Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA 17
akakaa kitandani na kuanza kuongea nae. Moyo wa mzee Lyimo ulimuuma zaidi, kamwe hakutarajia kama mzungu Wayne angeweza kuikataa mimba ile.
“Haiwezekani. Ameikataa?” Mzee Lyimo aliuliza huku akionekana kutokuamini.
“Ndio. Ameikataa” Happy alijibu.
Mzee Lyimo akasimama na kutoka nje ya chumba kile. Akauona mwili wake ukiwa umekufa ganzi kabisa. Hakuaamini kile ambacho alikuwa amekisikia kutoka kwa Happy, alitamani akutane na Wayne na kuongea nae ili aone kama alikuwa na ujasiri wa kuukataa ule ujauzito mbele ya macho yake.
Baada ya hapo, maisha ya Happy yakaendelea kama kawaida ingawa muda mwingi alikuwa akitawaliwa na huzuni. Alikuwa akijitahidi kula vyakula vizuri ambavyo vilikuwa vikimpa afya bora yeye pamoja na mtoto.
Mara kwa mara alikuwa akihudhuria kliniki kama ambavyo madaktari walivyotaka afanye. Kamwe hakulala katika kitanda kisichokuwa na neti, alikuwa akiyalinda maisha yake na ya mtoto wake ambaye alikuwa tumboni.
Ingawa ilikuwa ni vigumu sana lakini akaamua kujisahaulisha kuhusu Wayne, akaamua kuishi maisha yake peke yake, hakutamani kabisa kumuona Wayne mbele ya macho yake, alionekana kumchukia kuliko kiumbe chochote duniani.
Miezi tisa ikatimia na ndipo Happy akajifungulia shambani katika kipindi ambacho alikuwa akilima pamoja na wazazi wake hatua iliyowapelekea kumpeleka hospitalini.
Happy alikuwa amelala juu ya kitanda ndani ya chumba kimoja katika hospitali ya KCMC iliyokuwa Moshi mjini. Bado hakuwa ameongea kitu chochote kile. Dripu moja baada ya nyingine zilikuwa zikiingiza maji katika mishipa yake.
Happy alikuja kufumbua macho yake baada ya masaa nane kupita. Akayapeleka macho yake huku na kule, yakatua katika nyuso za wazazi wake. Tabasamu likaanza kuonekana usoni mwake. Mzee Lyimo na Bi Vanessa wakaanza kupiga hata kumfuata.
“Mtoto wangu yuko wapi?” Happy aliuliza kwa sauti ya chini.
“Kimaro. Tulikuja nae hapa. Amewekwa katika chumba maalumu” Mzee Lyimo alijibu.
“Silitaki jina hilo baba. Sitaki mtoto wangu aitwe Kimaro” Happy alisema kwa sauti ya chini.
“Sawa binti yangu. Unataka aitwe nani?”
“Aitwe Andy” Happy alijibu.
“Kwa hiyo aitwe Andy Wayne?”
“Hapana. Aitwe Andy Ryn. Hili ni jina la babu yake. Sitaki achukue jina la baba yake” Happy alisema.
Hicho ndicho kilichoamuliwa. Jina likawa limekwishapatikana. Baada ya siku mbili, Happy akaruhusiwa kurudi nyumbani. Kila wakati alikuwa pembeni ya mtoto wake, watu mitaani walikuwa wakishangaa namna mtoto yule alivyokuwa mweupe.
Afya yake ilikuwa bora hata zaidi ya watoto wengine ambao walikuwa wamezaliwa mitaani hapo. Happy alimthamini sana mtoto wake hata zaidi ya alivyojithamini yeye mwenye. Miezi ikakatika, Andy Ryn akaanza kujifunza kutembea.
Katika kila hatua ambayo alikuwa akiifikia, Happy alionekana kuwa na furaha.
akakaa kitandani na kuanza kuongea nae. Moyo wa mzee Lyimo ulimuuma zaidi, kamwe hakutarajia kama mzungu Wayne angeweza kuikataa mimba ile.
“Haiwezekani. Ameikataa?” Mzee Lyimo aliuliza huku akionekana kutokuamini.
“Ndio. Ameikataa” Happy alijibu.
Mzee Lyimo akasimama na kutoka nje ya chumba kile. Akauona mwili wake ukiwa umekufa ganzi kabisa. Hakuaamini kile ambacho alikuwa amekisikia kutoka kwa Happy, alitamani akutane na Wayne na kuongea nae ili aone kama alikuwa na ujasiri wa kuukataa ule ujauzito mbele ya macho yake.
Baada ya hapo, maisha ya Happy yakaendelea kama kawaida ingawa muda mwingi alikuwa akitawaliwa na huzuni. Alikuwa akijitahidi kula vyakula vizuri ambavyo vilikuwa vikimpa afya bora yeye pamoja na mtoto.
Mara kwa mara alikuwa akihudhuria kliniki kama ambavyo madaktari walivyotaka afanye. Kamwe hakulala katika kitanda kisichokuwa na neti, alikuwa akiyalinda maisha yake na ya mtoto wake ambaye alikuwa tumboni.
Ingawa ilikuwa ni vigumu sana lakini akaamua kujisahaulisha kuhusu Wayne, akaamua kuishi maisha yake peke yake, hakutamani kabisa kumuona Wayne mbele ya macho yake, alionekana kumchukia kuliko kiumbe chochote duniani.
Miezi tisa ikatimia na ndipo Happy akajifungulia shambani katika kipindi ambacho alikuwa akilima pamoja na wazazi wake hatua iliyowapelekea kumpeleka hospitalini.
Happy alikuwa amelala juu ya kitanda ndani ya chumba kimoja katika hospitali ya KCMC iliyokuwa Moshi mjini. Bado hakuwa ameongea kitu chochote kile. Dripu moja baada ya nyingine zilikuwa zikiingiza maji katika mishipa yake.
Happy alikuja kufumbua macho yake baada ya masaa nane kupita. Akayapeleka macho yake huku na kule, yakatua katika nyuso za wazazi wake. Tabasamu likaanza kuonekana usoni mwake. Mzee Lyimo na Bi Vanessa wakaanza kupiga hata kumfuata.
“Mtoto wangu yuko wapi?” Happy aliuliza kwa sauti ya chini.
“Kimaro. Tulikuja nae hapa. Amewekwa katika chumba maalumu” Mzee Lyimo alijibu.
“Silitaki jina hilo baba. Sitaki mtoto wangu aitwe Kimaro” Happy alisema kwa sauti ya chini.
“Sawa binti yangu. Unataka aitwe nani?”
“Aitwe Andy” Happy alijibu.
“Kwa hiyo aitwe Andy Wayne?”
“Hapana. Aitwe Andy Ryn. Hili ni jina la babu yake. Sitaki achukue jina la baba yake” Happy alisema.
Hicho ndicho kilichoamuliwa. Jina likawa limekwishapatikana. Baada ya siku mbili, Happy akaruhusiwa kurudi nyumbani. Kila wakati alikuwa pembeni ya mtoto wake, watu mitaani walikuwa wakishangaa namna mtoto yule alivyokuwa mweupe.
Afya yake ilikuwa bora hata zaidi ya watoto wengine ambao walikuwa wamezaliwa mitaani hapo. Happy alimthamini sana mtoto wake hata zaidi ya alivyojithamini yeye mwenye. Miezi ikakatika, Andy Ryn akaanza kujifunza kutembea.
Katika kila hatua ambayo alikuwa akiifikia, Happy alionekana kuwa na furaha.