The Boldly
JF-Expert Member
- May 21, 2017
- 2,377
- 5,147
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA TANO
Joe Awasili Pyongyang. Siri Nzito Yawashtua Habibu Na Pius.
“선량한 동지들” seonlyanghan dongjideul (Habari za asubuhi kamaradi). Ndugu En Ki, waziri anayehusika na masuala ya kigeni wa Korea Kaskazini aliwasalimia kiKorea Joe na ujumbe wake mara tu baada ya kuwapokea uwanja wa ndege wa Pyongyang.
“좋은 아침” joh-eun achim(Salama) Joe nae alijibu kiKorea huku akiwa ameshikana mkono na ndugu En wakiwa wameinamishiana vichwa. “평양에 오신 것을 환영합니다. pyeong-yang-e osin geos-eul hwan-yeonghabnida, (Karibuni Pyongyang), Waziri En aliendelea.
“고마워. 우리의 즐거움 동지 야”gomawo. uliui jeulgeoum dongji ya. (Asante sana. Ni furaha yetu kubwa sana kuwa hapa), Joe nae alijibu huku akitabasamu.
Joe akiwa mwanadiplomasia mbobevu alielewa itifaki za mataifa mengi. Alikuwa ni mtu makini ambaye ukikutana nae unajua kabisa kuwa ameiva kwelikweli katika masuala ya mahusiano ya kimataifa, diplomasia na hata lugha za kigeni.
Ndugu En aliwaongoza Joe na ujumbe wake mpaka kwenye magari yaliyoandaliwa kwa ajili ya msafara kuelekea Ikulu ya Pyongyang. Kutokea uwanja wa ndege wa kimataifa wa Pyongyang Sunan jijini Pyongyang mpaka makazi ya Rais Kim ni mwendo wa kama dakika 40 hivi kwa gari, hivyo msafara ulianza kwa kuifuataHeeecheon Expressway.
Yalikuwa jumla ya magari manne, la mbele likiwa linaongoza msafara, la pili alipanda Waziri En na Joe, la tatu alipanda Habibu na Pius na la nne likiwa ni la ulinzi. Wakiwa njiani, Joe alikuwa akiongea mawili matatu na En. En alikuwa ni mjuzi wa lugha nne ukiacha ya kiKorea.
Alizungumza kwa ufasaha kiingereza, kichina, kirusi na kifilipino. Alikuwa ni mtu mwenye uelewa mkubwa sana wa masuala ya kimataifa na mwenye akili nyingi sana. Aliaminiwa na Rais Kim Jon Un wa Korea Kaskazini tangu alipoingia madarakani kurithi mikoba ya baba yake alipofariki.
“Comrade Kim has high expectations of your visit”, (Rais Kim ana matarajio makubwa na ujio wenu huu). En alimwambia Joe huku akitabasamu kwa shauku. “Same to President Costa”, (Hata Rais Costa), Joe nae alijibu kwa ufupi. Joe alijua mbinu za mazungumzo, alijua wapi pa kuongea sana na wapi pa kuongea kwa uchache, alijua lipi la kujibu na lipi la kukaa kimya. Tangu anawasili Pyongyang kila jambo analofanya alitumia umakini mkubwa.
Safari iliendelea huku Joe akishangaa na kustaajabu namna barabara ilivyokuwa tupu na nyeupe. Hakuona hata mtu mmoja tokea walipouacha uwanja wa ndege. Alikuwa akistaajabu na alipouliza kwa En alijibiwa hivyo ndivyo wanavyowaheshimu wageni muhimu kwa taifa. Joe hakuelewa.
**************************************
Ryongsong ndilo jina la makazi ya Rais Kim. Wengine hupenda kuyaita Residence No. 55 auCentral Luxury Mansionkutokana na umaridadi wake. Ni makazi yanayosemekana kulindwa na kuwa salama kuliko makazi yoyote duniani. Ukubwa wa eneo yaliyopo makazi haya ni kilometa za mraba 12 pakiwa na kila aina ya kitu kinachohitajika kwa kiongozi mkuu wa nchi.
Wataalamu wa masuala ya ulinzi na ujasusi wanaamini kuwa askari kati ya 95,000 – 120,000 wapo maalumu kwa ajili ya kulinda eneo hili pamoja na usalama wa Rais Kim na maeneo mengine yote yalipo makazi ya familia ya Rais Kim. Wakiwa chini ya kikosi namba 963wakiongozwa na Jenerali Yun Jong-Rin, wanakifanya kikosi hiki kuwa moja ya vikosi vikubwa kabisa vya ulinzi wa Rais duniani.
Ryongsong imezungukwa na machimbo yaliyotegwa kulipuka kama kuna mvamizi yeyote atataka kusogelea makazi haya kwa njia ya ardhi, lakini pia kuna wigo mkubwa wa umeme pamoja na vituo vingi vya ukaguzi kwenye njia ya kuingilia na kuzunguka makazi haya. Makazi haya pia yamezungukwa na vituo vya kijeshi vyenye makombora makubwa ya maangamizi na ya masafa marefu na mitambo ya kunasa chochote kinachoikaribia eneo lile bila taarifa na kuweza kutuma kombora kukisambaratisha.
