Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,171
- 34,394
Nahisi yupo kajibadili id
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Lol unahisi !!? Kwanini uhisi wakati nimtu wako " !!? Ulipaswa kujua nasio kuhisi ...(nimestaajabu kidogo )
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkojoooooo[emoji85][emoji85][emoji85][emoji85]niliweka alama za nyayo zangu ili nisipotee
Tatizo unapotea sana ndio mana nakusahau[emoji30][emoji30] Shunie shangazi umewaza je kutoniita mwanao nije kupata huu utamu,?
Natamani nimzibe mdomo Joe asiendelee kumwamini huyo jamaa dah,
Sent using Jamii Forums mobile app
Tatizo unapotea sana ndio mana nakusahau
Tayari mkuu " .. your most welcomeAjahahaha ngoja nikucheki mie
OkDaah mpaka February ..si-nitakufa kwa arosto !!?
Haya bwana muandishi asante sana
Sent using Jamii Forums mobile app
The President And I(Mimi Na Rais)- Sehemu Ya Kumi
Lello Mmassy January 24, 2019

Kikulacho Ki Nguoni Mwako
“Mwambieni yule binti aje sasa ofisini”, Rais Costa alitoa agizo kwa mmoja wa wasaidizi wake kuwa Ketina aitwe ofisini kwake. Alitoa maagizo hayo huku akiingia ofisini kwake akitokea kuongea na askofu Begere.
“Kimweri, sijasikia kuhusu kina Joe. Kwa ratiba uliyonipa wanahitajika wawe wameshafika Beijing na Joe kuwasiliana nami. Nahitaji kusikia kutoka kwao kabla sijawasiliana na Mr. Kim”. Rais Costa alikuwa akiongea na simu huku akiketi kwenye kiti chake ofisi yake maalum pale Ikulu.
“Mh. Rais unachosema ni kweli lakini ni kuwa hawakuja na ndege niliotarajia waje nayo. Nimewasiliana na ubalozi wa Korea hapa China ambao ndio nashirikiana nao na wameniambia Joe wanakuja na ndege nyingine na kuwa wapo salama na ndani ya muda mfupi ujao watawasili hapa ubalozini”, Balozi Kimweri alimjibu Rais Costa.
“Sawa. Keep me posted”, (endelea kunijuza mambo yatakavyoendelea), Rais Costa alijibu kwa ufupi.
Rais Costa aliweka simu yake chini na kuhema kwa nguvu. Pamoja na madhaifu yake, nae ana akili fulani kama ya kunguru, yaani huhisi mambo na wakati wote hujiona hayupo salama hasa vitu vinapokwenda kinyume na matarajio yake hata kidogo tu.
Ilikuwa ni kawaida sana kufukuza mtu anapochelewa hata nusu dakika kutoka kwenye ule muda waliokubaliana kukutana. Huona kama kuchelewa kwako ni kwasababu fulani. Kwa ufupi ni mtu wa tahadhari iliyopitiliza.
Ni hulka hiyo ambayo Watoto wa mjini huiita ‘machale’ ndiyo humfanya salama, na ni hulka hiyo pia ilimsaidia kugundua mapema zaidi na katika hatua za awali sana jaribio la jeshi kutaka kumpindua kwenye awamu yake ya pili ya utawala. Hivyo kwake hii ni njia ya kumuweka salama.
“Meshack, niitie Macha mara moja”, Rais Costa aliagiza Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Stanza bwana Stanley Macha aitwe ofisini kwake. Wakati akimaliza kutoa maagizo hayo Ketina aliingia akiwa macho yamevimba na nywele kichwani zimevurugika.
“Nini tena?”, Rais Costa aliuliza kwa mshangao kwa jinsi alivyouona muonekano wa Ketina.
“Waulize hao vijana wako wamenifanyia nini”, Ketina alijibu kwa hasira na kupayuka.
“Sasa ongea kwa adabu. Unapaswa kuelewa upo ofisi ya nani hapa Keti”, Rais Costa alionekana nae kughadhibika kidogo.
“Adabu gani Costa? We si uliniacha hapa ili hawa vijana wako wanidhalilishe?”, Ketina alijibu nae kwa sauti ya juu.
