Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwa watakao miss vitu vya costa usiende mbali like hapa then kulingana na kiwango cha like tutadondosha kitu mbadala kwa ajili ya kumsubiria costaYajayo yanafurahisha.
Shukran mkuu
Ngoja apumzike kwanzaDuh mkuu kwa hiyo Stan ataendelea kushikiliwa hadi Feb? Aaah Costa si atakuwa kashammaliza? Utani kidogo kanzi nzuri mkuu tunasubiri msimu wa pili kwa shauku kubwa
Ila Costa alinifurahisha alivobonyeza kile kitufe kuwaita vijana wamtoe Ketie
Sent using Jamii Forums mobile app
Februari [emoji134][emoji134]asante mbaba wacha tuwe wapoleThe President And I(Mimi Na Rais)- Sehemu Ya Kumi
Lello Mmassy January 24, 2019

Kikulacho Ki Nguoni Mwako
“Mwambieni yule binti aje sasa ofisini”, Rais Costa alitoa agizo kwa mmoja wa wasaidizi wake kuwa Ketina aitwe ofisini kwake. Alitoa maagizo hayo huku akiingia ofisini kwake akitokea kuongea na askofu Begere.
“Kimweri, sijasikia kuhusu kina Joe. Kwa ratiba uliyonipa wanahitajika wawe wameshafika Beijing na Joe kuwasiliana nami. Nahitaji kusikia kutoka kwao kabla sijawasiliana na Mr. Kim”. Rais Costa alikuwa akiongea na simu huku akiketi kwenye kiti chake ofisi yake maalum pale Ikulu.
“Mh. Rais unachosema ni kweli lakini ni kuwa hawakuja na ndege niliotarajia waje nayo. Nimewasiliana na ubalozi wa Korea hapa China ambao ndio nashirikiana nao na wameniambia Joe wanakuja na ndege nyingine na kuwa wapo salama na ndani ya muda mfupi ujao watawasili hapa ubalozini”, Balozi Kimweri alimjibu Rais Costa.
“Sawa. Keep me posted”, (endelea kunijuza mambo yatakavyoendelea), Rais Costa alijibu kwa ufupi.
Rais Costa aliweka simu yake chini na kuhema kwa nguvu. Pamoja na madhaifu yake, nae ana akili fulani kama ya kunguru, yaani huhisi mambo na wakati wote hujiona hayupo salama hasa vitu vinapokwenda kinyume na matarajio yake hata kidogo tu.
Ilikuwa ni kawaida sana kufukuza mtu anapochelewa hata nusu dakika kutoka kwenye ule muda waliokubaliana kukutana. Huona kama kuchelewa kwako ni kwasababu fulani. Kwa ufupi ni mtu wa tahadhari iliyopitiliza.
Ni hulka hiyo ambayo Watoto wa mjini huiita ‘machale’ ndiyo humfanya salama, na ni hulka hiyo pia ilimsaidia kugundua mapema zaidi na katika hatua za awali sana jaribio la jeshi kutaka kumpindua kwenye awamu yake ya pili ya utawala. Hivyo kwake hii ni njia ya kumuweka salama.
“Meshack, niitie Macha mara moja”, Rais Costa aliagiza Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Stanza bwana Stanley Macha aitwe ofisini kwake. Wakati akimaliza kutoa maagizo hayo Ketina aliingia akiwa macho yamevimba na nywele kichwani zimevurugika.
“Nini tena?”, Rais Costa aliuliza kwa mshangao kwa jinsi alivyouona muonekano wa Ketina.
“Waulize hao vijana wako wamenifanyia nini”, Ketina alijibu kwa hasira na kupayuka.
“Sasa ongea kwa adabu. Unapaswa kuelewa upo ofisi ya nani hapa Keti”, Rais Costa alionekana nae kughadhibika kidogo.
“Adabu gani Costa? We si uliniacha hapa ili hawa vijana wako wanidhalilishe?”, Ketina alijibu nae kwa sauti ya juu.
Wakati Rais Costa akitaka kumjibu Ketina ghafla aliingia Meshack na kumtaarifu kuwa Stanley Macha amemuomba radhi kidogo atachelewa kufika kwani kuna taarifa ameipata kutoka Beijing China ambayo anaifanyia kazi hivyo ampe muda.
Rais Costa hapo hapo alinyanyua simu na kwa kutumia mtandao salama wa mawasiliano alimpigia Macha.
“Macha, tell me what’s going on”, (Macha niambie nini kinaendelea), Rais Costa alimuuliza Macha swali la moja kwa moja.
“Mkuu, Pius haonekani. Amewatoka wenzake katika mazingira ya kutatanisha”, Stanley Macha alijibu nae moja kwa moja.
“Amewatoka wapi? Kwani kina Joe wapo wapi? Wamefikaje China bila utaratibu Kimweri anaoufahamu na kwanini Joe awasiliane na wewe kabla yangu?”, Rais Costa aliuliza maswali mfululizo kwa kupaniki.
Stanley Macha aligundua kosa, kuwa Joe hakuwa amewasili na ndege ambayo balozi Kimweri anaifahamu na kuwa hakuwa Ubalozini mpaka muda ule. Lakini kosa la pili, kiutaratibu Joe alitakiwa kwanza awasiliane na Rais Costa kwani ndiye mkuu wa nchi na ndiye aliemtuma. Ilikuwa ni kosa kubwa sana kiutawala Joe kuongea na Stanley Macha kabla ya Rais.
“Mkuu umenipa kazi ya kuhakikisha wewe upo salama na taifa lipo salama. Ni kazi yangu ninayoifanya kwa moyo wote na naifanya usiku na mchana. Mimi kwa kutumia vyombo vya ulinzi na kikosi ulichonipa na nilichokula kiapo kukiongoza nilihakikisha namfuatilia Joe kila pahala na ni mimi niliegundua kuwa wamewasili China katika njia ambayo sio tuliyotegemea na nikachukua hatua kumuuliza Joe kulikoni na ndipo nilipogundua Pius hayupo na wenzake.
Mh. Rais nakuomba radhi kama nimekukwaza kwa kulifanya hili.” Stanley Macha alijitahidi kumjibu Rais kwa kumzunguka na kumtoa kwenye lengo. Rais Costa alionekana kukubali majibu ya Macha na yalimwongezea Imani nae.
“Macha nakuomba hapa ofisini kwangu sasa hivi nahitaji ufanye ufuatiliaji wa nini kinaendelea ukiwa hapa. Njoo na timu yako”, Rais Costa alimalizia. Alimtaka Macha afike haraka Ikulu.
“Kwahiyo unaniona mimi kinyago hapa sio?”, Ketina alimuuliza Rais Costa mara tu baada ya Rais Costa kumaliza kuongea na Macha kwa simu.
Wakati Ketina akiwa anauliza swali lake hilo, Rais Costa hakuwa anamsikiliza bali alikuwa akipiga simu nyingine kwa Mkuu wa Majeshi, Jenerali Ernest Nduta, wanajeshi wengi walizoea Kumuita Jemedari Mshua kwa aina ya maisha aliyoishi.
“Ernest, umewasiliana na Kijana wako Pius? Costa aliuliza.
“Hapana Mkuu, kuna tatizo?”, Jenerali Nduta aliuliza.
“Just find his whereabouts” (Mtafute yupo wapi), Rais Costa alijibu kiufupi na kukata simu na kuanza kupiga simu nyingine.
“Macha umefika wapi? Connect me with Joe, I can’t get hold of him” (Macha umefika wapi? Niunganishe na Joe mimi, nashindwa kumpata). Rais Costa alitoa maagizo huku akiwa amesimama akizunguka zunguka meza yake pale ofisini.
Macha alimpigia Joe simu na kumuunganisha na Rais.
“Joe, this is totally unethical. Mimi natakiwa nipate tabu kuwasiliana na wewe? Mimi ndio natakiwa nikutafute wewe? Wewe siku hizi bosi wako ni Stanley? Upo wapi? Nini kinaendelea kwa Pius? Yupo wapi? Mmefikaje China, kwanini hata Kimweri hajui mmeingiaje China? Hii inapaswa kuwa siri?” Rais Costa aliuliza kwa ghadhabu sana tena mfululizo.
“Salamu Mh. Rais. Kwanza niombe radhi kwa haya yanayotokea lakini yametokea kwa sababu ya heshima kubwa Rais Kim aliyotupatia kwa niaba yako na sisi tulishindwa kuikataa. Tumewasili China na ndege namba tano ya Rais Kim mkuu ndio maana unaona ni kama hakuna coordination nzuri na ubalozi wetu hapa China….”, Joe alianza kujieleza kwa utaratibu sana huku mapigo ya moyo yakienda kwa kasi.
“Joe, it’s ok Pius yupo wapi? Ninaambiwa hamjui halipo. Hili linawezekanaje?” Rais Costa alikatisha maongezi ya Joe yaliyoonyesha kumwingia kwa kiasi fulani na kumpa Tumaini lakini suala la Pius bado lilimsumbua.
“Nimetoa taarifa kwa Macha ili anisaide kufatilia kupitia mtandao wao wa usalama kwa kusaidiana na China, najua ndani ya muda mchache tu watajua nini kimetokea. Wameanza kufatilia kamera za hapa uwanja mdogo wa ndege kuonyesha ameelekea wapi”, Joe alijibu kwa ufupi.
“Macha nakusubiri sasa hivi”, Rais Costa aliongea kwenye simu kwa ufupi na kuikata.
“Kwa hiyo mimi hapa ni kinyago?”, Ketina aliekuwa ameketi pale ofisini kwa Rais aliuliza tena.
Rais Costa hakumjibu, aliminya kikengele kidogo kilicho chini ya meza yake kwenye kona na haraka waliingia vijana wawili wa usalama katika hali ya tahadhari na kumvaa Ketina na kumpiga shoti ya umeme kwa kifaa maalum kijulikanacho kitaalam kama compact stun gunswanachotembea nacho na alipopoteza fahamu Rais Costa aliwaagiza wamtoe mbele ya macho yake na kisha aliketi kwenye kiti.
Maskini binti Ketina alijua muda wote ni wa mahaba kwa Rais Costa, hakujua kwa muda ule Costa alikuwa kwenye shinikizo kubwa la kiakili juu ya kutoonekana kwa Pius katika hali ya kutatanisha na kuwa alihitaji majibu.
Pius ni mnadhimu mkuu wa Jeshi, kitendo cha yeye kupotea katika mazingira tata pale uwanja wa ndege tena baada ya kutoka safari nyeti kama ile kilimwacha na maswali mengi sana. Akili yake ya ‘kunguru’haikutulia
***********************************
Kwenye meza ya Rais Costa kwa chini kidogo tu upande anaokaa yeye huwa kuna kitufe kidogo sana cha alamu. Kwa sababu ofisi ya Rais imetengenezwa katika hali ambayo haitoi sauti na huwezi kusikia nini kinaongelewa ndani, kitufe kile kimewekwa kwa ajili ya usalama wa Rais.
Mgeni akiingia ofisini pale na kwasababu watu wa usalama wanabaki kwa nje na hivyo ikatokea kwa sababu yoyote ile Rais akahisi mgeni wake anahatarisha usalama wake, basi kwa siri atabonyeza kile kitufe na alamu itaita kwa nje na watu wa usalama wataingia moja kwa moja kumuokoa Rais.
Kitufe kile ni alama ya Rais kusema nipo hatarini na kuwa watu wa usalama hawaingii katika hali ya kuja kuuliza nini kinaendelea bali huingia katika hali ya kuja kumuokoa Rais na hivyo yule mgeni aliyeko ndani ya ofisi ya Rais huvamiwa moja kwa moja na kudhibitiwa na ndicho kilichotokea kwa Ketina.
Kwa kawaida mgeni kabla ya kuingia kwenye ofisi ya Rais Costa hukaguliwa sana na hupewa maelekezo ya namna ya kukaa kwenye meza ya Rais, kuwa wakati wote mikono yote miwili hutakiwa kukaa juu ya meza na kama unaingia na namna yoyote ya kifurushi basi japo kitakuwa kimekaguliwa sana lakini utatakiwa kukiweka juu ya meza pia kwa maana kuwa hutatakiwa uiname kunyanyua kitu chochote kutokea chini.