Hakuna ndege wala kifaa chochote kinachoruhusiwa kupita juu ya anga lililopo jengo hili la sivyo kitatunguliwa hapohapo. Ndani ya makazi haya, chini ya ardhi kuna Sehemu salama ya kumficha Rais ikiwa itaonekana yupo hatarini. Eneo hilo limejengwa kwa kuta za chuma kizito na zege zito lililofunikwa na madini ya leadili kuzuia nyumba hiyo kuathirika hata kwa shambulio la nyuklia.
Lead ni moja ya madini yenye myeyuko hafifu (Low melting point), hivyo huhitajika joto la kuanzia nyuzi joto 327 ili yaweze kuyeyuka. Ni katika Sehemu hiyo Rais Kim huweza kuishi huko kwa usalama bila chochote kutoka kwa maadui kuweza kumvamia ama kumdhuru kwa miaka zaidi ya mitatu mfululizo bila kutoka, huku akiweza kutoa maelekezo ya kivita na kiutawala.
Makazi haya pia yameunganishwa na makazi mengine ya Rais ya Changgyongau huitwa Residence No.26. Makazi haya yote yamewekewa mfumo utakaoruhusu kutumia njia iliyopo chini ya ardhi ikitokea kuna uvamizi. Pia chini ya ardhi kutokea kwenye nyumba hii kuna reli maalumu kwa ajili ya Rais tu na kitu cha kustaajabisha kwa wachambuzi wengi wa masuala ya kiusalama ya peninsula ya Korea ni kuwa reli hii ilitengenezwa kuelekea mahali kusikojulikana.
Inadhaniwa kuwa mwisho wa reli hii hubadilikabadilika kulingana na mahitaji ya wakati husika lakini lengo kuu likiwa kuhakikisha kuwa Rais na familia yake wanakuwa salama likitoea shambulio. Mbali na mambo mengine mengi ya kiulinzi na kiusalama, nyumba hii imepambwa sana kwa nakshi, taa na samani nzuri. Nje kukiwa na bustani nzuri na za maua zenye kuvutia, mito na maziwa ya bandia yaliyotengenezwa kupendezesha eneo hili. Hakika makazi haya yalivutia.
Joe, Habibu na Pius walikuwa wanakuja kuingia hapa kwa mara ya kwanza.
*******************************************
“Wananchi wenzangu mlinichangua ili nilete maendeleo na maendeleo ndiyo haya. Nimesema na nimemwagiza Waziri wa Kilimo na Chakula hapa kuwa Sitaki kusikia mkulima yeyote anakatwa tozo eti ya kusafirisha mazao. Mtu hata kuuza hajauza unamkata tozo kivipi? Vibali vya kusafirisha mazao vitolewe bure kama mtu amelima mazao yake kihalali anayatoa shamba anayapeleka mjini ama mkoa fulani kuuza unamwambia alipe, sasa alipe na nini wakati hata kuuza hajauza? Tena sitataka kusikia ukiritimba katika kutolewa vibali hivi.
Waziri upo hapa unanisikia na viongozi wengine wote hili nalifuta kuanzia leo”, Rais Costa alikuwa akiongea huku akishangiliwa kwa nguvu na wananchi wa Kisasampara, Jimbo la Kengwe alipokwenda kuzindua ghala kubwa za chakula za hifadhi ya Taifa.
“Tumeanza mazungumzo na serikali ya China na tutaingia nao ubia kutujengea soko kubwa la kimataifa la matunda. Soko letu likikamilika litakuwa la kwanza kwa ukubwa bara la Afrika, hivyo vijana anzeni kujikita kuzalisha matunda. Neema inakuja!” Rais Costa aliendelea huku umati mkubwa wa watu ukimshangilia. Alikuwa ameanza utekelezaji wa ushauri aliowahi kupewa na Joe siku za nyuma namna ya kujadiliana na Rais wa China juu ya kuingiza vijana wa kichina zaidi ya laki moja kuja nchini Stanza kufanya biashara ndogondogo.
Rais Sylvester Costa alimaliza kuhutubia na kushuka jukwaani na kusalimiana na wananchi wawili watatu kisha kuanza kutembea kuelekea kwenye zile ghala kuzikagua. Alikuwa amefuatana na mawaziri, viongozi wengine wa serikali kuu na ya Jimbo pia alikuwepo na bi. Eliza, mke wa Joseph ambae kwa wakati huo ni Mkurugenzi wa Benki ya Kilimo ya Stanza. Aliingia akayakagua na kuridhika kisha msafara uliondoka kuelekea kwenye nyumba ya mapumziko ya viongozi wa kiserikali kwa ajili ya mapumziko iliyopo pale Kengwe.
Wakiwa kwenye nyumba ya mapumziko Rais alipata chakula pamoja na Waziri wa Kilimo na Chakula, Waziri wa Fedha ambaye ndiye alikuwa Waziri wa zamu kwa wiki hiyo, Gideon, mshauri wa karibu wa Rais Costa na Eliza mke wa Joe.
“Eliza Watoto wanaendeleaje”, Rais Costa aliuliza. “Wanaendelea vizuri Mh Rais’’, Eliza alijibu pasi kumtazama Rais usoni. “Nimeipata mikakati yako ya kuboresha ufanisi wa benki na hakika taifa lilikumisi sana”, Rais Costa aliendela kuongea huku akikata kipande cha nyama kwa uma na kisu. “Nafurahi kutoa mchango wangu kwa taifa”, Eliza alijibu kishupavu na maongezi mengine yaliendelea. Mara baada ya kumaliza kula Eliza, Waziri wa Fedha na Waziri wa Kilimo na Chakula waliaga na kuondoka kuelekea mahali walipoandaliwa kupumzika.
