ndani ya uzio. Ubora zaidi wa kifaa hiki ni kuwa hata kama mtu yupo ndani ya jengo ama yupo ndani ya uzio, bado sauti itanaswa na cha zaidi ni kuwa unaweza kuzipa sauti majina. Mfano, kama una hakika sauti hii ni ya mtu fulani basi unaipa jina na kuhifadhi ndani ya hiki kifaa.


Ikitokea siku yoyote unataka kunasa Sauti ya huyo mtu kama yupo ndani ya jengo hivyo haonekani na una hakika kama yupo basi utakachotakiwa kufanya ni kutengeneza uzio kisha kuanza kunasa sauti za watu walioko huko ndani. Kama huyo mtu yupo na akazungumza basi kifaa kile kitakupa ishara kuwa huyu anaezungumza ni mtu fulani kutokana na lile jina ulilotumia kuhifadhia.


Teknolojia hii haihitaji mtu kutuma kifaa chochote kuwasogelea wale unaotakiwa kuwarekodi unachotakiwa kujua ni wapo eneo gani tu basi na kisha kukaa umbali usiozidi mita 500 kutokea mahali walipo.


Wakati huu Rais Costa alihakikisha hawakosi kuwasikia kina Joe. Alishapanga pia kijana huyo aje Stanza kumfatilia Joe kwa miezi sita mfululizo ndipo amwamini.

************************************

“Ulirudi kuongea nini na Rais Kim Joe?”, Alikuwa ni Pius akimuuliza Joe kwa kumnong’oneza mara tu alipotoka kwenye ofisi ya Rais Kim aliporudishwa mara ya pili.


“Nitawaambia Pius”, Joe aijibu kifupi.


Walitembea kwenye korido za Ryongsong wakiongozwa na Waziri En Ki. Walitoka na kuingia kwenye magari yaliyoandaliwa kuwapeleka uwanja wa ndege.


Wakiwa ndani ya magari huku viongozi wengine wa Korea wakiwa wamesimama kwenye varanda kubwa mbele ya jengo lile maridadi walipiga ishara ya saluti kuonyesha kuwaaga wageni wao kutoka Stanza. Joe na wenzake nao walifanya hivyo na msafara ulianza safari.


Jinsi walivyokaa ni vile vile kama walivyokuja. Gari moja akiwa Waziri En na Joe, gari la pili alipanda Habibu na Pius. Magari mawili yaliyobaki la mbele na nyuma yalikuwa ni ya ulinzi na usindikizaji tu.


“Habibu, Joe alirudi kuambiwa nini?”, Pius alimuuliza Habibu.


“Sasa mimi nitajuaje Pius?” Habibu alijibu kiufupi.


“Tumekuja wote kama ujumbe mmoja kwa nini alirudishwa mwenyewe? Huoni kama kuna jambo tunafichwa hapa Habibu?” Pius alihoji tena. Alihoji huku akijikuna kidevu na kuangalia dirishani upande wake badala ya kumwangalia Habibu.


“Pius kwani ulipomuuliza Joe pale si alisema atatuambia? Sasa wewe haraka ya nini? Au umeanza kuwa na mashaka nae?” Habibu alimuuliza Pius. Pius alikaa kimya.


Msafara uliwasili uwanja wa ndege Sunan Pyongyang. Waziri En aliwaongoza kina Joe moja kwa mmoja mpaka kwenye ndege ndogo iitwayo Chammae-5. Hii ni moja ya ndege wanazotumia viongozi tu wa serikali ya Korea Kaskazini kwa safari maalumu. Ipo kwenye mnyororo wa ndege maalum za Rais Kim ikiongozwa na ile ya Chammae-1 ambayo ndio haswa ndege ya Rais Kim. Ndege hizi ni zao la ndege za kisovieti za Jetliner Ilyushin Il-62M.


Walipofika waliagana na kuingia kwenye ndege. Pius na Habibu walionekana kushangaa heshima ile kubwa waliyopewa. Walikuwa wakijua wanarudi na ile ndege waliokuja nayo na kumbe sivyo wanarudishwa na moja ya ndege maalum za Rais. Joe alikuwa mkimya na ndege iliacha ardhi.


