Simulizi:The President and I(Mimi Na Rais)

Simulizi:The President and I(Mimi Na Rais)

imkakati
Ujumbe wa Gideon ulimfariji Joe, hakika aliona yupo na mshirika
mwaminifu na mwanamkakati wa dhati. Ujumbe aliousoma kwa Waziri
En ndio uliomtia wazimu kidogo.
“Comrade, what is the progress? We haven’t heard from you for some
days now. Is President Costa not happy with our agreement?”
(Kamaradi, maendeleo yakoje? Hatujasikia chochote kutoka kwako kwa
siku kadhaa sasa au Rais Costa hakuaϐikiana na makubaliano yetu?”
Ujumbe wa Waziri En uliuliza.
Ujumbe ule ulimchanganya kichwa Joe kwa sababu jibu atakalolitoa
hapo litaamua swali au hatua itakayofuata kwa Korea Kaskazini.
Alijua akisema mambo yapo sawa wakati hayapo sawa ingeleta shida.
Lakini akisema hayapo sawa ingezua maswali kwa En na hakuwa tayari
kwa hilo kujulikana kwa sasa. Aliwaza sana lakini mwisho alipata cha
kueleza. Aliwaza kuwa dawa ya moto ni kuumwagia maji na sio
kuwasha moto mwingine. Aliwaza, kama Pius aliamua kuwasaliti basi
acha ammalize kabisa kabisa kwenye sura ya Korea Kaskazini.
Alijua kwa vyovyote Rais Costa angemtumia Pius kuendelea na misheni
na yeye angekuwa hana maana tena hata kama akifa, wazungu
wanasema ‘He will be of no relevance’. Alijua hakuna kitu kibaya kwenye
maisha kama kupoteza thamani ya uwepo wako mahali fulani kwa
sababu utatemwa au wazungu wanasema ‘you will be rejected’.
Alifahamu hata ndoa huvunjika baada ya mwanandoa mmoja kupoteza
thamani mbele ya mwenzake, mtu hufukuzwa kazi baada ya kupoteza
thamani yake kwenye kampuni/shirika/oϐisi hiyo n.k
Joe hakukubali thamani yake kwenye serikali ya Stanza ipotezwe
kirahisi. Alijua ku ‘deal’ na matukio ya namna hiyo.
“Comrade, things are not ϐine. Pius has informed the president that I
have a secret mission with you that’s why we have agreed the
involvement of nucler weapons in our agreements. Now I am under the
extreme hunt together with Habibu to be terminated. This is the reason
why you don’t hear from me neither from the President”
(Kamaradi, mambo hayapo sawa. Pius amemtaarifu Rais kuwa nina
mpango wa siri na ninyi na ndio maana tumekubaliana nanyi juu ya
mpango wa silaha za kinyuklia. Sasa hivi nipo kwenye msako mkali ili
niuawe mimi na Habibu. Hii ndio sababu kwanini husikii lolote kutoka
kwangu wala kwa Rais). Joe alimjibu Waziri En.
“This is ridiculous, how could the soldier of the higher rank like Pius
behave like that? So you haven’t even arrived in Stanza?” (Hili jambo
linanishangaza sana, inawezekanaje askari wa cheo cha juu kama Pius
afanye mambo kama hayo? Kwa hiyo bado hujaϐika Stanza?) Waziri En
aliuliza kwa shangao.
“He has surprised all of us. Yes, We are still in Beijing” (Ametushangaza
wote. Ndio bado tupo Beijing) Joe alijibu.
“Africa has never stop to amaze us. So where are you and how can we
help you because you remember what we discussed?” (Africa haijawahi
kuacha kutushangaza. Kwa hiyo upo wapi na tukusaidieje kwa sababu
unakumbuka lile suala tulilojadili?) Waziri En alimuliza Joe.
Joe alianza kumwandikia Waziri En yote anayoona yanafaa ili
kuhakikisha yupo salama na misheni yake inaendelea. Mambo mengi En
alipingana nayo kwani kwa hakika yalikuwa yanaingilia uhuru na
utawala wa Stanza (Sovereignity interference). Waziri En alijua kwa
kufanya yale Joe aliyokuwa anamuomba angeibua hisia kubwa kwa
mataifa ya magharibi na ungekuwa ni uchokozi wa bayana kabisa
ambao ungekosa utetezi.
Waziri En alimwambia Joe asijali, kwanza atamtaarifu Rais Kim
kilichotokea na kisha atamrudia kumweleza nini wameϐikiria wanaweza
kusaidia. Waziri En alikuwa makini sana katika kila jambo alilopewa
kulisimamia na serikali yake ya Korea Kaskazini.
*******************************
“Mh. Rais umeona watu wanavyopiga kelele huko nje baada ya lile suala
la kodi kuanza kufanyiwa kazi?”, Gideon alikuwa akiongea na Rais Costa
asubuhi oϐisini kwake ambapo Rais Costa hupenda kupitia kila nyaraka
anayoikuta mezani kwake asubuhi, huo ukiwa ni utaratibu wake.
Gideon alikuwa akimkumbusha Rais juu ya ule mpango aliowahi
kumshauri wa kuhakikisha anaweka kodi koroϐi kwa wafanyabiashara
wa Stanza kwa kisingizio cha kuongeza mapato lakini hakika zikiwa
zinawatesa wananchi na kuua mitaji yao ya biashara. Agizo hilo lilikuwa
lipo katika utekelezaji na wananchi walikuwa wakilalamika na
kunyanyaswa sana na mamlaka ya makusanyo ya taifa wakishirikiana
na askari polisi pamoja na mgambo.
“Gideon, hizi kelele zimekuwa nyingi mpaka zinaanza kunipa hofu.
Ninataka bunge lipitishe muswada wa kutaka kubadili umri wa mtu
kugombea Urais ambapo tunauongeza, muswada huu utaleta kelele
nyingi kutoka kwa wapinzani sasa nahitaji wananchi wawe na amani na
mimi ili watu wangu watakapokuwa wanautetea wananchi waunge
mkono. Sasa, hili wazo lako naona linanichonganisha na wananchi tu
bila sababu”, Rais Costa alijibu huku akimalizia kusoma moja ya barua
alizozikuta pale mezani kwake ambayo aliiona haina maana akaiweka
kando.
“Mh. Rais, yani katika jambo litakupa ‘kiki’ ni hili, utakuja kunishukuru
baadaye. Wakati muswada ukiendelea kuandaliwa na huku tukisubiri
kipindi cha bunge kuanza ndio wakati huu wananchi watasumbuliwa
sana na watu wa Mamlaka ya Mapato na Makusanyo. Nimeona kila
halmashauri ya jimbo inawatumia mgambo kufanikisha makusanyo na
mgambo hawa wananyanyasa watu sana na kuzidisha chuki na hasira
kwa serikali na kwako.
Sasa hali hii iache iendelee na ikiwezekana kwenye mawasiliano yako
na wakuu wa mamlaka na wakuu wa mikoa na wilaya wasisitize kuwa
bado hujaona wakifanya jitihada vya kutosha ili wakazidi kutesa watu.
Sasa kipindi cha bunge kikianza tu ambapo muswada wako ndio
utajadiliwa wapinzani najua wataibuka na hoja nzito sana sasa wewe
ndio unatokea pale kuwavuruga kwa kusitisha kila aina ya manyanyaso
yanayoendelea kwa wafanya biashara juu ya ukusanyaji kodi. Tena ili
kuwamaliza kabisa toa tamko la kufuta mgambo wote kwenye miji yote.
Nakuhakikishia, ukifanya hivi utabadili upepo na muswada utapita bila
hata wananchi kuelewa na utapendwa kuliko ulivyowahi kupendwa.
Yani kwa ufupi ni kuwa, wakati wapinzani wakiwa na hoja ya muswada
wa umri wa kugombea uRais wewe unaibuka na suala la kutatua kero
za wananchi. Unakuwa ‘busy’ kupambana na hili suala la kodi koroϐi na
hivyo umakini wote wa wananchi unahamia kwako kama mkombozi
wao. Wakati wanagutuka tayari muswada umeshapita, na hapo
unakuwa umeua ndege wawili kwa jiwe moja. Kwanza umeongeza
mapenzi kwa wananchi na pili muswada wako umepita bila kelele.
Wapinzani utakuwa umewapiga kile tunaita ‘Bao la kisigino” Gideon
aliendelea ‘kumjaza upepo’ Rais Costa
“Hujawahi kuacha kunishangaza Gidi. Ha ha ha! Leo ndiyo nimekuelewa
vizuri, hasa hiyo ‘timing’ ulivyoiweka”, Rais Costa alionekana
kufurahishwa sana.
“Ndiyo kazi yangu Mh. Rais, kukushauri”. Gideon alijibu kwa nidhamu.
“Kha! Huyu kijana ameipata wapi hii ‘issue’ ya mimi kununua kisiwa cha
kitalii huko Uϐilipino?”. Rais Costa alionekana kuuliza kwa kushangaa na
hasira mara baada ya kusoma gazeti la kiingereza la STANZA TODAY
lililomnukuu Julius Kibwe akisema amepata Ushahidi kuwa Rais
Sylvester Costa anamiliki moja ya visiwa vya kitalii huko nchini
Uϐilipino.
“Kwani ni kweli mkuu habari hizi?”, Gideon alihoji.
“Hilo ni swali gani Gideon? Kuna kosa gani mimi kuwapa maendeleo
wananchi na mimi kujipa maendeleo?”, Rais Costa alijibu kiutu uzima.
Gideon aligutuka kuwa kuzidi kuuliza ni kukoroϐishana na Mh. Rais na
hilo si jambo lililompeleka oϐisini asubuhi ile.
“Mh. Rais huyu kijana yafaa adhibitiwe mapema na ninakumbuka mara
ya mwisho ulisema ungeongea na Macha na Waziri wa Polisi walifanyie
kazi, waliϐikia wapi?”, Gideon alidodosa.
“Macha ndiye aliyesema angemdhibiti sasa ndiyo huyohuyo tena
mhaini. Hauwezi kuwaaamini binadamu, hata kama ni ndugu zako wa
damu. Nadhani nitamwambia Waziri wa Polisi aendelee na mpango
wake”, Rais Costa alijibu huku akikazana kuisoma ile habari.
Kwa kawaida kila siku Rais huwa na kikao kidogo asubuhi ili kuelezwa