“Mh. Umeona wananchi wanavyokupenda? Umesikia walivyokuwa wapiga kelele uendelee kubaki madarakani? Mimi nadhani hata tulivyobadili katiba kuruhusu miula mitatu ya utawala tuliwarahisishia kazi sana”, Gideon alikuwa akimjaza upepo Rais Costa wakiwa pale sebuleni wakisoma magazeti huku wakitazama habari kwenye runinga.
“Ninaona hapa huyu Kibwe ameanza kupiga kelele juu ya azma yangu ya kubadili umri wa kugombea urais. Ni vyema tukamdhibiti mapema, si mtu wa kubeza, ana ushawishi mkubwa ndani na nje ya nchi. Hawa jamaa wa magharibi watatusumbua tukimwacha aliongelee ongelee”.
Badala ya kujibu aliloambiwa na Gideon, Rais Costa yeye alimwonyesha habari katika gazeti inayomwonyesha Julius Kibwe, kiongozi kijana na machachari wa upinzani akipinga vikali tetesi za muswada wa kutaka kubadili umri wa kugombea urais uongezwe kutoka miaka 40 mpaka miaka 55.
“Nitamshauri Waziri wa Sheria na Masuala ya Bunge njia nzuri ya kulipeleka hili, lakini wakati huo huo ni vema wewe ukazidi kuongeza imani na mapenzi kwa wananchi”, Gideon alimjibu Rais Costa.
‘’Umetoka kusema kuwa wananchi wananipenda. Hiyo Imani na mapenzi unayoshauri niongeze kwa wananchi ni kwa njia zipi?’’, Rais Costa alimuuliza Gideon akionekana wazi kuwa hajaelewa hilo lingefanyikaje kwani katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, pamoja na ukandamizaji wa demokrasia na kufunga wapinzani wake, lakini alianza kuhisi umaarufu wake umeshuka na kwa namna fulani wapinzani wake kisiasa walizidi kumkalia kooni wakimtaka aheshimu haki za binadamu, Sheria na Katiba ya nchi. Aliona kama alichosema Gideon hakiingii akilini kwa hali ya sasa.
‘’Tengeneza tatizo kupitia viongozi wa chini yako kisha wewe jiweke mbali nalo, hakikisha kuwa linamgusa kila mmoja au watu wengi, acha watu wapige kelele, wanasiasa waongee, kisha litatue na kulaumu watu wengine aidha kwa kuwataja hadharani au hata kwa kuwataja kwa ujumla tu katika makundi yao, ikiwezekana tumbua baadhi yao. Hii itakufanya wewe uonekane usiye na hatia, tena mkombozi haswa’’, Gideon alijibu na kumfanya Rais Costa kumpa usikivu zaidi na hata kubadilisha mkao.
“He he he he!”, Kwa mara ya kwanza baada ya kipindi kirefu, Rais Costa alicheka na kuonekana kuvutiwa na mipango ya Gideon ambayo ingemuongezea umaarufu na kupendwa. Rais Costa alipenda kusifiwa zaidi, hakutaka kusikia mtu anayemkosoa au asiyemuunga mkono. “Tatizo kama lipi kwa sasa?’’, Rais Costa alihoji kutaka kufahamu zaidi kuhusu mpango wa Gideon ambao ulishaanza kumvutia.
“Leo umetoka kuwafurahisha wakulima, ina maana vijijini tayari umezidi kupendwa kwani tozo hizi zilikuwa ni kero. Lakini ukumbuke kwa kufanya hivi umepunguza chanzo cha mapato kwa halmashauri nyingi hivyo ni lazima tutafute pa kulipia, sasa waite Waziri wa Fedha na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Taifa ya Mapato na Makusanyo. Wape maagizo waanze operesheni ya kukamata wote ambao hawajalipa kodi hata kama mhusika biashara yake mtaji ni wa chini ya shilingi laki moja, alazimishwe kulipa kodi kwanza kabla hajaanza bishara kwa kukadiriwa”, Gideon alishauri na kukaa kimya huku akimtazama Rais Costa.
“Ukweli kuna uliyosema ya msingi hasa kutafuta vyanzo mbadala vya mapato lakini hili la kulipisha watu kodi hata kabla ya biashara kuanza tena hata wenye mitaji ya chini kabisa sijaliunga mkono. Halina afya kwa mwananchi wa kawaida na tunajiua kiuchumi wenyewe”, Rais Costa alionekana kutoelewa.
Gideon alicheka sana kisha akamwambia Rais, “Hilo ndio litakuwa tatizo, na baada ya miezi mitatu hivi hadi sita ya watu kupata taabu na Mamlaka za Ukusanyaji Mapato na Kodi na kulalamika sana, utafuta huo utaratibu kwa kisingizo kuwa ni kumkandamiza mnyonge na wewe haupo kwa ajili ya kutesa wanyonge”, Gideon alimaliza.
Rais Costa alimwangalia Gideon kwa sekunde kama tatu akiwa kimya kisha aliangua kicheko kikubwa “Gideon you are a genius”, (Gideon una akili sana). Alifungua chupa ya wine na kuanza kummiminia Gideon.