Wakiwa angani Pius alikuwa wa kwanza kuuliza kulikoni na nini Joe aliongea na Rais baada ya kurudishwa ndani na wao kuachwa nje.


“Pius, kwanza lazima utambue mimi ni kiongozi wako katika msafara huu sawa kijana? Hivyo kuna mambo naweza ambiwa kwa msisitizo mimi kama kiongozi.


Kimsingi Rais Kim alitaka kunishukuru tena kwa niaba yenu kwa mazungumzo mazuri tuliyoyafanya. Amewapongeza ninyi na kusema ni hazina ya taifa la Stanza na hivyo amenishauri kuhakikisha Rais Costa anawathamini.


Pius, umeonyesha uwezo mkubwa sana wa masuala ya usalama na ameshangaa kuwa tuna vijana maridadi namna hii. Habibu, Waziri En mwenyewe amekiri kuwa una uelewa mpana na alinitania kuniambia kwanini kijana kama wewe usiwe Katibu mkuu wa Umoja wa Taifa badala ya wale waliokaa pale kuitumikia Marekani. Wamefurahi sana”.


Joe alimaliza kuwataarifu na kumfanya Habibu atabasamu na kujisikia vizuri sana. Kwa upande wa Pius alitabasamu kinafiki. Kwa taaluma yake ya usalama alisoma uso wa Joe kwa umakini na alitambua kuna maneno yamefichwa ambayo alitambua wazi Joe hatataka kumwambia. Alikwazika sana.


“Ndege hii itatua uwanja ule wa Kimataifa wa Beiijing tuliopandia wakati tunakuja ama uwanja tofauti?” Pius alihoji.


“Uwanja tofauti. Sasa hivi tutatua uwanja mdogo wa Shenyang kisha Korea wametuandalia usafiri kutupeleka kwenye ubalozi wetu”, Joe alijibu. Jibu hili lilizidi kumwacha Pius mwenye maswali.


Pius kwa taaluma yake ya usalama na intelijensia alikwiva kwelikweli. Alijua kusoma mwisho kutokea mwanzo, ilikuwa ni vigumu sana kumkwepa hasa akitaka kujua jambo na alijua kuunganisha nukta kwelikweli. Labda hiyo ndiyo sifa iliyomfanya aaminiwe na kupewa nafasi kubwa kabisa jeshini kama ile ya Unadhimu na Mkuu wa Kitengo cha Intelijensia cha Jeshi la watu wa Stanza.


“Kwa hiyo vipi kuhusu balozi Kimweri ana taarifa? Maana atakuwa na yeye ameandaa utaratibu wa kutupokea kule uwaja mwingine”, Pius alihoji.


“Tukifika tutamtaarifu” Joe alijibu kiufupi.


“Joe mbali ya shauku ya kutaka kufika na kumtumia Macha yale maneno ya siri, sasa tuambie nani mwingine anahusika na mipango hii itatekelezwaje. Yaani nataka nipate picha kamili”, Habibu alidakia mazungumzo.


“Haya sasa nitawaambia mpango mzima na niseme tu baada ya kuongea hapa tutapofika China hatutazungumza lolote mpaka tutakapofika Stanza. Na hata tukifika kule tutakuwa tukiendelea na utekelezaji na mazungumzo mengine tukiwa wote yaani mimi na ninyi Macha na huyu nitakaewatajia hapa tutayafanya kwa maelekezo maalum.


Nirudie, ninaamini hapa ni Sehemu salama maana tunatakiwa tuwe waangalifu kwa sababu najua tunafatiliwa.” Joe aliwaweka sawa kwanza.


Habibu na Pius walikaa kwa shauku kusubiri ni nini wangeambiwa kuhusu mpango ule mahsusi.

