Simulizi : Ukweli Wenye Kuuma (Painful Truth)

Simulizi : Ukweli Wenye Kuuma (Painful Truth)

Abdallahking

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2018
Posts
3,985
Reaction score
10,840
1.jpg


Simulizi: UKWELI WENYE KUUMA ( PAINFUL TRUTH )
Mwandishi: NYEMO CHILONGANI
Imeletwa kwenu na: BURE SERIES


SEHEMU YA 1

Msichana Happy alikuwa akilalamikia uchungu ambao ulikuwa umemshika katika kipindi ambacho alikuwa shambani akilima. Damu zikaanza kumtoka katika sehemu zake za siri, akalitupa jembe lake pembeni na kuanza kulishika tumbo lake ambalo aliliona kuwa katika maumivu makali.

Mama yake ambaye alikuwa pembeni pamoja na wakulima wengine wakaanza kumsogelea, Happy alionekana kuhitaji msaada kwa wakati huo. Wakatandika kanga zao chini na kisha kuanza kumzalisha pale pale shambani. Mpaka wanafanikiwa kumtoa mtoto, Happy alikuwa amepoteza damu nyingi sana mwilini mwake.

Mtoto mchanga alikuwa akilia, walipomwangalia vizuri, waligundua kwamba alikuwa mtoto wa kiume. Walichokifanya ni kumuinua Happy na kisha kumpeleka katika kivuli cha mti wa mwembe ambao ulikuwa pembeni kidogo ya shamba hilo.

Happy bado alikuwa akiendelea kulia, maumivu makali bado yalikuwa yamelikamata tumbo lake. Kwa haraka haraka mzee Lyimo akachukua baiskeli yake aliyokuwa ameiegesha pembeni na kisha kumpakiza Happy na safari ya kuelekea katika zahanati ya Machame kuanza.

Njia nzima Happy alikuwa akilia, maumivu yalikuwa yakiongezeka kadri muda ulivyozidi kwenda mbele. Mpaka wanafika Zahanati, Happy alikuwa hoi, hakuwa akiweza hata kusogeza kiungo chake chochote cha mwili wake.

Manesi ambao walikuwa nje wakipiga stori, wakaanza kuwasogelea, wakamteremsha Happy kutoka katika baiskeli ile na kisha kuelekea ndani ya Zahanati hiyo. Mama yake Happy, Vanessa alikuwa amembeba mjukuu wake huku akijitahidi kumbembeleza aache kulia.

Happy akaingizwa ndani ya moja ya chumba cha zahanati ile na kisha kulazwa kitandani. Bado alikuwa akiendelea kulia kutokana na maumivu makali ambayo alikuwa akiyasikia yakizidi kadri muda ulivyozidi kwenda mbele. Manesi wakaanza kumhudumia Happy mpaka pale ambapo dokta wa zahanati ile alipofika.

Mzee Lyimo na mkewe, Bi Vanessa walikuwa nje wakisubiri kusikilizia ni kitu gani ambacho kilikuwa kimeendelea ndani ya chumba kile.

Wala hazikupita dakika nyingi, dokta akatokea mahali pale. Akaanza kuwaangalia huku macho yake yakionyesha wasiwasi fulani, aliporidhika, akaiweka vizuri miwani yake.

“Mtoto wake yupo wapi?” Dokta aliuliza.

“Huyu hapa” Bi Vanessa alimwambia huku akimkabidhi dokta mtoto yule.

Dokta alibaki akishangaa, mtoto yule alikuwa mweupe kupita kawaida, kichwani hakuwa na nywele nyingi kama ambavyo watoto wengi wa kiafrika wanavyozaliwa. Dokta hakuonyesha mshangao wake waziwazi, alichokifanya ni kumchukua mtoto yule na kuingia nae ndani ya chumba kile.

Mzee Lyimo na Bi Vanessa waliendelea kukaa nje ya chumba kile kwa takribani dakika kumi, mlango ukafunguliwa na dokta kutoka.

Wote wakajikuta wakisimama kutoka katika viti vyao, dokta akawaomba wamfuate. Safari iliiishia ndani ya ofisi ya dokta yule.

“Kama msingemuwaisha binti yenu, hakika hali ingekuwa mbaya sana” Dokta aliwaambia.

“Kivipi?” Mzee Lyimo aliuliza.
 
SEHEMU YA 2

“Amepoteza damu nyingi sana mwilini katika kipindi cha kujifungua, mbaya zaidi njia yake haikuwa kubwa kabisa jambo ambalo lilikuwa linamletea matatizo sana” Dokta aliwaambia.

“Lakini anaendelea vipi?” Bi Vanessa aliuliza huku akionekana kuwa na wasiwasi.

“Anaendelea vizuri. Ila inabidi tumpeleke KCMC kwa matibabu zaidi kwa sababu kuna baadhi ya dawa hapa ambazo hatuna” Dokta aliwaambia.

“Sawa”

Kama ilivyoongelewa na ndivyo ilivyotokea, siku iliyofuata Happy akapelekwa katika hospitali ya mkoa ya KCMC mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya kupata matibabu zaidi.

*****
Happy alikuwa mtoto wa tatu katika familia ya mzee Lyimo ambaye alikuwa mkulima mkubwa aliyekuwa akivuma kuliko mtu yeyote Machame. Mzee huyu alikuwa akimiliki mashamba makubwa ya Migomba pamoja na mpunga. Kwake, ukulima ndio ilikuwa kazi yake kubwa ambayo alikuwa akiifanya akisaidiana na mke wake, Bi Vanessa.

Waliwasomesha watoto wao katika shule za kawaida sana ila waliwapatia kila kitu ambacho kilikuwa kikihitajika shuleni huko. Walitaka watoto wao wasome kwa sababu katika vipindi vyote vya maisha yao walikuwa wakiamini sana katika elimu.

Miaka ikazidi kukatika. Happy akaanza kubadilika na kuanza kuonekana mzuri. Weupe ambao alikuwa nao ulikuwa ukimvutia kila mwanaume ambaye alikuwa akimwangalia. Happy alikuwa akizidi kunawiri kadri siku zilivyokuwa zikizidi kwenda mbele.

Kama kawaida yao, wanaume hawakuwa nyuma, kila siku walikuwa wakijaribu kumuita Happy ambaye wala hakuonekana kuukubali wito. Kila mvulana akamuona Happy kama miongozi mwa wasichana ambao walikuwa wakiringa sana katika sehemu yote ya Machame.

Happy akafanikiwa kumaliza kidato cha nne katika shule ya Machame Girls Sekondary School. Hiyo ilikuwa ni faraja kwa wazazi wake, kumaliza shule kwa binti yao huyo ambaye alikuwa mtoto wao wa mwisho kulionekana kuwafurahisha. Mapenzi yao yalikuwa makubwa sana kwa Happy kuliko kwa watoto wao waliotangulia, David na Steve.

Wakamwandalia binti sherehe kubwa kama ya kumpongeza kwa kile ambacho alikuwa amekifanya. Kwenye sherehe, watu walikula na kunywa vya kutosha, kwa wale ambao walikuwa walevi, pombe ya ndizi ilikuwa nyingi na ya kutosheleza.

Kila kijana ambaye alikuwa mahali hapo alikuwa akihitaji kupata nafasi ya kuongea na msichana Happy. Nafasi hiyo ilionekana kuwa ngumu kwani muda wote Happy alikuwa pembeni mwa mama yake ambaye alionekana kuwa kila kitu katika maisha yake.

Sherehe ikaisha na kila mtu kuelekea nyumbani kwake. Siku iliyofuata asubuhi na mapema Happy akatakiwa kuondoka mkoani Kilimanjaro na kuelekea Jijini Arusha. Bila ubishi, Happy akaelekea huko kuanza maisha mapya huku akisubiri majibu ya kidato cha nne.