Zaidi ya hapo wakati mgeni anaingia huingizwa na mtu wa usalama na mtu wa usalama hatatoka mpaka umemaliza kusalimiana na Rais na Rais ameshakaa upande wake wa meza na wewe umeshaketi ndio mtu wa usalama atatoka nje. na sasa ikitokea mgeni unafanya miondoko yoyote ya mikono basi Rais nae hutakiwa ahamishe mkono wake na kuuelekeza kwenye kitufe kwa tahadhari.
Kwa hasira alizozipata Rais Costa kwa usumbufu wa Ketina na kilichokuwa kikiendelea China aliamua amtoe Ketina kama muhalifu. Atashughulika nae baadae. Nchi kwanza mahaba baadae.
**************************************
Katika watu ambao akili zao zinakimbia kwa kasi ya ajabu basi Stanley Macha ni mmoja wapo. Jasusi huyu akili zake zilikuwa si za kawaida.
Baada ya Joe kumpa taarifa zile za kutokomea kwa Pius huku akijua fika Joe alishampa mpango wote, basi haraka alijua nini Pius anataka kufanya.
Pius ni kijana aliye na maamuzi ya haraka tena asiyeweza kuvumilia mambo pale anapokuwa hajakubaliana nayo na kuwa yana athari kwa taifa. Si mara ya kwanza.
Macha alimjua Pius kuwa tayari ameshaujua mpango na kuwa hatavumilia hata afike Stanza, atataka kutoa taarifa kwa Rais. Alijua ametoweka ili alete taarifa kwa Rais, na sasa hata yeye Macha hayupo salama tena.
Mara tu baada ya Joe kumpa taarifa ile alimsihi Joe awe mtulivu na aelekee ubalozini yeye na Habibu kama walivyopanga na amwachie yeye kudili na Pius. Alimwagiza Joe amsihi Habibu awe na utulivu na kuwa asihofu kila kitu kitakuwa sawa.
Joe alimwamini Macha sana katika mambo mengi lakini katika hili hakika hakumwamini. Alimwitikia tu ila moyoni alijua mwisho wao umefika. Alijua ilikuwa ni ngumu kumfanya Pius asimfikie Rais na kumpa taarifa, ni ngumu. Ungeweza kuchelewesha tu ila sio kufanya Rais asijue.
Macha alizidi kumuhakikishia kuwa atulie na asikimbie kwani kufanya hivyo sio tu kutamuhakikishia kuwa mkimbizi wa daima bali familia yake itaingia kwenye tabu kubwa maisha yao yote. Joe alikubali kwa shingo upande.
Habibu alikuwa hana la kufanya alikuwa akimwangalia Joe kwa macho ya kutia huruma sana, ni kama mtu aliekuwa akijisema ‘najuta kukufahamu Joe’, maana alijua Pius ni lazima atamtaja na kusema kuwa yeye anahusika na amekubaliana na Joe.
“Nilijua tu hatutafika popote na mpango huu”, Ndiyo maneno ya mwisho Habibu aliyoweza kusema na alikaa kimya kuanzia hapo. Joe hakumjibu.
********************************
Pius baada ya kuwatoka kina Joe, hakwenda mbali. Alikimbilia chooni mulemule ndani ya uwanja. Kwake yeye aliona kabisa Rais Costa yupo hatarini na alitaka kumtaarifu akae katika hali ya tahadhari na Stanley Macha. Alidhani yale aliyoambiwa na Joe ni juu juu tu na kuwa kuna mpango wa ziada.
Hakuwa tayari na hakukubali Rais adhurike mbele ya macho yake. Kama yale yangetokea kazi yake ingekuwa nini basi? Hakukubali, kiapo chake cha kumlinda Rais kilimtesa sana.
Wakati akijitahidi kumpigia simu Rais simu ilikuwa ikiita lakini haipokelewi. Aliamua kumpigia Meshack kijana wa karibu wa usalama wa Rais nayo pia iliita bila kupokelewa. Pius alijaribu kumpigia bosi wake yaani mkuu wa Majeshi lakini pia simu haikupokelewa. Alishangaa.
Hakujua kuwa Stanley Macha mara baada tu ya Joe kumtaarifu kuwa Pius haonekani haraka alimwagiza kijana wake pale idara ya usalama wa taifa afanye mpango wa kitaalamu katika teknolojia ya mawasiliano unaoitwa ‘Connection scrambling’, yaani mtandao wa simu wa namba mahsusi zilizochaguliwa unavurugwa, ikiwa na maana kuwa simu zote zinazoingia kwenye namba hizo kutokea namba ya Pius basi yeye Pius atasikia zinaita lakini kihalisia huku kwa muhusika zinakuwa hazijafika na muhusika hatajua kama anapigiwa simu.
Vilevile ili kununua muda wa kuweza kukabiliana na Pius, aliagiza tena simu zote za watu ambao anajua watakuwa target ya Pius basi wakitaka kumpigia Pius wasimpate hewani, hii kitaalamu waliita ‘Connection proof’, halafu simu za wote ambao alihisi watakuwa tageti wa Pius alihakikisha hazitaingiza simu yoyote ambayo inatokea China, hii waliita ‘Connection blocking’.
Kwa kifupi Macha alifanya kila kinachowezekana kwa wakati huo kuhakikisha kuwa taarifa zozote hazifiki Stanza kutoka kwa Pius kabla hawajamdhibiti.
Macha alifanya yote haya kupitia kijana wake mbobezi wa masuala ya mitandao ya simu aliyeitwa Daudi Kigosi. Daudi ni kijana wa usalama wa taifa na mtii kwa Macha. Yeye yupo makao makuu ya Idara hiyo na wakati wote wa maongezi ya Macha na Rais Costa yeye ndiyo alikuwa akiunganisha.
Hata kitendo cha Macha kuomba kuchelewa kidogo ikulu ilikuwa ni ili ahakikishe anamwachia Daudi malekezo sawia na kupata muda wa kutosha kujua nini atafanya.
**********************************
“Salehe habari”, Pius alimsalimia Salehe kijana wa ngazi ndogo kabisa pale makao makuu ya jeshi lakini alieingia nae jeshini mwaka mmoja.
Salehe alikuwa akipatana sana na Pius. Macha hakuwahi kudhani kama Salehe anaweza kuwa tageti wa Pius hivyo katika namba alizoagiza zifanyiwe michakato ya kitaalam na kijana wake Daudi namba ya Salehe haikumjia akilini.
“Mkuu”, Salehe alisalimia kwa kupiga saluti japo alikuwa Stanza na Pius alikuwa China. Salehe alistaajabu kuona Pius anampigia simu. Pius kwa Salehe kwa nafasi za vyeo ni sawa na mbingu na ardhi.
“Salehe fanya unaloweza hakikisha unamfikia Jenerali na kumpa hii simu niongee nae sawa?”, Pius alimwagiza Salehe kwa ufupi sana.
Alifanya hivyo mara baada ya kuona simu yake haipokelewi na yeyote aliekuja kwenye akili yake alietaka kuwasiliana nae hata mke wake hata dereva wake. Hakika Macha alimuweza lakini sasa yeye alimuweza zaidi. Hakuna aliyejua kama Pius anaweza kuwa na namba ya simu ya mtu kama Salehe.
“Mkuu nitamfikiaje Jenerali? Mimi ni mdogo sana”. Salehe alijibu kwa kutetemeka. Ilikuwa ni ajabu, yani ni kitu asichowahi kuwaza na alijua angepata maswali mengi sana.
“Salehe usikate hii simu nenda ofisini kwa Jenerali na atakaekuuliza mpe simu nitampa maelekezo mpaka utamfikia Jenerali”, Pius alimwagiza.
Salehe alianza kutembea kwa kutetemeka kuelekea ofisi ya Mkuu wa Majeshi na kama alivyowaza alikuwa akizuiwa kuwa anataka kuonana nae kuna shida gani na kwanini asiwasiliane na kiongozi wake. Katika vizingiti vyote hivyo kitu Salehe alikuwa akifanya ni kuwapa simu na kila aliesikia sauti ya Pius alipiga saluti na kumruhusu kupita.
Ili kumuona mkuu wa majeshi Stanza ilikupasa upite milango sio chini ya mitatu ya wasaidizi wake. Ilikuwa si jambo jepesi. Pius akiwa Mnadhimu Mkuu wa jeshi ni mtu wa pili kicheo kutokea kwa mkuu wa majeshi. Kila aliesikia ile simu alistaajabu inakuwaje na kwanini na ilibidi msaidizi mmoja amchukue Salehe moja kwa moja mpaka kwa mkuu wa majeshi Jenerali Ernest Nduta.
“Mkuu Salehe ana simu ya Pius, anaomba akupe uongee nae”. Msaidi alitoa taarifa huku akiwa amesimama kikakamavu mbele ya mkuu wa majeshi. Mkuu wa Majeshi alionekana kustaajabu.
“Tumekuwa tukimtafuta Pius bila mafanikio imekuwaje? Embu nipe”, Jenerali Ernest Nduta aliuliza kwa mshangao na kuchukua ile simu na kusikiliza.
“Mkuu salamu. Naomba upakue programu tumishi ya WhatsApp kwenye simu yako tafadhali”, Pius aliongea moja kwa moja.
“Pius, nini kinaendelea?”, Jenerali Ernest Nduta alihoji kwa mshangao mkubwa.
“Mkuu sina muda mrefu sajili namba yako binafsi WhatsApp sasa hivi”, Pius alijibu kiufupi sana.
Jenerali Nduta hapo hapo alimpa msaidizi wake simu yake na kumpa maelekezo kuwa amsaidie kuweka programu ya WhatsApp kwenye simu yake. Hakuwa mtu wa mitandao ya kijamii hata kidogo, yani hata WhatsApp hakuwa anajua ni kitu gani. Ni mtu mhafidhina kwelikweli.
Wakiwa wanaendelea kuweka programu ya WhatsApp kwenye simu binafsi ya Jenerali huku akiwa amebaki na butwaa nini kinaendelea ghafla aliingia Meja Kotira. Meja Kotira ni mkuu wa mawasilino ya kiintelijensia katika idara ya intelijensia ya jeshi inayoongozwa na Pius. Aliingia katika hali isiyo ya kawaida.
“Mkuu tumegundua kuna mchujo wa simu unaendelea kwa baadhi ya watu wa jeshini na wewe ukiwemo pamoja na Ikulu. Mchujo huo ni baada ya kuona mkingamo na mwingiliano wa mawimbi kutoka kwenye mtambo wa mawasiliano wa idara ya Usalama wa Taifa.
Mchujo mkubwa umefanywa kwenye namba ya Luteni Jenerali Pius na simu zote zinazotoka China zilizojaribu kuingia kwenye hawa watu zilizuiwa”. Meja Kotira alieleza huku akitweta.
“Meja usiondoke…… asee tayari ushaweka hiyo makitu yenu?”, Jenerali alimsihi Meja asitoke huku akimuuliza msaidizi wake kama ameshamaliza kuweka hiyo programu ya WhatsApp. Alionekana kupagawa kidogo.
Yule msaidizi alimjibu kuwa tayari na Jenerali alimwambia amtumie ujumbe Pius kisha ampe yeye hiyo simu. Yule msaidizi alifanya hivyo na kumpa simu Jenerali na alimwamuru atoke nje na kumwacha na Meja Kotira.
“Kotira kuna mambo hayapo sawa”, Jenerali alimwambia Kotira huku akisubiri aone majibu ya Pius.
**************************
Wakati wote kijana wa Macha, Daudi Kigosi alikuwa akicheza na mawasiliano.
“Mkuu, tunaweza kukawa na tatizo kidogo. Nimefanya ‘phone triangulation’, nimegundua kuna simu kutoka China imeingia kwenye namba mojawapo pale makao makuu ya jeshi. Sio kati ya zile namba tulizoziainisha lakini naona hapa ilikaa hewani kwa dakika kama kumi hivi”, Daudi alimpigia simu Macha aliekuwa tayari kwenye korido za Ikulu kuingia kwenye ofisi ya Rais.
