Simulizi : Ukweli Wenye Kuuma (Painful Truth)

Simulizi : Ukweli Wenye Kuuma (Painful Truth)

SEHEMU YA 17

akakaa kitandani na kuanza kuongea nae. Moyo wa mzee Lyimo ulimuuma zaidi, kamwe hakutarajia kama mzungu Wayne angeweza kuikataa mimba ile.
“Haiwezekani. Ameikataa?” Mzee Lyimo aliuliza huku akionekana kutokuamini.
“Ndio. Ameikataa” Happy alijibu.
Mzee Lyimo akasimama na kutoka nje ya chumba kile. Akauona mwili wake ukiwa umekufa ganzi kabisa. Hakuaamini kile ambacho alikuwa amekisikia kutoka kwa Happy, alitamani akutane na Wayne na kuongea nae ili aone kama alikuwa na ujasiri wa kuukataa ule ujauzito mbele ya macho yake.
Baada ya hapo, maisha ya Happy yakaendelea kama kawaida ingawa muda mwingi alikuwa akitawaliwa na huzuni. Alikuwa akijitahidi kula vyakula vizuri ambavyo vilikuwa vikimpa afya bora yeye pamoja na mtoto.
Mara kwa mara alikuwa akihudhuria kliniki kama ambavyo madaktari walivyotaka afanye. Kamwe hakulala katika kitanda kisichokuwa na neti, alikuwa akiyalinda maisha yake na ya mtoto wake ambaye alikuwa tumboni.
Ingawa ilikuwa ni vigumu sana lakini akaamua kujisahaulisha kuhusu Wayne, akaamua kuishi maisha yake peke yake, hakutamani kabisa kumuona Wayne mbele ya macho yake, alionekana kumchukia kuliko kiumbe chochote duniani.
Miezi tisa ikatimia na ndipo Happy akajifungulia shambani katika kipindi ambacho alikuwa akilima pamoja na wazazi wake hatua iliyowapelekea kumpeleka hospitalini.
Happy alikuwa amelala juu ya kitanda ndani ya chumba kimoja katika hospitali ya KCMC iliyokuwa Moshi mjini. Bado hakuwa ameongea kitu chochote kile. Dripu moja baada ya nyingine zilikuwa zikiingiza maji katika mishipa yake.
Happy alikuja kufumbua macho yake baada ya masaa nane kupita. Akayapeleka macho yake huku na kule, yakatua katika nyuso za wazazi wake. Tabasamu likaanza kuonekana usoni mwake. Mzee Lyimo na Bi Vanessa wakaanza kupiga hata kumfuata.
“Mtoto wangu yuko wapi?” Happy aliuliza kwa sauti ya chini.
“Kimaro. Tulikuja nae hapa. Amewekwa katika chumba maalumu” Mzee Lyimo alijibu.
“Silitaki jina hilo baba. Sitaki mtoto wangu aitwe Kimaro” Happy alisema kwa sauti ya chini.
“Sawa binti yangu. Unataka aitwe nani?”
“Aitwe Andy” Happy alijibu.
“Kwa hiyo aitwe Andy Wayne?”
“Hapana. Aitwe Andy Ryn. Hili ni jina la babu yake. Sitaki achukue jina la baba yake” Happy alisema.
Hicho ndicho kilichoamuliwa. Jina likawa limekwishapatikana. Baada ya siku mbili, Happy akaruhusiwa kurudi nyumbani. Kila wakati alikuwa pembeni ya mtoto wake, watu mitaani walikuwa wakishangaa namna mtoto yule alivyokuwa mweupe.
Afya yake ilikuwa bora hata zaidi ya watoto wengine ambao walikuwa wamezaliwa mitaani hapo. Happy alimthamini sana mtoto wake hata zaidi ya alivyojithamini yeye mwenye. Miezi ikakatika, Andy Ryn akaanza kujifunza kutembea.
Katika kila hatua ambayo alikuwa akiifikia, Happy alionekana kuwa na furaha.
 
SEHEMU YA 18

Ila kamwe hakuweza kumsahau Wayne kwani kadri alivyokuwa akimwangalia Andy, alifanana sana na baba yake. Mpaka katika kipindi hicho hakujua ni kitu gani kilikuwa kimetokea katika maisha ya Wayne katika kipindi ambacho alikuwa ameondoka na kuelekea nchini Marekani.
Mwaka wa kwanza ukapita, wa pili ukaingia na kupita, Wayne hakuwa ameonekana kabisa mbele ya macho yake. Mwaka wa tatu ukaingia na kupita na mwaka wa nne kuingia. Hapo ndipo Happy akaamua kumuanzisha Andy katika shule ya chekechea iliyokuwa hapo Machame.
“Atakuwa na akili kama za mama yake” Happy alijisemea huku akimvarisha Andy nguo tayari kwa kumuanzisha shule.
Katika kipindi ambacho Happy alikuwa akiingia shuleni hapo pamoja na mtoto wake, walimu wote wakaonekana kushangaa, mtoto wa Happy alionekana kuwa tofauti kabisa. Alikuwa ni mzungu kwa asilimia themanini huku ishirini zilizobaki akiwa amechukua asili ya mama yake.
Andy akaanza kusoma katika shule hiyo. Kwa siku ya kwanza tu aliyofika shuleni hapo, uwezo wake ulijionyesha wazi. Ingawa alikuwa na umri mdogo lakini alikuwa na uwezo mkubwa sana kiasi ambacho kila mwalimu alikuwa akishangaa.
“Mmmh! Huyu mtoto ni wa maajabu nini?” Mwalimu Nuru alimuuliza mwalimu Leonila ambaye nae alikuwa akishangaa tu.
“Wala sijui. Ila uwezo wake unanishangaza sana. Nimewahi kufundisha watoto zaidi ya elfu tano katika shule hii, lakini mtoto huyu ameonekana kuwa wa kipekee sana” Mwalimu Leonila alimjibu mwalimu Nuru.
Mwaka wa tano na wa sita ukaingia. Andy akaanzishwa darasa la kwanza katika shule ya Machame Primary School. Kila mwanafunzi alikuwa akimshangaa, hawakuwahi kumuona mtoto wa kizungu akiwa anasoma katika shule kama ile.
Maswali mengi yalikuwa yakimiminika vichwani mwa walimu wa shule hiyo asili halisi ya mtoto huyo. Kila mmoja alikuwa akiongea lake. Mpaka amefikisha miaka sita, hakukuwa na mtu ambaye alikuwa akifahamu kama Andy alikuwa mtoto wa Wayne ambaye alikuwa ameikataa mimba yake kipindi cha miaka sita iliyopita.
****
Ilikuwa ni taarifa mbaya ambayo ilikuwa imesikika masikioni mwa Bwana Brown na mkewe, Bi Lydia. Waliiangalia simu ile ya mezani ambayo ilikuwa imepigwa na kupewa taarifa ile ya ajali mbaya huku wakionekana kutokuyaamini masikio yao.
Wakaonekana kuchanganyikiwa, wote walijiona kuwa kwenye ndoto iliyojaa huzuni ambapo baada ya muda wangeshtuka kutoka usingizini na kumuona Wayne akiendelea kujiandaa na harusi pamoja na mchumba wake, Kristen.
Hiyo haikuwa ndoto, lilikuwa ni tukio halisi ambalo lilikuwa limetokea katika maisha yao. Walichokifanya ni kuondoka na kuelekea katika hospitali ya Jackson Heights ambayo walikuwa wameelekezwa iliyokuwa katika mji wa Albertson hapo hapo jijini New York.
Gari likafunga breki ndani ya eneo la hospitali ile, wote wakateremka na
 