“Do you speak English? (Unaongea Kingereza?)” Ilisikika sauti ya mvulana mmoja wa kizungu akiwauliza vijana ambao walikuwa wamekaa kwenye
 
SEHEMU YA 3

benchi wakicheza drafti.

Hakukuwa na mvulana yeyote ambaye alilijibu swali lile kutokana na kutokuielewa lugha ya Kingereza, walibaki wakiangaliana tu huku kila mmoja akitamani mzungu huyo aondoke mbele ya macho yao.

Mzungu yule akabaki akiangalia huku na kule huku begi kubwa likiwa mgongoni mwake, kwa muonekano ambao alikuwa nao, alionekana kuhitaji msaada wa kitu fulani. Wala hazikupita dakika nyingi, Happy akaanza kuonekana mahali hapo. Mzungu yule akaonekana kushtuka, hakuamini kama msichana aliyefanana na Happy angeweza kuwa katika nchi kama Tanzania.

Umbo na uzuri wa Happy ukaonekana kumvutia, akaanza kupiga hatua kumfuata. Happy alipoyapeleka macho yake usoni mwa mzungu yule ambaye alikuwa akimfuata, akabaki akitetemeka. Alitamani kukimbia, ndio, lugha ya Kingereza alikuwa akiifahamu vilivyo ila kamwe hakujiamini kuongea na mzungu.

Akaanza kuongeza mwendo wake, mzungu nae akazidi kuongeza mwendo zaidi na zaidi. Happy akaonekana kutokuwa na ujanja, akaupiga konde moyo wake na kusimama. Mzungu yule akaanza kumsogelea zaidi, alipomkaribia, tabasamu pana likaanza kuonekana usoni mwake.

“Do you speak English? (Unaongea Kingereza?)” Mzungu yule aliuliza.

“I do (Naongea)” Happy alijibu. Mzungu akaonekana kufurahi zaidi.

“I need your help, can you just help me (Ninahitaji msaada wako, unaweza kunisaidia?)” Mzungu yule aliuliza.

“Yeah! I can help you (Yeah! Ninaweza kukusaidia)” Happy alijibu.

“Okey! Am a tourist from U.S.A. I come here in Tanzania for two main reasons, fistly, I want to visit Ngorongoro National Parks and secondly I wanna see mount Kilimanjaro (Mimi ni mtalii kutoka nchini Marekani. Nimekuja nchini Tanzania kwa sababu kuu mbili, kwanza ningependa kutembelea mbuga ya wanyama ya Ngorongoro na pili ninataka kuuona mlima Kilimanjaro)” Mzungu yule alimwambia Happy.

“So, what can I help you? (Kwa hiyo nikusaidie nini?)” Happy aliuliza.

Mzungu yule alibaki kimya kwa muda, akayagandisha macho yake usoni mwa Happy, kadri muda ulivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo uzuri wa Happy ulivyozidi kuonekana usoni mwake. Alijiona kuwa na kila sababu ya kumwambia Happy kile ambacho kilikuwa kimeanza kujengeka moyoni mwake.

“Helllow...” Happy aliita mara baada ya kumuona mzungu yule akiwa ameduwaa huku amemkodolea macho.

“Where were we? (Tulikuwa wapi?)” Mzungu yule aliuliza huku akionekana kutolewa katika lindi la mawazo.

Happy akaonekana kukasirika, alichokifanya ni kugeuka nyuma na kisha kuendelea na safari yake. Mzungu yule hakuweza kuvumilia hata kidogo, akaanza kupiga hatua kumfuata Happy ambaye alikuwa akitembea kwa mwendo wa haraka haraka kama mtu ambaye alikuwa akiwahi kitu fulani.

“Exccuse me (Samahani)” Mzungu yule alisema na Happy kusimama.

“Can you tell me your name? (Unaweza kuniambia jina lako?)” Mzungu
 
SEHEMU YA 4

alimuuliza.

“No. I can’t (Hapana. Siwezi)” Happy alisema na kisha kuendelea na safari yake.

Mzungu yule hakuonekana kushindwa, kumruhusu Happy aondoke katika mikono yake ingeonekana kuwa kosa kubwa ambalo angejutia katika kipindi chote cha maisha yake. Alijiona kuwa na sababu ya kufanya jambo lolote lile ili mladi tu amueleze Happy jinsi alivyojisikia moyoni.

“My name is Wayne Ryn. Am from U.S.A. What is your name? (Jina langu ni Wayne Ryn. Ninatokea nchini Marekani. Unaitwa nani?)” Wayne aliuliza.

Happy akasimama na kuanza kumwangalia Wayne usoni. Watu wote ambao walikuwa wakiendelea na shughuli zao wakazisimamisha na kuanza kuwaangalia. Uso wa Happy ukaonekana kukasirika lakini uso wa Wayne ukaonekana kutabasamu.

“Happy” Happy alijibu na kisha kuanza kupiga hatua tena kuondoka.

“Happy...Ok! Let me call you Happiness. You are a beautiful girl that I’ve never seen (Happy...Sawa! Acha nikuite Happiness. Wewe ni msichana mzuri ambaye sijawahi kumuona)” Wayne alimwambia Happy ambaye alikuwa akipiga hatua kuelekea nyumbani kwa shangazi yake alipokuwa akiishi hapo Arusha.

Wayne hakutaka kunyamaza wala kusimama, bado alikuwa akionekana kuwa king’ang’anizi kupita kawaida. Aliendelea kumfuatilia Happy mpaka katika kipindi ambacho aliingia ndani ya geti. Bila hiyana wala aibu, nae akaingia ndani huku begi likiwa mgongoni mwake.

“Naona umekuja na mgeni” Shangazi yake, Bi Selina alimwambia mara alipomuona Happy akiingia huku Wayne akiwa nyuma.

“Yaanii nashangaa kwa nini ananifuata fuata. Nimechoka. Yaani anakera sana” Hapy alisema huku akiingia ndani.

Wayne akaanza kuongea na Bi Celina huku akijaribu kumwambia kuhusu msaada ambao alikuwa akiuhitaji kutoka kwa Happy. Hapo hapo Bi Selina akamuita Happy na kuanza kuongea nae pembeni. Mara ya kwanza Happy alionekana kukataa lakini baadae akakubali.
“Sawa nimekubali” Happy alimwambia shangazi yake.

“Usiogope. Anachokitaka kutoka kwako ni msaada tu wa kumtembeza hapa na pale. Atatoa kiasi cha dola kumi kila siku. Hauoni kama hizo ni fedha nyingi kwako?” Shangazi yake alimwambia.

Wayne hakutaka kuingia moja kwa moja na kulielezea lengo lake, alichokitaka ni kuingia kwa lengo jingine kabisa la kuhitaji msaada wa Happy na kuwa kama mwenyeji wake. Malipo ya dola kumi kwa siku zilikuwa fedha nyingi sana hasa katika mwaka huo wa 1990.

Siku iliyofuata, Wayne akafika nyumbani hapo na kuondoka na Happy. Njia nzima Happy alikuwa na jukumu la kumuelekeza Wayne kila kitu alichokuwa akikiona. Mawazo ya Wayne yalikuwa pengine kabisa, kichwa chake kiliwaza mapenzi tu.

Walitembelea sehemu nyingi tu hapo Arusha, mwisho wa safari yao, wakaamua kwenda hotelini. Mara ya kwanza Happy alionekana kuogopa lakini kutokana na maneno mengi ya Wayne, akajikuta akikubali na kwenda
 
SEHEMU YA 5

nae hotelini.