Wakati Rais Costa akitaka kumjibu Ketina ghafla aliingia Meshack na kumtaarifu kuwa Stanley Macha amemuomba radhi kidogo atachelewa kufika kwani kuna taarifa ameipata kutoka Beijing China ambayo anaifanyia kazi hivyo ampe muda.
Rais Costa hapo hapo alinyanyua simu na kwa kutumia mtandao salama wa mawasiliano alimpigia Macha.
“Macha, tell me what’s going on”, (Macha niambie nini kinaendelea), Rais Costa alimuuliza Macha swali la moja kwa moja.
“Mkuu, Pius haonekani. Amewatoka wenzake katika mazingira ya kutatanisha”, Stanley Macha alijibu nae moja kwa moja.
“Amewatoka wapi? Kwani kina Joe wapo wapi? Wamefikaje China bila utaratibu Kimweri anaoufahamu na kwanini Joe awasiliane na wewe kabla yangu?”, Rais Costa aliuliza maswali mfululizo kwa kupaniki.
Stanley Macha aligundua kosa, kuwa Joe hakuwa amewasili na ndege ambayo balozi Kimweri anaifahamu na kuwa hakuwa Ubalozini mpaka muda ule. Lakini kosa la pili, kiutaratibu Joe alitakiwa kwanza awasiliane na Rais Costa kwani ndiye mkuu wa nchi na ndiye aliemtuma. Ilikuwa ni kosa kubwa sana kiutawala Joe kuongea na Stanley Macha kabla ya Rais.
“Mkuu umenipa kazi ya kuhakikisha wewe upo salama na taifa lipo salama. Ni kazi yangu ninayoifanya kwa moyo wote na naifanya usiku na mchana. Mimi kwa kutumia vyombo vya ulinzi na kikosi ulichonipa na nilichokula kiapo kukiongoza nilihakikisha namfuatilia Joe kila pahala na ni mimi niliegundua kuwa wamewasili China katika njia ambayo sio tuliyotegemea na nikachukua hatua kumuuliza Joe kulikoni na ndipo nilipogundua Pius hayupo na wenzake.
Mh. Rais nakuomba radhi kama nimekukwaza kwa kulifanya hili.” Stanley Macha alijitahidi kumjibu Rais kwa kumzunguka na kumtoa kwenye lengo. Rais Costa alionekana kukubali majibu ya Macha na yalimwongezea Imani nae.
“Macha nakuomba hapa ofisini kwangu sasa hivi nahitaji ufanye ufuatiliaji wa nini kinaendelea ukiwa hapa. Njoo na timu yako”, Rais Costa alimalizia. Alimtaka Macha afike haraka Ikulu.
“Kwahiyo unaniona mimi kinyago hapa sio?”, Ketina alimuuliza Rais Costa mara tu baada ya Rais Costa kumaliza kuongea na Macha kwa simu.
Wakati Ketina akiwa anauliza swali lake hilo, Rais Costa hakuwa anamsikiliza bali alikuwa akipiga simu nyingine kwa Mkuu wa Majeshi, Jenerali Ernest Nduta, wanajeshi wengi walizoea Kumuita Jemedari Mshua kwa aina ya maisha aliyoishi.
“Ernest, umewasiliana na Kijana wako Pius? Costa aliuliza.
“Hapana Mkuu, kuna tatizo?”, Jenerali Nduta aliuliza.
“Just find his whereabouts” (Mtafute yupo wapi), Rais Costa alijibu kiufupi na kukata simu na kuanza kupiga simu nyingine.
“Macha umefika wapi? Connect me with Joe, I can’t get hold of him” (Macha umefika wapi? Niunganishe na Joe mimi, nashindwa kumpata). Rais Costa alitoa maagizo huku akiwa amesimama akizunguka zunguka meza yake pale ofisini.
Macha alimpigia Joe simu na kumuunganisha na Rais.
“Joe, this is totally unethical. Mimi natakiwa nipate tabu kuwasiliana na wewe? Mimi ndio natakiwa nikutafute wewe? Wewe siku hizi bosi wako ni Stanley? Upo wapi? Nini kinaendelea kwa Pius? Yupo wapi? Mmefikaje China, kwanini hata Kimweri hajui mmeingiaje China? Hii inapaswa kuwa siri?” Rais Costa aliuliza kwa ghadhabu sana tena mfululizo.