***************************************
Msafara wa Joe na En uliwasili kwenye makazi ya Rais wa Korea. Rais Kim alikuwa mlangoni akiwasubiri na mara baada ya kushuka walipokelewa. Joe akiwa mbele ya Habibu na Pius alifika mbele ya Rais Kim kwa heshima kubwa, akainama kidogo na kumkabidhi nembo ya Rais wa Stanza (‘The Republic of Stanza’s Presidential Seal’), kama ishara haswa ya ujumbe maalumu wa Rais wa Stanza. “Karibuni sana”, kwa mshangao mkubwa Rais Kim aliwakaribisha kina Joe kwa kutumia Kiswahili. Walikumbatiana na kuelekea chumba maalum kwa ajili ya mazungumzo ya awali na kufikisha ujumbe Rais wa Stanza aliotaka umfikie Rais Kim.
Walifika na kuketi, Kim akiwa sambamba na En Waziri wake wa masuala ya kigeni huku kina Joe wakiwa wamepewa mkalimani waliulizana habari za hali na maendelo baina ya nchi hizo mbili. Joe alimkabidhi faili maalumu la siri alilopewa na Rais Costa lililo na barua na maelezo ya lengo la ujumbe ule. Hata hivyo maelezo yote aliyaandika Joe.
Baada ya Rais Kim kupokea faili lile alitoa maelekezo kuwa siku ile ya kwanza wangekutana ujumbe wa Joe na ujumbe wa serikali ya Korea Kaskazini. Joe na ujumbe wake wangeeleza kila jambo lililowapeleka Korea na kisha ujumbe wa Rais Kim ungeenda kutafakari na kisha kukutana nae kutafakari kabla ya kukutana tena wote kwa makubaliano na maazimio kesho yake.
Ilipangwa kuwa ni ugeni utakaodumu kwa siku mbili wakianza siku hiyo waliyowasili mpaka watakapoondoka. Mara baada ya kupata ratiba hiyo Joe na wenzake walielekezwa eneo la mapumziko na kuachwa hapo watatu wakiwa wamepewa kahawa kama walivyohitaji.
Joe akiwa na wenzake aliwaambia sasa muda wa kuonyesha vipawa vyao vya majadiliano ya kimataifa umefika. Wakiwa wanajadiliana, Pius alionekana kutotulia kiakili. Suala walilokuwa wamezungumza kwenye ndege lilikuwa likimsumbua sana.
“Upo sawa?”, Joe alimuhoji Pius. “Hapana, suala lile bado linanitafuna akili nataka kujua ni nani mwingine anafahamu”, Pius alimjibu Joe. Kwa kujua kuwa maongezi yao yaweza kuwa yanarekodiwa ndani ya makazi yale kwa kutumia vinasa sauti vyenye uwezo mkubwa ilikuwa ni lazima watumie maneno machache sana kuzungumza mambo yao au hata kwa ishara. Joe alishajua Pius anazungumzia nini, alijua anataka kujua ni nani mwingine yupo kwenye ule mpango aliowashirikisha wa kumpumzisha Rais Costa nje ya madaraka pasi yeye kutaka kwa hiari kuyaachia.
Joe aliwaangalia Habibu na Pius usoni. Aligundua kuwa bila kuwafumbulia fumbo hilo wasingefanya vizuri kwenye mazungumzo yao kwasababu akili zao zilitekwa na mpango ambao Joe aliwashirikisha kwa kifupi. “Ok, nitawaambia ili akili zenu mzirudishe hapa. Stanley Macha ni mmoja wapo kwenye mpango huu, mwingine sitawatajia kwa sasa” Joe aliwadokeza kwa kifupi.
Habibu na Pius walionekana kushtuka. Hawakuamini kama Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa nae yupo kwenye mpango huo. “This is serious guys”, (hili suala ni nyeti). Joe aliwaambia huku akiwatazama usoni. “Tutaamini vipi kama ni kweli?”, Habibu alihoji.
“Nitawapa namba za siri (codes). Sasa kila mtu kwa wakati wake na ikiwa umekubaliana na mpango huu kwa ustawi wa nchi yetu na kuwa mmoja kati ya watakaoleta chachu ya mabadiliko ya kweli, utamtumia Stanley hiyo namba ya siri kwa njia ya WhatsApp nae atajibu kama utakavyomwandikia, na baada ya hapo hamtaendelea na mazungumzo yoyote. Hiyo itakuwa ndio ishara kuwa nimeshawaambia na kuwa tupo pamoja”, Joe aliwaeleza.
“Tupe hizo codes”. Habibu na Pius walijikuta wakiuliza kwa pamoja. “Ego testor”, Joe aliwajibu (Hili ni neno la kilatini lenye maana ya kuapa/kula kiapo). Haraka Pius na Habibu walitoa simu zao za mkononi kwa shauku kutaka kuhakikisha kile wanachokisikia.
Waligundua simu zao hazinasi mtandao wowote, wapo ugenini lakini hata kama wangekua wanaweza kuwasiliana kwa wakati ule isingewezekana kwani ukikaribia tu makazi ya Rais Kim mawasiliano yote hukatika na ni mfumo wao tu maalumu wa mawasiliano ambao wanao watu wachache sana ndani ya makazi yale ndio hutumika. Walihema wote kwa pamoja na kutulia.
************************************
Je, Mazungumzo Jijini Pyongyang Yatafanikiwa?Vipi Usalama Wa Stanley Macha Baada Ya Kutajwa Na Joe?Usikose Sehemu Ya Sita
Joe Awasili Pyongyang. Siri Nzito Yawashtua Habibu Na Pius.