kwa ufupi mambo yote yanayoendelea kwenye habari na mitandaoni,
wananchi wanazungumza nini na kadhalika. Akiwa hapo oϐisini wakati
ule alikuwa akisubiriwa ili apewe taarifa kwa kina juu ya ile habari
aliyoisoma kwenye gazeti.
“Mh. Rais ulipomtaja Macha umenikumbusha jambo, mahojiano naye
yameϐikia wapi, yamevuna taarifa gani muhimu?”, Gideon aliuliza.
“Macha hataki kuongea, anadai kuwa hakukuwa na jaribio lolote la
mapinduzi. Nimemwagiza Majita amtese hadi aseme mpango wote, na
kama kufa afe tu, sitaki upumbavu. Joe nae nimeshatoa amri popote
atakapoonekana auawe. Sitaki hata kuona sura yake katika maisha
yangu”. Rais Costa alionekana kutibuliwa hasira na Gideon mara baada
ya kuulizwa habari juu ya Macha.
Gideon aliposikia Macha yupo chini ya Inspekta Majita roho ilimruka.
Anamfahamu Majita kwa uhodari wake wa kuua watu katika mateso,
hana mzaha. Suala la Rais kutoa amri ya Joe kuuawa popote
atakapopatikana lilimshtua pia. Alifahamu kuwa makachero wa Stanza
walishawahi kutumwa katika misheni mbalimbali duniani na kuua
maadui wa Rais Costa tena kwa kutumia njia ambayo haiachi alama
yoyote kuwa ni tukio la mauaji.
Gideon aliona amefanikiwa suala moja la kuhakikisha familia za Joe na
Macha hazibughudhiwi, lakini taarifa aliyoisikia kwa Mh Rais kuwa
ameagiza wauawe ilimpa mshtuko mkubwa. Alijiona kabisa ana haki ya
kuwasaidia wenzake katika misheni. Isitoshe suala la Rais Costa
kumiliki kisiwa Uϐilipino nalo lilimuacha mdomo wazi.
Alianza kuunganisha nukta kwa kujiuliza kumbe ndio maana Rais huwa
ana fedha za holela tu bila hata kujua anazipata wapi na wala
kutokuwapo kwenye utaratibu wa kawaida wa bajeti. Kwa mara ya
kwanza alijua huko anapozipata hizo za kugawa ndio huko huko
huchota za kwenda kununulia visiwa vya kitalii nchi za ughaibuni.
Kwasababu yeye huambatana na Rais Costa katika ziara zake nchini
Stanza, pia alikumbuka kuwa Rais hugawa mamilioni ya fedha kila
anapojisikia akiwa kwenye mikutano ya hadhara.
Alikumbuka pia taarifa ya Mwanamahesabu wa Serikali zilizotolewa
miaka mitatu iliyopita na kuonesha kuwa kuna fedha nyingi zilitumika
katika miradi hewa na matumizi yake hayakufuata sheria wala
utaratibu. Aliϐikiria masuala mengi, lakini pia alijifunza kuwa ukiwa
kwenye nafasi ya mamlaka ya juu unaweza kufanya jambo lolote bila
yeyote kukuuliza.
“Mh. Rais, ninaϐikiri inawezekana nikasaidia katika kupata taarifa
kutoka kwa Macha. Kama hutojali na inawezekana, ningependa
kufahamu ni wapi Macha ameshikiliwa na mkaniruhusu nizungumze
nae katika njia Raϐiki, pengine anaweza akanipa ushirikiano Zaidi ya
hapa na kunieleza kiundani zaidi”, Gideon aliomba.
“Sijui wapi wamempeleka ila Sabinasi atakuja asubuhi hii nitamwambia
akupe ‘clearance’ ya kwenda kuongea nae”. Rais Costa alijibu huku
akisimama ili watoke aelekee kwenye kikao cha kupata taarifa za
habari, wao hukiita Media Brieϔing.
Wakiwa ndio wanataka kutoka mara aliingia Sabinasi Paulo, Mkuu mpya
wa Idara ya Usalama Wa Taifa Stanza aliepewa nafasi hiyo mara tu
baada ya Stanley Macha kuwekwa chini ya Ulinzi.
“Mkuu, nimeleta ile orodha ningeomba unisaidie kuidhinisha”, Sabinasi
aliongea kwa ufupi.
Haraka Rais Costa alipokea ile karatasi na kuiweka mezani na kupitisha
macho kwa haraka. Ilikuwa na majina kama ya watu watano hivi na
chini kuna Sehemu ya Rais kuweka sahihi na yeye Sabinasi.
Gideon alikuwa amesimama kwa mbali kidogo hivyo alishindwa
kuisoma vizuri lakini alifanikiwa kusoma maneno ya juu yaliyoandikwa
‘Order to kill’ yenye maana Amri Ya Kuua. Halafu kwa sababu Rais
aliweka mkono juu ya ile karatasi hakuweza kusoma majina yote lakini
alifanikiwa kusoma jina moja la mwisho lililosomeka Sylvanus Majura.
Rais Costa alimaliza kusaini na kumpa Sabinasi na kisha kumwagiza
Sabinus ampeleke Gideon kwenye nyumba walipomuhifadhi Macha.
Baada ya Rais Costa kutoka kwanza kama utaratibu ulivyo, Gideon na
Sabinasi nao walitoka. Sabinasi alimwambia Gideon asubiri palepale
Ikulu na kuwa gari maalumu lingekuja kumchukua na kumpeleka
kuonana na Macha. Gideon aliaϐiki.
**********************************
Sara, mke wa Rais Costa alikuwa kwenye sintofahamu kubwa
alipotaariϐiwa kuwa anatakiwa kurudi Stanza haraka. Alimuuliza
msaidizi wake ambaye ni Sehemu ya Usalama wa Taifa Stanza kama
kuna lolote analolijua lakini msaidizi yule alisema kwa hakika hana
taarifa zozote.
Wakiwa Safarini kutokea Canada alijawa na mawazo mengi sana kwa
sababu hata alipoongea na mume wake Rais Costa alimwambia tu
anamtaka arudi nyumbani haraka na hakumpa sababu.
Alidhani labda mtoto wao wa pekee Brian Sylvester Costa amepata
tatizo lakini alipompigia simu Brian anayesoma nchini Denmark
alimwambia mama yake kuwa yupo salama. Sara alipata wasiwasi lakini
alishindwa kutambua tatizo ni lipi linalomfanya kutakiwa kurudi nchini
kwake haraka.
Asubuhi ile alitua uwanja wa Kimataifa wa ndege Stanza na msafara
ulimpokea kama kawaida ili kumpeleka Ikulu.
***********************************
“Tumsifu Yesu Kristu Baba Askofu”, Julius Kibwe alimsalimia
Muhashamu Baba Askofu Damian Begere alipomtembelea kwenye
makazi yake kama walivyokubaliana siku ya Jumapili.
“Milele amina Kibwe. Unaendeleaje?” Askofu Begere alimjibu Julius
huku akimshika mkono kumwelekeza mahali wanapokwenda kukaa
kwa mazungumzo kwenye bustani maridadi zilizozunguka makazi yale.
Makazi ya Askofu Begere yalivutia sana. Kulikuwa na usaϐi na utulivu wa
hali ya juu. Bustani zilishamiri maua ya kila aina na ya kuvutia. Kukiwa
kumetengenezewa njia maalumu za kutembelea ili kujivinjari kwenye
bustani zile, kulijaa ndege kama Tausi, Kanga na Kasuku
walioning’inizwa kwenye vivuli vya miti kwenye vitenga vyao.
Mathalini, katikati ya njia na kwenye bustani zile kuliwekwa sanamu
nzuri za kuvutia za watakatifu na taa nzuri zilizowaka na kuzifanya
sanamu zile zivutie sana. Tena hapakukosa kile wakatoliki wanaita
Groto, yaani Sehemu iliyotengenezwa vizuri kama pango hivi ambapo
kuna sanamu nzuri ya Bikira Maria na ambapo watu kama watano
huweza kukaa na kufanya ibada.
Upande wa kulia kuliwekwa sehemu inayorusha maji na kutiririka
kwenye njia zake maalumu zilizotengenezwa na kufanya kama vijito
hivi. Miti mingi ya vivuli na matunda ilizunguka makazi yale. Ukiϐika
kwenye makazi ya Askofu Begere basi ilikuwa ni vigumu sana
kutofautisha msimu wa kiangazi na wa mvua ama msimu wa joto na
baridi. Muda wote palijawa na unyevunyevu na kiubaridi. Ilikuwa ni
pepo iliyopo Stanza.
“Julius umeibuka na hili la Rais Costa kumiliki kisiwa cha kitalii huko
Uϐilipino. Limekaaje hili” Askofu Begere alimuuliza Julius katika hali ya
ucheshi.
Alirejea taarifa aliyoisoma na yeye kwenye gazeti la STANZA TODAY
lililomnukuu Julius akisema ana ushahidi usio na shaka wa Rais Costa
kumiliki kisiwa cha kitalii nchini Uϐilipino.
“Baba Askofu ndiyo maana Jumapili iliyopita nilishangaa mahubiri yako,
hayakuwa katika hali uliyotufundisha na ya ukweli. Labda wewe ndiyo
uanze kunieleza mimi nini kimekupata maana ulinijibu tu kuwa wakati
mwingine mtu huhitajika kubwaga manyanga chini”, Julius ni kijana
mdogo kiumri lakini mwenye uwezo mkubwa wa kujenga hoja katika
mijadala alimuuliza Askofu Begere kwa jicho la umakini.
“Hili lako ndilo la muhimu Julius. Ha ha ha!” Askofu Begere alisisitiza
huku akicheka.
“Baba Askofu, kwa kifupi tu ni kuwa kwa sasa tangu tuanze awamu hii
ya tatu ya Rais Costa, amekuwa akichukua pesa kwenye Kibubu Cha
Taifa kinyume na utaratibu. Amekuwa akitoa ‘Presidential Order’
kuidhinisha pesa kwa kisingizio kuwa anatekeleza miradi ya maendeleo
na kuwa taratibu za bunge ni ndefu na zinazorotesha kasi ya maendeleo
anayoitaka. Bahati mbaya bunge lina wabunge wengi wa chama chake
ambao hawataki kuhoji taarifa yoyote, ama kwa kuogopa au kwa
makusudi kwakuwa tu anayetenda hayo ni Mwenyekiti wa chama cha
Ukombozi Stanza.
Pesa hizi anazochota 25% anazichukua moja kwa moja ile 75%
inayobaki anaiingiza kwenye mradi lakini hao wanaotekeleza mradi