Ndani tena chumbani, Wayne akaonekana kubadilika. Akaanza kuongea mambo mengi ya mapenzi huku akijaribu kumbembeleza Happy. Muda wote huo, Happy alikuwa akiumauma vidole vyake tu. Happy hakuwa na nguvu za kumwangalia Wayne usoni, muda wote alikuwa akiangalia chini.

Hata alipoanza kushikwa bega alitulia tu, nguo yake ya juu ilipotolewa wala hakuleta ubishi wowote ule. Alikuja kushtuka mara alipojitazama na kujikuta akiwa mtupu. Akajaribu kuleta purukushani lakini akaonekana kushindwa.

Wayne akalala kifuani kwake, Happy akabaki akilia tu kwa maumivu makali. Bikira ambayo alikuwa nayo ndio ilikuwa siku ya mwisho kukaa mwilini mwake. Shuka likatapakaa damu. Happy akabaki akilia, hakuamini kama kweli kwa siku ile alikuwa amefanya mapenzi kwa mara ya kwanza.

“Mungu wangu! Kumbe niko kwenye tarehe zangu za kupata mimba” Happy alijisemea huku akionekana kushtuka katika kipindi ambacho Wayne akiwa pembeni akichukua taulo na kuelekea bafuni kuoga.

Macho ya Happy yakaanza kuwa mekundu, machozi yakaanza kujikusanya machoni mwake na baada ya sekunde kadhaa yakaanza kutiririka mashavuni mwake. Hakuamini kile ambacho kilikuwa kimetokea dakika chache zilizopita.

Alichokifanya huku akionekana kuchanganyikiwa ni kuanza kukimbia kuelekea nje ya chumba kile. Akaanza kushusha ngazi haraka haraka kuelekea chini huku akionekana kuchanganyikiwa.

Alipofika nje ya jengo la hoteli ile, akaanza kukimbia kuelekea nyumbani kwa shangazi yake. Njia nzima alikuwa akilia, moyoni alionekana kuumia kupita kawaida, kufanya mapenzi katika moja ya siku ambazo alikuwa na uhakika wa kupata mimba kulionekana kumuumiza kupita kawaida.

Alitumia dakika thelathini mpaka kufika nyumbani kwa shangazi yake, moja kwa moja akaingia chumbani na kujifungia. Hakutaka kutoka nje, aliamini kwamba kama angekaa ndani kwa muda mrefu basi angeweza kujisahaulisha na kile ambacho kilikuwa kimetokea.

Bi Selina akaonekana kumshangaa Happy, hakuelewa sababu ambayo ilimfanya kurudi nyumbani hapo huku akilia. Alichokifanya ni kuanza kumfuata chumbani kwake, alipoufikia mlango, akaanza kuugonga. Happy hakufungua mlango japokuwa alisikia fika kwamba Selina yake alikuwa akiugonga mlango ule.

Bi Selina aligonga mlango zaidi na zaidi, Happy akaamua kuufungua mlango. Selina akaanza kumfuatta happy pale kitandani alipokuwa na kisha kukaa pembeni yake. Kila alipojaribu kumuuliza, Happy hakujibu chochote kile zaidi ya kuendelea kulia.

“Tatizo nini Happy?” Bi Selina aliendelea kuuliza lakini Happy hakujibu kitu zaidi ya kuendelea kulia.

Bi Selina aliendelea kumbembeleza Happy zaidi na zaidi lakini Happy hakujibu kitu chochote kile. Alichokifanya Bi Selina mara baada ya kuona kwamba Happy haongei kitu chochote kile, akaamua kuondoka ndani ya chumba kile.

Happy hakujua afanye nini, hakujua kama angetakiwa kumwambia shangazi yake au la. Aliendelea kubaki chumbani kwa dakika kadhaa, baada ya muda
 
SEHEMU YA 6

akashtukia shangazi yake akianza kupiga hodi tena.

Mara hii akaingia huku akiwa katika hali ya kawaida, kwa mbali alionekana kukasirika. Akamfuata happy pale kitandani na kisha kukaa karibu nae. Akamwangalia Happy katika mtazamo ambao ukaonekana kumtia wasiwasi.

“Mbona umemkimbia yule mzungu?” Bi Selina aliuliza.

Happy hakujibu chochote kile, swali lile ambalo alikuwa ameulizwa likaonekana kuanza kukivuta tena kilio chake na kisha kuanza kulia tena. Alikumbuka vilivyo sababu iliyompelekea kumkimbia Wayne ndani ya chumba kile.

“Mbona umemkimbia mwezako?” Bi Selina aliendelea kuuliza.

“Nimeamua” happy alijibu.

“Alikupa hizo hela?” Bi Selina aliuliza.

“Ndio”

“Sasa kwa nini umemkimbia?” Shangazi alirudia swali lake.

Happy akashindwa ajibu nini, hakujua kama kulikuwa na sababu ya kumwambia shangazi yake kile ambacho kilikuwa kimetokea hotelini au la. Akayapeleka macho yake usoni kwa shangazi yake, akaanza kuyafuta machozi yake.

“Yule mzungu anakusubiri nje” Bi Selina alimwambia.

Happy akaonekana kushtuka kupita kawaida, hakuamini kile ambacho alikuwa amekisikia kutoka kwa shangazi yake. Alipanga moyoni mwake kwamba hakutaka kuonana tena na Wayne, kitendo kile alichokifanya cha kufanya nae mapenzi kilionekana kuanza kumuwekea aibu moyoni mwake.

“Yupo nje anakusubiri” Shangazi yake alimwambia mara baada ya kuona amekaa kimya kwa sekunde kadhaa.

“Sitaki. Sitaki kuonana nae” Happy alijibu.

Bi Selina alionekana kutokuelewa kitu chochote kile. Hakujua sababu ambazo zilimfanya Happy kukataa kuonana na Wayne na wakati nia asubuhi tu walikuwa wameondoka wote. Akaanza kuona kwamba kulikuwa na kitu ambacho kilikuwa kimetokea ila Happy hakutaka kumwambia.

“Niambie kuna kitu kimetokea?” Bi Selina alimuuliza.

“Hapana”

“Sasa kwa nini hautaki kuonana nae?”

“Nimeamua tu” Happy alijibu.

Bi Selina hakutaka kuendelea kubaki chumbani mule, alichokifanya ni kutoka chumbani mule na kuelekea nje.

****
Muda wote Wayne alikuwa akifurahia, hakuamini kwamba katika maisha yake angeweza kupata msichana ambaye alikuwa bikira na kuitoa yeye mwenye. Bikira ambayo alikuwa ameitoa kwa happy ilionekana kumchanganya kupita kawaida, muda wote bafuni alikuwa akiimba kwa furaha tu.

Akatoka bafuni na kisha kurudi chumbani. Akaanza kuangalia huku na kule, Happy hakuwepo. Wayne akaonekana kuchanganyikiwa, hakuelewa ni kitu gani ambacho kilimfanya Happy kuondoka ndani ya chumba kile pasipo kumuaga. Alichokifanya ni kuvaa nguo zake haraka haraka na kisha kutoka chumbani mule na kuelekea alipokuwa akiishi Happy.

Ingawa alikuwa akipata shida katika kuzikumbuka njia lakini alifanikiwa kufika. Akamkuta Bi Selina akiwa nje akifua nguo. Akamsalimia na kisha kumuulizia Happy. Alimueleza kila kitu ila hakumueleza kama alikuwa amefanya nae mapenzi.