SEHEMU YA 19

kuanza kuelekea ndani ya hospitali hiyo kubwa. Waandishi wengi wa habari walikuwa mahali hapo kwa ajili ya kupiga picha na kuandika kila kitu ambacho kilikuwa kinaendelea kwani tukio lile la ajaili lilikuwa limegusa hisia za watu wengi nchini Marekani.
Bwana Brown na mkewe wakaingia ndani ya jengo lile huku wakipigwa picha na waandishi wale waliokusanyika katika eneo la hospitali ile. Breki ya kwanza ilikuwa ni nje ya chumba cha wagonjwa mahututi ambacho alikuwa amelazwa Wayne.
Wote wawili wakajikuta wakitokwa na machozi hasa mara baada ya kuuangalia mlango wa chumba kile kilichoonekana kutisha. Wakakaa vitini huku bado machozi yakiendelea kuwatoka. Walitakiwa kusubiri mahali hapo mpaka pale ambapo wangeruhusiwa kuingia ndani ya chumba hicho kwa ajili ya kumuona mtoto wao.
Masaa yalikatika lakini hakukuwa na yeyote ambaye alikuwa ameruhusiwa kuingia, nao hawakutaka kuondoka mahali hapo, waliendelea kusubiri zaidi na zaidi. Usiku ukaingia na hata asubuhi kufika lakini bado hawakuruhusiwa zaidi ya madaktari kupishana mlangoni.
Hali ya Wayne ilionekana kuwa mbaya kiasi ambacho akatolewa chumbani akiwa juu ya machela na kisha kuanza kupelekwa katika hospitali ya St’ Albert ambayo ilikuwa kubwa sana nchini Marekani. Hawakutaka kubaki mahali hapo, walichokifanya ni kuanza kuifuatilia machela ile huku Bi Lydia akilia kama mtoto.
Katika maisha yao walikuwa wamepitia katika hali ngumu sana lakini kwa wakati huo, hali hiyo ndio ilikuwa ikionekana kuwa ngumu zaidi katika maisha yao. Wayne akapakizwa ndani ya helkopta ya hospitali ile na kisha kuanza kupelekwa katika hospitali ya St’ Albert huku dripu zikining’inia.
Bwana Brown na mkewe, Bi Lydia wakaingia katika gari lao na kisha kuanza kuelekea katika hospitali hiyo iliyokuwa katika mji wa RockVile uliokuwa karibu na uwanja wa ndege wa Kimataifa wa John F Kennedy.
Ni ndani ya dakika mia moja wakawa wamekwishafika katika eneo la hospitali hiyo. Wakateremka na kuanza kuingia ndani ya jengo la hospital hiyo. Kama kulia walikuwa wamelia sana na kama macho yao kuvimba yalikuwa yamevimba sana.
Miili yao ilikuwa ikitetemeka kupita kawaida, tayari hali ya wasiwasi ilikuwa imewashika, walikuwa wakiogopa kupita kawaida, waliona kwamba muda wowote ule wangeweza kumpoteza mtoto wao ambaye walikuwa wakimpenda sana hata zaidi ya walivyokuwa wakimpenda mtoto wao mwingine, Esther.
Mara baada ya oparesheni ya kuwekewa ngozi nyingine kufanyika ndani ya chumba maalumu na ndipo wakaruhusiwa kuingia ndani ya chumba kile. Hawakutakiwa kupiga kelele zozote zile kwa kuhofia kuleta matatizo mengine zaidi.
Wayne alikuwa kitandani kimya, dripu zilikuwa zikiendelea kuingiza maji mwilini mwake huku mashine ya hewa ya Oksijeni ikiwa imeziba mdomo na
 