wanamwingizia asilimia 15% tena kwenye akaunti zake zilizopo Uswizi.
Kwa hiyo kwa mradi mmoja pesa zinazotoka kwa amri yake karibu 40%
humrudia yeye mwenyewe.
Isitoshe kila kampuni kubwa hapa nchini imekadiriwa kodi ya kihalali
kabisa na baada ya kujua ni kiasi gani kwa uhalali kampuni inatakiwa
kulipa basi kwa kutumia vyombo vyake hurekodi kwenye mamlaka ya
makusanyo ya taifa 25% pungufu ya uhalisia. Hii asilimia 25
huchukuliwa na kuingizwa kwenye akaunti zake.
Kwa maneno mengine kama kodi ya kampuni husika inatakiwa ilipwe
Milioni mia moja katika mwaka wa fedha huo basi italipa Milioni 75 na
ile Milioni 25 iliyobaki itaingizwa kwenye akaunti binafsi za Rais Costa.
Najua hayo watu wengi hawafahamu, ila nimepenyezewa na watu
ninaowaamini kutoka Idara za Makusanyo ya kodi na hata wandani wa
Rais.
Lakini pia, toka tulipoingia awamu hii ya tatu ya utawala wa Rais Costa
amejikusanyia ukwasi mkubwa kuliko aliokusanya awamu zote mbili
alizokaa madarakani. Sasa basi, ninazo taarifa za visiwa alivyonunua
huko Uϐilipino na Majengo na makazi aliyonunua huko Finland. Tena
hisa zake kwenye makampuni ya hisa ya nchi za Scandinavia pia tayari
taarifa ninazo”, Julius alimalizia.
Askofu Begere alikuwa amebaki mdomo wazi asiamini anachokisikia.
“Nimeshangaa sana Julius kama haya ni kweli. Lakini sasa huogopi
kuyatamka haya? Huogopi atakudhuru?”. Askofu Begere alihoji kwa
sauti ya chini sana.
“Ataua wangapi? Mimi nimeaga kwetu kuwatumikia wana Stanza. Kama
ni kufa sote tutakufa, hata yeye. Sintokuwa binadamu wa kwanza kufa.
Hakuna haja ya kuwa na hofu”, Julius Kibwe alijibu kijasiri.
“Kwa kweli kijana wangu kama una moyo wa kijasiri namna hiyo
nakupongeza. Si wengi wameumbwa na ujasiri huo. Mpo wachache
sana. Mimi nilisikitika sana kwa kitendo alichonifanyia Costa.
Aliamua kuzuia miradi yote mikubwa ya maendeleo ninayotaka
kuifanya. Ile yote niliyoitangaza kanisani aliizuia na imebidi nikubaliane
na matakwa yake ili iendelee.” Askofu Begere alimalizia na kutulia
kimya.
“Baba Askofu kuliko kuongea vile ni bora ungekaa kimya ama
kumsukumia msaidizi wako aongee. Kauli yako ina uzito sana na sasa si
vyema kuharibu uzito ule katika siku zako hizi za mwisho za utumishi”,
Julius aliongea kwa kumshauri Askofu Begere.
“Julius, sisi Wajesuiti tuna msemo unaosema kwa kilatini ‘dum in sua
non est super’ yaani ‘hatujamalizana mpaka tumalizane’. Askofu Begere
alimwambia Julius huku akimninia chai iliyokuwa imeletwa pale
bustanini na mmoja wa masista wa makazi yale.
“Sijakuelewa baba”, Julius alitaka ufafanuzi.
“Ha ha ha ha! The ϐight for justice is not over, not just yet. My son,
resistance to tyranny is obedience to God. What is going to unfold next
is bigger than he ever expected”. (Ha ha ha ha! Mapambano kwa ajili ya
haki hayajaisha, bado. Mwanangu, kukataa udhalimu ni kumtii Mungu.
Kinachofuata ni zaidi ya alichowahi kukitarajia maishani mwake’’),
Askofu Begere alijibu tena kimafumbo.
Alimkaribisha Chai na waliendelea na habari nyingine mchanganyiko
ikiwemo Askofu Begere kumwelezea kwa kina kisa kizima cha yeye na
Rais Sylvester Costa.
*******************************
Jesuiti, kwa kimombo wakiitwa Jesuits au kwa maneno mengine Society
of Jesus ni moja ya mashirika makongwe sana ya mapadri. Shirika hili
likiwa limeanzishwa huko Ufaransa na Mtakatifu Ignatus wa Loyola ni
moja ya mashirika yanayoheshimika sana na lenye nguvu kwenye
kanisa katoliki.
Mathalani, hata Baba Mtakatifu Francis ni zao la shirika hili akiwa ndiye
Papa wa kwanza ambaye ni Jesuiti. Wenyewe hujiita Jeshi la Mungu la
Askari wa Nchi kavu na kwenye Maji au kizungu hujiita ‘God’s Marines’.
Labda hii imetokana na asili ya mwanzilishi wao kuwa na historia ya
jeshi.
Moja ya sifa yao nyingine ni usomi wa hali ya juu. Ni wasomi wa
kiwango cha juu sana na ndio maana wana shule nyingi duniani na vyuo
vikuu zaidi ya 189 tena vyenye hadhi za juu. Chuo kama Georgetown
huko Marekani (Georgetown University), Boston (Boston Collage), Loyola
(Loyola University), Fordham (Fordham University) na vingine vingi ni
vyuo vinavyomilikiwa na shirika hili.
Inaaminika kuwa shirika hili ndilo humtii Papa kuliko mapadri wowote
wale. Wao husema kuwa wapo tayari kufa kwa ajili ya Papa na kufanya
chochote atakachowaagiza. Kiapo hiki wanachokiita Kiapo cha nne
(Forth Vow) hutakikuta kwenye shirika lolote la mapadre wa kanisa
katoliki isipokuwa kwa wana Jesuiti. Wana mengi hawa. Itoshe tu
kusema Jesuiti ni zaidi ya watawa.
*************************
Mishale ya saa tano hivi Gideoni alikuja kuchukuliwa oϐisini kwake pale
Ikulu ili akakutanishwe na Stanley Macha. Alitolewa na kuingizwa
kwenye gari siti za nyuma. Alishangaa kuona kuwa hawezi kuona nje
kwa namna yoyote ile, yaani ni kama mtu aliyeingia kwenye pipa halafu
likafunikwa kwa juu.
Ndani ya gari lile siti aliyokaa kwa juu kulining’inia kipaza sauti
ambacho aliweza kuongea na kujibiwa na waliokaa mbele. Aliuliza ni
kwanini wanamsaϐirisha katika hali ile na kujibiwa kuwa sehemu
anayopelekwa ni siri na alitakiwa asijue ni eneo au nyumba gani na
kwamba ni watu maalumu tu wanaotakiwa kujua nyumba hiyo ipo
wapi.
Gideon aliposikia hivyo akaona isiwe tabu akachukua simu yake ili
awashe Google Map na angeweza kujua anapoelekea. Alishangaa kuona
mtandao ndani ya gari lile haupatikani na hata sauti za nje hazisikii
ndani.
Gari lilianza safari na Gideon aliona ujanja ni kuanza kuhesabu kona.
Alijaribu akidhani atafanikiwa lakini kuna mahali alichanganywa hadi
biashara ile ikamshinda.
“Mkuu usihesabu kona hutaweza”, alisikika dereva akimwambia Gideon
huku akicheka. Walijua ujanja ambao Gideon angeufanya.
“Huku ndipo mnapopaita Red Square?”, Gideon alihoji.
“Ilipokuwa Red square ya zamani maana tangu juzi imetoka amri Red
square imeshabadilishwa eneo. Sabinasi kabadili na bado ni siri kubwa”,
dereva alijibu.
Gideon alihisi kuishiwa nguvu. Kwa miaka yake saba akiwa Ikulu
hakuwahi kujua Red square, moja ya nyumba za siri za Idara ya Usalama
Wa Taifa Stanza ipo eneo gani. Hata Raϐiki yake kipenzi Stanley Macha
hakuwahi kumwambia.
Walitembea kwa dakika 40 na kisha Gideon alihisi kama wanaingia
shimoni ama kwenye handaki maana gari iliinama chini kwa dakika
kama tatu hivi na kisha mlango ulifunguliwa akashuka.
Eneo lile lilikuwa na taa nyingi na madirisha lakini ambayo yalikuwa
ndani ya jengo yaani usingeweza kuona anga.
Kijana mmoja alimwongoza Gideon wakiwa wanapita milango kadhaa
iliyofunguliwa kwa alama za vidole (ϔinger prints) mpaka mlango wa
mwisho uliofunguliwa kwa kuweka lenzi ya mboni ya jicho ya mmoja
wa wale madereva.
Waliingia ndani na Gideon alistaajabu hali aliyomkuta nayo Macha.
Stanley Macha alikuwa amechoka na mwenye maumivu makali. Alikuwa
amelazwa kwenye kitanda cha chuma akiwa amefungwa mikono, kiuno
na miguu vyote vikiwa vimefungamanishwa na kitanda kile kama vile
maiti inayotaka kwenda kuzikwa.
Mbele ya nyayo zake kuliwashwa mishumaa iliyokuwa ikiunguza nyayo
zake tartiiibu hivyo kusababisha malenge lenge makubwa. Mdomoni
alifungwa riboni ya gundi iliyomfanya asiweze kutoa sauti za kilio cha
maumivu.
Inspekta Majita alikuwa akiendesha kile wazungu wanakiita ‘enhanced
interogation’ yaani mahojiano ya mateso. Mahojiano ya namna hii
hufanyika mara baada ya jitihada za kumfanya mlengwa aongee jambo
unalotaka aϐichue zinaposhindikana.
Lakini pia kwa siku za karibuni mahojiano ya namna hiyo yamekuwa
yakipigwa vita kwani humfanya mtu kudanganya au kukubali jambo
ama kukataa hata kama si kweli ili tu ajiepushe na mateso. Kwa nchi
zilizoendelea wametengeneza mifumo na teknolojia zinazoweza
kumfanya anaehojiwa kugundulika kama anadanganya ama la bila hata
kumtesa.
Mashirika mengi ya kijasusi na ya kiuchunguzi katika nchi zilizoendelea
hutumia teknolojia inayoitwa ‘Polygraph’, almaarufu kama ‘lie detector
test’ ambacho ni kifaa maalumu kinachopima na kurekodi viashiria
mbalimbali vya kimwili kama vile msukumo wa damu, mapigo ya moyo,
upumuaji, na mienendo ya ngozi wakati ambao mtuhumiwa anaulizwa