Bi Selina akaonekana kukasirika, alichokifanya ni kuingia ndani ili amuite Happy. Wayne alibaki nje huku akionekana kuwa na furaha. Kitu pekee
 
SEHEMU YA 7

ambacho alikuwa akitaka kukiona kwa wakati huo ni kumuona Happy kwa mara nyingine tena.
Japokuwa kilikuwa kimepita kipindi kifupi lakini moyo wake ukaonekana kumkumbuka Happy. Hakutaka kuondoka mahali hapo pasipo kumuona Happy. Moyo wake tayari ulikuwa umekwishatekwa na binti huyo kiasi ambacho akaanza kumsahau Kristen , mchumba wake aliyekuwa nchini Marekani.
Bi Selina akarudi mahali hapo, Wayne bado alikuwa mvumilivu kusubiri, alipopewa taarifa kwamba Happy alikataa kutoka nje, moyo wake ukanyong’onyea kupita kawaida.
“But I want to see her (Lakini ninataka kumuona)” Wayne alimwambia Bi Selina.
“I know. She cried a lot. What happened when you left here? (Ninafahamu. Alilia sana. Nini kilitokea mlipoondoka mahali hapa?)” Bi Selina aliuliza.
“Nothing. We had some soft drinks somewhere but unfortunately she ran away. I tried to come after her but she disappered from my presence (Hakuna kitu. Tulikuwa tukipata vinywaji sehemu fulani, ghafla akaanza kukimbia. Nilijaribu kumfuatilia lakini akapotea katika uwepo wangu)” Wayne alimwambia Bi Selina.
“Ok! Dont worry. Just give me time, I will talk to her and tell you what happened to her (Sawa! Usijali. Nipe muda niongee nae na nitakuambia nini kilitokea)” Bi Selina alimwambia Wayne.
Wayne hakutaka kuendelea kubaki mahali hapo, alichokifanya ni kuanza kuondoka kurudi hotelini. Njia nzima alikuwa na mawazo, hakuamini kile ambacho kilikuwa kimetokea. Lengo lake kubwa lilikuwa ni kumuona Happy kwa mara nyingine kwa sababu alikuwa amemkumbuka sana, lakini mwisho wa siku alikuwa akirudi hotelini bila kuonana nae.
Akaingia ndani ya chumba kile na kisha kulala. Kwa wakati huo, Happy ndiye ambaye alikuwa amekitawala kichwa chake. Alimkumbuka sana Happy hata zaidi ya alivyokuwa akimkumbuka mpenzi wake aliyemuacha nchini Marekani, Kristen.
Simu yake ya mkononi ambayo ilikuwa imeunganishwa na mtandao wa kimataifa wa Tricom ikaanza kuita. Akainuka kivivu kitandani pale na kisha kuinyanyua simu ile kutoka mezani. Akakibonyeza kitufe cha kijani na kuanza kuongea.
“Rudi haraka sana nyumbani” Sauti ya upande wa pili ilisikika.
“Kuna nini baba?”
“Kuna tatizo. Kristen amezidiwa. Ugonjwa wa pumu umemuanza tena” Sauti ya baba yake ilisikika.
“Unasemaje! Sawa, nitakuja huko haraka iwezekanavyo” Wayne allijibu.
Tayari akaonekana kuchanganyikiwa, taarifa ambayo alikuwa amepewa ikaonekana kumchanganya kupita kawaida. Taarifa za kuumwa kwa mchumba wake zikaonekana kumshtua kupita kawaida. Mawazo juu ya Happy yakafutika na kuanza kumfikiria Kristen.
Ni kweli alikuwa akimpenda sana mchumba wake huyo japokuwa katika masaa machache yaliyopita alikuwa amemsaliti kwa kufanya mapenzi na Happy. Kristen hakuwa katika hali nzuri, mara kwa mara ugonjwa wa pumu ulikuwa ukimsumbua kupita kawaida.
 
SEHEMU YA 8

Aliona kulikuwa na kila sababu za kusafiri na kurudi nchini Marekani kwa ajili ya kumuona mpenzi wake. Alihitaji kukaa na mpenzi wake na kumuonyesha kwamba alikuwa akiendelea kumthamini japokuwa alikuwa na ugonjwa huo ambao ulikuwa umemtesa kwa kipindi kirefu.
Akapanga mipango ya safari, alitakiwa kurudi nchini Marekani haraka iwezekanavyo. Siku iliyofuata, akawa ndani ya ndege akirudi nchini Marekani. Kichwa chake kimoja kiilikuwa kikiwafikiria watu wawili tu, Kristen na Happy.
“Nitachagua wa kumuoa hapo baadae. Ila hata Happy nae anafaa sana. Mmh! Wazazi watanielewa vipi kama nikimuoa? Kwanza hawamjui hata mara moja, wataweza kuniunga mkono katika maamuzi yangu? Mmh! Huo nao uamuzi mgumu” Wayne alijisemea wakati ndege ikiwa imekwishafika katika ardhi ya Morocco tayari kwa kuendelea na safari ya kuingia Ulaya na kisha kuelekea Marekani.


Jina la Brown Michael Ryn lilikuwa jina kubwa miongoni mwa matajiri ambao walikuwa wakipatikana nchini Marekani. Mzee huyu alikuwa akimiliki miladi mikubwa nchini Marekani pamoja na mingine iliyokuwa katika mataifa makubwa kama Uingereza, Urusi na Ufaransa.
Huyu ndiye alikuwa mwasisi wa shirika la ndege la American Airways, ndiye alikuwa akimiliki kiwanda kikubwa cha kutengeneza makaratasi cha Brown Paper Company Limited, huyu ndiye ambaye alikuwa akiimiliki kampuni kubwa ya kutengeneza magazeti ya Independent ambayo yalikuwa yakitoka mara mbili kwa wiki nchini Marekani.
Tofauti na vitega uchumi hivyo, pia alikuwa na kampuni nyingi pamoja na visima vya mafuta nchini Qatar. Jina lake lillikuwa kubwa na kila siku alikuwa akiingiza kiasi kikubwa cha fedha katika maisha yake.
Mpaka inafika mwaka huo wa 1990, Bwana Brown alikuwa ameingiza kiasi cha dola bilioni sabini katika mwaka huo na kumfanya kuwa tajiri namba kumi na nane duniani. Maisha yake siku zote yalikuwa yametawaliwa na fedha, alikuwa akithamini sana fedha kuliko kitu kingine chochote kile.
Miaka ya nyuma katika kipindi ambacho alikuwa na umri mdogo, alikuwa kijana masikini ambaye alifiwa na wazazi wake na kuachwa akiwa hana kitu. Mchezo wa kamari wa Pluto Game ndio ambao ulimpatia fedha kiasi cha dola elfu themanini ambazo akazifanyia biashara ambayo ikaanza kumuingizia fedha.
Maisha yake yakabadilika na kumfanya kuongeza jitihada kwa kila biashara ambayo alikuwa akiifanya. Ni ndani ya mwaka mmoja tu, akafanikiwa kumiliki hisa ya asilimia arobaini katika kampuni ya kutengeneza magari ya Mc Lloyd.
Alipofikisha miaka ishirini na mbili akaamua kumuoa mwanamke mzuri, Ruth ambaye aliishi nae kwa miaka minne na kuachana nae. Hapo ndipo alipoamua kutulia ila baada ya miaka miwili akamuoa mwanamke mmoja ambaye alikuwa akiitwa Lydia.
Huyu ndiye ambaye alikuwa amedumu nae katika ndoa mpaka kumpatia
 