Phone tringuation ni namna unaweza kufanya uchakatuaji na uchambuzi wa simu zinazoingia mahali fulani na kuweza kujua imetoka wapi au umbali gani na kama kuna teknolojia ya juu uweza kusikia mpaka nini kiliongelewa.
Kuna simu zaidi ya mamilioni zinazokuwa hewani lakini kama mtu anafanya phone triangulationanaweza kuchagua anataka achuje simu zinazotoka wapi kwenda wapi au zinazoongea neno gani kama neno la umuhimu kwa mchujaji ambalo kitaalamu huliita ‘lead word’. Yaani kwa teknolojia hii unaweza kuchagua uchuje simu zote zilizopo hewani zinazotokea jimbo fulani au zinazotaja neno Rais n.k
Baada ya kusikia taarifa ile Macha aliishiwa nguvu. Alisimama katikati ya korido pale Ikulu.
**********************************
Baada ya kuhakikisha simu zote za Pius zinazuiwa Macha kwa kutumia nafasi yake aliwasiliana na uongozi wa kiwanja cha ndege Shenyang na kuwapa maelekezo yote na kuwaomba wafatilie.
Wakishirikiana na Joe na kijana mmoja kutoka ubalozi wa Korea Kaskazini pale China walianza kuangalia kamera kuwa Pius yupo wapi na walimuona yupo chooni. Walielekea moja kwa moja chooni kwani Joe aliwaambia kuwa yule ana taarifa nyeti na kuwa aliwatoka bila kuaga.
Walifika chooni na baada ya kugonga sana Pius alifungua na kuanza kutazamana na Joe.
“Pius unataka kufanya nini”, Joe aliuliza kwa sauti ya upole. Pius alibaki anamtazama.
“It’s too late Joe” (Umechelewa sana Joe), Pius alijibu kwa sauti ya kisaliti.
Kabla Joe hajaongea neno lolote aliona simu inaita na alipoangalia alikuwa ni Stanley Macha.
“Joe, we are cornered. Pius betrayed us. As I am speaking to you, I am in the middle of four security agents in the state house, they are approaching to arrest me. I think Pius managed to leak the info. See you Joe.” (Joe tumeshikwa. Pius ametusaliti. Hapa ninapozungumza nipo katikati ya vijana wa usalama wane, wananikaribia kuniweka chini ya ulinzi. Nadhani Pius amefanikiwa kupenyeza taarifa. Tutaonana Joe). Macha alionekana kuongea kwa huzuni sana.
“Do something Macha. Please!” (fanya jambo Macha tafadhali). Joe alionekana kuchanganyikiwa.
“Hakuna mnaloweza kufanya kaka. Nimemtumia Jenerali maongezi yetu yote”, Pius alionekana kujibu kwa kujiamini.
*********************************
Katika msafara ule, Pius ndiye alikuwa na kinasa sauti kilichokuwa na mfano wa kalamu. Kinasa sauti kile kina uwezo wa kuhifadhi maongezi kwa uwezo wa Terabyte 1japo ni kidogo sana.
Kinasa sauti kile hakikuwa siri na hata walipokuwa Korea walikiweka wazi na kuwa maongezi yote na majadiliano Rais Costa alitaka kuyasikia na hivyo wakati wote wa maongezi kalamu ile ilikuwa ikirekodi.
Ulikuwa unaweza kusoma dakika na kujua maongezi fulani yalizungumzwa katika dakika fulani kwa hivyo ukaweza kupeleka mbele ama nyuma na kusikiliza.
Ni kinasa sauti kile wakati wakiwa wanazungumza mambo yao ya siri na hasa Joe alipoanza kuwapa mpango wa kumpumzisha Rais Costa, yeye Pius alikuwa akikiwasha na kurekodi kwa siri. Hakuna aliyekuwa na shaka na Pius wala kuwaza kuwa anaweza kufanya jambo lile.
Baada ya Pius kuhakikisha Jenereali Nduta yupo kwenye WhatsApp alikuwa akisogeza mbele mazungumzo mpaka kwenye zile dakika alizozikariri kuwa ndipo walikuwa wakizungumza juu ya mkakati wa kumpumzisha Rais Costa basi alishikilia kitufe cha kurekodia sauti kwenye simu yake na kuiweka karibu na kile kinasa sauti na kila neno lilirekodiwa na simu na kumtumia Jenerali kama Ushahidi.
Pia alituma screenshot za yale maneno ya siri ya ‘ego testor’ kama ushahidi kuwa Macha anahusika. Ni rahisi kusema kama ni kusaliti tu basi Pius alisaliti wenzake kwa mikono na miguu yani mzima mzima.
Haikujulikana ni kwanini Pius alikuwa akimpenda Rais Costa kiasi cha kumsaliti mtu kama Joe. Ilibaki ni fumbo kubwa.
Baada ya kupata Ushahidi ule kutoka kwa Pius, Jenerali Nduta haraka alimtaarifu Rais kumuweka chini ya Ulinzi Stanley Macha na sasa vijana wa Usalama wa Taifa pale Ikulu walikuwa wakitekeleza amri hiyo. Macha alikuwa hana ujanja.
**************************************
“Macha, atleast we have tried” (Macha, angalau tumejaribu). Joe alimwambia Macha kwa simu kwa huzuni sana na kukata tamaa kuwa sasa hawana pa kutokea lakini angalau wamejaribu kutaka kutekeleza mpango wao walioona una manufaa kwa taifa.
“Yes Joe, we have tried. Goodluck friend” (Ni kweli Joe, tumejaribu. Nakutakia kila la heri Rafiki yangu) Macha alijibu na kabla hajamaliza vijana walishamfikia na kwa heshima kubwa kwa sababu yule ni bosi wao walimwambia kwa adabu….
“Kwa malekezo ya Rais wa Jamuhuri ya watu wa Stanza, naomba unikabidhi beji yako na kuanzia sasa upo chini ya ulinzi”, Meshack alimwambia bosi wake Stanley Macha.
“It’s ok kid, do your work” (Sawa, fanya kazi yako), Stanley Macha alimjibu Meshack kwa unyonge huku akimkabidhi beji na bastola anayotembea nayo.
****************************************
Joe na Habibu walibaki katika ardhi ya China huku wakiwa wamechanganyikiwa. Hawakuweza kuelekea ubalozini kwasababu waliamini kuwa taarifa zitakuwa zimeshawafikia.
Hali ya kutokujua pa kuanzia iliwakumba wote wawili. Joe alifikiri zaidi kuhusu familia yake aliyoiacha Stanza na namna ambavyo ilishaanza kuneemeka na msamaha wa Rais Costa na ni nini kingetokea.
Yeye Habibu alifikiri zaidi kuhusu kuharibu Maisha yake ya kitaaluma kwani ubalozi ni heshima ambayo kama ukiitumikia vyema basi haiondoki tena maishani mwako. Na kwa matukio ya siku moja tu, ameshapoteza hadhi ya ubalozi na uelekeo wa Maisha yake kwa ujumla upo mashakani.
Habibu na Joe waliangaliana kwa macho ya kukata tamaa pasi na kuongea suala lolote.
Muhudumu wa pale uwanja wa ndege aliwatazama bila kuelewa jambo lililokuwa linaotokea. Kwa mara nyingine wote walimuangalia Pius ambaye alionekana kuwa upande wa mawazo ya Joe safari nzima kumbe ni shushushu. Kwakuwa ni ardhi ya ugenini, Pius asingeweza kuwakamata au kufanya jambo lolote.
Ghafla, kama mtu aliyegutuka kutoka usingizini, Joe alimtizama Habibu machoni na kumwambia kwa sauti ya taratibu iliyoanza kuwa tulivu baada ya hofu kutanda, ‘’nina wazo, huu ndiyo mwanzo. Yajayo ni zaidi ya yaliyopita’’, Joe alisema.
“Unamaanisha nini Joe? Kila kitu kimeshaharibika hapa. Maisha yetu ni sawa na yamefikia mwisho” Habibu aliongea kwa sauti ya mtetemo kama mtu anaetaka kulia lakini anajikaza kume.
“No one has a problem with the first mile of a journey, even an infant could do fine for a while. But it isn’t the start that matters. It is the finish line’’ Joe aliendelea kuongea katika lugha ya kimombo kilichonyooka, na wakati huu alimnukuu mwanafalsafaJulien Smith.
Joe alianza kusogea kwa kuondoka huku Habibu akimfuata. Alizungumza kwa utaratibu na umakini na kusema ‘’It’s never over, it’s not over, not just yet. At best, it’s just paused for a moment. Pull up your socks boy and get ready to get started’’, Joe alimaliza na kumwacha Habibu akindelea kushangaa Joe anamaanisha nini?
Joe aliendelea kupiga hatua huku moyoni akimuwaza rafiki yake mpendwa Stanley Macha atakuwa katika hali gani ndani ya mikono ya Rais Sylvester Costa.
*************************************************************
Je, Umeipenda simulizi hii?.Tafadhali naomba uipe alama(Rate It) kwa kubofya hapa>>>
**************************************************************
Hii Ni Sehemu Ya Mwisho Ya Msimu Huu Wa Kwanza Wa Simulizi Hii.Ninashukuru Kwa Kuifuatilia.Baada Ya Kuipa Alama Na Kupata Maoni yako Nikusihi Usiache Kuifatilia Mara Tu Inapoanza Msimu Wa Pili Hapo Mwezi Februari.
Sent using Jamii Forums mobile app
[emoji1][emoji1]hii ni kufa hufi ila cha moto utakiona [emoji6]Daah mpaka February ..si-nitakufa kwa arosto !!?
Haya bwana muandishi asante sana
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkojoooooo[emoji85][emoji85][emoji85][emoji85]niliweka alama za nyayo zangu ili nisipotee
Sent using Jamii Forums mobile app
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Nimekusoma maana utashangaa unatoka tu ukirudi unakuta watu washakalia siti
Sent using Jamii Forums mobile app
Hehhe..miss you too hun[emoji8] (ukimisiwa wikiendi rahaa)
Hehhe..miss you too hun[emoji8] (ukimisiwa wikiendi rahaa)
Ulitekwa kwani Dume.?
Sent using Jamii Forums mobile app
Ntatekwa na nani mie laaziz wng?mambo ya kusaka rizki tuHehhe..miss you too hun[emoji8] (ukimisiwa wikiendi rahaa)
Ulitekwa kwani Dume.?
Sent using Jamii Forums mobile app
Masikini wakina JoeThe President And I(Mimi Na Rais)- Sehemu Ya Kumi
Lello Mmassy January 24, 2019

Kikulacho Ki Nguoni Mwako
“Mwambieni yule binti aje sasa ofisini”, Rais Costa alitoa agizo kwa mmoja wa wasaidizi wake kuwa Ketina aitwe ofisini kwake. Alitoa maagizo hayo huku akiingia ofisini kwake akitokea kuongea na askofu Begere.
“Kimweri, sijasikia kuhusu kina Joe. Kwa ratiba uliyonipa wanahitajika wawe wameshafika Beijing na Joe kuwasiliana nami. Nahitaji kusikia kutoka kwao kabla sijawasiliana na Mr. Kim”. Rais Costa alikuwa akiongea na simu huku akiketi kwenye kiti chake ofisi yake maalum pale Ikulu.
“Mh. Rais unachosema ni kweli lakini ni kuwa hawakuja na ndege niliotarajia waje nayo. Nimewasiliana na ubalozi wa Korea hapa China ambao ndio nashirikiana nao na wameniambia Joe wanakuja na ndege nyingine na kuwa wapo salama na ndani ya muda mfupi ujao watawasili hapa ubalozini”, Balozi Kimweri alimjibu Rais Costa.
“Sawa. Keep me posted”, (endelea kunijuza mambo yatakavyoendelea), Rais Costa alijibu kwa ufupi.
Rais Costa aliweka simu yake chini na kuhema kwa nguvu. Pamoja na madhaifu yake, nae ana akili fulani kama ya kunguru, yaani huhisi mambo na wakati wote hujiona hayupo salama hasa vitu vinapokwenda kinyume na matarajio yake hata kidogo tu.