“Salamu Mh. Rais. Kwanza niombe radhi kwa haya yanayotokea lakini yametokea kwa sababu ya heshima kubwa Rais Kim aliyotupatia kwa niaba yako na sisi tulishindwa kuikataa. Tumewasili China na ndege namba tano ya Rais Kim mkuu ndio maana unaona ni kama hakuna coordination nzuri na ubalozi wetu hapa China….”, Joe alianza kujieleza kwa utaratibu sana huku mapigo ya moyo yakienda kwa kasi.
“Joe, it’s ok Pius yupo wapi? Ninaambiwa hamjui halipo. Hili linawezekanaje?” Rais Costa alikatisha maongezi ya Joe yaliyoonyesha kumwingia kwa kiasi fulani na kumpa Tumaini lakini suala la Pius bado lilimsumbua.
“Nimetoa taarifa kwa Macha ili anisaide kufatilia kupitia mtandao wao wa usalama kwa kusaidiana na China, najua ndani ya muda mchache tu watajua nini kimetokea. Wameanza kufatilia kamera za hapa uwanja mdogo wa ndege kuonyesha ameelekea wapi”, Joe alijibu kwa ufupi.
“Macha nakusubiri sasa hivi”, Rais Costa aliongea kwenye simu kwa ufupi na kuikata.
“Kwa hiyo mimi hapa ni kinyago?”, Ketina aliekuwa ameketi pale ofisini kwa Rais aliuliza tena.
Rais Costa hakumjibu, aliminya kikengele kidogo kilicho chini ya meza yake kwenye kona na haraka waliingia vijana wawili wa usalama katika hali ya tahadhari na kumvaa Ketina na kumpiga shoti ya umeme kwa kifaa maalum kijulikanacho kitaalam kama compact stun gunswanachotembea nacho na alipopoteza fahamu Rais Costa aliwaagiza wamtoe mbele ya macho yake na kisha aliketi kwenye kiti.
Maskini binti Ketina alijua muda wote ni wa mahaba kwa Rais Costa, hakujua kwa muda ule Costa alikuwa kwenye shinikizo kubwa la kiakili juu ya kutoonekana kwa Pius katika hali ya kutatanisha na kuwa alihitaji majibu.
Pius ni mnadhimu mkuu wa Jeshi, kitendo cha yeye kupotea katika mazingira tata pale uwanja wa ndege tena baada ya kutoka safari nyeti kama ile kilimwacha na maswali mengi sana. Akili yake ya ‘kunguru’haikutulia
***********************************
Kwenye meza ya Rais Costa kwa chini kidogo tu upande anaokaa yeye huwa kuna kitufe kidogo sana cha alamu. Kwa sababu ofisi ya Rais imetengenezwa katika hali ambayo haitoi sauti na huwezi kusikia nini kinaongelewa ndani, kitufe kile kimewekwa kwa ajili ya usalama wa Rais.
Mgeni akiingia ofisini pale na kwasababu watu wa usalama wanabaki kwa nje na hivyo ikatokea kwa sababu yoyote ile Rais akahisi mgeni wake anahatarisha usalama wake, basi kwa siri atabonyeza kile kitufe na alamu itaita kwa nje na watu wa usalama wataingia moja kwa moja kumuokoa Rais.
Kitufe kile ni alama ya Rais kusema nipo hatarini na kuwa watu wa usalama hawaingii katika hali ya kuja kuuliza nini kinaendelea bali huingia katika hali ya kuja kumuokoa Rais na hivyo yule mgeni aliyeko ndani ya ofisi ya Rais huvamiwa moja kwa moja na kudhibitiwa na ndicho kilichotokea kwa Ketina.
Kwa kawaida mgeni kabla ya kuingia kwenye ofisi ya Rais Costa hukaguliwa sana na hupewa maelekezo ya namna ya kukaa kwenye meza ya Rais, kuwa wakati wote mikono yote miwili hutakiwa kukaa juu ya meza na kama unaingia na namna yoyote ya kifurushi basi japo kitakuwa kimekaguliwa sana lakini utatakiwa kukiweka juu ya meza pia kwa maana kuwa hutatakiwa uiname kunyanyua kitu chochote kutokea chini.
Zaidi ya hapo wakati mgeni anaingia huingizwa na mtu wa usalama na mtu wa usalama hatatoka mpaka umemaliza kusalimiana na Rais na Rais ameshakaa upande wake wa meza na wewe umeshaketi ndio mtu wa usalama atatoka nje. na sasa ikitokea mgeni unafanya miondoko yoyote ya mikono basi Rais nae hutakiwa ahamishe mkono wake na kuuelekeza kwenye kitufe kwa tahadhari.