SEHEMU YA 20

pua yake. Wote wakashindwa kuvumilia, hali ambayo ilionekana kwa mtoto wao ikaonekana kuwatisha, wakaanza kulia.
Hayo ndio yalikuwa maisha ya Wayne. Ajali ilionekana kubadili maisha yake kabisa. Ila kila siku wazazi wake walikuwa wakimshukuru Mungu kwa kumnusuru mtoto wao kutokana na Kristen kufariki pale pale. Wayne akaonekana kuwa na bahati katika maisha yake.
Miezi ilikatika lakini Wayne hakufumbua macho yake. Mwaka wa kwanza ukakatika, wa pili ukafuata. Mwaka wa tatu ukaingia, wa nne na hata wa tano ukaingia, bado alikuwa amefumba macho yake vile vile.
Mishipa yake ya fahamu ilikuwa imelegea sana kutokana na ajali ile kumletea matatizo na ilikuwa imechukua muda mrefu sana mpaka kukaa sawa. Waliamini kwamba ni lazima kuna siku Wayne angekuja kufumbua macho iwapo tu kama mishipa ile ya fahamu ingekaa sawa.
Kama kulia, wazazi wake walilia sana. Katika kipindi cha miaka mitano, kila siku walikuwa wakifika hospitali hapo huku wakiwa na mtoto wao, Esther ambaye alikuwa na majonzi zaidi ya wote. Maisha ya kitandani bado yalikuwa yakiendelea kwa Wayne.
Mwaka wa sita ukaingia na siku kumi na mbili, Wayne akayafumbua macho yake. Manesi hawakuamini kile ambacho walikuwa wamekiona, walichokifanya ni kwenda kumuita daktari ambaye alifika mahali hapo na kumwangalia Wayne.
“Glory to Almight God (Utukufu kwa Mungu Mkuu)” Dokta Carthebert alisema huku akiinyoosha mikono yake juu.
Walichokifanya ni kuwapigia simu wazazi wake ambao walifika mahali hapo huku wakiwa na furaha kupita kawaida. Kitendo cha mtoto wao kufumbua macho kilionekana kuwafurahisha kupita kawaida. Wakaanza kumshukuru Mungu kwa jambo kuu ambalo alikuwa amelifanya katika maisha ya mtoto wao, Wayne.
Japokuwa Wayne alikuwa amefumbua macho lakini hakuweza kuongea kitu chochote kile kitandani pale. Kumbukumbu zake zikaanza kurudi upya, akaanza kukumbuka kila kitu ambacho kilikuwa kimetokea siku ile alipopata ajali.
Alitamani kuongea kitu lakini hakuweza kuufumbua mdomo wake kabisa. Miezi sita ikakatika na ndipo Wayne alipoanza kufumbua mdomo wake na kuanza kuongea. Madaktari wakaonekana kuwa na furaha, walichokifanya ni kuwapigia simu wazazi wake na kuwapa taarifa.
Bwana Brown na Bi Lydia wakafika hospitalini hapo huku wakionekana kuwa na furaha kupita kawaida. Taarifa walizoambiwa kwamba Wayne alikuwa amefumbua mdomo wake na kuongea zilikuwa zimewapa faraja.
Wakaingia ndani ya chumba kile na macho yao kutua kwa mtoto wao, Wayne. Wote wakajikuta wakitoa tabasamu pana. Wayne alikuwa akiongea vitu fulani kwa sauti ya chini kabisa hali iliyomfanya Bwana Brown kumsogelea na kulipeleka sikio lake karibu na mdomo wa Wayne.
“Say something my son (Ongea kitu chochote kijana wangu)” Bwana Brown alisema huku akitabasamu.
“I want my kid....I want to see my kid (Ninamtaka mtoto wangu.... Ninataka kumuona mtoto wangu)” Wayne alisema maneno yaliyomfanya Bwana Brown kushangaa.
 
SEHEMU YA 21

Bwana Brown alionekana kuchanganyikiwa mara baada ya kuyasikia maneno yale ambayo alikuwa ameambiwa na kijana wake, Wayne. Kitu cha kwanza akazirudisha kumbukumbu nyuma na kuanza kukumbuka kama kuna siku yoyote Wayne alikuwa ametembea na msichana na kumpa mimba lakini hakupata jibu.
Hakuelewa ni mtoto gani ambaye Wayne alikuwa amemzungumzia mahali hapo. Akakiinua kichwa chake kutoka karibu na Wayne na kisha kuyapeleka macho yake usoni kwa mke wake, Bi Lydia. Uso wa Bwana Brown ulionyesha waziwazi kwamba ulikuwa umetawaliwa na maswali mengi, akaanza kupiga hatua na kumfuata mke wake.
“Vipi?” Bi Lydia aliuliza huku akionekana kuwa na hamu ya kutaka kufahamu kitu.
“Anamtaka mtoto wake” Bwana Brown alimjibu.
“Mtoto gani?”
“Sijui”
“Kwani katika kipindi ambacho alipata ajali, Kristen alikuwa mjauzito?” Bi Lydia aliuliza.
“Hapana”
“Sasa mtoto gani anayemtaka?”
“Hata mimi mwenyewe nashangaa. Ila nafikiri atakuwa hajakaa sawa, si unajua mishipa yake ya fahamu ndio inaanza kurudi katika hali yake”
“Inawezekana”
Hakukuwa na mtu ambaye alijisumbua kufuatilia maneno ambayo alikuwa ameyaongea Wayne kwani walijua kwamba akili yake wala haikuwa imekaa sawa. Daktari mmoja na manesi wawili wakaingia ndani ya chumba kile na kisha kuwataka Bwana Brown na Bi Lydia kutoka ndani ya chumba kile kwa ajili ya kuanza kazi yao.
Kila siku Wayne alikuwa akiwaambia maneno yale yale kwamba alikuwa akitaka kumuona mtoto wake. Maneno yale yakaendelea kuwashtua kupita kawaida kitu kilichowapelekea kuanza kufuatilia. Walifuatilia kwa muda wa mwezi mmoja lakini hawakufanikiwa kujua mtoto ambaye Wayne alikuwa akimzungumzia.
Hali ya Wayne ilikuwa ikizidi kutengemaa kadri siku zilivyokuwa zikizidi kwenda mbele. Kutokana na fedha nyingi ambazo alikuwa nazo Bwana Brown, madaktari kutoka katika hospitali kubwa wakaanza kuingia ndani ya hospitali ile kwa ajili ya kumtibia Wayne.
Miezi tisa ikakatika na ndipo hali ya Wayne ikarudi kabisa ila mwili wake ulikuwa na tofauti kubwa sana. Alichokifanya daktari ni kuwaita wazazi wake ndani ya ofisi yake na kisha kuanza kuongea nao huku kila mmoja akionekana kuyafurahia maendeleo ya Wayne.
“Tunamshukuru Mungu kwa kuwa Wayne anaendelea vizuri” Dokta aliwaambia huku akiyaweka vizuri miwani yake pamoja na kulichukua faili kubwa ambalo lilikuwa juu ya meza yake.
“Hata sisi tunashukuru” Bwana Brown alimwambia daktari huku akiwa amemshika mkono mkewe pale vitini walipokuwa wamekaa.
“Kuna mambo mawili ambayo yametokea katika mwili wake. Kwanza ninasikitika kuwaambia kwamba mtoto wenu Wayne hatoweza kutembea tena. Miguu yake pale ilipo ilikuwa imesagika kidogo. Katika kipindi chote tulikuwa tukiangaika nayo. Namshukuru Mungu kwamba tulifanikiwa kwa asilimia themanini kwani kama tungeshindwa kabisa, haina budi tungeikata miguu yake” Daktari aliwaambia.
Kila mmoja akaonekana kushtuka, maneno ambayo alikuwa ameyaongea daktari yalionekana kuwagusa kupita kawaida, walimwangalia daktari mara mbili mbili kana kwamba yeye ndeye ambaye alikuwa amesababisha yale yote.
“Ila tunashuru kwamba ni mzima” Bi Lydia alimwambia daktari.
“Jambo la pili ni kwamba tuligundua kwamba mtoto wenu amekatika mshipa mkubwa ambao unawezesha uume wake kusimama. Mshipa ule haufanyi kazi tena, kwa maana hiyo mtoto wenu hatoweza kusimamisha uume wake tena jambo ambalo halitoweza kumpa mtoto katika maisha yake yaliyobakia” Daktari aliwaambia.
Taarifa hiyo ndio ambayo ilionekana kumshtua zaidi kila mmoja. Wakamwangalia daktari kwa macho yaliyojawa na mshtuko, hawakuonekana
 