Ilikuwa ni kawaida sana kufukuza mtu anapochelewa hata nusu dakika kutoka kwenye ule muda waliokubaliana kukutana. Huona kama kuchelewa kwako ni kwasababu fulani. Kwa ufupi ni mtu wa tahadhari iliyopitiliza.
Ni hulka hiyo ambayo Watoto wa mjini huiita ‘machale’ ndiyo humfanya salama, na ni hulka hiyo pia ilimsaidia kugundua mapema zaidi na katika hatua za awali sana jaribio la jeshi kutaka kumpindua kwenye awamu yake ya pili ya utawala. Hivyo kwake hii ni njia ya kumuweka salama.
“Meshack, niitie Macha mara moja”, Rais Costa aliagiza Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Stanza bwana Stanley Macha aitwe ofisini kwake. Wakati akimaliza kutoa maagizo hayo Ketina aliingia akiwa macho yamevimba na nywele kichwani zimevurugika.
“Nini tena?”, Rais Costa aliuliza kwa mshangao kwa jinsi alivyouona muonekano wa Ketina.
“Waulize hao vijana wako wamenifanyia nini”, Ketina alijibu kwa hasira na kupayuka.
“Sasa ongea kwa adabu. Unapaswa kuelewa upo ofisi ya nani hapa Keti”, Rais Costa alionekana nae kughadhibika kidogo.
“Adabu gani Costa? We si uliniacha hapa ili hawa vijana wako wanidhalilishe?”, Ketina alijibu nae kwa sauti ya juu.
Wakati Rais Costa akitaka kumjibu Ketina ghafla aliingia Meshack na kumtaarifu kuwa Stanley Macha amemuomba radhi kidogo atachelewa kufika kwani kuna taarifa ameipata kutoka Beijing China ambayo anaifanyia kazi hivyo ampe muda.
Rais Costa hapo hapo alinyanyua simu na kwa kutumia mtandao salama wa mawasiliano alimpigia Macha.
“Macha, tell me what’s going on”, (Macha niambie nini kinaendelea), Rais Costa alimuuliza Macha swali la moja kwa moja.
“Mkuu, Pius haonekani. Amewatoka wenzake katika mazingira ya kutatanisha”, Stanley Macha alijibu nae moja kwa moja.
“Amewatoka wapi? Kwani kina Joe wapo wapi? Wamefikaje China bila utaratibu Kimweri anaoufahamu na kwanini Joe awasiliane na wewe kabla yangu?”, Rais Costa aliuliza maswali mfululizo kwa kupaniki.
Stanley Macha aligundua kosa, kuwa Joe hakuwa amewasili na ndege ambayo balozi Kimweri anaifahamu na kuwa hakuwa Ubalozini mpaka muda ule. Lakini kosa la pili, kiutaratibu Joe alitakiwa kwanza awasiliane na Rais Costa kwani ndiye mkuu wa nchi na ndiye aliemtuma. Ilikuwa ni kosa kubwa sana kiutawala Joe kuongea na Stanley Macha kabla ya Rais.
“Mkuu umenipa kazi ya kuhakikisha wewe upo salama na taifa lipo salama. Ni kazi yangu ninayoifanya kwa moyo wote na naifanya usiku na mchana. Mimi kwa kutumia vyombo vya ulinzi na kikosi ulichonipa na nilichokula kiapo kukiongoza nilihakikisha namfuatilia Joe kila pahala na ni mimi niliegundua kuwa wamewasili China katika njia ambayo sio tuliyotegemea na nikachukua hatua kumuuliza Joe kulikoni na ndipo nilipogundua Pius hayupo na wenzake.
Mh. Rais nakuomba radhi kama nimekukwaza kwa kulifanya hili.” Stanley Macha alijitahidi kumjibu Rais kwa kumzunguka na kumtoa kwenye lengo. Rais Costa alionekana kukubali majibu ya Macha na yalimwongezea Imani nae.
“Macha nakuomba hapa ofisini kwangu sasa hivi nahitaji ufanye ufuatiliaji wa nini kinaendelea ukiwa hapa. Njoo na timu yako”, Rais Costa alimalizia. Alimtaka Macha afike haraka Ikulu.
“Kwahiyo unaniona mimi kinyago hapa sio?”, Ketina alimuuliza Rais Costa mara tu baada ya Rais Costa kumaliza kuongea na Macha kwa simu.
Wakati Ketina akiwa anauliza swali lake hilo, Rais Costa hakuwa anamsikiliza bali alikuwa akipiga simu nyingine kwa Mkuu wa Majeshi, Jenerali Ernest Nduta, wanajeshi wengi walizoea Kumuita Jemedari Mshua kwa aina ya maisha aliyoishi.
“Ernest, umewasiliana na Kijana wako Pius? Costa aliuliza.
“Hapana Mkuu, kuna tatizo?”, Jenerali Nduta aliuliza.
“Just find his whereabouts” (Mtafute yupo wapi), Rais Costa alijibu kiufupi na kukata simu na kuanza kupiga simu nyingine.
“Macha umefika wapi? Connect me with Joe, I can’t get hold of him” (Macha umefika wapi? Niunganishe na Joe mimi, nashindwa kumpata). Rais Costa alitoa maagizo huku akiwa amesimama akizunguka zunguka meza yake pale ofisini.
Macha alimpigia Joe simu na kumuunganisha na Rais.
“Joe, this is totally unethical. Mimi natakiwa nipate tabu kuwasiliana na wewe? Mimi ndio natakiwa nikutafute wewe? Wewe siku hizi bosi wako ni Stanley? Upo wapi? Nini kinaendelea kwa Pius? Yupo wapi? Mmefikaje China, kwanini hata Kimweri hajui mmeingiaje China? Hii inapaswa kuwa siri?” Rais Costa aliuliza kwa ghadhabu sana tena mfululizo.
“Salamu Mh. Rais. Kwanza niombe radhi kwa haya yanayotokea lakini yametokea kwa sababu ya heshima kubwa Rais Kim aliyotupatia kwa niaba yako na sisi tulishindwa kuikataa. Tumewasili China na ndege namba tano ya Rais Kim mkuu ndio maana unaona ni kama hakuna coordination nzuri na ubalozi wetu hapa China….”, Joe alianza kujieleza kwa utaratibu sana huku mapigo ya moyo yakienda kwa kasi.
“Joe, it’s ok Pius yupo wapi? Ninaambiwa hamjui halipo. Hili linawezekanaje?” Rais Costa alikatisha maongezi ya Joe yaliyoonyesha kumwingia kwa kiasi fulani na kumpa Tumaini lakini suala la Pius bado lilimsumbua.
“Nimetoa taarifa kwa Macha ili anisaide kufatilia kupitia mtandao wao wa usalama kwa kusaidiana na China, najua ndani ya muda mchache tu watajua nini kimetokea. Wameanza kufatilia kamera za hapa uwanja mdogo wa ndege kuonyesha ameelekea wapi”, Joe alijibu kwa ufupi.
“Macha nakusubiri sasa hivi”, Rais Costa aliongea kwenye simu kwa ufupi na kuikata.
“Kwa hiyo mimi hapa ni kinyago?”, Ketina aliekuwa ameketi pale ofisini kwa Rais aliuliza tena.
Rais Costa hakumjibu, aliminya kikengele kidogo kilicho chini ya meza yake kwenye kona na haraka waliingia vijana wawili wa usalama katika hali ya tahadhari na kumvaa Ketina na kumpiga shoti ya umeme kwa kifaa maalum kijulikanacho kitaalam kama compact stun gunswanachotembea nacho na alipopoteza fahamu Rais Costa aliwaagiza wamtoe mbele ya macho yake na kisha aliketi kwenye kiti.
Maskini binti Ketina alijua muda wote ni wa mahaba kwa Rais Costa, hakujua kwa muda ule Costa alikuwa kwenye shinikizo kubwa la kiakili juu ya kutoonekana kwa Pius katika hali ya kutatanisha na kuwa alihitaji majibu.
Pius ni mnadhimu mkuu wa Jeshi, kitendo cha yeye kupotea katika mazingira tata pale uwanja wa ndege tena baada ya kutoka safari nyeti kama ile kilimwacha na maswali mengi sana. Akili yake ya ‘kunguru’haikutulia
***********************************
Kwenye meza ya Rais Costa kwa chini kidogo tu upande anaokaa yeye huwa kuna kitufe kidogo sana cha alamu. Kwa sababu ofisi ya Rais imetengenezwa katika hali ambayo haitoi sauti na huwezi kusikia nini kinaongelewa ndani, kitufe kile kimewekwa kwa ajili ya usalama wa Rais.
Mgeni akiingia ofisini pale na kwasababu watu wa usalama wanabaki kwa nje na hivyo ikatokea kwa sababu yoyote ile Rais akahisi mgeni wake anahatarisha usalama wake, basi kwa siri atabonyeza kile kitufe na alamu itaita kwa nje na watu wa usalama wataingia moja kwa moja kumuokoa Rais.
Kitufe kile ni alama ya Rais kusema nipo hatarini na kuwa watu wa usalama hawaingii katika hali ya kuja kuuliza nini kinaendelea bali huingia katika hali ya kuja kumuokoa Rais na hivyo yule mgeni aliyeko ndani ya ofisi ya Rais huvamiwa moja kwa moja na kudhibitiwa na ndicho kilichotokea kwa Ketina.
Kwa kawaida mgeni kabla ya kuingia kwenye ofisi ya Rais Costa hukaguliwa sana na hupewa maelekezo ya namna ya kukaa kwenye meza ya Rais, kuwa wakati wote mikono yote miwili hutakiwa kukaa juu ya meza na kama unaingia na namna yoyote ya kifurushi basi japo kitakuwa kimekaguliwa sana lakini utatakiwa kukiweka juu ya meza pia kwa maana kuwa hutatakiwa uiname kunyanyua kitu chochote kutokea chini.
Zaidi ya hapo wakati mgeni anaingia huingizwa na mtu wa usalama na mtu wa usalama hatatoka mpaka umemaliza kusalimiana na Rais na Rais ameshakaa upande wake wa meza na wewe umeshaketi ndio mtu wa usalama atatoka nje. na sasa ikitokea mgeni unafanya miondoko yoyote ya mikono basi Rais nae hutakiwa ahamishe mkono wake na kuuelekeza kwenye kitufe kwa tahadhari.
Kwa hasira alizozipata Rais Costa kwa usumbufu wa Ketina na kilichokuwa kikiendelea China aliamua amtoe Ketina kama muhalifu. Atashughulika nae baadae. Nchi kwanza mahaba baadae.
**************************************
Katika watu ambao akili zao zinakimbia kwa kasi ya ajabu basi Stanley Macha ni mmoja wapo. Jasusi huyu akili zake zilikuwa si za kawaida.
Baada ya Joe kumpa taarifa zile za kutokomea kwa Pius huku akijua fika Joe alishampa mpango wote, basi haraka alijua nini Pius anataka kufanya.
Pius ni kijana aliye na maamuzi ya haraka tena asiyeweza kuvumilia mambo pale anapokuwa hajakubaliana nayo na kuwa yana athari kwa taifa. Si mara ya kwanza.
Macha alimjua Pius kuwa tayari ameshaujua mpango na kuwa hatavumilia hata afike Stanza, atataka kutoa taarifa kwa Rais. Alijua ametoweka ili alete taarifa kwa Rais, na sasa hata yeye Macha hayupo salama tena.
Mara tu baada ya Joe kumpa taarifa ile alimsihi Joe awe mtulivu na aelekee ubalozini yeye na Habibu kama walivyopanga na amwachie yeye kudili na Pius. Alimwagiza Joe amsihi Habibu awe na utulivu na kuwa asihofu kila kitu kitakuwa sawa.
Joe alimwamini Macha sana katika mambo mengi lakini katika hili hakika hakumwamini. Alimwitikia tu ila moyoni alijua mwisho wao umefika. Alijua ilikuwa ni ngumu kumfanya Pius asimfikie Rais na kumpa taarifa, ni ngumu. Ungeweza kuchelewesha tu ila sio kufanya Rais asijue.