Kwa hasira alizozipata Rais Costa kwa usumbufu wa Ketina na kilichokuwa kikiendelea China aliamua amtoe Ketina kama muhalifu. Atashughulika nae baadae. Nchi kwanza mahaba baadae.
**************************************
Katika watu ambao akili zao zinakimbia kwa kasi ya ajabu basi Stanley Macha ni mmoja wapo. Jasusi huyu akili zake zilikuwa si za kawaida.
Baada ya Joe kumpa taarifa zile za kutokomea kwa Pius huku akijua fika Joe alishampa mpango wote, basi haraka alijua nini Pius anataka kufanya.
Pius ni kijana aliye na maamuzi ya haraka tena asiyeweza kuvumilia mambo pale anapokuwa hajakubaliana nayo na kuwa yana athari kwa taifa. Si mara ya kwanza.
Macha alimjua Pius kuwa tayari ameshaujua mpango na kuwa hatavumilia hata afike Stanza, atataka kutoa taarifa kwa Rais. Alijua ametoweka ili alete taarifa kwa Rais, na sasa hata yeye Macha hayupo salama tena.
Mara tu baada ya Joe kumpa taarifa ile alimsihi Joe awe mtulivu na aelekee ubalozini yeye na Habibu kama walivyopanga na amwachie yeye kudili na Pius. Alimwagiza Joe amsihi Habibu awe na utulivu na kuwa asihofu kila kitu kitakuwa sawa.
Joe alimwamini Macha sana katika mambo mengi lakini katika hili hakika hakumwamini. Alimwitikia tu ila moyoni alijua mwisho wao umefika. Alijua ilikuwa ni ngumu kumfanya Pius asimfikie Rais na kumpa taarifa, ni ngumu. Ungeweza kuchelewesha tu ila sio kufanya Rais asijue.
Macha alizidi kumuhakikishia kuwa atulie na asikimbie kwani kufanya hivyo sio tu kutamuhakikishia kuwa mkimbizi wa daima bali familia yake itaingia kwenye tabu kubwa maisha yao yote. Joe alikubali kwa shingo upande.
Habibu alikuwa hana la kufanya alikuwa akimwangalia Joe kwa macho ya kutia huruma sana, ni kama mtu aliekuwa akijisema ‘najuta kukufahamu Joe’, maana alijua Pius ni lazima atamtaja na kusema kuwa yeye anahusika na amekubaliana na Joe.
“Nilijua tu hatutafika popote na mpango huu”, Ndiyo maneno ya mwisho Habibu aliyoweza kusema na alikaa kimya kuanzia hapo. Joe hakumjibu.
********************************
Pius baada ya kuwatoka kina Joe, hakwenda mbali. Alikimbilia chooni mulemule ndani ya uwanja. Kwake yeye aliona kabisa Rais Costa yupo hatarini na alitaka kumtaarifu akae katika hali ya tahadhari na Stanley Macha. Alidhani yale aliyoambiwa na Joe ni juu juu tu na kuwa kuna mpango wa ziada.
Hakuwa tayari na hakukubali Rais adhurike mbele ya macho yake. Kama yale yangetokea kazi yake ingekuwa nini basi? Hakukubali, kiapo chake cha kumlinda Rais kilimtesa sana.
Wakati akijitahidi kumpigia simu Rais simu ilikuwa ikiita lakini haipokelewi. Aliamua kumpigia Meshack kijana wa karibu wa usalama wa Rais nayo pia iliita bila kupokelewa. Pius alijaribu kumpigia bosi wake yaani mkuu wa Majeshi lakini pia simu haikupokelewa. Alishangaa.
Hakujua kuwa Stanley Macha mara baada tu ya Joe kumtaarifu kuwa Pius haonekani haraka alimwagiza kijana wake pale idara ya usalama wa taifa afanye mpango wa kitaalamu katika teknolojia ya mawasiliano unaoitwa ‘Connection scrambling’, yaani mtandao wa simu wa namba mahsusi zilizochaguliwa unavurugwa, ikiwa na maana kuwa simu zote zinazoingia kwenye namba hizo kutokea namba ya Pius basi yeye Pius atasikia zinaita lakini kihalisia huku kwa muhusika zinakuwa hazijafika na muhusika hatajua kama anapigiwa simu.