“선량한 동지들” seonlyanghan dongjideul (Habari za asubuhi kamaradi). Ndugu En Ki, waziri anayehusika na masuala ya kigeni wa Korea Kaskazini aliwasalimia kiKorea Joe na ujumbe wake mara tu baada ya kuwapokea uwanja wa ndege wa Pyongyang.
“좋은 아침” joh-eun achim(Salama) Joe nae alijibu kiKorea huku akiwa ameshikana mkono na ndugu En wakiwa wameinamishiana vichwa. “평양에 오신 것을 환영합니다. pyeong-yang-e osin geos-eul hwan-yeonghabnida, (Karibuni Pyongyang), Waziri En aliendelea.
“고마워. 우리의 즐거움 동지 야”gomawo. uliui jeulgeoum dongji ya. (Asante sana. Ni furaha yetu kubwa sana kuwa hapa), Joe nae alijibu huku akitabasamu.
Joe akiwa mwanadiplomasia mbobevu alielewa itifaki za mataifa mengi. Alikuwa ni mtu makini ambaye ukikutana nae unajua kabisa kuwa ameiva kwelikweli katika masuala ya mahusiano ya kimataifa, diplomasia na hata lugha za kigeni.
Ndugu En aliwaongoza Joe na ujumbe wake mpaka kwenye magari yaliyoandaliwa kwa ajili ya msafara kuelekea Ikulu ya Pyongyang. Kutokea uwanja wa ndege wa kimataifa wa Pyongyang Sunan jijini Pyongyang mpaka makazi ya Rais Kim ni mwendo wa kama dakika 40 hivi kwa gari, hivyo msafara ulianza kwa kuifuataHeeecheon Expressway.
Yalikuwa jumla ya magari manne, la mbele likiwa linaongoza msafara, la pili alipanda Waziri En na Joe, la tatu alipanda Habibu na Pius na la nne likiwa ni la ulinzi. Wakiwa njiani, Joe alikuwa akiongea mawili matatu na En. En alikuwa ni mjuzi wa lugha nne ukiacha ya kiKorea.
Alizungumza kwa ufasaha kiingereza, kichina, kirusi na kifilipino. Alikuwa ni mtu mwenye uelewa mkubwa sana wa masuala ya kimataifa na mwenye akili nyingi sana. Aliaminiwa na Rais Kim Jon Un wa Korea Kaskazini tangu alipoingia madarakani kurithi mikoba ya baba yake alipofariki.
“Comrade Kim has high expectations of your visit”, (Rais Kim ana matarajio makubwa na ujio wenu huu). En alimwambia Joe huku akitabasamu kwa shauku. “Same to President Costa”, (Hata Rais Costa), Joe nae alijibu kwa ufupi. Joe alijua mbinu za mazungumzo, alijua wapi pa kuongea sana na wapi pa kuongea kwa uchache, alijua lipi la kujibu na lipi la kukaa kimya. Tangu anawasili Pyongyang kila jambo analofanya alitumia umakini mkubwa.
Safari iliendelea huku Joe akishangaa na kustaajabu namna barabara ilivyokuwa tupu na nyeupe. Hakuona hata mtu mmoja tokea walipouacha uwanja wa ndege. Alikuwa akistaajabu na alipouliza kwa En alijibiwa hivyo ndivyo wanavyowaheshimu wageni muhimu kwa taifa. Joe hakuelewa.
**************************************
Ryongsong ndilo jina la makazi ya Rais Kim. Wengine hupenda kuyaita Residence No. 55 auCentral Luxury Mansionkutokana na umaridadi wake. Ni makazi yanayosemekana kulindwa na kuwa salama kuliko makazi yoyote duniani. Ukubwa wa eneo yaliyopo makazi haya ni kilometa za mraba 12 pakiwa na kila aina ya kitu kinachohitajika kwa kiongozi mkuu wa nchi.
Wataalamu wa masuala ya ulinzi na ujasusi wanaamini kuwa askari kati ya 95,000 – 120,000 wapo maalumu kwa ajili ya kulinda eneo hili pamoja na usalama wa Rais Kim na maeneo mengine yote yalipo makazi ya familia ya Rais Kim. Wakiwa chini ya kikosi namba 963wakiongozwa na Jenerali Yun Jong-Rin, wanakifanya kikosi hiki kuwa moja ya vikosi vikubwa kabisa vya ulinzi wa Rais duniani.
Ryongsong imezungukwa na machimbo yaliyotegwa kulipuka kama kuna mvamizi yeyote atataka kusogelea makazi haya kwa njia ya ardhi, lakini pia kuna wigo mkubwa wa umeme pamoja na vituo vingi vya ukaguzi kwenye njia ya kuingilia na kuzunguka makazi haya. Makazi haya pia yamezungukwa na vituo vya kijeshi vyenye makombora makubwa ya maangamizi na ya masafa marefu na mitambo ya kunasa chochote kinachoikaribia eneo lile bila taarifa na kuweza kutuma kombora kukisambaratisha.