SEHEMU YA 22

kukiamini kile ambacho daktari alikuwa amekiongea mbele yao. Kwa mtoto wao Wayne kukosa uwezo wa kuwa na mtoto kulionekana kuwakosesha raha, waliyaona maisha yake kujaa giza huko mbeleni.
Hawakujua Wayne angeishi katika maisha gani, kutokutembea na kutokuwa na uwezo wa kusimamisha uume wake yalionekana kuwa matatizo makubwa ambayo yalikuwa yameupata mwili wake. Bi Lydia akashindwa kujizuia, akainamisha kichwa chake chini, alipokiinua, machozi yalikuwa yakimtoka.
Ni kweli kwamba walikuwa na mtoto mwingine, huyu alikuwa akiitwa Esther, lakini kwa upande wao walikuwa na mapenzi ya kweli kwa Wayne. Hata kama Esther angepata watoto kumi lakini furaha yao isingekamilika bila Wayne kutokuwa na mtoto.
Hawakujua ni kitu gani ambacho walitakiwa kukifanya, kukubaliana na matokeo yale ikaonekana kuwa kazi kubwa sana mioyoni mwao. Walichokifanya mara baada ya kutoka ndani ya hospitali ile ni kuanza kuwasiliana na madaktari waliokuwa wakubwa zaidi kutoka katika nchi mbalimbali.
Wayne akaanza kusafirishwa na kupelekwa katika nchi mbalimbali duniani kwa ajili ya kuangalia uwezekano wa kulitatua tatizo lile ambalo alikuwa nalo mwilini. Walitembea zaidi ya nchi kumi duniani tena kwa madktari mabingwa ambao walikuwa na uwezo mkubwa lakini kote huko hawakufanikiwa kabisa jambo lililowafanya kurudi nchini Marekani.
Wote wakakubaliana na matokeo. Wayne akaanza maisha mapya ya kuwa mlemavu wa miguu yake. Kila siku waandishi wa habari walikuwa wakielekea ndani ya nyumba hiyo na kuanza kuongea na Wayne ambaye siku zote hakuonekana kuwa na furaha.
Kitu ambacho alikuwa akitaka kuwaambia wazazi wake ni kuhusu Happy, msichana wa Kitanzania ambaye alimuacha akiwa mjauzito. Hakutaka kufanya haraka katika kuwaaambia hilo kwani aliamini kwamba ni lazima apate muda wa kutulia kabla ya kuongea kitu chochote kile.
Siku ziliendelea kukatika lakini Wayne hakuongea kitu chochote kile kwa wazazi wake. Kila siku alikuwa akijitahidi kutafuta njia mbalimbali za kumuwezesha kuwasiliana na Happy lakini ilishindikana kabisa. Miezi miwili ikakatika na ndipo hapo Wayne alipoamua kuwaita wazazi wake na kuanza kuongea nao.
“Nahitaji kwenda Tanzania” Wayne aliwaambia.
“Kuna nini?”
“Hapana. Ninahitaji tu kwenda Tanzania” Wayne aliwaambia.
“Hali yako si nzuri kusafiri masafa marefu. Tuambie kitu chochote kijana wetu tutakufanyia ila si kukuruhusu kuelekea nchini Tanzania” Bwana Brown alimwambia Wayne.
“Maisha yangu yametawaliwa na majonzi, kila siku nilikuwa nikikaa nikimfikiria msichana mmoja ambaye nilikutana nae katika mazingira ya kutatanisha na kumfanyia kitu ambacho kimekaa na kuniumiza moyoni” Wayne alisema huku akianza kulengwa na machozi.
Kila mmoja alikuwa kimya akimwangalia Wayne, maneno ambayo aliyaongea yalikuwa yamewagusa mioyoni mwao lakini pia yalikuwa yamewachanganya kupita kiasi. Wayne akaonekana kuwa na kitu kizito ambacho alikuwa akitaka kuwaambia kwa wakati huo.
“Unatuchanganya” Bwana Brown alimwambia.
“Nafahamu kama mmechanganyikwa na maneno yangu ila ninahitaji kwenda nchini Tanzania kuonana na Happy” Wayne aliwaambia. Wote wakaonekana kushtuka zaidi.
“Happy! Ndiye nani huyo?” Bi Lydia aliuliza kwa mshtuko.
“Msichana niliyemuacha akiwa na ujauzito wangu” Wayne alijibu.
Kwa mshtuko ambao walikuwa wameupata mioyoni mwao, walijihisi kwamba muda wowote ule wangeweza kuzimia. Maneno yale yaliwachanganya zaidi kuliko hata maneno mengine ambayo walikuwa wameyasikia kutoka kwa Wayne.
Wakamwangalia Wayne na kuanza kumsoma saikolojia yake kuona kwamba alikuwa akitania au alikuwa akimaanisha kile ambacho alikuwa akikiongea.
 