SEHEMU YA 9

watoto wawili, Wayne na msichana Esther. Watoto hawa ndio ambao walikuwa kila kitu katika maisha yake, aliwathamini kuliko hata alivyozithamini biashara zake.
Kijana wake, Wayne alionekana kuwa tofauti sana na watoto wa matajiri wengine. Yeye alikuwa akiishi maisha ya peke yake, kamwe hakuwahi kuchangamana na watoto wa matajiri. Maisha yake yalikuwa mitaani pamoja na watoto weusi ambako alikuwa akikaa nao na jioni kurudi nyumbani.
Maisha yake yalikuwa yakimkasirisha baba yake, kila siku alikuwa akimkaripia na hata kumpiga lakini Wayne hakuonekana kubadilika. Bwana Brown akaonekana kuchoka, akaamua kumuacha Wayne kuishi maisha ambayo alikuwa akitaka kuishi.
Hata Wayne alipoamua kumleta mchumba wake, Luciana, Bwana Brown akaonekana kukasirika. Kamwe hakutaka mtoto wake awe katika uhusiano na msichana yeyote wa kimasikini, alihitaji kijana wake awe katika uhusiano na msichana yeyote kutoka katika familia ya kitajiri.
Hapo ndipo alipoanza mipango yake ya chini chini kuhakikisha kwamba Wayne anaingia katika uhusiano na msichana yeyote kutoka katika familia ya kitajiri. Akafanikiwa kumuunganisha Wayne na msichana Kristen ambaye alikuwa ametoka katika familia ya kitajiri.
Wayne na Kristen wakaanza kuzoeana na hatimae kuanzisha uhusiano ambao ulionekana kuwafurahisha wazazi wao. Mipango ya harusi ikaanza kufanyika taratibu. Kila tarehe ya harusi ilipokuwa ikikaribia, harusi ilikuwa ikihahirishwa kwa sababu ambazo hazikujulikana vizuri.
Wayne akaonekana kukasirika, na hapo ndipo alipoamua kuomba muda wa kupumzika kwenda katika nchi yoyote abayo ilikuwa na vivutio vizuri. Hapo ndipo alipoisoma Tanzania katika ramani ya dunia na kuamua kuja nchini Tanzania.
Akatamani kuziona mbuga za wanyama ambazo zilikuwa zikitangazwa sana pamoja na mlima mrefu kuliko milima yote barani Afrika. Akasafiri tena akiwa peke yake, japokuwa baba yake alikuwa akimtaka atumie ndege ya kukodi lakini akaonekana kukataa kabisa.
Kwa sasa alikuwa ndani ya ndege kurudi nchini Marekani. Kichwa chake wala hakikutulia kwa mawazo, wasichana wawili ambao walikuwa kichwani mwake walionekana kumchanganya kupita kawaida.
Ndege ikaanza kupaa kutoka katika uwanja wa ndege wa Morocco na kuingia katika nchi za Ulaya. Kitu ambacho alikuwa akikitaka Wayne ni kufika nchini Marekani haraka iwezekanavyo ili apate kujua ni kitu gani alitakiwa kukifanya kwa wakati huo ambao mchumba wake alikuwa katika matatizo makubwa.
Kutoka nchini Morocco mpaka nchini Marekani, alitumia masaa ishirini na mbili na ndipo ndehe ikaanza kutua katika uwanja wa ndege jiji New York. Mara baada ya ndege kusimama, abiria wakaanza kuteremka na kuanza kupiga hatua kuelekea ndani ya jengo la uwanja huo wa ndege ambako baada ya mizigo yao kuchunguzwa, wakaichukua na kutoka nje.
Gari aina ya BMW ilikuwa ikimsubiri nje, alipoifikia, akaingia ndani ya hiyo
 
SEHEMU YA 10

gari na kisha safari ya kuelekea Eastchester kuanza huku ikiwa imetimia saa tano asubuhi. Ndani ya gari Wayne hakuonekana kuwa na furaha, muda wote alikuwa akimfikiria Kristen.
Gari likasimama nje ya jengo kubwa lililojengwa katika eneo kubwa lililokuwa na ukubwa wa mita mia moja na ishirini kwa urefu na upana wa mita sabini. Geti likajifungua na gari kuingizwa ndani. Wayne akateremka na kuanza kuelekea ndani ya nyumba hiyo.
Wazazi wake hawakuwepo, ni wafanyakazi wa ndani tu ndio ambao walikuwa wakizunguka zunguka ndani ya nyumba ile. Alipoulizia mahali walipokuwa, aliambiwa kwamba walikuwa katika hospitali ya St’ Mathew ambako mchumba wake, Kristen alikuwa amelazwa.
Wayne akatoka ndani ya nyumba ile, akaanza kuelekea katika sehemu za kupakia magari na kisha kulichukua gari lake aina ya Aston Martin na kuanza safari ya kuelekea katika hospitali hiyo ambayo ilikuwa kusini mwa jiji la New York karibu kabisa na bandari ya Hamilton.
Mawazo juu ya Happy yakafutika, Kristen ndiye ambaye alikuwa akimfikiria sana kwa wakati huo. Aliendesha gari kwa mwendo wa kasi, shida yake ilikuwa ni kutaka kufika hospitalini haraka iwezekanavyo. Ni ndani ya dakika thelathini tu, akawa analipaki gari lake katika eneo la hospitali hiyo.
Kwa haraka sana akateremka na kuanza kupiga hatua kuelekea ndani ya jengo la hospitali hiyo, sehemu ya kwanza kwenda ilikuwa mapokezi, akamulizia mgonjwa wake. Dada wa mapokezi akachukua kipanya cha kompyuta na kuanza kukipeleka huku na kule huku macho yake yakiwa katika kioo cha monita ya kompyuta.
Akaliandika jina la ‘Kristen’ na kisha kompyuta yenyewe kuanza kutafuta. Wayne alikuwa kimya akimwangalia yule dada wa mapokezi kwa jinsi alivyokuwa akicheza na kompyuta yake. Ni ndani ya sekunde kumi na tano tu, akaonekana kukipata kile alichokuwa akikitafuta.
“Yupo chumba namba 108 katika ghorfa ya sita” Dada yule alimwambia Wayne.
Wayne hakutaka kupoteza muda wake, alichokifanya ni kupanda lifti na kisha kuanza kuelekea katika ghorofa hiyo ambayo alikuwa ameelekezwa. Bado kichwa chake hakikutulia kabisa, mawazo juu ya Kristen yalikuwa yakimtesa kupita kawaida.
Alipofika katika ghorofa hiyo akateremka na kisha kuanza kupiga hatua kukitafuta chumba hicho. Alipokifikia, akakishika kitasa na kuanza kuufungua mlango. Kwa kuwa muda wa kuona wagonjwa ulikuwa umefika, akaruhusiwa kuingia.
Macho yake yakatua kitandani, Kristen alikuwa kimya kitandani pale huku mashine ya Oksijen ikiwa imefunika pua na mdomo wake. Wayne akajikuta akiishiwa na nguvu, akaanza kupiga hatua kuelekea katika kitanda kile.
Japokuwa pembeni ya kitanda kile walikuwepo wazazi wake pamoja na wazazi wa Kristen lakini yeye wala hakuonekana kuwaona, mtu aliyekuwa akimuona kwa wakati huo alikuwa Kristen tu. Alipokifikia kitanda kile, akapiga magoti chini, akauchukua mkono wa Kristen na kuubusu.
“Usiniache mpenzi...” Wayne alisema.
Machozi yakaanza kumtoka na kutiririka mashavuni mwake, hali ambayo alikuwa nayo Kristen ilionekana kumuumiza kupita kawaida. Katika maisha yake, ugonjwa wa pumu ndio ambao alikuwa akiuchukia kuliko ugonjwa wowote kwa kuwa ulikuwa ukimkosesha amani kupita kawaida.
“Lakini kwa nini mimi? Mbona maisha yangu ya uhusiano hayana furaha kabisa? Mbona kila siku ni mimi tu. Nani ameichukua furaha yangu?” Wayne alikuwa akijiuliza.
 