Hakuna ndege wala kifaa chochote kinachoruhusiwa kupita juu ya anga lililopo jengo hili la sivyo kitatunguliwa hapohapo. Ndani ya makazi haya, chini ya ardhi kuna Sehemu salama ya kumficha Rais ikiwa itaonekana yupo hatarini. Eneo hilo limejengwa kwa kuta za chuma kizito na zege zito lililofunikwa na madini ya leadili kuzuia nyumba hiyo kuathirika hata kwa shambulio la nyuklia.
Lead ni moja ya madini yenye myeyuko hafifu (Low melting point), hivyo huhitajika joto la kuanzia nyuzi joto 327 ili yaweze kuyeyuka. Ni katika Sehemu hiyo Rais Kim huweza kuishi huko kwa usalama bila chochote kutoka kwa maadui kuweza kumvamia ama kumdhuru kwa miaka zaidi ya mitatu mfululizo bila kutoka, huku akiweza kutoa maelekezo ya kivita na kiutawala.
Makazi haya pia yameunganishwa na makazi mengine ya Rais ya Changgyongau huitwa Residence No.26. Makazi haya yote yamewekewa mfumo utakaoruhusu kutumia njia iliyopo chini ya ardhi ikitokea kuna uvamizi. Pia chini ya ardhi kutokea kwenye nyumba hii kuna reli maalumu kwa ajili ya Rais tu na kitu cha kustaajabisha kwa wachambuzi wengi wa masuala ya kiusalama ya peninsula ya Korea ni kuwa reli hii ilitengenezwa kuelekea mahali kusikojulikana.
Inadhaniwa kuwa mwisho wa reli hii hubadilikabadilika kulingana na mahitaji ya wakati husika lakini lengo kuu likiwa kuhakikisha kuwa Rais na familia yake wanakuwa salama likitoea shambulio. Mbali na mambo mengine mengi ya kiulinzi na kiusalama, nyumba hii imepambwa sana kwa nakshi, taa na samani nzuri. Nje kukiwa na bustani nzuri na za maua zenye kuvutia, mito na maziwa ya bandia yaliyotengenezwa kupendezesha eneo hili. Hakika makazi haya yalivutia.
Joe, Habibu na Pius walikuwa wanakuja kuingia hapa kwa mara ya kwanza.
*******************************************
“Wananchi wenzangu mlinichangua ili nilete maendeleo na maendeleo ndiyo haya. Nimesema na nimemwagiza Waziri wa Kilimo na Chakula hapa kuwa Sitaki kusikia mkulima yeyote anakatwa tozo eti ya kusafirisha mazao. Mtu hata kuuza hajauza unamkata tozo kivipi? Vibali vya kusafirisha mazao vitolewe bure kama mtu amelima mazao yake kihalali anayatoa shamba anayapeleka mjini ama mkoa fulani kuuza unamwambia alipe, sasa alipe na nini wakati hata kuuza hajauza? Tena sitataka kusikia ukiritimba katika kutolewa vibali hivi.
Waziri upo hapa unanisikia na viongozi wengine wote hili nalifuta kuanzia leo”, Rais Costa alikuwa akiongea huku akishangiliwa kwa nguvu na wananchi wa Kisasampara, Jimbo la Kengwe alipokwenda kuzindua ghala kubwa za chakula za hifadhi ya Taifa.
“Tumeanza mazungumzo na serikali ya China na tutaingia nao ubia kutujengea soko kubwa la kimataifa la matunda. Soko letu likikamilika litakuwa la kwanza kwa ukubwa bara la Afrika, hivyo vijana anzeni kujikita kuzalisha matunda. Neema inakuja!” Rais Costa aliendelea huku umati mkubwa wa watu ukimshangilia. Alikuwa ameanza utekelezaji wa ushauri aliowahi kupewa na Joe siku za nyuma namna ya kujadiliana na Rais wa China juu ya kuingiza vijana wa kichina zaidi ya laki moja kuja nchini Stanza kufanya biashara ndogondogo.
Rais Sylvester Costa alimaliza kuhutubia na kushuka jukwaani na kusalimiana na wananchi wawili watatu kisha kuanza kutembea kuelekea kwenye zile ghala kuzikagua. Alikuwa amefuatana na mawaziri, viongozi wengine wa serikali kuu na ya Jimbo pia alikuwepo na bi. Eliza, mke wa Joseph ambae kwa wakati huo ni Mkurugenzi wa Benki ya Kilimo ya Stanza. Aliingia akayakagua na kuridhika kisha msafara uliondoka kuelekea kwenye nyumba ya mapumziko ya viongozi wa kiserikali kwa ajili ya mapumziko iliyopo pale Kengwe.
Wakiwa kwenye nyumba ya mapumziko Rais alipata chakula pamoja na Waziri wa Kilimo na Chakula, Waziri wa Fedha ambaye ndiye alikuwa Waziri wa zamu kwa wiki hiyo, Gideon, mshauri wa karibu wa Rais Costa na Eliza mke wa Joe.
“Eliza Watoto wanaendeleaje”, Rais Costa aliuliza. “Wanaendelea vizuri Mh Rais’’, Eliza alijibu pasi kumtazama Rais usoni. “Nimeipata mikakati yako ya kuboresha ufanisi wa benki na hakika taifa lilikumisi sana”, Rais Costa aliendela kuongea huku akikata kipande cha nyama kwa uma na kisu. “Nafurahi kutoa mchango wangu kwa taifa”, Eliza alijibu kishupavu na maongezi mengine yaliendelea. Mara baada ya kumaliza kula Eliza, Waziri wa Fedha na Waziri wa Kilimo na Chakula waliaga na kuondoka kuelekea mahali walipoandaliwa kupumzika.
“Mh. Umeona wananchi wanavyokupenda? Umesikia walivyokuwa wapiga kelele uendelee kubaki madarakani? Mimi nadhani hata tulivyobadili katiba kuruhusu miula mitatu ya utawala tuliwarahisishia kazi sana”, Gideon alikuwa akimjaza upepo Rais Costa wakiwa pale sebuleni wakisoma magazeti huku wakitazama habari kwenye runinga.
“Ninaona hapa huyu Kibwe ameanza kupiga kelele juu ya azma yangu ya kubadili umri wa kugombea urais. Ni vyema tukamdhibiti mapema, si mtu wa kubeza, ana ushawishi mkubwa ndani na nje ya nchi. Hawa jamaa wa magharibi watatusumbua tukimwacha aliongelee ongelee”.
Badala ya kujibu aliloambiwa na Gideon, Rais Costa yeye alimwonyesha habari katika gazeti inayomwonyesha Julius Kibwe, kiongozi kijana na machachari wa upinzani akipinga vikali tetesi za muswada wa kutaka kubadili umri wa kugombea urais uongezwe kutoka miaka 40 mpaka miaka 55.
“Nitamshauri Waziri wa Sheria na Masuala ya Bunge njia nzuri ya kulipeleka hili, lakini wakati huo huo ni vema wewe ukazidi kuongeza imani na mapenzi kwa wananchi”, Gideon alimjibu Rais Costa.
‘’Umetoka kusema kuwa wananchi wananipenda. Hiyo Imani na mapenzi unayoshauri niongeze kwa wananchi ni kwa njia zipi?’’, Rais Costa alimuuliza Gideon akionekana wazi kuwa hajaelewa hilo lingefanyikaje kwani katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, pamoja na ukandamizaji wa demokrasia na kufunga wapinzani wake, lakini alianza kuhisi umaarufu wake umeshuka na kwa namna fulani wapinzani wake kisiasa walizidi kumkalia kooni wakimtaka aheshimu haki za binadamu, Sheria na Katiba ya nchi. Aliona kama alichosema Gideon hakiingii akilini kwa hali ya sasa.
‘’Tengeneza tatizo kupitia viongozi wa chini yako kisha wewe jiweke mbali nalo, hakikisha kuwa linamgusa kila mmoja au watu wengi, acha watu wapige kelele, wanasiasa waongee, kisha litatue na kulaumu watu wengine aidha kwa kuwataja hadharani au hata kwa kuwataja kwa ujumla tu katika makundi yao, ikiwezekana tumbua baadhi yao. Hii itakufanya wewe uonekane usiye na hatia, tena mkombozi haswa’’, Gideon alijibu na kumfanya Rais Costa kumpa usikivu zaidi na hata kubadilisha mkao.
“He he he he!”, Kwa mara ya kwanza baada ya kipindi kirefu, Rais Costa alicheka na kuonekana kuvutiwa na mipango ya Gideon ambayo ingemuongezea umaarufu na kupendwa. Rais Costa alipenda kusifiwa zaidi, hakutaka kusikia mtu anayemkosoa au asiyemuunga mkono. “Tatizo kama lipi kwa sasa?’’, Rais Costa alihoji kutaka kufahamu zaidi kuhusu mpango wa Gideon ambao ulishaanza kumvutia.
“Leo umetoka kuwafurahisha wakulima, ina maana vijijini tayari umezidi kupendwa kwani tozo hizi zilikuwa ni kero. Lakini ukumbuke kwa kufanya hivi umepunguza chanzo cha mapato kwa halmashauri nyingi hivyo ni lazima tutafute pa kulipia, sasa waite Waziri wa Fedha na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Taifa ya Mapato na Makusanyo. Wape maagizo waanze operesheni ya kukamata wote ambao hawajalipa kodi hata kama mhusika biashara yake mtaji ni wa chini ya shilingi laki moja, alazimishwe kulipa kodi kwanza kabla hajaanza bishara kwa kukadiriwa”, Gideon alishauri na kukaa kimya huku akimtazama Rais Costa.
“Ukweli kuna uliyosema ya msingi hasa kutafuta vyanzo mbadala vya mapato lakini hili la kulipisha watu kodi hata kabla ya biashara kuanza tena hata wenye mitaji ya chini kabisa sijaliunga mkono. Halina afya kwa mwananchi wa kawaida na tunajiua kiuchumi wenyewe”, Rais Costa alionekana kutoelewa.
Gideon alicheka sana kisha akamwambia Rais, “Hilo ndio litakuwa tatizo, na baada ya miezi mitatu hivi hadi sita ya watu kupata taabu na Mamlaka za Ukusanyaji Mapato na Kodi na kulalamika sana, utafuta huo utaratibu kwa kisingizo kuwa ni kumkandamiza mnyonge na wewe haupo kwa ajili ya kutesa wanyonge”, Gideon alimaliza.
Rais Costa alimwangalia Gideon kwa sekunde kama tatu akiwa kimya kisha aliangua kicheko kikubwa “Gideon you are a genius”, (Gideon una akili sana). Alifungua chupa ya wine na kuanza kummiminia Gideon.
***************************************
Msafara wa Joe na En uliwasili kwenye makazi ya Rais wa Korea. Rais Kim alikuwa mlangoni akiwasubiri na mara baada ya kushuka walipokelewa. Joe akiwa mbele ya Habibu na Pius alifika mbele ya Rais Kim kwa heshima kubwa, akainama kidogo na kumkabidhi nembo ya Rais wa Stanza (‘The Republic of Stanza’s Presidential Seal’), kama ishara haswa ya ujumbe maalumu wa Rais wa Stanza. “Karibuni sana”, kwa mshangao mkubwa Rais Kim aliwakaribisha kina Joe kwa kutumia Kiswahili. Walikumbatiana na kuelekea chumba maalum kwa ajili ya mazungumzo ya awali na kufikisha ujumbe Rais wa Stanza aliotaka umfikie Rais Kim.
Walifika na kuketi, Kim akiwa sambamba na En Waziri wake wa masuala ya kigeni huku kina Joe wakiwa wamepewa mkalimani waliulizana habari za hali na maendelo baina ya nchi hizo mbili. Joe alimkabidhi faili maalumu la siri alilopewa na Rais Costa lililo na barua na maelezo ya lengo la ujumbe ule. Hata hivyo maelezo yote aliyaandika Joe.
Baada ya Rais Kim kupokea faili lile alitoa maelekezo kuwa siku ile ya kwanza wangekutana ujumbe wa Joe na ujumbe wa serikali ya Korea Kaskazini. Joe na ujumbe wake wangeeleza kila jambo lililowapeleka Korea na kisha ujumbe wa Rais Kim ungeenda kutafakari na kisha kukutana nae kutafakari kabla ya kukutana tena wote kwa makubaliano na maazimio kesho yake.
Ilipangwa kuwa ni ugeni utakaodumu kwa siku mbili wakianza siku hiyo waliyowasili mpaka watakapoondoka. Mara baada ya kupata ratiba hiyo Joe na wenzake walielekezwa eneo la mapumziko na kuachwa hapo watatu wakiwa wamepewa kahawa kama walivyohitaji.
Joe akiwa na wenzake aliwaambia sasa muda wa kuonyesha vipawa vyao vya majadiliano ya kimataifa umefika. Wakiwa wanajadiliana, Pius alionekana kutotulia kiakili. Suala walilokuwa wamezungumza kwenye ndege lilikuwa likimsumbua sana.
“Upo sawa?”, Joe alimuhoji Pius. “Hapana, suala lile bado linanitafuna akili nataka kujua ni nani mwingine anafahamu”, Pius alimjibu Joe. Kwa kujua kuwa maongezi yao yaweza kuwa yanarekodiwa ndani ya makazi yale kwa kutumia vinasa sauti vyenye uwezo mkubwa ilikuwa ni lazima watumie maneno machache sana kuzungumza mambo yao au hata kwa ishara. Joe alishajua Pius anazungumzia nini, alijua anataka kujua ni nani mwingine yupo kwenye ule mpango aliowashirikisha wa kumpumzisha Rais Costa nje ya madaraka pasi yeye kutaka kwa hiari kuyaachia.
Joe aliwaangalia Habibu na Pius usoni. Aligundua kuwa bila kuwafumbulia fumbo hilo wasingefanya vizuri kwenye mazungumzo yao kwasababu akili zao zilitekwa na mpango ambao Joe aliwashirikisha kwa kifupi. “Ok, nitawaambia ili akili zenu mzirudishe hapa. Stanley Macha ni mmoja wapo kwenye mpango huu, mwingine sitawatajia kwa sasa” Joe aliwadokeza kwa kifupi.
Habibu na Pius walionekana kushtuka. Hawakuamini kama Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa nae yupo kwenye mpango huo. “This is serious guys”, (hili suala ni nyeti). Joe aliwaambia huku akiwatazama usoni. “Tutaamini vipi kama ni kweli?”, Habibu alihoji.
“Nitawapa namba za siri (codes). Sasa kila mtu kwa wakati wake na ikiwa umekubaliana na mpango huu kwa ustawi wa nchi yetu na kuwa mmoja kati ya watakaoleta chachu ya mabadiliko ya kweli, utamtumia Stanley hiyo namba ya siri kwa njia ya WhatsApp nae atajibu kama utakavyomwandikia, na baada ya hapo hamtaendelea na mazungumzo yoyote. Hiyo itakuwa ndio ishara kuwa nimeshawaambia na kuwa tupo pamoja”, Joe aliwaeleza.
“Tupe hizo codes”. Habibu na Pius walijikuta wakiuliza kwa pamoja. “Ego testor”, Joe aliwajibu (Hili ni neno la kilatini lenye maana ya kuapa/kula kiapo). Haraka Pius na Habibu walitoa simu zao za mkononi kwa shauku kutaka kuhakikisha kile wanachokisikia.
Waligundua simu zao hazinasi mtandao wowote, wapo ugenini lakini hata kama wangekua wanaweza kuwasiliana kwa wakati ule isingewezekana kwani ukikaribia tu makazi ya Rais Kim mawasiliano yote hukatika na ni mfumo wao tu maalumu wa mawasiliano ambao wanao watu wachache sana ndani ya makazi yale ndio hutumika. Walihema wote kwa pamoja na kutulia.
************************************
Je, Mazungumzo Jijini Pyongyang Yatafanikiwa?Vipi Usalama Wa Stanley Macha Baada Ya Kutajwa Na Joe?Usikose Sehemu Ya Sita