SEHEMU YA 23

Wayne alionekana kumaanisha. Jina la Happy ndilo ambalo lilizua mjadala mkubwa vichwani mwao, wakatamani kumfahamu huyo Happy, mbali na huyo, pia walitaka kufahamu kuhusu huo ujauzito.
“Umesemaje?” Bwana Brown aliuliza huku akionekana kuwa na mshtuko uliojaa furaha.
Hapo ndipo Wayne akaanza kuwaadithia kila kitu ambacho kilikuwa kimetokea katika safari yake ya kwanza ya kitalii kuelekea nchini Tanzania miaka sita iliyopita. Hakuficha kitu chochote kile, alikuwa wazi kwa kila kitu ambacho alikuwa amekifanya kipindi kile.
Bwana Brown na mkewe, Bi Lydia wakaonekana kushtuka kwa furaha, hawakuamini kama kijana wao alikuwa na uwezekano wa kuwa na mtoto ambaye alikuwa nchini Tanzania. Wakajikuta wakisimama na kukumbatiana, machozi ya furaha yakaanza kuwatoka.
“Msifurahi kwa sasa mpaka pale ambapo mtakapomuona mtoto wangu mbele ya macho yenu. Hamuwezi kujua kwamba labda Happy alipata matatizo na mimba kutoka au hata mtoto kufariki” Wayne aliwaambia.
“Ni lazima nisafiri kuelekea huko Tanzania. Ni lazima nikamchukue mjukuu wangu” Bwana Brown alisema huku akionekana kuwa na furaha.
“Nami pia ninataka kwenda huko. Ninataka kumuona mjukuu wangu” Wayne aliwaambia.
“Wewe pumzika nyumbani. Tutakwambia kila kitu kitakachojili” Bwana Brown alimwambia Wayne.
Hakukuwa na cha kuchelewa, kwa haraka haraka viza zikaandaliwa na baada ya siku mbili safari ikaanza. Ndani ya ndege, Bwana Brown na mkewe, Bi Lydia walikuwa wakizungumzia kuhusu mtoto huyo ambaye walikuwa wakielekea kumuona nchini Tanzania.
Sala zao bado zilikuwa zikiendelea mioyo mwao kwa kumuomba Mungu awe Amemlinda mtoto yule mpaka katika kipindi ambacho watamchukua na kumpeleka kwa baba yake. Waliiona ndege ikienda kwa mwendo wa taratibu sana, walitamani wapotee kama wachawi na kujikuta ndani ya nyumba hiyo ambayo walikuwa wameelekezwa.
Mara baada ya ndege kutua katika uwanja wa Mwl Julius Nyerere, wakatoka nje ambako wakaomba kupelekwa katika ofisi za shirika la ndege la Precious Airlines na kukata tiketi ya ndege tayari kwa ajili ya kuelekea jijini Arusha.
Kutokana na kutokuwa na wasafiri wengi siku hiyo, wakapata ndege na saa tisa jioni safari ikaanza. Walichukua dakika arobaini na tano mpaka ndege kuanza kutua katika uwanja wa KIA ambapo wakaanza kuelekea katika moja ya hoteli ya nyota tano ya Jupiter iliyokuwa hapo Arusha.
Wakapata chumba na kutulia. Wakatoa ramani ambayo walikuwa wamechorewa na Wayne na kisha kuanza kuiangalia vizuri. Kila mmoja akaonekana kuridhika, ramani ya kuelekea nyumbani kwa Bi Selina ilionekana kueleweka vichwani mwao.
Siku iliyofuata asubuhi na mapema safari ya kuelekea nyumbani kwa shangazi yake Happy, Bi Selina ikaanza. Walikuwa wakiifuatilia ramani ile kama jinsi ilivyokuwa imeelekeza. Walipata tabu sana kutokana na nyumba nyingi kujengwa na hata mazingira kuwa tofauti sana, mwisho wa siku wakafanikiwa kuiona nyumba hiyo.
Wakaanza kuugonga mlango na baada ya muda fulani, mwanamke mmoja aliyekuwa na nywele zilizoanza kupatwa na mvi akafungua mlango, alikuwa Bi Selina. Wakajitambulisha kwake, wakaonekana kueleweka.
“Mmmhh!”
“Mbona umeguna?” Bwana Brown aliliza.
“Sidhani kama Happy atakubali kuonana nanyi” Bi Selina aliwaambia.
Hapo ndipo walipoanza safari ya kuelekea Machame. Njia nzima Bwana Brown na mkewe walikuwa wakijitahidi kuuliza maswali mengi kuhusu
 
SEHEMU YA 24

mjukuu wao lakini Bi Selina hakutaka kujibu chochote kile. Wakaingia ndani ya daladala, Bwana Brown hakujali kama alikuwa tajiri mkubwa, kitu ambacho alikuwa akikijali kwa wakati huo ni kumuona mjukuu wake tu.
Wakaanza kuingia katika eneo la nyumba ya mzee Lyimo. Bi Selina akaanza kuufuata mlango na kisha kuugonga, baada ya muda, Bi Vanessa akaufungua mlango ule. Wazungu ambao walikuwa wakionekana mbele yake hakuwa akiwafahamu lakini akaonekana kuhisi kitu fulani. Baada ya salamu, akawakaribisha ndani.
Maongezi yakaanzia hapo huku nae mzee Lyimo akiwa pembeni. Bwana Brown alijitahidi kujielezea kwamba alikuwa nani na alikuwa amefuata kitu gani mahali hapo. Hakukuwa na mtu ambaye alikuwa amemuelewa, walionekana kupinga kupita kawaida.
Kila walipokuwa wakikumbuka siku ambayo Wayne alikuwa amekuja hapo na kisha kuondoka kwa hasira mara baada ya kuambiwa kwamba Happy alikuwa mjauzito waliona hakukuwa na sababu za kuwakubalia ombi lao.
“Amechukua miaka sita na huu unakwenda kuwa mwaka wa saba, hajawahi kumjulia hali mtoto wake, mbaya zaidi alikataa mimba na kusema kwamba si ya kwake, iweje leo anakuja kudai mtoto? Hata kama ni mahakamani tutakwenda lakini Andy atabaki kuwa kwetu” Mzee Lyimo aliwaambia huku akionekana kukasirika.
Hapo ndipo Bwana Brown alipoanza kuelezea kila kitu ambacho kilikuwa kimtokea katika maisha ya Wayne toka katika kipindi kile alichokuwa amepata ajali na kulazwa kitandani kwa muda wa miaka sita. Wote wakaonekana kushtuka, hasira ambazo walikuwa nazo zikaonekana kupotea.
“Hapo alipo hawezi hata kutembea. Na kamwe hatoweza kutembea katika maisha yake” Bwana Brown aliwaambia.
“Furaha pekee ambayo imebaki kwake ni kumuona mtoto wake tu. Nafikiri ataweza kufanya jambo lolote baya kama tu hatutarudi na kile ambacho amekitarajia” Bi Lydia aliwaambia.
Habari za kupata ajali kwa Wayne zikaonekana kuwa mpya kwao, ni kweli kwamba Wayne alikuwa ameikataa mimba ile lakini katika upande wao mwingine wa moyo walijua kwamba kama asingepata ajali basi angekuwa amekwishafika nyumbani hapo siku nyingi.
Alichokifanya Bi Vanessa ni kuinuka na kuelekea chumbani kwa Happy ambaye alikuwa amelala. Ile kuufungua mlango, Andy akatoka huku akikimbilia pale sebuleni na kumfuata mzee Lyimo na kuishika miguu yake.
“Babu atata mma” Andy alisema katika lafudhi ya kitoto.
Bwana Brown na mkewe hawakuamini mara macho yao yalipotua kwa Andy. Andy alikuwa amefanana kwa kila kitu na mtoto wao, Wayne. Wote wakaonekana kufarijika, wakajikuta wakitokwa na machozi ya furaha.
“Ndiye yeye. Mwangalie alivyofanana na baba yake” Bi Lydia alisema huku akitamani kumfuata Andy na kumkumbatia.
Wala hazikupita dakika nyingi, Happy akatokea sebuleni hapo akiongozana na mama yake. Macho yake yakatua kwa Bwana Brown na Bi Lydia ambao macho yao bado yalikuwa yakimwangalia Andy. Alichokifanya Happy ni kumfuata mtoto wake, Andy kumchukua na kumpakata.
Mazungumzo yakaanza upya, walielezea kila kitu ambacho kilikuwa kimetokea katika maisha ya Andy mara baada ya kuondoka nchini Tanzania na kuelekea nchini Marekani. Tofauti na matarajio yao, Happy alikuwa akitabasamu muda wote ambao alikuwa akielezewa kuhusu Wayne.
“Hayo ndio malipo. Hivyo ndivyo Mungu alivyotaka iwe. Andy ni mtoto asiyekuwa na baba. Nafikiri huyo Wayne ambaye amewatuma mje kumchukua si yule Wayne ambaye nini baba yake. Kama mlivyokuja na ndivyo ninavyotaka muondoke. Mtakapomuona, naomba mmwambie kwamba baba
 