Macha alizidi kumuhakikishia kuwa atulie na asikimbie kwani kufanya hivyo sio tu kutamuhakikishia kuwa mkimbizi wa daima bali familia yake itaingia kwenye tabu kubwa maisha yao yote. Joe alikubali kwa shingo upande.
Habibu alikuwa hana la kufanya alikuwa akimwangalia Joe kwa macho ya kutia huruma sana, ni kama mtu aliekuwa akijisema ‘najuta kukufahamu Joe’, maana alijua Pius ni lazima atamtaja na kusema kuwa yeye anahusika na amekubaliana na Joe.
“Nilijua tu hatutafika popote na mpango huu”, Ndiyo maneno ya mwisho Habibu aliyoweza kusema na alikaa kimya kuanzia hapo. Joe hakumjibu.
********************************
Pius baada ya kuwatoka kina Joe, hakwenda mbali. Alikimbilia chooni mulemule ndani ya uwanja. Kwake yeye aliona kabisa Rais Costa yupo hatarini na alitaka kumtaarifu akae katika hali ya tahadhari na Stanley Macha. Alidhani yale aliyoambiwa na Joe ni juu juu tu na kuwa kuna mpango wa ziada.
Hakuwa tayari na hakukubali Rais adhurike mbele ya macho yake. Kama yale yangetokea kazi yake ingekuwa nini basi? Hakukubali, kiapo chake cha kumlinda Rais kilimtesa sana.
Wakati akijitahidi kumpigia simu Rais simu ilikuwa ikiita lakini haipokelewi. Aliamua kumpigia Meshack kijana wa karibu wa usalama wa Rais nayo pia iliita bila kupokelewa. Pius alijaribu kumpigia bosi wake yaani mkuu wa Majeshi lakini pia simu haikupokelewa. Alishangaa.
Hakujua kuwa Stanley Macha mara baada tu ya Joe kumtaarifu kuwa Pius haonekani haraka alimwagiza kijana wake pale idara ya usalama wa taifa afanye mpango wa kitaalamu katika teknolojia ya mawasiliano unaoitwa ‘Connection scrambling’, yaani mtandao wa simu wa namba mahsusi zilizochaguliwa unavurugwa, ikiwa na maana kuwa simu zote zinazoingia kwenye namba hizo kutokea namba ya Pius basi yeye Pius atasikia zinaita lakini kihalisia huku kwa muhusika zinakuwa hazijafika na muhusika hatajua kama anapigiwa simu.
Vilevile ili kununua muda wa kuweza kukabiliana na Pius, aliagiza tena simu zote za watu ambao anajua watakuwa target ya Pius basi wakitaka kumpigia Pius wasimpate hewani, hii kitaalamu waliita ‘Connection proof’, halafu simu za wote ambao alihisi watakuwa tageti wa Pius alihakikisha hazitaingiza simu yoyote ambayo inatokea China, hii waliita ‘Connection blocking’.
Kwa kifupi Macha alifanya kila kinachowezekana kwa wakati huo kuhakikisha kuwa taarifa zozote hazifiki Stanza kutoka kwa Pius kabla hawajamdhibiti.
Macha alifanya yote haya kupitia kijana wake mbobezi wa masuala ya mitandao ya simu aliyeitwa Daudi Kigosi. Daudi ni kijana wa usalama wa taifa na mtii kwa Macha. Yeye yupo makao makuu ya Idara hiyo na wakati wote wa maongezi ya Macha na Rais Costa yeye ndiyo alikuwa akiunganisha.
Hata kitendo cha Macha kuomba kuchelewa kidogo ikulu ilikuwa ni ili ahakikishe anamwachia Daudi malekezo sawia na kupata muda wa kutosha kujua nini atafanya.
**********************************
“Salehe habari”, Pius alimsalimia Salehe kijana wa ngazi ndogo kabisa pale makao makuu ya jeshi lakini alieingia nae jeshini mwaka mmoja.
Salehe alikuwa akipatana sana na Pius. Macha hakuwahi kudhani kama Salehe anaweza kuwa tageti wa Pius hivyo katika namba alizoagiza zifanyiwe michakato ya kitaalam na kijana wake Daudi namba ya Salehe haikumjia akilini.
“Mkuu”, Salehe alisalimia kwa kupiga saluti japo alikuwa Stanza na Pius alikuwa China. Salehe alistaajabu kuona Pius anampigia simu. Pius kwa Salehe kwa nafasi za vyeo ni sawa na mbingu na ardhi.
“Salehe fanya unaloweza hakikisha unamfikia Jenerali na kumpa hii simu niongee nae sawa?”, Pius alimwagiza Salehe kwa ufupi sana.
Alifanya hivyo mara baada ya kuona simu yake haipokelewi na yeyote aliekuja kwenye akili yake alietaka kuwasiliana nae hata mke wake hata dereva wake. Hakika Macha alimuweza lakini sasa yeye alimuweza zaidi. Hakuna aliyejua kama Pius anaweza kuwa na namba ya simu ya mtu kama Salehe.
“Mkuu nitamfikiaje Jenerali? Mimi ni mdogo sana”. Salehe alijibu kwa kutetemeka. Ilikuwa ni ajabu, yani ni kitu asichowahi kuwaza na alijua angepata maswali mengi sana.
“Salehe usikate hii simu nenda ofisini kwa Jenerali na atakaekuuliza mpe simu nitampa maelekezo mpaka utamfikia Jenerali”, Pius alimwagiza.
Salehe alianza kutembea kwa kutetemeka kuelekea ofisi ya Mkuu wa Majeshi na kama alivyowaza alikuwa akizuiwa kuwa anataka kuonana nae kuna shida gani na kwanini asiwasiliane na kiongozi wake. Katika vizingiti vyote hivyo kitu Salehe alikuwa akifanya ni kuwapa simu na kila aliesikia sauti ya Pius alipiga saluti na kumruhusu kupita.
Ili kumuona mkuu wa majeshi Stanza ilikupasa upite milango sio chini ya mitatu ya wasaidizi wake. Ilikuwa si jambo jepesi. Pius akiwa Mnadhimu Mkuu wa jeshi ni mtu wa pili kicheo kutokea kwa mkuu wa majeshi. Kila aliesikia ile simu alistaajabu inakuwaje na kwanini na ilibidi msaidizi mmoja amchukue Salehe moja kwa moja mpaka kwa mkuu wa majeshi Jenerali Ernest Nduta.
“Mkuu Salehe ana simu ya Pius, anaomba akupe uongee nae”. Msaidi alitoa taarifa huku akiwa amesimama kikakamavu mbele ya mkuu wa majeshi. Mkuu wa Majeshi alionekana kustaajabu.
“Tumekuwa tukimtafuta Pius bila mafanikio imekuwaje? Embu nipe”, Jenerali Ernest Nduta aliuliza kwa mshangao na kuchukua ile simu na kusikiliza.
“Mkuu salamu. Naomba upakue programu tumishi ya WhatsApp kwenye simu yako tafadhali”, Pius aliongea moja kwa moja.
“Pius, nini kinaendelea?”, Jenerali Ernest Nduta alihoji kwa mshangao mkubwa.
“Mkuu sina muda mrefu sajili namba yako binafsi WhatsApp sasa hivi”, Pius alijibu kiufupi sana.
Jenerali Nduta hapo hapo alimpa msaidizi wake simu yake na kumpa maelekezo kuwa amsaidie kuweka programu ya WhatsApp kwenye simu yake. Hakuwa mtu wa mitandao ya kijamii hata kidogo, yani hata WhatsApp hakuwa anajua ni kitu gani. Ni mtu mhafidhina kwelikweli.
Wakiwa wanaendelea kuweka programu ya WhatsApp kwenye simu binafsi ya Jenerali huku akiwa amebaki na butwaa nini kinaendelea ghafla aliingia Meja Kotira. Meja Kotira ni mkuu wa mawasilino ya kiintelijensia katika idara ya intelijensia ya jeshi inayoongozwa na Pius. Aliingia katika hali isiyo ya kawaida.
“Mkuu tumegundua kuna mchujo wa simu unaendelea kwa baadhi ya watu wa jeshini na wewe ukiwemo pamoja na Ikulu. Mchujo huo ni baada ya kuona mkingamo na mwingiliano wa mawimbi kutoka kwenye mtambo wa mawasiliano wa idara ya Usalama wa Taifa.
Mchujo mkubwa umefanywa kwenye namba ya Luteni Jenerali Pius na simu zote zinazotoka China zilizojaribu kuingia kwenye hawa watu zilizuiwa”. Meja Kotira alieleza huku akitweta.
“Meja usiondoke…… asee tayari ushaweka hiyo makitu yenu?”, Jenerali alimsihi Meja asitoke huku akimuuliza msaidizi wake kama ameshamaliza kuweka hiyo programu ya WhatsApp. Alionekana kupagawa kidogo.
Yule msaidizi alimjibu kuwa tayari na Jenerali alimwambia amtumie ujumbe Pius kisha ampe yeye hiyo simu. Yule msaidizi alifanya hivyo na kumpa simu Jenerali na alimwamuru atoke nje na kumwacha na Meja Kotira.
“Kotira kuna mambo hayapo sawa”, Jenerali alimwambia Kotira huku akisubiri aone majibu ya Pius.
**************************
Wakati wote kijana wa Macha, Daudi Kigosi alikuwa akicheza na mawasiliano.
“Mkuu, tunaweza kukawa na tatizo kidogo. Nimefanya ‘phone triangulation’, nimegundua kuna simu kutoka China imeingia kwenye namba mojawapo pale makao makuu ya jeshi. Sio kati ya zile namba tulizoziainisha lakini naona hapa ilikaa hewani kwa dakika kama kumi hivi”, Daudi alimpigia simu Macha aliekuwa tayari kwenye korido za Ikulu kuingia kwenye ofisi ya Rais.
Phone tringuation ni namna unaweza kufanya uchakatuaji na uchambuzi wa simu zinazoingia mahali fulani na kuweza kujua imetoka wapi au umbali gani na kama kuna teknolojia ya juu uweza kusikia mpaka nini kiliongelewa.
Kuna simu zaidi ya mamilioni zinazokuwa hewani lakini kama mtu anafanya phone triangulationanaweza kuchagua anataka achuje simu zinazotoka wapi kwenda wapi au zinazoongea neno gani kama neno la umuhimu kwa mchujaji ambalo kitaalamu huliita ‘lead word’. Yaani kwa teknolojia hii unaweza kuchagua uchuje simu zote zilizopo hewani zinazotokea jimbo fulani au zinazotaja neno Rais n.k
Baada ya kusikia taarifa ile Macha aliishiwa nguvu. Alisimama katikati ya korido pale Ikulu.
**********************************
Baada ya kuhakikisha simu zote za Pius zinazuiwa Macha kwa kutumia nafasi yake aliwasiliana na uongozi wa kiwanja cha ndege Shenyang na kuwapa maelekezo yote na kuwaomba wafatilie.
Wakishirikiana na Joe na kijana mmoja kutoka ubalozi wa Korea Kaskazini pale China walianza kuangalia kamera kuwa Pius yupo wapi na walimuona yupo chooni. Walielekea moja kwa moja chooni kwani Joe aliwaambia kuwa yule ana taarifa nyeti na kuwa aliwatoka bila kuaga.
Walifika chooni na baada ya kugonga sana Pius alifungua na kuanza kutazamana na Joe.
“Pius unataka kufanya nini”, Joe aliuliza kwa sauti ya upole. Pius alibaki anamtazama.
“It’s too late Joe” (Umechelewa sana Joe), Pius alijibu kwa sauti ya kisaliti.
Kabla Joe hajaongea neno lolote aliona simu inaita na alipoangalia alikuwa ni Stanley Macha.
“Joe, we are cornered. Pius betrayed us. As I am speaking to you, I am in the middle of four security agents in the state house, they are approaching to arrest me. I think Pius managed to leak the info. See you Joe.” (Joe tumeshikwa. Pius ametusaliti. Hapa ninapozungumza nipo katikati ya vijana wa usalama wane, wananikaribia kuniweka chini ya ulinzi. Nadhani Pius amefanikiwa kupenyeza taarifa. Tutaonana Joe). Macha alionekana kuongea kwa huzuni sana.