Vilevile ili kununua muda wa kuweza kukabiliana na Pius, aliagiza tena simu zote za watu ambao anajua watakuwa target ya Pius basi wakitaka kumpigia Pius wasimpate hewani, hii kitaalamu waliita ‘Connection proof’, halafu simu za wote ambao alihisi watakuwa tageti wa Pius alihakikisha hazitaingiza simu yoyote ambayo inatokea China, hii waliita ‘Connection blocking’.
Kwa kifupi Macha alifanya kila kinachowezekana kwa wakati huo kuhakikisha kuwa taarifa zozote hazifiki Stanza kutoka kwa Pius kabla hawajamdhibiti.
Macha alifanya yote haya kupitia kijana wake mbobezi wa masuala ya mitandao ya simu aliyeitwa Daudi Kigosi. Daudi ni kijana wa usalama wa taifa na mtii kwa Macha. Yeye yupo makao makuu ya Idara hiyo na wakati wote wa maongezi ya Macha na Rais Costa yeye ndiyo alikuwa akiunganisha.
Hata kitendo cha Macha kuomba kuchelewa kidogo ikulu ilikuwa ni ili ahakikishe anamwachia Daudi malekezo sawia na kupata muda wa kutosha kujua nini atafanya.
**********************************
“Salehe habari”, Pius alimsalimia Salehe kijana wa ngazi ndogo kabisa pale makao makuu ya jeshi lakini alieingia nae jeshini mwaka mmoja.
Salehe alikuwa akipatana sana na Pius. Macha hakuwahi kudhani kama Salehe anaweza kuwa tageti wa Pius hivyo katika namba alizoagiza zifanyiwe michakato ya kitaalam na kijana wake Daudi namba ya Salehe haikumjia akilini.
“Mkuu”, Salehe alisalimia kwa kupiga saluti japo alikuwa Stanza na Pius alikuwa China. Salehe alistaajabu kuona Pius anampigia simu. Pius kwa Salehe kwa nafasi za vyeo ni sawa na mbingu na ardhi.
“Salehe fanya unaloweza hakikisha unamfikia Jenerali na kumpa hii simu niongee nae sawa?”, Pius alimwagiza Salehe kwa ufupi sana.
Alifanya hivyo mara baada ya kuona simu yake haipokelewi na yeyote aliekuja kwenye akili yake alietaka kuwasiliana nae hata mke wake hata dereva wake. Hakika Macha alimuweza lakini sasa yeye alimuweza zaidi. Hakuna aliyejua kama Pius anaweza kuwa na namba ya simu ya mtu kama Salehe.
“Mkuu nitamfikiaje Jenerali? Mimi ni mdogo sana”. Salehe alijibu kwa kutetemeka. Ilikuwa ni ajabu, yani ni kitu asichowahi kuwaza na alijua angepata maswali mengi sana.
“Salehe usikate hii simu nenda ofisini kwa Jenerali na atakaekuuliza mpe simu nitampa maelekezo mpaka utamfikia Jenerali”, Pius alimwagiza.
Salehe alianza kutembea kwa kutetemeka kuelekea ofisi ya Mkuu wa Majeshi na kama alivyowaza alikuwa akizuiwa kuwa anataka kuonana nae kuna shida gani na kwanini asiwasiliane na kiongozi wake. Katika vizingiti vyote hivyo kitu Salehe alikuwa akifanya ni kuwapa simu na kila aliesikia sauti ya Pius alipiga saluti na kumruhusu kupita.
Ili kumuona mkuu wa majeshi Stanza ilikupasa upite milango sio chini ya mitatu ya wasaidizi wake. Ilikuwa si jambo jepesi. Pius akiwa Mnadhimu Mkuu wa jeshi ni mtu wa pili kicheo kutokea kwa mkuu wa majeshi. Kila aliesikia ile simu alistaajabu inakuwaje na kwanini na ilibidi msaidizi mmoja amchukue Salehe moja kwa moja mpaka kwa mkuu wa majeshi Jenerali Ernest Nduta.
“Mkuu Salehe ana simu ya Pius, anaomba akupe uongee nae”. Msaidi alitoa taarifa huku akiwa amesimama kikakamavu mbele ya mkuu wa majeshi. Mkuu wa Majeshi alionekana kustaajabu.