SEHEMU YA 25

yake Andy alikwishafariki hata kabla Andy hajazaliwa. Mtakapoona haelewi naomba mmwambie kwamba Andy alifariki kwa ugonjwa wa Tete kuwanga ambao ulikuwa umemsumbua sana utotoni” Happy alisema.
Bila kutarajia, Happy akajikuta akianza kutokwa na machozi, uwepo wa Bwana Brown na mkewe ulionekana kumkumbusha mbali sana tangu kipindi cha kwanza ambacho alikutana na Andy. Kamwe hakutaka kumuona mwanaume huyo, alikuwa akimchukia kupita kiasi. Ilikuwa ni afadhali kukutana na shetani angempenda kuliko kukutana na mwanaume ambaye alikuwa ameikimbia mimba yake.
“SITAKI KUONANA NAE WALA MTOTO WANGU KWENDA POPOTE” Happy alisema na kisha kuingia chumbani kwake pamoja na mtoto wake, Andy.
Walijaribu kuugonga mlango lakini wala mlango haukufunguliwa. Bwana Brown na mkewe wakakaa mahali hapo huku wakimtaka mzee Lyimo na Bi Vanessa waongee na Happy lakini hilo nalo halikuwezekana kwani Happy alikuwa amejifungia mlango na wala hakukuwa na dalili za kuufungua.
“NIMESEMA SITAKI....SITAKI....SITAKI......SITAKI...”Sauti ya Happy ilisikika kwa nguvu masikioni mwao.

Hakukuwa na mtu ambaye aliamini kama kweli Happy alikuwa amemaanisha kile ambacho alikuwa amekisema. Waliendelea kuugonga mlango lakini wala Happy hakuufungua, bado aliendelea kujifungia. Bwana Brown na mkewe bado walikuwa wamesimama mlangoni huku wakimtaka Happy kufungua mlango lakini bado Happy alikuwa king’ang’anizi, hakufungua mlango.
Walisimama mlangoni kwa zaidi ya nusu saa lakini hali haikuonekana kubadilika. Walichokifanya mara baada ya kuona Happy amekataa katakata kuufungua mlango ni kuaga mahali hapo na kurudi hotelini. Usiku hawakulala, vichwa vyao vilikuwa vikifikiria kuhusu mjukuu wao, Andy Ryn. Huyo ndiye alikuwa mtu pekee ambaye walikuwa wakimhitaji na kwenda nae nchini Marekani mpaka kwa baba yake.
Kutokuondoka na Andy kwenda nae Marekani waliona ingeweza kuleta tatizo fulani katika maisha ya baba yake, Wayne. Iliwabidi kupigana mpaka kufanikiwa, hata ikiwezekana kwa njia zisizokuwa za uhalali ili mladi tu Andy awe mikononi mwao.
Vichwa vyao vilikuwa vikisumbuka usiku kucha lakini hawakupata jibu juu ya kile ambacho walitakiwa kukifanya. Kwa wakati huo mioyo yao ilikuwa na furaha kumuona Andy lakini waliona furaha yao isingekamilika kama tu wasingerudi nchini Marekani pamoja na Andy.
“So what should we do? (Kwa hiyo tufanye nini?)” Bi Lydia aliuliza.
“Lets kidnap him (Tumteke)” Bwana Brown alijibu huku akionekana kumaanisha kile ambacho alikuwa amekisema.
“Do you think this is good idea? (Unafikiri hili ni wazo zuri?)”
“Things are not like we expected before. Everything goes wrong (Mambo hayapo kama tulivyotegemea. Kila kitu kinakwenda sivyo)” Bwana Brown alisema.
“I dont think if this is good idea. How can you kindnap your grandchild? (Sidhani kama hili ni wazo zuri. Utamteka vipi mjukuu wako?)” Bi Lydia alisema.
Wazo ambalo alikuwa amelitoa Bwana Brown lilionekana kutokumuingia akilini kabisa Bi Lydia, hakuona kama ilistahili Andy atekwe na kupelekwa nchini Marekani. Kitu ambacho alikuwa akikifikiria yeye ni maisha ya baadae hasa mara baada ya Andy kuja kuujua ukweli na kuambiwa kwamba alitekwa.
“Hapana mume wangu. Tutumie fedha” Bi Lydia alitoa wazo.
“Kivipi?”
“Kazi rahisi sana. Ninachoamini ni kwamba Happy anawasikiliza sana wazazi wake hata kama wakisema kitu gani. Kwa jinsi hali nilivyoiona, wazazi wale hawatotusaidia kwa nguvu zote, cha msingi tutumie fedha” Bi Lydia alielezea wazo lake.
 