“Do something Macha. Please!” (fanya jambo Macha tafadhali). Joe alionekana kuchanganyikiwa.
“Hakuna mnaloweza kufanya kaka. Nimemtumia Jenerali maongezi yetu yote”, Pius alionekana kujibu kwa kujiamini.
*********************************
Katika msafara ule, Pius ndiye alikuwa na kinasa sauti kilichokuwa na mfano wa kalamu. Kinasa sauti kile kina uwezo wa kuhifadhi maongezi kwa uwezo wa Terabyte 1japo ni kidogo sana.
Kinasa sauti kile hakikuwa siri na hata walipokuwa Korea walikiweka wazi na kuwa maongezi yote na majadiliano Rais Costa alitaka kuyasikia na hivyo wakati wote wa maongezi kalamu ile ilikuwa ikirekodi.
Ulikuwa unaweza kusoma dakika na kujua maongezi fulani yalizungumzwa katika dakika fulani kwa hivyo ukaweza kupeleka mbele ama nyuma na kusikiliza.
Ni kinasa sauti kile wakati wakiwa wanazungumza mambo yao ya siri na hasa Joe alipoanza kuwapa mpango wa kumpumzisha Rais Costa, yeye Pius alikuwa akikiwasha na kurekodi kwa siri. Hakuna aliyekuwa na shaka na Pius wala kuwaza kuwa anaweza kufanya jambo lile.
Baada ya Pius kuhakikisha Jenereali Nduta yupo kwenye WhatsApp alikuwa akisogeza mbele mazungumzo mpaka kwenye zile dakika alizozikariri kuwa ndipo walikuwa wakizungumza juu ya mkakati wa kumpumzisha Rais Costa basi alishikilia kitufe cha kurekodia sauti kwenye simu yake na kuiweka karibu na kile kinasa sauti na kila neno lilirekodiwa na simu na kumtumia Jenerali kama Ushahidi.
Pia alituma screenshot za yale maneno ya siri ya ‘ego testor’ kama ushahidi kuwa Macha anahusika. Ni rahisi kusema kama ni kusaliti tu basi Pius alisaliti wenzake kwa mikono na miguu yani mzima mzima.
Haikujulikana ni kwanini Pius alikuwa akimpenda Rais Costa kiasi cha kumsaliti mtu kama Joe. Ilibaki ni fumbo kubwa.
Baada ya kupata Ushahidi ule kutoka kwa Pius, Jenerali Nduta haraka alimtaarifu Rais kumuweka chini ya Ulinzi Stanley Macha na sasa vijana wa Usalama wa Taifa pale Ikulu walikuwa wakitekeleza amri hiyo. Macha alikuwa hana ujanja.
**************************************
“Macha, atleast we have tried” (Macha, angalau tumejaribu). Joe alimwambia Macha kwa simu kwa huzuni sana na kukata tamaa kuwa sasa hawana pa kutokea lakini angalau wamejaribu kutaka kutekeleza mpango wao walioona una manufaa kwa taifa.
“Yes Joe, we have tried. Goodluck friend” (Ni kweli Joe, tumejaribu. Nakutakia kila la heri Rafiki yangu) Macha alijibu na kabla hajamaliza vijana walishamfikia na kwa heshima kubwa kwa sababu yule ni bosi wao walimwambia kwa adabu….
“Kwa malekezo ya Rais wa Jamuhuri ya watu wa Stanza, naomba unikabidhi beji yako na kuanzia sasa upo chini ya ulinzi”, Meshack alimwambia bosi wake Stanley Macha.
“It’s ok kid, do your work” (Sawa, fanya kazi yako), Stanley Macha alimjibu Meshack kwa unyonge huku akimkabidhi beji na bastola anayotembea nayo.
****************************************
Joe na Habibu walibaki katika ardhi ya China huku wakiwa wamechanganyikiwa. Hawakuweza kuelekea ubalozini kwasababu waliamini kuwa taarifa zitakuwa zimeshawafikia.
Hali ya kutokujua pa kuanzia iliwakumba wote wawili. Joe alifikiri zaidi kuhusu familia yake aliyoiacha Stanza na namna ambavyo ilishaanza kuneemeka na msamaha wa Rais Costa na ni nini kingetokea.
Yeye Habibu alifikiri zaidi kuhusu kuharibu Maisha yake ya kitaaluma kwani ubalozi ni heshima ambayo kama ukiitumikia vyema basi haiondoki tena maishani mwako. Na kwa matukio ya siku moja tu, ameshapoteza hadhi ya ubalozi na uelekeo wa Maisha yake kwa ujumla upo mashakani.
Habibu na Joe waliangaliana kwa macho ya kukata tamaa pasi na kuongea suala lolote.
Muhudumu wa pale uwanja wa ndege aliwatazama bila kuelewa jambo lililokuwa linaotokea. Kwa mara nyingine wote walimuangalia Pius ambaye alionekana kuwa upande wa mawazo ya Joe safari nzima kumbe ni shushushu. Kwakuwa ni ardhi ya ugenini, Pius asingeweza kuwakamata au kufanya jambo lolote.
Ghafla, kama mtu aliyegutuka kutoka usingizini, Joe alimtizama Habibu machoni na kumwambia kwa sauti ya taratibu iliyoanza kuwa tulivu baada ya hofu kutanda, ‘’nina wazo, huu ndiyo mwanzo. Yajayo ni zaidi ya yaliyopita’’, Joe alisema.
“Unamaanisha nini Joe? Kila kitu kimeshaharibika hapa. Maisha yetu ni sawa na yamefikia mwisho” Habibu aliongea kwa sauti ya mtetemo kama mtu anaetaka kulia lakini anajikaza kume.
“No one has a problem with the first mile of a journey, even an infant could do fine for a while. But it isn’t the start that matters. It is the finish line’’ Joe aliendelea kuongea katika lugha ya kimombo kilichonyooka, na wakati huu alimnukuu mwanafalsafaJulien Smith.
Joe alianza kusogea kwa kuondoka huku Habibu akimfuata. Alizungumza kwa utaratibu na umakini na kusema ‘’It’s never over, it’s not over, not just yet. At best, it’s just paused for a moment. Pull up your socks boy and get ready to get started’’, Joe alimaliza na kumwacha Habibu akindelea kushangaa Joe anamaanisha nini?
Joe aliendelea kupiga hatua huku moyoni akimuwaza rafiki yake mpendwa Stanley Macha atakuwa katika hali gani ndani ya mikono ya Rais Sylvester Costa.
*************************************************************
Je, Umeipenda simulizi hii?.Tafadhali naomba uipe alama(Rate It) kwa kubofya hapa>>>
**************************************************************
Hii Ni Sehemu Ya Mwisho Ya Msimu Huu Wa Kwanza Wa Simulizi Hii.Ninashukuru Kwa Kuifuatilia.Baada Ya Kuipa Alama Na Kupata Maoni yako Nikusihi Usiache Kuifatilia Mara Tu Inapoanza Msimu Wa Pili Hapo Mwezi Februari.
Sent using Jamii Forums mobile app
Nipo juzi, jana na leo.....story nzuri inavutia, haichoshi kuisoma
Najifunzia kingereza kwenye hii story [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] big up The BookSEHEMU YA SITA
Mazungumzo Mazito Yarindima Pyongyang. Timu Ya Joe Na Timu Ya Waziri En Zaonyeshana Ujuzi
“Gentlemen, it’s time” (Ndugu, muda umefika), Waziri En, anayehusika na masuala ya kigeni na mahusiano ya kimataifa wa Korea Kaskazini aliingia akiwaita Joe na wenzake wamfuate.
Huku En akitangulia, Joe alifuata na kisha Habibu na Pius. Mara baada ya wote kutoka mlango wa chumba namba 315 ulijifunga lakini ghafla Pius aligundua kuwa amesahau simu yake juu ya meza ndogo ya kahawa iliyokuwa pembeni yake. Simu ile aliitoa mara baada ya kutaka kuwasiliana na Stanley Macha ili kujiridhisha kama kweli kuna mpango wa kumpumzisha Rais Costa nje ya madaraka kabla ya muda wake kuisha. Hivyo alipokumbuka alitaka kurudi ndani ya chumba kwa haraka ili aichukue.
“Aaaaaaaaaaaaaah”, alisikika Pius akilia kwa nguvu mara tu baada ya kugeuka na kuusogelea mlango ule wa chumba namba 315. Haraka En alitoa ishara fulani na hapo hapo walitokea askari wawili wa usalama kama upepo wa kisulisuli na kumnyakua Pius kumpeleka ambapo Joe hakupafahamika.
“What’s going on here?” (Nini kinaendelea?), Joe aliuliza kwa mshangao huku akimwangalia En.
“Relax, it is just a normal security measures that have been taken. He has been exposed to methylbenzene, a chemical substance that is irritants when contacted to an eye, so they have taken him to wash it out and he will join us soon. He should have told me that he was returning to the room, I would have given him security clearance. My apologies for the inconvenience”.
(Tulia, ni utaratibu wa kawaida wa kiusalama umechukuliwa. Ameingiwa machoni na kemikali iitwayo methylbenzene, ni kemikali ambayo ikikuingia machoni inawasha sana, kwahiyo wamemchukua kwenda kumuosha na ataungana nasi muda si mrefu. Alitakiwa anitaarifu kuwa anarudi kwenye chumba ili nimuombee kibali. Samahani sana kwa usumbufu huu). Alikuwa ni Waziri En akimwelezea Joe nini kimetokea huku wakiingia kwenye chumba cha mkutano.
***********************************
Jengo la makazi ya Rais Kim lilikuwa na ulinzi usio wa kawaida. Katika vyumba na korido zote kumefungwa kamera ambazo zina scan sura yako. Kila mtu aliyepo ndani ya jengo lile hupimwa nyuzi joto la mwili wake pamoja na mapigo ya moyo na sensors zilizofungwa kila kona, hivyo ni kusema joto lako likipanda ama mapigo ya moyo yakipanda ama kushuka kuliko kawaida haraka utaanza kufatiliwa nini kinaendelea kwenye mwili wako.
Si hivyo tu, ilikuwa hairuhusiwi kuelekea popote ambapo sio eneo lako la kazi bila kutoa taarifa kwenye chumba cha usimamizi (Control room) ili wakupe ruhusa na kuzuia hatua zozote za kiusalama kuchukuliwa dhidi yako la sivyo ni lazima udhibitiwe. Hivyo ni kusema mienendo ya kila mtu ndani ya jengo lile inajulikana kwa kila hatua na kila dakika.
Katika kila eneo kuna matundu madogo na sensors zinazofatilia lenzi ya macho ya mtu. Matundu hayo hurusha maji ya kuwasha pale tu mtu anapokatiza eneo ambalo hajapewa kibali. Maji hayo hupigwa moja kwa moja machoni kufuatana na mahali unapotazama labda uwe umeyafunga.
Milango yote hufunguliwa kwa rimoti kutoka chumba cha usimamizi. Hivyo ni kusema kamwe huwezi muona mtu yeyote akifungua mlango wowote na milango yote haina vitasa. Kuta za jengo lile zina unene sawa na mita moja zenye kujengwa na chuma kizito na juu kuweka simenti kali. Kuta na milango yote havipitishi risasi.
Kitendo cha En, Joe, Habibu na Pius kutoka ndani ya chumba namba 315 kilitoa taarifa chumba cha usimamizi kuwa watu hawa wametoka na wanaelekea chumba namba 441 hivyo kila hatua za kiusalama zilirudishwa kwenye chumba namba 315. Mlango ulifungwa,sensors za maji washa zilifunguliwa na za kupima joto zilifunguliwa kuonyesha kuwa eneo lile halihitaji tena kuwa na joto lolote bila taarifa.
Kitendo cha Pius kurudi kilasensor ilimdhania ni mvamizi na haraka kuchukua hatua. Mlango ulikuwa umebana na sensor inayofata macho ilifanya kazi na kuruhusu methylbenzenekurushwa moja kwa moja machoni mwa Pius. Ni sahihi kusema kuwa Ryongsong si makazi ya kawaida.