“Tumekuwa tukimtafuta Pius bila mafanikio imekuwaje? Embu nipe”, Jenerali Ernest Nduta aliuliza kwa mshangao na kuchukua ile simu na kusikiliza.
“Mkuu salamu. Naomba upakue programu tumishi ya WhatsApp kwenye simu yako tafadhali”, Pius aliongea moja kwa moja.
“Pius, nini kinaendelea?”, Jenerali Ernest Nduta alihoji kwa mshangao mkubwa.
“Mkuu sina muda mrefu sajili namba yako binafsi WhatsApp sasa hivi”, Pius alijibu kiufupi sana.
Jenerali Nduta hapo hapo alimpa msaidizi wake simu yake na kumpa maelekezo kuwa amsaidie kuweka programu ya WhatsApp kwenye simu yake. Hakuwa mtu wa mitandao ya kijamii hata kidogo, yani hata WhatsApp hakuwa anajua ni kitu gani. Ni mtu mhafidhina kwelikweli.
Wakiwa wanaendelea kuweka programu ya WhatsApp kwenye simu binafsi ya Jenerali huku akiwa amebaki na butwaa nini kinaendelea ghafla aliingia Meja Kotira. Meja Kotira ni mkuu wa mawasilino ya kiintelijensia katika idara ya intelijensia ya jeshi inayoongozwa na Pius. Aliingia katika hali isiyo ya kawaida.
“Mkuu tumegundua kuna mchujo wa simu unaendelea kwa baadhi ya watu wa jeshini na wewe ukiwemo pamoja na Ikulu. Mchujo huo ni baada ya kuona mkingamo na mwingiliano wa mawimbi kutoka kwenye mtambo wa mawasiliano wa idara ya Usalama wa Taifa.
Mchujo mkubwa umefanywa kwenye namba ya Luteni Jenerali Pius na simu zote zinazotoka China zilizojaribu kuingia kwenye hawa watu zilizuiwa”. Meja Kotira alieleza huku akitweta.
“Meja usiondoke…… asee tayari ushaweka hiyo makitu yenu?”, Jenerali alimsihi Meja asitoke huku akimuuliza msaidizi wake kama ameshamaliza kuweka hiyo programu ya WhatsApp. Alionekana kupagawa kidogo.
Yule msaidizi alimjibu kuwa tayari na Jenerali alimwambia amtumie ujumbe Pius kisha ampe yeye hiyo simu. Yule msaidizi alifanya hivyo na kumpa simu Jenerali na alimwamuru atoke nje na kumwacha na Meja Kotira.
“Kotira kuna mambo hayapo sawa”, Jenerali alimwambia Kotira huku akisubiri aone majibu ya Pius.
**************************
Wakati wote kijana wa Macha, Daudi Kigosi alikuwa akicheza na mawasiliano.
“Mkuu, tunaweza kukawa na tatizo kidogo. Nimefanya ‘phone triangulation’, nimegundua kuna simu kutoka China imeingia kwenye namba mojawapo pale makao makuu ya jeshi. Sio kati ya zile namba tulizoziainisha lakini naona hapa ilikaa hewani kwa dakika kama kumi hivi”, Daudi alimpigia simu Macha aliekuwa tayari kwenye korido za Ikulu kuingia kwenye ofisi ya Rais.
Phone tringuation ni namna unaweza kufanya uchakatuaji na uchambuzi wa simu zinazoingia mahali fulani na kuweza kujua imetoka wapi au umbali gani na kama kuna teknolojia ya juu uweza kusikia mpaka nini kiliongelewa.
Kuna simu zaidi ya mamilioni zinazokuwa hewani lakini kama mtu anafanya phone triangulationanaweza kuchagua anataka achuje simu zinazotoka wapi kwenda wapi au zinazoongea neno gani kama neno la umuhimu kwa mchujaji ambalo kitaalamu huliita ‘lead word’. Yaani kwa teknolojia hii unaweza kuchagua uchuje simu zote zilizopo hewani zinazotokea jimbo fulani au zinazotaja neno Rais n.k
Baada ya kusikia taarifa ile Macha aliishiwa nguvu. Alisimama katikati ya korido pale Ikulu.