na kujibu maswali mfululizo.
Mathalani, kuna vifaa vinavyopima mapigo ya moyo ukiwa unaongea
ukweli au uongo, vifaa vinavyopima mpepeso wa macho na njia
nyingine kama zile wazungu wanazoita ‘Logical deduction’ ambazo
hazimuumizi muhojiwa lakini humpelekea anaehoji kuujua ukweli.
Pamoja na teknolojia hizi kuwepo, bado nchi nyingi duniani ikiwamo
Stanza ziliendelea kupendelea mfumo wa zamani wa mahojiano
uliohusisha mateso kwa mlengwa hadi aseme lile anayehoji anataka
kusikia. Hali hii ilimkumba Macha, aliyekuwa bosi wa wale wanaofanya
kazi hizo. Lakini Stanley Macha akiwa mtaalaamu wa yote hayo
ilishindikana kumpata kwa lolote.
Gideon alipoingia na kumkuta Macha akiwa kwenye mateso makubwa
huku akigugumia wakati Majita akivuta sigara bila hata kumtazama
Macha alipiga kelele….
“Kwa amri ya Rais simamisha zoezi hili Majita”, Gideon alifoka huku
machozi yakikaribia kumtoka.
Majita bila hata kujibu kitu alisogea na kufungua zile kamba kisha bila
kusema na mtu alitoka nje ya kile chumba. Majita alikuwa ni kama
shetani aliejivika ng’ozi ya mtu.
Gideon alimsogelea Macha na kukosa la kutamka. Alibaki akimwangalia
na Macha hakika alikuwa akigugumia kwa uchungu wa kilio alichojikaza
kisitoke nje.
“It’s ok. I have got your back”, Gideon alinong’ona.
“Familia yangu ipo salama? Joe amekamatwa?”. Macha aliuliza haraka.
“Familia zipo salama na Joe bado hajakamatwa ila Costa ametoa amri ya
Majita kukutesa hata kifo kama hutasema chochote kuhusu mpango ule.
Hivi ninapoongea na wewe amesema pia atawatuma watu China
wakamsake Joe na popote watakapoweza kumuua basi wamuue”,
Gideon aliongea kwa haraka na yeye. Hawakuwa na muda wa kupoteza.
“Umejitahidi mpaka kuϐika hapa kuniona, umejitahidi sana. Sasa
utawasiliana na Meja Kairuki Byabato wa pale makao makuu ya Jeshi,
ukiϐika mwambie ‘Sienta-Go’ ataelewa. Lakini pia Rais akikuuliza
nimekuambia nini kwa ujio wako huu mwambie ninahitaji kuongea nae.
Sio huku, Ikulu ama Idarani. Lakini niambie nani amekaimishwa
kuongoza Idara?” Macha alihoji kwa haraka.
“Sabinasi, na amepangua watu wote Ikulu. Hivi jengo hili lipo wapi
nimeshindwa kupafahamu.” Gideon alihoji.
“Majengo haya yanaitwa Red square huwa ni siri kubwa kati ya watu
wanne. Rais, Mkuu wa Idara na wale madereva wawili. Hata Inpekta
Majita hajui hapa ni wapi ameletwa kama ulivyoletwa wewe.
Sasa sidhani kama jengo hili mimi nitakuwa najua lipo wapi kwa sababu
lazima wamebadilisha na ndio utaratibu. La zamani lilikuwa mtaa wa
Khanama lakini najua mkuu mpya wa Idara akiingia cha kwanza ni
kutafuta Red square yake na madereva wake wa kuwaleta watu huku.
Huku ndiko watu huweza kutoweka na wasipatikane maisha yao yote
na watu wakadhani wamekufa kumbe wapo huku. Watu wenye taarifa
muhimu huwezi kuwaua, unawatunza lakini unawatoa kabisa kwenye
macho ya dunia na mara baada ya kujiridhisha kuwa hawana faida tena
na wewe ndio huwaua. Gideon nimekwambia kuliko uliyotakiwa
kusikiliza, muda sio Raϐiki, kaendelee na taratibu za misheni.
Ila hakikisha haukamatwi kwani mateso haya huwezi kuyastahimili
hata kwa sekunde moja”, Macha aliongea kama mzazi kwa mwanae.
“Sasa wakati nilipotaka kutoka niliona Rais Costa akisaini jalada fulani
limeandikwa Presidential Order: Order to Kill. Sikuweza soma vizuri
linahusu nini ila kulikuwa na majina na jina moja wapo ni Sylvanus
Majura, unalifahamu hili jina?”, Gideon alihoji.
“Loh, huyo ni ‘Special assassin’ wa Idara. Kwa vyovyote ni kati ya
waliotumwa kumuua Joe. Jina hilo llikuwa la kwanza ama la mwisho?”,
Macha aliuliza.
“La Mwisho”, Gideon alijibu kwa haraka.
“Basi huyo ndio kiongozi wa misheni. Sisi huandikaga kutokea chini
kwenda juu. Sasa mtaarifu Joe awe makini”, Macha alishauri.
Kabla Gideon hajaongea jambo lingine, mlango ulifunguliwa na Majita
kwa sauti ya kukoroma na yenye besi nzito alimtaka Gideon kuondoka
eneo lile.
Gideon alitoka kwa kasi akiongozwa na wale madereva na kuingia
kwenye gari lililomleta ili kuelekea Ikulu.
Aliϐika Ikulu na kukuta Rais yupo na ratiba yake ya vikao hivyo alienda
oϐisini kwake na kuingia kwenye game ya Clash Royale na kuanza
kumpa Joe taarifa zote alizokusanya siku ile.
******************************
“Habibu muda wetu kukaa hapa umekwisha kesho twapaswa
kuondoka” Joe alimwambia Habibu aliyekuwa amejilaza kitandani
kwenye kile chumba.
“Tunaeleke wapi?”, Habibu alihoji.
“Sijajua bado. Najua Korea wataanza kumsumbua Rais Costa kuanzia
kesho”, Joe alijibu.
Wakiwa wanajadiliana mara mlio wa simu wa Joe uliita kuonyesha
kuwa kwenye game yake ya Clash Royale kuna ujumbe umeingia.
Alichukua na kuanza kusoma.
Alikuwa Gideon amempa taarifa na mipango yote. Alihuzunika sana
aliposikia hali ya Macha.
“Subiri niwasiliane na Meshack kuhusu huyu Sylvanus”, Joe alimjibu
Gideon.
“Kuna taarifa gani?”, Habibu alihoji.
“Tuwe makini kuna watu wametumwa kuja kunitafuta ili waniue. Bahati
nzuri wewe sio tageti wa Rais Costa. Sasa subiri niwasiliane na
Meshack”, Joe alijibu.
Joe alianza kumpigia Meshack Simu kwa njia ya WhatsApp kwenye
namba ambayo Meshack huitumia kwa kazi maalumu. Kwa kawaida
simu za WhatsApp ni salama kwasababu maongezi yake hayawezi
kudukuliwa na serikali au mashushuhu kwasababu tu zina mfumo wa
usalama wa usimbaji ϔiche wa mpigaji au mtumaji ujumbe na mpokeaji,
yaani end-to-end encryption. Simu iliita na mwishowe akaipokea.
“Kaka”, Meshack aliita.
“Got an intel kuwa Sylvanus ametumwa kuja kunimaliza.
Unamfahamu?”, Joe alihoji.
“Ndiyo. He is the master of silent killing. One of the worst assasins in
Stanza, I can conϐidently argue”. Meshack alionekana kuongea kwa sauti
ya taratibu.
“Now, you need to deal with him before he boards to China”, Joe
alimwambia Meshack kifupi.
“Do you mean killing him? No, that I can’t guarantee you Joe. He is a
very intelligent agent, If I poke him, I may compromise everything here.”
Meshack alijibu
“Meshack, wewe ndio ulikuwa unamlinda Rais Costa, iliwezekanaje
awekwe mtu asiye hodari kumlinda Rais? Macha ameniagiza nikwambie
‘umhandle’ Sylvanus”, Joe alimwambia Meshack.
Meshack alikaa kimya kidogo. Alitafakari ni namna gani anaweza
kumuua Sylvanus, kwanza bila yeye kuwahiwa na pili bila kujulikana.
Aliona sasa hapo ametiwa majaribuni na suala hili litaweka Maisha yake
kwenye mstari wa mauti.
“Hii ni mbwa kula mbwa kaka”, Meshack alinong’ona akijua Joe
hamsikii.
“Vyovyote utakavyoiita. Just do it” Joe wakati huu alionekana kuongoea
kwa kutoa amri. Alikata simu.
Mara baada ya Joe kukata simu alipokea ujumbe mwingine kwenye
simu yake. Aliusoma kwa makini kama vile unampa maelekezo Fulani
aliyopaswa kuyafuata kwa makini. Wakati huo Habibu alikuwa
anamuangalia kila kitu, akishangazwa na sura ya Joe iliyoonekana kuwa
na hasira mara baada ya mazungumzo yake na Meshack.
Mara baada ya Joe kusoma ujumbe ule na kumaliza, alimwambia Habibu
kuwa asimame waondoke. Habibu alitaka kutouliza, lakini akajikuta
anashindwa kuvumilia.
‘’Joe, ni nini kinaendela? umeshajua tunakwenda wapi na hatua gani
inafuata’’? Habibu aliuliza maswali mfululizo.
‘’The transfer window has just opened. Expect some new powerful
signings soon. Stanza will be turned upside down soon enough. We are
going to reclaim our country, the country that the founding fathers and
mothers fought to liberate from the yokes of colonialism. We cannot
allow to be colonized by our fellow countrymen’’.
(Dirisha la Usajili limefunguliwa. Tarajia uhamisho wa wenye nguvu hivi
karibuni. Stanza itageuzwa juu chini hivi karibuni, ingawa bila kumwaga
damu ya mtu. Lazima tuichukue nchi yetu, nchi ambayo wazee wetu
waliipigania kuondoa minyororo ya ukoloni. Hatuwezi kuruhusu
kufanyiwa ukoloni na Wanastanza wenzetu’’, Joe alimjibu Habibu kwa
mafumbo.
‘’So be it’’, Habibu hakuongezea neno bali kujibu kwa ufupi.
*************************
Usiache Kufuatilia Sehemu Ya 14 Itakayokujia Siku Ya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asanteee sana, ila haujamalizia tusubiri siku ya..?
 