Wakiwa wameketi, Joe na En pamoja na wajumbe wao walimwona Pius akiingia huku akitabasamu. “This place is crazy”, (Hili eneo ni la ajabu). Pius alimnong’oneza Joe akiwa anaketi upande wa kulia kwake.
“Gentlemen, my apologies once again, now we can start our conversation. Shall we?” (Ndugu, niwaombe radhi kwa mara nyingine tena na sasa tunaweza kuanza mazungumzo yetu. Au siyo?). Waziri En aliwaalika Joe na wenzake huku akitabasamu. “확실한” Hwagsilhan (Sawa), Joe alijibu kwa kiKorea.
Wakati Upande mmoja akiwa amekaa Joe, Habibu na Pius, upande wa pili wa meza alikaa Waziri En, Jenerali Uk In ambae ni Mkuu wa Jeshi la Ukombozi la Korea Kaskazini na wajumbe wengine wawili. Kikao kilianza.
***************************************
“Tetesi hizi ninazozisikia za chama Tawala kinachoongozwa na Rais Costa za kutaka kubadili umri wa kumruhusu mtu kugombea Urais kutoka miaka 40 mpaka 55 sisi kama wafanya siasa mbadala tunakataa na muswada huo ukija tutaupinga kwa nguvu zote, kwanza haufai hata kuingia bungeni, vuguvugu la kutaka kuruhusu Rais agombee muhula wa tatu tena kwa kipindi kirefu zaidi ya awali lilianza hivihivi’’. Alikuwa ni ndugu Julius Kibwe kiongozi mkuu wa chama kikuu cha upinzani nchini Stanza akizungumza wakati wa mahojiano katika kipindi cha Tarumbeta la Alasiri, kipindi cha Luninga kinachorushwa na stesheni ya MULIKA.
Akiwa ni miongoni mwa wageni walioalikwa kwenye mjadala huo akiwemo na Katibu Mkuu wa chama tawala ndugu Stanslaus Kaberege. Wote walikuwa wakimulika hali ya kisiasa na Uchumi nchini Stanza.
“Kwani shida ni nini”, Stansalaus aliuliza kwa kebehi.
“Ndugu yangu usijitie upofu kwa sababu upo hapo kutetea maslahi ya tumbo lako. Madhara yapo wazi kabisa katika hii hatua na tunajua lengo la Rais Costa ni kutaka kuminya upinzani katika uchaguzi ujao akijua fika wengi wa viongozi wa upinzani wenye matamanio na nafasi ya Urais watakuwa hawajafikia umri huo hivyo kutaka tupate wagombea wasiojulikana na kupunguza ushindani kwake.
Lakini la pili, hata ndani ya chama tawala na wewe mwenyewe unajua vijana wengi machachari na wenye uzoefu mkubwa wa uongozi watakuwa hawajafikia miaka 55. Vijana kama kina Habibu alioamua kuwanyamazisha kwa kuwapa ubalozi ni miongoni mwa watu aliowatoa kwenye ulingo wa kisiasa ili kupunguza upinzani dhidi yake hata ndani ya chama chenu”, Kibwe aliongea kwa msisitizo.
“Unajua ndugu mtangazaji, hata kama tetesi hizi zina ukweli maana nikiri wazi hazijafika kwenye meza yangu, sisi kama chama tunaamini na tunatambua kuwa uRais ni taasisi nyeti inayohitaji mtu aliyetulia kiakili na aliyekomaa, hivyo sioni shida kabisa kama wabunge wakipima wakaona hili linafaa wakaliafiki”. Stanslaus aliamua kujibu kiunyonge kwa kumuelekezea majibu mtangazaji badala ya Julias Kibwe alietoa hoja.
“Wakati nchi za wenzetu wakifikiri kupunguza umri ili kuwapa vijana nafasi ya kujiamulia hatma ya kizazi chao wewe unatetea kuongeza umri kuwapa wazee watuamulie hatma ya Maisha yetu? Hatutakubali.” Kibwe alionekana kukasirika kidogo na jibu la Stanslaus.
“Sawa, labda kwa sababu suala hilo ni tetesi tuliache na kwasasa tuangazie uchumi na hatua za maendeleo anazochukua Rais Costa, kwako katibu”, mtangazaji alimrushia Stanslaus swali.
“Juhudi zinaonekana. Tumeshuhudia mapinduzi makubwa ya kilimo, mapinduzi makubwa ya kibiashara katika bandari yetu. Leo tu Rais ametoka kuzindua maghala makubwa ya chakula na kutoa kodi zote sumbufu kwa wakulima achilia mbali mapinduzi makubwa yaliyotangazwa na benki ya kilimo kuwawezesha wakulima.
Tumeshuhudia miundombinu ikitengenezwa na mambo mengine mengi. Unajua ubaya wa wapinzani kama kina Kibwe, japo tunaheshimu michango yao lakini huwa hawaoni mazuri serikali inayofanya. Inawezekana ni kwasababu tu hawalitakii mema taifa letu au wana tamaa ya madaraka badala ya kuonesha uzalendo na kuungana na serikali kuwalete wananchi masikini maendeleo”, Stanslaus alionekana kujibu kwa bashasha.
“Miundombinu gani? Tuache kucheza na maisha ya watu. Hospitalini hakuna madawa wala madaktari, mashule hayana hata matundu ya vyoo, walimu wala madawati. Maji bado ni tatizo halafu mnasimama kusema maendeleo yanaonekana? Maendeleo ya Vitu na siyo maendeleo ya Watu ndugu Stanslaus.
Unawezaje kujenga uwanja mkubwa wa kimataifa wa ndege jimbo la Nungu kisa tu ndipo Rais alipotokea wakati ungeweza kufanya uwekezaji huo maeneo ya kimkakati ambayo yangekuza biashara za ndani za utalii na usafiri wa anga wa kikanda. Tija ipo kwenye uwekezaji wa kimkakati. Sasa kiwanja kile kimegeuka eneo la Kunguru kufanyia mashindano ya kuruka badala ya ndege, ndege gani itatua kule na ili iweje?
Mmejenga kituo kikubwa cha sayansi na teknolojia mkijinasibu mnataka Stanza iwe kitovu cha TEHAMA ukanda huu lakini mmewezaje kujenga kituo hicho huku mkijua elimu yetu bado ni tia maji tia maji? Kwanini tusingeanza kuimarisha kuanzia elimu ya msingi kuja juu hivyo kituo hiki kingekuja kuwa na manufaa?”, Kibwe alionekana kuongea mfululizo.
“Tatizo ni moja tu, ni wewe, sio Rais”, Stanslaus alionekana kujibu tena kwa kebehi.
“Ndio maana tutahakikisha Rais Costa harudi tena madarakani”, Julias alijibu kwa hasira tena kwa ufupi.
“Muda wetu unakaribia kufika ukingoni, labda kwa kumalizia ningependa kujua ni kwa vipi na hasa wewe Julius umejipanga kwa ajili ya kuchukua nafasi ya juu ya uongozi wa nchi, na Stansalaus kwa upande wa chama tawala mmejipangaje kuhakikisha vijana wanasimama na kugombea nafasi hii?” Mtangazaji alimalizia kuuliza.
“Kwanza, chama chetu kina uungwaji mkono mkubwa kutoka kwa vijana. Tumefanya utafiti na kugundua kuwa kama uchaguzi ungefanyika leo, chama tawala kingepata asilimia 22 tu ya kura katika nafasi ya Urais. Ninachoweza kusema ni kuwa, uchaguzi mkuu ujao hakutakuwa na wizi wa kura ambao chama tawala kimezoea kufanya. Kila kura itahesabiwa.
Tutaamkia na kulala kwenye kila kituo cha kupiga kura. Huu ni mwisho wa Costa na mabavu yake. Lakini pia tumejipanga kupigana kwa njia zozote zile kuhakikisha kuwa katiba haibadilishwi ili kuzuia wagombea vijana kuwania nafasi ya Urais. Mwambieni Costa kuwa hilo haliwezekani’’, alisema Kibwe akionekana waziwazi kujipanga haswa kwa uchaguzi mkuu ujao.
“Sisi tumejipanga. Chama chetu ni chama tawala na kitaendelea kuwa chama tawala milele kwasababu kinapambania maslahi ya nchi yetu. Namshauri tu Kibwe na wenzake wamuunge mkono Rais Costa ili tuwaletee maendeleo wanastanza’’. Alihitimisha Stanslaus akionekana kutokuwa na wasiwasi na utawala wa Rais Costa.
*************************************
Mazungumzo kati ya timu ya Joe na Waziri En yalikuwa mazito na ya ndani sana.
“I think the issue of establishing a secured communication system for Stanza should be handled by our Chinese friends who are more technologically advanced than us. Over the last few decades, China has been able to develop the best technology, second to none and they are our very good partners. We also use their technology in our communications. If that is something of interest to you, we can assist you to establish conversation with the Chinese who are also good friends with your country. So, lets put that aside and focus on the military assistance and technology”.
(Nafikiri suala la mtandao wa mawasiliano salama tuwaachie China. Wao wana teknolojia ya hali ya juu ya mawasiliano na ni marafiki zetu wazuri. Kwa kipindi cha miongo michache iliyopita, wao wameweza kuendeleza teknolojia kubwa ya mawasiliano salama ambayo haina mshindani. Tunaweza kusaidia mazungumzo nao maana hata sisi tunatumia teknolojia yao. Hivyo suala hili tuliweke pembeni kwa sasa na tuangazie suala la msaada wa kijeshi na teknolojia), alikuwa ni Waziri En akiweka sawa majadiliano baada ya kuona suala la masuala ya mawasiliano ni vema wakapewa China.
Alitoa maoni yale kwa sababu kuu mbili ambazo Joe alizing’amua lakini akamezea. Kwanza ni ukweli teknolojia ya mawasiliano wanayotumia Korea Kaskazini ni muunganiko wa teknolojia ya Uchina kwa asilimia kubwa na Urusi na yao kidogo. Lakini kiufundi, En hakutaka kuharibu wala kuleta sintofahamu kati ya taifa lake na China. China ni chanda na pete na Korea Kaskazini.
Kwake En aliona si sawa kwa Stanza kuivuka China au kwenda kuongea na Korea kuhusu masuala ya kusimika mifumo ya mawasiliano salama na kuiacha China, ambayo ni mbobevu wa siasa za Afrika na mwekezaji mkubwa.
En alitaka China ahusike katika mchakato huo. Korea haikutaka iwe katika sintofahamu na China hata kidogo hivyo En alionelea kwa namna moja ama nyingine hiyo iwe ni fursa kwa Korea kuiambia Rafiki yake wa karibu China kuwa kuna jambo tunataka kutekeleza Africa nchini Stanza. En alianza kutabiri mbele kurudi nyuma kwa kuelewa nguvu kubwa itakayoibuka kutoka mataifa ya magharibi mara tu mambo fulani yakianza kutekelezwa na sasa Korea ilihitaji iwe na mshirika mapema.
Joe alikubali kuwa wajadili kwanza kuhusu rada na misaada ya kijeshi kama ilivyopendekezwa na Waziri En. Waziri En alimwambia wana uwezo wa kuwapa rada zote za kuangazia usalama wa maji, hewa na nchi kavu.
“Comrade En, our priority is installing AN/SPF-71 generation radar’’. (Kamaradi En tungependa kupata rada kizazi cha AN/SPF-71 kama kipaumbele chetu cha kwanza), Luteni Jenerali Pius aliingilia kama eneo lake la uzoefu.
AN/SPF-71 ni kizazi cha rada za hali ya juu zenye uwezo wa kunasa aina zote za mawimbi na kwa maeneo yote. Huitwa kwa kizungu three surfaces radar detection, huweza kunasa mawimbi ya makombora ya masafa marefu yatupwayo angani, majini na nchi kavu. Pia kizazi hiki kina mfumo wa kunasa mazungumzo na uwezo mkubwa wa kuingilia mazungumzo mengine.