SEHEMU YA 11

Akashikwa bega lake kwa nyuma, alipoyageuza macho yake, alikuwa baba yake, Bwana Brown. Wayne akasimama na kisha kumkumbatia baba yake huku akilia tu. Mama yake, Bi Lydia nae akawasogelea na kisha kuwakumbatia. Wote walionekana kuumizwa na hali ile ambayo alikuwa nayo Kristen, kila siku sala zao zilikuwa ni kutaka Kristen apone kabisa ugonjwa ule.
Wazazi wa Kristen ambao walikuwa pembeni nao wakawasogelea na kuwakumbatia. Wote walionekana kuumizwa na hali ambayo alikuwa nayo Kristen, kwao waliona kwamba muda wowote ule msichana yule angepoteza uhai wake.
Walihangaika katika kila hospitali huku wakijitahidi kutumia kila aina ya dawa ambayo waliambiwa watumie lakini wala hali ya Kristen haikubadilika, kila siku alikuwa vile vile. Wote wakakata tamaa na maisha ya Kristen, sala zao ambazo kila siku walikuwa wakisali zikaonekana kukosa majibu kutoka kwa Mungu wao.
Kristen akakaa katika hospitali ile kwa muda wa wiki mbili, akaruhusiwa kurudi nyumbani huku akionekana kuwa mzima wa afya. Hatua hiyo ikaonekana kuwa ya furaha kwa Wayne ambaye alionekana kumthamini sana katika maisha yake.
Miezi mitano ikapita. Kitu alichokipanga pamoja nae ilikuwa ni kusafiri kuelekea nchini Tanzania huku sababu yake kubwa ikiwa ni kutaka kumuonyeshea mbuga mbalimbali za wanyama pamoja na kuuona mlima mkubwa kuliko wote barani Afrika.
Kristen hakutaka kupinga, kwake, matembezi ndio yalikuwa moja ya maisha yake. Akamkubalia mpenzi wake kwa moyo mmoja kusafiri nae kuelekea nchini Tanzania. Moyoni hakujua kwamba Wayne alitamani sana kuelekea nchini Tanzania kwa sababu moja tu, kumuona Happy ambaye tayari alikwishaanza kurudi kichwani mwake kwa kasi ya ajabu.
Siku tatu zilizofuata walikuwa ndani ya ndege ya Amerian Airlines wakianza safari ya kuelekea nchini Tanzania. Ndani ya ndege walikuwa wakiongea mengi lakini mudaa wote Wayne alikuwa katika mawazo mazito juu ya Happy.
Walichukua masaa ishirini na saba, ndege ikaanza kutua katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwl Julius Kambarage Nyerere. Wakateremka na kisha kukata tiketi ya ndege ya siku hiyo ya shirika la Precious kwa ajili ya safari ya kuelekea jijini Arusha ambako huko wangetembelea sehemu mbalimbali za mbuga za wanyama na pia kusafiri mpaka Kilimanjaro ambako wangeupanda mlima Kilimanjaro.
Ndani ya saa moja, ndege ya shirika la Precious ilikuwa ikitua katia uwanja wa ndege wa KIA ambako wakachukua teksi iliyowapeleka mpaka Arusha mjini ndani ya hoteli ya nyota tano ya Chui Chui.
Kila mmoja akaonekana kuwa na furaha, walitembea sehemu mbalimbali wakiwa pamoja huku wakinunua vinyago vingi kwa ajili ya kurudi navyo nchini Marekani. Katika vipindi vyote hivyo, Wayne alikuwa na mawazo ya kuonana na Happy tu.
 
SEHEMU YA 12

Asubuhi iliyofuata, saa moja akaamka na kuanza kuvaa nguo zake. Kitu alichokuwa akikitaka ni kuondoka na kuelekea kwa shangazi yake Happy ambapo angemuulizia Happy na kuonana nae. Hata kabla Kristen hajaamka, Wayne akaamka na kuanza safari ya kuelekea huko huku akihakikisha kwamba Kristen hakumuona katika kipindi ambacho aliondoka.
Njia nzima Wayne alikuwa na mawazo juu ya Happy. Aliukumbuka uzuri ambao alikuwa nao msichana huyo, kwake alionekana kuwa msichana wa ajabu ambaye hakustahili hata siku moja kukaa nchini Tanzania.
Alifika katika nyumba hiyo, Bi Selina alikuwa nje akifagia uwanja wa nyumba hiyo kwa kutumia ufagia mkubwa. Uso wa Wayne ukajaa tabasamu, kitendo cha kumuona Bi Selina kwake kikaonekana kumfariji kupita kawaida. Wakasalimiana kwa furaha hadi kukumbatiana.
“Aliondoka kuelekea nyumbani kwao” Bi Selina alimwambia Wayne.
“Siwezi kumuona kwa siku ya leo?” Wayne aliuliza huku akionekana kuwa na kiu ya kutaka kumuona Happy.
“Inawezekana. Inabidi tuondoke hata asubuhi hii. Ni mwendo wa dakika ishirini tu hadi kufika kwao kwa daladala” Bi Selina alimwambia.
Hakukuwa na kitu cha kusubiri, alichokifanya Bi Selina ni kujiandaa na kisha kuanza safari ya kueleka, Machame, Kilimanjaro. Ingawa ndani ya gari walikuwa wakiongea lakini Wayne alionekana kuwa na mawazo. Kitu cha kwanza alikuwa akimfiria Happy lakini kitu cha pili alikuwa akifikiria kuhusu Kristen katika kipindi ambacho angeamka na kumkosa kitandani.
“Nitahitaji kumuona tu ili mladi kiu yangu ikatike na hata ikiwezekana nifanye nae tena” Wayne alikuwa akijisemea moyoni katika kipindi ambacho safari ilikuwa ikiendelea.


Maisha ya Happy hayakuwa na furaha tena hali iliyompelekea kuondoka nyumbani kwa shangazi yake na kurudi nyumbani kwao Machame. Kichwa chake kilikuwa kikifikiria kuhusu mimba ambayo alikuwa nayo, hakujua ni kitu gani ambacho angekifanya mpaka kuanza kuwaeleza wazazi wake kuhusiana na mimba ile.
Moyo wake ulikuwa ukimuuma, akaanza kumchukia Wayne ambaye alikuwa amempa ujauzito ule na kisha kuondoka kurudi nchini Marekani. Alijiona kuwa mpweke, akakosa amani kabisa.
Mpaka katika kipindi ambacho alikuwa akiingia nyumbani kwao, Happy alikuwa akilia tu. Wazazi wake, Mzee Lyimo na Bi Vanessa wakabaki wakimshangaa Happy, hawakujua ni kitu gani ambacho kilikuwa kikimliza binti yao katika kipindi hicho.
Kila walipojaribu kumuuliza Happy kitu ambacho kilikuwa kimetokea, alikuwa kimya, hakutaka kuwaambia wazazi wake kitu ambacho kilikuwa kimetokea katika kipindi ambacho alikuwa jijini Arusha. Alibaki kimya, siri ya kwamba alikuwa mjauzito ikabakia moyoni mwake.
Siku zikakatika mpaka katika kipindi ambacho matokeo ya kidato cha nne yalipotangazwa. Happy alikuwa amefanya vizuri sana zaidi ya wanafunzi wote wa Machame Girls Secondary School. Matokeo hayo yaliinua furaha kwa wazazi wake,
 