SEHEMU YA 26

Ingawa mara ya kwanza lilionekana kuwa si wazo zuri kichwani mwa Bwana Brown lakini baadae akaliona kufaa sana. Walichokifanya siku iliyofuata ni kwenda nyumbani kwa mzee Lyimo, siku hiyo hawakutaka kabisa kuzungumzia kuhusu kumchukua Andy, siku hiyo walikuwa wakizungumzia namna ya kupatengeneza eneo hilo.
“Tumejifikiria sana, tena usiku kucha. Mjukuu wetu tumeamua kumuacha hapa hapa ili aendelee kupata malezi ya mama yake. Ila tunachokitaka ni kumtengenezea maeneo mazuri ya kukaa, kamwe hatutoweza kuacha eneo hili namna hii” Bwana Brown alisema maneno ambayo yalionekana kumfurahisha kila mtu, hata Happy mwenyewe.
Kiasi cha shilingi milioni hamsini kikatolewa na kisha ujenzi wa nyumba kubwa kuanza. Mafundi wakubwa waliokuwa na uwezo mkubwa wakaitwa mahai hapo na kisha kazi ya ujenzi kuanza. Kazi haikuwa ndogo hata mara moja, nyumba kubwa na ya kisasa ikaanza kutengenezwa.
Kwa mwaka huo wa 1996, kiasi cha shilingi milioni hamsini kilikuwa ni kiasi kikubwa sana cha fedha. Huku ujenz wa nyumba ile ukiendelea, Bwana Brown na mkewe, Bi Lydia wakaaga na kurudi nchini Marekani huku kila kitu kuhusu nyumba kikiwa kimetolewa na huku wakiwa wameacha kiasi cha shilingi milioni mia moja kwa ajili ya matumizi.
Mzee Lyimo na familia yake walionekana kushukuru kupita kawaida, kwao Andy alionekana kuwa na faida kubwa kiasi ambacho wakabaki wakimshukuru Mungu kwa hatua aliyoichukua Happy kuzaa na Wayne.
Kuanzia hapo, kazi kubwa ya mzee Lyimo na mkewe, Bi Vanessa ilikuwa ni kumbembeleza Happy akubali lile ambalo Bwana Brown na Bi Lydia walikuwa wakilitaka, kuondoka na Andy. Happy alikataa katakata, ila mwisho wa siku akajikuta akikubali ila kwa sharti na yeye kusafiri ili asikae mbali na mtoto wake.
Nchini Marekani, Wayne hakuwa na furaha hata kidogo, kitendo cha wazazi wake kurudi pasipo kuwa na mtoto wake, Andy kilimkosesha amani kabisa. Wayne hakutaka kukubali hata mara moja, moyoni aliamini kama angekwenda yeye mwenye nchini Tanzania basi kazi isingekuwa kubwa, ni lazima angerudi na mtoto wake.
Baada ya wiki mbili, Wayne akaanza safari pamoja na wazazi wake kwenda nchini Tanzania. Ndani ya ndege kiu yake ilikuwa ni kumuona mtoto wake ambaye alikuwa damu yake yeye mwenyewe. Walipofika jijini Dar es Salaam wakachukua ndege na kuelekea jijini Arusha.
Muda wote huo Wayne alikuwa na kiu kubwa ya kumuona mtoto wake ambaye alimuona kuwa wa thamani kuliko kitu chochote kile katika maisha yake. Wakafika Arusha na kuchukua vyumba hotelini huku Wayne akiendelea kuwa katika kibaiskeli chake cha walemavu.
Siku iliyofuata safari ya kuelekea Machame ikaanza. Nyumba kubwa na ya thamani ilikuwa imejengwa kiasi ambacho ilionekana kutokuwa na hadhi kubwa ya kujengwa nchini Tanzania. Magari mawili yalikuwa katika eneo hilo huku trekta kubwa likiwa limepaki pembeni kabisa, fedha zile zilizokuwa zimeachwa zilionekana kuyabadilisha maisha yao.
Wakati Bwana Brown na familia yake wanaingia ndani ya eneo la nyumba ile, walipokelewa kwa mapokezi makubwa. Happy hakuamini macho mara baada ya kumuona Wayne. Japokuwa mwanaume huyo alikuwa amemfanyia mambo mengi mabaya lakini akaonekana kuanza kuyasahau yote.
Akaanza kupiga hatua na kumfuata Wayne, alipomfikia, akamkumbatia. Wayne akashindwa kujizuia, akaanza kumuomba msamaha Happy huku akilia kama mtoto kiasi ambacho kilionyesha kwamba alikuwa akijutia kile ambacho alikuwa amekifanya maishani mwake miaka sita iliyopita.
 
SEHEMU YA 27

“Nimekusamehe” Happy alisema huku akijifuta machozi yake.
Andy akaletwa mahali hapo, Wayne akatamani kusimama, akaanza kukisukuma kibaiskeli chake na kumkumbatia Andy. Hakuamini kama tayari alikuwa ameiona damu yake, machozi yalizidi kuongezeka machoni mwake, kumuona Andy kulimpa faraja kuu maishani mwake.
Siku hiyo ilionekana kuwa siku ya furaha kuliko zote katika maisha ya Wayne, muda wote Andy alikuwa pembeni yake. Hakutaka kumuachia kwani aliona kama angemwacha aende kwa mtu mwingine basi asingerudi tena mikononi mwake.
Happy hakutaka kukumbuka maisha ambayo yalikuwa yamepita, alipanga maisha yajayo pamoja na mwanaume ambaye alikuwa aemkimbia miaka ya nyuma, Wayne. Kila kitu kilichokuwa kimepita kilionekana kuwa kama historia, alitakiwa kukisahau na kuanza kuandika historia nyingine.
Baada ya wiki mbili, safari ya kurudi nchini Marekani ikaanza, japokuwa walikuwa wamekuja watatu lakini kurudi walikuwa wakirudi watano, yaani Happy pamoja na Andy.
“Nitatumia fedha zangu zote, uwezo wangu wote mpaka mtoto wangu anafanikiwa” Wayne aliwaambia wazazi wake.
“Usijali. Tutakuwa pamoja nawe katika kila hatua utakayopitia” Bwana Brown alisema na kisha wote kukumbatiana.
****
Maisha mapya yakaanza nchini Marekani huku Wayne na Happy wakiishi kama mume na mke. Mapenzi yao yakarudi, wawili hao walionekana kupendana na kujaliana katika kila hali. Happy hakuangalia matatizo aliyokuwa nayo Wayne ya ulemavu au ya kutokusimamisha, ila kitu ambacho alikuwa akikiangalia ni mapenzi ya kweli.
Kila siku walikuwa na furaha kupita kawaida mpaka katika kipindi ambacho Andy alipoanzishwa katika shule ya St’ Augustine iliyokuwa Woodmere hapo hapo jijini New York. Shule hii ndio ambayo ilikuwa ikiongoza kusomwa na watoto waliotoka katika familia ya kitajiri jijini New York.
Wanafunzi wengi ambao walikuwa wakisoma katika shule hiyo walikuwa wazungu kitu ambacho kilisababisha wengi kumshangaa Andy ambaye alikuwa na mchanganyiko wa rangi. Ingawa wanafunzi weusi hawakuwa wengi katika shule hiyo lakini Andy alionekana kuwa tofauti kwao.
Masomo yakaanza kama kawaida, katika kipindi cha kwanza Andy alikuwa mgumu kuelewa kutokana na lugha ambayo ilikuwa ikitumika ila baada ya kukaa kwa miezi sita, akaanza kuelekewa kila kitu. Hapo ndipo ukali wake ulipoanza kuonekana.
Andy alionekana kuwa na uwezo mkubwa sana, alikuwa ni mtoto mwepesi kuelewa na alikuwa mtoto mgumu sana kusahau. Uwezo huo ndio ambao uliwafanya walimu kuanza kuona kitu cha tofauti, Andy alionekana kuwa mtoto wa ajabu.
Muda mwingi ambao alikuwa shuleni hapo, Andy alikuwa akipendelea kukaa karibu na wadudu. Wadudu ndio walikuwa sehemu ya maisha yake na kama ikatokea siku akamuona mdudu akiwa amekufa, siku hiyo haikuwa ya amani katika maisha yake.
Uwezo wake mkubwa ndio ambao uliwapelekea walimu kumpandisha darasa, alionekana kuwa mbele ya darasa lile ambalo alikuwa akilisoma. Huko alipopelekwa napo alikuwa moto mkali. Kila siku alikuwa akiongoza darasani, haikujalisha kama ilikuwa jaribio la kawaida au mtihani.
Andy hakuwa msomaji kabisa na wala haikuwahi kutokea hata siku moja kushika daftari kusoma. Muda mwingi shuleni alikuwa akishinda akiwaangalia wadudu. Hakujali alikuwa sehemu gani, hata kama alikuwa darasani, alikuwa akienda na kichupa ambacho kilikuwa na wadudu ndani yake.
Mara kwa mara Happy na Wayne walikuwa wakiitwa shuleni na kuambiwa kuhusu mtoto wao, wote walikuwa wakijivunia kupata mtoto ambaye alikuwa na uwezo mkubwa kama Andy. Miaka ikaendelea kukatika na ndipo Happy na
 