************************

the Legend☆
 
The President And I(Mimi Na Rais)- SEHEMU YA NANE
Cc. Ibney hearly kuku mweus Munamuge Atikinson samson nchimbi ram kisukari moneytalk Tater Litro Madame S BssU Shunie The Book baba swalehe nipo2 kanonb boy lanugo

Rais Kim Awaaga Joe Na Ujumbe Wake. Rais Costa Akarahishwa Na Utendaji Wa Waziri Wake


“Kinyamagoha huwa nakwazika sana na tabia ya mimi kutoa maagizo kisha nianze kufuatilia utekelezaji, ikiwa umechoka niambie nikupumzishe”. Alikuwa ni Rais Costa akiongea na Gambani Kimampala Kinyamagoha, Waziri wa Sheria na masuala ya Bunge wa Stanza.


“Samahani mkuu”, Kinyamagoha alijibu kwa utaratibu.


“Suala nililokupa la kuhakikisha muswada unaandaliwa wa marekebisho ya umri wa kugombea Urais umefikia wapi”, Rais Costa aliuliza.


“Mkuu, suala hili nilikuwa nafikiria njia nzuri ya kulienenda bila kuathiri hali ya kisiasa ya nchi…”


“Kinya acha ujinga”, Rais Costa aling’aka kwa hasira na kumkatiza Kinyamagoha kabla hajamaliza kujieleza.


“Unafikiria suala hili mara tatu tatu kwanini? Hivi nchi hii nani kiongozi?’’, Rais alihoji.


“Wewe mkuu”, Kinyamagoha alijibu.


“Bungeni Spika ni chama gani, na chama gani kina wabunge wengi”? Costa alihoji.


“Chama cha Ukombozi Stanza Mh. Rais” Kinyamagoha alijibu kwa upole.


Rais Costa aliendelea kuhoji kwa ghadhabu na kuonesha ukubwa wake ndani ya taifa la Stanza.


“Nani Mwenyekiti wa hicho chama Kinya?”, Rais Costa aliuliza.


“Ni wewe muheshimiwa”, Kinyamagoha alijibu tena kwa kutetemeka. Alishahisi kuwa Rais angeweza kumvua nafasi yake wakati uleule.


“Sasa wewe unavyoniambia unalitafakari hili una maanisha nini? Hii ni ishara tosha kuwa wewe ndio hutaki. Haya toka”, Rais Costa alimfukuza Kinyamagoha atoke.


“Mh. Rais nilikuwa naomba…….”, “Nimesema toka”, Rais Costa alimkatiza Kinyamagoha kwa hasira. Kinyamagoha aliondoka.


Rais Costa alibaki kimya akiwa amevimba kwa hasira kwa dakika kadhaa.


“Mh. Rais nina wazo”, Gideon mshauri na mpambe wa karibu wa Rais alidakia. Rais Costa alimwangalia Gideon machoni kuashiria kuwa anamsikiliza anachotaka kumwambia. Gideoni alijua haswa pa kujipatia sifa mbele ya Rais Costa. Alikuwa ni kama mkoba wake, hakumwacha kila alipoelekea. Alimwamini sana.


“Kuna watu wengi wenye uwezo sana wa kukusaidia hii kazi”, Gideon alianza kumshauri Rais.


“Kama nani”, Rais Costa alihoji.


“Yule binti, Katibu tawala wa Jimbo la Kichumbi, anaitwa Ketina nadhani angeweza sana kukusaidia hapa. Kwanza ni msomi wa sheria na ni mchapakazi kwelikweli”, Gideoni alimaliza.


Rais Costa alionekana kushtuka kusikia ushauri ule hasa ukizingatia Ketina ni kimada wake na alifanya siri kubwa watu wasijue. Alianza kuhisi kuwa Gideoni ameshajua nini? Ukweli ni kuwa Gideon alikuwa akicheza na akili ya Rais Costa. Alishapenyezewa taarifa na mmoja wa vijana wa usalama wanaotumiwa na Rais Costa kuwakutanisha na Ketina na hivyo Gideon aliamua atumie nafasi hiyo kuzidi kujipendekeza kwa Rais Costa.