SEHEMU YA 13

Kitu kilichowashangaza ni pale walipompa Happy matokeo yale. Badala ya Happy kuwa na furaha hata zaidi ya wao waliyokuwa nayo, akaanza kulia kwa uchungu. Kitendo kile kikaonekana kuwashangaza wazazi wake jambo ambalo liliwapelekea kumuuliza sababu ilikuwa nini. Happy hakutaka kuongea kitu chochote kile, tayari wazzi wake wakajua kwamba kulikuwa na tatizo limetokea.
“Kaongee nae. Nadhani ana tatizo” Mzee Lyimo alimwabia mkewe.
Bi Vanessa hakuwa na jinsi, alichokifanya ni kuanza kuelekea chumbani kwa Happy na kuanza kuongea nae. Alichukua saa moja kuongea nae lakini Happy hakuwa tayari kuufungua mdomo kueleza ni kitu gani ambacho kilikuwa kimetokea.
Bi Vanessa alitumia ujuzi wake wote na hatimae Happy kumwambia ukweli. Bi Vanessa akaonekana kama mtu aliyechanganyikiwa, hakuonekana kuyaamini maneno yale, alimwangalia binti yake mara mbili mbili huku akionekana kutokuamini.
“Una mimba?” Bi Vanessa aliuliza huku akionekana kutokuamini.
“Ndio” Happy aijibu huku akiangalia chini.
“Ya nani?”
“Wayne”
“Ndiye nani?”
“Mvulana mmoja hivi”
“Anakaa wapi? Hapa hapa Machame au Arusha?” Bi Vanessa aliuliza.
“Anakaa Marekani”
“Marekani!”
“Ndio”
Bi Vanessa hakutaka kubaki ndani ya chumba hicho, alichokifanya ni kutoka na kisha kwenda kumwambia mumewe, mzee Lyimo.
Mzee Lyimo akaonekana kuchanganyikiwa, hasira zikaanza kumshika, akaanza kuondoka kumfuata Happy chumbani kwake. Alipoingia tu, akajikuta hasira zake zote zikipotea haa mara baada ya kuyaona machozi ya Happy ambayo yalikuwa yakimtoka mfululizo.
Mzee Lyimo akaanza kupiga hatua kumfuata Happy pale kitandani alipokuwa na kisha kukaa karibu nae. Moyo wake ukaonekana kuumia, alijua kwamba alitumia kiasi kikubwa sana cha fedha kumsomesha Happy mpaka kufikia hatua hiyo ambayo alikuwa mefikia, kupata ujauzito hata kabla hajaendelea na masomo kulionekana kumuumiza.
Alijua fika kwamba kumchapa Happy au kumfukuza nyumbani isingekuwa suluhisho la kile ambacho kilikuwa kimetokea, aliona kuwa na umuhimu wa kuwa pamoja na Happy na kumfariji katika hali ambayo alikuwa nayo katika kipindi hicho.
“Wayne ndiye nani?” Mzee Lyimo aliuliza japokuwa alikuwa ameambiwa kila kitu na mkewe.
“Mwanaume kutoka Marekani” Happy alijibu.
“Ni mzungu?”
“Ndio” Happy alijibu.
Mzee Lyimo akaonekana kukosa nguvu, alichokifanya ni kuinuka mahali hapo na kwenda nje. Hakujua ni kitu gani ambacho alitakiwa kukifanya, kupata ujauzito kwa Happy kulionekana kumnyima furaha kabisa.
Huo ndio ukawa mwisho wa Happy kusoma, hakuendelea tena na elimu, akawa msichana wa kukaa nyumbani na kuwasaidia wazazi wake kazi mbalimbali hasa shambani. Miezi ilikuwa ikiendelea kukatika, Happy alikuwa akiutunza ujauzito wake huku wazazi wake wakimpa kila msaada ambao alikuwa akiuhitaji.
Dalili zote za kuwa mjamzito zikaanza kuonekana, akaanza kutapika mfululizo huku akipoteza hamu ya kula. Muda mwingi alikuwa akijisikia uchovu hali
 
SEHEMU YA 14

iliyompelekea kulala. Mpaka miezi mitano inatimia, hali ya ujauzito ikaanza kuonekana waziwazi.
Happy alikuwa amelala chumbani kwake huku pembeni yake kukiwa na maembe mabichi pamoja na udongo. Hivyo ndivyo vilikuwa vitu ambavyo alikuwa akipenda sana kuvitumia kila siku. Mara mama yake akaingia chumbani humo, uso wake ulikuwa umejaa tabaamu pana.
Maswali mfululizo yakaanza kujikusanya kichwani mwa Happy, hakujua sababu iliympelekea mama yake kuwa na tabasamu namna ile. Akainuka kitandani na kukaa. Mama yake akaja na kukaa pembeni yake huku tabasamu likiendelea kuonekana usoni mwake.
“Kuna nini?” Happy aliuliza.
“Amekuja” Bi Vanessa alijibu.
“Nani?”
“Wayne. Yupo nje anakusubiri” Bi Vanessa alimwambia Happy.
Badala ya kuonyesha furaha, Happy akaanza kutokwa na machozi. Hali ile ilionekana kumshangaza mama yake ambaye akaamua kuanza kumbembeleza. Alipoona Happy amenyamaza, akatoka chumbani mule na moja kwa moja kwenda kumuita Wayne ambaye alikuwa nje ya nyumba lle.
Ni ndani ya sekunde kumi tu, mlang wa chubani ukafunguliwa na Wayne kuingia ndani. Usowa Wayne ukaonekana kuwa na furaha mara baada ya kumuona Happy kwa mara nyingine tena. Huku akionekana kuwa na tabaamu pana, akakaa kitandani pale.
Happy akashindwa kuvumilia, akajikuta akimsogelea Wayne na kumkumbatia kwa furaha huku machozi yakiendelea kumtoka. Wayne akaipitisha mikono yake na kumkumbatia. Walikaa katika hali hiyo kwa dakika mbili, Wayne akayapeleka macho yake usoni mwa Happy, akaonekana kufarijika.
“Nimekukumbuka mpenzi” Wayne alimwambia Happy.
“Nimekukumbuka pia” Happy alijibu.
Furaha ya Wayne ikaonekana kurudi moyoni mwake, tayari alikuwa amekwishasahau kama alikuwa amemuacha Kristen hotelini. Alikaa pamoja na Happy kwa muda wa masaa mawili na ndipo walipoanza kupiga stori.
“Mbona ulikimbia chumbani siku ile?” Wayne alimuuliza Happy.
“Nilikuwa nikiogopa, kuna kitu nilikuwa nimekikumbuka” Happy alijibu.
“Kitu gani?”
“Kwamba nilikuwa katika siku zangu za kupata mimba” Happy alitoa jibu ambalo likaonekana kumshtua Wayne.
“Unasemaje?”
“Nilikuwa katika siku zangu za kupata mimba. Hapa unaponiona, nina ujauzito wako” Happy alimwambia Wayne.
Wayne akaonekana kushtuka, akamwangalia vizuri Happy, akaipandisha blauzi ambayo alikuwa ameivaa na kisha kuliangalia tumbolake, aliona mabadiliko makubwa lakini cha ajabu katika kipindi ambacho alikuwa akifanya nae mapenzi hakuyaona mabadilko hayo.
Wayne akaonekana kubadilika, wasiwasi ukaanza kuonekana machoni mwake, hakuamini kama alikuwa amempa ujauzito msichana wa kiafrika, akamwangalia Happy huku dhahiri uso wake ukionekana kuukataa ujauzito ule.
Wayne akainuka, akaanza kuvaa nguo zake na kuufungua mlango, kilichoendelea mahali hapo ni kuondoka huku akiwa kama mtu aliyechanganyikiwa. Hakujua ni kitu gani alitakiwa kukifanya, moyo wake haukuwa tayari kukubali kama alikuwa amempa mimba msichana wa Kiafrika.
“Haiwezekani. Ile sio mimba yangu. Siwezi kumpa mimba msichana wa
 