Et Rais hugawa hela ! [emoji4]

[emoji28][emoji28], wapi JOHN COSTA , mutu ya nyanza !

Sent using Jamii Forums mobile app
Kumbuka
Endapo tutaendelea kuhuwianisha yaliyomo ndani ya simulizi na mazingira halisia tutakuwa tunavunja sheria za nchi.Ikumbukwe kwamba Hii ni simulizi
Na tuache kutaja majina ya watu wanaotambulika kwenye jamii zetu. Tukiendelea hivyo huenda ikawa na ......ending of Presdent and I.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haha hii hadithi ina viwango vya series za mbele za intelligence
 
Dahhh huyu mtunga hadithi huko anapo ipost amejihakikishia kwamba yupo salama kweli !!?
 
Ni dhahma
The President And I(Mimi Na Rais)- Sehemu Ya Kumi Na Mbili

Lello Mmassy  February 12, 2019



Stanley Macha Ahojiwa. Askofu Begere Amvuruga Julius Kebwe


“Macha, mimi si mpelelezi wa shauri lako hili, lakini kwa heshima uliyokuwa nayo ndani ya vyombo vya ulinzi na usalama nimekuja mwenyewe. Nimekuja kusikia kutoka kwako mwenyewe, nataka uniambie ni nini kilikusibu, na utueleze kwa mapana ipi ilikuwa nia ya wewe na wenzako kutaka kumpindua Rais halali wa nchi yetu aliyechaguliwa kidemokrasia na kwa kufuata matakwa ya Kikatiba na anayeungwa mkono karibu na watu wote.


Mlikusudia nini na unashiriki wewe na nani? Ni vyema ukasema yote na kuwataja wenzako kabla njia nyingine hazijaanza kutumika’’, Alikuwa ni Inspekta Mabubi Majita akimhoji Stanley Macha kwa mara ya kwanza huku akimshushia na mkwara kidogo.


Stanley Macha alichukuliwa na kuwekwa ndani ya nyumba maalumu ya siri ya Idara ya Usalama wa Taifa Stanza, wenyewe wakiita‘safe house’ iliyopo karibu na fukwe za bahari katika eneo linalofahamika kama Khanama akiwa ameshikiliwa huko kwa kosa la uhaini kwa kushirikiana na Joe.


Pamoja na nyumba hii kuwa maeneo ya makazi wanapoishi matajiri na viongozi wa ngazi za juu serikalini, hakuna aliyekuwa anafahamu matumizi yake na wala hakuna aliyewahi kuitilia shaka. Hata baadhi ya viongozi wa juu wa serikali hawakuwa wanafahamu kazi yake zaidi ya maafisa usalama walioingia na kutoka mara kwa mara kwa shughuli maalumu.


Kabla ya kutumia njia za mateso, Jeshi la Polisi liliamua kujaribu mbinu za kidiplomasia kwani wanafahamu wazi ugumu wa kumfanya mwanausalama kusema lolote ambalo hataki kusema. Kuna wanausalama wengi hufa kwa mateso bila kusema hata tone la siri ambayo kwao wanaona haipaswi kumfikia mtu asiyepaswa.


Inspekta Majita alikuwa maarufu na mashuhuri sana katika kufuatilia masuala ya kiuchunguzi. Ni miongoni mwa ma afisa wa jeshi la Polisi watatu tu Stanza waliopata mafunzo nchini Pakistan, Cuba, Marekani na Israeli. Nchi zote katika nyakati tofauti.


Mathalani, Inspekta Majita ni miongoni mwa wataalamu wachache walioitwa kuunda kikosi cha kuchunguza tukio la ulipuaji wa balozi za Marekani katika nchi za Afrika ya Mashariki yaani Tanzania na Kenya mwaka 1998. Ni baada ya tukio lile Marekani ilimpa nafasi ya kwenda kuongeza ujuzi katika shirika lao la uchunguzi, Federal Bureau of Investigation maarufu kama FBI.