**********************************
Baada ya kuhakikisha simu zote za Pius zinazuiwa Macha kwa kutumia nafasi yake aliwasiliana na uongozi wa kiwanja cha ndege Shenyang na kuwapa maelekezo yote na kuwaomba wafatilie.
Wakishirikiana na Joe na kijana mmoja kutoka ubalozi wa Korea Kaskazini pale China walianza kuangalia kamera kuwa Pius yupo wapi na walimuona yupo chooni. Walielekea moja kwa moja chooni kwani Joe aliwaambia kuwa yule ana taarifa nyeti na kuwa aliwatoka bila kuaga.
Walifika chooni na baada ya kugonga sana Pius alifungua na kuanza kutazamana na Joe.
“Pius unataka kufanya nini”, Joe aliuliza kwa sauti ya upole. Pius alibaki anamtazama.
“It’s too late Joe” (Umechelewa sana Joe), Pius alijibu kwa sauti ya kisaliti.
Kabla Joe hajaongea neno lolote aliona simu inaita na alipoangalia alikuwa ni Stanley Macha.
“Joe, we are cornered. Pius betrayed us. As I am speaking to you, I am in the middle of four security agents in the state house, they are approaching to arrest me. I think Pius managed to leak the info. See you Joe.” (Joe tumeshikwa. Pius ametusaliti. Hapa ninapozungumza nipo katikati ya vijana wa usalama wane, wananikaribia kuniweka chini ya ulinzi. Nadhani Pius amefanikiwa kupenyeza taarifa. Tutaonana Joe). Macha alionekana kuongea kwa huzuni sana.
“Do something Macha. Please!” (fanya jambo Macha tafadhali). Joe alionekana kuchanganyikiwa.
“Hakuna mnaloweza kufanya kaka. Nimemtumia Jenerali maongezi yetu yote”, Pius alionekana kujibu kwa kujiamini.
*********************************
Katika msafara ule, Pius ndiye alikuwa na kinasa sauti kilichokuwa na mfano wa kalamu. Kinasa sauti kile kina uwezo wa kuhifadhi maongezi kwa uwezo wa Terabyte 1japo ni kidogo sana.
Kinasa sauti kile hakikuwa siri na hata walipokuwa Korea walikiweka wazi na kuwa maongezi yote na majadiliano Rais Costa alitaka kuyasikia na hivyo wakati wote wa maongezi kalamu ile ilikuwa ikirekodi.
Ulikuwa unaweza kusoma dakika na kujua maongezi fulani yalizungumzwa katika dakika fulani kwa hivyo ukaweza kupeleka mbele ama nyuma na kusikiliza.
Ni kinasa sauti kile wakati wakiwa wanazungumza mambo yao ya siri na hasa Joe alipoanza kuwapa mpango wa kumpumzisha Rais Costa, yeye Pius alikuwa akikiwasha na kurekodi kwa siri. Hakuna aliyekuwa na shaka na Pius wala kuwaza kuwa anaweza kufanya jambo lile.
Baada ya Pius kuhakikisha Jenereali Nduta yupo kwenye WhatsApp alikuwa akisogeza mbele mazungumzo mpaka kwenye zile dakika alizozikariri kuwa ndipo walikuwa wakizungumza juu ya mkakati wa kumpumzisha Rais Costa basi alishikilia kitufe cha kurekodia sauti kwenye simu yake na kuiweka karibu na kile kinasa sauti na kila neno lilirekodiwa na simu na kumtumia Jenerali kama Ushahidi.
Pia alituma screenshot za yale maneno ya siri ya ‘ego testor’ kama ushahidi kuwa Macha anahusika. Ni rahisi kusema kama ni kusaliti tu basi Pius alisaliti wenzake kwa mikono na miguu yani mzima mzima.
Haikujulikana ni kwanini Pius alikuwa akimpenda Rais Costa kiasi cha kumsaliti mtu kama Joe. Ilibaki ni fumbo kubwa.
Baada ya kupata Ushahidi ule kutoka kwa Pius, Jenerali Nduta haraka alimtaarifu Rais kumuweka chini ya Ulinzi Stanley Macha na sasa vijana wa Usalama wa Taifa pale Ikulu walikuwa wakitekeleza amri hiyo. Macha alikuwa hana ujanja.
**************************************
“Macha, atleast we have tried” (Macha, angalau tumejaribu). Joe alimwambia Macha kwa simu kwa huzuni sana na kukata tamaa kuwa sasa hawana pa kutokea lakini angalau wamejaribu kutaka kutekeleza mpango wao walioona una manufaa kwa taifa.
“Yes Joe, we have tried. Goodluck friend” (Ni kweli Joe, tumejaribu. Nakutakia kila la heri Rafiki yangu) Macha alijibu na kabla hajamaliza vijana walishamfikia na kwa heshima kubwa kwa sababu yule ni bosi wao walimwambia kwa adabu….
“Kwa malekezo ya Rais wa Jamuhuri ya watu wa Stanza, naomba unikabidhi beji yako na kuanzia sasa upo chini ya ulinzi”, Meshack alimwambia bosi wake Stanley Macha.
“It’s ok kid, do your work” (Sawa, fanya kazi yako), Stanley Macha alimjibu Meshack kwa unyonge huku akimkabidhi beji na bastola anayotembea nayo.
****************************************
Joe na Habibu walibaki katika ardhi ya China huku wakiwa wamechanganyikiwa. Hawakuweza kuelekea ubalozini kwasababu waliamini kuwa taarifa zitakuwa zimeshawafikia.
Hali ya kutokujua pa kuanzia iliwakumba wote wawili. Joe alifikiri zaidi kuhusu familia yake aliyoiacha Stanza na namna ambavyo ilishaanza kuneemeka na msamaha wa Rais Costa na ni nini kingetokea.
Yeye Habibu alifikiri zaidi kuhusu kuharibu Maisha yake ya kitaaluma kwani ubalozi ni heshima ambayo kama ukiitumikia vyema basi haiondoki tena maishani mwako. Na kwa matukio ya siku moja tu, ameshapoteza hadhi ya ubalozi na uelekeo wa Maisha yake kwa ujumla upo mashakani.
Habibu na Joe waliangaliana kwa macho ya kukata tamaa pasi na kuongea suala lolote.
Muhudumu wa pale uwanja wa ndege aliwatazama bila kuelewa jambo lililokuwa linaotokea. Kwa mara nyingine wote walimuangalia Pius ambaye alionekana kuwa upande wa mawazo ya Joe safari nzima kumbe ni shushushu. Kwakuwa ni ardhi ya ugenini, Pius asingeweza kuwakamata au kufanya jambo lolote.
Ghafla, kama mtu aliyegutuka kutoka usingizini, Joe alimtizama Habibu machoni na kumwambia kwa sauti ya taratibu iliyoanza kuwa tulivu baada ya hofu kutanda, ‘’nina wazo, huu ndiyo mwanzo. Yajayo ni zaidi ya yaliyopita’’, Joe alisema.
“Unamaanisha nini Joe? Kila kitu kimeshaharibika hapa. Maisha yetu ni sawa na yamefikia mwisho” Habibu aliongea kwa sauti ya mtetemo kama mtu anaetaka kulia lakini anajikaza kume.
“No one has a problem with the first mile of a journey, even an infant could do fine for a while. But it isn’t the start that matters. It is the finish line’’ Joe aliendelea kuongea katika lugha ya kimombo kilichonyooka, na wakati huu alimnukuu mwanafalsafaJulien Smith.
Joe alianza kusogea kwa kuondoka huku Habibu akimfuata. Alizungumza kwa utaratibu na umakini na kusema ‘’It’s never over, it’s not over, not just yet. At best, it’s just paused for a moment. Pull up your socks boy and get ready to get started’’, Joe alimaliza na kumwacha Habibu akindelea kushangaa Joe anamaanisha nini?
Joe aliendelea kupiga hatua huku moyoni akimuwaza rafiki yake mpendwa Stanley Macha atakuwa katika hali gani ndani ya mikono ya Rais Sylvester Costa.
*************************************************************
Je, Umeipenda simulizi hii?.Tafadhali naomba uipe alama(Rate It) kwa kubofya hapa>>>
**************************************************************
Hii Ni Sehemu Ya Mwisho Ya Msimu Huu Wa Kwanza Wa Simulizi Hii.Ninashukuru Kwa Kuifuatilia.Baada Ya Kuipa Alama Na Kupata Maoni yako Nikusihi Usiache Kuifatilia Mara Tu Inapoanza Msimu Wa Pili Hapo Mwezi Februari.
Sent using Jamii Forums mobile app