SEHEMU YA 15

Kiafrika” Wayne alisema katika kipindi ambacho alikuwa akielekea kituoni huku akiwaacha watu nyumbani pale wakiwa hawaelewi ni kitu gani ambacho kilikuwa kimetokea ndani ya chumba kile.
Wayne alifika hotelini baada ya saa moja. Kristen alikuwa na wasiwasi akimsubiri. Japokuwa Kristen alionekana kuwa na wasiwasi lakini hakuuliza kitu chochote kile. Tayari Wayne alikuwa amebadilika, uso wake ukaonekana kuwa na hasira kupita kawaida, kitendo cha kumpa mimba msichana wa Kiafrika kilionekana kumuumiza.
“Kuna nini?” Kristen alijikuta akiuliza.
“Tuondoke. Inatupasa turudi nyumbani haraka iwezekanavyo” Wayne alimwambia Kristen.
“Unasemaje? Mbona ni maamuzi ya haraka namna hiyo?”
“Ndio hivyo. Nakuomba usiulize kitu Kristen. Nimechanganyikiwa baada ya kusikia kwamba marafiki zangu kutoka Uingereza wameelekea Marekani tayari kwa kuhudhuria harusi yetu” Wayne alidanganya.
“Harusi gani? Mbona unaonekana kama umechanganyikiwa?”
“Ni lazima tufunge harusi haraka iwezekanavyo. Huo ni uamuzi ambao nimejiwekea. Najua ni uamuzi ulioamuliwa kwa haraka sana. Haina jinsi mpenzi. Wiki ijayo ni lazima tufunge ndoa” Wayne alimwambia Kristen.
Ni kweli. Ulikuwa ni uamuzi wa haraka sana, Wayne alionekana kuchanganyikiwa. Taarifa za ujauzito ambazo alikuwa amepewa zilionekana kumchanganganya kupita kawaida. Siku mbili zilizofuata, wakasafiri na kurudi tena nchini Marekani ambako huko mipango ya harusi ikaanza kufanyika.
Kila kitu kilikuwa kimepangwa kwa haraka haraka sana hali ambayo ilikuwa ikimshangaza kila mtu. Vyombo vya habari vikaanza kutangaza harusi kubwa ambayo ilitarajiwa kufanyika wiki ijayo. Kila mtu akawa na hamu ya kuiangalia harusi hiyo kwenye televisheni.
“Ni bora nioe ili nimsahau Happy. Haiwezekani kuzaa na msichana wa Kiafrika” Wayne alisema.
Kitu walichokifanya ni kuanza safari ya kuelekea Elmon, mji mdogo uliokuwa pembeni mwa jiji la New York kwa ajili ya kuwaona babu na bibi wa mchumba wake, Kristen kwa ajili ya kuwapa taarifa kile ambacho kilikuwa kinataka kutokea.
Ndani ya gari walikuwa wawili tu, Wayne na Kristen. Wayne ndiye ambaye alikuwa ameshikilia usukani, alikuwa akiendesha kwa mwendo wa kasi sana kwani alihitaji wafike katika mji huo haraka iwezekanavyo.
Bado kichwa chake hakikuwa sawa, muda wote alikuwa akimfikiria Happy na ujauzito ule ambao alikuwa nao. Mara kwa mara alikuwa akipiga usukani ule kuonyesha ni kwa jinsi gani alikuwa amechanganyikiwa.
“Happy.....haiwezekani...” Wayne alijikuta akisema kwa sauti kubwa iliyosikiwa na Kristen.
“Umesemaje?” Kristen aliuliza.
“Nini?” Wayne nae aliuliza.
“Nimekusikia umeongea kitu”
“Kitu gani?” Wayne aliuliza.
Bado Wayne alikuwa akiendesha gari kwa mwendo wa kasi hadi kutokukiona kibao ambacho kilimtaka kuendesha gari kwa mwendo wa taratibu kutokana na matengenezo ya barabara. Ghafla, mbele yake akaona gari kubwa likichimba barabara ile huku mainjiania wakitoa malelekezo kwa dereva wa
 
SEHEMU YA 16

gari lile kubwa la kutengeneza barabara.
Kutokana na mwendo mkali ambao walikuwa nao, ikawa ngumu kufunga breki na gari kusimama. Gari lao ambalo lilikuwa katika mwendo wa kasi likalivamia gari lile kubwa lililokuwa likitengeneza barabara.
Mlio mkubwa ukasikika, Kristen akarushwa kutoka ndani ya gari mpaka nje na kukibamiza kichwa chake katika chuma kikubwa cha gari lile lililokuwa likitengeneza barabara ile. Na Wayne akarushwa mpaka nje, akaburuzika katika marabara ile, sehemu kubwa ya ngozi yake tumboni ikabaki barabarani.
Ilikuwa ni ajali kubwa ambayo wala haikuwa na moyo kuitazama. Gari lao lilikuwa limebondeka, milango ya mbele haikuwa ikionekana kabisa, yaani gari lilikuwa limebaki nusu tu kuanzia milango ya nyuma.

Happy alionekana kuchanganyikiwa, hakuamini kama kweli Wayne alikuwa akitoka chumbani kwake huku akionekana kuwa na hasira mara tu alipothubutu kumwambia kuhusiana na ule ujauzito ambao alikuwa nao. Mshtuko mkubwa ukampata moyoni mwake hali iliyompelekea kuinuka pale kitandani na kuanza kumfuata Wayne.
Wayne alikuwa akitembea kwa mwendo wa haraka haraka, Happy akajitahidi kukimbia kumfuata huku akiita lakini Wayne hakugeuka nyuma. Happy hakutaka kuendelea kumfuata Wayne, akasimama na kisha kuanza kulia.
Tukio lile ambalo lilikuwa limetokea lilikuwa limemuumiza moyoni mwake zaidi ya tukio lolote ambalo liliwahi kutokea maishani mwake. Akaanza kupiga hatua kurudi nyumbani kwao, macho yake yalikuwa yakitoa machozi mfululizo.
Mama yake na shangazi yake wakaonekana kushangaa, hawakujua ni kitu gani ambacho kilikuwa kimetokea mpaka Wayne kutoka chumbani mule na kuondoka huku akionekana kubadilika. Hapo ndipo Happy alipoamua kuwaambia kile ambacho kilikuwa kimetokea.
“Yaani amekataa mimba yake?” Bi Vanessa aliuliza huku akionekana kushtuka.
Happy hakujibu kitu, bado alikuwa akiendelea kulia mfululizo. Alihisi kwamba kulikuwa na kitu kilichokuwa na ncha kali ambacho kilikuwa kimeuchoma moyo wake. Hakujua ni kitu gani ambacho alitakiwa kukifanya ili siku moja Wayne aamini kwamba mtoto yule alikuwa wake.
Happy akarudi chumbani na kujifungia, siku hiyo wala hakutaka kuongea na mtu yeyote yule, alikuwa akilia kwa uchungu. Kuna wakati alikuwa akinyamaza, ila kila alipokuwa akiliangalia tumbo lake, akaanza kulia zaidi na zaidi.
Mpaka katika kipindi ambacho mzee Lyimo alikuwa akitoka shambani na kuingia hapo nyumbani, bado Happy alikuwa amejifungia chumbani kwake. Alipopewa taarifa juu ya kilichoendelea, mzee Lyimo akaanza kupiga hatua kuufuata mlango wa kuingia chumbani kwa Happy.
Mlango ulikuwa umefungwa kwa ndani, akaanza kugonga lakini wala haukufunguliwa kitu ambacho kilimfanya kuanza kuliita jina la Happy huku akiendelea kugonga. Hazikupita hata dakika nyingi, Happy akafungua mlango na mzee Lyimo kuingia.
Macho ya Happy yalikuwa mekundu huku yakiwa yamevimba hali iliyoonyesha kwamba alikuwa amelia kwa muda mrefu sana. Mzee Lyimo
 
Back
Top Bottom