Inspekta Majita alikuwa ni mrefu, watoto wa mjini wangesema amepanda hewani, alipenda kufuga ndevu nyingi na kuvuta sana sigara hasa anapokuwa kwenye kazi maalumu. Alipendelea pia kuvaa shati lenye mikono mirefu na kisha kuikunja huku akivaa mkononi saa yake inayotumia mapigo ya moyo kutembea. Sauti yake ilikuwa nzito sana na yenye kukwaruza, hali hii ilichangiwa na uvutaji sana sigara uliopitiliza tangu akiwa mtoto wa miaka 16 tu.


Majita hakuwa muongeaji sana na hakuonekana mara kwa mara, hata serikalini na kwenye taasisi za kiusalama, wanausalama wenzake humuita Kakakuona, kwasababu kuonekana kwake kulikuwa kwasababu maalumu na kwa kazi maalumu tu. Alipendelea kufanya kazi bila kuonekana na watu wala vyombo vya habari.


Inspekta Majita hakuwa na magenge ya marafiki ndani au nje ya taasisi za usalama, alipendelea kuwa na mahusiano ya kikazi pekee. Tabia hii ilisababisha asioe na hakuwa na mtoto. Kwasababu hiyo hakuwa amezoeana na Stanley Macha hata kidogo japo walikuwa wakijuana na mara kadhaa Stanley Macha akiwa kama bosi wake alishawahi kumtuma kazi kadhaa na alizitekeleza vyema.


Stanley Macha anamfahamu fika inspekta Majita na uwezo wake. Leo ni zamu yake kuwekwa kitimoto.


“Majita, unajua unachofanya hapa ni kutaka kukamua maji kutoka kwenye mwamba. Hakuna mpango kama huo”, Macha alimjibu Majita wakiwa wamekaa meza ya mahojiano.


“Labda mimi ni nabii Mussa, huwezi kujua Macha. Nahitaji maji yatoke kwenye mwamba niwanyweshe wana wa Mungu. Rais Costa anahitaji majibu sasa, ukisema hakukuwa na mpango kama huo mimi siwezi kukuelewa na Rais hawezi kunielewa pia”, Majita nae alijibu kwa utaratibu huku akipuliza moshi wa sigara kutoka puani.


“Unajua nilitii na kuwa mkimya kwa sababu nilitaka kujiridhisha lakini ukweli ni kuwa mimi na Joe tulikuwa katika mpango wa kumpima Pius kama kweli yupo thabiti katika kumlinda na kumtetea Rais na Bahati nzuri matokeo ndio haya tumeona alivyo”, Macha alimjibu Majita.


“Macha stop that nonsense man. Both you and I know that is not it. Unampima mnadhimu mkuu wa Jeshi kama ana utii kwa Rais? Unampima kwa kibali cha nani? Kwanini? Kwanini umpime kwa njia hiyo?” Majita aliuliza huku akisimama na kuelekea dirishani.


“Majita zipo sababu nyingi. Kwanza ikumbukwe Pius yupo nafasi ya pili baada ya mkuu wa Majeshi na labda siku moja au siku za usoni yeye atashikilia nafasi hiyo kubwa ndani ya jeshi. Kwa kumbukumbu tu, mipango ya uasi wa jeshi miaka miwili iliyopita Pius alikuwa karibu na mkuu wa kikosi cha mizinga pamoja na anga ambao ilikuja kuthibitika kuwa ndiyo waliokuwa wapanga mipango ya kutaka jeshi liasi.


Ni mimi na Joe ndio tuliuzima mpango ule, unajua historia hiyo. Pius sasa hivi anahusika katika misheni ya kisualama ya Korea Kaskazini, yeye ndiye atakuwa akihusika sana kama kiungo ni muhimu tukajua ama kwa hakika yupo thabiti kumtetea Rais na kulitetea taifa na hana tamaa”, Macha alimalizia utetezi wake wa kuungaunga usio hata na kichwa wala miguu.


“Macha, wewe ndio ulinipendekeza kwa mara ya kwanza kwenda Cuba kusomea haya mambo. Ukanipeleka na Israel na Pakistan. Sasa leo unaponigeuza poyoyo unanikosea sana bosi wangu. I need the truth and only truth. Haya rudia tena”. Majita alimjibu Macha huku akiwa dirishani anaangalia nje. Hakuwa hata anamwangalia, alimpa kisogo. Majibu ya Macha yalimkera.


“Majita, unataka kuamini kweli kuwa mimi naweza kupanga njama za kumpindua Rais Costa? Kwasababu zipi? Ili nipate nini? Mimi nilimnusuru kwenye tukio la kwanza halafu tena leo nipange kumpindua? Come on guys mnanikosea sana. Hata Joe mnamkosea sana anafanya kazi kubwa iliyowashinda wote kwenye serikali hii”, Macha nae alijibu kwa dharau.


“Kama kweli ilikuwa ni kumpima Pius kwanini simu yako uliifanyiaHard reset? Kwanini taarifa zako za simu na za mawasiliano hazipatikani popote. Umezifuta. Faili hili hapa zimetoweka dakika tatu kabla ya kusimamishwa kwenye korido za Ikulu kwa kumtumia kijana wako Daudi.


Amefuta mpaka kwenye server za idara. Nikaagiza kufanyike hard backup nikakuta hakuna kitu. Kila kitu umefuta halafu unaniambia haukuwa mpango wenye nia mbaya? Macha ninakuheshimu, don’t push me to the corner that you would not wish for. Heshima ninayokupa itunze”, Majita aliongea kwa hasira jambo lililomshtua Macha.


“Majita, I have worked in intelligence community since I was in high school, keep that in mind. Maswali unayoniuliza hayana maana. Kuhakikisha taarifa zangu zipo salama ni kosa? Kwani hiyo si kanuni namba moja uliyofundishwa?”, Macha nae alijibu mapigo kwa kufoka.



“Sio ndani ya muda mfupi namna ile toka ujulikane mpango wako ovu” Majita alijibu.



“Kwa hiyo unasemaje”, Macha alijibu kwa hasira


“You are leaving me with no option than applying enhanced interrogation techniques on you Macha. I know both you and I do not wish for that”, Majita alijibu.


“Nimeihudumia serikali hii kwa miaka 30. Nimemlinda na kumtetea Rais Costa kwa mwaka wa 12 sasa. Kama hii ndiyo gharama ya uaminifu wangu kwa Mh Rais na kwa taifa hili, basi nipo tayari kuilipa”. Macha alijibu kwa kupayuka huku Inspekta Majita akiwa anatoka nje na kutotaka kumsikiliza.


“I will show you some love and you’ll fall in love with the show. I will be back to say hello soon”, Inspekta Majita alijibu na kutupa kipisi cha sigara chini na kisha kutoka.

**********************************


조에서 뭐 들었 니? o-eseo mwo deul-eoss ni? (Umesikia lolote kutoka kwa Joe?). Rais Kim alimuuliza Waziri En wakiwa wamesimama kibarazani kwenye jumba la Ryongsong, makazi maalum ya Rais Kim.


아니요, 그들이 베이징에 안전하게 도착했다고 확인되었지만 그의 탁월함aniyo, geudeul-i beijing-e anjeonhage dochaghaessdago hwag-indoeeossjiman geuui tag-wolham(Hapana Kamaradi, japo nilithibitishiwa kuwa walifika salama Beijing), Waziri En alijibu huku akiwa ameinamisha kichwa kidogo.


이것은 어색합니다. 코스타 대통령은 핵무기에 대한 생각을 좋아하지 않았습니까? igeos-eun eosaeghabnida. koseuta daetonglyeong-eun haegmugie daehan saeng-gag-eul joh-ahaji anh-assseubnikka? (Hii ni ajabu sana, au Rais Costa hakupenda wazo letu la silaha za kinyuklia?) Rais Kim alionesha mashaka yake kwa ukimya wa serikali ya Stanza.


나는 그의 탁월함을 확신하지 못한다.naneun geuui tag-wolham-eul hwagsinhaji moshanda. (Sina hakika Kamaradi), Waziri En alijibu kiufupi.


그것을 찾으십시오 . Joe와 논의한 내용이 여전히 유효한지 알고 싶습니다. geugeos-eul chaj-eusibsio. Joewa non-uihan naeyong-i yeojeonhi yuhyohanji algo sipseubnida. (Fuatilia na uje unihakikishie kuwa tuliyoyaongea na kuyapanga na Joe yapo katika mchakato au kuna mabadiliko yoyote), Rais Kim alimalizia.

Waziri En aliondoka.

******************************


Toka siku ile Waziri wa Sheria na Masuala ya Bunge bwana Kinyamagoha afukuzwe na Rais kwa sababu ya kushindwa kusukuma kwa nguvu muswada uingie bungeni wa kubadili umri wa mtu kugongea u Rais kutoka miaka 40 mpaka 55, hakuwahi hakuonekana hadharani tena.


Alitoka pale na moja kwa moja alielekea kijijini kwao Kwamchae ili kwenda kufanyiwa “maarifa”. Kama kuna mtu dunia hii aliamini uchawi na uganga basi Kinyamagoha aliongoza.