“No, that is an outdated generation, we have invented new version, TI/333-A. As our good partners, Stanza will be the first country outside Pyongyang to have such technology.’’ (Hapana, kizazi hicho ni cha zamani, tunacho kipya chaTI/333-A, kwasababu Stanza ni marafiki zetu wa kihistoria, tunaweza kuwapa kama nchi ya kwanza kuwa na teknolojia hiyo baada yetu). Jenerali Uk In Mkuu wa majeshi ya ukombozi wa Korea Kaskazini alidakia.
Pius hakuamini kama kuna kizazi kingine cha rada chenye uwezo zaidi ya AN/SPF-71. Kizazi hiki alielezwa kina uwezo wa kunasa mawimbi ya rada nyingine mfano ya adui na kuharibu kabisa isifanye kazi tena na uwezo mkubwa wa kunasa mawimbi ya targets mbalimbali kwa wakati mmoja yaani Multi-targets sensors detection.
“Excuse me, when did this invention happen? Because the latest generation even in the USA, China and Russia is AN/SPF-71.” (Ningependa kujua ugunduzi huu ulifanywa lini kwa sababu hata Marekani, China na Urusi kizazi chao cha mwisho ni kile cha AN/SPF-71). Pius alionekana kushangaa na kutokuamini. Kwa uchunguzi wake alijua hakuna rada zenye teknolojia ya hali ya juu zaidi ya zile za kizazi cha AN/SPF-71ambazo ndio hutumiwa na mataifa makubwa matatu ya Marekani, China na Urusi.
“You have no idea about the military supremacy of North Korea my friend, it is the very reason why we have managed to keep our country safe over the past 50 years. We develop our technology in utmost secrecy, arguably undetected. TI/333-A is more powerful than any radar generation in this world so far. With it’s Wang-C3NKR series, you can put your three neighbor countries in range all at once. Ha ha ha”.
(Hujui chochote kuhusu nguvu za kijeshi za Korea Kaskazini Rafiki yangu na ndiyo maana tumeweza kuifanya nchi yetu kuwa salama kwa kipindi cha miaka 50 sasa. Tunaendeleza teknolojia yetu kwa usiri mkubwa, naweza kusema bila kufahamika na washindani wetu. TI/333-A ni kizazi cha rada chanye nguvu kuliko kizazi chochote katika ulimwengu huu. Kwa kutumia toleo lake moja tu la Wang-C3NKR unaweza ukaziweka nchi zako tatu majirani kwenye uzio wako zote kwa wakati mmoja. Hahaha’’. Jenerali Uk In alimjibu Pius kwa majivuno ya kicheko.
Pius aliendelea kuwapa maombi mengine na kutaka kujua marekebisho yatakuwaje na nani atakuwa anazisimamia. Walikubaliana kuwa wanajeshi kutoka Stanza wangeenda Korea kupata mafunzo lakini zaidi ya hayo marekebisho yote yatakuwa yakifanyika na wa Korea wenyewe.
Maongezi yaliendelea na sasa walijadiliana misaada ya kijeshi.
“Well, president Costa is intending to mordenize the military. We require technical trainings backed up with high mordenised military equipments”. (Sasa, Rais Costa anakusudia kuliimarisha jeshi. Katika eneo hili tunahitaji mafunzo ya kijeshi na vifaa vya kisasa kabisa), Joe alitoa maoni.
“Mr. Joe, there is a lot of highly advanced military equipments that we can offer, but there is one which we think is more interesting and ofcourse unmatched by enemies, nucler weapons”. (Joe, kuna vifaa vingi vya kisasa vya kijeshi tunavyoweza kuwapa lakini kuna hii moja tunafikiri ni nzuri zaidi ya yote, silaha za nyuklia), Waziri En alijibu kwa haraka. Maneno ‘silaha za nyuklia’ iliwafanya Joe na wenzake waangaliane.
“Mmmh mmmh (Joe alisafisha koo). Comrade En…I don’t think if at all, we can handle such equipments. We can talk about other military equipements, that do not include nuclear weapons”. (En, sidhani kama tupo kwenye nafasi nzuri ya kumiliki silaha za nyuklia. Tuongelee vifaa vingine ambavyo havihusishi matumizi ya nyuklia), Joe alijibu kwa haraka.
“Are you afraid of America and her allies?”, (Mnawahofia Marekani na washirika wake?) Jenerali Uk In aliuliza.
“No we are not, but our visit here is rather focused on acquiring a new friend without jeopardizing friendship with others. (Hapana, lakini lengo la safari yetu ni kupata Rafiki mpya bila kuathiri urafiki tulio nao na mataifa mengine), Pius alidakia.
“You can’t have a friendship with North Korea without jeopardizing some of your other friendships even if that doesn’t include acquiring nuclear weapons from us”. (Huwezi kuwa na urafiki na Korea Kaskazini bila kuathiri urafiki na baadhi ya marafiki zako wengine hata bila kupata silaha za nyuklia kutoka kwetu), Waziri En aliwasisitizia kina Joe.
“If we take your proposal of acquiring nuclear weapons, how will you support us against pressure from international community, particularly from America?” (Kama tukichukua wazo lenu la kuwa silaha za nyuklia kwenye taifa letu, mnatuhakikishia vipi usalama wetu wakati tutakapoanza kupata vitisho vya kimataifa hasa Marekani?) Habibu alivunja ukimya wake wa muda mrefu.
“We should be able to ensure that Stanza remain safe against aggression of the West and so-called international community. In fact China and Russia has been secretly looking for an African country that will be able to join the East in balancing the world’s power by acquiring nuclear weapons technology. All you need to do is to escalate your relationship with China and Russia and, potentially India so that you will still be able to remain afloat if they sanction you, but security-wise you will be fine”.
(Tutawalinda kikamilifu dhidi ya tishio lolote kwa Stanza kutoka kwa magharibi na kinachoitwa Jumuiya ya Kimataifa.Hata hivyo China na Urusi zimekuwa zikitafuta mshirika imara kutoka Afrika atakayekuwa na teknolojia ya Nyuklia ili nchi ziheshimiane duniani. Mnachotakiwa kufanya ni kuongeza mashirikiano ya kiuchumi baina yenu na China na Urusi na labda India pia ili msitetereke kutokana na vikwazo vya kiuchumi vitakavyowekwa, lakini kiusalama mtakuwa sawa kabisa), Waziri En alimjibu Habibu.
“If I am correct, you haven't provided nuclear weapons to any country so far, we will be the first country in the world to get such a technology from you. So, you claim that you will ensure our country is safe against any aggression. Let us remind you a few things; where is Abdul Qadeer Khan, a Pakistanian nuclear scientist who was exporting nuclear technology to your country, Libya and Iran including centrifuges and consequently caught by Americans in 2004?. What did you do to assist India to clear the 2016 UN allegations that the country through her Technology Institute was giving specialized training on Space Instrumentation to one of your students that lead to the launch of Unha-3 rocket in 2012?”
(Kama nipo sahihi, hamjawahi kutoa silaha zozote za nyuklia kwa nchi yoyote, sisi tutakuwa taifa la kwanza duniani kupata teknolojia hiyo kutoka kwenu. Hivyo kama mnataka kutuaminisha kuwa mnaweza kutulinda, mnaweza kutuambia yupo wapi Abdul Qadeer Khan, mwanasanyansi wa nyuklia wa Pakistan aliyekuwa akiingiza teknolojia ya nyuklia hapa kwenu, Libya na Iran na hatimaye kukamatwa na Marekani mwaka 2004? Pia, mlifanya nini kusaidia India kusafisha jina lao mbele ya Umoja wa Mataifa uliotuhumu kuwa kwa kutumia chuo chao cha teknolojia walitoa mafunzo kwa mmoja wa wanafunzi wenu yaliyomsaidia akaongoza timu ya kutengeneza roketi aina yaUnha-3 mwaka 2012?). Habibu alionekana kuwa na taarifa za kutosha na aliuliza maswali mfululizo. Joe alionekana kutabasamu kwa uwezo wa vijana alioambatana nao.
“About Abdul Khan, he is fine. If you are more interested to know what happened, we can talk to him right now. He was put under house arrest by the then General Perves Musharaf and to correct you, he was never touched by the Americans. Do you know why? I can assure you that you will be fine.
Abdul was a double-agent, used by both Americans and UK for the same job, we managed to have him work for us while the Americans believed he was their covert asset. When they learned that he is working for us too they reacted, but we managed them.
About India, after the UN report, what happened next? Have you heard anyone talking about it again? Mr Habibu come on, you are better than that”
(Kuhusu Abdul Khan yupo salama na unaweza kuongea nae hata sasa kama ukitaka. Alihifadhiwa sehemu salama na aliyekuwa Jenerali Perves Musharaf na kukusahihisha tu hakuguswa na Marekani. Unajua ni kwa nini? Sasa unaweza kuelewa ninaposema tutahakikisha mpo salama.
Abdul alikuwa akitumiwa pia na Wamarekani na Uingereza kwa kuwapa teknolojia ya nyuklia. Wakati huohuo alifanya kazi na sisi huku wao wakiamini kuwa ni mtu wao. Walipofahamu kuwa anafanya na sisi pia wakachukia na kutaka kumkamata, lakini tuliweza kuwadhibiti.
Kuhusu India, baada ya ile tariifa ya UN ni nini kilifuata? Kuna yeyote unaemsikia akiiongelea tena. Habibu vipi bwana?). Waziri En alijibu kwa majigambo.
“Why is it necessary that we agree with you on this matter of nuclear weapons?”, (Kwanini inaonekana ni muhimu sisi kukubaliana nanyi katika suala hili la silaha za nyuklia?), Joe alidakia baada ya ukimya kidogo.
“Because this is one of the terms and condition of our partnership, along with others that Comrade Kim will suggest after we present our today’s deliberations’’. (Kwasababu hili ni mojawapo ya vigezo na masharti ya msaada na ushirika wetu nanyi, pamoja na mambo mengine ambayo kiongozi wetu Kamaradi Kim atatuambia baada ya kujadiliana nae, nasi tutawaambia kwanini tunahitaji hili liwe miongoni mwa mahitaji yetu), Wazir En alimjibu Joe.
Joe aliwaangalia wenzake na ilionekana ni vyema wakapewa muda kulijadili hivyo wapumzike halafu wakutane tena baadae kuendelea na mazungumzo. Walikubaliana na kurudishwa kwenye chumba namba 315.
Walipofika kila mmoja alipumua kwa nguvu. Kila mmoja alikaa kimya kwa dakika chache. Mazungumzo yale yalikuwa nyeti na mazito yaliyohitaji hekima kubwa. Suala la kukubali silaha za nyuklia kwenye taifa la Stanza lilikuwa kubwa. Kwanza sio jambo walilotumwa na lingeleta mtikisiko usio kawaida. Kila mmoja hakuwa tayari kuliingiza taifa la Stanza kwenye mtafakuru na robo tatu ya dunia kwa sababu tu ya kumiliki silaha hizo.
Waliwaza hivi siku ikatokea Korea wakawasusa itakuwaje? Maswali mengi yalirindima kwenye vichwa vyao. Lakini waliwaza kama hilo ndilo hitaji namba moja la Korea Kaskazini ili waweze kuwapa msaada walioufuata sasa wao wakakataa watarudi kumwambia Rais Costa kuwa wameshindwa? Joe hakutaka kukubali kushindwa.
Baada ya ukimya wa kama dakika tano nzima kila mmoja akiwa anamtegea mwenzake aanze kuongea Joe alivunja ukimya. “Guys come closer”, (Jamaa, sogeeni karibu). Joe aliwaita wamsogelee.
************************************
Joe Anataka kuwashauri Nini Wenzake? Kwanini Korea Inasisitiza Silaha Za Nyuklia Kwa Stanza?Usiache Kufuatana Nami Kwenye Msimu Wa Pili wa Simulizi Hii.
Imeandikwa na Lello Mmassy.
The Book.
With Great Pleasure.
Pius tutamnyamazisha faster[emoji28][emoji28][emoji28]Rais costa anafanana na mwafulani halafu huyu Pius huyu atawageuka wenzie