“Ketina bado hajakomaa. Atapata tabu kwenye kufanya lobbying ya wabunge, pia hajajua mambo mengi ya kiutawala. Ngoja akomae kwanza”, Rais costa alimjibu Gideon kiutu uzima.


“Kwani ni nani Rais? Spika wa bunge ni chama gani na chama gani kina wabunge wengi ndani ya bunge? Nani mwenyekiti wa chama hicho?” Gideoni alirudia maswali yote ambayo Rais Costa alimuhoji Kinyamagoha. Baada ya maswali hayo Rais Costa alibaki kimya.


“Sawa nipe muda”, Rais Costa alimjibu Gideon kwa ufupi.

**************************************

Mchana wa siku hiyo Rais Costa alikutana na Waziri wake wa Fedha ndugu Aidan Tamara akiwa ameambatana na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mapato na Makusanyo ya Taifa.


Aliwapa maagizo kuwa sasa waanze kukusanya kodi kwa nguvu. Wahahakikishe kila mtu anayefanya chochote kinachomwingizia kipato analipa kodi. Haijalishi ndio anaanza ama biashara imeshakua, kama anaanza alipe kodi kwanza ndio aanzishe biashara. Alitaka kodi kwa nguvu na kuwawekea lengo kubwa la makusanyo kuliko kawaida.


Katika kikao kile hakuna aliehoji, wote waliitikia na kuahidi utii na utekelezaji. Waliondoka.


Gideon alifurahi na kumwambia Rais sasa ategemee kilio kila kona ya nchi, asubirie kwa miezi michache kisha ajitokeze kukemea na kuagiza utaratibu mpya wa ukusanywaji wa kodi. Ni kwa namna hiyo atakuwa ametengeneza tatizo na kulitatua na hivyo kuzidi kupendwa na wananchi na kumwimbia nyimbo za ‘atawale milele’


Jioni, Macha aliingia akiwa ameambatana na Waziri wa Polisi na Magereza.


“Mnajua nilichowaitia right?’’ Rais Costa alikuwa amechoka na hakutaka kupoteza muda.


“Ndio Mkuu. Mimi nadhani tumpoteze kabisa huyu kijana”, Kirondori Rugara, Waziri wa Polisi na Magereza alijibu kwa pupa.


Rais Costa alikuwa akiwauliza wamefikia wapi na mpango alioagiza wa kuhakikisha kijana na kiongozi mkuu wa chama cha upinzani ndugu Julius Kibwe anadhibitiwa kwani anaonekana ataleta kelele nyingi kwenye muswada anaotaka upelekwe bungeni wa yeye kubadilisha umri wa kugombea uRais kutoka miaka 40 mpaka kuwa miaka 55.


“Tumpoteze vipi Kirondori? Acha kuwaza kama kichaa bwana”, Stanley Macha alijikuta akimkatiza kirondori kwa hasira.


Macha akiwa mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa alikuwa katika mipango ya siri na Joe. Lakini aliifanya katika weledi uliokithiri. Alichukizwa na jibu la Kirondori kuwa Julius Kibwe apotezwe. Kupotezwa ina maana auawe. Hakuwa tayari, hakutaka. Alijua fika Kirondori alijibu vile ili kujipendekeza kwa Rais na si vinginevyo.


“Mh. Rais mimi nilikuwa nawaza tofauti kwa sababu tukianza mambo ya kupotezana hapa tutawapoteza wangapi? Suala hili mbona ni dogo sana na huyu bado hajafikia kuwa tishio la kupoteza uhai wake.


Halafu nafikiri hawa jamaa wa magharibi wanatufuatilia kila hatua na wanajua kinachoendelea, kumpoteza kwa namna yoyote ile ni kukaribisha kufuatiliwa na kubughudhiwa na mataifa ya magharibi kila siku. Tusije kuishia kupunguza wahisani kabla bajeti yetu haijajitegemea kikamilifu’’, Macha alianza kuelezea kwa utofauti jinsi ya kukabiliana na Kibwe badala ya kummaliza kama ilivyoshauriwa.