Aliamini misukosuko ile ni kwasababu mwaka huu hakuwa ametoa kafara. Kafara ya Kinyamagoha ilihusisha watoto wachanga wasiozidi umri wa siku moja. Kinyamagoha akishirikiana na baadhi ya manesi anaowalipa pesa nyingi aliua watoto hasa wakati mama anapokuwa anajifungua. Wakati ule huhakikisha kwa namna yoyote hata kwa kumziba mtoto asipumue ama vinginevyo basi huua mtoto kama sehemu ya hitaji la waganga wake.


Baada ya kuua na mama aliejifungua kuambiwa na kuhuzunika nesi hujifanya anaenda kumsafisha ili wamfunge kwa mazishi lakini kabla ya humchanja yule mtoto na kutoa damu kiasi ambayo kuikinga na kupelekwa kwa Kinyamagoha kisha kuipekea kwa mganga.


Iikuwa ni ngumu kuamini hasa kutokana na tabia ya Kinyamagoha kupenda kuandaa makongamano ya dini akihusisha maaskofu ama mashehe. Tena mara kadhaa utamuona akiwa misikiti mbalimbali akishiriki swala ya Ijumaa ama kusaidia vituo vya watoto wasiojiweza.


Kinyamagoha alikuwa fisi ndani ya ngozi ya kondoo. Lakini pia, Kinyamagoha alikuwa ni kama alama ya wanasiasa walio wengi na hata wanajamii walio wengi kwa ujumla. Wengi walikuwa na dini zao lakini hawakuacha kushiriki masuala ya kishirikina au vinginevyo, kama si ya kishirikina basi waliendelea kutekeleza dini zao za asili, maarufu kama dini za Kiafrika zinazohusisha uganga na matambiko ya aina mbalimbali

********************************


“Tunamshuru sana Mh. Rais na serikali yake kwa kukubali kutoa kibali cha Ujenzi wa hospitali kubwa kule Kilungululu. Hii siyo tu inaonyesha nia njema ya Rais katika kuunga mkono jitihada za kanisa, lakini pia nia yake njema ya kutaka wananchi wa Stanza wapate huduma bora za afya.


Ni rai yangu basi waamini wenzangu kumuunga mkono Mh. Rais hata katika mambo mengine anayoyafanya ambayo ni tija kwa taifa letu. Hii tabia ya kumzodoa, kumkatisha tamaa na kumtusi tuiache, haisaidii wala haijengi.


Wapo wanaosema hafuati sheria wala katiba, tena haheshimu utawala bora. Mimi nasema Roma haijajengwa kwa siku moja, tutafika huko. Sasa hivi sio muda wa kufanya siasa, ni muda muafaka sasa wengine wote tuweke mikoba yetu na ya vyama vyetu chini tushirikiane na tuunge mkono juhudi njema za Mh Rais anazofanya kwa maslahi ya taifa letu. Hata nafsi tatu za Mungu hutenda kazi pamoja, kama kila moja ingekuwa ina kazi ya kumkosoa mwenzake basi hata leo tungekuwa hatujakombolewa”, Askofu Damian Begere aliendelea.


Ilikuwa ni siku ya Jumapili akiwa katika ibada ya kiaskofu akitoa mahubiri yake kikanisa huitwahomilia. Hakuna aliyeamini kama kweli maneno yale anayatamka Askofu Begere. Watu kanisani walikuwa wakinong’onezana sana wakiulizana kulikoni. Hakuna aliyemzoea askofu Begere na mahubiri ya mtindo ule yenye sifa kedekede kwa Rais Costa. Waswahili husema usilolijua ni sawa usiku wa giza.


Kama ilivyo ada, baada ya ibada ya misa Askofu hutoka nje ya saktestia(chumba maalumu cha Padri au Askofu kujiandaa kabla na baada ya ibada) na kisha kusalimiana na baadhi ya watu na kuongea nao mawili matatu.


Julius Kebwe, kiongozi mkuu wa siasa za upinzani nchini Stanza alienda kumsalimu Muhashamu baba Askofu Damiani Begere.


“Tumsifu Yesu Kristu baba Askofu”, Julius alisalimia huku akibusu pete ya askofu.


“Milele amina Julius. Haujambo?” Askofu Begere aliitikia huku akitabasamu.


Askofu Begere na Julius ni marafiki wakubwa. Urafiki wao ulianza tangu Julius akiwa kiongozi wa chama cha kitume cha wanafunzi wakatoliki mashuleni kijulikanacho kamaSYCMS (Stanza Catholic Movement for Students). Ni kutokea huko askofu Begere alimkuza Julius tena akitaka amfanye aingie seminari na kuwa padri lakini Julius alikataa.


Baada ya Julius kuingia kwenye siasa, askofu Begere amekuwa msaada mkubwa sana katika kumtia moyo na kumpa ushujaa na kumtaka kutoogopa kusimamia anayoamini ila tu iwe haki na kweli. Askofu Begere ni mtoa hamasa mkuu kwa Julius.


“Baba leo umeniacha njiani. Sijakuona kabisa”, Julius alianza kumtania askofu Begere.


“Siku zetu zinakaribia kwisha Juli”, Askofu Begere nae alijibu kiujanja kwani alijua Julius anamaanisha na kulenga nini.


“Lakini siku zikikaribia kwisha si ndo mnatakiwa wazee mtuachie wosia?” Julius nae alidodosa harakaharaka.


“Sometimes, you need to compromise for a greater cause”, askofu Begere alijibu kiutu uzima.


“Should I compromise as well?”, Julius nae alihoji.


“Njoo nyumbani tuzungumze Julius”, Askofu Begere alimwalika Julius kwenye makazi yake.


Julius alitabasamu na kumuhakikishia askofu kuwa ataenda kuonana nae kesho yake siku ya Jumatatu. Maswali ya Julius yalimwingia Askofu Begere na hakika aliona alichoongea kinajifunga sana na uhalisia wake na uhalisia wa mambo pia. Ila angefanyaje?

Anataka aonane na Julius.

*************************************


Joe alimwita Habibu asogee karibu na simu yake ili aweze kusoma mazungumzo watakayokuwa wanaandikiana Joe na huyo mtu mwingine kupitia game ya Clash Royale.


“Hii application inaitwaje Joe?”, Habibu alipoona tu kwanza aliuliza.


“Mapema kwa sasa wewe kufahamu ila subiri tuone kama atajibu kwanza”, Joe alimjibu Habibu huku akiwa ameandika salamu akisubiria jibu.


“Na huyu unayewasiliana nae ndio anaitwa Saddam Hussein?”, Habibu alihoji kwa mshangao.


“Hapana. Hilo ni jina analotumia huku”, Joe alijibu na ghafla ile salamu yake ilijibiwa.


“Aisee nimekwama na sijui naanzia wapi. Nimeambiwa Meshack nae kashapigwa pini, vipi Tigerwamempeleka wapi?” Joe aliandika kwenye ujumbe.


“Tiger yupo kama sio nyumba namba 3 basi ni wamempeleka red square”. Yule mtu alieandikwa kama Sadam Hussein alimjibu Joe kwa ujumbe.


Muda wote huo Habibu nae alikuwa akifuatilia mawasiliano yale akiwa ameachwa njiapanda asijue Joe anaongea na nani ila alijua nyumba namba 3 na red square ni kati ya nyumba za siri za Idara ya Usalama wa Taifa Stanza, kizungu wanaziitasecret detention facilities au kama zinatumika kwa kuhifadhi mtu kwa ajili ya usalama wake huitwa ‘safe houses.’


Alijaribu kuuliza Tiger ndio nani lakini Joe alimwambia atamwambia asijali.


“Kwa hivyo haujapata kujua chochote kinachoendelea kwa Tiger?”, Joe alihoji.


“Ndio, si unajua Sabinasi ndio sasa kapewa kitengo? Anajiona yeye niIgor Kostyukovu, pumbavu sana. Taarifa anazificha balaa”, Yule mtu alieandikwa kama Saddam Hussein alijibu.


Igor Kostyukovu ndio mkuu wa Idara ya Inteligensia ya Taifa la Urusi. Mmoja kati ya jasusi nguli duniani.


“Hakikisha familia yangu haiguswi Saddam. Wewe sasa ndiye uliebakia kunisaidia kumalizia kugurudumu hili. Nimeshapoteza mengi na siwezi kurudi nyuma maana haitosaidia tena. This time around ni mimi ama yeye.” Joe aliandika.


“Sawa Che, lakini huoni kama hakuna namna nyingine? Kwanza nakuomba mwache Habibu arudi. Hakuna sababu ya kumuharibia maisha huyo kinda”, Yule aliyejiita Sadam aliandika.


Joe alimwangalia Habibu aliekuwa akisoma kila kitu. Habibu alipoona ameangaliwa alitikisa kichwa kuashiria kuwa hataki kurudi na anataka awe pamoja na Joe.


“Una hakika Habibu”, Joe alimuuliza.


“Ndiyo”, Habibu alijibu na kupeleka macho kwenye simu ya Joe ili aone maongezi yataendeleaje?


“Habibu hayupo tayari kurudi Stanza.Ameamua kuendelea na mkakati huu”. Joe alimuandikia Saddam.


“Che, nitakurudia baadae kidogo” Saddam aliandika na kutoka hewani.


“Tiger na Che ndio kina nani?”, Habibu alihoji baada ya kuona la Sadam Hussein hajibiwi.