SEHEMU YA 30

Wayne wakaamua kufunga ndoa katika kanisa la St’Thabita lililokuwa Marrtson nje kidogo mwa jiji la New York.
Mapenzi yao yalikuwa makubwa, walikuwa wakiheshimiana kama mke na mume japokuwa Wayne hakuwa na uwezo wowote wa kufanya kazi kitandani. Happy hakutaka kuliangalia tatizo hilo, kitu ambacho alikuwa akikiangalia ni mapenzi ya kweli kwake.
Hali ile ikaanza kumuweka Wayne katika wakati mbaya, muda mwingi alikuwa akionekana kuwa na mawazo. Moyoni alitamani sana kufanya mapenzi na mke wake ila hakuwa na uwezo huo. Wayne alionekana kuwa kama kwenye msiba, alikuwa na kila kitu ambacho alikuwa akikihitaji katika maisha yake.
“Inatubidi tutumie uume wa bandia” Wayne alitoa wazo.
“Wa nini?”
“Kukusaidia mke wangu. Unajua hali hii inaniumiza sana, wakati mwingine najiona kama sitakiwi kuwa pamoja nawe, yaani najiona kutokuwa mwanaume mwenye sifa za kuwa na mwanamke mzuri kama wewe” Wayne alimwambia Happy.
“Haiwezekani. Siwezi kufanya mapenzi na uume wa bandia. Kama hali yako itaendelea milele, acha nami niwe hivi milele” Happy alimwambia Wayne.
Hivyo ndivyo walivyokuwa wakiishi. Kila siku walikuwa wakiangalia mikanda ya ngono huku Wayne akitaka kuona kama alikuwa na mabadiliko yoyote lakini bado hali ilikuwa vile vile. Kila kitu ambacho walikuwa wakikifanya hakikuwa kikiwasaidia.
Bado walikuwa wakiendelea kwenda katika mahospitali makubwa duniani kutafuta tiba lakini bado hali iliendelea kuwa vile vile. Ikafika kipindi wote wakaonekana kukata tamaa jambo ambalo liliwafanya kutulia na kusubiri muujiza wa Mungu.
Miaka ikakatika mpaka kufika kipindi ambacho Andy akaingia High School. Kwa sababu alikuwa akipenda sana wadudu, akaamua kuchagua somo la Bailojia liwe kama kichwa katika masomo yake aliyokuwa ameyachagua.
Kadri siku zilivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo uwezo wake darasani ulivyozidi kuongezeka. Alikuwa akifahamu mambo mengi kuhusu wadudu na hata sumu ambazo zilikuwa zikiwaua wadudu kwa muda mchache sana.
Andy akaona hiyo haitoshi, hapo ndipo alipoamua kuanza kuufuatilia mwili wa mwanadamu na jinsi damu ilivyokuwa ikifanya kazi kubwa mwilini. Hakuishia hapo bali vile vile akaanza kutafuta sababu ambazo zilikuwa zikimfanya binadamu kufa katika kipindi ambacho mwili wake ulikuwa ukiwekewa sumu fulani.
Katika kila kitu ambacho Andy alikuwa akijiuliza akaanza kupata jibu hali iliyoifanya akili yake kukua zaidi na zaidi. Ubora wake katika masomo ukaongezeka zaidi. Wanafunzi shileni hapo walikuwa wakizidi kumuogopa Andy ambaye toka ameanza masomo shuleni hapo hakuwa kushika namba zaidi ya namba moja.
Mwaka huu ndio ambao ulikuwa wa mwisho kabla kumaliza elimu ya juu kabla ya kuanza chuo. Katika maisha yake yote yote, Andy alikuwa akihofia sana kujiingiza katika mahusiano. Shuleni kulikuwa na wasichana wengi ambao walikuwa wakitamani sana kuwa na uhusiano na Andy lakini jambo hilo lilionekana kuwa gumu.
Maishani mwake alijifunza mengi kuhusiana na mahusiano ya kimapenzi, alikwishawahi kuwaona watu wakilia usiku na mchana huku wengine wakianza kuzichukia jinsia ambayo ilikuwa imemsababishia maumivu makali moyoni mwake, aliyachukia mapenzi na kamwe hakutaka kujiingiza katika mahusiano.
“Kamwe siwezi kupenda” Andy aliwaambia marafiki zake.
“Kwa nini?” Bruce aliuliza.
“Naogopa nitaua. Yaani sitaki kupenda kwa sababu nitaua” Andy alimwambia.
“Utaua! Kivipi?”
“Unafikiri nikipenda halafu nikasalitiwa, nitamuacha hai mtu aliyeuumiza moyo wangu?”
“Lakini si unajua kuna usahaulifu. Unachokifanya ni kuachana nae na kisha kutafuta mwingine” Bruce alimwambia.
 
Back
Top Bottom