‘’Ninafikiri kuwa kwasababu chama hiki hakina wabunge wengi, wabunge 100 kati ya 500 ni wachahe sana na hivyo sehemu kubwa ya mapato yao hutegemea misaada ya wahisani na hasa matajiri wawili wakubwa hapa nchini, ninapendekeza tuwabane hawa matajiri wakate pesa zao kwake.


Hatua hii itampunguza nguvu ya kuendesha chama chake na pia safari zake mikoani zitapungua. Hatua ya pili, tuongee na wamiliki wawili wa hivi vituo vya redio kuzuia mahojiano nae ama habari zake kuziandika katika hali ambayo hazitakuwa na hamasa. Hii ni njia rahisi sana ya kumpunguza nguvu”, Stanley Macha alishauri.


“Unajua ana wafuasi wangapi kwenye mitandao yake ya kijamii au unasema tu?”, Kirondori alihoji kwa haraka.


“Ulishawahi lini kuona Stanza watu wakafuatilia mambo kwa umakini huko kwenye mitandao? Kule wanapiga kelele tu yanaishia kule, Stanza mitandao ya kijamii bado haijawa tishio, wanapiga kelele tu.


Hata hivyo hao wafuasi ni wa hapa mjini hawana madhara hata kidogo. Mh. Rais hii kazi niachie mimi nitamdhibiti bila madhara kabisa. Labda Kirondori awe anamshikilia kila mara na kumpeleka mahakamani kwa kauli zake ama vikao visivyo halali, awe anashinda mahakamani Januari mpaka Disemba na kukosa muda wa kupambana na serikali. Wananchi watamsahau tu”, Macha alimalizia.


Rais Costa alionekana kukubaliana na Macha kwanza kwasababu ya uaminifu alionao kwake katika kuhakikisha usalama wake lakini pia kwa njia aliyopendekeza ambayo haitakuwa na utata hata kwa jumuiya za kimataifa. Kikao kilimalizika.

************************************

Siku ile ilikuwa ni ya msisimko mkubwa kwa Joe na wenzake. Ni siku ambayo walikuwa wanakutana na Rais Kim mwenyewe na ndipo hapo Rais Kim angesaini hati ya kukubali ama kukataa maombi yao na wao kundoka nayo kuelekea Stanza. Ilikuwa ni siku ya ama warudi Stanza kishujaa au kiunyonge. Joe alipenda la kwanza. Asingependa kabisa arudi na majibu kuwa imeshindikana.


Timu aliyoongozana nayo haikumuangusha, ilikuwa ni ya vijana Hodari kwelikweli. Katika mawazo yake wakiwa wanaelekea Upande wa mashariki mwa makazi namba 55, makazi rasmi ya Rais Kim na upande ambao ndio hasa zilipo ofisi zake, moyo wa Joe ulijawa furaha sana. Alijiona mshindi na mtu aliefikia Kilele cha mafanikio katika Nyanja ya kidiplomasia. Walifika wakaingia na Rais Kim akawapokea.


“힘들지만 좋은 토론을했다는 말을 들었습니다. 이것은 이정표이자 역사적인 이야기였습니다. 추가 할 내용이 없지만 모든 부분이 우리가 동의 한 부분에 서 있는지 확인합시다. 너무 잘 했어. En은 앞으로가는 길에 대해 계속 연락 할 것입니다”


himdeuljiman joh-eun tolon-eulhaessdaneun mal-eul deul-eossseubnida. geos-eun ijeongpyoija yeogsajeog-in iyagiyeossseubnida. chuga hal naeyong-i eobsjiman modeun bubun-i uliga dong-ui han bubun-e seo issneunji hwag-inhabsida. neomu jal haess-eo. Eneun ap-euloganeun gil-e daehae gyesog yeonlag hal geos-ibnida.


(Nimetaarifiwa kuwa mlikuwa na majadiliano magumu lakini mazuri. Majadiliano haya ni ya kihistoria na muhimu sana kwa pande zote mbili. Tunachotakiwa kuhakikisha ni kila upande kuona namna gani unakidhi matakwa ya mwenzake vyema. Hivyo niwatakieni heri na En ataendelea kuwasiliana nanyi kwa yote yanayofuata). Rais Kim alimaliza kuongea huku akimalizia kuweka sahihi kwenye nyaraka zile ziliandikwa vyema kabisa yote waliyojadiliana na kukubaliana kati ya ujumbe wa Joe na Waziri En.


“Thank you, Mr. President,” (Asante Mh. Rais), baada ya kupata tafsiri Joe alishukuru.


Ilikuwa ni hatua kubwa sana katika utumishi wa Joe. Habibu na Pius walionekana kutabasamu kwa kulifanikisha jambo lile. Kila mmoja alikuwa na mchango mkubwa katika makubaliano yale.


Joe asingekubali vifaa vya nyuklia vitengenezwe Stanza kama sio Pius kuwashirikisha nguvu ya Korea Kaskazini kijeshi na kuwahakikishia kuwa watalindwa. Habibu nae taarifa zake na umakini na uhodari wa kuhoji masuala uliwafungua macho kwa namna fulani Pius na Joe. Yeye Joe kama kiungo mchezeshaji alikuwa na kazi moja tu ya kuchuja na kuamua. Hakika walipongezana na baada ya dakika kadhaa waliagana na Rais Kim ili waondoke.


Wakiwa wanatoka jambo moja lilimshangaza Joe alivutwa nyuma na kurudishwa ndani ya ofisi alimokuwa Rais Kim na wenzake kubakia nje.


“If president Costa declines our offer, I will want you to make it happen in one way or another. Can I count on you? (Kama Rais Costa akikataa matakwa yetu nitakuhitaji wewe uyafanikishe kwa njia moja au nyingine. Naweza kukutegemea?). Rais Kim alimwambia Joe.


Joe alikosa la kujibu alipozungusha macho alikuta watu wote waliokuwa pale ofisini mwa Rais Kim wanamtazama yeye.


“Can I?” (Ninaweza kukutegemea?), Rais Kim alihoji tena. Joe hakujua ajibu nini.

*****************************************

“Kimweri, umeshapata nafasi ya kuwasiliana na kina Joe?”, Rais Costa alimuliza Kimweri balozi wa Stanza huko Beijing China.


“Hapana Mkuu lakini kutokana na ratiba watawasili leo saa kumi na moja jioni na ndege ya Air Koryo ile ile waliyoondoka nayo”. Kimweri alimjibu Rais Costa walipokuwa kwenye mazungumzo yao ya kufuatilia ujumbe wa Joe na wenzake.


Rais Costa alikuwa akimtumia Kimweri kufuatilia mazungumzo ya Joe na wenzake pindi wanapokuwa kwenye ardhi ya China. Alijua fika yapo watakayokuwa wanazungumza na japo hawezi yapata yote lakini machache yanaweza kumsaidia kuunganisha nukta na kujua kama Joe hana mpango mwingine ambao hauna maslahi mema kwake.


“Yule kijana umeshampanga hapo kiwanjani? Nataka wakati huu isishindikane”, Rais Costa alisisitiza.


“Sawa Mtukufu Rais”, Kimweri alijibu kwa kuinamisha kichwa japo yeye yupo China na Rais Costa yupo Stanza.


Kijana wa kiVietinam alishawekwa tayari kufatilia mienendo yote ya Joe na wenzake. Wakati huu wakitumia teknolojia ya MCC3G-R Voice ampliefier.


Hii ni teknolojia ya hali ya juu kabisa kutoka Vietnam ambayo mtu huweza kurekodiwa mazungumzo yake kwa anayerekodi kukaa mbali na kuweza kuelekeza kifaa hicho mahali anayerokodiwa alipo, kisha kifaa hicho huweza kuweka uzio wa mawimbi sauti katika eneo litakaloamuliwa na anaetaka kurekodi. Baada ya hapo chochote kitakachozungumzwa ndani ya uzio ule uliowekwa kitanaswa kutokea mbali na kisha sauti ile kukuzwa.


Kinachofanyika ni kuwa mtu yule anayerekodiwa akitembea ama kuhama ni shurti kifaa kile kigeuzwe ili mtu anayerekodiwa abakie ndani ya uzio. Ubora zaidi wa kifaa hiki ni kuwa hata kama mtu yupo ndani ya jengo ama yupo ndani ya uzio, bado sauti itanaswa na cha zaidi ni kuwa unaweza kuzipa sauti majina. Mfano, kama una hakika sauti hii ni ya mtu fulani basi unaipa jina na kuhifadhi ndani ya hiki kifaa.


Ikitokea siku yoyote unataka kunasa Sauti ya huyo mtu kama yupo ndani ya jengo hivyo haonekani na una hakika kama yupo basi utakachotakiwa kufanya ni kutengeneza uzio kisha kuanza kunasa sauti za watu walioko huko ndani. Kama huyo mtu yupo na akazungumza basi kifaa kile kitakupa ishara kuwa huyu anaezungumza ni mtu fulani kutokana na lile jina ulilotumia kuhifadhia.


Teknolojia hii haihitaji mtu kutuma kifaa chochote kuwasogelea wale unaotakiwa kuwarekodi unachotakiwa kujua ni wapo eneo gani tu basi na kisha kukaa umbali usiozidi mita 500 kutokea mahali walipo.


Wakati huu Rais Costa alihakikisha hawakosi kuwasikia kina Joe. Alishapanga pia kijana huyo aje Stanza kumfatilia Joe kwa miezi sita mfululizo ndipo amwamini.

************************************

“Ulirudi kuongea nini na Rais Kim Joe?”, Alikuwa ni Pius akimuuliza Joe kwa kumnong’oneza mara tu alipotoka kwenye ofisi ya Rais Kim aliporudishwa mara ya pili.


“Nitawaambia Pius”, Joe aijibu kifupi.


Walitembea kwenye korido za Ryongsong wakiongozwa na Waziri En Ki. Walitoka na kuingia kwenye magari yaliyoandaliwa kuwapeleka uwanja wa ndege.


Wakiwa ndani ya magari huku viongozi wengine wa Korea wakiwa wamesimama kwenye varanda kubwa mbele ya jengo lile maridadi walipiga ishara ya saluti kuonyesha kuwaaga wageni wao kutoka Stanza. Joe na wenzake nao walifanya hivyo na msafara ulianza safari.


Jinsi walivyokaa ni vile vile kama walivyokuja. Gari moja akiwa Waziri En na Joe, gari la pili alipanda Habibu na Pius. Magari mawili yaliyobaki la mbele na nyuma yalikuwa ni ya ulinzi na usindikizaji tu.


“Habibu, Joe alirudi kuambiwa nini?”, Pius alimuuliza Habibu.


“Sasa mimi nitajuaje Pius?” Habibu alijibu kiufupi.


“Tumekuja wote kama ujumbe mmoja kwa nini alirudishwa mwenyewe? Huoni kama kuna jambo tunafichwa hapa Habibu?” Pius alihoji tena. Alihoji huku akijikuna kidevu na kuangalia dirishani upande wake badala ya kumwangalia Habibu.


“Pius kwani ulipomuuliza Joe pale si alisema atatuambia? Sasa wewe haraka ya nini? Au umeanza kuwa na mashaka nae?” Habibu alimuuliza Pius. Pius alikaa kimya.


Msafara uliwasili uwanja wa ndege Sunan Pyongyang. Waziri En aliwaongoza kina Joe moja kwa mmoja mpaka kwenye ndege ndogo iitwayo Chammae-5. Hii ni moja ya ndege wanazotumia viongozi tu wa serikali ya Korea Kaskazini kwa safari maalumu. Ipo kwenye mnyororo wa ndege maalum za Rais Kim ikiongozwa na ile ya Chammae-1 ambayo ndio haswa ndege ya Rais Kim. Ndege hizi ni zao la ndege za kisovieti za Jetliner Ilyushin Il-62M.


Walipofika waliagana na kuingia kwenye ndege. Pius na Habibu walionekana kushangaa heshima ile kubwa waliyopewa. Walikuwa wakijua wanarudi na ile ndege waliokuja nayo na kumbe sivyo wanarudishwa na moja ya ndege maalum za Rais. Joe alikuwa mkimya na ndege iliacha ardhi.


Wakiwa angani Pius alikuwa wa kwanza kuuliza kulikoni na nini Joe aliongea na Rais baada ya kurudishwa ndani na wao kuachwa nje.


“Pius, kwanza lazima utambue mimi ni kiongozi wako katika msafara huu sawa kijana? Hivyo kuna mambo naweza ambiwa kwa msisitizo mimi kama kiongozi.


Kimsingi Rais Kim alitaka kunishukuru tena kwa niaba yenu kwa mazungumzo mazuri tuliyoyafanya. Amewapongeza ninyi na kusema ni hazina ya taifa la Stanza na hivyo amenishauri kuhakikisha Rais Costa anawathamini.


Pius, umeonyesha uwezo mkubwa sana wa masuala ya usalama na ameshangaa kuwa tuna vijana maridadi namna hii. Habibu, Waziri En mwenyewe amekiri kuwa una uelewa mpana na alinitania kuniambia kwanini kijana kama wewe usiwe Katibu mkuu wa Umoja wa Taifa badala ya wale waliokaa pale kuitumikia Marekani. Wamefurahi sana”.


Joe alimaliza kuwataarifu na kumfanya Habibu atabasamu na kujisikia vizuri sana. Kwa upande wa Pius alitabasamu kinafiki. Kwa taaluma yake ya usalama alisoma uso wa Joe kwa umakini na alitambua kuna maneno yamefichwa ambayo alitambua wazi Joe hatataka kumwambia. Alikwazika sana.


“Ndege hii itatua uwanja ule wa Kimataifa wa Beiijing tuliopandia wakati tunakuja ama uwanja tofauti?” Pius alihoji.


“Uwanja tofauti. Sasa hivi tutatua uwanja mdogo wa Shenyang kisha Korea wametuandalia usafiri kutupeleka kwenye ubalozi wetu”, Joe alijibu. Jibu hili lilizidi kumwacha Pius mwenye maswali.


Pius kwa taaluma yake ya usalama na intelijensia alikwiva kwelikweli. Alijua kusoma mwisho kutokea mwanzo, ilikuwa ni vigumu sana kumkwepa hasa akitaka kujua jambo na alijua kuunganisha nukta kwelikweli. Labda hiyo ndiyo sifa iliyomfanya aaminiwe na kupewa nafasi kubwa kabisa jeshini kama ile ya Unadhimu na Mkuu wa Kitengo cha Intelijensia cha Jeshi la watu wa Stanza.


“Kwa hiyo vipi kuhusu balozi Kimweri ana taarifa? Maana atakuwa na yeye ameandaa utaratibu wa kutupokea kule uwaja mwingine”, Pius alihoji.


“Tukifika tutamtaarifu” Joe alijibu kiufupi.


“Joe mbali ya shauku ya kutaka kufika na kumtumia Macha yale maneno ya siri, sasa tuambie nani mwingine anahusika na mipango hii itatekelezwaje. Yaani nataka nipate picha kamili”, Habibu alidakia mazungumzo.


“Haya sasa nitawaambia mpango mzima na niseme tu baada ya kuongea hapa tutapofika China hatutazungumza lolote mpaka tutakapofika Stanza. Na hata tukifika kule tutakuwa tukiendelea na utekelezaji na mazungumzo mengine tukiwa wote yaani mimi na ninyi Macha na huyu nitakaewatajia hapa tutayafanya kwa maelekezo maalum.


Nirudie, ninaamini hapa ni Sehemu salama maana tunatakiwa tuwe waangalifu kwa sababu najua tunafatiliwa.” Joe aliwaweka sawa kwanza.


Habibu na Pius walikaa kwa shauku kusubiri ni nini wangeambiwa kuhusu mpango ule mahsusi.

************************

the Legend☆
Rais costa anafanana na mwafulani halafu huyu Pius huyu atawageuka wenzie
 
Back
Top Bottom