“Tiger ni Stanley Macha na Che Guevara ni mimi”, Joe alimjibu kiufupi.


“Na huyo Sadam Hussein je?” Habibu aliuliza kwa hamu kubwa.


“Sadam Hussein ni Gideon”, Joe alijibu na kumwacha Habibu hoi asiamini alichosikia.

*******************************


Gideon Kalumanzila, mshauri wa karibu na kipenzi cha Rais Sylvester Costa na Joseph Kaduma ni marafiki wa siku nyingi. Urafiki wao haukuwa ukifahamika sana miongoni mwa wengi katika serikali ya Rais Costa. Hii ilitokana na ukweli kwamba ni watu waliokuwa wakisukuma agenda nyingi nyuma ya pazia katika serikali ya Stanza hivyo waliafiki kutokuweka wazi urafiki wao.


Ilikuwa ni ngumu kufatilia uhusiano wao na kujua umeanzia wapi maana kwenye rekodi zao hakuna mahali inaonekana kufahamiana kwa namna yoyote ile. Kuanzia makabila yao, shule walizosoma, vyuo na nchi walizowahi kuishi hakuna mahusiano hata kidogo. Ni hali hii iliwapa nafasi nzuri sana ya kusukuma mambo serikalini na mtu asijue kabisa kama ni nguvu ya pamoja.


Si hivyo tu, hata mitazamo yao mbele ya viongozi wenzao wa Stanza ilitofautiana sana. Yeye Gideoni alionekana kama mtu mwenye kuunga mkono kila haja ya Rais Costa wakati Joe yeye huhoji kila suala na wakati mwingine kupingana na Rais Costa.


Si mara moja wala mbili Gideon alionekana kumchongea Joe kwa Rais Costa ili achukuliwe hatua za kinidhamu katika masuala mbalimbali. Ni yeye aliyeshauri na kushupalia haswa Joe avuliwe ubalozi na kupewa kesi ya uhujumu uchumi iliyomtesa kwa miaka miwili. Jambo hili lilifanyika kwa umaridadi mkubwa ili Gideon azidi kuwekwa karibu na Rais Costa.


Kwa macho ya nje, Gideon alifanikiwa sana kujitenga na Joe na hakika kama tungekuwa kwenye medani za kishushushu basi Gideon alifuzu viwango vyote vya kuitwaundercover agent. Joe alihakikisha Gideon hagunduliki hata kwa thumni na hilo walifanikiwa sana.


Watu hawa walijuana vipi?


Ilikuwa ni katika miaka ya 1991 wakati Joe akichukua shahada ya Uzamili katika Diplomasia ya Kimataifa kutoka chuu kikuu chaWarwick huko Uingereza na Gideon akichukua shahada ya Uzamili katika Sayansi ya Siasa kutoka chuu kikuu cha Melbourne huko Australia walipokutana katika fainali za kombe la dunia la mchezo wa Rugbyzilizofanyika Ufaransa.


Gideon akiwa miongoni mwa waliounda kikosi cha timu ya Australia yeye Joe alikuwa ni mmoja wa kamati ya ufundi kwenye timu ya Uingereza. Ni katika mechi ile ambayo Australia waliibuka mabingwa wa dunia kwenye mchezo wa Rugby na kwa shauku kubwa Joe alipenda kujua muafrika mmoja tu aliyekuwa akiunda timu ile iliyoibuka na ushindi alitokea wapi.


Joe, alishangaa alipojua kuwa Gideon ni Mstanza. Gideon alikuwa ni Mstanza pekee labda mpaka nyakati hizi aliewahi kushiriki kombe la dunia la mchezo wa Rugby na timu yao kuibuka kidedea.


Ni baada ya mechi ile Joe aliongea na Gideon na kuanzisha mahusiano ya kirafiki. Japo hawakuwa wakiwasiliana mara kwa mara lakini mahusiano yao yalidumu. Ni Joe alieanza kurudi Stanza na kuingia serikalini. Baada ya miaka mitano Joe akiwa kwenye mkutano wa kimataifa Brusells Ubelgiji alikutana na Gideon kwenye moja ya migahawa ambapo wakati huo Gideo alikuwa Ubelgiji akifanya tafiti.


Joe aliongea kwa kirefu sana na Gideon juu ya siasa za Stanza na ni hapo Joe alivutiwa sana na mitazamo ya Gideon juu ya maendeleo ya nchi za kiAfrica. Alimsihi Gideon arudi Stanza na angefanya kila jitihada kumfanya awe mshauri wa Rais kwani aliona kabisa mawazo yake yangeisaidia Stanza kwa namna nyingi.


Gideon alirudi Stanza na kuteuliwa kuwa mshauri mdogo wa Rais Costa katika masuala ya kimataifa kwa ushawishi wa Joe. Wakati huo urafiki kati ya Rais Costa na Joe ulikuwa katika viwango vya hali ya juu labda kuliko mtu yeyote katika serikali ya Rais Costa.


Mienendo ya siasa na uendeshwaji wa nchi ya Stanza vilimchosha sana Gideon. Aliona ni bora arudi zake ughaibuni akaendelee na mambo yake kuliko kukaa kwenye nchi ambayo ushauri wa kitaalamu unaonekana ni takataka na badala yake umbea ndio unathaminiwa.


Joe alimsihi Gideon kuwa hapaswi kuondoka badala yake yafaa abaki ili wasaidiane kurekebisha hali ya utawala nchini Stanza. Ni hapo ndipo walipokubaliana namna bora ya kufanya.


Wakati wakiwa katika mpango ule ndipo Rais Costa alipoanzisha mpango wa yeye kuendelea kubaki madarakani kwa muhula wa tatu kwa kupeleka marekebisho ya katiba bungeni. Joe alipingana nae na kusababisha chuki dhidi yake na Rais Costa.


Joe alimsisitiza Gideon hata katika hali ile asiache kuwa karibu na Rais Costa na kuhakikisha analinda urafiki na ukaribu wake na Rais hata hapo muda muafaka utakapofika. Gideon alifanikiwa sana katika hilo na hakika kama kuna watu Rais Costa anawahusudu basi Gideon ni nambari moja.


Ni Gideon na Stanley Macha waliohakikisha wanamrudisha Joe kwenye picha na kumfanya aongoze ujumbe kule Korea Kaskazini. Baada ya yote kutokea ni yeye Gideon amebakia kama kimbilio la mwisho na mtu pekee anaeweza kuifanya misheni hii ya kumtoa Rais Costa madarakani ikamilike ama ishindikane. Gideon Kalumanzila, macho yote ya Joe, Habibu na Stanley Macha yanamwangalia yeye.

***********************************


Joe na Habibu waliendelea kubaki katika ardhi ya China. Walichagua kupumzika katika mgahawa waShenang, uliojengwa pembezoni mwa mto Chachiu ambao una vivutio vingi ikiwemo aina mbalimbali za ndege na maua.


Pamoja na kuwa katika msukumo mkubwa wa kiakili kufikiria ni hatua gani wangefuata baada ya mpango wa awali kukwama, Joe na Habibu waliamua kupumzika katika eneo hilo kusafisha akili zao na kupata mawazo mapya.


Wakati wakiendelea na tafakuri na kupata chakula cha mchana, Joe alisikia milio miwili tofauti katika simu yake kuashiria kuingia kwa jumbe mbili kwa mifumo miwili tofauti jambo lililomshtua kidogo.


Kupitia program ya Clash Royale, alipokea ujumbe kutoka kwa Gideon ulioandikwa kwa kifupi tu ‘’I have got an idea, let the movie begin. The plan B is taking off’’. Gideon alikuwa amemrudia Joe kama alivyomuahidi hapo awali.


Wakati Joe akiendelea kutafakari ujumbe wa Gideon, alikumbuka kuwa kuna ujumbe mwingine uliingia katika simu yake. Alipangusa kioo cha simu yake kwa kushusha chini na aliona ujumbe kutoka kwa Waziri En ukimuuliza ni nini kinaendelea na kwanini hawajasikia kutoka Stanza tangu waondoke Korea Kaskazini.


Ujumbe wa Waziri En ulitumwa kwa njia mahsusi, ni simu ya Joe peke yake iliwezeshwa kwa codesmaalumu ambazo ingeweza kupokea ujumbe akiwa sehemu yoyote duniani bila kujali kuwa ana mtandao au hana, hata kama amezima simu yake. Ujumbe ungekuja na mhuhusika akishausoma, basi ungetoweka katika simu yake. Ili aweze kujibu, ingempasa abofye namba maalumu alizopewa na kujibu kisha ujumbe wake ungefutika pia na kutoacha aina yoyote ya hustoria kuwa watu wao walishawasiliana.


Joe alikuwa na jumbe mbili za kujibu kutoka watu wawili muhimu katika kuleta matumaini mapya ya mkakati wa kuleta mabadiliko ya kiutawala nchini Stanza.

********************************

Gideon Amepata Plan Gani? Joe Amepokea Taarifa Zipi Kutoka Kwa Waziri En?.Sehemu Ya 13 Itakujia Ijumaa.

USISAHAU KU 'LIKE' NA KU 'FOLLOW' Ukurasa wetu



Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom